HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.0%

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s. Mwandishi:
Kundi: VITABU VYA HADITHI

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

Mwandishi: AMIRALY M.H.DATOO
Kundi:

Matembeleo: 27403
Pakua: 7868

Maelezo zaidi:

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 27403 / Pakua: 7868
Kiwango Kiwango Kiwango
HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

Mwandishi:
Swahili

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w) NA MA-IMAMU (a.s)

ZIMEKUSANYWA NA KUTARJUMIWA NA AMIRALY M.H.DATOO

UTANGULIZI

Allah swt anatuambia katika Al-Qur'an tukufu: Sura al-Nahl, 16, Ayah 43 Nasi hatukuwatuma kabla yako ila watu wanaume tulio wapa Wahyi (Ufunuo). Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui. Sura Al-Ambiya, 21, Ayah 7 Na kabla yako hatukuwatuma ila watu wanaume tulio wapa Wahyi (ufunuo). Bas waulizeni wenye ilimu ikiwa nyinyi hamjui. Ayah hii Tukufu inawasihi Waumini kujielekeza kwa Ahl-Dhikr yaani watu wenye busara na Wanazuoni wa Ummah ili kuweza kubainisha baina ya haki na batili, wakati ambapo Waumini wanapokumbana na shida au ugumu katika masuala mbalimbali, kwa sababu Allah swt baada ya kuwafundisha ilimu, aliwachagua hao kwa hayo. Hivyo, wao wamebobea katika ilimu na ambao ndio watu halisi wanaoielewa, kuifundisha na kuitekeleza kwa usahihi mafunzo ya Qur'an.

Ayah hii iliteremshwa kwa ajili ya kuwatambulisha Ahlul-Bayt(a.s) nao ni Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) Fatimah(a.s) , Al-Imam Hassan ibn Abi Talib(a.s) . na Al-Imam Husayn ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) , ambao kwa ujumla wanaitwa Watukufu watano au 'Al-i-'Aba ambapo pamoja na hao wameongezeka Ma-Imamu(a.s) . wengine tisa kutokea kizazi cha al-Imam Husayn ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) mara nyingi katika nyakati mbalimbali aliwatambulisha hao kuwa ni Ma-Imam waongozi, nuru katika kiza, na ni wale ambao wamebobea katika ilimu na bila shaka Allah swt amewajaalia Ilimu ya Kitabu Kitukufu. Ukweli huu, kama ilivyorejewa mahala pengi katika Ahadith mbalimbali kuanzia zama za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuanzia ufunuo hadi leo hii, na vile vile wanazuoni wengi na Wafasiri kutokea Ahl-Sunnah wamekiri waziwazi katika vitabu vyao kuwa Ayah hizi za Qur'an zilikuwa zimeteremshwa hususan kwa ajili ya kuelezea na kuwatambulisha Ahl-ul-Bayt (a.s) Baadhi ya mifano ya vitabu vyenyewe ni kama ifuatavyo:

1. Imam Tha'labi katika tafsiri ya kitabu chake juu ya Ayah hiyo ya 42 kutokea Sura An-Nahl, namba 16

2. Tafsir ibn Kathir, j.2, Uk.591

3. Tafsir at-Tabari, j.14, Uk.75

4. Tafsir-i-Alusi, ijukanavyo kama: Rahul-Bayan , j. 14, Uk. 134

5. Tafsir-i-Qartabi, j.11, Uk. 272

6. Tafsir-i-Hakim, au Shawahid-ut-Tanzil, j. 1, Uk. 334 7. Tafsir-i-Shabistrary, au: Ihqaq-ul-Haq, j.3, Uk.482 8. Yanabi'-ul-Muwaddah, cha Ghanduzi Hanafi, Uk. 119.

Kwa kutegemea ukweli huu, sisi lazima tujielekeze kwa Wananyumba ya Ahlul-Bayt(a.s) , na kutekeleza maneno yatuongozayo ili kuelekeza maisha yetu mema. Kwa sura hii, Imam-ul-Hadi(a.s) anasema katika Man la Yahdhuruh-ul-Faqih, Tahdhib na 'Uyun-i-Akh-bar-ur-Ridha: "Maneno yenu yenye busara yanatupa nuru, maamrisho yenu ni hidaya kwa watu na usia zenu ni Taqwa na usawa."

MUWE TAHADHARI ENYI WASOMAJI

Kwa kupitia Watukuu hawa ndipo sisi tunaweza kuokoka humu duniani na Aakhera na maisha yetu yakawa mema na salama. Twapata katika Man la Yahdhuruh-ul-Faqih, Tahdhib na 'Uyun-i-Akh-bar-ur-Ridha: "Ni kwa sababu yenu Allah swt ametutoa nje ya upotofu (wa ukafiri), ametufanya huru kutoka huzuni na masikitiko, na kutuchukua pa usalama dhidi ya maangamizo ya dunia na mioto ya Jahannam pia." Katika katika Man la Yahdhuruh-ul-Faqih, Tahdhib na 'Uyun-i-Akh-bar-ur-Ridha twasoma:

"Ni kwa sababu ya Ukuu na uongozi wenu kuwa Allah swt ametufundisha ilimu ya kanuni za Dini , na kuweka sawa na vyema yale yote yaliyovurugika na kufasidika katika dunia. (Naye ametuepusha na umasikini, udhalilifu na ujahili, na kututunukia ilimu, heshima na hadhi.) Kwa hakika, iwapo sisi tutawaacha hawa watukufu waliobarikiwa na kutukuzwa na Allah swt, basi hakuna shaka kuwa tutatumbukia katika upotoshi na maangamizi katika kila hali. Ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Mfano wa Ahlul-Bayt(a.s) yangu ni sawa na Safinah ya Mtume Nuhu(a.s) Yeyote yule atakaye ipanda basi kwa hakika ameokoka na yeyote yule atakayekhilafu kuipanda, basi kwa hakika amezama na kutokomea mbali." Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) :

"Inawezekana nikaitwa hivi karibuni nami nikaitikia. Hivyo, mimi ninawaachieni miongoni vitu viwili vilivyo vizito (vyenye thamani na maana kubwa mno): Kitabu cha Allah swt (yaani Qur'an) ni kamba iliyovutika kutoka mbinguni hadi ardhini, na Ahlul-Bayti(a.s) yangu; kwa hakika Allah swt, Mrehemevu, Mwenye kuwa Makini, amenijulisha kuwa kamwe, kamwe vitu hivi viwili havitatengana hadi kukutana na mimi hapo Hawdh-Kauthar (Chemchemi ya milele). Hivyo, muwe waangalifu mutakavyojishikiza navyo wakati ambapo mimi sitakuwapo." Na vile vile katika Hadith nyingineyo imeongezeka: "Kamwe, kamwe, hamtapotoka iwapo mutakuwa mumeshikamana navyo hivi vitu viwili." Hivyo, je ni heshima gani itakayopita kuliko Qur'an , Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Ahlul-Bayt(a.s) vikawa ni mifano yetu, waalimu na viongozi wetu? Na kwa sababu hizi ndipo sisi kwa moyo halisi na unyenyekevu tunasema:

Sisi tumefadhilika kwa sababu sisi ni wafuasi wa Madhehebu ambayo muasisi wake Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) (mja ambaye amekombolewa kutokana na minyororo ya udhalili na kuchaguliwa kuwa mkombozi wa binadamu wote kutoka utumwa mbali na ule wa Allah swt ) kwa kufuata mwongozo kutoka Allah swt. Sisi tumetukuzwa kwa kuwa na kitabu kitakatifu cha Nahjul-Balagha, ambacho ni kitukufu baada ya Qur'an Tukufu, chenye maandiko matukufu kwa ajili ya maisha yetu wanaadamu, ni kitabu kikubwa kwa ajili ya ukombozi wa mwandamu na maelekezo yake ya kiroho na kisiasa yanayo thamani kubwa kwa ukombozi na kimeandikwa na Ma'sum Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) Vile vile tumebarikiwa kwa Imam Al-Mahdi(a.s) atokanaye na Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .yu bado hai na kwamba anahabari na kujua habari zetu zote.

Sisi tumebarikiwa kuwa na Doa ambazo ndizo zilizofunzwa na Ma-Imam(a.s) kama Dua za Sha'baniyyah, Dua ya 'Arafah ya al-Imam Husayn ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) , Sahifa-i-Sajjadiyah ya al-Imam Zayn-al-'Aabediin(a.s) , na Sahifa-i-Fatimah. Vile vile sisi tumebarikiwa kuwa na Mwanazuoni mkubwa katika zama zetu ambaye hawezi kueleweka kwa watu wengine isipokuwa Allah swt, Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Ma-Imamu(a.s) kwa sababu ya kipaji chake kikubwa cha ilimu na hekima. Vile vile sisi tumebarikiwa kwa kuitwa Madhehebu ya Ja'afariyyah na kwamba Fiqh ambayo ni bahari isiyo na mwisho ( ya ilimu ), ambayo ni mchango mmojawapo wa Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) Vile vile sisi tunafakhari kubwa sana kwa kuwa na Ma-Imamu(a.s) wote, na tunawafuata kikamilifu. Sisi tumebarikiwa kwamba Maimam(a.s) wetu walikuwa wameteswa, kuwekwa mahabusu na vile vile kutolewa makwao kwa sababu wao walikuwa daima wamejitolea muhanga kuutetea ubinadamu na kuinua hali ya Dini ya Islam na kuyatekeleza maamrisho ya Qur'an yakiwemo maamrisho ya kutengeneza Serikali adilifu na hatimaye hao Ma-Imamu(a.s) waliuawa katika harakati zao za kutokomeza serikali dhalimu na Taghuti katika kila zama.

Sasa, ewe mpenzi kaka na dada Wewe ni shahidi wa macho, katika dunia hii ndogo, ndogo zaidi kuliko kijiji katika ulimwengu, unajionea kuwa hali ya binadamu inaendelea ipo inateketea katika jangwa la dhuluma na pasi na haki, wakati mwanadamu huyo yupo anatumbukia chini zaidi katika matingatinga ya kutokuhurumiwa na kukosekana kwa uadilifu. Wale wote wanaojidai kuhusu uhuru na raha ya mwanadamu wanashuhudia kwa makini kumomonyoka kwa maadili katika mazingira waliyoyaumba wao wenyewe. Wao hawana tena uwezo wa kudhibiti hali hiyo isipokuwa kuangamia kwa binadamu na ubinadamu. Lakini, je ni kweli kuwa huo ndio mwisho wa mstari huo? Jibu kwa kushangaa litakuwa ndiyo, hadi hapo mwanadamu atakaporejea katika uumbwaji kwake wa kiAllah swt, akimulika makosa na kasoro zake zilizopita kama ndiyo tochi kwa maisha yake ya mbeleni na akiitumia Islam kama ndiyo dawa ya matatizo yake yote.

Katika zama hizi, Islam ambayo ndiyo tukufu, na bora kabisa katika kutuongoza, bora katika katika historia, imetoa mikono yake kwa ajili ya kumnusuru mwananadamu ili asije akazama na kughalibiwa na maovu na kwa baraka za Allah swt, imesimama imara kumtibu mwanadamu dhidi ya magonjwa maovu kabisa ya maovu. Islam ipo kwa ajili ya kutuliza kiiu cha mwanadamu anayezurura katika majangwa ya chumvi kali zisizo na taqwa kwa kumnywisha maji matamu na baridi ya itikadi zilizonurishwa kwa ilimu na maarifa na utukufu wa Ahlul-Bayt(a.s) , ambayo ndiyo sura halisi ya tafsiri kamili ya ufunuo ambayo kamwe haikuwa na kosa au kasoro ya aina yoyote ile. Inatoa mwanga kwa hali zote na kimwili na kiroho ya maisha ya mwanandamu. Hivyo, imefungua milango kikamilifu kwa mwanadamu kukamilika kikamilifu. Lakini Ewe rafiki mpendwa NI jambo la muhimu na kwanza kabisa kwa kutaka kujua habari za shule yoyote ile pamoja na mafunzo yake, inatubidi sisi kutazama kwa undani maandiko na kuelewa mazungumzo na maneno ya viongozi wake. Na kwa njia hii ndipo sisi tutakapoweza kujua kuhusu itikadi na imani na malengo ya shule hiyo kuhusu dunia na matatizo yake na hivyo kuweza kufikia maamuzi na makisio ya upeo wake. Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema: "Rehema za Allah swt zimfikie mja ambaye huisha maamrisho yetu " Nami nilimwuliza ni vipi mtu anaweza kuziweka hai maamrisho yenu? Imam(a.s) alijibu "Yeye anaweza kujifunza ilimu na maarifa yetu na kuwafundisha wengineo. Kwa hakika, iwapo watu watazijua faida na mema za miihadhara na misemo yetu, basi kwa hakika watazifuata kuzitekeleza. "[1]

Matumaini mema Twategemea kuwa msomaji kwa kuyasoma na kuyazingatia maneno yenye thamani isiyosemekana, kuwa kwa kupitia maneno na maongozao ya Ahlul-Bayt(a.s) vizazi vyetu hususan vijana wataongoka na kamwe hawatapotoka wala kuvutiwa na mavutio yanayotuongoza kuelekea maangamizo ya milele na kwamba utamaduni wetu hautamomonyoka siku baada ya siku na badala yake tutatengeneza utamaduni wetu uwe utamaduni wa Kiislamu kwa baraka na miongozo za Ahlul-Bayt(a.s) na kwamba tutakuwa washupavu na maaskari kulinda imani na Din ya Islamu dhidi ya maadui wake walio ndani na nje. Tutakuwa Waislamu bora na mfano kwa watu wote. Amani na Salaam ziwafikie wale wote waliongoka.

1. MAIMAMU WA SHIA KATIKA UANDIKAJI NA UENEZAJI WA HADITH

Katika sehemu hii, twategemea kuzungumzia kwa mukhtasari msimamo wa Shia kuhusu uandikaji wa Hadith kutokea mwanzoni. Itaonekana kuwa ni kinyume na msimamo wa wengine kuhusu swala hili. Msimamo wa Kishia ulisisitiza mno juu ya uandikaji wa Hadith zikisaidia uhifadhi wake wakati ambapo Maulamaa mashuhuri wa Kisunni, hata kufikia mwanzoni mwa karne ya 3A.H./9 A.D. walikuwa wakipinga uandikaji wa Hadith. Ni baada ya uandikaji wa Hadith ulipokuwa dhahiri hao wanaopinga walipoanza kwenda kinyume na Hadith walizokuwa wamezitoa wakipinga uandishi na uenezaji wake na hapo wakaanza kuziandika. Alba ibn al-Ahmad ananakili kuwa mara moja Ali ibn Abi Talib(a.s) wakati akitoa Hotuba juu ya mimbar, alibainisha: "Je, ni nani atakayeinunua elimu kwa Dirhamu moja?" Al-Harith ibn al-A' war alinunua karatasi yenye thamani ya Dirhamu moja na kumwijia Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) na kuandika kiasi cha kutosha cha elimu juu yake. Riwaya hii inatuonyesha vile Imam(a.s) alivyokuwa akisisitiza juu ya uandikaji. Imam Hassan ibn Ali ibn Abi Talib(a.s) ameripotiwa akiwashauri watoto wake kama ifuatavyo:

"Nyinyi sasa ni watoto wa Ummah ambao katika maisha ya mbeleni mtakuwa wakubwa wao. Jielimisheni Elimu; na yeyote yule miongoni mwenu atakayeweza kuhifadhi (kukariri) elimu (yaani Hadith), basi aiandike na kuiweka nyumbani mwake." Imeripotiwa kuwa Hujr ibn Adi, mmoja wa Sahaba wa Mtume(s.a.w.w) na Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) , aliziandika Hadith za Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) katika kitabu na kuzirejea pale alipohitaji msaada wa mwongozo katika masuala mbalimbali Mifano hii inadhihirisha umuhimu aliokuwa ameuambatanisha Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) , watoto wake na Sahaba wake katika uandikaji wa Hadith. Mifano miwili ifuatayo itaonyesha dhahiri vile Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) alivyokuwa akisisitiza umuhimu wa Hadith na kuzihifadhi. Umar ibn Ali anaripoti kuwa mtu mmoja alimwuliza Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) ni vipi kuwa yeye (i.e. Ali) aliweza kunakili na kusimulia Hadith nyingi za Mtume(s.a.w.w) kuliko Sahaba wengineo. Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) alijibu: "Hii ni kwa sababu daima nilipokuwa nikimwuliza swali Mtume(s.a.w.w) , alikuwa akinijibu maswali yangu. Na pale nilipokuwa nikiwa kimya, basi Mtume(s.a.w.w) alianzisha mazungumzo mwenyewe." Ali ibn Hawshab anaripoti kutoka Makhul, mwanachuo kutokea Syria, kuwa Mtume(s.a.w.w) aliisoma Ayah (69:12).

Na hapo alimwambia Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) "Mimi nimemwomba Allah swt kuwa masikio hayo yawe ni yako." Baadaye Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) alisema: "Mimi kamwe sikusahau Hadith yoyote au chochote kile kilichosikilizwa na sikio langu kikisemwa na Mtume(s.a.w.w) Umar ibn al-Harith anasema: "Wakati mmoja Ali(a.s) aliuelekeza uso wake kuelekea mbinguni na kuurudisha chini akisema:"Mwenyezi Mungu na Mtume wake(s.a.w.w) wamesema kweli." "Je, kilikuwa nini?" Kikundi cha watu kiliuliza. Imam Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) . alisema: "Mimi ni mpiganaji wa vita na vita vinarithishia mtu ulaghai. Vivyo hivyo, ninaweza kukubali iwapo nitaporomoka kutokea mbinguni kwa ajili ya kunaswa na ndege kuliko kumsingizia uwongo Mtume wa Allah swt. Kwa hivyo fuateni chochote kile mukisikiacho kikitoka kwangu........" Kauli juu ya uandishi wa Hadith pia zimenakiliwa kutoka Maimamu wengine.

Al-Imam al-Sadiq(a.s) alisema: "Andikeni na kuieneza elimu yenu miongoni mwa ndugu zenu, na iwapo mtafariki basi watoto wenu watarithi vitabu vyenu. Itafika siku ambapo patatokea machafuko na hapatakuwapo na mtu wa kumfanya rafiki na wala hapatakuwa na chochote cha kuweza kutegemewa isipokuwa ni vitabu tu.... Al-Imam al-Sadiq(a.s) pia amenakiliwa kwa kusema: "Hifadheni vitabu vyenu kwani mutakuja kuvihitaji hivyo siku moja." Vile vile ameripotiwa akisema kuwa nguvu za moyo na kuhifadhi akilini inategemea mno juu ya maandishi. Abu Basir anaripoti kuwa aliambiwa na Imam al-Sadiq(a.s) : "Baadhi ya watu waliotoka Basrah walikuwa wakija na kuniuliza kuhusu Hadith na waliziandika. Je, kwa nini nawe hauziandiki?" Na aliongezea kusema, "Elewa wazi wazi kuwa wewe kamwe hautaweza kuhifadhi Hadith bila ya kuiandika." Idadi kubwa ya mapokezi yanaonyesha kuwa Maimamu(a.s) walikuwa navyo vitabu na maandishi ambavyo walirithi kutoka vizazi vilivyowatangulia.

Katika riwaya nyingine Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) ameripotiwa akiwa amesema: "Ikamateni elimu (kwa kuiandika)," ambavyo aliirejea mara mbili Imeripotiwa kutoka Ja'bir kuwa Abu Hanifa alikuwa akimwita al-Imam al-Sadiq(a.s) "Kutubi" (yaani mwenye vitabu) kwa sababu ya kutumia mno vitabu, na Imam(a.s) alifurahishwa kwa jina kama hilo. Vile vile imeripotiwa kuwa al-Imam Muhammad ibn Ali al-Baqir(a.s) ameziandika Hadith za Mtume(s.a.w.w) ambazo zilikuwa zikinakiliwa na Jaabir ibn Abdullah Ansaari. (Ingawaje taarifa hii inaonyesha kuwa siyo ya ukweli kwani Jaabir alikuwa ameshakwisha kufariki wakati Imam(a.s) alikuwa na umri wa miaka mitano tu, labda inawezekana kuwa Hadith ziliandikwa na mjumbe).

2. MASHIA NA UANDISHI WA HADITH

Kwa kuwa riwaya (desturi) ya uandishi wa Hadith ilikuwapo miongoni mwa Shia tangia mwanzoni, wao walikuwa wanaongoza katika uandishi wa Hadith na Fiqh. Dr. Shawqi Dayf anaandika: "Mwelekeo na umuhimu wa Mashia katika uandishi wa Fiqh umekuja daima ni madhubuti mno. Sababu nyuma yake ilikuwa ni imani yao katika Maimamu wao ambao walikuwa ni kiongozi wao (haad) na wakiwa wameo ngozwa na Allah swt (mahdi) na fatawa zao zimekuwa zimeshikamana. Kwa hivyo, wao walipatiwa uzito na umuhimu katika misemo ya Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) Na kwa sababu hiyo, mkusanyiko wa kwanza ulifanywa na Mashia, ulifanywa na Sulaym ibn Qays al-Hilali, katika zama za al-Hajjaj." Al-Allamah al-Sayyid Sharaf al-Din anaandika:

"Imam Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) na wafuasi wake walitilia mkazo na kufuatilia swala la uandishi kuanzia mwanzo kabisa. Jambo la kwanza kabisa lililotiliwa mkazo na kufuatiwa na Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) ilikuwa ni kuiandika Quran nzima, ambayo aliifanya baada ya kifo cha Mtume(s.a.w.w) kwa kuiandika kimpangilio wa ufunulio wa Aya za Qurani.Katika Qurani hiyo pia alikuwa ameonyesha ni aya zipi zilizokuwa 'amm au khass, mutlaq au muqayyad, muhkam au mutashabih. Baada ya kukamilisha hayo, aliendelea na kazi ya ukusanyaji wa kitabu kwa ajili ya Fatimah, ambacho kilikuwa kikijulikana kwa vizazi vyao kama Sahifat Fatimah. Baada ya hayo, aliandika kitabu juu ya diyat (fidia) ambacho kilijulikana kama Sahifah. Ibn Sa'id amenakili hivyo katika musnad kutoka kwa Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) . mwishoni mwa kazi yake mashuhuri al-Jami.' Mtunzi mwingine wa Kishia ni Abu Rafi, ambaye alikusanya maandiko yakiitwa kitab al-Sunan wa al-ahkam wa al-qadhaya. " Marehemu Sayyid Hassan al-Sadr anaandika kuwa Abu Rafi, aliyekuwa mawla wa Mtume(s.a.w.w) ndiye aliyekuwa wa kwanza miongoni mwa Mashia kwa kukikusanya kitabu. al-Najashi katika Fihrist ameelezea kuwa Abu Rafi alikuwa ni mtunzi katika kizazi cha kwanza cha Mashia. Mfuasi wa Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) Abu Rafi alishiriki katika vita vya Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) na alikuwa ni mwangalizi wa hazina ya Serikali huko Kufah. Kitabu chake kilichokuwa kikiitwa Kitab al-Sunan wa al-ahkam wa al-qadhaya, ambacho kilikuwa kimeanza kwa sura izungumziayo Salat, kufuatiwa na sura juu ya Saumu, Hajj, Zakat, kutolewa kutoka kwa Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) katika Kufah, Kitabu hiki kilinakiliwa na Zayb ibn Muhammad ibn Ja'afer ibn al-Mubarak katika nyakati za al-Najashi. Ali ibn Abi Rafi, mwana wa Abu Rafi, aliye tabi't na Mshia khalisi ameweza vile vile kukusanya kitabu kilichokuwa na sura mbali mbali juu ya mambo ya Sheria kama vile wudhuu, Salaat, n.k.

Kama ilivyoelezwa hapo awali, abu Hanifa alimwita al-Imam al-Sadiq(a.s) kutubi (akisema 'innahu kutubi' ) sifa ambayo ilimtambulisha na wengineo. Wakati Imam(a.s) aliposikia kuhusu hayo, alicheka na kusema, "...... lakini kila alichokisema kuwa kwangu suhufi ni kweli; mimi nimesoma suhuf (vitabu) vya mababu zangu." Riwaya hii inaonyesha kwa wazi wazi kuwa Imam(a.s) . alikuwanavyo vitabu fulani ambavyo alipewa na mababu zake, na hiki kilikuwa ni kipindi ambacho Ahl al-Sunnah walikuwa hawakutilia mkazo katika uandishi wa Hadith. Miongoni mwa mapokezi ambayo inatuonyesha kuwa ma-Imam(a.s) walikuwa navyo vitabu kama hivyo, ni mojawapo iliyoripotiwa na Muhammad ibn 'Udhafir al-Sayrafi anasema: "Mimi nilikuwa pamoja na al-Hakam ibn Utaybah na tulimtembelea al-Imam al-Baquir(a.s) Al-Hakam alimwuliza swali Imam(a.s) Abu Ja'afer(a.s) alikuwa akimstahi sana. Wao walitofautiana juu ya swala fulani na hapo Abu Ja'afer alisema: "Mwanangu (mtoto wake), inuka na ukilete kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) Huyo mtoto alimletea kitabu kikubwa, ambacho Imam(a.s) alikifungua, na kulipitishia macho hadi kulipata swala walilokuwa wakilizungumzia. Na hapo Abu Ja'afer(a.s) alisema: "Haya ni maandishi ya Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) na yaliyosemwa na Mtume(s.a.w.w) ..........." Katika riwaya nyingineyo ameripotiwa Imam al-Baquir(a.s) akisema: "Katika kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) nimepaona ambapo Mtume(s.a.w.w) akisema: 'Wakati zakat itakapokuwa hailipwi, basi baraka itapotea kutoka ardhi." Vile vile ipo imeripotiwa kuwa Imam al-Sadiq(a.s) amesema:

Baba yangu alisema: "Mimi nimesoma katika kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) kuwa Mtume(s.a.w.w) ameandika mkataba baina ya Muhajirun na Ansar na watu wengineo wa Yathrib ambao waliungana naye, ikisemwa humo hivi: "Jirani ni sawa na mtu mwenyewe; asitendewe visivyo haki au kutendewa madhambi. Utukufu wa jirani wa mtu ni sawa na ule utukufu wa mama yake." Katika riwaya nyingine al-Imam al-Sadiq(a.s) amesema: Imeelezwa katika kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) "Mfano wa dunia ni sawa na mfano wa nyoka: ngozi yake nyororo mno, lakini ndani yake ni sumu kali mno. Mtu aliye mwenye busara hujiweka naye mbali, lakini jahili anafanya kila aina ya jitihada ya kutaka kuikaribia." Kwa mujibu wa riwaya nyingineyo, habari ifuatayo imetoka katika kitab adab Amir al-Muminiin: Mtu yeyote asijaribu kurejea katika mithali katika masuala ya Din, kwani amri ya Allah swt haiwezi kutambuliwa kwa mithali. Watatokezea watu ambao watakuwa wakirejea katika mithali, na hao watakuwa na uadui pamoja na Din. Zurarah anaripoti:

Nilimwuliza al-Imam al-Baquir(a.s) kuhusu hisa ya babu katika urithi. Imam(a.s) alijibu: "Sijawahi kumwona mtu yeyote yule akilisemea swali hili bila ya kuongezea mawazo yake ya kibinafsi, isipokuwa Amir al-Muminiin Ali ibn Abi Talib(a.s) .." Mimi nilimwuliza: "Na jee alisema nini?" Imam(a.s) alinijibu: "Njoo kesho, mimi nitakusomea kutoka kitabuni." Mimi nilisema, "Mimi niwe fidia juu yako, naomba uiseme katika mtungo wa Hadith kwani Hadith zako ni afadhali kwangu kuliko kukisoma kitabu." Imam(a.s) alisema: "Tafadhali usikilize kile nilichokuambia. Njoo kesho na mimi nitakusomea kutoka kitabu hicho ." Siku ya pili mimi nilimwendea Imam(a.s) wakati wa adhuhuri. Jaafer ibn Muhammad mwanae Imam(a.s) alinikaribia na Imam(a.s) alimwambia kunisomea kitabu hicho........ Katika riwaya nyingine, Imam al-Sadiq(a.s) anasema: "Ipo imeelezwa katika Kitabu cha Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) kuwa mtu anywaye pombe na mwenye kumsaidia aliyelewa (muskir) basi wote wanastahili kuadhibiwa, ambavyo ni sawa katika sura zote mbili." Muhammad ibn Muslim, Sahaba wa Imam al-Baquir(a.s) asema: "Abu Jaafer alinisomea kitabu kitab al-faraidh, ambacho yalikuwemo yaliyosemwa na mtume(s.a.w.w) na kuandikwa na Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) "Habari zote zilizotajwa hapo juu, ambazo ni chache sana kutokea riwaya nyingi mno kama hizo, zinatudalilisha kuwa desturi ya Mashia ya kuandika Hadith imetangulia mawaidha ya ma-Imam(a.s) kwa sahaba wao kuhusu uandishi wa Hadith. Ilikuwa ni desturi ambayo ilianzia katika zama za Mtume Mtukufu(s.a.w.w) na ilikuwa imeanzishwa na Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) Zipo Hadith, nyingi katika desturi ya Mashia ambazo zimetimiza kanuni za tawatur, na vile vile yapo marejeo katika Sunni ambazo zinathibitisha na kushuhudia Hadith kama hizo.

Mambo yote hayo yanakuelekeza katika uimara na uhakikisho wa usahihi wa Hadith zilizonakiliwa na Mashia. Hii ni kwa sababu pamoja na kuendelea na maongozo ya Maimamu(a.s) hadi kufikia katikati ya karne 3 A.H./9 A.D., Hadith za Mashia zilitoa watunzi wengi mno na ambao maandishi yao kuanzia kipindi cha al-Imam al-Sadiq(a.s) yamekuwa kwa hakika ni katika idadi kubwa sana. Iwapo mtu ataweza kutupia macho Rijal al-Najashi, basi huyo ataweza kuona kuwa wafuasi wa Imam(a.s) wametupatia kazi kubwa ambazo zimetumika kama misingi ya Fiqh katika Ushia. Ukweli ni kwamba, Mashia idadi yao ndogo kwa upande mmoja na maisha ya hatari waliyokuwa wakiishi kwa upande wa pili ambayo iliwazuia watu waovu na wenye kuvizia majukumu kuingia katika Ushia pamoja na umuhimu uliosisitizwa na Maimamu(a.s) na wafuasi wao katika uandishi, ndivyo vilivyoleta matokeo ya utajiri na usahihi wa Fiqh ya Kishia. Haya ndiyo faida ambazo hazikupatikana kwa Ahl al-Sunnah kwani, kwanza, wingi wa idadi yao, pili, kwa kuwa madhehebu ya Sunni ndiyo iliyokuwa Dini ya utawala wa Dola, na tatu, kwa sababu ya ukosefu wa Hadith zilizoandikwa kwa Waislam kwa ujumla kuyafuatilia yale yanayotokana na ukweli wa misingi ya kihistoria.