TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU Juzuu 3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU 0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 16006
Pakua: 2425


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 12 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 16006 / Pakua: 2425
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU Juzuu 3

Mwandishi:
Swahili

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TATU

﴿تِلْكَ الرُّسُلُ فَضَّلْنَا بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ مِّنْهُم مَّن كَلَّمَ اللَّـهُ وَرَفَعَ بَعْضَهُمْ دَرَجَاتٍ وَآتَيْنَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ الْبَيِّنَاتِ وَأَيَّدْنَاهُ بِرُوحِ الْقُدُسِ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا اقْتَتَلَ الَّذِينَ مِن بَعْدِهِم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَاتُ وَلَـٰكِنِ اخْتَلَفُوا فَمِنْهُم مَّنْ آمَنَ وَمِنْهُم مَّن كَفَرَ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا اقْتَتَلُوا وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَفْعَلُ مَا يُرِيدُ ﴾

253. Mitume hao tumewafadhilisha baadhi yao zaidi kuliko wengine. Miongoni mwao yuko ambaye Mwenyezi Mungu alisema naye; na wengine akawapandisha vyeo, na tukampa Isa mwana wa Maryam dalili zilizo wazi na tukamtia nguvu kwa roho takatifu. Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana wale waliokuwa baada yao, baada ya kuwafikia dalili zilizo wazi; lakini walihitilafiana kuna katika wao walioamini na wengine katika wao waliokufuru, lakini Mwenyezi Mungu hufanya anayoyataka.

KUWAFADHILISHA MITUME

Aya ya 253

MAANA

Mitume hao tumewafadhilisha baadhi yao zaidi kuliko wengine.

Mwenyezi Mungu alimwambia Mtume Wake Muhammad(s.a.w.w) katika mwisho wa Aya iliyotangulia;"Na hakika wewe ni miongoni mwa Mitume," Halafu akafuatisha moja kwa moja na kauli Yake hii: "Mitume hao ..." Kwa hivyo basi, makusudio yanakuwa ni mitume wote ambao miongoni mwao ni Muhammad, sio kundi maalum, kama walivyosema wafasiri wengi.

Mitume wote ni sawa katika asili ya utume kuchaguliwa kwao na katika kufikisha ujumbe, wa Mwenyezi Mungu na kuongoza viumbe Vyake, lakini wanatofautiana katika mambo fulani. Yaani baadhi ya mitume wamekuwa mashuhuri kwa baadhi ya mambo fulani waliyohusika nayo, ambayo wengine hawakuwa nayo, ambayo Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewasifu nayo katika Kitabu chake. Kwa mfano Ibrahim alikuwa mashuhuri kwa kuitwa rafiki wa Mwenyezi Mungu (Khalilullah) kutokana na kauli Yake Mwenyezi Mungu:

﴿وَاتَّخَذَ اللَّـهُ إِبْرَاهِيمَ خَلِيلًا﴾

"Na Mwenyezi Mungu amemfanya Ibrahim kuwa ni rafiki" (4:125)

Musa naye akawa mashuhuri kwa jina la aliyesema na Mwenyezi Mungu (Kalimullah) kutokana na kauli Yake Mwenyezi Mungu:

﴿وَكَلَّمَ اللَّـهُ مُوسَىٰ تَكْلِيمًا﴾

"... Na Mwenyezi Mungu akasema na Musa maneno" (4:164)

Isa naye akawa mashuhuri kwa, roho wa Mwenyezi Mungu (Ruhullah); kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

﴿إِنَّمَا الْمَسِيحُ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ رَسُولُ اللَّـهِ وَكَلِمَتُهُ أَلْقَاهَا إِلَىٰ مَرْيَمَ وَرُوحٌ مِّنْهُ﴾

"Hakika Masihi Isa bin Maryam ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na neno lake alilompelekea Maryam. Na ni roho iliyotoka kwake ..." (4:171)

Muhammad naye akawa mashuhuri kwa, mwisho wa Mitume (khatamun nabiyyina) kwa kauli Yake Mwenyezi Mungu:

﴿وَلَـٰكِن رَّسُولَ اللَّـهِ وَخَاتَمَ النَّبِيِّينَ وَكَانَ اللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴾

"Na Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa Mitume ..." (33: 40)

Mwenyezi Mungu ametaja baadhi ya Mitume waliofadhilishwa au baadhi ya yanayohusika nao, kwa kauli Yake:

Miongoni mwao yuko ambaye Mwenyezi Mungu alisema naye.

Huyu ni Musa bin Imran kama walivyoafikiana wafasiri.

Na wengine akawapandisha vyeo.

Mwenye Tafsiri ya Al Manar amesema: "Wafasiri wamesema huyo ni Mtume wetu ..."Na amesema Razi: "Umekubaliana umma wote kwamba Muhammad ni bora ya Mitume," Ametoa dalili 19 juu ya hilo kwa dalili, Miongoni mwa dalili hizo ni kwamba Ali bin Abu Twalib siku moja alitokeza kwa mbali, Mtume akasema: "Huyu ni bwana wa Waarabu."Aisha akasema: "Siye wewe bwana wa Waarabu? "Mtume akasema: "Mimi ni bwana wa walimwengu na yeye ni bwana wa Waarabu" Dalili bora zaidi juu ya ubora wa Mtume kwa Mitume wote na watu wema wote ni sharia yake ilivyo na ukunjufu katika utukufu wake na utu wake.( [1] )

Na tukampa Isa mwana wa Maryam dalili zilizo wazi na tukamtia nguvu kwa roho takatifu.

Dalili zilizowazi hapa ni dalili ambazo zinadhihirisha haki; kama kufufua wafu, kuponyesha wagonjwa, kuumba ndege, n.k. Makusudio ya roho takatifu ni roho njema yenye kutakaswa. Imekwishapita tafsiri ya roho katika Aya ya 87 ya Sura hii.

Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana wale waliokuwa baada yao .

Yaani baada ya Mitume kuwajia na hoja zilizowazi na kuzifafanua haki kwa dalili, basi watu wao walihitalifiana baada yao.

Kuna katika wao walioamini na wengine katika wao waliokufuru.

Unaweza kuuliza: Kauli Yake Mwenyezi Mungu:"Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka wasingelipigana. Si inafahamisha kwamba binadamu ni mwenye kuendeshwa hana hiyari na kwamba kukaririka jumla hii ni kutilia mkazo kunasibika kupigana na matakwa ya Mwenyezi Mungu (s.w.t)?

Jibu : Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amempa uwezo mja na akambainishia heri na shari na kumkataza hili na kumwamrisha lile. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا﴾

"Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msiachane..." (3:103)

Mtu akifuata njia ya mshikamano na kupendana, atakuwa yeye mwenyewe ndiye anayenasibika na huko kufuata, kwa sababu kumetokana na yeye na kwa hiyari yake iliyomfanya aone bora njia hiyo kuliko njia ya kutoelewana; wakati huo huo huko kufuata njia hiyo ya mshikamano kunafaa kunasibishwe kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu ndiye aliyemwezesha kuifuata na ndiye aliyemwamrisha kuifuata.

Ama akifuata njia ya chuki na uhasama, basi njia hiyo itanasibika na mtu pekee wala hainasibiki na Mwenyezi Mungu, kwa sababu mtu ameifuata kwa radhi yake na akaiona ni bora kuliko njia ya maafikiano; wala haifai kuinasibisha kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Mwenyezi Mungu amemkataza. Unaweza kuuliza tena: Kwa nini Mwenyezi Mungu amemwezesha mtu kuifanya shari ambapo ilikuwa inatakikana ampe hima ya kuaacha na kufanya heri tu? Jibu: Lau Mwenyezi Mungu angelifanya hivi, binadamu asingebakiwa na fadhila yoyote wala vitendo visingekuwa na sifa ya heri na shari au vizuri na vibaya. Kwa sababu sifa hizi zinafungamana na matakwa ya mtu na hiyari yake. Bali lau Mwenyezi Mungu angelimfanya mtu kufanya kitu fulani tu, kusingelikuwako na tofauti ya mtu na mawe au tofauti na unyoya ulio katika mavumo ya pepo. Kwa ajili hii na kwa ajili ya kudumu mtu na utu wake, hakutaka Mwenyezi Mungu kuwalazimisha watu kwenye kitu fulani

"Na kama angelitaka wasingelipigana"

Kwa ufupi kupigana ambako kumepatikana kati ya watu sio kama kumekhalifu matakwa ya Mwenyezi Mungu yanayoitwa Kun fa yakun. Isipokuwa kumekhalifu matakwa ya Mwenyezi Mungu ya sharia yake, ambayo ni ubainifu na uongozi; na hekima yake imetaka kumpa mtu uwezo wa kutosha wa kufanya heri na shari, ili ajichagulie yeye mwenyewe uongozi na heri na awe ni mtu anayetofautiana na mawe na wanyama.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِمَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ يَوْمٌ لَّا بَيْعٌ فِيهِ وَلَا خُلَّةٌ وَلَا شَفَاعَةٌ وَالْكَافِرُونَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴾

254.Enyi mlioamini! Toeni katika vile tulivyowapa. Kabla haijafika siku ambayo hapatakuwa na biashara wala urafiki wala uombezi. Na makafiri ndio madhalimu.

KUTOA

Aya ya 254

MAANA

Mwenyezi Mungu amehimiza kutoa mali kwa mifumo mbali mbali. Yameshatangulia maelezo katika tafsiri ya Aya 245; na unakuja tena mfano wake katika Aya hii:

Enyi mlioamini! Toeni katika vile tulivyowapa.

Mwenyezi Mungu anahimiza kutoa pamoja na kuashiria kwamba mali iliyo na watu ni Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu 2. Sura Al-Baqarah 255. Mwenyezi Mungu hakuna mola ila Yeye Aliye hai msimamizi wa kila kitu. Hakumshiki kusinzia wala kulala. Ni Vyake vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni. Na ni nani huyo awezaye kuombea mbele Yake bila ya idhini Yake. Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawalijui lolote lililo katika elimu Yake ila kwa alitakalo. Elimu Yake imeenea mbingu na ardhi. Wala hakumshindi kuzilinda. Na Yeye ndiye Mtukufu aliye Mkuu.

mali Yake aliyoitoa Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t); na kwamba kesho fursa itakosekana, kwa hivyo ni juu ya mumin mwenye akili kuchukua fursa kabla ya kupitwa na wakati.

Kabla haijafika siku ambayo hapatakuwa na biashara wala urafiki wala uombezi.

Makusudio ya biashara hapa ni kulipa fidia ili kujikomboa na moto kwa mali; urafiki ni urafiki wa kusameheana na uombezi na kuombewa na mtu mwingine kuepukana na moto. Maana yake ni kwamba kesho mtu atakuja peke yake hana chochote isipokuwa amali njema Aya hii ina maana sawa na Aya ya 48 ya Sura hii. Tumeuzungumzia uombezi katika Aya hiyo.

Na makafiri ndio madhalimu.

Wamejidhulumu wenyewe kwa kuacha amali njema ambayo inawaokoa na adhabu. Kwa ujumla ni kuwa neno dhulma na ukafiri yanakuja katika matumizi ya maana mamoja. Mara nyingine hutumiwa ukafiri katika dhulma, kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t):

﴿إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ﴾

"... Hakika ushirikina ni dhulma kubwa" (31:13)

Na mara nyingine hutumiwa dhulma katika ukafiri, kama alivyosema Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

﴿وَلَـٰكِنَّ الظَّالِمِينَ بِآيَاتِ اللَّـهِ يَجْحَدُونَ﴾

"...Lakini madhalimu wanakanusha ishara za Mwenyezi Mungu..." (6:33)

﴿اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴾

255.Mwenyezi Mungu hakuna mola ila Yeye Aliye hai msimamizi wa kila kitu, Hakumshiki kusinzia wala kulala. Ni Vyake vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni. Na ni nani huyo awezaye kuombea mbele Yake bila ya idhini Yake. Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawalijui lolote lililo katika elimu Yake ila kwa alitakalo. Elimu Yake imeenea mbingu na ardhi, Wala hakumshindi kuzilinda. Na Yeye ndiye Mtukufu aliye Mkuu

AYA YA KURSIY

Aya ya 255

MAANA

Mwenyezi Mungu hakuna mola ila yeye aliye hai, Msimamizi wa kila kitu.

Mwanafalsafa mashuhuri wa elimu inayohusika na mambo ya Mungu, aitwaye Mulla Sadra anasema: Neno Allah (Mwenyezi Mungu) linafahamisha kupwekeka dhati Yake Mwenyezi Mungu na sifa Zake. Kufahamisha juu ya kupwekeka katika dhati, ni kwamba jina hili tukufu haliitiwi mtu mwingine kiuhakika wala majazi. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿فَاعْبُدْهُ وَاصْطَبِرْ لِعِبَادَتِهِ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا ﴾

"... Basi mwabudu Yeye tu na udumu katika ibada Yake. Je, unamjua (mwingine) mwenye jina lake?" (19:65)

Ama kufahamisha kupwekeka Kwake katika sifa, ni kwamba jina hili linafahamisha juu ya dhati yenye kukusanya kila sifa za ukamilifu na utukufu, kinyume cha majina mengine kama; Mjuzi, Mweza na Muumbaji, ambayo umoja wake haufahamishi isipokuwa umoja wa maana katika elimu, au uweza au utendaji. Unaweza kuuliza: Hakika sifa za ukamilifu na utukufu ni nyingi na zenye kubadilika kulingana na kueleweka kwake; vipi ifae kusema zimepwekeka na tunaziona zinahisabika na kubadilika?

Jibu : Ukisema huyu ni mtu mjuzi yataeleweka mambo mawili - Sifa na Mwenye kusifiwa; na vyote ni vitu tofauti. Mtu sio ujuzi na ujuzi sio mtu. Hayo ni kwa upande wa kiumbe. Ama kwa upande wa Muumbaji hakuna jingine isipokuwa kuweko kiutukufu; na huko kuweko ndiko ujuzi ndiko uwezo, na ndiko hekima, n.k. Hakuna sifa na mwenye kusifiwa vyote ni vimoja tu; na huku hakukufanana na kitu kingine.

Hakuna mola ila Yeye.

Inasemekana maana yake ni hakuna anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye. Lakini kueleweka kwake ni hakuna yoyote mwenye kukusanya sifa za uungu isipokuwa Yeye. Vyovyote iwavyo, maana zote mbili ni zenye kulazimiana.

Aliye hai Msimamizi wa kila jambo.

Ukiunasibisha uhai kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, maana yake yanakuwa ni kukua, kuhisi na utambuzi. Lakini ukiunasibisha kwa Mwenyezi Mungu unakuwa ni elimu na uweza. Makusudio ya kusimamia kila kitu ni kukisimamia katika mambo yake na kukipangilia vizuri. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قَالَ رَبُّنَا الَّذِي أَعْطَىٰ كُلَّ شَيْءٍ خَلْقَهُ ثُمَّ هَدَىٰ ﴾

"Akasema: Mola wetu ni Yule aliyekipa kila kitu umbo lake kisha akaongoza." (20:50)

Na amesema tena:

﴿وَخَلَقَ كُلَّ شَيْءٍ فَقَدَّرَهُ تَقْدِيرًا ﴾

"....Na ameumba kila kitu akakikadiria kipimo (chake)." (25:2)

Mulla Sadra anasema: Kauli ya Aliye Hai inafahamisha kwamba Yeye ni Mjuzi na Muweza. Na kauli ya Msimamizi wa kila kitu inafahamisha kuwa Yeye ni Mwenye kujisimamia Mwenyewe na kumsimamia mwingine. Kwa hiyo sifa mbili hizi ni zenye kuafikiana katika maana na ni zenye kuingiliana." Anakusudia kuwa usimamizi hauepukani na uhai; kama vile ambavyo uhai kwa maana ya uwezo na elimu hauepukani na usimamizi.

MWENYEZI MUNGU NA DESTURI YA MAUMBILE

Unaweza kuuliza: Je maana ya kusimamia Mungu juu ya mipango ya vitu vyote, ni kwamba mambo yote ya dhahiri ya kimaumbile mpaka mafungu yake yanasimamiwa na Mwenyezi Mungu moja kwa moja Yeye Mwenyewe bila ya kuweko kati sababu yoyote ya kimaada; kama inavyodhihiri katika Aya isemayo:

﴿ثُمَّ جَعَلْنَاهُ نُطْفَةً فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ ﴿١٣﴾ ثُمَّ خَلَقْنَا النُّطْفَةَ عَلَقَةً فَخَلَقْنَا الْعَلَقَةَ مُضْغَةً فَخَلَقْنَا الْمُضْغَةَ عِظَامًا فَكَسَوْنَا الْعِظَامَ لَحْمًا ثُمَّ أَنشَأْنَاهُ خَلْقًا آخَرَ فَتَبَارَكَ اللَّـهُ أَحْسَنُ الْخَالِقِينَ﴾

"Kisha tukamfanya tone la manii, katika makao madhubuti. Kisha tukaliumba tone hilo kuwa pande la damu, na tukaliumba pande la damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa na mifupa tukaivika nyama, kisha tukalifanya umbo jengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu mbora wa waumbaji" (23:13-14)

Kwa sababu yenye kuja haraka fahamuni katika Aya hii, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameingilia Yeye Mwenyewe moja kwa moja kwenye makuzi mbali mbali ya tone la manii; na tunajua kuwa nadharia ya kielimu inasema kuwa tone la manii linakuwa na kuzidi kulingana na kanuni maalum?

Katika kujibu hayo, hapana budi kupambanua kati ya jambo lisilokuwa la kawaida, kama vile kufufua wafu na kupatisha kitu bila ya kitu kingine, na matukio yanayo kuwa kulingana na kanuni za kimaumbile, kama kupatwa jua mwezi, n.k. Hili la aina ya kwanza linategemezwa kwake Mwenyezi Mungu moja kwa moja. Na hili la aina ya pili linategemea desturi ya maumbile na linategemezwa kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu Yeye ndiye aliyeweka desturi ya maumbile pamoja na vilivyomo ndani yake vikiwa ni pamoja na nguvu na viasili. Viasili hivi kwa kupitia njia zake vinafanya dhahiri za maumbile zikiwa ni pamoja na tone la manii.

﴿وَخَلَقَ كُلَّ شَيْءٍ فَقَدَّرَهُ تَقْدِيرًا﴾

"...Na ameumba kila kitu akakikadiria kipimo (chake)." (25:2)

Yaani anakipitisha katika desturi na kanuni za kitabia. Lau angelikuwa Yeye Mwenyezi Mungu ndiye anayesimamia umbile moja kwa moja bila ya kuweko kati kitu kingine, kusingelikuweko na sababu na msababishaji. Kwa hivyo basi, inatubainikia kuwa kila mwenye kuamini kwamba kila tukio la kimaumbile linategemea Mwenyezi Mungu moja kwa moja bila ya kuweko kati sababu yoyote yenye kuhisiwa ambayo imegunduliwa na utaalamu au inaweza kugunduliwa, mtu huyo atakuwa mjinga mwenye kukosea katika imani yake. Na lau ingelikuwa sahihi imani yake hii, kusingelikuweko na wajibu wa kitendo chochote na elimu isingelikuwa na faida yoyote; wala uvumbuzi na maendeleo ya mtu yasingekuwa na athari yoyote. Vile vile amekosa yule mwenye kuitakidi kwamba maumbile ndio kila kitu, kuwa ndiyo sababu ya kwanza na ya mwisho, wala hakuna kitu nyuma yake. Hayo ni makosa. Kwani kama ni hivyo kusingelikuwa na nidhamu wala athari yake na kungelikuwa na migongano na natija ingelikuwa kutokuwepo elimu wala uhai, Haya tumeyafafanua zaidi katika Aya ya 21 ya Sura hii, kifungu cha Tawhid.

Hakumshiki kusinzia wala kulala

Mwenyezi Mungu alipobainisha kwamba Yeye ni Hai Msimamizi wa kila jambo, ameendelea kulitilia mkazo hilo kwamba Yeye ni Mwenye kutukuka, haumzuwii usingizi wala kusahau au kitu chochote, katika kupanga kuumba K

wake kwa njia ya ukamilifu. Kwa sababu hilo linapingana na ukubwa Wake na kujitosha Kwake na kila kitu. Imam Ali amesema akimwambia Mola wake: "Sisi hatujui kiasi cha ukubwa wako, isipokuwa tunajua kuwa Wewe ni Aliye Hai wa Milele, Msimamizi wa kila jambo, hakukushiki kusinzia wala kulala; hutazamwi; wala halikuoni jicho, lakini Wewe unaliona; umezithibiti amali na ukazishika barabara."

Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini Makusudio ya vilivyomo ni ulimwengu wote na kila kilichomo ndani yake hakitoki nje ya ufalme Wake na mipangilio Yake.

Imam Ali(a.s) aliulizwa kuhusu:"Hapana hila wala nguvu isipokuwa kwa msaada wa Mwenyezi Mungu." Akajibu: "Sisi hatumiliki chochote mbele ya Mwenyezi Mungu, wala hatumiliki isipokuwa kile tulichomilikishwa; na anapomilikisha kile ambacho amekimiliki zaidi kuliko sisi, basi ametukalifisha nacho; na anapokiondoa, huwa ametuondolea taklifa."

Na ni nani huyo awezaye kuombea mbele Yake bila ya idhini Yake.

Umekuja mfumo wa swali kwa maana ya kukanusha; yaani hataombea yeyeote mbele Yake isipokuwa kwa amri Yake na hayo ni jibu na kubatilisha kauli ya washirikina kwamba masanamu ndiyo yanayowakurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anawasimulia hao kwa kusema:

﴿وَيَقُولُونَ هَـٰؤُلَاءِ شُفَعَاؤُنَا عِندَ اللَّـهِ قُلْ أَتُنَبِّئُونَ اللَّـهَ بِمَا لَا يَعْلَمُ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ﴾

"... Na wanasema: hao ndio waombezi wetu mbele ya Mwenyezi Mungu! Sema: 'Je, mnamwambia Mwenyezi Mungu asiyoyajua katika mbingu wala katika ardhi? ..." (10: 18)

Tumekwisha zungumzia uombezi katika Aya ya 48, Baadhi ya ulama wamesema kwamba siku ya Kiyama kutakuwa na aina mbalimbali za watu. Kama ifuatavyo:- Waliotangulia ambao ni wenye kukurubishwa; watakaokuwa upande wa kuume ambao ni watu wema watakaookoka, watakaokuwa upande wa kushoto ambao ni waovu watakao adhibiwa, na watakaokuwa na msamaha ambao amali zao njema zimechanganyika na maovu. Na hawa watakubaliwa kuombewa; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

﴿وَآخَرُونَ اعْتَرَفُوا بِذُنُوبِهِمْ خَلَطُوا عَمَلًا صَالِحًا وَآخَرَ سَيِّئًا عَسَى اللَّـهُ أَن يَتُوبَ عَلَيْهِمْ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴾

" Na wengine walikiri dhambi zao, wakachanganya vitendo vyema na vingine viovu, huenda Mwenyezi Mungu akapokea toba yao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusamehe Mwenye kurehemu" (9:102)

Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao.

Maana yake ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.), anajua yaliyokuwa na yatakayokuwa katika waja wake, iwe heri au shari; na anamjua mwombezi na anayeombewa na anayestahiki msamaha na thawabu au adhabu na mateso. Ikiwa mambo yako hivyo, basi uombezi (shafaa) hauna nafasi yoyote isipokuwa kwa amri Yake Mwenyezi Mungu kwenye mipaka Yake anayoridhia.

Wala hawalijui lolote lililo katika elimu Yake ila kwa alitakalo.

Dhamiri katika hawalijui inawarudia waja wote wakiwemo Malaika na Mitume. Makusudio ya elimu ni linalojulikana, Maana yako wazi. Ukipenda kujua zaidi unaweza kuangalia Aya hizi:

﴿عَالِمُ الْغَيْبِ فَلَا يُظْهِرُ عَلَىٰ غَيْبِهِ أَحَدًا ﴿٢٦﴾ إِلَّا مَنِ ارْتَضَىٰ مِن رَّسُولٍ﴾

"Yeye ni mjuzi wa siri; wala hamdhihirishii yoyote siri Yake isipokuwa Mtume aliyemridhia ..." (72: 26-27)

﴿سُبْحَانَكَ لَا عِلْمَ لَنَا إِلَّا مَا عَلَّمْتَنَا﴾

"...Utakatifu niwako! Hatuna elimu isipokuwa ile uliyotufundisha..." (2:32)

Elimu Yake imeenea mbingu na ardhi.

Kauli zimekuwa nyingi na zimegongana kuhusu maana ya neno Kursiy. Baadhi ya kauli hizo ni za kumzungumzia Mwenyezi Mungu bila ya elimu, lakini bora ya kauli ni mbili: Ya kwanza, ni fumbo la utukufu Wake Mwenyezi Mungu na cheo chake yaani enzi. Ya pili, ni elimu; yaani elimu Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) imezunguka kila kitu. Mpangilio wa maneno unarudia maana haya.

Wala hakumshindi kuzilinda na Yeye Ndiye Mtukufu aliye Mkuu.

Yaani hakumtii mashaka wala uzito wowote kuilinda mbingu na ardhi na kupangilia vizuri yaliyomo ndani yake. Vipi isiwe hivyo! Na hali kuumba nzi na kuumba ulimwengu Kwake ni sawa tu; maadamu Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.)

﴿إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ﴾

"... Akitaka chochote ni kukiambia kuwa, kikawa" (36:82)

KITU BILA YA KITU

Kutengeneza vitu kuko aina mbili: kutegeneza kitu kutokana na maada na kutengeneza bila ya maada. Na kunatofautiana kwa njia nyingi. 1. Anayetengeneza kwa maada anahitaji harakati na zana, lakini asiyetengeneza kwa maada hahitaji.

2. Wa maada anachoka, lakini asiyetumia maada hachoki.

3. Mwenye kutumia maada hawezi kupata kitu bila ya kitu kingine, lakini kwa asiyetumia, hilo sio jambo zito. Kwa hivyo inabainika kwamba kumlinganisha Muumbaji na Mwenye kuumbwa ni kulinganisha na kisicholingana. Itawezekana vipi kumfananisha mwenye kujitosha na mwenye kuhitajia; atakuwaje sawa na mwenye kushindwa?

﴿لَا إِكْرَاهَ فِي الدِّينِ قَد تَّبَيَّنَ الرُّشْدُ مِنَ الْغَيِّ فَمَن يَكْفُرْ بِالطَّاغُوتِ وَيُؤْمِن بِاللَّـهِ فَقَدِ اسْتَمْسَكَ بِالْعُرْوَةِ الْوُثْقَىٰ لَا انفِصَامَ لَهَا وَاللَّـهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴾

256. Hakuna kulazimisha katika dini; uongofu umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa taghuti na akamwamini Mwenyezi Mungu, hakika yeye ameshika kishiko madhubuti kisichovunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mjuzi.

﴿اللَّـهُ وَلِيُّ الَّذِينَ آمَنُوا يُخْرِجُهُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ وَالَّذِينَ كَفَرُوا أَوْلِيَاؤُهُمُ الطَّاغُوتُ يُخْرِجُونَهُم مِّنَ النُّورِ إِلَى الظُّلُمَاتِ أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴾

257. Mwenyezi Mungu ni mtawala wa wale walioamini; huwatoa gizani na kuwaingiza katika mwangaza, lakini walio kufuru watawala wao ni mataghuti. Huwatoa kwenye mwangaza, na kuwaingiza katika giza, hao ndio watu wa motoni, watadumu humo.

HAKUNA KULAZIMISHA KATIKA DINI

Aya ya 256 - 257

MAANA

Hakuna kulazimishwa katika dini

Lau tungeiangalia jumla hii peke yake, tungelifahamu kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuweka hukumu yenye aina yoyote ya kulazimisha na kwamba anayolazimishwa mtu katika kauli au vitendo hayaambatani na kitu chochote katika mtazamo wa sharia, si katika dunia wala akhera. Lakini kauli Yake Mwenyezi Mungu "Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu", ambayo ndiyo sababu ya kuacha kulazimisha, inaonyesha kuwa neno katika, hapa lina maana ya juu ya; Yaani uislamu haumlazimishi yeyote kukubali isipokuwa unamlazimisha mpinzani kwa hoja na dalili tu; kama inavyosema Qur'an:

﴿وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ فَمَن شَاءَ فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاءَ فَلْيَكْفُرْ﴾

"Na sema: (Huu) ni ukweli uliotoka kwa Mola wenu, basi anayetaka na aamini na anayetaka na akufuru ..." (18:29)

﴿أَفَأَنتَ تُكْرِهُ النَّاسَ حَتَّىٰ يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ﴾

"... Je, wewe utawashurutisha watu kwa nguvu wawe waumini? (10:99)

Unaweza kuuliza: Hakika dini haiwezekani kufungamana na kulazimishwa, kwa sababu dini ni katika mambo ya moyo yaliyo nje ya uwezo. Sawa na kuleta picha ya kitu akilini. Vinavyoweza kufungamana na kulazimishwa ni kauli na vitendo ambavyo inawezekana kutendeka bila ya matakwa ya msemaji na mtendaji, Kwa hivyo umepita njia gani mpaka ukasema habari ya kukataza kulazimishwa juu ya dini?

Jibu : Hakika kauli Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t):"Hakuna kulazimishwa katika dini" Imekuja kwa tamko la kuelezea habari. Kama hivyo ndivyo, basi swali litakuwa halina msingi, kwa sababu maana yatakuwa dini ni itikadi na hilo ni jambo linalorudia kwenye kukubali ambako mtu halazimishwi kukubali. Ikiwa tamko limekuja kwa kukusudiwa kukataza, basi maana yatakuwa ni: Enyi Waislamu msimlazimishe yeyote kusema "Lailaha illa Llahu Muhamadurasuli Llahi." baada ya kuwako hoja na dalili juu ya Tawhid na Utume.

Lakini jibu hili linaweza kuzalisha swali jipya kwamba hayo hayataafikiana na kauli ya Mtume(s.a.w.w) :"Nimeamrishwa nipigane na watu mpaka waseme: 'Laillahailla Ilah'; wakisema hivyo, basi damu zao na mali zao zimehifadhika na mimi."

Jibu : uislamu unaruhusu kupigana kwa sababu mbali mbali. Miongoni mwa sababu hizo ni: Kujikinga - Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَقَاتِلُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ الَّذِينَ يُقَاتِلُونَكُمْ وَلَا تَعْتَدُوا﴾

"Na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanaowapiga, wala msipituke mipaka." (2: 190).

Kudhulumiwa - Mwenyezi Mungu anasema:

﴿فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ﴾

"... Lipigeni (kundi) lile linaloonea (wenzao) mpaka lirudi katika amri ya Mwenyezi Mungu ..." (49:9)

Kupigana ili kuudhihirisha uislamu, ijapokuwa ni kwa ulimi. Hilo ni kwa ajili ya maslahi yanayowarudia wote, sio waislamu peke yao. Na maslahi haya anayakadiria aliye Masum au naibu wake; wala haifai kwa mwislamu yeyote, vyovyote alivyo, kupigana kwa ajili ya kutamkwa tamko la uislamu au kuueneza, isipokuwa kwa amri ya Masum au naibu wake, ambaye ni mujtahid ( [2] ) mwadilifu.

Ni kwa njia hii peke yake ndio inachukuliwa Hadith"Nimeamrishwa nipigane na watu..." ; Yaani mimi nitapigana nao nitakapoona mimi au kaimu wangu kwamba maslahi ya kiutu yanalazimisha kupigana kwa ajili ya 'Lailaha illa llah'. Hapo inaonyesha kuwa kupigana kwa kujikinga au kuikinga dini na haki, hakungojei idhini ya yeyote. Tumekwisha yaeleza hayo katika tafsiri ya Aya ya 193 kifungu cha 'Uislamu unapiga vita dhulma na ufisadi'

Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu.

Makusudio ya uongofu hapa ni imani na upotofu ni ukafiri. Mwenyezi Mungu amekwisha ibainisha haki kwa uwazi zaidi, na ubainifu na dalili zenye nguvu, mpaka kafiri akaishiwa na hoja au udhuru wowote. Mwenye kuijua njia ya haki na ya uongofu atakuwa amekwisha ijua njia ya upotofu na ya batili, Kwani hakuna kitu kingine baada ya haki isipokuwa upotofu.

Mulla Sadra anasema: Maana ya uongofu umekwisha pambanuka na upotofu ni kuitambua haki kutokana na batili na imani kutokana na ukafiri kwa dalili na hoja pamoja na kuzifahamu na kuziangalia vizuri. Yeyote mwenye kuikubali haki kwa kufuata tu, hana tofauti na mnyama. Hata hivyo mwenye kuwafuata watu wema kwa nia njema na kwa dhamiri nzuri atayapata yale watakayoyapata wao kesho.

Basi anayemkataa taghuti na akamwamini Mwenyezi Mungu, hakika yeye ameshika kishiko madhubuti kisichovunjika.

Kauli zimekuwa nyingi kuhusu tafsiri ya taghuti, baadhi ya wafasiri wamefikisha kauli tisa. Miongoni mwa hizo ni kuwa makusudio yake ni shetani. Nyingine ni dunia iliyo twevu. Iiliyo karibu na ufahamu na yenye kufahamisha kutokana na tamko lenyewe, ni kauli ya Sheikh Muhammad Abduh kwamba taghut ni yule ambaye kwa kumwabudu na kumwamini yeye, ndiyo sababu ya kupetuka mpaka na kutoka katika haki. Makusudio ya kishiko madhubuti, ni kwenda kwenye njia iliyonyooka ambayo hapotei mwenye kuifuata. Maana kwa ujumla ni kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni kishiko cha kutegemewa hakikatiki milele na kwamba mwenye kushikamana nacho hapotei. Katika Sahih Muslim anasema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema:Hakika mimi ninaacha kwenu vitu ambavyo kama mkishikamana navyo hamtapotea baada yangu, kimojawapo ni kikubwa kuliko kingine, nacho ni kitabu cha Mwenyezi Mungu kamba yenye kuvutwa kutoka mbinguni hadi ardhini na kizazi changu Ahlul Bait wangu, vitu viwili hivyo havitaachana mpaka vije kwangu kwenye birika." Hadith hiyo pia imepokewa na Tirmidhyi, Lakini hivi sasa vitu vyote hivyo viwili vimeachwa. Ndio Imam Ali(a.s) akasema:"Utakuja wakati Qur'an haitabaki isipokuwa maandishi yake na Uislamu utabaki jina lake tu."

Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia Mjuzi.

Anasikia tamko la Tawhid kutoka kwa waumini, na la kufuru kutoka kwa makafiri; na anajua yaliyo katika nyoyo za watu wawili na atamlipa kila mmoja kwa amali zake.

Mwenyezi Mungu ni mtawala wa wale walioamini; huwatoa gizani na kuwaingiza katika mwangaza.

Wafasiri wametofautiana sana katika Aya hii. Baadhi yao wakazalisha mushkeli wa kiitikadi; mpaka Mulla Sadra akasema: "Kuna mushkeli mkubwa ambao ni vigumu kuutatua kwa wenye fahamu." Sheikh Muhammad Abduh amesema: "Hakika baadhi ya tafsiri ni tafsiri za wafasiri wasiokuwa wataalamu ambao hawafahamu mifumo ya lugha ya hali ya juu, au ni tafsiri za wasiokuwa Waarabu ambao zaidi huwa hawafahamu." Ama sababu ya kutofautiana wafasiri na kuzalisha matatizo ya kiitikadi ni kwamba wao wamefahamu Aya kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni mtawala na mwangalizi wa mambo ya waumini tu; na wala sio kwamba waumini wanamfanya Yeye tu kuwa ni mtawala na mwangalizi wa mambo yao. Hapo kuna tofauti kubwa kati ya maana hizi mbili, Kuanzia hapa ndipo umekuja mushkeli katika wanavyofahamu wafasiri, kwamba utawala wa Mwenyezi Mungu na msaada Wake unakuwa kwa viumbe vyote katika nidhamu moja; na wala sio kwa waumini tu.

Vyovyote itakavyokuwa, kauli za wafasiri au wengi wao hazioani na mfumo, na kwamba maana yaliyo salama, ambayo hayana matatizo yoyote na yanayoafikiana na kauli Yake Mwenyezi Mungu, Basi anayemkataa taghuti na akamwamini Mwenyezi Mungu, hakika yeye ameshika kishiko madhubuti kisichovunjika ni kuwa waumini hawamfanyi mtawala asiyekuwa Mwenyezi Mungu wala hawamfanyi yeyote kuwa mlinzi wao isipokuwa Mungu pekee Yake; Kwake wanakimbilia, na kwa Kitabu Chake na sunna ya Mtume Wake wanaongoka katika itikadi zao, kauli zao na vitendo vyao. Wala hawategemei watu wapotevu na mataghuti, hata wawe vipi. Kinyume chake ni makafiri ambao wanawafanya mataghuti ndio watawala wao.

Hapana mwenye shaka kwamba mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na akaendelea kumtii na kuongoka kwa Aya Zake na ubainifu Wake kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu na msaada Wake atasalimika kutokana na giza la bid'a na upotevu, vilevile matamanio na ujinga. Na atapata mwanga kwa nuru ya maarifa ya kweli na imani sahihi. Hayo ndiyo maana ya Huwatoa gizani na kuwaingiza katika mwangaza.

Lakini waliokufuru, watawala wao ni mataghuti. Huwatoa kwenye mwangaza na kuwiangiza katika giza.

Maana kwa ujumla ni kuwa makafiri wanawafanya watu wapotevu na mataghuti kuwa watawala wao badala ya Mwenyezi Mungu; wanachukua amri zao na kuacha makatazo yao. Hawa wanakwenda katika njia ya kuhiliki na wanawatoa kwenye mwangaza wa akili na maumbile na kuwati katika giza ukafiri na uzushi.

KUDUMU MOTONI

Watadumu humo

Mara nyingi sana Qur'an imetaja kuwa kuna aina ya waasi watakaodumu motoni; na imebainisha kuwa miongoni mwa aina hii ni: Mwenye kumkufuru na akakadhibisha Aya zake. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

"Na wale ambao wamekufuru na kukadhibisha ishara zetu, hao ndio watakoakuwa watu wa motoni, humo watadumu." (2:39)

Mwenye kumua mumini kwa makusudi, Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا ﴾

"Na mwenye kumuua Muumin kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam, humo atadumu ..." (4:93)

Mwenye kumwasi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na kuruka mipaka. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَيَتَعَدَّ حُدُودَهُ يُدْخِلْهُ نَارًا خَالِدًا فِيهَا ﴾

"Na anayemuasi Mwenyezi Mungu na Mtume, na kuiruka mipaka ya Mwenyezi Mungu, atamwingiza motoni, humo atadumu." (4:14)

Mwenye kuzungukwa na makosa yake; Mwenyezi Mungu anasema:

﴿بَلَىٰ مَن كَسَبَ سَيِّئَةً وَأَحَاطَتْ بِهِ خَطِيئَتُهُ فَأُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

"Ndio wanaochuma ubaya na makosa yao yakawazunguka, hao ndio watu wa motoni, humo watadumu" (2:81)

Hapana mwenye shaka kwamba kwa mujibu wa uadilifu Wake Mwenyezi Mungu, hamwadhibu isipokuwa mwenye kustahili adhabu na adhabu yake inatofautiana kwa ukali na udhaifu kulingana na makosa na maasi. Kosa la mwenye kuhangaika akieneza ufisadi duniani, akaangamiza mimea na viumbe, si sawa na kosa la mwenye kuiba shillingi moja au aliyemsengenya anayeshindana naye katika kazi. Pamoja na haya tunaweza kujiuliza. kudumu katika moto kusikokuwa na mwisho, kugongwa kichwa kwa macheche yaliyo kama majumba, kuvurumishiwa marungu ya chuma mgongoni na kujazwa tumbo kwa maji ya usaha; kisha mtu asife akapumzika wala asipunguziwe angalau akapumua; mtu huyu ambaye anaumizwa na chawa na kufa kwa kusongwa koo na jasho humfanya anuke; kama alivosema Amirul Muminin Ali(a.s) . Tujiulize je machungu yote haya makubwa kwa mnyonge huyu mwenye kushindwa na chawa, yanaafikiana na dhati ya Mwenyezi Mungu ambaye ni heri tupu na rehema, ukarimu, neema, upole na hisani?" Je inaingilika akilini mtu huyu kuadhibiwa milele au kunyimwa kabisa neema Au huko kuwa milele na kila ngozi inapoiva kubadilishwa ngozi nyingine bila ya kupumzika, yote hayo ni ya kujiuliza.

Akisema msemaji: Hakuna adhabu ambayo itazidi ya mwenye kumuua Hussein bin Ali(a.s) au aliyetupa bomu la Atomic au Haidrojeni kwa watu na akawamaliza wote, au mwenye kuanzisha mambo mabaya, yakadumu na uovu wake ukazidi?

Jibu : Ni kweli kuwa hazidi yeyote katika uliowataja, lakini sio kila asi ni Yazidi wala sio kila bomu ni Atomic na Hadrojeni; wala sio kila desturi inawatawanya watu. Lakini swali halikuwa juu ya hawa, bali swali ni juu ya kudumu walio na daraja nyingine. Unaweza kusema: Maelezo ya Qur'an na Hadith za Mtume juu ya kudumu milele utazifanyaje?

Jibu : Hakuna katika hizo inayokataa Taawil.

Ukisema tena kuwa, kila kilicho elezwa ikiwa kukielewa kunawezekana kwa dhahiri, basi ni wajibu kudumu juu ya dhahiri yake, kwa hiyo kudumu wakosaji katika moto si muhali.

Jibu : Ndio, lakini lichukuliwe la kudumu muda mrefu badala ya milele, kwa kukusanya kati ya Qur'an na dalili za rehema ambako, hakukataliki wala hakupingwi na sharia na akili. Utasema mara ya tatu: Hakika mafaqihi hawawezi kuridhika na jawabu hili, kwa sababu wao hawaruhusu kuchukulia kinyume cha dhahiri ya tamko isipokuwa kwa sababu tatu: Kuunganisha na kitu kingine kwa kidesturi, kama vile kuchukulia mahsus kutoka katika jumla; au kisheria, kama kauli wazi yenye kuthibiti kutoka kwa Masum; au kiakili kusikokubali uwezekano wa kinyume, Na sisi hatuna chochote katika hivyo vitatu.

Jibu :Kwanza : Ninadhani kuwa mafaqihi waliozitambua dalili za rehema ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) wataafikiana nami, kwamba inawezekana kuziacha dhahiri za dalili za kudumu milele katika moto kwa baadhi ya wakosaji. Miongoni mwa dalili hizo ni Hadith Qudsi: "Rehema yangu imeshinda ghadhabu yangu." Vilevile Hadith tukufu inayosema: Hakika waombezi siku ya Kiyama ni wengi na mwisho wa waombezi ni mwenye kurehemu wenye kurehemu. Na kwamba rehema yake Mwenyezi Mungu itaenea siku ya Kiyama mpaka ibilisi atakuwa na tamaa na kunyoosha shingo yake. Katika baadhi ya riwaya ni kwamba Hassan al Basri alisema: "Si ajabu kwa aliyeangamia, kuwa vipi ameangamia. Lakini ajabu ni ya mwenye kuokoka vipi ameokoka." Imam Zainul Abidin(a.s) akasema: "Ama mimi ninasema; sio ajabu kwa aliyeokoka kuwa ameokoka vipi; isipokuwa ajabu ni kwa aliyeangamia kuwa ameangamia vipi pamoja na ukubwa wa rehema ya Mwenyezi Mungu!"

Tukiiunganisha riwaya hii na Aya inayosema:

﴿قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا﴾

"Sema! Enyi waja wangu waliojidhulumu! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu; hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote ..." (39:53).

Tunapata ulinganisho mkataa wa kuacha dhahiri ya dalili za kudumu milele motoni.

Pili : Sisi tunazungumza mambo ya kiitikadi mkataa, sio masuala ya matawi ya kudhania; na mafaqihi pamoja na kujichunga kwao na nguvu ya imani zao, wanakuwa ni wataalamu wa hukumu za Mwenyezi Mungu za kisharia sio mambo ya itikadi. Bali wengi katika wao wako katika daraja ya kufuata yale yanayorudia sifa za Mwenyezi Mungu na vitendo Vyake. Ama yale yanayorudia kwenye dalili za kuweko Muumbaji (s.w.t) ni dalili za mzunguuko na kuendelea. Hata hivyo ni lazima ieleweke kuwa sisi tunaamini kuswihi kufuata katika misingi ya itikadi ikiafikana na mambo yalivyo.

Tatu : Akili huona vibaya kukhalifu ahadi, lakini sio kiaga, Ukimwambia mtu mwingine nitakufanyia wema; kisha uvunje ahadi, basi utakuwa mwenye kulaumiwa mbele za wenye akili. Ama ukamwambia unayemdai haki: Nitachukua haki yangu tu kutoka kwako kisha umsamehe, basi wewe utakuwa mwenye kusifiwa mbele ya Mwenyezi Mungu na watu; hasa akiwa yule unayemdai ni fukara na wewe ni tajiri.

Na Mwenyezi Mungu ni tajiri kwa viumbe na adhabu zao. Na wao wana haja sana ya rehema Yake na msamaha wake.

Swali la nne na la mwisho: Kwa nini unaleta taawil ya Aya za kudumu motoni na ni maana gani unayoyachukulia?

Jibu : Inawezekana kuchukulia maana ya kudumu muda mrefu, lakini sio milele; au kudumu motoni bila ya adhabu; kama hema la Hatimtai ( [3] ) au kuwepo Ibrahim katika moto.

Haya yanatiliwa nguvu na yaliyopokewa katika baadhi ya Hadith kwamba baadhi ya watu wa motoni watakuwa wanacheza na makaa ya moto kama mpira wakirushiana. Hapana mwenye shaka kwamba mchezo huu hauwezi kuwa pamoja na adhabu hata hafifu sikwambii kali yake. Na Mungu si Mwenye kushindwa kuufanya moto baridi na salama kwa asiyekuwa Ibrahim kama alivyoufanya kwa Ibrahim(a.s) .

Muhhiddin Ibn al Arabi anasema katika al Futuhul Makkiyya J2 uk. 127: "Hatobaki motoni mwenye kumwamini Mungu mmoja katika waliopelekewa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , kwa sababu moto utarudi kuwa baridi na salama kwa wanaompwekesha Mwenyezi Mungu kwa baraka za Ahlul Bait katika akhera. Ni utukufu ulioje wa baraka za Ahlul Bait!