ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE0%

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE Mwandishi:
Kundi: Imam mahdi (a.s)

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

Mwandishi: Marehemu Mulla Muhammad Jaafar Sherif Dewj
Kundi:

Matembeleo: 20639
Pakua: 2907

Maelezo zaidi:

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 20 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 20639 / Pakua: 2907
Kiwango Kiwango Kiwango
ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

Mwandishi:
Swahili

13

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

SURA 18

BIBI, AZALI, BAHI KAMA VILE HUKO PUNJAB

Mirza alifanya daawa ya utume na umehdi, huko iran, kabla ya miaka 100, yalizuka madhehebu mapya ya babi, azali na bahai. wafuasi wa madhehebu hayo hadi leo wako iran na india. katika kitabu kidogo kama hiki haiyumkiniki kueleza maisha ya babi azali na bahai na ubatilisho wa madai yao. hata hivyo, tutaeleza kwa muhtasari historia ya madhehebu haya.

Mwanzilishi wa ubabi alikuwa mirza ali mohammad mirza raza shirazi. vichepuko vya madhehebu ya babi vikawa madhehebu ya azali na bahai yakimhesabu baab kuwa mtume na ishara ya habari njema kwa sababu alibashiria juu ya ndugu hao wawili. katika mabahai, baab hujulikana kuwa ni mtu mmoja tu aliyebaki hai kutokana na dhuria ya mtume(s.a.w.w) na mirza husseinali ni nabii issa wa pili anaye subiriwa. baada ya kifo cha mirza muhammad baab, wafuasi wake hawakumtambua au kumkubali mirza yahya subhe azal au mirza husseinali kama walivyomkubali baah. mirza alidai kwamba baab alitangaza kuja kwake (mirza yahya). Mirza husseinali baha mwanzoni alimkubali ndugu yake na kueneza madhehebu yake kwa niaba ya nduguye lakini baadaye akageuka na kutangaza kuwa madhehebu ya nduguye ni udanganyifu na kubatilisha madai yake kuwa ni ya uongo kuanza kueneza madhehebu yake mwenyewe ya ubahai.

Kutokana na mafarakano baina ya ndugu wawili hao, damu nyingi ilimwagika. Wafuasi wa mirza yahya wakajitambulisha kuwa maazali na wa mirza husseinali kuwa mabahai siku hizi wamisionari wa kibahai wameenea kote katika mabara ya asia, ulaya na afrika. Vipi mtu anaweza kuwa na daawa ya kuteremshiwa wahyi wakati yeye mwenyewe amebadilisha dini yake mara tatu! Kwanza alikuwa shia ithnaasheri, baadaye akaungana na madhehebu ya ubabi na baadaye kuwa misionari wa madhehebu ya nduguye mirza yahya azali. Hatimaye akawa mwanzilishi wa madhehebu yake na kujitangazia kuwa yeye ni mehdi anayesubiriwa. Madhehebu yake ni mchapuo wa madhehebu ya ubabi.

Albayan husemekana ni kitabu alichoteremshiwa mwanzilishi wa madhehebu ya baab. maadili kadhaa kutoka kitabu hicho yanaorodheshwa hapa. Itadhihiri kwamba maadili yote ni kinyume cha maagizo ya qur'an na hadithi.

1. Swala ya jamaa hukatazwa.

2. Badala ya raka 17 za kila siku mtu aswali rakaa tisa tu na kuna mabadiliko mengi katika hizo swala.

3. Kufunga katika mwezi wa ramadhan kumekatazwa na badala yake mtu afunge siku 19 tu kuanzia tarehe 1 machi (asrarul akaeed, uk. 830.

4. Kuoga tohara baada ya mtu kujamiiana na mwanamke au kutoka manii usingizini sio lazima.

5. Mwanamke yeyote, ila mama mzazi, huweza kufungwa naye ndoa.

mwanzoni, mwanzilishi wa madhehebu ya babi mirza muhammadali baab alikuwa shia ithnaasheri. alikuwa mwanazuoni wa kidini huko najaf-iraq. Baadaye alikwenda iran na akaanza uombezi. alikuwa akisimama kichwa wazi juani kwa muda mrefu. mwishowe, akapotelewa na akili na kujitangazia kila daawa. Katika 1844 a.d., mirza ali muhammad akaanza kutangaza dini yake. Akatangaza yeye ni mlango wa mungu (huwezi kumfikia mungu bila kupita kwake), mti wa toor, mehdi anayesubiriwa na mwishowe nabii.

Katika majadiliano bayana na mwanazuoni wa shia itbnaasheri akatangasza "kauli zangu ni bora na zenye ufasaha zaidi kuliko qur'ani. Madhehebu yangu hubatilisha uislaam. Tahadharini mimi nitawaua wapinzani wangu wote". Aliwaamuru wafuasi wake kuongeza katika adhana kauli ya ushahidi kwamba ali muhammad ni dalili ya mungu na vile vile natoa shahada kwamba ali muhammad ni mlango wa mungu".

Katika washabiki wakuu wa kueneza na kukubali madhehebu ya babi alikuwa mwanamke mmoja, kurratui ayn, ambaye alikuwa binti wa mwanazuoni naye aliolewa na mwanazuoni. Alikuwa mwanamke mjanja, aliyeelimika na msemaji hodari. Jina lake la mwanzo lilikuwa zarrin taj na alikuwa mwanamke mwenye sura nzuri sana. Kutokana na mafarakano na mumewe akaungana na madhehebu ya babi ili alipize kisasi dhidi ya mumewe. Kila alipopata fursa alionyesha umbo na uzuri wake kwa kuvua buibui lake hadharani. Siku moja alipanda juu ya mimbari mbele ya watu wengi, akavua buibui na kutangaza: "marafiki na maadui! Kutokeza kwa madhehebu ya babi kumebatilisha uislam.

Amri zote kuhusu swala, saumu, kutoa sadaka na kadhalika zimetanguliwa. Tahadharini hadhrat baab ataiteka dunia nzima na karibuni hakutakuwa na dini yoyote duniani ila ubabi na kwa hivyo kila mtu anawajibika kuungana nasi kwa wingi kadri iwezekanavyo." achilieni mbali buibui ambalo lawatenganisheni na wanawake. Mkumbuke kuwa mwanamke ni ua linalonukia la bustani la dunia hii. hivyo, lichume na kulistaladhi. ua huzawadiwa kwa marafiki. tamaa mbele giza. msikose kuwapa marafiki zenu, wake zenu na maana vikwazo kama hivyo vimekwisha ondolewa katika madhehebu ya ubabi. Staladhi raha zote za dunia maana hakuna lolote baada ya kifo." mwenye akili hahitaji maelezo zaidi kuhusu imani ya madhehebu hayo.

Ubahai ubahai ulianzishwa 1853 b.k. na mwanzilishi wake ni hussein ali ambaye hujulikana kama bahaullah, huko mazinderan iran baada ya kuacha madhehebu ya ubabi. Watu wengi waliuawa. Mwishowe kwa amri ya shah wa iran, nasiruddin, bahaullah akafungwa jela na kufia huko gerezani 1886. Alirithiwa na mwanawe abbas effendi ambaye alistakimu katika jiji la akka huko falestina.

Profesa browne aandika kwamba ubahai ni muundo mpya wa ubabi. kama vile mababi humtukuza ali mubammad (baab) kuwa mtukufu mno vivyo hiyyo mabahai vile vile humfikiria mirza husseinali bahauddin kuwa mtu mtukufu mno. mabahai huamini kwamba ali muhammad baab alibashiri tu juu ya kutokeza kikamilifu kwa amri ya mungu na hilo likafuatwa na kuzaliwa kwa bahauddin kwa sababu mirza hussein ali alikuwa kiwiliwili cha mungu. Hata bahaullah mwenyewe alipokuwa gerezani alitangaza kwamba "hakuna mungu ila mimi mwenyewe aliyefungwa na kukandamizwa." Mtu atamfikiria nini huyo mungu anayefungwa gerezani na anayekandamizwa? madhehebu hayo vipi huweza kuhesabiwa kuwa na uhusiano wowote na uislam?

Kitabu cha kwanza cha mabahai kilikuwa aykaan. baada ya kujitangazia kama yeye mwenyewe ndiye mungu akachapisha kitabu cha pili kiitwacho aqdas ambacho kinadaiwa kuwa ni bora kuliko vitabu vyote vya dini. Katika humo imearidhiwa: "mama zenu tu hamwezi kulala nao na ustaarabu tu unakataza kutoa kanuni kuhusu kumfeli mtoto mwanamume mwenye sura ya kupendeza". hivyo, inamaanisha kwamba mtu anaruhusiwa kuingiliana na kila mwanamke ila mama yake mzazi na vile vile kufeliana na mwanaume mwenzie. Uchochezi wa babi-bahai ulisababisha umwagaji mkubwa wa damu huko iran. wanazuoni, mawaziri na mwishowe shah wa iran nasirrudin shah waliuawa. Idadi kubwa ya mababi na mabahai waliokuwa iran ni mayahudi wa hamadan kashan na yazd waliokubali madhehebu hayo, na vile vile maparisi wa iran na india. waislamu wachache mno walikubali madhehebu hayo.

Mmisionari mkuu wa madhehebu ya bahai, mirza hassan niku, alikuwa mwakilishi wa abbas effendi, mwana wa bahaullah. Abbas ambaye alitunukiwa jina kuu la "jibrael" na mabahai. Jina lake la kiislaam lilikuwa abdulhussein ayni naye alikuwa mfuasi mkuu wa madhehebu hayo. Hao wote pamoja na wamisionari wakuu wa madhehbu hayo wakatubu na kuandika vitabu dhidi ya ubahai na kufichua mabaya ya madhehebu hayo. Avarah katika kitabu cha kashful hiyal amechapish kibayana picha zinazofichua siri za madhehebu hayo. Kwa sababu tu kuimarisha upinzani dhidi ya uislaam huko iran ndiyo mayahudi na maparisi walijiunga na madhehehbu hayo.

Mdai umehdi katika karne ya 13 na 14, mirza kadiani mwanzoni mwanazuoni mubalighi wa kisunni. pole pole, akaanza kudai umehdi, unabii na mwishowe uungu. Vile vile, mirza mohammad ali baab wa ubaabi na husseinali bahaullah wa ubahai mwanzoni walikuwa mashia kila mmoja akaanzisha madhehebu mapya na wakadai kuwa ni wawakilishi wa baab, mehdi, nabii na mwishowe mungu.

Babu zake his highness agakhan walikuja india kutoka iran wakiwa shia ithnaasheri na kuamini maimam kumi na wawili, watukufu kumi na wanne na wakifuata sheria za kuswali, kufunga ramadhaai na kanuni zote za madhehebu ya shia. Siku za mwanzoni, viongozi wa dini ya agakhan walijulikana kwa jina la 'peer' jamatini watu wa kiswali na kufunga ramadhani. Qur'an ikisomwa na watu wakiamini maimam kumi na wawili. Pole pole katika karne hii maaghakani ikaanza daawa ya umehdi, unabii na hatimaye kiwiliwili cha mungu.

Mwanzoni wafuasi wa agakhan wakijulikana kwa jina la bhagat na mashia ithnaasheri subhanya. baadaye waaghakani wakajigeuza kuwa maismaili na kitambo kidogo wamekuwa wakijitambulisha kama shia imami ismailia. kwa upande mwingine, kwa mujibu wa itikadi ya shia ithnaasheri, tangu kuja kwa uislam, imani katika qur'an, maimam kumi na wawili, kuzaliwa kwa hadhrat mehdi(a.s) , kughibu kwake na kutokeza mara ya pili kumethibitishwa kutokana na qur'an, hadithi na historia. Dalili madhubuti za uhakika huo na ufanunuzi wake umeelezwa kikamilifu katika kitabu hiki.

Waliodai umehdi walijitokeza mmoja baada ya mwingine, na kueleza nadharia zilizokuwa kinyume na tofauti na maadili ya kiislam kama ilivyoelezwa katika qur'an na hadithi. Hapana shaka wadai wote hao hawawezi kuwa wakweli kwa sababu ubashiri uliopo ni wa mehdi mmoja tu. Hadithi maarufu ya mtume mtukufu(s.a.w.w) kwamba watakuwa maimam kumi na wawili baada yake na wa mwisho ni hadhrat mehdi(a.s) imenakiliwa na wanazuoni maarufu wa kisunni katika vitabu vifuatavyo:

1. Kanzul umal, juzuu la 6, uk. 198

2. Sunan Abi Daud uk. 588

3. Jaamiu Tirmidhi uk. 269

4. Sahih Muslim, juzuu la pili, uk. 119

5. Sahih Bukhari, kitabul fitan, babul istikhlaf, juzuu la 29, uk.629

bila shaka mtume mtukufu(s.a.w.w) alitangaza hadithi hiyo kuhusu maimam kumi na wawili kutokana na amri ya mwenyezi mungu mwenyewe. Kwa hivyo, lazima wawe warithi 12 wa mtume(s.a.w.w) . Basi imani yoyote kuamini warithi zaidi ya kumi na wawili wa mtume(s.a.w.w) haiwezi kuwa na ridhaa ya mungu na mtume(s.a.w.w) .

Ifuatayo ni orodha ya madai ya warithi wa mtume(s.a.w.w) :

1. Msururu wa kwanza ni wa khulafaul rashidin ambao walikuwa wanne tu na sio kumi na wawili.

2. Msururu wa pili wa daawa ya urithi ni kutoka nasaba ya bani umayya ambao walikuwa kumi na wanne.

3. Msururu wa tatu ulikuwa wa bani abbasi ambao walikuwa 37 (thelalhini na saba).

4. Msururu wa nne ulikuwa mchanganyiko wa watu wa misri na bani abbas ambao walikuwa kumi na wanane. halaku khan alikomesha ukhalifa wa bani abbas huko baghdad, na mfalme wa misri alimtawaza mwana wa mfalme wa bani abbas kuwa khalifa na kufanya idadi yao iwe kumi na wanane.

5. Msururu wa tano unatokana na makhalifa wa kituruki. khalifa wa kwanza wa kituruki salim sultan aliiteka misri na kuanzisha ukhalifa wa kituruki. idadi ya makhalifa hao ilikuwa thelathini, lakini alipokuja mustafa kamal pasha akakomesha ukhalifa huo; kwa hivyo, duniani sasa hayupo khalifa wa kisunni.

Madai ya madhehebu mengine:

1. Madhehebu ya babi azali na bahai, ambayo yamejitenga mbali na itikadi ya uislam, hayawezi kufikiriwa kwamba ni madhehbu ya kiislaam.

2. Vile vile ukadiani hupinga moja kwa moja imani ya uislam na kwa hivyo madhehebu hayo pia siyo ya kiislaam.

3. Hata hivyo waumini wa madhehebu ya dawoodi bohora ni waislamu lakini huamini maimamu ishirini na mmoja na vile vile huamini hadi leo kuwa imam wao wa mwisho, imam tayab, amejificha, hivyo daawa yao huzidi idadi ya imam kumi na wawili.

4. Waismailia wafuasi wa agakhan, huamini imam wao wa kipindi hiki ni wa 49; kwa hiyyo, idadi yao buzidi idadi iliyotajwa na mtume(s.a.w.w) zaidi ya mara nne.

5. Ni shia ithnasharia peke yao tu ndio wanawaamini maimam kumi na wawili, kama ilivyosimuliwa na hadithi ya mtume(s.a.w.w) . imam wa kwanza ni hadhrat ali(a.s) na wa kumi na mbili ni hadhrat mehdi(a.s) kama ilivyoridhiwa katika vitabu vitano mashuhuri vya madhehebu ya kisunni na kutajwa katika vitabu vingi vingine. jina maalum la kila imam(a.s) lilitajwa na mwenyewe mtume(s.a.w.w) . ukweli huu vile vile umethibitishwa katika vitabu maarufu vya kisunni, k.m.

1. "Mawaddatul Qurba" uk. 34, kilicho andikwa na allama seyyid alihamdani, kilichochapishwa bombay press.

2. "Arjahul Matalib", uk. 402, lahore press.

3. Yanabiul Mawaddah", uk. 445, kilichoandikwa na allama

sheikh Suleiman Kanduzi, sheikh wa istanbul. istanbul turkish press.

4. Tarikhul Rawzatul Ahbab", Yanabiuel Mawadda juzuu 3, uk. 27. licha ya hivyo, kuna vitabu vingi vimetaja majina halisi ya imam mehdi(a.s) .

5. Babu zake agakhan wa siku hizo wakiamini maimam kumi na wawili kama ilivyoelezwa katika vitabu vyao ambavyo tumekwishavitaja.

14

ASIYEMTAMBUA IMAMU WA ZAMA ZAKE

SURA19

MAKAZI YA HADHRAT MEHDI (A.S) JAZIRATUL KHADHRAA NA MENGINEYO

Hadhrat Mahdi(a.s) yupo hai duniani na huwaokoa wafuasi wake wanapohitaji msaada wake. Mahala pengi pameainishwa kuwa ni makazi yake. Miongoni mwao ni rabwa huko yemen, zituwa n.k. kama ilivyoelezwa katika dua mbalimbali. Zaidi ya hayo, jaziratul khadhraa (kisiwa kijani) ni nchi kubwa mno katika ufalme wa imam(a.s) na kuna majiji mengi makubwa yenye umati mkubwa wa kishia. Hayo hutawaliwa na wana wa imam(a.s) kundi la visiwa linalojulikana kwa jina hilo lipo katikati ya bahari nyeupe (white sea) magharibi ya uingereza. Kwa amri ya mwenyezi mungu wengi wamekwishawahi kuzuru visiwa hivyo. Hata hivyo, kutokana na vitabu vya historia mizunguko mikali ya maji huzingira visiwa hivyo na huwa ngumu na hatari kwa vyombo kufika huko.

Kuna hoja inayotolewa kwamba ikiwa visiwa hivyo ni vikubwa kiasi hicho basi kutokana na maendeleo ya vyombo vya angani na vyombo vya kupigia picha vya ramani, kutoonekana kwa kisiwa hicho katika ramani ya dunia humfanya mtu asiamini kuwa kipo. kwa hivyo, kabla ya kueleza mahali penyewe, tunajibu hoja hiyo.

1. Amerika ambayo ni bara kubwa mno lililotanda karibu nusu ya dunia lilivumbuliwa katika karne ya 18. Je tunaweza kujenga hoja ya kusema kuwa bara hili halikuwapo kabla ya karne ya 18?

2. Ugunduzi wa nchi zilizofunikwa na barafu kwenye kizio cha kaskazini (north pole) bado unaendelea hadi leo.

3. kuna visiwa vingi katika bahari kuu na vichache tu vinajulikana.

4. kuna nchi nyingi ambazo kuwapo kwazo zimethibitika kihistoria, lakini mahala penyewe hapajulikani na hata ramani hazijachorwa; mathalan, kaskazini mwa afrika kuna eneo linalokaliwa na umati wa agog-magog nalo hujulikana kama saadal sikandari. nabii suleiman alijenga ngome kubwa huko kaskazini mwa afrika na kuficha hazina nyingi mno. tena kuna makazi ya masahaba wa gofu (as'habul kahf), bustani ya aden na janna ya shaddad. kuwepo pahala hapo pote pamethibitika kihistoria lakini hapawezi kufikiwa (ila tu watu wachache walioweza kufika huko); hata ndege za nchi zilizoendelea hazikufika huko.

5. Miaka michache iliyopita wakati vita vya korea vikiendelea habari zifuatazo ziliwasilishwa na shirika la habari la reuter. tadriki ya kusini kwenye kizio cha kusini cha dunia (south pole) baada ya vita vya korea. rear admiral byrd (mkuu wa jeshi la majini) mwenye umri wa miaka 64 ametangaza kwamba ataongoza tadriki nyingine kusini kwenye kizio cha kusini (south pole) mara tu baada ya vita vya korea kumalizika.

Yeye amesema: "kuna ardhi huko antarctic, yenye eneo kubwa kama amerika, ambayo mpaka leo halijafikiwa na mtu yeyote". "hivyo chemchem hiyo yenye mali asili isitekwe na adui yeyote." alizungumzia uwezekano wa kutumia bomu la haidrojeni au silaha nyingine ya nuklia kuyeyusha maeneo makubwa ya barafu ili aweze kupata mali iliyo chini ya ardhi. (reuter). kwa hivyo ni dhahiri kuwa kuna mahala pengi ambapo bado hapajagunduliwa. kadhalika, jaziratul khadhraa, ambayo habari zake kihistoria zimezungumzwa karne nyingi zilizopita na kuna ushahidi wa watu waliofika huko pamoja na majina na tarehe ya kufika.

Haramu za misri mwanazuoni mkuu wa kishia, allama majlis(a.s) na wanazuoni wengi wengine wameandika kwamba abdulhasan hammad bin ahmad aliwahi kuona hazina kubwa mno ambayo mtu yeyote hakuwahi kupata mali hapo kabla. kwa hivyo tama yake ilizidi na aliamrisha haramu za misri zibomolewe na mali yote iliyofukiwa chini yake ichukuliwe. washauri wake walijaribu kumsihi asibomoe haramu, kwa sababu maisha yake yatafupika. hata hivyo hakukubaliana nao na akawatuma watu elfu moja wafanye kazi hiyo.

Waliendelea kuchimba kwa muda wa mwaka mzima lakini hawakupata chochote. basi aliamua wasiendelee na uchimbaji. Siku ya mwisho wachimbaji waliona shimo refu na waliamua kuingia humo. kabla hawajafika mwisho wa hilo shimo wakaona bamba kubwa mno. Wakaling'oa hilo bamba. Ndani ya bamba hilo kulikuwa na michoro ambayo hakuwa hata mtu mmoja huko misri hakuweza kuifahamu.

hatimaye abi abdulla madini akasema kwamba anamjua mzee mmoja huko uhabeshi (ethiopia) mwenye umri wa miaka 360 ambaye angeweza kufafanua maana ya michoro hiyo. basi salaam zilitumwa kwa mfalme wa uhabeshi kumwomba ampeleke huyo mzee misri, lakini mfalme wa uhabeshi alisema hataweza kumwomba mtu mwenye umri kama huo asafiri maana safari hiyo ingeweza kusababisha kifo chake.

Mfalme alipendekeza kwamba masuala yote yanayotakiwa kumwuliza huyo mzee yatumwe kwa maandishi. kwa hivyo, hilo bamba likapelekwa uhabeshi. huyo mzee akatafsiri michoro hiyo katika lugha ya uahabeshi na tafsuru yake ikafanywa katika lugha ya kiarabu. bamba hilo lilisema kuwa limetoka kwa: rayan bin doneta mfalme wa misri, ambaye katika kipindi cha utawala wake nabii yusuf alikuwa nabii huko misri. azizi (mtawala wa misri) aliishi miaka 700 na baba yake rayyan 1700 na babu yake domag 3000. iliendelea "niliamua kuona chanzo cha mto wa nile. nilisafiri na masahibu wangu kw muda wa miaka minane. mwishonikafika pahala penye giza totoro. katika msafara huo masahibu wangu wote, ila 400, walikufa na kwa hivyo niliamua kurudi misri na kujenga haramu mbili. ndani humo nilificha mali yangu, vito vyenye thamani n.k mali hiyo wala vitabu vya elimu havitaharibika. baadaye ilifuata tafsiri ya maandiko yaliyoandikwa juu ya bamba: "elimu yangu imenipa mwanga juu ya undani wa maajabu machache.

Hata hivyo, mungu anajua kikamilifu habari za vitu vilivyojificha. mimi nilisafiri kwa muda wa miaka thamanini hata nikafika kwenye giza totoro. hatimaye nikafahamu kwamba sitaweza kwenda mbele na mtu yeyote mwingine hataweza kufika huko nilikofika. kwa hivyo, nilirudi nyumbani misri na nikajenga haramu mbili kama mfano wa nguvu na ujasiri wangu. hazitachakaa wala kuharibika. hakuna yeyote atakayeweza kufikia mali nyingi mno wala kufungua hilo shimo niliyofukia mali na niliyoimarisha, ila katikas siku za mwisho za dunia walii mmoja wa mungu atafichua hazina hii yangu ya ajabu.

Walii huyo ataonyesha hiyo mali katika kaaba. bila shaka, kila kitendo chake kitakuwa kikamilifu na atakuwa na uwezo wa kumdhibiti kila mtu. jina ka allah litaenea duniani kutokana na juhudi zake. huyo atapokuja watu 313 wataleta imani juu yake na yeyote atakayepinga atauwawa.baada ya hapo watu 99 walio kufa wa taif watafufuka na kuchimbua hiyo hazina niliyofukia ambayo itatumika katika vita vya dini. Hapa nimedokeza kuhusu mabao yatakayo tokea. kwa hakika wote tutakufa, hata mimi mwenyewe".

Baada ya kusoma hayo mfalme abdul hassan hammad aliyakinika kwamba hakuna mtu yeyote atakayeweza kufukua hiyo hazina ila hadhrat mahdi(a.s) . kwa hivyo, alirudisha hilo bamba pahala pake pa asili. katika muda mfupi wa miezi kumi na mbili hammad alipokuwa katika usingizi wa sakarani aliuliwa na mmoja wa watumwa wake, taher. hazina iliyofichwa na nabii suleiman katika ngome za shaba (madina-tunnahas) jiji la shaba.

Madinatunnahas ni mojawapo ya maajabu makuu ulimwenguni. ngome hiyo ilijengwa na nabii suleiman huko andolusia, afrika mashariki kwa msaada wa majini kwa kuyeyusha risasi. eneo lake ni maili kumi na mbili za mraba na kuta zake ni futi 75 kwa urefu. na ameficha mali ya ajabu yenye thamani kuu. ipo dokezo kuhusu hiyo katika qur'ani tukufu: "na kamyeyushia chemchem ya shaba. na kati ya majini walikuwepo wale waliofanya kazi chini ya uongozi wake kwa amri ya mola wake". (34:12).

Kwa amri ya allah kulitokeza chemchem ya shaba kujengea ngome. katika utawala wa khalifa bdul malik bin marwa wa bani umayya, mtu mmoja aliwahi kufika kwenye ngome hiyo. (ilikuwa niamri ya allah huyo mtu afike huko ili aje kuwasimulia watu wa bani umayya na waislaam wa wakati huo na watakaozaliwa baadaye alama zake (mungu) na hadhi ya hadhrat mehdi(a.s) . huyo mtu alimhadithia khalifa mambo yote ya ngome hiyo na khalifa papo hapo akamwamrisha gavana wa andolusia kuanza msafara wa kutafuta ngome hiyo na kupatiwa taarifa.

Gavana huyo alifunga hiyo safari. Alifika kwenye ngome lakini alishindwa kuingia ndani yake. Sauti za ajabu zilisikika kutoka ngomeni. karibu na ngome hiyo kulikuwa na ziwa moja ambamo maji yalikuwa yanajaa kila saa na maji hayo yalikuwa yakitoa povu kama vile maji ya moto yanapochemka. gavana akawaamrisha wapigambizi wazame ziwani, nao walileta vyombo duara vya mabati na risasi. juu ya hivyo vyombo vilikuwa mihuri. gavana akaamrisha vyombo hivyo vivunjwe. humo ndani ya vyombo vikatokeza masanamu yaliyopanda farasi yakipiga kelele." eh mtume wa mungu tunaomba amani kwako". Gavana alisadiki kwamba hao walikuwa majini wahalifu ambao walifungwa na nabii suleiman.

Gavana alimpatia khalifa taarifa kamili. vile vile aliongeza kwmba alitekeleza agizo lake la kwenda kwenye ngome dhidi ya ushauri wa wahenga ambao walimwonya kuwa kabla ya hapo hakuna mtu yeyote aliyefanikiwa kuingia ndani ya hiyo ngome., sikander mkuu (alexander the great) alijitahidi kufikia hiyo ngome na kutuma watu wake waingie humo lakini baada ya muda mrefu walirudi bila mafanikio. Kwa hiyo, sikander alikata tamaa na kuacha jambo hilo; hata hivyo, gavaha alipeleka watu waliojiandaa kikamilifu. Alikabili matatizo mengi na katika safari hiyo aliishiwa hata chakula. ijapokuwa aliifikia ngome hiyo lakini alishindwa kuingia ndani. Kuta za ngome zilikuwa na urefu wa futi sabini na tano ambazo zilizojengwa kwa shaba na juu ya hizo kuta kulikuwa maandishi maalum katika lugha ya kiarabu. Gavana aliagiza maandishi hayo yanakiliwe na kupelekwa kwa khalifa.

Hayo maandishi yalikuwa katika lugha ya kiarabu fasaha na kiini na muhtasari wake ulikuwa hivi: "hakuna kiumbe atakayeishi milele. iwapo kungekuwapo mtu mwenye nguvu na heshima ambaye angeweza kuishi milele basi pasina shaka kuwa nabii suleiman angeishi maisha marefu mno. mwenyenzi mungu alinitayarishia chemchem ya shaba na kukiamrisha kikundi cha majini kunijengea ngome kutokana na hiyo shaba iliyo yayuka na ambayo itadumu hadi siku ya hukumu (kiyama). Na haitachakazwa kwa urefu wa muda au umri. Mimi niliamrisha zijengwe kuta ndefu sana, ziimarishwe na shaba iliyoyayuka na kuhifadhi humo hazina yangu kubwa mno, ili muda wowote ukipita hata chembe moja ya hiyo hazina isiharibike. kwa hakika fahari (makuu) ya mfalme yeyote haiwezi kudumu daima.

Mwisho wa kila mfalme ni kulala peke yake kaburini. Na hivyo divyo itakuwa hali yangu. kwa hivyo, watu wajue kwamba ufalme wa milele ni wa mungu peke yake. Baada ya kufa kwangu kutakuja kipindi ambacho mtu aliye bora kuliko wote kutoka katika sulbi ya adrian na hashim atazaliwa. Mungu atamjalia miujiza, kudra yake na utume. Atakuwa mwongozi wa viumbe wote duniani. atakuwa na funguo zote za hazina za dunia nzima na warithi wake vile vile watakuwa na sifa hizo. Warithi hao watakuwa kumi na wawili-na wote watakuwa makhalifa wa mungu duniani. Mrithi wa mwisho atatokeza (baada ya kughibu kwa kipindi maalum) kwa amri ya mola. Jina lake litatangazwa kwa sauti kubwa huko mbinguni na huyo mtukufu atafungua hiyo ngome yangu na kudhihirisha hazina hii."

Alipomaliza kusoma hiyo taarifa, mjumbe aliyeleta barua, talib (bin mudrik, akaongezea na kusema kwamba yeye binafsi pamoja na gavana walifika kwenye hiyo ngome ya kusoma maandishi hayo juu ya kuta zake. kusikia hayo khalifa akamwuliza muhammmad bin shahad zohri aliyekuwa pale, na ambaye alikuwa mmojawapo wa masahaba wa imam wa nne (zainul abidiin a.s.) na mwenye kupenda familia ya mtume atoe maoni yake. Yeye (zohri) akasema kwamba hiyo ngome iko chini ya utawala wa majini ambao huzuia watu kuingia humo. hapo khalifa alisisitiza sana apatiwe jibu kwa sababu jambo hilo lilikuwa la muhimu mno na alimtaka zohri aelezee kinaga ubaga habari hizo bila kuchelea kuwa maelezo yatamuudhi khalifa kwa sababu mfalme alikuwa na hamu ya kujua jawabu.

Baadaye zohri akahadithia kwamba hadhrat ali bin hussein (imam wa nne a.s.) alimjulisha yeye kuwa huyo mehdi(a.s) atatokana na dhuria ya fatima(a.s) binti wa mtume mtukufu(s.a.w.w) , khalifa abdulmalik akamkata kauli na kwa hali ya kugugumia akasema: "nyinyi wote wawili waongo. mehdi atatokana na ukoo wa umayya". Zohri akamwambia kwamba anaweza kuthibitisha kutoka imam ali bin hussein(a.s) yote aliyosema lakini khalifa akajibu kuwa hapakuwa na dharura ya uthibitisho huo. Baadaye akamnong'oneza zohri, "tahadhari, mtu yeyote asipate kujua ukweli kuhusu hiyo ngome na maandishi yaliyokuwa ukutani". Zohri aliahidi kama hatamhadithia mtu yeyote maneno hayo.

Andolusia imeonyeshwa katika ramani ya afrika. waingereza walifika nchi hiyo lakini hawakufanikiwa kufikia hiyo ngome. Wangalifanikiwa kufikia hiyo ngome wangejitahidi kadri ya uwezo wao kupata hiyo hazina iliyohifadhiwa. kwa hivyo, si jambo la kuajabia kwamba jazeeratul khadhraa na nafasi nyingi zingine hazikugunduliwa na binadamu. Hadhrat Mahdi(a.s) ana makazi mengi lakini makazi hayo hayafikiwi na watu wa kawaida ila ayali yake na wahudumu wake wa karibu mno. Hata yeye (hadhrat mehdi(a.s) anapokuja kumwokoa mtu yeyote hatambuliki. baada ya kumuawini mtu na kutoweka, baada ya kutoa msaada kimuujiza huthibitika kwamba huo umetoka kwake hadhrat mahdi(a.s) na humfnya mtu awe na majonzi ya kukosa kumtambua imam wake.

katika mwezi mtukufu wa ramadhani imam pengine huhudhuria msikiti wa kufa, au wa najaf na vile vile kerbala. Katika kila msimu wa hija yeye huenda kuhiji. Baadhi ya makazi yake yametajwa katika vitabu vingi, k.m. majiji makubwa chini ya utawala wake ktika makundi ya visiwa vinavyojulikana kama jazeeratul khadhraa huko bahari nyeupe ambako huweza kufika baada ya safari ya siku kumi na tano hadi ishirini kwa meli kutoka mwambao wa kaskazini magharibi (northwest) ya afrika. majina ya majiji hayo ni haya yafuatayo:

1. Mubaraka: gavana wa kisiwa hicho ni hadharat tahir, mwana wa imam(a.s) na makao makuu ya kisiwa hiki ni jiji linaloitwa zahera.

2. Raequa: gavana wa huko ni mwana wa pili wa imam(a.s) , aitwaye hadhrat qassim.

3. Sfiya: lililo chini ya utawala wa hadhrat ibrahim ambaye vile vile ni mwana wa imam(a.s) .

4. Zaloom: hiko gavana ni hadhrat abdulraman ambaye pia ni mwana wa imam(a.s) .

5. Panatis: mtawala wa huko ni mwana wa imam.

mbali na visiwa hivi vitano, imamu anayo maskani mengine ya upekee huko yemen na iraq ambapo waumini wachache wameweza kuzuru na maelezo yake yametolewa kwingine katika kitabu hiki.

Masimulizi kuhusu visiwa hivyo

1. seyyid muhammad sharif rishtia ametuuusia kwamba katika kipindi cha ughaibu wa imam(a.s) waumini wajaribu kumkumbuka imam(a.s) mara kwa mara kwa sababu yeye hutupenda sisi na yu muhibu wetu kuliko wazazi wetu. tujitahidi mno kutenda mambo ya kumfurahisha yeye (imam a.s.). ameandika kwamba kila mara akimwomba imam(a.s) amwonyeshe jaziratul khadhraa, bahari nyeupe na nchi za ufalme wake ambazo yeye na wanawe wanatawala. anaendelea kusimulia kuwa: "safari moja usiku wa ghadir (siku ya kutangazwa kwa imam Ali(a.s) kuwa khalifa baada ya mtume(s.a.w.w) uliangukia usiku wa alhamisi kuamkia ijumaa. nilikuwa natembea bustanini mwangu baada ya ibada za usiku wa manane huko beedabad bazar katika mji wa isfahan (iran). ghafla nikakutana na seyyid mwenye haiba aliyevaa mavazi ya wanazuoni wa kiislamu. baada ya kunisalimu akaniuliza: "wewe una hamu ya kuona jaziratul khadraa kuongeza yakini yako na imani za wengine?" kwa unyenyekevu nikajibu, "bwana wangu, nina hamu sana ya kuiona."

Akaniambia nikamate mkono wake, kufumba macho yangu na kumswalia mtume(s.a.w.w) pamoja na dhuria yake mara 7. Mimi nilifanya hivyo. nilihisi mvumo mkali wa upepo huku nikipaa angani. Punde si punde, akaniambia nifungue macho yangu na kusifu uwezo wa kuumba wa mwenyezi mungu. Nilipofumbua macho yangu nilijikuta niko kwenye jiji zuri lenye barabara pana na majumba yaliyo karibu karibu. Chemchem za maji zilikuwa kote kote na mabustani ya kupendeza yaliyojaa aina nyingi ya miti iliyozagaa kwa matunda. Nilihisi nipo peponi.

Seyyid huyo alinionyesha msikiti uliotazamana na bustani na kunijulisha kwamba watu walikwisha kusanyika kwa ajili ya swala ya asubuhi ambayo itaongozwa na abdulrahman, mjukuu wa kizazi cha saba cha imam mehdi(a.s) . akanielekeza niswali nyuma ya huyo kiongozi wa swala na kuwa ataonana na mimi baada ya swala. mimi nilikwenda msikitini. Mashaallah! ulikuwa msikiti wa ajabu.

Nilipoingia tu niliona watu wamekwisha jiandaa kwa ajili ya swala itakayoongozwa na mcha mungu mwenye uso uliojaa nuru na ambaye alikuwa amekwishafika katika mihrab. Baada ya kujidukiza katika umati wa watu nikafika kwa kiongozi huyo na nikamsalimia na kumbusu mikono yake. Alinikaribisha kwa taadhima na kuniambia kwamba nilibarikiwa na allah kufika msikitini huko. Nilimwuliza maswali machache ambayo yalikuwa yakinitatanisha kwa muda mrefu na papo hapo nikapata majibu ya kunitosheleza. Punde ukafika wakati wa swala.

Baada ya swala nikakumbuka kwamba mimi huongoza swala katika msikiti wa isfahan na watu watakuwa wananisubiri na pengine kukata tamaa. Nilipotamka maneno hayo nikamkuta yule bwana aliyenileta kutoka isfahan amesimama karibu yangu na kunipa mkono wake na kuniambia nifumbe macho. Katika muda mfupi mno nilijikuta kwenye msikiti wa isfahan ambapo watu walikuwa wamekwishajiandaa na kunisubiri mimi. niliongoza swala na baada ya hapo sikumwona seyyid yule tena".