TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN0%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi: Muhammad Hussein Tabaatabaai
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 39401
Pakua: 2912

Maelezo zaidi:

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39401 / Pakua: 2912
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

19

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA INSHIRAAH (UKUNJUFU) (NA. 94)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenya kurehemu

أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ ﴿١﴾

1. Je, hatukukunjulia moyo wako?

وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ ﴿٢﴾

2. Tukakuondolea uzito wako.

الَّذِي أَنقَضَ ظَهْرَكَ ﴿٣﴾

3. Ambao uliuelemea mgongo wako?

وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ ﴿٤﴾

4. Tukakutukuzia utajo wako?

فَإِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا ﴿٥﴾

5. Hakika pamoja na uzito kuna wepesi.

إِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا ﴿٦﴾

6. Hakika pamoja na uzito kuna wepesi.

فَإِذَا فَرَغْتَ فَانصَبْ ﴿٧﴾

7. Basi ukishamaliza (amali yako) jitaabishe kwa ibada.

وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَارْغَب ﴿٨﴾

8. Na Mola wako (peke yake) mtake haja.

UBAINIFU

Ni amri ya kujitaabisha kwa ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kujipendekeza kwa kumtaka haja. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina, na mpangilio wa aya zake unawafikiana zaidi na Madina. Katika baadhi ya riwaya za Maimamu wa Ahlul Bait(a.s) zinasema kuwa Sura ya Adh-dhuha na Al-Inshiraah ni Sura moja. Na yamepokewa hayo vile vile kutoka kwa Twaaus na Umar bin Abdul-Aziz.

Amesema Arrazi katika Tafsiri Kabir baada ya kuwanakili hao wawili: Jambo lililofanya Twaaus na Umar kusema kuwa hizo ni Sura moja ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Je hatukukukunjulia moyo wako ?" Nikama linaungana na neno; "Je hakukukuta ni yatima akakuhifadhi?" Lakini sababu hiyo siyo, kwani neno la kwanza kushuka kwake, lilikuwa ni katika hali ya kuwa Mtume(s.a.w.w) yuko kwenye ghamu kutokana na maudhi ya makafiri, akawa katika hali ya misukosuko na dhiki ya moyo. Na neno la pili linahukumilia kuwa liliposhuka, Mtume alikuwa katika hali ya kukunjuka na kutulia moyo, basi yataungana vipi haya?

Katika hiyo hiyo Tafsiri Kabir imesemwa makusudio ya kuukunjua moyo wake Mtume(s.a.w.w) ni kufanywa Mtume anakunjukiwa na hakika zote anazopewa wala hapati dhiki yoyote kutokana na maarifa yanayomshukia na wala hapati dhiki kutokana na adha ya watu katika kuyafikisha hAya Na nayomshukia. Na wala sio kutulia moyo na furaha, kama yatakavyokuja maelezo zaidi (Inshallah). Yanafahamisha hayo yale yaliyopokewa na Ibn Abu Hatim kutoka kwa Said bin Jubayr naye kutoka kwa Ibn Abbas amesema: Amesema Mtume(s.a.w.w) : "Nilimuuliza Mola wangu masuala ambayo nilitamani nisingemuuliza. Nilimwambia "Ewe Mola wangu Mitume waliokuwa kabla yangu kuna katika wao waliofanyiwa upepo uwatii na waliokuwa wakiwafufua wafu. Ndio akasema Mwenyezi Mungu: "Je sikukuta ni yatima nikakuhifadhi?" Nikasema: "Kwa nini?" Akasema: "Je sikukuta umedangana nikakuongoza?" Nikasema: "Bila shaka ewe Mola wangu." Akasema: "Je sikukukunjulia Moyo wako na nikakuondolea uzito wako?" Nikasema "Bila shaka ewe Mola wangu." Maelezo zaidi yako katika Tafsiri ya Sura Quraish (Liiylafi Quraish).

Aya Na 1

Asili ya neno Nashrah ni kuichangua nyama na mfano wake, na miongoni mwa maana yake ni kukunjua moyo yaani kuukunjua kwa nuru ya Mungu na utuvu unaotokana upande wa Mwenyezi Mungu na Roho inayotoka kwake. Qur'an inasema: "Ewe Allah nikunjulie moyo wangu ." (20:25).

"Je hatukukunjulia moyo wako?" "Je ambaye amekunjuliwa moyo wake na Allah " (39:22).

Kuzifuatisha aya tatu za mwanzo katika madhumuni yake kisha kuzibainisha kwa kauli "Hakika pamoja na uzito kuna wepesi", kwa dhahiri inaonyesha kufungika hali yake Mtume katika mwanzo wa mlingano wake, katikati yake na mwisho wake. Kisha kukaririka kuthibitisha ila na kuzifanya aya mbili za mwisho kuwa ni sehemu yake. Yote hayo yanashuhudia kuwa makusudio ya kukunjua moyo wake Mtume(s.a.w.w) ni kuukunjua kiasi ambacho yatakunjuka yale yanayomfikia miongoni mwa wahyi, yale anayoamrishwa kuyafikisha na yale yanayompata katika maudhi na adha kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Kwa maneno mengine tunaweza kusema ni kuifanya nafsi yake tukufu ni yenye kujiandaa kwa ukamilifu kwa kukubali yale yanayoifikia hiyo nafsi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Aya Na 2-3

Makusudio ya kuondoa uzito wake kutokana na unavyofahamisha mpangilio wa maneno ni kutekeleza mlingano wake na kupitisha juhudi zake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kwa kuwafiki sababu. Kwani hakika ujumbe (Utume), na mlingano ndio uzito aliochukua mara tu! Baada ya kukunjuliwa moyo wake. Inasemekana kuwa kuondoa uzito kunaonyesha kunaelekeana na yale yaliyopokewa kwamba Malaika wawili walimshukia Mtume wakakipasua kifua chake na wakautoa moyo wake wakautoharisha, kisha wakaurudisha mahali pake. Maelezo zaidi yatakuja baadae.

Inasemekana makusudio ya uzito ni yale yaliyomtokea kabla ya kupewa utume, pia imesemwa ni kupatwa kwake na mshangao katika baadhi ya mambo kama kutekeleza haki ya ujumbe na imesemwa kuwa ni uadui wa watu wake na maudhi yao mengi. Pia imesemwa ni huzuni yake kwa kufiwa na ami yake Abu Twalib na mkewe Khadija. Na ikasemwa uzito ni maasi na kuondolewa uzito ni isma (kuhifadhiwa na dhambi) yake na imesemwa kuwa uzito ni dhambi za uma wake na kuondolewa uzito huo ni kusamehewa. Njia hizi baadhi yake ni za kipuuzi na baadhi yake ni dhaifu zisizoafikiana na mpangilio wa maneno. Nazo ziko kati ya imesemekana na inawezekana tu! Hazina uhakika wowote.

Aya Na 4

Kuutukuza utajo maana yake ni kutajwa sana jina lake kuliko mtu mwengine. Miongoni mwa kuutukuza utajo wake ni kukutanisha Mwenyezi Mungu jina lake pamoja na jina la Mtume. Kwani jina la Mtume liko pamoja na la Mola wake katika shahada mbili ambazo ndizo msingi wa dini na ni wajibu kwa kila muislamu kumtaja Mtume pamoja na Mola wake katika swala tano za wajibu kila siku. Ni katika wema kutokea kutukuzwa utajo baada ya kuondolewa uzito.

Aya Na 5

Siyo mbali kuwa ni sababu ya yale yaliyotangulia (kuondoa uzito na kulitukuza jina). Yale aliyobebeshwa na Mwenyezi Mungu na akaamrishwa kuyalingania - ambayo ni mazito kwa mtu kuyachukua - yalikuwa yamezidi. Vile vile watu wake walizidi kumfanya mwongo kwa mwito wake, kumdharau na kujitahidi kuuzima utajo wake (jina lake). Kwa hivyo Mwenyezi Mungu akamwondolea uzito wake ambao ameuchukua kwa kuwafanya watu kumwitikia mwito wake na akautukuza utajo wake ambao walikuwa wanataka kuuzima.

Hayo yanayotokana na desturi yake Mwenyezi Mungu katika ulimwengu kuleta wepesi baada ya uzito, kwa hiyo huenda kumwondolea shida kulikotajwa ni katika desturi yake. Basi kwa hali hii herufi lam katika neno Usri ni ya Jinsiya yaani jinsi ya uzito baadhi yake na wala sio kila uzito. Na huenda desturi na desturi ya kubadilisha matukio na hali isibakie milele.

Amesema Zamakh-Shari katika Kash-Shaff: Washirikishaji Mwenyezi Mungu walikuwa wakimkashifu Mtume(s.a.w.w) kwa ufukara na dhiki mpaka akatambua Mtume kuwa wao wanajiepusha na uislamu kwa sababu ya ufakiri wa watu wake. Kwa hiyo Mwenyezi Mungu anamkumbusha yale aliyomneemesha miongoni mwa neema nyingi kisha akasema: "Hakika pamoja na uzito kuna wepesi". Kana kwamba amesema: "Tumekufadhili yale tuliyokufadhili basi usikate tamaa na fadhila za Mwenyezi Mungu, kwani uzito ulio nao uko pamoja na wepesi." Kwa dhahiri herufi lam ni ya Ahdiyya na wala sio Jinsiyya yaani uzito maalum uliokusudiwa na kwamba makusudio ya wepesi ni ghanima nyingi walizoruzukiwa waumini na Mwenyezi Mungu.

Lakini hayo ni yenye kupingika kwani utambuzi wake Mtume (SAWW) ni mkubwa zaidi kuliko kuogopea hali zao. Kuwa wanajiepusha na usilamu kwa sababu ya ufakiri wa watu wake. Isipokuwa wao walikuwa wakiukataa mwito wake kwa kiburi tu! Na Mwenyezi Mungu alikwishamkatisha tamaa Mtume wake kuwa wengi wao hawataamini aliposema: "Hakika imehakikika kauli juu ya wengi katika wao; kwa hivyo hawaatamini " (36: 7-10).

Na aya hizo zilishuka Makka. Na aya nyengine iliyoshuka Madina inayosema: "Hakika wale ambao wamekufuru ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye hawataamini ". (1:6).

Lau inachukuliwa kuwa wepesi baada ya uzito ni nguvu ya kiislamu na kuinuka kwake baada ya kuwa chini pamoja na kuchukulia kuwa Sura imeshuka Makka, basi kusingekuwa na ubaya sana.

Aya Na 6

Ni kutilia mkazo na kusisitiza. Imesemekana kuwa ni kuanza upya na wametaja kwamba katika aya mbili hizo (5 na 6) kuna ufahamisho kuwa pamoja na hali nzito moja pana nyepesi mbili. Kwa kawaida jina lenye herufi lam likirudishwa mara ya pili katika maneno, linakuwa kama lile la kwanza kinyume cha jina lisilokuwa na lam. Lakini kawaida hii sio ya lazima, huwa ikabadilika.

Aya Na 7-8

Inatokana na yote yaliyobainishwa mwanzo, miongoni mwa kuchukua ujumbe na kumneemesha kwake Mwenyezi Mungu kwa kuukunjuwa moyo na kuondoa uzito na kuunyanyua utajo na yote hayo ni wepesi baada ya uzito. Kwa hiyo maana inakuwa, ikiwa uzito unafuatiwa na wepesi na mambo yote yanatokana na Mwenyezi Mungu tu! Basi ukimaliza yale uliyofaradhiwa, itaabishe nafsi yako kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kwa ibada zake na dua zake na umtake kukuneemesha raha baada ya taabu hii na wepese baada ya uzito huu.

Imesemwa makusudio yake ni ukiishamaliza faradhi, jitaabishe katika suna na pia imesemwa ukishaswali jitaabishe na dua. Na madhumuni ya kauli mbili hizi ni baadhi ya yanayokubalika. Imesemwa maana yake ni ukishamaliza vita, jitahidi katika ibada. Na pia imesemwa makusudio yake, ukisha maliza yale ya duniani jitaabishe katika akhera yako. Na yemesemwa zaidi na hayo, lakini zote hizo ni njia dhaifu.

Utafiti Wa Hadith Katika Durril Manthur ametoa Abdalla bin Ahmad katika Rawaid ez-zuhd kutoka kwa Ubayya bin Kaab kuwa Abu Hurayra alisema kumuuliza Mtume(s.a.w.w) : "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu ni jambo gani uliloona kwanza kuhusu utume?" Mtume(s.a.w.w) akakaa vizuri akasema: "Umeuliza swali ewe Abu Huraira. Mimi nilipokuwa na umri wa miaka ishirini na miezi kadhaa siku moja nilisikia maneno juu ya kichwa changu mara tu mmoja akawa anamwambia mwenzake ndiye huyu? Wakanikabili na sura ambazo sijaziona kwa kiumbe yoyote na roho ambao sijazipata kwa mtu yoyote na nguo sijaziona kwa mtu yoyote kabisa. Wakaja kila mmoja akanishika mkono.

Mmoja wao akamwambia mwenzake mlaze, akanilaza bila kuchelewa, mmoja akasema mpasue kifua chake, akashika kifua changu na kukipasua katika hali ambayo sikuona damu wala maumivu. Akamwambia mwenzake na mfundo wa hasadi, akatoa kitu mfano wa pande la damu kisha akikitupilia mbali akamwambia tia upole na huruma. Mara akatia kitu mfano wa kile kilichotolewa, lakini kikiwa mfano wa fedha, kisha akatingisha kidole gumba cha mguu wangu wa kulia na akasema: "Ondoka uko salama". Basi nikarudi nikawa nina mfanyia upole mdogo na kumuhurumia mkubwa."

Baadhi yao kama katika Rauhilmaani wamesema kwamba alikuwa na umri wa miaka kumi. Na katika baadhi ya riwaya kimenukuliwa kisa wakati wa kushuka Sura ya Alaq (96).

Na wengine kama katika Sahih ya Bukhari, Muslim, Tirmidhi na Nasai, kimenukuliwa kisa wakati wa Israi wa Mtume. Kisa hiki kwa hali yoyote ni cha kufananisha tu! Sio tukio la kweli na wamefanya upekuzi mrefu kwa madhumuni ya kuonyesha kuwa tukio la kweli wakautia nguvu hup upekuzi wao kwa njia ambazo hazina faida kujishughulisha nazo.

Katika hiyo Durril Manthur ametoa Abu Yaala, Jariyr, Ibn Mundhir, Ibn Hatim, Ibn Habban, Ibn Murdawayh na Abu Naim katika Dalail wamepokea kutoka kwa Abu Said El-Khudri naye kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) amesema: "Alinijia Jibril akasema: Hakika Mola wako akasema: "Je, unajua vipi alivyotukuza utajo wako?" Nikasema, "Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi ". Akasema: "Nikitajwa, unatajwa pamoja nami." Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Abdurrazzaq, Ibn Jariyr, Hakim na Bayhaqi, kutoka kwa Hassan amesema: Siku moja alitoka Mtume(s.a.w.w) akiwa na furaha na kucheka huku akisema: "Nzito moja haiwezi kushinda nyepesi mbili".

"Hakika pamoja na uzito kuna wepesi, hakika pamoja na uzito kuna wepesi." Katika Majmau kuhusu Aya Na 7 na 8 maana yake ukimaliza kuswali swala ya faradhi jitaabishe kwa Mola wako kwa dua na umtake haja. Na hayo pia yamepokewa kutoka kwa Abu Jaffar na Abu Abdiallah(a.s) .

20

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA TIN (TIN) (NA. 95)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

وَالتِّينِ وَالزَّيْتُونِ ﴿١﴾

1. Naapa kwa tini na zaituni.

وَطُورِ سِينِينَ ﴿٢﴾

2. Na kwa Mlima Sinai.

وَهَـٰذَا الْبَلَدِ الْأَمِينِ ﴿٣﴾

3. Na kwa mji huu wenye amani.

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ ﴿٤﴾

4. Hakika tumemuumba mwanadamu katika hali nzuri mno.

ثُمَّ رَدَدْنَاهُ أَسْفَلَ سَافِلِينَ ﴿٥﴾

5. Kisha tukamrudisha chini ya walio chini.

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ ﴿٦﴾

6. Ila wale walioamini wakatenda mema; wao wana malipo mema yasiyokoma.

فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِالدِّينِ ﴿٧﴾

7. Basi ni lipi baada ya hayo, linalokufanya ukadhibishe malipo?

أَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَحْكَمِ الْحَاكِمِينَ ﴿٨﴾

2. Je, Allah si bora ya mahakimu?

UBAINIFU

Sura hii inataja kufufuliwa na malipo, na inaeleza hayo kwa kufuata njia ya kueleza kuumbwa mtu katika hali nzuri, kisha kukhitalifiana watu; Wengine wakatoka na kuanguka chini ya waliochini. Pia inaeleza wajibu wa kihekima wa kupambanua kati ya hayo makundi mawili katika malipo. Sura hii imeshuka Makka, lakini inawezekana kuwa imeshuka Madina. Hata hivyo aya inayosema: "Na kwa mji huu wenye kuaminika," inatilia nguvu kuwa Sura hii imeshuka Makka.

Aya Na 1-3

Inasemekana makusudio ya Tini na Zaituni ni matunda maarufu na Mwenyezi Mungu ameapa kwa matunda hayo kwa sababu ya faida zake nyingi na majani yake yenye manufaa. Pia imesemwa makusudio yake ni mti wa Tini na wa Zaituni. Imesemwa makusudio ya Tini ni jabali iliyoko Damascus na Zaituni ni jabali liliyoko Al-Baytul Muqaddas (Palestina), na kwamba huenda makusudio ya hayo matunda mawili yaliyopo juu ya hayo majabali ni kwa vile hayo matunda yanaota katika majabali hayo na kwamba Mwenyezi Mungu ameapa kwa sehemu hizo kwa vile Mitume wengu wamepewa utume sehemu hizo. Na yamesemwa zaidi ya yaho.

Makusudio ya Turisinin ni jabali ambalo Mwenyezi Mungu Mtukufu alizungumza na Musa bin Imran(a.s) . Vile vile linaitwa Mlima Sinai. Makusudio ya mji huu wenye kuaminika, ni Makka kwa sababu Haram imepewa amani mahsus, ni kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Je, hawaoni ya kwamba tumeifanya ni nchi takatifu (Haram) na ya amani ." (29:67).

Na katika dua ya Ibrahim(a.s) , aliyoizungumzia Mwenyezi Mungu katika Qur'an tukufu: "Ewe Mola wangu, ufanye mji huu wa Makka uwe wa salama ". (2:126).

Kutumia tamko 'mji huu' ni kuthibitisha utukufu wake kwa kuuhusisha huo mji tu. Na kuusifu kwa neno amani inaweza kuwa ni kwa maana ya mji wenye amani au ni kwa maana ya mji wenye kuaminiwa, haohofiwi na shari.

Aya Na 4

Ni jawabu la kiapo. Makusudio ya kuwa mwanadamu ameumbwa katika hali nzuri, ni kuwa hali nzuri na bora katika mambo yake yote. Maana kwa ujumla ni kuwa mtu ameumbwa katika hali nzuri ya maumbile. Maana ya hali nzuri ya kimaumbile kutokana na ufahamisho wa aya inayofuatia (kisha tukamrudisha chini ya waliochini) ni kutengemaa kimaumbile kwa kupanda daraja ya juu na kufuzu kwa maisha ya milele mbele ya Mola wake, yaliyo mema na yasiyokuwa na uovu wowote. Hayo yametokana na vile alivyoandaliwa na Mwenyezi Mungu, pamoja na elimu yenye manufaa na kummakinisha kutokana na elimu hiyo katika amali njema; Mwenyezi Mungu anasema: "Na kwa nafsi na aliyeilingamanisha, akaifahamisha maasia yake na twaa yake ." (92:7-8).

Kwa hiyo akiamini lile alilolijua akaingilia kufanya amali njema Mwenyezi Mungu humnyanyua, kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

"Kwake hupanda maneno mazuri na amali njema huyapandisha (hayo maneno mazuri) " (35:10). "na lakini inamfikia twaa yenu " (22:37).

"Allah atawainua wale walioamini miongoni mwenu; na waliopewa elimu katika daraja ." (58:11).

Kuna aya nyengine zisizokuwa hizo zinazofahamisha kuwa kuinuka kwa mtu kufikia daraja ya juu ya kufikilia kwake imani na matendo mema ni zawadi isiyokatika. Na Mwenyezi Mungu ameiita 'malipo' kama alivyosema katika Sura hii. "Wana malipo mema yasiyokatika."

Aya Na 5

Makusudio ya chini ya waliochini ni mahali palipo chini kabisa pa watu waovu na wa hasara; yaani "kisha tukamrudisha chini ya walio chini" katika watu wa adhabu. Inawezekana kuwa maana ya kurudisha ni kufanya yaani kisha tukamfanya chini ya waliochini, au inaweza kuwa kwa maana ya kubadilisha yaani kisha tukambadilisha. Makusudio ya chini kwa hali yote ni ouvu na adhabu.

Imesemwa makusudio ya hali nzuri ni ujana, nguvu ukamilifu wa Sura na uzuri wa umbo. Na kwamba kurudishwa chini wa waliochini ni kurudishwa kwenye uzee kwa kudhoofika nguvu za binadamu za dhahiri za batini na kurudishwa nyuma umbo lake; kwa hiyo aya inakuwa sawa katika maana na aya inayosema: "Na tunaempa umri tunamrejeza nyuma katika umbo ". (36:68).

Lakini hayo hayakubaliani na aya inayofuatia "Ila wale waliomaini na wakatenda amali njema." Kwa sababu kusema kuwa waumini hawawi wazee ni upuuzi tu. Vile vile kusema kuwa makusudio ya mtu ni kafiri na kwamba kurudishwa ni kwa maana ya kurudishwa katika Jahannam au kubadilishwa umbo hakukubaliana na aya inayofuatia.

Aya Na 6

Hapo inavuliwa jinsi ya mtu. Neno "malipo yasiyokatika" linatilia nguvu kuwa makusudio ya chini ya waliochini ni kumrudisha kwenye uovu na adhabu.

Aya Na 7

Hapa anaulizwa mtu kwa kuzingatia jinsi ya mtu yeyote. Imesemwa ni Mtume(s.a.w.w) . Neno dini hapa limekuja kwa maana ya malipo. Na maana yake - kutokana na yale yaliyosemwa - ni, nilipi lilokufanya ukadhibishe malipo ya siku ya Kiyama baada ya kuwa tumewafanya watu makundi mawili: kundi lenya kurudishwa chini yawaliochini na kundi lenye kulipwa malipo yasiyokatika?

Aya Na 8

Kuhusu "Je Allah si hakimu bora wa mahakimu (wote)?" ni swali la kutaka kuthibitisha. Kuwa Mwenyezi Mungu ni hakimu bora na kwamba Yeye yuko juu ya mahakimu wote katika kuzingatia hukumu na haki yake na kuipitisha bila kutokea mgongano wowote au makosa yoyote. Kwa hiyo Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) anahukumu katika viumbe vyake kwani hekima inawajibisha kuhukumu kwa uzuri na kutekeleza hiyo hukumu. Ikiwa Mwenyezi Mungu ni hakimu bora wa mahakimu wote na watu wakiwa ni makundi mawili tofauti kwa kiitikadi na kimatendo, basi ni katika wajibu kihekima kupambanua kati ya hayo makundi mawili kwa malipo katika maisha yao yatakayobakia, ambayo ni ufufuo.

Kwa hivyo ikiwa watu wote wameumbwa katika hali nzuri (iliyo sawasawa); halafu wakatofautina, likapatikana kundi lililojitoa katika hali yake ya usawa ya umbile lake la kwanza, na kama Mwenyezi Mungu mwenye kuzingatia mambo yao ni hakimu bora wa mahakimu wote, na vile vile ikiwa ni lazima makundi hayo yatofautiane kimalipo, basi iko siku ambayo litalipwa kila kundi kutokana na yale liliyoyafanya, na hili ni jambo lisilokatalika. Aya hizi - kama unavyoziona - ziko katika maana ya aya zinazosema: "Je tuwajaalie wale walioamini na kutenda mema kuwa sawa na wale wafanyao uharibifu katika ardhi? Au tuwajaalie kuwa sawa na waovu? " (38:28).

"Je, wanafikiri wale ambao wamefanya maovu kuwa tutawafanya kama wale walioamini ." (45:21).

Baadhi ya wale wanaosema kuwa Mtume ndiye anaembiwa katika Aya Na "7" wameifanya Maa kuwa na maana na Man (nani), na neno Ahkam kwa maana ya kadhi (mwamuzi). Kwa hiyo maana kwa ujumla itakuwa: Ikiwa watu wanatofautiana, na hilo likalazimisha kutofautiana malipo yao katika siku ya malipo, basi ni nani anayekunasibishia uongo kwa malipo? Je, hakuwa Mwenyezi Mungu ni kadhi bora wa makadhi wote. Basi Yeye ataamua kati yako na ya wale wanaokadhibishia malipo." Lakini kama unavyoona, tafsiri hii ina taklifa isiyokuwa na lazima yeyote.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Aya Na 1-3: Tini ni Madina, Zaituni ni Baytul Muqadas, Turisinin ni Kuffa na mji wenye kuaminika ni Makka. Imepokewa hadith katika maana hayo hayo katika baadhi ya riwaya za Musa bin Jaffar kutokana na mababu zake(a.s) nao kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) . Na katika baadhi ya riwaya nyengine ni kwamba Tini na Zaituni ni Hassan na Hussein Tur ni Ali na mji wenye kuaminika ni Mtume(s.a.w.w) , lakini hayo hayamo katika tafsiri. Katika Durril-Manthur ametoa Ibn Murdawayh kutoka kwa Khuzayma bin Thabit (siye Ansari) alimuuliza Mtume(s.a.w.w) kuhusu mji wenye kuaminika akasema ni Makka.

21

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA ALAQ (PANDE LA DAMU) (NA. 96)

INA AYA 19

Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ ﴿١﴾

1. Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba

خَلَقَ الْإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴿٢﴾

2. Ameuumba mwanadamu katika pande la damu!

قْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ ﴿٣﴾

3. Soma na Mola wako ni Mkarimu mno.

الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ ﴿٤﴾

4. Ambaye amefunza (kuandika) kwa kalamu.

عَلَّمَ الْإِنسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ ﴿٥﴾

5. Amefunza mwanadamu asilolijua.

كَلَّا إِنَّ الْإِنسَانَ لَيَطْغَىٰ ﴿٦﴾

6. Si hivyo! Hakika mwanadamu hupetuka mipaka.

أَن رَّآهُ اسْتَغْنَىٰ ﴿٧﴾

7. Kwa kujiona amejitosha

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ الرُّجْعَىٰ ﴿٨﴾

8. Hakika marejeo ni kwa Mola wako.

أَرَأَيْتَ الَّذِي يَنْهَىٰ ﴿٩﴾

9. Je, umemwona ambaye humkataza.

عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰ ﴿١٠﴾

10. Mmja, ( wa Mungu) anaposwali?

أَرَأَيْتَ إِن كَانَ عَلَى الْهُدَىٰ ﴿١١﴾

11. Je, inaonaje! Ikiwa yuko katika uongofu.

أَوْ أَمَرَ بِالتَّقْوَىٰ ﴿١٢﴾

12. Au akawa anaamrisha wema?

أَرَأَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١٣﴾

13. Je, unaonaje! Akikadhi bisha na akaipa mgongo.

أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ اللَّـهَ يَرَىٰ ﴿١٤﴾

14. Je, hajui kwamba Allah anaona?

كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًا بِالنَّاصِيَةِ ﴿١٥﴾

15. Naakome! Naapa asipokoma, tutamkokota kwa nywele za utosi.

نَاصِيَةٍ كَاذِبَةٍ خَاطِئَةٍ ﴿١٦﴾

16. Utosi wenye kusema uongo, wenye kufanya makosa.

فَلْيَدْعُ نَادِيَهُ ﴿١٧﴾

17. Haya na awaite wanachama wenzake.

سَنَدْعُ الزَّبَانِيَةَ ﴿١٨﴾

18. Na sisi tutawaita Malaika wa adhabu.

كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَاسْجُدْ وَاقْتَرِب ﴿١٩﴾

19. Naakome! Usimtii (bali) sujudu (swali) na ujikurubishe ( kwa Mola wako).

UBAINIFU

Amri kwa Mtume kupokea Qur'an kwa Wahyi utokao kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) Hii ni ndio Sura ya kwanza kushuka katika Qur'an na mpangilio wake wa maneno haukatai kwa imeshuka kwa mpigo (mkupuo mmoja) kama tutakavyoeleza - Nayo imeshuka Makka , bila ya shaka yoyote.

Aya Na 1

Amesema Raghib kusoma ni kukusanya herufi na matamko, lakini sio mkusanyiko wowote ni kusoma. Haiwezekani kusema umewasomesha watu kwa kuwa umewakusanya. Kwa vyovyote iwavyo husemwa umesoma kitabu kama ukizikusanya herufi na matamko na kuyachunguza katika bongo hata kama hukuyatamka. Na husemwa umesomea mtu kama ukimkusanyia herufi na matamko katika usikizi wake; vile vile hutumiwa neno Tilawa kwa maana ya kisomo kama alivyolitumia Mwenyezi Mungu neno hilo katika Sura ya (98:2): Naye (ni) Mtume aliyetoka kwa Allah anayewasomea madaftari yenye kutakasika.

Kwa dhahiri maana ya neno Soma ni amri ya kupokea yale anayopewa wahyi na Malaika. Kwa ujuma ni amri ya kusoma kitabu ambayo inatokana na kitabu hichi hicho; kama alivyosema msemaji mmoja katika mwanzo wa kitabu chake kwa yule aliyempeleka "Soma kitabu changu hiki na ukifanyie kazi" kwa hivyo hiyo amri ya kusoma kitabu, imetokana na kitabu chenyewe. Mpangilio huu wa maneno:

Kwanza : unatilia nguvu yale yaliyopokewa kwamba Sura hii ni ya kwanza kayika Qur'an kwa Mtume(s.a.w.w) .

Pili : Kwamba makusudio yake ni kusoma Qur'an au yaliyo katika maana yake, na sio makusudio ya kusoma chochote au kuwasomea watu ijapokuwa hilo ni miongoni mwa lengo la kushuka kwake, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na Quran tumeigawanya sehemu mbali mbali. Ili uwasomee watu kwa kituo ".(17:106)

Na pia sio makusudio yakuwa lisome jina la Mola wako. Makusudio hasa ni kwamba jumla ya "kwa jina la Moa wako" inafungamana na kitu kilichoondolewa; kukadiriwa kwake ni hali ya kuanza na hali ya kufungua. Hilo halipingi Bismillahi inayoanza katika Sura hiyo, kuwa ni fungu katika Sura, kwani hayo ni katika maneno ya Mwenyezi Mungu aliyoanzia na kuamrisha kuanzia nayo. Kuhusu "Mola wako ambaye ameumba; inaonyesha milki ya Mwenyezi Mungu kwa viumbe vyote, kwani wanaoamshirikisha Mungu walikuwa wakisema Mwenyezi Mungu kazi yake ni kuumba na kupatisha vitu tu! Lakini hana ufalme wowote juu yake. Mwenyezi Mungu analipinga hilo kwa kusema 'Mola wako ambaye ameumba' kwa kutumia neno Rabb ambalo limaana ya kumiliki na kukiangalia vizuri kile kinachimilikiwa kwa hiyo kuumba na kumiliki ni kwake Yeye peke yake.

Aya Na 2

Neno Alaq lina maana ya damu iliyoganda na makusudio yake ni ile inayogeuka kutoka tone la manii katika mfuko wa uzazi. Hiyo inaonyesha vile Mwenyezi Mungu anavyoangalia vizuri na kupanga mambo ya mtu, tangu anapokuwa pande la damu mpaka anapokuwa mtu kamili kwa namna ya kiajabuajabu kiasi ambacho akili zinakwama kujua hilo. Hivyo mtu hatimii wala hakamiliki ila kwa mipangilio inayotokana na Mungu ambayo ni kutoka umbo moja baada ya jingine. Kwa hiyo mtu hana budi kumfanya Mungu pekee ndiye mlezi. Na maneno haya ni hoja ya kuwa Mmoja Mlezi (Mungu).

Aya Na 3

Amri ya kusoma hapa ni ya kusisitiza ile amri ya kwanza. Imesemwa makusudio yake hapo ni kuamrisha kisomo kwa watu yaani kuwafikishia (Tabligh) kama ilivyosemwa kwamba amri ya kwanza ya kusoma na hii ya pili zote ni kwa ajili ya kuwasomea watu. Lakini njia zote mbili hizi haziko wazi

Aya Na 4-5

Herufi Ba ni yakusababisha, kwa maana ya amemfundisha mtu kusoma au kuandika kupitia kalamu. Maneno haya ni kwa ajili ya kuitia nguvu nafsi ya Mtume(s.a.w.w) na kumwondoa kiherehere; kwa kuamrisha kusoma na hali ya kuwa yeye ni ummiy haandiki wala hasomi. Kama vile ameambiwa; soma kitabu cha Mola wako anachokufunulia wala usipogope na hali ya kuwa Mola wako ni Mtukufu ambaye amefundisha mtu kusoma kupitia kalamu, kwa hiyo yeye anaweza kukufundisha kusoma maandishi yake na hali ya kuwa wewe ni ummiy (usiyejua kusoma wala kuandika).

Kisha akaeneza Mwenyezi Mungu (s.w.t) neema, akataja kumfundisha kwke mtu asilolijua akasema: Amemefundisha mtu asilolijua. Hilo ni kuzidisha kuutia nguvu moyo wa Mtume(s.a.w.w) .

Makusudio ya mtu kwa dhahiri ni jinsi ya mtu yoyote. Imesemwa makusudio yake ni Mtume(s.a.w.w) . Na imesemwa ni Mtume Idris(a.s) kwa sababu yeye ndiye mtu wa kwanza kuandika kwa kalamu; Pia imesemwa ni kila Mtume aliyekuwa akiandika. Lakini njia zote ni dhaifu zilizo mbali na ufahamu.

Aya Na 6-7

Makatazo ya kukufuru neema, baada ya Mwenyezi Mungu kumneemesha mtu kwa neema kubwakubwa; mfano kumfundisha kwa kalamu na mengineyo. Ni juu ya mtu kumshukuru juu ya hilo, lakini mtu hukufuru neema zake Mwenyezi Mungu Mtukufu na kupetuka mpaka. Na hiyo ni kutokana na kwamba yeye anajishughulisha na sababu za kidhahir ambazo zinamfikisha kwenye makusudio yake. Kwa hiyo anaghafilika na Mola wake na kuona kuwa hana haja na kumkumbuka na kumshukuru juu ya neema yake, ndipo anamsahau na kupetuka mpaka.

Aya Na 8

Kwa dhahiri maana ya neno marejeo hapa ni kiaga cha mauti na kufufuliwa. Hapa anaambiwa Mtume(s.a.w.w) na imesemwa anaambiwa mtu. Kauli ya kwanza ndiyo iliyodhahiri zaidi.

Aya Na 9-13

Yanatajwa baadhi ya mambo ya mtu mwenye kupetuka mpaka. Makusudio ya mja anayeswali hapa ni Mtume(s.a.w.w) kutokana na unavyofahamisha mwisho wa aya za mwisho wakati Mwenyezi Mungu anapomwamrisha Mtume(s.a.w.w) kusujudu na kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu na kumkataza kumtii huyo anayekataza. Mpangilio wa aya hizi kwa kukadiri kuwa Sura ni ya kwanza kushuka na kushuka kwake mara moja, basi unafahamisha kuwa Mtume alikuwa akiswali kabla ya kushuka Qur'an na pia unafahamisha utume wake kabla ya risala yake ya Qu'an. Ama yale waliyoyataja baadhi yao kwamba swala haikufaradhiwa mwanzo wa utume isipokuwa ilifaradhiwa usiku wa Miraj kwa kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Simamisha swala jua linapopinduka mpaka giza la usiku na Qur'an ya Alfajiri "(17:78).

Hiyo inafahamisha kuwa swala tano za kila siku zilifaradhiwa kwa namna yake hasa rakaa mbili mbili, katika usiku wa Miraji, lakini hakuna linalofahamisha kuwa haikuweko kabla yake. Na zimeshuka Sura nyingi kuwa haikuweko kabla yake. Na zimeshuka Sura nyingi kabla ya sura ya 17 (Israi) zinazotaja swala kama Al- Muddathtir, Al-Muzammil nk. kwa ibara tofauti ijapokuwa namna ya swala yenyewe haikudhihirishwa, isipokua ilikuwa ni namna ya kusoma Qur'an na kusujudu, vile vile zimepokewa baadhi ya riwaya za swala ya Mtume(s.a.w.w) pamoja na Khadija bin Ali katika mwanzo wa utume, ingawaje haikutajwa namna ya swala yenyewe. Kwa ujumla maana ya aya ni kumfahamisha yule ambaye anamkataza mja anaposwali na huyo anayekataza anajua kuwa Mwenyezi Mungu anamwona yale anayoyafanya. Nifahamishe huyo anaemkataza mja anayeswali aliye juu ya uongofu au anayeamrisha kumcha Mwenyezi Mungu anamwona?, Je, hastahiki adhabu?

Aya Na 14

Kuhusu "Hivi hajui kuwa Mwenyezi Mungu anamwona ". Makusudio ya kujua hapa yamekuja kwa njia ya kulazimsha kujua. Kwa sababu kuitakidi kuwa Mwenyezi Mungu ni Muumba wa kila kitu kunalizimisha kuitakidi kuwa Yeye (Mwenyezi Mungu) ana ujuzi wa kila kitu. Na huyo mkatazaji alikuwa ni mshirikishaji Mungu anayeabudu masananmu, na wanaobudu masanamu wanakubali kuwa Mwenyezi Mungu ndiye muumba wa kila kitu na wanamtakasa na sifa za upuungufu, kwa hiyo wanaona kuwa Mwenyezi Mungu hapitwi na kitu wala kushindwa na kitu chochote.

Aya Na 15 - 16

Kuusifu utosi wenye kusema uongo ni kwa njia ya fumbo kwa maana ya uongo wa mwenye utosi huo. Maana ya aya kwa jumla ni makemeo na utisho; nikuwa mambo hayako kama anavyotaka yeye. Ninaapa kama hatajizuia na makatazo yake, tutamchukua kidhalili na kumkokota mwenye adhabu ya utosi ambao mwenye utosi huo ni mwongo kwa anayosema na mkosaji kwa anayofanya. Imesemwa maana yake ni tutautia kovu utosi wake kwa moto na kuufanya mweusi.

Aya Na 17-18

Anaeleza Mwenyezi Mungu udhaifu ya huyo mwenye kukataza mja kuswali, kwa kusema: Haya na awaite hao watu wa baraza lake (wanachama wenzake) na sisi tutawaita Malaika wa motoni, wakali wenye nguvu, ambao hawana wa kuwazuyiwa.

Aya Na 19

Ni kusisitiza makemeo. Makusudio ya "Usimtii " ni usimtii anayekukataza swala. Hii inafahamisha kuwa makusudio ya kusujudu ni swala. Huenda swala aliyokuwa akiiswali Mtume(s.a.w.w) wakati huo ni tasbih na kumsujudia Mwenyezi Mungu. Imesemwa makusudio yake ni kusujudu kwa ajili ya kisomo cha Sura hi ambayo ni moja ya Sura nne za Azaim ( zenye sijda za wajib). Na kujikurubisha ni kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Imesemwa ni kujikurubisha kutokana na thawabu za Mwenyezi Mungu.

Utafiti Wa Hadithi Katika Durril-Manthur ametoa Abdurrazzaq, Ahmad, Abdu bin Hamid, Bukhari, Muslim, Ibn Jariyr na Ibn Ambari katika Masahif. Vile vile Ibn Murdawayh na Bayhaqi katika njia ya Ibn Shihab kutoka kwa Urwa bin Zubeir naye kutoka kwa Aisha mama wa waumin amesema "mwanzo wa kudhihirikiwa Mtume(s.a.w.w) na wahyi ni ndoto njema katika usingizi. Na alikuwa haoti ndoto ila itadhihiri mfano wa Falaq (nyota ya asubuhi).

Kisha akawa anapendelea kukaa mbali na alikuwa akipendelea kwenda Jabal Hiraa na kuabudu huko kwa idadi ya nyusiku kadhaa akiwa amechukua chakula, kisha hurudi kwa Bibi Khadija kuchukua chakula. Alikuwa akifanya hivyo mpaka ilipomjia haki naye akiwa huko Jabal Hiraa. Akamjia Malaika akasema: "Soma" akamwambia "Mimi si msomaji". Mtume anasema: Akanishika na kunikamua mpaka nikafikiwa na kughumiwa, kisha akaniacha, akasema "Soma" nikasema "mimi si msomaji" akanishika tena na kunikamua kama kwanza kisha akaniacha akaniambia "Soma" nikamwambia "mimi si msomaji". Akanishika tena mara ya tatu kisha akaniwacha akaniambia: "Soma kwa jina la Mola wako ambaye ameumba (kila kitu). Amemuumba Mtu kutokana na pande la damu. Soma na hali yakuwa Mola wako ni Mkarimu. Ambaye amemfundisha (mtu) kuandika kwa kalamu".

Akarudi Mtume(s.a.w.w) kwa Bibi Khadija akiwa anatetemeka moyo wake, akasema: "Nifunikeni, nifunikeni" wakamfunika mpaka ilipomwondokea fazaa, akamuhadithia Khadija habari hiyo na akamwambia 'ninaogopa juu ya nafsi yangu' Khadija akamwambia 'Hapana Mwenyezi Mungu hakukufedhehesha kabisa. Hakika wewe utaunga udugu, utachukua taabu, utawakaribisha wageni na utasaidia upande wa haki'.

Akaondoka Khadija mpaka kwa binamu yake anayeitwa Waraqah bin Naufal bin Asad bin Abdulaziz naye alikuwa ni mkristo katika zama za ujahili na alikuwa akiandika Kiibrania, akawa anaandika Injili kwa Kiibrania; wakati huo alikuwa mzee sana na kipofu. Khadija akamwambia "Ewe binamu nisikilize". Akamwambia "umeona nini?". Akamfahamisha yale aliyoyaona Mtume(s.a.w.w) . Akamwambia "huyo ni msiri ambaye alimshukia Musa! Natamani ningelikuwa kijana, natamani niwe hai wakati watakapokutoa watu wako!" Akasema Mtume(s.a.w.w) "hivi watanitoa?" Akasema, "ndio hakuna mtu yeyote aliyekuja na mfano wa uliyokuja nayo wewe ila hupingwa na nikiwahi siku yako hiyo nitakusaidia." Lakini hakuendelea kuishi Waraqah na akafa katika kipindi cha wahyi.

Amesema Ibn Shihab: "Amenifahamisha Abu Salama bin Abdurrahman kwamba Jabir bin Abdillahi El-Ansari amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) - akiwa anazungumzia kipindi cha wahyi akasema katika mazungumzo yake mbiguni, nikanyanyua macho yangu, nikamwoma Malaika yule aliyenijia katika Jabal Hiraa kwenye kiti kati ya mbingu na ardhi, nikamwogopa na kurudi nyumbani, nikasema nifunikeni nguo! Nifunikeni! Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha aya: "Ewe mwenye kujifunika maguo, simama uonye (watu) na Mola wako umtukuze. Na nguo zako uzisafishe na mabAya Na puuze ." (74:1-5).

Katika hiyo hiyo Durril-Manthur ametoa Ibn Abu Shaybah, Ibn Jariyr nna Abu Naim kutoka kwa Abdalla bin Shaddad amesema: "Jibril alimjia Muhammad(s.a.w.w) akasema: "Ewe Muhammad "Soma". Akasema "Nisome nini?" Akamshika kisha akasema ewe Muhammad "Soma". Akasema "nisome nini?" Akasema : "Soma kwa jina la Mola wako ambaye ameumba (kila kitu) mpaka akafikia amemfunza mwanadamu asilolijuwa."

Mtume akaja kwa Khadija akamwambia, "Ewe Khadija naona amenidhuru." Akasema Khadija: "Hapana Mola wako hawezi kukufanya hivyo na wala kukufanyia ubaya wowote". Basi Khadija akamwendea Waraqh bin Naufal, akampa habari hiyo akasema. "Ukiwa unasema kweli, basi mumeo ni Mtume na atapata tabu kutokana na umati wake nakama nikimuwahi nitamwamini."

Kisha akachelewa Jibril kumjia, akasema Khadija naona Mola wako amechukia ndio Mwenyezi Mungu akateremsha: "Naapa kwa mwanzo wa mchana. Na kwa usiku unapotulia hakukuacha Mola wako wala hakukukasirikia ". (93:1-3).

Lakini kisa chote hiki hakiwezi kuepukana na shaka. Miongoni mwa shaka yake ni vile kutia shaka Mtume(s.a.w.w) kuwa yule aliyoyaona ni wahyi wa Mwenyezi Mungu kutoka kwa Malaika wa Mbinguni, bali hata kudhani kuwa ameshikwa na shetani aliyemtia wazimu. Na shaka zaidi ni vile kumtegemea Mkristo Mtawa kuwa ndiye atakayemtuliza nafsi yake kwa kumfahamisha kuwa yeye ni Mtume, na hali Mwenyezi Mungu amesema: "Sema hii ni njia yangu ninailingania kwa Allah kwa ujuzi wa kweli, mimi na wanaonifuata. (12:108). "Sasa je, ujuzi wa kweli ndio huko kutulizwa moyo na neno la Waraqah? Na amesema Mwenyezi Mungu:

"Sema mimi ninayodalili wazi itokayo kwa Mola wangu ". (6:57)

Sasa dalili gani iliyo wazi katika neno la Waraqah? Na amesema tena Mwenyezi Mungu: "Hakika sisi tumekuletea wahyi kama tulivyowapelekea Nuh na Manabii (wengine) baada yake ." (4:163). Je hao Mitume wengine walikuwa wakitegemea kupata utume wao mfano wa kisa hiki?

Ilivyo ni kwamba wahyi wa utume unalazimisha kuwepo yakini kutoka kwa Mtume mwenyewe kuwa umetokana na Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hayo ndio yaliyopokewa kutokana na Maimamu wa Ahlul Bait. Katika Majmau kuhusu Aya Na tisa; ni kuwa Abu Jahl alisema; "Je Muhammad anaweka uso wake mchangani (anaswali) mbele yenu?" Wakasema "ndio". Akasema "Ninaapa kwa yule anayeapiwa, nikimwona nitaikanyaga shingo yake". Akaambiwa "huyo anaswali". Akawa anakwenda kumkanyaga mara akawa anarudi nyuma huku akijikinga kwa mikono yake wakasema: "Unanini ewe Abul Hakam?" Akasema: "Hakika kati yangu na yake kuna handaki la moto na hawa wenye mbawa". Akasema Mtume: "Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko katika uweza wake, lau angelinikurubia tu! Wangelimchanachana Malaika. Ndipo akateremsha Mwenyezi Mungu Aya Na tisa mpaka mwisho wa Sura. Hayo ameyapokea Muslim katika Sahih.

Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu aya hiyo hiyo nikuwa ilishuka juu ya Walid bin El-Mughira aliyekuwa akiwakataza watu kuswali na kutiiwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Ufahamisho wa hayo haupingi kuwa mwenye kuswali ni Mtume(s.a.w.w) .

Katika Majmau kwenye hadith ya Abdallah bin Masud kwamba Mtume(s.a.w.w) amesema: "Mja anakuwa karibu zaidi na Mwenyezi Mungu anapokuwa amesujudu". Katika Kafi kwa isnadi wa Wash-shai amesema: "Nimemsikia Arridhaa(a.s) akisema: "Karibu zaidi anapokuwa mja na Mwenyezi Mungu ni anaposujudu, ndio maana akasema Mwenyezi Mungu "Sujudu na ujikurubishe (kwa Mola wako)".

Katika Majmau amepokea Abdulla bin Sinan kutoka kwa Abu Abdillahi amesema: Al - Azaim (Sura Sajda za wajibu) ni nne (Sura ya 32, 41, 52 na 96), zisizokua hizo katika Qur'an ni sunna tu, kusujudu!.