TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA13%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Mwandishi:
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Juzuu 9 Juzuu 10 Juzuu 11
  • Anza
  • Iliyopita
  • 20 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 39073 / Pakua: 4816
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA KWANZA Juzuu 1

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

13

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تَذْبَحُوا بَقَرَةً قَالُوا أَتَتَّخِذُنَا هُزُوًا قَالَ أَعُوذُ بِاللَّـهِ أَنْ أَكُونَ مِنَ الْجَاهِلِينَ ﴾

67.Na Musa alipowaambia watu wake: Hakika Mwenyezi Mungu anawaamrisha mchinje ng’ombe. Wakasema: Je! Unatufanyia mzaha? Akasema: Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga.

﴿قَالُوا ادْعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا هِيَ قَالَ إِنَّهُ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٌ لَّا فَارِضٌ وَلَا بِكْرٌ عَوَانٌ بَيْنَ ذَٰلِكَ فَافْعَلُوا مَا تُؤْمَرُونَ ﴾

68.Wakasema: Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni ng’ombe gani? Akasema: Hakika yeye anasema kwamba ng’ombe huyo si mpevu wala si mchanga, ni wa katikati baina ya hao. Basi fanyeni mnavyoamrishwa.

﴿قَالُوا ادْعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا لَوْنُهَا قَالَ إِنَّهُ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٌ صَفْرَاءُ فَاقِعٌ لَّوْنُهَا تَسُرُّ النَّاظِرِينَ ﴾

69.Wakasema: Tuombee kwa Mola wako atupambanulie rangi yake ni ipi? Akasema: Yeye anasema ng’ombe huyo ni wa manjano, na rangi yake imeiva sana, huwapendeza wanaomtazama.

﴿قَالُوا ادْعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا هِيَ إِنَّ الْبَقَرَ تَشَابَهَ عَلَيْنَا وَإِنَّا إِن شَاءَ اللَّـهُ لَمُهْتَدُونَ ﴾

70.Wakasema: Tuombee kwa Mola wako atupambanulie ni vipi hali yake; hakika ng’ombe wamefanana na hakika sisi kama Mwenyezi Mungu akipenda (tutakuwa) ni wenye kuongoka.

﴿قَالَ إِنَّهُ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٌ لَّا ذَلُولٌ تُثِيرُ الْأَرْضَ وَلَا تَسْقِي الْحَرْثَ مُسَلَّمَةٌ لَّا شِيَةَ فِيهَا قَالُوا الْآنَ جِئْتَ بِالْحَقِّ فَذَبَحُوهَا وَمَا كَادُوا يَفْعَلُونَ ﴾

71.Akasema: Yeye anasema: Kuwa huyo si ng’ombe anayefanyishwa kazi ya kulima ardhi wala kutilia maji mimea, mzima, hana kipaku. Wakasema: Sasa umeleta haki. Basi wakamchinja, na walikaribia wasifanye.

﴿وَإِذْ قَتَلْتُمْ نَفْسًا فَادَّارَأْتُمْ فِيهَا وَاللَّـهُ مُخْرِجٌ مَّا كُنتُمْ تَكْتُمُونَ ﴾

72.Na mlipoiua nafsi, kisha mkahitilafiana kwa hayo, na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuyatoa hayo mliyokuwa mkiyaficha.

﴿فَقُلْنَا اضْرِبُوهُ بِبَعْضِهَا كَذَٰلِكَ يُحْيِي اللَّـهُ الْمَوْتَىٰ وَيُرِيكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴾

73.Tukasema: Mpigeni kwa kipande chake (huyo ng’ombe). Ndivyo hivi Mwenyezi Mungu huwahuisha wafu; na anawaonyesha ishara zake ili mpate kufahamu.

MWENYEZI MUNGU ANAWAAMRISHA MCHINJE NG’OMBE

Aya 67 - 73

MUHTASARI WA KISA

Aya hizi tukufu haziwezi kufahamika maana yake bila ya kufahamu tukio lililoteremshiwa. Kwa ufupi tukio lenyewe ni hili: Mzee mmoja tajiri katika Waisrail aliuliwa na binamu yake kwa tamaa ya kurithi mali yake; kisha akadai kuwa ameuliwa na watu wengine, na wakatakiwa walipe fidia. Ukazuka ubishi mkubwa na wakamwendea Musa(a.s) . Kwa vile hakukuwa na ushahidi wowote wa kugundua mambo walimtaka Musakama kawaida yao - kumwomba Mwenyezi Mungu awabainishie muuaji. Ndipo Mwenyezi Mungu akampa wahyi kuwa wachinje ngombe na sehemu ya huyo ngombe wampige yule aliyeuliwa atafufuka na ataeleza yule aliyemuua. Baada ya udadisi mwingi walifanya vile walivyotakiwa kufanya na yule aliyeuliwa akafufuka na akamtaja aliyemuua.

MAANA

Wakasema: Je unatufanyia mzaha? Yaani tunakuuliza kuhusu kuuliwa mtu nawe unatuamrisha kuchinja ngombe hakika huu ni mzaha. Akasema: Najikinga kwa Mwenyezi Mungu kuwa miongoni mwa wajinga. Yaani mimi sifanyi mzaha, hata katika mambo yasiyokuwa ya kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu, sembuse hayo ya kufikisha neno la Mungu ambaye umetukuka msemo Wake? Ilikuwa inatosha tu wamchinje ngombe yoyote, kwa sababu waliamrishwa wachinje ngombe tu; lakini kwa udadisi wao.

Wakasema:Tuombee Mola wako atupambanulie ni ng’ombe gani? Wakajibiwa kuwa ni ambaye yuko katikati si mkubwa wala si mdogo, basi fuateni amri wala msingoje, lakini wakarudia tena kuuliza Wakasema:Tuombee Mola wako atupambanulie rangi yake ni ipi? Akasema: ni wa manjano, lakini tena wakazidi kudadisi na kuuliza swali mara ya tatu, kwa sababu ngombe walio katika rangi hii na umri huu ni wengi. Akawaambia kuwani yule asiyefanyishwa kazi na asiyekuwa na kasoro yoyote. Wakamtafuta mpaka wakampata, wakamchinja; kisha wakampiga maiti kwa kipande cha nyama akafufuka na siri ikafichuka baada ya kumtaja aliyemuua. Ndivyo hivi Mwenyezi Mungu huwahuyisha wafu na anawaonyesha ishara zake ili mpate kufahamu.

Yaani huku kumfufua huyu aliyeuliwa ni ushaidi wazi na dalili wazi ya kufufuliwa watu baada ya kufa, kwa sababu mwenye kuweza kufufua nafsi moja hawezi kushindwa na nyingine. Je, baada ya ushahidi huu wa kuona kwa macho mnaweza mkakanusha na kutia shaka na kuasi? Lakini pamoja na hayo na yasiyokuwa hayo nyoyo zenu zimesusuwaa, bali zimesusuwaa zaidi na zimekuwa ngumu zaidi kuliko jiwe, kama itakavyoeleza Aya inayofuatia. Baada ya maelezo tuliyoyaeleza kuhusu Mayahudi haiwezekani tena kuuliza swali lolote kuwa,kwa nini Mwenyezi Mungu hakumfufua yule aliyeuliwa tangu mwanzo, na hali Mwenyezi Mungu alikuwa anaweza kufanya hivyo? Vipi anaweza kufufuka mtu kwa kupigwa na nyama ya ngombe? Kwa nini ilikuwa lazima ngombe huyo? Kisha kuna faida gani ya kumpiga na ngombe huyo aliyeuliwa?

Maswali yote haya hayana nafasi baada ya kuthibitisha kuwa Mwenyezi Mungu aliwafanyia Mayahudi mambo maalum wao tu; na kwamba Yeye kwa upande huu ndio amewafadhilisha juu ya watu wote.

﴿ ثُمَّ قَسَتْ قُلُوبُكُم مِّن بَعْدِ ذَٰلِكَ فَهِيَ كَالْحِجَارَةِ أَوْ أَشَدُّ قَسْوَةً وَإِنَّ مِنَ الْحِجَارَةِ لَمَا يَتَفَجَّرُ مِنْهُ الْأَنْهَارُ وَإِنَّ مِنْهَا لَمَا يَشَّقَّقُ فَيَخْرُجُ مِنْهُ الْمَاءُ وَإِنَّ مِنْهَا لَمَا يَهْبِطُ مِنْ خَشْيَةِ اللَّـهِ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴾

74. Kisha nyoyo zenu zikawa ngumu baada ya hayo, zikawa kama mawe au ngumu zaidi; kwani kuna mawe mengine yanayobubujika mito ndani yake, na kuna mengine yanayopasuka yakatoka maji ndani yake; na kuna mengine huanguka kwa sababu ya kumwogopa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu si Mwenye kughafilika na mnayoyafanya.

KUWA NGUMU NYOYO

Aya 74

Kisha nyoyo zenu zikawa ngumu baada ya hayo. Yaani ilikuwa ni wajibu kwa wazee wenu - enyi Mayahudi wa Madina - wazingatie na zilainike nyoyo zao baada ya kushuhudia waliyoyashuhudia katika miujiza na maajabu; ambayo miongoni mwake ni kufufua aliyeuliwa, lakini, kwa ukhabithi wao, wakafanya kinyume na vile inavyotakiwa; wakafanya ufisadi na nyoyo zao zikasusuwaa kama kwamba zimetokana na mawe, bali baadhi yake ni ngumu zaidi kuliko mawe, kwani kuna mawe, mengine yanayobubujika mito ndani yake, na kuna mengine yanayopasuka yakatoa maji. Unaweza kuuliza: Mito ni maji, sasa mbona yametajwa maji na mito? Inawezekana kutofautisha jengo na nyumba? Jibu: Hakika Aya tukufu imegawanya maji kwenye mafungu mawili mengi ambayo ni mto, na machache ambayo ni chemchem. Ibara ya mgawanyiko imekuja kwa tamko la maji, kwa hivyo kumetajwa kububujika maji kwa maana ya wingi na kupasuka kwa maana ya uchache.

Vyovyote iwavyo, lengo la Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuwa amefadhilisha aina za majabali na mawe kuliko nyoyo za Mayahudi, ni kwa sababu jiwe linaweza kupasuka likatoa maji, na kwamba jiwe mara nyingine huwa linatikisika likaondoka pale lilipokuwa. Lakini nyoyo za Mayahudi hazina hata chembe ya kheri wala hazitikiswi na uzuri wowote na hazielekei kwenye uongofu. Unaweza kuuliza kuwa mawe hayana uhai wala utambuzi, kwa hiyo hayawezi kumwogopa Mwenyezi Mungu, sasa kuna wajihi gani katika kauli yake Mwenyezi Mungu: Na kuna mengine huanguka kwa sababu ya kumwogopa Mwenyezi Mungu.

Swali hilo limejibiwa kwa majibu mengi, yaliyo karibu zaidi ni mawili: Kwanza, hayo ni makisio kwamba lau kama mawe yangelikuwa na fahamu na akili kama Mayahudi, yangelianguka kwa kumwogopa Mwenyezi Mungu. Mifano hii ni mingi sana katika maneno ya waarabu. Jibu jingine, ni kwamba ni kawaida ya mawe kumnyenyekea Mwenyezi Mungu ambaye ndiye aliyeumba maumbile yote. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿تُسَبِّحُ لَهُ السَّمَاوَاتُ السَّبْعُ وَالْأَرْضُ وَمَن فِيهِنَّ وَإِن مِّن شَيْءٍ إِلَّا يُسَبِّحُ بِحَمْدِهِ وَلَـٰكِن لَّا تَفْقَهُونَ تَسْبِيحَهُمْ إِنَّهُ كَانَ حَلِيمًا غَفُورًا﴾

Zinamsabihi (zinamtakasa) mbingu zote saba na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake, na hakuna chochote ila kinamsabihi kwa sifa Zake njema. (17:44)

Utakuja ufafuanuzi tutakapofika Aya hiyo inshallah.

TOFAUTI YA HULKA

Anaweza kuuliza muulizaji: Je ndani ya binadamu kuna nguvu inayompa msukumo wa harakati; au yanayompa harakati ni matukio ya nje, kiasi ambacho ndani ni tawi lakini nje ndio shina? Au kila moja ni shina hiyo yenyewe peke yake, kwamba mtu mara nyingine hupata msukumo kutoka ndani na mara nyingine nje au mara nyingine ndani na nje? Kama tutafaradhia kuwa ndani ya binadamu kuna msukumo wa aina ya peke yake usioshirikiana na kitu kingine, Je msukumo huo ni wa aina moja kwa watu wote au kila mtu ana wa aina yake? Jibu: Hakika mtu anakuwa mtu kwa silika yake na nguvu yake ya kiroho. Lau tunavitoa vitu hivyo au tanavizuia utendaji kazi wake, basi binadamu atakuwa ni kama ganda tupu au unyoya katika mavumo ya upepo. Ndio! Ni kweli kwamba nguvu za kindani zinafanya kazi pamoja na matukio ya nje na kuathirika nazo, lakini kufanya kazi ni kitu kingine na kuathirika ni kitu kingine. Kwa mfano, silika ya kuchunguza inakuwa pamoja na mtu na ndio maana mtoto anakuwa mdadisi kwa umbile lake; bali sili- ka hiyo ni katika mambo yanayomuhusu mtu. Kisha silika hii inakua na kukoma kwa kuona matukio ya nje vilevile kwa utafiti na uvumbuzi; na kwa kukua kwake binadamu anaweza kuathirika vitu vya nje kulingana na haja yake na matakwa yake. Kwa hivyo harakati za binadamu zinachimbuka kutoka ndani na nje, yaani kutoka katika nafsi yake na kutoka katika matukio.

Hapa kuna kifungu cha tatu ambacho nimekigundua kutokana na majaribio yangu maalum; Kifungu hicho nimekipa jina Tawfik katika heri na kufaulu. Kifungu hiki hakitokani na nafsi wala matukio, bali kinatokana na nguvu iliyojificha ambayo iko katika ulimwengu uliojificha (usiojulikana), inawaandalia baadhi ya watu njia ya heri na inaingia katika kuwaelekeza watu kwenye lile linalomridhshia Mwenyezi Mungu bila ya mtu kutambua. Ni kawaida kwamba hatanikubalia juu ya hili isipokuwa yule anayemwamini Mwenyezi Mungu na hekima yake na kumpa cheo kinachomstahiki. Ninakiri kwamba mimi sina ufahamu wa ujumla wa kifungu hiki, isipokuwa nimekifahamu kutokana na majaribio yangu; kama nilivyotangulia kueleza.23 Ama jawabu la kuwa je, watu wanakuwa na namna moja katika silika na sifa za kinafsi, linataka ufafanuzi. Katika sifa za kinafsi kuna zile ambazo watu wanashir-ikiana; kama vile utambuzi wa kupambanua kati ya haki na batili, heri na shari, na kati ya baya na zuri.

* 23 Jambo la kushangaza lilotokea kwa sadfa.Baada ya kuandika maneno haya nikasoma nakala fulani, kuwa kiongozi mmoja wa kijeshi wa Kiingereza maarufu sana anayeitwa Montgomery alijieleza kwa kusema: Hakika yeye ni askari mdogo chini ya uongozi wa nguvu kuu; na kwamba yeye hakushinda katika vita isipokuwa kwa matakwa ya kudra hiyo; na kwamba bila ya kuamini nguvu hii kubwa yenye akili, haiwezekani kushinda katika vita vya dunia vya pili. Yeye anaamini kwamba kuna nguvu iliyofichika ambayo iliwaandalia njia ya kumshinda Romel, ambaye alikuwa akiitwa mbweha wa jangwani, naye alikuwa amirijeshi mkubwa wakati huo. Lau si ushirikiano huu isingeliwezekana kwa vyovyote vile kuthibitisha uovu na wema na isingelifaa kwetu kumlaumu au kumsifu mtu kwa kufanya jambo fulani. Vile vile kuna ushirikiano katika kujipenda na upendo wa mzazi na mwana, na mengineyo ambayo wanayo watu wote, ijapokuwa kuna tofauti ya wingi na uchache.

Kuna sifa nyingine za kinafsi, ambazo watu wanatofuatiana kama vile; ushujaa, woga, ukarimu, ubahili, ugumu wa moyo, ulaini wa moyo, udhaifu wa matakwa na nguvu yake na kupondokea kwenye heri au shari. Watu katika sifa hizi wanatofuatiana, kila mtu sio karimu au bahili,wala mwoga au mshari. Unaweza kuuliza: Hakika kauli yako si inakhalifu kawaida maarufu iliyozoeleka, kuwa hakuna mtu yoyote isipokuwa ana pande mbili, mzuri na usiokuwa mzuri; na wewe umetilia mkazo upande mmoja tu, na ukaufinyia jicho upande mwingine?. Jibu: Hakika uvivio wa heri ambao mara nyengine tunauona kwa baadhi ya watu wa shari, unakuwa umeingia kighafla tu, bila ya kukusudiwa; na kwamba suala la kuwa kila mtu ana pande mbili linawezekana kwa wasiokuwa Mayahudi.Kwa sababu, Mayahudi hawana lolote wao isipokuwa uovu tu; hawana wema kabisa. Ushahidi wa hayo ni Tawrat yao, Quran tukufu na historia sahihi. Vile vile vitendo vyao katika Palestina na kwingineko, mambo ambayo ni dalili wazi kwamba dini, maadili na mfungamano wote wa kiutu, kwao ni biashara na manufaa tu.Maudhui haya tutayarudia kila itakapolazimika.

﴿أَفَتَطْمَعُونَ أَن يُؤْمِنُوا لَكُمْ وَقَدْ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْهُمْ يَسْمَعُونَ كَلَامَ اللَّـهِ ثُمَّ يُحَرِّفُونَهُ مِن بَعْدِ مَا عَقَلُوهُ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴾

75.Je mna matumaini ya kwamba wataamini na hali baadhi yao walikuwa wanasikia maneno ya Mwenyezi Mungu kisha wanayabadili baada ya kuwa wameyafahamu na hali wanajua?

HAKUNA MATUMAINI

Aya 75

MAELEZO

Kila mwenye ujumbe fulani huwa anapupia watu wauamini ujumbe huo. Kwa hivyo anaueneza kwa matumaini ya kupata wafuasi wengi, na anahimili taabu na mashaka katika hilo, kama alivyofanya Mtume(s.a.w.w) na sahaba zake, waliueneza mwito wa Uislamu katika pembe zote kwa kutaraji kupata wafuasi. Kulikuwa na mfungamano wa kijirani, kibiashara na hata kunyonyeshana watoto kati ya Ansar na Mayahudi. Hivyo wakawalingania kwenye Uislamu kwa amri ya Mtume. Wakawatolea dalili kwa hoja zinazoingia akilini na kwa mantiki mazuri, wakatumai kwamba nyoyo zao zitashtuka, hasa kwa kuzingatia kwamba wao ni watu wa Kitabu na kwamba sifa za Muhammad(s.a.w.w) zimetajwa kwa uwazi katika Tawrat yao. Walipoendelea Wayahudi kukaidi mwito wa Uislamu na kuendelea kukufuru na kuipinga haki, ndipo Mwenyezi Mungu alipomwambia Mtume wake kwa kusema: Je mnatumaini nyinyi Waislamu ya kwamba watawaamini hao Mayahudi, na hali wazee wao hawa Mayahudi walikuwa wakisikia maneno ya Mwenyezi Mungu kutoka kwa Nabii Musa(a.s) pamoja na miujiza, lakini wakiyabadilisha na kuyageuza vile matamanio yao yanavyotaka pamoja na kujua kuwa hayo maneno ni ya haki?

Kwa hivyo, hali ya Wayahudi wa Madina ni kama hali ya wazee wao waliopita, ambao walibadilisha halali ikawa haramu na haramu kuwa halali kwa kufuata matamanio yao na wakabadilisha sifa za Muhammad(s.a.w.w) zilizopokewa katika Tawrat, ili isiweko hoja juu yao. Mwenye Majmaul-Bayan anasema: Katika Aya hii kuna dalili juu ya ukubwa wa dhambi ya kuibadilisha sheria. Na dhambi hiyo inapatikana katika kuleta Bida katika fatwa au hukumu na mambo yote ya kidini. Kuongezea juu ya maneno hayo ya mwenye Majmau ni kuwa Aya hii ni dalili juu ya kuwa mwenye kufuata upotevu kwamba sio kuwa anajifanyia uovu yeye mwenyewe tu, bali athari yake inaenea kwa vizazi, kama ilivyoelezwa katika Hadith.

﴿وَإِذَا لَقُوا الَّذِينَ آمَنُوا قَالُوا آمَنَّا وَإِذَا خَلَا بَعْضُهُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ قَالُوا أَتُحَدِّثُونَهُم بِمَا فَتَحَ اللَّـهُ عَلَيْكُمْ لِيُحَاجُّوكُم بِهِ عِندَ رَبِّكُمْ أَفَلَا تَعْقِلُونَ﴾

76. Na wanapokutana na wale walioamini husema: Tumeamini. Na wanapokuwa peke yao, wao kwa wao husema: Mnawaambia yale aliyowahukumia Mwenyezi Mungu ili wapate kuhojiana nanyi mbele ya Mola wenu? Je,hamna akili?

﴿أَوَلَا يَعْلَمُونَ أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ﴾

77.Hawajui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua wanayoyayafanya siri na wanayoyadhihirisha?

WANAPOKUTANA NAWALE WALIOAMINI

Aya 76 - 77

MAELEZO

Baadhi ya Mayahudi walikuwa wakifanya unafiki na uwongo kwa Waislamu na wakisema: Sisi tunaamini yale mnayoyaamini nyinyi na tunashuhudia kuwa Muhammad ni mkweli katika maneno yake, kwani tumekuta katika Tawrat sifa zake. Lakini wanafiki hao wanapochanganyikana na viongozi wao, basi viongozi wanawalaumu kwa kusema: Vipi mnawahadithia wafuasi wa Muhammad yale aliyowahukumia Mwenyezi Mungu? Hivi hamfahamu kwamba huko ni kukubali nyinyi wenyewe kwamba mko katika batili na wao wako katika haki? Hawajui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua wanayoyafanya siri na wanayoyadhihirisha? Yaani kwa vyovyote watakavyojaribu wanafiki, kuficha unafiki wao na viongozi wapotevu wanavyowaelekeza wafuasi wao, lakini kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hakifichiki chochote. Basi nyinyi Mayahudi mnaficha njama zenu, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamfahamisha Mtume wake Muhammad(s.a.w.w) na anavifagia vitimbi vyenu.

﴿وَمِنْهُمْ أُمِّيُّونَ لَا يَعْلَمُونَ الْكِتَابَ إِلَّا أَمَانِيَّ وَإِنْ هُمْ إِلَّا يَظُنُّونَ ﴾

78.Na wako miongoni mwao wasiojua kusoma; hawajui kitabu isipokuwa matamanio tu nao hawana isipokuwa kudhani tu!

﴿فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ يَكْتُبُونَ الْكِتَابَ بِأَيْدِيهِمْ ثُمَّ يَقُولُونَ هَـٰذَا مِنْ عِندِ اللَّـهِ لِيَشْتَرُوا بِهِ ثَمَنًا قَلِيلًا فَوَيْلٌ لَّهُم مِّمَّا كَتَبَتْ أَيْدِيهِمْ وَوَيْلٌ لَّهُم مِّمَّا يَكْسِبُونَ﴾

79.Basi ole wao wanaoandika kitabu kwa mikono yao. Kisha wakasema hiki kimetoka kwa Mwenyezi Mungu ili wachukue kwacho thamani ndogo. Basi ole wao kwa yale iliyoyaandika mikono yao. Na ole wao kwa yale wanayoyachuma.

WAKO MIONGONI MWAO WASIOJUA KUSOMA

Aya 78 79

MAELEZO

Na wako miongoni mwao wasiojua kusoma. Yaani katika Mayahudi kuna wale waliokuwa hawakusoma; hawajui chochote katika dini ya Mwenyezi Mungu na kwamba mambo yao zaidi ni ya kudhania dhania tu, bila ya kutegemea elimu. Kimsingi ni kwamba ingawa maelezo haya yamekuja kwa sababu ya Wayahudi, lakini shutumu inamwendea kila mjinga.

TAFSIRI INA MISINGI NA KANUNI

Katika Aya hii kuna dalili wazi kwamba haifai kufasiri Quran na Hadith kwa kudhania na kukisia, bali hapana budi lazima mfasiri awe na elimu ya kanuni za tafsiri na misingi yake, na kuchunga kanuni hizi katika kubainisha makusudio ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa kujihadhari na kuwazulia. Sharti la kwanza la kufaa kufasiri ni kujua kusoma na kuandika; kisha hujua elimu za Kiarabu kwa aina zake zote, ambazo ni kujua msamiati, Sarfa, Nahw, Bayan, Fiqh na misingi yake. Vile vile kujua elimu ya Tawhid na kuongezea elimu nyingine ambazo zitamsaidia katika kufasiri baadhi ya Aya. Yote haya mfasiri anaweza kuyajua kwa kuwaendea wenye kuhusika nayo. Basi ole wao wanaoandika kitabu kwa mikono yao. Hapa Mwenyezi Mungu anamkemea kila anayemnasibishia yale asiyokuwa nayo kwa ajili ya kuchukua thamani kwa shetani. Si lazima thamani iwe ni mali (pesa) tu; inaweza kuwa ni kupata jaha au chochote katika anasa za kidunia.

Mwenyezi Mungu amekariri makemeo mara tatu katika Aya moja kwa kutilia mkazo kwamba kumzulia yeye Mwenyezi Mungu na Mtume ni katika maasi makubwa na yenye adhabu kali; kama alivyosema mahali pengine:

﴿قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ وَيْلَكُمْ لَا تَفْتَرُوا عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا فَيُسْحِتَكُم بِعَذَابٍ وَقَدْ خَابَ مَنِ افْتَرَىٰ﴾

Ole wenu msimzulie uwongo Mwenyezi Mungu asije akawafutilia mbali kwa adhabu, Na ameruka utupu anayezua uwongo. (20:61)

MWANACHUONI HAWEZI KUHUKUMU KWAMATUKIO

Tunadokeza kwa mnasaba huu kwamba mwanachuoni, kwa namna yoyote atakavyokuwa na elimu, ni juu yake kutomnasibishia chochote Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kwamba kitu hicho kinatoka katika Lawh Mahfudh. Akitoa fatwa kwa uhalali au uharamu; au kuhukumia kitu kuwa ni haki; au kufasiri Aya au Hadith, basi ni juu yake kuifanya hukumu yake hiyo, fatwa yake au tafsiri yake kuwa ni rai yake tu. Inaweza kuwa ni makosa au sawa. Hapo ndio atakuwa anakubaliwa msamaha mbele ya Mwenyezi Mungu kama akijitahidi kadiri ya uwezo wake. Lakini kama hakujitahidi sana au amejitahidi sana, lakini akasema kuwa kauli yake hiyo ni kauli ya

* 24 W amethibitisha wenye kuhusika na historia ya lugha na ada zake kwamba Tawrat ya sasa, ambayo Wayahudi wanaitakidi kuwa iliteremshwa na Mwenyezi Mungu kwa Musa, imetungwa. W atafiti wametoa hakika hii kutokana na muundo wa lugha ulivyo na ustawi wa kijamii na wa kisiasa ambao uko kinyume na Tawrat. Tutarudia kueleza maudhui haya kwa upana zaidi Inshallah. Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi atakuwa ni sawa na wale wanaomzulia Mwenyezi Mungu uwongo, ajapokuwa ni mwanachuoni wa wanachuoni. Kwa sababu mwanachuoni hatoi fatwa ya kweli wala hukumu ya kweli,bali anaitikadi tu kuwa ni haki. Huu ndio msingi wa kwamba yeye sio maasum.

﴿وَقَالُوا لَن تَمَسَّنَا النَّارُ إِلَّا أَيَّامًا مَّعْدُودَةً قُلْ أَتَّخَذْتُمْ عِندَ اللَّـهِ عَهْدًا فَلَن يُخْلِفَ اللَّـهُ عَهْدَهُ أَمْ تَقُولُونَ عَلَى اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ﴾

80.Na walisema: Hautatugusa moto isipokuwa kwa siku chache tu. Sema: Je, mmepata ahadi kwa Mwenyezi Mungu Kwa hivyo hatakhalifu ahadi yake.Au mnamsingizia Mwenyezi Mungu mambo msiyoyajua?

﴿بَلَىٰ مَن كَسَبَ سَيِّئَةً وَأَحَاطَتْ بِهِ خَطِيئَتُهُ فَأُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

81. Ndiyo, wanaochuma ubaya na makosa yao yakawazunguka, hao ndio watu wa motoni; humo watadumu.

﴿وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

82.Na wale walioamini na kutenda mema, hao ndio watu wa peponi, watadumu humo.

WALISEMA HAUTATUGUSA MOTO WA JAHANNAM

Aya 80 - 82

Na walisema: Hautatugusa moto isipokuwa kwa siku chache tu Mayahudi wanadai kwamba wao ni watoto wa Mungu na taifa lake teule na kwamba watu wote ni watoto wa shetani, isipokuwa wao tu, na ni mataifa yaliyotupiliwa mbali. Kwa hivyo ati Mwenyezi Mungu hatawaweka milele motoni, isipokuwa atawaadhibu kwa adhabu hafifu tena kwa muda mfupi, kisha atawaridhia. Yaani kwamba Mwenyezi Mungu anawaendekeza na kuuendekeza ukoloni wa kizayuni ambao unaikalia ardhi ya Palestina. Sema: Je, mmepata ahadi kwa Mwenyezi Mungu. Yaani waambie ewe Muhammad, kwamba madai yao haya ni porojo tu, na kama si hivyo, basi ni ahadi gani mliyowekeana na Mwenyezi Mungu? Madai yao haya, hayafahamishi chochote zaidi ya kudharau kwao madhambi na kufanya uovu.

Mtume mtukufu(s.a.w.w) anasema:Hakika mumini anaona dhambi yake ni kama jiwe anaogopa lisimwangukie na kwamba kafiri anaona dhambi yake ni kama nzi tu aliyepitia kwenye pua yake....

Anasema Amirul Muminin(a.s) :Dhambi kubwa zaidi ni ile iliyodharauliwa na mwenye kuifanya.

Kauli yake Mtume mtukufu(s.a.w.w) : Kama kwamba dhambi ni nzi anayepita juu ya pua ya mwenye dhambi. Inafanana kabisa na ya Mayahudi ambao wanadai kwamba wao ni watoto wa Mwenyezi Mungu wenye kutendekezwa. Huenda haya yakamnufaisha na kumzindua yeyote ambaye anapuuza dhambi kwa kutegemea utukufu wa nasabu. Mwenye kujitegemea yeye mwenyewe tu wala asihisi makosa ya nafsi yake, na asikubali nasaha za mwingine, basi ni muhali kuweza kuongoka kwenye heri. Hakika mwenye akili hajiangalii mwenyewe tu kwa kujihadaa na ndoto zake, bali daima anakuwa na msimamo wa kujilaumu makosa yake na kupambanua yale aliyonayo na yale anayotakiwa awe nayo. Vile vile huitoa nafsi yake na fikra za kitoto na mawazo ya kishetani. Kwa hali hii pekee ndio atakuwa anafaa kuitwa mtu kwa maana sahihi. Kuna hadith tukufu inayosema: Mwenye kujiona kwamba yeye ni mwovu, basi ni mwema.

Ndiyo, wanaochuma ubaya na makosa yao yakawazunguka, hao ndio watu wa motoni na humo watadumu. Ubaya ni shirk na madhambi mengineyo, lakini makusudio yake hapa yanahukumu shirk tu! Kwa kulinganisha na kauli yake Mwenyezi Mungu hao ndio watu wa motoni humo watadumu. Mwenye Majmaul-Bayan anasema: Makusudio ya ubaya kuwa ni shirk ndiyo yanayoafiki, kwa sababu dhambi nyingine yoyote haiwajibishi kudumu motoni. Na wale walioamini na kutenda mema hao ndio watu wa peponi watadumu humo. Aya hii tukufu inafahamisha kuwa kuokoka na adhabu ya Mwenyezi Mungu kesho kutatokana na imani sahihi ikiambatana na matendo mema. Hadith tukufu inasema: Abu Sufyani Athaqafiy, alisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Niambie neno katika Uislamu ambalo sitamuuliza yeyote baada yako.Akasema Mtume:Sema: Nimemwamini Mwenyezi Mungu, kisha ufuate unyoofu (msimamo).

Katika hadith yake hii Mtume(s.a.w.w) anaelezea Aya inayosema:

﴿إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ﴾

Wale waliosema: Mola wetu ni Mwenyezi Mungu kisha wakawa na unyoofu hao huwateremkia malaika (wakawambia): Msiogope wala msihuzunike, na furahini kwa pepo mliyokuwa mkiahidiwa. (41:30).

Makusudio ya kuwa na unyoofu katika Aya na Hadith, ni kuwa katika msimamo wa kufanya amali kwa mujibu wa Quran na hadith za Mtume(s.a.w.w) .

MWISLAMU NA MUUMINI

Mwislamu kwa kuangalia muamala wake na kuthibiti Uislamu wake, anagawanyika kwenye mafungu mawili:

Kwanza : kumkubali Mwenyezi Mungu kuwa ni mmoja na kukubali Utume wa Muhammad bila ya kuangalia itikadi yake na amali (matendo) yake. Lakini ni sharti asikanushe zile dharura za dini, kama ulazima wa swala na uharamu wa zinaa na pombe. Huyu ndiye anayejulikana kwa Waislamu kuwa yeye ni Mwislamu atafanya na kufanyiwa mambo ya Kiislamu; kama kurithi, kuoa, na kuzikwa kiislamu, ikiwa ni pamoja na kumwosha, kumtia sandani, kumswalia na kumzika katika makaburi ya Waislalmu, anafanyiwa hayo kwa vile amepiga shahada.

Pili : ni kuamini na kushikamana na Uislamu kwa misingi na matawi; hakanushi hukumu yoyote katika hukumu za Kiislamu, wala hafanyi uasi wa hukumu katika hukumu za sheria. Huyu ndiye Mwislamu wa kweli (muumin) mbele ya Mwenyezi Mungu na watu, bali ni Mwislamu mwadilifu ambaye zimethibiti kwake athari zote za uadilifu wa Kiislamu duniani na akhera. Athari za dunia ni kukubaliwa ushahidi wake, kufaa kuswalisha, kuchukua hukumu zake na fatwa zake akiwa ni mujtahidi. Ama athari za kiakhera ni kule kuwa juu hadhi yake na thawabu. Mumin ni yule mwenye kukiri kwa ulimi na kusadikisha kwa moyo wake shahada mbili, wala haitoshi kukiri kwa ulimi tu au kusaidikisha kwa moyo tu, bali hapana budi yote mawili yaende sambamba. Kwa hivyo kila mumin ni Mwislamu, lakini si kila Mwislamu ni mumin.

Hapa inatubainikia kwamba amali njema haiitwi imani, kwa dalili kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Ameleta kiunganishi baina ya imani na amali njema kwa maana ya kuwa ni vitu viwili tofauti. Hata hivyo amali njema inaingia katika ufahamu wa uadilifu kama tulivyoonyesha. Utakuja ufafanuzi wake mahali pake. Mafaqihi wa kishia wanahusisha tamko la mumin kwa yule anayeamini Maimamu kumi na wawili, wakisema zaka inapewa mumin, na mwenye kuswalisha awe mumin, basi wanakusudia yule mwenye kuamini maimamu kumi na wawili tu. Istilahi hii wanahusika nayo mafaqih tu. Lakini hata huyo fakihi wa Kishia kama akizugumzia mumin katika mswala yasiyokuwa ya kifikihi, basi huwa anakusudia kila mwenye kukiri shahada mbili na kuzisadikisha kwa moyo; hata kama siye mwenye kuamini Maimamu kumi na wawili.

Kwa vyovyote ilivyo Uislamu na imani kwa maana tuliyoyaelezea, hautamuokoa mtu na adhabu ya Mwenyezi Mungu kesho, isipokuwa uwe pamoja na unyoofu ambao ni kufanya amali kulingana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna za Mtume Wake(s.a.w.w) .

MWENYE MADHAMBI MAKUBWA

Mafakihi wameyagawanya madhambi katika mafungu mawili Makubwa; kama kunywa pombe. Na madogo kama kukaa kwenye meza ya pombe bila kunywa. Utakuja ufafanuzi wa madhambi makubwa na madogo Inshallah, katika Aya isemayo:Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu; isipokuwa makosa hafifu...

Wamehitalifiana Waislamu katika yule mwenye kukiri shahada mbili na akafanya madhambi makubwa, Je, yeye ni kafiri atakayebakia milele motoni au yeye ni mwislamu fasiki ambaye ataadhibiwa kiasi anachostahili, kisha atiwe peponi? Khawarij wamesema kuwa atabakia milele motoni.Shia, Ashari, Masahaba wengi na Tabiin, wamesema atatolewa motoni. Mutazila wamezusha fikra ya tatu ya kuthibitisha mawili, yaani hatakuwa kafiri wala Mumin. Allama Hilli ametoa dalili katika sherehe ya Tajrid juu ya ushahidi wa kauli ya kuwa mwenye madhambi makubwa ni fasiki hatokaa milele motoni, kuwa: Lau atabakishwa milele motoni, ingelazimika mwenye kumwabudu Mwenyezi Mungu muda wa umri wake wote; kisha akamuasi mwisho wa umri wake mara moja tu, pamoja na kubakia na imani yake, aingie motoni milele, awe sawa na yule aliyemshirikisha Mwenyezi Mungu katika umri wake wote. Na hilo ni muhali na haliingii akilini.

Hapana mwenye shaka kwamba ovu moja haliwezi kuondoa mema yote, bali ni kinyume; kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t). Kwa ajili hiyo basi, inapasa kulichukulia neno ubaya katika Aya (Na wanaochuma ubaya na makosa yao yakawazunguka, hao ndio watu wa motoni, watadumu humo), kuwa na maana ya shirk. Kama ambavyo Aya inayofuatia hiyo (Na wale walioamini na kutenda mema hao ndio watu wa peponi, watakaa humo milele) inafahamisha kwamba mwenye kufanya madhambi makubwa ataingia peponi,

* 25 Aya hii tukufu inakuwa ni jibu la yule anayesema: Katika madhambi hakuna kubwa wala dogo, bali yote ni makubwa. Jibu lenyewe ni tamko,Lamam, lenye maana ya uhafifu. wala hatakaa milele motoni. Kwa sababu Aya ile inamhusu pia mwenye kuamini na akafanya amali njema kisha akafanya madhambi makubwa na wala asitubie.

MAYAHUDI TENA

Madai ya Mayahudi kwamba wao ni watoto wa Mungu na taifa teule, ni kwamba dini na maadili yake, katika itikadi yao, ni kazi ya kibiashara na manufaa ya kiutu. Vinginevyo itakuwa ni bure tu. Unaweza kusema, hayo hayahusiani na Mayahudi tu, bali wako watu wa namna hiyo. Jibu, ndio, lakini tofauti iliyopo ni kwamba Mayahudi wana hasadi kwa watu wote isipokuwa wao.

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KWANZA

AL - BAQARAH (NG’OMBE)

﴿ وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ﴾

34.Na tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adam, wakamsujudia wote isipokuwa Iblis; alikataa na akajivuna; na akawa miongoni mwa makafiri.

MSUJUDIENI ADAM

Aya 34

Mwenyezi Mungu aliwaamrisha malaika kumsujudia Adam kwa kudhihirisha ubora wake kuliko wao na kuliko viumbe vyake vyote. Hapana tafsiri ya ubora huu isipokuwa ubora wa elimu au ubora wa aliye nayo. Kwa sababu elimu, kama ilivyothibiti, ndiyo kipimo cha kila hatua anayopiga mtu ya maendeleo na ukamilifu; kama vile ambavyo ujinga ni msingi wa kurudi nyuma. Hawezi kuwa juu isipokuwa kwa elimu. Mwenye elimu siku zote hufuatwa, na mjinga siku zote hufuata. Kwa ajili hii Uislamu umewajibisha elimu kwa kila Mwislamu mwanamume na mwanamke.

Wafasiri wengi wamesema kwamba sijda ilikuwa ni ya ki-maamkuzi tu; Kama kuinama na kuinua mkono. Kwa sababu kumsujudia asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni haramu. Lakini haya sio kweli kwa mujibu wa mwenye tafsiri ya Majmaul-Bayan, kwani kama ingelikuwahivyo,basi, Iblis asingelikataa kumsujudia. Kimsingi sijda ilikuwa ni kwa amri ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kumtii Mwenyezi Mungu sio kwa ajili ya Adam.

Amri ya kumsujudia Adam iliwahusu Malaika wote bila ya kumvua yoyote, hata Jibril na Mikail pia, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ كَانَ مِنَ الْجِنِّ فَفَسَقَ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِ﴾

Na tulipowaambia Malaika, msujudieni Adam.Basi wakamsujudia isipokuwa Iblis; yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake. (18:50)

Hakuna njia ya kumjua Iblis, shetani na jini, isipokuwa kwa njia ya wahyi tu; kama ilivyo katika kuwajua Malaika.Maelezo yamekwishaelezwa katika Aya iliyotangulia.

Wafasiri wameonyesha utafiti usiokuwa na manufaa. Kwa hivyo tumeuacha kwa kufupiliza yale yanayofahamishwa na dhahiri ya maneno. Tumekwishaonyesha katika kurasa zilizotangulia baadhi ya yale yanayona- sibishwa kwa Iblis katika vigano. Ni picha iliyo wazi ya watu wengi wa siku hizi katika kuchezea kwao matamko, ambako hakutimizi elimu au fani yoyote zaidi ya kubobokwa tu.

﴿ وَقُلْنَا يَا آدَمُ اسْكُنْ أَنتَ وَزَوْجُكَ الْجَنَّةَ وَكُلَا مِنْهَا رَغَدًا حَيْثُ شِئْتُمَا وَلَا تَقْرَبَا هَـٰذِهِ الشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ الظَّالِمِينَ ﴾

35.Na tukasema: Ewe Adam! kaa wewe na mkeo katika Pepo (bustani); na kuleni humo maridhawa popote mpendapo, wala msiukurubie mti huu; msije mkawa miongoni mwa waliodhulumu (nafsi zao).

﴿ فَأَزَلَّهُمَا الشَّيْطَانُ عَنْهَا فَأَخْرَجَهُمَا مِمَّا كَانَا فِيهِ وَقُلْنَا اهْبِطُوا بَعْضُكُمْ لِبَعْضٍ عَدُوٌّ وَلَكُمْ فِي الْأَرْضِ مُسْتَقَرٌّ وَمَتَاعٌ إِلَىٰ حِينٍ﴾

36.(Lakini) Shetani akawatelezesha wote wawili na akawatoa katika ile hali waliyokuwa nayo. Tukasema: nendeni hali yakuwa maadui nyinyi kwa nyinyi, na mtapata katika ardhi makazi na starehe kwa muda (maalum).

﴿ فَتَلَقَّىٰ آدَمُ مِن رَّبِّهِ كَلِمَاتٍ فَتَابَ عَلَيْهِ إِنَّهُ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ ﴾

37.Akapokea Adam maneno kutoka kwa Mola wake na Mola wake akapokea toba yake; hakika Yeye ni Mwingi wa kukubali toba, Mwenye kurehemu.

﴿ قُلْنَا اهْبِطُوا مِنْهَا جَمِيعًا فَإِمَّا يَأْتِيَنَّكُم مِّنِّي هُدًى فَمَن تَبِعَ هُدَايَ فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴾

38.Tukasema: Tokeni humo nyote: Na kama ukiwafikia uongozi wangu basi watakaoufuata mwongozo wangu haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

﴿ وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴾

39.Na ambao wamekufuru na kukadhibisha ishara zetu, hao ndio watakaokuwa watu wa motoni, humo watadumu.

ADAMU PEPONI

Aya 35

Mwenyezi Mungu aliamwamrisha Adam na Hawa kukaa peponi; akawahalalishia kula yaliyomo ndani yake isipokuwa mti mmoja tu, waliokatazwa kuula. Lakini shetani aliwahadaa kwa kuwataka waule. Walipokubaliana naye ilipita hekima yake Mwenyezi Mungu ya kuwatoa pepo ni kuwapeleka ardhini na akawatia mtihani kwa taklifa na kazi, uzima na ugonjwa, shida na raha, kisha mauti muda wake unapofika.

Adam alihisi msiba na akajuta. Akamwomba Mola wake kwa ikhlasi amtakabalie toba yake, akamkubalia na akamsamehe, kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kukubali toba Mwenye rehema. Nadhani kwamba Hawa pia alitubia pamoja na Adam, lakini Mwenyezi Mungu hakuitaja toba yake. Hakuna tofauti kati ya Mwanamume na mwanamke. Mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na akafanya amali njema, Mwenyezi Mungu atamuweka peponi, na mwenye amali mbaya atamwingiza motoni awe mume au mke.

Wamejiingiza wafasiri wengi kuelezea pepo aliyotoka Adam,ilikuwa wapi?Mti ulikuwa mtini au ngano? Kuhusu nyoka ambaye aliingia Iblis ndani yake, na mahali aliposhukia Adam, je palikuwa India au Hijaz? Na mengineyo yaliyokuja katika hadithi za Kiisrail.Quran haikudokeza lolote katika hayo; wala haikuthibiti katika hadithi kwa njia sahihi. Pia akili haiwezi kujua chochote katika hayo, na hayo hayaambatani na maisha kwa karibu au mbali. Hata hivyo hakuna budi kutanabahisha mambo yafuatayo:-

HAWA NA UBAVU WA ADAM

Imeenea habari kwamba Hawa aliumbwa kutokana na ubavu wa Adam, lakini hakuna maelezo sahihi ya kutegemewa. Na habari zilizoelezea hilo si za kutegemewa. Ikiwa tutazichukulia kuwa ni sahihi basi ni kwamba makusudio yake ni kuonyesha usawa na kukosa kutofautisha kati ya mume na mke, yaani mke ametokana na mume na mume naye ametokana na mke. Katika kitabu Malla yahdhur hul-faqih, imesemwa, Imam Sadiq(a.s) wakati alipoulizwa usahihi wa uvumi huu, aliukanusha na akasema:Mwenyezi Mungu Ametukuka na hayo kabisa.

Je Mwenyezi Mungu alishindwa kumuumbia Adam mke isipokuwa kutokana na ubavu wake mpaka ikabidi Adam aoe sehemu yake ya mwili?

MTAKA YOTE HUKOSA YOTE

Hekima ya Mwenyezi Mungu ilipitisha kuwa Adam akae na mkewe peponi wakati fulani, kisha atoke kwa sababu maalum ambayo wao wawili ndio walioifanya kwa matakwa yao na hiyari yao; lau si hivyo wangelibaki peponi milele wakistarehe bila ya taabu yoyote.

Vile vile hekima yake Mwenyezi Mungu ilipitisha kuwa Adam na Hawa wabaki katika ardhi hii mpaka watakapozaana na kupatikana koo na vizazi, wakati ambapo wataulizwa wote, kauli na vitendo walivyovifanya. Kama ilivyohukumilia hekima yake kurudi Adam na mkewe peponi baada ya kufa na wadumu humo milele.

Unaweza kuuliza: Kuna hekima gani ya kuingia Adam peponi na kutoka kuja ardhini, kisha kuitoka hiyo ardhi na kurudi tena peponi mara ya pili baada ya kufa?

Jibu : Huenda hekima iliyopo ni kuwa Adam apitie majaribio atakayonufaika nayo na kufaidika nayo, yeye na watoto wake, na kurudi kwenye pepo hii akiwa amejaa majaribio yenye kunufaisha. Yaani ni kwamba mtu hawezi kuishi milele bure bure tu vile anavyotaka na kwamba mwenye kuyachunga hayo majaribio kwa kuyamiliki matakwa yake bila ya kukubali kusukumwa na matamanio yake, basi ataishi maisha mazuri ya wema usiokuwa na mwisho. Na mwenye kuwa na msimamo hafifu na akawa mdhaifu mbele ya matamanio yake, atakuwa amepata aliyoyapata Adam majuto, kujaribiwa, taabu na mashaka.

ISMA (KUHIFADHIWA MITUME)

Wameafikiana Waislamu wote kwamba Adam ni katika Mitume, na Mitume kama inavyofahamika ni wenye kuhifadhiwa na madhambi na makosa.Sasa nini maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu; Akawahadaa shetani katika hali waliyokuwa nayo? Kwa ajili hiyo ndio wameonelea wanachuoni kuwa iko haja kubwa ya kufanya utafiti juu ya Isma ya Mitume; kisha kuifasiri Aya hii katika hali ambayo italeta natija. Nasi tunakusanya kauli juu ya hilo kama ifuatavyo ili iwe ni asili katika kila linaloambatana na maudhui haya. Maana ya Isma ya Mtume ni kutakata na makosa katika kila jambo

*15 Kuna maelezo yanayosema kuwa Adam ana jina la kubandikwa peponi la Abu Muhammad kwa heshima na kutukuzwa, na hakuna mtu mwenye jina la kubandikwa peponi ispokuwa yeye tu. linaloambatana na dini na hukumu zake, kiasi ambacho atafikilia Mtume utakatifu na elimu na kumjua Mwenyezi Mungu na yale anayoyataka kwa waja wake; kwa hali ambayo inakuwa muhali kuikhalifu, iwe kwa makusudi au kwa kusahau. Mwenye kuthibitisha Isma kwa Mitume kwa maana hayo na kwa mafungu yake yote yatakayokuja, ataifanyia taawil Aya inayopingana na dhahiri ya msingi huu, kwa kwenda na kanuni ya kiujumla ambayo ni wajibu wa kufanya taawil kwa kuafikiana na dhahiri ya akili. Na, mwenye kukanusha Isma kwa mitume, atabakisha dhahiri kwa dhahiri yake.

Wanavyuoni wa madhehebu mbali mbali wana kauli nyingi katika Isma, zenye kukhitalifiana kwa tofauti za mafungu yafuatayo:

1. Isma katika itikadi na misingi ya dini; yaani kutakasika kwa Mtume kutokana na ukafiri na ulahidi. Hilo ni lenye kuthibiti kwa kila Mtume kimisingi na kwa maafikiano.Kwani haiingii akilini kuwa Mtume amkanushe yule aliyempa Utume.

2. Isma katika kufikisha amri za Mwe-nyezi Mungu. Akisema, Mwenyezi Mungu anaamrisha hili na anakataza lile, basi amri itakuwa ile ile aliyoisema. Wameafikiana Shia Imamiya kuthibiti Isma hii kwa kila Mtume. Kwa sababu lengo la kufikisha ni kuwachukua wale wanaokalifiwa na sharia kwenye haki.Akikosea mwenye kufikisha itakuwa lengo la kufikisha limebatilika. Hayo yanatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ﴾

Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi yake) (53:3)

Na kauli yake:

﴿ وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا﴾

Na anachowapa Mtume kipokeeni na anachowakataza jiepusheni nacho. (59:7)

Kwa maneno mengine Isma ya Mitume haiwezi kuepukana kabisa na kusema kuwa kauli yao, kitendo na uthibittisho wao ni hoja na dalili. Baada ya Razi kusema katika tafsiri yake: Wameafikiana Waislamu kwamba kukosea katika kufikisha hakujuzu kwa kusudi au kusahau, aliendelea kusema: Wako watu wanaojuzisha hilo kwa kusahau. Sijui aliwakusudia watu gani.

3. Isma katika Fatwa; yaani Mtume kufutu kitu cha wote; kama kuharamisha riba na kuhalalisha biashara. Razi ametaja kifungu hiki katika tafsiri yake kwa kusema: Wameafikiana kwamba kukosea Mtume katika hilo hakujuzu kwa kukusudia ama kwa kusahau, wengine wamejuzisha na wengine hawakujuzisha. Kifungu hiki kinarudi katika kifungu cha pili cha kufikisha. Inatakikana kifanywe kifungu cha tatu ni Isma katika hukumu sio fatwa.16 Wameafikiana Imamiya kwamba Mtume ni mwenye kuhifadhiwa na makosa katika hukumu kama ilivyo katika kufikisha; pamoja na kwamba kwao wamenakili kutoka kwa Mtume mtukufu(s.a.w.w) kwamba yeye amesema:

*16 Tofauti ya hukumu na Fatwa ni kwamba maudhui ya hukumu yanakuwa ni mahsusi kama kadhi kuhukumu mapatano yaliyopita kati ya Zaid na Bakari ni batili. Ama maudhui ya Fatwa yanakuwa ni kwa wote kama kuhalalisha biashara na kuharamisha riba. Hakika mimi ninahukumu kati yenu kwa hoja (ushahidi) na yamini. Mimi ni mtu. Nyinyi mkiwa na ugomvi, huenda mmoja akawa mjanja kuliko adui yake - kwa hiyo nitahukumu kutokana na nilivyosikia kutoka kwake, basi kama mtu nikimpa haki ya ndugu yake asichukue; kwani ninamkatia kipande cha moto. Kama ni kosa hapo katika hukumu yake, imetokana na hoja au kiapo n.k. yaani katika kutegemea hukumu sio katika hakimu mwenyewe.

4. Isma katika vitendo vya Mitume na mwenendo wao hasa. Amesema Iji katika Mawaqif Juz.5; Hakika Hashawiya wanajuzisha kwa Mitume kufanya madhambi makubwa; kama uwongo, kwa makusudi au kusahau; na wamekataa Ashaira - yaani Sunni - kwa kusudi sio kusahau. Ama madhambi madogo inajuzu kwao hata kwa kusudi wachilia mbali kusahau.

Wamesema Imamiya: Hakika Mitume ni wenye kuhifadhiwa katika kila wanayoyasema na wanayoyatenda; kama vile ambavyo wamehifadhiwa katika itikadi na kufikisha. Ni muhali kwao kufanya madhambi madogo, wachilia mbali makubwa, na wala hayawezi kuwatokea kabisa, si kwa kukusudia wala kusahau, si kabla ya Utume wala baada yake. Aya yoyote ambayo haiafikiani dhahiri yake na msingi huu, basi wameiletea taawil.Wakasema katika Adam kula tunda, kwamba kukatazwa kule hakukua ni kwa uharamu au kwa ibada, kama vile kukatazwa kuzini na kuiba, bali kulikuwa ni kimwongozo na nasaha tu; kama kumwambia mtu unayemtakia heri, usinunue nguo hii kwa sababu sio nzuri, ikiwa hakukusikia, basi atakuwa hakufanya haramu wala hakumdhulumu mtu; atakuwa amejidhulumu yeye mwenyewe na amefanya jambo ambalo ilikuwa ni vizuri asilifanye.

Kimsingi kula tunda hakuambatani na kumdhulumu mtu yeyote isipokuwa kula tu. Kwa hivyo maana ya toba ya Adam inakuwa ni toba ya kuacha kutenda jambo lenye kupendekezwa na lililo bora. Na, jambo la toba ni jepesi sana, kwani mara nyingi Mitume na watu wema hulikariri neno Namtaka msamaha Mwenyezi Mungu na ninatubia. Inatosha kuwa ni dalili juu ya hilo dua ya Imam Zainul-Abidin katika Sahifa Sajjadiyya yenye kujulikana kwa dua ya toba akisema: Ninaomba msamaha kutokana na ujinga wangu.

AHLUL- BAIT

Amesema Muhyiddini anayejulikana kwa jina Ibnul Arabi katika kitabu chake Futuhatul Makkiya Juz. 1;Uk. 196 chapa ya zamani. Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemtoharisha Mtume wake na kizazi chake kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

﴿ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ﴾

...Mwenyezi Mungu anawatakia kuwaondolea uchafu enyi watu wa nyumba (ya Mtume) na kuwatakasa kabisa. (33:33)

Hakuna kitu kichafu zaidi ya dhambi kwa hivyo hakutegemewi kwa watu wa nyumba (ya Mtume) isipokuwa usafi na utohara, bali wao ni dhati ya utohara. Kisha akasema Ibnul Arabi kwamba Salmanul Farisi ni mwenye kuhifadhiwa na dhambi kwa ushahidi wa Mwenyezi Mungu, na imethibiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwamba yeye amesema: Salman ni katika sisi Ahlul Bait. Kwa hiyo Salman ni mwenye kuhifadhiwa na dhambi kwa ushahidi wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Katika juzuu ya pili ya kitabu hicho hicho Uk. 127, amesema: Hatabaki katika moto mwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika waliotumwa na Mwenyezi Mungu, kwa sababu moto kwao unakuwa ni baridi na salama kwa baraka ya Ahlul Bait katika akhera. Ni utukufu ulioje wa baraka za Ahlul Bait!

﴿ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اذْكُرُوا نِعْمَتِيَ الَّتِي أَنْعَمْتُ عَلَيْكُمْ وَأَوْفُوا بِعَهْدِي أُوفِ بِعَهْدِكُمْ وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ﴾

40.Enyi wana wa Israil! Kumbukeni neema yangu niliyowaneemesha; na tekelezeni ahadi yangu nitatekeleza ahadi yenu; na niogopeni Mimi tu.

﴿ وَآمِنُوا بِمَا أَنزَلْتُ مُصَدِّقًا لِّمَا مَعَكُمْ وَلَا تَكُونُوا أَوَّلَ كَافِرٍ بِهِ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي ثَمَنًا قَلِيلًا وَإِيَّايَ فَاتَّقُونِ﴾

41.Na aminini niliyoyateremsha ambayo yanasadikisha mliyonayo wala msiwe wa kwanza kuyakataa, wala msiuze ishara zangu kwa thamani ndogo; na niogopeni Mimi tu.

﴿ وَلَا تَلْبِسُوا الْحَقَّ بِالْبَاطِلِ وَتَكْتُمُوا الْحَقَّ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴾

42. Wala msichanganye haki na batili, na mkaficha haki na hali mnajua.

﴿ وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَارْكَعُوا مَعَ الرَّاكِعِينَ ﴾

43.Na simamisheni swala na toeni zaka na inameni pamoja na wanaoinama.

﴿ أَتَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبِرِّ وَتَنسَوْنَ أَنفُسَكُمْ وَأَنتُمْ تَتْلُونَ الْكِتَابَ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴾

44.Je, mnawaamrisha watu kutenda mema na mnajisahau, hali mnasoma Kitabu? Basi je,hamfahamu?

﴿ أَتَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبِرِّ وَتَنسَوْنَ أَنفُسَكُمْ وَأَنتُمْ تَتْلُونَ الْكِتَابَ أَفَلَا تَعْقِلُونَ﴾

45.Na takeni msaada kwa kusubiri na kwa kuswali na kwa hakika jambo hilo ni gumu isipokuwa kwa wanyenyekevu.

﴿ الَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَاقُو رَبِّهِمْ وَأَنَّهُمْ إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ﴾

46.Ambao wana yakini kwamba wao watakutana na Mola wao na kwamba watarejea Kwake.

ZIKUMBUKENI NEEMA ZANGU

Aya 40 - 46

Mwenyezi Mungu amewataja Mayahudi katika Aya nyingi za Quran tukufu.Zimebainisha Aya hizo neema za Mwenyezi Mungu na kuua kwao Mitume bila ya haki. Vile vile zimebainisha uadui wao kwa Musa na Harun(a.s.) , kuabudu kwao ndama na kufanywa watumwa na Mafirauni, kisha kukombolewa. Vile vile Aya zimeeleza walivyookoka wasife maji na kuteremshiwa Manna na Salwa. Pia zimeelezea chuki yao hao Mayahudi kwa Mtume Muhammad(s.a.w.w) , au njama zao dhidi yake na uadui wao mkubwa kwa Waislamu, kuchukia kwao haki na mengineyo ambayo yatakuja maelezo yake kwa ufafanuzi. Surah ya Ngombe, waliyemchinja, hii inaelezea kwa upana sifa na matendo yao.

DHAHIRI YA MAISHA

Aina nyingi za hali ya maisha wanayoishi watu ni natija ya Historia ndefu. Aina ya mavazi tunayovaa, mapishi ya chakula tunachokila na ujenzi wa nyumba tunazokaa, vyote hivi ni kutokana na usanifu wa waliotangulia. Hata meli zinazotumia mashine zimeundwa baada ya majahazi yanayotumia matanga,baada ya kupita vipindi vya maendeleo. Hakika maigizo ya kihistoria yanafanya kazi kama desturi za kitabia; sawa na mawimbi yanayotulia kutokana na msukosuko wa kupwa maji na kujaa. Kwa hivyo matukio yanayotumika katika maisha yetu ya kila siku na mfungamano tunaokuwa nao na watu wengine, mbaya au mzuri, ni natija ya yaliyopita zamani sana au hivi karibuni.

Hapa ndipo wanafalsafa wakasema: Historia ni miongoni mwa njia za maarifa. Na Aya hizi ambazo Mwenyezi Mungu anawazungumzia Mayahudi, zina mfungamano mkubwa na Historia yao, kama tutakavyoona.

ISRAIL

Israil: ni jina jingine la Yaqub bin Is-haq bin Ibrahim(a.s.) , Khalilullah. Ishaq ni ndugu wa Ismail, babuye Mtume Muhammad(s.a.w.w) . Waarabu na Wayahudi wote wamekutana kwa Ibrahim. Mwenyezi Mungu amesema:

﴿ مِّلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ﴾

Mila ya baba yenu Ibrahim (22:78).

Katika Majmaul-Bayan imesemwa kwamba: Waarabu wote ni uzao wa Ismail; na wengi wasiokuwa Waarabu ni uzao wa Is-haq. Maana ya Israil katika lugha ya Kiebrania ni Abdullah (mja wa Mungu), Isra: ni mja, il: ni Mwenyezi Mungu. Alitumia upole Mwenyezi Mungu katika kuwazungumzia Wayahudi kwa kuwategemeza na Mtume mtukufu Israil ili kuwakumbusha nasaba hii tukufu. Huenda wakahisi utukufu ikiwa umo ndani ya nafsi zao; sawa na kusema: Ewe mtoto wa watu wema! Kuwa kama baba zako na babu zako. Ama sababu ya kuitwa kwao Yahudi ni kwamba ukoo mmoja kati yao unatokana na Yahudha ambaye ni mtoto wa nne wa Nabii Yaqub. Sehemu ifuatayo tutaeleza kwa muhtasari historia ya Mayahudi kutokana na Aya tuliyonayo.

HISTORIA YA MAYAHUDI

Yatakuja maelezo katika Sura ya Yusuf kwamba Mtume Yaqub(a.s) alihama na watoto wake kutoka Palestina kwenda Misri alipo mtoto wake Yusuf(a.s) akiwa waziri wa Firaun wakati huo. Firaun akawakatia kipande cha ardhi yenye rutuba kwa heshima ya Yusuf. Kikaendelea kizazi cha Yakub kwa muda kiasi. Lakini Mafiraun waliokuja baadaye waliwakandamiza na kuwapa adhabu na mateso; waliwachinja watoto wao wa kiume wakawaacha wa kike; na wakawafanya watumwa. Kisha Mwenyezi Mungu akawapelekea Mtume aliyekuwa mmoja wao ambaye ni Musa bin Imran, kuwak-omboa na dhulma na utumwa; akawataka warudi Palestina kupigana na akawaahidi ushindi. Wakakataa kwa woga. Mwenyezi Mungu akawapangia kutangatanga katika jangwa la Sinai miaka arobaini. Utakuja ufafanuzi Inshallah.

Katika kipindi hiki Harun alikufa kisha Musa pia akafa. Akachukua uongozi mpwawe Yashua bin Nun. Ilipofika karne ya 13 kabla ya kuzaliwa Nabii Isa(a.s) walivamia ardhi ya Palestina wakiongozwa na Yoshua wakawafukuza wenyeji; kama kilivyofanya kizazi chao (Wazayuni) katika Palestina mwaka 1948.17 Baada ya Yoshua Mwenyezi Mungu alituma mitume wengi waliotokana na wao.

* 17 Tutaje mifano miwili: kwanza, Wazayuni waliwakusanya wanawake 25 wenye mimba katika kijiji cha Dair Yasin, wakawapasua matumbo yao kwa mabisu na mikuki. Pili, waliwakusanya watu wa kijii cha Zaituni msikitini, kisha wakawalipua kwa baruti. Mnamo mwaka 596 kabla kuzaliwa Nabii Isa(a.s) , Mfalme wa Babil Nebukadnezzar aliwashambulia akaondoa utawala wao katika Palestina, akawachinja wengi na kuwachukua mateka wengi. Wakaendelea kuwa chini ya utawala wa Nebukadnezzar mpaka mwaka 538 kabla ya kuzaliwa Isa(a.s) aliposhindwa na mfalme wa Fursi (Iran ya sasa), ndipo Mayahudi wakapumua. Wakaendelea kuwa chini ya utawala wa Fursi kiasi cha miaka mia mbili, baadaye wakatawaliwa na makhalifa wa Alexandria mkuu. Kisha wakawa chini ya utawala wa Roma.

Ilipofika mwaka 135 kabla ya kuzaliwa Isa(a.s) , Mayahudi walifanya mapinduzi kwa Warumi, lakini hayakufanikiwa. Walifukuzwa Palestina, wakakimbilia sehemu mbali mbali za mashariki na magharibi; wengine Misri na wengine Lebanon na Syria, wengine wakaenda Iraq na wengine Hijaz. Ama Yemen walikujua Mayahudi na kuhamia huko kwa ajili ya biashara tangu zama za Nabii Suleiman ambaye alimwoa Malkia wa Yemen, Bilqis (Malkia wa Sheba).

Neema za Mwenyezi Mungu kwao ambazo Mwenyezi Mungu amezitaja kwa kauli yake; Zikumbukeni neema Zangu nilizowaneemesha, ni nyingi; zikiwa ni pamoja na kuwachagua Mitume kutoka katika kabila lao; kama Musa, Harun, Yoshua, Daud, Suleiman, Ayub, Uzair, Zakaria, Yahya n.k. Ama Maryam, mama yake Isa pia ni Mwisrail, nasaba yake inaishia kwa Nabii Daud(a.s) , lakini Mayahudi hawamkubali Masih mwana wa Maryam na wanadai kwamba Masih aliyetajwa katika Tawrat hajakuja bado.

MUHAMMAD NA MAYAHUDI WA MADINA

Mtume(s.a.w.w) alipohamia Madina kutoka Makka, Mayahudi walikuwa na koo tatu: Bani Qaynuqa, Bani Quraydha na Bani Nadhir. Walikuwa wana vilabu vya pombe, madanguro na sehemu za kufugia nguruwe. Na walikuwa wakihodhi dhahabu na fedha, kutengeneza silaha na kufanya biashara ya riba. Kwa ujumla wao ndio waliokuwa wakuu katika mambo ya uchumi mjini Madina, kama walivyo sasa (duniani).

Alipofika Mtume(s.a.w.w) , Mayahudi walihisi hatari kwa faida zao na mapa to yao ya kibiashara, kwa sababu vijana wa Madina wasingekwenda kwenye maduka na mabucha yao na watu wa Madina wasingekula nyama za nguruwe. Maana yake ni kwamba mayahudi wangepoteza vitega uchumi vyote. Kwa ajili hiyo wakawa wanamchimbia vitimbi Mtume mtukufu(s.a.w.w) na kupanga njama pamoja na makafiri dhidi ya Waislamu, kama zinavyofanya leo nguvu za dola kubwa zinavyolinda maslahi yake.

Mtume naye ni kama aliyejua hilo pale alipoingia Madina, akataka kuwatafutia hoja na kuwaadhibu kwa kauli zao. Kwa hiyo akawachukulia upole, akawekeana nao mkataba: kwamba wao wana uhuru katika dini yao na Mahekalu yao kwa masharti ya kuwa wasimsaidie adui na kama wakiamua kupigana pamoja na Waislamu, basi watapata fungu katika ngawira. Ni juu yao kushirikiana na Waislamu, kuulinda mji wa Madina, kwa sababu mji ni wa wote sio wa kundi maalum.Lakini walivunja ahadi upesi sana.Tangu lini ahadi ikasimama mbele ya maslahi? Je inaingia akilini usalama na hadaa kuwa pamoja? Vipi anaweza kuishi mbwa mwitu pamoja na punda kwa amani? Kutafaa nini kukumbushwa neema, hadhari na nasaha kama zikigongana na maslahi ya kiutu na mapatano ya kibiashara?

Imeelezwa katika kitabu Muhammad Rasullul-huriyya (Muhammad Mtume wa Uhuru) hivi: Mtume aliwaambia wafanyabiashara wa Kiislamu waanzishe soko jipya mjini Madina, wakaanzisha; likawa na nguvu soko hilo; wafanyi biashara wageni wakawa wanaelekea huko, na soko la Mayahudi likaathirika. Kwa sababu biashara katika soko la waislamu ilikuwa ya uadilifu sana kwa muuzaji na mteja. Hiyo peke yake ilitosha kujaza nyoyo za Mayahudi hasadi na chuki kwa Muhammad(s.a.w.w) na kuwafanya wavunje ahadi.

MAELEZO

Mwenyezi Mungu ameanza kuwaambia Mayahudi kukumbuka neema zake kwao.Miongoni mwa hizo neema ni kuwaletea Mitume wengi na kuwatukuza kwa Tawrat na Zabur. Vile vile kuwakomboa katika utumwa wa Firaun, kuokoka kwao kutokana na kufa maji, kuwateremshia Manna na Salwa, kuwapa milki na ufalme katika zama za Mtume Suleiman na mengineyo ambayo yanawajibisha kuamini na kushukuru na wala sio kukanusha na kukufuru. Unaweza kuuliza: Kwa nini msemo unawaelekea Mayahudi wa Madina pamoja na kujua kuwa neema zinazoelezwa zilikuwa kwa baba zao na sio kwao? Jibu: Neema kwa baba ni neema kwa watoto vile vile; ambapo mtoto anapata utukufu kutokana na baba yake. Zaidi ya hayo ni kwamba umma wote ni mmoja.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwakumbusha neema zake aliwaambia: Tekelezeni ahadi yangu nitatekeleza ahadi yenu. Ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kuchukua yale yanayofahamiwa na maumbile na yale ambayo vimeteremshwa vitabu kwayo, ikiwa ni pamoja na kumwamini Mwenyezi Mungu na Mitume yake na kufanya amali kwa hukmu zake. Mwenye Majmaul-Bayan anasema: Hakika Mwenyezi Mungu aliwaahidi katika Tawrat kwamba Yeye atawapelekea Mtume anayeitwa Muhammad. Fikra hii ndiyo wanayoielezea wafasiri wengi nayo ndiyo inayotolewa ushahidi na Quran. Ama ahadi ya Mayahudi ni ile ahadi ya Mwenyezi Mungu kwao. Na,kila mwenye kuamini akafanya amali njema basi Mwenyezi Mungu atamlipa thawabu siku ya Kiyama.

Imesemekana maana yake ni kwamba kama wakimcha Mwenyezi Mungu, basi atawainua katika maisha haya ya duniani.Tutaeleza fikra ya malipo katika dunia mahali pake Inshaallah. Kisha Mwenyezi Mungu amewaamrisha kuamini Quran na wasifanye haraka kuikanusha, kumkanusha Muhammad na kutaka maslahi tu. Na kwamba ni juu yao kuisimamisha swala na kutoa zaka ili wazitakase nafsi na mali zao.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu: Je, mnawaamrisha watu kutenda mema na mnajisahau, hali mnasoma kitabu, inawaelekea viongozi na wakubwa, sio kwa watu wote, kwa sababu watu wengine ni wafuasi, na viongozi ndio wenye kufuatwa. Wao ndio wanaoficha haki na hali wanaijua na wanatoa mawaidha lakini hawayafuati. Tunakariri tena kwamba mawaidha na nasaha haziendi pamoja na kutaka maslahi; na hayawezi kuacha athari yoyote isipokuwa katika nafsi isiyotaka maslahi na isiyokuwa na lengo lolote zaidi ya haki.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Na takeni msaada kwa kusubiri na kwa kuswali Imeelezwa tena katika Aya ya 153 ya Sura hii, kwa hivyo utakuja ufafanuzi wake huko Inshallah. Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Kwanza 2 Sura Al-Baqara


7

8

9

10

11

12

13

14

15