MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE 14%

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE Mwandishi:
: SALMANI SHOU
Kundi: Misingi mikuu ya Dini

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE
  • Anza
  • Iliyopita
  • 28 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 29999 / Pakua: 4254
Kiwango Kiwango Kiwango
MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

Mwandishi:
Swahili

5

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA TANO

KUONEKANA MWENYEZI MUNGU KATIKA MAUMBILE

Dunia ya maada na maumbile, inayochukuliwa kama kitu kizima kilichoumbwa, ndio ushahidi mzuri sana, wa dhahiri na ulioenea sana, bila upinzani, juu ya ujuzi wa Mwenyezi Mungu. Utashi wenye busara ya Kanuni ya Milele unaweza kugundulika kutoka kwenye kutendeka huku hasa kwa mabadiliko ya vitu. Ni dhahiri kwamba miale Yake ya milele inatoa uhai na mahitaji kwa viumbe vyote, na kwamba viumbe wote wanapata uhai na maendeleo yao kutoka Kwake.

Kuchunguza viumbe tofauti ulimwenguni, siri za kitabu cha uumbaji, kurasa ambazo zote zina shahidilia kwenye shughuli za akili ya juu sana katika uumbaji wake, hutoa, halafu ushahidi ambao wakuegemeza elimu na imani juu ya Muumba mwenye hekima, Ambaye uwezo wake huonekana kidogo tu kwenye mpangilio wa viumbe kwa utukufu wao wote na ukubwa wao. Zaidi ya haya, ni uthibitisho ulio rahisi na kueleweka kwa urahisi ambao unakosa utata na uzito mkubwa wa ushahidi wa kifalsafa. Ni njia ya uchunguzi na tafakuri ambayo ipo wazi kwa wote; kila mtu anaweza kunufaika nayo, wanafikra na wanazuoni na umati wa watu wa kawaida.

Kila mtu, kwa kadiri anavyoruhusiwa na uwezo wake na upeo wa kuona kwake, anaweza kuona katika jambo zima la uumbaji dalili za uunganikaji, utulivu, umasukusudi wa dhati kabisa, na kukuta katika kila moja ya chembechembe zisizo idadi za maumbile, uthibitisho thabiti wa kuwepo kwa chanzo cha viumbe. Marekebisho kamili ya kila aina ya mnyama kufuatana na hali za maisha yake ni ishara kubwa ya Mwenyezi Mungu; kila aina imeumbwa pamoja na vifaa vyote muhimu vinavyohitajika katika hali ya maisha yake. Musa, (amani iwe juu ya Mtume wetu pamoja na yeye), ambaye alizungumza na Mwenyezi Mungu, alitumia ushahidi huu ili aoneshe kuwepo kwa Mwenyezi Mungu kwa Firauni. Yeye Firauni akawaambia Musa na nduguze:

قَالَ فَمَن رَّبُّكُمَا يَا مُوسَىٰ ﴿٤٩﴾ قَالَ رَبُّنَا الَّذِي أَعْطَىٰ كُلَّ شَيْءٍ خَلْقَهُ ثُمَّ هَدَىٰ ﴿٥٠﴾

"Ni nani Mola Wenu ewe Musa? Akasema "Mola Wetu ni yule aliyekipa kila kitu umbo lake. ." (20:49-50).

Vivyo hivyo Imam Sadiq(a.s.) alimwambia Mufadhal, "Tazama kwa uangalifu lile umbo la maumbile ya ndege; uone jinsi alivyoumbwa mwepesi na mdogo katika ujazo ili kumwezesha kuruka. Ndege alipewa miguu miwili tu badala ya minne ambayo wanyama wengine wamepewa na vidole vinne tu kati ya vitano ambavyo wanavyo katika kila mguu. Ndege wana vifua nyembamba vilivyochongoka, ili waweze kuelea hewani na kuruka kwa urahisi kuelekea kila upande. Miguu mirefu ya ndege imekaa vizuri chini ya mkia wake na mabawa yake, na mwili wake wote umefunikwa na manyoya ili hewa iweze kupenya humo na kumwezesha kuruka. Kwa kuwa chakula cha ndege ni pamoja na mbegu na minovu ya wanyama ambavyo wanavila bila kutafuna, basi hawana haja ya meno.

Badala yake, Mwenyezi Mungu amewambia ndege mdomo mgumu na wenye ncha kali ambao hauwezi kuvunjiki wakati unaponyofoa nyama au kuumia wakati wa kukusanya nafaka. Ili kumuwezesha kiumbe huyu kukisaga chakula ambacho hakukitafuna, amepewa mfumo wa kusagia chakula wenye nguvu na mwili wenye joto. Zaidi ya hayo, ndege huzaana kwa kutaga mayai ili waweze kubakia wepesi kiasi cha kutosha kuwawezesha kuruka; endapo watoto wao wangekuwa wakulie matumboni mwao, wangekuwa wazito sana kuweza kuruka."

Halafu Imam akarejea kwenye kanuni ya jumla, akisema,"Kwa hiyo upekee wote wa umbile la ndege huendana na mazingira yake na namna ya maisha yake." [14] Suala la lugha ya wanyama - ile njia ambayo kwamba wanyama wanawasiliana wao kwa wao - ni dalili nyingine ya ki-ungu. wanyama wanayo aina maalumu ya lugha ambayo huwawezesha kuwasiliana wao kwa wao.

Qur'ani Tukufu inaelezea kisa cha mdudu chungu akiongea na Nabii Suleiman(a.s) :

قَالَتْ نَمْلَةٌ يَا أَيُّهَا النَّمْلُ ادْخُلُوا مَسَاكِنَكُمْ لَا يَحْطِمَنَّكُمْ سُلَيْمَانُ وَجُنُودُهُ وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿١٨﴾

"Akasema mdudu chungu: Enyi wadudu chungu! Ingieni majumbani mwenu, asikupondeni Suleiman na majeshi yake, hali hawatambui." (Naml: 27: 18).

Wanasayansi wa sasa wamegundua mtandao changamano wa mawasiliano miongoni mwa wanyama ambao ni mgumu zaidi na uliosahihi kuliko mfumo wetu wenyewe wa mawasiliano. Crissy Morrison anaandika: "Kama tukimweka nondo jike karibu na dirisha la chumba chetu, hutoa ishara nyororo ambazo nondo dume huzipokea kutoka kwenye umbali wa kuangaza na kutuma ishara zake mwenyewe katika kujibu. Kwa kiasi chochote utakachoweza kutaka wewe kuvuruga mawasiliano haya, hutaweza Mwenyezi Mungu na sifa zake 51 kufanya hivyo. Je, kiumbe huyu mnyonge anabebea aina fulani ya transimita, au huyu nondo dume anacho kinasio kilichojificha kwenye kipapasi chake?

"Senene husugua miguu yake kwa pamoja, na sauti inaweza kusikika kwa umbali wa kilomita moja wakati wa usiku wa kimya na mtulivu. Ili aweze kumwita mwenzi wake, nondo dume huweka tani sitini za hewa katika mwendo na senene jike hupeleka jibu la kusisimua kwa kuposa kwake kwa kwa njia ya kimwili, pamoja na kwamba inavyoonekana hakuna sauti inayosikika kutoka kwake. "Kabla ya kuvumbuliwa kwa radio, wanasayansi walidhani kwamba wanyama waliwasiliana wao kwa wao kwa njia ya harufu. Endapo dhana hii ingekuwa kweli, bado ingekuwa ni jambo la muujiza, kwa sababu harufu ingekwenda kupitia hewani ili iweze kufika kwenye pua za mdudu jike. Hali hii ni mbali kabisa na suala la ama upepo unavuma au hapana na jinsi gani mdudu jike angeipata harufu na kutambua inatoka wapi, na kumwezesha kujua mwenzi wake aliko.

"Leo hii, shukrani kwa njia changaman za hali ya juu za kitaalamu, tumepata uwezo wa kuwasiliana na kila mmoja wetu kwa masafa marefu sana. Radio ni uvumbuzi wa kipekee kabisa, unaotuwezesha kuwasiliana mara moja. Lakini matumizi ya uvumbuzi huu hutegemea waya na sisi kuwepo mahali fulani. Nondo bado yupo mbali sana na sisi kwa mbele yetu."[15] Kuchagua sayansi za kimajaribio kama njia ya kuchunguza miujiza ya dunia isiyo na kikomo kuna manufaa mengine ndani yake zaidi ya kuwa karibu na kila mtu. Ni ule utambuzi wa maajabu ya maumbile na utaratibu uliomo ndani yake ambao kwa kawaida humuunganisha mwanadamu na Mwenyezi Mungu Ambaye ameuumba; utambuzi wa aina hii humuonesha binadamu sifa za ukamilifu, ujuzi na uwezo usio na kikomo ambao humuainisha Muumba na Chanzo cha viumbe wote.

Mpangilio huu ulio sahihi unaashira lengo fulani, mpango, hekima pana na kubwa. Ubunifu gani, uwezo gani, ujuzi gani ambao Yeye Ameuwekeza katika dunia yote ya uhai, katika udogo kabisa na ukubwa kabisa wa uumbaji wake wenye kulandana - katika ardhi, katika angahewa, katika maumbile ya ki-mbinguni, katika moyo wa mawe, na kwenye viini vya chembehai! Tunapozungumzia juu ya 'Mpango' lazima ieleweke kwamba fikira hii ya mpangilio inatumika kwa kitu ambapo sehemu zake mbali mbali kwa namna fulani zinahusiana kwa namna ambavyo kwa ulinganifu zinafuatia lengo maalum; ushirikiano wa sehemu hizo lazima pia uwe umezingatiwa. Ingawa wale wanaokanusha kuwepo kwa mpangilio katika ulimwengu kwa ujumla hawakatai kuwepo kwa chanzo hai (kwa vile wanakubali kanuni za usababisho), kinachomaanishwa na kanuni ya ujuzi wa pande mbili katika maumbile ni ile sababu ya msingi, na hii - ikimaanisha kama ifanyavyo kuingilia kati kwa lengo na makusudi kwenye jambo asilia - wao hukataa.

Kwenye Ayah zake nyingi sana, Qur'anii Tukufu inamualika binadamu kutafakari kuhusu mpangilio wa uumbaji ili kwamba watu walio wengi waweze, kwa njia rahisi iwezekavyo, kutambua kuwepo kwa Muumba wa Pekee. Hizi ni baaadhi ya Ayah husika:

إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ وَالْفُلْكِ الَّتِي تَجْرِي فِي الْبَحْرِ بِمَا يَنفَعُ النَّاسَ وَمَا أَنزَلَ اللَّـهُ مِنَ السَّمَاءِ مِن مَّاءٍ فَأَحْيَا بِهِ الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا وَبَثَّ فِيهَا مِن كُلِّ دَابَّةٍ وَتَصْرِيفِ الرِّيَاحِ وَالسَّحَابِ الْمُسَخَّرِ بَيْنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَعْقِلُونَ ﴿١٦٤﴾

"Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kuhitilafiana usiku na mchana, na marikebu ambazo hupita baharini pamoja na viwafaavyo watu, na maji aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mawinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayoamrishwa kupita baina ya mbingu na ardhi, bila shaka zimo ishara kwa watu wenye kuzingatia." (Baqarah: 2:164).

اللَّـهُ الَّذِي رَفَعَ السَّمَاوَاتِ بِغَيْرِ عَمَدٍ تَرَوْنَهَا ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ كُلٌّ يَجْرِي لِأَجَلٍ مُّسَمًّى يُدَبِّرُ الْأَمْرَ يُفَصِّلُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُم بِلِقَاءِ رَبِّكُمْ تُوقِنُونَ ﴿٢﴾

"Mwenyezi Mungu aliyeziinua mbingu bila ya nguzo mnazoziona; kisha akatawala kwenye Arshi, na akalitiisha jua na mwezi, kila kimoja kinaendelea mpaka muda uliowekwa. Yeye ndiye anayeliendesha kila jambo, na anazipambanua Ayah ili mpate kuwa na yakini kukutana na Mola wenu." (Rad: 13:2).

وَهُوَ الَّذِي مَدَّ الْأَرْضَ وَجَعَلَ فِيهَا رَوَاسِيَ وَأَنْهَارًا وَمِن كُلِّ الثَّمَرَاتِ جَعَلَ فِيهَا زَوْجَيْنِ اثْنَيْنِ يُغْشِي اللَّيْلَ النَّهَارَ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ ﴿٣﴾

"Na ndiye aliyeitandaza ardhi na akaweka humo milima na mito. Na katika kila matunda akafanya dume na jike. Huufunika usiku juu ya mchana. Hakika katika haya zimo Ishara kwa wenye kufikiri." (Rad; 13:3).

Endapo tunakubali na kukimbilia kila nadharia ambayo imewekwa na wataalam na watafiti, hata ile nadharia ya mabadiliko kuhusu kutokeza kwa spishi za aina mbali mbali zinazoonekana duniani, hakuna hata nadharia moja itakayoeleweka bila kuwepo kwa nguvu kamili, uingiliaji kati wa utashi, utambuzi, na lengo na makusudio ya mwisho. Uumbaji wa pole pole katika mpangilio wa maumbile pia unaonesha kwa uwazi uingiliaji kati kwa utashi na utambuzi katika utaratibu wake; hatua zote katika mwendo na maendeleo ya maumbile zimetegemezwa kwenye chaguo na azimio sahihi kabisa, na maumbile kamwe hayajatofautiana kwenye njia yake yaliyowekewa hata kidogo katika mamilioni ya miaka.

Ni kweli kwamba katika hatua za mwanzo za kupata uthibitisho wa kuwepo kwa Mwenyezi Mungu kutoka kwenye mpangilio wa ulimwengu zimetumika kumbukumbu za majaribio, na kwamba sehemu za hoja zimejengwa kwa msaada wa hisia, uchunguzi wa maumbile na uchunguzi wa majaribio. Hata hivyo, kwa kweli hoja hiyo si ya majaribio lakini hasa zaidi ni ya kimantiki, ambayo inatuongozea nje ya maumbile na kutuelekeza kwenye ukweli ulio nje ya uwezo wa binadamu ambao uko mbali na maumbile. Uthibitisho wa majaribio unahusu uhusiano baina ya sehemu mbili za maumbile, ambazo kila moja lazima iwe ya utambuzi wa kihisia ili kuruhusu uhusiano baina ya sehemu hizo mbili kuanzishwa.

Tunapokisia kiwango cha ujuzi na utambuzi wa mtu kwa kupima kazi zake na mafanikio yake, hatupo katika uvumbuzi wa majaribio, kwani kiwango cha ujuzi na akili za mtu sio kitu chenye wingi wa kugusika kwa ajili ya sisi kutegemea majaribio moja kwa moja upande wetu sisi.Bila shaka, mtu moja kwa moja anapata utashi, akili, na fikira ndani ya nafsi yake mwenyewe, lakini huwa hana utambuzi kama huo wa kuwepo kwa vitu hivyo kwa wengine; hawezi kuvifikia.

Tunatambua kuwepo kwa akili na fikira ndani ya watu kwa kuangalia kazi zao na mafanikio yao, ingawaje hakuna uthibitisho wa kimajaribio juu ya kuwepo kwa vitu hivyo ndan ya watu hao. Sasa ugunduzi wa akili ndani ya watu wengine kwa njia ya kazi zao na mafanikio yao, upo kwenye ushahidi wa kimantiki, sio matokeo ya majaribio kwa maana ya akili na kazi zake kuwa vyenye kuvutika moja kwa moja kwenye uchunguzi wa moja kwa moja ili kwamba uhusiano wao uweze kugundulika. Ugunduzi huu pia haupo kwenye ulinganishaji wa kimantiki kwa maana ya kuonesha utambulisho baina ya mtu mmoja na wengine wote.

Ikiwa basi, kwamba utambuzi wa fikira na akili ndani ya watu haufanyiki kwa njia ya uthibitisho wa kimajaribio, ni dhahiri kwamba hoja ya mpangilio katika ulimwengu na uhusiano wake na chimbuko la ki-Mungu pia haipo katika jamii ya uthibitisho wa kimajaribio.

Kutoka kwenye mtazamo mwingine, kwa kuwa mwanadamu siye muumbaji wa maumbile bali yeye ni sehemu yake, matendo yake katika dunia ya maumbile yanawakilisha kuanzishwa kwa uhusiano baina ya sehemu tofauti za dunia hiyo. Lengo na madhumuni yanayotafutwa na mwanadamu katika ukusanyaji wa mlolongo wote wa elementi za kimaada (kwa mfano, katika kujenga jengo, kutengeneza motokaa, au kiwanda) kuna husiana na nafsi yake mwenyewe, ni kusema kwamba, lengo na makusudio ya mwisho ni mtengenezaji mwenyewe, sio kile kitu kilichotengenezwa. Uhusiano baina ya sehemu ya vile vitu vilivyotengenezwa, kwa hiyo ni uhusiano ambao si wa kimaumbile; kwa kuthibitisha uhusiano huo, mtengenezaji anataka kutimiza malengo yake mwenyewe na kukumbukia mapungufu yake mwenyewe, kwani juhudi zote za mwanadamu ni msongo wa kutoka kwenye uwezekano na kwenda kwenye hali halisi na kutoka kwenye mapungufu kwenda kwenye ukamilifu.

Hata hivyo, sifa hizi mbili hazitumiki katika uhusiano baina ya vitu vilivyoumbwa, na yule muumbaji - Mwenyezi Mungu. Uhusiano baina ya seheMwenyezi mu tofauti na kazi za Mwenyezi Mungu ni wa kimaumbile, na lengo la kiumbe kilichoumbwa halina uhusiano na Muumbaji. Yakiwekwa mbalimbali, makusudio ya matendo ya Mwenyezi Mungu yote yanahusiana na matendo yenyewe, si kwa Wakala, kwa kuwa hekima ya Mwenyezi Mungu inalazimu kwamba Yeye apaswe kusababisha viumbe wote kufikia ukamilifu wao.

Wakati wa kutengenezwa hoja ya mpangilio wa ulimwengu tunajaribu kuthibitisha kuwepo kwa mtengenezaji afananaye na mtengenezaji binadamu, mtengenezaji wa ki-Mungu, kwa kweli, pia atakuwa kiumbe kilichoumbwa kwa kiwango cha mwanadamu; kuthibitisha kuwepo kwa mtengenezaji kama huyo ni jambo tofauti kabisa na kuthibitisha kuwepo kwa Mtengenezaji na Muumbaji wa viumbe wote. Kwa mtazamo wa kisayansi, kujianzisha mwenyewe kwa jambo hakuwezekani; ile nadharia ya ki-Marx kwamba dunia ya kimaada wakati wote anabadilika na kuelekea kwenye hali za juu zaidi ni dhahiri inapingana na kumbukumbu za kisayansi na ukweli wa kimaumbile. Mielekeo yote na misongo katika nyanja ya madini ninatokana ama kwa sababu ya kuingilia kati kwa utashi nje ya vitu au mvutano, kubadilishana, na ukusanyikanaji na maumbo mengine.

Katika ulimwengu wa mimea, maendeleo, kukua na kuongezeka hutokea kama matokeo ya kunyesha mvua, mwanga wa jua na kupata yale madini muhimu kutoka kwenye udongo. Hali ni ile ile kwa ulimwengu wa wanyama. Hali ni ile ile kwa ulimwengu wa wanyama, isipokuwa kwamba hapo kipengele cha mwendo wa hiari kuelekea kile chenye manufaa na muhimu lazima kiongezwe. Katika mifano yote iliyotajwa hivi punde, kuna ushirikiano wa wazi baina ya vitu na viumbe, kwa upande mmoja, na mambo yaliyopo nje yao kwa upande mwingine. Kwa mujibu wa sifa pekee za asili ndani ya kila kiumbe na sheria na kanuni ambazo zinakitawala, haziwezi kukiuka amri ambazo zimepigwa mhuri katika umbile lake.

Ukweli wa kwamba mwanadamu hutambua kwa hisia zake una sifa fulani za pekee. Tunatambua wazi kwamba viumbe katika dunia hii vinapatwa na mabadiliko ya mara kwa mara na hali ya kutokudumu. Kakita kipindi chote cha kuwepo kwake, kiumbe chochote cha kimaada ama kinakwenda kwa kupitia mkondo wa kukua na kuendelea au kuelekea kwenye kuoza na kudhoofika. Kwa ufupi, hakuna kiumbe cha kimaada katika hatua ya uhai wake kinabakia kama kilivyo na hakibadiliki.

Kuwa na kikomo ni sifa nyingine ya uhai wa kihisia. Kutoka kwenye chembechembe ndogo sana hadi kwenye kundi kubwa la nyota, vitu vyote vinahitaji nafasi na muda; ni kawaida kwamba vitu fulani huchukua nafasi kubwa zaidi au muda mrefu zaidi; na vingine, huchukua muda mfupi zaidi na nafasi ndogo zaidi. Zaidi ya hayo, viumbe vyote vya kimaada vina uhusiano kwa mtazamo wa kuwepo kwao na pia sifa vilivyonazo; sifa yoyote ile kama vile uwezo, utukufu, uzuri na hekima ambazo tunazozitoa kwa vitu, tunafanya hivyo kwa kulinganisha na vitu vingine.

Kutegemea na hali ya kimasharti pia ni miongoni mwa sifa za viumbe hivi. Kuwepo kwa kiumbe chochote tunakowezakutambua kunategemea na ni kwa masharti ya vipengele vingine, na kwa hiyo, kinakuwa kwenye kuvihitajia vipengele hivyo. Hakuna kiumbe kinachoweza kuonekana duniani ambacho kinajitegemea chenyewe tu, ambacho hakina haja na kitu kingine chochote isipokuwa chenyewe tu. Kuhitaji na kutegemea, kwa hiyo, huvizingia viumbe vyote.

Akili na fikara ya mwanadamu vinaweza kuvuka mapazia ya muonekano wa nje, tofauti na hisia zake, na kupenya vina na kadiri za ndani zaidi za kiumbe; vitu hivyo haviwezi kukubali kwamba uhai lazima uwekewe mipaka kwenye viumbe vyenye uhusiano, kikomo, mabadiliko na utegemezi. Kinyume chake, uwezo wa kufikiri kwa dhahiri hutambua umuhimu wa kuwepo, nje ya uwezekano wa kuchunguzika, ukweli thabiti, usiopingika na wenye kujitosheleza ambao juu yake viumbe vingine vinatumainia na kutegemea. Ukweli huu upo wakati wote na mahali popote, endapo haungekuwepo, ukamilifu wa dunia ungekoma kuwepo na ungepoteza ulingano wote wa uhai.

Mara tunapoona utegemezi wa dunia iliyoumbwa na kutambua kwamba hakuna kitu kinachoweza kuwepo bila ya kusaidiwa, tunahitimisha kwamba kuna "Kilichopo kwa Lazima," kwani tunalazimika kuhoji, "ni juu ya kitu gani ambacho kila kiumbe hatimae hutegemea?" Endepo tutajibu, "Hutegemea kiumbe kingine," halafu lazima tuulize, "kiumbe hicho na chenyewe hutegemea nini?" endapo basi jibu litatolewa "Hutegemea kitu ambacho sisi hatujui asili yake," swali linajitokeza, "Je kitu hicho ni cha peke au changamani?"

Kama jibu litakuwa "changamani" halafu tunajibu kwamba changamani pia ni tegemezi juu ya sehemu zake, kwani kwanza kabisa hizo sehemu lazima ziwepo ilihiyo changamani itokee kuwepo. Kwa kuwa maumbile ni changamani, hayawezi kuwa ndiyo 'Kilichopo kwa Lazima.' Kwa hiyo, tunalazimika kusema kwamba kisababisho cha kwanza lazima kiwe peke. Pia lazima kiwe ndani ya mpaka au maana moja na kile 'Kilichopo kwa Lazima,' kwani mlolongo wa kisababisho hauwezi kuendelea bila mpaka.

Ujumla wa dunia, kwa hiyo, unahitaji ukweli ambao unajitegemea na ambao humo ndimo vitu vyote vyenye masharti, ukomo na uhusiano vinamotegemea. Vitu vyote vinauhitaji ukweli huo ili kuvijaza uhai, na viumbe vyote vyenye uhai vinakuwa na dalili ya uhai wake wa milele, ujuzi, uwezo na hekima. Kwa hiyo, vinaturuhusu sisi kupata ujuzi wenye manufaa kuhusu ukweli huo na kumwezesha kila mtu aliye na akili, mdadisi kufasiri kuwepo kwa Muumbaji.

Kutegemeana kwa pande mbili kwa maada na kanuni za uhai kwa namna yoyote ile hakuelekezi kwenye kujitegemea kwa vitu vya kimaada. Kinyume chake, mambo tofauti yanayotokea kwenye maada, pamoja na uhusiano wao wa karibu, yanaonesha kwamba maada, katika namna yake ya maisha, hulazimika kukubali na kufuata kanuni fulani na desturi ambazo huyasukuma kwenye utaratibu na uelewano. Uhai unategemea juu ya vipengele viwili muhimu. Maada na utaratibu, ambavyo vinahusiana kwa karibu sana na huzaa dunia inayoeleweka na yenye utulivu. Baadhi ya watu huchukulia maada kama yenye kujitegemea na hudhania kwamba yenyewe imepata uhuru huu na kufafanua zile kanuni ambazo zinaitawala. Lakini ni vipi wanaweza kuamini kwamba haidrojeni na oksijeni, elektroni na protoni, zipaswe kwanza kujizalisha zenyewe, halafu ziwe chanzo cha viumbe vingine vyote, na hatimaye kuamuru kanuni zinazojirekebisha zenyewe na ulimwengu wote wa maada?

Uyakinifu unadhania kwamba vitu duni ndio chanzo cha kutokeza vitu vya hali ya juu bila ya kusumbuka kuhakikisha kama kile kitu cha hali ya juu kwa kweli, kinakuwepo katika kiwango cha kile duni. Kama mata ya kiwango duni haiwezi - hata katika kiwango cha juu sana cha maendeleo yake yaani fikra na tafakuri - ama kujiumba yenyewe au kukiuka mojawapo ya kanuni ambazo hutawalia juu yake, kwa hiyo ina maana isiopingika kwamba haiwezi kuumba viumbe vingine na kanuni zinazovirekebisha. Ni vipi, basi inaweza kuaminika kwamba mata duni ingejishughulisha katika uumbaji na uanzishaji wa viumbe vya hali ya kiwango cha juu au kuwa na uwezo wa kutoa uhai kwa vitu vya juu sana? Katika sayansi mpya ya mifumo, kanuni imethibitisha kwamba mifumo yenye elementi zenye uhai ambazo zina lengo au mifumo iliyopangika kwa nje kwa msingi wa programu iliyowekwa, zinaweza kuendelea kwenye mwelekeo wa kupanuka, utaratibu mkubwa zaidi na uboreshaji. Hata hivyo, mifumo yote, ama ya peke au changamani, inahitaji kusaidiwa na, na kuhusishwa na vipengele vya nje yao yenyewe, haziwezi kujijenga zenyewe. Hakuna mfumo au kitu humu duniani kitakachoweza kuumba au kutia utashi kwenye kiungo kinachotembea na kukua isipokuwa kiwe kina kiwango fulani cha dhamira na ufahamu.

Yakiwa yametegemezwa kwenye kanuni ya uwezekano, matokeo ya hamasa huru ya fani zote yanaweza kuwa tu ya mtawanyiko na vurugu, yakielekea kwenye kifo cha namna moja. Kanuni ya uwezekeano pia inakanusha wazi wazi kutokea kwa dunia kwa njia ya kubahatisha, na kuiona kuwa haina mantiki na haiwezekani. Hata makadirio yaliyofanywa kwa msingi wa kanuni ya kimahesabu ya uwezekano yanathibitisha umuhimu wa mwongozo ulio sahihi na upangaji kwa ajili ya dunia, kwa kukubaliana na programu iliyo sahihi na dhamira ya fahamu.

Kwa kweli kanuni ya uwezekano inatoa pigo la uhakika kwa wale wanaoamini nadharia ya kutokea kwa dunia kwa bahati. Endapo tutajaribu kutumia nadharia ua ajali kwenye mfumo wa kawaida au tarakimu ndogo, utumikaji wake ni wenye kuwezekana, ingawaje hauelekei kabisa. Lakini haieleweki kwamba mtu aweze kubahatisha kamwe kwa njia ya ajali ya kijometri kuelezea mpangilio imara na wenye utulivu uliopo kwenye mfumo changamani wa dunia. Mabadiliko ya kiasi na ya kawaida kwenye mpangilio wa maisha pia hayawezi kuuelezea mgeuko wa dunia; muungano wa elementu zilizo tofauti, na mchanganyiko wa chembechembe za asili kuunda mchanganyiko unaowiana.

Ikiwa kama wakati fulani maumbile yalijishughulisha kwa kujitawala katika kazi za sanaa na utengenezaji, kwa nini sasa hayaonyeshi hatua yoyote katika mwelekeo wa kujibadilisha yenyewe zaidi ya hapo; kwa nini hayaonyeshi tena mabadiliko makubwa yanayojiendesha yenyewe? Hata matukio madogo na ya kawaida hapa duniani husababishia uumbikaji wa sura za kipekee ambazo zinawiana na kuafikiana na lengo la maumMwenyezi bile.

Hii peke yake, yenyewe ni dalili ya ule ukweli kwamba nyuma ya mabadiliko yote makubwa, kuna nguvu makini na yenye uwezo mkubwa inayojishughulisha katika kuumba na kuzalisha mpangilio wa maajabu ya ulimwengu: inatoa umbo kwenye udhahiri wa kipekee wa dunia ya maumbile na kuashiria mpango na utaratibu wa uhai.

Uwiano na upatanishikaji wa mamilioni ya vitu vya maumbile na uhusiano wao kwenye uhai unaweza kuelezwa juu ya msingi wa nadharia moja tu - yaani kwamba tunamtambua kuwepo kwa Muumbaji juu ya mfumo huu mpana Ambaye ameasisi chembe zinazotofautiana za uhai juu ya duniani hii kwa njia ya uwezo usio na mipaka na ukomo na kutayarisha programu kwa ajili ya kila mojawapo ya chembechembe hizo za uhai. Nadhari hii ni kwa kulingana na uhusiano mtulivu ambao tunaouona umewekwa ndani ya viumbe.

Kama hatutakubaliana na nadharia hii, upo uwezekano gani kwamba utulivu wa aina hii ungetokea - ki-ajali na bila madhumuni - miongoni mwa taratibu nyingi za uhai? Ingeaminikaje kwamba mata yenyewe iwe chanzo cha mamilioni ya sifa na tabia na kwa hiyo kuwa inayolingana na Muumbaji mwenye madhumuni, hekima na mjuzi wa yote? Endapo dunia ya uhai isingekuwepo, pamoja na maajabu yake ambayo yanastaajabisha akili na uzuri ambao ujuzi wa mwanadamu hauwezi kufahamu kikamilifu, na endapo ulimwengu ungekuwa na kiumbe cha seli moja tu hai, bado uwezekano kwamba kitu kidogo na kisichokuwana thamani, pamoja na mpangilio uliopo juu yake na hali ya lazima na vifaa kingekuja kuwepo kama bahati tu, uwezekano, ajali, uwezekano kama huo unaashira, tarakimu ndogo sana ambayo haiwezi kueleweka kimahesabu, kwa mujibu wa bingwa wa baiolojia Mswisi aitwaye Charles Unguy.

Chembe zote za viumbe hai, katika maumbo yao ya ndani na uhusiano wao, zinategemea mpangilio ulioimarika. Kujengeka kwao na uhusuano uliopo baina yao ni wa namna ambayo husaidiana zenyewe ili ziendelee kwenye njia zao husika hadi kwenye malengo yaliyoko mbele yao. Zikinufaika kutokana na uhusiano zilionao kwa viumbe vingine hai na kutokana na kuambukizana athari kwao kama livyodhamiriwa na uundwaji wao wenyewe, zina uwezo wa kuelekea kwenye malengo na mwisho wa safari yao.

Mafanikio makubwa ya sayansi ya maada ni kutambua sura na sifa za nje za dunia; kutambua asili na mumbile hailsi ya viumbe vilivyoumbwa na matukio kupo nje ya upeo wa uelewa wa sayansi hizo. Mathalani, mafanikio makubwa sana ambayo mnajimu anaweza kupata, ni kujua kama mabilioni ya matufe kule angani hayabadiliki wa kusogea kwa sababu ya kani-pewa au kama yanaendelea kubiringika ambapo nguvu ya uvutano huyazuia yasigongane na kudumisha utulivu wao. Inaweza pia kupima umbali wao kutoka hapa ardhini na kasi ya mwendo wao na ukubwa kwa njia ya zana za kisayansi. Hata hivyo, hatima ya matokeo ya ujuzi huu wote na majaribio hayavuki upeo wa tafsiri ya nje na ya juujuu ya vipengele vya maumbile, kwani mnajimu (bingwa wa elimu ya anga) hawezi kutambua asili halisi ya nguvu ya mvutano, chimbuko la kani-pewa au namna ya jinsi zilivyo na ule mfumo ambao zinauatumikia vilivyojitokeza kuwepo.

Wanasayansi wanaweza kutafsiri mashine bila kutambua tafsiri ya hiyo nguvu mwendo. Sayansi asilia vivyo hivyo hazina uwezo wa kutafsiri na kuchanganua mamilioni ya mambo ya ukweli ambayo yamewekwa katika maumbile na ndani ya mwanadamu. Mwanadamu amechimba kwenye kiini cha chembe lakini ameshindwa kupata ufumbuzi wa miujiza migumu na iliofichika ya chembe hai moja. Kwa ufupi, ni ngome hizi za miujiza ambazo mabingwa wa sayansi asilia wamekuwa hawana uwezo wa kuzishinda.

Mojawapo ya maajabu ya maumbile ni ule uwiano wa maafikiano uliopo baina ya vitu viwili ambavyo sio vya wakati mmoja. Ulinganifu huu ni wa hali ambayo kwamba mahitaji ya kitu ambacho bado hakijatokeza na kuwepo, tayari yameandaliwa kwenye umbile la kitu kingine. Mfano mzuri wa aina hii ya uwiano unaweza kuonekana kwenye uhusiano baina ya mama na mwana. Miongoni mwa binadamu na mamalia wengine, mara mwanamke anapobeba mimba na jinsi kilenge kinavyokua ndani ya nyumba ya uzazi, tezi ambazo hutengeneza maziwa - aina nzuri na changamani ya lishe - huanza kufanya kazi kwa mvuto wa homoni maalumu. Jinsi kilenge kinavyoendelea kukua, ndivyo lishe hii yenye virutubisho inavyoongezeka wingi wake ili kwamba pindi kilenge kinapokuwa kwenye mlango wa kizazi na kipo tayari kuingia katika dunia hii pana isiyo na mipaka, kirutubisho hiki kinachohitajiwa na mtoto na kinachofaa kwa mahitaji yake yote ya kimwili kinakuwa kipo tayari.

Kirutubisho hiki kilichokwishatengenezwa tayari, kimepatanishwa kabisa na mfumo ambao bado mchanga, wa kusaga chakula wa mtoto. Kimehifadhiwa kwenye ghala iliyofichika - titi la mama, ghala ambayo alipewa mama miaka mingi kabla kichanga hakijapata umbo. Ili kuwezesha ulishaji wa mtoto alliyezaliwa mara, vijitundu vidogo na laini vimewekwa kwenye chuchu za titi lenyewe - kwa kipimo kinacholingana na mdomo wa mtoto - ili maziwa yasitiririke moja kwa moja kwenye mdomo wa mtoto ambaye kwa wakati huo hana uwezo wa kuyameza mwenyewe. Badala yake mtoto anayapata riziki ya kila siku anayoihitaji kutoka kwenye hazina hiyo kwa njia ya kunyonya.

Jinsi mtoto aliyezaliwa anavyozidi kukua, ndivyo mabadiliko yanavyofanyika kwenye maziwa ambayo yanaunganishwa na umri wake. Ni kwa sababu hii kwamba madaktari wa tiba wanaamini kwamba kunyonyeshwa mtoto mchanga aliyezaliwa punde na mama mwingine ambaye siye aliyemzaa, wakati mwingine si jambo la busara kushauriwa. Hapa swali linajitokeza; si kweli kwamba mahitaji ya kiumbe kutengenezwa kwenye umbile la kiumbe kimoja, kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya kiumbe kingine ambacho bado hakipo, ni jambo ambalo kimepangwa na kutabiriwa kwa msingi wa hekima na usahihi? Je, sio kwamba matayarisho haya kwa ajili ya siku zijazo, uhusiano huu wa kistadi na wa kushangaza baina ya viumbe viwili, ni kazi ya nguvu yenye uwezo na hekima isiyo na mfano? Si kwamba hii ni dalili ya wazi ya kuingilia kati kwa nguvu isiyo na kikomo, mbunifu na mpangaji mkuu, ambaye makusudio yake ni kuendeleza uhai na kukua kwa vitu vyote kuelekea kwenye ukamilifu? Tunatambua vizuri kwamba mahesabu sahihi tunayoyaona kwenye misingi ya mashine zote na zana za viwandani ni matokeo ya vipaji na fikra zilizoingizwa kwenye usanifu na utengenezwaji wao. Vivyo hivyo, kwa kutegemea uchunguzi wetu wa busara tunaweza kufikia uamuzi wa jumla wa kifalsafa kwamba popote pale ambapo mpangilio na ukusanyaji unaotegemea uwiano na makadirio unapotakiwa kufuatwa, dhamira, akili na mawazo lazima pia vitafutwe.

Usahihi huo huo ambao unaweza kuonekana kwenye mashine za viwandani ndio utakaoonekana katika kiwango cha juu zaidi na kipekee katika viumbe asili na uumbwaji wao. Hakika kiwango cha maandalizi na mpangilio unaoonekana kwenye maumbile upo katika daraja ya juu sana hivyo kwamba usahihi alioumaliza mwanadamu katika ubunifu wake hauwezi kwa hali yoyote ile kulinganishwa nacho. Wakati bila kusita, tunapotambua kwamba utaratibu wetu wa viwanda ni matokeo ya fikira na mawazo, hatupaswi sisi kuutambua utendaji wa akili isiyo na kikomo, dhamira na ujuzi uliopo kwenye mpango sahihi wa maumbile?

Katika zama hizi, elimu ya madawa imefika katika kiwango cha maendeleo ambacho kinakiruhusu kuondoa figo kutoka kwenye mwili wa binadamu na kuipandikiza kwenye mwili wa mtu ambaye figo zake zimekwama kufanya kazi na ambaye anakaribia kufa. Maendeleo haya kwa uhakika si matokeo ya juhudi ya daktari moja pekee; hii inatokana na urithi wa milenia kadhaa. Shughuli ya upandikizaji sasa ndio hatua ya mwisho katika mlolongo mrefu ambao hatua zake za mwanzo zilikamilishwa na wanasayansi wa siku za mwanzo; mawazo na utambuzi wa wanasayansi yalikuwa yakusanywe kwa miaka elfu kadhaa kabla ya kupandikiza figo kuweza kutokea.

Je, inawezekana kwamba matokeo haya yaweze kupatikana bila ujuzi? Bila shaka hapana: akili za binadamu uwezo mkubwa zililazimika kufanya kazi kwa miaka elfu kadhaa ili upandikizaji wa figo upate kuwezekana. Sasa na tuulize swali jingine. Ni lipi linahitaji ujuzi mwingi na akili zaidi: ni kubadilisha tairi kwenye gurudumu la gari - kazi ambayo inahitaji kiasi fulani cha ufundi stadi - au utengenezaji wa tairi lenyewe? Kazi ipi iliyo ya umuhumu: kutengeneza tairi au kubadilisha tairi? Ingawaje kupandikiza figo ni kazi muhimu katika tiba, inafanana na kubadilisha tairi kwenye gurudumu la motokaa; kazi hii inakosa umuhimu ikilinganishwa na ile ya kutengeneza umbo la figo yenyewe na ile miujiza, ustadi na mahesabu iliyonayo.

Mwanasayansi gani halisi, aliyetawaliwa na uaminifu katika kutafuta ukweli anayeweza kudai leo hii kwamba, wakati ambapo upandikizaji wa figo ni matokeo ya mfululizo wa utafiti wa majaribio ya kisayansi ya karne nyingi, umbo la figo yenyewe halioneshi dalili ya akili bunifu na dhamira, kuwa ni matokeo ya maumbile tu - maumbile yasiyo na ujuzi zaidi au utambuzi kuzidi mwanafunzi wa shule ya chekechea?

Haitakuwa na mantiki zaidi kuweka nadharia ya kuwepo kwa akili, dhamira na maandalizi katika uumbaji na utaratibu wa ulimwengu kuliko kuhusisha uumbaji kwenye mata kitu ambacho hakina akili, mawazo, umakini na uwezo wa kuanzisha mambo mapya? Imani juu ya kuwepo kwa muumbaji mwenye hekima bila shaka ina mantiki zaidi kuliko kuamini katika ubunifu wa mata, kitu kisichokuwa na ama utambuzi, umakini wala uwezo wa kupanga, hatuwezi kuzihusisha kwamba zitokane kwenye maada, tabia na sifa zote za akili tuzionazo hapa duniani na utashi wa mpangilio inaouonyesha.

Mufadhal alimwambia Imam Sadiq(a.s) : "Bwana! baadhi ya watu hudhani kwamba huu utaratibu na usahihi tuuonao hapa duniani ni kazi ya maumbile." Imamu akamjibu:"Waulize kama maumbile hufanya kazi zake zote zilizokadiriwa kwa usahihi kwa mujibu wa elimu, mawazo na uwezo wake yenyewe. Kama watasema kwamba maumbile yana elimu na uwezo, kuna kitu gani kinachozuia wao kupinga lile chimbuko la milele la ki-ungu na wakakiri kuwepo kwa hiyo kanuni kuu? Endapo kwa upande mwingine watasema kwamba maumbile hufanya kazi zake kwa kawaida na kwa usahihi bila matumizi ya ujuzi na utashi basi kinachofuata ni kwamba shughuli zote za hekima na zilizo sahihi, sheria zilizopangwa vizuri ni kazi ya muumbaji mjuzi na mwenye hekima. Kile ambacho wao wanakiita maumbile, kwa kweli, ni sheria na kawaida zilizowekwa na mkono wa uwezo wa ki-mungu ili zitawale maumbile." [16] Ustadi wa maumbile.

Mfikirie mbu wa malaria. Hakuna haja ya kutumia darubini; unaweza kutambua mpangilio sahihi na changamano uliomo kwenye kiumbe kile kisicho na thamani kwa matumizi ya kawaida ya jicho tupu. Ndani ya kiumbe hiki dhaifu mnakuwemo na seti kamili ya viungo na milango ya fahamu, ya kipekee kwa usahihi wao: mfumo wa kusaga chakula tumboni, mfumo wa mzunguko wa damu, mfumo wa neva, mfumo wa kupumua. Mbu anayo maabara iliyoandaliwa kwa vifaa: kwa usahihi na kasi ya ajabu, itengeneza vitu vyote anavyovihitaji. Mlinganishe mbu na maabara ya kisayansi: pamoja na nguvu zote za kibinadamu na kiuchumi zilizomwagwa juu yake, maabara hiyo haiwezi kamwe kupata kasi, umakini na usahihi wa maabara inayodharaulika ya mbu. Ni muda kiasi gani, tafakuri na akili vinavyohitajika, kwa mfano, kutengeneza tiba kwa ajili ya ule uumaji wa mbu tu!

Wakati ambapo upangaji mwingi, mawazo na usahihi vinahitajika kwa mtu kufanya kazi kama hii, hivi huu ustadi, usahihi na utaratibu unaoonekana duniani, sio uthibitisho wa chimbuko linalotokana na akili, maandalizi bunifu na busara ya kiwango cha juu ya huyo muumbaji? Hivi inawezekana hata kidogo kufikiria jometri yote sahihi, utendaji wa mwendo wa ulimwengu kuwa ni matokeo ya mata, na kukosa elimu kwake? Tunatamka kwa dhati kabisa kwamba jambo la maumbile linaonyesha mpangilio na utaratibu; haya hayatangazi kutokuwa na lengo, vurugu na machafuko.

Endapo nyakati fulani tunaona dalili za dosari katika maumbile hii haina maana ya kuwepo kwa upungufu au kasoro kwenye kitabu kikubwa cha uumbaji. Fikira na utambuzi wetu haviwezi kupaa na kuruka angani na uwezo wa akili zetu ni mfupi mno kuweza kuelewa miujiza na vitendawili vyote vya ulimwengu. Akili zetu haziwezi kuvumbua azma na malengo yote ya uhai. Kama hatuwezi kuelewa kazi ya skrubu ndogo kwenye mashine kubwa, sasa basi, hali hii inatupatia sisi haki ya kumshutumu na kumlaani mbunifu kwamba ni mbumbumbu? Au ni kwamba upeo wetu wa kukodoa macho ni mfinyu mno kuweza kuelewa lengo na madhumuni halisi ya mashine hiyo?

Bahatisho haliwezi kufanya kazi ya elimu, elimu, ambayo zaidi ya hayo, haikuchanganyika na ujinga kwa hali yoyote ile. Ikiwa, kama wayakinifu wanavyodhani, dunia ya maumbile haikutokana na elimu na utashi (licha ya dalili za uumbaji na ubunifu unaoonekana wazi katika kila kiumbe) halafu, mwanadamu pia ili aweze kufanikisha malengo yake atalazimika kuacha maendeleo yake kwenye mkondo wa elimu na kujifunga mwenyewe kwenye ujinga ili aweze kutenda kufuatana na kule kutokujitambua kwa maumbile yenyewe. Ile hali halisi inayoongoza na kuelekeza utendaji wa dunia kwa utaratibu na mpangilio wa namna hiyo una lengo, madhumuni na dhamira, mambo ambayo hayawezi kukanushwa. Haiwezi kudhaniwa kwamba mlolongo wa utendaji usiokatika na athari zake huendelea kuelekea upande maalum bila uingiliaji na uangalizi wa akili fulani.

Baada ya miaka mingi ya maandalizi yaliyofanywa kwa uangalifu na kazi ya kuchosha mabingwa wa sayansi ya biokemia wamefaulu katika kugundua mfumo fulani wa majaribio katika kiwango cha kawaida na cha chini ambao kutoka humo dalili zote za uhai zinakosekana. Ushindi huu wa kisayansi ulionekana kuwa na manufaa sana na ulipokelewa kwa shauku kubwa katika duru za kisayansi, na hakuna mtu aliyedai kwamba uumbaji huu wa maabara wenye upungufu mkubwa na wa kiwango cha chini sana uliotokeza kuwepo kama matokeo ya bahati, bila ya mwelekeo, maandalizi na usahihi.

Hali ikiwa ni hivi, wale wanaohusisha viumbe vyote viliyomo kwenye mfumo mpana wa ulimwengu, pamoja na sifa zake changamani na za kimwujiza kwenye nguvu povu na zisizo na fahamu za mata, kwa kweli wanaifanyia vurugu na udhalimu mantiki na akili ya binadamu na kuendesha vita vya wazi dhidi ya ukweli. Weka mazingatio yako kwa dakika moja tu juu ya mtayarishaji wa chapa kwenye kiwanda cha uchapishaji. Yeye anachukua hadhari na uangalifu mkubwa anapozipanga herufi zinazotakiwa kwa ajili ya ukurasa mmoja wa kitabu, lakini anapoirudia kazi yake, anakutana na makosa madogo madogo yatokanayo na kukosa umakini kidogo tu. Mtayarishaji wa chapa angekuwa achukue herufi chache kiganjani na kuzisambaza kwenye bamba badala ya kuzipanga kwa uangalifu katika mistari, je, itawezekana kwa vyovyote vile kwamba ukurasa utakaotokea uweze kuwa sahihi katika maudhui na kutokuwa na kosa lolote?

Itakuwa bado ni upumbavu zaidi kudai kwamba kila mia moja za risasi iliyoyeyushwa, ikashindiliwa kwenye tyubu, itatokeza katika hali ya herufi ambazo zimetengenezwa tayari; na kwamba dhoruba kali iweze kuzichukua herufi hizo na kuzipanga kwenye mpangilio na utaratibu maalum unaokubalika, kwenye maelfu ya mabamba ya chuma, na kwamba mabamba haya yaishie kwenye kuchapishwa kitabu chenye kurasa elfu moja chenye maudhui nyingi sahihi za kisayansi na maelezo ya kuvutia na kushawishi, yote haya yafanyike bila hata kosa dogo kutokea. Kuna mtu yoyote anayeweza kuiunga mkono nadharia hii?

Wayakinifu ambao hukanusha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu wana nini cha kusema kuhusu kutokeza kwa maumbo tofauti ya herufi za maumbile na uhusiano ulio sahihi na changamani ambao hudhibiti viumbe vya mbinguni, maumbile asilia na vitu vyote vya kimaada? Je, herufi za maumbile (yaani atomu na chembechembe zinazoziunda) zinaweza kuwa hazina maana kuliko herufi zitumikazo katika uchapishaji? Inawezekana kukubalika kwa namna yoyote ile kwamba hizi herufi zenye mpangilio na maana, jometri hii iliyo sahihi na iliyoandaliwa vizuri maumbo ya kushangaza yanayofafanuliwa kwenye kitabu cha uumbaji, iwe ni kazi ya kijinga na isiyo na malengo? Kwamba nguvu kuu na yenye hekima, kanuni ya mpangilio ya kimwujiza, isiwepo kwenye muonekano wenyewe wa dunia? Je, mambo yote sio kwamba yanachipukia kutokana kudhihiri kwa ufahamu, utambuzi na uwezo?

Endapo uwezo uliofichika kwenye vina vya mata hautokani na akili ya fani zote, ni jambo gani linauongozo kwenye ufafanuzi wa maumbile, kwenye utaratibu na uwiano wa kushangaza? Ikiwa uwezo huo ni wakala asiye na akili na fahamu, kwa nini basi haujaangukia kamwe kwenye vurugu, na kwa nini mchanganyiko wake wa mata kamwe hausababishi mgongano na maangamizi? Hapa ndipo ambapo imani ya kuwepo kwa muumbaji inaleta maana juu ya maada yote na hujaalia dunia kuwa na maana na kutosheka. Wale wenye mtazamo wa mbali na fikra safi za wazi hutambua dhahiri kwamba uwezo usio na ukomo ndio unaohakikisha utunzaji wa mpangilio wa dunia kwa njia ya usimamizi ulio madhubuti na mamlaka kamili.

Zamani, kila mtu alikuwa akimwongoza na kumdhibiti mnyama wake wa kipando, na vile vile alikuwa na desturi, katika zama zote, ya kumuona mmiliki au msimamizi anayesimamia sehemu ya rasilimali, kila kipande cha ardhi isiyotumika, kila kundi au chama. Sasa mambo yamebadilika. Mwanadamu wa kisasa anaweza kutengeneza setilaiti inayoendeshwa toka mbali, ala za elektroni na ndege zisizo na rubani, vyote hivi vikiwa vimetayarishwa kwa vifaa vinavyojiendesha vyenyewe. Kila mtu anajua kwamba inawezekana kutengeneza mashine yenye vifaa vyote ambayo inaweza kufanya kazi kwa namna nyingi zinazofaa kwenye hali yoyote itakayojitokeza, bila mtengenezaji wa chombo hicho kuwepo au kuonekana. Kwa hiyo, hatuna tena haki ya kukataa kuwepo kwa Mwenyezi Mungu kwa ukaidi tu kwa sababu mkono Wake hauonekani haufanyi kazi kwa kuonekana katika mambo ya uumbaji - kwa kuonekana, yaani kwa uelewa na elimu yetu yenye upungufu.

Kwa kweli, ungekuwa ni ufananishaji wenye upungufu mkubwa endapo tungemlinganisha mtengenezaji setilaiti au roketi bandia, ambaye ameketi kwenye kituo chenye vifaa vyote hapa ardhini na kwa msaada wa vifaa changamani anaongoza na kudhibiti njia na mwendo wa chombo cha angani. Lakini kama uingiliaji kati wa mkono wa Mwenyezi Mungu kwenye mpangilio wa maumbile hauonekani kwa jicho letu la kawaida na utambuzi wetu (ingawaje tunaweza kuona dalili na ishara ambazo zinafanana na mwale unaoendelea kutoka kwenye fahari ya utukufu wake) tunaweza kwa sababu hiyo kutotilia maanani kuwepo kwa mpangaji na mwendeshaji ambaye peke yake ndiye elimu ya dhati, uwezo na utashi halisi, kwa sababu tu kwamba hawezi kudhibitiwa ndani ya mfumo finyu wa muda na nafasi.

Ni kweli kwamba uwezo wetu wa kuelewa nafsi ambayo haifanani wala haina mfano na chochote katika himaya ya hisia na ambayo lugha ya kibinadamu haiwezi kuieleza kikamilifu na kwa usahihi ni mfinyu sana. Taa ya akili zetu hutoa mwanga mdogo kwenye uwanda huu usio na ukomo, au - kwa lugha nyingine tofauti - unakabiliana na kuta za mipaka. Wakati huo huo uhusiano wetu katika dunia hii upo juu ya matukio; lile ambalo litajiingiza lenyewe kwenye akili zetu linakuwa na miali ambayo hugunduliwa na kaida za dunia yenye busara. Lakini katika kuitambua dunia hiyo, tatizo la kuidhania linaondolewa kwetu; hakuna kipingamizi kilichopo baina ya fikira zetu na kile kiasi muhimu cha ufahamu.

Hata hivyo, watu fulani wenye kushuku ambao wameutelekeza mtindo thabiti wa fikra ambao unatokana na asili ya msingi ya mwanadamu na ambao wamekuwa, kimipaka kabisa, na mazoea ya uhai wenyewe hasa wa maumbile wakati wote wakingojea kutokea muujiza kutoka kwa Mwenyezi Mungu ambao utavunja utaratibu uliopo wa muumbo ili kufanya zawadi kwao ya itikadi na imani, na kufanya kuwepo Kwake (Mwenyezi Mungu) kueleweka na kukubalika bila kusita. Hata hivyo, watu hao hawatilii maanani kwamba dalili na ishara zozote mpya za Mwenyezi Mungu zinazoweza kutokea zitasababisha msisimko mashaka ya muda tu, na kwa kupita muda, yatakuwa mambo ya 'kawaida' na hayatavuta nadhari tena.

Ingawa mambo yote sasa yamejumuishwa kwenye muundo wa mpangilio wa maumbile, yalianza kwa kuvunja mpango wa asilia, na kwa kuwa viumbe vyote vimerudiwa katika hatua za dunia tangu kudhihiri kwa mara ya kwanza, sasa vinaonekana kuwa vya kawaida na kuzoeleka. Kinyume chake, kiumbe kisichoweza kutambulika kihisia - kiumbe, ambacho zaidi ya hayo kimejaa fahari na utukufu na kilichojaa utakatifu na ukuu - kila mara kitavutia roho za wanadamu. Mazingatio yao kwa kiumbe kama hicho, kwa kweli kila wakati utaongezeka na wakati wote watakiangalia kwa kuhitajia.

Ni kutawaliwa na nafsi ya ukaidi, ya uamuzi uliotengenezwa kwenye mantiki isiyopatana, ambayo huifungia fikira ya kibinadamu kwa mipaka. Kwa kila kiumbe katika mpangilio wa kuwepo ni uthibitisho unaotosha kwa ajili ya wale wanaobana na kuweka tupu akili zao za ukaidi na sababu za ukanushaji.

2

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA PILI

UNDANI WA NAFSI YA MWANADAMU HUMLAZIMISHA KUMTAFUTA MWENYEZI MUNGU

Nje ya mfumo wa hisia za mwili wake, mwanadamu anayo maeneo makubwa mno na muhimu ambayo kwa hali yoyote ile hayakufungiwa katika utaratibu wa mwili wake. Ili kuweza kugundua vipengele hivyo na hatua zilizo nje ya muundo wa mwili na ukubwa wa kiwiliwili chake, mtu lazima atafute muundo wa ndani na wa kiroho wa binadamu na kufahamu ule upeo mpana wa asili yake yenye mambo mengi, pamoja na udhihiri nyeti na wa kiungwana wa hisia na silika zake.

Mlolongo wa namna maalumu za ufahamu zinakuwemo katika nafsi ya binadamu ambazo zimejiotea mizizi ndani yake zenyewe, zinachomoza kutoka kwenye namna hasa ya hulka ya mwanadamu, na na kuchomoza kwao hakupasiki na jambo lolote la nje ya mwili wake. Miongoni mwa tambuzi hizi ni hisia za kuwajibika kwenye amana, haki, kuwa mkweli na mwaminifu. Kabla hajaingia kwenye uwanja wa sayansi na ujuzi na vyote vinavyohusika navyo, mtu ana uwezo wa kutambua ukweli fulani kwa njia ya utambuzi huu wa asili. Lakini baada ya kuingia kwenye eneo la sayansi na falsafa na kuujaza ubongo wake na shuhuda mbali mbali na tasfiri ya mambo, anaweza akasahau tambuzi zake za kawaida na za asili au akaanza kuzitilia mashaka. Ni kwa sababu hii kwamba binadamu anapokwenda kinyume na tabia yake ya asili kufafanua imani kwa maneno, tofauti huanza kujitokeza.

Kuelekea kwenye dini na kumuamini Mwenyezi Mungu, katika hatua zake za mwanzo huvutia kwenye sababu za kisilika na tambuzi za asili, lakini halafu huendelea kukua na kugeuka kwa msaada wa mantiki na tafakari. Mizizi ya hisia asili katika silika za mwanadamu imekwenda ndani mno na wakati huo huo, huonekana wazi na dhahiri sana hivyo kwamba endapo mtu anatakasa akili yake na roho yake kuhusu fikira za kidini na zisizo za kidini na halafu akajiangalia mwenyewe na dunia ya viumbe, kwa wazi kabisa ataona kwamba anasonga kuelekea upande fulani akiwa na msafara mzima wa viumbe. Bila ya utashi wowote au hiari upande wake, huanza maisha yake mahali fulani, na halafu tena bila hiari yake husonga mbele kwenda mahali pengine ambapo hapajui. Na ukweli huu huu unaweza kuonekana juu ya viumbe vyote vya asili, vikijiendesha kwa namna ya usahihi na kwa mpango.

Endapo mtu anayeona vizuri, akiwa bado yu katika hali ya kimaumbile, atayaangalia mazingira yanayomzunguka, kwa wazi kabisa atahisi kuwepo kwa nguvu kuu ambayo inamzunguka yeye na dunia yote. Katika umbile lake mwenyewe, ambalo ni sehemu ndogo sana ya dunia kubwa, ataona ujuzi, nguvu na utashi wa kuishi, na atajiuliza ni vipi ujuzi, nguvu na utashi havingeweza kuwepo katika dunia kwa jumla. Ni huu mpango uliofanyiwa mahesabu kwa ustadi mkubwa na mwendo wa dunia ambao humlazimisha mwanadamu kukubali kuwepo kwa uwezo wa akili ya fani zote ambayo, ikiwa ipo nje ya dunia ya kimaumbile, lakini hata hivyo inaisanifu na kuiamuru, isipokuwa kwa kukubalika hili, mpangilio huu wa dunia hauwezi kuelezeka. Mtu yeyote anaye tathmini nafasi yake hapa duniani anaweza kutambua kwamba kuna nguvu inayomuumba yeye, ikamleta yeye hapa, inayomtia usongefu ndani mwake, na halafu tena humwondoa, bila ya ruhusa au msaada wake kutakiwa kwa ajili ya lolote katika haya.

Kiongozi mkuu wa mashahidi, Hussein bin Ali(a.s) alisema katika dua yake ya siri kwa Muumba wake; "Inawezekanaje kufasiri kuweko Kwako kutoka kwenye kitu ambacho kinakutegemea Wewe kwa kuwepo kwake? Kwa nini huna hali ya kudhihirika kama wengine wasio wewe waliyonayo, ili kwamba iweze kukufanya Wewe uwepo dhahiri? Ni lini ulifichika kamwe kutoka kwenye jicho la ndani ili labda uweze kuhitaji uthibitisho uwe kama mwongozo wa kuelekea kwako Wewe? Ni lini ambapo ulikuwa kamwe mbali na sisi hivyo kwamba ishara na dalili Zako labda zingeweza kutusogeza karibu na Wewe? Limepofuka jicho ambalo halikuoni Wewe unapolitazama kulilinda na kuliongoza!

"Ee Mwenyezi Mungu, Wewe ambaye umejidhihirisha Mwenyewe kwa ufahari wako, unawezaje kuwa umefichika ambapo unaonekana na kudhihirika? Unawezaje kuwa haupo ambapo kwa kuonekana kwako kusiko na ukomo unawaangalia waja Wako?"[3] Hapana mahali popote na wakati wowote ambapo kitu kimetengenezwa bila mtengenezaji wake kuonekana, wala tendo bila mtendaji. Utafutaji wa kiungo baina ya chanzo na athari hujitokeza kutokea kwenye silika ya ndani ya mwanadamu; utambuzi wa uhusiano hauwezi kuondolewa kutoka kwa mtu yeyote.

Vivyo hivyo, hisia za kidini, kumtafuta Muumba, pia haiwezekani kuondolewa kutoka kwa mtu yeyote. Hata mtoto ambaye hana uzoefu wa dunia, wakati wowote asikiapo sauti au aonapo msongo, ki-silika atageuzia nadhari yake kwenye chanzo cha sauti au msongo. Misingi yote ya maisha halisi na ujuzi inasimama kwenye kukubali sababu kwa kila athari. Kanuni ya uhusiano, kwa kweli ni dhahiri kabisa ambayo haitoi mwanya wowote. Jiolojia, fizikia, Kemia, elimujamii, uchumi - katika hizi na elimu zingine, utafiti una lengo la kubainisha sababu na mambo yanayoamua uhusiano. Kwa ufupi, ni dhahiri kwamba elimu na ujuzi si lolote zaidi ya utafutaji wa vyanzo; maendeleo na kusonga mbele katika mambo ya binadamu hutokana na uchunguzi unaofanywa na wasomi kuhusu vyanzo vya mambo.

Kama ingekuwa inawezekana sisi kugundua kutoka kwenye kiumbe kimoja au pembe moja ya ulimwengu alama ya kujianzisha au kujiumba chenyewe kikamilifu, tungeridhika katika kueneza mfano huo moja kwa mpangilio wote wa viumbe. Kama mambo yalivyo, si muhimu kwamba kanuni ya usababisho kila mara ijioneshe kwetu katika miundo inayojulikana. Aina mbalimbali na wingi wa vyanzo viko kiasi kwamba mtafiti anayejihusisha na jambo moja tu labda atashindwa kupambanua visababisho vyote. Hata hivyo, katika mambo yote ya mwanadamu, maalum na ya kawaida, yaliyopita na yajayo, katika mazingira ya mtu mmoja au ya jamii, hakuna nukta hata moja inyoweza kuonekana kuwa ya bahati mbaya.

Si tu kwamba upo mpangilio mahususi ambao ni wa asili katika kuumbwa kwa kila kitu peke yake; pia kunakuwepo na ya kuonekana katika uhusiano wa kila jambo na jambo jingine, vile vile na uhusiano wa kila kitu na mazingira ambamo kinakuwemo, utaratibu stadi uliokokotolewa vizuri sana. Mathalani, katika kuukuza mti, kanuni za anga na ardhi zinafanya kazi katika uelewano kamili na muundo wa mizizi na matawi yake. Pia upo uhusiano wa wanyama na mti ule kwa vile wanapata chakula kutoka humo. Inawezekanaje kwamba pawepo na bahati mbaya katika asili ya utaratibu wa uhusiano wa aina hiyo?

Endapo jambo lingepata umbo katika ngazi fulani katika muundo wa kiumbe, bila kufahamu na katika misingi ya kubahatisha, hali hii ingetoa maandalizi mazuri sana kwa ajili ya kutoweka na kuangamia kwa dunia. Kwa sababu hitilafu ndogo sana katika usawa wa vitu asili na dosari ndogo sana katika kanuni angavu za ulimwengu ingetosha kusababisha vitu kukosa amari zao na viumbe vya angani kugongana, na kutokea kwa mlipuko mkubwa na kuangamia kwa dunia. Kama asili ya dunia ingeegemea kwenye kuweko bahati mbaya, kwa nini nadharia hata za wapenda anasa za dunia zimetegemewa kwenye kufikiria kupanga, mpangilio uliopangwa, kukosekana hali ya bahati mbaya? Kama dunia yote ni matokeo ya kubahatisha na bahati mbaya, ni kitu gani kile ambacho hakikutokea kwa msingi wa kubahatisha? Endapo kitu kilichopo sasa kilikuja kuwepo kama kiumbe si kwa sababu ya kubahatisha, ni sehemu gani muhimu na sifa zake zake ambazo zinazokibainisha na je zinaweza kutumika katika vitu vingi na vya namna nyingi mbali mbali vya ulimwengu?

Sasa kwa kuwa kubahatisha kunapingana na mpangilio na upatanifu, inaonekana kwamba kitu chochote kinachokuwa na mabaki ya upangaji, ubunifu na ukokotozi kitakuwa hakitangamani vizuri na hakiendelei, kwa sababu dhana za upangaji, usanii na mpangilio mzuri zimepingana na kubahatisha na hali ya uwezekano. Kudhani kwamba mfumo wa kubahatisha ndio muundombinu kwa ajili ya ulimwengu na kanuni yake inayotawala haitegemei uthibitisho wowote wa kimantiki au ushahidi wa kisayansi haiwezi kukubaliwa kuwa ni ufumbuzi wa uhakika kwenye jiometri ya muundo wa maumbile.

Wakati ambapo sayansi za majaribio zinaonyesha kwamba elementi na vipengele vya asili haviwezi kutoa mvuto wowote wa kujitegemea na havina uumbaji; ambapo uzoefu wetu wote, hisia zetu za fahamu na mafuhum zetu za kimantiki yanaelekeza kwenye maamuzi kwamba katika maumbile hakuna kinachotokea bila ya sababu na chanzo na kwamba vitu vyote vimetengenezwa kwenye mfumo madhubuti na kanuni maalum - ikiwa yote haya ndio hali halisi yenyewe, inashangaza kuona watu wengine wanageuzia migongo yao kwenye kanuni za kisayansi, mafuhum muhimu na mapendekezo yaliyo egemezwa kwenye tafakuri, na kukataa kuwepo kwa Muumba.

Elimu na vipengele vya kimazingira ni miongoni mwa sababu ambazo ama huzuia fahamu za asili za binadamu zisijioneshe, au kinyume chake, kuziimarisha. Kila chenye kujionyesha chenyewe kutoka kwenye chanzo cha silika hufanana katika mpangilio wake na mlolongo wa asili. Wale ambao wameachwa huru na kufuata mwelekeo wa asili wa maumbile yao bila ya kufungwa na mazoea na ambao tabia yao ya kina zaidi haikupambwa na maneno na muonekano, wanaweza kusikiliza vizuri zaidi wito wa nafsi zao za ndani zaidi na kuweza kupambanua baina ya matendo mema na mabaya, imani za kweli na za uongo. Kutokuwa na maadili ya dini, hali ambayo kwa kweli ni kuipa kisogo asili ya maumbile, kwa hiyo, ni nadra sana kuonekana miongoni mwa watu kama hao.

Endapo mtu anawaambia kwamba dunia haina mpangilio wenye kukaa ndani na kwamba inatokana na hali ya kutukia (isiyo ya uhakika), akiyapamba maneno yake kwa istilahi za kifalsafa, hatakuwa na athiri juu ya watu kama hao, kwa sababu watazikataa nadharia zake kwa ajili ya asili yao ya kimaumbile. Watu ambao wamenasa katika mitandao ya sayansi wanaweza kuwa mateka wa shaka na utatanishi kama matokeo ya istilahi zenye ushawishi. Elimu finyu ambayo hutia msukumo wa kiburi kwa binadamu ni kama mfano wa kipande cha kioo kilichopakwa rangi ka kuwekwa mbele ya kiupenyo cha akili na maumbile ya asili; yeyote mwenye akili hii huona dunia imetiwa rangi kidogo na ujuzi wake na elimu yake. Hudhania kwamba ukamilifu wa ukweli ni ule anaouona kupitia kwenye kipenyo chembamba cha fahamu zake na akili ambavyo ni nyara rahisi ya rangi. Kama hali ilivyo, hatuna maana kwamba binadamu aache kuendeleza akili yake ili ajiepushe na upotovu. Hata hivyo, asije akawekewa mipaka na ujuzi wake na elimu yake au asijigambe kwa hiyo elimu na ujuzi wake wenye kikomo.

Watu walio wengi, badala ya kufanya maarifa na ujuzi wao kuwa ngazi ya kunyanyua uwezo wa akili zao ili waweze kufikia kiwango cha juu zaidi, wanabaki wametulia na kufungiwa kwenye uzio wa kuta nne za dhana na masharti. Hali ya asili ya mwanadamu, pindi anapohisi hatari, haraka hukimbilia kwenye msaada wake. Mtu anapobanwa na shida na matatizo makubwa sana, wakati mambo ya kilimwengu yanapompa kisogo, anapokuwa hana njia yoyote ya kuzifikia rasilimali za kimaisha na anazama kama bua kwenye machafuko ya mabadiliko na kifo kipo karibu sana naye - ndipo dhamira ya kutoka moyoni humwongoza kisilika na kumwelekeza kwenye chanzo cha msaada kisichokuwa cha kilimwengu. Hutafuta msaada kutoka kwa yule ambaye uwezo wake upo juu ya uwezo wowote ule, na huelewa kwamba ni yule Muumba mwenye huruma na mwenye nguvu zote ambaye anaweza kumsaidia kwa kutumia uwezo wake usio wa kawaida na kumwokoa.

Kwa sababu ya utambuzi wake, kwa nguvu zake zote binadamu hutafuta msaada wa yule aliye mtakatifu sana ili amwondoshe kwenye hatari na kwenye faragha ya moyo wake, anahisi uwezo na nguvu ya muweza huyo zikifanya kazi kwqa ajili ya mwokovu wake. Mtu mmoja wakati fulani alimuomba Imamu Sadiq(a.s) amwongoze kuelekea kwa Mola wake Mlezi, akasema kwamba maneno ya wapinzani yalimtatanisha. Imamu akamuuliza, "Umewahi kusafiri kwa meli? Akajibu, "Ndio."

Imamu: "Je, imewahi kutokea kwamba meli ikaingiza maji na hapakuwepo na mtu wa kuwaokoeni ili msizame kwenye mawimbi ya tufani ya bahari?"

Jibu: "Ndio." Imamu: "Wakati huo wa hatari na katika hali hiyo ya kukatisha tamaa, je, ulikuwa na hisia kwamba nguvu isiyopimika na yenye uwezo mkubwa ingeweza kuwakuokoeni kwenye balaa lenu la kutisha?"

Jibu: "Ndio, hivyo ndivyo ilivyokuwa."

Imamu:"Ni Mwenyezi Mungu Mwenye uwezo ambaye ndio chanzo cha mategemeo na kwake Yeye watu ndiko wanakotazamia kwa matumaini pale ambapo milango yote inapokuwa imefungwa." [4] Hata watu waasi na wapenda dunia wenye uwezo ambao hawautambui uwezo usio na kikomo wa Mwenyezi Mungu, wanapofurahia utawala wao, hubadilika wanaponasa kwenye mtego wa kushindwa na kuangamia. Husahau kumkana kwao Mwenyezi Mungu ambako madhehebu yao ya mazingira na ya kianasa za dunia ulivyojipandikiza ndani yao na kwa moyo mkunjufu kabisa hugeukia kwenye asili ya viumbe vyote na chanzo cha nguvu zote.

Historia imeorodhesha mifano mingi sana ya watu kama hao ambao walipata kuwa waathirika wa matatizo na hali za mitihani hivyo kwamba vumbi la upotofu liliondolewa ghafla kutoka kwenye tabia zao za asili na kutoka kwenye vina vya nafsi zao na wakarejea kwa Muumba asiye na kifani. Kwa kuongezea kwenye rasilimali za ndani ambazo ni za asili katika nafsi ya binadamu na humsaidia yeye kugundua ukweli hivyo kwamba, akiwa huru kutokana na dhana na vikwazo vya kiakili husonga mbele akifuata njia ya tabia yake ya asili, na kiwango cha nje cha mwongozo na maonyo pia ni muhimu kwa ajili ya kumwelekeza njia na kuimarisha hali yake ya asili. Ni mwongozo ndio unaorekebisha sifa za ki-uasi na kuilinda akili na tabia ya asili kutoka kwenye upotovu na utiifu kwa miungu wa uwongo. Mitume walipelekwa kwa madhumuni ya kuwafanya watu wajihadhari na utambuzi wenye utatanishi, wa tabia zao za asili, ili kuufanya mwelekeo wao wa ki-Mungu ufuate mkondo unaostahili, na kuyanyanyua matarajio yao makubwa.

Amirul-Mu'minina(a.s) amesema:"Mwenyezi Mungu aliwatuma Wajumbe Wake miongoni mwa watu ili waweze kuwahoji kuhusu ahadi yao na Mwenyezi Mungu, kuwakumbusha watu kuhusu neema za Mwenyezi Mungu zlizosahaulika, kuzungumza nao kwa namna ya kuwaonya, kuzindua hekima iliyojificha ndani mwao, na kuwaonesha ishara za uwezo wa Mwenyezi Mungu." [5]

Mwongozo na nasaha za aina hiyo kwa jinsi yoyote ile haimaanishi kuzimwa kwa nuru ya dhamira endelevu ya mwanadamu kumnyima uhuru na uwezo wake wa kufikiri na kuchagua. Hii, kinyume chake, ni aina ya msaada kwenye mielekeo na silika bayana, kuziwezesha kukua na kuendelea. Ni kupitia mwongozo na nasaha ambapo wanadamu wanaondolewa kwenye vifungo na kuwezeshwa kunufaika kutokana na mpanuko wote wa maumbile yao ya asili na kusitawi pamoja na viumbile wenzao wote. Qur'anii inasema:

وَيَضَعُ عَنْهُمْ إِصْرَهُمْ وَالْأَغْلَالَ الَّتِي كَانَتْ عَلَيْهِمْ فَالَّذِينَ آمَنُوا بِهِ وَعَزَّرُوهُ وَنَصَرُوهُ وَاتَّبَعُوا النُّورَ الَّذِي أُنزِلَ مَعَهُ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٥٧﴾

". . Anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyokuwa juu yao. Basi wale waliomuamini yeye, na wakamtukuza, wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyoteremshwa pamoja naye, hao ndio wenye kufaulu."[6]

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ ﴿٢٤﴾

"Enyi mlioamini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapokuiteni kwa yale yatakayokupeni uzima."[7]

يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَتْكُم مَّوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَشِفَاءٌ لِّمَا فِي الصُّدُورِ ﴿٥٧﴾

"Enyi watu! Yamekufikieni mawaidha kutoka kwa Mola wenu Mlezi, pozo la yale yaliyomo vifuani, .[8]

Watu wa kwanza waliokubali wito wa Mitume walikuwa watu wenye mioyo safi na dhamira zilizoongoka. Safu za washindani wao zilikuwa na wale waliotegemea juu ya mamlaka bandia na utajiri au walijawa na kiburi kwa sababu ya ujuzi wao mdogo na wenye mapungufu, akili zilizochafuliwa na udanganyifu, kwa namna ambayo kwamba jeuri yao isiyo na msingi, ilizuia uwezo wa kina na matamanio yao kustawi.

Mwanazuoni fulani amesema hivi: "Katika mambo ya kiroho, pia kanuni ya usambazaji na kuhitaji huwepo. Kama haja ya dini isingekuepo katika tabia ya asili ya binadamu, mahitaji yaliyotolewa na Mitume yangepotea bure. Tunaona kwamba ugawaji wa Mitume ulipata wateja; mawazo yao yenye mipango mingi, yasiyo na shaka na sahihi kabisa yalipata wafuasi na waunga mkono wengi. Huu ni uthibitisho kwamba haja ya dini inakuwepo ndani ya mwanadamu na dhamiri yake ya kina kabisa."[9]

Kwa kweli, mafundisho ya msingi ya Mitume wote yalikuwa wito wa kumwamini Mwenyezi Mungu mmoja, sio ya kuthibitisha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu. Walibatilisha thamani ya masanamu, jua, mwezi na nyota kuabudiwa, ili kwamba kiu ya ya mwanadamu ya kina na ya kimaumbile kwa ajili ya ibada isitoshelezwe na kuvikimbilia vitu vya maumbo ya nje kama hivi na wanaweza, badala yake, kutafuta malengo na maadili yao kwenye safina imara na kupanda kwenye madhumuni halisi ya ibada. Mioyo yao inapaswa ifungamane na ulinzi usio na kikomo, na kwa imani ambayo daima inapanda, wao wanapaswa wakati wote kusonga mbele kuelekea kwenye chanzo cha maadili yote na wema, hatimaye kufikia kwenye malengo yao.

Aina zote za kuabudu miungu wengi za ukana dini - mfumo wa kale ambao ni kuabudu masanamu namuundo ulioendelea, wa kisasa, ambao tamaa ya anasa - ni matokeo ya kukengeuka asili ya maumbile. Maendeleo ya elimu kuhusu uzoefu wa kidini ambayo yanatokea pote duniani yamesababisha ugunduzi mwingi ambao unaruhusu maamuzi muhimu ya uhakika yaweze kufikiwa.

Ikiegemezwa kwenye takwimu nyingi kiasi zilizokusanywa na wataalamu wa sosholojia, wanaakiologia (wachambuzi wa elimu ya kale), wana anthropogia (elimu ya asili ya binadamu), historia ya dini sasa ina changanua silika ya kidini, pamoja na uanzishwaji, imani, desturi na vipengele ambavyo vinaijenga jamii, kwa namna mpya ambayo inatofautiana sana na maelezo yaliyotolewa kabla ya hapo. Sasa hivi kuna wimbi la fikra ambalo kwa muda wote linaendelea kuwavutia wafuasi wapya kutoka kwenye madhehebu mbali mbali wanaosema kwamba hisia za kidini ni kijenzi cha msingi, cha asili na madhubuti cha roho ya binadamu na kwamba ni njia ya asili ya kutambua yaliyo ghaibu. Mnamo kama mwaka wa 1920, mwanafalsafa wa Kijerumani aitwaye Rudolf Otto aliweza kudhibitisha kwamba sambamba na dalili za kiakili na maadili ndani ya mwanadamu, pia zipo dalili za kimantiki ya hali ya juu sana ambazo hujenga hisia za kidini. Sifa zinazomhusu Mwenyezi Mungu kama vile uwezo, ukuu na zenye kuvuka mipaka zina madhumuni ya kusisitiza kwamba utakatifu hauwezi kurahisishwa kuwa dhana nyingine. Hii ni namna inayojitegemea ambayo haiwezi kupatikana kutokana na namna nyingine na haiwezi kuhusishwa na dhana nyingine yoyote, kimantiki au vinginevyo.

Mojawapo ya upekee wa zama hizi kwa kweli, ni utafutaji wa kipimo cha nne katika dunia ya asili kiitwacho "Wakati". Kama vilivyo vipimo vingine, ni lazima kiingiliane na miili, na kwa hiyo hakuna mwili uliopo katika duniani ambacho kimeepukana na wakati ambao unatokana na msongo na mabadiliko. Vivyo hivyo ni sifa ya zama hizi kwamba tafiti za wanachuo zimeongozea kwenye ugunduzi wa 'kipimo cha nne' cha nafsi ya mwanadamu - hisia za kidini[10] .

Vipimo vingine vitatu au hisia vinakuwa na hisia ya dadisi, hisia ya maadili na hisia ya ubora. Hisia ya kidini au dhana ya utakatifu, ni kipimo cha nne na cha msingi zaidi cha hisia. Kihulka kila mtu anao mvuto na mwelekeo kwa kile kilichoko nje ya maumbile, tofauti na huru kutokana na zile hisia zingine tatu. Kwa kugunduliwa kwa hisia ya kidini, jela ya nafsi yake, yenye nyuso tatu, iliporomoka na ikathibitika kwamba mielekeo ya kidini ya mwanadamu imeota mizizi kwa kujitawala kabisa ndani ya utu wake. Ilijitokeza yenyewe hata nyakati zile ambazo watu walikuwa wanaishi ndani ya misitu na mapangoni.

Licha ya ubora wake, kujitawala na kufaa kwa hisia za udadisi, maadili, ubora na nafasi zilizoichukua katika kutokeza kwa elimu, maadili na ujuzi, ilikuwa ni hisia ya kidini iliyoandaa mazingira kwa ajili ya utendaji wa hisia hizi tatu, ikizisaidia kusonga mbele katika njia yao na kugundua siri za ulimwengu ulioumbwa. Kwa mtazamo wa muumini, dunia imesanifiwa katika msingi wa kanuni na mpango sahihi uliokusudiwa vizuri. Imani hii kwa Mwenyezi Mungu mwenye kuamuru na mwenye hekima huzindua hisia ya udadisi kwa lengo la kutafuta na kugundua kanuni na siri za maumbile ambazo zimeegemea kwenye mlolongo wa sababu namotokeo yake. Mchango wa hisia ya kidini katika kukuza na kuendeleza tabia tukufu kabisa za binadamu, katika kurekebisha hisia zake na kurutubisha silika zake za maadili na wema, haupingiki. Wale wanaofuata maamrisho ya dini wanauona kama mmoja wa wajibu wao muhimu sana wa kidini, kudhibiti silika zao na kupata sifa nzuri za hali ya juu. Fikra ya kidini pia imekuwa kipengele chenye kulea hisia za kisanaa. Watu wa kale walitengeneza kazi zao za kisanaa endelevu sana ili kuwatukuza miungu wao. Mahekalu ya ajabu ya China, mapiramidi makubwa ya Misri, masanamu ya aina ya kipekee ya Mexico, usanifu majengo ulioboreshwa na wakustaajabisha ya Mashariki ya Kiislamu -yote haya yalitegemea sana kwenye hisia ya kidini.

Wanasaikolojia wanaamini kwamba upo uhusiano baina ya hali ya balehe na kujitokeza kwa ghafla kwa hisia za kidini. Katika kipindi hiki cha maisha, hata kwa watu ambao siku za nyuma hawakujali mambo ya dini, hisia ya kidini inachukua mkazo maalum. Hapana shaka kwamba, wito wa ndani hujionyesha kwa jinsi ambayo kwamba hakuna kizuizi kinachoweza kuzuia njia yao. Hata hivyo vipengele fulani kama vile propaganda za upinzani vinaweza kupunguza hisia za ndani kwa ndani na fikra sahihi, ingawa vishawishi kama hivyo haviwezi kuishia kwenye ung'oaji kabisa wa uwelekeo huo. Endapo vikwazo kama hivyo vitaondolewa, hisia zilizo imara huanza tena utendaji wao na kujionesha kwa namna ya jitihada zao endelevu za ndani kwa ndani.

Tunafahamu kwamba zaidi ya nusu karne imepita tangu mapinduzi ya kikomunisti ya Jumuiya ya Kisovieti, lakini mizizi ya dini ipo hai kwenye vina virefu vya nafsi za watu wa Sovieti. Licha ya juhudi zote ambazo zimefanywa katika kipindi hiki kirefu na watawala za kuifuta dini, wameshindwa kuondoa hisia ya kidini kutoka kwa watu.

Kuwapo kwa fikra za maslahi ya kidunia, kwa hiyo, hakupingani na ukweli kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni jambo la kawaida kwa mwanadamu. Endapo madhehebu fulani itaondoka kwenye mkondo wa maumbile ya asili na hapo ikajifanya ya kipekee kusuiana na madhehebu zingine, kwa dunia ya sasa na katika nyakati zilizopita, hali hii haiwezi kufikiriwa kama ni kukanusha ile hoja kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni kawaida kwa binadamu; tofauti inakuwepo katika nyanja zote. Kile ambacho historia inakionesha na kwamba madhehebu ya tamaa za kidunia ilianzishwa mnamo karne ya sita na saba kabla ya Yesu Isa(a.s) .

3

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA TATU

MWENYEZI MUNGU NA MANTIKI YA JARIBIO (JARABA)

Bila shaka, hali ya kijamii, mambo ya kihistoria na kielimu, na aina mbali mbali za kazi za binadamu ni mambo ambayo haviwezi kuwa bila mvuto juu ya uonyeshaji kwa vitendo wa mwelekeo wa ndani wa mtu na tabia zake za kiroho na kihisia. Ingawa hali hizi mbali mbali hazisababishi ulazima wowote au umuhimu katika uchaguzi wa mwelekeo wa mtu, zinaweza kusababisha kuwepo kwa mazingira yanayofaa zaidi kwa ajili ya uchaguzi wa aina fulani, kwa hiyo kutoa mchango muhimu kuhusu jinsi binadamu anavyoviona vitu. Hali hizi wakati mwingine zinaweza hata kujionesha katika umbo la kikwazo kwenye uhuru wa mtu na uwezo wa kuchagua. Kama matokeo ya uzoefu zaidi wa maamuzi ya kisayansi na ya kimajaribio, akili ya binadamu kwa kawaida huelekea kuonea haya kwa kiasi fulani maamuzi halisi ya kiakili kabisa, hususan kama jambo linalofanyiwa uchunguzi sio yakinifu na halina maana.

Kwa ujumla, uwezo wa kiakili za mtu hupata nguvu na ustadi kwenye eneo ambamo zinatumiwa sana. Mambo yaliyoko nje ya eneo hilo, kwake (binadamu) huonekana kuwa si ya kweli au si halisi au vizuri zaidi ni jambo la hatua ya pili au linalohusika kidogo sana na jambo analolishughulikia maalum hasa. Kwa hiyo, mwanadamu huelekea kuhukumu kila kitu kwa namna ya kipekee. Mojawapo ya vipengele viharibifu na vinavyo potosha sana katika fikra zihusuzo Mwenyezi Mungu ni kuziwekea mipaka fikra ndani ya mantiki ya elimu za kimajaribio na kushindwa kutambua viwango na mipaka ya mantiki hiyo. Kwa kuwa wataalamu wa sayansi za majaribio kutumia nguvu zao zote za kiakili kwenye elimu za kihisia, wanakuwa wageni kwa mambo yaliyoko nje ya utambuzi wa hisia.

Ugeni huu, umbali huu kutoka kwenye mambo yasiyohusiana na hisia, imani hii isiyo ya kawaida juu ya data zinazotokana na sayansi za majaribio, hufikia kiwango kiasi kwamba kupima na kufanya majaribio huunda muundo wote wa akili na mtazamo wa dunia wa wataalamu kama hao. Wanaona majaribio kama ndio nyenzo pekee inayokubalika na njia ya utambuzi, kama kigezo pekee Wanakitegemea hicho kutatua matatizo yote. Kazi ya sayansi hizo ni kufafanua uhusiano baina ya mambo; lengo lao ni kuthibitisha uwiano baina ya matukio, si baina ya Mwenyezi Mungu na matukio. Katika sayansi za majaribio, mwanadamu hahusiki kabisa na Mwenyezi Mungu. Mtu asiwe na matumaini ya kuweza kutambua ukweli wa hisia za juu kwa kutumia kigezo cha hisia, au kamuona Mwenyezi Mungu ndani ya maabara.

Sayansi hizo haziwezi kufanya majaribio ya maabara juu kuwepo kwa Mwenyezi Mungu na halafu wafikie uamuzi kwamba endapo kitu hakionekani kimwili na hakiwezi kuthibitishwa kwa njia ya majaribio ya maabara na ukokotozi wa kimahesabu, kwa hiyo, kitu hicho hakina ukweli. Kwa kweli hakuna jaribio lolote linaloweza kufanywa na kupambanua kama kitu kisicho cha ki-maada kipo au hakipo, kwa sababu ni kitu hicho tu ambacho kinaweza kukanushwa kwa njia ya majaribio kinachoweza kuthibitishwa kwa njia ya majaribio. Sayansi na metafizikia ni aina mbili za elimu ambazo zina kiwango sawa cha uhalali na usahihi. Kanuni ya metafizikia haitokani na majaribio wala haiwezi kukanushwa na majaribio.

Maelfu ya majaribio ya kisayansi yanabuniwa ili yathibitishe kwamba vitu vyote ni vya ki-maada, yote yatashindwa kufikia malengo yao. Mwanasayansi wa majaribio anayo haki ya kusema, "Nimevumbua hiki na hiki," au "Sijagundua hiki na hiki." Hana haki ya kusema, "Kitu hiki na kile havipo." Mbinu za maabara, pamoja na utata wao na hali ya juu ya maendeleo, haziwezi kupata njia kupitia yasiyojulikana, giza na dunia iliyopanuka ya vitu vya asili, ambavyo ndio kiini cha majaribio, haziwezi kufahamu ukweli wote uliojificha katika kiini cha chembe zisizo na kikomo na haziwezi kuvumbua hata asili halisi ya kitu.

Mbinu inayotegemea majaribio imekuwa na manufaa sana katika kuendeleza utambuzi wa mwanadamu wa mpangilio sahihi wa maumbile, na inaweza kutoa msingi ulio dhahiri na mpya kwa ajili ya kumwamini Mola Mlezi kupita kwenye uchunguzi wake wa utaratibu wa uumbaji, kwani inaashiria kuwepo kwa Muumba mtambuzi na mwenye uwezo. Hata hivyo, nia na madhumuni ya wana sayansi katika utafiti na uchunguzi katika masuala ya maumbile na siri za dunia kwa ujumla si kwa sababu ya kumtambua Muumbaji wa uhai. Ikiwa katika mkondo wa kuendelea kukua kwake katika mikono ya watafiti, sayansi wakati wote imekuwa inagundua siri za kuwepo kwa maumbile bila ya wanasayansi kujitokeza, kwa njia ya sayansi yao, kutoka kwenye ujuzi mfinyu na wenye mipaka ambao wameupata kutoka kwenye hatua yao ya utafiti wa sasa.

Endapo wangelikuwa wafanye hivyo, wangelifahamu uunganishwaji wa mambo na kujiweka chini kwa vitu vyote kwenye utaratibu uliowekwa, na kwa hiyo, kupata hatua nyingine mbili za ziada za ujuzi na utambuzi. Kwanza wangeweza kuwianisha data zao zote za kihisia na majaribio, na halafu wangeweza kutoa uamuzi wa busara na kufanya tafsiri. Bila kukubali kuwepo kwa Muumba mwenye busara, haiwezekani kutoa tafsiri kwa kusadikisha ukamilifu wa data zenye tofauti zinazotokana na elimu mbalimbali na uhusiano uliopo baina yao.

Kwa matendo, hata hivyo, kazi na mbinu za fikra ya kisayansi ni kuunda kanuni na kufanya utafiti bila marejeo kwa Mwenyezi Mungu, hivyo kwamba mfumo wa fikra ambamo Mwenyezi Mungu hahusishwi unakuwa mhimili ambao juu yake kazi ya kisayansi huugeukia, na kusababisha mwanadamu kuwa mgeni na chochote kilichopo nje ya upeo wa fikra hiyo. Wakati huo huo, maisha ya kivitendo ya mwanadamu yanasihusiana na elimu bila kuepukika. Matokeo yanayotokana na ujuzi unaotegemea majaribio yanajumuisha mielekeo yote ya ki-maada ya maisha, kuwafunga wanadamu kwenye kuta zao nne zisizopenyeka, na ni vigumu sana kupata nyenzo yoyote ya kawaida miongoni mwa njia za maisha ya mwanadamu.

Hali hii kwa ulazima huongeza kuamini kwa binadamu katika sayansi na huathiri tabia yake, kumdukizia nafsini mwake hali ya mashaka na wasiwasi. Juu ya hayo, manufaa ya hali ya asili ya kitu kilichofanyiwa uchunguzi kwa kutumia sayansi ya majaribio kinagusika na kiko dhahiri kwa kila mtu, kwa tofauti kubwa sana ikilinganishwa na masuala ya metafizikia. Vivyo hivyo, vitu vya kimaada ambavyo vimechunguzwa kwa kutumia sayansi ya majaribio vinaeleweka sana, ambapo kinyume chake ni kweli katika masuala ya metafizikia.

Kuwasilisha masuala ya kidini kwa kutumia mbinu isiyo sahihi iliyofuatwa na kanisa la zama za kati (1100-1500A.D), ikichanganywa na uadui kwenye udhihirikaji wote wa sayansi, ilikuwa ndio jambo muhimu sana katika kuifanya sayansi ya majaribio kuonekana yenye kupendelewa zaidi kuliko yale ya mambo kifalsafa na ya kimaada. Kwa ufupi, sayansi ilionekana kupingana cha dini, si kwenda sambamba nayo. Mara mantiki ya majaribio ilipofuzu katika kumwaga fikra zote ndani ya umbo lake, ilibadili sura ya mtazamo wa wanadamu juu ya dunia kwa kiwango ambacho kwamba walisadiki kwamba huo tu ndio ulikuwa msingi kwa ajili ya kukubali ukweli wa kitu. Waliiteua kuwa ndio mamlaka ya mwisho na wakaona kwamba haiwezekani kuthibitisha kuwepo kwa kitu chochote ambacho hakitambuliki kwenye akili.

Hivyo, mwana sayansi anayetegemea majaribio, ambaye hafahamu utaratibu wa watu wanaomjua Mwenyezi Mungu, anakubali na kuona kuwa ni sawa katika maisha yake, kila kinacholingana na mantiki na fikra ya kisayansi. Hujichukulia mwenyewe haki ya kukanusha chochote kisichochukuana na desturi yake ya kisayansi. Utaratibu wake ni imani kamili katika majaribio na kuiona kuwa ni ndio uthibitisho pekee wa usahihi wa maamuzi yoyote. Katika hali kama hii, ambapo msingi wote wa fikra za kidini unapuuzwa, mwanasayansi anajikuta hana kanuni zozote za kumwezesha kutafsiri yale masuala madogo madogo ya kidini ambayo hujitokeza katika namna ya amri na makatazo. Akiwa amezoea kabisa lugha ya kisayansi na kutegemea kanuni, anakuwa amejifunga kabisa kwenye desturi yake na kudhani amri za dini zinazoshurutisha, zilizo rahisi na zinazoeleweka, kuwa hazina maudhui au thamani.

Njia hii ya fikira ina dosari na si sahihi. Ingawa sayansi zina fomula (kanuni) changamani za ajabu na sahihi, ambazo kuzielewa kwake huhitaji uchunguzi wa kina na mgumu, fomula hizo hizo huondoka kwenye nyanja ya sayansi mara ziingiapo katika maisha yetu ya kawaida, hujitenga na lugha ya kifundi ya wana sayansi. Kama isingekuwa hivi, zingedhibitiwa kutumika kwenye vituo vya kisayansi na viwanda, maktaba na vituo vya utafiti.

Kila mtu anaweza kutumia vifaa kama simu na radio. Hali ni hiyo hiyo kwa nyenzo na zana za kisayansi. Juu ya usahihi na uchangamano wao, maelekezo kidogo yenye utaalamu yatamwezesha mtu yeyote kuzitumia. Mtu aliyebobea na mtaalam huwa hawatoi maarifa ya umakenika na ya ufundi kwa wanunuzi wa kifaa, badala yake, hufupisha maelezo yao katika sentensi fupi fupi yale matokeo ya kazi ngumu zilizovumiliwa na wavumbuzi. Kwa hiyo, si haki na ni kinyume cha mantiki ya kisayansi kujaribu kulazimisha amri za dini (ambazo haziwezi kufupishwa kuwa fomula za kisayansi, ambapo zikiwa rahisi na za kila mahali) kwenye tabia ya dhana na maoni ya mtu, na halafu zitangazwe kwamba hazina thamani na si za maana, huku wakipuuza wajibu wao wa kimaamuzi na athari zao za maana sana katika maisha yetu. Maelezo ya kivitendo huzaa matunda yao wakati yanapotamkwa katika lugha inayoeleweka kwa ujumla na kuwa na mguso kwa kila mtu na maisha ya kijamii.

Zaidi ya hayo, endapo ingedhaniwa kwamba amri na maelekezo ya dini yangeamuliwa na ufahamu, uelewa na muonjo wetu hapangekuwepo na haja ya wahyi na Mitume; tungeweza kuanzisha dini zetu wenyewe! Mara nyingi mwanadamu huwa hazioni dosari zake, akishughulishwa kama alivyo na nguvu zake. Mwenye kuabudu sayansi wa dunia ya leo anajivunia sana pia ujuzi wake kama matokeo na maendeleo ambayo yameyapatikana kutoka kwenye sayansi za majaribio kiasi kwamba anajidhania yeye mwenyewe kwamba ameshinda na kwa ushindi huo amechukua umiliki wa dunia ya ukweli. Lakini, hapana mtu ambaye wakati wowote ameweza kudai kwamba amepata ujuzi wa siri zote za ulimwengu na kuondosha mapazia yote kutoka kwenye dunia ya maumbile ya asili.

Mtu lazima achukuwe mtazamo mpana zaidi juu ya hali halisi na atambue ni jinsi gani tone la elimu yake lilivyo dogo likilinganishwa na bahari ya siri zilizofichika ambazo zinatukabili sisi. Baada ya kila ugunduzi wa kisayansi, msururu zaidi wa mambo yasiyojulikana hujitokeza. Katika karne zote ambapo mwanadamu amekuwa akifanya kazi bila kupumzika pamoja na rasilimali zake zote ili aweze kuijua dunia kwa kadiri iwezekanavyo, matokeo pekee ya jitihadi zake yamekuwa ugunduzi wa mambo machache miongoni kwa siri nyingi za ulimwengu. Ni hatua chache tu zimechukuliwa katika njia hii, na kuna lundo kubwa la yasiyojulikana yaliyoizunguka elimu ya mwanadamu kama wingu.

Kwa hiyo, mtu lazima atathimini kwa uhakika zaidi upeo wa utambuzi wa sayansi za hisia na sehemu zao zinazofaa kwa shughuli na athari. Mawazo yote yaliyokuwepo hapo kabla ambayo ni kama vizuizi kwenye njia ya kwenye ukweli lazima yaachwe kwa ajili ya uchambuzi sahihi.

Bila shaka, sayansi za majaribio zinaweza kutujulisha vipengele vya nje tu vya jambo; ni vitu vya ki-maada na mambo yakinifu ambavyo vinakuja kwenye upeo wa uchunguzi wao na vinaweza kuathirika kwenye majaribio ya maabara. Utaratibu wa sayansi katika kufanikisha malengo yao, wakiwa wanatafuta kupata faida kutoka kwenye kila ongezeko dogo katika ujuzi, ni uchunguzi na majaribio. Kwa kuwa shughuli ya msingi wa sayansi ya majaribio ni uchunguzi wa dunia ya nje, ili kuweza kuwa na uhakika kwamba nadharia fulani ya kisayansi ni sahihi, lazima tuilinganishe na ulimwengu wa nje ili kuijaribu. Endapo dunia ya nje inathibitisha kwa kufaa zaidi, sisi tunaikubali; laa kama sivyo, basi hatuikubali.

Kwa hiyo, kuzingatia lengo na utaratibu wa sayansi ya majaribio, lazima tuhoji endapo kama ukweli wa metafizikia unategemea kwenye kipimo cha hisia na kufanyiwa majaribio? Hivi hoja yoyote ya majaribioya kisayansi lazima ina haki ya kuingilia kati masuala ya imani na itikadi? Je, kuna sehemu yoyote ya sayansi ya majaribio inayohusika na Mwenyezi Mungu? Ili kuweza kugundua usahihi na kutokuwa sahihi kwa jambo katika sayansi za majaribio, ni muhimu kufanya matumizi ya mabadiliko na ya kuondoa vipengele tulivyopewa, pamoja na mazingira yake. Utaratibu huu hautumiki kwenye uhai wa ki-mungu, wa milele, usiobadilika na wa vitu vingi.

Ujuzi yakinifu ni taa ambayo inaweza kumulika baadhi vitu visivyojulikana kwa miale yake lakini si taa ambayo inaweza kuondosha giza lote. Kwani elimu ya mfumo hutegemea kuufahamu ujumla wake wote kabisa na namna ya ufahamu ambayo inaweza kuunganisha wenyewe sehemu zote za utambuzi, na kusababisha mtazamo wa mbali mtimilifu kabisa. Sasa kuifungia elimu ya mwanadamu kwenye kikomo cha sayansi za hisia hauwezi kumfikisha mtu kwenye mtazamo wa mbali kamili, bali kwenye ufahamu wa eneo la ndani zaidi la nafsi.

Kama tunamwamini Mwenyezi Mungu au laa, kwa kweli haina uhusiano na sayansi za majaribio, kwa sababu kwa kuwa kiini cha uchunguzi wao ni maada, sayansi zinazojihusisha na mambo yanayoonekana hayana haki ya kujieleza yenyewe kwa kukubali au kukataa kuhusu jambo lolote lisilokuwa la ki-maada. Kwa mujibu wa imani ya kidini ya madhehebu mbali mbali, Mwenyezi Mungu sio mtu - hana mwili. Hawezi kufahamika kwa kutumia milango ya fahamu. Yeye ameupindukia muda na nafasi (havihitajii). Yeye ni Ambaye kuwepo kwake hakutawaliwi na mipaka ya kidunia na nafasi haiwezi kumbana. Kwa hiyo, Yeye ameepukana na kuhitaji na ametukuka katika dhati yake juu ya upungufu wa aina yoyote.

Anavijua vipengele vya ndani sana na vya nje vya ulimwengu. Dunia ipo wazi mbele Yake. Mwisho kabisa, Anacho kiwango cha juu kabisa cha ukamilifu na ametukuka zaidi kuliko chochote kinachomhusu Yeye kinachoweza kuingia kwenye akili ya mwanadamu. Hatuwezi kabisa kuujua msingi wa dhati Yake, tukiwa tuna upungufu wetu wenyewe na wa uwezo wetu, akili na nyenzo za upambanuzi. Kwa sababu hii; endapo ukivichunguza vitabu vyote vya sayansi ya majaribio, hutakuta utajo hata kidogo wa majaribio kuhusu Mwenyezi Mungu au uamuzi wowote umetolewa kuhusu Mwenyezi Mungu.

Hata kama tutachukulia utambuzi wa hisia kuwa ndio njia pekee ya kugundua ukweli, hatuwezi kuthibitisha kwa kutegemea utambuzi wa hisia, kwamba hakuna kitu chochote kinachokuwepo nje ya ulimwengu wa hisia. Madai kama hayo, yenyewe yatakuwa si ya kutegemea majaribio, yakiegama kwenye ushahidi usiokuwa wa hisia au majaribio. Hata kama wafuasi wa madhehebu ya kidini walikuwa hawana uthibitisho wa kutetea madai yao, kuhitimisha kwa uthabiti na kwa nguvu kwamba visivyokuwana uhai, vimeenea nje ya upeo wa hisia, ungekuwa ni uchaguzi usio wa kisayansi, ulio tegemea kwenye dhana na minong'ong'oni.

Watu wengine hujaribu kutangaza njozi hizi kwa kuisingizia sayansi na kuonyesha uchaguzi wao kuwa umetokana na fikra ya kisayansi. Hata hivyo, katika mchanganuo wa mwisho, ukanushaji unaohusishwa kwenye madai kama hayo hayana thamani ya sayansi na falsafa, na vilevile yanapingana na mantiki ya majaribio. Kwenye kitabu kiitwacho 'The Elementary Principles of Philosophy'. George Pulitzer anasema, "kukidhania kitu ambacho hakikalii muda na nafasi na hakiathiriwi na mabadiliko wala maendeleo, ni jambo lisilowezekana."

Ni wazi ya kwamba maneno haya yanaakisi njia fulani ya fikra ambayo haijui inatafuta nini. Kama ingejua inachokitafuta, pia ingeelewa namna ya kukitafuta. Kwa kuwa shughuli ya aina hii ya fikra inazunguka kwenye maumbile na himaya ya hisia, ni kawaida kwamba itachukulia kama ni kitu ambacho hakiwezekani, kila kile kilichopo nje ya eneo la shughuli yake na kuwepo kwake ambako hakuwezi kuthibitishwa kwa njia ya majaribio ya hisia. Itaiona imani katika ukamilifu wake hasa kama ni kinyume na muundo wa fikara ya kisayansi. Hata hivyo, wasomi wanaojishughulisha na elimu asilia wanakabiliwa na lundo kubwa la vitu visivyojulikana kuhusu dunia hii hasa, na vya dhahiri, visivyo na uhai ingawaje wakati wote vina mawasiliano nayo (mbali na ulimwengu wa maada, wenye miujiza na siri nyingi zisizo na idadi, haihusishi hili tufe la dunia tunayoishi tu). Wasomi kama hao, kwa hiyo, wanayo haki yakusema tu, "Kwa vile nyanja za kimiujiza zipo nje ya upeo wa zana zangu za kitaalamu, ninanyamaza kimya na sitakanusha. Wangewezaje kujiruhusu kutoa madai ambayo yangesababisha elimu pana kiasi cha kama mpango wa ulimwengu wote, ambapo ujuzi wao wa mpango wote wa uhai unakaribia sufuri?

Kuna uthibitisho gani wa kuhakikisha madai kwamba uhai ni sawa na kitu cha ki-maada na kwamba dunia yote ya uhai imejaa vitu vya kimaada? Ni mwanasayansi gani anayeikataa metafizikia ambaye ameweza kusimamisha kanusho lake juu ya mantiki au ushahidi, au kutoa ushahidi kwamba nje ya kutokuwepo uhai, hakuna kitu kilichopo nje ya uwanja wa hisia? Ingawa sayansi haikatai kwa uwazi na uhakika kabisa kila kitu kisichojulikana kwa sababu tu kwamba haina uwezo wa kukifikia kwa kutumia nyenzo na vifaa vyake, badala yake inangojea kwa uvumilivu siku ambapo kitu hicho kitavumbuliwa, wapenda anasa za dunia wala hawaliendei suala la kuwepo kwa Mwenyezi Mungu kwa shaka na wasi wasi, kwa misingi ya maoni yao ya kimakosa na haraka, wanatangaza uamuzi wao kwamba hakuna Muumbaji!

Watu kama hawa huanzisha vigezo na viwango fulani kwa ajili ya matumizi yao; na hawapo tayari kutumia kigezo kingine kilichoanzishwa kwa makusudi fulani katika eneo lililokusudiwa. Mathalan, kamwe hawatatumia kigezo ambacho kinatumika kwenye uso wa kitu kupimia mwili, lakini inapokuja kwenye kupima dunia ya hisia nyingi wanajaribu kumpima Mwenyezi Mungu, roho na msukumo, kwa kutumia nyenzo hizo hizo wanazotumia kupima dunia yakinifu. Wanapojikuta hawawezi kupata ujuzi wowote wa viumbe kamili husika, wanaendelea kukana kuwepo kwa vitu hivyo.

Sasa kama mtu aliyefungwa kwenye mantiki ya majaribio atapenda kukubali ukweli wa ulimwengu kwa kadiri tu alivyoruhusiwa na uzoefu wa hisia na kukanusha chochote kilichopo nje ya hilo, lazima atambue kwamba hii ni njia ambayo amejichagulia mwenyewe, si matokeo ya uchambuzi wa majaribio ya kisayansi. Aina hii ya itikadi bandia ya usomi na uwezo wa kiakili hutokana na uasi wa kisomi na mtu kuacha asili yake halisi.

Huyo Mwenyezi Mungu ambaye mwanasayansi wa kawaida, anataka "kuthibitisha" kwa kutumia nyenzo zake na vifaa vyake, kwa hali yoyote ile, sio mungu asilani kwa mtazamo wa wale wanaomcha Mwenyezi Mungu.


3

4

5

6

7

8

9

10

11

12

13

14