• Anza
  • Iliyopita
  • 6 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 17443 / Pakua: 3988
Kiwango Kiwango Kiwango
UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

Mwandishi:
Swahili

1

2

UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

KIMEANDIKWA NA: ALLAMAH SAYYID SA'EED AKHTAR RIZVI

KIMETARJUMIWA NA: AL-AKHY SALMAN SHOU

NENO LA MCHAPISHAJI WA KWANZA

TOLEO LA KIINGEREZA

Kitabu hiki kimerudiwa kimechapishwa tena kwa ruhusa ya waandishi, ili kuafikiana na Kongamano la Kilimwengu la Umoja wa Mataifa dhidi ya Ubagazi wa Rangi, (United Nations World Conference against Racism) ambalo lilitege-mewa kufanyika katika jiji la Durban, Afrika ya Kusini, mwezi Augosti, 2001. Mada mbili zilizo pendekezwa kuwepo kwenye agenda zilisababisha migongano ya kimataifa. Agenda hizi zilikuwa: Malipo ya fidia kwa utumwa na biashara yake ambayo ilifanywa na mataifa ya Ulaya na Marekani (U.S.A) hapa Afrika na nyingine ilikuwa kulin-ganisha Uzayuni (Zionism) na ubaguzi wa rangi. Suala la malipo ya fidia kwa Afrika kutoka kwa mataifa yaliyojihu-sisha na utumwa limeachwa kushugulikiwa kwa muda kwa makubaliano baina ya mataifa yanayodaiwa na Afrika, kuweka nguvu na msukumo mkubwa katika kuisaidia Afrika kuendeleza mpango wake wa kurejesha hali nzuri ya uchu-mi. Mpango mmoja wapo unaojulikana sana ni ule wa: Millenium Africa Recovery Plan, ambao unasimamiwa na Rais Thabo Mbeki wa Afrika ya Kusini. Msaada unaozungumziwa hapa bila shaka unaeleweka kwamba ni aina ya ukandamizaji wa kiuchumi kwa kuendeleza utumwa wa kiuchumi hapa Afrika daima milele. Wayahudi wapatao milioni tatu (3) waliuawa wakati wa vita kuu ya Pili ya Dunia - ambapo zaidi ya Waafrika milioni kumi (10) walichukuliwa kuwa watumwa. Malipo ya fidia kwa ajili ya mauaji ya Halaiki ya Wayahudi yanaendelea hadi leo. Msaada wa ruzuku kwa serikali ya Uyahudi (Israeli) kutoka Marekani ambao ulianza kutolewa tangu 1948 sasa umefika kiwango cha dola za Kimarekani billion 18. Utafutaji wa watu watuhumiwa wa "makosa ya kivita" ambao yasemekana ndio walio husika kuwaua Wayahudi tangu 1939 hadi 1943 unaendelea hadi leo. Kwa mara ya kwanza Wayahudi walidai fidia mnamo mwaka wa 1951 kiasi cha dola za Kimarekani bilioni (1.5) moja na nusu. Madai haya yalifanyika miaka sita baada ya kukoma Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Ni takribani miaka 140 tangu kupig-wa marufuku utumwa katika nchi za Magharibi. Makubaliano yalisainiwa na Chansela akiwakilisha Ujerumani mnamo tarehe 10 Septemba, 1952. Je uhai wa Mwafrika hauna thamani ya kutosha ili ulipiwe fidia? Majumba ya makumbusho na makaburi makubwa yanajeng-wa kwa madhumuni ya kuhuisha kumbukumbu ya wale wanaodaiwa "kuuawa kikatili na Manazi wa Kijerumani." Dunia inalazimishwa kutubu dhambi zake dhidi ya Wayahudi, na pamoja na kisingizio hiki bandia, hakuna uha-lali wa hata kidogo unoifanya Israeli kulundika silaha nyin-gi kiasi hicho kisicho linganishwa. Yeshayahou Lebowtz (Israel and Judaism, Jerusalem, 1987) ameandika kwa ufupi: "Israeli si dola yenye kumiliki jeshi, bali ni jeshi lenye kumiliki dola."

UTUMWA MAMBO LEO

Uendelezaji wa wazi wa aina za utumwa unaweza kufaniki-wa kwa njia ya kusaidia Mipango kama vile "Millenium African Recovery Plan." Utandawazi kupitia umiliki wa nguvu za uzalishaji unaofanywa na"Muungano wa Kimataifa wa Wakiritimba" (Multi Ntional Cartels) tayari upo. Mfumo huu hupenya kwenye kila tabaka la uchumi wa dunia, iwe ni bidhaa zinazo zalishwa, kama sukari, silaha za kivita, madawa ya tiba au biashara ya dhahabu na madini ya platinamu. Utumwa wa kiuchumi kupitia udhibiti mkali wa mtiririko wa mitaji ulimwenguni uko imara mikononi mwa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF). Uharibifu kwa Afrika ulitokea kwa njia ya utawala wa mabavu wa kikoloni wa moja kwa moja, uliofanywa na Uingereza, Udachi, Ufaransa, Ureno na Ubeligiji. Hii ilifu-atiwa na udhibiti wa nje ya Afrika, kwa kuanzisha serikali kidhalimu ili kuendelea kudhibiti kwa njia za hila zaidi. Kwa kufichuliwa vibaraka hawa kwa ajili ya ulimwengu kuwaona, ikawa vigumu zaidi kuendelea kwa uwazi kusaidia vitendo vyao viovu dhidi ya jamaa zao. Vurugu zilidhibitiwa ili kuhakikisha kuendelea uingiaji kwenye hak-iba kubwa za madini. Njia changamano ilikuwepo kazini kwa zaidi ya miaka 30, ambayo ni kulitumbukiza bara hili (la Afrika) kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe visivyo na maana yoyote. Ahadi za "kusamehe madeni" zinatolewa kwa lengo la kuendeleza utumwa kwa Waafrika. Huu "Utumwa Mpya" unaweza kuonekana tofauti kwa nje na ule wa "West African Slave Trade " (Biashara ya utumwa ya Afrika ya Magharibi), lakini misingi yake inafanana. Kwa kuanzishwa kwa mfumo wa makao makuu ya fedha (Benki ya Dunia na shirika la Fedha la Kimaraifa), Polisi wa Dunia (North Atlantic Treaty Organization), imewarahisishia wakoloni kazi ya kuwa na mamlaka ya kuitawala Afrika. Mfano wa wazi unaoonyeshwa na nguvu hizi za wakoloni na washirika wake, ni kuunda taifa la Israeli katikati ya Rasi ya Arabia. Kwa hiyo ni muhimu sisi kuchambua na kuonye-sha ulinganifu huu baina ya Uzayuni (Zionism) na washirika wake na ukubwa na vipimo vya utumwa unaoendelezwa na nguvu za wanyonyaji.

Kwa hiyo, tumeona ni muhimu kukichapisha kitabu hiki, kiitwacho: "Utumwa, kwa Mtazamo wa Kiislamu na Usio wa Kiisilamu", kilichoandikwa na Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi (ambacho kilichapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1972). Kwa madhumuni ya: Kuwataarifu kwa mara nyingine washiriki kwenye Kongamano hili kuujua uovu halisi wa utumwa ambao umekuwa unaendelea kwa karne tano zilizopita. Kupanua akili za wasomaji na hivyo kutambua jinsi utumwa ulivyogeuzwa na kuwa kama ulivyo sasa katika hali yake ya udanganyifu zaidi, na njama za nchi ya Israeli na Marekani zenye sera za kuuendeleza ili ziweze kutimiza malengo yao ya siri. "Ahlul Bait(a.s) Foundation of South Africa" inaona fahari kuitambulisha kazi hii rasmi yenye thamani na wanayo matumaini kwamba usiri unaogubika akili zetu utaondolewa na kuamsha akili za watu wote wenye msimamo unaostahili. Kwa kweli sisi ni wadeni kwa Muadhama Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi (Dar es salaam, Tanzania) na kwa unyenyekevu tunashukuru juhudi zake za miongo michache katika kueneza mafundisho ya Uislamu hapa Afrika. Tabia yake ya kisomi imeonekana kwenye mfululizo wa mada nyingi zilizo chapishwa zikijumuisha maelekezo ya jumla kama vile "Haja ya Dini", hadi kufikia kazi za kisomi kama hii. Bilal Muslim Mission of Tanzania, imefanya kazi kubwa ya kueneza kazi hii na zingine nyingi za maandishi na akawatia moyo Waislamu na wasio Waislamu duniani kote pamoja na Afrika ya Kusini katika kipindi cha zaidi ya miaka 50 iliyopita.

Mwenyezi Mungu amzidishie neema hapa duniani na akhera, na tunamwomba Muweza wa yote amjaalie nafasi kubwa zaidi ya kutunufaisha kwa kutumia kalamu yake, Insha- Allah.

Syed Aftab Haider

Ahlul Bait Foundation of South Africa

August 2001.

NENO LA MCHAPISHAJI TOLEO LA KISWAHILI

Kitabu kilichoko mikononi mwako, ni tarjuma ya kitabu cha Kiingereza, kwa jina la "Slavery - Islamic & Western Perspectives kilichoandikwa na Mwanachuoni mkubwa Mar hum Allamah Sayyid Sa'eed Akhtar Rizvi. Kitabu hiki kwa ufupi kinaelezea juu ya biashara ya utumwa ilivyokuwa ikiendeshwa na wazungu hapa Afrika, waki-saidiwa na Kanisa Katoloki na Makinisa mengine yaliyofu-atia. Mwandishi kwa kutumia elimu, akili, mantiki na utafi-ti wa kina, amefichua ukweli wote uliokuwa umejificha nyuma ya biashara hii ya udhalilishaji wa binadamu. Hapa Afrika na duniani kote, watu wangali wanaamini kwamba biashara ya utumwa hapa Afrika (hususan Afrika ya Mashariki) ilianzishwa na kuendeshwa na Waraabu waki-ungwa mkono na Uislamu. Kwa hiyo mbele za watu Uislamu ulionekana kama dini isiyojali ubinadamu, iliy-owaswaga mababu zetu kama wanyama na kuwafanya watumwa kwenye nchi zao. Mwandishi anayakanusha yote haya, na kuonyesha jinsi gani Uislamu ulivyokuwa dhidi ya biashara hii ya tumwa, na ulivyofanya ili kukomesha biashara hii. Na kuonyesha jinsi gani Wazungu walivy-oing'ang'ania biashara hii, na jinsi Mapadre na Maaskofu walivyozibariki meli zilizokuwa zimebeba watumwa. Tumeona tukitoe kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ili kizidishe mwanga wa elimu kwa Waislamu (na wasio kuwa Waislamu) wazungumzaji wa Kiswahili, na hili likiwa ndilo lengo kubwa la Taasisi yetu ya 'AFItrah Foundation' kati-ka kuwahudumia Waislamu hususan wazungumzaji wa Kiswahili. Tunamshukuru Ndugu yetu al-Akh Salman Shou kwa kukubali jukumu hili la kukifanyia tarjuma kitabu hiki. Vile vile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki. Ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitakuwa ni mwanga kwa wasomaji wetu na kuzidisha upeo wao wa elimu, na kuondokana na dhana hii potofu juu ya biashara ya utumwa. Mchapishaji: Al-Itrah Foundation S. L. P. 1017 Dar-es-Salaam Tanzania.

NENO LA MCHAPISHAJI TOLEO LA KISWAHILI

Utumwa ni moja wapo ya maovu ambayo yamekuwepo katika jamii tangu kuwepo kwa mwanadamu hapa duniani na jitihada za wanamageuzi kujaribu kuuzuia zimeshindwa kwa karne nyingi sana. Ustaarabu wa kale haukuweza kuondoa utumwa, kwa hiyo jamii za wakati huo ziliafiki kuwa nao. Baadhi ya jamii hizo za kistaarabu ziliulea utumwa. Makanisa ya Kikristo yalishiriki katika biashara ya utumwa. Mapadri wao walizibariki meli zilizokuwa zin-abeba shehena za binadamu na waliwaonya watumwa kuwa watiifu, lakini hawakuwasihi mabwana wenye kumiliki watumwa kuwa wapole kwa shehena hizo za watu. Hivi karibuni mnamo mwaka 1970 Kanisa Katoliki lilinunua wasichana 1500 kutoka India, eti kwa sababu wasichana wa kizungu huko Ulaya hawakutaka kuishi maisha ya kitawa (usista). Miongoni mwa dini zote ni Uislamu tu ndio ulio-haribu misingi yote ya uovu huu. Lakini, ni kejeli ya histo-ria kwamba watu walio rutubisha utumwa wakasaidia uen-deleaji wake na walifaidika nao, baadaye ndio wakawa mabingwa wa kuukomesha. Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi, Mhubiri Mkuu wa Bilal Muslim Missioni of Tanzania, amekiandika kitabu hiki kwa uwezo mkubwa na jitihada. Kama ilivyo kwa msomi mtafi-ti kama yeye, ameshuhgulikia mada ya kitabu hiki bila upen-deleo, Ameupanga ukweli baada ya ukweli kutoka kwenye historia; amenukuu kutoka kwenye Qur'ani, hadithi na waandishi wa zama za leo kuhusu somo hili, na ameonyesha sheria za Kiislamu na zile zilizotumika kabla ya Uislamu. Ameonyesha waziwazi kwamba ustaarabu wa Kimagharibi sio bingwa mkubwa kiasi hicho wa kuwaokoa watumwa kama unavyojionyesha. Kwa kweli kitabu hiki kitathibitisha kuwa kifungua macho kwa wale ambao hukubali bila kuchunguza kuhusu propaganda ya ubinadamu wa Kimagharibi. Peermahomed Ebrahim Trust kwa fahari kubwa wanakileta kitabu hiki kwa wasomaji na wana matumaini kitakubaliwa na jamii. Wadhamini, Peermahomed Ebrahim Trust Karachi, Pakistan 15 Jamadi, 1392 27 June, 1972.

UTANGULIZI WA MWANDISHI KWA TOLEO LA PILI

Kitabu hiki kiliandikwa kwa ombi la marehemu Haji Hasanali P. Ebrahim, ambaye ndiye aliye kichapisha kutoka kwa Peermahomed Ebrahim Trust, Karachi, mnamo mwaka 1972. Mara baada ya kuchapishwa, nakala zote zilinunuli-wa, lakini mahitaji yakawa bado yanaendelea. Kwa kukid-hi mahitaji hayo, mwanangu, Hujjatul Islam Sayyid Muhammad Rizvi sasa ametayarisha toleo la pili. Baadhi ya mabadiliko madogo madogo yamefanywa katika mpangilio wa Sura; ibara zimeongezwa hapa na pale; na mwanangu ametayarisha maelezo ya ufafanuzi chini ya kurasa, ambayo yameongeza ubora wa kitaaluma wa kitabu hiki. Mwenyezi Mungu na amrefushie maisha na amwongeze nguvu za kuendelea kuutumikia Uislamu wa kweli kwa uaminifu. Pia ninawashukuru marafiki ambao wamenisaidia kwa namna yoyote ile katika kufanikisha kuchapishwa toleo hili: S.S. A. Rizvi Gopalpur (India) 28 Novemba 1987.

UTUMWA KATIKA ZAMA ZA KALE

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿١٣﴾

"Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na wana-mume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni aliye mchamungu zaidi katika nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye khabari." (Qur'an 49:13).

Utumwa sio taasisi iliyoanzishwa na Ukristo au Uislamu. Ni Utumwa ulikuwepo kwa muda mrefu hata kabla ya kuanzishwa hizi dini mbili. Kwa mtazamo wa haraka kuhusu utumwa wa kale, ninamnukuu Jaji Ameer Ali: "Shughuli ya Utumwa ina rika moja sawa na kuwepo kwa binadamu. Kihistoria dalili zake zinaonekana katika kila zama na kila taifa... Wayahudi, Wayunani, Warumi na Wajerumani wa kale, watu ambao taasisi zao za kisheria na za kijamii zilizoathiriwa mno na tabia na desturi za kisasa, walizitambua na kuzifanya aina zote za utumwa, utumwa wa kazi za kiuchumi na wa kazi za nyumbani. Baada ya kuanzishwa kwa makundi ya washenzi wa Magharibi na Kaskazini katika mabaki ya dola ya Warumi, zaidi ya utumwa wa mtu binafsi, utumwa wa taifa moja kulifanya taifa lingine kuwa mtumwa, ambao haukujulikana sana kwa Warumi, ukashamiri kwenye nchi zote mpya zilizo kaliwa... kanuni za kishenzi, kama zile za Warumi, ziliona utumwa kama hali ya kawaida ya binadamu; na kama mtumwa alipewa ulinzi, ilikuwa kwa sababu mtumwa alikuwa mali inayo milikiwa na bwana wake, ambaye ni yeye peke yake baada ya nchi, alikuwa na mamlaka juu ya uhai na kifo kwa mtumwa.1 Katika nchi ya Uajemi (Persia) ikulu ya Mfalme ilikuwa na watumwa wanawake elfu kumi na mbili. Wakati Mfalme wa Byzantine anaketi kwenye kiti chake cha enzi, maelfu ya watumwa walikuwa tayari kutoa huduma kamili na mamia ya watumwa waliinama kuonyesha heshima wakati mfalme anainama kuvaa viatu. Huko Ugiriki au Uyunani, idadi ya watumwa ilikuwa kubwa zaidi ya watu walio kuwa huru, licha ya kwamba Ugiriki ilitoa watetezi wakubwa wa ubi-nadamu na haki. Kila jeshi la Kiyunani ambalo lilirudi nyumbani na salamu za ushindi, lilifuatwa na kuindi la watumwa. Aristotle, mwanasalsafa maarufu wa zamani, alipokuwa anazungumzia suala la iwapo kila mtu alikusudi-wa na maumbile kuwa mtumwa au la, anasema: "Hakuna ugumu katika kujibu swali hili, katika misingi yote miwili, ya akili na kweli.

Ya kwamba watu baadhi fulani watawale na wengine watawaliwe si tu kwamba ni jambo muhimu bali ni kitu chenye manufaa kuanzia saa ya kuzaliwa kwao, watu wengine wameumbwa ili wawe watumwa, wako kwa ajili ya kutii tu, na wengine wameumbwa kwa ajili ya kutawala." Halafu anahitimisha; "... watu wengine kwa asili wako huru, na wengine ni watumwa, na kwa utumwa huu (uliotajwa) wa mwisho, wote ni wenye manufaa na haki."2 Katika utawala wa Rumi, utumwa wa kale ulifika kilele chake, lakini Dola ya Kirumi ilipoanza kuanguka, watumwa wengi wakaanza kuwa na hali nzuri kwa kiwango kidogo.

1 Ameer Ali, Spirit of Islam (London: University paper back, 1965), PP. 259-261; pia angalia Will Duratnt, The Story ofa Civilisation, juzuu ya III (New York, 1944), P.397. Aristotle, Politics, Book one, Sura ya 5 (New York: Modern Library, 1943), uk. 58-60.

Lakini uovu wa utumwa ulionekana wazi kabisa. Uovu huu ulishinda ujuzi wa uhalali wa Kiyunani kama ambavyo imeshinda falasfa stadi ya Kigriki. Kuonyesha mapenzi kwa watumwa lilionekana si tendo la hisia za kawaida lakini ilikuwa tabia pekee ya mtu mwenyewe binafsi. Mtumwa hakuonekana kama binadamu, hakuwa na haki, hakuwa na roho.3 Wakati huo wa ujio wa Uislamu (mnamo karne ya 7 CE) utumwa ulikwisha enea kote kote huko India, Ajemi, Rumi, Rasi ya Arabia, Romania na Ugiriki. Watu waliokuwa na hali nzuri na nafasi nzuri na wasomi wa nchi hizi hawakuwatilia maanani watumwa kustahiki kupatiwa hata angalao pia haki za msin-gi za kibinadamu. Mtumwa alikuwa anaonekana kama bid-haa isiyo na thamani zaidi kuliko hata ya ng'ombe.4 Mara nyingi mtumwa aliuzwa kwa bei rahisi kuliko kondoo na mbuzi. Kwenye hafla maalum za kijamii wageni waheshimiwa wa nchi walikuwa na tabia ya kukusanyika pamoja na Kiongozi wa Nchi kutazama michezo ya kupi-gana watu na katika michezo hii watumwa walifanywa wapigane kwa kutumia mapanga na mikuki kama vile maonyesho ya mapigano ya jongoo wawili na kware katika kipindi cha zamani cha jamii ya kikabaila. Watu walis-hangilia kwa kupiga makofi hadi mtu mmoja miongoni mwa wapiganaji aliuawa. Watazamaji walimshangilia sana mshindi.5 Kwa upande mwingine, Rasi ya Arabia ilizunguukwa na nchi ambazo bado zilikuwa na dalili za ufahari wa ustaaraabu wa Kirumi na Kiyunani uliokuwa unaporomoka, 3 Durant, W., op.cit., Juzuu ya III uk. 397, Juzuu IV (New York), uk. 29). 4 Ibid 5 ibid. na kwa upande mwingine, ilizunguukwa na nchi zilizogu-bikwa na imani za dini za "Zoroastria" na "Uhindi." Kama ilivyo tajwa hapo juu, kwenye nchi zote hizi utumwa ni taasisi iliyo tambuliwa. Vibao kumi na mbili vya maandiko (ya sheria zao) vilitoa mhuri wake rasmi kuithibitisha taasisi hii. Ukali usiopungu-ka wa matatizo na ukatili ambao watumwa walifanyiwa, haukupungua, lakini, kwa namna yoyote ile, watumwa sasa walikubaliwa kama wanyama (hayawani) ambao hatima yao ilikuwa ni kufanya kazi na kufa tu kwa manufaa ya hao walio wamiliki. Sina nia ya kukifanya kitabu hiki kuwa his-toria ya unyama waliofanyiwa watumwa lakini itoshe tu kusema kwamba mtu lazima siku zote abebe hatia katika dhamira yake kwamba wakati fulani alijiingiza kwenye uovu wa utumwa.

UKRISTO NA UTUMWA

Ingawaje utumwa ulikuwa taasisi ya kale ambayo ilianza kabla ya historia ya binadamu haijaanza kuandikwa, ni sala-ma kusema kwamba ukubwa wa biashara hii ulifika kilele chake kwa kuendelezwa na mataifa ya Kikristo ya Ulaya na Amerika ambao kama ilivyo kawaida yao, waliigeuza kuwa biashara yenye utaratibu uliopangwa kwa uangalifu sana na wakaanza kuwakamata watumwa kwa maelfu. Kabla hatu-jaanza kutoa maelezo ya biashara hii mbaya sana ya utumwa ambayo ilianzishwa na Wareno, Wahispania na mamlaka zingine za kiubaharia za Kikristo kutoka Magharibi kwa ajili ya makoloni yao mapya, hebu tuangalie kwanza tuone kama Ukristo, kama mfumo na imani, ulifanya lolote wakati wa siku za mwanzo sana kupunguza ukali wa mateso kwa wengi wa watumwa. Jaji Ameer Ali anaandika kuhusu Ukristo: Ukristo uliona utumwa kuwa ni taasisi iliyo tambuliwa na himaya (dola); na wenyewe ukakubali mfumo huu bila ya hata kujaribu kupunguza uovu wake, au kuahidi kukomesha polepole, au kuboresha hadhi ya watumwa. Chini ya sheria ya nchi, watumwa walikuwa kama mali inayo hamishika. Waliendelea kuwa hivyo chini ya utawala wa Kikristo. Utumwa ulishamiri miongoni mwa Warumi tangu zama za kale. Watumwa hao ama wamezaliwa wazalendo au wamezaliwa kutoka nje, ama walipatikana kutokana na ushindi wa vita au kununuliwa, walijulikana kama mali tu ya kuhamishika. Mabwana zao walikuwa na mamlaka na uwezo wa kuamua juu ya uhai au kifo kwao. Ukristo ulishindwa kabisa kukomesha utumwa au kupunguza uovu wake.6 Will Durant anatoa maelezo kuhusu nafasi ya Kanisa kama ifuatavyo. Kanisa halikulaani utumwa. Kanisa la Orthodox na waasi, Kanisa la Rumi na washenzi wote walidhani taasisi hii ilikuwa ya kawaida na haingeharibiwa. Sheria za kipagani zilimwingiza utumwani mwanamke yeyote aliye huru ambaye aliolewa na mtumwa; sheria za Mfalme Constantine (Mfalme Mkristo) ziliamuru mwanamke wa aina hiyo kuuawa kwa kukatwa kichwa, na mtumwa mwanamume kuchomwa moto akiwa bado yu hai. Mfalme Gratian alitoa amri kwamba mtumwa yeyote aliye mshitaki bwana wake kuhusu kosa lolote isipokuwa uhaini dhidi ya serikali, lazima achomwe moto akiwa bado yu hai 6 ameer Ali, op. cit., uk. 260-261 mara moja bila hata kufanya uchunguzi ili kupata uhalali wa shitaka.7

Rekebisho moja tu lililoagizwa na Ukristo linaonekana kati-ka barua ya Mtakatifu Paulo kwa mtu fulani aitwaye Filemoni alipomrudisha mtumwa wake, aliyeitwa Onesimo, na kupendekeza amfanyie wema. Hakuna zaidi ya hapo. Inavutia kuona kwamba neno "slave " ("mtumwa") la asili ya lugha ya Kiebrania limebadilishwa na kuwa "mtumishi wa nyumbani" kwenye toleo la Biblia liitwalo "Authorised Version of the Bible," na likabadilishwa kuwa "mtumwa mtumishi" katika toleo liitwalo "Revised Standard Version," kwa sababu, katika maneno ya "The Concise Bible Commentary," neno hili (yaani mtumwa) limeachwa kutumiwa kwa sababu ya maana yake.8 Mtu hushanga iwapo mtarjumi anayo haki ya kubadilisha asili ya neno kwa sababu tu ya maana zake au ukumbusho wake?" Itavutia kuona hapa kwamba neno "slave" ("mtumwa") ni la asili ya Wazungu. Lilianza kuwapo na kutumika wakati Wajerumani (Franks) walipokuwa wanajishughulisha na kulipatia "Washenzi" soko la watumwa la Wahispania, na mateka hao walio wengi walikuwa Waturuki kutoka jimbo la Slovakia (sasa ni sehemu ya Czecoslovakia). Watu hawa huitwa "Slav" na kwa hiyo mateka wote wakaitwa "slaves." Nukuu ifuatayo inaonyesha dhahiri mtazamo wa Uislamu na Ukristo kuhusu suala la utumwa na rangi ya ngozi: 7.leeky, W.E. History of European Morals, Juzuu ya II ( New Yolk, 1926), kama ilivyonukuliwa na Will Durant, op. cit., juzuu ya IV, uik. 77. 8. Clarke, Rev. W. K. L, The Concise Commentary (London: S.P.C.K, 1952) uk. 976.

"Mwondoshe mtu mweusi! Siwezi kuzungumza naye," alisema Archbishop Mkristo aliyeitwa Cyrus wakati Waarabu walioshinda walipowatuma wawakilishi wao wenye uwezo mkubwa ili wazungumze kuhusu makubaliano ya kusalimu amri mji mkuu wa Misri, ujumbe huu wa wawakilishi hawa uliongozwa na mtu mweusi aliyeitwa Ubaydah kama mtu mwenye uwezo mkubwa sana kuliko wote. Archbishop, alishangaa alipoambiwa kwamba mtu huyo mweusi alipewa ukubwa na maelekezo na Generali Amr, na kwamba Waislamu huwapa watu weusi na weupe heshima na daraja sawa na huwahukumia watu kwa tabia na si kwa rangi.9 Tukio hili linakupa tu maelezo kwa ufupi kile ninachotaka kueleza kwa urefu zaidi katika kitabu hiki.

1

UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

5. Bilal al-Habashi: Bilal al-Habashi (mtu wa Ethiopia) alikuwa muadhini wa kwanza wa Mtume. Baba yake alikuwa Riyah, na mama yake Jumanah, na lakabu yake ni Abu Abdillah na Abu Umar. Alikuwa mmojawapo wa kundi la watu waliosilimu mwanzoni kabisa. Alishiriki katika vita ya Badr, Uhud, Khandaq na zingine.86. 86. Ibn Sa'd, op. cit., j.3:1, uk. 170; Ibn Hajar, op. cit., j. 1, uk. 336.

Bilal alikuwa mtumwa wa kwanza wa Safwan bin Umayyah. Wakati wa utumwa wake, aliteswa kinyama kwa sababu ya imani yake. Aliamuriwa kulala chini kwenye mchanga wa jangwa la Arabia unaounguza akiwa uchi, jiwe zito liliwekwa juu ya kifua chake na kumfanya asipumue kwa urahisi. Na kama vile hiyo haikutosha, watu wane sana walitumia kuruka juu ya jiwe hilo, katika jaribio la kutaka kumuua kwa njia hiyo. Hata hivyo, sauti moja tu ilisikika kutoka kwa Bilal nayo ni (Mungu Mmoja! Mungu Mmoja!) Ahad! Ahad! 87. Mtume alipoona ukatili aliokuwa anafanyiwa Bilal, alisiki-tika sana. Abu Bakr akamnunua na kumwachia huru Bilal. Mnamo mwaka wa 2 A.H. wakati adhana (wito wa kwenda kusali) ilipoamriwa, Bilal alipewa heshima ya kuadhini.88. Baadaye, watu fulani walishauri kwamba heshima hii angepewa mtu mwingine, kwa sababu Bilal hakuweza kutamka herufi ya Kiarabu "shin" kwa lafudhi ya Kiarabu. Mtume akasema; "Hii 'sin' ya Bilal ni 'shin' inayosikika kwa Mungu." Mwenyezi Mungu hatazami umbile lilivyo, Yeye hupendezwa na utakatifu wa moyo. Wakati mmoja Bilal alikwenda kwa Mtukufu Mtume na akakariri beti ya shairi kwa lugha yake akimsifu Mtume. Mtume akamtaka Hassan bin Thabit al-Ansari kutafsiri katika lugha ya Kiarabu. Hassan akasema: "Tabia bora zinapoelezwa nchini kwetu, Wewe unaonekana kuwa kigezo chetu." 87. Ibn Sa'd, op. cit., j. 166; Abu Na'im, op. cit., j. 1, uk. 336. 88. Ibid, uk. 167.

Ni ukweli unaojulikana sana kwamba Mtume alikuwa na tabia ya ucheshi inayopendeza licha ya kwamba hata kwenye misemo ya uchekeshaji alikuwa mkweli. Siku moja bimkubwa mmoja hapo Madina alimwomba amwombee kwa Mwenyezi Mungu ampatie sehemu ya makazi huko Peponi. Mtume akasema; "Wanawake wazee (vikongwe) hawataingia Peponi." Bi kizee huyo aliondoka akiwa ana-lia. Bilal akamwona na akamuuliza kwa nini alikuwa ana-lia. Bimkubwa huyo akasimulia mkasa wote. Bilal akaenda naye kwa Mtume, na akasema: "Mwanamke huyu ames-imulia hivi na hivi kutoka kwako?" Mtume akasema: "Hata watu weusi hawataingia Peponi." Sasa hata Bilal akaanza kulia. Halafu Abbas, mjomba wake Mtume akafika hapo na alipoelewa kuhusu mkasa huo, akajaribu kuingilia kati kwa kuzungumza na Mtume, ambaye alimwambia kwamba hata mzee mwanamume hataingia peponi. Abbas naye alipoju-muika katika kundi la wenye kulia, Mtume akawaambia wawe na furaha kwa sababu Mwenyezi Mungu atawaumba kuwa vijana tena na wenye nyuso zinazo ng'ara na halafu wataingia peponi. 89. Bilal alikuwa mpenzi wa Ahlul Bayt. Imamu Jafar al-Sadiq amenukuliwa kusema: "Mungu na amneemeshe Bilal! Alitupenda sisi, watu wa Nyumba ya Mtume, na alikuwa mchaji Mungu bora sana miongoni mwa waja wake Mwenyezi Mungu." Imeandikwa katika Kamil Bahai kwamba Bilal hakuadhini au kukimu sala wakati wa ukhalifa wa Abu Bakr,90. na haku-toa kiapo cha utii kwa Abu Bakr kama Khalifa. Shaykh Abu 89. al-Majilisi, Hayatu'l-Qulub, uk. 129-130; Biihar, j. 16, uk. 295. 90. Shustari, Nurullah, Majalisu'l-Mu'minin (Tehran, 1268 AH.) uk. 54; na vile vile angalia Ibn Sa'd, op. cit., j. 3:1, uk. 169

Jafar al-Tusi amesimulia kwenye Ikhtiyar al-Rijal taarifa isemayo kwamba Bilal alikataa kutoa kiapo cha utii kwa Abu Bakr; na Umari alikamata vazi lake lililotengenezwa kwa ngozi na akasema: "Hii ni zawadi ya Abu Bakr; alikuachia huru na sasa unakataa kutoa kiapo cha utii kwake?" Bilal akasema: "Kama Abu Bakr alinikomboa kwenye utumwa kwa ajili ya radhi ya Mwenyezi Mungu, basi na aniachie niendelee na kumcha Mwenyezi Mungu; na kama aliniachia huru kwa sababu ya kumtumikia yeye, basi nipo tayari kumpatia huduma zihitajikazo. Lakini sitatoa kiapo cha utii kwa mtu ambaye Mjumbe wa Mungu hakum-teua kuwa Khalifa wake." Umari akamkaripia sana akasema: "Hutakiwi kuwa na sisi hapa." Hii ndio sababu baada ya kutawafu Mtume, Bilal akahamia Syria. Baadhi ya mashairi yake kuhusu mada hii ni kama ifu- atavyo: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu! Sikumgeukia Abu Bakr, Kama Mwenyezi Mungu hangenilinda, fisi wangesimama miguuni mwangu.

Mwenyezi Mungu amenipa wema na Ameniheshimu, Hakika kuna wema mwingi sana kwa Mwenyezi Mungu. Hutaniona nina mfuata mtu wa bidaa, Kwa sababu mimi siendekezi bidaa kama wao." Mwandishi wa Istiab anaandika, "Alipo tawafu Mtume, Bilal alitaka kwenda Syria. Abu Bakr akamwambia abaki Madina ili amtumikie yeye (binafsi). Bilal akasema: "Kama umenipa uhuru kwa ajili ya kukutumikia wewe, basi nikamate niwe mateka tena; lakini kama uliniondoa kwenye utumwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi niache niende katika njia ya Mwenyezi Mungu." Abu Bakr akamwacha aendelee na mipango yake."

91. Bilal alifariki dunia huko Dameski kwa ugonjwa wa tauni mnamo mwaka wa 18 A.H. au 20 A.H. na akazikwa huko Bab Saghir.92. Kaburi lake huko Dameski hutembelewa na maelfu ya Waisilamu waaminifu kila mwaka.

6. FIZZAH

Fizzah al-Nubiyyah (kutoka Nuba, sasa iko ndani ya nchi ya Sudan) pia amepata sifa njema ya milele kwa ajili ya kuji-tolea kwake katika Uislamu na kuwapenda Ahlul Bayt. Mwanzoni, alimtumikia Fatimah, binti yake Mtume. Ilipangwa na Mtume kwamba siku moja Fatimah angefanya kazi za ndani wakati Fizzah angepumzika, na siku iliyofua-ta Fizzah afanye kazi ambapo Fatima naye anapumzika. Baada ya kifo cha Fatimah, Ali akamuoza Fizzah kwa Abu Thalabah al-Habashi. Akazaa naye mtoto wa kiume, na halafu Abu Thalabah akafariki dunia. Baadaye Fizzah akaolewa na Malik al-Ghatathan. Siku moja Malik akalalamika kwa Umari kuhusu Fizzah. Umari akasema; "Unywele ambao chimbuko lake ni familia ya Abu Talib unayo elimu zaidi kuliko Adi."93. (Adi lilikuwa kabila la Umari) 91.Shushtari, op. cit., j. 1, uk. 150. 92. Shushtari, op. cit., uk. 54; vile vile tazama Ibn Sa'd, 0p. cit., j.3:1, uk. 170; Ibn Hajar, op. cit., j. 1, uk. 336-337. 93. Shubar, S. 'Abdullah, Masabihul Anwar, j. 2 (Najaf: Matba'ah al-'Ilmiyyah, 1952/1371) uk. 425-6 akinukuu Manaqib ya Ibn Shahr Ashub.

Fizzah alikuza familia yake mwenyewe; lakini aliendelea kuwapenda Ahlul Bayt. Yeye, kwa hiyari yake mwenyewe, alikwenda na Husein hadi Karbala naye akapata masum-buko makali na mateso yaliyo wapata familia ya Imamu Husein. Elimu yake ya Kitabu Kitukufu, cha Qur'an, anasifiwa kati-ka dunia ya Kiisilamu. Imetaarifiwa kwamba angalau kwa miaka yake ishirini ya mwisho wa uhai wake, hakutamka neno lingine lolote isipokuwa Qur'an; na kila mara alizungumza kwa kukariri aya za Qur'an. Kipande kimoja cha kuvutia cha mazungumzo kinanukuliwa hapa kwa lengo la kuonyesha ujuzi wake wa pekee. Abul Qasim al-Qushayri anamnukuu mtu wa kuaminika kwamba wakati mmoja aliachwa nyuma na msafara wake na akawa anasafiri peke yake. Katika jangwa, alimwona mwanamke na akamuuliza yeye alikuwa nani. Mwanamke akakariri aya ya Qur'an:

"Basi wasamehe na uwaambie (maneno ya) Amani: Hivi karibuni watajua ." (43:89)

Akagundua kosa lake, na halafu akauliza: Unafanya nini hapa?" Mwanamke:

"Na wale ambao Mungu huwaongoza hakuna atakaye wapotosha ." (39:37)

Mwanamume: "Wewe ni jini au mwanadamu?" Mwanamke:

يَا بَنِي آدَمَ خُذُوا زِينَتَكُمْ عِندَ كُلِّ مَسْجِدٍ ﴿٣١﴾

"Enyi wana wa Adamu! Vaeni mavazi yenu mazuri kila wakati wa sala na mahali pa sala." (7: 31)

Mwanamume: "Unatoka wapi?" Mwanamke: "Hao wanaitwa na hali ya kuwa wako mbali kabisa " (41:44)

Mwanamume: "Unakwenda wapi?" Mwanamke:

وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ﴿٩٧﴾

"Na Mwenyezi Mungu, amewajibishia watu wafanye Hija katika Nyumba hiyo, kwa wale wenye uwezo wa kugharamia safari." (3:97)

Mwanamume:

وَلَقَدْ خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ﴿٣٨﴾

"Siku ngapi zimepita tangu uachwe na msa-fara?" Mwanamke: "Na kwa hakika tuliumba mbingu na dunia na vyote viliv yomo ndani humo kwa muda wa siku sita." (50:38)

Mwanamume: "Unataka chakula?" Mwanamke: "Wala hakuwapa wao miili ambayo haikuhitaji chakula ." (21:8)

Hivyo mwanamume akampa mwanamke huyo chakula. Baada ya hapo mwanamume akamwambia mwanamke akimbie haraka. Mwanamke akasema: "Mungu haibebeshi nafsi yoyote mzigo isiyoweza kuubeba ." (2:286)

Hivyo mwanamume akamwambia mwanamke aketi kwenye ngamia nyuma yake. Lilikuwa jibu lililotoka kwa mwanamke huyo:

لَوْ كَانَ فِيهِمَا آلِهَةٌ إِلَّا اللَّـهُ لَفَسَدَتَا ﴿٢٢﴾

"Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipo kuwa Mwenyezi Mungu basi bila ya shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. (21:22).

Aliposikia hivi alishuka chini kutoka kwenye ngamia na akamwomba mwanamke apande juu ya ngamia, na amwen-deshe yeye. Alipoketi juu ya ngamia, mwanamke huyo akakariri aya hii:

سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَـٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِينَ ﴿١٣﴾

"Utukufu uwe kwake Yeye ambaye amemtiisha kiumbe huyu ili tumtumie, kwani hatungeweza kusafiri mwendo mrefu sisi wenyewe." (43:13)

Baada ya muda si mrefu, wakaungana na msafara. Mwanamume akamuuliza mwanamke kama alikuwa na ndugu miongoni mwa wasafiri kwenye msafara huo. Mwanamke akasema: "Ewe Dawud! Hakika tumekufanya wewe uwe khalifa hapa duniani; Muhammad ni Mtume tu; Ewe Yahya kishike kitabu kwa nguvu zote; Ewe Musa, Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi!" (38:26, 3:144, 19:21, 20:11-12.) Mwanamke akaita majina haya, na akawaona vijana wanne wanakimbia kuelekea kwake. Hapo hapo akamuuliza mwanamke huyo uhusiano wake na vijana hao.

Mwanamke huyo alisoma ay a hii: "Mali na wana ni pambo la maisha ya dunia hii ." (18:46)

Wakati huo watoto hao wakafika hapo; mama akawaambia watoto wake: "Ewe baba yangu! Muajiri huyu. Hakika mbora wa kumua-jiri ni mwenye nguvu na mwaminifu ." (28:26).

Watoto wa mama huyo wakampa mwanamume aliyekuja hapo na mama yao ujira kwa ajili ya usumbufu na huduma. Lakini mama wa watoto hao akaona ujira huo ulikuwa mdogo, kwa hiyo akasema:

"Na Mwenyezi Mungu humzidishia amtakaye ." (2:261).

Kwa hiyo, wanawe wakaongeza ujira wa mwanamume. (Upo uwezekano mkubwa sana kwamba watoto hawa wa kiume baba yao ni mume wa pili wa Fizzah, Malik al- Ghatathani.) Mwanamume huyo akawauliza watoto hao wa kiume mama huyo alikuwa nani. Wakamwambia kwamba alikuwa Fizah, mtumishi wa Fatimah, binti yake Mtume na kwamba tangu miaka ishirini iliyopita alikuwa hajasema neno lolo isipokuwa Qur'an 94. 7. Qambar: Mara nyingi jina la Qambar limetajwa kwenye hadithi. Na amepewa sifa za daima na beti za shairi lifuatalo la Imamu Ali: "Nilipoona jambo ambalo ni kinyume cha sheria, Niliwasha moto na kumwita Qambar.

Mtu mmoja alimuuliza Qambar bwana wake alikuwa nani. Qambar alielezea sifa za Imamu Ali bin Abi Talib kwa namna ya dhahiri na ya kupendeza hivyo kwamba lime-nakiliwa na muhadithin bila kubadili hata kidogo.95. Kwa sababu haki haiwezi kutendeka kwayo katika kulitafsiri, ninaiacha hotuba hiyo. Nimekwisha sema jinsi Qambar alivyokuwa anatendewa wema kwa mapenzi na Imamu Ali. Baada ya kifo cha Imamu, Qambar alikuwa na desturi ya kusimulia kwamba alikuwa ana mtumikia bwana wake mara chache sana kwa sababu Imamu Ali alikuwa akifanya kazi zake yeye mwenyewe; alikuwa anachota maji kwa ajili ya matumizi ya kila siku, alikuwa anafua nguo zake mwenyewe, alikuwa hata anashona nguo zake mwenyewe wakati ihitajikapo; alikuwa anachota maji kisimani yeye 94. Majilisi, Bihar,)A3 (Beirut, 1983/1403) uk. 86-7; Ibn Shahr Ashub, Manaqib Aal Abi Talib, j. 4 (Bombay, 1313 AH.) uk. 15 95.Kashshi, Rijal kama ilvyonukuliwa na Qummi, op. cit., j. 1, uk. 153 mwenyewe kwa matumizi yake ya kila siku; alikuwa anawalisha chakula kizuri na nguo nzuri lakini yeye mwenyewe alikuwa anavaa na kula kama mtu fukara. Mara nyingi alitumia usemi wa: "jihisi upo nyumbani mtoto." Qambar alikuwa na desturi ya kusema: "Ni katika siku moja tu alinikasirikia. Ilikuwa wakati nilipomwonyesha fedha nilizoziweka kama akiba yangu ya matumizi ya baadaye. Fedha hiyo ilikuwa mafungu ya kipato nilichopewa na watu wengine na zawadi nilizopewa na watu wa familia yake. Nilikuwa nimekusanya dinari mia moja. Nilipo mwonyesha kiasi hicho cha fedha, alionekana kukasirika, na kilicho niu-miza mimi zaidi, Ali alionekana na huzuni." Qambar aka-muuliza kwa nini alikuwa na huzuni hivyo. Ali akajibu, 'Qambar, kama ulikuwa huna utumizi na fedha, je, hakuna watu jirani yako ambao wana hitaji fedha? Baadhi yao pengine wanakufa njaa, wengine pengine ni wagonjwa na walio dhaifu. Je, usingeweza kuwasaidia (kwa fedha hiyo?). Sikufikiria kama ungekuwa huna huruma kiasi hicho na unapenda utajiri kwa ajili ya kuwa tajiri. Qambar nina hofu hufanyi jitihada ya kujaribu kupata faida kutoka kwenye Uislamu; jaribu sana kwa dhamira hasa na kwa moyo safi. Ziondoe sarafu hizo nyumbani mwangu." Qambar akagawa fedha hizo kwa masikini haraka sana na kwa wahitaji, Qambar alikwisha achwa huru na Imamu Ali, lakini aliamua kuendelea kubaki naye.

Hajjaj bin Yusuf al-Thaqafi, gavana aliyeteuliwa na Abdul Malik bin Marwan kutawala Iraq, alikuwa katili aliyekuwa na tabia ya kujivuna kwamba, "Kitu kitamu kuliko vyote hapa duniani ninacho kitamani ni kuua." Jina lake limekuwa methali kwenye uovu. Aliua watu 120,000 ambao kosa lao lilikuwa kumpenda Ali bin Abi Talib na Ahlu Bayt. Idadi hii haijumuishi wale watu walio uawa na yeye kwenye vita. Alijaribu sana kuwamaliza Shia wa Ali kutoka Iraq. Said bin Jubayr na Kumayl bin Ziyad ni waathirika wake wawili. Wakati fulani Hajjaj aliuliza, "Yupo aliye bakia miongoni mwa wafuasi wa Abu Turab (yaani Ali) ili niweze kumrid-hisha Mwenyezi Mungu kwa kumuua?" Akajibiwa kwa kuambiwa kwamba alikuwepo Qambar, mtumwa wake. Hivyo Qambar, aliye mtu mzee sana, alikamatwa na akafik- ishwa kwake. Halafu mazungumzo yalikuwa kama ifu- atavyo baina ya Hajjaj na Qambar: Hajja: "Wewe ni mtumwa wa Ali?" Qambar: "Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi na Ali ni mfadhili wangu." Hajjaj: "Kazi yako ilikuwa nini ulipokuwa unamtumikia Ali." Qambar: "Kazi yangu ilikuwa kumpa maji ya kutawadha ili apate udhu." Hajjaj: "Ali alikuwa akikariri nini baada ya kutawadha?" Qambar: "Ali alikuwa na tabia ya kukariri aya hii: "Basi walipo sahau walio kumbushwa, tuliwafungulia milango ya kila kitu. Mpaka walipo furahia yale waliyo pewa tuli- washika kwa ghafla, na mara wakawa wenye kukata tamaa." (6:44) Hajjaj: "Nadhani ni sisi alio maanisha kujumuishwa kwenye aya hii?" Qambar: "Ndio."

Hajjaj: "Ni vema uache dini ya Ali." Qambar: "Kabla sijaacha dini hii, niambieni dini gani ni nzuri zaidi kuliko yake." Hajjaj: "Utafanya nini kama nikikukata kichwa chako?" Qambar: "Basi itakuwa ni bahati njema kwangu na bahati mbaya kwako." Kwenye hadithi nyingine swali hili la mwisho na jibu lake limenukuliwa tofatui. Hajjaj: "Hakika nina taka kukuua. Ni vema uchague namna yako mwenyewe ya kufa." Qambar: "Ni juu yako. Niue kwa namna yoyote unayota-ka, kwa sababu nitakuua kwa njia hiyo hiyo Siku ya Hukumu. Na, ni jambo la ukweli kwamba bwana wangu alikwisha niambia kwamba ungeniua kwa kunikata kichwa." Hajjaj akaamuru akatwe kichwa Qambar aliuawa kifo cha kishahidi kwa ajili ya imani yake. Leo hii kaburi lake huko Baghdad ni mahali panapotembelewa na maelfu ya mahuja-96. 8. Said: Said, mtumwa mwingine wa Ali bin Abi Talib, anasema kwamba ilikuwa siku moja ya joto kali, Ali alikuwa na shughuli ya kuandika barua. Akataka kumtuma Said aende kuwaita baadhi ya maofisa wake. Akamwita mara ya kwan-za, pili, tatu, na kila mara alipoitwa Said alinyamaza kimya kwa kukusudia. 96. Abu Na'im, op. cit., j. 1, uk. 153; Ibn Hajar, op. cit., j. 3, uk. 514. Imamu alisimama mwenyewe na akamuona Said amekaa mahali ambapo si mbali na alipokaa. Akamuuliza kwa nini haitiki wito wake. Saidi akajibu, "Bwana, nilitaka kujua ni mahali gani, wakati gani na kwa jinsi gani ungeweza kukasirika." Ali akatabasamu na akamwambia Said kwamba hangeweza kuamsha hisia za kukasirisha na hivyo kumkasirisha kwa kutumia hila hizo za kitoto. Imamu Ali akamwachia huru, lakini akaendelea kumsaidia hadi kifo chake. 9. Watumwa: Wasaidizi wa Imani. Kama ambavyo Mtume wa Uislamu alileta ujumbe wa undugu ulimwengu mzima, ilikuwa ni dhahiri kwamba ujumbe huu wa kuikomboa roho ya mwanadamu unge-wavutia na kuwapendezesha watu wa mataifa yote na imani; lakini hususan yale makundi yenye kuonewa na kudhulumi-wa. Ilikuwa kawaida kwamba sehemu kubwa zaidi ya wafuasi wake wa mwanzo ilikuwa ya watumwa. Wapinzani walihofu; katika hali ya kukata tamaa, wakaanza kuwatesa watu walioingia kwenye Uislamu mwanzoni. Zaidi ya hayo majina ambayo maelezo yake yamekwisha tolewa hapo juu, yafuatayo ni majina yanayohitaji kuangali-wa kwa makini. Suhayb bin Sinan wa Roma alikuwa mtumwa aliyesilimu na kuwa Mwisilamu wakati wa siku za mwanzo wa Uislamu. Mtu huyu alikuwa mfua chuma stadi, akiten-geneza deraya na panga. Kwa hiyo, alikusanya akiba kubwa ya fedha. Baada ya kuwa Mwisilamu, pia alikutana na mateso ya kikatili aliyofanyiwa na makafiri.97. 97.Ibn Hajar, op. cit., j. 3, uk. 514 Alipotaka kuhamia Madina, makafiri wakamkamata na wakamnyang'anya fedha yake yote. Kwa hiyo, alifika Madina akiwa fukara. Umari, Khalifa wa pili, alimpa dhamana ya kuongoza sala ya jamaa, baada ya kifo chake hadi hapo Khalifa mwingine atakapochaguliwa. - Khabbab bin al-Arrat - alikuwa sahaba maarufu wa Mtume. Alikuwa mtu wa sita k ukubali Uislamu. Alitoka bara la Afrika; na akateswa kwa sababu ya ukweli. 9

Alikuwa miongoni mwa wale walioitwa "Shia (wafuasi wenye ari) wa Ali." Mtoto wake wa kiume, Abdullah pamo-ja na watu wote wa familia yake, waliuawa kishahidi na Makhariji mwaka wa 40 A.H. 100 Kujitolea mhanga kukubwa kabisa kw ajili ya Uislamu kuli-fanyika huko Karbala mnamo mwaka wa 61 A.H. kuliko-fanywa na Imamu Husein na masahaba wake. Kundi la roho 120-lilikabiliana na jeshi la Yazid bin Muawiyah (wapi-ganaji wasiopungua 30,000.) Ni jambo la kuzingatia kwam-ba kwenye kundi hilo la waumini 120, takriban watu 16 walikuwa watumwa au watumwa walioachiwa huru. Walikuwa kama ifuatavyo: Shawadhab - Mwafrika aliyekufa kishahidi, alikuwa mmoja wapo wa wasomi walio heshimiwa sana wa sheria za Kiisilamu na hadithi. Watu walikuwa na kawaida ya kusafiri kutoka mbali kumsikiliza yeye. 1 98. Ibn Sa'd, op. cit., j. 3:1, uk.161-4; Ibn Hajar, op. cit., j. 3, uk. 516. 99. Ibn Sa'd, op. cit., j. 3:1, uk. 116-7; Abu Na'im, op. cit., j. 1, uk. 144. 100. Ibn Sa'd, op. cit., j. 3:1, uk. 21; Ibn Hajar, op. cit., j. 4, uk. 739. 101. Qummi, op. cit., j. I, uk. 266. Aliposikia taabu ya Husein, Shawadhab na bwana wake wa zamani (na sasa ni sabaha) Abis Shakiri waliungana pamoja na wakaingia kwenye uwanja wa vita wa Karbala na wakafia humo. Jonh (Yahya) bin Huwai, - Wa kutoka Ethiopia, inawezekana alisilimu kutoka dini ya Kikristo kama jina lake linavyoonyesha. Alikuwa mtumwa wa Abu Dharr al-Ghifari, sahaba maarufu wa Mtume. Baada ya kifo cha Abu Dharr, aliambatana na Ahlul Bayt ambao walikuwa wanamwangalia. Akafuatana na Imamu Husein huko Karbala, na mbali ya kwamba kwa wakati huo alikuwa mtu mzee, alijaribu kwenda kuingia kwenye uwanja wa vita kupigana. Imam Hussein kwanza alikata; lakini John aling'ang'ania na mwishowe Imam alimruhusu kwenda kwenye uwanja wa mapambano. Alipoanguka Imamu Husein alikwenda kwenye maiti yake, akaweka paji la uso wake kwenye mapaja yake, na akamwomba Mungu ang'ar-ishe uso wa John. Watu wa kabila la Asad walipofika hapo baada ya siku tatu kuwazika mashahidi, walishangaa kuona maiti iliyokuwa inang'aa kwa nuru ya peponi na kufunikwa na mafuta mazuri ya peponi. Hii ilikuwa maiti ya John.

Salim, Zahir bin Amr, Qarib bin Abdullah Du Ali, Mumjih bin Sahm, Sa'd bin Harth, Nasr bin Abi Naizar, Aslam bin Amr na Sulayman walikuwa miongoni mwa waathirika wa "shambulio la kwanza" jaribio lililofanywa na kikosi cha Yazid kukimaliza kikundi kidogo cha Imamu Husein kwa kuwazidi nguvu kwa uwingi, uwezo, uwepesi na masham-bulizi ya kushtua. Jeshi la Yazid lilishindwa katika jaribio lake la kwanza kwa sababu ya ubora wa mbinu za kundi la Husein na utii kamili kwake. Kikosi cha Yazid kilirudi nyuma, na kuacha nyuma, wapiganaji wengi waliouawa. Lakini ushindi huu wa wafuasi wa Imamu Husein uli-patikana kwa gharama kubwa. Masahaba wa Imam Hussein walikuwa wamelala katika uwanja wa mapambano, mion-goni mwao wakiwemo mashahidi sita waliotajwa hapo juu ambao walikuwa watumwa. Pia palikuwepo na watumwa wengine sita waliokufa kishahidi hapo Karbala. Majina yao ni: Harith bin Nabhan, Said, Nafi, Salim, Shabib na Wadih. Maelezo pia yanapatikana kwenye historia za mtumwa wa Kituruki wa Imamu Zaynul Abidin ambaye alipigana na jeshi la Yazid na akajitoa mhanga kwa ajili ya Uislamu. 102.

Aqabah bin Saman, - pia ni mtumwa, alikuwa miongoni mwa masahaba walioaminiwa sana wa Imamu Husein. Imamu alimwachia sahaba huyu nyaraka zake muhimu zote azitunze yeye. Kwa istilahi ya kisasa, tunaweza kusema kwamba alikuwa katibu wa Imamu Husein. Sahaba huyu alijeruhiwa kwenye uwanja wa vita wa Karbala na akatekwa na kuwa mfungwa wa kivita pamoja na familia ya Imamu Husein. Akiwa mmoja wapo wa mashahidi walioona kwa macho wenyewe mauaji ya halaiki ya watu huko Karbala, maandiko ya Aqabah bin Samem ni chanzo muhimu sana cha historia. Bin Jarir al-Tabari, mwanahistoria maarufu Mwisilamu, ameandika maelezo ya Aqabah kwenye kitabu chake kiitwacho Tarikh al-umam wa al-muluk. Orodha hiyo ya matukio ilitenganishwa kutoka kwenye orodha ya matukio ya al-Tabari na kuchapishwa huko India pamoja na maelezo kutoka kwa marhum Mujtaba Husein Kamunpuri wa Aligarh Muslim University. 102. Kwa maelezo zaidi juu ya Imamu Husein na Karbala, tazama Rizvi, S.M., Imam Husayn, the Saviour of Islam, (Vancouver: 1984). Waisilamu wakati wote wamekuwa na fahari kwa mihanga ilyotolewa na mashahidi wa Karbala kwa ajili ya Uislamu. Dhuria wa Imamu Husein wakati wote wamekuwa wana wapa salaam mashahidi hao, wakati mwingine wanawataja mmoja baada ya mwingine, wakati mwingine wanawataja kwa pamoja. Shia Ithna Asharia, wakiongozwa na Maimamu wao, kila mara huwapa salaamu mashahidi hawa kwa tamko lifuatalo, Karibuni siku zote:- Salaamu kwenu, Enyi watakatifu wa Allah na mlio wapendwa wake; Salaamu kwenu, Enyi wateule wa Allah na wapenzi wake;

Salaamu kwenu, Enyi wasaidizi wa Dini (imani) Wazazi wangu nawafidie maisha kwa ajili yenu, Mlio tohara na safi, na imekuwa tohara na safi ardhi mliyozikiwa; kwa hakika mumepata mafanikio (ushindi) makubwa kabisa; Ningependa kwa Mwenyezi Mungu kwamba ningekuwa pamoja nanyi katika kushiriki mafanikio hayo. 103. 10. Watoto wa watumwa: Maimamu na Makhalifa Tangu ujilio wake hadi kipindi cha ukoo wa Umayya, Uislamu uli-pata ushindi wa kiwango cha mafanikio katika vita yake ya wema dhidi ya utumwa. Watumwa hawakuwa tena binadamu wa daraja la kudharauliwa kama wanyama, bali walikuwa watu wanaume na wanawake wenye hadhi na hes-hima. Watumwa wengi walioachiwa na kuwa huru, wali-weza kupata kazi za juu na kupata vyeo vikubwa. Dhuria wa Mtume na wafuasi wao waliendeleza msimamo wa Kiisilamu kwa utumwa. Maimamu kadhaa walioa wanawake watumwa ambao baadaye wakawa mama wa Maimamu. 103. Qummi, Mafatihu'l-Jinan ( Tehran, n.d.) uk. 427. Madhehebu ya Kaysaniyyah yaliamini Muhammad al-Hanafiyyah (mtoto wa Imamu Ali) kuwa ndivyo Imamu baada ya Imamu Husein. Mama yake Muhammad al-Hanafiyyah, Khawla bint Jafar bin Qays alikuwa mateka ambaye Ali alimuoa. Lakini hapana mtu alitoa ushauri kwamba kuzaliwa na mama aliyekuwa mateka, ilikua dosari katika imani ya madhehebu ya Kaysaniyyah. Vivyo hivyo, Madhehebu ya Zaydiyyah wana amini kwamba Imamu, baada ya Imamu Zaynul Abidin, alikuwa ni mwanae Zayd ambaye alizaliwa na mama msichana mtumwa kutoka Sindhi, jina lake Huriya.

Hata Shahr Banu, binti yake Yazd Jurd (mfalme wa mwisho wa Iran) ambaye aliolewa na Imamu Husein na akamzaa Imamu Zaynul Abidin, alifika Arabuni akiwa mateka. Hata hivyo sifa zake binafsi zilimpa fursa ya kupewa cheo cha "Mkuu wa wanawake." Hamidah Khatun, mama yake Imamu Musa al-Kazim alikuwa msichana mtumwa kutoka Berber. Anasifiwa kwa elimu yake na uchamungu wake. Akawa anaitwa Hamidah mtakatifu. Imamu Jafar al-Sadiq alikuwa na desturi ya kuwapeleka wanawake kujifunza kanuni za dini kutoka kwa Hamidah na alikuwa na tabia ya kusema kwamba, "Hamidah ni mtakatifu kutokana na uchafu wote kama kipande cha dhabahu." Mama yake Imamu Ali al-Riza pia alikuwa msichana mtumwa kutoka Afrika Magharibi Kaskazini. Jina lake Taktum (au Najma) na alijulikana kama Tahirah, aliye takaswa. Alijulikana kwa elimu yake na uchamungu wake. Imamu Muhammad al-Taqi alikuwa mtoto wa Sabikah, aliyejulikana zaidi kama Khayzurah, mtumwa msichana kutoka Nuba. Imamu Musa al-Kazim alimwambia Yazid bin Sabt kupeleka salam zake kwa Sabikah. Kwenye hadithi anaitwa Tayyibah. Mama yake Imamu Ali al-Naqi, Sammanah, wa Maghrib, alikuwa mtumwa, lakini alikuwa anaitwa Sayyidah (mkuu wa wanawake) hakuwa na mtu wa kulingana naye kwa uchaji Mungu, mapenzi na kumuogopa Mwenyezi Mungu. Alikuwa akifunga saumu karibu mwaka wote. Imamu Ali al-Naqi alimwambia kwamba alikuwa analindwa na Mwenyezi Mungu na alikuwa wa kwanza miongoni mwa wakweli na waadilifu. Imamu Hasan al-Askari pia alizaliwa na mama ambaye alikuwa mtumwa msichana, Hudayth (au Salil.) Katika kumwonyesha hadhi yake ya juu miongoni mwa Shia, inatosha kusema kwamba baada ya kifo cha Imamu Hasan al-Akari yeye alikuwa mtu wa katikati kabisa ndani ya Ushia na jamii yote ilikusanyika kumzunguuka yeye na ali-waongoza katika njia iliyo bora kabisa. Shia walikuwa wakimwita "Jaddah," bimkubwa. Narjis Khatun, mama yake Imamu wetu wa 12 ambaye yupo hai mpaka sasa, alikuwa mtoto wa mfalme wa himaya ya Byzantine. Lakini pia alifika kwa Imamu Hasan al-Askari kama mtumwa.

Kiasi hiki kitatosha kwa upande wa kiroho. Tukiangalia upande wa siasa, tunaona watumwa wasio hesabika waliofi-ka katika kazi za vyeo vya juu sana vya uwajibikaji, uki-jumlisha na makamanda wa majeshi, kufanya kazi ya uga-vana, na uhakimu. Si tu kwenye utawala, pia tunawaona wataalam wa theolojia (elimu ya dini), wafasiri wa Qur'an, muhadithi, wana sheria na waandishi, ambao ama walikuwa watumwa au watoto wa watumwa, au watumwa walio achwa huru. Ukiwaondoa khalifa wa kwanza, tatu, nne na tano, makhalifa wote wa ukoo Abbas walizaliwa na wanawake watumwa. al-Mansur (khalifa wa pili wa ukoo wa Abbas) maarufu, alikuwa ndiye khalifa wa kwanza kuza-liwa na mama aliyekuwa mtumwa, Salamah, aliyetoka Berber. Kuanzia kwa Mamun al-Rashid (khalifa wa sita wa Banu Abbas) hadi wa mwisho wote walikuwa watoto wa wasichana watumwa. Yafuatayo ni majina ya makhalifa na mama zao watumwa: Mamun al-Rashid: Murajil, mtumwa msichana mweusi Mutasim Billah: Mtumwa msichana kutoka Kufah, jina lake aliitwa Maridah Wathiq Billah: Mrumi, jina lake ni Qaratis Mutawakkil Allallah: Mtoto wa Shuja Muntasir Billah: Mrumi, jina lake ni Habashiyyah Mustin Billah: Mukhariq Mutazz Billah: Mrumi, jina lake ni Qabihah Muhtadi Billah; Wards au Qurb. Mutamid Allallah: Mrumi, jina lake ni Fityan. Mutazid Billah: Sawab (au Hirz au Dhirar) Muktafi Billah: Mturuki mtumwa msichana, jina lake ni Jyaq au Khudi. Muqtadir Billah: Mrumi au Mturuki, mtumwa msichana, Gharib au Shaghab Qahir Billah: Fitnah Radhi Billah: Mrumi, jina lake ni Zalum. Muttaqi Lillah: Khalub au Zuhra Mustakfi Billah: Awjahun Naa au Ghusm. Muti Lillah: Mashalah Attai Lillah: Hazar au Atab. Qadir Billah: Dumanah au Tamami Qaim Billah: Kutoka Armenia, jina lake ni, Badrudduja au Qatrunnada Muqtadi Bi Amrillah: Arjwan Mustazhir Billah: Mtumwa (jina halikuandikwa) Mustarshid Billah: Mtumwa (jina halikuandikwa) Rashid Billah: Mtumwa (jina halikuandikwa Muqtafi Li Amrillah: Kutoka Ethiopia, mtumwa msichana Mustanjid Billah: Kutoka Karjiyya, mtumwa, jina lake ni Taus Mustadi Bi Amrillah: Kutoka Armenia, jina lake ni Dhaddha Nasir Li Dinillah: Mturuki, mtumwa, jina lake ni, Zamurrad Zahir Bi Amrillah: Jina halikuandikwa. Munstansir Billah: Mturuki mtumwa (jina halikuandikwa) Mustasim Billah: Hajir104.

Hata wakati wa karibu sana wa falme ya Ottoman ya Uturuki, familia ya Kifalme inaweza kujumuishwa katika familia ya kitumwa kwa sababu mama wa watoto wa hao masultani walikuwa watumwa. Muda mrefu kabisa kabla ya utawala wa Sulayman, Sultani ama alikwisha acha kuchukua mke kutoka kwenye familia za Kisultani au alimpa daraj a la mke kwa mama wa watoto wao. Mfumo wa utawala wa Ottoman kwa makusudi ulichukua watumwa na kuwafanya mawaziri wa nchi. Ufalme huo ulichukua watoto wa kiume kutoka kwenye zizi la kondoo shambani na kuwafanya washauri wa Sultani na kuwaoza mabinti wa kifalme, waliwachukua wanaume vijana wa nhi ambayo wahenga wao walikuwa na majina ya Kikristo kwa karne nyingi, na kuwafanya watumwa wa nchi kubwa kabisa za Kiislam. 104. Tizama sura zinazohusika za kitabu Rawdatu 's-Safa cha Muhammad Khawind Shah ; vile vile Ibn Rabbih al-Undulusi, al-Iqdu'l-Farid, j. 5 (Beirut: 1983) uk. 113-131.

1

MASOMO YA KI-ISLAMU

MUONGOZO KWA WASOMAJI

WANAOTHIBITISHA KUWA IPO

A . Amepokea Ibnu Abbas kwamba: "Umar bnul Khattab, siku moja alipokuwa juu ya Mimbar alisema: "Sisi tulikuwa tukisoma katika Qur'an: AN LAA TARGHABU A'N ABAAIKUM FAINNAHU KFRUN BIKUM AN TARGHABU A'N ABAAIKUM"...[27]

B . Umar bnul Khattab alileta Ayatur rajmi ili itiwe katika msahafu, lakini haikuandikwa, kwa sababu Umar alikuwa peke yake hakuwa na shahidi.[28]

Aya yenyewe aliyoileta Umar inasomeka hivi: ASH'SHAYKHU WASH'SHAYKHATU IDHA ZANAYAA FARTUMUHUMAA ALBATTATA NAKAALAN MINALLAHI WALLAHU A'ZIZUN HAKIMUN".[29]

C . Inasimuliwa kuwa: katika mbao za Mwana Aisha ilikuwako Qur'an ikisomeka hivi: "INNA LLAHA WAMALAIKA TAHU YUSWALLUNA A'LAN NABIYY YA AYYUHA LLADHINA AMANU SWALLU A'LAYHI WASALLIMU TASLIIMA WA A'LALLADHI NA YUSWALLUNA ASSUFUFAL AWWALA" Mwana Aisha (mkewe Mtume) alikuwa nayo Qur'an hiyo kabla Uthman bin Affan hajabadilisha misahafu![30]

D . Anasema Mwana Aisha (mkewe Mtume) katika zama za Mtume(s.a.w.w) Suratul Ahzabi ilikuwa inafikia Aya mia mbili, lakini, ulipoandikwa msahafu Aya zikawa hivi kama zilivyo sasa ambazo ni sabini na tatu tu!! Aya mia moja ishirini na saba zimepotea![31]

WALIOSEMA KUWA HAIPO

Mizani ya kupima riwaya zilizo tajwa hapo juu kuonyesha kuwa kuna baadhi ya amma sura au aya zilizopotea, riwaya hizo na za mfano wa kama hizo ni batili, Mwenyeezi Mungu anasema: (Qur'an) "Haitaifikia batili mbele yake wala nyuma yake " 41:42

"Hakika sisi tumeiteremsha Qur'an, na hakika sisi ndio wenye kuilinda " 15:9. Hii ndio itikadi ya Shia Ithna Ashar.[32]

KUSOMA QUR'AN KWA AJILI YA MAITI

Wako baadhi ya Waislamu wanapinga kumsomea Qur'an maiti, wakisema kwamba kufanya hivyo ni bid'a na bid'a mahala pake ni motoni. Katika kupinga jambo hili wanatoa hoja zao kama ifuatavyo:

A . Imethibiti kuwa: Mtume(s.a.w.w) hakumsomea Qur'an maiti yeyote katika uhai wake, kama jambo hilo ni jema Mtume asingeliacha kufanya kheri hiyo. Kwa hiyo, yeyote leo anae soma Qur'an kwa ajili ya mait, akaamini kuwa itamnufaisha, bila shaka mtu huyo anadai kuwa Mtume amefanya khiyana katika umma huu. Na hilo ni kosa kubwa kuamini kuwa Mtume hakufikisha baadhi ya mambo katika umma wake.

B . Mwenyeezi Mungu anasema: "Na ya kwamba mtu hatapata isipokuwa aliyoyafanyia juhudi " 53:39.

Na kwa Aya hii Imam Shafi amesema kuwa: Kisomo (anachosomewa maiti) thawabu za kisomo hicho hazifiki kwa maiti. Kwa sababu hilo haliko katika matendo yake, na kwa sababu hii, Mtume hakuwawekea umma wake, wala hakuhimiza (wafanye) kwa mtu yeyote. Wala hakupendekeza, wala sahaba yeyote hakuna aliyepokea (jambo hili) [33]

C . Amesema Mtume(s.a.w.w) : "Anapokufa mwanadamu, matendo yake humalizika yote isipokuwa mambo matatu: sadaka ya kudumu, au elimu yenye kunufaisha, au mtoto mwema atakaemuombea baada yake ".

Kwa hiyo, wasomaji wa khitima hupoteza bure muda wao, kwa kufanya jambo haliko katika Uislamu.

MAJIBU YETU

Kabla ya kuingia katika majadiliano hayo ni vyema kuzingatia jambo mmoja, nalo ni "NINI QUR'AN"? Taarif ya Qur'an ni: "Maneno ya Mwenyeezi Mungu aliyoyateremsha kwa Mtume wake Muhammad(s.a.w.w) hali yakuwa ni muujiza wake" sasa, Ikisemwa kuwa: Mtume(s.a.w.w) hakuwasomea Qur'an maiti wake, huwa inakusudiwa Qur'an gani?? Kwa sababu, katika salatiil maiti mna Suratul Fatiha, na Mtume(s.a.w.w) aliwasalia mauti wake. Isipokuwa, ikithibitishwa kwa dalili kuwa: Suratul Fatiha si Qur'an[34] . Kuhusu Aya iambiwayo kuwa inazuia thawabu za Qur'an kumfikia maiti 53:39.

Tuangalie matni yake: "WA AN LAYSA LIL'INSANI ILLA MASAA", yaani, "Na yakwamba mtu hatapata isipokuwa aliyo yafanyia juhudi." Hivi ndivyo ananyosema Mwenyeezi Mungu na wala hasemi: "LA YANTAFIU'UL INSANU ILLA MASAA", yaani, "Hanufaiki mwanadamu isipokuwa kwa yale aliyoyafanyia juhudi". Hapa pana tofauti kubwa kati ya ibara ya kwanza na hii ya pili. Ibara ya kwanza inafidisha kuwa: "Mwanadamu atalipwa thawabu kwa mujibu wa matendo yake". Na ibara ya pili inafidisha kuwa: "Mwanadamu hanufaiki kwa chochote isipokuwa kwa matendo aliyoyatenda mwenyewe." Kwa ibara hizi ni sawa na kusema kuwa: "Athumani ana kibanda kidogo cha makuti, na humo ndimo anamoishi. Kwa hiyo, Athumani hana nyumba nyingine yoyote atakayoishi isipokuwa katika kipanda hicho. Lakini hali hii haizuii yeyote mkarimu kumjengea Athumani nyumba kubwa na bora. Mkarimu kama atajenga nyumba iliyo bora na kubwa, kisha akampa Athumani, haiwezi kusemwa: Athumani hawezi kukaa katika nyumba hiyo eti kwa sababu hakuijenga yeye. Amma Hadithi iamiwayo kuwa iazuia thawabu ya Qur'an kumfikia maiti isemayo: "IDHA MATA IBNU ADAMA IN'QATAA A'MALUHU ILLA MIN THALATHA..." yaani, "Anapokufa Mwanadamu matendo yake yote hukatika isipokuwa mambo matatu...." wala Hadithi haisemi: "IDHA MATA IBNU ADAMA IN'QATAA INTIFAU'HU" yaani, "Anapo kufa Mwanadamu humalizika kunufaika kwake". Ibara ya kwanza inafidisha kuwa: "Kinachomalizika ni matendo yake". Na ibara ya pili inafidisha kuwa: "Kinachomalizika ni kunufaika". Kwa mizani ya somo hili, natija inaonyesha kuwa Qur'an ikisomwa kwa ajili ya maiti, lazima thawabu ya kisomo hicho zitamfikia maiti, na hapa tutaonyesha hali tatu zilizo hai:

a . Mtume(s.a.w.w) amesema: "Man Mata Wa A'layhi Siyam Sama A'nhu Waliyyuhu ". yaani,atakae kufa na juu yake kuna saumu atafunga kwa niaba yake walii wake ". Hadithi hii imekubaliwa na Waislamu wote na hata Imam Shafi naye ameikubali. Je! Kama mlango wa kunufaika umefungwa, thawabu ya funga anayofanyiwa maiti na walio hai ingemfikiaje?

b . Mtume(s.a.w.w) alimwambia mwanamke mmoja: "Mhijie mama yako". Na akamwambia mwanamume: "Mhijie baba yako". Hadithi hii pia imekubaliwa na Waislamu wote, Je! Thawabu za hija anayohijiwa na walio hai zinamfikiaje maiti, kumbe mlango wa kunufaika umefungwa?

c . Mwenyeezi Mungu anasema: "Zinamtukuza mbingu saba na ardhi (saba) na vilivyomo ndani yake, na hakuna chochote isipokuwa kinamsabihi kwa sifa zake njema lakini nyinyi hamfahamu kutukuza kwao" 17:44.

Iliposemwa: "Na hakuna chochote isipokuwa kinamsabihi kwa sifa zake njema". Hii inafidisha kuwa: Vitu vyote vinamsabihi Mwenyeezi Mungu, na kwa kuelewa zaidi hili tumsikilize Mtume(s.a.w.w) . Imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Mtume(s.a.w.w) alipita kwenye makaburi mawili akasema: Hawa waliomo katika makaburi haya wanaadhibiwa... Mara akaagiza kuti la mtende, akalipasua vipande viwili kisha akachimbiaa kimoja katika kaburi hili na kingine akachimbia katika kaburi lile, halafu akasema: Bila shaka vitawapunguzia (adhabu) madam havijakauka". Hiposemwa: "Madam havijakauka" inafidisha kuwa: Wakati wote vitakapokuwa vibichi (vipande vya kuti Ia mtende) vitakuwa vinamsabihi Mwenyezi Mungu. Hapa Mtume(s.a.w.w) ana thibitisha kuwa: Tasbihi za kuti zina mpunguzia adhabu maiti, kupunguziwa adhabu ni hatua ya kuingia mtu katika neema (pepo). Mpenzi msomaji! Tasbihi za kuti la mtende zitampa nafuu maiti, lakini Mwislamu akisoma Qur'an kwa ajili ya kumuombea maiti itakosa kumfikia?[35]

Kisha Sheikh Mkuu wa Tanzania alitoa fat'wa kwa kupitia Redio Tanzania kuwa: "Qur'an haikuchanwa" ingawa kwa maelezo yao - kama yalivyo kwenye kitabu: "Taarifa ya ujumbe wa Sheikh Mkuu" ukurasa 14 inasema: "Irshadul Muslimina kilichanwa kwa dharau" mwisho wa kunukuu. Kwa hiyo, Irshadul Muslimina iliyochanwa kwa dharau, ukikifunua kitabu hicho ukurasa wapili katika mlango wa kwanza utaiona Aya ya kumi na nane na ya kumi na tisa nusu yake, za Suratul Jathia. Bakwata inasema: Qur'an haikuchanwa lakini aya mbili katika Suratul Jathia zimechanwa kwa dharau! Sijui kwa Bakwata Qur'an inathubutu kwa vipi! Kwa kukamilika Sura ngapi au Aya ngapi hata isemwe ni QUR'AN? Kwa nini washutumiwe na kulaniwa watu wanaopendekeza kuwa: Sharia ya Mirathi na ya ndoa zifanyiwe marekebisho? Katika Mirathi wanachoomba iondolewe ni Aya isemayo "Lidh'dhakari Mithlu H'adh'dhil Unthayayni " 4:11

katika Ndoa wanaomba iondolewe Aya: "Mathna Wathulatha Warubaa " 4:4, sasa, unaweza kuhesabu silabi za Aya hizi, kisha uhesabu silabi za Aya zilizomo katika vitabu vilivyochanwa. Ndipo utamjua nani mwenye kosa wakufaa kushutumiwa na kulaaniwa! Kwakuwa sheria ni msumeno, hapa napenda kukumbusha baadhi ya matukio kama haya yalioyofanywa na wakubwa. Baada ya kufariki Mtume(s.a.w.w) sheria isemayo kuwa "Katika mafungu manane ya sadaka, fungu moja kati ya haya ni la wale wanaoingia Uislamu. Fungu hili lilifutwa! Na Aya inasomeka hivi: "Wal'muallafati Qulubuhum "[36]

Hukumu ya Aya hii imefutwa, kwa hiyo, maasi ya kunyanyasa sheria ya Mwenyeezi Mungu hayakuanza juzi katika Tarafa ya Nyakato, bali yameanza mbali huko baada ya kufariki tu Mtume(s.a.w.w) .

ISRAA NA MIIRAJI

Israa ni: Mwendo wa usiku, kama ilivyokuja katika Qur'an: "Utukufu ni wa yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku, kutoka Msikiti mtukufu (wa Makka) mpaka Msikiti wa mbali (Falastin) ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumuonyeshe baadhi ya ishaara zetu " 17:1.

Miiraji ni: Msafara ulioanzia katika Msikiti wa Falastin kwenda juu. Tukio la Israa limepokewa na waandishi wa Tarikh kwa njia tofauti, kuna wanaosema kuwa Israa ilitokea mwaka wa kumi na mbili baada ya kupewa Utume, Wengine wanasema ilikuwa mwaka wa kumi na moja, wengine mwaka wa kumi, wengine mwaka wa tano, wengine mwaka wa tatu na wengine mwaka wa pili.[37]

Kauli ya sawa katika mjadala huu ni: Israa imetokea katika mwaka wa tatu kwa sababu zifuatazo"

a . Mtume(s.a.w.w) alikuwa akipendelea sana kumbusu binti yake Mwana Fatima(a.s) mpaka Mwana Aisha (mkewe Mtume) likamuudhi sana hilo, akasema: "Ewe Mtume wa Mwenyeezi Mungu! Una nini? Kila mara ninakuona sana unambusu Mwana Fatima kama unayekula asali! Mtume(s.a.w.w) akamjibu: "Ni kweli, ewe Aisha! Mimi nilipopelekwa juu (Miiraji) Malaika Jibril(a.s) aliniingiza Peponi humo nilikula Tunda fulani, likabaki mgongoni, niliposhuka nilimwingillia Khadija (mkewe) mara akapata ujauzito wa Mwana Fatima kutokana na hilo tunda. Na yeye ndiye Tunda bora, kila ninapokumbuka Peponi, humbusu Fatima".[38]

Katika hadithi hii tunajifunza kuwa: Mwana Fatima(a.s) amezaliwa mwaka wa tano baada ya Biitha (kupewa Utume) kwa hiyo, Israa na Miiraji ilikuwa kabla ya kuzaliwa Mwana Fatima, kwa sababu Mwana Fatima ni Tunda la peponi alilokula Mtume siku aliyopelekwa Miiraji. Tunda lililobaki mgongoni kwake hata baada ya miaka miwili akazaliwa Fatima, Bibi bora kabisa katika mabibi wa Peponi - Hadithi. b. Mtume(s.a.w.w) alipopelekwa juu (Miiraji) Malaika walikuwa wakiuliza kila mahala Je! Muhammad amekwisha pewa Utume? Hili linaonyesha kuwa Tukio la Israa na Miiraji lilitokea katika miaka ya awali ya Utume, wala siyo baada ya miaka kumi na mbili. Kwa sababu ingekuwa hivyo bila shaka suala la Utume lingekwisha eleweka zamani pasingekuwepo haja ya kuliuliza. Israa na Miiraji ilitokea kabla ya kusilimu Abubakr bin Abi Quhafa, kwa sababu, Abubakr amesilimu baada ya miaka mitano ya biitha.[39]

Ikiwa Israa na Miiraji imetokea kabla ya kusilimu Abubakr, basi madai ya Laqabu isemwayo kuwa alipata Abubakri ya "SIDDIQ" yanatupwa: Kwa sababu ikiwa laqabu hiyo (kama inavyodaiwa) alupata baada ya kusadikisha msafara wa Mtume(s.a.w.w) aliopelekwa katika Israa na Miiraji. Litawezekanaje hilo, ilihali wakati wa tukio la Israa na Miiraji Abubakri alikuwa kafiri! Hapo tasdiq itapatikana?!

MTUME ALIKWENDA MWENYEWE AU NI NJOZI?

Tukio la Israa, wako baadhi ya Waislamu wanao ona kuwa Mtume(s.a.w.w) alioteshwa na wala hakwenda mwenyewe akiwa macho. Na mategemeo yao ni ile habari aliyoisimulia Mwana Aisha kuwa: "Siku hiyo hakukikosa kiwiliwili cha Mtume".[40]

MAJIBU YETU

a . Mwana Aisha wakati wa tukio hilo alikuwa hajaolewa na Mtume, bali yaelekea hata kuzaliwa alikuwa bado!!

b . Mwenyeezi Mungu anasema: "Utukufu ni wa yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku, kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa mbali " 17:1. lliposemwa: "Asraa Bia'bdihi " tamko la "A'BD" hutumiwa kwa roho na kiwiliwili pamoja. Kwa hiyo, Mtume(s.a.w.w) alikkwenda mwenyewe akiwa macho. c. Kama Israa ingelikuwa kwa njozi, basi kusingekuwako na upinzani mkubwa hivyo, na watu wasingeritarddi.[41]

d . Kama Israa ingelikuwa kwa njozi, basi Abu Talib na Bani Hashim wasingetoka kumtafuta, kwa sababu Bani Hashim walitoka kumtafuta siku hiyo.[42]

MUSA NA SALA TANO

Imepokewa katika riwaya kuwa: Sala tano zimefaradhiwa wakati Mtume(s.a.w.w) alipopelekwa katika msafara wa Miiraji huko juu Inasemwa kuwa, zilifaradhiwa sala hamsini kwa kila siku, na Mtume(s.a.w.w) alipokuwa akirudi na agizo hilo, alipofika mbingu ya sita akakutana na Nabii Musa(a.s) akamshauri Mtume Muhammad(s.a.w.w) arudi kwa Mola wake amuombe ampunguzie Sala hizo. Mtume alirudi kwa Mola wake na akapunguziwa Sala kumi, aliposhuka katika mbingu ya sita akakutana na Nabii Musa akiwa na sala arobaini. Nabii Musa akamrudisha kwa Mola wake apunguziwe Sala hizo, Mtume akafanya hivyo, Mwenyeezi Muungu akapunguza Sala kumi. Mtume alipofika kwa Nabii Musa, akamrudisha kwa Mola wake akaombe takhfif; Mtume alifanya hivyo, Mwenyeezi Mungu akapunguza sala kumi Mtume akashuka alipofika kwa Nabii Musa akiwa na sala ishirini, Nabii Musa akamtaka arudi kwa Mola wake akampunguzie, kwa sababu umma wake hawawezi hilo. Mtume(s.a.w.w) alifanya hivyo, Mwenyeezi Mungu akapunguza Sala kumi, Mtume akashuka akiwa na sala kumi, alipokutana na Nabii Musa akamrudisha kwa Mola wake ili apunguziwe, Mtume alifanya hivyo, Mwenyeezi Mungu akapunguza Sala tano, Mtume(s.a.w.w) aliposhuka kwa Nabii Musa(a.s) akiwa na sala tano, alipotaka kumrudisha kwa Mola wake, Mtume(s.a.w.w) alisema:- "Kwa hakika, nimerudi kwa Mola wangu mara tano, kuomba takhfif mpaka sasa naona aibu kubwa". Ndipo aliposhuka Mtume(s.a.w.w) akiwa sala tano, ambazo wanapaswa Waislamu kuzisali kwa kila siku.

UCHUNGUZI

Tunaamini kuwa: "Mwenyeezi Mungu haweki sheria yoyote isipokuwa ina maslahi ndani yake. Kwa mantiq hii, Mtume(s.a.w.w) asingehitaji kurudi mara zote hizo kwa ajili ya kupunguziwa. Kwa sababu kufanya hivyo ni kutaka sheria isiyo na maslahi, kama ambavyo sababu zilizompelekea Nabii Musa kutaka zipunguzwe Sala hamsini ni kushindwa kuzitekeleza sala hizo. Kama kwamba Nabii Musa anaamini kuwa Sheria hii (ya Sala hamsim) inakwenda kunyume na maslahi, na hilo ni muhali (haliwezekani) kwa Mwenyeezi Mungu. Aidha, vipi Mwenyeezi Mungu hakujua kuwa: Umma wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) hauwezi hilo, bali Musa yeye alijue hilo?? Au tuseme, ni takhfif kwa jambo lisilowezekana, vipi, Mwenyeezi Mungu anatwambia wakati wote: "Mwenyeezi Mungu huwatakieni yaliyo mepesi wala hawatakieni yaliyo mazito ". 2: 185. "Wala hakuweka juu yenu dhiki katika dini " 22:78.

Na vipi Nabii Ibrahim hakushitushwa na misafara ya nenda rudi ya Mtume Muhammad, asimuulize kuna nini! Maana kwa mujibu wa riwaya zinzosimulia tukio hili zinasema kuwa, Nabii Ibrahim(a.s) alikuwa katika mbingu ya saba na Nabii Musa(a.s) mbingu ya sita. Aidha, kwanini Mwenyeezi Mungu asimpe moja kwa moja Mtume wake Sala tano, kuliko usumbufu huu alioupata Mtume wa nenda rudi mpaka akaingiwa na aibu kubwa akashuka kwa shingo upande na sala zake tano!?

LENGO LA ISRAA NA MIRAJI

Tukitaka kujuwa shabaha na hekima na muujiza wa Israa na Miiraji, lazima kusoma nassi zake na vipengele vyake kwa undani na makini. Na hapa tutaonyesha mambo yafuatayo:

a . Israa na Miiraji ni muujiza mkubwa wa kudumu, na leo katika karne hii ya ishirini tukio hili linakubaliwa na elimu ya sayansi na Teknolojia. Mwanadamu hashangai tena leo kusikia kuwa mtu amekwenda umbali wa maili nyingi zaidi katika upeo wa juu.

b . Mwenyezi Mungu ametaja wazi lengo la msafara huo aliposema: "Linuriyahu Min Ayaatina ", yaani, "Ili tumuonyeshe baadhi ya Aya (ishara) zetu" 17:1. Kwahiyo, lengo ni kumuonyesha Mtume(s.a.w.w) baadhi ya ishara za utukufu wa Mwenyeezi Mungu. Na kwakupelekwa Mtume Israa na Miiraji, kumefunguwa moyo wake na akili yake zaidi kwa kupata taaluma kubwa katika ulimengu huu anaouongoza.

c . Mwanadamu (hasa Mwarabu) wakati huo aijishi katika ulimwengu finyu sana, na akili duni iliyofungwa katika tundu dogo. Kwa sabaha hii ikawa dharura kufunguliwa macho yake na moyo wake ili aujue ulimwengu anaoishi, ambao Mwenyeezi Mungu amemfanya awe khalifa wake.

KHADIJA ALIOLEWA NA YEYOTE KABLA YA MTUME?

Inasemekana kuwa: Mtume(s.a.w.w) hakuoa mke yeyote aliye bikira isipokuwa Mwana Aisha tu. Wanasema kuwa: "Mwana Khadija kabla ya kuolewa na Mtume(s.a.w.w) alikwisha olewa na waume wawili kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w.w) na amepata watoto wawili. Tutataja kidogo hapa baadhi ya hoja zinazosemwa juu ya Mwana Khadija kuhusu watoto aliopata kwa waume wengine kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w.w) ni kama ifuatavyo:

i. Wanasema: Shahidi wa kwanza katika Uislamu ni mtoto wa Mwana Khadija aitwae Harithi bin Abi Hala, alipata shahada pale Mtume(s.a.w.w) alipotangaza Uislamu hadharani.[43]

ii. Lakini, hoja hii inaangushwa na riwaya ya Qatada inayosema kuwa: Shahidi wa kwanza katika Uislamu ni Sumayya, mama yake Ammar bin Yasir.[44]

Imepokewa kuwa: Mwana Khadija(a.s) alikuwa na nduguye akiitwa Hala, aliolewa na mtu mmoja katika Koo ya Al'Makhzumi, akazaa mtoto wa kike jina lake Hala, Kisha aliachika akaolewa na mtu mmoja katika Koo ya At'Tamim aitwaye Abu Hindi, akamzalia mtoto jina lake Hind. Huyu Abu Hindi, alikuwa na mke mwingine ambaye alimzalia watoto wawili: Zaynab na Ruqayya. Hatimae Abu Hindi na mkewe wa pili walikufa,akabakia Bi Hala ndugu ya Mwana Khadija, pamoja na watoto wawili: Zaynab na Ruqayya. Yule mtoto wake wa kuzaa: Hind, alikwenda kwa jamaa za mumewe. Ndipo Mwana Khadija alipowakusanya wote akawa nao, Bi Hala na watoto wawili walioachwa na mama yao: Zaynab na Ruqayya. Mwana Khadija alipoolewa na Mtume(s.a.w.w) Bi Hala alifishwa, wakabaki Zaynab na Ruqayya wakilelewa na Mtume(s.a.w.w) . Katika mila za Kiarabu, walikuwa wakiamini kuwa mtoto wa kufikia ni mtoto wako halisi, kwa hiyo, watoto hawa wakapewa ubinti wa Mtume(s.a.w.w) (Zaynab binti Muhammad na Ruqayya binti Muhammad).[45]

MAJIBU YETU

a. Katika kitabu "Asha'shaafy" na "At Talkhis" inasema Mtume(s.a.w.w) amemuoa Mwana Khadija akiwa bikira.

b. b. Amesema Abulqasim Alkufy: Mtume(s.a.w.w) alipomuoa Mwana Khadija(a.s) wanawake wa kikuraishi walimkasirikia sana Mwana Khadija wakisema: Wamekuposa mabwana wa kikuraishi wenye heshima, umekataa kuolewa na yeyote kati yao, umekubali kuolewa na Muhammad, yatima wa Abu Talib Lofa hana mali![46]

POTE LENYE KUOKOKA

Amesema Mtukufu Mtume(s.a.w.w) "Watafarakana umma wangu makundi sabini na tatu, kundi moja tu kati ya hayo litaokoka, na yaliyobaki yatatiwa motoni . Ali akauliza: "Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu! Kundi gani litakalookoka? Mtume(s.a.w.w) akajibu: "Wewe na watu wako".[47]

Mfarakano kwa mara ya kwanza ulitokea kwa Waislamu pale tu alipofariki Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Mtume(s.a.w.w) kabla ya kufariki dunia, aliweka sera kamili ya uongozi katika Uislamu. Iliposhuka Aya: "Hakika wale walioamini na wakatenda mema, basi hao ndio wema kushinda viumbe vyote " 98:7.

Mtume(s.a.w.w) akamwambia Ali: "Wewe Ali na kundi (pote) lako ".[48]

Mtume(s.a.w.w) amesema: "Ali yu pamoja na Qur'an, na Qur'an ipamoja na Mi, hawataachana mpaka wanifikie katika Haudh ".[49]

Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mimi ninakuachieni vizito viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, Qur'an na Ahlul Bayt wangu, viwili hivi havitaachana mpaka vitakaponifikia katika Haudh".[50]

Imam Ali(a.s) mmoja katika Ahlul Bayt wa Mtume(s.a.w.w) tazama pale iliposhuka Ayatut Tat'hir: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana " 33:33.

Na mke wa Mtume(s.a.w.w) (Ummu Salama) alipotaka kuingia katika nguo hiyo Mtume akamzuia![51]

AHLUL BAYT WALIO PAMOJA NA QUR'AN

1. Imam Ali bin Abi Talib(a.s) amezaliwa ndani ya Al' Kaaba siku ya Ijumaa, tarehe kumi na tatu Rajab mwaka wa thalathini (mwaka wa ndovu). Wamekhitilafiana waandishi wa tarikh kujuwa tarehe aliyopigwa dharba Imam Ali, baadhi ya kauli hizo zasema:

a. Alipigwa dharba tarehe 17 usiku wa kuamkia Ijumaa mwezi wa Ramadhan, akafishwa usiku wa kuamkia Jumapili tarehe 19 Ramadhan.

b. Alipigiwa dharba tarehe 19 usiku, akafishwa tarehe 21 Ramadhan mwaka 40.

c. Alipigwa dharba kuamkia tarehe 21, akafishwa tarehe 23 Ramadhani.

d. Alipigwa dharba kuamkia tarehe 23, akafishwa tarehe 25 Ramadhan.[52]

Riwaya nyingine zinasema kuwa:

a. Alipigwa dharba asubuhi ya tarehe 17 Ramadhan.

b. Alipigwa dharba asubuhi ya tarehe 19 Ramadhan, mwaka 40 Hijra.[53]

Abdur Rahman bin Muljam alikutana na msichana mmoja katika khawariji aitwaye Qatwam, ambaye baba yake na kaka yake waliuliwa na Imam Ali katika vita vya Nahrwan. Msichana huyo alikuwa mzuri kupita kiasi, Abdur Rahman alipomtaka Qatwam, alimjibu: "Kama utaweza kunipoza moyo wangu utanipata" Akamuuliza: "Ni lipi litakalo kupoza moyo wako?" Akajibu: "Unipe dirham alfu tatu, mtumishi mmoja, mjakazi, mwimbaji, na umuue Ali bin Abi Talib. Abdur Rahman bin Muljam akasema: "Hayo mengine yote ni mepesi sana, lakini hili la kumuua Ali, ni dalili ya kuwa umenikataa. Kwa sababu haiwezekani kumuua Ali nami nikasalimika, tukaweza kuoana". Ilipofika siku hiyo, kwa kauli zilivyo khitilafiana, kama ulivyoona hapo juu, Abdur Rahman bin Muljam akatimiza lengo lake. Imam Ali amezikwa Kufa katika nchi ya Iraq.[54]

2. Imam Hasan bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina, tarehe kumi na tano Ramadhan mwaka wa tatu Hijra'. Mu'awiya alipotaka kumtawalisha mwanawe Yazid, alitumia mbinu, akamjenga Juuda bint Al'ash'a'th bin Qays. Huyu alikuwa mke wa Imam Hasan(a.s) . Muawiya akampa sumu ili amtilie Imam Hasan. Na endapo atamuua, basi atamfanyia mambo mawili, la kwanza atampa dirham laki moja na la pili atamuoza mwanawe, Yazidi. Imam Hasan akapewa sumu hiyo na baada ya hapo alibaki siku arobainni akafariki dunia! Amekufa mfungo tano mwaka 50 Hijra.[55]

Wengine wanasema: Amekufa mfungo sita mwaka 49 Hijra.[56]

Baada ya kufa Imam Hasan Juu'da alipeleka ujumbe kwa Yazidi wa kutaka kuolewa naye kama walivyoahidiana na baba yake Mu'awiya, Yazidi aliruka na kusema: "Hukuweza kumhurumia Hasan utanihurumia mimi!? Kama umeweza kumuua yeye mimi utanimaliza mara moja, Yazid akakataa kumuoa.

3. Imam Husein bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe tatu Shaaban mwaka wa nne Hijra. Imam Husein(a.s) ameuliwa mwezi kumi Muharram siku ya Ijumaa (wengine wanasema Jumamosi) mwaka wa sitini na moja Hijra. Imepokewa kutoka kwa Anas kwamba Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mwanangu Husein atauliwa katika nchi ya Iraq, yeyote miongoni mwenu atakaekuwapo, basi asimame kumnusuru.[57]

Imepokewa kwa mama Ummu Salama (mkewe Mtume) anasema: "Nilimuona Mtume(s.a.w.w) akikipangusa kichwa cha Imam Husein na huku akilia. Nikamuuliza: "Unalilia nini!" Akasema: "Hivi sasa amenijulisha Malaika Jibril kuwa: Mtoto wangu huyu atauliwa katika ardhi litwayo "KARBALA" kisha akanipa gao la udongo na akaniambia: 'Huu udongo ndipo mahala atakapouliwa, utunze, siku yoyote utakapogeuka kuwa mwekundu basi jua yakwamba amekwisha uliwa".[58]

Kama ambavyo, siku aliyouliwa Imam Husein mbingu zilimlilia, na alama ya kuonyesha kuwa zinamlilia ni wekundu unao onekana kwenye mawingu. Kwa hiyo, Imam Husein(a.s) analiliwa na mbingu mpaka leo hii.[59]

4. Imam Ali bin Husein(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe tano Shaaban mwaka thalathini na nane Hijra, kabla ya kufishwa babu yake (Imam Ali) kwa miaka miwili. Imam Ali bin Husein amefariki mwaka wa tisini na nne Hijra, akazikwa katikamji wa Madina katika kiwanja kitakatifu cha Baqii.

5. Imam Muhammad bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe tatu mfungo tano (wengine wanasema tarehe moja Rajab) mwaka hamsini na saba Hijra, kabla ya kuuliwa babu yake Imam Husein kwa miaka mitatu. Wamekhitilafiana mwaka aliofia kama hivi:

a. Amefishwa mwaka 114 Hijra.

b. Amefishwa mwaka 117 Hijra.

c. Amefishwa mwaka 118 Hijra.

6. Imam Ja'far bin Muhammad(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe 16 mfungo sita (wengine wanasema tarehe moja Rajab) mwaka 80 Hijra. Imam amefishwa katika mji wa Madina mwaka 149 Hijra, amezikwa pamoja na baba yake na babu yake katika viwanja vitakatifu vya Baqii.[60]

7. Imam Musa bin Ja'far(a.s) amezaliwa katika kijiji cha "AB'WAA" kilicho kati ya Makka na Madina, mahala ambapo kaburi la Mwana Amina bint Wahab mama yake Mtume(s.a.w.w) lilipo. Amezaliwa mwaka 128 Hijra (wengine wanasema mwaka 129). Imam Musa amefariki mwaka 188 Hijra baada ya kutiwa jela na Haruna Rashid kwa miaka kumi moja.[61]

8. Imam Ali bin Musa(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina. Wamekhitilafiana kujuwa tarehe aliyozaliwa kama hivi:

a. Amezaliwa mfungo pili mwaka 148.

b. Amezaliwa mfungo tatu mwaka 148.

c. Amezaliwa mfungo sita mwaka 148.

d. Amezaliwa mwaka 153. Kifo cha Imam Ali bin Musa kimetokana na maji ya matunda yenye sumu aliyopewa na Maamun. Baada ya kunywa Imam alibaki siku mbili kisha akafariki dunia, mwaka 203 wengine wanasema mwaka 202 na wengine wanasema mwaka 206.[62]

9. Imam Muhammad bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina, tarehe kumi na tisa Ramadhan mwaka 195 Hijra. Amefariki Imam Muhammad mwaka 220 wengine wanasema mwaka 225[63]

10. Imam Ali bin Muhammad(a.s) amezaliwa Rajab mwaka 214 Hijra umbali wa maili tatu hivi kutoka katika mji wa Madina. Imam Ali bin Muhammad ameuliwa kwa sumu mwaka 254 Hijra.

11. Imam Hasan bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina mwaka 231 Hijra. Imam Hasan bin Ali amefariki siku ya Ijumaa tarehe nane mfungo sita mwaka 260 na akazikwa mahala alipozikwa Baba yake.

12. Imam Muhammad bin Hasan(a.s) amezaliwa tarehe kumi na tano Shaaban mwaka 255 Hijra, wengine wanasema tarehe ishirini na tatu Ramadhan mwaka 258 Hijra. Imam Muhammad bin Hasan yuko hai mpaka sasa, alipofiwa Baba yake alikuwa na umri wa miaka mitano. Hawa ni Maimam kumi na wawili katika AhIul Bayt(a.s) walio pamoja na Qur'an. Amesema Mtume(s.a.w.w) "Dini itaendelea kuwa imara mpaka isimame kiama, na mtasimamiwa na viongozi kumi na wawili, wote katika Maquraishi ".[64]

Na ameonya Mtume(s.a.w.w) kwa yeyote ambaye hatawatambua Maimam hawa: "Yeyote atakaekufa na asimjue Imam wa zama zake, atakufa kifo cha kipagani ".[65]

SERA ZA UTAWALA BAADA YA MTUME

Ukisoma Terikh, na kisha ukafuatilia sera za utawala wa makhalifa watatu, utajua wazi kwamba mabwana hao walizuia kuandikwa Hadithi za Mtume Muhammad(s.a.w.w) bali walikataza hata kuzizungumza mbele za watu. Kwa sababu walijua wazi kuwa sera za utawala wao haziendi sambamba na uongozi wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Abubakr amekataza kuzungumza chochote juu ya Mtume(s.a.w.w) na amesema:Yeyote atakaewauliza mseme: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an, basi, halalisheni halali yake na haramisheni haramu yake ". [66]

Kauli hii ya Abubakr imekuja baada ya muda mfupi wa tukio la karatasi, Umar bnul Khattab alipomjibu Mtume kuwa: "Mtume anaweweseka, ipo Qur'an inatutosha", Abubakr anasema: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an"..... Qur'an iliyo kati yetu na Abubakr inasema kuhusu wanaozuia zaka: "Na miongoni mwao wako walio mwahidi Mwenyeezi Mungu, akitupa katika fadhili zake bila shaka tutatoa sadaka na lazima tutakuwa miongoni mwa watendao mema. Lakini alipowapa katika fadhili zake, wa kayafanyia ubakhili na wakageuka, nao ndio wakengeukao. Kwa hiyo akawalipa unafiki mioyoni mwao mpaka siku ya kukutana naye, kwa sababu ya kumkhalifu Mwenyezi Mungu ahadi waliyo mwahidi, na kwa sababu walikuwa wanasema uongo". 9:75-77.

Aya hizi zimeshuka kwa ajili ya Thaalaba aliyezuia zaka wakati wa Mtume(s.a.w.w) . Lakini pamoja na yote hayo Mtume(s.a.w.w) hakumpiga wala hakumnyang'anya mali yake, ingawa Mtume yote haya alikuwa na uwezo nayo. Ambapo suala la Malik bin Nawyira na wenzake waliodaiwa kuwa walizuia Zaka katika utawala wa Abubakr. Huo ni msimamo waliouonyesha dhidi ya utawala wa Abubakr aliyepora madaraka yasiyo kuwa yake. Kwa hiyo, kitendo cha kuzuia zaka kutoupa utawala wa Abubakr ni tafsiri halisi ya kupinga utawala huo na wala si kupinga hukumu ya faradhi ya zaka. Sasa, Abubakr yuko wapi na aya hizi aliyedai kuwa ndiyo sera yake?? Mbona amewaua watu waliozuia zaka kwa kigezo gani? Sera ya Abubakr inasema: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an".

Qur'an inasema: "Wanaume wana sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio wakaribia, Na wanawake wanayo sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio wakaribia " 4:7.

Mwana Fatima bint Muhammad(s.a.w.w) alipokwenda kwa Abubakr kutaka mirathi iliyoachwa na baba yake, Abubakr akakataa kumpa akidai kuwa amemsikia Mtume akisema: "Sisi Mitume haturithiwi". Hapa Qur'an hana haja nayo, ameshika lile asilokuwa na haja nalo tokea awali, hata hivyo, Abubakr kweli maneno ya Mtume anayakubali? MwanaAisha (Mwanawe) anasimulia tukio hili: Baba yangu alizikusanya Hadithi za Mtume(s.a.w.w) ambazo zilikuwa mia tano, akakesha kucha akizigeuzageuza......kulipokucha akasema: Mwanangu! Niletee Hadithi ulizonazo, ni kampa, akazichoma moto![67]

Je! Ni kweli Abubakr anaitegemea Qur'an tu peke yake? Mwenyeezi Mungu anasema: "Sadaka ni kwa mafakiri tu na masikini na wanaozitumikia na waungiwao.......mioyo yao.....9:60. Iliposemwa: "Na waungiwao mioyo yao" ni wale waislamu wapya ambao ndio kwanza wanasilimu. Abubakr alipotawala, hukumu ya kifungu cha Aya hii akaifuta![68]

SHARTI YA KUCHAPA

Sharti ya kuchapa au kusambaza ni kutaja rejeo hili. haki zote zimehifadhiwa na Taasisi ya Al-Hasanain Taasisi ya Imamu Husein(a.s)

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini(a.s) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini.

MWISHO WA KITABU

YALIYOMO

MASOMO YA KI-ISLAMU 1

MUONGOZO KWA WASOMAJI 1

KIMEANDIKWA NA: OMAR JUMAA MAYUNGA 1

UTANGULIZI 1

MASOMO YA KI-ISLAMU 2

MUONGOZO KWA WASOMAJI 2

MWANZO WA WAHY 2

MJADALA WA RIWAYA ZA WAHY 4

MUHARRAM SI MWANZO WA MWAKA 5

KUONEKANA KWA MWENYEEZI MUNGU 6

MAJIBU YETU 6

HADITHI ZISEMAZO KUWA ATAONEKANA 7

MAJIBU YETU 8

QUR'AN IMEUMBWA 8

TAQIYYA 8

TAHRIFUL QUR'AN 10

MASOMO YA KI-ISLAMU 12

MUONGOZO KWA WASOMAJI 12

WANAOTHIBITISHA KUWA IPO 12

WALIOSEMA KUWA HAIPO 12

KUSOMA QUR'AN KWA AJILI YA MAITI 13

MAJIBU YETU 13

ISRAA NA MIIRAJI 15

MTUME ALIKWENDA MWENYEWE AU NI NJOZI? 16

MAJIBU YETU 16

MUSA NA SALA TANO 17

UCHUNGUZI 17

LENGO LA ISRAA NA MIRAJI 18

KHADIJA ALIOLEWA NA YEYOTE KABLA YA MTUME? 18

MAJIBU YETU 19

POTE LENYE KUOKOKA 19

AHLUL BAYT WALIO PAMOJA NA QUR'AN 20

SERA ZA UTAWALA BAADA YA MTUME 23

SHARTI YA KUCHAPA 24

MWISHO WA KITABU 24

YALIYOMO 25


[1] . Taz: Sahihi Bukhari Juz.I uk: 5-6. Sahihi Muslim Juz. I, uk: 97 Almuswannaf Juz. 5, uk: 322. Tarikhut Tabari Juz. 2, uk: 47.

[2] . Taz; Albidayatu Wannihaya Juz. 3, Uk: 9 Assiratun Nabawiyya Juz. 1 uk: 83. Assiratul Halabiyya Juz. 1, uk: 250. Siiratu Mughlataya uk, 15.

[3] . Taz: Albidayatu Wannihaya Juz.3 uk, 12. Siiratu Ibn Hisham Juz. 1 uk, 238 Assiratul Halabiyya Juz. 1, Uk. 239.

[4] . Taz: Assiratul Halabiyya Juz. 1, Uk. 252.

[5] . Taz: Tarikhul Yaa'quby Juz. 2, Uk. 23.

[6] . Taz: Tarikhul Khamisi Juz. 1, Uk. 284. Assiratul Halabiyya Juz. 1, Uk. 243. Assiratun Nabawiyya Juz. 1. Uk. 83.

[7] . Taz: Almuswannaf Juz. 5, Uk. 323.

[8] . Taz: Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 13.

[9] . Taz: Qamusir Rijal Juz. 6, Uk. 300 Algharat Juz. 2, Uk. 558-560.

[10] . Taz: Mustadrakul Hakim Juz. 3, Uk. 121. Musnad Ahmad Juz. 5, Uk. 30. Alfusulul Muhimma Uk. 111. Tarikh Ibn Asakir Juz. 2, Uk. 184. Manaqibu Ali Uk. 394.

[11] . Taz: Sahihi Muslim, katika kitabul Iman. Sahihat Tirmidhi Juz. 2, Uk. 301. Musnad Ahmad Juz. 1, Uk. 84. Tarikh Bughdad Juz. 2, Uk. 255. Hilyatul Awliyaa Juz. 4, Uk. 185. Kanzul Ummal Juz. 6, Uk. 394. Mustadrakul Hakim Juz. 3, uk 129. Al Istiab Juz. 2, Uk. 214. Addurrul Manthur Aya ya 25 sura 47.

[12] . Taz: Magatilut Talibina Uk. 27. Aljamal, Uk. 83-84.

[13] . Taz: Sahihi Bukhari Juz. 1, Uk. 152. Sahihi Muslim Jz. 7, Uk. 100. Musnad Ahmad Juz. 2, Uk. 315. Almuswannaf Juz. 11, Uk. 274. Sunannun Nasai Juz. 4, Uk. 118. Albidayatu Wannihaya Juz. 1, Uk. 317. Tarikhut Tabari Juz. 1, Uk. 305.

[14] . Taz: Alkharaj Uk. 81. Jamharatu Rasailil ar'b Juz. 1, Uk. 82.

[15] . Taz: Albidayatu Wannihaya Juz. 3, Uk. 207.

[16] . Taz: AI'i'lanu Uk. 78.

[17] . Taz: U'nwanul Maa'rif Uk. 11.

[18] . Taz: Sahihi Bukhari J. 4 Uk. 92 Sahihi Muslim J. 1 Uk. 86 Tafsirul Khazin J. 7 Uk. 137.

[19] . Taz: At'targhib Wat'tarhib J. 4 Uk. 551.

[20] . Taz: Tafsirul Qurtubi, J. 4, Uk. 57.

[21] . Taz: Tafsir ibn Kathir J.1, Uk. 365 Safwatut Tafasir J.1, Uk.196.

[22] . Taz: Tafsir Ibn Kathir J. 2 Uk. 609 Tafsirul Qurtubi J. 10 Uk. 180 Tafsirul Khaazin J. 4 Uk. 117 Tafsirul Maraghi J. 14 Uk. 146.

[23] . Taz: Tafsirul Qurtubi J. 9 Uk. 76.

[24] . Taz: Tafsir Qurtubi J. 14 Uk. 290.

[25] . Taz: Manahilul I'r fani Juz. 1 Uk. 253 3.

[26] . Taz: Tafsirul Alus Juz. 1 Uk: 39 Tafsir lbn Kathir Juz. 1 Uk: 17 Tafsirul Khazin Juz. 1 Uk: 18 Tafsirush Shawkan Juz. 1 Uk; 7.

[27] . Taz: Sahihi Bukhari J. 8 Uk. 26 Sahihi Muslim Juz. 5 Uk. 116.

[28] . Taz: Al' It'qan Juz. 1 Uk. 101.

[29] . Taz: Tafsirul Qurtubi J. 14 Uk. 113 Al' It'qan Juz.2 Uk.32.

[30] . Taz: Al' It'qan Juz. 2 Uk. 33.

[31] . Taz: Tafsirul Qurtubi Juz. 14 Uk. 113.

[32] . Taz: Al'I'tigad Juz. 1 Uk. 16. Tafsir Aalair Rahman Juz. 1 Uk. 25. Albayan fit'tafsiril Qur'an Uk. 213. Tafsirul Qur'an, assayid shubbar Uk. 17.

[33] . Taz: Tafsir ibn Kathir Juz. 4 Uk. 276.

[34] . Tarehe 18-8-1984 katika mkoa wa Mwanza Tarafa ya Nyakato Kijiji cha Buzuruga, kulitokea tatizo kubwa lililosababishwa najeshi la jadi Ia sungusungu. Jeshi la jadi la sungusungu kwa makusudi kabisa, ililiivamia nyumba ya MwisIamu, likaingia ndani na kuchanachana vitabu vitano vitakatifu vya Kiislamu. Yasin Ndogo (B) Majmuul Mubarak (C) Irshadul Muslimina (D) Hadithi Za Mtume (E) Ahlul Badr.

[35] . Taz: Tafsirul Qurtubi J. 10 Uk. 267.

[36] . Taz: Tafasirut Tabari Juz. 10, Uk. 113.

[37] . Taz: Albidayatu Wannihaya Juz. 3, Uk. 108 Tarikhul Khamisi Juz. 1, Uk. 307 Assahihu Minsiiratin Nabi Juz. 1, Uk. 269.

[38] . Taz: Tarikh Bughdad Juz. 5 Uk. 87. Mizanul'itidal Juz. 2 Uk. 297. Mustadrakul Hakim Juz. 3 Uk. 156. Majmauz Zawaid Juz. 9 Uk. 202. Kanzul Ummal Juz. 14 Uk. 97. Dhakhaairul U'qbaa Uk. 36.

[39] . Taz: Assahihu Minsiiratin Nabii Juz. 1, Uk. 274 Usudul Ghaba Juz. 4, Uk. 18.

[40] . Taz: Tarikhul Khamisi Juz. 1 Uk. 308. Al' mawahibul laduniyya Juz. 2 Uk.2.

[41] . Taz: Tafsir ibn Kathir Juz. 3 Uk. 24. Tarikhul Khamisi Juz. 3 Uk. 308. Almuswannaf Juz. 5, Uk. 327.

[42] . Taz: Assahihu Minsiiratin Nabii Juz. 1 Uk. 276.

[43] . Taz: Al' Isaba Juz. 1, Uk. 293 Al'Awaail Juz. 1, Uk. 311-312.

[44] . Taz: Al' Isaba J. 4 Uk. 335.

[45] . Taz: As' Sahihu Minsiiratin Nabi Juz. I, Uk. 123.

[46] . Taz: Al' Istighatha Juz. 1, Uk. 70.

[47] . Taz: Ithbatul Hudat Juz. 2, Uk. 260.

[48] . Taz: Tafsirut Tabari Juz. 30 Uk. 171.

[49] . Taz: Faidhul Qadir Juz. 4 Uk. 358. Musnad Ahmad Juz. 5 Uk. 31. Alfat'hul Kabir Juz. 2, Uk.21. Tarikhul Khulafai Uk. 174. Majmauz Zawaid Juz. 9, Uk. 134. Kifayatut Talibi Uk. 399. Asnal matalibi Uk 136.

[50] . Taz: Tafsir ibn Kathir J. 4 Uk. 122 Tafsir ul Kazin J. 1 Uk. 4 Tarikhu Bughdad J. 8 Uk. 442 Sahihi Muslim Juz. 4 Uk. 1873. Jamiul Usul Juz. 1, Uk. 187. Albidayatu Wannihaya Juz. 7 Uk. 362. Majmauz Zawaid Juz. 9 Uk. 163. Musnad Ahmad Juz. 2 Uk. 17-26. Al Mustadrak Juz. 4 Uk. 109.

[51] . Taz: Sahihi Muslim Juz. 4 Uk. 127. Sahihi Tirmidhi Juz. 4 Uk. 304. Alkhasais Uk. 4. Tarikh Bughdad J. 9 Uk. 126 Al' Isaba J. 1 Uk. 27 Usudul Ghaba J. 5 Uk. 521 Al Mustadrak Juz. 2 Uk. 416. Tafsirut Tabari Juz. 22 Uk. 5-7. Tafsirul Khazin Juz. 5 Uk. 259. Addurrul Manthur Juz. 5 Uk. 198.

[52] . Taz: Kashful Ghumma Juz. 2, Uk. 63.

[53] . Taz: Suratul Aimmatil Ithna Ashar Juz. 1, Uk 452.

[54] . Taz: Kashful Ghumma Juz. 2, Uk. 62. Tabaqatul Kubra, Juz. 6, Uk. 12. Tadhkiratul Khawas Uk. 179 2.

[55] . Taz: Kashful Ghumma Juz. 2 Uk. 207. Tadhkiratul Khawas Uk. 211.

[56] . Taz: Tadhkiratul Khawas Uk. 211.

[57] . Taz: Dhakhairul Uq'baa Uk. 146.

[58] . Taz: Dhakhairul' U'qbaa Uk. 147 Albidayatu Juz. 3 Uk. 174. Albidayatu Wannihaya Juz. 6 Uk. 230. Tarikhul Islam Juz. 3 Uk. 10. Almustadrak Juz. 3 Uk. 176.

[59] . Taz: Tafsirul Qurtubi Juz. 16 Uk. 14.

[60] . Taz: Siiratul' Aimmatil Ithna Ashar Juz. 2, Uk. 225.

[61] . Taz: Tadhkiratul Khawas Uk. 350.

[62] . Taz: Siiratul' Aimmatil' Ithna Ashar Juz. 2, Uk. 341.

[63] . Taz: Siiratul' Aimmatil' Ithna Ashar Juz. 2, Uk. 448.

[64] . Taz: Sahihi Muslim Juz. 6 Uk. 3-4 Sahihi Bukhari Juz. 4, Uk. 165. Sunan Abi Daud Juz. 3, Uk. 106 Musnad Ahmad Juz. 5, Uk. 86-90. Kanzul Ummal Juz. 13 Uk. 26-27. Hilyatul Awliyaa Juz. 4, Uk. 333.

[65] . Taz: Sharhul Maqasid Juz. 2, Uk. 275. Al'mirqat Juz. 2 Uk. 509. Al'ghaadir Juz. 10, Uk. 260.

[66] . Taz: Tadh'kiratul hufaadh Juz. 1, Uk. 3.

[67] . Taz: Kanzul Ummal. Juz. 5, Uk. 237 Tadh'kiratul hufaadh Juz. 1, uk, 5.

[68] . Taz: Tafsirut Tabari Juz. 10, Uk. 113.

1

MASOMO YA KI-ISLAMU

MUONGOZO KWA WASOMAJI

WANAOTHIBITISHA KUWA IPO

A . Amepokea Ibnu Abbas kwamba: "Umar bnul Khattab, siku moja alipokuwa juu ya Mimbar alisema: "Sisi tulikuwa tukisoma katika Qur'an: AN LAA TARGHABU A'N ABAAIKUM FAINNAHU KFRUN BIKUM AN TARGHABU A'N ABAAIKUM"...[27]

B . Umar bnul Khattab alileta Ayatur rajmi ili itiwe katika msahafu, lakini haikuandikwa, kwa sababu Umar alikuwa peke yake hakuwa na shahidi.[28]

Aya yenyewe aliyoileta Umar inasomeka hivi: ASH'SHAYKHU WASH'SHAYKHATU IDHA ZANAYAA FARTUMUHUMAA ALBATTATA NAKAALAN MINALLAHI WALLAHU A'ZIZUN HAKIMUN".[29]

C . Inasimuliwa kuwa: katika mbao za Mwana Aisha ilikuwako Qur'an ikisomeka hivi: "INNA LLAHA WAMALAIKA TAHU YUSWALLUNA A'LAN NABIYY YA AYYUHA LLADHINA AMANU SWALLU A'LAYHI WASALLIMU TASLIIMA WA A'LALLADHI NA YUSWALLUNA ASSUFUFAL AWWALA" Mwana Aisha (mkewe Mtume) alikuwa nayo Qur'an hiyo kabla Uthman bin Affan hajabadilisha misahafu![30]

D . Anasema Mwana Aisha (mkewe Mtume) katika zama za Mtume(s.a.w.w) Suratul Ahzabi ilikuwa inafikia Aya mia mbili, lakini, ulipoandikwa msahafu Aya zikawa hivi kama zilivyo sasa ambazo ni sabini na tatu tu!! Aya mia moja ishirini na saba zimepotea![31]

WALIOSEMA KUWA HAIPO

Mizani ya kupima riwaya zilizo tajwa hapo juu kuonyesha kuwa kuna baadhi ya amma sura au aya zilizopotea, riwaya hizo na za mfano wa kama hizo ni batili, Mwenyeezi Mungu anasema: (Qur'an) "Haitaifikia batili mbele yake wala nyuma yake " 41:42

"Hakika sisi tumeiteremsha Qur'an, na hakika sisi ndio wenye kuilinda " 15:9. Hii ndio itikadi ya Shia Ithna Ashar.[32]

KUSOMA QUR'AN KWA AJILI YA MAITI

Wako baadhi ya Waislamu wanapinga kumsomea Qur'an maiti, wakisema kwamba kufanya hivyo ni bid'a na bid'a mahala pake ni motoni. Katika kupinga jambo hili wanatoa hoja zao kama ifuatavyo:

A . Imethibiti kuwa: Mtume(s.a.w.w) hakumsomea Qur'an maiti yeyote katika uhai wake, kama jambo hilo ni jema Mtume asingeliacha kufanya kheri hiyo. Kwa hiyo, yeyote leo anae soma Qur'an kwa ajili ya mait, akaamini kuwa itamnufaisha, bila shaka mtu huyo anadai kuwa Mtume amefanya khiyana katika umma huu. Na hilo ni kosa kubwa kuamini kuwa Mtume hakufikisha baadhi ya mambo katika umma wake.

B . Mwenyeezi Mungu anasema: "Na ya kwamba mtu hatapata isipokuwa aliyoyafanyia juhudi " 53:39.

Na kwa Aya hii Imam Shafi amesema kuwa: Kisomo (anachosomewa maiti) thawabu za kisomo hicho hazifiki kwa maiti. Kwa sababu hilo haliko katika matendo yake, na kwa sababu hii, Mtume hakuwawekea umma wake, wala hakuhimiza (wafanye) kwa mtu yeyote. Wala hakupendekeza, wala sahaba yeyote hakuna aliyepokea (jambo hili) [33]

C . Amesema Mtume(s.a.w.w) : "Anapokufa mwanadamu, matendo yake humalizika yote isipokuwa mambo matatu: sadaka ya kudumu, au elimu yenye kunufaisha, au mtoto mwema atakaemuombea baada yake ".

Kwa hiyo, wasomaji wa khitima hupoteza bure muda wao, kwa kufanya jambo haliko katika Uislamu.

MAJIBU YETU

Kabla ya kuingia katika majadiliano hayo ni vyema kuzingatia jambo mmoja, nalo ni "NINI QUR'AN"? Taarif ya Qur'an ni: "Maneno ya Mwenyeezi Mungu aliyoyateremsha kwa Mtume wake Muhammad(s.a.w.w) hali yakuwa ni muujiza wake" sasa, Ikisemwa kuwa: Mtume(s.a.w.w) hakuwasomea Qur'an maiti wake, huwa inakusudiwa Qur'an gani?? Kwa sababu, katika salatiil maiti mna Suratul Fatiha, na Mtume(s.a.w.w) aliwasalia mauti wake. Isipokuwa, ikithibitishwa kwa dalili kuwa: Suratul Fatiha si Qur'an[34] . Kuhusu Aya iambiwayo kuwa inazuia thawabu za Qur'an kumfikia maiti 53:39.

Tuangalie matni yake: "WA AN LAYSA LIL'INSANI ILLA MASAA", yaani, "Na yakwamba mtu hatapata isipokuwa aliyo yafanyia juhudi." Hivi ndivyo ananyosema Mwenyeezi Mungu na wala hasemi: "LA YANTAFIU'UL INSANU ILLA MASAA", yaani, "Hanufaiki mwanadamu isipokuwa kwa yale aliyoyafanyia juhudi". Hapa pana tofauti kubwa kati ya ibara ya kwanza na hii ya pili. Ibara ya kwanza inafidisha kuwa: "Mwanadamu atalipwa thawabu kwa mujibu wa matendo yake". Na ibara ya pili inafidisha kuwa: "Mwanadamu hanufaiki kwa chochote isipokuwa kwa matendo aliyoyatenda mwenyewe." Kwa ibara hizi ni sawa na kusema kuwa: "Athumani ana kibanda kidogo cha makuti, na humo ndimo anamoishi. Kwa hiyo, Athumani hana nyumba nyingine yoyote atakayoishi isipokuwa katika kipanda hicho. Lakini hali hii haizuii yeyote mkarimu kumjengea Athumani nyumba kubwa na bora. Mkarimu kama atajenga nyumba iliyo bora na kubwa, kisha akampa Athumani, haiwezi kusemwa: Athumani hawezi kukaa katika nyumba hiyo eti kwa sababu hakuijenga yeye. Amma Hadithi iamiwayo kuwa iazuia thawabu ya Qur'an kumfikia maiti isemayo: "IDHA MATA IBNU ADAMA IN'QATAA A'MALUHU ILLA MIN THALATHA..." yaani, "Anapokufa Mwanadamu matendo yake yote hukatika isipokuwa mambo matatu...." wala Hadithi haisemi: "IDHA MATA IBNU ADAMA IN'QATAA INTIFAU'HU" yaani, "Anapo kufa Mwanadamu humalizika kunufaika kwake". Ibara ya kwanza inafidisha kuwa: "Kinachomalizika ni matendo yake". Na ibara ya pili inafidisha kuwa: "Kinachomalizika ni kunufaika". Kwa mizani ya somo hili, natija inaonyesha kuwa Qur'an ikisomwa kwa ajili ya maiti, lazima thawabu ya kisomo hicho zitamfikia maiti, na hapa tutaonyesha hali tatu zilizo hai:

a . Mtume(s.a.w.w) amesema: "Man Mata Wa A'layhi Siyam Sama A'nhu Waliyyuhu ". yaani,atakae kufa na juu yake kuna saumu atafunga kwa niaba yake walii wake ". Hadithi hii imekubaliwa na Waislamu wote na hata Imam Shafi naye ameikubali. Je! Kama mlango wa kunufaika umefungwa, thawabu ya funga anayofanyiwa maiti na walio hai ingemfikiaje?

b . Mtume(s.a.w.w) alimwambia mwanamke mmoja: "Mhijie mama yako". Na akamwambia mwanamume: "Mhijie baba yako". Hadithi hii pia imekubaliwa na Waislamu wote, Je! Thawabu za hija anayohijiwa na walio hai zinamfikiaje maiti, kumbe mlango wa kunufaika umefungwa?

c . Mwenyeezi Mungu anasema: "Zinamtukuza mbingu saba na ardhi (saba) na vilivyomo ndani yake, na hakuna chochote isipokuwa kinamsabihi kwa sifa zake njema lakini nyinyi hamfahamu kutukuza kwao" 17:44.

Iliposemwa: "Na hakuna chochote isipokuwa kinamsabihi kwa sifa zake njema". Hii inafidisha kuwa: Vitu vyote vinamsabihi Mwenyeezi Mungu, na kwa kuelewa zaidi hili tumsikilize Mtume(s.a.w.w) . Imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Mtume(s.a.w.w) alipita kwenye makaburi mawili akasema: Hawa waliomo katika makaburi haya wanaadhibiwa... Mara akaagiza kuti la mtende, akalipasua vipande viwili kisha akachimbiaa kimoja katika kaburi hili na kingine akachimbia katika kaburi lile, halafu akasema: Bila shaka vitawapunguzia (adhabu) madam havijakauka". Hiposemwa: "Madam havijakauka" inafidisha kuwa: Wakati wote vitakapokuwa vibichi (vipande vya kuti Ia mtende) vitakuwa vinamsabihi Mwenyezi Mungu. Hapa Mtume(s.a.w.w) ana thibitisha kuwa: Tasbihi za kuti zina mpunguzia adhabu maiti, kupunguziwa adhabu ni hatua ya kuingia mtu katika neema (pepo). Mpenzi msomaji! Tasbihi za kuti la mtende zitampa nafuu maiti, lakini Mwislamu akisoma Qur'an kwa ajili ya kumuombea maiti itakosa kumfikia?[35]

Kisha Sheikh Mkuu wa Tanzania alitoa fat'wa kwa kupitia Redio Tanzania kuwa: "Qur'an haikuchanwa" ingawa kwa maelezo yao - kama yalivyo kwenye kitabu: "Taarifa ya ujumbe wa Sheikh Mkuu" ukurasa 14 inasema: "Irshadul Muslimina kilichanwa kwa dharau" mwisho wa kunukuu. Kwa hiyo, Irshadul Muslimina iliyochanwa kwa dharau, ukikifunua kitabu hicho ukurasa wapili katika mlango wa kwanza utaiona Aya ya kumi na nane na ya kumi na tisa nusu yake, za Suratul Jathia. Bakwata inasema: Qur'an haikuchanwa lakini aya mbili katika Suratul Jathia zimechanwa kwa dharau! Sijui kwa Bakwata Qur'an inathubutu kwa vipi! Kwa kukamilika Sura ngapi au Aya ngapi hata isemwe ni QUR'AN? Kwa nini washutumiwe na kulaniwa watu wanaopendekeza kuwa: Sharia ya Mirathi na ya ndoa zifanyiwe marekebisho? Katika Mirathi wanachoomba iondolewe ni Aya isemayo "Lidh'dhakari Mithlu H'adh'dhil Unthayayni " 4:11

katika Ndoa wanaomba iondolewe Aya: "Mathna Wathulatha Warubaa " 4:4, sasa, unaweza kuhesabu silabi za Aya hizi, kisha uhesabu silabi za Aya zilizomo katika vitabu vilivyochanwa. Ndipo utamjua nani mwenye kosa wakufaa kushutumiwa na kulaaniwa! Kwakuwa sheria ni msumeno, hapa napenda kukumbusha baadhi ya matukio kama haya yalioyofanywa na wakubwa. Baada ya kufariki Mtume(s.a.w.w) sheria isemayo kuwa "Katika mafungu manane ya sadaka, fungu moja kati ya haya ni la wale wanaoingia Uislamu. Fungu hili lilifutwa! Na Aya inasomeka hivi: "Wal'muallafati Qulubuhum "[36]

Hukumu ya Aya hii imefutwa, kwa hiyo, maasi ya kunyanyasa sheria ya Mwenyeezi Mungu hayakuanza juzi katika Tarafa ya Nyakato, bali yameanza mbali huko baada ya kufariki tu Mtume(s.a.w.w) .

ISRAA NA MIIRAJI

Israa ni: Mwendo wa usiku, kama ilivyokuja katika Qur'an: "Utukufu ni wa yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku, kutoka Msikiti mtukufu (wa Makka) mpaka Msikiti wa mbali (Falastin) ambao tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake, ili tumuonyeshe baadhi ya ishaara zetu " 17:1.

Miiraji ni: Msafara ulioanzia katika Msikiti wa Falastin kwenda juu. Tukio la Israa limepokewa na waandishi wa Tarikh kwa njia tofauti, kuna wanaosema kuwa Israa ilitokea mwaka wa kumi na mbili baada ya kupewa Utume, Wengine wanasema ilikuwa mwaka wa kumi na moja, wengine mwaka wa kumi, wengine mwaka wa tano, wengine mwaka wa tatu na wengine mwaka wa pili.[37]

Kauli ya sawa katika mjadala huu ni: Israa imetokea katika mwaka wa tatu kwa sababu zifuatazo"

a . Mtume(s.a.w.w) alikuwa akipendelea sana kumbusu binti yake Mwana Fatima(a.s) mpaka Mwana Aisha (mkewe Mtume) likamuudhi sana hilo, akasema: "Ewe Mtume wa Mwenyeezi Mungu! Una nini? Kila mara ninakuona sana unambusu Mwana Fatima kama unayekula asali! Mtume(s.a.w.w) akamjibu: "Ni kweli, ewe Aisha! Mimi nilipopelekwa juu (Miiraji) Malaika Jibril(a.s) aliniingiza Peponi humo nilikula Tunda fulani, likabaki mgongoni, niliposhuka nilimwingillia Khadija (mkewe) mara akapata ujauzito wa Mwana Fatima kutokana na hilo tunda. Na yeye ndiye Tunda bora, kila ninapokumbuka Peponi, humbusu Fatima".[38]

Katika hadithi hii tunajifunza kuwa: Mwana Fatima(a.s) amezaliwa mwaka wa tano baada ya Biitha (kupewa Utume) kwa hiyo, Israa na Miiraji ilikuwa kabla ya kuzaliwa Mwana Fatima, kwa sababu Mwana Fatima ni Tunda la peponi alilokula Mtume siku aliyopelekwa Miiraji. Tunda lililobaki mgongoni kwake hata baada ya miaka miwili akazaliwa Fatima, Bibi bora kabisa katika mabibi wa Peponi - Hadithi. b. Mtume(s.a.w.w) alipopelekwa juu (Miiraji) Malaika walikuwa wakiuliza kila mahala Je! Muhammad amekwisha pewa Utume? Hili linaonyesha kuwa Tukio la Israa na Miiraji lilitokea katika miaka ya awali ya Utume, wala siyo baada ya miaka kumi na mbili. Kwa sababu ingekuwa hivyo bila shaka suala la Utume lingekwisha eleweka zamani pasingekuwepo haja ya kuliuliza. Israa na Miiraji ilitokea kabla ya kusilimu Abubakr bin Abi Quhafa, kwa sababu, Abubakr amesilimu baada ya miaka mitano ya biitha.[39]

Ikiwa Israa na Miiraji imetokea kabla ya kusilimu Abubakr, basi madai ya Laqabu isemwayo kuwa alipata Abubakri ya "SIDDIQ" yanatupwa: Kwa sababu ikiwa laqabu hiyo (kama inavyodaiwa) alupata baada ya kusadikisha msafara wa Mtume(s.a.w.w) aliopelekwa katika Israa na Miiraji. Litawezekanaje hilo, ilihali wakati wa tukio la Israa na Miiraji Abubakri alikuwa kafiri! Hapo tasdiq itapatikana?!

MTUME ALIKWENDA MWENYEWE AU NI NJOZI?

Tukio la Israa, wako baadhi ya Waislamu wanao ona kuwa Mtume(s.a.w.w) alioteshwa na wala hakwenda mwenyewe akiwa macho. Na mategemeo yao ni ile habari aliyoisimulia Mwana Aisha kuwa: "Siku hiyo hakukikosa kiwiliwili cha Mtume".[40]

MAJIBU YETU

a . Mwana Aisha wakati wa tukio hilo alikuwa hajaolewa na Mtume, bali yaelekea hata kuzaliwa alikuwa bado!!

b . Mwenyeezi Mungu anasema: "Utukufu ni wa yeye ambaye alimpeleka Mja wake usiku, kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa mbali " 17:1. lliposemwa: "Asraa Bia'bdihi " tamko la "A'BD" hutumiwa kwa roho na kiwiliwili pamoja. Kwa hiyo, Mtume(s.a.w.w) alikkwenda mwenyewe akiwa macho. c. Kama Israa ingelikuwa kwa njozi, basi kusingekuwako na upinzani mkubwa hivyo, na watu wasingeritarddi.[41]

d . Kama Israa ingelikuwa kwa njozi, basi Abu Talib na Bani Hashim wasingetoka kumtafuta, kwa sababu Bani Hashim walitoka kumtafuta siku hiyo.[42]

MUSA NA SALA TANO

Imepokewa katika riwaya kuwa: Sala tano zimefaradhiwa wakati Mtume(s.a.w.w) alipopelekwa katika msafara wa Miiraji huko juu Inasemwa kuwa, zilifaradhiwa sala hamsini kwa kila siku, na Mtume(s.a.w.w) alipokuwa akirudi na agizo hilo, alipofika mbingu ya sita akakutana na Nabii Musa(a.s) akamshauri Mtume Muhammad(s.a.w.w) arudi kwa Mola wake amuombe ampunguzie Sala hizo. Mtume alirudi kwa Mola wake na akapunguziwa Sala kumi, aliposhuka katika mbingu ya sita akakutana na Nabii Musa akiwa na sala arobaini. Nabii Musa akamrudisha kwa Mola wake apunguziwe Sala hizo, Mtume akafanya hivyo, Mwenyeezi Muungu akapunguza Sala kumi. Mtume alipofika kwa Nabii Musa, akamrudisha kwa Mola wake akaombe takhfif; Mtume alifanya hivyo, Mwenyeezi Mungu akapunguza sala kumi Mtume akashuka alipofika kwa Nabii Musa akiwa na sala ishirini, Nabii Musa akamtaka arudi kwa Mola wake akampunguzie, kwa sababu umma wake hawawezi hilo. Mtume(s.a.w.w) alifanya hivyo, Mwenyeezi Mungu akapunguza Sala kumi, Mtume akashuka akiwa na sala kumi, alipokutana na Nabii Musa akamrudisha kwa Mola wake ili apunguziwe, Mtume alifanya hivyo, Mwenyeezi Mungu akapunguza Sala tano, Mtume(s.a.w.w) aliposhuka kwa Nabii Musa(a.s) akiwa na sala tano, alipotaka kumrudisha kwa Mola wake, Mtume(s.a.w.w) alisema:- "Kwa hakika, nimerudi kwa Mola wangu mara tano, kuomba takhfif mpaka sasa naona aibu kubwa". Ndipo aliposhuka Mtume(s.a.w.w) akiwa sala tano, ambazo wanapaswa Waislamu kuzisali kwa kila siku.

UCHUNGUZI

Tunaamini kuwa: "Mwenyeezi Mungu haweki sheria yoyote isipokuwa ina maslahi ndani yake. Kwa mantiq hii, Mtume(s.a.w.w) asingehitaji kurudi mara zote hizo kwa ajili ya kupunguziwa. Kwa sababu kufanya hivyo ni kutaka sheria isiyo na maslahi, kama ambavyo sababu zilizompelekea Nabii Musa kutaka zipunguzwe Sala hamsini ni kushindwa kuzitekeleza sala hizo. Kama kwamba Nabii Musa anaamini kuwa Sheria hii (ya Sala hamsim) inakwenda kunyume na maslahi, na hilo ni muhali (haliwezekani) kwa Mwenyeezi Mungu. Aidha, vipi Mwenyeezi Mungu hakujua kuwa: Umma wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) hauwezi hilo, bali Musa yeye alijue hilo?? Au tuseme, ni takhfif kwa jambo lisilowezekana, vipi, Mwenyeezi Mungu anatwambia wakati wote: "Mwenyeezi Mungu huwatakieni yaliyo mepesi wala hawatakieni yaliyo mazito ". 2: 185. "Wala hakuweka juu yenu dhiki katika dini " 22:78.

Na vipi Nabii Ibrahim hakushitushwa na misafara ya nenda rudi ya Mtume Muhammad, asimuulize kuna nini! Maana kwa mujibu wa riwaya zinzosimulia tukio hili zinasema kuwa, Nabii Ibrahim(a.s) alikuwa katika mbingu ya saba na Nabii Musa(a.s) mbingu ya sita. Aidha, kwanini Mwenyeezi Mungu asimpe moja kwa moja Mtume wake Sala tano, kuliko usumbufu huu alioupata Mtume wa nenda rudi mpaka akaingiwa na aibu kubwa akashuka kwa shingo upande na sala zake tano!?

LENGO LA ISRAA NA MIRAJI

Tukitaka kujuwa shabaha na hekima na muujiza wa Israa na Miiraji, lazima kusoma nassi zake na vipengele vyake kwa undani na makini. Na hapa tutaonyesha mambo yafuatayo:

a . Israa na Miiraji ni muujiza mkubwa wa kudumu, na leo katika karne hii ya ishirini tukio hili linakubaliwa na elimu ya sayansi na Teknolojia. Mwanadamu hashangai tena leo kusikia kuwa mtu amekwenda umbali wa maili nyingi zaidi katika upeo wa juu.

b . Mwenyezi Mungu ametaja wazi lengo la msafara huo aliposema: "Linuriyahu Min Ayaatina ", yaani, "Ili tumuonyeshe baadhi ya Aya (ishara) zetu" 17:1. Kwahiyo, lengo ni kumuonyesha Mtume(s.a.w.w) baadhi ya ishara za utukufu wa Mwenyeezi Mungu. Na kwakupelekwa Mtume Israa na Miiraji, kumefunguwa moyo wake na akili yake zaidi kwa kupata taaluma kubwa katika ulimengu huu anaouongoza.

c . Mwanadamu (hasa Mwarabu) wakati huo aijishi katika ulimwengu finyu sana, na akili duni iliyofungwa katika tundu dogo. Kwa sabaha hii ikawa dharura kufunguliwa macho yake na moyo wake ili aujue ulimwengu anaoishi, ambao Mwenyeezi Mungu amemfanya awe khalifa wake.

KHADIJA ALIOLEWA NA YEYOTE KABLA YA MTUME?

Inasemekana kuwa: Mtume(s.a.w.w) hakuoa mke yeyote aliye bikira isipokuwa Mwana Aisha tu. Wanasema kuwa: "Mwana Khadija kabla ya kuolewa na Mtume(s.a.w.w) alikwisha olewa na waume wawili kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w.w) na amepata watoto wawili. Tutataja kidogo hapa baadhi ya hoja zinazosemwa juu ya Mwana Khadija kuhusu watoto aliopata kwa waume wengine kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w.w) ni kama ifuatavyo:

i. Wanasema: Shahidi wa kwanza katika Uislamu ni mtoto wa Mwana Khadija aitwae Harithi bin Abi Hala, alipata shahada pale Mtume(s.a.w.w) alipotangaza Uislamu hadharani.[43]

ii. Lakini, hoja hii inaangushwa na riwaya ya Qatada inayosema kuwa: Shahidi wa kwanza katika Uislamu ni Sumayya, mama yake Ammar bin Yasir.[44]

Imepokewa kuwa: Mwana Khadija(a.s) alikuwa na nduguye akiitwa Hala, aliolewa na mtu mmoja katika Koo ya Al'Makhzumi, akazaa mtoto wa kike jina lake Hala, Kisha aliachika akaolewa na mtu mmoja katika Koo ya At'Tamim aitwaye Abu Hindi, akamzalia mtoto jina lake Hind. Huyu Abu Hindi, alikuwa na mke mwingine ambaye alimzalia watoto wawili: Zaynab na Ruqayya. Hatimae Abu Hindi na mkewe wa pili walikufa,akabakia Bi Hala ndugu ya Mwana Khadija, pamoja na watoto wawili: Zaynab na Ruqayya. Yule mtoto wake wa kuzaa: Hind, alikwenda kwa jamaa za mumewe. Ndipo Mwana Khadija alipowakusanya wote akawa nao, Bi Hala na watoto wawili walioachwa na mama yao: Zaynab na Ruqayya. Mwana Khadija alipoolewa na Mtume(s.a.w.w) Bi Hala alifishwa, wakabaki Zaynab na Ruqayya wakilelewa na Mtume(s.a.w.w) . Katika mila za Kiarabu, walikuwa wakiamini kuwa mtoto wa kufikia ni mtoto wako halisi, kwa hiyo, watoto hawa wakapewa ubinti wa Mtume(s.a.w.w) (Zaynab binti Muhammad na Ruqayya binti Muhammad).[45]

MAJIBU YETU

a. Katika kitabu "Asha'shaafy" na "At Talkhis" inasema Mtume(s.a.w.w) amemuoa Mwana Khadija akiwa bikira.

b. b. Amesema Abulqasim Alkufy: Mtume(s.a.w.w) alipomuoa Mwana Khadija(a.s) wanawake wa kikuraishi walimkasirikia sana Mwana Khadija wakisema: Wamekuposa mabwana wa kikuraishi wenye heshima, umekataa kuolewa na yeyote kati yao, umekubali kuolewa na Muhammad, yatima wa Abu Talib Lofa hana mali![46]

POTE LENYE KUOKOKA

Amesema Mtukufu Mtume(s.a.w.w) "Watafarakana umma wangu makundi sabini na tatu, kundi moja tu kati ya hayo litaokoka, na yaliyobaki yatatiwa motoni . Ali akauliza: "Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu! Kundi gani litakalookoka? Mtume(s.a.w.w) akajibu: "Wewe na watu wako".[47]

Mfarakano kwa mara ya kwanza ulitokea kwa Waislamu pale tu alipofariki Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Mtume(s.a.w.w) kabla ya kufariki dunia, aliweka sera kamili ya uongozi katika Uislamu. Iliposhuka Aya: "Hakika wale walioamini na wakatenda mema, basi hao ndio wema kushinda viumbe vyote " 98:7.

Mtume(s.a.w.w) akamwambia Ali: "Wewe Ali na kundi (pote) lako ".[48]

Mtume(s.a.w.w) amesema: "Ali yu pamoja na Qur'an, na Qur'an ipamoja na Mi, hawataachana mpaka wanifikie katika Haudh ".[49]

Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mimi ninakuachieni vizito viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, Qur'an na Ahlul Bayt wangu, viwili hivi havitaachana mpaka vitakaponifikia katika Haudh".[50]

Imam Ali(a.s) mmoja katika Ahlul Bayt wa Mtume(s.a.w.w) tazama pale iliposhuka Ayatut Tat'hir: "Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni sana sana " 33:33.

Na mke wa Mtume(s.a.w.w) (Ummu Salama) alipotaka kuingia katika nguo hiyo Mtume akamzuia![51]

AHLUL BAYT WALIO PAMOJA NA QUR'AN

1. Imam Ali bin Abi Talib(a.s) amezaliwa ndani ya Al' Kaaba siku ya Ijumaa, tarehe kumi na tatu Rajab mwaka wa thalathini (mwaka wa ndovu). Wamekhitilafiana waandishi wa tarikh kujuwa tarehe aliyopigwa dharba Imam Ali, baadhi ya kauli hizo zasema:

a. Alipigwa dharba tarehe 17 usiku wa kuamkia Ijumaa mwezi wa Ramadhan, akafishwa usiku wa kuamkia Jumapili tarehe 19 Ramadhan.

b. Alipigiwa dharba tarehe 19 usiku, akafishwa tarehe 21 Ramadhan mwaka 40.

c. Alipigwa dharba kuamkia tarehe 21, akafishwa tarehe 23 Ramadhani.

d. Alipigwa dharba kuamkia tarehe 23, akafishwa tarehe 25 Ramadhan.[52]

Riwaya nyingine zinasema kuwa:

a. Alipigwa dharba asubuhi ya tarehe 17 Ramadhan.

b. Alipigwa dharba asubuhi ya tarehe 19 Ramadhan, mwaka 40 Hijra.[53]

Abdur Rahman bin Muljam alikutana na msichana mmoja katika khawariji aitwaye Qatwam, ambaye baba yake na kaka yake waliuliwa na Imam Ali katika vita vya Nahrwan. Msichana huyo alikuwa mzuri kupita kiasi, Abdur Rahman alipomtaka Qatwam, alimjibu: "Kama utaweza kunipoza moyo wangu utanipata" Akamuuliza: "Ni lipi litakalo kupoza moyo wako?" Akajibu: "Unipe dirham alfu tatu, mtumishi mmoja, mjakazi, mwimbaji, na umuue Ali bin Abi Talib. Abdur Rahman bin Muljam akasema: "Hayo mengine yote ni mepesi sana, lakini hili la kumuua Ali, ni dalili ya kuwa umenikataa. Kwa sababu haiwezekani kumuua Ali nami nikasalimika, tukaweza kuoana". Ilipofika siku hiyo, kwa kauli zilivyo khitilafiana, kama ulivyoona hapo juu, Abdur Rahman bin Muljam akatimiza lengo lake. Imam Ali amezikwa Kufa katika nchi ya Iraq.[54]

2. Imam Hasan bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina, tarehe kumi na tano Ramadhan mwaka wa tatu Hijra'. Mu'awiya alipotaka kumtawalisha mwanawe Yazid, alitumia mbinu, akamjenga Juuda bint Al'ash'a'th bin Qays. Huyu alikuwa mke wa Imam Hasan(a.s) . Muawiya akampa sumu ili amtilie Imam Hasan. Na endapo atamuua, basi atamfanyia mambo mawili, la kwanza atampa dirham laki moja na la pili atamuoza mwanawe, Yazidi. Imam Hasan akapewa sumu hiyo na baada ya hapo alibaki siku arobainni akafariki dunia! Amekufa mfungo tano mwaka 50 Hijra.[55]

Wengine wanasema: Amekufa mfungo sita mwaka 49 Hijra.[56]

Baada ya kufa Imam Hasan Juu'da alipeleka ujumbe kwa Yazidi wa kutaka kuolewa naye kama walivyoahidiana na baba yake Mu'awiya, Yazidi aliruka na kusema: "Hukuweza kumhurumia Hasan utanihurumia mimi!? Kama umeweza kumuua yeye mimi utanimaliza mara moja, Yazid akakataa kumuoa.

3. Imam Husein bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe tatu Shaaban mwaka wa nne Hijra. Imam Husein(a.s) ameuliwa mwezi kumi Muharram siku ya Ijumaa (wengine wanasema Jumamosi) mwaka wa sitini na moja Hijra. Imepokewa kutoka kwa Anas kwamba Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mwanangu Husein atauliwa katika nchi ya Iraq, yeyote miongoni mwenu atakaekuwapo, basi asimame kumnusuru.[57]

Imepokewa kwa mama Ummu Salama (mkewe Mtume) anasema: "Nilimuona Mtume(s.a.w.w) akikipangusa kichwa cha Imam Husein na huku akilia. Nikamuuliza: "Unalilia nini!" Akasema: "Hivi sasa amenijulisha Malaika Jibril kuwa: Mtoto wangu huyu atauliwa katika ardhi litwayo "KARBALA" kisha akanipa gao la udongo na akaniambia: 'Huu udongo ndipo mahala atakapouliwa, utunze, siku yoyote utakapogeuka kuwa mwekundu basi jua yakwamba amekwisha uliwa".[58]

Kama ambavyo, siku aliyouliwa Imam Husein mbingu zilimlilia, na alama ya kuonyesha kuwa zinamlilia ni wekundu unao onekana kwenye mawingu. Kwa hiyo, Imam Husein(a.s) analiliwa na mbingu mpaka leo hii.[59]

4. Imam Ali bin Husein(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe tano Shaaban mwaka thalathini na nane Hijra, kabla ya kufishwa babu yake (Imam Ali) kwa miaka miwili. Imam Ali bin Husein amefariki mwaka wa tisini na nne Hijra, akazikwa katikamji wa Madina katika kiwanja kitakatifu cha Baqii.

5. Imam Muhammad bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe tatu mfungo tano (wengine wanasema tarehe moja Rajab) mwaka hamsini na saba Hijra, kabla ya kuuliwa babu yake Imam Husein kwa miaka mitatu. Wamekhitilafiana mwaka aliofia kama hivi:

a. Amefishwa mwaka 114 Hijra.

b. Amefishwa mwaka 117 Hijra.

c. Amefishwa mwaka 118 Hijra.

6. Imam Ja'far bin Muhammad(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina tarehe 16 mfungo sita (wengine wanasema tarehe moja Rajab) mwaka 80 Hijra. Imam amefishwa katika mji wa Madina mwaka 149 Hijra, amezikwa pamoja na baba yake na babu yake katika viwanja vitakatifu vya Baqii.[60]

7. Imam Musa bin Ja'far(a.s) amezaliwa katika kijiji cha "AB'WAA" kilicho kati ya Makka na Madina, mahala ambapo kaburi la Mwana Amina bint Wahab mama yake Mtume(s.a.w.w) lilipo. Amezaliwa mwaka 128 Hijra (wengine wanasema mwaka 129). Imam Musa amefariki mwaka 188 Hijra baada ya kutiwa jela na Haruna Rashid kwa miaka kumi moja.[61]

8. Imam Ali bin Musa(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina. Wamekhitilafiana kujuwa tarehe aliyozaliwa kama hivi:

a. Amezaliwa mfungo pili mwaka 148.

b. Amezaliwa mfungo tatu mwaka 148.

c. Amezaliwa mfungo sita mwaka 148.

d. Amezaliwa mwaka 153. Kifo cha Imam Ali bin Musa kimetokana na maji ya matunda yenye sumu aliyopewa na Maamun. Baada ya kunywa Imam alibaki siku mbili kisha akafariki dunia, mwaka 203 wengine wanasema mwaka 202 na wengine wanasema mwaka 206.[62]

9. Imam Muhammad bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina, tarehe kumi na tisa Ramadhan mwaka 195 Hijra. Amefariki Imam Muhammad mwaka 220 wengine wanasema mwaka 225[63]

10. Imam Ali bin Muhammad(a.s) amezaliwa Rajab mwaka 214 Hijra umbali wa maili tatu hivi kutoka katika mji wa Madina. Imam Ali bin Muhammad ameuliwa kwa sumu mwaka 254 Hijra.

11. Imam Hasan bin Ali(a.s) amezaliwa katika mji wa Madina mwaka 231 Hijra. Imam Hasan bin Ali amefariki siku ya Ijumaa tarehe nane mfungo sita mwaka 260 na akazikwa mahala alipozikwa Baba yake.

12. Imam Muhammad bin Hasan(a.s) amezaliwa tarehe kumi na tano Shaaban mwaka 255 Hijra, wengine wanasema tarehe ishirini na tatu Ramadhan mwaka 258 Hijra. Imam Muhammad bin Hasan yuko hai mpaka sasa, alipofiwa Baba yake alikuwa na umri wa miaka mitano. Hawa ni Maimam kumi na wawili katika AhIul Bayt(a.s) walio pamoja na Qur'an. Amesema Mtume(s.a.w.w) "Dini itaendelea kuwa imara mpaka isimame kiama, na mtasimamiwa na viongozi kumi na wawili, wote katika Maquraishi ".[64]

Na ameonya Mtume(s.a.w.w) kwa yeyote ambaye hatawatambua Maimam hawa: "Yeyote atakaekufa na asimjue Imam wa zama zake, atakufa kifo cha kipagani ".[65]

SERA ZA UTAWALA BAADA YA MTUME

Ukisoma Terikh, na kisha ukafuatilia sera za utawala wa makhalifa watatu, utajua wazi kwamba mabwana hao walizuia kuandikwa Hadithi za Mtume Muhammad(s.a.w.w) bali walikataza hata kuzizungumza mbele za watu. Kwa sababu walijua wazi kuwa sera za utawala wao haziendi sambamba na uongozi wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Abubakr amekataza kuzungumza chochote juu ya Mtume(s.a.w.w) na amesema:Yeyote atakaewauliza mseme: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an, basi, halalisheni halali yake na haramisheni haramu yake ". [66]

Kauli hii ya Abubakr imekuja baada ya muda mfupi wa tukio la karatasi, Umar bnul Khattab alipomjibu Mtume kuwa: "Mtume anaweweseka, ipo Qur'an inatutosha", Abubakr anasema: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an"..... Qur'an iliyo kati yetu na Abubakr inasema kuhusu wanaozuia zaka: "Na miongoni mwao wako walio mwahidi Mwenyeezi Mungu, akitupa katika fadhili zake bila shaka tutatoa sadaka na lazima tutakuwa miongoni mwa watendao mema. Lakini alipowapa katika fadhili zake, wa kayafanyia ubakhili na wakageuka, nao ndio wakengeukao. Kwa hiyo akawalipa unafiki mioyoni mwao mpaka siku ya kukutana naye, kwa sababu ya kumkhalifu Mwenyezi Mungu ahadi waliyo mwahidi, na kwa sababu walikuwa wanasema uongo". 9:75-77.

Aya hizi zimeshuka kwa ajili ya Thaalaba aliyezuia zaka wakati wa Mtume(s.a.w.w) . Lakini pamoja na yote hayo Mtume(s.a.w.w) hakumpiga wala hakumnyang'anya mali yake, ingawa Mtume yote haya alikuwa na uwezo nayo. Ambapo suala la Malik bin Nawyira na wenzake waliodaiwa kuwa walizuia Zaka katika utawala wa Abubakr. Huo ni msimamo waliouonyesha dhidi ya utawala wa Abubakr aliyepora madaraka yasiyo kuwa yake. Kwa hiyo, kitendo cha kuzuia zaka kutoupa utawala wa Abubakr ni tafsiri halisi ya kupinga utawala huo na wala si kupinga hukumu ya faradhi ya zaka. Sasa, Abubakr yuko wapi na aya hizi aliyedai kuwa ndiyo sera yake?? Mbona amewaua watu waliozuia zaka kwa kigezo gani? Sera ya Abubakr inasema: "Kati yetu sisi na nyinyi ni Qur'an".

Qur'an inasema: "Wanaume wana sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio wakaribia, Na wanawake wanayo sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio wakaribia " 4:7.

Mwana Fatima bint Muhammad(s.a.w.w) alipokwenda kwa Abubakr kutaka mirathi iliyoachwa na baba yake, Abubakr akakataa kumpa akidai kuwa amemsikia Mtume akisema: "Sisi Mitume haturithiwi". Hapa Qur'an hana haja nayo, ameshika lile asilokuwa na haja nalo tokea awali, hata hivyo, Abubakr kweli maneno ya Mtume anayakubali? MwanaAisha (Mwanawe) anasimulia tukio hili: Baba yangu alizikusanya Hadithi za Mtume(s.a.w.w) ambazo zilikuwa mia tano, akakesha kucha akizigeuzageuza......kulipokucha akasema: Mwanangu! Niletee Hadithi ulizonazo, ni kampa, akazichoma moto![67]

Je! Ni kweli Abubakr anaitegemea Qur'an tu peke yake? Mwenyeezi Mungu anasema: "Sadaka ni kwa mafakiri tu na masikini na wanaozitumikia na waungiwao.......mioyo yao.....9:60. Iliposemwa: "Na waungiwao mioyo yao" ni wale waislamu wapya ambao ndio kwanza wanasilimu. Abubakr alipotawala, hukumu ya kifungu cha Aya hii akaifuta![68]

SHARTI YA KUCHAPA

Sharti ya kuchapa au kusambaza ni kutaja rejeo hili. haki zote zimehifadhiwa na Taasisi ya Al-Hasanain Taasisi ya Imamu Husein(a.s)

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini(a.s) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini.

MWISHO WA KITABU

YALIYOMO

MASOMO YA KI-ISLAMU 1

MUONGOZO KWA WASOMAJI 1

KIMEANDIKWA NA: OMAR JUMAA MAYUNGA 1

UTANGULIZI 1

MASOMO YA KI-ISLAMU 2

MUONGOZO KWA WASOMAJI 2

MWANZO WA WAHY 2

MJADALA WA RIWAYA ZA WAHY 4

MUHARRAM SI MWANZO WA MWAKA 5

KUONEKANA KWA MWENYEEZI MUNGU 6

MAJIBU YETU 6

HADITHI ZISEMAZO KUWA ATAONEKANA 7

MAJIBU YETU 8

QUR'AN IMEUMBWA 8

TAQIYYA 8

TAHRIFUL QUR'AN 10

MASOMO YA KI-ISLAMU 12

MUONGOZO KWA WASOMAJI 12

WANAOTHIBITISHA KUWA IPO 12

WALIOSEMA KUWA HAIPO 12

KUSOMA QUR'AN KWA AJILI YA MAITI 13

MAJIBU YETU 13

ISRAA NA MIIRAJI 15

MTUME ALIKWENDA MWENYEWE AU NI NJOZI? 16

MAJIBU YETU 16

MUSA NA SALA TANO 17

UCHUNGUZI 17

LENGO LA ISRAA NA MIRAJI 18

KHADIJA ALIOLEWA NA YEYOTE KABLA YA MTUME? 18

MAJIBU YETU 19

POTE LENYE KUOKOKA 19

AHLUL BAYT WALIO PAMOJA NA QUR'AN 20

SERA ZA UTAWALA BAADA YA MTUME 23

SHARTI YA KUCHAPA 24

MWISHO WA KITABU 24

YALIYOMO 25


[1] . Taz: Sahihi Bukhari Juz.I uk: 5-6. Sahihi Muslim Juz. I, uk: 97 Almuswannaf Juz. 5, uk: 322. Tarikhut Tabari Juz. 2, uk: 47.

[2] . Taz; Albidayatu Wannihaya Juz. 3, Uk: 9 Assiratun Nabawiyya Juz. 1 uk: 83. Assiratul Halabiyya Juz. 1, uk: 250. Siiratu Mughlataya uk, 15.

[3] . Taz: Albidayatu Wannihaya Juz.3 uk, 12. Siiratu Ibn Hisham Juz. 1 uk, 238 Assiratul Halabiyya Juz. 1, Uk. 239.

[4] . Taz: Assiratul Halabiyya Juz. 1, Uk. 252.

[5] . Taz: Tarikhul Yaa'quby Juz. 2, Uk. 23.

[6] . Taz: Tarikhul Khamisi Juz. 1, Uk. 284. Assiratul Halabiyya Juz. 1, Uk. 243. Assiratun Nabawiyya Juz. 1. Uk. 83.

[7] . Taz: Almuswannaf Juz. 5, Uk. 323.

[8] . Taz: Albidayatu Wannihaya J. 3 Uk. 13.

[9] . Taz: Qamusir Rijal Juz. 6, Uk. 300 Algharat Juz. 2, Uk. 558-560.

[10] . Taz: Mustadrakul Hakim Juz. 3, Uk. 121. Musnad Ahmad Juz. 5, Uk. 30. Alfusulul Muhimma Uk. 111. Tarikh Ibn Asakir Juz. 2, Uk. 184. Manaqibu Ali Uk. 394.

[11] . Taz: Sahihi Muslim, katika kitabul Iman. Sahihat Tirmidhi Juz. 2, Uk. 301. Musnad Ahmad Juz. 1, Uk. 84. Tarikh Bughdad Juz. 2, Uk. 255. Hilyatul Awliyaa Juz. 4, Uk. 185. Kanzul Ummal Juz. 6, Uk. 394. Mustadrakul Hakim Juz. 3, uk 129. Al Istiab Juz. 2, Uk. 214. Addurrul Manthur Aya ya 25 sura 47.

[12] . Taz: Magatilut Talibina Uk. 27. Aljamal, Uk. 83-84.

[13] . Taz: Sahihi Bukhari Juz. 1, Uk. 152. Sahihi Muslim Jz. 7, Uk. 100. Musnad Ahmad Juz. 2, Uk. 315. Almuswannaf Juz. 11, Uk. 274. Sunannun Nasai Juz. 4, Uk. 118. Albidayatu Wannihaya Juz. 1, Uk. 317. Tarikhut Tabari Juz. 1, Uk. 305.

[14] . Taz: Alkharaj Uk. 81. Jamharatu Rasailil ar'b Juz. 1, Uk. 82.

[15] . Taz: Albidayatu Wannihaya Juz. 3, Uk. 207.

[16] . Taz: AI'i'lanu Uk. 78.

[17] . Taz: U'nwanul Maa'rif Uk. 11.

[18] . Taz: Sahihi Bukhari J. 4 Uk. 92 Sahihi Muslim J. 1 Uk. 86 Tafsirul Khazin J. 7 Uk. 137.

[19] . Taz: At'targhib Wat'tarhib J. 4 Uk. 551.

[20] . Taz: Tafsirul Qurtubi, J. 4, Uk. 57.

[21] . Taz: Tafsir ibn Kathir J.1, Uk. 365 Safwatut Tafasir J.1, Uk.196.

[22] . Taz: Tafsir Ibn Kathir J. 2 Uk. 609 Tafsirul Qurtubi J. 10 Uk. 180 Tafsirul Khaazin J. 4 Uk. 117 Tafsirul Maraghi J. 14 Uk. 146.

[23] . Taz: Tafsirul Qurtubi J. 9 Uk. 76.

[24] . Taz: Tafsir Qurtubi J. 14 Uk. 290.

[25] . Taz: Manahilul I'r fani Juz. 1 Uk. 253 3.

[26] . Taz: Tafsirul Alus Juz. 1 Uk: 39 Tafsir lbn Kathir Juz. 1 Uk: 17 Tafsirul Khazin Juz. 1 Uk: 18 Tafsirush Shawkan Juz. 1 Uk; 7.

[27] . Taz: Sahihi Bukhari J. 8 Uk. 26 Sahihi Muslim Juz. 5 Uk. 116.

[28] . Taz: Al' It'qan Juz. 1 Uk. 101.

[29] . Taz: Tafsirul Qurtubi J. 14 Uk. 113 Al' It'qan Juz.2 Uk.32.

[30] . Taz: Al' It'qan Juz. 2 Uk. 33.

[31] . Taz: Tafsirul Qurtubi Juz. 14 Uk. 113.

[32] . Taz: Al'I'tigad Juz. 1 Uk. 16. Tafsir Aalair Rahman Juz. 1 Uk. 25. Albayan fit'tafsiril Qur'an Uk. 213. Tafsirul Qur'an, assayid shubbar Uk. 17.

[33] . Taz: Tafsir ibn Kathir Juz. 4 Uk. 276.

[34] . Tarehe 18-8-1984 katika mkoa wa Mwanza Tarafa ya Nyakato Kijiji cha Buzuruga, kulitokea tatizo kubwa lililosababishwa najeshi la jadi Ia sungusungu. Jeshi la jadi la sungusungu kwa makusudi kabisa, ililiivamia nyumba ya MwisIamu, likaingia ndani na kuchanachana vitabu vitano vitakatifu vya Kiislamu. Yasin Ndogo (B) Majmuul Mubarak (C) Irshadul Muslimina (D) Hadithi Za Mtume (E) Ahlul Badr.

[35] . Taz: Tafsirul Qurtubi J. 10 Uk. 267.

[36] . Taz: Tafasirut Tabari Juz. 10, Uk. 113.

[37] . Taz: Albidayatu Wannihaya Juz. 3, Uk. 108 Tarikhul Khamisi Juz. 1, Uk. 307 Assahihu Minsiiratin Nabi Juz. 1, Uk. 269.

[38] . Taz: Tarikh Bughdad Juz. 5 Uk. 87. Mizanul'itidal Juz. 2 Uk. 297. Mustadrakul Hakim Juz. 3 Uk. 156. Majmauz Zawaid Juz. 9 Uk. 202. Kanzul Ummal Juz. 14 Uk. 97. Dhakhaairul U'qbaa Uk. 36.

[39] . Taz: Assahihu Minsiiratin Nabii Juz. 1, Uk. 274 Usudul Ghaba Juz. 4, Uk. 18.

[40] . Taz: Tarikhul Khamisi Juz. 1 Uk. 308. Al' mawahibul laduniyya Juz. 2 Uk.2.

[41] . Taz: Tafsir ibn Kathir Juz. 3 Uk. 24. Tarikhul Khamisi Juz. 3 Uk. 308. Almuswannaf Juz. 5, Uk. 327.

[42] . Taz: Assahihu Minsiiratin Nabii Juz. 1 Uk. 276.

[43] . Taz: Al' Isaba Juz. 1, Uk. 293 Al'Awaail Juz. 1, Uk. 311-312.

[44] . Taz: Al' Isaba J. 4 Uk. 335.

[45] . Taz: As' Sahihu Minsiiratin Nabi Juz. I, Uk. 123.

[46] . Taz: Al' Istighatha Juz. 1, Uk. 70.

[47] . Taz: Ithbatul Hudat Juz. 2, Uk. 260.

[48] . Taz: Tafsirut Tabari Juz. 30 Uk. 171.

[49] . Taz: Faidhul Qadir Juz. 4 Uk. 358. Musnad Ahmad Juz. 5 Uk. 31. Alfat'hul Kabir Juz. 2, Uk.21. Tarikhul Khulafai Uk. 174. Majmauz Zawaid Juz. 9, Uk. 134. Kifayatut Talibi Uk. 399. Asnal matalibi Uk 136.

[50] . Taz: Tafsir ibn Kathir J. 4 Uk. 122 Tafsir ul Kazin J. 1 Uk. 4 Tarikhu Bughdad J. 8 Uk. 442 Sahihi Muslim Juz. 4 Uk. 1873. Jamiul Usul Juz. 1, Uk. 187. Albidayatu Wannihaya Juz. 7 Uk. 362. Majmauz Zawaid Juz. 9 Uk. 163. Musnad Ahmad Juz. 2 Uk. 17-26. Al Mustadrak Juz. 4 Uk. 109.

[51] . Taz: Sahihi Muslim Juz. 4 Uk. 127. Sahihi Tirmidhi Juz. 4 Uk. 304. Alkhasais Uk. 4. Tarikh Bughdad J. 9 Uk. 126 Al' Isaba J. 1 Uk. 27 Usudul Ghaba J. 5 Uk. 521 Al Mustadrak Juz. 2 Uk. 416. Tafsirut Tabari Juz. 22 Uk. 5-7. Tafsirul Khazin Juz. 5 Uk. 259. Addurrul Manthur Juz. 5 Uk. 198.

[52] . Taz: Kashful Ghumma Juz. 2, Uk. 63.

[53] . Taz: Suratul Aimmatil Ithna Ashar Juz. 1, Uk 452.

[54] . Taz: Kashful Ghumma Juz. 2, Uk. 62. Tabaqatul Kubra, Juz. 6, Uk. 12. Tadhkiratul Khawas Uk. 179 2.

[55] . Taz: Kashful Ghumma Juz. 2 Uk. 207. Tadhkiratul Khawas Uk. 211.

[56] . Taz: Tadhkiratul Khawas Uk. 211.

[57] . Taz: Dhakhairul Uq'baa Uk. 146.

[58] . Taz: Dhakhairul' U'qbaa Uk. 147 Albidayatu Juz. 3 Uk. 174. Albidayatu Wannihaya Juz. 6 Uk. 230. Tarikhul Islam Juz. 3 Uk. 10. Almustadrak Juz. 3 Uk. 176.

[59] . Taz: Tafsirul Qurtubi Juz. 16 Uk. 14.

[60] . Taz: Siiratul' Aimmatil Ithna Ashar Juz. 2, Uk. 225.

[61] . Taz: Tadhkiratul Khawas Uk. 350.

[62] . Taz: Siiratul' Aimmatil' Ithna Ashar Juz. 2, Uk. 341.

[63] . Taz: Siiratul' Aimmatil' Ithna Ashar Juz. 2, Uk. 448.

[64] . Taz: Sahihi Muslim Juz. 6 Uk. 3-4 Sahihi Bukhari Juz. 4, Uk. 165. Sunan Abi Daud Juz. 3, Uk. 106 Musnad Ahmad Juz. 5, Uk. 86-90. Kanzul Ummal Juz. 13 Uk. 26-27. Hilyatul Awliyaa Juz. 4, Uk. 333.

[65] . Taz: Sharhul Maqasid Juz. 2, Uk. 275. Al'mirqat Juz. 2 Uk. 509. Al'ghaadir Juz. 10, Uk. 260.

[66] . Taz: Tadh'kiratul hufaadh Juz. 1, Uk. 3.

[67] . Taz: Kanzul Ummal. Juz. 5, Uk. 237 Tadh'kiratul hufaadh Juz. 1, uk, 5.

[68] . Taz: Tafsirut Tabari Juz. 10, Uk. 113.


6

7