TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE Juzuu 4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE27%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18039 / Pakua: 4401
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE Juzuu 4

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU, MWINGI WA REHEMA, MWENYE KUREHEMU

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London. Kama lilivyo jina la Tafsiri yenyewe ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo. Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana. Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea, hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho 'Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah' (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka hivi karibuni Inshaallah). Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasyansi kama kina Enstein, Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa. Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji. Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

Masahihisho Katika Juzuu ya pili: Uk 23- Aya ya 177 badala ya kusoma Lissaailina soma Walissaailina Uk. 23-25 Aya ya 177 tarjuma ya Kiswahili, mwisho kabisa wa Aya, badala "Hao ndio waliothubutu (katika Imani) soma: "Hao ndio wasemao" Uk. 29- Aya 184, Msitari wa tano- tarjuma ya Kiswahili "Na wale wasioweza, "Soma: "Wanaoweza kwa shida" Uk. 35- Aya ya 192- badala ya kusoma Ghafu soma Ghafuur

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa. Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo, Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa. Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswatu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146). Imeandikwa La Ya'alamuun,(hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki. Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa "Fawqahum ila yawmil qiyama badala ya Fawqahum yawamal qiyama". Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu jabal amail 'Makosa ya chapa.' Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: "Hatta idaha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidaha balagha ashuddahu arbai ' na sanah" Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko ya kuufungia macho uzuri wa maana. Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa, kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi. Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu" Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyoyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿ لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴾

92.Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda; na chochote mnachokitoa, basi hakika Mwenyezi Mungu anakijua.

MALI NDIO SABABU YA UGOMVI

Aya 92

MAANA

Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda, na chochote mnachokitoa, basi Mwenyezi Mungu anakijua.

Makusudio ya wema hapa, ni utukuzo wa Mwenyezi Mungu na fadhila kwa mja wake, Zimetangulia tafsir za Aya kadha kuhusu kutoa. Lakini Aya hii imetofautiana kabisa na Aya zingine zinazoelezea maudhui haya. Kwa sababu, haitosheki na kuamrisha kutoa tu, kama Aya nyinginezo, bali imeunganisha baina ya kupata mtu daraja ya juu mbele za Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kujitolea anavyovipenda. Kwa hiyo ibada isiyokuwa ya kujitolea, haikurubishi kwa Mwenyezi Mungu - kwa mujibu wa Aya hii- isipokuwa ikiambatana na kujitolea katika njia ya Mwenyezi Mungu.

Kwa hivyo basi, kauli yake Mwenyezi Mungu; "Hamtaufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda," ni tafsiri na ubainufu wa kila Aya na Riwaya inayohimiza kufanya amali kwa ajili ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu na kujikurubisha kwake hali ya kuwa ni ufafanuzi kwamba, kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu hakupatikani wala hakutapatikana ila kwa kujitolea mtu nafsi yake na mali yake anayoipenda. Ni kama kwamba Imam Ali(a.s) alichukua kutokana na Aya hii, kauli yake:"Hapana haja ya Mungu kwa ambaye katika nafsi yake na mali yake hakuna fungu la Mungu"

Kutoa ni kugumu na hasa mali ambayo ndiyo mgomvi anayeipambanua imani ya asili. Mali ilikuwa na inaendelea kuwa ni yenye kuabudiwa na mamilioni ya watu. Watu wengi wanawazishwa na shetani kwamba wao wanamwabudu Mwenyezi Mungu (s.w.t), kumbe kwa hakika wanaabudu pesa, lakini wenyewe hawatambui. Kuna kisa kimoja kwamba Iblis, kabla ya kuanzishwa mfumo wa pesa, alikuwa na shughuli kubwa sana ya kuwapoteza watu na kuwaepusha na ibada ya Mwenyezi Mungu wawe waabudu sanamu. Kwa hiyo ikawa hana raha usiku na mchana. Baada ya kupita masiku, ukaja mfumo wa pesa ndipo Ibilisi akapumua, akafurahi sana, akaandaa hafla ya taarabu, akawa anacheza huku ameweka Dirham kwenye jicho moja na Dinar kwenye jicho jengine. Akasema: (kuziambia pesa hizo) mmenipumzisha sasa, sitojali kama watu wanawaabudu nyinyi au wataabudu masanamu. Kisa hiki kiwe ni cha kweli au uongo au hata kama ni katika vigano, lakini ni picha ya kweli. Kwa sababu hakuna tofauti kati ya kuabudu mali na kuabudu masanamu, kila moja inamwepusha mtu na Mungu na haki. Bali kuabudu mali kuna athari mbaya zaidi, na kuna madhara zaidi. Kwa sababu, mara nyingi sana mali ndio kiini cha matamanio na ni chimbuko la ufisadi. Wale waliozihaini nchi zao wamefanya hivyo kwa sababu ya pesa. Na wale waliowapiga vita Mitume na watu wema na kuibadilisha dini na sharia ya Bwana wa Mitume, walifanya hivyo baada ya kupata chochote.

Kadiri nitakavyotia shaka, lakini siwezi kutia shaka kuwa walahidi na waabudu masanamu ambao hawakuzifanyia hiyana nchi zao wala kuwafanyia njama watu wema, kuwa ni bora mara elfu, kuliko mwenye kufunga, kuswali, kuhiji na kutoa zaka lakini anapanga njama pamoja na maadui kuuza nchi na riziki za waja. Kwa hiyo hapana ajabu kwa mtu kupata daraja mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kujitolea kwa mali, ambapo kutokana na kutoa huku kunaonyesha haki kuwa juu ya batili na akhera juu ya ulimwengu,

Unaweza kuuliza kuwa : mbona kauli yake Mwenyezi Mungu"Hamtapata wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda." Kwa dhahiri inafahamisha kuwa pepo haipati ila yule aliye nazo atakayejitolea vizuri katika mali, ambapo watu wengi hawamiliki chochote.

Jibu : Msemo katika Aya tukufu unamhusu mwenye nacho. Ama asiyekuwa nacho, yeye ndio anapasa achukue sio kutoa, bali yeye ni sehemu mojawapo ya kutolea hiyo mali. Zaidi ya hayo ni kwamba, ambao wanapigana jihadi kwa nafsi zao, wana cheo zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko wale ambao wanapigana jihadi kwa mali zao. Kwa sababu, kuitoa nafsi ni ukomo wa kutoa. Kama ambavyo Aya imefahamisha, kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kumedhaminiwa na kutoa na kujitolea. Basi vile vile imefahamisha kwamba, mali ni chimbuko la kheri na ni njia ya kumtii Mwenyezi Mungu; kama ambavyo pia ni kiini cha matamanio na ni ya kumridhisha shetani. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema:"Mwenye kuitafuta dunia kwa ajili ya kujilimbikizia na kujifaharisha atakutana na Mwenyezi Mungu akiwa amekasirika. Na mwenye kuitafuta kwa kujistahi na kuichunga nafsi yake, atakuja siku ya Kiyama uso wake ukiwa kama mbalamwezi." Imam Ali(a.s) anasema:"Hakupewa yeyote kitu katika dunia ila hupungua fungu lake katika akhera" Mmoja wa waliokuwepo akasema: 'Sasa sisi tunaitafuta dunia (Itakuaje?)' Imam akasaili:"Mnaifanyia nini?" Akajibu: 'Kujikimu mimi, wanangu na kutoa sadaka na kuhiji.' Imam akasema: "huku si kutafuta dunia, bali ni kutafuta Akhera"

﴿ كُلُّ الطَّعَامِ كَانَ حِلًّا لِّبَنِي إِسْرَائِيلَ إِلَّا مَا حَرَّمَ إِسْرَائِيلُ عَلَىٰ نَفْسِهِ مِن قَبْلِ أَن تُنَزَّلَ التَّوْرَاةُ قُلْ فَأْتُوا بِالتَّوْرَاةِ فَاتْلُوهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴾

93.Kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israil ila alichojiharamishia Israil mwenyewe kabla ya kuteremshwa Tawrat. Sema: Leteni Tawrat muisome mkiwa ni wakweli.

﴿ فَمَنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴾

94.Basi wenye kumzulia uongo Mwenyezi Mungu baada ya hayo, basi hao ndio madhalimu.

﴿ قُلْ صَدَقَ اللَّـهُ فَاتَّبِعُوا مِلَّةَ إِبْرَاهِيمَ حَنِيفًا وَمَا كَانَ مِنَ الْمُشْرِكِينَ﴾

95.Sema: Amesema kweli Mwenyezi Mungu. Basi fuateni mila ya Ibrahim aliyeshikamana na haki; wala hakuwa katika washirikina

WANA WA ISRAIL NA CHAKULA

Aya 93 - 95

MAANA

Kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israel.

Aya hii kwa ufupi inasimulia kwamba, Aya nyingi zinaonyesha wazi kuwa Muhammad(s.a.w.w) na walio pamoja naye wako kwenye mila ya Ibrahim; wanamwamini Mwenyezi Mungu na aliyoteremshiwa Ibrahim, Ismail, Is-haq,Yakub na kizazi chake. Vile vile Musa, Isa na Mitume wengineo.

Maana yake kwa dhahiri ni kwamba, kila lililokuwa haramu katika dini ya Mitume hiyo basi ni haramu katika dini ya Kiislamu. Mayahudi walikuwa wakiitakidi kuwa nyama ya ngamia na maziwa yake ni haramu katika dini ya Mitume iliyotajwa. Wakamwona Muhammad anaihalalisha na kwamba, uhalalishaji huo unapingana na kauli yake kuwa yeye yuko kwenye mila ya Ibrahim, na kwamba yeye anaamini alichoteremshiwa Ibrahim na Mitume walio baada yake.

Kwa kutegemea madai haya, wakatangaza na kueneza habari kwa makusudio ya kutia ila na kuleta shaka katika Uislamu kwamba Muhammad anajipinga mwenyewe. Anahalalisha chakula kilichokuwa haramu katika mila ya Ibrahim, na wakati huo huo anadai kwamba yuko katika mila ya Ibrahim.

Ndipo Mwenyezi Mungu akawajibu kwa kusema: "Kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israel." Yaani Ibrahim na waliomfuata, hawakuharamisha nyama ya ngamia na maziwa yake, bali kila chakula kilikuwa halali kwao. Na mayahudi ni wakadhibishaji na ni wazushi katika kuwanasibishia Mitume kuwa ndio wenye kuharamisha.

Ila alichojiharamishia Israil mwenyewe.

Israel ni Yakub bin Is-haq bin Ibrahim. Alikuwa hatumii baadhi ya vyakula kwa sababu zake zinazomhusu yeye tu, si kwa sababu ya kuharamishiwa na Mwenyezi Mungu.

Ni kama mtu akiamua kutovuta sigara kwa sababu za kiafya n.k. Lakini alipojizuia ikawa ni desturi ya Wana wa Israil kumfuata baba yao katika yale aliyojizuilia mwenyewe na hilo lilikuwa kabla ya kuteremshwa Tawrat.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja hivyo, kwa sababu aliwaharamishia vitu vingi baada ya Tawrat kutoka na dhambi walizozifanya; kama asemavyo Mwenyezi Mungu:

﴿ فَبِظُلْمٍ مِّنَ الَّذِينَ هَادُوا حَرَّمْنَا عَلَيْهِمْ طَيِّبَاتٍ أُحِلَّتْ لَهُمْ وَبِصَدِّهِمْ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ كَثِيرًا﴾

"Basi kwa dhuluma ya Mayahudi tuliwaharamishia vitu vizuri walivyohalalishiwa, na kwa sababu ya kuzuilia kwao njia ya Mwenyezi Mungu kwa wingi" (4:160).

Ama aina ya vitu walivyoharamishiwa baada ya kuteremshwa Tawrat vimetajwa na Aya hii:

﴿وَعَلَى الَّذِينَ هَادُوا حَرَّمْنَا كُلَّ ذِي ظُفُرٍ وَمِنَ الْبَقَرِ وَالْغَنَمِ حَرَّمْنَا عَلَيْهِمْ شُحُومَهُمَا إِلَّا مَا حَمَلَتْ ظُهُورُهُمَا أَوِ الْحَوَايَا أَوْ مَا اخْتَلَطَ بِعَظْمٍ ذَٰلِكَ جَزَيْنَاهُم بِبَغْيِهِمْ وَإِنَّا لَصَادِقُونَ﴾

"Na kwa wale walio mayahudi tuliharamisha kila(mnyama) mwenye kucha, na katika ng’ombe na kondoo tukawaharamishia mafuta yao isipokuwa yale iliyobeba migongo yao au matumbo au ile iliyogandamana na mifupa. Tuliwalipa hivyo kwa uasi wao, "Na hakika sisi ndio wa kweli." (6:146)

Ufafanuzi zaidi utakuja mahali pake

Kwa ujumla ni kuwa Waislamu wameafikiana kwa kauli moja kwamba asili ya kila kitu ni halali mpaka ithibiti kinyume chake.

Sema: Leteni Tawrat muisome mkiwa ni wenyewe kusema kweli.

Hii ni kujadiliana na mayahudi kwamba walete Tawrat ambayo ndiyo wanayoitegemea waisome kadamnasi, wakiwa wanasema kweli katika madai yao ya uharamu wa ngamia au wengineo. Lakini wao baada ya pambano hili waliingia gizani na hawakuwa na ushujaa wa kuileta Tawrat, kwa sababu wao walikuwa wana yakini kabisa na ukweli wa Mtume(s.a.w.w) na uongo wao.

Mwenye kumzulia uongo Mwenyezi Mungu baada ya hayo

Yaani baada ya kudhihiri hoja na kusimama dalili ya haki.

Basi hao ndio madhalimu

Kwa sababu wamepotea na kuwapoteza wengine kwa kuing'ang'ania na kuipinga haki.

Sema: amesema kweli Mwenyezi Mungu.

Kwamba kila chakula kilikuwa halali kwa wana wa Israil na kwamba Muhammad ni Mtume wa haki.

Basi fuateni mila ya Ibrahim aliyeshikamana na haki.

Hapana budi kuashiria kwamba Muhammad(s.a.w.w) alikuwa katika mila ya Ibrahim na mila ya Mitume yote katika itikadi na misingi. Ama katika sharia alikuwa ni tofauti, ingawaje sharia zote zinasimamia masilahi, lakini masilahi yanatofautiana kulingana na hali ya mazingira na mnasaba.

Kuafikiana sharia katika kuhalalisha chakula, hakuwezi kukulazimisha kuwa sharia moja katika pande zote

Vyovyote iwavyo, ni kwamba makusudio ya Aya tulizozifafanua ni kuwakadhibisha mayahudi yale waliyowasingizia Mitume katika kuharamisha baadhi ya vyakula.

﴿ إِنَّ أَوَّلَ بَيْتٍ وُضِعَ لِلنَّاسِ لَلَّذِي بِبَكَّةَ مُبَارَكًا وَهُدًى لِّلْعَالَمِينَ﴾

96.Hakika nyumba ya kwanza waliyowekewa watu ni ile iliyoko Makka yenye kubarikiwa na mwongozo kwa viumbe.

﴿ فِيهِ آيَاتٌ بَيِّنَاتٌ مَّقَامُ إِبْرَاهِيمَ وَمَن دَخَلَهُ كَانَ آمِنًا وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ ﴾

97.Mna humo ishara zilizo wazi: Mahali aliposimama Ibrahim. Na mwenye kuingia humo huwa katika amani; Na ni haki ya Mwenyezi Mungu juu ya watu kuhiji nyumba hiyo kwa mwenye kuweza njia ya kuiendea. Na atakayekufuru, basi Mwenyezi Mungu si muhitaji wa viumbe.

NYUMBA YA KWANZA

Aya 96 -97

LUGHA

Neno 'Awwal' (Mwanzo) ni jina la kitu ambacho kimepatikana kwanza, ni sawa kipatikane kingine baadaye au la. Husemwa 'Ni mara yangu ya kwanza kuja hapa, na hii ndiyo mali yangu ya kwanza kuipata'.

Neno: Bakka lina maana ya Makka mara nyingi herufi 'Ba, huja mahali pa Miim. Na Maana ya neno Bakka ni msongamano: watu huko Makka hupigana vikumbo kwa sababu ya wingi wao.

Arrazi katika Tafsir yake amenakili Riwaya kwamba Imam Baqir(a.s) alikuwa akiswali Al-Kaaba, Mwanamke mmoja alipita mbele yake, Mtu mmoja akataka kumzuwia, Imam akamwambia: Mwache, hapa Makka panaitwa Bakka (msongamano) kwa sababu watu wanasongamana. Mtu anapita mbele ya mwanamke akiwa anaswali na Mwanamke naye anapita mbele ya mwananamume. Hilo halina ubaya kwa hapa.

MAANA

Hakika nyumba ya kwanza waliyowekewa watu ni ile iliyoko Makka.

Yameshatangulia maelezo kwa ufafanuzi zaidi - katika kufasiri Aya ya 142 na zinazofuatilia katika Sura ya Pili (Baqara) - kuhusu waliyosema Mayahudi juu ya kugeuza Qibla kutoka Baytul-Muqaddas na kuwa Al-Kaaba.

Aya hii tuliyonayo inafugamana na Aya hizo za Sura ya (Baqara), hasa kauli ya wapumbavu:

"Nini kilichowageuza kutoka Qibla chao walichokuwa wakikielekea?." (2:142)

Kauli yake Mwenyezi Mungu "Hakika nyumba ya kwanza waliyowekewa watu" haina maana kwamba hiyo ndiyo nyumba ya kwanza duniani, Bali kwa dhahiri ni nyumba ya kwanza ya ibada, Kwa sababu watu wote wanashirikiana ndani yake. Kimsingi ni kwamba watu wote hawashirikiani katika nyumba moja, isipokuwa masuala ya kiujumla; kama vile ibada na twaa.

Baadhi ya wafasiri wamechafua kurasa katika kupekua na kunukuu kauli kuhusu Al-Kaaba, kwamba je, ndiyo nyumba ya kwanza kujengwa duniani au sio. Kwa hakika, hakuna faida yoyote ya utafiti huu, Kwa sababu hayaungani na msingi wa dini au matawi yake, Wala hakutakiwi kuitakidi ndio au hapana.

Yenye kubarikiwa,na mwongozo kwa viumbe.

Makusudio ya baraka hapa ni kuzidishiwa thawabu. Mtume(s.a.w.w) amesema: "Fadhila za Masjidul-haram, juu ya Msikiti wangu ni kama fadhila za msikiti wangu juu ya misikiti mingine." "Swala ya Msikiti wangu huu ni bora kuliko swala elfu za misikiti mwingine." "Mwenye kuhiji na asifanye uchafu au ufasiki, atatakasika kutokana na dhambi zake kama siku aliyozaliwa na mama yake" "Hijja safi haina malipo ila pepo" Na mengineyo mengi.

Ama kwamba ni uongofu kwa viumbe ni kwamba inakumbusha Mwenyezi Mungu na inaleta unyeyekevu.

Mna humo ishara zilizo wazi: Mahali aliposimama Ibrahim.

Ni kama vile muulizaji ameuliza ni ipi dalili ya kwamba Al-Kaaba ni ya zamani, na kwamba ndiyo nyumba ya kwanza ya ibada na wala sio Baitul-Muqadas?

Aya hii inafaa kuwa ni jibu la swali hili, kwa sababu Ibrahim ni wa zamani naye ndiye aliyejenga Al-Kaaba. Kwa hiyo itakuwa ndiyo ya kale iliyotangulia kutokana na ukale wa mjenzi wake. Ama Baitul-Muqadas, ilijengwa na Nabii Suleiman nayo inaitwa mahali pa kuabudia pa Suleiman' mpaka sasa. Na kati ya Suleiman na Ibrahim kulipita karne nyingi. Mwenye tafsir Al-Manar amenukuu kutoka vitabu vya Mayahudi kwamba Suleiman alijenga Baitul-Muqadas miaka 1005 B.C. (Kabla ya kuzaliwa Isa)

Dalili ya kwamba Ibrahim ndiye aliyeijenga Al-Kaaba, ni athari za waziwazi zilizoko mpaka sasa; kama vile Maqam Ibrahim (Mahali aliposimama Ibrahim). Waarabu bado wananukuu kwa njia Mutawatir kutoka vizazi na vizazi kwamba sehemu hii maalum ya Msikiti ni sehemu aliyokuwa akisimama Ibrahim kuswali na kufanya ibada.

Kwa hivyo, kama linavyofahamisha jina la Msikiti wa Suleiman kwamba aliyeijenga Baitul Muqadas ni Suleiman, vile vile jina la Maqam Ibrahim, linafahamisha kuwa yeye ndiye aliyeijenga Al-Kaaba; na kwamba hiyo Al-Kaaba ndiyo iliyotangulia, kwa kuwa Ibrahim ametangulia.

Na mwenye kuingia humo huwa katika amani

Imekwishapita tafsir yake katika (2:125) Na hayo ni fadhila ya dua ya Ibrahim.

Na ni haki ya Mwenyezi Mungu juu ya watu kuhiji nyumba hiyo kwa mwenye kuweza njia ya kuiendea.

Uwezo uko namna mbili: Kiakili, ambao ni uwezekano wa kufika Makka, Hilo sio sharti. Na wa Kisheria, ambao ni uwezo wa kiafya, usalama wa nafsi, mali na uwezekano. Hayo yakikamilika, Hijja inakuwa ni lazima, Ufafanuzi uko katika vitabu vya Fiqhi.

Na atakayekufuru, basi Mwenyezi Mungu si muhitaji wa viumbe.

Makusudio ya neno 'Kufru' hapa ni kukanusha kama tukilirudisha kwenye Al- Kaaba kwamba ndiyo nyumba ya kwanza ya ibada, au kwenye kutoitakidi wajibu wa Hijja. Na yatakuwa makusudio yake ni ufasiki kama tukilirudisha kwenye kuacha Hijja kwa kupuuza.

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لِمَ تَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَاللَّـهُ شَهِيدٌ عَلَىٰ مَا تَعْمَلُونَ﴾

98.Sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnazikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na hali Mwenyezi Mungu ni shahidi juu ya muyatendayo!

﴿قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لِمَ تَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ مَنْ آمَنَ تَبْغُونَهَا عِوَجًا وَأَنتُمْ شُهَدَاءُ وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴾

99.Sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnawazuilia njia ya Mwenyezi Mungu walioamini ? Mkaitafutia kosa na nyinyi mnashuhudia. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na muyatendayo

KUKANUSHA DALILI NA ISHARA ZA MWENYEZI MUNGU

Aya 98 -99

MAANA

Qur'an imejishughulisha sana na watu wa Kitabu, ikawateremeshia Aya kadha wa kadha zinazowakumbusha Tawrat na Injil na kuwaaibisha, kwa sababu ya kuzigeuza; ikawajadili kwa namna nzuri na kuwaelezea makosa yao mengi na dhambi zao. Miongoni mwa Aya hizo, ni Aya hizi mbili:

Ya kwanza ni : "Sema:Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnazikanusha ishara za Mwenyezi Mungu ambazo zimefahamisha Utume wa Muhammad(s.a.w.w) ; na kwamba Al-Kaaba ndiyo nyumba ya kwanza kuwekewa watu kwa ibada, pamoja na kuwa ishara hizo na hoja hizo ziko wazi kama jua, na hawezi kuzikanusha isipokuwa mwenye kiburi"

Ya pili ni "sema: Enyi watu wa Kitabu! Kwa nini mnawazuilia njia ya Mwenyezi Mungu walioamini Mkaitafutia kosa?." Hawakutosheka na kufanya ufisadi hao wenyewe, mpaka wakajishughulisha kuwaharibu wengine na kuwapoteza. Kwa hiyo wamechanganya upotevu na kupoteza, na ufisadi na kuwafanya wengine wawe wafisadi. Kila mfisadi anatamani na kufanya kadiri ya uwezo wake ili kuwe na mafisadi wengi kwa kutumia misingi ya Iblis aliposema:

﴿قَالَ رَبِّ بِمَا أَغْوَيْتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمْ فِي الْأَرْضِ وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ ﴾

"Kwa kunihukumu kupotea, basi nitawapambia katika ardhi na nitawapoteza wote" (15:39)

Tusisahau ishara ya aina hii ya upole wa kuwaambia watu wa Kitabu, na kuwakumbusha vizuri kuwa wao ni watu wa dini na Kitabu, ili angalau waweze kusikia mawaidha na kuongoka.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن تُطِيعُوا فَرِيقًا مِّنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ يَرُدُّوكُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ كَافِرِينَ﴾

100.Enyi mlioamini! Mtakapotii kikundi katika watu wa Kitabu watawarudisha kuwa makafiri baada ya kuamini kwenu.

﴿وَكَيْفَ تَكْفُرُونَ وَأَنتُمْ تُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ آيَاتُ اللَّـهِ وَفِيكُمْ رَسُولُهُ وَمَن يَعْتَصِم بِاللَّـهِ فَقَدْ هُدِيَ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴾

101.Na vipi mnakufuru na nyinyi mnasomewa Aya za Mwenyezi Mungu na Mtume wake mnaye? Na mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu basi ameongozwa katika njia iliyonyooka.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ ﴾

102.Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu ipasavyo kumcha; wala msife isipokuwa mmekuwa waislamu.

﴿وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا وَاذْكُرُوا نِعْمَتَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ إِذْ كُنتُمْ أَعْدَاءً فَأَلَّفَ بَيْنَ قُلُوبِكُمْ فَأَصْبَحْتُم بِنِعْمَتِهِ إِخْوَانًا وَكُنتُمْ عَلَىٰ شَفَا حُفْرَةٍ مِّنَ النَّارِ فَأَنقَذَكُم مِّنْهَا كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ﴾

103.Na Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarikiane; na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu mlipokuwa maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; hivyo kwa neema yake mkawa ndugu; na mlikuwa ukingoni mwa shina la moto naye akawaokoa nalo. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyozibainisha Aya Zake ili mpate kuongoka.

KUWATII MAKAFIRI

Aya 100 - 103

MAANA

Enyi mlioamini! Mtakapotii kikundi katika watu wa Kitabu, watawarudisha kuwa makafiri baada ya kuamini kwenu.

Katika Aya mbili zilizotangulia, Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewahadharisha watu wa Kitabu kuipinga haki pamoja na kuwazuia waumini na njia Yake Mwenyezi Mungu. Katika Aya hii, Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawahadharisha waumini wasiwasikilize makafiri katika watu wa Kitabu wanaojaribu kuwapoteza waumini na kuwafitini na dini yao. Imepokewa Riwaya kwamba, sababu za kushuka Aya hii ni kuwa baadhi ya mayahudi walikusudia kuirudisha tena fitna iliyokuwepo baina ya kabila la Ansar na Khazraj wasiwe na umoja baada ya Mwenyezi Mungu kuwaweka pamoja kwenye Uislamu. Kwa hiyo, makafiri wakawa wanawakumbusha uadui na mapigano waliyokuwa nayo wakati wa ujahiliya. Hasa siku ya vita ya Bughat ambayo Aus na Khazraj waliuana, na ushindi ukawa wa Aus. Mori ukawapanda wakawa karibu wapigane kama si kuwahi Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Aya inafungamana na tukio hili, kama ambavyo inafungamana na jaribio la wahubiri wa Kikristo wakati huu; na majaribio yote ambayo baadhi ya watu wa Kitabu na wengineo katika kutawanya umoja wa waislamu na kuwaepusha na dini yao, uzalendo wao, na uhuru wao na kuwa windo la kila mnyang'anyi.

Haya ndiyo wayafanyao wakoloni wa Kimagharibi kwa waarabu. Na kazi hiyo hawaifanyi peke yao, bali wanashirikiana na vibaraka duni ambao wanawatii na kuwafuata; na waliokufuru dini yao baada ya kuamini na kuiuza nchi yao. Kwa hivyo basi, Aya inafungamana na vibaraka hawa na pia inafungamana na wanaohubiri fitina na ufisadi na wakapendelea ukafiri na upotevu. Ni sawa wawe ni katika watu wa Kitabu au wengineo; wa Mashariki na Magharibi. Vile vile, Aya hii inafungamana na wanawake wetu wanavyoiga wanawake wa kimagharibi katika kujiremba na kujipodoa, na vijana wetu katika kudharau dini na mwendo wa dini. Vile vile desturi zote za madhara na haramu tulizoziiga kutoka kwa wageni. Aya kwa dhahiri inakataza kuwatii makafiri katika kufuru na kurtadi. Lakini, linalosababisha hilo linaenea katika kila uigaji unaomkasirisha Mwenyezi Mungu na Mtume.

Na vipi mnakufuru na nyinyi mnaosomewa Aya za Mwenyezi Mungu na Mtume Wake mnaye?

Yaani, haitakikani kwa Mwislamu kuathirika na kuwa katika upotevu wa wapotezaji, na kuwafuata makafiri katika desturi zao na hulka zao wakati ambapo yeye mwislamu anasoma Qur'an Tukufu na kumsikiliza Mtume Mtukufu, anayembainishia haki na kumuondolea kila shubha. Anasema Nidhamuddin Al-Hasan Muhammad Annaisaburi katika Tafsir, Gharaibul- Qur'an: "Ama Kitabu kitabaki milele. Na Mtume(s.a.w.w) ingawaje amekwenda kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu, lakini nuru yake imebaki, Kwa sababu, kizazi na warithi wake wanakaimu nafasi yake. Kwa sababu hii ndipo Mtume akasema:"Mimi ninawaachia vizito viwili ambavyo kama mkishikamana navyo hamtapotea: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu"

Na mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu, basi ameongozwa katika njia iliyonyooka.

Kushikamana na Mwenyezi Mungu ni kushikamana na dini; dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni uislamu, nayo ndiyo hasa njia iliyonyooka. Makusudio ni kuwa mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu kwa haki kabisa, hawezi wala hataweza kuuwacha uislamu kwa namna yoyote ya majaribio na hadaa zitakavyokuwa.

Unaweza kuuliza : Imekuja Aya isemayo:

"Hakika Mola wangu yuko juu ya njia iliyonyooka" (11:56)

Na wewe unafasiri kuwa njia iliyonyooka ni uislamu, Kwa hiyo itakuwa Mwenyezi Mungu yuko kwenye dini ya kiislamu.

Jibu : Hakika njia iliyoonyooka ikinasibishwa kwa mja, inakusudiwa uislamu. Ama ikinasibishwa kwa Mwenyezi Mungu inakusudiwa uadilifu na hekima; yaani yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu anapanga mambo kwa uadilifu na hekima Yake.

Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu ipasavyo kumcha; wala msife isipokuwa mmekuwa waislamu

Kila mwenye kufanya ya wajibu na kujiepusha na mambo ya haramu, basi ndio amemcha Mwenyezi Mungu ipasavyo kumcha. Haya ndiyo maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

"Mcheni Mwenyezi Mungu muwezavyo" (64:16)

Kwa sababu, lisilowezekana halikalifiwi na sharia, Na kila lisilowezekana kukalifiwa, basi liko nje ya kumcha Mwenyezi Mungu. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu "Msife isipokuwa mmekuwa waislamu;" ni kukataza kuacha uislamu na kuamrisha kuwa imara nao mpaka siku ya kifo.

Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarikiane.

Kamba ni maarufu; na makusudio yake hapa ni uislamu. Maana ya Aya nzima, ni kuwa maadam waislamu ni wafuasi wa dini moja, Mtume mmoja na Kitabu kimoja, basi ni juu yao wote kuuchunga mfungamano huu wa kidini ambao ndio wenye nguvu zaidi kuliko mfungamano wa nasaba, na kuwa na hima nao; wala wasigawanyike vikundi.

Unaweza kuuliza : Je, mwito huu wa muungano wa kidini si aina ya ubaguzi wa dini?

Jibu : Hapana, mwito huu wa mshikamano wa wafuasi wa dini moja ni sawa na mwito wa mshikamano wa wanachama wa chama kimoja, au wa wafamilia moja, Mshikamano huu haulazimishi kuwabagua wengine. Bali ni kinyume na hivyo katika uislamuu, ambapo unatoa mwito wa kuwapenda na kuwahurumia watu wengine bila ya kuangalia dini zao, fikra zao au kabila zao. Kwa hivyo basi undugu wa Kiislamu ni nguzo ya udugu wa kibinadamu.

Kwa ujumla ni kwamba kundi ambalo ni wajibu kusaidiana nalo, ni lile lililojikusanya na kusaidiana katika jambo lililo na radhi ya Mwenyezi Mungu na masilahi ya watu. Ama kukutana kusikokuwa na faida yoyote ya kuridhisha hakutakikani. Imam Ali(a.s) anasema:"Utengano ni kwa watu wa batili hata wakiwa wengi, Na kuungana ni kwa watu wa haki hata wakiwa wachahe." Na hiyo ndiyo tafsir ya Hadith mashuhuri:"Msaada wa Mwenyezi Mungu uko pamoja na wengi." Yaani kuwahusu wanaojumuika na kusaidiana kwa jambo la haki. Ama ikiwa ni kwa jambo la batili; basi hawatakuwa na yeyote zaidi ya shetani.

Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu mlipokuwa maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; hivyo kwa neema yake mkawa ndugu.

Mwenyezi Mungu anawakumbusha waislamu wa kwanza vile walivyokuwa na misukusuko ya vita, bughudha na vita vya kuendelea, kama vile vita vya Aus na Khazraj vilivyodumu kwa muda wa miaka mia moja na ishirini, kama ilivyoelezwa kwenye Tafsir Tabari. Basi Mwenyezi Mungu akaziunganisha nyoyo zao kwa baraka ya uislamu mpaka wakawa ni ndugu wanaohurumiana na kunasihiana. Jafar bin Abu Talib katika mazungumzo yake na Najjash alimwambia: "Tulikuwa watu wa ujahilia (ujinga) tukiabudu masanamu, tukila mizoga, tukifanya maovu, kuvunja undugu, kumfanyia uovu jirani na mwenye nguvu akimuonea mnyonge. Tulikuwa hivyo mpaka Mwenyezi Mungu akatuletea Mtume atokanaye na sisi; tunayemjua nasaba yake, ukweli wake, uaminifu na usafi wake.

Akatulingania kwa Mwenyezi Mungu ili tumwabudu yeye peke yake na tuachane na kuabudu wasiokuwa Yeye - mawe na masanamu. Akatuamrisha kusema kweli, kutekeleza amana, kuunga undugu, kumfanyia wema jirani na kujizuia na haki za watu na damu (zao). Akatukataza kufanya maovu, kusema uongo, uzushi, kula mali ya yatima na kuwavunjia heshima wanawake wanaojistahi. Akatuamrisha tumwabudu Mwenyezi Mungu na kutomshirikisha na chochote. Pia akatuamrisha kuswali, kutoa Zaka na kufunga"

Na mlikuwa ukingoni mwa shimo la moto naye akawaokoa nalo

Yaani mlikuwa karibu na moto wa Jahannam, kwa ukafiri wenu, Mwenyezi Mungu akawaokoa nao kwa baraka ya Muhammad(s.a.w.w) .

﴿وَلْتَكُن مِّنكُمْ أُمَّةٌ يَدْعُونَ إِلَى الْخَيْرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ﴾

104.Na liwepo miongoni mwenu kundi lenye kulingania kwenye heri, na kuamrisha mema na kukataza maovu. Na hao ndio wenye kufaulu

KUAMRISHA MEMA

Aya 104

Makusuido ya heri hapa ni uislamu, na mema ni kumtii Mwenyezi Mungu, na maovu ni kumwasi. Maana yanayopatikana ni kwamba hapana budi kupatikane kundi la watu litakalowalingania wasiokuwa waislamu kwenye uislamu; kwenye lile linalomridhisha Mwenyezi Mungu, analolilipa thawabu na kuacha lile linalomkasirisha analoliletea adhabu. Tamko kutokana na nyinyi katika Aya hii inafahamisha wajibu wa kuamrisha mema kwa njia ya kutosheana (kifaya). Yaani, wakilisimamia hilo baadhi, utakuwa wajibu umewaondokea wengine, Wala si lazima kuwa mwenye kutekeleza umuhimu huu, awe mwadilifu. Hapana, si hivyo, kwa sababu mbili:

Kwanza : kwamba sharti ya hukumu ni sawa na hukumu yenyewe, haithibiti ila kwa dalili wala hakuna dalili ya sharti ya uadilifu hapa; si kutoka katika Qur'an, Hadith au kutoka katika akili.

Pili : hukumu ya kuamrisha mema haitegemei maasi au utiifu wa mwengine katika hukumu. Mafakihi wengi wameshartisha wajibu wa kuamrisha mema kuwa mwenye kuamrisha awe atakuwa salama, kiasi ambacho hatapata madhara yoyote kwa kuamrisha mema na kukataza maovu. Lakini sharti hili haliingi sehemu zote, kwani, kupigana na anayetupiga kwa ajili ya dini yetu na nchi yetu ni wajibu, ingawaje tunafahamu kwamba, kwa kawaida kupigana huleta madhara.

Inafaa kwa kila mtu kuyatoa mhanga maisha yake, akiwa na yakini kwamba kujitoa mhanga huku kuna maslahi ya umma. Faida ya watu na nchi ni muhimu na adhimu zaidi kuliko maisha yake, bali hilo linashukuriwa mbele ya Mwenyezi Mungu na kwa watu. Kuna Hadith isemayo:"Jihadi bora zaidi ni tamko la haki mbele za Sultan dhalimu."

Kwa ufupi ni wajibu kukinga madhara yakiwa hayatakuwa na faida yoyote. Vyenginevyo, itajuzu kuyavumilia; kama inavyojuzu kwa mtu kukata kiungo kibovu katika viungo vyake kwa kupigania uhai wake na kuhofia kumalizika. Zaidi ya hayo, mifumo inaathari zake, Baadhi ya mifumo inaifukuza haki na kumsababishia mtu matatizo. Na mingine inalazimisha fikra kwa msikilizaji bila ya kujitambua. Mwenye akili na hekima anafanya kulingana na hali ilivyo ya taratibu au ya nguvu.

Firaun alikuwa na ukomo wa Usultani na kupetuka mipaka; Musa na Harun hawakuwa hata na msaidizi, lakini pamoja na hayo waliamrishwa kumlingania kwenye haki. Lakini kwa njia ya upole. Hata Muumba wa ulimwengu, (ambaye limetukuka neno lake) mara nyingine amewaambia waja wake kwa vitisho na kusema:

"Hakika nyinyi hamtanusuriwa nasi" (23:65) Mara nyingine hutumia upole na kusema:

﴿أَلَا تُحِبُّونَ أَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَكُمْ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

"Je, hampendi Mwenyezi Mungu awasamehe na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe Mwenye kurehemu." (24:22)

Kwa ujumla kutangaza mwito wa uislamu kwa watu, na waislamu kuamrishana mema na kukatazana mabaya, ni katika nguzo za uislamu. Kwa hiyo kunawajibisha kuwapo kwa kikundi kitakachosimamia umuhimu huu, sawa na kulazimika kuwapo uongozi utakaosimamia amani na nidhamu, wafanya kazi wa viwandani, wakulima na wengineo ambao wanachangia maisha.

Huu ni msingi wa kila dini, kila dhehebu na kila fikra. Kwa sababu, hiyo ndiyo njia nzuri ya kueneza mwito, kupata ushindi na kuwazuia maadui. Angalia jinsi watu wa siasa na uchumi wanavyotilia umuhimu vyombo vya habari, kuvikuza na kuvitolea mamilioni ya mapesa na kufanya mizinga na habari kuwa bega kwa bega. Hawakufanya hivyo ila ni kwamba wametambua, kutokana na uzowefu wao, kwamba habari ni silaha yenye nguvu kuliko mizinga na mabomu. Mmoja wa wakuu wa mapatano alisema baada ya kufaulu kwao katika vita vya ulimwengu: "Tumeshinda katika vita kwa mabomu ya karatasi." Yaani magazeti.

Unaweza kuuliza : kwamba unawezaje kuziunganisha Aya hizi mbili: "Na wawepo katika nyinyi watu wanaolingania kwenye heri na wanaoamrisha mema na kukataza maovu." Na Aya isemayo:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ﴾

"Enyi mlioamini! Jiangalieni nafsi zenu hatawadhuru aliyepotea ikiwa mmeongoka" (5:105)

Ambapo ya kwanza imefahamisha wajibu wa kuamrisha mema na ya pili imefahamisha kutokuwepo wajibu huo kutokana na neno "Jiangalieni nafsi zenu."

Jibu : Makusudio ya Aya ya pili, ni kwamba mwenye kutekeleza wajibu wa kuamrisha mema na kukataza mabaya, hatadhuriwa na upotevu wa aliyepotea wala upinzani wa mpinzani, maadamu yeye anaetekeleza wajibu wake tu,

"Hakika ni juu yako kufikisha tu, na juu yetu ni kuhisabu" (13:40)

Swali la pili : kuna Hadith mashuhuri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) isemayo: "Mwenye kuona katika nyinyi uovu, na auondoe kwa mkono wake, akishindwa, basi (auondoa) kwa ulimi wake, akishindwa basi ni kwa moyo wake na hilo ni katika udhaifu zaidi wa imani." Mpangilio huu unapingana na ilivyo desturi ya sharia, kiakili na kimazoweya; kwamba kuondoa uovu kunaanzia kwa ulimi halafu ndio vita. Sasa kuna wajihi gani wa kauli hii ya Mtume?

Jibu : Kuna tofauti kubwa sana baina ya kuondoa uovu na kukataza uovu, kwani kukataza uovu aghlabu ni kabla ya kutokea uovu wenyewe; ni kama vile kukinga, kama kuona kuwa mtu fulani anafikiria kuiba, ukamkataza kufanya wizi huo, Ama kuondoa uovu, kunakuwa baada ya kutokea uovu wenyewe. Kwa mfano umejua kuwa mtu fulani ameiba mfuko wa mtu mwengine, hapo ukiwa unaweza kumnyang'anya na kumrudushia mwenyewe, basi ni wajibu kwako kulifanya hilo wewe mwenyewe, ikiwa kuna uwezekano wa kumyang'anya mwizi; na wewe usiweze kupata madhara. Kama hukuweza ni wajibu kwako kumwamrisha mwizi aurudishe kwa mwenyewe na kumkataza kuuzuwia. Kama utashindwa na vishindo vya mwizi, basi usikiridhie kitendo chake - baina yako na Mola wako. Kwa hivyo maudhui ya Hadith ni kugeuza uovu, si kukataza uovu([1] ) .

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Sura Ya Ishirini Na Nane: Surat Al-Qasas. Tabrasi amesema imeshuka Makka. Ina Aya 88.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

طسم ﴿١﴾

1. Twaa Siin Miim.

تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ ﴿٢﴾

2. Hiyo ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

نَتْلُو عَلَيْكَ مِن نَّبَإِ مُوسَىٰ وَفِرْعَوْنَ بِالْحَقِّ لِقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿٣﴾

3. Tunakuosomea habari za Musa na Firauni kwa haki kwa ajili ya watu wanaoamini.

إِنَّ فِرْعَوْنَ عَلَا فِي الْأَرْضِ وَجَعَلَ أَهْلَهَا شِيَعًا يَسْتَضْعِفُ طَائِفَةً مِّنْهُمْ يُذَبِّحُ أَبْنَاءَهُمْ وَيَسْتَحْيِي نِسَاءَهُمْ إِنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُفْسِدِينَ ﴿٤﴾

4. Hakika Firauni alitakabari katika nchi akagawa watu wake makundi. Akidhoofisha taifa moja miongoni mwao, akiwachinja watoto wao wa kiume na akiwaacha watoto wao wa kike. Hakika yeye alikuwa katika wafisadi.

وَنُرِيدُ أَن نَّمُنَّ عَلَى الَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا فِي الْأَرْضِ وَنَجْعَلَهُمْ أَئِمَّةً وَنَجْعَلَهُمُ الْوَارِثِينَ ﴿٥﴾

5. Na tunataka kuwafadhili waliodhoofishwa katika ardhi na kuwafanya wawe ni viongozi na kuwafanya ni warithi.

وَنُمَكِّنَ لَهُمْ فِي الْأَرْضِ وَنُرِيَ فِرْعَوْنَ وَهَامَانَ وَجُنُودَهُمَا مِنْهُم مَّا كَانُوا يَحْذَرُونَ ﴿٦﴾

6. Na kuwamakinisha katika ardhi. Na kumuonyesha Firauni na Hamana na majeshi yao yale waliyokuwa wakiyahadhari kwao.

AYA ZA KITABU

Aya 1 – 6

TWAA SIIN MIIM.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1)

Hiyo ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

Hiyo ni ishara ya Sura hii, Kitabu ni Qur’an na kubainisha ni kupambanua baina ya upotevu na uongofu.

Tunakuosomea habari za Musa na Firauni kwa ajili ya watu wanaoamini.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsomea Mtume wake mtukufu habari mara kwa mara. Katika Juz. 16 kifungu cha ‘Kukaririka Kisa’ (20:9) tumeeleza lengo la kukaririka kisa cha Musa.

Hakika Firauni alitakabari katika nchi akagawa watu wake makundi.

Alipetuka mipaka na akajifanya jabari, akawagawa wananchi wake kwenye makundi wakigombana, ili udumu utawala wake.

Akidhoofisha taifa moja miongoni mwao, akiwachinja watoto wao wa kiume na akiwaacha watoto wao wa kike. Hakika yeye alikuwa katika wafisadi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:49) na Juz. 9 (7:127).

KWA NINI FIRAUNI ALIWAKANDAMIZA WANA WA ISRAIL?

Mmoja katika wafasiri wa kisasa anasema: “Firauni aliwakandamiza wana wa Israil kwa sababu walikuwa na itikadi isiyoafikiana na itikadi yake. Wao walikuwa wakifuata dini ya babu yao Ibrahim na Ya’qub. Ingawa itikadi yao ilikuwa na upotofu, lakini walibakia na itikadi ya Mungu mmoja.”

Sisi tunamuuliza mfasiri huyu mpya: Umejua vipi kuwa mayahudi waliokuwa wakati wa Firauni walikuwa kwenye dini ya Ibrahim(a.s) na kwamba walibaki na itikadi ya Mungu mmoja? Je, umepata kujua kutokana na kuli yao: “Ewe Musa! Hebu nasi tufanyie waungu kama hawa walivyo na waungu.” Au kauli yao: “Hatutakuamini mpakae tumwone Mungu wazi wazi.”

Au ni kutokana na kuabudu kwao ndama au kwa kuwaua kwao mitume? Ikiwa Firauni aliwakandamiza kwa sababu ya itikadi yao, kwa nini Mtume wao na mwenye ikhlasi zaidi, Musa aliwapa wasifa huu ufuatao? Ufuska, Juz. 6 (5:25), wapumbavu, Juz. 9 (7:155), wabatilifu Juz. 9 (7:153) na ujinga Juz. 9 (7:138). Kama amabavyo Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya kadhaa amewasifu kwa ufisadi, uovu na kwa kila aina ya hatia?

Qur’an imetaja kwamba Firauni aliwakandamiza wana wa isaril na kwam- ba yeye alipituka mpaka katika dhulma yake, lakini haikuashiria sababu.

Kwa hiyo maulama wametofautiana katika kuielezea. Kuna waliosema kuwa kuhani alimwambia Firauni kuwa atazaliwa mtoto katika wana waisrail, atakayekuja mvua ufalme wake, wengine wakasema kuwa mitume waliokuwa kabla yake walitoa bishara ya kuja kwake.Firauni alipojua hivyo akahofia na kuanza kuwachinja watoto wa kiume wa wana wa israil. Na sikuona yoyote aliyesema kuwa Firauni aliwakandamiza kwa sababu ya kuwa kwenye dini ya Ibrahim.

Tukiangalia sera ya wana wa israil kwa Mtume wao Musa(a.s) na mitume wengine waliokuja baada ya Musa; ambapo walikuwa wakikadhibisha wengine na wengine wakiwaua. Pia tukiangalia sera yao katika miji wanayoiteka jinsi wanavyoleta fitna, kupanga njama, kujaribu kutawala nyenzo na propaganda zote.

Tukiangalia yote haya basi tunakubaliana na Sheikh Maraghi aliyesema: “Firauni aliwakandamiza wana wa israil kwa vile aliwahofia wanaume ambao walikuwa na ufundi na mikononi mwao mlikuwa na hatamu za uchumi; kuwa muda ukiendelea watakuwa juu kiuchumi waje wawashinde wamisri. Na uchumi ndio wenye nguvu kiutawala.”

Ni kweli kuwa Firauni alipetuka mpaka katika dhulma kwa kuwachinja watoto wa kiume na kuwafanya watumwa watoto wa kike wa wana wa israil, lakini sababu ya yote haya ni wayahudi.

Kwa hiyo lawama ni la wote wawili. Mayahudi kwa sababu ya chuki yao, tabia yao na malengo yao mabaya na pia kwa Firauni kwa sababu aliwatesa wasiokuwa na hatia kwa sababu ya wenye hatia.

LINI MWENYEZI MUNGU ATAWAFADHILI WALIODHOOFISHWA?

Na tunataka kuwafadhili waliodhoofishwa katika ardhi.

Waliodhoofishwa katika ardhi ni wale waliokandamizwa na wenye nguvu, waliotawala nyenzo zao na nguvu zao kimabavu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawafadhili uhuru na kujikomboa kwenye ukandamizaji ikiwa watafanya juhudi na kujitolea kwa ajili ya maisha yao na heshima yao; sawa na mgonjwa atapona ikiwa atafanya matibabu mazuri na mkulima atapata mavuno akilima vizuri.

Mwenyezi Mungu ana desturi katika maumbile yake, na wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu kabisa. Kila mwenye kufuata njia atafika, awe mumin au kafiri. Ama malipo ya kafiri na mumin ni siku ya Kiyama, si katika maisha haya.

Basi atakayemnyenyekea dhalimu, Mwenyezi Mungu humdhalilisha na humwachia atakayemdhulumu, hata kama ataswali, kufunga na kuhiji. Kwa sababu ameidhalilisha haki na akisaidia batili na akhera hana kitu.

Na mwenye kujikomboa kutoka kwa dhalimu na watu wake, na akajitolea mhanga kwa ajili ya heshima yake, Mungu humpa nusra kuwashinda mad- halimu na wababe; kwa sababu atakuwa amekutana na utashi wa Mwenyezi Mungu na amri yake, kwa jihadi na uimara.

Hatuna haja ya kurudia historia ya mbali kutafuta ushahidi wa hakika hii. Kwani ukakamavu wa wananchi wa Vietnam mbele ya taifa hilo na nguvu kubwa ya shari na ufisadi, ni dalili kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja na mwenye kudhulumiwa anayepigana jihadi aliye mvumilivu, kwa namna yoyote ile atakayokuwa.

Kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu hapigani kwa ajili ya waliodhoofishwa, lakini anakuwa nao na kuwapa msaada wake, ikiwa watapigana na kupinga kwa lengo la haki, uadilifu na kujikomboa kutoka kwenye makucha ya ukoloni na dhulma. Mwenyezi Mungu yuko pamoja na hawa, kwa sababu, yuko pamoja na kila mwenye kufanya juhudi na akatenda kwa ajili ya maisha.

Haya tumeyafafanua zaidi katika Juz. 13 (13:11).

Unaweza kuuliza : Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimwangamiza Firauni na watu wake, akawaokoa wana wa israil na adhabu yao na ukandamizwaji wao. Hii inamaanisha kuwa Mwenyezi Mungu anapigana kwa ajili ya wanyonge; bali kuna Aya isemayo:

إِنَّ اللَّـهَ يُدَافِعُ عَنِ الَّذِينَ آمَنُوا ﴿٣٨﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu huwakinga walioamini.” Juz. 17 (22:38)?

Jibu : Mwenyezi Mungu Mtukufu alimwangamiza Firauni na watu wake kwa sababu ya shirki yao na kuwakadhibisha kwao mitume na sio kuwasaidia wana wa israili; sawa na alivyoangamiza kaumu ya Nuh na washirikina wengineo.

Kwa hiyo wana wa israil na wengineo wakapona na dhulma na ukandamizwaji. Ama makusudio ya walioamini, wanaokingwa na Mwenyezi Mungu ni wale wanopigana jihadi. Na wavivu wako kwenye dini ya wale waliomwambia Musa:

فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ ﴿٢٤﴾

“Nenda wewe na Mola wako mkapigane, hakika sisi ni wenye kukaa hapa.” Juz. 6 (5:24)

Na kuwafanya wawe ni viongozi.

Yaani tuwafanye mitume miongoni mwao.

Na kuwafanya ni warithi na kuwamakinisha katika ardhi.

Mwenyezi Mungu anawafanya huru kwa muda mrefu baada ya kuwa utumwani.

Na kumuonyesha Firauni na Hamana na majeshi yao yale waliyokuwa wakiyahadhari kwao.

Kwao ni kwa hao wana wa israil. Maana ni kuwa Firauni na watu wake walihofia utawala wao usiingie mikononi mwa wana wa israil, ndio wakachukua hadhari, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawaingiza kwenye yale waliyoyahofia.

وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ أُمِّ مُوسَىٰ أَنْ أَرْضِعِيهِ فَإِذَا خِفْتِ عَلَيْهِ فَأَلْقِيهِ فِي الْيَمِّ وَلَا تَخَافِي وَلَا تَحْزَنِي إِنَّا رَادُّوهُ إِلَيْكِ وَجَاعِلُوهُ مِنَ الْمُرْسَلِينَ ﴿٧﴾

7. Na tulimpa wahyi mama wa Musa kuwa mnyonyeshe. Na utakapomhofia basi mtie mtoni. Na usihofu wala usihuzunike. Hakika sisi tutamrudisha kwako na tutamfanya miongoni mwa mitume.

فَالْتَقَطَهُ آلُ فِرْعَوْنَ لِيَكُونَ لَهُمْ عَدُوًّا وَحَزَنًا إِنَّ فِرْعَوْنَ وَهَامَانَ وَجُنُودَهُمَا كَانُوا خَاطِئِينَ ﴿٨﴾

8. Basi wakamwokota watu wa Firauni aje kuwa adui kwao na huzuni. Hakika Firauni na Hamana na majeshi yao walikuwa wenye makosa.

وَقَالَتِ امْرَأَتُ فِرْعَوْنَ قُرَّتُ عَيْنٍ لِّي وَلَكَ لَا تَقْتُلُوهُ عَسَىٰ أَن يَنفَعَنَا أَوْ نَتَّخِذَهُ وَلَدًا وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿٩﴾

9. Akasema mke wa Firaun: Ni kiburudisho cha macho kwangu na kwako. Msimuuwe! Huenda akatufaa au tumfanye kuwa mtoto wetu. Wala wao hawakutambua

وَأَصْبَحَ فُؤَادُ أُمِّ مُوسَىٰ فَارِغًا إِن كَادَتْ لَتُبْدِي بِهِ لَوْلَا أَن رَّبَطْنَا عَلَىٰ قَلْبِهَا لِتَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١٠﴾

10. Moyo wa mamake Musa ukawa mtupu. Alikuwa karibu kudhihirisha, lau tusingeliuimarisha moyo wake ili awe miongoni mwa waumini.

وَقَالَتْ لِأُخْتِهِ قُصِّيهِ فَبَصُرَتْ بِهِ عَن جُنُبٍ وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿١١﴾

11. Akamwambia dadake (Musa) mfuatie. Basi akawa anamwangalia kiupande upande na wao hawatambui.

وَحَرَّمْنَا عَلَيْهِ الْمَرَاضِعَ مِن قَبْلُ فَقَالَتْ هَلْ أَدُلُّكُمْ عَلَىٰ أَهْلِ بَيْتٍ يَكْفُلُونَهُ لَكُمْ وَهُمْ لَهُ نَاصِحُونَ ﴿١٢﴾

12. Na tukamharamishia wanyonyeshaji tangu mwanzo. Akasema (dadake): Je, niwaonyeshe watu wa nyumba watakaowalelea na watakuwa wema kwake?

فَرَدَدْنَاهُ إِلَىٰ أُمِّهِ كَيْ تَقَرَّ عَيْنُهَا وَلَا تَحْزَنَ وَلِتَعْلَمَ أَنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿١٣﴾

13. Basi tukamrudisha kwa mama yake ili yaburudike macho yake na ajue kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Lakini watu wengi hawajui.

MAMA WA MUSA

Aya 7 – 13

MAANA

Na tulimpa wahyi mama wa Musa kuwa mnyonyeshe.

Makusudio ya wahyi hapa ni ilhamu; ni mfano kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na Mola wako akampa wahyi nyuki.” Juz. 14 (16:68). Katika Juz. 9 (7: 103 -112).

Tumenukuu kutoka kitabu Qisasul-qur’an, kwamba jina la mama yake Musa ni Yukabid (Jochebed). Kisha tukasoma katika Tawrat kuwa hilo ndilo jina lake na kwamba aliolewa na Amram, mtoto wa kaka yake. Musa ndiye mdogo katika watoto wa baba yake, akiwa ni watatu, baada ya Maryam na Harun.

Na utakapomhofia basi mtie mtoni.

Makusudio ya mto hapa ni mto Nile. Maana ni akimhofia kuchinjwa amtie mtoni kwa mkono wake! Itakuwaje, mwenye akili aweze kujitupa motoni?

Lakini akaambiwa: Na usihofu wala usihuzunike. Hakika sisi tutamrudisha kwako na tutamfanya miongoni mwa mitume.

Usimhofie, hakika Mwenyezi Mungu ndiye mhifadhi na mlinzi. Yule ambaye ameujaalia moto kuwa baridi na salama kwa Ibrahim, ataijalia bahari kuwa amani kwa Musa. Alimpa habari ya usalama wa mtoto wake na kwamba yeye atamlea na pia akampa habari njema kuwa amemchagua kwa risala yake na kumhusu kwa rehema yake. Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:38).

Basi wakamwokota watu wa Firauni aje kuwa adui kwao na huzuni.

Walimwokota na kumlea kwa kumfanya mtoto wao, lakini akaja akawa ni adui wa itikadi yao na desturi yao. Akaingiza huzuni nyoyoni mwao na mwisho wa ufalme wao ukawa mikononi mwake.

Hakika Firauni na Hamana na majeshi yao walikuwa wenye makosa, wapotevu katika vitendo vyao vyote; hasa kuua maelefu ya vijana ili kujiepusha na Musa, lakini ikawa wao wanamwepusha Musa na mauti ili aje awamalize. Katika kamusi ya Kitabu kitakatifu[4] , imeelezwa kuwa maisha ya Musa katika nyumba ya Firauni hayakujulikana kwa ufafanuzi na kwamba wanahistoria wametofautiana kuhusu wakati wake alioishi. Wengine wakasema ni wakati wa Firauni Amenophis (Amenhotep II) (1411 – 1436 Bc), wengine wakasema ni Ramesses II (1223 – 1290 Bc). Pia kuna waliosema ni wakati wa Mernptsh ( 1211 – 1223 Bc).

Akasema mke wa Firaun: Ni kiburudisho cha macho kwangu na kwako. Msimuue! Huenda akatufaa au tumfanye kuwa mtoto wetu. Wala wao hawakutambua.

Kuburudika macho ni furaha. Mke wa Firauni ni Asiya bint Muzahim. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsifu pale aliposema:

وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا لِّلَّذِينَ آمَنُوا امْرَأَتَ فِرْعَوْنَ إِذْ قَالَتْ رَبِّ ابْنِ لِي عِندَكَ بَيْتًا فِي الْجَنَّةِ وَنَجِّنِي مِن فِرْعَوْنَ وَعَمَلِهِ وَنَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿١١﴾

“Na Mwenyezi Mungu amewapiga mfano walioamini – mke wa Firauni, aliposema: “Mola wangu! Nijengee kwako nyumba Peponi na uniokoe na Firauni na vitendo vyake na uniokoe na watu madhalimu.” (66:11).

Na katika Hadith imesemwa kuwa wanawake bora ni wane: Maryam binti Imran, Asiya binti Muzahim, Khadija bint Khuwaylid na Fatima bint Muhammad. Firauni alipomwangalia mtoto alishtuka na kusema, imekuaje huyu mtoto wa ki Hebrew amepona kuchinjwa? Majasusi hawakumuona au wamenificha?

Mkewe akamtuliza na akamfanya ampende mtoto ili awe kiburudisho cha macho yao, lakini akawa ni kero ya macho yao na huzuni ya nyoyo zao.

Moyo wa mamake Musa ukawa mtupu. Alikuwa karibu kudhihirisha, lau tusingeliuimarisha moyo wake ili awe miongoni mwa waumini.

Alimtupa mtoto wake baharini akiwa na matumaini ya kuukotwa na ambaye atamwepusha na Firauni. Mara kadari ikamtoa baharini hadi nyumbani kwa Firauni!

Alipopata habari kuwa ameanguka mikononi mwa mchinjaji, alijua mtoto wake amekwisha.

Akafazaika sana na akajisahau na ahadi aliyoahidiwa na Mungu kuwa atamrudisha kwake; akawa karibu adhihirishe fazaa yake kwa kutamka jina la kipenzi chake, lakini Mwenyezi Mungu akampa utuvu, akaufanya thabiti moyo wake ili awe miongoni mwa wanaoamini ahadi yake. Kwa hiyo akawa na subira na akatulia.

Akamwambia dadake (Musa), mfuatie na uchunguze habari yake.

Akaenda na akamkuta kwa Firauni.

Basi akawa anamwangalia kiupande upande na wao hawatambui.

Wengine wamefasiri alimwangalia kwa mbali.

Maana ni kuwa alimwangalia kama vile hataki wala hamkusudii yeye, huku watu wa Firauni hawajui lengo lake au kuwa yeye ni dada wa mtoto waliyemuokota ufukweni.

Na tukamharamishia wanyonyeshaji tangu mwanzo.

Firauni alimsikiliza mkewe, akamwacha mtoto baada ya Mwenyezi Mungu kutia mahaba moyoni mwake na akaamrisha atafutwe mnyonyeshaji atakayemlea na kumtunza.

Wakaletwa wanyonyeshaji kutoka huku na huko, kila mmoja anapendelea akubali matiti yake ili apate hadhi mbele ya Firauni. Lakini mtoto aliwakataa wote.

Akasema (dadake): Je, niwaonyeshe watu wa nyumba watakaowalelea na watakuwa wema kwake.

Dadake Musa alipoona kuduwaa kwa watu wa Firauni kuhusu mtoto alijitokeza kuwaelekeza atakayekubali matiti yake na kumshughulikia bila ya kuzembea. Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:40).

Basi tukamrudisha kwa mama yake ili yaburudike macho yake.

Vile vile umetangulia mfano wake katika Juzuu hiyo hiyo.

Na ajue kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli.

Yaani mamake Musa ajue kuwa ahadi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ya kurudishiwa mwanawe na kuwa miongoni mwa mitume, ni kweli.

Lakini watu wengi hawajui, mipangilio yake Mwenyezi Mungu Mtukufu na undani wa hekima yake.

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

وَلَمَّا بَلَغَ أَشُدَّهُ وَاسْتَوَىٰ آتَيْنَاهُ حُكْمًا وَعِلْمًا وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿١٤﴾

14. Na alipofikilia kukomaa kwake na akastawi, tulimpa hukmu na elimu. Na hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

وَدَخَلَ الْمَدِينَةَ عَلَىٰ حِينِ غَفْلَةٍ مِّنْ أَهْلِهَا فَوَجَدَ فِيهَا رَجُلَيْنِ يَقْتَتِلَانِ هَـٰذَا مِن شِيعَتِهِ وَهَـٰذَا مِنْ عَدُوِّهِ فَاسْتَغَاثَهُ الَّذِي مِن شِيعَتِهِ عَلَى الَّذِي مِنْ عَدُوِّهِ فَوَكَزَهُ مُوسَىٰ فَقَضَىٰ عَلَيْهِ قَالَ هَـٰذَا مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ إِنَّهُ عَدُوٌّ مُّضِلٌّ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾

15. Na akaingia mjini wakati wenyeji wake wako kwenye mghafala. Akakuta humo watu wawili wanapigana – huyu ni katika kundi lake na huyu ni katika adui zake. Yule aliye katika kundi lake alimtaka msaada dhidi ya yule aliye katika adui zake. Musa akampiga, akammaliza. Akasema: Hiki ni kitendo cha shetani; hakika yeye ni adui mpotezaji dhahiri.

قَالَ رَبِّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي فَغَفَرَ لَهُ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿١٦﴾

16. Akasema: Mola wangu! Hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu, basi nisamehe. Akamsamehe; hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

قَالَ رَبِّ بِمَا أَنْعَمْتَ عَلَيَّ فَلَنْ أَكُونَ ظَهِيرًا لِّلْمُجْرِمِينَ ﴿١٧﴾

17. Akasema: Mola wangu! Kwa ulivyonineemesha, sitakuwa msaidizi wa wakosefu.

فَأَصْبَحَ فِي الْمَدِينَةِ خَائِفًا يَتَرَقَّبُ فَإِذَا الَّذِي اسْتَنصَرَهُ بِالْأَمْسِ يَسْتَصْرِخُهُ قَالَ لَهُ مُوسَىٰ إِنَّكَ لَغَوِيٌّ مُّبِينٌ ﴿١٨﴾

18. Akapambaukia mjini akiwa na hofu na hadhari, mara yule aliyemtaka msaada jana anampigia kelele. Musa akamwambia: Hakika wewe ni mpotevu dhahiri.

فَلَمَّا أَنْ أَرَادَ أَن يَبْطِشَ بِالَّذِي هُوَ عَدُوٌّ لَّهُمَا قَالَ يَا مُوسَىٰ أَتُرِيدُ أَن تَقْتُلَنِي كَمَا قَتَلْتَ نَفْسًا بِالْأَمْسِ إِن تُرِيدُ إِلَّا أَن تَكُونَ جَبَّارًا فِي الْأَرْضِ وَمَا تُرِيدُ أَن تَكُونَ مِنَ الْمُصْلِحِينَ ﴿١٩﴾

19. Basi Musa alipotaka kumkamata kwa nguvu, yule aliye adui yao akasema: Ewe Musa! Unataka kuniua, kama ulivyomuua mtu jana? Hutaki ila kuwa jabari katika ardhi, wala hutaki kuwa miongoni mwa wema.

ALIPOFIKIA KUKOMAA

Aya 14 – 19

MAANA

Na alipofikilia kukomaa kwake na akastawi, tulimpa hukmu na elimu. Na hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 12 (12:22). Kule imekuja kwa wasifu wa Yusuf na hapa ni wa Musa.

Na akaingia mjini wakati wenyeji wake wako kwenye mghafala. Akakuta humo watu wawili wanapigana – huyu ni katika kundi lake na huyu ni katika adui zake. Yule aliye katika kundi lake alimtaka msaada dhidi ya yule aliye katika adui zake. Musa akampiga, akam- maliza.

Makusudio ya mji hapa ni mji wa Misri.

Siku moja Musa aliingia mitaani bila ya kujulikana na yeyote. Akawaona watu wawili wanagombana na kupigana – mmoja ni Mkibti katika wafuasi wa Firauni na mwingine ni Mwisrail katika jamaa za Musa. Kwa ujumla Wakibti walikuwa wakiwakandamiza waisrail na wakiwahisabu ni watumishi na watumwa wao.

Basi yule Mwisrail akamtaka msaada Musa. Musa naye akampiga ngumi au fimbo kwa kukusudia kumtia adabu na kukinga dhulma, si kwa kukusudia kuua na yule akaanguka ni maiti. Huku kunaitwa kuua kimakosa.

Akasema: Hiki ni kitendo cha shetani; hakika yeye ni adui mpotezaji dhahiri.

Anakusudia kile kitendo cha kugombana wale wawili sio pigo alilopiga Musa. Maana ni kuwa mapigano baina ya wawili, chanzo chake ni wasi-wasi wa shetani na hadaa yake ya kuingiza kwenye uasi na madhambi.

Akasema: Mola wangu! Hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu, basi nisamehe. Akamsamehe; hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mitume na mawili wanajiona mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa ni wapungufu. Hiyo ni katika aina ya kunyenyekea na dua. Hilo halifahamishi kuweko dhambi wala upungufu.

Kwa sababu anayemjua Mwenyezi Mungu kisawasawa huwa anaituhumu nafsi yake kuwa na upungufu wa kumtii Mwenyezi Mungu na kumwabudu.

Ndio maana humwomba msamaha wa dhambi. Wa kale walisema: “Uovu wa watu wema ni wema wa waovu.” Tazama tuliyoyaeleza kwa anuani ya ‘Toba na maumbile’ katika Juz. 4 (4:17-18).

Akasema: Mola wangu! Kwa ulivyonineemesha, sitakuwa msaidizi wa wakosefu.

Musa alimuomba msamaha Mola wake na akamwahidi kuwa atawapiga vita mataghuti na wakosefu; kama vile Firauni na jeshi lake na kumsaidia kila mumin.

Akapambaukia mjini akiwa na hofu na hadhari.

Musa alihofia kuuawa kwa sababu ya Mkibti na kutarajia shari kutoka kwa Firauni na watu wake.

Wakati akiwa katika hali hiyo, mara yule aliyemtaka msaada jana anampigia kelele. Anampigia kelele za kumtaka msaaada. Musa akamwambia: Hakika wewe ni mpotevu dhahiri.

Wewe kazi yako ni kugombana na Wakibti na kutusababishia matatizo. Hebu chunga upotevu wako!

Basi Musa alipotaka kumkamata kwa nguvu yule aliye adui yao,

Musa alitaka kumkamata Mkibti, kwa sababu wakibti ndio waliokuwa wakiwachokoza waisrail na kuwachukulia kuwa ni watumwa wao, kama tulivyoashiria mwanzo. Mkibti alidhani kuwa Musa anataka kumuua, kwa hiyo akasema:

Ewe Musa! Unataka kuniua, kama ulivyomuua mtu jana? Hutaki ila kuwa jabari katika ardhi, wala hutaki kuwa miongoni mwa wema.

Jana ulimuua mtu na leo unataka kuniua mimi, je wewe ni mbabe au mtu mwema? Hii inaashiria kwamba Musa alikuwa ni katika watu wema mwenye tabia nzuri na kwamba kuua hakuendani na tabia yake.

وَجَاءَ رَجُلٌ مِّنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ يَسْعَىٰ قَالَ يَا مُوسَىٰ إِنَّ الْمَلَأَ يَأْتَمِرُونَ بِكَ لِيَقْتُلُوكَ فَاخْرُجْ إِنِّي لَكَ مِنَ النَّاصِحِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na akaja mtu kutoka mwisho wa mji akaipiga mbio, akasema: Ewe Musa! Wakubwa wanapanga kukuua. Basi toka! Hakika mimi ni katika wanaokupa nasaha.

فَخَرَجَ مِنْهَا خَائِفًا يَتَرَقَّبُ قَالَ رَبِّ نَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٢١﴾

21. Basi akatoka mjini akiwa na hofu na hadhari. Akasema: Mola wangu! Niokoe na watu madhalimu.

وَلَمَّا تَوَجَّهَ تِلْقَاءَ مَدْيَنَ قَالَ عَسَىٰ رَبِّي أَن يَهْدِيَنِي سَوَاءَ السَّبِيلِ ﴿٢٢﴾

22. Alipoelekea upande wa Madyana alisema: Asaa Mola wangu akaniongoza njia iliyo sawa.

وَلَمَّا وَرَدَ مَاءَ مَدْيَنَ وَجَدَ عَلَيْهِ أُمَّةً مِّنَ النَّاسِ يَسْقُونَ وَوَجَدَ مِن دُونِهِمُ امْرَأَتَيْنِ تَذُودَانِ قَالَ مَا خَطْبُكُمَا قَالَتَا لَا نَسْقِي حَتَّىٰ يُصْدِرَ الرِّعَاءُ وَأَبُونَا شَيْخٌ كَبِيرٌ ﴿٢٣﴾

23. Alipoyafikia maji ya Madyana alikuta umati wa watu wakinywesha (wanyama wao), na akakuta nyuma yao wanawake wawili wanazuia (wanyama wao). Akasema: Mna nini? Wakasema: Hatunyweshi mpaka wamalize hao wachunga na baba yetu ni mzee sana.

فَسَقَىٰ لَهُمَا ثُمَّ تَوَلَّىٰ إِلَى الظِّلِّ فَقَالَ رَبِّ إِنِّي لِمَا أَنزَلْتَ إِلَيَّ مِنْ خَيْرٍ فَقِيرٌ ﴿٢٤﴾

24. Basi akawanyweshea kisha akarudi kivulini na akasema: Mola wangu! Hakika mimi ni mhitaji wa kheri utakayoniteremshia.

فَجَاءَتْهُ إِحْدَاهُمَا تَمْشِي عَلَى اسْتِحْيَاءٍ قَالَتْ إِنَّ أَبِي يَدْعُوكَ لِيَجْزِيَكَ أَجْرَ مَا سَقَيْتَ لَنَا فَلَمَّا جَاءَهُ وَقَصَّ عَلَيْهِ الْقَصَصَ قَالَ لَا تَخَفْ نَجَوْتَ مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٢٥﴾

25. Basi mmoja wa wale wanawake wawili akamjia naye anatembea akiona haya. Akasema: Baba yangu anakuita akulipe ujira wa kutunyweshea.Basi alipomjia na kumsimulia visa vyake, alisema: Usiogope; umekwishaokoka na watu madhalimu.

قَالَتْ إِحْدَاهُمَا يَا أَبَتِ اسْتَأْجِرْهُ إِنَّ خَيْرَ مَنِ اسْتَأْجَرْتَ الْقَوِيُّ الْأَمِينُ ﴿٢٦﴾

26. Akasema mmoja katika wale wanawake: Ewe baba! Muajiri huyu. Hakika mbora wa kumwajiri ni mwenye nguvu na mwaminifu.

قَالَ إِنِّي أُرِيدُ أَنْ أُنكِحَكَ إِحْدَى ابْنَتَيَّ هَاتَيْنِ عَلَىٰ أَن تَأْجُرَنِي ثَمَانِيَ حِجَجٍ فَإِنْ أَتْمَمْتَ عَشْرًا فَمِنْ عِندِكَ وَمَا أُرِيدُ أَنْ أَشُقَّ عَلَيْكَ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّـهُ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴿٢٧﴾

27. Akasema: Mimi ninataka kukuoza mmoja wa mabinti zangu hawa wawili kwa kunifanyia ajira ya miaka minane na kama ukitimiza kumi hiyari yako. Mimi sitaki kukutaabisha. Inshaallah utanikuta miongoni mwa watu wema.

قَالَ ذَٰلِكَ بَيْنِي وَبَيْنَكَ أَيَّمَا الْأَجَلَيْنِ قَضَيْتُ فَلَا عُدْوَانَ عَلَيَّ وَاللَّـهُ عَلَىٰ مَا نَقُولُ وَكِيلٌ ﴿٢٨﴾

28. Akasema: Hayo yamekwishakuwa baina yangu na yako. Muda wowote kati ya miwili nitakoumaliza nisifanyiwe ubaya na Mwenyezi Mungu ni wakili juu ya haya tunayoyasema.

NJAMA

Aya 20 – 28

MAANA

Na akaja mtu kutoka mwisho wa mji akaipiga mbio, akasema: Ewe Musa! Wakubwa wanapanga kukuua. Basi toka! Hakika mimi ni katika wanaokupa nasaha.

Firauni na wapambe wake walijua yaliyotokea baina ya Musa na Mkibti wa kwanza aliyemuua kimakosa na wa pili aliyemwambia unataka kuniua. Kwa hiyo wakashauriana kuhusu mambo ya Musa na kuazimia kumuua. Mmoja wa waumini alipojua hilo alikimbia kwa Musa kumpa habari na akamshauri awakimbie madhalimu.

Wafasiri wengi wamesema kuwa mumin huyu ni yule aliyeashiriwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu:

“Na akasema mumin aliyekuwa mmoja katika watu wa Firauni aliyeficha imani yake: Mtamuua mtu kwa kusema Mola wangu ni Mwenyezi Mungu naye amewajia na hoja zilizo wazi?” (40:28).

Basi akatoka mjini akiwa na hofu na hadhari. Akasema: Mola wangu! Niokoe na watu madhalimu.

Musa alitoka mjini bila ya maandalizi yoyote; hana chakula wala maji, au yeyote wa kuongozana naye. Alitoka kwa hadhari akihofia asionekane na chinjachinja wa Firauni. Zaidi ya hayo alikuwa hajui anakwenda wapi? Basi akamkimbilia Mola wake, akamwachia Yeye mambo yake na akamwomba kuongoka na kuokoka na Firauni na watu wake.

Alipoelekea upande wa Madyana alisema: Asaa Mola wangu akaniongoza njia iliyo sawa.

Musa alitembea bila ya kujua anakwenda wapi, lakini ana yakini kuwa Mola wake atamwongoza njia iliyo sawa ambayo itampelekea kuokoka na kufaulu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamshika mkono na kumwelekeza Madyana, mji wa Shua’yb, ambao baina yake na Misri pana masafa ya mwendo wa siku nane katika jangwa pana sana.

Basi Musa akakata mbuga kwa tawfiki ya Mwenyezi Mungu. Alikuwa akila mimea ya ardhini. Jana alikuwa ikulu ya Firauni akistarehe. Mimea ya ardhi na hofu ni bora mara elfu kwa wenye ikhlasi kuliko starehe pamoja na dhulma; kama alivyosema Imam Husein(a.s) : “Wallahi! Sioni mauti ila ni wema; na sioni kuishi pamoja na madhalimu ila ni uovu.”

Alipoyafikia maji ya Madayana alikuta umati wa watu wakinywesha (wanyama wao) na akakuta nyuma yao wanawake wawili wanazuia (wanyama wao). Akasema: Mna nini? Wakasema: Hatunyweshi mpaka wamalize hao wachunga na baba yetu ni mzee sana.

Mwendo wa Musa uliishia kwenye kisima. Akakuta kundi la watu waki-wanywesha maji wanyama wao na akawaona wanawake wawili pembeni wakiwa na kondoo wao wanataka kunywa maji, lakini wao wanawazuia.

Musa akashtuliwa na hali hii, akawauliza, kwa nini mnawazuia nao wana kiu? Wakasema sisi ni wanawake dhaifu, hatuwezi kusukumana na wanaume. Tunangoja mpaka wamalize ndio nasi tupate nafasi, na baba yetu ni mzee sana, hawezi kuja kuchota maji. Nafsi ya Musa ikataharaki kidini na kiubinadamu, akawasaidia.

Hakuna ajabu kwa Musa kuwasaidia wanawake dhaifu; wala si ajabu kwa Shua’yb na mabinti zake kuishi kwa jasho lao.

Hii ndiyo sera ya mitume na makhalifa wao wenye takua, tangu zamani na baadaye. Bali ajabu ni kuwa roho hii ya Qur’an haina athari yoyote katika nafsi zetu sisi tunaodai kumjua Mwenyezi Mungu, Kitabu chake, na sera ya mitume wake. Ajabu ya maajabu ni kwamba tunashindana katika kuitafuta dunia na mapambo yake.

Basi akawanyweshea, kisha akarudi kivulini na akasema: Mola wangu! Hakika mimi ni mhitaji wa kheri utakayoniteremshia.

Musa aliwapatia maji wanyama wa wasichana wawili, kisha akaenda chini ya mti kupata kivuli, akiwa na uchovu na njaa. Akamwomba Mwenyezi Mungu fadhila na ukarimu wake. Wala hakung’angania sana au kuomba zaidi, kwa sababu alichokitaka ni kuziba tumbo tu.

Kama angelikuwa anaomba akhera angeling’ang’ania. Katika Nahjul balagha imeelezwa: “Wallahi hakumuomba isipokuwa mkate wa kula tu. Rangi ya kijani ya majani ilikuwa ikionekana kwenye ngozi ya tumbo lake kwa wembamba wake na kutengana na nyama yake.”

Basi mmoja wa wale wanawake wawili akamjia naye anatembea akiona haya. Akasema: Baba yangu anakuita akulipe ujira wa kutunyweshea.

Wale wasichana wawili walirudi kwa baba yao na wakamwelezea yaliyotokea. Basi akamwambia mmoja wao: Nenda kamwite tuje tumlipe hisani yake. Basi akaenda msichana akiwa amegubikwa na haya, ustahi na heshima na kumweleza alivyosema baba yake.

Basi alipomjia na kumsimulia visa vyake, alisema: Usiogope; umekwishaokoka na watu madhalimu.

Musa alikubali mwito, na mzee akamkaribisha na kumshukuru kwa kitendo chake. Musa alipotulia na kumwamini yule mzee, alimsimulia yaliyompitia kwa Firauni na watu wake. Yule mzee akamwambia usihofu, umefika. Hapa kwetu ni ngome ya amani, haifikiwi na Firauni wala mfano wake katika madhalimu.

Wafasiri wametofautiana kuhusu mzee huyu ni nani? Wengi wao wamesema ni Shuaib na wengine wakasema siye. Hakuna ya kutegemewa kwa hawa wala wale. Nasi hatuna haja na tofauti hizi madam hazina uhusiano wowote na imani wala maisha.

Sisi tumechagua jina la Shua’yb kiasi cha kumwelezea huyo mzee tu, sio kuwa tumekubaliana na jina hilo na pia kwa kuwa ni jina liloenea kwa wengi; kama lilivoenea baina ya wanafunzi na ulamaa wa Najaf.

Akasema mmoja katika wale wanawake ambaye alimwita kwa baba yake: Ewe baba! Muajiri huyu. Hakika mbora wa kumwajiri ni mwenye nguvu na mwaminifu.

Tunasema aliyesema ni yule aliyemwita kutokana na kauli yake ‘mwenye nguvu’ pale alipowasaidia kuchota maji na ‘mwaminifu’ pale alipokuwa na staha wakati wakielekea kwa baba yake.

Akasema: Mimi ninataka kukuoza mmoja wa mabinti zangu hawa wawili kwa kunifanyia ajira ya miaka minane na kama ukitimiza kumi hiyari yako. Mimi sitaki kukutaabisha. Inshaallah utanikuta miongoni mwa watu wema.

Musa mkimbizi, fukara asiyekuwa na chochote, ambaye kwa siku kadhaa, ameishi kwa kula mimea ya ardhi; mpaka akamuomba Mola wake tonge ya kumwezesha kuishi, leo anahiyarishwa kuchagua mke amtakaye. Bila shaka hapa kuna siri ya utu wa Musa na utukufu wake uliomgusa mzee na mabinti zake. Vile vile katika masimulizi yake na sera yake kwa Firauni na watu wake.

Mzee alitambua, kutokana na akili yake safi, kwamba mtu huyu atakuwa na athari ya mbali. Kwa sababu matendo ya mtu aghlabu yanatoka kwenye chimbuko moja. Kwa hiyo mzee, hapa alifuzu kutokana na ukwe huu. Kuna faida gani kubwa zaidi ya kuwa mkwe wa Mtume na mwenye takua.

SHARIA YA KIISLAMU IMEFUTA SHARIA ZOTE

Mafaqihi wamezungumza mengi kuhusiana na Aya hii, wakaitolea dalili kuwa walii wa mwanamke ndiye atakayetamka tamko la ndoa. Lakini ilivyo ni kuwa inafaa kwa mwanamume au mwanamke mwenyewe kutam- ka. Hilo linafahamika kimsingi bila ya kuhitaji nukuu. Shafii na Imamiya wamesema kuwa ndoa haifungiki isipokuwa kwa tamko la ziwaj na nikah. Hii ni baada ya kuiunganisha Aya hii, yenye tamko la nikah, na ile yenye tamko la ziwaj.

فَلَمَّا قَضَىٰ زَيْدٌ مِّنْهَا وَطَرًا زَوَّجْنَاكَهَا ﴿٣٧﴾

“Basi Zaid alipokwisha haja naye tulikuoza wewe” (33:37).

Malik na Hambal wakasema pia ndoa inafungika kwa neno hiba, kutokana na Aya yenye neno hiba:

وَامْرَأَةً مُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلنَّبِيِّ ﴿٥٠﴾

“Na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii.” (33:50).

Hanafi naye akasema kuwa ndoa inafungika kwa neno lolote linalofahamisha kutaka kuoana.

Mafaqihi wengi wamesema kuwa muda wa kuchunga wanyama miaka minane au kumi haukuwa mahari au sehemu yake. Bali mahari yalikuwa mbali; na kwamba kauli ya mzee: “kunifanyia ajira” maana yake ni kuwa ukichunga wanyama kwangu kwa ajira, nitakuoza mmoja wa mabinti zangu kwa mahari; sawa na kusema: ‘Ukifanya hivi nami nitafanya hivyo.’

Haya ndio maana sahihi ya Aya. Kwa vyovyote iwavyo, hakuna hoja yoyote, katika Aya hii kwa, waliyoyasema mafaqihi. Kwa sababu hizo ni simulizi za sharia zilizotangulia. Nasi tuna uhakika kwamba sharia ya Kiisalmu imefuta sharia zote zilizotangulia, wala haifai kutumia hukumu yoyote miongoni mwa hukumu hizo zilizotangulia, isipokuwa kwa dalili maalum au ya kiujmla kutoka katika Kitab au Sunna. Na hapo itakuwa ni kukitumia Kitab au Sunna, sio kuitumia sharia hiyo.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ ﴿٣٨﴾

“Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote.” Juz. 7 (6:38).

Na kauli yake:

وَنَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ تِبْيَانًا لِّكُلِّ شَيْءٍ ﴿٨٩﴾

Na tumekuteremshia Kitabu hiki kubainisha kila kitu.” Juz.14: (16:89),

Yaani kila kitu katika misingi ya kiislamu na sharia yake.

Mtume(s.a.w.w) naye anasema: “Hakuna kitu kitakachowakurubisha nyinyi Peponi isipokuwa nimewaamrisha, na hakuna kitu kitakachowaweka mbali na moto isipokuwa nimewakataza.”

Akasema: Hayo yamekwishakuwa baina yangu na yako. Muda wowote kati ya miwili nitakoumaliza nisifanyiwe ubaya na Mwenyezi Mungu ni wakili juu ya haya tunayoyasema.

Haya ni maneno ya Musa. Muda wa kwanza ni Hijja nane na wa pili ni Hijja kumi. Maana ni kuwa Musa alimwambia mzee, nimekubali na kuridhia kuoa na kuchunga wanyama.

Mimi nitakuwa na hiyari ya kumaliza nane au kumi. Muda wowote nitakaoumaliza basi usiwe na hoja kwangu na Mwenyezi Mungu ndiye shahidi juu ya haya uliyojiwajibishia na niliyojiwajibishia.

Kuna Hadith isemayo kuwa Musa alichagua muda wa kumi. Wafasiri wengi wanasema kuwa yeye alimchagua mdogo naye ndiye aliyesema, baba yangu anakuita. Na pia kumwambia baba yake, hakika yeye ana nguvu na ni mwaminifu.

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Sura Ya Ishirini Na Nane: Surat Al-Qasas. Tabrasi amesema imeshuka Makka. Ina Aya 88.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

طسم ﴿١﴾

1. Twaa Siin Miim.

تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ ﴿٢﴾

2. Hiyo ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

نَتْلُو عَلَيْكَ مِن نَّبَإِ مُوسَىٰ وَفِرْعَوْنَ بِالْحَقِّ لِقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿٣﴾

3. Tunakuosomea habari za Musa na Firauni kwa haki kwa ajili ya watu wanaoamini.

إِنَّ فِرْعَوْنَ عَلَا فِي الْأَرْضِ وَجَعَلَ أَهْلَهَا شِيَعًا يَسْتَضْعِفُ طَائِفَةً مِّنْهُمْ يُذَبِّحُ أَبْنَاءَهُمْ وَيَسْتَحْيِي نِسَاءَهُمْ إِنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُفْسِدِينَ ﴿٤﴾

4. Hakika Firauni alitakabari katika nchi akagawa watu wake makundi. Akidhoofisha taifa moja miongoni mwao, akiwachinja watoto wao wa kiume na akiwaacha watoto wao wa kike. Hakika yeye alikuwa katika wafisadi.

وَنُرِيدُ أَن نَّمُنَّ عَلَى الَّذِينَ اسْتُضْعِفُوا فِي الْأَرْضِ وَنَجْعَلَهُمْ أَئِمَّةً وَنَجْعَلَهُمُ الْوَارِثِينَ ﴿٥﴾

5. Na tunataka kuwafadhili waliodhoofishwa katika ardhi na kuwafanya wawe ni viongozi na kuwafanya ni warithi.

وَنُمَكِّنَ لَهُمْ فِي الْأَرْضِ وَنُرِيَ فِرْعَوْنَ وَهَامَانَ وَجُنُودَهُمَا مِنْهُم مَّا كَانُوا يَحْذَرُونَ ﴿٦﴾

6. Na kuwamakinisha katika ardhi. Na kumuonyesha Firauni na Hamana na majeshi yao yale waliyokuwa wakiyahadhari kwao.

AYA ZA KITABU

Aya 1 – 6

TWAA SIIN MIIM.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1)

Hiyo ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

Hiyo ni ishara ya Sura hii, Kitabu ni Qur’an na kubainisha ni kupambanua baina ya upotevu na uongofu.

Tunakuosomea habari za Musa na Firauni kwa ajili ya watu wanaoamini.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsomea Mtume wake mtukufu habari mara kwa mara. Katika Juz. 16 kifungu cha ‘Kukaririka Kisa’ (20:9) tumeeleza lengo la kukaririka kisa cha Musa.

Hakika Firauni alitakabari katika nchi akagawa watu wake makundi.

Alipetuka mipaka na akajifanya jabari, akawagawa wananchi wake kwenye makundi wakigombana, ili udumu utawala wake.

Akidhoofisha taifa moja miongoni mwao, akiwachinja watoto wao wa kiume na akiwaacha watoto wao wa kike. Hakika yeye alikuwa katika wafisadi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:49) na Juz. 9 (7:127).

KWA NINI FIRAUNI ALIWAKANDAMIZA WANA WA ISRAIL?

Mmoja katika wafasiri wa kisasa anasema: “Firauni aliwakandamiza wana wa Israil kwa sababu walikuwa na itikadi isiyoafikiana na itikadi yake. Wao walikuwa wakifuata dini ya babu yao Ibrahim na Ya’qub. Ingawa itikadi yao ilikuwa na upotofu, lakini walibakia na itikadi ya Mungu mmoja.”

Sisi tunamuuliza mfasiri huyu mpya: Umejua vipi kuwa mayahudi waliokuwa wakati wa Firauni walikuwa kwenye dini ya Ibrahim(a.s) na kwamba walibaki na itikadi ya Mungu mmoja? Je, umepata kujua kutokana na kuli yao: “Ewe Musa! Hebu nasi tufanyie waungu kama hawa walivyo na waungu.” Au kauli yao: “Hatutakuamini mpakae tumwone Mungu wazi wazi.”

Au ni kutokana na kuabudu kwao ndama au kwa kuwaua kwao mitume? Ikiwa Firauni aliwakandamiza kwa sababu ya itikadi yao, kwa nini Mtume wao na mwenye ikhlasi zaidi, Musa aliwapa wasifa huu ufuatao? Ufuska, Juz. 6 (5:25), wapumbavu, Juz. 9 (7:155), wabatilifu Juz. 9 (7:153) na ujinga Juz. 9 (7:138). Kama amabavyo Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya kadhaa amewasifu kwa ufisadi, uovu na kwa kila aina ya hatia?

Qur’an imetaja kwamba Firauni aliwakandamiza wana wa isaril na kwam- ba yeye alipituka mpaka katika dhulma yake, lakini haikuashiria sababu.

Kwa hiyo maulama wametofautiana katika kuielezea. Kuna waliosema kuwa kuhani alimwambia Firauni kuwa atazaliwa mtoto katika wana waisrail, atakayekuja mvua ufalme wake, wengine wakasema kuwa mitume waliokuwa kabla yake walitoa bishara ya kuja kwake.Firauni alipojua hivyo akahofia na kuanza kuwachinja watoto wa kiume wa wana wa israil. Na sikuona yoyote aliyesema kuwa Firauni aliwakandamiza kwa sababu ya kuwa kwenye dini ya Ibrahim.

Tukiangalia sera ya wana wa israil kwa Mtume wao Musa(a.s) na mitume wengine waliokuja baada ya Musa; ambapo walikuwa wakikadhibisha wengine na wengine wakiwaua. Pia tukiangalia sera yao katika miji wanayoiteka jinsi wanavyoleta fitna, kupanga njama, kujaribu kutawala nyenzo na propaganda zote.

Tukiangalia yote haya basi tunakubaliana na Sheikh Maraghi aliyesema: “Firauni aliwakandamiza wana wa israil kwa vile aliwahofia wanaume ambao walikuwa na ufundi na mikononi mwao mlikuwa na hatamu za uchumi; kuwa muda ukiendelea watakuwa juu kiuchumi waje wawashinde wamisri. Na uchumi ndio wenye nguvu kiutawala.”

Ni kweli kuwa Firauni alipetuka mpaka katika dhulma kwa kuwachinja watoto wa kiume na kuwafanya watumwa watoto wa kike wa wana wa israil, lakini sababu ya yote haya ni wayahudi.

Kwa hiyo lawama ni la wote wawili. Mayahudi kwa sababu ya chuki yao, tabia yao na malengo yao mabaya na pia kwa Firauni kwa sababu aliwatesa wasiokuwa na hatia kwa sababu ya wenye hatia.

LINI MWENYEZI MUNGU ATAWAFADHILI WALIODHOOFISHWA?

Na tunataka kuwafadhili waliodhoofishwa katika ardhi.

Waliodhoofishwa katika ardhi ni wale waliokandamizwa na wenye nguvu, waliotawala nyenzo zao na nguvu zao kimabavu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawafadhili uhuru na kujikomboa kwenye ukandamizaji ikiwa watafanya juhudi na kujitolea kwa ajili ya maisha yao na heshima yao; sawa na mgonjwa atapona ikiwa atafanya matibabu mazuri na mkulima atapata mavuno akilima vizuri.

Mwenyezi Mungu ana desturi katika maumbile yake, na wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu kabisa. Kila mwenye kufuata njia atafika, awe mumin au kafiri. Ama malipo ya kafiri na mumin ni siku ya Kiyama, si katika maisha haya.

Basi atakayemnyenyekea dhalimu, Mwenyezi Mungu humdhalilisha na humwachia atakayemdhulumu, hata kama ataswali, kufunga na kuhiji. Kwa sababu ameidhalilisha haki na akisaidia batili na akhera hana kitu.

Na mwenye kujikomboa kutoka kwa dhalimu na watu wake, na akajitolea mhanga kwa ajili ya heshima yake, Mungu humpa nusra kuwashinda mad- halimu na wababe; kwa sababu atakuwa amekutana na utashi wa Mwenyezi Mungu na amri yake, kwa jihadi na uimara.

Hatuna haja ya kurudia historia ya mbali kutafuta ushahidi wa hakika hii. Kwani ukakamavu wa wananchi wa Vietnam mbele ya taifa hilo na nguvu kubwa ya shari na ufisadi, ni dalili kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja na mwenye kudhulumiwa anayepigana jihadi aliye mvumilivu, kwa namna yoyote ile atakayokuwa.

Kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu hapigani kwa ajili ya waliodhoofishwa, lakini anakuwa nao na kuwapa msaada wake, ikiwa watapigana na kupinga kwa lengo la haki, uadilifu na kujikomboa kutoka kwenye makucha ya ukoloni na dhulma. Mwenyezi Mungu yuko pamoja na hawa, kwa sababu, yuko pamoja na kila mwenye kufanya juhudi na akatenda kwa ajili ya maisha.

Haya tumeyafafanua zaidi katika Juz. 13 (13:11).

Unaweza kuuliza : Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alimwangamiza Firauni na watu wake, akawaokoa wana wa israil na adhabu yao na ukandamizwaji wao. Hii inamaanisha kuwa Mwenyezi Mungu anapigana kwa ajili ya wanyonge; bali kuna Aya isemayo:

إِنَّ اللَّـهَ يُدَافِعُ عَنِ الَّذِينَ آمَنُوا ﴿٣٨﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu huwakinga walioamini.” Juz. 17 (22:38)?

Jibu : Mwenyezi Mungu Mtukufu alimwangamiza Firauni na watu wake kwa sababu ya shirki yao na kuwakadhibisha kwao mitume na sio kuwasaidia wana wa israili; sawa na alivyoangamiza kaumu ya Nuh na washirikina wengineo.

Kwa hiyo wana wa israil na wengineo wakapona na dhulma na ukandamizwaji. Ama makusudio ya walioamini, wanaokingwa na Mwenyezi Mungu ni wale wanopigana jihadi. Na wavivu wako kwenye dini ya wale waliomwambia Musa:

فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ ﴿٢٤﴾

“Nenda wewe na Mola wako mkapigane, hakika sisi ni wenye kukaa hapa.” Juz. 6 (5:24)

Na kuwafanya wawe ni viongozi.

Yaani tuwafanye mitume miongoni mwao.

Na kuwafanya ni warithi na kuwamakinisha katika ardhi.

Mwenyezi Mungu anawafanya huru kwa muda mrefu baada ya kuwa utumwani.

Na kumuonyesha Firauni na Hamana na majeshi yao yale waliyokuwa wakiyahadhari kwao.

Kwao ni kwa hao wana wa israil. Maana ni kuwa Firauni na watu wake walihofia utawala wao usiingie mikononi mwa wana wa israil, ndio wakachukua hadhari, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawaingiza kwenye yale waliyoyahofia.

وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ أُمِّ مُوسَىٰ أَنْ أَرْضِعِيهِ فَإِذَا خِفْتِ عَلَيْهِ فَأَلْقِيهِ فِي الْيَمِّ وَلَا تَخَافِي وَلَا تَحْزَنِي إِنَّا رَادُّوهُ إِلَيْكِ وَجَاعِلُوهُ مِنَ الْمُرْسَلِينَ ﴿٧﴾

7. Na tulimpa wahyi mama wa Musa kuwa mnyonyeshe. Na utakapomhofia basi mtie mtoni. Na usihofu wala usihuzunike. Hakika sisi tutamrudisha kwako na tutamfanya miongoni mwa mitume.

فَالْتَقَطَهُ آلُ فِرْعَوْنَ لِيَكُونَ لَهُمْ عَدُوًّا وَحَزَنًا إِنَّ فِرْعَوْنَ وَهَامَانَ وَجُنُودَهُمَا كَانُوا خَاطِئِينَ ﴿٨﴾

8. Basi wakamwokota watu wa Firauni aje kuwa adui kwao na huzuni. Hakika Firauni na Hamana na majeshi yao walikuwa wenye makosa.

وَقَالَتِ امْرَأَتُ فِرْعَوْنَ قُرَّتُ عَيْنٍ لِّي وَلَكَ لَا تَقْتُلُوهُ عَسَىٰ أَن يَنفَعَنَا أَوْ نَتَّخِذَهُ وَلَدًا وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿٩﴾

9. Akasema mke wa Firaun: Ni kiburudisho cha macho kwangu na kwako. Msimuuwe! Huenda akatufaa au tumfanye kuwa mtoto wetu. Wala wao hawakutambua

وَأَصْبَحَ فُؤَادُ أُمِّ مُوسَىٰ فَارِغًا إِن كَادَتْ لَتُبْدِي بِهِ لَوْلَا أَن رَّبَطْنَا عَلَىٰ قَلْبِهَا لِتَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١٠﴾

10. Moyo wa mamake Musa ukawa mtupu. Alikuwa karibu kudhihirisha, lau tusingeliuimarisha moyo wake ili awe miongoni mwa waumini.

وَقَالَتْ لِأُخْتِهِ قُصِّيهِ فَبَصُرَتْ بِهِ عَن جُنُبٍ وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿١١﴾

11. Akamwambia dadake (Musa) mfuatie. Basi akawa anamwangalia kiupande upande na wao hawatambui.

وَحَرَّمْنَا عَلَيْهِ الْمَرَاضِعَ مِن قَبْلُ فَقَالَتْ هَلْ أَدُلُّكُمْ عَلَىٰ أَهْلِ بَيْتٍ يَكْفُلُونَهُ لَكُمْ وَهُمْ لَهُ نَاصِحُونَ ﴿١٢﴾

12. Na tukamharamishia wanyonyeshaji tangu mwanzo. Akasema (dadake): Je, niwaonyeshe watu wa nyumba watakaowalelea na watakuwa wema kwake?

فَرَدَدْنَاهُ إِلَىٰ أُمِّهِ كَيْ تَقَرَّ عَيْنُهَا وَلَا تَحْزَنَ وَلِتَعْلَمَ أَنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿١٣﴾

13. Basi tukamrudisha kwa mama yake ili yaburudike macho yake na ajue kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Lakini watu wengi hawajui.

MAMA WA MUSA

Aya 7 – 13

MAANA

Na tulimpa wahyi mama wa Musa kuwa mnyonyeshe.

Makusudio ya wahyi hapa ni ilhamu; ni mfano kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na Mola wako akampa wahyi nyuki.” Juz. 14 (16:68). Katika Juz. 9 (7: 103 -112).

Tumenukuu kutoka kitabu Qisasul-qur’an, kwamba jina la mama yake Musa ni Yukabid (Jochebed). Kisha tukasoma katika Tawrat kuwa hilo ndilo jina lake na kwamba aliolewa na Amram, mtoto wa kaka yake. Musa ndiye mdogo katika watoto wa baba yake, akiwa ni watatu, baada ya Maryam na Harun.

Na utakapomhofia basi mtie mtoni.

Makusudio ya mto hapa ni mto Nile. Maana ni akimhofia kuchinjwa amtie mtoni kwa mkono wake! Itakuwaje, mwenye akili aweze kujitupa motoni?

Lakini akaambiwa: Na usihofu wala usihuzunike. Hakika sisi tutamrudisha kwako na tutamfanya miongoni mwa mitume.

Usimhofie, hakika Mwenyezi Mungu ndiye mhifadhi na mlinzi. Yule ambaye ameujaalia moto kuwa baridi na salama kwa Ibrahim, ataijalia bahari kuwa amani kwa Musa. Alimpa habari ya usalama wa mtoto wake na kwamba yeye atamlea na pia akampa habari njema kuwa amemchagua kwa risala yake na kumhusu kwa rehema yake. Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:38).

Basi wakamwokota watu wa Firauni aje kuwa adui kwao na huzuni.

Walimwokota na kumlea kwa kumfanya mtoto wao, lakini akaja akawa ni adui wa itikadi yao na desturi yao. Akaingiza huzuni nyoyoni mwao na mwisho wa ufalme wao ukawa mikononi mwake.

Hakika Firauni na Hamana na majeshi yao walikuwa wenye makosa, wapotevu katika vitendo vyao vyote; hasa kuua maelefu ya vijana ili kujiepusha na Musa, lakini ikawa wao wanamwepusha Musa na mauti ili aje awamalize. Katika kamusi ya Kitabu kitakatifu[4] , imeelezwa kuwa maisha ya Musa katika nyumba ya Firauni hayakujulikana kwa ufafanuzi na kwamba wanahistoria wametofautiana kuhusu wakati wake alioishi. Wengine wakasema ni wakati wa Firauni Amenophis (Amenhotep II) (1411 – 1436 Bc), wengine wakasema ni Ramesses II (1223 – 1290 Bc). Pia kuna waliosema ni wakati wa Mernptsh ( 1211 – 1223 Bc).

Akasema mke wa Firaun: Ni kiburudisho cha macho kwangu na kwako. Msimuue! Huenda akatufaa au tumfanye kuwa mtoto wetu. Wala wao hawakutambua.

Kuburudika macho ni furaha. Mke wa Firauni ni Asiya bint Muzahim. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsifu pale aliposema:

وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا لِّلَّذِينَ آمَنُوا امْرَأَتَ فِرْعَوْنَ إِذْ قَالَتْ رَبِّ ابْنِ لِي عِندَكَ بَيْتًا فِي الْجَنَّةِ وَنَجِّنِي مِن فِرْعَوْنَ وَعَمَلِهِ وَنَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿١١﴾

“Na Mwenyezi Mungu amewapiga mfano walioamini – mke wa Firauni, aliposema: “Mola wangu! Nijengee kwako nyumba Peponi na uniokoe na Firauni na vitendo vyake na uniokoe na watu madhalimu.” (66:11).

Na katika Hadith imesemwa kuwa wanawake bora ni wane: Maryam binti Imran, Asiya binti Muzahim, Khadija bint Khuwaylid na Fatima bint Muhammad. Firauni alipomwangalia mtoto alishtuka na kusema, imekuaje huyu mtoto wa ki Hebrew amepona kuchinjwa? Majasusi hawakumuona au wamenificha?

Mkewe akamtuliza na akamfanya ampende mtoto ili awe kiburudisho cha macho yao, lakini akawa ni kero ya macho yao na huzuni ya nyoyo zao.

Moyo wa mamake Musa ukawa mtupu. Alikuwa karibu kudhihirisha, lau tusingeliuimarisha moyo wake ili awe miongoni mwa waumini.

Alimtupa mtoto wake baharini akiwa na matumaini ya kuukotwa na ambaye atamwepusha na Firauni. Mara kadari ikamtoa baharini hadi nyumbani kwa Firauni!

Alipopata habari kuwa ameanguka mikononi mwa mchinjaji, alijua mtoto wake amekwisha.

Akafazaika sana na akajisahau na ahadi aliyoahidiwa na Mungu kuwa atamrudisha kwake; akawa karibu adhihirishe fazaa yake kwa kutamka jina la kipenzi chake, lakini Mwenyezi Mungu akampa utuvu, akaufanya thabiti moyo wake ili awe miongoni mwa wanaoamini ahadi yake. Kwa hiyo akawa na subira na akatulia.

Akamwambia dadake (Musa), mfuatie na uchunguze habari yake.

Akaenda na akamkuta kwa Firauni.

Basi akawa anamwangalia kiupande upande na wao hawatambui.

Wengine wamefasiri alimwangalia kwa mbali.

Maana ni kuwa alimwangalia kama vile hataki wala hamkusudii yeye, huku watu wa Firauni hawajui lengo lake au kuwa yeye ni dada wa mtoto waliyemuokota ufukweni.

Na tukamharamishia wanyonyeshaji tangu mwanzo.

Firauni alimsikiliza mkewe, akamwacha mtoto baada ya Mwenyezi Mungu kutia mahaba moyoni mwake na akaamrisha atafutwe mnyonyeshaji atakayemlea na kumtunza.

Wakaletwa wanyonyeshaji kutoka huku na huko, kila mmoja anapendelea akubali matiti yake ili apate hadhi mbele ya Firauni. Lakini mtoto aliwakataa wote.

Akasema (dadake): Je, niwaonyeshe watu wa nyumba watakaowalelea na watakuwa wema kwake.

Dadake Musa alipoona kuduwaa kwa watu wa Firauni kuhusu mtoto alijitokeza kuwaelekeza atakayekubali matiti yake na kumshughulikia bila ya kuzembea. Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:40).

Basi tukamrudisha kwa mama yake ili yaburudike macho yake.

Vile vile umetangulia mfano wake katika Juzuu hiyo hiyo.

Na ajue kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli.

Yaani mamake Musa ajue kuwa ahadi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ya kurudishiwa mwanawe na kuwa miongoni mwa mitume, ni kweli.

Lakini watu wengi hawajui, mipangilio yake Mwenyezi Mungu Mtukufu na undani wa hekima yake.

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

وَلَمَّا بَلَغَ أَشُدَّهُ وَاسْتَوَىٰ آتَيْنَاهُ حُكْمًا وَعِلْمًا وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿١٤﴾

14. Na alipofikilia kukomaa kwake na akastawi, tulimpa hukmu na elimu. Na hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

وَدَخَلَ الْمَدِينَةَ عَلَىٰ حِينِ غَفْلَةٍ مِّنْ أَهْلِهَا فَوَجَدَ فِيهَا رَجُلَيْنِ يَقْتَتِلَانِ هَـٰذَا مِن شِيعَتِهِ وَهَـٰذَا مِنْ عَدُوِّهِ فَاسْتَغَاثَهُ الَّذِي مِن شِيعَتِهِ عَلَى الَّذِي مِنْ عَدُوِّهِ فَوَكَزَهُ مُوسَىٰ فَقَضَىٰ عَلَيْهِ قَالَ هَـٰذَا مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ إِنَّهُ عَدُوٌّ مُّضِلٌّ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾

15. Na akaingia mjini wakati wenyeji wake wako kwenye mghafala. Akakuta humo watu wawili wanapigana – huyu ni katika kundi lake na huyu ni katika adui zake. Yule aliye katika kundi lake alimtaka msaada dhidi ya yule aliye katika adui zake. Musa akampiga, akammaliza. Akasema: Hiki ni kitendo cha shetani; hakika yeye ni adui mpotezaji dhahiri.

قَالَ رَبِّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي فَغَفَرَ لَهُ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿١٦﴾

16. Akasema: Mola wangu! Hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu, basi nisamehe. Akamsamehe; hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

قَالَ رَبِّ بِمَا أَنْعَمْتَ عَلَيَّ فَلَنْ أَكُونَ ظَهِيرًا لِّلْمُجْرِمِينَ ﴿١٧﴾

17. Akasema: Mola wangu! Kwa ulivyonineemesha, sitakuwa msaidizi wa wakosefu.

فَأَصْبَحَ فِي الْمَدِينَةِ خَائِفًا يَتَرَقَّبُ فَإِذَا الَّذِي اسْتَنصَرَهُ بِالْأَمْسِ يَسْتَصْرِخُهُ قَالَ لَهُ مُوسَىٰ إِنَّكَ لَغَوِيٌّ مُّبِينٌ ﴿١٨﴾

18. Akapambaukia mjini akiwa na hofu na hadhari, mara yule aliyemtaka msaada jana anampigia kelele. Musa akamwambia: Hakika wewe ni mpotevu dhahiri.

فَلَمَّا أَنْ أَرَادَ أَن يَبْطِشَ بِالَّذِي هُوَ عَدُوٌّ لَّهُمَا قَالَ يَا مُوسَىٰ أَتُرِيدُ أَن تَقْتُلَنِي كَمَا قَتَلْتَ نَفْسًا بِالْأَمْسِ إِن تُرِيدُ إِلَّا أَن تَكُونَ جَبَّارًا فِي الْأَرْضِ وَمَا تُرِيدُ أَن تَكُونَ مِنَ الْمُصْلِحِينَ ﴿١٩﴾

19. Basi Musa alipotaka kumkamata kwa nguvu, yule aliye adui yao akasema: Ewe Musa! Unataka kuniua, kama ulivyomuua mtu jana? Hutaki ila kuwa jabari katika ardhi, wala hutaki kuwa miongoni mwa wema.

ALIPOFIKIA KUKOMAA

Aya 14 – 19

MAANA

Na alipofikilia kukomaa kwake na akastawi, tulimpa hukmu na elimu. Na hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 12 (12:22). Kule imekuja kwa wasifu wa Yusuf na hapa ni wa Musa.

Na akaingia mjini wakati wenyeji wake wako kwenye mghafala. Akakuta humo watu wawili wanapigana – huyu ni katika kundi lake na huyu ni katika adui zake. Yule aliye katika kundi lake alimtaka msaada dhidi ya yule aliye katika adui zake. Musa akampiga, akam- maliza.

Makusudio ya mji hapa ni mji wa Misri.

Siku moja Musa aliingia mitaani bila ya kujulikana na yeyote. Akawaona watu wawili wanagombana na kupigana – mmoja ni Mkibti katika wafuasi wa Firauni na mwingine ni Mwisrail katika jamaa za Musa. Kwa ujumla Wakibti walikuwa wakiwakandamiza waisrail na wakiwahisabu ni watumishi na watumwa wao.

Basi yule Mwisrail akamtaka msaada Musa. Musa naye akampiga ngumi au fimbo kwa kukusudia kumtia adabu na kukinga dhulma, si kwa kukusudia kuua na yule akaanguka ni maiti. Huku kunaitwa kuua kimakosa.

Akasema: Hiki ni kitendo cha shetani; hakika yeye ni adui mpotezaji dhahiri.

Anakusudia kile kitendo cha kugombana wale wawili sio pigo alilopiga Musa. Maana ni kuwa mapigano baina ya wawili, chanzo chake ni wasi-wasi wa shetani na hadaa yake ya kuingiza kwenye uasi na madhambi.

Akasema: Mola wangu! Hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu, basi nisamehe. Akamsamehe; hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mitume na mawili wanajiona mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa ni wapungufu. Hiyo ni katika aina ya kunyenyekea na dua. Hilo halifahamishi kuweko dhambi wala upungufu.

Kwa sababu anayemjua Mwenyezi Mungu kisawasawa huwa anaituhumu nafsi yake kuwa na upungufu wa kumtii Mwenyezi Mungu na kumwabudu.

Ndio maana humwomba msamaha wa dhambi. Wa kale walisema: “Uovu wa watu wema ni wema wa waovu.” Tazama tuliyoyaeleza kwa anuani ya ‘Toba na maumbile’ katika Juz. 4 (4:17-18).

Akasema: Mola wangu! Kwa ulivyonineemesha, sitakuwa msaidizi wa wakosefu.

Musa alimuomba msamaha Mola wake na akamwahidi kuwa atawapiga vita mataghuti na wakosefu; kama vile Firauni na jeshi lake na kumsaidia kila mumin.

Akapambaukia mjini akiwa na hofu na hadhari.

Musa alihofia kuuawa kwa sababu ya Mkibti na kutarajia shari kutoka kwa Firauni na watu wake.

Wakati akiwa katika hali hiyo, mara yule aliyemtaka msaada jana anampigia kelele. Anampigia kelele za kumtaka msaaada. Musa akamwambia: Hakika wewe ni mpotevu dhahiri.

Wewe kazi yako ni kugombana na Wakibti na kutusababishia matatizo. Hebu chunga upotevu wako!

Basi Musa alipotaka kumkamata kwa nguvu yule aliye adui yao,

Musa alitaka kumkamata Mkibti, kwa sababu wakibti ndio waliokuwa wakiwachokoza waisrail na kuwachukulia kuwa ni watumwa wao, kama tulivyoashiria mwanzo. Mkibti alidhani kuwa Musa anataka kumuua, kwa hiyo akasema:

Ewe Musa! Unataka kuniua, kama ulivyomuua mtu jana? Hutaki ila kuwa jabari katika ardhi, wala hutaki kuwa miongoni mwa wema.

Jana ulimuua mtu na leo unataka kuniua mimi, je wewe ni mbabe au mtu mwema? Hii inaashiria kwamba Musa alikuwa ni katika watu wema mwenye tabia nzuri na kwamba kuua hakuendani na tabia yake.

وَجَاءَ رَجُلٌ مِّنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ يَسْعَىٰ قَالَ يَا مُوسَىٰ إِنَّ الْمَلَأَ يَأْتَمِرُونَ بِكَ لِيَقْتُلُوكَ فَاخْرُجْ إِنِّي لَكَ مِنَ النَّاصِحِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na akaja mtu kutoka mwisho wa mji akaipiga mbio, akasema: Ewe Musa! Wakubwa wanapanga kukuua. Basi toka! Hakika mimi ni katika wanaokupa nasaha.

فَخَرَجَ مِنْهَا خَائِفًا يَتَرَقَّبُ قَالَ رَبِّ نَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٢١﴾

21. Basi akatoka mjini akiwa na hofu na hadhari. Akasema: Mola wangu! Niokoe na watu madhalimu.

وَلَمَّا تَوَجَّهَ تِلْقَاءَ مَدْيَنَ قَالَ عَسَىٰ رَبِّي أَن يَهْدِيَنِي سَوَاءَ السَّبِيلِ ﴿٢٢﴾

22. Alipoelekea upande wa Madyana alisema: Asaa Mola wangu akaniongoza njia iliyo sawa.

وَلَمَّا وَرَدَ مَاءَ مَدْيَنَ وَجَدَ عَلَيْهِ أُمَّةً مِّنَ النَّاسِ يَسْقُونَ وَوَجَدَ مِن دُونِهِمُ امْرَأَتَيْنِ تَذُودَانِ قَالَ مَا خَطْبُكُمَا قَالَتَا لَا نَسْقِي حَتَّىٰ يُصْدِرَ الرِّعَاءُ وَأَبُونَا شَيْخٌ كَبِيرٌ ﴿٢٣﴾

23. Alipoyafikia maji ya Madyana alikuta umati wa watu wakinywesha (wanyama wao), na akakuta nyuma yao wanawake wawili wanazuia (wanyama wao). Akasema: Mna nini? Wakasema: Hatunyweshi mpaka wamalize hao wachunga na baba yetu ni mzee sana.

فَسَقَىٰ لَهُمَا ثُمَّ تَوَلَّىٰ إِلَى الظِّلِّ فَقَالَ رَبِّ إِنِّي لِمَا أَنزَلْتَ إِلَيَّ مِنْ خَيْرٍ فَقِيرٌ ﴿٢٤﴾

24. Basi akawanyweshea kisha akarudi kivulini na akasema: Mola wangu! Hakika mimi ni mhitaji wa kheri utakayoniteremshia.

فَجَاءَتْهُ إِحْدَاهُمَا تَمْشِي عَلَى اسْتِحْيَاءٍ قَالَتْ إِنَّ أَبِي يَدْعُوكَ لِيَجْزِيَكَ أَجْرَ مَا سَقَيْتَ لَنَا فَلَمَّا جَاءَهُ وَقَصَّ عَلَيْهِ الْقَصَصَ قَالَ لَا تَخَفْ نَجَوْتَ مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٢٥﴾

25. Basi mmoja wa wale wanawake wawili akamjia naye anatembea akiona haya. Akasema: Baba yangu anakuita akulipe ujira wa kutunyweshea.Basi alipomjia na kumsimulia visa vyake, alisema: Usiogope; umekwishaokoka na watu madhalimu.

قَالَتْ إِحْدَاهُمَا يَا أَبَتِ اسْتَأْجِرْهُ إِنَّ خَيْرَ مَنِ اسْتَأْجَرْتَ الْقَوِيُّ الْأَمِينُ ﴿٢٦﴾

26. Akasema mmoja katika wale wanawake: Ewe baba! Muajiri huyu. Hakika mbora wa kumwajiri ni mwenye nguvu na mwaminifu.

قَالَ إِنِّي أُرِيدُ أَنْ أُنكِحَكَ إِحْدَى ابْنَتَيَّ هَاتَيْنِ عَلَىٰ أَن تَأْجُرَنِي ثَمَانِيَ حِجَجٍ فَإِنْ أَتْمَمْتَ عَشْرًا فَمِنْ عِندِكَ وَمَا أُرِيدُ أَنْ أَشُقَّ عَلَيْكَ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّـهُ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴿٢٧﴾

27. Akasema: Mimi ninataka kukuoza mmoja wa mabinti zangu hawa wawili kwa kunifanyia ajira ya miaka minane na kama ukitimiza kumi hiyari yako. Mimi sitaki kukutaabisha. Inshaallah utanikuta miongoni mwa watu wema.

قَالَ ذَٰلِكَ بَيْنِي وَبَيْنَكَ أَيَّمَا الْأَجَلَيْنِ قَضَيْتُ فَلَا عُدْوَانَ عَلَيَّ وَاللَّـهُ عَلَىٰ مَا نَقُولُ وَكِيلٌ ﴿٢٨﴾

28. Akasema: Hayo yamekwishakuwa baina yangu na yako. Muda wowote kati ya miwili nitakoumaliza nisifanyiwe ubaya na Mwenyezi Mungu ni wakili juu ya haya tunayoyasema.

NJAMA

Aya 20 – 28

MAANA

Na akaja mtu kutoka mwisho wa mji akaipiga mbio, akasema: Ewe Musa! Wakubwa wanapanga kukuua. Basi toka! Hakika mimi ni katika wanaokupa nasaha.

Firauni na wapambe wake walijua yaliyotokea baina ya Musa na Mkibti wa kwanza aliyemuua kimakosa na wa pili aliyemwambia unataka kuniua. Kwa hiyo wakashauriana kuhusu mambo ya Musa na kuazimia kumuua. Mmoja wa waumini alipojua hilo alikimbia kwa Musa kumpa habari na akamshauri awakimbie madhalimu.

Wafasiri wengi wamesema kuwa mumin huyu ni yule aliyeashiriwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu:

“Na akasema mumin aliyekuwa mmoja katika watu wa Firauni aliyeficha imani yake: Mtamuua mtu kwa kusema Mola wangu ni Mwenyezi Mungu naye amewajia na hoja zilizo wazi?” (40:28).

Basi akatoka mjini akiwa na hofu na hadhari. Akasema: Mola wangu! Niokoe na watu madhalimu.

Musa alitoka mjini bila ya maandalizi yoyote; hana chakula wala maji, au yeyote wa kuongozana naye. Alitoka kwa hadhari akihofia asionekane na chinjachinja wa Firauni. Zaidi ya hayo alikuwa hajui anakwenda wapi? Basi akamkimbilia Mola wake, akamwachia Yeye mambo yake na akamwomba kuongoka na kuokoka na Firauni na watu wake.

Alipoelekea upande wa Madyana alisema: Asaa Mola wangu akaniongoza njia iliyo sawa.

Musa alitembea bila ya kujua anakwenda wapi, lakini ana yakini kuwa Mola wake atamwongoza njia iliyo sawa ambayo itampelekea kuokoka na kufaulu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamshika mkono na kumwelekeza Madyana, mji wa Shua’yb, ambao baina yake na Misri pana masafa ya mwendo wa siku nane katika jangwa pana sana.

Basi Musa akakata mbuga kwa tawfiki ya Mwenyezi Mungu. Alikuwa akila mimea ya ardhini. Jana alikuwa ikulu ya Firauni akistarehe. Mimea ya ardhi na hofu ni bora mara elfu kwa wenye ikhlasi kuliko starehe pamoja na dhulma; kama alivyosema Imam Husein(a.s) : “Wallahi! Sioni mauti ila ni wema; na sioni kuishi pamoja na madhalimu ila ni uovu.”

Alipoyafikia maji ya Madayana alikuta umati wa watu wakinywesha (wanyama wao) na akakuta nyuma yao wanawake wawili wanazuia (wanyama wao). Akasema: Mna nini? Wakasema: Hatunyweshi mpaka wamalize hao wachunga na baba yetu ni mzee sana.

Mwendo wa Musa uliishia kwenye kisima. Akakuta kundi la watu waki-wanywesha maji wanyama wao na akawaona wanawake wawili pembeni wakiwa na kondoo wao wanataka kunywa maji, lakini wao wanawazuia.

Musa akashtuliwa na hali hii, akawauliza, kwa nini mnawazuia nao wana kiu? Wakasema sisi ni wanawake dhaifu, hatuwezi kusukumana na wanaume. Tunangoja mpaka wamalize ndio nasi tupate nafasi, na baba yetu ni mzee sana, hawezi kuja kuchota maji. Nafsi ya Musa ikataharaki kidini na kiubinadamu, akawasaidia.

Hakuna ajabu kwa Musa kuwasaidia wanawake dhaifu; wala si ajabu kwa Shua’yb na mabinti zake kuishi kwa jasho lao.

Hii ndiyo sera ya mitume na makhalifa wao wenye takua, tangu zamani na baadaye. Bali ajabu ni kuwa roho hii ya Qur’an haina athari yoyote katika nafsi zetu sisi tunaodai kumjua Mwenyezi Mungu, Kitabu chake, na sera ya mitume wake. Ajabu ya maajabu ni kwamba tunashindana katika kuitafuta dunia na mapambo yake.

Basi akawanyweshea, kisha akarudi kivulini na akasema: Mola wangu! Hakika mimi ni mhitaji wa kheri utakayoniteremshia.

Musa aliwapatia maji wanyama wa wasichana wawili, kisha akaenda chini ya mti kupata kivuli, akiwa na uchovu na njaa. Akamwomba Mwenyezi Mungu fadhila na ukarimu wake. Wala hakung’angania sana au kuomba zaidi, kwa sababu alichokitaka ni kuziba tumbo tu.

Kama angelikuwa anaomba akhera angeling’ang’ania. Katika Nahjul balagha imeelezwa: “Wallahi hakumuomba isipokuwa mkate wa kula tu. Rangi ya kijani ya majani ilikuwa ikionekana kwenye ngozi ya tumbo lake kwa wembamba wake na kutengana na nyama yake.”

Basi mmoja wa wale wanawake wawili akamjia naye anatembea akiona haya. Akasema: Baba yangu anakuita akulipe ujira wa kutunyweshea.

Wale wasichana wawili walirudi kwa baba yao na wakamwelezea yaliyotokea. Basi akamwambia mmoja wao: Nenda kamwite tuje tumlipe hisani yake. Basi akaenda msichana akiwa amegubikwa na haya, ustahi na heshima na kumweleza alivyosema baba yake.

Basi alipomjia na kumsimulia visa vyake, alisema: Usiogope; umekwishaokoka na watu madhalimu.

Musa alikubali mwito, na mzee akamkaribisha na kumshukuru kwa kitendo chake. Musa alipotulia na kumwamini yule mzee, alimsimulia yaliyompitia kwa Firauni na watu wake. Yule mzee akamwambia usihofu, umefika. Hapa kwetu ni ngome ya amani, haifikiwi na Firauni wala mfano wake katika madhalimu.

Wafasiri wametofautiana kuhusu mzee huyu ni nani? Wengi wao wamesema ni Shuaib na wengine wakasema siye. Hakuna ya kutegemewa kwa hawa wala wale. Nasi hatuna haja na tofauti hizi madam hazina uhusiano wowote na imani wala maisha.

Sisi tumechagua jina la Shua’yb kiasi cha kumwelezea huyo mzee tu, sio kuwa tumekubaliana na jina hilo na pia kwa kuwa ni jina liloenea kwa wengi; kama lilivoenea baina ya wanafunzi na ulamaa wa Najaf.

Akasema mmoja katika wale wanawake ambaye alimwita kwa baba yake: Ewe baba! Muajiri huyu. Hakika mbora wa kumwajiri ni mwenye nguvu na mwaminifu.

Tunasema aliyesema ni yule aliyemwita kutokana na kauli yake ‘mwenye nguvu’ pale alipowasaidia kuchota maji na ‘mwaminifu’ pale alipokuwa na staha wakati wakielekea kwa baba yake.

Akasema: Mimi ninataka kukuoza mmoja wa mabinti zangu hawa wawili kwa kunifanyia ajira ya miaka minane na kama ukitimiza kumi hiyari yako. Mimi sitaki kukutaabisha. Inshaallah utanikuta miongoni mwa watu wema.

Musa mkimbizi, fukara asiyekuwa na chochote, ambaye kwa siku kadhaa, ameishi kwa kula mimea ya ardhi; mpaka akamuomba Mola wake tonge ya kumwezesha kuishi, leo anahiyarishwa kuchagua mke amtakaye. Bila shaka hapa kuna siri ya utu wa Musa na utukufu wake uliomgusa mzee na mabinti zake. Vile vile katika masimulizi yake na sera yake kwa Firauni na watu wake.

Mzee alitambua, kutokana na akili yake safi, kwamba mtu huyu atakuwa na athari ya mbali. Kwa sababu matendo ya mtu aghlabu yanatoka kwenye chimbuko moja. Kwa hiyo mzee, hapa alifuzu kutokana na ukwe huu. Kuna faida gani kubwa zaidi ya kuwa mkwe wa Mtume na mwenye takua.

SHARIA YA KIISLAMU IMEFUTA SHARIA ZOTE

Mafaqihi wamezungumza mengi kuhusiana na Aya hii, wakaitolea dalili kuwa walii wa mwanamke ndiye atakayetamka tamko la ndoa. Lakini ilivyo ni kuwa inafaa kwa mwanamume au mwanamke mwenyewe kutam- ka. Hilo linafahamika kimsingi bila ya kuhitaji nukuu. Shafii na Imamiya wamesema kuwa ndoa haifungiki isipokuwa kwa tamko la ziwaj na nikah. Hii ni baada ya kuiunganisha Aya hii, yenye tamko la nikah, na ile yenye tamko la ziwaj.

فَلَمَّا قَضَىٰ زَيْدٌ مِّنْهَا وَطَرًا زَوَّجْنَاكَهَا ﴿٣٧﴾

“Basi Zaid alipokwisha haja naye tulikuoza wewe” (33:37).

Malik na Hambal wakasema pia ndoa inafungika kwa neno hiba, kutokana na Aya yenye neno hiba:

وَامْرَأَةً مُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلنَّبِيِّ ﴿٥٠﴾

“Na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii.” (33:50).

Hanafi naye akasema kuwa ndoa inafungika kwa neno lolote linalofahamisha kutaka kuoana.

Mafaqihi wengi wamesema kuwa muda wa kuchunga wanyama miaka minane au kumi haukuwa mahari au sehemu yake. Bali mahari yalikuwa mbali; na kwamba kauli ya mzee: “kunifanyia ajira” maana yake ni kuwa ukichunga wanyama kwangu kwa ajira, nitakuoza mmoja wa mabinti zangu kwa mahari; sawa na kusema: ‘Ukifanya hivi nami nitafanya hivyo.’

Haya ndio maana sahihi ya Aya. Kwa vyovyote iwavyo, hakuna hoja yoyote, katika Aya hii kwa, waliyoyasema mafaqihi. Kwa sababu hizo ni simulizi za sharia zilizotangulia. Nasi tuna uhakika kwamba sharia ya Kiisalmu imefuta sharia zote zilizotangulia, wala haifai kutumia hukumu yoyote miongoni mwa hukumu hizo zilizotangulia, isipokuwa kwa dalili maalum au ya kiujmla kutoka katika Kitab au Sunna. Na hapo itakuwa ni kukitumia Kitab au Sunna, sio kuitumia sharia hiyo.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ ﴿٣٨﴾

“Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote.” Juz. 7 (6:38).

Na kauli yake:

وَنَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ تِبْيَانًا لِّكُلِّ شَيْءٍ ﴿٨٩﴾

Na tumekuteremshia Kitabu hiki kubainisha kila kitu.” Juz.14: (16:89),

Yaani kila kitu katika misingi ya kiislamu na sharia yake.

Mtume(s.a.w.w) naye anasema: “Hakuna kitu kitakachowakurubisha nyinyi Peponi isipokuwa nimewaamrisha, na hakuna kitu kitakachowaweka mbali na moto isipokuwa nimewakataza.”

Akasema: Hayo yamekwishakuwa baina yangu na yako. Muda wowote kati ya miwili nitakoumaliza nisifanyiwe ubaya na Mwenyezi Mungu ni wakili juu ya haya tunayoyasema.

Haya ni maneno ya Musa. Muda wa kwanza ni Hijja nane na wa pili ni Hijja kumi. Maana ni kuwa Musa alimwambia mzee, nimekubali na kuridhia kuoa na kuchunga wanyama.

Mimi nitakuwa na hiyari ya kumaliza nane au kumi. Muda wowote nitakaoumaliza basi usiwe na hoja kwangu na Mwenyezi Mungu ndiye shahidi juu ya haya uliyojiwajibishia na niliyojiwajibishia.

Kuna Hadith isemayo kuwa Musa alichagua muda wa kumi. Wafasiri wengi wanasema kuwa yeye alimchagua mdogo naye ndiye aliyesema, baba yangu anakuita. Na pia kumwambia baba yake, hakika yeye ana nguvu na ni mwaminifu.


4

5

6

7

8

9

10

11