TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA Juzuu 7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA 22%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: tafsiri ya Qurani

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 14674 / Pakua: 3584
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASIF JUZUU YA SABA Juzuu 7

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿قُلْ أَنَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُنَا وَلَا يَضُرُّنَا وَنُرَدُّ عَلَىٰ أَعْقَابِنَا بَعْدَ إِذْ هَدَانَا اللَّـهُ كَالَّذِي اسْتَهْوَتْهُ الشَّيَاطِينُ فِي الْأَرْضِ حَيْرَانَ لَهُ أَصْحَابٌ يَدْعُونَهُ إِلَى الْهُدَى ائْتِنَا قُلْ إِنَّ هُدَى اللَّـهِ هُوَ الْهُدَىٰ وَأُمِرْنَا لِنُسْلِمَ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ﴾

71.Sema: Je, tuwaabudu wasiokuwa Mwenyezi Mungu ambao hawatunufaishi wala kutudhuru? Na turudishwe nyuma baada ya Mwenyezi Mungu kutuongoza? Kama yule ambaye mashetani wamempoteza; akiwayawaya katika ardhi, Anao marafiki wanaomwita kwenye uongofu: Njoo kwetu. Sema: Mwongozo hasa ni mwongozo wa Mwenyezi Mungu. Na tumeamrishwa tusilimu kwa Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe vyote.

﴿وَأَنْ أَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَاتَّقُوهُ وَهُوَ الَّذِي إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ﴾

72.Na simamisheni Swala na mcheni yeye; naye ndiye ambaye kwake mtakusanywa.

﴿وَهُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ وَيَوْمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُ قَوْلُهُ الْحَقُّ وَلَهُ الْمُلْكُ يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ﴾

73.Naye ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi kwa haki, Na siku anayosema 'kuwa' basi huwa. Kauli yake ni haki. Na ufalme ni wake siku itakapopulizwa parapanda.

SEMA: JE: TUWAABUDU WASIOKUWA MWENYEZI MUNGU?

Aya 71-73

MAANA

Sema: Je, tuwaabudu wasiokuwa Mwenyezi Mungu ambao hawatunufaishi wala kutudhuru?

Mtume(s.a.w.w) aliwalingania washirikina katika kumwabudu Mwenyezi Mungu; nao wakamtaka aabudu masanamu yao. Inasemekana kwamba walitoa rai ya kuwa waabudu nao waungu wao na wao waabudu naye Mola wake.

Kwa vyovyote itakavyokuwa ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwamrisha, katika Aya hii, kuwaambia kwa kukanusha, vipi tuache kumwabudu Mwenyezi Mungu anayenufaisha na kudhuru na tuabudu wale wasiojiweza wao wenyewe kujinufaisha au kujikinga na madhara?

Na turudishwe nyuma baada ya Mwenyezi Mungu kutuongoza.

Kurudi nyuma ni neno linalotumiwa kwa mtu aliyeiacha haki akafuata batili.

Kama yule ambaye mashetani wamempoteza; akiwayawaya katika ardhi. Anao marafiki wanaomwita kwenye uongofu: Njoo kwetu.

Huu ni mfano anaoutoa Mwenyezi Mungu kwa aliyekataa Tawhid na kwenda kwenye ushirikina au ulahidi. Kwa ufupi nikuwa mfano wa mtu huyu ni kama mfano wa mtu aliyekuwa katika msafara unakwenda kwa amani na salama.

Akauacha na akafuata njia yake jangwani bila ya mwelekeo wowote; kama ambaye amezungwa na mashetani. Basi wenzake wakamhurumia na kumwita: 'Njoo kwetu, hii ndiyo njia ya uongofu', lakini asiwajibu kwa kubabaika kwake. Ikawa mwisho wake ni balaa na maangamivu.

Mjuzi wa ghaibu na yanayoonekana, Naye ndiye mwenye hekima mwenye habari.

Sema: Mwongozo hasa ni mwongozo wa Mwenyezi Mungu.

Muundo huu wa kiubainifu unafahamisha kuwa mwongozo wa Mwenyezi Mungu haungiliwi na shaka yoyote; kama ambavyo unafahamisha kuwa mwongozo ni wa Mwenyezi Mungu peke yake katika kila kitu - katika itikadi sharia maadili na hali. Itikadi yoyote au fikra yoyote au kazi yoyote isiyokutana na mwongozo wa Mwenyezi Mungu basi ni ujinga na upotevu.

Na tumeamrishwa tusilimu kwa Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe vyote.

Hii ni katika kutaja mahsusi baada ya ujumla. Kwa sababu mwongozo wa Mwenyezi Mungu unaingia katika kila aliloamrisha Mwenyezi Mungu na kulikataza. Makusudio ya kuuhusisha Uislamu ni kukumbusha utukufu wake.

Na simamisheni swala.

Kwani hakuna mwongozo wala Uislam ila kwayo; ndiyo nguzo ya dini, ikikubaliwa hukubaliwa mengine na ikikataliwa hukataliwa mengine.

Na mcheni yeye Mwenyezi Mungu Mola wa walimwengu. Ameamrisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) takua baada ya kuamrisha swala, Kwa sababu hakuna swala wala imani sahihi bila ya takua, Kumwabudu Mwenyezi Mungu kweli ni kwenda kwenye njia yake na kumtii katika hukumu zote, sio baadhi tu.

Naye ndiye ambaye kwake mtakusanywa.

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:"Na itakuja kila nafsi pamoja na mwendeshaji na shahidi" (50:21).

Mwendeshaji atakayeiendesha hadi mahshar (watakapokusanya watu) na shahidi atakayeishuhudilia kwa yale yaliyoandaliwa kwa siku hii.

Naye ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi kwa haki.

Haki hapa ni ishara ya kuwa ulimwengu una kanuni zinazouhukumu na desturi inayokwenda nao kwa mpangilio bila ya mkorogano wowote. Hii ni dalili fasaha ya kuweko mpangaji wa mambo na atakayeilipa kila nafsi ililochuma.

Na siku anayosema 'kuwa' basi huwa, Kauli yake ni haki.

Katika maneno haya kuna kukadiriwa, kutangulizwa, na kuwekwa nyuma. Asili yake ni hivi: Kauli yake ni haki siku anapokiambia kitu kuwa, huwa. Maana yake ni kuwa kauli ya Mwenyezi Mungu inakuwa tu; na hudhihirika wazi hilo siku anapokiambia kitu kuwa, kikawa, Ni sawa aliyasema haya siku alipoanza kuumba viumbe au siku atakapowarudisha.

Kwa maneno mengine ni kuwa kauli ya Mwenyezi Mungu ndiyo kitendo chake katika kupatikana kitu bila ya kitu, na katika kukirudisha jinsi kilivyokuwa baada ya kuharibika na kuchangukana.

Na ufalme ni wake siku itakapopulizwa parapanda.

Kupulizwa parapanda ni fumbo la kufufuliwa walio makaburini. Na maana ya ufalme wa ufufuo huu ni kwamba yeye ndiye anayerudisha wafu kwenye uhai.

MASUFI

Mjuzi wa ghaibu na yanayoonekana.

Ghaibu ni mambo ya siri yaliyojificha, kama vile Malaika, ufufuo na mambo anayoyaficha mtu nafsini mwake. Na dhahiri ni yale yanayoonekana kidhahiri, kama vile ardhi, mbingu na anayoyafanya mtu wazi wazi.

Haya kwa binadamu ni sawa; ama kwa Mwenyezi Mungu hakuna ghaibu si katika mbingu wala ardhi, Hata hivyo masufi wanadai kuwa nafsi zao zinafichua ghaibu.

Ibn Al-Arabi, katika Futuhatil- makkiya mlango wa 302, anasema: "Hakika watu wa Mwenyezi Mungu wana macho wanayoonea na masikio wanayosikizia na nyoyo wanazofahamia na ndimi wanazosemea; si macho haya wala masikio au nyoyo na ndimi hizi. Kwa macho hayo wanaona na kwa masikio hayo wanasikia na kwa nyoyo hizo wanafahamu na kwa ndimi hizo wanasema na maneno yao yanapatia"

Naye ndiye mwenye hekima mwenye habari.

Yeye tu peke yake hana mshirika katika kupangilia mamabo ya viumbe vyake kulingana na heima yake na katika kujua siri zote. Basi hebu naamuogope Mwenyezi Mungu yule anayedai kuwa ana nyoyo mbili, ndimi mbili, macho mane na masikio mane.

﴿وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ لِأَبِيهِ آزَرَ أَتَتَّخِذُ أَصْنَامًا آلِهَةً إِنِّي أَرَاكَ وَقَوْمَكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ﴾

74.Na Ibrahim alipomwambia baba yake Azar: Unawafanya masanamu kuwa waungu? Hakika ninakuona wewe na watu wako mko katika upotofu ulio wazi.

﴿وَكَذَٰلِكَ نُرِي إِبْرَاهِيمَ مَلَكُوتَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَلِيَكُونَ مِنَ الْمُوقِنِينَ﴾

75.Na namna hii tukamwonyesha Ibrahim ufalme wa mbingu na ardhi ili awe katika wenye yakini.

﴿فَلَمَّا جَنَّ عَلَيْهِ اللَّيْلُ رَأَىٰ كَوْكَبًا قَالَ هَـٰذَا رَبِّي فَلَمَّا أَفَلَ قَالَ لَا أُحِبُّ الْآفِلِينَ﴾

76.Na usiku ulipomwingilia, akaona nyota, alinena: Hii ni Mola wangu. Ilipotua akasema: Sipendi wanaotua.

﴿فَلَمَّا رَأَى الْقَمَرَ بَازِغًا قَالَ هَـٰذَا رَبِّي فَلَمَّا أَفَلَ قَالَ لَئِن لَّمْ يَهْدِنِي رَبِّي لَأَكُونَنَّ مِنَ الْقَوْمِ الضَّالِّينَ﴾

77.Na alipouona mwezi unachomoza alisema: Huu ni Mola wangu. Ulipotua alisema: Asiponiongoza Mola wangu, hakika nitakuwa katika watu waliopotea.

﴿فَلَمَّا رَأَى الشَّمْسَ بَازِغَةً قَالَ هَـٰذَا رَبِّي هَـٰذَا أَكْبَرُ فَلَمَّا أَفَلَتْ قَالَ يَا قَوْمِ إِنِّي بَرِيءٌ مِّمَّا تُشْرِكُونَ﴾

78.Na alipoliona jua linachomoza alisema: Hili ndilo Mola wangu. Hili ni kubwa kabisa. Lilipotua alisema: Enyi watu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha.

﴿إِنِّي وَجَّهْتُ وَجْهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ حَنِيفًا وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ﴾

79.Hakika mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Hali ya kuwa nimeacha dini za upotevu, tena mimi si katika washirikina.

IBRAHIM NA BABA YAKE NAWATU WAKE

Aya 74-79

MAANA

Na Ibrahim alipomwambia baba yake Azar: Unawafanya masanamu kuwa waungu? Hakika ninakuona wewe na watu wako mko katika upotofu ulio wazi.

Dhahiri ya Aya inafahamisha waziwazi kuwa Azar ni baba hasa wa Ibrahim Khalil(a.s) ; na kwamba alikuwa mshirikina muabudu masanamu; na kwamba Ibrahim alimkataza ushirikina na akamlingania kwenye Tawhid. Huu ndio ufahamisho wa Aya unaofahamika mara moja kwenye fahamu ya mjuzi na mjinga, bila ya kuweko ufafanuzi au tafsir.

Pamoja na hayo wafasiri wamerefusha maneno na wakatofautiana kuwa je, Azar ni baba hasa wa Ibrahim au ni baba yake kimajazi.

Tofauti hii inazalisha tofauti nyingine kuwa je mababa na mababu wote wa Muhammad(s.a.w.w) waliamini Mungu mmoja na wala haifai kuweko mshirikina hata mmoja, au inawezekana kuweko washirikina na wapwekeshaji? Baadhi ya maulama wametunga vitabu maalum vya hilo tu.

Shia wanasema baba na mababu zake wote Muhammad ni wapwekeshaji Mungu kutokana na Hadith isemayo:"Niliendelea kugura kutoka migongo ya watakatifu mpaka kwenye mifuko ya uzazi ya watakatifu hadi akanitoa Mwenyezi Mungu kwenye ulimwengu wenu huu."

Wakasema kuwa baba hasa wa Ibrahim anaitwa Tarik na kwamba Azar ni ndugu wa baba yake au babu yake wa upande wa mama yake, amepewa jina la baba kimajazi tu[8] .

Al-Alusi anasema, "Kundi kubwa la Sunni pia wanasema hivyo" Lakini mwenye Tafsir Al-manar na Razi wanasema: "Sunni hawaafikiani na Shia kwenye rai yao hii na wanasema inawezekana kuweko washirikina au walahidi katika mababu wa Mtume."

Dhahiri ya Qur'an iko pamoja nao, hasa kauli yake Mwenyezi Mungu:

﴿وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِبْرَاهِيمَ إِنَّهُ كَانَ صِدِّيقًا نَّبِيًّا ﴿٤١﴾ إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ لِمَ تَعْبُدُ مَا لَا يَسْمَعُ وَلَا يُبْصِرُ وَلَا يُغْنِي عَنكَ شَيْئًا﴾

"Na mtaje Ibrahim katika Kitab, Hakika yeye alikuwa mkweli sana, Nabii, Alipomwambia baba yake: Ee baba yangu! Kwa nini unaabudu visivyosikia na visivyoona na visivyokufaa chochote" (19: 41-42)

Kwa vyovyote iwavyo hakuna faida ya mzozo huu, kwa sababu hauna uhusiano wowote na itikadi ya Kiislamu. Kwa sababu linalotakikana kwa Mwislamu ni kuamini Utume wa Muhammad(s.a.w.w) na Isma yake na kwamba yeye ni bwana wa Mitume na ni wa mwisho wao. Ama kuamini kuwa baba na mababu zake wote ni wapwekeshaji Mwenyezi Mungu, na kwamba Azar ni ami wa Ibrahim na sio baba yake, Yote haya si chochote katika itikadi ya Kiislamu.

Na namna hii tukamwonyesha Ibrahim ufalme wa mbingu na ardhi.

Makusudio ya 'namna hii' ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kama ambavyo alimfichulia Ibarahim upotevu wa watu wake wa kuabudu kwao masanamu, pia alimfunulia maajabu ya mbingu na ardhi ili atoe dalili, kwa ustadi wa nidhamu yake na ufundi wa utengenezwaji wake, juu ya kuweko Mwenyezi Mungu, umoja wake na utukufu wake na awe miongoni mwa wenye yakini.

Aya hii inafahamisha mambo mawili:

Kwanza : itikadi ya Uislamu inaismamia uhuru wa rai na akili. Kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuwajibisha mtu kumwamini ila baada ya kumwekea hoja na akataka afanye uchunguzi.

Pili : kuwa dalili aliyoiweka juu ya kuweko kwake ni nyepesi na sahali kufahamiwa na watu wote bila ya kuhitaji juhudi wala sayansi au falsafa. Yatosha mtu kuangalia maajabu ya ulimwengu na utaratibu wake ili aweze kuongoka kwa Muumbaji wake na mtegenezaji wake.

Na usiku ulipomwingilia, akaona nyota, alinena: Hii ni Mola wangu.

Watu wa Ibrahim walikuwa wakiabudu nyota badala ya Mwenyezi Mungu. Akataka kuwavuta kidogo kidogo kwenye haki na kuwaelekeza kwenye mantiki ya kiakili na kimaumbile kwa upole na ulaini. Akangoja mpaka usiku ulipoingia na kufunga giza, akaona nyota wanazoziabudu. Akasema kwa kuigiza madai yao: 'Huyu ni Mola wangu'. Wakamwamini, lakini ilipotua na kupotea pambizoni, akili zao zilizinduka na mtazamo wao ukaona kuwa Mwenyezi Mungu habadiliki wala kugeuka na wala hifichwi na chochote.

Na alipouona mwezi unachomoza alisema kwa kutaka kuwavuta:Huu ni Mola wangu , kwa sababu ni mkubwa na una mwangaza zaidi kuliko ule wa kwanza.

Ulipotua alisema: Asiponiongoza Mola wangu, hakika nitakuwa katika watu waliopotea.

Anaashiria kuwa yeye bado hajatulizwa nafsi yake na nyota hizii; na kwamba yeye bado hajaongoka kwenye njia na akamtaka Mwenyezi Mungu amwokoe.

Na alipoliona jua linachomoza alisema: Hili ndilo Mola wangu. Hili ni kubwa kabisa. Lilipotua alisema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika hayo mnayoyashirikisha.

Jaribio la kwanza, la pili na la tatu yamepita na shaka ikabakia kama ilivyokuwa. Kwa hiyo hapana budi kujiepusha na kuabudu nyota, Kwani hazistahiki kuabuduiwa wala kutukuzwa. Baada ya kutangaza kujitoa katika waungu wao aliuelekeza moyo wake kwa Muumba wa ulimwengu na akasema:

Hakika mimi nimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimeacha dini za upotevu, tena mimi si katika washirikina.

Hii ndiyo natija ya utafiti na kufikiria katika kitu chochote miongoni mwa vitu vya ulimwengu huu. Mtazamo mmoja tu, wa kuangalia sura yoyote katika sura za ulimwengu huu, lazima utapelekea kwenye yakini ya mkato kuwa Mwenyezi Mungu pekee yake ndiye Muumba wa mbingu na ardhi.

﴿وَحَاجَّهُ قَوْمُهُ قَالَ أَتُحَاجُّونِّي فِي اللَّـهِ وَقَدْ هَدَانِ وَلَا أَخَافُ مَا تُشْرِكُونَ بِهِ إِلَّا أَن يَشَاءَ رَبِّي شَيْئًا وَسِعَ رَبِّي كُلَّ شَيْءٍ عِلْمًا أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ﴾

80.Na watu wake wakamhoji. Akasema: Je, mnanihoji juu ya Mwenyezi Mungu na hali yeye ameniongoza? Wala siogopi wale mnaowashirikisha naye; isipokuwa Mola wangu akitaka kitu, Mola wangu ana wasaa wa kujua kila kitu. Je, hamkumbuki.

﴿وَكَيْفَ أَخَافُ مَا أَشْرَكْتُمْ وَلَا تَخَافُونَ أَنَّكُمْ أَشْرَكْتُم بِاللَّـهِ مَا لَمْ يُنَزِّلْ بِهِ عَلَيْكُمْ سُلْطَانًا فَأَيُّ الْفَرِيقَيْنِ أَحَقُّ بِالْأَمْنِ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴾

81.Nitaogopaje hao mnaowashirikisha, na hali nyinyi hamwogopi kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kile ambacho hakukiteremshia dalili kwenu? Basi kundi gani katika mawili haya linastahiki kupata amani kama nyinyi mnajua?

﴿الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ الْأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُونَ﴾

82.Wale walioamini na hawakuchanganya imani yao na upotevu, hao ndio watakaopata amani na ndio walioongoka. 83. Na hiyo ndiyo hoja yetu tuliyompa Ibrahim juu ya watu wake. Tunamuinua kwa vyeo yule tumtakaye, Hakika Mola wako ndiye mwenye hekima, Mjuzi.

JE, MNANIHOJI JUU YA MWENYEZI MUNGU

Aya 80 – 83

LUGHA

Neno 'hoja' linatumika kwa maana ya dalili zenye kuthibitisha haki; na hutumiwa kwa maana yale anayoyatolea hoja mdai kuthibitisha madai yake.

MAANA

Na watu wake wakamhoji.

Baada ya Ibrahim kuwapatia watu wake hoja inayoingia akilini kutokana na mantiki ya kiakili na kimaumbile, na kuthibitisha uharibifu na ibada yao ya mizimu na nyota, baada ya yote hayo nao walileta hoja zao dhaifu. Wakasema miongoni mwa waliyoyasema:

﴿قَالُوا وَجَدْنَا آبَاءَنَا لَهَا عَابِدِينَ﴾

"Tumewakuta baba zetu wakiyaabudu" (21:53)

Ndipo Ibrahim akawajibu kwa kusema:

Je, mnanihoji juu ya Mwenyezi Mungu na hali yeye ameniongoza?

Yaani ni hoja gani hizi kuhusu Mwenyezi Mungu na hali yeye ameniongoza kumjua kutokana na nafsi yangu na ulimwengu. Imetangulia katika sura hii Aya ya 71:

﴿قُلْ إِنَّ هُدَى اللَّـهِ هُوَ الْهُدَىٰ﴾

"Sema: Mwongozo hasa ni mwongozo wa Mwenyezi Mungu" (6:71) Ambao hauna shaka yoyote, vinginevyo ni ujinga na upotevu. Ama kuhofisha waungu wao alikujibu kwa kusema:Wala siogopi wale mnaowashirikisha naye wasiokuwa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu hawadhuru wala hawanufaishi, hawoni wala hawasikii,Isipokuwa Mola wangu akitaka chochote kwa kuniangushia sanamu kichwani kwangu linivunje fuvu, au kimondo cha nyota kitakachoniunguza.

Mola wangu ana wasaa wa kujua kila kitu.

Kwa hiyo siogopi kuwa nitapatwa na jambo lolote baya bila ya kujua yeye au kutaka.

Je, hamkumbuki kuwa miungu yenu si chochote na kwamba Mwenyezi Mungu peke yake ndiye mwenye kudhuru na kunufaisha. Kwa sababu yeye ni Muumbaji wa kila kitu.

Nitaogopaje hao mnaowashirikisha, na hali nyinyi hamwogopi kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kile ambacho hakukiteremshia dalili kwenu?

Makusudio ya mliowashirikisha ni masanamu na nyota mnaoziabudu. Maana nikuwa mnataka niwaogope waungu wenu walioumbwa wanaoshindwa na nyinyi hamwogopi madai yenu ya kumfanyia Mungu washirika, madai ambayo ni uzushi usiokuwa na hoja wala dalili!

Kwa maneno mengine, Ibrahim aliwaambia je, mnanihofisha kwa wale wasiokuwa na uwezo, na nyinyi mmejiamini na kumfanyia uzushi yule mwenye nguvu na uwezo kwa wote?

Basi kundi gani katika mawili haya linastahiki kupata amani kama nyinyi mnajua?

Kundi linalomwamini Mwenyezi Mungu mwenye nguvu, mwenye kushinda, au linaloamini udhaifu ulio dhalili?

Wale walioamini na hawakuchanganya imani yao na upotevu, hao ndio watakaopata amani na ndio walioongoka.

Huu ni ubainifu wa kundi lililookoka katika makundi mawili na kwamba wao ndio waliomfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu katika imani yao na hawakuchanganya na imani hii kushirikisha katika itikadi wala katika kutii hawaa za kiumbe yeyote awaye. Hawa peke yao ndio waliosalimika, wenye kuongoka.

Na hiyo ndiyo hoja yetu tuliyompa Ibrahim juu ya watu wake.

Yaani hizo ndizo hoja ambazo tumemtia ilham Ibrahim , zinazoingia bongoni ambazo aliwahshinda nazo Ibrahim watu wake. Aya hii ni dalili wazi kwamba Mitume na wale wanaoongozwa na mwongozo wao katika maulama, ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ubainifu wake; na kwamba kuwapinga ni kumpinga Mwenyezi Mungu hasa; kama ilivyoelezwa katika Hadith.

Tunamuinua kwa vyeo yule tumtakaye.

Utaipata Tafsir yake katika Juz 28 (58:11.) inshaallah Sababu ya kuinuliwa mtu kwa Mwenyezi Mungu ni imani na elimu, na kila moja katika hayo ina daraja ya juu na ya juu zaidi. Ibrahim alifikia ile ya juu zaidi mpaka akawa rafiki wa Mwenyezi Mungu (Khalilullah).

Hakika Mola wako ndiye mwenye hekima, Mjuzi.

Mwenye hekima aliyetakata na mchezo na matamanio, anajua anayostahiki kila mtu katika daraja na vyeo.

12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿وَوَهَبْنَا لَهُ إِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ كُلًّا هَدَيْنَا وَنُوحًا هَدَيْنَا مِن قَبْلُ وَمِن ذُرِّيَّتِهِ دَاوُودَ وَسُلَيْمَانَ وَأَيُّوبَ وَيُوسُفَ وَمُوسَىٰ وَهَارُونَ وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ﴾

84.Na tukampa Is-haq na Yaqub Kila mmoja tulimuongoza, Na Nuh tulimwongoza zamani. Na katika kizazi chake Daud na Suleiman na Ayyub na Yusuf na Musa na Harun. Na kama hivyo tunawalipa wafanyao mema.

﴿وَزَكَرِيَّا وَيَحْيَىٰ وَعِيسَىٰ وَإِلْيَاسَ كُلٌّ مِّنَ الصَّالِحِينَ﴾

85.Na Zakariya na Yahya na Isa na Ilyas; wote ni katika wema.

﴿وَإِسْمَاعِيلَ وَالْيَسَعَ وَيُونُسَ وَلُوطًا وَكُلًّا فَضَّلْنَا عَلَى الْعَالَمِينَ﴾

86.Na Ismail na Al-yasaa na Yunus na Lut; na kila mmoja tulimfadhilisha juu ya walimwengu wote.

﴿وَمِنْ آبَائِهِمْ وَذُرِّيَّاتِهِمْ وَإِخْوَانِهِمْ وَاجْتَبَيْنَاهُمْ وَهَدَيْنَاهُمْ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴾

87.Na katika baba zao na vizazi vyao na ndugu zao na tukawachagua na kuwaongoza katika njia iliyonyooka.

﴿ذَٰلِكَ هُدَى اللَّـهِ يَهْدِي بِهِ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

88.Huo ni uongozi wa Mwenyezi Mungu, Kwa huo humwongoza amtakaye katika waja wake. Na kama wangelishirikisha bila shaka yangeliporomoka yale waliyokuwa wakiyatenda.

﴿أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ وَالْحُكْمَ وَالنُّبُوَّةَ فَإِن يَكْفُرْ بِهَا هَـٰؤُلَاءِ فَقَدْ وَكَّلْنَا بِهَا قَوْمًا لَّيْسُوا بِهَا بِكَافِرِينَ﴾

89.Hao ndio tuliowapa Kitab na hukumu na utume. Kama hawa wakiyakataa, basi tumekwisha yawakilisha kwa watu wasioyakataa.

﴿أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ هَدَى اللَّـهُ فَبِهُدَاهُمُ اقْتَدِهْ قُل لَّا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْعَالَمِينَ﴾

90.Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaongoza, basi fuata mwongozo wao. Sema: Siwaombi ujira juu ya haya. Haikuwa hiyo ila ni mawaidha kwa waimwengu wote.

NA TUKAMPA IS-HAQ NA YAQ'UB

Aya 84 - 90

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya hizi ametaja Mitume 18 akiwemo Ibrahim, Baadhi akawaashiria kwa baba zao, vizazi vyao na ndugu zao. Na amewasifu wote kwa hisani, wema na uongofu, na kwamba yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu amewaneemesha Mitume waliotajwa kwa hekima na Unabii na baadhi yao akawaneemesha kwa kuteremshiwa Kitab.

Makusudio katika hayo ni kutoa hoja Muhammad(s.a.w.w) kwa Waarabu kwamba babu yao ni Ibrahim na wanawe wengi walikuwa wenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu.

Vilevile Mtume afuate nyayo za Mitume waliotangulia katika kulingania kwa Mwenyezi Mungu na kuvumilia adha. Huu ndio muhtasari wa madhumuni ya Aya hizi saba.

Uko wazi usiohitaji ubainifu wa kurefusha na ufafanuzi, lakini baadhi ya wafasiri wamekataa ila kurefusha, wakatoka nje ya maudhui ya Tafsir kufikia ambako hakuna uhusiano wowote na maisha.

Ni vizuri ifahamike kuwa majina ya Mitume yaliyotajwa katika Aya hayakuja kwa mpangilio wa wakati au ubora; kama ambavyo wametajwa kwa njia ya mifano tu.

Na tukampa Is-haq na Yaqub.

Dhamir ya 'tukampa' inamrudia Ibrahim. Is-haq ni mwanawe wa kumzaa na mama yake ni Sara. Yaqub ni mwana wa Is-haq, na mwana wa mwana ni mwana. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿فَبَشَّرْنَاهَا بِإِسْحَاقَ وَمِن وَرَاءِ إِسْحَاقَ يَعْقُوبَ﴾

"Basi tukambashiria Is-haq na baada ya Is-haq ni Yaqub." (11:71)

Kila mmoja Is-haq na Yaqubtulimuongoza .

Na Nuh tulimwongoza zamani kwani yeye ni wa zamani kuliko Ibrahim.

Na katika kizazi chake.

Dhamir inamrudia Nuh, yaani na kizazi cha Nuh, kwa sababu ndiye wa karibu kutajwa, Imesemekana kuwa inamrudia Ibrahim.

Daud na Suleiman na Ayyub na Yusuf na Musa na Harun.

Yaani wote hawa tumewaongoa kama tulivyomwongoza Nuh, Is-haq na Yaqub.

Na kama hivyo tunawalipa wafanyao mema.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamlipa mwema kwa wema, awe Mtume au sio Mtume; kama anavyomlipa mwovu kwa amali yake awe mweupe au mweusi. Na Zakariya na Yahya na Isa na Ilyas. Hawa vilevile ni katika aliowaongoza Mwenyezi Mungu.

Wote ni katika watu wema.

Na kila mwenye kutumia kipawa chake kwa kheri yake na kheri ya watu basi yeye ni mwema na mtengenevu.

HASAN NA HUSEIN NI WANAWA MTUME

Anasema Razi katika Tafsir yake kuhusu Aya hii: "Hakika Aya hii inafahamisha kuwa Hasan na Hussein ni katika kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) .

Kwa sababu Mwenyezi Mungu amemjaalia Isa ni katika kizazi cha Ibrahim, ingawaje yeye amenasibiana na Ibrahim kwa upande wa mama tu. Vilevile Hasan na Hussein ni katika kizazi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu ingawaje wananasibika na Mtume kwa mama. Inasemekana kuwa Abu Jafar Al-Baqir, aliitolea dalili Aya hii mbele za Hajjaj bin Yusuf."

Mwenye Tafsir Al-Manar anasema: "Ninasema katika mlango wa Hadith Abu Bukra kwa Bukhari, iliyo Marfu'. (Hakika mwanangu, huyu ni Sayyid) yaani Hassan. Na neno mwanangu, kwa Waarabu, halitajwi kwa watoto wa binti. Na Hadith ya Umar katika Kitab Ma'rifatu Sahaba cha Abu Naim, iliyo marfu'; (kuwa kila mtoto wa Adam ukoo wao unatokana na baba yao, isipokuwa watoto wa Fatima, mimi ndiye baba yao na ni ukoo wao). Watu wakazoea haya, wakawa wanasema kuhusu watoto wa Fatima kuwa ni watoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) na ni kizazi chake na Ahlu bait (watu wa nyumbani) wake."

Maana ya maneno haya ni kuwa watoto wa Fatima(a.s) si watoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu kilugha, lakini ni watoto wake kisharia, kutokana na kauli ya Mtume 'mimi ni baba yao na ukoo wao.' Vilevile ni watoto wake kimazoweya, kwa sababu watu walizoweya kuwaita kuwa ni watoto wa mtume.

Wamekongamana kwa kauli moja maulama wa Sunni na Shia kwamba sharia inatangulia ufahamisho wa matamko kimazowea na kilugha; na kwamba mazoea yanaitangulia lugha. Kwa sababu, mwenye hekima huzungumza na watu kwa lile wanalolifahamu haraka sio kwa lile lililoandikwa katika kamusi za lugha.

Likija neno katika Aya au Hadith, na tukakuta Tafsir maalum ya maana yake katika Qur'an au Hadith, basi tamko hilo litachukuliwa katika maana haya maalum; na huitwa maana ya kisharia na kupuuzwa ile ya kilugha na kimazoea. Ikiwa hatukupata maana maalum, basi tutalichukulia kwa maana wanayoifahamu watu; na huitwa maana ya mazoea. Wakitolifahamu watu kwa maana hayo, basi itachukuliwa maana yake kutoka kwenye kamusi za lugha.

Kwa hiyo basi maana ya sharia yanakuwa katika ngazi ya kwanza, ya mazoea katika ngazi ya pili na ya kilugha katika ngazi ya tatu. Na imethibiti kisharia na kimazoea kuwa Hassan na Hussein ni watoto wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, Hivyo ikapuuzwa maana ya kilugha. Kwa sababu lugha inahukumiwa na sharia na mazoea.

Ama siri ya kuwa Hasan na Husein ni wana wa Mtume ingawaje si wanawe kilugha, ataipata mpekuzi katika sifa za hao wawili na hulka zao. Inamtosha mwenye kufanya utafiti wa sera ya Hasan kuwa Muawiya bin Abu Sufian hakupata wasaa wa Ufalme aliokuwa nao na huku Hassan bado yu hai. Na inamtosha mwenye kutafiti sera ya Hussein kwamba Yazid bin Muawiya dunia ilimzonga kwa kuweko Husein, kama ilivyomzonga baba yake, Muawiya kwa kuweko Hasan.

Na Ismail na Al-yasaa na Yunus na Lut , Vilevile tuliwaongoa.

Na kila mmoja tulimfadhilisha juu ya walimwengu wote katika zama zake.

Na katika baba zao na vizazi vyao na ndugu zao.

'Katika' hapa ni ya kubaadhisha; yaani baadhi yao Kwa sababu katika vizazi vyao na ndugu zao walikuwako makafiri; bali Isa na Yahya hawakuwa na kizazi.

Na tukawachagua na kuwaongoza katika njia iliyonyooka.

Sifa hizi ni utanguluzi wa kauli yake Mwenyezi Mungu:

Huo ni uongozi wa Mwenyezi Mungu, Kwa huo humwongoza amtakaye katika waja wake.

Yaani uongozi ambao ni wajibu kufuata ni ule waliokuja nao Mitume, wala hafuati mwongozo huu ila aliyepewa tawfiki na Mwenyezi Mungu.

Na kama wangeshirikisha, bila shaka yangeliporomoka yale waliyokuwa wakiyatenda.

Yaani hawa Mitume pamoja na ubora wao na utukufu wao wa vyeo, lau ingelitokea kufanya chembe ya kitu inayofahamisha shirk, basi bila shaka yangelibatilika yale waliyokuwa wakiyatenda na kuwa ni bure tu.

Lengo la ishara hii ni kuzindua kuwa Mwenyezi Mungu atawafanyia watu kulingana na amali zao si kulingana na vyeo vyao, na kwa watakavyoishilia wanapokufa, si kwa walivyoanzia uhai wao.

Hao ndio tuliowapa Kitab na hukumu na utume.

Hao, ni wale Mitume waliotangulia kutajwa. Na Kitab, ni jinsi ya Kitab inayochanganya vitabu vyote vya Mwenyezi Mungu vilivyoitangulia Qur'an, kama vile Mbao za Ibrahim, Tawrat, Zabur na Injil. Makusudio ya 'Hukumu' ni kujua kuhukumu na kila lile aliloliwekea sharia Mwenyezi Mungu katika halali na haramu.

Kama hawa wakiyakataa, basi tumekwisha yawakilisha kwa watu wasioyakataa.

Hawa, ni washirikina wa Kiquraish ambao wameukana Utume wa Muhammad(s.a.w.w) na kumfanyia uadui. Wanayoyakataa ni Utume. Makusudio ya watu ambao hawayakanushi ni Muhajirina na Ansari[9] ambao walimwamini Muhammad na wakamsaidia.

Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaongoza, basi fuata mwongozo wao.

Hao wanaotajwa hapa ni Mitume waliotangulia kutajwa. Mwenyezi Mungu amemwamrisha Mtume wake mtukufu kufuata nyao zao katika kuilingania haki na kuvumilia adha katika njia yake.

Sema: Siwaombi ujira juu ya haya.

Kwa sababu dini haikuwekwa kuwa ni chumo na biashara.

Haikuwa hiyo ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.

Dhamir ya hiyo ni Qur'an. Maneno haya ni dalili wazi kuwa Muhammad ametumwa kwa watu, wakati wote na mahali pote.

﴿وَمَا قَدَرُوا اللَّـهَ حَقَّ قَدْرِهِ إِذْ قَالُوا مَا أَنزَلَ اللَّـهُ عَلَىٰ بَشَرٍ مِّن شَيْءٍ قُلْ مَنْ أَنزَلَ الْكِتَابَ الَّذِي جَاءَ بِهِ مُوسَىٰ نُورًا وَهُدًى لِّلنَّاسِ تَجْعَلُونَهُ قَرَاطِيسَ تُبْدُونَهَا وَتُخْفُونَ كَثِيرًا وَعُلِّمْتُم مَّا لَمْ تَعْلَمُوا أَنتُمْ وَلَا آبَاؤُكُمْ قُلِ اللَّـهُ ثُمَّ ذَرْهُمْ فِي خَوْضِهِمْ يَلْعَبُونَ﴾

91.Na hawakumkadiria Mwenyezi Mungu kwa haki ya kadri yake, waliposema: Mwenyezi Mungu hakuteremshia chochote juu ya binadamu yoyote. Sema: nani aliyekileta Kitab alichokuja nacho Musa chenye nuru na mwongozo kwa watu? Mlichokifanya nyaraka- nyaraka, mkizidhihirisha na mkificha mengi, Na mkafundishwa msiyoyajua nyinyi wala baba zenu. Sema: Ni Mwenyezi Mungu, Kisha waache wacheze katika porojo zao.

﴿وَهَـٰذَا كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ مُّصَدِّقُ الَّذِي بَيْنَ يَدَيْهِ وَلِتُنذِرَ أُمَّ الْقُرَىٰ وَمَنْ حَوْلَهَا وَالَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ يُؤْمِنُونَ بِهِ وَهُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ﴾

92.Na hiki ni kitab tulichokiteremsha, kilichobarikiwa, chenye kusadikisha yale yaliyokitangulia. Na ili uwaonye (watu wa) Ummul qura na walio pambizoni mwake. Na wale wanaoamini akhera, wanakiamini, Nao huzihifadhi Swala zao.

HAWAMHESHIMU MWENYEZI MUNGU KAMA INAVYOTAKIWA

Aya 91 - 92

MAANA

Na hawakumkadiria Mwenyezi Mungu kwa haki ya kadiri yake, waliposema: Mwenyezi Mungu hakuteremshia binadamu chochote.

Aya hii inafahamisha kuwa katika wakati wa Mtume wa Mwenyezi Mungu kulikuwa na watu wanaokanusha wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa mtu yoyote, na wakisema kuwa Mwenyezi Mungu hakumtuma mtu yeyote kuwa mjumbe.

Lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakubainisha ni akina nani waliokanusha na kusema hivyo, Kwa ajili hii waliotofautiana wafasiri, kuhusu waliokusudiwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu. Je, ni washirikina wa Kiarabu au Mayahudi wa Hijaz?

Kuna kundi la wafasiri waliosema kuwa ni washirikina wa Kiarabu. Kauli hii inapingwa, kwanza kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwamrisha Mtume wake kuwakabili na swali hili:

Sema: Ni nani aliyekileta Kitab alichokuja nacho Musa chenye nuru na mwongozo kwa watu?

Kimsingi ni kuwa swali hili linaelekezwa kwa yule anayekubali Utume wa Musa na Tawrat; na yajulikana kuwa washirikina wa Kiarabu hawakubali Utume wa Musa na Tawrat yake; vinginevyo wangelikuwa ni katika watu wa Kitab.

Pili, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewatahayariza wakanushaji kwa kauli yake:

Mlichokifanya nyaraka-nyaraka, mkizidhihirisha na mkificha mengi.

Yaani kuwa nyinyi mmeibadilisha Tawrat, mkadhihirisha yale yanayoafikiana na hawaa zenu na mkaficha yale yasiyoafikiana nayo. Inajulikana kuwa walioibadilisha Tawrat ni Mayahudi, sio washirikina wa Kiarabu.

Kundi jingine la wafasiri limesema kwamba waliosema kuwa Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote kwa mtu, ni Mayahudi. Wakatoa dalili kwa mambo mawili: Kuwa Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake Muhammad amjibu anayesema hivi kwa Utume wa Musa na Tawrat, nalo ni jibu sahihi, kisha akatilia mkazo jibu hili kwa kuipotosha kwao Tawrat akasema: "Mlichokifanya nyaraka-nyaraka."

Kauli hii iko karibu na dhahiri ya Aya kuliko ile ya kwanza.

Na mkafundishwa msiyoyajua nyinyi wala baba zenu.

Msemo huu unaelekezwa kwa Mayahudi vilevile; na maana yake ni, vipi mnasema - Enyi Mayahudi - kuwa Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote kwa mtu yeyote na hali nyinyi mnaitakidi kwamba Musa ni mwanadamu na kwamba Tawrat imeteremshwa kwake? Na mmejua kutokana nayo yale mliyokuwa hamyajui nyinyi na baba zenu.

Miongoni mwayo ni kuwa nyinyi mlikuwa mkisoma katika Tawrat sifa za Muhammad kabla ya kutumwa kwake, wala hamkuwa mkimjua kwa ufafanuzi aliyekusudiwa. Mwenyezi Mungu alipomtuma na mkamjua aliyekusudiwa hasa, kwa kiburi na inadi yenu mkageuza na kuondosha yale yanayomwelezea.

Sema: Ni Mwenyezi Mungu.

Hili ni jawabu la swali lililotangulia (Sema: Ni nani aliyeteremsha Kitab alichokuja nacho Musa?

Jibu : hili ndilo lenyewe hasa na halikimbiliki. Kwa sababu Mayahudi wanakiri kuwa Tawrat inatoka kwa Mwenyezi Mungu. Na kwa ajili ya kukiri kwao huku ndio inawasimamia hoja na kuwajibu kauli yao ya kuwa Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote kwa mtu.

Kisha waache wacheze katika porojo zao.

Yaani sema haki Ewe Muhammad, na waache Mayahudi katika batili zao wala usijishughulishe na inadi zao na ria zao.

Huku ni kuwapa onyo na kuwapa kiaga, kama ambavyo pia ni kuwadharau na kuwapuuza.

Utauliza : Mayahudi wanaukubali Utume wa Musa(a.s) na kuteremshwa Tawrat, kama yalivyotangulia maelezo. Kwa hiyo imekuwaje Mwenyezi Mungu akawanasibishia kukanusha wahyi na Utume?

Jibu : Wao wanakanusha wahyi na Utume kwa dhahiri, kwa inadi na kiburi kwa Muhammad(s.a.w.w) na si kwa undani hasa.

﴿وَجَحَدُوا بِهَا وَاسْتَيْقَنَتْهَا أَنفُسُهُمْ ظُلْمًا وَعُلُوًّا﴾

"Na wakazikakataa kwa dhuluma na kujivuna, na hali ya kuwa nafsi zao zina yakini nazo" (27:14)

MITUME WA MWENYEZI MUNGU NA WANASAYANSI

Wanasayansi wengi wakati huu wanaamini kuweko Mwenyezi Mungu, Kwa sababu wameona kuwa ulimwengu huu unakwenda kulingana na kanuni thabiti, na iliyowazi inayohukumu, haiepukani nao kwa hali yoyote ile.

Kwa ajili hii imewezekana kuichunguza, kuikisia na kufaidika nayo. Huku ni kuthibitika kuweko nguvu ya hali ya juu nyuma ya ulimwengu inayofanya uhandisi na kujenga; na nguvu hiyo ndio Mwenyezi Mungu.

Kwa maneno mengine, si lazima mtu akitaka kujua kuweko kila kitu afanye majaribio katika vyombo na kukiona kwa macho, bali inatosha kwa kujua kwa elimu isiyo na shaka na dhana, ni sawa elimu hiyo iwe imetokana na majaribio na macho au imetokana na natija ya akili ya kiasili. Mwenye fikira na uchunguzi akitaamali ulimwnengu huu kwa taamuli ya kielimu isiyo na shaka shaka, lazima atakomea kwenye kumjua Mwenyezi Mungu.

Lakini Wanasayansi waliojua kuweko Mwenyezi Mungu kwa Kisayansi, wamekanusha kuwa ana wajumbe katika watu anaowapa wahyi na wakasema: Nguvu-asili (nature) peke yake ndio Kitab cha Mwenyezi Mungu na wala sio Tawrat, Injil na Qur'an.

Sina shaka kwamba wataalam hawa, lau wangelipa somo la Qur'an wakati mdogo tu katika muda ule ule walioutoa kwa kusoma sayansi wangelikinai kuwa Mwenyezi Mungu ana vitabu viwili: Ulimwengu na wahyi, Na kwamba mtu anavihitajia vyote viwili.

Kutokana na Kitab cha ulimwengu atajua Ufalme wa Mwenyezi Mungu na kumwamini. Na kutokana na Kitab cha wahyi atajua sharia ya Mwenyezi Mungu ambayo itamwangazia njia ya maisha, kusonga mbele na kujiepusha na maangamizo na matatizo ambayo yatachelewesha safari yake ya kwenda mbele.

Mtu ameumbwa ili afanye kazi katika maisha haya, kwa hivyo basi, hapana budi kwa kila anayefanya amali kuwa na njia anayoifuata katika kufanya kazi, Kwa sababu kujifanyia mambo ovyo ovyo hakupelekei kheri yoyote. Na Mwenyezi Mungu ndiye aliyememuumba mtu, anajua siri yake na dhahiri yake, nguvu yake na udhaifu wake na yale yanayomnufaisha na kumdhuru.

Kwa hiyo basi ni lazima kuwa yeye ndiye marejeo ya kwanza ya njia ambayo inapasa mtu kuifuata katika kazi yake; sawa na ilivyo kwa mgunduzi wa ndege na gari na mengineyo; ambapo inakuwa lazima kumrejea yeye katika kutaka kuitumia na kufaidika nayo. Kwa sababu yeye ndiye Ayajuae zaidi masilahi ya ndege na madhara yake.

Hakuna mwenye shaka kwamba kuifikisha njia ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake na kuwafahamisha kunafungika na Mitume na Manabii, kwa sababu wao ndio lugha ya Mwenyezi Mungu na ubainifu wake. Huu ndio wahyi hasa.

Anayetaka ufafanuzi na arejee kitab chetu Al-Islam wal-aql (Uislamu na akili) sehemu ya Utume na akili.

Na hiki ni kitab tulichokiteremsha, kilichobarikiwa, chenye kusadikisha yale yaliyokitangulia.

Hii, ni Qur'an Tukufu; na maana ni kuwa kama tulivyoteremsha Tawrat kwa Musa, Vilevile tumeiteremsha hii Qur'an Kwa Muhammad(s.a.w.w) nayo ina manufaa na faida nyingi kwa anayejua hukumu zake na siri zake na akazitumia.

Nayo Vilevile inasadikisha vitabu vya Mwenyezi Mungu ambavyo vimeteremshiwa Mitume wa Mwenyezi Mungu tangu zamani. Imam Ali anasema: "Jifundisheni Qur'an kwani hiyo ni mazungumuzo mazuri, na ifahamuni kwani hiyo ni utuvu wa nyoyo, na ifanyeni dawa kwa nuru yake kwani hiyo ni ponyo la nyoyo, na isomeni vizuri kwani hiyo ina visa vizuri."

Na ili uwaonye (watu wa) Ummul qura na walio pambizoni mwake.

Ummul-qura (Mama wa miji) ni Makka. Imeitwa hivyo kwa sababu mna nyumba ya kwanza iliyowekwa kwa ajili ya watu kumwabudu Mwenyezi Mungu.

Wastashriki (Wataalamu wa kimagharibi juu ya mambo ya uislamu) na kabla yao Mayahudi walidai kuwa Muhammad(s.a.w.w) ametumwa kwa Waarabu tu, kwa kutolea hoja Aya hii, na kusahau Aya nyingine; kama vile:

﴿وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا رَحْمَةً لِّلْعَالَمِينَ﴾

"Na hatukukutuma ila uwe ni rehema kwa walimwengu wote" (21:107)

﴿وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ﴾

"Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mbashiri na muonyaji; lakini watu wengi hawajui" (34:28)

Wamejitia purukushani na Aya hizo na hali chimbuko la Qur'an ni moja. maneno yake yanajifasiri hayo yenyewe na Aya mbili hizi ni ubainifu wa kauli yake Mwenyezi Mungu: 'Na ili uwaonye (watu wa) Ummul qura na walio pembezoni mwake.'

Na Vilevile makusudio yake ni kuanza mwito wa Uislam, mwanzo kabisa, katika mji wa mwenye mwito huo; yaani Makka.

Mpaka utakapopata wafuasi ndipo uwape bishara walio kando kando yake; kama vile mwito wowote unavyoanza, ambapo unazaliwa kisha unatembea mabara yote.

Zaidi ya hayo imethibiti riwya kwa njia ya Mutawatir kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) aliwaandikia Wafalme na viongozi wote akiwalingania kwenye Uislamu, miongoni mwao ni Mfalme Kisra wa Fursi (Iran) na Kaizari wa Roma. Wastashriki wanajua hayo, lakini baadhi yao wanaficha wanayoyajua.

Na wale wanaoamini akhera, wanakiamini.

Dhamiri ya wanakiamini inarudia Kitabu ambacho ni Qur'an. Yeyote atakayeisoma Qur'an kwa uchunguzi na kuzingatia maana hutoka na kitu. Akiwa anamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, basi huzidi imani, na akiwa anamwamini Mwenyezi Mungu tu, basi ataamini wahyi na ufufuo; akiwa anamwamini Mwenyezi Mungu na ufufuo bila wahyi, basi ataamini Mitume na vitabu vya Mwenyezi Mungu, na hasa Utume wa Muhammad na Qur'an.

Akiwa anamkanusha Mwenyezi Mungu atamwamini; Kwa sababu Qur'an itamwonyesha dalili za hilo na kumhimiza kuichunguza. Nayo kwa asili yake humpeleka mtafiti, anayechunga haki, kwenye elimu.

Nao huzihifadhi Swala zao.

Ili daima wawe na mawasiliano ya kutegemewa na Mwenyezi Mungu. Ameihusisha kutaja Swala kinyume cha ibada nyinginezo kwa sababu ndiyo nguzo kubwa ya dini na inayodumisha imani. Miongoni mwa kazi za swala ni kumkataza mwenye kuswali uovu na mambo mabaya.

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ يَعْرِفُونَهُ كَمَا يَعْرِفُونَ أَبْنَاءَهُمُ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ﴾

20.Wale tuliowapa Kitab wanamjua kama wanavyowajua wana wao, Wale ambao wamezitia hasarani nafsi zao hawaamini.

﴿وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا أَوْ كَذَّبَ بِآيَاتِهِ إِنَّهُ لَا يُفْلِحُ الظَّالِمُونَ﴾

21.Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule amzuliaye Mwenyezi Mungu uwongo, Au azikadhibishaye ishara zake? Hakika madhalimu hawatafaulu.

﴿وَيَوْمَ نَحْشُرُهُمْ جَمِيعًا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشْرَكُوا أَيْنَ شُرَكَاؤُكُمُ الَّذِينَ كُنتُمْ تَزْعُمُونَ﴾

22.Na siku tutakapowakusanya wote, kisha tutawaaambia wale walioshirikisha: Wako wapi washirikishwa wenu mliokuwa mnadai?

﴿ثُمَّ لَمْ تَكُن فِتْنَتُهُمْ إِلَّا أَن قَالُوا وَاللَّـهِ رَبِّنَا مَا كُنَّا مُشْرِكِينَ﴾

23.Kisha hautakuwa udhuru wao ila kusema Wallahi, Mola wetu! Hatukuwa washirikina.

﴿انظُرْ كَيْفَ كَذَبُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَضَلَّ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَفْتَرُونَ﴾

24.Angalia jinsi wanavyojisemea uwongo wenyewe, Na yamepotea waliyokuwa wakiyazua.

WANAMFAHAMU KAMAWANAVYO WAFAHAMU WANAWAO

Aya ya 20 - 24

MAANA

Wale tuliowapa Kitab wanamjua kama wanavyowajua wana wao. Waliopewa Kitab ni Mayahudi na Wakristo, Dhamiri ya wanamjua inamrudia Muhammad(s.a.w.w) . Aya hii inawakabili maulama wa watu wa Kitab kwamba wao wanamjua vizuri Mtume wa mwisho, kama wanavyowajua wana wao, lakini wao wanaficha yale wanayoyajua. Maana haya yamekaririka katika Aya kadhaa, zikiwemo hizi zifuatazo:

﴿الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الرَّسُولَ النَّبِيَّ الْأُمِّيَّ الَّذِي يَجِدُونَهُ مَكْتُوبًا عِندَهُمْ فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ﴾

"Ambao wanamfuata Nabii asiyesoma wala kuandika ambaye wanamwona ameandikwa kwao katika Tawrat na Injil" (7:157)

﴿أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ﴾

Je, haikuwa ishara kwao kwamba wanayajua haya maulama wa wana wa Israil? (26:197)

Yamekwishapita maelezo kwa ufafanuzi katika Juz. 2 (2:146) na Juz. 4 (4:164). Si lazima kwa watu wa Kitab, katika kuujua ukweli wa Muhammad(s.a.w.w) , wakute jina lake limeandikwa kwao katika Tawrat na Injil. Kila mwenye kuusoma Uislamu kwa somo sawa sawa na upekuzi, ataamini kwa imani isiyokuwa na tashwishi yoyote kwamba Uislamu ni haki na ukweli.

Na mawili hayo (haki na ukweli) ndiyo johari za Uislamu, nguzo yake na lengo lake kutokana na neno Lailaha illa Ilah (Hakuna Mungu isipokuwa Allah) ambalo linamaanisha usawa baina ya watu, kumpa mtu msimamo wa misingi ya kufanya amali na ikhlasi na wala sio kwa misingi ya mali, jaha na nasabu. Na vilevile mshikamano na majukumu ya kila kiongozi kwa wachini wake katika mwito wa amani na usalama, maendeleo na utulivu usiokuwa na mwisho.

Wale ambao wamezitia hasarani nafsi zao hawaamini.

Imepita, punde tu Tafsir yake katika Aya 12 ya Sura hii.

Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule amzuliaye Mwenyezi Mungu uwongo.

Makusudio ya dhulma hapa ni Ukafiri. Kwa sababu kila anayemzulia Mwenyezi Mungu uwongo, basi yeye ni kafiri. Hakuna tofauti yoyote baina ya anayemshirikisha na yule mwenye kugeuza hukumu yoyote katika hukumu zake kwa makusudi na kujua; na yule mwenye kudai unaibu wa maasum au kuwaombea viumbe haki, na hali anajua kuwa yeye ni mzushi na mwongo. Wote hawa ni makafiri waovu kwa Ijmai (kongamano), Kitab na Hadith.

Au azikadhibishaye ishara zake? Hakika madhalimu hawatafaulu.

Jumla iliyotangulia imeashiria yule anayeleta yasiyokuwepo; kama mwenye kumfanyia Mwenyezi Mungu washirika au mtoto. Na jumla hii inaashiria yule mwenye kukanusha vilivyopo, kama vile anayemkana

Mwenyezi Mungu kabisa. Hukumu ya wote wawili ni moja, kila mmoja wao ni dhalimu:

﴿مَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ حَمِيمٍ وَلَا شَفِيعٍ يُطَاعُ﴾

"Madhalimu hawana rafiki mpenzi wala muombezi anayetiiwa" (40:18) "Na siku tutakapowakusanya wote, kisha tutawaambia wale walioshirikisha: Wako wapi washirikishwa wenu mliokuwa mnadai" Wanaomwamini Mwenyezi Mungu wako aina mbili: Kuna wale wanaoamini uungu wake na kuwa ni mmoja tu. Hawa wanaitwa wanaompwekesha Mungu (watu wa Tawhid). Na kuna wale wanaoamini uungu wake na uungu mwingine. Hawa ndio wale walioharibu imani yao kwa mchanganyiko huu; na wakawa sawa na wale wanaomkana Mwenyezi Mungu. Kwa sababu kumjaalia Mwenyezi Mungu mfano maana yake hasa ni kumkana Mwenyezi Mungu kabisa. Kwani ilivyo nikuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hana mshabaha wala mfano:

"Hakuna kama mfano wake kitu chochote." (42:11)

Mwenyezi Mungu atawakabili washirikina na swali hili (wako wapi washirikishwa mliokuwa mnadai na mkiwataka msaada, kama mnavyomtaka msaada Mwenyezi Mungu) kwa njia ya kutahayariza na kukaripia, na wala sio kwa njia ya kuhakikisha.

Unaweza kuuliza : kwa nini Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema wako wapi washirikishwa wenu na wala hakusema wako wapi washirikishwa wangu, pamoja na kuwa makafiri ndiyo waliosema kuwa Mungu ana washirika na sio wao?

Jibu : Ni kwa kuwa wao ndiyo wako karibu zaidi na mnasaba huo; kwani wao ndio waliozusha ushirikina ambao hauna athari kabisa.

Kisha hautakuwa udhuru wao ila kusema Wallahi, Mola wetu! Hatukuwa washirikina.

Makusudio ya udhuru wao ni udhuru wao wa kushirikisha na kuabudu mizimu. Maana ni kuwa mwisho wa ushirikina waliozusha ni kiapo chao cha uovu kwamba wao hawakuwa washirikina.

Unaweza kuuliza : Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwasimulia watu hao: 'Wallahi Mola wetu! Hatukuwa washirikina' inapingana na kauli yake yake."Wala hawatamficha Mwenyezi Mungu na mazungumzo (yao)" (4:42)

Zaidi ya hayo ni kuwa inajulikana kuwa mtu hawezi kusema uongo Siku ya Kiyama.

Jibu : Katika Kiyama kutakuwa na vituo kadhaa, baadhi yake mtu ataweza kukana na ambapo katika kituo hicho miguu yake na mikono yake haitamtolea ushahidi wa yale aliyokuwa akiyafanya. Kwenye kituo hicho ndipo huchukuliwa kauli yake Mwenyezi Mungu: 'Wallahi Mola wetu! Hatukuwa washirikina' Na katika kituo kingine, atakiri ambapo hapatakuwa na nafasi ya kukana. Hapo ndipo huchukuliwa kauli yake Mwenyezi Mungu: "Wala hawataweza kumficha Mwenyei Mungu neno lolote" Ama kauli ya kuwa mtu atashindwa kabisa kusema uwongo siku ya Kiyama, inakanushwa na Aya isemayo:

﴿يَوْمَ يَبْعَثُهُمُ اللَّـهُ جَمِيعًا فَيَحْلِفُونَ لَهُ كَمَا يَحْلِفُونَ لَكُمْ وَيَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ عَلَىٰ شَيْءٍ أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ الْكَاذِبُونَ﴾

"Siku atakayowafufua Mwenyezi Mungu wote; wamuapie kama wanavyoapa kwenu, na watadhani kwamba wamepata kitu. Kwa hakika hao ndio waongo hasa" (58: 18)

Swali la pili linatokana na jibu la swali la kwanza nalo ni kuwa: ikiwa mtu ataweza kusema uwongo kesho, bali hata kuapa, kama ilivyo katika maisha haya ya duniani. Basi kuna wajihi gani kuita akhera nyumba ya ukweli na kuiita nyumba yetu hii (dunia) nyumba ya uwongo?

Jibu : Makusudio ya kutofautisha huku ni kwamba uwongo hapa duniani unaweza ukamletea mtu manufaa au kumkinga na madhara, Ama huko akhera hautafaa chochote. Kwa maneno mengine, kushindwa kusema uwongo, ni kitu kingine na kuweza kusema bila ya manufaa ni kitu kingine.

Angalia jinsi wanavyojisemea uwongo wenyewe.

Msemo unaelekezwa kwa Mtume(s.a.w.w) na makusudio yake ni kwa wote, nako ni kusataajabu kutokana na kukana kwao ushirikina na hali wamekufa juu ya ushirikina. Kila mwenye kukana jambo alilonalo au kudai asiyokuwa nayo kwa makusudi, basi amejidaganya mwenyewe, Mwenyezi Mungu na watu:

Na yamepotea waliyokuwa wakiyazua.

Hiyo inaungana na 'wanavyojisemea uwongo.' Maana yake ni angalia Ewe Muhammad vipi yamewapotea washirikina yale waliyokuwa wakiyatarajia kuwa yatawasaidia na kuwaombea.

﴿وَمِنْهُم مَّن يَسْتَمِعُ إِلَيْكَ وَجَعَلْنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ أَكِنَّةً أَن يَفْقَهُوهُ وَفِي آذَانِهِمْ وَقْرًا وَإِن يَرَوْا كُلَّ آيَةٍ لَّا يُؤْمِنُوا بِهَا حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوكَ يُجَادِلُونَكَ يَقُولُ الَّذِينَ كَفَرُوا إِنْ هَـٰذَا إِلَّا أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ﴾

25.Na miongoni mwao wako wanaokusikiliza, na tumezitia pazia nyoyo zao wasije kuyafahamu na mna uziwi masikioni mwao, Na wakiona kila Ishara hawaiamini. Hata wakikujia kujadaliana nawe wanasema waliokufuru: Hizi si chochote isipokuwa ni ngano za watu wa kale.

﴿وَهُمْ يَنْهَوْنَ عَنْهُ وَيَنْأَوْنَ عَنْهُ وَإِن يُهْلِكُونَ إِلَّا أَنفُسَهُمْ وَمَا يَشْعُرُونَ﴾

26.Nao wanamkatazia na wenyewe wanajitenga naye. Na hawaangamizi ila nafsi zao na hawatambui.

NYOYO ZAO ZINA PAZIA

Aya 25 - 26

MAANA

Na miongoni mwao wako wanaokusikiliza, na tumezitia pazia nyoyo zao wasije kuyafahamu na mna uziwi masikioni mwao.

Mwenyezi Mungu anamwambia Mtume wake katika Aya hii, baada ya kumwamrisha kuwambia hoja zinazowasimamia, Maana ni kuwa kundi katika hawa wapinzani wanamsikiliza Mtume, nao wanasoma Qur'an, lakini wao hawanufaiki nayo wala hawanufaiki na dalili na hoja nyingine- zo.

Kwa sababu wao tangu mwanzo waling'anga'ania inadi na kiburi, mpaka kung'angania huko kukapofua akili zao zisione haki na kukatia uziwi kwenye masikio yao.

Unaweza kuuliza : Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu ndiye aliyezipofua nyoyo zao akatia uziwi masikio yao. Kwa nini basi wastahiki shutuma na adhabu na hali ya kuwa wamelazimishwa hawana hiyari?

ibu: Kwa vile nyoyo za wapinzani hazikuitambua Qur'an na kunufaika nayo, na masikio yao hayakuisikiliza kwa usikizi wa kufahamu na kuzingatia, imesihi kusema, kimajazi, kwamba nyoyo zao zimefumba na katika masikio yao mna uziwi.

Na kwa vile Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye aliyeumba nyoyo na masikio, imesihi kunasibisha upofu na uziwi kwake yeye kimajazi vilevile.

Ama kulingana na hali halisi ilivyo ni kuwa washirikina ndio wenye jukumu. Kwa sababu wao waliipinga haki kwa kutaka wenyewe. Yamekwishatangulia maelezo ya hayo katika Juz. 1(2:7)

Ni vizuri kuashiria kuwa Aya hii inafahamisha kwa uwazi kwamba Uislam hauna mfano na chochote kwa ulivyo; bali kwa natija zake na athari zake. Kwa hiyo usikizi na uoni ni utekelezaji wa akili, na akili ndiyo inayopanga matendo. Ikiwa kitendo hakikufanyika, basi usikizi na uoni utakuwa hauna maana yoyote; kwa dhahiri au si kwa dhahiri.

Kwa maneno mengine katika Uislamu, mambo yote ya ndani na ya nje, na ya ardhini na ya angani ni nyenzo za manufaa ya watu katika kupangilia maisha yao na kutatua matatizo yao.

Imam Ali(a.s) anasema:"Anadai kwamba yeye anamtaraji Mwenyezi Mungu. Amesema uwongo kwa nini matarajio yake hayaonekani katika vitendo vyake, na kila mwenye kutarajia (Mwenyezi Mungu) hujulikana matarajio yake katika vitendo vyake."

Na wakiona kila Ishara hawaiamini.

Muhammad(s.a.w.w) alifichua hakika ya waongo katika watu wapendao mali na jaha. Wakataharuki na kuhisi hatari ya masilahi yao wakakimbilia kukadhibisha na wakasema kuhusu Aya za Mwenyezi Mungu kuwa ni ngano za watu wa kale, na hali wao wana yakini kwamba Qur'an hii ni mwongozo, lakini wakawa wanaitia njia za shaka shaka na makosa ili wawatumie watu kutokana na upotevu wao na ubatilifu; sawa na wanavyofanya leo watu wa serikali ovu na kanuni za dhuluma.

Na wanamkatazia na wenyewe wanajitenga naye.

Dhamiri ya neno nao inawarudia wale waliopinga haki kwa kupupia masilahi yao. Dhamiri ya wanamkatazia na kujiweka mbali naye, inamrudia Muhammad(s.a.w.w) .

Waongo walikataza watu wasimfuate Muhammad(s.a.w.w) na wakampinga, vilevile walijaribu kumtesa na wakakusanya majeshi kwa ajili ya kumpiga vita. Si kwa lolote ila ni kwamba yeye amefichua mabaya yao.

Na hawaangamizi ila nafsi zao na hawatambui.

Walitaka kuufanyia vitimbi Uislamu na Mtume wake, balaa ikawafikia wao, walipoangamia baadhi yao siku ya Badr wengine wakajisalimisha wakiwa madhalili na wanyonge siku ya kutekwa Makka. Huu ndio mwisho wa kila mwenye kuzama na kung'ang'ania dhuluma na inadi.

﴿وَلَوْ تَرَىٰ إِذْ وُقِفُوا عَلَى النَّارِ فَقَالُوا يَا لَيْتَنَا نُرَدُّ وَلَا نُكَذِّبَ بِآيَاتِ رَبِّنَا وَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ﴾

27.Na ungeliona watakapoonyeshwa moto wakawa wanasema. Laiti tungerudishwa (duniani) wala hatutakadhibisha ishara za Mola wetu na tutakuwa katika wanaoamini.

﴿بَلْ بَدَا لَهُم مَّا كَانُوا يُخْفُونَ مِن قَبْلُ وَلَوْ رُدُّوا لَعَادُوا لِمَا نُهُوا عَنْهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ﴾

28.Bali yamewadhihirikia waliyokuwa wakiyaficha zamani. Na kama wangalirudishwa, bila shaka wangeyarudia yale waliyokatazwa na hakika wao ni waongo.

﴿وَقَالُوا إِنْ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا الدُّنْيَا وَمَا نَحْنُ بِمَبْعُوثِينَ﴾

29.Na kusema: Hakuna kingine ila maisha yetu ya dunia, wala sisi hatutafufuliwa.

﴿وَلَوْ تَرَىٰ إِذْ وُقِفُوا عَلَىٰ رَبِّهِمْ قَالَ أَلَيْسَ هَـٰذَا بِالْحَقِّ قَالُوا بَلَىٰ وَرَبِّنَا قَالَ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴾

30.Na ungeliona watakaposimamishwa mbele ya Mola wao, Akasema: Je, si kweli haya? Watasema: Kwa nini? Tunaapa kwa Mola wetu. Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakataa.

﴿قَدْ خَسِرَ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِلِقَاءِ اللَّـهِ حَتَّىٰ إِذَا جَاءَتْهُمُ السَّاعَةُ بَغْتَةً قَالُوا يَا حَسْرَتَنَا عَلَىٰ مَا فَرَّطْنَا فِيهَا وَهُمْ يَحْمِلُونَ أَوْزَارَهُمْ عَلَىٰ ظُهُورِهِمْ أَلَا سَاءَ مَا يَزِرُونَ﴾

31.Hakika wameshahasirika wale waliokadhibisha kukutana na Mwenyezi Mungu, na wamefuzu wale waliomwamini, mpaka itakapowajia ghafla saa (Kiyama) watasema: Oo! Majuto yetu juu ya yale tuliyoyapuuza! Nao watabeba mizigo yao migongoni mwao. Angalieni! Ni mabaya mno wanayoyabeba.

﴿وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَعِبٌ وَلَهْوٌ وَلَلدَّارُ الْآخِرَةُ خَيْرٌ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَ أَفَلَا تَعْقِلُونَ﴾

32.Na maisha ya dunia si kitu ila mchezo na upuzi. Na hakika nyumba ya akhera ni bora zaidi kwa wenye takua. Basi je hamtii akili?

WATAKAPOSIMAMISHWA MOTONI

Ay 27 - 32

MAANA

Na ungeliona watakapoonyeshwa moto.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amerudia kuelezea hali ya wakadhibishaji Siku ya Kiyama, na kwamba wao watakapoona adhabu waliyoandaliwa na thawabu walizoandaliwa waumini, watasema:

Laiti tungerudishwa duniani wala hatutakadhibisha ishara za Mola wetu na tutakuwa katika wanaoamini.

Yaani tutatubia na tufanye amali njema. Lakini masikitiko na mazingatio hayafai chochote ila ikiwa kumwogopa Mwenyezi Mungu na adhabu yake ni kabla ya kutokea adhabu. Ama baada ya kutokea, basi ni kulilia maiti na kusikitika yaliyofutu.

Bali yamewadhihirikia waliyokuwa wakiyaficha zamani.

Hataokoka kesho na adhabu ya Mwenyezi Mungu ila ambaye yuko wazi katika maisha haya, vitendo vyake vinaambatana na kauli yake; yote mawili yawe ni picha ya dhati yake na hali yake, mpaka viwe vyote ni kama kitu kimoja tu mbele ya Mwenyezi Mungu na watu.

Ama yule mwenye kuzibaziba, ambaye Muumba anayajua yale ayafanyayo na watu hawayajui, miongoni mwa ria na unafiki, huyu yatamdhihirikia malipo ya ria yake na unafiki wake; na nafsi yake itajutia uovu wake na kutamani kujisafisha kwa kurudishwa duniani, lakini wapi!

Na kama wangalirudishwa, bila shaka wangeyarudia yale waliyokatazwa na hakika wao ni waongo.

katika kusema kwao: Laiti tungerudishwa wala hatutakadhibisha ishara za Mola wetu na tutakuwa katika wanaoamini.

Tumesoma habari za wakosaji kadhaa ambao wanatubia wakiwa gerezani, lakini wanapotoka hurudia makosa yao. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿وَإِذَا مَسَّكُمُ الضُّرُّ فِي الْبَحْرِ ضَلَّ مَن تَدْعُونَ إِلَّا إِيَّاهُ فَلَمَّا نَجَّاكُمْ إِلَى الْبَرِّ أَعْرَضْتُمْ وَكَانَ الْإِنسَانُ كَفُورًا﴾

"Na inapowafikia dhara katika bahari hupotea wale mnawaomba isipokuwa Yeye tu, lakini anapowaokoa mkafika salama nchi kavu mnageuka; na mwanadamu ni mkanushaji mno" (17:67)

Na kusema: Hakuna kingine ila maisha yetu ya dunia, wala sisi hatutafufuliwa.

Yaani lau wangelirudishwa kwenye maisha yao ya mwanzo wangalisema waliyoyasema mwanzo: Hakuna ufufuo wala hisabu wala malipo.

Unaweza kuuliza : Vipi watakanusha na hali wao watakuwa wameshuhudia vituko vikubwa na wakaonyeshwa, mpaka wakataka kujitakasa nayo na kuahidi kuwa hawatarudia?

Jibu : Wao wanajua fika kwamba hisabu na adhabu itakuwa tu, hapana budi. Wakati huo huo wanajua kuwa lau wataitangaza haki na kuinyenyekea, chumo na faida zao watazikosa. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

﴿وَجَحَدُوا بِهَا وَاسْتَيْقَنَتْهَا أَنفُسُهُمْ ظُلْمًا وَعُلُوًّا﴾

"Na wakazikanusha (ishara zetu) na hali yakuwa nafsi zao zina yakini nazo kwa dhulma na kujivuna" (27:14)

Na ungeliona watakaposimamishwa mbele ya Mola wao , baada ya kukadhibisha kukutana naye. Atasema: Je, si kweli haya? Katika kufasiri Aya ya nne katika Sura hii tulisema kuwa Mwenyezi Mungu analingania kuamini haki pamoja na kusimamisha dalili yake. Mpingaji akiipinga, hoja inakuwa juu yake. Na Aya hii inatilia mkazo hilo na kutaja dalili na hoja walizozikanusha na kuzikadhibisha. Watasema: Kwanini? Tunaapa kwa Mola wetu. Hivi sasa yamepita yaliyopita na hakuna kilichobaki isipokuwa malipo yenye kulingana na adhabu kwa mwenye kukufuru na kukanusha.

Akasema: "Basi onjeni adhabu kwa sababu ya mliyokuwa mkikataa. Haya ni malipo ya kila mwenye kuiweka mbele dunia na kuiacha Akhera na akaificha haki kwa hawa ya nafsi yake.

Utauliza : Kauli yake Mwenyezi Mungu kwa Makafiri: 'Je, si kweli haya?' Na kauli yake: "Onjeni adhabu" mbona haziafikiani na kauli yake:"Wala hatawasemeza Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama" ? (2:174)

Jibu : Makusudio ni kwamba Mwenyezi Mungu hatawasemesha yale yanayowafurahisha, bali atawasemeza yanayowaudhi, kama ilivyo katika Aya hii, na ilivyo katika Aya isemayo:

"Atasema: Tokomeeni humo wala msinisemeze." (23:108)

Hakika wamekwishahasirika wale waliokadhibisha kukutana na Mwenyezi Mungu na wamefuzu wale waliomwamini, mpaka itakapowajia ghafla saa (Kiyama) watasema: Oo! Majuto yetu juu ya yale tuliyoyapuza!

Imam Ali anasema:"Matunda ya kupuuza ni majuto, na matunda ya uthabiti ni amani."

Nao watabeba mizigo yao migongoni mwao. Angalieni! Ni mabaya mno wanayoyabeba.

Mizigo ni dhambi na kuibeba mgongoni ni fumbo, yaani kuwa nayo; kama vile isemwavyo: "Amepandwa na shetani." Yaani yuko naye hamwachi. Maana ni kuwa wanaoikadhibisha haki ndio watu wenye hali mbaya zadi huko akhera.

Mmoja wa wafasiri wapya anasema: "Bali mnyama ana hali nzuri zaidi kwa sababu hubeba mizigo mizito,; na mnyama huutua mzigo wake akaenda kupumzika, lakini hawa watakwenda na mizigo yao kwenye Jahannam wakisindikizwa na dhambi."

Na maisha ya dunia si kitu ila mchezo na upuzi." Umetangulia mfano wake katika Juz 4 (3:185)

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA SABA

﴿قَدْ نَعْلَمُ إِنَّهُ لَيَحْزُنُكَ الَّذِي يَقُولُونَ فَإِنَّهُمْ لَا يُكَذِّبُونَكَ وَلَـٰكِنَّ الظَّالِمِينَ بِآيَاتِ اللَّـهِ يَجْحَدُونَ﴾

33.Hakika tunajua kwamba yanakuhuzunisha yale wanayoyasema, Basi hakika hao hawakukadhibishi wewe, lakini madhalimu wanakataa ishara za Mwenyezi Mungu.

﴿وَلَقَدْ كُذِّبَتْ رُسُلٌ مِّن قَبْلِكَ فَصَبَرُوا عَلَىٰ مَا كُذِّبُوا وَأُوذُوا حَتَّىٰ أَتَاهُمْ نَصْرُنَا وَلَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَاتِ اللَّـهِ وَلَقَدْ جَاءَكَ مِن نَّبَإِ الْمُرْسَلِينَ﴾

34.Na hakika walikadhibishwa Mitume kabla yako, wakavumilia juu ya kukadhibishwa na kuudhiwa, mpaka ikawafikia nusura yetu. Na hakuna wa kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu, Na bila shaka zimekujia baadhi ya habari za Mitume hao.

﴿وَإِن كَانَ كَبُرَ عَلَيْكَ إِعْرَاضُهُمْ فَإِنِ اسْتَطَعْتَ أَن تَبْتَغِيَ نَفَقًا فِي الْأَرْضِ أَوْ سُلَّمًا فِي السَّمَاءِ فَتَأْتِيَهُم بِآيَةٍ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَجَمَعَهُمْ عَلَى الْهُدَىٰ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْجَاهِلِينَ﴾

35.Na ikiwa ni makubwa kwako huku kukataa kwao, basi kama unaweza kutafuta njia ya chini kwa chini katika ardhi au ngazi kwendea mbinguni na kuwaletea ishara. Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka, bila shaka angeliwakusanya kwenye uongofu. Basi usiwe miongoni mwa wajinga

﴿إِنَّمَا يَسْتَجِيبُ الَّذِينَ يَسْمَعُونَ وَالْمَوْتَىٰ يَبْعَثُهُمُ اللَّـهُ ثُمَّ إِلَيْهِ يُرْجَعُونَ﴾

36.Hakika wanaokubali ni wale tu wanaosikia, Na wafu Mwenyezi Mungu atawafufua kisha watarejeshwa kwake.

﴿وَقَالُوا لَوْلَا نُزِّلَ عَلَيْهِ آيَةٌ مِّن رَّبِّهِ قُلْ إِنَّ اللَّـهَ قَادِرٌ عَلَىٰ أَن يُنَزِّلَ آيَةً وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ﴾

37.Na husema: Kwa nini hakuteremshiwa ishara kutoka kwa Mola wake? Sema: Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye uweza wa kuteremsha ishara yoyote, lakini wengi wao hawajui.

TUNAJUA KUWA YANAKUHUZUNISHA

Aya 33 - 37

MAANA

Hakika tunajua kwamba yanakuhuzunisha yale wanayoyasema.

Msemo unaelekezwa kwa Mtume(s.a.w.w) , Dhamir ya 'wanayoyasema' inawarudia wale waliomkadhibisha Mtume(s.a.w.w) . Ama yale wanayoyasema bali waliyasema hasa, ni yale yaliyoashiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w.t):

﴿ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ﴾

Kisha wakampa mgongo na wakasema: Amefunzwa (na) ni mwendawazimu." (44:14)

"Wakasema Makafiri: Hakika huyu ni mchawi dhahiri." (10:2) Na mengineyo.

Basi hakika hao hawakukadhibishi wewe, lakini madhalimu wanakataa ishara za Mwenyezi Mungu.

Kila mwenye kumpiga vita mwenye haki, basi ameipiga vita haki yenyewe, na kila mwenye kumdharau Mtume kwa kuwa yeye anachukua risala ya aliyemtuma, basi atakuwa amemdharau yule aliyemtuma na sio Mtume mwenyewe.

Washirikina wa Makka walikuwa wakimwita Muhammad(s.a.w.w) mkweli mwaminifu, kabla ya Utume. Alipowaletea risala ya Mwenyezi Mungu na kuwasimamishia hoja, walimpiga vita na wakamwita mwendawazimu, mchawi nk.

Kwa hiyo kumkadhibisha kwao huku na hali hii, ni kukadhibisha risala ya Mwenyezi Mungu na hoja zake. Hakuna linalofahamisha hilo kwa dalili zaidi ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

﴿إِنَّ الَّذِينَ يُبَايِعُونَكَ إِنَّمَا يُبَايِعُونَ اللَّـهَ يَدُ اللَّـهِ فَوْقَ أَيْدِيهِمْ﴾

"Hakika wale wanaokubai, kwa hakika wanambai Mwenyezi Mungu; mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao" (48:10)

Na hakika walikadhibishwa Mitume kabla yako, wakavumilia juu ya kukadhibishwa na kuudhiwa, mpaka ikawafikia nusura yetu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamwambia Mtume wake ikiwa watakukadhibisha, basi wamekadhibishwa Mitume kabla yako na wakaudhiwa katika kufikisha risala yake, wakavumilia juu ya maudhi mpaka ikawajia nusura. Kwa hiyo nawe vumilia kama walivyovumilia; na Mwenyezi Mungu atakunusuru kama alivyowanusuru.

Huu ndio mzunguko wa maisha - mvutano baina ya kheri na shari na haki na batili. Ni muhali kwa mpigania haki asipate maudhi kutoka katika maadui wa haki. Vilevile haki haiwezi kushinda ila wapatikane watakaoinusuru wavumilivu katika jihadi ya haki na wainunue kwa nafsi zao, watu wao na mali zao.

Ni desturi ya Mwenyezi Mungu, wala huwezi kupata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu, Hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Na hakuna wa kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu.

Wala sijui wakati ambao wabatilifu wamekuwa na nguvu kuliko wakati huu tunaoishi. Wameweka vituo vya kijeshi kila mahali, vituo vya kuharibu, silaha kali za kumaliza watu na kubomoa. Wanatawala nyenzo za wananchi wadhaifu, mabenki, magazeti, uchapishaji na usambazaji, Mpaka yule mtu aliye mwaminifu mwenye ikhlasi anajikuta ametupwa hawezi kutoa makala huru au kutangaza haki kupitia kwenye Idhaa. Lakini mhaini, popote atakapoelekea atapata mapokezi na kutukuzwa [7] .

Na bila shaka zimekujia baadhi ya habari za Mitume hao.

Yaani tumekusimulia kabla yale yaliyowapata Mitume kutokana na watu wao na jinsi walivyovumilia katika kukadhibishwa na maudhi, na kwamba mwisho ushindi ulikuwa wao.

Na desturi hii itakupitia wewe, kama iliyowapita wao, wala hakuna mwenye kubadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu.

Na ikiwa ni makubwa kwako huku kukataa kwao, basi kama unaweza kutafuta njia ya chini kwa chini katika ardhi au ngazi kwendea mbinguni na kuwaletea ishara.

Aya hii ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu kumwambia Mtume wake Mtukufu:

﴿فَلَا تَذْهَبْ نَفْسُكَ عَلَيْهِمْ حَسَرَاتٍ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ بِمَا يَصْنَعُونَ﴾

"Basi roho yako isitoke kwa majonzi juu yao; hakika Mwenyezi Mungu anayajua yote wanayoyafanya." (35:8)

Aya zote hizi mbili zinatoa picha jinsi Mtume(s.a.w.w) alivyokuwa akipata jakamoyo na uchungu kutokanana upinzani wa washirikina kwa mwito wake.

Yaliyompata Mtume kutoka kwa watu wake ni yale yanayoondoa upole wa mpole. Lakini yeye akavumilia na kuwa na matumaini; wala hakuwaapiza bali aliwaombea, akisema:"Ewe Mola wangu! Wasamehe watu wangu, hakika wao hawajui"

Pamoja na hayo yote alikuwa akihisi uchungu kwa kufuru zao. Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia kwa Aya hii, ili kumpoza na kumwondolea matumaini na aachane nao; kisha angoje kidogo, aone vile utakavyokuwa mwisho wa wakadhibishaji.

Na kama Mwenyezi Mungu angelitaka, bila shaka angeliwakusanya kwenye uongofu.

Razi anasema kuwa: "Hii inafahamisha kuwa yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu hataki makafiri waamini, bali anataka kuwabakisha kwenye ukafiri.

Lakini hii itakuwa ni dhuluma hasa, na Mwenyezi Mungu hawadhulumu waja. Usahihi wa maana ya jumla hii, ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hataki kumlazimisha yeyote katika kumwamini, bali anamwachia hiyari yake baada ya kumsimamishia hoja kwa dalili na ubainifu. Lau angelitaka waja wake waamini kwa kusema 'kuwa ikawa', basi asingelikufuru yeyote katika wao. Lakini hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ilitaka ajiingize katika mambo ya watu kama mwamrishaji na mwenye kutoa nasaha, si kama Muumba mwenye nguvu, Umetangulia ufafanuzi katika Juz. 1 (2:26)

Basi usiwe miongoni mwa wajinga.

Atakuwaje Mtume Mtukufu miongoni mwa wajinga na hulka zake ni hulka za Qur'an? Msemo huu umefaa kuelekezwa kwa mtukufu wa viumbe, kwa vile unatoka kwa Muumba wa viumbe na sio kwa kwa aliye kama yeye.

Wanaokubali ni wale tu wanaosikia, Na wafu Mwenyezi Mungu atawafufua kisha watarejeshwa kwake.

Aya hii ni mfano wa Aya isemayo:

﴿إِنَّكَ لَا تُسْمِعُ الْمَوْتَىٰ وَلَا تُسْمِعُ الصُّمَّ الدُّعَاءَ إِذَا وَلَّوْا مُدْبِرِينَ﴾

"Hakika huwezi kuwasikilizisha wafu wala huwezi kuwasikilizisha viziwi mwito wanapogeuka kurudi nyuma" (27:80)

Maana ni kuwa: Ewe Muhammad! Wale unaopupia waonyeke hawakusikii kwa kufahamu na kuzingatia. Kwa sababu kupenda dunia kumewafanya kama wafu, na wafu haitakikani kuwaambia chochote; bali wanaachwa na mambo yao mpaka siku ya kiyama, watakapoiona adhabu ambayo hawataweza kuikimbia.

Na husema: Kwa nini hakuteremshiwa ishara kutoka kwa Mola wake?

Utauliza : vipi wanasema hivi na hali Mwenyezi Mungu amemteremshia Muhammad(s.a.w.w) ishara na hoja kadhaa na ubainifu.

Jibu : Makusudio ya ishara hapa ni muujiza ule walioutaka wao kuwa ni sharti la wao kumwamini Muhammad(s.a.w.w) ; hawakusudii muujiza unaomkinaisha mwenye kuitafuta haki, Lau wangeliutaka huo wasingelisema hivyo.

Sema: Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye uweza wa kuteremsha ishara yoyote , ile wanayotaka, lakini yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu haiteremshi kwa kuitikia matakwa na hawaa zao; isipokuwa anateremsha miujiza kulingana na inavyopitisha hekima yake.

Lakini wengi wao hawajui , kuwa anateremsha miujiza kulingana na hekima Yake na sio hawa za watu.

﴿وَمَا مِن دَابَّةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا طَائِرٍ يَطِيرُ بِجَنَاحَيْهِ إِلَّا أُمَمٌ أَمْثَالُكُم مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يُحْشَرُونَ﴾

38.Na hakuna mnyama katika ardhi wala ndege arukaye kwa mbawa zake, ila ni umma kama nyinyi, Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote. Kisha watakusanywa kwa Mola wao.

﴿وَالَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا صُمٌّ وَبُكْمٌ فِي الظُّلُمَاتِ مَن يَشَإِ اللَّـهُ يُضْلِلْـهُ وَمَن يَشَأْ يَجْعَلْهُ عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴾

39.Na wale waliokadhibisha ishara zetu ni viziwi na mabubu wako gizani. Amtakaye Mwenyezi Mungu humpoteza na amtakaye humweka katika njia iliyonyooka.

WANYAMA NA NDEGE NI UMMA

Aya 38-39

LUGHA

Mnyama, ni kila anayetembea katika ardhi wakiwa ni: Watu, wanyama na wadudu.

MAANA

Na hakuna mnyama katika ardhi wala ndege arukaye kwa mbawa zake, ila ni umma kama nyinyi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anabainisha katika Aya hii kwamba baina yetu na wanyama kuna aina ya kufanana, lakini hakufafanua aina yenyewe. Je, tunafanana katika kuwa wao ni viumbe wa Mwenyezi Mungu; au katika kumwamini Mwenyezi Mungu na kumsifu kwa sifa zake njema? Au tunafanana katika kuwa wao ni aina zinazojulikana kwa majina; kama zinavyojulikana koo na kabila? Au ni katika kupanga maisha yao na kufanya mambo kulingana na masilahi?

Kwa hali yoyote iwayo ni kuwa wataalamu wengi wamechunguza tabia na kazi za wanyama, wadudu na ndege na wakafikia kwenye siri za ajabu zinazoshuhudia kuweko mpangaji mwenye hekima, Tutataja baadhi ya mifano.

Ndovu huweka mahakama kwa mhalifu na ndovu aliyekosea huhukumiwa kwa kutengwa na kundi la wengine ili aishi peke yake katika upweke.

Kunguru anapohisi hatari itakayowapata wenzake huwaonya kwa sauti maalum. Ama katika hali ya furaha hutoa sauti iliyo karibu na kicheko.

Utauliza : Kuna faida gani katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kusema arukaye kwa mbawa zake ambapo kumtaja Ndege kunafahamisha moja kwa mja kuruka kwa mbawa?

Jibu : Hakuna faida, tuijuayo, isipokuwa ufasaha wa maneno.

Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote.

Imesemekana kuwa makusudio ya Kitab hapa ni lawhim-mahfudh (ubao maalum wenye kuhifadhiwa) wenye kukusanya yaliyokuwa na yatakayokuwa.

Kauli ya pili, inasema ni fumbo la ujuzi wa Mwenyezi Mungu kujua makusudio ya mtu, na kauli zake na vitendo vyake.

Kauli ya tatu, inasema ni Qur'an na kwamba Mwenyezi Mungu amebainisha ndani yake kila yapasayo kubainishiwa watu, miongoni mwa misingi ya dini na matawi yake na yanayofungamana nayo, Nasi tumeichagua kauli hii katika kufasiri Aya ya (2:2) Juz. 1, kifungu Qur'an na sayansi.

Kisha watakusanywa kwa Mola wao.

Dhahiri ya maneno inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu atawakusanya wanyama na ndege siku ya Kiyama, kama atakavyowakusanya watu. Vilevile Aya isemayo:"Na wanyama mwitu watakapokusanywa." (82:5)

Maulama wengi wamesema hivyo kwa kutegemea Aya hizo mbili na Hadith isemayo: "Hakika Mwenyezi Mungu atawachukulia kisasi watu kutokana na wenye pembe."

Sisi tuko pamoja na Ibn Abbas aliyesema kuwa makusudio ya kukusanywa wanyama ni mauti yao; kama ilivyopokewa katika Hadith: "Anayepatwa na kifo ndiyo kiama chake." Kwa sababu hisabu na adhabu ni baada ya kukalifiwa na sharia na kuzihalifu. Wala hakuna kukalifiwa na sharia ila pamoja na akili; na wanyama na ndege hawana akili, kwa hiyo hawakalifiwi na sharia.

Kwa sababu hizo basi, hawatakusanya kwa ajili ya hisabu. Lau wanyama wangelichukuliwa hisabu basi ingefaa zaidi watoto wadogo wachukuliwe hisabu. Ama Hadith ya 'kuchukua kisasi', ni fumbo la uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na kwamba yeye hataacha kidogo wala kikubwa ila atakidhibiti.

Ikiwa Mwenyezi Mungu atawaadhibu wenye pembe wakimpiga mtu, basi vizuri zaidi ni kutuharimishia sisi kuwachinja wanyama. Ama kauli ya anayesema kuwa Mwenyezi Mungu atayabadilisha maumivu ya mtu kwa mnyama, hiyo ni kumsemea Mwenyezi Mungu bila ya ujuzi wowote.

Na wale waliokadhibisha ishara zetu ni viziwi na mabubu wako gizani. Yaani wao ni kama viziwi, kwa sababu wao hawasikii mwito wa haki, na ni kama mabubu kwa sababu wao hawaitamki haki waliyoijua na wako katika giza la kufuata na giza la ushirikina, ukafiri, ufasiki na dhambi.

Amtakaye Mwenyezi Mungu humpoteza na amtakaye humweka katika njia iliyonyooka.

Yametangulia maelezo kuhusu uongofu na upotevu katika Juz.1 (2:26) na Juz.2 (4:88).

﴿قُلْ أَرَأَيْتَكُمْ إِنْ أَتَاكُمْ عَذَابُ اللَّـهِ أَوْ أَتَتْكُمُ السَّاعَةُ أَغَيْرَ اللَّـهِ تَدْعُونَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴾

40.Sema: niambieni, kama ikiwafikia adhabu ya Mwenyezi Mungu au ikiwafikia ile saa, je, mtamuomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wakweli?

﴿بَلْ إِيَّاهُ تَدْعُونَ فَيَكْشِفُ مَا تَدْعُونَ إِلَيْهِ إِن شَاءَ وَتَنسَوْنَ مَا تُشْرِكُونَ﴾

41.Bali yeye tu ndiye mtakayemuomba, Atawaondolea mnayomuomba akitaka, Na mtawasahau mnaowashirikisha .

﴿وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا إِلَىٰ أُمَمٍ مِّن قَبْلِكَ فَأَخَذْنَاهُم بِالْبَأْسَاءِ وَالضَّرَّاءِ لَعَلَّهُمْ يَتَضَرَّعُونَ﴾

42.Kwa hakika tulipeleka (Mitume) kwa umma zilizokuwa kabla yako; kisha tukawatia katika shida na madhara ili wapate kunyenyekea.

﴿فَلَوْلَا إِذْ جَاءَهُم بَأْسُنَا تَضَرَّعُوا وَلَـٰكِن قَسَتْ قُلُوبُهُمْ وَزَيَّنَ لَهُمُ الشَّيْطَانُ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

43.Basi mbona wasinyenyekee ilipowafikia adhabu yetu? Lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu na shetani akawapambia waliyokuwa wakiyafanya.

﴿فَلَمَّا نَسُوا مَا ذُكِّرُوا بِهِ فَتَحْنَا عَلَيْهِمْ أَبْوَابَ كُلِّ شَيْءٍ حَتَّىٰ إِذَا فَرِحُوا بِمَا أُوتُوا أَخَذْنَاهُم بَغْتَةً فَإِذَا هُم مُّبْلِسُونَ﴾

44.Basi waliposahau yale waliyokumbushwa tuliwafungulia milango ya kila kitu, mpaka walipofurahia yale waliyopewa tuliwakamata kwa ghafla; na mara wakawa wenye kukata tamaa.

﴿فَقُطِعَ دَابِرُ الْقَوْمِ الَّذِينَ ظَلَمُوا وَالْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴾

45.Ikakatwa mizizi ya watu waliodhulumu; na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote.

SEMA NIAMBIENI

Aya 40 - 45

MAANA

Sema: niambieni, kama ikiwafikia adhabu ya Mwenyezi Mungu au ikiwafikia ile Saa, je, mtamuomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wakweli?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamwamrisha Mtume wake awaambie washirikina: Niambieni kama ikiwafikia adhabu, kama ile iliyoteremshiwa wale waliokadhibisha Mitume yao; au yakiwafikia maumivu makubwa ya mauti na vitisho vya Kiyama, je katika hali hii, mtayaita masanamu na mizimu mliyokuwa mkiabudu na kudai kuwa itawaondolea fazaa na adhabu?

Makusudio ya Aya hii ni kuwa Makafiri kesho watajivua na yale waliyokuwa wakiyaabudu na kukimbilia kwa Mwenyezi Mungu baada ya kuwabainikia kuwa hakuna hila wala nguvu ila kwa msaada wake Yeye tu peke yake bila ya kuwa na mshirika.

MWENYEZI MUNGU NA MAUMBILE

Bali yeye tu ndiye mtakayemuomba.

Baada ya kuwauliza kuwa mtamwomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu siku ya vituko vikubwa, amelithibithisha jibu kwa kusema kwake:(Bali yeye tu ndiye mtakayemuomba) .

Hilo ndilo jibu linaloaminiwa na kujibiwa na umbile ambalo Mwenyezi Mungu amewaumbia watu, katika dunia na akhera, Na sio maana ya umbile la Mwenyezi Mungu kuwa mtu atamtambua Muumba hivi hivi tu bila ya dalili. Hapana! Kama ni hivo basi kusingelitokea mtu yeyote wa kumkanusha Mwenyezi Mungu.

Hakika maana ya umbile hili ni kuwa Mwenyezi Mungu amempa mtu maandalizi ya kufahamu dalili zinazofahamisha kuweko Mwenyezi Mungu, na dalili hizi haepukani nazo kwa hali yoyote. Anayekufuru anakufuru kwa kuzembea na kupuuza kwa kuepuka kuchunguza dalili na hoja. Kwa hiyo ndipo akastahiki adhabu kwa kupuuza huko.

Kwani hakuna tofauti kabisa katika mtazamo wa akili, baina ya mwenye kuacha kufanya amali, kwa makusudi, na huku anajua; na yule mwenye kuiacha haki akafuta batili kwa kutojua lakini ana uwezo wa kujua na kupambanua uongufu na upotevu, lakini akaacha kwa kupuuza na kudharau.

Inawezekana maandalizi hayo yakajificha nyuma ya pazia la kufuata maelezo na matamanio; sawa na linavyojificha jua nyuma ya mawingu, ikafikiriwa kwa yule asiyejua sitara hizo kuwa yeye amemkana Mwenyezi Mungu kwa kukosa dalili na dalili iko katika dhati yake na maumbile yale ambayo amemuumbia Mwenyezi Mungu. Na siku ya Kiyama sitara hii iliyozuka itaondoka na kudhihiri hakika iliyo wazi wala hakutasalia nafasi ya shaka na ukanusho.

Atawaondolea mnayomuomba akitaka.

Yaani nyinyi washirikina mtaacha siku ya Kiyama, kuomba masanamu mliyokuwa mkiyaabudu duniani na mtamwomba Mwenyezi Mungu peke yake, wakati hakika ya kila jambo itakapodhihiri.

Na mtawasahau mnaowashirikisha.

Yaani nyinyi washirikina siku ya Kiyama mtaacha kuyaomba masanamu mliyokuwa mkiyaabudu duniani na kumwomba Mwenyezi Mungu peke yake wakati itakapodhihiri hakika ya kila kitu.

Kwa hakika tulipeleka (Mitume) kwa umma zilizokuwa kabla yako; kisha tukawatia katika shida na madhara ili wapate kunyenyekea.

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) hawaadhibu waja wake ila baada ya kuwapelekea mjumbe atakayewaongoza kwenye njia ya uongofu. Kama hawakuongoka anawapa fursa ili wajirudi wenyewe, na kuwatia katika mtihani kwa mabalaa ili wanyenyekee na watubie, lakini wao waling'ang'ania maasi; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Aya inayofuatia hii.

Basi mbona wasinyenyekee ilipowafikia adhabu yetu? Lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu na shetani akawapambia waliyokuwa wakiyafanya.

Mwenyezi Mungu, ambaye zimetukuka sifa zake, anasema kuwa wao hawakunyenyekea ilipowafikia shida duniani wala hawakumdhalilikia Mwenyezi Mungu kwa kuacha inadi yao, bali waling'ang'ania ukafiri, na shetani akawa nyuma yao akiwapambia upotevu na ufisadi.

Aya hii inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamkubali kila anayekimbilia kwake, hata kama kukimbia kwake ni kwa vikwazo vya shida na balaa. Hivi ndivyo alivyo aliye mkarimu na adhimu. Hamnyimi mwenye kuomba wala hamkatishi tamaa, kwa namna yoyote lengo na msukumo wake utakavyokuwa.

Basi waliposahau yale waliyokumbushwa tuliwafungulia milango ya kila kitu mpaka walipofurahia yale waliyopewa tuliwakamata kwa ghafla; na mara wakawa wenye kukata tamaa.

Aliwaonya kwanza kwa kauli kupitia kwa Mitume. Pili, kwa vitendo alipowapa mtihani kwa shida na madhara.

Waliponga'ang'ania ukafiri na inadi aliwafungulia milango ya riziki na raha, ili kuwasimamishia hoja na kuwavuta kidogo kidogo kwa neema baada ya mtihani wa nakama.

Walipofurahia raha na kuzidi kiburi na wala wasielekee kwenye uongofu, basi Mwenyezi Mungu aliwaadhibu kwa namna wasiyofikiria, wakajuta kwa kuzembea na wakakata tamaa ya kuokoka.

Kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) mara nyingine aliwapa dhiki na mara nyingine furaha kwa kupenda waongoke; sawa na afanyavyo mzazi kumhurumia mwanawe akitaka atengenekewe.

Lakini wala hawakushukuru raha wala kuwaidhika na balaa. Wakang'olewa wote asibakie yeyote katika wao, ili wapate funzo watakaokuja baada yao.

Ikakatwa mizizi ya watu waliodhulumu; na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote.

Kwa sababu ya kuwaneemesha kwake waumin na kuwanusuru na watu wa kufuru na ufisadi.


6

7

8

9