TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU Juzuu 3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU 30%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 12 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 17918 / Pakua: 3852
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TATU Juzuu 3

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TATU

﴿وَمِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ مَنْ إِن تَأْمَنْهُ بِقِنطَارٍ يُؤَدِّهِ إِلَيْكَ وَمِنْهُم مَّنْ إِن تَأْمَنْهُ بِدِينَارٍ لَّا يُؤَدِّهِ إِلَيْكَ إِلَّا مَا دُمْتَ عَلَيْهِ قَائِمًا ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَالُوا لَيْسَ عَلَيْنَا فِي الْأُمِّيِّينَ سَبِيلٌ وَيَقُولُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴾

75.Na katika watu wa Kitabu yuko ambaye ukimwamini na mrundo wa mali atakurudishia. Na katika wao yuko ambaye ukimpa amana ya dinari moja hakurudishii, isipokuwa ukimsimamia hayo ni kwa kuwa walisema: "Hatuna lawama kwa wasiojua kusoma" Na wanamzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na hali wanajua.

﴿بَلَىٰ مَنْ أَوْفَىٰ بِعَهْدِهِ وَاتَّقَىٰ فَإِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُتَّقِينَ ﴾

76.Sivyo hivyo, bali anayetimiza ahadi na akamcha Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu huwapenda wacha Mungu

KUNA WAAMINIFU NA WAHAIN I KATIKA WATU WA KITABU

Aya 75 - 76

MAANA

Na katika watu wa Kitabu yuko ambaye ukimwamini na mrundo wa mali atakurudishia katika wao, Na yuko ambaye ukimpa amana ya dinar moja hakurudishii.

Makusudio ni kwamba katika watu wa Kitabu kuna ambao wako katika upeo wa uaminifu, hata ukiwaamini na mali nyingi, basi watatekeleza amana. Na pia wako walio katika upeo wa hiyana hawaaminiki hata kwa dinar moja tu. Umetajwa uaminifu wa mali, kwa sababu ndiyo mtihani sahihi wa kujua ubovu na uzima wa moyo wa mtu.

HAKUNA MAISHA ILA KWA UKAKAMAVU WA KUTOJALI MAUTI

Isipokuwa ukimsimamia

Mwenye hiyana hutaka zaidi ya haki yake wala hatekelezi haki ya watu, kwa sababu ni maiti wa dhamiri. Wala hakuna njia ya kuipata haki kutoka kwake isipokuwa kwa kumsimamia, kama alivyosema mwenye hekima kubwa. Maana ya kumsimamia mwenye hiyana mnyang'anyi ni kumsonga na kugombana naye kwa silaha yoyote uliyo nayo. Walikwishasema wahenga: "Uhuru huchukuliwa, wala hautolewi." Kumsonga mhaini ni faradhi ya lazima; vinginevyo ufisadi ungelienea duniani. Kosa la kunyamaza mdhulumiwa, ni sawa na kosa la dhalimu. Kwa sababu wote wawili wanaandaa kueneza dhulma na ufisadi. Lau dhalimu angelijua kuwa mdhulumiwa ana hisia za kutojali kufa kugombea haki yake,basi asingelidhulumu.

Majaribio yametufahamisha kuwa hakuna haki katika Umoja wa mataifa wala Baraza la usalama isipokuwa kwa kutumia nguvu; na kwamba hakuna maisha katika karne ya ishirini hasa Mashariki ya kati na hasa hasa waarabu, isipokuwa kwa ukakamavu wa kutojali mauti.

Hayo ni kwa kuwa walisema: Hatuna lawama kwa wasiojua kusoma.

Maana yake ni kuwa watu wa Kitabu walijihalalisha mali za waarabu, kwa sababu wao walidai kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hatawaadhibu kwa unyang'anyi huo.( [13] ) Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu uzushi wao, kwa kusema:

Na wanamzulia Mwenyezi Mungu uwongo na hali wanajua.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kumzulia Mwenyezi Mungu kwa kukusudia, hiyana yake ni kubwa na kosa lake ni ovu zaidi. Unaweza kuuliza: Mataifa yote na watu wa dini zote, bali hata walahidi pia, kuna waaminifu na wenye hiyana; wakweli na waongo. Kuna walahidi kadhaa walio wakweli na kutekeleza amana kuliko wanaofunga na kuswali. Sasa kuna wajihi gani wa kuwahusisha watu wa Kitabu na kifungu hiki?

Jibu :Kwanza : katika Aya Mwenyezi Mungu amesema kuwa baadhi ya watu wa Kitab wanataka kuwapoteza, akasema tena wanataka kuamini asubuhi na kukufuru jioni. Na katika aya hizi anabainisha kuwa kuna waaminifu na wahaini, Na hii haimaanishi hakuna wengine wasiokuwa hivyo.

Pili : Inawezekana tuadhanie watu wa Kitabu wote wana hiyana; ndipo Mwenyezi Mungu akaondoa tuhuma hii, kwamba wao ni kama vikundi vingine na watu wa dini nyingine.

Si hivyo, bali anayetimiza ahadi yake na akamcha Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu huwapenda wacha mungu.

Ni kuthibitisha yale waliyoyakana watu wa Kitabu waliposema: Hatuna lawama kwa wasiojua kusoma na kwamba wao ni waongo katika madai haya.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuthibitisha njia ya mwenye kujihalalishia mali za watu, anaeleza kuwa mwenye kutekeleza ahadi na akaogopa yaliyoharamishwa, basi yeye ni mwenye kupendeza mbele ya Mwenyezi Mungu. Imepokewa Hadith, Mtume amesema:"Hakuna kitu kilichokuwa wakati wa ujahiliya isipokuwa kiko chini ya wayo wangu, isipokuwa amana; kwani hiyo inatekelezewa mwema na muovu". Imam Zainul-abidin(a.s) anasema:"Lau aliyemuua baba yangu Hussein ataniwekea amana upanga aliomuulia baba yangu, basi nitamtekelezea amana yake." Imam Jaffer Assadiq(a.s) anasema:"Mambo matatu hayana udhuru kwa yeyote: Kutekeleza amana kwa mwema au muovu, kuwatendea wema wazazi wawili wema au waovu na kutekeleza ahadi na mwema au muovu." Kwa sababu hiyo ndipo mafakihi wa Shia Imamia wakaafikiana kuwa Kafiri akitangaza vita na waislam, ni halali damu yake lakini haijuzu kumfanyia hiyana. Kwa mfano lau alikuwa ametoa mali yake kwa mwislam, ni lazima arudishe amana pamoja na kujua kuwa inajuzu kumuua na kuchukua mali yake, lakini sio ile aliyoiweka amana.

﴿إِنَّ الَّذِينَ يَشْتَرُونَ بِعَهْدِ اللَّـهِ وَأَيْمَانِهِمْ ثَمَنًا قَلِيلًا أُولَـٰئِكَ لَا خَلَاقَ لَهُمْ فِي الْآخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ اللَّـهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيْهِمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴾

77.Hakika wale wanaouza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapo vyao kwa thamani ndogo. Hao hawatakuwa na sehemu yoyote akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watapata adhabu iumizayo.

ASIYE NA AHADI HANA DINI

Aya 77

MAANA

Arrazi anasema katika kufasiri Aya hii: "Yanaingia katika Aya hii yote aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu, yale aliyoyatolea hoja, yaliyochukuliwa kutoka upande wa Mtume na Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Tatu 2. Sura Al-Imran yanaingia yale yanayomlazimu mtu mwenyewe. Kwa sababu yote hayo ni katika ahadi ya Mwenyezi Mungu ambayo ni lazima kuitekeleza." Katika Hadith imeelezwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) hakuhutubia hotuba yoyote isipokuwa alisema: "Asiye kuwa na uaminifu hana imani na asiyekuwa na ahadi hana dini." Aya hii na Hadith hii na nyinginezo zinatufahamishia kuwa Uislam unafungamana na tabia na maadili; ndipo ukawajibisha kutekeleza mambo yote ya lazima ya kuamiliana na wengine; na ukakuzingatia kuwa ni kuamiliana na Mwenyezi Mungu, hata kama ni kuamiliana na mlahidi kwa sharti ya kuwa muamala wenyewe usipingane na misingi ya kimaadili; vinginevyo kutakuwa ni batili hakufai.

Vilevile kwa upande wa hukumu, ambapo uislam umemwajibishia kadhi kusikiliza sauti ya dhamiri na hoja ya kitabia kabla ya kusikiliza kauli ya wanaogombana. Nadharia ya tabia; ndio mkazo wa kwanza wa sharia za kiislamu kwa kawaida zake zote na hukmu zake. Kwa ajili hii Mwenyezi Mungu amewatishia wale wanaovunja ahadi na wasiokuwa na uaminifu kwa kitisho ambacho hakumtisha yeyote katika wafanyao madhambi makubwa; pale aliposema:

Hao hawatakuwa na sehemu yoyote akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama siku ya kiyama wala hatawatakasa, nao watapata adhabu iumizayo.

Ama siri ya kuhimiza huku na kutoa tisho kwa wasiotekeleza ahadi ni kuchunga maslahi ya watu, kuweko kutegemeana kati ya watu na kuchunga haki, mambo ambayo ndio msingi wa amani na nidhamu.

﴿وَإِنَّ مِنْهُمْ لَفَرِيقًا يَلْوُونَ أَلْسِنَتَهُم بِالْكِتَابِ لِتَحْسَبُوهُ مِنَ الْكِتَابِ وَمَا هُوَ مِنَ الْكِتَابِ وَيَقُولُونَ هُوَ مِنْ عِندِ اللَّـهِ وَمَا هُوَ مِنْ عِندِ اللَّـهِ وَيَقُولُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴾

78.Na hakika miongoni mwao kuna kundi linalopinda ndimi zao kwa Kitabu ili mpate kuyadhani hayo kuwa ni ya Kitabu wala si ya Kitabu. Na wanasema: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu, na hali hayakutoka kwa Mwenyezi Mungu; na wanasema uwongo juu ya Mwenyezi Mungu na hali wanajua

WANAPINDA NDIMI ZAO KWA KITABU

Aya 78

Aya hii ni mwendelezo wa Aya 75. Makusudio ya kupinda ni kugeuza. Kuna Aya nyingi zinazoelezea kugeuza kwao maneno ya Mwenyezi Mungu,

﴿تَجْعَلُونَهُ قَرَاطِيسَ تُبْدُونَهَا وَتُخْفُونَ كَثِيرًا﴾

"Miongoni mwa hizo ni: Mmekifanya kurasa mlizoonyesha baadhi na kuficha nyingi."( 6:91)

﴿وَقَدْ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْهُمْ يَسْمَعُونَ كَلَامَ اللَّـهِ ثُمَّ يُحَرِّفُونَهُ مِن بَعْدِ مَا عَقَلُوهُ وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴾

"Baadhi yao walikuwa wakisikia maneno kisha wakiyabadili baada ya kuwa wameyafahamu." (2:75)

Mtu atakayeiona Tawrat yao, atakubali kuwa wamezua, ambapo Mwenyezi Mungu amena sibishiwa kula na kupigana hata miereka; kama ambavyo mitume wamenasibishiwa ulevi, na kuzini na mabinti zao.

Kugeuza kunathibiti kwa kuongeza au kupunguza; kama kuzidisha katika maandishi au kupunguza. Vilevile kunathibiti kwa kugeuza irabu, kama kumfanya mtendaji kuwa ndiye mtendwa. Pia kugeuza kunaweza kuthibiti kwa tafsir; kwa kufasiri kiuhakika badala ya kimajazi; mfano mkono wa Mwenyezi Mungu badala ya uwezo wa Mwenyezi Mungu. Wafasiri wametofautiana kuhusu aina ya mageuzi iliyokusudiwa katika Aya hii.Sheikh Muhammad Abduh amesema kuwa makusudio ya kugeuza hapa ni kugeuza tafsir na kulipa tamko maana yasiyokusudiwa; akatoa mfano wa hilo kwa neno liliosemwa na Masih (Baba yetu aliye mbinguni) akiwa na makusudio ya huruma na upole wa Mwenyezi Mungu kwa waja wake, lakini baadhi ya wakubwa wa kikristo wamefasiri kuwa Mwenyezi Mungu ni baba wa Isa (Yesu) kiuhakika.

Tunavyoona sisi katika tafsir ya Aya hii ni kwamba kikundi hicho cha watu wa kitabu kilikuwa kikipindua tamko lenyewe na kuzusha fikra nyingine na kuwafanya watu wafikirie kuwa ni kitabu cha Mwenyezi Mungu ili wawe na itikadi ya batili. Kwa hiyo, tamko la kwanza la Kitabu katika Aya ni kinachodaiwa kuwa ni kitabu; na tamko la pili na la tatu ni sifa ambayo. Kukadiri kwake ni wanapinda ndimi zao kwa kinachodaiwa kuwa ni Kitabu ambacho kimegeuzwa, ili nyinyi watu, mkifikirie kuwa kinatokana na Kitabu cha hakika cha asili, na wala sio Kitabu kamwe.

Ama kauli Yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Na wanasema hayo yanatoka kwa Mwenyezi Mungu na wala hayatoki kwa Mwenyezi Mungu , ni kutilia mkazo kauli yake: na wala hayatokani na kitabu. Imesemekana kuwa hayo ni kutilia mkazo upande wa kuunganisha ujumla juu ya umahusus. Kwa sababu kitabu kinahusika na wahyi ulioteremshiwa Mtume. Ama yale yanayotoka kwa Mungu yanakuwa ni Hadith za Mtume na hukumu ya kiakili.

﴿مَا كَانَ لِبَشَرٍ أَن يُؤْتِيَهُ اللَّـهُ الْكِتَابَ وَالْحُكْمَ وَالنُّبُوَّةَ ثُمَّ يَقُولَ لِلنَّاسِ كُونُوا عِبَادًا لِّي مِن دُونِ اللَّـهِ وَلَـٰكِن كُونُوا رَبَّانِيِّينَ بِمَا كُنتُمْ تُعَلِّمُونَ الْكِتَابَ وَبِمَا كُنتُمْ تَدْرُسُونَ ﴾

79.Haiwezekani kwa mtu aliyepewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hekima na Unabii, kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu. "Kuweni watumishi wa Mwenyeezi Mungu. Kwa kuwa mnafundisha Kitabu na kwa sababu mnakisoma .

﴿وَلَا يَأْمُرَكُمْ أَن تَتَّخِذُوا الْمَلَائِكَةَ وَالنَّبِيِّينَ أَرْبَابًا أَيَأْمُرُكُم بِالْكُفْرِ بَعْدَ إِذْ أَنتُم مُّسْلِمُونَ﴾

80. Wala hatawaamrisha kuwafanya Malaika na manabii kuwa waungu. Je,atawaamrisha ukafiri baada ya kuwa nyinyi waislamu?

KUWENI WATUMISHI WA MUNGU

Aya 79 - 80

MAANA

Haiwezekani kwa mtu aliyepewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hekima na Unabii kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu.

Hapana mwenye shaka kwamba haiwezekani kwa mtu kupewa kitabu, hukumu na utume kuwaambia watu wamwabudu, kwa sababu hiyo ni kufuru na Mwenyezi Mungu hawachagui makafiri. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

"Na hakika tumewachagua kwa ujuzi juu ya walimwengu wote" (44:32) Aya hii Tukufu ni jibu la wale wanaowawekea mitume na mawali baadhi ya sifa za Mungu. Vilevile ni ushahidi kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwatakasa Mitume. Kwamba Mtume ana yakini kuwa yeye ni mja miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu pekee ndiye mwenye kuabudiwa. Sasa itawezekanaje yeye awatake waja wamwabudu yeye au waaabudu Malaika. Yeye anawaamrisha wawe waalimu na watumishi wa Mwenyezi Mungu kwa vitendo.

Imeelezwa katika Hadith kwamba mtu mmoja alimwambia Mtume: "Tukusujudie?" Mtume akajibu: "La, haitakikani kusujudiwa yeyote zaidi ya Mwenyezi Mungu." Mwengine naye alisema: "Je unataka tukuabudu na tukufanye Mungu." Akasema Mtume: "Mwenyezi Mungu anihifadhi na hilo! Sikuamrishwa hivyo wala sisemi hivyo" Ama kisa cha Imam Ali kuwachoma moto wale waliomnasibisha uungu ni mashuhuri kiasi cha kutohitajiwa kutajwa. Kila mwenye kuwataka watu wamwabudu, basi ni kafiri; na kila mwenye kuwataka wamtukuze kwa makusudio ya kujitukuza na kujiweka juu, basi ni fasiki. Unaweza kuuliza: "Aya imekusanya matamko matatu: Kitabu, hekima na unabii: na kila tamko maana yake yako wazi hayahitaji tafsir kama yakiwa peke yake. Lakini yakiwa pamoja katika jumla moja na yakaunganishwa, basi yanahitaji tafsir. Kwa sababu, maana yake yanaingiliana; hasa kupewa kitab na unabii. Na tunajua kuwa kuungana maneno kunamaanisha tofauti na kubadilika. Sasa kuna njia gani ya kutofautisha matamko hayo matatu?

Jibu : Makusudio ya Kitabu ni Kitabu kilichoteremshwa na Mwenyezi Mungu kama Tawrat, Zabur, Injil na Qur'an. Makusudio ya hekima ni elimu na sunna za utume. Mwenyezi Mungu anasema Kuhusu Yahya:

"Na tulimpa hekima akiwa mtoto (19:12)

Ama unabii maana yake ni maarufu; nao ingawaje unalazimisha kujua Kitabu na Sunna, lakini kuyajua hayo mawili hakulazimishi unabii. Kila nabii anajua Kitabu na Sunna, lakini sio kila anayejua Kitabu na Sunna ni nabii. Aya hii iko katika mfano wa Aya isemayo:

"Hao ndio ambao tumewapa Kitabu na hekima na unabii" (6:89)

Lakini kuweni watumishi wa Mwenyezi Mungu kwa kuwa mnafundisha kitabu na kwa kuwa mnakisoma.

Yaani Mtume anawaambia watu kuweni wajuzi wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu, wenye kukitumia na wenye kuwafundisha wengine, Sheikh Muhammad Abduh anasema: "Aya inafahamisha kuwa mtu atakuwa mtumishi wa Mwenyezi Mungu kwa kukijua Kitabu, kukifundisha kwa watu na kukitangaza. Na ni uthibitisho kuwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu hakuwi kwa elimu pekee, bali ni lazima kuwa pamoja na vitendo"

Wala hatawaamrisha kuwafanya Malaika na manabii kuwa waungu.

Yaani Mtume haamrishi wala hatamwamrisha yeyote kuwafanya wengine kuabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu.

Je,atawaamrisha ukafiri baada ya kuwa nyinyi Waislamu?

Wao ni Waislamu kwa sababu wao wamemwamini nabii na wakachukua kauli yake. Mwenye kumwamini nabii yeyote wakati wowote yeye ni mwislamu kwa mujibu wa istilahi ya Qur'an. Ufafanuzi wa hilo umetangulia katika kufasiri Aya ya 19 ya Surah hii. Mwenye kufuatilia Aya za Qur'an na Hadith za Mtume wa Mungu, ataona kuwa miongoni mwa mambo ya asili yanayojitokeza zaidi, ambayo uislam unatofautiana na dini nyengine, ni kusisitiza kuwa haifai kwa hali yoyote kuinasibisha sifa ya Mungu kwa kiumbe, awe mtume, mfalme au walii. Siri ya kulitilia mkazo hilo ni kwamba umbile la mtu linapondokea sana kwenye kutopea kama tunavyoshuhudia hilo kwa baadhi ya watu wa dini. Pamoja na sisitizo hilo, lakini utawakuta waislam waliotopea (Ghulat) na kwamba Waislam leo- tukiwa katika karne ya ishirini - wanawanasibishia wafu mambo ambayo hayafai kuyanasibisha isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu peke yake, asiyekuwa na mshirika.

﴿وَإِذْ أَخَذَ اللَّـهُ مِيثَاقَ النَّبِيِّينَ لَمَا آتَيْتُكُم مِّن كِتَابٍ وَحِكْمَةٍ ثُمَّ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مُّصَدِّقٌ لِّمَا مَعَكُمْ لَتُؤْمِنُنَّ بِهِ وَلَتَنصُرُنَّهُ قَالَ أَأَقْرَرْتُمْ وَأَخَذْتُمْ عَلَىٰ ذَٰلِكُمْ إِصْرِي قَالُوا أَقْرَرْنَا قَالَ فَاشْهَدُوا وَأَنَا مَعَكُم مِّنَ الشَّاهِدِينَ﴾

81.Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi kwa manabii. Nikiwapa kitabu na hekima; kisha akawajia mtume msadikishaji wa yale yaliyo pamoja nanyi, ni juu yenu kumwamini na kumsaidia. Akasema: Je, mmekubali na mmechukua ahadi yangu kwa hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema: basi shuhudieni, na mimi ni pamoja nanyi katika mashahidi.

﴿فَمَن تَوَلَّىٰ بَعْدَ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ ﴾

82.Na atakayegeuka baada ya hayo, basi hao ndio mafasiki.

﴿أَفَغَيْرَ دِينِ اللَّـهِ يَبْغُونَ وَلَهُ أَسْلَمَ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ طَوْعًا وَكَرْهًا وَإِلَيْهِ يُرْجَعُونَ ﴾

83.Je, wanataka dini isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu na hali waliomo mbinguni na ardhini wanamtii yeye wapende wasipende, Na kwake yeye watarejeshwa.

MSHIKAMANO WA MITUME

Aya 81 - 83

MTUME NA MREKEBISHAJI

Hakuna tofauti kati ya mtume na mrekebishaji katika ukweli wa nia na ikhlasi katika amali. Lakini wanatofautiana kwa kuwa mtume hakosei. Kwa vile yeye anasema na kutenda kwa wahyi utokao kwa Mwenyezi Mungu. Ama mrekebishaji, hufanya kwa kutegemea mtazamo wake na jitihadi yake. Na mwenye kujitahidi hukosea na kusibu. Kwa hivyo upo uwezekano wa kutofautiana katika jitihadi na mtazamo, Na imesihi kumwondokea jukumu akikosea. Ama kutofautiana mitume kabisa, hilo haliwezekani, Kwa sababu wote wanategemea chimbuko moja - wahyi unaowaelekea wote. Kwa hivyo mitume ni sawa na wafanyikazi wa serikali katika kufikisha amri kwa wananchi.

Haya yanafungamana na kuwa Mwenyezi Mungu anapopeleka manabii wawili kwenye umma mmoja, wakati mmoja, basi watakuwa ni wenye kuafikiana katika kila kitu; kama ilivyotokea kwa Musa na Harun(a.s) . Na kama watakuwa katika nyakati mbalimbali, watakuwa wanaafikiana wote katika fikra na misingi; kama vile kumwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Ikiwa kutakuwa na tofauti, basi ni tofauti katika picha yake na katika hukumu za matendo ambazo zinakwenda na wakati. Hata hiyo nayo wanaikubali Manabii wote kuwa ni ukweli na haki na ni dharura. Kwa hivyo basi hakuna tofauti kabisa kati ya manabii wote na ni kwa ajili hiyo ndipo kila mtume alisadikisha nabii mwenzake aliyemtangulia, Unaweza kuuliza kuwa inawezekana nabii kumsadikisha nabii mwenzake aliyemtangulia. Bali ndivyo ilivyo hasa: sisi tunaamini utume wa Isa na Muhammad; Ibrahim naye akaamini aliyokuja nayo Nuh; Musa akaamini waliyo kuja nayo wote wawili; Isa akaamini waliyokuja nayo wote watatu na Muhammad(s.a.w.w) akaamini waliyokuja nayo wote. Hili linaingilika akilini sana. Lakini litaingilikaje akili kuwa nabii aliyetangulia amwamini atakayekuja baadae,ambaye bado hajapatikana?

Jibu : Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) anaampa wahyi Mtume aliyetangulia kwamba Yeye atamtuma Mtume baada yake na kubainisha jina lake na sifa zake. Na ni juu ya yule aliyetangulia kuwatangazia watu wa kizazi alicho yeye katika uma wake ili nao wawatangazie watakaofuatia. Kwa hivyo akija anayefuatia anakuta njia ya kusadikisha imani yake na ujumbe wake imeandaliwa. Tumeyaeleza haya kuwa ni utangulizi na kurahisisha ufahamu Aya hizi zifuatazo.

IRABU

Inawezekana kusoma Lima kwa kuifanya herufi Lam ni ya Jarri. Kwa maana ya kuwa Mwenyezi Mungu alipochukuwa ahadi kwa manabii kwa kwa ajili kuwapa Kitabu na hikima. Na inawezekana kusoma Lama, kwa fat-ha kuifanya lamu ni ya kuanzia (Mubtada). kwa maana ya, Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi kwa manabii: Nikiwapa Kitabu na hekima.

MAANA

Na Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi kwa Manabii: Nikiwapa kitabu na hekima; kisha akawajia mtume msadikishaji wa yale yaliyo pamoja nanyi, ni juu yenu kumwamini na kumsaidia.

Kutokana na mfumo wa maneno ulivyo inafahamika kuwa makusudio ya manabii hapa ni manabi na wafuasi wao na wala si manabii peke yao. Na makusudio ya mtume ni mtume Muhammad(s.a.w.w) ; kama ilivyo Aya nyengine isemayo:

﴿وَلَمَّا جَاءَهُمْ رَسُولٌ مِّنْ عِندِ اللَّـهِ مُصَدِّقٌ لِّمَا مَعَهُمْ نَبَذَ فَرِيقٌ مِّنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ كِتَابَ اللَّـهِ وَرَاءَ ظُهُورِهِمْ كَأَنَّهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴾

"Na walipojiwa na mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu mwenye kusadikisha yale yaliyo pamoja nao kundi moja miongoni mwa wale waliopewa Kitabu lilitupa Kitabu cha Mwenyezi Mungu nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui." (2:101).

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) baada ya kuwabainishia mitume na umma unaowafuata, katika misingi na matawi, alichukua ahadi kwao wote kwamba wamwamini Muhammad(s.a.w.w) na wamsaidie; kama ambavyo naye Muhammad anawasadikisha waliomtangulia na vitabu walivyoviacha, kama vile Tawrat na Injil. Kuchukua ahadi kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa mitume ni kwa njia ya wahyi. Ama kwa wafuasi wa mitume ni kwa kupitia mitume. Yaani kila mtume anachukua ahadi kwa ulama wa umma wake kumwamini Muhammad na kumsaidia. Kwa maelezo ya ndani zaidi ni kwamba kuchukua ahadi kwa anayefuatwa ni lazima kuwe kwa mfuasi. Ikiwa ni wajibu kwa nabii kumwamini Muhammad basi imekuwa wajibu kwa wanaomfuata nabii huyo. Maana ya umma kumwamini Muhammad na kumsaidia, ni kuitakidi kwamba yeye atakuja baada yao na walibashirie hilo. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَإِذْ قَالَ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُم مُّصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيَّ مِنَ التَّوْرَاةِ وَمُبَشِّرًا بِرَسُولٍ يَأْتِي مِن بَعْدِي اسْمُهُ أَحْمَدُ﴾

"Na Isa aliposema: "Enyi wana wa Israil mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu; nisadikishaye yaliyokuwa kabla yangu katika Tawrat na kutoa bishara ya mtume atakayekuja baada yangu jina lake ni Ahmad (61:6)"

Imam Ali(a.s) anasema:"Mwenyezi Mungu hakupeleka Mtume yeyote ila huchukua ahadi naye kuhusu Muhammad (s.a.w.w) na kumwamrisha kuchukua ahadi na watu kuwa watamwamini na kumsaidia, kama watazikuta zama zake"

Maana ya Umma kumwamini Muhammad(s.a.w.w) na kumsaidia ni kumsadikisha wanavyuoni wao na viongozi wa dini zao na kuwatangazia wale wanaowategemea kwamba Muhammad bin Abdullah ndiye Mtume aliyebashiriwa na mitume, na kwamba jina lake liko katika Vitabu vya dini zao kama asemavyo Mwenyezi Mungu Mtukufu.

﴿الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الرَّسُولَ النَّبِيَّ الْأُمِّيَّ الَّذِي يَجِدُونَهُ مَكْتُوبًا عِندَهُمْ فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ﴾

"Ambao humfuata mtume ummi ambaye humkuta ameandikwa kwao katika Tawrat na Injil (7:157)

Na wala wasiyapindue maneno ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru na inadi, kama alivyowaelezea Mwenyezi Mungu (s.w.t):

﴿وَقَدْ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْهُمْ يَسْمَعُونَ كَلَامَ اللَّـهِ ثُمَّ يُحَرِّفُونَهُ مِن بَعْدِ مَا عَقَلُوهُ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴾

Hali ya kuwa baadhi yao walikuwa wanasikia maneno ya Mwenyezi Mungu kisha wanayabadili baada ya kuwa wanayafahamu; na hali wanajua. (2:75)

Akasema: Je, mmekubali na mmechukua ahadi yangu kwa hayo? Wakasema: Tumekubali.

Swali hapa ni la kuthibitisha na kutilia mkazo. Maana yake ni Mwenyezi Mungu aliziambia Umma kwa ndimi za mitume yao: Je, mmemkubali Muhammad na mmekubali ahadi? Umma ukasema: Ndio tumekubali wajibu wa kumwamini kumsaidia. Tumelikubali hilo na tumelazimiana nalo. Makusudio ya umma ni viongozi wa dini na wanavyuoni wao wanaojua vitabu vya dini. Akasema: Shuhudieni; yaani akasema Mwenyezi Mungu kwa ndimi za mitume Yake kwa umma shuhudizaneni kwamba mmekubali utume wa Muhammad(s.a.w.w) na wajibu wa kumsaidia.

Mimi ni pamoja nanyi katika mashahidi.

Mwenyezi Mungu na Malaika wake na mitume Yake wanashuhudia kuchukuliwa kwa ahadi ya wanavyuoni wa kidini, na kumkubali kwao Muhammad(s.a.w.w) , lakini pamoja na hayo wanavyuoni wa kiyahudi na wa Kinaswara walikana ahadi hii; wakamkadhibisha Muhammad na kumfanyia vitimbi na kiburi kama zilivyofafanua Aya zilizotangulia,

Na atakayegeuka baada ya hayo.

Yaani atakayegeuza kumwamini Muhammad baada ya kuchukua ahadi ya kumkubali na kumsaidia,

Basi hao ndio mafasiki.

Makusudio ya mafasiki hapa ni makafiri. Kwa sababu kila mwenye kugeuza Aya kutoka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu na akakanusha utume miongoni mwa mitume ya Mwenyezi Mungu huku akijua utume wake basi yeye ni kafiri.

Je, wanataka dini isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu na hali waliomo mbinguni na ardhini wanamtii yeye wapende wasipende.

Watu wote wanamwamini Mwenyezi Mungu bila ya kutofautiana mwema na muovu, isipokuwa kwamba mwema humwamini Mwenyezi Mungu kwa hiyari katika maisha haya. Na muovu atamwamini kwa nguvu siku ya kiyama itakapoondoka pazia, na kila mkanushaji ataona adhabu kinaga ubaga. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿فَلَمَّا رَأَوْا بَأْسَنَا قَالُوا آمَنَّا بِاللَّـهِ وَحْدَهُ وَكَفَرْنَا بِمَا كُنَّا بِهِ مُشْرِكِينَ﴾

"Walipoiona adhabu yetu wakasema: Tunamwamini Mwenyezi Mungu pekee na tunawakataa tuliokuwa tukiwashirikisha naye." (40:84).

Haya ndiyo maana ya 'wapende wasipende' tulivyofasiri ambayo si mazito kufahamiwa na yeyote vyovyote alivyo. Lakini Razi amefasiri kwa tafsiri ya kifalsafa. Aliyoyasema yako karibu, lakini ni kwa watu maalum watakaoelewa sio wote. Na hapa tunayanakili kwa ajili yao sio kwa ajili ya hawa: "Kila kisichokuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kinawezekana kwa dhati yake; na kila chenye kuwezekana kwa dhati yake hakipatikani ila kwa kukipatisha yeye na hakikosekani ila kwa kukikosesha yeye. Kwa hiyo, kila kisichokuwa Mwenyezi Mungu ni chenye kumnyeyekea Mwenyezi Mungu Mtukufu katika njia zote mbili za kupatikana kwake na kukosekana kwake, Na, huo ndio ukomo wa kunyenyekea"

﴿قُلْ آمَنَّا بِاللَّـهِ وَمَا أُنزِلَ عَلَيْنَا وَمَا أُنزِلَ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ وَالْأَسْبَاطِ وَمَا أُوتِيَ مُوسَىٰ وَعِيسَىٰ وَالنَّبِيُّونَ مِن رَّبِّهِمْ لَا نُفَرِّقُ بَيْنَ أَحَدٍ مِّنْهُمْ وَنَحْنُ لَهُ مُسْلِمُونَ﴾

84.Sema tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa na yale aliyoteremshiwa Ibrahim na Ismail na Is-haq na Yaqub na wajukuu zao na alichopewa Musa na Isa na manabii kutoka kwa Mola wao; hatutofautishi baina yao hata mmoja na sisi ni wenye kusilimu kwake.

﴿وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الْإِسْلَامِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الْآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ ﴾

85.Na mwenye kutaka dini isiyokuwa uislam haitakubaliwa kwake, naye katika akhera ni miongoni mwa wenye kupata hasara.

TUMEAMINI MITUME YOTE

Aya 84 - 85

MAANA

Aya hii ya 85 imekwishapita pamoja na tafsiri yake katika Sura ya Baqara Aya 136. Kwa ufupi ni kwamba mayahudi na manaswara wanaamini baadhi ya manabii na wanawakanusha baadhi yao, Ama waislam, wao wanaamini wote. Kwa sababu, mwito wa manabii ni mmoja na lengo lao pia ni moja. Kwa hiyo, kujaribu kuwatofautisha ni sawa na kusema ndiyo na hapana kwa jambo moja tofuati ya kuamini unabii wao ni sawa na kitu kimoja, kwamba sawa ni hapana kwa pamoja, Na mwenye kutaka dini isiyokuwa Uislamu haitakubaliwa kwake.

Makusudio ya Aya hii yatajulikana kwa kurudia tafsiri ya Aya ya 19 ya Sura hii. Nimewaona baadhi ya watu wakitoa dalili kuwa hakuna tofauti baina ya mwislam, myahudi na mkristo maadam wote wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, kwa Aya isemayo:

﴿إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَادُوا وَالنَّصَارَىٰ وَالصَّابِئِينَ مَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَعَمِلَ صَالِحًا فَلَهُمْ أَجْرُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ وَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ﴾

"Hakika wale ambao wameamini na mayahudi na manaswara na wasabai, yeyote atayemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na akatenda mema, basi watapata malipo yao kwa Mola wao, wala haitakuwa hofu juu yao, wala hawatahuzunika." (2:62)

Hilo ni kosa kwa njia mbili:

Kwanza : kwamba makusudio ya waliotajwa katika Aya ni kila aliyekufa akiwa na imani na amali njema katika watu wa dini zilizomtangulia Muhammad(s.a.w.w) . Tumeyafafanua hayo wakati wa kufasiri Aya hiyo.

Pili : Hata kama dhahiri ya tamko la Aya inaonyesha kuwa inaenea wakati wote, lakini kauli yake Mwenyezi Mungu: Na mwenye kutaka dini isiyokuwa uislam hatakubaliwa," inaihusisha Aya hiyo na wale waliokuwa kabla ya wakati wa Muhammad tu. Ama mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na asimwamini Muhammad baada ya kupewa kwake utume na ukawa mwito wake umemfikia, basi imani yake si chochote na yeye huko akhera atakuwa katika wenye kupata hasara.

﴿كَيْفَ يَهْدِي اللَّـهُ قَوْمًا كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ وَشَهِدُوا أَنَّ الرَّسُولَ حَقٌّ وَجَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ﴾

86.Atawaongozaje Mwenyezi Mungu watu waliokufuru baada kuamini kwao, na wakashuhudia kwamba mtume ni wa haki na zikawafikia hoja zilizo wazi, Na Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.

﴿أُولَـٰئِكَ جَزَاؤُهُمْ أَنَّ عَلَيْهِمْ لَعْنَةَ اللَّـهِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ﴾

87.Hao malipo yao ni kushukiwa na laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika, na ya watu wote.

﴿خَالِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنْهُمُ الْعَذَابُ وَلَا هُمْ يُنظَرُونَ﴾

88.Ni wenye kudumu humo, Hawatapunguziwa adhabu wala hawatapewa nafasi.

﴿إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ وَأَصْلَحُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴾

89.Isipokuwa wale ambao wametubia baada ya hayo, na wakasahihisha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe mwenye kurehemu.

ATAWAONGOZAJE MAKAFIRI

Aya 86 - 89

MAANA

Atawaongozaje Mwenyezi Mungu watu waliokufuru baada ya kuamini kwao, na wakashuhudia kwamba mtume ni wa haki na zikawafikia hoja zilizo wazi wazi.

Makusudio ya Mtume ni Muhammad(s.a.w.w) ; na watu, ni wanavyuoni wa kiyahudi na wa kinaswara kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewataja kuwa ni watu walioamini na wakashuhudia utume wake, lakini baada ya kuletwa na kuwajia wao ubainifu na dalili wazi juu ya utume wake, walimkanusha na wakakataa kumfuata. Sifa hizi zinalingana kabisa na wanavyuoni wa kiyahudi na wa kinaswara, kwa sababu, wao walikuta jina la Muhammad limeandikwa katika Tawrat na Injil, kwa hivyo wakawa wamemwamini kabla ya kuja kwake isipokuwa tu alipoletwa na kuwajia wao dalili walikufuru kwa chuki na hasadi na wakaifuta kila Aya inayofahamisha kwa uwazi au kwa umbali.

Unaweza kuuliza kuwa dhahiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu; Atawaongozaje Mwenyezi Mungu watu waliokufuru baada ya kuamin kwao, inaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu hataki warudie tena kwenye uislamu hata kama watajaribu kutubia; jambo ambalo litawafanya wasistahili adhabu wala kuwa na lawama yoyote. Jibu: Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamsimamishia mja dalili za haki, akiamini, basi atakuwa katika wenye kuongoka; na uongofu wake utatokana na Mwenyezi Mungu, Kwa sababu, Mwenyezi Mungu ndiye aliyemsimamishia dalili za haki. Vile vile uongofu utakuwa umetokana na mja mwenyewe. Kwa sababu yeye ameongoka kwa hiyari yake. Akirtadi baada ya uongofu kwa kiburi na inadi, basi Mwenyezi Mungu atamwachilia mbali katika maisha haya, na wala hatamwekea dalili mpya. Vilevile hawezi kumlazimishia uongofu kwa sababu hakuna taklifu ikiwa kuna kulazimisha.

Hao malipo yao ni kushukiwa na laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika, na ya watu wote.

Yaani wanastahili hilo. Laana ya Mwenyezi Mungu ni kuelezea ghadhabu yake na machukivu yake. Na laana ya watu wote na Malaika ni dua yao ya kumtaka Mwenyezi Mungu awaadhibu na kuwaweka mbali na rehema yake, Katika Nahjul-balagha imeelezwa kwamba Ali(a.s) alikuwa akihutubu katika mimbari Kufa. Ash'ath akamkatiza na kumwambia "Laana ikushukie" Amirul-Muminini akasema: "Wajuaje laana itanipata au la, Mungu akulaani wewe na wakulani wanaolaani." Sheikh Muhammad Abduh katika kulifafanua hilo anasema: "Ash'ath katika masahaba wa Ali alikuwa kama Abdullah bin Ubayy katika masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) wote walikua viongozi wa wanafiki,

Ni wenye kudumu humo, hawatapunguziwa adhabu wala hawatapewa nafasi.

Dhamiri ya humo ni ndani ya Jahannam. Hawatapewa nafasi, yaani hawatapewa muda, bali wataadhibiwa haraka sana.

Isipokuwa wale ambao wametubia baada ya hayo, na wakasahihisha. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu.

Imekuja Hadith isemayo: "Mwenye kutubia ni kama asiyekuwa na dhambi." Imam Ali anasema: Mungu hamfungulii mja mlango wa toba, akamfungia wa msamaha." Unaweza kuuliza: Mtu akisilimu, kisha akartadi, kisha akarudi kwenye Uislamu lakini akapuuza hukumu sio misingi; kama vile kuacha Swala na Saumu kwa uvivu na kupuuza, Je, toba yake itakubaliwa? Jibu: Ndio, atakubaliwa, Kwa sababu, toba ilikuwa ya kukufuru, sio ya Swala au Saumu. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na wakasahihisha, ni kuzitengeneza dhamiri zao na kuthibiti kwenye uislam na kutortadi mara ya pili.

﴿إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ ثُمَّ ازْدَادُوا كُفْرًا لَّن تُقْبَلَ تَوْبَتُهُمْ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الضَّالُّونَ ﴾

90.Hakika wale ambao wamekufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, haitatakabliwa toba yao; na hao ndio waliopotea.

﴿إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَمَاتُوا وَهُمْ كُفَّارٌ فَلَن يُقْبَلَ مِنْ أَحَدِهِم مِّلْءُ الْأَرْضِ ذَهَبًا وَلَوِ افْتَدَىٰ بِهِ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ وَمَا لَهُم مِّن نَّاصِرِينَ ﴾

91.Hakika wale ambao wamekufuru na wakafa hali ya kuwa wao ni makafiri, basi haitakubaliwa kwa yeyote katika wao hata fidia ya dhahabu kwa kujaza ardhi yote lau angeliitoa. Hao watapata adhabu iumizayo wala hawatakuwa na msaidizi.

KISHA WAKAZIDI KUKUFURU

Aya 90 – 91

MAANA

Hakika wale ambao wamekufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, haitatakabliwa toba yao.

Maana ya kukufuru baada ya kuamini yako wazi. Ama kuzidisha kukufuru, kunakuwa kwa dhambi anazozifanya mwenye dhambi hasa kueneza ukafiri na kuwapiga vita waumini kwa kuwa tu ni waumini. Unaweza kuuliza; Hakika Mwenyezi Mungu amehukumu - katika Aya iliyotangulia - kumtakabalia toba mwenye kukufuru baada ya imani; na katika Aya hii amehukumu kutomtakabalia. Kuna wajihi gani wa kuungana haya? Wafasiri wamejibu kwa majibu mengi. Yenye nguvu zaidi ni kwamba kukufuru baada ya kuamini kuko mafungu matatu.

Kwanza : Kutubia toba ya kweli ambayo Mwenyezi Mungu ameitaja kwa kusema: Isipokuwa wale waliotubia.

Pili : Toba isiyo ya kweli ambayo Mwenyezi Mungu ametaja kwa kusema: Haitotakabaliwa toba yao."

Tatu : Ni kufa juu ya ukafiri kulikotajwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Hakika wale ambao wamekufuru na wakafa hali ya kuwa wao ni makafiri. Jibu tunaloliona sisi, ni kwamba mtu anaweza akahisi usahihi wa jambo au kutokuwa sahihi. Kisha akachangayikiwa na kuwaza kuwa hisia zake zimebadilika na kuwa si sahihi au kuwa ni sahihi baada ya kutokuwa sahihi; ingawaje hisia zake hasa hazijabadilika; ambapo kuitakidi kwake kuwa zimebadilika ni kwa mawazo tu. Vilevile mapenzi na chuki, mfano, mtoto wako anaweza kukufanyia ubaya na ukachukulia kuwa yeye ni mtu anayemchukia zaidi kuliko watu wote, na kwamba unataka aangamie, lakini huruma za ubaba bado ziko kwenye nafsi yako bila ya kutambua, mara ngapi tunashuhudia mtu akifanya jambo au kuliacha kwa kufuata desturi, kuiga au kwa kwa kuhurumia huku mwenyewe kiitakidi kuwa ni kwa njia ya dini.

Pia inaonyesha watubiaji wengi wa dhambi zao kuwa ni wa kweli, lakini kwa ndani bado wamebakia nayo waliyokuwa nayo. Watubiaji hawa ndio walielezwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hawatatakabaliwa toba yao. Ama wale walioelezwa na Aya iliyotangulia (Isipokuwa wale waliotubia), ni wale watubiaji wa kweli na wa haki.

Hakika wale ambao wamekufuru na wakafa hali ya kuwa wao ni makafiri, basi haitakubaliwa kwa yeyote katika wao hata fidiya ya dhahabu kwa kujaza ardhi yote.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kuishiliza maisha yake kwa ukafiri atahisabiwa hisabu ya makafiri.

Unaweza kuuliza; kuwa hakuna dhahabu siku ya kiyama wala hakuna njia yoyote ya kuweza kuimiliki wala kuitoa. Sasa kuna faida gani ya kuitaja.

Jibu : Makusudio ni kwamba hakuna njia ya kujikomboa kwa namna yoyote ile. Kimsingi ni kuwa kukadiri muhali si muhali. Katika aliyoyasoma Imam Ali, kuisifu Jahannam ni: "Haondoki mkazi wake wala hakombolewi mateka wake."

MWISHO WA JUZUU YA TATU

10

SHARTI YA KUCHAPA

sharti ya kuchapa au kusambaza ni kutaja rejeo hili. haki zote zimehifadhiwa na Taasisi ya Al-Hasanain Taasisi ya Imamu Husein(a.s)

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini(a.s) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini

2

MUANDAMO WA MWEZI

SURA YA PILI

JAWABU KWA WANAFUNZI WA BACHOO JAWABU YA UTANGULIZI

Wahusika ndugu zetu wa Masjid Al-Sunna Zanzibar, wameanza kitabu chao hicho kwa utangulizi wenye kumshukuru na kumuhimidi Allah na kumtakia rehema na amani Bwana wetu Muhammad (s.a.w.) kama zilivyo khutuba na vitabu vya kiislamu. Na hayo yote yamefanyika chini ya utangulizi wenye anwani:

UKWELI JUU YA KUANDAMA KWA MWEZI

Na hii ndio sehemu ya kwanza ya kitabu chao. Wakasema katika utangulizi huo: Msisitizo wetu mkubwa katika kitabu hiki ni ile nukta muhimu ya kwamba suala la kufunga na kufungua kwa muandamo mmoja kwa dunia nzima si jambo jipya kama wanavyodhani baadhi ya watu, ni jambo la kale mno ambalo linaweza kutekelezeka na kwamba huo ndio uliokuwa msimamo wa 'Jamhur' ya wanavyuoni.

Jawabu Nakubali kuwa hili ni jambo la zamani, lakini kudai kuwa hii ni kauli ya Jumhuri ni madai hewa: hayana ushahidi. Leo hii duniani hakuna madhehebu yoyote ambayo inaitendea kazi kauli hio kama ni madhehebu nzima, bali kuna baadhi ya watu tu katika kila madhehebu ambao wanafata kauli hio. Hata zile madhehebu ziliotajwa kuwa ni zenye kufata kauli hio kama vile Malik, Hanbal na Hanafi, basi hawaitendei kazi kauli hio ila baadhi yao tu. Libya, Algeria na nchi nyengine za Afrika Kaskazini na Magharibi - kwa mfano - ni nchi za wafuasi wa madhehebu ya Malik, nao wanafata miandamo yao wenyewe. Kwa hivyo, dai kuwa hii ni kauli ya Jumhur ya wanavyuoni, si dai sahihi.

SEHEMU YA PILI

Katika sehemu ya pili, ndugu waandishi wanasema:

2. Si Fikra Za Shaykh Naaswir Bachuu "Ndugu yetu Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui amejitahidi kuandika kitabu alichokiita: "Ushahidi Uliowekwa Wazi Katika Suala La Miandamo Ya Mwezi. Makusudio yake yalikuwa ni kutaka kukijibu kitabu kilichoandikwa na Shaykh Naaswir Abdullah Bachuu kinachojulikana kwa jina la "Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi."

Jawabu Kidogo na mimi naomba niweke wazi kwamba kitabu changu hakikuwa kabisa na lengo la kujibu kitabu cha Sheikh Nassor Bachoo. Hili la kunukuu maneno yake na kuyajadili lilikuwa ni jambo la kutokea tu baada ya mtu Fulani kuniletea kitabu chake. Kwa havyo, kama mulivyosema nyinyi katika kitabu chenu kwamba: Kitabu hiki ni kama nasaha kwa Waislamu wote ili kuweza kudumisha umoja wetu hususan pale ambapo pamejitokeza misimamo tofauti katika mambo ya ibada. Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili.

Basi na mimi nakuombeni munielewe hivyo hivyo, kwamba wakati mimi naikubali fikra Fulani na kuikataa fikra Fulani, hakuna budi ninukuu fikra pinzani na kuonesha kwanini siikubali; na kwa upande wa pili ni lazima nioneshe kwanini naikubali fikra ninayoikubali. Na nitaposema kuwa kuna watu wana fikra hii, basi nadhani haitokuwa jambo la busara kama watu hao sikuwataja na nikiwataja ni lazima nitaje marejeo. Kwa sababu hii ndio maana nimekuwa nikinukuu maelezo ya Sheikh wetu Nassor Bachoo na kumjadili mule nisimokubaliana naye. Naomba musihuzunike kwani kujibizana katika kutafuta ukweli ni suala mashuhuri katika uwanja wa elimu. Wanavyuoni wakubwa wa kale na wa sasa wamekuwa wakijibizana ili kutafuta ukweli na hatimae huwabainikia woa pamoja na wasomaji. Kwa hivyo, hamukuwa na haja ya kutumia lugha: "Wala hapakuwa na lengo la kumkashifu": hii si kashfa hata kidogo: hii ni elimu.

Lakini, hakuna haja ya kufichana; kitabu chenu mumeandika kwa kujibu kitabu changu. Hamuna haja ya kusema: "Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili", kwani kitabuchenu kimeanza kwa kunitaja mimi mwanzo hadi mwisho na kuniaga kwa kunipa nasaha mimi. Ama mimi naandika jawabu hii kukujibuni nyinyi: sikufichini wala sisemi uwongo.

Munasema Kutokana na jambo hilo , sisi kwa upande mmoja tunashukuru kwa juhudi yake hiyo na kwa upande wa pili tunatuma masikitiko yetu kwake kwa kutokuwa makini na muadilifu katika kulifafanua jambo hilo muhimu. Kwani kitabu chake hicho kimeandikwa katika mfumo wa chuki, kibri, kejeli na malumbano huku akisisitiza kwa mara nyingi kauli chafu ambazo muandishi hapaswi kuzitumia katika kitabu au katika mijadala ya Dini. Jawabu Hizi chuki, kibri na kejeli, mimi nimezisoma kwenu, kwa hivyo na iwe kama msemo wa Waswahili: "Papa akipea mafuta huwapa wanawe". Je nyinyi munayakumbuka haya:

1) Munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo ambao alisema kuwa wasionyanyua mikono katika sala wanasali kama mipopoo? Jamani! Hii si kejeli? Je katika nyinyi yuko aliyetoa muhadhara au kuandika kitabu ili kumjibu Sheikh wetu. Sasa uadilifu uko wapi?

2) Je munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo aliozungumzia mas-ala ya udhu kasha akasema: "Wengine wakitia udhu kiungo hiki huomba dua hii na kiungo hiki huoma dua hii; upumbavu mtupu". Je haya si matusi? Je hii si kejeli?

3) Siku moja palikuwa na maziko. Maiti alisaliwa msikiti wa wajiitao "Watu wa Sunna". Kijana mmoja akasimama akasema: "Leo tunataka kukuonesheni vipi Mtume (s.a.w.) kamsalia maiti: si kama wanavyofanya Ibadhi na Shia.

4) La nne ni kuwa ikiwa nyinyi mumethubutu kunita mjeuri, mwenye kibri na kejeli; maneno ambayo mimi sikukwambieni wala kumwambia Sheikh Nassor; mimi nimemtoa makosa tu Sheikh wetu: na hii ni kawaida katika uwanja wa elimu; sasa je na nyinyi pia ni majeuri, wenye kibri na kejeli? Katika uwandishi wenu, pia mumesema: "Hatujui dhana hii potofu ameitoa wapi." Mwenye dhana potufu naye ni mpotufu, kwa hivyo na nyinyi hamukutoa nasaha bali mumetukana. Nakupeni mifano hii mitatu ya Sheikh wetu na mmoja wenu nyinyi wenyewe enyi wenye kuandika Radan mardudan na mifano iko mingi. Inatosha kuwaita kwenu watu wengine kuwa ni watu wa bidaa na nyinyi ndio watu wa Sunna. Kwa hivyo, hii hali mumeiuda nyinyi wenyewe: Zanzibar bali Afrika Mashariki na Dunia kwa ujumla haikuwa hivi. Chuki mumeziunda nyinyi; mukijirekebisha kwa kutumia lugha nzuri nadhani hakuna atayekwambieni jambo kwa lugha nzito.

Mnasema Mfano wa kauli zake mbaya ni kama zifuatazo:

(vuta-nikuvute) [uk. 6]

(hii ni ajabu katika ajabu za dunia!) [uk. 124]

(Kwa hivyo, uwezekano huo alioutoa Sheikh hauwashi wala hauzimi [uk. 124]

(Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja,)

(Utaona kwamba masuala yote haya si yenye kima katika soko la elimu, bali ni masuala ya kuwababaisha watu wasiojua nini cha kujadiliwa katika mas-ala haya ya funga) [uk. 167]

(Hoja nyengine - nayo pia ni hoja ya mitaani - ni kuwa watu wengi wa kawaida wanapouona mwezi mkubwa husema: "E basi ule ndio mwezi wa leo ule?!!!")

(Jawabu hii ya mwisho, inaufanya upinzani mzima wa Sheikh Bachoo kuwa hauna maana yoyote.) [uk. 132]

(Kwa ufupi ni kuwa hicho walichokidai watetezi wa rai pinzan) [uk. 32]

(utaona jinsi gani mwanamume alivyokuwa bingwa wa kubadilika! Na hili si jengine bali ni lile Waswahili wanalolisema: "Mfa maji hukamata maji.") [uk. 128]

(Hakuna hapa kinachoonesha mas-ala ya kufunga kwa muandamo mmoja wala kumi na moja.)) [uk. 125] (haina maana kwamba usiku ukiingia sehemu moja ndio umeingia dunia nzima. Kwa ufupi ni kuwa hii ni hoja ambayo haina faida yoyote ya kielimu, lakini tunaijadili kwa ajili ya watu wa mitaani tu.)

Jawabu Sikubaliani na nyinyi kwamba humu muna maneno mabaya. Lakini hata nikikubali basi nasema kwamba lugha ya namna hii sababu ni nyinyi, na kwa hivyo, utaona kwamba ninapojadiliana na watu wengine basi lugha yangu hubadilika. Kwa hivyo, tujirekebisheni sote na tujadili tafauti zetu kwa lugha ya kiungwana. Ama ukinita mpopoo, basi usinilaumu na wewe nikikwita mnazi: unanilaumu nini na wewe unakifanya kile kile nikifanyacho?! Bali hata katika kitabu hiki munachonijibu, basi nanyi mumetumia lugha hizo hizo. Katika baadhi ya sehemu umesema: "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti..". Na mwishoni mwa kitabu mumesema: "Dhana ya pili ya ndugu Juma imejengeka katika msingi dhaifu wala haina nafasi katika uwanja wa fani (kitaalamu) nao ni kule kusukuma kwake juu ya elimu ya Jiografia". Na yamo mengi katika kitabu chenu. Sasa nyinyi mwasema nini na mwatenda nini?

Munasema "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti: Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi i likuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini? Na ni nani aliyemwambia kwamba jambo lenye khitilafu halizungumzwi? Yeye angezungumza nini katika kitabu chake kama si masuala ya ikhtilafu? Pia anatwambia haya ni katika mambo ya furui (matawi) za Kidini, kwa hivyo zisizungumzwe. Kwani ni nani aliyemwambia kuwa furui za Kidini hazizungumzwi?"

Jawabu Ikiwa lugha hii ndogo hamukuweza kuifahamu, vipi mutaweza kufahamu kitu chenye kuhitaji fani za lugha na usuli na mengineo. Ikiwa mimi niliingia msikitini kwenu Raha Leo nikakuta juu ya ubao wenu munawasomesha vijana na katika darsa hio Mubtadaa mumemwita Fa'il (vipi mutaweza kujadili masuala haya?!!! Mimi nimempongeza Sheikh Bachoo kwa juhudi au moyo wake; na sikumpong eza kwa kulikuza suala ambalo:

1) Ni la furuu'i

2) Lina khilafu. Na hii haina maana kuwa Furu'i zisizungumzwe; suala la Furu'i huwa halishadidiwi; bali unawaacha watu kama walivyo tu. Lakini yeye anapenda kushadidia katika mas-ala kama haya; ndio maana akashadidi hata katika suala la kufunga mikono hata kuwaita watu mipopoo bali na kuwambia kuwa hawana Sala. Kwa hivyo, nieleweni kwamba ninachokipinga ni kushadidia au kuwakoroga watu katika kitu ambacho ni furu'i za dini ilhali yeye kawakuta na msimamo tafauti tangu zamani. Katika mas-ala ya furu'i, wanavyuoni huwa hawashadidi juu ya Mas-ala kama haya. Mimi leo nikisimama nikaanza kufanya kampeni kwamba watu wasiitikie amina wa kisali, nalo ni jambo la furu'i, si nitakuwa natia fitna tu? Jambo kama hili huwachwa wasomi wakalitafiti kaiha kila mmoja akafanya vile ilivyombainikia. Lakini kufanya kampeni maalumu na da'awa kana kwamba waliotangulia wote ni wapotovu, hili ndilo jambo la kulaumiwa.

Ama kauli yenu: "Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi ilikuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini?" Mwisho wa kunukuu. Na mimi nikuulizeni nyinyi mumenishukuru kwa juhudi yangu kisha mwisho wa kitabu mukaniambia: "Mwisho tunachukua fursa hii kumuonya ndugu Juma kuwa amuogope Mwenyezi Mungu hususan katika mas-ala ya kielimu. Akumbuke kuwa Mwenyezi Mungu Ameonya juu ya mtu kusema jambo au kufanya asilolijua. Aelewe kwamba ataulizwa juu ya hilo. Lingekuwa jambo la busara kama ndugu Juma angalikubali kuuliza na kufanya utafiti zaidi juu ya mas-ala haya kama agizo la Mwenyezi Mungu linavyotutaka". Sasa na nyinyi munanishukuru nini?

Munasema "Sisi tunapenda kumfahamisha kuwa suala hili la kwamba mwezi ukiandama sehemu moja unatosheleza kufuatwa kwa kufunga au kufungua ulimwengu mzima, si suala jipya bali ni jambo la kale. Tunasikitika kwamba hakuangalia vizuri maoni ya Wanavyuoni wakubwa walivyoelezea msimamo huo. Angalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 51-58. Hapa tunanukuu baadhi ya kauli hizo:

Imamun-Nawawy aliyekisherehesha Kitabu cha Sahihi Muslim anasema:

"Na jambo lililo sahihi kwa wenzetu (Mashaffi) ni kuwa muandamo mmoja hauwahusu watu wote bali unawahusu wale walio karibu kwa kiasi ambacho hawaruhusiki kupunguza Sala (Sala ya safari). Pia imesemwa kuwa iwapo matlai ni mamoja watalazimika (watu) kufunga pamoja. Pia imesemwa kuwa ikiwa (wanaishi) katika eneo la Iklimu moja (maili 72 au km 89) (watalazimika kufunga pamoja) vyenginevyo kila mmoja atafunga kwa muandamo wake. Na wakasema wenzetu wengine (Mashaffi) kuwa muandamo katika sehemu moja utawahusu wote wa dunia nzima".

Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar katika kitabu chake "Bayaanullinnas" J. 2 uk 203 - 204 ameandika yafuatayo juu ya kauli hiyo ya Imamun-Nawawy:

"Hapa Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasari kauli zilizomo katika madhehebu ya Kishaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu mengine ya Kiislamu. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika maf ungu matatu makuu: "...Hapo Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasar kauli zilizomo katika madhehebu ya Shaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu nyengine za Kiislam. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika mafungu matatu makuu: Kauli ya kwanza: "Kila nchi iwe na matlai yake, wala muandamo wa nchi moja hautalazimu nchi nyengine ya mbali wala karibu". Kauli ya pili: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi zote za dunia hata kama ziko mbali".

Kauli ya tatu: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi iliyo karibu nayo au inayowafikiana kimatlai". Kisha, Shaykh Jaadul-Haq akaendelea kusema kwamba:

"Na (kauli) zote hizo ni maoni yatokanayo na Ijtihaadi ambazo hazikusimama juu ya hoja kat-ii, si sanad wala matni. Kwa hivyo ingefaa ichaguliwe kauli ambayo inakubaliana na maslahi ya (Waislam wote wa) dunia nzima kwa jumla"."

Jawabu Sikubaliani na mtazamo wa Sheikh Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar, kwamba zote hizi ni rai na itihad kwani kanuni ni kuwa "Hakuna ijtihadi mbele ya andiko" Ijtihad mwahala mwake ni musimo andiko. Wakatika katika suala hili, utaona kwamba asemaye kuwa tufunge kwa muandamo mmoja, hoja yake ni Hadithi "Fungeni kwa kuuona"; na anayesema kuwa kila mahala na muandamo wake, anatoa ushahidi wake ni Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib. Kwa hivyo, ijtihad ni katika kuyafahamu maandiko: si ijtihad kwa maana ya rai tupu pasi na andiko kama alivyosema Sheikh. Kilichobaki ni kuzijadili riwaya mbili hizi zina maana gani?

Munasema Tungependa kumueleza ndugu yetu kwamba hata hapa Afrika ya Mashariki jambo hili hakulianzisha Shaykh Naaswir Bachuu kama alivyodai mwenyewe (Nd. Juma) kwamba: (Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro)) Inasikitisha hakuweza kuangalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 161-163 wametajwa walioonyesha kwa vizuri kabisa misimamo hiyo tofauti. Mashaykh wenyewe ni hawa wafuatao: Al-marhuum Shaykh Juma Abdul Waduud (wa Zanzibar), Shaykh Abdillahi Naaswir ( Nairobi Kenya ), na Shaykh Naaswir Khamis Abdul Rahman ( Mombasa Kenya ).

Jawabu Kwani wapi katika kitabu changu nilisema kuwa Sheikh Nassor Bchoo ndiye aliyeanzisha fikra hii hapo Afrika ya Mashariki hata mukaleta dai hili? Mimi nimeeleza kuwa zamani Afrika Mashariki watu wote wakifata muandamo mmoja. Nilisema: Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo. Dr. Ramadhan Al-butti - miongoni mwa wanavyuoni wakubwa wa ulimwengu wa sasa - anaona kwamba harakati hizi hazisifiki kama ni madhehebu: bali ni hatua (phase) katika mapito ya Historia.

Na katika uk. 97, nimesema:

Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya. Kwa hivyo, ni wazi kwamba mimi nazungumzia Afrika Mashariki. Na mfano wa hilo pia kalisema Sheikh Nassor Bachoo, lakini yeye hamukumjibu. Anasema: "Pamoja na kuwa mgogoro wa kuandama kwa mwezi umeanza kuonekana hadharani katika jamii za Waislam wa hapa Afrika ya Mashariki katika miaka ya hivi karibuni". Inasikitisha kwamba hata maneno yangu mumeyakata na kuchukua yale ambayo hayakamilishi maana nilioilenga. Maneno "Karne zimepita" hamukuyataka kwani hayakufikisheni kule mutakako!

Pili narejea tena kusema kwamba hao wanavyuoni aliowataja Sheikh Nassor, hawajathibitisha habari za kuwa watu wafunge au wakifunga kwa muandamo mmoja Africa Masharik, ukimtoa Sheikh Nassir Khamis wa Mombasa ambaye naye pia ni mtu wa sasa. Ama sheikh Juma Abdu-Wadood yeye, kwa mujibu wa nakala hio ya Sheikh Nassor Bachoo, kasema hivi: Kuona huku kwa mwezi kumekusudiwa kuonekana na Waislam, na kuonekana na Waislamu huko, sio lazima kuonekana na Waislamu wote. Bali inatosha shahada ya mtu mmoja muadilifu".

Pia inampasa mtu mmoja pekee kama ameuona mwezi yeye afunge na kila aliyemuamini; hata akiwa haijakubaliwa shahada yake. Haya ndio maneno ya Sheikh Juma Abdu-Wadood kwa mujibu wa alivyomnukuu Sheikh Bachoo. Sasa ikiwa ndugu zetu mumeshindwa kuyafahamu maneno haya ya Sheikh Juma Abdu-Wadood, bado mutaendelea kupoteza watu bila ya elimu?! Sheikh Juma Abdul-Wadood hapa anazungumzia mas-ala ya ushahidi kwamba si lazima - katika suala la kuonekana kwa mwezi - kwamba kila mmoja auone: bali akiona mtu mmoja basi inatosha kwa wengine kufunga. Hii ndio kauli ya Sheikh Juma Abdul-Wadood na hili nimelieleza kwa urefu katika kitabu changu.

Kisha Sheikh Juma Abdul-Wadood akazungumzia suala la kufunga kwa muandamo mmoja akasema: "Rai za Maimamu wengine wameifasiri hadithi isemayo: (Fungeni kwa kuuona Mwezi) kwamba ukionekana popote mashariki au magharibi (watu) wafunge; hapana kutazama masafa fulani au nini. Hii ni rai nayo na wengi wamesema (hivyo) kama Imamu Malik , Ahmad na kundi kubwa la Hanafi. Inakurubia kuwa n dio rai ya Jamhuri - kufata rai hii ni kuhakikisha umoja wa dunia nzima. Wala hatuwezi kusema kwamba rai ya Shaffiy ndio ya Jamhur". Hapa Sheikh Juma anasimulia rai za Maimamu wengine: si rai za Maulamaa wa Afrika Mashariki. Mimi dai langu nililodai ni kuwa jambo hili la kufunga kwa muandamo mmoja, napenda munifahamu: ni jipya kwa Africa Mashariki. Mimi sikusudii jambo la wanazuoni kuzungumzia rai mbali mbali: bali nazungumzia jambo la watu kufata muandamo mmoja kwamba karne zimepita ya sikio la Muafrika Mashariki wa Kawaida halijiapata kusikia. Na nimetumia maneno "Muafrika wa Mashariki wa kawaida" ili kuwatoa wanavyuoni wao hata kama walikuwa hawafati kauli hio, lakini wanaijua. Kwa hali yoyote ile:

1) Sheikh Juma Abdul-Wadoo hajazungumzia kwamba Afrika Mashariki watu walikuwa wakifunga au wafunge kwa muandamo mmoja, bali kazungumzia rai za wanavyuoni wasio wa Afrika Mashariki - Al-Imamu Shafi, Hanbal n.k. Na mimi sijakanusha tafauti hizi.

2) Kauli yake ilikuwa ni kuhusu suala la mashahidi.

Ama Sheikh Abdillahi Nassir, yeye ni mwanachuoni wa sasa. Na mimi sijasema kuwa sasa hakuna rai hizo. Pili ni kuwa nakala alizotupa Sheikh Bachoo za kitabu cha Sheikh Abdillahi utaona kwamba Sheikh Abdillahi hazungumzii kuwa kauli ya kufatwa ni ile ya muandamo mmoja; bali yeye kasema kuwa hili ni suala la khilafu kwa hivyo tusigombane kila mtu afate rai anayoiona kuwa ni sawa. Sheikh Abdillah kayasema haya baada ya kutokea mizozo hii ya sasa. Kwa hivyo tunarudi pale pale kwamba "Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo". Kwa hivyo, nukta hii hamukuuijibu: na wala sioni kuwa kuna haja ya kuijibu kwani haina umuhimu katika maudhui yetu. Bali kitabu chenu chote, munachagua mambo yasio na umuhimu "Juma kantutukana; Juma kanfanya hivi" nyinyi ndio munajibu baada ya kuzungumzia dalili za kielimu.

Ama Sheikh Nassor: yeye pia ni mtu wa sasa na ni mfuasi wa skuli hio hio munayoifuata nyinyi, kwa hivyo kusema kwake alivyosema hakujapindua nilioyasema kuwa - kimatendo - hili ni suala jipya kwa kwetu Afrika ya Mashariki. Wala mimi sikusema kuwa Sheikh Nassor Bachoo ndiye muasisi wa fikra hio huko kwetu. Naomba munifahamu ninachokisema kwanza kisha ndio munijibu. Na sijui munapinga nini kitu ambacho watu wote wanakijua. Bila ya kusahau kwamba mimi sikusudii kusema kuwa kitu sahihi ni kilichofanywa zamani au kilichofanywa leo: laa! Bali kitu sahihi ni chenye ushahidi sahihi uliojengeka juu ya misingi sahihi ya kielimu. Na kielimu, suala la kuzingatia muandamo mmoja - hamutoweza kulithibitisha.

MNASEMA

Pia Shaykh Ahmad Al Khalil, Mufti wa Omani amethibitisha kwamba Ikhtilaf hii ya muandamo wa mwezi katika hukmu ya kufunga au kufungua ipo na kwamba ni jambo la kale. Kama alivyosema maneno yake yaliyotafsiriwa na Shaykh Muniir Sulayman 'Aziz kwamba: "Hakuna madhehebu iliyokuwa imesalimika na kuwa na Khitilafu baina ya Wanavyuoni wake juu ya suala la kutafautiana miandamo ya mwezi." Jee ndugu Juma anataka kusema kwamba Shaykh Naaswir Bachuu ndiye mwalimu aliyeanzisha madhehebu zote? Au ndiye aliyeanzisha mtafaruku huu kama alivyouita mwenyewe ndugu Juma?

JAWABU

Suala hilo jiulizeni wenyewe; mujijibu wenyewe; kwani nyinyi ndio mulioliunda: mimi sikusema hivyo kamwe bali nilichokisema ni hiki: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nami sikusudii kusema kwamba upya huo ni katika kuzungunzwa au kusomwa suala hilo katika vitabu; nakusudia kimatendo sula hili lilikuwa halipo Afrika Mashariki. Sasa ili muwe mumenijibu, twambieni nani alikuwa akifata muandamo mmoja hapa Afrika Mashariki. Jamani! Tafuteni hoja mujadili: musijadili kitu kisichokuwa na umuhimu. Kama hamuna hoja nyamzeni musijitie aibu!

MNASEMA

Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani; Ndugu Juma anasema: (Kama tunavyojua kwamba Sheikh Nassor Bachoo, ni mmoja wa wenye kusisitiza ulazima wa kuwa na muandamo mmoja.) Sisi kwa upande wetu tunasema: Katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu hakuna pahala alipolazimisha watu wafuate huo aliouita ndugu Juma (msimamo wa Shaykh Naaswir). Bali yeye ameonesha mitizamo ya Wanavyuoni kwa kutumia Aya za Qur-aan, Hadiythi na vitabu vinavyokubalika. Lugha aliyotumia Shaykh Naaswir katika huo unaonekana ni msimamo wake ni maneno yaliyozimuliwa kilugha (polite language) kama vile: (inawezekana) ((inaonyesha) .

JAWABU

Na mimi hapa sijasema kuwa Sheikh Nassir Bachoo kalazimisha watu wafunge kwa muandamo mmoja. Nimesema "Anasisitiza ulazima" yaani yeye analingania msimamo huo kwani kwake ndio msimamo sahihi na ndio wajibu kuufata. Naomba tena tuelewane musiseme kitu kinyume na nilivyosema. Wala musitafute kitu kisicho na maana mukajadili eti ndio jawabu! Pili maneno yenu: "Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani". Sasa je na nyinyi pia munaonesha udhaifu huo huo kwa kumuandama mtu fulani katika kitabu chenu?

MNASEMA

Aliyelazimisha rai ni ndugu Juma mwenyewe kama anavyosema: (Lakini kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali) [uk. 112]

JAWABU

Bali hata Sheikh Bachoo pia kalazimisha kwani ukidai kuwa huu ndio msimamo wa haki au ndio msimamo sahihi au ndio wajibu kufatwa, bila kusema kuwa rai zote zinafaa basi na wewe huwa umelazimisha rai yako. Sasa je Sheikh Bachoo anakubali hivyo kuwa rai zote ni sawa? Mimi kweli sisemi kuwa rai zote ni sawa: nasema kuwa nyinyi mumekosea na sahihi ni kinyume na munavyofanya, na kwa hivyo bado nipo katika msimamo wangu huo huo kwamba: "Kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali".

MUNASEMA

"Kisha katika uk 85 ndugu Juma anataja kwamba msimamo huu wa muandamo mmoja kwa dunia nzima ni ((kitu kipya)) na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu baada ya kutaja baadhi ya nchi zinazofuata miandamo yao - yaani kila nchi na muandamo wake kama Al-yaman , Oman , Misri na Saudia. Kisha hapo hapo akataja: ((isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.)) Inafaa ndugu Juma aulizwe masuala yafuatayo:

i) Kama ni jambo lisilotekelezeka vipi tena Imarat wanalitekeleza?

ii) Je hawa wa Imarat nao ni wanafunzi wa Shaykh Naaswir Bachuu?

iii) Kwani hiyo sio kauli ya Jamhuur ambayo ndio msimamo wa maimamu wakubwa wakiwemo Ahmad bin Hanbal, Malik na Abu Hanifa? (Angalia pia sehemu ya 11 na 13 za kitabu hiki)

JAWABU

Kwanza mumemefanya ghushi: maneno yangu hamukuyanukuu yote. Mimi nimesema: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nyinyi maneno "Kwa kwetu Afrika Mashariki" mumeyatoa ili ionekane kuwa mimi nasema kuwa hili ni suala jipya kila pahala. Watu kama nyinyi vipi tutakuamini katika dini yenu na uadilifu wenu, ikiwa munaghushi maandiko hivi? Hii ndio kamati ya Msikiti Sunna na hii ndio suna yenyewe?! Halafu mukaendelea na tadlis (ghushi) yenu mukasema: "Na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu". Mimi sikusema hapa kuwa "Halitekelezeki", bali nimesema:

Lakini ukweli ni kuwa hata katika nchi nyengine zote za dunia taqriban kauli kwamba tufunge kwa muandamo mmoja, ni kauli ilioishia katika vitabu tu, kimatendo (practically) kauli hio haitumiwi isipokuwa na mtu mmoja mmoja. Hadi leo hii: watu Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao, Misr wanafata muandamo wao na nchi zote taqriban ni hivyo, isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.

Haya nionesheni hapa maneno "Halitekelezeki". Mimi nimesema kuwa kimatendo kauli hii, hadi leo haitendewi kazi isipokuwa na baadhi ya watu. Nyinyi mumebadilisha na kuweka ghushi yenu mukasema nimesema halitekelezeki. Kwa hivyo, hilo Sula (a na b) jibuni wenyewe kwani mumesema kinyume na nilivyosema. Suala (d), najibu kuwa sio: hio si kauli ya jumhur bali jumhur kauli yao ni kinyume na hivyo na hili nimelithibitisha katika uk. 189-193 wa chapa ya pili ya kitabu changu au uk. 171 wa kitabu hicho chapa ya kwanza. Na Al-Imamu Malik riwaya zake zimegongana na riwaya kwamba kila watu na muandamo wao ndio ilio bora kwani ni riwaya ya Madina aliko kuweko Al-Imamu Malik, wakati riwaya nyengine ni ya watu wa Irak kulikokuwa na viwanda vya kutunga riwaya!

MNASEMA

Na sisi tunamuongezea habari moja ambayo ni vyema kuielewa, kwamba nchi ya Uganda iliyo katika Afrika ya Mashariki pia inafuata rasmi muandamo mmoja wa duniani. Pia aelewe kwamba huo msimamo wa kila nchi na mwezi wake huku Afrika ya Mashariki haukuwepo tokea zamani. Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja. Yeye anaendelea kushika msimamo wake: (Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka.

JAWABU

1) Kitu rasmi Uganda hakizingatiwi kwani Uganda kimsingi sin chi ya Kiislamu wala ya Waislamu: Waislamu ni wachache ukilinganisha na Wasio Waislamu. Kwa hivyo, hakuna kitu rasmi. Na jambo hilo ni jambo la sasa. Na mimi sijapinga kwamba sasa fikra hio ipo Afrika Mashariki.

2) Ama kauli yenu: "Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja". Ndio maana nikatumia lafdhi "Kwa kwetu Afrika Mashariki" nikijua kuwa wanavyuoni wote wa kwetu Afrika Mashariki wana msimamo huo. Ama kauli yenu: "Yeye anaendelea kushika msimamo wake: ((Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao,)). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka". Mwisho wa kunukuu. Inaonesha kuwa kitabu changu mumekijibu bila ya kukifahamu. Nilichosema ni kuwa, ijtihadi ifanywe katika kubainisha wapi hadi wapi watu wafunge pamoja. Kwa vile, hakuna andiko lililobainisha hivyo. Ama muandamo mmoja kwa dunia nzima hili ni kinyume na andiko. Kwa hivyo, wakiwa wanavyuoni wa zamani wamefanya ijtihad hio, sisi tunafata ijtihad yao kwa vile hapa ni mahala pa ijtihad na haikugongana na andiko. Ama madai yenu nyinyi ni kinyume na andiko lilivyoonesha.

MNASEMA

"Kuna suala moja la nyongeza tunapenda tumuulize ndugu yetu Juma: Hata kama hizo nchi alizozitaja ( Al-Yaman , Oman , Misri na Saudia) hazijakubaliana kufuata muandamo mmoja, je hakuna uwezekano (japo wa sadfa) unaoweza kutokea kufunga siku moja ijapokuwa kila mmoja ameona mwezi katika nchi yake? Sasa tuseme kila nchi katika hizo imeona mwezi usiku wa Alkhamisi kuamkia Ijumaa - Wote si watafunga siku moja ya Ijumaa? Basi huo ndio utekelezaji aliosema hautekelezeki. Ni wazi kuwa unatekelezeka.

JAWABU

Munaendelea kuuliza masula haya kwa sababu masuala yenu mumeyajenga katika kitu nisichokisema kamwe. Wapi nimesema kuwa "Hilo halitekezeki" hata mukauliza masuala haya?

2

MUANDAMO WA MWEZI

SURA YA PILI

JAWABU KWA WANAFUNZI WA BACHOO JAWABU YA UTANGULIZI

Wahusika ndugu zetu wa Masjid Al-Sunna Zanzibar, wameanza kitabu chao hicho kwa utangulizi wenye kumshukuru na kumuhimidi Allah na kumtakia rehema na amani Bwana wetu Muhammad (s.a.w.) kama zilivyo khutuba na vitabu vya kiislamu. Na hayo yote yamefanyika chini ya utangulizi wenye anwani:

UKWELI JUU YA KUANDAMA KWA MWEZI

Na hii ndio sehemu ya kwanza ya kitabu chao. Wakasema katika utangulizi huo: Msisitizo wetu mkubwa katika kitabu hiki ni ile nukta muhimu ya kwamba suala la kufunga na kufungua kwa muandamo mmoja kwa dunia nzima si jambo jipya kama wanavyodhani baadhi ya watu, ni jambo la kale mno ambalo linaweza kutekelezeka na kwamba huo ndio uliokuwa msimamo wa 'Jamhur' ya wanavyuoni.

Jawabu Nakubali kuwa hili ni jambo la zamani, lakini kudai kuwa hii ni kauli ya Jumhuri ni madai hewa: hayana ushahidi. Leo hii duniani hakuna madhehebu yoyote ambayo inaitendea kazi kauli hio kama ni madhehebu nzima, bali kuna baadhi ya watu tu katika kila madhehebu ambao wanafata kauli hio. Hata zile madhehebu ziliotajwa kuwa ni zenye kufata kauli hio kama vile Malik, Hanbal na Hanafi, basi hawaitendei kazi kauli hio ila baadhi yao tu. Libya, Algeria na nchi nyengine za Afrika Kaskazini na Magharibi - kwa mfano - ni nchi za wafuasi wa madhehebu ya Malik, nao wanafata miandamo yao wenyewe. Kwa hivyo, dai kuwa hii ni kauli ya Jumhur ya wanavyuoni, si dai sahihi.

SEHEMU YA PILI

Katika sehemu ya pili, ndugu waandishi wanasema:

2. Si Fikra Za Shaykh Naaswir Bachuu "Ndugu yetu Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui amejitahidi kuandika kitabu alichokiita: "Ushahidi Uliowekwa Wazi Katika Suala La Miandamo Ya Mwezi. Makusudio yake yalikuwa ni kutaka kukijibu kitabu kilichoandikwa na Shaykh Naaswir Abdullah Bachuu kinachojulikana kwa jina la "Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi."

Jawabu Kidogo na mimi naomba niweke wazi kwamba kitabu changu hakikuwa kabisa na lengo la kujibu kitabu cha Sheikh Nassor Bachoo. Hili la kunukuu maneno yake na kuyajadili lilikuwa ni jambo la kutokea tu baada ya mtu Fulani kuniletea kitabu chake. Kwa havyo, kama mulivyosema nyinyi katika kitabu chenu kwamba: Kitabu hiki ni kama nasaha kwa Waislamu wote ili kuweza kudumisha umoja wetu hususan pale ambapo pamejitokeza misimamo tofauti katika mambo ya ibada. Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili.

Basi na mimi nakuombeni munielewe hivyo hivyo, kwamba wakati mimi naikubali fikra Fulani na kuikataa fikra Fulani, hakuna budi ninukuu fikra pinzani na kuonesha kwanini siikubali; na kwa upande wa pili ni lazima nioneshe kwanini naikubali fikra ninayoikubali. Na nitaposema kuwa kuna watu wana fikra hii, basi nadhani haitokuwa jambo la busara kama watu hao sikuwataja na nikiwataja ni lazima nitaje marejeo. Kwa sababu hii ndio maana nimekuwa nikinukuu maelezo ya Sheikh wetu Nassor Bachoo na kumjadili mule nisimokubaliana naye. Naomba musihuzunike kwani kujibizana katika kutafuta ukweli ni suala mashuhuri katika uwanja wa elimu. Wanavyuoni wakubwa wa kale na wa sasa wamekuwa wakijibizana ili kutafuta ukweli na hatimae huwabainikia woa pamoja na wasomaji. Kwa hivyo, hamukuwa na haja ya kutumia lugha: "Wala hapakuwa na lengo la kumkashifu": hii si kashfa hata kidogo: hii ni elimu.

Lakini, hakuna haja ya kufichana; kitabu chenu mumeandika kwa kujibu kitabu changu. Hamuna haja ya kusema: "Wala lengo la kitabu hiki sio kuendeleza malumbano baina ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe hata kwa wale wenye misimamo tofauti. Kutajwa ndugu yetu Juma Muhammad Rashid lilikuwa ni jambo lisilobudi wala hapakuwa na lengo la kumkashifu au kumuumbua bali ni kutokana na kuwa hapakuweza kupatikana njia mbadala kwa vile ameshaandika kitabu ambacho ameshakichapisha chapa ya kwanza na ya pili", kwani kitabuchenu kimeanza kwa kunitaja mimi mwanzo hadi mwisho na kuniaga kwa kunipa nasaha mimi. Ama mimi naandika jawabu hii kukujibuni nyinyi: sikufichini wala sisemi uwongo.

Munasema Kutokana na jambo hilo , sisi kwa upande mmoja tunashukuru kwa juhudi yake hiyo na kwa upande wa pili tunatuma masikitiko yetu kwake kwa kutokuwa makini na muadilifu katika kulifafanua jambo hilo muhimu. Kwani kitabu chake hicho kimeandikwa katika mfumo wa chuki, kibri, kejeli na malumbano huku akisisitiza kwa mara nyingi kauli chafu ambazo muandishi hapaswi kuzitumia katika kitabu au katika mijadala ya Dini. Jawabu Hizi chuki, kibri na kejeli, mimi nimezisoma kwenu, kwa hivyo na iwe kama msemo wa Waswahili: "Papa akipea mafuta huwapa wanawe". Je nyinyi munayakumbuka haya:

1) Munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo ambao alisema kuwa wasionyanyua mikono katika sala wanasali kama mipopoo? Jamani! Hii si kejeli? Je katika nyinyi yuko aliyetoa muhadhara au kuandika kitabu ili kumjibu Sheikh wetu. Sasa uadilifu uko wapi?

2) Je munaukumbuka muhadhara wa Sheikh Bachoo aliozungumzia mas-ala ya udhu kasha akasema: "Wengine wakitia udhu kiungo hiki huomba dua hii na kiungo hiki huoma dua hii; upumbavu mtupu". Je haya si matusi? Je hii si kejeli?

3) Siku moja palikuwa na maziko. Maiti alisaliwa msikiti wa wajiitao "Watu wa Sunna". Kijana mmoja akasimama akasema: "Leo tunataka kukuonesheni vipi Mtume (s.a.w.) kamsalia maiti: si kama wanavyofanya Ibadhi na Shia.

4) La nne ni kuwa ikiwa nyinyi mumethubutu kunita mjeuri, mwenye kibri na kejeli; maneno ambayo mimi sikukwambieni wala kumwambia Sheikh Nassor; mimi nimemtoa makosa tu Sheikh wetu: na hii ni kawaida katika uwanja wa elimu; sasa je na nyinyi pia ni majeuri, wenye kibri na kejeli? Katika uwandishi wenu, pia mumesema: "Hatujui dhana hii potofu ameitoa wapi." Mwenye dhana potufu naye ni mpotufu, kwa hivyo na nyinyi hamukutoa nasaha bali mumetukana. Nakupeni mifano hii mitatu ya Sheikh wetu na mmoja wenu nyinyi wenyewe enyi wenye kuandika Radan mardudan na mifano iko mingi. Inatosha kuwaita kwenu watu wengine kuwa ni watu wa bidaa na nyinyi ndio watu wa Sunna. Kwa hivyo, hii hali mumeiuda nyinyi wenyewe: Zanzibar bali Afrika Mashariki na Dunia kwa ujumla haikuwa hivi. Chuki mumeziunda nyinyi; mukijirekebisha kwa kutumia lugha nzuri nadhani hakuna atayekwambieni jambo kwa lugha nzito.

Mnasema Mfano wa kauli zake mbaya ni kama zifuatazo:

(vuta-nikuvute) [uk. 6]

(hii ni ajabu katika ajabu za dunia!) [uk. 124]

(Kwa hivyo, uwezekano huo alioutoa Sheikh hauwashi wala hauzimi [uk. 124]

(Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja,)

(Utaona kwamba masuala yote haya si yenye kima katika soko la elimu, bali ni masuala ya kuwababaisha watu wasiojua nini cha kujadiliwa katika mas-ala haya ya funga) [uk. 167]

(Hoja nyengine - nayo pia ni hoja ya mitaani - ni kuwa watu wengi wa kawaida wanapouona mwezi mkubwa husema: "E basi ule ndio mwezi wa leo ule?!!!")

(Jawabu hii ya mwisho, inaufanya upinzani mzima wa Sheikh Bachoo kuwa hauna maana yoyote.) [uk. 132]

(Kwa ufupi ni kuwa hicho walichokidai watetezi wa rai pinzan) [uk. 32]

(utaona jinsi gani mwanamume alivyokuwa bingwa wa kubadilika! Na hili si jengine bali ni lile Waswahili wanalolisema: "Mfa maji hukamata maji.") [uk. 128]

(Hakuna hapa kinachoonesha mas-ala ya kufunga kwa muandamo mmoja wala kumi na moja.)) [uk. 125] (haina maana kwamba usiku ukiingia sehemu moja ndio umeingia dunia nzima. Kwa ufupi ni kuwa hii ni hoja ambayo haina faida yoyote ya kielimu, lakini tunaijadili kwa ajili ya watu wa mitaani tu.)

Jawabu Sikubaliani na nyinyi kwamba humu muna maneno mabaya. Lakini hata nikikubali basi nasema kwamba lugha ya namna hii sababu ni nyinyi, na kwa hivyo, utaona kwamba ninapojadiliana na watu wengine basi lugha yangu hubadilika. Kwa hivyo, tujirekebisheni sote na tujadili tafauti zetu kwa lugha ya kiungwana. Ama ukinita mpopoo, basi usinilaumu na wewe nikikwita mnazi: unanilaumu nini na wewe unakifanya kile kile nikifanyacho?! Bali hata katika kitabu hiki munachonijibu, basi nanyi mumetumia lugha hizo hizo. Katika baadhi ya sehemu umesema: "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti..". Na mwishoni mwa kitabu mumesema: "Dhana ya pili ya ndugu Juma imejengeka katika msingi dhaifu wala haina nafasi katika uwanja wa fani (kitaalamu) nao ni kule kusukuma kwake juu ya elimu ya Jiografia". Na yamo mengi katika kitabu chenu. Sasa nyinyi mwasema nini na mwatenda nini?

Munasema "Kwa hakika katika kitabu chake hicho kwenye uk 6, anajionyesha alivyo na kauli mbili tofauti: Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi i likuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini? Na ni nani aliyemwambia kwamba jambo lenye khitilafu halizungumzwi? Yeye angezungumza nini katika kitabu chake kama si masuala ya ikhtilafu? Pia anatwambia haya ni katika mambo ya furui (matawi) za Kidini, kwa hivyo zisizungumzwe. Kwani ni nani aliyemwambia kuwa furui za Kidini hazizungumzwi?"

Jawabu Ikiwa lugha hii ndogo hamukuweza kuifahamu, vipi mutaweza kufahamu kitu chenye kuhitaji fani za lugha na usuli na mengineo. Ikiwa mimi niliingia msikitini kwenu Raha Leo nikakuta juu ya ubao wenu munawasomesha vijana na katika darsa hio Mubtadaa mumemwita Fa'il (vipi mutaweza kujadili masuala haya?!!! Mimi nimempongeza Sheikh Bachoo kwa juhudi au moyo wake; na sikumpong eza kwa kulikuza suala ambalo:

1) Ni la furuu'i

2) Lina khilafu. Na hii haina maana kuwa Furu'i zisizungumzwe; suala la Furu'i huwa halishadidiwi; bali unawaacha watu kama walivyo tu. Lakini yeye anapenda kushadidia katika mas-ala kama haya; ndio maana akashadidi hata katika suala la kufunga mikono hata kuwaita watu mipopoo bali na kuwambia kuwa hawana Sala. Kwa hivyo, nieleweni kwamba ninachokipinga ni kushadidia au kuwakoroga watu katika kitu ambacho ni furu'i za dini ilhali yeye kawakuta na msimamo tafauti tangu zamani. Katika mas-ala ya furu'i, wanavyuoni huwa hawashadidi juu ya Mas-ala kama haya. Mimi leo nikisimama nikaanza kufanya kampeni kwamba watu wasiitikie amina wa kisali, nalo ni jambo la furu'i, si nitakuwa natia fitna tu? Jambo kama hili huwachwa wasomi wakalitafiti kaiha kila mmoja akafanya vile ilivyombainikia. Lakini kufanya kampeni maalumu na da'awa kana kwamba waliotangulia wote ni wapotovu, hili ndilo jambo la kulaumiwa.

Ama kauli yenu: "Kwanza anakubali kwamba suala la muandamo wa mwezi lina ikhtilafu katika kufunga kwa kumuelezea Shaykh Naaswir Bachuu kwamba: (Tunampongeza kwa juhudi) Kisha pale pale anageuka kwa kusema: (madamu hili ni suala la khilafu - basi ilikuwa ni kutolizungumza kabisa,) Sasa hebu tumuulize ndio anapongeza nini?" Mwisho wa kunukuu. Na mimi nikuulizeni nyinyi mumenishukuru kwa juhudi yangu kisha mwisho wa kitabu mukaniambia: "Mwisho tunachukua fursa hii kumuonya ndugu Juma kuwa amuogope Mwenyezi Mungu hususan katika mas-ala ya kielimu. Akumbuke kuwa Mwenyezi Mungu Ameonya juu ya mtu kusema jambo au kufanya asilolijua. Aelewe kwamba ataulizwa juu ya hilo. Lingekuwa jambo la busara kama ndugu Juma angalikubali kuuliza na kufanya utafiti zaidi juu ya mas-ala haya kama agizo la Mwenyezi Mungu linavyotutaka". Sasa na nyinyi munanishukuru nini?

Munasema "Sisi tunapenda kumfahamisha kuwa suala hili la kwamba mwezi ukiandama sehemu moja unatosheleza kufuatwa kwa kufunga au kufungua ulimwengu mzima, si suala jipya bali ni jambo la kale. Tunasikitika kwamba hakuangalia vizuri maoni ya Wanavyuoni wakubwa walivyoelezea msimamo huo. Angalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 51-58. Hapa tunanukuu baadhi ya kauli hizo:

Imamun-Nawawy aliyekisherehesha Kitabu cha Sahihi Muslim anasema:

"Na jambo lililo sahihi kwa wenzetu (Mashaffi) ni kuwa muandamo mmoja hauwahusu watu wote bali unawahusu wale walio karibu kwa kiasi ambacho hawaruhusiki kupunguza Sala (Sala ya safari). Pia imesemwa kuwa iwapo matlai ni mamoja watalazimika (watu) kufunga pamoja. Pia imesemwa kuwa ikiwa (wanaishi) katika eneo la Iklimu moja (maili 72 au km 89) (watalazimika kufunga pamoja) vyenginevyo kila mmoja atafunga kwa muandamo wake. Na wakasema wenzetu wengine (Mashaffi) kuwa muandamo katika sehemu moja utawahusu wote wa dunia nzima".

Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar katika kitabu chake "Bayaanullinnas" J. 2 uk 203 - 204 ameandika yafuatayo juu ya kauli hiyo ya Imamun-Nawawy:

"Hapa Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasari kauli zilizomo katika madhehebu ya Kishaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu mengine ya Kiislamu. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika maf ungu matatu makuu: "...Hapo Imamu An-Nawawy ametaja kwa mukhtasar kauli zilizomo katika madhehebu ya Shaffi (juu ya kuandama kwa mwezi) na ambazo pia zimo katika madhehebu nyengine za Kiislam. Kauli hizo tunaweza kuzigawa katika mafungu matatu makuu: Kauli ya kwanza: "Kila nchi iwe na matlai yake, wala muandamo wa nchi moja hautalazimu nchi nyengine ya mbali wala karibu". Kauli ya pili: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi zote za dunia hata kama ziko mbali".

Kauli ya tatu: "Muandamo wa nchi moja unalazimu nchi iliyo karibu nayo au inayowafikiana kimatlai". Kisha, Shaykh Jaadul-Haq akaendelea kusema kwamba:

"Na (kauli) zote hizo ni maoni yatokanayo na Ijtihaadi ambazo hazikusimama juu ya hoja kat-ii, si sanad wala matni. Kwa hivyo ingefaa ichaguliwe kauli ambayo inakubaliana na maslahi ya (Waislam wote wa) dunia nzima kwa jumla"."

Jawabu Sikubaliani na mtazamo wa Sheikh Shaykh Jaadul Haq wa chuo kikuu cha Al-Azhar, kwamba zote hizi ni rai na itihad kwani kanuni ni kuwa "Hakuna ijtihadi mbele ya andiko" Ijtihad mwahala mwake ni musimo andiko. Wakatika katika suala hili, utaona kwamba asemaye kuwa tufunge kwa muandamo mmoja, hoja yake ni Hadithi "Fungeni kwa kuuona"; na anayesema kuwa kila mahala na muandamo wake, anatoa ushahidi wake ni Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib. Kwa hivyo, ijtihad ni katika kuyafahamu maandiko: si ijtihad kwa maana ya rai tupu pasi na andiko kama alivyosema Sheikh. Kilichobaki ni kuzijadili riwaya mbili hizi zina maana gani?

Munasema Tungependa kumueleza ndugu yetu kwamba hata hapa Afrika ya Mashariki jambo hili hakulianzisha Shaykh Naaswir Bachuu kama alivyodai mwenyewe (Nd. Juma) kwamba: (Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro)) Inasikitisha hakuweza kuangalia katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu uk 161-163 wametajwa walioonyesha kwa vizuri kabisa misimamo hiyo tofauti. Mashaykh wenyewe ni hawa wafuatao: Al-marhuum Shaykh Juma Abdul Waduud (wa Zanzibar), Shaykh Abdillahi Naaswir ( Nairobi Kenya ), na Shaykh Naaswir Khamis Abdul Rahman ( Mombasa Kenya ).

Jawabu Kwani wapi katika kitabu changu nilisema kuwa Sheikh Nassor Bchoo ndiye aliyeanzisha fikra hii hapo Afrika ya Mashariki hata mukaleta dai hili? Mimi nimeeleza kuwa zamani Afrika Mashariki watu wote wakifata muandamo mmoja. Nilisema: Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo. Dr. Ramadhan Al-butti - miongoni mwa wanavyuoni wakubwa wa ulimwengu wa sasa - anaona kwamba harakati hizi hazisifiki kama ni madhehebu: bali ni hatua (phase) katika mapito ya Historia.

Na katika uk. 97, nimesema:

Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya. Kwa hivyo, ni wazi kwamba mimi nazungumzia Afrika Mashariki. Na mfano wa hilo pia kalisema Sheikh Nassor Bachoo, lakini yeye hamukumjibu. Anasema: "Pamoja na kuwa mgogoro wa kuandama kwa mwezi umeanza kuonekana hadharani katika jamii za Waislam wa hapa Afrika ya Mashariki katika miaka ya hivi karibuni". Inasikitisha kwamba hata maneno yangu mumeyakata na kuchukua yale ambayo hayakamilishi maana nilioilenga. Maneno "Karne zimepita" hamukuyataka kwani hayakufikisheni kule mutakako!

Pili narejea tena kusema kwamba hao wanavyuoni aliowataja Sheikh Nassor, hawajathibitisha habari za kuwa watu wafunge au wakifunga kwa muandamo mmoja Africa Masharik, ukimtoa Sheikh Nassir Khamis wa Mombasa ambaye naye pia ni mtu wa sasa. Ama sheikh Juma Abdu-Wadood yeye, kwa mujibu wa nakala hio ya Sheikh Nassor Bachoo, kasema hivi: Kuona huku kwa mwezi kumekusudiwa kuonekana na Waislam, na kuonekana na Waislamu huko, sio lazima kuonekana na Waislamu wote. Bali inatosha shahada ya mtu mmoja muadilifu".

Pia inampasa mtu mmoja pekee kama ameuona mwezi yeye afunge na kila aliyemuamini; hata akiwa haijakubaliwa shahada yake. Haya ndio maneno ya Sheikh Juma Abdu-Wadood kwa mujibu wa alivyomnukuu Sheikh Bachoo. Sasa ikiwa ndugu zetu mumeshindwa kuyafahamu maneno haya ya Sheikh Juma Abdu-Wadood, bado mutaendelea kupoteza watu bila ya elimu?! Sheikh Juma Abdul-Wadood hapa anazungumzia mas-ala ya ushahidi kwamba si lazima - katika suala la kuonekana kwa mwezi - kwamba kila mmoja auone: bali akiona mtu mmoja basi inatosha kwa wengine kufunga. Hii ndio kauli ya Sheikh Juma Abdul-Wadood na hili nimelieleza kwa urefu katika kitabu changu.

Kisha Sheikh Juma Abdul-Wadood akazungumzia suala la kufunga kwa muandamo mmoja akasema: "Rai za Maimamu wengine wameifasiri hadithi isemayo: (Fungeni kwa kuuona Mwezi) kwamba ukionekana popote mashariki au magharibi (watu) wafunge; hapana kutazama masafa fulani au nini. Hii ni rai nayo na wengi wamesema (hivyo) kama Imamu Malik , Ahmad na kundi kubwa la Hanafi. Inakurubia kuwa n dio rai ya Jamhuri - kufata rai hii ni kuhakikisha umoja wa dunia nzima. Wala hatuwezi kusema kwamba rai ya Shaffiy ndio ya Jamhur". Hapa Sheikh Juma anasimulia rai za Maimamu wengine: si rai za Maulamaa wa Afrika Mashariki. Mimi dai langu nililodai ni kuwa jambo hili la kufunga kwa muandamo mmoja, napenda munifahamu: ni jipya kwa Africa Mashariki. Mimi sikusudii jambo la wanazuoni kuzungumzia rai mbali mbali: bali nazungumzia jambo la watu kufata muandamo mmoja kwamba karne zimepita ya sikio la Muafrika Mashariki wa Kawaida halijiapata kusikia. Na nimetumia maneno "Muafrika wa Mashariki wa kawaida" ili kuwatoa wanavyuoni wao hata kama walikuwa hawafati kauli hio, lakini wanaijua. Kwa hali yoyote ile:

1) Sheikh Juma Abdul-Wadoo hajazungumzia kwamba Afrika Mashariki watu walikuwa wakifunga au wafunge kwa muandamo mmoja, bali kazungumzia rai za wanavyuoni wasio wa Afrika Mashariki - Al-Imamu Shafi, Hanbal n.k. Na mimi sijakanusha tafauti hizi.

2) Kauli yake ilikuwa ni kuhusu suala la mashahidi.

Ama Sheikh Abdillahi Nassir, yeye ni mwanachuoni wa sasa. Na mimi sijasema kuwa sasa hakuna rai hizo. Pili ni kuwa nakala alizotupa Sheikh Bachoo za kitabu cha Sheikh Abdillahi utaona kwamba Sheikh Abdillahi hazungumzii kuwa kauli ya kufatwa ni ile ya muandamo mmoja; bali yeye kasema kuwa hili ni suala la khilafu kwa hivyo tusigombane kila mtu afate rai anayoiona kuwa ni sawa. Sheikh Abdillah kayasema haya baada ya kutokea mizozo hii ya sasa. Kwa hivyo tunarudi pale pale kwamba "Karne zimepita bila ya sikio la Muafrika wa Mashariki wa kawaida kusikia sauti ya mgogoro juu ya suala la muandamo wa mwezi. Harakati za elimu zilipobadilika na kuelekea zaidi - kwa kujua au bila kujua - katika mrengu wa Kihanbali na Kiwahabi, pakajitokeza mapinduzi ya ghafla ya fikra na matendo". Kwa hivyo, nukta hii hamukuuijibu: na wala sioni kuwa kuna haja ya kuijibu kwani haina umuhimu katika maudhui yetu. Bali kitabu chenu chote, munachagua mambo yasio na umuhimu "Juma kantutukana; Juma kanfanya hivi" nyinyi ndio munajibu baada ya kuzungumzia dalili za kielimu.

Ama Sheikh Nassor: yeye pia ni mtu wa sasa na ni mfuasi wa skuli hio hio munayoifuata nyinyi, kwa hivyo kusema kwake alivyosema hakujapindua nilioyasema kuwa - kimatendo - hili ni suala jipya kwa kwetu Afrika ya Mashariki. Wala mimi sikusema kuwa Sheikh Nassor Bachoo ndiye muasisi wa fikra hio huko kwetu. Naomba munifahamu ninachokisema kwanza kisha ndio munijibu. Na sijui munapinga nini kitu ambacho watu wote wanakijua. Bila ya kusahau kwamba mimi sikusudii kusema kuwa kitu sahihi ni kilichofanywa zamani au kilichofanywa leo: laa! Bali kitu sahihi ni chenye ushahidi sahihi uliojengeka juu ya misingi sahihi ya kielimu. Na kielimu, suala la kuzingatia muandamo mmoja - hamutoweza kulithibitisha.

MNASEMA

Pia Shaykh Ahmad Al Khalil, Mufti wa Omani amethibitisha kwamba Ikhtilaf hii ya muandamo wa mwezi katika hukmu ya kufunga au kufungua ipo na kwamba ni jambo la kale. Kama alivyosema maneno yake yaliyotafsiriwa na Shaykh Muniir Sulayman 'Aziz kwamba: "Hakuna madhehebu iliyokuwa imesalimika na kuwa na Khitilafu baina ya Wanavyuoni wake juu ya suala la kutafautiana miandamo ya mwezi." Jee ndugu Juma anataka kusema kwamba Shaykh Naaswir Bachuu ndiye mwalimu aliyeanzisha madhehebu zote? Au ndiye aliyeanzisha mtafaruku huu kama alivyouita mwenyewe ndugu Juma?

JAWABU

Suala hilo jiulizeni wenyewe; mujijibu wenyewe; kwani nyinyi ndio mulioliunda: mimi sikusema hivyo kamwe bali nilichokisema ni hiki: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nami sikusudii kusema kwamba upya huo ni katika kuzungunzwa au kusomwa suala hilo katika vitabu; nakusudia kimatendo sula hili lilikuwa halipo Afrika Mashariki. Sasa ili muwe mumenijibu, twambieni nani alikuwa akifata muandamo mmoja hapa Afrika Mashariki. Jamani! Tafuteni hoja mujadili: musijadili kitu kisichokuwa na umuhimu. Kama hamuna hoja nyamzeni musijitie aibu!

MNASEMA

Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani; Ndugu Juma anasema: (Kama tunavyojua kwamba Sheikh Nassor Bachoo, ni mmoja wa wenye kusisitiza ulazima wa kuwa na muandamo mmoja.) Sisi kwa upande wetu tunasema: Katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu hakuna pahala alipolazimisha watu wafuate huo aliouita ndugu Juma (msimamo wa Shaykh Naaswir). Bali yeye ameonesha mitizamo ya Wanavyuoni kwa kutumia Aya za Qur-aan, Hadiythi na vitabu vinavyokubalika. Lugha aliyotumia Shaykh Naaswir katika huo unaonekana ni msimamo wake ni maneno yaliyozimuliwa kilugha (polite language) kama vile: (inawezekana) ((inaonyesha) .

JAWABU

Na mimi hapa sijasema kuwa Sheikh Nassir Bachoo kalazimisha watu wafunge kwa muandamo mmoja. Nimesema "Anasisitiza ulazima" yaani yeye analingania msimamo huo kwani kwake ndio msimamo sahihi na ndio wajibu kuufata. Naomba tena tuelewane musiseme kitu kinyume na nilivyosema. Wala musitafute kitu kisicho na maana mukajadili eti ndio jawabu! Pili maneno yenu: "Katika kudhihirisha udhaifu wake wa kumuandama mtu fulani". Sasa je na nyinyi pia munaonesha udhaifu huo huo kwa kumuandama mtu fulani katika kitabu chenu?

MNASEMA

Aliyelazimisha rai ni ndugu Juma mwenyewe kama anavyosema: (Lakini kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali) [uk. 112]

JAWABU

Bali hata Sheikh Bachoo pia kalazimisha kwani ukidai kuwa huu ndio msimamo wa haki au ndio msimamo sahihi au ndio wajibu kufatwa, bila kusema kuwa rai zote zinafaa basi na wewe huwa umelazimisha rai yako. Sasa je Sheikh Bachoo anakubali hivyo kuwa rai zote ni sawa? Mimi kweli sisemi kuwa rai zote ni sawa: nasema kuwa nyinyi mumekosea na sahihi ni kinyume na munavyofanya, na kwa hivyo bado nipo katika msimamo wangu huo huo kwamba: "Kilicho lazima na ambacho tunatakiwa tukubaliane ni kuwa muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali".

MUNASEMA

"Kisha katika uk 85 ndugu Juma anataja kwamba msimamo huu wa muandamo mmoja kwa dunia nzima ni ((kitu kipya)) na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu baada ya kutaja baadhi ya nchi zinazofuata miandamo yao - yaani kila nchi na muandamo wake kama Al-yaman , Oman , Misri na Saudia. Kisha hapo hapo akataja: ((isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.)) Inafaa ndugu Juma aulizwe masuala yafuatayo:

i) Kama ni jambo lisilotekelezeka vipi tena Imarat wanalitekeleza?

ii) Je hawa wa Imarat nao ni wanafunzi wa Shaykh Naaswir Bachuu?

iii) Kwani hiyo sio kauli ya Jamhuur ambayo ndio msimamo wa maimamu wakubwa wakiwemo Ahmad bin Hanbal, Malik na Abu Hanifa? (Angalia pia sehemu ya 11 na 13 za kitabu hiki)

JAWABU

Kwanza mumemefanya ghushi: maneno yangu hamukuyanukuu yote. Mimi nimesema: "Kwa kwetu - Afrika Mashariki - kusema kwamba mwezi muandamo wa nchi moja ni muandamo kwa nchi nyengine zote za dunia ni kitu kipya". Nyinyi maneno "Kwa kwetu Afrika Mashariki" mumeyatoa ili ionekane kuwa mimi nasema kuwa hili ni suala jipya kila pahala. Watu kama nyinyi vipi tutakuamini katika dini yenu na uadilifu wenu, ikiwa munaghushi maandiko hivi? Hii ndio kamati ya Msikiti Sunna na hii ndio suna yenyewe?! Halafu mukaendelea na tadlis (ghushi) yenu mukasema: "Na kwamba jambo hilo halitekelezeki na ni kauli iliyobaki vitabuni tu". Mimi sikusema hapa kuwa "Halitekelezeki", bali nimesema:

Lakini ukweli ni kuwa hata katika nchi nyengine zote za dunia taqriban kauli kwamba tufunge kwa muandamo mmoja, ni kauli ilioishia katika vitabu tu, kimatendo (practically) kauli hio haitumiwi isipokuwa na mtu mmoja mmoja. Hadi leo hii: watu Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao, Misr wanafata muandamo wao na nchi zote taqriban ni hivyo, isipokuwa Imarati katika miaka ya mwisho wamekuwa wakifata Saudia.

Haya nionesheni hapa maneno "Halitekelezeki". Mimi nimesema kuwa kimatendo kauli hii, hadi leo haitendewi kazi isipokuwa na baadhi ya watu. Nyinyi mumebadilisha na kuweka ghushi yenu mukasema nimesema halitekelezeki. Kwa hivyo, hilo Sula (a na b) jibuni wenyewe kwani mumesema kinyume na nilivyosema. Suala (d), najibu kuwa sio: hio si kauli ya jumhur bali jumhur kauli yao ni kinyume na hivyo na hili nimelithibitisha katika uk. 189-193 wa chapa ya pili ya kitabu changu au uk. 171 wa kitabu hicho chapa ya kwanza. Na Al-Imamu Malik riwaya zake zimegongana na riwaya kwamba kila watu na muandamo wao ndio ilio bora kwani ni riwaya ya Madina aliko kuweko Al-Imamu Malik, wakati riwaya nyengine ni ya watu wa Irak kulikokuwa na viwanda vya kutunga riwaya!

MNASEMA

Na sisi tunamuongezea habari moja ambayo ni vyema kuielewa, kwamba nchi ya Uganda iliyo katika Afrika ya Mashariki pia inafuata rasmi muandamo mmoja wa duniani. Pia aelewe kwamba huo msimamo wa kila nchi na mwezi wake huku Afrika ya Mashariki haukuwepo tokea zamani. Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja. Yeye anaendelea kushika msimamo wake: (Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka.

JAWABU

1) Kitu rasmi Uganda hakizingatiwi kwani Uganda kimsingi sin chi ya Kiislamu wala ya Waislamu: Waislamu ni wachache ukilinganisha na Wasio Waislamu. Kwa hivyo, hakuna kitu rasmi. Na jambo hilo ni jambo la sasa. Na mimi sijapinga kwamba sasa fikra hio ipo Afrika Mashariki.

2) Ama kauli yenu: "Mashaykh wote wa huku wanakubaliana mwezi ukionekana popote katika nchi hizi tatu ( Kenya , Uganda na Tanzania ) wanafunga pamoja". Ndio maana nikatumia lafdhi "Kwa kwetu Afrika Mashariki" nikijua kuwa wanavyuoni wote wa kwetu Afrika Mashariki wana msimamo huo. Ama kauli yenu: "Yeye anaendelea kushika msimamo wake: ((Al-yaman wanafata muandamo wao, Oman wanafata muandamo wao, Saudia wanafata muandamo wao,)). Lile analoliona yeye halitekelezeki, basi ndio linatekelezeka". Mwisho wa kunukuu. Inaonesha kuwa kitabu changu mumekijibu bila ya kukifahamu. Nilichosema ni kuwa, ijtihadi ifanywe katika kubainisha wapi hadi wapi watu wafunge pamoja. Kwa vile, hakuna andiko lililobainisha hivyo. Ama muandamo mmoja kwa dunia nzima hili ni kinyume na andiko. Kwa hivyo, wakiwa wanavyuoni wa zamani wamefanya ijtihad hio, sisi tunafata ijtihad yao kwa vile hapa ni mahala pa ijtihad na haikugongana na andiko. Ama madai yenu nyinyi ni kinyume na andiko lilivyoonesha.

MNASEMA

"Kuna suala moja la nyongeza tunapenda tumuulize ndugu yetu Juma: Hata kama hizo nchi alizozitaja ( Al-Yaman , Oman , Misri na Saudia) hazijakubaliana kufuata muandamo mmoja, je hakuna uwezekano (japo wa sadfa) unaoweza kutokea kufunga siku moja ijapokuwa kila mmoja ameona mwezi katika nchi yake? Sasa tuseme kila nchi katika hizo imeona mwezi usiku wa Alkhamisi kuamkia Ijumaa - Wote si watafunga siku moja ya Ijumaa? Basi huo ndio utekelezaji aliosema hautekelezeki. Ni wazi kuwa unatekelezeka.

JAWABU

Munaendelea kuuliza masula haya kwa sababu masuala yenu mumeyajenga katika kitu nisichokisema kamwe. Wapi nimesema kuwa "Hilo halitekezeki" hata mukauliza masuala haya?