TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI Juzuu 2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 19034
Pakua: 2869


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 19034 / Pakua: 2869
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI Juzuu 2

Mwandishi:
Swahili

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿ يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَإِثْمُهُمَا أَكْبَرُ مِن نَّفْعِهِمَا وَيَسْأَلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَ قُلِ الْعَفْوَ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ تَتَفَكَّرُونَ ﴾

219.Wanakuuliza kuhusu ulevi na kamari. Sema: Katika hivyo mna madhara makubwa na manufaa kwa watu, na madhara yake ni makubwa zaidi kuliko manufaa yake. Na wanakuuliza watoe nini? Sema: Vilivyowazidia. Namna hii Mwenyezi Mungu anawabainishia Aya mpate kufikiri.

﴿ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْيَتَامَىٰ قُلْ إِصْلَاحٌ لَّهُمْ خَيْرٌ وَإِن تُخَالِطُوهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ الْمُفْسِدَ مِنَ الْمُصْلِحِ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَأَعْنَتَكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾

220.Katika dunia na akhera. Na wanakuuliza kuhusu mayatima. Sema: Kuwatengenezea ndiyo heri. Na kama mkichanganyika nao, basi ni ndugu zenu. Na Mwenyezi Mungu anamjua fisadi na mtengenezaji. Na kama angelitaka Mwenyezi Mungu angeliwatia katika dhiki. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu,Mwenye hekima.

ULEVI NA KAMARI

Aya 219 – 220

LUGHA

Limetumiwa neno Khamri, lenye maana ya kufunika, kwa maana ya ulevi, kwa sababu ulevi unafunika akili. Na limetumiwa neno Maysir, lenye maana ya wepesi, kwa maana ya kamari, kwa sababu chumo la kamari linakuwa jepesi bila ya jasho.

MAANA

Wanakuuliza kuhusu ulevi na kamari.

Waliuliza baadhi ya Waislamu kuhusu hukumu ya ulevi na kamari katika Madina; yaani zaidi ya miaka 13 tangu ulipoanza mwito wa Kiislamu. Hiyo inafahamisha kuwa hukumu ya pombe ilikuwa imenyamaziwa muda mrefu, kama zilivyonyamaziwa baadhi ya hukumu za haramu mpaka wakati wake maalum, kulingana na masilahi. Mara nyingine kubainisha hukumu kunataka hekima ya kuchukulia mambo pole pole. Inasemekana kuwa ubainifu wa hukumu ya pombe ulikuwa hivi, kwa sababu Waislamu walikuwa wameizoweya wakati wa Ujahiliya (kabla ya kuja Uislamu); lau wangelizuiliwa mara moja tu, ingelikuwa uzito kwao. Bali Mwenyezi Mungu aliwakumbusha Waislamu walipokuwa Makka kwamba katika jumla ya neema zake ni kwamba wao wanafanya ulevi na kupata riziki kutokana na tende na zabibu. Anasema Mwenyezi Mungu:

﴿ وَمِن ثَمَرَاتِ النَّخِيلِ وَالْأَعْنَابِ تَتَّخِذُونَ مِنْهُ سَكَرًا وَرِزْقًا حَسَنًا﴾

"Na kutokana na matunda ya mitende na mizabibu mnatengeneza ulevi na riziki nzuri..." (16:67)

Waliuliza baadhi ya Waislamu kuhusu hukumu ya pombe na kamari, Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake kuwajibu: Katika hivyo madhara makubwa na manufaa kwa watu na madhara yake ni makubwa zaidi kuliko manufaa yake. Jawabu hili peke yake halitoshi kuwa ni dalili ya uharamu wa ulevi. Kwa sababu hakusema kuwa ni haramu; linafahamisha kawaida ya kujikinga na madhara ni bora kuliko maslahi, na muhimu inatanguliwa na muhimu zaidi. Lakini tukiangalia Aya isemayo:

﴿ قُلْ إِنَّمَا حَرَّمَ رَبِّيَ الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ وَالْإِثْمَ وَالْبَغْيَ بِغَيْرِ الْحَقِّ﴾

"Sema: Mola wangu ameharimisha mambo maovu yaliyodhihirika na yaliyofichika na madhara na uasi pasipo haki..." (7:33)

Tukiiunganisha Aya hiyo na hii tunayoizungumzia tutapata dalili ya kuharimishwa ulevi waziwazi na kwa mkato. Kwa sababu natija inayopatikana ni kuwa ulevi ni madhara na madhara ni haramu, kwa hivyo ulevi ni haramu.

Hiyo ni pamoja na kuongezea Aya inayosema:

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾ إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ﴾

"Enyi mlioamini! Hakika ulevi na kamari na masanamu na mishale ya kutizamia (ramli) ni uchafu katika kazi ya Shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufaulu. Hakika Shetani anataka kuwatilia uadui na bughudha baina yenu kwa ulevi na kamari kuwazuilia na kumkumbuka Mwenyezi Mungu na Kuswali. Basi je, mtaacha?" (5:90 - 91)

Kwa hiyo kusema jiepusheni navyo ni amri ya kujiepusha, na amri inafahamisha wajibu. Na kusema basi je mtaacha! Ni kukataza, na kukataza kunafahamisha uharamu. Ndipo Waislamu waliposikia Aya hii wakasema: "Tumeacha."Ama ile Aya inayosema:

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْرَبُوا الصَّلَاةَ وَأَنتُمْ سُكَارَىٰ﴾

"Enyi mlioamini msiikurubie swala hali mmelewa..." (4:43)

ilishuka kabla ya Aya (5:90-91), ambazo zina uzito mkubwa. Tumeeleza kwamba huenda ilikuwa ni hekima ya kuchukulia mambo pole pole katika kubainisha uharamu, kwa vile kutoikurubia swala hali mme-lewa haina dalili yoyote ya kuonyesha uhalali wa pombe katika isiyokuwa swala. Tutafafanua Inshaallah tutakapofikia Aya hizo.

Zaidi ya hayo Waislamu wote tangu mwanzo hadi hivi leo wamekongamana kwa kauli moja tu! Kuwa ulevi ni katika madhambi makubwa, na kwamba mwenye kuuhalalisha siye Mwislamu. Na mwenye kuinywa kwa kupuuza ni fasiki na atapigwa (Had) viboko themanini. Imekuja Hadith Mutawatir kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba amelaaniwa mwenye kupanda mti wa (hiyo pombe), mwenye kuigema, mwuzaji, mnunuzi, mwenye kuhudumia wanywaji na mnywaji. Na imeelezwa katika baadhi ya hadith kwamba hakuna sharia yoyote ya mbinguni ila imekataza ulevi. Tumeyaeleza kwa ufafanuzi zaidi maudhui haya katika juzuu ya nne ya kitabu: Fiqhul Imam Jaffar Sadiq katika mlango wa vyakula na vinywaji.

Na madhara yake ni makubwa zaidi kuliko manufaa yake.

Makusudio ya ithm hapa ni madhara. Madhara ya pombe yanadhihirika katika mwili, akili na mali na vile vile kuacha kumkumbuka Mwenyezi Mungu, kugom-bana na kufanya mambo yaliyoharamishwa.Wanahistoria wanasema kwamba baadhi ya walevi walizini na mabinti zao. Abbas bin Mirdas, alikuwa kiongozi wa watu wake, katika zama za Jahiliya (kabla ya Uislamu) alijiharimishia pombe yeye mwenye tu kwa maumbile yake. Alipoulizwa sababu, akasema: "Siwezi kuchukua ujinga kwa mkono wangu nijiingize mwenyewe, wala siko radhi asubuhi niwe bwana mkubwa wa watu na jioni niwe mpuzi wao." Daktari mmoja mashuhuri wa Kijerumani alisema: "Fungeni nusu ya mabaa na mimi ninawadhaminia kuwa hamtahitajia nusu ya zahanati na mahospitali na majela."

Ama kamari inaleta uadui na chuki na inazuia kutajwa Mwenyezi Mungu; kama ilivyoonyesha Aya tukufu, inaharibu tabia kwa kuzoeya uvivu na kutafuta riziki kwa ndoto tu! Pia inavunja majumba na inamtia mtu kwenye umasikini ndani ya saa moja tu. Inatosha kuwa haramu kamari, kule kuchukua mali bure bure tu.

Na wanakuuliza watoe nini? Sema: Vilivyowazidia.

Yaani: Toeni vilivyozidi haja zenu na za familia yenu. Amri ya kutoa hapa ni ya suna sio ya wajibu, isipokuwa inakuwa wajibu kutoa kama zikithibiti sharti za khumsi na zaka. Tutaelezea kwa ufafanuzi, Inshaallah.

Aya hii ni kama Aya isemayo:

﴿ وَلَا تَجْعَلْ يَدَكَ مَغْلُولَةً إِلَىٰ عُنُقِكَ وَلَا تَبْسُطْهَا كُلَّ الْبَسْطِ فَتَقْعُدَ مَلُومًا مَّحْسُورًا ﴾

"Wala usifanye mkono wako ni wenye kufungwa shingoni mwako, wala usiukunjue ovyo ovyo utakuwa ni mwenye kulaumiwa mwenye kufilisika." (17:29)

Imeelezwa katika Hadith kwamba mtu mmoja alikwenda kwa Mtume(s.a.w.w) na kibonge cha dhahabu kama yai, akamwambia Mtume: "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu chukua hii ni sadaka Wallah sina chochote zaidi ya hiyo." Mtume akaachana naye; kisha akamfuata tena na kurudia kumwambia, kisha Mtume akakichukua na kumrudishia mwenyewe akisema: "Mtu ananijia na mali yake naye hana kitu kingine chochote; kisha aombe watu! Hakika sadaka inatokana na kujitosha; chukua mwenyewe hatuna haja nayo." Iko Hadith pia kwamba Mtume(s.a.w.w) alikuwa akiiwekea familia yake matumizi ya mwaka mzima.

Namna hii anawabainishia Mwenyezi Mungu Aya mpate kufikiri katika dunia na akhera.

Yaani Mwenyezi Mungu anawabainishia hukumu yake katika pombe na kamari, na hukumu yake katika vile ambavyo tunatakikana kuvitoa sadaka katika mali zetu kwa misingi ya maslahi yetu. Yeye haamrishi isipokuwa lile ambalo lina maslahi ya kidunia na askhera, na wala hakatazi isipokuwa lile lenye uharibifu.

Yatupasa kuuzingatia na kuuchunga uhakika huu tusimwasi Mwenyezi Mungu katika jambo lolote miongoni mwa amri na makatazo yake. Kwa hivyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu:"Mpate kufikiri katika dunia na akhera" ni kwamba tufanye amali kwa ajili ya zote mbili (dunia na akhera) bila ya kuacha moja.

Na wanakuuliza kuhusu mayatima.

Wakati wa ujahilia (kabla ya Uislamu) watu walizowea sana kunufaika na mali za mayatima; pengine mtu aliweza kumwoa yatima au kumwoza mtoto wake kwa tamaa ya mali yake tu. Ulipokuja Uislamu, Mwenyezi Mungu alimterem-shia Mtume wake Aya hizi:

﴿ إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا﴾

"Hakika wale ambao wanakula mali ya mayatima kwa dhulma, hakika wanakula moto matumboni mwao..." (4:10)

﴿ وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ﴾

"Wala msikaribie mali ya yatima isipokuwa kwa njia ya wema kabisa..."( 6:152)

Basi ziliposhuka Aya hizo waliacha kuchanganyika na kuwasimamia mayatima. Hapo maslahi yao yakaharibika na maisha yao yakawa mabaya. Ndipo baadhi ya Waislamu wakauliza kuhusu hali hiyo. Likaja jawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu:

Sema: Kuwatengenezea, ndio heri.

Maana yake msijizuilie na kuchanganyika na mayatima na kuzikurubia mali zao, kama mnataka kuwatengenezea uzuri katika malezi yao, adabu zao na kusimamia mali zao. Bali hilo lina malipo na thawabu. Lenye kuharamishwa ni kuzifuja na kuzila mali zao.

Na kama mkichanganyika nao basi ni ndugu zenu.

Kundi la wafasiri limesema: "Hii ni idhini kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa anayesimamia yatima kumshirikisha pamoja na familia yake katika kula na kunywa ikiwa hilo ni sahali kwa msimamizi na achukue kutoka katika mali ya yatima kiasi kile cha malezi.

Na Mwenyezi Mungu anamjua fisadi na mtengezaji.

Fisadi ni yule anayesimamia yatima ili afuje mali zake: Na mtengezaji ni yule anayesimamia mali ya yatima kwa maslahi ya yatima kwa dhati. Kwa hivyo kauli yake hiyo Mwenyezi Mungu ni kemeo kwa mwenye kutaka kufuja na kufanya ufisadi.

Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka angeliwatia katika dhiki.

Makusudio hapa ni kwamba Mwenyezi Mungu amehalalisha kuchanganyika yatima na familia ya msimamizi na kuchukua katika mali ya yatima thamani ya kile alichompatia posho, ili yasipatikane mashaka na uzito. Kwa sababu Mwenyezi Mungu anawatakia watu wepesi wala hawatakii uzito. Hapa inaonyesha kuwa si lazima kuwe na usawa wa kutopungua hata kidogo kati ya kile alichokula yatima pamoja na familia ya msimamizi na kile atakachochukua badali kutoka katika mali ya yatima. Kwani Mwenyezi Mungu (s.w.t.) husamehe tofauti ndogo isiyoepukika, bali msimamizi anaweza hata kula katika mali kwa wema akiwa fukara. Hayo ni kwa kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿ وَمَن كَانَ غَنِيًّا فَلْيَسْتَعْفِفْ وَمَن كَانَ فَقِيرًا فَلْيَأْكُلْ بِالْمَعْرُوفِ﴾

"...Na mwenye kuwa tajiri basi ajiepushe, na atakayekuwa mhitaji basi ale kwa kadri ya ada. (4:6)

﴿ وَلَا تَنكِحُوا الْمُشْرِكَاتِ حَتَّىٰ يُؤْمِنَّ وَلَأَمَةٌ مُّؤْمِنَةٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكَةٍ وَلَوْ أَعْجَبَتْكُمْ وَلَا تُنكِحُوا الْمُشْرِكِينَ حَتَّىٰ يُؤْمِنُوا وَلَعَبْدٌ مُّؤْمِنٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكٍ وَلَوْ أَعْجَبَكُمْ أُولَـٰئِكَ يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ وَاللَّـهُ يَدْعُو إِلَى الْجَنَّةِ وَالْمَغْفِرَةِ بِإِذْنِهِ وَيُبَيِّنُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴾

221.Wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini. Na mjakazi muumini ni bora kuliko mshirikina hata akiwa-pendeza. Wala msiwaoze wanaume washirikina mpaka waamini. Na mtumwa muumini ni bora kuliko mshirikina hata akiwapendeza. Hao wanaita kwenye Moto, na Mwenyezi Mungu anaita kwenye Pepo na maghufira, kwa idhini Yake. Naye hubainisha Aya Zake kwa watu ili wapate kukumbuka.

MSIWAOE WANAOMSHIRIKISHA MWENYEZI MUNGU

Aya 221

MAANA

Aya hizi ni miongoni mwa Aya za hukumu, na zinaingia katika mlango wa ndoa. Kabla ya kuingilia madhumuni ya Aya, kwanza tutajaribu kufasiri neno. Nikah, Mushrikina, Amah, Neno: (Nikaha) lina maana mbili: Kufunga ndoa na kumwingilia mwanamke. Neno: Mushrikina (washirikina) imesemekana kuwa ni kila asiyeamini utume wa Muhammad(s.a.w.w) . Kwa kauli hii watakuwa wanaingia watu wa Kitabu ambao ni Mayahudi, na Wakristo. Na inasemekana kuwa Qur'an haikusudii watu wa Kitabu, japo wanasema kuwa Issa ni Mwana wa Mungu na utatu wa Mungu. waliosema haya wametoa dalili kwa Aya hizi:

﴿ مَّا يَوَدُّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَلَا الْمُشْرِكِينَ﴾

"Hawapendi waliokufuru miongoni mwa watu wa Kitabu wala washirikina..." ( 2:105)

﴿ لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ ﴾

"Hawakuwa, wale ambao wamekufuru katika watu wa Kitabu na washiririkina..." (98:1)

Katika Aya hizo kuna viunganishi kati ya watu wa kitabu na washirikina, na kiunganishi kinafahamisha tofauti. Kwa sababu kitu hakiwezi kuunganishwa na kitu hicho hicho.

Neno: Amah (mjakazi) na Abd linatumiwa kwa mtumwa na hata aliyehuru. Unaweza kumwambia aliyehuru: "Ewe mjakazi wa Mwenyezi Mungu," vile vile mtumwa kwa sababu binadamu wote ni watumwa wa Mwenyezi Mungu. Maana ya Aya ni kuwa enyi Waislamu msioane na washirikina, bali oaneni na wanaotokana nanyi hata kama sio bora kama washirikina kwa umbo na tabia au kwa jaha na mali. Hao wanaiita kwenye moto. Yaani hao washiikina. hikima ya kukataza kuoana ni hiyo ya mwito wa motoni, na kwamba muungano wa kuiondoa unapelekea uharibifu wa itikaTafsir di na dini. Kwa ufupi unapelekea ufasiki na kupuuzwa hukumu ya Mwenyezi Mungu. Tunashuhudia hivi leo vijana wetu wengi wako katika hali mbaya kuliko makafiri na washirikina, kutokana na kudharau kwao, kuipuuza dini na kujivua kabisa katika athari za dini. Wanawalea watoto wao malezi yasiyokuwa ya dini wala ya tabia njema. Lau sikuwa walishuhudia kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja na Muhammad ni Mtume wake, basi tungeliwafanyia muamala wa walahidi na washirikina.

Lakini kwa sababu ya tamko hili tu (la shahada), ndilo limehifadhi damu, mali na kusihi kuoana na kurithiana nao hata kama haya yanatokana na njia za taqlid na kurithi( [11] ).

Na Mwenyezi Mungu anaita kwenye pepo na maghufira.

Hapa kuna miito miwili:

• Mwito wa kwanza: Ni wa wanaoshirikisha - kufanya yale yanayoingiza motoni na kwenye ghadhabu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.)

• Mwito wa pili: Ni wa Mwenyezi Mungu - kufanya yanayoleta maghufira na kuingia peponi. Miongoni mwa hayo ni kuoa mwenye kuamini na wala sio mwenye kushirikisha. Hapana mwenye shaka kwamba wanaoamini ndio wanaoitika mwito wa Mwenyezi Mungu na wanapata maghufira yake na hatimae kuingia pepo Yake kwa idhini Yake; yaani kwa uongofu na tawfiki yake.

KUOA MWENYE KITABU (AHLUL-KITAB)

Wameafikiana Waislamu kwamba haijuzu kwa Mwislamu kuoa au kuolewa na asiyekuwa na kitabu; kama vile kuoa wale wanaoabudu masanamu, jua na moto, n.k. kwa ufasaha zaidi yule asiyeamini.

Vile vile haijuzu kumuoa au kuolewa na Majusi, hata kama imesemwa Majusi ni shabihi ya wenye kitabu. Wameafikiana madhehebu manne ya Ahli Sunna juu ya kusihi kumuoa mwenye kitabu, na wamehitalifiana Mafaqihi wa Kishia. Wengi wao wamesema kuwa haijuzu kwa Mwislamu kumuoa Yahudi au Mkristo. Na wengine wamesema inajuzu. Miongoni mwa Ulamaa wakubwa waliosema hivyo ni Sheikh Muhammad Hassan katika Jawahir, shahidi wa Pili katika Masalik na Sayyid Abul Hassan katika Wasilah, wamesema inajuzu. Na sisi tuko pamoja na rai hii kwa dalili hizi:

1. Dalili zinazohalalisha ndoa zimemtoa Mwislamu mwanamume kumwoa Mshirikina, na Mwislamu mwanamke kuolewa na mshirikina na mwenye kitabu. Kwa hivyo inafahamisha kuwa wasiokuwa hao inajuzukuoa.

2 Kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿الْيَوْمَ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ وَطَعَامُ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ حِلٌّ لَّكُمْ وَطَعَامُكُمْ حِلٌّ لَّهُمْ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الْمُؤْمِنَاتِ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ ﴾

"Leo mmehalalishiwa kula vilivyo vizuri na chakula cha wale waliopewa kitabu ni halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao na wanawake wasafi waumini na wanawake wasafi katika wale waliopewa kitabu kabla yenu..." (5:5)

Kuhusu kauli yake Mwenyezi Mungu:Wala msiwaweke wanawake makafiri katika kifungo cha ndoa (zenu), makusudio ya makafiri hapo ni washirikina sio wenye Kitabu. Kwa sababu Aya iliwashukia wanawake waliosilimu na kuhama na Mtume wakiwaacha waume zao washirikina; na mfumo mzima wa Aya unafahamisha hivyo. Aya yenyewe ni hii:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا جَاءَكُمُ الْمُؤْمِنَاتُ مُهَاجِرَاتٍ فَامْتَحِنُوهُنَّ اللَّـهُ أَعْلَمُ بِإِيمَانِهِنَّ فَإِنْ عَلِمْتُمُوهُنَّ مُؤْمِنَاتٍ فَلَا تَرْجِعُوهُنَّ إِلَى الْكُفَّارِ لَا هُنَّ حِلٌّ لَّهُمْ وَلَا هُمْ يَحِلُّونَ لَهُنَّ وَآتُوهُم مَّا أَنفَقُوا وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ أَن تَنكِحُوهُنَّ إِذَا آتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ وَلَا تُمْسِكُوا بِعِصَمِ الْكَوَافِرِ ﴾

"Enyi mlioamini! Watakapowajia wanawake walioamini wanaohama, basi wafanyieni mtihani; Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye zaidi imani yao. Mkiwajua ni waumini basi msiwarudishe kwa makafiri. Hawa si halali kwa hao (wanaume makafiri) wala wao (wanaume makafiri) si halali kwao. Na warudishieni (waume zao) (mahari) waliyotoa. Wala kwenu si vibaya kuwaoa ikiwa mtawapa mahari yao (hao wanawake) kwenu. Wala msiwaweke katika kifungo cha makafiri..." (60:10)

Pia ziko Hadith sahihi kutoka kwa Mtume (s.a.w.w.) katika kusihi kumuoa mwanamke katika wenye kitabu, na haya tumeyafafanua zaidi katika juzuu ya tano ya kitabu. Fiqhul Imam Jafar Sadiq. Mlango yaliyoharamu, kifungu cha kutofautiana dini

﴿وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْمَحِيضِ قُلْ هُوَ أَذًى فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي الْمَحِيضِ وَلَا تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطْهُرْنَ فَإِذَا تَطَهَّرْنَ فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللَّـهُ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ ﴾

222.Wanakuuliza kuhusu hedhi; waambie ni udhia. Basi jitengeni na wanawake wakati wa hedhi wala msiwakaribie mpaka watoharike. Wakisha toharika basi waendeni pale alipowaam-risha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubia na huwapenda wanaojitoharisha.

﴿ نِسَاؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُوا حَرْثَكُمْ أَنَّىٰ شِئْتُمْ وَقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّكُم مُّلَاقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ ﴾

223.Wake zenu ni mashamba yenu. Basi yaendeeni mashamba yenu mpendavyo, na tangulizieni nafsi zenu; na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba mtakutana Naye, na wape habari njema wenye kuamini.

HEDHI

Aya 222 - 223

MAANA

Baada ya kumuuliza Mtume mtukufu(s.a.w.w) kuhusu miezi mitakatifu, ulevi, kamari watakachotoa na mayatima; kisha walimuuliza kuhusu hedhi. Amesema Razi: "Imepokewa habari kuwa Mayahudi na Majusi walikuwa wakikaa mbali sana na wanawake wakati wa hedhi; Wakristo walikuwa wakiwaingilia bila ya kujali hedhi; na watu wa zama za Jahiliya (kabla ya Uislamu) walikuwa hawali, hawanywi, hawakai kitanda kimoja wala hawakai nyumba moja na mwanamke mwenye hedhi; kama walivyokuwa wakifanya Majusi na Mayahudi.

Wanakuuliza kuhusu hedhi; waambie ni udhia. Basi jitengeni na wanawake wakati wa hedhi.

Swali linahusu kuchanganyika na wanawake wakati wa hedhi, ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake mtukufu kuwajibu waulizaji kwamba: wajitenge na wanawake siku za hedhi; yaani wasiwaingilie. Imekuja Hadith inayosema;"Fanyeni kila kitu isipokuwa kuingilia tu." Makusudio ya neno 'Adha' (udhia) ni madhara kwa kuwa ni uchafu na najisi.

Wala msiwakurubie mpaka watoharike.

Wamehitalifiana juu ya makusudio ya kutoharika kuwa je, ni kukatika damu tu bila ya kuoga au ni pamoja na kuoga? Yaani inajuzu kuingiliwa kabla ya kuoga au la? Wamesema Shia inajuzu kumwingilia hata kabla ya kuoga kwa vile ndio ufahamu wa tamko Tuhr watoharike. Ama kujitoharisha hiyo ni kazi ya wanawake ambayo inakuwa baada ya tohara (kwisha damu). Amesema Malik na Shafii: Haijuzu ila baada ya kuoga. Na wanasema Hanafi: Ikiendelea damu kwa muda wa siku kumi, inajuzu kumkurubia kabla ya kuoga, lakini ikakatika damu kabla ya siku kumi haijuzu mpaka aoge. Mwenye tafsiri ya Al Manar ameelezea juu ya ufafanuzi huu kwa kusema: "Huu ni ufafanuzi wa kushangaza.

"Wakishatoharika, basi waendeeni pale alipowaamrisha Mwenyezi Mungu.

Neno: pale ni uhakika wa mahali, kwa maana ya tupu ya mbele, kama inavyofahamika. Masuala ya hedhi na hukumu zake tumeyazungumzia kwa ufafanuzi zaidi katika kitabu Fiqhul Imam Jaffar Sadiq na kitabu Al Fiqhu ala Madhahibil Khamsa

Wake zenu ni mashamba yenu, Basi yaendeeni mashamba yenu mpendavyo.

Neno: Anna, Kulingana na sarufi (nahw ya Kiarabu) lina maana ya vyovyote, wakati wowote au popote. Zimekuja kauli nyingi kuhusu maana ya neno hilo Anna katika Aya hii: Kuna mwenye kusema: Ni kwa maana ya wakati wowote; yaani muwaendee (muwaingilie) wakati wowote usiku au mchana. Wengine wakasema ni kwa maana ya popote yaani mna hiyari ya kuwaingilia popote tupu ya mbele au nyuma. Vile vile kuna mwenye kusema ni kwa maana ya vyovyote; yaani hali yoyote kukaa, kulala, n.k.

Limesema kundi la wafasiri, miongoni mwao akiwa ni mwenye Tafsiri ya Al Manar ambaye ni miongoni mwa wanachuoni wa Kisunni na mwenye Tafsiri ya Bayanu Ssada ambaye ni miongoni mwa wanachuoni wa Kishia, kwamba Neno: shamba linafungamana na mazao na ni tupu ya mbele tu, ndiyo ambayo inaweza kuoteshwa mazao (Mtoto ). Kuongezea kuwa kuendea tupu ya nyuma ni udhia. Sisi tunaiunga mkono rai hii kwa sababu mbili: Kwanza, mazao hayapatikani isipokuwa kwa kupitia tupu ya mbele tu, kama walivyotaja wafasiri hao. Pili, kauli yake Mwenyezi Mungu "Waendeni pale alipowaamrisha Mwenyezi Mungu inaonyesha makusudio yake ni mbele baada ya kufasiri hayth kwa maana ya mahali.

Kuna baadhi ya Mafaqihi wa Kishia wanaojuzisha kumwendea mke nyuma lakini kwa makuruhu makubwa sana. Wengine wamedai ati kuwa hayo yanahusika na Shia tu! Na kwamba hawaafikiani na yeyote katika hilo; na inajulikana kuwa Razi (mwanachuoni wa kisunni) amenakili katika kuifasiri Aya hii kwamba, Ibn Umar na Malik walikuwa wakisema: "Makusudio ya Aya ni kujuzisha kuwaendea wanawake nyuma." Na Al- Hafidh Abu Bakr Al-Andalusi wa madhehebu ya Kimalik (Sunni) - aliyekufa mwaka 542 Hijriya - katika juzuu ya kwanza ya kitabu Ahkamul Qur'an ukurasa 73 chapa ya mwaka 1331 A.H.; alisema hivi ninamnukuu: Wamehitalifiana wanavyuoni katika kujuzu kumwendea mke nyuma, wengi wamejuzisha."

Ameyaeleza hayo Ibn Shaban katika Jimau nnis-wan wa Ahkamul Qur'an. Sunni Na akategemeza, riwaya nyingi kujuzu kwake, kwenye kundi tukufu la masahaba, na Tabiina na kwa Malik. Bukhari ametaja kutoka kwa Ibn Aun, kutoka kwa Nafi kwamba Ibn Umar alikuwa akisoma Sura ya Baqara mpaka alipoishia 'Anna shiitum' alisema: "Je unajua imeteremka kwenye nini?" Nikasema: "La." Akasema: "Imeshuka katika kadha na kadha"; yaani tupu za nyuma za wanawake.

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿وَلَا تَجْعَلُوا اللَّـهَ عُرْضَةً لِّأَيْمَانِكُمْ أَن تَبَرُّوا وَتَتَّقُوا وَتُصْلِحُوا بَيْنَ النَّاسِ وَاللَّـهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ﴾

224.Wala msimfanye Mwenyezi Mungu ni pondokeo la viapo vyenu, (ili) mfanye mema na mumche (Mwenyezi Mungu) na muwe wema kati ya watu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.

﴿لَّا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا كَسَبَتْ قُلُوبُكُمْ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴾

225. Mwenyezi Mungu hatawashika kwa sababu ya kuapa kwenu kwa upuzi upuzi, lakini atawashika katika yaliyokusudiwa na nyoyo zenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghufira Mpole

﴿لِّلَّذِينَ يُؤْلُونَ مِن نِّسَائِهِمْ تَرَبُّصُ أَرْبَعَةِ أَشْهُرٍ فَإِن فَاءُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴾

226.Kwa wale ambao wanaapa kujitenga na wake zao ni kungojea miezi minne. Na kama wakirejea basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghufira Mwenye kurehemu.

﴿وَإِنْ عَزَمُوا الطَّلَاقَ فَإِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴾

227.Na wakiazimia talaka, basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

YAMINI

Aya 224 - 227

Wala msimfanye Mwenyezi Mungu ni pondokeo la viapo vyenu.

Mwenyezi Mungu amekataza kutangulizwa katika kila jambo kwa kuapa sana. Kwa sababu mwenye kukitaja kitu sana amekijaalia ni pondokeo lake. Mwenyezi Mungu ameshutumu kuapa sana kwa kauli yake.

﴿وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَهِينٍ ﴾

Wala usimtii kila mwenye kuapa sana aliye dhalili." (68:10)

Mwenye kuapa sana haiba yake hupungua, huzidi dhambi zake na atatuhumiwa uongo.

(Ili) mfanye mema na mumche (Mwenyezi Mungu) na muwe wema kati ya watu.

Hili ndio sababu ya kukatazwa kuapa; maana yake Mwenyezi Mungu anawakataza kuapa bila ya dharura, ili muwe wema wanaomcha Mungu, wenye kufanya wema duniani na wala sio wenye kufanya ufisadi.

Mwenyezi Mungu hatawashika kwa sababu ya kuapa kwenu kwa upuzi upuzi.

Baada ya kukataza Mwenyezi Mungu kuapa bila ya dharura amebainisha kwamba mengi yanayowapitia watu katika ulimi mfano 'Wallahi vile' au 'sio hivyo Wallahi', n.k. hayo siyo viapo vya uhakika isipokuwa ni mchezo tu unaokuja kwenye ulimi bila ya kukusudia, wala hayana athari yoyote. Kwa hivyo Mwenyezi Mungu hakuwajibisha kafara katika dunia wala hakuna adhabu katika akhera.

Lakini atawashika katika yaliyokusudiwa na nyoyo zenu.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu Ambaye umetukuka utukufu wake, haangalii sura na kauli, bali huangalia nia na vitendo, kama anavyosema:

﴿لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ﴾

"Mwenyezi Mungu hatawashika kwa viapo vyenu vya upuzi, lakini atawashika kwa viapo mlivyoapa kwa nia mliyoifunga (barabara). Basi kafara yake ni kuwalisha masikini kumi kwa chakula cha wastani mnachowalisha watu wa majumbani mwenu au kuwavisha, au kumwacha huru mtumwa. Asiyeweza kupata hayo, basi afunge siku tatu. Hiyo ndiyo kafara ya viapo vyenu mnapoapa...." (5:89)

Mtu aliyebaleghe, mwenye akili timamu mwenye kukusudia na aliye na hiyari, akiapa na akakhalifu, basi itampasa kutoa kafara ya kumwacha huru mtumwa au kuwalisha au kuwavisha maskini kumi. Akishindwa hivyo atafunga siku tatu. Tumezungumzia zaidi kuhusu kiapo, sharti zake na hukumu zake katika juzuu ya tano ya Fiqhul-Imam Jaffar Sadiq.

Kwa wale ambao wanaapa kujitenga na wake zao ni kungojea miezi minne. Na kama wakirejea basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. Na wakiamua talaka basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

Kuapa kujitenga katika sharia ni kuapa mtu kuwa hatamwingilia mkewe. Mafaqihi wa Kishia wameshartiza kuwa mke awe ameingiliwa; kama si hivyo hakitakuwa kiapo; na kuwe ni kuapa mume kuacha kumwingilia mkewe muda wa maisha yake au muda unaozidi miezi minne, kwa sababu mke anayo haki ya kuingiliwa angalau mara moja kila miezi minne kwa uchache.

Wamesema: Kama atamwingilia kabla ya miezi minne atatoa kafara na kizuizi kitaondoka; kama vile hakikuwa kitu, na ikipita zaidi ya miezi minne wala asimwingilie; kama mke akisubiri na akaridhia, hiyo ni juu yake wala haifai kwa yeyote kumpinga. Na kama akishi-ndwa atamshtaki mume kwa hakimu wa sheria. Baada ya kupita miezi minne atalazimishwa kumrudia au kumwacha, akikataa atafungwa mpaka achague moja wapo ya mambo mawili; wala si haki kwa hakimu kumwachisha kwa nguvu. Kama mume ataamua kurudi, basi atatoa kafara iliyotajwa.

﴿وَالْمُطَلَّقَاتُ يَتَرَبَّصْنَ بِأَنفُسِهِنَّ ثَلَاثَةَ قُرُوءٍ وَلَا يَحِلُّ لَهُنَّ أَن يَكْتُمْنَ مَا خَلَقَ اللَّـهُ فِي أَرْحَامِهِنَّ إِن كُنَّ يُؤْمِنَّ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَبُعُولَتُهُنَّ أَحَقُّ بِرَدِّهِنَّ فِي ذَٰلِكَ إِنْ أَرَادُوا إِصْلَاحًا وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾

228.Na wanawake waliopewa talaka wangoje tohara tatu wala si halali kwao kuficha alichokiumba Mwenyezi Mungu katika matumbo yao, ikiwa wanamwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na waume zao wana haki zaidi ya kuwarudia katika muda huo, kama wakitaka kufanya suluhu. Nao (wanawake) wanayo haki sawa na ile iliyo juu yao kwa sharia. Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao. Mwenyezi Mungu ana nguvu, Mwenye hekima.

WALIOTALIKIWA

Aya 228

MAANA

Na wanawake waliopewa talaka wangoje tohara tatu.

Tamko la waliopewa talaka kwa dhahiri ni lenye kuenea kwa yeyote yule aliyepewa talaka, awe anatoka hedhi au amekoma, muungwana au kijakazi mwenye mimba au asiyekuwa nayo, mkubwa au mdogo asiyetimiza miaka tisa. Lakini dhahiri hiyo siyo makusudio yake. Kwa sababu baadhi ya wanaotalikiwa hawana eda, kwa tamko la Qur'an;

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَكَحْتُمُ الْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ طَلَّقْتُمُوهُنَّ مِن قَبْلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ فَمَا لَكُمْ عَلَيْهِنَّ مِنْ عِدَّةٍ تَعْتَدُّونَهَا﴾

"Enyi mlioamini Mtakapowaoa wanawake wenye kuamini kisha mkawapa talaka kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakayaoihisabu..." ( 33:49)

Pia aliyekoma. Mafaqihi wa Kishia wanasema kwamba hana eda hata kama ameingiliwa na mume; vile vile mtoto mdogo chini ya miaka tisa. Na kuna wanawake wanaokaa eda kwa tohara mbili kama mjakazi. Wengine wanakaa miezi mitatu sio tohara tatu; huyo ni yule ambaye yuko katika rika la kutoka hedhi, lakini hatoki; kama ambavyo mwenye mimba muda wake wa kukaa eda unaisha wakati atakapozaa. Mwenyezi Mungu anasema;

﴿وَأُولَاتُ الْأَحْمَالِ أَجَلُهُنَّ أَن يَضَعْنَ حَمْلَهُنَّ﴾

"...Na wenye mimba eda yao ni mpaka watakapozaa..." (65:4)

Kwa hivyo basi makusudio ya waliopewa talaka katika Aya, ni yule aliyeingiliwa akiwa na umri wa zaidi ya miaka tisa, asiwe na mimba na awe mwenye kutoka hedhi.

Wamefasiri Shia, Malik na Shafii neno Qurui kwa maana ya tohara na makusudio ya tohara ni siku za kutoharika baina ya hedhi mbili. Kama akiachwa wakati wa mwisho mwisho wa tohara yake, itahisabiwa pia katika eda na atakamilisha tohara mbili. Ama Hanafi na Hambal wamefasiri neno Qurui kwa maana ya hedhi tatu.

Wala haijuzu kwao kuficha alichokiumba Mwenyezi Mungu katika matumbo yao.

Ili kufahamu hakika ya jumla hii itabidi kuanza kueleza haya yafuatayo: Mafaqihi wa Kisunni wameigawa talaka kwenye mafungu mawili: ya sunna na bid'a (uzushi). Hebu tuwaachie wenyewe tafsiri ya Sunna na Bid'a (talaka ya kawaida na uzushi)

Katika kitabu Al-Mughni cha Ibn Quddam Juzuu 7 Uk. 98 chapa ya tatu anasema: "Maana ya talaka ya sunna ni talaka ambayo inaafiki amri ya Mwenyezi Mungu na amri ya Mtume wake, nayo ni talaka katika hali ya tohara asiyomwingilia." Na katika kitabu hicho hicho Uk. 99 amesema: "Hakika talaka ya Bid'a ni talaka katika hali ya hedhi au katika hali ya tohara aliyomwingilia."Amesema Razi katika tafsiri ya Aya ya 1 katika Sura ya 86; "Utohara katika talaka ni lazima, vyinginevyo haitakuwa ya sunna." Kwa hali hiyo basi, kupewa talaka mke katika hali ya hedhi au katika hali ya utohara ambapo mke ameingiliwa, siyo talaka ya kisheria, bali ni Bid'a (uzushi) na kila uzushi ni upotevu na kila upotevu ni motoni. Ama kumtaliki mke katika tohara asiyoingiliwa na mumewe, inakuwa ndiyo talaka iliyofuata sharia ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hapo ndio inafafanulika siri ya kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.): "wala haijuzu kwao kuficha alichokiumba Mwenyezi Mungu katika matumbo yao." Kwa sababu maarifa ya kutokea talaka kwa njia ya kawaida au uzushi ndiyo yatakayofahamisha hali ya mwenye kuachwa, na kwamba je ana hedhi au yuko tohara.

Kimsingi njia ya kujua sifa mbili hizi (tohara na hedhi) inamtegemea mwanamke mwenyewe. Kwa hivyo itabidi aaminiwe maadamu haujajuliwa uwongo wake. Imam Jaffar Sadiq amesema;Mwenyezi Mungu amewachia wanawake mambo matatu: Tohara, hedhi na mimba." Katika riwaya ya pili imeongezewa eda. Shia wanaafikiana na Sunni kwamba talaka ikiwa katika hedhi au katika tohara aliyoingiliwa, inakuwa ya uzushi na ikiwa ni katika tohara ambayo hakuingiliwa inakuwa ni ya sharia ya Mtume(s.a.w.w) . Lakini Shia wamesema Talaka ya uzushi sio talaka kabisa; yaani si sahihi. Na talaka sahihi inayomtenganisha mume na mke, ni talaka ya kawaida; yaani inayotokea katika tohara asiyoingilwa. Sunni wanasema hapana; talaka ya uzushi ni sahihi na inahusika na athari zote za talaka, isipokuwa tu yule mwenye kuacha atapata dhambi.

Hiyo ni kusema kuwa Sunni hawatofautishi kati ya talaka ya kawaida na ya uzushi katika kusihi kwake, isipokuwa wanatofautisha katika kupata madhambi na uasi tu. Ama Shia wametofautisha kati ya hizo mbili, kwa upande wa usahihi, na si upande wa dhambi.

Ikiwa wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho.

Hii ni kuogopesha na kuweka utisho kwa wenye kuficha yaliyo tumboni na wala sio sharti la kuwajibisha kusadiki. Kwa sababu maana yake ni kwamba imani inazuwiya uongo; kama vile kumwambia mtu: "Ikiwa unamuogopa Mwenyezi Mungu usiseme uongo." Tumetangulia kueleza kuwa mwenye kutalikiwa ndiye atakayeaminiwa katika tohara, hedhi na mimba. Maana yake ni kuwa itakayotegemewa ni kauli yake katika kubaki eda na kwisha kwake. Ilivyo ni kwamba haki ya mume katika kurejea, itategemea kutokwisha kwa eda; kama ambavyo muungano (wa nasaba mtoto) unaambatana na utohara na hedhi.

Vile vile kusihi talaka na kutosihi kwa upande wa mafaqihi wa kishia. Akiwa na hedhi na akasema kuwa ni tohara, basi talaka haitakuwa, na atabaki ni mke wa mtu; kama akisema eda yake imekwisha kwa tohara na kumbe bado, haki ya mume ya kurejea itafutika. Lakini akiolewa katika hali hiyo atakuwa mzinifu. Kwa sababu hii na nyinginezo, ndio Mwenyezi Mungu akawakataza wanawake kuficha vilivyo katika matumbo yao na akawakemea kwa hilo.

Na waume zao wana haki ya kuwarudia katika muda huo, kama wakitaka kufanya suluhu.

Kauli yake Mwenyezi Mungu "katika muda huo" ni ule muda wa kungojea (muda wa eda). Maana yanayopatikana ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) baada ya kubainisha wajibu wa eda, ametaja haki ya mwenye kutaliki kumrejea mtalaka wake katika muda wa eda ikiwa ni talaka rejea. Hiyo ni haki yake awe mke hakuridhia au ameridhia; wala kurejea mke hakuhitaji kufunga ndoa tena na mahari, kama vile ambavyo hakuhitajii ushahidi kwa mafaqihi wa Kishia. Utakuja ubainifu wake zaidi kwenye Sura ya Talaka (65).

Makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu "kama wakitaka kufanya suluhu" ni suluhu kati ya mume na mke bila ya kukusudia madhara katika kurejea. Unaweza kuuliza: Kama mume akimrejea mtalaka wake ndani ya eda kwa kukusudia madhara sio suluhu, je kurejea kutakuwa sahihi au la? Jibu: Kutaswihi kurejea, lakini mume atapata dhambi, kwa sababu kukusudia suluhu ni hukumu ya taklifa ambayo ni kuhalalisha kurejea na wala sio sharti ya maudhui yenyewe ya kurejea na kuswihi kwake.

Nao (wanawake) wanayo haki sawa na ile iliyo juu yao kwa sharia.

Makusudio ya kufanana haki hapa sio ya kufanana kijinsia, kwamba yanayostahiki kwa mume kama vile mahari na posho, basi na mke pia naye atoe, la; isipokuwa makusudio hapa ni kuwa sawa wajibu na yanayostahiki. Mafaqihi wanasema haki ya mume kutoka kwa mkewe ni kutiiwa kitandani, na haki ya mke kutoka kwa mume ni kumlisha na kumvisha. Mwenye tafsiri Al Manar anasema haki ya mume kwa mke na haki ya mke kwa mume ni ile kawaida ya mambo ya watu, isipokuwa yale yaliyoharimishwa katika sharia. Linaloonekana kikawaida kuwa ni haki kwa mke na mume, basi litakuwa ni sawa mbele za Mwenyezi Mungu. Yanayodhihirikia kutokana na mfumo wa Aya ni kwamba haki iliyo kwa mke ni eda, ukweli katika kuitolea habari eda na kuacha kupinga kurejea kulikokamilisha masharti. Na iliyo juu ya mume ni kukusudia suluhu katika kurejea na usuhuba mzuri na wala sio madhara. Ama haki nyingine za mume na mke ziko mbali na Aya hii.

Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao.

Wamehitalifiana wanavyuoni na wafasiri katika makusudio ya daraja hii inayomtofautisha mwanamume na mwanamke. Ikasemwa kuwa ni akili na dini; ikasemwa ni mirathi na pia ikasemwa kuwa ni ubwana; yaani inampasa mke kumtii mume na kumsikiliza. La kushangaza ni kwamba wengine wamefasiri daraja ya juu kwa maana ya ndevu; kama ilivyoelezwa katika kitabu Ahkamul-Qur'an cha Abu bakr Al- Andalusi. Sio mbali na maana kuwa makusudio ya daraja ni kuijaalia talaka na kurejea mikononi mwa mume na wala sio mwa mke.

MWANAMUME NA MWANAMKE KATIKA SHARIA YA KIISLAMU

Uislamu umezitangulia sharia na kanuni zote katika kumkomboa mwanamke na kuzithibitisha haki zake, baada ya kuwa mwanamume alimtumia mwanamke kama bidhaa tu, akamfanya kama mnyama, ambapo mpaka hivi karibuni Ulaya na Marekani walikuwa wakifanya hivyo. Uislamu unapomtofautisha mwanamke na mwanamume unamtofautisha kwa tofauti za kimaumbile au maslahi ya jamii. Ni jambo lisiloingia akilini wala uadilifu kufanya usawa katika kila kitu kati ya yule mwenye kujishughulisha zaidi na magauni, mitindo ya mavazi, kuchana nywele, n.k.; na yule anayehisi majukumu ya mwenzake (mkewe) na watoto na kustahamili mashaka kwa ajili yake (mke) na kwa ajili yao wote. Mafaqihi wa Kiislamu wamezitaja tofauti kati ya mwanamume na mwanamke katika hukumu za kisharia kama ifuatavyo:

1. Fidia ya kuuliwa mwanamke ni nusu ya mwanamume.

2. Kutoa talaka na kurejea kuko mikononi mwa mume sio mke.

3. Haijuzu kwa mke kusafiri, na kutoka nyumbani kwake isipokuwa kwa kukubali mume, lakini mume anaweza kufanya hivyo.

4. Si wajibu kwa mwanamke kuswali Ijumaa, hata yakitimia masharti.

5. Haijuzu mwanamke kutawalia jambo wala kuwa Kadhi, isipokuwa kwa Abu Hanifa anasema inafaa katika haki za watu lakini sio za Mungu.

6. Hawezi kuwa Imam wa swala ya wanaume, lakini mwanamume anaweza kuwa Imam wa wanawake.

7. Ushahidi wake haukubaliwi katika mambo yasiyo husiana na mali; hata akiwa pamoja na waume, isipokuwa katika maswala ya uzazi, unakubaliwa akiwa pamoja na waume kwa kuchukulia kuwa ushahidi wa wanawake wawili ni sawa na wa mwanamume mmoja.

8. Katika mirathi mtoto wa kike anapata nusu ya fungu la mtoto wa kiume.

9. Ni lazima ajifunike mwili wake wote - hata nywele - mbele za waume wasio maharimu, lakini kwa mwanamume mbele za wanawake wajibu wake ni kustiri tupu mbili tu.

10. Hapigani jihadi wala hatoi kodi wala hauliwi vitani iwapo hajapigana. 11. Mama hashirikiani na baba katika usimamizi (uwalii) wa mtoto mdogo au katika matumizi ya mali yake (mtoto). 12. Haifai kushindana mashindano ya farasi na kulenga shabaha. 13. Mafaqihi wametoa fatwa kuwa fidia ya aliyeuawa kimakosa inachukuliwa na ndugu zake wa karibu kwa upande wa baba tu; kama vile kaka, ami na watoto wao lakini sio wakike. 14. Mwanamke akimuua mwanamume, atauliwa bila ya kutoa fidia, lakini kama mwanamume akimuua mwanamke, basi hawezi kuuliwa mpaka walii wa mwanamke atoe nusu ya fidia kwa warithi wa muuaji.