TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Mwandishi:
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
Kundi:

Matembeleo: 35766
Pakua: 3060


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Juzuu 9 Juzuu 10 Juzuu 11
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 20 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 35766 / Pakua: 3060
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

Mwandishi:
Swahili

14

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ لَا تَعْبُدُونَ إِلَّا اللَّـهَ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَقُولُوا لِلنَّاسِ حُسْنًا وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ ثُمَّ تَوَلَّيْتُمْ إِلَّا قَلِيلًا مِّنكُمْ وَأَنتُم مُّعْرِضُونَ﴾

83.Na tulipochukua ahadi na wana wa Israil: Hamtamwabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu; na muwafanyie wema wazazi na jamaa na mayatima na maskini; na semeni na watu kwa uzuri na simamisheni swala na toeni zaka. Kisha mkageuka isipokuwa wachache tu katika nyinyi na nyinyi mnakengeuka.

AHADI NAWANAWA ISRAIL

Aya 83

AYA HII IMEKUSANYA MAMBO YAFUATAYO

I. Kuwatendea wema wazazi wawili Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameikutanisha shukrani ya wazazi wawili na yake na akawajibisha kuwatendea wema na ku-wafanyia hisani; sawa na alivyowajibisha kuabudiwa kwake. Kuanzia hapa ndio mafakihi wamesema kwa kauli moja kwamba kuwaasi wazazi wawili ni katika madhambi makubwa, na kwamba mwenye kuwaasi ni fasiki hauwezi kukubaliwa ushahidi wake. Hadith tukufu inasema: Hakika mwenye kuwaudhi wazazi wawili hatapata harufu ya pepo. Makusudio ya kuwatendea wema wazazi wawili ni kuwatii na kuwachukulia upole.

Kuna kisa cha mwanamke mmoja aliyembeba baba yake mgongoni kutoka Yemen mpaka Makka. Akatufu naye katika Al-Kaaba. Mtu mmoja akamwambia Mwenyezi Mungu akulipe heri, umetekeleza haki yake. Akasema: Hapana sijatekeleza; yeye alikuwa akinibeba huku akinitakia uhai (niishi) na mimi hivi sasa ninambeba huku nikimtakia mauti (afe).

II. Jamaa, Mayatima na Maskini Aya imewajibisha muungano wa udugu kwa kuungana kwake na wazazi wawili. Pia imewajibisha kumchunga yatima na mali yake kwa yule ambaye atakuwa ni walii (msimamizi) au wasii wa yatima huyo. Vile vile Aya imemwajibishia fakiri fungu katika mali za matajiri.

III. Kuchukulia usahihi Kama mtu akifanya amali yoyote au akisema kauli yoyote inawezekana iwe sahihi au isiwe sahihi. Sasa je, uchukuliwe usahihi juu ya kitu chochote au la; au ni lazima iweko dalili mkataa? Mfano kumwona mtu pamoja na mwanamke, hujui kama ni mkewe au ni mtu kando. Au usikie maneno nawe hujui kuwa msemaji alikusudia wewe au la. Mafakihi wameafikiana kuchukulia usahihi katika hilo (afanyalo si kosa) na mfano wake. Wametolea dalili hilo kwa kauli yake Mwenyezi Mungu: Na semeni na watu kwa uzuri.

Amirul Muminin Ali(a.s) naye amesema:Liweke jambo la ndugu yako juu ya uzuri wake.

Vile vile kwa kauli ya Imam Jafar Sadiq(a.s) :Yakadhibishe masikio yako na macho yako kwa ndugu yako. Wakitoa ushahidi kwako watu hamsini kwamba yeye amesema kadhaa, na yeye akuambie sikusema, basi mwamini yeye na uwachukulie kuwa ni waongo wale watu hamsini.

Huu ndio msingi wa kiutu hasa. Kwa sababu unajenga heshima ya mtu na unatilia mkazo mfungamano wa kusaidiana na kuchukuliana upole kati ya watu, na unawaepusha na yale yanayoleta chuki. Kwa hivyo basi, inabainika kuwa Uislamu haujishughulishi na itikadi na ibada pekee, bali unajishughulisha na utu na heri zake na unaonyeshea njia itakayopelekea uhai wenye matunda ya kufaulu. Lakini wale ambao wameiuza dini yao kwa shetani wameupoteza msingi huu wa kiutu, wakaenda kombo na malengo yake; na wakaboresha kazi ya uharamia na kuchukua riba. Ilivyo hasa kama tulivyoonyesha ni kwamba msingi wa kuchukulia usahihi haufungamani na kazi ya unyanganyi, ujambazi, kupoteza na mengineyo yanayofanana na hayo, ambayo tunayajua kwa yakini kuwa ni katika mambo ya haramu na yenye kuangamiza. Isipokuwa msingi huo tuliotaja unakuwa katika mambo ambayo yana uwezekano wa kuwa kweli au uwongo, usawa au upotevu.

﴿وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَكُمْ لَا تَسْفِكُونَ دِمَاءَكُمْ وَلَا تُخْرِجُونَ أَنفُسَكُم مِّن دِيَارِكُمْ ثُمَّ أَقْرَرْتُمْ وَأَنتُمْ تَشْهَدُونَ﴾

84.Na tulipochukuwa ahadi yenu kuwa Hamtamwaga damu zenu, wala hamtatoana majumbani mwenu; nanyi mkakubali na hali mnashuhudia.

﴿ثُمَّ أَنتُمْ هَـٰؤُلَاءِ تَقْتُلُونَ أَنفُسَكُمْ وَتُخْرِجُونَ فَرِيقًا مِّنكُم مِّن دِيَارِهِمْ تَظَاهَرُونَ عَلَيْهِم بِالْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ وَإِن يَأْتُوكُمْ أُسَارَىٰ تُفَادُوهُمْ وَهُوَ مُحَرَّمٌ عَلَيْكُمْ إِخْرَاجُهُمْ أَفَتُؤْمِنُونَ بِبَعْضِ الْكِتَابِ وَتَكْفُرُونَ بِبَعْضٍ فَمَا جَزَاءُ مَن يَفْعَلُ ذَٰلِكَ مِنكُمْ إِلَّا خِزْيٌ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يُرَدُّونَ إِلَىٰ أَشَدِّ الْعَذَابِ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴾

85.Kisha nyinyi hao hao, mnajiua watu na mnawatoa baadhi yenu majumbani mwao, mkisaidiana dhidi yao kwa (njia ya) dhambi na uadui. Na wakiwajia mateka mnawakomboa na hali kumeharamishwa kwenu kuwatoa. Je mnaamini baadhi ya kitabu na kukataa baadhi? Basi hakuna malipo kwa mwenye kufanya haya katika nyinyi ila fedheha katika maisha ya dunia, na siku ya Kiyama watarudishwa kwenye adhabu kali; na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayoyatenda.

﴿أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ اشْتَرَوُا الْحَيَاةَ الدُّنْيَا بِالْآخِرَةِ فَلَا يُخَفَّفُ عَنْهُمُ الْعَذَابُ وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ ﴾

86.Hao ndio walionunua maisha ya dunia kwa akhera, kwa hivyo hawatapunguziwa adhabu wala hawatanusuriwa.

HAMTAMWAGA DAMU ZENU

Aya 84 - 86

MAELEZO

Mazungumzo ya Mayahudi na matatizo yao hayajakwisha; na yanayokuja ni mengi. Kwa muhtasari wa Aya za Mayahudi, ni kwamba: wao kila wanapopewa mwito wa uongofu na msimamo mzuri wanakakamia katika kueneza ufisadi duniani na wanaendelea katika upotevu, kama kwamba wao wameumbwa kumuasi Mwenyezi Mungu na kuikhalifu haki. Tawrat yao inawaamrisha kumwabudu Mwenyezi Mungu, wao wanaabudu ndama; Musa anawaambia: Hii Tawrat kutoka kwa Mwenyezi Mungu, wao wanasema; Tuonyeshe huyo Mwenyezi Mungu wazi wazi. Tena Musa anawaambia: Zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu kwenu na mumwombe msamaha, wao wanafanya mzaha na stihizai.

Ikiwa Nabii Musa(a.s) tu walimfanyia hivyo naye ni Mwisrail mwenzao, je mwingine watamfanyiaje? Mfalme Edward I aliwafukuza Uingereza na wakateswa na Hitler huko Ujerumani baada ya kuwajua walivyo.Wao wanastahili zaidi ya hayo. Tumekwishaeleza vile walivyofanyiwa na Firaun, Nebukadnezzar na Warumi. Kwa vyovyote ilivyo ni kwamba miongoni mwa ahadi alizozichukua Mwenyezi Mungu kwa Mayahudi katika Tawrat ni kutouana wenyewe kwa wenyewe wala wasimtoe yeyote katika nyumba yake. Na Mayahudi hawakanushi ahadi hizi, bali hawana nafasi ya kuzikanusha kwa sababu zinapatikana katika Tawrat ambayo wanaiamini kwa ukweli na kwamba hiyo ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Lakini pamoja na hayo yote waliikhalifu kwa makusudi, kwa hivyo ikawasimamia hoja.

MAANA

Na tulipochukuwa ahadi yenu kuwa hamtamwaga damu zenu wala hamtatoana majumbani mwenu. Anarudia Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuwakumbusha Wana wa Israil ahadi walizoziweka kwa ulimi wa Musa na Mitume wengine waliokuwa baada yake. Miongoni mwa ahadi hizo ni kutomwaga damu na kutotoana majumbani mwao.Nanyi mkakubali na hali mnashuhudia . Yaani mlikubali ahadi na kushuhudiana nyinyi wenyewe. Unaweza kuuliza: Kukubali na kushuhudia ni kitu kimoja, sasa vipi ikafaa kuunganisha kitu kwa kitu chenyewe?

Jibu : Inawezekana kuwa ni katika upande wa kutilia mkazo. Vile vile inawezekana kuwa makusudio ya kukubali ni kukubali Mayahudi wa zamani na kushuhudia ni kwa watakaokuja. Kwa sababu wa zamani walikubali na wakakiri ahadi.

Kisha nyinyi hao hao mnajiua, na mnawatoa baadhi yenu majumbani mwao. Yaani nyinyi baada ya kukiri kwenu ahadi, mnaivunja wenyewe, mwenye nguvu anamuua mnyonge na kumtoa katika nyumba yake. Mkisaidiana dhidi yao kwa (njia ya) dhambi na uadui. Aya inaonyesha kugawanyika Mayahudi na kusaidiana kila kikundi na Waarabu dhidi ya kikundi kingine cha Mayahudi.

KISA

Kwa ufupi kisa kilikuwa hivi: Aus na Khazraj ni koo mbili za Kiarabu zenye asili moja, kwa sababu Aus na Khazraj walikuwa ndugu. Koo mbili hizi zilikuwa na uadui na vita kati yao kabla ya Uislamu na walikuwa wakimshirikisha Mwenyezi Mungu, hawajui pepo wala moto wala Kiyama au Kitabu.

Na Mayahudi nao walikuwa na koo tatu: Bani Qaynuqaa, Bani Quraidha na Bani Nadhir, nao walikuwa na uadui na vita kama ilivyokuwa kati ya Aus na Khazraj pamoja na kuwa hawa Mayahudi walikuwa katika asili moja na dini yao ni moja. Wote hao, Mayahudi na Waarabu walikuwa ni wakazi wa Madina. Bani Qaynuqaa walikuwa wakisaidiana na Aus dhidi ya Bani Nadhir na Quraidha; kama ambavyo Bani Nadhir na Bani Quraidha walikuwa wakisaidiana na Khazraj dhidi ya Qaynuqaa. Vita vinapochacha Myahudi alikuwa akimuua ndugu yake Myahudi na kumtoa nyumbani kwake akiweza. Lakini kama Yahudi akitekwa na Mwarabu, basi Mayahudi hukomboana hata kama ni adui yake mkubwa.

Kwa ufupi ni kwamba Mayahudi hawaoni kizuizi kuwaua Mayahudi wenzao kiasi cha kusaidiana na Waarabu, lakini Mwarabu akimteka nyara Yahudi, basi Yahudi mwenzake huingiwa na huruma na kutoa fidia kumkomboa mwenzake ingawaje ni adui yake. Kwa hivyo Yahudi anahalalisha kumuua ndugu yake na kumfukuza, lakini asiwe mateka. Walikuwa wakidai kwamba Tawrat yao ndiyo inayowaamrisha kukomboa mateka wa Kiyahudi. Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu kwamba Tawrat yao vile vile imewaamrisha kutouana na kutotoana majumbani; sasa vipi mmeiasi Tawrat katika kuua, na kuitii katika kukomboa mateka? Hii ndiyo tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na wakiwajia mateka mnawakomboa na hali kumeharamishwa kwenu kuwatoa. Je mnaamini baadhi ya kitabu na kukataa baadhi?

Walilolikataa ni kule kukatazwa kuua, kusaidiana katika dhambi na uadui na kutoana majumbani. Waliloamini, ni lile la kutoleana fidia mateka. Na hii ndiyo istihzai hasa na kucheza na dini.

Unaweza kuuliza, lenye kuharamishwa kwao ni kuua na kusaidiana na kutoana majumbani; kwa nini Mwenyezi Mungu amehusisha kutoana majumbani katika Aya hii?

Jibu : Ndio yote ni haramu, lakini Mwenyezi Mungu amehusisha kutoana kwa kutaja mara ya pili kwa sababu ya kutilia mkazo tu. Kwa sababu kutoana majumbani huendelea, kinyume na kuua kama walivyosema wafasiri wengine.Basi hakuna malipo kwa mwenye kufanya haya katika nyinyi ila fedheha katika maisha ya duniani. Malipo yanaweza kuwa ya heri au ya shari; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

﴿ وَجَزَاهُم بِمَا صَبَرُوا جَنَّةً وَحَرِيرًا ﴾

Na malipo yao kutokana na vile walivyosubiri ni pepo na nguo za hariri. (76:12)

﴿ وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا﴾

Na mwenye kumuua mumin kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam, humo atadumu... (4:93)

Hao ndio walionunua maisha ya dunia kwa akhera; kwa hivyo hawatapunguziwa adhabu wala hawatanusuriwa. Mwenyezi Mungu hakuharamisha, katika Aya hii wala nyingine chakula kizuri na mavazi ya kifahari, isipokua anamkemea mwenye kuiuza dini yake kwa ajili ya dunia yake na akaishi maisha ya kidhulma na upotevu. Hakika Mwenyezi Mungu anakataza ufisadi duniani na sio vipambo na neema za dunia, bali hakika Yeye Mwenyezi Mungu amekanusha sana kuharamisha neema na ladha katika dunia hii; kama anavyosema:

﴿ قُلْ مَنْ حَرَّمَ زِينَةَ اللَّـهِ الَّتِي أَخْرَجَ لِعِبَادِهِ وَالطَّيِّبَاتِ مِنَ الرِّزْقِ قُلْ هِيَ لِلَّذِينَ آمَنُوا ﴾

Sema: Ni nani aliyeharimisha pambo la Mwenyezi Mungu ambalo amewatolea waja wake.Na, vitu vizuri katika riziki? Sema: hivyo ni kwa walioamini.... (7:32)

Yaani ni halali kwa aliyevichuma kwa njia ya halali na ni haramu kwa anayevitafuta kwa kunyanganya, kuhadaa na utapeli. Kwa ufupi ni kwamba misingi ya ki-Quran ni kuishi watu katika kusaidiana yale yaliyo na wema kwa wote. Ama misingi ya Kizayuni ya kikoloni, ni Maadamu mimi ninaishi basi na uangamie ulimwengu na kila mwenye kwenda na msingi huu, basi ni Mzayuni akijua au asijue; hana budi kukumbana na uadilifu wa mbingu na ardhi na kuteremkiwa na mateso na balaa.

MAYAHUDI NA UKOMUNISTI NA UBEPARI

Inadhihiri kutokana na Aya tukufu kwamba kugawanyika Mayahudi katika makundi mawili ni mambo waliyoyarithi kutoka kwa mababa na mababu zao ili wazidishe moto kuwaka kwa upande fulani na wapate masilahi yao kwa upande wa pili. Kama ilivyo kuwa kugeuka geuka kwao ndio asili yao na ada yao. Kabla ya nusu karne walikuwa wakilingania ukomunisti na ndio wao leo wanaoulemea ubepari. Hawana lengo lolote isipokuwa kuugawa ulimwengu na kuanzisha vita na fitina ili watekeleze siasa zao za ukandimizaji na ukupe wa kunyonya jasho la watu.

﴿ وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ وَقَفَّيْنَا مِن بَعْدِهِ بِالرُّسُلِ وَآتَيْنَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ الْبَيِّنَاتِ وَأَيَّدْنَاهُ بِرُوحِ الْقُدُسِ أَفَكُلَّمَا جَاءَكُمْ رَسُولٌ بِمَا لَا تَهْوَىٰ أَنفُسُكُمُ اسْتَكْبَرْتُمْ فَفَرِيقًا كَذَّبْتُمْ وَفَرِيقًا تَقْتُلُونَ﴾

87.Na hakika tulimpa Musa Kitabu na tukawafuatisha Mitume baada yake; na tukampa Isa, mwana wa Maryam, hoja zilizo wazi wazi, na tukamtia nguvu kwa roho takatifu. Kila alipowafikia Mtume kwa yale yasiyoyapenda nafsi zenu, mlijivuna, kundi moja mkalikadhibisha na kundi jingine mkaliua!

﴿ وَقَالُوا قُلُوبُنَا غُلْفٌ بَل لَّعَنَهُمُ اللَّـهُ بِكُفْرِهِمْ فَقَلِيلًا مَّا يُؤْمِنُونَ ﴾

88.Na walisema: Nyoyo zetu zimefunikwa, bali Mwenyezi Mungu amewalaani kwa kufuru zao; kwa hivyo ni kidogo tu wanayoyaamini!

TULIMPA MUSA KITABU

Aya 87 - 88

LUGHA

Neno Maryam, lina maana ya mtumishi kwa lugha ya kiebrania. Kwa sababu mama yake Maryam aliweka nadhiri ya kumtoa awe mtumishi wa Baitul -Maqdis (Quds). Na hakika tulimpa Musa Kitabu na tukawafuatisha Mitume baada yake.Yaani tumempa Musa Tawrat; kisha tukawapeleka Mitume baada yake, mmoja baada ya mwengine. Inasemekana kuwa hazikupita zama kati ya Musa na Isa ambaye ndiye Mtume wa mwisho wa Kiisrail, isipokuwa kulikuwa na Mtume Mursal au Mitume tofauti wanaoamrisha mema na kukataza mabaya. Imesemwa katika Tafsirul Razi na ya Abu Hayan El-Andalusi kwamba Mitume hao ni Yoshua, Samuel, Shamun, Daud, Suleiman, na Shiau. Vile vile Armiya, Uzayr, Ezekiel, Eliyas, Yunus, Zakaria na Yahya.

Na tukampa Isa mwana wa Maryam, hoja zilizo wazi wazi na tukamtia nguvu kwa roho takatifu.

Isa(a.s) ndiye Mtume wa mwisho wa wana wa Israil, na kati yake na Musa kulikuwa na karne 14.Ni kidogo tu wanayoamini. Yaani hawakuamini katika Mayahudi isipokuwa wachache tu, kama Abdallah bin Salam na wafuasi wake. Mwenye Majmaul-Bayan amechagua kusema kuwa maana ya:ni kidogo tu wanayoamini, kwamba hakuamini yoyote katika wao, si wachache wala wengi; kama vile inavyosemwa ni nadra kufanya. Kwa maana ya kutofanya kabisa. Lakini maana tuliyoyaeleza mwanzo ndiyo yaliyo sahihi zaidi, kwa kuangalia kauli yake Mwenyezi Mungu: ﴿ وَقَوْلِهِمْ قُلُوبُنَا غُلْفٌ بَلْ طَبَعَ اللَّـهُ عَلَيْهَا بِكُفْرِهِمْ فَلَا يُؤْمِنُونَ إِلَّا قَلِيلًا﴾

...Na kwa kusema kwao nyoyo zetu zimefumbwa, bali Mwenyezi Mungu amezipiga mhuri kwa kufuru yao, basi hawataamini ila wachache tu. (4:155).

MKWELI NA TAPELI

Inatakikana tuangalie tena kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu:Kila walipowafikia Mitume mpaka mwisho.

Hakika Aya hii tukufu pamoja na kuwa na madhumuni ya kumsuta mwenye kuwaasi Mitume na kuikataa haki, kama haikuafikiana na matakwa yake, pia vile vile ina madhumuni ya kumsuta mwenye kuwapuuza watu na asiwakabili kwa tamko la haki kwa kutaka kujipendekeza kwao kwa tamaa ya cheo nk. Hakika mtengenezaji wa kweli anaizungumza haki wala haogopi lawama katika kazi ya Mwenyezi Mungu. Kwa sababu lengo lake la kwanza na la mwisho ni kumridhisha Mwenyezi Mungu peke yake. Kwa ajili hiyo ndio anajitoa muhanga na kufa shahidi kwa ajili ya kuwapelekea na kuwaonyesha haki umma. Ama mharibifu aliye mwongo anakuwa na lengo la kuwaridhisha watu ili wanunue bidhaa yake: Imam Ali(a.s) anasema:Usimchukize Mwenyezi Mungu kwa kumridhisha yeyote katika viumbe vyake.

﴿ وَلَمَّا جَاءَهُمْ كِتَابٌ مِّنْ عِندِ اللَّـهِ مُصَدِّقٌ لِّمَا مَعَهُمْ وَكَانُوا مِن قَبْلُ يَسْتَفْتِحُونَ عَلَى الَّذِينَ كَفَرُوا فَلَمَّا جَاءَهُم مَّا عَرَفُوا كَفَرُوا بِهِ فَلَعْنَةُ اللَّـهِ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴾

89.Na kilipowajia kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu kisadikishacho yaliyo pamoja nao, na zamani walikuwa wakiomba ushindi juu ya makafiri. Lakini yalipowafikia yale waliyoyajua waliyakataa. Basi laana ya Mwenyezi Mungu iko juu ya makafiri.

﴿ بِئْسَمَا اشْتَرَوْا بِهِ أَنفُسَهُمْ أَن يَكْفُرُوا بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ بَغْيًا أَن يُنَزِّلَ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ فَبَاءُوا بِغَضَبٍ عَلَىٰ غَضَبٍ وَلِلْكَافِرِينَ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴾

90.Kibaya kabisa walichokiuzia nafsi zao ni kule kukataa kile alichokiteremsha Mwenyezi Mungu kwa kuona maya kuwa Mwenyezi Mungu amemteremshia fadhila zake amtakaye katika waja wake. Kwa hiyo wakastahili ghadhabu juu ya ghadhabu, na watakuwa nayo makafiri adhabu idhalilishayo.

﴿ وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ آمِنُوا بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ قَالُوا نُؤْمِنُ بِمَا أُنزِلَ عَلَيْنَا وَيَكْفُرُونَ بِمَا وَرَاءَهُ وَهُوَ الْحَقُّ مُصَدِّقًا لِّمَا مَعَهُمْ قُلْ فَلِمَ تَقْتُلُونَ أَنبِيَاءَ اللَّـهِ مِن قَبْلُ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ﴾

91.Na wakiambiwa: Yaaminini aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu husema: Tunaamini yaliyoteremshwa juu yetu; na hukataa yaliyo nyuma yake; na hali yakuwa hii ndiyo haki inayosadikisha yaliyo pamoja nao. Sema: Mbona mliwaua Mitume wa Mwenyezi Mungu hapo zamani kama mlikuwa mkiamini

KILIPOWAFIKIA KITABU

Aya 89 - 91

MAELEZO

Mayahudi wa Madina walikuwa wamejipa tumaini la kujiwa na Mtume na walikuwa wakimtaja Muhammad, wakiwaambia Aus na Khazraj: Kesho atakuja Mtume ambaye sifa zake tumezikuta katika Tawrat na atawashinda waarabu na washirikina wote. Mayahudi walikuwa wakifikiria kuwa huyo Mtume ni Mwisrail sio Mwarabu. Basi Mwenyezi Mungu alipomtuma Muhammad Mwarabu, waliona unyonge, wakaingiwa na ubaguzi na kuupinga Utume wake na kukanusha yale waliyokuwa wakiyasema kwa Muhammad. Ikawa baadhi ya Aus na Khazraj wanawambia: Enyi Mayahudi, jana mlikuwa mkitutisha kwa Muhammad(s.a.w.w) kuwa sisi ni watu wa shirk: mlikuwa mkimsifu na kumtaja kwamba yeye ni Mtume. Sasa mbona sisi ndio tunaomwamini na nyinyi mmegeuka na kurudi nyuma? Wakajibu Mayahudi: Hakutujia na kitu tunachokijua na wala yeye siye yule tuliyekuwa tukiwatajia. Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii:Na kilipowajia kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu kisadikishacho yaliyo pamoja nao.

Yaani ilipowajia Quran walikanusha. Quran waliyoikanusha ndani yake mna usadikisho wa yale yaliyo katika Tawrat yao iliyobashiri kuja Muhammad(s.a.w.w) . Kwa hiyo wanamfanya mwongo yule anayewasadikisha wao, bali wanajikadhibisha wenyewe. Hili si geni wala si ajabu kwa yule anayefanya matakwa yake na mapenzi yake ndiyo kigezo cha kuhalalisha, kusadikisha na kukadhibisha. Kila mwenye kujihalalishia yale yaliyo haramu kwa wengine, basi anaingia katika mkumbo huu. Ewe Mwenyezi Mungu tukinge na shari ya kutojifahamu sisi wenyewe.

Na hapo mbele walikuwa wakiomba ushindi juu ya makafiri lakini yalipowafikia yale waliyokuwa wakiyajua waliyakataa. Mayahudi kabla ya kuja Mtume Muhammad(s.a.w.w) walikuwa wakiwaonya Aus na Khazraj kwa Muhammad. Lakini alipokuja mambo yaligeuka, Aus na Khazraj wakamwamini na wakamsaidia mpaka wakaitwa Ansar (wasaidizi) na Mayahudi wakamkanusha; wakaangamizwa na kufukuzwa na hao Ansar kupitia kwa Muhammad; kama vile walivyokuwa wao wakiwaonya Ansar. Namna hii wanapata wenye vitimbi vibaya, na balaa humshukia yule anayemtakia mwenzake hiyo balaa.

Unaweza kuuliza: Kwa nini Mayahudi waligeuza imani waliyokuwa nayo kwa Muhammad?

Jibu : Walikuwa wakiitakidi kwamba Mtume atakayekuja atakuwa Mwisrail kutoka katika kizazi cha Is-haq, kwa kufikiria wingi wa Mitume Waisrail. Walipomwona ni Mwarabu kutoka katika kizazi cha Ismail, walimkanusha kwa uhasidi na ubaguzi tu wa Kiyahudi. Na kila mwenye kuipinga haki kwa ubaguzi wa kikabila au vinginevyo, basi huyo ni sawa na Mayahudi hao ambao walikataa kumkiri Muhammad, si kwa lolote isipokuwa kwamba yeye ni Mwarabu tu. Kibaya kabisa walichokiuzia nafsi zao ni kule kukataa alichokiteremsha Mwenyezi Mungu.

Quran tukufu mara nyingi hutumia tamko la kuuza na kununua na biashara, kuhusu amali njema na mbaya. Kwa vile mtu akiamini na akafanya amali njema, ni kama kwamba amefanya biashara ya nafsi yake na kuiokoa; na kama akikufuru na kuacha kunufaika, ni kama kwamba ameiuza nafsi yake kwa shetani kwa thamani duni kabisa. Kuziuzia nafsi zao hapa ni kwa maana ya kuwa Mayahudi wameziuzia shetani nafsi zao na wame-

* 26 Haya ndiyo waliyoyataja wafasiri kwa kuangalia dhahiri ya Aya. Utakuja ubainifu wa sababu za hakika za kumkanusha kwao Muhammad(s.a.w.w) katika Aya ya 91 ambazo ni manufaa na chumo lililotokana na uasherati, udanganyifu, riba, na mengineyo yaliyoharamishwa na Uislamu. jiangamiza; wala hapana thamani ya nafsi zao isipokuwa hasadi na ubaguzi wa Kiyahudi tu. Kwa hivyo ndiyo Mwenyezi Mungu akasema:Kwa kuona maya kuwa Mwenyezi Mungu humteremshia fadhila zake amtakaye katika waja wake. Yaani walimkanusha Muhammad(s.a.w.w) si kwa jingine isipokuwa wao walitaka kuhodhi wahyi na fadhila kwao tu peke yao. Hawakubali kutoka kwa Mwenyezi Mungu wala kwa mwengine isipokuwa yale yanayoafiki mapenzi na manufaa yao. Kwa hiyo wao wanastahili adhabu mara mbili, kwa kukanusha na kwa ubinafsi wao.

Na wanapoambiwa: Yaaminini aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu. Yaani aminini wahyi kama ulivyo bila ya kuangalia utu wa mwenye kuufikisha wahyi huo. Kwa sababu Mtume ni wasila tu wa kufikisha. Ama sharti lenu la kuamini wahyi kuwa uteremshwe kwa taifa la Kiisrail tu, na kama ukiteremshiwa mwengine basi hamwamini, sharti hili linafichua kukosa kuamini wahyi kimsingi. Isitoshe, itakuwa nyinyi mnatoa hukumu kwa Mwenyezi Mungu kwa mapenzi yenu. Maana yake nyinyi mnataka Mwenyezi Mungu awanyenyekee na mnakataa kumnyenyekea.

Husema: Tunaamini yaliyoteremshwa juu yetu. Huku ni kukiri wazi kwamba wao hawaamini wala hawataamini isipokuwa kwa sharti la kuteremshwa wahyi kwao, na hawataamini wahyi utakaoteremshwa kwa mwingine, hata kama kutakuwa na dalili elfu.Sema: Mbona mliwaua Mitume wa Mwenyezi Mungu hapo zamani kama mlikuwa mkiamini.

Hakuna hoja yenye nguvu zaidi ya hii; yaani sema ewe Muhammad kuwaaambia Mayahudi: Nyinyi ni waongo katika madai yenu ya kuamini wahyi kwa kuuhusisha na taifa la Kiisrail, bali nyinyi hamwamini wahyi kabisa, hata ule uliowahusu nyinyi! Dalili ya hayo ni kwamba Mwenyezi Mungu amepeleka Mitume kutoka kwenu na kwa ajili yenu na akawajibisha muwasadiki na kuwatii, lakini pamoja na hayo wengine mliwafanya waongo; kama vile Isa(a.s) na wengine mkawaua kama vile Zakaria na Yahya. Hii inafahamisha uongo wenu na kugongana vitendo vyenu na maneno yenu na kujidaganya wenyewe.

Imekuwa sawa kuuelekeza msemo wa kuua kwa Mayahudi wa Madina pamoja na kuwa walioua ni mababu zao. Hiyo ni kwa sababu umma wao ni mmoja kwa kushiriki kuridhia kuua.

WALIOFANANA NA MAYAHUDI

Mayahudi walimkataa Muhammad(s.a.w.w) , kwa sababu alikuwa si Mwisrail; Naye Abu Sufian alimkanusha na kuongoza jeshi kumpinga kwa sababu Mtume ni katika ukoo wa Hashim. Alikataa kwa sababu ukoo wa Hashim utapata utukufu wa Utume kuliko ukoo wake yeye Abu Sufiani wa Umayya. Vile vile Maquraish waliukana ukhalifa wa Ali(a.s) , kwa sababu walichukia kukusanyika Utume na Ukhalifa katika nyumba ya Hashim. Baadhi ya wasiokuwa Waarabu wanaona uzito kuwa Marjaa (Mufti) wa kwanza awe Mwarabu; kama ambavyo baadhi ya waarabu nao wanaona uzito kuwa Marjaa (Mufti) ambaye si Mwarabu. Mimi nawajua watu ambao wako tayari kubaki kwenye upotevu lau wanahiyarishwa kuifuata haki kwa wasiokuwa wao. Vile vile lau wanahiyarishwa kati ya kusikiliza sifa za mwingine, basi wangeona bora kusikiliza za Yazid.

Kwa ajili hiyo ndipo ukaona mtu anafanya juhudi ya kutafuta aibu ya mwenzake akipata chembe tu, huikuza na kuifanya jabali, na akiikosa huizusha. Mwenye kuona fadhila kuwa ndio msingi, huikuza vyovyote iwavyo na njia yoyote itakavyokuwa na humwonyesha mwingine kama anavyoona yeye; bali hufanya kazi ya kuieneza. Ama mwenye kuikanusha, hutumia muundo huo ambao wameutumia Mayahudi kwa inadi.

﴿ وَلَقَدْ جَاءَكُم مُّوسَىٰ بِالْبَيِّنَاتِ ثُمَّ اتَّخَذْتُمُ الْعِجْلَ مِن بَعْدِهِ وَأَنتُمْ ظَالِمُونَ ﴾

92.Na aliwajia Musa na hoja zilizo wazi wazi, kisha mkafanya ndama baada yake na hali nyinyi ni madhalimu.

﴿ وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَكُمْ وَرَفَعْنَا فَوْقَكُمُ الطُّورَ خُذُوا مَا آتَيْنَاكُم بِقُوَّةٍ وَاسْمَعُوا قَالُوا سَمِعْنَا وَعَصَيْنَا وَأُشْرِبُوا فِي قُلُوبِهِمُ الْعِجْلَ بِكُفْرِهِمْ قُلْ بِئْسَمَا يَأْمُرُكُم بِهِ إِيمَانُكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴾

93.Na tulipochukua ahadi yenu na tukauinua mlima juu yenu: Kamateni kwa nguvu haya tuliyowapa na sikilizeni. Wakasema: Tumesikia na tumekataa na wakanyweshwa nyoyoni mwao (imani ya) ndama kwa kufuru yao. Sema: Ni kibaya kabisa kilichowaamrishia imani yenu; mkiwa ni wenye kuamini.

﴿ قُلْ إِن كَانَتْ لَكُمُ الدَّارُ الْآخِرَةُ عِندَ اللَّـهِ خَالِصَةً مِّن دُونِ النَّاسِ فَتَمَنَّوُا الْمَوْتَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴾

94.Sema: Ikiwa nyumba ya akhera iliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni yenu nyinyi tu bila ya watu wengine, basi tamanini mauti kama nyinyi ni wa kweli.

﴿ وَلَن يَتَمَنَّوْهُ أَبَدًا بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالظَّالِمِينَ﴾

95. Wala hawatayatamani kabisa kwa sababu ya yale yaliyotangulizwa na mikono yao, na Mwenyezi Mungu anawajua madhalimu.

﴿ وَلَتَجِدَنَّهُمْ أَحْرَصَ النَّاسِ عَلَىٰ حَيَاةٍ وَمِنَ الَّذِينَ أَشْرَكُوا يَوَدُّ أَحَدُهُمْ لَوْ يُعَمَّرُ أَلْفَ سَنَةٍ وَمَا هُوَ بِمُزَحْزِحِهِ مِنَ الْعَذَابِ أَن يُعَمَّرَ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِمَا يَعْمَلُونَ ﴾

96.Na Utawaona wanapupia zaidi maisha kuliko watu wengine na kuliko wale wamshirikishao Mwenyezi Mungu. Kila mmoja katika wao anapenda lau angelipewa umri wa miaka elfu. Na huko kupewa kwake umri mwingi hakuwezi kumwondoshea adhabu; na Mwenyezi Mungu anayaona wanayoyatenda .

MUSAALIWAJIA NA HOJA

Aya 92 - 96

MAELEZO

Aya hizi ziko wazi na zinayakariri yaliyotangulia. Kwa hiyo tutaeleza maana kwa ujumla. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimwamrisha Mtume wake kujadiliana kwa uzuri na wapinzani. Maana ya kujadiliana kwa uzuri ni kuzungumza na moyo na akili. Hoja zote za Quran ziko namna hiyo; imewataka wakanushaji wajifikiriie wao wenyewe na kuumbwa mbingu na ardhi; akamwambia mwenye kumnasibisha Bwana Masih uungu, kuwa yeye Masih na mama yake walikuwa wakila chakula. Na inazungumza na nyoyo za Mayahudi kwa Aya hizi kwa kuwakumbusha neema ya Mwenyezi Mungu ya kuwapelekea Tawrat ambayo ndani yake mna uongofu na nuru; kama zilivyowakumbusha Aya zilizotangulia kukombolewa kwao kutoka kwenye minyororo ya Firaun, n.k.

Kisha Mwenyezi Mungu akawakemea kwa kuabudu kwao ndama wakaikufuru na kuipinga neema Yake, amekariri kutaja kuinuliwa jabali juu yao kutokana na uasi wao na mantiki ya kiakili ikayakadhibisha madai yao ya kuwa wao ni watoto na wapenzi wa Mwenyezi Mungu, na kwamba pepo inawahusu wao tu hataingia mwengine zaidi yao. Vilevile amewaamrisha kutamani mauti ikiwa wao ni wakweli. Kwa sababu mwenye kuitakidi kwamba pepo ni yake, basi atachagua mauti yenye raha kuliko kuwa na maisha ya balaa na mashaka. Kisha Quran ikatoa habari kwamba wanapupia sana dunia na wana pupa zaidi kuliko wale wasioamini pepo wala moto. Bali hata mtu katika wao anaweza kutamani lau angeliishi miaka elfu. Lakini kurefusha kwake umri hakutamfaa kitu wala hakutamwokoa na adhabu.

Lengo la majadiliano haya ya kimantiki ya akili yaliyo salama ni kuwathibitishia Mayahudi hoja kwamba wao ni waongo wanavyodai kuwa wanaamini Tawrat, na kudai kwao kuwa wao ni taifa teule la Mwenyezi Mungu. Sheikh Maraghi katika tafsir yake anasema: Imekuja Hadith kwamba Abdalla bin Rawaha alipokuwa akipigana na Warumi alikuwa akiimba: Kwa hamu naitamani, Pepo ilokaribia Yenye vinywaji laini, Vilo baridi jamia Na Ammar bin Yasir katika vita vya Siffin alisema: Hapo kesho twaazimu, Kukutana na wapenzi Muhammad muadhamu, Na swahabaze wa enzi

Ikiwa Mayahudi hawatatamani mauti basi wao si wakweli wa imani. Hoja hii inawahusu watu wote. Kwa hivyo ni wajibu kwa Waislamu kuifanya hoja hiyo ni mizani watakayopimia madai yao ya imani na kusimamia haki za Mwenyezi Mungu. Wakiwa wanaona raha kujitolea roho zao kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, watakuwa ni waumini wa kweli, vinginevyo watakuwa kinyume na madai yao.

MASLAHI NDIO SABABU

Hatuna shaka kabisa kwamba suala la kumkadhibisha Muhammad (s.a.w.) sio suala la kuhusiana na ubaguzi tu. Isipokuwa sababu hasa ni maslahi yao ya kiutu na manufaa yao ya kimaada. Kwani wao wanaishi kwa utapeli, riba, na uasherati; na Muhammad(s.a.w.w) anayaharamisha hayo. Vipi wataamwamini? Ushahidi wa hayo ni kwamba wao hawana sababu nyingine isipokuwa pupa ya manufaa ya kibinafsi. Na kila mwenye kupupia manufaa yake, haumfai mjadala mzuri. Na kaui yake Mwenyezi Mungu: Na utawaona wanapupia zaidi maisha, inafahamisha hilo.