TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA13%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Mwandishi:
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Juzuu 9 Juzuu 10 Juzuu 11
  • Anza
  • Iliyopita
  • 20 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39797 / Pakua: 5102
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَنِّي فَضَّلْتُكُمْ عَلَى الْعَالَمِينَ ﴾

47.Enyi wana wa Israil, ikumbukeni neema Yangu niliyowaneemesha, na nikawatukuza kuliko viumbe wengine.

﴿ وَاتَّقُوا يَوْمًا لَّا تَجْزِي نَفْسٌ عَن نَّفْسٍ شَيْئًا وَلَا يُقْبَلُ مِنْهَا شَفَاعَةٌ وَلَا يُؤْخَذُ مِنْهَا عَدْلٌ وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ﴾

48.Na iogopeni siku ambayo nafsi haitafaa nafsi kwa lolote.Wala hayatakubaliwa kwake maombezi (shufaa), wala hakitapokelewa kikomboleo; wala hawatanusuriwa.

WANAWA ISRAIL TENA!

Aya 47 - 48

MAELEZO

Enyi wana wa Israil ikumbukeni neema Yangu.

Aya hii inatilia mkazo Aya iliyotangulia, na ni maandalizi kwa yatakayokuja baada yake. Tutaonyesha katika sehemu itakayofuatia hekima ya kukaririka. Makusudio ya kukumbuka hapa ni kushukuru; yaani zishukuruni neema zangu kwa usikizi na twaa. Na nikawatukuza kuliko viumbe wengine.

Mwenyezi Mungu aliwafadhilisha kuliko mataifa mengine ya wakati huo. Herufi lam katika neno Alamin ni ya kuenea kwa kawaida, sio kuenea kwa kiuhakika. Inatosha kuwa ubora ni katika upande mmoja na sio pande zote. Upande ambao Waisrail wamepambanuka na watu wengine ni kwamba Mwenyezi Mungu aliwapelekea idadi ya Mitume; kwa mfano Musa, Harun, Yoshua, Zakaria na Yahya na wengineo. Wote hao ni Waisrail. Vyovyote ilivyo, kuwa bora kwao kwa watu wa zama zao kwa upande fulani, hakufahamishi kuwa bora katika kila upande kwa watu wa wakati huo; wala sio kwamba mtu wao ni bora kuliko mtu mwingine. Bali kule kuwa Mitume wengi wamekuja kutokana na kabila lao ni hoja juu yao na wala sio hoja yao, kwa sababu hilo linafahamisha kwamba wao walikuwa katika upotevu sana, ikawa kuna haja sana wapate waonyaji na wahadharishaji. Na ogopeni siku mbayo nafsi haitaifaa nafsi nyingine kwa lolote. Yaani kila mtu na lake hakuna dhahiri wala batini, hakuna kusaidiana wala kuoneana huruma.

﴿ يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ ﴾

Siku ambayo mtu atamkimbia ndugu yake. (80:34).

Wala hayatakubaliwa kwake (hiyo nafsi) maombezi (shufaa), wala hakitapokelewa kikomboleo; wala hawatanusuriwa. Yaani Kiyama ni sawa na mauti, haufai usaidizi wowote, haitafaa fidiya yoyote, hata ikiwa ghali, wala haitazuia nguvu yoyote hata iwe kubwa kiasi gani. Hakuna chochote isipokuwa Rehema ya Mwenyezi Mungu:

﴿ لَئِن لَّمْ يَرْحَمْنَا رَبُّنَا وَيَغْفِرْ لَنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ ﴾

Kama hataturehemu Mola wetu na kutusamehe, bila shaka tutakuwa miongoni mwa waliopata hasara. (7:149)

KUKARIRIKA KATIKA QURAN

Mara ya pili Mwenyezi Mungu anawaku-mbusha wana Israil neema Zake na amerudia baada ya Aya tano. Hiyo siyo Aya peke yake iliyorudiwa katika Quran, zimeka-ririka Aya nyingi hasa zile zinazofungamana na wana wa Israil pamoja na Musa(a.s.) . Wengi hujiuliza sababu ya kukaririka Aya.Wameafikiana wafasiri kwamba hekima ya kukaririka ni kutilia mkazo. Baada ya kupita siku, wakuu wa vyama, wanasiasa, wafanyibiashara na wenye mashirika wamegundua kwamba, kukar-irika jambo ndio njia nzuri ya kulipendekeza, kulikinaisha na kulifanyia propaganda. Kwa ajili hiyo ndio wakaweka mitindo mbali mbali ya matangazo, kukawa na watu maalum wa kuhusika nayo na yakawa ghali sana.

Gustave Lebon anasema katika kitabu chake kiitwacho The man and his work: Mwenye kulikariri tamko mara kwa mara hulibadilisha kuwa itikadi. Dr Gibson katika kitabu kilichotarjumiwa kwa kiarabu kayfa tufakkir (Vipi utafikiri) anasema Ibara zina sumaku zinapokaririka mara kwa mara mbele ya macho yetu na masikio yetu, zinapumbaza akili zetu kabisa. Kwa hivyo basi Quran inakariri kwa mfumo mwingine pamoja na kuzidisha makemeo na mengineyo kwa kiasi cha hekima inavyotaka.

SHUFAA (UOMBEZI)

Hapana budi shufaa iwe na pande tatu: Mwenye kuombwa, mwenye kuombewa na muombezi ambaye anakuwa kati ya hao wawili, anaomba kwa yule wa kwanza ili amsaidie wa pili ni sawa apate idhini ya yule mwenye kuombwa au la. Hiyo ndiyo Shufaa kwa viumbe. Ama shufaa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) maana yake ni msamaha na maghufira kwa mwenye dhambi; haitakuwa shufaa mbele ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa idhini yake.

Amesema mwenye Majmaul-Bayan Shufaa kwetu ni yenye kuhusika na kuondoa madhara na kuondoa mateso kwa mumin mwenye dhambi. Muutazila na Khawarij wamekanusha Shufaa ya Muhammad(s.a.w.w) kwa wenye madhambi makubwa katika umati wake, kwa maana hii tuliyoinakili kutoka kwa mwenye Majmaul-Bayan, lakini Imamiya na Ashaira wameithibitisha kwamba iko.Akili haihukumu kutokea Shufaa au kutotokea, lakini haioni pingamizi yoyote ya kupatikana. Kwa hiyo, kusihi kwake na kuthibiti kwake kutategemea kunakili kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Ambaye kumemthibitikia kunakili huko, basi ni wajibu kwake kuamini Shufaa, na kama hakuthibitikiwa basi atasamehewa. Kwa hali hiyo inatubainika kuwa shufaa si msingi wa dini na kwamba mwenye kuikanusha na huku anamwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi huyo ni Mwislamu bila shaka.

Tukirudi kwenye Aya za Quran tunakuta nyingine zinakanusha; kama ile inayosema:

﴿ يَوْمٌ لَّا بَيْعٌ فِيهِ وَلَا خُلَّةٌ وَلَا شَفَاعَةٌ ﴾

...Siku ambayo hapatakuwa na bishara wala urafiki wala Shufaa (uombezi).... (2:254)

Hapo inaonyesha kukanusha Shufaa kabisa.Na Aya nyingine zinathibitisha kwa sharti; kama ile inayosema:

﴿لَا تُغْنِي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا إِلَّا مِن بَعْدِ أَن يَأْذَنَ اللَّـهُ لِمَن يَشَاءُ وَيَرْضَىٰ ﴾

....Hautafaa chochote uombezi (shufaa) wao isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia. (53:26)

Tukiziunganisha Aya mbili hizi na tukazikusanya pamoja, natija itakuwa, Mwenyezi Mungu atakubali Shufaa kutoka kwa mwombezi baada ya kumpa idhini. Sio lazima kupatikana idhini ya Mwenyezi Mungu kwa jina la mmoja mmoja, bali inatosha tu kwa Mtume kujua kwamba Shufaa ni halali ikiwa yule mwenye kuombewa si katika wenye kuwakandamiza watu na kunyanganya riziki zao; bali ni katika watu wa kawaida tu, ambao wanafanya madhambi ya kawaida.

Kwa maneno mengine ni kwamba makusudio ya idhini ya Mwenyezi Mungu kwa Shufaa ni kumpa wahyi Mtume wake kwamba Mimi nimekuruhusu kuwaombea uwatakao katika Umma wako ambao wamefanya mad- hambi maalum. Hapo basi mambo ya hao wenye madhambi yatakuwa mikononi mwa Mtume(s.a.w.w) ; naye atamwombea yule mwenye kustahiki kuombewa. Imethibiti kwamba yeye amesema: Nimeuweka akiba uombezi wangu kuwaombea wenye madhambi makubwa katika Umma wangu.

Sisi tuna yakini kuthibiti Shufaa katika Uislamu.Lakini hatujui kwa ufafanuzi; wakati huo huo tunaamini kwa imani ya mkato, kwamba mwombezi bora wa mtu ni matendo yake, na kwamba kitakachowaombea wenye dhambi ni toba. Hakika Mwenyezi Mungu haweki kizuizi kwa mwenye kutaka kuokoka akiwa na ikhlasi na akakimbilia kwenye ukarimu wa Mwenyezi Mungu hali ya kunyenyekea.

﴿وَإِذْ نَجَّيْنَاكُم مِّنْ آلِ فِرْعَوْنَ يَسُومُونَكُمْ سُوءَ الْعَذَابِ يُذَبِّحُونَ أَبْنَاءَكُمْ وَيَسْتَحْيُونَ نِسَاءَكُمْ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَاءٌ مِّن رَّبِّكُمْ عَظِيمٌ ﴾

49.Na tulipowaokoa kwa watu wa Firaun waliowapa adhabu mbaya; wakiwachinja watoto wenu wakiume na kuwaacha hai wakike; na katika hayo ulipatikana mtihani mkubwa uliotoka kwa Mola wenu.

﴿وَإِذْ فَرَقْنَا بِكُمُ الْبَحْرَ فَأَنجَيْنَاكُمْ وَأَغْرَقْنَا آلَ فِرْعَوْنَ وَأَنتُمْ تَنظُرُونَ﴾

50.Na tulipoitenga bahari kwa ajili yenu na tukawaokoa, na tukawazamisha watu wa Firaun na hali mwatizama.

NA TULIPOWAOKOA

Aya 49 - 50

LUGHA

Neno: Aal, lina maana ya kurudi; kwa hiyo kila mwenye kurudiwa kwa nasaba, rai au itikadi basi yeye ni Aal wa wale wanaomrudia, kisha likawa linatumiwa zaidi kwa maana ya watu wa nyumba ya huyo mtu atakayetajwa, lakini hawezi kuitwa mtu Al mpaka awe na utukufu fulani. Makusudio ya Al-Firaun hapa ni wafuasi wake ambao walikuwa wakiwatesa wana wa Israil kwa amri yake. Abu-Hayan Al-Andalusi (Mhispania) amesema: Katika tafsir yake kubwa Al-Bahrul Muhit; Firaun ni lakabu (msimbo) ya wafalme wa Misri wakati huo; kama vile Kisra wa Fursi, Kaizari wa Roma, Najashi wa Uhabeshi, Tubba wa Yemen na Khaqani wa Uturuki.

Lakini alhamdulillah misimbo hii yote imebakia kuwa ni vigano tu!

MAELEZO

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwakumbusha neema zake kwao kwa ujumla, sasa anawakumbusha kwa ufafanuzi. Bora zaidi ya neema aliyoidokeza ni kuwaokoa na Firaun na wafuasi wake ambao waliwapa Mayahudi adhabu kali. Mwenyezi Mungu ameifasiri adhabu hiyo kwa kusema: wakiwachinja watoto wenu wakiume na kuwaacha hai wakike. Yaani wanawaua watoto wanaume na kuwaacha wanawake waje kuwafanya watumishi.

* 18 Mwenye Majmaul Bayan anasema: Firaun aliota mambo yaliyomtisha. Wakamfasiria makuhani kuwa atazaliwa kijana wa kiume kutoka kwa wana wa Israil ambaye atakuja muua, ndipo Firaun akawafanyia hivyo wana wa Israil. Zaidi ya hayo Wamisri walikuwa wakiwadhalilisha Wayahudi kwa kuwatuma kazi za kuvunja mawe, kuchimba mifereji na kazi nyinginezo za sulubu. Msemo umewaelekea Mayahudi waliokuwepo zama za Mtume Muhammad(s.a.w.w) , kwa sababu wao walikuwa kwenye dini ya mababu zao na waliridhia amali zao. Na,mwenye kupenda amali ya watu wengine anakuwa ameshirikiana nao.

Na katika hayo ulipatikana mtihani mkubwa uliotoka kwa Mola wenu: Yaani, Enyi wana wa Israil, Mwenyezi Mungu amewatahini katika shida na raha, ili ijulikane kuwa je mtapigana jihadi na kuwa wavumilivi katika shida? Na je,mtashukuru raha? Au mtasalimu amri katika shida na mkufuru katika neema? Kwa hakika Mwenyezi Mungu hamtahini mtu ili ajue, la! Yeye anajua lenye kuwa kabla ya kuwa; isipokuwa yeye anamtahini mtu kwa ajili ya kusimamisha hoja juu yake. Kwani hakuna madai kwa asiyekuwa na hoja, hata kama yenye kudaiwa yanathibiti katika elimu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.). Mwenyezi Mungu amewaonyesha Waisrail neema ya pili aliposema: Na tulipoitenga bahari kwa ajili yenu na tukawaokoa, na tukawazamisha watu wa Firaun

Yaani tulitenga bahari na tukafanya njia kumi na mbili kwa hisabu ya wajukuu. Wajukuu katika wana wa Israil ni koo katika kizazi cha Yaqub(a.s) Kwa ufupi Wayahudi walikuwa katika unyonge na udhalili wa hali ya juu; na adui yao alikuwa na nguvu za hali ya juu. Lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akabadilisha hali hiyo kupitia mikononi mwa Mtume wake Musa(a.s) , wao wakawa ndio wenye nguvu; na adui yao akawa dhalili, hilo wakaliona kwa macho yao; kama inavyosema Aya: Na hali nyinyi mnaangalia. Mwenyezi Mungu alimdhalilishia yule aliyewadhalilisha na akamwangamiza yule aliyetaka kuwaangamiza. Kwa hivyo basi wamelazimiana na hoja na imewalazimu kuwaidhika na kuzingatia, wala wasiwafanyie wengine yale waliyofanyiwa na wengine.

Lakini hivi leo mfano ule ule waliokuwa wakifanyiwa na Firaun ndio wanawafanyia Wapelestina. Na waendelee hivyo, lakini wajue hali itakuja wabadilikia tu, na yatawafika yale yaliyompata Firaun. Na waangalie ilivyokuwa kwa Nebukadnezzar na Warumi; na kwamba shujaa huvuma kisha akaisha. Jambo la kustaajabisha sana kwa mtu ni kwamba anapokuwa kwenye shida, kisha akaokolewa na Mwenyezi Mungu, basi hupetuka mipaka akafanya uovu na kusahau kila kitu. Wafasiri wengi wamesema, kwamba bahari iliyotajwa ni Bahari nyekundu (Red Sea).

﴿وَإِذْ وَاعَدْنَا مُوسَىٰ أَرْبَعِينَ لَيْلَةً ثُمَّ اتَّخَذْتُمُ الْعِجْلَ مِن بَعْدِهِ وَأَنتُمْ ظَالِمُونَ﴾

51. Na tulipomwahidi Musa masiku arobaini mkafanya ndama (kuwa Mungu) badala ya Mwenyezi Mungu mkawa madhalimu (wa nafsi zenu).

﴿ثُمَّ عَفَوْنَا عَنكُم مِّن بَعْدِ ذَٰلِكَ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴾

52.Kisha tukawasamehe baada ya hayo ili mpate kushukuru.

﴿وَإِذْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ وَالْفُرْقَانَ لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ﴾

53.Na tulipompa Musa kitabu na upambanuzi ili mpate kuongoka.

NA TULIPOMWAHIDI

Aya 51 - 53

LUGHA

Neno: Musa kwa lugha ya Kiarabu lina maana ya: kifaa cha kunyolea nywele kilichotengezwa kutokana na chuma; lakini maana yanayokusuduwa kwa Musa bin Imran siyo ya Kiarabu, bali ni ya Kikibti ambayo ni matamko mawili: Mu lenye maana ya maji na Sa lenye maana ya mti. Kwa hiyo maana ya Musa ni maji ya mti, Ama maana ya kuitwa Maji ya mti, kama ilivyoelezwa katika Majmaul-Bayan, ni kwamba wajakazi wa Asiya(mke wa Firaun), walitoka kwenda kuoga wakakuta sanduku lililokuwa na Musa ndani yake baina ya maji na mti; wakawa naye.

MAELEZO

Baada ya Firaun kuangamizwa na Mwenyezi Mungu na waliokuwa pamoja naye, Waisrail Walipumua, wakarudi Misri wakiwa salama; kama livyoelezwa katika Majmau.Wakati huo, Tawrat ilikuwa bado haijateremshwa, wakamtaka Musa awaletee kitabu kutoka kwa mola wao. Basi Mwenyezi Mungu akamwahidi kumteremshia Tawrat na akamwekea wakati. Musa akawaambia: Hakika Mola wangu ameniahidi kitabu ambacho ndani yake mna ubainifu wa ambayo ni wajibu kwenu kuyafanya na kuyaacha. Akawambia wakati wake ambao ni masiku arobaini, na masiku hayo - kama ilivyosemwa - ni mwezi wa Dhul-Qaada, na siku kumi za mwezi wa Dhul- Hijja.

Musa akenda kwa Mola wake ili awachukulie watu wake kitabu; ndugu yake Harun akawa naibu wake. Kabla ya kwisha muda wa kuja Musa, walianza kuabudu ndama badala ya Mwenyezi Mungu, wakajidhulimu wao wenyewe.

Hiyo ndiyo maana ya dhahiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na tulipomwahidi Musa masiku arobaini mkafanya ndama (kuwa Mungu) badala ya Mwenyezi Mungu mkawa madhalimu ( wa nafsi zenu).

Baada ya Musa kurejea kwa watu wake, walitubia na wakarudi kwa Mola wao; Mwenyezi Mungu akawakubali toba yao, na hii ni neema ya tatu ambayo imeelezewa katika Aya:Kisha tukawasamehe baada ya hayo .

Ama neema ya nne ni; kitabu cha Mwenyezi Mungu:Na tulipompa Musa kitabu na upambanuzi ili mpate kuongoka. Kitabu chenyewe ni Tawrat; yenye kukusanya kila kitu kwa ajili ya kubainisha haki na batili, na halali na haramu.

Kunganisha kati ya neno, kitabu na kupambanua, ni kuunganisha sifa kwenye kile kinashosifiwa. Kwa muhtasari ni kwamba: Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewakumbusha Waisrail katika Aya zilizotangulia, neema nne, Kuwaokoa kuchinjiwa watoto wao wa kiume na kuachwa wa kike wawe watumwa, kuangamia kwa Firaun, kusamehewa na kuletewa Tawrat.

Maelezo mazuri zaidi niliyoyasoma kuhusu maudhui haya, ni kauli ya Abu Hayan Al-Andulusi katika Tafsir Al -Bahrul Muhit; namnukuu: Tazama uzuri wa safu hizi ambazo zimepangika kwa mpango wa mtungo wa lulu na wa sayari katika falaki zake, kila safu katika hizo, yaani neema, imeishia kwa mnasaba wake na ikafikia daraja ya juu ya ufasaha ukitoka kwa Mwenyezi Mungu kupitia mdomoni mwa Muhammad mwaminifu wake, bila ya kusoma kitabu chochote kabla yake, wala kuandika kwa mkono wake.

Abu Hayan anaonyesha kuwa mpangilio huo wenye kupangika vizuri ni katika miujiza ya Muhammad; kwamba yeye anauelezea bila ya kujifundisha. Mwenyezi Mungu awarehemu wahenga, awasamehe na awape neema nyingi. Kwani hakika wao hawakuona chochote chenye harufu ya kuitilia mkazo dini hii na Mtume wake mtukufu isipokuwa walikinyooshea shingo kwa pupa na shauku; wakafanya haraka kukisherehesha, kukifafanua na kukitolea dalili. Lakini tuko wapi sisi wanavyuoni wa sasa ambao twapupia zaidi dunia; hatuoni umuhimu wowote isipokuwa umuhimu wetu tu; wala matatizo isipokuwa matatizo ya watoto wetu tu! Tuko wapi sisi na hao watukufu waliojitolea kila kitu kwa ajili ya kuutukuza Uislamu na Mtume wa Uislamu? Mwenyezi Mungu awasamehe na awainue, na kila mwenye kuitumikia dini, kwenye daraja ya juu.

﴿وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ يَا قَوْمِ إِنَّكُمْ ظَلَمْتُمْ أَنفُسَكُم بِاتِّخَاذِكُمُ الْعِجْلَ فَتُوبُوا إِلَىٰ بَارِئِكُمْ فَاقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ عِندَ بَارِئِكُمْ فَتَابَ عَلَيْكُمْ إِنَّهُ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ ﴾

54.Na Musa alipowaambia watu wake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmejidhulumu kwa kufanya kwenu ndama (kuwa ni Mungu). Basi tubuni kwa Muumba wenu na jiueni; hilo ni bora kwenu mbele ya Muumba wenu.Basi akapokea toba yenu.Hakika Yeye ndiye apokeaye toba Mwenye kurehemu.

﴿وَإِذْ قُلْتُمْ يَا مُوسَىٰ لَن نُّؤْمِنَ لَكَ حَتَّىٰ نَرَى اللَّـهَ جَهْرَةً فَأَخَذَتْكُمُ الصَّاعِقَةُ وَأَنتُمْ تَنظُرُونَ ﴾

55.Na mliposema: Ewe Musa! Hatutakuamini mpaka tumwone Mungu waziwazi.Ukawanyakua ukelele na hali mwatizama.

﴿ثُمَّ بَعَثْنَاكُم مِّن بَعْدِ مَوْتِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ﴾

56.Kisha tukawafufua baada ya kufa kwenu ili mpate kushukuru.

﴿وَظَلَّلْنَا عَلَيْكُمُ الْغَمَامَ وَأَنزَلْنَا عَلَيْكُمُ الْمَنَّ وَالسَّلْوَىٰ كُلُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ وَمَا ظَلَمُونَا وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ ﴾

57.Tukawatilia kivuli kwa mawingu na tukawateremshia Manna na Salwa: Kuleni katika vitu vizuri tulivyowaruzuku.Na hatukuwadhulumu, lakini wamejidhulumu wenyewe.

MUSA ALIPOWAAMBIAWATU WAKE

Aya 54 - 57

LUGHA

Manna ni kitu fulani kinachonata mithili ya asali, na Salwa ni tombo (aina ya ndege wa jamii ya kware, kama kuku).

MAELEZO

Na Musa alipowaambia watu wake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mumejidhulumu kwa kumfanya kwenu Ndama (kuwa ni Mungu). Basi tubuni kwa Muumba wenu. Maana yoyote inayofahamika kwa kusikia tu haihitaji tafsiri, bali kuifasiri na kuisherehesha ni ufedhuli tu! Na Aya hii iko katika hali hiyo.

Na jiueni Makusudio ya kujiua yako wazi, ni kujitoa roho: wala hapana haja ya kufasiri vingine, kwa maana ya kuhalifu mapenzi na kuidhalilisha nafsi kwa kukiri dhambi na makosa au kumwabudu sana Mwenyezi Mungu; kama ilivyosemwa. Makusudio ya kujiua hapa, ni baadhi wawaue wengine. Kwa hivyo yule ambaye hakurtadi dini yake kwa kuabudu ndama ndio atamuua yule aliyertadi dini yake. Sawa na kusema kwake Mwenyezi Mungu:

﴿فَإِذَا دَخَلْتُم بُيُوتًا فَسَلِّمُوا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ ﴾

...Mnapoingia katika majumba jitoleeni salamu.... (24:61).

Na vile vile kusema kwake

﴿وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ ﴾

...Wala msijikejeli: yaani msikejeliane (49:11)

Amesema Tabrasi katika Majmaul-Bayan kwa upande wa Shia, na Razi katika Tafsir Al-Kabir, kwa upande wa Sunni, kuwa Mwenyezi Mungu aliijaalia toba yao ni huko kujiua, sio kwamba wajiue baada ya kutubia. Hukumu hii ina mfano wake katika sharia ya Kiislamu, pale ulipozingatia kuua kuwa ni hadi na adhabu ya kosa la kurtadi.Hilo tutalieleza katika kifungu cha kurtadi kinachofuatia. Zinaendelea Aya kueleza maovu ya Waisrail: Na mliposema: Ewe Musa! Hatutakuamini mpake tumwone Mungu waziwazi Wakati Musa alipowaendea na Tawrat, baadhi yao walisema: Hatuamini kuwa kitabu hiki kinatoka kwa Mungu mpaka tumwone kwa macho; bila ya kizuwizi chochote kati yetu sisi na Yeye; na atueleze ana kwa ana kuwa Yeye amekutuma na kitabu hiki.

Sijui kama wale wanaokanusha kuwepo Mwenyezi Mungu wakati huu, kwa kuwa tu hawajamuona kwa wazi, wanategemea Waisrail na inadi yao? Au vipi? Mayahudi walimwambia Musa: Hatutakuamini mpaka tumwone Mungu. Hawa wa sasa nao wanasema: Hakuna chochote chenye kupatiana isipokuwa kile tunachoweza kukiona kwa jicho, kukigusa kwa mkono, kukinusa kwa pua au kukionja kwa mdomo. Hivyo ndivyo inavyokaririka historia ya picha ya upinzani wa haki katika kila kizazi.

Yakawanyakua mauti ya ghafla na hali mwalizania Yaani adhabu kutoka mbinguni iliwapata wale waliomwambia Musa hatukuamini mpaka tumwone Mungu wazi wazi, wakaangamizwa mbele ya macho ya wale wasiopinga. Kisha tukawafufua baada ya kufa kwenu ili mpate kushukuru. Baadhi ya wafasiri kama vile Muhamad Abduh, katika tafsiri Al-Manar, amesema: Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakuwarudishia uhai mara ya pili baada ya kuchukuliwa na ukelele; na kwamba makusudio ya kufufuliwa kwao ni kizazi chao kuwa kingi. Wengine wakasema kuwa sio hivyo, hayo hayafahamiki kutokana na dhahiri yake ilivyo, na kwamba waliorudishwa ni wale wale waliouliwa na ukelele.Na hii ndiyo sawa, kwani hapana sababu inayolazimisha taawil, madamu kurudishwa kuwa hai kunawezekana kiakili. Na hilo lilimtokea Uzair, kama inavyofahamisha Aya:

﴿قَالَ أَنَّىٰ يُحْيِي هَـٰذِهِ اللَّـهُ بَعْدَ مَوْتِهَا فَأَمَاتَهُ اللَّـهُ مِائَةَ عَامٍ ثُمَّ بَعَثَهُ﴾

Akasema: Mwenyezi Mungu atauhuisha vipi (mji) huu baada ya kufa kwake? Mwenyezi Mungu Akamfisha kwa miaka mia, kisha akamfufua.... (2:259)

Kimsingi,lililotokea haliwezi kuwa muhali. Kwa hakika inaonyesha kwamba makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu: Yakawanyakua mauti ya ghafla, na kauli yake tukawafufua ni wale waliokuwa wakati wa Musa waliosema: Mpaka tumwone Mungu waziwazi Kwa hiyo, kauli haiwahusu Mayahudi waliokuwa na mtume, msemo umeele-kezwa kwao kwa kuangalia kuwa wanatokana na kizazi kilichosema hivyo.

Tukawatilia kivuli cha mawingu na tukawateremshia Manna na Salwa. Hayo yaliyotokea wakati Waisrail walipotoka Misri wakahangaika katika jangwa la Sinai, kusikokuwa na majengo; wakamlalamikia Musa kwa joto la jua; Mwenyezi Mungu akawaneemesha kwa wingu lililowafunika na kuwakinga na joto la jua kali. Vile vile Mwenyezi Mungu akawaneemesha kwa Manna na Salwa ili wale. Yatakuja maelezo katika tafsiri ya Aya ya 60 kuwa maji yaliwabubujikia kutoka katika jiwe alilolipiga Musa kwa fimbo yake. Inashangaza kuona baadhi ya wafasiri, wakifasiri yale aliyoyanyamazia Mwenyezi Mungu kuyabainisha; kama vile idadi ya waliojiua kwa toba ya kuabudu ndama, kuwa ni watu elfu moja; vile vile walionyakuliwa kuwa ni watu sabini. Ama kuhusu Manna, wanadai kila mtu alikuwa akipata pishi moja na kwamba Salwa ilikuwa ikishuka kutoka mbinguni ikiwa moto moto huku ikifuka moshi, na mengineyo ambayo hayana kauli yoyote iliyopokewa au kudhaniwa.

Imethibiti Hadith kutoka kwa Mtume mtukufu(s.a.w.w) :Hakika Mwenyezi Mungu amenyamazia mambo si kwa kusahau, ni kwa kuwaonea huruma, kwa hiyo msijikalifishe nayo.

Katika Nahjul-Balagha amesema Imam Ali(a.s) :Hakika Mwenyezi Mungu amewafaradhisha faradhi msizipoteze, na amewawekea mipaka msipetuke; na ameyakataza mambo basi msifanye; na ameyanyamazia mambo si kwa kusahau, basi msijikalifishe (nayo).

Na hawakutudhulumu sisi, lakini wamejidhulumu wenyewe .Kukanusha dhulma kwa Mwenyezi Mungu ni sawa na kukanusha kuwa na watoto na mshirika; yaani kumwepusha kabisa na hilo; sawa na kumwambia mseja kuwa hana mtoto. Ama kujidhulumu kwa Mayahudi ni kwa sababu ya usafihi wao na kuzikanusha neema za Mwenyezi Mungu ambaye hanufaiki na twaa ya mwenye kumtii wala hayamdhuru maasi ya mwenye kuasi na madhara ya uasi yanamrudia mwasi. Anasema Ali bin Abu Twalib (a.s.):Ewe mwanadamu ukiona Mola wako anaendelea kukuneemesha nawe unamwasi, basi mhadhari.

Kwa ufupi Aya hizi zinaonyesha ibada ya Waisrail kwa ndama, kutubia kwao kwa kujiua na kutaka kwao kumwona Mwenyezi Mungu. Vile vile kuangamia kwao na kufufuliwa kwao, kufunikwa na kiwingu na kulishwa Manna na Salwa.. Tutaelezea kisa cha Nabii Musa na Waisrail katika surah ya Maida (5) Inshallah. Waliposema kumwambia Musa:

﴿فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ﴾

...Basi nenda wewe na Mola wako mkapigane sisi tutakaa hapa (5:24).

Hilo ni tamko linaloonyesha ukhabithi na uduni wa Mayahudi. Wa kwanza waliogundua uhabithi na uduni wao ni watu wa Firaun ambao waliwachinja watoto wao wa kiume na kuwaacha wa kike. Kumwona Mungu Kutokana na Aya tukufu:Mpaka tumwone Mungu waziwazi.

Tutaonyesha mzozo uliopo katika madhehebu ya Kiislamu na tofauti zao kuwa akili inajuzisha kuonekana Mwenyezi Mungu kwa macho au la?!

Wamesema Ashari (Sunni): Hakika kuonekana Mungu kwa macho kunawezekana kiakili, kwa sababu Yeye yupo na kila kilichopo kinawezekana kuonekana.

Imamiya na Mu’utazila wamesema; Haijuzu kuonekana Mwenyezi Mungu kwa macho katika hali yoyote ile, si duniani wala akhera, kwa sababu Yeye si umbo hata akaonekana, wala haingii katika umbo wala upande fulani.

Baada ya akili kuthibitisha kutoonekana, wamechukulia kwamba ataonekana kiakili sio kwa macho na kwa hakika ya imani sio ya viungo vya mwili, kwa mujibu wa alivyosema mwanafalsafa mkubwa na mashuhuri, Muhammad bin Ibrahim Shirazi, maarufu kwa jina la Mulla Sadra. Katika aliyoyatolea dalili Mulla Sadra kuhusu kutoonekana, ni kauli yake: Kuhisi kitu ni hali inayozuka kwa kile kinachohisi kikikutanishwa na kinachohisiwa kilichozuka. Hivyo basi, kulazimisha kitu ambacho hakikuzuka kuwa kinahisiwa ni kama kulazimisha kitu kisicho na upande kuwa kina upande.

Kauli yake hii - kama ninavyoona - ni kwamba jicho haliwezi kuona kitu isipokuwa kwa sharti mbili:

Liwe linaweza kuona na kiwe kile kinachoangaliwa kinaweza kuonekana kwa jicho. Hilo ni jambo la msingi; likikosa jicho uwezo wa kuona, au kikiwa kitu hakina uwezo wa kuonekana; itakuwa kuona hakuko. Jicho ni dogo na duni zaidi kuweza kuona dhati tukufu; kama vile ambavyo, Mwenyezi Mungu ni mkubwa wa kuonekana na jicho. Nilipokuwa nasoma ibara hii, tukufu akili yangu ilienda kwa mwanafalsafa wa Kiingereza John Luk, anayesema kuwa: kitu kina sifa yake ya kwanza yenye kukithibitikia, ambayo haipambanuki nayo, ni sawa mtu aitambue au asiitambue; kama vile vitu vinavyosimamisha kitu hicho.

Vile vile kuna sifa ya pili ambayo haiwezi kuepukana na kuhisiwa au kujulikana; kama rangi, sauti na ladha. Rangi siyo sifa ya kitu, kama inavyoonekana, isipokuwa ni mawimbi ya kimwangaza yanayohusika kati ya kitu na jicho; kama wasemavyo wataalamu. Vile vile sauti ni mawimbi ya kihewa; na ladha isingekuweko kama si mdomo. Kwa hiyo ladha inahitilafiana kwa uzima wa mdomo na ugonjwa.Kwa ufupi anataka kueleza kuwa hakuna rangi bila ya jicho; wala sauti bila ya sikio; au ladha bila ya mdomo. Hakuna mwenye kutia shaka kwamba nuru ya Mwenyezi Mungu imezidi mawimbi ya kimwanga na mengineyo.Kwa hivyo yakikosekana mawimbi haya, ndio kumekosekana kuona.

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿ كَيْفَ تَكْفُرُونَ بِاللَّـهِ وَكُنتُمْ أَمْوَاتًا فَأَحْيَاكُمْ ثُمَّ يُمِيتُكُمْ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴾

28.Vipi mnamkanusha Mwenyezi Mungu na hali mlikuwa wafu akawafufua! Kisha atawafisha tena atawafufua,kisha kwake mtarejeshwa.

﴿ هُوَ الَّذِي خَلَقَ لَكُم مَّا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ اسْتَوَىٰ إِلَى السَّمَاءِ فَسَوَّاهُنَّ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴾

29.Yeye ndiye aliwaumbia vyote vilivyomo katika ardhi tena akakusudia kuumba mbingu na akazifanya saba. Naye ni mjuzi wa kila kitu.

MWANADAMU KWA DHATI YAKE NI HOJA

Aya 28 - 29

Vipi mnamkanusha Mwenyezi Mungu!

Kwa dhahiri ya mfumo wa maneno inaonyesha kwamba msemo katika Aya mbili hizi unaelekezwa kwa yule ambaye hanufaiki na chochote katika kupigiwa mfano, lakini ilivyo hasa msemo unamhusu kila anayemkufuru Mwenyezi Mungu pamoja na kuweko dalili hizi zisizokuwa na idadi ambazo ni pamoja na huyo kafiri mkanushaji. Kwani yeye kwa dhati yake ni dalili iliyo wazi ya kupatikana aliyemuumba.

Kama si hivyo ni nani basi aliyemfanya katika nidhamu hii kali kabisa, akakiweka kila kitu mahala pake panapohusika, kuanzia chembe hai za ubongo na moyo mpaka kwenye utumbo na maini, kwenye usikizi na uoni na mpaka kwenye miishilio isiyokuwa na mwisho. Kila kimoja kinatekeleza umuhimu wake kwa uangalifu bila ya usimamizi wowote kutoka kwa kiumbe.

Vile vile ni kutoka wapi umekuja ufahamu huu na akili ambayo mtu analikurubisha lililo mbali, kulisahilisha zito na kukusanya yaliyo katika ardhi katika nyumba moja, kisha akaendelea zaidi na kuweka athari zake mwezini.

Je haya na mengineyo yamekuja kibahati na (kisadfa) tu?Je kuna vitu hasa vinavyoendesha mpangilio huo? Je Sayansi inaweza kujibu hayo? Na je majibu yatatokana na kuhusika na majaribio ya Kisayansi?(14:34)

Walijaribu wenye kujaribu kujibu,lakini yakajitokeza maelfu ya maswali. Sisi hatukanushi kabisa kwamba wataalamu wa kisayansi wamefikilia kwenye ukweli wa kushangaza katika tiba, ukulima na viwanda, lakini wataalamu wa uhai wameambulia patupu wakitafuta siri ya uhai na asili yake; na hawana chochote isipokuwa dhana tu, ambayo haitoshei haki. Kimsingi, kila Sayansi inaposhindwa kutafsiri jambo hulihukumia kwa kinyume chake.

Ikawa kupatikana mtu ni nguvu ya hoja kuhusu kuwapo Mwenyezi Mungu (s.w.t.), inakuaje hoja hii ipinge hoja inayolazimiana nayo? Vipi mtu aliye na fasihi aweze kupinga fikra ya fasihi na balagha? Basi hapo ndio inakuwa siri ya kustaajabisha katika kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

Vipi mnakanusha Mwenyezi Mungu na hali mlikuwa wafu akawafufua.

Yaani ni maajabu yaliyoje ya kumkanusha kwenu Mwenyezi Mungu na hali nyinyi kwa dhati kabisa ni dalili wazi ya kuwepo Mwenyezi Mungu. Vyovyote mtakavyokanusha, je, mnaweza kukanusha kwamba nyinyi hamkuwa kitu chochote kisha ndipo mkawa kitu kinachosikia, kuona, kuhisi na kutambua, pamoja na kusema na kutenda? Je,hiyo si dalili inayoeleza kupatikana nguvu iliyoumba?

Kweli kabisa.Hakika binaadamu ni dhalimu mkubwa mwenye kukanusha mno! Hakukuwa kumkanusha Mwenyezi Mungu isipokuwa ni kukanusha na kutojijua huyo mkanushaji.11 Na asiyejijua, basi ndio hamjui mwingine. Kwa hali hiyo ndiyo tunapata tafsiri ya hadith tukufu: Anayejijua zaidi ni yule anayemjua zaidi Mola wake. Unaweza kuuliza: Ni akili gani inayoweza kujikanusha yenyewe?Je hayo yanaingia akilini? Tunajibu: Hakika hoja inalazimiana na chenye kutolewa hoja; na kukanusha ulazima kunapelekea kukanusha chenye kulazimiwa. Kwa hivyo mwenye kukanu-sha dalili ya matamko, kwa mfano, kutokana na maana iliyowekwa, atakuwa ameyakanusha matamko yenyewe atake asitake, wala hakumfalii yeye kuyakubali wakati anakanusha dalili zake.

Hivi ndivyo ilivyo kwa mwenye kumka-nusha Mwenyezi Mungu. Kwani kuwapo kwake ni dalili ya kuwapo muumbaji, na kupatikana muumbaji kunatolewa dalili na kupatikana kwake yeye mkanushaji. Basi akikanusha chenye kutolewa dalili ndio amekanusha dalili yenyewe, ambayo ndiyo huyo mkanushaji kwa dhati yake bila ya kujijua wala kujitambua. Hivyo ndivyo anavyofanya mjinga anayejiepusha na maumbile anayoishi nayo na kumpa uhai, kupinga dalili zilizo wazi na kuamini vigano na mambo ya kijinga.

MAUTI NA UHAI MARA MBILI

Makusudio ya kufa kwa kwanza kunak-oonyesha na neno Mlikuwa wafu ni kutokuwapo kwa mara ya kwanza, Na makusudio ya uhai wa kwanza, Akawafufua ni kuumbwa baada ya kutokuwapo.

* 11 Anasema Charlie Champlin, mchezaji sinema mashuhuri wa kimataifa, ambaye umashuhuri wake umezidi ule wa Gandi: Katika mamlaka isiyojulikana kuna nguvu isiyokuwa na mpaka. Na anasema Kierkegaard Hakika Mwenyezi Mungu anajitokeza kwenye nafsi yenye kukata tamaa katika wakati mgumu wa kukata tamaa na katika lindi la makosa. Mauti ya pili, Kisha atawaua, ni mauti haya yaliyozoeleka; na kufufuliwa mara ya pili ni kufufuliwa kwa ajili ya hisabu na malipo.

TENA ATAWAFUFUA

Unaweza kuuliza, je roho inafarikiana na mwili baada ya kwisha nguvu zake za uhai, kwa namna ambayo lau nguvu zingebakia, basi roho ingelibaki na bina -damu milele? Au ni kwamba inawezekana roho kufarikiana na mwili hata ukiwa na nguvu za kuishi kwa ukamilifu bila ya kutokea uharibifu wowote mwilini? Jibu: Watu wa kimaada wamechukulia kauli ya kwanza na wengine wamechukulia kauli ya pili. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

﴿ فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ لَا يَسْتَأْخِرُونَ سَاعَةً﴾

...Utakapofika muda wao hawatakawia (hata) saa moja wala hawatatangulia (7:34)

Inaweza kuchukuwa njia zote mbili. Kwani haikubainisha sababu ya kufika muda wao.Je ni kuharibika mwili au ni kitu kingine. Kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ الَّذِينَ خَرَجُوا مِن دِيَارِهِمْ وَهُمْ أُلُوفٌ حَذَرَ الْمَوْتِ فَقَالَ لَهُمُ اللَّـهُ مُوتُوا﴾

...ambao walitoka katika majumba yao nao walikuwa maelfu wakiogopa mauti? Mwenyezi Mungu akawaambia Kufeni (2:243)

Na kauli yake:

﴿قَالَ أَنَّىٰ يُحْيِي هَـٰذِهِ اللَّـهُ بَعْدَ مَوْتِهَا فَأَمَاتَهُ اللَّـهُ مِائَةَ عَامٍ﴾

Akasema: Mwenyezi Mungu atuuhuisha vipi (mji) huu baada ya kufa kwake? Basi Mwenyezi Mungu alimfisha kwa miaka mia... (2:259)

Aya mbili hizo zinahusu matukio fulani tu.Haziingii katika matukio mingine.

Vyovyote iwavyo hatuna kitu kinachotuthibitishia, lakini tunayoshuhudia ni kwamba watu wengi wanafikiwa na mauti nao bado wabichi wakiwa na afya nzuri na kwamba wengi wanatembea na kufurahi nao wako katika umri mkubwa na magonjwa tele. Madaktari wengi mahodari wanamwambia mgonjwa utakufa baada ya saa chache tu, lakini akaishi muda mrefu!

UFUFUO

Ufufuo katika Uislamu ni msingi wa tatu baada ya Tawhid na Utume, misingi ambayo tumeshaielezea. Mwenyezi Mungu ameyatolea habari marejeo (ufufuo) aliposema:

﴿ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴾

Kisha atawafufua kisha kwake mtarejeshwa.

Ametoa dalili au kuukurubisha uwezekano wa ufufuo katika Aya nyingi. Miongoni mwazo ni:

﴿أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلَمْ يَعْيَ بِخَلْقِهِنَّ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ﴾

Je! hawaoni kwamba Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi na hakuchoka kwa kuziumba, ana uwezo wa kuwafufua wafu? (46:33)

﴿يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِن كُنتُمْ فِي رَيْبٍ مِّنَ الْبَعْثِ فَإِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن تُرَابٍ ثُمَّ مِن نُّطْفَةٍ ثُمَّ مِنْ عَلَقَةٍ ﴾

Enyi watu! Kama mmo katika shaka juu ya ufufuo, basi kwa hakika tuliwaumba kutokana na udongo, kisha kutokana na manii, kisha kutokana na kipande cha damu... (22:5)

Hakuna anayetia shaka kwamba Mwenye kuumba kitu huwa rahisi kwake kuvikusanya viungo vyake baada ya kuwa mbali mbali; bali kukusanya ni rahisi zaidi kuliko kuumba tena. Mwenye kujenga jumba kubwa ni rahisi kwake kujenga kibanda.12

Ninacho kitabu maalum nilichoandika cha maudhui haya kinachoitwa Alakhira wal aql kisha nikayalinganisha na kitabu Al-Islam wal aql ambavyo vimechapishwa mara nyingi sana.

YALIYO KATIKA ARDHI

Baada ya Mwenyezi Mungu kumkumbusha mtu neema ya kupatikana kwake, anamtajia wingi wa neema alizonazo, ikiwa ni pamoja na kula na kunywa, mavazi, vipando, mandhari na mengineyo katika starehe za ardhi na heri zake zisizohisabika. Wametoa dalili mafakihi kwa kauli ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

﴿ هُوَ الَّذِي خَلَقَ لَكُم مَّا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ث﴾

Yeye ndiye aliyewaumbia vyote vilivyo katika ardhi.

Kwamba vitu vyote kabla ya kuja sharia ni halali, na kwamba haimfailii kiumbe kuharamisha kitu isipokuwa kwa dalili. Mwenyezi Mungu anasema:

*12 Mnamo mwaka 1959 Mustafa Mahmud, Mmisri, alitunga kitabu Allahu Wal-insan (Mungu na mtu) katika kitabu hicho alikana Mungu na ufufuo, nami nikamjibu kwa kutunga kitabu Allahu wal-Aqli (Mungu na Akili) mpaka sasa kimechapishwa mara tano. Ilipofika tarehe 10.4.1967 nilimsomeya makala Mustafa Mahmud katika jarida la Ruz Al-Yusuf, inayosema: Imani yangu inashikilia kwamba mimi nilikuwako kabla ya maisha yangu haya kwa jina jingine, na kwamba mimi sitaisha baada ya kufa kwangu isipokuwa nitarudi kwenye uhai kwa namna nyingine, na maisha yanaendelea.

﴿قُلْ أَرَأَيْتُم مَّا أَنزَلَ اللَّـهُ لَكُم مِّن رِّزْقٍ فَجَعَلْتُم مِّنْهُ حَرَامًا وَحَلَالًا قُلْ آللَّـهُ أَذِنَ لَكُمْ أَمْ عَلَى اللَّـهِ تَفْتَرُونَ﴾

Sema: Je, mnaonaje zile riziki alizowateremshia Mwenyezi Mungu kisha mkafanya katika hizo (kuwa) haram na (nyingine) halali. Sema, Je, Mwenyezi Mungu amewaruhusu au mnamzulia Mwenyezi Mungu tu? (10:59)

Pengine hutolewa dalili kwa Aya hii kwamba ardhi haimilikiwi. Kinachofaa kumilikiwa ni kile kinachozalishwa na ardhi. Kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema: Amewaumbia vilivyomo ardhini na hakusema amewaumbia ardhi.

MBINGU SABA

Maana ya neno istawa hapa ni kukusudia. Kuzihusisha mbingu saba hakufahamishi kuwa ndio hizo hizo tu wala hakukanushi kabisa kuwapo nyinginezo. Wamethibitisha wanavyuoni wa elimu ya usul na lugha kwamba idadi sio ufahamisho, mwenye kusema mimi ninamiliki vitabu saba haimaanishi kwamba hamiliki vingine. Analitilia nguvu hilo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alipomwambia Mtume wake(s.a.w.w) :

﴿إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَهُمْ﴾

Hata ukiwaombea msamaha mara sabini, Mwenyezi Mungu hatawasamehe. (9:80)

Mtume(s.a.w.w) akasema:Lau ningelijua kuwa Mwenyezi Mungu atawasamehe nikizidisha sabini ningelifanya. Huenda ikawa sababu ya kutaja saba ni kwamba hizo saba zina mambo maalum yasiyopatikana katika mbingu nyingine.

﴿ وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي جَاعِلٌ فِي الْأَرْضِ خَلِيفَةً قَالُوا أَتَجْعَلُ فِيهَا مَن يُفْسِدُ فِيهَا وَيَسْفِكُ الدِّمَاءَ وَنَحْنُ نُسَبِّحُ بِحَمْدِكَ وَنُقَدِّسُ لَكَ قَالَ إِنِّي أَعْلَمُ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴾

30. Na Mola wako alipowaambia Malaika mimi nitaweka Khalifa katika ardhi. Wakasema (Malaika) utaweka humo watakaofanya uharibifu humo na kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na kukutaja kwa utakatifu wako? Akasema Mwenyezi Mungu: Hakika mimi nayajua msiyoyajua.

﴿ وَعَلَّمَ آدَمَ الْأَسْمَاءَ كُلَّهَا ثُمَّ عَرَضَهُمْ عَلَى الْمَلَائِكَةِ فَقَالَ أَنبِئُونِي بِأَسْمَاءِ هَـٰؤُلَاءِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴾

31.Na akamfundisha Adam majina ya vitu vyote, kisha akaviweka mbele ya Malaika akasema: Niambieni majina ya vitu hivi ikiwa mnasema kweli.

﴿ قَالُوا سُبْحَانَكَ لَا عِلْمَ لَنَا إِلَّا مَا عَلَّمْتَنَا إِنَّكَ أَنتَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ ﴾

32.Wakasema: Utakatifu ni wako hatuna elimu isipokuwa ile uliyotufundisha; hakika wewe ndiwe mjuzi, mwenye hekima.

﴿ قَالَ يَا آدَمُ أَنبِئْهُم بِأَسْمَائِهِمْ فَلَمَّا أَنبَأَهُم بِأَسْمَائِهِمْ قَالَ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ إِنِّي أَعْلَمُ غَيْبَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَأَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا كُنتُمْ تَكْتُمُونَ ﴾

33.Akasema: Ewe Adam waambie majina yake. Alipowaambia majina yake. Alisema (Mwenyezi Mungu): Sikuwaambia kwamba mimi ninajua siri za mbinguni na za ardhini; tena najua mnayoyadhihirisha na mliyokuwa mkiyaficha.

MOLAWAKO ALIPOWAAMBIA MALAIKA

Aya 30 - 33

MAKUSUDIO YA MAJINA

Makusudio ya majina katika kauli yake Mwenyezi Mungu: Na Mwenyezi Mungu akamfundisha Adam majina ya (vitu) vyote, ni: maana ya majina, nayo ni ya vitu vya ulimwengu na sifa zake. Mwenye Majmaul-Bayan anasema: Hakika majina bila ya maana hayana faida wala kuonyesha ubora wake. Imam Sadiq(a.s) Aliulizwa kuhusu hayo majina akasema:Ni milima na mabonde. Kisha akaonyesha busati lililokuwa chini yake akasema: Hili ni miongoni mwayo, yaani kila kitu mpaka busati hili pia.

MALAIKA

Hakuna njia ya kuwajua Malaika na hakika yao kwa hisia na majaribio wala kwa akili na kukisia au kwa kitu chochote isipokuwa kwa njia ya wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu kupitia midomoni mwa Mitume yake. Mwenye kukanusha wahyi kimsingi haifai kumzungumzia habari ya Malaika kwa hali yoyote. Kwa sababu wao ni tawi na wahyi ni asili (shina). Ikiwa hapana budi kulumbana naye basi ni lazima iwe ni kuhusu fikra ya wahyi na kuswihi kwake tu.

Hapa hatukusudii kulumbana na anayekanusha wahyi, kwa vile tumekwishafafanua; isipokuwa tunamwambia yule mwenye kukanusha: Si haki kulazimisha rai yako juu ya yule mwenye kuamini wahyi; kama si hivyo basi ingelijuzu kwake kulazimisha rai yake kwako. Kama ukimwambia mwenye kuamini wahyi kuwa imani yake ni batili kwa vile yeye hategemei majaribio, atakujibu kwamba kuamini kwako kuwa wahyi ni batili vilevile hakukutegemea kwenye majaribio, kwa sababu kukanusha kwako na uthibitisho wa mwenye kuamini, maudhui yake ni mamoja, nayo ni wahyi.Ikiwa majaribio, hayathibitishi wahyi pia hayaukanushi.

Kwa maneno mengine kuamini kutokuwepo ghaibu ni sawa na kuamini kuwepo, yote mawili ni ghaibu katika ghaibu. Kimsingi ni kwamba ghaibu haifai kuipinga kwa ghaibu. Sartre, mwandishi na mwanafalsafa mashuhuri wa Kifaransa akiwajibu wanaoamini maada alisema: Nyinyi mnapokanusha kuwepo Mwenyezi Mungu ndio mnafafanua ghaibu kwa ukamilifu, kama wanaoamini mifano ambao wanakubali kuwepo kwa Mwenyezi Mungu. Hakika yakini ya kimaada ya kukanusha ghaibu, inategemea dalili ile ile anayoitegemea mwenye kuamini kuswihi ghaibu.Kwa hivyo basi imebainika kwamba imani ya kimaada inajipinga yenyewe.

KHALIFA

Makusudio ya Khalifa katika Aya ni Adam, baba wa watu na kila mtu aliyeko na atakayekuwako katika kizazi chake wakati wowote na mahali popote. Wajihi wa kumwita Khalifa ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimpa nafasi ya kuchukua hatamu za uongozi wa ardhi hii na kutafuta yaliyomo ndani yake miongoni mwa nguvu na manufaa na kufaidika nayo. Katika kauli ya Malaika:

* 13 Angalia kifungu cha Sartre na madhehebu ya kimaada katika kitabu chetu Falsafatul- Mabdai Wal-Maad, tulichokitunga kuwajibu wenye Falsafa ya kimaada. Utaweka humo watakaofanya uharibifu na kumwaga damu. Inaonyesha kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) aliwafahamisha Malaika kwa njia fulani kabla ya kumuumba Adam, kwamba lau binadamu atakuwa katika ardhi hii angeliasi kwa ufisadi na kumwaga damu. Kutokana na hali hiyo ndio wakaona ajabu vipi Mwenyezi Mungu amlete ambaye atamuasi na wao wanamtukuza kwa sifa zake na kumtaja kwa utakatifu wake? Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akawabainishia hekima ya kuumbwa mtu na kwamba huko ni kuandaa kujulisha lile wasilolijua na uharibifu wake katika ardhi hauwezi kuondoa faida ya kupatikana kwake. Hapo Malaika wakatosheka na wakatii.

Kwa hivyo Mwenyezi Mungu Mtukufu hakumuumba mwanaadamu ili afanye maasi na maovu, bali amemuumba kwa ajili ya elimu na amali yenye manufaa na akamkataza ufisadi na madhara. Akikhalifu na kuasi basi huadhibiwa kadri anavyostahiki. Aya hii inafahamisha kwamba elimu na yanayoambatana nayo, ina cheo kikubwa mbele za Mwenyezi Mungu na Malaika wake, kwa sababu Mwenyezi Mungu amefanya bora kumuumba mtu kwa ajili ya elimu na maarifa na alipowaonyesha hilo, Malaika walitoa udhuru kwa kusema: Utakatifu ni wako hatuna elimu isipokuwa ile uliyotufundisha. Ikiwa lengo la kuumbwa mtu ni elimu na amali, basi mwenye kuiacha atakuwa ameivunja hekima ya kuwepo.

Naogopa kusema kuwa lau Malaika wakati huo wangejua athari ya mabomu ya kitonoradi (Nuclear) na mabomu ya sumu (Napalm) waliyotumia Wamarekani huko Vietnam, basi wasingelikinai kabisa...

*14 Inasemekana kuwa katika ardhi walikuwepo watu kabla ya Adam wetu, na kwamba wao walifanya uharibifu kisha wakaangamia wote na Malaika walikuwa wakilijua hilo.Namuomba msamaha Mwenyezi Mungu ambaye anajua vile tusivyovijua sisi wenyewe.

SOMO WAZI

Somo ambalo ni lazima tufaidike nalo katika majibizano ya Mwenyezi Mungu na Malaika wake, ni kwamba mtu, vyovyote atakavyofikia katika elimu, nguvu na ukubwa, hawezi kuepuka kufanyiwa majibizano, malumbano na kushauriwa. Mwenyezi Mungu mwenyewe tu aliye mtukufu alitoa nafasi kwa Malaika ajadiliane nao na kujibizana ambako kunafanana na upinzani; na wao hawakujizuia na hilo, bali walijitia ushujaa wa elimu.

Mwenyezi Mungu akawachukulia upole katika kuwajibu na kuwabainishia dalili kwa upole wakakubali kwa kuridhia na kukinai, sio kwa kukemewa. Pia Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akafungua mlango wa majibizano pamoja na Iblis mwenye laana ambaye alijibizana naye kwa kusema: Umeniumba kwa moto na yeye umemuumba kwa udongo..., kama yatakavyokuja maelezo.

Basi ni juu ya wale wanaojiona kuwa hawawezi kupingwa wachukue faida ya somo hili la wazi. Wakijitoa na kujibiwa watakuwa wanajifanya juu zaidi ya Mwenyezi Mungu, bila ya kujua. Anasema Amirul Muminin Ali(a.s) :Msinich-anganye na watu wenye kujifanya wala msinidhanie kuwa nitaona uzito kwa haki niliyoambiwa wala kujifanya mkubwa. Kwani mwenye kuona uzito wa haki anayoambiwa au uadilifu atakaoonyeshwa, basi kuyafanya hayo mawili itakuwa uzito zaidi kwake. Msijizuwie na haki iliyosemwa au ushauri wa uadilifu. (Nahjul-Balagha, Khutba Na. 213).


6

7

8

9

10

11

12

13

14

15