TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA13%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Mwandishi:
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Juzuu 9 Juzuu 10 Juzuu 11
  • Anza
  • Iliyopita
  • 20 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39983 / Pakua: 5154
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

Mwandishi:
Swahili

1

2

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿ وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ﴾

34.Na tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipokuwa Iblis; alikataa na akajivuna; na akawa miongoni mwa makafiri.

MSUJUDIENI ADAM

Aya 34

Mwenyezi Mungu aliwaamrisha malaika kumsujudia Adam kwa kudhihirisha ubora wake kuliko wao na kuliko viumbe vyake vyote. Hapana tafsiri ya ubora huu isipokuwa ubora wa elimu au ubora wa aliye nayo. Kwa sababu elimu, kama ilivyothibiti, ndiyo kipimo cha kila hatua anayopiga mtu ya maendeleo na ukamilifu; kama vile ambavyo ujinga ni msingi wa kurudi nyuma. Hawezi kuwa juu isipokuwa kwa elimu. Mwenye elimu siku zote hufuatwa, na mjinga siku zote hufuata. Kwa ajili hii Uislamu umewajibisha elimu kwa kila Mwislamu mwanamume na mwanamke.

Wafasiri wengi wamesema kwamba sijda ilikuwa ni ya ki-maamkuzi tu; Kama kuinama na kuinua mkono. Kwa sababu kumsujudia asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni haramu. Lakini haya sio kweli kwa mujibu wa mwenye tafsiri ya Majmaul-Bayan, kwani kama ingelikuwahivyo,basi, Iblis asingelikataa kumsujudia. Kimsingi sijda ilikuwa ni kwa amri ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kumtii Mwenyezi Mungu sio kwa ajili ya Adam.

Amri ya kumsujudia Adam iliwahusu Malaika wote bila ya kumvua yoyote, hata Jibril na Mikail pia, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ كَانَ مِنَ الْجِنِّ فَفَسَقَ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِ﴾

Na tulipowaambia Malaika, msujudieni Adam.Basi wakamsujudia isipokuwa Iblis; yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake. (18:50)

Hakuna njia ya kumjua Iblis, shetani na jini, isipokuwa kwa njia ya wahyi tu; kama ilivyo katika kuwajua Malaika.Maelezo yamekwishaelezwa katika Aya iliyotangulia.

Wafasiri wameonyesha utafiti usiokuwa na manufaa. Kwa hivyo tumeuacha kwa kufupiliza yale yanayofahamishwa na dhahiri ya maneno. Tumekwishaonyesha katika kurasa zilizotangulia baadhi ya yale yanayona- sibishwa kwa Iblis katika vigano. Ni picha iliyo wazi ya watu wengi wa siku hizi katika kuchezea kwao matamko, ambako hakutimizi elimu au fani yoyote zaidi ya kubobokwa tu.

﴿ وَقُلْنَا يَا آدَمُ اسْكُنْ أَنتَ وَزَوْجُكَ الْجَنَّةَ وَكُلَا مِنْهَا رَغَدًا حَيْثُ شِئْتُمَا وَلَا تَقْرَبَا هَـٰذِهِ الشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ الظَّالِمِينَ ﴾

35.Na tukasema: Ewe Adam! kaa wewe na mkeo katika Pepo (bustani); na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, wala msiukurubie mti huu; msije mkawa miongoni mwa waliodhulumu (nafsi zao).

﴿ فَأَزَلَّهُمَا الشَّيْطَانُ عَنْهَا فَأَخْرَجَهُمَا مِمَّا كَانَا فِيهِ وَقُلْنَا اهْبِطُوا بَعْضُكُمْ لِبَعْضٍ عَدُوٌّ وَلَكُمْ فِي الْأَرْضِ مُسْتَقَرٌّ وَمَتَاعٌ إِلَىٰ حِينٍ﴾

36.(Lakini) Shetani akawatelezesha wote wawili na akawatoa katika ile hali waliyokuwa nayo. Tukasema: nendeni hali yakuwa maadui nyinyi kwa nyinyi, na mtapata katika ardhi makazi na starehe kwa muda (maalum).

﴿ فَتَلَقَّىٰ آدَمُ مِن رَّبِّهِ كَلِمَاتٍ فَتَابَ عَلَيْهِ إِنَّهُ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ ﴾

37.Akapokea Adam maneno kutoka kwa Mola wake na Mola wake akapokea toba yake; hakika Yeye ni Mwingi wa kukubali toba, Mwenye kurehemu.

﴿ قُلْنَا اهْبِطُوا مِنْهَا جَمِيعًا فَإِمَّا يَأْتِيَنَّكُم مِّنِّي هُدًى فَمَن تَبِعَ هُدَايَ فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴾

38.Tukasema: Tokeni humo nyote: Na kama ukiwafikia uongozi wangu basi watakaoufuata mwongozo wangu haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

﴿ وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴾

39.Na ambao wamekufuru na kukadhibisha ishara zetu, hao ndio watakaokuwa watu wa motoni, humo watadumu.

ADAMU PEPONI

Aya 35

Mwenyezi Mungu aliamwamrisha Adam na Hawa kukaa peponi; akawahalalishia kula yaliyomo ndani yake isipokuwa mti mmoja tu, waliokatazwa kuula. Lakini shetani aliwahadaa kwa kuwataka waule. Walipokubaliana naye ilipita hekima yake Mwenyezi Mungu ya kuwatoa pepo ni kuwapeleka ardhini na akawatia mtihani kwa taklifa na kazi, uzima na ugonjwa, shida na raha, kisha mauti muda wake unapofika.

Adam alihisi msiba na akajuta. Akamwomba Mola wake kwa ikhlasi amtakabalie toba yake, akamkubalia na akamsamehe, kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kukubali toba Mwenye rehema. Nadhani kwamba Hawa pia alitubia pamoja na Adam, lakini Mwenyezi Mungu hakuitaja toba yake. Hakuna tofauti kati ya Mwanamume na mwanamke. Mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na akafanya amali njema, Mwenyezi Mungu atamuweka peponi, na mwenye amali mbaya atamwingiza motoni awe mume au mke.

Wamejiingiza wafasiri wengi kuelezea pepo aliyotoka Adam,ilikuwa wapi?Mti ulikuwa mtini au ngano? Kuhusu nyoka ambaye aliingia Iblis ndani yake, na mahali aliposhukia Adam, je palikuwa India au Hijaz? Na mengineyo yaliyokuja katika hadithi za Kiisrail.Quran haikudokeza lolote katika hayo; wala haikuthibiti katika hadithi kwa njia sahihi. Pia akili haiwezi kujua chochote katika hayo, na hayo hayaambatani na maisha kwa karibu au mbali. Hata hivyo hakuna budi kutanabahisha mambo yafuatayo:-

HAWA NA UBAVU WA ADAM

Imeenea habari kwamba Hawa aliumbwa kutokana na ubavu wa Adam, lakini hakuna maelezo sahihi ya kutegemewa. Na habari zilizoelezea hilo si za kutegemewa. Ikiwa tutazichukulia kuwa ni sahihi basi ni kwamba makusudio yake ni kuonyesha usawa na kukosa kutofautisha kati ya mume na mke, yaani mke ametokana na mume na mume naye ametokana na mke. Katika kitabu Malla yahdhur hul-faqih, imesemwa, Imam Sadiq(a.s) wakati alipoulizwa usahihi wa uvumi huu, aliukanusha na akasema:Mwenyezi Mungu Ametukuka na hayo kabisa.

Je Mwenyezi Mungu alishindwa kumuumbia Adam mke isipokuwa kutokana na ubavu wake mpaka ikabidi Adam aoe sehemu yake ya mwili?

MTAKA YOTE HUKOSA YOTE

Hekima ya Mwenyezi Mungu ilipitisha kuwa Adam akae na mkewe peponi wakati fulani, kisha atoke kwa sababu maalum ambayo wao wawili ndio walioifanya kwa matakwa yao na hiyari yao; lau si hivyo wangelibaki peponi milele wakistarehe bila ya taabu yoyote.

Vile vile hekima yake Mwenyezi Mungu ilipitisha kuwa Adam na Hawa wabaki katika ardhi hii mpaka watakapozaana na kupatikana koo na vizazi, wakati ambapo wataulizwa wote, kauli na vitendo walivyovifanya. Kama ilivyohukumilia hekima yake kurudi Adam na mkewe peponi baada ya kufa na wadumu humo milele.

Unaweza kuuliza: Kuna hekima gani ya kuingia Adam peponi na kutoka kuja ardhini, kisha kuitoka hiyo ardhi na kurudi tena peponi mara ya pili baada ya kufa?

Jibu : Huenda hekima iliyopo ni kuwa Adam apitie majaribio atakayonufaika nayo na kufaidika nayo, yeye na watoto wake, na kurudi kwenye pepo hii akiwa amejaa majaribio yenye kunufaisha. Yaani ni kwamba mtu hawezi kuishi milele bure bure tu vile anavyotaka na kwamba mwenye kuyachunga hayo majaribio kwa kuyamiliki matakwa yake bila ya kukubali kusukumwa na matamanio yake, basi ataishi maisha mazuri ya wema usiokuwa na mwisho. Na mwenye kuwa na msimamo hafifu na akawa mdhaifu mbele ya matamanio yake, atakuwa amepata aliyoyapata Adam majuto, kujaribiwa, taabu na mashaka.

ISMA (KUHIFADHIWA MITUME)

Wameafikiana Waislamu wote kwamba Adam ni katika Mitume, na Mitume kama inavyofahamika ni wenye kuhifadhiwa na madhambi na makosa.Sasa nini maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu; Akawahadaa shetani katika hali waliyokuwa nayo? Kwa ajili hiyo ndio wameonelea wanachuoni kuwa iko haja kubwa ya kufanya utafiti juu ya Isma ya Mitume; kisha kuifasiri Aya hii katika hali ambayo italeta natija. Nasi tunakusanya kauli juu ya hilo kama ifuatavyo ili iwe ni asili katika kila linaloambatana na maudhui haya. Maana ya Isma ya Mtume ni kutakata na makosa katika kila jambo

*15 Kuna maelezo yanayosema kuwa Adam ana jina la kubandikwa peponi la Abu Muhammad kwa heshima na kutukuzwa, na hakuna mtu mwenye jina la kubandikwa peponi ispokuwa yeye tu. linaloambatana na dini na hukumu zake, kiasi ambacho atafikilia Mtume utakatifu na elimu na kumjua Mwenyezi Mungu na yale anayoyataka kwa waja wake; kwa hali ambayo inakuwa muhali kuikhalifu, iwe kwa makusudi au kwa kusahau. Mwenye kuthibitisha Isma kwa Mitume kwa maana hayo na kwa mafungu yake yote yatakayokuja, ataifanyia taawil Aya inayopingana na dhahiri ya msingi huu, kwa kwenda na kanuni ya kiujumla ambayo ni wajibu wa kufanya taawil kwa kuafikiana na dhahiri ya akili. Na, mwenye kukanusha Isma kwa mitume, atabakisha dhahiri kwa dhahiri yake.

Wanavyuoni wa madhehebu mbali mbali wana kauli nyingi katika Isma, zenye kukhitalifiana kwa tofauti za mafungu yafuatayo:

1. Isma katika itikadi na misingi ya dini; yaani kutakasika kwa Mtume kutokana na ukafiri na ulahidi. Hilo ni lenye kuthibiti kwa kila Mtume kimisingi na kwa maafikiano.Kwani haiingii akilini kuwa Mtume amkanushe yule aliyempa Utume.

2. Isma katika kufikisha amri za Mwe-nyezi Mungu. Akisema, Mwenyezi Mungu anaamrisha hili na anakataza lile, basi amri itakuwa ile ile aliyoisema. Wameafikiana Shia Imamiya kuthibiti Isma hii kwa kila Mtume. Kwa sababu lengo la kufikisha ni kuwachukua wale wanaokalifiwa na sharia kwenye haki.Akikosea mwenye kufikisha itakuwa lengo la kufikisha limebatilika. Hayo yanatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ﴾

Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi yake) (53:3)

Na kauli yake:

﴿ وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا﴾

Na anachowapa Mtume kipokeeni na anachowakataza jiepusheni nacho. (59:7)

Kwa maneno mengine Isma ya Mitume haiwezi kuepukana kabisa na kusema kuwa kauli yao, kitendo na uthibittisho wao ni hoja na dalili. Baada ya Razi kusema katika tafsiri yake: Wameafikiana Waislamu kwamba kukosea katika kufikisha hakujuzu kwa kusudi au kusahau, aliendelea kusema: Wako watu wanaojuzisha hilo kwa kusahau. Sijui aliwakusudia watu gani.

3. Isma katika Fatwa; yaani Mtume kufutu kitu cha wote; kama kuharamisha riba na kuhalalisha biashara. Razi ametaja kifungu hiki katika tafsiri yake kwa kusema: Wameafikiana kwamba kukosea Mtume katika hilo hakujuzu kwa kukusudia ama kwa kusahau, wengine wamejuzisha na wengine hawakujuzisha. Kifungu hiki kinarudi katika kifungu cha pili cha kufikisha. Inatakikana kifanywe kifungu cha tatu ni Isma katika hukumu sio fatwa.16 Wameafikiana Imamiya kwamba Mtume ni mwenye kuhifadhiwa na makosa katika hukumu kama ilivyo katika kufikisha; pamoja na kwamba kwao wamenakili kutoka kwa Mtume mtukufu(s.a.w.w) kwamba yeye amesema:

*16 Tofauti ya hukumu na Fatwa ni kwamba maudhui ya hukumu yanakuwa ni mahsusi kama kadhi kuhukumu mapatano yaliyopita kati ya Zaid na Bakari ni batili. Ama maudhui ya Fatwa yanakuwa ni kwa wote kama kuhalalisha biashara na kuharamisha riba. Hakika mimi ninahukumu kati yenu kwa hoja (ushahidi) na yamini. Mimi ni mtu. Nyinyi mkiwa na ugomvi, huenda mmoja akawa mjanja kuliko adui yake - kwa hiyo nitahukumu kutokana na nilivyosikia kutoka kwake, basi kama mtu nikimpa haki ya ndugu yake asichukue; kwani ninamkatia kipande cha moto. Kama ni kosa hapo katika hukumu yake, imetokana na hoja au kiapo n.k. yaani katika kutegemea hukumu sio katika hakimu mwenyewe.

4. Isma katika vitendo vya Mitume na mwenendo wao hasa. Amesema Iji katika Mawaqif Juz.5; Hakika Hashawiya wanajuzisha kwa Mitume kufanya madhambi makubwa; kama uwongo, kwa makusudi au kusahau; na wamekataa Ashaira - yaani Sunni - kwa kusudi sio kusahau. Ama madhambi madogo inajuzu kwao hata kwa kusudi wachilia mbali kusahau.

Wamesema Imamiya: Hakika Mitume ni wenye kuhifadhiwa katika kila wanayoyasema na wanayoyatenda; kama vile ambavyo wamehifadhiwa katika itikadi na kufikisha. Ni muhali kwao kufanya madhambi madogo, wachilia mbali makubwa, na wala hayawezi kuwatokea kabisa, si kwa kukusudia wala kusahau, si kabla ya Utume wala baada yake. Aya yoyote ambayo haiafikiani dhahiri yake na msingi huu, basi wameiletea taawil.Wakasema katika Adam kula tunda, kwamba kukatazwa kule hakukua ni kwa uharamu au kwa ibada, kama vile kukatazwa kuzini na kuiba, bali kulikuwa ni kimwongozo na nasaha tu; kama kumwambia mtu unayemtakia heri, usinunue nguo hii kwa sababu sio nzuri, ikiwa hakukusikia, basi atakuwa hakufanya haramu wala hakumdhulumu mtu; atakuwa amejidhulumu yeye mwenyewe na amefanya jambo ambalo ilikuwa ni vizuri asilifanye.

Kimsingi kula tunda hakuambatani na kumdhulumu mtu yeyote isipokuwa kula tu. Kwa hivyo maana ya toba ya Adam inakuwa ni toba ya kuacha kutenda jambo lenye kupendekezwa na lililo bora. Na, jambo la toba ni jepesi sana, kwani mara nyingi Mitume na watu wema hulikariri neno Namtaka msamaha Mwenyezi Mungu na ninatubia. Inatosha kuwa ni dalili juu ya hilo dua ya Imam Zainul-Abidin katika Sahifa Sajjadiyya yenye kujulikana kwa dua ya toba akisema: Ninaomba msamaha kutokana na ujinga wangu.

AHLUL- BAIT

Amesema Muhyiddini anayejulikana kwa jina Ibnul Arabi katika kitabu chake Futuhatul Makkiya Juz. 1;Uk. 196 chapa ya zamani. Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemtoharisha Mtume wake na kizazi chake kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

﴿ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ﴾

...Mwenyezi Mungu anawatakia kuwaondolea uchafu enyi watu wa nyumba (ya Mtume) na kuwatakasa kabisa. (33:33)

Hakuna kitu kichafu zaidi ya dhambi kwa hivyo hakutegemewi kwa watu wa nyumba (ya Mtume) isipokuwa usafi na utohara, bali wao ni dhati ya utohara. Kisha akasema Ibnul Arabi kwamba Salmanul Farisi ni mwenye kuhifadhiwa na dhambi kwa ushahidi wa Mwenyezi Mungu, na imethibiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwamba yeye amesema: Salman ni katika sisi Ahlul Bait. Kwa hiyo Salman ni mwenye kuhifadhiwa na dhambi kwa ushahidi wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Katika juzuu ya pili ya kitabu hicho hicho Uk. 127, amesema: Hatabaki katika moto mwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika waliotumwa na Mwenyezi Mungu, kwa sababu moto kwao unakuwa ni baridi na salama kwa baraka ya Ahlul Bait katika akhera. Ni utukufu ulioje wa baraka za Ahlul Bait!

﴿ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَوْفُوا بِعَهْدِي أُوفِ بِعَهْدِكُمْ وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ﴾

40.Enyi wana wa Israil! Kumbukeni neema yangu niliyowaneemesha; na tekelezeni ahadi yangu nitatekeleza ahadi yenu; na niogopeni Mimi tu.

﴿ وَآمِنُوا بِمَا أَنزَلْتُ مُصَدِّقًا لِّمَا مَعَكُمْ وَلَا تَكُونُوا أَوَّلَ كَافِرٍ بِهِ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي ثَمَنًا قَلِيلًا وَإِيَّايَ فَاتَّقُونِ﴾

41.Na aminini niliyoyateremsha ambayo yanasadikisha mliyonayo wala msiwe wa kwanza kuyakataa, wala msiuze ishara zangu kwa thamani ndogo; na niogopeni Mimi tu.

﴿ وَلَا تَلْبِسُوا الْحَقَّ بِالْبَاطِلِ وَتَكْتُمُوا الْحَقَّ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴾

42. Wala msichanganye haki na batili, na mkaficha haki na hali mnajua.

﴿ وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَارْكَعُوا مَعَ الرَّاكِعِينَ ﴾

43.Na simamisheni swala na toeni zaka na inameni pamoja na wanaoinama.

﴿ أَتَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبِرِّ وَتَنسَوْنَ أَنفُسَكُمْ وَأَنتُمْ تَتْلُونَ الْكِتَابَ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴾

44.Je, mnawaamrisha watu kutenda mema na mnajisahau, hali mnasoma Kitabu? Basi je,hamfahamu?

﴿ أَتَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبِرِّ وَتَنسَوْنَ أَنفُسَكُمْ وَأَنتُمْ تَتْلُونَ الْكِتَابَ أَفَلَا تَعْقِلُونَ﴾

45.Na takeni msaada kwa kusubiri na kwa kuswali na kwa hakika jambo hilo ni gumu isipokuwa kwa wanyenyekevu.

﴿ الَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَاقُو رَبِّهِمْ وَأَنَّهُمْ إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ﴾

46.Ambao wana yakini kwamba wao watakutana na Mola wao na kwamba watarejea Kwake.

ZIKUMBUKENI NEEMA ZANGU

Aya 40 - 46

Mwenyezi Mungu amewataja Mayahudi katika Aya nyingi za Quran tukufu.Zimebainisha Aya hizo neema za Mwenyezi Mungu na kuua kwao Mitume bila ya haki. Vile vile zimebainisha uadui wao kwa Musa na Harun(a.s.) , kuabudu kwao ndama na kufanywa watumwa na Mafirauni, kisha kukombolewa. Vile vile Aya zimeeleza walivyookoka wasife maji na kuteremshiwa Manna na Salwa. Pia zimeelezea chuki yao hao Mayahudi kwa Mtume Muhammad(s.a.w.w) , au njama zao dhidi yake na uadui wao mkubwa kwa Waislamu, kuchukia kwao haki na mengineyo ambayo yatakuja maelezo yake kwa ufafanuzi. Surah ya Ngombe, waliyemchinja, hii inaelezea kwa upana sifa na matendo yao.

DHAHIRI YA MAISHA

Aina nyingi za hali ya maisha wanayoishi watu ni natija ya Historia ndefu. Aina ya mavazi tunayovaa, mapishi ya chakula tunachokila na ujenzi wa nyumba tunazokaa, vyote hivi ni kutokana na usanifu wa waliotangulia. Hata meli zinazotumia mashine zimeundwa baada ya majahazi yanayotumia matanga,baada ya kupita vipindi vya maendeleo. Hakika maigizo ya kihistoria yanafanya kazi kama desturi za kitabia; sawa na mawimbi yanayotulia kutokana na msukosuko wa kupwa maji na kujaa. Kwa hivyo matukio yanayotumika katika maisha yetu ya kila siku na mfungamano tunaokuwa nao na watu wengine, mbaya au mzuri, ni natija ya yaliyopita zamani sana au hivi karibuni.

Hapa ndipo wanafalsafa wakasema: Historia ni miongoni mwa njia za maarifa. Na Aya hizi ambazo Mwenyezi Mungu anawazungumzia Mayahudi, zina mfungamano mkubwa na Historia yao, kama tutakavyoona.

ISRAIL

Israil: ni jina jingine la Yaqub bin Is-haq bin Ibrahim(a.s.) , Khalilullah. Ishaq ni ndugu wa Ismail, babuye Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Waarabu na Wayahudi wote wamekutana kwa Ibrahim. Mwenyezi Mungu amesema:

﴿ مِّلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ﴾

Mila ya baba yenu Ibrahim (22:78).

Katika Majmaul-Bayan imesemwa kwamba: Waarabu wote ni uzao wa Ismail; na wengi wasiokuwa Waarabu ni uzao wa Is-haq. Maana ya Israil katika lugha ya Kiebrania ni Abdullah (mja wa Mungu), Isra: ni mja, il: ni Mwenyezi Mungu. Alitumia upole Mwenyezi Mungu katika kuwazungumzia Wayahudi kwa kuwategemeza na Mtume mtukufu Israil ili kuwakumbusha nasaba hii tukufu. Huenda wakahisi utukufu ikiwa umo ndani ya nafsi zao; sawa na kusema: Ewe mtoto wa watu wema! Kuwa kama baba zako na babu zako. Ama sababu ya kuitwa kwao Yahudi ni kwamba ukoo mmoja kati yao unatokana na Yahudha ambaye ni mtoto wa nne wa Nabii Yaqub. Sehemu ifuatayo tutaeleza kwa muhtasari historia ya Mayahudi kutokana na Aya tuliyonayo.

HISTORIA YA MAYAHUDI

Yatakuja maelezo katika Sura ya Yusuf kwamba Mtume Yaqub(a.s) alihama na watoto wake kutoka Palestina kwenda Misri alipo mtoto wake Yusuf(a.s) akiwa waziri wa Firaun wakati huo. Firaun akawakatia kipande cha ardhi yenye rutuba kwa heshima ya Yusuf. Kikaendelea kizazi cha Yakub kwa muda kiasi. Lakini Mafiraun waliokuja baadaye waliwakandamiza na kuwapa adhabu na mateso; waliwachinja watoto wao wa kiume wakawaacha wa kike; na wakawafanya watumwa. Kisha Mwenyezi Mungu akawapelekea Mtume aliyekuwa mmoja wao ambaye ni Musa bin Imran, kuwak-omboa na dhulma na utumwa; akawataka warudi Palestina kupigana na akawaahidi ushindi. Wakakataa kwa woga. Mwenyezi Mungu akawapangia kutangatanga katika jangwa la Sinai miaka arobaini. Utakuja ufafanuzi Inshallah.

Katika kipindi hiki Harun alikufa kisha Musa pia akafa. Akachukua uongozi mpwawe Yashua bin Nun. Ilipofika karne ya 13 kabla ya kuzaliwa Nabii Isa(a.s) walivamia ardhi ya Palestina wakiongozwa na Yoshua wakawafukuza wenyeji; kama kilivyofanya kizazi chao (Wazayuni) katika Palestina mwaka 1948.17 Baada ya Yoshua Mwenyezi Mungu alituma mitume wengi waliotokana na wao.

* 17 Tutaje mifano miwili: kwanza, Wazayuni waliwakusanya wanawake 25 wenye mimba katika kijiji cha Dair Yasin, wakawapasua matumbo yao kwa mabisu na mikuki. Pili, waliwakusanya watu wa kijii cha Zaituni msikitini, kisha wakawalipua kwa baruti. Mnamo mwaka 596 kabla kuzaliwa Nabii Isa(a.s) , Mfalme wa Babil Nebukadnezzar aliwashambulia akaondoa utawala wao katika Palestina, akawachinja wengi na kuwachukua mateka wengi. Wakaendelea kuwa chini ya utawala wa Nebukadnezzar mpaka mwaka 538 kabla ya kuzaliwa Isa(a.s) aliposhindwa na mfalme wa Fursi (Iran ya sasa), ndipo Mayahudi wakapumua. Wakaendelea kuwa chini ya utawala wa Fursi kiasi cha miaka mia mbili, baadaye wakatawaliwa na makhalifa wa Alexandria mkuu. Kisha wakawa chini ya utawala wa Roma.

Ilipofika mwaka 135 kabla ya kuzaliwa Isa(a.s) , Mayahudi walifanya mapinduzi kwa Warumi, lakini hayakufanikiwa. Walifukuzwa Palestina, wakakimbilia sehemu mbali mbali za mashariki na magharibi; wengine Misri na wengine Lebanon na Syria, wengine wakaenda Iraq na wengine Hijaz. Ama Yemen walikujua Mayahudi na kuhamia huko kwa ajili ya biashara tangu zama za Nabii Suleiman ambaye alimwoa Malkia wa Yemen, Bilqis (Malkia wa Sheba).

Neema za Mwenyezi Mungu kwao ambazo Mwenyezi Mungu amezitaja kwa kauli yake; Zikumbukeni neema Zangu nilizowaneemesha, ni nyingi; zikiwa ni pamoja na kuwachagua Mitume kutoka katika kabila lao; kama Musa, Harun, Yoshua, Daud, Suleiman, Ayub, Uzair, Zakaria, Yahya n.k. Ama Maryam, mama yake Isa pia ni Mwisrail, nasaba yake inaishia kwa Nabii Daud(a.s) , lakini Mayahudi hawamkubali Masih mwana wa Maryam na wanadai kwamba Masih aliyetajwa katika Tawrat hajakuja bado.

MUHAMMAD NA MAYAHUDI WA MADINA

Mtume(s.a.w.w) alipohamia Madina kutoka Makka, Mayahudi walikuwa na koo tatu: Bani Qaynuqa, Bani Quraydha na Bani Nadhir. Walikuwa wana vilabu vya pombe, madanguro na sehemu za kufugia nguruwe. Na walikuwa wakihodhi dhahabu na fedha, kutengeneza silaha na kufanya biashara ya riba. Kwa ujumla wao ndio waliokuwa wakuu katika mambo ya uchumi mjini Madina, kama walivyo sasa (duniani).

Alipofika Mtume(s.a.w.w) , Mayahudi walihisi hatari kwa faida zao na mapa to yao ya kibiashara, kwa sababu vijana wa Madina wasingekwenda kwenye maduka na mabucha yao na watu wa Madina wasingekula nyama za nguruwe. Maana yake ni kwamba mayahudi wangepoteza vitega uchumi vyote. Kwa ajili hiyo wakawa wanamchimbia vitimbi Mtume mtukufu(s.a.w.w) na kupanga njama pamoja na makafiri dhidi ya Waislamu, kama zinavyofanya leo nguvu za dola kubwa zinavyolinda maslahi yake.

Mtume naye ni kama aliyejua hilo pale alipoingia Madina, akataka kuwatafutia hoja na kuwaadhibu kwa kauli zao. Kwa hiyo akawachukulia upole, akawekeana nao mkataba: kwamba wao wana uhuru katika dini yao na Mahekalu yao kwa masharti ya kuwa wasimsaidie adui na kama wakiamua kupigana pamoja na Waislamu, basi watapata fungu katika ngawira. Ni juu yao kushirikiana na Waislamu, kuulinda mji wa Madina, kwa sababu mji ni wa wote sio wa kundi maalum.Lakini walivunja ahadi upesi sana.Tangu lini ahadi ikasimama mbele ya maslahi? Je inaingia akilini usalama na hadaa kuwa pamoja? Vipi anaweza kuishi mbwa mwitu pamoja na punda kwa amani? Kutafaa nini kukumbushwa neema, hadhari na nasaha kama zikigongana na maslahi ya kiutu na mapatano ya kibiashara?

Imeelezwa katika kitabu Muhammad Rasullul-huriyya (Muhammad Mtume wa Uhuru) hivi: Mtume aliwaambia wafanyabiashara wa Kiislamu waanzishe soko jipya mjini Madina, wakaanzisha; likawa na nguvu soko hilo; wafanyi biashara wageni wakawa wanaelekea huko, na soko la Mayahudi likaathirika. Kwa sababu biashara katika soko la waislamu ilikuwa ya uadilifu sana kwa muuzaji na mteja. Hiyo peke yake ilitosha kujaza nyoyo za Mayahudi hasadi na chuki kwa Muhammad(s.a.w.w) na kuwafanya wavunje ahadi.

MAELEZO

Mwenyezi Mungu ameanza kuwaambia Mayahudi kukumbuka neema zake kwao.Miongoni mwa hizo neema ni kuwaletea Mitume wengi na kuwatukuza kwa Tawrat na Zabur. Vile vile kuwakomboa katika utumwa wa Firaun, kuokoka kwao kutokana na kufa maji, kuwateremshia Manna na Salwa, kuwapa milki na ufalme katika zama za Mtume Suleiman na mengineyo ambayo yanawajibisha kuamini na kushukuru na wala sio kukanusha na kukufuru. Unaweza kuuliza: Kwa nini msemo unawaelekea Mayahudi wa Madina pamoja na kujua kuwa neema zinazoelezwa zilikuwa kwa baba zao na sio kwao? Jibu: Neema kwa baba ni neema kwa watoto vile vile; ambapo mtoto anapata utukufu kutokana na baba yake. Zaidi ya hayo ni kwamba umma wote ni mmoja.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwakumbusha neema zake aliwaambia: Tekelezeni ahadi yangu nitatekeleza ahadi yenu. Ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kuchukua yale yanayofahamiwa na maumbile na yale ambayo vimeteremshwa vitabu kwayo, ikiwa ni pamoja na kumwamini Mwenyezi Mungu na Mitume yake na kufanya amali kwa hukmu zake. Mwenye Majmaul-Bayan anasema: Hakika Mwenyezi Mungu aliwaahidi katika Tawrat kwamba Yeye atawapelekea Mtume anayeitwa Muhammad. Fikra hii ndiyo wanayoielezea wafasiri wengi nayo ndiyo inayotolewa ushahidi na Quran. Ama ahadi ya Mayahudi ni ile ahadi ya Mwenyezi Mungu kwao. Na,kila mwenye kuamini akafanya amali njema basi Mwenyezi Mungu atamlipa thawabu siku ya Kiyama.

Imesemekana maana yake ni kwamba kama wakimcha Mwenyezi Mungu, basi atawainua katika maisha haya ya duniani.Tutaeleza fikra ya malipo katika dunia mahali pake Inshaallah. Kisha Mwenyezi Mungu amewaamrisha kuamini Quran na wasifanye haraka kuikanusha, kumkanusha Muhammad na kutaka maslahi tu. Na kwamba ni juu yao kuisimamisha swala na kutoa zaka ili wazitakase nafsi na mali zao.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu: Je, mnawaamrisha watu kutenda mema na mnajisahau, hali mnasoma kitabu, inawaelekea viongozi na wakubwa, sio kwa watu wote, kwa sababu watu wengine ni wafuasi, na viongozi ndio wenye kufuatwa. Wao ndio wanaoficha haki na hali wanaijua na wanatoa mawaidha lakini hawayafuati. Tunakariri tena kwamba mawaidha na nasaha haziendi pamoja na kutaka maslahi; na hayawezi kuacha athari yoyote isipokuwa katika nafsi isiyotaka maslahi na isiyokuwa na lengo lolote zaidi ya haki.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Na takeni msaada kwa kusubiri na kwa kuswali Imeelezwa tena katika Aya ya 153 ya Sura hii, kwa hivyo utakuja ufafanuzi wake huko Inshallah. Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Kwanza 2 Sura Al-Baqara

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NGOMBE)

﴿يَا أَيُّهَا النَّاسُ اعْبُدُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ﴾

21.Enyi watu! Mwabuduni Mola wenu ambaye amewaumba nyinyi na wale wa kabla yenu; ili mpate kuokoka.

﴿الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ فِرَاشًا وَالسَّمَاءَ بِنَاءً وَأَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجَ بِهِ مِنَ الثَّمَرَاتِ رِزْقًا لَّكُمْ فَلَا تَجْعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ﴾

22.Ambaye amewafanyia ardhi kuwa tandiko busati na mbingu kuwa paa na akateremsha kutoka mawinguni maji, na kwayo akatoa matunda yawe riziki zenu. Basi msimfanyizie Mwenyezi Mungu washirika na hali nyinyi mwajua.

MWABUDUNI MOLA WENU

Aya 21 22

Baada ya Mwenyezi Mungu kutaja waumini, makafiri na wanafiki kwa alama zao na sifa zao na yale yanayofafanua hali zao, aligeukia kuwaambia wote waliobaleghe wenye akili, wawe waumini au la, waliokuwepo wakati wa maneno na watakao kuwepo baadaye, wote aliwaamrisha kumwabudu Mwenyezi Mungu peke yake.

Amri hiyo kwa waumini ni kutaka uthabiti na kuendelea na imani na twaa. Kwa upande wa makafiri na wanafiki ni kuwataka watubie. Unaweza kuuliza, kwa nini umewajumlisha watakaopatikana, wakati ambapo maneno ni ya ana kwa ana, hayawezi kumhusu asiyekuwepo? Jibu: Kila jambo lina pande mbili: Upande wa nje ambao unahusika na yule aliyepo tu; kwa mfano kusema: Ameangamia yule aliye katika jahazi. Upande wa pili ni wa maana ya undani; kama kusema: Fanyeni uadilifu enyi watawala. Hapa amri itakuwa inafungamana na kila mtawala. Kwa hiyo Aya iko katika upande huu wa pili.

TAWI HUFUATA SHINA

Mwenye kufuatilia Aya za Quran na akazifikiria vizuri kwa undani ataona kuwa zikitaja msingi wowote katika misingi ya itikadi; kama Tawhid, Utume au Ufufuo, basi huuambatanisha na hoja na dalili, lakini kama zikitaja hukumu za sheria kama kuharamisha zinaa huwa bila ya dalili yoyote, je kuna siri gani? Jibu: Kukithibiti kupatikana kwa Muumba na Utume wa Muhammad(s.a.w.w) kwa hoja ya kiakili, basi kauli zao zinatosha kuwa ni hoja, wala haijuzu kuzikhalifu kwa hali yoyote. Kwa sababu kukhalifu kauli ya Mwenyezi Mungu na Mtume ni kupinga dalili ya kiakili juu ya Tawhid na Utume.

Yeyote mwenye kuamini na akakubali mashina haya mawili, basi ni juu yake kukubali kila lilothibitishwa na Quran na Hadith katika hukumu za sharia na tanzu zake bila ya maswali. Mwenye kuzikanusha hapana haja ya kujadiliana naye katika sharia na tanzu zake. Kwa ajili hiyo Quran imejihimu zaidi kuleta dalili juu ya Tawhid, Utume na Ufufuo (mambo ya msingi - shina). Imeanza kwa Tawhid kwa sababu ndio msingi mkubwa. Kwa hiyo anayeamini shina ni lazima aamini tawi la shina hilo.

TAWHID

Dini za Mwenyezi Mungu zote zinasimamia misingi mitatu: Tawhid, Utume na Ufufuo.Hakuna Mtume yeyote kuanzia Adam(a.s) mpaka Muhammad(s.a.w.w) ambaye hakusimamia mambo matatu haya. Yale yanayofuatia yanatokana na hayo. Kwa hiyo uadilifu, kudura na hekima zake ni sehemu ya Tawhid; Uimamu na Quran ni sehemu ya Utume; na hisabu pepo na moto ni sehemu ya Ufufuo. Quran tukufu imeanza na msingi wa Tawhid na ikaongoza kwenye dalili Zake; ikiwaambia watu: Mwabuduni Mola wenu ambaye amewaumba...

Kimsingi ni kwamba kumwabudu Mwenyezi Mungu kunataka kumjua kwanza kwa njia ya mkataa, sio njia ya kudhani kwa sababu dhana haiwezi kuitoshea haki na chochote; kwa ushahidi wa hiyo Quran yenyewe.

Ni njia gani inayopelekea kumjua Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa uwazi kabisa? Wanavyuoni wanahitilafiana katika namna ya njia hii, kila mmoja amethibitisha kwa vile alivyoona ni sawa. Kuna wale waliotegemea dalili ya kilimwengu ambayo wameielezea kwa namna hii ifuatayo:

* 7 Uislamu ni itikadi na Sharia. Itikadi ni kama kumwamini Mwenyezi Mungu na sifa zake; utume na isma yake, ufufuo na mengineyo katika mfano wake yaliyo katika ghaibu. Halithibiti jambo lolote katika masuala ya kiitikadi isipokuwa kwa njia ya mkataa: Ndio maana Ijtihad haiko katika itikadi. Ama sheria; kama vile ibada, mahusiano ya jamii,hukumu za makosa nk,inajuzu kuzithibitisha kwa njia ya dhana na ijtihad kwa sharti ya kuwepo dalili mkataa ya kusihi amali kwa njia hii hasa.

Hakika maumbile na matukio yake yenye kukaririka na yenye kutokea upya yanahitaji kuweko na sababu yake, na haiwezekani kuwa sababu iwe ni maumbile hayo yenyewe. Kama ingekuwa hivyo, basi ingelikuwa sababu na chenye kusababishiwa ni kitu kimoja; na huo ni mzunguko ulio batili kama tulivyoonyesha katika vifungu vilivyotangulia katika Aya ya 4 ya Surah hii.

Ikiwa sababu iko nje ya maumbile tutauliza; je, sababu hiyo ni natija ya sababu iliyotangulia au ni kwamba imepatikana yenyewe bila ya sababu? Kama kuna sababu, je na hiyo sababu nayo imepatikana na sababu ipi? Hivyo yataendelea maswali; na mlolongo huu wa maswali ni muhali. Kwa hiyo, inakuwa ni sababu ya pili ambayo ni kupatikana kwa dhati yake na kwake zinaishia na kukoma sababu zote; wala yenyewe haishilii kwa nyengine, nayo ni tamko la Mwenyezi Mungu, kukiambia kitu kuwa kikawa kun fayakun.

Dalili hii inasimamia kukubali nadharia ya sababu (Al-illiyyah) kwamba kila athari lazima iwe na mwenye kuileta athari hiyo na kila sababu ni lazima iwe na mwenye kuisababisha; kama vile elimu lazima iwe imetokana na mwenye elimu, na maandishi lazima yawe yameandikwa na mwandishi.8 Ili tuiweke wazi zaidi fikra ya ubatilifu wa mlolongo, na kulazimika kukomea kwenye sababu isiyokuwa na sababu, tutakupigia mfano: Hii michoro waliyoweka wahandisi wa michoro kwa ajili ya ndege, magari majengo, n.k. haina budi ikomee kwa mgunduzi wa kwanza ambaye ameweka huo mchoro; hata kama wengine wameuchukua kutoka kwake, na wala yeye hakuuchukua kutoka kwa mwingine.

Lau tukikadiria kuwa hakuna mgunduzi wa kwanza wa mchoro, basi lazima kusingekweko na ugunduzi wala mchoro.

* 8 Mwanafalsafa mmoja wa Kiingereza anayeitwa Hume anakanusha misingi ya sababu kwa kusema: Hakuna dalili kwamba kupatikana kitu lazima kuwe na sababu. Hatuna la kujibu kauli hii zaidi ya kusema kuwa kuondoa msingi wa sababu nikuondoa msingi wa akili za watu wote.Hakuna yoyote anayeweza kufikiria kupatikana kitu bila ya sababu. Kwa hivyo basi haifai kwa yeyote kusema na kuuliza: Mgunduzi wa kwanza aliuchukua wapi huu mchoro? Kwa sababu, maana ya ugunduzi ni kwamba, amegundua yeye mwenyewe bila ya kuchukua kutoka kwa mwingine. Hakika hii inajifahamisha yenyewe,kama linavyojifahamisha jua kwa mwanga wake.

Basi hivyo ndivyo ilivyo kwa upande wa Mwenye kuumba na Mwenye kuruzuku. Maana yake ni kuwa Yeye anaumba, lakini hakuumbwa, anaruzuku lakini haruzukiwi.Ndio ikawa Leibnitz anamwita Mwenyezi Mungu Mhandisi yaani mvumbuzi; Plato naye anamwita Mtengenezaji. Yote hayo ni kuonyesha kuwa yeye ni Muumbaji lakini si Mwenye kuumbwa. Wengine wanatolea dalili ya kuweko Mwenyezi Mungu kwa nidhamu ya ulimwengu na kupangika kwake kunakaoendelea.Dalili hiyo inaitwa dalili ya ukomo Al-ghai.

MAELEZO

Wataalamu wengi wapya wa elimu ya maumbile wanaona dhahiri ya maumbile haifai kuifasiri kwa sababu ya ukomo wake, bali ni lazima kuifasiri kwa sababu za kiutendaji. Jibu: sisi tunagundua kupatikana sababu ya kitendo kwa kupatikana sababu ya ukomo wake sawa na vile tunavyogundua seremala hodari kutokana na kupangika kitanda kifundi. Jibu linaweza kufunuka zaidi kutokana na maelezo yajayo. Kuna wengine waliotegemea wataalamu wa elimu ya maumbile na wengineo katika kugundua hakika nyingi. Kutokana na makadirio haya ndio ikaja nadharia ya mvutano (Force of gravity) aliyogundua Newton kutokana na kuanguka tofaa juu ya ardhi. Kwamba makadirio yote yasiyokuwa mvutano ni batili na makadirio ya mvutano ni sahihi.

Ama kuifuatilia dalili hii juu ya suala tulilonalo, ni kwamba sisi tunashuhudia nidhamu ya ulimwengu na mshikamano wake unaoendelea; kila tunavyokadiria kuwa nidhamu hii imepatikana bila ya Muumba mwenye hekima, basi hayo ni makadirio ya kipuuzi yasiyokubaliwa na akili, wala haikubali akili isipokuwa lazima awepo Muumbaji mwenye hekima na kuwa yeye ndiye ambaye amepangilia. Hebu angalia mfano huu: Kama ukiona jina lako limeandikwa angani kwa herufi za nuru; halafu usimwone mtu yeyote, huna budi kukadiria kuwa kuna mtu mwenye akili ana chombo kinachomwezesha kuchora herufi za nuru zenye kushikamana katika anga. Ni makadirio gani yasiyokuwa haya yanayowezwa kukadiriwa? Sadfa au kugongana gari mbili au kupatikana volkano, yote hayo yanakupeleka kwenye makosa. Akili yako haiwezi kutulia isipokuwa utakadaria tu kuwa kuna aliyefanya hivyo.

Basi hivyo ndiyo ilivyo kuhusu ulimwengu. Neno la kufikiria na lililo wazi zaidi ni lile la Voltaire aliposema: Hakika fikra ya kuwepo Mwenyezi Mungu ni dharura. Kwa sababu fikra inayopinga hiyo ni upumbavu. Nimesoma kitabu Adhahiratul-Quraniyya ukurasa wa 91 chapa ya 1958. Kuna aina fulani ya sisimizi katika Amerika huondoka nyumbani mwao kabla ya kulipuka moto kwa usiku mmoja. Vyovyote utakavyokadiria katika makadirio yote na tafsiri zote, haiwezi kutulia nafsi yako milele isipokuwa kwa kukadiria kupatikana mwenye kuzingatia vizuri mambo, mwenye hekima aliyeipa kila nafsi mwongozo wake.

Wengine wanategemea dalili ya kimaumbile na wanasema: Lau si Imani ya kupatikana Mwenyezi Mungu yangeliangamia makadirio yote ya kimaumbile na kusingelikuwa na wa kuwaepushia watu shari wala kusingelikuwa na wa kuwafahamisha heri. Dalili hii iko karibu zaidi na kukanusha kuliko kuthibitisha, kwani inaonyesha kuwa kumwamini Mwenyezi Mungu na hali hii ni wasila na sio lengo, kiasi ambacho lau ingekadiriwa kupatikana mtu anayefanya yale yanay-

otakikana kuyafanya na kuacha yale yasiyotakikana kuyafanya, basi asingelikuwa na wajibu wa kumwamini Mwenyezi Mungu. Hakuna mwenye kutia shaka kuwa kumfanya Mwenyezi Mungu ni chombo tu ni kubaya zaidi kuliko kumkanusha. Wengine hutegemea dalili ya hisia ya moyo; nayo ni hisia za moyo moja kwa moja. Wanasema kuwa moyo wa mtu unapata kumjua Muumbaji moja kwa moja bila ya dalili yoyote, sawa na vile unavyohisi mapenzi na chuki.Yamekw-ishatangulia maelezo kuhusu hayo katika tafsiri ya Aya ya 3.kifungu cha maarifa.

Njia bora zaidi ya zote ni ile aliyoitolea dalili Mwenyezi Mungu juu ya kupatikana Kwake. Kwa ufupi ni kuangalia na kufikiri katika kuumbwa mbingu na ardhi, mtu, mauti na uhai na neema kubwa. Na mengineyo yaliyokuja katika Quran tukufu, hadith za Mtume na Nahjul-Balagha. Ingawaje dailili hii hakika yake inarudi kwenye dalili ya Kawni (kupatikana ulimwengu) na dalili ya Al-ghai (ya ukomo), lakini mpangilio wa maelezo unafahamika upesi na unaweka karibu zaidi kufahamu vitu mahsusi na vya kiujumla. Asiyekinaika na Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa dalili za kupatikana Kwake alizozileta yeye mwenyewe, je anaweza kukinaishwa na mtu aliye mfano wake?

Ajabu ya maajabu ni kwamba anayemkanusha Mungu anaamini kabisa na kuitakidi kuwa shati alilolivaa - kwa mfano - limetokana na mbegu aliyoipanda mkulima kwa mpangilio; akaifuma mfanya kazi kwa umakini, akaiuza mfanya biashara kwa maarifa, baadaye mshonaji akaipasua na akaishona kwa kipimo kinachohitajika. Lakini haamini kupatikana aliyetengeneza vizuri huu ulimwengu na kila kitu.

Kwa kuongezea dalili ya kuweko Mwenyezi Mungu ambayo inaingia kwa ujumla, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amempa kila mtu dalili ya kuwepo yeye Mungu inayomuhusu yeye tu bila ya kushirikiana na mwingine. Mtu yeyote, vyovyote vile atakavyokuwa, akikumbuka mambo na majaribio yaliyompitia, na kama akiyapeleleza ni lazima atakuta katika

maisha yake amepitiwa na vitu visivyo na maelezo yoyote isipokuwa matakwa ya Mwenyezi Mungu tu. Mimi sikubali kabisa kuwa kuna mtu yeyote vyovyote alivyo, ijapokuwa ni kafiri, kuwa anaweza kuishi kipindi fulani cha maisha bila ya kupitiwa na kipindi kimoja katika maisha yake asiweze kumrejea Mwenyezi Mungu tena bila ya kukusudia wala kutambua. Atamwuelekea nani katika kipindi cha shida? Bila shaka atarudi katika maumbile ya Mwenyezi Mungu aliyowaumbia watu na yakapiga chapa kwa kila mwenye kuzaliwa, ambayo si baba anayeyajua wala mama.Mzandiki mmoja alimuuliza Imam Jafar Sadiq(a.s.) : Ni ipi dalili ya kuweko muumbaji? Imam akamwambia:

Lau unapanda chombo na mabaharia wote wakafa ukabaki wewe peke yako,je utakuwa unataraji kuokoka? Mzandiki akasema: Ndio Imam akasema: Hakika muumbaji (Mungu) ndiye yule utakayemtarajia wakati huo. Basi mimi ninampa nasaha yule anayetia shaka ya kuweko Mwenyezi Mungu asome dalili za wakanushaji na watu wa maada, bila shaka yoyote ataishilia kwenye kumwamini Mwenyezi Mungu; ambapo atakuta dalili ya kukanusha ni kwamba wao wanataka kumwuona Mwenyezi Mungu kwa macho na kumgusa kwa mkono na kumnusa kwa pua.

Nimetaja dalili nyingi sana katika maudhui haya katika kitabu Mwenyezi Mungu na akili na Falsafa ya mwanzo na marejeo ambacho nilikihusisha na kujibu Falsafa ya kimaada Vile vile katika kitabu Baina ya Mwenyezi Mungu na Mtu, Elimu ya Falsafa, Uislamu pamoja na Maisha, Uimamu wa Ali na Akili na mengineyo katika vitabu na makala.

Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuombwa kuzitwaharisha nafsi zetu na shaka na kuzikinga kwa tawfiki yake na radhi zake. Tumerefusha maneno katika msingi wa kwanza ambao ni Tawhid, ili uwe kama mdhibiti wa yote ambayo yatarudia kwake katika Aya zinazoambatana nao. Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Kwanza 2 Sura Al-Baqara 46

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿وَإِن كُنتُمْ فِي رَيْبٍ مِّمَّا نَزَّلْنَا عَلَىٰ عَبْدِنَا فَأْتُوا بِسُورَةٍ مِّن مِّثْلِهِ وَادْعُوا شُهَدَاءَكُم مِّن دُونِ اللَّـهِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴾

23. Na ikiwa mna shaka kwa (hayo) tuliyomteremshia mtumwa wetu, basi leteni sura moja iliyo mfano wake, na muwaite mashahidi wenu badala ya Mwenyezi Mungu ikiwa mnasema kweli.

﴿فَإِن لَّمْ تَفْعَلُوا وَلَن تَفْعَلُوا فَاتَّقُوا النَّارَ الَّتِي وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ أُعِدَّتْ لِلْكَافِرِينَ ﴾

24.Na msipofanya, na hamtafanya, basi uogopeni moto ambao kuni zake ni watu na mawe, uliowekewa makafiri.

﴿وَبَشِّرِ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أَنَّ لَهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ كُلَّمَا رُزِقُوا مِنْهَا مِن ثَمَرَةٍ رِّزْقًا قَالُوا هَـٰذَا الَّذِي رُزِقْنَا مِن قَبْلُ وَأُتُوا بِهِ مُتَشَابِهًا وَلَهُمْ فِيهَا أَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ وَهُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

25.Na wabashirie walioamini na wakafanya vitendo vizuri, kwamba watapata mabustani yapitayo mito chini yake; kila mara watakapopewa matunda humo kuwa riziki, watasema: Haya ndiyo yale tuliyopewa mwanzo, kwani wataletewa hali yakuwa yamefanana na humo watapata wake waliotakasika; na watakaa milele humo.

LETENI SURA

Aya 23-25

Kama ambavyo Quran imeongoza njia ya kujua kuweko Mwenyezi Mungu Mtukufu vilevile imeongoza njia ya kujua utume wa Muhammad(s.a.w.w) miongoni mwazo ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshia mtumwa wetu, yaani Muhammad(s.a.w.w). Basi leteni sura moja iliyo mfano wake.

Makusudio yake ni kushindwa kuleta mazungumzo yaliyo mfano wa Quran, wakiwa wao ndio mabingwa katika fasihi na shughuli yao kubwa ni fasihi, lakini si lazima walete yale yanayolingana nayo kwa idadi na umbo. Walipewa hiyari,wakipenda walete yote; Sura kumi au Sura moja. Vile vile hawakulazimishwa kuleta mfano wa maana yake katika kanuni za tabia, misingi ya sharia na habari za ghaibu, bali walitakiwa walete wanayoyaweza katika maana yoyote na lengo lolote mradi tu ubainifu wake uwe kama wa Quran.

Matakwa haya, kama unavyoyaona yasingeliwashinda kama ingelikuwa Quran haitoki kwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu wao hawakutakiwa wainue jabali au wakaushe bahari, isipokuwa walitakiwa maneno tu. Na wala hakuna kitu rahisi kama hicho kwao. Kwa hivyo kulipothibiti kushindwa kwao, imethibiti kwamba kuna siri fulani na wala hakuna tafsiri ya siri hii isipokuwa wahyi na Utume.Vilevile kila linaloshinda kutafsiriwa katika elimu halina budi kutafsiriwa na lile lililo juu ya maumbile. Hakuna kitu chenye nguvu zaidi katika kufahamisha ukweli wa Quran kuliko mkatao huu wa kauli yake Mwenyezi Mungu: Na hamtafanya mpaka hivi leo hajafanya yeyote baada yao. Na mlango bado umefunguliwa kwa anayetaka kujaribu mpaka mwisho.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwataja makafiri na adhabu ya moto waliyo nayo, amefuatisha kuwataja waumini, neema na thawabu; kama ilivyo desturi ya Quran, kukutanisha mapendekezo na vitisho na ahadi na kiaga kikali, kwa kusisitiza mwongozo na mawaidha. Wafasiri wengi wamesema kuwa dhamiri katika neno,Mfano wake inarudia Quran; yaani mfano wa Quran, kwa maana ya kuwa leteni sura iliyo na sifa za Quran na muundo wake.

Wengine wamesema, bali hiyo dhamiri inarudia mja wetu; yaani mfano wa mja wetu ambaye ni Muhammad(s.a.w.w) . Kwa maana ya kuwa mleteni Ummiy (mtu asiyesoma),kama Muhammad, aweze kuleta mfano wa Quran hii ambayo ameileta mtu huyu Ummiy.

Maana zipo sawasawa kwa kauli zote mbili ingawaje kauli ya kwanza ndiyo mashuhuri na dhahiri zaidi, ambapo Mwenyezi Mungu amesema: Ikiwa mna shaka kwa tuliyomteremshia...Na wala hakusema; ikiwa mna shaka katika Muhammad(s.a.w.w) . Hata hivyo kauli ya pili ina maana yenye nguvu, kwani lau yakadiriwa kuwa mtu mwenye uwezo analeta mfano wa Quran lisingelikuwa hilo ni ushindi. Kwa sababu wajihi wa kushinda unakuja kwa kuletwa na asiyesoma (Ummiy) sio kwa mjuzi mwenye uwezo.

Makusidio ya kuni ni chochote kinachowashiwa moto. Watu ni wale waasi, na mawe ni masanamu waliyokuwa wakiyaabudu washirikina.

SIRI YA MUUJIZAWA QURAN

Utume ni ubalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, anamhusisha nao anayemtaka katika waja wake ili awafikishiye yale wasiyoweza kuyajua; Mwenyezi Mungu amempa nguvu kila Mtume kwa ubainifu ulio wazi juu ya ukweli wa utume wake, ili iwe ni hoja kwa wale waliopelekewa Mtume. Sharti la msingi la ubainifu huo, ni kuwa uwe katika namna maalum inayodhihiri katika mkono wa Mtume na sio mwingine. Hiyo ni kwa kuchukuwa hadhari ya kutatizika kati ya Mtume na asiyekuwa Mtume. Muhammad(s.a.w.w) naye ana ubainifu na dalili juu ya utume wake. Miongoni mwa dalili zake ni hii Quran ambayo nakala zake zimeenea kila mahali na Aya zake zinasikika katika vipaaza sauti na katika idhaa za radio mashariki na magharibi, hata Israel.

Njia inayofahamisha kwamba hiyo Quran imeshinda, ni kuwa kila mkanushaji alishindwa na anaendelea kushindwa kuleta kitu kama Quran au kuleta Sura kama hiyo. Haijanakiliwa habari kuwa kuna mtu aliyeweza kuanzia zamani hadi sasa; ingawaje wapinzani na maadui wa Uislamu na Waislamu ni wengi. Kwa hiyo kimsingi kuthibiti muujiza ndio kuthibiti kwa Utume wa Muhammad(s.a.w.w) .

Baada ya wanavyuoni kuafikiana kwamba Quran ni muujiza wametofatiana katika njia ya muujiza wenyewe na siri yake. Je, ni maajabu na uzuri wa muundo wake? Au ni madhumuni yake mkusanyiko wa elimu, kanuni za sheria na kutolea habari mambo ya ghaibu, n.k.? Au ni mambo yote mawili pamoja?

Wamerefusha maneno katika kubainisha wajihi wa muujiza na kuweka vitabu mahsusi. Sitaki kurefusha yale yaliyosemwa, nafupiliza yale niliyoyaona yana mwelekeo. Kwa ufupi ni kwamba mtu anaweza kumwiga mtu aliye mfano wake kwa kauli na vitendo. Lakini kumwiga Muumba wake katika athari yoyote miongoni mwa athari Zake, ni muhali. Kwa sababu mtu hawezi kupetuka mpaka wake akiwa kama muumbwa, vyovyote atakavyokuwa na nguvu au mkubwa. Ni vizuri kufafanua kama ifuatavyo:

KUSHINDA

Tumedokeza kwamba Muhammad aliwashinda wapinzani kwa Quran. Hapana shaka kwamba ushindi unatimu na unakubalika ikiwa kitendo chenyewe anakiweza mtu aliyekusudiwa kushindwa; Kama kumtaka mwenye mkono mzima auweke juu ya kichwa chake, au aondoe unyayo ard- hini. Lakini ukimtaka asiyejua kusoma asome na asiyekuwa tabibu atibu au asiyekuwa malenga atunge shairi, haitakuwa ni kushindwa. Muhammad(s.a.w.w) amewashinda wapinzani jambo wanaloliweza (maneno) likawashinda, na kushindwa kwao huko kumeongezea Quran sifa ya muujiza. Unaweza kuuliza: Je, muujiza wa Quran ni kwa yule fasihi wa lugha ya Kiarabu au asiyejua Kiarabu au mtu dhaifu?

Jibu:Quran ni muujiza kwa kuwa ni maneno ya Mwenyezi Mungu bila ya kumwangalia fasihi na asiyekuwa fasihi, isipokuwa tunajua kwamba ni muujiza kwa kushindwa mwarabu aliye na ufasaha; sawa, na tunapogundua bingwa wa kuogelea anaposhindwa kuogelea kwenye bahari ya mawimbi, kuwa ni kigezo kwamba mwingine asiye bingwa haiwezi bahari hiyo. Yaani ikiwa fasihi ameshindwa basi mwingine ndio kabisa. Kwa maelezo yetu sisi mafaqihi ni kwamba kushindwa kwa fasihi ni sababu ya kujua muujiza wa Quran na wala sio fungu au sharti lake.

JE, MUHAMMAD ANAMUUJIZAMWINGINE ZAIDI YAQURAN?

Wengine wanaona kuwa Muhammad(s.a.w.w) hana muujiza mwingine isipokuwa Quran Ama mimi niko pamoja na wanaoamini kwamba miujiza yake haina ya idadi. K wa sababu hekima ya kiungu inapelekea kupatikana namna namna za miujiza kwa kutofautiana hali na watu; kama ilivyofanya hekima yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ya kuapizana Mtume wake na Wakristo wa Najran. Hayo ni ikiwa mwenye kutaka muujiza anautaka kwa kusadikisha.

Ama mwongo mkaidi asiyetoshwa na chochote, anatoshewa na Quran tu. Kwa sababu muujiza wa Quran ni msingi wa yote, si wa wakati fulani wala na kundi fulani au mtu fulani. Mara nyingine hekima inataka kutoonyeshwa mtu muujiza kabisa; kama vile kutosheka kwa utambuzi na hisia tu, au kwa kuapa Mtume tu. Imekuja hadith kueleza kwamba mtu mmoja alimwambia Muhammad(s.a.w.w) : Nina haja gani na muujiza? Apa tu kwa Mwenyezi Mungu, kwamba wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mimi nitakuamini. Mtume Akasema:Naapa kwa Mwenyezi Mungu mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu . Yule mtu akasema: Nashuhudia kwamba hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Ambalo linatufahamisha kwamba miujiza ya Muhammad(s.a.w.w) haina idadi, ni kwamba mtu wa dini zamani alikuwa akitoa dalili za Utume wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) kutokana na hadith za kusema na mawe, kujiwa na miti na kuchimbuka maji katika vidole vyake na watu walikuwa wakiyakubali wakati huo. Ama leo ambapo watu wamejitokeza katika maisha bora (na teknolojia), sisi twatoa dalili Utume wake kwamba yeye alisimama pamoja na wanyonge na kuwapiga vita wadhalimu. Na kwa fadhila zake na fadhila za sheria yake yalivuliwa mataji kutoka katika vichwa vya wastakbari na kutupwa chini ya miguu ya wachunga ngamia na zikagawanywa hazina za wafalme kwa mafukara na maskini.

Kwa vyovyote ilivyo ni kwamba miujiza yote ya Mtume mtukufu ni muhimu na mikubwa, lakini muhimu zaidi katika kukadiria kwangu ni mambo mawili:

Kwanza : sheria ya Quran ambayo imepanga haki za watu na ufungamano wa watu kati yao juu ya misingi ya uadilifu na kusaidiana. Nitaonyesha kila kitu mahali pake Inshaallah.

Pili : maapizano ya Mtume pamoja na ujumbe wa Najran, ambayo ameyataja Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika Sura ya Al-Imran (3).

Hakika maapizano haya ni dalili mkataa na ni mpaka wenye kupambanua, ambao unamweka mpinzani mbele ya adhabu na maangamizo ana kwa ana Maangamizo atakayoyateremsha Muhammad (s.a.w.) kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kwa tamko moja tu linalotoka katika mdomo wake mtakatifu.

Hakika ushindi huu hauna mfano wake katika historia ya binadamu. Utakuja ufafanuzi mahali pake Inshaallah.Tumerefusha maneno katika msingi wa pili (Utume) ili uwe ni uthabiti wenye kuenea wa kila linaloambatana nao katika Aya. Nimetunga kitabu maalum kuhusu Utume nilichokiita Anubuwa wal-Aql (Utume na Akili), kimechapishwa mara nne.

﴿ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَسْتَحْيِي أَن يَضْرِبَ مَثَلًا مَّا بَعُوضَةً فَمَا فَوْقَهَا فَأَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا فَيَعْلَمُونَ أَنَّهُ الْحَقُّ مِن رَّبِّهِمْ وَأَمَّا الَّذِينَ كَفَرُوا فَيَقُولُونَ مَاذَا أَرَادَ اللَّـهُ بِهَـٰذَا مَثَلًا يُضِلُّ بِهِ كَثِيرًا وَيَهْدِي بِهِ كَثِيرًا وَمَا يُضِلُّ بِهِ إِلَّا الْفَاسِقِينَ ﴾

26.Hakika Mwenyezi Mungu haoni haya kupiga mfano wowote wa mbu na ulio wa zaidi yake. Ama wale walioamini, wao hujua ya kwamba hiyo ni haki iliyotoka kwa Mola wao; lakini wale waliokufuru husema: Nini analotaka Mwenyezi Mungu kwa mfano huu? Mwenyezi Mungu huwapoteza kwa mfano huo wengi na huwaongoza kwa mfano huo wengi na hawapotezi kwa (mfano) huo isipokuwa wale mafasiki.

﴿ الَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهْدَ اللَّـهِ مِن بَعْدِ مِيثَاقِهِ وَيَقْطَعُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ ﴾

27.Wanaovunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kwisha kuifunga na kuyakata aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu kuungwa, na kufanya ufisadi katika ardhi. Hao ndio wenye hasara.

HAKIKA MWENYEZI MUNGU HAONI HAYA KUPIGA MFANO WOWOTE

Aya 26 – 27

HAYA

Haya ikinasibishwa kwa mtu maana yake ni kubadilika hali yake ya tabia kuwa hali nyingine, kwa sababu fulani.Haya ya mtu inaweza kuwa nzuri au mbaya. Nzuri, ni ile kuona haya mtu kufanya mambo maovu na machafu. Kwa hivyo ndio ikawa inasemwa kwa yule anayefanya uovu bila ya kujali: Kama huoni haya fanya unavyopenda. Imam Jafar Sadiq(a.s) amesema;Hana haya asiyekuwa na Imani.

Ama ubaya wa haya, ni mtu kuacha kufanya yale yanayotakikana kwa kuogopa; kama vile mtu kuona haya kujifun-disha, kutafuta maarifa, n.k. Amirul Muminin amesema: Woga uko pamoja na kushindwa; kukosa huletwa na haya, na wakati unapita kama mawingu (ya kiangazi). Ilisemwa zamani: Hakuna haya katika dini.

Hiyo ni haya kwa upande wa binadamu. Ama ikinasibishwa kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.), inakuwa makusudio yake ni kuacha kitendo. Kama ilivyoelezwa katika hadith: Hakika Mwenyezi Mungu anamuonea haya mzee, yaani anaacha kumwadhibu.

Makusudio ya kupiga mfano ni kuiweka wazi fikra na kuondoa mikanganyo. Makusudio ya ahadi ya Mwenyezi Mungu ni hoja iliyosimama kwa waja wa Mwenyezi Mungu; ni sawa iwe matokeo ya hoja hiyo ni maumbile na akili au kunakili kwenye kuthibiti kutoka katika kitabu chenye kuteremshwa au kutoka kwa Mtume.

Makusudio ya kufunga hapa ni kukata na kuhukumu. Ahadi kubwa zaidi ya Mwenyezi Mungu iliyopitishwa ni kumfanya peke Yake na kumfanyia ikhlas jambo ambalo linafahamika kutokana na akili na kuthibitishwa na sharia.

Makusudio ya kukata aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu kuungwa ni maamrisho yake na makatazo yake. Kwa mujibu wa irabu za kinahaw (sarufi) inawezekana kuwa maana yake ni, Hakika Mwenyezi Mungu haachi kujaalia mbu kuwa mfano. Pia inawezekana, kuwa maana yake ni, Hakika Mwenyezi Mungu haachi kujaalia kitu chochote kuwa mfano, hata kama kitu hicho ni mbu.

UONGOFU NA UPOTEVU

Uongofu una maana nyingi; kama ifuatavyo:-

Kubainisha na kuongoza. Aya nyingi katika Quran zina maana hiyo; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

﴿ وَمَا مَنَعَ النَّاسَ أَن يُؤْمِنُوا إِذْ جَاءَهُمُ الْهُدَىٰ ﴾

Na hapana lililozuilia watu kuamini ulipowajia uongofu (17:94)

Vile vile kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ الْهُدَىٰ﴾

Hakika umewajia uongofu kutoka kwa Mola wao (53:23)

Yaani; wala hapana ubainifu wa Mwenyezi Mungu isipokuwa ule waliokuja nao Mitume au uliohukumiwa na hukumu ya wazi isiyokuwa na shaka.

Kukubali mtu nasaha na kunufaika nayo; kama asemavyo Mwenyezi Mungu:

﴿ قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَكُمُ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ فَمَنِ اهْتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهْتَدِي لِنَفْسِهِ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيْهَا﴾

Sema: Enyi watu! Haki imekwisha wajia kutoka kwa Mola wenu, basi anayeongoka anaongoka kwa nafsi yake na anayepotea anapotea kwa nafsi yake. (10:108).

Tawfiq na msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa njia mahsusi; kama anavyosema Mwenyezi Mungu:

﴿ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ﴾

...lakini Mwenyezi Mungu humuongoza amtakaye.. .(2:272)

Na kauli yake:

﴿ وَأَنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يُرِيدُ﴾

...na hakika Mwenyezi Mungu humuongoza amtakaye... (22:16)

Yaani anamwafikisha kwenye amali kwa uongofu na kumwandalia njia ya kuendea. Kimsingi ni kwamba uongofu kwa maana ya ubainifu tu haulazimishi kuwafikisha kwenye amali; kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

﴿ لَّيْسَ عَلَيْكَ هُدَاهُمْ ﴾

Si juu yako uongofu wao. (2:272)

yaani si juu yako wafanye amali kwa uongofu wako au wasifanye; isipokuwa ni juu yako kubainisha tu Thawabu; kama kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ يَهْدِيهِمْ رَبُّهُم بِإِيمَانِهِمْ تَجْرِي مِن تَحْتِهِمُ الْأَنْهَارُ فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ﴾

Hakika wale walioamini na kufanya vitendo vizuri, Mola wao atawaongoza kwa sababu ya Imani yao; itakuwa inapita mito mbele yao katika mabustani yenye neema. (10:9)

Yaani atawapa thawabu kwa sababu ya imani yao.

Mwenye Kuongoza na mwenye kubainisha, kwa kuangalia kwamba uongofu umepatikana kwa sababu yake.Hayo ndiyo makusudio katika Aya hii tunayoizungumzia. Amesema mwenye Majmaul-Bayan: Kauli yake Mwenyezi Mungu: Huongoza wengi kwa mfano huo,anakusudia wale ambao wameamini. Kwa kuwa uongofu umepatikana kwa sababu ya Mwenyezi Mungu, basi umetengenezwa kwake.

Hukumu; kama kusema: Kadhi amehukumu sawa sawa; yaani amehukumu kwa uadilifu wake. Maana haya yanafaa kuyanasibisha kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Upotevu, nao pia una maana nyingi: Miongoni mwayo ni haya yafuatayo:-

Kutia mashaka, kuingiza katika ufisadi na kuizuilia dini na haki. Maana haya hayategemezwi kwa Mwenyezi Mungu kwa hali yoyote; bal hunasibishwa kwa Iblis na wafuasi wake; kama asemayo Mwenyezi Mungu akimzungumzia Iblis, Firaun na Samiri:

﴿ وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ﴾

kwa hakika nitawapoteza na nitawatamanisha... (4:119)

﴿ وَأَضَلَّ فِرْعَوْنُ قَوْمَهُ وَمَا هَدَىٰ﴾

Na Firaun akawapoteza watu wake na hakuwaongoza. (20:79)

﴿ وَأَضَلَّهُمُ السَّامِرِيُّ﴾

...Na akawapoteza Samiri (20:85)

ADHABU

Aya nyingi katika Quran zimekuja kwa maana haya; kama vile:

﴿ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللَّـهُ الْكَافِرِينَ ﴾

Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu huwapoteza makafiri (40:74)

﴿ وَيُضِلُّ اللَّـهُ الظَّالِمِينَ﴾

...Na Mwenyezi Mungu huwapoteza madhalimu... (14:27)

﴿ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللَّـهُ مَنْ هُوَ مُسْرِفٌ مُّرْتَابٌ﴾

Kama hivyo Mwenyezi Mungu humpoteza aliyepita kiasi mwenye shaka (40:34)

Yaani anawaadhibu waongo, makafiri na madhalimu.

Kukusudiwa jina la mpotezaji,kama kusema Amepotezwa na fulani Ukikusudia kumnasibisha kwenye upotevu na kumzingatia kuwa ni katika wapotevu.

Kujitenga mtu na nafsi yake. Mwenye kumpuuza mtoto wake bila ya malezi yoyote au usaidizi wowote,inafaa kuambiwa amempoteza mtoto wake.

Kupoteza kitu. Husemwa: Fulani amepoteza ngamia wake. Maana haya vile vile hayanasibishwi kwa Mwenyezi Mungu. Majaribio na mitihani, kwa namna ambayo hupatikana upotevu kwenye ubainifu ambao Mwenyezi Mungu humtahini mja wake. Mwenye Majmau anasema: Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu anawatahini kwa mifano hii waja wake, kwa hiyo huwapoteza watu wengi na huwaongoza watu wengi.

MAELEZO

Maana yanayopatikana kutokana na Aya mbili hizi ni kwamba Mwenyezi Mungu haachi kupiga mifano kwa vitu ambavyo wajinga wanaviona ni duni; kama buibui, nzi, mbu na wengineo. Kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Muumba na Mola wa kila kitu; kwake bawa la mbu na ulimwengu mzima ni sawa tu.

Zaidi hayo kupiga mifano kunapatikana katika lugha zote ili kuziweka wazi fikra kwa kuzikutanisha na vyenye kuhisiwa. Kwa hivyo, kila linalohakikisha kupatikana kwa lengo hili linafaa kufanywa ni mfano, liwe dogo au kubwa; na kwalo inatimu hoja kwa kila mpinzani. Mwenyezi Mungu amewatahini watu kwa mifano hii, kama alivyowatahini kwa mambo mengine miongoni mwa dalili na ishara. Wengi wakaitumia na wengi wakapinga. Wale walioitumia ni wale wema walio waumini na waliopinga ni wale mafasiki waliopotea.

Kumesihi kuutegemeza uongofu na upotevu kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kwa kuangalia kuwa Yeye ndiye aliyepiga mifano ambayo imekuwa ni rehema kwa aliyewaidhika na ni mateso kwa asiyewaidhika. Ni vizuri kuleta mfano ili kufafanua fikra hii: Mwanachuoni alipata elimu na ikamwinua, halafu akahusudiwa na hasadi ikadhuru kiwiliwili na akili yake; kama alivyosema Imam Ali(a.s) :Siha ya mwili ni husuda kuwa chache . Inafaa kusema kuwa mwanachuoni huyu ndiye aliyemfanya hasidi kufanya uovu huu; au kama vile unavyosema: Uzuri wa mwanamke fulani umeharibu akili ya mwanamume fulani. Pengine wawili hao hata hawajuani.

Kwa mtazamo huu ndipo umenasibishwa upotevu kwa Mwenyezi Mungu kimajazi. Kwa vile Yeye ndiye aliyebainisha hoja na kuziweka wazi, na mhalifu alipozikhalifu akapotea. Lau Mwenyezi Mungu asingelibainisha, basi kusingekuwepo na suala la utiifu na uasi na asingelikuwako mpotevu na mwongofu. Mwenyezi Mungu amemwita yule asiyepata onyo kwa mifano: Fasiki, mvunja ahadi na mkataji wa yale aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu ya ungwe, ambayo ni kufuatilia mambo ya heri na kuungana na watu wa heri na mengineyo ya kusaidiana kwenye heri.

KUUMBA NA KUWEKA SHARIA

Mwenyezi Mungu ana matakwa mawili: Matakwa ya kuumba ibara yake ni Kun fayakun (kuwa na ikawa).Kwa matakwa haya kinapatikana ambacho hakikuweko. Matakwa ya pili, ni ya kuweko sharia ambayo yanakuwa katika ibara ya kuamrisha na kukataza na kulingania kwenye heri na kuacha shari. Mja akifanya heri huifanya kwa matakwa yake na hiyari yake bila ya kulazimishwa. Vile vile akifanya shari na kuacha heri.

Ikiwa utekelezaji wa hukumu zote za dini unafungamana na matakwa ya wale wenye kukalifiwa na hukumu hizo na hiyari, wala kusiweko mwenye kuwachunga isipokuwa wao wenyewe, basi itakuwa ni kosa kusema kuwa dini imeathiri katika kuanguka wafuasi wake na wenye kunasibika nayo. Ndio, lau wangeliitumia dini na wakaifuata kwa ukamilifu kwenye vitendo vyao, ingelifaa kufanywa dini ni kipimo cha kupanda na kuanguka kwao. Kwa hali hiyo basi ndio inabainika hasadi na chuki dhidi ya Uislamu katika kauli ya aliyesema; Unyonge wa Waislamu ni dalili ya unyonge wa Uislamu na mafundisho yake.

Kutokana na matamko ya mkosaji, inajuzu kwetu kunasibisha katika dini ya Kikristo kila ufasiki, uovu, na kuvunjiana heshima katika Ulaya na Amerika. Vile vile kunasibisha uharibifu wa vita vyote vilivyoathiri dola za Kikristo katika Mashariki na Magharibi ya dunia mpaka kulipuka bomu la Atomiki katika Hiroshima, na mabomu yaliyotupwa Veitnam; na hata kubadili maumbile 9 na kuongezeka idadi ya makosa na maovu siku baada ya siku katika Ulaya na Amerika mpaka kufikia hatua ya kuhalalisha ulawiti katika Uingereza kikanuni na kikanisa.

* 9 Sehemu kubwa ya Hiroshima na Nagasaki zilizopigwa bomu la Atomiki ardhi yake haimei kitu, na watoto wengi hadi leo huzaliwa na kasoro mwilini kutokana na athari ya bomu hilo - Mfasiri Je, yote hayo na mengi mengineyo yanafaa kunasibishwa kwa Masih (a.s.)? Hapana! Ametakasika na uchafu wote huu. Kama tungechukulia uzushi wa huyo mzushi, angelikuwa Myahudi wa Yemen ni sawa na Myahudi wa New York na Mkristo wa Misri ni sawa na wa Paris kimaendeleo.

Kuacha kuendelea miji kuna sababu nyingi sana zisizokuwa za dini; hasa ujinga, Historia ya kubakia katika unyonge na matatizo ya mazingira, na kukosa kuchangayika miji iliyoendelea na ile isiyoendelea.10 Lau kama si kuchanganyika Waislamu wa kwanza na mataifa mengine isingebaki athari yoyote ya maendeleo ya kiislamu. Naam! Uislamu ulikuwa ndio msukumo wa mchanganyiko huo.

Kwa ufupi sababu za kutoendelea hazitokani na tabia ya Uislamu wala ya Ukristo au wasiokuwa na dini, bali ni kutokana na hali za kijamii. Tutarudia kufafanua zaidi tutakapofika kwenye Aya za maudhui ya Jabri na Tafwidh (kutenzwa nguvu na kuachiwa). Na hayo tumeyaelezea kwa ufafanuzi katika kitabu Maalimul Falsafatul Islamiya na kitabu Maashiatul Imamiya.

* 10 Dini ni sawa na baraza la kutunga sharia. Ama utekelezaji ni wa mwingine. Umoja wa mataifa umefeli katika maazimio yake mengi muhimu na baraza la usalama nalo likafeli kuyatekeleza. Vile vile haikufaulu mikutano ya uongozi wa siasa zisizofungamana na upande wowote na wengineo. Mara ngapi wameshindwa, lakini lawama halikuwa lao. Sasa itakuwaje Uislamu ulaumiwe kwa sababu ya wanaoitwa Waislamu.


5

6

7

8

9

10

11

12

13

14

15