10
TAFSIRI YA QURANI AL-MIIZAAN
SURA BURUJ (BURUJI) (NA. 85)
INA AYA 22
Kwa jina la Allah, Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu.
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْبُرُوجِ ﴿١﴾
1. Naapa kwa mbingu zenye buruji.
وَالْيَوْمِ الْمَوْعُودِ ﴿٢﴾
2. Na siku iliyotolewa kiaga.
وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ ﴿٣﴾
3. Na shahidi na chenye kushuhudiwa.
قُتِلَ أَصْحَابُ الْأُخْدُودِ ﴿٤﴾
4. Wamelaaniwa wenye handaki.
النَّارِ ذَاتِ الْوَقُودِ ﴿٥﴾
5. (Lenye) moto wenye kuni.
إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ ﴿٦﴾
6. Walipokuwa pambizoni mwake wamekaa.
وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِالْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ ﴿٧﴾
7. Na wao, kwa yale wanayowatendea wenye kuamini washuhudia.
وَمَا نَقَمُوا مِنْهُمْ إِلَّا أَن يُؤْمِنُوا بِاللَّـهِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿٨﴾
8. Wala hapana lililowachukiza kwao ila kwamba walimwamini Allah. Mwenye kushinda Mwenye kusifiwa.
الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ ﴿٩﴾
9. Ambaye ni wake ufalme wa mbingu na ardhi. Na Allah ni mwenye kushuhudia kila kitu.
إِنَّ الَّذِينَ فَتَنُوا الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ الْحَرِيقِ ﴿١٠﴾
10. Hakika wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na wanaumini wanawake, kisha wasitubie watapata adhabu ya kuungua.
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْكَبِيرُ ﴿١١﴾
11. Hakika wale ambao wameamini wakatenda amali njema, watapata mabustani yanayopita mito chini yake; huko ndiko kufaulu kukubwa.
إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ ﴿١٢﴾
12. Hakika mashiko ya Mola wako ni makubwa.
إِنَّهُ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ ﴿١٣﴾
13. Hakika Yeye ndiye anayeanza na kurejeza
وَهُوَ الْغَفُورُ الْوَدُودُ ﴿١٤﴾
14. Naye ndiye Mwingi wa kusamehe, Mwenye mapenzi.
ذُو الْعَرْشِ الْمَجِيدُ ﴿١٥﴾
15. Mwenye ufalme mkubwa.
فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ ﴿١٦﴾
16. Mwingi wa kutenda alipendalo.
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْجُنُودِ ﴿١٧﴾
17. Jee, imekujia habari ya majeshi.
فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ ﴿١٨﴾
18. (Ya) Firaun na Thamud.
بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي تَكْذِيبٍ ﴿١٩﴾
19. Lakini ambao wamekufuru wamo katika kukadhibisha.
وَاللَّـهُ مِن وَرَائِهِم مُّحِيطٌ ﴿٢٠﴾
20. Na Allah kwa nyuma yao amewazunguka.
بَلْ هُوَ قُرْآنٌ مَّجِيدٌ ﴿٢١﴾
21. Bali hii ni Qur'an tukufu.
فِي لَوْحٍ مَّحْفُوظٍ ﴿٢٢﴾
22. Katika ubao uliohifadhiwa.
UBAINIFU
Sura ya maonyo na biashara, ndani yake mna makamio kikali kwa wale wanaowaadhibu waumini wanaume na waumini wanawake kwa sababu ya kumwamini kwao Mwenyezi Mungu; kama walivyokuwa washirikina wa Makka wakiwafanyia hivyo wale waliomwamini Mtume(s.a.w.w)
. Wanawaadhibu ili warudie shirki yao ya kwanza. Wakawa katika wao kuna ambao walikuwa wakisubiri wala hawarudi kwa hali yoyote ile na kuna katika wao walikuwa wakirudi na kurtadi nao ni wale wadhaifu wa imani, kama kunavyoonyesha kusema kwake Mwenyezi Mungu:
"Na katika watu kuna wanaosema: tumemwamini Allah lakini wanapoudhiwa katika (njia ya) Allah hufanya vile vituko vinavyowakuta kwa watu kama ni adhabu ya Allah
" (29:10).
Na kusema kwake: "Na katika watu wako wanaomwabudu Allah ukingoni. Ikiwafikia heri hutulia kwayo na ikiwafikia fitina (misukosuko) hubwatika juu ya uso wake (akasunukia, hataki kuuna tena uislamu)
." (22:11). Ametanguliza Mwenyezi Mungu S.W.T. ishara hiyo katika kisa cha wenye handaki, kuwahimiza waumini kuwa na subira katika upande wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) Na akafuatisha kuishiria habari ya askari wa Firaun na Thamud na hilo ni kuituliza nafsi ya Mtume kwa kiaga cha ushindi na kuwatisha wanaomshirikisha Mwenyezi Mungu.
Sura hii imeshuka
Makka kwa ushahidi wa mpangilio wa aya zake.
Aya Ya 1
Neno Buruj lina maana ya kudhihiri, aghlabu kutumiwa kwa jumba kubwa kwa vile linawadhirikia watazamaji. Na jengo lenye kujengwa juu ya ukuta wa mji kwa ajili ya kujikinga huitwa Buruji. Hayo ndiyo makusudio katika aya hii, kutokana na kusema kwake Mwenyezi Mungu: "Na hakika tumeweka katika mbingu, buruj (vituo vya nyota) na tumezipamba kwa ajili ya wale wanaozitazama
". (15:16).
Basi makusudio ya Buruj ni mahali pa nyota katika mbingu. Kwa hivyo inadhihiri kwamba kutafsiri Buruj kuwa ni nyota 12 zilizokubaliwa katika elimu ya nyota sio sawa. Katika aya kuna kiapo kwa mbingu yenye kuhifadhiwa na buruji na kiapo hicho kinanasibiana sana na kisa kitakachoelezewa. Pia kunafuatia kiapo cha makamio na kiaga.
Aya Na 2
Inaungana na Aya Na kwanza. Siku iliyoagwa ni siku ya Kiyama ambayo Mwenyezi Mungu ametoa kiaga kwa kuhukumu baina ya waja wake.
Aya Na 3
Pia inaungana na aya mbili zilizotangulia. Viapo vyote hivyo viko juu ya yale yaliyokusudiwa kubainishwa katika Sura, nayo-kama ilivyotangulia kuelezwa - ni makamio kikali kwa mwenye kuwaudhi waumini wanaume na waumini wanawake kwa sababu ya imani yao. Na kiaga kizuri kwa wale waliomini na wakatenda amali njema. Ni kama vile kusema: "Ninaapa kwa mbingu zenye buruji" ambazo kwa buruj hizo Mwenyezi Mungu anazikinga mbingu hizo na mashetani, hakika Mwenyezi Mungu anaikinga imani ya waumini ni vitimbi vya mashetani na marafiki zao katika makafiri. "Na ninaapa kwa siku iliyotolewa kiaga ambayo watalipwa watu matendo yao. Na ninaapa kwa shahidi anayeshuhudia matendo ya hao makafiri na vile wanavyowafanyia waumini kwa sababu ya imani yao kwa Mwenyezi Mungu. Na ninaapa kwa kile chenye kushuhudiwa atakachokishuhudia kila mmoja".
Juu ya hivyo basi inakubalika kuwa "Shahid" ni Mtume kwa kushuhudia kwake vitendo vya umma wake, kisha atavitolea ushahidi siku ya Kiyama. Na inakubalika kuwa chenye kushuhudiwa ni adhabu ya makafiri kwa sababu ya hawa waumini na yale waliyofanyiwa katika maudhi. Ukipenda unaweza kusema ni malipo yake au unaweza kusema juu ya yale yatakayotukia siku wa Kiyama katika mateso na thawabu kwa hao madhalimu na wadhulimiwa. Kuna kauli nyingi juu ya tafsiri ya shahidi na chenye kushuhudiwa; baadhi yao wamefikisha kauli thelathini (30). Kama vile kuwa shahidi ni siku ya Ijumaa na chenye kushuhudiwa ni siku ya Arafa, Siku ya Idd na siku ya Arafa, siku ya Arafa na siku ya Kiyama, kuwa shahidi ni Malaika wanaowashuhudia wanaadamu na chenye kushuhudiwa ni siku ya Kiyama, kuwa shahidi ni ni siku ya Kiyama. Na kuwa shahidi ni wale wanaowashuhudia watu na chenye kushudiwa ni wale wanaoshuhudiwa.
Vile vile kuwa shahidi ni umma huu na chenye kushuhudiwa ni umma wengineo. Shahidi ni viungo vya binadamu na chenye kushuhudiwa ni nafsi zao. Shahidi ni jiwe jeusi (Hajarul-Aswad) na chenye kushuhudiwa ni mwenye kuhiji. Shahid ni Mitume na chenye kushuhudiwa ni Mtume Muhammad(s.a.w.w)
ni kwamba shahidi ni Mwenyezi Mungu na chenye kushudiwa ni tamko la Lailah illa llah. Pia iko kauli kuwa shahidi ni Mwenyezi Mungu na chenye kushuhudiwa ni siku ya Kiyama. Shahidi ni Adam na kizazi chake na chenye kushuhudiwa ni siku ya Kiyama. Shahidi ni siku ya Tarwiya na chenye kushudiwa ni siku ya Arafa, siku ya Jumatatu na Ijumaa. Shahidi ni wenye kukurubisha na chenye kushuhudiwa ni illiyuuna. Shahidi ni mtoto ambaye alimwambia mama yake. "Subiri hakika wewe uko kwenye haki" katika kisa cha wenye handaki na chenye kushuhudiwa ni tukio lenyewe na kauli kuwa shahid ni Malaika wanaofuatilia kuandika vitendo, na chenye kushudiwa ni Qur'an ya Al-fajr na kauli nyengine nyingi.
Nyingi katika kauli hizi zinachukulia ushahidi kwa maana ya kutekeleza yale yaliyochukuliwa katika ushahidi na baadhi yake zinatofautisha kati ya shahidi na chenye kushuhudiwa katika maana ya ushahidi na umekwishajua udhaifu wake. Linalonasibu zaidi ni kuchukua ushahidi kwa maana ya kuona ijapokuwa unalazimisha maana ya kutekeleza siku ya Kiyama na kwamba ushahidi unakubaliana kufungamana na Mtume(s.a.w.w)
. Vipi isiwe hivyo na hali Mwenyezi Mungu amemwita shaahid aliposema: "Ewe Mtume hakika sisi tumekutuma (uwe) shahidi na mtoaji habari nzuri na mwonyaji
". (33:45).
Na amemwita shaahid aliposema: "ili awe Mtume shahidi juu yenu
." (22:78). Kisha jawabu la kiapo limeondolewa linajulishwa na kusema kwake: "Hakika wale ambao wamewaudhi waumini wanaume na waumini wanawake" mpaka mwisho wa aya mbili. Vile vile hilo jawabu la kiapo linafahamishwa na kusema kwake: "Wamelaaniwa wenye handaki
." na hicho ni makamio cha wale wanaoudhi na ni ahadi kwa waumini wema kwamba Mwenyezi Mungu atawawafikisha kwa subira na atawapa nguvu juu ya kuhifadhi imani yao kutokana na vitimbi vya wachimba vitimbi, ikiwa watafanya Ikhlas (kumtakashia Mwenyezi Mungu amali) kama walivyofanya waumini katika kisa cha handaki.
Aya Na 4
Ni ishara ya kisa cha handaki ili iwe ni mwanzo wa yatayokuja katika kauli yake "Hakika wale ambao wamewaudhi
" na sio jawabu la kiapo kabisa. Watu wa handaki ni wale waliochimba handaki na kuwasha moto ndani yake, kisha wakawaumuru waumini waingie ndani yake wakawachoma kwa kuwatesa kwa ajili ya imani yao. Na neno Wamelaaniwa ni dua ua kuwaombea laana. Imesemwa kwa makusudio ya watu wa handaki ni waumini wanaume na waumini wanawake waliochomwa ndani ya handaki na kwamba neno Qutila ni kwa maana ya kuuliwa yaani kuuliwa hao waumini kwa kuchomwa, na wala sio dua ya laana. Lakini hayo yanadhoofishwa na kudhihiri dhamiri katika jumla ya walipokuwa pambizoni mwake, wao kwa yale wayatendayo na hapana lililowachukiza kwao. Dhamiri zote hizo haziwezi kuwarudia waumini.
Aya Na 5
Kuusifu moto wenye kuni ni ishara ya kuonyesha ukali wa moto na mwako wake.
Aya Na 6
Pambizoni mwake ni huo moto yaani hao watu makatili wenye kiburi walikuwa wamekaa pambizoni mwa huo moto.
Aya Na 7
Yaani waumini wanaona na kushuhudia kuunguzwa kwao.
Aya Na 8-9
Yaani walichukizwa na imani yao. Kuanzia mwenye kushinda mpaka mwisho wa Aya Na 9 ni sifa zenye kupita katika jina la Mwenyezi Mungu zinazoonesha kuwa hao waumini. Walikuwa juu ya haki katika imani, wenye kudhulumiwa katika waliyofanyiwa, haijifichi hali yao kwa Mwenyezi Mungu na atawalipa malipo mema na kwamba hao makatili walikuwa kwenye batili wenye kumkosea Mwenyezi Mungu, madhalimu kwa waliyoyafanya na wataonja ubaya wa mambo yao. Hilo ni kwamba Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kushinda, mwenye kusifiwa, yaani yeye ni mshindi asiyeshindika kwa hali yoyote, ni mzuri katika vitendo vyake, ni wake peke yake kila utukufuru na uzuri. Kwa hivyo ni wajibu kumnyenyekea na kutompinga. Ikiwa ni wake ufalme wa mbingu na ardhi basi yeye ni mwenye kumiliki hali zote, amri ni yake na hukumu ni yake, Yeye ni bwana wa viumbe vyote. Hivyo ni wajibu kumfanya ni Mola wa kuabudiwa na kutomshirikisha na yoyote. Basi waumini wako kwenye haki na makafiri wako katika upotevu.
Kisha hakika Mwenyezi Mungu- ambaye ndiye aliyepatisha kila kitu- juu ya kila kitu ni mwenye kushuhudia, hakifichiki kwake kitu chochote katika viumbe vyake wala vitendo vyovyote katika vitendo vya viumbe vyake wala haifichiki hisani na mwenye kufanya hisani au uovu wa mwenye kufanya uovu, atamlipa kila mmoja kwa aliyoyafanya. Kwa ujumla, ikiwa Mwenyezi Mungu mwenye kutukuka ndiye mwenye kusifika na sifa hizi tukufu itakuwa ni juu ya hao waumini kumwamini, na ni jambo lisilotakikana kwa hao maharamia kuwaingilia waumini wala kuwafanyia uovu wowte.
Baadhi ya wafasiri wamesema kuhusu makusudio ya kuleta sifa katika aya: Hao watu ikiwa walikuwa ni washirikina, basi jambo liliokuwa likiwaudhi kutokana na waumini halikuwa ni kumwamini Mwenyezi Mungu Mtukufu, bali lilikuwa ni kukanusha yale yasiyokwuwemo katika ibada zao batilifu. Na kama walikuwa ni wakanushaji wa sifa za Mwenyezi Mungu, basilinalowaudhi ni kuthibitisha Mwenye kuabudia wasiyemzoea. Lakini ilivyokuwa makusudio ya mambo yote hayo mawili (kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kukanusha sifa), ni kumkanusha mwenye kuabudiwa kwa haki mwenye kusifika na sifa za uungu na utukufu, basi ndipo zikaletwa ibara za sifa za Mwenyezi Mungu (s.w.t).
Katika mghafala waliokuwa nao makafiri ambao ni waabudu masanamu, hawakuwa wakinasibisha kwa Mwenyezi Mungu isipokuwa kutengeneza na kupatisha tu! Ama uungu ambao unawajibisha ibala walikuwa wakitosheka na waungu wao tu! Mwenyezi Mungu kwao alikuwa ni Mungu wa waungu tu! Na sio zaidi ya hapo.
Aya Na 10
Neno Fitna hapa ni kwa maana ya misukosuko na adhabu, na hilo linaenea kwa watu wa handaki na makafiri wa kiquraysh waliokuwa wakiwaadhibu wenye kumwamini Mtume(s.a.w.w)
katika waumini wanaume na waumini wanawake kwa aina za adhabu ili warudi katika dini yao. Amesema katika Majmau "pameulizwa vipi kutofautisha kati ya adhabu ya Jahannam na adhabu ya kuungua? Pakajibiwa kwamba makusudio yake ni kwamba wao wana aina za adhabu katika Jahannam ambazo sio kuungua mfano Zakkum(mti wa uchungu), maji ya ushaha na marungu, pamoja na hayo watachomwa kwa moto.
Aya Na 11
Kiaga kizuri kwa waumini cha kuzituliza nafsi zao.
Aya Na 12
Aya hiyo na zinazofuatia mpaka kutimia Aya Na saba ni kuhakikisha na kutilia mkazo yaliyotangulia katika makamio na kiaga kwa makafiri na ahadi ya waumini. Kutegemeza neno "Mashiko" Kwa Mola na kutegemeza neno mola kwa dhamiri ya mwenye kuambiwa ni kuituliza nafsi ya Mtume(s.a.w.w)
kwa kumpa nguvu na ushindi na kuonyesha kuwa watu wenye kiburi katika umati wake, vile vile wana fungu katika makamio yaliyotangulia kuelezwa.
Aya Na 13
Neno Yubdiu kwa kulilinganisha na Yuid lenye maana ya kurejeza, lina maana ya kuanza. Wamesema halikusikika neno hilo kwa waarabu, lakini kisomo kiko hivyo. Katika baadhi ya visomo vyengine visivyokuwemo katika istihali husomwa kwa fatha ya yei na dali Yabdau. Kwa vyovyote iwavyo aya iko mahali pa ila (sababu) ya ukali wa mashiko yake Mwenyezi Mungu (s.w.t).
Hilo ni kwamba yeye Mwenyezi Mungu mwenye kutukuka ni mwenye kuanza. Hupatisha kila anachokikusudia kupatisha kwa kuanza bila ya kumtegemea mwengine. Yeye Mwenyezi Mungu atarudisha kila kilichokuwa vile kilivyokuwa. Yeye Mwenyezi Mungu S.W.T hazuiliki na alilokusudia wala halimpiti. Ikiwa ni hivyo, basi yeye ni muweza wa kumchukulia hatua ya adhabu ya zaidi ya uwezo wake yule mwenye kupetuka mpaka wake, na kumhifadhi juu ya yale aliyo nayo, ili aonje adhabu, Mwenyezi Mungu anasema: "Na wale ambao wamekufuru wana wao moto wa Jahannam, hawatahukumiwa kufa, wala kawatapunguziwa adhabu yake
" (35:36).
Yeye nu muweza juu ya kurudisha vile vilivyoharibiwa na adhabu katika hali yake ya kwanza, ili aonje mkosaji adhabu bila ya kwisha; Mwenyezi Mungu anasema: "Hakika wale ambao wamezikanusha aya zetu, tutawaingiza katika moto. Kila ngozi zao zitakapoiva, tutawabadilisha ngozi nyingine ili wawe wanaonja (uchungu wa) adhabu
." (4:56).
Kwa ubainifu huu yanafunuka mamba hAya Na fuatayo:
kwanza
: Mpangilio wa kauli yake "Hakika yeye" mpaka mwisho unafahamisha kuwa kuanzisha kupatisha na kurudisha ni kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t), kwa sababu matengenezo na kupatisha kunakomea kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) peke yake.
Pili
: Mipaka ya vitu vyote iko kwake Mwenyezi Mungu akitaka kitu kisiwe na mpaka, huwa; au kubadilisha mpaka mwengine. Yeye ndiye ambaye ameweka mpaka (ukomo) wa adhabu ya dunia kuwa ni mauti, na lau asingelitaka kuiweka ukomo angefanya kama ilivyo katika ahabu ya akhera. Tatu: Kwamba makusudio ya mashiko makubwa ni kwamba hakuna wa kumzuia Mwenyezi Mungu na adhabu yake wala haukna wa kuipinga hukumu yake vyovyote vile anavyohukumu.
Aya Na 14
Yaani ni mwingi wa maghufira na mapenzi kwa kuangalia ahadi ya waumini; kama ilivyo katika aya iliyotangulia kwa kuangalia kiaga cha makafiri.
Aya Na 15-16
Arshi ni arshi ya ufalme. Kusema: Mwenye arshi ni fumbo la ufalme yaani Yeye ni mfalme anaweza kufanya vile atakavyo katika mamlaka yake. Mwenye kutenda alipendalo yaani haligeuki analolitaka, si kwa sababu ya ndani kama vile uvivu au kuchoka, wala kwa sababu za nje kwa kizuizi kitakachoingia kati yake na kati ya analolitaka. Kwa hivyo anaweza kuwapa kiaga wale waliowaadhibu waumini wanaume na waumini wanawake kwa moto na kuwaahidi wale walioamini na wakatenda amali njema kwa pepo kwa sababu Yeye ndiye mwenye arshi tukufu, wala hawezi kuvunja ahadi yake, kwa sababu Yeye ni mwingi wa kutenda alipendalo.
Aya Na 17-18
Ni tikrari ya yaliyotangulia katika mashiko yake Mwenyezi Mungu Mtukufu, kuwa Yeye ni mfalme mkubwa mwenye kutenda alitakalo. Na hilo nikuituliza nafsi ya Mtume(s.a.w.w)
Aya Na 19
Sio mbali kutokana na mpangilio wa aya kuwa makusudio ya wale ambao wamekufuru ni katika kaumu ya mtume Muhammad(s.a.w.w)
. Aya inaonyesha kususiwa mauidha yaliyotangulia, yaani haitakikani kutarajia kwao kuamini aya hizi zilizowazi, kwani wale ambai wamekufuru ni wenye kuendelea na kukabidhisha kwao, hawatanufaika na mawaidha au joha.
Aya Na 20
Nyuma ya kitu ni pambizoni mwake mnamokizunguuka. Inaonyesha kawaba wao hawawezi kumshinda Mwenyezi Mungu Yeye ni Mwenye kuwazuguuka ni muweza juu yao kwa kila upande. Na hilo pia ni katika kuituliza nafsi ya Mtume(s.a.w.w)
.
Aya Na 21-22
Ni kupinga kuendelea kwao Kuikadhibisha Qur'an. Maana yake nikuwa sio kama wanavyodai, bali Qur'an ni kitabu kikubwa katika maana yake chenye kushinda katika maarifa yake kiko katika ubao wenye kuhifadhiwa na uongo na batili, na yeye ni yenye kuhifadhiwa kuguswa na shetani.
Utafiti Wa Hadith Katika Durril Manthur ametoa Ibnu Murdawayh kutoka kwa Jabir bin Abdillah kwamba Mtume(s.a.w.w)
aliulizwa kuhusu mbingu yenye buruji akasema ni nyota. Akaulizwa kuhusu "ambaye amejaaliwa katika mbingu buruji" akasema ni nyota. Akaulizwa kuhusu Buruujum mushayyadah akasema ni majumba makubwa. Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Abdu bin Hamid Attrimidhiy na Ibn Abidduniya katika Usuul; Ibn Jariyr, Ibn Al-Mundhir, Ibn Hatim, Ibn Murdawayh na Bayhaqi katika Sunan yake kutoka kwa Abu Huraira amesema: Amesema Mtume(s.a.w.w)
: siku iliyoagwa ni siku ya Kiyama na siku yenye kushuhudiwa ni siku ya Arafa na shahidi ni siku ya Ijumaa.
Imepokea hadith mfano wa hiyo kwa njia nyengine kutoka Abu Malik Said Bin Al-Musabbib na Jubayr bin Mut'imu kutoka kwake Mtume(s.a.w.w)
; Shahid ni siku ya Ijumaa na chenye kumshuhudiwa ni siku ya Arafa. Imepokewa kwa tamko hili kutoka kwa Abdurrazzaq, Fariyabiyy, Abdu bin Hamid, Ibn Jariyr na Ibn Mundhir kutoka kwa Ali bin Abu Twalib. Katika hiyo hiyo Durril Manthur ametoa Ahmad bin Hamid, Ibn Al-Mundhir kutoka kwa Ali amesema: siku iliyoagwa ni siku ya kiyama, shahidi ni siku ya ijumaa na chenye kushuhudiwa ni siku ya Idd ((Idd-el-Hajj)
Katika Majmau imepokewa kwamba mtu mmoja alingia katika msikiti wa Mtume(s.a.w.w)
mara ikawa mtu mmoja anazungumzia Mtume(s.a.w.w)
. Amesema: "nikaamuliza kuhusu Shahid na mwenya "kushuhudiwa", akasema: Ndio shahidi ni siku ya Ijumaa na chenye kushuhudiwa ni siku ya Arafa, nikampita na kumfuata mwengine naye pia anamzungumzia Mtume(s.a.w.w)
nikamuuliza hilo, akasema: "ama shahid ni siku ya Arafa na chenye kushuhudiwa ni siku ya Idd." Nikawapita wote hao wawili nikaenda kwa kijana uso wake kama Dinar naye anamzungumzia Mtume(s.a.w.w)
, nikamwambia: "nifahamishe kuhusu shahidi na chenye kushuhudiwa", akasema: ndio ama shahidi ni Muhammad na chenye kushuhudiwa ni siku ya Kiyama kwani hukusikia kauli yake Mwenyezi Mungu?: "Ewe Mtume hakika sisi tume kutuma (uwe) shahidi na mtoaji habari nzuri na mwonyaji
?" (33:45)
Akaendelea kusema: hiyo siku ya kukusanya watu, ndiyo siky yenye kushuhudiwa. Nikauliza ni nani yule wa kwanza? Wakasema: ni Ibn Abbas, wapili ni Ibn Amr na watu wakasema ni Hasan bin Ali." Hadith hiyo ni yenye kupokewa kwa njia tofauti na matamko yenye kukurubiana. Imetangulia katika tafsir ya aya kwamba aliyoyasema Hasan
ndiyo yaliyo wazi zaidi kwa kuangalia mpangilio wa aya, ingawaje tamko la shahidi na chenye kushuhudiwa halikatai kufungamana na jambo jengine vile vile.
Katika Tafsir ya Qummi kuhusu "wamelaaniwa wenye handaki" anasema: sababu yake ni kwamba yule ambaye aliitingisha Uhabeshi kwenye vita vya Yaman ni Dhu Nawas naye ndiye mfalme wa mwisho katika ukoo wa Himyar, aliingia katika dini ya Uyahudi na akawakusanya watu wa kabila ya Himyar na kuwafanya kuufuata Uyahudi. Yeye akajiita Yusuf na alidumu hivyo kwa muda mrefu. Akapata habari kwamba huko Najran kuna watu wamebaki kwenye dini ya Unasara (Ukristo) na wanahukumu kwa Injili na kiongozi wa dini hiyo ni Abdallah bin Baryam. Kwa hiyo akachukuwa watu wa dini yake kuwaendea hao Manasara ili wawaingize katika dini ya Kiyahudi. Alipofika Najran akawakusanya wale waliokuwa katika dini ya Kinasara kisha akawelezea dini ya Kiyahudi na kuwahimiza waingie. Akajadiliana nao na akatoa jitahad zake zote lakini walikataa na wakajizulia kuingia dini ya Kiyahudi.
Basi akafanya handaki, akakusanya kuni na akawasha moto. Kuna katika wao waliounguzwa wengine waliouliwa kwa upanga na akawafanyia vya kufanya, ikafikia iadadi ya waliouawa 20,000 (ishirin elfu). Akawaponyoka mtu mmoja anyeitwa Dawshi Dhu Thaalaban na farasi wake, wakamfuata mpaka akawashinda kwa mbio, akarudi Dhu nuwasi kwa askari wake. Ndio Mwenyezi Mungu akasema "wamelaaniwa wenye handaki mpaka mwisho wa Aya Na 8."Katika Majmau amepokea Said bin Jubayr amesema: waliposhindwa watu wa Isfand-han alisema Umar bin Al-Khattab: wao sio wayahudi wala wanasara wala hawana kitabu chochote na walikuwa ni Majusiy, akasema Ali bin Abi Twalib: Hapana wao walikuwa nacho kitabu, lakini kikaondolewa. Sababu ya kuondokwa kitabu nikwamba mfalme wao siku moja alilewa akamwingilia binti yake au dada yake, ulevi ulipomtoka akamwambia: "Itakuwaje kwa nililyoyanfanya? Akamjibu: "Wakusanye watu na mamlaka yako na uwaambie kwamba wewe unapendekeza watu kuonana na mabinti zao na kwamba wewe unawaamrisha walihalilishe hilo."
Kwa hivyo akawakusanya na akawapa habari ya hilo. Wakakataa kumfuata. Akawachimbia handaki katika ardhi na akawasha moto. Ikawa mwenye kukataa humtupa katika moto na mwenye kukubali humwacha. Imepokewa hadith kwa maana haya katika Durril Manthur kutoka kwa Abd bin Hamid kutokana naye Ali
. Katika Tafsir ya Iyashi, imepokewa kutoka kwa Jabir
amesema: Alitumwa Ali
kwa askofu wa kinajrani kumuuliza kuhusu wnye handaki, akamuelezea, kisha Ali
akamwambia sio kama ulivyosema, lakini nitakueleza: "Hakika Mwenyezi Mungu alimpa utume mtu mmoja wa Kihabeshi, wakamkadhibisha na kupingana naye. Wakawaua wafuasi wake, wakateka nyara na wafuasi wake. Kisha wakamjengea boma wakalijaza moto.
Wakawakusanya watu wakawaambia: "Ambaye yuko kwenye dini yetu na mambo yetu na ajitenge na ambaye tuko kwenye dini ya hawa na ajitupe mwenyewe moto. Wakawa wafuasi wake wanashindana kujitupa katika moto. Akaja mwanamke na mtoto mdogo wa mwezi mmoja. Alipotaka kujitupa aliogopa na akamuhurumia mtoto wake. Mtoto akanadi: 'usiogope nitupe mimi wa wewe katika moto kwani hakika Wallahi adhabu hii kwa Mwenyezi Mungu ni chache'. Akajitupa katika moto pamoja na mwanawe. Na huyo mtoto akawa miongoni mwa waliozungumza uchangani." Imepokewa hadith kwa maana haya katika Durril Manthur kutoka kwa Ibn Murdawayh, naye kutoka kwa Abdillahi bin Naja naye kutokana na Ali
. Vile vile imepokewa kutoka kwa Ibn Hatim, Ibn Al-Mundhir katika njia ya Hasan kutokana na Ali
kuhusu "wenye handaki" amesema hao ni wahabeshi.
Sio mbali kufahamika kwamba hadith ya wenye handaki ni matukio mbali mbali yaliyotukia uhabeshi, Yemen na Uajemi. Ziko hadith zinazozungumzia kisa chake bila ya kutaja mahali maalum pa tukio lenyewe. Katika Tafsiri ya Qummi kuhusu aya "bali hii ni Qur'an tukufu katika ubao uliohifadhiwa" una ncha mbili kuumeni mwa Arshi kwenye paji la Israfil, anaposema Mwenyezi Mungu ambaye umetukuka utajo wake - wahyi, ubao hupiga paji la Israfil naye huangalia kwenye ubao na kuupeleka wahyi kwa Jibril".
Katika Durril Manthur ametoa Abu Shaykh, na Ibn Murdawayh kutoka kwa Ibn Abbas amesema: 'amesema Mtume(s.a.w.w)
: ameumba Mwenyezi Mungu ubao kutokana na lulu nyeupe. Umezungushiwa Zabrajad ya kijani, maandishi yake ni ya nuru, huchunguzwa mara mia tatu na sitini (360) kila siku. Anahuisha na kufisha. Anaumba na kuruzuku. Anatukuza na kudhalilisha na anafanya analotaka.' Riwaya kuhusu Lawh ni nyingi zenye kuhitalifiana, nazo ziko juu ya namna ya kufananisha tu!.