MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU 0%

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU Mwandishi:
Kundi: Vitabu mbali mbali

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi: NDUGU ZETU WA KISUNNI
Kundi:

Matembeleo: 44524
Pakua: 3487

Maelezo zaidi:

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 22 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 44524 / Pakua: 3487
Kiwango Kiwango Kiwango
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi:
Swahili

8

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

(iv) SIKU YA KUFUFULIWA

Baada ya kipindi cha Barzakh watu watafufuliwa na kuelekea kwenye uwanja wa Hisabu - kama tunavyojifunza katika Qur'an:

﴿ وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ الْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ ﴿٥١﴾ قَالُوا يَا وَيْلَنَا مَن بَعَثَنَا مِن مَّرْقَدِنَا هَـٰذَا مَا وَعَدَ الرَّحْمَـٰنُ وَصَدَقَ الْمُرْسَلُونَ ﴿٥٢﴾ إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ ﴿٥٣﴾ فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

Na kisha litapigwa baragumu (la kufufuliwa), tahamaki hao wanatoka makaburini kwenda mbio mbio kwa Mola wao. (Na huku) wanasema: Ole wetu, (Eee adhabu yetu)!Nani aliyetufufua malaloni petu?" (Waambiwe): "Haya ndiyo yale aliyoahidi (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema na waliyoyasema kwa haki Mitume". Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, tahamaki wote wamehudhurishwa mbele yetu. (Waambiwe) "Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa chochote kile wala hamtalipwa ila yale mliyokuwa mkiyatenda".[36:51-54]

Aya hizi zinatufahamisha kuwa hali ya siku hiyo itakuwa ni tofauti kabisa na hali ya hapa ulimwenguni na kwa ujumla itakuwa ni hali ya kutisha na ngumu kwa wanadamu (na majini). Muelekeo wa watu wote baada ya kufufuliwa utakuwa kwa Mola wao katika uwanja wa Hisabu. Japo katika aya nyingi za Qur'an siku ya kufufuliwa imeunganishwa moja kwa moja na siku ya hisabu, bado katika Hadith tunawekwa wazi kuwa patapita muda mrefu wa taabu na mashaka kabla ya kufikia katika hisabu. Patakuwa na jua kali na joto kali sana. Ardhi na mbingu vitakuwa vya shaba kama tunavyofahamishwa katika aya hii:

﴿ يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ﴾

"Siku mbingu zitakapokuwa kama shaba iliyoyeyuka". [70:8].

Katika hali hii joto na jua kali watu watabubujikwa na jasho litakalofurika kama tunavyofahamishwa katika hadithi zifuatazo:

Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:Siku ya kufufuliwa (Siku ya Kiyama) watu watatokwa na jasho kwa kiasi ambacho jasho lao litafurika juu (litakuwa na kina) kiasi cha dhiraa sabini na litawazamisha watu mpaka kufikia masikioni. [Bukhari na Muslim]

Mbubujiko na mafuriko haya ya jasho yatategemeana na matendo waliyoyatanguliza waja. Kama tunavyopata ufafanuzi katika Hadith ifuatayo: Miqdad amesimulia: Nimemsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: Siku ya Kiyama jua litashushwa karibu na viumbe kiasi cha umbali wa maili moja. Watu watatokwa na jasho kulingana na matendo yao. Kwa watu wengine litafika kwenye fundo za miguu, wengine litafika mpaka magotini na katika watu kuna wale watakaozamishwa mzamisho mkubwa na jasho lao, akiashiria mdomoni mwake kwa mkono wake" [Muslim]

Watu wataangalia mbinguni juu kwa juu kwa muda wa miaka arobaini. Matumbo yataungua kwa njaa na midomo itapasuka kwa kiu. Kila mmoja siku hiyo atahakikisha kuwa siku aliyoahidi Allah (s.w.) na kuikariri mara nyingi katika ujumbe wake, ndio hiyo iliyowadia na hapana popote pa kukimbilia isipokuwa kwa Mola wako.Kila mmoja ataona matendo yake yamehudhurishwa. Na katika hali hii Qur'an inauliza:

﴿ وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ ﴿١٧﴾ ثُمَّ مَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الدِّينِ ﴿١٨﴾ يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌ لِّنَفْسٍ شَيْئًا وَالْأَمْرُ يَوْمَئِذٍ لِّلَّـهِ﴾

Ni nini kitakachokujulisha siku ya malipo ni siku gani hiyo. Tena nini kitakachojulisha siku ya malipo ni siku gani hiyo?Ni siku ambayo nafsi hitamilikia nafsi (nyingine) chochote. Na amri siku hiyo itakuwa ya Mwenyezi Mungu tu" [82:17-19]

Kwa ujumla kipindi kati ya kufufuliwa na kufikia hisabu, kitakuwa kigumu sana na kila mtu atahisi ugumu wake na kiasi ambacho hata Mitume wa Allah (s.w.) ambao ni vipenzi vyake watahisi. Hapana nafsi itakayojiamini, kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo:

Aysha amesimulia kuwa alikumbuka moto na akaangusha kilio. Mtume(s.a.w.w) akauliza:Ni kitu gani kinachokuliza? Akajibu: "Nimekumbuka moto na nikaanza kulia. Je utawakumbuka wake zak siku ya Kiyama?" Mtume (s.a.w.) akasema: "Sikiliza: Katika sehemu tatu (zifuatazo) hakuna atakayemkumbuka yeyote yule - karibu na mizani (hisabu) mpaka ajue kuwa mizani yake itakuwa nyepesi au nzito, na karibu na kupewa kitabu kilichorikodiwa matendo mpaka utakapoitwa: Njoo, soma kitabu chako, na mpaka atakapopewa kitabu chake kwa mkono wa kulia au kushoto au nyuma ya mgongo wake, na karibu na njia nyembamba (siratwa) inakayowekwa baina ya ncha mbili za moto wa Jahannam". [Abuu Daud]

Hata hivyo, tunafahamishwa katika Hadith kuwa katika hicho kipindi kigumu cha baina ya kufufuliwa na kuhukumiwa, waumini waliotenda matendo mema watawekewa kivuli cha Allah (s.w.) na kila Mtume atapewa kisima au haudhi ya maji ya kuwanywesha watu wa ummah wake walioamini pamoja naye. Mtume(s.a.w.w) ameahidiwa Kauthar katika Qur'an:

﴿ إِنَّا أَعْطَيْنَاكَ الْكَوْثَرَ ﴾

"Hakika Tumekupa kheri nyingi" [108:1]

Kutokana na Hadith, Kauthar ni Birika (haudhi) aliloahidiwa Mtume(s.a.w.w) ambalo maji yake ni matamu kuliko asali na meupe kuliko maziwa na yanakata kiu milele - yaani kila mwenye kunywa maji hayo hasikii kiu tena.

Hadith ifuatayo inatufahamisha Kauthar ni nini: Abdullah bin Amr amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.w.) amesema: "Haudhi yangu ina urefu wa safari ya mwezi mmoja na ni pembe mraba na maji yake ni meupe kuliko maziwa, na harufu yake ni nzuri kuliko misk na vikombe vyake vinang'ara kama nyota angani. Yeyote yule anywaye maji yake hasikii kiu daima . [Bukhari na Muslim]

Watakaonyweshwa maji haya na Mtume(s.a.w.w) katika kipindi hicho kigumu cha joto kali lisilo kifani, njaa inayounguza matumbo na kiu kikali kisicho kifani, ni wale tu katika waumini waliomfuata Mtume(s.a.w.w) bila ya kumzumulia lolote. Waliozusha jambo lolote katika dini, Mtume(s.a.w.w) atawafukuza na kuwanyima maji yake kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifautayo:

Sahl bin Sa'ad amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema: Hakika nitawatangulia katika Haudhi. Yeyote atakayepita kwangu atakunywa, na yeyote atakayekunywa hatasikia kiu daima. Watu wale nitakaowajua na watakaonijua hapana shaka watakuja kwangu kunywa lakini patakuwa na kizuizi kati yangu na wao, kisha nitasema: "Hakika hawa ni wangu". Patasemwa: Hakika hujui ni uzushi gani waliokuzulia baada yako. Kisha nitasema: Ondokeni, ondokeni nyinyi mlionizulia (mliozua mambo na kuyaingiza kwenye dini) baada ya yangu. [Bukhari na Muslim]

(V) SIKU YA HUKUMU

Siku ya Hukumu ndio Siku Kuu ambapo Ufalme wa Allah (s.w.) utaonekana kwa wazi kwa kila mtu. Kila mtu atayakinisha kuwa Ufalme ni wa Allah (s.w.) Peke Yake hata kwa wale waliokanusha hapo awali katika maisha ya dunia. Hata hivyo Allah (s.w.) atauliza: Leo Ufalme ni wa nani? Wote watakuwa kimya, halafu atajibu Mwenyewe swali hili kama ilivyo katika aya ifuatayo:

﴿ يَوْمَ هُم بَارِزُونَ لَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِنْهُمْ شَيْءٌ لِّمَنِ الْمُلْكُ الْيَوْمَ لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ﴾

Siku watakayodhihiri (mbele ya Mwenyezi Mungu), na haitafichika habari yao yoyote kwa Mwenyezi Mungu. Leo Ufalme ni wa nani? Ni wa Mwenyezi Mungu Mmoja, Mwenye Nguvu (za kufanya Atakalo). [40:16]

Hukumu itatolewa katika ardhi iliyotambarare kabisa ambapo viumbe vyote vitahudhurishwa.Malaika wote watasimama katika safu:

﴿ يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَـٰنُ وَقَالَ صَوَابًا﴾

"Siku ambayo zitasimama Roho (za viumbe wote) na Malaika safu safu; hatasema siku hiyo ila yule ambaye (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema amempa idhini ( ya kusema) na atasema yaliyo sawa". [78:38]

Kisha kiti cha Enzi cha Allah (s.w.) cha kutolea Hukumu kitahudhurishwa pale na Nuru Yake itazagaa kila mahali na kila mmoja atakuwa na uhakika kuwa Allah (s.w.) yupo kwa kuchukua Hisabu. Qur'an tukufu inatupa picha ya Siku hiyo kuwa:

﴿ وَأَشْرَقَتِ الْأَرْضُ بِنُورِ رَبِّهَا وَوُضِعَ الْكِتَابُ وَجِيءَ بِالنَّبِيِّينَ وَالشُّهَدَاءِ وَقُضِيَ بَيْنَهُم بِالْحَقِّ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ﴾

Na ardhi (siku hiyo) itang'ara kwa nuru ya Mola wake, na madaftari (ya vitendo) yatawekwa, na wataletwa Manabii na mashahidi na kutahukumiwa baina yao kwa haki wala hawatadhulumiwa". [39:69]

Kila mmoja atapita katika hisabu, japo wengine hisabu zao zitakuwa ngumu sana na wengine nyepesi sana. Hebu tuzingatie Hadith zifuatazo: Aysha amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.w.) amesema: Yeyote atakayehisabiwa (atakayeulizwa) katika siku ya Hukumu, ataangamia. Nikauliza (Aysha) Je, Allah hakusema:

﴿ فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا ﴾

"Basi Yeye Atahisabiwa hisabu nyepesi?" [84:8]

Akajibu: Hayo kwa hakika ni maelezo ya ujumla lakini atakayehisabiwa kila kitu kwa undani wake, ataangamia. [Bukhari na Muslim] Hadith inatufundisha kuwa kila mmoja atahisabiwa, lakini yule ambaye hisabu yake haitafanywa nyepesi, hataweza kufaulu kutokana na maelezo yake na bila shaka atakuwa ni mtu wa motoni. Pia Hadith ifuatayo inasisitiza juu ya kila mtu kuulizwa na Allah (s.w.):

Ad bin Haatim amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:Hapana yeyote kati yenu ambaye hataongea na Mola wake. Hapatakuwa na mkalimani yeyote kati ya Allah na yeye na hapatakuwa na pazia ya kumzuia Allah asionekane. Mja ataangalia kuliani kwake,lakini hatoona chochote isipokuwa matendo yake aliyoyatanguliza.Ataangalia mbele yake, lakini hataona chochote isipokuwa moto unaomjia usoni mwake. Kwa hiyo jikinge na moto (na kutoa sadaka) angalau kipande cha tende. [Bukhari na Muslim] Vile vile tunafahamishwa katika Hadith kuwa hapana yeyote atakayetoka kwenye uwanja wa Hisabu bila ya kuulizwa mambo matano yafuatayo:

1. Ujana wako umeutumiaje?

2. Umri wako umeutumiaje?

3. Mwili wako na vipaji vyako umevitumiaje?

4. Mali yako umeipataje na umeitumiaje?

5. Elimu yako umeitumiaje ?

Maswali haya yataulizwa mbele ya viumbe vyote vilivyoumbwa tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka mwisho wake.Kila mchunga (kila kiongozi katika ngazi yoyote ile) ataulizwa juu ya uchungaji (uongozi) wake. Mitume ndio watakaokuwa wa kwanza kuulizwa. Allah (s.w.) atawauliza Mitume: Ni lipi jibu lenu. Watajibu: Hatuna ujuzi.Hakika Wewe Ndiye Mjuzi wa siri (ghaibu)". Mitume watapumbaa kwa woga baada ya kuulizwa swali hili: Kisha Mtume Nuhu(a.s.) ataitwa na kuulizwa kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo: Abu Sayyid amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema: Nuhu(a.s.) atahudhurishwa katika siku ya hukumu. Ataulizwa: Je, umefikisha (ujumbe wangu)? "Ndiyo" atajibu.Kisha wafuasi wake wataulizwa: Aliwafikishia (ujumbe wangu)? Watajibu: "Hapana mwonyaji aliyetujia". Ataulizwa (Nuhu ni nani mashahidi wako? Atajibu: Muhammad na Umma wake. Mtume(s.a.w.w) amesema: Kisha mtaitwa (mtahudhurishwa) na mtatoa ushahidi kuwa kwa hakika alifikisha ujumbe (wa Allah kwa watu wake).

Kisha Mtume(s.a.w.w) akasoma (aya ifuatayo): Na hivyo ndivyo Tumekufanyeni umati bora (kama Kibla chenu tulivyokifanya bora) ili muwe mashahidi juu ya watu, na Mtume(s.a.w.w) awe shahidi juu yenu. Na hatukukifanya Kibla ulichokuwa nacho (mara ya kwanza kuwa ndio Kibla chako sasa na mwisho wa ulimwengu) ili tupate anayegeuka akarejea nyuma. Na kwa yakini ilikuwa jambo gumu isipokuwa kwa wale aliowaongoza Mwenyezi Mungu. Kwani Mwenyezi Mungu. Kwa watu ni mpole sana (na) mwenye rehma. (2:143) [Bukhari]

Habari juu ya kuulizwa kwa Nabii Issa(a.s.) inatolewa katika Qur'an: Na (kumbukeni) Mwenyezi Mungu atakaposema: Ewe Issa bin Maryam Je, wewe uliwaambia watu 'Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu? Aseme (Nabii Issa): "Wewe umetakasika na kuwa na mshirika. Hainijuzii mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uwongo).Kama ningalisema bila shaka ungalijua; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini siyajui yaliyo nafsini mwako; hakika Wewe ndiye ujuaye mambo ya ghaibu".

﴿ ن يَدْعُونَ مِن دُونِهِ إِلَّا إِنَاثًا وَإِن يَدْعُونَ إِلَّا شَيْطَانًا مَّرِيدًا ﴿١١٧﴾ لَّعَنَهُ اللَّـهُ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿١١٨﴾ وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا﴾

"Sikuwaambia lolote ila yale uliyoniamrisha: Ya kwamba mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu'. Na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao, na uliponikamilisha muda wangu, wewe ukawa mchungaji juu yao, na wewe shahidi juu ya kila kitu. "Ikiwa utawaadhibu basi bila shaka hao ni waja wako, na ukiwasamehe basi kwa hakika wewe ndiye mwenye nguvu na mwenye hikima; (hutaambiwa kuwa wamekushinda kuwatia adabu).Mwenyezi Mungu atasema: Hii ndiyo siku ambayo wakweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata Bustani zipitazo mbele yake mito. Humo watakaa milele.Mwenyezi Mungu amewawia (amewapa) radhi,nao wawe radhi naye.Huku ndiko kufaulu kukubwa. [4:117-119)

Waovu na madhalimu watapiga kelele na kila mmoja katika waumini (wa kweli) atasema:

"Nafsi yangu Nafsi yangu" Watakapokuwa katika hali hii moto utalisambaza tena joto lake mara ya pili, na watarudi katika hali ya kuogopa na kutetemeka. Katika mara ya tatu, watu wataanguka kifudifudi na hapo baba atamkimbia mtoto, ndugu atamkimbia ndugu yake na mume atamkimbia mkewe.

﴿ وَلَا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا﴾

"Wala jamaa hatamuuliza jamaa (yake)" [70:10]

Kisha watu watahudhurishwa mmoja mmoja mbele ya Mola wao kuulizwa. Hapana yeyote atakayeongea bila ya kuulizwa. Hapatakuwa na ndugu wala rafiki wa kumsaidia au kumuonea huruma mtu mwingine. Mahojiano na Allah (s.w.) itakuwa kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo: Abu Hurairah amehadithia: Ewe Mtume(s.a.w.w) Tutamuona Bwana wetu Siku ya Kiyama? Akauliza (Mtume(s.a.w.w) Je, mnaona ugumu kuona mwanga wa jua katikati ya mchana wakati halikufunikwa na mawingu?" Hapana" walijibu. Akauliza (tena): Mnaona vigumu kuona mwanga wa mwezi katikati ya mbalamwezi kali wakati ambapo hamna mawingu? Wakajibu: Hapana. Akasema: Naapa kwa yule ambaye maisha yangu yamo mikononi mwake, hamtapata shida katika kumuona Bwana wenu bali mtamuona kama msivyoona shida kuona jua katikati ya mchana na mwezi wakati wa mbalamwezi kali. Kisha (Allah) atakutana na mja na kumuuliza: Ewe fulani sikukutukuza na nikakupa nguvu, na nikakuozesha, na nikakutiishia farasi na ngamia, na sikukupa uongozi na bora (ya ngawira)? Ulifikiria kuwa utakutana na Mimi. 'Hapana'. Atajibu. Atasema Allah (s.w.) Sasa nimekusahau kama ulivyonisahau. Qur'an inatueleza:

﴿ وَقِيلَ الْيَوْمَ نَنسَاكُمْ كَمَا نَسِيتُمْ لِقَاءَ يَوْمِكُمْ هَـٰذَا وَمَأْوَاكُمُ النَّارُ وَمَا لَكُم مِّن نَّاصِرِينَ﴾

Na itasemwa:"Leo tunakusahauni kama nyinyi mlivyotusahau siku yenu hii, na mahali penu ni motoni, wala hamna wa kukunusuruni". [45:34]

Kisha Allah atakutana na mtu wa pili. (Mtume(s.a.w.w) akatekeleza habari zake kama yule wa kwanza. Kisha Allah (s.w.) akakutana na mtu wa tatu atamuuliza maswali yale yale: Mja huyo atajibu: Ee Bwana, nilikuamini na nikaamini kitabu chako, na Mitume wako, na niliswali, nikafunga na kutoa zaka. Atataja matendo mema aliyoyafanya kwa kiasi atakachoweza.

Allah atamwambia: Njoo hapa (kama unavyosema ndivyo).Sasa tunakuletea mashahidi. Atajiuliza ni nani atakayetoa ushahidi dhidi yangu? Kisha mdomo wake utafungwa na makalio yake yatapewa amri: Sema. Makalio yake, nyama yake na mifupa yake itaongea juu ya vitendo vyake na kwa hivyo ataomba msamaha na huyo atakuwa ni mnafiki ambaye amekasirikiwa na Allah (s.w.). [Muslim]

Kwa ujumla kabla ya kuulizwa na kisha kujitetea kote huku, kila mja atapewa uwezo wa kuona matendo yake aliyoyatanguliza ambayo yamehifadhiwa katika kitabu maalum ambacho atapewa aambiwe akisome mwenyewe kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿وَكُلَّ إِنسَانٍ أَلْزَمْنَاهُ طَائِرَهُ فِي عُنُقِهِ وَنُخْرِجُ لَهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ كِتَابًا يَلْقَاهُ مَنشُورًا ﴿١٣﴾ اقْرَأْ كِتَابَكَ كَفَىٰ بِنَفْسِكَ الْيَوْمَ عَلَيْكَ حَسِيبًا﴾

"Na kila mwanadamu tumemfungia (jaza ya) vitendo vyake shingoni mwake, tutamtolea siku ya kiyama daftari (iliyoandikwa ndani yake kila alilolifanya) atakayoikuta imekunjuliwa (aambiwe): Soma daftari yako.Nafsi yako inatosha leo kukuhisabu" [17:13-14]

Daftari hili ni daftari la ajabu, litakuwa limenukuu kila kitu mja alichokitenda katika maisha yake. Tunaweza kukiangalia kitabu hiki zaidi ya mfano wa televisheni ya matendo ya mtu ya kila siku kutokea kwenye baleghe yake mpaka kufariki kwake dunia. Televisheni hii itaonesha hata fikra zilizofichikana akilini na siri zilizohifadhiwa vifuani. Kila kitu kitaonekana kwa uwazi katika kitabu hicho. Kitabu hiki kinatolewa picha yake na Qur'an katika aya ifuatayo:

﴿ وَوُضِعَ الْكِتَابُ فَتَرَى الْمُجْرِمِينَ مُشْفِقِينَ مِمَّا فِيهِ وَيَقُولُونَ يَا وَيْلَتَنَا مَالِ هَـٰذَا الْكِتَابِ لَا يُغَادِرُ صَغِيرَةً وَلَا كَبِيرَةً إِلَّا أَحْصَاهَا وَوَجَدُوا مَا عَمِلُوا حَاضِرًا وَلَا يَظْلِمُ رَبُّكَ أَحَدًا ﴾

Na madaftari yatawekwa (mbele yao). Utaona wabaya wanavyoogopa kwa sababu ya yale yaliyomo (madaftarini) na watasema: "Ole wetu, (Ee kuangamia kweli leo). Namna gani madaftari haya!Haliachi dogo wala kubwa ila yamelidhibiti (yameliandika)!"Na watakuta yote yale waliyoyafanya yamehudhuria hapo, na Mola wako hamdhulumu yeyote. [18:49]

Pia tumefahamishwa katika Qur'an:

﴿فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾ وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُ﴾

Basi anayefanya wema (hata) kwa kiasi cha uzito wa mdudu chungu (atom's weight) ataona jaza yake. Na anayefanya uovu (hata) wa uzito wa mdudu chungu (atom's weight) ataona jaza yake" [99:7-9]

Pia tunafahamishwa katika Qur'an kuwa dalili ya kufaulu au kufeli kwa mtu itaonekana hata kabla mja hajasoma kitabu chake. Atakayekabidhiwa kitabu chake kwa mkono wa kulia atakuwa ni miongoni mwa wenye kufaulu na atakayekabidhiwa kitabu chake kwa mkono wa kushoto atakuwa miongoni mwa waliofeli kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ فَيَقُولُ هَاؤُمُ اقْرَءُوا كِتَابِيَهْ ﴿١٩﴾ إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَاقٍ حِسَابِيَهْ ﴿٢٠﴾ فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ ﴿٢١﴾ فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ ﴿٢٢﴾ قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ ﴿٢٣﴾ كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الْأَيَّامِ الْخَالِيَةِ ﴿٢٤﴾ وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِشِمَالِهِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيَهْ ﴿٢٥﴾ وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ ﴿٢٦﴾ يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ ﴿٢٧﴾ مَا أَغْنَىٰ عَنِّي مَالِيَهْ ﴿٢٨﴾ هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيَهْ ﴿٢٩﴾ خُذُوهُ فَغُلُّوهُ ﴿٣٠﴾ ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ ﴿٣١﴾ ثُمَّ فِي سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَاسْلُكُوهُ ﴿٣٢﴾ إِنَّهُ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ الْعَظِيمِ﴾

Basi ama yule atakayepewa daftari lake kwa mkono wake wa kuume (kulia) atasema (kwa furaha) "haya someni daftari langu (nililopewa sasa hivi). Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu (kwa vizuri)". Basi yeye atakuwa katika maisha ya raha katika pepo tukufu.Vishada vya matunda yake vitakuwa karibu;(vinachumika bila tabu). (Waambiwe) "Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya vitendo mlivyofanya katika siku zilizopita".Walakini atakayepewa daftari lake katika mkono wake wa kushoto basi yeye atasema: "Oh Laiti nisingalipewa daftari langu.Wala nisingelijua nini hisabu yangu.Laiti (mauti) yangemaliza (kila kitu changu). Mali yangu haikunifaa.Usultani (ukubwa) wangu umenipotea.(Kusemwe): "Mkamateni na mtieni makongwa.Kisha mtupeni motoni. Tena katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini muingizeni, (mtatizeni). Hakika yeye alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu" [69:19-33]

Baada ya kupewa daftari, tukio kubwa litakalofuata ni kupimwa amali katika mizani. Jambo ambalo litakuwa pia ni lenye kutisha sana kwa waja kama tulivyofahamishwa katika Hadith. Patakuwa na makundi matatu ya watu. Kuna watakaoingia peponi moja kwa moja bila hesabu. Hili litakuwa kundi la watu wachache waliojizatiti katika kutenda mema kwa ajili ya kupata radhi ya Allah (s.w.). Atawakaribisha moja kwa moja baada ya kuwafanyia wepesi katika hesabu yao kwa kuwaita:

﴿يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ﴿٢٧﴾ ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ﴿٢٨﴾ فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ﴿٢٩﴾ وَادْخُلِي جَنَّتِي﴾

"Ewe nafsi yenye kutua: Rudi kwa Mola wako, hali ya kuwa umeridhika (kwa utakayoyapata), na (Mwenyezi Mungu) aridhike na wewe. Basi ingia katika (kundi la) waja wangu (wazuri) uingie katika Pepo Yangu" [89:27-30]

Kundi la pili la wale ambao hawakumuamini Allah (s.w.) hata chembe, hawa wataingizwa motoni moja kwa moja bila ya amali zao kupimwa katika mizani kwani chochote atakachokifanya kafiri au mushriki, au kitakachofanywa kwa ria au kwa unafiki hakitakuwa na malipo yoyote kutoka kwa Allah (s.w.). Hivyo kafiri, mushriki na mnafiki hawatakuwa na lao mbele ya Allah (s.w.) kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿أَفَحَسِبَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَن يَتَّخِذُوا عِبَادِي مِن دُونِي أَوْلِيَاءَ إِنَّا أَعْتَدْنَا جَهَنَّمَ لِلْكَافِرِينَ نُزُلًا ﴿١٠٢﴾ قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُم بِالْأَخْسَرِينَ أَعْمَالًا ﴿١٠٣﴾ الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا ﴿١٠٤﴾ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ وَلِقَائِهِ فَحَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَلَا نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَزْنًا ﴿١٠٥﴾ ذَٰلِكَ جَزَاؤُهُمْ جَهَنَّمُ بِمَا كَفَرُوا وَاتَّخَذُوا آيَاتِي وَرُسُلِي هُزُوًا﴾

Je,wale waliokufuru wanadhani ya kwamba kule kuwafanya waja wangu kuwa walinzi (wao) badala Yangu (kutawafaa kitu kufanya hivyo)?Hakika Sisi Tumeiandaa Jahannamu iwe ndio mahala pa kuteremkia makafiri. Sema:Je!Tukujulisheni wenye hasara katika vitendo (vyao)? Hao ambao bidii yao hapa duniani imepotea bure katika maisha ya dunia, nao wanafikiri kwamba wanafanya amali njema? Hao ni wale waliozikataa (waliozikanusha) ishara za Mola wao na (wakakataa) naye.Kwa hiyo vitendo vya vimeruka patupu, wala hatutawasimamishia mizani siku ya kiyama. Hivyo Jahannamu ni malipo yao kwa sababu walikufuru na kuzifanyia mzaha aya zangu na Mitume wangu. [18:102-106]

﴿ وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴾

"Na kwa yakini imefunuliwa kwako na kwa wale waliokuwa kabla yako (maneno haya): "Kama ulimshirikisha (Mwenyezi Mungu) bila shaka amali zako zitaruka patupu (hatazipatia thawabu japo ni amali njema), na lazima utakuwa miongoni mwa wenye hasara". [39:65]

Kundi la tatu ni lile la watu walimuamini Allah (s.w.) lakini katika utendaji wakawa wamechanganya mema na maovu. Mema yao na maovu yao itabidi yapimwe katika mizani ya haki ili kila mmoja alipwe kwa haki kutokana na matendo yake aliyoyatanguliza. Qur'an inatufahamisha juu ya hili:

﴿وَنَضَعُ الْمَوَازِينَ الْقِسْطَ لِيَوْمِ الْقِيَامَةِ فَلَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَإِن كَانَ مِثْقَالَ حَبَّةٍ مِّنْ خَرْدَلٍ أَتَيْنَا بِهَا وَكَفَىٰ بِنَا حَاسِبِينَ﴾

Nasi tutaweka mizani za uadilifu siku ya Kiyama na nafsi yeyote haitadhulumiwa hata kidogo. Na hata kama ikiwa (jambo hilo lina) uzito mdogo wa chembe ya hardali nalo tutalileta. Nasi tunatosha kuwa wajuzi (wazuri kabisa) wa hisabu. [21:47]

Wale watakaokuwa na mizani nzito upande wa wema au wale ambao uzito wa mema yao utazidi uzito wa uovu wao, hawa watakuwa ni wenye kufaulu watastahiki pepo. Na wale ambao mizani itaonyesha kinyume chake, utakapokuwa umezidi uzito wa mema yao, hao watakuwa ni watu wa motoni kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿ فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٠٢﴾ وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ﴾

Ama wale ambao mizani ya amali zao (nzuri) itakuwa nzito,hao ndio wenye kufaulu. Na wale ambao mizani yao itakuwa nyepesi, hao ndio waliozitia hasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watakaa muda mrefu. [23:102-103]

Ukweli wa mambo ni kwamba, mizani anayo mtu katika maisha yake yote ya hapa ulimwenguni. Kila mja ameshajulishwa ni tabia ipi au mwenendo upi wa maisha akiufuata atafaulu hapa duniani na akhera, na ni tabia ipi au mwenendo upi wa maisha atakapoufuata mja utamhilikisha hapa duniani na huko akhera. Hivyo kila mja anao uwezo wa kukisia kuwa mizani yake itakuwaje kwa kuiangalia tabia yake jinsi anavyolandana na inavyopingana na utaratibu wa Sharia aliyoiweka Allah (s.w.). Makisio haya tutayafanya kwa kutumia mizani aliyotuletea Allah (s.w.) kama Qur'an inavyofufahamisha:

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ﴾

Kwa hakika Tuliwapeleka Mituma wetu kwa dalili wazi wazi na tukaviteremsha vitabu na mizani (ya mema na maovu) ili watu wasimamie uadilifu [57:25]

Hivyo kila mmoja anao uwezo wa kuiweka mizani yake ikaelemea upande unastahili kwa kulipima kila jambo analolifanya katik a maisha yake kwa mizani aliyoiweka Allah (s.w.) ya kuyaweka bayana mabaya na mazuri kisha mtu akajihukumu. Mafundisho tunayoyapata kutokana na Hadith ifuatayo:

Aysha amesimulia kuwa, alikuja mtu mmoja na kukaa mbele ya Mtume(s.a.w.w) na kuuliza: "Ewe Mtume(s.a.w.w) wa Allah nimeweka mkataba wa watumwa ambao wananikadhibisha na wananifanyia hila na kunidanganya na hawanitii, ninawakemea na kuwapiga.Niwafanyeje? Mtume(s.a.w.w) akasema: "Siku ya malipo itakapofika, hisabu itachukuliwa dhidi yao kiasi walichokuhadaa kwa hila, kiasi walichokataa kukutii na kiasi walichokughadhibisha. Kama adhabu uliyowapa (ya kuwakemea na kuwapiga) itakuwa ni sawa na makosa yao, sawa kwako na kwao, na kama adhabu uliyowapa itakuwa ni ndogo kuliko makosa yao, utaongezewa ufidie sehemu iliyobaki, na kama adhabu uliyowapa itazidi makosa yao basi itabidi fidia itoke (kwenye amali yako) kwkao uwape.". Yule mtu aligeuka pembeni na akaanza kusikitika na kulia. Kisha Mtume(s.a.w.w) akasema:" Hujasoma aya za Allah (s.w.):

﴿وَنَضَعُ الْمَوَازِينَ الْقِسْطَ لِيَوْمِ الْقِيَامَةِ فَلَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَإِن كَانَ مِثْقَالَ حَبَّةٍ مِّنْ خَرْدَلٍ أَتَيْنَا بِهَا وَكَفَىٰ بِنَا حَاسِبِينَ﴾

"Tutaweka mizani kwa uadilifu siku ya Kiyama na nafsi yoyote haitadhulumiwa hata kidogo na hata kama likiwa na uzito ndogo wa chembe yardali nalo tutalileta, Nasi tutatosha kuwa wajuzi wa kuhisabu". [21:47].

Yule mtu akasema: "Ewe Mtume wa Allah: Ninaona kuwa hapana jambo lililo bora zaidi kwangu mimi na kwa hawa watumwa, isipokuwa kuachana nao.Ninashuhudia mbele yako kuwa wote sasa wako huru". [Tirmidh]

Hadith inatupa fundisho kubwa kuwa, pamoja na mtu kukosewa, si vema kutoa hukumu kwani anaweza kutoa hukumu isiyolingana na kosa. Kwa ujumla Mtume (s.a.w.w) ametuusia kuwa tujihisabu wenyewe kabla hatujahisabiwa. Huku kujihesabu si lingine bali ni kutubu kikweli kweli kwa moyo mkunjufu kwa makosa yote mtu aliyoyafanya na kwa yale yote aliyoacha kuyatekeleza katika yale aliyoamrishwa. Na kurudisha haki ya aliyedhulumiwa hata kama ni punje moja iliyochukuliwa kwa makosa au kinyume na idhini yake, kumtaka msamaha kwa haki iliyochukuliwa, na wale walioumizwa kwa uonevu kwa ulimi au mkono. Kama mtu aliyefanya makosa haya atafariki bila ya kutubia na kuwaomba msamaha wale aliowakosea au kuwarudishia haki zao kama zinarudishika, atawakuta karibu na mizani katika siku ya hisabu wakidai haki zao na kushitaki: "Ulinigombeza (ulinikemea) bila ya sababu yoyote, ulinitukana, uliniteta, ulinifanyia ubaya ukiwa kama jirani, mtumishi, Rais, hukunihudumia ipasavyo nilipokuwa mgonjwa, ulinikuta nina njaa na hukunilisha na ilihali ulikuwa na uwezo, unilikuta nina kiu hukuninyeshwa, ulinikuta ni uchi hukunivisha, hukuondoa dhulma na ili hali ulikuwa na madaraka na kadhalika. Hapa Allah (s.w.) atasema:

﴿الْيَوْمَ تُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ لَا ظُلْمَ الْيَوْمَ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ﴾

"Leo kila nafsi italipwa kwa kila ilichokitanguliza.Hapana atakayedhulumiwa leo".[40:17]

Kwa muhtasari kutokana na haya tuliyojifunza juu ya Siku ya Kiyama mambo matano yafuatayo yamejitokeza:

Kwanza : hukumu itakuwa ya haki na kwamba hakuna mtu hata mmoja atakayedhulumiwa chochote kama Qur'an inavyosisitiza:

﴿الْيَوْمَ تُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ لَا ظُلْمَ الْيَوْمَ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ﴾

Leo kila mtu atapewa malipo ya yale aliyoyatenda, hakuna dhulma leo, bila shaka Allah ni Mwepesi kuhisabu. [40:17]

﴿إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ النَّاسَ شَيْئًا وَلَـٰكِنَّ النَّاسَ أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ﴾

Hakika Allah hawadhulumu watu chochote, lakini watu wanajidhulumu nafsi zao [10:44]

Pili : mambo yote siku hiyo yatakuwa wazi kiasi cha kuweza mtu kujihesabu mwenyewe

Tatu : kabla ya hukumu kwa kawaida hutakikana ushahidi. Ushahidi wa siku hiyo ni daftari la amali za mtu ambalo limedhibitiwa vyema na malaika waandishi hodari wa amali za waja kama tunavyofahamishwa katika Qur'an:

﴿مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴾

Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu naye yuko mngojeaji tayari (kuandika) [50:18]

﴿وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَافِظِينَ ﴿١٠﴾ كِرَامًا كَاتِبِينَ ﴿١١﴾ يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ﴾

Na hakika juu yenu kuna wenye kuwatunza (Malaika) watukufu wenye kuandika.Wanayajua yote mnayoyatenda.[82:10-12].

Nne : mashahidi siku hiyo ni viungo vyake mtu. Macho yatasema yalichokitazama kinyume na sheria ya Allah (s.w.), mikono itachoiba, miguu iliko kwenda na kadhalika. Maadam mtu hatendi jema wala ovu ila atatumia kiungo fulani cha mwili wake basi ajue hao ni mashahidi waadilifu ambao hawapokei rushwa, na ataitoa wapi rushwa siku hiyo? Tunafahamishwa katika Qur'an:

﴿يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ وَأَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yao na miguu yao kwa yale waliyokuwa wakifanya. [24:24]

﴿لْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰ أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ﴾

Siku hiyo tutaviziba vinywa vyao, itazungumza mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa yale waliyokuwa wakiyachuma. [36:65]

﴿وَمَا كُنتُمْ تَسْتَتِرُونَ أَن يَشْهَدَ عَلَيْكُمْ سَمْعُكُمْ وَلَا أَبْصَارُكُمْ وَلَا جُلُودُكُمْ وَلَـٰكِن ظَنَنتُمْ أَنَّ اللَّـهَ لَا يَعْلَمُ كَثِيرًا مِّمَّا تَعْمَلُونَ﴾

Na hamkuwa mkijificha hata masikio yenu na macho yenu na ngozi zenu zisiweze kutoa ushahidi juu yenu, bali mlidhani ya kwamba Allah hayajui mengi katika (hayo) mnayoyafanya. [41:22]

Tano : kutakuwa na mizani ya kupimia amali za waja. Mizani hii haitapima amali zenyewe bali thamani ya amali. Uzito siku hiyo utakuwa ni kweli na haki. Yaani kweli au haki ndivyo vitakavyokuwa na uzito. Allah (s.w.) amesema:

﴿وَالْوَزْنُ يَوْمَئِذٍ الْحَقُّ فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿٨﴾ وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُم بِمَا كَانُوا بِآيَاتِنَا يَظْلِمُونَ﴾

Na siku hiyo kipimo (uzito) kitakuwa ni haki. Basi watakaokuwa na uzani mzito, hao ndio watakaofaulu. Na watakaokuwa na uzani hafifu, basi hao ndio waliozitia hasarani nafsi zao kwa sababu ya kuzifanyia jeuri Aya zetu. [7:8-9]

"Na siku hiyo uzito utakuwa ni haki Msemo huu wa Allah (s.w.) una maana kuwa, siku ya Hukumu katika mizani ya haki, hakuna chochote isipokuwa Haki na Ukweli ndivyo vitakavyokuwa na uzito. Uzito utazidi au kupungua kulingana na ukweli utakaokuwa nao mja juu ya nafsi yake na atahukumiwa kwa kipimo cha ukweli huo na si kwa kitu kingine chochote. Maisha ya kinafiki na uasi hata kama yatakuwa marefu na hata kama mtu atakuwa amefanya mambo mengi ambayo yeye atadhani kuwa ni makubwa katika mizani ya Allah (s.w.) hayatakuwa na uzito wowote.