TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN0%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi: Muhammad Hussein Tabaatabaai
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 39394
Pakua: 2908

Maelezo zaidi:

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39394 / Pakua: 2908
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

22

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA QADR (QADR) (NA. 97)

INA AYA 5

Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾

1. Hakika sisi tumeiteremsha Qur'an katika Laylatul Qadri.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ ﴿٢﴾

2. Na ni lipi la kukujulisha wewe ni nini Laylatul Qadri?

لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ ﴿٣﴾

3. Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ ﴿٤﴾

4. HushukaMalaika na Roho katika (usiku) huo kwa amri ya Mola wao kwa ajili ya kila jambo.

سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ ﴿٥﴾

5. (Ni) amani mpaka alfajiri.

Ubainifu Sura hii inaelezea kushuka Qur'an katika usiku wa "Laylatul -qadr" na kuutukuza usiku huo kwa kuufanya bora kuliko miezi elfu. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina, lakini yale yaliyopokewa kwa Maimamu katika Ahlul Bait wa Mtume(s.a.w.w) kuhusu sababu za kushuka kwake, yanatilia nguvu kuwa Sura hii imeshuka Madina.

Aya Na 1

Dhamira katika neno "tumeiteremsha" ni ya Qur'an. Kwa dhahiri inaonyesha kushuka Qur'an yote na wala sio baadhi ya aya zake. Hilo linatiliwa nguvu na ibara ya neno "Anzalnahu" ambalo kwa dhahir lina maana ya kushuka kwa mkupuo mmoja; kinyume cha neno "Tanziyl" ambalo kwa dhahiri lina maana ya kushuku kwa awamu nyingi. Katika maana ya aya hiyo Mwenyezi Mungu anasema: "Naapa kwa kitabu kinachobainisha. Hakika sisi tumeiteremsha (Qur'an) katika usiku uliobarikiwa ". (44:2-3).

Kwa dhahiri hapo Mwenyezi Mungu anaapa kwa jumla ya kitabu chote kisha anatolea habari ya kila kilichoapiwa. Kwa hiyo ufahamisho wa aya ni kuwa Qur'an imeshuka jumla kwa Mtume.

Hakuna katika manen ya Mwenyezi Mungu yanayobainisha kuwa usiku huo ni usiku wowote na kwamba sio usiku ulio katika neno lake Mwenyezi Mungu: "Ni Mwezi wa Ramadhan ambao imeteremshwa ndani yake Qur'an " (2:185) kwa sababu aya hii ikichanganywa na Aya Na Sura ya Al-Qadr (tunayoizungumza) inafahamisha kuwa usiku huo ni katika nyusiku za Ramadhan. Mwenyezi Mungu ameuita usiku huo Laylatul Qadri. Kwa dhahiri inaonyesha kwamba makusudio ya neno Qadri ni kukadiria. Kwa hiyo ni usiku wa kukadiria ambao anakadiria Mwenyezi Mungu matukio ya mwaka mzima kama vile uhai, mauti na riziki. Vile vile wema, uovu nk, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Katika usiku huo hubainishwa kila jambo la hekima. Ndio hukumu inayotoka kwetu; kwa hakika sisi ni waletao mitume. Ni rehema itokayo kwa Mola wako " (44:4-6).

Kwa hivyo hakukuwa kubainisha jambo la hekima ila ni hekima za matukio yenye kutuka katika sehemu zake zinazohusika kwa kukadiria. Hilo linafahamisha kwamba usiku huo unakaririka kwa kukaririka miaka. Kwa hiyo katika mwezi wa Ramadhan wa kila mwaka kuna usiku unaokadiriwa mambo ya mwaka. Kwa sababu hakuna maana ya kuukadiria usiku mmoja (ulioshuka Qur'an) kwamba umekadiriwa ndani yake matukio ya kabla yake na baada yake. Na neno 'hubainisha' ambalo kwa dhahiri linaonyesha kuendelea vile vile neno 'hushuka' Malaika yanatilia nguvu hilo.

Basi hakuna njia inayoonyesha yale yaliyosemwa kuwa usiku huo ni ule usiku mmoja tu ulioteremshwa Qur'an. Au kwamba ulikuwa ukikaririka katika miaka ya zama za Mtume(s.a.w.w) kisha Mwenyezi Mungu akauondoa. Vile vile hakuna njia inayoonyesha kuwa usiku huo upo katika miaka yote, lakini unabadilika kwa kukaririrka miaka; kwamba mwaka mwengine uwe katika mwezi wa Ramadhan, mwengine uwe katika mwezi wa Shaaban, nk. Imesemwa neno Qadr limekuja kwa maana ya hadhi na heshima na kwamba umeitwa usiku wa hadhi kutokana na umuhimu wa hadhi yake, au kwa hadhi ya wale wenye kuabudu katika usiku huo. Imesemwa tena Qadr ni kwa maana ya ufinyu, na kwamba umeitwa usiku finyu kwa sababu ardhi inakuwa finyu kutkana na kushuka Malaika.

Maana ya aya ni kwamba huo ni usiku ulio katika mwezi wa Ramadhan katika kila mwaka ambao ndani yake mnahukumiwa mambo kwa kiasi cha makadiro. Hilo halikanushi kutokea mabadiliko katika muda wa mwaka kwa sababu kuhakikika kile chenye kukadiriwa ni jambo jengine na mbadiliko katika kukadiria ni jambo jengine; kama vile kutokea mabadiliko ya matukio ya kilimwengu kwa kiasi cha matakwa ya Mungu, hakukanushi kuainiwa kwake katika "Lauhil Mahfudh"! Amesema Mwenyezi Mungu: "Na asili ya hukumu zote iko kwake " (13:39).

Uwezekano wa kutokea mambo kwa kuhakikika kwake kuna mipangilio kwa kutimia na kupungua. Inawezekana kutokea baadhi ya mipangilio katika Laylatul-Qadr na kuchelewa kutimia kupitishwa mpaka wakati mwengine, lakini hadithi zitakazokuja haziwafiki hilo.

Aya Na 2

Ni fumbo la utukufu wa cheo cha usiku na daraja yake kubwa. Hilo linatiliwa nguvu na kudhihiri kwa jina la huo usiku mara kwa mara, pale iliposemwa: "Nini Laylatul-Qadr, Laylatul-Qadr ni bora ". Na wala isisemwe nini huo, huo ni bora.

Aya Na 3

Ni ubainifu wa kijumla kwa lile limaloishiriwa na aya tatu katika ukubwa wa jambo la huo usiku. Makusudio ya kuwa ni bora kuliko miezi elfu ni ubora wa ibada kama walivyofasiri wafasiri. Hilo ni lenye kunasibiana na makusudio ya Qur'an na kuwatia hima watu kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kuufanyia ibada ni bora kuliko ibada ya miezi elfu na baraka iliyotajwa katika Sura ya (44:3) inafahamisha hilo. Na kuna maana mengine yatakayokuja katika utafiti wa hadith (Inshallah).

Aya Na 4

Kwa dhahiri roho hapa ni roho iliyotajwa katika Aya Na (85:17) "Sema roho ni jambo linalohusika na Mola wangu ". Herufi Min katika neno Min Kulli imesemwa kuwa imekuja kwa maana ya herufi Ba yaani kwa kila jambo. Na imsemwa ni ya kuanzia makusudio na kufahamisha sababu yaani kwa sababu ya kila jambo la Mungu. Pia imesemwa ina maana ya sababu ya lengo, yaani kwa ajili ya kuzingatia kila jambo katika mambo. Kwa kweli hasa ikiwa makusudio ya neno Amr ikiwa ni amri ya Mungu inayofasiriwa na neno lake Mwenyezi Mungu katika Sura (36:82): "Hakika amri yake anapotaka chochote ni kukiambia kuwa kikawa". Basi Min ni ya kuanza na kufahamisha sababu kwa maana ya "Hushuka Malaika na Roho katika Laylatul-Qadr kwa idhini ya Mola wao hali ya kuanza kushuka kwao kutokana na kila amri ya Mungu ".

Ikiwa Amr ina maana ya kilimwengu, basi itakuwa kwa maana ya Lam ya kwa ajili, yaani kwa idhini ya Mola wao kwa ajili ya kuzingatia kila jambo katika mambo ya kilimwengu.

Aya Na 5

Amesema katika Mufradat neno Salaam lina maana ya kuepukana na maafa ya nje na ndani. Kwa hivyo neno hilo katika aya linaonyesha hifadhi ya Mungu kwa kueneza rehema kwa waja wake wenye kuelekea kwake na kuziba mlango wa mateso. Aya mbili hizi za mwisho ni tafsiri ya Aya Na tatu.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Bur'han kutoka kwa Sheikh Tusi naye kutoka kwa Abu Dharri amesema: Nilimuuliza Mtume(s.a.w.w) : "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu Laylatul-Qadr ni jambo linalokuwa katika zama za Mitume, wakiondoka nalo linaondoka?" Akasema "La! bali Laylatul-Qadr inaendelea mpaka siku ya Kiyama". Na imekuja hadithi hiyo katika maana mbali mbali katika njia ya Ahli Sunnah. Katika Majmau kutoka kwa Hammad bin Uthman, naye kutoka kwa Hassan bin Abu Ali amesema, "nilimuuliza Abu Abdillahi(a.s) kuhusu Laylatul-Qadr akasema: 'Utafute katika usiku wa 19, 21 na 23". Katika baadhi ya habari zilizopokewa ni kuwa kati ya usiku wa 21 na 23 kama inavyoeleza riwAya Na Iyashi kutoka kwa Abdul-Wahid naye kutoka kwa Baqir(a.s) .

Imefahamika kutoka katika riwaya kwamba haukuainiwa (haukutajwa) kwa ajili ya kuutukuza ili usidharauliwe kwa kufanyiwa maasi. Katika hiyo hiyo Majmau katika riwAya Na Abdillahi bin Bakir kutoka kwa Zurara kutokana na mmoja wa Maimamu wawili (Abu Abdillahi na Baqir) amesema: "Hakika usiku wa Laylatul-Qadr ni usiku wa "Jahaniy". Hadith ya Jahaniy ni kwamba yeye alisema kumwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Hakika nyumba yangu nimeijenga nje ya mji niamrishe usiku wa kuingia kwenye nyumba hiyo, akamwamrisha usiku wa 23. Hadith ya Jahaniy imepokewa kwa njia ya Ahli Sunnah vile vile katika Durril Manthur kutoka kwa Malik na Bayhaqi. Katika Kafi kwa isnadi ya Zurarah amesema; "Amesema Abu Abdillahi(a.s) kukadiria ni mwezi 19, kukata hukumu ni mwezi 21, na kutia saini ni mwezi 23." Na kuna riwaya nyengine zenye maana hiyo.

Zimeafikiana habari za Ahlul Bait kwamba usiku huo ni wenye kubakia ukikaririka kila mwaka na kwamba huo ni usiku katika usiku wa mwezi wa Ramadhan na kwamba uko katika moja ya nyusiku tatu. Ama kwa upande wa Ahli sunnah riwaya zimehitalifiana kiajabu kiasi kisicho dhibitika na lililo maarufu ni kwamba huo ni usku wa mwezi 27 ambao imeshuka Qur'an. Katika Durril Manthur ametoa Hatib kutoka kwa Ibn El-Musabbib amesema: "Amesema Mtume(s.a.w.w) niliona katika ndoto Bani Umayya wakipanda mimbari yangu likanitia dhiki hilo, ndio akateremsha Mwenyezi Mungu Sura ya Qadr.

Imepokewa mfano wa hadith hiyo kutoka kwa Hatib katika Tarekh yake naye kutoka kwa Ibn Abbas, vile vile imepokewa katika maana hayo kutoka kwa Tirmidhi, ibn Jariyr, Tabrani Ibn Murdawahyh na Bayhaqi katoka kwa Hassan bin Ali. Na ziko riwaya nyingi katika maana haya kwa upande wa Shia kutoka kwa Maimam wa Ahlul Bait(a.s) . Katika riwaya hizo ni kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu alimfariji Mtume wake(s.a.w.w) kwa kumpa Laylatul Qadr na kuifanya bora kuliko miezi elfu ambao ni muda wa ufalme wa Bani Umayya. Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Ibn Abu Umayya naye kutoka kwa watu zaidi ya mmoja nao kutoka kwa Abu Abdillah(a.s) kwamba walimuuliza baadhi ya sahaba zetu wala simjuwi ila Said Assiman: "Vipi itakua Laylatul Qadr ni bora kuliko miezi elfu?' "Akasema amali katika usiku huo ni bora kuliko amali ya miezi elfu bila Laylatul Qadr".

Katika hiyo hiyo Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Fadhili, Zurara na Muhammad bin Muslim, kutoka kwa Humran kwamba yeye alimuuliza Abu Jaffar(a.s) kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika sisi tumeiteremsha (Qur'an) katika usiku uliobarikiwa". Akasema: "Ndio Laylatul Qadr nao uko katika kila mwaka katika mwezi wa Ramadhan katika kumi la mwisho, haikushuka Qur'an illa katika Laylatul Qadr, amesema Mwenyezi Mungu: "Katika (usiku) huo hubainishwa kila jambo la hekima ." (44:4).

Akaendelea kusema: "Hukadiriwa katika Laylatul Qadr kila kitu kinachokuwa mwaka huo kwa mkabala wake; heri na shari, utii na uasi na kuzaliwa na ajali au riziki. Kinachokadiriwa katika usiku huo na kupitishwa basi kimekwishapitishwa. Na Mwenyezi Mungu ana matakwa yake katika hilo. Akasema tena: "Na amali njema katika usiku huo kama vile swala, zaka na namna ya mambo ya heri, ni bora kuliko amali katika miezi elfu isiyokuwa na Laylatul Qadr."

Kuhusu jumla ya "Mwenyezi Mungu ana matakwa yake katika hilo" anakusudia uhuru wa kudura yake. Anaweza kufanya analotaka hata kama amelipitisha. Kwani kuwajibisha jambo hakuwezi kuufunga uweza, kwa hiyo anaweza kuichangua hukumu aliyoipitisha. Katika Majmau amepokea Ibn Abbas kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba yeye Mtume amesema: "Unapokuwa Laylatul Qadr hushuka Malaika ambao ni wakazi wa Sidratul Muntaha miongoni mwao akiwa ni Jibril. Anashuka pamoja na bendera, bendera moja anaisimamisha kwenye kaburi yangu, nyengine kwnye Baytul-Muqadas, nyengine Masjidul-Haram, na nyengine anaisimamisha Mlima Sinai. Wala hamwachi yeyote mwanamume au mwanamke ila humpa salam isipokuwa, mnywaji tembo, mwenye kula nyama ya nguruwe na mwenye kujipaka zafarani".

Katika Tafsiri ya Bur'han kutoka kwa Said bin Abdillahi naye kutoka kwa Abu Baswiyr amesema. "Nilikuwa pamoja na Abu Abdillahi(a.s) akataja kitu kuhusu kuzaliwa Imam, akasema inawajibisha kuzidi Roho katika Laylatul Qadr , nikamwambia: niwe mkombozi wako kwani Roho si Jibril? Akasema Jibril ni katika Malaika na Roho ni mkubwa kuliko Jibril huoni Mwenyezi Mungu anasema: "Hushuka Malaika na Roho". Riwaya ni nyingi sana zinazoeleza ubora wa Laylatul Qadr na baadhi yake zimetaja alama ambazo tumezifungia jicho; kama kutokeza mwanga wa jua na kulingana sana hewa, nk.

SURA BAYYINA ( HOJA) (NA. 98)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah. Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأْتِيَهُمُ الْبَيِّنَةُ ﴿١﴾

1. Hawakuwa wale ambao wamekufuru katika watu wa kitabu na washirikina, ni wenye kuachana na waliyonayo mpaka iwajie hoja.

رَسُولٌ مِّنَ اللَّـهِ يَتْلُو صُحُفًا مُّطَهَّرَةً ﴿٢﴾

2. (Nayo) ni Mtume atokaye kwa Allah awasomee kurasa zilizotakaswa.

فِيهَا كُتُبٌ قَيِّمَةٌ ﴿٣﴾

3. (Ambazo) ndani yake mna maandishi yaliyosawasawa

وَمَا تَفَرَّقَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَةُ ﴿٤﴾

4. Wala hawakutengana wale waliopewa kitabu ila baada ya kuwajia hiyo hoja.

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ ﴿٥﴾

5. Na hawakuamrishwa ila wamuabudu Allah kwa kumtakasia yeye dini, hali wameshikamana na haki na wasimamishe swala na watoe zaka na hiyo ndiyo dini iliyo sawasawa

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا أُولَـٰئِكَ هُمْ شَرُّ الْبَرِيَّةِ ﴿٦﴾

6. Hakika wale ambao wamekufuru katika watu wa kitabu na wenye kushirikisha (wataingia) katika moto wa Jahannam watakaa humo milele na hao ndio waovu wa viumbe.

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ هُمْ خَيْرُ الْبَرِيَّةِ ﴿٧﴾

7. Hakika wale amabo wameamini wakatenda (amali) njema hao ndio bora wa viumbe.

جَزَاؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِيَ رَبَّهُ ﴿٨﴾

8. Malipo yao kwa Mola wao ni mabustani ya milele yanayopita mito chini yake watakaa humu milele. Allah yuradhi nao na wao waradhi naye. Na hayo ni kwa mwenye kumcha Mola wake.

UBAINIFU

Sura hii inasajili ujumbe wa Muhammad kwa wote wale waliopewa kitabu na washirikina. Kwa maneno mengine, kwa wote wale wenye mila na wasiokuwa na mila. Ujumbe huo ni katika utaratibu wa Mwenyezi Mungu - desturi za uongofu - ambazo zimeelezwa katika Qur'an; kwa mfano kamanalivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Hakika sisi tumemuongoa (tumembainishia) njia, basi ama atakua mwenye kushukuru au mwenye kukufuru ." (76:3).

Na amesema tena Mwenyezi Mungu : "Na hakuna umma wowote ila alipitia humo muonyaji ." (35:24).

Ujumbe wa Muhammad(s.a.w.w) unatoa hoja kuwa ni kwa ajili ya watu wote, kwa vile unakusanya maslahi ya jamii ya binadamu ikiwa ni pamoja na itikadi na matendo; kama utakavyokuja ufafanizi (Inshallah). Sura hii inauwezekano wa kuwa imeshuka Makka au Madina, ingawaje mpangilio wake unaonyesha kuwa imeshuka Madina.

Aya Na 1

Ayah hii ambayo ndiyo kichwa cha maneno ya Sura, inaonyesha kusimama hoja juu ya wale ambao wamekufuru na wale waliopewa kitabu wakati walipoanza kuhitalifiana. Makusudio hasa ni kuwa Mtume(s.a.w.w) ni mmojawapo wa waliyothibitisha hoja ya Mwenyezi Mungu ana wajibu wa kuleta mwokozi kwa watu. Hii ni kutokana na (uadilifu) wa mwenendo wake. Makusudio ya 'waliokufuru' hapa ni waliokanusha mwito wa utume wa kiislamu. Herufi: min ni ya kuelezea baadhi, yaani baadhi ya waliopewa kitabu. Washirikina ni wale wanaoabudu masanamu na wengineo.

Kwa ujumla ni kuwa; wale walioukanusha ujumbe wa Mtume(s.a.w.w) walikuwa ni wenye kuhitajia kusimamishiwa hoja wakati wote, mpaka alipokuja Mtume(s.a.w.w) wajibu huo wa kupatiwa hoja ulikwisha. Wamehitalifiana kiajabu katika tafsiri ya ayah ii na maana yake, mpaka baadhi yao wakasema kwamba aya hiyo ndiyo ngumu zaidi katika Qur'an kimpangilio na kitafsiri. Maana haya tuliyoyaleta ndiyo yanayolingana sawa na mpangilio wote wa Sura bila ya kupingana na aya. Mwenye kutaka maelezo zaidi na ayatafute haya katika vitabu vilivyorefushwa maelezo.

Aya Na 2

Neno Suhuf lina maana ya kitu kinacho andikiwa juu yake. Makusudio yake hasa ni mafungu ya Qur'an yanayoshuka kwa ujumla. Neno hili limekaririka katika maneno yake Mwenyezi Mungu kwa maana ya mafungu ya vitabu vya mbinguni; kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Huo waadhi umo katika kurasa tukufu. Zenye kutukuzwa (na) zenye kutakaswa. Zimo katika mikono ya waandishi. Watukufu watenda mema ." (8:13-16).

Makusudio ya kuwa kurasa. Zimetakaswa, ni kuwa imetakaswa na uchafu wa ubatilishi kwa kuguswa na shetani. Na imekaririwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwamba hayo ni maandishi ya haki yenye kuhifadhiwa na muingilio wa kishetani. Mwenyezi Mungu kasema: "Hapana aigusaye ila waliotakaswa na mabaya" (56:79).

Aya Na 3

Neno kutubu lina maana ya kila chenye kuandikwa, iwe ni ubao au karatasi nk. Vile vile lina maana ya hukumu: Kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t); "Mmehukumiwa (mmelazimishwa) kufunga ".(2:183).

"Na mmehukumiwa (mmelazimishwa) kupigana vita " (2:216).

Kwa dhahiri ni kuwa makusudio yake ni maandishi yaliyomo katika kurasa zenye hukumu za Mungu zenye kufungamana na itikadi na matendo. Dalili yake ni kuyasifu kwa neno Qayyima linalotokana kusimamia kitu kwa maana ya kukihifadhi, kuchunga maslahi yake na kudhamini wema wake. Inajulikana kuwa vitabu vya mbinguni vinasimamia mambo ya jamii ya watu, na kuchunga maslahi yake kutokana na hukumu zake zenye kufungamana na itikadi na amali. Kwa hiyo maana ya aya hizi mbili ni kuwa: hoja iliyowazi ambayo amewaletea Mtume(s.a.w.w) kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwasomea vitabu vya mbiguni vyenye kutakaswa na batili, ni hukumu zenye kusimamia mambo ya jamii ya watu, zenye kuchunga maslahi yake.

Aya Na 4

Aya Na kwanza ilikuwa inaonyesha kumkanusha kwao Mtume na kitabu chake chenye kudhamini mlingano (mwito) wa haki. Aya hii inaonyesha kukhitalifiana kwao juu ya mlingano wa Kiislamu. Hayo yameonyweshwa kwenye sehemu nyengine katika Qur'an kama: "Na hawakukhitalifiana waliopewa kitabu ila baada kuwajia elimu ". (3:19).

Kuwajia hoja ni ubainifu wa utume ambao umewabainikia katika vitabu vyao au ule waliofafanuliwa na mitume yao, kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t): "Na alipofika Isa kwa dalili zilizo wazi, alisema "Nimekujieni na elimu (yenye nafuu na nyie), na ili nikuelezeni baadhi ya yule mliyohitalifiana; basi mcheni Allah na nittini. Kwa hakika Allah ndiye Mola wenu; basi muabuduni, hii ndiyo njia iliyonyooka, lakini yalihitalifiana makundi wao kwa wao ". (43:63-65).

Kama ukiuliza, kwa nini imeelezwa kutengana kwa watu wa kitabu na haikuelezewa kutengana kwa washirikina.

Jibu ni kuwa, sio mbali kuwa neno: wale ambao wamepewa kitabu, lililoko katika ayah ii linawachanganya watu wa kitabu na washirikina. Limebadilishwa neno 'watu wa kitabu' ambao katika Qur'an wanajulikana kuwa ni Mayahudi, Wakristo na Majusi, kuwa wale ambao 'wamepewa kitabu'. Bila shaka ibara hizi mbili zinatofautiana. Mwenyezi Mungu amefafanua kuwa Yeye ameteremsha kitabu ambacho ni sharia iliyofaradhaiwa juu yao yenye kuhukumu katika hitilafu za mambo yao ya kimaisha - tangu mwanzo zilipodhihiri hitilafu zao za kimaisha wao wakahitalifiana katika dini baada ya kuwabainikia wao haki na kuwasimamia wao hoja. Kwa hiyo watu wote wameletewa kitabu; kisha wakahitalifiana, kuna katika wao waliosahau kile walichopewa, kuna waliochukulia kimakosa na kuna wale waliohifadhi kile walichopewa wakakiamini. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema: "Watu wote walikuwa wa dini moja (kisha wakahitalifiana). Basi Allah akawaleta manabii watoao habari njema na waonyao na pamoja nao akawateremshia vitabu vilivyoshikamana na haki ili vihukumu baina ya watu katika yale waliyokhitalifiana na hawakuhitalifiana katika hayo ila wale waliopewa vitabu hivyo; baada ya kuwafikia hoja zilizo wazi kwa sababu ya uhasidi (uliokuwa) baina yao ." (2:213).

Katika maana hayo Mwenyezi Mungu anasema: - mpaka aliposema- Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana wale waliokuwa baada yao (baada ya mitume) baada ya kuwafikia hoja zilizowazi. Lakini walihitalifiana, kwa hiyo wako katika wao walioamini na wako katika wao waliokufuru.. (2:253).

Kwa ujumla neno wale ambao wamepewa vitabu linaenea kwa wote, watu wa kitabu na washirikina.

Aya Na 5

Dhamira katika neno hawakuamrishwa inawarudia wale waliokanusha katika waliopewa kitabu na washirikina. Makusudio yake ni kuwa, ujumbe wa Mtume(s.a.w.w) na maandishi yaliyomo katika kurasa na wahyi, hayakudhamini kitu isipokuwa ibada ya Mwenyezi Mungu kwa kuifunga pamoja na Ikhlas katika dini na kutomshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu chochote. Neno Hunafaa lina maana ya kuondoka kwenye upande wa kupetuka mipaka na kuelekea kwenye kulingana sawa (kuwa ndani ya mipaka ya Mwenyezi Mungu). Na Mwenyezi Mungu ameiita Dini ya Kiislamu Hanifa kwa vile Uislamu unaamrisha 'uwastani' katika mambo yote na kujiepusha na kukiuka vipimo. "Kisha wasimamshe swala na watoe zaka". Baada ya kuelezea dini kwa ujumla anaelezea mafungu ya dini yenye kuhusikana. Swala na kutoa zaka ni miongoni mwa nguzo za Uislamu ambazo ni mwelekeo wa kiibada unaomhusu Mwenyezi Mungu na kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya dini iliyo sawasawa ni dini ya maandishi yenye msimamo ulio sawasawa kama walivyofasiri. Ikiwa makusudio ya maandishi ni maandishi yote ya mbiguni kama maandishi ya Nuh na wengineo katika mitume, maana yake yatakuwa hAya Na liyoamriwa na kulinganiwa katika mlingano (mwito) wa Muhammad, ndio yale yale waliyoamriwa katika vitabu vyao vyenye msimamo na wala sio jambo la kuzusha, kwani dini ya Mwenyezi Mungu ni moja na ni juu yao kuifuata dini hiyo, kwa sababu ndiyo yenye msimamo. Na ikiwa makusudio ya maandishi yenye msimamo ni yale wanayosemewa na Mtume(s.a.w.w) kutoka katika maandishi yaliyomo katika kurasa zenya kutoharishwa, basi itakuwa maana yake ni kuwa wao hawakuamrishwa ila kufuata hukumu zenye msimamo na zenye maslah ya jamii ya kiutu.

Kwa vyovyote iwavyo aya inaishiria dini ya Tawhid (kumpwekesha Mwenyezi Mungu) ambayo inadhaminiwa na Qur'an inayosadikisha vitabu vilivyo kabla yake na kuhukumia yale yanayoamrisha jamii ya watu, hali ya kusimamia mambo yao na kuchunga maslahi ya maisha yao; kama alivyo lifafanua hilo Mwenyezi Mungu kwa uwazi katika neno lake: "Basi uelekeze uso wako katika dini iliyosawasawa, ndilo umbile ambalo Allah amewaumbia watu (dini iliyosawa). Hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Allah. Hiyo ndiyo dini ya sawa (30:30).

Kwa aya hii basi, yanakamilika ubainifu wa kuenea ujumbe wa Mtume(s.a.w.w) na kuenea mwito wa Kiislamu kwa watu wote. Kwa hiyo neno lake Mwenyezi Mungu: "Hawakuwa wale ambao wamekufuru katika watu wa kitabu" mpaka mwisho, linaonyesha kuwa kuna ulazimu kutokana na desturi ya uongozi wa Mungu, kutimiza hoja kwa yule mwenye kuukanusha mwito miongoni mwa watu wa kitabu na washirikina. Kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu "Mtume atokae kwa Allah" inaonyesha kuwa hiyo hoja ni Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Kufarikiana kwao na kukanusha kwao haki kwa zamani, pia kuliendelea baada ya kuja Mtume Mhuhammad(s.a.w.w) kama anavyosema Mwenyezi Mungu katika Sura hii: "Wala hawakutengana".

Aya Na 6-7

Baada ya kuelezea ukanushaji wao wa hoja na mambo wanayolinganiwa, sasa anaingilia kutoa onyo kwa wale wakanushaji na kuwapa biashara waumini. Maana ya Aya Na ko wazi hakuna haja ya ufafanuzi.

Aya Na 8

Maana halisi ya neno Adn ni kutulia na kuthibiti, kwa hiyo makusudio yake ni pepo ya kudumu. Mwenyezi Mungu analisisitiza hilo kwa kusema: "Watakaa humo milele".

Mwenyezi Mungu kuwa radhi nao ni uhakika wa thawabu alizowapa, ikiwa ni malipo ya imani zao na matendo yao. "Hayo ni ya mwenye kumuogopa Mola wake" hiyo ndio chapa ya wema wa akhera na Mwenyezi Mungu amesema: "Kwa hakika wale wanaomuogopa Allah miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu (wanavyuoni) ". (35:28).

Kwa hiyo kumjua Mwenyezi Mungu kunafuatia kumuogopa na kumuogopa kunafuatia kumuamini kwa maana ya kuamini kimoyo uungu wake kisha kutenda amali njema. Kuna hitilafu kubwa sana katika kufasiri aya hizi. Hitilafu hizi hazina umuhimu wa kuzielezea. Mwenye kutaka kuzijua na aangalie vitabu vyenye maelezo marefu.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsiri ya Qumii katika riwAya Na Abu-Jarud kutoka kwa Abu Jaffar(a.s) anasema: Hoja ni Muhammad(s.a.w.w) . Katika Durril Manthur ametoa Ibn Murdawy kutoka kwa Aisha amesema: "Nilimuuliza ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu" Ni nani Mtukufu zaidi wa viumbe kwa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ewe Aisha kwani hukusoma aya inayosema: Hakika wale ambao wameamini na wakatenda matendo mema hao ndio bora wa watu?" Katika hiyo hiyo Durril-Manthur ametoa Ibn Asaki, kutoka kwa Jabir bin Abdillahi amesema: "Tulikuwa mbele ya Mtume akaja Ali akasema Mtume(s.a.w.w) . "Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake hakika huyu na wafuasi wake ndio wenye kufuzu siku ya Kiyama." Kisha ikashuka aya hiyo, ikiwa masahaba wa Mtume(s.a.w.w) wakijiwa na Ali husema: "Amekuja bora wa watu."

Imepokewa hadith kwa maana hiyo kutoka kwa Addi kutoka kwa Ibn Abbas, vile vile kutoka kwa Ibn Murdawayh, naye kutoka kwa Ali(a.s) . Na imepokewa vile vile katika Bur'han kutoka kwa Muwaffaq bin Ahmad katika kitabu Manaqib kutoka kwa Yazid bin Sharahiyl El-Ansari, vile vile katika Majmau kutoka katika kitabu cha Shawahiduttanzil cha Hakim naye kutoka kwa Yazid bin Sharahiyl kutoka kwa Ali amesema: Wakati Mtume(s.a.w.w) akikaribia kufa, na mimi nimemwigamiza katika kifua changu, aliniambia: "Ewe Ali hivi hukusikia neno la Mwenyezi Mungu. "Hakika wale ambao wameamini na wakatenda (amali) njema hao ndio bora wa viumbe". Wao ni wafuasi wako na kukutana kwangu na nyinyi ni kwenye birika wakati utakapokusanyika umati kwa ajili ya hisabu. Wafuasi wako watakuwa wana mapako yenye kung'aa (katika viungo vya udhu).

Katika Majmau kutoka kwa Muqatil bin Salman, naye kutoka kwa Adh-dhah-hak naye kutoka kwa Ibn Abbas kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu: "Hao ndio bora wa viumbe" amesema ilishuka kwa Ali na Ahlul Bait wake.

23

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA SILZAAL ( TETEMEKO)(NA. 99)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema , Mwenye kurehemu

إِذَا زُلْزِلَتِ الْأَرْضُ زِلْزَالَهَا ﴿١﴾

1. Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake.

وَأَخْرَجَتِ الْأَرْضُ أَثْقَالَهَا ﴿٢﴾

2. Na ikatoa ardhi mizigo yake.

وَقَالَ الْإِنسَانُ مَا لَهَا ﴿٣﴾

3. Na akasema mwanadamu ina nini?

يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا ﴿٤﴾

4. Siku hiyo itatoa habari zake.

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا ﴿٥﴾

5. Kwa kuwa Mola wako ameiamrisha.

يَوْمَئِذٍ يَصْدُرُ النَّاسُ أَشْتَاتًا لِّيُرَوْا أَعْمَالَهُمْ ﴿٦﴾

6. Siku hiyo wataondoka watu wametawanyika tawanyika ili kuonyeshwa amali zao.

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

7. Basi atakayefanya wema (hata) uzani wa sisimizi atauona.

وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُ ﴿٨﴾

8. Na atakayefanya uovu (hata) uzani wa sisimizi atauona.

UBAINIFU

Sura hii inaelezea Kiyama, kutolewa watu kwa ajili ya malipo ya sharti za kiyama ambazo ni tetemeko la ardhi na kuzungumza habari zake. Sura hii inawezekana kuwa imeshuka Makka au Madina.

Aya Na 1

Mwenyezi Mungu anasema "Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake" kwa maana ya kuwa tetemeko hilo ni la aina yake, kutokana na ukubwa wake.

Aya Na 2

Neno athqal lina manna ya mizigo. Kwa vyovyote vile iwavyo makusudio ya aya ni kuwa ardhi itatoa mizigo yake iliyoichukua ambayo ni wafu kama ilivyosemwa au hazina za madini au vyote hivyo. Kauli ya kwanza (wafu) ndyo iliyokaribu zaidi na maana.

Aya Na 3

Yaani mtu atapigwa na mshangao wa ajabu kutokana na tetememko hilo kiasi cha kujiuliza: Ina nini ardhi? Mbona inatetemeka hivi? Imesemwa kuwa makusudio ya mtu hapa ni kafiri asiyeamini ufufuo, na yamesemwa zaidi ya hayo kama yatakavyokuja maelezo (Inshallah).

Aya Na 4 -5

Ardhi itakuwa shahidi wa vitendo vya mwanadamu, kama vile vitavyokuwa shahidi viungo vya binadamu na maandishi ya Malaika. Hiyo ni kutokana na amri ya Mwenyezi Mungu. Na hii inafahamisha kuwa vitu vina uhsai na hisia, ijapokuwa sisi hatujui hilo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na hakuna chochote ila kinamsabihi (Mwenyezi Mungu) kwa sifa zake njema lakini nyinyi hamfahamu kusabihi (kutukuza) kwake.." (17:44).

Akasema tena: "Hata watakapoujia (huo moto), hapo ndipo masikio yao, na macho yao na ngozi zao zitakapotoa ushahidi juu yao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda.. Na wao waziambie ngozi zao; "Mbona mnatushuhudilia? "Nazo ziwaambie: "Allah aliyekitamkisha kila kitu ndiye aliyetutamkisha, naye ndiye aliyekuumbeni mara ya kwanza. Na kwake hivi sasa) mnarudishwa (41:20-21).

Kumekuwa na hiitilafu kubwa juu ya maana ya kuzungumza ardhi; kuwa itapewa uhai na hisia au itaumbwa sauti tu! Lakini hatuna haja na hitilafu hizo, kwa sababu vyovyote iwavyo ni kwamba ardhi itatoa ushahidi.

Aya Na 6

Makusudio ya kuondoka kutawanyika tawanyika, ni kuenda zao kwenye makazi yao katika pepo na katika moto. Na kuona matendo yao ni kuona malipo ya matendo ya au kuona umbo halisi la hayo matendo. Imesemwa kuwa makusudio yake ni kutoka makaburini mwao kuelekea kwenye mkusanyiko wakitofautina kwa nyuso nyeusi na nyeupe,na kwa fazaa na amani, ili yafahamike malipo yao kwa kuangalia tu!, kama alivyosema Mwenyezi Mungu; "Siku ambayo kila nafsi itakuta mema iliyoyafanya yamehudhurishwa, na pia ubaya iliofanya .(3:30).

Kauli ya kwanza ndiyo iliyo karibu zaidi na maana.

Aya Na 7-8

Dharra ni chembe ndogo za vumbi zinaonekana katika mwanga wa jua au sisimizi wadogo. Aya hiyo inatilia mkazo yaliyotangulia kuwa amali yoyote hata iwe ndogo kiasi gani, itaonekana. Lakini aya hizo hazikanushi kuharibika kwa amali, au kugura amali kwenda kwenye nafsi nyingine; kama kugura mema ya mwuuaji kwenda kwa mwenye kuuwa, au kubadilika maovu kuwa mema kwa baadhi ya wenye kutubia, nk; kama ilivyoelezwa katika Sura zilizotangulia kama aya inayosema: "Ili Allah apate kuwapambanua walio wabaya na walio wazuri ." (8:37).

Kwa hiyo aya hizo zinahukumia aya hizi mbili, kwani mwenye kuharibikiwa na amali yake ya heri, ni kuwa hana amali ya heri atakayoiona. Na juu ya mfano huu unaweza kukisia na kufahamu..

Utafiti Wa Hadith Katika Durril Manthur, ametoa Ibn Murdawayh na Bayhaqi kutoka jwa Anas bin Malik, kwamba Mtume(s.a.w.w) amesema: "Hakika Ardhi itatoa habari siku ya Kiyama kila lililofanywa juu ya mgongo wake, na akasoma Mtume(s.a.w.w) : "Itakapotetemeshwa ardhi huo mtetemeko wake" mapaka alipofikia: "Siku hiyo itatoa habari zake" akasema " Je, mnajua habari yake? Jibril amenijia akaniambia kuwa; kitakapokuwa Kiyama ardhi itatoa habari ya kila yaliyofanywa juu ya mgongo wake". Na imepokewa hadith ya mfano huo kwa Abu Huraira.

Ametoa Hussein bin Sufiani na Abu Naim kutoka kwa Shaddad bin Aus; amesema: Nimemsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: "Enyi watu, hakika dunia ni maonyesho ya sasa hivi anakula mwema na muovo. Na hakika Akhera ni kiaga cha kweli, atahukumu huko Mfalme muweza, itathibiti haki na itabatilika batili, Enyi watu kuweni watoto wa akhera wala msiwe watoto wa dunia, kwani kila mtoto humfuata mama yake. Fanyeni amali kwa tahadhari. Jueni kwamba mtaonyeshwa amali zenu na mtakutana na Mwenyezi Mungu. Basi mwenye kufanya wema (hata) uzani wa sisimizi atauona na mwenye kufanya uovu (hata) uzani wa sisimizi atauona! Katika Tafsiri ya Qummi, kuhusu Aya Na 2, amesema: Mizigo ni watu. Na kuhusu aya 4-6 amesema: Yatakuja makundi ya waumin, makafiri na ya wanafiki ili waone matendo yao. Katika riwAya Na Abu Jarudi kutoka kwa Ab Jaffar(a.s) kuhusu Aya Na 7-8 anasema: Ikiwa mtu ni katika watu wa motoni na amefanya amali ya heri ya uzani wa sisimizi itakuwa ni majuto ikiwa ameifanya siyo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Na akiwa ni mtu wa peponi na amefanya amali ya shari ya uzani wa sisimizi, ataonyeshwa shari hiyo, kisha atasamehewa.

SURA ADIYAAT (FARASI) (NA. 100)

INA AYA 11

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema , Mwenye kurehemu.

وَالْعَادِيَاتِ ضَبْحًا ﴿١﴾

1. Naapa kwa farasi wanaokwenda mbio wakihema.

فَالْمُورِيَاتِ قَدْحًا ﴿٢﴾

2. Wanaotoa moto, kwa kupiga kwata.

فَالْمُغِيرَاتِ صُبْحًا ﴿٣﴾

3. Wanaowashambulia maadui ghafla wakati wa asubuhi.

فَأَثَرْنَ بِهِ نَقْعًا ﴿٤﴾

4. Wakatifua vumbi wakati huo.

فَوَسَطْنَ بِهِ جَمْعًا ﴿٥﴾

5. Wakaliingilia kati wakati huo kundi (la maadui).

إِنَّ الْإِنسَانَ لِرَبِّهِ لَكَنُودٌ ﴿٦﴾

6. Hakika mwanadamu ni mwenye utovu wa shukrani sana kwa Mola wake.

وَإِنَّهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ ﴿٧﴾

7. Na yeye ni shahidi wa hilo.

وَإِنَّهُ لِحُبِّ الْخَيْرِ لَشَدِيدٌ ﴿٨﴾

8. Na hakika yeye kwa sababu ya kupenda mali ni bakhili.

أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِي الْقُبُورِ ﴿٩﴾

9. Je, hajuwi watakapofufuliwa waliomo makaburini.

وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ ﴿١٠﴾

10. Yakadhihirishwa yalipo nyoyoni.

إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّخَبِيرٌ ﴿١١﴾

11.Hakika Mola wao siku hiyo ni mjuzi mno wa hali zao.

UBAINIFU

Sura inataja ukanushaji wa mtu kwa neema ya Mola wake na kupenda kwake sana heri. Na yeye atahisabiwa juu ya hayo. Sura hii imeshuka Madina kwa ushahidi wa habari ya vita inayoelezwa katika Sura hiyo kwa mfano: "Naapa kwa farasi wa wapigania Jihadi"; kama yatakavyokuja maelezo yake. Na vita vya jihadi vilianza baada ya Hijra. (kuhama wa Mtume(s.a.w.w) . Hayo yanatiliwa nguvu na hadith zilizopokewa na Shia kutoka Maimamu wa Ahlul Bait kuwa, Sura hiyo ilishuka kwa ajili ya Ali(a.s) katika vita vya Salasil (Minyororo). Yatakuja maelezo yake katika utafiti wa hadith (Inshallah) kwa kufuatana na mapokezi ya Ahli Sunnah.

Aya Na 1

Mwenyezi Mungu anaapa kwa farasi wanaokwenda mbio wakihema; yaani wakitoa sauti ya pumzi mbele ya maadui na hali hiyo ni maarufu kwa farasi, ingawaje inadaiwa kuwa wanyama wengine wanayo. Maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu anaapa kwa jeshi lililo na farasi wa namna hiyo. Imesemwa kuwa makusudio yake ni ngamia wa mahujaji wanapokuwa Mina siku wa Nahr (ya kuchinja). Na pia imesemwa kuwa ni ngamia wa vita. Lakini aya zinazofuata hazionyeshi kuwa makusudio yake ni ngamia !

Aya Na 2

Yaani farasi wanaotoa moto kwa kupiga kwato katika mawe au ardhi ngumu. Imesemwa kuwa makusudio ya kuwasha moto hapa ni hila za wanaume katika vita. Na imesemwa kuwa ni kuwasha moto tu! Na pia imesemwa kuwa makusudio ni ndimi za wanaume zinazowasha moto kutokana na uzito wa yale wanayoyasema. Lakini njia zote hizo ni dhaifu kwa dhahiri kabisa.

Aya Na 3

Wanatajwa farasi kuwa ndiyo wenye kushambulia maadui kwa njia ya fumbo kwa maana ya wenye farasi hao.

Aya Na 4

Watawatimulia vumbi maadui kutokana na mashambulizi.

Aya Na 5

Yaani kuliingilia kati kundi la maadui. Imesemwa kuwa maana yake ni kuingia kati ngamia katika Mina siku ya Hijja. Lakini kuzifikiria aya zote tano kuwa na maana ya ngamia wa mahujaji wanaomiminika kwenda Mina, ni kinyume kabisa. Ilivyo hasa makusudio yake ni farasi wa vitani. Na mpangilio wa aya inayosema: (Wanaoshambulia maadui ghafla wakati wa asubuhi:) na (wakaingia katikati ya kundi), unafahamishwa kuwa Mwenyezi Mungu anaapa kwa farasi wa vita. Ne herufi fa katika aya nne, inafahamisha mpangilio wa kufuatana kila moja baada ya nyingine.

Aya Na 6

Ni jawabu ya Qasam (kiapo) inayotolea habari yale yaliyo katika tabia ya mtu, kama kufuata matamanio, kuyavamia na mambo ya dunia yanayokwisha na kuacha kumshukuru Mola wake juu ya alivyomneemesha. Inaonyesha aina ya watu wanaoshambuliwa. Inaonyesha kuwa makusudio ya kukanusha kwao, ni kukanusha neema ya uislamu aliyowaneemesha Mwenyezi Mungu juu yao. Nayo ni neema kubwa waliyopewa na kutengeneza vizuri maisha yao ya dunia na wema wa maisha yao mengine ya milele.

Aya Na 7

Dhamira katika neno "na yeye" inamrudia mtu, kwa hiyo makusudio yanakuwa: mtu yeye mwenyewe anashuhudia juu ya kukanusha na kukufuru kwake. Kwa hiyo aya iko katika maana ya aya nyengine inayosema: "Bali mtu juu ya nafsi yake ni mwenye kushuhudia ". (75:14).

Na imesemwa kuwa dhamira inamrudia Mwenyezi Mungu, kwa maana kuwa yeye Mwenyezi Mungu ni shahidi. Lakini mpangilio wa dhamira hauliwafiki hilo.

Aya Na 8

Neno Khayr hapa limekuja kwa maana ya mali, yaani mtu kwa ajili ya kupenda sana mali anakuwa bakhili. Imesemwa kuwa makusudio yake ni hakika mtu ni mwingi wa kupenda mali na hilo linampelekea kujuzuwiya na kutoa haki ya Mwenyezi Mungu na kutoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Namna hii wamefasiri. Lakini hayo hayaweki mbali kuwa makusudio ya Khayr ni kheri ya aina yoyote. Na kwamba kupenda kheri ni maumbile ya kiutu, ndipo mtu anaona anasa za dunia ndio kheri, kwa hiyo zinamuingia na zinamsahauliza kumshukuru Mola wake.

Aya Na 9 – 10

Yaliyo katika nyoyo ni sifa ya imani au ukafiri, kama alivyosema Mwenyezi Mungu "Siku itakayofuniliwa siri ". (87:9).

Na maana kwa ujumla - na Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi - ni kuwa; hivi hajui mtu kuwa kwa sababu ya kukanusha kwake na kumkufuru kwake Mola wake atalipwa? Wakati watakapotolewa waliomo makaburini na kudhihirishwa siri za nafsi, miongoni mwa imani na kufuru na utii na uasi. Hakika Mola wao, siku hiyo ni mjuzi mno wa hali zao, kwa hiyo atawalipa.

Utafiti Wa Hadith Katika Majmau imesemwa kuwa; Mtume(s.a.w.w) alipeleka kikosi katika makao ya ukoo wa Kinana kikiongozwa na El-Mundir bin Amri El-Ansari mmoja wa Makamanda. Walipochelewa kurudi, Mwenyezi Mungu akampa khabari Mtume(s.a.w.w) kwa kusema: "Naapa kwa farasi wenye kwenda mbio wenye kuhema." Imesemwa kuwa Sura hii ilishuka wakati Mtume(s.a.w.w) alipompeleka Ali(a.s) kwa Dhatus-Salasil (Wenye Minyororo) na akawashinda. Na hilo ni baada ya kuwapeleka masahaba wengine mara nyingi. Wote wakarudi kwa Mtume bila ya kufaulu. Hadith hii imepokewa kutoka kwa Abu Abdillah(a.s) katika hadith ndefu. Na vita hivyo viliitwa vya minyororo kwa sababu baadhi yao walitekwa, wakauawa na wakafungwa mateka kwa kamba za mikoni kama vile wamefungwa na nyororo.

Utafiti Wa Hadith Iliposhuka Sura hii Mtume(s.a.w.w) alitoka akawaswalisha watu swala ya asubuhi na akasoma katika swala Sura hiyo. Alipomaliza kuswali masahaba zake wakasema: "Sura hii haituijui", Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ndio hakika Ali amewashinda maadui wa Mwenyezi Mungu na Jibrail amenifahamisha hilo usiku huu. Baada ya siku kidogo Ali akafika pamoja na ngawira na mateka kadhaa ."