TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TANO Juzuu 5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TANO15%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TANO Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 19949 / Pakua: 4440
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TANO

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA TANO Juzuu 5

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TANO

﴿فَمَا لَكُمْ فِي الْمُنَافِقِينَ فِئَتَيْنِ وَاللَّـهُ أَرْكَسَهُم بِمَا كَسَبُوا أَتُرِيدُونَ أَن تَهْدُوا مَنْ أَضَلَّ اللَّـهُ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَلَن تَجِدَ لَهُ سَبِيلًا﴾

88.Mna nini nyinyi mmekuwa makundi mawili katika (habari ya) wanafiki, na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa yale waliyoyachuma? Je,mnataka kumwongoza ambaye Mwenyezi Mungu amemuacha kupotea? Na ambaye Mwenyezi Mungu amemuacha kupotea, hatampatia njia

﴿وَدُّوا لَوْ تَكْفُرُونَ كَمَا كَفَرُوا فَتَكُونُونَ سَوَاءً فَلَا تَتَّخِذُوا مِنْهُمْ أَوْلِيَاءَ حَتَّىٰ يُهَاجِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَإِن تَوَلَّوْا فَخُذُوهُمْ وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ وَجَدتُّمُوهُمْ وَلَا تَتَّخِذُوا مِنْهُمْ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا﴾

89.Wanapenda lau mngekufuru kama walivyokufuru wao mkawa sawasawa, Basi msifanye katika wao marafiki mpaka wahame katika njia ya Mwenyezi Mungu. Wakikataa wakamateni na muwaue popote muwakutapo, wala msifanye katika wao rafiki wala msaidizi.

﴿إِلَّا الَّذِينَ يَصِلُونَ إِلَىٰ قَوْمٍ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُم مِّيثَاقٌ أَوْ جَاءُوكُمْ حَصِرَتْ صُدُورُهُمْ أَن يُقَاتِلُوكُمْ أَوْ يُقَاتِلُوا قَوْمَهُمْ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَسَلَّطَهُمْ عَلَيْكُمْ فَلَقَاتَلُوكُمْ فَإِنِ اعْتَزَلُوكُمْ فَلَمْ يُقَاتِلُوكُمْ وَأَلْقَوْا إِلَيْكُمُ السَّلَمَ فَمَا جَعَلَ اللَّـهُ لَكُمْ عَلَيْهِمْ سَبِيلًا﴾

90.Ila wale waliofungamana na watu ambao baina yenu na wao mna ahadi, au wakawajia hali ya vifua vyao vina dhiki kupigana nanyi au kupigana na watu wao, Lau Mwenyezi Mungu angelitaka angewasaliti nao wakapigana nanyi. Watakapojitenga nanyi, wasipigane nanyi na wakawapa amani, basi Mwenyezi Mungu hakuwafanyia njia ya kupigana nao.

IMEKUWAJE KUWA MAKUNDI MAWILI KATIKA HABARI YA MAKAFIRI

Aya 88-90

MAANA

Mna nini nyinyi mmekuwa makundi mawili katika habari ya wanafiki

Aya hii ilishuka kuwahusu wanafiki waliobaki katika mji wa Makafiri na wala wasihame kwenda Madina, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu: "Mpaka wahame." Kwa sababu Hijra (kuhama) inakuwa ni kutoka mji wa ukafiri kwenda kwenye mji wa uislam tu. Na kabla ya kutekwa Makka, mji wa Madina pekee ndio uliokuwa mji wa uislam.

Dhahiri ya Aya hii ni wazi kuwa hukumu ya aliyekuwa mnafiki, akabaki katika mji wa ukafiri sio hukumu ya mnafiki anayekaa katika mji wa kiislamu. Kwani Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameamrisha kuuawa hao na kuwateka, kinyume cha hawa.

Kabla ya kushuka amri hii Masahaba walitofautiana, wakagawanyika makundi mawili kuhusu hukumu ya wanafiki ambao wamebaki kwenye mji wa ukafiri. Kundi moja likaonelea kuwa ni lazima kuvunja uhusiano nao na kuacha kuwasaidia na chochote, tena kuwatangazia vita; sawa na aliyedhihirisha ushirikina na uadui kwa waislamu. Kundi jingine likaonelea kuweko kuvumiliana kuwasamehe na kuwafanyia muamala wa waislamu. Inaonyesha kuwa Mtume(s.a.w.w) alinyamaza kuhusu tofauti hizi mpaka Mwenyezi Mungu alipompa ufumbuzi kwa kusema kwake:

Mna nini nyinyi mmegawanyika makundi mawili katika habari ya wanafiki.

Yaani haitakikani mtofautiane kuhusu mambo yao, bali ni juu yenu kuwa na kauli moja ya kutovumiliana nao kwa hali yoyote ile; na Mwenyezi Mungu akabainisha sababu ya hilo kwa kusema kwake:

Na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa yale waliyoyachuma.

Yaani amewarudisha kwenye hukumu, ya makafiri wanaopiga vita, ya kujuzu kuwaua na kuwateka. Kwa sababu hao ni kama kafiri anayepiga vita tu, au wana madhara zaidi kwa kubakia kwao kwenye mji wa ushirikina ambao hana faida nao isipokuwa adui wa uislamu.

UPOTEVU

Je, mnataka kumwongoza ambaye Mwenyezi Mungu amemuacha kupotea.

Hii inafahamisha kwamba lile kundi lililotaka kuwavumila lilikuwa na matumaini ya kuwa hao wanafiki watarudi kwenye uongofu, Mwenyezi Mungu akaikata tamaa yao kwa kusema:

Na ambaye Mwenyezi Mungu amemwacha kupotea hatampatia njia.

Unaweza kuuliza : Kwanza Mwenyezi Mungu -uliotukuka usemi wake - ameeleza kwamba Yeye amewageuza hao wanafiki kwa sababu ya kuchuma kwao na kuchagua kwao kubaki katika mji wa makafiri, kisha tena anasema kwamba Yeye ndiye aliyewapoteza, Kwa hiyo upotevu ameutegemeza kwake baada ya kuutegemeza kwao, Sasa kuna wajihi gani katika kukusanya yote mawili?

Jibu : Makusudio ya aliyeachwa kupotea na Mwenyezi Mungu sio kuwa ni kuumba upotevu kwao, la isipokuwa ni kwamba mwenye kukengeuka na njia ya haki na uongofu kwa matakwa yake akifuata njia ya batili na upotevu kwa hiyari yake, basi Mwenyezi Mungu ataachana naye na atamwacha na mambo yake. Hapana mwenye shaka kwamba mtu anayeachiwa na Mwenyezi Mungu, hatapata njia ila ya upotevu. Maana haya ndiyo yanayooana na kauli yake Mwenyezi Mungu:"Na hali Mwenyezi Mungu amewageuza kwa yale waliyoyachuma."

Kwa ufasaha zaidi ni kwamba kila mwenye kufuata njia ya haki, hakika Mwenyezi Mungu anamwingiza katika usaidizi wake na kumchunga kwa tawfiki yake:

﴿إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الَّذِينَ اتَّقَوا وَّالَّذِينَ هُم مُّحْسِنُونَ﴾

"Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wale wanaomcha na wale wafanyao mema" (16:128)

Usaidizi huu, kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa wanaomcha unaitwa uongofu, tawfiki, mapenzi na utegemezi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Na kila mwenye kufuata njia ya upotevu, Mwenyezi Mungu huachana naye wala hamrudishi kwenye uongofu kwa kumlazimisha. Kuachana naye huku kunaitwa upotevu, utwezaji na kugeuzwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Kwa ibara moja ni kwamba upotevu kutoka kwa Mwenyezi Mungu maana yake ni ukombo sio usawa: na maana ya uongofu kutoka kwake Mwenyezi Mungu ni upole na upangaji wa mambo. Hapana budi kuwa hekima ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) inapelekea upole kwa mja wake na kutoepukana naye; sawa na mama asivyoepukana na mwanawe.

Ila itakapokuwa mja ndio sababu inayowajibisha kuepukana na Mwenyezi Mungu kwa njia ya kumwasi; kama mama anavyoepukana na mtoto wake aliyezidi sana kumwudhi.

Wanapenda lau mngekufuru kama walivyokufuru wao mkawa sawasawa.

Kila mtu anapendelea watu wote wawe upande wake, Imetangulia tafsiri yake katika 2:109

Basi msifanye katika wao marafiki mpaka wahame katika njia ya Mwenyezi Mungu, Baada ya kuhama Mtume(s.a.w.w) kwenda Madina, Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwajibisha kuhama (Hijra) kwenda Madina kwa kila mwislamu ila akishindwa au kupewa idhini na Mtume kubaki kwa masilahi yanayowarudia waislam.

Miongoni mwa Aya zilizohimiza kuhama ni:

﴿وَالَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يُهَاجِرُوا مَا لَكُم مِّن وَلَايَتِهِم مِّن شَيْءٍ حَتَّىٰ يُهَاجِرُوا﴾

"Na wale walioamini lakini hawakuhama hamna haki ya kuwalinda hata kidogo mpake wahame" (8:72)

Siri ya hilo - kama uonavyo - ni kw amba Waislamu walikuwa wachache kabla ya kutekwa Makka. Kama wakitengana huku na huko watakuwa wanyonge na maadui watavamia. Lakini kama wakikusanyika mahali pamoja karibu na Mtume(s.a.w.w) watakuwa na nguvu na kuogopewa. Zaidi ya hayo kuna faida nyingi zinazotokana na kuwa pamoja na mshikamano.

Kukaendela kuhama kwenda Madina ni wajibu mpaka ilipotekwa Makka na Mtume, Mwenyezi Mungu akamnusuru mja wake na maadui zake na kuingia watu kwenye dini ya Mwenyezi Mungu makundi makundi, na kukawa hakuna sababu ya kuhama.

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema"Hapana kuhama baada ya kutekwa (Makka)."

Wakikataa wakamateni na muwaue popote muwakutapo.

Yaani hao wanafiki kama hawatawacha mji wa ukafiri na kuhama kwenda Madina na kuungana na Mtume na waislamu, basi wakamateni na muwaue popote mtakapowapata.

Wala msifanye katika wao rafiki wala msaidizi.

Yaani achaneni nao kabisa, msiwasaidie wala kuwalinda katika chochote.

Unaweza kuuliza : Uislamu ni dini ya uhuru na kuvumiliana na vikundi vyote na watu wa dini zote na sharia yake, ikilinda maisha ya watu, tena watu wote, na haki zao za kimaana na kimaada, bila ya kuangalia rai, maoni yao na itikadi zao. Sasa imekuwaje hapa unaamrisha kuwateka wanafiki na kuwaua popote watapopatikana?

Jibu : Kuna tofauti baina ya makundi na watu wa dini, bali hata na walahidi wanaotangaza maoni yao na itikadi zao kwa watu na wasidhamirie uadui kwa watu wala wasipange njama au kuwasaidia wanaovunja haki; kuna tofauti kubwa sana baina ya hawa na wanafiki ambao wamedhihirisha uislamu na kufichika na neno la uislamu na wakabaki katika mji wa makafiri kwa makusudio ya kuwafanyia vitimbi waislamu, kuwafanyia njama na kuwasaidia maadui. Kwa hiyo amri ya kuwateka na kuwaua ni malipo ya uadui wao na njama zao kwao. Ama kuvumiliana kwa uislamu na vikundi vingine na watu wa dini nyingine, kunafungamana na msingi wake katika kuuhami uhuru wa kila mtu na kuacha kulazimisha katika maoni na itikadi, iwe ya haki au ya batili, maadamu kila mtu ana mzigo wake, na watu wako katika amani.

Swali la pili lililotokana na jibu la swali la kwanza: Uislam unavumiliana na wanafiki; sawa na unavyovumilia na makundi mengine na watu wa dini nyingine kwa dalili ya kuwa Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake kujipurukusha nao; kama ilivyotangulia katika Aya 63 ya Sura hii: "Basi achana nao na uwape mawaidha"

Jibu : Aya hiyo ilishuka kwa wanafiki waliokuwa pamoja na Mtume(s.a.w.w) Madina. Hawakuwa na wasaa wa kushirikiana na washirikina kwa kuwa mbali nao na kuwa karibu na Mtume na vile vile nguvu za waislamu. Na Aya tuliyonayo (89) ilishuka kwa wanafiki waliong'anga'nia kubakia katika mji wa makafiri kwa ajili ya kuwachimba waislamu.

Zaidi ya hayo Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume kuwafanyia amani wanafiki wakati waislamu walipokuwa dhaifu wenye wasaidizi wachache, Kisha akamwamrisha kuwaua baada ya kuwa uislamu una nguvu na wasaidizi (Ansari) wengi; sawa na alivyowaamuru kuvumilia kule Makka na kupigana jihadi walipokuwa Madina.

Baada ya kuamrisha Mwenyezi Mungu kuadhibiwa hao wanafiki maadui, aliwavua kutokana nao sehemu mbili: Sehemu ya Kwanza ni wale aliowaashiria kwa kauli yake:

Ila wale waliofungamana na watu ambao baina yenu na wao mna ahadi.

Hapa Mwenyezi Mungu Mtukufu anakusudia kwamba katika hao wanafiki mwenye kukimbilia kwa watu ambao wana mkataba wa amani na waislamu, basi mkimbizi huyu hatatekwa wala kuuawa kwa sababu yeye - katika hali hii - anakuwa ana salama na waislamu, sawa na aliyekimbilia kwao; Kwa hiyo hawatamwingilia.

Ni vizuri hapa tumnukuu Razi, anasema: "Jua kwamba hii inadhamini bishara kubwa kwa watu wenye imani. Kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu, aliondoa upanga kwa aliyewakimbilia waislamu, basi kumwondolea adhabu huko akhera aliyekimbilia kwenye mahaba ya Mwenyezi Mungu na mahaba ya Mtume wake ni zaidi." Hapana mwenye shaka kwamba kuwapenda Ahlul bait wa Mtume ni kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿قُل لَّا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِلَّا الْمَوَدَّةَ فِي الْقُرْبَىٰ﴾

Sema: "Siwaombi malipo yoyote isipokuwa kuwapenda ndugu(kizazi changu) ." (42: 23)

Sehemu ya pili Mwenyezi Mungu amewaashiria kwa kusema:

Au wakawajia hali ya kuwa vifua vyao vina dhiki kupigana na nyinyi au kupigana na watu wao.

Yaani wale ambao wanaona uzito kupigana na waislamu pamoja na watu wao washirikina au kupigana na watu wao pamoja na waislamu, na wakaja kwa Mtume(s.a.w.w) kutaka awaridhie wawe katika msimamo usiofungamana na upande wowote, hawa vile vile wataachwa, hawatauawa wala hatatekwa yeyote katika wao; Kwa sababu hao si wapiga vita.

Mfano bora unaofasiri Aya hii ni ule uliokuja katika Majmaul-bayan kuwa jamaa katika Ashjai walikuja kwa Mtume(s.a.w.w) wakamwambia: "Nyumba yetu iko karibu na yako na tunachukia kukupiga vita na kuwapiga vita watu wetu; na tumekuja il tupatane. Akawakubalia na akapatana nao wakarudi.

Hakuna nguvu na ukweli wa dalili ya kuwa uislamu ni amani kwa mwenye amani na inampiga vita mwenye kupiga vita, kuliko dalili hii.

Lau Mwenyezi Mungu angelitaka angewasaliti nao wakapigana nanyi

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) hajiingizi kwa matakwa yake ya Takwin[12] Katika mambo ya watu isipokuwa anakusudia kwa kauli yake hii kuwakumbusha waislamu fadhila zake kwao na kwamba inawezekana kuwakusanya wote kwa maadui wa waislamu, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaondolea hilo kwa wao kuwa na msimamo wa kutofungamana na sehemu yoyote. Kwa hiyo kusema kwake Lau Mwenyezi Mungu angelitaka angewasaliti nao wakapigana nanyi, maana yake ni angeliwafanya wawashambulie na wala asingewajalia na moyo wa kupatana. Na hii si katika matakwa ya Takwin, bali ni matakwa yaTawfiki kama sikosei.

Watakapojitenga nanyi, wasipigane nanyi na wakawapa amani, basi Mwenyezi Mungu hakuwafanyia njia ya kupigana nao.

﴿إِنَّمَا السَّبِيلُ عَلَى الَّذِينَ يَظْلِمُونَ النَّاسَ وَيَبْغُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ﴾

"Hakika njia iko kwa wale wanaodhulumu watu na wakawafanyia jeuri katika ardhi pasipo haki" (42: 42)

﴿لَّا يَنْهَاكُمُ اللَّـهُ عَنِ الَّذِينَ لَمْ يُقَاتِلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَلَمْ يُخْرِجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ أَن تَبَرُّوهُمْ وَتُقْسِطُوا إِلَيْهِمْ ﴾

"Mwenyezi Mungu hawakatazi kuwafanyia hisani na uadilifu wale ambao hawakupigana nanyi kwa ajili ya dini wala hawakuwafukuza katika nchi zenu" (60: 8)

"Na wakielekea katika amani, nawe pia ielekee" (8: 61)

Na Aya nyinginezo zinatoa mwito wa mapenzi, udugu na usawa, vilevile kusaidiana katika kila jambo lenye masilahi ya watu kwa njia yoyote. Kuchunga zaidi kwa haki kuliko katika uislamu ni kwamba unazingatia kuutumikia ubinadamu kuwa ndio uti wa mgongo wa dini, bali ndio njia pekee ya kumwelekea Mwenyezi Mungu.

﴿ سَتَجِدُونَ آخَرِينَ يُرِيدُونَ أَن يَأْمَنُوكُمْ وَيَأْمَنُوا قَوْمَهُمْ كُلَّ مَا رُدُّوا إِلَى الْفِتْنَةِ أُرْكِسُوا فِيهَا فَإِن لَّمْ يَعْتَزِلُوكُمْ وَيُلْقُوا إِلَيْكُمُ السَّلَمَ وَيَكُفُّوا أَيْدِيَهُمْ فَخُذُوهُمْ وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ ثَقِفْتُمُوهُمْ وَأُولَـٰئِكُمْ جَعَلْنَا لَكُمْ عَلَيْهِمْ سُلْطَانًا مُّبِينًا ﴾

91. Mtawakuta wengine wanataka wapate amani kwenu na wapate amani kwa watu wao; kila wakirejezwa kwenye fitna hudidimizwa humo.

Wasipojitenga nanyi na kuwapa amani wala kuzuia mikono yao, basi wakamateni muwaue popote muwakutapo; na hao ndio ambao tumewafanyia hoja zilizo wazi juu yao.

MTAWAKUTA WENGINE

Aya 91

HAKUNA KUUANA WALA VITA KATIKA UISLAM

Aya zilizotangulia zimeonyesha namna mbali mbali za wale ambao Mtume(s.a.w.w) alipata kutoka kwao aina za vitimbi na uasi kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Aya hii inaonyesha sura nyingine ya kundi la watu ambao ni wengi kila wakati na kila mahali. Yaani wale wenye dhambi ambao hawana msimamo isipokuwa kugeukageuka tu; wanaamini msimamo fulani kwa muda tu; kisha wanaukanusha.

Sisi hatukatai kuwa binadamu anageuka kutokana na hali zake, hilo hutokea mara nyingi kama tulivyoeleza katika kufasiri 2: 143, kifungu cha 'Kubadilika hulka na fikra.' Lakini pamoja na yote haya tunaitakidi - kulingana na hali ilivyo - kwamba baadhi ya watu wana tabia ya kigeugeu wanabadilika kutoka hali hii hadi nyingine, hata kama wakiwa katika hali moja tu.

Mtawakuta wengine wanataka wapate amani kwenu na wapate amani kwa watu wao; kila wakirejezwa kwenye fitna hudidimizwa humo.

Makusudio ya kurejezwa ni kuitwa, fitna ni ukafiri na kudidizwa ni kuingia. Maana yake ni kuwa kundi hili kila linapoitwa kwenye ukafiri na kurtadi wanakubali na kuwa wabaya zaidi ya kafiri uliyethibiti ukafiri wake. Maelezo mazuri hasa kuelezea hali yao, ni yale waliyoyasimulia baadhi ya wafasiri kuwa, wao walikuwa wanaporudi kwa watu wao, mmoja wao huambiwa sema kombamwiko (mende) ni Mungu wangu na nyani ni Mungu wangu, naye hukubali na kusema hivyo hivyo.

Kadiri wanavyofikia watu hawa katika hali ya kuporomoka, kukosa utu, na kigeugeu baina ya ukafiri na imani, lakini Uislam unawaacha tu na mambo yao, maadam hawajafanya uadui wala vita. Ikiwa watafanya uchokozi na wakapigana, basi uislam unaamrisha kupigana nao popote walipo, ikiwa watakuwa wanaendelea na vita. Haya ndiyo aliyoyakusudia Mwenyezi Mungu kwa kusema kwake.

Wasipojitenga nanyi na kuwapa amani wala kuzuia mikono yao, basi wakamateni muwaue popote muwakutapo.

Hii ni dalili miongoni mwa dalili kadhaa zinazoelezewa na Qur'an na Hadith za Mtume kwamba msingi wa dini ya Kiislamu ni kutoua wala kupigana vita ila kwa kumzuia mwenye kupigana na kueneza ufisadi duniani.

Kwa hivyo basi uislamu umeruhusu vita kwa namna ile ile iliyoruhusu sheria za zamani na za sasa na kukubaliwa na akili zote. Pamoja na dalili zote hizi, maadui wa uislamu bado wanang'ania kusema kuwa uislam ni dini ya upanga; sawa na yule aliyesema: "Ni mbuzi tu hata kama akiruka."

Angalia Aya iliyotangulia kisha uikutanishe na hii, utaona kila moja inatilia mkazo kuwa vita havikukubaliwa katika sharia ila kwa kujikinga na kuondoa ufisadi.

﴿ وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ أَن يَقْتُلَ مُؤْمِنًا إِلَّا خَطَأً وَمَن قَتَلَ مُؤْمِنًا خَطَأً فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ وَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ إِلَّا أَن يَصَّدَّقُوا فَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ عَدُوٍّ لَّكُمْ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ وَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُم مِّيثَاقٌ فَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ وَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ شَهْرَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ تَوْبَةً مِّنَ اللَّـهِ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴾

92.Wala haiwi kwa muumini kumwua muumini (mwenzake) ila kwa kukosea. Na mwenye kumwua muumini kwa kukosea, basi amwache huru mtumwa mwislamu na atoe diya kwa watu wake ila watakapoifanya sadaka. Na ikiwa ni mmoja wa watu walio maadui zenu, naye ni muumin, basi ni kuacha huru mtumwa muumini. Na ikiwa ni katika watu ambao baina yenu nyinyi na wao pana ahadi, basi ni diya kwa watu wake na kumwacha huru mtumwa muumini. Na ambaye hakupata basi ni kufunga miezi miwi li yenye kufuatana. Ni kitubio kitokacho kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye hekima.

﴿ وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ وَأَعَدَّ لَهُ عَذَابًا عَظِيمًا﴾

93.Na mwenye kumuua muumini kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam, ni mwenye kudumu humo; na Mwenyezi Mungu amemughadhibikia na amemlaani na amemwandalia adhabu kubwa.

KUUA KWA KUTOKUSUDIA NA KUKUSUDIA

Aya 92-93

MAANA

Wala haiwi kwa muumin kumwua muumin (mwenzake) ila kwa kukosea. Na mwenye kumwua muumin kwa kukosea, basi amwache huru mtumwa mwislamu na atoe diya kwa watu wake ila watakapoifanya sadaka.

Kuua kuko aina tatu:

1. Kukusudia: Ni kudhamiria mtu mwenye akili aliyebaleghe kumwua mwingine moja kwa moja; kama vile kuchinja na kunyonga. Au kwa kusababisha; kama vile kutia sumu kwenye chakula au kumzuilia mtu asile mpaka afe na njaa.

Ukithibiti usawa wa muuaji na muuliwa kidini na kiungwana, na wala muuaji asiwe ni baba wa muuliwa, hapo msimamizi wa aliyeuliwa atakuwa na hiyari ya kumuua kwa kulipiza kisasi au kuchukua fidia ikiwa muuaji atakubali kuitoa.

Hiyari ya kulipiza kisasi na kuchukua fidia ni ya msimamizi (walii) katika kuua kwa makusudi, Akichagua fidia, basi muuaji anayo hiyari ya kutoa fidia au ajitolee kuuawa, Kwa hiyo msimamizi hawezi kumlazimisha muuaji kutoa fidia wala muuaji hawezi kumlazimisha msimamizi kuchuka fidia.

Fidia ya kisheria ni Dinar elfu moja ambazo ni sawa na 3.529 Kg za dhahabu.

2. Bila ya kukusudia: Ni kuwa muuaji amekusudia kitendo, lakini akakosea makusudio; kama kumpiga mototo kwa kumtia adabu akafa. Kuua kwa aina hii kunawajibisha fidia sio kisasi. Fidia yake ni Dinar elfu moja; kama fidia ya kukusudia. Tumezungumza kuhusu kuua kwa makusudi na shabihi - kusudio, katika kufasiri (2: 178 - 179)

3. Kukosea: Ni kuwa muuaji alikosea kitendo na makusudio; kama mwenye kupiga mshale mnyama ukampata mtu ukamuua, Hapo mtu siye aliyekusudiwa kufumwa wala kuuliwa. Haya ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na mwenye kumwua mwislamu kwa kukosea, basi amwache huru mtumwa mwislamu na diya kwa watu wake ila watakapoifanya sadaka.

Qur'an na Hadith kwa pamoja zimefahamisha kuwa mwenye kumuua mwislam kwa maksudi, basi ni wajibu kwake atoe kafara ya kumwacha huru mtumwa, kufunga miezi miwili yenye kufuatana na kuwalisha masikini sitini; atakusanya yote matatu, Hili ndilo linaloitwa kafara la kuchanganya.

Ikiwa kuua ni bila ya kukusudia au kukosea, basi atatoa kafara la kumwacha huru mtumwa; akishindwa afunge miezi miwili inayofuatana, akishindwa awalishe masikini sitini.

Fidia ya kuua kwa makosa mzigo wake utabebwa na walio baleghe wenye akili na walio na uwezo katika ndugu wa karibu wa upande wa baba; kama vile kaka, ami na watoto wao wanaume. Kiasi cha fidia ni 1000 Dinar. Fidia ni haki ya walii (wasimamizi) wa aliyeuliwa; wakipenda wataidai na wakitaka wataisamehe Ndipo Mwenyezi Mungu akasema,

ila wakiifanya sadaka .

Mafakihi wanasema limewajibishwa kafara kwa mwenye kuua bila kukusidia ili kuwa ni onyo la uzembe na h imizo la kuchukua tahadhari katika mambo yote. Imewajibishwa fidia kwa ndugu zake kwa kumuhurumia aliyekosea. Na kumewajibishwa kuchukuliwa kisasi kwa aliyeua makusdi, ili kumtia adabu kwa kukusudia haramu.

Na ikiwa ni mmoja wa watu walio maadui zenu, naye ni muumin, basi ni kuacha huru mtumwa muumin.

Makusudio ya watu walio maadui ni makafiri wenye vita na waislamu. Dhamiri ya 'naye' inarudia kwa aliyeuawa. Maana yake ni kuwa mwislamu akiua mtu kwa kuitakidi kwamba yeye ni kafiri, kisha ikabainika kuwa yeye ni mwislamu anayekaa kwa watu wake waliomakafiri, hapo hapatakuwa na chochote kwa muuaji zaidi ya kumwacha huru mtumwa; hakutakuwa na fidia. Kwa sababu watu wa aliyeuliwa ni makafiri, wakipewa fidia itawongezea nguvu kuwapiga vita waislamu.

Na ikiwa ni katika watu ambao baina yenu nyinyi na wao pana ahadi, basi ni diya kwa watu wake na kumwacha huru mtumwa muumin. Na ambaye hakupata basi ni kufunga miezi miwili yenye kufuatana.

Yaani ikiwa mwislamu aliyeuawa kimakosa anatokana na watu makafiri, lakini hawana vita na waislam kwa vile wana mkataba wa amani na waislamu, hapa itatolewa fidia kwa watu wake, hata kama ni makafiri, kwa sababu hukumu yao katika hali hii ni sawa na hukumu ya waislamu katika wajibu wa fidia.

Na ni juu ya muuaji kutoa kafara la kumwacha huru mtumwa, akishindwa afunge miezi miwli inayofuatana. Imewekwa sharia hii ya kafara kwa muuaji ili iwe ni toba kwa aliyoyafanya.

Na mwenye kumuua muumin kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannam, ni mwenye kudumu humo; na Mwenyezi Mungu amemughadhibikia na amemlaani na amemwandalia adhabu kubwa.

Tumeeleza mwanzo wa maelezo namba (1) kuhusu hukmu ya aliyeua makusudi na kwamba yeye atauwawa ila akisamehe walii. Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anataja kwamba malipo yake huko akhera ni kukaa milele motoni, ghadhabu na laana ya Mwenyezi Mungu na adhabu kubwa.

Adhabu zote hizi nne ni kutilia mkazo. Makusudio ya ukubwa wa adhabu kutokana na kosa hili ni kuwa ni kosa kubwa la kutisha na kwamba ni katika madhambi makubwa ambayo hayana mfano wake zaidi ya ukafiri, Baadhi ya mafakihi wamesema: Ni udhihirisho zaidi wa ukafiri na maana yake.

Utakuja ufafanuzi wa kuua nafsi kwa dhulma 'Inshaallah' katika kufasiri (5:32), Na yemetangulia maelezo ya kudumu motoni katika kufasiri (2, 257) kifungu cha 'kudumu motoni.'

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا ضَرَبْتُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَتَبَيَّنُوا وَلَا تَقُولُوا لِمَنْ أَلْقَىٰ إِلَيْكُمُ السَّلَامَ لَسْتَ مُؤْمِنًا تَبْتَغُونَ عَرَضَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فَعِندَ اللَّـهِ مَغَانِمُ كَثِيرَةٌ كَذَٰلِكَ كُنتُم مِّن قَبْلُ فَمَنَّ اللَّـهُ عَلَيْكُمْ فَتَبَيَّنُوا إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا ﴾

94.Enyi mlioamini! Mtakaposafiri katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi hakikisheni wala msimwambie mwenye kuwapa Salaam: Wewe si mwislam. Mnataka mafao ya duniani na kwa Mwenyezi Mungu kuna ngawira nyingi! Hivi ndivyo mlivyokuwa nyinyi hapo mbeleni, na Mwenyezi Mungu akawafanyia hisani. Basi hakikisheni; hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa mnayoyatenda.

KUUDHIHIRISHA UISLAM KUNATOSHA KUWA NI KUUTHIBITISHA

Aya 94

MAANA

Enyi mlioamini! Mtakaposafiri katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi hakikisheni, wala msimwambie mwenye kuwapa salamu: Wewe si mwislamu.

Wameafikiana wafasiri na wapokezi wa Hadith sababu iliyowajibisha kushuka Aya hii ni kuwa Mtume alituma kikosi katika Masahaba wakakutana na mtu mmoja mwenye mali; kama kondoo n.k. Wakamdhania ni kafiri; akatamka neno la kufahamisha uislamu wake, katika maamkuzi au tamko la shahada n.k. Baadhi wakaona hiyo ni kutaka kujiokoa na kifo, waka mwua.

Mtume alipolijua hili alihisi taabu na kumlaumu muuaji akasema: Hakika amehifadhika na kuuliwa kwa tamko hilo. Akamwambia - kama inavyoelezwa katika baadhi ya riwaya - "Huoni kuwa umeupiga mapande moyo wake!"

Matamshi ya Aya hayakatai maana haya, Kwani kauli yake, mtakaposafiri katika njia ya Mwenyezi Mungu, basi thibitisheni, Maana yake mtakapokwenda kwen ye Jihadi pelelezeni; msikimbilie kumua ambaye mnamtilia shaka katika dini yake na uadui wake; wala msimwambie mwenye kuwapa salamu wewe si mwislamu. Kwa sababu kila mwenye kudhihirisha uislamu anayo haki waliyonayo waislam; hasa katika mambo ya kuhifadhi damu na mali ama batini yake inajulikana kwa Mungu peke yake.

Mnataka mafao ya duniani na kwa Mwenyezi Mungu kuna ngawira nyingi!

Inafahamisha kuwa lililowapelekea kuua ni tamaa ya mali aliyokuwa nayo. Hilo ndilo lililowafanya wawaze kuwa kudhihirisha kwake tamko la uislamu kulikuwa na makusudio ya kuokoka. Ni mara nyingi sana mtu kufikiria yale yasiyo ya uhakika. Inakuwa hali ilivyo ni vingine, hata kama anajua ndivyo hivyo, Haya ndiyo maajabu ya mtu.

kwa hali yoyote Mwenyezi Mungu amewatanabahisha makosa yao haya na kwamba wao wameharakia ngawira na ngawira za Mwenyezi Mungu na neema zake hazina idadi, ambazo atawabadilishia na mali ya aliyeuwa wa zaidi na zaidi,

Hivyo ndivyo mlivyokuwa nyinyi zamani

Hili ni jibu lao na kukivunja kitendo chao kwa mantiki ya kiakili na ya hali halisi.

Taarifa yake ni kuwa nyinyi hapo mwanzo mlikuwa washirikina, kisha mkaingia katika Uislam kwa tamko lile lile alilolitamka yule aliyeuliwa; na Mtume alilikubali kutoka kwenu. Kwa tamko hili zimehifadhiwa damu zenu na mali zenu. Kwa hiyo ilikuwa ni juu yenu kumkubalia yule mliyemuua kama vile Mtume alivyowakubalia nyinyi, Hivi ndivyo walivyo watu wengi, wanataka wengine waridhie uchache, lakini wao wenyewe hawaridhii.

Na Mwenyezi Mungu akawafanyia hisani

Kwa kuwakubalia uislam na kuwafanya ni katika Masahaba kwa kutamka tu tamko la shahada, wala Mtume hakuyachunguza yaliyo nyoyoni mwenu. Kwa nini hamkufanyia mwingine vile alivyowafanyia Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w)

Basi hakikisheni; hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa mnayoyatenda.

Yaani kuanzia sasa msifanye kitu mpaka muwe na uhakika nacho wala msimwadhibu yeyote kwa tuhuma au dhana. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa matukio yenu na ana hisabu kwa mnavyostahiki. Mafakihi wameiingiza Aya hii katika Aya za hukumu[13] na wakatoa hukumu mbili za sharia.

Kwanza : Wajibu wa kuhakikisha katika kila kitu, hasa katika hukumu za kisharia na zaidi hasa katika damu na mali; ambapo wamewajibisha mafakihi katika mawili hayo kujichunga na kufanya ihtiyat na wakaongezea pia kuhusiana na tupu.

Pili : Kila mwenye kutamka tamko la uislamu na akasema mimi ni mwislamu, basi hukumu yake ni hukumu ya waislam katika ndoa urithi na mengineyo ambayo yanafungamana na mtu akidhihirisha uislamu tu. Sio kwa undani.

﴿لَّا يَسْتَوِي الْقَاعِدُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ غَيْرُ أُولِي الضَّرَرِ وَالْمُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فَضَّلَ اللَّـهُ الْمُجَاهِدِينَ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ عَلَى الْقَاعِدِينَ دَرَجَةً وَكُلًّا وَعَدَ اللَّـهُ الْحُسْنَىٰ وَفَضَّلَ اللَّـهُ الْمُجَاهِدِينَ عَلَى الْقَاعِدِينَ أَجْرًا عَظِيمًا ﴾

95.Hawawi sawa waumini waliokaa - wasiokuwa wenye madhara - na wenye kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao. Amewatukuza Mwenyezi Mungu katika cheo wale wapiganao katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao kuliko waliokaa, Na wote Mwenyezi Mungu amewaahidi wema. Na amewatukuza Mwenyezi Mungu wenye kupigana Jihadi kwa malipo makubwa kuliko waliokaa.

﴿دَرَجَاتٍ مِّنْهُ وَمَغْفِرَةً وَرَحْمَةً وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴾

96.Ni vyeo kutoka kwake na maghufira na rehema. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

WENYE KUPIGANA JIHAD NA WENYE KUKAA

Aya 95 - 96

MAANA

Hawawi sawa waumini waliokaa - wasiokuwa wenye madhara - na wenye kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao.

Mwenye kubaki nyuma asiende katika jihadi kwa udhuru wa kisheria; kama vile upofu, ulemavu na mengineyo, basi amesamehewa, bali atapata malipo mema akiwa ni muumin mwenye ihlasi anayependa ushindi wa dini, na heri ya watu wake; na anayependelea lau angalikuwa mzima akashiriki na wanaopigana jihadi.

Kuna Hadith isemayo:"Mtu yuko pamoja na anayempenda." Yaani, mwenye kumpenda mwenye kupigana jihadi si kwa chochote ila kwa kuwa yeye ni mwanajihadi, basi naye ana malipo ya wapigania jihadi; mwenye kumpenda mkweli kwa sababu ya ukweli wake basi yeye yuko katika cheo chake; mwenye kumpenda dhalimu katika dhulma yake; basi yeye ni mshirika wake na mwenye kumpenda kafiri kwa ukafiri, basi ni kama yeye. Hii ndiyo hukumu ya wenye kukaa wasiokuwa na siha nzuri.

Ama wale wasiokuwa na udhuru katika wao wataangaliwa. Wakikaa bila ya kwenda kwenye jihadi ambayo wamewajibishiwa wao na wengineo; yaani kuwa vita ni vya wote. Hapo hawatasamehewa, bali watalaumiwa na ni wenye kustahili adhabu.

Kwa sababu wao wameasi, kwa hiyo haifai kuwalinganisha na wapiganaji kwa hali yoyote kwa sababu kulinganisha ni kushirikisha; na hawa hawakushirikiana na wapigana jihadi katika kitu chochote; hata kama ikiwa jihadi ni faradhi kifaya (ya kutosheana), isiyokuwa na haja ya kushiriki wote, lakini bado wapigana jihadi ni bora kuliko waliokaa. Kwa sababu wao wamechagua uvivu - kujiuzulu na vita. Hawa ndio waliokusudiwa na kauli yake Mwenyezi Mungu: "Hawawi sawa waumini waliokaa"

Kwa hiyo maana yanakuwa ni hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu waliokaa, walio wazima na wale wapigania Jihadi ambao haikuwa jihadi ni wajibu kwao tu, bali ilikuwa wajibu kwa wote kwa njia ya kifaya, lakini wao ndio walioziba wajibu huu na wakautekeleza kwa ukamilifu na kuuondoa kwa waliobaki. Ni maana haya ambayo ameyakusudia Mwenyezi Mungu na kuyafafanua kwa kauli yake:

Amewatukuza Mwenyezi Mungu katika cheo, wale wapiganao katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao kuliko waliokaa.

Baada ya Mwenyezi Mungu kukanusha usawa baina yao na baina ya wale waliokaa anabainisha yale yaliyowapambanua wapigania Jihadi; ambayo ni ubora wao katika cheo kuliko waliokaa.

Kwa hiyo inakuwa kauli yake hii ni ufafanuzi baada ya kueleza kwa ujumla. Na siri ya kutukuzwa ni kama tulivyoeleza, kuchukua majukumu ya ulinzi peke yao; sawa na lau adui anashambulia mji, kukatokea kikundi kuwazuiwa kinyume cha kikundi kingine, hapo kimsingi kikundi cha kwanza kitatofautika na kikundi cha pili.

Ingawaje kikundi cha pili hakitaadhibiwa baada ya cha kwanza kusimamia wajibu na kupatikana lengo lililotakikana. Kwa hiyo ndio Mwenyezi Mungu akasema:

Na wote Mwenyezi Mungu amewaahidi wema

Lakini tena akarudia kutilia mkazo na kuhimiza Jihadi kwa kusema:

Na amewatukuza Mwenyezi Mungu wenye kupigana Jihadi kwa malipo makubwa kuliko waliokaa.

Na akabainisha malipo haya makubwa kuwa:Ni vyeo kutoka kwake na maghufira na rehema .

Cheo kimoja tu kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni bora kuliko ulimwengu na vilivyomo ndani yake, je itakuwaje vyeo vingi! Ama rehema yake, hakuna kitu bora zaidi kuliko hiyo ila ambaye imetokana naye. Na inatosha kwa maghufira yake kuwa ni kusalimika na adhabu yake na machukivu yake.

Haya ndiyo maghufira, rehema na cheo kwa Mwenyezi Mungu. Mwenye kupata moja tu, atakuwa katika walio juu, sikwambii atakayeyapata yote! "Ewe Mola wangu! Hakika mimi nakuomba wepesi katika rehema yako na maghufira yako; na wewe wajua kuwa mimi naihitajia.

Kwani itakuwaje kama utanineemesha na kunikwasisha? Kwani unahofia maghufira yako yatakwisha na hazina ya rehema yako (itakwisha)? Au ni nini ewe Mola wangu! Au ni kwa kuwa mimi nina dhambi? Ndio, lakini hujui kwamba mimi najua kuwa hakuna kimbilio ila kwako tu na kwamba kunanifurahisha mimi kunisamehe! Ewe Mola wangu! Ikiwa mimi ni muongo kwa niliyosema, basi nifanyie vile ninavyostahiki, na ikiwa ni mkweli kwa niliyoyasema, basi fanya vile unavyostahiki"

ALI NA ABU BAKR

Amesema Razi (ninamnukuu): "Wamesema Shia kuwa Aya hii: Amewatukuza Mwenyezi Mungu wenye kupigana Jihadi kwa malipo makubwa kuliko wenye kukaa. Inafahamisha kuwa Ali bin Abu Twalib ni bora kuliko Abu Bakr. Kwa vile Ali alipigana Jihadi zaidi ya Abu Bakr" Kipimo cha utofauti ni kuwa Ali alikuwa ni katika waliopigana Jihadi katika alivyomzidi Abu Bakr, na Abu Bakr alikuwa katika waliokaa. Ikiwa hivyo basi imewajibika kuwa Ali(a.s) ni bora kuliko Abu Bakr." Kisha Razi akawajibu Shia kwa kuse ma: "Tunawaambia: Kuua kwa Ali makafiri kulitokana na Mtume, kwa hiyo itawalazimu kwa hukumu yenu hii ya Aya, kuwa Ali ni bora kuliko Muhammad(s.a.w.w) . Na haya hayasemwi na mwenye akili. Kama mkisema: Kupigana Jihadi kwa Mtume pamoja na Makafiri ni kukubwa zaidi kuliko kwa Ali, kwa sababu Mtume alikuwa akipigana kutokana na dalili na ubainifu, kuondoa shubha na upotevu, na kwamba jihadi hii ni kamilifu zaidi kuliko hiyo. Basi tunasema: Na sisi tukubalieni kuhusu Abu Bakr kama mfano wake."

Huku ni ni kulala kabisa kwa mwanafalsafa wa wafasiri na wala siwezi kukuita kusinzia. Kwa sababu hizi zifuatazo:-

Kwanza : kila mwenye kumlinganisha Muhammad(s.a.w.w) na mmoja wa maswahaba zake, katika kuleta dalili na ubainifu, basi atakuwa ametoka katika uislamu, atake asitake. Kwa sababu Muhammad anatoa ubainifu kwa wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu -kama tutakavyoeleza- na maswahaba wanatoa kutokana na mafunzo yake. Kwa hiyo basi cheo cha kwanza ni cha Mwenyezi Mungu peke yake hana mshirika, cha pili ni cha Muhammad peke yake hana mwenzake na kuwamini wote wawili kuko daraja moja.

Kwa vile kumwamina Mungu na mitume yake ni nguzo moja katika nguzo zinazousimamisha uislam, haitoshi moja peke yake. Ukhalifa na uswahaba ni matawi ya kumwamini Mungu na Mitume, na tawi haliwezi kufananishwa na shina.

Pili : Maana yaliyo wazi ya neno wenye kupigana Jihadi katika Aya, ni Jihadi kwa upanga, si kwa kingine kwa kukiri Razi katika tafsiri yake. Lakini yeye ameghafilika na aliyoyasema na akajipinga mwenyewe.

Hebu tuiache dhahiri ya Aya na tafsiri zote, tumrudie yule ambaye Qur'an imeteremshwa kwenye moyo wake na tumwulize, ni yupi mbora wa watu? Tumsikilize atajibu nini, Amepokea Muslim katika sahih yake, kwamba mtu mmoja alimwuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) : "Ni nani mbora wa watu?" Akasema:"Ni mtu anayepigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa nafsi yake na mali yake."

Sote tunajua kuwa Ali alipigana zaidi Jihadi; kama alivyosema Razi, kwa hivyo anakuwa mbora wa watu, isipokuwa Mtume(s.a.w.w) ; ambapo hakuna chochote zaidi ya daraja ya utume ila Uungu - kama tulivyobainisha - Na kila mmoja anajua kwa uwazi kwamba Jihadi kwa nafsi ni bora na kubwa kuliko Jihadi kwa mali. Kwa sababu mali hutolewa katika njia ya Jihadi kwa nafsi, lakini nafsi haitolewi katika njia ya mali.

Tatu : Hakika Mtume Mtukufu(s.a.w.w) - kama tulivyotangulia kueleza - hakutoa dalili na hakubainisha,wala hakuondoa utatanishi yeye mwenyewe; bali yote yanatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) alikuwa akimwelezea Muhammad(s.a.w.w) naye akifikisha kwa kunukuu kwa herufi, Muhammad anaambiwa.

"Sema: Ataihuisha yule aliyeiumba mara ya kwanza" (36:79)

"Sema: Je, yuko katika washirika wenu aongozaye katika haki?" (10: 35)

﴿قُلْ فَأْتُوا بِسُورَةٍ مِّثْلِهِ وَادْعُوا مَنِ اسْتَطَعْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴾

"Sema: Hebu leteni Sura moja mfano wake na muwaite muwezao asiyekuwa Mwenyezi Mungu mkiwa mnasema kweli." (10: 38)

﴿قُلْ أَفَاتَّخَذْتُم مِّن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ لَا يَمْلِكُونَ لِأَنفُسِهِمْ نَفْعًا وَلَا ضَرًّا﴾

"Sema: Je, mnawafanya wengine badala yake kuwa ni walinzi na hawajifai wenyewe kwa nafuu wala dhara" (13: 16)

Na Aya nyingine kadha, Jambo la ajabu ni kuwa Razi ameghafilika nazo baada ya kurefusha ufafanuzi na tafsiri zake. Ajabu ya maajabu ni pale aliposema: "Basi na sisi tukubalieni kuhusu Abu Bakr kama mfano wake;" yaani kama mlivyomkubalia Muhammad.

Hapana! tena hapana mara elfu! Si sisi wala mwislam yeyote atakayekukubalia wewe au mwengine kuwa Abu Bakr awe na mfano wa aliyo nayo Muhammad(s.a.w.w) (katika kuleta dalili, hoja na kuondoa utatanishi na upotevu. Ila ikiwa Abu Bakr ni Mtume anayeteremshiwa Wahyi.

Zaidi ya haya cheo cha Ali katika elimu hakikurubiwi na yeyote katika Masahaba. Inatosha kuwa ni ushahidi wa hilo. Hadith mutawatir iliyopokewa kutoka kwa Mtume inayosema: "Mimi ni jiji la elimu na Ali ni mlango wake." Zimehifadhiwa turathi za kiislam kutokana na elimu ya Ali, kiasi ambacho hakikuhifadhiwa kutoka kwa Abu Bakr wala Sahaba mwengineo.

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA TANO

﴿ إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴾

97.Hakika wale ambao Malaika wamewafisha hali ya kuwa wamezidhulumu nafsi zao, wataambiwa: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa wanyonge katika ardhi, wataambiwa: Kwani ardhi ya Mwenyezi Mungu haikuwa pana mkahamia humo? Basi hao makazi yao ni Jahannam; nayo ni marejeo mabaya.

﴿إِلَّا الْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ لَا يَسْتَطِيعُونَ حِيلَةً وَلَا يَهْتَدُونَ سَبِيلًا﴾

98.Isipokuwa wale wanyonge katika wanaume na wanawake na watoto (ambao) hawawezi kufanya hila yoyote wala kufuata njia.

﴿فَأُولَـٰئِكَ عَسَى اللَّـهُ أَن يَعْفُوَ عَنْهُمْ وَكَانَ اللَّـهُ عَفُوًّا غَفُورًا ﴾

99.Basi hao huenda Mwenyezi Mungu akawasamehe; na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa maghufira.

﴿وَمَن يُهَاجِرْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ يَجِدْ فِي الْأَرْضِ مُرَاغَمًا كَثِيرًا وَسَعَةً وَمَن يَخْرُجْ مِن بَيْتِهِ مُهَاجِرًا إِلَى اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ يُدْرِكْهُ الْمَوْتُ فَقَدْ وَقَعَ أَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴾

100.Na mwenye kuhama katika njia ya Mwenyezi Mungu atapata katika ardhi mahali pengi pa kukikimbilia na wasaa. Na mwenye kutoka nyumbani kwake ili kuhamia kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kisha yakamfika mauti, basi yamethibiti malipo yake kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

ARDHI YA MWENYEZI MUNGU NI PANA

Aya 97 - 100

MAANA

Waislamu zama za Mtume(s.a.w.w) walikuwa na Hijra mbili kutoka Makka. Ya kwanza ilikuwa ni ile ya kuelekea Uhabeshi (Ethopia), na ilikuwa miaka mitano tangu Mtume kuutangaza utume wake, Ya pili ilikuwa ile ya kuelekea Madina iliyokuwa miaka minane baadaye.

Wako Masahaba ambao walifanya Hijra mbili kama Jafar bin Abu Twalib ambaye maisha yake yaliishia kwa kufa shahid baada ya kukatwa mikono yake. Mwenyezi Mungu akamkirimu kutokana na mikono hiyo mbawa mbili atakazoruka nazo katika pepo; na ndio akatiwa 'Attwayyar' (Mrukaji).

Ama sababu ya Hijra (kuhama) ni kujiepusha na kuingia katika maangamivu, kukimbilia mahali pa amani kupanga mipango ya Jihadi na kuipinga batili. Kwa kutokana na Hijra (kuhama) na fadhila zake, uislamu umeshinda maadui zake. Lau si hiyo ungelizimika mwenge wake na kugeuka jivu linalopeperuka. Kwa ajili hii Hijra ikawa wakati huo ni fadhila kubwa na ni kitendo cha fahari cha kwanza ambacho hakikurubiwi na kitu chochote.

Mtume(s.a.w.w) alihama kutoka Makka kwenda Madina na akawaamrisha waislamu wahamie huko. Wengi wakamwitikia na wengine wakabaki kwa kung'ang'ania mali zao na masilahi yao. Kwa sababu washirikina walikuwa hawamwachi mwenye kuhama kuchukua chochote katika mali yake.

Washirikina walikuwa wakimwudhi sana anayebaki hapo na kumzuilia na dini yake, akiwa hawezi kujitetea. Lakini alikuwa anaweza kujiepusha na vikwazo hivyo na kuisimamisha dini kwa njia za ukamilifu, kwa kuhama kutoka katika mji ulio na vita na waislam kwenda mji wa uislamu na amani (Madina) aliko Mtume na Sahaba. Kwa hiyo Mwenyezi Mungu aliwatahayariza wale walioona kuwa ni heri kubaki katika nyumba ya ukafiri na kuipiga vita dini na watu wake. Aliwatahayariza na akawazindua kupitia Malaika kwa kusema:

Hakika wale ambao Malaika wamewafisha hali ya kuwa wamezidhulumu nafsi zao.

Kwa kuacha Jihadi na kuhama kwenda kwenye mji wa kiislamu, wakaridhia kubaki katika nyumba ya ukafiri, udhalili na kuharibu wajibu wa dini,Wataambiwa; mlikuwa katka hali gani? Yaani Malaika wa mauti watawaam- bia wale walioacha kuhama; mlikuwa vipi? Hili hasa si swali, isipokuwa ni lawama na kusutwa. Ilivyo hasa ni kuwa lawama zinakuwa kwenye tukio maalum, ambalo hapa ni kule kukaa kwao nyuma ya ndugu zao wahamiaji ambao wamemtii Mtume katika kutekeleza mipango ya kuumaliza ushirikina na kuliinua neno la Mungu.

Akiuliza muulizaji; Je, makaripio haya na masuto kutoka kwa Malaika kwa wale waliorudi nyuma yalikuwa wakati wa kukata roho au ni baada yake?

Tutajibu kuwa ujuzi wa haya uko kwa Mola; yeye amelinyamazia hilo. Kwa hiyo na sisi tunalinyamazia vilevile. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema:"Hakika Mwenyezi Mungu amenyamazia mambo si kwa kusahau, basi msijikalifishe nayo"

Watasema: Tulikuwa ni wanyonge katika ardhi.

Huu ni udhuru na kutafuta sababu kwa waliorudi nyuma. Maana yake ni kuwa waliorudi nyuma wanawajibu Malaika wanaowalaumu kwa uzembe wao katika mambo ya dini. Wanawajibu kwa kusema: Tulikuwa tumeshindwa, tunaonewa katika mji wa makafiri, kusimamia wajibu wa kidini.

Kwa sababu washirikina walitukandamiza na kutuzuia kufanya tuliyokuwa tukiitakidi, Malaika wakajibu udhuru huu. Watasema: - Kwa kuwasuta –

Kwani ardhi ya Mwenyezi Mungu haikuwa pana mkahamia humo? Yaani mlikuwa mnaweza kuhamia mji wa kiislamu ambako mtaepukana na udhalili na kuweza kuitekeleza dini kwa uhuru; kama walivyofanya waislamu wengine.

Kama kuna kitu kinachofahamisha zaidi kuhusu malumbano haya, basi ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hamwadhibu yeyote ila baada ya kukamilisha hoja, bali ila baada ya kurundikana hoja kwake; kiasi ambacho kinamwacha mwenye dhambi asiwe na kimbilio ila msamaha wake Mwenyezi Mungu (s.w.t) na rehema yake ambayo imeenea katika kila kitu, "Ewe Mola wangu na mimi ni kitu zinienee rehema zako."

Basi hao - yaani waliorudi nyuma -makazi yao ni Jahannam, na ni marejeo mabaya. Isipokuwa wale wanyonge katika wanaume na wanawake na watoto (ambao) hawawezi kufanya hila yoyote wala hawawezi kufuata njia.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwakemea waliorudi nyuma, aliwavua walio na udhuru kwa ugonjwa au kukosa posho na akawaondolea takilifa ya Hijra. Kwa sababu Mwenyezi Mungu hakalifishi ila uweza wake.

Unaweza kuuliza : kuwa kutolewa wanaume na wanawake wenye udhuru kuna mwelekeo maalum. Sasa kuna mwelekeo gani wa kutolewa watoto na inajulikana kuwa watoto hawakalifiwi na kitu?

Swali hili limejibiwa kuwa : maana ya neno Wildan ni watumwa na wajakazi. Ama sisi tunajibu kuwa watoto wengine wanaweza kuhama hasa vijana wadogo, bali baadhi yao wana uwezo zaidi ya watu wakubwa. Kwa ajili hii mtu anaweza akadhania kuwa kuhama ni wajibu kwa kila anayeweza. Hivyo Mwenyezi Mungu ameiondoa dhana hiyo na kubainisha kuwa Hijra ni wajibu kwa kila mwenye uweza ila akiwa ni katika watoto.

MAFAKIHI NA WAJIBU WA HIJRA

Mafakihi wameitolea dalili Aya hii kwamba mwislamu haijuzu kwake kukaa kwenye mji wa ukafiri ikiwa hawezi kuitekeleza dini, hata kama ni mji wake akiwa na milki na masilahi, Lakini hukumu hii siku hizi haina maudhui. Kwa sababu kila mtu katika kila mji anaweza kumwabudu Mwenyezi Mungu kwa namna yoyote atakayo, Akiacha, basi yeye peke yake ndiye mwenye jukumu.

Unaweza kuuliza : Mtu akijua kuwa kukaa kwake katika mji usiokuwa wa kiislamu kunasababisha kuacha faradhi, si kwa kuwa mtu anamzuia, bali kwa udhaifu wa kukabiliana na msukumo; kama vile mchezo n.k. Je, inafaa kukaa katika mji huu?

Jibu : Akijua kwa yakini kwamba kwenda mahali popote, pawe ni mjini, kikao au sokoni ambako lazima kutamfanya aache wajibu au kufanya haram basi ni wajibu kwake kuepukana nako. Kwani sababu inayolazimu uharamu basi ni haramu. Mwenyezi Mungu anasema:"Basi baada ya kukumbuka usikae pamoja na watu madhalimu." (6: 68)

Amirul Mumin(a.s) anasema: "Hijra (kuhama) bado iko kwenye mipaka yake ya kwanza." Yaani, bado ipo hukumu yake ya wajibu kwa yule ambaye imekuwa uzito kutekeleza hukumu za dini yake ila katika mji wa waislamu.

Ama kauli ya Mtume(s.a.w.w) :Hapana Hijra (kuhama) baada ya kutekwa Makka," makusudio yake ni kuhama kutoka Makka. Hilo linafahamishwa na neno kutekwa Makka.

Na mwenye kuhama katika njia ya Mwenyezi Mungu atapata katika ardhi mahali pengi pa kukimbilia na wasaa.

Riziki haziko nyumbani tu na kuhama hakuwajibishi kukosa. Miji ya Mwenyezi Mungu ni mingi, riziki yake ni pana na neema katika kila mji hazihisabiki, na kwamba mafukara wengi wamejikusanyia mali kule walikohamia kiasi ambacho walikuwa hawaoti kupata hata sehemu ndogo tu walipokuwa nyumbani kwao.

Lau wale waliorudi nyuma wangelihama, wangelipata riziki na utukufu kiasi cha kuwadhalilisha washirikina waliowapa aina kwa aina za udhalili na vikwazo. Lakini waliorudi nyuma walilikataa hilo, wakachukua udhalili na utwevu kutoka kwa maadui wa dini yao, si kwa lolote ila ni kuwa shetani aliwatisha na ufukara iwapo watahama wakategemea vitisho vyake na wakaathirika kuacha maghufira ya Mwenyezi Mungu:

﴿الشَّيْطَانُ يَعِدُكُمُ الْفَقْرَ وَيَأْمُرُكُم بِالْفَحْشَاءِ وَاللَّـهُ يَعِدُكُم مَّغْفِرَةً مِّنْهُ وَفَضْلًا وَاللَّـهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ ﴾

"Shetani anawatisha na ufukara na anawaamrisha ubakhili; na Mwenyezi Mungu anawaahidi msamaha utokao kwake na fadhila na Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu, Mjuzi" (2: 268).

Na mwenye kutoka nyumbani kwake ili kuhamia kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kisha yakamfikia mauti, basi yamethibiti malipo yake kwa Mwenyezi Mungu.

Kila mwenye kukusudia kwa kujitahidi na kufanya ikhlasi kwa amali yoyote katika amali za twaa kisha akashindwa, basi Mwenyezi Mungu (s.w.t) humwandikia thawabu kamili kwa fadhila na ukarimu kutoka kwake Mwenyezi Mungu. Tumelifafanua hilo katika kufasiri Aya (3: 144) kifungu, kila mtu ana alilonuia.

Imepokewa kuwa Jundub bin Dhumra, aliposikia Aya ya Hijra aliwaambia wanawe; "Wallahi silali Makka mpaka nitoke, kwa sababu ninahofia kufa Makka;" naye alikuwa mgonjwa sana, wakatoka nae wakimchukua kitandani, Alipofika mahali panapoitwa Tan'im akafariki, Ndipo ikashuka Aya hii.

BAINA YA KUHAMA MTUME KUTOKA MJI MTUKUFU WA MAKKA NA KUHAMA WAPALESTINA KUTOKA ARDHI TAKATIFU

Katika maajabu ya sadfa ni kuafikiana - bila ya kukusudia - kufikia kwangu kufasiri Qur'an kwenye Aya ya Hijra mwanzo wa mwaka 1388 A.H. na Israel inakalia ardhi yetu takatifu, watu wetu wanahama wakikimbia mateso na mauaji waliyoyafanya waisrael na wanayoendelea kuyafanya.

Sadfa hii imenifanya nilinganishe tukio la uchokozi wa washirikina katika Makka kwa waislamu na kutolewa kwao mijini mwao, na tukio la uchokozi wa waisrael; au kwa usahihi zaidi uchokozi wa kikoloni kwenye ardhi takatifu na kuwatoa wenyeji mijini mwao.

Kisha nikatoka kwenye mlinganisho huu kufikia Ibra na mazingatio kutokana na jihadi ya Mtume(s.a.w.w) na waislamu katika kuhama kwao na kupanga mipango iliyowapeleka waislamu kwenye kilele cha ushindi kwa maadui zao, kuuvunja utaghuti na uchokozi wake na kuwasimamisha mamwinyi wa kiquraish, waliowatoa Makka mbele ya Mtume wakiwa madhalili, wenye kusalimu amri wakimsikiliiza akiwaambia "Mnadhani nitawafanya nini?"

Baadhi ya watu wanaweza kudhani kuwa lengo la kwanza la Mtume na waislamu ni kuikimbiza tu dini yao kutoka kwa washirikina ambao waliwaingilia kwa kuwaudhi na kuwazuia kutekeleza nembo za dini yao na amali za kidini; sawa na anavyokimbilia Daruweshi msikitini ili aswali vizuri kwa kuepuka fujo na kelele. Hapana! Hijra ya waislamu ilikuwa mbali na kuwa na undani zaidi ya hilo.

Dalili ya hilo ni natija na malengo yaliyotekelezwa na Hijra hiyo. Hijra hiyo zaidi ya kuikimbiza dini, ilikuwa na mipango iliyopangwa vizuri ya uandalizi wa vita; sawa na jeshi linapojitenga kutoka uwanja wa vita kwenda mahali pengine ili kujiandaa kwa shambulio kubwa la kummaliza adui. Mtume(s.a.w.w) baada ya kufika Madina aliwafanya ndugu Masahaba na akazichanganya pamoja nyoyo za mahasimu na akayeyusha vinyongo na vidonge walivyokuwa navyo.

Baada ya kukamilisha kazi hiyo aliwahimiza waislamu jihadi na kuwahimiza kulinda heshima yao na itikadi yao, na kumdhaminia pepo atakayepigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, na kupata utukufu na cheo duniani na akhera kwa atakayepona kifo.

Baada ya mafunzo haya kuwaingia, Mtume akaanza kuwaunganisha kijeshi na kuwazoesha vita vidogo vidogo akiwapeleka huku na huko; mara nyingi akiviongoza mwenyewe. Waislamu wakawa na amani na raha; na amani ya Maquraish ikaingia kwenye wasiwasi. Hatimaye vita vidogo vikageuka na kuwa vita vikubwa, huku waislamu wakijitolea roho zao na mali zao, mpaka ukaja msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi.

﴿وَجَعَلَ كَلِمَةَ الَّذِينَ كَفَرُوا السُّفْلَىٰ وَكَلِمَةُ اللَّـهِ هِيَ الْعُلْيَا ﴾

"Na akalifanya neno la waliokufuru kuwa chini na neno la Mwenyezi Mungu ndilo la juu" (9: 40)

Nadhani ishara hii inatosha kuchukua ibra ambayo ni wajibu kunufaika nayo katika balaa letu na israel na wanaoisaidia

Mtume(s.a.w.w) alihama kutoka Makka kwa sababu ya uchokozi wa washirikina waliokuwa wakimfanyia yeye na masahaba wake. Na wapalestina nao walihama kutoka ardhi takatifu kwa uchokozi wa kizayuni na kutaka kuwatawala wao wanawake wao na watoto wao. Hijra ya waislamu wakati huo ilikuwa ni kujiepusha na maangamizo na kujitenga kutoka uwanja wa vita ili kukusanya nguvu na kujiandaa kwa shambulio la kummaliza adui.

Kwa hiyo basi ni wajibu kuwa kutoka kwa wapalestina mijini kwao kuwe ni kwa makusudio haya na kwa lengo hili; sio kwa kuwaachia wanyang'anyi Baitul- Maqdis waichezee.

Mtume alianza Hijra yake kwa kufanya udugu baina ya masahaba zake. Kwa hiyo ni juu ya viongozi wa kiarabu na waislamu, kuanza kufanyiana udugu na kusafiana nyoyo; wawe wamoja ili waweze kumkabili adui; sawa na alivyofanya Mtume kabla ya kukabiliana na washirikina. Mwenye kuepuka njia hii basi amekutana na waisrael na ametekeleza malengo yao, atake asitake.

Mtume alituma vikosi vidogo kubabaisha washirikina, alivipa vikosi hivyo mahitaji yao. Ni wajibu kwa waarabu na waislamu kuwashujaisha wanaojitolea mhanga na wengineo na kusaidiana nao hadi mwisho, ili kuwatia wasiwasi waisrael.

Mtume aliwaandaa waislamu wote kwa vita vikubwa na kuung'oa ushirikina na mizizi yake baada ya kuota mizizi, karibu karne nzima, katika kila sehemu ya ardhi ya Bara Arabu. Na hivyo ndivyo inavyopasa kwa kila kiongozi wa waarabu na waislam.

Ikiwa hatutalizingatia somo hili kutokana na turathi zetu na Historia yetu na kuwa sote ni askari katika askari wa Mwenyezi Mungu na wa nchi, basi hatutastahiki jina la uarabu na warabu, wala la uislamu na waislam; hata kwa jina za binadamu na ubinadamu; baada ya kuwa hizi ni zama za kujitolea na kutekeleza; na kujikomboa na kila aina ya dhulma na unyonyaji.

Tumalizie kwa kuwapa salaam watoto wetu wapiganaji waliojitolea mhanga ambao wameonyesha mfano mzuri wa kishujaa katika nchi yetu iliyovamiwa, wakauthibitishia ulimwengu wote kwamba sisi tuko katika zama za kujitolea na kupigania uhuru na heshima.

﴿وَإِذَا ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَقْصُرُوا مِنَ الصَّلَاةِ إِنْ خِفْتُمْ أَن يَفْتِنَكُمُ الَّذِينَ كَفَرُوا إِنَّ الْكَافِرِينَ كَانُوا لَكُمْ عَدُوًّا مُّبِينًا ﴾

101.Na mnaposafiri katika ardhi, si vibaya kwenu kama mkifupisha Swala, ikiwa mnaogopa kuwa wale waliokufuru watawaletea balaa. Hakika makafiri ni maadui wenu walio wazi.

﴿وَإِذَا كُنتَ فِيهِمْ فَأَقَمْتَ لَهُمُ الصَّلَاةَ فَلْتَقُمْ طَائِفَةٌ مِّنْهُم مَّعَكَ وَلْيَأْخُذُوا أَسْلِحَتَهُمْ فَإِذَا سَجَدُوا فَلْيَكُونُوا مِن وَرَائِكُمْ وَلْتَأْتِ طَائِفَةٌ أُخْرَىٰ لَمْ يُصَلُّوا فَلْيُصَلُّوا مَعَكَ وَلْيَأْخُذُوا حِذْرَهُمْ وَأَسْلِحَتَهُمْ وَدَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ تَغْفُلُونَ عَنْ أَسْلِحَتِكُمْ وَأَمْتِعَتِكُمْ فَيَمِيلُونَ عَلَيْكُم مَّيْلَةً وَاحِدَةً وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن كَانَ بِكُمْ أَذًى مِّن مَّطَرٍ أَوْ كُنتُم مَّرْضَىٰ أَن تَضَعُوا أَسْلِحَتَكُمْ وَخُذُوا حِذْرَكُمْ إِنَّ اللَّـهَ أَعَدَّ لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا﴾

102.Na utakapokuwa kati yao, ukawasimamishia Swala, basi kundi moja miongoni mwao wasimame pamoja nawe na washike silaha zao. Watakaposujudu na wawe nyuma yenu; Na lije kundi jingine ambalo halijaswali, waswali pamoja na wewe na washike hadhari yao na silaha zao. Wanataka wale waliokufuru lau kama nyinyi mwasahau silaha zenu na vifaa vyenu ili wawavamie mvamio wa ghafla. Wala hapana vibaya kwenu ikiwa mnaona udhia kwa sababu ya mvua au mkiwa wagonjwa kuweka silaha zenu, Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha.

﴿فَإِذَا قَضَيْتُمُ الصَّلَاةَ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمْ فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا﴾

103.Mtakapomaliza Swala, basi mtajeni Mwenyezi Mungu kwa kusimama na kwa kukaa na kwa (kulala) ubavu. Mtakapopata amani, basi simamisheni Swala, Hakika Swala kwa waumin ni faradhi iliyoekewa wakati maalum.

SWALA YA HOFU

Aya 101- 103

MAANA

Swala haiachwi kwa hali yoyote; hata kwa maradhi, vita, au safarini. Anaitekeleza kila mwenye kukalifiwa na sharia kiasi cha uwezo wake; iwe ni kusimama au kukaa; akishindwa ataitekeleza hali ya kulala ubavu. Hata bubu pia ni wajibu kwake kutingisha ulimi wake na kuishiria kwa mkono wake badala ya kutamka, Ufafanuzi uko katika vitabu vya Fiqh.

Na mnaposafiri katika ardhi, si vibaya kwenu kama mkifupisha swala ikiwa mnaogopa kuwa wale waliokufuru watawaletea balaa.

Aya hii imeshuka katika hukumu ya jihadi na hofu; sawa na Aya zilizotangulia, kwani mfumo wa zote ni mmoja. Uwazi zaidi wa kuwa mfumo mmoja ni kauli yake Mwenyezi Mungu: Ikiwa mtaogopa kuwa wale waliokufuru watawaletea balaa. Kwa sababu makusudio ya balaa hapa ni kuua. Ama safari imekuja mahali pa aghalabu, sio kuwa ni sharti.

Ama kauli yake 'si vibaya kwenu' makusudio yake ni wajibu na lazima sio ruhusa na kuhalalisha. Kwa sababu Hadith zimefasiri ulazima; kama vile Aya ya Tawaf:

﴿فَمَنْ حَجَّ الْبَيْتَ أَوِ اعْتَمَرَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِ أَن يَطَّوَّفَ بِهِمَا﴾

"Basi anayehiji katika nyumba hiyo, au kufanya umra, si vibaya kwake kuvizunguka (vilima) hivyo viwili" (2:158)

Kwa kuwa Aya imekuja katika Swala ya hofu si Swala ya kupunguza ya msafiri, basi makusudio ya kauli yake Mwen yezi Mungu kufupisha Swala ni kupunguza idadi ya rakaa na kugeuza umbo la Swala, kulingana na dharura iliyopo.

Swala ya hofu ina sharti. Sharti lake muhimu ni kuwa upande wa maadui kuna nguvu zinazowawezesha kuhujumu na kuvamia. Ama aina yake, Shahid wa pili amesema katika Lum'a: ni nyingi zinazofikia kumi inasihi kwa jamaa na kwa mmoja mmoja.

Ifuatayo ni namna y a Swala ya hofu kwa mtu pekee aliyoielezea mwenye Kitab Ash-sharai: "Ama Swala ya hofu ni mfano wa hali ya kufikia kuuana. Ataswali kiasi atakachoweza, iwe ni kwa kusimama, kwenda au kupanda.

Ataelekea Qibla kwa Takbira ya kuhirimia; kisha ataendelea ikiwezekana kuendelea, vinginevyo, ataelekea Qibla kwa itakavyowezekana kwake, na ataswali kwa udhuru wa kuelekea popote patakapomwezekania. Ikiwa hakuweza kushuka, ataswali akiwa amepanda na atasujudu juu ya kiti cha saruji yake; kama hakuweza basi ataashiria, kama atakuwa (anazidi) kuhofia basi ataswali kwa tasbih, bila ya kurukuu na kusujudu. Atasema badala ya kila rakaa "Subhanullah Wal-hamdulillaah wa Lailaha illa Ilah Wallahu Akbar."

Sura hii inatosha kuwa ni dalili kwamba Swala ni laizma, hasamehewi hata katikati ya mapigano na wala wakati wa kukata roho. Na kwamba mtu ataitekeleza kwa namna na hali yoyote atakavyoweza.

Na utakapokuwa kati yao, ukawasimamishia Swala, basi kundi moja miongoni mwao wasimame pamoja nawe na washike silaha zao.

Huu ni ubainifu wa Swala ya hofu ya jamaa. Maana yake, ukitaka Ewe Muhammad kuswali jamaa na wapiganaji, basi gawa makundi mawili: Moja liswali na wewe wakiwa na silaha zao; na la pili lisimame kulinda; kama ambavyo inaswihi jamaa pamoja na Mtume(s.a.w.w) ; vile vile inaswihi pamoja na mtu mwingine.

Watakaposujudu na wawe nyuma yenu.

Yaani watakaposujudu wale wanaoswali na Mtume(s.a.w.w) , lisimame kundi linalolinda nyuma ya wenye kuswali.

Na lije kundi jingine ambalo halijaswali, waswali pamoja na wewe na washike hadhari yao na silaha zao. Yaani baada ya kumaliza kundi la kwanza kuswali, kundi la pili lichukue mahali pa kundi la kwanza katika Swala na kundi la kwanza lichukue mahali pa ulinzi.

Wanataka wale waliokufuru lau kama nyinyi mwasahau silaha zenu na vifaa vyenu ili wawavamie mvamio wa ghafla.

Huu ni ubainifu wa hekima iliyofanya kuwekwa Swala ya aina hii. Hekima yenyewe ni kutopata fursa adui ya kuwavamia wakati wanaswali.

Wala hapana vibaya kwenu ikiwa mnaona udhia kwa sababu ya mvua au mkiwa wagonjwa kuweka silaha zenu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwaamrisha walioswali kuchukua silaha, akawapa ruhusa ya kuziacha ikiwa wanaona uzito wa kuzichukua kwa sababu ya mvua au ugonjwa, lakini Mwenyezi Mungu Mtukufu amewalazimisha wajilinde na wawe macho na adui asijewaingilia ghafla.

Mtakapomaliza Swala, basi mtajeni Mwenyezi Mungu kwa kusimama na kwa kukaa na kwa (kulala) ubavu.

Makusudio ya Swala hapa ni Swala ya hofu. Maana ni kuwa kumtaja Mwenyezi Mungu ni vizuri katika hali yoyote si katika Swala tu. Imam Ali(a.s) amesema:"Amefaradhisha Mwenyezi Mungu katika ndimi zenu dhikri na akawausia takwa na akaijaalia ndio mwishilio wa haja yake kwa viumbe vyake."

Anasema Ibn Al-arabi katika Futuhatil-Makkiyya J.5: "Mwenye kumtaja Mwenyezi Mungu katika kisimamo chake kukaa kwake na kulala kwake, basi amekusanya yote."

Mtakapopata amani, basi simamisheni Swala; Hakika Swala kwa Waislamu ni faradhi iliyowekewa wakati maalum.

Yaani wakati wowote vita itakapotulia na hofu ikiwaondokea basi ni juu yenu kutekeleza Swala kwa wakati wake wala msipuuze.

Tumezungumzia kuhusu Swala na jinsi uislamu ulivyoipa kipaumbele, katika Aya zilizotangulia; kama vile (2: 238- 239).

Unaweza kuuliza : Aya imewajibisha Swala ya hofu, ambapo vita vilikuwa vya panga na mikuki. Lakini hivi sasa kuna maendeleo ya silaha za vita kiasi ambacho hatufahamu katika silaha za kuangamiza, Kwa hiyo si inapasa Swala ya hofu iondolewe kwa vile maudhui yake hayapo?

Jibu : Lililosababisha Swala hii ni hofu, bila ya kuangalia vita na ala zake, ziwe za zamani au za kisasa. Kwa hiyo ikipatikana kwa sababu zisizokuwa za vita, basi imejuzu kuifupiliza Swala kwa idadi ya rakaa na kwa aina.

Mwenye Al-jawahiri anasema: "Kukiwa na hofu ya mafuriko, wanyama, nyoka, moto au mengineyo, basi inajuzu kuswali Swala ya shida ya hofu. Kwa hiyo atapunguza idadi na namna, Kwa kukosekana tofauti katika sababu ya hofu iliyoruhusiwa, Kwani aliulizwa Imam Jafar as-Sadiq(a.s) kuhusu anayehofia wanyama au wezi ataswali vipi? Akasema: "Atapiga Takbira na kuashiria."

Tunasisitiza tena kuwa Swala haiwezi kumwondokea mtu kwa hali yoyote. Na kwamba kila mtu anaitekeleza kwa namna anavyoweza katika maneno na vitendo, Akishindwa ataashiria, akishindwa kuashiria ataleta picha ya Swala moyoni mwake.

﴿وَلَا تَهِنُوا فِي ابْتِغَاءِ الْقَوْمِ إِن تَكُونُوا تَأْلَمُونَ فَإِنَّهُمْ يَأْلَمُونَ كَمَا تَأْلَمُونَ وَتَرْجُونَ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا يَرْجُونَ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴾

104.Wala msilegee katika kuwafuatia hao watu. Ikiwa mnaumia basi na wao wanaumia kama mnavyoumia nyinyi. Na nyinyi mwataraji kwa Mwenyezi Mungu ambayo wao hawayataraji. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi mwenye hekima.

MSILEGEE KATIKA KUWAFUATA

Aya 104

MAANA

Wala msilegee katika kuwafuatia hao watu, Ikiwa mnaumia basi na wao wanaumia kama mnavyoumia nyinyi. Na nyinyi mwataraji kwa Mwenyezi Mungu ambayo wao hawayataraji.

Lau kama Wahyi ungelishuka hivi sasa katika hali yetu na waisrael, basi usingezidi hata herufi moja ya Aya hii. Haja kubwa iliyopo sasa ya kupambana na adui huyu mwovu na fedhuli na kukomesha dhulma yake, ni kujifunga kib webwe na kumtegemea Mwenyezi Mungu na sisi wenyewe na kutowasikiliza wakoloni wanaotaka kutunyonya; wanaofanya propaganda ili watudanganye tuache nguvu zetu.

Kumtetemekea adui tu kunampa faida na kunamsaidia, sikwambii kumwogopa. Kwa ajili hii ndipo Mwenyezi Mungu akatukataza kumwogopa adui wa Mwenyezi Mungu na wa ubinadamu kwa hali yoyote ilivyo na itakavyokuwa; na kutuamrisha udhabiti katika kupambana naye.

Vilevile ametuzindua kuwa tunamwumiza adui, kama anavyotuumiza, lakini sisi tuko zaidi kuliko yeye, kwa sababu sisi twamwamini na kumtegemea Mwenyezi Mungu.

Ama Israel inawategemea wakoloni na ndugu zao mashetani walioitengeneza; wakawasheheni silaha na mali, wakawahimiza kufanya uchokozi na kuwasaidia katika Umoja wa mataifa na katika Baraza la usalama.

Hapana shaka yoyote kuwa kama tukijitegemea na kuwa na msimamo imara wa ikhlasi na tukafanya juhudi zetu zote, kama alivyotuamrisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, ushindi utakuwa wetu tu. Mwenyezi Mungu Mtukufu, katika Aya nyingine anasema:

﴿فَلَا تَهِنُوا وَتَدْعُوا إِلَى السَّلْمِ وَأَنتُمُ الْأَعْلَوْنَ وَاللَّـهُ مَعَكُمْ ﴾

Wala msilegee na kutaka suluhu na nyinyi ndio mko juu na Mwenyezi Mungu yuko pamoja nanyi. (47:35)

Waislamu wako juu kwa itikadi yao historia yao na uwezo wao, Nguvu hizo haziendi wala hazitakwenda bure. Kwa hiyo hapana budi kuwa athari zake zitadhihiri kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, iwe sasa au baadaye.

﴿إِنَّا أَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ لِتَحْكُمَ بَيْنَ النَّاسِ بِمَا أَرَاكَ اللَّـهُ وَلَا تَكُن لِّلْخَائِنِينَ خَصِيمًا﴾

105.Hakika tumekuteremshia Kitabu kwa haki ili upate kuhukumu baina ya watu kwa alivyokufahamisha Mwenyezi Mungu; wala usiwe mtetezi wa wenye kufanya hiyana.

﴿وَاسْتَغْفِرِ اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا﴾

106.Na muombe maghufira Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu.

﴿وَلَا تُجَادِلْ عَنِ الَّذِينَ يَخْتَانُونَ أَنفُسَهُمْ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ خَوَّانًا أَثِيمًا ﴾

107.Wala usiwatetee wale ambao wamezihini nafsi zao, Hakika Mwenyezi Mungu hampendi aliye haini mwenye dhambi.

﴿يَسْتَخْفُونَ مِنَ النَّاسِ وَلَا يَسْتَخْفُونَ مِنَ اللَّـهِ وَهُوَ مَعَهُمْ إِذْ يُبَيِّتُونَ مَا لَا يَرْضَىٰ مِنَ الْقَوْلِ وَكَانَ اللَّـهُ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطًا ﴾

108.Wanajificha kwa watu wala hawajifichi kwa Mwenyezi Mungu, na yeye yu pamoja nao walipokula njama usiku kwa maneno asiyoyapenda. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyajua vyema muyatendayo.

﴿هَا أَنتُمْ هَـٰؤُلَاءِ جَادَلْتُمْ عَنْهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فَمَن يُجَادِلُ اللَّـهَ عَنْهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَم مَّن يَكُونُ عَلَيْهِمْ وَكِيلًا ﴾

109.Nyinyi ndio ambao mnawatetea katika maisha ya duniani, basi ni nani atakayewatetea kwa Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama au ni nani watakayemtegemea?

﴿وَمَن يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ يَسْتَغْفِرِ اللَّـهَ يَجِدِ اللَّـهَ غَفُورًا رَّحِيمًا﴾

110.Na mwenye kutenda uovu au akadhulumu nafsi yake, kisha akaomba maghufira kwa Mwenyezi Mungu atamkuta Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu.

﴿وَمَن يَكْسِبْ إِثْمًا فَإِنَّمَا يَكْسِبُهُ عَلَىٰ نَفْسِهِ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴾

111.Na mwenye kuchuma dhambi, basi anajichumia mwenyewe. Na Mwenyezi Mungu ni mjuzi mwenye hekima.

﴿ وَمَن يَكْسِبْ خَطِيئَةً أَوْ إِثْمًا ثُمَّ يَرْمِ بِهِ بَرِيئًا فَقَدِ احْتَمَلَ بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴾

112.Na mwenye kuchuma kosa au dhambi, kisha akamisingizia asiye na kosa, basi hakika amejitwika dhuluma na dhambi iliyo wazi.

﴿وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكَ وَرَحْمَتُهُ لَهَمَّت طَّائِفَةٌ مِّنْهُمْ أَن يُضِلُّوكَ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّا أَنفُسَهُمْ وَمَا يَضُرُّونَكَ مِن شَيْءٍ وَأَنزَلَ اللَّـهُ عَلَيْكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمْ تَكُن تَعْلَمُ وَكَانَ فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكَ عَظِيمًا﴾

113.Na lau si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yako na rehema yake, lingedhamiria kundi katika wao kukupoteza; wala hawazipotezi ila nafsi zao; wala hawatakudhuru na lolote. Na amekuteremshia Mwenyezi Mungu Kitabu na hikima na amekufunza uliyokuwa huyajui. Na fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yako ni kubwa.

KUWATETEA WAHAINI

Aya 105 - 113

MAANA

Mwenye kufuatilia tafsir, akachunguza Aya hizi na kufikiri vizuri maana yake atakubali kuwa zilishuka kuhusiana na mwislamu mmoja aliyeiba bidhaa, akamsingizia mtu asiyekuwa na hatia; na kwamba jamaa wa mwizi walimwendea Mtume(s.a.w.w) na kujaribu kumkinaisha kwa mbinu mbalimbali wamkinge mtu wao kumwepushia janga la wizi; na kama hakufanya hivyo, basi mtu wao ataangamia.

Karibu Mtume aitikie maombi ya wapotevu hao lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimlinda mchukuzi mwaminifu wa wahyi wake na mfikishaji wa sharia yake. Akamhifadhi na njama zao na kumfichulia uhakika. Akafichuka mwizi na kusalimika yule aliyesingiziwa. Inasemekana pia kuwa aliyesingiziwa alikuwa ni myahudi na mwizi ni ansari; na kwamba yeye baada ya kufichuka alikimbia na kujiunga na washirikina. Dhahiri ya Aya inafungamana kabisa na tukio hili. Ufuatao ndio ubainifu wake:

Hakika tumekuteremshia Kitabu kwa haki ili upate kuhukumu baina ya watu kwa alivyokufahamisha Mwenyezi Mungu.

Tunasema - Tukimwomba msamaha Mwenyezi Mungu - kwamba msemo huu unatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa Mtume wake mtukufu ukiashiria aina ya lawama.

Kama kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu anamwambia: Nimekuchagua mimi mwenyewe, nikakuteremshia Qur'an ili uhukumu baina ya watu kwa lile unalojua kwa yakini kuwa ni hukumu kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Sasa wadanganyifu wamekurubia kukuhadaa, lakini Mwenyezi Mungu amekulinda na walivyokupangia - kumtia hatiani asiye na makosa - kwa kukufichulia uhakika na njama zao.

Hakuna linalofahamishwa na hali hii zaidi ya kuwa kuhifadhiwa na dhambi (Isma) si jambo la kulazimishwa; kama urefu na ufupi; isipokuwa ni wasifu unaomwepusha huyo maasum kufanya haramu, ingawaje anaweza kufanya, na kumpa msukumo wa kufanya wajibu, ingawaje anaweza kuuacha.

Aya hii ni jibu na kubatilisha kauli ya wasemao kuwa Mtume ana hukumu katika baadhi ya masuala kwa ijtihadi yake. Aya inaonyesha wazi kuwa yeye hahukumu ila kwa wahyi utokao kwa Mwenyezi Mungu. Zaidi ya hayo ni kwamba mwenye kujitahidi anapata na kukosa, na Mtume ni mwamuzi wa tofauti za wenye kujitahidi na kubainisha kosa la mwenye kukosea na usawa wa mwenye kupatia.

Wala usiwe ni mtetezi wa wenye kufanya hiyana.

Mtume hakuwatetea, na ni muhali kwa Mtume kuwatetea wanaofanya hiyana. Na kukatazwa kwake kutetea hakulazimishi kutokea hilo kwake, bali ni kwamba kukatazwa haramu kunatokea kabla ya kuifanya, Lau kungekuwa kunakuja baada ya kutokea lengo la kukatazwa basi litabatilika.

Unaweza kuuliza : Ikiwa kufanya haramu ni muhali kwa Mtume kutokana na kuhifadhiwa kwake na dhambi, kwa nini akakatazwa?

Jibu : Mwenyezi Mungu anaweza kuielekeza amri yake kwa Mtume wake katika hali zote. Kwa sababu ni amri kutoka kwa aliye juu kwenda kwa aliye chini yake. Zaidi ya hayo, ni kwamba amri ya wajibu na katazo la haramu mara nyingi huelekea kwa Mitume kwa kuelewesha hukumu tu.

Na muombe maghufira Mwenyezi Mungu, Hakika Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

Anasema Tabari katika Tafsir yake kuwa Mwenyezi Mungu amemwamrisha Mtume wake kuomba maghufira ya kusamehewa dhambi za kumtetea mhaini, Na sisi tunaomba maghufira kutokana na tafsir hii. Kwani Mtume(s.a.w.w) - kama tulivyotangulia kueleza - hakumtetea mhaini. Kwa dalili ya Aya itakayofuatia (113):

Ama amri ya kutaka maghufira ya dhambi hailazimishi kupatikana dhambi, Tafsiri ya Aya tunavyoiona ni kuwa Mtume(s.a.w.w) kwa kuwa ni mtu, anaweza akadhania vizuri jambo lisilostahiki; ikamdhihirikia hakika kwa njia ya wahyi au nyingine kabla ya kuchukua uamuzi wowote wa dhana yake nzuri. Ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha kuomba maghufira kutokana na ile dhana nzuri iliyomtokea ambayo haikuwa mahali pake. Makusudio ni kujichunga na kujitoa shakani na kutotegemea lolote ila baada ya yakini.

Wala usiwatetee wale ambao wamezihini nafsi zao, Hakika Mwenyezi Mungu hampendi aliye haini, mwenye dhambi.

Kwa dhahiri msemo unaelekezwa kwa Mtume(s.a.w.w) , lakini ulazima wake unamhusu kila aliye baleghe mwenye akili, hasa makadhi na mahakimu.

Ama waliozihini nafsi zao ni wale waliofanya dhambi na kuwasingizia watu wengine wasio na hatia; na mwenye kuwatetea basi yeye ni kama wao. Maana ya mtu kujihini yeye mwenyewe ni kujibebesha mzigo wa adhabu kwa kuharibu mambo ya wajibu na kufanya haramu.

Tumetangulia kueleza kuwa Mtume(s.a.w.w) hakutetea wala hatawatetea wahaini, na Aya hii inatilia mkazo kauli yake:Wala usiwe ni mtetezi wa wenye kufanya hiyana ; Vilevile inabainisha kuwa mwenye kumdhulumu mwingine amejidhulumu yeye mwenyewe na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu atamwadhibu kila haini, mwenye kujidhulumu na anayewadhulumu wengine.

Wanajificha kwa watu wala hawajifichi kwa Mwenyezi Mungu, naye yu pamoja nao walipokula njama usiku kwa maneno asiyoyapenda.

Mfanya makosa huficha makosa na kujificha gizani asionekane na watu kwa kutaka sifa au kuogopa shutuma zao. Ambapo ilikuwa afanye kinyume - ajifiche na Mwenyezi Mungu - kama anaweza, na wala asijishughulishe na watu kabisa. Kwa sababu Mwenyezi Mungu peke yake ndiye mwenye kumiliki madhara na manufaa.

Asiyekuwa Mwenyezi Mungu hawezi kumtosheleza binadamu na kitu chochote. Sifa za watu na shutuma zao ni maneno yanayokwenda na upepo. Ikiwa kujificha na Mwenyezi Mungu hakuwezekani, basi kumtii ni lazima, sio pendekezo.

Nyinyi ndio ambao mnawatetea katika maisha ya duniani, basi ni nani atakayewatetea kwa Mwenyezi Mungu siku ya Kiyama au ni nani watakayemtegemeea?

Msemo unaelekezwa kwa watu wa yule mwizi mhaini. Kwa sababu wao peke yao ndio waliomtetea na kumgombea.

Kwa hiyo Mwenyezi Mungu - ambaye limetukuka neno lake - amewafahamisha kuwa kumtetea mhaini hakuwezi kumfaa mhaini siku atakayofichuliwa na Mwenyezi Mungu:"Na jitengeni leo enyi waovu" (36:59)

Na mwenye kutenda uovu au akadhullumu nafsi yake, kisha akaomba maghufira kwa Mwenyezi Mungu atamkuta Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira mwenye kurehemu.

Huyo ndiye mwenye kutoka katika dhambi mwenye kuikiri na kutubia. Kama ambavyo Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni mkali wa adhabu, basi pia ni mwenye kumghufiria mwenye kutubia, mwenye kumrehemu anayekimbilia kwake.

Kuna hadith inayosema:"Hakika Mwenyezi Mungu hachoki, mpaka mchoke; mkiacha naye huacha."

Yaani mkiacha kutubia dhambi naye huacha kusamehe, Kwa hiyo la sawa kwa wale waliomtetea mwenye hatia, ni kumzindua kutokana na kosa lake na kumpa nasaha ya kutubia, kama wangelikuwa ni wanasihi waumin wa kweli.

Katika Aya hizi nne kuna maneno ambayo hapana budi kuyafafanua ili ieleweke tofauti yake ambayo kwa dhahiri inaonekana kama ni moja tu inayokaririka: Neno la kwanza ni dhambi, lilioko katika Aya ya 107, 111 na 112. La pili na la tatu ni uovu na kujidhulumu, yaliyo katika 111. La nne ni kosa, lililotajwa katika Aya ya 112.

Maneno yote haya yanakusanya maana moja ambayo ni maasi. Tofauti ni kuwa uovu ni ule unaofanyiwa mtu mwingine, kujidhulumu ni kujiingiza katika madhara kwa kuacha wajibu au kutenda haramu na kosa ni lile linalofanywa bila ya udhuru wowote; kama vile mzembe asiyejua anayekosea kutekeleza wajibu kwa kutojua ingawaje ana uwezo wa kujifundisha. Hukumu yake ni kama hukumu ya mwenye kukusudia makosa. Kwa sababu amepuuza kufanya utafiti na kuuliza.

Na dhambi ni kufanya kosa pamoja na kujua na kung'angania kulifanya. Dhambi ni ujumla inakusanya uovu na kujidhulumu. Kwa hiyo maana yanakuwa:Mwenye kutenda uovu au akadhulumu nafsi yake… mpaka mwisho " ni kuwa mwenye kumfanyia uovu mwingine kwa kumtukana au ku piga na mengineyo au kuifanyia nafsi yake tu; kama vile yamini ya uongo kisha akatubia, Mwenyezi Mungu humkubalia toba yake; kama vile hakufanya uovu wowote au kudhulumu.

Na maana ya:Mwenye kuchuma dhambi, basi anajichumia mwenyewe . Ni kwamba; mwenye kufanya dhambi, basi amejifanyia uovu mwenyewe, ni sawa awe amefanya uzembe kwa uovu huu yeye peke yake au alimfanyia mwingine.

Maana ya:Mwenye kuchuma kosa au dhambi, kisha akamsingizia asiye na kosa, basi hakika amejitwika dhuluma na dhambi iliyo wazi , ni kuwa mwenye, kumsingizia mtu mwingine kwa kosa asilokuwa nalo, ataadhibiwa adhabu ya uzushi wa makusudi; ni sawa alifanya kosa hilo akamsingizia mwingine kwa makusudi, (hilo linafahamishwa na neno 'dhambi'), au hakulifanya yeye, lakini akamsingizia mwingine kabla ya kuthibitisha, (hilo linafa- hamishwa na neno 'kosa') Lengo ni kuwa haifai kwa yeyote kumbandika mtu mwingine jambo lolote, mpaka awe na yakini nalo kama jua.

Na lau si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yako na rehema yake, lingedhamiria kundi katika wao kukupoteza; wala hawazipotezi ila nafsi zao; wala hawatakudhuru na lolote.

Makusudio ya kundi ni wale waliomtetea mwizi; na dhamiri ya katika wao inawarudia watu wake na wasaidizi wake. Makusudio ya kukupoteza ni kukuhadaa kwa maneno ya makosa na masilahi. Wala hawazipotezi ila nafsi zao, kwa sababu kujaribu kupoteza kunalazimisha upotevu; na mwenye kupoteza ni mpotevu na ziada.

Maana kwa ujumla ni kuwa kundi katika wasaidizi wa mwizi na jamaa zake, walikula njama ya kukuhadaa na haki na kujaribu uwe upande wao katika kumwokoa mtu wao nawe ulikaribia kuwakubalia kwa yale mazuri waliyokudhihirishia, lakini Mwenyezi Mungu akakuhifadhi nao; akakufichulia njama zao na kurudisha vitimbi vyao kwao.

Aya hii ni jibu la wazi kwa wale wanaodai kwamba Mtume(s.a.w.w) aliwatetea wahaini. Kwani kauli yake Mwenyezi Mungu "Na rehema yake" na "Wala hawatokudhuru na chochote," hazikubali taawili yoyote na shaka yeyote kuwa Mtume hakumtetea mwizi na mhaini. Na kwamba aliyefanya haya ni mwingine.

Na amekuteremshia Mwenyezi Mungu Kitabu na hikima na amekufunza uliyokuwa huyajui. Na fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yako ni kubwa.

Kitabu ni Qur'an na hekima ni utume. Ikiwa Mwenyezi Mungu amewajibisha Muhammad kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumfanya ni mwisho wa Mitume na bwana wa Mitume wote na kumfundisha asiyoyajua, basi ni wajibu kwa waarabu kumshukuru Muhammad kwa kuwa wamekuwa ni wenye kutajika baada ya ujinga wao wa wajinga. Vilevile wamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjaalia mtukufu zaidi wa viumbe kuwa ametokana na wao sio kwa wengine.


10

11

12

13