MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU 0%

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU Mwandishi:
Kundi: Vitabu mbali mbali

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi: NDUGU ZETU WA KISUNNI
Kundi:

Matembeleo: 44519
Pakua: 3484

Maelezo zaidi:

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 22 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 44519 / Pakua: 3484
Kiwango Kiwango Kiwango
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi:
Swahili

10

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MAISHA YA MOTONI

Moto umetumiwa katika Qur'an na Hadithi kuonyesha makazi mabaya watakaposhukia waovu, walioamua kumpinga Allah (s.w.) na kuendesha maisha yao ya hapa duniani kinyume na kanuni na taratibu alizoziweka Allah (s.w.). Maisha ya motoni ni kinyume na maisha ya peponi ambayo picha yake tumeshaiona. Hebu tuelekeze kamera yetu motoni na kupiga picha ya maisha ya huko. Kwanza kabisa tunafahamishwa na Qur'an kuwa motoni kuna daraja au milango saba.

﴿ وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوْعِدُهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٤٣﴾ لَهَا سَبْعَةُ أَبْوَابٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنْهُمْ جُزْءٌ مَّقْسُومٌ ﴾

"Na bila shaka Jahannam ndipo mahali pao walipoahidiwa Ina milango saba, na kwa kila mlango iko sehemu yao iliyogawanywa" [15:43-44]

Daraja hizi za moto zimepewa majina kama tusomavyo katika Qur'an: Jahannam: Jina hili limetumiwa katika aya nyingi za Qur'an kama jina la ujumla la maisha ya motoni. Hutwamah:

﴿كَلَّا لَيُنبَذَنَّ فِي الْحُطَمَةِ ﴾

"Moto wa kuvunja vunja - moto uliowashwa kwa ukali barabara". [104:4]

Moto mkali wa kuunguza [4:55]

Moto unaobabua. [74:26]

Moto mkali. Qur'an (26:9 na 102:6]

Moto uwakao kwa ukali. Qur'an (101:9]

Mioto hii itawaunguza wakosaji kulingana na makosa yao.

Kwa ujumla aina yoyote ya moto ulioandaliwa makafiri hata ukiwa na daraja ya chini namna gani, utakuwa ni mkali usiokifani na usiovumilika hata kwa muda mfupi sana kama Allah anavyotufahamisha:

﴿إِنَّهَا سَاءَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا ﴾

"Hakika hiyo (Jahannam) ni kituo kibaya na mahali (pabaya kabisa) pa kukaa (hata kwa muda mfupi) " [25:66]

Hebu tuone pia anavyotufahamisha Mtume(s.a.w.w) juu ya kiwango cha ukali wa adhabu ya motoni: Nuuman bin Bashir amesimulia kuwa, Mtume(s.a.w.w) amesema:Hakika atakayekuwa na adhabu nyepesi kabisa katika wakazi wa motoni atakuwa yule atakayekuwa na viatu vya moto. Kwa moto huu (wa nyayoni) utachemsha ubongo wake kama maji yachemkayo kwenye birika. Haitaonekana kuna mwenye adhabu kali kuliko hii, lakini hiki ndio kiwango cha chini kabisa cha adhabu .[Bukhari na Muslim]

Kwa ujumla moto wa adhabu aliouandaa Allah (s.w.) kwa watu waovu ni mkali sana wenye miale yenye kupanda juu kwa hasira. Moto huu umeunguzwa kwa ukali kwa muda wa miaka elfu moja mpaka ukabadilika kuwa mwekundu. Uliunguzwa tena kwa muda wa miaka mingine elfu moja mpaka ukabadilika kuwa mweupe. Kisha uliunguzwa tena kwa miaka mingine elfu moja mpaka ukabadilika kuwa mweusi. Hivi ndivyo tunavyofahamishwa katika Hadithi ifuatayo:Abu Hurairah amesimulia kutoka kwa Mtume (s.a.w.w) ambaye amesema: Moto uliunguzwa kwa muda wa miaka elfu moja mpaka ukawa mwekundu. Kisha uliunguzwa kwa muda mwingine wa miaka elfu moja mpaka ukawa mweupe. Tena uliunguzwa kwa mara nyingine kwa muda wa miaka elfu moja mpaka ukawa mweusi. Sasa ni mweusi tii. [Tirmidh]

Pia tunafahamishwa kuwa Jahannam kutakuwa shimoni kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo: Uthman bin Ghazwaan amesimulia: Imesimuliwa kwetu na Mtume(s.a.w.w) kuwa jiwe litatupwa kutoka ukingoni mwa moto. Litaendelea kuanguka kwa miaka sabini bila kufika chini. Naapa kwa jina la Allah kuwa itajazwa. Na tulifamishwa kuwa umbali katika kati ya milango miwili ya moto na mwendo wa siku arubaini na patakuja siku ambapo itajaa watu. [Muslim]

Humo ndani ya shimo la moto wa Jahannam patakuwa na mashimo (mabonde) na shimo baya kabisa kuliko yote ni "Jabal- Huzn", ambapo Jahannam yenyewe inaomba kukingwa na moto huo wa "Jabal-Huzn" mara sabiini kwa siku. Ndani ya mazingira ya motoni pia patakuwa na miti michungu, na miti maarufu kwa uchungu wake hujulikana kwa jina la "Zaquum". Tumefahamishwa katika Hadith kuwa: Ibn Abbas amesimulia kuwa Mtume (s.a.w.w) alisoma aya hii:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ ﴾

"Enyi mlioamini muogopeni Allah kama ipasavyo kumuogopa,wala msife isipokuwa mmeshakuwa Waislamu kamili". (3:102).

Mtume(s.a.w.w) alisema:Kama tone la Zaquum lingeanguka kwenye nyumba ya dunia hii, lingelitosha kuharibu vitu vyote wanavyovitumia wakazi wa dunia. Sasa itakuwaje kwa yule ambaye hicho kitakuwa ndio chakula chake? [Tirmidh]

Tunapata maelezo kamili ya mti wa Zaquum. Ambao umemea katikati ya Jahannam na watakaostahiki kuula katika aya zifuatazo:

﴿ أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ ﴿٦٢﴾ إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ ﴿٦٣﴾ إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ ﴿٦٤﴾ طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ ﴿٦٥﴾ فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ ﴿٦٦﴾ ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ ﴾

"Je, karibisho la namna hii silo bora au kupata mti wa Zuqquum? (Mti mchungu kabisa watakaolishwa watu wa motoni). Kwa yakini sisi tumeufanya ni adhabu ya (hao) madhalimu (wa nafsi zao). Hakika huo ni mti unaotoka (unaoota) katikati ya Jahannam. (Panda za) matunda yake (zinatisha) kama kwamba ni vichwa vya mashetani. Bila shaka wao watakula katika (mti) huo, na kwa huo wajaze matumbo (yao). Kisha bila shaka utawathubutikia, juu ya uchungu wa mti huo, mchanganyiko wa maji ya moto". [37:62-67]

Pia katika mazingira ya motoni patakuwa na nyoka na nge wakubwa wenye sumu kali ambao watakuwa wanauma wakazi wa humo kama sehemu ya adhabu yao kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo:

Abdullah bin Harith bin Jazin amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:"Kuna nyoka huko motoni wakubwa kama ngamia. Mmoja wao akikuuma mara moja, uchungu wake hubaki kwa miaka arobaini. Kuna nge huko motoni wakubwa kama nyumba. Mmoja wao atamuuma mtu na uchungu wake utabakia kwa muda wa miaka arobaini . [Ahmad]

Kwa vyovyote itakavyokuwa maisha ya motoni yatakuwa magumu sana kwa wakazi wake. Chakula chao kitakuwa cha moto wa kuunguza kila kitu tumboni, mavazi yao yatakuwa ya moto, kinywaji chao cha moto kitakachochemsha matumbo yao. Picha halisi ya mazingira ya motoni, maisha ya wakazi wake na sifa zitakazowafanya wastahiki kuingia humo, aya zifuatazo zinafafanua zaidi:

﴿وَقَالُوا أَإِذَا ضَلَلْنَا فِي الْأَرْضِ أَإِنَّا لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ بَلْ هُم بِلِقَاءِ رَبِّهِمْ كَافِرُونَ ﴿١٠﴾ قُلْ يَتَوَفَّاكُم مَّلَكُ الْمَوْتِ الَّذِي وُكِّلَ بِكُمْ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمْ تُرْجَعُونَ ﴿١١﴾وَلَوْ تَرَىٰ إِذِ الْمُجْرِمُونَ نَاكِسُو رُءُوسِهِمْ عِندَ رَبِّهِمْ رَبَّنَا أَبْصَرْنَا وَسَمِعْنَا فَارْجِعْنَا نَعْمَلْ صَالِحًا إِنَّا مُوقِنُونَ ﴿١٢﴾ وَلَوْ شِئْنَا لَآتَيْنَا كُلَّ نَفْسٍ هُدَاهَا وَلَـٰكِنْ حَقَّ الْقَوْلُ مِنِّي لَأَمْلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ ﴿١٣﴾ فَذُوقُوا بِمَا نَسِيتُمْ لِقَاءَ يَوْمِكُمْ هَـٰذَا إِنَّا نَسِينَاكُمْ وَذُوقُوا عَذَابَ الْخُلْدِ بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴾

"Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?" (Ndio) Bali wao hawakiri kwamba watakutana na Mola wao. Sema: "Atakufisheni malaika wa mauti aliyewakilishwa kwenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu".Na ungaliwaona waovu wakiinamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao, (na kusema): "Mola wetu! Tumekwishakuona na tumekwisha kusikia, basi turudishe tutafanya vitendo vizuri, hakika (sasa) tumeyakinisha.Na tungalitaka tungempa kila mtu uwongofu wake (kwa lazima kama tulivyowapa malaika, lakini binadamu amepewa nguvu ya kufanya alitakalo lililo jema na baya), lakini imehakikika kauli iliyotoka Kwangu: Kwa yakini nitaijaza Jahannam kwa wote hawa; majini na watu (ambao ni wabaya). "Basi ionjeni (adhabu) kwa sababu ya kusahau makutano ya siku yenu hii, na sisi tutakusahauni (humo motoni) na onjeni adhabu idumuyo kwa yale mliyokuwa mkiyatenda". [32:10-14]

﴿ إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا ﴿٢١﴾ لِّلطَّاغِينَ مَآبًا ﴿٢٢﴾ لَّابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا ﴿٢٣﴾ لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا ﴿٢٤﴾ إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا ﴿٢٥﴾ جَزَاءً وِفَاقًا ﴿٢٦﴾ إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا ﴿٢٧﴾ وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا ﴿٢٨﴾ وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا ﴿٢٩﴾ فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا ﴾

"Kwa hakika Jahannam inawangoja wabaya.Ni makazi ya maasi.Wakae humo dahari nyingi (karne baada ya karne) Hawataonja humo baridi (wala usingizi) wala kinywaji.Ila maji yachemkayo sana na usaha (wanalipwa) malipo yaliyo sawa (na amali zao).Hakika wao hawakuwa wakiogopa hisabu (ya Mwenyezi Mungu).Na wakikadhibisha aya zetu kukadhibisha (kukubwa kabisa). Na (hali ya kuwa) kila kitu tumekidhibiti kwa kukiandika. Basi onjeni (leo adhabu yangu). Nasi Hatutakuzidishieni (kitu) ila adhabu (juu ya adhabu) ". [78:21-30]

﴿وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ﴿٢٣﴾يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ﴿٢٤﴾ فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ﴿٢٥﴾ وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ ﴾

"Basi siku hiyo italetwa Jahannam.Siku hiyo mwanadamu atakumbuka,lakini kukumbuka huko kutamfaa nini? Atasema:"Laiti ningalitanguliza (wema) kwa ajili ya uhai wangu (huu wa leo)".Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu Kwake (Mwenyezi Mungu). Wala hatafunga yeyote jinsi ya kufunga Kwake (Mwenyezi Mungu) " [89:23-26]

Aya hizi kwa ujumla zimesisitiza kuwa, watakaostahiki adhabu ya motoni ni wanadamu na majini waovu ambao waliendesha maisha yao ya hapa duniani kwa kibri na kinyume na utaratibu aliouweka na kuuridhia Allah (s.w.). Kuhusu adhabu yenyewe itakavyokuwa tunafahamishwa katika aya zifuatazo:

﴿إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا سَوْفَ نُصْلِيهِمْ نَارًا كُلَّمَا نَضِجَتْ جُلُودُهُم بَدَّلْنَاهُمْ جُلُودًا غَيْرَهَا لِيَذُوقُوا الْعَذَابَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَزِيزًا حَكِيمًا ﴾

"Hakika wale waliozikataa Aya zetu, tutawaingiza katika moto. Kila ngozi zao itakapowiva, tutawabadilishia ngozi nyingine badala ya zile, ili wawe wanaonja (uchungu wa) adhabu (maisha). Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu (na Mwenye Hikima) " [4:56]

Hawa mahasimu wawili waliohasimiana kwa ajili ya Mola wao. Basi wale waliokufuru watakatiwa nguo za moto na yatamiminwa juu ya vichwa vyao maji yachemkayo.

﴿هَـٰذَانِ خَصْمَانِ اخْتَصَمُوا فِي رَبِّهِمْ فَالَّذِينَ كَفَرُوا قُطِّعَتْ لَهُمْ ثِيَابٌ مِّن نَّارٍ يُصَبُّ مِن فَوْقِ رُءُوسِهِمُ الْحَمِيمُ ﴿١٩﴾ يُصْهَرُ بِهِ مَا فِي بُطُونِهِمْ وَالْجُلُودُ ﴿٢٠﴾ وَلَهُم مَّقَامِعُ مِنْ حَدِيدٍ ﴿٢١﴾ كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا مِنْ غَمٍّ أُعِيدُوا فِيهَا وَذُوقُوا عَذَابَ الْحَرِيقِ ﴾

"Kwa (maji) hayo vitayayushwa vilivyomo matumboni mwao na ngozi zao (pia). Na kwa ajili yao (yatakuwapo) marungu ya chuma. Kila mara watakapotaka kutoka humo (adhabuni) kwa sababu ya uchungu watarudishwa humo na (kuambiwa): "Ionjeni adhabu ya kuungua".[22:19-22]

﴿وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ ﴿١٠٣﴾ تَلْفَحُ وُجُوهَهُمُ النَّارُ وَهُمْ فِيهَا كَالِحُونَ ﴿١٠٤﴾أَلَمْ تَكُنْ آيَاتِي تُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ فَكُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ ﴿١٠٥﴾ قَالُوا رَبَّنَا غَلَبَتْ عَلَيْنَا شِقْوَتُنَا وَكُنَّا قَوْمًا ضَالِّينَ ﴿١٠٦﴾ رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْهَا فَإِنْ عُدْنَا فَإِنَّا ظَالِمُونَ ﴿١٠٧﴾ قَالَ اخْسَئُوا فِيهَا وَلَا تُكَلِّمُونِ ﴾

"Na wale ambao mizani yao itakuwa nyepesi, hao ndio waliozitia hasarani nafsi zao, na katika Jahannam watakaa muda mrefu. Moto utababua (utaziunguza) nyuzo zao, nao watakuwa humo wenye kukenya (meno yao kwa adhabu).(Waambie): Je! Hazikuwa aya zangu mkisomewa na nyinyi mkizikadhibisha? Watasema:"Mola wetu: Tulizidiwa na ubaya wetu na tukawa watu wenye kutopea. Mola wetu! Tutoe humu (motoni, uturejeshe ulimwenguni, tukafanye amali nzuri), na tufanyapo tena bila shaka tutakuwa madhalimu (wa nafsi zetu kweli kweli). Atasema (Mwenyezi Mungu):"Hizikeni humo wala msinisemeshe (msiseme nami) ". [23:103-108]

﴿إِنَّ شَجَرَتَ الزَّقُّومِ ﴿٤٣﴾ طَعَامُ الْأَثِيمِ ﴿٤٤﴾ كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ ﴿٤٥﴾ كَغَلْيِ الْحَمِيمِ ﴿٤٦﴾ خُذُوهُ فَاعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَاءِ الْجَحِيمِ ﴿٤٧﴾ ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِهِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ ﴿٤٨﴾ ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ ﴿٤٩﴾ إِنَّ هَـٰذَا مَا كُنتُم بِهِ تَمْتَرُونَ ﴾

"Bila shaka mti wa Zaqquum, ni chakula cha (kuliwa na) maasi,(kwa umoto wake ni) kama shaba iliyoyayushwa; huchemka matumboni kama chemko la maji ya moto kabisa. (Kuambiwe):"Mkamateni (huyo asi) na mumtupie katikati ya Jahannam.Kisha mwagieni juu ya kichwa chake (aonje) adhabu ya maji ya moto. (Aambiwe): Onja! Ulikuwa (ukijidai kuwa) wewe ni mwenye nguvu, mhishimiwa, (onyesha leo nguvu zako).Hakika hii ndiyo ile (adhabu) mliyokuwa mkibishana (mkiitilia shaka) ". [44:43-50]

﴿ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ ﴿٥١﴾ لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ ﴿٥٢﴾ فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ ﴿٥٣﴾ فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ ﴿٥٤﴾ فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ ﴿٥٥﴾ هَـٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ ﴾

"Kisha nyinyi, mliopotea (na kukadhibisha) kwa yakini mtakula mti wa Mzaqquum, na kwa huo mtajaza matumbo (yenu).Na juu yake mtakunywa maji ya moto yanayochemka. Tena mtakunywa kama wanywavyo ngamia wenye kiu sana.(Na kila wakinywa kiu haiweshi). Hiyo ni karamu yao siku ya malipo". [56:51-56]

﴿هَـٰذَا وَإِنَّ لِلطَّاغِينَ لَشَرَّ مَآبٍ ﴿٥٥﴾ جَهَنَّمَ يَصْلَوْنَهَا فَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴿٥٦﴾ هَـٰذَا فَلْيَذُوقُوهُ حَمِيمٌ وَغَسَّاقٌ ﴿٥٧﴾ وَآخَرُ مِن شَكْلِهِ أَزْوَاجٌ ﴾

"Hivyo (ndivyo itakakavyokuwa).Na kwa hakika wale warukao mipaka, pa kurudia pao patakuwa pabaya: Jahannam - wataingia. Nayo ni matengenezeo mabaya kabisa.(Ndivyo hivyo itakavyokuwa). Basi waonje (wanywe) maji ya moto na usaha. Na (adhabu) nyingine za namna hii nyingi.(Kila likitiwa jeshi jingine huko motoni waambiwe wale waliotangulia". [38:55-58]

﴿وَلِلَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ ﴿٦﴾ إِذَا أُلْقُوا فِيهَا سَمِعُوا لَهَا شَهِيقًا وَهِيَ تَفُورُ ﴿٧﴾ تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ الْغَيْظِ كُلَّمَا أُلْقِيَ فِيهَا فَوْجٌ سَأَلَهُمْ خَزَنَتُهَا أَلَمْ يَأْتِكُمْ نَذِيرٌ ﴿٨﴾ قَالُوا بَلَىٰ قَدْ جَاءَنَا نَذِيرٌ فَكَذَّبْنَا وَقُلْنَا مَا نَزَّلَ اللَّـهُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ كَبِيرٍ ﴿٩﴾ وَقَالُوا لَوْ كُنَّا نَسْمَعُ أَوْ نَعْقِلُ مَا كُنَّا فِي أَصْحَابِ السَّعِيرِ ﴿١٠﴾ فَاعْتَرَفُوا بِذَنبِهِمْ فَسُحْقًا لِّأَصْحَابِ السَّعِيرِ ﴾

"Na kwa waliomkufuru Mola wao iko adhabu ya Jahannam (inawaongojea). Na ni marejeo mabaya yaliyoje: Watakapotupwa humo watasikia rindimo (mngurumo) lake, na hali ya kuwa inafoka. Unakaribia kupasuka kwa hasira (yake juu ya wabaya).Kila mara litakapotupwa humo kundi (la wabaya) walinzi wake watawauliza: Je! Hakukufikieni mwonyaji? Watasema: Kwanini? Alitujia muonyaji, lakini tulikadhibisha na tulisema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote, nyinyi hamumo ila katika upotofu (upotevu) mkubwa. Na watasema: Kama tungalikuwa tunasikia au tungalikuwa na akili tusingalikuwa katika watu wa motoni (leo). Watakiri dhambi zao; (lakini hapana faida).Basi kuangamia kumewastahikia watu wa motoni". [67:6-11]

﴿إِنَّهُ مَن يَأْتِ رَبَّهُ مُجْرِمًا فَإِنَّ لَهُ جَهَنَّمَ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ﴾

Hakika atakayekuja kwa Mola wake, hali ya kuwa mkosa, basi kwa yakini atapata moto wa Jahannam, hatakufa humo wala hataishi (maisha mazuri). [20:74]

﴿فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ﴾

Basi siku hiyo hataadhibu yoyote namna ya kuadhibu Kwake(Mwenyezi Mungu). [89:25]

Aya hizi chache zimetupa picha ya kutisha ya maisha ya Motoni ambapo wakazi wake hawatakuwa na hata chembe ya furaha na hawatakufa japo watatamani wafe. Na hasara kubwa zaidi watakayoipata ni kutomuona Allah (s.w.). Kwani kumuona Allah (s.w.) ni kilele cha furaha na ilihali watu wa motoni wameharamishwa hata chembe ya furaha. Kwa ujumla marejeo ya motoni ni marejeo mabaya kabisa na kila mja mwema hana budi daima aombe:

﴿وَالَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا اصْرِفْ عَنَّا عَذَابَ جَهَنَّمَ إِنَّ عَذَابَهَا كَانَ غَرَامًا ﴿٦٥﴾ إِنَّهَا سَاءَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا﴾

"Mola wetu: Tuondolee adhabu ya Jahannam, bila shaka adhabu yake ni yenye kuendelea. Hakika hiyo (Jahannam) ni kituo kibaya na mahali (pabaya kabisa) pa kukaa (muda mfupi au mrefu). [25:65-66]

11

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MAANANA YA KUAMINI SIKU YA MALIPO KATIKA MAISHA YA KILA SIKU

Muumini wa kweli wa Siku ya Mwisho ni yule atakaye jitahidi kwa jitihada zake zote kufanya yafuatayo:

1. Kufanya wema kwa kadiri ya uwezo wake ili apate radhi za Allah (s.w) ili astahiki kupata makazi mema katika maisha ya akhera.

Huingia katika biashara na Allah (s.w):

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا هَلْ أَدُلُّكُمْ عَلَىٰ تِجَارَةٍ تُنجِيكُم مِّنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ ﴿١٠﴾ تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَتُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ بِأَمْوَالِكُمْ وَأَنفُسِكُمْ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١١﴾ يَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَيُدْخِلْكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ وَمَسَاكِنَ طَيِّبَةً فِي جَنَّاتِ عَدْنٍ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ﴿١٢﴾ وَأُخْرَىٰ تُحِبُّونَهَا نَصْرٌ مِّنَ اللَّـهِ وَفَتْحٌ قَرِيبٌ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ﴾

Enyi mlioamini! Je! Nikujulisheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo? (Basi biashara yenyewe ni hii):- Muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na piganieni dini ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu, haya ni bora kwenu; ikiwa mnajua (kuwa ni bora, basi fanyeni).(Mkifanya haya) Atakusameheni dhambi zenu na atakuingizeni katika Mabustani yapitayo mito mbele yake na (atakupeni) maskani mazuri mazuri katika Bustani za milele: huku ndiko kufuzu kukubwa. Na (atakupeni) kingine mnachokipenda: Nayo ni nusura itokayo kwa Mwenyezi Mungu na ushindi ulio karibu! Na wapashe habari njema waumini (61:10 -13)

﴿إِنَّ اللَّـهَ اشْتَرَىٰ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ أَنفُسَهُمْ وَأَمْوَالَهُم بِأَنَّ لَهُمُ الْجَنَّةَ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَيَقْتُلُونَ وَيُقْتَلُونَ وَعْدًا عَلَيْهِ حَقًّا فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ وَالْقُرْآنِ وَمَنْ أَوْفَىٰ بِعَهْدِهِ مِنَ اللَّـهِ فَاسْتَبْشِرُوا بِبَيْعِكُمُ الَّذِي بَايَعْتُم بِهِ وَذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ﴾

Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata Pepo. Wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu - wanauwa na wanauwawa. Hii ni ahadi aliyo jilazimisha kwa Haki katika Taurati na Injili na Qur'ani.Na nani atimizae ahadi kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa biashara yenu mliyo fanya naye. Na huko ndiko kufuzu kukubwa, (9: 111)

2. Kujiepusha na maovu kwa kadiri ya uwezo wake na kila mara kuleta Istighfar na dua, kumuomba Mola wake amuepushe na adhabu ya akhera. Katika Qur-an tunafahamishwa waja wa Rahman (Waumini wa kweli) ni wale waombao:

﴿وَالَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا اصْرِفْ عَنَّا عَذَابَ جَهَنَّمَ إِنَّ عَذَابَهَا كَانَ غَرَامًا ﴿٦٥﴾ إِنَّهَا سَاءَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا﴾

"Mola wetu tuondolee adhabu ya Jahannam, bila shaka adhabu yake ni yenye kuendelea. Hakika hiyo (Jahannam) ni kituo kibaya na mahali (pabaya kabisa) pa kukaa" (25:65-66)

3. Kuleta toba ya kweli atakapoteleza kwa kufanya jambo lolote lile kinyume na radhi ya Allah (s.w). Mwenyewe Allah (s.w) anatuamrisha:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللَّـهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا عَسَىٰ رَبُّكُمْ أَن يُكَفِّرَ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَيُدْخِلَكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ﴾

"Enyi mlioamini! Tubuni kwa Allah toba ya kweli, huenda Mola wenu Atakufutieni maovu yenu na kukuingizeni katika pepo zipitazo mito mbele yake,.." (66:8)

﴿وَاسْتَغْفِرُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴾

"Na ombeni msamaha kwa Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa Kurehemu." (73:20)

﴿إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يُبَدِّلُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٠﴾ وَمَن تَابَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَإِنَّهُ يَتُوبُ إِلَى اللَّـهِ مَتَابًا﴾

Allah (s.w) ameahidi kuwasamehe wale watakao leta toba ya kweli kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo: Ila yule atakayetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri; basi hao ndio Mwenyezi Mungu atawabadilishia maovu yao kuwa mema; na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu. Na aliyetubia na kufanya wema, basi kwa hakika yeye anatubu kweli kweli kwa Mwenyezi Mungu.(25:70-71)

﴿ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ عَمِلُوا السُّوءَ بِجَهَالَةٍ ثُمَّ تَابُوا مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ وَأَصْلَحُوا إِنَّ رَبَّكَ مِن بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

Kisha hakika Mola wako kwa wale waliofanya ubaya kwa ujinga, kisha wakatubia baada ya hayo na wakatenda mema; bila shaka Mola wako baada ya hayo ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu (16:119)

﴿وَإِذَا جَاءَكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِآيَاتِنَا فَقُلْ سَلَامٌ عَلَيْكُمْ كَتَبَ رَبُّكُمْ عَلَىٰ نَفْسِهِ الرَّحْمَةَ أَنَّهُ مَنْ عَمِلَ مِنكُمْ سُوءًا بِجَهَالَةٍ ثُمَّ تَابَ مِن بَعْدِهِ وَأَصْلَحَ فَأَنَّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴾

Na (wewe Mtume) wanapofika wale wanaoamini Aya zetu(na hali wamekosa kidogo; wanakuja kutubia) waambie "Amani iwe juu yenu, Mola wenu amejilazimisha rehema, kwamba atakayefanya miongoni mwenu uovu kwa ujinga, Mwenyezi Mungu atamghufiria kwani yeye ni Mwingi wa Rehema. (6:54)

﴿قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴾

Sema,"Enyi waja wangu mliojidhulumu nafsi zenu! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu; bila shaka Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote; hakika yeye ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu." (39:53)

Kutokana na aya hizi, tunajifunza kuwa toba ya kweli itapatikana kwa kuzingatia masharti yafuatayo:

1. Mwenye kuleta toba awe amefanya kosa kwa ujinga au kwa kutelezeshwa na vishawishi vya mazingira ya kishetani bila ya kudhamiria.

2. Baada ya kutanabahi kuwa amemuasi Mola wake, Muumini wa kweli atajuta na kuilaumu nafsi yake, na kulalama kwa Mola wake, kama walivyolalama wazazi wetu, Adam(a.s) na Hawwa (r.a):

﴿قَالَا رَبَّنَا ظَلَمْنَا أَنفُسَنَا وَإِن لَّمْ تَغْفِرْ لَنَا وَتَرْحَمْنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴾

"Mola wetu!Tumedhulumu nafsi zetu, na kama hutatusamehe na kuturehemu,bila shaka tutakuwa miongoni mwa wenye khasara." (7:23)

Pia katika Hadithi iliyosimuliwa na Abubakar Swidiq (r.a) na kukubaliwa na Maimamu wote wa hadith, Mtume (s.a.w) ametufundisha kuleta majuto moyoni mwetu kwa kuomba: "Ewe Mwenyezi Mungu! Hakika nimedhulumu nafsi yangu dhulma kubwa.Hapana yeyote mwenye kusamehe dhambi isipokuwa wewe tu.Basi nakuomba unipatie msamaha utukao kwako na unihurumie.Hakika wewe ni Msamehevu, Mrehemevu."

3. Kuazimia moyoni kuacha maovu.

4. Iwapo makosa yake yamehusiana na kudhulumu haki za watu, itabidi awatake radhi wale aliowakosea na kuwarejeshea haki zao zile zinazorejesheka.

5. Kuzidisha kufanya amali njema kwa kuzidisha kutoa sadaqa, kuzidisha kuleta swala na funga za sunnah, na kuzidisha juhudi ya kupigania dini ya Allah kwa mali na nafsi. Rejea Qur-an (61:10-13) na (9:111).

Shufaa Ni muhimu baada ya mada hii ya "maana ya kuamini siku ya mwisho", tuiangalie shufaa kwa mtazamo wa Kiislamu. Ni muhimu kwa sababu imetokea kwa baadhi ya watu wanaoitakidi kuwa ni waumini, kwa kupenda kwao njia ya mkato, wanaacha kutekeleza wajibu wao wa kuishi kama anavyotakiwa kuishi muumini wa kweli na badala yake wanaendesha maisha yao ya kila siku kama wafanyavyo makafiri na wakati huo huo wanamatumaini makubwa ya kupata neema za peponi kwa njia ya shufaa.

Maana ya Shufaa: Kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah shufaa ni uombezi wa watu wema kuwaombea msamaha watu watakaokuwa katika hali ya udhalili katika maisha ya akhera ili Allah (s.w) awatoe katika hali hiyo ya udhalili na kuwapeleka katika hali bora. Patakuwa na shufaa ya:

(i) Kuwaombea watu hisabu nyepesi na wachukue muda mfupi katika hisabu.

(ii) Kuwaombea waja wema waingie peponi moja kwa moja bila ya hisabu ili kuepukana na mazito ya siku ya Hisabu.

(iii) Kuwaombea waingizwe peponi wale ambao mizani ya mema na mabaya yao imekuwa sawa sawa.

(iv) Kuwaombea watu watolewe kutoka motoni na waingizwe peponi.

(v) Kuwaombea watu wema wapandishwe daraja katika Pepo; watolewe katika pepo ya daraja ya chini na kupandishwa katika pepo ya dara ya juu.

Masharti ya Shufaa: Pamoja na shufaa kuwepo katika siku hiyo ya malipo, Uislamu hauichukulii shufaa kwa mtazamo wa kikristo au mtazamo wa dini nyingine, ambapo hao watakaoshufaia wameitakidiwa kuwa watakuwa na uwezo wa kuwaokoa watu na adhabu ya Allah (s.w) na kuwaingiza Peponi. Katika Qur-an tunafahamishwa kuwa Shufaa haitafanyika ila kwa idhini ya Allah (s.w). Ni lazima kwanza Allah (s.w) aridhike kuwa mkosaji anastahiki ndio atoe ruhusa ya shufaa kwa yule aliyemridhia na kisha baada ya msamaha huo kuombwa ni khiari yake Allah (s.w) kusamehe au kutosamehe. Msimamo huu juu ya shufaa umewekwa bayana katika Qur-an:

﴿مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ﴾

" Nani huyo awezaye kushufaia mbele yake (Allah) bila ya idhini yake?" (2:255)

"Na wako Malaika wangapi mbingu ni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia." (53:26). Pia rejea Qu r-an (6:51, 10:3, 19:87, 39:44, 43:86 na 74:48).

Kwa ujumla shufaa ni rehema ya Allah (s.w) atakayo ikunjua kwa wale watakaostahiki kuipata kutokana na jitihada zao za kutenda mema hapa duniani kwa ajili ya Allah (s.w) japo wakati mwingine wanaweza kutekeleza na kumuasi. Muumini wa kweli wa siku ya malipo atajitahidi kwa kadri ya uwezo wake kutenda mema kwa ajili ya Allah (s.w), kujiepusha na maovu kwa kuchelea ghadhabu za Allah (s.w) na kuomba maghfira kwa haraka haraka kila atakapomkosea Allah (s.w) au kumkosea mwanaadamu mwenziwe. Udhaifu utakaompitia muumini huyu, Allah (s.w) atamsamehe kwa njia mbali mbali na hii ya kuombewa shufaa ikiwa ni mojawapo.

Nani watakao shufaia? Watakaoombea waumini shufaa kama tulivyoona katika aya zilizotangulia ni pamoja na Malaika, Mitume, watu wema ikiwa ni pamoja na watoto wachanga na amali njema kama Swala, Swaumu, Qur-an, n.k. Wa kwanza kushufai katika siku ya kutisha, siku ya Kiyama atakuwa ni Mtume(s.a.w.w) kama tunavyofahamishwa katika hadith nyingi. Baada ya Hukumu kupita,Mitume watawaombea shufaa miongoni mwa wafuasi wao ambao watakuwa wamehukumiwa kuingia motoni. Pia waumini watakoingia Peponi watapewa fursa ya kuwaombea shufaa waumini wenzao ambao kwa njia moja au nyingine walifeli mtihani na ikabidi waingie motoni.

Hebu tuzingatie hadith zifuatazo: Uthman bin Affan amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) kasema: "Watatu watashufaia katika siku ya Kiyama: Mitume, kisha wanachuoni, kisha waliokufa mashahidi". (Ibn Majah). Abu Sayyid amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:Kati ya Umma wangu patakuwa na watakaoshufaia makundi mengi ya watu kati yao kuna watakaoomba shufaa kwa kabila (moja) na kati yao kuna wakaoomba shufaa ya mtu mmoja, mpaka wangie Peponi." (Tirmidh)

Anas kasema: Wakazi wa motoni watapangwa katika mistari, kisha mmoja wa wakazi wa Peponi atawapitia. Mmoja katika wao atasema: Ewe Fulani, hunitambui?Nilikuwa yule niliyekupa maji. Na wengine watasema: Tulikuwa ni wale tuliyekupa maji ya kutawadhia. Hivyo atamuombea (kila mmoja) kwa Allah (s.w) na kumwingiza peponi. (Ibn Majah). Abu Sayyed al-Khudry amesimulia kuwa Mtume(s.a.w.w) amesema:"Kila mwenye imani uzito wa hardali (atom weight) atatolewa motoni". (Tirmidh).

Jambo la kuzingatia na kusisitiza sana hapa ni kwamba shufaa haitaombwa kwa misingi ya udugu, ukoo, utaifa au kwa misingi ya upendeleo wa aina yeyote, bali itajuzu tu kwa wale Allah (s.w) atakaoridhia waombewe na akatoa idhini juu ya kuombewa kwao. Kwa maana nyingine shufaa itategemeana na matendo mema ya mtu aliyoyatanguliza. Mitume watashufaia wafuasi wao waliowafuata kwa uadilifu, watu wema watawashufaia jamaa zao, jirani zao, rafiki zao, wananchi wenzao, waliowatendea wema kwa ajili ya wema wao, watoto wadogo wawashufaia wazazi wao waliokuwa wema kwao, n.k. Shufaa hizi zitapata ruhusa na kukubaliwa tu iwapo wale wanaoombewa walikuwa waumini ambao kwa njia moja au nyingine waliteleza na kumuasi Allah na wakastahiki kuwa katika hali hiyo ya dhiki. Kwa kafiri au mushriki shufaa ya aina yeyote haitakubaliwa hata kama shufaa hiyo itaombwa na Mitume au vipenzi vya Allah (s.w). katika Qu-an tumeona kukataliwa kwa maombi ya Nabii Muhu juu ya mwanawe aliyestahiki kuangamizwa pamoja na walioangamizwa kwa ukafiri wao:

"Ikiwa hiyo (jahazi) inakwenda nao katika mawimbi kama milima. Na Nuhu akamwita mwanawe aliyekuwa mbali (kakataa kuingia jahazini): "Ewe mwanangu!Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri". Akasema (huyo mtoto): "Nitaukimbilia mlima utakaonilinda na maji". Akasema (Nuhu): "Hakuna leo kulindwa na amri ya Mwenyezi Mungu isipokuwa yule atakayemrehemu (Mwenyezi Mungu)". Mara mawimbi yakaingia baina yao na akawa miongoni mwa waliogharikishwa. Na (baada ya kuangamizwa wote na vyote alivyotaka Mwenyezi Mungu viangamie) ikasemwa:P "Ewe ardhi: Meza maji yako. Na ewe Mingu jizuie (na kuteremsha mvua). Basi maji yakadidimia chini na amri ikapitishwa (ya kuangamizwa makafiri), na (jahazi) likasimama juu ya (jabali linaloitwa) Judi.Na ikasemwa likasimama juu ya (jabali linaloitwa) Judi. Na ikasemwa "Wameangamiliziwa mbali madhalimu"

Na Nuhu alimwomba Mola wake (alipomwona mwanawe anaangamia) akasema:

﴿ وَنَادَىٰ نُوحٌ رَّبَّهُ فَقَالَ رَبِّ إِنَّ ابْنِي مِنْ أَهْلِي وَإِنَّ وَعْدَكَ الْحَقُّ وَأَنتَ أَحْكَمُ الْحَاكِمِينَ ﴿٤٥﴾قَالَ يَا نُوحُ إِنَّهُ لَيْسَ مِنْ أَهْلِكَ إِنَّهُ عَمَلٌ غَيْرُ صَالِحٍ فَلَا تَسْأَلْنِ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِنِّي أَعِظُكَ أَن تَكُونَ مِنَ الْجَاهِلِينَ﴾

"Ewe Mola wangu! Mwanangu ni katika watu wa nyumbani kwangu (mbona anaangamia)? Na hakika ahadi yako ni haki; nawe ni Mwenye haki kuliko mahakimu (wote): Akasema (Mwenyezi Mungu): Ewe Nuhu! Huyu si miongoni mwa watu wako. Yeye ni (mwenye) mwendo usiokuwa mzuri. Basi usiniombe ambayo huyajui Mimi nakunasihi usiwe miongoni mwa wajinga" (11:45-46)

Pia tunafahamishwa katika Hadith jinsi Nabii Ibrahim (a.s) atakavyokataliwa maombi yake kwa Allah (s.w) kumuombea baba yake Azar aepushwe na adhabu kali waliyoandaliwa washirikina: Abu Hurairah amesimulia kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) aliyesema: Ibrahim atakutana na baba yake. Azar katika siku ya Kiyama. Uso wa Azar utakuwa umefunikwa na lami na mavumbi.

Ibrahimu atamsemesha: "Sikukuambia kuwa usiache kunitii (usinikadhibishe)?" Baba yake atamjibu: "Leo sitaaacha kukutii". Ibrahim ataomba: Ewe Mola! Hakika umeniahidi kuwa hutanifedhehesha siku watakapofufuliwa watu.Sasa ni fedheha gani zaidi kuliko kuwekwa mbali na baba yangu? Allah (s.w) atasema: Hakika Nimeiharamisha Pepo kwa Washirikina. Kisha itasemwa kwa Ibrahimu: Angalia ni kitu gani kilichoko miguuni mwako. Ataangalia, hamaki: shingo kubwa itatokeza. Ataburuzwa (Azar) kwa miguu yake na kutupiwa motoni. (Bukhari)

Vile vile tukirejea tena Qur-an tunaona jinsi Mtume(s.a.w.w) alivyokataliwa maombi yake alipowaombea wanafiki:

﴿اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَهُمْ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ﴾

Waombee msamaha au usiwaombee.Hata ukiwaombea msamaha mara sabiini,Mwenyezi Mungu hatawasamehe. Hayo ni kwa sababu ya kuwa wao wamemkataa Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wapotofu.(9:80)

Hivyo kutokana na maelezo haya, tumeona kuwa shufaa itakuwepo, lakini itawanufaisha tu walioamini na sio makafiri, washirikina na wanafiki. Jambo muhimu kwa Muislamu ni kujitakasa kwa kutenda mema na kuacha maovu na kuwa mwepesi na kurejea kwa Allah (s.w) kwa toba baada ya Kumkosea au kuhisi Kumkosea. Si vyema kwa Muislamu kuzembea katika kufanya mema na kuendelea kufanya maovu kwa matarajio ya kupata shufaa ya Mtume(s.a.w.w) au ya yeyote yule amtegemeaye kuwa atamshufaia. Kuna mambo mawili muhimu ya kuzingatia kwa wale wanaoacha kujitahidi kutekeleza wajibu wao kama anavyoridhia Allah (s.w) na badala yake wakaishi watakavyo kwa tegemeo la kupata uokovu kutokana na shufaa:

Kwanza kutegemea shufaa ni jambo la kubahatisha mno, kwani si jambo lililoko kwenye mamlaka ya yeyote isipokuwa Allah (s.w) pekee. Pili, shufaa nyingine itakuja baada ya mja kuadhibiwa kwanza, adhabu ambayo ni kali mno, inayodhalilisha au kuhilikisha hata kama mja atakaa humo muda mfupi sana. Ni vyema tuzingatie sana aya ifuatayo:

﴿فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ﴾

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu Kwake (Allah) (89:25)

Hivyo, jambo la busara ni Muislamu kujitahidi kuepukana na adhabu kali ya Allah (s.w) aliyowaandalia watu maasi na badala yake ayaendee kwa juhudi kubwa iliyoambatana na subira na yale yatakayompelekea kustahiki kuingizwa peponi moja kwa moja.