• Anza
  • Iliyopita
  • 3 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 3978 / Pakua: 3187
Kiwango Kiwango Kiwango
PAMOJA NA MITUME KATIKA NJIA YA MASHAKA

PAMOJA NA MITUME KATIKA NJIA YA MASHAKA

Mwandishi:
Swahili

PAMOJA NA MITUME KATIKA NJIA YA MASHAKA

MTUNGAJI: SAYYID MUHAMMAD TAQI MUDARRISI

MFASIRI: HASSAN A MWALUPA

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Mpenzi msomaji! Assalaamu alaykum wa rahmatullahi wa barakaatuh! Je, imetokea siku moja kuwa na shaka na ukahisi upweke katika njia ya haki kwa sababu ya uchache wa wafuasi wake? Je, umejikuta siku moja uko peke yako katika uwanja wa mapambano? Je, umewahi kuzunguka huku na huko ukimtafuta mtu atakayekusaidia kutatua matatizo ya maisha na njia yake ngumu? Je, umewahi siku moja kuhitajia akiba ya chakula kwa ajili ya safari ya maisha ya mashaka? Je, yamekutokea yote hayo?

Sitangoja jibu kutoka kwako! Kwan i jibu la watu wote litakuwa moja tu, nalo ni: "Ndiyo. Mambo hayo yote yametufika." Ndugu yangu Mwislamu! Hakika hukuwa peke yako katika njia iliyokupwekesha; wametangulia katika njia hiyo Mitume watukufu, wanaharakati na wanamapinduzi wa mwanzoni. Hakika hukuwa peke yako katika uwanja wa mapambano uliosimama kuutetea Uislamu na itikadi za Waislamu, bali walitangulia mawalii na watu wema katika uwanja huohuo na mahali hapohapo ambapo ulisimama kwa lengo hilohilo na matumaini hayohayo uliyokuwa nayo. Basi njia ni moja kufuatana na malengo na matumaini yake. Kwa hivyo, hukuwa peke yako. Pengine umekuwa peke yako katika wakati wako ambao ulifuata njia hiyo, lakini hukuwa peke yako katika nyakti zote ambazo amefaradhia Mwenyezi Mungu kukata mbuga ya maisha yenye miba. Mitume watukufu, maimamu wema, wanaitikadi (wenye kubeba ujumbe) wa mwanzoni na mashahidi watukufu, kila mmoja wao ameingia katika majaribio hayo magumu ya kiitikadi, akayakabili na kuyavumilia kwa msimamo thabiti. kwa hivyo, Mwenyezi Mungu akamlipa malipo yake bila ya kupungua chochote. Basi makusudio yetu tunapokwenda katika njia yenye kudumu ya hao waliotutangulia ni kuwafuata na kuchukua mwanga wa taa yao na azma, subira na msimamo wao.

Ewe ndugu yangu Mwislamu! Hakika kitabu hiki kitakuonyesha visa vya Mitume na Manabii jinsi walivyopambana na mashaka na matatizo ya maisha na jinsi usafi wao ulivyozidi na ukatoa johari ambazo zinadhihirisha hakika yao safi isiyokuwa na vumbi. Vilevile kitabu hiki kinaonyesha kwamba kila mashaka ya njia ya Manabii yalivyozidi ndivyo azma na uthabiti wa njia yao ya haki ulivyozidi. Mafanikio hayo yanatokana na kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na kuhakikisha malengo yao ya kiitikadi. Visa vya Mitume vilivyotajwa katika kitabu hiki vimenukuliwa kutoka Qur'ani Tukufu na vitabu vya kihistoria na vya kiitikadi. Kwa hakika fikra za kitabu hiki na darasa zake zinawezekana kuzingatiwa kuwa ni mwanga utakaotuongoza kushika njia ya kujenga hadi ya mwislamu kufuatana na maoni ya Qur'ani. Hakika uzoefu wao ni mali waliyoturithisha ili tugharamie mahitaji yote katika njia ya kiitikadi. Kuirudisha hadhi ya Kiislamu katika tukio la maisha huhesabiwa na katika mambo muhimu zaidi ya wanaofanyia kazi Uislamu leo. Kwa hivyo, halipatikani hilo ila kwa kupatikana kiigizo chema, nacho ni Mitume. Kutikana na umuhimu na haja kubwa ya kitabu hiki, Jumuia ya Udugu wa Kiislamu imekichapisha tena kitabu hiki kama ni mojawapo ya kazi zake za kuitamaduni na kimaarifa.

Chapa ya kwanza ya kitabu hiki (kwa kugha ya Kiarabu) kilichapishwa zaidi ya miaka 20 iliyopita, lakini pamoja na kupita muda huo mrefu bado kitabu hiki kinatoa pumzi ya uhai. Kwa nini kisiwe hivyo ilhali mishipa yake imeambatana na mishipa ya historia ya kiitikadi iliyo hai? Mtungaji wa kitabu hiki ni mwanachuoni mtukufu Sayyid Muhammad Taqi al-Mudarrisi ambaye ameingia katika nyanja mbalimbali za kazi za Kiislamu kama vile kujenga shule na vyuo vya kidini vya kisasa. Vilevile amejiendeleza katika kutunga vitabu vya darasa na utafiti wa Kiislamu pamoja na huduma nyinginezo za Kiislamu ambazo anaendelea kuzitoa katika Umma wa Kiislamu. Kitabu hiki chenye fasaha ni miongoni mwa natija zake za mwanzoni, na amekiandika akiwa na umri wa miaka ishirini.

Ifuatayo ni orodha ya vitabu vyake vya darasa vilivyokwishachapishwa ambavyo vinajadili kwa mapana katika fani mbalimbali za Kiislamu:

1) fikra za Kiislamu: Mwelekeo wa Kisasa

2) Mantiki ya Kiislamu: Misingi na Njia Zake

3) Amali za Kiislamu: Asili na Malengo Yake

4) Jamii ya Kiislamu: Asili na Malengo Yake

5) Historia ya Kiislamu

6) Ufufuo wa Kiislamu

7) Fiqihi ya Kiislamu

8) Mijadala katika Qur'ani Tukufu

9) Tafsiri ya Qur'ani. Mwongozo katika Qur'ani.

Kuna vitabu kadhaa vya Kiislamu na mamia ya kaseti za Mihadhara yake ambayo anaendelea kutoa. Vyote ni katika lugha ya asili ya Kiarabu. Mchapishaji wa kitabu hiki ni Maktab As-Sayyid al-Mudarrisi ambayo ni taasisi ya utamaduni wa Kiislamu yenye lengo la kueneza fikra za Kiislamu yenye lengo la kueneza fikra za Kiislamu miongoni mwa wana wa Umma wa kiislamu na kuingiza roho ya udugu wa Kiislamu. Jumuia hii inafanya kazi nyingi za Kiislamu. Mwishowe, tunapenda kuwakumbusha ndugu zetu mambo mawili:

1) Kitabu hiki kinatoa zingatio, faida na kielelezo, kwa kuwa Mitume ni kiigizo chetu.

2) Saidia kueneza kitabu hiki wa upana zaidi, kisome, kisha mpe rafiki yako afaidike. Tunakuombea mafanikio mema na kabuli njema kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Maktab as-Sayyid al-Mudarrisi

UTANGULIZI WA MTUNGAJI

Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na rehema na amani zimshukie Mtume Wake Muhammad(s.a.w.w) , Nabii wa Mwisho, na juu ya kizazi chake kitakatifu. Hakika Umma wa Kiislamu umeshindwa kabisa, na kushindwa huko kunafuatia machungu na mateso; kisha ukosefu mkubwa katika pande mbili: upande wa kimaada (kidunia) na upande wa kimaanawi (kiroho). Kukosekana upande wa kimaanawi ni sababu ya kukosekana upande wa kimaada, kwani umaada sio nguvu inayojileta yenyewe kwa mtu na kuweza kubaki au kuondoka wakati wowote, bali ni natija ya kazi ya mtu na mapato ya juhudi yake. Mtu hafanyi bidii ila baada ya kujua maana ya juhudi yake. Kwa hivyo, kukosekana umaanawi katika Umma wa Kiislamu ndiko ambako kunapasa kuupiga vita na kuupigania ili urudi utukufu na ushindi na Umma uishi katika neema baada ya kuwa katika adhabu. Hatuwezi kuupiga vita ukosefu huu bila ya kueneza mwamko sahihi wa Kiislamu kwa kutafsiri Qur'ani, kueneza maarifa yake. kuelezea maisha ya mashujaa wa Kiislamu, n.k. Kitabu hiki kidogo ni jaribio dogo katika kutimiza lengo hili, kwani tumenakili mifano michache ya visa vya Mitume.

KILELE CHA UTUKUFU

Hakika Mitume (amani iwe juti yao) wamekumbana na matatizo mengi na wamepita katika njia ya miiba (mashaka) kuelekea kwenye utukufu wa kitu hadi wakafika kwenye kilele cha ukamilifu na utukufu. Wakawa ni watu wa ngazi za juu kwa kufikia kwenye kilele cha ubinadamu. Kwa hivyo, wao walijua njia, wakaongoka na wakajua malengo ya njia hizo na wakalingania watu na kuwaongoza wale waliopotea kwenye lile walilolijua. Waliwafungulia watu njia ambazo zilikuwa hazijulikani kwa kuwa walikuwa wenyeji katika mambo hayo na walikuwa na nguvu na uwezo kutokana na bahari yao ya elimu, upole na sifa zao za uvumilivu na uthabiti. Hatuwezi kuvipima vipawa vyao vinavyoshindania kheri, utiifu na utukufu. Hatuwezi kuvipima kwa vipawa vyetu. Nguvu yao ya uwezo, udhibiti wao wa nafsi, matamanio, dunia na udanganyifu wake, na kuvumilia kwao misiba, ni muujiza wa Mwenyezi Mungu kwa viumbe Vyake.

Kwa hakika, Mitume wametuachia athari nyingi na mazingatio mengi ambazo ndizo zinazotusaidia. Wao ndio waliotufundisha namna ya kuvumbua vitu visivyojulikana na kutosalimu amri mbele va vitu hivyo. Wametufundisha namna ya kupambana na kuyashinda matamanio, kuwa na msimamo mzuri katika kuyakabili matamanio na kuwa na azma imara. Lau tusingefuata ushauri wao tusingekuwa watu kama tulivyo. Lau tungekubali ujinga tangu siku ya kwanza na kutawaliwa na matamanio, tungejikuta tumo katika pango la ushenzi na tungelikuwa kama wanyama tu! Ni lazima tulizingatie an tufaidike kutokana na ibra au mafunzo ya mambo yetu muhimi ya kidini na kidunia. Mazingatio hayo hayawezi kutekelezwa bila ya sisi wenyewe kutaka kuelekea na hayawezi kutuhimiza bila ya sisi wenyewe kujihimiza. Mfano wake ni kama umeme unaotoa mwangaza wakati ule tunapotaka utoe mwangaza.

Mazingatio haya huunda nguvu, uwezo na azma katika harakati, huimarisha kazi na hutakasa utiifu; na kila mmoja katika misimamo hiyo mitukufu ya kiutu hutukuza athari zake katika maisha na hutoa matumaini makubwa kwa maazimio yake. Haya ndiyo mapinduzi ya hakika ambayo kipimo cha utukufu wake yanaonekana katika malengo yake.

1. Vipi Tutazingatia? Vipi tutazingatia visa vya Mitume na Manabii? Vipi tutaweza kuilinganisha historia ya zamani na matatizo yetu ya sasa? Hakika swali hili linataka jibu pana. Hakika mtu ana tabia ya kuogopa vitu asivyovijua na hujihadhari na upotofu. Kwa hivyo, hujiepusha na mambo yasiyojulikana. Mitume wameondoa tatizo hili katika maisha ya kiutu kwa kujiingiza katika mambo yasiyojulikana, na huko ni kwa kuomba msaada wa Mwenyezi Mungu. Wameweza kumthibitishia mtu kwamba utafiti wa mambo yasiyojulikana ndiyo njia ya pekee ya maendeleo katika maisha; kisha wakamfundisha mtu ushujaa katika kazi hii tukufu kukabiliana na kitu kisichojulikana.

Mitume wamewashajaisha watu kuvunja vikwazo vya matamanio ambavyo vimemzunguka mtu kila upande mpaka kumfanya mnyonge kabisa ilhali Mwenyezi Mungu amemuumba mtukufu. Unyonge ni udhalilifu mfano wa kuni zinazomchoma. Ikiwa ni hivyo, basi ni juu yetu kujifunza mwenendo wao uliojaa jihadi iliyoimarika na bidii ya amali (utendaji) katika njia ya kujikomboa kifikra na kumpeleka mtu kwenye kheri. Hebu tuangalie mambo haya mawili matukufu ambayo ni ushujaa na ujasiri katika kuyapetuka mambo yasiyojulikana, na ushujaa katika kuondoa vikwazo vya matamanio.

2. Kiigizo Kizuri Tumesema kuwa maisha ya Mitume ni kiigizo cha mambo ya kheri walivoyafanya, kuyafundisha, kuyawekea mpaka mambo ya shari na kuthibitisha bidii ya jihadi na harakati za kudumu. Kwa hivyo, tunajifunza kutoka kwao mambo haya:

1. Namna ya kujikomboa kutokana na shari na washari. Vilevile namna ya kujikomboa kutoka katika makucha ya mataghuti (madhalimu) na wanyonyaji wa nchi.

2. Namna ya kuvumilia udhalilifu, unyonge, uduni, mateso, adhabu na machukivu ili tusikwame katika shabaha yetu wala zisidhoofike nishati zetu.

3. Namna ya kuendelea daima katika jihadi na mapambano dhidi ya adui wetu. Ijapokuwa natija yake itachelewa, lakini ni lazima tuendeleze mapambano hata kama mauti yatatufikia njiani na kuwaigiza walioendeleza harakati zao kwa bidii mpaka wakapata yale waliyoyatamani kabla ya kufikia mwisho.

4. Namna ya kumnyenyekea Mwenyezi Mungu kwa moyo safi bila ya kutegemea malipo au shukrani kutoka kwa viumbe.

5. Namna ya kutatua maelfu ya matatizo yaliyozidi ambayo yanatuongoja katika harakati zifanywazo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na ambayo Mitume wameyapatia ufumbuzi wake kamili.

3. Sababu za Kijinga Kuna baadhi ya watu wanaopendelea uvivu, wanaostahabu udhaifu na kupendelea kungojangoja bila ya kufanya bidii yoyote. Husema: "Hakika harakati huleta matatizo", au husema: "Hatuna uwezo wa kufanya kazi fulani za kiharakati." Wakijibiwa: "Mbona Mitume waliweza kuwa na harakati licha ya matatizo waliyokuwa nayo?" Husema "Mitume walikuwa wakipata msaada wa wahyi (ufunuo) na wakilindwa kwa nguvu za Kiungu. Isitoshe, wameumbwa wakiwa na ujuzi, hekima, usafi, uwerevu na mengineyo ambayo yaliwaandalia njia na kuwawekea msingi mzuri; kisha wao walikuwa na miujiza iliyowaandaa kwa tablighi na kuhami nafsi zao na za wasaidizi wao." Ninawaambia watu hawa: "Ukweli ni kuwa sababu hizi haziwezi kukuteteeni, enyi wavivu! Wenyewe mnasema kinagaubaga kuwa hamwezi kuwa na harakati, hivi ni kwa sababu mnadharau na ni wazembe."

Bila shaka sababu hizi zinaweza kuwapa faida wale walio tayari kupiga mbizi katika mawimbi makubwa ya bahari. Kwa hivyo, si Mitume peke yao ndio wenye kulindwa na kusaidiwa, bali yeyote yule mwenye kufanya kazi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hupata taufiki na msaada Wake. Qur'ani inasema:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن تَنصُرُوا اللَّـهَ يَنصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ ﴿٧﴾

''Mkimsaidia Mwenyezi Mungu atakusaidieni na ataithibitisha miguu (hatua) yenu." (47:7).

Uzoefu umeonyesha kwamba mwenye kuwa na harakati kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hana budi kupata nusura kutoka Kwake. Vivyo hivyo, vipawa vyao (Mitume) wameviweka wazi katika vitendo vyao, maneno yao, visa vyao na utukufu wao wamevibakisha kwetu kama ni hazina safi ambayo tunaweza kutoa kiasi tunachotaka na tunachohitajia. Qur'ani inasema: "Hakika katika visa vyao kuna mazingatio kwa wenye akili ." (12:111).

Kuna mifano mingi katika Qur'ani ya uzoefu katika maisha ya Mitume na maadili yao. Vivyo hivyo, katika vitabu vya sira kuna hekima nyingi zilizotolewa na Mitume katika karne nyingi zilizopita. Madai ya baadhi ya watu kwamba Mitume walikuwa na miujiza ni sawa, lakini ukweli ni kuwa Mitume hawakuutumia uwezo huu ila kwa nadra sana. Mara nyingi walijadiliana na watu kwa dalili za kiakili, na walipoanza kuwalingania watu walikuwa wakifukuzwa na kuadhibiwa wao pamoja na masahaba zao. Lau wangelikuwa wakitegemea miujiza ya kujikinga, basi kazi yao ingekuwa nyepesi sana na wala wasingeadhibiwa. Kwa hivyo, miujiza ilikuwa ni kwa ajili ya kubainisha Utume wao na hoja ya Mwenyezi Mungu kwa watu ili katika siku ya Kiyama watu wasidai na kusema: "Ewe Mola wetu! Sisi tumemkanusha mtu aliyetaka kututawala na kuchukua milki zetu." Mitume hawakuzitatua kazi nyinginezo kwa kutumia miujiza, bali kwa kufuata maumbile ya Mwenyezi Mungu anayowaumbia viumbe Vyake na neon Lake wakati alipokadiria kila kitu kwa mujibu wa sababu zake. Wao ni kama watu wengine - hula. huenda sokoni, hufanya tablighi, na hujitahidi kufuata mwendo wa watu wa kawaida. Tukiangalia mfano mmoja tu utatosha kutupa dalili dhahiri ya hoja hiyo.

4. Njia ya Mashaka Mitume (amani iwe juu yao) wamekumbana na mashaka (miiba) katika mwendo wao wa kuwaongoza watu kwenye njia ya uongofu. Ni watu wachache sana miongoni mwa wanaofanya kazi za daawa (tablighi) wanaopata mashaka kama hayo. Hakika Mitume wamepata shida na misukosuko mingi sana, matusi na tuhuma. lakini wao walitegemea nguzo ya haki mbele ya batili, mwanga mbele ya giza na ukweli mbele ya hadaa na vitimbi. Wakathibiti katika hali hiyo kama jabali mbele ya kimbunga, na walikwenda katika njia hiyo ngumu ya mashaka kwa mwendo wa kasi bila ya kuogopa wala kujali masumbuko yaliyokuwa yakiwangoja njiani. Tunathibitisha hapa visa vichache vya Mitume hao ambavyo vinaonyesha msimamo wao thabiti katika njia ya daawa (tablighi), visa ambavyo vina mazingatio na ukumbusho kwa waumini.

Tutadondoa hapa visa vya maisha yao yaliyojaa jiihadi na mapambano, na tunataraji kwamba wasomaji watagundua njia yao pana ya kufuata jihadi yao tukufu ili iwe ni somo kwao. Jambo hili ni wajibu kwa kila binadamu mwema kulifanya mbele ya ubatilifu na watu wake. Wasomaji wazingatie kwamba lau wangechukua nafasi ya Mitume na wangeitakidi itikadi yao, je. wangefanya nini mbele ya ubatilifu unaotawala? Hebu tuchukulie kwamba hii ni zama za Mitume na watu ndio haohao na matatizo ndiyo hayohayo, nasi tunataka kutenda kama walivyotenda wao ili kuiga mifano yao.

VISA VYA JIHADI NDEFU

1. NABII IDRIS(a.s)

Kuna watu wengine ambao wanapotiwa hima na tamaa, na wanapodanganywa na makosudio yao, mara huanza kufanya bidii na kutafuta kila njia ili wapate matamanio na makusudio haya. Kuna wengine ambao kazi yao ni vitimbi, hila na wizi, na wengine kazi yao ni kutafuta utawala na uongozi wa kuhukumu watu na miji. Watu hao hujitahidi kwa kila njia ili kufikia malengo yao. Hakika watu wa aina hii ni waovu sana, kwa sababu wameharibika na wanawaharibu wengine, wamepotea na wanawapoteza wengine. Hao ndio viongozi waovu wanaowaongoza watu kwenye Moto.

Mfano mmojawapo wa aina ya watu tuliyowataja alikuwa dhalimu mmoja aliyeishi katika zama za Nabii Idris(a.s) ambaye aliwamiliki watu na kuwafanya watumishi wanyonge wanaomtumikia kwa kila analolitaka na kulitamani. Ikiwa mmoja wao alionyesha upinzani wowote basi alikuwa akimtesa kwa adhabu mbaya sana. Siku moja alipokua akitembea njiani aliona shamba zuri lenye rutuba lililokuwa ni mali ya mja mwema wa Mwenyezi Mungu ambaye alikuwa akijipatia maisha ya ukoo wake kwa kulimia ardhi hiyo. Mfalme dhalimu alivutiwa sana na shamba hilo, na alipouliza ni la nani, akaambiwa kuwa ni la mpinzani mmoja fulani. Akataka kulinunua, lakini yule mtu akakataa kwa kumjibu "Ardhi hii wanahitaji zaidi ukoo wangu kuliko wewe." Mfalme akarudi nyumbani kwake akiwa amekasirika. Akamhadithia mkewe habari hiyo. Mkewe akamwambia: "Usikasirike, ikiwa unashindwa kumwua kwa kukosa sababu, mimi nitafanya mpango."

Mwanamke yule akawaita watu na kuwaamrisha washuhudie kwamba mtu fulani ni mpinzani wa dini ya mfalme. Kwa hivyo, mfalme akapata sababu. Akamwua yule mja mwema na akachukua ardhi na kuwafukuza wajane na mayatima wake. Mwenyezi Mungu akakasirika kwa kitendo hicho. Akampa wahyi (ufunuo) Nabii Idris(a.s) kuwa aende kwa mfalme. Akamwendea mfalme na ujumbe wa Mwenyezi Mungu unaosema: "Hivi umeridhia kumwua mja Wangu muumini na kuitia ufakiri familia yake ili uchukue ardhi yake? Naapa kwa Utukufu Wangu, nitakutesa nitaondoa ufalme wako, nitauharibu mji wako na nitawalisha mbwa nyama ya mke wako."

Mfalme aliposikia maneno hayo kutoka kwa Nabii Idris(a.s) , akamwambia: "Toka, ewe Idris nisije nikakuua." Mkewe akamwambia: "Usikofazaishe ujumbe wa Mungu wa Idris. Mimi nitatuma watu wakamwue, hivyo, utabatilika ujumbe wa Mungu wake" Mfalme akamwamrisha mkewe atekeleze njama hiyo. Akatuma watu arobaini wakamwue Nabii mwaminifu. Nabii Idris(a.s) akakimbia mwituni na akawa akiishi humo na kumwabudu Mwenyezi Mungu kwa tahadhari. Baada ya muda, mfalme taghuti akafa. Mke wake akafa pia, na mwili wake ukawa chakula cha mbwa. Mji wake ukaharibika kama alivyoahidi Mwenyezi Mungu kupitia ulimi wa Nabii Idris(a.s) .

Akatawala dhalimu mwingine na akawa kama yule wa kwanza kwa ushenzi na kiburi. Ikapita miaka ishirini baada ya kuondoka Nabii ldris(a.s) na mvua haikunyesha. Hali ya watu ikawa mbaya sana na wakawa wanatafuta chakula kutoka katika miji jirani. Kisha watu wa mji ule wakakusanyika kumwomba Mwenyezi Mungu awaepushe na balaa iliyowasibu. Wakajua kuwa hakuna wa kutegemewa isipokuwa Mwenyezi Mungu. Wakanaza kutubia na wakafikiri namna ya kumwabudu Mungu. Je, wangeweza kumtii Mwenyezi Mungu bila ya kuongozwa? Mwenyezi Mungu akamleta Nabii ldris(a.s) kutoka mahali pake alipokuwa akimwabudu. Nabii Idris(a.s) akawaombea mvua, ikanyesha sana mpaka ikakaribia kuwagharikisha. Pamoja na mwujiza huo, Nabii Idris(a.s) alikuwa ni mtu wa pekee aliyeweza kuandika na kushona nguo, na vilevile alikuwa ni mwenye maarifa ya ujuzi wn hesabu na nyota.

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿جَعَلَ اللَّـهُ الْكَعْبَةَ الْبَيْتَ الْحَرَامَ قِيَامًا لِّلنَّاسِ وَالشَّهْرَ الْحَرَامَ وَالْهَدْيَ وَالْقَلَائِدَ ذَٰلِكَ لِتَعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴾

97.Mwenyezi Mungu amefanya Al-Kaaba nyumba tukufu, kuwa ni kisimamo cha watu na miezi mitukufu na wanyama wa kuchinja na vigwe; hayo ni kwa sababu mjue kuwa Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

﴿اعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ وَأَنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

98. Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu na kwamba Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwingi wa kurehemu.

﴿مَّا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا تَكْتُمُونَ﴾

99.Haimlazimu Mtume ila kufikisha tu, na Mwenyezi Mungu anajua mnayo yadhihirisha na mnayoyaficha.

NYUMBA TAKATIFU

Aya 97-99

MAANA

Mwenyezi Mungu ameifanya Al-Kaaba, nyumba takatifu, kuwa ni kisimamo cha watu na miezi mitakatifu na wanyama wa kuchinja na vigwe.

Kisimamo cha watu; yaani mahali pa ibada na ibada za Hijja. Miezi mitakatifu ni ile minne Rajab, Dhul-qa'da, Dhul-Hijja na Muharram[5] Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameharamisha kupigana huko na katika miezi hiyo; ispokuwa kutetea nafsi au mali. Anasema:

﴿وَلَا تُقَاتِلُوهُمْ عِندَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ حَتَّىٰ يُقَاتِلُوكُمْ فِيهِ﴾

"Wala msipigane nao karibu na Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko" (2:191) Na akasema tena:

﴿الشَّهْرُ الْحَرَامُ بِالشَّهْرِ الْحَرَامِ وَالْحُرُمَاتُ قِصَاصٌ فَمَنِ اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ فَاعْتَدُوا عَلَيْهِ بِمِثْلِ مَا اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ ﴾

"Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu; na vitu vitakatifu vina kisasi. Basi wanaowachokoza, pia nanyi wachokozeni kwa kadiri walivyowachokoza" (2:194)

Mnyama wa kuchinja, ni wale wanaochinjwa Makka. Na kigwe ni ukambaa anaofungwa nao mnyama wa kuchinja kuwa ni alama ya kufahamisha kuwa ni wa Al-Kaaba ili asitaradhiwe na yeyote. Kwa hiyo kuunganisha vigwe kwa wanyama ni kuunganisha maalum katika ujumla.

Makusudio ya kutaja chinjo pamoja na Nyumba takatifu na miezi mitakatifu ni kwamba mnyama wa kuchinja inapasa awe salama yeye na anayemchunga, kwa sababu yeye anakusudia Haram tukufu.

Bali ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewapa amani ndege na wanyama walio katika haramu yake; isipokuwa mwewe, kipanga, kunguru, panya, nge, mbwa anayeuma watu na kila tunayemuona anaudhi.

Hayo ni kwa sababu mjue kuwa Mwenyezi Mungu anayajua yaliomo mbinguni na yaliyomo ardhini na kwamba Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kubainisha miko ya Al-Kaaba, miezi mitukufu na wanyama wa kuchinja, anaashiria kwamba hekima ya sharia hii ni kuwa watu wajue kwamba Mwenyezi Mungu anajua ufafanuzi wa mambo katika ardhi na katika mbingu; na ambayo yana masilahi kwa watu katika dini yao na dunia yao.

Kuna masilahi gani makubwa zaidi ya usalama wa maisha ya mtu na mali yake ijapokuwa ni kwa kipindi fulani. Tumeyaona mataifa makubwa yanayotwangana, wakati huu, yakiafikiana kuwa baadhi ya miji iwe ni maeneo maalumu ya amani, haijuzu kwa taifa linalopigana kuishirikisha katika vita wala kuweka vituo vya kijeshi katika ardhi hiyo au kupita wanajeshi wake.

Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu na kwamba Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekutanisha adhabu na rehema na maghufira ili mja awe anahofia adhabu yake na kutaraji rehema yake. Kwa sababu mja, akiwa na hofu atajiepusha na maasi na akiwa na matarajio atajitahidi katika twaa.

Razi anasema: "Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja kuwa yeye ni mkali wa kuadhibu, kisha akafuatishia kwa wasifu wa rehema na maghufira. Na huu ni uzinduzi juu ya undani kuwa kupatikana kiumbe ni kwa ajili ya rehema. Na kwa dhahiri ni kuwa mwisho hauwi ila kwa rehema" Hiyo ni kweli kabisa.

Haimlazimu Mtume ila kufikisha tu.

Hatakiwi jingine zaidi ya hilo, ambapo hapana udhuru baada ya kufikisha kwa anayepuuza na kupetuka mpaka. Ama hisabu na adhabu hiyo ni juu ya Mwenyezi Mungu pekee Yake. Mwenyezi Mungu anasema:

"Hakika ni juu yako kufikisha tu, na ni juu yetu hisabu." (13:40)

Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyadhihirisha katika kauli na vitendo na mnayoyaficha. Haya ni makemeo kwa anayeinyamazia haki, na hasa yule anayeifanyia biashara kwa kujipanua na jina la dini na la nchi.

﴿قُل لَّا يَسْتَوِي الْخَبِيثُ وَالطَّيِّبُ وَلَوْ أَعْجَبَكَ كَثْرَةُ الْخَبِيثِ فَاتَّقُوا اللَّـهَ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴾

100.Sema: Hawi sawa habithi na mwema, hata ukikupendeza wingi wa habith, Basi mcheni Mwenyezi Mungu enyi wenye akili ili mpate kufaulu.

WINGI WA MWOVU

Aya 100

MAANA

Aya hii inarudufu Aya ile isemayo:

﴿لَا يَسْتَوِي أَصْحَابُ النَّارِ وَأَصْحَابُ الْجَنَّةِ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمُ الْفَائِزُونَ﴾

"Hawawi sawa watu wa Motoni na watu wa Peponi, watu wa Peponi ndio wenye kufuzu" (59:20)

Wingi wa habithi ni anayoyamiliki miongoni mwa jaha na mali. Mwenye akili hawezi kumweka sawa habithi, na mwema hata kama ana mali nyingi na jaha kubwa. Kwa sababu jaha na mali hazimfanyi mwovu kuwa mwema; wala ufakiri na udhaifu haumfanyi mwema kuwa mwovu.

Mtu habith katika kipimo cha dini ni yule anayeasi hukumu za Mwenyezi Mungu katika kitabu chake na Sunna za Mtume wake. Na katika desturi ya watu ni yule wanayemhofia kwa shari yake na wasiyemwamini kwa jambo lolote na kutomsadiki katika kauli au vitendo vyake. Kimsingi ni kwamba mwenye sifa hizi, ni mbaya pia mbele ya Mwenyezi Mungu. Mtume wa Mwenyezi Mungu anasema:"Utukufu zaidi wa imani ni kuaminiwa na watu." Ama mtu mwema ni yule aliye kinyume cha mtu habithi katika sifa zake zote.

JE RIZIKI NI BAHATI AU MAJAALIWA?

Unaweza kuuliza : Ikiwa habithi anachukiwa na Mwenyezi Mungu na mwema anaridhiwa na Mwenyezi Mungu, kwa nini basi habithi anafaulu katika maisha haya na kuneemeshwa kwa jaha na utajiri, na mwema anaanguka na wala hapati matakwa yake?

Jibu : Maisha yana desturi na kanuni zinazokwenda nayo, na hazigeuki kwa hali yoyote ile. Kwa sababu hisia na uoni unakataa mkorogano katika ulimwengu. Desturi na kanuni hizi ni katika matengenezo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: Kwa sababu yeye ni muumbaji wa asili na vilivyomo katika asili.

Kimsingi ni kuwa desturi ya kawaida ya tabia inakataa kuwa mali, afya na ilimu, vishuke tu kutoka mbinguni. Isipokuwa vitu hivi na mfano wake vinakuja kwa njia zake na sababu zake za kimaumbile. Elimu inatokana na kujifundisha, afya inatokana na lishe na kinga, na mali inatokana na kazi. Kwa hiyo mwenye kujifunza hujua, mwenye kujiepusha na visababishi vya maradhi husalimika, mwenye kujinyonga atakufa tu; awe mwema au mwovu, mumin au kafiri.

Kwa hiyo wema au imani hauoteshi ngano wala hauponeshi ugonjwa wala haumfanyi asiyejua kuwa mjuzi, Yote haya na mfano wake yanakwenda kwa desturi ya tabia na desturi ya tabia inakwenda kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, hilo halina shaka.

Kwa sababu yeye ndiye aliyejaalia kujifundisha ndio sababu ya elimu na kujikinga ndio sababu ya afya na kupanda kuwa ndio sababu ya kuvuna. Yeye ni Muumba wa kila kitu na kwake yeye ni mwishilio wa kila jambo.

Ndiyo! kuchuma mali kuna njia nyingi, na milango mingi, nyingine Mwenyezi Mungu amezihalalisha na nyingine akaziharamisha. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehalalisha biashara, kilimo na viwanda; na akaharamisha riba, utapeli, rushwa, kupora na ulanguzi.

Mwenye kuchuma mali kwa njia ya halali hunasibishwa chumo lake kwake, kwa sababu yeye amejitahidi na kufanya bidii kuitafuta, na vilevile hunasabishwa kwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu yeye ndiye aliyepitisha sababu hizi na kuzihalalisha kwa kila azitakaye, awe mwema au mwovu.

Ama mwenye kuchuma mali kwa njia za haramu; kama vile riba na unyang'anyi; chumo lake litanasibishwa kwake na kwa hali aliyoitumia, wala halinasibishwi kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu ameharamisha njia hizi kwa mwema na mwovu.

Utasema : Haya yote ni kweli, lakini hayajibu swali wala hayatatui mushkeli. Tumewahi kumuona mwema na mwovu wote wakifuata njia za sharia za riziki, na kuzitafuta riziki kwa njia zile alizozihalalisha Mwenyezi Mungu na kuziharamisha, lakini pamoja na hayo, riziki inakuwa zaidi kwa mwovu aliye habith na kuwa dhiki kwa mwema, pengine huyu mwema ametoa juhudi maradufu ya yule mwovu, bali mara nyingine riziki humjia mwovu bila ya kutazamia wala maandalizi au juhudi, na inazuilika kumwendea mwema anapoitazamia na kuifanyia maandalizi na juhudi?

Jibu : Baadhi ya watu wanakimbilia kulifasiri hilo kwa kusema ni sadfa au bahati. Hakuna kinachofahamika kutokana na maelezo hayo zaidi ya kushindwa kwao kutoa tafsiri sahihi. Vinginevyo wasingelikimbilia kwenye maelezo ya kubahatisha tu.

Kwa hiyo sisi tunapinga Sadfa na bahati na tunaamini kwa imani ya mkato kwamba kuna chaguo la juu linajiingiza kwa sababu tusizozijua. kwa vile elimu katika masuala hayo na mfano wake, bado ni changa. Na kushindwa kwa elimu hakumaanishi kuwa kitu hakiko. Imani yetu hii inatiliwa mkazo na kauli zake Mwenyezi Mungu zifuatazo:

﴿وَاللَّـهُ فَضَّلَ بَعْضَكُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ فِي الرِّزْقِ﴾

"Na Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine katika riziki" (16:71)

﴿اللَّـهُ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ﴾

"Mwenyezi Mungu hukunjua riziki kwa amtakaye na huidhikisha (13:26) Ay a hii imekuja kwa herufi zake katika 17:30, 28:82, 29:62, 30:37, 34: 36, 34: 39, 39:52, 42:12.

Kwa hiyo basi aliyesema au anayesema: Mwenyezi Mungu amemtajirisha fulani kwa kuwa yeye ni mwema basi atakuwa anazungumza mantiki ya Firaun na kupima kwa kipimo cha Shetani. Hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu imetaka kumlipa mwema malipo mazuri na kumwadhibu mwovu katika akhera inayobakia sio katika hii dunia inayokwisha. Hii ni Nyumba ya matendo na ile ni Nyumba ya Hisabu. Zaidi ya haya ni kuwa wingi wa mali wa mwovu huenda ukawa ni balaa kwake na sababu ya kuadhibiwa kwake. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا وَيَتَمَتَّعُوا وَيُلْهِهِمُ الْأَمَلُ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ﴾

"Waache wale na wafurahi na iwazuge tamaa, watakuja jua." (15:3)

﴿يَتَمَتَّعُونَ وَيَأْكُلُونَ كَمَا تَأْكُلُ الْأَنْعَامُ وَالنَّارُ مَثْوًى لَّهُمْ﴾

"Hujistarehesha na hula kama walivyo wanyama, na moto ndio makazi yao." (47:12)

Kwa ufupi ni kwamba riziki inategemea mambo mawili. Kuhangaika na matakwa ya Mwenyezi Mungu. Asiyehangaika ataishi omba omba; na mwenye kuhangaika Mwenyezi Mungu humruzuku kutokana na bidii yake, akitaka humpa nyingi na akitaka humpa chache.

Uhakika huu umo katika maumbile ya binadamu na anaufanya bila ya kujitambua. Mfanya biashara humwomba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amruzuku kupata soko zuri la bidhaa zake na watu wazikubali. Mkulima anamwomba Mungu aiteremshie mimea yake mvua; wala hamuombi kumwoteshea mimea bila ya mvua.

Mimi hapa namwomba Mwenyezi Mungu ampe tawfiq mwanangu katika masomo yake na kufaulu mtihani; wala si mwombi akipe mawazo chuo kikuu kimpatie shahada bila ya kusoma na kufanya mtihani. Iko methali isemayo: Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.

Pengine inawezekana mahangaiko yasiambulie kitu, lakini pamoja na hayo inatakikana kupanga mipango na kuongeza juhudi. Kwa sababu kuongeza juhudi, kutumia mipango, na kuvumilia tabu ni sababu ya matakwa ya kufaulu kutoka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ﴾

101.Enyi Mlioamini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatawachukiza. Na mnapoyauliza inapoteremshwa Qur'an mtabainishiwa. Mwenyezi Mungu ameyasamehe hayo. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira Mpole.

﴿قَدْ سَأَلَهَا قَوْمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ثُمَّ أَصْبَحُوا بِهَا كَافِرِينَ﴾

102.Waliyauliza watu waliokuwa kabla yenu kisha wakawa makafiri kwayo.

MSIULIZEULIZE MAMBO

Aya 101-102

MAANA

Enyi Mlioamini! Msiulize mambo ambayo mkidhihirishiwa yatawachukiza.

Kauli yake Mwenyezi Mungu 'Msiulize' inaishiria kuwa baadhi ya Masahaba walikuwa waking'ang'ania kuuliza mambo yasiyokuwa na dharura yoyote kuyajua na huenda jibu lake likawaudhi waulizaji. Kuna riwaya isemayo kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume(s.a.w.w) : "Ni nani baba yangu?" Mtume akamwambia, "baba yako ni Fulani" Mwingine akauliza "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Baba yangu yuko wapi? Mtume akajibu: "Yuko motoni," ndipo ikashuka Aya hiyo.

Riwaya nyingine inasema kuwa Mtume alisema: "Mwenyezi Mungu amewafaradhishia kuhiji, basi hijini." Wakauliza: "Kila mwaka ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Mtume akanyamaza. Wakarudia kuuliza, akasema La; lau ningelisema naam, ingelikuwa wajib." Ndipo ikashuku Aya hii. Riwaya hii ndiyo yenye nguvu kuliko ile ya kwanza.

Na mnapoyauliza inapoteremshwa Qur'an mtabainishiwa.

Yaani msijikalifishe kuuliza mambo ila baada ya kuteremshwa Qur'an. Mtakapoanza kuuliza Mtume(s.a.w.w) atawadhirishia mliyokuwa mkiyauliza.

Kwa hali hii, inatubainikia kuwa riwaya ya Hija ndiyo yenye nguvu katika sababu ya kushuka Aya, kuliko riwaya ya kuuliza mababa na wahenga wa Masahaba. Kwa sababu Qur'an inaanza kuleta itikadi na sharia na wala sio kuanzia kwa mababa na mababu wa Masahaba. Katika Hadith imeelezwa:"Hakika Mwenyezi Mungu ameweka mipaka msiikiuke; amewafaradhishia faradhi msizipoteze; ameharamishia vitu msivifanye; na ameacha vitu vingine si kwa kusahau, lakini ni kwa kuwahurumia, basi vikubalini wala msivifanyie utafiti".

Mwenyezi Mungu amesamehe hayo

Yaani maswali yenu yaliyotangulia, kwa hiyo msiyarudie. Imesemekana kuwa maana yake ni amezuia kutaja vitu mlivyoviulizia, basi nanyi jizuieni wala msijikalifu kuviulizia. Tafsir zote mbili zina uwezekano hazikataliwi na dhahiri ya tamko.

Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mpole.

Humsamehe mkosaji akikosea tena.

Waliyauliza watu waliokuwa kabla yenu kisha wakawa makafiri kwayo.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwakataza kuuliza mambo wasiyokuwa na haja nayo, anawapigia mfano wa watu waliokuwa kabla yao, waliuliza wakang'ang'ania kuuliza. Walipobainishiwa na Mwenyezi Mungu walichukia wakaasi na wakastahiki adhabu. Lau wangeliacha kuuliza ingelikuwa bora kwao.

Wafasiri wamerefusha maneno katika kubainisha makusudio ya watu waliouliza, kisha wakawa makafiri kwa sababu ya kuuliza, lakini Aya haikubainisha. Pamoja na hivyo, tunaweza kusema kuwa watu waliouliza wakawa makafiri kwa sababu ya kuuliza ni wana wa Israil, kwa sababu ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwasimulia:

﴿فَقَدْ سَأَلُوا مُوسَىٰ أَكْبَرَ مِن ذَٰلِكَ فَقَالُوا أَرِنَا اللَّـهَ جَهْرَةً ﴾

"Hakika walimtaka Musa makubwa kuliko hayo, Walisema: Tuonyeshe Mwenyezi Mungu waziwazi" (4:153)

﴿مَا جَعَلَ اللَّـهُ مِن بَحِيرَةٍ وَلَا سَائِبَةٍ وَلَا وَصِيلَةٍ وَلَا حَامٍ وَلَـٰكِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ وَأَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ﴾

103.Mwenyezi Mungu hakujaalia Bahira wala Saiba wala Waswila wala Hami; Lakini waliokufuru wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na wengi wao hawafahamu.

﴿وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ قَالُوا حَسْبُنَا مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ﴾

104.Wakiambiwa njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kwa Mtume, husema: Yanatutosha yale tuliyowakuta nayo babu zetu. Je hata kama baba zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

105.Enyi mlioamini! Jiangalie nafsi zenu. Hawawadhuru waliopotea ikiwa mmeongoka. Marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu. Atawaambia yale mliyokuwa mkiyatenda.

HAKUNA BAHIRAWALA SAIBA

Aya 103-105

MAANA

Mwenyezi Mungu hakujaalia Bahira wala Saiba wala Waswila wala Hami.

Bahira, ni ngamia aliyetobolewa masikio, watu wa wakati wa Jahilia walikuwa wakifanya hivyo, ikiwa ngamia atazaa mimba kumi ; na inasemekana ni mimba tano. Wanamwacha bila ya kutumiwa na mtu yoyote. Saiba ni ngamia waliyemwekea nadhiri kwa waungu, na wana mwacha akijilisha mwenyewe popote bila ya kufungwa wala kuwa na mchungaji sawa na Bahira.

Wasila ni mbuzi anayezaa mtoto wa kiume na wa kike pamoja. Desturi yao ilikuwa kama akizaa mume wanamfanya ni wa waungu na akizaa mke ni wao. Iwapo atazaa mume na mke pamoja, hawamchinji mume wakisema kuwa ameunganishwa na dada yake. Hami ni dume aliyezalisha mimba kumi, wanamwacha hazuiliwi na maji wala malisho, wakisema ameuhami mgongo wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anabainisha kwamba yote hayo hayamo katika dini, na kwamba dume, jike na mbuzi, vyovyote wanavyofanyiwa, wanabakia na uhalali wake kama walivyokuwa mwanzo na wala hawaharamishwi na porojo hizo.

Lakini waliokufuru wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na wengi wao hawafahamu.

Watu wa kijahilia walikuwa wakikubali kuweko kwa muumba kwa dalili kwamba wao wamenasibishia uharamu wa Hami, Saiba, Bahira na Waswila, lakini pamoja na hayo Mwenyezi Mungu amewanasibishia ukafiri.

Kwa sababu wao wamemnasibishia uharamu kwa uwongo na uzushi. Kwa hiyo, basi kila anayemnasibishia Mwenyezi Mungu na yasiyokuwa na dalili ya Kitab wala Hadith ya Mtume wake basi huyo ni kafir kwa sharti ya kutegemea kumnasibishia Mungu, huku akijua kutokuwepo dalili.

Hii, kwa lugha ya watu wa sharia, huitwa Bid'a (uzushi). Kuna Hadithi isemayo: "Kila bid'a ni upotevu na kila upotevu ni motoni".

Ilivyo ni kuwa kufaradhia huko kuko mbali na hali halisi ilivyo, Ni nani anayemnasibishia hukumu Mwenyezi Mungu huku akijua kuwa hakuna dalili. Pengine anaweza akadhani ni dalili, lakini kumbe sio dalili.

Wakiambiwa njooni katika yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu na kwa Mtume, husema: "Yanatutosha yale tuliyowakuta nayo babu zetu. Je hata kama babu zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?

Razi anasema: "Maana yanajulikana, nayo ni jibu la kuwapinga watu wa Taqlid (kufuata)". Tumezungumzia kuhusu Taqlid katika Juz.2 (2:170)

Enyi mlioamini! Jiangalieni nafsi zenu, Hawawadhuru waliopotea ikiwa mmeongoka, Marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu.

Razi ametaja njia nane za kufasiri Aya hii. Mmoja wa wafasiri wapya ameandika kurasa 33. Lililowafanya wawili hawa na wengineo kurefusha mambo hivi ni kuwa kuamrisha mema ni wajibu na dhahiri ya Aya inafahamisha kutokuwa wajib na kwamba ni juu ya mtu kujishughulikia mwenyewe. Ama wengine wana majukumu yao juu ya nafsi zao wala si wajibu kwa yoyote kuiongoza au kuikanya nafsi ya mwingine.

Ilivyo tafsir ya Aya hii ni kwamba, ni juu ya mtu kuamrisha mema. Kuamrisha kwake kukinufaisha basi hayo ndiyo yanayotakikana. Vinginevyo basi atakuwa ametekeleza lile aliloamrishwa wala hautamdhuru upotevu wa aliyepotea.

Mwenye jukumu baada ya kuamrisha ni yule aliyepotea na wala sio mwamrishaji. Tafsir hii imetilia mkazo wajibu wa kuamrisha mema na sio kupinga.