• Anza
  • Iliyopita
  • 6 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 16340 / Pakua: 2221
Kiwango Kiwango Kiwango
UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

Mwandishi:
Swahili

3

UTUMWA KATIKA MTIZAMO WA KIISLAMU NA KIMAGHARIBI

Katika kipindi chote cha historia ya Kiislamu, tunaona watumwa wakipanda siyo tu katika nyadhifa za utawala bali hata katika Ufalme pia. Katika maneno ya Will Durant, "Inashangaza ni watoto wangapi wa watumwa wamepanda katika nafasi za juu katika usomi (kitaaluma) na Kisiasa, katika ulimwengu wa Kiislamu; ni wangapi, kama vile Mahmud na wale Mamelik wa mwanzo, walikuja kuwa Wafalme. o Subktagin wa Ghazni na mtoto wake, Mahmud (mfalme mpiganaji maarufu ambaye aliishambulia India mara kumi na saba) walikuwa watumwa na watoto wa watumwa mtawalia. Utawala wa kwanza wa Kinasaba wa Kiislamu wa nchini India nao pia uliundwa na utawala wa kinasaba wa watumwa. Kabla ya kuifunga sura hii, ni lazima nisisitize nukta moja: Wale wafungwa wote au watoto wa wafungwa ambao wali-fika kilele cha heshima kiroho au Kisiasa -hawakufanywa hivyo kamwe kwa sababu ya kuwa watumwa au watoto wa watumwa; bali walifikia daraja hizo kwa sababu walikuwa Waislamu waliokuwa na uwezo. Daraja zao za kiutumwa au kuachiwa huru kamwe halikuongezeka au kupunguza nafasi za mafanikio yao; kamwe haukurahisisha wala kuzuia kufikia lengo lao la maisha. Jamii ya Kiislamu, shukurani kwa sheria madhubuti za Uislamu na Mtume Muhammad, walikuwa vipofu-kirangi na vipofu-kihadhi (yaani Uislamu haufadhilishi rangi au hadhi ya mtu). Jambo moja tu lililo-husika lilikuwa ni uwezo wa kufanya jambo au kitu ambao mwanamume au mwanamke alikuwa nao.

Mafanikio haya, yaliyo patikana miaka 1400 iliyopita, ni kilio cha tofauti sana kutokaka na kushindwa kwa dhahiri 105. Durant, W., The Story of Civilization, j. 4, uk. 209. kwa Ukristo katika miaka hii ya 1960 ambako, katika nchi ya Kikristo ya Amerika (U.S.A) kama mtu mweusi (Mnegro) anakuwa Meya (wa Jiji) inaonekana ni habari kubwa; na wakati ambapo katika mwaka 1971 serikali ili-panga kumpandisha cheo mwanajeshi wake wa kwanza mtu mweusi kuwa admiral (mkuu wa jeshi la wana maji), aliyeitwa Kapteni Samwel Lee Granely. Unaona kidokezi cha habari hizi. Mtu fulani kutoka jamii ya watu weusi (Manegro) anachaguliwa na kupandishwa cheo kwa misingi ya kisiasa kwa sababu ni mtu mweusi (Mnegro). Lakini ingekuwa hasa hasa ni sifa zake tu za kib-inafsi, jina hili lisingekuwa ni jambo la kutangazwa na kuenezwa kila mahali! Aina kama hiyo ya ubaguzi wa rangi na kujiona ilikuwa, na hata sasa haifikiriki katika Uislamu.

Hivyo basi, ni dhahiri kwamba Uislamu ulifanikiwa mahali ambapo kila dini nyingine na mifumo imeshindwa mpaka sasa. Uislamu uliwachanganisha watumwa katika jamii ya Waislamu bila kujali rangi zao au asili. Kuamua kutokana nakumbu kumbu zake zenyewe (zilizo za kweli), hatuwezi ila kushanga mafanikio makubwa ya Uislamu katika uwan-ja wa nyanja hii.

CHIMBUKO LA WATUMWA WEUSI

Sasa tumeona msimamo wa Uislamu kuhusu utumwa, hebu ngoja tuuangalie Ukristo na wafuasi wake, na tuone wali-fanya nini kuhusu suala hili. Inashangaza kuona kwamba Wakristo, ambao kwa sababu wanazo zijua wao, siku hizi wanajifanya kama mabingwa wa uhuru wa mwanadamu, kumbe wao ndiyo mawakala wa dhahiri na watetezi wakub-wa wa mfumo huu wa utumwa. Walivumbua falsafa na uthibitisho wa kimaadili, kama sababu za kuwafanya watumwa watu "wasio staarabika." Mojawapo ya hoja zao ni kwamba walikuwa wana waokoa watu hao (watumwa) kutoka kwa majirani zao wanaokula watu hapa duniani, na kutoka kwenye fedheha ya daima milele baada ya uhai wa hapa duniani. Uislam na wafuasi wake kamwe hawakuwa na fikira kama hizo. Wingi mno wa maandiko ya Kiisilamu hauna kitu kama hicho, kutokana na aina hii ya jitihada ya uadilishi wa kusikitisha. Lakini waandishi wa Kikiristo kila mara hutaja biashara ya utumwa kama vile wao hawakuhusika kwa vyovyote vile na tatizo hili, na kwamba ni Uislam ndio ambao "ulihimiza na kuhalalisha utumwa" ambapo wao, Wakristo, kila mara walijaribu kukomesha mpango huu mbaya sana! Haya ndiyo maelezo ya waandishi wa Kikristo.

Ni jambo la kuvutia kuona kwamba wakati wanapo zungumzia kuhusu biashara ya watumwa ya Afrika ya Magharibi ambayo ilifanywa kikamilifu na Wakristo peke yao, waandishi na wanahistoria wa Kikristo, wameipa biashara hii jina la "West African Slave trade," Yaani biashara ya utumwa ya Afrika ya Magharibi au "Atlantic Slave - Trade" yaani biashara ya utumwa ya Atlantic, lakini wanapotoa maelezo kuhusu suala hili kwa upande wa Afrika ya Mashariki, hubadili maneno na kuandika "Arab Slave Trade" yaani biashara ya utumwa ya Waarabu. Ukristo, kwa kutumia propanganda ya udanganyifu wa jinsi hii, umefaulu kwa kiwango kikubwa kupanua uwanja wa athari zake miongoni mwa Waafrika ambao humo umeweka mkakati wa propaganda yake na wanafurahi sana lakini hawatambui ukweli kwamba makanisa ya Kikristo yalikuwa washiriki wenye bidii sana kwenye "African Slave Trade" (biashara ya utumwa ya Kiafrika). Sura zifuatazo zitaonye-sha picha ya kweli kwa wasomaji.

Mnamo mwaka wa 1492, ambapo Columbus, akiwakilisha ufalme wa Hispania aligundua "New World" (Dunia mpya), alianzisha mfululizo mrefu na mchungu wa ushindani wa kimataifa katika kujipatia makoloni, ambao hadi sasa baada ya karne nne na nusu, hakuna suluhu iliyopatikana. Ureno, ambayo ndio iliasisi kitendo cha kujipanua kimataifa, ilidai hizo nchi mpya kwa hoja ya kwamba zilikuwa kwenye eneo la madaraka ya amri ya baba mtakatifu (papal bull) wa 1455 inayowaruhusu wareno (ambao ni Wakristo) kuwafanya watumwa wapagani wote. Katika kujaribu kuepuka ubis-hani, mamlaka hizi mbili, zilitafuta suluhisho, na kwa sababu zote zilikuwa katika madhehebu ya Ukatoliki, zil-imwelekea Baba Mtakatifu - hatua ambayo ilikuwa ya kawaida na ya mantiki katika kipindi ambapo madai ya wakati wote ya Kipapa yalikuwa bado hayana upinzani ama kutoka kwa mtu binafsi au serikali ya nchi. Baada ya kuchunguza kwa makini madai ya washindani, Baba Mtakatifu, katika mwaka 1493, alitoa mfululizo wa amri za kipapa ambazo ziliweka mipaka ya kuaua kati ya makoloni yanayomilikiwa na dola hizo mbili za Ulaya: Mashariki ilichukuliwa na Ureno na Magharibi ilichukuliwa na Hispania. Mgawanyo huo, hata hivyo, haukukidhi mategemeo ya Ureno na mwaka uliofuata washindani hao wawili walifanikiwa kuhitimisha mwafaka wa maridhiano zaidi kwenye Mkataba wa Tordesillas ambao ulirekebisha uamuzi wa Baba Mtakatifu kuiruhusu Ureno kumiliki B 106. Williams, Dk. Eric, Capitalism and Slavery (London, 1964) P. 4. kama koloni lake.

Lakini maamuzi haya hayakuweza kuzifunga mamlaka zingine ambazo zilikuwa zina wania kunyakua makoloni mengi iwezekanavyo; Uingereza, Ufaransa, na hata Uholanzi zilianza kudai sehemu zao (makoloni) hapa duni-ani. Mtu mweusi, pia, alikuwa apate sehemu yake, licha ya kwamba hakuomba; ilikuwa uanzishwaji na upanukaji wa mashamba makubwa ya miwa, tumbaku na pamba ya ulimwengu Mpya. "Kwa mujibu wa Adam Smith, maendeleo ya koloni jipya yalitegemea jambo moja rahisi la kiuchumi- 'ardhi pana yenye rutuba.' Hata hivyo, umiliki wa makoloni wa Uingereza hadi 1776, kwa ujumla unaweza kugawanywa katika aina mbili. Aina ya kwanza ni wakulima wadogo wanao jitosheleza na kushughulika na uchumi wa bidhaa mbalimbali. Aina ya pili ni koloni ambalo limesheheni hali iwezeshayo mtu kuzalisha bidhaa kuu mbali mbali kwa wingi kwa madhumuni ya kuuza nje. Katika aina ya kwanza, yalikuwemo makoloni ya Kaskazini ya bara la Marekani; katika aina ya pili, yalikuwepo makoloni ya tumbaku na visiwa vya miwa vya Caribbean. Kwenye makoloni; ardhi na mtaji havikuwa na manufaa bila ya kuwepo nguvu kazi ya musuli. Kibarua, lazima awepo wakati wote na lazima afanye kazi, au ahimizwe kufanya kazi, katika kundi moja. Bila ya sharti hili, kibarua angeamua kuwa na mwelekeo wake binafsi na kufanya kazi katika ardhi yake mwenyewe. Hadithi moja inasimuliwa mara nyingi kuhusu kabaila mmoja wa Uingereza, Bwana Pell, ambaye alichukua pauni za Kiingereza elfu hamsini (50,000) na vibarua mia tatu akaenda nao kwenye koloni la Swan River huko Australia.

Mpango wake ulikuwa kwamba vibarua hao wangefanya kazi kwake, kama iliyvokuwa Uingereza. Bwana Pell akawasili Australia ambapo ardhi ilikuwa pana sana vibarua wakapendelea kufanya kazi kwenye mashamba yao madogo kwa manufaa yao kama wamiliki wadogo, badala ya kufanya kazi chini ya kabaila kwa kulipwa ujira. Austaralia haikuwa Uingereza, na kabaila huyo alibaki hana mtumishi wa kumtandikia kitanda au wa kumchotea maji." CHIMBUKO LA WATUMWA WEUSI "Ni njia ya kuchukiza," ingawa inaweza kuwa hivyo, kama Merivalle alivyoiita, utumwa ulikuwa taasisi ya kiuchumi yenye muhimu wa kwanza. Utumwa ulikuwa ndiyo msingi wa uchumi wa Ugiriki na ukajenga Ufalme wa Kirumi. Katika zama hizi utumwa ulizalisha sukari kwa ajili ya chai, na vikombe vya kahawa vya dunia ya Magharibi. Ulizalisha pamba ikiwa ndiyo msingi wa Ukabaila mambo leo. Utumwa ulijenga Marekani (US) ya Kusini na visiwa vya Caribbean."108. "Ulaya ikiwa na watu wachache katika karne ya kumi na sita, hivyo kwamba, vibarua wa kulima bidhaa muhimu kama miwa, tumbaku na pamba katika Dunia Mpya hawangepatikana kwa idadi ya kutosheleza kuruhusu uzal-ishaji wa kiwango kikubwa. Utumwa ulikuwa muhimu kwa lengo hili na ili kuweza kuwapata watumwa, wazungu walianza kwanza kuwatumia Waaborigine kama watu- 107. Ibid uk. 4-5 108. Ibid 109. Ibid, uk. 6 Lakini utumwa wa Kihindi kamwe haukuwa mkubwa kwenye makoloni ya Uingereza... Kwa upande wa Wahindi... utumwa ulionekana kama jambo lilotokealo mara chache, kama kinga ya adhabu na si kama ndiyo hali ya kawaida na ya kudumu. Katika makoloni ya New England, utumwa wa Wahindi haukuwa na faida, kwani utumwa wa aina yoyote ulikuwa hauna faida kwa sababu haukustahili kwenye kilimo cha mazao mbalimbali ya makoloni haya. Juu ya haya, mtumwa wa Kihindi alikuwa hawezi kufanya kazi kwa bidii. Wahispania waligundua kwamba mtumwa mweusi mmoja alikuwa sawa na watumwa wanne wa Kihindi. Afisa mmoja mashuhuri wa Hispaniola alisisitiza mnamo mwaka 1581 kwamba itolewe ruhusa ya kuwaleta watu weusi, jamii iliyo kakamavu kwa kazi badala ya wazawa ambao ni dhaifu sana hivyo kwamba wanaweza kuajiriwa kwenye kazi ndogo zisizo hitaji matumizi ya nguvu nyingi kama vile kutunza mashamba ya mahindi.... Bidhaa za siku za usoni za "New World," yaani miwa na pamba, zilihitaji nguvu ambazo watumwa wa Kihindi walipungukiwa na wakataka "mtu mweusi wa pamba" aliye mkakamavu kama ambavyo miwa inahitaji nyumbu wenye nguvu ambao hupatikana Louisiana, wenye kisifa cha jina la 'nyumbu wa sukari.' Kwa mujibu wa Lauber, inapolinganishwa kiasi cha malipo kilichotolewa kwa mtu mweusi (Mnegro) kwa wakati huo huo na kwa mahali hapo hapo, utaona kwamba bei za watumwa wa Kihindi zinaonekana kuwa za chini mno.

Wingi wa nguvu kazi ya Kihindi, pia, ilikuwa ndogo, ambapo vibarua wa Kiafrika walikuwa hawaishi. Kwa hiyo, watu weusi (Manegro) waliibiwa kutoka hapa Afrika kwen-da kufanya kazi kwenye ardhi, iliiyoporwa (na kuibiwa) kutoka kwa wazalendo wa Kihindi (Wahindi wekundu) huko Marekani. Misafara ya baharini ya Prince Henry the Navigator (Mfalme Henry Baharia mvumbuzi) ilikamilisha ile ya Columbus, historia ya Afrika ya Magharibi ikawa kamilisho la historia ya West Indians." (Wahundi wa Magharibi)110.

WAKRISTO WANAPANGA BIASHARA YA UTUMWA

Watumwa walikuwa wanachukuliwa kutoka hata katika wakati wa Ufalme wa Kirumi, lakini "biashara halisi ya Utumwa" ilianza mnamo karne ya 16 baada ya ujio wa mataifa ya Kikristo ya Ulaya. Edward A. Alpers wa Chuo Kikuu cha Dar- es Salaam, anaandika kwamba; "kama tunavyoleta utofautisho baina ya biashara inayoambatana katika watumwa ambayo ilichuruzika katika sahara kutoka magharibi mpaka kaskazini ya Afrika kuanzia siku za nyuma sana za wakati wa utawala wa Ufalme wa Kirumi, kwa upande mmoja, na kioja tunacho kiita The West African Slave Trade kwa upande mwingine, kwa hiyo lazima tulete tofauti hiyo hiyo kwa Afrika ya Mashariki." 111 Walter Rodney pia wa Chuo, Kikuu cha Dar es Salaam, anaanza kuandika kijitabu chake "West Africa and the Atlantic Slave-Trade kwa maneno yafuatayo: - Wakati wote lazima ikumbukwe kwamba biashara ya utumwa iliyo;fanyi-ka katika bahari ya Atlantiki" lilikuwa ni tukio katika historia ya dunia, iliyo husisha mabara matatu - Ulaya, Afrika na Marekani. 110. Ibid, UK. 8-9 111. Alpers, Edward A., East Africa Slave-Trade (Dar-es-Salaam: The Historical Association of Tanzania, 1967) Watu walio toka kwa dhamira ya kutafuta watumwa walikuwa Wazungu waliotoka katika kila nchi kati ya Sweeden kwa upande wa Kaskazini na Ureno kwa upande wa magharibi. Wareno walifika Afrika ya Magharibi muda mfupi kabla ya kuingia nusu karne ya kumi na tano. Mara moja na kwa haraka sana walianza kukamata (watumwa) Waafrika na kuwapeleka kufanya kazi Ulaya kama watumwa, hususan katika Ureno na Hispania. Lakini maendeleo muhimu sana kwa biashara hii ya utumwa yalikuwa katika karne ya kumi na sita, ambapo mabepari wa Kizungu walitambua kwamba wangepata faida kubwa sana kwa kutumia nguvu-kazi ya Waafrika kuujenga na kuuen-deleza utajiri wa nchi zote za Amerika. Matokeo yake, Waafrika walipelekwa Amerika ya kaskazini, Amerika ya kati, Amerika ya kusini na Visiwa vya Caribbean kwa ajili ya kukidhi haja ya nguvu-kazi ya watumwa kwenye machimbo ya dhahabu na shaba, na kwenye mashamba ya kilimo cha mazao ya miwa, pamba na tumbaku. Biashara hii mbaya ya kununua na kuuza binadamu ilidumu kwa kipindi cha miaka (400) mia nne, kwani Atlantic slave-Trade (Biashara ya Utumwa wa kupitia bahari ya Atlantiki) ilikoma mwishoni mwa miaka ya 1870.

"Mambo mengi yanaweza kusemwa kuhusu jinsi Biashara ya Utumwa katika bahari ya Atlantiki ilivyopangwa huko Ulaya, na kuhusu faida kubwa iliyokusanywa na nchi kama Uingereza na Ufaransa. Mambo mengi yanaweza kusemwa kuhusu safari za kutisha kutoka Afrika hadi Marekani kuvu-ka bahari ya Atlantic. Waafrika walipangwa kama dagaa kwenye meli za kubeba watumwa, na matokeo yake walik-ufa wengi sana." 112. 112. Rodney, Walter., West African and the Atlantic slave-trade (Dares-Salaam: The Historical Association of Tanzania, 1967) Na dagaa walioje! Kwa maelezo zaidi kuhusu upakiaji huu wa watumwa kwenye meli, soma taarifa ifuatayo: -Moja ya hati yenye kuuvunja moyo sana katika nyaraka zote zinazotisha ni "Plan of the Brookes," mpango mbaya sana wa karne ya kumi na nane wa kupanga watumwa kwenye meli ya kubeba watumwa 'Brookes'... Kwa mahesabu sahi-hi, teknolojia ya kushtua ilitengenezwa - futi na inchi, chumba cha kusimama na nafasi ya kupumua iliwekwa kwa matumaini ya faida kubwa. Mtu mmoja Bwana Jones anapendekeza kwamba wanawake watano wahesabiwe kama wanaume wanne, na wavulana watatu au wasichana watatu wafanywe kuwa sawa na watu wazima wawili kila mtumwa mwanaume aruhusiwe futi sita kwa futi moja na inchi nne (1'4"x6') kama nafasi ya chumba chake, kila mwanamke alipewa nafasi ya upana wa futi tano na inchi kumi na futi moja na inchi nne.... (5'10"x1'4"); na inaen-delea hivyo mpaka kila mtu anapata nafasi - watumwa 451. Lakini Muswada wa Bunge unaruhusu watumwa 454. Kwa hiyo hati hiyo inahitimisha kwamba kama watumwa watatu zaidi wangeweza kuwekwa kwa kubanwa katikati ya wale waliotamkwa kwenye mpango, mpango huu ungeweza kuchukua idadi ile ile ambayo imeelekezwa kwenye muswada. 113.

Mara Waafrika walipofikishwa upande mwingine wa bahari ya Atlantic, kwa hakika walikuwa katika "Dunia Mpya", iliyojaa ukandamizaji na ukatili. Taarifa ifuatayo inaweza kusaidia kuelewa hali ilivyokuwa wakati huo. Rodney anaandika: 113. Newsweek (March 15, 1965) uk. 106 "Kuanzia wakati walipofika (Wakristo) Wazungu hadi 1600, takriban Waafrika milioni moja (1, 000,000) walichukuliwa kwenye meli za kubeba watumwa. Wakati wa kipindi hicho, Wareno walikuwa ndio wafanya biashara wakuu wa biashara ya watumwa huko Afrika ya Magharibi. Ama wali-wapeleka Waafrika huko Brazil, ambayo nchi hiyo ilikuwa koloni lao, au vinginevyo waliwauza kwa waloezi wa Kihispania huko Mexico, Amerika ya kati, Amerika ya Kusini na visiwa vya Caribbean. Mnamo karne ya kumi na saba, kiasi cha Waafrika wapatao milioni saba hadi nane kutoka Afrika ya magharibi walivushwa bahari ya Atlantic. Wadachi walijumuika na Wareno kama wafanya biashara wakuu wa biashara ya utumwa mnamo karne ya kumi na saba, na karne iliyofuata Waingereza wakawa wafanya biashara wakubwa kushinda wote wa biashara ya utumwa. Wakati biashara ya Utumwa katika bahari ya Atlantiki ilipofikia kileleni mnamo karne ya kumi na nane, meli za Kiingereza zilikuwa zinachukua zaidi ya nusu ya jumla yote ya watumwa na idadi iliyobaki iligawanywa baina ya Wadachi, Wafaransa, Wareno na Wadane (Danish).

"Ilipofika karne ya kumi na tisa, palikuwepo na mabadiliko mengine ya watu ambao walishika nafasi mbele katika kuinyonya Afrika. Nchi za Ulaya zenyewe hazikushiriki kikamilifu kwenye biashara ya utumwa, lakini badala yake Wazungu ambao waliloea Brazil, Cuba, na Amerika ya Kaskazini ndio ambao walipanga sehemu kubwa ya biashara. waamerika (U.S.A) ndiyo katika kipindi hicho hicho tu walipata uhuru kutoka kwa Waingereza, hili lilikuwa taifa jipya (U.S.A.) ambalo lilikuwa na mgawo mkubwa kabisa kuliko wote katika biashara ya watumwa katika biashara ya Atlantiki katika kipindi cha miaka hamsi-ni ya mwisho, kwa kuchukua kiwango kikubwa zaidi cha watumwa kuliko ambavyo imewahi kufanya huko nyuma. "Ilipoanza "biashara ya watumwa ya Atlantiki kwenye pwani ya Afrika ya Magharibi, ilichukua utaratibu wa kutu-mia nguvu moja kwa moja wa Wazungu kuwashambulia Waafrika waliokuwa wanaishi karibu na pwani. Mabaharia wa kwanza wa Kireno walipofika kwenye pwani inayoju-likana leo kama Mauritania, waliacha meli zao na kuanza kuwawinda watu waitwao, Moors watu walioishi katika jimbo hilo. Kwa kweli, hii haikuwa biashara hata kidogo -ilikuwa uvamizi wa nguvu. Hata hivyo, baada ya masham-bulizi kadhaa ya kushtukizwa, Waafrika wa pwani wakawa na kawaida ya kulinda kwa zamu na walijilinda kwa nguvu dhidi ya washambuliaji wao Wazungu. Katika kipindi kifupi tu, Wareno walitambua kwamba uvamizi haikuwa mbinu inayofaa na iliyo salama katika kujaribu kuwapata watumwa. Zaidi ya hayo, pia walitaka dhahabu na bidhaa zingine za Kiafrika, ambazo wangeweza tu kuzipata kwa njia ya kununuliana na kuuziana kwa amani.

Kwa hiyo badala ya kuvamia, Wareno waliona afadhali kutumia bidhaa zilizo tengenezwa kiwandani ili kuwatia moyo Waafrika kubadilishana na bidhaa zao na hata kuweza kuwafikisha mateka wa Kiafrika kwenye meli za Wazungu kwa urahisi. Mpango huu haukufanywa na Wareno pekee, lakini hata wazungu wengine wote walitambua na kukubali kwamba huo ulikuwa mpango mzuri zaidi wa kupata bidhaa hapa Afrika; na ilikuwa kwa njia hii waliweza kupata mamilioni mengi ya Waafrika." 114 114. Rodney, op. cit., uk.4-5 Akifafanua juu ya kipengele hiki cha biashara ya watumwa, mwandishi anasema: "Moja ya vitu muhimu sana ni kutam-bua jambo liumalo sana na lisilo pendeza kwamba walikuwepo Waafrika ambao waliwasaidia na kushirikiana na Wazungu katika kuwafanya Waafrika wenzao kuwa watumwa. Maana yake ni kwamba hatuwezi kuchukua msi-mamo dhaifu na kusema kwamba watu weupe walikuwa wabaya sana na watu weusi walikuwa waathirika (katika kuangamia). Mfano unaofaa na sambamba ambao ungeweza kusaidia kuelewa yale yaliyotokea katika Afrika ya Magharibi wakati wa kipindi cha karne za biashara za watumwa unaweza kuonekana hapa Afrika leo, ambapo viongozi wengi wanashirikiana na mabeberu wa Ulaya na Marekani (U. S. A.) kwa lengo la kuwanyonya na kuwakan-damiza Waafrika walio wengi.

Hatimaye, Waafrika wa Afrika ya Magharibi walifikishwa kwenye hali ya "uza au uuzwe." Hapa suala la bunduki lilikuwa na umuhimu maalum. Kuwa na nguvu, serikali ili-hitaji bunduki, lakini ili kupata bunduki kutoka kwa wazungu, Waafrika ilibidi kuwapa Wazungu watumwa na wao kupewa bunduki. Watawala wa Kiafrika walijikuta wenyewe wanawauza watumwa ili wapate bunduki ambazo ziliwawezesha kuwakamata raia wao na kuwauza kama watumwa ili wanunue bunduki nyingi zaidi. Hali hii inaweza kuelezewa, kama "ubaya juu ya ubaya (mzun-guuko unaoashiria kukwama)." Watawala wa Kiafrika ambao waliwasaidia wazungu hawasameheki moja kwa moja, lakini inafafanua jinsi gani mwishoni hawakuwa washirika halisi wa Wazungu bali walikuwa watumishi au vibaraka wa Wazungu." 11 116. Ibid, uk. 7f.

Na kanisa lilikuwa linafanya nini wakati wote huo? Msikilize mwandishi huyu huyu anasema; "Kwa sababu faida kubwa sana ilikuwa inapatikana kwa kuwachukua watumwa kutoka Afrika, Wazungu walikataa kuzisikiliza dhamiri zao. Walifahamu kuhusu mateso yaliyo wapata watu katika Afrika, ndani ya meli za kubebea watumwa na kwenye mashamba yaliyokuwa yanalimwa na watumwa ya Waamerika, na walitambua kwamba kuwauza binadamu wenzao ni jambo ambalo halingethibitishwa kimaadili. Hata hivyo kanisa la Kikristo lilijitokeza na kutoa sababu nyingi likijitetea kuingia kwake katika biashara ya watumwa. Wachungaji wengi walifanya biashara ya watumwa, hasa katika Angola, na wengine wengi walimili-ki watumwa, katika nchi za Amerika. Sababu moja tu ambayo ilitolewa na kanisa Katoliki kuhusu vitendo vyake ilikuwa kwamba lilikuwa kinajaribu kuziokoa roho za Waafrika kwa kuwabatiza watumwa. Waprotestanti walikuwa wabaya zaidi, kwani wala hawakuweka wazi kwamba walikubali kwamba Waafrika walikuwa na roho. Badala yake, walikubaliana na fikira kwamba mtumwa wa Kiafrika alikuwa sehemu ya rasilimali kama fenicha au hayawani wa kufugwa. Hakuna sehemu ya historia ya Kanisa la Kikristo ambayo inafedhehesha zaidi kuliko kusaidia "Biashara ya Utumwa katika Bahari ya Atlantiki."116. Kwa mujibu wa orodha ya Lloyd, iliamuliwa kwamba watumwa walikuwa ni bidhaa, na wenye thamani sana. Hati za bima zilizochukuliwa kutoka Lloyd waliwakatia watumwa hati za bima hadi kufika kiasi cha pauni za Kiingereza 45 kila mtumwa - kiasi hicho cha fedha ni kikubwa katika kipindi hichi cha mwanzoni mwa karne ya 116. Ibid uk.22. 18 huko Uingereza.

Ili kuwazuia watumwa wasitoroke, au kuwaadhibu, nyenzo zisizo za kawaida kama zilivyoorodheshwa hapa zilitumiwa katika Afrika ya Magharibi na katika visiwa vya West-Indies. 117. Siku zote kulikuwepo watu wachache ambao walipinga Biashara ya Utumwa katika Bahari ya Atlantiki. tangu mwanzo; lakini serikali mbalimbali na wafanya biashara hawakuwajali, wakati wa karne ya kumi na tano, kumi na sita na kumi na saba. Haikuwa hivyo, hadi mwishoni mwa karne ya kumi na nane wakati majaribio ya dhati yalifanywa kwa lengo la kukomesha biashara hii. James Boswell, akijaribu kukana hoja za watu waliotaka biashara ya watumwa ikomeshwe, anaandika katika kitabu chake kiitwacho "Life of Johnson." Kwamba: Jaribio la kinyama na la hatari ambalo kwa muda fulani limeendelea kuwepo kwa lengo la kupata sheria ya bunge letu, ili kukomesha tawi la maana sana na muhimu la faida kibi-ashara, lazima lingekwisha amuliwa mara moja, kama isin-gelikuwa kundi lisilo na maana la washabiki waliokuwa msitari wa mbele kwalo bila kufaulu, ndilo ambalo linaunda kundi kubwa la Wakulima, Wafanya biashara na wengineo ambao rasilimali yao imetumbukizwa na kuhusishwa kwenye biashara hiyo, kwa sababu zao kujikinaisha, hufikiria kwamba hapangekuwepo na hatari. 117. Lloyd's list, 250th Anniversary (1734-1984) April 17,1984, London, uk. 149.

Ujasiri ambao jaribio hilo limepata msisimko mshangao wangu na hasira, na ingawa watu fulani wenye uwezo mkubwa wameliunga mkono, ama kwa sababu ya kutaka umaarufu wa muda mfupi, wakati wanao utajiri, au kupenda kujumuika kwenye fitina, wakati hawana kitu, maoni yangu hayatetereki. Kukomesha hali ya kuwepo utumwa ambayo katika zama zote, MUNGU ameruhusu, na binadamu akaen-deleza, haingekuwa unyang'anyi tu kwa tabaka la raia wetu wasio hesabika; lakini pia ingekuwa ukatili mno kwa Washenzi wa Kiafrika, ambao sehemu kutoka miongoni mwao inaokolewa kutoka kwenye mauaji ya kinyama, au kutoka kwenye utumwa isiyovumilika katika nchi yao wenyewe, na huwaingiza kwenye maisha ya hali ya furaha zaidi, hasa zaidi sasa kupita kwao kwenda katika visiwa vya West-Indies na wanavyotendewa huko katika hali ya udhibiti wa kibinadamu. Kukomesha biashara hiyo itakuwa sawa na kufunga milango ya huruma kwa binadamu."H -Marekebisho ya takrima ya kibinadamu wanayofanyiwa na huruma, hujionyesha yenyewe kwenye maelezo ya kina na picha iliyoonyeshwa hapo juu!