TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA Juzuu 7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA 33%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 14671 / Pakua: 3584
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA Juzuu 7

Mwandishi:
Swahili

1

2

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ يَعْرِفُونَهُ كَمَا يَعْرِفُونَ أَبْنَاءَهُمُ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ﴾

20.Wale tuliowapa Kitab wanamjua kama wanavyowajua wana wao, Wale ambao wamezitia hasarani nafsi zao hawaamini.

﴿وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا أَوْ كَذَّبَ بِآيَاتِهِ إِنَّهُ لَا يُفْلِحُ الظَّالِمُونَ﴾

21.Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule amzuliaye Mwenyezi Mungu uwongo, Au azikadhibishaye ishara zake? Hakika madhalimu hawatafaulu.

﴿وَيَوْمَ نَحْشُرُهُمْ جَمِيعًا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشْرَكُوا أَيْنَ شُرَكَاؤُكُمُ الَّذِينَ كُنتُمْ تَزْعُمُونَ﴾

22.Na siku tutakapowakusanya wote, kisha tutawaaambia wale walioshirikisha: Wako wapi washirikishwa wenu mliokuwa mnadai?

﴿ثُمَّ لَمْ تَكُن فِتْنَتُهُمْ إِلَّا أَن قَالُوا وَاللَّـهِ رَبِّنَا مَا كُنَّا مُشْرِكِينَ﴾

23.Kisha hautakuwa udhuru wao ila kusema Wallahi, Mola wetu! Hatukuwa washirikina.

﴿انظُرْ كَيْفَ كَذَبُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَضَلَّ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَفْتَرُونَ﴾

24.Angalia jinsi wanavyojisemea uwongo wenyewe, Na yamepotea waliyokuwa wakiyazua.

WANAMFAHAMU KAMAWANAVYO WAFAHAMU WANAWAO

Aya ya 20 - 24

MAANA

Wale tuliowapa Kitab wanamjua kama wanavyowajua wana wao. Waliopewa Kitab ni Mayahudi na Wakristo, Dhamiri ya wanamjua inamrudia Muhammad(s.a.w.w) . Aya hii inawakabili maulama wa watu wa Kitab kwamba wao wanamjua vizuri Mtume wa mwisho, kama wanavyowajua wana wao, lakini wao wanaficha yale wanayoyajua. Maana haya yamekaririka katika Aya kadhaa, zikiwemo hizi zifuatazo:

﴿الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الرَّسُولَ النَّبِيَّ الْأُمِّيَّ الَّذِي يَجِدُونَهُ مَكْتُوبًا عِندَهُمْ فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ﴾

"Ambao wanamfuata Nabii asiyesoma wala kuandika ambaye wanamwona ameandikwa kwao katika Tawrat na Injil" (7:157)

﴿أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ﴾

Je, haikuwa ishara kwao kwamba wanayajua haya maulama wa wana wa Israil? (26:197)

Yamekwishapita maelezo kwa ufafanuzi katika Juz. 2 (2:146) na Juz. 4 (4:164). Si lazima kwa watu wa Kitab, katika kuujua ukweli wa Muhammad(s.a.w.w) , wakute jina lake limeandikwa kwao katika Tawrat na Injil. Kila mwenye kuusoma Uislamu kwa somo sawa sawa na upekuzi, ataamini kwa imani isiyokuwa na tashwishi yoyote kwamba Uislamu ni haki na ukweli.

Na mawili hayo (haki na ukweli) ndiyo johari za Uislamu, nguzo yake na lengo lake kutokana na neno Lailaha illa Ilah (Hakuna Mungu isipokuwa Allah) ambalo linamaanisha usawa baina ya watu, kumpa mtu msimamo wa misingi ya kufanya amali na ikhlasi na wala sio kwa misingi ya mali, jaha na nasabu. Na vilevile mshikamano na majukumu ya kila kiongozi kwa wachini wake katika mwito wa amani na usalama, maendeleo na utulivu usiokuwa na mwisho.

Wale ambao wamezitia hasarani nafsi zao hawaamini.

Imepita, punde tu Tafsir yake katika Aya 12 ya Sura hii.

Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule amzuliaye Mwenyezi Mungu uwongo.

Makusudio ya dhulma hapa ni Ukafiri. Kwa sababu kila anayemzulia Mwenyezi Mungu uwongo, basi yeye ni kafiri. Hakuna tofauti yoyote baina ya anayemshirikisha na yule mwenye kugeuza hukumu yoyote katika hukumu zake kwa makusudi na kujua; na yule mwenye kudai unaibu wa maasum au kuwaombea viumbe haki, na hali anajua kuwa yeye ni mzushi na mwongo. Wote hawa ni makafiri waovu kwa Ijmai (kongamano), Kitab na Hadith.

Au azikadhibishaye ishara zake? Hakika madhalimu hawatafaulu.

Jumla iliyotangulia imeashiria yule anayeleta yasiyokuwepo; kama mwenye kumfanyia Mwenyezi Mungu washirika au mtoto. Na jumla hii inaashiria yule mwenye kukanusha vilivyopo, kama vile anayemkana

Mwenyezi Mungu kabisa. Hukumu ya wote wawili ni moja, kila mmoja wao ni dhalimu:

﴿مَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ حَمِيمٍ وَلَا شَفِيعٍ يُطَاعُ﴾

"Madhalimu hawana rafiki mpenzi wala muombezi anayetiiwa" (40:18) "Na siku tutakapowakusanya wote, kisha tutawaambia wale walioshirikisha: Wako wapi washirikishwa wenu mliokuwa mnadai" Wanaomwamini Mwenyezi Mungu wako aina mbili: Kuna wale wanaoamini uungu wake na kuwa ni mmoja tu. Hawa wanaitwa wanaompwekesha Mungu (watu wa Tawhid). Na kuna wale wanaoamini uungu wake na uungu mwingine. Hawa ndio wale walioharibu imani yao kwa mchanganyiko huu; na wakawa sawa na wale wanaomkana Mwenyezi Mungu. Kwa sababu kumjaalia Mwenyezi Mungu mfano maana yake hasa ni kumkana Mwenyezi Mungu kabisa. Kwani ilivyo nikuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hana mshabaha wala mfano:

"Hakuna kama mfano wake kitu chochote." (42:11)

Mwenyezi Mungu atawakabili washirikina na swali hili (wako wapi washirikishwa mliokuwa mnadai na mkiwataka msaada, kama mnavyomtaka msaada Mwenyezi Mungu) kwa njia ya kutahayariza na kukaripia, na wala sio kwa njia ya kuhakikisha.

Unaweza kuuliza : kwa nini Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema wako wapi washirikishwa wenu na wala hakusema wako wapi washirikishwa wangu, pamoja na kuwa makafiri ndiyo waliosema kuwa Mungu ana washirika na sio wao?

Jibu : Ni kwa kuwa wao ndiyo wako karibu zaidi na mnasaba huo; kwani wao ndio waliozusha ushirikina ambao hauna athari kabisa.

Kisha hautakuwa udhuru wao ila kusema Wallahi, Mola wetu! Hatukuwa washirikina.

Makusudio ya udhuru wao ni udhuru wao wa kushirikisha na kuabudu mizimu. Maana ni kuwa mwisho wa ushirikina waliozusha ni kiapo chao cha uovu kwamba wao hawakuwa washirikina.

Unaweza kuuliza : Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwasimulia watu hao: 'Wallahi Mola wetu! Hatukuwa washirikina' inapingana na kauli yake yake."Wala hawatamficha Mwenyezi Mungu na mazungumzo (yao)" (4:42)

Zaidi ya hayo ni kuwa inajulikana kuwa mtu hawezi kusema uongo Siku ya Kiyama.

Jibu : Katika Kiyama kutakuwa na vituo kadhaa, baadhi yake mtu ataweza kukana na ambapo katika kituo hicho miguu yake na mikono yake haitamtolea ushahidi wa yale aliyokuwa akiyafanya. Kwenye kituo hicho ndipo huchukuliwa kauli yake Mwenyezi Mungu: 'Wallahi Mola wetu! Hatukuwa washirikina' Na katika kituo kingine, atakiri ambapo hapatakuwa na nafasi ya kukana. Hapo ndipo huchukuliwa kauli yake Mwenyezi Mungu: "Wala hawataweza kumficha Mwenyei Mungu neno lolote" Ama kauli ya kuwa mtu atashindwa kabisa kusema uwongo siku ya Kiyama, inakanushwa na Aya isemayo:

﴿يَوْمَ يَبْعَثُهُمُ اللَّـهُ جَمِيعًا فَيَحْلِفُونَ لَهُ كَمَا يَحْلِفُونَ لَكُمْ وَيَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ عَلَىٰ شَيْءٍ أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ الْكَاذِبُونَ﴾

"Siku atakayowafufua Mwenyezi Mungu wote; wamuapie kama wanavyoapa kwenu, na watadhani kwamba wamepata kitu. Kwa hakika hao ndio waongo hasa" (58: 18)

Swali la pili linatokana na jibu la swali la kwanza nalo ni kuwa: ikiwa mtu ataweza kusema uwongo kesho, bali hata kuapa, kama ilivyo katika maisha haya ya duniani. Basi kuna wajihi gani kuita akhera nyumba ya ukweli na kuiita nyumba yetu hii (dunia) nyumba ya uwongo?

Jibu : Makusudio ya kutofautisha huku ni kwamba uwongo hapa duniani unaweza ukamletea mtu manufaa au kumkinga na madhara, Ama huko akhera hautafaa chochote. Kwa maneno mengine, kushindwa kusema uwongo, ni kitu kingine na kuweza kusema bila ya manufaa ni kitu kingine.

Angalia jinsi wanavyojisemea uwongo wenyewe.

Msemo unaelekezwa kwa Mtume(s.a.w.w) na makusudio yake ni kwa wote, nako ni kusataajabu kutokana na kukana kwao ushirikina na hali wamekufa juu ya ushirikina. Kila mwenye kukana jambo alilonalo au kudai asiyokuwa nayo kwa makusudi, basi amejidaganya mwenyewe, Mwenyezi Mungu na watu:

Na yamepotea waliyokuwa wakiyazua.

Hiyo inaungana na 'wanavyojisemea uwongo.' Maana yake ni angalia Ewe Muhammad vipi yamewapotea washirikina yale waliyokuwa wakiyatarajia kuwa yatawasaidia na kuwaombea.

﴿وَمِنْهُم مَّن يَسْتَمِعُ إِلَيْكَ وَجَعَلْنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ أَكِنَّةً أَن يَفْقَهُوهُ وَفِي آذَانِهِمْ وَقْرًا وَإِن يَرَوْا كُلَّ آيَةٍ لَّا يُؤْمِنُوا بِهَا حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوكَ يُجَادِلُونَكَ يَقُولُ الَّذِينَ كَفَرُوا إِنْ هَـٰذَا إِلَّا أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ﴾

25.Na miongoni mwao wako wanaokusikiliza, na tumezitia pazia nyoyo zao wasije kuyafahamu na mna uziwi masikioni mwao, Na wakiona kila Ishara hawaiamini. Hata wakikujia kujadaliana nawe wanasema waliokufuru: Hizi si chochote isipokuwa ni ngano za watu wa kale.

﴿وَهُمْ يَنْهَوْنَ عَنْهُ وَيَنْأَوْنَ عَنْهُ وَإِن يُهْلِكُونَ إِلَّا أَنفُسَهُمْ وَمَا يَشْعُرُونَ﴾

26.Nao wanamkatazia na wenyewe wanajitenga naye. Na hawaangamizi ila nafsi zao na hawatambui.

NYOYO ZAO ZINA PAZIA

Aya 25 - 26

MAANA

Na miongoni mwao wako wanaokusikiliza, na tumezitia pazia nyoyo zao wasije kuyafahamu na mna uziwi masikioni mwao.

Mwenyezi Mungu anamwambia Mtume wake katika Aya hii, baada ya kumwamrisha kuwambia hoja zinazowasimamia, Maana ni kuwa kundi katika hawa wapinzani wanamsikiliza Mtume, nao wanasoma Qur'an, lakini wao hawanufaiki nayo wala hawanufaiki na dalili na hoja nyingine- zo.

Kwa sababu wao tangu mwanzo waling'anga'ania inadi na kiburi, mpaka kung'angania huko kukapofua akili zao zisione haki na kukatia uziwi kwenye masikio yao.

Unaweza kuuliza : Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu ndiye aliyezipofua nyoyo zao akatia uziwi masikio yao. Kwa nini basi wastahiki shutuma na adhabu na hali ya kuwa wamelazimishwa hawana hiyari?

ibu: Kwa vile nyoyo za wapinzani hazikuitambua Qur'an na kunufaika nayo, na masikio yao hayakuisikiliza kwa usikizi wa kufahamu na kuzingatia, imesihi kusema, kimajazi, kwamba nyoyo zao zimefumba na katika masikio yao mna uziwi.

Na kwa vile Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye aliyeumba nyoyo na masikio, imesihi kunasibisha upofu na uziwi kwake yeye kimajazi vilevile.

Ama kulingana na hali halisi ilivyo ni kuwa washirikina ndio wenye jukumu. Kwa sababu wao waliipinga haki kwa kutaka wenyewe. Yamekwishatangulia maelezo ya hayo katika Juz. 1(2:7)

Ni vizuri kuashiria kuwa Aya hii inafahamisha kwa uwazi kwamba Uislam hauna mfano na chochote kwa ulivyo; bali kwa natija zake na athari zake. Kwa hiyo usikizi na uoni ni utekelezaji wa akili, na akili ndiyo inayopanga matendo. Ikiwa kitendo hakikufanyika, basi usikizi na uoni utakuwa hauna maana yoyote; kwa dhahiri au si kwa dhahiri.

Kwa maneno mengine katika Uislamu, mambo yote ya ndani na ya nje, na ya ardhini na ya angani ni nyenzo za manufaa ya watu katika kupangilia maisha yao na kutatua matatizo yao.

Imam Ali(a.s) anasema:"Anadai kwamba yeye anamtaraji Mwenyezi Mungu. Amesema uwongo kwa nini matarajio yake hayaonekani katika vitendo vyake, na kila mwenye kutarajia (Mwenyezi Mungu) hujulikana matarajio yake katika vitendo vyake."

Na wakiona kila Ishara hawaiamini.

Muhammad(s.a.w.w) alifichua hakika ya waongo katika watu wapendao mali na jaha. Wakataharuki na kuhisi hatari ya masilahi yao wakakimbilia kukadhibisha na wakasema kuhusu Aya za Mwenyezi Mungu kuwa ni ngano za watu wa kale, na hali wao wana yakini kwamba Qur'an hii ni mwongozo, lakini wakawa wanaitia njia za shaka shaka na makosa ili wawatumie watu kutokana na upotevu wao na ubatilifu; sawa na wanavyofanya leo watu wa serikali ovu na kanuni za dhuluma.

Na wanamkatazia na wenyewe wanajitenga naye.

Dhamiri ya neno nao inawarudia wale waliopinga haki kwa kupupia masilahi yao. Dhamiri ya wanamkatazia na kujiweka mbali naye, inamrudia Muhammad(s.a.w.w) .

Waongo walikataza watu wasimfuate Muhammad(s.a.w.w) na wakampinga, vilevile walijaribu kumtesa na wakakusanya majeshi kwa ajili ya kumpiga vita. Si kwa lolote ila ni kwamba yeye amefichua mabaya yao.

Na hawaangamizi ila nafsi zao na hawatambui.

Walitaka kuufanyia vitimbi Uislamu na Mtume wake, balaa ikawafikia wao, walipoangamia baadhi yao siku ya Badr wengine wakajisalimisha wakiwa madhalili na wanyonge siku ya kutekwa Makka. Huu ndio mwisho wa kila mwenye kuzama na kung'ang'ania dhuluma na inadi.

﴿وَلَوْ تَرَىٰ إِذْ وُقِفُوا عَلَى النَّارِ فَقَالُوا يَا لَيْتَنَا نُرَدُّ وَلَا نُكَذِّبَ بِآيَاتِ رَبِّنَا وَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ﴾

27.Na ungeliona watakapoonyeshwa moto wakawa wanasema. Laiti tungerudishwa (duniani) wala hatutakadhibisha ishara za Mola wetu na tutakuwa katika wanaoamini.

﴿بَلْ بَدَا لَهُم مَّا كَانُوا يُخْفُونَ مِن قَبْلُ وَلَوْ رُدُّوا لَعَادُوا لِمَا نُهُوا عَنْهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ﴾

28.Bali yamewadhihirikia waliyokuwa wakiyaficha zamani. Na kama wangalirudishwa, bila shaka wangeyarudia yale waliyokatazwa na hakika wao ni waongo.

﴿وَقَالُوا إِنْ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا الدُّنْيَا وَمَا نَحْنُ بِمَبْعُوثِينَ﴾

29.Na kusema: Hakuna kingine ila maisha yetu ya dunia, wala sisi hatutafufuliwa.

﴿وَلَوْ تَرَىٰ إِذْ وُقِفُوا عَلَىٰ رَبِّهِمْ قَالَ أَلَيْسَ هَـٰذَا بِالْحَقِّ قَالُوا بَلَىٰ وَرَبِّنَا قَالَ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴾

30.Na ungeliona watakaposimamishwa mbele ya Mola wao, Akasema: Je, si kweli haya? Watasema: Kwa nini? Tunaapa kwa Mola wetu. Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakataa.

﴿قَدْ خَسِرَ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِلِقَاءِ اللَّـهِ حَتَّىٰ إِذَا جَاءَتْهُمُ السَّاعَةُ بَغْتَةً قَالُوا يَا حَسْرَتَنَا عَلَىٰ مَا فَرَّطْنَا فِيهَا وَهُمْ يَحْمِلُونَ أَوْزَارَهُمْ عَلَىٰ ظُهُورِهِمْ أَلَا سَاءَ مَا يَزِرُونَ﴾

31.Hakika wameshahasirika wale waliokadhibisha kukutana na Mwenyezi Mungu, na wamefuzu wale waliomwamini, mpaka itakapowajia ghafla saa (Kiyama) watasema: Oo! Majuto yetu juu ya yale tuliyoyapuuza! Nao watabeba mizigo yao migongoni mwao. Angalieni! Ni mabaya mno wanayoyabeba.

﴿وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَعِبٌ وَلَهْوٌ وَلَلدَّارُ الْآخِرَةُ خَيْرٌ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَ أَفَلَا تَعْقِلُونَ﴾

32.Na maisha ya dunia si kitu ila mchezo na upuzi. Na hakika nyumba ya akhera ni bora zaidi kwa wenye takua. Basi je hamtii akili?

WATAKAPOSIMAMISHWA MOTONI

Ay 27 - 32

MAANA

Na ungeliona watakapoonyeshwa moto.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amerudia kuelezea hali ya wakadhibishaji Siku ya Kiyama, na kwamba wao watakapoona adhabu waliyoandaliwa na thawabu walizoandaliwa waumini, watasema:

Laiti tungerudishwa duniani wala hatutakadhibisha ishara za Mola wetu na tutakuwa katika wanaoamini.

Yaani tutatubia na tufanye amali njema. Lakini masikitiko na mazingatio hayafai chochote ila ikiwa kumwogopa Mwenyezi Mungu na adhabu yake ni kabla ya kutokea adhabu. Ama baada ya kutokea, basi ni kulilia maiti na kusikitika yaliyofutu.

Bali yamewadhihirikia waliyokuwa wakiyaficha zamani.

Hataokoka kesho na adhabu ya Mwenyezi Mungu ila ambaye yuko wazi katika maisha haya, vitendo vyake vinaambatana na kauli yake; yote mawili yawe ni picha ya dhati yake na hali yake, mpaka viwe vyote ni kama kitu kimoja tu mbele ya Mwenyezi Mungu na watu.

Ama yule mwenye kuzibaziba, ambaye Muumba anayajua yale ayafanyayo na watu hawayajui, miongoni mwa ria na unafiki, huyu yatamdhihirikia malipo ya ria yake na unafiki wake; na nafsi yake itajutia uovu wake na kutamani kujisafisha kwa kurudishwa duniani, lakini wapi!

Na kama wangalirudishwa, bila shaka wangeyarudia yale waliyokatazwa na hakika wao ni waongo.

katika kusema kwao: Laiti tungerudishwa wala hatutakadhibisha ishara za Mola wetu na tutakuwa katika wanaoamini.

Tumesoma habari za wakosaji kadhaa ambao wanatubia wakiwa gerezani, lakini wanapotoka hurudia makosa yao. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَإِذَا مَسَّكُمُ الضُّرُّ فِي الْبَحْرِ ضَلَّ مَن تَدْعُونَ إِلَّا إِيَّاهُ فَلَمَّا نَجَّاكُمْ إِلَى الْبَرِّ أَعْرَضْتُمْ وَكَانَ الْإِنسَانُ كَفُورًا﴾

"Na inapowafikia dhara katika bahari hupotea wale mnawaomba isipokuwa Yeye tu, lakini anapowaokoa mkafika salama nchi kavu mnageuka; na mwanadamu ni mkanushaji mno" (17:67)

Na kusema: Hakuna kingine ila maisha yetu ya dunia, wala sisi hatutafufuliwa.

Yaani lau wangelirudishwa kwenye maisha yao ya mwanzo wangalisema waliyoyasema mwanzo: Hakuna ufufuo wala hisabu wala malipo.

Unaweza kuuliza : Vipi watakanusha na hali wao watakuwa wameshuhudia vituko vikubwa na wakaonyeshwa, mpaka wakataka kujitakasa nayo na kuahidi kuwa hawatarudia?

Jibu : Wao wanajua fika kwamba hisabu na adhabu itakuwa tu, hapana budi. Wakati huo huo wanajua kuwa lau wataitangaza haki na kuinyenyekea, chumo na faida zao watazikosa. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

﴿وَجَحَدُوا بِهَا وَاسْتَيْقَنَتْهَا أَنفُسُهُمْ ظُلْمًا وَعُلُوًّا﴾

"Na wakazikanusha (ishara zetu) na hali yakuwa nafsi zao zina yakini nazo kwa dhulma na kujivuna" (27:14)

Na ungeliona watakaposimamishwa mbele ya Mola wao , baada ya kukadhibisha kukutana naye. Atasema: Je, si kweli haya? Katika kufasiri Aya ya nne katika Sura hii tulisema kuwa Mwenyezi Mungu analingania kuamini haki pamoja na kusimamisha dalili yake. Mpingaji akiipinga, hoja inakuwa juu yake. Na Aya hii inatilia mkazo hilo na kutaja dalili na hoja walizozikanusha na kuzikadhibisha. Watasema: Kwanini? Tunaapa kwa Mola wetu. Hivi sasa yamepita yaliyopita na hakuna kilichobaki isipokuwa malipo yenye kulingana na adhabu kwa mwenye kukufuru na kukanusha.

Akasema: "Basi onjeni adhabu kwa sababu ya mliyokuwa mkikataa. Haya ni malipo ya kila mwenye kuiweka mbele dunia na kuiacha Akhera na akaificha haki kwa hawa ya nafsi yake.

Utauliza : Kauli yake Mwenyezi Mungu kwa Makafiri: 'Je, si kweli haya?' Na kauli yake: "Onjeni adhabu" mbona haziafikiani na kauli yake:"Wala hatawasemeza Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama" ? (2:174)

Jibu : Makusudio ni kwamba Mwenyezi Mungu hatawasemesha yale yanayowafurahisha, bali atawasemeza yanayowaudhi, kama ilivyo katika Aya hii, na ilivyo katika Aya isemayo:

"Atasema: Tokomeeni humo wala msinisemeze." (23:108)

Hakika wamekwishahasirika wale waliokadhibisha kukutana na Mwenyezi Mungu na wamefuzu wale waliomwamini, mpaka itakapowajia ghafla saa (Kiyama) watasema: Oo! Majuto yetu juu ya yale tuliyoyapuza!

Imam Ali anasema:"Matunda ya kupuuza ni majuto, na matunda ya uthabiti ni amani."

Nao watabeba mizigo yao migongoni mwao. Angalieni! Ni mabaya mno wanayoyabeba.

Mizigo ni dhambi na kuibeba mgongoni ni fumbo, yaani kuwa nayo; kama vile isemwavyo: "Amepandwa na shetani." Yaani yuko naye hamwachi. Maana ni kuwa wanaoikadhibisha haki ndio watu wenye hali mbaya zadi huko akhera.

Mmoja wa wafasiri wapya anasema: "Bali mnyama ana hali nzuri zaidi kwa sababu hubeba mizigo mizito,; na mnyama huutua mzigo wake akaenda kupumzika, lakini hawa watakwenda na mizigo yao kwenye Jahannam wakisindikizwa na dhambi."

Na maisha ya dunia si kitu ila mchezo na upuzi." Umetangulia mfano wake katika Juz 4 (3:185)

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿قَدْ نَعْلَمُ إِنَّهُ لَيَحْزُنُكَ الَّذِي يَقُولُونَ فَإِنَّهُمْ لَا يُكَذِّبُونَكَ وَلَـٰكِنَّ الظَّالِمِينَ بِآيَاتِ اللَّـهِ يَجْحَدُونَ﴾

33.Hakika tunajua kwamba yanakuhuzunisha yale wanayoyasema, Basi hakika hao hawakukadhibishi wewe, lakini madhalimu wanakataa ishara za Mwenyezi Mungu.

﴿وَلَقَدْ كُذِّبَتْ رُسُلٌ مِّن قَبْلِكَ فَصَبَرُوا عَلَىٰ مَا كُذِّبُوا وَأُوذُوا حَتَّىٰ أَتَاهُمْ نَصْرُنَا وَلَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَاتِ اللَّـهِ وَلَقَدْ جَاءَكَ مِن نَّبَإِ الْمُرْسَلِينَ﴾

34.Na hakika walikadhibishwa Mitume kabla yako, wakavumilia juu ya kukadhibishwa na kuudhiwa, mpaka ikawafikia nusura yetu. Na hakuna wa kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu, Na bila shaka zimekujia baadhi ya habari za Mitume hao.

﴿وَإِن كَانَ كَبُرَ عَلَيْكَ إِعْرَاضُهُمْ فَإِنِ اسْتَطَعْتَ أَن تَبْتَغِيَ نَفَقًا فِي الْأَرْضِ أَوْ سُلَّمًا فِي السَّمَاءِ فَتَأْتِيَهُم بِآيَةٍ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَجَمَعَهُمْ عَلَى الْهُدَىٰ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْجَاهِلِينَ﴾

35.Na ikiwa ni makubwa kwako huku kukataa kwao, basi kama unaweza kutafuta njia ya chini kwa chini katika ardhi au ngazi kwendea mbinguni na kuwaletea ishara. Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka, bila shaka angeliwakusanya kwenye uongofu. Basi usiwe miongoni mwa wajinga

﴿إِنَّمَا يَسْتَجِيبُ الَّذِينَ يَسْمَعُونَ وَالْمَوْتَىٰ يَبْعَثُهُمُ اللَّـهُ ثُمَّ إِلَيْهِ يُرْجَعُونَ﴾

36.Hakika wanaokubali ni wale tu wanaosikia, Na wafu Mwenyezi Mungu atawafufua kisha watarejeshwa kwake.

﴿وَقَالُوا لَوْلَا نُزِّلَ عَلَيْهِ آيَةٌ مِّن رَّبِّهِ قُلْ إِنَّ اللَّـهَ قَادِرٌ عَلَىٰ أَن يُنَزِّلَ آيَةً وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ﴾

37.Na husema: Kwa nini hakuteremshiwa ishara kutoka kwa Mola wake? Sema: Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye uweza wa kuteremsha ishara yoyote, lakini wengi wao hawajui.

TUNAJUA KUWA YANAKUHUZUNISHA

Aya 33 - 37

MAANA

Hakika tunajua kwamba yanakuhuzunisha yale wanayoyasema.

Msemo unaelekezwa kwa Mtume(s.a.w.w) , Dhamir ya 'wanayoyasema' inawarudia wale waliomkadhibisha Mtume(s.a.w.w) . Ama yale wanayoyasema bali waliyasema hasa, ni yale yaliyoashiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w.t):

﴿ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ﴾

Kisha wakampa mgongo na wakasema: Amefunzwa (na) ni mwendawazimu." (44:14)

"Wakasema Makafiri: Hakika huyu ni mchawi dhahiri." (10:2) Na mengineyo.

Basi hakika hao hawakukadhibishi wewe, lakini madhalimu wanakataa ishara za Mwenyezi Mungu.

Kila mwenye kumpiga vita mwenye haki, basi ameipiga vita haki yenyewe, na kila mwenye kumdharau Mtume kwa kuwa yeye anachukua risala ya aliyemtuma, basi atakuwa amemdharau yule aliyemtuma na sio Mtume mwenyewe.

Washirikina wa Makka walikuwa wakimwita Muhammad(s.a.w.w) mkweli mwaminifu, kabla ya Utume. Alipowaletea risala ya Mwenyezi Mungu na kuwasimamishia hoja, walimpiga vita na wakamwita mwendawazimu, mchawi nk.

Kwa hiyo kumkadhibisha kwao huku na hali hii, ni kukadhibisha risala ya Mwenyezi Mungu na hoja zake. Hakuna linalofahamisha hilo kwa dalili zaidi ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿إِنَّ الَّذِينَ يُبَايِعُونَكَ إِنَّمَا يُبَايِعُونَ اللَّـهَ يَدُ اللَّـهِ فَوْقَ أَيْدِيهِمْ﴾

"Hakika wale wanaokubai, kwa hakika wanambai Mwenyezi Mungu; mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao" (48:10)

Na hakika walikadhibishwa Mitume kabla yako, wakavumilia juu ya kukadhibishwa na kuudhiwa, mpaka ikawafikia nusura yetu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamwambia Mtume wake ikiwa watakukadhibisha, basi wamekadhibishwa Mitume kabla yako na wakaudhiwa katika kufikisha risala yake, wakavumilia juu ya maudhi mpaka ikawajia nusura. Kwa hiyo nawe vumilia kama walivyovumilia; na Mwenyezi Mungu atakunusuru kama alivyowanusuru.

Huu ndio mzunguko wa maisha - mvutano baina ya kheri na shari na haki na batili. Ni muhali kwa mpigania haki asipate maudhi kutoka katika maadui wa haki. Vilevile haki haiwezi kushinda ila wapatikane watakaoinusuru wavumilivu katika jihadi ya haki na wainunue kwa nafsi zao, watu wao na mali zao.

Ni desturi ya Mwenyezi Mungu, wala huwezi kupata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu, Hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Na hakuna wa kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu.

Wala sijui wakati ambao wabatilifu wamekuwa na nguvu kuliko wakati huu tunaoishi. Wameweka vituo vya kijeshi kila mahali, vituo vya kuharibu, silaha kali za kumaliza watu na kubomoa. Wanatawala nyenzo za wananchi wadhaifu, mabenki, magazeti, uchapishaji na usambazaji, Mpaka yule mtu aliye mwaminifu mwenye ikhlasi anajikuta ametupwa hawezi kutoa makala huru au kutangaza haki kupitia kwenye Idhaa. Lakini mhaini, popote atakapoelekea atapata mapokezi na kutukuzwa [7] .

Na bila shaka zimekujia baadhi ya habari za Mitume hao.

Yaani tumekusimulia kabla yale yaliyowapata Mitume kutokana na watu wao na jinsi walivyovumilia katika kukadhibishwa na maudhi, na kwamba mwisho ushindi ulikuwa wao.

Na desturi hii itakupitia wewe, kama iliyowapita wao, wala hakuna mwenye kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu.

Na ikiwa ni makubwa kwako huku kukataa kwao, basi kama unaweza kutafuta njia ya chini kwa chini katika ardhi au ngazi kwendea mbinguni na kuwaletea ishara.

Aya hii ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu kumwambia Mtume wake Mtukufu:

﴿فَلَا تَذْهَبْ نَفْسُكَ عَلَيْهِمْ حَسَرَاتٍ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ بِمَا يَصْنَعُونَ﴾

"Basi roho yako isitoke kwa majonzi juu yao; hakika Mwenyezi Mungu anayajua yote wanayoyafanya." (35:8)

Aya zote hizi mbili zinatoa picha jinsi Mtume(s.a.w.w) alivyokuwa akipata jakamoyo na uchungu kutokanana upinzani wa washirikina kwa mwito wake.

Yaliyompata Mtume kutoka kwa watu wake ni yale yanayoondoa upole wa mpole. Lakini yeye akavumilia na kuwa na matumaini; wala hakuwaapiza bali aliwaombea, akisema:"Ewe Mola wangu! Wasamehe watu wangu, hakika wao hawajui"

Pamoja na hayo yote alikuwa akihisi uchungu kwa kufuru zao. Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia kwa Aya hii, ili kumpoza na kumwondolea matumaini na aachane nao; kisha angoje kidogo, aone vile utakavyokuwa mwisho wa wakadhibishaji.

Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka, bila shaka angeliwakusanya kwenye uongofu.

Razi anasema kuwa: "Hii inafahamisha kuwa yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu hataki makafiri waamini, bali anataka kuwabakisha kwenye ukafiri.

Lakini hii itakuwa ni dhuluma hasa, na Mwenyezi Mungu hawadhulumu waja. Usahihi wa maana ya jumla hii, ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hataki kumlazimisha yeyote katika kumwamini, bali anamwachia hiyari yake baada ya kumsimamishia hoja kwa dalili na ubainifu. Lau angelitaka waja wake waamini kwa kusema 'kuwa ikawa', basi asingelikufuru yeyote katika wao. Lakini hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ilitaka ajiingize katika mambo ya watu kama mwamrishaji na mwenye kutoa nasaha, si kama Muumba mwenye nguvu, Umetangulia ufafanuzi katika Juz. 1 (2:26)

Basi usiwe miongoni mwa wajinga.

Atakuwaje Mtume Mtukufu miongoni mwa wajinga na hulka zake ni hulka za Qur'an? Msemo huu umefaa kuelekezwa kwa mtukufu wa viumbe, kwa vile unatoka kwa Muumba wa viumbe na sio kwa kwa aliye kama yeye.

Wanaokubali ni wale tu wanaosikia, Na wafu Mwenyezi Mungu atawafufua kisha watarejeshwa kwake.

Aya hii ni mfano wa Aya isemayo:

﴿إِنَّكَ لَا تُسْمِعُ الْمَوْتَىٰ وَلَا تُسْمِعُ الصُّمَّ الدُّعَاءَ إِذَا وَلَّوْا مُدْبِرِينَ﴾

"Hakika huwezi kuwasikilizisha wafu wala huwezi kuwasikilizisha viziwi mwito wanapogeuka kurudi nyuma" (27:80)

Maana ni kuwa: Ewe Muhammad! Wale unaopupia waonyeke hawakusikii kwa kufahamu na kuzingatia. Kwa sababu kupenda dunia kumewafanya kama wafu, na wafu haitakikani kuwaambia chochote; bali wanaachwa na mambo yao mpaka siku ya kiyama, watakapoiona adhabu ambayo hawataweza kuikimbia.

Na husema: Kwa nini hakuteremshiwa ishara kutoka kwa Mola wake?

Utauliza : vipi wanasema hivi na hali Mwenyezi Mungu amemteremshia Muhammad(s.a.w.w) ishara na hoja kadhaa na ubainifu.

Jibu : Makusudio ya ishara hapa ni muujiza ule walioutaka wao kuwa ni sharti la wao kumwamini Muhammad(s.a.w.w) ; hawakusudii muujiza unaomkinaisha mwenye kuitafuta haki, Lau wangeliutaka huo wasingelisema hivyo.

Sema: Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye uweza wa kuteremsha ishara yoyote , ile wanayotaka, lakini yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu haiteremshi kwa kuitikia matakwa na hawaa zao; isipokuwa anateremsha miujiza kulingana na inavyopitisha hekima yake.

Lakini wengi wao hawajui , kuwa anateremsha miujiza kulingana na hekima Yake na sio hawa za watu.

﴿وَمَا مِن دَابَّةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا طَائِرٍ يَطِيرُ بِجَنَاحَيْهِ إِلَّا أُمَمٌ أَمْثَالُكُم مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يُحْشَرُونَ﴾

38.Na hakuna mnyama katika ardhi wala ndege arukaye kwa mbawa zake, ila ni umma kama nyinyi, Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote. Kisha watakusanywa kwa Mola wao.

﴿وَالَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا صُمٌّ وَبُكْمٌ فِي الظُّلُمَاتِ مَن يَشَإِ اللَّـهُ يُضْلِلْـهُ وَمَن يَشَأْ يَجْعَلْهُ عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴾

39.Na wale waliokadhibisha ishara zetu ni viziwi na mabubu wako gizani. Amtakaye Mwenyezi Mungu humpoteza na amtakaye humweka katika njia iliyonyooka.

WANYAMA NA NDEGE NI UMMA

Aya 38-39

LUGHA

Mnyama, ni kila anayetembea katika ardhi wakiwa ni: Watu, wanyama na wadudu.

MAANA

Na hakuna mnyama katika ardhi wala ndege arukaye kwa mbawa zake, ila ni umma kama nyinyi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anabainisha katika Aya hii kwamba baina yetu na wanyama kuna aina ya kufanana, lakini hakufafanua aina yenyewe. Je, tunafanana katika kuwa wao ni viumbe wa Mwenyezi Mungu; au katika kumwamini Mwenyezi Mungu na kumsifu kwa sifa zake njema? Au tunafanana katika kuwa wao ni aina zinazojulikana kwa majina; kama zinavyojulikana koo na kabila? Au ni katika kupanga maisha yao na kufanya mambo kulingana na masilahi?

Kwa hali yoyote iwayo ni kuwa wataalamu wengi wamechunguza tabia na kazi za wanyama, wadudu na ndege na wakafikia kwenye siri za ajabu zinazoshuhudia kuweko mpangaji mwenye hekima, Tutataja baadhi ya mifano.

Ndovu huweka mahakama kwa mhalifu na ndovu aliyekosea huhukumiwa kwa kutengwa na kundi la wengine ili aishi peke yake katika upweke.

Kunguru anapohisi hatari itakayowapata wenzake huwaonya kwa sauti maalum. Ama katika hali ya furaha hutoa sauti iliyo karibu na kicheko.

Utauliza : Kuna faida gani katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kusema arukaye kwa mbawa zake ambapo kumtaja Ndege kunafahamisha moja kwa mja kuruka kwa mbawa?

Jibu : Hakuna faida, tuijuayo, isipokuwa ufasaha wa maneno.

Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote.

Imesemekana kuwa makusudio ya Kitab hapa ni lawhim-mahfudh (ubao maalum wenye kuhifadhiwa) wenye kukusanya yaliyokuwa na yatakayokuwa.

Kauli ya pili, inasema ni fumbo la ujuzi wa Mwenyezi Mungu kujua makusudio ya mtu, na kauli zake na vitendo vyake.

Kauli ya tatu, inasema ni Qur'an na kwamba Mwenyezi Mungu amebainisha ndani yake kila yapasayo kubainishiwa watu, miongoni mwa misingi ya dini na matawi yake na yanayofungamana nayo, Nasi tumeichagua kauli hii katika kufasiri Aya ya (2:2) Juz. 1, kifungu Qur'an na sayansi.

Kisha watakusanywa kwa Mola wao.

Dhahiri ya maneno inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu atawakusanya wanyama na ndege siku ya Kiyama, kama atakavyowakusanya watu. Vilevile Aya isemayo:"Na wanyama mwitu watakapokusanywa." (82:5)

Maulama wengi wamesema hivyo kwa kutegemea Aya hizo mbili na Hadith isemayo: "Hakika Mwenyezi Mungu atawachukulia kisasi watu kutokana na wenye pembe."

Sisi tuko pamoja na Ibn Abbas aliyesema kuwa makusudio ya kukusanywa wanyama ni mauti yao; kama ilivyopokewa katika Hadith: "Anayepatwa na kifo ndiyo kiama chake." Kwa sababu hisabu na adhabu ni baada ya kukalifiwa na sharia na kuzihalifu. Wala hakuna kukalifiwa na sharia ila pamoja na akili; na wanyama na ndege hawana akili, kwa hiyo hawakalifiwi na sharia.

Kwa sababu hizo basi, hawatakusanya kwa ajili ya hisabu. Lau wanyama wangelichukuliwa hisabu basi ingefaa zaidi watoto wadogo wachukuliwe hisabu. Ama Hadith ya 'kuchukua kisasi', ni fumbo la uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na kwamba yeye hataacha kidogo wala kikubwa ila atakidhibiti.

Ikiwa Mwenyezi Mungu atawaadhibu wenye pembe wakimpiga mtu, basi vizuri zaidi ni kutuharimishia sisi kuwachinja wanyama. Ama kauli ya anayesema kuwa Mwenyezi Mungu atayabadilisha maumivu ya mtu kwa mnyama, hiyo ni kumsemea Mwenyezi Mungu bila ya ujuzi wowote.

Na wale waliokadhibisha ishara zetu ni viziwi na mabubu wako gizani. Yaani wao ni kama viziwi, kwa sababu wao hawasikii mwito wa haki, na ni kama mabubu kwa sababu wao hawaitamki haki waliyoijua na wako katika giza la kufuata na giza la ushirikina, ukafiri, ufasiki na dhambi.

Amtakaye Mwenyezi Mungu humpoteza na amtakaye humweka katika njia iliyonyooka.

Yametangulia maelezo kuhusu uongofu na upotevu katika Juz.1 (2:26) na Juz.2 (4:88).

﴿قُلْ أَرَأَيْتَكُمْ إِنْ أَتَاكُمْ عَذَابُ اللَّـهِ أَوْ أَتَتْكُمُ السَّاعَةُ أَغَيْرَ اللَّـهِ تَدْعُونَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴾

40.Sema: niambieni, kama ikiwafikia adhabu ya Mwenyezi Mungu au ikiwafikia ile saa, je, mtamuomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wakweli?

﴿بَلْ إِيَّاهُ تَدْعُونَ فَيَكْشِفُ مَا تَدْعُونَ إِلَيْهِ إِن شَاءَ وَتَنسَوْنَ مَا تُشْرِكُونَ﴾

41.Bali yeye tu ndiye mtakayemuomba, Atawaondolea mnayomuomba akitaka, Na mtawasahau mnaowashirikisha .

﴿وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا إِلَىٰ أُمَمٍ مِّن قَبْلِكَ فَأَخَذْنَاهُم بِالْبَأْسَاءِ وَالضَّرَّاءِ لَعَلَّهُمْ يَتَضَرَّعُونَ﴾

42.Kwa hakika tulipeleka (Mitume) kwa umma zilizokuwa kabla yako; kisha tukawatia katika shida na madhara ili wapate kunyenyekea.

﴿فَلَوْلَا إِذْ جَاءَهُم بَأْسُنَا تَضَرَّعُوا وَلَـٰكِن قَسَتْ قُلُوبُهُمْ وَزَيَّنَ لَهُمُ الشَّيْطَانُ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

43.Basi mbona wasinyenyekee ilipowafikia adhabu yetu? Lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu na shetani akawapambia waliyokuwa wakiyafanya.

﴿فَلَمَّا نَسُوا مَا ذُكِّرُوا بِهِ فَتَحْنَا عَلَيْهِمْ أَبْوَابَ كُلِّ شَيْءٍ حَتَّىٰ إِذَا فَرِحُوا بِمَا أُوتُوا أَخَذْنَاهُم بَغْتَةً فَإِذَا هُم مُّبْلِسُونَ﴾

44.Basi waliposahau yale waliyokumbushwa tuliwafungulia milango ya kila kitu, mpaka walipofurahia yale waliyopewa tuliwakamata kwa ghafla; na mara wakawa wenye kukata tamaa.

﴿فَقُطِعَ دَابِرُ الْقَوْمِ الَّذِينَ ظَلَمُوا وَالْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴾

45.Ikakatwa mizizi ya watu waliodhulumu; na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote.

SEMA NIAMBIENI

Aya 40 - 45

MAANA

Sema: niambieni, kama ikiwafikia adhabu ya Mwenyezi Mungu au ikiwafikia ile Saa, je, mtamuomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wakweli?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamwamrisha Mtume wake awaambie washirikina: Niambieni kama ikiwafikia adhabu, kama ile iliyoteremshiwa wale waliokadhibisha Mitume yao; au yakiwafikia maumivu makubwa ya mauti na vitisho vya Kiyama, je katika hali hii, mtayaita masanamu na mizimu mliyokuwa mkiabudu na kudai kuwa itawaondolea fazaa na adhabu?

Makusudio ya Aya hii ni kuwa Makafiri kesho watajivua na yale waliyokuwa wakiyaabudu na kukimbilia kwa Mwenyezi Mungu baada ya kuwabainikia kuwa hakuna hila wala nguvu ila kwa msaada wake Yeye tu peke yake bila ya kuwa na mshirika.

MWENYEZI MUNGU NA MAUMBILE

Bali yeye tu ndiye mtakayemuomba.

Baada ya kuwauliza kuwa mtamwomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu siku ya vituko vikubwa, amelithibithisha jibu kwa kusema kwake:(Bali yeye tu ndiye mtakayemuomba) .

Hilo ndilo jibu linaloaminiwa na kujibiwa na umbile ambalo Mwenyezi Mungu amewaumbia watu, katika dunia na akhera, Na sio maana ya umbile la Mwenyezi Mungu kuwa mtu atamtambua Muumba hivi hivi tu bila ya dalili. Hapana! Kama ni hivo basi kusingelitokea mtu yeyote wa kumkanusha Mwenyezi Mungu.

Hakika maana ya umbile hili ni kuwa Mwenyezi Mungu amempa mtu maandalizi ya kufahamu dalili zinazofahamisha kuweko Mwenyezi Mungu, na dalili hizi haepukani nazo kwa hali yoyote. Anayekufuru anakufuru kwa kuzembea na kupuuza kwa kuepuka kuchunguza dalili na hoja. Kwa hiyo ndipo akastahiki adhabu kwa kupuuza huko.

Kwani hakuna tofauti kabisa katika mtazamo wa akili, baina ya mwenye kuacha kufanya amali, kwa makusudi, na huku anajua; na yule mwenye kuiacha haki akafuta batili kwa kutojua lakini ana uwezo wa kujua na kupambanua uongufu na upotevu, lakini akaacha kwa kupuuza na kudharau.

Inawezekana maandalizi hayo yakajificha nyuma ya pazia la kufuata maelezo na matamanio; sawa na linavyojificha jua nyuma ya mawingu, ikafikiriwa kwa yule asiyejua sitara hizo kuwa yeye amemkana Mwenyezi Mungu kwa kukosa dalili na dalili iko katika dhati yake na maumbile yale ambayo amemuumbia Mwenyezi Mungu. Na siku ya Kiyama sitara hii iliyozuka itaondoka na kudhihiri hakika iliyo wazi wala hakutasalia nafasi ya shaka na ukanusho.

Atawaondolea mnayomuomba akitaka.

Yaani nyinyi washirikina mtaacha siku ya Kiyama, kuomba masanamu mliyokuwa mkiyaabudu duniani na mtamwomba Mwenyezi Mungu peke yake, wakati hakika ya kila jambo itakapodhihiri.

Na mtawasahau mnaowashirikisha.

Yaani nyinyi washirikina siku ya Kiyama mtaacha kuyaomba masanamu mliyokuwa mkiyaabudu duniani na kumwomba Mwenyezi Mungu peke yake wakati itakapodhihiri hakika ya kila kitu.

Kwa hakika tulipeleka (Mitume) kwa umma zilizokuwa kabla yako; kisha tukawatia katika shida na madhara ili wapate kunyenyekea.

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) hawaadhibu waja wake ila baada ya kuwapelekea mjumbe atakayewaongoza kwenye njia ya uongofu. Kama hawakuongoka anawapa fursa ili wajirudi wenyewe, na kuwatia katika mtihani kwa mabalaa ili wanyenyekee na watubie, lakini wao waling'ang'ania maasi; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Aya inayofuatia hii.

Basi mbona wasinyenyekee ilipowafikia adhabu yetu? Lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu na shetani akawapambia waliyokuwa wakiyafanya.

Mwenyezi Mungu, ambaye zimetukuka sifa zake, anasema kuwa wao hawakunyenyekea ilipowafikia shida duniani wala hawakumdhalilikia Mwenyezi Mungu kwa kuacha inadi yao, bali waling'ang'ania ukafiri, na shetani akawa nyuma yao akiwapambia upotevu na ufisadi.

Aya hii inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamkubali kila anayekimbilia kwake, hata kama kukimbia kwake ni kwa vikwazo vya shida na balaa. Hivi ndivyo alivyo aliye mkarimu na adhimu. Hamnyimi mwenye kuomba wala hamkatishi tamaa, kwa namna yoyote lengo na msukumo wake utakavyokuwa.

Basi waliposahau yale waliyokumbushwa tuliwafungulia milango ya kila kitu mpaka walipofurahia yale waliyopewa tuliwakamata kwa ghafla; na mara wakawa wenye kukata tamaa.

Aliwaonya kwanza kwa kauli kupitia kwa Mitume. Pili, kwa vitendo alipowapa mtihani kwa shida na madhara.

Waliponga'ang'ania ukafiri na inadi aliwafungulia milango ya riziki na raha, ili kuwasimamishia hoja na kuwavuta kidogo kidogo kwa neema baada ya mtihani wa nakama.

Walipofurahia raha na kuzidi kiburi na wala wasielekee kwenye uongofu, basi Mwenyezi Mungu aliwaadhibu kwa namna wasiyofikiria, wakajuta kwa kuzembea na wakakata tamaa ya kuokoka.

Kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) mara nyingine aliwapa dhiki na mara nyingine furaha kwa kupenda waongoke; sawa na afanyavyo mzazi kumhurumia mwanawe akitaka atengenekewe.

Lakini wala hawakushukuru raha wala kuwaidhika na balaa. Wakang'olewa wote asibakie yeyote katika wao, ili wapate funzo watakaokuja baada yao.

Ikakatwa mizizi ya watu waliodhulumu; na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote.

Kwa sababu ya kuwaneemesha kwake waumin na kuwanusuru na watu wa kufuru na ufisadi.

9

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w) NA MA-IMAMU (a.s)

KUSEMA UONGO

498. Anas Ibn Maliki Khisal-i-Sadduq, Uk. 321: Anaelezea kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Chukueni mambo sita kutoka kwangu, na mimi nakubalia, na kutoa dhamana (Ya wewe kuingizwa Jannat)

1. Usiseme uongo

2.Unapo toa ahadi, usivunje

3. Unapo pewa amana na wengine, basi uwemuaminifu

4. Tazama chini ( usitende dhambi ).

5. Chunga heshima yako

6. Idhibiti mikono yako na ulimi wako.

499. Amesema Imam Al Hassan al-'Askari(a.s) : "Iwapo maovu yote yatawekwa katika nyunba moja, basi ufunguo ( wa milango yake ) itakuwa ni uongo ."[213] .

500. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Jiepusheni na kusema uongo hata kama ni uongo mgogo au mkubwa, kama kwa wadilifu au unasema kwa kdhihaki, kwasababu mtu anapo sema uongo mdogo basi anaweza kudiriki kusema uongo mkubwa pia.[214] .

501. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : Wakati mmoja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliulizwa kuhusu umbali baina ya ukweli na uongo naye akiwa akionyesha umbali huo baina ya macho yake na maskio yake kwa vidole vinne katika kutoa jibu hilo, "Kile majo yako yanayooonani ukweli na mengi na yale yanayo sikilizwa na maskio yako ni sehemu kubwa ni uongo."[215] .

502. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameyawekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[216]

503. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wasema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[217]

504. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameya wekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[218] .

505. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wa sema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[219] .

MARAFIKI NA URAFIKI

506. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Mtu anaathirika kwa imani ya marafiki zake. Kwa hivyo, muwe waangalifu kabisa katika urafiki wenu pamoja nao . " [220]

507. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) , Amesema: "Uwe rafiki wa yule ambaye atakuwa ndio heshima yako, si wewe uwe heshima yake. (Ufanye urafiki na wale walio juu yako ili wewe uweze kupata maendeleo kutokana na urafiki huo).[221] .

508. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Ndugu yangu mpenzi ni yule (anayenitambulisha) makosa na kasoro zangu.[222]

509. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kwa hakika kuna marafiki wa aina tatu kwa ajili ya Muislam:

1. Rafiki anayesema mimi niko pamoja nawe iwapo upo hai au umekufa: Na hili ndio matendo yake.

2. Rafiki anayesema mimi nipo rafiki wako hadi ukingoni mwa kaburi na nitakuacha:hawa ni watoto wake.

3. Rafiki anayesema mimi nitakuwa nawe hadi pale utakapo kufa:hii ni mali ambayo ataiacha humu duniani kwa warithi wake baada ya kifo chake.[223]

Tanbih Kutokana na riwaya hii, na kama hizi sisi tunaelewa kuwa kitu ambacho kitakuwa pamoja na huyo mtu aliye kufa na kuaga dunia hii katika siku ya Qiyamah imani na matendo yake mema. Na suala hili limezungumziwa katika ahadithi nyingi sana za Kiislam na vile vile katika ayah za Qur'an tukufu, kwa mfano:

510. Allah swt anatuambia: Wale walio amini na wakatenda mema watakuwa na raha na marejeo mazuri. (Qur'an, 13:29).

511. Allah swt anatuambia: Hakika wale walio amini na wakatenda mema - hakika Sisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema. (Qur'an,18: 30).

512. Allah swt anatuambi: Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi. (Qur'an, 18: 107).

513. Allah swt anatuambia:" Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi. (Qur'an,19: 96).

514. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Muwe waangalifu katika kutafuta marafiki wa kweli na mujaribu kuwafanyia majaribio, kwa sababu wao watakuwa ndio msaada wenu pale mnapokuwa katika hali nzuri na watetezi wenu pale mtapokuwa katika shida na matatizo."[224]

515. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Kukutana pamoja na wacha Mungut kunawaleteeni mema ."[225]

516. Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) . Amesema: "Jitahadharisheni na urafiki wa watendao madhambi, na kuwasaidia madhalimu ."[226]

MARAFIKI WASIO WEMA

517. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Anayetafuta uhusiano na marafiki wa wale wanao wadhalilisha wapenzi wa Allah swt basi watambue kuwa wao wamemuasi Allah swt ."[227]

518. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Mnapojulishwa kuhusu marafiki zenu wanapotenda maovu, nendeni mumwambie: Ewe fulani bin fulani ! Ama acha kutenda madhambi au ukae mbali nasi: Na hapo utengane naye hadi atakapo acha kutenda maovu.[228]

519. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili kutoka baba yake Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . ambaye Amesema kuwa baba yake Al Imam Hussein ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Ewe mwanangu! Jichunge na makundi matano na kamwe usifanye urafiki nao, wala usiongee nao na wala usifanye urafiki pamoja nao. Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . alimuuliza baba yake Je ni makundi gani hayo matano. Imam(a.s) . alimujibu: Jitahadharishe na wala usifanye urafiki pamoja na yule msema uongo kwa sababu yeye ni kama mazua mazua anaye kufanyia vitu vya mbali vikawa karibu, na anakifanya kiwe mbali kile ambacho kiko karibu nawe.[229]

Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na mtu ambaye hana tabia njema, kwa sababu atakuuza kwa thamani kwa tonge moja au hata chini ya hiyo. Jihadhari na wala usifanye uhusiano na bahili kwa sababu yeye atakunyima kutoka mali yake pale wewe utakapo hitaji hasa. Jihadhari na usifanye urafiki pamoja na mpumbavu, kwa sababu yeye atataka kukufaidisha wewe lakini kwa uhakika anakudhuru zaidi. Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na yule ambaye hawajali ndugu na maJama'a zake, kwa sababu mimi nimemona mtu kama huyo akilaaniwa katika kitabu cha Allah swt (yaani Qur'an Tukufu) katika sehemu tatu.

Nayo ni: Sura Al Baqarah, 2, Ayah ya 27; Wanao vunja ahadi ya Allah swt baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo amrisha Allah swt kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye Khasara. Sura Al-Raa'd, 13, ayah ya 25 Na wale wano vunja ahadi ya Allah swt baada ya kuzifunga, na wanakata aliy amrisha Allah swt yaungwe, na wanafanya fisadi katika nchi: Hao ndio watakao pata laana, na watapata Nyumba mbaya. Sura Muh'ammad, 47, ayah 22 Basi yanayo tarajiwa kwenu mkitawala ndio mfisidi katika nchi na mwatupe Jama'a zenu ?

520. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Ewe Kumail ! sema kile kilichopo katika hali yoyote ile. Uwe marafiki pamoja na wacha Allah swt na jiepushe na watendao maovu, jiweke mbali na wanafiki na usiwe pamoja na wadanganyifu na wahalifu na wahaini ."[230]

KUWAHUDUMIA WATU

521. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye mpuuzia ndugu yake Muislam mwenzake matatizo na shida za dunia hizi, basi Allah swt atampunguzia shida na matatizo yake huko Akhera ." [231]

522. Amesema Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Kwa hakika, maombi ya shida za watu zinazokuijia wewe ni miongoni mwa neema na baraka za Allah swt juu yako. Hivyo usisikitike kwa sababu ya neema na baraka hizi ."[232]

523. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Popote pale utakapoona ndugu yako Muislam ana shida, jaribu kuangalia kama utaweza kumusaidia. (Usimpuuze mpaka akutamkie shida zake.) "[233]

524. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa amenakili kutoka mababu zake(a.s) . ambao wamemnakili Mtume Muhammad(s.a.w.w) akisema: "Yeyote yule anayemlisha muumin aliye na njaa akashiba basi Allah swt atamlisha mpaka ashibe kutoka matunda ya Jannah; Na yeyote yule atakaye mvisha nguo yule aliye na shida za nguo, Allah swt atamvisha nguo zilizofumwa na za hariri, na yeyote yule atakaye mumalizia kiu muumin basi Allah swt atamjaalia kinywaji kilichopigwa lakiri; Na yeyote atakaye msaidia muumin kupunguza shida yake, basi Allah swt atamweka chini ya Arshi yake siku ya Qiyama siku ambayo hakutakuwa na kivuli chochote isipokuwa kivuli cha Arshi yake."[234]

525. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Watu wanamtegemea Allah swt kwa ajili ya riziki, kwa hiyo mpenzi miongoni mwa watu kwake Allah swt ni yule ambaye anawasaidia wale watu wanaomtegemea Allah swt na kuwafanya watu wa familia ya nyumbani wakawa na furaha."[235] .

526. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye wasaidia Waislam ndugu zake wakati wa shida, Allah swt atamwondolea shida na matatizo sabini na tatu, moja ambayo ni ambayo iko humu duniani na sabini na mbili zingine zitakazo kuwa wakati wa shida kubwa, ambapo watu watakuwa mashughuli katika mambo yao ya binafsi (katika Akhera) ." [236]

KUTOA MIKOPO

527. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayeijiwa na ndugu yake Muislam kwa ajili ya kukopa na kama yeye hampi mkopo, basi Allah swt atamharamishia kuingia Jannat siku ambayo waja mema watakuwa wakilipwa na kufidiwa ." [237]

528. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayetakiwa na ndugu yake Muislam kwa kukopeshwa na kama yeye hamkopeshi mkopo, Allah swt atamzuia kuingia Jannat siku ambayo waja wema watakuwa wakilipwa mema yao ." [238]

KUWASAIDIA WENYE SHIDA

529. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Waulizeni maswali walio elimika, muongee pamoja na wale wenye hekima, na mujihusishe pamoja na masikini."[239]

530. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Sababu mojawapo ya kuteketea na kupotea kwa mali na utajiri wa mtu ni kule kutowajali na kutowasaidia wale wenye shida."[240]

531. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mtume Muhammad (s.a.w.w) amemnakili Allah swt kwa kuameambiwa usiku wa Mi'raj: Ewe Ahamad! Mapenzi yangu ni kule kuwapenda masikini. Wafanye masikini wawe karibu nawe na uwaweke karibu nawe ili mimi niweze kukufikia wewe .."[241]

532. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Yeyote yule anayemmalizia muumin njaa yake kiasi kwamba akaridhika kikamilifu, basi hakuna binadamu yeyote miongoni mwetu au miongoni mwa Malaika wanaojua kiasi cha thawabu yake siku ya Qiyamah isipokuwa Allah swt mmiliki wa Malimwengu yote. Na aliongezea: Kumlisha Muislam aliye na njaa ni njia moja kubwa sana ya kuomba Tawba( usamehevu)."[242]

Baada ya hapo alisoma ayah ya Qur'an Tukufu Sura Al-Balad, 90, ayah 14 - 16. Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye Jama'a, Au masikini aliye vumbini.

ZAWADI NA KUWAFURAHISHA MUUMIN

533. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Wakati sadaka inapotolewa na mtu kutoka mikononi mwake, basi hiyo sadaka inasema: Mimi nilikuwa kitu cha kwisha, lakini wewe umenipa maisha; Mimi nilikuwa sina thamani sasa wewe umenifanya niwe na thamani kubwa; mimi nilikuwa ni adui nawe umenifanya mie kuwa rafiki; Wewe ulikuwa daima ukinilinda na kunihifadhi lakini sasa mimi nitakulinda na kukuhifadhi hadi siku ya Qiyamah ." [243]

534. Amesema Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) : "Yeyote yule atakaye mfurahisha Muumin, basi kwa hakika kwanza kabisa amemfurahisha Allah swt, na pili amemfurahisha Mtume Muhammad (s.a.w.w) na tatu ametufurahisha sisi Ahlul Bayt (a.s) "[244]

535. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Allah swt ameweka mahitaji ya wale wasio na uwezo katika mali ya matajiri. Kwa hivyo atakapokuwa mtu asiye na uwezo akabakia katika hali ya njaa basi ni kwa sababu matajiri wamemnyima haki yake ."[245] .

536. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Kwa kiapo cha Allah swt! Yeyote yule anayeizuia mali yake isiwasaidie Mumin wenye shida basi siku ya Qiyamah kamwe hawataonja chakula cha Jannat wala Kinywaji kilichopigwa Lakiri."[246]

SADAKA NA MISAADA

537. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah ."

538. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya ."

539. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema." Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akaendelea kusema: "Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika barak a."

540. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya .

541. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . katika kuelezea tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl, 92, Ayah ya 5 na 6: Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu. Ndipo amesema kuwa; Allah swt ndivyo anavyo walipa wale watendao mema, kwa mema yao mara kumi, au hata mara laki moja na hata zaidi ya hapo. Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi."

542. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa."

543. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka ."

544. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu ."

545. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjipatie riziki ."

546. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu. Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali kwa kile huyu mtu akitoacho katika mali yake ."

547. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu! Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi ".

548. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Kuwa mali halisi ya mtu ni ile ambayo yeye ametolea sadaka ."

549. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima ."

550. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam ."

551. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa akisema: "Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka ."

552. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . katika Nahjul Balagha amesema kuwa: "Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt ."

553. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima, "Awe na tabia njema, "Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa "Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo) " Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji (anaotoa katika njia ya Allah swt ).

554. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na nikawarudishia heshima yao miongoni mwa watu, basi mimi ninaona jambo hili ni afadhali na bora zaidi kuliko hata kwenda kuhiji Hijja sabini. "

555. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . aliijiwa na mtu mmoja na aliyeuliza, "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w)! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru ?"

556. Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimjibu kuwa: "Kuwa mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi."

557. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Siku moja Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Maimuna binti Harun, Je Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , 'Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi nimemfanya huru.' Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwambia "Iwapo kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea huruma basi ingekuwa afadhali zaidi."

558. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini ."

559. Siku moja walikuja wagonjwa wakilalamikia magonjwa yao mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ., naye akawaambia; "Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya ."

560. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . aliulizwa na Sahaba mmoja: "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo." Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . kamwambia: "Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo." Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alipomtembelea huyo mtu akamwambia, "Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata kama kitakuwa ni kipande kidogo tu. Utambue wazi kuwa kiasi chochote kile hata kikiwa kiasi gani kama kitatolewa kwa roho safi basi mbele ya Allah huwa ni kipenzi, kwani Allah swt ameelezea kuwa: Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! (Qur'an,99: 7 – 8).

561. Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alimwelezea kuwa: "Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Balad,90, Ayah11 - 16 Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? Kumkomboa mtumwa; Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye jamaa, Au masikini aliye vumbini

"Hivyo ewe Sahabi uelewe kuwa Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au watakao walisha yatima na masikini."

562. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu: "Toa Sadaka kwa niaba yake." Na mtu huyo akajibu kuwa "Sasa mtoto wake amekuwa na umri yaani amekuwa kijana." Basi Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimwambia kuwa "Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . kuwa: "Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo. Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza 'Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?' Kwa hayo mtoto akajibu "Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.' Kwa hayo baba yake akasema "Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo."

563. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia 'ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe."

564. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua ".

565. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) katika hadith zake amesema kuwa: "Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji ."

566. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Kuna aina tatu ya mikono wa " kwanza ni mkono ule wa Allah swt ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt, " mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na " mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt na musikalifishe nafisi zenu".

567. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.

Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt."

568. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa' ya tende, na kama sa' moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka. Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia 'Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe umejiandalia nini?' Na hapo wewe utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt."

569. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu." Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa katika mali yenu. Na miongoni mwa jamaa zenu wanapokuwa na shida muwasaidiapo hiyo siyo Sadaka bali hiyo ni wajibu wenu."

570. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka themanini. Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake. Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba. Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake. Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu."

571. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amesema kuwa; " Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi. Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba: 'Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.

Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt ni kwamba, Allah swt alimtuma Malaika Jibrail(a.s) kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili(a.s) . akamwambia 'Ewe bibi kizee! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake."

572. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: " Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka. Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo (mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana."

573. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa : "Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza, kama vile mwanadamu anavyowatunza watoto wake.

Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud, milima mikubwa sana."

574. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima ."

575. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima ."

576. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka ."

577. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s).! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri .

Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka hao haitakuwa ni Sadaka. Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .!Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka ."

578. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza mtu mmoja "Je leo umefunga Saumu?" Mtu huyo alijibu "La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza: "Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?" Naye akajibu: "Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.

579. Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza: "Je umemlisha masikini yeyote?" Naye akajibu: "Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) !" Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwambia huyo mtu: "Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee na uwe nao kwa mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka yako kwao."

580. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ambaye ameseama: "kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu."

581. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ili kutaka kuepukana na shari za madhalimu basi toeni Sadaka ."

582. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake : "Myahudi huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka. Myahudi huyo kama kawaida yake alikata kuni na alijitwisha kichwani mwake na akarud akiwa salama. Na tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini. Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali sana huku akiuma kuni. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Myahudi yule,'Je wewe leo umefanya jambo gani?' Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka. Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya."

583. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahaba wake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote. Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema: "Mimi nilipotoka nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za tende. Na kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa kama Sadaka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . akajibu "Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza."

584. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . siku mmoja alimwambia Sahabi wake Mayassari kuwa: "Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi."

585. Al Imam Hasan al-'Askary(a.s) . anasema kuwa: " Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . je tufanyeje sasa? Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: 'Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya mali yenu basi yeye kila siku atawarudishia pamoja na nyongeza yake. ' Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza : "Je ni nani huyo?" Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: "Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt." Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza kumkabidhi vipi mali zetu hizi? Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawaambia: Toeni Sadaka muwape wale wanaostahiki. Kwa kusikia hayo wakauliza ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Hapa tulipo tutawatoa wapi hawa masikini na mafakiri tutawatafuta wapi? Basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwajibu: munuie kuwa sehemu moja ya mali yenu mtatoa Sadaka basi na msiwe na wasiwasi Allah swt atailinda mali yenu yote.

"Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alivyowaambi,a na Imam(a.s) . akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao. Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi."

586. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema "mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue". Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia "Allah swt atakuzidishia" na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . na akamwambia Imam(a.s) . "Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa." Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam(a.s) . hakumpa chochote.

Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu mwingine kuja kuomba, na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alichota mikono ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia mtumwa wake kama tuna pesa zozote zile tulizo nazo kwetu mpe huyo. Na huyo mfanyakazi wa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa amri yake alimpa Dirham Ishirini alizokuwa nazo. Mwombaji akiwa anachukua Dirham akasema: 'Ewe Allah swt! Nakushukuru mno sana na hakuna mwingine wa kushirkishwa nawe. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . nguo aliyokuwa amejifunika akampa huyo mwombaji na huyo mwombaji baada ya kuivaa na kujifunika na hiyo nguo akamshukuru Allah swt ambaye amemjaalia nguo ya kujifunika. 'Ewe Aba 'Abdillah! Allah swt akulipe kila la heri. Na baada ya kusema hayo akaondoka zake. Kwa kuona haya Ma-sahaba wakamwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa kila alivyoendelea yeye kumsifu Allah swt ndivyo wewe ulivyoendelea kumpa na kama asinge omba kwa kutaja jina la Al Imam(a.s) . lazima angeendelea kumpa chochote zaidi ya hayo."

9

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w) NA MA-IMAMU (a.s)

KUSEMA UONGO

498. Anas Ibn Maliki Khisal-i-Sadduq, Uk. 321: Anaelezea kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Chukueni mambo sita kutoka kwangu, na mimi nakubalia, na kutoa dhamana (Ya wewe kuingizwa Jannat)

1. Usiseme uongo

2.Unapo toa ahadi, usivunje

3. Unapo pewa amana na wengine, basi uwemuaminifu

4. Tazama chini ( usitende dhambi ).

5. Chunga heshima yako

6. Idhibiti mikono yako na ulimi wako.

499. Amesema Imam Al Hassan al-'Askari(a.s) : "Iwapo maovu yote yatawekwa katika nyunba moja, basi ufunguo ( wa milango yake ) itakuwa ni uongo ."[213] .

500. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Jiepusheni na kusema uongo hata kama ni uongo mgogo au mkubwa, kama kwa wadilifu au unasema kwa kdhihaki, kwasababu mtu anapo sema uongo mdogo basi anaweza kudiriki kusema uongo mkubwa pia.[214] .

501. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : Wakati mmoja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliulizwa kuhusu umbali baina ya ukweli na uongo naye akiwa akionyesha umbali huo baina ya macho yake na maskio yake kwa vidole vinne katika kutoa jibu hilo, "Kile majo yako yanayooonani ukweli na mengi na yale yanayo sikilizwa na maskio yako ni sehemu kubwa ni uongo."[215] .

502. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameyawekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[216]

503. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wasema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[217]

504. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameya wekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[218] .

505. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wa sema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[219] .

MARAFIKI NA URAFIKI

506. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Mtu anaathirika kwa imani ya marafiki zake. Kwa hivyo, muwe waangalifu kabisa katika urafiki wenu pamoja nao . " [220]

507. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) , Amesema: "Uwe rafiki wa yule ambaye atakuwa ndio heshima yako, si wewe uwe heshima yake. (Ufanye urafiki na wale walio juu yako ili wewe uweze kupata maendeleo kutokana na urafiki huo).[221] .

508. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Ndugu yangu mpenzi ni yule (anayenitambulisha) makosa na kasoro zangu.[222]

509. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kwa hakika kuna marafiki wa aina tatu kwa ajili ya Muislam:

1. Rafiki anayesema mimi niko pamoja nawe iwapo upo hai au umekufa: Na hili ndio matendo yake.

2. Rafiki anayesema mimi nipo rafiki wako hadi ukingoni mwa kaburi na nitakuacha:hawa ni watoto wake.

3. Rafiki anayesema mimi nitakuwa nawe hadi pale utakapo kufa:hii ni mali ambayo ataiacha humu duniani kwa warithi wake baada ya kifo chake.[223]

Tanbih Kutokana na riwaya hii, na kama hizi sisi tunaelewa kuwa kitu ambacho kitakuwa pamoja na huyo mtu aliye kufa na kuaga dunia hii katika siku ya Qiyamah imani na matendo yake mema. Na suala hili limezungumziwa katika ahadithi nyingi sana za Kiislam na vile vile katika ayah za Qur'an tukufu, kwa mfano:

510. Allah swt anatuambia: Wale walio amini na wakatenda mema watakuwa na raha na marejeo mazuri. (Qur'an, 13:29).

511. Allah swt anatuambia: Hakika wale walio amini na wakatenda mema - hakika Sisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema. (Qur'an,18: 30).

512. Allah swt anatuambi: Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi. (Qur'an, 18: 107).

513. Allah swt anatuambia:" Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi. (Qur'an,19: 96).

514. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Muwe waangalifu katika kutafuta marafiki wa kweli na mujaribu kuwafanyia majaribio, kwa sababu wao watakuwa ndio msaada wenu pale mnapokuwa katika hali nzuri na watetezi wenu pale mtapokuwa katika shida na matatizo."[224]

515. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Kukutana pamoja na wacha Mungut kunawaleteeni mema ."[225]

516. Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) . Amesema: "Jitahadharisheni na urafiki wa watendao madhambi, na kuwasaidia madhalimu ."[226]

MARAFIKI WASIO WEMA

517. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Anayetafuta uhusiano na marafiki wa wale wanao wadhalilisha wapenzi wa Allah swt basi watambue kuwa wao wamemuasi Allah swt ."[227]

518. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Mnapojulishwa kuhusu marafiki zenu wanapotenda maovu, nendeni mumwambie: Ewe fulani bin fulani ! Ama acha kutenda madhambi au ukae mbali nasi: Na hapo utengane naye hadi atakapo acha kutenda maovu.[228]

519. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili kutoka baba yake Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . ambaye Amesema kuwa baba yake Al Imam Hussein ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Ewe mwanangu! Jichunge na makundi matano na kamwe usifanye urafiki nao, wala usiongee nao na wala usifanye urafiki pamoja nao. Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . alimuuliza baba yake Je ni makundi gani hayo matano. Imam(a.s) . alimujibu: Jitahadharishe na wala usifanye urafiki pamoja na yule msema uongo kwa sababu yeye ni kama mazua mazua anaye kufanyia vitu vya mbali vikawa karibu, na anakifanya kiwe mbali kile ambacho kiko karibu nawe.[229]

Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na mtu ambaye hana tabia njema, kwa sababu atakuuza kwa thamani kwa tonge moja au hata chini ya hiyo. Jihadhari na wala usifanye uhusiano na bahili kwa sababu yeye atakunyima kutoka mali yake pale wewe utakapo hitaji hasa. Jihadhari na usifanye urafiki pamoja na mpumbavu, kwa sababu yeye atataka kukufaidisha wewe lakini kwa uhakika anakudhuru zaidi. Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na yule ambaye hawajali ndugu na maJama'a zake, kwa sababu mimi nimemona mtu kama huyo akilaaniwa katika kitabu cha Allah swt (yaani Qur'an Tukufu) katika sehemu tatu.

Nayo ni: Sura Al Baqarah, 2, Ayah ya 27; Wanao vunja ahadi ya Allah swt baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo amrisha Allah swt kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye Khasara. Sura Al-Raa'd, 13, ayah ya 25 Na wale wano vunja ahadi ya Allah swt baada ya kuzifunga, na wanakata aliy amrisha Allah swt yaungwe, na wanafanya fisadi katika nchi: Hao ndio watakao pata laana, na watapata Nyumba mbaya. Sura Muh'ammad, 47, ayah 22 Basi yanayo tarajiwa kwenu mkitawala ndio mfisidi katika nchi na mwatupe Jama'a zenu ?

520. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Ewe Kumail ! sema kile kilichopo katika hali yoyote ile. Uwe marafiki pamoja na wacha Allah swt na jiepushe na watendao maovu, jiweke mbali na wanafiki na usiwe pamoja na wadanganyifu na wahalifu na wahaini ."[230]

KUWAHUDUMIA WATU

521. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye mpuuzia ndugu yake Muislam mwenzake matatizo na shida za dunia hizi, basi Allah swt atampunguzia shida na matatizo yake huko Akhera ." [231]

522. Amesema Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Kwa hakika, maombi ya shida za watu zinazokuijia wewe ni miongoni mwa neema na baraka za Allah swt juu yako. Hivyo usisikitike kwa sababu ya neema na baraka hizi ."[232]

523. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Popote pale utakapoona ndugu yako Muislam ana shida, jaribu kuangalia kama utaweza kumusaidia. (Usimpuuze mpaka akutamkie shida zake.) "[233]

524. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa amenakili kutoka mababu zake(a.s) . ambao wamemnakili Mtume Muhammad(s.a.w.w) akisema: "Yeyote yule anayemlisha muumin aliye na njaa akashiba basi Allah swt atamlisha mpaka ashibe kutoka matunda ya Jannah; Na yeyote yule atakaye mvisha nguo yule aliye na shida za nguo, Allah swt atamvisha nguo zilizofumwa na za hariri, na yeyote yule atakaye mumalizia kiu muumin basi Allah swt atamjaalia kinywaji kilichopigwa lakiri; Na yeyote atakaye msaidia muumin kupunguza shida yake, basi Allah swt atamweka chini ya Arshi yake siku ya Qiyama siku ambayo hakutakuwa na kivuli chochote isipokuwa kivuli cha Arshi yake."[234]

525. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Watu wanamtegemea Allah swt kwa ajili ya riziki, kwa hiyo mpenzi miongoni mwa watu kwake Allah swt ni yule ambaye anawasaidia wale watu wanaomtegemea Allah swt na kuwafanya watu wa familia ya nyumbani wakawa na furaha."[235] .

526. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye wasaidia Waislam ndugu zake wakati wa shida, Allah swt atamwondolea shida na matatizo sabini na tatu, moja ambayo ni ambayo iko humu duniani na sabini na mbili zingine zitakazo kuwa wakati wa shida kubwa, ambapo watu watakuwa mashughuli katika mambo yao ya binafsi (katika Akhera) ." [236]

KUTOA MIKOPO

527. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayeijiwa na ndugu yake Muislam kwa ajili ya kukopa na kama yeye hampi mkopo, basi Allah swt atamharamishia kuingia Jannat siku ambayo waja mema watakuwa wakilipwa na kufidiwa ." [237]

528. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayetakiwa na ndugu yake Muislam kwa kukopeshwa na kama yeye hamkopeshi mkopo, Allah swt atamzuia kuingia Jannat siku ambayo waja wema watakuwa wakilipwa mema yao ." [238]

KUWASAIDIA WENYE SHIDA

529. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Waulizeni maswali walio elimika, muongee pamoja na wale wenye hekima, na mujihusishe pamoja na masikini."[239]

530. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Sababu mojawapo ya kuteketea na kupotea kwa mali na utajiri wa mtu ni kule kutowajali na kutowasaidia wale wenye shida."[240]

531. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mtume Muhammad (s.a.w.w) amemnakili Allah swt kwa kuameambiwa usiku wa Mi'raj: Ewe Ahamad! Mapenzi yangu ni kule kuwapenda masikini. Wafanye masikini wawe karibu nawe na uwaweke karibu nawe ili mimi niweze kukufikia wewe .."[241]

532. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Yeyote yule anayemmalizia muumin njaa yake kiasi kwamba akaridhika kikamilifu, basi hakuna binadamu yeyote miongoni mwetu au miongoni mwa Malaika wanaojua kiasi cha thawabu yake siku ya Qiyamah isipokuwa Allah swt mmiliki wa Malimwengu yote. Na aliongezea: Kumlisha Muislam aliye na njaa ni njia moja kubwa sana ya kuomba Tawba( usamehevu)."[242]

Baada ya hapo alisoma ayah ya Qur'an Tukufu Sura Al-Balad, 90, ayah 14 - 16. Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye Jama'a, Au masikini aliye vumbini.

ZAWADI NA KUWAFURAHISHA MUUMIN

533. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Wakati sadaka inapotolewa na mtu kutoka mikononi mwake, basi hiyo sadaka inasema: Mimi nilikuwa kitu cha kwisha, lakini wewe umenipa maisha; Mimi nilikuwa sina thamani sasa wewe umenifanya niwe na thamani kubwa; mimi nilikuwa ni adui nawe umenifanya mie kuwa rafiki; Wewe ulikuwa daima ukinilinda na kunihifadhi lakini sasa mimi nitakulinda na kukuhifadhi hadi siku ya Qiyamah ." [243]

534. Amesema Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) : "Yeyote yule atakaye mfurahisha Muumin, basi kwa hakika kwanza kabisa amemfurahisha Allah swt, na pili amemfurahisha Mtume Muhammad (s.a.w.w) na tatu ametufurahisha sisi Ahlul Bayt (a.s) "[244]

535. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Allah swt ameweka mahitaji ya wale wasio na uwezo katika mali ya matajiri. Kwa hivyo atakapokuwa mtu asiye na uwezo akabakia katika hali ya njaa basi ni kwa sababu matajiri wamemnyima haki yake ."[245] .

536. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Kwa kiapo cha Allah swt! Yeyote yule anayeizuia mali yake isiwasaidie Mumin wenye shida basi siku ya Qiyamah kamwe hawataonja chakula cha Jannat wala Kinywaji kilichopigwa Lakiri."[246]

SADAKA NA MISAADA

537. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah ."

538. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya ."

539. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema." Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akaendelea kusema: "Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika barak a."

540. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya .

541. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . katika kuelezea tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl, 92, Ayah ya 5 na 6: Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu. Ndipo amesema kuwa; Allah swt ndivyo anavyo walipa wale watendao mema, kwa mema yao mara kumi, au hata mara laki moja na hata zaidi ya hapo. Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi."

542. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa."

543. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka ."

544. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu ."

545. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjipatie riziki ."

546. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu. Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali kwa kile huyu mtu akitoacho katika mali yake ."

547. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu! Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi ".

548. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Kuwa mali halisi ya mtu ni ile ambayo yeye ametolea sadaka ."

549. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima ."

550. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam ."

551. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa akisema: "Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka ."

552. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . katika Nahjul Balagha amesema kuwa: "Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt ."

553. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima, "Awe na tabia njema, "Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa "Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo) " Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji (anaotoa katika njia ya Allah swt ).

554. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na nikawarudishia heshima yao miongoni mwa watu, basi mimi ninaona jambo hili ni afadhali na bora zaidi kuliko hata kwenda kuhiji Hijja sabini. "

555. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . aliijiwa na mtu mmoja na aliyeuliza, "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w)! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru ?"

556. Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimjibu kuwa: "Kuwa mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi."

557. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Siku moja Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Maimuna binti Harun, Je Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , 'Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi nimemfanya huru.' Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwambia "Iwapo kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea huruma basi ingekuwa afadhali zaidi."

558. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini ."

559. Siku moja walikuja wagonjwa wakilalamikia magonjwa yao mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ., naye akawaambia; "Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya ."

560. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . aliulizwa na Sahaba mmoja: "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo." Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . kamwambia: "Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo." Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alipomtembelea huyo mtu akamwambia, "Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata kama kitakuwa ni kipande kidogo tu. Utambue wazi kuwa kiasi chochote kile hata kikiwa kiasi gani kama kitatolewa kwa roho safi basi mbele ya Allah huwa ni kipenzi, kwani Allah swt ameelezea kuwa: Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! (Qur'an,99: 7 – 8).

561. Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alimwelezea kuwa: "Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Balad,90, Ayah11 - 16 Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? Kumkomboa mtumwa; Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye jamaa, Au masikini aliye vumbini

"Hivyo ewe Sahabi uelewe kuwa Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au watakao walisha yatima na masikini."

562. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu: "Toa Sadaka kwa niaba yake." Na mtu huyo akajibu kuwa "Sasa mtoto wake amekuwa na umri yaani amekuwa kijana." Basi Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimwambia kuwa "Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . kuwa: "Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo. Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza 'Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?' Kwa hayo mtoto akajibu "Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.' Kwa hayo baba yake akasema "Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo."

563. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia 'ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe."

564. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua ".

565. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) katika hadith zake amesema kuwa: "Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji ."

566. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Kuna aina tatu ya mikono wa " kwanza ni mkono ule wa Allah swt ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt, " mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na " mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt na musikalifishe nafisi zenu".

567. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.

Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt."

568. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa' ya tende, na kama sa' moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka. Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia 'Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe umejiandalia nini?' Na hapo wewe utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt."

569. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu." Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa katika mali yenu. Na miongoni mwa jamaa zenu wanapokuwa na shida muwasaidiapo hiyo siyo Sadaka bali hiyo ni wajibu wenu."

570. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka themanini. Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake. Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba. Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake. Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu."

571. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amesema kuwa; " Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi. Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba: 'Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.

Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt ni kwamba, Allah swt alimtuma Malaika Jibrail(a.s) kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili(a.s) . akamwambia 'Ewe bibi kizee! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake."

572. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: " Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka. Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo (mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana."

573. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa : "Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza, kama vile mwanadamu anavyowatunza watoto wake.

Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud, milima mikubwa sana."

574. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima ."

575. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima ."

576. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka ."

577. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s).! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri .

Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka hao haitakuwa ni Sadaka. Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .!Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka ."

578. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza mtu mmoja "Je leo umefunga Saumu?" Mtu huyo alijibu "La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza: "Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?" Naye akajibu: "Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.

579. Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza: "Je umemlisha masikini yeyote?" Naye akajibu: "Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) !" Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwambia huyo mtu: "Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee na uwe nao kwa mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka yako kwao."

580. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ambaye ameseama: "kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu."

581. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ili kutaka kuepukana na shari za madhalimu basi toeni Sadaka ."

582. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake : "Myahudi huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka. Myahudi huyo kama kawaida yake alikata kuni na alijitwisha kichwani mwake na akarud akiwa salama. Na tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini. Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali sana huku akiuma kuni. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Myahudi yule,'Je wewe leo umefanya jambo gani?' Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka. Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya."

583. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahaba wake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote. Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema: "Mimi nilipotoka nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za tende. Na kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa kama Sadaka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . akajibu "Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza."

584. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . siku mmoja alimwambia Sahabi wake Mayassari kuwa: "Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi."

585. Al Imam Hasan al-'Askary(a.s) . anasema kuwa: " Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . je tufanyeje sasa? Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: 'Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya mali yenu basi yeye kila siku atawarudishia pamoja na nyongeza yake. ' Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza : "Je ni nani huyo?" Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: "Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt." Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza kumkabidhi vipi mali zetu hizi? Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawaambia: Toeni Sadaka muwape wale wanaostahiki. Kwa kusikia hayo wakauliza ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Hapa tulipo tutawatoa wapi hawa masikini na mafakiri tutawatafuta wapi? Basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwajibu: munuie kuwa sehemu moja ya mali yenu mtatoa Sadaka basi na msiwe na wasiwasi Allah swt atailinda mali yenu yote.

"Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alivyowaambi,a na Imam(a.s) . akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao. Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi."

586. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema "mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue". Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia "Allah swt atakuzidishia" na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . na akamwambia Imam(a.s) . "Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa." Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam(a.s) . hakumpa chochote.

Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu mwingine kuja kuomba, na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alichota mikono ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia mtumwa wake kama tuna pesa zozote zile tulizo nazo kwetu mpe huyo. Na huyo mfanyakazi wa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa amri yake alimpa Dirham Ishirini alizokuwa nazo. Mwombaji akiwa anachukua Dirham akasema: 'Ewe Allah swt! Nakushukuru mno sana na hakuna mwingine wa kushirkishwa nawe. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . nguo aliyokuwa amejifunika akampa huyo mwombaji na huyo mwombaji baada ya kuivaa na kujifunika na hiyo nguo akamshukuru Allah swt ambaye amemjaalia nguo ya kujifunika. 'Ewe Aba 'Abdillah! Allah swt akulipe kila la heri. Na baada ya kusema hayo akaondoka zake. Kwa kuona haya Ma-sahaba wakamwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa kila alivyoendelea yeye kumsifu Allah swt ndivyo wewe ulivyoendelea kumpa na kama asinge omba kwa kutaja jina la Al Imam(a.s) . lazima angeendelea kumpa chochote zaidi ya hayo."


6

7

8

9