MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU 0%

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU Mwandishi:
Kundi: Vitabu mbali mbali

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi: NDUGU ZETU WA KISUNNI
Kundi:

Matembeleo: 44540
Pakua: 3490

Maelezo zaidi:

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 22 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 44540 / Pakua: 3490
Kiwango Kiwango Kiwango
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi:
Swahili

9

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Je, mtu hufuzu kwa amali zake au kwa rehema ya Mwenyezi Mungu? Kutokana na msisitizo mkubwa wa Qur'an wa kuwahimiza watu kufanya amali njema ili wafuzu huko Akhera, baadhi ya Wakristo mara nyingi huuliza: "Je, Wailsamu mnategemea kunusurika na adhabu kwa sababu tu ya vitendo vyenu na siyo kwa sababu tu ya huruma ya Mwenyezi Mungu kwenu? Ikiwa ni hivyo mtawezaji kuokoka?

Hapana shaka yoyote kuwa, katika mafundisho ya Uislamu ipo nafasi kubwa sana ya rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini rehema hiyo wanaipata wale tu wanaostahiki. Na wanaostahiki kuipata ni wale ambao pamoja na udhaifu wao wa kibinadamu wanajitahidi kadri ya uwezo wao kumtii Mola wao na wanaolipigania neno lake kwa hali na mali. Hivyo rehema hiyo haitolewi holela tu. Atakuwa ni mwislamu wa ajabu yule atakayewaambia wanafunzi wake: "Yeyote yule anaweza kufaulu na si muhimu kabisa kama anajitahidi kuhudhuria masomo au la, au kama anafanya mazoezi, ninayotoa au la, atafaulu kwa huruma yangu tu".

Uislamu unafundisha kuwa kumuamini Mwenyezi Mungu siyo kwa kusema tu; bali aisadikishe hiyo imani yake kwa kufanya aliyoamrishwa na Mola wake na kujiepusha na yale aliyomkataza. Lakini hata mja akifanya hivyo bado hatakiwi kujigamba na kujipiga kifua kuwa eti Pepo ni mali yake kwa sababu ya mambo kadhaa anayoyafanya. Bali aombe rehema ya Mola wake ili ayazidishe mema yake, na amghufirie makosa yake.

Watu wanapata wokovu kutokana na rehema ya Mwenyezi Mungu kwa sababu anaulipa uovu kwa uwiano wa moja kwa moja.Lakini anapoilipa amali njema huilipa malipo bora zaidi thamani ya amali hiyo. Mwenyezi Mungu anatufahamisha katika Qur'an:

﴿مَن جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ خَيْرٌ مِّنْهَا وَمَن جَاءَ بِالسَّيِّئَةِ فَلَا يُجْزَى الَّذِينَ عَمِلُوا السَّيِّئَاتِ إِلَّا مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

Atakayefanya mema atapata jaza bora kuliko huo (wema alioufanya) na atakayefanya ubaya, basi hawatalipwa wale wafanyao ubaya ule ila sawa na yale waliyokuwa wakiyafanya. [28:84]

﴿إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ وَإِن تَكُ حَسَنَةً يُضَاعِفْهَا وَيُؤْتِ مِن لَّدُنْهُ أَجْرًا عَظِيمًا﴾

Hakika Mwenyezi Mungu hawadhulumu (viumbe vyake hata kitu kilicho sawa na) uzito wa mdudu chungu, na kama likiwa ni jambo jema atalizidisha na kutoa ujira mkubwa unaotoka kwake. [4:40]

﴿وَهُوَ الَّذِي يَتَوَفَّاكُم بِاللَّيْلِ وَيَعْلَمُ مَا جَرَحْتُم بِالنَّهَارِ ثُمَّ يَبْعَثُكُمْ فِيهِ لِيُقْضَىٰ أَجَلٌ مُّسَمًّى ثُمَّ إِلَيْهِ مَرْجِعُكُمْ ثُمَّ يُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

Afanyaye kitendo kizuri,atalipwa mfano wake mara kumi. Na afanyaye kitendo kibaya hatalipwa ila sawa nacho tu (basi), Nao hawatadhulumiwa. [6:160]

Rehema hii ya Allah (s.w.) pia imetajwa katika Qur'an ifuatavyo:

﴿ذَٰلِكَ الَّذِي يُبَشِّرُ اللَّـهُ عِبَادَهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ قُل لَّا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِلَّا الْمَوَدَّةَ فِي الْقُرْبَىٰ وَمَن يَقْتَرِفْ حَسَنَةً نَّزِدْ لَهُ فِيهَا حُسْنًا إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ شَكُورٌ﴾

Hii ndiyo habari nzuri ambayo Mwenyezi Mungu anawaambia waja wake walioamini na kufanya vitendo vizuri. Sema: "Kwa haya (ninayokufundisheni) siombi, (sitaki) malipo yoyote kwenu; lakini (nataka) myapende mambo ya kukusogezeni (kwa Mwenyezi Mungu). Na anayefanya wema tutamzidishia wema; kwa hakika Mwenyezi Mungu ni mwingi wa msamaha, mwingi wa shukrani. [42:23]

﴿لِيَجْزِيَهُمُ اللَّـهُ أَحْسَنَ مَا عَمِلُوا وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ وَاللَّـهُ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴾

Ili Mwenyezi Mungu Awalipe (malipo) mazuri kwa yale waliyoyafanya na kuwazidishia katika fadhila zake, na Mwenyezi Mungu Humruzuku Amtakaye pasipo hisabu. [24:38]

Ni dhahiri kuwa, ili mtu aipate rehema hii ya Mwenyezi Mungu itabidi kwanza liwemo hilo jambo jema ambalo Allah (s.w.) atalizidisha. Ndiyo maana Mtume(s.a.w.w) amesema, mtu akitakiwa kutoa hisabu yake reja reja yaani kwa kuangalia kila kipengele kimoja kimoja, basi mtu huyo ameangamia. Hii ni kwa sababu watu wema hutoa hisabu ya jumla na mema yao hufuta makosa yao. Mwenyezi Mungu amesema:

﴿وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُكَفِّرَنَّ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ وَلَنَجْزِيَنَّهُمْ أَحْسَنَ الَّذِي كَانُوا يَعْمَلُونَ﴾

"Na walioamini na wakafanya vitendo vizuri, kwa yakini tutawasamehe maovu yao, na tutawalipa mema ya yale waliyokuwa wakiyafanya". [29:7]

Hivyo hisabu ya watu wema itakuwa nyepesi na ya waovu itakuwa nzito kama anavyozidi kututhibitishia Mwenyezi Mungu kwa kusema:

﴿فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ ﴿٧﴾ فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا﴿٨﴾وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ ﴿١٠﴾ فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا ﴾

"Ama atakayepewa daftari lake katika mkono wake wa kulia, basi Naye atahisabiwa hisabu nyepesi, lakini atakayepewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake, basi yeye atayaita mauti (yamjie ili afe apumzike, wala hayatamjia)". [84:7-8 na 10-11]

Hivyo lililo muhimu kwetu ni kujitahidi upeo wa uwezo wetu ili tustahili kupata rehema ya Mwenyezi Mungu, na tutakuwa tunajidanganya wenyewe iwapo tutaitaraji rehema hiyo kwa kuchapa usingizi tu.

Maisha ya Peponi Kabla hatujaeleza maisha ya Peponi yatakavyokuwa hebu tuangalie maana ya neno Jannat (Pepo) Jannat ilivyoelezwa katika Qur'an na Hadith ni Bustani nzuri zilizo na matunda na miti mizuri ya kila aina, yenye kupitwa na mito ya maji mazuri na matamu kuliko asali na meupe kuliko maziwa na yenye harufu nzuri kuliko miski. Pia ndani ya bustani hii nzuri isiyo na kifani ni yenye fenicha nzuri zisizo hadithika. Maelezo ya Qur'an na Hadith katika kuelezea uzuri wa pepo ni kama mfano tu kwani vipaji hivi vya fahamu tulivyo navyo ni vya hapa hapa duniani tu na havina uwezo kabisa kuyaingiza katika picha sahihi matukio yote ya maisha ya akhera. Katika maisha hayo ya akhera watu watakuwa na maumbile na vipaji vinavyolingana na maisha hayo na kila mja ataona na kuyahisi maisha ya huko kwa uhakika. Hivi ndivyo anavyotufahamisha Mtume(s.a.w.w) katika Hadith ifuatayo:

Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume wa Allah kasema:Allah (s.w.) kasema: Nimewaandalia waja wangu mema ambayo hapana jicho lililowahi kuona, na hapana sikio lililowahi kusikia, na hapana moyo wa mtu uliopata kufahamu (kufikiri). Na soma kama unapenda: "Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika hayo yanayofurahisha macho (huko Peponi) ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyafanya".

Kwa maana ya ujumla, neno Jannat limetumiwa katika lugha ya Kiislamu kama kielelezo cha mazingira mazuri katika maisha ya Akhera ambapo watu wema, walioishi hapa duniani kwa wema, kwa kufuata barabara kanuni za maisha ya kila siku kama zilivyowekwa na Allah (s.w.) wataishi milele kwa furaha na amani. Hebu tujaribu kupiga picha ya mazingira ya peponi kwa kutumia mifano iliyotolewa katika Qur'an na Hadith inayolingana na mazingira haya:

Abu Mussa amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema:"Hakika kwa waumini patakuwa na hema moja kubwa la lulu katika pepo. Upana wake (urefu wake) utakuwa maili sitini. Katika kila kona patakuwa na wakaaji ambao hawatawaona wengine. Waumini watayazungukia ambapo patakuwa na bustani mbili ambamo vyombo vyake vyote na kila kilichomo ndani yake kitakuwa cha dhahabu, na kati ya watu na uoni wao kwa Allah patakuwa na pazia ya utukufu wa uso wake itakavyoonekana katika Pepo ya daraja ya juu". [Bukhari na Muslim]

Hizi bustani nne zimeelezewa katika Qur'an katika aya zifuatazo:

﴿وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ﴾

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake atapata mabustani (Pepo) mawili. [55:46]

﴿وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ﴾

Na zaidi ya hizo yako mabustani mawili (mengine) [55:62]

Katika Hadith nyingine, tunafahamishwa kuwa Pepo imegawanywa kwa uzuri katika daraja mia moja na daraja ya juu ndio bora kuliko zote. Ubaidah bin Samit amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.w.) amesema:Pana milango mia moja katika Pepo. Umbali kati ya kila milango miwili ni kama umbali kati ya mbingu na ardhi,na Firdausi ndiyo yenye mlango ulio juu kabisa kuliko yote. Mito minne ya peponi inamiminika kutoka humo na juu yake ipo arshi. Kwa hiyo,unapomuomba Allah (akuruzuku pepo), muombe Firdausi. [Tirmidh]

Katika Qur'an tunapewa sifa za watu watakaofuzu kuingia katika Firdaus:

﴿قَدْ أَفْلَحَ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١﴾ الَّذِينَ هُمْ فِي صَلَاتِهِمْ خَاشِعُونَ ﴿٢﴾ وَالَّذِينَ هُمْ عَنِ اللَّغْوِ مُعْرِضُونَ ﴿٣﴾ وَالَّذِينَ هُمْ لِلزَّكَاةِ فَاعِلُونَ ﴿٤﴾ وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ ﴿٥﴾ إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ ﴿٦﴾ فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ ﴿٧﴾ وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ ﴿٨﴾ وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَوَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ ﴿٩﴾ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَ ﴿١٠﴾ الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴾

Hakika wamefuzu Waumini.Ambao katika sala zao huwa ni wanyenyekevu. Na ambao hujiepusha na mambo ya kipuuzi.Na ambao (nguzo ya) Zaka wanaitekeleza.Na ambao tupu zao wanazilinda. Isipokuwa kwa wake zao na kwa (wanawake) wale iliyomiliki mikono yao ya kuume (kulia). Basi hao ndio wasiolaumiwa.(Lakini) anayetaka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka (ya Mwenyezi Mungu). Na ambao amana zao na ahadi zao wanaziangalia wanazitekeleza).Na ambao Sala zao wanazihifadhi.Hao ndio warithi. Ambao watarithi Firdaus wake humo milele. [23:1-11]

Hali ya mazingira ya maisha ya wenyeji au wakazi wa peponi inafafanuliwa katika Hadith zifuatazo: Jabir anasimulia kuwa Mtume wa Allah (s.w.) amesema:Hakika wakazi wa peponi watakula na kunywa lakini hawatakuwa wanatema, wala kwenda haja ndogo au kubwa, wala kutokwa na uchafu puani. Waliuliza (Masahaba): Kitakuwaje chakula? Alijibu (Mtume s.a.w.w) kitabu kama utamu wa miski na watakuwa wamejazwa na Tasbihi na Tahmid kama walivyojaaliwa kupumua. [Muslim]

Abu Sayyid na Abu Hurairah wasimulia kuwa, Mtume (s.a.w.) amesema:Mwenye kunadi atanadi: Kwenu pana afya ya kudumu na daima hamtakuwa wagonjwa, na kwenu kuna maisha ya milele na hapana kufa, na kwenu kuna ujana unaoendelea na daima hamtazeeka, na kwenu mna neema ziendeleazo na daima hamtapungukiwa na mahitaji. [Muslim]

Pamoja na Hadith hizi, Qur'an inatuchorea picha ya maisha ya peponi pamoja na wakazi wake na sifa zitakazowawezesha kuingia humo. Hebu tuzingatie aya chache zifuatazo:

﴿إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ ﴿٥٥﴾ هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِئُونَ ﴿٥٦﴾ لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ ﴿٥٧﴾ سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ﴾

Kwa yakini watu wa Peponi leo wamo katika shughuli (zao), wamefurahi. Wao na wake zao wamo katika vivuli, wameegemea juu ya viti vya fahari. Watapata humu (kila namna ya) matunda na watapata watakavyovitaka.Salama (tu juu yao), ndio neno litokalo kwa Mola (wao) Mwenye Rehema. [36:55-58]

﴿قُلْ أَؤُنَبِّئُكُم بِخَيْرٍ مِّن ذَٰلِكُمْ لِلَّذِينَ اتَّقَوْا عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَأَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ وَرِضْوَانٌ مِّنَ اللَّـهِ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِالْعِبَادِ﴾

Sema: "Nikwambieni yaliyo bora kuliko hivyo?" Kwa ajili ya wamchao Allah ziko bustani kwa Mola wao, zipitazo mito mbele yake. Watakaa humo milele na wake (zao) waliotakaswa (na kila uchafu na kila ubaya). Na wana radhi ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu anawaona (wote) waja (wake). [3:15]

﴿أُولَـٰئِكَ لَهُمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهِمُ الْأَنْهَارُ يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ وَيَلْبَسُونَ ثِيَابًا خُضْرًا مِّن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَّكِئِينَ فِيهَا عَلَى الْأَرَائِكِ نِعْمَ الثَّوَابُ وَحَسُنَتْ مُرْتَفَقًا﴾

Hao watapata mabustani ya milele yanayopita mito (ya maji) mbele yake. Humo watapambwa kwa mavazi ya mikononi ya dhahabu na watavaa nguo za kijani za hariri laini na za hariri nzito; wanaegemea humo juu ya vitanda vilivyopambwa (makochi).Ni malipo mazuri yaliyoje hayo. Na mahali bora palioje hapo (Pa kupumzika) [18:31]

﴿إِنَّ اللَّـهَ يُدْخِلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ وَلُؤْلُؤًا وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ﴾

Hakika Mwenyezi Mungu atawaingiza wale walioamini na kufanya vitendo vizuri (katika) mabustani yapitayo mito mbele yake.humo watavishwa mapambo ya mikononi ya dhahabu na lulu, na mavazi yao humo yatakuwa hariri. [22:23]

﴿وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَا نُكَلِّفُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٤٢﴾ وَنَزَعْنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ تَجْرِي مِن تَحْتِهِمُ الْأَنْهَارُ وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي هَدَانَا لِهَـٰذَا وَمَا كُنَّا لِنَهْتَدِيَ لَوْلَا أَنْ هَدَانَا اللَّـهُ لَقَدْ جَاءَتْ رُسُلُ رَبِّنَا بِالْحَقِّ وَنُودُوا أَن تِلْكُمُ الْجَنَّةُ أُورِثْتُمُوهَا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴾

Na wale wanaoamini na kufanya vitendo vizuri - hatumkalifishi mtu yeyote ila kwa kiasi cha uweza wetu - hao ndio watu wa Peponi. Wao watakaa humo daima.Na tutaiondoa bughudha vifuani mwao (wawe wanapendana wote kweli kweli, mbele yao iwe inapoita mito. Na watasema (katika kushukuru kwao): Sifa zote njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu ambaye ametuongoza katika (neema) hizi. Na hatukuwa wenye kuongoka wenyewe kama asingetuongoza Mwenyezi Mungu. Mitume wa Mola wetu wameleta haki. Na watanadiwa (wataambiwa) ya kwamba: Hii ndiyo pepo mliyorithishwa kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyafanya". [7:42-43]

﴿إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿٤٥﴾ ادْخُلُوهَا بِسَلَامٍ آمِنِينَ ﴿٤٦﴾ وَنَزَعْنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ إِخْوَانًا عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ ﴿٤٧﴾ لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ﴾

"Na hakika wanaomcha Mwenyezi Mungu watakuwa katika Mabustani na chemchem (zinazoita mbele yao huko; waambiwe): "Yaingieni salama salimini (kwa salama na muwe katika amani)". Na tutaondoa mifundo iliyokuwa vifuani mwao, na (watakuwa) ndugu (wenye kupendana) (waliokaa) juu ya viti vya kifalme, wameelekeana (wanazungumza kwa furaha kubwa).Haitawagusa humo taabu wala pia humo hawatatolewa". [15:45-48]

﴿جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ وَلُؤْلُؤًا وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ ﴿٣٣﴾ وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي أَذْهَبَ عَنَّا الْحَزَنَ إِنَّ رَبَّنَا لَغَفُورٌ شَكُورٌ ﴿٣٤﴾ الَّذِي أَحَلَّنَا دَارَ الْمُقَامَةِ مِن فَضْلِهِ لَا يَمَسُّنَا فِيهَا نَصَبٌ وَلَا يَمَسُّنَا فِيهَا لُغُوبٌ﴾

"Bustani ya milele wataingia humo, humo watapambwa vikuku vya dhahabu, na lulu, na nguo zao humo zitakuwa za hariri. Na watasema (katika kushukuru kwao) "Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu Aliyetuondolea huzuni, kwa yakini Mola wetu ni Mwingi wa msamaha (na) Mwenye shukurani". Ambaye kwa fadhila zake ametuweka katika nyumba ya kukaa daima, humo haitugusi taabu wala humo hakutugusi kuchoka". [35:33-35]

﴿يَا عِبَادِ لَا خَوْفٌ عَلَيْكُمُ الْيَوْمَ وَلَا أَنتُمْ تَحْزَنُونَ ﴿٦٨﴾ الَّذِينَ آمَنُوا بِآيَاتِنَا وَكَانُوا مُسْلِمِينَ ﴿٦٩﴾ ادْخُلُوا الْجَنَّةَ أَنتُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ تُحْبَرُونَ ﴿٧٠﴾ يُطَافُ عَلَيْهِم بِصِحَافٍ مِّن ذَهَبٍ وَأَكْوَابٍ وَفِيهَا مَا تَشْتَهِيهِ الْأَنفُسُ وَتَلَذُّ الْأَعْيُنُ وَأَنتُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٧١﴾ وَتِلْكَ الْجَنَّةُ الَّتِي أُورِثْتُمُوهَا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٧٢﴾ لَكُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ كَثِيرَةٌ مِّنْهَا تَأْكُلُونَ﴾

"Enyi waja wangu (mlio wazuri) Hamtakuwa na hofu siku hiyo wala hamtahuzunika.(Waja wangu) ambao waliziamini aya zetu na walikuwa Waislamu kamili. Ingieni bustanini (peponi) nyinyi na wake zenu, mtafurahishwa (humo). Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe (vya dhahabu) na vitakuwemo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele. Na hii ni bustani (pepo) mliyorithishwa kwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.Muna (nyingi) humo matunda mengi mtakayoyala" [43:68-73]

﴿مَّثَلُ الْجَنَّةِ الَّتِي وُعِدَ الْمُتَّقُونَ فِيهَا أَنْهَارٌ مِّن مَّاءٍ غَيْرِ آسِنٍ وَأَنْهَارٌ مِّن لَّبَنٍ لَّمْ يَتَغَيَّرْ طَعْمُهُ وَأَنْهَارٌ مِّنْ خَمْرٍ لَّذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ وَأَنْهَارٌ مِّنْ عَسَلٍ مُّصَفًّى وَلَهُمْ فِيهَا مِن كُلِّ الثَّمَرَاتِ وَمَغْفِرَةٌ مِّن رَّبِّهِمْ كَمَنْ هُوَ خَالِدٌ فِي النَّارِ وَسُقُوا مَاءً حَمِيمًا فَقَطَّعَ أَمْعَاءَهُمْ﴾

Mfano wa pepo waliyoahidiwa wacha Mungu (itakuwa hivi): Imo mito ya maji yasiyovunda, na mito ya maziwa isiyoharibika ladha yake, na mito ya ulevi wenye ladha kwa wanywao, na mito ya asali iliyosafishwa, tena humo watapata matunda ya kila namna, na samahani kutoka kwa Mola wao. Basi hao watakuwa sawa na wale watakaokaa motoni, na kunyeshwa maji yachemkayo yatakayokata chango zao? [47:15]

﴿نَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَعِيمٍ ﴿١٧﴾ فَاكِهِينَ بِمَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَاهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ ﴿١٨﴾ كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿١٩﴾ مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَّصْفُوفَةٍ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ ﴿٢٠﴾ وَالَّذِينَ آمَنُوا وَاتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَانٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَا أَلَتْنَاهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَيْءٍ كُلُّ امْرِئٍ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ ﴿٢١﴾ وَأَمْدَدْنَاهُم بِفَاكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ ﴿٢٢﴾ يَتَنَازَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَّا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ ﴿٢٣﴾ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَّكْنُونٌ ﴿٢٤﴾ وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ﴿٢٥﴾ قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ ﴿٢٦﴾ فَمَنَّ اللَّـهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ ﴿٢٧﴾ إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ﴾

"Kwa yakini wamchao Mwenyezi Mungu watakuwa katika mabustani na neema. Wakifurahia yale Aliyowapa Mola wao, na Mola wao amewalinda na adhabu ya moto utakao (kwa nguvu kabisa). (Wataambiwa watu wema):"Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya hayo mliyokuwa mkiyatenda, watakuwa wameegemea juu ya viti vya fahari vilivyopangwa safu safu, na Tutawaoza wanawake wanaopendeza wenye macho ya vikombe (makubwa). Na wale walioamini na wakafuatwa na wazee wao na watoto wao katika imani. Tutawakutanisha nao hao jamaa zao, wala hatutawapunja kitu katika (thawabu) vitendo vyao, kila mtu atalipwa kwa kila alichokichuma. Na tutawapa (kila namna ya) matunda na (kila namna za) nyama, kama vile watakavyopenda.Watapeana humo gilasi (zilizojaa vinywaji) visivyoleta maneno ya upuuzi wala dhambi. Iwe wanawapitia watumishi wao (wanaopendeza) kama kwamba ni lulu zilizomo ndani ya chaza. Wataelekeana wao kwa wao wanauliza (wanazungumza).Waseme: "Tulikuwa zamani pamoja na watu wetu tukimuogopa (Mwenyezi Mungu). Basi Mwenyezi Mungu ametufanyia ihsani (ametutia peponi) na ametuokoa na adhabu ya pepo za moto". Hakika sisi zamani tulikuwa tukimuabudu yeye (tu Mwenyezi Mungu): Hakika Yeye Ndiye Mwema, Mwenye Rehema". [52:17-28]

﴿إِنَّ الْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا ﴿٥﴾عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا عِبَادُ اللَّـهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفْجِيرًا ﴿٦﴾ يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا ﴿٧﴾ وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا ﴿٨﴾ إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ اللَّـهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَاءً وَلَا شُكُورًا ﴿٩﴾ إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوْمًا عَبُوسًا قَمْطَرِيرًا ﴿١٠﴾ فَوَقَاهُمُ اللَّـهُ شَرَّ ذَٰلِكَ الْيَوْمِ وَلَقَّاهُمْ نَضْرَةً وَسُرُورًا ﴿١١﴾ وَجَزَاهُم بِمَا صَبَرُوا جَنَّةً وَحَرِيرًا ﴿١٢﴾ مُّتَّكِئِينَ فِيهَا عَلَى الْأَرَائِكِ لَا يَرَوْنَ فِيهَا شَمْسًا وَلَا زَمْهَرِيرًا ﴿١٣﴾ وَدَانِيَةً عَلَيْهِمْ ظِلَالُهَا وَذُلِّلَتْ قُطُوفُهَا تَذْلِيلًا ﴿١٤﴾ وَيُطَافُ عَلَيْهِم بِآنِيَةٍ مِّن فِضَّةٍ وَأَكْوَابٍ كَانَتْ قَوَارِيرَا ﴿١٥﴾ قَوَارِيرَ مِن فِضَّةٍ قَدَّرُوهَا تَقْدِيرًا ﴿١٦﴾ وَيُسْقَوْنَ فِيهَا كَأْسًا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا ﴿١٧﴾ عَيْنًا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلْسَبِيلًا ﴿١٨﴾ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيْتَهُمْ حَسِبْتَهُمْ لُؤْلُؤًا مَّنثُورًا ﴿١٩﴾ وَإِذَا رَأَيْتَ ثَمَّ رَأَيْتَ نَعِيمًا وَمُلْكًا كَبِيرًا ﴿٢٠﴾ عَالِيَهُمْ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضْرٌ وَإِسْتَبْرَقٌ وَحُلُّوا أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٍ وَسَقَاهُمْ رَبُّهُمْ شَرَابًا طَهُورًا ﴿٢١﴾ إِنَّ هَـٰذَا كَانَ لَكُمْ جَزَاءً وَكَانَ سَعْيُكُم مَّشْكُورًا ﴾

"Hakika watu wazuri watakunywa kinywaji kilichochanganyika na kafuri. (Hiyo kafuri) ni mto watakaokunywa waja wa Mwenyezi Mungu, watautiririsha mtiririsho ( mzuri namna watakavyo). (Watu hao ni hawa) wanaotimiza wajibu (wao) na wanaiogopa siku ambayo shari yake itaenea (sana). Na huwalisha chakula masikini na mayatima na wafungwa, na hali ya kuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho). (Husema wenyewe katika nyoyo zao wanapowapa chakula hicho): "Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu (tu) hatutaki kwenu malipo wala shukurani".Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu". Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema na furaha. Na atawajazia Mabustani (ya peponi) na maguo ya hariri, kwa sababu ya kusubiri (kwao). Humo wataegemea viti vya enzi, hawataona humo jua (kali) wala baridi (kali), Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yake yataning'inia mpaka chini.Na watapitishwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae. Vigae vya fedha, wamevijaza kwa vipimo. Na humo watanyweshwa kinywaji kilichochanganyika na tangawizi. Huo ni mto ulio humo (peponi) unaitwa Salsabili. Na watawazungukia (kuwatumikia) wavulana wasiochakaa, ukiwaona utafikiri ni lulu zilizotawanywa. Na utakapoyaona (yaliyoko) huko utaona neema (zisizo kuwa na mfano) na ufalme mkubwa. Juu yao wana nguo za hariri laini, za kijani kibichi na za hariri nzito. Na watavikwa vikuku vya fedha na Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa (Awaambie):"Hakika haya ni malipo yenu, na amali zenu zinakubaliwa" [76:5-22]

Hizi ni baadhi tu ya aya zinazotoa sifa za Peponi na sifa za wale wanaostahiki kuingia Peponi. Kwa ujumla kilele cha lengo la maisha ya mwanadamu ni kukutana na Allah (s.w.) akiwa radhi naye. "Ee Allah! Tuongoze katika njia iliyonyooka na tujaalie tuwe miononi mwa waja wako wema watakaostahiki kuingia peponi"