TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN0%

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi: Muhammad Hussein Tabaatabaai
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 39012
Pakua: 2740

Maelezo zaidi:

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39012 / Pakua: 2740
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

Mwandishi:
Swahili

24

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA QAARIA ( KIYAMA) (NA. 101)

INA AYA 11

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehemai, Mwenye kurehemu

الْقَارِعَةُ ﴿١﴾

1. Kiyama!

مَا الْقَارِعَةُ ﴿٢﴾

2. Ni nini Kiyama?

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْقَارِعَةُ ﴿٣﴾

3. Na nini lipi lakukujulisha ni nini Kiyama?

يَوْمَ يَكُونُ النَّاسُ كَالْفَرَاشِ الْمَبْثُوثِ ﴿٤﴾

4. Ni siku ambayo watu watakuwa kama panzi waliotawanywa.

وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ الْمَنفُوشِ ﴿٥﴾

5. Na yakawa majabali kama sufi iliyopurwa.

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ ﴿٦﴾

6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito.

فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ ﴿٧﴾

7. Yeye atakuwa katika maisha yenye kuridhiwa.

وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ ﴿٨﴾

8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa nyepesi.

فَأُمُّهُ هَاوِيَةٌ ﴿٩﴾

9. Basi makaza yake yatakuwa ni Hawiya.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا هِيَهْ ﴿١٠﴾

10. Na ni lipi la kujulisha wewe nini hiyo ( Hawiya).

نَارٌ حَامِيَةٌ ﴿١١﴾

11. (Hawiya) ni moto uliomkali mno.

UBAINIFU

Sura hii inatoa onyo juu ya Kiyama.Imeshuka Makka.

Aya Ya 1-3

Neno Qari'ah linatokana na Qur'u lenye maana ya kugonga sana, nalo ni mojawapo katika majina ya Kiyama. Imesemwa kuwa Kiyama kimeitwa hivyo, kwa sababu kinagonga nyoyo fazaa na kinawagonga maadui wa Mwenyezi Mungu kwa adhabu.

Aya Ya 4

Yaani siku hiyo ya Kiyama watu watakuwa kama panzi waliotapanyika, kutokana na mfazaiko. Imesemwa kuwa watu siku ya kufufuliwa wamefananishwa na panzi, kwa vile panzi wanaporuka hawaeleki upande mmoja kama desturi ya ndege wengine. Bsi vile vile watu watakapotoka makaburini mwao watakuwa wameshikwa na fazaa; wataelekea pande mbali mbali; au wataelekea sehemu zao mbalimbali za uovu au wema.

Aya Ya 5-7

Inaashiria juu ya uzani wa amal ( Matendo); kwamba kuna matendo mazito ambayo yana daraja mbele ya Mwenyezi Mungu nayo ni iman na twaa (Utii) na kuna yale ambayo hayana uzani wowote nayo ni kufuru na uasi. Kwa hiyo mwenye kuwa na amali zenye uzani uzito atakuwa katika maisha atakayoyaridhia.

Aya Ya 8

Neno Hawiya lenye maana ya kuporomoka ni mojawapo ya majina ya Jahannam; imeitwa hivyo kwa vile mtu atakayeingizwa humo ataporomoka hadi chini ya waliochini; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Kisha tukamrudisha chini ya waliochini, ila wale walioamini "(95:5-6)".

Kuusifu moto kwa neno Hawiya ni fumbo kama fumbo la kuyasifu maisha ya kuridhiwa kuileta ibara ya makazi kwa neno Ummu lenye maana ya mama, ni kwa sababu ndiyo marejeo ya huyo mwenye uzani mwepesi, kama anavyorejea mtoto kwa mama yake. Imesemwa kuwa makusudio ya Ummu ni Ummur- ra'as yaani fuvu la kichwa chake, kwa maana yakuwa ataangukia kichwa chake katika Jahannam, lakini kauli inawekwa mbali na kubakia dhamiri bila ya mahali inapoashiria katika neno Maahiya inayofasiriwa na aya 11.

Aya Ya 10

Jumla hiyo ni kulifanya kubwa jambo la huo moto.

Aya Ya 11

Moto mkali, yaani wenye kuchomwa sana. Na hilo ni jawabu na tafsiri ya aya 1.

Utafiti Wa Hadith Katika Tafsri ya Qummi katika neno lake Mwenyezi Mungu " Na yule ambaye mizani yake itakuwa nyepesi". Yaani wepesi katika mambo mema. Na kuhusu Ummu amesema ni fuvu la kichwa chake yaani atatupwa katika Jahannam kichwa- kichwa.

Katika Durril Manthur ametoa Ibn Murdawayah kutoka kwa Abu Ayyub El- Ansari, kwamaba Mtume(s.a.w.w) amesema: " Hakika nafsi ya muumin inapochukuliwa hukutana na watu wa rehema katika waja wa Mwenyezi Mungu na watu wema kutoka duniani; watasema: Mwaangalieni mwenzenu anastarehe kwani yeye alikuwa katika mashaka makubwa; kisha watamuuliza: fulani na fulani wamefanya nini? Je Fulani ameolewa? Na watakapomuulizia mtu aliyekufa kabla yake, atasema: huyo amekufa kabla yangu. Halafu watasema: " Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea. Amekwishapelekwa kwenye makazi yake ya Hawiya, ni makazi mabaya na malezi mabaya." Na imepokewa hadith kwa maana haya kutoka kwa Anas bin Malik, na kutoka kwa Hassan na Ash'ath bin Abdalla Ama.

SURA TAKATHUR ( KUTAKA WINGI WA MALI) (NA. 102)

INA AYA 8

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

أَلْهَاكُمُ التَّكَاثُرُ ﴿١﴾

1. Kumewashughulisha mno kutaka wingi wa mali.

حَتَّىٰ زُرْتُمُ الْمَقَابِرَ ﴿٢﴾

2. Mpaka mzuru makaburi.

كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ ﴿٣﴾

3. Komeni! Hapo mtajua.

ثُمَّ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ ﴿٤﴾

4. Kisha komeni! Hapo mtajua.

كَلَّا لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ الْيَقِينِ ﴿٥﴾

5. Si hivyo! lau mngejua ujuzi wa yakini (msinge jishughulisha na hayo).

لَتَرَوُنَّ الْجَحِيمَ ﴿٦﴾

6. Hakika mtauona moto.

ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيْنَ الْيَقِينِ ﴿٧﴾

7. Kisha mtauona kwa jicho la yakini.

ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ ﴿٨﴾

8. Lisha mtaulizwa siku hiyo matumizi ya neema mlizopewa.

UBAINIFU

Makaripio makubwa kwa watu kutokana na kujishughulisha kwao kwa wingi wa mali na watoto na kusahau mambo yanayofuatia miongoni mwa hasara na adhabu. Vile vile ni utisho kwamba wao watajua, wataona adhabu na kuulizwa neema waliyopewa ili washukuru, lakini wakabadilisha neema hiyo kuwa kufuru. Sura hii uinaweza kuwa imeshuka Makka au Madina Maelezo zaidi yatakuja katika utafiti wa hadithi kuhusu sababu za kushuka kwake, (Inshallah).

Aya Ya 1-2

Maana ya aya hizi mzunguko ni kuwa: mmeshughulika sana na kuzama katika starehe za dunia na vipambo vyake na kushindana katika wingi wa vitu, jambo ambalo limewafanya muache jambo muhimu la kumtaja Mwenyezi Mungu, mpaka mkafikiwa na kifo. Kughafilika kwenu kumewatia upofu katika maisha yenu yote. Imesemwa kuwa maana yake ni kuwa kumewashughulisha nyinyi kujifaharisha kwa wingi wa watu. Hawa wanasema "Sisi tuna watu wengi zaidi". Na wengine wanasema "Sisi tuna watu wengi hata mlipomaliza kuhisabu waliohai mkaenda makaburini kuwahesabu waliokufa katika watu wenu. Hivyo basi mkashindana pia kuwahisabu wafu wenu".

Maana haya ndiyo yaliyoko katika mpangilio wa yale yaliyopokewa kuhusu sababu za kushuka Sura hii, kwamba makabila mawili katika Ansar yalijifakharisha waliohai na waliokufa. Katika baadhi ya yaliyopokewa ni kwamba hayo yalikuwa Makka kati ya Abdu Manaaf na Bani Sahm. Kitakuja kisa chake katika utafiti wa hadithi (Inshallah).

Aya Ya 3

Makemeo na vitisho kutokana na kujishughulisha na mambo yasiyokuwa na umuhimu wowote.

Aya Ya 4

Kusisitiza yale yaliyotangulia katika aya ya 3. Imesemwa kuwa makusudio ya aya ya 3 ni kwamba watayojua hayo wakati wa kufa, na aya ya 4 kuwa watayajua wakati wa kufufuliwa.

Aya Ya 5

Makemeo baada ya makemeo, kwa kusisitiza. Na 'yakini' ni elimu ambayo haina shaka yoyote. Jawabu la 'Lau' limeondolewa, ambalo makadirio yake ni "Lau mngejua ujuzi wa yakini msingejishughulisha na hayo".

Aya Ya 6

Ni jumla nyengine inayoanza, na wala siyo jawabu la lau ya aya ya 5. Makusudio yake ni kuuona moto kwa moyo kabla ya kuuona kwa macho siku ya Kiyama, kutokana na inavyoonyesha katika neno lake Mwenyezi Mungu: "Na utadhihirishwa moto kwa mwenye kuona ". (79:36).

Aya Ya 7

Makusudio yake ni kuona kabisa kwa macho siku ya Kiyama, kutokana na dalili ya aya ya mbele (Kisha ataulizwa siku hiyo neema zote). Kuna kauli zinazosema: Kuuona kwa kwanza ni kabla ya kuuingia moto na kuuona kwa pili ni baada ya kuuingia. Kauli nyengine inasema, kwanza ni kuujua huo moto na pili ni kuuona. Na imesemwa makusudio yake ni kuuona baada ya kuuona, kwa kuonyesha kuendelea na kudumu. Na mengine zaidi ya hayo yamesemwa.

Aya Ya 8

Mzunguko wote wa maneno, unaonyesha kuwa maneno haya yanaelekezwa kwa watu wote wale ambao neema za Mwenyezi Mungu zimewafanya wamsahau Mwenyezi Mungu. Na binadamu ni mwenye kuulizwa juu ya neema zote alizopewa na Mwenyezi Mungu. Neema-Jambo ambalo linamuafiki yule mwenye kuneemeshwa na kumpa heri na manufaa-inakuwa neema kulingana na yule mwenye kuneemeshwa anavyoitumia. Kinyume cha hivyo, basi itakua ni balaa, ijapokuwa yenyewe nineema. Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemuumba mtu na akajaalia makusudio ya kumuumba kwake, ni kumuabudu. Kama alivyosema: "Sikuumba majini na watu ila waniabudu " (51:56).

Huo ndio utawala wa Mungu kwa mja wake, na Mwenyezi Mungu amemuandalia huyo mja wake, kila linalomnufaisha katika kulifikia lengo ambalo amemuumbia kwalo.

Kwa hivyo kuitumia neema hii katika njia anayoiridhia Mwenyezi Mungu na itakayomfikisha mtu kwenye lengo lake analolitaka, ndiyo njia ya kufikia lengo muhimu ambalo ni twaa (Utii). Kuitumia neema kinyume cha anavyoridhia Mwenyezi Mungu na kusahau lengo lake, ni upotevu na kukosa kulifikia lengo. Mwenyezi Mungu amekwishatoa hukumu ambayo haibadilishwi, kuwa mtu atarudi kwake na kumuuliza juu ya amali (matendo) yake, kisha amuhisabie na kumlipa. Matendo (amali) yake ni matumizi ya neema ya Mwenyezi Mungu. Kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Na kwamba mtu hatapata isipokuwa yale aliyoyatenda. Na kwamba matendo yake yataonekana. Kisha atalipwa malipo yaliyo kamili. Na kwamba mwisho (wa kila jambo) unarejea kwa Mola wako ." (53:39-42).

Utafiti Wa Hadithi Katika Majmau imesemwa kuwa Sura hii ilishuka kwa Mayahudi waliosema: "Sisi ni wengi zaidi kuliko ukoo fulani". Na ukoo fulani ni zaidi ya ukoo fulani". Wengine wamesema kuwa ilishuka kwa makabila mawili katika Ansar walipojifaharisha, na imesemwa kuwa imeshuka kwa Maquraish ukoo wa Abdu Manaaf bin Quswai na wa Sahm bin Amr wakajifaharisha na wakahesabu watukufu wao, Abdu Manaaf wakawa wengi. Kisha wakasema twendeni makaburini, tuwahisabu wafu wetu. Wakawa wengi ukoo wa Sahm, kwa sababu wao walikuwa wengi wakati wa ujahili. Katika Tafsiri ya Bur'han kutoka kwa Barqi kutoka kwa baba yake kutoka kwa Ibn Abu Umayr, kutoka kwa Hisham bin Salim naye kutoka kwa Abu Abdillahi, kuhusu neno la Mwenyezi Mungu "Lau mngelijua kujua kwa yakini". Amesema: Nikuona kwa macho. Na riwaya hii inatilia nguvu yale tuliyotangulia kuyaeleza katika maana ya aya". Katika Tafsiri ya Qummi kwa isnadi yake kutoka kwa Jamil naye kutoka kwa Abu Abdillahi(a.s) amesema: "Nilimwambia kuhusu mtaulizwa siku hiyo neema zote" akasema: "Utaulizwa uma huu juu ya neema aliyowaneemesha Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kisha kwa Ahlul Bayt wa Mtume(s.a.w.w) .

Katika Kafi kwa isnadi yake kutoka kwa Abu Khalid El-Kabili amesema: "Nilliingia kwa Abu Jafar(a.s) akaniita chakula cha mchana nikala pamoja naye chakula ambacho sijapata kukila kwa uzuri wake. Tulipomaliza kula akasema: "Ewe Abu Khalid umekionaje chakula chetu?" Nikasema, "Sijakula chakula kizuri na kisafi kama hicho, lakini nimekumbuka aya ambayo iko katika kitabu cha Mwenyezi Mungu (s.w.t) inayosema: "Kisha mtaulizwa siku hiyo neema zote". Abu Jaffar akasema: "Hakika mtaulizwa yale mliyo na haki nayo ".

Katika hiyo hiyo Kafi kutoka kwa Abu Hamza amesema: "Tulikuwa kundi kwa Abu Abdillahi(a.s) akatuita chakula ambacho hatujapata kuona mfano wake, kutokana na ladha yake na kupendeza kwake, na akatuletea tende zilizo nzuri na safi, mtu mmoja akasema: "Mtaulizwa neema hii mliyoneemeshwa nyumbani kwa mtoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema Abu Abdillahi(a.s) : Hakika Mwenyezi Mungu ni mkarimu sana, hawezi kuwalisha chakula kisha awaulize, isipokua atawauliza neema aliyowaneemesha kwa Muhammad na kizazi cha Muhammad(s.a.w.w) ." Zimepokewa riwaya zenye maana haya kwa njia nyengine na ibara zenya kukhitalifiana. Baadhi ya riwaya zinasema kwamba neema ni wilaya (Utawala) wa Ahlul Bait wa Mtume na imetafsiriwa, kuwa ni neema zote alizozineemesha Mwenyezi Mungu.

Ubainifu wa hayo, ni kwamba neema hiyo sio kuwa itaulizwa kama kitu kwa mfano nyama, mkate, tende au maji baridi. Au kwamba neema hiyo ni usikizi, uoni, mkono au mguu. Hapana sio hivyo; isipokuwa itaulizwa neema ambayo Mwenyezi Mungu amemuumbia mtu, kama ameitumia katika njia ya ukamilifu wake na kupata ukaribisho na ibada, na akahimiza kuitumia kwa kushukuru, sio kuikufuru. Neema itaulizwa vipi ilivyotumiwa? Inayoelezea jinsi ya kutumia neema, ni dini aliyokuja nayo Mtume(s.a.w.w) na kuusimamisha ubainifu wake, na maimamu kutoka katika Ahlul Bayt wake Mtume.

Kwa hiyo kuulizwa neema, maana yake ni kuulizwa amali ya dini katika harakati zote. Na kuulizwa juu ya Mtume(s.a.w.w) na Maimamu walio baada yake ambao amewajibisha Mwenyezi Mungu kuwatii na akawajibisha kuwafuata katika njia ya kumuendea yeye Mwenyezi Mungu, ambayo njia yenyewe nu kuitumia neema kama ilivyobainishwa na Maimamu. Kuulizwa neema maana yake ni kuulizwa dini, kunaonyeshwa na riwaya ya Abu Khalid inayosema: "Hakika mtaulizwa yale mliyo na haki nayo". Kuulizwa dini maana yake ni kuulizwa juu ya Mtume na Ahlul Bayt wake, hili linaonyeshwa na riwaya mbili za Jamil na Abu Hamza zinazosema. "Atauliza Mwenyezi Mungu umma huu juu ya alivyowaneemesha kwa Mtume wake na Ahlul Bait wake".

Kuna baadhi ya riwaya zinazosema neema ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa watu wa ulimwengu kuwaokoa na upotevu. Na neema ni utawala wa Ahlul Bait, na utawala wa Ahlul Bait, unawajibisha kuwatii na kuwafuata katika ibada. Katika Majmau, imesemwa kuwa neema ni uzima na wasaa juu ya marifa. Riwaya hii inasaidiwa na riwaya iliyopokewa na Ibn Abbas kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) amesema: "Watu wengi wamehadaiwa na neema mbili, uzima na wasaa".

Katika hiyo hiyo Majmau imesemwa kuwa neema ni amani na uzima. Riwaya hii imepokewa kutoka kwa Abdallah bin Masud na Mujahid. Katika riwaya nyingine kutoka katika njia ya Ahli Sunnah zinasema: "Neema ni tende, maji baridi, nk. Na katika hadithi nyingine kutoka katika njia hiyo hiyo ya Sunni inasema: "Mambo matatu hataulizwa mtu; kitambaa kinachousitiri uchi wake, kipande cha tonge kinachozuiya njaa yake au nyumba inayomsitiri joto na baridi". Na Mwenyezi Mungu ndie mjuzi zaidi.

SURA ASR (ZAMA) (NA. 103)

INA AYA 3

Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu

وَالْعَصْرِ ﴿١﴾

1. Naapa kwa zama.

إِنَّ الْإِنسَانَ لَفِي خُسْرٍ ﴿٢﴾

2. Hakika mwanadamu yumo katika hasara.

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ ﴿٣﴾

3. Ila wale ambao wameamini wakatenda amali (matendo) njema, wakausiana (kushikamana na) haki, wakausiaana kusubiri.

UBAINIFU

Sura hii Muhtasari wa maarifa yote ya Kiqur'an na imekusanya makusudio ya Qur'an kwa maelezo mafupi (Muhtasar). Sura hii inawezekana kwa imeshuka Makka na Madina, lakini inavyoelekea imeshuka Makka.

Aya Ya 1

Ni kuapa kwa majira maalum. Na hii ndiyo tafsiri nzuri, kwa vile aya mbili zinazofuatia, zimejumlisha watu wote wa ulimwengu katika kupata hasara, isipokuwa wale waliofuata ukweli na wakasubiri. Sifa hizo ni za waumini wanaofanya mema. Hivyo makusudio ya majira (asr) yanakuwa ni zama za Mtume(s.a.w.w) ambazo ni zama za kutokeza Uislamu kwa jamii ya watu na kudhihiri haki juu ya batili. Inasemekana pia kuwa makusudio ya Asr hapa ni wakati wa Alasiri ambao ni sehemu ya mwisho katika mchana, kwa kufahamisha mipangilio ya Mungu kwa kuchwa jua na kuja usiku pamoja na kuondoka ufalme wa jua. Na imesemwa kuwa makusudio ya Asr hapa ni swala ya Alasiri ambayo ni swala katikakati na ni bora katika swala za faradhi za kila siku.

Pia inasemeka makusido ya Asr ni usiku na mchana, na imesemwa kuwa makusudio ni zama ndefu za maisha kutokana na matukio ya kiajabu yanayofahamisha uwezo wa Mungu nk Imepokewa kutoka katika baadhi ya riwaya kwamba makusudio yake ni zama za kudhiri Mahdi(a.s) kwa kutumia kudhihiri haki juu ya batili.

Aya Ya 2

Yaani hasara ya kupungua raslimali ya mtu.

Aya Ya 3

Mwenyezi Mungu anawatoa katika hasara wale wenye kuvaana na imani na matendo mema, hao ni wenye kusalimika na hasara. Hapa kitabu cha Mwenyezi Mungu kinabainisha kuwa mtu anayo maisha ya milele ambayo hayakatiki kwa kifo, bali kifo ni kugura kutoka ulimwengu mmoja mpaka ulimwengu mwengine, kama alivyosema Mwenyezi Mungu "(Hatutashindwa) kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyingi katika umbo (jengine) msilolijua ".(56:61).

Qur'an inabainisha kwamba sehemu ya maisha hayo ambayo ni maisha ya dunia ni mtihani wa sehemu ya mwisho ya maisha ambayo ni akhera ya milele; kuwa yatakuwa mazuri au mabaya anasema Mwenyezi Mungu: "Na uhai wa dunia kwa mkabala wa akhera si kitu isipokuwa ni starehe ndogo tu ".(13:26).

Na amesema tena: "Kila nafsi itaonja mauti, na tuna kufanyieni mitihani kwa (mambo ya) shari na ya kheri, na kwetu (nyote) mtarejea " (21:35).

Vile vile inabainisha kwamba kitu cha kukitanguliza katika maisha haya ya dunia kwa ajli ya maisha ya akhera ni itikadi na vitendo. Kwa hiyo itikadi ya kweli na amali njema ndivyo vyenye kumiliki wema wa akhera, na ukafiri na ufasiki utasababisha uovu akhera. Mwenyezi Mungu amesema: "Na kwamba mtu hatapata ila yale aliyoyatenda. Na kwamba matendo yake yataonekana. Kisha atalipwa malipo yaliyo kamili ." (41:39-41)

Amesema tena: "Anayekufuru, (madhara) ya kufuru yake ni juu yake (mwenyewe); na wafanyao mema (hao) wanazitengeza nafsi zao ".(44:46). Kwa hali hiyo basi, imebainika kwamba uhai wa dunia ni rasilimali ya mtu, anachuma yale atakayoishi nayo katika maisha ya akhera. Kama akifuata haki katika itikadi na amal (vitendo) basi amepata faida katika biashara yake, amebarikiwa katika chumo lake na amesalimika na shari katika mustakabali wake. Kama akiifuata batili na akaacha imani na matendo mema, basi biashara yake itakuwa na hasara na atazuiliwa heri katika mwisho wake. Hilo ndilo neno lake Mwenyezi Mungu. " Hakika wanadamu wote wako katika hasara, isipokuwa wale ambao wameamini na wakatenda amali njema". Makusudio ya imani, ni kuamini Mwenyezi Mungu na miongoni mwa mambo ya kumuamini Mwenyezi Mungu ni kuamini Mitume yako yote na kuamini siku ya mwisho.

Mwenyezi Mungu ameeleza katika Sura ya (4:150-151), kuwa yule asiyeamini baadhi ya Mitume yake au siku ya mwisho, basi sio muumin. Kukusiana (kushikamana na) haki na kuusiana kusubiri, ni kuusiana watu kushika hiyo haki, kuifuata na kudumu nayo. Dini ya kweli haiwi isipokuwa kwa kuifuata haki kwa itikadi na vitendo. Na kuusiana kushikamana na haki ni kukubwa zaidi ya kuamrisha mema na kukataza mabaya, kwa sababu kunakusanya itikadi na kuhimiza amali njema.

Kisha kuusiana haki na katika amali njema, na kumetajwa baada ya amali njema kutokana na umuhimu wake. Na kuusiana kusubiri ni katika kuusiana haki, limetajwa neno kuusiana mara mbili kwa ajili ya kusisitiza. Kumetajwa kuusiana baada ya kutajwa iman na amali njema, kwa kuashiria kwanza kwenye uhai wa nyoyo zao na kukunjuka nyoyo zao kwa Uislamu, kisha kuieneza haki hiyo kwa watu wote. Subira imeelezwa kwa ujumla, kama kusubiri juu ya kumtii Mungu, kusubiri juu ya kuacha maasai na kusubiri juu ya misiba inayompata kwa kadari ya Mungu.

Utafiti Wa Hadithi Katka Tafsri ya Qummi kwa isnadu yake kutoka kwa Abdurrahman bin Kathiyr naye amepokea kutoka kwa Abu Abdillahi(a.s) katika neno lake Mwenyezi Mungu "Ila wale ambao wameamini" amewavua Mwenyezi Mungu watu wa ikhlas katika viumbe vyake. Katika Durril Manthur, ametoa Ibn Murdawayh, kutoka kwa Ibn Abbas kuhusu neno lake Mwenyezi Mungu: "Hakika wanadamu wote wako katika hasara" anakusudia Abu Jahl bin Hisham. Na kuhusu "Ila wale ambao wameamini na wakatenda mambo mema" ametajwa Ali na Salman.

25

TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN

SURA HUMAZA (MRAMBA KISOGO) (NA. 104)

INA AYA 9

Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ ﴿١﴾

1. Ole wake kila anyeramba kisogo, anayesengenya.

الَّذِي جَمَعَ مَالًا وَعَدَّدَهُ ﴿٢﴾

2. Ambaye amekusanya mali na kuyahesabu.

يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُ أَخْلَدَهُ ﴿٣﴾

3. Anadhani kwamba mali yake itambakisha milele.

كَلَّا لَيُنبَذَنَّ فِي الْحُطَمَةِ ﴿٤﴾

4. Na akome! Atatupwa katika Hutama!

مَا أَدْرَاكَ مَا الْحُطَمَةُ ﴿٥﴾

5. Na ni lipi la kukujulisha nini hiyo Hutama?

نَارُ اللَّـهِ الْمُوقَدَةُ ﴿٦﴾

6. Ni moto wa Allah uliowashwa.

الَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى الْأَفْئِدَةِ ﴿٧﴾

7. Ambao hupanda mpaka nyoyoni.

إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌ ﴿٨﴾

8. Hakika (Moto) huo utafungiwa juu yao.

فِي عَمَدٍ مُّمَدَّدَةٍ ﴿٩﴾

9. Kwa magogo marefu marefu.

UBAINIFU

Sura hii inatoa makamio makali ya Mwenyezi Mungu kwa wale wenye kuzama katika kukusanya mali, wakajifanya juu kuliko watu wengine, wakatakabari na kuwaaibisha wenzao. Sura hii imeshuka Makka.

Aya Ya 1

Amesema katika Majmau: "Neno Humaza lina maana ya mwingi wa kuwaaibisha na kuwashutumu wengine kwa mambo wasiyokuwa nayo. Asili ya neno hilo ni kuvunja na humaza ni aibu. Vile vile amesema kwamba humaza na lumaza ni kwa maana moja. Lakini imesemwa kuwa kuna tofauti kati ya maneno hayo mawili, humaza ni yule anayeaibisha mtu akiwa hayupo na lumaza ni yule anayeaibisha mtu mbele yake. Pia imesemwa kuwa humaza ni yule anayemuudhi mtu aliekaa naye kwa maneno mabaya na lumaza ni yule anaye mvunjia macho mtu aliyekaa naye huku akiashiria kwa macho yake na kichwa chake. Kwa hiyo maana kamili ya aya ni: "Ole wake kila anaewatia aibu watu sana, mwenye kusengenya sana." Wengine wamefasiri kwa maana nyengine kulingana na tafsiri zao.

Aya Ya 2

Ni ubainifu wa yule mwenye kuramba kisogo mwenye kusengenya. Pia ni ubainifu wakuidunisha mali. Kwani mali ijapokuwa nyingi kiasi gani, haiwezi kumfaa mwenye kuwa nayo na kitu chochote zaidi ya matumizi ya nafsi ya kitabia, kama vile kula, kunywa, nk. Neno Addadah lina maana ya hesabu yaani kwa sababu ya kuipenda mali sana, basi anaikusanya na kuihesabu mara kwa mara huku akifurahiwa wa wingi wake. Na imesemwa kuwa maana yake ni kuirundika mali, kwa kutaraji itamfaa wakati wa shida (akiba).

Aya Ya 3

Yaani anafikiria kuwa mali yake hiyo itamzuia kufa? Mtu huyu kwa sababu ya kutaka kuishi kwake katika ardhi, na kuzama kwake katika tama ndefu, hakinai na mali ambayo inamuondoshea haja za maisha yake mafupi na siku zake zenye kuhesabiwa, bali kadiri mali inavyozidi ndivyo anavyozidi kuwa na tamaa isiyokua na mwisho. Hivyo hali yake inaonyesha kwamba yeye anaona kua hiyo mali itambakisha ulimwenguni. Na kwa sababu ya mapenzi yake ya kitabia ya kutaka kubaki, basi anajishughulisha na kuikusanya mali na kuihesabu. Baada ya kuipata hiyo mali na kujiona tajiri, anajifanya mkubwa mbele za watu kama alivyosema Mwenyezi Mungu: "Hakika mwanadamu hupetuka mpaka, kwa vile kujiona ametajirika." Na kiburi hicho ndicho kinachomfanya arambe visogo vya watu.

Neno akhladah limekuja kwa njia ya muda uliopita lakini hapa lina maana ya muda ujao kutokana na kukutana na neno yahsabu ambalo ni la muda ujao.

Aya Ya 4

Inapinga fikra za kudhania kudumu milele kwa mali. Neno hutama hapa limekuja kwa maana ya kula. Na hiyo hutama ni moja kati ya majina ya moto kama inavyo fasiriwa na aya ya 6. Yaani ayah hii inakusudia kusema kwa: Mtu huyo hataweza kubakishwa milele na mali, bali atakufa kisha atupwe katika Hutama.

Aya Ya 5

Ni utisho na kulifanya kubwa jambo.

Aya Ya 6

Ni kwa ajili ya kulifanya kubwa jambo na kuogopesha.

Aya Ya 7

Moto huo utatokeza kwenye nyoyo, kwa vile moyo ndiyo msingi wa utambuzi wa mtu na fikra yake nao ndiyo nafsi ya kiutu. Inaelekea kuwa makusudio ya kutokeza juu ya nyoyo, ni kwamba unamchoma banadamu ndani na nje alvyosema Mwenyezi Mungu: "Kuni zake ni watu na mawe ." (2:24).

Aya Ya 8

Yaani moto huo utatiwa komeo amabyo hawataweza kutoka wala kuokoka.

Aya Ya 9

Maguzo marefu; Imesemwa kuwa ni maguzo ambayo yatakua ni komeo ya moto. Pia imesemwa kuwa ni miti ambayo watafungiwa watu wa motoni kama ile miti inayofungiwa wezi. Na yamesemwa zaidi ya hayo.

Utafiti Wa Hadithi Katika Ruwhel Maani kuhusu aya ya 1 kutokana na alivyotoa Ibn Hatim kutoka katika njia ya Ibn Ishaq kutoka kwa Athman bin Umar, kwamba imeshuka juu ya Ubayya bin Khalaf. Na kutokana na aliyo yatoa Sudiyy, kuwa imeshuka juu ya Ubayya bin Amru El-Thaqafi, mashuhuri kwa jina la Akhnas bin Shariq, kwani yeye alikuwa akimsengenya Mtume katika matukio mengi. Na kutokana na yale aliyoyasema Ibn Ishaq kuwa imeshuka kwa Umayya bin Khalaf El-Jamhi ambaye alikuwa akimramba kisogo Mtume(s.a.w.w) .

Kutokana na aliyotoa Ibn Jariyr na wengineo kutoka kwa Mujahid, ni kwamba ayah ii imeshuka juu ya Jamil bin Amir, na imesemwa pengine, kwamba imeshuka juu ya Walid bin Mughirah kwa kumsengenya kwame Mtume(s.a.w.w) na pia imesemwa kuwa imeshuka kwa Asi bin Wail. Kisha amesema katika hiyo Ruwhel Maani kuwa inawezekana kuwa imeshuka kwa wote hao waliotajwa. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu aya ya 1 amesema ni yule ambaye anawakonyeza watu na kuwadharau mafakiri. Kuhusu neno humaza ni yule ambaye anageuza shingo yake na kichwa chake (anabeza) na anachukia anapomuona fukara au muombaji.

Kuhusu aya ya 2 ni yule aliyeiandaa mali na kuiweka. Katika Majmau amepokea Iyashi kwa isnadi yake kutoka kwa Muhammad bin Annu'man El-Ahwal, naye kutoka kwa Hamran bin aa'yan naye kutoka kwa Abu Jaffar (AS) amesema: "Hakika makafiri na washirikina watawaaibisha watu wa Tawhid katika moto huku wakisema: "Tunaona Tawhid yenu haiwafai chochote, nyinyi na sisi tuko sawa tu!" Basi hapo Mwenyezi Mungu atawatoa aibu kwa kuwaambia Malaika: "Waombeeni". Nao watawaombea. Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawambia Mitume: "Waombeeni" Mitume nao watawaombea. Tena Mwenyezi Mungu atawaambia waumini, "Waombeeni" basi waumini watawaombea Mwenyezi Mungu atasema: "mimi ni Mwingi wa rehema wenye kurehemu, tokeni kwa Rehema Yangu." Ndiyo watatoka kama wanavyotoka panzi; kasha itavutwa nguzo na wale watu wa motoni watatiliwa komeo kama walivyokuwa".

SURA FIL (NDOVU) (NA.105)

INA AYA 5

Kwa jina ya Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصْحَابِ الْفِيلِ ﴿١﴾

1. Je, hukujua jinsi Mola wako alivyowafanya wenye ndovu?

أَلَمْ يَجْعَلْ كَيْدَهُمْ فِي تَضْلِيلٍ ﴿٢﴾

2. Je, hakukifanya kitimbi chao nichenye kupotea bure?

وَأَرْسَلَ عَلَيْهِمْ طَيْرًا أَبَابِيلَ ﴿٣﴾

3. Akawepelekea ndege makundi makundi.

تَرْمِيهِم بِحِجَارَةٍ مِّن سِجِّيلٍ ﴿٤﴾

4. Wakiwatupia kwa mawe ya udongo mkavu.

فَجَعَلَهُمْ كَعَصْفٍ مَّأْكُولٍ ﴿٥﴾

5. Akawafanya kama ganda tupu lililoliwa ( kokwa yake)

UBAINIFU

Sura hii inaeleza kisa cha watu wenye ndovu, walipokwenda Makka, ili kuharibu Al-Ka'aba tukufu, lakini Mwenyezi Mungu akawaangamiza kwa kuwapelekea makundi ya ndege. Kisa hicho kilichowazi ni katika alama ya Mwenyezi Mungu. Na Majahili walikitaja katika Sura hii imeshuka Makka.

Aya Na 1

Neno Alamtara hapa lina maana ya kujua kuliko dhahir, kwa maana ya kuwa, je hukujua namna gani alivyowafanya Mola wako watu wenye ndovu? Tukio hili lilikuwa mwaka aliozaliwa Mtume(s.a.w.w) .

Aya Na 2

Makusudio ya vitimbi vyao ni makusudio yao mabAya Na kwenda Makka kutaka kuivunja nyumba tukufu (Al-Ka'aba), lakini vitimbi vyao vilipotea bure. Walikwenda kwa ajili ya kuivunja Al-Ka'aba, wakaishilia kuangamia wao wenywe.

Aya Na 3 -4

Neno Ababil lina maana ya makundi makundi, yaani Mwenyezi Mungu aliwapeleka hao waliotaka kuivunja Al-Ka'aba makundi ya ndege, waliowatupia mawe.

Aya Na 5

Asf ni jani la mmea ambao mbegu yake imeliwa, au ganda tupu la tembe ambayo imeliwa kokwa yake. Yaani wao walirudi kuwa viwiliwili bila ya roho, au kwamba vile vijiwe kutokana na joto lake, viliunguza miili yao kwa ndani. Imesemwa kuwa makusudio yake ni majani yaliyoliwa na wadudu. Na imefasiriwa aya hii baadhi ya njia ambazo hazilingani na fasihi ya Qur'an.

Utafiti Wa Hadithi Katika Majmau wapokezi wamesema mfalme wa Yemen ambaye alikusudua kuivunja Al-Ka'aba ni Abraha bin Assabahi El-Ashram, na inasemekana alikuwa akijulikana zaidi kwa jina la "Abu Yaksum". Imenukuliwa kutoka kwa Waqidi kuwa yeye ni babu wa Mfalme Najashi aliyekuwa katika zama za Mtume(s.a.w.w) . Kisa kinaendelea kueleza kuwa huyo mfalme alijenga Ka'aba huko Yemen akaweka makuba ya dhahabu, na akaamrisha watu wa mamlaka yake kuhiji hapo, kwa kuifananisha na ile ya Makka.

Mtu mmoja katika Bani Kinana, alikwenda Yemen akaangalia jingo hilo, kisha akaenda kunya humo ndani. Abraha alipoingia na kukuta uchafu huo , alisema: Ni nani aliyenionyesha jeuri hii? Ninaapa kwa Ukristo wangu nitaivunja ile Al-Ka'aba yao ili wasiende tena watu kuhiji milele". Basi akaitisha ndovu na akatoka pamoja wa wafuasi wake katika watu wa Yemen. Wafuasi wake zaidi walikuwa ni makabila ya Akka, Ash-Aruun na Khath'am. Alipokuwa njiani, akamtuma mtu mmoja katika Bani Salim, ili awalinganie watu kwenda kuhiji nyumba yake aliyoijenga. Basi huyo mjumbe akakutana na mtu mwengine kutoka katika Bani Kinana akauliwa. Hilo likamzidisha mori zaidi wa kwenda.

Alipofika Taif, akawaomba wampatie muonyeshaji njia, wakampatia mtu mmoja katika ukoo wa Hudhayl anayeitwa Nufayl. Akawa anawaongoza mpaka walipofika Maghmas maili 6 kutoka Makka, wakatua, kisha wakapeleka watangulizi. Maquraish wakatoka makundi wakasema : Hatuna nguvu za kukabiliana na watu hawa, " hakubaki hapo Makka isipokuwa Abdul Mutwalib bin Hashim akiwa mahali pake pa kunywesha maji na Shaybah bin Uthman bin Abdiddar akiwa kwenye kizuizi cha Al-Ka'aba. Akawa Abdul Mutwalib anashika mihimili ya mlango huku akisema: 'Ewe Mwenyezi Mungu hakika mtu anataka kuzuwiya utukufu wako basi uzuwiye msafara wake, ili usiweze kushinda msalaba wao na uadui wao. Wasiweze kuingia mji huu mtukufu basi jambo limekudhihirikia."

Wale watangulizi wakapora ngamia wa Maquraish na wakapora ngamia mia mbili wa Abdul Mutwalib. Abdul Mutwalib alipopata habari hizo, akawaendea. Mlinzi wa Abraha alikuwa ni mtu mmoja katika Ash'an ambaye alikuwa akimjua Abdul Mutwalib. Basi yule mlinzi akamtaka idhini mfalme, akimwaambia: "Ewe Mfalme amekujia Bwana wa Maquraish, ambaye huwalisha binadamu mjini na wanyama majabalini. Akamwambia mwache aingie.

Abdul Mutwalib alikuwa ni mtu mwenye umbo kubwa, mzuri. Basi Abu Yaksum (Abraha) alipomwona hakuona vyema kumkalisha chini yake wala hakupendelea kumkalisha juu ya kitanda chake. Kwa hivyo akashuka chini akakaa pamoja na Abdul Mutwalib, kisha akamuuliza: "Nini haja yako?" akajibu: " Haja yangu ni ngamia mia mbili walioporwa na watu wako". Akasema Abu Yaksum: " Hakika umenishangaza sana". Akasema: " kwa nini ewe Mfalme". Akasem:" " Mimi nimekuja kwenye nyumba ya utukufu wenu, ya ubora wenu kwa watu na ya dini yenu ambayo mnaabudia. Nimekuja niivunje na ni nikapora ngamia wako mia mbili, sasa ninakuuliza nini haja yako, unaniambia ni ngamia tu! Wala huukulizia habari ya nyumba yenu (Al-Ka'aba)."

Abdul Mutwalib akamwambia: "Ewe mfalme mimi ninakusemesha katika mali yangu na hii nyumba ina mwenyewe ( Mungu) mwenye kuilinda. Mimi si lolote si chochote. HAya Na limshtusha Abu Yaksum. Basi Abu Yaksum akaamrisha kurudishwa ngamia wa Abdul Mutwalib, kisha akarudi na wale wakakesha katika usiku ambao anga yake ilichafuka, wakawa wanahisi adhabu.

Jua lilipochomoza, wakatokewa na ndege wakiwa wamechukua mawe, wakawa wanawatupia, kila ndege katika mdomo wake kuna jiwe moja na kwenye miguu kuna mawe mawili. Ndege akitupa jiwe likimpata mtu kwenye tumbo linampasua na linatoboa mifupa. Abu Yaksum akaamua kurudi, huku akiwa amepatwa na baadhi ya mawe akawa kila anapopiga hatua hukatika kiungo mpaka alipofika Yemen hakubakiwa na kiungo chochote. Alipofika, kikachanika kifua chake na likapasuka timbo lake akaangamia. Kunahitilafu kubwa katika kisa hiki, mwenye kutaka zaidi na asome vitabu vya sera na historia vyenye kueleza kwa urefu.

SURA QURAISH (QURAISH)(NA. 106)

INA AYA 4

Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.

لِإِيلَافِ قُرَيْشٍ ﴿١﴾

1. Kwa ajili ya kuzowea Maquraish.

إِيلَافِهِمْ رِحْلَةَ الشِّتَاءِ وَالصَّيْفِ ﴿٢﴾

2. Kuzowea kwao safari ya kusi na kaskazi.

فَلْيَعْبُدُوا رَبَّ هَـٰذَا الْبَيْتِ ﴿٣﴾

3. Na wamwabudu Mola wa nyumba hii.

الَّذِي أَطْعَمَهُم مِّن جُوعٍ وَآمَنَهُم مِّنْ خَوْفٍ ﴿٤﴾

4. Ambaye amewalisha wakati wa njaa, na akawasalimisha na khofu.

UBAINIFU

Sura hii inaeleza neema ya Mwenyezi Mungu juu ya Maquraish kwa kuweza kusafiri katika wakati wa kusi na kaskazi na kufanya biashara kwa usalama, kwa hivyo wambudu Mola wa nyumba tukufu (Al-Ka'aba). Sura hii imeshuka Makka. Kwa kuwa madhumuni ya Sura hii yanafungamana na madhumuni ya Sura ya Fil, basi wamesema jamaa katika Shia na Ahli Sunnah kuwa Fil na Quraish ni Sura moja; kama ilivyosemwa katika Sura Adhuha na Alamnashrah (Al Inshirahi).

Kwa upande wa Ahli Sunnah waemetegemea mapokezi yao kuwa Ubayya bin Kaab, hakuweka Bismillah kati ya Sura ya Fil na Quraish katika msahafu wake. Na pia mapokezi yaliyotokana na Maymun El-Azadi amesema: "Niliswali maghrib nyuma ya Umar bin El-Khattab akasoma katika rakaa ya kwanza Sura ya Wattin na katika rakaa ya pili akasoma Alamtara na Liilafi bila ya kusoma Bismillahi kati yake. Lakini riwAya Na kwanza imejibiwa kuwa riwaya hiyo inapingana na riwaya nyingine inayosema kuwa Bismillah ipo katika huo msahafu wa El-Azadi. Na riwAya Na pili imejibiwa kuwa inawezekana huyo mpokeaji wa riwaya hiyo hakusikia tu! Au pengine hiyo Bismillah ilisomwa bila sauti.

Ama kwa upande wa Shia wametegemea yale yaliyo katika Majmau: Kutoka kwa Abul Abbas, naye kutoka kwa mmoja wa Maimamu(a.s) amesema: "Alamtara na Lillafi ni Sura moja". Na wametegema yale yaliyo katika Tahdhib kwa isnadi ya Alaa, kutoka kwa Zaid Shaham amesema: "Abu Abdillahi(a.s) alituswalisha Alfajiri, akasoma Alamnashrah na Adhuha katika rakaa moja. Na yaliyo katika Majmau, kutoka kwa Iyash naye kutoka kwa Mufadhil bin Saleh kutoka kwa Abu Abdillahi(a.s) amesema: "Nimemsikia akisema huyo Abu Abdillahi(a.s) : Hazichanganywi Sura mbili katika rakaa moja illa Alamtara na Ilafi na Alamnashra na Adhuha. Na amepokea Muhakkik kwa kunakili kutoka katika kitabu Jamiu cha Ahmad Muhammad bin Abu Nasr. Lakini riwAya Na Abul Abbas ni dhaifu. Ama riwAya Na Shahham, imepokewa kutoka kwake kwa njia mbili nyengine Ya kwanza ni ile iliyo katika Tahdhib kutoka kwa Ibn Miskan, naye kutoka kwa Zaid Shahham amesema: "Abu Abdillahi alituswalisha, akasoma Sura ya Wadhuha na Alamnashra.

Na riwAya Na pili imepokewa kutoka kwa Ibn Abdi Umar naye kutoka kwa baadhi ya masahaba zetu, kutoka kwa Zaid Shham amesema: " Abu Abdillah(a.s) alituswalisha akasoma katika rakaa ya pili Sura ya Wadhuha na katika rakaa ya pili Sura ya Alamnashrah." Kwa hali yeyote itakayokuwa ni kwamba riwaya hizo, zinafahamisha kujuzu kusoma Sura mbili Alamnashrah na Adhuha katika rakaa moja au Alamtara na Liilafi katika rakaa moja, jambo ambalo halijuzu katika Sura nyengine.

Aya Na 1-2

Maquraish ni ukoo wa Mtume(s.a.w.w) , wao ni kizazi cha Nadhr bin Kinanah aliyekuwa akijulikana kwa jina la Quraish, "Msafara wa kusi na kaskazi" ni msafara wa Maquraish wakawa wanaishi kwa biashara tu! Walikuwa wana misafara miwili kwa kila mwaka, msafara wakusi ulikuwa wa Yemen na msafara wa kaskazi ulikuwa wa Sham (Syria). Na walikuwa wakiishi kwa hilo na watu wakiwaheshimu, hawaulizwi njiani, wala mji hauvamiwi, kwa sababu ya nyumba tukufu (Al-Ka'aba). Herufi Fa katika neno Fal-ya'abudu ni ya kueleza maana ya sharti yaani: kwa vyovyote iwavyo, basi wamwabudu Mola wa nyumba hii kwa ajili ya kuwazowesha kwake misafara miwili. Kwa ujumla maana ya aya hizi tatu ni kuwa; Maquraish wamwabudu Mola wa nyuba hii(Al-Ka'aba) kwa ajili ya kuwazowesha msafara wa kusi na kaskazi huku wakiwa katika amani.

Hii ni kwa kuangalia kuwa Sura hii imeepukana na Sura ya Alamtara. Ama kwa kukadiri kua Sura hii ni sehemu ya Sura ya Alamtara, basi herufi Lam katika Liilafi, itakuwa ni Ya taalil yenye kufungamana na yale yaliyo katika Sura ya Alamtara, kwa maana ya kuwa tumefanya hayo tuliyowafanyia watu wenye ndovu, hali yakuwa ni neema itokayo kwetu juu ya Maquraish kuongezea neema ya misafara yao ya kusi na kaskazi. Yaani kama vile amesema kutoka neema moja mpaka neema nengine kwa hivyo ndio maana kasema kuwa herufi lam inatekeleza maana ya Ilaa (mpaka). Na hilo ni neno lake Farra (Mwanachuoni wa kinahaw) Pia imesemwa kuwa: tumewafanyia hilo watu wenye ndovu ili wazoee Maquraish Makka na waweza kukaa hapo. Au ili wazowee Maquraish hapo kwa vile walimkimbia Abraha alipoikusudia Al-Ka'aba, hivyo tukawangamiza Abraha na watu wake, ili warudi Maquraish Makka, wazowee hapo na azaliwe Muhammad(s.a.w.w) awe muonyaji kwa watu.

Aya Na 4

Inaishiria yale yaliyomo katika neema zilizo wazi, amabazo ni kupata chakula katika ardhi iliyo kame na kuwa katika amani, jambo ambalo halikuweko kwa watu wengine, kwa hiyo basi na wamwabudu Mola anayezingatia vizuri mambo yao ambaye ndiye huyo Mola wa hiyo nyumba (Al-Ka'aba)

Utafiti Wa Hadithi Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu Sura hii anasema " Imeshuka kwa ajili ya Maquraish, kwa sababu maisha yao yalikuwa yakitokana na misafara miwili msafara katika kusi kuelekea Yemen na msafara katika kaskazi kuelekea Sham (Syria) na walikuwa wakichukua kutoka Makka siagi, lozi na vitu vinavyoota pembeni mwa bahari, kama pilipili na vyenginevyo, na walikuwa wakinunua nguo, unga mweupe na nafaka huko Sham, na walikuwa wakitembea vikundi, kila kikundi kina kiongozi katika viongozi wa Kiquraish.

Basi Mwenyezi Mungu alipompeleka Mtume wake wakawa hawana haja na hayo tena, kwani walikuwa watu wakija kwa Mtume(s.a.w.w) na kuhiji Al-Ka'aba, kwa hivyo ndio Mwenyezi Mungu akasema: " Na wamwabudu mola wa nyumba hii, ambaye amewalisha kwa ajili ya njaa na akawasilimisha na khofu" (yaani hofu ya njiani)". Lakini maneno haya (kuanzia Mwenyezi Mungu alipompeleka Mtume?.) yamefichika katika anuani ya aya za Sura hii, au huenda huyo Qummi ameyachukua kutokana na baadhi ya yaliyopokewa kutoka kwa Ibn Abbas.