TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE Juzuu 4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE27%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18056 / Pakua: 4424
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA NNE Juzuu 4

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿أَوَلَمَّا أَصَابَتْكُم مُّصِيبَةٌ قَدْ أَصَبْتُم مِّثْلَيْهَا قُلْتُمْ أَنَّىٰ هَـٰذَا قُلْ هُوَ مِنْ عِندِ أَنفُسِكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾

165.Hivi mlipopata msiba - na nyinyi mmekwisha watia mara mbili yake - mnasema: imekuaje? Waambie hayo yanatokana na nyinyi wenyewe. Hakika Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu.

﴿وَمَا أَصَابَكُمْ يَوْمَ الْتَقَى الْجَمْعَانِ فَبِإِذْنِ اللَّـهِ وَلِيَعْلَمَ الْمُؤْمِنِينَ ﴾

166.Na yaliyowasibu siku ya kukutana makundi mawili ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na ili wajue waumini.

﴿وَلِيَعْلَمَ الَّذِينَ نَافَقُوا وَقِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا قَاتِلُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أَوِ ادْفَعُوا قَالُوا لَوْ نَعْلَمُ قِتَالًا لَّاتَّبَعْنَاكُمْ هُمْ لِلْكُفْرِ يَوْمَئِذٍ أَقْرَبُ مِنْهُمْ لِلْإِيمَانِ يَقُولُونَ بِأَفْوَاهِهِم مَّا لَيْسَ فِي قُلُوبِهِمْ وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا يَكْتُمُونَ﴾

167.Na ili awajue wale ambao walifanya unafiki, na wakaambiwa njooni mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu au mjikinge. Wakasema: Lau tungelijuwa ni vita tungeliwafuata, wao siku ile walikuwa karibu na ukafiri kuliko imani. Wanasema kwa midomo yao yale yasiyokuwa nyoyoni mwao, Na Mwenyezi Mungu anayajua vizuri wanayoyaficha.

﴿الَّذِينَ قَالُوا لِإِخْوَانِهِمْ وَقَعَدُوا لَوْ أَطَاعُونَا مَا قُتِلُوا قُلْ فَادْرَءُوا عَنْ أَنفُسِكُمُ الْمَوْتَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴾

168.Wale waliosema kuhusu ndugu zao na wao wakiwa wamebaki nyuma: Lau wangelitutii wasingeuawa. Sema jizuilie na mauti (msife) ikiwa mnasema kweli.

ULIPOWAFIKA MSIBA

Aya 165-168

MAANA

Hivi mlipopata msiba - na nyinyi mmekwisha watia mara mbili yake - mnasema: imekuaje?

aani, ulipowapata msiba siku ya vita vya Uhud na nyinyi mlikwisha watia msiba zaidi ya huo siku ya Badr, mnasema imekuaje, na sisi tunapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu? Kwa ufafanuzi zaidi, ni kwamba vita vya Badr vilikuwa mwaka wa tatu. Katika Badr, waislamu walipata ushindi kwa kuwaua washirikina sabini na kuwateka sabini. Vilevile waislamu walipata ushindi katika sehemu ya kwanza ya vita vya Uhud, na wakapata hasara sehemu ya pili, kwa sababu wapiga mishale walikhalifu amri ya Mtume(s.a.w.w) , hapo waislamu sabini wakauawa. Tukilinganisha ushindi wa Waislamu siku ya Badr na ushindi wa washirikina siku ya Uhud, tunapata kuwa Waislamu ni mara mbili zaidi, kwa sababu maiti sabini kwa sabini. Waislamu wanabaki na mateka sabini Sasa kwa nini wanafiki na baadhi ya waislamu washikwe na mshangao kiasi hiki? Tena pamoja na kuuliza wameshindwaje na washirikina, na wao ni maadui wa Mwenyezi Mungu. Kwa nini basi wanafiki wanasahau ushindi wa Badr ambao ulikuwa zaidi?

Waambie: hayo yanatokana na nyinyi wenyewe.

Hili ni jawabu la kauli yao: 'Imekuaje'? maana yake nyinyi ndio sababu ya yaliyowapata, Mtume alionelea kuwa watu wabaki Madina wasitoke, lakini mkakataa. Na mlipotoka, akawalazimisha mbakie sehemu alizowapangia, mkaondoka kwa sababu ya tamaa. Kwa ufupi ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hayo yanatokana na nyinyi wenyewe". Ni sawa na kauli yake:

﴿ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيكُمْ وَأَنَّ اللَّـهَ لَيْسَ بِظَلَّامٍ لِّلْعَبِيدِ﴾

"Hayo ni kwa sababu ya yaliyotangulizwa na mikono yenu na kwamba Mwenyezi Mungu si mwenye kuwadhulumu waja." (3:182)

Na yaliyowasibu siku ya kukutana makundi mawili, ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya 'siku' ni 'siku ya Uhud,' 'makundi mawili', ni waislamu na washirikina, na makusudio ya neno 'idhini' ya Mwenyezi Mungu, ni kujua kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu, kama alivyolitumia Mwenyezi Mungu neno hilo kwa maana ya kujua katika (2:179)

wala haijuzu kuwa makusudio ya idhini iwe kuhalalisha kwa sababu Mwenyezi Mungu hawahalalishii makafiri kuwaua waislamu.

Na ili Mwenyezi Mungu awajue waumini na ili awajue wanafiki.

Yaani, masaibu ya Uhud yalikuwa na faida, kama vile kudhihirisha elimu yake Mwenyezi Mungu, kuwa watu watambue imani ya waumini na unafiki wa wanafiki. Wanafiki kabla ya tukio la Uhud hawakuwa wakijulikana wala kutofautiana na waumini. Kwenye tukio hilo walijulikana, kwa hiyo makusudio ya elimu ya Mwenyezi Mungu hapa ni kudhihirisha elimu yake ijulikane kwa wengine, Sio kwamba yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu alipata kujua baada ya tukio la Uhud; Kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua mambo kabla ya kutukia kwake, Maelezo ya Aya yameshatangulia katika kufasiri Aya ya 141 ya Sura hii.

Wakaambiwa njooni mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu au mjitetee.

Mwenyezi Mungu hubainisha nani aliyeyasema hayo kwa wanafiki. Kwa sababu yeye ameleta kauli kwa tamko la mbali na si kwa majina. Lakini wafasiri wengi wamesema kuwa Abdullah bin Ubayya alitoka pamoja na Mtume(s.a.w.w) siku ya Uhud akiwa na wapiganaji 300. Walipofika katikati ya njia Abdallah alirudi na genge lake akakataa kupigana. Alifanya hivyo kwa ajili ya kuwavunja nguvu wengine wasipigane vita. Abdullah (babake Jabir Ansari) akawauliza: "Kwa nini mnarudi nyuma? Mkiwa na dini basi piganieni dini yenu.

Haya ndiyo maana ya; 'mpigane katika njia ya Mwenyezi Mungu' Na kama hamna dini, basi mzitetee nafsi zenu, watu wenu na mali zenu. Haya ndiyo maana ya 'au mjitee' Watu wa historia pia wametaja kujitoa huku kwa bin Ubayya na watu wake na kauli ya Abdullah. Na tamko la Aya linafungumana na kitendo chao, Lakini haikutaja majina ya waliofanya wala jina la msemaji. Kwa vyovyote itakavyokuwa lakini wanafiki walijibu kauli ya mumini na wakasema:"Lau tungelijua ni vita bila shaka tungeliwafuata" Yaani, kwamba Waislamu na washirikina hawatapigana, lau tungelihakikisha kuwa watapigana, basi tungelipigana pamoja na nyinyi. Wengine wanasema kwamba makusudio ya jibu hilo la wanafiki ni kwamba kukabiliana na washirikina sio kupigana, bali ni kujipeleka machinjioni kwa sababu ya idadi kubwa ya maadui. Tamko la Aya linakubali maana zote mbili, lakini maana ya kwanza iko karibu zaidi na tamko la Aya.

Wao siku ile walikuwa karibu zaidi na kufuru kuliko imani.

Yaani, wanafiki waliposema lau tungelijua ni vita tungeliwafuata, walikusudia kuficha unafiki wao na kujiepusha na tuhuma. Lakini kauli yao ndiyo inayofahamisha zaidi unafiki wao, na ni kauli ya kuwasaidia washirikina; kwa sababu inafuata maslahi yao kutokana na inavyowavunja nguvu waliokuwa pamoja na Mtume(s.a.w.w) .Wanasema kwa midomo yao lau tungelijua ni vita tungeliwafuata yale yasiyokuwa nyoyoni mwao bali ni uongo na unafiki.Na Mwenyezi Mungu anajua vizuri wanayoyaficha ambayo ni kumkufuru Mwenyezi Mungu na kumkanusha Mtume wake. Imam Ali(a.s) anasema "Ulimi wa Mu'min uko nyuma ya moyo wake na moyo wa mnafiki uko nyuma ya ulimi wake," Yaani, kauli ya Mu'min ni kioo cha yaliyo moyoni mwake, kwa sababu yeye husema kile anachokiamini. Ama mnafiki ulimi wake uko mbali na moyo wake na ulimi wake unafuata maslahi yake tu, na kutengeneza maneno vile yanavyotaka maslahi yake.

Wale waliosema kuhusu ndugu zao na wao wakiwa wamebaki nyuma, "Lau: wangelitutii wasingeuawa."

Yaani, wanafiki walisema lau wale waliouawa siku ya Uhud wangelitufuata sisi wakabaki, asingeliuawa yeyote, kama vile ambavyo sisi tumebaki. Yameshatangulia maelezo yake katika tafsir ya Aya ya 156 ya Sura hii.

Sema: Jizuilieni na mauti (msife) ikiwa mnasema kweli.

Hapana! Hakuna anayeweza kuyakimbia mauti wala hayamwachi yanayemtaka.

Imam Ali(a.s) amesema:"Mauti yanafuata, hayamkosi aliyekaa wala hayamshindi mwenye kuyakimbia, mauti ya utukufu ni kuuliwa, Naapa kwa ambaye nafsi ya mwana wa Abu Talib iko mikononi mwake, mapigo elfu kwangu si chochote kuliko kufa kitandani"

﴿وَلَا تَحْسَبَنَّ الَّذِينَ قُتِلُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أَمْوَاتًا بَلْ أَحْيَاءٌ عِندَ رَبِّهِمْ يُرْزَقُونَ﴾

169.Na usiwadhanie kabisa wale waliouawa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa wamekufa, bali wako hai mbele ya Mola wao wanaruzukiwa.

﴿فَرِحِينَ بِمَا آتَاهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ وَيَسْتَبْشِرُونَ بِالَّذِينَ لَمْ يَلْحَقُوا بِهِم مِّنْ خَلْفِهِمْ أَلَّا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴾

170.Wanafurahia aliyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake, na wanawashangilia wale ambao hawajajiunga nao, walio nyuma yao, ya kwamba haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

﴿يَسْتَبْشِرُونَ بِنِعْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ وَفَضْلٍ وَأَنَّ اللَّـهَ لَا يُضِيعُ أَجْرَ الْمُؤْمِنِينَ ﴾

171.Wanashangilia neema na fadhila za Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa waumini.

WAKO HAI MBELE YA MOLA WAO WAKIRUZUKIWA

Aya 169-171

MAANA

Na usiwadhanie kabisa wale waliouawa katika njia ya Mwenyezi Mungu kuwa wamekufa, bali wako hai mbele ya Mola wao wanaruzukiwa.

Anayeambiwa 'usiwadhanie' ni kila mwenye akili. Makusudio ya waliouwawa wako katika njia ya Mwenyezi Mungu, ni kila aliyeuawa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu; ni sawa awe amekuwa shahidi mbele za Mtume, kabla yake, au baada yake. Dhahiri ya Aya ni kwamba mashahidi wako hai hivi sasa, na wala sio kuwa watakuwa hai pamoja na wengine siku ya ufufuo. Na wao wako hai kihakika, sio kimajazi, kama kutajwa vizuri n.k. Hii ndio dhahiri ya Aya, na yapasa kuitegemea, Kwa sababu hakuna la kuwajibisha kutafuta maana nyingine, maadam uhai uko mikononi Mwenyezi Mungu Mtukufu anampa amtakaye wakati wowote autakao. Wala hatujui dini au Umma uliotukuza mashahidi katika njia ya haki na uadilifu kama uislamu. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema:"Kuchwewa na jua na kupambaukiwa ukiwa katika njia ya Mwenyezi Mungu ni bora kuliko dunia na vilivyo ndani yake." Na akasema:"Pepo iko kwenye ncha za mikuki." Ambayo itamaliza dhulma, shari na batili.

Ama wale wanaokufa shahidi katika njia ya haki, wao na haki ni sawa katika mtazamo wa kiislamu, kwa sababu mwenye kuutoa uhai wake kwa ajili ya haki, utakatifu wake ni utakatifu wa haki yenyewe.

Wanafurahia aliyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake

Furaha yao ya fadhila hizi iko mara mbili.

Kwanza : Kwa kuwa wao wanastarehe kwa fadhila hiyo.

Pili : Kwamba hili linafahamisha radhi ya Mwenyezi Mungu kwa wale waliojitolea uhai wao kwa ajili yake, sawa na zawadi ya mpenzi inayofahamisha upendo wake.

Na wanawashangilia wale ambao hawajajiunga nao, walio nyuma yao, ya kwamba haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika.

Kila Mumin anampendelea ndugu yake katika imani lile analolipendelea nafsi yake, lakini kwa sababu ya matatizo na kwa sababu fulani huenda mtu asifikie makusudio. Lakini wale waliokufa shahid katika njia ya Mwenyezi Mungu, wanao ndugu katika imani wanaowajua kwa majina wakiwa na iman na ikhlas kama wao, nao wamewaacha bado wako hai. Basi mashahidi watakapoona fadhila za Mwenyezi Mungu kwao, watafurahi na watashangilia kutokana na waliyoyapata, vilevile kwa ajili ndugu zao wanafuata njia yao katika iman, ikhlas na jihadi. Mashahidi Watashangilia kwa sababu, ndugu zao walio hai watapata kama waliyoyapata wao miongoni mwa fadhila na karama. Aya hii ni dalili ya wazi kwamba mashahidi wako hai kabla ya siku ya kiama kwa sababu kushangilia kwao ndugu zao walio hai kumekwishapatikana, na wala sio kuwa kutapatikana kesho.

Wanashangilia fadhila na neema za Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa waumini.

Unaweza kuuliza : kwa nini limerudiwa neno kushangilia na fadhila?

Jibu : Mashahidi wana furaha tatu:

Furaha ya kwanza : ni kwa yale waliyoyapata wao, kulikoelezwa na kauli yake Mwenyezi Mungu. Wanafurahia aliyowapa Mwenyezi Mungu kutokana na fadhila zake. Furaha ya

Furaha ya pili : ni kwa ajili ya ndugu zao wanaowajua ambao watajiunga nao, kama linavyoonyeshwa hilo na kauli yake Mwenyezi Mungu. "Na wanawashangilia wale ambao hawajajiunga nao."

Furaha ya tatu : ni kwa ajili ya kila Mumini wanayemjua na wasiyemjua shahidi na asiye shahidi. Hilo linaelezwa na kauli yake Mwenyezi Mungu: "Wanashangilia neema za fadhila za Mwenyezi Mungu." Linalotilia nguvu kuwa furaha hii ni kwa ajili ya waumini wote, ni kauli yake Mwenyezi Mungu:"Na Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa waumini."

Swali la pili : Mwenyezi Mungu ameunganisha fadhila na neema: na kuunganisha kunamaanisha tofauti. Tunavyoona sisi ni kwamba hakuna tofauti, sasa tofauti ni ipi hiyo?

Razi amejibu kuwa, neema ni thawabu na ujira anaostahiki mtenda amali kuwa ni malipo ya amali yake. Na fadhila ni ziada (Bahashishi) anayoitoa Mwenyezi Mungu kwa ukarimu sio kwa kustahiki. Jibu hili la Razi halifungamani na chochote, isipokuwa kupendelea tu kuwepo tofauti. Tunavyoona sisi ni kwamba hakuna tofauti yoyote kati ya kusema: "Amenineemesha" na kusema: "Amenifadhili." Ilivyo hasa ni kwamba misamiati inaungana na kutofautiana tamko tu, kunatosha. Kuungana huku kunaitwa 'muungano wa tafsir' (Atfu Tafsir)

﴿الَّذِينَ اسْتَجَابُوا لِلَّـهِ وَالرَّسُولِ مِن بَعْدِ مَا أَصَابَهُمُ الْقَرْحُ لِلَّذِينَ أَحْسَنُوا مِنْهُمْ وَاتَّقَوْا أَجْرٌ عَظِيمٌ﴾

172.Wale waliomwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume baada ya majeraha yaliyowapata; kwa waliofanya wema na kumcha Mwenyezi Mungu wana ujira mkubwa.

﴿الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ﴾

173.Wale ambao waliambiwa na watu: Hakika watu wamewakusanyikia kwa hivyo waogopeni. Lakini yakawazidishia imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha na bora ya mwenye kutegemewa ni Yeye.

﴿فَانقَلَبُوا بِنِعْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ وَفَضْلٍ لَّمْ يَمْسَسْهُمْ سُوءٌ وَاتَّبَعُوا رِضْوَانَ اللَّـهِ وَاللَّـهُ ذُو فَضْلٍ عَظِيمٍ ﴾

174.Basi wakarudi na neema za Mwenyezi Mungu na fadhila haukuwagusa ubaya na wakafuata radhi ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.

﴿إِنَّمَا ذَٰلِكُمُ الشَّيْطَانُ يُخَوِّفُ أَوْلِيَاءَهُ فَلَا تَخَافُوهُمْ وَخَافُونِ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴾

175.Hakika huyo ni shetani, anawatia hofu marafiki zake, basi msiwaogope na niogopeni Mimi, ikiwa nyinyi ni waumini.

WALIOMWITIKIA MWENYEZI MUNGU

Aya 172-175

MAANA

Wale waliomwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume baada ya majeraha yaliyowapata, kwa waliofanya wema na kumcha Mwenyezi Mungu wana ujira mkubwa.

Inaelezwa katika vitabu vya Sera na Tafsir kuwa washirikina walipomaliza vita vya Uhud, walipokuwa wakirudi Makka, njiani walirudia kufikiria, wakajuta na kulaumiana. Wakaambiana: "Hatukuwamaliza Waislamu, kwa hiyo wataungana tena na watarudia mara nyingine tena." Hapo wakaazimia kumrudia Muhammad(s.a.w.w) , ili kumpiga vita, Mtume aliposikia hilo, alirudia kuwapanga watu wake haraka. Mpigaji mbiu akanadi, "Asitoke na sisi yeyote isipokuwa yule tuliyokuwa naye jana!" Hapo wakakusanyika waislamu wakiwamo waliojeruhiwa, wakaenda kupiga kambi sehemu ya Hamraul Asad, kiasi cha maili nane kutoka Madina, wakimngoja Abu Sufian na wenzake. Mkusanyiko huo ulifaulu, kwa sababu washirikina walipojua kuwa waislamu wamejikusanya upya, waliogopa na wakarudi Makka haraka sana. waislamu wakarudi Madina wakiwa na nguvu kwa upande fulani.

Wale ambao waliambiwa na watu: Hakika watu wamewakusanyikia, kwa hivyo waogopeni. Lakini yakawazidishia imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha na bora ya mwenye kutegemewa ni yeye.

Makusudio ya neno 'watu' la kwanza ni wale waliorudi wasiende vitani pamoja na Mtume(s.a.w.w) hao ndio waliowambia waumini waliotakiwa na Mtume(s.a.w.w) kupambana na washirikina kwa mara ya pili "Watu wamekusanyika, kwa hivyo waogopeni." Na makusudio ya neno 'watu' la pili ni washirikina waliojaribu kuwarudia waislamu. Maana ni kuwa waumini pamoja na majeraha yao mabichi, lakini waliitika wito wa Mtume(s.a.w.w) wa kukabiliana na Abu Sufian na jeshi lake bila ya kuwasikiliza wale waliowatia woga, Waliowaambia kuwa msitoke na Muhammad kwa sababu adui ana nguvu zaidi yenu. Badala yake kauli hii iliwazidishia imani kwa Mwenyezi Mungu na kuwa na imani na miadi yake, wakaendelea kumtii Mtume(s.a.w.w) na kutaka kupigana na adui potelea mbali itakavyokuwa, kwa kusema: "Mwenyezi Mungu anatutosha na bora ya mwenye kutegemewa ni yeye." Hivi ndivyo unavyokuwa msimamo na mshikamano wa mumini pamoja na imani yake, Haogopi kifo, kutekwa nyara au kuadhibiwa. Mtu mmoja wa ukoo wa Abdulash- hal anasema: "Mimi na ndugu yangu tulikuwa katika vita vya Uhud na kujeruhiwa. Mwito wa Mtume(s.a.w.w) wa kutoka ulipotolewa, tulitoka pamoja na Mtume. Jeraha langu lilikuwa nafuu kuliko la ndugu yangu kwa hiyo akibaki nyuma nilikuwa nikimbeba"

Basi wakarudi na neema za Mwenyezi Mungu na fadhila, haukuwagusa ubaya na wakafuata radhi ya Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.

Waumini walitoka pamoja na Mtume hadi Hamral-Asad, kama walivyoamriwa lakini hawakupata lolote kutoka kwa adui. Hiyo ndiyo maana ya kusema: Haukuwagusa na ubaya" Kwa sababu adui alipojua kuwa wamejikusanya tena, aliogopa na kurudi.

Baada ya adui kurudi, Waislamu wakarudi kwao na neema nyingi za Mwenyezi Mungu zikiwa ni salama, twa'a ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kumtisha adui. Kuna neema gani inayolingana na kutukuzwa na Mwenyezi Mungu na kusajiliwa fahari hii katika Lawh Mahfudh na katika Kitabu chake ambacho wanakisoma watu duniani hadi siku ya ufufuo?

Hakika huyo ni shetani anawatia hofu marafiki zake, basi msiwaogope na niogopeni Mimi, ikiwa nyinyi ni waumini.

Kila anayemtii Mwenyezi Mungu, basi ni katika vipenzi vya Mwenyezi Mungu, na kila anayemwitikia shetani, basi ni katika marafiki zake. Mwenyezi Mungu anawaamrisha na anawakataza shari na kuwahadharisha nayo. Ama shetani yeye ni kinyume. Anawaamrisha nayo na anawakataza mema na kuwahofisha nayo, mfasiri Muhammad bin Ahmad Al-Kalabiy anasema katika Tafsir Tashil, makusudio ya shetani hapa ni Abu Sufian au aliyetumwa na Abu Sufian au Iblis. Kauli ya aliyewaambia waumini "Hakika watu wamekusanyikia" Inatokana na mawazo ya shetani na kuhofisha kwake, Hakuna anayemsikiza isipokuwa rafiki zake wanaomtii. Ama wapenzi wa Mwingi wa rehema, kauli hii huwazidishia imani kwa kupigana jihadi na kujitolea mhanga kwa ajili ya uislamu na Mtume wa Uislamu.

Hayo ndiyo maana ya 'shetani anawatia hofu marafiki zake' Ama marafiki wa Mwenyezi Mungu hawamwogopi shetani akiwahofisha. Na maana ya msiwaogope, ni msiwaogope washirikina kwa sababu wao ni marafiki wa shetani wenye kuogopewa kwa kuwapa sifa ya nguvu, ili wapate nafasi ya kueneza ufisadi duniani, Na Mu'min hamuogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu.

SHETANI NI OMBAOMBA NA NI HODARI

Shetani ana majina mengi, kama: mlaaniwa, mwenye kuwekwa mbali na rehma, mpotevu na mpotezaji. Unaweza kumwita ombaomba, kwa sababu yeye husimama kwenye mlango wa moyo kwa kutia huruma na kubisha pole pole akitaka idhini ya kuingia, ukichelewa kumfungulia, hukuomba kwa unyenyekevu na maneno matamu ya kukufanya umfungulie japo kidogo. Ukifanya hivyo tu huingia na kuanza kukutolea hadaa na upotevu kutoka mfukoni mwake. Hapo ataanza kuufinika uhakika na kukubabaisha, na kuupamba uovu na kuufanya uonekane mzuri. Vilevile ataleta sura ya kazi njema kuwa mbaya, kupigania kuondoa batili kuwa kufuru, maovu kuyafanya mema na mema kuyafanya maovu. Pia atamvisha mhaini nguo ya mwema na mwenye ikhlas atamvisha nguo ya mfisadi, na mengineyo yenye hila na upotevu. Njia kubwa anayoitumia kufikia malengo yake ni kutengeneza hofu kwa kuleta nguvu za marafiki zake ambao ndio watekelezaji wa miradi yake. Shetani ni fundi aliye hodari. Ama nguvu zake za utekelezaji ni wafuasi wake ambao wanaeneza ufisadi duniani. Kwa ajili hii anawakuza na kuwatengenezea njia ya utekelezaji na kuwavisha kivazi cha utukufu na cheo, ili wasiwe na sauti au fikra yoyote ya kujitoa, usije ukadhoofika utawala wake na kukatika matarajio yake, shari na ufisadi wake kwa kuondoka athari yao.

Kwa ufupi ni kwamba kila anayewaogopa watu wa ufisadi na wapotevu lakini akapatana na mmoja wao, basi atakuwa amepatana na upotevu wenyewe na atakuwa amesaini mkatataba wa mapenzi na udugu kati yake na shetani. Hiki ni kipimo kisichokosea kabisa katika kumpambanua mwenye kulingania kumwamini Mwenyezi Mungu na kumwogopa Yeye tu, na yule mwenye kumtawalisha shetani na kuathirika na twa'a yake, wala hakuna kitu kinachofahamisha uhakika huu kuliko kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t), 'msiwaogope na niogopeni Mimi,' ikiwa nyinyi ni waumini. Kwani maana yake ni kwamba mwenye kuacha kuwapiga jihadi wafisadi na wapotevu kwa kuwaogopa, basi yeye ni katika marafiki wa shetani na wala hana chochote kwao. Aya hii iko karibu na kauli ya Mtume Mtukufu(s.a.w.w) "Mwenye kuinyamazia haki ni shetani bubu."

﴿وَلَا يَحْزُنكَ الَّذِينَ يُسَارِعُونَ فِي الْكُفْرِ إِنَّهُمْ لَن يَضُرُّوا اللَّـهَ شَيْئًا يُرِيدُ اللَّـهُ أَلَّا يَجْعَلَ لَهُمْ حَظًّا فِي الْآخِرَةِ وَلَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾

176.Wala wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia ukafiri, Hakika wao hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu anataka asiwawekee fungu lolote huko akhera, Nao wana adhabu kubwa.

﴿إِنَّ الَّذِينَ اشْتَرَوُا الْكُفْرَ بِالْإِيمَانِ لَن يَضُرُّوا اللَّـهَ شَيْئًا وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴾

177.Hakika wale walionunua ukafiri kwa imani, hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu na wana adhabu iumizayo.

﴿وَلَا يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا أَنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ خَيْرٌ لِّأَنفُسِهِمْ إِنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ لِيَزْدَادُوا إِثْمًا وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴾

178.Wala wasidhanie kabisa wale waliokufuru kwamba muda tunaowapa ni heri kwa nafsi zao. Hakika tunawapa muda na wanazidi tu katika dhambi na wana adhabu idhalilishayo.

WANAOKIMBILIA UKAFIRI

Aya 176-178

MAANA

Wala wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia ukafiri, hakika hao hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu.

Yametangulia maelezo kuwa washirikina walikusanya makundi, wakaandaa jeshi la kumpiga vita Mtume(s.a.w.w) na wanafiki walikuwa wakiwasaidia na wakiwapangia njama waislamu. Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewataja wanafiki na washirikina kuwa ni waasi na wanafanya bidii kuipinga haki na kuipiga vita. Na Mtume(s.aw.w) alikuwa akihuzunika na kuona uchungu kutokana na vitendo vyao hivi. Ndipo Mwenyezi Mungu Mtukufu akamwambia: Usihuzunike, wao hawatakudhuru na chochote wewe, wala Waislamu na dini ya Mwenyezi Mungu, na kwamba njama zao hizo zitapotea tu. Ama dini itakuwa na utukufu. Na kweli hazikupita siku nyingi Mwenyezi Mungu akaumakinisha uislamu Mashariki na Magharibi kwa watu ambao jana walikuwa wakikimbilia kuupiga vita.

Mwenyezi Mungu anataka asiwawekee fungu lolote huko akhera. Nao wana adhabu kubwa.

Huu ndio ukweli wa kila mwenye kuendelea na upotevu mpaka akafa.Unaweza kuuliza : kuwa dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa shari inatokana na Mwenyezi Mungu, kwa sababu, adhabu ya Jahannam ni shari, na Mwenyezi Mungu amewatakia hiyo adhabu, itakuwaje?

Jibu : ni kweli kuwa Mwenyezi Mungu amewatakia adhabu, lakini ni baada ya kustahili, kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaamrisha kuamini na akawakataza kukufuru na akawaachia hiyari. Hivyo wakachagua ukafiri badala ya imani. Maana yake ni kwamba washirikina na wanafiki ndio waliosababisha adhabu. Baada ya wao kusababisha kwa hiyari yao, ndipo Mwenyezi Mungu akawatakia adhabu sawa na hakimu anayemtakia kifungo mwenye hatia baada ya kufanya makosa.

Hakika wale walionunua ukafiri kwa imani, hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu.

Neno:'walionunua' linafahamisha hiyari. Kwa sababu mnunuzi anachagua bidhaa na kuridhia anachokichukua badala ya thamani. Na kafiri ameridhia ukafiri badala ya imani, ndipo akastahili adhabu kali.

Unaweza kuuliza : kwa nini Mwenyezi Mungu amelikariri neno'hawatamdhuru Mwenyezi Mungu kitu' katika Aya mbili, kuna siri gani?

Jibu : makusudio ya Aya ya kwanza ni makafiri wa kiquraishi walioandaa jeshi la kumpiga Mtume(s.a.w.w) na wale wanafiki waliokuwa wakiwasaidia. Aya ya pili, makusudio yake ni kila kafiri kuanzia wa mwanzo hadi wa mwisho, awe mpiga vita au la. Kwa hiyo Aya ya kwanza inakuwa ni mahsusi, na ya pili ni kutaja kiujumla. Mara nyingi inakuwa hivi katika maneno ya watu ambao husema "Fulani amecheza kamari akajimaliza na kila mwenye kufanya hivyo ataangamia"

Wala wasidhanie kabisa wale waliokufuru kwamba muda tunaowapa, ni heri kwa nafsi zao. Hakika tunawapa muda na wanazidi tu katika (kufanya) dhambi na wana wao adhabu idhalilishayo.

Umri wa mtu ni kama mali yake, akiitumia vizuri yeye, kwa watu wake na pia kwa watu wengine au jamaa zake wanaohitaji, basi atarudiwa na heri na wema. Kila mali yake inapozidi ndiyo kunavyozidi kutoa kwake na ndipo wema wake unavyozidi. Na kama akiitumia vibaya na kuitoa katika maasi, basi humrudia mabaya, na kila inavyozidi na kukuwa ndivyo anavyozidi uasi na ufisadi. Umri nao ni hivyo hivyo. Mtu hufikilia wema kama akifanya amali nzuri na unakuwa ni sababu ya uovu wake, kama akifanya uovu. Hiyo ndiyo desturi ya Mungu kwa kijamii. Kila desturi iliyozoeleka inayojulikana kimaumbile au kijamii, basi ni desturi ya Mwenyezi Mungu katika viumbe vyake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amepitisha desturi yake kwa makafiri na watu wote. Amewapa muda kwa kurefusha umri ili mtu ajichagulie mwenyewe, kheri au shari. Lakini kafiri akaghurika kwa kupewa muda na akajiachia katika upotevu. Kwa hiyo ikawa natija ya kupewa kwake muda, ni uovu wake na adhabu yake. Kinyume na Mumini, Mwenyezi Mungu akichelewesha ajali yake kheri yake huzidi na wema huwa mwingi. Bali mwenye kufanya wema katika sehemu iliyobakia katika umri wake, hataadhibiwa kwa dhambi zake zilizopita, kama ilivyoelezwa katika Hadith tukufu. Kwa hali hiyo basi, inatubainikia kuwa herufi Lam katika neno liyazdaadu ni ya mwishilio, sio ya sababu, yaani wanazidi tu na sio 'ili' wazidi.

KAFIRI NA AMALI NJEMA

Unaweza kuuliza : baadhi ya makafiri hufanya kheri kwa ajili ya kheri, na kila umri wao unavyozidi ndivyo wanavyozidi kuwanufaisha watu kwa elimu zao na juhudi zao zilizo nzuri kabisa. Je, hii haipingani na kauli yake Mwenyezi Mungu, na wanazidi tu, katika dhambi?

Jibu : mfumo wa Aya unakusudia dhambi tu, na kuwa wao kwa upande huu wanazidi ukafiri, na wala sio katika hali zote, kwani huenda wakawa ni wema katika baadhi ya matendo yao.

Swali la pili : Je kafiri akifanya wema na kuwanufaisha watu, atapata thawabu, au wema wake huo ni sawa na kutofanya chochote?

Jibu : mtu kwa mtazamo wa imani na matendo (amali), atakuwa katika mojawapo ya hali nne zifuatazo: -

1. Kuamini na kutenda amali njema, hali hii inafuatana na kauli ya Mwenyezi Mungu:

﴿إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ﴾

"Hakika wale wanaosema mola wetu ni Mwenyezi Mungu, kisha wakawa na msimamo, wao huteremkiwa na Malaika (na kuwaambia): msiogope wala msihuzunike na furahieni pepo mliyokuwa mkiahidiwa" (41:30)

2. Kutomuamini Mwenyezi Mungu na kutofanya amali njema, hawa ni katika wale ambao:

﴿اسْتَحْوَذَ عَلَيْهِمُ الشَّيْطَانُ فَأَنسَاهُمْ ذِكْرَ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ حِزْبُ الشَّيْطَانِ أَلَا إِنَّ حِزْبَ الشَّيْطَانِ هُمُ الْخَاسِرُونَ﴾

"Shetani amewatawala, kwa hivyo akawasahaulisha kumkumbuka Mwenyezi Mungu, Hao ndio kundi la shetani ni lenye kupata hasara" (58:19)

3. Kuamini bila ya kufanya amali njema, hawa ni katika wanachama wa shetani kama wale waliotangulia. Lau angelikuwa ni mumin wa kweli, basi zingeonekana alama za imani. Mtume(s.a.w.w) anasema: "Hakuna inayookoa isipokuwa amali. Lau ningeasi ningeliangamia" Ama ikiwa amali yake njema imechanganyika na mbaya na akatubia, basi atakuwa katika Aya isemayo:

﴿وَآخَرُونَ اعْتَرَفُوا بِذُنُوبِهِمْ خَلَطُوا عَمَلًا صَالِحًا وَآخَرَ سَيِّئًا عَسَى اللَّـهُ أَن يَتُوبَ عَلَيْهِمْ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

"Na wako wengine waliokiri dhambi zao, wakachanganya vitendo vizuri na vingine vibaya, Huenda Mwenyezi Mungu akapokea toba zao, Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kusamehe mwenye kurehemu" (9:102)

4. Kufanya amali njema bila ya kuamini, kama kafiri amlishaye mwenye njaa au amvishaye aliye uchi, atengenezaye barabara, kujenga nyumba za mayatima, au hospitali, kwa njia ya kheri ya kibinadamu.

Imesemekana amali yake hii, kuwepo kwake na kutokuwepo ni sawa tu. Kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللَّـهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ ﴾

"Hakika Mwenyezi Mungu anawakubali wamchaye tu." (5:27)

Hapa Tunajibu hivi:

Kwanza : Makusudio ya kauli ya Mwenyezi Mungu: "Hakika Mwenyezi Mungu huwakubalia wamchaye tu," sio kuwa mtu akimwasi Mwenyezi Mungu katika jambo fulani, basi hamkubalii akimtii katika jambo jingine. Kama ni hivyo basi wasingekubaliwa isipokuwa waliohifadhiwa kutotenda dhambi (Maasum) tu, jambo ambalo linapingana na uadilifu wake na hekima yake. Isipokuwa makusudio ya Aya kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakubali isipokuwa amali safi isiyokuwa na uchafu wowote wa kidunia na kwamba mwenye kufanya tendo lolote kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu na kwa kheri basi atatosheka na aliyemfanyia. Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kufanya kheri kwa ajili ya kheri na ubinadamu, basi amefanya kheri hiyo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu ni sawa awe amekusudia hivyo au la. Na mwenye kufanya amali kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi malipo yake yako kwa Mwenyezi Mungu.

Ama makusudio ya 'hapana dhambi zaidi ya ukafiri' ni kuwa ukafiri ni dhambi kubwa na kwamba dhambi yoyote kadiri itakavyokuwa kubwa haishindi ukafiri. Lakini hili - la kuwa ukafiri ni dhambi kubwa - ni jambo jingine, na malipo ya wema ni jambo jingine. Pili: Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni mwadilifu, katika jumla ya uadilifu wake ni kwamba mwema na muovu hawako sawa bali mwema ana malipo yake na mwovu ana malipo yake.

Wala sio lazima malipo ya mtenda mema asiyekuwa mu'min yawe akhera

Inawezekana yakawa duniani kwa kuondolewa madhara na balaa, kama asemavyo Mtume(s.a.w.w) : "Kufanya wema ni kinga ya mambo maovu" Na pia sio kuwa malipo ya akhera ni pepo tu, inawezekana kuwa ni kwa kupunguziwa adhabu, au kutokuwa na adhabu wala malipo kama ilivyo hali ya A'raf. Kwa ufupi ni kuwa mtu atalipwa kwa vitendo vyake, vikiwa ni kheri basi atalipwa kheri na vikiwa ni shari atalipwa shari. Kafiri anastahili adhabu kutokana na ukafiri wake, na huenda akafanya kheri kwa ajili ya kheri akastahiki malipo mema, Kila tendo lina hisabu.

Ndio, ni kweli sisi hatujui aina ya malipo atakayolipwa mtenda wema asiyekuwa mu'min. Pia hatujui ni lini na wapi, duniani au akhera. Haya yanategemezewa kwenye ujuzi wa Mwenyezi Mungu na hekima Yake. Na kuyapanga hayo ni kama kushirikiana na Mwenyezi Mungu katika elimu yake. Basi na amwogope Mwenyezi Mungu mwenye kumwamini. Kwa mnasaba huu tutataja maneno ya Sayyid Kadhim mwenye kitab U'rwathul- Wuthqa mlango wa waqf, maswala ya sharti ya niya ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Ninamnuku: "Inawezekana kusema kwamba, thawabu zinathibiti kwa matendo mema, hata kama hayakusudiwa kwa ajili ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu anayeyatenda anastahiki kusifiwa kwa wenye akili, hata kama hakukusudia kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Basi ikiwa hivyo, sio mbali kustahiki fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu mtukufu"

Kwa hiyo mwanachuoni huyu mkubwa anasema wazi kwamba inawezekana mtu kulipwa malipo mema kwa vitendo vizuri hata kama hakukusudia radhi ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kutakuwa na uwezekano mkubwa zaidi kupewa malipo mema anayekusudia njia ya kheri na ubinadamu. Imekwishaelezwa mara nyingi kwamba akili haikatai kuwa yawezekana mwenye dhambi aneemeshwe kwa fadhila za Mwenyezi Mungu, isipokuwa linalokataliwa na akili ni kuadhibiwa na Mwenyezi Mungu yule asiyestahili adhabu.

﴿مَّا كَانَ اللَّـهُ لِيَذَرَ الْمُؤْمِنِينَ عَلَىٰ مَا أَنتُمْ عَلَيْهِ حَتَّىٰ يَمِيزَ الْخَبِيثَ مِنَ الطَّيِّبِ وَمَا كَانَ اللَّـهُ لِيُطْلِعَكُمْ عَلَى الْغَيْبِ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَجْتَبِي مِن رُّسُلِهِ مَن يَشَاءُ فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ وَإِن تُؤْمِنُوا وَتَتَّقُوا فَلَكُمْ أَجْرٌ عَظِيمٌ ﴾

179.Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kutaka kuwaacha waumini juu ya hali mliyo nayo mpaka awapambanue wabaya na wazuri. Na hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwafunulia mambo ya ghaibu, lakini Mwenyezi Mungu humchagua amtakaye katika Mitume yake. Basi mwaminini Mwenyezi Mungu na Mitume Yake. Na kama mtaamini na kuogopa basi mtakuwa na ujira mkubwa.

KUPAMBANUA WEMA NA UOVU

Aya 179

MAANA

Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwaacha waumini juu ya hali mliyonayo mpaka awapambanue wabaya na wazuri.

Maadui wa Mtume(s.a.w.w) walikuwa aina mbili: Kwanza ni washirikina, nao ni wale walioukataa uislamu kwa ndani na nje, wakatangaza vita tangu mwanzo wakaishia kuunda vikundi,wakajiandaa kwa nguvu wanazoziweza. Wakawa ni maadui wanaojulikana wazi wakitofautika na waislamu. Aina ya pili ni wanafiki, nao ni wale walioficha ukafiri na uadui kwa Mtume na sahaba zake, wakadhihirisha mapenzi. Kazi yao ilikuwa ni njama dhidi ya Mtume(s.a.w.w) ndani ya safu za waislamu mara wanawababaisha watu kwa uongo, mara nyingine wanawavuta waislamu kwenye maasi, au kuwavunja nguvu za kupambana na adui na kuwatia hofu. Na katika baadhi ya vita walikuwa pamoja na jeshi la waislamu, kisha wakajitoa njiani.

Wanafiki walimsumbua sana Mtume kuliko alivyosumbuliwa na washirikina. Kwa sababu, washirikina walikuwa maadui wanaoonekana wazi, lakini wanafiki walikuwa wakifanya vitimbi kwa kujificha na kuleta madhara kichinichini. Na hivyo ndivyo walivyo kwa yeyote anayelingania kheri, wakati wowote na mahali popote. Wanajaribu kuchafua katika safu za watu wazuri, Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewataja katika Aya nyingi, kama vile Aya ya 173 ya Sura hii, na katika Aya hii tuliyTafsir onayo na pia katika Aya isemayo:

﴿وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَا لِكُلِّ نَبِيٍّ عَدُوًّا شَيَاطِينَ الْإِنسِ وَالْجِنِّ يُوحِي بَعْضُهُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ زُخْرُفَ الْقَوْلِ غُرُورًا﴾

"Na namna hii tumefanyia kila Nabii adui, mashetani katika watu wa majini, Baadhi yao wanawafunulia wengine maneno ya kuwapamba pamba kwa kuwahadaa" (6:112)

Mtume aliamrishwa kuwafanyia hao wanafiki na kila aliyetamka shahada muamala wa kiislamu. Kuhifadhia damu zao na mali zao, kushirikiana nao katika vita na hata katika ngawira. Kwa sababu uislamu ulikuwa bado ni mchanga, lau atawaua au kuwafukuza wangelisema wakuzaji mambo kwamba Muhammad hampendi anayemwamini na asiyemwamini. Na washirikina wangelifanya hilo ni njia ya kuutangazia vibaya uislamu na Mtume wake.

Kwa sababu hiyo Mtume akawa hana la kufanya, Akiwakubali wataharibu na kuwaweka mbali waislamu na jihad, na akiwakataa alihofia mlinganio wake usipungukiwe na wasaidizi na wafuasi. Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii: "Mwenyezi Mungu hakuwa mwenye kuwaacha waumini" Yaani sio hekima ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwaacha katika hali hiyo, wanafiki wajifiche kwenye pazia la kudai Uislamu. La sivyo hivyo, bali anawafichua ili wajulikane na wafedheheshwe mbele ya watu na wasibakiwe na pa kutolea vitimbi na ufisadi. Na jambo la kuwafedhehesha sio kutamka shahada, kurukuu na kusujudu, na mambo mengine ambayo ni mepesi kuyafanya. La! Bali ni jambo zito ambalo litawafichua wanafiki na wasibakie na nafasi yoyote ya ria na hadaa au vitimbi na kutia sumu. Kwa mtihani huu mzito na amri ya kuwa na subira na kuwa na uthabiti katika vita vya Uhud, mtajua enyi waumini neema ya Mwenyezi Mungu kwenu na kwamba Yeye hakuwaacha katika hali mliyokua nayo, ya kuchanganyikana na maadui ambao mlitosheka nao hapo mwanzo kwa jina la uislamu. Makusudio ya wazuri ni waumini na wabaya ni wanafiki.

Na hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwafunulia mambo ya ghaibu.

Yaani si katika hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu wala si katika desturi Yake kuwafahamisha watu elimu Yake na awaambie hili ni zuri na hili ni baya; bali ni juu yenu kuyafahamu hayo kupitia majaribio ya shida na misukosuko, kama ilivyotokea Uhud wakati Mtume(s.a.w.w) alipowaita maswahaba warudi kwa adui mara ya pili katika Hamraul Asad. Yaani Mwenyezi Mungu hamfahamishi yeyote yaliyo katika nyoyo za watu kuwa ni imani au unafiki, isipokuwa kuwaamrisha kujitoa mhanga kwa hali na mali, na kwenye utekelezaji ndipo anajulikana mwenye kujitiatia na mwenyewe hasa.

Ndio, Mwenyezi Mungu anawafichulia baadhi ya Mitume yake juu ya unafiki wa huyu na imani ya yule, kwa hekima ambayo yeye mwenyewe Mungu anaijua zaidi, Haya ndiyo maana ya kauli yake,

Lakini Mwenyezi Mungu huchagua katika Mitume yake amtakaye.

Kauli hiyo inafanana na kauli yake Mwenyezi Mungu isemayo:

﴿عَالِمُ الْغَيْبِ فَلَا يُظْهِرُ عَلَىٰ غَيْبِهِ أَحَدًا ﴿٢٦﴾ إِلَّا مَنِ ارْتَضَىٰ مِن رَّسُولٍ﴾

"Mjuzi wa ghaibu, wala hamdhihirishi ghaibu Yake yeyote isipokuwa Mtume aliyemridhia" (72: 26- 27)

﴿وَلَا يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ يَبْخَلُونَ بِمَا آتَاهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ هُوَ خَيْرًا لَّهُم بَلْ هُوَ شَرٌّ لَّهُمْ سَيُطَوَّقُونَ مَا بَخِلُوا بِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلِلَّـهِ مِيرَاثُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴾

180.Na wasidhanie kabisa wale ambao wanafanyia ubakhili vile alivyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake kuwa ni bora kwao, bali ni shari kwao. Watatiwa mandakozi ya hivyo walivyofanyia ubakhili siku ya kiyama; na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ana habari ya mnayoyatenda.

﴿لَّقَدْ سَمِعَ اللَّـهُ قَوْلَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ فَقِيرٌ وَنَحْنُ أَغْنِيَاءُ سَنَكْتُبُ مَا قَالُوا وَقَتْلَهُمُ الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ وَنَقُولُ ذُوقُوا عَذَابَ الْحَرِيقِ ﴾

181.Hakika Mwenyezi Mungu amekwishasikia kauli ya wale waliosema: Hakika Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri. Tutaandika yale waliyoyasema; na kuua kwao Mitume; na tutawaambia: onjeni adhabu ya kuungua.

﴿ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيكُمْ وَأَنَّ اللَّـهَ لَيْسَ بِظَلَّامٍ لِّلْعَبِيدِ ﴾

182.Hayo ni kwa sababu ya yale yaliyotangulizwa na mikono yenu na kwamba Mwenyezi Mungu si dhalimu kwa waja.

URITHI WA MBINGU NA ARDHI NI WA MWENYEZI MUNGU

Aya 180-182

MAANA

Na wasidhanie kabisa wale ambao wanafanyia ubakhili vile alivyowapa Mwenyezi Mungu katika fadhila zake kuwa ni bora kwao, bali ni shari kwao.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuhimiza kujitolea mhanga kwa nafsi, amefuatishia kuhimiza kujitolea kwa mali. Makusudio ya Aya hii ni wale wanaojizuia kutoa Zaka na Khumsi ambazo ni wajibu, na wala sio kutoa sadaka ya sunna. Kwa sababu kiaga kikali ambacho kinaelezwa na Aya kinaonyesha kuacha wajibu, sio kuacha sunna. Imesemekana pia kuwa makusudio ni mwenye kuficha jina la Muhammad(s.aw.w) na sifa zake zilizokuja katika Taurat na Injil. Vilevile imesemekana ni kufanya ubakhili wa elimu kwa anayeihitajia. Lakini linalokuja haraka kwenye fahamu, ni kufanya ubakhili kwenye mali. Hilo linaonyeshwa na kauli yake Mwenyezi Mungu.Watatiwa mandakozi ya hivyo walivyovifanya ubakhili siku ya kiyama, Hii ni tafsiri ya;'na ni shari kwao.' Kutiwa mandakozi, hapa ni fumbo la adhabu kali, kama vile Mwenyezi Mungu alivyosema. Siku (mali) itakapotiwa moto katika moto wa Jahannam na vichomwe vipaji vyao vya nyuso na mbavu zao na migongo.yao kwa mali hiyo. (9:35)

MATAJIRI NI MAWAKALA SIO WENYEWE

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehimiza kutoa mali katika Aya kadhaa, nyingi katika hizo ameonyesha kuwa mali zote sio miliki ya aliyenazo, isipokuwa ni miliki ya Mwenyezi Mungu peke Yake na kwamba mtu amewekewa amana tu kuruhusiwa kuitumia kwa mipaka maalum bila ya kuikiuka kama alivyo wakala, hufuata matakwa ya mwenye mali katika matumizi yote. Miongoni mwa Aya nyingine zilizotaja hayo ni:

﴿وَابْتَغِ فِيمَا آتَاكَ اللَّـهُ الدَّارَ الْآخِرَةَ﴾

"Na tafuta - kwa yale aliyokupa Mwenyezi Mungu - makazi mazuri ya akhera" (28:77).

"Toeni katika yale aliyowapa Mwenyezi Mungu" (36:47)

Aya iliyo wazi zaidi ni ile isemayo.

﴿وَأَنفِقُوا مِمَّا جَعَلَكُم مُّسْتَخْلَفِينَ فِيهِ﴾

"Na toeni katika yale ambayo (Mwenyezi Mungu) amewafanya kuwa makhalifa kwenye hayo" (57:7)

maana ya kuwa khalifa ni kuwa kaimu. Katika Hadith Qudsi anasema:"Mali (zote) ni zangu, na matajiri ni mawakala wangu, mafukara ni watu wangu (wanaonitegemea) basi mwenye kuwafanyia ubakhili watu wangu, nitamwingiza motoni bila ya kujali"

Kwa hivyo, Aya na Hadith zinafahamisha kuwa Uislamu haukubali miliki ya mtu kwa aina yoyote ile, ni sawa iwe ni miliki ya mtu binafsi kabisa, kama ulivyo mfumo wa kibepari, au milki ya kiwango maalum, kama ulivyo mfumo wa kijamaa, au hata miliki ya umma, kama ulivyo mfumo wa kikomunist. Aina zote hizi zinakanushwa na uislamu na kubakia milki ya kihakika ya Mwenyezi Mungu peke Yake, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehalalishia mtu kutumia mali kwa ajii yake na watu wake kwa uzuri, na pia kuitumia katika njia ya kheri kwa sharti ya kuipata kwa njia ya halili siyo ya haramu; kama vile kughushi, kuhadaa, kunyang'anya, rushwa, riba, ulanguzi na kufanya biashara ya ulevi. Kwa hivyo ruhusa ya kuitawala mali na kutumia ni kwa kiwango maalum.

Unaweza kuuliza , baadhi ya Aya zinafahamisha kuwa mali ni milki ya mtu,kama "Piganeni jihadi kwa mali yenu" "Wapeni mayatima mali zao" Katika Hadith imeelezwa: "Damu zenu na mali zenu ni haramu (kwa mwengine)." Na "watu ni wenye mamlaka juu ya mali zao." Na bei na urithi ni katika mambo ya lazima ya dini na sheria ya kiislamu. Kwa hivyo basi, si haifai kusema kuwa uislamu hautambui milki ya mtu kwa aina zote?

Jibu : kutegemeza mtu kitu kunafaa kwa mnasaba ulio karibu. Kwa mfano kumwambia mgeni sahani yako au kumwambia mpotea njia, "hii ndiyo njia yako" Hapa inajulikana wazi kwamba mgeni hana sahani, isipokuwa makusudio ni mgeni ale kwa kutumia sahani hiyo `na mpotea njia, hana njia isipokuwa ni kufuata hiyo njia. Kwa hiyo mali inaegemezwa kwa mtu kwa kutumia kwa njia ya halali na kwa ruhusa sio kwa njia ya milki; kama kauli yake Mwenyezi Mungu.

"Na Mwenyezi Mungu amewafanyia wake katika jinsi yenu." (16:72)

Na kauli ya Mtume(s.a.w.w) "Wewe na mali yako ni ya babako." Kwa dhahiri ni kwamba mke siye milki ya mume kabisa wala mtoto si milki ya kihakika ya mzazi. Ama mauzo na mirathi ni utambulisho wa haki; yaani uislamu umemjaalia mwenye mali kuitambulisha itumiwe na mwengine, wakati huo huo umehalalisha haki maalumu kwenda kwa mrithi na mnunuzi. Na tofauti kati ya milki ya utambulisho na milki ya hakika ni kubwa.

Kwa ufupi ni kwamba uislamu umehalalishia mtu kuhodhi mali kwa sharti maalumu na kuitoa kwa sharti mahsusi, ukasisitiza sana juu ya masharti haya na kuharamisha kuyakiuka. Hii peke yake inatosha na ni dalili wazi kwamba mwanadamu ni wakala wa mali na si mwenye mali, kama si hivyo, basi ingelijuzu kwake kutumia bila ya masharti yoyote. Ni vizuri tumalizie mlango huu kwa kauli ya Imam Jafar as-Sadiq(a.s) :"Mali ni ya Mwenyezi Mungu, nayo ni amana kwa waja wake. Amewaruhusu kula bila ya kuifuja, kuvaa bila ya kuifuja, kuoa bila ya kuifuja na kupanda (k.v. farasi) bila ya kuifuja. Itakayozidi hapo itarudi kwa mafukara waumini kurekebisha hali yao. Atakayefanya hivyo, basi anachokila ni halali, anachokinywa ni halali, anachokipanda ni halali na aliyemuoa ni halali, zaidi ya hivyo ni haram"

Hakika Mwenyezi Mungu amekwisha sikia kauli ya wale waliosema: Hakika Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri.

Aya haikutaja majina ya waliotamka kufuru hii, lakini wafasiri wamenakili kuwa Mtume alipoteremshiwa Aya hii:

"Ni nani atakayemkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mzuri" (2:245)

Wayahudi wa Madina waliwokuwako wakati wa Mtume, walisema "Fukara tu, ndiye anayetaka mkopo kwa tajiri. Kwa hivyo Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri" Hili sio la kushangaza kwa Mayahudi hasa wale matajiri. Kwa sababu misingi yao na kazi zao zinafahamisha wazi uovu huu na kutojali misimamo ya kibinadamu. Na mwenye kufuatilia historia ataona kuwa hakuna sehemu yoyote duniani isipokuwa imeathiriwa na ufisadi wao na malengo yao maovu.

Hakuna ufasaha unaofahamisha taswira ya hakika ya ukweli wa Uyahudi kuliko kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿وَتَرَىٰ كَثِيرًا مِّنْهُمْ يُسَارِعُونَ فِي الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ وَأَكْلِهِمُ السُّحْتَ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٦٢﴾ لَوْلَا يَنْهَاهُمُ الرَّبَّانِيُّونَ وَالْأَحْبَارُ عَن قَوْلِهِمُ الْإِثْمَ وَأَكْلِهِمُ السُّحْتَ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَصْنَعُونَ ﴿٦٣﴾ وَقَالَتِ الْيَهُودُ يَدُ اللَّـهِ مَغْلُولَةٌ غُلَّتْ أَيْدِيهِمْ وَلُعِنُوا بِمَا قَالُوا﴾

"Na utawaona wengi wao wanakimbilia kwenye dhambi na uadui na ulaji wao haramu, Hakika ni mabaya kabisa wayafanyayo, Mbona watawa wao na wanavyuoni wao hawakatazi maneno yao ya dhambi na ulaji wao haramu. Hakika ni mabaya kabisa wayafanyao. Na Mayahudi walisema: mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba. Mikono yao ndiyo iliyofumba, na wamelaaniwa kwa yale waliyoyasema" (5: 62-64)

Sina shaka kabisa kwamba kila mwenye kuingilia hekima ya Mwenyezi Mungu na akasema kwa ulimi wake maneno, kwa mfano, 'Ilikuwa haifai kwa Mwenyezi Mungu kufanya hivi, isipokuwa angefanya hivi' sina shaka kuwa anayesema hivyo atakuwa pamoja na waliosema. Mkono wa Mwenyezi Mungu umefumba; atake asitake.

Tutaandika yale waliyoyasema.

Hili ni kemeo la kiaga cha wale waliosema: "Hakika Mwenyezi Mungu ni fukara na sisi ni matajiri" Kwa sababu kuandika dhambi kunapelekea adhabu, Na kuuwa kwao Mitume. Pia tutaandika wa kale wao walivyowaua Mitume. Kumenasibishwa kuua kwao, ingawaje walioua ni wa kale wao, Hayo yamekwishaelezwa katika tafsir ya Aya 21 ya Sura hii.

Hayo ni kwa sababu ya yaliyotangulizwa na mikono yenu; na kwamba Mwenyezi Mungu si dhalimu sana kwa waja.

Vipi atadhulumu na Yeye amekataza dhulma na kuifanya kuwa ni kubwa ya madhambi makubwa na katika Aya nyingi akiita kuwa ni kufuru?

Zaidi ya hayo dhalimu anadhulumu kwa sababu tu anahitajia hicho anachokifanyia dhulma. Na Mwenyezi Mungu amejitosheleza na kila kitu. Kwa msingi huu wa kuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kujitosha na hahitajii kitu, kunathibitisha uadilifu wake Mwenyezi Mungu (s.w.t) vilevile kunathibitisha kwamba yeye hana mwili, kwa sababu mwili unahitaji vitu.

Kwa hivyo, inatubainika kubatilikia kwa madhehebu ya wanaosema kuwa shari inatokana na Mwenyezi Mungu, na kwamba yeye anamtengenezea maasi mja, kisha amwadhibu, Pengine watafute njia ya kuhepa kauli hii ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Hakika Mwenyezi Mungu si dhalimu wa waja. Kwa vile ametumia neno Dhallam lenye maana kudhulumu sana iwe anaweza kudhulumu kidogo, lakini sio sana! Mwenyezi Mungu ametakasika kabisa na wayasemayo madhalimu.

1

VAZI LA MWANAMKE

BIBI FATIMA (A.S) KIIGIZO CHEMA KWA WANAWAKE

Bibi Fatimah(a.s) ni mwanamke anayezingatiwa kuwa ni mwanamke wa kutolea mfano katika dini ya ki-Islamu, na pia ni kiigizo chema kwa kila mwanamke anayetafuta mafanikio katika maisha yake. Bibi Fatimah binti Muhammad(s.a.w.w) ndiye mwanamke bora ulimwenguni aliyezaliwa na kupata malezi katika nyumba iliyokuwa ikishuka ndani yake Wahyi kutoka mbingu-ni.

9 Hadithi hii imenukuliwa kutoka ndani ya kitabu kiitwacho Tuhaful- Uquul. Katazo hili linajumuisha mambo mengi na khususan mambo yote ambayo Mwenyezi Mungu hayaridhii na yanatendwa na maadui wa Mwenyezi Mungu. Mwislamu inamuwajibikia kujiepusha nayo vinginevyo hapatakuwa na tofauti kati ya Muumini na adui wa Mwenyezi Mungu. Mtarjumi.

Si hivyo tu bali Bibi Fatimah alihitimu mafunzo ya Uislamu katika madrasa ya Utume, na kutokana na mafunzo hayo aliweza kufikia daraja ya juu na tukufu. Katika kuthibitisha ubora wa Bibi Fatimah, Mtume(s.a.w.w) amepata kusema,"Hakika Mwenyezi Mungu huwa radhi kwa radhi ya Fatimah, na huchukia kutokana na kuchukia kwa Fatimah. " 10 Kwa ajili ya daraja kubwa aliyonayo Bibi Fatimah katika Umma wa Nabii Muhammad(s.a.w.w) imekuwa ni wajibu kwa kila mwanamke duniani kuiga mwenendo wa Bibi huyu katika maisha yake, ajing'arishe kwa nuru yake nzuri na afuate nyayo zake ambazo zitamuelekeza kwenye mafanikio na utukufu. Hakika Bibi Fatimah(a.s) , ni mfano wa kila utukufu na kila jema. Mwanamke yeyote atafanikiwa iwapo ataamua kufuata mwenendo wa Bibi Fatmah (a.s.) , na kinyume chake ni kuwa, kila mwanamke ataangamia iwapo ataamua kujichagulia mwenendo wake au kuiga usiyokuwa mwenendo wa Bibi Fatimah. Pia Fatimah(a.s.) alikuwa Mchaji Mungu na mwenye kutekeleza vilivyo maamrisho ya Mwenyezi Mungu. Pia ile maana nzima ya Hijabu aliifahamu vema na kuitekeleza kama ilivyoamriwa na Mwenyezi Mungu.

Hivyo utekelezaji wake katika maamrisho ya Mwenyezi Mungu ulikuwa wa hali ya juu, kwani hakupata kutoka nje ila huwa amevaa vazi la kumsitiri mwili wake wote tangu kichwani hadi miguuni. Isitoshe alikuwa akiichukia mno tabia ya wanawake kutoka majumbani mwao bila kujisitiri kisheria. Bibi Fatimah alichukizwa na tabia hiyo kwa sababu Mwenyezi Mungu pia anaichukia tabia ya kutokujisitiri na hasa kwa kuwa kukosa sitara ya kishera kwa wanawake ni ufunguo wa kuyaendea maovu na ni miongoni mwa vitangulizi vinavyosababisha watu kuteleza, bali wanaaanguka kabisa. 10Mustadrak Alhakim juz 3 uk , Al isabah ya Ibn Hajar Al asqalani juz 4 uk. 10 Sasa hivi tunawaletea baadhi ya mafundisho kuhusu Hijabu na tutaona pia utukufu wa Bibi Fatimah katika mafunzo hayo.

NI KITU GANI KILICHO BORA KWA MWANAMKE?

Inasimuliwa katika historia kwamba, Mtume(s.a.w.w) siku moja aliwauliza Masahaba suali lifuatalo:"Je! ni kitu gani kilicho bora kwa mwanamke?" Masahaba walinyamaza kwa kuwa jibu la mkato na sahihi hawakulifahamu, ikawa kama kwamba akili zao zinahangaika baina ya kuwa kilicho bora kwa mwanamke ni mali, uzuri wake, kuolewa au kitu gani? Kipindi chote hiki Bibi Fatimah alikwisha lisikia swali hilo, na baada ya kimya cha kukosekana jibu, Bibi Fatimah alimtuma mtu aende kwa Mtume(s.a.w.w) aka-toe jibu sahihi la swali hili nalo ilikuwa;"Kilicho bora kwa mwanamke ni yeye mwanamke asimuone mwanaume na mwanaume naye asimuone mwanamke." 11

Baada ya jibu la bibi Fatimah Masahaba walikuwa wakisubiri jibu la Mtume atasema nini kuhusu jawabu alilotoa Binti yake. Mtume(s.a.w.w) akasema "Amesema kweli Fatimah." Na akaongeza kusema,"Fatimah ni sehemu iliyotokana na mwili wangu." Maana ya maneno ya Mtume yalimaanisha kwamba hilo ndilo jawabu sahihi na hiyo ndiyo imani. Kutokana na jawabu hili, Bwana Mtume(s.a.w.w) akawa ameitangazia dunia nzima kwamba; Utu, heshima, utukufu, na wema wa mwanamke unapatikana ndani ya Hijabu, na kinyume chake ni uovu na shari, isitoshe hasara hum-fika mwanamke anapoitupa Hijabu. 11Hapana shaka makusudio yaliyomo ndani ya jawabu la bibi Fatimah(a.s) ni kwamba, waw-ili hawa yaani mwanamke na mwanaume ni wale wasiokuwa na uhsiano wa kisheria. Watu wenye uhusiano kisheria ni kama hawa wafuatao: Mama, dada, shangazi na au Baba, kaka, mjomba na wengine ambao wametajwa katika vitabu vinavyohusika na sheria. Ama mume na mke, wawili hawa uhusiano kati yao hauna haja ya kutolewa maelezo. Mtarjumi.

MAZUNGUMZO YA KUSTAAJABISHA

Historia inaendelea kutufahamisha kwamba Bibi Fatimah(a.s) alikuwa amekaa na baba yake ambaye ndiye Mtume(s.a.w.w) , mara alibisha hodi Sahaba Abdalla ibn Ummi Maktum ambaye alikuwa kipofu. Kabla Sahaba huyu hajaingia Bibi Fatimah(a.s) alisimama akaondoka mahali hapo. Baada ya kwisha mazungumzo baina ya Mtume na Sahaba huyu, Sahaba Abdallah ibn Ummi Maktum aliondoka. Bibi Fatima alirudi na akaendelea kuzungumza na Mtume(s.a.w.w) Bwana Mtume(s.a.w.w) .wakamuuliza Binti yake sababu ya kuondoka wakati alipoingia Sahaba Abdallah ibn Ummi Maktum hali kuwa anafahamu kabisa kwamba yule ni kipofu haoni.12

Bibi Fatimah alijibu kama ifuatavyo."Ikiwa yeye hanioni basi mimi namuona na yeye ananusa harufu ya wanawake. " Mtume(s.a.w.w) alifurahishwa mno na jawabu la Binti yake ambalo linaonyesha kipimo cha Uchamungu na utukufu unaotoka kwa Binti yake Mwenye hekima. Isitoshe kwa jawabu hilo, Bwana Mtume hakumlaumu binti yake kutokana na mkazo huu mkali unaohusu Hijabu, bali furaha ya Mtume iliendelea kwa upeo mkubwa na akaunga mkono kwa dhati kabisa kisha akasema;"Nashuhudia kwamba wewe ni sehemu iliyotokana nami" 13.

12 Ni vyema ikaeleweka wazi kwamba Bwana Mtume(s.a.w.w) alimuuliza Binti yake suali hilo hali ya kuwa yeye mwenyewe anajua wazi kuwa Sahaba yule alikuwa haoni, lakini lengo la Bwana Mtume (s.a.w) kuuliza suali hilo alitaka aone namna Binti yake atakavyo toa jawabu la suali hilo ili historia ipate kusajili mazungumzo haya ya kiimani na ubakie kuwa ni mfano mzuri wa kuigwa siku zote.

13 Mustadrak Al-Wasail Kitabun-Nikah. Biharul-An-Waar juz 104 uk 38.

TUKIO MUHIMU NDANI YA MSIKITI WA MTUME (S.A.W.W.)

Siku moja Bibi Fatimah(a.s.) alitaka kutoa mhadhara ndani ya msikiti wa Mtume(s.a.w.w) Kabla ya kuanza kuhadhiri aliten-genezewa sitara humo Msikitini, akakaa yeye na Waumini wengine wakike upande mmoja na Waumini wanaume wa Kiansari na Muhajirina nao wakakaa upande wa pili. Sitara hii aliyotengenezewa Bibi Fatimah(a.s) ilikuwa ina maana nyingi ndani yake. Kwanza ilikuwa ni kutekeleza sheria inayohusu Hijabu katika sura ya kuweka kizuizi, ambapo pande mbili hizo zilitenganishwa. Pili, hali hiyo ilikuwa ni kuonesha kutokuukubali kwa vitendo mchanganyiko wa wanaume na wanawake, jambo ambalo maadui wa Uislamu wanatumia kila mbinu kulihalalisha kwa kuli-tolea hoja batili.

Sasa nakutazama ewe dada yangu wa ki-Islamu, nikitarajia umeiona mifano hii mitatu inayohusu maisha ya Bibi Fatimah(a.s.) ambaye ni mwanamke bora kuliko wanawake wote duniani, na ni mwanamke anayestahiki kuigwa katika Uislamu. Inafaa uige na ujifunze kwake ili upate kupambika kwa umbile la kike ( yaani kuwa na haya) na utukufu, kadhalika ifanye nafsi yako iwe ya mwanamke Mchamungu mwenye kushika mafunzo ya ki-Islamu na hukmu za Qur'an. Ewe dada wa ki-Islamu hebu shikamana na mafunzo ya ki-Islamu ambayo Mwenyezi Mungu amekupa ili ufanikiwe duniani na akhera. Mafunzo haya yatakupandisha kwenye daraja tukufu la wenye imani na mafanikio. Fahamu kwamba hutafanikiwa isipokuwa uwe umeshikamana na kuyatu-mia mafunzo hayo kwa kuyatekeleza maishani mwako.

KUJIHESHIMU NDIYO PAMBO LA MWANAMKE

Bwana Mtume(s.a.w.w) amesema,"Kujiheshimu ndiyo pambo la Mwanamke." Hapana shaka kwamba pambo limegawanyika sehemu mbili: Pambo lisilo halisi na pambo halisi. Ama pambo lisilo halisi ni lile ambalo linaloonekana wazi, na ni lenye kubakia kwa muda maalum, kisha hutoweka bila hata ya kumuongezea kitu muhusi-ka katika utu wake. Ama lile pambo halisi, ni lile ambalo hubakia muda wote na pia humfanya mwanamke aupate ule utu wake kamili na kumfikisha kwenye daraja ya ukamilifu. Ukweli usiokuwa na shaka ni kuwa, pambo halisi ndilo lenye umuhimu mno kuliko lile jingine, bali ndilo lengo analopaswa kulishughulikia kila mtu. Endapo mtu atakosa kuwa na fungu fulani katika pambo hili halisi, basi pia huwa hana faida yoyote ndani ya lile pambo la dhahiri.

Hapana shaka kwamba kujiheshimu ndilo pambo pekee linalom-faa mwanamke kama alivyosema Bwana Mtume(s.a.w.w) . Pambo hilo humjengea mwanamke utu, heshima na utukufu hapa duniani na kesho akhera. Ama madawa ya kujirembesha, manukato na mengineyo miongoni mwa mapambo, yote hayo ni mapambo ya nje tu na hayana maana yoyote khususan mwanamke mwenyewe atakapokuwa si Mchajimungu; Mwenyezi Mungu apishe mbali.

Hijabu ndiyo alama pekee inayoweza kutambulisha Uchaji Mungu wa mwanamke na pia heshima yake na utu wake. Wakati huo huo tabia ya kutokuwa na Hijabu huchafua heshima ya mwanamke na kuacha maswali chungu nzima kuhusu Uchaji Mungu wake na kujiheshimu kwake kwa jumla. 14Kalimatur-Rasuli uk 110 cha Sayyid Shirazi.

Yote haya yanakuja kwa sababu yeye mwenyewe kauweka mwili wake kuwa maonesho mbele ya maelfu ya watu siku zote. Kutokana na hali kama hiyo, hata huwezi kutambua ni mikono mingapi iliyowahi kuushika mwili wake kwa kuuacha wazi na kutokujisitiri kwa mujibu wa sheria!! Hivi unadhani watu wa kale na hata wa leo hii, nyoyo zao zitasal-imika vipi katika mazingira hayo ya wanawake kuicha wazi miili yao? Kamwe hawatasalimika kabisa, kwani wanawake wanapoiacha wazi miili yao ni jambo linalopelekea tuhuma mbaya kwa wanawake. Imam Ali(a.s.) anasema"Yeyote mwenye kui-weka nafsi yake mahala penye tuhuma mbaya, basi asimlaumu mtu atakaye mdhania vibaya." 15

Hapana shaka kwamba, mwanamke asiyekuwa na Hijabu huwa anaidhuru nafsi yake mwenyewe kwa sababu; Kwanza, huwa anapata hasara mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Pili, heshi-ma yake ndani ya jamii huwa inaporomoka. Hasara anayoipata mwanamke huyo mbele ya Mwenyezi Mungu inakuja kwa sababu mwanamke huyo huwa amekwenda kinyume na kanuni za mbinguni na kukosa utiifu kwa Mwenyezi Mungu. Baadaye tutaeleza adhabu za huko akhera atakazozipa-ta mwanamke asiyejali kujisitiri kwa mujibu wa sheria ya KiIslamu.

Ama hasara atakayoipata mwanamke kutoka na na heshima yake kuporomoka ndani ya jamii, hali hiyo inasababishwa na yeye mwenyewe kutokana na tabia yake ya kuyaacha wazi maungo yake yaonekane kwa kila mtu, hali ambayo humuingiza ndani ya kila aina ya uovu na ufisadi na hatimaye akadhalilika vibaya. 15 Al-kafi juz uk 152. Miongoni mwa dhana mbaya atakayodhaniwa mwanamke asiyejali sitara ya kisheria ni kuwa, wakati wote huonekana yuko tayari kufanya ufisadi. Kama si hivyo, amtazamaye hushawishika kumtendea uovu. Mtarjumi.

Na tukirejea kwa mwanamke mwenye kujisitiri kwa mujibu wa sheria ya ki-Islamu, huyu hupata faida za aina mbili kwa pamoja: Faida aipatayo mbele ya Mwenyezi Mungu ni kwamba, yeye huwa ni mwanamke mtukufu mbele ya Mwenyezi Mungu na Malaika wake pamoja na Mawalii wa Mwenyezi Mungu. Utukufu huu anaupata kwa kuwa amemtii Mola wake, ametekeleza maamrisho yake na ameyasitri maungo ambayo Mwenyezi Mungu ameamrishsa yasitiriwe. Na kwa ajili hii basi, mwanamke kama huyu kamwe hatonyanyua unyayo wake bali rehma za Mwenyezi Mungu huwa ziko pamoja naye, pia radhi za Mwenyezi Mungu humbatana naye, na wakati huo huo Malaika wa Mwenyezi Mungu wanamuombea msamaha. Mwenyezi Mungu anasema; "Kilichoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora na ni chenye kubakia." 16 Ama faida atakayoipata ndani ya jamii, ni pale mwanamke huyo anapokuwa ni mwenye kuheshimiwa na kutukuzwa, yote haya anayapata kwa kuwa yeye amejipamba kwa pambo la kuji-heshimu na kuuhifadhi utu wake, kisha akausitiri uzuri huo aliopewa na Mwenyezi Mungu.

MAJADILIANO NA MSICHANA WA KIKRISTO

Msichana mmoja wa Kikristo alikwenda kwa mwanachuoni wa ki-Islamu na kumwambia. "Mimi nimefahamu mambo mengi kuhusu Uislamu na kwa hakika dini hii imenishangaza sana kwa kanuni zake na miongozo yake, na nimeupenda Uislamu kwa mapenzi ya kweli. Lakini kanuni moja tu kwangu mimi imekuwa ni kikwazo kuingia katika Uislamu. Nimewauliza watu wengi kuhusu kanuni hiyo, mpaka sasa sijapata jawabu la kunitosheleza. 16 Qur'an 42:36.

Iwapo wewe Sheikh utaweza kunibainishia hekima iliyomo ndani ya kanuni hii, basi nakuthibitishia kuwa nitaingia katika Uislamu." Yule Mwanachuoni akasema, "Ni ipi kanuni hiyo?" Msichana aka-jibu. "Kanuni ya kuvaa Hijabu, ni kwa nini Uislamu haumuachi mwanamke akatoka nje apendavyo kama ilivyo kwa wanaume.?" Mwanachuoni yule wa ki-Islamu akasema, "Je umepata kumuona sonara ameweka dhahabu na johari nyinginezo katika sanduku la kioo, kisha akalifunga sanduku hilo kwa kufuli? Msichana akajibu, "Ndiyo." Sheikh huyu akamwambia tena yule msichana, "Je, ni kwanini sonara hakuziacha johari hizo zikawa zinashikwa na kila mtu ajaye kutaka kununua? Kwa nini amezihifadhi ndani ya sanduku la kioo lililofungwa?" Msichana akasema; "Amefanya hivyo ili azilinde johari zake kutokana na wezi na mikono yenye khiyana." Yule Mwanachuoni akamwambia msichana; "Hii ndiyo hekima ya Hijabu, fahamu kwamba mwanamke ni johari ya thamani ambayo ni lazima kuilinda kutokana na waovu na wahaini.

Pia ni wajibu kumhifadhi mwanamke kutokana na macho ya watu waovu ndani ya kitu ambacho kitamsitiri barabara kama inavy-olindwa lulu katika kola lake, ili asije akaangukia mikononi mwa watu hao na kumgeuza kuwa ngawira yao." Hakuna njia bora isipokuwa Hijabu, hicho ndiyo kizuwizi na ni mlinzi wa mwanamke. Kwa hakika mwanamke mwenye Hijabu huwa sala-ma kutokana na shari. kwa kuwa mwili wake umesitirika, na mapambo yake nayo hayaonekani mbele ya kila mtu.

Hali ya kuvaa Hijabu inawafanya watu wasimtamani mwanamke huyo kwa kuwa hakuna wakionacho cha kuwafanya wamtamani. Kutokana na hali hiyo huwa wanamuepuka, wala hakiwageuzi kitu chochote cha kuwafanya wamuangalie mwanamke huyo, bali humuogopa na kumuheshimu. Mwisho wa yote watu humuogopa na kumpa heshima yake kama anavyostahiki. Yote hayo yatap-atikana kwa ajili ya kuvaa Hijabu, na hali hii inamaanisha kwam-ba, Hijabu ndiyo mlinzi wako na ni hifadhi ya heshima, na utuku-fu wako. Ewe msichana huu ndio upande mmoja wa falsafa ya Hijabu."

Baada ya maelezo hayo ya Sheikh, msichana yule wa Kikristo alionesha furaha na akaridhishwa na maelezo ya Sheikh kisha akasema, "Sasa nimetosheka na falsafa iliyomo ndani ya kanuni hii ya ki-Islamu, na pia nimefahamu hekima iliyomo na ninapen-dezwa kuingia katika Uislamu." Baada ya hapo msichana akatoa Shahada mbili na akawa Muislamu. Majadiliano haya mazuri ya kidini yanatubainishia kwamba Uislamu unakusudia kuihifadhi hehsima na utukufu wa mwanamke, pia Uislamu unataka kuilinda jamii. Na kwa sababu hizo basi, Uislamu umewajibisha Hijabu kama sharti la msingi kuweza kutimiza malengo hayo.

TOFAUTI YA MWANAMKE MWENYE HIJABU NA ASIYE NA HIJABU

Mmoja wa marafiki zangu alinisimulia tukio la kufurahisha lililom-tokea Muumini mmoja wa ki-Islamu. Tukio hili lilikuwa kama ifu-atavyo. Siku moja Muumini huyo alikuwa akitembea pamoja na mkewe aliyekuwa kavaa Hijabu. Matembezi hayo yalimfikisha katika moja ya bustani zinazotembelewa na watu wa aina tofauti. Ghafla Muumini huyo alijiwa na mtu fulani ambaye naye alikuwa na mkewe. Mke wa mtu huyu hakuwa amevaa vazi la Hijabu na hivyo basi kwa dharau na kejeli alimwambia yule Muumini. "Kwa nini umemvalisha mkeo Hijabu, kwa nini hukumuacha akatoka bila Hijabu kama jinsi alivyo mke wangu? Hijabu ina faida gani?" Jawabu alilotoa Muumini yule lilikuwa la kushangaza na la kishu-jaa. Alimwambia.

"Je unafahamu tofauti ya mwanamke mwenye Hijabu na asiyekuwa na Hijabu? Bwana yule mwenye kejeli akasema "Nini tofauti yake?" Yule Muumini akajibu kwa njia ya kuuliza, je, kuna tofauti gani baina ya taxi na gari ambalo mtu hulitumia yeye binaf-si? Yaani kwa matumizi yake pekee yake." Bwana yule akajibu akasema, "Taxi hutumiwa na kila mtu, wakati ambapo gari maalum linamuhusu mwenyewe peke yake. Hii ndiyo tofauti iliyopo." Basi yule Muumini akasema, "Hali hiyo ndio iliyopo baina ya mwanamke aliyevaa Hijabu na yule asiye na Hijabu.

Mwanamke asiye na Hijabu ni sawa na taxi ambayo kila mtu anaweza kuikodisha na kuitumia. Mwili wa mwanamke huyo huwa wazi na kuonesha mapambo yake na uzuri wake, na kuwafanya watu wavutike kutokana naye, jambo ambalo linaweza kusababisha kutendewa maovu, kama ambavyo mara kwa mara hali hii inavyowapata wanawake wa aina hii. Ama mwanamke aliyevaa Hijabu yeye ni bibi aliyemtukufu, ni maalum kwa ajili ya mumewe, mapambo yake na uzuri wake havionekani kwa kila mtu. Pia watu wenye nyoyo chafu na dhaifu hawamuangalii, na uso wake na mapambo yake havikutani na macho yenye khiana, kwa kuwa amehifadhiwa ndani ya Hijabu.

Kwa hiyo utukufu wa mwanamke huyu na mwili wake vimo ndani ya hifadhi bora, pia bibi huyu hupendwa na kupendeza mbele ya mumewe na kum-fanya mume kuwa na imani na mkewe, kwa sababu ya hifadhi hiyo inayomkinga kuwa na mahusiano na watu wengine kwa njia mbaya." Baada ya maelezo yaliyotolewa na yule Muumini wa kiIslamu, bwana yule mwenye kejeli aliona haya na akaanza kumwambia yule Muumini, "Najuta kwa kukuudhi, kwani maneno yako ni ukweli mtupu, na mifano uliyonipa ni sawa kabisa naom-ba samahani kwa haya niliyokutamkia na pia natubia kwa Mwenyezi Mungu kwa kitendo nilichokitenda na sasa...Kabla bwana huyu hajamaliza kujieleza mkewe alimkatiza na kusema. "Naam; naapa maneno haya aliyosema bwana huyu ni sawa na mfano aliotoa ni mzuri sana, kwani kabla ya leo nilikuwa sijasikia mawaidha kama haya. Mfano huu umeniingia moyoni nami pia natubia kwa Mwenyezi Mungu."

Baadaye yule mume akarudia kukamilisha usemi wake akasema, "Na mimi sasa naiamini Hijabu na kuanzia leo mke wangu atain-gia katika uwanja mtukufu kwa kuvaa Hijabu. Kamwe sikubali mke wangu atoke bila Hijabu, kwani ndiyo vazi la amani na imani. Nafsi yangu haipendi kabisa kumuona mke wangu akidhihiri mbele za watu kama kwamba yeye ni kwa ajili ya kila mtu."

NI LIPI LENGO LA WANAOPINGA HIJABU?

Baada ya kuusoma Uislamu kwa undani, maadui wa Uislamu wameandaa mikakati ya kuuangamiza Uislamu na Waislamu kidogo kidogo, bila Waislamu kuigundua hali hii isipokuwa wachache. Na miongoni mwa mikakati yao ya kishetani katika kutilia mkazo kuiondoa Hijabu, wametumia na bado wanatumia kila njia za kuvutia na madai batili kutimiza lengo lao hilo. Kuna mambo mengi machafu wanayoyaeneza katika jamii ya Waislamu, chini ya kiza kinene chenye ibara zinazovutia na kam-peni ambazo matokeo yake ni mabaya.

Kwa kutumia mbinu za kimaendeleo na utaalamu, wamefaulu kuwapotosha Waislamu, na wakasambaza uovu mwingi. Kwa madai hayo hayo ya maen-deleo na kupigania uhuru na haki za binadamu., uchafu wao umeenea ndani ya jamii zetu za ki-Islamu. Kwa hakika wamefaulu kuzinyang'anya jamii zetu maumbile ya kuwa na haya na heshi-ma. Ibara hizi zimewahadaa Waislamu wengi, wake kwa waume.

Masikini Waislamu hawa wamekuwa wafuasi wa itikadi hizi zenye sumu kali inayovuja kuelekea kwenye maovu na maangamio. Wanawake wa ki-Islamu na mabinti wa ki-Islamu wanafanya upin-zani hadharani dhidi ya vazi hili la ki-Islamu. Wametoka katika nyumba ya utukufu na imani na kuingia katika nyumba ya kiza na upotovu.

Wanawake wetu na wasichana wetu wameathiriwa na mavazi ya Kiyahudi na Kikristo yatokayo kwa wapinzani wa kimagharibi na makafiri wa mashariki. Maadui na wavamizi hawa wamefanikisha kwa kiasi kikubwa lengo lao, kwa kuwa sasa hivi jamii ya ki-Islamu imekwisha tumbukia na kuzama katika dimbwi la matendo machafu. Jamiii ya ki-Islamu ambayo asili yake ni adil-ifu na yenye muruwa, leo imegeuka na kushika bendera ya maovu ya kila aina.

Matukio ya kubaka,17 kupora, udanganyifu, dhulma, kutoa mimba na mengineyo, yameivamia jamii yetu tukufu. Watu hawa wa Ulaya magharibi na mashariki yake, hawali wakashiba wala hawalali wakapata usingizi, ila mpaka watimize lengo lao la kutu-achisha utamaduni wetu wa ki-Islamu. Ni wazi kabisa kwamba watu hao wanaomtaka mwanamke wa ki-Islamu avue Hijabu lengo lao wanataka wamuone mwanamke huyu anafanya ufisadi kwa kumlazimisha akae uchi. Nia yao ni kumuangamiza na kuipotosha jamii kwa jumla. Kumtaka mwanamke asivae Hijabu ni kumuondolea heshima yake na uchamungu wake.

Ewe msomaji wangu, iwapo utataka kuyafahamu vizuri maneno yangu, muulize mzee yeyote katika wazee wa makamo na mababu ambao bado wanayo kumbukumbu ya hali ya mambo ilivyokuwa hapo zamani. Waulize kwa kusema, "Hivi maovu haya yaliyopo sasa hivi ya kuwavunjia heshima wanawake na kuwaba-ka, na watu kudhulumia, mambo haya yakulikuwepo hapo zamani kabla ya miaka ishirini au thelathini iliyopita?" Watakujibu kwa nguvu zao zote, kwa kusema, Hapana kabisa hayakuwako."

17 Kwa asili mia kubwa wakazi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba, pwani ya Kenya inay-ojumuisha Mombasa, Lamu n.k, Visiwa vya Ngazija na miji mingi ya Tanganyika (Tanzania bara) kwa kipindi kirefu imekuwa ni miji ya amani na utulivu. Mazingira haya mazuri yali-jengeka kutokana na wakazi hao kuwa ni wafuasi wa dini ya ki-Islamu iliyowajenga katika maadili mema ya ki-Islamu. Ni ukweli usiyopingika kwamba hapo zamani hapakuwa na matukio ya kuwavunjia heshima wanawake kama tunavyoyashuhudia mambo hayo leo hii ndani ya miji yetu. Misamiati ya kufadhaika na kubaka haikuwako hapo zamani. Utoaji mimba na kutupa watoto ni mambo mageni kwetu hayakuwako. Ujambazi, utapeli na kutokuaminiana ni misamiati mipya. Lakini haya yote ni mipango ya maadui wa dini ya ki-Islamu, na kwa bahati mbaya Waislamu wamehadaika na mbinu za kikafiri na kujikuta wanapoteza dini yao na hata hiyo dunia waliyopambiwa imewatupa mkono hawana nayo asilani. Msiba uliyoje kwa Umma wa Ki-Islamu!! Mtarjumi.

Sasa yametoka wapi mambo haya maovu na matukio ya kuhuzu-nisha? Watakuambia, "Hali hii imetokana na mambo mengi, mion-goni mwake ni wanawake wenyewe kutembea mabarabarani bila sitara ya kisheria." Hili ndilo jibu sahihi kwa matatizo kama haya ya ubakaji ambayo takwimu zake zinaongezeka kila siku. Iwapo utataka uhakika zaidi, waulize wakazi wa miji michache ambayo wakazi wake bado wanashikamana na sheria za ki-Islamu na imani zao zingali hai na uwaambie, "Hivi katika miji yenu kuna matukio maovu ya kubaka na unyang'anyi kama inavyotokea katika miji mikubwa?" Bila shaka watakujibu hapana. Sababu kubwa ya kutokuwepo maovu kwa wingi katika sehemu hizo, ni kwa kuwa jamii bado inauheshimu na kuulinda Uislamu na kanuni zake zenye hekima.

Maovu mengi zaidi yanajitokeza katika miji au sehemu ambazo zinadai kuwa zimeendelea. Miji hiyo imehusika kwa kiwango kikubwa na ongezeko la maovu ambayo yanakithiri kwa kasi ya kutisha, licha ya serikali zao kutoa adhabu kali kwa wanaohusika kila wanapobainika na kukamatwa.18

Hali hii inaonyesha wazi kwamba kanuni peke yake hazitoshelezi, wala hazinufaishi katika kuirekebisha jamii, bali kinachotakiwa ni kuing'oa mizizi ya maovu kwanza, ili maovu hayo yapate kunyau-ka yenyewe. Kwa kawaida kila kitu kina asili yake, na asili ya maovu yaliyozikumba jamii zetu sasa hivi, ni hizi picha za video wanazooneshwa vijana wetu, 18 Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimekumbwa kwa kiasi kikubwa na matatizo ya mmomonyoko wa maadili, na zinatungwa sheria kali kila leo ili labda? itawezekana kureke-bisha hali hii, lakini bila mafanikio. Tunachokiona ni ongezeko la maovu ambayo yanatende-ka wazi wazi na kila mtu anayashuhudia wakiwemo hao wanaokaa na kutunga sheria hizo kwa matumaini ya kukomesha maovu. Hakuna njia inayoweza kukomesha hali hiyo isipokuwa ni kushikamana na mafunzo bora ya ki-Islamu. Ni muhimu kwa viongozi wetu wakatambua mambo yanayochangia uharibifu wa mwenendo wa jamii na kuhakikisha kuwa wanaing'oa mizizi yake. Mtarjumi.

picha ambazo huwa zinaonesha hali ya maumbile ya siri, isi-toshe huonesha pia matendo ya jinsiya baina ya mke na mume bila kuona aibu wala huzuni kuuchezea na kuudhalilisha uanadamu ambao ni kitu cha thamani, kutokana na kuwa na uwezo wa kutambua nini cha kufanya na nini si cha kufanya. Kitu kingine kinachochangia ni nchi zetu zinaporuhusu uingizaji wa magazeti na majarida yanayochapisha picha zinazoonesha sehemu za siri na kisha magazeti hayo na majarida yanasam-bazwa katika jamii. Maadam asili ya maovu bado ipo kama mifano ya picha za video na majarida tuliyoyataja hapo kabla, basi maovu na matukio machafu yataendelea kutokea siku hadi siku, na kamwe hayataondoka kwa kutegemea kanuni hizi za kidunia.

2

VAZI LA MWANAMKE

NI YUPI MWANAMKE BORA

Sasa napenda kutoa mifano miwili ya wanawake wawili ambao kila mmoja anao mwelekeo wake na mwenendo tofauti na mwenzake, lakini wote wanaishi katika jamii moja. Wa kwanza ni yule mwanamke mwenye kuvaa Hijabu ambayo ni sitara ya imani na ni vazi la ki-Islamu, tena ni vazi la heshima na humpa utukufu mvaji. Kwa kuvaa Hijabu, mwanamke huyu atakuwa amepata radhi za Mola wake na kupata utukufu wa watu wa peponi. Kwa vazi hili mwanamke huyu huvutia mvuto wa ucha Mungu na heshima.

Pia dalili za utulivu hujitokeza kwa mwanamke huyu na dhana njema kwake hutawala fikra za kila amuonaye. Amtazamapo mwenye kumtazama, huwa ni shida kutambua, je, mwanamke huyu ni msichana au ni mtu mzima? Sura yake ikoje nzuri au la? Hutatizika wanaomuangalia. Matokeo yake watu humuangalia kwa jicho la heshima, hakuna awezaye kumkabili kwa maneno chafu au maudhi, kwani anafahamu wazi kwamba mwanamke huyo ameshikamana na dini yake na anaheshimu utu wake. Isitoshe mwanamke kama huyu huwa amejitenga na matendo ya aibu na kujiepusha na wanawake wasio na sitara, na kwa ajili hiyo hayuko tayari kuidhalilisha nafsi yake.

Huo ndiyo mfano wa mwanamke mmoja na namna alivyojiweka katika jamii yake. Kwa upande wa yule mwanamke wa pili, ni yule asiyejali kujisitiri uso wake amevua vazi la la stara, hana aibu wala haya. Kwa maana hiyo ameing'oa imani yake, kwa sababu Mtume anasema: "Mtu kuwa na haya ni sehemu ya imani, na mtu asiye na haya hana imani." Kwa mwenendo wake mwanamke huyu, huwa ni mpinzani mkubwa wa muongozo wa Qur'an na huwa anajidhalilisha kwa kuonesha mapambo yakem, kama walivyokuwa wakionesha mapambo yao wanawake wa zama za kijahiliya kabla ya kuja Uislamu. Isitoshe kwa mwanamke huyu, hali aliyo nayo huwa amejifananisha na wanawake wa Kiyahudi na Kikristo, na huwa yuko mbali na heshima yake na utu wake. Kutokana na kuudhihirisha mwili wake na uso wke na mikono yake, pia kifua chake na sehemu nyingine katika maumbile ya kike. Watu waovu na wenye tamaa huyaona wazi wazi maumbile yake na hapo tayari anakuwa mfano wa bidhaa zilizotandazwa sokoni, kwani kila mtu ana uhuru wa kuziangalia bila mipaka.

Matokeo ya uovu wa mwanamke huyu, ni kupata usumbufu toka kwa wahuni ambapo hatimaye wanaweza kumtendea matendo machafu yanayoweza kumharibia tohara yake. Na iwapo itafikia hali ya kuharibiwa tohara yake, basi atakuwa amepoteza heshima yake na utu wake katika jamii. Hii ni kwa sababu ameacha kuulin-da mwili wake ndani ya vazi la kisheria. Baada ya kuwa mmefahamu namna za wanawake hawa wawili sasa tuwe pamoja kaitka kulinganisha hali zao kati yao na tujiulize masuali yafuatayo.

1.Je ni yupi mwanamke bora baina yao? 2.Yupi kati yao ni mtulivu na anayevutia, 3.Mwenye kujilinda au yule anayeuacha wazi mwili wake? 4.Ni yupi mwenye kuheshimika kati yao, mwenye Hijabu au yule asiye na Hijabu? Bila shaka, mwanamke mwenye Hijabu na ucha Mungu ni bora na ni mtukufu tena ni mwenye thamani kuliko yule mwingine.

KIPINDUPINDU NDANI YA JAMII

Miongoni mwa maradhi yanayoua haraka ni kipindupindu kwa mujibu wa taarifa ambazo huwa zinatolewa baada ya maradhi hayo kuingia katika kijiji au mji. Kila yanapodhihiri maradhi haya, hutangazwa hali ya hatari katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na kuwekwa karantini. Kama ilivyo katika kuzuia kipindupindu kisie-nee katika mji au kijiji, na fisadi nyingine ni hivyo hivyo. Sasa basi mtazamo wa Uislamu katika kuitazama jamii ni mtazamo wenye hekima kubwa, na ni mtazamo ambao lengo lake ni kujenga jamii nzuri na safi isiyokuwa na maovu ndani yake. Miongoni mwa mambo yanayoweza kudhibiti amani na ubora wa jamii ni mavazi. Siyo kweli kwamba kila vazi linaweza kukidhi haja hii, bali Hijabu pekee ndiyo jawabu, kwa sharti ya kuwa mvaaji aivae kwa kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu na siyo kinyume chake.19

baadhi ya watu wanajaribu kulitia dosari vazi la Hijabu kuwa eti ni vazi linalovaliwa ili kuficha maovu ya hao wanovaa. Upo ukweli fulani kuhusu madai haya, lakini upotoshaji huu wa vazi la Hijabu usiwe miongoni mwa sababu za kuwakatisha tamaa wanawake wa kiIslamu wanaovaa Hijabu kwa kumtii Mola wao, kwani ni mara ngapi watu wanautumia usiku kwa mambo maovu wakati Mwenyezi Mungu ameuweka kuwa ni kipindi cha mapumziko baada ya kazi za kutwa nzima? Kwa hiyo matumizi mabaya ya kitu kizuri hayawi ni sababu ya kukifanya kitu hicho kuwa kibaya. Mtarjumi.

Hijabu humlinda mwanamke kutokana na ufasiki na inamzuia kukhalifu maumbile yake aliyopangiwa kuishi ndani yake. Kwa kanuni hii ya Hijabu, Uislamu unakuwa umeisalimisha jamii na kuilinda isije ikajikuta imeteleza na kuvamiwa na maovu. Hali hal-isi inayojitokeza katika malengo ya msingi kuhusu kanuni hii ya Hijabu, ni kuitakasa jamii na kuisafisha, pindi wanawake watakapofuata sheria ya kuvaa Hijabu. Kinyume chake haitawezekana kabisa kudai kwamba jamii yetu ni safi, wakati wanawake zetu wanatembea bila kujali ni nguo gani wamevaa, kwa kuwa suala la mavazi kwa wanawake linataka litazamwe kwa mapana na marefu isiwe mradi kuvaa tu. Ni mara ngapi tunashuhudia mambo ya aibu na ya kuhuzunisha wanafanyiwa wanawake? Hivyo uchafu unasambaa haraka na kuleta madhara kwa wingi, kama kipindupindu kilichoingia mjini au kijijini. Na kwa ajili hiyo karantini inahitajika kuwekwa na kufuatwa kwa mujibu wa maelekezo ya wataalamu.

Uislamu kwa upande wake unataka kukata na kung'oa mizizi ya fitina na maovu kwa kutumia njia mbali mbali ikiwemo kusisitiza vazi la Hijabu. Pia Uislamu kwa nafsi yake unapinga kwa nguvu uovu na kila jambo linalokuwa ni sababu ya kueneza uchafu ndani ya jamii, miongoni mwa sababu hizo ni mwanamke kutokuwa na Hijabu ambayo ni vazi la kisheria.

KUKOSEKANA SITARA KUNALETA MAOVU

Miongoni mwa maovu na athari mbaya katika jamii, ni wanawake kuacha kuisitiri miili yao ipasavyo, kitu ambacho kimesababisha vijana wetu wa kiume kuteleza na kujikuta wanafanya mambo machafu bila kukusudia. Imam Ali ibn Musa Ar-ridha anasema,"....Imeharamishwa kuangalia nywele za wanawake, kwani katika kuziangalia nywele hizo kunasababisha kuamsha hisia za wanaume ambazo huwafanya waingie katika maovu na mambo yasiyo halali na yasiyopendeza." 20 Hapana shaka kwamba, mwanamke anayetoka nyumbani mwake na kwenda sokoni bila kujali ni vazi gani alilovaa, hajali kama limemsitiri vizuri au hapana, ni wazi kabisa huko njiani ataonekana kwa watu wa aina mbali mbali wakiwemo vijana ambao ndiyo kwanza wanaingia katika rika la ujana na nafsi zao bado hazijaweza kujimiliki kuhusu suala la kijinsiya.

Hali kama hii ni lazima itaamsha hisia za kimaumbile za vijana hao kutokana na jinsi mwanamke huyo atakavyokuwa amevaa na umbile lake linavyoonekana kwa jumla pindi atakapopita mbele yao. Hisia hizi za kimaumbile ni lazima ziamke kwa kuwa ndivyo ilivyo hali halisi. Kwa hali hii basi nafsi za vijana hawa kwa tabia ya maumbile ya mwanaadamu huanza kuhangaika kutafuta njia za kuyatosheleza maumbile yao.

Suala la kujiuliza hapa ni je, vijana hawa watafanya nini? Ikiwa wao sio watu walioshikamana na mafunzo ya dini wala hawafuati miongozo ya ki-Islamu, basi watajaribu kutosheleza hamu zao kwa njia ya siri ambayo ni kujitoa manii jambo ambalo ni hasara na aibu. Ama wengine hufanya baya zaidi ambalo ni kinyume cha utaratibu aliotuwekea Mwenyezi Mungu, hawa hufanya liwati. Kundi jingine wao huamua kuzini na katika huko kuzini huwa wanatumia kila njia kufanikisha azma yao hiyo, ikiwa ni kwa hila au hata kwa nguvu ambayo ni kubaka wanawake mitaani. Matokeo ya ubakaji ni kuvunja heshima za watu na kuwadhalil-isha wanawake.

20 Biharul Anwaar juz 6 uk 130. Kilichokusudiwa hapa bila shaka ni nywele za mwanamke ambaye si maharim wako wala siyo mkeo. Ikiwa nywele tu zinatosha kumuingiza mwanaume ndani ya madhambi, basi ikoje hali ya watu leo hii kwa namna wanawake wa kileo wanavy-ovaa.? Je! Ni kwa kiasi gani wanatuingiza katika madhambi? Leo hii siyo nywele tu bali vifua vya wanawake vinaonekana kwa kila mtu na maungo mengi yanakashifiwa na kila mtu. Hivi kweli kwa hali kama hii vijana wetu watasalimika na maovu? Pia hao kina dada nao watam-laumu nani watakapovunjiwa heshima? Mtarjumi.

Pamoja na matendo haya kwenda kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu, pia yanasababisha maradhi hatari na vifo vya ghafla..21 Inakadiriwa kwamba idadi ya hospitali zinazo shughulikia maradhi ya uasherati peke yake inafikia hospitali mia sita hamsini. Hesabu hii ni kwa nchi ya Marekani peke yake. Chanzo cha balaa lote hili ni kwa wale wanawake wasiojali kutenganisha maumbile yao na ya wanaume mpaka wakawa wanaona miili yao haistahiki kulindwa na kupewa hadhi ya pekee. Lakini kila mwanamke asiyezingatia suala la mavazi kisheria ni lazima atambue kwamba, yeye ni mshiriki mkubwa anayesababisha madhambi na mis-iba hii, na anayo sehemu yake ya adhabu mbele ya Mwenyezi Mungu.

Yote yaliyotajwa hapa sasa hivi, yanatokana na vijana ambao wao siyo watu wa dini wala hawashikamani na Uislamu. Kwa upande wa pili inawezekana vijana hao wakawa ni watu wa dini na wanaambatana na mafunzo ya ki-Islamu na sheria zake, basi vijana hao huzuia hisia zao zisivuke mipaka ya Mwenyezi Mungu na hupambana na matamanio ya nafsi zao na kumlaani shetani asije akawahadaa. Vijana hawa huvumilia kero ya maumbile na kubeba mzigo mzito ambao hawakutarajia kuubeba. Kwa mara nyingine tena mwanamke au wanawake wasiojali sheria ya mavazi kama Mwenyezi Mungu alivyoamrisha, wanabeba uzito wa taabu na maudhi yanayowapata watu hawa wa dini.

21 Asili ya yote hayo ni mwanamke au wanawake ambao kwa makusudi kabisa wanaamua kuvaa nguo ambazo zitahatarisha usalama wao na usalama wa jamii yote. Kuhatarisha usala-ma wao na wa jamii peke yake haitoshi, bali waelewe kwamba wanasababisha vijana wetu wa kiume kuchuma madhambi makubwa, na wakati mwingine kuwaharibia maisha yao ya baadaye kwa kufungwa jela kutokana na hatia ya kubaka. Madhara mengine yaletwayo na matukio ya zinaa na liwati ni pamoja na kuambukizwa maradhi hatari kama vile kisonono, kaswende, na leo ukimwi. Maradhi haya hatari yameleta huzuni na misiba inayotisha katika ulimwengu. Mtarjumi.

KUTOKUVAA HIJABU NA MADHAMBI YA UBAKAJI

Miongoni mwa athari mbaya zinazosababishwa na tabia ya wanawake ya kutokuvaa Hijabu ni yale makosa ya jinai ya kuwabaka wanawake na kuwaingilia kwa nguvu bila hiyari yao. Ni jambo lisilofichikana pindi mwanamke anapouacha wazi mwili wake na mapambo yake, hali hiyo huamsha hisia za kijinsia kwa wanaume. Kwa hakika ni juu ya mwanamke mwenyewe kuulinda mwili wake, mapambo yake na utu wake kutokana na hatari hiyo inayoweza kumkabili.

Hapana shaka kwamba, macho ya vijana wasiokuwa na msi-mamo wa dini, pindi wanpomuangalia mwanamke ni sawa na macho ya mbwa mwitu anapomuangalia kondoo. Pia tunaweza kuyalinganisha macho hayo na macho ya paka anapomuona panya, au tuseme yanafanana na macho ya mnyama mkali wa porini, anapomuona mnyama mwingine au kitu kimngine amba-cho kinamfaa kwa chakula. Siyo ajabu kabisa kwa mazingira kama haya kumkuta mwanamke amenasa ndani ya mtego alio-jitegea mwenyewe kutokana na tabia ya kujitangaza mbele ya watu waovu.

Tabia hii ya ubakaji mara nyingi inatokea katika sura ya kutisha huko kwenye nchi za magharibi ambazo zimeporomoka mno katika suala zima la maadili. Katika ripoti moja kati ya matoleo ya gazeti la The Gurdian la nchini Uingereza iliandikwa kwamba; "Takwimu za polisi zinaonesha kuwa, makosa ya jinai ya kubaka yanaongezeka mwaka hadi mwaka. Katika mji wa Washington peke yake kila baada ya dakika kumi na tano huwa kuna tukio la kubaka, na katika mji mkuu wa Uingereza (London) yalitokea matukio 2095 ya kubaka wanawake na wasichana mnamo mwaka wa 1970 peke yake."22 Haya ni machache katika mengi ambayo tungeweza kukuorodheshea.

22Majallatud-Dastuur Lebanon.

Na miongoni mwa matukio ya kubaka kutokana na wanawake kutokujali kujisitiri kwa mujibu wa sheria na maumbile yao, mimi nimesikia kwamba, kuna rais fulani anayeongoza nchi moja miongoni mwa nchi za Kiarabu, yeye hufanya ziara za mara kwa mara kuvitembelea vyuo vikuu akitafuta mabinti katika vyuo hivyo na kuwachagua wale wazuri na wanaopendeza. Kisha humtoa nje ya msitari binti anayemuona kuwa atamfaa. Baada ya muda mfupi askari wa usalama wa taifa huwa wanakwenda nyumbani kwa binti huyo na kumweleza baba yake kwamba rais wa jamhuri anamtaka binti yake akakeshe naye katika usiku wa siku hiyo!!

Hali kama hii husababisha msiba mkubwa kwa baba, mama, binti huyu na hata familia nzima huingia ndani ya mtihani huu. Msiba huu huwagubika watu hawa kwa sababu wanafahamu wazi kwamba rais huyu ataishi na binti yao kwa usiku huo mmoja tu!! Sasa je, watu hawa watalikataa ombi la rais? Na je, inawezekana kwa watu hawa kuuepuka unyanyasaji unaowasubiri kutoka kwa rais wao? Basi je, matokeo ya jambo hili yatakuwaje? Hapana jambo jingine litakalotokea hapo isipokuwa msichana itamlazimu kuuendea uovu kwa miguu yake mwenyewe. Ataifuata fedheha na aibu hiyo kubwa bila kupenda, na kisha atarudi nyumbani hali ya kuwa amekwishapata hasara ya kuvunjika kwa heshima yake na utu wake pia kagubikwa na kiza la ulimwengu machoni mwake.

Ewe msomaji mpendwa, hapana shaka kwamba watu wanaoso-ma au kusikia unyanyasaji huu, utawaona wanamlaani na kumsh-tumu rais huyu muovu. Lakini hebu tufikiri kidogo juu ya misingi inayosababisha mateso haya na tujiulize swali lifuatalo: Je! Ni nani mwenye makosa? Hivi kweli mwenye makosa siyo yule baba ambaye toka hapo mwanzo alimruhusu binti yake atoke ndani hali ya kuwa maungo yake yako wazi na uzuri wake unaonekana kwa kila mtu? Lau binti huyo angekuwa ni mwenye kujisitiri, hivi unadhani yule rais mpumbavu angelimtamani na kumfanya kuwa kiwindo chake?

Ni baba ndiyo mwenye kustahili lawama tangu ile siku aliponunua television (ambayo ni adui mkubwa muovu aliye-mo ndani) ili kuistarehesha familia yake kwa kuangalia vipndi viit-wavyo kuwa ni vya watu walioendelea!! Baba huyo huyo ndiyo mwenye lawama siku zile alipokuwa akiichukua familia yake kwa ajili ya kwenda sinema kuangalia filamu za watu walio uchi. Na mama pia anastahili lawama... Je ! Siyo yeye yule ambaye alikuwa akizifumua nywele za binti yake na kumpamba utadhani siku hiyo ndiyo siku ya harusi yake na kisha akamwacha kwenda shuleni akiwa katika mazingira kama hayo?

Ni huyo mama aliyekuwa akimchagulia binti yake asiyejuwa kitu mavazi mafupi yanayobana mwilini ambayo hayamsitiri inavy-opasa? Binti naye anapaswa kulaumiwa kutokana na matokeo hayo yenye kiza kinene cha majonzi kwa kuwa ni yeye mwenyewe ndiye aliyechagua tabia ya kuuweka wazi mwili wake, na pia akachagua kupita njia ngumu iliyojaa miba na mawe. Naam, watu hawa ndiyo tabaka la mwanzo la kulaumiwa, na baada ya hapo ndio mnapaswa kumlaani rais yule!!

KUTOKUVAA HIJABU NA MADHAMBI YA UTOAJI MIMBA

Ni vema pia kutaja mambo mengine ambayo yanaletwa na makosa ya jamii inapokuwa imepuuza na kuacha Hijabu. Yapo mengi, lakini yanayotajwa ndani ya kijitabu hiki ndiyo ya msingi. Suala la kutoa au kuharibu mimba ni miongoni mwa athari mbaya ziletwazo na ukosefu wa sitara bora ya kisheria kwa wanawake. Ni mara nyingi inatokea kwa wanawake wasio na Hijabu kuvunji-wa heshima zao na utu wao.

Mwanamke asiyekuwa na sitara bora pindi anapodhihiri mbele ya vijana wenye dhiki ya kukidhi haja zao za kijinsia, hapana shaka vijana hao hushindwa kuyazuwia matamanio yao na hapo ndipo huamua kumbaka. Hapo mwanamke huwa anajikuta ametum-bukia mikononi mwao bila hiyari, na huenda ikatokea bahati mbaya mwanamke huyo anaweza kubeba mimba haramu ambayo hakuitarajia. Kutokana na uovu huu aliofanyiwa hulaz-imika kuitoa au kuiharibu mimba hiyo. Leo hii katika anga la dunia yetu matukio kama haya ni mengi mno. Yako wazi kila mahali na hasa nchi za Ulaya Magharibi na zile zote zinazojaribu kuiga ustaraabu wa magharibi.

Tarehe 28 Februari mwaka 1972. jarida la An Nahaar la Lebanon lilichapisha katika ukurasa wake wa makala maalum kama ifu-atavyo. "Katika mji wa London idadi ya utoaji mimba imeongezeka kutoka wanawake hamsini elfu mwaka 1969 hadi kufikia wanawake themanini na tatu elfu mwaka 1970 na idadi inayokaribia laki mbili mwaka 1971. Na huko Ufaransa hali hii imeongezeka na kufikia kutolewa mimba arobaini na sita hadi mia moja arobaini na tatu katika kila mimba mia mbili wanazobeba wanawake kwa mwaka. Ama huko Urusi, kuna mimba zipatazo milioni sita zinazotolewa kila mwaka.23 Kwa hakika takwimu na taarifa hizi zinatisha, na yote haya ni matokeo ya tabia ya wanawake kuyaonesha wazi maumbile yao na uzuri wao mbele ya kila mtu. Hakuna njia ya kuzuwia mad-hambi haya isipokuwa vazi la Hijabu iwapo litavaliwa kwa mujibu wa sheria na kutunza mipaka ya dini.

1

VAZI LA MWANAMKE

BIBI FATIMA (A.S) KIIGIZO CHEMA KWA WANAWAKE

Bibi Fatimah(a.s) ni mwanamke anayezingatiwa kuwa ni mwanamke wa kutolea mfano katika dini ya ki-Islamu, na pia ni kiigizo chema kwa kila mwanamke anayetafuta mafanikio katika maisha yake. Bibi Fatimah binti Muhammad(s.a.w.w) ndiye mwanamke bora ulimwenguni aliyezaliwa na kupata malezi katika nyumba iliyokuwa ikishuka ndani yake Wahyi kutoka mbingu-ni.

9 Hadithi hii imenukuliwa kutoka ndani ya kitabu kiitwacho Tuhaful- Uquul. Katazo hili linajumuisha mambo mengi na khususan mambo yote ambayo Mwenyezi Mungu hayaridhii na yanatendwa na maadui wa Mwenyezi Mungu. Mwislamu inamuwajibikia kujiepusha nayo vinginevyo hapatakuwa na tofauti kati ya Muumini na adui wa Mwenyezi Mungu. Mtarjumi.

Si hivyo tu bali Bibi Fatimah alihitimu mafunzo ya Uislamu katika madrasa ya Utume, na kutokana na mafunzo hayo aliweza kufikia daraja ya juu na tukufu. Katika kuthibitisha ubora wa Bibi Fatimah, Mtume(s.a.w.w) amepata kusema,"Hakika Mwenyezi Mungu huwa radhi kwa radhi ya Fatimah, na huchukia kutokana na kuchukia kwa Fatimah. " 10 Kwa ajili ya daraja kubwa aliyonayo Bibi Fatimah katika Umma wa Nabii Muhammad(s.a.w.w) imekuwa ni wajibu kwa kila mwanamke duniani kuiga mwenendo wa Bibi huyu katika maisha yake, ajing'arishe kwa nuru yake nzuri na afuate nyayo zake ambazo zitamuelekeza kwenye mafanikio na utukufu. Hakika Bibi Fatimah(a.s) , ni mfano wa kila utukufu na kila jema. Mwanamke yeyote atafanikiwa iwapo ataamua kufuata mwenendo wa Bibi Fatmah (a.s.) , na kinyume chake ni kuwa, kila mwanamke ataangamia iwapo ataamua kujichagulia mwenendo wake au kuiga usiyokuwa mwenendo wa Bibi Fatimah. Pia Fatimah(a.s.) alikuwa Mchaji Mungu na mwenye kutekeleza vilivyo maamrisho ya Mwenyezi Mungu. Pia ile maana nzima ya Hijabu aliifahamu vema na kuitekeleza kama ilivyoamriwa na Mwenyezi Mungu.

Hivyo utekelezaji wake katika maamrisho ya Mwenyezi Mungu ulikuwa wa hali ya juu, kwani hakupata kutoka nje ila huwa amevaa vazi la kumsitiri mwili wake wote tangu kichwani hadi miguuni. Isitoshe alikuwa akiichukia mno tabia ya wanawake kutoka majumbani mwao bila kujisitiri kisheria. Bibi Fatimah alichukizwa na tabia hiyo kwa sababu Mwenyezi Mungu pia anaichukia tabia ya kutokujisitiri na hasa kwa kuwa kukosa sitara ya kishera kwa wanawake ni ufunguo wa kuyaendea maovu na ni miongoni mwa vitangulizi vinavyosababisha watu kuteleza, bali wanaaanguka kabisa. 10Mustadrak Alhakim juz 3 uk , Al isabah ya Ibn Hajar Al asqalani juz 4 uk. 10 Sasa hivi tunawaletea baadhi ya mafundisho kuhusu Hijabu na tutaona pia utukufu wa Bibi Fatimah katika mafunzo hayo.

NI KITU GANI KILICHO BORA KWA MWANAMKE?

Inasimuliwa katika historia kwamba, Mtume(s.a.w.w) siku moja aliwauliza Masahaba suali lifuatalo:"Je! ni kitu gani kilicho bora kwa mwanamke?" Masahaba walinyamaza kwa kuwa jibu la mkato na sahihi hawakulifahamu, ikawa kama kwamba akili zao zinahangaika baina ya kuwa kilicho bora kwa mwanamke ni mali, uzuri wake, kuolewa au kitu gani? Kipindi chote hiki Bibi Fatimah alikwisha lisikia swali hilo, na baada ya kimya cha kukosekana jibu, Bibi Fatimah alimtuma mtu aende kwa Mtume(s.a.w.w) aka-toe jibu sahihi la swali hili nalo ilikuwa;"Kilicho bora kwa mwanamke ni yeye mwanamke asimuone mwanaume na mwanaume naye asimuone mwanamke." 11

Baada ya jibu la bibi Fatimah Masahaba walikuwa wakisubiri jibu la Mtume atasema nini kuhusu jawabu alilotoa Binti yake. Mtume(s.a.w.w) akasema "Amesema kweli Fatimah." Na akaongeza kusema,"Fatimah ni sehemu iliyotokana na mwili wangu." Maana ya maneno ya Mtume yalimaanisha kwamba hilo ndilo jawabu sahihi na hiyo ndiyo imani. Kutokana na jawabu hili, Bwana Mtume(s.a.w.w) akawa ameitangazia dunia nzima kwamba; Utu, heshima, utukufu, na wema wa mwanamke unapatikana ndani ya Hijabu, na kinyume chake ni uovu na shari, isitoshe hasara hum-fika mwanamke anapoitupa Hijabu. 11Hapana shaka makusudio yaliyomo ndani ya jawabu la bibi Fatimah(a.s) ni kwamba, waw-ili hawa yaani mwanamke na mwanaume ni wale wasiokuwa na uhsiano wa kisheria. Watu wenye uhusiano kisheria ni kama hawa wafuatao: Mama, dada, shangazi na au Baba, kaka, mjomba na wengine ambao wametajwa katika vitabu vinavyohusika na sheria. Ama mume na mke, wawili hawa uhusiano kati yao hauna haja ya kutolewa maelezo. Mtarjumi.

MAZUNGUMZO YA KUSTAAJABISHA

Historia inaendelea kutufahamisha kwamba Bibi Fatimah(a.s) alikuwa amekaa na baba yake ambaye ndiye Mtume(s.a.w.w) , mara alibisha hodi Sahaba Abdalla ibn Ummi Maktum ambaye alikuwa kipofu. Kabla Sahaba huyu hajaingia Bibi Fatimah(a.s) alisimama akaondoka mahali hapo. Baada ya kwisha mazungumzo baina ya Mtume na Sahaba huyu, Sahaba Abdallah ibn Ummi Maktum aliondoka. Bibi Fatima alirudi na akaendelea kuzungumza na Mtume(s.a.w.w) Bwana Mtume(s.a.w.w) .wakamuuliza Binti yake sababu ya kuondoka wakati alipoingia Sahaba Abdallah ibn Ummi Maktum hali kuwa anafahamu kabisa kwamba yule ni kipofu haoni.12

Bibi Fatimah alijibu kama ifuatavyo."Ikiwa yeye hanioni basi mimi namuona na yeye ananusa harufu ya wanawake. " Mtume(s.a.w.w) alifurahishwa mno na jawabu la Binti yake ambalo linaonyesha kipimo cha Uchamungu na utukufu unaotoka kwa Binti yake Mwenye hekima. Isitoshe kwa jawabu hilo, Bwana Mtume hakumlaumu binti yake kutokana na mkazo huu mkali unaohusu Hijabu, bali furaha ya Mtume iliendelea kwa upeo mkubwa na akaunga mkono kwa dhati kabisa kisha akasema;"Nashuhudia kwamba wewe ni sehemu iliyotokana nami" 13.

12 Ni vyema ikaeleweka wazi kwamba Bwana Mtume(s.a.w.w) alimuuliza Binti yake suali hilo hali ya kuwa yeye mwenyewe anajua wazi kuwa Sahaba yule alikuwa haoni, lakini lengo la Bwana Mtume (s.a.w) kuuliza suali hilo alitaka aone namna Binti yake atakavyo toa jawabu la suali hilo ili historia ipate kusajili mazungumzo haya ya kiimani na ubakie kuwa ni mfano mzuri wa kuigwa siku zote.

13 Mustadrak Al-Wasail Kitabun-Nikah. Biharul-An-Waar juz 104 uk 38.

TUKIO MUHIMU NDANI YA MSIKITI WA MTUME (S.A.W.W.)

Siku moja Bibi Fatimah(a.s.) alitaka kutoa mhadhara ndani ya msikiti wa Mtume(s.a.w.w) Kabla ya kuanza kuhadhiri aliten-genezewa sitara humo Msikitini, akakaa yeye na Waumini wengine wakike upande mmoja na Waumini wanaume wa Kiansari na Muhajirina nao wakakaa upande wa pili. Sitara hii aliyotengenezewa Bibi Fatimah(a.s) ilikuwa ina maana nyingi ndani yake. Kwanza ilikuwa ni kutekeleza sheria inayohusu Hijabu katika sura ya kuweka kizuizi, ambapo pande mbili hizo zilitenganishwa. Pili, hali hiyo ilikuwa ni kuonesha kutokuukubali kwa vitendo mchanganyiko wa wanaume na wanawake, jambo ambalo maadui wa Uislamu wanatumia kila mbinu kulihalalisha kwa kuli-tolea hoja batili.

Sasa nakutazama ewe dada yangu wa ki-Islamu, nikitarajia umeiona mifano hii mitatu inayohusu maisha ya Bibi Fatimah(a.s.) ambaye ni mwanamke bora kuliko wanawake wote duniani, na ni mwanamke anayestahiki kuigwa katika Uislamu. Inafaa uige na ujifunze kwake ili upate kupambika kwa umbile la kike ( yaani kuwa na haya) na utukufu, kadhalika ifanye nafsi yako iwe ya mwanamke Mchamungu mwenye kushika mafunzo ya ki-Islamu na hukmu za Qur'an. Ewe dada wa ki-Islamu hebu shikamana na mafunzo ya ki-Islamu ambayo Mwenyezi Mungu amekupa ili ufanikiwe duniani na akhera. Mafunzo haya yatakupandisha kwenye daraja tukufu la wenye imani na mafanikio. Fahamu kwamba hutafanikiwa isipokuwa uwe umeshikamana na kuyatu-mia mafunzo hayo kwa kuyatekeleza maishani mwako.

KUJIHESHIMU NDIYO PAMBO LA MWANAMKE

Bwana Mtume(s.a.w.w) amesema,"Kujiheshimu ndiyo pambo la Mwanamke." Hapana shaka kwamba pambo limegawanyika sehemu mbili: Pambo lisilo halisi na pambo halisi. Ama pambo lisilo halisi ni lile ambalo linaloonekana wazi, na ni lenye kubakia kwa muda maalum, kisha hutoweka bila hata ya kumuongezea kitu muhusi-ka katika utu wake. Ama lile pambo halisi, ni lile ambalo hubakia muda wote na pia humfanya mwanamke aupate ule utu wake kamili na kumfikisha kwenye daraja ya ukamilifu. Ukweli usiokuwa na shaka ni kuwa, pambo halisi ndilo lenye umuhimu mno kuliko lile jingine, bali ndilo lengo analopaswa kulishughulikia kila mtu. Endapo mtu atakosa kuwa na fungu fulani katika pambo hili halisi, basi pia huwa hana faida yoyote ndani ya lile pambo la dhahiri.

Hapana shaka kwamba kujiheshimu ndilo pambo pekee linalom-faa mwanamke kama alivyosema Bwana Mtume(s.a.w.w) . Pambo hilo humjengea mwanamke utu, heshima na utukufu hapa duniani na kesho akhera. Ama madawa ya kujirembesha, manukato na mengineyo miongoni mwa mapambo, yote hayo ni mapambo ya nje tu na hayana maana yoyote khususan mwanamke mwenyewe atakapokuwa si Mchajimungu; Mwenyezi Mungu apishe mbali.

Hijabu ndiyo alama pekee inayoweza kutambulisha Uchaji Mungu wa mwanamke na pia heshima yake na utu wake. Wakati huo huo tabia ya kutokuwa na Hijabu huchafua heshima ya mwanamke na kuacha maswali chungu nzima kuhusu Uchaji Mungu wake na kujiheshimu kwake kwa jumla. 14Kalimatur-Rasuli uk 110 cha Sayyid Shirazi.

Yote haya yanakuja kwa sababu yeye mwenyewe kauweka mwili wake kuwa maonesho mbele ya maelfu ya watu siku zote. Kutokana na hali kama hiyo, hata huwezi kutambua ni mikono mingapi iliyowahi kuushika mwili wake kwa kuuacha wazi na kutokujisitiri kwa mujibu wa sheria!! Hivi unadhani watu wa kale na hata wa leo hii, nyoyo zao zitasal-imika vipi katika mazingira hayo ya wanawake kuicha wazi miili yao? Kamwe hawatasalimika kabisa, kwani wanawake wanapoiacha wazi miili yao ni jambo linalopelekea tuhuma mbaya kwa wanawake. Imam Ali(a.s.) anasema"Yeyote mwenye kui-weka nafsi yake mahala penye tuhuma mbaya, basi asimlaumu mtu atakaye mdhania vibaya." 15

Hapana shaka kwamba, mwanamke asiyekuwa na Hijabu huwa anaidhuru nafsi yake mwenyewe kwa sababu; Kwanza, huwa anapata hasara mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Pili, heshi-ma yake ndani ya jamii huwa inaporomoka. Hasara anayoipata mwanamke huyo mbele ya Mwenyezi Mungu inakuja kwa sababu mwanamke huyo huwa amekwenda kinyume na kanuni za mbinguni na kukosa utiifu kwa Mwenyezi Mungu. Baadaye tutaeleza adhabu za huko akhera atakazozipa-ta mwanamke asiyejali kujisitiri kwa mujibu wa sheria ya KiIslamu.

Ama hasara atakayoipata mwanamke kutoka na na heshima yake kuporomoka ndani ya jamii, hali hiyo inasababishwa na yeye mwenyewe kutokana na tabia yake ya kuyaacha wazi maungo yake yaonekane kwa kila mtu, hali ambayo humuingiza ndani ya kila aina ya uovu na ufisadi na hatimaye akadhalilika vibaya. 15 Al-kafi juz uk 152. Miongoni mwa dhana mbaya atakayodhaniwa mwanamke asiyejali sitara ya kisheria ni kuwa, wakati wote huonekana yuko tayari kufanya ufisadi. Kama si hivyo, amtazamaye hushawishika kumtendea uovu. Mtarjumi.

Na tukirejea kwa mwanamke mwenye kujisitiri kwa mujibu wa sheria ya ki-Islamu, huyu hupata faida za aina mbili kwa pamoja: Faida aipatayo mbele ya Mwenyezi Mungu ni kwamba, yeye huwa ni mwanamke mtukufu mbele ya Mwenyezi Mungu na Malaika wake pamoja na Mawalii wa Mwenyezi Mungu. Utukufu huu anaupata kwa kuwa amemtii Mola wake, ametekeleza maamrisho yake na ameyasitri maungo ambayo Mwenyezi Mungu ameamrishsa yasitiriwe. Na kwa ajili hii basi, mwanamke kama huyu kamwe hatonyanyua unyayo wake bali rehma za Mwenyezi Mungu huwa ziko pamoja naye, pia radhi za Mwenyezi Mungu humbatana naye, na wakati huo huo Malaika wa Mwenyezi Mungu wanamuombea msamaha. Mwenyezi Mungu anasema; "Kilichoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora na ni chenye kubakia." 16 Ama faida atakayoipata ndani ya jamii, ni pale mwanamke huyo anapokuwa ni mwenye kuheshimiwa na kutukuzwa, yote haya anayapata kwa kuwa yeye amejipamba kwa pambo la kuji-heshimu na kuuhifadhi utu wake, kisha akausitiri uzuri huo aliopewa na Mwenyezi Mungu.

MAJADILIANO NA MSICHANA WA KIKRISTO

Msichana mmoja wa Kikristo alikwenda kwa mwanachuoni wa ki-Islamu na kumwambia. "Mimi nimefahamu mambo mengi kuhusu Uislamu na kwa hakika dini hii imenishangaza sana kwa kanuni zake na miongozo yake, na nimeupenda Uislamu kwa mapenzi ya kweli. Lakini kanuni moja tu kwangu mimi imekuwa ni kikwazo kuingia katika Uislamu. Nimewauliza watu wengi kuhusu kanuni hiyo, mpaka sasa sijapata jawabu la kunitosheleza. 16 Qur'an 42:36.

Iwapo wewe Sheikh utaweza kunibainishia hekima iliyomo ndani ya kanuni hii, basi nakuthibitishia kuwa nitaingia katika Uislamu." Yule Mwanachuoni akasema, "Ni ipi kanuni hiyo?" Msichana aka-jibu. "Kanuni ya kuvaa Hijabu, ni kwa nini Uislamu haumuachi mwanamke akatoka nje apendavyo kama ilivyo kwa wanaume.?" Mwanachuoni yule wa ki-Islamu akasema, "Je umepata kumuona sonara ameweka dhahabu na johari nyinginezo katika sanduku la kioo, kisha akalifunga sanduku hilo kwa kufuli? Msichana akajibu, "Ndiyo." Sheikh huyu akamwambia tena yule msichana, "Je, ni kwanini sonara hakuziacha johari hizo zikawa zinashikwa na kila mtu ajaye kutaka kununua? Kwa nini amezihifadhi ndani ya sanduku la kioo lililofungwa?" Msichana akasema; "Amefanya hivyo ili azilinde johari zake kutokana na wezi na mikono yenye khiyana." Yule Mwanachuoni akamwambia msichana; "Hii ndiyo hekima ya Hijabu, fahamu kwamba mwanamke ni johari ya thamani ambayo ni lazima kuilinda kutokana na waovu na wahaini.

Pia ni wajibu kumhifadhi mwanamke kutokana na macho ya watu waovu ndani ya kitu ambacho kitamsitiri barabara kama inavy-olindwa lulu katika kola lake, ili asije akaangukia mikononi mwa watu hao na kumgeuza kuwa ngawira yao." Hakuna njia bora isipokuwa Hijabu, hicho ndiyo kizuwizi na ni mlinzi wa mwanamke. Kwa hakika mwanamke mwenye Hijabu huwa sala-ma kutokana na shari. kwa kuwa mwili wake umesitirika, na mapambo yake nayo hayaonekani mbele ya kila mtu.

Hali ya kuvaa Hijabu inawafanya watu wasimtamani mwanamke huyo kwa kuwa hakuna wakionacho cha kuwafanya wamtamani. Kutokana na hali hiyo huwa wanamuepuka, wala hakiwageuzi kitu chochote cha kuwafanya wamuangalie mwanamke huyo, bali humuogopa na kumuheshimu. Mwisho wa yote watu humuogopa na kumpa heshima yake kama anavyostahiki. Yote hayo yatap-atikana kwa ajili ya kuvaa Hijabu, na hali hii inamaanisha kwam-ba, Hijabu ndiyo mlinzi wako na ni hifadhi ya heshima, na utuku-fu wako. Ewe msichana huu ndio upande mmoja wa falsafa ya Hijabu."

Baada ya maelezo hayo ya Sheikh, msichana yule wa Kikristo alionesha furaha na akaridhishwa na maelezo ya Sheikh kisha akasema, "Sasa nimetosheka na falsafa iliyomo ndani ya kanuni hii ya ki-Islamu, na pia nimefahamu hekima iliyomo na ninapen-dezwa kuingia katika Uislamu." Baada ya hapo msichana akatoa Shahada mbili na akawa Muislamu. Majadiliano haya mazuri ya kidini yanatubainishia kwamba Uislamu unakusudia kuihifadhi hehsima na utukufu wa mwanamke, pia Uislamu unataka kuilinda jamii. Na kwa sababu hizo basi, Uislamu umewajibisha Hijabu kama sharti la msingi kuweza kutimiza malengo hayo.

TOFAUTI YA MWANAMKE MWENYE HIJABU NA ASIYE NA HIJABU

Mmoja wa marafiki zangu alinisimulia tukio la kufurahisha lililom-tokea Muumini mmoja wa ki-Islamu. Tukio hili lilikuwa kama ifu-atavyo. Siku moja Muumini huyo alikuwa akitembea pamoja na mkewe aliyekuwa kavaa Hijabu. Matembezi hayo yalimfikisha katika moja ya bustani zinazotembelewa na watu wa aina tofauti. Ghafla Muumini huyo alijiwa na mtu fulani ambaye naye alikuwa na mkewe. Mke wa mtu huyu hakuwa amevaa vazi la Hijabu na hivyo basi kwa dharau na kejeli alimwambia yule Muumini. "Kwa nini umemvalisha mkeo Hijabu, kwa nini hukumuacha akatoka bila Hijabu kama jinsi alivyo mke wangu? Hijabu ina faida gani?" Jawabu alilotoa Muumini yule lilikuwa la kushangaza na la kishu-jaa. Alimwambia.

"Je unafahamu tofauti ya mwanamke mwenye Hijabu na asiyekuwa na Hijabu? Bwana yule mwenye kejeli akasema "Nini tofauti yake?" Yule Muumini akajibu kwa njia ya kuuliza, je, kuna tofauti gani baina ya taxi na gari ambalo mtu hulitumia yeye binaf-si? Yaani kwa matumizi yake pekee yake." Bwana yule akajibu akasema, "Taxi hutumiwa na kila mtu, wakati ambapo gari maalum linamuhusu mwenyewe peke yake. Hii ndiyo tofauti iliyopo." Basi yule Muumini akasema, "Hali hiyo ndio iliyopo baina ya mwanamke aliyevaa Hijabu na yule asiye na Hijabu.

Mwanamke asiye na Hijabu ni sawa na taxi ambayo kila mtu anaweza kuikodisha na kuitumia. Mwili wa mwanamke huyo huwa wazi na kuonesha mapambo yake na uzuri wake, na kuwafanya watu wavutike kutokana naye, jambo ambalo linaweza kusababisha kutendewa maovu, kama ambavyo mara kwa mara hali hii inavyowapata wanawake wa aina hii. Ama mwanamke aliyevaa Hijabu yeye ni bibi aliyemtukufu, ni maalum kwa ajili ya mumewe, mapambo yake na uzuri wake havionekani kwa kila mtu. Pia watu wenye nyoyo chafu na dhaifu hawamuangalii, na uso wake na mapambo yake havikutani na macho yenye khiana, kwa kuwa amehifadhiwa ndani ya Hijabu.

Kwa hiyo utukufu wa mwanamke huyu na mwili wake vimo ndani ya hifadhi bora, pia bibi huyu hupendwa na kupendeza mbele ya mumewe na kum-fanya mume kuwa na imani na mkewe, kwa sababu ya hifadhi hiyo inayomkinga kuwa na mahusiano na watu wengine kwa njia mbaya." Baada ya maelezo yaliyotolewa na yule Muumini wa kiIslamu, bwana yule mwenye kejeli aliona haya na akaanza kumwambia yule Muumini, "Najuta kwa kukuudhi, kwani maneno yako ni ukweli mtupu, na mifano uliyonipa ni sawa kabisa naom-ba samahani kwa haya niliyokutamkia na pia natubia kwa Mwenyezi Mungu kwa kitendo nilichokitenda na sasa...Kabla bwana huyu hajamaliza kujieleza mkewe alimkatiza na kusema. "Naam; naapa maneno haya aliyosema bwana huyu ni sawa na mfano aliotoa ni mzuri sana, kwani kabla ya leo nilikuwa sijasikia mawaidha kama haya. Mfano huu umeniingia moyoni nami pia natubia kwa Mwenyezi Mungu."

Baadaye yule mume akarudia kukamilisha usemi wake akasema, "Na mimi sasa naiamini Hijabu na kuanzia leo mke wangu atain-gia katika uwanja mtukufu kwa kuvaa Hijabu. Kamwe sikubali mke wangu atoke bila Hijabu, kwani ndiyo vazi la amani na imani. Nafsi yangu haipendi kabisa kumuona mke wangu akidhihiri mbele za watu kama kwamba yeye ni kwa ajili ya kila mtu."

NI LIPI LENGO LA WANAOPINGA HIJABU?

Baada ya kuusoma Uislamu kwa undani, maadui wa Uislamu wameandaa mikakati ya kuuangamiza Uislamu na Waislamu kidogo kidogo, bila Waislamu kuigundua hali hii isipokuwa wachache. Na miongoni mwa mikakati yao ya kishetani katika kutilia mkazo kuiondoa Hijabu, wametumia na bado wanatumia kila njia za kuvutia na madai batili kutimiza lengo lao hilo. Kuna mambo mengi machafu wanayoyaeneza katika jamii ya Waislamu, chini ya kiza kinene chenye ibara zinazovutia na kam-peni ambazo matokeo yake ni mabaya.

Kwa kutumia mbinu za kimaendeleo na utaalamu, wamefaulu kuwapotosha Waislamu, na wakasambaza uovu mwingi. Kwa madai hayo hayo ya maen-deleo na kupigania uhuru na haki za binadamu., uchafu wao umeenea ndani ya jamii zetu za ki-Islamu. Kwa hakika wamefaulu kuzinyang'anya jamii zetu maumbile ya kuwa na haya na heshi-ma. Ibara hizi zimewahadaa Waislamu wengi, wake kwa waume.

Masikini Waislamu hawa wamekuwa wafuasi wa itikadi hizi zenye sumu kali inayovuja kuelekea kwenye maovu na maangamio. Wanawake wa ki-Islamu na mabinti wa ki-Islamu wanafanya upin-zani hadharani dhidi ya vazi hili la ki-Islamu. Wametoka katika nyumba ya utukufu na imani na kuingia katika nyumba ya kiza na upotovu.

Wanawake wetu na wasichana wetu wameathiriwa na mavazi ya Kiyahudi na Kikristo yatokayo kwa wapinzani wa kimagharibi na makafiri wa mashariki. Maadui na wavamizi hawa wamefanikisha kwa kiasi kikubwa lengo lao, kwa kuwa sasa hivi jamii ya ki-Islamu imekwisha tumbukia na kuzama katika dimbwi la matendo machafu. Jamiii ya ki-Islamu ambayo asili yake ni adil-ifu na yenye muruwa, leo imegeuka na kushika bendera ya maovu ya kila aina.

Matukio ya kubaka,17 kupora, udanganyifu, dhulma, kutoa mimba na mengineyo, yameivamia jamii yetu tukufu. Watu hawa wa Ulaya magharibi na mashariki yake, hawali wakashiba wala hawalali wakapata usingizi, ila mpaka watimize lengo lao la kutu-achisha utamaduni wetu wa ki-Islamu. Ni wazi kabisa kwamba watu hao wanaomtaka mwanamke wa ki-Islamu avue Hijabu lengo lao wanataka wamuone mwanamke huyu anafanya ufisadi kwa kumlazimisha akae uchi. Nia yao ni kumuangamiza na kuipotosha jamii kwa jumla. Kumtaka mwanamke asivae Hijabu ni kumuondolea heshima yake na uchamungu wake.

Ewe msomaji wangu, iwapo utataka kuyafahamu vizuri maneno yangu, muulize mzee yeyote katika wazee wa makamo na mababu ambao bado wanayo kumbukumbu ya hali ya mambo ilivyokuwa hapo zamani. Waulize kwa kusema, "Hivi maovu haya yaliyopo sasa hivi ya kuwavunjia heshima wanawake na kuwaba-ka, na watu kudhulumia, mambo haya yakulikuwepo hapo zamani kabla ya miaka ishirini au thelathini iliyopita?" Watakujibu kwa nguvu zao zote, kwa kusema, Hapana kabisa hayakuwako."

17 Kwa asili mia kubwa wakazi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba, pwani ya Kenya inay-ojumuisha Mombasa, Lamu n.k, Visiwa vya Ngazija na miji mingi ya Tanganyika (Tanzania bara) kwa kipindi kirefu imekuwa ni miji ya amani na utulivu. Mazingira haya mazuri yali-jengeka kutokana na wakazi hao kuwa ni wafuasi wa dini ya ki-Islamu iliyowajenga katika maadili mema ya ki-Islamu. Ni ukweli usiyopingika kwamba hapo zamani hapakuwa na matukio ya kuwavunjia heshima wanawake kama tunavyoyashuhudia mambo hayo leo hii ndani ya miji yetu. Misamiati ya kufadhaika na kubaka haikuwako hapo zamani. Utoaji mimba na kutupa watoto ni mambo mageni kwetu hayakuwako. Ujambazi, utapeli na kutokuaminiana ni misamiati mipya. Lakini haya yote ni mipango ya maadui wa dini ya ki-Islamu, na kwa bahati mbaya Waislamu wamehadaika na mbinu za kikafiri na kujikuta wanapoteza dini yao na hata hiyo dunia waliyopambiwa imewatupa mkono hawana nayo asilani. Msiba uliyoje kwa Umma wa Ki-Islamu!! Mtarjumi.

Sasa yametoka wapi mambo haya maovu na matukio ya kuhuzu-nisha? Watakuambia, "Hali hii imetokana na mambo mengi, mion-goni mwake ni wanawake wenyewe kutembea mabarabarani bila sitara ya kisheria." Hili ndilo jibu sahihi kwa matatizo kama haya ya ubakaji ambayo takwimu zake zinaongezeka kila siku. Iwapo utataka uhakika zaidi, waulize wakazi wa miji michache ambayo wakazi wake bado wanashikamana na sheria za ki-Islamu na imani zao zingali hai na uwaambie, "Hivi katika miji yenu kuna matukio maovu ya kubaka na unyang'anyi kama inavyotokea katika miji mikubwa?" Bila shaka watakujibu hapana. Sababu kubwa ya kutokuwepo maovu kwa wingi katika sehemu hizo, ni kwa kuwa jamii bado inauheshimu na kuulinda Uislamu na kanuni zake zenye hekima.

Maovu mengi zaidi yanajitokeza katika miji au sehemu ambazo zinadai kuwa zimeendelea. Miji hiyo imehusika kwa kiwango kikubwa na ongezeko la maovu ambayo yanakithiri kwa kasi ya kutisha, licha ya serikali zao kutoa adhabu kali kwa wanaohusika kila wanapobainika na kukamatwa.18

Hali hii inaonyesha wazi kwamba kanuni peke yake hazitoshelezi, wala hazinufaishi katika kuirekebisha jamii, bali kinachotakiwa ni kuing'oa mizizi ya maovu kwanza, ili maovu hayo yapate kunyau-ka yenyewe. Kwa kawaida kila kitu kina asili yake, na asili ya maovu yaliyozikumba jamii zetu sasa hivi, ni hizi picha za video wanazooneshwa vijana wetu, 18 Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimekumbwa kwa kiasi kikubwa na matatizo ya mmomonyoko wa maadili, na zinatungwa sheria kali kila leo ili labda? itawezekana kureke-bisha hali hii, lakini bila mafanikio. Tunachokiona ni ongezeko la maovu ambayo yanatende-ka wazi wazi na kila mtu anayashuhudia wakiwemo hao wanaokaa na kutunga sheria hizo kwa matumaini ya kukomesha maovu. Hakuna njia inayoweza kukomesha hali hiyo isipokuwa ni kushikamana na mafunzo bora ya ki-Islamu. Ni muhimu kwa viongozi wetu wakatambua mambo yanayochangia uharibifu wa mwenendo wa jamii na kuhakikisha kuwa wanaing'oa mizizi yake. Mtarjumi.

picha ambazo huwa zinaonesha hali ya maumbile ya siri, isi-toshe huonesha pia matendo ya jinsiya baina ya mke na mume bila kuona aibu wala huzuni kuuchezea na kuudhalilisha uanadamu ambao ni kitu cha thamani, kutokana na kuwa na uwezo wa kutambua nini cha kufanya na nini si cha kufanya. Kitu kingine kinachochangia ni nchi zetu zinaporuhusu uingizaji wa magazeti na majarida yanayochapisha picha zinazoonesha sehemu za siri na kisha magazeti hayo na majarida yanasam-bazwa katika jamii. Maadam asili ya maovu bado ipo kama mifano ya picha za video na majarida tuliyoyataja hapo kabla, basi maovu na matukio machafu yataendelea kutokea siku hadi siku, na kamwe hayataondoka kwa kutegemea kanuni hizi za kidunia.

2

VAZI LA MWANAMKE

NI YUPI MWANAMKE BORA

Sasa napenda kutoa mifano miwili ya wanawake wawili ambao kila mmoja anao mwelekeo wake na mwenendo tofauti na mwenzake, lakini wote wanaishi katika jamii moja. Wa kwanza ni yule mwanamke mwenye kuvaa Hijabu ambayo ni sitara ya imani na ni vazi la ki-Islamu, tena ni vazi la heshima na humpa utukufu mvaji. Kwa kuvaa Hijabu, mwanamke huyu atakuwa amepata radhi za Mola wake na kupata utukufu wa watu wa peponi. Kwa vazi hili mwanamke huyu huvutia mvuto wa ucha Mungu na heshima.

Pia dalili za utulivu hujitokeza kwa mwanamke huyu na dhana njema kwake hutawala fikra za kila amuonaye. Amtazamapo mwenye kumtazama, huwa ni shida kutambua, je, mwanamke huyu ni msichana au ni mtu mzima? Sura yake ikoje nzuri au la? Hutatizika wanaomuangalia. Matokeo yake watu humuangalia kwa jicho la heshima, hakuna awezaye kumkabili kwa maneno chafu au maudhi, kwani anafahamu wazi kwamba mwanamke huyo ameshikamana na dini yake na anaheshimu utu wake. Isitoshe mwanamke kama huyu huwa amejitenga na matendo ya aibu na kujiepusha na wanawake wasio na sitara, na kwa ajili hiyo hayuko tayari kuidhalilisha nafsi yake.

Huo ndiyo mfano wa mwanamke mmoja na namna alivyojiweka katika jamii yake. Kwa upande wa yule mwanamke wa pili, ni yule asiyejali kujisitiri uso wake amevua vazi la la stara, hana aibu wala haya. Kwa maana hiyo ameing'oa imani yake, kwa sababu Mtume anasema: "Mtu kuwa na haya ni sehemu ya imani, na mtu asiye na haya hana imani." Kwa mwenendo wake mwanamke huyu, huwa ni mpinzani mkubwa wa muongozo wa Qur'an na huwa anajidhalilisha kwa kuonesha mapambo yakem, kama walivyokuwa wakionesha mapambo yao wanawake wa zama za kijahiliya kabla ya kuja Uislamu. Isitoshe kwa mwanamke huyu, hali aliyo nayo huwa amejifananisha na wanawake wa Kiyahudi na Kikristo, na huwa yuko mbali na heshima yake na utu wake. Kutokana na kuudhihirisha mwili wake na uso wke na mikono yake, pia kifua chake na sehemu nyingine katika maumbile ya kike. Watu waovu na wenye tamaa huyaona wazi wazi maumbile yake na hapo tayari anakuwa mfano wa bidhaa zilizotandazwa sokoni, kwani kila mtu ana uhuru wa kuziangalia bila mipaka.

Matokeo ya uovu wa mwanamke huyu, ni kupata usumbufu toka kwa wahuni ambapo hatimaye wanaweza kumtendea matendo machafu yanayoweza kumharibia tohara yake. Na iwapo itafikia hali ya kuharibiwa tohara yake, basi atakuwa amepoteza heshima yake na utu wake katika jamii. Hii ni kwa sababu ameacha kuulin-da mwili wake ndani ya vazi la kisheria. Baada ya kuwa mmefahamu namna za wanawake hawa wawili sasa tuwe pamoja kaitka kulinganisha hali zao kati yao na tujiulize masuali yafuatayo.

1.Je ni yupi mwanamke bora baina yao? 2.Yupi kati yao ni mtulivu na anayevutia, 3.Mwenye kujilinda au yule anayeuacha wazi mwili wake? 4.Ni yupi mwenye kuheshimika kati yao, mwenye Hijabu au yule asiye na Hijabu? Bila shaka, mwanamke mwenye Hijabu na ucha Mungu ni bora na ni mtukufu tena ni mwenye thamani kuliko yule mwingine.

KIPINDUPINDU NDANI YA JAMII

Miongoni mwa maradhi yanayoua haraka ni kipindupindu kwa mujibu wa taarifa ambazo huwa zinatolewa baada ya maradhi hayo kuingia katika kijiji au mji. Kila yanapodhihiri maradhi haya, hutangazwa hali ya hatari katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na kuwekwa karantini. Kama ilivyo katika kuzuia kipindupindu kisie-nee katika mji au kijiji, na fisadi nyingine ni hivyo hivyo. Sasa basi mtazamo wa Uislamu katika kuitazama jamii ni mtazamo wenye hekima kubwa, na ni mtazamo ambao lengo lake ni kujenga jamii nzuri na safi isiyokuwa na maovu ndani yake. Miongoni mwa mambo yanayoweza kudhibiti amani na ubora wa jamii ni mavazi. Siyo kweli kwamba kila vazi linaweza kukidhi haja hii, bali Hijabu pekee ndiyo jawabu, kwa sharti ya kuwa mvaaji aivae kwa kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu na siyo kinyume chake.19

baadhi ya watu wanajaribu kulitia dosari vazi la Hijabu kuwa eti ni vazi linalovaliwa ili kuficha maovu ya hao wanovaa. Upo ukweli fulani kuhusu madai haya, lakini upotoshaji huu wa vazi la Hijabu usiwe miongoni mwa sababu za kuwakatisha tamaa wanawake wa kiIslamu wanaovaa Hijabu kwa kumtii Mola wao, kwani ni mara ngapi watu wanautumia usiku kwa mambo maovu wakati Mwenyezi Mungu ameuweka kuwa ni kipindi cha mapumziko baada ya kazi za kutwa nzima? Kwa hiyo matumizi mabaya ya kitu kizuri hayawi ni sababu ya kukifanya kitu hicho kuwa kibaya. Mtarjumi.

Hijabu humlinda mwanamke kutokana na ufasiki na inamzuia kukhalifu maumbile yake aliyopangiwa kuishi ndani yake. Kwa kanuni hii ya Hijabu, Uislamu unakuwa umeisalimisha jamii na kuilinda isije ikajikuta imeteleza na kuvamiwa na maovu. Hali hal-isi inayojitokeza katika malengo ya msingi kuhusu kanuni hii ya Hijabu, ni kuitakasa jamii na kuisafisha, pindi wanawake watakapofuata sheria ya kuvaa Hijabu. Kinyume chake haitawezekana kabisa kudai kwamba jamii yetu ni safi, wakati wanawake zetu wanatembea bila kujali ni nguo gani wamevaa, kwa kuwa suala la mavazi kwa wanawake linataka litazamwe kwa mapana na marefu isiwe mradi kuvaa tu. Ni mara ngapi tunashuhudia mambo ya aibu na ya kuhuzunisha wanafanyiwa wanawake? Hivyo uchafu unasambaa haraka na kuleta madhara kwa wingi, kama kipindupindu kilichoingia mjini au kijijini. Na kwa ajili hiyo karantini inahitajika kuwekwa na kufuatwa kwa mujibu wa maelekezo ya wataalamu.

Uislamu kwa upande wake unataka kukata na kung'oa mizizi ya fitina na maovu kwa kutumia njia mbali mbali ikiwemo kusisitiza vazi la Hijabu. Pia Uislamu kwa nafsi yake unapinga kwa nguvu uovu na kila jambo linalokuwa ni sababu ya kueneza uchafu ndani ya jamii, miongoni mwa sababu hizo ni mwanamke kutokuwa na Hijabu ambayo ni vazi la kisheria.

KUKOSEKANA SITARA KUNALETA MAOVU

Miongoni mwa maovu na athari mbaya katika jamii, ni wanawake kuacha kuisitiri miili yao ipasavyo, kitu ambacho kimesababisha vijana wetu wa kiume kuteleza na kujikuta wanafanya mambo machafu bila kukusudia. Imam Ali ibn Musa Ar-ridha anasema,"....Imeharamishwa kuangalia nywele za wanawake, kwani katika kuziangalia nywele hizo kunasababisha kuamsha hisia za wanaume ambazo huwafanya waingie katika maovu na mambo yasiyo halali na yasiyopendeza." 20 Hapana shaka kwamba, mwanamke anayetoka nyumbani mwake na kwenda sokoni bila kujali ni vazi gani alilovaa, hajali kama limemsitiri vizuri au hapana, ni wazi kabisa huko njiani ataonekana kwa watu wa aina mbali mbali wakiwemo vijana ambao ndiyo kwanza wanaingia katika rika la ujana na nafsi zao bado hazijaweza kujimiliki kuhusu suala la kijinsiya.

Hali kama hii ni lazima itaamsha hisia za kimaumbile za vijana hao kutokana na jinsi mwanamke huyo atakavyokuwa amevaa na umbile lake linavyoonekana kwa jumla pindi atakapopita mbele yao. Hisia hizi za kimaumbile ni lazima ziamke kwa kuwa ndivyo ilivyo hali halisi. Kwa hali hii basi nafsi za vijana hawa kwa tabia ya maumbile ya mwanaadamu huanza kuhangaika kutafuta njia za kuyatosheleza maumbile yao.

Suala la kujiuliza hapa ni je, vijana hawa watafanya nini? Ikiwa wao sio watu walioshikamana na mafunzo ya dini wala hawafuati miongozo ya ki-Islamu, basi watajaribu kutosheleza hamu zao kwa njia ya siri ambayo ni kujitoa manii jambo ambalo ni hasara na aibu. Ama wengine hufanya baya zaidi ambalo ni kinyume cha utaratibu aliotuwekea Mwenyezi Mungu, hawa hufanya liwati. Kundi jingine wao huamua kuzini na katika huko kuzini huwa wanatumia kila njia kufanikisha azma yao hiyo, ikiwa ni kwa hila au hata kwa nguvu ambayo ni kubaka wanawake mitaani. Matokeo ya ubakaji ni kuvunja heshima za watu na kuwadhalil-isha wanawake.

20 Biharul Anwaar juz 6 uk 130. Kilichokusudiwa hapa bila shaka ni nywele za mwanamke ambaye si maharim wako wala siyo mkeo. Ikiwa nywele tu zinatosha kumuingiza mwanaume ndani ya madhambi, basi ikoje hali ya watu leo hii kwa namna wanawake wa kileo wanavy-ovaa.? Je! Ni kwa kiasi gani wanatuingiza katika madhambi? Leo hii siyo nywele tu bali vifua vya wanawake vinaonekana kwa kila mtu na maungo mengi yanakashifiwa na kila mtu. Hivi kweli kwa hali kama hii vijana wetu watasalimika na maovu? Pia hao kina dada nao watam-laumu nani watakapovunjiwa heshima? Mtarjumi.

Pamoja na matendo haya kwenda kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu, pia yanasababisha maradhi hatari na vifo vya ghafla..21 Inakadiriwa kwamba idadi ya hospitali zinazo shughulikia maradhi ya uasherati peke yake inafikia hospitali mia sita hamsini. Hesabu hii ni kwa nchi ya Marekani peke yake. Chanzo cha balaa lote hili ni kwa wale wanawake wasiojali kutenganisha maumbile yao na ya wanaume mpaka wakawa wanaona miili yao haistahiki kulindwa na kupewa hadhi ya pekee. Lakini kila mwanamke asiyezingatia suala la mavazi kisheria ni lazima atambue kwamba, yeye ni mshiriki mkubwa anayesababisha madhambi na mis-iba hii, na anayo sehemu yake ya adhabu mbele ya Mwenyezi Mungu.

Yote yaliyotajwa hapa sasa hivi, yanatokana na vijana ambao wao siyo watu wa dini wala hawashikamani na Uislamu. Kwa upande wa pili inawezekana vijana hao wakawa ni watu wa dini na wanaambatana na mafunzo ya ki-Islamu na sheria zake, basi vijana hao huzuia hisia zao zisivuke mipaka ya Mwenyezi Mungu na hupambana na matamanio ya nafsi zao na kumlaani shetani asije akawahadaa. Vijana hawa huvumilia kero ya maumbile na kubeba mzigo mzito ambao hawakutarajia kuubeba. Kwa mara nyingine tena mwanamke au wanawake wasiojali sheria ya mavazi kama Mwenyezi Mungu alivyoamrisha, wanabeba uzito wa taabu na maudhi yanayowapata watu hawa wa dini.

21 Asili ya yote hayo ni mwanamke au wanawake ambao kwa makusudi kabisa wanaamua kuvaa nguo ambazo zitahatarisha usalama wao na usalama wa jamii yote. Kuhatarisha usala-ma wao na wa jamii peke yake haitoshi, bali waelewe kwamba wanasababisha vijana wetu wa kiume kuchuma madhambi makubwa, na wakati mwingine kuwaharibia maisha yao ya baadaye kwa kufungwa jela kutokana na hatia ya kubaka. Madhara mengine yaletwayo na matukio ya zinaa na liwati ni pamoja na kuambukizwa maradhi hatari kama vile kisonono, kaswende, na leo ukimwi. Maradhi haya hatari yameleta huzuni na misiba inayotisha katika ulimwengu. Mtarjumi.

KUTOKUVAA HIJABU NA MADHAMBI YA UBAKAJI

Miongoni mwa athari mbaya zinazosababishwa na tabia ya wanawake ya kutokuvaa Hijabu ni yale makosa ya jinai ya kuwabaka wanawake na kuwaingilia kwa nguvu bila hiyari yao. Ni jambo lisilofichikana pindi mwanamke anapouacha wazi mwili wake na mapambo yake, hali hiyo huamsha hisia za kijinsia kwa wanaume. Kwa hakika ni juu ya mwanamke mwenyewe kuulinda mwili wake, mapambo yake na utu wake kutokana na hatari hiyo inayoweza kumkabili.

Hapana shaka kwamba, macho ya vijana wasiokuwa na msi-mamo wa dini, pindi wanpomuangalia mwanamke ni sawa na macho ya mbwa mwitu anapomuangalia kondoo. Pia tunaweza kuyalinganisha macho hayo na macho ya paka anapomuona panya, au tuseme yanafanana na macho ya mnyama mkali wa porini, anapomuona mnyama mwingine au kitu kimngine amba-cho kinamfaa kwa chakula. Siyo ajabu kabisa kwa mazingira kama haya kumkuta mwanamke amenasa ndani ya mtego alio-jitegea mwenyewe kutokana na tabia ya kujitangaza mbele ya watu waovu.

Tabia hii ya ubakaji mara nyingi inatokea katika sura ya kutisha huko kwenye nchi za magharibi ambazo zimeporomoka mno katika suala zima la maadili. Katika ripoti moja kati ya matoleo ya gazeti la The Gurdian la nchini Uingereza iliandikwa kwamba; "Takwimu za polisi zinaonesha kuwa, makosa ya jinai ya kubaka yanaongezeka mwaka hadi mwaka. Katika mji wa Washington peke yake kila baada ya dakika kumi na tano huwa kuna tukio la kubaka, na katika mji mkuu wa Uingereza (London) yalitokea matukio 2095 ya kubaka wanawake na wasichana mnamo mwaka wa 1970 peke yake."22 Haya ni machache katika mengi ambayo tungeweza kukuorodheshea.

22Majallatud-Dastuur Lebanon.

Na miongoni mwa matukio ya kubaka kutokana na wanawake kutokujali kujisitiri kwa mujibu wa sheria na maumbile yao, mimi nimesikia kwamba, kuna rais fulani anayeongoza nchi moja miongoni mwa nchi za Kiarabu, yeye hufanya ziara za mara kwa mara kuvitembelea vyuo vikuu akitafuta mabinti katika vyuo hivyo na kuwachagua wale wazuri na wanaopendeza. Kisha humtoa nje ya msitari binti anayemuona kuwa atamfaa. Baada ya muda mfupi askari wa usalama wa taifa huwa wanakwenda nyumbani kwa binti huyo na kumweleza baba yake kwamba rais wa jamhuri anamtaka binti yake akakeshe naye katika usiku wa siku hiyo!!

Hali kama hii husababisha msiba mkubwa kwa baba, mama, binti huyu na hata familia nzima huingia ndani ya mtihani huu. Msiba huu huwagubika watu hawa kwa sababu wanafahamu wazi kwamba rais huyu ataishi na binti yao kwa usiku huo mmoja tu!! Sasa je, watu hawa watalikataa ombi la rais? Na je, inawezekana kwa watu hawa kuuepuka unyanyasaji unaowasubiri kutoka kwa rais wao? Basi je, matokeo ya jambo hili yatakuwaje? Hapana jambo jingine litakalotokea hapo isipokuwa msichana itamlazimu kuuendea uovu kwa miguu yake mwenyewe. Ataifuata fedheha na aibu hiyo kubwa bila kupenda, na kisha atarudi nyumbani hali ya kuwa amekwishapata hasara ya kuvunjika kwa heshima yake na utu wake pia kagubikwa na kiza la ulimwengu machoni mwake.

Ewe msomaji mpendwa, hapana shaka kwamba watu wanaoso-ma au kusikia unyanyasaji huu, utawaona wanamlaani na kumsh-tumu rais huyu muovu. Lakini hebu tufikiri kidogo juu ya misingi inayosababisha mateso haya na tujiulize swali lifuatalo: Je! Ni nani mwenye makosa? Hivi kweli mwenye makosa siyo yule baba ambaye toka hapo mwanzo alimruhusu binti yake atoke ndani hali ya kuwa maungo yake yako wazi na uzuri wake unaonekana kwa kila mtu? Lau binti huyo angekuwa ni mwenye kujisitiri, hivi unadhani yule rais mpumbavu angelimtamani na kumfanya kuwa kiwindo chake?

Ni baba ndiyo mwenye kustahili lawama tangu ile siku aliponunua television (ambayo ni adui mkubwa muovu aliye-mo ndani) ili kuistarehesha familia yake kwa kuangalia vipndi viit-wavyo kuwa ni vya watu walioendelea!! Baba huyo huyo ndiyo mwenye lawama siku zile alipokuwa akiichukua familia yake kwa ajili ya kwenda sinema kuangalia filamu za watu walio uchi. Na mama pia anastahili lawama... Je ! Siyo yeye yule ambaye alikuwa akizifumua nywele za binti yake na kumpamba utadhani siku hiyo ndiyo siku ya harusi yake na kisha akamwacha kwenda shuleni akiwa katika mazingira kama hayo?

Ni huyo mama aliyekuwa akimchagulia binti yake asiyejuwa kitu mavazi mafupi yanayobana mwilini ambayo hayamsitiri inavy-opasa? Binti naye anapaswa kulaumiwa kutokana na matokeo hayo yenye kiza kinene cha majonzi kwa kuwa ni yeye mwenyewe ndiye aliyechagua tabia ya kuuweka wazi mwili wake, na pia akachagua kupita njia ngumu iliyojaa miba na mawe. Naam, watu hawa ndiyo tabaka la mwanzo la kulaumiwa, na baada ya hapo ndio mnapaswa kumlaani rais yule!!

KUTOKUVAA HIJABU NA MADHAMBI YA UTOAJI MIMBA

Ni vema pia kutaja mambo mengine ambayo yanaletwa na makosa ya jamii inapokuwa imepuuza na kuacha Hijabu. Yapo mengi, lakini yanayotajwa ndani ya kijitabu hiki ndiyo ya msingi. Suala la kutoa au kuharibu mimba ni miongoni mwa athari mbaya ziletwazo na ukosefu wa sitara bora ya kisheria kwa wanawake. Ni mara nyingi inatokea kwa wanawake wasio na Hijabu kuvunji-wa heshima zao na utu wao.

Mwanamke asiyekuwa na sitara bora pindi anapodhihiri mbele ya vijana wenye dhiki ya kukidhi haja zao za kijinsia, hapana shaka vijana hao hushindwa kuyazuwia matamanio yao na hapo ndipo huamua kumbaka. Hapo mwanamke huwa anajikuta ametum-bukia mikononi mwao bila hiyari, na huenda ikatokea bahati mbaya mwanamke huyo anaweza kubeba mimba haramu ambayo hakuitarajia. Kutokana na uovu huu aliofanyiwa hulaz-imika kuitoa au kuiharibu mimba hiyo. Leo hii katika anga la dunia yetu matukio kama haya ni mengi mno. Yako wazi kila mahali na hasa nchi za Ulaya Magharibi na zile zote zinazojaribu kuiga ustaraabu wa magharibi.

Tarehe 28 Februari mwaka 1972. jarida la An Nahaar la Lebanon lilichapisha katika ukurasa wake wa makala maalum kama ifu-atavyo. "Katika mji wa London idadi ya utoaji mimba imeongezeka kutoka wanawake hamsini elfu mwaka 1969 hadi kufikia wanawake themanini na tatu elfu mwaka 1970 na idadi inayokaribia laki mbili mwaka 1971. Na huko Ufaransa hali hii imeongezeka na kufikia kutolewa mimba arobaini na sita hadi mia moja arobaini na tatu katika kila mimba mia mbili wanazobeba wanawake kwa mwaka. Ama huko Urusi, kuna mimba zipatazo milioni sita zinazotolewa kila mwaka.23 Kwa hakika takwimu na taarifa hizi zinatisha, na yote haya ni matokeo ya tabia ya wanawake kuyaonesha wazi maumbile yao na uzuri wao mbele ya kila mtu. Hakuna njia ya kuzuwia mad-hambi haya isipokuwa vazi la Hijabu iwapo litavaliwa kwa mujibu wa sheria na kutunza mipaka ya dini.


7

8

9

10

11