AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 0%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi: Ali ibn al - Husayn Imam Zaynul al - Abidin (a.s.)
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 18351
Pakua: 2868

Maelezo zaidi:

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18351 / Pakua: 2868
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

10

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S) KATIKA KUJIKINGA NA VITIMBI VYA MAADUI NA KUONDOWA MACHUNGU YAO

Mola wangu uliniongoza nikabeuwa. Uniwaidhi moyo wangu ukawa mgumuUlinitaribu kwa uzuri nimeasi. Baadaye nilitambuwa uliyo amrisha uliponitambulisha. Nikaomba ghofirani ukaondowa nikarudia ukasitiri. Zako Mola wangu ni sifa njema. Nimetosha katika bonde za kuangamiza nimejiweka kwenye hatari ya dhahbu zako na ni mashukio ya adhabu zako. Njia yangu kwako ni Tawheed. Nasababu zangu za kufika kwako ni kuwa sija kushirikisha na kitu chochote sijaambatanisha pamoja na wewe Mungu nimekimbilia kwako na nafsi yangu. Kwako ndio kimbilio la mtenda maovu aliyepoteza hadhi ya nafsi yake na kuomba kimbilio. Kiasi gani cha aduwi amechoomowa kwa ajili yangu upanga wa uaduwi wake! Na amechongowa makali ya ncha ya upanga wake kwa ajili yangu! Na kunowa kwa ajili yangu bapa la makali yake. Ameichanganya sumu yake iuwayo kwa ajili yangu. Na kuelekeza kwangu mishale yake iliyonyooka irukayo. Wala halikulala jicho lake linichungalo. Na kisiri siri akakusudia kunifanyia makuruuhi. Ana nitakia mimi uchungu wa chuki yake umeona O Mungu wangu udhaifu wangu kuibeba mizigo mizito na kushindwa kwangu kupata ushindi dhidi ya aliyenikusudia kwa kupigana naye. Na upeka wangu mbele ya idadi kubwa ya aliye na uaduwi na mimi. Anivizia kwa balaa ambalo sikuliwazia fikrani mwangu.

Ulianza kunisaidia kwa nusura yako uliimarisha mgongo wangu kwa nguvu zako. Uliyafanya butu makali yake. Baada ya mkusanyiko mwingi umemfanya abakiye peke. Umekiinua kisigino changu juu yake na kumfanya aliyonilenga yamrudie ulimrudisha nyuma. Hakuzituliza ghadhabu zake. Hakukoza kiu chake. Ameuma kidole chake. Aligeuza mgongo na kukimbia mpango wake haukutimia. Ni mara ngapi mdhalimu amenifanyia udhalimu kwa vitimbi vyake amenitegea mtego wake. Akaniwekea uangalizi wa walinzi wake akaniwinda uwindaji wa mnyama mkali awindapo windo lake.

Naye unidhihirishia tabasamu ya mwenye kujipendekeza. Huku akiniangalia kwa ghadhabu kali ulipoona Ewe Mungu wangu! Umebarikiwa na umetukuka ubaya wa fikra zake za siri na ubaya wa aliyo nayo. Ulimtupa kichwa chini ndani ya shimo lake mwenyewe. Na umemtumbukiza katika maporomoko aliyochimba. Alidogeshwa dhahili baada ya kujitukuza kwake ndani ya tanzi la mtego wake ambao alipanga anione nimenasa humo. Kama si Rehema zako yangenifika yaliyomfika. Wangapi miongoni mwa hasidi amenisonga koo kwa maumivu makubwa sana. Kwa ukali wake amenihuzunisha amenikata kwa ncha ulimi wake alinifanyia kijicho heshima yangu ilikuwa lengo lake ili kuiharibu. Amenivisha utepe wa aibu ambao ungalipo. Amenifanyia vitimbi ameniknga na hila zake. Hivyo basi nikakuita Oh Mungu wangu nikiomba msaada kwako. Nikiwa na uhakika wa haraka ya jibu lako. Nikijua kuwa hatendewi vibaya mwenye kukimbilia kwenye kivuli cha hifadhi yako. Hatofadhaika mwenye kukimbilia kwenye ngome ya ushindi wako. Ukanihifadhi na ukali wake kwa uwezo wako. Kiasi gani cha mawingu makuruhi umeniondolea mbali. Na mawingu ya neema umenyeshesha rehema zake juu yangu. Vijimto vya rehema umevitiririsha na halki njema umenivika nayo macho ya misiba umeyapofowa. Mfululizo wa mfuniko wa majonzi umeitanduwa. Dhana nzuri ngapi umeithibitisha na ukosefu umesawazisha ugonjwa umeuponya. Umasikini umeubadilisha. Yoote hayo ni neema na ufadhili kutoka kwako. Na katika hali yoote hiyo umeendelea ushupavu kutoka kwangu wa kukuasi. Matendo yangu maovu hayatakuzuiya kutimiza ihsani ufanyayo.

Hakika uliombwa ukatowa usipo ombwa ulianza (kutowa) uliombwa ufadhili wako haukutowa kwa unyimivu. Umekataa Oh Mungu wangu isipokuwa kufanya ihsani na ufadhili na kuneemesha. Nimekataa kila kitu isipokuwa kujitosa katika yaliyoharamisha. Na kuvuka mipaka yako. Na kutotiliya mananni makamio yako. Yako ni sifa njema Oh Mungu wangu! muweza asiye shindwa. Na saburi hafanyi haraka. Hiki ni kisimamo cha mwenye kutambuwa wingi wa neema na umeikabili kwa kiwango cha chini ya vile inavyobidi. Na amejishuhudiya binafsi kutowajibika. Oh Allah mimi najikurubisha kwako kupitia daraja ya juu ya Muhammad na kwa mwanga wa daraja ya juu ya Aali. Naelekea kwako kupitia wao wawili unilinde kutokana na shari fulani na fani. Hakika hayo hayakutii dhiki katika utajiri wako. Wala haikupi taabu katika nguvu zako na wewe ni muweza juu ya kila kitu. Basi nipe Oh Mungu wangu katika rehema zako na taufiki yako ya kudumu ambayo nitaifanya ngazi niipandayo ili kuifikia ridhaa yako. Ili niwe na amani mbali na adhabu yako. Oh Mwingi wa rehema kuliko wote wenye kurehemu.

NA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA HALI YA WOGA

Oh Allah hakika wewe umeniumba katika hali sawa bila dosari. Umenikuza nilipokuwa mdogo, uliniruzuku vya kutosha. Oh Allah hakika mimi nimekuta katika uliyoteremsha kitabuni mwako na umewabashiria hayo waja wako umesema: Oh! Waja wangu ambao wamezifuja nafsi zao, musikate tamaa na rehema za Allah. hakika Mungu hughofiria dhambi zote. Na yametangulia toka kwangu katika uliyoyajuwa na ambayo wewe ni mjuzi zaidi kuliko mimi. Aibu iliyoje kwa yale ambayo kitabu chako kimeyahifadhi dhidi yangu. Lau kama si sehemu ambazo nina matumaini ya msamaha wako ambao umeenea kila kitu ningejitupa chini (nikikata tamaa). Lau kama yeyote angeweza kumkimmbia Mola wake ningekuwa na haki zaidi ya kukukimbia. Na wewe hakifichiki kwako chenye kujificha kiwe ardhini au mbinguni ila utakileta. Wewe ni mwenye kujaza tosha na wewe ni mhasibu tosha. Oh Allah! hakika wewe utanitafuta endapo nitakimbi utanipata endapo nitapiga mbio hivyo basi mimi ni huyo ni mbele yako mnyenyekevu dhalili mwenye kujitweza. Ukiniadhibu ninastahiki, nayo Oh! Mola wangu ni uadilifu kutoka kwako. Na ukinisamehe toka zamani nimeingizwa katika msamaha wako. Na umenivika hali njema yako. Hivyo basi nakuomba Oh Allah! kwa majina yako yaliyo katika hazina na kwa utukufu wako uliyo nyuma ya pazia, ikiwa hautoihurumia nafsi hii yenye mashaka na hii mifupa iliyo sumbuka ambayo haiwezi joto la jua lako, itawezaje joto kali la moto wako ambayo haiwezi kuvumilia sauti ya radi yako. Vipi itaweza kuivumilia sauti ya ghadhabu yako. Hivyo basi nihurumie. Oh Allah! mimi ni mtu mnyonge, thamani yangu ndogo, kuniadhibu kwako hakuuzidishii ufalme wako uzito hata kama ule wa chembe ya vumbi.. Lau kama kuniadhibu kwako mimi kungezidisha chochote katika ufalme wako, ningekuomba niiivumiliye (adhabu), na ningependa iwe yako. Lakini mamlaka yako Allahumma ni Mtukufu mno, na ufalme wako ni wa kudumu mno kuliko ule wa kuongezwa na utii wa watii au upunguzwe na maasi ya watenda dhambi. Nihurumiye Ewe mwenye rehema zaidi ya woote wenye kurehemu. Nivumiliye Ewee mwenye enzi na ukarimu. Nirejelee, hakika wewe ni mwingi wa kukubali toba mwenye huruma kuliko wote.

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUSIHI NA KUNYENYEKEA

Oh Mungu wangu nakuhimidi na wewe ni mwenye kustahiki kuhimidiwa, kwa ihisani yako kwangu, na wingi wa neema zako kwangu, na kwa wingi wa utowaji wako kwangu, na kwa uliyonifadhili katika rehema zako. Umenikamilishia neema zako.Umenitendea mema kwa kiwango nashindwa kutekeleza shukurani yake. Lau kama si ihisani yako kwangu, na wingi wa neema zako kwangu, nisingeifikia hadhi yangu, wala nisingeiweka nafsi yangu sawa. Lakini wewe ulianza kunihisani na uliniruzuku vya kutosha katika mambo yangu yote. Uliniondolea taabu ya balaa. Uliziwiya kwa ajili yangu maamuzi yako yakuogofya.

Mungu wangu, balaa ngapi zitaabishazo umeniondolea. Neema ngapi za ukarimu umeniletea karibu. Matendo yako mangapi ya ukarimu kwangu! Wewe ndiye ambaye ulinijibu wakati wa dharura ombi langu. Na ulidogesha nilipojikwaa mtelezo wangu na ulinichukulia kutoka kwa maaduwi niliodhulumiwa. Oh! Mungu wangu sijakukuta bakhili nikuombapo. Wala mwenye kujikunja nilipo kutaka, bali nilikukuta mwenye kusikiliza DU'A yangu. Na mpaka wa matakwa yangu. Nimekuta neema zako kwangu nyingi. Katika kila jambo miongoni mwa mambo yangu. Na kila zama katika zama zangu wewe kwangu ni mwenye kuhimidiwa na matendo mema yako kwangu yenye kuheshimiwa. Nafsi yangu, ulimi wangu, akili yangu, vya kuhimidi himidi ifikiye tekelezo na hakika ya kushukuru. Himidi iwe kiwango cha ridhaa zako kwangu. Niokowe toka kwenye makasiriko yako. Oh! Mwokozi wangu nijikwaapo, lau si kama sitara yako aibu yangu, ningekuwa miongoni mwa wenye kufedheheka. Oh! Muungaji wangu mkono kwa msaada kama si msaada wako kwangu ningekuwa miongoni mwa wenye kushindwa. Oh! We ambaye wafalme wamemwekea kongwa ya udhalili shingoni mwao wakiogopa adhabu zake.

Oh! Mwenye stahiki ya kutukuzwa. Oh! Mwenye majina mema. Nakuomba unisamehe na unighofiriye siko mweupe bila dhambi, ili niweze kutowa udhuru. Wala sina nguvu, niwe na weza kupata ushindi wala sina kimbilio niweze kukimbilia. Ninakuomba uniokowe toka kwenye kujikwaa kwangu. Najitenga mbele yako na dhambi zangu ambazo zimeniweka pabaya na zimenizunguka na kunihilikisha. Kutokana nazo nimekimbilia kwako Mola wangu mwenye kutubu nikubaliye toba yangu. Najikinga kwako nipe kinga. Nikiomba hifadhi usiniache. Nikiomba usininyime. Nikishikilia usiniache. Nikiomba usinirudishe mikono mitupu. Nimekuomba Ewe Mola wangu niko hali mbaya mnyonge. Mwenye hofu mwoga. Mwenye kutapatapa fakiti. Nimedharurika kwako. Nakulalamikia Ewe Mola wangu, udhaifu wa nafsi yangu kutoharakia kwenye kile ulichowaahidi marafiki zako. Nakujiepusha na ulicho wahadharisha maadui zako. Na kukithiri mayonzi yangu na wasiwasi wa nafsi yangu. Mola wangu hujanifedhehesha kwa ajili ya fikra zangu za siri, wala hujanihilikisha kwa maovu yangu, nakuita wanijibu japo nipo goigoi unaponiita. Nakuomba nipendapo haja zangu. Popote niwapo naweka siri zangu kwako. Simwombi yeyote bali ni wewe tu. Simtumainii yeyote asiyekuwa wewe. Labeika Labeika. Wamsikia anayekunung'unikia, wampokea akutegemeaye. Wamwokoa mwenye kuomba hifadhi kwako. Wamfariji akimbiliyae kwako. Mola wangu usininyime mwisho mwema na mwanzo mwema kwa uchache wa shukrani wangu. Nighofirie ujuayo katika dhambi zangu. Ukiadhibu ni kwa kuwa mimi ni dhalimu, mzembe, mwenye kupuuza, mwenye dhambi, mwenye kuachwa mvivu. Mwenye kughafirika na hisa yake binafsi. Ukinisamehe ni kwa sababu wewe ni mwenye huruma mno kuliko wenye huruma wote.

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUMSIHI ALLAH (s.w.t)

Oh Allah! ambaye hakifichiki kitu chochote kwake katika ardhi au mbinguni. Vipi kifichike kwako Ewee Mola wangu ambacho wewe umekiumba? Vipi usijuwe idadi ya ambacho wewe umekiumba! Au vipi kisionekane kwako ambacho wewe wakimiliki. Oh Allah! Hapana kirudishacho ghadhabu zako isipokuwa huruma zako. Wala kiirudishacho kasiriko lako ispokuwa msamaha wako. Wala hakuna atowaye kimbilio la kuepuka adhabu ila ni Rehema zako. Hakuna kitakachoniokoa kutoka kwako isipokuwa kunyenyekea kwako mbele yako. Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad na utupe kutoka kwako Ewe Mola wangu Faraja kwa nguvu ambazo kwayo wa Huisha wafu wa waja. Na kwayo unarudisha uhai wa wafu na wala usinihilikishe Ewe Mola wangu katika majonzi kabla hujanijibu na kunijulisha jibu katika duwa yangu. Nionjeshe utamu wa kuwa na hali njema mpaka mwisho wa muda wangu. Usimpe fursa kunisimanga aduwi yangu, wala usiiweke shingo yangu chini ya uwezo wake usimpe mamlaka juu yangu. Oh Mungu! Wangu ukiniinuwa ni nani atanitweza? ukinitweza ni nani ataniinuwa? Ukinipa heshima ni nani atakayenidunisha ukinidunisha ni nani atakayenipa heshima? Ukiniadhibu ninani atakayenihurumia? Ukinihilikisha ni nani atakayekupinga katika mja wako au akuulize kuhusu mambo yalee? Nijuavyo ni kwamba hapana dhulma katika hukumu yako, wala haraka katika malipizi yako. Kwa kuwa hufanya haraka aogopaye kukosa na ni hakika kabisa kuwa aihitajie dhuluma ni yule ambaye ni dhaifu. Na hakika umetukuka Ewe Mola wangu! Umbali na hayo utukufu wa juu kabisa. Oh Allah mrehemu Muhammad na Aali wake. Usinifanye kuwa shabaha ya mabalaa wala nisiwe lengo la kisasi chako nipe muda nipe raha. Niondoshee kujikwaa kwangu Watambuwa udhaifu wangu na uhaba wa hila yangu na maombi yangu kwako. Na maombi yangu kwako na jikinga kwako Oh Allah dhidi ya ghadhabu yako hii leo. Mrehemu Muhammad na Aali wake ni kinge na kuomba amani ili niwe mbali na adhabu yako. Mrehemu Muhammad na Aali wake, na unipe amani. Nakuomba mwongozo basi mrehemu Muhammad na Aali wake na ni ongoze. Naomba kwako msaada basi mrehemu Muhammad na Aali wake na unisaidiye na kuomba rehema, basi mrehemu Muhammad na aali wake na unirehemu. Nakuomba kujitosheleza basi mrehemu Muhammad na Aali wake na unitosheleze. nakuomba riziki basi mrehemu Muhammad na Aali wake na uniruzuku. Nakuomba mssada basi mrehemu muhammad na Aali wake na unisaidie. Nakuomba msamaha kwa yaliyopita katika dhambi zangu mrehemu Muhammad na Aali wake na unisamehe. Nihifadhi basi mrehemu Muhammad Na Aali wake na unihifadhi. Kwa kuwa sitorudia kitu ulichokichukia kutoka kwangu ukipenda hivyo. Yaa Rabbi yaa Rabbi Oh Mola wangu! Oh Mola wangu! Yaa Hannaan yaa Hannan mpenda wote ya Dhal-Jalaal Wal-Ikram Oh Mwenye Ufalme na ukarimu.Mrehemu Muhammad na Aali zake na nijibu kwa yote niliyokuomba na nimeyataka kutoka kwako na nilio kulondea agiza, gadiria, nihukumiye nipitishiye. Nipe kizuri katika ukipitishacho, nibariki nacho. Nifadhili nacho, Nifanye niwe na furaha na unipacho nizidishie fadhila zako na wasaa kwa uliyo nayo. Kwani wewe ni mwenye wasaa mpaji na unganisha hayo na heri ya Ahera na Neema Zake. Ewe Mwenye Rehema sana miongoni mwa wenye kurehemu (hapo omba upendayo na utamsalia Mtume Muhammad na Ahli wake mara 1000 elifu moja. Hivi ndivyo alivyokuwa afanya amani iwe juu yake).

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUJIDHALILISHA KWA MUNGU MWENYE ENZI MTUKUFU

Oh Mola wangu zimeninyamazisha dhambi zangu maneno yangu yamekatika sina hoja nimekuwa mateka wa balaa yangu. Niko rehani kwa matendo yangu. Mwenye kutaradadi katika makosa yangu nimechanganyikiwa katika makusudio yangu. Nimezuilika. Nimejikwamisha binafsi mahali pa madhalili wenye dhambi. Mahali pa wenye hali mbaya wanaothubutu dhidi yako, ambao waifanyao ahadi yako nyepesi. Sub'haanaka-utakatifu ni wako. Ni ufedhuli ulioje nimekufanyia! Kudanganyika gani nimejidanganya nafsi yangu Mola wangu uhurumiye mtelezo wangu ulioniweka fudi fudi. Na kuteleza kwa nyayo yangu nitendee kwa upole wako kulingna na kutojuwa kwangu. Na kwa ih'sani yako juu ya uovu wangu. Mimi ni mwenye kukiri dhambi yangu.Mwenye kutambuwa makosa yangu. Huu mkono wangu na paji langu la uso. Najitoa kwa malipizi nafsi yangu, zihurumie mvi zangu na kwisha kwa siku zangu. Na kukurubia muda wangu, udhaifu wangu taabu yangu, na uchache wa hila yangu Mola wangu nihurumie pindi athari yangu ikatikapo duniani. Na kufutika kwa viumbe utajo wangu nikawa miongoni mwa waliosahaulika kama ambaye amekwisha sahauliwa. Mola wangu nihurumie libadilikapo umbo langu na hali yangu uozapo mwili wangu na kutawanyika viungo vyangu. Oh! mghafala ni wangu kwa yaliyotakiwa kwangu. Oh Mola wangu! nihurumie siku ya kukusanywa kwangu na kufufuka kwangu. Jaalia siku ile kisimamo changu niwe pamoja na mawalii wako. Matokeo yangu yawe pamoja na wapenzi wako. Makazi yangu yawe karibu yako. OhMola wa ulimwengu.

11

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

MIONGONI MWA DU'A ZAKE KUONDOWA MASHAKA

Oh mfariji wa mashaka, muondoa huzuni mwenye reh'ma ya dunia na akhera na mwenye huruma kwa zote mbili (dunia na akhera). Mrehemu Muhammad na Ali wa Muhammad. Nifariji mashaka yangu. Niondolee huzuni yangu. Oh we! mmoja Oh wee pekee! Oh we kimbilio la kudumu! Oh we ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa halingani na mmoja yeyote. Ni hifadhi, nifanye niwe safi niondolee balaa langu. Na hapa watakiwa isome;Ayatal-Kursiyi Na Qul Audhu Birabil-Falaq Na Qul-Audhu Bira Binnasi Na Qul-Huwallahu Ahadu.

Kisha soma DU'A hii: Oh Allah hakika mimi nakuomba ombi la ambaye hajja yake ni kubwa sana, nguvu zake zimedhoofu dhambi zake zimekithiri ombi la ambaye hampati wakumsaidia mahitaji yake, wala wakurudisha nguvu kwenye udhaifu wake wala wa kumghofiria dhambi zake asiyekuwa wewe, Oh mwenye utukufu na ukarimu. Nakuomba amali ambayo waipenda mwenye kuitenda na yakini itamfaa mwenye kuwa na yakini ya kweli katika kutekeleza amri yako. Oh Allah mrehemu Muhammad na Ali wa Muhammad ichukuwe nafsi yangu ikiwa katika hali ya kusadikisha, iondolee hajja yangu ya dunia na jaalia upendo wangu uwe katika yale yaliyo kwako nikiwa na shauku ya kukutana na wewe. Nipe ukweli wa kukutegemea na kuomba kheri iliyoachwa na kitabu kitakatifu na ninajikinga kwako na shari ya iliyoachwa na kitabu kitakatifu.

Nakuomba hofu ya wanao kuabudu na ibada ya wakunyenyekeao kukuogopa na yakini ya wanaokutegemea na kukutegemea kwa waumini. Oh Allah ufanye utashi wangu katika maombi yangu mfano wa utashi wa mawalii wako katika maombi yao. Na woga wangu mfano wa woga wa mawalii wako. Nitumikishe katika maridhawa yako aamali sitoacha pamoja nayo kitu chochote katika dini yako kwa kumwogopa yeyote katika viumbe wako. Oh Allah hii ni hajja yangu ukuze utashi wangu humo, dhihirisha humo udhuru wangu, nifundishe humo hoja yangu na humo kipe afya kiwili wili changu. Oh Allah mwenye kufikiwa na asubuhi akiwa na matumaini au tarajio kwa asiyekuwa wewe, nimefikiwa na asubuhi na wewe ni matumaini yangu na ndio tarajio langu katika mambo yote niamulie ambalo linamwisho mwema na uniepushe na fitna potovu, kwa huruma yako, ewe mwenye huruma zaidi ya wenye huruma wote. Mungu mbariki muheshimiwa wetu Muhammadi na mjumbe wa Mungu mteule na wabariki ali zake waliotahirika.

MIONGONI MWA TASBEEHI ZAKE NAMKUSUDIA ZAYNUL-AABIDEENA(A.S) ALAYHIS-SALAAM

Utakatifu ni wako Oh Allah na ninakuomba uangalizi wako wenye upendo. Utakatifu ni wako Oh Allah na umetukuka juu kabisa. Adhama ni yako Oh Allah na enzi ni shuka yako utakatifu ni wako Oh Allah na dhama ni joho lako utakatifu ni wako Oh Allah na ukubwa ni mamlaka yako. Utakatifu ni wako, ulioje utukufu wako! Utakatifu ni wako umetukuzwa juu, wasikia na waona kilicho chini ya udongo. Utakatifu ni wako washuhudia kila nong'ono, utakatifu ni wako mahali ambapo malalamiko yote huwekwa hapo. Utakatifu ni wako uko hadhiri katika kila mkusanyiko. Utakatifu ni wako ni lengo la kila matumaini. Utakatifu ni wako wakiona kilicho chini kabisa ya maji. Utakatifu ni wako wasikia pumzi za samaki waliochini kabisa ya bahari. Utakatifu ni wako wajuwa uzito wa mbingu. Utakatifu ni wako wajuwa uzito wa ardhi zote. Utakatifu ni wako wajuwa uzito wa jua na wa mwezi. Utakatifu ni wako wajuwa uzito wa giza na nuru. Utakatifu ni wako wajuwa uzito wa kivuli na wa hewa. Utakatifu ni wako wajuwa uzito wa upepo mara ngapi kubwa kuliko uzito wa chembe ya vumbi. Utakatifu ni wako Qudusu Qudusu utakatifu ni wako mwenye kukutambuwa vipi asikuogope. Utakatifu ni wako Oh Allah sifa njema ni zako. Utakatifu ni wa Mungu mtukufu mkubwa.

Zuh'riy alieleza habari kutoka kwa Saeedi bin Musayyib amesema: Qaumu ya watu walikuwa hawatoki nje ya mji wa Makka mpaka atoke Aliy bin Husayn bwana wa wafanya ibada amani iwe juu yake. Hivyo basi alitoka nikatoka pamoja naye alisimama katika moja ya vituo akasali rakaa mbili akawa yu afanya tasbihi hii: (hapo juu) haukubaki mti wala kidongo isipokuwa kilifanya tasbihi pamoja naye. Tukafazaika, akainuwa kichwa chake akasema: Ewe Saeed umefadhaika? Nikasema ndiyo ewe mwana wa Mjumbe wa Mungu! Akasema hii ni tasbihi tukufu amenihadithia baba yangu kutoka kwa babu yangu mjumbe wa Mungu(s.a.w.w) dhambi haitobaki pamoja na tasbihi hii, kwamba mungu umetukuka utukufu wake alipomuumba Jibrail alimfundisha tasbihi hii nayo ni jina kubwa la Mungu.

DU'A NA KUMADHIM KWAKE

Sifa njema ni za Allah ambaye amejitokeza nyoyoni kwa utukufu. Na amejificha kando na macho kwa nguvu akajiwezesha juu ya vitu kwa uwezo macho hayathubutu kumwona, wala mawazo hayafikii kiini cha utukufu wake. Ameonyesha nguvu zake na ukubwa amejizinga nguvu wema, na utukufu na amejitakasa kwa wema na uzuri. Ametukuka kwa fahari na uzuri. Amejitanda utukufu na neema. Amejichagulia nuru na mwanga. Muumbaji asiye na kifani pekee hana mpinzani, kimbilio la milele halingani mungu hana wa pili pamoja naye. Mwanzilishi hana mshirika, mtowa rizki hana msaidizi. Wa kwanza bila ya kutoweka wadaima bila kutoweka. Msimamizi bila taabu, mtowa amani bila mwisho, mwanzilishi bila muda, mtengenezaji bila ya kitu, bwana mwenye bila mshirika, muumbaji bila ya takalifu, mtekelezaji bila ya ajizi hana mpaka wa mahali, hana upeo katika zama, alikuwapo, yupo, ataendelea kuwa yupo kama alivyo, bila kikomo. Yeye ni Allah yu hai mwenye kujisimamia wa daima wa tangu, muweza mwenye busara, mungu wangu mbele yako watetemeka watetemekaji wa chaji. Na kwako wamekuwa na ikhlasi waliaji wakikuogopa na wakitarajia msamaha wako ewe Mungu wa haki. Ihurumiye DU'A ya waliowakiomba msaada, samehe dhambi za walioghafilika, zidisha ihisani za warejeao siku ya kuja kwako Oh mkarim.

DU'A ZAKE KATIKA KUWATAJA ALI WA MUHAMMAD(A.S)

Oh Allah ambaye umemteuwa Muhammad na Ali wake kwa heshima na kuwapendelea kwa risala na kuwachagua makhsusi kwa uombezi na kuwafanya kuwa ni mawarithi wa Manabiy na kwao ndio umehitimishwa uwasii na Maimamu na amewafundisha elimu ya mambo yaliyokuwa na yanayoendelea, na kuzifanya nyoyo za watu zielemee kwao mrehemu Muhammad na Ali zake waliotahirika tufanyiye yale ambayo wewe ni mwenye kustahiki katika dini na dunia na akhera, hakika wewe ni muweza wa kila kitu.

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE KATIKA KUMTAKIA REHMA ADAM(A.S)

Oh Allah Adamu ni shani ya maumbile yako, wa kwanza kuumbwa kutokana na udongo mwenye kutambua ubwana wako, mwanzo wa haja yako kwa waja wako na viumbe wako, na dalili ya kuomba hifadhi ya msamaha wa adhabu yako, na ni mfunguzi wa njia za toba yako, na ni wasila kati ya viumbe na kukujuwa wewe na ambaye umemfikishia uliyoyaridhia kwake kwa huruma yako kwake na rehema zako, ni mwenye kurejea kwako ambaye hakung'ng'ania kukuasi, mtangulizi wa wajidhalilishao kwa kunyoa kichwa chake katika haram yako, mwenye kutafuta wasila baada ya uasi kukutii ili aufikiye msamaha wako, baba wa Manabiy ambaye ambao wameudhiwa kwa ajili yako, ambaye amepambana sana kati ya wakazi wa ardhini katika kukutii. Hivyo mrehemu Oh we mwingi wa rehema na malaika wako na wakazi wa mbingu zako na ardhi yako, kama alivoadhimisha amri zako zisizoweza vurugwa, ametujulisha sisi njia za ridha zako Oh we mwingi wa rehema miongoni mwa wenye kurehemu.

MIONGONI MWA DU'A ZAKE KATIKA USUMBUFU NA KUOMBA FARAJA

Oh Mola wangu usimwache adui wangu anisimange, wala usimuumize mpenzi na rafiki yangu kupitia mimi. Mola wangu nipe mtazamo miongoni mwa mitazamo yako uniondolee humo uliyonisibu nayo. Ili unirudishe kwenye kawaida yako iliyo nzuri zaidi kwangu, nikubalie maombi yangu na maombi ya ambaye mwenye ikhilasi kwako ombi lake.Hakika nguvu zangu zimedhoofika werevu wangu ni mdogo, hali yangu imekuwa mbaya, nimekata tamaa na yaliyo kwa viumbe wako hakuna lililobaki kwangu isipokuwa kukutumainia wewe. Oh Mola wangu, hakika uwezo wako wa kuniondolea nilionayo ni kama uwezo wako juu ya yaliyonisibu, hakika kukumbuka mazuri yako kwangu kwanipa raha, na kutumainia fadhila zako na neema zako kwanipa nguvu, kwa sababu sijapata kuwa bila ya neema zako toka ulivoniumba, wewe ndio Mungu wangu ndio kimbilio langu ngome yangu, muhifadi wangu mlinzi wangu, mwenye upendo kwangu, mwenye rehema kwangu, mlinzi wa rizki yangu. Katika amri yako imekuwa yaliyo halali kwangu, kwa elimu yako ndiyo nilivyojaalia ee bwana wangu Sayyidi wangu ulichokikadiria na kuamuwa kwa ajili yangu, ulichokifanya hapana budi, kwa hali njema yangu ambacho ndani yake kuna manufaa yangu na kupata faraja kwa kuepukana na niliyo nayo. Mimi simtarajii yeyote kuzuwia hilo asiyekuwa wewe, simtegemei kwa hilo isipokuwa kwako basi ewe mwenye utukufu na heshima kuwa kwenye dhana yangu nzuri mno kwako.

Uhurumie udhaifu wangu na uchache wa werevu wangu, niondolee shida zangu, nikubaliye maombi yangu, niokowe toka kwenye kujikwaa kwangu, nionyeshe huruma kwa hilo na kila mwenye kukuomba, umeniamuru ewe bwana wangu kuomba na ulijipa jukumu la kuikubali ahadi yako ni thabiti haikhalifu wala kubadilika. Hivyo basi mrehemu Muhammad Nabiy wako na mja wako, na waliotahirika katika Ahli-Bayt wake. Nisaidie kwa kuwa wewe ni msaada kwa asiyekuwa na msaada na ngome kwa asiyekuwa na hifadhi. Nami ni mwenye dhiki ambaye umewajibisha kumjibu na kumwondolea aliyo nayo miongoni mwa maovu. Nijibu niondolee huzuni yangu irejeshe hali yangu kwenye ubora zaidi kuliko ilivyokuwa. Usinilipe kama ninavostahiki lakini nilipe kwa kulingana na rehema zako ambazo zimeenea juu ya kila kitu, ewe mwenye utukufu na heshima mrehemu Muhammad na Ali wa Muhammad sikiliza na ujibu owe mwenye enzi.

DU'A ZAKE A.S. KWA AYAHOFIAYO NA KUYAOGOPA

Oh Mola wangu hakuna liwezalo kuziwiya ghadhabu zako isipokuwa huruma zako, wala liokowalo toka kwenye adhabu yako isipokuwa msamaha wako. Hakuna liwezalo kuokowa kutoka kwako isipokuwa rehma zako na kunyenyekea kwako. Hivyo basi nipe ewe Mola wangu faraja kwa nguvu ambazo kwazo wahuisha mauti wa nchi na kwayo wazifufuwa roho za waja, wala usiniangamize na unipe maarifa ya jibu. Ewe Mola wangu niinuwe usinirudishe chini, nisaidie nipe rizki, ewe Mola wangu, ukiniinuwa nani atanirudisha chini, ukinirudisha chini nani ataniinuwa? Nimejuwa ewe Mola wangu katika hukumu yako hakuna dhuluma wala hapana haraka katika malipizi yako. Afanyaye haraka yule ahofiaye kukosa na aihitajiaye dhulma ambaye ni dhaifu, nawe uko juu kabisa mbali na hayo ewe bwana wangu. Mola wangu usinifanye kuwa lengo la shabaha ya balaa wala nisiwe ndio kiguzo cha malipizi yako, nipe muhula nipe raha, niokowe toka kwenye kujikwaa kwangu usinifuatilie kwa balaa baada ya balaa. Umeona udhaifu wangu na uchache wawerevu wangu, nipe uvumilivu kwa hakika mimi ni dhaifu nanyenyekea kwako ewe Mola wangu, ninajikinga kwako kutoka kwako basi nipe kinga. Naomba hifadhi kwako kutokana na kila balaa nipe kimbilio, najisitiri na wewe nipe sitara ewe bwana wangu na ambayo nayaogopa na kujihadhari nayo, wewe ni mtukufu mno u mtukufu kuliko kila kitukufu, bika bika bika nimejisitir ya Allah yaa Allah ya Allah (kariri hiyo mara kumi) Mrehemu Muhammad na Ali zake wataharifu.

MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUJIDHALILISHA

Mola wangu Mola wangu, wewe ni Mola na mimi ni mja yeyote amrehemu mja! Ni Mola tu Mola wangu Mola wangu, wewe u mtukufu namimi ni dhalili, yeyote amuhurumia dhalili ni mwenye utukufu tu. Mola wangu Mola wangu, wewe ni muumba na mimi ni kiumbe amuhurumia kiumbe ni muumba tu, Mola wangu Mola wangu, wewe ndio mpaji na mimi ni mwombaji, anayemuhurumia mwombaji ni mpaji tu. Mola wangu Mola wangu, wewe ni msaidiaji na mimi nimtaka msaada, anayemuhurumia mtaka msaada ni msaidiaji tu. Mola wangu Mola wangu, wewe ni mwenye kubakia na mimi ni mwenye kuhiliki, anayemrehemu mwenye kuhiliki ni mwenye kubaki tu. Mola wangu Mola wangu, wewe ni wa daima na mimi ni wakutoweka, anamrehemu mwenye kutoweka isipokuwa ni wa daima. Mola wangu Mola wangu, wewe u hai na mimi ni mayiti, anayemrehemu mayiti isipokuwa aliyehai. Mola wangu Mola wangu, wewe ni mwenye nguvu na mimi ni dhaifu amrehemu dhaifu isipokuwa mwenye nguvu, Mola wangu Mola wangu, wewe ni tajiri na mimi ni miskini anayemuhurumia miskini isipokuwa tajiri. Mola wangu Mola wangu, wewe ni mkubwa na mimi ni mdogo, anamrehemu mdogo isipokuwa mkubwa. Mola wangu Mola wangu, wewe ni mwenye kumiliki na mimi ni mwenye kumilikiwa, amuhurumiaye mmilikiwa ni mmiliki tu.

DU'A ZAKE SIKU YA JUMAPILI

Kwa Jina la Mwenjzi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenje Kurehemu. Kwa jina la Allah ambaye siitarajii isipokuwa fadhila zake. Wala siogopi isipokuwa uadilifu wake, sitegemei isipokuwa kauli yake sishikamani isipokuwa na kamba yake. Kwako naomba hifadhi , Oh mwenye msamaha na ridhaa kutokana na dhulma na uaduwi na kutokana na mabadiliko ya zama na kurudia rudia kwa huzuni na kutokana na pigo la matokeo mabaya nakwisha kwa muda kabla ya maandalizi na utayarifu. Kwako tunaomba mwongozo kwa ambayo ndani yake kuna wema na marekebisho, kwako naomba msaada wa ambalo lina mafungamano na mafanikio na jibu muwafaka, na kwako tunaloendea vazi la hali njema na ukamilifu wake na kuenea kwa amani na kudumu kwake. Ninajikinga kwako Oh Mola wangu na shinikizo la shetani, na ninaomba ulinzi kwa mamlaka yako na dhulma ya watawala, hivyo basi zikubali sala zangu zilizopita na swaumu yangu, na ijaaliye siku yangu ya kesho na ya baadaye iwe bora kuliko saa yangu hii na siku yangu, nienzi mimi katika ukoo wangu na kaumu yangu, ni hifadhi nikiwa macho na nikiwa nimelala. Wewe ni Allah muhifadhi bora na wewe ni mwingi mno wa rehma kuliko wote wenye kurehemu Oh Allah hakika mimi nina uhama ushirikina na kufuru, katika siku yangu hii na baada yake miongoni mwa siku za jumapili ninakuomba kwa unyofu kabisa ili nipate jibiwa, mrehemu Muhammad na Ali wa Muhammad, viumbe wako bora mwitaji wa kwenye ukweli wako, nitukuze kwa utukuzo wako ambao haudhuriwi, nihifadhi kwa jicho lako ambalo halilali, hitimisha mambo yangu kwa kujikata na mengine yoote isipokuwa kwako nahitimisha maisha yangu kwa ghofira hakika wewe ndio mghofiri mwingi wa huruma.

DU'A YAKE YA SIKU YA JUMATATU

Kwa Jina la Mwenjezi Mungu, Mwingi wa Kehema Mwenye Kurehemu. Hakumruhusu yeyote kushuhudia alipoziumba mbingu na ardhi, wala hakumchukuwa msaidizi alipoziumba nafsi, hakushirikisha katika uungu wala hakukusaidiwa katika umoja, ndimi ziko butu kufikia kikomo cha sifa yake. Akili zimeshindwa kumtambuwa yeye, wadhalimu wamenyenyekea kwa kumwogopa yeye, nyuso zimenyenyekea kwa kumwogopa kila mtukufu ametii utukufu wake (Mungu). Wako ni utukufu tena na tena wenye uwiano mfululizo kwa utaratibu ziwe baraka zake kwa mjumbe wake milele. Na amani yake ya daima bila mwisho Oh Allah jaalia mwanzo wa siku yangu hii iwe njema na kati yake iwe ya ufanisi. Mwisho wake uwe wa mafanikio na ninajikinga kwako na siku mwanzo wake ni hofu na katikati yake ni mashaka na mwisho wake maumivu Oh Allah kwa hakika mimi nakuomba msamaha kwa kila nadhiri nimeifanya na kila ahadi nimeiahidi kisha sikuitekeleza kwa ajili yako. Na ninakuomba kuhusu malalamiko ya waja wako kwangu hivyo basi mja yeyote katika watumwa wako au mjakazi miongoni mwa vijakazi wako alikuwa na malalmiko dhidi yangu nimemtendea vibaya yeye mwenyewe au katika heshima yake au katika mali yake, au katika ahli wake au mtoto wake au nimemsengenya au kumsingizia kwa kuelemea upande fulani dhidi yake au utashi wa moyo wivu, kujionyesha au upendeleo awe yupo hayo yakitendeka au hayupo, akiwa hai au amekufa. Kwa namna ambayo mkono wangu ulishindwa au sikuwa na wasaa wa kumrudishia na kujitowa kuwa dhidi yake. Nakuomba ewe mwenye kumiliki haja nazo hutolewa kwa utashi wake na ziko haraka kwenye irada yake, umrehemu Muhammad na Ali wa Muhammad, umridhishe kwa ajili yangu upendavyo nipe rehema kutoka kwako hakika yeye hapungukiwi kwa kughofiri kutoa hakumdhuru. Ewe mwingi wa rehema miongoni mwa wenye kurehemu. Oh Allah nipe mimi kila siku ya jumatatu neema mbili kutoka kwako, heri mwanzoni mwake kwa kukutii wewe na neema mwishoni mwake kwa msamaha wako, Oh ambaye ndiyo Allah. Haghofiri dhambi asiyekuwa yeye.