TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN0%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi: Muhammad Hussein Tabaatabaai
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 39412
Pakua: 2919

Maelezo zaidi:

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39412 / Pakua: 2919
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

16

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA SHAMS (JUA) (NA. 91)

INA AYA 15

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu

وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا ﴿١﴾

1. Naapa kwa jua na mwanga wake.

وَالْقَمَرِ إِذَا تَلَاهَا ﴿٢﴾

2. Na (kwa) mwezi unapoliandamana.

وَالنَّهَارِ إِذَا جَلَّاهَا ﴿٣﴾

3. Na (kwa) mchana unapoifunia.

وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَاهَا ﴿٤﴾

4. Na (kwa) usiku unapoifunika.

وَالسَّمَاءِ وَمَا بَنَاهَا ﴿٥﴾

5. Na (kwa) mbingu na aliyeziweka.

وَالْأَرْضِ وَمَا طَحَاهَا ﴿٦﴾

6. Na (kwa) ardhi na aliyeitandika.

وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا ﴿٧﴾

7. Na (kwa) nafsi na aliyelingamanisha.

فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا ﴿٨﴾

8. Akaifahamisha maasia yake na twaa yake.

قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا ﴿٩﴾

9. Hakika amefaulu mwenye kuitakasa.

وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا ﴿١٠﴾

10. Na hakika amepata hasara mwenye kuitweza.

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَاهَا ﴿١١﴾

11. Ilikadhibisha (kabila ya) thamud kwa kupetuka mipaka.

إِذِ انبَعَثَ أَشْقَاهَا ﴿١٢﴾

12. Wakati walipomshakiza mwovu wao (kumuua ngamia).

فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اللَّـهِ نَاقَةَ اللَّـهِ وَسُقْيَاهَا ﴿١٣﴾

13. Akawaambia Mtume wa Allah, (tahadharini na) ngamia wa Allah na maji yake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنبِهِمْ فَسَوَّاهَا ﴿١٤﴾

14. Wakamkadhibisha (na) wakamchinja. Mola wao akaeneza (adhabu) kwa sababu ya madhambi yao, na akaifanya sawa.

وَلَا يَخَافُ عُقْبَاهَا ﴿١٥﴾

15. Wala haogopi matokeo yake.

UBAINIFU

Sura inataja kwamba kufaulu kwa mtu ni kuitakasa nafsi yake na kuikuza makuzi mema kwa kuipamba na takua na kuitakasa na uovu. Na kupata hasara na kuzuiliwa wema ni kwa mwenye kuitweza. Yanatolea ushahidi hilo yale yaliyowapitia kabila la Thamud walipong'olewa na adhabu pale walipomkadhibisha Mtume was Saleh na kumchinja ngamia. Hilo ni kuwaonyesha watu wa Makka. Sura imeshuka Makka kwa ushahidi wa mpangilio wake wa maneno.

Aya Na 1

Maana ya neno Dhuhaa ni kukunjuka jua na kuenea mchana na neno hilo limetumiwa kwa wakati. Katika aya hii kuna kiapo kwa jua na kuangaza kwake juu ya Ardhi.

Aya Na 2

Inaungana na Aya Na kwanza na nikuapa kwa mwezi hali yakuwa unaandamia jua. Makusudio ya kuandamia ikiwa inamaanisha kule kupata mwezi nuru yake kutoka kwa jua, basi itakuwa ni kuapa kwa wakati wote wa mwezi. Na ikiwa ni kuchimbuka kwa mwezi baada ya kutua jua, basi itakuwa kuapa ni tangu kuwa mwezi mchanga mpaka kuwa mpevu.

Aya Na 3

Maana ya neno Jallaha ni kudhihirisha na dhamir ni ya Ardhi kwa maana ya kuwa: ninaapa kwa mchana unapoidhirisha ardhi kwa macho. Inasemekana kuwa dhamir ya (mtendaji) ni ya mchana na dhamir ya (mtendwa) ni ya jua, kwa maana ya kuwa, ninaapa kwa mchana wakati Mwenyezi Mungu anapolidhihirisha jua, na hiyo ni njia iliyo mbali.

Aya Na 4: Yaani unapoifunika ardhi, dhamir ni ya ardhi kama katika aya iliyotangulia. Na inasemekana kuwa ni ya jua na hiyo pia ni njia iliyo mbali, kwa sababu usiku haufuniki jua isipokuwa unafunika ardhi na vilivyo juu yake. Ibara ya kufunika ardhi imekuja kwa (kitendo cha sasa) kinyume cha aya zilizotangulia ambapo ibara zake zimekuja kwa kitendo cha muda uliopita. Hiyo ni kufahamisha kufunika uovu wa ardhi kwa wakati uliopo ambao ndio mwanzo wa kudhihiri mlingano (mwito) wa Kiislamu, kutokana na yaliyotangulia kuwa kuna muungano kati ya kuapa na mwenye kuapiwa.

Aya Na 5-6

Herufi Maa katika neno Maabanaaha na Maatwahaaha ni kiwakilishi yaani na ambaye ameziweka na kuitandika ni Mwenyezi Mungu. Kuleta ibara bila ya kumtaja Mwenyezi Mungu ni athari ya kuficha kunakofahamisha ukubwa na ajabu, kwa maana ya kuwa; Ninaapa kwa mbingu na kitu chenye nguvu cha ajabu kilichoziweka. Na ninaapa kwa ardhi na kitu chenye nguvu cha ajabu kilichoitandika. Imesemwa kuwa Maa ni kiarifa chenye kutumika kama jina kwa maana ninaapa kwa mbingu na kuziweka kwake. Na ardhi na kuitandika kwake, lakini mpangilio wa maneno katika Sura kama vile aya inayofuatia haulisaidii hilo.

Aya Na 7

Yaani ninaapa kwa nafsi na kitu chenye uwezo, ujuzi na hekima ambacho kimeilingamanisha, kuipanga umbo lake na viungo vyake na kuilingamanisha sawa nguvu yake. Makusudio na nafsi ni nafsi ya mtu yoyote. Imesemwa kuwa makusudio ni nafsi na Nabii Adam(a.s) , lakini mpangilio wa maneno hauafikiani na hilo hasa Aya Na tisa na kumi.

Aya Na 8

Neno Fujuur kama alivyotaja Raghib ni kupasua sitara ya dini. Makatazo ya Mungu ya kufanya au kuacha, ni sitara iliyowekwa kati ya binadamu na Mwenyezi Mungu na kufanya yaliyokatazwa ni kupasua sitara hiyo. Neno Taqwa kama alivyotaja Raghib ni kuifanya nafsi katika kinga ya yanayohifiwa. Makusudio ya Taqwa kwa kuilinganisha na aya inayofuatia ni kujiepusha na maovu na kujilinda na yaliyo katazwa. Imefasiriwa katika hadith kwamba ni kujichunga ya yaliyoharamishwa.

Kuifunga silika (Ilham) juu ya anuani mbili za uovu wa nafsi na takua yake, ni kwa ajili ya kufahamisha kwamba makusudio ni kwamba Mwenyezi Mungu anamfahamisha mtu sifa ya kitendo chake kuwa ni kizuri au kibaya, baada ya kumfahamisha kitendo chenyewe hasa, kwa kuangalia asili yake ya mwenzo, ambapo kitendo kinaweza kuwa ni kizuri na kibaya wakati mmoja. Kwa mfano kula mali ya yatima ambako ni kuovu na kula mali yake mwenyewe ambako ni kitendo kizuri au kuvaana na mwanamke ambako kunashirikiana kati ya zina ambayo ni uovu na ndoa ambayo ni takua. Kwa ujumla makusudio na kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemfahamisha mtu kuwa kitendo anachokifanya ama kitakuwa cha uovu au cha takua na akampambanulia takua na uovu.

Kuifuatisha silika juu ya usawa katika kauli yake: "na mwenye kuilingamanisha. Akaifahamisha." ni kuashiria kuwa (mtu) kufahamu uovu na heri - ambapo ndiyo akili ya kimatendo - ndiyo kusawazisha nafsi. Na hiyo ni miongoni mwa sifa za umbile la hiyo nafsi; kama alvyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Basi uelekeze uso wako katika dini iliyo sawasawa ndiyo umbile Allah alilowaumbia watu; hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Allah. Hiyo ndiyo dini iliyo haki " (30:30).

Kutegemeza uovu na takua kwenye dhamir na nafsi ni kuonyesha kwamba makusudio ya uovu na takua zinafahamishwa hapa ni uovu na wema kuhusika na hii nafsi iliyoelezewa ya mtu na zile za majini kama ilivyodhihiri katika Qur'an tukufu kuwa wao ni wenye kukalifiwa na imani na kutenda amali njema.

Aya Na 9 -10

Kufaulu ni kushinda matakwa na kupata matakwa, kinyume chake ni kupata hasara. Kutakata ni kukua kwa makuzi mema yenye baraka. Na kutweza ni kuingiza kitu katika kitu chengine, makusudio yake kwa kukutanisha na aya, inayokabiliana na kutakasa, ni kuikuza nafsi katika misingi inayohitalifiana na tabia yake na kuipandanisha nayo. Aya hizo mbili ni jawabu la kiapo na Aya Na pili inaungana na ya kwanza. Kuleta ibara ya kutengenea nafsi na kuharibika kwake kwa neno kutakasa na kutweza ni udhihirisho wa inavyofahamisha kauli yake Mwenyezi Mungu. Akaifahamisha maasi yake na twaa yake, kwamba ni katika ukamilifu wa nafsi ya kiutu kwamba hiyo nafsi kimaumbile inapambanua uovu kutokana na twaa, yaani dini ya Kiislamu ni dini ambayo Mwenyezi Mungu anaikusudia kwa maumbile ya mtu, kwa hiyo kuipamba nafsi kwa twaa ni kuitakasa.

Aya Na 11

Aya hii na zinazofuatia mpaka mwisho wa Sura ni ushuhuda na uthibitisho wa yaliyotangulia katika kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa ".

Aya Na 12

Makusudio ya mwovu wa Thamud ni yule aliyemchinja ngamia. Jina lake kutokana na yaliyo katika riwaya ni Qidar bin Salif. Na kushakiza kulikuwa na kushakiza kwa watu kama zinavyofahamisha aya zinazofuatia kutokana na dhamir zake za wingi.

Aya Na 13

Makusudio ya Mtume wa Mwenyezi Mungu hapa ni Saleh(a.s) Mtume wa Thamud. Maana yake: akawaambia Mtume Saleh kwa ujumbe utokao kwa Mwenyezi Mungu: "Tahadharini na ngamia wa Allah na maji yake wala msimtaaradhi kuwa kutaka kumuua au kumzuwia na zamu yake ya kunywa maji ." Mwenyezi Mungu amekifafanua kisa hiki katika Sura ya II (Hud) na nyenginezo.

Aya Na 14

Kusema kwake akaifanya sawa, kwa dhahiri dhamir ni ya Thamud kwa kuzingatia kuwa ni kabila yaani akalifanya sawa na ardhi hilo kabila au ni kufanya sawa kwa maana ya kuitandaza hiyo ardhi. Inasemekana kuwa dhamir ni ya neno kueneza kwa maana ya kuwa akawaeneza adhabu na akaifanya sawa kwa wote hila ya kuangalia mwenye nguvu, wala myonge au mkubwa wala mdogo.

Aya Na 15

Dhamir ni ya kueneza au kufanya sawa yaani Mola wao haogopi mwisho wa kueneza adhabu na kuifanya sawa, kama wanavyoogopa wafalme na wenye nguvu mwisho wa mateso kwa maadui zao; kwa sababu mwisho wa mambo ni vile anavyotaka yeye Mwenyezi Mungu na kuafikiana na anavyoidhinisha. Aya hii iko karibu katika maana na aya inayosema: "Haulizwi anayoyafanya, lakini wao wataulizwa " (21:23).

Inasemekana kuwa dhamir ya neno haogopi ni ya mwovu kwa maana ya kuwa haogopi mchinjaji ngamia mwisho wa aliofanya. Na pia imesemekana kuwa dhamir ya haogopi ni ya Saleh na dhamir ya mwisho wake ni ya kueneza adhabu kwa kutegemea kuokoka. Udhaifu wa njia zote hizo mbili uko wazi.

Utafiti Wa Hadith Katka Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na saba amesema: Akaiumba na kuitia Sura. Katika Majmau amepokea Zurarah na Hamran, na Muhammad bin Muslim kutoka kwa Abu Jaffar na Abu Abdillah(a.s) katika kauli yake Mwenyezi Mungu: Akaifahamisha maasis yake na twaa yake, ni kuwa ameibanisha yale ya kufanya na ya kuwacha. Na katika kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa". Amesema: "Hakika amefaulu mwenye kutwii" Na kuhusu na hakika amepata hasara mwenye kuitweza. Amesema: "Hakika amepata hasara mwenye kuasi".

Katika Durril Manthur ametoa Ahmad, Muslim, Ibn Jariyr, Ibn Mundhir, Ibn Murdawayh kutoka kwa Amran bin Haswiyn kwamba mtu mmoja alisema: "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaona wanayoyafanya watu leo wanajitahidi katika jambo ambalo limekwisha hukumuliwa na kupitishwa katika kadar iliyotangulia? Au katika ambayo wanamkubalia Mtume wao"? Akasema: "Bali ni jambo lililokwisha pitishwa.' Akasema huyo mtu kwa nini wanafanya basi? Akasema Mtume: "Ambaye Mwenyezi Mungu amemuumbia kwa moja ya daraja mbili humuandalia kuifanya. Na ukweli wa hayo ni katika kitabu cha Mwenyezi Mungu: "Na (kwa) nafsi na aliyelingamanisha akaifahamisha maasia yake na twaa yake ."

Ufafanuzi Wa Hadith Hiyo Aliposema au katika wanayomkubalia Mtume wao, inaungana na sehemu ya kwanza kama swali yaani, Je, katika kumtii Mtume wao kumepitishwa na kukadiriwa tayari? Aliposema: "Kwa nini wanafanya basi, yaani nini maana ya amali yao na kutugemezwa kitendo kwao"? Na aliposema; "Ambaye Mwenyezi Mungu amemuandalia " Maana yake ni kuwa: Matokeo ya kutenda wema au uovu yanatokana na wao pamoja na kuangalia kuwa yamekwishapitishwa na kukadiriwa; huko hakukanushi kutokea kwake kwa kumwangalia mtu na hiyari yake. Na hayo yamefafanuliwa mara nyingi. Katika utafiti uliotangulia katika kitabu hiki.

Katika hiyo Durril Manthur, ametoa Ibn Abu Hatim,Abu Shakh, Ibn Murdawayah na Addilami kutoka kwa Juwaybir naye kutoka Adh-dhahak naye kutoka kwa Ibn Abbas amesema: Nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) akisema: "Hakika amefaulu mwenye kuitakasa". Imefaulu nafsi aliyoitakasa Mwenyezi Mungu na imepata hasara nafsi aliyoihasirisha Mwenyezi Mungu na kila heri".

Kunasibisha utakaso na hasara kwa Mwenyezi Mungu S.W.T. ni kwa njia ambayo haikanushi kunasababishwa twaa na maasi kwa mtu. Na hakika hunasababishwa upotevu kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa njia ya fumbo; kaa S.W.T. kwa njia ya fumbo; kama alivyosema Mwenyezi Mungu "Na hamwachii yoyote kupotea kwa mfano huo isipokuwa wale wavunjao amri zake (mafasiki) " (2:26).

Katika Majmau anasema: " Imesihi riwaya kwa kutegemeza Uthman bin Suhaib naye kutoka kwa baba yake amesema" "Mtume(s.a.w.w) alisema kuumuliza Ali bin Abu Twalib: ni nani mwovu zaidi wa watu wa mwanzo?" Akasema: " aliyemchinja ngamia". Mtume akasema, "umepata". "Na nani mwovu wa watu wa mwisho?" Akasema "sijuwi ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu." Akasema Mtume: "Ambaye atakupiga kwenye huu (akaonyesha utosi wake)". Na imepokewa hadith nyengine kwa maana haya haya kutoka kwa Ammar bin Yassir. Katika Tafsiri ya Burhan amepokea Thalaabi ne Wahidi kwa kutegemezwa kwao, kutoka kwa Ammar na kutoka kwa Athman Bin Suhaib na kutoka kwa Adh-dhahhak.

Na amepokea Ibn Murdawayh kutoka kwa Jabir bin Samra; na kutoka kwa Ammar kutoka kwa Ibn Adi na amepokea Attabari na Muswili. Amepokea Ahmad kutoka kwa Adh- dhahhak naye kutoka kwa Ammar kwamba yeye amesema: Amesema Mtume(s.a.w.w) : "Ewe Ali mwovu zaidi wa kwanza ni mchinja ngamia na mwovu zaidi wa mwisho ni muuaji wako ".

17

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA LAYL (USIKU) (NA. 92)

INA AYA 21

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa usiku unapofunika

وَالنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ ﴿٢﴾

2. Na (kwa) mchana unapofunuka.

وَمَا خَلَقَ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ ﴿٣﴾

3. Na (kwa) mwenye kuumba kiume na kike.

إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ ﴿٤﴾

4. Hakika matendo yenu ni mbali mbali.

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾

5. Ama mwenye kutoa akamcha (Mwenyezi Mungu).

وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾

6. Akalisadiki jambo jema.

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧﴾

7. Tutamsahilishia njia ya wepesi.

وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾

8. Ama mwenye kufanya ubakhili akajiona hana haja.

وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾

9. Akalikadhibisha jambo jema.

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾

10. Tutamfanyia nyepesi njia ya uzito.

وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ ﴿١١﴾

11. Hayatamfaa mali yake atakapopomoka.

إِنَّ عَلَيْنَا لَلْـهُدَىٰ ﴿١٢﴾

12. Hakika na juu yetu kuongoza.

وَإِنَّ لَنَا لَلْآخِرَةَ وَالْأُولَىٰ ﴿١٣﴾

13. Na hakika ni yetu sisi akhera na ulimwengu.

فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًا تَلَظَّىٰ ﴿١٤﴾

14. Basi ninawahadharisha na moto unaowaka kwa nguvu.

لَا يَصْلَاهَا إِلَّا الْأَشْقَى ﴿١٥﴾

15. Hatauingia ila mwovu mno!

الَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١٦﴾

16. Ambaye amekadhibisha akapa mgongo.

وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾

17. Na ataepushwa nao mwenye kucha (Mungu).

الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾

18. Ambaye hutoa mali yake kwa (kutaka) kujitakasa.

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾

19. Na hali ya kuwa hakuna yoyote aliyemfanyia hisani ili awe anamlipa.

إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠﴾

20. Isipokuwa ni kwa kutaka radhi ya Mola wake aliye Mtukufu mno.

وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١﴾

21. Basi hapo ataridhia.

UBAINIFU

Lengo la Sura hii ni kuonya. Inaelezea huko kuonya kwa kufuata njia ya kuonyesha tofauti ya matendo ya watu: Kwamba katika wao, mwenye kutoa, akamcha Mwenyezi Mungu na akalisadiki jambo jema, basi Mwenyezi Mungu atammanikisha katika maisha mema ya milele. Na katika wao mwenye kufanya ubakhili, akajiona hana haja na akalikadhibisha jambo jema, basi Mwenyezi Mungu atamwelekeza kwenye uovu. Sura hii inatilia umuhimu zaidi jambo la kutoa mali. Kulingana na mpangilio wake inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina.

Aya Na 1

Mwenyezi Mungu anaapa kwa usiku unapofunika mchana; kama alivyosema: "Huufunika usiku kwa mchana " (7:54). Inawezekana kuwa makusudio yake ni kufunika ardhi au jua.

Aya Na 2

Inaungana na Aya Na (1). Maana ya neno Tajallaa ni kudhihiri kitu baada ya kujificha. Amesema katika Majmau ni kudhihiri huo mchana kutoka katika giza. Hili ni neema kubwa, kwani lau wakati wote ungekuwa ni giza, basi watu wasingeweza kutafuta maisha.

Aya Na 3

Pia inaungana na aya iliyotangulia herufi Maa ni kiwakilishi na makusudio yake ni Mwenyezi Mungu Mtukufu. Imekuja ibara hiyo bila ya kumtaja Mwenyezi Mungu kwa kutambulisha utukufu wake; Maana yake; ninaapa kwa kitu cha ajabu ambacho kimeleta kiume na kike ambavyo ni namna moja, lakini vimetofautina. Imesemwa kuwa herufi Maa ni kiarifa chenye kutumika kama jina; Maana yake ni ninaapa kwa kuumba kiume na kike lakini njia hii ni dhaifu. Mukusudio ya kiume na kike hapa ni aina yoyote ya kiume na kike. Imesemwa kuwa ni mtu mume na mke na pia imesemwa kuwa ni Adam na mkewe Hawa, lakini njia iliyo na nguvu zaidi, ni hiyo ya kwanza.

Aya Na 4

Neno Saa'ya lina maana ya kwenda haraka, na makusudio yake hapa ni ketendo kwa vile mtu anajihimu nacho, nalo liko katika maana ya wingi. Jumla hiyo ni jawabu la kiapo na maana yake; Ninaapa kwa vitu hivi vyenye kutofautiana kwa umbo na athari, hakika matendo yenu ni yenye kutofautiana hayo yenyewe na athari zake. Kuna katika hayo ni ya kutoa, kumcha Mwenyezi Mungu na kusadikisha, yana athari inayohusika nayo. Na kuna katika hayo ni ya ubakhili, kujitosheleza na kukadhibisha nayo yana athari inayohusika nayo.

Aya Na 5-6

Ni ufafanuzi wa kutofautiana matendo yao na kutofautiana athari yake. Makusudio ya kutoa ni kutoa mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kinyume chake ni ubakhili wa kujizuia kutoa mali. Na kusema kwake: "Hayatamfaa mali yake atakapopomoka." Na kusema kwake : "Na akamcha Allah" ni kama anafasiri kutoa, makusudio yake ni kutoa kwa njia ya (taqwa) uchaji Mungu. "Jambo jema" ni sifa yenye kusimama mahali pa chenye kusufiwa, kwa dhahiri kukadiriya kwake ni maandalizi mema ambayo ameyatolea ahadi Mwenyezi Mungu Katika thawabu ya kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) Na huko kutoa ni kusadikisha ufufuo na kuamini Mwenyezi Mungu na kulazimisha imani kwa umoja wake Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika ubwana na kuuamini utume. Hiyo ndiyo njia ya kufikia yale aliyoyatolea ahadi Mwenyezi Mungu kupitia kwenye ulimi wa Mtume wake.

Aya Na 7

Makusudio ya kumsahilishia njia ya wepesi ni kumwafikisha kwa mali njema kwa kuzifanya nyepesi bila ya uzito wowote. Au kumfanya ni mwenye kujiandaa kwa maisha mema mbele ya Mola wake na kuingia peponi kwa sababu ya amali njema anazozifanya. Hii njia ya pili ni karibu na iko wazi zaidi kutokana na yale yaliyotolewa ahadi katika viaga vya Qur'an.

Aya Na 8 -10

Ubakhili ni kunyume cha kutoa. Makusudio ya kukadhibisha jambo jema ni kukanusha mambo mema na thawabu za Mwenyezi Mungu ambazo wamezielezea Mitume. Na hayo yanarudia kukanusha ufufuo. Makusudio ya 'kusahilishiwa uzito' ni kutofanikiwa kwake kwa kukosa kuwafikishwa kwenye amali njema, kwa kuwa nzito na kukosa kukunjuliwa moyo wake na imani au ni kuandaliwa adhabu.

Aya Na 11

Herufi Maa ni swali yaani mali yake itamfaa namna gani atakapokufa na kuangamia. Au ni ya kukanusha, yaani haitamfaa mali yake atakapoangamia.

Aya Na 12-13

Ni sababu ya yaliyotangulia katika kuzungumzia wepesi na uzito Au nikuelezea kwa ufafanuzi zaidi kwamba hakika sisi tunafanya huu wepesi au tunaubainisha ubainifu huu, kwa sababu unatokana na uongofu na ni juu yetu kuongoza na wala hakituzuii kitu chochote. Kwa hivyo kusema kwake "Hakika ni juu yetu kuongoza", kunamaanisha kwamba kuongoza watu alikokupitisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) amejiwabisha mwenyewe kwa mujibu wa hekima, na hilo ni kwamba yeye amewaumba ili wamwabudu; kama alivyosema: "Sikuumba majini na watu ila waniabudu ". (51:56).

Kwa hiyo amefanya kumwabudu ndiyo lengo la kuumbwa kwao na akaifanya hiyo ibada ni njia yenye kunyooka ya kumwendea yeye; kama alivyosema: "Hakika Allah ni Mola wangu na ni Mola wenu, basi mwabuduni hii ndiyo njio iliyonyooka " (3:51) "Hakika wewe unaongoza njia iliyonyooka " (42:52).

Mwenyezi Mungu amejihukumilia kuwabainishia watu njia yake na kuwaongoza kwake, kwa maana ya kuwaonyeshea njia, ikiwa wataifuata au wataiwacha, kama alivyosema: "Na Allah ndiye anayesema kweli, naye kuongoa njia (ya uongofu) (33:4). Amesema tena: "Hakika sisi tumemuongoa njia, basi ama atakuwa mwenye kushukuru au kukufuru ". (76:3).

Hayo yote hayapingi kuwa mtu mwengine asiyekuwa Mwenyezi Mungu kuweza kusimamia jambo hili kwa idhini yake Mwenyezi Mungu, kama vile mitume; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Hakika wewe (Muhammad) unaongoza njia iliyonyooka " (42:52). Amesema tena: "Sema, hii ndiyo njia yangu ninailingania kwa Allah kwa ujuzi wa kweli, mimi (ninafanya hivi) na wanaonifuata " (12:108)

Hayo ni ikiwa uongozi ni kwa maana ya kuonyesha njia. Ama ikiwa uongozi ni kwa maana ya kufikisha kwenye matakwa - na matakwa ni athari nzuri ambazo zinafuatana na kuongoka kwa uongofu wa Mwenyezi Mungu kama maisha mema ya dunia na ya akhera ya milele - basi kwa ubainifu zaidi itakuwa ni kwa upande wa kutengeneza na kupatisha ambako anahusika nako Mwenyezi Mungu (s.w.t) Hayo ni katika yale aliyoyahukumilia Mwenyezi Mungu na kujiwajibishia na kuyasajili kwa kiaga chake cha haki; Mwenyezi Mungu anasema: "Basi atakayeufuata uongofu wangu hatapotea wala hatataabika ." (20:123).

"Mwenye kufanya mema miongoni mwa wanaume au wanawake na hali ya kuwa yeye ni muu'min tutamuhuyisha maisha mema na tutawapa ujira wao mkubwa kwa sababu ya yale mema waliyokuwa wakiyatenda ." (16:97).

Amesema tena: "Na wale waliomaini na wakatenda njema tutawaingiza katika mabustani yapitayo mito chini yake watakaa humo milele. Ndiyo ahadi ya Allah iliyokweli. Na ninani mkweli zaidi kwa usemi kuliko Allah ? (4:122). Kunasibishiwa uongozi mtu mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu, kwa kuingia kati huyo mtu na hayo yanayonasibishwa kwa Mwenyezi Mungu. Hii ikiwa ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Hivyo Mwenyezi Mungu atakuwa ndiyo asili ya uongozi, na mtu huyo ni mfuasi. Maana ya aya, ikiwa makusudio ya uongofu ni kuonyesha njia, ni: hakika sisi tunawabainisha yale tunayoyabainisha, kwa sababu ni juu yetu kuonyesha njia ya kuabudu. Ikiwa ni kwa makusudio ya kufikisha kwenye matakwa, ni: hakika tunawasahilishia hawa wepesi wa amali njema, au na maisha mepesi ya milele na kuingia peponi; kwa sababu hilo ni katika kuvifikisha vitu kwenye lengo lake, na hilo ni juu yetu. Ama kusahilishia njia ya uzito ni kuzuilika na kupata wepesi, "Ili Allah apate kuwapambanua walio wabaya na walio wazuri na kuwaweka wabaya juu ya wabaya wengine na kuwarundika wote pamoja na kuwatupa katika Jahanam ". (8:37).

Mwenyezi Mungu amekwishasema: "Na tunateremsha katika Qur'an (Hayo mafundisho yake) ambayo ni ponyo na rehema kwa wanaoamini wala hayawazidishi (mafundisho hayo) madhalimu ila hasara tu! (kwani hawakubali kufuata) ." (17:82).

Inawezekana kuwa maana ya ungozi hapa - kwa vile tamko 'uongozi' halikutegemezewa sharti yeyote - ni kwamba huu uongozi, pasi na kutajwa katika jambo gani, una maana mapana zaidi kuliko uongozi uliotajwa kama katika mazingatio ya sheria n.k. - kwa hiyo Mwenyezi Mungu ni wake uongozi wa kiuhakika kama alivyosema: "ambaye amekipa kila kitu umbo lake kisha akakiongoza ." (20:50).

Na ni wake uongofu wa kimazingatio, kama alivyosema: "Hakika sisi tumemuongoa (tumembainishia) njia (ya kheri nay a shari) , basi (mwenyewe tena) atakuwa mwenye kushukuru au kukufuru .(76:3).

Kuhusu Aya Na (13) ni ulimwengu wa mwanzo na ulimwengu wa kurudi; kila kinachohisabika ni kitu basi ni milki yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa milki ya uhakika ambayo inasimamia kupatikana kwa kiti hicho, kisha ndipo inakuja milki wa kimazingatio ambayo katika athari zake ni kujuzu kukifanya lolote.

Kwa hiyo yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamiliki kila kitu kwa kila upande hakuna mpinzani anayempinga wala mzuwiyaji atakayemzuwiya, wala hakuna kitu kinachomshinda, kama alivyosema: "Na Allah huhukumu hakuna wa kupinga hukumu yake "(13:41).

Na amesema tena: "Na Allah hufanya apendavyo." (14:27).

Na amesema tena: "Na Allah ndiye mwenye kushinda juu ya jambo lake (alitakalo lazima liwe) ." (12:21).

Aya Na 14-16

Ni mtiririko wa yaliyotangulia; yaani ikiwa uongofu ni juu yetu, basi ninawatahadharisha na moto wa Jahannam. Na kwa hilo anauelekeza msemo katika kauli yake (ninawatahadharisha) kutoka katika wenye kusema wengi kwenda kwa mwenye kusema mmoja pekee, yaani ikiwa uongofu ni wenye kupitishwa, basi muhadharishaji wa asili ni Mwenyezi Mungu ijapokuwa ni kupitia kwa ulimi wa Mtume wake. Makusudio ya moto uwakao ni Jahannam kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Lakini wapi! Kwa hakika huo ni moto uwakao ". (70:15).

Makusudio ya mwovu mno ni kafiri yeyote ambaye anakufuru kwa kukadhibisha na kupa mgongo. Kwani yeye ni mwovu zaidi ya waovu wengine. Mwenye kuwa na balaa katika mwili wake amepata uovu, mwenye kupatwa na balaa katika mali yake au mtoto wake pia amepata uovu na mwenye kupata hasara katika mambo yake ya akhera amekuwa mwovu, lakini huyu ni mwovu zaidi ya wengine kwa vile uovu wake ni wa milele hakuna tamaa ya kuepukana nao. Kinyume cha uovu wa mambo ya kidunia, kwa sababu uovu unakatika na ni wenye kutarajiwa kuondoka haraka.

Kwa hiyo makusudio ya mwovu mno hapa ni kafiri mwenye kukadhibisha mlingano wa haki, kama alivyomwelezea Mwenyezi Mungu kwa kusema: "Ambaye amekadhibisha na akapa mgongo." Ama kusema muovu zaidi ni kwa maana ya muovu wa watu wote ni jambo ambalo halisaidiwi kabia na mpangilio wa maneno. Makusudio ya neno Yaswlaaha ni kuufuata huo moto na kulazimiana nao (kuwa nao) kwa hiyo inafahamisha kudumu kwenye huo moto. Hayo ni katika aliyoyahukumilia Mwenyezi Mungu katika haki ya kafiri, kama alivyosema: "Na wale ambao wamekufuru na wakayakadhibisha maneno yetu hao ni watu wa motoni, watakaa milele humo ." (2:39).

Hilo basi linapinga yale yaliyosemwa kwamba maana ya neno: "Hatauingia ila mwovu mno" kwamba mafasiki katika waislamu hawataingia motoni, isipokuwa inaonyesha kuwa asiyekuwa kafiri hatadumu , lakini atauingia.

Aya Na 17-19

Makusudio ya neno Atqaa ni yule mwenye kumcha Mungu zaidi: Wako watu hucha kupotea nafsi kama kwa kifo au kuuawa, na wengine hucha kuharibika mali na wengine hucha ufakiri, kwa hiyo wanajizuia kutoa mali. Na wengine humcha Mwenyezi Mungu tu; kwa hiyo wanatoa mali. Basi huyu ndiye mwenye kucha zaidi ya wote, anatoa mali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Ukipenda unaweza kusema: hucha hasara ya akhera , kwa hiyo anajitakasa kwa kutoa. Yule ambaye hachi kwa kutoa mali anashindwa na huyo anayetoa mali, ijapokuwa hucha mambo ya kidunia au humcha Mungu kwa baadhi ya matendo mema.

Ayah ii inaenea kwa wote na sio mahsusi kwa mtu, kulingana na inavyofahamisha, na kunafahamisha hilo, kumsifu mwenye kucha zaidi kwa aya inayofuatia. "Ambayo hutoa mali yake" hiyo ni sifa ya yeyote yule amayetoa, lakini hili halikanushi kuwa aya au Sura yote imeshuka kwa sababu mahsusi kama ilivyopokewa katika sababu za kushuka. Ama kumuhusisha mbora zaidi mmoja tu! Juu ya watu wote, wabaya au wema katika wote au katika kila zama na iwe maana ni "ataepushwa nao mwenye kucha zaidi ya watu wote, na hatauingia ila mwovu zaidi ya watu wote", ni jambo ambalo halisaidiwi na mpangilio wa aya za mwanzo wa Sura vile vile hakuna maana ya kusema "Ninawahadharisha nyote na moto ambao hatadumu ndani yake ila mmoja katika nyinyi na hataokoka ila mmoja katika nyinyi".

Aya Na (18) ni sifa ya yule mwenye kumcha zaidi yaani ambaye anatoa mali yake hali ya kutaka kwa hilo ziada njema.

Aya Na (19) ni ya kuthibitisha madhumuni ya aya iliyotangulia yaani hana yoyote mbele zake ihsani itakayolipa hiyo ihsani yake isipokuwa anatoa kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu. HAya Na natiliwa nguvu na aya inayofuatia.

Aya Na 20

Maana yake ni lakini yeye anatoa mali yake hali ya kutaka radhi ya Mola wake Mtukufu. Maelezo zaidi ya Mola Mtukufu yako katika Sura ya 87.

Aya Na 21

Yaani huyu mchaji zaidi ataridhia yale anayopewa na Mola wake Mtukufu kutokana na malipo mema yaliyo mazuri. Kutaja sifa mbili za Mola na Utukufu, ni kufahamisha kwamba yale malipo anayopewa ni malipo ya neema zaidi na ya utukufu zaidi (juu zaidi) nayo ni yenye kunasibiana na Uungu na Utukufu.

Utafiti Wa Hadith Katika Kafi kutoka kwa Muhammad bin Muslim amesema: "Nilimuuliza Abu jaffar(a.s) kuhusu maneno ya Mwenyezi Mungu: "Naapa kwa usiku unapofunika, na naapa kwa nyota zinapoanguka (zinapokuchwa) " na mifano ya hayo. Akaniambia: "Hakika Mwenyezi Mungu anaweza kuapia chochote anachotaka katika viumbe vyake, lakini viumbe haviwezi kumwapia asiyekuwa Yeye (Mwenyezi Mungu). Imepokewa katika Faqih kutoka kwa Ali bin Mahziyar kutoka kwa Abu Jaffar wa pili(a.s) na katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na kwanza anasema: Ni wakati unapofunikwa mchana, na hicho ni kiapo. Kutoka kwa Humayri naye kutoka kwa Ahmad bin Muhammad naye kutoka kwa Ahmad bin Muhammad bin Abu nasr naye kutoka kwa Abul-Hassan Arridhaa(a.s) kuhusu tafsiri ya Sura ya Al-layl anasema:

"Hakika mtu mmoja alikuwa na mtende katika ukuta wa Mtu mwengine na huyo mwenye mtende alikuwa akimdhuru huyo mwengine; akamshtakia Mtume akaitwa yule mwenye na Mtume akamwambia nipe mtende wako kwa mtende wa peponi, akakataa. Na kulikuwepo mtu mwengine anayeitwa Abu Dahdaah aliyesikia hayo akamwendea mwenye mtende akamwambia niuzie mtende wako kwa ukuta wangu akamuuzia. Abu Dahdaah akwamwendea Mtume akamwambia nimeununua mtende fulani: kwa ukuta wangu. Mtume akamwambia "utapata badala yake mtende katika peponi ndipo akateremsha Mwenyezi Mungu: "Na mwenye kuumba kike na kiume. Hakika matendo yenu ni mbalimbali. Ama mwenye kutoa (yaani mtende) na akamcha Allah na akalisadiki jambo jema (yaani lililo mbele ya Mtume(s.a.w.w) mpaka Aya Na 11.

Katika Tafsiri ya Qummi mwenye kucha Mwenyezi Mungu zaidi ni Abu Dahdaah. Hayo ni kwa upande wa Shia kutokana na Maimamu wa Ahlul Bait. Kwa upande wa Ahli Sunna amepokea Tabrasi katika Majmau kwamba kisa hicho kimepokewa kwa Wahidi naye kutoka kwa Akrama naye kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Ansari mmoja alipiga bei na mwenye mtende akaununua kwa mitende arubaini, kisha akampa Mtume naye Mtume akampa mwenye nyumba. Amepokea Tabrasi kutoka kwa Ata kwamba jina la huyo mtu ni Abu Dahdaah. Na amepokea Assuyuti katika Durril Manthur kisa hicho kutoka kwa Ibn Abu Hatim naye kutoka kwa Ibn Abbas, lakini ameifanya dhaifu riwaya hiyo.

Imepokewa tena, katika njia ya Ahli Sunna kwamba Sura hii ilishuka kwa Abu Bakr. Amesema Arrazi katika Tafsiri Kabir: "Wamekongamana wafasiri katika sisi kwamba makusudio katika aya ni Abu Bakr. Anaendelea kusema Arrazi: "Jua kwamba Mashia wote wanakanusha riwaya hii, wanasema imeshuka katika haki ya Ali bin Abu Twalib na dalili juu ya hilo ni juu ya aya inayosema: "Na hutoa zaka na hali yakua wao wanaswali " (5:55).

Kwa hiyo neno lake Mwenyezi Mungu: "Mwenye kumcha (Mungu) zaidi ambaye hutoa mali yake kwa kujitakasa " linaishiria kwenye aya hiyo (5:55).

Ama yale yaliyonasibishwa kwa Mashia wote, yenye kutegemewa katika njia zao ni Sahihi ya Al-Himyariyy iliyotangulia kueleza yaliyo katika riwAya Na nayofahamisha kushuka aya kwa Abu-Dahdaah El- Ansari.

Ndio, imekuja riwaya dhaifu kutoka kwa Barqi naye kutoka kwa Ismail bin Mahraan naye kutoka kwa Ayman bin Muhriz naye kutoka kwa Abu Basiyr naye kutoka kwa Abu Abdillah amesema: Ama kauli yake: Na ataepushwa nao mwenye kumcha (Mungu) zaidi, mwenye kumcha (Mungu) zaidi ni Mtume(s.a.w.w) na wafuasi wake na Ambaye hutoa mali yake kwa (kutaka) kujitakasa, huyo ni Amiirul-Mui'miniin Ali(a.s) na ndiyo kauli yake Mwenyezi Mungu: "Na wanatoa zaka na hali wao ni wenye kuswali ." (5:55).

Na kuhusu aya "Na hali ya kuwa hakuna yoyote aliyemfanyia hisani ili awe anamlipa " huyo ni Mtume(s.a.w.w) ambaye hana yoyote wa kumlipa hisani na hali hisani zake ni zenye kuenea kwa watu wote.

Riwaya hiyo ni dhaifu kwa upande wa mapitio yake na kufuatilia kwake bila ya kuangalia tafsir. Dalili iliyowazi ya udhaifu wake ni vile kufuatilia kwake kuwa mwenye kusifiwa ni Mtume na sifa iwe juu ya Ali(a.s) kisha aya inayofuatia tena juu ya Mtume. Na kama hilo lingekuwa katika tafsiri ingeliharibika nidhamu yake kabisa. Na huyo Ayman bin Muhriz hajulikani.

Imepokjewa kutoka kwa Al Himyariyy kutoka kwa Ahmad bin Muhammad bin Abu Nasr naye kutoka kwa Abul hassan Arridha(a.s) amesema: Niliulizwa kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika Allah humwongoza anayemtaka na kumpoteza anayetaka. Nikamwambia: Mwenyezi Mungu akufanye uwe mwema "Hakika watu katika watu wetu wanadai mwamba maarifa ni yenye kuchumwa na kwamba wao wakiangalia vizuri wanapata heri". Akakanusha hilo na akasema: "Hawa watu hawachumi heri wao wenyewe, hakuna yeyote katika watu isipokuwa ni wajibu kuwa heri inatokana na yule ambaye heri inatoka kwake.

Ama uongofu ambao makusudio yake ni kufikisha kwenye matakwa, huo ni wa Mwenyezi Mungu kwa sababu ni katika mambo ya Mungu. Ama upotevu ambao makusudio yake ni kupoteza kwa upande wa njia na wala sio kupoteza kwa kuanzia ambako hakuegemezwi kwa Mwenyezi Mungu, ni kwa Mwenyezi Mungu pia, kwa kuwa yeye ni mwenye kuzuwiya kushusha rehema na kukosekana uongofu. Ikiwa uongofu unatokana naye basi kuzuilika nako pia kunatokana naye.

18

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA ADHUHAA (DHUHA)(NA. 93)

INA AYA 11

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa mwanzo wa mchana.

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na kwa usiku unapotuwa.

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Hakukuacha Mola wako wala hakukukasirikia.

وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ الْأُولَىٰ ﴿٤﴾

4. Hakika akhera ni bora kwako kuliko ulimwengu.

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ ﴿٥﴾

5. Na atakupa Mola wako utaridhia.

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَآوَىٰ ﴿٦﴾

6. Je, hakukuta ni yatima akakuhifadhi?

وَوَجَدَكَ ضَالًّا فَهَدَىٰ ﴿٧﴾

7. Akakukuta umedangana akakuongoza?

وَوَجَدَكَ عَائِلًا فَأَغْنَىٰ ﴿٨﴾

8. Akakukuta ufakiri akakutajirisha.

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ ﴿٩﴾

9. Basi yatima usimdhalilishe.

وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ ﴿١٠﴾

10. Na mwenye kuoma usimkaripie.

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ ﴿١١﴾

11. Na neema ya Mola wako, izungumze.

UBAINIFU

Inasemekana kuwa Mtume(s.a.w.w) alikatikiwa na wahyi kwa siku kadhaa mpaka watu wakawa wanasema: "Hakika Mola wake amemwachilia mbali". Basi ndio akateremsha Mwenyezi Mungu Sura hii kuituliza nafsi yake. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina.

Aya Na 1-2

Maana ya neno Dhuhaa ni kuangaza jua na kuenea mchana na neno Sajaa nikutulia yaani kuingia giza.

Aya Na 3

Ni jawabu la kiapo. Mnasaba wa nuru ya mchana na giza la usiku kwa kushuka wahyi na kukatika kwake uko dhahiri.

Aya Na 4

Maana yake kutokana na inavyofahamisha aya iliyotangulia ni kama vile anaambiwa Mtume: Yale uliyonayo miongoni mwa fadhila na rehema ni muda wa kuwa uko hai katika dunia na uhai wako wa akhera ni bora kwako kuliko maisha yako ya dunia.

Aya Na 5

Ni uthibitisho wa aya iliyotangulia na imekusanya kiaga cha kutoa kutakakofuatiwa na kuridhia. Imesemwa aya hii inaangalia pande zote mbili (maisha ya dunia na akhera) na wala sio akhera tu!

Aya Na 6

Inaishiria baadhi ya neema zake Mwenyezi Mungu kwa Mtume; alifiwa na baba yake akiwa tumboni mwa mama yake, kisha akafa mama yake akiwa na miaka miwili, tena akafa (mlezi wake) babu yake naye akiwa na miaka minane, basi ndio akachukuliwa na ami yake kumlea. Inasemekana makusudio ya yatima hapa ni yule mtu aliye peke yake. Kwa hiyo maana inakuwa; Je hakukuta peke yako kati ya watu, akawakusanya watu kwako?

Aya Na 7

Makusudio ya neno Dhwallan ni kudangana kukosa ungofu na makusudio ya kudangana kwake Mtume(s.a.w.w) ni ila hali ya kukatikiwa na ungofu wake Mwenyezi Mungu Mtukufu na hapana uongofu kwa Mtume(s.a.w.w) wala kwa yoyote katika viumbe ila kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo nafsi yake ilikuwa imedangana, ijapokuwa uongofu wa Mwenyezi Mungu ni wenye kulazimiana naye. Aya hii iko katika maana na aya inayosema: "Ulikuwa hujui kitabu nini wala imani " (42:52).

Vile vile iko katika maana ya neno la Musa, kama anavyosimulia Mwenyezi Mungu katika Qur'an. "nimeyafanya hayo nilipokuwa miongoni mwa waliodangana ." (26:20) yaani wakati bado sijapata uongofu wa utume.

Yanakurubia maana hayo na yale yaliyosemwa kuwa makusudio ya Dhwallan ni kuondokewa na elimu (kutokujua) kama ilivyo katika kauli yake Mwenyezi Mungu."..ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwengine " (2:282).

Hayo yanatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu: "na hakika ulikuwa kabla ya haya ni miongoni mwa wasio na habari hizi ." (12:3).

Imesemwa maana yake ni akakukuta umepotea kati ya watu hawajui haki yako akawaongoza kwako na akawajulisha kuhusu wewe.

Imesemwa ni ishira ya kupotea njia ya Makka alipokuwa mdogo. Pia imesemwa ni ishara ya kupotea kwake ndani ya msafara wa Maysara mtumishi wa Khadija, wakati alipokwenda Sham pamoja na ami yake, Abu Twalib. Na yamesemwa zaidi ya hayo ni hizo zote ni njia dhaifu.

Aya Na 8

Fukara ni yule ambaye hana mali. Alikuwa Mtume(s.a.w.w) ni fukara akatajirishwa na Mwenyezi Mungu baada ya kumuoa Bibi Khadija ambaye alikuwa na mali nyingi akampa Mtume.

Aya Na 9-11

Aya zote hizi tatu zinatokana na aya zilizotangulia na zinataja wema wake Mwenyezi Mungu (s.w.t), ni kama anasema: "Umeyapata yale yanayompata yatima katika udhalili na upweke kwa hiyo basi usimdhalilishe yatima kwa kuidhalilisha nafsi yake au mali yake." Na mara nyingi umeipata haja ya mwenye kupotea vile anavyohitajia uongofu na fakiri anavyohitajia utajiri, basi usimkaripie mwenye kuomba kuondolewa haja yake ya uongofu au maisha. Vile vile umeona kuwa neema ulizonazo amekuneemesha Mola wako kwa ukarimu wake, basi ishukuru neema yake kwa kuizungumza wala usiifiche. Maamrisho yote haya ni kwa watu wote ingawaje yanaelekezwa kwa Mtume.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu neno la Mwenyezi Mungu Dhuhaa anasema ni wakati wa kupanda jua na Sajaa anasema ni wakati wa giza. Na kuhusu neno la Mwenyezi Mungu Maqalaa anasema ni "hakukukasirikia". Katika Durril Manthur kuhusu Aya Na tano, ametoa Ibn Abu Shayba kutoka kwa Ibn Masud amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) "Sisi Ahlul Bait Mwenyezi Mungu ametuchagulia akhera kuliko dunia ."

Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Askary katika Mawaidh, Ibn Laali na Ibn Najjar kutoka kwa Jabir bin Abdillahi amesema; "Mtume(s.a.w.w) aliingia kwa Fatima akiwa anatwanga kwa jiwe huku amevaa nguo za sufu za ngamia". Alipomwangalia akasema: "Ewe Fatima fanya haraka umeze uchungu wa dunia kwa neema na akhera kesho." Akateremsha Mwenyezi Mungu aya hiyo ya tano. Riwaya hii inachukulia kuwa aya hiyo ilishuka peke yake baada ya kushuka aya zilizo kabla yake katika Sura hii kisha kuunganishwa. Kuna uwezekano wa Aya hiyo kushuka peke yake kwa mara nyingi.

Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Ibn El Mundhir,Ibn Murdawayh na Abu naim katika Hilyat kutoka katika njia ya Harb bin Sharih amesema:"Nilimwambia Abu jaffar Muhammad bin Ali bin Hussein(a.s) unaonaje hii Shafaa (uombezi) wanayoizungumzia watu wa Iraq ni kweli? Akasema: "Kabisa Wallah". Alinizungumzia Ami yangu Muhammad bin El-Hanafiya kutoka kwa Ali kwamba Mtume(s.a.w.w) alisema: "nitauombea shafaa umati wangu mpaka Mola wangu anisemeshe: Umeridhika ewe Muhammad? Na nisema: Ndio ewe Mola wangu nimeridhika." Kisha akanikabili na kuniambia: "Hakika nyinyi watu wa Iraq mnasema: Hakika aya yenye kutarajiwa zaidi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ni ile inayosema: "Sema, enyi waja wangu mliojidhulumu nafsi zenu! Msikate tamaa na Rehema ya Allah; Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote " (39:53). Nikasema ndio sisi tunasema hivyo. Akasema: Basi sote sisi Ahlul Bait tunasema: "Hakika aya inayotarajiwa zaidi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ni ile inayosema: "Na atakupa Mola wako nawe utaridhia". Yaani uombezi. (Aya Na tano katika Sura hii).

Katika Tafsiri ya Burhan kutoka kwa Baabwayh kwa isnadi ya Ibn Jaham kutoka kwa Ridhaa(a.s) katika kikao pamoja ya Maamun alisema huyo Ridhaa; "Anasema Mwenyezi Mungu (s.w.t) kumwambia Mtume wake Muhammad(s.a.w.w) . "Je hakukuta ni yatima akakuhifadhi?" Anasema: "Je hakukuta peke yako akakusanyia watu? Na akakukuta umedangana yaani mbele ya watu wako "akakuongoa" yaani akawongoa watu wakakufahamu. Na akakukuta ufakiri akakutajirisha". Anasema "akakutajirisha kwa kujaalia dua yako ni yenye kutakabaliwa?" Akasema Maamun: "Mwenyezi Mungu akubarikie ewe mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu".

Katika hiyo hiyo Tafsiri ya Burhan kutoka kwa Barqi kwa isnadi yake kutoka kwa Amru bin Abu Nasr amesema: Alinizungumzia mtu mmoja katika watu wa Basra akasema: "Nilimuona Hussein bin Ali(a.s) na Abdallah bin Umar wanatufu Al-Kaaba. Nikamuuliza Ibn Umar: Kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu "Na neema ya Mola wako izungumze", Akasema : "Ni kuzungumza aliyoneemesha Mwenyezi Mungu." Kisha nikamuuliza Hussein bin Ali(a.s) akasema: "Nikuzungumza aliyoneemesha Mwenyezi Mungu katika dini yake." Katika Durril Manthur kutoka kwa Bayhaqi naye kutoka kwa Hassan bin Ali kuhusu ayay hiyo ya 11 akasema: "Ukipata heri wazungumzie ndugu zako".

Katika hiyo Durril Manthur ametoa Abu Dawud kutoka kwa Jabir bin Abdillahi kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mwenye kujaribiwa kwa kupewa misukosuko akaizungumza, hakika huyo amemshukuru Mwenyezi Mungu, na mwenye kuficha atakuwa amemkanusha (uweza) wa Mwenyezi Mungu. Na mwenye kujinasibishia asilokuwa nalo, hakika yeye ni kama amevaa nguo za uzushi.