UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI0%

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI Mwandishi:
: SHEIKH MUSABBAH SHA'ABANI
Kundi: Vitabu mbali mbali

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

Mwandishi: SHEIKH JA'AFAR SUBHANY
: SHEIKH MUSABBAH SHA'ABANI
Kundi:

Matembeleo: 48407
Pakua: 4205

Maelezo zaidi:

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 24 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 48407 / Pakua: 4205
Kiwango Kiwango Kiwango
UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

Mwandishi:
Swahili

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

KIMEANDIKWA NA SHEIKH JA'FAR SUBHANI

KIMETAFSIRIWA NA MUSABBAH SHAABANI MAPINDA

KIMETOLEWA NA AHLUL BAYT ASSEMBLY OF TANZANIA

Dar es Salaam - Tanzania

MUHTASARI

Afrika ya Mashariki imefaidi mazingira ya amani sana kiasi cha karne mbili zilizopita. Watu wa imani na itikadi zote waliishi pamoja kwa upendo na mapenzi. Kila mmoja akishiriki kwenye shughuli za mwenzake za kijamii na za Kidini. Ukiangalia kwenye Jumuiya za Kiislamu, wote wakihudhuria kwenye Misikiti ya kila mmoja, waliungana pamoja katika Maulidi na hafla za Muharram, na kupanua ushirikiano wao katika miradi ya kila mmoja. Kama Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi alivyosema katika hotuba moja ya hadhara; "Misikiti mingi ya Waislamu wa (Madhehebu ya) Shafi'i iliyoko Zanzibar na Pemba ilijengwa na kutolewa na Shia Ithna-ashariyya" Hatimaye Wahhabi walianza Tabligh (Mahubiri) yao hapa. Badala ya kujaribu kuwaleta mapagani au wasio waislamu kwenye boma ya Uislamu, nia yao kabisa ilikuwa na bado inakaziwa katika kuwabadilisha Mashafii wawe Mawahabi. Kwa lengo hili, hujifanya kama wao ni Masunni, na kuchanganyika pamoja na Masunni. Mawahabi hao wamepanda mbegu ya fitina na chuki kati ya Madhehebu mbali mbali za Kiislamu, na hususan kati ya Sunni na Shia. Wanazungumza dhidi ya Shia, na kusambaza vitabu na vijitabu (vya mambo ya dini) dhidi ya itikadi ya Shia ambavyo vimejaa mambo ya uwongo na uzushi. Kishawishi chao kiko wazi, kwa kuwatenganisha Masunni na Mashia, wakitumaini kupata urahisi wa kuingia katika jamii ya Sunni na Misikiti yao, ingawaje tumaini hili lingali bado kukamilishwa katika Tanzania.

Hebu tuangalie katika mzizi wa uovu wa kampeni hii. Huenda hapo nyuma katika mwaka 1979, ambapo Mapinduzi ya Ki-Islamu yalipotokea katika nchi ya Iran, na watawala wa Kiwahaabi wa Saudia walihadharishwa vikali mno, hata kabla ya tukio la Mapinduzi ya Kiislamu, wakati Ayatullah al-'uzma al-Khomeini (r.a.) akiwa bado Najaf (Iraq). Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Saudi Arabia, akizungumza katika hadhara moja ya Waarabu, aliuonya ulimwengu wa Waarabu kwamba kama Khomeini ataruhusiwa kuendeleza harakati zake kutoka Iraq kama hapo nyuma, sio tu kwamba utawala wa Shaha utaangushwa, lakini, hali katika eneo lote vile vile itakuwa imetibuliwa. Hivyo wakaishinikiza Iraq kuweka vikwazo juu ya Khomeini kwa hofu ya kwamba, kama juhudi zake zitafanikiwa katika Iran, zitatingisha tawala zao wenyewe zisizo imara. Haikushangaza kwamba mara tu Mapinduzi ya Kiislamu yalipoimarika nchini Iran, hawa Wahhabi wakuanza propoganda kali yenye chuki dhidi ya Khomeini, dhidi ya Iran na dhidi ya Ushia. Kalamu za kukodisha zikuanza mchakato kutoa vitabu, makala na vijitabu (vya mambo ya dini) dhidi ya Shia. Shia waliitwa Makafiri, na pengine mtu angeuliza: Kama ni Makafiri, basi kwa nini wanapewa viza kwa ajili ya Hija na Umra? Wairani waliitwa Majus (Waabudu Moto) kwa nini? Kwa sababu kabla ya kuja kwa Uislamu waliabudu moto. Kwa hoja hii nasi hatuna haki ya kuwaita Wahhabi Mushrikuna? Kwa sababu kabla ya kuja kwa Uislamu wata wa Najd walikuwa wakiabudu Masanamu.

Baadhi ya waajiriwa wao wa ngazi za juu walikuwa ni (marehemu) Ihsan Ilahi Zaheer wa Pakistan, na Manzoor Ahmad Nu'mani na Abul Hasan Ali Nadwi wa India. Sauti itokayo kwenye vinywa vyao ni katika watakiwayo na mabwana zao kuyasema, na jambia la uzayuni lilichovywa kwenye damu ya waislamu linatumika kama kalamu yao. Kitabu kinachoandikwa dhidi ya Shia na watumwa hawa, kwa miezi michache tu kinatarujumiwa katika lugha zote kubwa za ulimwengu wa Kiislamu; na hufanywa kipatikane kila mahali, kadhalika husambazwa bure miongoni mwa Mahujaji: Nimeandika majibu kwa kitabu kimoja kama hicho, ambacho kilichapishwa katika mwaka 1994 nchini Tanzania na Marekani kwa jina la "Wahhabi's Fitna Exposed". Kimevunja habari za uwongo wao wote na masingizio yasiyo na msingi dhidi ya Shia. Tarjuma yake ya Kiswahili (Fitina za Wahhabi Zafichuliwa) imechapishwa na Bilal Muslim Mission of Tanzania, Dar es Salaam.

Bado inahisiwa haja ya kuweko kitabu katika sehemu hizi za ulimwengu ambacho kitaangalia katika mawazo yote na mafundisho ya Uwahhabi na kushughulika nayo katika mwanga wa Qur'an na Hadithi, ili kufichua uwongo na itikadi yao na mtizamo wao juu ya vita vitakatifu vya Kiislamu. Ahlul-Bayt(a.s) Assembly of Tanzania, ina furaha kutoa kitabu kama hiki kwa wata wazungumzao Kiswahili. Nimechagua kwa ajili ya madhumuni haya kitabu (kitwacho) "Al-Wahhabiyah Fil-Mizan" kilichoandikwa na Mwanachuoni mashuhuri wa dini na mtunzi, aitwaye Shaykh Ja'far Subhani, Profesa wa Chuo cha dini Qum (Iran). Kitabu hiki kwa hakika (bila kupendelea) kinaangalia katika hoja zote zilizotolewa na Wahhabi na kutahini kusihi kwake kutoka kwenye Qur'an na Sunnah.

Shaykh Musabbah Shaabani Mapinda, wa Dar-es-Salaam kwa ushauri wangu amefanya tarjuma ya kitabu hiki kutoka Kiarabu kwenda kwenye Kiswahili, kinachoitwa "Uchunguzi juu ya Uwahhabi". Nimekikagua kwa utaratibu ili kuhakikisha kwamba mafuhumu ya Kiarabu kwa uaminifu na ukweli yametolewa kwenda kwenye Kiswahili. Hiki ni kitabu cha kwanza cha "Ahlul-Bayt(a.s) Assembly of Tanzania", na nina fahari kwa kushirikishwa katika kila hatua. Namuomba Allah Subhanahu Wa Ta'ala atoe malipo yake kwa Mtunzi, mtarjumi na wale wote ambao wamesaidia katika kuchapishwa kwake kwa njia yoyote ile. Wa Ma Tawfeeq Illa Billah

Syed Saeed Akhtar Rizvi

Mwenyekiti,

Ahlul-Bayt (A.S.) Assembly

P.O. Box 75215,

Dar- es- Salaam, Tanzania

UCHUNGUZI JUU YA UWAHABI

UTANGULIZI WA CHAPA YA KWANZA

KUHUSU MAWAHABI NA ITIKADI ZAO

Shukurani zote Anastahiki Mwenyezi Mungu ambaye ni Mtangu na hapana kitu kilichokuwepo kabla yake, naye ndiye wa mwisho hapana baada yake chochote. Na yeye ni dhahiri hapana kilicho dhahiri kuliko yeye, naye ni batin hapana kilicho Batin kuliko yeye. Na Sala na Salamu zimshukie Mtume wake na mbora wa viumbe wake ambaye alimtuma katika kipindi ambacho watu walikuwa ndani ya upotevu wakihangaika na wamezama ndani ya Fitna, na wametekwa na matamanio yao na wamepotoshwa na ujeuri na akili zao zimepotoshwa na Ujahili uliopita kiasi, wakihangaika katika mambo yaliyovurugika na balaa linalotokana na ujinga, basi Mtume[s .a.w.w ] akatoa nasaha kwa upeo, akaitengeneza njia na akalingania kwa hekima na mawaidha mazuri.

Mwenyezi Mungu alimtuma kuitimiza ahadi yake na kukamilisha Utume wake. Alichukua ahadi yake toka kwa Manabii na alama zilikuwa Mashuhuri na mazazi yake yalikuwa matukufu hali ya kuwa walimwengu katika zama hizo wakiwa na mila tofauti tofauti, na fikra mbali mbali na ni vikundi vingi wakiwemo wanaomshabihisha Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake au walikuwa wakifanya kufuru na shiriki katika jina lake au wakimuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Basi Mwenyezi Mungu akawaongoa kupitia kwa Mtume[s.a.w.w] kutoka kwenye upotovu na akawaokoa kutokana na ujinga kwa njia yake na ni nguzo ya dini yake. Na Rehma za (Mwenyezi Mungu) zimshukie Mtume na kizazi chake (watu) ambao ndiyo wa ndani wake na ni tegemeo la dini yake na ni chombo cha elimu yake, na ni rejea ya hekima zake na ni hazina ya vitabu vyake.

Kwao wao Mwenyezi Mungu aliimarisha dini yake, na ni watu ambao Mwenyezi Mungu amewaondoshea uchafu na kuwatakasa mno. Na (Pia) ziwashukie Masahaba wake ambao waliisoma Qur'an na wakazitumia hukmu zake na wakazizingatia faradhi kisha wakazisimamisha. Waliihuyisha Sunna na kuuwa Bid'a, walilinganiwa kwenye jihadi wakaitika, na walimuamini kiongozi wao (ambaye ni Mtume[s.a.w.w] , kisha wakamfuata. Wamekutana na Mwenyezi Mungu na akawalipa ujira wao, na amewapa makazi ya amani baada ya khofu waliyokuwa nayo, waliendelea katika njia ya Dini na wakaifuata haki, Rehma ziwashukie daima milele muda wote wa kudumu mbingu na ardhi. Amma baad, bila shaka umma wa Kiislamu tangu mwanzoni umeshikamana juu ya Tauhudi katika nyanja zake mbali mbali, ukaafikiana juu ya kuipwekesha dhati ya Mwenyezi Mungu na kwamba, yeye ni mmoja hana mshirika wake na ni mpweke hana mfano. Kama ambavyo umeafikiana ya kwamba, yeye ni uumba na hapana muumba asiyekuwa yeye. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Je, kuna muumba asiyekuwa Mwenyezi Mungu " Qur'an, 35:3.

Na Amesema tena: "Waambie, Mwenyezi Mungu ndiye muumba wa kila kitu " Qur'an, 13:16.

Vile vile umekubaliana juu ya Tauhidi yake katika Rububiya yake na kwamba hapana Mola wala mwenye kusimamiya (mambo yao) asiyekuwa yeye. Amesema Mwenyezi Mungu: Yeye ndiye anayesimamia mambo yote hakuna muombezi ila baada ya idnini yake, huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu basi muabuduni yeye, Je, hamna kumbukumbu? Pia wamekubaliana kempwekesha Mwenyezi Mungu katika Ibada na kwamba, yeye Mwenyezi Mungu ndiye Mola ambaye anastahiki kuabudiwa na hukuna wa kuabudiwa asiyekuwa Yeye. Mwenyezi Mungu Amesema:

قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ تَعَالَوْا إِلَىٰ كَلِمَةٍ سَوَاءٍ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ أَلَّا نَعْبُدَ إِلَّا اللَّـهَ وَلَا نُشْرِكَ بِهِ شَيْئًا وَلَا يَتَّخِذَ بَعْضُنَا بَعْضًا أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَإِن تَوَلَّوْا فَقُولُوا اشْهَدُوا بِأَنَّا مُسْلِمُونَ ﴿٦٤﴾

"Waambie, Enyi mliopewa Kitabu, njooni kwenye neno lililo sawa kati yetu na ninyi ya kwamba, tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, na wala tusimshirikishe na chochote, wala baadhi yeta tusiwafanye kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu". Qur 'an, 3:64.

Bali hizi ndizo nukta ambazo zenye kuafikiana baina ya sheria zote za mbinguni, na yote haya yanaonekana kuwa ni miongoni mwa mambo ya kipekee kwa baadhi ya wafuasi wa sheria zilizopita. Basi mtazamo uliyo kinyume na misingi hii ni miongoni mwa vitendo vya uchafuzi na kupotosha vinavyotokana na wanachuoni, Watawa na Makasisi (wao).

MAWAHABI NA MSIMAMO WAO KWA UNDANI KATIKA QADHIYYAH ZA TAUHID

Cha ajabu, (na midhali uhai utona maajabu zaidi) in kwamba, Uwahabi unatokana na fikia ya Sheikh mpotofu aitwaye Ibn Taimiyyah ambaye ametuarifisha maana ya Tauhidi katika kitabu chake aliposema: "Hakika Mwenyezi Mungu yuko juu ya mbingu yake kwenye arshi yake, yuko juu ya viumbe wake".[1] Na amesema tena: "Mola wete hushuka mpaka kwenye mbingu ya dunia kila siku inapobakia theluthi ya mwisho ya usiku kisha husema; Nani ataniomba (saa hizi) nami nitamkubalia (maombi yake) nani ataniomba nami nitampa, ni nani atanitaka msamaha nami nitamsamehe".[2] Haya ndiyo maarifa ya mtu huyo (Ibn Taimiyyah) na huku ndiko kumtakasa kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu na (yote haya aliyoyasema) inajulisha wazi kabisa kuwa yeye anaitakidi kuwa Mwenyezi Mungu anao mwili na anapatikana upande fulani. Na (huyu Ibn Taimiyyah) amesema hayo kutokana na kung'ang'ania kwake dhahiri ya aya na hadithi za Mtume bila ya kuzitafiti kwa undani aya zilizokuja kuhusu maudhui hiyo, na bila ya kufanya uhakiki katika isnadi za hadithi na madhumuni yake.

Basi iwapo haya ndiyo maoni ya mwalimu (wa Mawahabi) basi itakuwaje hali ya watu wanaoramba vikombe vyake na wanakaa katika meza zake kama kina Ibn Al-Qayyim na Muhammad bin Abdul-Wahhab. Na cha ajabu ni kwamba, hawa nao wanataka wawe ni waalimu wa Tauhidi na walinganiaji wa Tauhid. Na Mwenyezi Mungu amrehemu mshairi aliyesema: "Katika maajabu ya duniani ni kwamba, mwenye ugonjwa wa manjano anadai kuwa ni mganga na mwenye macho mabovu awe mwenye kutengeneza dawa ya macho na kipofu awe mnajimu, na msomaji wetu wa Qur'an awe Mturuki na Khatibu wetu awe Muhindi, basi njooni tulie na tupige vifuajuu ya Uislamu, (Tuulilie kwa msiba uliyoufika). Hii ndiyo itikadi ya jamaa hawa kuhusu Mwenyezi Mungu, basi iwapo tutataka kuzipima fikra hizi, basi tunawajibika kulinganisha kati ya maelezo hayo na yale yaliyopokelewa kutoka kwa Maimamu wa nyumba ya Mtume[s.a.w.w] kuhusu makusudio hayo (ya Tauhid), kisha tuone ni lipi kati ya makundi haya mawili lenye haki ya kufuatwa.

Je, ni yule amsifuye Mwenyezi Mungu kwamba, yeye ana mwili na anakaa upande fulani na kuteremka mpaka mbingu ya dunia, (ndiye wa kufuatwa) au yule amsifuye Mwenyezi Mungu kwa kusema: "Shukurani zote anastahiki Mwenyezi Mungu ambaye hawafikii kikamilifu sifa zake wenye kuzisema, wala hawazidhibiti neema zake wenye kuhesabu, na wala hawatekelezi ipasavyo haki yake wenye kujitahidi, Mwenyezi Mungu ambaye fikra hazimfikii hate ziende umbali kiasi gani, wala akili hazimfikii japo ziende ndani kiasi gani, ambaye sifa zake hazina mpaka, wala hakuna maneno yatakayoeleza sifa zake kikamilifu. Na yeye hana wakati uliohesabiwa wala muda uliopangwa, mwenye kumsifu Mwenyezi Mungu kwa mujibu wa fikra zake atakuwa kamfanyia mwenza, na mwenye kumfanyia mwenza atakuwa kanifanya wawili na mwenye kumfanya wawili basi atakuwa kamgawa. Na mwenye kumgawa hakumjua, na asiyemjua atamuashiria na mwenye kumuashiria atakuwa kamuwekea mipaka, na mwenye kumuwekea mipaka atakuwa kamfanya kuwa zaidi ya mmoja, na atakayeuliza yuko katika kitu gani, basi yeye atakuwa kamuweka ndani ya kitu, na atakayemuuliza kuwa yuko juu ya kitu gani, basi yeye atapafanya mahala pengine pote kuwa Mwenyezi Mungu hayupo. Yeye yupo lakini si kwamba hapo kabla hakuwepo. Yupo pamoja na kila kitu, lakini si kwa kuambatana naye yu mbali na kila kitu lakini si kwa kuondoka.[3]

(Ndugu msomaji), utakapolinganisha yale yaliyonakiliwa kutoka kwa As-Habul-Hadithi kuhusu Tauhidi ya Mwenyezi Mungu na kumtakasa kwake utastaajabu, kwani Imam Al-Ash-Ari amenakili toka kwao kwamba, maana ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika kuomba ni kuwa: Maovu ya waja anayaumba Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuwa matendo ya waja anayeyaumba ni Mwenyezi Mungu na waja hawawezi kufanya chochote.[4] Bila shaka ibn Taimiyyah na wale walioko kama yeye wanajisifu wenyewe kuwa ni Ahlul-hadithi na wanaitafsiri Tauhidi inayohusu kuumba kwa maana hii. Basi Je, baada ya hali hii itawezekanaje kwao (kina ibn Taimiyyah) kumtakasa Mwenyezi Mungu kutokana na dhulma na ujeuri na kuvuka mipaka. Basi iwapo Mwenyezi Mungu ndiye anayeumba maovu ya waja, na waja hao wakawa hawana walichokifanya katika maovu hayo, si kwa uwezo wao wala kwa kuiga basi ni kwa nini Mwenyezi Mungu awaadhibu? Je, hali hii siyo miongoni mwa kauli za msemaji fulani aliposema: "Amefanya makosa mwingine nami ninaadhbiwa."

Nawe unatambua kwamba Tauhid inayohusu kuumba haimaanishi kama walivyoileza Ahlul-Hadithi, na kabla na baada yao (waliyasema kama hayo) Jabriyyah na ibn Taimiyyah na wafuasi wake. Bali maana yake ni kwamba: Muumba mwenye kujitosheleza na mtendaji asiyehitaji kitu chochote ni yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu. Lakini wako watendaji wanaotenda kwa idhini yake na wanaumba kwa amri yake na husimama na kukaa kwa uwezo wake na nguvu zake, hivyo basi mtu analo jukumu lake kutokana na matendo yake na kazi zake: "Kila nafsi itafungika kwa yale iliyoyatenda ". Qur'an, 74:38.

WANACHUONI WA KIWAHABI WANAJIPENDEKEZA KWA WATAWALA

Tunaona kwamba wanachuoni wa Kiwahabi nchini Saudia na sehemu zingine wanajipendekeza kwa watawala na Makhalifa wajeuri, wanajaribu kuyatakasa matendo ya dhulma ya watawala hao na msimamo wao wakijeuri, na wanajitahidi kutoa kibali cha kisheria kwa kila kinachotokana na watawala wao na wenye mamlaka juu yao (mtawala huyo) awe mwema au muovu. Na hilo siyo jambo la ajabu (kwao) kwani wao (Mawahabi) ndiyo wanaoona kuwa kusali nyuma ya kila Imam mwema au muovu sala inasihi, na kuwaombea wema viongozi wa Waislamu ni faradhi, na kuwapinga wanapopotoka ni haramu.[5] Wanaichukuliaje kauli ya Mtume wa Mwenyezi Mungu [s.w.t] kama alivyoinakili toka kwake mjukuu wake Husein bin Ali[a.s] "Abu-Shuhadaa" pale aliposema: "Enyi watu, hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu [s.w.t] amesema; mtu yeyote atakayemuona mtawala muovu anayehalalisha haramu ya Mwenyezi Mungu, mwenye kutengua ahadi ya Mwenyezi Mungu, mwenye kwenda kinyume cha Sunna ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, anawatendea uovu na uadui waja wa Mwenyezi Mungu, kisha mtu huyo akaacha kumkataza kwa kitendo au kauli, basi Mwenyezi Mungu atakuwa na haki ya kumuingiza motoni mtu huyo." [6] [6] Hebu niambie kweli, ni ipi baina ya kauli mbili na ni ipi baina ya njia mbili inayotokana na Uislamu halisi na inaonyesha picha ya nadharia ya Uislamu halisi?

Mwenyezi Mungu amesema: "Wala msiwategemee (mkawa pamoja nao) wale wanaodhulumu usije kukupateni moto ." Qur'an, 11:113.

MAPINDUZI YA KIISLAMU NA HUJUMA ZA KIWAHABI

Kwa hakika Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran yameleta mshituko mkubwa katika ghuba, na kuzisononesha tawala zote zilizoko sehemu hiyo na hasa hasa zile zinazohusiana na mataifa makubwa na kuyategemea kwa kila hali, na kwa upande mwingine madola hayo ya kikoloni yanazitegemea nchi hizo na miongoni mwa tawala hizi ni ule utawala wa Kiwahabi unaotawala nchi kubwa miongoni mwa nchi za Kiislamu, nchi ambayo inasifika kwa utajiri mkubwa wa asili na inufaika kwa hali maalum ya kijiografia. Basi ukoloni mbaya na vibaraka wake na watendaji wake wakiongozwa na waliaganiaji wa Kiwahabi wamekusudia kupinga mapinduzi ya Kiislamu na kimbunga chake kwa njia mbali mbali, miongoni mwa upinzani huo ni kuzusha wasi wasi ndani yake na kuwasha mioto ya vita dhidi yake na kulazimisha vikwazo vya kiuchumi dhidi ya mapinduzi hayo. Na njama zote hizi za upinzani dhidi ya mapinduzi ziliposhindwa, wakakusudia kuleta picha mbaya ya utamaduni wa mapinduzi an kuondosha Mafhumu yake na kuuzushia uongo na kuupakazia uzushi ili kuwazuia watu kufuata muongozo wake na kumfuata kiongozi wa mapinduzi hayo. Kwa hakika njama hii ya kiadui dhidi ya utamaduni wa mapinduzi ya Kiislamu, inabainika katika mambo yafuatayo:

1. Kueneza matangazo na magazeti aina nyingi katika nchi mbali mbali za ulimwengu ili kuzungumzia dhidi ya mapinduzi na kufanya ushawishi dhidi yake na kuonyesha sura mbaya ya utamaduni wake halisi.

2. Kuchapisha vijitabu na vitabu vingi mno kuhusu utamaduni huo kwa kupitia mikono ya watu na waandishi ambao wameuza nafsi zao na hawajali isipokuwa mlo wao na pengine vyeo vyao vya kidunia, wakiongozwa na yule muongo mkubwa ih-Sa'an ilahi dhahiri[7] ambaye ni miongoni mwa watu wanaopata mali nyingi kutoka Saudia. Mtu huyu amesimama kidete kwa nguvu zake zote na kwa kila kile ambacho Suudia inakitoa ili kutoa picha mbaya ya taaluma ya mapinduzi miongoni mwa Waislamu.

Na huyu Bwana ni masikini kwa kila kitu hata katika madai yake kuwa anayafahamu madhhebu ya Shia Imamiyyah, basi anachanganya na kuvuruga na wala hapambanui baina ya Asili na Far-i. Wala baina ya Aqida na Riwaya, na anatoa ushahidi kwa kutumia riwaya kuwa eti ndiyo madhhebu ya Shia (yalivyo). Yapo mengi zaidi ya hayo, katika uongo wake na uzushi wake na natija mbovu atoazo, hivyo basi sisi tutahusika naye mahala pengine ndani ya kitabu pekee.

3. Kuyaeneza Madhhebu ya Kiwahabi miongoni mwa vijana katika Eneo hilo kwa njia mbali mbali huku wakibainisha wazi kuwa Mawahabi ndiyo Waislamu na kwamba wao ndiyo wanaompwekesha Mwenyezi Mungu na ndiyo wanaoitumia Qur'an na sunna kwa usahihi, na wasiyokuwa wao wako mbali mno na hayo. Basi kwa ajili hiyo tumeweka risala hiyo kuyabainisha madhhebu ya Kiwahabi, na kuweka bayana ndani yake upeo wa yale wayasemayo Mawahabi na upeo wa kuwa kwao mbali na Qur'an na Sunna na sera ya Waislamu.

Mwisho, tunatoa ushauri kwa wanachuoni wa Kiislamu walioko ulimwenguni kwanza, na pili kwa waandishi wa Kiwahabi, wasimamie kuitisha mkutano wa Ulimwengu wa Kiislamu, mkutano ambao utawakusanya wanachuoni wa Kiislamu kutoka vikundi vyote vya Kiislamu ili kuyachambua Mas-ala haya kwa mujibu wa Qur'an na Sunna na kuyasambaza matokeo ya mkutano huo kwa Waislamu wote ili haki iwabainikie kwa uwazi na ifuatwe, na iliyo haki ndiyo yenye haki mno kufuatwa, na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuwafikisha na ndiye msaidizi. Jaafar Subhani

Qum Takatifu

1/Mfunguo Tano/1405