ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE0%

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE Mwandishi:
Kundi: Imam mahdi (a.s)

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

Mwandishi: Marehemu Mulla Muhammad Jaafar Sherif Dewj
Kundi:

Matembeleo: 20827
Pakua: 3023

Maelezo zaidi:

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 20 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 20827 / Pakua: 3023
Kiwango Kiwango Kiwango
ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

Mwandishi:
Swahili

10

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

SURA 13

MAISHA MAREFU YA HADHRAT MAHDI IMAM WETU WA ZAMA HIZI

Hadhrat Mahdi(a.s) alizaliwa mwaka 255(a.s) na yu hai hadi leo. watu hutilia shaka juu ya maisha yake marefu ya zaidi ya miaka elfu moja. ubishi upo kwamba mtu akitimiza miaka mia huwa mdhoofu, hajiwezi na pungwani, kwa hivyo vipi mtu mwenye umri wa zaidi ya miaka 1100 huweza kuwa na afya nzuri? suala hili hujibiwa kwa aya nyingi za qur'an, hadithi na kwa dalili za kiakili. kwanza, ni jambo dhahiri lililothibitishwa kihistoria kwamba watu wengi wakiwemo waumini na makafiri miongoni mwao, wanajulikana kuwa wameishi zaidi ya miaka elfu moja, kwa hakika tutathibitisha katika sura hii kwamba baadhi ya hao wapo hai hadi leo.

Qur'an tukufu inapozungumzia juu ya nabii yunus imeeleza:

فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ ﴿١٤٣﴾ لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ﴿١٤٤﴾

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu. Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa." (37:143 - 144).

Nabii Yunus alikuwa binadamu. Ikiwa allah kwa uwezo wake anaweza kumweka hai binadamu tumboni mwa samaki bila huyo binadamu kupata mwangaza, upepo, chakula hata maji mpaka siku ya kiyama, kwa nini haiwezekani kwake kumweka mtume wake (au mrithi wa mtume wake) hai kwa muda wa miaka 1,000 au 2,000? hakuna mtu anayeweza kutia shaka juu ya uwezo wa mungu. kwa hivyo, swali linaloweza kuulizwa ni je, ni kweli hadhrat mehdi(a.s) yu hai, na kama yupo hai kwa nini haonekani? masuala hayo yamezungumziwa katika sura nyingine ya kitabu biki. hata masunni wamekubali na kuandika juu ya maisha marefu ya hadhrat mehdi(a.s) hayo pia katika sura nyingine katika kitabu hiki. wafuatao ni binadamu, mitume watukufu na vile vile washirikina na makafiri ambao walijaliwa maisha marefu mno: mitume na waumini:

Nabii Nuh miaka 2,000 hadhrat lukman miaka 3,800 nabii suleiman miaka 700 miaka nabii hood miaka 464 nabii adam ambaye aliishi miaka 930 na kuacha ayali ya watu .40,000 nabii shish miaka 900 bibi hawa (mke wa nabii adam) miaka 930 manabii wanne ambao wangali hai hadi leo mbinguni kwa maelfu ya miaka: nabii idris alichukuliwa mbinguni wakati umri wake ulikuwa umekwishatimia miaka 890 na yupo huko kwa miaka elfu kwa maelfu. nabii issa yupo mbinguni kiasi cha miaka 2,000. makafiri na washirikina: iblis tangu milele, anak binti wa nabii adam, miaka 3,000. ouj bin anak, miaka 3,600 mfalme jamshed miaka 1,000 zahaq tazi (mpwa wa jamshed) miaka 1,000 aaad bin our bin irem saam bin nooh miaka 1,200 shaddaad, miaka 900. cyrus, mfalme wa iran miaka 1,000 dajjal, miaka 1,375 na yu hai hadi leo.

Duniani nabii khidhr yu hai leo miaka 4,000 na hutembea dunia nzima. nabii elias yu hai kiasi cha miaka 4,000-5,000 na hutembea dunia nzima. hatimaye, hoja moja ya kirazini. ikiwa atatokea mtu mmoja akada kwamba anaweza kutembea juu ya maji, bila shaka watu wote watamzunguka na kuona kwamba kweli huyo anatembea juu ya maji na kushangazwa na kumwamini yeye kama mtu mtakatifu. lakini ikiwa baada ya rnuda mfupi atatokea mtu mwingine na kudai hilo, mshangao wa watu utapungua na hawatakuwa wengi kumwangalia mdai wa pili kama walivyomwangalia wa kwanza. dai kama hilo halitakuwa tena jambo la kushangaza. kama akitokea mdai wa tatu watu hawatashangazwa hata kidogo na hakitakuwa kitu kipya tena.

Vile vile, ikiwa watu wengi wamekwishaishi maisha ya maelfu ya miaka ya maelfu na kwa hakika manabii khidhr na elias wamekwishaishi maisha zaidi ya miaka 4,000-5,000, na wakiwa na afya nzuri huku wakitembea dunia nzima, basi haliwezi kuwa jarnbo la kustaajabisha kuwepo hai na mwenye afya nzuri kwa imam wetu wa kumi na mbili(a.s) kwa miaka 1,110-1,200. si ajabu wala kustaajabisha tena wakati wakristo na waislamu hukubali iblis na dajjal wapo hai hadi leo na agog magog wapo hai kwa tangu maelfu ya miaka ya zama ya alexander mkuu.

Kwa hakika manabii khidhr na elias wapo hai ijapokuwa kipindi chao cha unabii na uongozi umemalizika. hiki ni kipindi cha unabii wa mtume muhammad(s.a.w.w) na kanuni za kiislamu zilizopangwa kutokana na aya za qur'an zitadumu hadi siku ya kiyama. kwa hivyo, muda mrefu wa uhai wa manabii na mfano bora sana kuhusu maisha marefu ya imam wa zama hizi, hadhrat mehdi(a.s) aliyejaliwa na mungu.

Idadi kubwa ya wanazuoni wa kisunni wamenakili katika vitabu vyao habari juu ya kuzaliwa kwa hadhrat mehdi(a.s) katika mwaka 255 a.h. na kuwepo hai kwake hadi leo na vile vile kunakili habari za watu walionana naye. hata hivyo, wengi wao huamini kwamba hadhrat mehdi(a.s) hajazaliwa bado na atazaliwa katika siku za mwisho na yeye ndiye atatawala kwa insafu na usawa. sababu kuu kuhusu itikadi hii ni kwamba wakimkubali kuwa hadhrat mehdi(a.s) amekwishazaliwa watalazimika kumkubali kama yu hai na ameghibu na bidhaa yake itakuwa kuacha imani juu ya makhalifa kumi na wawili wanaowakubali, na kufuata itikadi ya ithnaasheri ambayo inaamini kwamba ukhalifa unakomea kwa hadhrat mehdi(a.s) , imam wa kumi na mbili.

Kwa wanaomkataa hadhrat mehdi(a.s) amekwishazaliwa na yungali hai, kuwa ana pahala pake anapoishi, watoto na wahudumu wake na kukutana na watu kwa sababu tu kwamba pahala anapoishi hapakuonyeshwa katika ramani na si rahisi kufika ni kujidanganya nafsi zao. papo hapo, hao wanaomkataa imam mehdi(a.s) wenyewe wanawaamini wale waliojificha na hawaonekani na kwamba maskani yao hayajaweza kutambulika. kwa mfano, katika kitabu cha "rehla eibne battuta" (ibne battutta aliyefariki 779 a.h.), ambacho kinaeleza juu ya safari yake ndefu kwenda arabuni, iraq, asia na china, katika juzuu la pili ukurasa 64 imenakiliwa kuwa: "katika safari yangu nilifika had! china ambako nilisimuliwa juu ya sheikh wa ajabu mwenye umri wa miaka 200, lakini hakuna mtu yeyote aliyemwona akila, kunywa wala kuzungumza na mtu mwingine. alikuwa na afya nzuri lakini hakufunga ndoa, akiishi ndani ya pango lakini akitoka nje wakati akitaka kufanya ibada. hivyo niliamua kwenda pamoja na sahibu zangu kumwona huyo sheikh pangoni mwake.tuiipofika tulimwona amesimama nje ya pango lake. Nilimsalimu na akanijibu. Baadaye akaushika mkono wangu na maneno yake yalifasiriwa kwangu na mkalimani kwamba mimi ninaishi upande wa magharibi wa dunia na yeye anaishi upande wa mashariki wa dunia.

Tena akaniambia kwamba katika safari yangu nimeona vitu vya kumstaajabisha na ninakumbuka kuzuru kisiwa ambamo kulikuwa hekalu moja na humo ndani nilimwona mtu ambaye alinipa sarafu kumi za dhahabu. nikamjibu kwamba tukio hilo nakumbuka vizuri sana. akanijibu kwamba mtu yule alikuwa yeye mwenyewe (sheikh). papo hapo nilimbusu mkono wake, naye akanyamaza kimya kwa muda mrefu. ghafla yeye akaingia ndani ya pango. tulimsubin nje kwa muda mrefu sana lakini hakutokea, kwa hivyo tuliamua kumfuata ndani lakini tuliambiwa kwamba hatutaweza kumwona tena. mtumishi wake alikuwa na vipande vya karatasi ambavyo alinikabidhi na humo ndani kuliandikwa kwamba sheikh amemkabidhi zawadi kwa ajili ya wageni na kwa hivyo mimi niondoke. niliposisitiza kutaka kumwona huyo sheikh mhudumu akaniambia kwamba hata nikisubiri miaka kumi sitaweza kumwona tena kwa sababu yeye haonani na mtu yeyote mara ya pili.

Mimi nilihisi kuwa huyo mtu alikuwa pale pale na mimi, ila alikuwa haonekani tu. sisi tuliduwazwa na tukatoka kwenye hilo pango. mwandishi aliendelea kusema "mimi niliwasimulia tukio hakimu shaikhul islam na awahududin bukhari nao walithibitisha kwamba mtu yeyote aliyemwona huyo sheikh (huko china) mara ya kwanza hawezi kumwona tena na yule mhudumu aliyewakabidhi hiyo bahasha ni huyo mtu mwenyewe lakini alibadilisha sura yake. sahaba wake mmojawapo alithibitisha kwamba aliwahi kujificha kwa miaka 50 na kujitokeza ghafla. hakuna cho chote katika pango hilo lakini mhitaji yeyote aombapo msaada hupatiwa pesa. huyo sheikh (wa china) alisimulia hadithi ya mtume(s.a.w.w) na kuzungumza mambo yaliyopita. yeye hudai kwamba angalikuwa wakati wa mtume mtukufu(s.a.w.w) angalimsaidia bila wasiwasi wowote. naye huwalaani vikali mno muawiya na yazid.

Zaidi ya hayo katika kitabu hicho hicho juu ya safari zake mwandishi aandika kwamba awahuddin bukhari alimwambia kwamba yeye (bukhari) aliwahi kuingia ndani ya hilo pango na huyo sheik alipeana naye mkono. anakumbuka kwamba alikuwa katika kasri kubwa iliyopambwa sana na sheikh huyo alikaa juu ya kiti cha enzi na kuvaa taji kichwani mwake huku akizungukwa na magashi. aliona mito hupita na vile vile miti yenye matunda matamu. aliokota tunda moja ili ale lakini ghafla alijikuta yuko peke yake nje ya hilo pango. mandhari yale yalipotea na akajikuta peke yake. papo hapo akaondoka. mambo ya kustaajabisha kama hayo yanayomhusu sheikh yamenakiliwa katika vitabu vya sunni na huonekana kwamba waislamu wapo tayari kumwamini huyo sheikh, kuhusu kujificha kwake na miujiza ya kustaajabisha wakati hata jina lake halifahamiki. lakini, bado wanatia shaka juu ya hadhrat mehdi(a.s) , wakati qur'ani tukufu, hadithi na historia na vitabu vilivyoandikwa na waandishi wa kiislamu hutoa maelezo ya kutosheleza juu yake, kughibu kwake na miujiza yake.

SURA 14

KUGHIBU KWA MITUME

Sheikh Abu Jaafer Muhammad bin Babawayhi anayejulikana kwa jina la S heikh Saduq amenakili kwamba: aliambiwa na sheikh Najmuddin Abu Said Muhammad bin Hassan kuandika kitabu juu ya hadhrat Mahdi(a.s) na aliahidi kuandika atakapo rudi nyumbani tehran. aliporudi tehran hakuweza kuitimiza ahadi hiyo kwa sababu alishughulikia familia yake na matatizo mengine. siku moja aliota ndoto kwamba yuko makkah anatufu kaaba. 'alipomaliza kutufu mara yasaba na kubusu hajaril aswad (jiwe jeusi) alimwona mtu mtukufu mwenye uso uliokuwa unatoa nuru karibu na mlango wa kaaba. yeye alitia shaka kwamba huyo ni imam wake na akamwamkia ipasavyo. huyo mtu akamjibu na kumwuliza kwa sababu gani hakuandika kitabu juu ya kughibu (ghaibat). Sheikh akajibu kwamba amekwishaandika mengi kuhusu ghaibat lakini huyo mtu akasema: "la, sasa katika kitabu hicho eleza ghaiba ya manabii waliotangulia". huyo sheikh akaamka usingizini mwake na akalia. usiku kucha akakesha katika ibada na siku ya pili akaanza kuandika kitabu kuhusu [kughibu kwa imam(a.s) .

Katika sura hii, tutaelezea kwa ufupi kuhusu kujificha kwa manabii wawili. kujificha kwa Nabii Musa(a.s) sheikh sadooq ananakili kutoka kwa imam wa nne(a.s) kuwa kabla ya kufariki dunia nabii yusuf aliwakusanya ayali wake na wafuasi wake na kubashiri yatakayo tokea. akawaambia kwamba watapata rnateso makubwa katika utawala wa firaun. firaun atawafanya wanaume wao watumwa na kuwachinja na ataamrisha matunbo ya wake zao yakatwe ili watoto wauawe kabla ya kuzaliwa. allah atamwamrisha hadhrat mussa mwana wa lavi bin yakub kutokeza. atakuwa rnrefu wa kimo na mwenye uso wa rangi ya hudhurungi.

kwa muda wa miaka 400 chini ya utawala dhalimu wa firaun, waisraeli waliteseka. mtume alikaa mafichoni. Waisraeli waliomba mungu kwa bidii sana kuja kwa nabii mussa. baada ya muda mrefu walipata ishara ya kuz.aliwa kwa nabii mussa ambayo iliwapatia matumaini makuu. miongoni mwa hao waisraeli alikuwa mwanazuoni mcha mingu ambaye akiwatuliza hao waisraeli kuwabashiria juu ya kuzaliwa kwa nabii musa na ushindi wake juu ya firaun. Mateso ya firaun yaliendelea na ilimlazimu huyo mwanazuoni kujificha pangoni mwituni. Baada ya waisraeli kuchoka kuendelea kuvumilia mateso ya kubebeshwa magogo na mapande mazito mazito ya mawe walituma ujumbe kwa huyo mwanazuoni kuhusu mateso waliyopata. Wakamweleza kwamba maneno yake kuhusu ushindi ulikuwa 'faraja kwao na wakamwomba arudi kuishi nao na kuwafariji tena katika mateso.

Mwanazuoni huyo akawaalika Waisraeli hao kwake msituni. Wachache wakaenda kumtembelea. Usiku mmoja wenye mwangaza akatabiri kwamba wakati wa kuja. kwa mkombozi ulikaribia. walipokuwa wame.shughulika katika mazungumzo yao. wakamwona kijana mmoja mrefumwenye uso mwangavu mbele yao. Huyo mwanazuoni ambaye akizijua sifa za nabii musa papo hapo akasujudu kumshukuru mungu na waisraeli wote walienda sijda kumshukuru mola. walibusu miguu ya nabii musa na kueleza mateso waliyopata kutoka kwa firaun. Nabii Musa akawatuliza na kuwahakikishia kwamba ushindi umekaribia na akapoteamachoni mwao. Nabii Musa akaelekea madyan nyumbani kwa nabii shuaib na akafunga ndoa na binti wa nabii shuaib kwa sharti ya kumtumikia nabii shuaib kwa muda wa miaka kumi.

Kipindi cha kwanza cha kujificha kwa nabii musa ni sawa na kughibu kwa hadhrat mehdi(a.s) kwa muda mfupi. usumbufu kwa waisraeli ulizidi kuongezeka na subira ilikuwa inapungua. kwa hivyo, baada ya miaka kumi walienda kamwona huyo mwanazuoni ambaye aliwaarifu kuwa alikuwa amepata ilhamu kutoka kwa mwenyezi mungu ya kuwa ushindi wao ungepatikana katika miaka arobaini. kusikia hivyo, wao wakatamka "alhamdulillah" (sifa zote ziwe kwa mungu). Kushukuru huku kulimfurahisha mungu. naye akawapunguzia muda wa kuteseka uwe wa miaka ishirini. habari hii njema alipashwa mwanazuoni huyo na mungu. mwanazuoni akawaeleza waisraeli kuwa shukraini zao zimeleta faida hiyo. kusikia tu hivyo, waisraeli wakasema "rehema na huruma zote hutoka kwa mwenyezi mungu peke yake". Hapo tena mwanazuoni huyo akapata ilhamu ya kuwa mwenyezi mungu amewapunguzia huo muda uwe wa miaka kumi. waliposikia hayo wakasema kuwa hapakuwa na mwingine ila mwenyezi mungu mwenye uwezo wa kuwakomboa.

Punde si punde, wakamwona nabii musa ametokeza. wakasujudu kwa mwenyezi mungu na kumbusu miguu nabii musa ambaye aliwafikishia habari njema ya kuwa aliamrishwa na allah kujitokeza ra kumkabili firaun na akawaamrisha waondoke. baada ya hapo nabii mussa akaelekea kwenye kasri ya firaun ambaye akaamrisha wachawi wake wahudhurie. nabii musa akatoka misri na waisraeli 600,000, wake kwa waume, wazee na vijana, na akavuka mto. lakini firaun na wafuasi wake wengi walipojaribu kuuvuka mto wakazama. Hivyo inathibitika kujificha kwa hadhrat musa na majaribio na mitihani kwa wafuasi wake. vivyo hivyo wafuasi wa mtume muhammad(s.a.w.w) hujaribiwa na kutahiniwa. kujificha kwa nabii suleiman nabii dawood alirithiwa ufalme na nabii suleiman. baadaye nabii suleiman kwa amri ya mungu akajificha kutoka wafuasi wake na tatika kipindi hicho akapata taji ya ufalme. hadithi yake ni kama ifuatayo: nabii dawood aliimarishwa na mungu kumteua mwanawe wa mwisho suleiman kuwa mrithi wake. nabii dawood aliwajulisha wanawe na wafuasi wote juu ya uamuzi huo. waisraeli hawakupendezwa na uamuzi huo eti ulikuwa sio wa insafu kwa sababu nabii suleiman alikuwa mdogo kuliko wote na kaka zake walikuwa wenye uwezo na ujuzi.

Nabii Daudi akawaambia kwamba: hakuna yeyote anayeweza kutengua amri ya Mungu. Lakini kuwatosheleza akawaomba wanawe kuweka vitawi vilivyoandikwa majina yao katika chumba maalum, na vile vile akamwomba nabii suleiman kuweka vitawi vilivyo andikwa jina lake katika chumba hicho maalum. Siku ya pili wote walitakiwa wafike kuangalia kwamba vitawi gani vime mea na kuota majani na matunda. mwenye vitawi vilivyo mea na kuota majani na matunda ndiye atakuwa mrithi wake. wote waliridhika na wazo hilo na wakaleta vitawi. Siku ya pili walipofungua hicho chumba ilionekana kuwa vitawi vya nabii suleiman tu vilikuwa vimeota majani na kuzaa matunda. kwa hivyo wote walikubali uteuzi wa nabii suleiman.

Kuthibitisha zaidi ustahilifu wa Nabii Suleiman, nabii Daudi akamtahini elimu yake na uwezo wake kadamnasi ya waisraeli. akamwuliza "kitu gani humpa mtu furaha na utulivu wa moyo?" nabii suleiman akajibu "kusamehewa na mungu na kusameheana watu wenyewe". nabii dawood tena akamwuliza: "kitu gani chenye ladha mno?" "huba na urafiki wa ukweli kwani upendo na urafiki wa ukweli ni zawadi na rehema kutoka kwa mungu juu ya viumbe wake." (katika zamana hii zawadi ya mungu ya mapendano na urafiki imepotea na badala yake uadui, husuda na dhuluma imezagaa ambayo ni adhabu kutoka kwa mwenyezi mungu). nabii dawood alifurahishwa sana na ubora na usahihi wa jibu kutoka kwa mwanae. akawauliza waisraeli kama wameridhika kwamba nabii suleiman alistahili urithi kwa kila njia.

Baada ya kifo cha nabii dawood, nabii suleiman kutokana na amri ya mungu alienda kujificha. Katika kipindi hicho wafuasi wake waliteseka na kupata shida. nabii suleiman alikwenda kujificha katika nchi ya jirani ambako aliolea na kuishi na wakwe zake. Siku moja mkewe akamwambia kwamba anampenda sana kwa tabia zake, sifa na ukarimu wake. lakini huona dhila kutegemea wazazi wake na alimpa wazo la kujitafutia maisha yake na kujitetegemea kimapato. Nabii Suleiman akajibu kwamba: hakuwa na ujuzi wa kazi yoyote ya kujikimu kistahiki kwa sababu hakuhitajika kufanya kazi (kwa muda alikuwa mwana wa mfalme). Hata hivyo, aliahidi kwamba siku ifuatayo atakwenda sokoni kujitafutia mapato. alijiandaa kwenda kufanya kazi, lakini hakufanikiwa chochote. mkewe mwema akamtuliza moyo na akampa hima kwamba ajaribu sikuya pili.

Siku ya apili vile vile nabii suleiman akarudi mikono mitupu. tena mkewe akamsihi asivunjike moyo na kumhakikishia kwamba kutokana na rehema ya mungu atafanikiwa. siku ya tatu nabii suleiman akenda pwani na kumwomba amtumikie mvuvi kwa ujira wowote, mvuvi akakubali ombi na jioni yake akampa nabii suleiman samaki wawili kama ujira wake. nabii suleiman alifurahi na akamshukuru mungu nabii suleiman akamkata samaki huyo vipande na kumsafisha. tumboni mwa samaki mmoja nabii suleiman akapata pete moja. kwa vile alikuwa nabii, akatambua kuwa hiyo pete ni dalili yq ufalme. akasafisha hiyo pete akaiweka kwenye leso na kuweka mfukoni mwake. baadaye, akawachukua hao samaki wawili na kwenda nyumbani, ambako akamwona mkewe amefurahi sana.

Huyo mkewe akamwita baba yake akamwonyesha samaki wawili, nabii suleiman hapo akamwuliza baba mkwe " unajua mimi nani" huyo baba mkwe akajibu kwamba nabii suleiman alikuwa mtu mwema na yeye (bab mkwe) akimhesabu kama mwanawe lakini alikuwa hamjui kama yeye ni nani. Hapo nabii Suleiman akamsimulia kwamba yeye ni mwana wa Nabii dawood, mwana wa mfalme na mriuthi wa kiti cha ufalme. akatoa hiyo pete kutoka mfukoni mwake na kuivaa. papo hapo, majini na ndege kutoka pande zote walikusanyika bele yake. Nabii Suleiman akaelekea kwenda mji mkuu pamoja na mkewe na wakwe zake. Wafuasi wake walifurahi sana kumwona nabii Suleiman na wakamshukuru Mungu. Hii ni mifano miwili kuhusu kujificha kwa mitume. Wafuasi wa kila mtume walijaribiwa. kujificha kwa manabii Yusuf Ibrahim na Idris kumeelezwa katika vitabu vingine. Kwa kufupisha kitabu hiki hatuandiki habari hiyo humu.

11

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

SURA 15

HADHARAT MAHDI (A.S) NA WSIO WAISLAM

Allamah Gulam Husein Kanturi ameandika katika kitabu chake Intisarul islam (1917) kwamba: jamaa yake wa karibu Hakim Seyyid Zafer Mahdi alirudi lahore baada ya kwenda kuhiji pamoja naye. Mnajimu mmoja wa kihindi alimjia na akamwomba Seyyid amwulize swali. Seyyid alimwomba apokee zawadi bila ya kumuuliza swali, lakini huyo mnajimu alikataa kupokea zawadi bila kuulizwa swali. Huyo Seyyid alikerwa sana kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa mnajimu. lakini, hata hivyo, alimwuliza ili aweze kujua kwamba huyo mnajimu alikuwa anaweza kubashiri juu ya mambo yajayo, mambo ya kale na kumweleza nini alikuwa anafikiria.

Huyo mnajimu aliendelea kueleza juu ya jambo gumu; Seyyid huyo akamwomba amweleze juu ya mtu anayemfikiria kwa wakati huo. huyo mnajimu akafikiria na kufanya hesabu kwa uwezo wake wote lakini bila mafanikio. mwishowe akaweza kupata undani wa habari ya huyo anayefikiriwa; sura yake na sifa zake ambazo zilimshangaza yeye mwenyewe. huyo mnajimu akamwambia seyyid kwamba huyo mtu anayefikiriwa ni mfalrne wa dunia na akhera. ameng'amua kwamba hata akijitahidi maisha yake yote hataweza kujua habari kamili ya buyo mtu. akaeleza kwamba huyo ni mfalme wa duniani na akhera, na vile vile mfalme wa wafalme duniani.

Kusikia hivyo, huyo seyyid alifurahishwa sna na akasema kwakmba kwa wakati huo alikuwa akimfikiria imam mahdi(a.s) ambaye mnajimu aliweza kumtambua. hapo sayyid akamwamrisha mhudumu wake kuleta kashida nzuri sana na kumvika begani. mnajimu huyo alikataa kupokea zawadi yoyote na machozi yalimlenga lenga. "sitaki ,sitaki, sihitaji zawadi ya kashida. leo kutokana na suala lako nimepata ufumbuzi mkubwa na wenye thamani kuliko ufalme wowote duniani. Nimeongozwa kwenye njia ya ukweli na nimemfahamu bwana wangu wa kweli. Sina tama ya kitu chochote duniani" hapo mnajimu akalia sana na seyyid na wenzake wote pia wakalia.

Mwandishi (hayati) wa kitabu hiki alitembelewa katika mwaka 1930 a.d. na mnajimu mmoja kutoka bombay ambaye alikuwa na umri mkubwa, ndevu nyeupe na akijitambulisha kuwa ni husein brahmin. baniani wa aina ya brahmin alietokana na kizazi cha wafuasi wa iamam husein (a.s) alimwomba mwandishi amwulize suali lakini kwa vile hayati alikuwa na shughuli nyingi hakumjali. hata hivyo, mnajimu huyo aliendelea kukaa hapo na baada ya muda mfupi akaanza kumweleza habari ya maisha yake yaliyopita nay a baadaye, biashara yake, burudani, tabia zake njema na mbaya na vilevile afya yake, mwandishi alishangazwa; kwa hiyo, alianza kumsikiliza kwa makini. asilimia tisini na tisa ya aliyoeleza yalikuwa ya kweli. kwa hivyo, mwandishi akasema: "nimejishughulisha kwa muda mrefu sasa kujua habari za rafiki yangu. Nataka kujua yuko wapi, ana hali gani, yu hai au amefariki dunia, ana raha au ana shida na kama kuna uwezekano wowote wa kuonana naye. ukinipa jibu la kunitosheleza nitakupa rupia 25 za kihindi."

Kusikia hayo, mnajimu huyo akaanza kupiga mahesabu yake juu ya karatasi. kabla ya hayo alimsimulia mwandishi mambo mengi bila ya kufanya mahesabu yoyote. Mwandishi alipomwuliza kwa nini anafanya hivyo, mnajimu akamjibu kwamba aliweza kutoa habari zote kwa kutazama paji la uso wake, lakini sasa anahitaji msaada wa kalamu ili aweze kutafuta habari za rafiki yake. baada ya michoro mingi juu ya karatasi na mahesabu ya vidole na kuinamisha kichwa mara kwa mara kwa muda wa robo saa akasema: "Bila shaka rafiki yako unayemfikiria ni mtu mkubwa sana. yeye hutawala juu ya ulimwengu na mbinguni, hana wasiwasi wala shida yoyote ila fikra juu ya dini ya jadi yake. bila shaka yu hai na ana raha ya kila aina. karibu atajitokeza kutawala india, asia na dunianzima, na akaendelea kueleza sifa nyingi njema ya huyo rafiki (imam Mahdi a.s) ambazo zilimfurahisha mwandishi kiasi cha kumpa mnajimu rupia 25. mwandishi tena akamwuliza siku gani huyo mfalme atajitokeza ? akafanya mahesabu na akasema karibu sana katika muda wa miaka 25 au 30 atajitokeza na kushinda dunia nzima. (tanbihi: hakuna mtu yeyote anayeweza kutoa taarifa kwa uhakika siku gani mungu ataamua kumwamrisha imam mehdi(a.s) kujitokeza.

Hata hivyo mahesabu ya wanajimu yamethibitisha kuweko na kughibu kwa hadhrat mehdi(a.s) . muhaki-el-tusi, mwanazuoni maarufu wa shia ithnaasheria, alisumbuliwa sana na suala la "upekee wa mungu", ambalo aliulizwa na mlahidi (asiye amini mungu). alifanya mahesabu ya kinajimu kutafuta wapi hadhrat mehdi(a.s) atakuwa kwa wakati huo na akaona kwamba atakuwepo masjid-ul-kufa. kwa hivyo papo hapo aliondoka najaf, akakutana na imam(a.s) na akapata jibu la kumtosheleza na kutatua tatizo lake.

Imam(a.s) akamwuliza vipi alijua kwamba yeye yupo pale (masjid-ul-kufa). akamjibu kuwa kutokana na mahesabu yake, imam(a.s) akamsihi kwamba asirudie tena jambo hilo na muhakiki Attusi aliomba msamaha na kueleza kwamba alifanya hivyo kwa sababu ya tatizo alilo nalo na kuahidi kuwa asingerudia padri mmoja wa kiingereza alichapisha kitabu kiitwacho "maajabu arubaini ya siku zijazo" kutokana na kitabu cha nabii. daniel, kubusu vita, njaa na alama zingine zitakazo jitokeza katika siku za mwisho wa dunia. Kitabu hicho kilipendwa sana na kilichapishwa 1925 a.d., ambacho "hayati mwandishi alikisoma mwenyewe. padri huyo kaandika kuwa kutakuwa vita kuu katika siku zijazo na nchi tisa tu za ulaya zitasalimika.

Nchi ya kumi itakuwa syria ambayo mfalme wake yumkini atakuwa muhammad mehdi. huyo mehdi atakuwa mpinzani mkali wa ukristo. atavamia ulaya, atashinda na hatimaye kushinda dunia nzima. lakini atatawala kwa miaka saba tu na baadaye nabii issa atatokeza na ukristo utaenea duniani kote. hapo nabii issa atatawala miaka elfu moja. mwandishi (hayati) mwenyewe binafsi amekiona kitabu hicho toleo la l6 na kusoma yaliyomo, lakini katika matoleo yaliyo fuata jina la. mehdi limefutwa. padri huyo labda alitanabahi kwamba jina hilo huthibitisha ukweli wa uislam na wa imam mehdi(a.s) . Hata hivyo, ufutaji wa jina la Mahdi(a.s) hauwezi kukanusha ukweli. yeyote ambaye anaweza kupata nakala ya toeo la 16 la kitabu hicho ataweza kuhakikisha kwa dhati jina la imam mehdi(a.s) lilivyotajwa bayana.

Kwamba hadhrat mehdi(a.s) atatawala dunia nzima ni ushahidi madhubuti kuhusu kujitokeza kwake. kwamba baada ya utawala wake wa miaka saba utafuata uenezi wa ukristo duniani na nabii issa atatawala kwa miaka elfu moja si jambo la kuwababaisha wafuasi wa hadhrat mehdi(a.s) . ni imani yetu kwamba nabii issa atakuja baada ya muda mfupi wa kujitokeza kwa hadhrat mehdi(a.s) na dini pekee ya ukweli, uislam, itaenea dunia nzima. nabii isa kamwe hakudai kuwa mwana wa mungu na hakufundisha kwamba kuna mungu zaidi ya mmoja na huyu mungu ana mshirika yeyote. yeyote anaye amini katika upekee wa mungu, mtume muhammad(s.a.w.w) pamoja na manabii wote ni mwislamu. waumini wa nabii adam na manabii waliofuata ambao wamezingatia mafundisho yao, na kujizuia na maasi wote ni waislamu. katika qur'an tukufu kuhusu nabii Ibrahim Mungu anasema: "Amewaiteni jina la waislam ." (22:78).

Katika zaburi aliyoteremshiwa nabii dawood, aya ya nne, sura 19, murmuz, imeandikwa kwamba katika siku za rnwisho za dunia atakuja mtu mmoja ambaye atakuwa na kivuli cha wingu juu yake na ambaye ataeneza usawa na insafu.

katika kitabu cha mtume safyay, aya ya 3, imeandikwa: "Tahadharini kwamba katika siku za mwisho duniani atatokeza mtu mmoja ambaye atasababisha watu wote kumwabudu mungu mtindo mmoja (wote wataamini katika upekee wa mungu). Katika kitabu cha mabaniani (hindoo) fat ankal imeandikwa kuwa, "maisha duniani yatagawanyika katika vipande vinne, na kila kipindi kitagawanyika katika mida maalum na kila muda utakuwa wa kipindi cha miaka elfu nne. dunia itaendelea kwa muda wa miaka 256,000 na mwisho atatokeza mtu rnmoja muadham. huyo atatokana na kizazi cha viongozi wakuu wawili, mtume wa mwisho(s.a.w.w) na mrithi wake ajulikanaye kwa jina la bishan. Jina la huyo mtu atakaye tokeza itakuwa mwongozi (Mahdi) na atakuwa walii wa ram (Mungu).yeye atatawala dunia kama walivyotawala mitume walio pita na ataonyesha miujiza mingi; yeyote atakayemkubali huyo (Mahdi) ataokoka. Atakuwa na maisha marefa na ataishinda dunia nzima, atabomoa jumba la masanamu somnath na kutokana na amri yake sanamu kuu jaganath litapata uwezo wa kusema na baadaye litaporomoka. mwishowe kwa agizo lake masanamu yote yatavunjwa duniani kote.

Katika kitabu cha dini ya hindoo kiitwacho nasak, imeandikwa kuwa: "wakati dunia itakapo karibia kwisha kutakuwa ufalme ambamo ukweli na insafu itatawala. hazina zilizojificha chini ya bahari kuu, majabali au ardhi zitajitokeza na kuanza kuelezea siri zitajitokeza na kuanza kuelezea siri zote za duniani na mbinguni. katika kitabu cha dini ya waabudu moto "zand vapa zand" ambacho huaminiwa kama kataremshiwa nabii zardosh, kuhusu hadhrat mehdi(a.s) . vile vile katika vitabu vingine "kosab na azwasan' imeandikwa juu ya habari za imam mehdi(a.s) . Hakim jamasap katika kitabu kuhusu Mtume(s.a.w.w) na warithi wake amearidhia: "mtume mmoja atazaliwa katika milima ya uarabuni, atapanda ngamia na atakaa na kula na watumwa (hatakuwa mtu mwenye kiburi).

Yeye atafuta dini zingine zote, atashinda iran na kubatilisha dini ya waabudu moto. mrithi wa mwisho wa huyo mtume(s.a.w.w) atakayetokana na kizazi cha binti wa mtume(s.a.w.w) atatawala dunia nzima kwa uwezo aliopewa na mungu. utawala wake utaanzia makkah na utaendelea mpaka siku ya kiama. Atamkamata na kumfunga adui wa mungu, aharman (iblisi) na malaika kutoka mbinguni watafika kwake. atawafufua (waliokufa na kupata uhai kwa amri ya mungu) wema na waovu. atawapa jazaa wema na kuwaadhibu waovu. atamfufua baba yake nabii khidhr, nabii elias, mahras, lafvas baba wa ahasata lalis, nuh, shamasun na solan shamueel. Vile vile atawafufua namrood, firaun, hamman na kuwachoma moto."

Mengi yameandikwa kuhusu huyo mfalme (hadhrat Mahdi a.s.) wa siku za mwisho za dunia. katika vitabu vingi vya manabii wa zamani na vile vile katika vitabu vitukufu: torat, injiil na zabur na vile vile katika vitabu vingine vya dini zingine (zisizokuwa za kiislamu). zaidi ya hayo, wakristo, mayahudi, waabudu moto na mabaniani wanamsubiri mwongozi. wakristo humsubiri nabii issa na mayahudi nabii mussa. kwa hivyo, dunia nzima humsubiri huyo 'hadi' ambaye atasafisha dunia hii kutokana na maovu, fitina, ugomvi, vita, maafa, mateso au ulahidi na kueneza usawa wa uadilifu. kwa jumla, imani ya watu wote duniani huthibitisha imani yao juu ya "anayesubiriwa" na huimarisha hoja ya kwamba hao wote waliodai kuwa mehdi ni wadanganyifu tu. hawakuweza kutimiza chochote kama anavyotarajiwa kutimiza mehdi wa kweli.

Bayasajee aliandika kitabu 'bothiran sandhram' na gosai tulsidasji alitafsiri hicho kitabu katika lugha ya kihindi. Katika sura ya 12; ya tafsiri hiyo, ukurasa 212, ameandika: "Mimi sitaandika chochote kutokana na maoni yangu lakini ukweli mtupu ulioandikwa katika ved na purana. Katika muda wa miaka kumi nguvu zote zitamalizika na hakuna yeyote atakuwa na nguvu kama hiyo tena. badala ya hayo nyota itang'aa pahala patakatifu duniani. Miujiza yasiyoaminika yatafanyika na walii aliyekamilika atateuliwa duniani. yeyote atakayetamani kupata ridhaa ya mungu atawajibika kumtii muhammad. baadaye atatoka mtu atayejulikana kwa jina la mehdi. uwezo wote utakuwa wake (imenakiliwa kutoka gazeti la kisunni molvi-delhi- rasool, safar/rabiul awwal. 135z ah).

12

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

SURA 16

HADITHI KUHUSU MUDA WA KUSUBIRI (INTIDHAR) NA MAJARIBIO YA MUDA HUO

1. Hadhrat imam Ali Ridhaa(a.s) amessema kwamba: katika qur'ani Mwenyezi Mungu amezungumzia juu ya kugojea:

"Basi ngojeni; ngojea hapo. mimi vilevile nitakuwemo katika wale wanaongojea" (7:71).

2. Hadhrat Ali(a.s) amesema:"ngojea (msubiri) kutokeza imam mehdi; hivyo, yeyote atakayesubiri amri zetu atazawadiwa cheo cha shahidi anayegalagala katika damu yake" .

3. Hadhrat imam Jaafar Sadiq(a.s) ameeleza: "kutakuwa kipindi ambamo imam(a.s) atakuwa haonekani kwa wafuasi wake ambao itawabidi wavumilie mateso kutoka maadui wao kwa muda mrefa mmo siku ya kiyama watapewa habari njema kutokana na imani yao juu ya imam aliyeghibu, madhambi yao yatasamehewa na mema yao yatazawadiwa, na kwa sababu ya hao waumini duniani kutanyesha mvua na kuota vyakula. wasingekuwepo allah aangeliwateremshia adhabu hao wahalifu.

4. Imam Jaafar Sadiq(a.s) amesema kwamba:"Mwumini yeyote atakaye msubiri imam wake aliyeghibu kwa makini akifariki dunia atapewa jazaa ya kuishi na imam mehdi (a.s)." .

5. Imenakiliwa kutoka abdulhamid wasti kwamba yeye alilalamika kwa imam hadhrat muhammad baqir(a.s) kwamba kusubiri daima usiku na mchana kwa ajili ya mwokozi wa mwisho huathiri shughuli za kila siku maishani. imam akajibu "yeyote mwenye imani kuwa mungu atamwokoa kwa mkono wa wokovu, mungu mwenyewe humtimizia mambo yake. mwenyezi mungu amteremshie rehema huyo mwumini ambaye huvumilia shida kwa ajili yetu na hueneza hdithi zetu (mambo ya dini) kwa waumini wengine." adbulhamid akauliza tena, kama huyo mtu akifariki dunia kabla kujitokeza imans(a.s) je? imam akamjibu kwamba yeyote anaetamani kwamba atakapojitokeza hadhrat mehed(a.s) yeye awe mmoja wa wasaidizi wake kwenda vitani naye, atapata daraja kama ya mtu yule ambaye aliyeishi pamoja na hadhrat mehdi(a.s) na kupigana vita vya dini kutokana na amri yake (imam mehdi).

6. Mtume mtukufu(s.a.w.w) aliwaambia masahaba wake: " katika siku za mwisho za dunia wema wa mwumini mmoja utazidi wema wa watu 25 wenu". Masahaba wakalalamika kwamba wao walikuwa pamoja na mtume(s.a.w.w) na wamekwenda vitani naye. lakini mtume(s.a.w.w) akajibu, "siku za mwisho duniani waumini watakuwa wamezingirwa na maadui, kuzungukwa na maafa yaliyo sababishwa na maadui wao, lakini hata hivyo watakuwa imara katika imani yao kiasi hata nyinyi hamtaweza kulingana nao.

7. Imam wa tano, hadhrat muhammad baqir(a.s) . akiwahutubia marafiki na mashia juu ya dhuria ya mtume(s.a.w.w) akasema:"kumbukeni kwamba bila shaka rntatahiniwa katika uthabiti wa imani yenu na hiyo imani itatoweka bila nyinyi kufahamu. hilo jambo litakuwa kama mfano wa wanja, unapokuwa machoni hudhihirisha athari yake lakini hutoweka (yeyuka) bila mtu mwenyewe kufahamu. vilevile kati yenu watakuwa watu ambao asubuhi wataamka waumini lakini magharibi watakuwa wamepotelewa na imani yao bila wao wenyewe kufahamu" .

8. Hadhrat imam Jaafar Sadiq(a.s) amesema:"Wakati waovu namakafiri watakapoeleza (julikana) imani yao kadamnasi na waumini kudhihirisha imaniyao na tofauti baina ya waumini na makafiri kudhihirika, na watu kukata tamaa na kufa moyo ndipo imam (a.s) atajitokeza." maana ya hadithi hii ni kuwa yatakuwa majaribio magumu mno. wale watu ambao hawajali dini yao na kwa hivyo ni wazembe wa kuswali, au kufunga na kutekeleza maagizo mengine ya kidini, waliojishughulisha katika mambo ya dunia, na ni wadhalimu watafedheheka, na kwa upande mwingine wale wacha mungu waswalihina, wanaofunga mwezi wa ramadhani na kutekeleza maagizo mengine, wema, waoambao toba, wenye huruma na wathabiti katika imani yao watafaulu majaribio hayo.

9. Zaidi ya hayo imam Jaafar Sadiq(a.s) alimwambia Abu Basir kwamba: theluthi mbili ya wafuasi wa hadhrat hujjat(a.s) wataacha dini (kwa sababu ya dhambi zao na uzembe wao watakata tamaa na kwanza kuuliza ikiwa imam(a.s) yupo ughaibuni kwanini hajitokezi? Kwa hivyo, watapoteza imani yao juu ya imam(a.s) .

10. hadhrat imam muhammad baqir(a.s) amesisitiza kwamba bidii ifanywe ya kuwasimulia waumini hadithi ya kughibu na kuonekana tena kwa hadhrat imam mehdi(a.s) na wale wasioamini waache walivyo.

11. Hadhrat Ali(a.s) ameserna: "Nyinyi waumini ni kama nyuki. Watu duniani watafikiri nyinyi wanyonge, wanyenyekevu, na msiothaminika. hawatatambua sifa zenu. kumbukeni kwamba imam wenu hatatokeza mpaka nyinyi mtapo gombana na kila mtu kumwita mwenzie mwongo kutokana na mafarakano baina yenu. katika siku hizo za majaribio na mitihani wachache mno watabakia juu ya imani yao kwa uthabiti".

SURA 17

ALAMA ZITAKAZO DHIHIRIKA KATIKA SIKU ZA MWISHO ZA DUNIA

Wakati huu, yaani siku za mwisho (Akhiru Zamani) dunia imezingirwa na ulahidi, ukafiri, udhalimu, uovu na ukandamizi. binadamu amezongwa na ugomvi, vita, jefule na amepoteza imani juu ya mungu. Hata hivyo, kipindi hiki kinajulikana kama ni kipindi cha ustaarabu, elimu, utafiti, ufumbuzi na hekima. jumuia zingine zimefuata nyayo ya maendeleo ya kipindi hiki nasi twashawishika tufuate mtindo huo. Hata hiyyo, maendeleo yote ya zamana hii humezwa na ugomvi, vita na dhuluma.

Hadhrat Ali(a.s) amesema kwamba:katika siku za mwisho za dunia binadamu atapoteza busara yake na kupotoshwa katika mawazo yake, kila kilichokuwa chema atakiona kibaya na kiovu, lakini uzushi (bidaat) katika mambo ya dini, uasherati, uhayawani utatukuzwa . kuna hadithi nyingi zinazoeleza alama za siku za mwisho za dunia. nyingi zimekwisha dhihirika na zingine zinadhihirika. alama muhimu zitadhibirika katika muda mfupi kabla ya kujitokeza kwa imam(a.s) .

Hadithi chache kuhusu alama hizo ni kama zifuatazo:

1. Mtume mtukufu(s.a.w.w) ameridhia kuwa utafika wakati:

a) Mtu atamthamini mwanazuo (Aalim) kufuatana na mavazi mazuri yake.. (wataangalia mapambo ya mwanazuoni, mwanazuoni wa kweli atadharauliwa na atabaki fukara).

b) watu watatamani kusikia qur'ani kutokana na uzuri wa sauti ya wasomaji (qur'ani husikilizwa katika redio, na kaseti kutokana na uzuri wa sauti ya wasomaji).

c) watu watamwabudu mungu katika mwezi wa ramadhani tu. (katika miezi mingine usomaji wa qur'ani, ibada na saumu vitasahaulika). ukija wakati kama huo watu watateseka kutokana na watawala dhalimu.

2. hadhrat ali (a.s) amesema kwamba: "katika siku za mwisho za dunia mfalme wa iran atapinduliwa. ataomba msaada kutoka wasio waislamu. mashavu ya miguu yake yatakuwa membamba (yeye kwa maumbile atakuwa mnene mno). jina la mfalme huyo litakuwa ahmed (huyo alikuwa mfalme wa mwisho katika ukoo wa kajar). alipopinduliwa alikimbilia paris (ufaransa) na kufia huko huko. hata jina lake lilibashiriwa miaka 1300 kabla ya hadhrat ali(a.s) .

3. Hadhrat ali(a.s) vile vile alisema katika siku hizo waislamu watavaa vitambaa vya rangi shingoni mwao.

4. Vilevile amesema: "tehran itakuwa kama gereza na jahannam kwa waumini, lakini pepo kwa wale wasio na imani. hapatakuwa kitu chochote cha dini (uislam), wanaume watakuwa na tabia za kike na wanawake watadharau buibui, watatembea uso wazi masokoni na kujazana barabarani.

5. katika vyuo watakuwa wanafunzi wa aina mbili:

a) Wale ambao wanajifunza falsafia.

b) Wale ambao wanajifunza mambo yasiyo husiana na uislamu.

6. Hadhrat imam Jaafar Sadiq(a.s) amesisitiza kuwa: "Wakati nchi zinazingirwa na balaa, fitina na uovu inafaa mtu ahame kwenda kuishi katika jiji la qum, iran, ambalo litakuwa pahala pa amani na kuepukana na maafa, vyuo vya elimu vitahamia qum kutoka najaf, karibu na wakati wa kujitokeza kwa imam mehdi(a.s) . qum kutakuwa makao makuu ya kujipatia masomo ya dini ya kiislam.

7. Namna wanawake wanaotembea bila haya na kutojifunika huku kujipamba ni mojawapo ya alama za mwisho wa dunia. kuna hadithi nyingi kuhusu alama kama hii na tunazinakili chache tu.

a) Hadhrat Ali(a.s) amesema"Wanawake watakuwa hawana haya. watajihusisha na wanaume wasiokuwa waume zao. mitindo ya usukaji wa nywelie utafanana na nundu iliyojitokeza ya ngamia. wanawake hao katu hawataingia peponi" (kitu kilichobashiriwa na mtume(s.a.w.w) na maimamu kabla ya miaka 1300 kinaonekana dhahiri kabisa na kuthibitisha ukweli wa hadithi hizo, na wa uislaam).

Mwanazuoni huyo akawaalika waisraeli hao kwake msituni. wachache wakaenda kumtembelea. usiku mmoja wenye mwangaza akatabiri kwamba wakati wa kuja. kwa mkombozi ulikaribia. walipokuwa wame.shughulika katika mazungumzo yao. wakamwona kijana mmoja mrefumwenye uso mwangavu mbele yao. huyo mwanazuoni ambaye akizijua sifa za nabii musa papo hapo akasujudu kumshukuru mungu na waisraeli wote walienda sijda kumshukuru mola. walibusu miguu ya nabii musa na kueleza mateso waliyopata kutoka kwa firaun. nabii musa akawatuliza na kuwahakikishia kwamba ushindi umekaribia na akapoteamachoni mwao. nabii musa akaelekea madyan nyumbani kwa nabii shuaib na akafunga ndoa na binti wa nabii shuaib kwa sharti ya kumtumikia nabii shuaib kwa muda wa miaka kumi.

Kipindi cha kwanza cha kujificha kwa nabii musa ni sawa na kughibu kwa hadhrat mehdi(a.s) kwa muda mfupi. usumbufu kwa waisraeli ulizidi kuongezeka na subira ilikuwa inapungua. kwa hivyo, baada ya miaka kumi walienda kamwona huyo mwanazuoni ambaye aliwaarifu kuwa alikuwa amepata ilhamu kutoka kwa mwenyezi mungu ya kuwa ushindi wao ungepatikana katika miaka arobaini. kusikia hivyo, wao wakatamka "alhamdulillah" (sifa zote ziwe kwa mungu). kushukuru huku kulimfurahisha mungu. naye akawapunguzia muda wa kuteseka uwe wa miaka ishirini. habari hii njema alipashwa mwanazuoni huyo na mungu. mwanazuoni akawaeleza waisraeli kuwa shukraini zao zimeleta faida hiyo. kusikia tu hivyo, waisraeli wakasema "rehema na huruma zote hutoka kwa mwenyezi mungu peke yake". hapo tena mwanazuoni huyo akapata ilhamu ya kuwa mwenyezi mungu amewapunguzia huo muda uwe wa miaka kumi. waliposikia hayo wakasema kuwa hapakuwa na mwingine ila mwenyezi mungu mwenye uwezo wa kuwakomboa.

Punde si punde, wakamwona nabii musa ametokeza. wakasujudu kwa mwenyezi mungu na kumbusu miguu nabii musa ambaye aliwafikishia habari njema ya kuwa aliamrishwa na allah kujitokeza ra kumkabili firaun na akawaamrisha waondoke. baada ya hapo nabii mussa akaelekea kwenye kasri ya firaun ambaye akaamrisha wachawi wake wahudhurie. nabii musa akatoka misri na waisraeli 600,000, wake kwa waume, wazee na vijana, na akavuka mto. lakini firaun na wafuasi wake wengi walipojaribu kuuvuka mto wakazama. hivyo inathibitika kujificha kwa hadhrat musa na majaribio na mitihani kwa wafuasi wake. vivyo hivyo wafuasi wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) hujaribiwa na kutahiniwa.

Kujificha kwa nabii suleiman nabii dawood alirithiwa ufalme na nabii suleiman. baadaye nabii suleiman kwa amri ya mungu akajificha kutoka wafuasi wake na tatika kipindi hicho akapata taji ya ufalme. hadithi yake ni kama ifuatayo: nabii dawood aliimarishwa na mungu kumteua mwanawe wa mwisho suleiman kuwa mrithi wake. nabii dawood aliwajulisha wanawe na wafuasi wote juu ya uamuzi huo. waisraeli hawakupendezwa na uamuzi huo eti ulikuwa sio wa insafu kwa sababu nabii suleiman alikuwa mdogo kuliko wote na kaka zake walikuwa wenye uwezo na ujuzi.

Nabii dawood akawaambia kwamba hakuna yeyote anayeweza kutengua amri ya mungu. Lakini kuwatosheleza akawaomba wanawe kuweka vitawi vilivyoandikwa majina yao katika chumba maalum, na vile vile akamwomba nabii suleiman kuweka vitawi vilivyo andikwa jina lake katika chumba hicho maalum. siku ya pili wote walitakiwa wafike kuangalia kwamba vitawi gani vime mea na kuota majani na matunda.

Mwenye vitawi vilivyo mea na kuota majani na matunda ndiye atakuwa mrithi wake. wote waliridhika na wazo hilo na wakaleta vitawi. siku ya pili walipofungua hicho chumba ilionekana kuwa vitawi vya nabii suleiman tu vilikuwa vimeota majani na kuzaa matunda. kwa hivyo wote walikubali uteuzi wa nabii suleiman.

Kuthibitisha zaidi ustahilifu wa nabii suleiman, nabii dawood akamtahini elimu yake na uwezo wake kadamnasi ya waisraeli. akamwuliza "kitu gani humpa mtu furaha na utulivu wa moyo?" nabii suleiman akajibu "kusamehewa na mungu na kusameheana watu wenyewe". nabii dawood tena akamwuliza: "kitu gani chenye ladha mno?" "huba na urafiki wa ukweli kwani upendo na urafiki wa ukweli ni zawadi na rehema kutoka kwa mungu juu ya viumbe wake." (katika zamana hii zawadi ya mungu ya mapendano na urafiki imepotea na badala yake uadui, husuda na dhuluma imezagaa ambayo ni adhabu kutoka kwa mwenyezi mungu).

Nabii daudi alifurahishwa sana na ubora na usahihi wa jibu kutoka kwa mwanae. akawauliza waisraeli kama wameridhika kwamba nabii suleiman alistahili urithi kwa kila njia. baada ya kifo cha nabii dawood, nabii suleiman kutokana na amri ya mungu alienda kujificha. katika kipindi hicho wafuasi wake waliteseka na kupata shida. nabii suleiman alikwenda kujificha katika nchi ya jirani ambako aliolea na kuishi na wakwe zake. siku moja mkewe akamwambia kwamba anampenda sana kwa tabia zake, sifa na ukarimu wake. lakini huona dhila kutegemea wazazi wake na alimpa wazo la kujitafutia maisha yake na kujitetegemea kimapato. nabii suleiman akajibu kwamba hakuwa na ujuzi wa kazi yoyote ya kujikimu kistahiki kwa sababu hakuhitajika kufanya kazi (kwa muda alikuwa mwana wa mfalme).

Hata hivyo, aliahidi kwamba siku ifuatayo atakwenda sokoni kujitafutia mapato. alijiandaa kwenda kufanya kazi, lakini hakufanikiwa chochote. mkewe mwema akamtuliza moyo na akampa hima kwamba ajaribu sikuya pili. siku ya apili vile vile nabii suleiman akarudi mikono mitupu. tena mkewe akamsihi asivunjike moyo na kumhakikishia kwamba kutokana na rehema ya mungu atafanikiwa. siku ya tatu nabii suleiman akenda pwani na kumwomba amtumikie mvuvi kwa ujira wowote, mvuvi akakubali ombi na jioni yake akampa nabii suleiman samaki wawili kama ujira wake. nabii suleiman alifurahi na akamshukuru mungu nabii suleiman akamkata samaki huyo vipande na kumsafisha. tumboni mwa samaki mmoja nabii suleiman akapata pete moja.

Kwa vile alikuwa nabii, akatambua kuwa hiyo pete ni dalili yq ufalme. akasafisha hiyo pete akaiweka kwenye leso na kuweka mfukoni mwake. baadaye, akawachukua hao samaki wawili na kwenda nyumbani, ambako akamwona mkewe amefurahi sana. huyo mkewe akamwita baba yake akamwonyesha samaki wawili, nabii suleiman hapo akamwuliza baba mkwe " unajua mimi nani" huyo baba mkwe akajibu kwamba nabii suleiman alikuwa mtu mwema na yeye (bab mkwe) akimhesabu kama mwanawe lakini alikuwa hamjui kama yeye ni nani. hapo nabii suleiman akamsimulia kwamba yeye ni mwana wa nabii daudi, mwana wa mfalme na mriuthi wa kiti cha ufalme. akatoa hiyo pete kutoka mfukoni mwake na kuivaa. papo hapo, majini na ndege kutoka pande zote walikusanyika bele yake.

Nabii Suleiman akaelekea kwenda mji mkuu pamoja na mkewe na wakwe zake. wafuasi wake walifurahi sana kumwona nabii suleiman na walimshukuru mungu. hii ni mifano miwili kuhusu kujificha kwa mitume. wafuasi wa kila mtume walijaribiwa. kujificha kwa manabii yusuf ibrahim na idris kumeelezwa katika vitabu vingine. kwa kufupisha kitabu hiki hatuandiki habari hiyo humu.