TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI Juzuu 2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI25%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 21192 / Pakua: 4681
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA PILI Juzuu 2

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿الطَّلَاقُ مَرَّتَانِ فَإِمْسَاكٌ بِمَعْرُوفٍ أَوْ تَسْرِيحٌ بِإِحْسَانٍ وَلَا يَحِلُّ لَكُمْ أَن تَأْخُذُوا مِمَّا آتَيْتُمُوهُنَّ شَيْئًا إِلَّا أَن يَخَافَا أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ اللَّـهِ فَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ اللَّـهِ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا فِيمَا افْتَدَتْ بِهِ تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ فَلَا تَعْتَدُوهَا وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ اللَّـهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴾

229.Talaka ni mara mbili; kisha ni kushika kwa wema au kuacha kwa ihsani. Wala si halali kwenu kuchukua chochote katika mlichowapa, isipokuwa wakiogopa (wote wawili) ya kwamba hawataweza kusimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu. Basi mkiogopa kwamba hawataweza kusimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu, itakuwa hapana ubaya kwao kupokea ajikomboleacho mke. Hii ndiyo mipaka ya Mwenyezi Mungu; basi msiipetuke. Na watakao-ipetuka mipaka ya Mwenyezi Mungu, hao ndio madhalimu.

﴿فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا تَحِلُّ لَهُ مِن بَعْدُ حَتَّىٰ تَنكِحَ زَوْجًا غَيْرَهُ فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا أَن يَتَرَاجَعَا إِن ظَنَّا أَن يُقِيمَا حُدُودَ اللَّـهِ وَتِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ يُبَيِّنُهَا لِقَوْمٍ يَعْلَمُونَ﴾

230.Na kama amempa talaka ( ya tatu) basi si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine. Na akimwacha, basi hapo si vibaya kwao kurejeana waki-ona kuwa watasimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na hii ni mipaka ya Mwenyezi Mungu anayoibainisha kwa watu wajuao.

TALAKA NI MARA MBILI

Aya 229 - 230

MAANA

Talaka ni mara mbili.

Waarabu katika zama za Ujahiliya (kabla ya Uislamu) walikuwa na talaka, eda na kurejeana katikati ya eda. Lakini talaka haikuwa na idadi maalum. Mtu aliweza kumwacha mkewe mara mia na kumrudia. Kwa hivyo mwanamke anakuwa ni kitu cha kuchezewa mikononi mwa mwanamume. Kuna riwaya inayoeleza kuwa mtu mmoja alimwambia mkewe: "Sitakukur-ubia milele, na pamoja na hivyo utabaki kwangu tu, hutaweza kuolewa na mwingine." Mke akauliza: "Itakuwaje hivyo?" Mume akajibu: "Nitakuacha mpaka ukikaribia muda wa kwisha eda nikurudie, halafu nikuache tena, n.k." Mwanamke akamshtakia Mtume(s.a.w.w) . Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii:"Talaka ni mara mbili" yaani talaka ambayo mnaruhusiwa kurejea ni talaka ya kwanza na ya pili tu! Ama ya tatu si halali kurejea, mpaka mke aolewe na mume mwingine; kama alivyosema Mwenyezi Mungu;"Na kama amempa talaka si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine."

Kisha ni kushika kwa wema au kuacha kwa ihsani.

Mume akimwacha mkewe mara ya pili ana hiyari kati ya mambo mawili akiwa katika eda. Jambo la kwanza ni kumrejea kwa kukusudia kupatana na kutangamana. Huku ndiko kumweka kwa wema. Jambo la pili, ni kumwacha mpaka ishe eda yake, amtekelezee haki yake asimtaje kwa ubaya baada ya kutengana wala asimkatishe anayetaka kumwoa baada yake. Huko ndiko kumwacha kwa ihisani. Unaweza kuuliza, wafasiri wengi wamefasiri kumwacha kwa ihisani ni talaka ya tatu na wakatoa ushahidi wa Hadith ya Mtume(s.a.w.w) . Sasa imekuwaje wewe kuipinga kauli yao na kufasiri kuacha, kuwa ni kupuuza kumrejea katika muda wa eda?

Jibu : Neno kumwacha, kwa dhati yake linawezekana kuwa ni talaka ya tatu na linawezekana kuwa ni kumnyamazia mtalaka na kuwacha kumrejea. Lakini kwa kuchunga mfumo ulivyo, maana ya neno inarudia maana ya pili; yaani kuacha kurejea, kwa sababu kauli yake Mwenyezi Mungu "Kama amempa talaka basi mwanamke huyo si halali kwake baada ya hapo." Inatokana na kumweka; maana yake yanakuwa ni akimwacha baada ya kumweka na akamrejea katikati ya talaka ya pili itakuwa talaka ni ya tatu wala si halali kwa mwenye kuacha kumwoa mpaka aolewe na mume mwingine. Kwa hivyo haiwezekani kuwa imetokana na kumweka kwa maana ya talaka ya tatu, kwa sababu maana itakuwa alimwacha mara ya nne baada ya kumwacha mara ya tatu. Na ilivyo ni kwamba hakuna talaka ya nne katika Uislamu. Ama Hadith iliyofasiri kumweka kwa maana ya talaka ya tatu si thabiti.

TALAKA TATU

Madhehebu manne ya Kisunni yameafikiana kuwa atakaye mwambia mkewe: Nimekuacha talaka tatu au akisema: Nimekuacha, nimekuacha, nimekuacha, basi itakuwa ni talaka tatu na itakuwa haramu mpaka aolewe na mume mwingine. Shia wamesema itakuwa ni talaka moja tu, na ni halali kumrejea, maadamu yuko katika eda. Katika tafsiri ya Al Manar imepokewa kutoka kwa Ahmad bin Hambal katika Musnad yake, na Muslim katika Sahih yake kwamba talaka tatu zilikuwa moja katika zama za Mtume(s.a.w.w) , za Abu Bakr na baadhi ya miaka ya ukhalifa wa Umar, lakini Umar ikamdhihirikia fikra nyingine akasema; "Hakika watu wamefanya haraka katika jambo lililokuwa na upole kwao, lau tungelipitisha."Basi akapitisha (kuwa kusema talaka tatu ni tatu).

Kisha amenakili mwenye tafsiri Al Manar kutoka kwa Al Qayyim kwamba masahaba wote walikuwa wakikubali kwamba talaka tatu hazikutokea kwa pamoja tangu mwanzo wa Uislamu mpaka miaka mitatu ya ukhalifa wa Umar. Vile vile walifutu hivyo jamaa katika masahaba, Tabiina (waliokuwapo baada ya maswahaba) na waliokuja baada ya hao Tabiina (Tabii-Tabiina), na kwamba fatwa juu ya hilo inaendelea kila wakati hata baadhi ya wafuasi wa Maimamu wanne walifutu hivyo.

Wala si halali kwenu kuchukua chochote katika mlichowapa.

Katika mlichowapa hapa ina maana kiwe kingi au kichache; yaani ikiwa mume ndiye asiyemtaka mke na akapendelea kumpa talaka, basi si haki kwake kuchukua vile alivyompa zawadi mke au mahari. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَإِنْ أَرَدتُّمُ اسْتِبْدَالَ زَوْجٍ مَّكَانَ زَوْجٍ وَآتَيْتُمْ إِحْدَاهُنَّ قِنطَارًا فَلَا تَأْخُذُوا مِنْهُ شَيْئًا أَتَأْخُذُونَهُ بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا﴾

"Na kama mkitaka kubadilisha mke mahali pa mke na hali mmoja wao mmempa rundo mali, basi msichukue chochote katika hiyo. Je, mnachukua kwa dhuluma na kwa dhambi iliyo wazi" (4:20)

Hiyo ni ikiwa mume ndiye asiyemtaka mke. Ama ikiwa mke ndiye asiyemtaka mume, basi hapana kizuwizi cha mke kumpa mume kile kinachomridhia ili amwache, ni sawa chenye kutolewa kiwe ni kiasi cha mahari au kichache au zaidi ya mahari. Talaka hii inaitwa Khul'u (kujivua); na mume katika talaka hii hana haki ya kumrejea katika eda maadamu anaendelea kulipwa. Isipokuwa kama huyo mke atabadilisha katikati ya eda.

Kuhusu talaka hii ya khul'u Mwenyezi Mungu anasema:

Isipokuwa wakiogopa (wote wawili) ya kwamba hawataweza kusimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu. Basi mkiogopa kwamba hawataweza kusimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu, itakuwa hapana ubaya kwao kupokea ajikomboleacho mke.

Hii ni kuelezea uwezekano wa kuchukua kitu kutoka kwa mke. Mipaka ya Mwenyezi Mungu ni haki na wajibu wa kila mmoja kwa mwenzake (mke na mume).

Maana yake: Enyi waume! Msichukue kitu kutoka kwa watalaka wenu kwa sababu yoyote ile, isipokuwa sababu moja tu, ambayo ni ikiwa mke ndiye anayemchukia mume, wala hawezi kuishi naye, kiasi ambacho hali itapelekea kumwasi Mwenyezi Mungu katika kutia dosari haki za unyumba, na huenda mume naye akaogopa kumkabili mke kwa uovu. Katika hali hii, itafaa kwa mke kudai talaka kutoka kwa mume na kumlipa ridhaa; kama vile ambavyo inajuzu kwa mume kuichukua ridhaa hiyo.

Imekuja Hadith kwamba Thabit bin Qays alikuwa amemuoa bint wa Abdulla bin Ubay. Naye alikuwa akimpenda, lakini mke hampendi mume. Na alikuwa amempatia shamba. Mke akaja kwa Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Mimi na Thabit kichwa changu hakipatani na chake." Thabit akasaili: "Na lile shamba?" Mtume akamwambia bint Abdulla: "Unasemaje?" Akasema: "Ndio, tena na ziada nitampa." Mtume akasema: "Hapana, shamba tu," Basi wakafanyiana khul'u. Linakuja swali katika aya hii: Kwa nini ikaja dhamiri ya wawili katika "Isipokuwa wakiogopa (wote wawili) ya kwamba hawataweza kusimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu." Kisha ikaja dhamiri ya wengi kwa kusema: "Na kama mkiogopa". Kwa nini dhamiri zisiafikiane katika jumla mbili?

Jibu : Dhamiri ya wote wawili ni ya mke na mume na dhamiri ya 'mkiogopa' ni ya mahakimu na wasuluhishi; yaani wakiogopa, mahakimu na wasuluhishi kuacha kusimamishwa mipaka ya Mwenyezi Mungu. Makusudio hasa ni kuondoa hofu ya kutoa na kuchukua kwa wote. Swali la pili: Kwa nini ikaja dhamiri ya wawili katika: Si dhambi juu yao (mume na mke), na tunajua kuwa anayepokea ni mume tu. Jibu: Hapa inaonyesha kuwa si vibaya kutoa na kuchukua; kwa kufahamu kuwa kujuzu kutoa kunalazimisha kujuzu kupokea. Swali la tatu: Ikiwa mke na mume wameridhiana kufanya khul'u, mke akatoa mali ili aachwe; lakini uhusiano wao ni mzuri, je, itaswihi khul'u na itafaa mume achukue fidia? Madhehebu zote nne zimesema khul'u itafaa na itafungamana na athari zote za khul'u.

Shia Imamia wamesema haiswihi hiyo khul'u wala mtaliki hawezi kumiliki fidia, lakini talaka itaswihi na itakuwa ni talaka rejea kwa sharti zake. Wametoa dalili ya kuharibika khul'u na kutojuzu kuchukua fidia kwamba Aya imeshartisha kujuzu hilo kwa kuogopa kuingia katika maasi, kama ndoa ikiendelea. Ama Aya inayosema:

﴿وَآتُوا النِّسَاءَ صَدُقَاتِهِنَّ نِحْلَةً فَإِن طِبْنَ لَكُمْ عَن شَيْءٍ مِّنْهُ نَفْسًا فَكُلُوهُ هَنِيئًا مَّرِيئًا﴾

"Na wapeni wanawake mahari yao hali ya kuwa ni zawadi, kama wakiwatunikia kwa ridhia ya nafsi zao, katika hayo (mahari) basi kuleni kwa raha." (4:4)

Makusudio ya Aya hiyo ni kwamba anachotoa mke hapo ni zawadi tu, sio badali ya talaka. Hivyo Aya iko mbali na khul'u.

Swali la nne: Kama mume akifanya makusudi ubaya ili apate mali kutoka kwa mke, na mke naye akatoa mali na ikatolewa talaka kwa misingi hii; je, khul'u itakuwa halali? Na je, ni halali kuchukua mali? Abu Hanifa anasema: "Khul'u ni sahihi, mali ni lazima itolewe na mume ana dhambi." Shafi na Malik wamesema: "Khul'u ni batili na mali irudishwe kwa mke, kwa sababu ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿وَلَا تَعْضُلُوهُنَّ لِتَذْهَبُوا بِبَعْضِ مَا آتَيْتُمُوهُنَّ﴾

"... Wala msiwataabishe ili mpate kuwanyang'anya baadhi ya vile mlivyowapa..." (4:19)

Hayo yamo katika kitabu Al- Mughni, cha Ibn Quddama Juz 7, Uk 55 chapa ya 7. Shia Imamia wamesema: "Haiswihi khul'u, ni haramu kuchukua mali, lakini itakuwa ni talaka rejea kwa kukamilika sharti zake." Ama sisi tuko katika fikra ya kuwa talaka hiyo ni upuzi tu, sio khul'u wala talaka rejea. Kwa sababu kinachojengeka kwa uharibifu ndio kimeharibika chote. Hayo tumeyafafanua zaidi katika kitabu Fiqhul Imam Jaffar Sadiq Juz 6 mlango wa khul'u kifungu cha Hukumu za khul'u. Na kama amempa talaka (ya tatu) basi si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine. Na akimwacha (mume wa pili), basi hapo hapana ubaya kwao kurejeana wakiona kuwa watasimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu.

Maana ni kuwa mwenye kumwacha mkewe mara tatu, basi si halali kwake kumwoa tena mpaka aolewe na mume mwingine kwa ndoa sahihi tena amwingilie. Imekuja Hadith inayosema: "Si halali kwa mume wa kwanza mpaka wa pili amwonje (amwingilie)." Huyu mume wa pili ndiye anayeitwa muhallil (mhalalishaji); Ni lazima awe ni baleghe, na ndoa iwe ya daima sio ya Mut'a. Zikitimia sharti; kisha mume wa pili akatalikiana naye kwa mauti au talaka na ikaisha eda, basi itafaa kwa mume wa kwanza kufunga ndoa naye tena.

﴿وَإِذَا طَلَّقْتُمُ النِّسَاءَ فَبَلَغْنَ أَجَلَهُنَّ فَأَمْسِكُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ أَوْ سَرِّحُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ وَلَا تُمْسِكُوهُنَّ ضِرَارًا لِّتَعْتَدُوا وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَقَدْ ظَلَمَ نَفْسَهُ وَلَا تَتَّخِذُوا آيَاتِ اللَّـهِ هُزُوًا وَاذْكُرُوا نِعْمَتَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَمَا أَنزَلَ عَلَيْكُم مِّنَ الْكِتَابِ وَالْحِكْمَةِ يَعِظُكُم بِهِ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴾

231.Na mtakapowapa wanawake talaka, wakafikia muda wao, basi washikeni kwa wema au waacheni kwa wema. Wala msiwaweke kwa kudhuriana mkafanya uadui. Na atakayefanya hivyo, amejidhulumu mwenyewe. Wala msizifanyie mzaha Aya za Mwenyezi Mungu. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu, na Kitabu alichowateremshia na hekima, kwa kuwaonya. Na mcheni Mwenyezi Mungu, na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

﴿وَإِذَا طَلَّقْتُمُ النِّسَاءَ فَبَلَغْنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا تَعْضُلُوهُنَّ أَن يَنكِحْنَ أَزْوَاجَهُنَّ إِذَا تَرَاضَوْا بَيْنَهُم بِالْمَعْرُوفِ ذَٰلِكَ يُوعَظُ بِهِ مَن كَانَ مِنكُمْ يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ذَٰلِكُمْ أَزْكَىٰ لَكُمْ وَأَطْهَرُ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴾

232.Na mtakapowapa wanawake talaka na wakafikia muda wao, msiwazuie kuolewa na waume zao, ikiwa wamepatana kwa wema. Hayo anaonywa nayo yule, miongoni mwenu, anaye-mwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ni mazuri mno kwenu na safi kabisa. Na Mwenyezi Mungu anajua, na nyinyi hamjui.

MNAPOWAPATALAKAWANAWAKE

Aya 231 - 232

MAANA

Na mtakapowapa wanawake talaka, wakafikia muda wao, basi washikeni kwa wema au waacheni kwa wema.

Msemo huu unaelekezwa kwa waumini wote au kwa watu wote; ni kama vile Mwenyezi Mungu ametaka kusema: Enyi waumini! Atakapompa talaka mmoja wenu mkewe. Baada ya kubainisha Mwenyezi Mungu kwamba mwenye kupewa talaka ni lazima akae eda, kwamba anaweza kurudiwa na mumewe zikikamilika sharti, kwamba ni haramu baada ya talaka ya tatu mpaka aolewe na mume mwingine, na kwamba si halali kuchukua kitu kwa mke kwa ajili ya talaka, isipokuwa ikiwa mke ndiye asiyemtaka mume, baada ya kuyabainisha yote hayo, anatubainishia vile tunavyotakiwa kuchunga haki ya anaekaa eda.

Kuchunga haki kutathibitika kwa kuazimia mwenye kuacha moja kati ya mawili: Kumrejea mtalaka wake wakati inapokaribia kumalizika eda, kwa kukusudia usuluhishi na utangamano mzuri. Na huku ndiko kurejea kwa wema. Au kumwacha bila ya kumtaaradhi kwa ubaya pamoja na kumtekelezea kila analostahiki. Na huku ndiko kumwacha kwa wema. Kwa hivyo inatubainikia kuwa makusudio ya Aya iliyotangulia siyo makusudio ya Aya hii tuliyonayo. Aya ile iliyotangulia inabainisha kuwa kurejeana ni talaka ya kwanza na ya pili na siyo ya tatu. Na hii inabainisha vile tunavyotakiwa kuwafanyia waliopewa talaka; kama ambavyo makusudio ya kufikilia muda wao ni kukurubia sio kufika hasa.

Wala msiwaweke kwa kudhuriana mkafanya uadui.

Yaani msiwarudie kwa kukusudia kuwaudhi au kuwafanyia ubaya; muwareTafsir jee tu kwa makusudio ya kutekeleza haki za unyumba na kusaidiana yale yaliyo na maslahi kwa wote.

Unaweza kuuliza kwa nini imesemwa kudhuriana, ambapo makusudio ni kuepusha madhara ya mume kwa mke?

Jibu : Kumdhuru mke kunasababisha kudhurika kwa mume pia, kwa sababu ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu juu yake, shutuma za watu kwake, na mke kulipiza kisasi. Hapo ndio unyumba unageuka kuwa Jahannam kwa mume na mke na huenda moto ukaenea kwa jamaa na ndugu. Ndio maana Mwenyezi Mungu anasema:

Na atakayefanya hivyo, amejidhulumu mwenyewe. Yaani si kumdhulumu mke peke yake.

Wala msizifanyie mzaha Aya za Mwenyezi Mungu.

Hiki ni kiaga na kemeo kwa yule mwenye kukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu katika haki za unyumba. Njia ya kuzifanyia mzaha Aya za Mwenyezi Mungu, ambaye limetu-kuka neno lake, ni kwamba kila mwenye kudai kumwamini Mwenyezi Mungu na hakufuata dini kwa sharia zake, halafu akapuuza hukumu zake, halali yake na haramu yake, basi atakuwa amefanya mzaha, atake asitake. Sawa na anayem-uahidi mtu kitu hali akiwa na niya ya kutotekeleza. Baadhi ya wahenga wamesema: "Mwenye kutubu dhambi na huku anaendelea nayo ni kama mwenye kumcheza shere Muumba wake."(Mungu apishie mbali!)

Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu.

Miongoni mwa hizo ni kuwa Mwenyezi Mungu ametuumbia wanawake ili tupate utulivu kwao na tusaidiane nao katika yale yenye utengeneo wa familia. Ikiwa tunamwamini Mwenyezi Mungu na tunafuata amri zake kweli, basi ni juu yetu kufanya lile litakaloleta lengo hili na kujie-pusha na kila linaloleta uovu katika familia na kuchafua usafi wa maisha ya ndoa.

Na mtapowapa talaka wanawake na wakafikia muda wao, msiwazuie kuolewa na waume zao.

Makusudio ya kufikia muda katika Aya iliyotangulia ni kukaribia kwisha eda na makusudio yake hapa ni kwisha kabisa hiyo eda. Katika Aya hii kuna mielekezo miwili ya misemo (mnapowapa talaka, na msiwazuie) ambayo wafasiri wamehitilafiana; kwamba, je yote inaelekezwa upande mmoja au pande tofauti? Kuna wenye kusema kuwa unaelekezwa kwa upande mmoja tu wa waume; na maana yake ni: Enyi waume, mnapowapa talaka wanawake na eda yao ikaisha, basi msiwazuwie kuolewa na waume wengine wanaowaridhia. Kwa sababu mwanamume alikuwa akimhukumu mtalaka wake na kumzuia, kuolewa na mume mwingine baada yake. Wengine wanasema: Msemo wa kwanza Mtakapowapa talaka, unaelekezwa kwa waume, na wapili msiwazuie, unaelekezwa kwa mawalii; kwa maana ya: Enyi waume, mnapowapa talaka wanawake, basi nyinyi mawalii msiwazuwie watoto wenu kurudiana na waume zao wa kwanza, ikiwa eda imekwisha. Wanaosema hivi wametoa ushahidi wa Hadith ya Mu'ukil bin Yasir( [12] ).

Inaeleweka kwamba kauli yake Mwenyezi Mungu: "Mtakapowapa talaka wanawake na wakafikia muda wao msiwazuwie" ni jumla ya pamoja iliyo na sharti, na jawabu lake ni msiwazuie. Ikiwa sharti ya mwenye kumwambia ni mwingine na jawabu liwe kwa mwingine na maana yawe ni: Enyi waume mtakapowapa talaka wanawake basi nyinyi mawalii msiwazuie, hapa kutakuwa na mkorogano ambao haupaswi kuwapo katika maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Usahihi hasa ni misemo miwili (sharti na jawabu lake) inaelekezwa kumoja tu kwa waumini wote;

sio waume peke yao wala mawalii tu, wala pia sio kwa wote, bali ni kwa waumini. Hali hii inakuja mara nyingi katika maneno yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.), na maana yanakuwa: Enyi mlioamini mmoja wenu akimpa talaka mkewe, eda ikaisha na akataka kuolewa na mume mwingine au kurudiwa na mumewe wa kwanza, basi msimzuie kama wakipatana kwa wema; yaani wakiazimia kuoana. Na kauli yake Mwenyezi Mungu: Ikiwa wamepatana kwa wema inafahamisha kuwa mke anaweza kujioza yule anayemridhia, bila ya kumngoja walii.

Unaweza kusema: hakika Aya imeuondoa uwalii (usimamizi) kwa wanawake walioachwa tu, na wala haikuutaaradhi usimamizi kwa wengineo. Kwa hivyo kuuondoa usimamizi kwa wanawali kunahitajia dalili. Jibu: Kuthibitisha usimamizi ndiko kunakohitajia dalili; ama kuondoa, dalili yake ni ya asili kwamba kila aliyebaleghe mwenye akili mume au mke ni huru katika mambo yake wala hatawaliwi na yeyote, kwa vyovyote atakavyokuwa isipokuwa tu kama atakiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.)

Hayo anawaonywa nayo yule, miongoni mwenu, anayemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho.

Hayo ni ishara ya hayo aliyoyataja Mwenyezi Mungu katika hukumu zake. Anaonywa nayo, yaani wanaonyeka nayo wenye imani sahihi. Ama wengineo katika wenye imani mbovu, masikioni mwao mna vizuwizi, hawasikii mawaidha ya Mwenyezi Mungu na hukumu Zake wala uongozi Wake. Aya hii ni dalili ya wazi kwamba hakuna imani bila ya ucha Mungu na imani sahihi haiepukani na mawaidha, na asiye waidhika wala kunufaika na amri za Mwenyezi Mungu hana hata chembe ya imani.

Hayo ni mazuri mno kwenu na safi kabisa.

Hayo ni ishara ya mawaidha na kutumia hukumu ya Mwenye-zi Mungu katika maisha ya ndoa kwa ujumla na hasa katika waliopewa talaka. Hakuna mwenye shaka kwamba ndoa yenye lengo la utu na kusaidiana katika heri, inaleta ongezeko na usafi katika riziki, usafi wa tabia, heshima na ufanisi kwa watoto. Ama makusudio yakiwa mabaya, basi mwisho wake ni ukafiri, uharibifu, balaa na mashaka katika maisha ya wazazi na watoto.

Na Mwenyezi Mungu anajua, na nyinyi hamjui.

Makusudio sio kutupa habari kuwa Yeye ni mjuzi au mjuzi zaidi, hapana. Hilo liko wazi halihiitaji mafunzo wala ufafanuzi. Makusudio hasa ni kutilia mkazo na kuhimiza kutekeleza hukumu Zake Mwenyezi Mungu; hata kama haikutubainikia njia ya manufaa yapatikanayo katika hukumu hiyo. Kwa sababu Mwenyezi Mungu ambaye imetukuka hekima yake, haamrishi isipokuwa lenye heri na maslahi na wala si lazima tuijue heri hiyo kwa ufafanuzi; bali inatosha tu kujua kuwa Mwenye kuamrisha na Mwenye kukataza, ni Mjuzi Mwenye hekima, halijifichi lolote Kwake liwe ardhini au mbinguni. Kwa ujumla ni kuwa kuna tofauti kati ya mumin na asiyekuwa mumin. Mumin anaabudu kulingana na kauli ya Mwenyezi Mungu na anafanya amali katika hali ya kuyakinisha kupatikana manufaa, hata kama atashindwa kuyafahamu kwa ufafanuzi.

Ama asiyekuwa mumin hafanyi kitu mpaka ajue au adhani kuwa kuna manufaa anayoyajua yeye mwenyewe kwa akili yake au aongozwe na kiumbe kama yeye, ambapo mara nyingi anaruka patupu na kubainikiwa na kinyume, lakini mumin anakuwa katika amani ya Mwenyezi Mungu na hifadhi Yake.

5 UKWELI WA USHIA

KUYAJENGEA MAKABURI

FUADI : Ewe Jaafar, je unaniruhusu nikuulize kuhusiana na maudhui ya Shia na Sunni?[13]

JAAFAR : Uliza kwani nina penda sana kila mtu awe ni mwenye kufahamu mambo, mwenye elimu na anae fahamu mambo kutokana na utafiti na kwa kupata yakinina hawi ni mwenye msimamo legelege na mwenye kufuata kila akisikiacho na kipepeacho angani, au kila sauti ijitokezayo na kutangaa anganibila ya kufahamu usahihi wake na ubatilifu wake au ufisadi wake.

FUADI : Je maneno yangu utayaamini ikithibitika kuwa sisi (Ahli sunna) ndio wenye haki?

JAAFAR : Kwa hakika mimi niko msitari wa mbele kati ya wale wenye kuamini mambo ya kweli haraka pale wanapo yafahamu, na mimi sikushikamana na ushia isipokuwa ni baada ya kuuona kuwa ni haki na wewe unafahamu ya kuwa baba yangu na mama yangu na ndugu zangu na watu wa kabila langu wote ni masunni na kati yao hakuna Shia hata mmoja, na mimi sikufuata Ushia isipokuwa ni kwa ajili ya ukweli nilio uona na kuukuta ndani ya madhehebu hayo.. na lau nitafahamu usahihi wa maneno yako mimi ni wa mwanzo kuyaamini.

FUAD : Nyie Mashia mnayajengea makaburi ya Manabii, Maimamu, Maulamaa na watu wemamajengo makubwa, mnasali kwenye makaburi, wakati jambo hilo ni shirki, kama washirikina wanavyo abudu masanamu nanyi Mashia mnaaabudu majengo ya makaburi ya mawalii.

JAAFAR : Ni wajibu sisi tuwe wakweli na tunao kwenda sambamba na uhakika wa mambo, tusiwe ni watu wachukuao maganda na kuacha kiini, tusiangalie yasemwayo na fulani au fulani, bali tuangalie ukweli ulio wazi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake(s.a.w.w) , na mwenendo wa watu wema walio tangulia.

FUAD : Ndio, nami ni hivyo hivyo, ninapenda kufahamu ukweli wa mambo kupitia njia za kielimu na ufahamu sahihi, si kufuata mambo ufuataji wa kipofu.

JAAFAR : Kwanza kabisa: Sio sisi Mashia pekee tuhusikao na suala la kuyajengea makaburi, kwani waislaam wote wanayajengea makaburi ya Manabii na Maimam na wanazuoni wakubwa au viongozi wao, na ifuatayo ni mifano juu ya hayo: Kaburi la Mtume(s.a.w.w) na makaburi ya makhalifa wawili bado hadi hivi sasa yamejengewa kwa jengo kubwa na yenye kuba kubwa na ya hali ya juu kabisa.

Makaburi ya Mitume kadhaa, kama vile kaburi la Nabii Ibrahim(a.s) lililoko Jodan katika mji wa (Al-khaliil) makaburi hayo yana dharihi (yamejengewa) na juu yake kuna kuba na majengo makubwa. Kaburi la Nabi Mussa(a.s) lililoko Jodan kati ya mji wa (Qudsi) na (Omman) lina jengo kubwa. Kaburi la Abi Hanifa lililoko Baghdad hadi leo bado limejengewa kwa jengo kubwa, na juu yake kuna kuba. Kaburi la Abi Hurairah katika (Misri) hufanyiwa ziara na limejengewa na juu yake kuna kuba. Kaburi la Abdul-qaadir lililoko (Baghdaad) kaburi hilo lina uwanja mkubwa na dharihi na juu yake kuna kuba.

Na makaburi mengine ya Mitume, na makaburi ya Maimamu na wanazuoni wakubwa wa madhehebu, yote hayo yana majengo na juu yake kuna kuba, na yana waqfu maalum ambapo waqfu hizo faida zake hutumika kuyaimarisha na kuyakarabati makaburi hayo na kuyalinda yasiharibike.

Na Miji ya kiislaam imejawa na majengo kama hayo.. na Waislaam wote pamoja na tofauti za madhehebu yao tangu siku ya kwanza hadi leo huyapenda mambo hayo, na huwaamrisha watu kuyatekeleza hayo, na hawakukataza kufanya hivyo hata siku moja, kwa hivyo si sisi Mashia pekee tuhusikao na hukumu hii, bali wanakubaliana nasi na kuwafikiana nasi Waislaam wengine wote, na wao pia huyajengea makaburi ya maimamu wao na wakati wote huyatembelea.

Pili: Sisi- Mashia- au waislaam wengine wakati tunapo Sali pembezoni mwa makaburi ya mawali, hatusali kwa ajili ya mawalii hao bali tunasali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee. Na liwezalo kukujulisha hilo ni kuwa sisi tunapokuwa katika sala huelekea kibla na wala hatuyaelekei makaburi hayo, na lau kama tunge kuwa tukiyasalia makaburi yale, na kuelekea kwenye ibada zatu kwenye dharihi zile (majengo yale ya makaburi), ingewajibika kuyaelekea, na tusinge elekea kwenye kibla.

FUAD : Kwa nini mnasali nyuma ya makaburi hayo, mpaka mkayafanya kuwa ni kibla chenu?

JAAFAR : Hakika sisi wakati tunapo Sali nyuma ya makaburi, tunaelekea kibla na wala hatuyaelekei makaburi, bali makaburi yale-imetokea tu- yakawa mbele yetu, bila ya sisi kukusudia kuyaelekea.

Na hili halitokei isipokuwa kwa mtu anae Sali akiwa ameelekea kibla katika sehemu fulani na ikatokea kwa mfano kukawa na jengo kubwa mbele yake, je kusali katika sehemu hiyo kunamaanisha kuwa mwenye kusali anaabudu jengo hilo?! Na zaidi ya hayo Maulamaa wote wa Waislaam wanasema kuwa: Inajuzu kusalia katika majumba ya ibada za washirikina hali ya kuwa umeelekea kibla hata kama mbele ya mwenye kusali kutakuwa na sanamu lenye kuabudiwa kinyume cha Mwenyezi Mungu, Kwani mwenye kusali humuelekea Mwenyezi Mungu na wala halielekei sanamu. Je hii inamaana kuwa mwenye kusali analiabudu sanamu lile?

FUAD : Ikiwa kuyajengea makaburi si shirki- kama unavyo sema- na waislam wote wanasema ya kuwa inajuzu kufanya hivyo, ilikuwaje wakavunja madharihi (majengo ya makaburi) na makuba yaliyo jengwa juu ya makaburi ya maimamu na wengineo, kwa hoja ya kuwa kufanya hivyo ni shirki na ni kumuabudu asie kuwa Mwenyezi Mungu, na maulamaa wa Hijazi wakatoa fat'wa ya kufanya hivyo?

JAAFAR : Kwa hakika ni baadhi tu walio toa fat'wa kama hiyo kati ya maulamaa wa Hijazi katika zama zile, kwani kuna baadhi ya Mashekhe waishio katika mji wa Madina walio nihadithia na kunisimulia kwa kusema: Kwa hakika wakati huo walipo toa amri ya kubomoa makuba na majengo ya makaburi, maulamaa wenyewe wa Hijazi walipinga amri hiyo, wakitoa hoja kuwa hilo si shirki bali vitu kama hivyo ni sunna katika sheria ya kiislaam, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:jambo lililo pelekea kufukuzwa kwa maulamaa wale, na kuwauz ulu wengine katika nyadhifa zao na kuwatenga. Kwa hivyo basi: Fat'wa hiyo haikutolewa isipokuwa na baadhi tu ya maulamaa wa Hijaz.

FUAD: Kwa hakika mimi nilikuwa nikifikiria na kujiuliza ya kuwa: Ikiwa kujenga madharihi na makuba ni haram na shirki, kwa nini maulamaa wa Waislaam hawakuzinduka na kuliona hilo tangu zama za Mtume(s.a.w.w) hadi leo, na kwanini hawakuzuwia kufanya hivyo? Na ilikuwaje Waislaam wasilifahamu hilo kwa muda wa karne kumi na tatu?

JAAFAR: Nitakuongezea elimu na maarifa: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alikiri na kukubali kujengea makaburi, madharihi na makuba na hakukataza kufanya hivyo. Kwa mfano hili ni jengo la hijri Ismail mahala alipo zikwa Nabi (Ismail) na sehemu alipo zikiwa mama yake Haajar. Na haya hapa makaburi ya Manabii wengine-kama Ibrahim Musa na wengineo- walio zikiwa pembezoni mwa baytul-maqdas, yalikuwa ni yenye majengo makubwa katika zama za Mtume(s.a.w.w) na hadi zama zetu hizi, na wala hakuzuwia yeyote si Mtume Mwenyewe (s.a.w) wala mmoja wapo kati ya makhalifa wake.

Na lau kama tendo hilo linge kuwa haram au linge kuwa ni shirki basi Mtume ange amuru kuvunjwa na kubomolewa kwa majengo na makuba hayo, na ange kataza kufanya hivyo. Na kutokana na ukweli kuwa hakufanya hivyo tunafahamu na kuwa na yakini ya kuwa mfano wa vitu kama hivyo au kufanya hivyo ni kitu kinacho juzu na kinafaa.

Hivyo hivyo baada ya kufariki Mtume(s.a.w.w) , kwani Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo chukuliwa roho yake alizikwa katika chumba chake, na mlango wa chumba kufungwa, na kaburi lake likawa katikati ya chumba kilicho jengewa kuta na dari, na lau kama sahaba yeyote ange sikia kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kuwa tendo kama hilo ni haram basi wasinge thubutu kumzika Mtume katika chumba hicho kilicho jengewa, na lau kama ingelazimika kumzika chumbani mwake basi ingekuwa wajibu kubomoa chumba hicho ili kaburi hilo lisiwe na jengo au lisiwe ni lenye kujengewa.

Na kutokana na kutofanya kwao hivyo, tukafahamu ya kuwa kujenga juu ya makaburi si haram, sasa vipi itakuwa ni shirki?.

FUAD: Ninakushukuru kwa wema wako kwani umeniongoza kwenye ukweli (haki), na kunijulisha ya kuwa kujenga juu ya makaburi si haram wala shirki, na kwamba wale ambao wanaharamisha jambo hilo hawana dalili yoyote katika sheria wawezayo kuitegemeza kwayo kauli yao.Na kwa hakika mimi nitakushukuru daima juu ya hili.

JAAFAR: Nami ninakushukuru kwa kukubali kwako ukweli na haki baada ya kuifahamu, na kuufuata kwako uongofu pale ulipo uona, kwani wewe ni mwenye kufuata muongozo wa akili na mantiki sahihi, kwa hivyo basi ninapenda kukuzidishia maarifa zaidi kuhusiana na haki na ukweli, na kukupatia maarifa mbali mbali katika dini, je unawakati zaidi ili niweze kuzungumza na wewe?

FUAD: Kwa hakika mimi ninapenda sana maneno ya kweli, zungumza ulitakalo, hakika mimi niko tayari kukusikiliza na kuyajaza masikio yangu kwa maarifa.

JAAFAR: Kutokana na mazungumzo yetu yaliyo pita imethibiti kuwa kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni jambo linalo faa na inajuzu kufanya hivyo, na jambo hilo si haram.

FUAD: Ndio.. nami niko pamoja nawe katika hilo.

JAAFAR : Hivi sasa nataka kusema hivi: Hakika kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu na kuweka madharihi juu yake na kujenga makuba.. yote hayo ni sunna, hupewa thawabu mwenye kuyafanya hayo yote, si tu kwamba inajuzu.

FUAD : Vipi inakuwa sunna?

JAAFAR : Mwenyezi Mungu mtukufu amesema:( Na anayeziheshimu alama za Mwenyeezi Mungu basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo). Kwa hivyo kila kitu ambacho huzing atiwa na kuhesabiwa kuwa ni katika shiari za Mwenyezi Mungu kukitukuza ni sunna katika Uislaam.

FUAD: Ndio..lakini vipi itakuwa kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni katika shiari za Mwenyezi Mungu?

JAAFAR: Shiari ni vitu ambavyo huitukuza dini katika mtizamo wa ulimwengu bila kuwepo dalili juu ya uharamu wake.

FUAD: Je dini hutukuzwa kwa majengo na makuba hayo?

JAAFAR : Ndio.

FUAD: Ki vipi?

JAFAAR: Kujengea makaburi ya maulamaa na viongozi watukufu wa kiislaam, na kujenga makuba juu yake, na kuyahifadhi yasiharibike na yasibomoke, ni kuwatukuza watukufu hao bila shaka yoyote. Kwa mfano: Akijitokeza mtu fulani na kupanda uwa waridi kwenye kaburi la mtu alie kufa, je mtu huyu haonekani kuwa amemtukuza maiti yule, na kuwa amemuenzi?

FUAD : Ni sahihi.

JAAFAR : Vipi ikiwa atajenga juu ya kaburi lake jengo kubwa na kuweka kuba juu yake, hakika kufanya hivyo ni kumtukuza na kumuenzi maiti huyo bila shaka yoyote. Na kuwatukuza viongozi na maulamaa wa kiislaam pia maimamu na mawalii.. ni kuutukuza Uislaam, na kuitukuza na kuienzi dini ambayo watu hawa walikuwa wakiilingania, na wakiwaelekeza watu kwenye dini hiyo. Je mtu fulani anapo mtukuza Raisi wa chama fulani, au walinganiaji wa itikadi za chama hichohuzingatiwa kuwa ni mwenye kukitukuza chama kile na itikadi ile au laa?

FUAD: Ndio ni kama usemavyo.

JAAFAR: Kwa hivyo basi kuyajengea makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni kuwatukuza wao na kumtukuza Mwenyezi Mungu, na ni kuuinua na kuutukuza Uislamm, na kila kitu ambacho kukifanya kutakuwa ni kumtukuza Mwenyezi Mungu na ndani yake kuna kuuinua Uislaam, kitu hicho ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo anahimiza kuzifanya, kwani anasema:Suratul- haji aya 32.

FUAD: Kwa hivyo..kuvunja na kubomoa maka buri ya mawalii na Mitume na maimam, inakuwa ni kuidhalilisha dini, na kuutia dosari utukufu wa kiislaam.. kwani kuyabomoa ni kuwadharau viongozi wetu, na ni kuwahini wao.. na kuwahini wao ni kuihini dini, na kuutia dosari utukufu wao ni kuutia dosari utukufu wa Uisalaam.

JAAFAR: Na mimi pia nimekuwa Shia, na nimefuata madhehebu ya Ahlil-bayti (a.s) na nimebadilisha jina kutoka jina la Waliid na kuwa Jaafarkwa sababu hii hii? Kwa hakika mimi wakati nilipo kuwa nikifuata rai za watu wengine sikuwa nikidha nia ya kuwa hakuna alie kwenye haki kinyume changu mimi, lakini nimeitafuta haki na kuifuata hadi kuifikia. Na mtu wakati wote anapo acha nyuma na kuzitupilia mbali asabia za madhehebu, na kukifungua kifua chake kwa ajili ya kuikubali haki, na kuitafuta haki.. hapana budi ataifikia haki hiyo na kuipata.

FUAD: Mimi, na baada ya msimamo na mawkifu haya, nitakuwa makini katika mambo mbali mbali, na nitakuwa ni mwenye kuitafuta haki, mpaka niweze kuifuata haki kokote nitako ikuta. Na kwa hakika nitakushukuru kwa muda wote.. Basi niruhusu nende zangu kwani nina ahadi na mtu fulani.

JAAFAR: Nenda, Mwenyezi Mungu akulinde.

FUAD : Fii amani llahi.

JAAFAR : Uwe katika amani ya Mwenyezi Mungu.

Abu haatam Ar-raziy katika kitabu chake (Az-ziinah) anasema: Kwa hakika jina la kwanza lililo dhihiri katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu ni Shia, na jina hili ndilo lililo kuwa jina mashuhuri (Laqab) la masahaba wane nao ni: Abu Dharri Salman Miqdaad na Ammar.

Na Shekh Mohammad Husein Kaashiful-Ghitaa katika kitabu chake kiitwacho (Aslush-shia wa Usuuliha) anasema: Hakika mbegu ya mwanzo ya Ushia iliwekwa na kupandikizwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) tangu zama za mwanzo kuanza kueneza Uislaam bila ya kutofautisha kati ya vitu viwili hivyo na vikiwa sawa.

Na ushahidi ni hadithi zake tukufu si kupitia njia za Mashia na upokezi wa wapokezi wa Kishia Imamiyyah pekee bali ni hadithi za maulamaa wa kisunni na wanazuoni wao na kupitia njia zao wanazo ziamini ambazo hazidhaniwi kuwa zina chembe ya uongo, na katika hadithi hizo ni hadithi iliyo pokelewa na Suyuut katika kitabu chake (Ad-durrul-manthuur fii tafsiri kitabillahi bil-ma'athur) katika kuitafsiri kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:(Hao ndio viumbe bora) (suratul bayyinah aya 7). Ame sema: Ametoa hadithi Ibn Asakir kutoka kwa Jaabir bin Abdillahi amesema: Tulikuwa kwa Mtume(s.a.w.w) mara akatokea Ali na kuingia na Mtume(s.a.w.w) akasema: Nina apa kwa haki ya yule ambae nafsi yangu iko mikononi mwake hakika huyu na wafuasi (Mashia) wake ndio walio faulu na kufuzu siku ya kiama. Na hapo ikatelemka aya isemayo:(Hakika wale ambao waliamini na kufanya matendo mema hao ndio viumbe bora). (Suratul-bayyinah aya 7). Ibnu Hisham katika Siir atun-nabawiyyah anasema:Hakika umma wa kiarabu uligawanyika katika makundi mawili Masunni na Mashia tangu siku ya Sakifa.

Muhammad Abu Zuhra anasema katika kitabu chake kiitwacho Taarikhul-madhaahibil-islaamiyyah:(Ushia ni madhehebu ya kiislaam ya kisiasa ya tangu muda mrefu na Mashia walidhihiri na madhehbu yao hayo tangu mwishoni mwa zama za Uthuman na kukua na kupata nguvu katika zama za ukhalifa wa Ali, kwani kila alipo pata nafasi ya kuchanganyika na watu walizidi kupendezewa na kuvutiwa kutokana na kipawa chake na kutokana na nguvu ya Imani yake ya dini na elimu yake).

Ibnu Abil-hadiid anasema katika kitabu chake Sharhu Nahjul-balagha:(Hakika Mashia katika zama za dola na utawala wa Muawia walikuwa wakifadhilisha kuitwa Al-kitabiy na wasiitwe Shia. Kwani Ushia anwani yake na shiari yake ni kushikamana na Ahlul-bayti na kufuata elimu yao na kujiepusha na watu wa Bidaa (Uzushi) na kushikamana na kizazi kitwaharifu na kilicho pambika na tabia njema na bora kabisa) (Rejea kitabu Taarikhul-firaqil-islaamiyyah cha Shekh Muhammad Khaliil Az-zayni ukurasa wa 108-109).

Neno Sunnah: Lenye shadda, asili ya neno hilo ni njia, na neno hilo limepanuka maana yake katika makundi tofauti, na linapo tumika huwa lina maana ya aliyo yafanya Mtume (s.a.w) kama kauli vitendo au aliyo yakataza na kuyakemea, na hutumika katika maana hizo kupitia ndimi za wanazuoni na hadithi za Mtume(s.a.w.w) . Na katika zama za hivi karibuni neno Sunnah limekuwa likitumika katika mukabala wa neno Shia, na Husemwa: As-sunnatu wal-jamaah katika mukabala wa watu maalum, na katika ufahamu wa Shekh wa madhehebu ya Hanbali Ibnu Taimiyyah: Neno Sunnah: lina maana ya kumpenda Ali Uthmani na kumtanguliza Abubakar na Omar kwa wawili hao walio tangulia.

Na madhehebu yalipokithiri na makundi kuwa mengi, baadhi wakashikamana na rai isemayo kuwa tamko Sunni lilikuwa likitumika kwa mtu ambae anafuata dini kwa kuwapenda na kuwatawalisha mashekhe wawili, (Abubakar na Omar), na ilikuwa ikisemwa Sunaatul-umariyyh) Rejea kitabu Tariikhul-firaqil-islaamiyyah ukurasa 44-45).

6 UKWELI WA USHIA

KUPAMBWA KWA MAKABURI YA MAIMAM

KHALID : Salaamun alaykum.

BAAQIR : Wa alaykumus-salaam warahmatullahi wabarakatuhu.KHALID : Umefanya vizuri umekuja lini?

BAAQIR : Nimekuja kumtembelea mtoto wa ami yangu anaishi hapa.KHALID : Nakuomba leo hii ukaribie nyumbani kwetu.

BAAQIR : Kwa hakika ninakazi nyingi nilizo ziacha kwa ajili ya kuwatembelea ndugu (kuunga udugu) na kuomba unisamehe sana kwa wito huo.

KHALID : Haiwezekani..marafiki wawili baada ya kutengana kwa muda wa miaka kumi wanakutana kisha wasibakie na kufuatana walau kwa muda wa saa moja. Hakika mimi -pia nina haki ya udugu wa kiislaam. Kisha kulitokea mazungumzo kati yangu na ndugu yangu mmoja muumini kuhusiana na maudhui ya Shia na Sunna na kutokana na kuwa mimi ninamatumaini na imani na wewe ninataka na ninakusudia kufanya mazungumzo na wewe kuhusu maudhui hayo ili niweze kuelewa ukweli na uhaki katika maudhui hayo.

BAAQIR : Hakuna shaka. Walifuatana pamoja hadi nyumbani kwa Khalid, na kufika nyumbani kwake, na kila mmoja akaketi pembezoni mwa mwenziwe. Na baada ya kuzungumza kuhusiana na mambo yanayo wahusu na yaliyo maalum kwa ajili yao wawili, Baaqir akamuwahi mwenzie kwa kumuuliza swali na kusema: Ni mazungumzo gani yaliyo fanyika kati yenu?

KHALID : Mazungumzo yalikuwa yakihusiana na kuyapamba makaburi ya Manabii, maimam, maulamaa, waumini na watu wema na mfano wa hao, kwa Dhahabu na Fedha na mapambo mengineyo.

BAAQIR : Ni tatizo gani lililopo kuhusiana na jambo hilo?

KHALID : Je kufanya hivyo si haram?

BAAQIR : Kwanini iwe haram?

KHALID : Je maiti anafaidika na mapambo hayo?

BAAQIR : Hapana, hafaidiki nayo.

KHALID : Kwa hivyo, hayo yote ni Israfu na matumizi mabaya, na Mwenyezi Mungu anasemaWala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu. Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu za mashetani. suratul- israai aya 26-27.

BAAQIR : Unasemaje kuhusiana na nguo ifunikwayo juu ya Kaaba na mapambo yake, na Dhahabu Fedha na vitu ambavyo vipo juu ya Kaaba na ndani ya Kaabah?

KHALID: Sijui.

BAAQIR : Ndio, Kaaba ina nguo ambayo hufunikwa juu yake, na kuna Dhahabu nyingi, ambayo watu huitoa zawadi kwa ajili ya Kaaba kutoka sehemu tofauti za Dunia tangu zama za ujahilia hadi katika zama zetu hizi. Ibnu Khaladuni[14] anasema katika utangulizi wa kitabu chake:

[15] Kwa hakika tangu zama za Ujahilia kaumu mbali mbali walikuwa wakiitukuza Kaaba, na wafalme walikuwa wakituma mali na vitu vya thamani kwenye nyumba hiyo kama vile Kisraa na wengineo, Na kisa cha mapanga na nguo zilizo fumwa kwa dhahabu, vitu ambavyo Abdulmutwalib alivikuta chini alipo chimba kisima cha Zamzam ni maarufu sana).

Na Mtume(s.a.w.w) alipo ikomboa Makka alikuta katika kisima kirefu kukiwa na Awqiyah sabini elfu za Dhahabu vitu ambavyo wafalme walikuwa wakizitoa zawadi kwa ajili ya nyumba ya Allah. Na kulikuwa na dinari milioni moja, yaani zenye uzito wa Kintwari milioni mbili. Na Ali(a.s) alisema kumwambia Mtume: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaonaje ukitumia mali hii ikakusaidia katika vita vyako? Mtume hakufanya hivyo. Kisha akamwambia Abubakar nae hakuzitoa. (hadi akasema)

(Amesema Abu waail): Niliketi kwa Shaibah bin Othuman nae akasema Aliketi kwa Omar bin Khattab, akasema: Niliazimia nisibakishe katika nyumba hiyo chembe yoyote ya Dhahabu wala Fedha isipokuwa nitaigawa kati ya Waislaam. Nikasema Hutafanya hivyo?

Akasema: Kwanini nisifanye hivyo?

Nikasema: Sahiba wako hakufanya hivyo.

Akasema: Hao wawili ndio ambao hufuatwa nyendo zao.[16]

Je Kaabah ilikuwa ikifaidika na Dhahabu na Fedha hizo ewe Khalid?

Au -Mwenyezi Mungu -ametakasika na hili- alikuwa akifaidika na vitu hivyo viwili?

KHALID : Hapana.

BAAQIR : Pamoja na hayo Mtume(s.a.w.w) hakuunyoosha mkono wake kwenye mali hiyo iliyo kuwa imelimbikizana, wala hakutumia hata chembe moja ya mali hiyo, pamoja na kuwa wakati ule Uislaam ulikuwa ukihitajia sana mali na pesa nyingi wakati ambapo hazina ilikuwa imejaa, kwa ajili ya kuimarisha nguzo zake katika miji na nchi mbali mbali. Kwa nini hakufanya hivyo? Ni kwa sababu mali hiyo nyingi ilikuwa ni mali ya Kaabah na huiongezea Kaabah utukufu na heba yake machoni mwa watu, japokuwa utukufu na daraja yake ya kweli iko kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, utukufu ambao haupungui wala kuongezeka, sawa iwe na mali zote za dunia, au isiwe na chochote.

Na maneno ni hayo hayo kuhusiana na makuba ya Dhahabu, na milango ya Dhahabu na Fedha, na nguo ifunikwayo juu yake na mapambo yatolewayo zawadi na kupambwa nayo makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu mtukufu kama vile: Amirul-muuminiin, Imam hasan na Imam Husein, Imam Ridhaa na wengineo juu yao rehma na amani. Watu hawa cheo na daraja yao ya kweli waliyo pewa na Mwenyezi Mungu haipungui wala kuzidi kwa kuwepo madini hayo ya thamani kwenye makaburi yao, na wala haipungui ikiwa hayakuwepo, kwa mfano Imam Hasan bin Ali(a.s) ni bora kuliko nduguye Husein(a.s) japokuwa kaburi la Imam Hasan(a.s) hupigwa na jua katika jangwa la Bakii'i likiwa halikujengewa juu yake au juu yake kukiwa hakuna jengo lolote, na likiwa halikupambwa na pambo la aina yoyote, na kaburi la Imam Husein(a.s) lilikuwa na majengo makubwa makubwa ya dhahabu halisi iangazayo angani na kuyaondoa mawingu.

Lakini tumeyafanya hayo kwa ajili yao, na kutoa zawadi ya mapambo ya Dhahabu kwenye makaburi yao, na makuba ya makaburi yao kuyatia dhahabu na mengineyo, yote hayo kwa ajili ya kuwaenzi na kuwatukuza wao.

KHALID : Je vitu hivi vinawapatia hawa utukufu katika macho ya watu?BAAQIR : Ndio. Na hivi sasa nitakufanya ukiri jambo hilo. Kwa mfano ukienda kwa Mayahudi na kuyaona makaburi ya maulamaa wao yakiwa yameharibika, yakipigwa na jua, hakuna kizuizi chochote juu yake au chumba ambacho mwenye kuyatembelea anaweza kujikinga jua kwenye kivuli chake. Kisha ukenda kwa Wakiristo, na ukakuta makaburi ya maulamaa wao yakiwa yamejengewa vizuri na kuhifadhika, yakiwa yamejengewa makuba na yakiwa yamepambwa kwa dhahabu na fedha, na mapambo mengine ya madini mbali mbali. Je ni maulamaa gani utakao waona kuwa ni wenye utukufu, ni maulamaa wa Mayahudi au Wakiristo, pamoja na kuwa unafahamu ya kuwa wewe ni Muislaam na unafahamu ya kuwa wote wawili wako kwenye batili?

KHALID : Bila shaka kutokana na mandhari ya makaburi ya pande mbili niliyo yaona nitachukua picha fulani ya utukufu wa maulamaa wa Wakiristo, na picha ya udhalili wa maulamaa wa Mayahudi.

BAAQIR : Kwa hivyo basi wayafanyayo Mashia na Masunni kwa kujenga madharihi juu ya makaburi, na kujenga haram na makuba na mengineyo juu ya makaburi ya maimamu na Mitume.. ni kwa ajili ya kuwatukuza wao na kuwaenzi, kwa sababu hiyo huyapamba kwa Dhahabu Fedha na mapambo mengine ya madini mbali mbali.

KHALID : Yote hayo ni sahihi lakini je jambo hilo linakitoa kitendo hicho kwenye sifa ya israfu na matumizi mabaya na yasiyo ya lazima?.BAAQIR : Ndio, na zaidi ya hapo. Ikiwa itathibiti kuwa matendo haya ni kuwatukuza mawalii wa Mwenyezi Mungu, wakati huohuo ni kuutukuza Uislaam, kwani kuwatukuza viongozi na watukufu wa Uislaam ni kuutukuza Uislaam, na kila kitu ambacho ndani yake kuna kuutukuza Uislaam basi kitu hicho ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo Mwenyezi Mungu amesema kuhusiana nazo:Kwa hivyo basi kuyapamba makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo ni sunna kuzifanya na kufanya kazi kwa ajili yake, na mtu mwenye kufanya hivyo hupewa thawabu kwa matendo yake hayo. KHALID : Nakuomba samah ani, kwa kuchukua kiasi hiki cha wakati wako lakini mbele ya Mwenyezi Mungu ni mwenye malipo, kwani umenitoa kwenye kiza cha ujinga na kuniweka kwenye nuru ya elimu na ufahamu, ni kwa kiasi gani nilikuwa nikifikiria kuhusiana na upambaji huu wa makaburi na nisielewe siri yake na faida yake na usahihi wake, kwa hakika hivi leo-wewe- umenitia nuru kwa elimu yako hii, na umenifikisha niliko kuwa nikipakusudia.

BAAQIR : Sasa shaka yote uliyo kuwa nayo kuhusiana na kupamba makaburi imetoweka?

KHALID : Ndio.. hakuna shaka yoyote niliyo bakia nayo kwani kufanya hivyo ni sunna na jambo lililo himizwa na Qur'ani tukufu kwa kauli yake Mwenyezi Mungu:

BAAQIR : Alaa ayyi hal (Kwa hali yoyote ele):Hakika mimi niko tayari kufahamiana nawe katika maudhui kama haya ili niweze kufaidika, au wewe pia ufaidike, na wote kwa pamoja tuwe ni wenye kuyafahamu mambo kwa ufahamu mzuri na wenye mazingatio.

KHALID : Ninakushukuru sana sana, na ninamuomba Mwenyezi Mungu mtukufu akuwafikishe kwa yale ayaridhiayo.

7 UKWELI WA USHIA

KUBUSU MADHARIHI (MAKABURI)

MAALIK: Ewe Swaadiq ni sababu gani iwafanyayo kubusu Dharihi ya kaburi la Mtume na maimam na kutoacha kitendo hicho?

SWAADIQ: Je kuna tatizo (ishkali) lolote kufanya hivyo?

MAALIK: Inasemekana kuwa kufanya hivyo ni miongoni mwa matendo ya shirki.

SWADIQ: Nani asemae kuwa kufanya hivyo ni shirki?

MAALIK: Waislaam ndio wasemao hivyo.

SWADIQ: Ajabu! Basi ni watu gani ambao wanabusu madharihi?MAALIK: Inasemekana kuwa ni kikundi kidogo cha Mashia.

SWADIQ: Je umewahi kwenda hija?

MAALIK: Ninamshukuru Mwenyezi Mungu.. ndio nimefanikiwa kwenda hija.

SWADIQ: Je umelitembelea kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) katika mji wa Madinah?

MAALIK: Ninamshukuru Mwenyezi Mungu nimefanikiwa kulitembelea.SWAADIQ: Je hukuwaona maelfu ya waislaam wa madhehebu ya sunni wakikusudia na kutaka kulibusu dharihi la kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu na huku wakipigwa na walinzi wa kikundi cha (Hay'atu amri bil-maarufi)?!!

MAALIK: Ndio..

SWAADIQ: Kwa maana hiyo si sisi Mashia pekee tunao busu madharihi ya Mitume wa Mwenyezi Mungu, bali waislaam wote huyabusu.

MAALIK: Sasa kwanini baadhi wanasema kuwa kufanya hivyo ni haram, na kwamba kufanya hivyo ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu?

SWAADIQ: Hawa ni watu wachache wa kikundi fulani kati ya makundi ya waislaam, wajionao kuwa wao ndio wenye haki, na kwamba wao ndio waislam wa kweli na wanawaona waislaam wengine kuwa ni makafiri na washirikina wanamuabudu asie kuwa Mwenyezi Mungu, na hawawaoni watu wengine kuwa ni waislaam walio kosea, kwa hivyo ndio maana huwaona wakiyakufurisha madhehebu (makundi) mengine yote ya kiislaam. Je hukuona ile kamati ya (Al-amri bil-maarufi)!! katika nchi ya Hijazi wakimpiga anaekusudia na kutaka kubusu dharihi la kaburi la Mtume(s.a.w.w) na kumwambia:Ewe kafiri! Ewe mshirikina! Ewe zindiki! Ewe nguruwe! Ewe mbwa! Na mengineyo kati ya aina mbali mbali za matusi na tuhuma zilizo mbaya kabisa.

Na matusi hayo humuelekea kila mtu: Sawa awe Shia, Hanafiy, Maalikiy, Shafiiy, Hanbaliy, Zaydiah, na waislaam wengine..[17]

MAALIK: Ndio.. yote hayo nimeyaona, na yaliyo mabaya zaidi kuliko hayo: Kwa hakika mimi niliwaona wakimpiga kichwani mtu mmoja alie ng'ang'ania kufanya hivyo kwa fimbo kiasi kwamba huenda pigo hilo lilipelekea kumpasua na kutoka damu, na wakati mwingine huwapiga kwa mikono yao-kwa nguvu- na wakiwapiga vifuani waislaam walio kuja kufanya ziara mapigo ambayo huwaumiza na kuwadhuru vifua vyao na kuwasababishia maumuvu na maradhi miili yao! Na ni kwa kiwango gani niliumia kwa kuyao mambo hayo na vitendo hivyo!!.

Hija ambayo Mwenyezi Mungu ameifanya kuwa ni kongamano la waislaam wote ulimwenguni ili waweze kuzungumza katika kongamano hilo kuhusu mambo yao mbali mbali, hivi leo imekuwa ni mahala pa kutia tofauti kati ya waislaam kutokana na matendo ya kikundi hicho kidogo kinacho jiita kuwa ni (hay'atul-amri bil-maaruf wannahyi anil-munkar)!!!.SWAADIQ: Ala ayyi hal, ewe Maalik.. je wewe unambusu mwanao?MAALIK: Ndio!

SWADIQ: Je unamshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu kwa kumbusu mwanao?

MAALIK: Hapana, hapana.. kamwe simshirikishi Mwenyezi Mungu.SWADIQ: Vipi usimshirikishe Mwenyezi Mungu kwa kumbusu mwanao?MAALIK: Kwa hakika mimi ninambusu mwanangu kwa ajili ya mapenzi yangu kwake, na hilo si shirki.

SWADIQ: Je wewe unaibusu Qur'ani?

MAALIK: Ndio.

SWADIQ: Je kwa kufanya kwako hivyo humshirikishi Mwenyezi Mungu?

MAALIK: Hapana.

SWADIQ: Je jalada la Qur'ani unalo libusu si ngozi ya mnyama?MAALIK: Ndio.

SWADIQ: Kwa hivyo wewe unamshirikisha Mwenyezi Mungu, na unaifanya ngozi ya mnyama kuwa ni mshirika wa Mwenyezi Mungu.. ametakasika Mwenyezi Mungu na hilo.

MAALIK: Si hivyo. Kwa hakika mimi ninaibusu Qur'ani kwa sababu imekusanya maneno ya Mwenyezi Mungu, kutokana na mapenzi ya maneno ya Mwenyezi Mungu ndio maana ninalibusu jalada lililo ifunika Qur'ani hiyo, na hii ni kutokana na mapenzi mengi, na wingi wa shauku yangu kwa Qur'ani, ni tofauti iliyoje kati ya kitendo hiki na kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

Kisha ninapo ibusu Qur'ani ninapata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa kufanya hivyo, kwa sababu kuibusu Qur'ani ni kuitukuza na kuienzi na kuiinua daraja yake, na kuitukuza Qur'ani kuna thawabu na malipo mbele ya Mwenyezi Mungu, kwa hivyo ni tofauti iliyoje iliyopo kati ya tendo hili na kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

SWADIQ: Kwa nini maneno kama hayo usiyasema katika kubusu dharihi la Mtume(s.a.w.w) na madharihi ya maimam(a.s) [18] au unadai ya kuwa wale ambao wanabusu madharihi huvifanya vyuma hivyo kuwa ni washiriki wa Mwenyezi Mungu mtukufu?! Ikiwa ni hivyo kwanini hawabusu vyuma mbali mbali vilivyoko huku na kule katika ardhi? Lakini..kutokana na ukweli kuwa dharihi hilo limefunika kaburi la Mtume(s.a.w.w) au kaburi la mmoja wapo kati ya maimamu(a.s) , kutokana na mapenzi ya Mtume(s.a.w.w) na maimamu na kutokana na shauku yao kwao ndio maana wanalibusu dharihi la kaburi lake kwa sababu wao hawawezi kumfikia Mtume na imamu mwenyewe(a.s).

Pamoja na kufanya kwao hivyo hakika wao hupata malipo kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, na hupawa thawabu kwa kufanya hivyo, kwani kulibusu dharihi la mtu fulani ni kumtukuza mtu yule. Na kumtukuza Mtume(s.a.w.w) au mmoja wapo kati ya maimamu(a.s) , ni kuutukuza Uislaam ambao huyu alikuwa ni Mtume wake(s.a.w.w) au alikuwa ni imamu wake alie kuwa akilingania watu kwenye Uislaam huo.

Na jambo lolote litakapo kuwa na sura ya kuutukuza Uislaam basi jambo hilo ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo amezizungumzia kwa kusema:suratul-haji aya 32.

MAALIK: Ikiwa ukweli ni huo basi kwanini baadhi ya watu wanasema kuwa nyinyi ni wenye kumshirikisha Mwenye zi Mungu?

SWAADIQ: Imepokelewa katika Hadithi tukufu kama ifuatavyo:(Kwa hakika matendo hufanyika kutokana na Nia) [19] ikiwa mtu yeyote anabusu dharihi na katika kubusu kwake huko anakusudia kumshirikisha Mwenyezi Mungu bila shaka mtu huyo ni mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu (mshirikina). Na ikiwa kubusu huku kunatokana na mapenzi mengi, na kwa ajili ya kupata thawabu kwa ajili ya kuadhimisha na kutukuza shiari za Mwenyezi Mungu kwa kufanya hivyo, basi hupewa thawabu yule mwenye kuyatekeleza matendo hayo. Na wewe waulize wote wale ambao wanayabusu madharihi kati ya Mashia na Masunni kama ifuatavyo: Kwa nini mnabusu madharihi?

Hata kujibu yeyote kati yao isipokuwa kwa kusema tunafanya hivyo kutokana na mapenzi makubwa na shauku kubwa tuliyo nayo na kwa ajili ya kupata thawabu, na huwezi kumsikia yeyote kamwe-bila shaka yoyote- akisema ya kuwa anabusu dharihi kwa ajili ya jambo lingine tofauti na hili tulilo litaja.

MAALIK: Ni kweli, maneno yako ni sahihi.

SWADIQ: Na ikiwa kubusu peke yake bila kukusudia kumshirikisha Mwenyezi Mungu kunamfanya mtu kuwa mshirikina, bila shaka huwezi kumpata mwanadamu yeyote asie mshirikina, kwani waislaam imma wanabusu madharihi, au wanabusu Qur'ani.. kwa msingi wa hali mbili hizi wao-wote-ni washirikina. Sasa ikiwa hali ni kama hiyo Muislaam ni nani?

MAALIK: Ninakushukuru sana, na kwa hakika mimi nitafanya mazungumzo na majadiliano na baba yangu alie kuwa akinilisha na kunifundisha mambo kama haya ya asabia yasiyo na maana yoyote, na sinto sikiliza maneno ya mtu yeyote wa madhehebu mengine, kwa hakika nimefahamu ya kuwa haki na ukweli uko pamoja nanyi-nyinyi Mashia- na wewe unahaki juu yangu milele, kwa sababu umenionyesha njia, si katika jambo hili tu bali katika mambo yote, ili nisifuate kila kinifikiacho masikioni mwangu, bila ya kufikiria kuhusu usahihi wake na ubatilifu wake.

5 UKWELI WA USHIA

KUYAJENGEA MAKABURI

FUADI : Ewe Jaafar, je unaniruhusu nikuulize kuhusiana na maudhui ya Shia na Sunni?[13]

JAAFAR : Uliza kwani nina penda sana kila mtu awe ni mwenye kufahamu mambo, mwenye elimu na anae fahamu mambo kutokana na utafiti na kwa kupata yakinina hawi ni mwenye msimamo legelege na mwenye kufuata kila akisikiacho na kipepeacho angani, au kila sauti ijitokezayo na kutangaa anganibila ya kufahamu usahihi wake na ubatilifu wake au ufisadi wake.

FUADI : Je maneno yangu utayaamini ikithibitika kuwa sisi (Ahli sunna) ndio wenye haki?

JAAFAR : Kwa hakika mimi niko msitari wa mbele kati ya wale wenye kuamini mambo ya kweli haraka pale wanapo yafahamu, na mimi sikushikamana na ushia isipokuwa ni baada ya kuuona kuwa ni haki na wewe unafahamu ya kuwa baba yangu na mama yangu na ndugu zangu na watu wa kabila langu wote ni masunni na kati yao hakuna Shia hata mmoja, na mimi sikufuata Ushia isipokuwa ni kwa ajili ya ukweli nilio uona na kuukuta ndani ya madhehebu hayo.. na lau nitafahamu usahihi wa maneno yako mimi ni wa mwanzo kuyaamini.

FUAD : Nyie Mashia mnayajengea makaburi ya Manabii, Maimamu, Maulamaa na watu wemamajengo makubwa, mnasali kwenye makaburi, wakati jambo hilo ni shirki, kama washirikina wanavyo abudu masanamu nanyi Mashia mnaaabudu majengo ya makaburi ya mawalii.

JAAFAR : Ni wajibu sisi tuwe wakweli na tunao kwenda sambamba na uhakika wa mambo, tusiwe ni watu wachukuao maganda na kuacha kiini, tusiangalie yasemwayo na fulani au fulani, bali tuangalie ukweli ulio wazi katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake(s.a.w.w) , na mwenendo wa watu wema walio tangulia.

FUAD : Ndio, nami ni hivyo hivyo, ninapenda kufahamu ukweli wa mambo kupitia njia za kielimu na ufahamu sahihi, si kufuata mambo ufuataji wa kipofu.

JAAFAR : Kwanza kabisa: Sio sisi Mashia pekee tuhusikao na suala la kuyajengea makaburi, kwani waislaam wote wanayajengea makaburi ya Manabii na Maimam na wanazuoni wakubwa au viongozi wao, na ifuatayo ni mifano juu ya hayo: Kaburi la Mtume(s.a.w.w) na makaburi ya makhalifa wawili bado hadi hivi sasa yamejengewa kwa jengo kubwa na yenye kuba kubwa na ya hali ya juu kabisa.

Makaburi ya Mitume kadhaa, kama vile kaburi la Nabii Ibrahim(a.s) lililoko Jodan katika mji wa (Al-khaliil) makaburi hayo yana dharihi (yamejengewa) na juu yake kuna kuba na majengo makubwa. Kaburi la Nabi Mussa(a.s) lililoko Jodan kati ya mji wa (Qudsi) na (Omman) lina jengo kubwa. Kaburi la Abi Hanifa lililoko Baghdad hadi leo bado limejengewa kwa jengo kubwa, na juu yake kuna kuba. Kaburi la Abi Hurairah katika (Misri) hufanyiwa ziara na limejengewa na juu yake kuna kuba. Kaburi la Abdul-qaadir lililoko (Baghdaad) kaburi hilo lina uwanja mkubwa na dharihi na juu yake kuna kuba.

Na makaburi mengine ya Mitume, na makaburi ya Maimamu na wanazuoni wakubwa wa madhehebu, yote hayo yana majengo na juu yake kuna kuba, na yana waqfu maalum ambapo waqfu hizo faida zake hutumika kuyaimarisha na kuyakarabati makaburi hayo na kuyalinda yasiharibike.

Na Miji ya kiislaam imejawa na majengo kama hayo.. na Waislaam wote pamoja na tofauti za madhehebu yao tangu siku ya kwanza hadi leo huyapenda mambo hayo, na huwaamrisha watu kuyatekeleza hayo, na hawakukataza kufanya hivyo hata siku moja, kwa hivyo si sisi Mashia pekee tuhusikao na hukumu hii, bali wanakubaliana nasi na kuwafikiana nasi Waislaam wengine wote, na wao pia huyajengea makaburi ya maimamu wao na wakati wote huyatembelea.

Pili: Sisi- Mashia- au waislaam wengine wakati tunapo Sali pembezoni mwa makaburi ya mawali, hatusali kwa ajili ya mawalii hao bali tunasali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee. Na liwezalo kukujulisha hilo ni kuwa sisi tunapokuwa katika sala huelekea kibla na wala hatuyaelekei makaburi hayo, na lau kama tunge kuwa tukiyasalia makaburi yale, na kuelekea kwenye ibada zatu kwenye dharihi zile (majengo yale ya makaburi), ingewajibika kuyaelekea, na tusinge elekea kwenye kibla.

FUAD : Kwa nini mnasali nyuma ya makaburi hayo, mpaka mkayafanya kuwa ni kibla chenu?

JAAFAR : Hakika sisi wakati tunapo Sali nyuma ya makaburi, tunaelekea kibla na wala hatuyaelekei makaburi, bali makaburi yale-imetokea tu- yakawa mbele yetu, bila ya sisi kukusudia kuyaelekea.

Na hili halitokei isipokuwa kwa mtu anae Sali akiwa ameelekea kibla katika sehemu fulani na ikatokea kwa mfano kukawa na jengo kubwa mbele yake, je kusali katika sehemu hiyo kunamaanisha kuwa mwenye kusali anaabudu jengo hilo?! Na zaidi ya hayo Maulamaa wote wa Waislaam wanasema kuwa: Inajuzu kusalia katika majumba ya ibada za washirikina hali ya kuwa umeelekea kibla hata kama mbele ya mwenye kusali kutakuwa na sanamu lenye kuabudiwa kinyume cha Mwenyezi Mungu, Kwani mwenye kusali humuelekea Mwenyezi Mungu na wala halielekei sanamu. Je hii inamaana kuwa mwenye kusali analiabudu sanamu lile?

FUAD : Ikiwa kuyajengea makaburi si shirki- kama unavyo sema- na waislam wote wanasema ya kuwa inajuzu kufanya hivyo, ilikuwaje wakavunja madharihi (majengo ya makaburi) na makuba yaliyo jengwa juu ya makaburi ya maimamu na wengineo, kwa hoja ya kuwa kufanya hivyo ni shirki na ni kumuabudu asie kuwa Mwenyezi Mungu, na maulamaa wa Hijazi wakatoa fat'wa ya kufanya hivyo?

JAAFAR : Kwa hakika ni baadhi tu walio toa fat'wa kama hiyo kati ya maulamaa wa Hijazi katika zama zile, kwani kuna baadhi ya Mashekhe waishio katika mji wa Madina walio nihadithia na kunisimulia kwa kusema: Kwa hakika wakati huo walipo toa amri ya kubomoa makuba na majengo ya makaburi, maulamaa wenyewe wa Hijazi walipinga amri hiyo, wakitoa hoja kuwa hilo si shirki bali vitu kama hivyo ni sunna katika sheria ya kiislaam, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:jambo lililo pelekea kufukuzwa kwa maulamaa wale, na kuwauz ulu wengine katika nyadhifa zao na kuwatenga. Kwa hivyo basi: Fat'wa hiyo haikutolewa isipokuwa na baadhi tu ya maulamaa wa Hijaz.

FUAD: Kwa hakika mimi nilikuwa nikifikiria na kujiuliza ya kuwa: Ikiwa kujenga madharihi na makuba ni haram na shirki, kwa nini maulamaa wa Waislaam hawakuzinduka na kuliona hilo tangu zama za Mtume(s.a.w.w) hadi leo, na kwanini hawakuzuwia kufanya hivyo? Na ilikuwaje Waislaam wasilifahamu hilo kwa muda wa karne kumi na tatu?

JAAFAR: Nitakuongezea elimu na maarifa: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alikiri na kukubali kujengea makaburi, madharihi na makuba na hakukataza kufanya hivyo. Kwa mfano hili ni jengo la hijri Ismail mahala alipo zikwa Nabi (Ismail) na sehemu alipo zikiwa mama yake Haajar. Na haya hapa makaburi ya Manabii wengine-kama Ibrahim Musa na wengineo- walio zikiwa pembezoni mwa baytul-maqdas, yalikuwa ni yenye majengo makubwa katika zama za Mtume(s.a.w.w) na hadi zama zetu hizi, na wala hakuzuwia yeyote si Mtume Mwenyewe (s.a.w) wala mmoja wapo kati ya makhalifa wake.

Na lau kama tendo hilo linge kuwa haram au linge kuwa ni shirki basi Mtume ange amuru kuvunjwa na kubomolewa kwa majengo na makuba hayo, na ange kataza kufanya hivyo. Na kutokana na ukweli kuwa hakufanya hivyo tunafahamu na kuwa na yakini ya kuwa mfano wa vitu kama hivyo au kufanya hivyo ni kitu kinacho juzu na kinafaa.

Hivyo hivyo baada ya kufariki Mtume(s.a.w.w) , kwani Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo chukuliwa roho yake alizikwa katika chumba chake, na mlango wa chumba kufungwa, na kaburi lake likawa katikati ya chumba kilicho jengewa kuta na dari, na lau kama sahaba yeyote ange sikia kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kuwa tendo kama hilo ni haram basi wasinge thubutu kumzika Mtume katika chumba hicho kilicho jengewa, na lau kama ingelazimika kumzika chumbani mwake basi ingekuwa wajibu kubomoa chumba hicho ili kaburi hilo lisiwe na jengo au lisiwe ni lenye kujengewa.

Na kutokana na kutofanya kwao hivyo, tukafahamu ya kuwa kujenga juu ya makaburi si haram, sasa vipi itakuwa ni shirki?.

FUAD: Ninakushukuru kwa wema wako kwani umeniongoza kwenye ukweli (haki), na kunijulisha ya kuwa kujenga juu ya makaburi si haram wala shirki, na kwamba wale ambao wanaharamisha jambo hilo hawana dalili yoyote katika sheria wawezayo kuitegemeza kwayo kauli yao.Na kwa hakika mimi nitakushukuru daima juu ya hili.

JAAFAR: Nami ninakushukuru kwa kukubali kwako ukweli na haki baada ya kuifahamu, na kuufuata kwako uongofu pale ulipo uona, kwani wewe ni mwenye kufuata muongozo wa akili na mantiki sahihi, kwa hivyo basi ninapenda kukuzidishia maarifa zaidi kuhusiana na haki na ukweli, na kukupatia maarifa mbali mbali katika dini, je unawakati zaidi ili niweze kuzungumza na wewe?

FUAD: Kwa hakika mimi ninapenda sana maneno ya kweli, zungumza ulitakalo, hakika mimi niko tayari kukusikiliza na kuyajaza masikio yangu kwa maarifa.

JAAFAR: Kutokana na mazungumzo yetu yaliyo pita imethibiti kuwa kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni jambo linalo faa na inajuzu kufanya hivyo, na jambo hilo si haram.

FUAD: Ndio.. nami niko pamoja nawe katika hilo.

JAAFAR : Hivi sasa nataka kusema hivi: Hakika kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu na kuweka madharihi juu yake na kujenga makuba.. yote hayo ni sunna, hupewa thawabu mwenye kuyafanya hayo yote, si tu kwamba inajuzu.

FUAD : Vipi inakuwa sunna?

JAAFAR : Mwenyezi Mungu mtukufu amesema:( Na anayeziheshimu alama za Mwenyeezi Mungu basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo). Kwa hivyo kila kitu ambacho huzing atiwa na kuhesabiwa kuwa ni katika shiari za Mwenyezi Mungu kukitukuza ni sunna katika Uislaam.

FUAD: Ndio..lakini vipi itakuwa kujenga juu ya makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni katika shiari za Mwenyezi Mungu?

JAAFAR: Shiari ni vitu ambavyo huitukuza dini katika mtizamo wa ulimwengu bila kuwepo dalili juu ya uharamu wake.

FUAD: Je dini hutukuzwa kwa majengo na makuba hayo?

JAAFAR : Ndio.

FUAD: Ki vipi?

JAFAAR: Kujengea makaburi ya maulamaa na viongozi watukufu wa kiislaam, na kujenga makuba juu yake, na kuyahifadhi yasiharibike na yasibomoke, ni kuwatukuza watukufu hao bila shaka yoyote. Kwa mfano: Akijitokeza mtu fulani na kupanda uwa waridi kwenye kaburi la mtu alie kufa, je mtu huyu haonekani kuwa amemtukuza maiti yule, na kuwa amemuenzi?

FUAD : Ni sahihi.

JAAFAR : Vipi ikiwa atajenga juu ya kaburi lake jengo kubwa na kuweka kuba juu yake, hakika kufanya hivyo ni kumtukuza na kumuenzi maiti huyo bila shaka yoyote. Na kuwatukuza viongozi na maulamaa wa kiislaam pia maimamu na mawalii.. ni kuutukuza Uislaam, na kuitukuza na kuienzi dini ambayo watu hawa walikuwa wakiilingania, na wakiwaelekeza watu kwenye dini hiyo. Je mtu fulani anapo mtukuza Raisi wa chama fulani, au walinganiaji wa itikadi za chama hichohuzingatiwa kuwa ni mwenye kukitukuza chama kile na itikadi ile au laa?

FUAD: Ndio ni kama usemavyo.

JAAFAR: Kwa hivyo basi kuyajengea makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni kuwatukuza wao na kumtukuza Mwenyezi Mungu, na ni kuuinua na kuutukuza Uislamm, na kila kitu ambacho kukifanya kutakuwa ni kumtukuza Mwenyezi Mungu na ndani yake kuna kuuinua Uislaam, kitu hicho ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo anahimiza kuzifanya, kwani anasema:Suratul- haji aya 32.

FUAD: Kwa hivyo..kuvunja na kubomoa maka buri ya mawalii na Mitume na maimam, inakuwa ni kuidhalilisha dini, na kuutia dosari utukufu wa kiislaam.. kwani kuyabomoa ni kuwadharau viongozi wetu, na ni kuwahini wao.. na kuwahini wao ni kuihini dini, na kuutia dosari utukufu wao ni kuutia dosari utukufu wa Uisalaam.

JAAFAR: Na mimi pia nimekuwa Shia, na nimefuata madhehebu ya Ahlil-bayti (a.s) na nimebadilisha jina kutoka jina la Waliid na kuwa Jaafarkwa sababu hii hii? Kwa hakika mimi wakati nilipo kuwa nikifuata rai za watu wengine sikuwa nikidha nia ya kuwa hakuna alie kwenye haki kinyume changu mimi, lakini nimeitafuta haki na kuifuata hadi kuifikia. Na mtu wakati wote anapo acha nyuma na kuzitupilia mbali asabia za madhehebu, na kukifungua kifua chake kwa ajili ya kuikubali haki, na kuitafuta haki.. hapana budi ataifikia haki hiyo na kuipata.

FUAD: Mimi, na baada ya msimamo na mawkifu haya, nitakuwa makini katika mambo mbali mbali, na nitakuwa ni mwenye kuitafuta haki, mpaka niweze kuifuata haki kokote nitako ikuta. Na kwa hakika nitakushukuru kwa muda wote.. Basi niruhusu nende zangu kwani nina ahadi na mtu fulani.

JAAFAR: Nenda, Mwenyezi Mungu akulinde.

FUAD : Fii amani llahi.

JAAFAR : Uwe katika amani ya Mwenyezi Mungu.

Abu haatam Ar-raziy katika kitabu chake (Az-ziinah) anasema: Kwa hakika jina la kwanza lililo dhihiri katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu ni Shia, na jina hili ndilo lililo kuwa jina mashuhuri (Laqab) la masahaba wane nao ni: Abu Dharri Salman Miqdaad na Ammar.

Na Shekh Mohammad Husein Kaashiful-Ghitaa katika kitabu chake kiitwacho (Aslush-shia wa Usuuliha) anasema: Hakika mbegu ya mwanzo ya Ushia iliwekwa na kupandikizwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) tangu zama za mwanzo kuanza kueneza Uislaam bila ya kutofautisha kati ya vitu viwili hivyo na vikiwa sawa.

Na ushahidi ni hadithi zake tukufu si kupitia njia za Mashia na upokezi wa wapokezi wa Kishia Imamiyyah pekee bali ni hadithi za maulamaa wa kisunni na wanazuoni wao na kupitia njia zao wanazo ziamini ambazo hazidhaniwi kuwa zina chembe ya uongo, na katika hadithi hizo ni hadithi iliyo pokelewa na Suyuut katika kitabu chake (Ad-durrul-manthuur fii tafsiri kitabillahi bil-ma'athur) katika kuitafsiri kauli yake Mwenyezi Mungu mtukufu:(Hao ndio viumbe bora) (suratul bayyinah aya 7). Ame sema: Ametoa hadithi Ibn Asakir kutoka kwa Jaabir bin Abdillahi amesema: Tulikuwa kwa Mtume(s.a.w.w) mara akatokea Ali na kuingia na Mtume(s.a.w.w) akasema: Nina apa kwa haki ya yule ambae nafsi yangu iko mikononi mwake hakika huyu na wafuasi (Mashia) wake ndio walio faulu na kufuzu siku ya kiama. Na hapo ikatelemka aya isemayo:(Hakika wale ambao waliamini na kufanya matendo mema hao ndio viumbe bora). (Suratul-bayyinah aya 7). Ibnu Hisham katika Siir atun-nabawiyyah anasema:Hakika umma wa kiarabu uligawanyika katika makundi mawili Masunni na Mashia tangu siku ya Sakifa.

Muhammad Abu Zuhra anasema katika kitabu chake kiitwacho Taarikhul-madhaahibil-islaamiyyah:(Ushia ni madhehebu ya kiislaam ya kisiasa ya tangu muda mrefu na Mashia walidhihiri na madhehbu yao hayo tangu mwishoni mwa zama za Uthuman na kukua na kupata nguvu katika zama za ukhalifa wa Ali, kwani kila alipo pata nafasi ya kuchanganyika na watu walizidi kupendezewa na kuvutiwa kutokana na kipawa chake na kutokana na nguvu ya Imani yake ya dini na elimu yake).

Ibnu Abil-hadiid anasema katika kitabu chake Sharhu Nahjul-balagha:(Hakika Mashia katika zama za dola na utawala wa Muawia walikuwa wakifadhilisha kuitwa Al-kitabiy na wasiitwe Shia. Kwani Ushia anwani yake na shiari yake ni kushikamana na Ahlul-bayti na kufuata elimu yao na kujiepusha na watu wa Bidaa (Uzushi) na kushikamana na kizazi kitwaharifu na kilicho pambika na tabia njema na bora kabisa) (Rejea kitabu Taarikhul-firaqil-islaamiyyah cha Shekh Muhammad Khaliil Az-zayni ukurasa wa 108-109).

Neno Sunnah: Lenye shadda, asili ya neno hilo ni njia, na neno hilo limepanuka maana yake katika makundi tofauti, na linapo tumika huwa lina maana ya aliyo yafanya Mtume (s.a.w) kama kauli vitendo au aliyo yakataza na kuyakemea, na hutumika katika maana hizo kupitia ndimi za wanazuoni na hadithi za Mtume(s.a.w.w) . Na katika zama za hivi karibuni neno Sunnah limekuwa likitumika katika mukabala wa neno Shia, na Husemwa: As-sunnatu wal-jamaah katika mukabala wa watu maalum, na katika ufahamu wa Shekh wa madhehebu ya Hanbali Ibnu Taimiyyah: Neno Sunnah: lina maana ya kumpenda Ali Uthmani na kumtanguliza Abubakar na Omar kwa wawili hao walio tangulia.

Na madhehebu yalipokithiri na makundi kuwa mengi, baadhi wakashikamana na rai isemayo kuwa tamko Sunni lilikuwa likitumika kwa mtu ambae anafuata dini kwa kuwapenda na kuwatawalisha mashekhe wawili, (Abubakar na Omar), na ilikuwa ikisemwa Sunaatul-umariyyh) Rejea kitabu Tariikhul-firaqil-islaamiyyah ukurasa 44-45).

6 UKWELI WA USHIA

KUPAMBWA KWA MAKABURI YA MAIMAM

KHALID : Salaamun alaykum.

BAAQIR : Wa alaykumus-salaam warahmatullahi wabarakatuhu.KHALID : Umefanya vizuri umekuja lini?

BAAQIR : Nimekuja kumtembelea mtoto wa ami yangu anaishi hapa.KHALID : Nakuomba leo hii ukaribie nyumbani kwetu.

BAAQIR : Kwa hakika ninakazi nyingi nilizo ziacha kwa ajili ya kuwatembelea ndugu (kuunga udugu) na kuomba unisamehe sana kwa wito huo.

KHALID : Haiwezekani..marafiki wawili baada ya kutengana kwa muda wa miaka kumi wanakutana kisha wasibakie na kufuatana walau kwa muda wa saa moja. Hakika mimi -pia nina haki ya udugu wa kiislaam. Kisha kulitokea mazungumzo kati yangu na ndugu yangu mmoja muumini kuhusiana na maudhui ya Shia na Sunna na kutokana na kuwa mimi ninamatumaini na imani na wewe ninataka na ninakusudia kufanya mazungumzo na wewe kuhusu maudhui hayo ili niweze kuelewa ukweli na uhaki katika maudhui hayo.

BAAQIR : Hakuna shaka. Walifuatana pamoja hadi nyumbani kwa Khalid, na kufika nyumbani kwake, na kila mmoja akaketi pembezoni mwa mwenziwe. Na baada ya kuzungumza kuhusiana na mambo yanayo wahusu na yaliyo maalum kwa ajili yao wawili, Baaqir akamuwahi mwenzie kwa kumuuliza swali na kusema: Ni mazungumzo gani yaliyo fanyika kati yenu?

KHALID : Mazungumzo yalikuwa yakihusiana na kuyapamba makaburi ya Manabii, maimam, maulamaa, waumini na watu wema na mfano wa hao, kwa Dhahabu na Fedha na mapambo mengineyo.

BAAQIR : Ni tatizo gani lililopo kuhusiana na jambo hilo?

KHALID : Je kufanya hivyo si haram?

BAAQIR : Kwanini iwe haram?

KHALID : Je maiti anafaidika na mapambo hayo?

BAAQIR : Hapana, hafaidiki nayo.

KHALID : Kwa hivyo, hayo yote ni Israfu na matumizi mabaya, na Mwenyezi Mungu anasemaWala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu. Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu za mashetani. suratul- israai aya 26-27.

BAAQIR : Unasemaje kuhusiana na nguo ifunikwayo juu ya Kaaba na mapambo yake, na Dhahabu Fedha na vitu ambavyo vipo juu ya Kaaba na ndani ya Kaabah?

KHALID: Sijui.

BAAQIR : Ndio, Kaaba ina nguo ambayo hufunikwa juu yake, na kuna Dhahabu nyingi, ambayo watu huitoa zawadi kwa ajili ya Kaaba kutoka sehemu tofauti za Dunia tangu zama za ujahilia hadi katika zama zetu hizi. Ibnu Khaladuni[14] anasema katika utangulizi wa kitabu chake:

[15] Kwa hakika tangu zama za Ujahilia kaumu mbali mbali walikuwa wakiitukuza Kaaba, na wafalme walikuwa wakituma mali na vitu vya thamani kwenye nyumba hiyo kama vile Kisraa na wengineo, Na kisa cha mapanga na nguo zilizo fumwa kwa dhahabu, vitu ambavyo Abdulmutwalib alivikuta chini alipo chimba kisima cha Zamzam ni maarufu sana).

Na Mtume(s.a.w.w) alipo ikomboa Makka alikuta katika kisima kirefu kukiwa na Awqiyah sabini elfu za Dhahabu vitu ambavyo wafalme walikuwa wakizitoa zawadi kwa ajili ya nyumba ya Allah. Na kulikuwa na dinari milioni moja, yaani zenye uzito wa Kintwari milioni mbili. Na Ali(a.s) alisema kumwambia Mtume: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaonaje ukitumia mali hii ikakusaidia katika vita vyako? Mtume hakufanya hivyo. Kisha akamwambia Abubakar nae hakuzitoa. (hadi akasema)

(Amesema Abu waail): Niliketi kwa Shaibah bin Othuman nae akasema Aliketi kwa Omar bin Khattab, akasema: Niliazimia nisibakishe katika nyumba hiyo chembe yoyote ya Dhahabu wala Fedha isipokuwa nitaigawa kati ya Waislaam. Nikasema Hutafanya hivyo?

Akasema: Kwanini nisifanye hivyo?

Nikasema: Sahiba wako hakufanya hivyo.

Akasema: Hao wawili ndio ambao hufuatwa nyendo zao.[16]

Je Kaabah ilikuwa ikifaidika na Dhahabu na Fedha hizo ewe Khalid?

Au -Mwenyezi Mungu -ametakasika na hili- alikuwa akifaidika na vitu hivyo viwili?

KHALID : Hapana.

BAAQIR : Pamoja na hayo Mtume(s.a.w.w) hakuunyoosha mkono wake kwenye mali hiyo iliyo kuwa imelimbikizana, wala hakutumia hata chembe moja ya mali hiyo, pamoja na kuwa wakati ule Uislaam ulikuwa ukihitajia sana mali na pesa nyingi wakati ambapo hazina ilikuwa imejaa, kwa ajili ya kuimarisha nguzo zake katika miji na nchi mbali mbali. Kwa nini hakufanya hivyo? Ni kwa sababu mali hiyo nyingi ilikuwa ni mali ya Kaabah na huiongezea Kaabah utukufu na heba yake machoni mwa watu, japokuwa utukufu na daraja yake ya kweli iko kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, utukufu ambao haupungui wala kuongezeka, sawa iwe na mali zote za dunia, au isiwe na chochote.

Na maneno ni hayo hayo kuhusiana na makuba ya Dhahabu, na milango ya Dhahabu na Fedha, na nguo ifunikwayo juu yake na mapambo yatolewayo zawadi na kupambwa nayo makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu mtukufu kama vile: Amirul-muuminiin, Imam hasan na Imam Husein, Imam Ridhaa na wengineo juu yao rehma na amani. Watu hawa cheo na daraja yao ya kweli waliyo pewa na Mwenyezi Mungu haipungui wala kuzidi kwa kuwepo madini hayo ya thamani kwenye makaburi yao, na wala haipungui ikiwa hayakuwepo, kwa mfano Imam Hasan bin Ali(a.s) ni bora kuliko nduguye Husein(a.s) japokuwa kaburi la Imam Hasan(a.s) hupigwa na jua katika jangwa la Bakii'i likiwa halikujengewa juu yake au juu yake kukiwa hakuna jengo lolote, na likiwa halikupambwa na pambo la aina yoyote, na kaburi la Imam Husein(a.s) lilikuwa na majengo makubwa makubwa ya dhahabu halisi iangazayo angani na kuyaondoa mawingu.

Lakini tumeyafanya hayo kwa ajili yao, na kutoa zawadi ya mapambo ya Dhahabu kwenye makaburi yao, na makuba ya makaburi yao kuyatia dhahabu na mengineyo, yote hayo kwa ajili ya kuwaenzi na kuwatukuza wao.

KHALID : Je vitu hivi vinawapatia hawa utukufu katika macho ya watu?BAAQIR : Ndio. Na hivi sasa nitakufanya ukiri jambo hilo. Kwa mfano ukienda kwa Mayahudi na kuyaona makaburi ya maulamaa wao yakiwa yameharibika, yakipigwa na jua, hakuna kizuizi chochote juu yake au chumba ambacho mwenye kuyatembelea anaweza kujikinga jua kwenye kivuli chake. Kisha ukenda kwa Wakiristo, na ukakuta makaburi ya maulamaa wao yakiwa yamejengewa vizuri na kuhifadhika, yakiwa yamejengewa makuba na yakiwa yamepambwa kwa dhahabu na fedha, na mapambo mengine ya madini mbali mbali. Je ni maulamaa gani utakao waona kuwa ni wenye utukufu, ni maulamaa wa Mayahudi au Wakiristo, pamoja na kuwa unafahamu ya kuwa wewe ni Muislaam na unafahamu ya kuwa wote wawili wako kwenye batili?

KHALID : Bila shaka kutokana na mandhari ya makaburi ya pande mbili niliyo yaona nitachukua picha fulani ya utukufu wa maulamaa wa Wakiristo, na picha ya udhalili wa maulamaa wa Mayahudi.

BAAQIR : Kwa hivyo basi wayafanyayo Mashia na Masunni kwa kujenga madharihi juu ya makaburi, na kujenga haram na makuba na mengineyo juu ya makaburi ya maimamu na Mitume.. ni kwa ajili ya kuwatukuza wao na kuwaenzi, kwa sababu hiyo huyapamba kwa Dhahabu Fedha na mapambo mengine ya madini mbali mbali.

KHALID : Yote hayo ni sahihi lakini je jambo hilo linakitoa kitendo hicho kwenye sifa ya israfu na matumizi mabaya na yasiyo ya lazima?.BAAQIR : Ndio, na zaidi ya hapo. Ikiwa itathibiti kuwa matendo haya ni kuwatukuza mawalii wa Mwenyezi Mungu, wakati huohuo ni kuutukuza Uislaam, kwani kuwatukuza viongozi na watukufu wa Uislaam ni kuutukuza Uislaam, na kila kitu ambacho ndani yake kuna kuutukuza Uislaam basi kitu hicho ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo Mwenyezi Mungu amesema kuhusiana nazo:Kwa hivyo basi kuyapamba makaburi ya mawalii wa Mwenyezi Mungu ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo ni sunna kuzifanya na kufanya kazi kwa ajili yake, na mtu mwenye kufanya hivyo hupewa thawabu kwa matendo yake hayo. KHALID : Nakuomba samah ani, kwa kuchukua kiasi hiki cha wakati wako lakini mbele ya Mwenyezi Mungu ni mwenye malipo, kwani umenitoa kwenye kiza cha ujinga na kuniweka kwenye nuru ya elimu na ufahamu, ni kwa kiasi gani nilikuwa nikifikiria kuhusiana na upambaji huu wa makaburi na nisielewe siri yake na faida yake na usahihi wake, kwa hakika hivi leo-wewe- umenitia nuru kwa elimu yako hii, na umenifikisha niliko kuwa nikipakusudia.

BAAQIR : Sasa shaka yote uliyo kuwa nayo kuhusiana na kupamba makaburi imetoweka?

KHALID : Ndio.. hakuna shaka yoyote niliyo bakia nayo kwani kufanya hivyo ni sunna na jambo lililo himizwa na Qur'ani tukufu kwa kauli yake Mwenyezi Mungu:

BAAQIR : Alaa ayyi hal (Kwa hali yoyote ele):Hakika mimi niko tayari kufahamiana nawe katika maudhui kama haya ili niweze kufaidika, au wewe pia ufaidike, na wote kwa pamoja tuwe ni wenye kuyafahamu mambo kwa ufahamu mzuri na wenye mazingatio.

KHALID : Ninakushukuru sana sana, na ninamuomba Mwenyezi Mungu mtukufu akuwafikishe kwa yale ayaridhiayo.

7 UKWELI WA USHIA

KUBUSU MADHARIHI (MAKABURI)

MAALIK: Ewe Swaadiq ni sababu gani iwafanyayo kubusu Dharihi ya kaburi la Mtume na maimam na kutoacha kitendo hicho?

SWAADIQ: Je kuna tatizo (ishkali) lolote kufanya hivyo?

MAALIK: Inasemekana kuwa kufanya hivyo ni miongoni mwa matendo ya shirki.

SWADIQ: Nani asemae kuwa kufanya hivyo ni shirki?

MAALIK: Waislaam ndio wasemao hivyo.

SWADIQ: Ajabu! Basi ni watu gani ambao wanabusu madharihi?MAALIK: Inasemekana kuwa ni kikundi kidogo cha Mashia.

SWADIQ: Je umewahi kwenda hija?

MAALIK: Ninamshukuru Mwenyezi Mungu.. ndio nimefanikiwa kwenda hija.

SWADIQ: Je umelitembelea kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) katika mji wa Madinah?

MAALIK: Ninamshukuru Mwenyezi Mungu nimefanikiwa kulitembelea.SWAADIQ: Je hukuwaona maelfu ya waislaam wa madhehebu ya sunni wakikusudia na kutaka kulibusu dharihi la kaburi la Mtume wa Mwenyezi Mungu na huku wakipigwa na walinzi wa kikundi cha (Hay'atu amri bil-maarufi)?!!

MAALIK: Ndio..

SWAADIQ: Kwa maana hiyo si sisi Mashia pekee tunao busu madharihi ya Mitume wa Mwenyezi Mungu, bali waislaam wote huyabusu.

MAALIK: Sasa kwanini baadhi wanasema kuwa kufanya hivyo ni haram, na kwamba kufanya hivyo ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu?

SWAADIQ: Hawa ni watu wachache wa kikundi fulani kati ya makundi ya waislaam, wajionao kuwa wao ndio wenye haki, na kwamba wao ndio waislam wa kweli na wanawaona waislaam wengine kuwa ni makafiri na washirikina wanamuabudu asie kuwa Mwenyezi Mungu, na hawawaoni watu wengine kuwa ni waislaam walio kosea, kwa hivyo ndio maana huwaona wakiyakufurisha madhehebu (makundi) mengine yote ya kiislaam. Je hukuona ile kamati ya (Al-amri bil-maarufi)!! katika nchi ya Hijazi wakimpiga anaekusudia na kutaka kubusu dharihi la kaburi la Mtume(s.a.w.w) na kumwambia:Ewe kafiri! Ewe mshirikina! Ewe zindiki! Ewe nguruwe! Ewe mbwa! Na mengineyo kati ya aina mbali mbali za matusi na tuhuma zilizo mbaya kabisa.

Na matusi hayo humuelekea kila mtu: Sawa awe Shia, Hanafiy, Maalikiy, Shafiiy, Hanbaliy, Zaydiah, na waislaam wengine..[17]

MAALIK: Ndio.. yote hayo nimeyaona, na yaliyo mabaya zaidi kuliko hayo: Kwa hakika mimi niliwaona wakimpiga kichwani mtu mmoja alie ng'ang'ania kufanya hivyo kwa fimbo kiasi kwamba huenda pigo hilo lilipelekea kumpasua na kutoka damu, na wakati mwingine huwapiga kwa mikono yao-kwa nguvu- na wakiwapiga vifuani waislaam walio kuja kufanya ziara mapigo ambayo huwaumiza na kuwadhuru vifua vyao na kuwasababishia maumuvu na maradhi miili yao! Na ni kwa kiwango gani niliumia kwa kuyao mambo hayo na vitendo hivyo!!.

Hija ambayo Mwenyezi Mungu ameifanya kuwa ni kongamano la waislaam wote ulimwenguni ili waweze kuzungumza katika kongamano hilo kuhusu mambo yao mbali mbali, hivi leo imekuwa ni mahala pa kutia tofauti kati ya waislaam kutokana na matendo ya kikundi hicho kidogo kinacho jiita kuwa ni (hay'atul-amri bil-maaruf wannahyi anil-munkar)!!!.SWAADIQ: Ala ayyi hal, ewe Maalik.. je wewe unambusu mwanao?MAALIK: Ndio!

SWADIQ: Je unamshirikisha Mwenyezi Mungu mtukufu kwa kumbusu mwanao?

MAALIK: Hapana, hapana.. kamwe simshirikishi Mwenyezi Mungu.SWADIQ: Vipi usimshirikishe Mwenyezi Mungu kwa kumbusu mwanao?MAALIK: Kwa hakika mimi ninambusu mwanangu kwa ajili ya mapenzi yangu kwake, na hilo si shirki.

SWADIQ: Je wewe unaibusu Qur'ani?

MAALIK: Ndio.

SWADIQ: Je kwa kufanya kwako hivyo humshirikishi Mwenyezi Mungu?

MAALIK: Hapana.

SWADIQ: Je jalada la Qur'ani unalo libusu si ngozi ya mnyama?MAALIK: Ndio.

SWADIQ: Kwa hivyo wewe unamshirikisha Mwenyezi Mungu, na unaifanya ngozi ya mnyama kuwa ni mshirika wa Mwenyezi Mungu.. ametakasika Mwenyezi Mungu na hilo.

MAALIK: Si hivyo. Kwa hakika mimi ninaibusu Qur'ani kwa sababu imekusanya maneno ya Mwenyezi Mungu, kutokana na mapenzi ya maneno ya Mwenyezi Mungu ndio maana ninalibusu jalada lililo ifunika Qur'ani hiyo, na hii ni kutokana na mapenzi mengi, na wingi wa shauku yangu kwa Qur'ani, ni tofauti iliyoje kati ya kitendo hiki na kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

Kisha ninapo ibusu Qur'ani ninapata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa kufanya hivyo, kwa sababu kuibusu Qur'ani ni kuitukuza na kuienzi na kuiinua daraja yake, na kuitukuza Qur'ani kuna thawabu na malipo mbele ya Mwenyezi Mungu, kwa hivyo ni tofauti iliyoje iliyopo kati ya tendo hili na kumshirikisha Mwenyezi Mungu?

SWADIQ: Kwa nini maneno kama hayo usiyasema katika kubusu dharihi la Mtume(s.a.w.w) na madharihi ya maimam(a.s) [18] au unadai ya kuwa wale ambao wanabusu madharihi huvifanya vyuma hivyo kuwa ni washiriki wa Mwenyezi Mungu mtukufu?! Ikiwa ni hivyo kwanini hawabusu vyuma mbali mbali vilivyoko huku na kule katika ardhi? Lakini..kutokana na ukweli kuwa dharihi hilo limefunika kaburi la Mtume(s.a.w.w) au kaburi la mmoja wapo kati ya maimamu(a.s) , kutokana na mapenzi ya Mtume(s.a.w.w) na maimamu na kutokana na shauku yao kwao ndio maana wanalibusu dharihi la kaburi lake kwa sababu wao hawawezi kumfikia Mtume na imamu mwenyewe(a.s).

Pamoja na kufanya kwao hivyo hakika wao hupata malipo kwa Mwenyezi Mungu mtukufu, na hupawa thawabu kwa kufanya hivyo, kwani kulibusu dharihi la mtu fulani ni kumtukuza mtu yule. Na kumtukuza Mtume(s.a.w.w) au mmoja wapo kati ya maimamu(a.s) , ni kuutukuza Uislaam ambao huyu alikuwa ni Mtume wake(s.a.w.w) au alikuwa ni imamu wake alie kuwa akilingania watu kwenye Uislaam huo.

Na jambo lolote litakapo kuwa na sura ya kuutukuza Uislaam basi jambo hilo ni katika shiari za Mwenyezi Mungu ambazo amezizungumzia kwa kusema:suratul-haji aya 32.

MAALIK: Ikiwa ukweli ni huo basi kwanini baadhi ya watu wanasema kuwa nyinyi ni wenye kumshirikisha Mwenye zi Mungu?

SWAADIQ: Imepokelewa katika Hadithi tukufu kama ifuatavyo:(Kwa hakika matendo hufanyika kutokana na Nia) [19] ikiwa mtu yeyote anabusu dharihi na katika kubusu kwake huko anakusudia kumshirikisha Mwenyezi Mungu bila shaka mtu huyo ni mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu (mshirikina). Na ikiwa kubusu huku kunatokana na mapenzi mengi, na kwa ajili ya kupata thawabu kwa ajili ya kuadhimisha na kutukuza shiari za Mwenyezi Mungu kwa kufanya hivyo, basi hupewa thawabu yule mwenye kuyatekeleza matendo hayo. Na wewe waulize wote wale ambao wanayabusu madharihi kati ya Mashia na Masunni kama ifuatavyo: Kwa nini mnabusu madharihi?

Hata kujibu yeyote kati yao isipokuwa kwa kusema tunafanya hivyo kutokana na mapenzi makubwa na shauku kubwa tuliyo nayo na kwa ajili ya kupata thawabu, na huwezi kumsikia yeyote kamwe-bila shaka yoyote- akisema ya kuwa anabusu dharihi kwa ajili ya jambo lingine tofauti na hili tulilo litaja.

MAALIK: Ni kweli, maneno yako ni sahihi.

SWADIQ: Na ikiwa kubusu peke yake bila kukusudia kumshirikisha Mwenyezi Mungu kunamfanya mtu kuwa mshirikina, bila shaka huwezi kumpata mwanadamu yeyote asie mshirikina, kwani waislaam imma wanabusu madharihi, au wanabusu Qur'ani.. kwa msingi wa hali mbili hizi wao-wote-ni washirikina. Sasa ikiwa hali ni kama hiyo Muislaam ni nani?

MAALIK: Ninakushukuru sana, na kwa hakika mimi nitafanya mazungumzo na majadiliano na baba yangu alie kuwa akinilisha na kunifundisha mambo kama haya ya asabia yasiyo na maana yoyote, na sinto sikiliza maneno ya mtu yeyote wa madhehebu mengine, kwa hakika nimefahamu ya kuwa haki na ukweli uko pamoja nanyi-nyinyi Mashia- na wewe unahaki juu yangu milele, kwa sababu umenionyesha njia, si katika jambo hili tu bali katika mambo yote, ili nisifuate kila kinifikiacho masikioni mwangu, bila ya kufikiria kuhusu usahihi wake na ubatilifu wake.


10

11

12