HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 2

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 20%

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 2 Mwandishi:
Kundi: VITABU VYA HADITHI

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 2

Mwandishi: AMIRALY M.H.DATOO
Kundi:

Matembeleo: 19991
Pakua: 3232

Maelezo zaidi:

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 2
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 11 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 19991 / Pakua: 3232
Kiwango Kiwango Kiwango
HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 2

HADITH ZA MTUME s.a.w.w.NA MA-IMAMU a.s.V0L 2

Mwandishi:
Swahili

9

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w) NA MA-IMAMU(a.s)

SEHEMU YA PILI

UBASHIRI WA IMAM JAAFER AS-SADIQ(a.s)

1684. Mazungumzo yafuatayo yamefanywa na Imam Jaafer as-Sadiq(a.s) . ambamo ameripoti ubashiri wa siku za mwisho wa dunia hii. Yametolewa kutoka Darul Islam,Bihar-ul-Anwar na Raudhat-ul-Kafi. Wanaoripoti habari hizo ni Allamah Naraqi na Sheikh Kulaini r.a. kutokea kwa Himran. Imam(a.s) . alisema:

1. "Haki itakuwa imetokomezwa na watu walio katika haki hawatapatikana.

4. Dhulma na uonevu utaenea katika miji yote.

5. Kufuata Qur'an kimatendo itajulikana kama tabia ya kizamani.

6. Zitatolewa maana ya Aya za Qur'an kwa mujibu wa matakwa ya watu,hivyo mafhum ya Qur'an itakuwa imebadilishwa na kupotoshwa.

7. Wadhalimu watakuwa wakiwa kandamiza wale walio katika haki.

8. Uchokozi na uchochezi utatokea kutoka kila pande na pembe.

9. Matendo maovu na kukosa aibu vitaenea na kuzagaa kila mahala.

10. Ulawiti utakuwa ni jambo la kawaida.

11. Muumin atakuwa akionekana kama mtu dhalili ilhali waovu watakuwa wakiheshimiwa

12. Vijana hawatakuwa wakiwaheshimu wakubwa wao.

13. Huruma itakuwa imepotea kabisa.

14. Waovu watakuwa wakitukuzwa kwa udhalimu wao na hakutakuwapo na mtu yeyote wa kuwapinga.

15. Wanaume watafurahishwa mno kwa kuingiliana na wanaume wenzao.

16. Wanawake watawaoa wanawake wenzao.

17. Mapesa yatatumika kwa ajili ya matumizi yale yaliyo haramishwa na Allah swt.

18. Starehe, anasa na zinaa zitashamiri.

19. Zinaa itajulikana kama maadili yaliyopitwa na muda.

20. Muumin atatengwa kwa sababu ya kufanya ibada za Allah swt.

21. Jirani mmoja atafurahi mno kwa kumuudhi na kumbughudhi jirani mwenzake.

22. Wazushi (kama Salman Rushdie wa Uingereza) watatukuzwa na kusifiwa katika kueneza fitina na yale wanayozusha.

23. Ushauri mzuri utakanwa.

24. Milango ya wema yatafungwa wakati milango ya maovu yatafunguliwa.

25. Al-Kaaba haitatumika au haitafikika kwa sababu ya vikwazo na ugumu utakaowekewa mahujaji.

26. Watu watalazimishwa kuacha kwenda Makkah kuhiji.

27. Watu hawatakuwa wakitimiza ahadi zao watakazokuwa wakizitoa.

28. Wanaume watakuwa wakitumia dawa za kuamsha tamaa za kiume kwa ajili kulawiti na wanawake watakuwa wakitumia vyakula vya mafuta ili kujitayarisha kwayo.

29. Baadhi ya wanaume watakuwa wakiishi kwa kujipatia mapesa kwa kuuza mikundu yao.

30. Na wanawake watakuwa wakijipatia mapesa kwa kufanyisha biashara kuma zao.

31. Wanawake wataunda vilabu vyao,mashirika na umoja wao.

32. Wanaume atajigeuza kama wanawake na watavutia na wanawake.

33. Wanaume watajirembesha kama wanawake.

34. Ulawiti utachukuliwa kama ndiyo ustaarabu na starehe ya kweli.

Na Banu Abbas watalipia ulawiti.

35. Wanawake wataona fakhari kwa kuwa na waume nje ya mume mmoja wa ndoa na vivyo hivyo wanaume watakuwa hivyo hivyo.

36. Heshima itakuwa ikitolewa kwa utajiri wa mtu na wala si ucha Mungu.

37. Riba ndiyo itakayokuwa biashara ya kila siku.

38. Ushahidi wa uongo utakuwa ukIssadikiwa mno.

39. Kile alichokiharamisha Allah swt kitachukuliwa ni halali na chochote kile alichokihalalisha Allah swt kitachukuliwa ni haramu.

40. Maamrisho ya Dini yatageuzwa kwa mujibu wa matakwa yao.

41. Wachokozi na waovu watatenda maovu kwa udhahiri bila ya khofu yoyote ile na Muumin hawataweza kuwazuia vyovyote vile.

42. Watawala watawapenda mno Makafiri kuliko Muumiin.

43. Rushwa ndiyo itakuwa njia ya kujitimizia kazi kutoka maofIssa wanaohusika.

44. Wanaume wata walawiti wake zao.

45. Watu watakuwa wakiuawa kwa visingizio vidogo vidogo na magomvi madogo madogo.

46. Wanawake watawafanyia wanaume dhihaka, nao watashawishiwa kufanya uhusiano na wanawake.

47. Wanaume wataishi kwa mapato ya wake zao zitakazopatikana kwa zinaa.

48. Wanawake watakuwa wakiendesha hukumu majumbani huku wanaume wakiwatii wake zao kwa sababu wanawake hao ndio watakuwa wenye mapato.

49. Wanawake watatumiwa katika kupatikana huduma mbalimbali.

50. Kula kiapo kwa jina la Allah swt litakuwa ni jambo lililowekwa ulimini.

51. Pombe na kamari vitapatikana kila mahala na vitakuwa vimezagaa.

52. Wanawake wa Kiislamu wataingiliana na Makafiri,ambapo Waislamu hawataweza kuwazuia na wala hawatakuwa na uwezo kama huo.

53. Maadui wetu watasaidiwa na watawala na marafiki zetu watadhalilishwa kiasi kwamba hata kiapo chao hakitakubaliwa.

54. Udanganyifu na hila ndizo zitakuwa desturi miongoni mwa watu.

55. Usomaji na usikilizaji wa Qur'an utakuwa ni bughudha kwa watu.

56. Kusikiliza mambo fidhuli ndiyo itakuwa ikipendelewa na watu.

57. Jirani hatamstahi jirani mwenzake illa kwa khofu ya ulimi mkali na mchafu.

58. Sheria na kanuni za Allah swt hazitatambuliwa na waovu hawataadhibiwa kwa maamrisho hayo.

59. Ghiba na kulaghaiana ndivyo vitakuwa vitu vya kawaida.

60. Madhumuni ya Hajj na Jihad yatakuwa mbali na yale ya Kiislamu.

61. Misikiti itarembeshwa kwa dhahabu.

62. Watawala watawataka ushauri kwa nia ya Makafiri.

63. Litakuwa ni jambo la kawaida kuibia katika uzani na vipimo vya biashara.

64. Kumwaga damu ya watu wegine litakuwa ni jambo la kawaida.

65. Watu watajigamba kwa ndimi zao chafu zenye matusi mabaya ili kuwatishia watu wengine.

Imam(a.s) . aliendelea kusema:

66. "Watu watakuwa wakipuuzia sala na kutojali.

67. Watu hawatakuwa wakilipa zaka ingawaje watakuwa na utajiri mkubwa.

68. Sanda za maiti zitakuwa zikiibiwa na kuuzwa tena.

69. Mauaji yatakithiri mno kiasi kwamba hata wanyama pia wataanza kuuana wenyewe kwa wenyewe.

70. Watu watakuwa wakIssali katika mavazi ya kiajabu.

71. Macho na mioyo itapoteza nuru zao za heshima na huruma.

72. Watu watakuwa wamejishughulisha na maswala ya kutafuta mali na mapesa tu.

73. Watu watasali kwa kuonyesha tu.

74. Watu watatafuta ilimu ya Dini kwa ajili ya kujipatia mali ya dunia.

75. Ushirika katika makundi yatakuwa ndiyo mambo ya maisha.

76. Wale watakaojipatia riziki kwa njia ya halali,watasifiwa kwa midomo tu.

77. Matendo maovu na machafu yataenea hata Makkah na Madina.

78. Watu waliokufa watafanyiwa mizaha na vichekesho.

79. Mwaka hadi mwaka hali itakuwa ikiendelea kuharibika kuwa mbaya zaidi.

80. Matajiri wataigwa.

81. Masikini, mafukara watafanyiwa dhihaka na kufedheheshwa.

82. Matukio ya kudura kama yale ya mitetemeko,maporomoko n.k. yatakuwapo lakini watu watakuwa hawaviogopi.

83. Matendo maovu yatakuwa yakitendwa kiwaziwazi.

84. Wazazi watatupa watoto wao na watoto watawatusi wazazi wao na daima watakuwa wakitaka mali na utajiri wa wazazi wao.

85. Wanawake hawatawatii na kuwafuata waume wao.

86. Siku itakayopita bila ya mtu kutenda madhambi,basi itachukuliwa ni siku yenye nuksi.

87. Watu wenye uwezo wataficha mali muhimu na kuviuza kwa bei ya ulanguzi.

88. Waombaji na walaghai watajumuika katika kucheza kamari na kulewa.

89. Pombe itatumika kama ni kitu chenye kuponya i.e.dawa.

90. Makafiri watatukuzwa juu ya watu wengine na Muumin watadhalilishwa na kupuuzwa.

91. Kutafanywa malipo kwa ajili ya kutoa Adhan na sala.

92. Misikiti itajaa kwa watu wasiokuwa na khofu ya Allah swt.

93. Watu wenye fahamu na akili kasoro ndio watakaokuwa wakiongoza sala za jamaa' na watu kama hao kamwe hawatashutumiwa au kusutwa na badili yake wataheshimiwa."

VIFO VYEUPE NA VYEKUNDU

1685. Kuhusu kifo cheupe na chekundu, Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . alisema: "Kabla ya kudhihiri kwa al-Qaim (a.s). kutatokezea kwa aina mbili za vifo - nyekundu na nyeupe. Kwa nyekundu kunamaanisha damu yaani kumwagika kwa damu nyingi mno kwa sababu za vita na mauaji ya aina mbalimbali. Na kifo cheupe kinamaanisha kuzuka kwa maafa ya magonjwa ambayo yatakuwa daima yakienea na kuzuka kila mahala ."

Tanbihi : Kwa vifo vyekundu hapo juu tunaelewa kuwa kutakuwapo na vita vya kutisha mno ambapo damu itakuwa ikimwagika kutoka kila pembe ya dunia.Tunasikia kila siku katika maredio na televisheni vile dunia yetu hii ilivyokumbwa na mauaji kila pande. Na ama kuhusiana na kifo cheupe, tunasikia vile magonjwa mbalimbali ya saratani, ukimwi n.k. yanavyoua watu kwa mamilioni.

UBASHIRI WA IMAM 'ALI

1686. Imam Ali ibn Abi Talib(a.s) . alianza kuelezea: "Kumbukeni kuwa kabla ya kuja kwake,

1. Watu watakuwa wakiiona Sala kama jambo hafifu kabisa.

2. Amana zitakuwa zikichukuliwa kiwizi.

3. Kusema uongo ndio itakuwa ikichukuliwa kuwa sahihi.

4. Waislamu wataanza kuchukua riba.

5. Rushwa itakuwa ni jambo la kawaida.

6. Majumba makubwa makubwa na ya fakhari yatakuwa yakijengwa.

7. Dini itauzwa kwa matakwa ya dunia.

8. Watu watawafanya waovu na hakiri kuwa watawala au viongozi wao.

9. Wanaume watawataka wanawake ushauri na uongozi.

10. Hakutapatikana huruma kokote pale,dunia itakuwa imejaa kwa udhalimu.

11. Utumwa utakuwa ni jambo la kawaida.

12. Mauaji na umwagaji wa damu utachukuliwa kama jambo la kawaida na ubabe.

13. Watu wenye ilimu watakuwa wadhaifu na wadhalimu watakuwa wenye nguvu.

14. Watawala watakuwa watu waovu na Mawaziri wao watakuwa wadhalimu.

15. Wasufi na wasomaji wa Qur'an watakuwa wapumbavu.

16. Kutakuwa kukitolewa ushahidi wa kughushiwa.

17. Qur'an Tukufu itakuwa ikirembeshwa kwa nyuzi za dhahabu.

18. Misikiti itakuwa ikijengewa minara mirefu.

19. Watu waovu watakuwa wakiheshimwa.

20. Idadi ya watu itaongezeka lakini wakiikhtilafiana baina yao.

21. Ahadi na mikataba itakuwa ikivunjwa kila hapa na pale.

22. Wanawake watakuwa wakishirikiana pamoja na wanaume wao kwa uroho wa mali.

23. Sauti za Wakomunisti na wapingamizi wa Dini zitakuwa zina nguvu sana.

24. Nao watakuwa wakisikilizwa na kila mtu

25. Viongozi wa Jumuiya watakuwa ndio watu waovu kabisa.

26. Watu waendeshao biashara za Mabenki watakuwa wabadhirifu na wadhulumaji.

27. Ala za muziki zitakuwa zikipatikana kila mahala na kupindukia idadi.

28. Wanawake watakuwa wakipanda mafarasi na wakiendesha magari.

29. Kuiga, hali ya mtu mwingine itaonekana ni kama desturi ya kawaida yaani mwanamme atapenda awe kama mwanamke (ajifanye mwanamke) na mwanamke atapenda ajifanye kama mwanamme

30. Utatolewa ushahidi katika mambo ya mahakama ingawaje mtoa ushahidi mwenyewe atakuwa haelewi kitu chochote kuhusu kesi inayoendelea lakini atatoa ushahidi wa kiuongo katika kesi yoyote ile itakayokuwa ikiendelea.

31. Mbwamwitu watakuwa wengi ,katika makundi ya kondoo.

32. Unafiki utakuwa ndio mambo ya kujivunia

33. Nyoyo za watu zitakuwa zikinuka kuliko hata maiti na mbaya kabisa kuliko kitu chochote kile.

34. Na mahali pa kuishi pema kabisa wakati huo itakuwa ni Jerusalem.Utafika wakati huo mtu atatamani laiti angelikuwa mkazi wa Jerusalem.

Asbagh ibn Nabata alisimama na kusema

"Ewe Bwana, naomba utwambie Dajjal atakuwa ni mtu wa aina gani?"

Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . alimjibu "Yeye atakuwa ni Sayyed .Laana iwe kwa mtu atakaye mkubalia Dajjal na atakuwa mtu mwenye bahati yule ambaye atakuwa amemkana Dajjal .

35. Yeye atatokea karibu na Kijiji kinachojulikana kama Isbahan kutokea eneo la Judea, kutakuwa na toto la jicho katika jicho la kulia .Jicho lake la kushoto litakuwa juu ya paji lake la uso na litakuwa liking'ara kama nyota ya alfajiri, na hapo kutakuwa kipande cha nyama kilichojaa kwa damu. Baina ya macho yake mawili kutakuwa na herufi zilizoandikwa katika Kiarabu Kafir yeye atapita katika mabahari makubwa makubwa.

36. Jua litakuwa pamoja naye.

37. Wingu la moshi litakuwa mbele yake na mlima mweupe utakuwa nyuma yake.

38. Watu waliofikwa na majanga ya njaa watafikiria hiyo milima kama ni chakula,

39. Na punda wake mwekundu atakuwa akitembea mamaili na miguu yake itakuwa ikirefuka na kuwa mifupi kufuatana na ardhi ilivyotambaa.

40. Maji yoyote atakayokuwa akiyapitia yeye Dajjal yatakauka hadi siku ya Qiyama,

41. Baadaye atapiga sauti kwa nguvu kwamba kila kiumbe kitamsikia, atasema"Enyi marafiki! Mimi ndiye yule mliyekuwa mkinisubiri,mimi ndiye niliyewaumba,na niliyewafanya nyie mkawa wazuri.Na mimi ndiye mpaji wenu mkubwa sana. "

42. Huyu mwehu wa jicho moja atakuwa mwongo mkubwa sana.

43. Ole wenu, wafuasi wake wengi watakuwa ni wanaharamu na wale waliozaliwa kwa zinaa,

44. Wao watakuwa wakijivika vitambaa vya silki,

45. Huyo Dajjal atauawa mahala panapoitwa Aqba huko Syria, atauawa siku ya Ijumaa mchana,

46. Mtume Issa(a.s) . atasali nyuma ya Imam Mahdi(a.s) .

47. Na baadaye jambo la ajabu kabisa litatokezea.

UDONDOZI WA UBASHIRI

1687. Kutoka dalili na mabashiri ya kudhihiri kwa Imam Mahdi(a.s) . hapa kuna madondoo machache ambayo yamechambuliwa:

1. Uasi wa Sufiani,

2. kuuawa kwa Hasan,

3. Ikhitilafu baina ya Bani Abbas kwa matakwa ya dunia.

4. Kupatwa kwa jua katika mwezi wa Ramadhani, ikifuatiwa na kupatwa kwa mwezi mwishoni mwa mwezi huo wa Ramadhani.

5. Beda (mahala baina ya Makkah na Madina) itadidimia ardhini,

6. Ardhi katika upande wa Mashariki na upande wa Magharibi zitadidimia,

7. Jua wakati wa asubuhi litaonekana liko papo hapo bila kutembea hadi wakati wa mchana na baadaye litachomoza kutoka Magharibi.

8. Mcha Mungu atauawa nyuma ya msikiti wa Kufa pamoja na watu sabini wengine.

9. Mtu mwema kutoka ukoo wa Bani Hashim atachinjwa baina ya Rukn na Makam huko Makkah.

10. Kuta za Msikiti wa Kufa zitaporomoka.

11. Bendera nyeusi zitatokezea huko Khorasan.

12. Mtu kutoka Yemen ataongoza uasi.

13. Mtu atakayetokea nchi za Maghreb ataonekana huko Misri na ambapo atapata mamlaka makubwa.

14. Warusi watafika Bara la Arabia,

15. Wazungu watafika Palestina.

16. Upande wa Mashariki kutaonekana kwa nyota yenye mkia. Mwanga wake utaonekana kama ule wa mwezi na ncha zake zote zitakuwa moja (zitaungana).

17. Kutaonekana uwekundu mkubwa sana mbinguni.

18. Kutazuka moto mkubwa sana katika Mashariki ya kati ambayo itadumu kwa muda wa siku tatu hadi saba.

19. Wale wasio Waarabu watawafukuza Waarabu kutoka ardhi zao.

20. Utawala wa kifalme utakwisha nchini Iran.

21. Wamisri watamuua kiongozi wao.

22. Bendera tatu zitakusanyika Syria.

23. Kutazuka mizozo mikubwa na Syria itateketezwa.

24. Bendera za Waarabu na Bani Qais zitatoka Misri.

25. Bendera ya Banu Kinda itapepea Khorasan.

26. Jeshi kubwa sana litapita Hira.

27. Mabango meusi yatafika kutokezea Mashariki.

28. Maji ya mito ya Furat yatafurika katika mitaa ya Kufa.

29. Kutatokezea watu sitini watakaodai kuwa wao ni Mitume.

30. Sayyid kumi na wawili watadai kuwa wao ni Imamu Mahdi

31. Mtu mwenye heshima kubwa kutoka Bani Abbas atachomwa moto hai karibu na Khankin.

32. Kutajengwa na daraja katika Baghdad katika sehemu za Kharah.

33. Kutakuwa na tufani ya upepo mkali katika Baghdad wakati wa asubuhi na kutafuatiwa na kupasuka kwa ardhi ambamo baadhi ya sehemu itadidimia ardhini.

34. Mauti,vifo na maangamizo yatakithiri huko Iraq kiasi kwamba watu watakuwa kama wamewehuka.

35. Vikundi vitapigana mno huko Iran.

36. Sura za jumuia zitachafuliwa.

37. Watumwa wataanza kutawala nchi za Mabwana wao.

38. Sura kama ya binadamu itaonekana karibu na jua.

39. Makaburi yatafumuliwa na

40. Waliokufa watapewa uhai.

41. Kutakuwa na mvua itakayonyesha kwa mfululizo wa siku ishirini na nne ambayo itahuisha ardhi iliyokuwa imekufa. Kwa hakika wakati huo ndio utakuwa wakati wa kudhihiri kwa Imam Mahdi Sahib az-Zamaan (a.s).

MUKHTASARI WA DALILI

1688.1. Baghdad itateketezwa kabisa.

2. Basra itazama.

3. Waarabu watatawaliwa na mfalme wa ukoo mmoja tu kwa nguvu.

4. Msikiti wa Borasa (baina ya Baghdad na Kazmain) utadhoofika.

5. Kutakuwa na nchi nyingi za Kiislamu na kutakuwa na soko la kawaida

6. Qum itakuwa ni kitovu cha mafunzo ya Kiislamu, kitakuwa ni kituo kipya kuliko kile cha Najaf (Iraq). Na hapo ndipo kutakuwa kukitolewa ahkamu za dini.

7. Kutakuwapo na reli kupitia katika nchi za Kiislamu.

8. Azarbaijan itakumbwa na vita.

9. Wanawake watakosa heshima kabisa.

10. Duniani kote kutaenea sheria za kidemokrasia.

11. Kutakithiri kizazi cha wanaharamu.

12. Kutakithiri riba na rushwa.

13. Kuzaliwa kwa wanawake waovu katika familia nzuri.

14. Watu wenye hali ya chini wataweza kujenga majumba makubwa.

15. Watu wema na waaminifu watakuwa wakiomba mauti ili waepukane na maudhi wanayoyapata.

16. Watoto na majahili watapanda juu ya Mimbar, na watajulikana kama khatib.

17. Wanazuoni watajiingiza katika mambo ya dunia.

18. Madhumuni ya kutafuta Elimu itakuwa ni kutaka kutafuta pesa.

19. Badala ya kusalimiana matusi ndiyo yatakayo kuwa yakitumika watu watakapokuwa wakikutana.

20. Watu watatoka katika dini zao kwa sababu ya ulafi wa vitu.

21. Dini ya Kiislamu itakuwa dhaifu.

22. Mambo ya kuingiliana yatakuwa yakifanyika kidhahiri kama vile wafanyavyo wanyama.

23. Wanawake watasuka nywele zao kama nundu za ngamia.

24. Kupatwa kwa mwezi na jua na mitetemeko vitatokea Mashariki na Magharibi na baadaye katika Bara la Arabia.

25. Kutakuwa na ongezeko katika kuzaliwa watoto wa kike.

26. Ulawiti na pombe vitakuwa ni vitu vya kawaida.

27. Mitetemeko ya kila mara itaongezeka.

28. Wanawake watakuwa na taasisi zao.

29. Wanawake watafanya kazi pamoja na wanaumme katika kutafuta maisha yao.

30. Usafiri utakuwa wa haraka sana.

31. Kutakuwa na muongezeko wa ajali za njiani.

32. Mavazi yatakuwa mafupi.

33. Mwanamme na Mwanamke watajaribu kuonana sawa kijinsia

34. Kutakuwa na ndoa za kuoa jinsia yake yaani mwanamme atamuoa mwanamme mwenzake na mwanamke atamuoa mwanamke mwenzake (na mambo haya hasa yanatokea katika nchi za Ulaya).

35. Wakazi wa Kufa na Najaf watakuwa wamekaribiana sana.

36. Wakazi wa Makkah na Madina wataongezeka.

37. Hijab itakuwa imepotea (hijab, bubui).

38. Maji yataanza kujaa katika ziwa Sawa.

39. Kutakuwapo na nyota yenye mkia karibu na Capricorn.

40. Watu wengi sana watakufa kwa sababu ya kuenea kwa vita

41. Misikiti na Qur'an itarembeshwa kwa dhahabu.

42. Kutatokea na moto mkubwa sana katika mashariki na utaendelea kuwaka kwa siku saba.Na moto huo utatia khofu kubwa sana kwa mioyo ya watu.

43. Kutakusanyika bendera tofauti tofauti huko Kufa na kusababisha mifarakano mikubwa.

44. Utawala wa Kifalme utakwisha huko Iran.

45. Kutatokea na mivurugo katika nchi za Kiaarabu. Kila nyumba ya mwarabu na nchi zote za Kiislamu zitahusishwa humo.

46. Kukosa Imani kutaenea kote.

47. Waislamu wataiga tamaduni na mila za maadui zao.

48. Vifo vya ajali vitaongezeka.

49. Ala za muziki zitaenea kiasi kwamba hakutakuwa na mtu hata mmoja atakayesalimika kwa sauti zao.

50. Watu wataanza kukataa kuwapo kwa Imam Mahdi(a.s) .

51. Kutaonekana sura katika jua, na sauti zao zitasikika duniani kote.

52. Mwanadamu atafika mwezini.

53. Sufiani atatokezea na kueneza utawala wake wa vitisho.

54. Sayyed Hassan atatokezea huko Iran.Na yeye atafika Multan kwa kupitia Kirman huku akiteka sehemu zote. Yeye atamfikia Imam(a.s) . Yeye atamfikia Imam Mahdi(a.s) . na kujIssalimisha mbele yake.

55. Kutatokezea wazushi wa mtume sitini.

56. Mtume Issa(a.s) .atateremka kutoka mbinguni.

57. Maafa, magonjwa ya kuambukiza na ukame utaenea kote.

58. Nafsi ibn Zakia atauawa katika al- Khaaba (mtu mcha Mungu atauawa katika al-Kaaba).

59. Jua litachomoza kutoka Magharibi kwa siku moja.

60. Warusi wataingia Bara la Arabia na watu weupe wataingia Bara la Parestina.Nao baadaye watapambana.

61. Wachina wataingia Bara la Arabia na kusababisha maangamio na maafa ambayo yatakuwa ni mambo ya kawaida.

62. Baadhi ya miji itateketezwa kwa sababu ya maafa na misukosuko.

63. Sauti ya kutisha itasikika kutoka mbinguni.

64. Kutokezea kwa Dajjal.

65. Moto na moshi itakuwa kawaida duniani.

66. Mvua zitatokezea pasipo na misimu yake.

67. Kuongezeka kwa joto katika anga za juu.

68. Kulipuka kwa moto mkubwa katika Aden.

69. Baadhi ya makundi ya wanaume yatakuwa yamegeuka maumbo.

70. Kutatokea na mabadiliko ya ajabu katika sayari ya Capricorn

71. Mkuu wa Dola ya Misri atauawa.

72. Kutakuwapo na mvua ya mfululizo kwa muda wa siku ishirini na nne(24).Dunia nzima itakuwa imejaa michafuko, maafa na maangamizo n.k.

1689. Hadith hii ifuatayo inatuonyesha dhahiri kuwa kuna haja ya kuwapo kwa Imam wa zama na kumtii yeye ni faradhi kwetu sisi,kama vile wanavyoinakili Maimamu wa Kishiah na vile vile Wanazuoni wa Ahli Sunna pia wananakili vivyo hivyo katika vitabu vyao. Hadithi mashuhuri ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . inayopokelewa na madhehbu yote ni kama ifuatavyo: "yeyote yule atakayekufa bila ya kumtambua na kumjua Imam wa zama zake basi mtu huyo atakufa mauti ya ujahili (yaani atakufa kifo cha ukafiri)."

HADITH YA PILI

1690. Madhehebu yote ya Islam kwa pamoja yanaelezea Hadith ifuatayo na ambayo ni uthibitisho wa ukweli wa Kiislamu na vile vile Sahih Bukhari na vitabu vingine vyote vya Hadith pia vinaelezea kuwa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . alisema: "Baada yangu watakuwapo Maimamu kumi na wawili ambao watatokana na Maqureish. "

HADITH YA TATU

1691. 'Allamah Syed Jamal ud-Din Muhaddath ambaye ni mwachuoni mkubwa wa Ahli Sunna,anaandika katika kitabu chake Rawdhat ul-Ahbaab kwa kumnakili Sahaba Ja'abir ibn 'Abdullahi Ansari wakati Allah swt alimfunulia Aya hii Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) :

"Enyi mlioleta Imani! Mtiini Allah swt na Mtume wake na vile vile mumtiini 'ulil Amr'." "Basi mimi (anaendelea Bwana Ja'abir) niliuliza "Ewe Mtume wa Allah swt! Sisi tunaelewa Allah swt pamoja na Mtume wake.Lakini jee ni wakina nani hao ambao wanajulikana kama 'ulil Amr" ambao utiifu wao umefaradhishwa kwetu sisi?" Hapo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alitoa majibu haya yafuatayo: "Wao watakuwa Makhalifa baada yangu na wa kwanza miongoni mwao ni Ali ibn Abi Talib na amfuataye atakuwa ni mwanae Hasan na atamfuatia Hussein na baadaye atafuatia Ali ibn al-Hussein na baadaye Mohammad ibn Ali na anatambulika katika Tawrati kwa umashuhuri wa jina la Baqir na ewe Jaabir! Karibu utafikia zama zake na hapo tafadhali naomba unifikishie salamu zangu. Baada yake atakuja Ja'afer as-Sadiq bin Mohammad na baadaye Musa ibn Ja'afer na baadaye Ali ibn Musa na baadaye Muhammad ibn Ali na baadaye Ali ibn Mohammad na baadaye Hasan ibn Ali na baadaye Muhammad ibn al-Hasan ambaye atakuwa juu ya ardhi hii kama hujjatillah na bakiyallah katika wamchao Allah swt. Huyo ndiye atakayepata ushindi wa mashariki hadi wa magharibi wa dunia hii. Na yeye mwenyewe ambaye atakuwa hayupo mbele ya wafuasi (Mashiah) wake na wale wampendaye hadi kwamba hao hawatabakia katika itikadi ya Uimamu illa wale tu ambao Allah swt ameshawachukulia mitihani ya nyoyo zao." Ja'abir r.a. anaelezea kuwa: Mimi sikusita kumwuliza Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . "Ewe Mtume wa Allah swt! Je katika zama za Ghaibat, wafuasi (Mashiah) wake wataweza kufaidika naye?" Hapo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . alijibu: "Naam! Kwa kiapo cha Allah swt ambaye amenituma nikiwa Mtume wake,kuwa katika zama zake za Ghaibat ,Mashiah wake watang'arika kwa nuru yake na kufaidika kwa Ukhalifa wake kama vile watu wanavyofaidika na jua hata kama litakuwa limejificha katika mawingu."

HADITH YA NNE

1692. Imam bu Dawud ameandika katika kitabu chake Sunan na Imam Tirmidhi anaandika katika Sahih Tirmidhi kwa kumnakili Abu Said Khudhri,kuwa: "Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . amesema: "Mahdi anatokana nami na mwenye uso unaong'aa na pua yake iliyo ndefu ataijaza ardhi kwa uadilifu na haki kama vile itakavyokuwa imeshajaa kwa dhuluma na ufIssadi, na atatawala kwa kipindi cha miaka saba. "

HADITH YA TANO

1693. Imam Abu Dawuud katika Sunan amendika kwa kumnakili Sayyidina Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . amesema kuwa iwapo kwisha kwa dunia hata kama ni siku moja itakayobakia,hivyo pia Allah swt atamtuma mtu mmoja kutokana na Ahlul Bayt yangu (kizazi changu) humu duniani ambaye ataijaza dunia kwa uadilifu na haki kama vile itakavyokuwa imejaa kwa dhuluma na ufIssadi."

HADITH YA SITA

1694. Imam Abu Dawud amemnakili Ummul Moominiina kufuatilia mfululizo huo wake kuwa: Mtume Mtukufu(s.a.w.w) amesema kuwa 'Mahdi atatokana na Itrati (kizazi) yangu,yaani atatokana na kizazi cha Fatimah az-Zahra(a.s) ."

HADITH YA SABA

1695.Imam Bukhari katika Sahih Bukhari , Imam Muslim katika Sahih Muslim na Kadhi ibn Mas'ud Baghawi katika Tasnif Sharh al-Sunnah. Wote wanamnakili Abu Hurayrah akisema: "Amesema Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . 'Je hali yenu itkuwaje wakati Mtume Issa(a.s) .atakapoteremka kwenu na Imam wenu atakuwapo ametokea miongoni mwenu? "

HADITH YA NANE

1696. Imam Tirmidhi katika Sahih Tirmidhi na Imam Abu Dawud katika Sunan Abu Dawud wanamnakili Abdullah Ibn Mas'ud akinakili riwaya: Amesema Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . "Kuwa dunia haitakwisha hadi hapo mfalme wa Kiarabu hatatokea kutokana na kizazi changu,na ambaye jila lake litakuwa kama jina langu. "

HADITH YA TISA

1697. Imenakiliwa na Maimamu wa Ahli Sunna katika Sahih zao,riwaya ifuatayo: Amesema Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . "Atatokezea mtu mmoja katika Ahlul Bayt yangu,atakayetawala na jina lake litakuwa kama jina langu. "

HADITH YA KUMI

1698. Imam Abu Is-haq Tha'alabi katika tafsir yake anamnakili Anas bin Malik kuwa:Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . amesema kuwa "Sisi wana wa Abdul Muttalib ni viongozi wa watu wa Jannah,yaani mimi , Hamza, Ja'afer na Ali na Hasan , Hussein na Mahdi. "

1699. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Hakuna watu wanaopoteza utajiri wao isipokuwa kwa kutokana na madhambi yao, kwani Allah swt kamwe hawadhulumu viumbe vyake ."

1700. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . amesema: "Wale wote wanaotukuzwa na kuheshimiwa kwa woga wa maovu yao, kwa hakika wao watakuwa miongoni mwa watu waovu kabisa siku ya Qiyama. "

1701. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Hamaki huziba (nuru ya) moyo wa mwenye hekima. Asiyeweza kudhibiti hamaki yake hawezi kuitawala akili yake. "

1702. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Mwenye kuiacha hamaki yake ipande, huharakisha mauti yake ."

1703. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Jihadhari na hamaki, kwani mwanzo wake ni wendawazimu na mwisho wake ni majuto ."

1704. Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Hamaki ni moto uliokokwa, mwenye kuipoza hamaki huuzima (moto wake); na mwenye kuiachilia huwa ni wa kwanza kuungua humo ."

1705. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Jilindeni kutokana na ukali wa hamaki na jiandaeni kupambana nao kwa kuvunja hamaki na kwa kuvumilia. "

1706. Vile vile Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . amesema: "Kujidhibiti wakati wa kushikwa na hasira humsalimisha mtu wakati wa maangamizo ."

1707. Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . amesema: "Kitu gani kilicho kiovu zaidi kuliko hamaki wakati mtu aliyepandwa na hamaki hutoa roho iliyoharamishwa na Allah swt ."

1708. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . amesema: "Ikiwa mmoja wenu atapandwa na hamaki, kama amesimama akae chini, na kama amekaa alale. Na kama hamaki haikupoa baada ya kufanya hivyo, basi atawadhe kwa maji baridi au aoge kwani moto hauzimiki ila kwa maji."

1709. Mtu mmoja alimwambia Al Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . na kusema: "Mimi mpaka hivi punde tu nilikuwa nikiamini kwamba wewe na baba yako ni watu wabaya kabisa, lakini sasa ninahisi kwamba huo moyo wangu uliokuwa umejaa chuki na uadui dhidi yenu, sasa umejaa mapenzi na ikhlasi. Hakika hakuna mwingine anayestahiki cheo hiki kitukufu isipokuwa wewe tu.

1710. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema: "Jiepusheni na ghadhabu, kwani huleta mashaka. "

SHARTI YA KUCHAPA

Sharti ya kuchapa au kusambaza ni kutaja rejeo hili. haki zote zimehifadhiwa na Taasisi ya Al-Hasanain Taasisi ya Imamu Husein(a.s)

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini(a.s) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini.

MWISHO WA KITABU