AKIDA

AKIDA0%

AKIDA Mwandishi:
: AMIR ALY DATOO
Kundi: Misingi mikuu ya Dini

  • Anza
  • Iliyopita
  • 4 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 3089 / Pakua: 2287
Kiwango Kiwango Kiwango
AKIDA

AKIDA

Mwandishi:
Swahili

AKIDA

MSAMIATI

Adilisha: tendea haki, wema na uadilifu.

Daawa: utangazaji wa mafundisho ya dini ya Kiislamu;

Tablighi: Uhubiri.

Mwanadaawa: mtu anayetangaza mafundisho ya dini ya Kiislamu;

Mubalighi; mhubiri.

Dhahania: mawazo.

hasi: -a kukana; -a kinyume kabisa.

Irfani: mafundisho au imani inayohusiana na maarifa ya hakika ya Mwenyezi Mungu yapatikanayo kwa njia ya mtu kujisahau nafsi yake na kumwabudu Mwenyezi Mungu tu; usufii; uwalii.

Maada: asili au dhati ya kila kitu; meta.

Maadili: (elimu inayohusiana na) tabia njema au mwenendo sahihi wa mtu; akhlak.

Hekima, kauli; fani ya utumiaji wa akili.

Maono: fikra, ufahamu au uonaji wa kimoyomoyo (wa dini moja au mfumo mmoja wa kiitikadi) juu ya ulimwengu mzima,viumbe na vitu; nadharia.

Metafizikia: elimu ihusikanayo na asili ya mwanzo wa uhai, Uungu, n.k.

Nara: matamko mafupi au mwito maalum wa kikundi cha watu, chama au dini ambao unatolewa aghlab katika medani za vita, mikutano, misafara, n.k. kwa lengo la kutia shime, kuhamasisha au kutangaza shabaha yake, n.k. Pia shaari.

Radiamali: jambo au kitendo kinachofanywa kurudia kitendo fulani kilichotendewa.

Shaari:taz.nara.

Shirki: hali ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kiumbe au kitu chochote katika ibada, uumbaji na tadbiri Yake ya ulimwengu; ushirikina.

Stadhaafika:kuwa katika hali ya kukandamizwa kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni.

Ustadhaafu: hali ya kustadhaafika.

Mustadhaafu:(wastadhaafu/mustadhaafina): mtu mwenye kukandamizwa kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni; mnyonge; mwenye kudhoofishwa au kustadhaafishwa.

Takabari (stakabari); fanya jeuri au kiburi na kuona wengine si kitu; kandamiza watu kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni. Utakabari (ustakabari): hali ya kutakabari au kustadhaafisha. Mtakabari/mstakabari (watakabari/ was-takabari): mtu mwenye kukandamiza watu kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni.

Taghuti:(ma-) kitu au kiumbe ambacho ni sababu ya uasi au uvunjaji wa sheria za Mwenyezi Mungu, k.v. miungu, masanamu, mashetani, viongozi madhalimu, utawala wa haramu, n.k.; mtu yeyote anayefuatwa bila ya idhini ya Mwenyezi Mungu; mtu anayependelea mambo yenye kukiuka mipaka (sheriaya Mwenyezi Mungu).

Tasnifu: ithibati (thesis).

Tawhidi:Umoja na Upweke wa Mwenyezi Mungu katika dhati, sifa, vitendo na ibada Zake.

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

Ndugu Msomaji ! Kitabu ulichonacho mkononi mwako kimetafsiriwa na mfasiri wetu mmoja.

Taasisi hii ya Fikra za Kiislamu imo katika jitahada za kutafsiri na kuchapisha vitabu vya maarifa na utamaduni wa Kiislamu katika lugha mbalimbali za dunia ili viwe mwongozo katika maisha ya mashaka ya ndugu zetu ambao ni viungo vya kiwiliwili kimoja cha Uislamu; na vilevile viwe ni mnara wa baharini wenye kuwamulika wasio Waislamu ambao wametweka tanga zao kukata mawimbi ya bahari ili kutafuta ukweli, au viwe kama motisho kuzidisha raghba ya msomaji. Tunataraji kwamba jitahada zetu za kidhati zitajibu maswali yanayowatatiza wasomaji wetu. Kwa hakika tumeangalia kwamba vitabu tunavyochagua kuchapishwa vimeandikwa na waandishi mashuhuri katika ulimwengu wa Kiislamu.

Huenda unaelewa kwamba utamaduni wa Kiislamu na fasihi yake umetajirika kwa maneno mahsusi na ya asili kwa sababu chemchemi yake ambayo ni Qur'ani, Kitabu cha Mwenyezi Mungu - hububujisha maneno hayo na kuufurisha. Kwa hivyo, huwa ni vigumu kuyazuia mafuriko hayo katika maziwa ya lugha nyinginezo. Inatubidi tuchimbe mifereji kadhaa ili kupunguza uzito na kuhifadhi mito. Na hilo ndilo tulilolifanya. Wakati wowote tulipoona kwamba haiwezekani kutumia neno fulani na wakati huohuo likatoa maana hasa iliyokusudiwa katika lugha ya asili ya Kiarabu na katika istilahi ya Qur'ani, hapo tukatumia neno lake laasili na kulifafanua katika ukurasa wa msamiati na istilahi. Kwa njia hii, utaelewa vizuri maudhui na ujumbe uliokusudiwa katika kitabu hicho, na kwa wakati huohuo utatajirisha msamiati wako wa Kiislamu.

Mwishowe, tunakuomba ukisome kwa makini kitabu hiki ambacho maudhui yake ni msingi muhimu na wa kwanza wa dini ya Kiislamu, nao ni Tawhidi - kumpwekesha Mwenyezi Mungu. Somo la Tawhidi linaweza kujadiliwa kwa mapana na marefu katika kila kipengee, lakini Sayyid Ali Khamenei, mwandishi wa kitabu hiki, ameashiria baadhi tu ya vipengee vya kijamii, kiuchumi na kisiasa ambavyo tunaamini kwamba havikujadiliwa vya kutosha katika mihafala ya Afrika Mashariki.

Kama kuna makosa yoyote humu ni yetu wenyewe na wala si ya mwandishi; hivyo, tunawaomba wasomaji watuonyeshe ili tuweze kusahihisha katika chapa nyingine.

Tunamwomba Mwenyezi Mungu awaunganishe Waislamu wote duniani. Amin.

TAASISI YA FIKRA ZA KIISLAMU KUHUSU MTUNGAJI

Mtungaji wa kitabu hiki, Hujjatulislam Sayyid Ali Khamenei, amezaliwa tarehe 15 julai 1939 (28 Safar 1358 Hijria) katika mji mtakatifu wa Mashhad, mashariki mwa Iran. Wazazi wake wote wawili wanatokana na koo za wanazuoni. Babake Ayatullah HaJ Sayyid Jawad Khamenei, alikuwa ni miongoni mwa wanavyuoni wachaMungu katika Mashhad.

Mamake alikuwa binti wa mwanachuoni Hujjatulislam Sayyid Hashim Najafabadi.

Akiwa na umri wa miaka minne, aliingia chuoni kusoma Qur'ani na baadaye akasoma na kumaliza shule ya msingi. Alipokuwa akisoma katika shule ya sekondari, alijiunga katika chuo cha kidini cha Nawab. Alipokuwa na umri wa miaka 18 alimaliza masomo ya kati kwa babake na wanavyuoni wengine wa Mashhad, kama vile Marehemu Haj Hashim Qazwini, Haj Sayyid Ahmad Mudarrisi na Marehemu Haj Sayyid Mahmud Damad.

Baada ya hapo, akaanza kuhudhuria darasa za kharij (darasa za juu) za Hawza (Chuo) ya Mashhad. Maustadhi wake walikuwa Marehemu Haj Hashim Qazwini na Ayatu-llah Milani.

Katika mwaka 1957, alikwenda Najaf (lraq) kwa ajili ya kuzuru maziara ya watukufu ambapo alishiriki na kufaidika na darasa za Ayatullah Sayyid Muhsin Hakim, Ayatullah Sayyid Abul Qasim Khui, Ayatullah Sayyid Mahmud Shah-rudi, Ayatullah Aqa Mirza Baqir Zanjani, Ayatullah Mirza Hasan Yazdi na Ayatullah Mirza Yahya Yazdi.

Katika mwaka 1958, aliendelea na masomo yake katika mji wa Qum (Iran) pamoja na Hujjatulislam Hashimi Rafsan-jani, Rais wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

WALIMU WAKE

Walimu wake walikuwa: Marehemu Ayatu-llah Burujerdi na Imam Khomeini ambaye wakati huo alikuwa akifundisha falsafa katika Madrasa ya Fayziyyah.

Hujjatulislam Khamenei alisomafalsafa ya Mandhumah ya Haj Mulla Hadi Sabziwari kwa Marehemu llyasi na Haj Mirza Jawad Aqa Tehrani. Alisoma kwa Marehemu Ayatullah Allamah Tabatabai faslu kadhaa za vitabu vya kifalsafa vya Asfaar na Shifaa; pia alisoma kwa Ayatullah Muntadhari sehemu ya vitabu vya kifalsafa vya Asfaar na Sharh /shaaraat.

Wakati harakati za kisiasa za maulamaa (wanavyuoni) zilipoanza katika mwaka 1962, Hujjatulislam Khamenei alikuwa miongoni mwao pia. Alishiriki katika harakati za mwaka 1963 zilizoongozwa na Imam Khomeini dhidi ya utawala wa Shah wakati askari wa Shah walipoishambulia Madrasa Fayziyyah mjini Qum. Alikamatwa akiwa na risala ya Imam Khomeini aliyomwandikia Ayatullah Milani kuhusu mauaji ya siku ya Ashura. Kwa jumla, Hujjatulislam Khame-nei alikamatwa na kutiwa ndani mara saba kati ya mwaka 1963 na 1978. Alikamatwa katika mji wa Birjand mahali ambapo Asadullah Alam, Waziri Mkuu wa Shah alipokuwa na nguvu kubwa na mahali ambapo Shah alikuwa akistarehe katika mkoa wa Khurasan. Vilevile alikamatwa katika mji wa Zanjan na akabaidishwa katika mji wa Iranshahr kwa muda mrefu.

Wakati mmoja alianzisha chama cha siri cha Kiislamu, na kilipogunduliwa akakamatwa yeye pamoja na Ayatullah Muntadhari na Marehemu Ayatullah Rabbani Shirazi. Lakini Khamenei aliweza kukimbia jela yeye pamoja na wengine, na akarejea Mashhad katika mwaka 1965. Vifungo hivyo

vya ndani na vya kuhamishwa vilimpatia uzoefu mzuri na kuimarisha harakati zake za Mapinduzi ya Kiislamu. Alitumia fursa ya kuwepo. kifungoni kwa kufasiri Qur'ani Tukufu na kufundisha maarifa ya Kiislamu pamoja na kuandika na kufasiri vitabu kadhaa. Darasa zake za tafsiri ya Qur'ani ziliwavutia sana vijana.

Katika mwaka 1978, yeye pamoja na mashekhe wanaharakati wenzake waliunda Jumuiya ya Wanavyuoni Wakakamavu.

Wakati Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Khomeini alipokuwa uhamishoni mjini Paris (Ufaransa), alimteua Hujjatul islam Khamenei kuwa ni mwanachama wa Baraza la Mapinduzi; na baada ya kuundwa serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliteuliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Mapinduzi katika jeshi, na msaidizi wa mambo ya kimapinduzi katika Wizara ya Ulinzi.

Katika mwaka 1980, Imam Khomeini alimteua Sayyid Ali Khamenei kuwa mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (Pasdar) na Imamu wa Ijumaa waTehran.

Katika uchaguzi wa kwanza wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu (Bunge), Khamenei alichaguliwa kuwa mwakilishi (mbunge) wa wakazi wa Tehran na katika mwaka huohuo, Imam Khomeini alimteua kuwa mwakilishi wake katika Baraza Kuu la Ulinzi.

Yeye ni miongoni mwa waanzilishi wa Chama cha Jamhuri ya Kiislamu (Hizbe jamhuriye Islami), na kitabu chake kiitwacho Msimamo Wetu alichokiandika pamoja na Hujjatul-islam Hashimi Rafsanjani kimetumika kuratibu sera ya chama hicho. Sasa ni Katibu Mkuu wa tatu wa chama hicho, na mchapishaji wa gazeti la chama liitwalo jamhuriye Islami.

Mnamo tarehe 27 Julai 1981, wakati Hujjatulislam Sayyid Ali Khamenei alipokuwa akitoa mawaidha baada ya kusalisha sala ya jamaa katika Msikiti wa Abu Dhar, alijeruhiwa sana kwenye mkono na kifua wakati bomu lililokuwa limetegwa na wanafiki katika tepurikoda lilipo ripuka juu ya meza aliyokuwa akihutubia.

Katika uchaguzi wa tatu wa Urais wa jamhuri ya Kiislamu ya Iran uliofanyika katika mwezi wa Oktoba 1981, Khamenei alichaguliwa kuwa Rais kwa asilimia 95 ya kura zote. Katika kipindi cha kwanza cha'miaka minne ya Urais wake, mafanikio mengi yalipatikana ingawa nchi ilikabiliwa na vita na matatizo mengi.

Katika uchaguzi wa nne wa Urais uliofanyika katika mwezi wa Agosti 1985, Hujjatulislam Khamenei alichaguliwa kwa mara ya pili kuwa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Alishinda kwa kura, 12,203,870 kati ya kura 14,244,630.

Mnamo Septemba 4, 1985, Imam Khomeini aliufawidhi (aliuthibitisha) Urais wa Sayyid Ali Khamenei, na mnamo tarehe 10 Oktoba aliapishwa katika Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu.

Rais Khamenei ni khatibu mahiri, mwandishi hodari, mwanafikra na mwanafasihi. Ameandika na kufasiri vitabu kadhaa katika uwanja wa maarifa ya Kiislamu na historia. Ametarjumi kwa lugha ya Kifarsi (Kiajemi) tafsiri ya Qur'ani ya Shahid Qutb iitwayo Fii Dhilaalil Qur'an.

Hujjatulislam Sayyid Ali Khamenei ameoa binti wa mwanachuoni mmoja katika mwaka 1964 na ana watoto wanne wa kiume na wawili wa kike.

Kwa jina la Allah, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

Siku ambayo Mtume wa Uislamu, Muhammad(s.a.w.w) , alipotangaza mwito (nara) wa : ("Hakuna mungu ila Allah") ili kuwaokoa wanadamu, watu wa kwanza waliosimama kumpinga walikuwa viongozi, wakuu na watu watukufu wa makabila. Mwanzoni, maadui hao walitumia silaha ndogo san a, yaani kumfanyia mzaha na kumtukana, lakini baadaye kila harakati ya Kitawhidi ilipozidi kuimarika na kuratibika, silaha zao pia zikawa kali zaidi. Watu wengine pia walishawishiwa na wapinzani hao, na wakasimama kumpinga na kumfanyia uhasama Mtume Mtukufu na wafuasi wake; na kwa mara nyingine tena mandhari ya kifedheha katika historia iliyokuwepo katika miaka ya kumi na mitatu kabla ya Hijria ikakaririwa.

Uhakika huu wa kihistoria unahitaji kuchunguzwa kwa makini sana kwa ajili ya kuufahamu Uislamu kwa jumla, na hasa Tawhidi ambayo ni kiini cha mafundisho ya Kiislamu.

Katika zama zetu, mojawapo kati ya mambo yenye kusikitisha sana ambalo ni msiba mkubwa kwa zama zetu, ni kupotoshwa maana halisi ya ujumbe wa Mitume wa Mwenyezi Mungu ambayo ni Tawhidi. Kupotoshwa maana ya Tawhidi ni kupotosha msingi halisi wa mafundisho ya dini, kwa sababu hakuna itikadi yoyote nyingine katika historia

nzima ambayo inaweza kwa kadiri hii kuwaokoa watu na kuwakomboa waliokandamizwa.

Kwa kadiri tunavyojua, ujumbe wote wa Mitume ulikusudiwa kuleta mabadiliko ya kimapinduzi kwa faida ya watu, kuwakomboa wanyonge na wanaokandamizwa, na kupinga udhalimu, ubaguzi na uonevu. Kiini cha maadili ya dini zote kuu, kama alivyosema Erich Fromm, ni kuthibitika malengo ya elimu, mapenzi ya kindugu, kupungua shida za watu, uhuru na hisia za majukumu. (Hapana shaka kwamba malengo yaliyo bora zaidi hayawezi kutambuliwa kwa macho ya mchunguzi wa kimaada.)

Malengo yote hayo yanategemea msingi wa Tawhidi. Kwa kupiga nara ya Tawhidi, Mitume walikuwa wakitangaza makusudio na malengo yao yote, na kwa wakati huohuo, kwa kupiga nara hiyo walikuwa wakiandalia mapambano kwa ajili ya kutekeleza malengo hayo katika dunia au kuyakaribia.

Kwa hakika ni jambo la kusikitisha sana, si tu kwa wenye kuitakidi Tawhidi, bali hata kwa wale wote wenye kuyapigania malengo hayo, kuona kwamba katika zama hizi wakati ambapo malengo hayo huhitajika kwa haraka na kwa dharura zaidi - kuna ujinga na upotoshi wa msingi.na maana ya Tawhidi, na kwamba watu hutosheka na tafsiri yake ya juujuu na ya kimawazo tu.

Tumesema kwamba mkabala na upinzani uliokuwepo mwanzoni mwa Uislamu unaweza kufafanua uhakika muhimu wa maana halisi ya Tawhidi.

Uhakika wenyewe ni huu, kwamba shaari (nara) ya Laa ilaaha illallaah - ("Hakuna mungu ila Allah"), kwa hatua ya kwanza, ni pigo zito kwa walewale watu ambao wali-simama kuipinga, yaani tabaka la wenye mamlaka na utawala katika jamii.

Vitendo vya uhasama dhidi ya fikra moja na harakati moja, vinabainisha misimamo yake ya kijamii, kiwango na kina cha taathira zake katika misimamo hiyo. Kwa njia hii, tunaweza kujua misrmamo ya kitabaka na ya kijamii ya harakati hizo kwa kusoma nyuso za maadui wa harakati hizo. Vilevile tunaweza kupima kina na taathira za harakati hizo kwa kuangalia ushadidi na ukali wa upinzani wao.

Kwa sababu hii, njia mojawapo inayoaminika kutumiwa kwa ajili ya kutambua barabara daawa za Mitume, ni kuzichunguza safu za waungao mkono na safu za wapingao harakati hizi.

Tunapoona kwamba tabaka la wenye nguvu na mamlaka katika jamii ni watu wa kwanza waliosimama kupinga dini bila ya kusita hata kidogo katika upinzani wao, hapo ndipo tunapotambua waziwazi kwamba kwa kawaida dini na harakati za kidini zinapinga tabaka hilo. Kimsingi, Mitume walikuwa wakipinga ujeuri na ubepari wao, na nafsi ya tabaka lenyewe ambalo lilikuwa likijitenga mbali na wengine.

lli tuweze kuzingatia suala la Tawhidi katika kipengee hiki cha kuupinga utawala wa kitabaka katika jamii, ni lazima kwanza tujue kwamba kinyume na vile inavyodhaniwa na watu wa kawaida, Tawhidi si nadharia ya kifalsafa na kidhahania peke yake, bali ni nadharia ya kimsingi kuhusu binadamu na ulimwengu, na ni itikadi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa pia.

Miongoni mwa istilahi za kidini na zisizo za kidini, ni taabu sana kupata istilahi kama hii iliyojaa maana ya kimapinduzi na kiurekibishaji yenye kuzingatia vipengee mbalimbali vya kimaisha, kijamii na kihistoira vya binadamu. Haikuwa sadfa kwamba miito yote ya Mitume wa Mwenyezi Mungu katika historia nzima ilianzia kwa kutangazwa Upweke na Umoja wa Mwenyezi Mungu na umilikaji Wake Peke Yake.

Ifuatayo ni muhtasari wa vipengee mbalimbali vya maudhui ya Tawhidi:

1) Tawhidi katika Kipengee cha Nadharia juu ya Ulimwengu na Maisha

a) Tawhidi maana yake ni umoja na ufungamano wa ulimwengu mzima na vitu vyote vilivyomo humo.

llivyokuwa mfumo wa uumbaji ni mmoja, na kila kitu kimeanza na kutokana na chanzo na asili moja bila ya kuwepo miungu na waumba wengi tofauti; hivyo, vitu vyote hivyo vinaingia katika mkusanyiko na mfumo mmoja,na ulimwengu mzima ni mmoja, na wote una mwelekeo mmoja.

مَّا تَرَىٰ فِي خَلْقِ الرَّحْمَـٰنِ مِن تَفَاوُتٍ

"Huoni hitilafu yoyote kati'ka uumbaji wa Mwingi wa rehema." (alMulk, 67:3)

أَوَلَمْ يَتَفَكَّرُوا فِي أَنفُسِهِم مَّا خَلَقَ اللَّـهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَأَجَلٍ مُّسَمًّى

"Je, hawatafakari juu ya nafsl zao? Allah hakuumba mbingu na ardhl, na vlllvyomo baina yao ila kwa [mfumo wa] haki na kwa muda maalum. "(ar-Rum, 30:8).

Kufuatana na mtazamo huu, ulimwengu huonekana kama msafara mmoja ambao wasafiri wake wote hufanya kazi kwa pamoja kuelekea kwenye mahali na lengo moja kama mnyororo ulioshikamanishwa pamoja kwa vikuku na kama vipande vidogo na vikubwa vya mashine. Kila kitu katika mfumo huo hufanya kazi kufuatana na hali na nafasi yake, maana na sababu iliyowekewa. Hivyo, katika mwendo huu wa ukamilifu, kila kitu hukisaidia na kukikamilisha kitu kingine, na vyote ni vitu vya lazima katika mjumuiko huo. Kusimama, kuharibika, kupanguka au kwenda kombo kimojawapo katika vitu hivyo kutasababisha kuharibika, kuparaganyika na kwenda kombo mfumo mzima. Kwa hivyo, ufungamano halisi na wa kiroho wa mfumo

mmoja ndio unao unganisha vitu vyote hivyo.

b) Tawhidi maana yake ni kuwepo shabaha katika uumbaji. Ulimwengu umeumbwa kwa mpango, hesabu na utaratibu maalum; na kila kitu chake kina maana na roho (dhati) pia. llivyokuwa ulimwengu umeumbwa na Muumba Mwenye hekima, hivyo, ni lazima kuwepo hekima, lengo na shabaha katika asili ya kuumbwa kwake kama inavyoonekana katika vitu vingi vya hapa ulimwenguni.

وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاءَ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ ﴿١٦﴾

"Nu hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yao kwa mchezo [na bila shabaha]." (al-Am- biyaa, 21:16)

Kwa mtazamo huu, hakuna kitu chochote katika ulimwengu kilichoumbwa bila ya kuwa na shabaha au maana yoyote, bali mfano wake ni kama mashine iliyotengenezwa kwa ajili ya kufanya kazi maalum. Tunaweza kuuliza kuhusu shabaha yake, lakini hatuwezi kuuliza kuhusu asili ya shabaha hiyo. Mfano wake ni kama shairi moja la maana ambalo unaweza kulifahamu kwa kuzingatia maana yake, lakini huwezi kulifahamu kwa kutegemea sauti au mizani yake tu.

c) Tawhidi maana yake kubwa zaidi ni kunyenyekea vitu na viumbe vyote vya ulimwengu mbele ya Mwenyezi Mungu. Hakuna kitu chochote katika mkusanyiko huo chenye hiari yake yenyewe. Kanuni zote za ulimwengu (maumbile) na kila kitu kinachofuata kanuni hizo ni lazima kitii, kijitolee na kisalimu amri kwa Mwenyezi Mungu tu.

Kwa hivyo, kuwepo kanuni za kimaumbile katika ulimwengu mzima hakumaanishi kwamba hakuna Mwenyezi Mungu na Muumba wa ulimwengu.

إِن كُلُّ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ إِلَّا آتِي الرَّحْمَـٰنِ عَبْدًا ﴿٩٣﴾

"Hakuna yeyote aliyemo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Mwingi wa rehema hali ni mtumwa." (Maryam, 19:93)

بَل لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ كُلٌّ لَّهُ قَانِتُونَ ﴿١١٦﴾

"Bali ni vyake vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Vyote vinamnyenyekea Yeye." (al-Bagarah, 2:116)

وَمَا قَدَرُوا اللَّـهَ حَقَّ قَدْرِهِ وَالْأَرْضُ جَمِيعًا قَبْضَتُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَالسَّمَاوَاتُ مَطْوِيَّاتٌ بِيَمِينِهِ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَىٰ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٦٧﴾

"Hawakumheshimu Allah heshima anayostahiki, na (katika) Sfku ya Kiyama ataidhibiti ardhi yote, na mbingu zitakunjwa kwa uwezo Wake. Ameepukana na upungufu na Yu mbali na yale wanayomshirlkishiya." (az-Zumar, 39:67)

2) Tawhidi katika Kipengere cha Uchunguzi na Uamuzi kuhusu Binadamu

a) Tawhidi maana yake ni kwamba: wanadamu wote ni wamoja na ni sawa katika kuhusiana na Mwenyezi Mungu. Yeye ni Mola wa wanadamu wote. Hakuna mtu aliyekuwa na uhusiano mahsusi na Mwenyezi Mungu kwa sababu ya umbile lake la kibinadamu tu, wala hakuna mwenye ujamaa Naye. Yeye si Mungu wa taifa, umma au kabila fulani. Hakuumba wala hakufadhilisha jamii moja kuliko nyingine. Wote ni sawa mbele ya Mwenyezi Mungu. Hakuna mtu mwenye utukufu mahsusi mbele ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kutokana na jitahada zake. Kila mtu anaweza kupata utukufu na fadhila zaMwenyezj Mungu akijitahidi zaidi kutoa huduma njema kwa wanadamu na kwa kutekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu ambayo ni dhamana ya pekee ya kumtukuza binadamu.

وَقَالُوا اتَّخَذَ اللَّـهُ وَلَدًا سُبْحَانَهُ بَل لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ كُلٌّ لَّهُ قَانِتُونَ ﴿١١٦﴾

"Wanasema 'Allah amejipangia mwana.' Ameepukana na hilo; bali ni Vyake vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Vyote vina mnyenyekea Yeye. " (al-Baqa-rah, 2:116)

فَمَن يَعْمَلْ مِنَ الصَّالِحَاتِ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَا كُفْرَانَ لِسَعْيِهِ وَإِنَّا لَهُ كَاتِبُونَ ﴿٩٤﴾

"Na atakayefanya vitendo vizuri na hali ni muumini, bas/ haitokataliwa juhudi yake; na kwa hakika Sisi tutamwandiki'a." (al-Ambiyaa, 21:94)

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ﴿١٣﴾

"Enyi watu! Kwa hakika tumekuunbeni nyote kutokana na mwanamume na mwanamke, na tumekufanyeni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika anae heshimiwa sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule anayemcha Mungu zaidi katika nyinyi." (al-Hujaraat, 49:13).

b) Tawhidi maana yake ni kwamba wanadamu wote ni wamoja na ni sawa katika kuumbwa kwao na katika asili yao ya ubinadamu. Ubinadamu ni asili moja inayopatikana katika wanadamu wote bila ya kutofautiana. Wanadamu waliogawika katika matabaka mbalimbali ya kijamii si waja wala viumbe wa waungu mbalimbali hata asili na maumbile yao yakatofautiana pia, na matokeo yake ukakuwepo mpaka usiovukika baina yao. Wala hakuna mungu wa tabaka aali (tukufu) aliyekuwa na nguvu zaidi kuliko mungu wa tabaka la chini. Wote ni viumbe wa Mwenyezi Mungu Mmoja, na wote wameumbwa sawa katika maumbile yao ya asili.

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ ...﴿١﴾

"Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi aliye kuumbeni kutokana na nafsi moja..." (an-Nisaa, 4:1)

c) Tawhidi maana yake ni kwamba wanadamu wote ni sawa na wamoja katika kuweza kujiendeleza na kujikamilisha. Wanadamu wote ni sawa katika asili na maumbile yao ya kibinadamu. llivyokuwa Mwenyezi Mungu Mwenye hekima amempa kila mtu umbile la kibinadamu, hivyo, hakuna mtu yeyote asiyekuwa na uwezo katika dhati na umbile lake wa kufuata njia iliyonyooka na njia ya kujikamilisha. Kwa sababu hii ndiyo maana mwito wa Mwenyezi Mungu ukawa ni kwa watu wote bila ya kuwa ni mahsusi kwa watu, taifa au tabaka fulani. Ingawa mazingira tofauti yanaleta athari tofauti kwa binadamu, lakini athari hasi za mazingira haziwezi kabisa kumfanya binadamu daima awe shetani au malaika, au kumfungia njia ya kujiamulia yeye mwenyewe. Qur'ani inamhutubu hivi Mtume Mtukufu:

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢٨﴾

"Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mbashiri, na mwonyaji. Lakini watu wengi hawajui." (Sabaa, 34:28)

"Na tumekutuma kwa watu wote kuwa Mtume." (an-Nisaa, 4:79)

يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَكُم بُرْهَانٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَأَنزَلْنَا إِلَيْكُمْ نُورًا مُّبِينًا ﴿١٧٤﴾ فَأَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَاعْتَصَمُوا بِهِ فَسَيُدْخِلُهُمْ فِي رَحْمَةٍ مِّنْهُ وَفَضْلٍ وَيَهْدِيهِمْ إِلَيْهِ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا ﴿١٧٥﴾

"Enyi watu! Umekufikieni ushahidi kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na tumekuteremshieni Nuru iliyo wazi. Ama wale walio muamini Mwenyezi Mungu, na wakashikamana naye, basi atawatia katika rehema yake na fadhila, na atawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka." (An-Nisaa, 174 - 175)

d) Tawhidi maana yake ni kuwakomboa wanadamu wote kutoka katika utumwa n.a unyenyekevu wa yeyote asiyekuwa Mwenyezi Mungu, na kwa maana nyingine ni ulazima (wajibu) wa kumwabudu Mwenyezi Mungu tu. Tawhidi inapinga mwanadamu kuingia katika utumwa na utiifu usiokuwa wa Mwenyezi Mungu. Kwa kuzingatia maana pana ya ibada, utumwa huo unaweza kuwa ni wa kifikra, kitamaduni, kiuchumi au kisiasa. Tawhidi inakataza kuishi maisha kama haya ya kujichukulia mtu mwingine kuwa ni mshirika na sawa katika ibada ya Mwenyezi Mungu. Tawhidi humchukulia binadamu kuwa ni mja wa Mwenyezi Mungu tu, na humkomboa kutoka katika utumwa na utiifu wa kila mtu, mfumo au nguvu yoyote ambayo humfanya amshirikishe katika ibada ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo, Tawhidi maana yake ni kukubali utawala wa Mwenyezi Mungu tu na kukana na kupinga utawala wowote mwingine usiokuwa wa Mwenyezi Mungu, uwe na sura au umbo la aina yoyote.

إِنِ الْحُكْمُ إِلَّا لِلَّـهِ أَمَرَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٤٠﴾

"Hapana hukumu ila ya Mwenyezi Mungu tu. Yeye ameamrisha msimuabudu yeyote isipo kuwa Yeye tu. Hiyo ndiyo Dini Iliyo Nyooka. Lakini watu wengi hawajui." (Yusuf, 12:40)

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ ﴿٢٣﴾

"Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu...." (al-lsraa, 17:23).

e) Tawhidi maana yake ni kumheshimu na kumthamini binadamu. Umbile tukufu na la fahari la binadamu lina thamani zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu na wala halina haja ya kufanywa mnyonge, dhalili au mtumwa mbele ya yeyote ghairi ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu tu Mwenye ukamilifu na jamala mutlaki Ndiye Ambaye anastahiki kuabudiwa na binadamu, kusifiwa na kupendwa. Kutukuza huko ni daraja moja ya mja kupata utukufu.Ghairi ya Dhati Takatifu hakuna kitu wala kiumbe chochote chenye utukufu na hadhi ambayo kwayo inamstahikisha amfanye binadamu kuwa mtumwa wake. Masanamu yote yenye uhai na yasiyo

na uhai ambayo yamejipachika katika fikra, moyo na kiwiliwili cha binadamu na yamechukua kwa nguvu utawala wa Mwenyezi Mungu katika maisha ya binadamu, ni najisi na uchafu unaochafua usafi wa umbile la binadamu. Masanamu hayo humletea binadamu madhila na uduni, hivyo, inambidi ayaangamize na ayasafishe katika ibada yake ili apate kurejesha hadhi yake tukufu. Hakuna mawazo yoyote ya kimaada ya binadamu yaliyoweza kujadili kwa undani na ufasaha utukufu na thamani ya binadamu, kamaTawhidi inavyojadili.

فَاجْتَنِبُوا الرِّجْسَ مِنَ الْأَوْثَانِ وَاجْتَنِبُوا قَوْلَ الزُّورِ ﴿٣٠﴾حُنَفَاءَ لِلَّـهِ غَيْرَ مُشْرِكِينَ بِهِ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَكَأَنَّمَا خَرَّ مِنَ السَّمَاءِ فَتَخْطَفُهُ الطَّيْرُ أَوْ تَهْوِي بِهِ الرِّيحُ فِي مَكَانٍ سَحِيقٍ ﴿٣١﴾

"Basi jiepusheni na uchafu wa masanamu na maneno ya uwongo; mhalisike kwa Allah bila kumshirikisha. Na anae mshirikisha Allah basi ni kana kwamba ameanguka kutoka mbinguni k'isha ndege [tai] wakamnyakua au upepo umemtupa mahali pa mbali." (al-Hajj, 22:30, 31)

لَّا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَقْعُدَ مَذْمُومًا مَّخْذُولًا ﴿٢٢﴾

"Usimfanye mungu mwingine pamoja na Allah, usije ukawa mwenye kushutumiwa (na) kutupwa." (al-lsraa, 17:22)

ذَٰلِكَ مِمَّا أَوْحَىٰ إِلَيْكَ رَبُّكَ مِنَ الْحِكْمَةِ وَلَا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتُلْقَىٰ فِي جَهَنَّمَ مَلُومًا مَّدْحُورًا ﴿٣٩﴾

"Wala usimfanye mungu mwingine pamoja na Allah, usije kutupwa katika jahannam hali ya kuwa mwenye kulaumiwa (na) mwenye kufukuzwa." (al-lsraa, 17:39)

f) Tawhidi maana yake ni ulinganifu na umoja baina ya maisha ya binadamu na kuwepo kwake. Maisha ya binadamu yamefanyika kwa dhamiri na uhakika, fikra na amali (matendo). Ikiwa kimojawapo kati ya vitu viwili hivo, au sehemu moja yake itaathiriwa na nguvu zilizo kinyume cha Uungu kama vile dhamiri ya kumwamini Mungu kuambatana na uhakika usiokuwa wa Kiungu, au uhakika wa kumpenda Mungu kuambatana na moyo wa kutomjua Mungu basi matokeo yake yatakuwa ni kupatikana hali mbili zinazopingana katika maisha ya binadamu na kufanyika shirki (ushirikina) katika kumwabudu Mwenyezi Mungu. Katika hali kama hiyo, binadamu huwa kama akrabu ya dira ambayo huelekea sehemu nyingine kwa sababu ya kuvutwa na uvutano usio wa kawaida, hivyo, kama haitoelekea kwenye ncha ya kawaida itaharibika. Kwa hivyo, ikiwa binadamu atapotoka kwenye njia iliyonyooka na mwelekeo ulio sawa ambao ni umbile aliloumbiwa, basi atapotoka kwenye njia ya Mwenyezi Mungu.

أَفَتُؤْمِنُونَ بِبَعْضِ الْكِتَابِ وَتَكْفُرُونَ بِبَعْضٍ فَمَا جَزَاءُ مَن يَفْعَلُ ذَٰلِكَ مِنكُمْ إِلَّا خِزْيٌ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يُرَدُّونَ إِلَىٰ أَشَدِّ الْعَذَابِ ...﴿٨٥﴾

"Je, mnaamini baadhi ya Kitabu [maarifa na maam-risho ya dini] na kuyakataa mengine? Basi' hakuna malipo kwa mwenye kufanya hivyo kati'ka nyinyi ila fedheha katika maisha ya dunia, na Si'ku ya Kiyama watarudishwa kwenye adhabu kali kabisa. " (Al-Baqa-rah, 2:85)

g) Tawhidi maana yake ni kwenda sambamba binadamu na mazingira yake ya ulimwengu. Upana usio na kikomo wa ulimwengu ni uwanja wa amali na radiamali zisizohesabika za kanuni za ulimwengu. Hakuna tukio au jambo lolote, liwe dogo vipi, ambalo linaweza kuepukana na kanuni hizo. Kutokana na ulingano, utaratibu na umoja wa kanuni za ulimwengu ndipo unapopatikana mfumo wenye utaratibu na umoja katika ulimwengu. Binadamu ni sehemu moja ya mfumo huo, hivyo, yeye pia hutawaliwa na kanuni hizo za kawaida pamoja na kanuni maalum ambazo zinakwenda

sambamba na kanuni nyinginezo.

Lakini binadamu, kinyume cha viumbe vinginevyo ambavyo vinalazimika kufuata maumbile bila ya kuwa na hiari yoyote, ana uwezo wa kuchagua na kujiamulia mwenyewe. Inambidi binadamu achague njia ya asili na ya umbile lake ambayo ndiyo njia inayomnyanyua, kumwendeleza na kumkamilisha. Hii pia ina maana kwamba ana uwezo wa kwenda kinyume na njia hiyo ya umbile (fikra).

"Basi anayetaka aamini, na anayetaka akufuru ." (al-Kahf, 18:29)

Tawhidi humtaka binadamu afuate njia ya kiasili na ya kimaumbile ambayo pia inafuatwa na ulimwengu mzima. Binadamu akiwa ni kiungo muhimu katika ulimwengu, hujitahidi kujiunganisha na kujiambatanisha na viungo vingine vya ulimwengu ili upatikane umoja na ufungamano kamili kati ya binadamu na ulimwengu.

أَفَغَيْرَ دِينِ اللَّـهِ يَبْغُونَ وَلَهُ أَسْلَمَ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ طَوْعًا وَكَرْهًا وَإِلَيْهِ يُرْجَعُونَ ﴿٨٣﴾

"Je, wanataka dini ghairi ya Allah na hali kila kilichomo mbinguni na ardhini kinamtii Yeye kwa upendo au karaha, na Kwake watarejeshwa?" (Aali 'lmraan, 3:83)

أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ يَسْجُدُ لَهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَمَن فِي الْأَرْضِ وَالشَّمْسُ وَالْقَمَرُ وَالنُّجُومُ وَالْجِبَالُ وَالشَّجَرُ وَالدَّوَابُّ وَكَثِيرٌ مِّنَ النَّاسِ ...﴿١٨﴾

"Je, huoni kwamba kinamsujudia Allah kila kilichomo mbinguni na kllicbomo ardhini, na jua na mwezi na nyota na milima na miti na wanyama na miongoni rnwa watu walio wengi?" (al-Hajj, 22:18)

3 ) Tawhidi katika Kipengee cha Sera ya Kijamii, Kiuchumi na Kisiasa

a) Tawhidi maana yake ni kwamba hakuna mtu yeyote ghairi ya Mwenyezi Mungu anayefaa peke yake kupanga na kuamua mambo ya ulimwengu na binadamu. Hii ni haki ya Mwenyezi Mungu tu Ambaye Ndiye Muumba wa binadamu na ulimwengu na Mratibu wa vitu vyake vyote. Yeye tu anajua uwezo na mahitaji yao yote. Kwa hakika, Yeye tu hujua kwa ukamilifu nguvu, uwezo na nishati zilizomo katika kiwiliwili na roho ya binadamu, na vilevile hazina zisizohesabika katika ulimwengu, kadiri na matumizi yake na vipi kuvisawazisha.

Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu Peke Yake tu Ndiye anayeweza kuratibu ratiba ya maisha ya binadamu na sera ya uhusiano wake katika mfumo wa ulimwengu. Yeye tu anaweza kupanga mifumo ya kisheria na kijamii katika maisha ya binadamu.

Haki hii ya pekee ya Mwenyenzi Mungu inatokana na uhakika huu wa kiasili na kimantiki kwamba Yeye ni Muumba. Kwa hivyo, aina yoyote ya uingiliaji katika kuamua sera ya kimatendo ya wanadamu utakaotokana na wengine, utakuwa ni sawa na kuingilia utawala wa Mwenyezi Mungu na kudai Uungu, na huko kutachukuliwa kuwa ni shirki.

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٦٥﴾

"La! Naapa kwa Mola wako Mlezi! Hawataamini mpaka wakufanye wewe ndiye muamuzi katika yale wanayo khitalifiana, kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu ya hukumu utayo toa, na wanyenykee kabisa." (an-Nisaa, 4:65)

وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّـهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا ﴿٣٦﴾

"Haiwi kwa Muumini mwanamume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika jambo, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapo kata shauri katika jambo lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi hakika amepotea upotofu ulio wazi. " (al-Ahzaab, 33:36)