MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE 14%

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE Mwandishi:
: SALMANI SHOU
Kundi: Misingi mikuu ya Dini

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE
  • Anza
  • Iliyopita
  • 28 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 29966 / Pakua: 4222
Kiwango Kiwango Kiwango
MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

Mwandishi:
Swahili

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

KIMEANDIKWA NA

SAYYID MUJTABAA MUUSAWIY LARI

KUHUSU MWANDISHI

Sayyid Mujtaba Mussawi Lari ni mtoto wa marehemu Ayatullah Sayyid Ali Asghar Lari mmojawapo wa wanachuoni na watu mashuhuri katika jamii ya Iran. Babu yake alikuwa marehemu Ayatullah Hajj Sayyid Abd ul- Husayn Lari ambaye alipigania uhuru wakati wa mapinduzi ya kikatiba. Wakati wa kipindi kirefu cha mapambano yake dhidi ya serikali dhalimu ya wakati huo, alijaribu kuanzisha serikali ya Kiislamu na alifaulu kufany hivyo kwa kipindi kifupi huko Larestan.

Sayyid Mujtaba Musawi Lari alizaliwa mwaka 13/4/1935 kwenye jiji la Lar ambako alihitimu elimu yake ya Msingi na masomo ya mwanzo ya Kiislamu. Mnamo mwaka wa 1332/1953, aliondoka Lar na akaenda Qum kuendelea na masomo yake ya elimu ya Kiislamu, akiwa anafundishwa na maprofesa na waalimu wa taasisi ya Kidini, pamoja na wanazuoni wakuu katika maarifa ya sheria (maraji).

Mnamo mwaka wa 1341/ 1962, akawa mshiriki katika Maktabil-Islam, gazeti la kidini na kisayansi lililokuwa lianaandika mfululizo wa makala kuhusu maadili ya Kiislamu. Makala hizi baadaye zilikusanywa na kuchapishwa kitabu kilichoitwa Ethical and psychological Problems. Matoleo tisa katika kitabu hiki kwa lugha ya kiajemi (Fursi) yamechapishwa, na pia kimetafsiriwa katika lugha ya Kiarabu na hivi karibuni kwa Kifaransa.

Mnamo mwaka 1342/1963. Alisafiri kwenda Ujerumani kutibiwa, na alirudi Iran baada ya miezi kadhaa, aliandika kitabu kiitwacho 'The face of Western Civilization'. Kitabu hiki kinajumuisha mazungumzo ya kulinganisha ustaarabu wa Kimagharibi na Kiisilamu, ndani ya kitabu hiki, mwandishi anataka kuthibitisha, kwa njia ya utambuzi, kifikira na ulinganisho kamili, ubora wa utambuzi na mambo mengi ya ustaarabu wa Uislamu kwa ule wa Magharibi. Kitabu hiki hivi karibuni tu kimechapishwa tena kwa mara ya saba. Mnamo 1349/1970, kitabu hiki kilitafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza na mtaalam wa mambo ya nchi za Mashariki, F.G. Goulding, na kilichochea hisia za watu huko Ulaya. Makala kuhusu kitabu hiki zilionekana kwenye magazeti kadhaa ya kimagharibi na BBC ilifanya mpango wa mahojiano na mtarjumi huyo ambapo sababu za kutafsiri na jinsi kilivyopelekwa hapo Uingereza zilizungumziwa. Tafsiri ya Kiingereza ya kitabu hiki hadi sasa imechapishwa mara tatu huko Uingereza, mara tano Iran na mara mbili Marekani.

Mnamo takriban miaka mitatu baada ya kuchapishwa tafsiri ya Kiingereza, Rudolf Singler, profesa wa chuo Kikuu wa Kijerumani alikitafsiri katika lugha ya Kijerumani, na tafsiri hiyo ilithibitisha kuwa yenye kuvutia huko Ujerumani. Mmojawapo wa viongozi wa chama cha Social Democratic Party alimtaarifu Mtarjumi katika barua kwamba kitabu hicho kimeacha mvuto wa kina juu yake yeye, na kusababisha yeye kubadilisha maoni yake kuhusu Uislamu, na kwamba angelipendekeza Kitabu hicho kisomwe na marafiki zake. Tarjuma ya lugha ya Kijerumani imerudiwa kuchapishwa mara tatu hadi sasa.

Tafsiri za Kiingereza na Kijerumani za kitabu hiki zilichapishwa na Wizara ya Mwongozo wa Kiislamu kwa ajili kuisambaza zaidi nje ya Iran kupitia Wizara ya mambo ya Nje na taasisi ya mafunzo ya Kiislamic nchi za nje. Wakati huo huo ilipochapishwa tafsiri ya kwanza ya lugha ya Kijerumani, mwanachuo Muislamu wa asili ya kihindi aitwaye Maulana Raushan Ali alikitarjumi kitabu hiki katika lugha ya Urdu kwa lengo la kukisambaza India na Pakistani. Tarjumi hii ya Urdu imechapishwa mara tano hadi sasa. Sayyid Mujtaba Musawi Lari pia ameandika kijarida kuhusu Tawhid (upweke wa Mwenyezi Mungu), ambacho kilitafsiriwa Uingereza na kuchapishwa mara kadhaa Marekani.

Mnamo mwaka 1343/1964, aliasisi taasisi ya kutoa msaada huko Lar kwa madhumuni ya kueneza Uislamu, kutoa mafunzo ya Kiislamu kwa vijana walioko vijijini, na kuwasaidia wasiojiweza. Taasisi hii iliendelea kufanya kazi hadi 1346/1967. Taasisi hii ilitekeleza mambo makuu kama kuwapeleka wanafunzi wa sayansi za Kidini vijijini kufundisha Uislamu kwa watoto na vijana, kuwagawia maelfu ya watoto wa shule nguo, vitabu, vifaa vya kuandikia, kujenga idadi ya misikiti, mashule, zahanati mijini na vijijini, na huduma nyingine nyingi.

Sayyid Mujtaba Musawi Lari aliyaandama matakwa yake katika maadili ya Kiislamu, akiandika makala mpya kuhusu somo hilo. Mnamo mwaka wa 1353/1974, mkusanyiko wa makala hizi, zilizopitiwa upya na kuongezewa maneno, zilitoka katika muundo wa kitabu kilichoitwa 'The Function of Ethics in Human Development.' Kitabu hiki kimechapishwa mara sita hadi sasa.

Mnamo mwaka 1357/1978, alisafiri hadi Marekani kwa mwaliko wa Taasisi ya Kiislamu nchini humo. Halafu akaenda Uingereza, Ufaransa na baada ya kurudi Iran alianza kuandika mfululizo wa makala kuhusu itikadi za Uislamu kwa ajili ya gazeti la Sorouch. Makala hizi baadaye zilikusanywa na kutengenezwa kitabu chenye juzuu nne kuhusu imani za misingi za Uislamu (tauhid, uadilifu wa Mwenyezi Mungu, utume, uimamui, na ufufuo) kwa jina la 'The Foundations of Islamic Doctrine.' Kitabu hiki chenye juzuu nne kimetafsiriwa katika lugha ya Kiarabu, sehemu zake zingine zikiwa tayari zimekwisha chapishwa mara tatu. Tafsiri ya Kiingereza ya juzuu ya kwanza ya kazi hii ndio imetengeneza kitabu hiki cha sasa; juzuu zilizosalia pia zitatafsiriwa na kuchapishwa. Tafsiri za Urdu, Hindi na Kifaransa pia zimo katika mpango wa kutayarishwa; juzuu mbili za lugha ya Kifaransa zimekwishatokea.

Mnamo mwaka wa 1359/1980, Sayyid Mujtaba Musawi Lari aliasisi Taasisi huko Qum iitwayo 'Office for The Diffusion of Islamic Culture Abroad.' Husambaza bure nakala za vitabu vyake vilivyotafsiriwa kwa watu wapendao kuzisoma duniani pote. Taasisi hii pia imechukua shughuli ya kuchapisha Qur'ani kwa lengo la kuisambaza kwa Waislamu binafsi, Taasisi na shule za Kidini hapa Afrika.

NENO LA MCHAPISHAJI

Kitabu kilichoko mikononi mwako, ni tarjuma ya kitabu cha Kiingereza, kwa jina la: "God and His Attributes." Sisi tumekiita: "Mwenyezi Mungu na Sifa Zake." Kitabu hiki, "Mwenyezi Mungu na Sifa Zake" ni kazi ya kielimu iliyofanywa na Mwanachuoni mahiri, Sayyid Mujtaba Musawi Lari. Mwandishi wa kitabu hiki ameichambua itikadi ya Kiislamu na Umoja wa Mungu (tawhid) kwa kutumia uhojaji wa kifilosofia na maneno mepesi. Ili kukamilisha kazi yake hii ametegemea sana juu ya Sunna na nukuu nyingi kutoka kwenye Qur'an Tukufu.

Kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote. Kutokana na ukweli huu, Taasisi yetu ya 'Al-Itrah Foundation' imeona ikitoe kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yale yale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili, ili kuongeza ujuzi wao katika masuala ya dini na ya kijamii.

Tunamshukuru ndugu yetu, Salman Shou kwa kukubali jukumu hili la kukifanyia tarjuma kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki.

Mchapishaji:

Al-Itrah Foundation

S. L. P. 19701

Dar-es-Salaam, Tanzania.

UTANGULIZI

Ombwe la kielimu na kiitikadi linazidi kumsogeza mwanadamu mbali na utambuzi wa ukweli kuelekea kwenye dimbwi la upotovu. Leo tunashuhudia nguvu nyingi za ubunifu wa mwanadamu zikipotea bure pale anapofumbia macho ile bahari yenye utajiri na mawimbi ya utamaduni na fikra ambayo dini inaitengeneza na vile anavyoyaruhusu maisha yake ya kisomi kunyongwa na itikadi za dunia ya kisasa.

Leo, mawazo mbali mbali yanawasilishwa kwenye kizazi cha wakati wetu chenye kiu na ambacho kimechanganyikiwa, mawazo ambayo yanatokana na dhana potovu za juu juu za wanafalsafa na wanazuoni wenye peo finyu. Mawazo haya yanajifanya kujaribu kujibu mahitaji ya kizazi cha sasa, lakini hayapendekezi maana yoyote au lengo la maisha. Muundo wa mwelekeo mmoja wa fikira ambao ndio msingi wa mawazo haya sio malezi yanayofaa kwa ajili ya akili nyeti za zama zetu hizi, na wala haustahili hata kufikiriwa katika mazingira yoyote yale ambamo akili na busara bado vinakuwa na mshiko juu ya uhai.

Hapawezi kuwa na wasiwasi kwamba tofauti mbalimbali kubwa, ukatili, mateso na ghasia ambayo yanaweza kuonekana katika historia yote, yanatokana na ikhtilafu ambazo zinaitawala dunia yenyewe na maisha ya mwanadamu.

Tunaamini kwamba Uislamu na itikadi yake, iliyoegemea kwenye tawhiid, ikiwa na, kama ilivyo, mlolongo mpana wa chambuzi za kifalsafa na kisayansi za kina za dunia yenye madhumuni na uhalisia wa nje, na kumfahamisha mwanadamu juu ya mielekeo yote ya uhai wake, una uwezo wa kutatua kimsingi ikhtilafu zote na kutowiana kote na kummuongoza mwanadamu katika mwelekeo wa kitendo cha ubunifu kilichokubalika cha kumhakikishia mustakabali wake.

Kila mfumo wa imani, ingawa kanuni zake zinaweza kuwa zimeenea na misingi yake ikawa ya kudumu, inahitaji kuwasilishwa upya kwa kila kizazi kwa mujibu wa mazingira ya zama hizo. Wenye fikra na walezi wa kiroho, ambao wamezoena na ari ya wakati na wenye kuelewa haja ya utafiti zaidi katika shughuli za msingi ili kukabiliana na mageuzi yanayoletwa na falsafa na sayansi za kisasa, ni lazima kwa hiyo, watoe mazingatio ya uangalifu, makini na yenye upeo mpana juu ya maswali haya, wakichukua vyanzo vya Kiislamu. Ni lazima wawasilishe ukweli, kama mwelekeo mpana na endelevu wa Uislamu unavyotaka kwamba uwasilishwe, na kuizoesha dunia na kanuni za kimantiki za Uislamu.

Kitabu hiki cha sasa ni juhudi za kuwasilisha, kwa njia fupi na hai, uchunguzi wa misingi ya kiimani ya Uislamu, kwa kuchanganya mantiki ya kifalsafa kwa urahisi wa maneno. Kwa vile lengo letu limekuwa ni kuwasilisha kazi fupi kiasi, tumejizuia kutokana na kunukuu maoni ya wanafalsafa na wanasayansi mbalimbali kwa kirefu. Sehemu ya kwanza ya kazi yetu inashughulika na mada za tawhid na uadilifu. Tunategemea kwamba itakuwa ni mchango wa kufanya yajulikane maoni ya Uislamu juu ya maswali haya ya msingi. Sayyid Mujtaba Musavi Lari, Qum, Julai 15, 1981.

1

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LAKWANZA

USTAWI WA IMANI KATIKA VIPINDI MBALIMBALI

Miongoni mwa mada za msingi za kielimu zinazohusu maisha ya binadamu, masuala ya kidini yanachukua umuhimu wa pekee. Kwa kweli, kila mara zimekuwa zinazingatiwa kama tatizo la msingi kwa ustawi na hatima ya mwanadamu na zimetengeneza utambuzi wa kina sana na ujuzi mkubwa. Wanachuo na watafiti wamefanya uchunguzi mpana sana kuhusu sababu za asili zilizomfanya binadamu ajihusishe na mambo ya Kidini, kufuatilia utafiti wao kwa mtazamo wa pekee na utaratibu ambao hutawala maamuzi na maoni yao.

Ukweli wa jambo hili ni kwamba tangu nyakati za kabla ya historia, itikadi na imani kila mara vimekuwa ndio sehemu ya mtindo wa jamii ya wanadamu; sio zamani au wakati huu ambapo inawezekana kukuta jamii ambayo ndani yake masuala ya kidini hayakulelewa. Qur'ani Tukufu imetaja kwenye Aya kadhaa kuhusu ukweli wa kihistoria kwamba Mitume waliotumwa toka mbinguni siku zote walijitokeza kwenye umma zilizopita ambako, pamoja na athari zao za kiroho zenye manufaa, vile vile walichukua nafasi muhimu katika kubuni ustaarabu wa kibinadamu.

Uchunguzi wa jinsi ambavyo maisha ya mwanadamu yameendelea taratibu na ujuzi kupanuka, pamoja na ujuzi uliotokana na upeo wa mbali sana wa historia, unaonyesha kwamba binadamu aliambatana na imani ya kidini kabla hajawa na utambuzi kamili wa mbinu za maamuzi ya busara. Kipindi cha kwanza cha ujuzi na utendaji wa mwanadamu, kwa hiyo, hakuchukui ubora juu ya vipindi vya mwanzoni kabisa vya dini na imani. Inawezekana hata kudaiwa kwamba jitihada za mwanadamu katika nyanja

za dini na imani zimeonyesha bidii kubwa sana na za kudumu zaidi kuliko juhudi zake katika eneo la ujuzi na sanaa, kwani elimu ya ukweli unaokuvuka mipaka ambao ndio kiini cha cha dunia ya uhai ni mgumu zaidi na inayopatikana kwa taabu kuliko kiini cha vitu vile ambavyo ujuzi na sanaa daima huhangaikia kuvipata. Hali halisi ya msingi ya jua lenye utukufu, ambalo ndio kitu dhahiri kuliko vitu vyote, ilibakia bila kujulikana kwa binadamu kwa karne nyingi na mwenendo na athari zake vilipewa tafsiri za kila aina; ingawa hapana mtu aliyeweza kukanusha kuhusu kung'ara kwa miale yake, akili za watu wengi zilibakia gizani kuhusu kujulikana kwake.

Kwa hiyo, utambuzi wa ukweli mkubwa hauwezekani bila uchunguzi wa kimantiki, maamuzi na kusoma kunakoeleweka. Endapo ushirikina na visa-asili (hekaya) vya kidini vinaweza kupatikana miongoni mwa watu wa kale, na muda wote vikiingizwa kwenye tabia mpya kwa sababu ya upungufu na udhaifu wa kifikira na mipaka finyu ya ujuzi, hii haimaanishi kwamba dini pamoja na kiwango chake cha nadharia, ni udanganyifu. Kwa usahihi zaidi, dini huonyesha ubora na uhuru wa matamanio ya Kidini katika vina vya nafsi na moyo wa mwanadamu. Zaidi ya hayo, kutoka kwenye sayansi ambayo inatafuta kuchunguza nyakati za kabla ya historia, hatuwezi kutegemea kwamba itagundua zaidi kuhusu dini za kale kuliko masalia ya hekaya na ushirikina unaoweza kufumbulika kwenye mabaki ya mtu wa kale na chini ya ardhi.

Kwa kuwa mwenendo wa binadamu na shughuli zake daima huambatana na sifa mbili zilizo wazi; ubora na uhuru, kwa upande moja, na ufahamikaji na ueneaji pote duniani miongoni mwa jamii ya spishi, kwa upande mwingine - kimantiki, moja kwa moja inaonyesha kwamba tunatakiwa tutoe namna ya chimbuko kwa ajili ya mwenendo na shughuli hiyo kutoka katika kina cha moyo wa mwanadamu. Kuwepo kwa jambo endelevu la aina hiyo kwenye hali ya umilele na kilimwengu, muda wote wa historia na kabla ya historia haliwezi kuchukuliwa kama athari za desturi na mazoea; ni udhihirashaji wa kiu ya dahari na silika ya lazima kwa ajili ya ukweli. Imani zote za kidini na vipengele na aina zao zinazotofautiana zinatoka kwenye chanzo kimoja kinachobubujika na chenye hazina kubwa - ni asili ya dahari ya mwanadamu, ambao haukulazimishwa kutoka nje wala haikuwa ajali.

Kwanza kunakuja kuwepo katika moyo wa binadamu, uwezo wa kukubali imani, na halafu imani yenyewe kuchukua muundo wake. Mwelekeo huo huo wa ndani unaomlazimisha mtu kufanya uchunguzi na utafiti wa kisomi ili aweze kufahamu ukweli ndio dalili ya binadamu kuhitaji elimu ya kidini. Hii, kwa kweli, haina maana kwamba hali ya ndani na maelekezo ni lazima yaambatane na imani sahihi na iliyoundwa kikamilifu. Kama vile ambavyo mwili unavyohitaji viini rutubishi bila ya tamaa hii, haionyeshi uzuri na ukamilifu wa chakula, roho nayo pia hutafuta chakula chake - yaani imani na itikadi - kwa msisitizo ikitafuta utambuzi wa Mola wake na kutamani kuomba kwenye lango lake. Lakini silika ambayo inailazimisha roho kutafuta haiwezi kutambua na kutathmini imani na kanuni za imani, kubainisha ukweli na uwongo.

Wanachuo wanakubaliana kwamba imani za kidini kila mara zimefungamanishwa na maisha ya binadamu. Hata hivyo, maoni yao yanatofautiana kuhusu viini vya misingi vya dini na mambo ambayo yameshika nafasi muhimu katika kuanzishwa na kuendelea kwake. Uamuzi wao katika jambo hili, kwa ujumla umetegemezwa kwenye uchunguzi wa dini za kishirikina na imani za kale, na matokeo yake ni kwamba, maamuzi yao, kwa uchambuzi wa mwisho, yanakuwa na mapungufu na bila mantiki. Ni kweli kwamba dini fulani, zisizofungamana na kanuni za ufunuo wa ki- Mwenyezi Mungu, zimeathiriwa katika muonekano na kukua kwao na mazingira ya kijamii na mambo mengine yanayofanana na hayo. Hata hivyo, haina mantiki kuhusisha misingi yote ya imani na mielekeo ya kidini na mazingira ya kinyenzo au hali ya kiuchumi na mahitaji, kwa hofu ya nguvu zinazoogofya za kiasili, kwa ujinga au kwa fikira zilikataliwa na sayansi.

Bila shaka, moja wapo ya mambo katika kujitokeza kwa mawazo ya kinyume na dini na kundi la watu wanaomkana Mwenyezi Mungu, ni mafundisho ya udanganyifu, upungufu na upotovu wa kiakili wa wafuasi wa baadhi ya dini. Upekee na tofauti za tabia za kila dini, kwa hiyo lazima zichambuliwe moja baada ya nyingine wakati wa kuchunguza sababu ambazo zimemfanya binadamu kuwa mfuasi wa dini hiyo.

Katika matukio mengi ya kihistoria, dini inaweza kuonekana kutawala mahusiano yote. Endapo dini ingekuwa si jambo la msingi, ingekuwa imefungika moja kwa moja kwenye dhamira za kimaada. Hata hivyo, ni jambo gani ambalo lingewapa watu wa dini uimara na ushupavu wa aina hiyo kwa ajili ya kukidhi malengo yao ya kidini? Je, ilikuwa ni kwa sababu ya mategemeo ya manufaa ya utajiri wa kidunia na manufaa mengine ya kibinafsi ambayo yalifanya matatizo machungu yaliyotokana na balaa na shida kuwa na ladha tamu katika nafsi zao? Kinyume chake, tunaona kwamba walitoa utajiri wao wote, maendeleo yao na utashi wa kibinafsi, kwenye hisia na maadili ya kidini, hadi kufika kiasi cha kujitolea nafsi zao kwa mapenzi makubwa.

Kwenye hadithi inayomhusu Firauni na wachawi wake, tunasoma kwamba aliwaita waganga wake wote wa mazingaombwe ili wamshinde Musa(a.s) yule mtu aliyesemeshwa na Mwenyezi Mungu, wakiwa na matumaini kwamba kwa werevu na uwezo wao wa kichawi, wangeweza kumlazimisha kusalimu amri. Lakini shukurani kwa uwezo wa kimiujiza aliopewa Musa, walishindwa na wakarejea kwenye imani ya kweli. Firauni mwenye hasira, ambaye kiburi chake kilivunjwa, akaanza kuwakashifu na kuwatishia, akiwaambia kwamba angewaadhibu kwa mateso mabaya kuzidi yote - yaani kuwakata miguu yao. Lakini, mageuzi ya kina sana yalikwisha kufanyika katika nyoyo zao; walibakia kuwa imara na madhubuti mbele ya vitisho na kurairai kwa Firauni na mateso yake makali. Wachawi hao wakajibu, kwa ushupavu sana;

فَاقْضِ مَا أَنتَ قَاضٍ إِنَّمَا تَقْضِي هَـٰذِهِ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا ﴿٧٢﴾

"....basi fanya unavyotaka kufanya, unaweza kutoa hukumu inayohusiana na maisha haya ya dunia tu." (Surat-Twaha; 20:72).

Hili lilikuwa ni onyesho la wazi la nguvu ya utashi wa asili wa kutaka kupata ukweli na uhalisi ndani ya binadamu anapokabiliwa na dhuluma uonevu na nguvu za kikatili. Watu ambao waliishi kati kati ya chombo cha Firauni na walikuwa wanafaidika nacho, walinyanyua vichwa vyao na kuasi na walikuwa tayari kujitoa mhanga. Mwelekeo maalum wa mtu kwenye masuala ya kidini, kwa hiyo hauwezi kuelezwa kwa kigezo cha tafsiri ya manufaa ya kidunia; kinyume chake matukio kama lile la wachawi huonyesha ubora wa maana za kidini kwa binadamu.

Imani zisizo na mantiki hazifungamani na masuala ya kidini tu. Kabla hazijasafishwa sawasawa, elimu nyingi zilikuwa zimechanganywa na ushirikina. Watu waliona njia yao kutoka kwenye upandisha mashetani na uchawi kwenda kwenye tiba za kweli na zenye manufaa na kutoka kwenye alkemi za uongo kuja kwenye kemia halisi. Hapana mtu anayeweza kudai kwamba endapo mtu alifanya kosa mara moja wakati wa kutafuta kitu, kwa hiyo, analazimika kubakia kwenye makosa wakati wote na kamwe hatapata njia ya kuufikia ukweli. Wale watu wanaoamini katika falsafa za kisayansi na ubora na mbinu ya majaribio, wanakubali kwamba majaribio yao yanaweza kuleta matokeo yasiyo sahihi ingawa kwa namna moja au nyingine watayapatia hadhi ya ukweli.

Watu wanaomkana Mwenyezi Mungu husisitiza uamuzi wa kwamba Mwenyezi Mungu ni matokeo ya fikira ya mwanadamu. Kwa mfano, mwanafalsafa Mwingereza, Betrand Russell, anauona woga wa nguvu za asili kutokea kuwa chanzo cha dini. "Kwa maoni yangu, dini zaidi ya yote imetokana na woga wa kisichojulikana, woga wa kifo, woga wa kushindwa, hofu ya mambo ya siri na yaliyofichikana. Kwa nyongeza, kama ambavyo imekwisha kuandikwa, hisia hujitokeza na kumwezesha kila mtu kudhani kwamba anaye msaidizi katika matatizo yake yote na jitihada zake."[1]

Haya ni madai tu, ambayo hayaungwi mkono na ushahidi wowote. Samuel King anasema, "Chanzo cha dini kimegubikwa na usirisiri. Miongoni mwa nadharia zisizo na idadi za wasomi kuhusu somo hili, baadhi huonekana zenye mantiki kuzidi zingine, lakini hata ile bora kuliko zote inakabiliwa na upinzani kutoka katika mta zamo wa uthibitisho wa kisayansi. Haziwezi kuvuka mipaka ya mazingira ya makisio ya kimantiki. Kwa hiyo, kupo kutokukubaiana kukubwa sana miongoni mwa wataalamu wa elimu ya jamii kuhusu chanzo cha dini."[2] Hata hivyo, tunaweza kujibu kwamba hata kama tunakubali chanzo na msingi wa hamasa ya imani ya binadamu juu ya kuwepo muumba imeonekana kuwa ni hofu, hii haithibitishi kwa vyovyote vile kwamba kuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni mzaha mzaha usio na ukweli.

Endapo hofu ilimsukuma binadamu kutafuta kimbilio na kama katika kutafuta huko aligundua ukweli yakini, yaani Mwenyezi Mungu, je, kuna haja ya kufanya upinzani wowote dhidi ya hilo? Kama hofu ni sababu ya ugunduzi wa kitu fulani, hivi tunaweza kusema kwamba kitu hicho ni cha kubuni na si cha kweli kwa sababu woga ndio uliomsukuma binadamu kukitafuta kitu hicho? Kwa hakika haingekuwa na mantiki kushikilia, kwa mfano, kwamba elimu ya tiba haina ukweli kwa sababu binadamu ameitafuta na kuivumbua kwa sababu ya woga yaani hofu ya maradhi na kifo? Ukweli wa jambo hili ni Katika mambo yote na matukio ya maisha, kuamini Mungu Mmoja aliye na hekima ni hifadhi halisi na msaada madhubuti.

Hili ni jambo tofauti kabisa mbali na kama ndivyo au sivyo kwamba msukumo wa binadamu kutafuta kitu hiki ni woga wa mabadiliko ya maisha na kutafuta kimbilio au hapana. Mambo haya mawili yapo mbali mbali kabisa na lazima yachunguzwe kila moja kwa upande wake. Bila shaka katika hatua za zamani za maisha yake, binadamu kwa kweli alikuwa mateka wa hofu ya kufedhehesha na kuumiza alipokabiliwa na matukio ya kimaumbile ya kutisha kama vile mafuriko, matetemeko ya ardhi na maradhi. Jinamizi la hofu lilitupa kivuli chake chenye kisirani katika vipengele vyake vyote vya maisha yake na fikira zake, na katika mapambano yasiyoisha aliyoyaendesha dhidi ya udhaifu na hofu, alitafuta msaada ambapo angeweza kupata hifadhi kutoka kwenye mazingira yake ya kuogofya na kupata amani ya kina. Hatimaye, kwa bidii kali, alilishinda jinamizi la unyonge na hofuna akapata ushindi wa dhahiri.

Uchunguzi wa hatua tofauti tofauti kuhusu maisha ya binadamu wa kale, na ugunduzi wa ushahidi kwamba woga ulikuwepo katika fikira za binadamu, hauthibitishi kwamba woga na ujinga ndio tu mambo ya msingi yaliyomfanya binadamu aielekee dini. Dai la aina hii litakuwa ni matokeo ya kuona eneo moja tu la jambo hili. Uamuzi wa jumla unaweza tu kufanywa kutokana na utafiti na uchunguzi wa kihistoria ambapo utimilifu wa historia, pamoja na vipindi tofauti vyote katika maisha ya binadamu, umechunguzwa na kufanyiwa utafiti, si pembe moja ya kihistoria yake pana na yenye sura mbalimbali.

Hofu kutawala mambo ya binadamu na unyonge wao katika vipindi maalum na vyenye mipaka si lazima vifanywe kuwa msingi wa uamuzi wa jumla kuhusu vipindi vyote. Haitakuwa ni uamuzi wa haraka mno kusema kwamba fikira zote za kidini na hisia ya mwanadamu, mwelekeo wa kumwabudu Mwenyezi Mungu katika nyakati zote tangu zama za kale pamoja na huu wa sasa, zimesababishwa hivi hivi tu na hou, kwa kuogopa ghadhabu ya maumbile, ya vita na magonjwa? Kwa kweli hasa, wale ambao wameridhika kwa uthabiti hasa miongoni mwa watu kwa hali yoyote ile sio wale wanyonge mno. Wale ambao, jinsi wakati unavyopita, wamenyanyua juu bendera ya dini ni wale wenye nguvu sana na imara katika watu. Imani ya mtu kamwe haiongezeki kwa kuwiana na unyonge wake, na kiongozi wa watu katika mambo ya imani ya kidini si mtu wa mbele sana miongoni mwao katika udhaifu, unyonge na kuishiwa nguvu.

Je, Imani katika dini ya maelfu ya wanachuo na wanafikra ni matokeo ya woga wao juu ya dhoruba, matetemeko ya ardhi na magonjwa? Inawezekana mwelekeo wao kwenye dini, uchunguzi wa kisomi, wa mantiki na uthibitisho madhubuti, kudhaniwa kuwa ni kwa sababu ya ujinga wao na kutokutambua kwao sababu asilia za matikio? Ni lipi litakuwa jibu la mtu mwenye akili?

Zaidi ya hayo mtu kuingia kwenye dini si kwa sababu ya kupata amani ya aina fulani. Badala yake, mtu huanza kufurahia matunda mazuri ya dini - amani na utulivu, baada ya kupata imani na kusadikisha. Kwa maoni ya wanazuoni waliongozwa Ki-Mungu, dunia ni ufupisho kamili wa sababu na hoja zilizopangwa uzuri, mfumo sahihi wa ulimwengu unaoshuhudia kuwepo kwa chanzo kitambulikanacho kwa elimu na uwezo. Michirizi ya upakaji rangi usioeleweka na unaotatiza haiwezi kuchukuliwa kuwa dalili ya msanii stadi, lakini michirizi iliyo sahihi na ubunifu wenye maana huo ndio ushahidi wa hakika wa kuwepo kwa fundi rangi mwenye ujuzi.

Pia wapo watu wanaoiangalia imani katika ukweli ulioko nje ya mipaka ya asili kuwa kama matokeo ya mambo ya uchumi. Hufanya juhudi kubwa kuanzisha uhusiano fulani baina ya dini na uchumi. Wanadai kwamba wakati wote dini imekuwa katika huduma ya ubeberu na unyonyaji na kwamba ilikuwa uvumbuzi wa tabaka utawala na unyonyaji kama njia ya kuvunja upinzani wa umma unaonyonywa. Wanadai kwamba, dini imekuwa ikitumiwa kuwapumbaza wavuja jasho wasiojiweza na kuwahimiza waendelee kuridhia kutojiweza kwao. Hapana shaka kwamba, kama kwa kitu kingine chochote kile hapa duniani, dini inaweza kutumiwa vibaya. Inapobadilishwa kutoka kwenye malengo yake ya kweli, inakuwa ni silaha mikononi mwa wenye kufaidika ambao wanataka kuyaweka mataifa utumwani. Hata hivyo, huku kutumika vibaya kwa dini kusiwape wabinafsi kisingizio cha kushambulia kidhalimu kila kitu chenye jina la dini. Lazima pawepo na utenganisho uliowazi baina ya dini potovu zilizobuniwa na ubeberu kwa lengo la kuwapumbaza watu, na zile halisi za kweli na zenye kujenga.

Inawezekana kwamba katika jamii nyingi za binadamu, hali mbaya ya kiuchumi, kuvia na kukosa maendeleo vinaweza kuwepo sambamba na imani ya kidini. Lakini, kuwepo pamoja huku hakuwezi kulazimisha kuwepo uhusiano wa kawaida; mmoja hauwezi kuwasilishwa kama sababu ya mwingine. Wakati fulani tunaona jamii inafaidi maendeleo na ustawi kiuchumi ambao umeambatana kwa kina sana na dini, ambapo jamii nyingine ambayo inafaidi vivyo hivyo hali nzuri ya kiuchumi iko kinyume kabisa na dini. Vivyo hivyo, kwenye mazingira ya umasikini na kukosa maendeleo, nuru ya dini inaweza kutoweka ambapo kwenye mazingira mengine kama hayo, mvuto wa dini unaweza kuwa kwenye kilele chake. Kutokuwepo kwa ulingano wa wazi baina ya hali ya uchumi na kuwepo au kuanguka kwa mvuto wa kidini na uthibitisho uliowazi wa ukweli kwamba kutokea kwa wakati mmoja (kwa mambo mawili) hakutoshi kuanzisha uhusiano wa kawaida. Jambo fulani maalum lazima liwepo kusababisha kutokeza au kutoweka kwa mojawapo kuunganishwa na kuwepo au kutokuwepo kwa jingine.

Tunaweza kuona wazi kabisa huku kutokuwepo kwa ulingano katika jamii mbili ambazo zote zipo kwenye utawala dhalimu wa tabaka la wanyonyaji. Katika mojawapo ya hizo jamii mbili, dini imeondoka kabisa kwenye mazingira yake, ambapo kwenye jamii nyingine mvuto wake umepanuka. Uhalisi wa lengo unatuonyesha kwa hiyo kwamba, mtu anavutwa kwenye dini na mazingira mbalimbali ya nje. Popote pale ambapo dini inaonyesha mvuto wake, mtu lazima atafute dhamira ya msingi ya ndani kabisa katika hali asili hususia ya dini, sio katika mazingira ya uchumi. Kwa nyongeza, tunapoyachunguza yale malengo ya dini za ki-Mungu, tunafikia uamuzi kwamba mahitaji ya kuwepo kwa ustawi na kuanzishwa kwa mfumo wa uchumi wa haki ambao unaegemezwa kwenye dini yamekuwa mojawapo ya sababu za kutumwa Mitume. Hii, pia ni sababu mojawapo ambayo imewafanya watu wamevutiwa kwenye dini na ni moja wapo ya manufaa ambayo jamii ya binaadamu imepata kutoka humo.

2

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA PILI

UNDANI WA NAFSI YA MWANADAMU HUMLAZIMISHA KUMTAFUTA MWENYEZI MUNGU

Nje ya mfumo wa hisia za mwili wake, mwanadamu anayo maeneo makubwa mno na muhimu ambayo kwa hali yoyote ile hayakufungiwa katika utaratibu wa mwili wake. Ili kuweza kugundua vipengele hivyo na hatua zilizo nje ya muundo wa mwili na ukubwa wa kiwiliwili chake, mtu lazima atafute muundo wa ndani na wa kiroho wa binadamu na kufahamu ule upeo mpana wa asili yake yenye mambo mengi, pamoja na udhihiri nyeti na wa kiungwana wa hisia na silika zake.

Mlolongo wa namna maalumu za ufahamu zinakuwemo katika nafsi ya binadamu ambazo zimejiotea mizizi ndani yake zenyewe, zinachomoza kutoka kwenye namna hasa ya hulka ya mwanadamu, na na kuchomoza kwao hakupasiki na jambo lolote la nje ya mwili wake. Miongoni mwa tambuzi hizi ni hisia za kuwajibika kwenye amana, haki, kuwa mkweli na mwaminifu. Kabla hajaingia kwenye uwanja wa sayansi na ujuzi na vyote vinavyohusika navyo, mtu ana uwezo wa kutambua ukweli fulani kwa njia ya utambuzi huu wa asili. Lakini baada ya kuingia kwenye eneo la sayansi na falsafa na kuujaza ubongo wake na shuhuda mbali mbali na tasfiri ya mambo, anaweza akasahau tambuzi zake za kawaida na za asili au akaanza kuzitilia mashaka. Ni kwa sababu hii kwamba binadamu anapokwenda kinyume na tabia yake ya asili kufafanua imani kwa maneno, tofauti huanza kujitokeza.

Kuelekea kwenye dini na kumuamini Mwenyezi Mungu, katika hatua zake za mwanzo huvutia kwenye sababu za kisilika na tambuzi za asili, lakini halafu huendelea kukua na kugeuka kwa msaada wa mantiki na tafakari. Mizizi ya hisia asili katika silika za mwanadamu imekwenda ndani mno na wakati huo huo, huonekana wazi na dhahiri sana hivyo kwamba endapo mtu anatakasa akili yake na roho yake kuhusu fikira za kidini na zisizo za kidini na halafu akajiangalia mwenyewe na dunia ya viumbe, kwa wazi kabisa ataona kwamba anasonga kuelekea upande fulani akiwa na msafara mzima wa viumbe. Bila ya utashi wowote au hiari upande wake, huanza maisha yake mahali fulani, na halafu tena bila hiari yake husonga mbele kwenda mahali pengine ambapo hapajui. Na ukweli huu huu unaweza kuonekana juu ya viumbe vyote vya asili, vikijiendesha kwa namna ya usahihi na kwa mpango.

Endapo mtu anayeona vizuri, akiwa bado yu katika hali ya kimaumbile, atayaangalia mazingira yanayomzunguka, kwa wazi kabisa atahisi kuwepo kwa nguvu kuu ambayo inamzunguka yeye na dunia yote. Katika umbile lake mwenyewe, ambalo ni sehemu ndogo sana ya dunia kubwa, ataona ujuzi, nguvu na utashi wa kuishi, na atajiuliza ni vipi ujuzi, nguvu na utashi havingeweza kuwepo katika dunia kwa jumla. Ni huu mpango uliofanyiwa mahesabu kwa ustadi mkubwa na mwendo wa dunia ambao humlazimisha mwanadamu kukubali kuwepo kwa uwezo wa akili ya fani zote ambayo, ikiwa ipo nje ya dunia ya kimaumbile, lakini hata hivyo inaisanifu na kuiamuru, isipokuwa kwa kukubalika hili, mpangilio huu wa dunia hauwezi kuelezeka. Mtu yeyote anaye tathmini nafasi yake hapa duniani anaweza kutambua kwamba kuna nguvu inayomuumba yeye, ikamleta yeye hapa, inayomtia usongefu ndani mwake, na halafu tena humwondoa, bila ya ruhusa au msaada wake kutakiwa kwa ajili ya lolote katika haya.

Kiongozi mkuu wa mashahidi, Hussein bin Ali(a.s) alisema katika dua yake ya siri kwa Muumba wake; "Inawezekanaje kufasiri kuweko Kwako kutoka kwenye kitu ambacho kinakutegemea Wewe kwa kuwepo kwake? Kwa nini huna hali ya kudhihirika kama wengine wasio wewe waliyonayo, ili kwamba iweze kukufanya Wewe uwepo dhahiri? Ni lini ulifichika kamwe kutoka kwenye jicho la ndani ili labda uweze kuhitaji uthibitisho uwe kama mwongozo wa kuelekea kwako Wewe? Ni lini ambapo ulikuwa kamwe mbali na sisi hivyo kwamba ishara na dalili Zako labda zingeweza kutusogeza karibu na Wewe? Limepofuka jicho ambalo halikuoni Wewe unapolitazama kulilinda na kuliongoza!

"Ee Mwenyezi Mungu, Wewe ambaye umejidhihirisha Mwenyewe kwa ufahari wako, unawezaje kuwa umefichika ambapo unaonekana na kudhihirika? Unawezaje kuwa haupo ambapo kwa kuonekana kwako kusiko na ukomo unawaangalia waja Wako?"[3] Hapana mahali popote na wakati wowote ambapo kitu kimetengenezwa bila mtengenezaji wake kuonekana, wala tendo bila mtendaji. Utafutaji wa kiungo baina ya chanzo na athari hujitokeza kutokea kwenye silika ya ndani ya mwanadamu; utambuzi wa uhusiano hauwezi kuondolewa kutoka kwa mtu yeyote.

Vivyo hivyo, hisia za kidini, kumtafuta Muumba, pia haiwezekani kuondolewa kutoka kwa mtu yeyote. Hata mtoto ambaye hana uzoefu wa dunia, wakati wowote asikiapo sauti au aonapo msongo, ki-silika atageuzia nadhari yake kwenye chanzo cha sauti au msongo. Misingi yote ya maisha halisi na ujuzi inasimama kwenye kukubali sababu kwa kila athari. Kanuni ya uhusiano, kwa kweli ni dhahiri kabisa ambayo haitoi mwanya wowote. Jiolojia, fizikia, Kemia, elimujamii, uchumi - katika hizi na elimu zingine, utafiti una lengo la kubainisha sababu na mambo yanayoamua uhusiano. Kwa ufupi, ni dhahiri kwamba elimu na ujuzi si lolote zaidi ya utafutaji wa vyanzo; maendeleo na kusonga mbele katika mambo ya binadamu hutokana na uchunguzi unaofanywa na wasomi kuhusu vyanzo vya mambo.

Kama ingekuwa inawezekana sisi kugundua kutoka kwenye kiumbe kimoja au pembe moja ya ulimwengu alama ya kujianzisha au kujiumba chenyewe kikamilifu, tungeridhika katika kueneza mfano huo moja kwa mpangilio wote wa viumbe. Kama mambo yalivyo, si muhimu kwamba kanuni ya usababisho kila mara ijioneshe kwetu katika miundo inayojulikana. Aina mbalimbali na wingi wa vyanzo viko kiasi kwamba mtafiti anayejihusisha na jambo moja tu labda atashindwa kupambanua visababisho vyote. Hata hivyo, katika mambo yote ya mwanadamu, maalum na ya kawaida, yaliyopita na yajayo, katika mazingira ya mtu mmoja au ya jamii, hakuna nukta hata moja inyoweza kuonekana kuwa ya bahati mbaya.

Si tu kwamba upo mpangilio mahususi ambao ni wa asili katika kuumbwa kwa kila kitu peke yake; pia kunakuwepo na ya kuonekana katika uhusiano wa kila jambo na jambo jingine, vile vile na uhusiano wa kila kitu na mazingira ambamo kinakuwemo, utaratibu stadi uliokokotolewa vizuri sana. Mathalani, katika kuukuza mti, kanuni za anga na ardhi zinafanya kazi katika uelewano kamili na muundo wa mizizi na matawi yake. Pia upo uhusiano wa wanyama na mti ule kwa vile wanapata chakula kutoka humo. Inawezekanaje kwamba pawepo na bahati mbaya katika asili ya utaratibu wa uhusiano wa aina hiyo?

Endapo jambo lingepata umbo katika ngazi fulani katika muundo wa kiumbe, bila kufahamu na katika misingi ya kubahatisha, hali hii ingetoa maandalizi mazuri sana kwa ajili ya kutoweka na kuangamia kwa dunia. Kwa sababu hitilafu ndogo sana katika usawa wa vitu asili na dosari ndogo sana katika kanuni angavu za ulimwengu ingetosha kusababisha vitu kukosa amari zao na viumbe vya angani kugongana, na kutokea kwa mlipuko mkubwa na kuangamia kwa dunia. Kama asili ya dunia ingeegemea kwenye kuweko bahati mbaya, kwa nini nadharia hata za wapenda anasa za dunia zimetegemewa kwenye kufikiria kupanga, mpangilio uliopangwa, kukosekana hali ya bahati mbaya? Kama dunia yote ni matokeo ya kubahatisha na bahati mbaya, ni kitu gani kile ambacho hakikutokea kwa msingi wa kubahatisha? Endapo kitu kilichopo sasa kilikuja kuwepo kama kiumbe si kwa sababu ya kubahatisha, ni sehemu gani muhimu na sifa zake zake ambazo zinazokibainisha na je zinaweza kutumika katika vitu vingi na vya namna nyingi mbali mbali vya ulimwengu?

Sasa kwa kuwa kubahatisha kunapingana na mpangilio na upatanifu, inaonekana kwamba kitu chochote kinachokuwa na mabaki ya upangaji, ubunifu na ukokotozi kitakuwa hakitangamani vizuri na hakiendelei, kwa sababu dhana za upangaji, usanii na mpangilio mzuri zimepingana na kubahatisha na hali ya uwezekano. Kudhani kwamba mfumo wa kubahatisha ndio muundombinu kwa ajili ya ulimwengu na kanuni yake inayotawala haitegemei uthibitisho wowote wa kimantiki au ushahidi wa kisayansi haiwezi kukubaliwa kuwa ni ufumbuzi wa uhakika kwenye jiometri ya muundo wa maumbile.

Wakati ambapo sayansi za majaribio zinaonyesha kwamba elementi na vipengele vya asili haviwezi kutoa mvuto wowote wa kujitegemea na havina uumbaji; ambapo uzoefu wetu wote, hisia zetu za fahamu na mafuhum zetu za kimantiki yanaelekeza kwenye maamuzi kwamba katika maumbile hakuna kinachotokea bila ya sababu na chanzo na kwamba vitu vyote vimetengenezwa kwenye mfumo madhubuti na kanuni maalum - ikiwa yote haya ndio hali halisi yenyewe, inashangaza kuona watu wengine wanageuzia migongo yao kwenye kanuni za kisayansi, mafuhum muhimu na mapendekezo yaliyo egemezwa kwenye tafakuri, na kukataa kuwepo kwa Muumba.

Elimu na vipengele vya kimazingira ni miongoni mwa sababu ambazo ama huzuia fahamu za asili za binadamu zisijioneshe, au kinyume chake, kuziimarisha. Kila chenye kujionyesha chenyewe kutoka kwenye chanzo cha silika hufanana katika mpangilio wake na mlolongo wa asili. Wale ambao wameachwa huru na kufuata mwelekeo wa asili wa maumbile yao bila ya kufungwa na mazoea na ambao tabia yao ya kina zaidi haikupambwa na maneno na muonekano, wanaweza kusikiliza vizuri zaidi wito wa nafsi zao za ndani zaidi na kuweza kupambanua baina ya matendo mema na mabaya, imani za kweli na za uongo. Kutokuwa na maadili ya dini, hali ambayo kwa kweli ni kuipa kisogo asili ya maumbile, kwa hiyo, ni nadra sana kuonekana miongoni mwa watu kama hao.

Endapo mtu anawaambia kwamba dunia haina mpangilio wenye kukaa ndani na kwamba inatokana na hali ya kutukia (isiyo ya uhakika), akiyapamba maneno yake kwa istilahi za kifalsafa, hatakuwa na athiri juu ya watu kama hao, kwa sababu watazikataa nadharia zake kwa ajili ya asili yao ya kimaumbile. Watu ambao wamenasa katika mitandao ya sayansi wanaweza kuwa mateka wa shaka na utatanishi kama matokeo ya istilahi zenye ushawishi. Elimu finyu ambayo hutia msukumo wa kiburi kwa binadamu ni kama mfano wa kipande cha kioo kilichopakwa rangi ka kuwekwa mbele ya kiupenyo cha akili na maumbile ya asili; yeyote mwenye akili hii huona dunia imetiwa rangi kidogo na ujuzi wake na elimu yake. Hudhania kwamba ukamilifu wa ukweli ni ule anaouona kupitia kwenye kipenyo chembamba cha fahamu zake na akili ambavyo ni nyara rahisi ya rangi. Kama hali ilivyo, hatuna maana kwamba binadamu aache kuendeleza akili yake ili ajiepushe na upotovu. Hata hivyo, asije akawekewa mipaka na ujuzi wake na elimu yake au asijigambe kwa hiyo elimu na ujuzi wake wenye kikomo.

Watu walio wengi, badala ya kufanya maarifa na ujuzi wao kuwa ngazi ya kunyanyua uwezo wa akili zao ili waweze kufikia kiwango cha juu zaidi, wanabaki wametulia na kufungiwa kwenye uzio wa kuta nne za dhana na masharti. Hali ya asili ya mwanadamu, pindi anapohisi hatari, haraka hukimbilia kwenye msaada wake. Mtu anapobanwa na shida na matatizo makubwa sana, wakati mambo ya kilimwengu yanapompa kisogo, anapokuwa hana njia yoyote ya kuzifikia rasilimali za kimaisha na anazama kama bua kwenye machafuko ya mabadiliko na kifo kipo karibu sana naye - ndipo dhamira ya kutoka moyoni humwongoza kisilika na kumwelekeza kwenye chanzo cha msaada kisichokuwa cha kilimwengu. Hutafuta msaada kutoka kwa yule ambaye uwezo wake upo juu ya uwezo wowote ule, na huelewa kwamba ni yule Muumba mwenye huruma na mwenye nguvu zote ambaye anaweza kumsaidia kwa kutumia uwezo wake usio wa kawaida na kumwokoa.

Kwa sababu ya utambuzi wake, kwa nguvu zake zote binadamu hutafuta msaada wa yule aliye mtakatifu sana ili amwondoshe kwenye hatari na kwenye faragha ya moyo wake, anahisi uwezo na nguvu ya muweza huyo zikifanya kazi kwqa ajili ya mwokovu wake. Mtu mmoja wakati fulani alimuomba Imamu Sadiq(a.s) amwongoze kuelekea kwa Mola wake Mlezi, akasema kwamba maneno ya wapinzani yalimtatanisha. Imamu akamuuliza, "Umewahi kusafiri kwa meli? Akajibu, "Ndio."

Imamu: "Je, imewahi kutokea kwamba meli ikaingiza maji na hapakuwepo na mtu wa kuwaokoeni ili msizame kwenye mawimbi ya tufani ya bahari?"

Jibu: "Ndio." Imamu: "Wakati huo wa hatari na katika hali hiyo ya kukatisha tamaa, je, ulikuwa na hisia kwamba nguvu isiyopimika na yenye uwezo mkubwa ingeweza kuwakuokoeni kwenye balaa lenu la kutisha?"

Jibu: "Ndio, hivyo ndivyo ilivyokuwa."

Imamu:"Ni Mwenyezi Mungu Mwenye uwezo ambaye ndio chanzo cha mategemeo na kwake Yeye watu ndiko wanakotazamia kwa matumaini pale ambapo milango yote inapokuwa imefungwa." [4] Hata watu waasi na wapenda dunia wenye uwezo ambao hawautambui uwezo usio na kikomo wa Mwenyezi Mungu, wanapofurahia utawala wao, hubadilika wanaponasa kwenye mtego wa kushindwa na kuangamia. Husahau kumkana kwao Mwenyezi Mungu ambako madhehebu yao ya mazingira na ya kianasa za dunia ulivyojipandikiza ndani yao na kwa moyo mkunjufu kabisa hugeukia kwenye asili ya viumbe vyote na chanzo cha nguvu zote.

Historia imeorodhesha mifano mingi sana ya watu kama hao ambao walipata kuwa waathirika wa matatizo na hali za mitihani hivyo kwamba vumbi la upotofu liliondolewa ghafla kutoka kwenye tabia zao za asili na kutoka kwenye vina vya nafsi zao na wakarejea kwa Muumba asiye na kifani. Kwa kuongezea kwenye rasilimali za ndani ambazo ni za asili katika nafsi ya binadamu na humsaidia yeye kugundua ukweli hivyo kwamba, akiwa huru kutokana na dhana na vikwazo vya kiakili husonga mbele akifuata njia ya tabia yake ya asili, na kiwango cha nje cha mwongozo na maonyo pia ni muhimu kwa ajili ya kumwelekeza njia na kuimarisha hali yake ya asili. Ni mwongozo ndio unaorekebisha sifa za ki-uasi na kuilinda akili na tabia ya asili kutoka kwenye upotovu na utiifu kwa miungu wa uwongo. Mitume walipelekwa kwa madhumuni ya kuwafanya watu wajihadhari na utambuzi wenye utatanishi, wa tabia zao za asili, ili kuufanya mwelekeo wao wa ki-Mungu ufuate mkondo unaostahili, na kuyanyanyua matarajio yao makubwa.

Amirul-Mu'minina(a.s) amesema:"Mwenyezi Mungu aliwatuma Wajumbe Wake miongoni mwa watu ili waweze kuwahoji kuhusu ahadi yao na Mwenyezi Mungu, kuwakumbusha watu kuhusu neema za Mwenyezi Mungu zlizosahaulika, kuzungumza nao kwa namna ya kuwaonya, kuzindua hekima iliyojificha ndani mwao, na kuwaonesha ishara za uwezo wa Mwenyezi Mungu." [5]

Mwongozo na nasaha za aina hiyo kwa jinsi yoyote ile haimaanishi kuzimwa kwa nuru ya dhamira endelevu ya mwanadamu kumnyima uhuru na uwezo wake wa kufikiri na kuchagua. Hii, kinyume chake, ni aina ya msaada kwenye mielekeo na silika bayana, kuziwezesha kukua na kuendelea. Ni kupitia mwongozo na nasaha ambapo wanadamu wanaondolewa kwenye vifungo na kuwezeshwa kunufaika kutokana na mpanuko wote wa maumbile yao ya asili na kusitawi pamoja na viumbile wenzao wote. Qur'anii inasema:

وَيَضَعُ عَنْهُمْ إِصْرَهُمْ وَالْأَغْلَالَ الَّتِي كَانَتْ عَلَيْهِمْ فَالَّذِينَ آمَنُوا بِهِ وَعَزَّرُوهُ وَنَصَرُوهُ وَاتَّبَعُوا النُّورَ الَّذِي أُنزِلَ مَعَهُ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٥٧﴾

". . Anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyokuwa juu yao. Basi wale waliomuamini yeye, na wakamtukuza, wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyoteremshwa pamoja naye, hao ndio wenye kufaulu."[6]

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ ﴿٢٤﴾

"Enyi mlioamini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapokuiteni kwa yale yatakayokupeni uzima."[7]

يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَتْكُم مَّوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَشِفَاءٌ لِّمَا فِي الصُّدُورِ ﴿٥٧﴾

"Enyi watu! Yamekufikieni mawaidha kutoka kwa Mola wenu Mlezi, pozo la yale yaliyomo vifuani, .[8]

Watu wa kwanza waliokubali wito wa Mitume walikuwa watu wenye mioyo safi na dhamira zilizoongoka. Safu za washindani wao zilikuwa na wale waliotegemea juu ya mamlaka bandia na utajiri au walijawa na kiburi kwa sababu ya ujuzi wao mdogo na wenye mapungufu, akili zilizochafuliwa na udanganyifu, kwa namna ambayo kwamba jeuri yao isiyo na msingi, ilizuia uwezo wa kina na matamanio yao kustawi.

Mwanazuoni fulani amesema hivi: "Katika mambo ya kiroho, pia kanuni ya usambazaji na kuhitaji huwepo. Kama haja ya dini isingekuepo katika tabia ya asili ya binadamu, mahitaji yaliyotolewa na Mitume yangepotea bure. Tunaona kwamba ugawaji wa Mitume ulipata wateja; mawazo yao yenye mipango mingi, yasiyo na shaka na sahihi kabisa yalipata wafuasi na waunga mkono wengi. Huu ni uthibitisho kwamba haja ya dini inakuwepo ndani ya mwanadamu na dhamiri yake ya kina kabisa."[9]

Kwa kweli, mafundisho ya msingi ya Mitume wote yalikuwa wito wa kumwamini Mwenyezi Mungu mmoja, sio ya kuthibitisha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu. Walibatilisha thamani ya masanamu, jua, mwezi na nyota kuabudiwa, ili kwamba kiu ya ya mwanadamu ya kina na ya kimaumbile kwa ajili ya ibada isitoshelezwe na kuvikimbilia vitu vya maumbo ya nje kama hivi na wanaweza, badala yake, kutafuta malengo na maadili yao kwenye safina imara na kupanda kwenye madhumuni halisi ya ibada. Mioyo yao inapaswa ifungamane na ulinzi usio na kikomo, na kwa imani ambayo daima inapanda, wao wanapaswa wakati wote kusonga mbele kuelekea kwenye chanzo cha maadili yote na wema, hatimaye kufikia kwenye malengo yao.

Aina zote za kuabudu miungu wengi za ukana dini - mfumo wa kale ambao ni kuabudu masanamu namuundo ulioendelea, wa kisasa, ambao tamaa ya anasa - ni matokeo ya kukengeuka asili ya maumbile. Maendeleo ya elimu kuhusu uzoefu wa kidini ambayo yanatokea pote duniani yamesababisha ugunduzi mwingi ambao unaruhusu maamuzi muhimu ya uhakika yaweze kufikiwa.

Ikiegemezwa kwenye takwimu nyingi kiasi zilizokusanywa na wataalamu wa sosholojia, wanaakiologia (wachambuzi wa elimu ya kale), wana anthropogia (elimu ya asili ya binadamu), historia ya dini sasa ina changanua silika ya kidini, pamoja na uanzishwaji, imani, desturi na vipengele ambavyo vinaijenga jamii, kwa namna mpya ambayo inatofautiana sana na maelezo yaliyotolewa kabla ya hapo. Sasa hivi kuna wimbi la fikra ambalo kwa muda wote linaendelea kuwavutia wafuasi wapya kutoka kwenye madhehebu mbali mbali wanaosema kwamba hisia za kidini ni kijenzi cha msingi, cha asili na madhubuti cha roho ya binadamu na kwamba ni njia ya asili ya kutambua yaliyo ghaibu. Mnamo kama mwaka wa 1920, mwanafalsafa wa Kijerumani aitwaye Rudolf Otto aliweza kudhibitisha kwamba sambamba na dalili za kiakili na maadili ndani ya mwanadamu, pia zipo dalili za kimantiki ya hali ya juu sana ambazo hujenga hisia za kidini. Sifa zinazomhusu Mwenyezi Mungu kama vile uwezo, ukuu na zenye kuvuka mipaka zina madhumuni ya kusisitiza kwamba utakatifu hauwezi kurahisishwa kuwa dhana nyingine. Hii ni namna inayojitegemea ambayo haiwezi kupatikana kutokana na namna nyingine na haiwezi kuhusishwa na dhana nyingine yoyote, kimantiki au vinginevyo.

Mojawapo ya upekee wa zama hizi kwa kweli, ni utafutaji wa kipimo cha nne katika dunia ya asili kiitwacho "Wakati". Kama vilivyo vipimo vingine, ni lazima kiingiliane na miili, na kwa hiyo hakuna mwili uliopo katika duniani ambacho kimeepukana na wakati ambao unatokana na msongo na mabadiliko. Vivyo hivyo ni sifa ya zama hizi kwamba tafiti za wanachuo zimeongozea kwenye ugunduzi wa 'kipimo cha nne' cha nafsi ya mwanadamu - hisia za kidini[10] .

Vipimo vingine vitatu au hisia vinakuwa na hisia ya dadisi, hisia ya maadili na hisia ya ubora. Hisia ya kidini au dhana ya utakatifu, ni kipimo cha nne na cha msingi zaidi cha hisia. Kihulka kila mtu anao mvuto na mwelekeo kwa kile kilichoko nje ya maumbile, tofauti na huru kutokana na zile hisia zingine tatu. Kwa kugunduliwa kwa hisia ya kidini, jela ya nafsi yake, yenye nyuso tatu, iliporomoka na ikathibitika kwamba mielekeo ya kidini ya mwanadamu imeota mizizi kwa kujitawala kabisa ndani ya utu wake. Ilijitokeza yenyewe hata nyakati zile ambazo watu walikuwa wanaishi ndani ya misitu na mapangoni.

Licha ya ubora wake, kujitawala na kufaa kwa hisia za udadisi, maadili, ubora na nafasi zilizoichukua katika kutokeza kwa elimu, maadili na ujuzi, ilikuwa ni hisia ya kidini iliyoandaa mazingira kwa ajili ya utendaji wa hisia hizi tatu, ikizisaidia kusonga mbele katika njia yao na kugundua siri za ulimwengu ulioumbwa. Kwa mtazamo wa muumini, dunia imesanifiwa katika msingi wa kanuni na mpango sahihi uliokusudiwa vizuri. Imani hii kwa Mwenyezi Mungu mwenye kuamuru na mwenye hekima huzindua hisia ya udadisi kwa lengo la kutafuta na kugundua kanuni na siri za maumbile ambazo zimeegemea kwenye mlolongo wa sababu namotokeo yake. Mchango wa hisia ya kidini katika kukuza na kuendeleza tabia tukufu kabisa za binadamu, katika kurekebisha hisia zake na kurutubisha silika zake za maadili na wema, haupingiki. Wale wanaofuata maamrisho ya dini wanauona kama mmoja wa wajibu wao muhimu sana wa kidini, kudhibiti silika zao na kupata sifa nzuri za hali ya juu. Fikra ya kidini pia imekuwa kipengele chenye kulea hisia za kisanaa. Watu wa kale walitengeneza kazi zao za kisanaa endelevu sana ili kuwatukuza miungu wao. Mahekalu ya ajabu ya China, mapiramidi makubwa ya Misri, masanamu ya aina ya kipekee ya Mexico, usanifu majengo ulioboreshwa na wakustaajabisha ya Mashariki ya Kiislamu -yote haya yalitegemea sana kwenye hisia ya kidini.

Wanasaikolojia wanaamini kwamba upo uhusiano baina ya hali ya balehe na kujitokeza kwa ghafla kwa hisia za kidini. Katika kipindi hiki cha maisha, hata kwa watu ambao siku za nyuma hawakujali mambo ya dini, hisia ya kidini inachukua mkazo maalum. Hapana shaka kwamba, wito wa ndani hujionyesha kwa jinsi ambayo kwamba hakuna kizuizi kinachoweza kuzuia njia yao. Hata hivyo vipengele fulani kama vile propaganda za upinzani vinaweza kupunguza hisia za ndani kwa ndani na fikra sahihi, ingawa vishawishi kama hivyo haviwezi kuishia kwenye ung'oaji kabisa wa uwelekeo huo. Endapo vikwazo kama hivyo vitaondolewa, hisia zilizo imara huanza tena utendaji wao na kujionesha kwa namna ya jitihada zao endelevu za ndani kwa ndani.

Tunafahamu kwamba zaidi ya nusu karne imepita tangu mapinduzi ya kikomunisti ya Jumuiya ya Kisovieti, lakini mizizi ya dini ipo hai kwenye vina virefu vya nafsi za watu wa Sovieti. Licha ya juhudi zote ambazo zimefanywa katika kipindi hiki kirefu na watawala za kuifuta dini, wameshindwa kuondoa hisia ya kidini kutoka kwa watu.

Kuwapo kwa fikra za maslahi ya kidunia, kwa hiyo, hakupingani na ukweli kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni jambo la kawaida kwa mwanadamu. Endapo madhehebu fulani itaondoka kwenye mkondo wa maumbile ya asili na hapo ikajifanya ya kipekee kusuiana na madhehebu zingine, kwa dunia ya sasa na katika nyakati zilizopita, hali hii haiwezi kufikiriwa kama ni kukanusha ile hoja kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni kawaida kwa binadamu; tofauti inakuwepo katika nyanja zote. Kile ambacho historia inakionesha na kwamba madhehebu ya tamaa za kidunia ilianzishwa mnamo karne ya sita na saba kabla ya Yesu Isa(a.s) .

3

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA TATU

MWENYEZI MUNGU NA MANTIKI YA JARIBIO (JARABA)

Bila shaka, hali ya kijamii, mambo ya kihistoria na kielimu, na aina mbali mbali za kazi za binadamu ni mambo ambayo haviwezi kuwa bila mvuto juu ya uonyeshaji kwa vitendo wa mwelekeo wa ndani wa mtu na tabia zake za kiroho na kihisia. Ingawa hali hizi mbali mbali hazisababishi ulazima wowote au umuhimu katika uchaguzi wa mwelekeo wa mtu, zinaweza kusababisha kuwepo kwa mazingira yanayofaa zaidi kwa ajili ya uchaguzi wa aina fulani, kwa hiyo kutoa mchango muhimu kuhusu jinsi binadamu anavyoviona vitu. Hali hizi wakati mwingine zinaweza hata kujionesha katika umbo la kikwazo kwenye uhuru wa mtu na uwezo wa kuchagua. Kama matokeo ya uzoefu zaidi wa maamuzi ya kisayansi na ya kimajaribio, akili ya binadamu kwa kawaida huelekea kuonea haya kwa kiasi fulani maamuzi halisi ya kiakili kabisa, hususan kama jambo linalofanyiwa uchunguzi sio yakinifu na halina maana.

Kwa ujumla, uwezo wa kiakili za mtu hupata nguvu na ustadi kwenye eneo ambamo zinatumiwa sana. Mambo yaliyoko nje ya eneo hilo, kwake (binadamu) huonekana kuwa si ya kweli au si halisi au vizuri zaidi ni jambo la hatua ya pili au linalohusika kidogo sana na jambo analolishughulikia maalum hasa. Kwa hiyo, mwanadamu huelekea kuhukumu kila kitu kwa namna ya kipekee. Mojawapo ya vipengele viharibifu na vinavyo potosha sana katika fikra zihusuzo Mwenyezi Mungu ni kuziwekea mipaka fikra ndani ya mantiki ya elimu za kimajaribio na kushindwa kutambua viwango na mipaka ya mantiki hiyo. Kwa kuwa wataalamu wa sayansi za majaribio kutumia nguvu zao zote za kiakili kwenye elimu za kihisia, wanakuwa wageni kwa mambo yaliyoko nje ya utambuzi wa hisia.

Ugeni huu, umbali huu kutoka kwenye mambo yasiyohusiana na hisia, imani hii isiyo ya kawaida juu ya data zinazotokana na sayansi za majaribio, hufikia kiwango kiasi kwamba kupima na kufanya majaribio huunda muundo wote wa akili na mtazamo wa dunia wa wataalamu kama hao. Wanaona majaribio kama ndio nyenzo pekee inayokubalika na njia ya utambuzi, kama kigezo pekee Wanakitegemea hicho kutatua matatizo yote. Kazi ya sayansi hizo ni kufafanua uhusiano baina ya mambo; lengo lao ni kuthibitisha uwiano baina ya matukio, si baina ya Mwenyezi Mungu na matukio. Katika sayansi za majaribio, mwanadamu hahusiki kabisa na Mwenyezi Mungu. Mtu asiwe na matumaini ya kuweza kutambua ukweli wa hisia za juu kwa kutumia kigezo cha hisia, au kamuona Mwenyezi Mungu ndani ya maabara.

Sayansi hizo haziwezi kufanya majaribio ya maabara juu kuwepo kwa Mwenyezi Mungu na halafu wafikie uamuzi kwamba endapo kitu hakionekani kimwili na hakiwezi kuthibitishwa kwa njia ya majaribio ya maabara na ukokotozi wa kimahesabu, kwa hiyo, kitu hicho hakina ukweli. Kwa kweli hakuna jaribio lolote linaloweza kufanywa na kupambanua kama kitu kisicho cha ki-maada kipo au hakipo, kwa sababu ni kitu hicho tu ambacho kinaweza kukanushwa kwa njia ya majaribio kinachoweza kuthibitishwa kwa njia ya majaribio. Sayansi na metafizikia ni aina mbili za elimu ambazo zina kiwango sawa cha uhalali na usahihi. Kanuni ya metafizikia haitokani na majaribio wala haiwezi kukanushwa na majaribio.

Maelfu ya majaribio ya kisayansi yanabuniwa ili yathibitishe kwamba vitu vyote ni vya ki-maada, yote yatashindwa kufikia malengo yao. Mwanasayansi wa majaribio anayo haki ya kusema, "Nimevumbua hiki na hiki," au "Sijagundua hiki na hiki." Hana haki ya kusema, "Kitu hiki na kile havipo." Mbinu za maabara, pamoja na utata wao na hali ya juu ya maendeleo, haziwezi kupata njia kupitia yasiyojulikana, giza na dunia iliyopanuka ya vitu vya asili, ambavyo ndio kiini cha majaribio, haziwezi kufahamu ukweli wote uliojificha katika kiini cha chembe zisizo na kikomo na haziwezi kuvumbua hata asili halisi ya kitu.

Mbinu inayotegemea majaribio imekuwa na manufaa sana katika kuendeleza utambuzi wa mwanadamu wa mpangilio sahihi wa maumbile, na inaweza kutoa msingi ulio dhahiri na mpya kwa ajili ya kumwamini Mola Mlezi kupita kwenye uchunguzi wake wa utaratibu wa uumbaji, kwani inaashiria kuwepo kwa Muumba mtambuzi na mwenye uwezo. Hata hivyo, nia na madhumuni ya wana sayansi katika utafiti na uchunguzi katika masuala ya maumbile na siri za dunia kwa ujumla si kwa sababu ya kumtambua Muumbaji wa uhai. Ikiwa katika mkondo wa kuendelea kukua kwake katika mikono ya watafiti, sayansi wakati wote imekuwa inagundua siri za kuwepo kwa maumbile bila ya wanasayansi kujitokeza, kwa njia ya sayansi yao, kutoka kwenye ujuzi mfinyu na wenye mipaka ambao wameupata kutoka kwenye hatua yao ya utafiti wa sasa.

Endapo wangelikuwa wafanye hivyo, wangelifahamu uunganishwaji wa mambo na kujiweka chini kwa vitu vyote kwenye utaratibu uliowekwa, na kwa hiyo, kupata hatua nyingine mbili za ziada za ujuzi na utambuzi. Kwanza wangeweza kuwianisha data zao zote za kihisia na majaribio, na halafu wangeweza kutoa uamuzi wa busara na kufanya tafsiri. Bila kukubali kuwepo kwa Muumba mwenye busara, haiwezekani kutoa tafsiri kwa kusadikisha ukamilifu wa data zenye tofauti zinazotokana na elimu mbalimbali na uhusiano uliopo baina yao.

Kwa matendo, hata hivyo, kazi na mbinu za fikra ya kisayansi ni kuunda kanuni na kufanya utafiti bila marejeo kwa Mwenyezi Mungu, hivyo kwamba mfumo wa fikra ambamo Mwenyezi Mungu hahusishwi unakuwa mhimili ambao juu yake kazi ya kisayansi huugeukia, na kusababisha mwanadamu kuwa mgeni na chochote kilichopo nje ya upeo wa fikra hiyo. Wakati huo huo, maisha ya kivitendo ya mwanadamu yanasihusiana na elimu bila kuepukika. Matokeo yanayotokana na ujuzi unaotegemea majaribio yanajumuisha mielekeo yote ya ki-maada ya maisha, kuwafunga wanadamu kwenye kuta zao nne zisizopenyeka, na ni vigumu sana kupata nyenzo yoyote ya kawaida miongoni mwa njia za maisha ya mwanadamu.

Hali hii kwa ulazima huongeza kuamini kwa binadamu katika sayansi na huathiri tabia yake, kumdukizia nafsini mwake hali ya mashaka na wasiwasi. Juu ya hayo, manufaa ya hali ya asili ya kitu kilichofanyiwa uchunguzi kwa kutumia sayansi ya majaribio kinagusika na kiko dhahiri kwa kila mtu, kwa tofauti kubwa sana ikilinganishwa na masuala ya metafizikia. Vivyo hivyo, vitu vya kimaada ambavyo vimechunguzwa kwa kutumia sayansi ya majaribio vinaeleweka sana, ambapo kinyume chake ni kweli katika masuala ya metafizikia.

Kuwasilisha masuala ya kidini kwa kutumia mbinu isiyo sahihi iliyofuatwa na kanisa la zama za kati (1100-1500A.D), ikichanganywa na uadui kwenye udhihirikaji wote wa sayansi, ilikuwa ndio jambo muhimu sana katika kuifanya sayansi ya majaribio kuonekana yenye kupendelewa zaidi kuliko yale ya mambo kifalsafa na ya kimaada. Kwa ufupi, sayansi ilionekana kupingana cha dini, si kwenda sambamba nayo. Mara mantiki ya majaribio ilipofuzu katika kumwaga fikra zote ndani ya umbo lake, ilibadili sura ya mtazamo wa wanadamu juu ya dunia kwa kiwango ambacho kwamba walisadiki kwamba huo tu ndio ulikuwa msingi kwa ajili ya kukubali ukweli wa kitu. Waliiteua kuwa ndio mamlaka ya mwisho na wakaona kwamba haiwezekani kuthibitisha kuwepo kwa kitu chochote ambacho hakitambuliki kwenye akili.

Hivyo, mwana sayansi anayetegemea majaribio, ambaye hafahamu utaratibu wa watu wanaomjua Mwenyezi Mungu, anakubali na kuona kuwa ni sawa katika maisha yake, kila kinacholingana na mantiki na fikra ya kisayansi. Hujichukulia mwenyewe haki ya kukanusha chochote kisichochukuana na desturi yake ya kisayansi. Utaratibu wake ni imani kamili katika majaribio na kuiona kuwa ni ndio uthibitisho pekee wa usahihi wa maamuzi yoyote. Katika hali kama hii, ambapo msingi wote wa fikra za kidini unapuuzwa, mwanasayansi anajikuta hana kanuni zozote za kumwezesha kutafsiri yale masuala madogo madogo ya kidini ambayo hujitokeza katika namna ya amri na makatazo. Akiwa amezoea kabisa lugha ya kisayansi na kutegemea kanuni, anakuwa amejifunga kabisa kwenye desturi yake na kudhani amri za dini zinazoshurutisha, zilizo rahisi na zinazoeleweka, kuwa hazina maudhui au thamani.

Njia hii ya fikira ina dosari na si sahihi. Ingawa sayansi zina fomula (kanuni) changamani za ajabu na sahihi, ambazo kuzielewa kwake huhitaji uchunguzi wa kina na mgumu, fomula hizo hizo huondoka kwenye nyanja ya sayansi mara ziingiapo katika maisha yetu ya kawaida, hujitenga na lugha ya kifundi ya wana sayansi. Kama isingekuwa hivi, zingedhibitiwa kutumika kwenye vituo vya kisayansi na viwanda, maktaba na vituo vya utafiti.

Kila mtu anaweza kutumia vifaa kama simu na radio. Hali ni hiyo hiyo kwa nyenzo na zana za kisayansi. Juu ya usahihi na uchangamano wao, maelekezo kidogo yenye utaalamu yatamwezesha mtu yeyote kuzitumia. Mtu aliyebobea na mtaalam huwa hawatoi maarifa ya umakenika na ya ufundi kwa wanunuzi wa kifaa, badala yake, hufupisha maelezo yao katika sentensi fupi fupi yale matokeo ya kazi ngumu zilizovumiliwa na wavumbuzi. Kwa hiyo, si haki na ni kinyume cha mantiki ya kisayansi kujaribu kulazimisha amri za dini (ambazo haziwezi kufupishwa kuwa fomula za kisayansi, ambapo zikiwa rahisi na za kila mahali) kwenye tabia ya dhana na maoni ya mtu, na halafu zitangazwe kwamba hazina thamani na si za maana, huku wakipuuza wajibu wao wa kimaamuzi na athari zao za maana sana katika maisha yetu. Maelezo ya kivitendo huzaa matunda yao wakati yanapotamkwa katika lugha inayoeleweka kwa ujumla na kuwa na mguso kwa kila mtu na maisha ya kijamii.

Zaidi ya hayo, endapo ingedhaniwa kwamba amri na maelekezo ya dini yangeamuliwa na ufahamu, uelewa na muonjo wetu hapangekuwepo na haja ya wahyi na Mitume; tungeweza kuanzisha dini zetu wenyewe! Mara nyingi mwanadamu huwa hazioni dosari zake, akishughulishwa kama alivyo na nguvu zake. Mwenye kuabudu sayansi wa dunia ya leo anajivunia sana pia ujuzi wake kama matokeo na maendeleo ambayo yameyapatikana kutoka kwenye sayansi za majaribio kiasi kwamba anajidhania yeye mwenyewe kwamba ameshinda na kwa ushindi huo amechukua umiliki wa dunia ya ukweli. Lakini, hapana mtu ambaye wakati wowote ameweza kudai kwamba amepata ujuzi wa siri zote za ulimwengu na kuondosha mapazia yote kutoka kwenye dunia ya maumbile ya asili.

Mtu lazima achukuwe mtazamo mpana zaidi juu ya hali halisi na atambue ni jinsi gani tone la elimu yake lilivyo dogo likilinganishwa na bahari ya siri zilizofichika ambazo zinatukabili sisi. Baada ya kila ugunduzi wa kisayansi, msururu zaidi wa mambo yasiyojulikana hujitokeza. Katika karne zote ambapo mwanadamu amekuwa akifanya kazi bila kupumzika pamoja na rasilimali zake zote ili aweze kuijua dunia kwa kadiri iwezekanavyo, matokeo pekee ya jitihadi zake yamekuwa ugunduzi wa mambo machache miongoni kwa siri nyingi za ulimwengu. Ni hatua chache tu zimechukuliwa katika njia hii, na kuna lundo kubwa la yasiyojulikana yaliyoizunguka elimu ya mwanadamu kama wingu.

Kwa hiyo, mtu lazima atathimini kwa uhakika zaidi upeo wa utambuzi wa sayansi za hisia na sehemu zao zinazofaa kwa shughuli na athari. Mawazo yote yaliyokuwepo hapo kabla ambayo ni kama vizuizi kwenye njia ya kwenye ukweli lazima yaachwe kwa ajili ya uchambuzi sahihi.

Bila shaka, sayansi za majaribio zinaweza kutujulisha vipengele vya nje tu vya jambo; ni vitu vya ki-maada na mambo yakinifu ambavyo vinakuja kwenye upeo wa uchunguzi wao na vinaweza kuathirika kwenye majaribio ya maabara. Utaratibu wa sayansi katika kufanikisha malengo yao, wakiwa wanatafuta kupata faida kutoka kwenye kila ongezeko dogo katika ujuzi, ni uchunguzi na majaribio. Kwa kuwa shughuli ya msingi wa sayansi ya majaribio ni uchunguzi wa dunia ya nje, ili kuweza kuwa na uhakika kwamba nadharia fulani ya kisayansi ni sahihi, lazima tuilinganishe na ulimwengu wa nje ili kuijaribu. Endapo dunia ya nje inathibitisha kwa kufaa zaidi, sisi tunaikubali; laa kama sivyo, basi hatuikubali.

Kwa hiyo, kuzingatia lengo na utaratibu wa sayansi ya majaribio, lazima tuhoji endapo kama ukweli wa metafizikia unategemea kwenye kipimo cha hisia na kufanyiwa majaribio? Hivi hoja yoyote ya majaribioya kisayansi lazima ina haki ya kuingilia kati masuala ya imani na itikadi? Je, kuna sehemu yoyote ya sayansi ya majaribio inayohusika na Mwenyezi Mungu? Ili kuweza kugundua usahihi na kutokuwa sahihi kwa jambo katika sayansi za majaribio, ni muhimu kufanya matumizi ya mabadiliko na ya kuondoa vipengele tulivyopewa, pamoja na mazingira yake. Utaratibu huu hautumiki kwenye uhai wa ki-mungu, wa milele, usiobadilika na wa vitu vingi.

Ujuzi yakinifu ni taa ambayo inaweza kumulika baadhi vitu visivyojulikana kwa miale yake lakini si taa ambayo inaweza kuondosha giza lote. Kwani elimu ya mfumo hutegemea kuufahamu ujumla wake wote kabisa na namna ya ufahamu ambayo inaweza kuunganisha wenyewe sehemu zote za utambuzi, na kusababisha mtazamo wa mbali mtimilifu kabisa. Sasa kuifungia elimu ya mwanadamu kwenye kikomo cha sayansi za hisia hauwezi kumfikisha mtu kwenye mtazamo wa mbali kamili, bali kwenye ufahamu wa eneo la ndani zaidi la nafsi.

Kama tunamwamini Mwenyezi Mungu au laa, kwa kweli haina uhusiano na sayansi za majaribio, kwa sababu kwa kuwa kiini cha uchunguzi wao ni maada, sayansi zinazojihusisha na mambo yanayoonekana hayana haki ya kujieleza yenyewe kwa kukubali au kukataa kuhusu jambo lolote lisilokuwa la ki-maada. Kwa mujibu wa imani ya kidini ya madhehebu mbali mbali, Mwenyezi Mungu sio mtu - hana mwili. Hawezi kufahamika kwa kutumia milango ya fahamu. Yeye ameupindukia muda na nafasi (havihitajii). Yeye ni Ambaye kuwepo kwake hakutawaliwi na mipaka ya kidunia na nafasi haiwezi kumbana. Kwa hiyo, Yeye ameepukana na kuhitaji na ametukuka katika dhati yake juu ya upungufu wa aina yoyote.

Anavijua vipengele vya ndani sana na vya nje vya ulimwengu. Dunia ipo wazi mbele Yake. Mwisho kabisa, Anacho kiwango cha juu kabisa cha ukamilifu na ametukuka zaidi kuliko chochote kinachomhusu Yeye kinachoweza kuingia kwenye akili ya mwanadamu. Hatuwezi kabisa kuujua msingi wa dhati Yake, tukiwa tuna upungufu wetu wenyewe na wa uwezo wetu, akili na nyenzo za upambanuzi. Kwa sababu hii; endapo ukivichunguza vitabu vyote vya sayansi ya majaribio, hutakuta utajo hata kidogo wa majaribio kuhusu Mwenyezi Mungu au uamuzi wowote umetolewa kuhusu Mwenyezi Mungu.

Hata kama tutachukulia utambuzi wa hisia kuwa ndio njia pekee ya kugundua ukweli, hatuwezi kuthibitisha kwa kutegemea utambuzi wa hisia, kwamba hakuna kitu chochote kinachokuwepo nje ya ulimwengu wa hisia. Madai kama hayo, yenyewe yatakuwa si ya kutegemea majaribio, yakiegama kwenye ushahidi usiokuwa wa hisia au majaribio. Hata kama wafuasi wa madhehebu ya kidini walikuwa hawana uthibitisho wa kutetea madai yao, kuhitimisha kwa uthabiti na kwa nguvu kwamba visivyokuwana uhai, vimeenea nje ya upeo wa hisia, ungekuwa ni uchaguzi usio wa kisayansi, ulio tegemea kwenye dhana na minong'ong'oni.

Watu wengine hujaribu kutangaza njozi hizi kwa kuisingizia sayansi na kuonyesha uchaguzi wao kuwa umetokana na fikra ya kisayansi. Hata hivyo, katika mchanganuo wa mwisho, ukanushaji unaohusishwa kwenye madai kama hayo hayana thamani ya sayansi na falsafa, na vilevile yanapingana na mantiki ya majaribio. Kwenye kitabu kiitwacho 'The Elementary Principles of Philosophy'. George Pulitzer anasema, "kukidhania kitu ambacho hakikalii muda na nafasi na hakiathiriwi na mabadiliko wala maendeleo, ni jambo lisilowezekana."

Ni wazi ya kwamba maneno haya yanaakisi njia fulani ya fikra ambayo haijui inatafuta nini. Kama ingejua inachokitafuta, pia ingeelewa namna ya kukitafuta. Kwa kuwa shughuli ya aina hii ya fikra inazunguka kwenye maumbile na himaya ya hisia, ni kawaida kwamba itachukulia kama ni kitu ambacho hakiwezekani, kila kile kilichopo nje ya eneo la shughuli yake na kuwepo kwake ambako hakuwezi kuthibitishwa kwa njia ya majaribio ya hisia. Itaiona imani katika ukamilifu wake hasa kama ni kinyume na muundo wa fikara ya kisayansi. Hata hivyo, wasomi wanaojishughulisha na elimu asilia wanakabiliwa na lundo kubwa la vitu visivyojulikana kuhusu dunia hii hasa, na vya dhahiri, visivyo na uhai ingawaje wakati wote vina mawasiliano nayo (mbali na ulimwengu wa maada, wenye miujiza na siri nyingi zisizo na idadi, haihusishi hili tufe la dunia tunayoishi tu). Wasomi kama hao, kwa hiyo, wanayo haki yakusema tu, "Kwa vile nyanja za kimiujiza zipo nje ya upeo wa zana zangu za kitaalamu, ninanyamaza kimya na sitakanusha. Wangewezaje kujiruhusu kutoa madai ambayo yangesababisha elimu pana kiasi cha kama mpango wa ulimwengu wote, ambapo ujuzi wao wa mpango wote wa uhai unakaribia sufuri?

Kuna uthibitisho gani wa kuhakikisha madai kwamba uhai ni sawa na kitu cha ki-maada na kwamba dunia yote ya uhai imejaa vitu vya kimaada? Ni mwanasayansi gani anayeikataa metafizikia ambaye ameweza kusimamisha kanusho lake juu ya mantiki au ushahidi, au kutoa ushahidi kwamba nje ya kutokuwepo uhai, hakuna kitu kilichopo nje ya uwanja wa hisia? Ingawa sayansi haikatai kwa uwazi na uhakika kabisa kila kitu kisichojulikana kwa sababu tu kwamba haina uwezo wa kukifikia kwa kutumia nyenzo na vifaa vyake, badala yake inangojea kwa uvumilivu siku ambapo kitu hicho kitavumbuliwa, wapenda anasa za dunia wala hawaliendei suala la kuwepo kwa Mwenyezi Mungu kwa shaka na wasi wasi, kwa misingi ya maoni yao ya kimakosa na haraka, wanatangaza uamuzi wao kwamba hakuna Muumbaji!

Watu kama hawa huanzisha vigezo na viwango fulani kwa ajili ya matumizi yao; na hawapo tayari kutumia kigezo kingine kilichoanzishwa kwa makusudi fulani katika eneo lililokusudiwa. Mathalan, kamwe hawatatumia kigezo ambacho kinatumika kwenye uso wa kitu kupimia mwili, lakini inapokuja kwenye kupima dunia ya hisia nyingi wanajaribu kumpima Mwenyezi Mungu, roho na msukumo, kwa kutumia nyenzo hizo hizo wanazotumia kupima dunia yakinifu. Wanapojikuta hawawezi kupata ujuzi wowote wa viumbe kamili husika, wanaendelea kukana kuwepo kwa vitu hivyo.

Sasa kama mtu aliyefungwa kwenye mantiki ya majaribio atapenda kukubali ukweli wa ulimwengu kwa kadiri tu alivyoruhusiwa na uzoefu wa hisia na kukanusha chochote kilichopo nje ya hilo, lazima atambue kwamba hii ni njia ambayo amejichagulia mwenyewe, si matokeo ya uchambuzi wa majaribio ya kisayansi. Aina hii ya itikadi bandia ya usomi na uwezo wa kiakili hutokana na uasi wa kisomi na mtu kuacha asili yake halisi.

Huyo Mwenyezi Mungu ambaye mwanasayansi wa kawaida, anataka "kuthibitisha" kwa kutumia nyenzo zake na vifaa vyake, kwa hali yoyote ile, sio mungu asilani kwa mtazamo wa wale wanaomcha Mwenyezi Mungu.


3

4

5

6

7

8

9

10

11

12

13

14