MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE 14%

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE Mwandishi:
: SALMANI SHOU
Kundi: Misingi mikuu ya Dini

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE
  • Anza
  • Iliyopita
  • 28 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 30026 / Pakua: 4269
Kiwango Kiwango Kiwango
MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

11

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA KUMI NA MOJA

KUTOLINGANISHIKAKWA SIFA ZA KI-MUNGU

Katika jitihada zetu za kumwelezea alivyo Muumba na kupata kujua sifa zake, tunahitaji kwa ukamilifu kuwa na dhana na maelezo ambayo yako nje ya uwezo wetu. Yale maneno tunayotumia hayatatuwezesha kufikia lengo letu, maelezo halisi juu ya Mwenyezi Mungu, kwani uchache wa kuelewa kwetu hauwezi kuzingatia utambuzi wa asili hasa ya sifa za Mwenyezi Mungu zisizo na ukomo. Ametukuka juu ya dhana na fikra zote zinazobuniwa na kuundwa na akili ya binadamu.

Mwanadamu, ambaye ameumbwa na kuwekewa mipaka katika kila hali, asitumainie kuwa na uwezo wa kukadiria na kuelezea kitu kisicho cha kimaumbile kwa njia ya sifa na tabia za kimaumbile. Uhakika ambao ni kinyume na viumbe vinavyoweza kutokea na vile vya kawaida, ambao mamlaka yake kamili na elimu isiyo na ukomo vinafunika vitu vyote, ambao kwa maneno ya Qur'ani:

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ ﴿١١﴾

"Hakuna kitu chochote mfano Wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona." (42:11).

Dhati ya aina hii kwa kawaida haiwezi kujadiliwa kwa haraka kama mada zingine za kawaida. Ali(a.s) Bwana wa wacha-Mungu, alisema: "Yeyote anayemlinganisha na kumchanganya Mwenyezi Mungu na kitu au anakihusisha kwenye asili yake takatifu atakuwa kwa uhakika bado hajamuona Yeye. Chochote anachokijua mwanadamu kuwa ni msingi wa asili Yake ni lazima kiwe kimeumbwa. Mwenyezi Mungu ndiye Muumbaji na Mtengenezaji. Chochote kinachotegemea kitu kingine zaidi ya chenyewe hicho kimesababishwa na kimeumbwa. Ni Mwenyezi Mungu peke Yake tu ambaye ndiye sababu pekee (na sio athari).

Yeye anashughulikia uumbaji bila ya kutumia namna yoyote ya vitendea kazi. Hupima bila msaada wa fikira na tafakuri. Yeye si mhitaji na hapati manufaa kutokana na kitu chochote. Wakati na nafasi haviandamani Naye. Vyombo na vifaa havimsaidii Yeye. Kuwepo kwake hutangulia nyakati zote na ukabla wa umilele Wake ulitangulia mwanzo wote.

"Yeye habanwi na mipaka, kwani ni viumbe ndivyo huwekea mipaka maumbile yao kwa njia ambazo ni maalum kwao, na miili yao ndio inayoonyesha aina zao. Dhati Yake takatifu haikubali dhana ya mwendo na ile ya kutokuwa na mwendo, inawezekanaje kwamba kitu kilichoumbwa ndani ya kiumbe pia kiwepo ndani ya Dhati Yake? Kama pangekuwepo mwendo na kutuama kimya katika Dhati Yake, Angelazimika kukumbwa na mabadiliko na marekebisho; angeweza kugawanyika na kutokuwa na mwanzo kwake kungekanushwa. Yeye ni chanzo cha nguvu zote, kwa hiyo hakuna kiumbe ambacho kingeweza kumwathiri.Mwisho kabisa, Yeye ni Muumba Ambaye habadiliki au kutoweka na Ambaye kamwe hafichikani kwa watu wa ujuzi na umaizi."[33]

Ukweli kwamba sifa za Mwenyezi Mungu zimejitenga kabisa na zile za kwetu na haziwezi kupimwa kwa kulinganishwa na sifa zetu ni kwa sababu sifa za hicho chanzo cha viumbe ni tofauti na sifa za viumbe vingine vyote. Mathalani, sisi tunao uwezo wa kufanya kazi fulani, lakini hii sio sawa na ule uwezo wa Mwenyezi Mungu; kwa upande wetu, sifa ni kitu kimoja na kitu hasa kinachozungumziwa ni kingine. Tunapojivunia elimu zetu, hatuko kitu kimoja na kufanana na elimu zetu. Wakati wa utoto wetu hapakuwapo na dalili ya ujuzi au elimu katika utu wetu, lakini baadaye tulianza polepole kupata kiasi fulani cha elimu kwa kujifunza. Elimu na uwezo vinaunda pembe mbili tofauti za utu wetu, pembe hizi hazifanani na asili yetu na wala kuunganishwa pamoja katika maisha yetu. Sifa ni matokeo ya bahati na asili yetu ndio kiini; kila kimoja hakitemgemei mwenzie.

Lakini suala la sifa za ki-Mungu kimsingi ni tofauti: tunaposema kwamba Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa yote na ni Muweza wa yote, tunachokimaanisha ni kwamba Yeye ndiye chanzo cha elimu na uwezo. Sifa hizo sio kitu kingine mbali na kile inachokielezea ingawaje kifikra vinatofautiana. Kwa hali halisi, sifa Zake zinafanana na Dhati Yake; kwani Dhati Yake haiundwi na kitu ambamo mambo ya kubahatisha yanaweza kushikilia. Yeye ni Dhati halisi, yenye kufanana na elimu, uwezo, uhai, uthabiti na utambuzi; Yeye hatawaliwi na mipaka yoyote ya kiakili au ya kutoka nje au kizuizi.

Kwa kuwa tunalelewa katika kiini hasa cha maumbile, na kwa hiyo tuna uzoefu nayo wakati wote, na kwa kuwa chochote tunachokiona kina kipimo na umbo maalumu, wakati na mahali na sifa zingine zote za miili - kwa ufupi, kwa sababu ya mazoea ya akili zetu kwenye maumbile ya kawaida - tunajaribu kupima vitu vyote kwa kigezo cha maumbile, hata dhana za kiakili na kihekima. Kigezo cha maumbile kwa hiyo, kinakuwa kituo cha kuanza kuondokea cha uchunguzi wote wa kisayansi na kifalsafa. Kuidhania nafsi ambayo haina hata sifa moja ya kimaada na ambayo ni tofauti kabisa ni vile akili zetu zinavyoweza kutambua na kuelewa sifa ambazo hazitenganishiki na dhati hiyo, sio tu kunahitaji usahihi lakini pia kunatutaka tusafishe kabisa akili zetu na mambo ya maumbile.

Ali(a.s) amesema kwa ufasaha kabisa, kwa kina na kwa umuhimu mkub- wa kuhusu jambo hili. Anasisitiza kwamba mwanadamu hawezi kumfunga Mwenyezi Mungu katika maelezo, akisema: "Upwekeshaji halisi wa Mwenyezi Mungu (Tawhiid) na imani halisi vinategemea katika kuacha, kukana na kuondoa kabisa kutoka kwenye asili Yake tukufu, sifa zote za viumbe vilivyoumbwa. Mwenyezi Mungu apishie mbali kwamba Angeweza kuelezwa kwa sifa zozote kama hizo, kwa sababu akielezewa hivyo, itaonekana kama vile kila sifa imejitenga na mwenye sifa hiyo na ni mgeni nayo. Kwa hiyo mtu anayesema chochote katika kumuelezea Muumbaji akimdhania Yeye kuwanazo sifa fulani ambazo zimeongezwa na kukithirishwa kwenye ile dhati, tayari zimemfanya Yeye kuwa mshirika wa kitu fulani na kushauri kwamba anazo sehemu mbili. Jaribio la namna hii la kumwelezea Mwenyezi Mungu husababishwa na kutokujua na kutokutambua."[34]

Dhana za kiakili haziwezi kumwelezea Mwenyezi Mungu kwa kukimbilia sifa zenye ukomo, kwa kuwa na mipaka kwao, basi hazifai kumwelezea Mwenyezi Mungu. Kila sifa, kwa kuhusiana na ile maana maalum inayoiwasilisha, iko tofauti na sifa zingine zote. Kwa mfano; sifa ya uhai ni tofauti kabisa na sifa ya uwezo; hazibadilishaniki. Inawezekana kwamba mifano fulani huenda ikakusanya sifa zote hizi mahali pamoja, lakini kila moja ina maana yake kimsamiati.

Wakati akili ya mwanadamu inapotaka kukipatia sifa kitu fulani, lengo lake ni kuanzisha, katika mfano maalum, aina ya ushirikiano baina ya sifa na kitu inachokielezea. Lakini kwa kuwa sifa kimawazo inatofautiana na kitu chenyewe, akili bila kukwepa inaamuru kwamba vibakie mbali mbali. Njia moja tu ya kujua vitu ni kuvieleza kwa kutumia fikra za kiakili, ambazo kimawazo kila moja imetengana na mwenziwe, na kwa hiyo lazima viwe na ukomo. Dhana hizo haziwezi kwa hiyo, kutumiwa kupatia elimu juu ya ule Uhakika wa Hali ya Juu zaidi. Yeye ametukuka juu ya uwezekano na kujulikana kwa maelezo, na yeyote anayemwekea mipaka Mwenyezi Mungu kwa kutumia sifa fulani, huyo ameshindwa kupata

Kwa kutaja mifano michache tunaweza kuelewa kwa kiwango fulani jinsi ambavyo sifa hazikithirishwi kwenye dhati hiyo. Hebu zingatia kwamba miale ya joto inayotoka kwenye moto inafikisha joto kwenye kila kitu, hivyo kwamba mojawapo ya tabia na sifa ya moto ni kuwaka na kusambaza joto. Je, tabia hii imekalia pembe moja katika mwili wa umbile la moto? Kwa kweli, jibu ni hapana; uhai wote wa moto kwa jumla una sifa ya uwakaji na ugawaji wa joto. Imam Jafar as-Sadiq(a.s) alisema katika kumjibu mtu ambaye alimuuliza kuhusu hali halisi ya Mwenyezi Mungu: "Mwenyezi Mungu ni kitu tofauti kabisa na vitu vingie vyote; ni Yeye peke yake ndiye anayelingana na dhati halisi ya asili ya uhai wote. Yeye si mwili na wala hana umbile. Milango ya fahamu haiwezi kumtambua Yeye na hawezi kutafutwa. Yeye ameepukana na utambuzi aina yoyote wa milango mitano ya fahamu; njozi na dhana havimtambui Yeye. Kupita kwa wakati na kupishana kwa zama havimpunguzi Yeye kwa hali yoyote, na ameepukana na mabadiliko na kigeugeu cha aina yoyote."[35]

UPWEKE WA MWENYEZI MUNGU (TAWHIID)

Wakati suala la upweke wa Mwenyezi Mungu linapojitokeza kwenye mazungumzo ya kidini, linachukuliwa kujumuisha mada nyingi, ikiwemo pamoja na imani ya upweke wa hiyo dhati, hivyo pia mkusanyiko wa sifa na tofauti baina ya dhati na sifa imewekwa pembeni kabisa kuhusiana na umoja wa sifa. Upambanuzi na utofautishaji unatokana na uwekaji mipaka. Kama tunatanguliza tofauti miongoni mwa sifa za ki-Ungu, inakuwa ni halali tu kwa mtazamo wa mawazo na tafakuri zetu za kawaida; ongezeko la mielekeo na sifa zilizokithirishwa haziwezi kuathiri hiyo dhati tukufu

Endapo katika ulimwengu wa maumbile tutatazama kiwiliwili kwa kutumia vipande vya kioo vyenye rangi tofauti; kiwiliwili hicho kitaonekana katika mfululizo wa rangi tofauti. Hivyo hivyo, tunapotafakari dhati tukufu ya kipekee kwa busara zetu, wakati mwingine tunaihusisha elimu na hiyo dhati isiyokuwa na ukomo kwa kuzingatia ukweli kwamba viumbe vyote wakati wote vipo mbele yake; halafu tunasema Yeye ni Mjuzi wa Yote. Wakati mwingine tunatambua uwezo wake wa kuumba vitu vyote, na halafu tunazungumzia juu ya Yeye kuwa Mwenye Nguvu zote. Kwa hiyo, pale tunapotambua kupitia kwenye vipenyo hivi mbali mbali, zile sifa tofauti zinazoonekana kufanana na uhai wetu wenye ukomo, tunajaribu kuzitenga kutoka kwenye dhati Yake isiyo na ukomo. Hata hivyo, bila upendeleo, dhana zote zilizowasilishwa na sifa hizo tofauti zinakuwepo mahali pamoja na unawasilisha ukweli moja, ukweli ambao hauna dosari na upungufu wowote, wenye ukamilifu wote kama vile uwezo, huruma, ujuzi, neema, hekima na ufahari.

Amirul-Muminin Ali(a.s) anasema katika hotuba ya kwanza ya Nahjul- Balagha,"Mwanzo wa dini ni kumtambua, na ukamilifu wa kumtambua ni kumsadiki. Imani ukamilifu wa kumsadiki ni kumpwekesha, na ukamilifu wa kumpwekesha ni kuwa na Ikhlasi Naye, na ukamilifu wa kuwa na Ikhlasi Naye ni kumuondolea sifa, kwa ushuhuda wa kila sifa ni si chenye kusifiwa, na ushuhuda wa kuwa kila chenye kusifiwa sio sifa. Hivyo basi mwenye kumsifu Mungu swt. Amemfanyia mwenzi, na mwenye kumfanyia mwenzi amemfanya kuwa wawili, na mwenye kumfanya wawili amemfanya kuwa mwenye sehemu sehemu, na mwenye kumfanya kuwa mwenye sehemu sehemu anakuwa hamjui, na ambaye hamjui anakuwa amemuashiria, na mwenye kumuonyesha amemuwekea mpaka, na mwenye kumwekea mpaka amemfanya wa idadi. Na mwenye kusema yuko ndani ya nini amemfanya yuko ndani ya; na mwenye kusema yuko juu ya nini amemtoa humo."

Kwa hiyo, kila sifa haina ukomo na inakuwa na uhai mrefu wa pamoja na umilele wa dhati yenyewe. Mwenyezi Mungu ametakasika na kuondokana na sifa zinazoweza kuwa tofauti na nyingine na kutenganishwa na dhati yenyewe. Pindi tutakapotambua kwamba dhati ya Mwenyezi Mungu inatokana na Yeye mwenyewe, hiyo ina maana kwamba kuna nafsi kamilifu isiyopimika katika namna zote. Kama kiumbe hai na kisichokuwa na uhai vyote vinaweza kufikiriwa sawa kwa ajili ya maisha, lazima kipate uhai kutoka kwenye kitu kingine ili kiweze kuwa hai; kitu kujianzisha chenyewe, hata hivyo, haiwezekani. Kwa hiyo, ni dhati kamilifu tu ndio inayoweza kutokana na yenyewe; hali halisi nyingine zote ziko chini yake na zinajulikana tu kwa njia yake. Pindi dhati itakapofanana na uhai wake, inakuwa isiyopimika kuhusu ujuzi, uwezo, kutojianzisha na hali ya kudumu milele, kwani zote hizi ni aina za viumbe na chimbuko ambalo linafanana na asili yake kwa hali yoyote ni lazima kuwa na ukamilifu wote huu kwenye kiwango kikubwa sana.

Upweke wa Mwenyezi Mungu (Tauhiid) ni mojawapo ya sifa Zake za mwanzo kabisa. Dini zote za mbinguni, katika mafundisho yao ya asili na yasiyopotoshwa, yamemlingania mwanadamu kwenye uthibitisho halisi wa upweke wa Mwenyezi Mungu, usiotiwa dosari na kushirikishwa na miungu wenza. Kupachikwa washirika huko, kwa namna zote za miundo na mielekeo ndio kosa baya sana ambalo mwanadamu anawajibika kwalo kisheria. Imetokea katika historia yote kama matokeo ya ujinga, kutokutambua, na kukengeuka toka kwenye mwongozo wa akili na mafundisho ya Mitume.

Kama mwanadamu alimwamini Mwenyezi Mungu kwa mujibu wa fikra sahihi, uthibitisho wa akili na mwongozo wa mitume, isingewezekana kwa wao kukubali vitu vyovyote vya kubahatisha au vitu vilivyoumbwa, kusimama mahali Pake, na kudhani kwamba kiumbe kingine chochote kinaweza kuwa mshirika wake au kuwa sawa katika kuamuru na kuthibiti hali za dunia, au hata kuwa na sehemu katika uendeshaji wa mpango wa ulimwengu. Kama miungu wengi wangeitawala dunia na kila mmoja wa miungu hawa angefanya anavyotaka na kutoa amri kufuatana na utashi wake, mpangilio wa ulimwengu ungetambukia kwenye uawala huria. Qur'ani inasema:

وَلَمَّا بَلَغَ أَشُدَّهُ آتَيْنَاهُ حُكْمًا وَعِلْمًا وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿٢٢﴾

"Na (Yusuf) alipofikilia utu uzima, tulimpa hukumu na elimu na hivyo ndivyo tunavyo walipa watendao mema." (12:22)

Kama tunasema kwamba Mwenyezi Mungu ni mmoja, ni kwa sababu Yeye sio mwili. Kuimbe ni mkusanyiko wa mlolongo wa elementi, ambazo kuunganika kwao husababisha kiumbe kuwepo. Kuchanganyika, mgawanyiko na kuzaana zote hizi ni sifa za viumbe na miili inayotegemewa kuweko au kutokea; kwa hiyo tunaiondoa kwenye mfano wa Mwenyezi Mungu na tunathibitisha kwamba chochote ambacho kimekuwepo, kama matokeo ya uchanganyikaji na uzaanaji, wala hakiwezi kuwa Mwenyezi Mungu ama kufanana Naye.

Inawezekana kufikiria juu ya u-wingi ndani ya namna fulani maalum pindi tunapozungumzia mipaka kama vile wingi, ubora na muda. Hata hivyo, Mwenyezi Mungu habanwi kimipaka na lolote kati ya haya, na kwa hiyo haiwezekani kumfikiria Yeye kuwa na wa kufanana Naye au mwenza. Kama tunajaribu kudhania asili ya maji, bila sifa yoyote ya ukomo au mpaka, na tukalirudia zoezi hili mara kadhaa, hakuna kitakachoongeka kwenye dhana yetu ya awali. Kwa sababu mwanzoni tuliyafikiria maji katika maana yake halisi, bila kuweka ufinyu wowote katika hali, wingi au ubora, haiwezekani kwamba katika majaribio yetu yatayofuata ya kutafakari juu yake, nadharia mpya itajitokeza kwetu sisi.

Lakini tunapoongeza kwenye asili ya maji sifa fulani zenye ukomo ambazo sio za msingi juu yake, aina tofauti na mifano ya maji itatokea na pamoja nayo, ni uwingi. Mifano ya hili ingekuwa maji ya mvua, maji ya chemchem, maji ya mto, maji ya bahari, yote haya yakionekana nyakati na sehemu tofauti hapa na pale. Kama tukiondoa masharti yote haya na kuangalia tena asili ya msingi ya maji, tutaona kwamba yameondokana na aina zote za uwili mchanganyiko na sasa ni asili moja tu.

Lazima tutambue kwamba kiumbe chochote ambacho kinaweza kuwekwa na kuenea kwenye sehemu fulani, basi kwa lazima sana kinaihitaji sehemu hiyo, na kitu chochote ambacho kitakuwa ndani ya wakati fulani, uhai wake yenyewe unategemea mazingira bainifu ya wakati huo: uhai wake utatambuliwa tu ndani ya muundo maalum wa kiwakati ambamo mazingira hayo yanaupata.

Kwa hiyo, tunapokuja kuitambua nafsi ambayo ipo wakati wote na kila mahali na ambayo ina kiwango cha juu sana cha ukamilifu wa kueleweka, na ambayo mbali na hiyo hakuna kitu kingine ambacho ni kikamilifu au halisi na kisicho na walakini, lazima tuelewe kwamba kupachika uwili juu ya dhati ya juu kiasi hicho ni kukifanya kiwe chenye mwisho na ukomo. Hakika Mwenyezi Mungu si mmoja kwa maana ya kimahesabu, hivyo kwamba tunaweza kudhania kwamba Yeye ni wa kwanza wa aina ambayo anafuatiwa na wa pili. Upweke wake ni kiasi kwamba kama tukidhania kuwepo wa pili pamoja Naye, yule wa pili lazima afanane na yule wa kwanza.

Kwa kuwa uongezekaji wa vitu hutokana na mazingira yenye kuweka mipaka ambayo huvitofautisha kimoja na kingine, itakuwa haina mantiki kabisa kuleta nadharia ya wa pili juu ya kiumbe kisichokuwa na mipaka na vifungo. Kuwepo kwa wa pili itamaanisha kwamba wa kwanza alikuwa na mipaka na vifungo, na endapo mipaka na vifungo vikiondolewa, hatuwezi kuwa na viumbe viwili; dhana yetu ya kiumbe cha pili itakuwa ni marudio ya kile cha kwanza.

Mafundisho ya upweke wa Mwenyezi Mungu yana maana kwamba kama tukimchukulia Mwenyezi Mungu peke yake bila kuvihusisha viumbe vingine vyote vinavyotambulika, dhati yake tukufu inathibitika kikamilifu. Vivyo hivyo, endapo tunafikiria kuwepo kwake, pamoja na kuvihusisha viumbe vingine vyote, hapo tena, kuwepo kwake kutakuwa kumethibitika kikamilifu. Lakini kama, kwa kinyume chake, tunaviangalia vitu vinavyotokea bila kutarajiwa bila kumhusisha Mwenyezi Mungu basi vitu hivyo haviwezi kusemekana kwa njia yoyote ile kwamba vipo, kwa sababu kuwepo kwao kunategemea juu ya Muumba kwa ajili ya chimbuko lao na kuongezeka kwao.

Kwa hiyo wakati wowote tunapomwekea Mwenyezi Mungu mipaka na masharti, maana yake ni kwamba Mwenyezi Mungu atakoma kuwepo wakati wowote ambapo mpaka na sharti hilo litakoma kuwepo. Hata hivyo, kuwepo kwa Mwenyezi Mungu hakutawaliwi na sharti au wingi, na kwa hiyo akili haiwezi kuleta nadharia ya wa pili katika namna yake. Hebu natutoe mfano mmoja: Tuchukulie kwamba dunia haina ukomo; haina mipaka na katika upande wowote tutakaoelekea kamwe hatufikii mwisho wake. Kwa fikra kama hii kuhusu dunia ya maumbo, mipanuko yake yote ikiwa haina mwisho, tunaweza kudhania kuwepo kwa dunia nyingine zaidi yake, imma yenye ukomo au isiyo na ukomo. Hakika hatuwezi, kwa sababu dhana ya dunia ya viumbe isiyo na mwisho inalazima kuondoa kuwepo kwa dunia nyingine kama hiyo. Endapo tunajaribu kufikiria dunia nyingine kama hii, ama itafanana na ile ya kwanza au iwe ni sehemu yake.

Kwa hivyo, kufikiri kwamba asili tukufu ni kiumbe kilicho kamilika, kudhania kuwepo kwa kiumbe cha pili kinachofanana na Yeye ni sawa kabisa na kudhani dunia ya pili ya viumbe kuwepo kwa wakati mmoja huohuo na dunia ya viumbe isiyo na mwisho. Kwa maneno mengine, hiyo haiwezekani. Kwa hiyo, ni dhahiri kwamba maana ya Mwenyezi Mungu kuwa Mmoja sio kwamba Yeye sio wawili; ni kwamba, wa pili hafikiriki kuwepo na kwamba umiliki pekee wa utukufu unalazimishwa na asili Yake. Anakuwa tofauti na mwingine asiyekuwa Yeye Mwenyewe, sio kwa namna ya mpaka wowote bali kwa namna ya asili Yake yenyewe ambayo inaweza kutofautishwa wazi wazi na zingine zote. Viumbe vingine vyote, vinapolinganishwa, hupata ubainishwaji wao, sio kutoka kwenye asili zao bali hasa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Tunaona dhahiri kwamba uhusiano na upatanifu mkubwa unakuwepo miongoni mwa vijenzi vyote vya dunia. Binadamu huzalisha gesi ya asidi ya kaboni ambayo huiwezesha mimea kuvuta hewa hiyo, na miti na mimea, kwa kubadilishana hurudisha hewa ya oksijeni ambayo humwezesha binadamu kuivuta. Kwa matokeo ya kubadilishana hivi baina ya binadamu na mimea, kiasi cha hewa ya oksijeni huhifadhiwa wakati wote; kama isingekuwa hivyo, hakuna dalili za maisha ya mwanadamu yangebaki juu ya duniani.

Kiasi cha joto kinachopokelewa na dunia kutoka kwenye jua huwa kinakubaliana na mahitaji ya viumbe hai kwa ajili ya kupata joto. Kasi ya mbiringiko wa dunia kuzunguuka jua na umbali inaouweka kutoka kwenye chanzo hicho cha nishati na joto vimekadiriwa katika kiwango kinachofanya uhai wa binadamu juu ya dunia uwezekane. Umbali wa dunia kutoka kwenye jua ndio unaoamua kiwango cha nyuzi joto ambacho hasa ndicho kinachokubaliana na mahitaji ya uhai juu ya ardhi. Kama kasi sya mbiringiko wa dunia kuzunguka jua ingekuwa maili 100 kwa saa badala ya maili 1000 kwa saa, kama ilivyo sasa, vipimo vya usiku na mchana wetu vingekuwa mara kumi zaidi kwa urefu, na ukali wa joto la jua ungepanda na kufika kiwango ambacho uhai wote wa mimea ungeunguzwa na usiku wa baridi wa kila siku ya majira ya kipupwe ungegandisha machipu yote mapya ardhini.

Endapo, kwa upande mmoja, miale ya jua ingepunguzwa kwa nusu, viumbe hai vyote vingegandishwa pale vilipo na baridi iliyokithiri sana. Endapo, kwa upande mwingine, miale ya jua ingeongezwa na kuwa maradufu, mbegu ya uhai kamwe isingeweza kufanikisha matunda yake. Kama mwezi ungekuwa mbali sana kutoka duniani, mawimbi ya bahari yangekuwa na nguvu na makali kiasi cha kutosha kuweza kung'oa milima. Inapooonekana kwa mtazamo huu, dunia huonekana kama msafara ambao wasafiri wake wote wameungana pamoja kama viungo katika mnyororo. Sehemu zake zote, kubwa na ndogo zinajitahidi kwa pamoja kusonga mbele kwenye muelekeo mmoja. Katika mfumo wote huu, kila kitu kinatimiza kazi yake mahsusi na vitu vyote husaidiana na kukamilishana. Kiungo kikubwa na kisichoonekana huunganisha kila atomu moja na atomu zingine zote.

Dunia ambayo imejaa umoja kiasi hicho lazima iwe imeunganishwa na chimbuko na kanuni moja. Uhai unatokana na chanzo kimoja, kama ujumla wote wa ulimwengu ni mmoja, muumbaji wake pia lazima awe mmoja. Ule ukweli kwamba muumbaji ameleta umoja katika uwingi wa dunia iliyoumbwa, huo peke yake ni uthibitisho wa kutosha wa Upweke wake, uwezo na hekima Yake.

Qur'ani inasema:

قُلْ أَرَأَيْتُمْ شُرَكَاءَكُمُ الَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَرُونِي مَاذَا خَلَقُوا مِنَ الْأَرْضِ أَمْ لَهُمْ شِرْكٌ فِي السَّمَاوَاتِ أَمْ آتَيْنَاهُمْ كِتَابًا فَهُمْ عَلَىٰ بَيِّنَتٍ مِّنْهُ بَلْ إِن يَعِدُ الظَّالِمُونَ بَعْضُهُم بَعْضًا إِلَّا غُرُورًا ﴿٤٠﴾

"Sema: mmewaona washirika wenu mnaowaabudu badala ya Mwenyezi Mungu? Nionyesheni ni sehemu gain ya ardhi waliyoiumba au wanayo shirika katiaka mbingu? Au tumewapa kitabu na wao ambacho kwacho wakawa na dalili za wazi? Lakini madhalimu hawaahidiani wao kwa wao ila udanganyifu tu. Kwa hakika Mwenyezi Mungu huzuia mbingu na ardhi zisiondoke, na kama zikiondoka hakuna yeyote wa kuzizuia baada yake. Bila shaka yeye ni Mpole, Mwingi wa kusamehe." (35:40-41).

Asili yetu ya kimaumbile, ambayo ni kipimo cha msingi wa maisha yetu pia inathibitisha upweke wa Mwenyezi Mungu. Katika nyakati za hali mbaya sana na taabu, matakwa yetu yote huelekezwa mahali pamoja; tunageukia upande mmoja na kukabidhi nyoyo zetu Kwake. Mmojawapo wa wanafunzi wa Imamu Jafar as-Sadiq(a.s) alimwuliza, "Kuna uthibitisho gani juu ya upweke wa Mwenyezi Mungu?" Imamu alimjibu: "Uthibitisho wa upweke Wake ni uhusianaji mwendelezo wa maumbile yote, mpangilio muhimu wa uhai ambao unatawala juu ya kila kitu. Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qur'ani:

"Angekuwepo muumba mbinguni na katika ardhi, mbali na yule Mungu Mmoja, mpango wao ungetoweka na dunia ingeangamia."[36] Kwa hiyo, utaratibu na uelewekaji wa mpangilio uliotawala vitu vyote unaikanusha ile nadharia ya kuwa panaweza kuwepo na miungu wengine kadhaa, wanaotawala maeneo yale au maeneo mengine tofauti.

Ingawa Qur'ani inasisitiza upweke wa Mwenyezi Mungu katika uumbaji na hekima, pia inatamka wajibu wa visababisho na njia ambazo zinatekeleza amri ya Mwenyezi Mungu. Inasema:

وَاللَّـهُ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَحْيَا بِهِ الْأَرْضَ بَعْدَ مَوْتِهَا إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّقَوْمٍ يَسْمَعُونَ ﴿٦٥﴾

"Na Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka mbinguni na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, kwa hakika katika hayo mna mazingatio kwa watu wanaosikia." (16:65)

Pindi tunapofikia kwenye hitimisho kwamba Mwenyezi Mungu peke Yake ndiye anayeshughulika na uumbaji, upangaji na uendeshaji wa ulimwengu wote, na kwamba vyanzo vyote vya athari na uhusiano baina yao viko chini ya utashi na amri Yake, kila kimoja kikiwa na kazi yake maalum ilichopangiwa na Mwenyezi Mungu - pindi tunapofikia uamuzi huo, tunawezaje kudhania kiumbe kingine chochote kuwa katika daraja sawa na Mwenyezi Mungu na kuinama katika kukiabudia mbele yake?

Qur'ani inasema:

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ وَلَوْ يَرَى الَّذِينَ ظَلَمُوا إِذْ يَرَوْنَ الْعَذَابَ أَنَّ الْقُوَّةَ لِلَّـهِ جَمِيعًا وَأَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعَذَابِ ﴿١٦٥﴾

"Na miongoni mwa watu wako ambao huwafanya miungu wasiokuwa Mwenyezi Mungu, wanawapenda kama kumpenda Mwenyezi Mungu. Lakini wale walioamini wanampenda sana Mwenyezi Mungu zaidi (2: 165)

وَمِنْ آيَاتِهِ اللَّيْلُ وَالنَّهَارُ وَالشَّمْسُ وَالْقَمَرُ لَا تَسْجُدُوا لِلشَّمْسِ وَلَا لِلْقَمَرِ وَاسْجُدُوا لِلَّـهِ الَّذِي خَلَقَهُنَّ إِن كُنتُمْ إِيَّاهُ تَعْبُدُونَ ﴿٣٧﴾

"Na miongoni mwa ishara zake ni usiku na mchana, na jua na mwezi. Basi msilisujudie jua wala mwezi, bali msujudieni Mwenyezi Mungu aliyeviumba, ikiwa ninyi mnamuabudu Yeye t u." (41:37).

12

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA KUMI NA MBILI

UWEZO WA MWENYEZI MUNGU USIOPIMIKA

Uwezo wa Mwenyezi Mungu Usiopimika,haun uthibitisho wa wazi zaidi kuliko ule unaopatikana kwa njia ya uchunguzi na kuhoji maumbile ya ulimwengu ulioumbwa na mifumo mingi ya mpangilio wa rangi za maumbile ambazo kamwe haziwezi kuelezewa kukamilifu.

Tunapo tazama viumbe wa Mwenyezi Mungu tunajikuta tunakabiliwa na nguvu kubwa mno hivyo kwamba hapana ukomo unaoweza kufikiriwa juu yake. Kutazama uumbaji na mamilioni ya ukweli yaliofichika kwenye maajabu ya maumbile na vina vya ndani vya utu wake mwanadamu mwenyewe kunatoa dalili za wazi kabisa za kipimo cha uwezo wa yule Mmoja Aliyeuumba huo, kwani mpangilio mzito wa uhai na mgumu kuelezeka haukubali maelezo mengine.

Ni uwezo wa Mwenyezi Mungu usiolinganishika ambao humlazimisha binadamu kuinama kwa unyenyekevu mbele ya Muumbaji wa mpango huu mkubwa. Hakuna neno la kuweza kuelezea kadiri ya vipimo vya uwezo Wake, dhati hiyo ya pekee ina uwezo mkubwa mno ambao kwamba wakati wowote Anapolitaka jambo, hutosha kwa ile amri, 'Kuwa' itoke kwake na kitu kilichoambiwa hivyo, kitakuwa. Qur'ani inasema:

إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ ﴿٨٢﴾

"Hakika amri yake, anapolitaka jambo lolote ni kuliambia tu: 'KUWA' na linakuwa. (36:82).

Sheria iliyofafanuliwa katika Aya hii ni ishara nzuri zaidi ya uwezo Wake usio na mpaka na udhihirisho wa mamlaka wa utukufu Wake usio na mwisho. Inabatilisha mpaka wowote ambao unaweza kuwekwa juu ya uwezo wa Mwenyezi Mungu na kutangaza kutotoshekeza kwa vigezo vyote na vipimo, vinapokabiliwa na sheria hii tukufu.

Mabingwa wa sayansi ya viumbe, watu wa maabara, licha ya maendeleo yote ambayo wamepata, hawajapata elimu kamili ya siri za ndani kabisa za kiumbe mmoja pekee miongoni mwa viumbe vingi na vyenye kutofautiana vya ulimwengu ulioumbwa. Hata hivyo, ile sehemu ya elimu na yenye dosari ambayo mwanadamu ameipata kuhusu viumbe vichache vilivyopo hapa ulimwenguni inamtosha yeye kutambua kwa nafsi yake yote kwamba ile nguvu kubwa ambayo imeumba aina mbalimbali na nyingi kama hizi hapa duniani lazima iwe haina ukomo.

Fikiria wingi wa viumbe Vyake: viumbe vidogo sana na madubwana yenye sura za ajabu kwa pamoja wakiishi katika vina vya baharini; ndege wanaopendeza wenye sauti za kuvutia wenye mabawa yenye rangi mbalimbali, ambao uzuri wao, wasanii stadi huiga, kama mapambo ya kazi yao; nyota zing'arazo mbinguni na jua lichomozalo na kuzama; alfajiri na mwanga wa mwezi; sayari, galaksi na jamii ya nyota nyingi za mbali sana kila moja yao wakati mwingine kwenye kiini chake huwa na mamilioni ya nyota kubwa sana zing'arazo na kufanya maruweruwe ukosa ukomo wake wa dhahiri.

hivi maumbile kama haya, yanayoshangaza kwa utukufu wake, hayaashirii uwezo usio na ukomo wa mtengenezaji wake? Je, mtu anaweza kudharau uwezo wa Muumbaji Ambaye anatoa mabadiliko mbali mbali kama haya kwenye maisha, akafanya miundo dhahiri, ya mabadiliko hayo, yenye ukomo kujitokeza kwenye mpango wote huu mpana wa matukio. Sasa baada ya ukweli kwamba aina zote hizi za viumbe za kuvutia hatimaye zinachipukia kutoka kwenye atomu, suala la uhai haliwezi kuelezewa isipokuwa kwa kurejea kwenye mamlaka yenye muongozo na yasiyo na ukomo. Ni Yeye Ambaye huvichochea vitu vyote kuelekea kwenye dhana ya muundo wenye kuleta uhai na anao uwezo na akili ya kupanga na kubuni mpango huu mpana na sahihi.

Kubwa na ndogo, ngumu na rahisi ni tabia zinayofungamana na viumbe vyenye ukomo; katika ufalme wa milele wa dhati na sifa za Mwenyezi Mungu, hakuna suala la ukubwa na udogo, nyingi na chache. Unyonge na udhaifu husababishwa na ukomo wa nishati katika haki ya utumiaji wa wakala, kwa kuwepo kipingamizi katika njia yake, au kwa kukosekana njia na vifaa, hayo ni yasiyowazika katika suala la uwezo usio na ukomo. Qur'ani inasema:

وَمَا كَانَ اللَّـهُ لِيُعْجِزَهُ مِن شَيْءٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ إِنَّهُ كَانَ عَلِيمًا قَدِيرًا ﴿٤٤﴾

" Na hakuna kitu kiwezacho kumshinda Mwenyezi Mungu mbinguni wala ardhini, Bil a shaka yeye ni Mwenye kujua, Mwenye uwezo." (Fatir: 35:44).

Ingawa Mwenyezi Mungu anaweza kufanya vitu vyote, Ameumba ulimwengu kulingana na mpango usahihi na maalum katika mfumo ambao kwamba jukumu lililopangwa maalum, limewekwa juu ya viumbe fulani katika uanzishaji wa vingine. Viumbe hivyo, moja kwa moja na bila shaka yoyote viko chini ya amri Yake wakati vinapotimiza jukumu hilo na kamwe havikiuki amri Zake japo kidogo. Qur'ani inasema:

وَالشَّمْسَ وَالْقَمَرَ وَالنُّجُومَ مُسَخَّرَاتٍ بِأَمْرِهِ أَلَا لَهُ الْخَلْقُ وَالْأَمْرُ تَبَارَكَ اللَّـهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ ﴿٥٤﴾

"Na jua na mwezi na nyota vimetiishwa kwa amri Yake. Fahamuni kuumba na amri zote na Zake. Amebarikiwa Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu wote. (A'aaraf: 7:54).

Kusema kweli, hapana kiumbe katika mpango wa ulimwengu kinachoweza kuwa udhihirisho wa mamlaka au kuwa na fungu lolote katika utashi na amri Yake, kwani kama vile ambavyo Mwenyezi Mungu hana mshirika katika dhati Yake, vivyo hivyo, pia, hana mshirika katika uwakala Wake. Kama vile ambavyo viumbe vyote duniani vinavyokosa uhuru katika asili zao na vikawa vinamtegemea Yeye, pia vinaukosa vilevile katika kutoa vitendo na athari. Kila kiwakilishi na kisababishi hupata dhati ya uhai wake kutoka kwa Mwenyezi Mungu na pia uwezo wake wa kutenda na kutoa athari.

Kila anapotaka na kukilazimisha, amri ambayo inahusu viumbe vyote hutelekeza wajibu wake, kwani utaratibu huo wenyewe upo chini ya utashi Wake, hata kama uwe wenye thamani na imara vipi. Muumbaji Ambaye ameweka athari mahsusi kwa kila kitu na chanzo, anaweza kuitangua na kuahirisha athari hiyo wakati wowote. Kama vile ambavyo amri moja ilivyosababisha utaratibu wa ulimwengu kuwepo, amri nyingine hunyang'anya maumbile athari zao za desturi.

Hivyo, Qur'ani inasema:

قَالُوا حَرِّقُوهُ وَانصُرُوا آلِهَتَكُمْ إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ ﴿٦٨﴾ قُلْنَا يَا نَارُ كُونِي بَرْدًا وَسَلَامًا عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ ﴿٦٩﴾

"Wakasema; mchomeni (Ibrahim) na muiokoe miungu yenu, ikiwa ninyi ni watu wenye kutenda. Tukasema; Ewe moto! Kuwa baridi na salama juu ya Ibrahim. (21:68-69).

Ingawaje ule mvuto wenye nguvu sana utolewao na jua na ardhi unaenea kwenye nafasi kubwa mno, bado maumbo yote hayo yako chini ya utashi Wake. Mara tu Anapompa ndege mdogo nguvu za lazima, ndege huyo anakuwa na uwezo wa kuzuia mvuto wa ardhi na akaruka zake. Qur'an inasema:

أَلَمْ يَرَوْا إِلَى الطَّيْرِ مُسَخَّرَاتٍ فِي جَوِّ السَّمَاءِ مَا يُمْسِكُهُنَّ إِلَّا اللَّـهُ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿٧٩﴾

"Je, hawawaoni ndege waliotiishwa katika anga la mbingu? Hakuna awazuiaye (wasianguke) isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hakika katika hayo mna mazingatio kwa watu wanaoamini. (16:79).

Kiumbe chochote kinachoweza kufikiriwa kuwepo katika dunia ya maumbile kinakuta mahitaji yake ya riziki na maisha yanatimizwa na Muumbaji. Kwa hiyo, uwezo wowote na nafasi inayoonekana kwenye mpango wa maumbile inabidi lazima kurudi kwenye uwezo usio na kikomo wa Mwenyezi Mungu. Amirul-Mu'minin Ali(a.s) anasema kwenye hotuba iliyoandikwa kwenye Nahju al-Balagha:

"Ee Mwenyezi Mungu, hatuwezi kupenya vina vya ubora utukufu wako. Tunajua kwamba Wewe uko hai daima na unajitosheleza, kwamba wewe huhitajii kula wala kulala usingizi. Hakuna akili inayoweza kukutambua Wewe na hakuna jicho linaloweza kukuona wewe. Bali Wewe unayaona macho yote, Unajua kipindi cha uhai wa kila kiumbe, na Wewe ni Muweza wa kila kitu.

"Ingawa hatujatambua lolote katika uumbaji Wako, tunashangazwa na uwezo Wako na tunakutukuza sana Wewe. Kile kilichofichika kwetu na macho yetu hayawezi kukiona wala fikra na akili haviwezi kukipata, ambacho kimefichwa kwetu kwa mapazia ya ghaib (yasiyoonekana) ni kikubwa zaidi kuliko kile tunachokiona." [37] Mtu anapoamua kujenga kitu - mfano hospitali - hukusanya vitendea kazi muhimu na vifaa vingine ambavyo havina uhusiano wowote muhimu kati ya kimoja na kingine, na halafu anaviunganisha kwa kutumia mlolongo wa uhusiano wa bandia ili kutimiza lengo lake.

Ili aweze kutengeneza uhusianao wa bandia kama huo, hutumia nguvu tofauti tofauti na vitu vingine ambavyo anavikuta tayari vipo. Kazi na shughuli ya mtu huyu ni sehemu ya mfumo wa maumbile, sio shughuli ya ubunifu kwa kusema kweli, bali ni namna ya msogeo tu ambao unafanyika ndani ya vitu vilivyopo. Uumbaji wa ki-Mungu unakuwa na aina tofauti kabisa na ule uzalishaji wa uhusiano wa bandia baina ya vitu visivyo husiana. Mwenyezi Mungu huanzisha vitu vikiwa na tabia zao zote, nguvu, nishati na sifa bainifu.

Tunaposema Mwenyezi Mungu ni mweza wa yote, lazima tuelewe kwamba uwezo wake unavutika au kuitikia tu kwenye vitu vinavyowezekana. Vitu ambavyo haviwezekani kimantiki vipo nje ya nyanja (fani) ya uwezo Wake na kutumia neno 'Uwezo' kuhusiana na vitu ambavyo haviwezekani sio sahihi na haina maana yoyote. Ingawa uwezo wa Mwenyezi Mungu kwa kweli hauna ukomo, uwezo wa mapokezi wa vitu na uwezo wao wa kutumika kama kituo maalum kwa ajili ya udhihirishaji wa uwezo wa ki- Mungu lazima ufikiriwe. Utekelezaji wa utashi wa Mwenyezi Mungu unasokotana na uhusiano baina ya chanzo na athari, na mfumo mgumu wa sababu na vyanzo usioelezeka kwa urahisi. Ili kitu kiweze kuwa lengo la utashi wa ki-Mungu, lazima kisiwe ni kisichowezekana na lazima, katika asili yake, kiwe na uwezo wa kupokea; utashi wa ki-Mungu unatimizwa kwa njia ya wepesi wa upokeaji vitu vyenyewe. Ni kweli, kwamba nuru ya ki-ungu haina ukomo na wakati wote inazidi kufurika, lakini sehemu inayotakiwa kuipokea nuru hiyo inaweza kuwa na dosari na kwa hiyo inashindwa kufyonza mgawo huo wa kudumu ambao unatolewa na chanzo hicho chenye ukwasi tele.

Bahari ni chanzo kikubwa sana cha maji, chenye maji mengi sana, lakini meli ya kubebea vimiminika ina nafasi ndogo tu ya kuchukua maji yake; kwa kweli ni kiasi kidogo sana cha maji hayo kitakachoweza kupakiwa kwenye meli hiyo. Kwa uwazi wa kutosha kabisa ni kwamba chenye mpaka na kikomo katika mfano huu ni nafasi ya meli, sio maji katika bahari hiyo.

Mtu mmoja wakati fulani alimuuliza Ali, Amirul-Mu'minin(a.s) : "Je, Mola wako anaweza kuijaza dunia yote kwenye yai la kuku?"

Akajibu:Mwenyezi Mungu Mweza wa Yote, kwa hakika anaweza kufanya chochote, lakini kile ulichouliza ni kitu kisichowezekana." [38] Kwa hiyo ingawa dhati tukufu ya Mwenyezi Mungu ipo huru kabisa kutokana na kutokuwa na nguvu na uwezo, haina maana na mantiki kuuliza kama Mwenyezi Mungu anaweza kufanya jambo ambalo kwa asili haliwezekani.

Mtu ambaye moyo wake hudunda kwa kumpenda Mwenyezi Mungu na ukawa umejawa na imani juu ya Muumbaji wa vitu vyote kamwe hatokata tamaa, kujihisi mpweke na asiye na matumaini hata katikati ya matatizo magumu sana. Tendo lolote analolifanya, anafanya huku akitambua kwamba yupo kwenye kivuli cha ulinzi cha nguvu kubwa ambayo inaweza kumfanya yeye aweze kupata ushindi juu ya matatizo yote. Mtu anayemtambua Mwenyezi Mungu na anajua kwamba anafaidi msaada Wake anaweza kujizuia na kustahamili matatizo ya kila aina. Kwake yeye mtu huyo matatizo ni kama sehemu ya povu iliyomo kwenye povu linalotoweka haraka juu ya uso wa maji. Moto unaowaka ndani mwake huendelea kuwaka na kuangaza zaidi na anatokea kuwa na nguvu zaidi kuliko mwanzo kutoka kwenye kalibu (kikaango) ya mateso.

Wakati wote binadamu wa kazi ngumu anazostahimilia, analiwazwa na kutiwa nguvu na huruma na upendeleo wa Mwenyezi Mungu, hali hii ndiyo inayo tengeneza nguvu ya shughuli yake. Kushindwa hakumzibii njia yake na kusababisha asalimu amri badala yake, kwa nia njema na juhudi za uchapakazi, huendelea kufanya bidii kwake hadi mwishowe anapopata ushindi.

Anaelewa vema kabisa kwamba juhudi zake haziwezi kukosa kuleta matokeo mazuri na kwamba ushindi huenda kwa yule anayestahili. Kila anaporidhia, Mwenyezi Mungu humshika mkono yule aliyeanguka na mwenye kudhulumiwa ambao hawana kimbilio jingine mbali na Kwake na kuwanyanyua na kuwafikisha kwenye kilele cha uwezo. Pia wakati mwingine Mwenyezi Mungu, huzipaka vumbi la udhalilishaji na mabalaa, zile pua za wenye uwezo na madhalimu wenye kiburi ambao huamini kwenye vurugu tu na mantiki ya mabavu na kuwatendea watu kama vile hawana thamani.

Ni madikteta wangapi wenye kiburi wametupwa chini na mabalaa katika historia ya mwanadamu, wakazama na kutoweka katika wimbi la aibu. Mfululizo wa kisa cha mitume wa Mwenyezi Mungu unawakilisha mfano kamili na bora wa maadili mema ya binadamu. Sote tunajua jinsi mitume walivyosimama peke yao dhidi ya nguvu za dhuluma za wakati wao ili waweze kuwaongoza wanadamu kwenye ukombozi, kuibadili jamii yao, na kuwafundisha maadili ya kiwango cha juu. Kwa kufanya hivyo, waliwasha cheche ya kwanza ambayo hatimaye iliangamiza ushirikina.

Majibu yaliyoamshwa na imani zao yalisababisha vurugu ya uhakika hivyo, kiasi kwamba waliweza kubadili sura na mwelekeo wa historia. Waliweka misingi ya ibada ya Mungu mmoja (Tawhiid) na waliasisi kanuni za maadili kwa njia pana zaidi. Ni nani anayeweza kukanusha wajibu waliofanya kwa kujitolea kwao na imani zao katika mapambano yasiyochokesha waliyoyafanya? Ni umbali gani nguvu ya utashi peke yake inaweza kumfikisha wanadamu na kwa kiasi gani itamwezesha kustahamili na kujitolea mhanga?

Uchambuzi wa haraka wa historia ya kujivunia ya maisha ya Mitume unatuwezesha sisi sote kutazama, kwa namna ya dhahiri kiasi iwezekanavyo, ule uaminifu na utiifu waliouonyesha, huruma zao na uvumilivu wao na tamaa yao kubwa ya kuwaongoza na na kuwabadilisha wanaadamu.

Siri yao kuu juu ya mafanikio yao ni ukweli kwamba kamwe hawakujifiria wao wenyewe binafsi hata mara moja, kwa uaminifu walizikana nafsi zao, na kuzifanya wakfu katika njia ya Mwenyezi Mungu. Halafu Mwenyezi Mungu akajibu kwa kuwajaalia Mitume uhai na umaarufu wa milele daima.

6

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA SITA

HAJA YA ULIMWENGU KUMHITAJI YULE ASIYEHITAJI CHOCHOTE

Kanuni ya usababisho ni ya kawaida na fani zote na msingi wa juhudi zote za mwanadamu, katika kutafuta elimu na katika shughuli zake za kawaida vilevile. Jitihada za wanazuoni kuvumbua sababu za kila jambo, ama liwe la kimaumbile au la kijamii, hutokana na imani kwamba hakuna kitu kinachojianzisha ndani yake, au chenyewe tu bila sababu na asili kuingilia kati.

Utafiti wa wanafikra duniani pote umewapa wao uwezo wa kufahamu vizuri zaidi mpangilio wenye nguvu sana wa maumbile; jinsi wanavyozidi kusonga mbele kwenye mkondo wa maarifa ndivyo wanavyozidi kujifunga kwenye kanuni ya usababisho. Kiungo baina ya sababu na athari, na kanuni kwamba hakuna kitu kitakachotokea chenyewe kwenye uwanja wa uwepo bila sababu, ni miongoni mwa maamuzi yenye nguvu sana ambayo yamepata kufanywa na mwanadamu na kuthaminiwa kama sharti la kimsingi kwa shughuli za kitaalamu. Yanawakilisha kitu ambacho ni kawaida na cha asili, kinachofyonzwa na akili zetu moja kwa moja bila kukwepa.

Hata mwanadamu aliyeishi kabla ya historia kuanza kuandikwa alielekea kugundua sababu za mambo, na kwa kweli, wanafalsafa waliipata dhana hai ya uhusiaino kati ya sababu na athari kutoka kwenye asili yenyewe na silika ya mwanadamu kabla ya kuiweka katika kalibu (chungu) ya kifalsafa. Kufungiwa kama tulivyo kwenye kuta nne mata, hatukabiliani kamwe na kitu chochote cha kutuka chenyewe kwenye uhai, na kwa kweli, hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kamwe kukabiliana, katika historia ya ulimwengu, na kutuka kwa jambo ambalo halitokani na sababu. Kama hali isingekuwa hivyo, tungeweza labda kuwa kisingizio cha kuufikiria ulimwengu kuwa ni kitu cha kutuka chenyewe katika asili yake. Itakuwa ni aina gani ya kutuka kiajali ambako tangu mwanzo wa kuwepo kwa uhai hadi sasa, kumeongoza muingilano huo usiopimika wa vitu vyote, katika mfumo na mtindo wa kushangaza kiasi hicho? Je, inawezekana mpangilio huu tunaoufahamu ukawa ni kuakisi kwa jambo la kutuka na sadifa ya hivi hivi tu?

Kitu chochote kinachoweza kudhaniwa hapa ulimwenguni kilikuwa kimezamishwa kwenye giza la kutokuwepo kabla hakijapata umbile la kiumbe. Hakiwezi kupenya giza la kutokuwepo na kujitokeza kwenye uwanja wa uhai kama kitu kilichopo hadi mkono wa kisababisho wenye uwezo mkubwa uingie kazini.

Uhusianao baina ya chanzo na athari ni uhusiano baina ya vitu viwili vilivyopo, kwa maana kwamba kuwepo kwa kimoja chao kunategemea juu ya kuwepo kwa kile kingine. Kila athari ina uhusiano wa mvuto na uwiano na chanzo chake, kwa kuwa athari hupata kuwepo kwake kutoka kwenye chanzo. Uhusiano huu maalum hauwezi kuharibiwa au kubadilishwa na mwingine.

Wakati wowote unapofikiria asili ya kitu chenye uhusiano wenye kufanana kwa kiumbe hai na kisichokuwa hai, na vyote vikiwa hakuna ambacho ni muhimu kimsingi kwa ajili ya kitu hicho, kitu hicho huitwa 'dharura' kwa maana kwamba hakuna chochote katika asili yake kinachosababisha ama uhai au kutokuwa hai. Kama kitu katika asili yake kinahitaji kutokuwa hai kwake, basi kuwa hai kwake hakuwezekani. Hatimaye, endapo uhai utajitokeza kutoka ndani ya asili ya kitu kwa namna ambayo kwamba akili haiwezi kukiona kwamba ni tegemezi kwa kitu kingine chochote, uhai wa kitu hicho unafanywa kuwa muhimu. Ni kiumbe hai kinachojitegemea, kisichohitaji chochote na kinajikimu kwa njia za asili yake binafsi, kuwepo kwake ndicho chanzo cha viumbe vingine vyote ambapo chenyewe hakitawaliwi na haja au hali yoyote.

Inapaswa kuongezwa hapa kwamba kuwepo kwa maada hakuwezi kupata sifa ya "muhimu" kwa sababu kuwepo kwa kitu chochote cha mchanganyiko wa maada kunategemea kuwepo kwa sehemu zinazokiunda kitu hicho; kinakuwa ni tegemezi juu ya sehemu zake chenyewe kwa ajili ya chanzo na kuendelea kwa uhai wake. Mata ina mielekeo tofauti na ukubwa mbalimbali; yenyewe imetumbukizwa kwenye kiasi na kuongezeka, na inapata ukubwa wake mbali mbali kwa namna ya sifa na tabia. Kiumbe muhimu, kwa kinyume chake, hakihitajii tabia zote hizi.

Vitu vyote ambavyo wakati fulani havikuwepo halafu vikajakuwepo, wakati mmoja vilitawaliwa na dhana ya kufikirika ya uhai na kutokuwa hai. P ale vilipokimbilia kwenye hatua ya uhai, hii ilikuwa ni matokeo ya chanzo ambacho kilivilazimisha mwelekeo huo, kilikuwa ni kichocheo, kipengele cha nje ambacho kilivisukuma vyote kwenye mwelekeo mmoja badala ya ule mwingine. Kwa mneno mengine, kuwepo kwa chanzo ilikuwa ni wakala wa kiumbehai, kama vile kutokuwepo, au kukosekana sababu ni asili ya kutokuwepo kiumbe.

Kwa kawaida, kitu ambacho kinakuja kuwepo kama matokeo ya kuwepo kwa chanzo kamwe hakipotezi asili yake ya kuhitaji, wakati wote kitabia kiumbe chenye kuainishwa na kuhitaji. Kwa sababu hii, haja ya kitu juu ya kuwepo chanzo ni ya kudumu na isiyotanguka, uhusiano wake na chanzo hicho hautakatika japo mara moja. Endapo uhusiano huo ungekatishwa, uhai wa kitu hicho ungesalimu amri mara moja na kutokuwepo, kwa namna ile ile ambayo kwamba, mara jenereta ya umeme inapoacha kufanya kazi, taa zote angavu zilizounganishwa hapo hizimika. Ni kwa sababu hii kwamba chanzo na athari, uhuru kutokana kuhitaji na kutawaliwa na mahitaji ni hali ambazo zinahusiana wakati wote, endapo uhusiano huo ungekatizwa, kusingebakia chochote isipokuwa giza na kutokuwepo uhai.

Hivyo, hakuna jambo linaloweza kuonekana dhahiri hapa duniani mpaka uwezo maalum uwe umewekwa juu yake na kimoja ambacho asili yake iko huru kutokana na kuhitaji na chenyewe ndio chanzo haswa ambacho uhai hububujika kutoka humo. Kama uhai ungekuwa ni sehemu ya asili za vitu, kamwe usingefuata mkondo wa kukoma na kutoweka. Lakini ni ile tabia ya kuhitaji ndio tabia ya msingi kwenye asili zao, ili hata baada ya uhai wao kuanzishwa kwenye mpangilio wa viumbe, sifa yao ya kuhitaji huendelea kuwepo kwa hali yoyote ile. Haviko huru kamwe na kutohitaji chanzo; haiwezekani kwamba athari iweze kupata uhai kwa uhuru kabisa au iendelee kuwepo japo kwa nukta moja bila kutegemea juu ya chanzo. Kwa hiyo inakuwa dhahiri juu yetu kwamba vitu vyote - viumbe hai vyote vinavyoweza kutokea - vinapata wakati wote na kwa kila mara kutoka kwenye asili isiyo na ukomo ambayo ndio hugawa uhai - yaani, ile Nafsi Muhimu, ya Pekee na Muumbaji Muweza - ule uwezo na uhai unaoviruhusu kuwa hai na kubakia kuwepo hai.

Qur'anii Tukufu inasema:

يَا أَيُّهَا النَّاسُ أَنتُمُ الْفُقَرَاءُ إِلَى اللَّـهِ وَاللَّـهُ هُوَ الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ ﴿١٥﴾

"Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kujitosha, Msifiwa (Fatir:35:15).

Na tuzingatie pia wito huu wa Qur'ani:

أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ ﴿٣٥﴾

"Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?" ( Tur: 52:35).

أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بَل لَّا يُوقِنُونَ ﴿٣٦﴾

"Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini" (Tur: 52:36).

أَمْ لَهُمْ إِلَـٰهٌ غَيْرُ اللَّـهِ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٤٣﴾

"Au wanae mungu mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametakasika Mwenyezi Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye." (Tur: 52:43).

تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١﴾

"Ametukuka ambaye mkononi mwake umo Ufalme wote; na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu." (Almulku: 67:1).

Chanzo cha viumbe vyote chenyewe hakihitajii kuwa na Asili Wafuasi wa uyakinifu wanatoa uangalifu wa ukosoaji sana kwenye kanuni ya kwamba Mwenyezi Mungu hahitaji kuwa na Asili. Wao wanasema endapo tutadhani Muumbaji ndiye chimbuko la ulimwengu na ndiye anayeweka uhai juu yake, viumbe vyote vikipata vyanzo vyao na uhai wa kuendelea kutoka kwake, ni sababu gani imemuondolea yeye haja ya kuwa na muumbaji, ni kiwakilishi gani kilichosababisha yeye mpaka kuja kuwepo? Katika hotuba iliyotolewa kwenye jumuiya ya 'Londoni Atheist Sosiety,' mwandishi maarufu, Betrand Russell, alisema; "Siku moja, nilipokuwa na umri wa miaka kumi na nane, nilikuwa ninasoma wasifu wa John Stuart Mill. Sentenso moja mahsusi ilinivutia sana: Mill aliandika kwamba siku moja alimuuliza baba yake, ni nani aliyemleta yeye kwenye uhai duniani, na baba yake hakuweza kumjibu." Sababu yake ni kwamba papo hapo aliuliza swali la ni nani aliyesababisha Mwenyezi Mungu kuwepo?

Halafu Russell anaongeza: "Bado ninasadiki kwamba sentenso ile rahisi inadhihirisha ile ghiliba ya chanzo cha msingi. Kwani kama kila kitu lazima kiwe na sababu na chanzo, hali hiyo lazima itumike juu ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu. Kama, kinyume chake, kitu kinaweza kuwepo bila ya sababu au chanzo, kitu hicho inawezekana kiwe ama Mwenyezi Mungu au ulimwengu, na mjadala wote unakuwa hauna maana."[17] Kwa bahati mbaya, wanafalsafa fulani wa nchi za Magharibi ambao wanakubali kuwepo kwa Mwenyezi Mungu wameshindwa kufumbua tatizo hili. Mwana falsafa wa Uingereza Herbet Spencer amesema yafuatayo

kuhusiana na suala hili: Tatizo ni kwamba, kwa upande mmoja, akili ya binadamu hufuata sababu ya kila kitu na, kwa upande mwingine, hukataa fhana zote zisizo na mantiki (kwa vile ukweli wa dhana hizo hauwezi kuthibitishwa bila kurejea kwenye hitimisho). Haitambui wala kuelewa chanzo kisichosababishwa. Mchungaji anapomwambia mtoto kwamba Mwenyezi Mungu ameumba ulimwengu, mtoto huuliza nani aliyemuumba Mwenyezi Mungu?[18] Mahali pengine mwanafalsafa huyu anasema: "Myakinifu hujaribu kujisadikishia mwenyewe kuhusu dunia ambayo ipo na imetokana na yenyewe, milele bila ya kisababisho. Hata hivyo, hatuwezi kukiamini kitu ambacho hakina mwanzo wala asili. Mwanatheolojia huyo anayapeleka mambo haya hatua moja zaidi nyuma kwa kusema kwamba Mwenyezi Mungu aliuumba ulimwengu. Lakini mtoto anamuuliza swali lisilojibika: Nani aliyemuumba Mwenyezi Mungu?[19] .

Tunaweza kuleta hasa upinzani kama huo huo dhidi ya wayakinifu na kuwauliza, endapo tukifuata mlolongo wa usababishaji kinyumenyume, hatimaye tutafika penye chanzo cha msingi. Natuseme kwamba chanzo si Mwenyezi Mungu, bali ni mata. Sasa hebu tuambieni ni nani aliyeiumba mata ya msingi. Ninyi mnaoamini katika kanuni ya usababisho, tujibuni sisi swali hili. Kama mata ndio chanzo halisi cha vitu vyote, ni nini chanzo cha mata? Mnasema kwamba asili ya vitu vyote ni nguvu ya mata, ni nini sababu na asili ya nguvu ya mata? Kwa kuwa mlolongo wa usababisho hauwezi kurudi kwenye kutokuwa na ukomo, jibu pekee wanaloweza kutoa ni kwamba mata ni kitu kisicho na wakati na chenye umilele ambacho hakiwezi kuwekewa mwanzo: mata ni kitu kisichoumbwa, hakina mwanzo wala mwisho, kuwepo kwake hutukia ndani ya asili yake yenyewe.

Hii ina maana kwamba wayakinifu wanakiri kuwepo kwa kanuni ya umilele na kukosa chimbuko; wanaamini kwamba vitu vyote vilitukia kwenye maada ya milele na kwamba uhai unatukia kutoka ndani ya asili yenyewe hasa ya maada, bila ya haja yoyote ya muumbaji. Russell anelezea wazi imani hii kwenye hotuba iliyonukuliwa hapo juu. Yeye anasema; "Hakuna uthibitisho kwamba dunia ilipata kuwa na mwanzo kamwe. Hii fikira ya kwamba vitu lazima wakati fulani vilikuwa vina mwanzo inatokana na ufinyu wa fikra zetu."[20] .

Kwa namna ile ile ambayo Russell anafikiria mata kuwa ni ya milele, wanaomwamini Mwenyezi Mungu wanahusisha sifa ya umilele kwa Mwenyezi Mungu. Imani katika kitu chenye umilele kwa hiyo ni ya shirika, ya kawaida kwa wanafalsafa wa kiyakinifu na kidini. Makundi yote mawili yanaafiki kwamba kuna chanzo cha msingi, lakini wanaomwamini Mwenyezi Mungu wanakiachukulia chanzo cha msingi kama ni chenye hekima, ujuzi wote, na chenye kumiliki uwezo wa kuamua na utashi, ambapo kwa maoni ya wayakinifu, hicho chanzo cha msingi hakina busara wala akili, utambuzi ama uwezo wa maamuzi. Hivyo, kumwondoa Mwenyezi Mungu, kwa hali yoyote ile hakuleti ufumbuzi wa tatizo linaloletwa na suala la kiumbe cha milele.

Zaidi ya hayo, maada ni kituo cha mwendo na mabadiliko, na mwendo wake ni wenye nguvu na imewekwa ndani ya asili yake yenyewe. Sasa, mwendo muhimu hauendani na umilele, na mata na utulivu muhimu ni jinsi mbili ambazo zote ni za kipekee ambazo haziwezi kuunganishwa kwenye kituo kimoja. Chochote kile ambacho kimetulia na hakibadiliki katika asili yake hakiwezi kupokea mwendo na mabadiliko katika asili hiyo.

Ni vipi wenye fikira za ki-Marx, ambao wanaamini kwamba mata inaandamana na tamathali yake yenye dhana ya kutofautiana (tabaini), wanavyoweza kuthibitisha umilele wa maada? Umilele maana yake ni umadhubuti na kutobadilika kwa asili, kutowezekana kwa ukomo, lakini maada katika asili yake ni ufupisho makini wa nguvu na uwezekano; inawiana yenyewe, ikiwa imenasa kabisa katika kuishi na kufariki. Umilele hauendani na mtindo wa uhai uliomo kwenye mata na vipengele na sifa zilizolazimishwa na asili yake. Itikadi ya wale walio na imani juu ya Mwenyezi Mungu kuhusu kanuni isiyobadilika na ya dhahiri inahusika kwa kiumbe ambacho ndani, na, kwa asili yake kinaweza kukubali utulivu na kutobadilika; asili yake hainazo kabisa - na iko mbali nazo - sifa za maada. Asili yenyewe hasa ya maada inakataa kudumu, umilele na uendelevu, kwani kamwe haiwezi kujitenga yenyewe na mwendo, kuwiana na inakataa kuwa chanzo cha msingi au kisichobadilika.

Itakuwa na manufaa hapa kusimulia mazungumzo baina ya Imamu Sadiq(a.s) na mmoja wa wayakinifu wa wakati wake. Myakinifu: "Viumbe viliumbwa kutokana na nini? Imamu: "Havikuumbwa kutokana na kitu chochote (yaani kiasili havikuwa viumbe)." Myakinifu: "Sasa vinakua vipi na kujitokeza kutoka kwenye kutokuwa kiumbe?"

Imamu: "Je, sikusema kwamba vitu vyote duniani havikuumbwa kutokana na chochote? Maana yangu ni hii, kwamba viumbe vyote ki-asili havikuwa viumbe, na halafu vikaja kuwepo. Unataka kusema kwamba dunia ni ya milele, lakini fhana hii si sahihi kwa sababu zifuatazo:

"Kwanza, kama dunia hii ya maada ni ya milele, ina maana kwamba kitu chenye umilele lazima kipatwe na kubadilika na ukomo, jambo ambalo haliwezekani.

"Pili: endapo elementi zinazotengeneza dunia ni vya milele kwa sababu ya asili yao, inawezekanaje basi ziingie kwenye mkumbo wa kifo na kutoweka? Na kama, katika kinyume chake, zinakuwa hazina uhai katika asili zao, ni namna gani uhai unavyoweza kuchomoza kutoka ndani yao? Endapo utasema kwamba viumbe hai hutokana na elementi hai na viumbe visivyo hai hutokana na elementi zisizo hai, tunajibu kwamba asili isiyona uhai ndani mwake na utokanao ndani mwake haiwezi kuwa ya milele na haiwezi kuwa chanzo cha uhai." Myakinifu: "Kama maada iko kama vile usemavyo, kwa nini viumbe vinasemekana kuwa na umilele?" Imamu: "Imani katika umilele wa ulimwengu inashikiliwa na wale wanaokanusha kuwepo kwa mtawala na mpangaji wa maumbile, wanawakataa mitume wa Mwenyezi Mungu, wanafikiria vitabu wanavyokuja navyo wajumbe ni ngano za kale, na kubuni itikadi zinazowaridhisha wao wenyewe."[21] .

Sasa tunasema kwamba, kuwepo kwa kitu hakuwezekani bila ya chanzo cha kitu chenye upungufu, yaani, ambacho majaaliwa yake yamo mikononi mwa chanzo chake na ambacho kudumu kwake kunategemea kuwepo hai kwa chanzo chake. Hali hii haiwezi kutumika kwa kitu ambacho, kinafahamu uhalisi wake na hakioneshi dalili yoyote ya upungufu na ukomo.

Chanzo cha msingi ni chanzo msingi kwa sababu ya kuwa na uhai kamilifu na usiokuwa na kikomo; bila kutawaliwa na asili yoyote, kimeepukana na kuhitaji, mazingira na utegemezi, na hakina dalili ya kugeuka au kubadilika.

Tunapozungumzia kuhusu sababu ya mwanzo na wakati huo huo tunasema kwamba Mwenyezi Mungu ameepukana na haja yote ya kuwa na chanzo, hatuna maana ya kwamba Yeye kwa ujumla anashirikiana na viumbe vilivyoumbwa ile haja ya kuwa na chanzo lakini wakati fulani alikuwa, kama ilivyokuwa, aliondokana na kanuni ya usababisho. Mwenyezi Mungu sio athari kwamba ahitaji chanzo; Yeye si kiumbe kwamba ahitajie muumbaji. Kinyume chake, dalili zote na maajabu ya uhai vinatokana na Yeye, chanzo cha milele cha uhai. Kanuni ya usababisho hutumika kipekee kwenye mazingira ya vile vitu ambavyo kutokuwepo kwao kulitangulia - kabla ya kuwepo kwao.

Vivyo hivyo, maana ya sababu ya mwanzo si kwamba Mwenyezi Mungu alijibuni Mwenyewe, kwamba Yeye alikuwa ndio chanzo chake mwenyewe. Mahitaji ya athari kwa ajili ya chanzo yamo kwenye aina ya uhai ambao kile kilichotangulia kinao; kinakuwepo sio kwa sababu kina uhai kimsingi bali ni kama matokeo ya uhai utokanao na kitu kingine na ulio tegemezi kinaoupata kutoka kwenye chanzo. Lakini kiumbe ambacho asili yake haitawaliwi na hali yoyote na kinaonyesha kutokuwepo kabisa kwa utegemezi na uhusiano umeondolewa kabisa kutoka kwenye mazingira ambamo ile kanuni ya usababisho inafanya kazi.

Endapo kiumbe kwa sababu ya ukamilifu na kutokuhitaji kwa asili yake, kinakuwa hakihitaji chanzo, maana yake ni kwamba hakuna chanzo kilichokiweka katika kiwango maalumu cha uhai na kwamba hakuna sababu inayoweza kuingilia ndani yake. Mlolongo wa kisababisho hauwezi kurefushwa kurudi nyuma bila kikomo, na kukosekana kwa uhusiano ni kwa asili katika dhana yenyewe hasa ya chanzo cha awali. Swali kama: "Hicho chanzo cha awali kilijitokeza lini?" kwa hiyo, huwa halijitokezi; hivyo maswali kama haya hutumika tu juu ya vyanzo vya vitu na tabia zao za kutegemea.

Kuwepo kwa chanzo cha kwanza kunatambulika kwa dhati yake; kuwa kwake chanzo cha kwanza chenyewe, kwa hakika pia kunattmbulikana kwa dhati yake. Tabia zote hizi zinaashiria kujitosheleza, ambapo vitu ambavyo kuwepo kwao kumetokana na vitu vingine huwa vinahitaji chanzo, kwa sababu vinajulikana kwa tabia za kubadilik na kugeuka, kwa kuchipukia kutoka kwenye kutokuwepo na kuingia kwenye kuwepo. Inawezekanaje kudhaniwa kwamba imani katika kuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni kukiri kuwepo kwa kuhitilafiana, ambapo imani juu ya asili isiyoanzishwa ya athari kama vile maada iwe haipingani?

Tunaishi kwenye dunia ambayo vitu vyote vimeachwa wazi kwenye kubadilika na kuharibika; ipo dalili ya kutokudumu, kutawaliwa na kufadhiliwa kulikochapwa kwenye kila chembechembe yake. Kuhitaji na kutegemeana kumeota mizizi imara katika uhai wetu na ule wa kila kitu kilichomo duniani na mbinguni. Uhai wetu sio wa kudumu na haukuzuka kutoka ndani ya asili yetu wenyewe; hatukuwa, na halafu tulifunikwa kwenye joho la kuwepo na tukaja kuwa hai. Ili kuweza kuja kwenye uhai, viumbe kama vile sisi lazima tuwe wenye kuomba sana kumfikia mwenye kutoa uhai.

Lakini Yeye Ambaye ni wa milele nawa kudumu, ambaye kuwepo kwake kunatokana ndani ya asili Yake Mwenyewe, na Ambaye kuonekana kwake kuko nje ya wakati, ni wazi kabisas hana haja ya chanzo. Maana ya chanzo katika falsafa ni kile kinacholeta athari kutoka kwenye kutokuwepo kitu hadi kuwepo kwake na kukifunika na vazi la uhai. Uumbaji huu hauwezi kutolewa hoja kwa ajili ya vyanzo vya kimaada, na jukumu moja tu la mata ni kuacha umbile moja ili kuweza kupokea umbo lingine.

Ni kweli kwamba kila kiumbe cha kimaada hupata tabia mpya na iliyo tofauti katika kila nukta kama matokeo ya maendeleo ya ndani kwa ndani. Hata hivyo, usogevu wa kimaumbile wa dunia na mifuatano ya uletaji na uchafuzi inadai mahitaji kudumu ya msaada kwa yule ambaye huumba mwendo, msaada ambao hulea msafara wa haraka wa uhai na kuusukuma kwenda mbele.

7

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA SABA

UKOMO WA NYORORO YA USABABISHO

Wayakinifu wanaweza kung'ang'ania kwa ukaidi kabisa katika kukanusha ukweli na kuleta hoja nyingine yenye kuonekana kama ni nzuri. Wanaweza wakasema, "Hatuikatishi nyororo ya usababisho lakini, kinyume chake tunaiendeleza isiwe na mwisho; tunatetea kanuni ya asili isiyo na ukomo ya kiungo sababishi."

Kama ni hivyo, wanapaswa kujibiwa kama ifuatavyo: Kuchambua dunia ya maumbile kwa namna hii kunasimama kwenye kufikiria juu ya nyororo ya visababisho na athari na mkunjuko wa kudumu wa mfuatano wa vyanzo usio na ukomo. Hata hivyo, kwa vile kila chanzo pia ni athari, kinakosa chenyewe kuwa kwenye asili yake; kinakuwa hakiwezi kuchukua sehemu ya uhai, mbali na chanzo bora zaidi na kilichokitangulia kabla.

Kwa hiyo, ni jinsi gani kila sehemu ya nyororo hiyo, ambayo imetawaliwa na tabia ya kuhitaji kutoka mwisho mmoja hadi mwingine, ilivyoibuka kutoka kwenye hali ya kutokuwa kiumbe? Kuwepo kwa kila sehemu ya nyororo hiyo huonyesha upungufu, kutokuwa na nguvu na chimbuko ndani ya muda uliowekwa, kuwepo kwake kulianza lini? Inawezekanaje vitu vikubwa na vyenye vijisehemu kuibuka kutoka viunganisho vya vitu visivyokuwepo? Je, uhai hububujika kutoka kwenye muungano wa vipengele vingi ambavyo husababisha kifo?

Hata kwa umbali kiasi gani nyororo hii isiyo na ukomo ingerefushwa, bado itakuwa na zile sifa za uhitaji, utegemezi na uibukaji kwa wakati. Nyororo kutoka kwenye ile asili hasa ambayo kwamba kujitawala na uhuru kutokana na kuhitaji hakujitokezi kamwe haiwezi kuchukua sura ya kuwepo hadi itakapoungana na yule ambaye katika asili yake yuko huru kabisa kutokana na kuhitaji - na kiumbe ambaye anazo sifa za utakatifu na ambaye yeye ni kisababisho tu na sio athari. Bila ya kuwepo kwa kitu kama hicho kisichotawaliwa na masharti yoyote, chanzo cha sababu zote na msingi wa uhai wote, mpangilio wa maumbile hauwezi kuelezeka.

Tuseme kwamba kwenye uwanja wa kivita, kikosi cha wapiganaji kinaazimia kumshambulia adui lakini hakuna hata mmoja wao ambaye yupo tayari kuanza vita kwa kurukia katikati ya jeshi la adui. Yeyote anayepewa amri kufanya hivyo jibu lake ni: "Sitashambulia hadi fulani wa fulani aanze kupigana." Kila mpiganaji anajibu hivyo; hapana hata mmoja wao ambaye yupo tayari kushambulia bila kuweka sharti.

Je, katika hali kama hiyo, shambulizi litaweza kutokea kamwe? Kwa vyovyote vile halitatokea, kwa sababu kupigana kwa kila askari ni kwa masharti juu ya kupigana kwa mwenzake. Ni dhahiri kwamba mfululizo wote wa mashambulizi ya masharti hautatokea bila kutimizwa kwa sharti lenyewe, kitu kisichowezekana chini ya mazingira hayo, na matokeo yake, shambulizi halitafanyika.

Kama tukiiendeleza nyororo ya chanzo na athari milele, kuwepo kwa kila kiunganishi kwenye nyororo hiyo kutakuwa kwa sharti la kiunganishi kilichotangulia ambacho nacho baadaye kitakuwa kwa sharti la kuwepo kwa kiunganishi kilichotangulia. Inakuwa kana kwamba kila kiunganishi kwenye nyororo hiyo ya usababishaji kingekuwa kitangaze kwa sauti kubwa kutoka vina vya nafsi zao: "Sitachukua sura ya kuwepo hadi hapo yule mwingine atakapokuwa amekanyaga uwanja wa viumbe." Kila kiunganishi kinategemea juu ya sharti ambalo halijatimizwa, na kila kimojawapo, kwa hiyo, kikiwa kimezuiwa kupata baraka za kuwepo.

Kwa kuwa tunauona ulimwengu wote ukiwa umetapakaa aina tofauti za viumbe, lazima duniani pawepo na chanzo ambacho sio athari, sharti ambalo halitawaliwi na sharti jingine; vinginevyo uso wa dunia usingekuwa umefunikwa hivi na vitu vingi. Chanzo cha msingi ni mmoja, ambaye katika asili yake yu huru na kuhitajia chochote, ambaye anaweza kujiweka mbali na vipengele vyote tofauti vya uhai, na ambaye anaweza kusababisha kutokea mambo ya maajabu kabisa na dalili za asili kabisa. Ni muumbaji ambaye hupanga yote haya na halafu huyaweka kwenye utekelezaji, ambaye huunganisha maumbile yote kwenye utaratibu wa dunia, ambaye wakati wote hutawanyisha uzuri wa uhai juu ya dunia, na ambaye huisukuma mbele ile mandhari kubwa ya maumbile kuelekea kwenye kutimiza lengo la mpangilio wa uhai. Kwa kuifanya dunia si yenye kuumbwa na ya milele, wayakinifu wanajaribu kukanusha haja ya kudumu ya dunia juu ya muumbaji na hapo kuweka uhai wa kujitegemea juu ya dunia. Utaratibu wao, hata hivyo, hauleti matokeo ya kuridhisha.

Wayakinifu wanadhani kwamba dunia inahitaji muumbaji pale wakati wa mwanzo wa uumbaji tu; mara lengo hilo likitimizwa, Mwenyezi Mungu na ulimwengu hawategemeani na hawana kiunganisho baina yao. Kwa matokeo ya itikadi hii, wayakinifu wanaendelea kukanusha hata ule wakati wa mwanzo wa haja, na kwa kukataa wazo la kuwepo mwanzo wa uumbaji, wanadhani wamepata ufumbuzi wa suala la Mwenyezi Mungu na maumbile na wameikomboa dunia kutokana na haja juu ya muumbaji. Hii ni kwa sababu wanadhani kwamba mahitaji juu ya dunia, kuwa ni ya muda na ya mpito tu, ambapo mahitaji hayo ni ya msingi katika asili ya dunia - dunia si chochote bali ni mwendo, muundo wa mwendo wenye ukomo na utegemezi.

Kwa kweli, kila nukta ni mwanzo wa uumbaji; kila muda; kila atomu hapa duniani inajishughulisha na uanzilishi. Ina maana kwamba kitu kizima ambacho hizo atomu ni kama sehemu yake, hivyo hivyo kimeanzika katika muda; hakina asili na nafsi ambayo imejitenga na huru kutokana na ile ya atomu ambazo zinakijenga. Kwa hiyo dunia bado inayo haja ile ile juu ya kuwepo muumbaji ambayo ilikuwa nayo muda uumbaji ulipoanza. Hata kwa kudhaniwa dunia kuwa ya milele, bado isingepata kujitawala kwa uhai. Jibu la wanasayansi juu ya hoja ya Umilele wa dunia.

Kama vile ambavyo binadamu hupoteza uwezo wa kiakili kadiri muda unavyopita hivyo kwamba siku moja taa ya uhai wake inazimika; viivyo hivyo pia ulimwengu nao wakati wote unaelekea kwenye kuporomoka na kukoma. Kwani nishati zilizopo duniani zinaendelea kufifia pole pole; atomu zimegeuka kuwa nishati na nishati hai inazima na kutulia. Mara tu atomu zinapogawanyika kwa ulinganifu na usawa, hakuna kinachobakia isipokuwa ukimya na kutosogea kwa dhahiri. Kwa hiyo, haiwezekani kuichukulia mata kama ni asili ya milele au maudhui ya uhai, na hakuna jinsi nyingine isipokuwa kuiona dunia kama ni kitu kilichoumbwa. Kanuni ya pili ya mwendojoto, kipimo cha ukosekanaji wa nguvu ya joto katika mfumo (entropy) au kupungua kwa nishati ya joto, inatufundisha kwamba ingawaje hatuwezi kuweka tarehe maalum ya kutokeza kwa dunia, kwa hakika dunia ilikuwa na mwanzo. Joto hapa duniani linapungua polepole na kuanguka, kama kipande cha chuma kilichoyeyushwa ambacho hutawanya joto lake hewani hadi mwishowe joto la chuma hicho litakuwa sawa na lile la vitu na hewa inayokizunguka.

Kama ingekuwa hakuna mwanzo au mahali pa kuondokea kwa ajili ya dunia, Atomu zote zilizopo zingemumunyuka na kugeuzwa kuwa nishati kipindi cha miaka isiyokikomo iliyopita nyuma. Katika kipindi cha muda mrefu uliopita joto la dunia lingeweza kufikia kuisha kabisa, kwani kuhusu mata, katika mkondo wa mabadiliko ya mfululizo muendelezo, hatimaye hubadilika kuwa nishati yenye kuharibika. Haiwezekani kwa nishati yote iliyosambaa kugeuka kuwa mata na bonge lenye starehe kwa dunia ya uhai.

Kufuatana na kanuni ambayo imetajwa hapo juu, mara tu nishati itumikayo ikimalizika nguvu yake, utendaji na hisia za kikemikali haziwezi kuendelea kutokea. Lakini kama ilivyo bayana kwamba utendaji na hisia za kemikali vinatokea, kwamba maisha yanawezekana duniani, na kwamba kitu kikubwa sana kama jua hugawanyika kila siku mchana na usiku kwenye tani milioni mia tatu elfu, ni dhahiri kwamba dunia ilianza wakati fulani. Kuangamia kwa sayari na nyota na kutokuweka majua ni uthibitisho wa kifo na mabadiliko katika mpangilio uliopo; vinaonyesha kwamba dunia inaelekea kwenye kutoweka na hatima isiyoepukika.

Halafu tunaona kwamba, sayansi asilia zimeiondoa mata kwenye ngome ya umilele. Sayansi si tu kwamba inathibitisha kuumbwa kwa dunia lakini pia hushuhudia kwamba dunia ilikuja kuwepo katika wakati maalum. Wakati wa kuumbwa kwake, dunia ilijikuta inahitaji nguvu zisizo za kawaida kwani mwanzoni, vitu vyote havikuwa na umbile na havikutofautiana. Ilikuwa muhimu kwa cheche asili ya mwendo na uhai kutua juu ya ulimwengu wa maumbile. Ingewezekanaje mazingira yasiyokuwa na nishati hai, yanayoainishwa na ukimya kabisa na ukosa maumbile, yangekuwa ndio chanzo cha usongevu na uhai?

Umakanika unatuambia kwamba kitu kisichosogezeka wakati wowote kinakuwa kimetulia isipokuwa kinapopatwa na nguvu ya nje yake. Kanuni hii inawakilisha kanuni isiyoweza kukiukwa katika dunia yetu ya maada, na kwa hiyo, hatuwezi kuamini nadharia ya uwezekano au kubahatisha.

Hakuna kitu kisichosogezeka hata kimoja hadi sasa ambacho kimeingia katika mwendo bila ya kusukumwa na nguvu ya nje yake. Hivyo kwa msingi wa kanuni hii ya kimakanika, lazima pawepo na nguvu ambayo ikiwa ni nyingine mbali na dunia hii ya kimaada, inayoumba dunia hiyo na kuipatia nguvu hivyo kwamba inachukua maumbile, inayojitofautisha yenyewe, na inayojipatia sifa mbali mbali. Mwanasayansi mashuhuri Frank Allen, anapendekeza hoja ya kuvutia ifuatayo yenye msimamo wa kukubali kuumbwa kwa dunia na Mwenyezi Mungu: "Watu wengi wamejaribu kuonyesha kwamba dunia hii ya kimaada haihitaji kuwa na muumbaji. Kilicho juu zaidi ya mashaka yote ni kwamba dunia ipo na maelezo ya aina nne yanaweza kupendekezwa kuhusu chanzo chake: "Kwanza, ni kwamba licha ya hayo ambayo tumeyasema hivi punde, tunaiona dunia kama ndoto na madanganyo (kiini-macho) tupu. Ya pili ni kwamba dunia imechomoza kutoka kwenye hali ya utupu kabisa, yenyewe tu hivihivi. Ya tatu ni kwamba dunia haikuwa na mwanzo na kwamba imekuwepo daima. Ya nne ni kwamba dunia imeumbwa.

"Nadharia tete ya kwanza inategemea katika kukubali kwamba hakuna, kiukweli, tatizo linalotakiwa kupatiwa ufumbuzi mbali na tatizo la metafizikia la utambuzi wa mwandamu juu ya nafsi, ambalo pia linaweza kupuuzwa kama ndoto, njozi na kiini macho. Inawezekana kwamba mtu anaweza kusema kwamba treni za kubuniwa, zilizojaa watu wa kubuniwa zinavuka mito hewa ya kubuniwa kupitia kwenye madaraja yasiyo ya kimaada.

"Nadharia tete ya pili, kwamba dunia ya mata na nishati iliyojitokeza na kuwepo yenyewe tu hivihivi, haina maana na ya kipumbavu kama ile ya kwanza, haifai hata kufikiriwa kwa mazungumzo. "Nadharia tete ya tatu, kwamba dunia imekuwepo wakati wote ina ele - menti moja inayofanana na ile dhana ya kuumbwa, kwani ama mata isiyokuwa na uhai, na hiyo nishati vilichanganika nayo au amekuwepo muumbaji wakati wote. Wala uhusishaji wa umilele hauleti tatizo lolote maalum ndani yake yenyewe. Hata hivyo, mwendojoto umethibitisha kwamba dunia inasogea kuelekea kwenye hali ambayo joto la vitu vyote litakuwa kwenye kiwango cha chini kinachofanana na nishati ya kutumika itakuwa haipatikani tena. Kwa hiyo, uhai utakuwa hauwezekani.

"Kama dunia haingekuwa na chimbuko na ilikuwepo tangu milele yote, hali kama ya kifo na kutokuwepo uhai tayari ingekwishatokea. Jua ling'aralo na lenye joto, nyota na dunia iliyojaa uhai vinabeba ushahidi wa kuaminika wa dunia kuanzilika katika wakati; muda maalum katika wakati ulianisha mwanzo wa uumbaji. Hapo basi, dunia haiwezi kuwa vinginevyo mbali na kuwa imeumbwa; lazima ilikuwa kisababisho kikubwa, cha tangu dahari, muumba wa milele, mwenye ujuzi wa kila kitu na kudra, ambaye ndiye aliyeileta dunia kwenye kuwepo."[22]

Kama mwanadamu atafikiria kwa kina japo kidogo na akatafakari kuhusu ukweli kwa mtazamo mpana, ataelewa kwamba akiwa amekabiliwa na maeneo mapana sana ya kijiografia ya maisha na haja ya namna fulani ya kuyatambua, hawezi hata kidogo kuuona uwezo wake binafsi kama wenye kugetosha kwa kazi hiyo. Elimu juu ya mpango wa maumbile iliokusanywa na mwanadamu kupitia juhudi zake zisizochokesha zinakuwa kama ni bure kabisa. Ingawa sayansi imepiga hatua kubwa sana mbele, kuna hitilafu kabisa baina ya wanadamu, ni nini mwanadamu amejifunza, na ni yapi ambayo bado hayajui.

Kwa kiasi ambacho vile vipindi vilivyopita vinahusika ambavyo vimefunikwa na giza nene, kwa jinsi tujuavyo, maelfu au hata mamilioni ya jamii za wanadamu zilizo bora zaidi ya hii iliopo sasa zinaweza kuwa zilikuwepo. Jamii kama hizo bado zinaweza kuja kuwepo tena hapo baadaye. Kile kinachoitwa sayansi na wale wanaoabudu sayansi wa zama hizi za sasa na wao wakaziona kuwa sawa na jumla yote ya ukweli, ni mkusanyiko tu wa sheria zinazotumika kwa upande mmoja tu wa dunia. Matokeo ya bidii zote za binadamu na majaribio ni sehemu ya ujuzi inayohusu nukta moja ndogo ing'arayo - inayoweza kulinganishwa na mwanga hafifu wa mshumaa - uliozungukwa na usiku wa giza uliofunika jangwa pana sana la ukubwa usio na mpaka.

Kama tukirudi nyuma mamilioni ya miaka vumbi la vurugu litafunika njia yetu ikiwa kama moja ya dalili ya nguvu ya udhaifu na ujinga wa mwanadamu anapokabiliwa na utukufu na ukubwa wa maumbile. Inaweza kuwa kwamba kipindi ambamo mwanadamu amekuwepo si chochote zaidi ya muda kidogo tu katika uhai wa dunia; ni hakika kwamba palikuwepo na bahari nyeusi isiyokuwa na uhai ambamo hamkuwepo na dalili ya mwanadamu. Kwa ufupi tunajua kiasi kidogo sana cha mwanzo wa safari yetu na hatujui chochote kuhusu mustakabali wake. Wakati huo huo, ni vigumu kuamini kwamba mazingira muhimu kwa ajili ya uhai yapo kwenye sayari hii ndogo pekee tu. Wanasayansi wengi wa kipindi hiki wanaona eneo la maisha ni kubwa na pana mno; wanawasilisha mamilioni yasiyo na idadi ya sayari kwenye kukodoa macho kwetu na tunazitazama kwa namna mbalimbali. Lakini kile tunachowezeshwa kuona si chochote zaidi ya umbali wa maono ya mdudu mchwa pale inapolinganishwa na ukubwa wa ulimwengu.

Kuelezea safari ya kufikirika tu kwenye dunia isiyo na ukomo, mwanasayansi mashuhuri; Camille Flammarion, anasema yafuatayo katika kitabu chake cha elimu ya nyota: "Tunaendelea kusonga mbele kwa miaka elfu moja, kwa miaka elfu kumi, kwa miaka mia moja elfu, kwa kasi ile ile, bila kutetereka, bila kupunguza kasi ya mwendo wa gari yetu, wakati wote tukienda mbele katika msitari ulionyooka. Tunasonga mbele kwa kasi ya kilomita mia tatu elfu kwa sekunde. Tunadhani kwamba baada ya kusafiri kwa kasi hiyo kwa miaka milioni moja tutakuwa tumefika kwenye mipaka ya ulimwengu huu unaoonekana?

"Hapana, zipo anga kubwa mno za mbali zaidi zenye giza nene ambazo lazima zipitiwe, na huko pia, nyota mpya zinazoonekana katika mipaka ya mbingu. Tunaziendelea hizo, lakini je, tutazifikia kamwe? "Mamilioni zaidi ya miaka, uvumbuzi mpya zaidi, fahari na ukubwa zaidi, ardhi na dunia nyingine zaidi mpya, viumbe vipya vingine zaidi na vitu vya kiroho vinginevyo - je, kavitakwisha kamwe? Upeo haujifungi kamwe; mbingu daima hazizuii njia yetu; anga yenye kuendelea, pengo inayoendelea. Tupo wapi sisi? Ni njia gani ambayo sisi tumepita? Bado tungalipo katikati ya ile nukta - sehemu ya katikati ya duara ipo kila mahali, mzingo wake hauonekani popote.

Hiyo ndio dunia isiyo na mwisho ambayo inaonekana kukaa wazi mbele yetu na ambayo uchunguzi wake ndio kwanza umeanza. Bado hatujaona chochote, na tunageuka nyuma kwa woga, tukianguka kwa kuchoka kutokana na safari hii isiyo na mafanikio. Lakini tutaangukia wapi? Tunaweza kuangukia kwenye umilele kwenye madimbwi yasiyo na kikomo ambamo kina chake hatukifikii kamwe, kama vile ambavyo, hatuwezi kuvifikia vilele vyao. Kaskazini inakuwa kusini; hakuna mashariki wala magharibi, hakuna juu wala chini, hakuna kushoto wala kulia.

Kokote kule tutakapotazama hatuoni mwisho, na ndani ya eneo hili lisilokuwa na mwisho, ulimwengu wetu si chochote zaidi ya kisiwa kidogo kwenye mkusanyiko mkubwa wa visiwa vilivyoenea kwenye bahari isiyo na mwisho. Maisha yote ya mwanadamu, kwa fahari yote ambayo mwanadamu anajigamba nayo katika historia yake kisiasa na kidini, au hata uhai wote wa sayari yetu pamoja na ufahari wake wote, ni sawa na ndoto ya kitambo kinachopita kwa kasi kubwa.

Kama tungependa kuandika tena kazi zote za utafiti ambazo zimeandikwa na mamilioni ya wasomi kwenye mamilioni ya vitabu, wino ambao unahitajika kwa kazi hiyo ni sawa na ujazo ambao hautazidi ujazo wa tenki moja dogo. Lakini kuelezea na kupanga kwa mtindo wa utaratibu, ile miundo ya vitu vyote vilivyopo duniani na mbinguni, katika vipindi visivyoonekana vilivyopita na kwenye mustakabali usiopimika - kuandika, kwa ufupi, miujiza yote ya maumbile - inaweza kuhitaji wino mwingi zaidi kuliko bahari kuwa na maji."[23] .

Kama asemavyo Profesa Ravaillat; "Ili kuwa na utambuzi uliokamilika wa dunia, inatosha kujua kwamba idadi ya kundi la nyota na sayari kwenye anga pana isiyopimika ya ulimwengu ni kuwa zaidi kuliko ile ya chembechembe za mchanga katika pwani zote za dunia hii."[24] Fikra za aina hiyo kuhusu yale tunayoyajua na tusiyoyajua zinatuwezesha kuepuka kifungo katika kifukofuko cha maisha yetu finyu; ili tuweze kutambua kwa unyonge kuhusu tupo wadogo kiasi gani; kwenda zaidi ya haya maisha yetu yenye ukomo, kwa kiwango ambacho tunaweza na kutafakari ukweli kwa uangalifu mkubwa na kwa kuzama zaidi.


6

7

8

9

10

11

12

13

14