AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 0%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi: Ali ibn al - Husayn Imam Zaynul al - Abidin (a.s.)
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 18401
Pakua: 2896

Maelezo zaidi:

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18401 / Pakua: 2896
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

8

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 45

ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KUUAGA MWEZI WA RAMADHANI

Oh Allah! Ewe ambaye hapendi alipwe, Ewe ambaye hajutii kwa sababu ya kutoa. Ewe ambaye hamlipi mja wake sawa kwa sawa. Huruma zako ndio mwanzo, Msamaha wako ni ufadhili, Adhabu yako ni uadilifu, Hukumu yako ni uchaguzi mwema. Ukitoa huutii doa utowaji wako kwa masimbulizi. Ukiziwiya (kutoa) hauwi uziwiyaji wako uchokozi. Wamshukuru anayekushukuru na wewe ndiye uliyempa ilhamu ya kushukuru wamlipa mwenye kukuhimidi na wewe ndiye uliyemfundisha kukuhimidi wamsitiri ambaye lau ungependa ungemfedhehesha. Wamfanyia hisani ambae lau ungependa ungemnyima. Wote hao wawili wastahiki kutoka kwako fedheha na kunyimwa, isipokuwa wewe umefanya msingi wa matendo yako kufadhili. Umepitisha uwezo wako katika msamaha. Umemlaki aliye kuasi kwa huruma umempa muhula mwenye kukusudia kujidhulumu nafsi yake. Unawangoja kurejea kwa saburi yako. Unaacha kuwa harakia kwenye toba ili mwangamiaji asije angamia kwa sababu yako mwenye kuangamia miongoni mwao. Na asije kuwa na hali mbaya kwa neema zako mwenye hali mbaya wao isipokuwa kwa ajili ya udhuru wako mrefu kwake, na baada ya mfululizo wa hoja dhidi yake. Ikiwa ni ukarimu wa msamaha wako Ewe Mkarimu! Na ni tendo la huruma Ewe mpole. Wewe ndie uliyefungua mlango wa msamaha wako kwa waja wako, na umeuita "TOBA" na umeweka juu ya mlango huo dalili kwa ufunuo wako ili wasiupotee ndipo ulisema - jina lako limebarikiwa: (Tubuni kwa Mungu toba isiyo ya kurudi nyuma huwenda Mola wenu akakuondoleeni maovu yenu na akakuingizeni katika Jannah ambazo chini yake mito yatiririka. Siku ambayo Mungu hatomwaibisha huyu Nabii na walioamini pamoja naye nuru yao yakimbia (pita) mbele yao na kuliani kwao wakisema Mola wetu tutimiziye nuru yetu na tughofirie kwa hakika wewe umuweza juu ya kila kitu). Basi ni udhuru gani atakuwa nao mwenye kughafilika kuingia nyumba ile baada ya mlango kufunguliwa na kuwepo dalili?

Na wewe ndiye ambaye ulijizidishia bei dhidi yako mwenyewe kwa faida ya waja wako ukiwatakia faida yao kwa biashara yao na wewe. Na kufuzu kwao kwa kukufika wewe na ziada kutoka kwako. Ukasema jina lako limebarikiwa na uko ngazi ya juu (mwenye kuleta tendo jema atapata malipo yaliyo sawa na mema kumi, na mwenye kuleta tendo ovu moja hatolipwa ila sawa na malipo ya ovu hilo moja) na umesema: (mfano wa ambao watoao mali zao katika njia ya Mungu ni mfano wa punje moja imetoa masuke saba katika kila suke kuna punje mia moja Mungu humzidishia amtakaye). Na ulisema: (nani ambaye atamkopesha Mungu mkopo mzuri? Naye atamzidishia zidisho jingi. Na ulizoteremsha fano wao katika Qur'ani miongoni mwa aya zielezazo miongoni mwa ongezeko la malipo ya matendo mema. Na wewe ndiye uliyewajulisha kwa kauli yako toka ghaibu yako na himizo lako ambalo lina hadhi yao ndani yake, lau ungelificha kwao macho yao yasingelidiriki. Masikio yao yasingelisikia. Akili zao zisingelifikia. hivyo basi ulisema: (Nikumbukeni nitawakumbuka nishukuruni wala musinikufuru) na ulisema: (mukiwa wenye kushukuru nitawazidishieni lakini mkikufuru (kuacha shukrani) hakika adhabu yangu ni kali). Na ulisema: (Niombeni nitakujibuni hakika wanaofanya kibri kuniabudu mimi wataingia Jehannam wakiwa duni) umeiita DU'A yako Ibada, na kuacha kukuomba ni kibri, na umekamia mwenye kuacha kukuomba ataingia jehannam akiwa duni.

Hivyo basi wamekutaja kwa ukarimu wako. Na wamekushukuru kwa fadhila zako na wamekuomba kwa amri yako. Na wametoa sadaka wakitaka ziada yako. Na katika yote hayo umekuwa uokozi wao kwa kuepukana na ghadhabu zako na kufuzu kwao kupata ridhaa zako. Lau kiumbe mwenyewe angemwongoza kiumbe mwingine mfano wa yale uliyowaongoza waja wako angekuwa asifike kuwa ni muhisani na angesifika kuwa ni mwema na angehimidiwa na kila ulimi. Sifa njema ni zako. Kipatikanacho katika mwenendo wa sifa zako hapana tamko libakialo kwa sifa usifiwazo na maana ya sifa ya kuelekea wewe. Oh yule ambaye amesifika kwa waja wake kwa hisani na ufadhili. Na amewaeneza ukarim na umbuji wingi ulioje wa neema zako zilizotuenea? Ukarimu wako mwingi mno kwetu umetufanya makhsusi kwa wema wako. Umetuongoza kwenye dini yako ambayo umeichagua. Na mila yako uliyoiridhia, na njia yako uliyoirahisisha. Na umetuoneysha ukaribu kwako, nafika kwenye ukarimu wako. Oh Allah! Miongoni mwa teule mno katika nyadhifa hizo na zilizo makhsusi sana miongoni mwa faradhi hizo ni mwezi wa Ramadhani ambao umeufanya kuwa makhsusi kwa kuulinganisha na miezi mingine. Umeuchagua toka zama zote na nyakati zote. Umeupenda kuliko nyakati zote za mwaka kwa sababu umeteremsha humo Qur'an na nuru. Humo umezidisha imani na umewajibisha humo (mwezi wa Rama...) Funga, na umependezewa humo kisimamo cha sala Na umeutukuza kwa Laylatul-qadir ambayo ni bora kuliko usiku elfu moja. Kisha umetupendelea sisi kwayo kuliko umma zingine. Kwa ubora wake umetuchagua mbali na watu wa mila. Tumefunga kwa amri yako mchana wake tumesimama tukisal usiku wake tukijishughulisha kuufunga na kusali humo. Kwa vile umetuonesha kwa ajili yake rehema zako. Kwa ajili yake tumekuwa na sababu kuelekea thawabu zako. Na wewe uko daraja la juu zaidi kuliko kile kwa ajili yake watakiwa. Umkarimu uombwacho kwa fadhila zako.

Ukaribu kwa mwenye kujaribu kuupata ukaribu wako. Mwezi huu umetusimamishia msimamo wa sifa njema, umesuhubiana na sisi usuhuba wa mtu mwema. Umetufidisha faida bora ya viumbe wa ulimwengu. Kisha umetuacha ulipotimia wakati wake na kukatika kwa muda wake na kutimiza idadi yake. Nasi tu wenye kuuaga uwagaji wa ambaye kujitenga nae kwake kwa umiza juu yetu. Kumetusononesha na kutuacha peka, kutoweka kwake, mbali na sisi, kwa ajili yake umetulazimu ulinzi ulihifadhika. na heshima yenye kuangaliwa, na haki tekelezwa. Hivyo twasema: Assalaamu Alayka Ewe mwezi wa Mungu mkubwa kabisa Ewe Iddi ya wapenzi wake (Mungu). Assalaamu Alayka, Ewe wakati ulio bora kuwa nao miongoni mwa nyakati. Ewe mbora wa miezi katika siku na saa Assalaamu Alayka mwezi matumaini yamekurubia. Kazi njema humo zimetawanywa. Assalaamu Alayka Ewe rafiki ambaye thamani yake iliyopo imetukuka. Kutoweka kwake kwa tia simanzi. Machungu ya kutengana naye kwake yatazamiwa. Assalaamu Alayka msuhuba ambaye ujaji wake huleta raha hufurahisha ambaye aondokapo huleta kitwea. Assalaamu Alayka jirani ambaye nyoyo hulainika kwa ajili yake. Dhambi mwake zimepungua. Assalaamu Alayka msaidizi asaidiae dhidi ya shetani. Mwezi arahisishaye njia za ihsani. Assalaamu Alayka wengi walioje wakombolewa wa Mungu ndani yako.

Furaha iliyoje kwa wenye kuchunga heshima yako kwa msaada wako. Assalaamu Alayka umekuwa mfutaji mno wa dhambi. Umesitiri sana wa aina mbali mbali za aibu. Assalaamu Alayka umekuwa na uvumilivu kwa watenda dhambi wa tisha mno mioyoni mwa waumini. Assalaamu Alayka mwezi ambao siku hazishindani nao. Assalaamu Alayka mwezi ambao amani katika kila jambo. Assalaamu Alayka mwezi ambao kuwa pamoja nao kwake hakuchukizi, wala kuchanganyika pamoja nao kwake hakulaumiki. Assalaamu Alayka kama ulivyoingia kwetu kwa baraka nyingi na umetoa uchafu wa makosa. Assalaamu Alayka si muagwa achukizaye wala hakichoshi kilichoachwa na saumu yake. Assalaamu Alayka mtafutwa kabla ya wakati wake. Na muhuzunikiwa kabla ya kwisha kwake. Assalaamu Alayka maovu mangapi yamezuiliwa yasitufike kwa wewe. Mema mangapi tumebubujishiwa kwa sababu yako. Assalamu Alayka wa Alaa Laylatil Qadr ambayo ni bora kuliko miezi elfu moja. Assalamu Alayka tulipupia sana jana tutakuwa na shaka sana na wewe kesho. Assalaamu Alayka na juu ya fadhila zako zilizo haramishwa kwetu na juu ya baraka zako zilizopita ambazo hivi sasa tumepokonywa. Oh Allah! Sisi ni wana, mwezi huu ambao umetuboresha kwako (kwa huo mwezi). Na kwa huruma yako umetupa taufiki. walipokosa kuujua wakati wake. Na wamenyimwa fadhila zake kwa ajili ya uovu wao. Na wewe ndiye mfadhili wa elimu zake ambazo umetupendelea maarifa yake.

Umetuongoza kwenye utekelezaji wa sunna zake. Kwa tawfiki yako tumebeba jukumu la kuufunga na kusali kwa kiwango kidogo sana. Tumetekeleza humo kidogo sana miongoni mwa kingi. Oh Allah! sifa njema zote ni zako. Twakiri maovu. Twatambua kuzembea. Katika nyoyo zetu kuna fundo la majuto kwako. Ulimini mwetu kuna ukweli wa kukuomba udhuru. Tupe thawabu kwa yaliyotupata ingawaje tumezembea. Huenda tutaifikia kwayo fadhila itakiwayo na kwayo tufanikiwe aina mbali mbali za vifaa vilivyohifadhiwa. Wajibisha kwa ajili yetu udhuru wako kwa tuliyoshindwa kutekeleza ipasavyo miongoni mwa haki zako. Umri wetu tulio nao ufikishe mwezi wa Ramadhani ujao tukiufikia tusaidiye kufanya ibada unayostahiki. Tufanye tuwe twatekeleza yapasayo (ndani ya) mwezi huu yastahikiyo katika utii. Tutunukiye Amali njema itayotekeleza haki yako katika miezi miwili miongoni mwa miezi ya Dahar. Oh Allah! Tuliyoyatenda katika mwezi wetu huu miongoni mwa dhambi ndogo au kubwa. Au dhambi tumeangukia Emo na kosa tulilotenda makusudi au kwa kusahau. Tumejidhulumu nafsi zetu. Au tumemvunjia heshima mtu mwingine. Mswaliye Muhammad na Aali zake. Na utusitiri kwa sitira yako. Tusamehe kwa msamaha wako wala usituweke mbele ya macho ya wasimbuliaji. Wala usitukunjulie ndimi za wa umbuwaji. Tutumikishe kwa yatakayokuwa ndiyo punguzo na kafara ya usilolikubali kutoka kwetu. Kwa huruma yako isiyokwisha na fadhila yako isiyopanguliwa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake uuponye msiba wetu kwa mwezi wetu. Utubariki siku ya Iddi yetu na siku yetu ya kwanza kufunguliwa.

Ijaaliye kuwa miongoni mwa siku ya kheri mno imetupitia yenye kuleta msamaha sana na yenye kufuta mno dhambi. Tughofiriye zilizojificha katika dhambi zetu na zilizotangazika. Oh Allah! tutowe kwa kutoweka mwezi huu makosa yetu tuvuwe kwa kutoweka kwake maovu yetu. Tufanye miongoni mwa watu wenye heri mno kwa huwo (mwezi). Na wenye hisa kubwa mno humo na wenye hadhi mno humo. Oh Allah! mwenye kuchunga haki ya mwezi huu kwa haki, na kuhifadhi heshima yake kwa haki, na kutekeleza mipaka yake kwa haki. Na kuchelea dhambi zake kwa haki yake. Au akajikurubisha kwako kwa ujikurubishaji uwajibishao ridhaa yako kwake na huruma yako ikamwelekea juu yake. Tupe sisi mfano wake kutoka kwenye ukwasi wako. Tupe na sisi zaidi yake kwa fadhila zako. Hakika fadhila zako hazipunguwi kwa hakika hazina zako hazipunguwi bali huzidi. Ni kweli kabisa kuwa chimbuko la hisani zako hazishi. Upaji wako ni upaji wapendeza sana. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake, tuandikie ujira mfano wa ujira wa mwenye kuufunga au amekuabudu ndani yake mpaka siku ya Kiyama.

Oh Allah! Hakika twatubu kwako siku ya kwanza ya kufuturu kwetu ambayo umeifanya kwa waumini kuwa ni Idi na furaha. Na kwa watu wa mila yako wakati wa mkusanyiko na mjumuiko kutokana na kila dhambi tumeitenda au ovu tumelitanguliza, au fikra ya shari tumeificha iwe toba ya asiyeficha dhamira ya kurudi kwenye dhambi wala harejei baada yake kwenye makosa. Toba ya nasuha iliyeepukana na shaka na wasiwasi. Ikubali kutoka kwetu tu iridhiye tuimarishe juu yake. Oh Allah! Turuzuku kuogopa adhabu za kamio na shauku ya thawabu iliyo ahidiwa ili tuipate ladha ya kile tukuombacho kwa ajili yake na huzuni ya tukuombeacho kimbilio kwa ajili yake. Tujaaliye tuwe miongoni mwa walio tubu kwako. Ambao umewajibisha mapenzi yako. Oh! Umwadilifu mno wa waadilufu, Oh Allah! Wavumilie baba zetu na mama zetu na watu wote wa Dini yetu waliotangulia kati yao na watakaopita mpaka siku ya Kiyama. Oh Allah! Mrehemu Muhammad Nabii wetu na Aali Zake kama ulivyowarehemu malaika wako waliokurubishwa. Na umswali yeye na Aali zake. Kama ulivyowasalia Manabii wako wajumbe. Mswaliye yeye na Aali zake kama ulivyowasalia waja wako wema na bora zaidi kuliko hivyo Ewe Bwana wa Ulimwengu Swala Baraka zake zitufikie. Nafu yake ihifike, kwayo DU'A zetu zijibiwe. Hakika wewe u umkarimu mno wa waombwao. Na umtoshelezaji mno wa wanaotegemewa. Na umpaji mno wa waombwao fadhila yake. Na u muweza juu ya kila kitu.

DUA YA 46

DU'A ZAKE(A.S) KATIKA SIKU YA IYDI AL-FITRI

Akimaliza kusali husimama kuelekea Qibla na siku ya Ijumaa husema: Ewe! Unayemrehemu asiyerehemewa na waja. Ewe ambaye humkubali asiyekubaliwa na nchi. Ewe ambaye hawadharau wenye haja kwake. Ewe ambaye hamtowi matumaini mwenye kumsihi sana. Ewe ambaye hawakabili kwa kutowakubalia wenye msimamo mgumu kwake. Ewe ambaye akusanyae kidogo apewacho na ashukurue kidogo atendewacho. Ewe ashukuruye kidogo na hulipa kikubwa. Ewe ambaye humsogelea kwa amwendaye karibu yake. Ewe ambaye humwita kwake mwenye kumtumbia mgongo! Oh we! ambaye haibadilishi neema wala aharakii kulipizi. Oh We! ambaye huzalisha jema ili likuwe na hufumbia macho ovu ili asamehe hurudi tumaini kutoka kwake na haja yake bila kufikia uelewa na kiwango cha ukaribu wako. Vyombo vya haja vimejaa upaji wako sifa zimeshindwa kufikia sifa zako katika kukusifu. Ujuu wa juu kabisa ni wako uko juu kabisa kuliko kila aliyejuu. Utukufu mkubwa kabisa juu ya utukufu wote. Kila mtukufu kwako ni mdogo kila kitukufu kwenye utukufu wako ni kinyonge. Wameshindwa kupata waya tarajiayo wa mwenoeaye asiyekuwa wewe. Wamehasirika wajipelekao mbele isipokuwa kwako. Wamepotea wakaao ispokuwa na wewe wamekuwa wa kiwa wenye kukimbilia isipokuwa waliokimbilia fadhila zako. Mlango wako uko wazi kwa waronga - Rongao. Upaji wako kwa ajili ya waombao msaada wako ukaribu na waombao msaada. Wenye matumaini hawa katishwi tamaa wajiletao kwako hawatokwi na matumaini na upaji wako. Hawapatwi na hali mbaya kwa ajili ya lipizi lako wenye kuomba ghofirani.

Riziki yako imekunjuka mpaka kwa wanaokuasi. Huruma yako ya mwendea akupingaye, tabia yako ni kuwatendea hisani waovu desturi yako kuwabakisha wachokozi, mpaka kuwangojea kwako kumewadanganya wasirejee. Kuwapa kwako muhla kunawazuia kukoma. Hakika hukuwafanyia haraka ili warudi kwa amri yako. Mwenye kuwa miongoni mwa wema mulihitimishia. Na mwenye kuwa miongoni mwa anayestahiki hali mbaya wa mwacha bila msaada wako wote hao watakuwa kwenye hukumu yako, na mambo yao yazuilika na amri yako. Mamlaka yao hayadhoofiki kwa muda wao mrefu wote. Dalili yako haikuvunjwa kwa kuacha kuwaharakia! Hoja yako ipo haivunjwi, na ufalme wako uko thabiti haitoweki. Ole wake yule atakayeelemea mbali na wewe. Kuachwa kusiko kuwa na msaada ni kwa yule mwenye kuachwa na wewe shakawa iliyo mbaya sana ni ya aliye danganyika nawe. Atafanyaje ndani ya adhabu yako? Mahangaiko yake marefu yaliyoje ndani ya adhabu yako? Upeo wake wa faraja umbali ulioje? Kukatishwa tamaa kwake kulioje na urahisi wa kutoka? Ni uadilifu kutokana na uamuzi wako hudhulumu katika maamuzi.

Ni usawa wa hukumu yako huwezi muonea. Umesaidia hoja na kuzijaribu nyudhuru. Ulianza na tishio. Umekuwa mpole katika kuhimiza na umefanya mifano. Na umerefusha kutoa muhla. Umechelewesha ukiwa muweza wa kufanya haraka. Umefanya bila haraka hali ukiwa umejaa haraka. Kutoharakia kwako hakukuwa kwa sababu ya kushindwa, wala kutoa muhla kwako ni unyonge wala kujiziwia kwako si mghafala. Wala kungoja kwako si upendeleo, bali ili hoja yako iwe yenye nguvu zaidi na ukarimu wako uwe kamili na ihsani yako iwe ya kutosha. Neema zako ziwe timilifu. Yote hayo yamekuwa na yangali yataendelea kuwa haitokoma. Hoja yako ni kubwa mno kuliko vile vya weza kuelezwa yote. Utukufu wako uko juu zaidi hauwezi kufanyiwa mipaka kwa kiini chake. Neema zako nyingi haziwezi kuhesabiwa zote. Hisani zako nyingi kuliko vile zishukuruwe hata kwa kiasi chake kidogo. Ukimya umenifanya nishindwe kukuhimidi. Kujizuiya kumenifanya nishindwe kukutukuza. Niwezalo kulifanya ni kukiri kushindwa kwangu. Si kwa kupenda Ewe Mola wangu! Bali ni kutoweza, Mimi ni huyu hapa naja tena mbele yako. Nakuomba usaidizi mwema. Mrehemu Muhammad na Aali zake. sikiliza mnong'ono wangu. Kubali duwa yangu, wala usiihitimishe siku yangu kwa kukatishwa matumaini. Wala usinikabili kwa kurudisha ombi langu bila jibu. Uheshimu utokaji wangu kwako. Marejeo yangu ni kwako. Hakika wewe hudhikiki na ulipendalo. Na si mshindwi wa uombwalo We u muweza juu ya kila kitu. Hapana hila wala nguvu isipokuwa kuwezeshwa na Allah Mtukufu mkubwa.

9

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 47

DUWA ZAKE(A.S) SIKU YA ARAFA

Sifa Njema Ni Zake Allah Bwana Wa Ulimwengu. Oh Allah! Sifa Njema ni Zako. Mbuni wa mbingu na Ardhi. Mwenye Utukufu na ukarimu. U bwana wa Mabwana. Mwabudiwa wa kila mfanya ibada. Muumba wa kila kiumbe. Mrithi wa kila kitu (Hapana kitu mfano wake) wala kwake haifichiki elimu ya kitu. Na yeye akizunguka kila kitu. Yeye akichunga kila kitu. Wewe ndiye Allah..Hapana Miungu Ila ni wewe. Huna kifani peke yako. Mmoja mwenye kujitenga. Wewe u Allah! Hapana miungu isipokuwa wewe. U mkarimu mpaji! U Mtukufu mwenye kutukuka. U mkubwa mwenye kujitukuza. Wewe ndiye Allah hapana miungu isipokuwa ni wewe. Ungazi ya juu kabisa mwenye kujinyanyuwa. Mwenye Nguvu Stadi. Wewe ndiyo Allah. Hapana Miungu isipokuwa wewe. Mwingi wa Rehema mwenye huruma. Mjuzi wa kila kitu mwenye hekima. Wewe ndiye Allah. hapana Miungu isipokuwa wewe. Msikiaji Muonaji. Wa Tangu na Elewa. Wewe ndiye Allah. Hapana Mingu isipokuwa wewe. Mkarimu mkarimu mno.

Wa milele wamilele mno! Wewe ndiyo Allah. hapana Miungu isipokuwa wewe. Huna mwanzo upo kabala ya chochote. Utaendelea kuwa baada ya kila idadi. Wewe ndiye Allah. hapana Miungu isipokuwa Wewe. Aliye karibu katika kuwa kwake ngazi ya juu. Na u Daraja ya juu katika ukaribu wake. Na wewe ndiyo Allah. hapana miungu isipokuwa wewe. Mwenye uzuri na Utukufu. Mwenye Utukufu na sifa njema. Wewe ni Allah hapana miungu isipokuwa Wewe ambaye amevifanya vitu viwe bila ya asili. Umevianzisha ulivyo vianzisha bila kuiga. Wewe ndiye ambaye umekadiria kila kitu makadirio. Umekirahisisha kila kitu rahisisho. Umekipanga kilicho chini yako kwa mpango. Wewe ndiye ambaye hakukusaidia katika kuumba kwako mshirika. Wala hakukusaidia katika amri yako waziri. Wala hujawa na shahidi wala kifani. Wewe ndiye ambaye umetaka likawa ulilotaka bila muhali. Umehukumu ikawa hukumu yako adilifu. Wewe ndiye ambaye mahali hapawezi kukufanya uwe ndani yake. Haijapata kuwa mamlaka mbele ya mamlaka yako. Wewe ndiye ambaye umekihesabu kila kitu kwa idadi. Umekifanyia kila kitu muda, umekifanyia kila kitu makadirio. Wewe ndiye ambaye akili zimeshindwa kuitambuwa dhati yako. Zimehemewa fahamu kutambuwa namna yako. Macho yameshindwa kudiriki ulipo! Wewe ndiye ambaye huwekewi mipaka. usijezingirwa ndani ya mipaka Hujafanyiwa mfano usije kuwa upo ndani ya mifano. Hukuzaa usije kuwa mzaliwa. wewe ndiye ambaye huna aliye kinyume nawe asije kukupinga.

Hapana kilicho sawa na wewe kisije kukushinda. Wala huna mpinzani ili akupinge. Wewe ndiye ambaye aliyeanzisha na kubuni. Amezusha na kuanzisha. Amefanya vizuri kutengeneza aliyotengeneza. Utakatifu ni wako. utukufu ulioje washani yako. Miongoni mwa mahali. mahali pako ni pa juu sana. Imeipasua haki furkani yako, Utukufu ni wako umpole ulioje upole wako? Mwenye huruma ilioje huruma yako! Mwenye hekima ulioje ujuzi wako! Utakatifu ni wako Mfalme huonekani mpaji mwenye wasaa. Uko wa daraja ya juu, ilioje daraja yako ya juu! Mwenye Uzuri na utukufu, ukubwa na sifa njema. Utakatifu ni wako umekunjuwa mikono yako kwa mema. Mwongozo umejulikana kutoka kwako mwenye kukuomba. Dini au dunia atakukuta. Utakatifu ni wako. Atanyenyekea mwenye kukutambuwa. Walio chini ya arshi yako wamenyenyekea kwa ajili ya utukufu wako. Wamefuata ili kusalimu amri kwako viumbe wako wote. Utakatifu ni wako, uhisiwi wala huguswi. Huguswi wala hudanganywi. Hutolewi wala hupingwi, hukurubiwi wala hubishwi. Uhadaiwi wala hufanyiwi vitimbi Utakatifu ni wako. Njia yako ni ardhi laini amri yako ni ongofu nawe uko hai kimbilio la milele. Utakatifu ni wako. kauli yako ni maamuzi thabiti. Na hukumu yako hapana budi. Utashi wako thabiti. Utakatifu ni wako. hapana wakukataa utashi wako. Wala hapana mbadilishaji wa maneno yako. Utakatifu ni wako, mwenye alama zitiazo kiwi macho. Muumba wa mbingu. muumba wa Roho, Himidi ni yako, himidi ya kudumu kwa kudumu kwako. Sifa njema ni zako. sifa njema za kudumu kwa neema zako. Sifa njema ni zako sifa njema iendayo sambamba na fadhila zako. Sifa njema ni zako. sifa njema zazidisha radhi zako. Sifa njema ni zako. sifa njema zi pamoja na kila mwenye kukuhimidi. Shukrani huwa ndogo mbele yake shukrani ya kila mwenye kushukuru. Sifa njema haipaswi kwa yeyote isipokuwa wewe. Hautafutwi ukaribu kwa yoyote isipokuwa ukaribu kwako. Sifa njema ambayo kwayo huidumisha (Fadhila) ya kwanza. Na huwa ni sababu ya kudumu ya mwisho. Sifa njema huongezeka kila zinapokariri zama. Sifa njema wanashindwa wahifadhi kuihesabu, inazidi ile walioihesabu katika kitabu chako waandishi. Sifa njema itauzidi uzito wa arshi yako Tukufu, na kulingana na kiti chako kilichoinuka. Sifa njema ambazo malipo yake yatakamilishwa na wewe malipo yake yataenea juu ya malipo yote. Sifa njema ambazo sehemu yake ya nje ina uwiano na ya ndani. Na sehemu yake ya ndani yalingana na ukweli wa nia. Sifa njema hajakusifu hajapata kukusifu kiumbe mfano wake. Wala fadhila zake hazijui yeyote asiyekuwa wewe. Sifa njema ambazo mwenye kujitahidi kuzizidisha husaidiwa.

Haitokuwa Rehema ikiwa kuishinda. mrehemu Rehema yenye kuridhisha ambayo haitokuwa rehma juu yake. Mola wangu Mrehemu Muhammad na Aali zake. Rehema itakayomridhisha na itayozidisha juu ya ridhaa yake. Mrehemu Rehema itakayokuridhisha na itazidisha Radhi yako kwake. Mrehemu Rehema ambayo hutomridhia ila kwayo. Wala hautoiona nyingine kuwa na thamani. Mola wangu mrehemu Muhammad na aali zake. Rehema ambayo itakayoivuka ridhaa zako. Na itaungana na muungano wa kubaki kwako. Wala haitokwisha kama vile maneno yako hayatokwisha. Bwana wangu mrehemu Muhammad na Aali zake. Rehema zitakazo jinadhimu na Rehema za Malaika wako na Manabii wako na Mitume wako na watii wako na ndani yake mutakuwa na swala za waja wako miongoni mwa majini wako na wanaadamu wako na za wenye kukubaliwa nawe. Na zitaungana na sala za kila ulichokiumba miongoni mwa jinsi ya viumbe wako. Mola wangu Mrehemu yeye na Aali zake Rehema itayoizunguka kila Rehema iliyopita na itakayo kuja. Mrehemu yeye na watu wa nyumbani mwake. Rehema ikuridhishayo na kila aliye chini yako italeta pamoja na hiyo Rehema utaongezeka pamoja nayo Rehema hizo. Na kuzidi kwa kadiri siku zinavyorudia ziada yenye kuongezeka. Hatoweza kuihesabu asiyekuwa wewe. Mola wangu warehemu walio wema zaidi katika Aali zake. Ambao umewachagua kwa ajili ya amri yako. Uliowafanya kuwa hazina ya Elimu yako. Na walinzi wa Dini yako. Ni Makhalifa wako katika ardhi yako. Wao ndio hoja yako dhidi ya viumbe (waja) wako.

Umewatakasa kutokana na uchafu na ujusi na kuwafanya tohara kwa utashi wako. Na umewafanya njia ya kwenye Jannah yako. Mola wangu mrehemu Muhammad na Aali zake Rehema itayowakithirishia kitu katika kipaji chako na ufadhili wako. Itayowajazia hadhi ya huruma zako na manufaa yako kwao. Mola wangu Mrehemu Muhammad na Aali zake Rehema ambayo mwanzo wake kikomo wala muda wake hauna mwisho. Mwendeleo wake hauna mwisho. Mola wangu warehemu Rehema inayolingana na uzito wa arshi yako na walio chini yake. Rehema zijaazo mbingu zako na vilivyo juu yake, (zenye) kulingana na idadi ya ardhi zako na vilivyo chini yake na vilivyo kati yake Rehema itakayowasogeza karibu yako. Itakayokuridhisha na wao wataridhika. Na kuungana na walio mfano wako milele. Oh Allah! Hakika wewe umeiunga mkono dini yako nyakati zote kwa Imamu uliomweka akiwa mwongozo kwa waja wako na mnara katika nchi yako. Baada ya kuwa umeunga kamba yao na yako. Na umeifanya kuwa ni sababu ya kuifikia ridhaa zako. Na umewajibisha utii wake. Na umehadharisha kumuasi. Umeamrisha kutekeleza amri zake. Na kujiziwiya na katazo lako, na asimtanguliye mwenye kumtanguliya wala asibaki nyuma yake mwenye kubaki nyuma. Yeye ni kinga ya waombao hifadhi na ni kimbilio la waumini na kishiko cha wenye kushikamana. Ni mwanga wa ulimwengu. Oh Allah! mwongoze walii wako kushukuru juu ya uliyomneemesha nayo. Wasituongoze mfano wake kumuhusu yeye. Mjaalie kutoka kwako uwezo wa kumsaidia. Mfunguliye ufunguzi rahisi. Msaidie kwa nguzo yako yenye uwezo mkubwa. Uzidishe nguvu mgongo wake. Utie nguvu mkono wake. Msaidie kwa Malaika wako. Mwongozee Malaika Askari wako washindi, kupitia yeye kiimarishe kitabu chako na mipaka yako na sheria yako na Sunna za Mjumbe wako. Rehema zako.

Oh Allah! iwe juu yake na Aali zake. Kupitia yeye huisha walichokifisha wadhalimu miongoni mwa mwongozo wa dini yako. Kupitia yeye isuguwe kutu ya dhuluma itoweke mbali na njia yako Kupitia yeye iondowe shida iwe mbali na njia yako. Kupitia yeye waondolee mbali waliopotoka kombo na njia yako. Wafuate kupitia yeye waitakiao njia yako iliyonyooka kupinda pinda. Lainisha upande wake kwa ajili ya marafiki zake. Mkunjuliye mkono wake juu ya maadui zako. Tupe huruma yake, Rehema zake upendo wake. Tujaaliye kuwa wenye kumsikiliza watii kwake wenye bidii kwa limridhishalo, wenye kuungana katika kumsaidia na kumlinda. Tuwe karibu nawe na kwa Rasuli wako. Rehema zako Oh Allah! ziwe juu yake na Aali zake. Oh Allah! warehemu wapenzi wao watambuwao daraja yao. Wafuatao njia yao, wafuatiliao athari zao, wenye kushikamana na mashiko yao, wenye kushikamana na wilaya yao, wafuatao Uimamu wao, wenye kusalimu amri yao, wenye kujitahidi kuwatii, wenye kungoja siku zao, wenye kuelekeza macho yao kwao, Rehema na baraka zenye kuongezeka safi mpya mpya zenye kunukia, uwape wao usalama na wa roho zao, yaweke pamoja mambo yako katika Ta'kwaa, iweke sawa hali yao. Warejelee. Hakika wewe ni mwingi wa kurejea mwenye Rehema na mbora wa wenye kusamehe na tujaaliye tuwe pamoja nao katika nyumba ya salama. Kwa Rehema zako. Ewe Mrehemu zaidi kuliko warahimu wote. Oh Allah hii ni siku ya Arafa. siku ulioipa Utukufu, heshima, na ukubwa, umetawanya humo Rehema zako, umeonesha humo wema kwa msamaha wako. Umekithirisha humo upaji wako kwayo umewafadhili waja wako. Allah nami ni mja wako ambaye ulimneemesha kabla hujamuumba, na baada ya ulivyomuumba ukajaaliya kuwa miongoni mwa uliowaongoza kwa ajili ya Dini yako. Na ulimuwafikisha kwa ajili ya haki yako, ulimuhifadhi kwa kamaba yako, ulimwingiza katika kundi lako na umemwongoza kuwa rafiki wa rafiki zako. Na kuwa adui kwa maadui zako, kisha ulimwamuru hakufuata amri yako, ulimkemea hakukemeka, umemkataza asikuasi, amekhalifu katazo lako na kutenda katazo lako, si kwa kukupinga wala kuonesha kiburi dhidi yako, bali matamanio yake yamemtuma afanye ulichokitenga na kumuhadharisha akisaidiwa kwa hilo na adui yako na adui wake. Akajitosha kwenye hilo (katazo) hali yu atambua fika kamio lako akiwa na ithibati na uvumilivu wako ingawaje alilazimika mno katika waja wako kwa ajili ya uliyompa asingethubutu kufanya. Mimi ni huyo mbele yako! mwenye kudharaulika, dhalili mnyenyekevu, duni mwenye woga nakiri mzigo mkubwa wa dhambi nimeubeba na makosa makubwa nimeyatenda naomba hifadhi ya msamaha wako nakusihi sitara katika rehema zako nikiwa na yakini kuwa hakuna awezae kunilinda dhidi yako mlinzi. Wala hawezi kuniziwiya dhidi yako mziwiyaji, hivyo basi ni hurumiye kama umuhurumiavyo mwenye kutenda dhambi, nikirimu kama unavyomkirimu mwenye kujitupa mbele yako kwa msamaha wako. Ni hurumie kwa ambalo haliwi kubwa kwako kumhurumia mwenye kukutazamia kutokana na msamaha wako. Nijaaliye katika siku hii sehemu natapatapa kwa ajili yake, hadhi katika ridhaa zako wala usinirudishe mikono mitupu kama ambavyo warudivyo wafanya Ibada yako miongoni mwa waja wako. Ingawaje sijatanguliza mema kulinganisha na waliyotanguliza miongoni mwa mema. Hakika nimetanguliza Tawheed yako na kukanusha dhidi na kufanana na wewe na nimekuja kwako kupitia milango ambayo umeamrisha ujiwe. Na nimejikurubisha kwako kwa namna ambayo hajikurubishi yeyote kwako ila kwa kujikurubisha kwayo. Kisha nimefatilia hayo kwa kurejea kwako kwa kujidhalilisha na kujitweza kwako na kwa dhana njema kwako na kuwa na imani na ambayo uliyonayo, nimefanya jozi ya matumaini kwako ambayo mara chache hukosa mwenye kukutumainia. Nimekuomba ombi la mtu duni, dhalili, msikitikiwa, misikini, mwenye woga, mwomba hifadhi, yote hayo akiwa na woga akijitetea akiomba kinga na kusitiriwa. Si mwenye ufedhuli kwa kiburi cha wafanyao kibri. Si mwenye kujitukuza na utashi wa watii wala mwenye kutumainia uombezi wa waombezi ningali mnyonge wa wanyonge. Dhalili wa madhalili. Ni mfano wa chembe ndogo mno ya vumbi. Oh! We ambaye hawaharakii watenda maovu wala hawaziwii wenye maisha ya raha. Oh! yule ambaye atendea ihsani kwa kuwaokoa waliojikwaa. Na huwafadhili kwa kuwapa muda. Watenda makosa:

Mimi ni mtenda maovu, mwenye kukiri mkosefu. Mwenye kujikwaa. Mimi ndiye ambaye nimethubutu mbele yako. Mimi ndiye ambaye amekuasi makusudi. Mimi ndiye ambaye nimejificha nisikuabudu na kujitokeza mbele yako kwa majivuno. Mimi ndiye ambaye amewaogopa waja wako na kujiaminisha kwako. Mimi ndiye ambaye hakuogopa adhabu yako wala kuhofia ukali wako. Mimi ni mwenye kujikosea binafsi. Mimi niko rehani wa kujisibu kwangu. Mimi sina haya. Mwenye taabu sana, kwa haki ya uliyemuainisha katika viumbe wako. Na kwa uliyemchaguwa kwa ajili yako. Kwa haki ya uliye mteua kutoka viumbe wako. Na uliyempembuwa kwa kazi yako. Kwa haki uliye unganisha utii wake na utii wako. Na uliyemfanya kumuasi yeye ni kama kukuasi wewe. Kwa haki ya uliyeunganisha kumpenda kwake na kukupenda kwako. Na uliyeambatanisha kumfanyia uadui ni kukufanyia uadui. Nikinge katika siku yangu hii kwa kile ambacho wamkinga nacho mwenye kukuomba kwa shauku kubwa akijitakasa. Akiomba hifadhi kwa msamaha wako akitibu nichunge kwa ambacho unawachunga nacho watu wako watii na wakaribu kwako na wenye daraja kwako. Nipembuwe kwa unachowapembulia wenye kutekeleza ahadi yako. Na aliyejitaabisha nafsi yake kwa ajili yako ameishughulisha katika ridha zako. Usinichukuliye makosa kwa kuzembea kwangu kuhusu haki yako. Na kuvuka kadiri yangu kwenye mipaka yako. Na kukiuka hukumu zako. Usinivute kwa kunipa muda (huku ukijaza maovu yangu kwenye daftari ya maovu) mvuto wa aliyeniziwiya kheri zilizo kwake wala hakukushirikisha katika kuteremsha neema zake kwangu. Nizinduwe kutoka usingizi wa walio ghafilika na usingizi wa wafujaji na sinzio la waliotupiliwa mbali. Uchukuwe moyo wangu kwenye lile ulilo watumikisha wafanya ibada waliojitowa. Na ulikowatiisha wachamungu na kwayo umewaokoa wenye kuzembea. Nikinge mbali na kitacho niweka mbali na wewe. Na kitakachoziwiya kati yangu na hadhi yangu kwako. Na ziwiya juhudi yangu kwako Nirahisishiye njia ya kheri kuelekea kwako.

Na kupambana kuzielekea kama ulivyoamuru usinifute katika uwafutao miongoni mwa wanaopuuza uliyoahidi. Wala usiniangamize pamoja na uwaangamizao miongoni mwa wajitiao katika hatari ya chuki yako. Wala usinitanguwe katika uwatanguwao miongoni mwa waliopotoka toka kwenye njia zako. Niokoe kutoka kwenye funiko la fitina. Niepushe toka kwenye umio la balaa. Nikinge na kuchukuliwa na kuwepwa muda. Zuwia kati yangu na adui anipotezaye na upuuzi uniangamizao na dosari inipatayo. Usinigeuziye uso mgeuzo wa usiye mridhia baada ya ghadhabu yako. Usinikatishe tamaa kukutumainia ili nisije zidiwa na kutokwa na matumaini ya rehema zako. Wala usinipe mtihani ulio zaidi ya uwezo wangu ili usije ukanifanya nizidiwe na uzito wa unitwishacho kutokana na fadhila za mahaba yako. Usinitume kutoka mkononi mwako utumwaji wa asiyekuwa na kheri yeyote, wala umuhitajii wala harejei kwako. Usinitupe mtupo wa aliyetoka nje ya jicho la uangalizi wako. Aliyezingirwa na udhalilisho wako. Ni afadhali unishike mkono ili uniokowe kutokana na hamaniko la waliopotoka, na kuteleza kwa waliodanganyika, na hali mbaya ya walioangamia. Ni feleti kutokana na balaa ulio waonjesha tabaka za waja wako na vijakazi wako. Nifikishe ngazi za uliyemtilia manani uliyemneemesha, uliyemridhia, umemfanya aishi kwa sifa njema. Na ukamchukua kwako kwa heri, univike utepe wa kujitoa kwenye (mambo) yanayo haribu matendo mema, yaondoayo baraka. Ufunulie moyo wangu kujiziwiya na matendo mabaya, matendo yafedheha.

Usinishughulishe kufanya ambalo siwezi lifikia isipokuwa kupitia kwako, kwa kuwa mbali na ambalo huridhiki na mimi isipokuwa kwa hilo. Ondoa moyoni mwangu kupenda dunia nyonge iziwiayo kilicho kwako, inaziba kumpata mtetezi kwako, inaondoa jaribio la kupata ukaribu na wewe. Na pambambiye kubakia peka kwa ajili ya ibada yako usiku na mchana. Nipe hifadhi itakayo nikurubisha kukuogopa wewe. Itakayo niweka mbali na kutenda uliyo yaharamisha. Itakayonikomboa kutokana na utumwa wa dhambi kubwa itishayo. Nipe utakaso kutokana na uchafu wa maaswi. Niondolee uchafu wa makosa. Nivike na vazi la hali njema. Nivishe joho la msamaha wako. Niviringishe katika wingi wa neema zako. Nivishe na fadhila zako na ihsani yako. Nipe nguvu kwa tawfiki yako na mwongozo wako. Nisaidiye kuwa na nia njema na kauli ya kuridhisha, na kazi ikubaliwayo. Wala usiniwakilishe kwenye uwezo wangu na nguvu zangu, mbali na uwezo wako na nguvu zako. Usinidhili siku utakayonifufua kukutana na wewe. Usiniumbuwe mbele ya wapenzi wako, wala usinisahaulishe kukukumbuka. Usiniondolee shukrani yako, bali nilazimishe nayo katika hali ya kusahau wakati wa mghafala wa wasio zijua neema zako. Niongoze (moyoni) kusifu ulionitendea, na niyatambue uliyonitunukia nayo.

Jaalia londeo langu kwako zaidi kuliko londeo la wa londeawo. Na himidi yangu kwako iwe zaidi kuliko himidi ya wenye kukuhimidi. Usinitupe wakati wa haja yangu kwako. Usiniangamize kwa ajili ya niliyokutendea. Usinichape kofi kama ulivyowachapa kofi wakupingao. Kwani mimi nasalimu amri kwako. Najua kuwa hoja ni yako, na wewe ni mbora wa fadhila, mzoefu wa kufanya ihsani. Ni mwenye kustahiki kuogopwa, wastahiki kutoa msamaha, na kwamba kwako msamaha bora kuliko uadhibu. Na kwamba wewe kusitiri kwako ni karibu mno kuliko kufichuwa sitara. Nihuishe maisha mema yatakayo lingana na nitakayo, na yatayafikia niyapendayo kwa namna ambayo siyafanyi uyachukiayo, wala sitendi uliyoyakataza. Nifishe kifo cha ambaye nuru yake yapita mbele yake na kuliani kwake. Nidhalilishe mbele yako nitukuze mbele ya viumbe wako. Niteremshe nikiwa peke yangu kwako, ninyanyuwe kati yawaja wako. Nitosheleze kwa asiye na haja na mimi nizidishiye haja na ufakiri kwako. Nikinge na masimbulizi ya maadui na kushukiwa na balaa, udhalili na shida. Nikinge na lile ulionalo kwangu kwa ajikingacho nacho mwenye uwezo wa kupiga kwa nguvu lau si huruma yake. Nakushika kwa sababu ya dhambi lau kama si saburi yake. Uwafanyiapo gumu mtihani au uovu niokoe kwa kuwa naomba sitara yako. Kwa kuwa hujasimamisha kisimamo cha fedheha katika dunia yako, usinisimamishe kisimamo mfano wake katika akhera yako. Nifanyie ihsani mbili ya mwanzo kwa ya mwisho wake. Mafao yako yametangulia kwa matukio yake. Usinirefushie muda ambao moyo wangu utakuwa mgumu kwa ajili yake. Usinigonge na kigongo ambacho kunawiri kwangu kutatoweka. Usinitupe udhalili ambao utaidogesha hadhi yangu wala upungufu kwa ajili yake tamaa haitojulikana nafasi yangu. Usinihofishe hofu ambayo itanikatisha wala woga ambao kwa ajili yake nitabakia na woga. Jaalia woga wangu uwe katika tishio lako, na hadhari yangu iwe katika kutoacha kwako kwangu udhuru na onyo lako. Woga wangu uwe nisomapo aya zako usitawishe usiku wangu kwa kuamka humo kwa ibada yako. Nakubaki peke yangu nikikesha kwa ajili yako. Utulivu wangu ni kwako tu, na kuzileta haja zangu kwako. Na kukulalamikia wewe katika kuikomboa shingo yangu iepukane na moto wako. Na unipe kimbilio kutoka mahali ambapo watu wake ana adhambu. Usiniache kipofu nikitangatanga katika ujeuri wangu, wala katika mfadhaiko wangu mpaka muda.

Usinifanye niwe onyo kwa mwenye kuonyeka. Wala mfano wa adhabu kwa mwenye kuzingatia. Wala usiwe jaribio kwa mwenye kuangalia. Usinifanyie vitimbi pamoja na uwafanyiao vitimbi. Usinibadilishe na mwingine. Usinibadilishe jina, wala usinibadilishe mwili, usinifanye kichekesho kwa viumbe wako wala kuwa mfuasi wa chochote isipokuwa ridhaa zako. Wala kuwa mtumishi kwa yeyote isipokuwa kulipiza kisasi kwa ajili yako. Nionyeshe ubaridi wa msamaha wako, na utamu wa rehema zako, na raha zako, utulivu wako, na bostani ya kipeo cha raha yako. Nionjeshe utamu wa kuwa na faragha kwa uyapendayo, kwa wasaa katika wasaa wako. Na kufanya juhudi katika mambo ambayo yaletayo ukaribu na wewe na kwako. Nizawadie kwa zawadi miongoni mwa zawadi zako. Ifanikishe biashara yangu; rejeo langu lisiwe la hasara. Nihofishe mahali pako, nipe shauku ya kukutana na wewe. Ipokee toba yangu toba isio rejelewa dhambi usibakishe pamoja nayo dhambi ndogo wala kubwa. Usiache kosa pamoja na (Toba) lawazi wala la siri. Niondolee chuki kifuani mwangu kwa waumini lifanye moyo wangu uelemee kwa wanyenyekevu. Kuwa kwangu kama uwavyo kwa watu wema ni pambe na mapambo ya wachamungu nijaalie usemi mkweli kwa waliopita na utajo wenye kukuwa katika wakati ujao nichukuwe kwenye uwanda wa watu wa kwanza. Nikamilishiye neema yako, nidhihirishiye ukarimu wako. Ijaze mikono yangu faida zako. Nisongezee zawadi ya ukarimu wako. Nifanye jirani wa watu wema miongoni mwa mawalii wako, katika janna uliyoipamba kwa ajili ya wateule wako. Nizingirishe kwenye zawadi zako tukufu mahali palipo andaliwa kwa ajili ya wapenzi wako. Nijaalie kwako mahali nitakuwa nakimbilia nikiwa mtulivu. Na marejeo nitarejeako na macho yangu kupata utulivu. usinipime kwa ukubwa wa maovu yangu wala usinihilikishe siku siri zitakapo fichuliwa. Niondowe kila aina ya shaka na hali isiokuwa wazi. Nijaalie njia katika ukweli kutoka kila aina ya rehema. Nizidishie sehemu ya zawadi katika ukitowacho. Nipe hadhi kubwa ya ihsani katika utoaji wako wa ufadhili. Ujaalie moyo wangu kuwa na itibari na yaliyopo kwako. Hima yangu iwe kwa ajili ya ambalo ni lako. Nitumikishe kwa yale uwatumikishayo wenye ikhilaasi kwako. Unyweshe moyo wangu utii wako wakati nyoyo zitakapovutwa vingine.

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) SIKU YA KUCHINJA, SIKU YA IJUMAA

O h Allah! Hii ni siku yenye baraka yenye heri. Waislamu katika siku hii wamejikusanya katika sehemu ya ardhi yako. Miongoni mwao akiwemo mwombaji, atafutaye alondeaye mwenye woga. Nawe ukiwa mwangaliaji wa haja zao kwa hiyo nakuomba kwa upaji wako na ukarimu wako na urahisi wa nilichokuomba. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na ninakuomba Oh Allah Mola wetu. Kwa sababu ufalme ni wako na zako ni sifa njema. Hapana Mungu isipokuwa ni wewe. Mwenye huruma mkarimu. Mpendwa wa wote mwema kwa wote. Mwenye Enzi na upaji. Mwanzilishi wa mbingu na ardhi. Ugawanyapo kati ya waja wako waumini miongoni mwa heri au hali bora, au baraka au mwongozo au kazi ya utii wako au heri kwa tunukiayo unawaongoza kwayo kuja kwako. Au unawanyanyua kwako daraja au unawapa kwayo heri miongoni mwa heri ya dunia na akhera. Nizidishiye hisa yangu na sehemu yangu. Nakuomba Oh Allah Mola wetu kwa kuwa wako ni ufalme na zako ni sifa njema hapana muabudiwa ila ni wewe. Mrehemu Muhamrnad (Na Ali zake) mja wako na mjumbe wako mpenzi wako mteule wako mchaguliwa wako katika viumbe wako na ziwe juu ya Ali wa Muhammad watu wasafi wateuliwa. Rehema ambazo hana uwezo yeyote wa kuzihesabu isipokuwa wewe. Tushirikishe na wema waliokuomba katika siku hii miongoni mwa waja wako waumini.

Oh Bwana wa Walimwengu wote. Tusamehe sisi na wao. Hakika wewe ni Muweza juu ya kila kitu. Oh Allah! Kwako nimekusudia kwa haja zangu. Kwako nimekabidhi hii leo umaskini wangu haja zangu na taabu yangu. Kwani kwenye msamaha wako na rehema zako naani mno kuliko aamali yangu (Kazi). Msamaha wako na rehema zako zinawasaa zaidi kuliko dhambi zangu. Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad shikilia kukidhi kila haja ambayo ni yangu. Kwa uwezo wako juu yake na urahisi wa hilo kwako. Na kwa sababu ya ufakiri wangu kwako, na kwa sababu ya kutonihitajia kwako. Sipati heri kabisa isipokuwa kutoka kwako. Haniondolei yeyote ovu kabisa isipokuwa wewe. Simtumainii kwa mambo ya akhera yangu na dunia yangu asiyekuwa wewe. Oh Allah! Mwenye kujiandaa na kujitayarisha kumwendea kiumbe akitarajia msaada wake na jaalio lake na kutaka kupata na tuzo lake. Basi kwako Ewe Mola wangu , ndio maandalizi yangu na utayarifu wangu hii leo. Maandalizi yangu na kuwa tayari kwangu kutaraji msamaha wako na msaada wako na kukupata wewe na kupata zawadi zako.

Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad usinitowe matumaini leo, hayo ndiyo matarajio yangu. Oh yule ambaye hasumbuliwi na mwombaji wala hapunguzwi na mpata (mahitaji). Hakika mimi sikukujia kwa kujiamini kuwa nina aamali njema nimeitanguliza au uombezi wa kiumbe niutarajiao. Isipokuwa uombezi wa Muhammad na Ahl-Bayt wake. Juu yake na juu yao amani iwafikie amani yako. Nimekujia nikiwa mwenye kutambua makosa na maovu kwa ajili ya nafsi yangu. Nimekujia nikitaraji kupata utukufu wa msamaha wako ambao kwa huwo umewasamehe wakosefu. Kisha muda mrefu wa kubaki kwao katika madhambi makubwa haukukuzuia kuwa rejelea na Rehema na msamaha. Oh yule ambaye rehema zake zinawasaa na msamaha wake mkubwa. Ewe Mtukufu Ewe Mtukufu. Ewe Mkarimu Ewe Mkarimu! Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad. Nirudilie kwa Rehema zako kuwa mpole kwangu kwa fadhila zako nienezee msamaha wako. Oh Allah! Hakika nafasi hii ni ya makhalifa wako wateule kwako.

Na nafasi ya waaminifu kwako katika daraja ya juu ambayo umeifanya kuwa ni mahususi kwao wamenyang'anywa wewe ndio mpangaji wa hayo. Amri yako hailemewi. Wala hauvukwi mpango wako wa lazima. Upendavyo wakati upendao. Kwa ambalo wewe wajuwa zaidi, hutuhumiwi kwa kuumba kwako wala kwa utashi wako. Kitabu chako kimebeuliwa. Faradhi zako zimepotoshwa toka malengo ya sheria zako sunna za Nabii wako zimeachwa. Oh Allah! walaani maadui toka wa mwanzo mpaka wa mwisho pamoja na aridhikaye. Pamoja na mwenye kuridhika na vitendo vyao na wenye kuambatana nao na wafuasi wao. Oh Allah mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad. Hakika ewe ni mwenyestahiki ya kuhimidiwa na kutukuzwa. Mfano wa Rehema zako na baraka zako na maamkizi yako kwa wateule wako Ibrahimu na wana wa Ibrahim. Oh Allah! waharakishie faraja Raha, msaada, imarisho na kuungwa mkono. Oh Allah! nifanye mimi niwe miongoni mwa wenye kukupwekesha na kukuamini na kumsadiki mtumishi wako na maimamu ambao umeamuru utii wao miongoni mwa ambaye kwake wapitisha hayo na mkononi mwake. Ameen Rabbal-Alameen.

Oh Allah! Hapana kirudishacho ghadhabu zako isipokuwa huruma zako. Wala kiirudishacho kasiriko lako ispokuwa msamaha wako. Wala hakuna atowaye kimbilio la kuepuka adhabu ila ni Rehema zako. Hakuna kitakachoniokoa kutoka kwako isipokuwa kunyenyekea kwako mbele yako. Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad na utupe kutoka kwako Ewe Mola wangu Faraja kwa nguvu ambazo kwayo wa Huisha wafu wa waja. Na kwayo unarudisha uhai wa wafu wa wala usinihilikishe Ewe Mola wangu katika majonzi kabla hujanijibu na kunijulisha jibu katika duwa yangu. Nionjeshe utamu wa kuwa na hali njema mpaka mwisho wa muda wangu. Usimpe fursa kunisimanga aduwi yangu, wala usiiweke shingo yangu chini ya uwezo wake usimpe mamlaka juu yangu. Oh Mungu! Wangu ukiniinuwa ni nani atanitweza? ukinitweza ni nani ataniinuwa? Ukinipa heshima ni nani atakayenidunisha ukinidunisha ni nani atakayenipa heshima? Ukiniadhibu ninani atakayenihurumia? Ukinihilikisha ni nani atakayekupinga katika mja wako au akuulize kuhusu mambo yalee? Nijuavyo ni kwamba hapana dhulma katika hukumu yako, wala haraka katika malipizi yako. Kwa kuwa hufanya haraka aogopaye kukosa na ni hakika kabisa kuwa aihitajie dhuluma ni yule ambaye ni dhaifu. Na hakika umetukuka Ewe Mola wangu! Umbali na hayo utukufu wa juu kabisa. Oh Allah mrehemu Muhammad na Aali wake. Usinifanye kuwa shabaha ya mabalaa wala nisiwe lengo la kisasi chako nipe muda nipe raha. Niondoshee kujikwaa kwangu Watambuwa udhaifu wangu na uhaba wa hila yangu na maombi yangu kwako. Na maombi yangu kwako najikinga kwako Oh Allah dhidi ya ghadhabu yako hii leo. Mrehemu Muhammad na Aali wake ni kinge na kuomba amani ili niwe mbali na adhabu yako.

Mrehemu Muhammad na Aali wake, na unipe amani. Nakuomba mwongozo basi mrehemu Muhammad na Aali wake na ni ongoze. Naomba kwako msaada basi mrehemu Muhammad na Aali wake na unisaidiye na kuomba rehema, basi mrehemu Muhammad na aali wake na unirehemu. Nakuomba kujitosheleza basi mrehemu Muhammad na Aali wake na unistosheleze. nakuomba riziki basi mrehemu Muhammad na Aali wake na uniruzuku. Nakuomba mssada basi mrehemu muhammad na Aali wake na unisaidie. Nakuomba msamaha kwa yaliyopita katika dhambi zangu mrehemu Muhammad na Aali wake na unisamehe. Nihifadhi basi mrehemu Muhammad Na Aali wake na unihifadhi. Kwa kuwa sitorudia kitu ulichokichukia kutoka kwangu ukipenda hivyo. Yaa Rabbi yaa Rabbi Oh Mola wangu! Oh Mola wangu! Yaa Hannaan yaa Hannan mpenda wote ya Dhal-Jalaal Wal-Ikram Oh Mwenye Ufalme na ukarimu.

Mrehemu Muhammad na Aali zake na nijibu kwa yote niliyokuomba na nimeyataka kutoka kwako na nilio kulondea agiza, gadiria, nihukumiye nipitishiye. Nipe kizuri katika ukipitishacho, nibariki nacho. Nifadhili nacho, Nifanye niwe na furaha na unipacho nizidishie fadhila zako na wasaa kwa uliyo nayo. Kwani wewe ni mwenye wasaa mpaji na unganisha hayo na heri ya Ahera na Neema Zake. Ewe Mwenye Rehema sana miongoni mwa wenye kurehemu (hapo omba upendayo na utamsalia Mtume Muhammad na Ahli wake mara 1000 elifu moja. Hivi ndivyo alivyokuwa akifanya amani iwe juu yake).