HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.18%

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s. Mwandishi:
Kundi: VITABU VYA HADITHI

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 30830 / Pakua: 10404
Kiwango Kiwango Kiwango
HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

3

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w)NA MA-IMAMU (a.s)

SALA ZA USIKU WA MANANE

25. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Heshima ya Mumiin ipo katika kukesha kwake usiku na utukufu wake upo katika kujitawala mwenyewe miongoni mwa watu ." [25]

26. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Yeyote yule alale zaidi wakati wa usiku, lazima atapoteza kitu mujimu kabisa katika matendo yake (i.e. sala ya usiku) ambayo hataweza kuipata wakati wa mchana ."[26]

27. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : Allah swt katika ufunuo wake kwa Mtume Musa(a.s) ., mwana wa 'Imran(a.s) . alisema: "Ewe Mwana wa 'Imran! Wale tu ambao wanadai kunipenda mimi, wasema uongo, kwani usiku unapoingia wao hulala huku wakiniacha mimi ."[27]

28. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Kamwe usiikose Sala ya usiku wa manane! Kwa sababu, ukweli ni kwamba, mpotezaji ni yule anayeikosa (faida zake) Sala za usiku wa manane. "[28]

29. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alimwambia Jibrail amwambie chochote, naye alimwambia: "Ishi utakavyo huku ukitambua kuwa utakuja kufa; penda chochote kile utakacho lakini utatengana nacho; tenda utakavyo lakini utakutana nacho ( na kulipwa malipo yake). Heshima ya Mumin ni Sala yake ya Layl (usiku wa manane), na utukufu wake upo katika kujiepusha (na kuangamiza) sifa za watu. " [29] .

30. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Vipo vitu vitatu ambavyo ndivyo sifa za Muumin na ndivyo vito vya thamani kwake humu duniani na Aakhera. Navyo ni: Sala katika sehemu ya mwisho wa usiku (Salat ul-Layl), kutotamani au kuwa na wivu kwa kile kidogo kilicho mikononi mwa watu, na mapenzi (na uongozi ) wa Imam kutokana na kizazi cha Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) "[30] .

31. Amesema al-Imam Muhammad ibn Ali al-Jawad ul- 'A'immah(a.s) : "Yeyote yule aliye na imani kamili juu ya Allah swt, anaona furaha; na yeyote amwaminiaye, basi anatosheleza matendo yake ."[31] .

KUMWAMINI ALLAH NA KUIPATA FURAHA YAKE

32. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Baba yangu aliniambia kuhusu baba yake kuwa mtu mmoja kutoka mji wa Kufa alimwandikia baba yake viz. Al-Husayn ibn Ali(a.s) ., akimwuliza(a.s) . kumjulisha yeye kuhusu mema ya dunia hii na mema ya Akhera. Kwa hayo Imam(a.s) . alimwandikia (katika majibu): "Kwa jina la Allah,aliye Rahmaan na Rahiim'. Baadaye akiendelea 'Kwa hakika yeyote yule atakaye furaha ya Allah swt hata wakati wa kutokuwafurahisha watu, Yeye humtosheleza katika masuala ya watu. Lakini, yule ambaye hutaka furaha za watu wakati anamuudhi Allah swt, basi Allah swt humwachia watu ( na yeye atakuwa mbali na baraka za Allah swt), Wassalaam' ."[32]

33. Amesema Al-Imam Zayn Al-Abedin(a.s) : "Yeyote yule atendaye matendo yake kwa mujibu wa vile alivyoamrisha Allah swt, ni miongoni mwa watu bora ."[33] .

34. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Yeyote yule aliye na mapenzi ya Allah swt,anachukia kwa ajili yake Allah swt, na anatoa msaada kwa ajili ya Allah swt, basi huyo ni miongoni mwa wale ambao Imani yao imekamilika ."[34]

35. Amesema Al-Imam Al-Hasaan Al-Askari, Imam wa Kumi na Moja,(a.s) : "Hakuna sifa zaidi ya hizi mbili: Kuwa na Imani kwa Allah swt na kuwa mwenye manufaa kwa Waislamu ."[35] .

TAQWA NA UMUHIMU WAKE KWA WAISLAMU

36. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Miongoni mwa kitu kilicho muhimu kabisa kwa kuwafikisha watu hadi kufikia Peponi ni taqwa na tabia njema ." [36] .

37. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Wakati wa kutoa uamuzi wa kitu, fikiria matokeo yake. Iwapo ni nzuri kwako wewe kuendelea na maendeleo, fuata hivyo, lakini iwapo inakupotosha, uiachilie mbali ."[37] .

38. Aliulizwa Al-Imam As - Sadique(a.s) . kuhusu maana ya Taqwa, na alijibu: "Allah swt hakukosi mahala pale alipokuamrisha wewe uwepo, na hakuoni pale ambapo amekuharamishia wewe kuwepo ."[38]

39. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Onyesha heshima zako kwa ajili ya Allah swt kama vile utakavyoonyesha heshima zako mbele ya mtu mwema miongoni mwa ukoo wako ." [39]

40. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s): "Kwa mtu kuinamisha macho yake kutamwia kama kizuizi dhidi ya matamanio (shahwa) yake ."[40]

41. Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amewaambia wana wake Al Imam Hassan ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . na Al Imam Hussein ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . wakati 'Abdur Rahman ibn Muljim (Allah amla'ani) alipokuwa amempiga dharuba ya upanga kichwani mwake, katka Nahjul Balagha, Barua no. 47: "Ninawasihini nyote mumwogope Allah swt na nyinyi wala musiwe na uchu wa starehe za dunia hii hata kama itawakimbilia nyinyi. Wala musikisikitikie kitu chochote cha dunia hii ambacho mumekikosa. Semeni ukweli na mutende (kwa kutumai) malipo. Muwe adui wa mdhalimu na msaidizi wa mdhulumiwa ."

42. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Ninawauusieni kumwogopa Allah swt, Ewe mwana wangu, kubakia katika Amri Zake, kuujaza moyo wako kwa ukumbusho Wake na kubakia katika kumtegemea Yeye tu. Hakuna Hakuna ushikamano unaotegemewa kuwa madhubuti baina yako na Allah isipokuwa wewe iwapo utaishikilia menyewe .[41]

43. Abi Osama Amesema kuwa alimsikia Al Imam Ja'afer as- Sadiq(a.s) . alisema: "Muwe nakhofu za Allah, taqwa, ijtihadi, kusema ukweli, uaminifu katika amana, tabia njema na ujirani mwema. Muwaite wengine kwenu (kwa tabia zenu njema), wala si kwa maneno tu. Muwe watu wenye kupendeza na kamwe musiwe watu wa kutuaibisha. Ninawausieni murefushe rukuu' na sujuda zenu. Kwani kila mmoja wenu anaporefusha rukuu' na sujuda basi Shaytani hulia nyuma yenu kwa kusea 'Ole wako! yeye ametii; amesujudu na mimi nilikataa ."[42]

44. Al Imam Zaynul 'Abediin ibn Hussein bin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kwa hakika marafiki wa Allah hawatakuwa na khofu yoyote juu yao wala hawatakuwa watu wenye kuhuzunika) iwapo watadumisha yaliyofaradhishwa na Allah swt, wakafuata Sunnah za Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w)wakajiepusha na yale yaliyoharamishwa na Allah swt, wakawa wacha Allah swt wema katika kile walichonacho katika utajiri na wadhifa wa humu duniani, wakajitahidi kujitafutia kile kilicho halali, wakaamua kutojifakharisha wala kutojilimbikia katika mali na utajiri isipokuwa katika kutoa misaada na kutoa malipo ya kulipa yaliyofaradhishwa kwake. Basi kwa hakika hao ndio waliobarikiwa katika mapato yao na watalipwa mema kwa yale waliyoyatanguliza huko Aakhera. "[43]

45. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Kwa hakika Wana wa Adam wapo sawa na meno ya kitana kuanzia zama za Mtume Adam (a.s) . hadi leo, na wala hakuna utukufu wa Mwarabu juu ya asiye Mwarabu, wala Mwekundu juu ya Mweusi isipokuwa kwa Taqwa ."[44]

46. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Kwa hakika, tendo dogo kabisa lifanywalo pamoja na Taqwa ni bora kabisa kuliko tendo kubwa (au matendo mengi) lifanywalo bila Taqwa. "[45]

KUOMBA DUA

47. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Dua yoyote inayoombwa kwa Allah swt, inakuwa imezuiwa na mbingu hadi hapo iwe imeshirikishwa na Salawat i.e. kumsaliwa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w)pamoja na Ahlil Bayt (a.s) . "[46]

48. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Muminiin waombao Dua zao hazikukubaliwa humu duniani watatmani kuwa dua zao hata moja zisingelikubaliwa pale watakapoonyeshwa hapo Aakhera, mema kupita kiasi ya thawabu (akipewa yeye kwa kutokujibiwa Dua zake na kwa mateso na shida alizozipata akiwa humu duniani) ."[47]

49. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Tendo lipendwalo sana mbele ya Allah swt humu duniani ni Dua na ibada iliyo bora kabisa mbele Yake ni unyenyekevu na ucha-Allah swt. "[48]

50. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Milango ya Peponi ipo wazi kwa nyakati tano: wakati mvua inyeshapo; wakati wa Vita vitukufu; wakati wito wa Sala utolewapo (wanapotoa Adhaan) ; wakati wa kusoma Qur'an Tukufu wakati ambapo jua linazama na linachomoza alfajiri ."[49]

51. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mujiweke tayari kuomba Dua katika nyakati tano: Wakati usomwapwo Qur'an; Wakati utolewapwo Aadhaan; Wakati unaponyesha mvua; Wakati wa kwenda kupigana katika vita vitakatifu kwa ajili ya kuwa shahidi; Wakati madhulumu anapoomba dua, kwa sababu yeye hana kizuizi cha aina yoyote chini ya mbingu ."[50]

52. Amesema Al Imam Hussain ibn 'Ali bin Abi Talib(a.s) . , katika Dua 'Arafah: "Ewe Mola Wangu! Wewe U karibu kabisa wa kuombwa; Na mwepesi wa kujibu; na Wewe Mkarimu wa kutoa; na unamtosheleza umpaye; unamsikia vyema akuulizae; Ewe Uliye Rahmaan wa dunia na Aakhera na Mremehevu kote !"

53. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Anayejaaliwa vitu vinne hanyimwi vinne: Anayejaaliwa kuomba Dua hanyimwi kukubalika kwake; anayejaaliwa kufanya Tawba hanyimwi kukubalika kwake; anayejaaliwa kuomba msamaha hanyimwi kusamehewa kwake; anayejaaliwa kutoa shukuurani zake hanyimwi kuongezewa kwake ."[51]

54. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Siku ya Qiyama, Allah swt atazihesabu Dua zote alizokuwa akiziomba Mja wake na kuuzibadilisha katika matendo mema na kwa hayo atawapandisha daraja katika Jannat (Peponi) ."[52]

55. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Ponyesheni magonjwa yenu kwa kutoa Sadaka na mujiepushe na balaa za kila aina kwa Dua "[53]

56. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) .

60: "Mwombe Allah swt maombi yako na daima uwe ukisisitiza katika kumwomba kwani Allah swt mwenyewe anapenda mno kubakia kwa kumsisitiza miongoni mwa waja wake Muminiin ."[54]

57. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Ninakuusieni muombe Dua', kwa sababu hamtaweza kumkaribia Allah swt kwa vinginevyo kama hivyo ."[55]

58. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Inawezekana kuwa wewe umemwomba Allah swt Dua ya kitu fulani ambacho yeye hakukujaalia kwa sababu yeye anataka kukupa kitu kilicho bora zaidi ya kile ulichokuwa umekiomba, hapo mbeleni(unatakiwa kufanya subira - mtarjum) ."[56]

AHLUL BAYT (A.S)

59. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Mfano wa Ahlul-Bayt yangu kwa Ummah wangu ni sawa na Safina ya Mtume Nuh (a.s). Wote wale watakaoipanda ndani yake basi wameokolewa na wote wale waupingao, basi wamezama na kupotea ."[57]

60. Amesema Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) ., Imam wa tano: "Ahadith zetu (za Alhul Bayt) zinahuisha nyoyo ."[58]

61. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Muhuishe mikutano na mikusanyiko yenu kwa makumbusho ya Ali ibn Abi Talib (a.s) ." [59]

62. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : na yenye maana yakaribiayo katika Yanabi-ul- Muwaddah, uk. 117: Ipo riwaya kupitia Jabir-il-Ju'fi iliyopokelewa kutoka Jabir-ibn-Abdillah isemayo: Mimi nilisema: Ewe Mtume wa Allah swt, sisi tunamwelewa Allah swt na Mtume wake(s.a.w.w) Sasa jee hawa 'Ulul-Amr ni wakina nani ambao utiifu wao umefardhishwa sawa na wako?

Hapo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alisema: "Ewe Ja'abir! Wao ni, baada yangu, Makhalifa wangu na Ai'mmah wa Waisilamu; wa kwanza miongoni mwao ni Ali ibn Abi Talib(a.s) ; atafuatia (Imam) Hassan, na (Imam) Husayn; atafuatia Ali ibn il Husayn; atafuatia Muhammad ibn Ali; ajulikanaye katika Tawrati kama Baqir, ambaye utakutana naye, Ewe Ja'abir! Pale utakapomtembelea, umpe salaam zangu. Baada yake Musa ibn Ja'afar; atafuatia Ali ibn Musa, atafuatia Muhammad ibn Ali; atafuatia Ali ibn Muhammad, atafuatia Hassan ibn Ali; na baada yake (atakuja) Al-Qaim, ambaye jina lake ni sawa na jina langu. Yeye ndiye atakaye kuwa Mamlaka Ya Allah swt juu ya ardhi hii na Aliyebakia miongoni mwa Waja wake. Yeye ndiye mwana wa (Al-Imam) Hassan ibn Ali ( al-'Askari). Huyu ndiye shakhsiyyah ambaye Allah swt atafungua Dhikiri zake Mashariki na Magharibi na huyu ndiye Shakhsiyyah ambaye atakuwa ghaibu kwa wafuasi na wapenzi wake ambavyo hakuna nyoyo zozote zile zinazoweza kukubali isipokuwa nyoyo za wale tu ambao Allah swt ameshakwishakuzijaribu kwa ajili ya Imani."[60]

Ja'abir alisema: "Mimi nilimwuliza 'Ewe Mtume wa Allah swt! Je wafuasi wake watafaidika naye wakati akiwa ghaibu? Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alijibu: 'Naam. Kwa kiapo cha Yule aliyenichagua kuwa Mtume, wao watafaidika kwa nuru yake na watafaidika kwa ibada akiwa ghaibu kama vile kufaidika kwa watu kutokana na (nuru ya ) jua hata pale linapofunikwa kwa mawingu.'"

63. Amesema Malik ibn Anas kuhusu mema ya Imam As-Sadique(a.s) : "Hakuna macho yaliyowahi kuona, hakuna masikio yaliyokwisha kusikia, na wala hakuna moyo uliyokwisha shtushwa kwamba kunaweza kuwapo na mtu yeyote aliye bora zaidi kuliko (Imam) Ja'afar as- Sadique(a.s) . katika Taqwa, elimu, ibada na Ucha-Allah swt."[61]

64. Amesema Al Imam Hussain ibn 'Ali bin Abi Talib(a.s) ., Al-Irshaad, Uk. 204: "Kwa roho yangu, hakuna Imam isipokuwa ni Hakimu kwa Kitabu, anaimarisha uadilifu, anaamini katika Dini ya Ukweli, na anajizuia nafsi yake pamoja na njia ya Allah swt ."

MAPENZI YA AHLUL-BAYT (A.S).

65. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , Al-Jami'- ul-Saghir, J. 1 Uk. 14: "Wafunzeni watoto wenu vitu vitatu: Mapenzi ya Mtume wenu, Mapenzi ya Ahlul-Bayt, usomaji wa Qur'an ."

66. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Mtu yeyote ambaye hawezi kutufanyia wema wowote sisi Ahlul-Bayt basi wawafanyie mema wafuasi wetu walio wema; na yeyote yule asiyeweza kutuzuru, basi wanaweza kuwazuru wafuasi wetu walio wema ambavyo thawabu za kutuzuru sisi zitaandikiwa yeye ."[62]

67. Amesema al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) : "Kwa kile kilicho bora kabisa kwa mja kumkaribia Allah swt ni utiifu kwake Allah swt, utiifu kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . na utiifu kwa ulil Amr." Aliendelea kusema: "Mapenzi yetu (ya Ahlul-Bayt) ni Imani na chuki dhidi yetu ni kufr." [63]

68. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Kwa hakika zipo daraja za ibada, lakini mapenzi yetu , Ahlul-Bayt, ni ibada iliyo bora kabisa ."[64]

SIFA NA TABIA ZINAZOKUBALIKA

69. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Je niwatambulisheni Mu'miin ni nani? Muumin ni yule ambaye waumini wengine wanamwamini kwa nyoyo zao na mali pia. Je niwatambulisheni Mwislamu ni nani ? Mwislamu ni yule ambaye Waislamu wengine wanakuwa wamehifadhika kwa ulimi na mikono yake.. Ni haramu kwa Mumiin kumfanyia ubaya mumin mwenzake, au kumwacha katika hali ya shida, au kumsengenya au kumkataa kwa ghafla ."[65]

70. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Haimpasi Mwislamu kuhudhuria au kushiriki katika mikutano au mikusanyiko ambapo Sharia za Allah swt zinavunjwa na kwamba yeye (huyo Mwislamu) hana uwezo wa kuyazuia hayo ."[66] .

71. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Yeyote yule kwa tabia yake husema ukweli, basi matendo yake yametakasika; Na allah swt humwongezea riziki yule aliye na nia njema; na yeyote yule awatendeaye mema familia yake, Allah swt humwongezea umri mrefu ."[67]

72. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alijiwa na mtu mmoja aliyeomba kufundishwa tendo kwayo ataweza kupendwa na Allah swt pamoja na watu, utajiri wake utaongezeka, mwili wake utakuwa na siha nzuri, umri wake utaongezeka na atainuliwa Siku ya Qiyama pamoja na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alimjibu: 'Hizi ndizo njia sita zinazohitaji sifa sita: Iwapo wataka Allah swt akupende, lazima umwogope na ujiepushe na madhambi,Iwapo wataka watu wakupende, lazima uwe mkarimu kwao na ukatae walichonacho mikononi mwao, Iwapo wataka Allah swt akuongezee utajiri wako, hunabudi kutoa malipo yaliyofaradhishwa kwako i.e. Zaka, Khums, na zinginezo.

Iwapo wataka Allah swt aupatie mwili wako afya njema, basi uwe ukitoa sadaqa kila mara iwezekanavyo, Iwapo wataka Allah swt aurefushe umri wako, basi uwe ukiwajali maJama'a zako, Iwapo wataka Allah swt akuinue pamoja nami Siku ya Qiyama, basi ni lazima urefushe sujuda zako mbele ya Allah swt, aliye Pekee na Mmiliki."[68]

73. Amesema Al-Imam Ar-Ridhaa(a.s) . Imam wa Nane: "Mumin hawezi kuwa mumin kamili hadi hapo atakapokuwa na mambo matatu: Sunna za Allah swt, Sunna za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . na Sunna za Imam(a.s) . wake. Ama Sunna za Allah swt ni kuzificha siri zake; kama vile Allah swt anavyosema katika Sura Al-Jinn, 72, Ayah 26 & 27. Yeye ndiye mwenye kujua ya siri, wala hamdhihirishii yeyote siri yake, Usipo kuwa Mtume wake aliye mridhia. Naye huyo humwekea walinzi mbele yake na nyumba yake.[69]

Na ama Sunnah za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni kule kupatana na kuelewana na watu, wakati ambapo Allah swt alimtuma Mtume wake kuwapenda watu na Amesema: 'Uzoee usamehevu na uwafundishe mema na ujiondoe kutoka majaheli Ama kuhusu Sunnah za Imam(a.s) . (kuwa imara na) mwenye subira katika siku nzuri na siku mbaya na nzito, ambavyo Allah swt anatuambia katika Sura Al-Baqara, 2, Ayah 177. Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni wa anaye muamini Allah swt na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na anawapa mali, kwa kupenda kwake, Jama'a na mayatima na masikini na wasafiri, na akawa anashika Sala, na akatoa Zaka, na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanao vumilia katika shida na dhara na wakati wa vita; hao ndio walio sadikisha, na hao ndio wajilindao.

74. Amesema Al Imam Muhammad al-Taqi(a.s) . (al-Jawad Imam wa Tisa), Muntah al-'Amal, Uk.229: "Mumin anahitaji mambo matatu: mafanikio yatokayo kwa Allah swt, mwenye kujipa mawaidha, kukubaliwa na yule ampaye nasiha. "

75. Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Imam wa Nne, aliulizwa "Ewe mwana wa Mtume! Huanzaje siku yako?" Na Imam(a.s) . alijibu: "Mimi huanza siku yangu huku nikitakiwa kutimiza mambo manane (8): Allah swt ananitaka nitimize yaliyafaradhiwa juu yangu; Na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . ananitaka nitimize yale yaliyo Sunna yake; Familia yangu inanitaka mimi niwatimizie mahitaji yao kama chakula n.k.; Nafsi yangu inanitaka niitimizie matamanio yangu; Shaytani aninitaka mimi nitende madhambi; Malaika wawili wanaonihifadhi wananitaka mimi nitende matendo kwa moyo halisi, Malaika wa Mauti anataka roho yangu na Kaburi inautaka mwili wangu. Basi mimi ndivyo nilivyo baina ya mzunguko wa matakwa hayo."[70]

76. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Kwa hakika kila kitu kinashawishiwa na Mumin kwa sababu Dini ya Allah swt inamfanya yeye awe ni mtu mwenye nguvu, na wala yeye kamwe hashawishiwi na kitu chochote kile, na kwa hakika hii ndiyo dalili ya kila Mumin ." [71]

4

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w)NA MA-IMAMU (a.s)

WAFUASI HALISI WA AHLUL-BAYT (A.S) NA SIFA ZAO

77. Al Imam Muhammad al Baqir(a.s) . alimwambia, Ja'bir: "Je inatosheleza kwa mtu kujiita Shia na mfuasi wetu ati kwa kudhihirisha mapenzi yetu, Ahlul Bayt? Kamwe sivyo hivyo!, Kwa kiapo cha Allah swt, huyo mtu kamwe hawezi kuwa mfuasi wetu isipokuwa yule ambaye amejawa khofu ya Allah swt na kumtii ipasavyo. Ewe Ja'abir! Wafuasi wetu hawawezi kutambuliwa isipokuwa kwa sifa zifuatazo watakazokuwanazo kama unyenyekevu, kujitolea; uadilifu; kumsifu Allah kupita kiasi; kufunga saumu na kusali; kuwatii wazazi; kuwasaidia masikini, wenye shida, wenye madeni, na mayatima wanaoishi karibu naye; kusema ukweli; kusoma Qur'an; kuuzuia ulimi kusema chochote kuhusu watu isipokuwa kwa mapenzi; na kuwa mwaminifu kwa majama'a kwa maswala yote ."[72]

78. Amesema Sulayman Ibn Mahran kuwa Yeye alimtembelea Imam Ja'afer as-Sadique(a.s) . wakati ambapo baadhi ya wafuasi (Mashiah) walikuwa karibu naye na alimsikia Imam(a.s) . akiwaambia:"(Mujiheshimu) muwe kama vito vya thamani kwa ajili yetu na wala kamwe musiwe wenye kutuaibisha sisi. Waambieni watu kuhusu mema, na muizuie ndimi zenu zisizungumze mneno maovu na mambo yasiyo na maana ."[73] .

79. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Kwa hakika, sisi huwapenda wale walio na busara, wenye kuelewa, wenye elimu, wenye kufanya subira, waaminifu na wenye imani. Kwa hakika Allah swt aliwajaaliwa Mitume(a.s) . kwa tabia njema. Kwa hivyo yeyote yule aliye na sifa hizo basi amshukuru Allah swt, lakini yule ambaye hana hayo basi amlilie Allah swt, Aliye Mkuu na Mwenye uwezo, na amwombe hayo. "Ja'abir kwa unyenyekevu alimwuliza Imam(a.s) . ndiyo yapi hayo", na Imam(a.s) . alimjibu: "Nayo ni: Ucha-Allah swt, kutosheka, subira, kushukuru, kuvumilia, tabia njema, furaha, hima, bidii, shauku, mkarimu, mkweli na mwaminifu katika amana ."[74] .

80. Amesema Al-Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Yeyote yule anamtii Allah swt basi ni mpenzi wetu, na yeyote yule asiyemtii Allah swt basi ni adui wetu (sisi Ahlul-Bayt) .."[75] .

MADHAMBI NA ATHARI ZAKE

81. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Msitazame udogo wa dhambi, lakini muangalie mliyemuasi (Allah swt) ." [76] .

82. Amesema Al-Imam Amir-ul-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Iwapo mtu anapenda kujiona vile alivyo mbele ya Allah swt, basi ajitathmini kwa madhambi na maasi yake mbele ya Allah swt; basi kwa kipimo hicho ndivyo alivyo huyo mtu mbele ya Allah swt ."[77] .

83. Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) . aliwauliza watu ni kwa nini wanamwudhi Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) Basi mmoja wa watu alimwuliza Imam(a.s) . vipi, naye Imam(a.s) . aliwaambia: "Je hamujui kuwa matendo yenu yapoyanajulishwa kwa Mtume Mtukufu (s.a.w.w) na pale aanapoona madhambi dhidi ya Allah swt miongoni mwao, basi husikitishwa mno. Kwa hivyo musimuudhi Mtume wa Allah swt na badala yake munatakiwa kumfurahisha (kwa kutenda mema) ."[78] .

84. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Kukosa kusamehe ni kasoro moja kubwa kabisa na kuwa mwepesi katika kulipiza kisasi ni miongoni mwa madhambi makubwa kabisa "[79] .

85. Kutokea Asbaghi bin Nabatah kutokea kwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa:Allah swt anapoukasirikia Ummah na kama hakuiadhibu basi bei za vitu vitapanda juu sana yaani maisha yatakuwa ghali, maisha yao yatakuwa mafupi, biashara zao hazitaingiza faida, mazao yao hayatukuwa mengi, mito yao haitakuwa imejaa maji, watanyimwa mvua (itapungua), na watatawaliwa na waovu miongoni mwao ." [80] .

(Yaani Hadith hiyo juu inatubainishia kuwa iwapo kutakuwa na jumuiya ambayo imejitumbukiza katika madhambi basi wanabashiriwa kupatwa na mambo saba hayo yaliyotajwa.).

86. Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . Amesema kuwa amekuta katika kitabu cha Al-Amir al-Muminiin Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . akisema kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) Amesema: "Wakati zinaa itakapokithiri katika jumuiya basi idadi za mauti za ghafla zitakithiri; na patakapokuwa na uovu basi Allah swt atawatumbukiza katika maisha ya ghali na hasara. Wakati watu watakapoacha kulipa zaka , basi ardhi itazinyakua baraka zake kutokea mazao, matunda, madini na vitu vyote kama hivyo. Wakati watakapotenda bila haki kwa mujibu wa Shariah, basi itakuwa sawa na kumsaidia dhalimu na ugaidi. Na watakapozikiuka ahadi zao, basi Allah swt atawafanya maadui wao kuwasaliti na kuwakandamiza. Wakati watakapoacha uhusiano pamoja na ndugu na Jama'a zao, basi yote yale wayamilikiayo yatakwenda mikononi mwa waovu. Na wakati watakapojiepusha na kutoa nasiha ya mambo mema na kuyakataza maovu na kama hawatawafuata waliochaguliwa Ahl-ul-Bayt(a.s) , basi Allah swt atawasalitisha kwa walio wenye shari miongoni mwao na katika hali hii, wataomba duaa lakini hazitakubalika."[81] .

87. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Machozi hayaishi illa kwa nyoyo kuwa ngumu, na nyoyo haziwi ngumu illa kukithiri kwa madhambi .[82] "

88. Allah swt alimwambia Mtume Dawud(a.s) : "Ewe Dawud! Wabashirie habari njema wale watendao madhambi kuhusu msamaha wangu, ambayo inajumuisha kila kitu kilichopo humu duniani, ili wasikate tamaa ya msamaha wangu; na waonye wale watendao mema kwa adhabu zangu ili wasije wakajifanyia ufakhari kwa utii wao, kwani ufakhari ni dhambi mbaya kabisa."[83] .

ELIMU NA THAMANI YAKE

89. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Waalimu pamoja na wanafunzi wanashirikiana katika kuulipwa mema wakati watu wengine hawabahatiki.."[84] .

90. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Yeyote yule aienezaye Din kwa watu bila ya yeye mwenyewe kuwa na ilimu ya kutosha, basi anaidhuru Din zaidi kuliko vile anavyoitumikia."[85] .

91. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Thamani ya kila kitu ni katika ubora wake." Yaani thamani ya mtu ni katika ilimu yake. Cheo na utukuzo wake utakuwa katika kiwango cha ilimu aliyonayo. Macho yetu hayaangali sura, urefu ukubwa wa mwili wa mtu bali humthamini kwa kufuatana na kiwango cha ilimu aliyonayo. Hivyo inatubidi sisi sote tujitahidi katika kutafuta na kuipata ilimu kwa kiasi tuwezacho.[86] .

92. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Elimu ni amana ya Allah swt juu ya ardhi hii na wanazuoni ndio wenye amana hii. Hivyo yeyote yule atebdaye kwa mujibu wa ilimu yake, basi kwa hakika ameiwakilisha amana vile ipasavyo"[87] .

93. Al-Imam Muhammad Baqir(a.s) . amesema: "Jitafutieni ilimu kwa sababu kujifunza ni matendo mema na kusoma kwenyewe ni 'ibada ."[88] .

94. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) Amesema: "Mtu ambaye anatafuta ilimu, ni sawa na mpiganaji vita katika njia ya Allah swt ."[89]

95. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Uichunge sana ilimu yako na utazame ni kwa nani unaitoa ."[90] .

96. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Muitafute ilimu na kuipamba kwa subira na ukuu ; na uwe mnyenyekevu kwa yule ambaye anaitafuta ilimu kutoka kwako "[91] .

97. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) katika, Al-Kafi, J. 1, Uk. 35: "Yeyote yule ajifunzae ilimu na kutenda vilivyo, na kuifundisha kwa ajili ya Allah swt, basi Malaika watatmukuza mbinguni ."

98. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Wema wa duniani humu pamoja na Aakhera ni pamoja na ilimu ." [92] .

ILIMU NA FADHILA ZA KUJIFUNZA

99. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Yeyote yule atafutaye ilimu ni sawa na mtu anayefunga saumu mchana na akikesha macho usiku kucha akifanya ibada. Iwapo atajifunza ilimu kwa sehemu fulani, basi itakuwa kwake ni afadhali kabisa hata kuliko kuwa na dhahabu ya ukubwa wa mlima Abu Qubais na ambayo itagawiwa sadaqa katika njia ya Allah swt ." [93] .

100. Al-Imam Zaynul 'Aabediin(a.s) . Amesema: "Iwapo watu wangalikuwa wakitambua kile kilichopo ndani ya kutafuta ilimu, basi wao wangaliitafuta hata kama itawabidi kusafiri na hata kuhatarisha maisha yao katika kuipata ."[94] .

101. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kutafuta ilimu haitawezakana wakati mwili unastareheshwa ."[95] .

(yaani mtu hataki kutaabika)

102. Amesema Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) : "Hifadhini maandiko na vitabu vyenu kwa sababu hautapita muda mutakapovihitaji ."[96] .

103. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kwa hakika, kukamilika kwa Din ni kule kuitafuta ilimu na kuitekeleza ipasavyo, na muelewe waziwazi kuwa kutafuta ilimu ni faradhi zaidi kwenu nyinyi kuliko kutafuta mali na utajiri. "[97] .

104. Amesema al-Imam al-Hassan ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Wafundisheni watu wengine ilimu muliyonayo na mujaribu kujifunza ilimu waliyonayo wengineo "[98] .

105. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Fadhila za ilimu zinapendwa zaidi na Allah swt hata kuliko fadhila za ibada ." [99] .

ILIMU NA FADHILA ZA KUIFUNDISHA

106. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Mtu yeyote aliyekuwa na ilimu kuhusu swala fulani na akaificha pale atkapoulizwa basi Allah swt atamkasirikia kwa ghadhabu za moto."[100] .

(yaani mtu anapokuwa na habari ambazo zitamsaidia mtu aliyepatwa na shida na ikaweza kumsaidia kuimarisha hali yake, badala ya kumsaidia yeye akaificha, basi hapo kwa hakika ametenda dhambi kubwa.)

107. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Qur'an Tukufu ni chuo kikuu ; hivyo jielimisheni kiasi muwezavyo kutokea chuo hiki ." [101] .

108. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Kwa hakika, kile kitakachoendelea kumfikia mtu hata baada ya kufa kwake, miongoni mwa matendo yake mema ni: ilimu ambayo yeye amewafundisha na kuieneza kwa wengineo, mtoto mwema aliyemwacha, kuacha Qur'an Tukufu ikapatikana ." [102] .

109. Amesema al-Imam Ali ar-Ridha(a.s) : "Rehema za Allah swt ziwe juu ya yule ambaye anazihuisha amri zetu." Na halikuwapo mtu akamwuliza Imam(a.s) . ni vipi wanaweza kuhuisha amri zao, na Imam(a.s) . alimjibu: "Anaweza akijifunza ilimu zetu na akawafundisha watu. Kwa hakika, iwapo watu wangelikuwa wamezijua faida na mema ya semi zetu, basi kwa hakika wangalitufuata sisi ."[103] .

ELIMU - HEKIMA - MA'ARIFA

110. Elimu ni fidia kwa juhudi za akili.

111. Wema ni sababu kuu ya elimu.

112. Kumwogopa Allah swt ni matokeo ya elimu.

113. Jumla ya utukufu wote, ni elimu au ma'arifa.

114. Yeyote afundishaye herusi moja, amenifunganisha nae minyororo.

115. Elimu iliyo bora ni ile inayomfaa mwenye kuwa nayo.

116. Elimu ni hazina na maisha.

117. Unyenyekevu ni matokeo ya elimu na ma'arifa.

118. Mtu mwenye elimu yu hai hata kama amekufa.

119. Dini ni ghala na elimu ni mwongozo wa kuifikia ghala.

120. Ili kupata ufanisi itikia elimu na kupuuzia ujahiliya.

121. Wengi wanaelezea ma'arifa, lakini ni wachache waiingizayo akilini mwao.

122. Bakhshishi iliyo kamili ya Allah swt ni ile maisha iliyotegemea elimu na hekima.

123. Wapumbavu wengi mno wanawafanya wasomi kuwa wachache.

124. Aliyeelimika anamwelewa vyema mjinga kwani yeye binafsi alikuwa mjinga awali.

125. Na mtu aliye jahili hataweza kumwelewa mtu aliyeelimika kwani hajaelimika mwenyewe.

126. Wana elimu wanaishi katika kiwiliwili kilichokufa cha ujahili.

127. Ma'arifa huuwa ujahili.

128. Elimu ndiyo iipatiayo maisha Roho.

129. Ma'arifa chache (ya Allah swt) huharibu mwenendo wa mtu.

130. Hakuna chochote kile pasi na nuru ya kweli tu itakayokutakasisha.

131. Kuwaheshimu waliosoma ni kumheshimu Allah swt.

132. Ma'arifa ni chanzo cha khofu ya Allah swt (--inaletwa na )

133. Kile kikomazacho ma'arifa ni matendo kwa kutumia hekima na ma'arifa hayo.

134. Kufundisha ndiko kujifunza.

UMUHIMU WA MAARIFA

135. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alielekea Msikitini na huko akakuta makundi mawili ya Waislamu. Kikundi cha kwanza kilikuwa kikijifunza ilimu ya Dini, na kikundi cha pili kilikuwa kinafanya 'ibada. Kwa kuona hayo Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Vikundi vyote viko katika kheri, ama hawa wanamwomba Allah swt na hawa wanajifundisha na kuwafundisha wengine wasio na ilimu, kwa hakika hawa ndio bora, nimetumwa kwa watu ili kuwafundisha." Kisha akakaa pamoja nao .

136. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Ewe Kumail ! Hakuna harakati zozote utakazozifanya, ila unahitaji kuwa na maarifa ."

137. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Kukosa macho ni jambo jepesi kuliko kukosa mwanga (maarifa) ".

138. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Usizungumzie usilolifahamu ".

139. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Elimu ni msingi wa kila heri ".

140. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Katika hadith inayotokana na mababa zake, toka kwa Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . ambae ameipokea toka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) "Watu wengine walio na thamani (qimmah) kwa watu ni wale walio na elimu nyingi kati yao, na wale wenye thamani duni kati yao ni wale wachache wao wa elimu ".

KUTAFUTA ELIMU

141. Amesema Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) : "Kutafuta elimu ni faradhi (lazima) kwa kila Mwislamu Mwanamme na Mwislamu Mwanamke ".

142. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Kujitolea nafsi yake mtu kwa ajili ya kutafuta elimu, mfano wake ni kama anaepigana vita kwa ajili ya Allah swt .".

143. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . "Watu ni aina mbili; Aalimu (mwenye elimu) na mwenye kujifundisha, ama watu wengine ni upumbavu na wapumbavu mahala pao ni motoni ".

144. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kuwa mwenye elimu au mwenye kujifundisha elimu, jiepushe kuwa mwenye kupumbazika na kuona ladha ( ya kutojihangaisha kutafuta elimu.)

145. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . "Sikupenda kumwona kijana, kijana kati yenu ila amekuwa kati ya moja ya hali mbili; Ima awe mwenye elimu au mwenye kutafuta elimu, na kama hakufanya hivyo basi amepoteza nafasi yake, na aliye poteza nafsi yake amefanya dhambi na anayefanya dhambi ndio amekaa motoni. "

AKILI. 146. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema "Hakika heri yote hupatikana kwa akili ".

147. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Akili ni jahazi ya elimu. "

148. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Hakugawa Allah swt kwa waja wake kitu kilicho bora kuliko akili, usingizi wa mwenye akili ni bora kuliko kukesha kwa mtu mjinga, kufuturu (kutofunga) kwa mtu mwenye akili ni bora kuliko Saumu ya mtu mjinga, na kutosafiri kwa mtu mwenye akili ni bora kuliko safari ya mtu mjinga ".

149. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema "Ubinadamu wa mtu hutokana na akili yake ."

150. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : Kumwambia mtoto wake Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Ewe Mwanangu! Hakika ya utajiri ni utajiri wa akili na ufakiri mkubwa ni kuwa mtu mpumbavu ."

151. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Akili ndio mjumbe wa haki. "

152. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Rafiki wa kila mtu ni akili yake, na adui ni ujinga wake ".

153. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Mwenye kutekeleza (vitendo) kutokana na kile anachojua, Allah swt humrithisha (humjalia) elimu ambayo haijui ."

154. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Akili ni kitu cha maumbile, huzidi kwa elimu na majaribio ."

155. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Asiejaribu mambo hudanganyika ."

156. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Na majaribio ya muda mrefu ni nyongeza ya akili ."

157. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema: "Ewe Hisham! Hakika kwa Allah swt juu ya watu kuna dalili (burhani) mbili: Dalili ya wazi, na dalili ya ndani. Na ama ile ya wazi ni Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) , Manabii na Maimamu (a.s). na ama ya ndani ni akili ."

158. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema "Mwenye kuwa nayo akili, amekuwa na dini. "

159. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Mwenye kuijua nafsi yake, hakika amemjua Allah swt ."

160. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Huzijua mtu aibu za nafsi yake, ni maarifa yenye kunufaisha zaidi ."

161. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Na akili ni ngao (ngome) ya majaribu ."

162. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema "Na kila ujuzi unahitaji majaribio ."

163. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Kutafuta elimu ni bora kuliko kufanya ibada. Amesema Allah swt, Hakika wanaomwogopa Allah swt miongoni mwa waja wake ni wanachuoni .

164. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema "Hakuna zaka iliyo bora katika elimu kuliko kuifanyia kazi ."

165. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Mweney kuwa na yakini (uhakika wa Jambo) hufanya amali (kazi) hali ya kuwa yeye ni mwenye kupigania Jihadi. "

166. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Lau (mtihani wa Allah swt) husubiri, na asiyefahamu hakanushi ."

167. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Hasubiri mtu yeyote katika uchungu wa haki ila yule anae kuwa na yakini (uhakika) wa matokeo yake. "

168. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Hakuna kitu chochote kile ila kina upeo wake," akaulizwa" Ni nini upeo wa Yaqini (kuwa na uhakika)?. Akasema "Usiogope kitu chochote ."

169. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Kutoa majabali kutoka mahali pake ni rahisi kuliko kuutoa moyo kutoka katika chochote ."

170. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Haisafiki kazi mpaka isihi (iwe sahihi) elimu ."

171. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Mwanachuoni katika zama zake, hayamhujumu matatizo. "

172. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Aliye kamilika kiakili hayawi mazito kwake matatizo ."

173. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Akili iliyokamilika, ndiyo yenye kuvunja mabaya ."

174. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Lengo la elimu ni kufanya kazi vizuri ".

MAELEZO

1. Katika nadharia za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Mawasii wake, elimu ni kitu bora kuliko kitu kingine chochote kile, kiasi kwamba jambo hili limeweza kuwastajaabisha watu wengi kutokana na hadithi nyingi zilizo pokewa zinazo sifa ubora wa elimu, hadithi kadhaa zimesikiwa toka kwenye ulimi wake Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Maimamu (a.s) . Lakini je! Mshangao huo utabaki mpaka lini? Mshangao mbele ya uhakika wa mambo yalivyo hausaidii kitu. Je hatuamini kwamba maendeleo ya Dunia na Akhera hupatikana kwa elimu?. Jibu liko wazi kwamba kwa elimu hupatikana na maendeleo. Kwahiyo tunajionea wazi kuwa thamani ya elimu iko juu sana.

MAELEZO

2. Mwanadamu hutokea akajifunza elimu, lakini elimu yake ikawa ni upuuzi mtupu na balaa kwa watu, kutokana na kule kuvuka mpaka kwake na kuitumia elimu yake isivyo ndivyo na kinyume cha mtu mwenye akili, matokeo ya mtu wa ina hii ni kugundua mambo ambayo hayana faida yoyote kwa wengine, elimu kama hii humpoteza yeye mwenyewe na ummah pia katika dunia na akhera, hatimaye mtu huyu hugunduwa utengenezaji wa pombe na mabomu.

175. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Inamtosha mtu kuwa mjinga kwa kutokuzijua aibu zake ."

176. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Enyi watu! Hakuna heri katika dini isiyo na mafunzo ndani yake ."

177. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Mfanya ibada bila ya mafunzo ni kama punda mwenye kuzunguka, anazunguka na wala hachoki .''

178. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Mwenye kueneza elimu basi anao ujira mfano wa mwenye kutekeleza kwa hiyo (kutokana na elimu hiyo) ."

179. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Upingeni ujinga kwa elimu ."

180. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Katika kuwasifu waja wa Allah swt: Nawakasimamisha masikio yao (kwakusikiliza ) elimu yenye manufaa kwao ."

181. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema: "Nimekuta elimu ya watu iko katika mambo manne: Kwanza kati ya hayo manne ni kumjua Mola wako, Pili kujuwa alicho kiumba, Tatu kujuwa anacho taka kwako, Nne kujuwa chenye kukutoa katika dini yako ."

182. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Lau ningeijiwa na kijana miongoni mwa vijana wa ki-Shi'a hajifunzi (elimu ya dini) ninge mtia adabu. "

183. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Rafiki wa kila mtu ni akili yake na adui wake ni ule ujinga wake. "

184. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Mwenye akili ni kufikiri ataona (kuona muongozo)

185. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema: "Kila kitu kina dalili, dalili ya mwenye akili ni kufikiri na dalili ya kufikiri ni kunyamaza ."

186. Mtume Mtukufu Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Kufikiri kwa muda wa saa moja ni bora kuliko ibada ya mwaka ."

187. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Kufikiri ni kioo kilicho safi. "

188. Al Imam Hassan al-'Askari(a.s) . amesema: "Haikuwa ibada kwa uwingi wa kufunga na kusali, hakika ya ibada ni kufikiri (na kuzingatia) kuhusu Allah swt ."

189. Mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Elimu ndio kichwa cha kila heri na ujinga ndio kichwa cha kila shari ."

190. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Ujinga ni Umauti ."


6

7

8

9

10

11