MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU 0%

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU Mwandishi:
Kundi: Vitabu mbali mbali

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi: NDUGU ZETU WA KISUNNI
Kundi:

Matembeleo: 44190
Pakua: 3347

Maelezo zaidi:

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 22 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 44190 / Pakua: 3347
Kiwango Kiwango Kiwango
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Mwandishi:
Swahili

5

MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

MAFUNDISHO YA MITUME

Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s.w).Dalili zinazodhihirisha kuwepo Allah (s.w) katika eneo hili ni pamoja na:

(a) Umoja wa ujumbe wa mitume

(b) Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

(c) Upeo wa elimu waliyokuwa nayo mitume.

(a)Umoja wa Ujumbe wa Mitume

Kitu kinachodhihirisha kuwa Mitume ambao baadhi yao ulimwengu mzima una shuhudia historia yao, kama vile historia ya Nabii Ibrahim (a.s), Musa(a.s) , Isa(a.s) na Muhammad(s.a.w.w) kuwa ni wajumbe kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) wenye ujuzi na hekima, ni kule kufanana kwa ujumbe wao. Kama dhana ya kutokuwepo Mwenyezi Mungu (s.w) ingelikuwa kweli, ingelikuwa muhali kwa Mitume waliotokea sehemu tofauti nyakati tofauti, kutoa ujumbe unaofanana. Turejee katika Qur-an mifano michache ya mafundisho ya msingi waliyotoa Mitume kwa watu wao:

(I) NUHU(A.S)

﴿لَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ فَقَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ﴾

Tulipompeleka Nuhu kwa watu wake, naye akasema:"Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu.Nyinyi hamna Mungu ila Yeye.Hakika mimi ninakuhofieni adhabu ya siku (hiyo) iliyo kuu"(7:59).

(II) HUD(A.S)

﴿وَإِلَىٰ عَادٍ أَخَاهُمْ هُودًا قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ أَفَلَا تَتَّقُونَ﴾

"Na kwa Adi (tulimpeleka) ndugu yao Hudi, akasema: "Enyi kaumu yangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mungu ila Yeye.Basi hamuogopi? "(7:65).

(III) SALIH(A.S)

﴿وَإِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمْ صَالِحًا قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ قَدْ جَاءَتْكُم بَيِّنَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ هَـٰذِهِ نَاقَةُ اللَّـهِ لَكُمْ آيَةً فَذَرُوهَا تَأْكُلْ فِي أَرْضِ اللَّـهِ وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ﴾

"Na kwa thamud (tulimpeleka) ndugu yao, Saleh.Akasema "Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mola ila Yeye. Hakika umekwisha kukufikieni muujiza ulio dhahiri kutoka kwa Mola wenu. Huyu ni ngamia jike wa Mwenyezi Mungu aliye na ishara kwenu (ya Utume wangu). Basi muacheni ale katika ardhi ya Mungu, wala msimtie katika dhara yoyote, isije ikakushikeni adhabu iumizayo" (7:73)

(IV) SHU'AYB(A.S)

﴿وَإِلَىٰ مَدْيَنَ أَخَاهُمْ شُعَيْبًا قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ قَدْ جَاءَتْكُم بَيِّنَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ فَأَوْفُوا الْكَيْلَ وَالْمِيزَانَ وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ بَعْدَ إِصْلَاحِهَا ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴾

Na kwa watu wa Madyan (tulimpeleka) ndugu yao, Shu'ayb, akasema: 'Enyi kaumu yangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu, hamna Mungu mwingine isipokuwa Yeye. Zimekwisha kufikieni hoja dhahiri kutoka kwa Mola wenu. Basi kamilisheni sawa sawa vipimo (vya vibaba) na mizani (pia) wala msiwapunguzie watu vitu vyao wala msifanye uharibifu katika ardhi badala ya kutengenea kwake.Hivi ndivyo bora kwenu ikiwa nyinyi mumeamini. (7:85).

(V) ISA(A.S)

﴿وَإِنَّ اللَّـهَ رَبِّي وَرَبُّكُمْ فَاعْبُدُوهُ هَـٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ ﴾

Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu na Mola wenu. Basi muabuduni.Hii ni njia iliyonyooka. (19:36)

(VI) MUHAMMAD(S.A.W.W)

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ النَّبِيِّ الْأُمِّيِّ الَّذِي يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَكَلِمَاتِهِ وَاتَّبِعُوهُ لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ﴾

Sema (ewe Muhammad): "Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote; (Mungu) ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi, hakuna aabudiwaye (kwa haki) ila yeye, yeye ndiye ahuishaye na ndiye afishaye.Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, aliye Nabii Ummiyyi (asiyejua kusoma wala kuandika) ambaye humuamini Mwenyezi Mungu na maneno yake. Na mfuateni yeye ili mpate kuongoka". (7:158)

﴿وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ فَمِنْهُم مَّنْ هَدَى اللَّـهُ وَمِنْهُم مَّنْ حَقَّتْ عَلَيْهِ الضَّلَالَةُ فَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَانظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُكَذِّبِينَ﴾

"Na bila shaka tulimpeleka mtume katika kila umma ya kwamba, Muabuduni Mwenyezi Mungu na mwepukeni twaghuti. Basi wako miongoni mwao ambao Mwenyezi Mungu amewaongoa na wako miongoni mwao ambao upotofu umethubutu juu yao. Basi tembeeni katika ardhi na mwangalie ulikuwaje mwisho wa wale waliokadhibisha" (16:36)

Ukirejea katika Qur-an utaona kuwa Mitume wote kwa ujumla wamefundisha yafuatayo:-

(i)TAWHIID

Wamewafundisha watu juu ya kuwepo Allah (s.w) na upweke wake kwa kuwaonyesha dalili zilizo waziwazi.

(II)LENGO

Waliwafundisha watu kuwa lengo la kuumbwa kwao ni kumuabudu Allah (s.w) na kusimamisha ukhalifa wake hapa ulimwenguni na kisha waliwafundisha namna ya kumuabudu Mola wao katika kila kipengele cha maisha.

(III) KUBASHIRIA

Waliwabashiria watu malipo mema ya kudumu ya huko Peponi kwa wale watakaoamini vilivyo na kutenda mema katika maisha yao ya hapa duniani.

(IV) KUHOFISHA

Waliwahofisha watu juu adhabu kali watakayopata huko Akhera wale watakao mkufuru Allah (s.w) na kumwabudu twaghuti. Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, wala hawakuingiza utamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.w). Kwa mfano, maquraishi walipomjia Mtume(s.a.w.w) na rai ya kuchanganya haki na batili katika ibada, Mtume(s.a.w.w) aliamuriwa na Mola wake awape msimamo wa Uislamu kama ifuatavyo:

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ ﴿١﴾ لَا أَعْبُدُ مَا تَعْبُدُونَ ﴿٢﴾ وَلَا أَنتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ ﴿٣﴾ وَلَا أَنَا عَابِدٌ مَّا عَبَدتُّمْ ﴿٤﴾ وَلَا أَنتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ ﴿٥﴾ لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِيَ دِينِ﴾

"Sema: Enyi makafiri, siabudu mnachoabudu. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.Wala sintaabudu mnachoabudu.Wala nyinyi hamtamuabdudu ninayemuabudu.Nyinyi mna dini yenu nami nina dini yangu" (109:1-6)

Upeo wa Elimu waliyokuwa nayo Mitume Mitume walikuwa na upeo wa fikra na hekima kuliko mtu yeyote katika jamii zao. Hawakusoma kwa mtu bali walifunuliwa elimu kwa njia ya Wahay kutoka kwa Mola wao. Kwa mfano juu ya Nabii Daudi na Suleimani tunasoma katika Qur-an: "Na bila shaka tuliwapa Daudi na Suleimani elimu (kubwa kabisa na wakamshukuru Allah) wakasema, "Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu aliyetufadhilisha kuliko wengine katika waja wake waliomuamini" (27:15) Sifa za Allah (s.w) Kuthibitisha kuwepo kwa Mungu muumba baada ya kutafakari ishara mbali mbali zilizotuzunguka katika kuiendea Imani ya kweli juu ya Allah (s.w) ni hatua ya kwanza. Hatua ya pili ni kuzifahamu sifa (Attributes) za Allah (s.w). Sifa za Allah (s.w) ni nyingi kiasi kwamba hapana yeyote awezaye kuzimaliza kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

﴿قُل لَّوْ كَانَ الْبَحْرُ مِدَادًا لِّكَلِمَاتِ رَبِّي لَنَفِدَ الْبَحْرُ قَبْلَ أَن تَنفَدَ كَلِمَاتُ رَبِّي وَلَوْ جِئْنَا بِمِثْلِهِ مَدَدًا﴾

"Sema hata bahari ingelikuwa ndio wino kwa kuyaandika maneno ya Mola wangu, basi bahari ingelikwisha kabla ya kwisha maneno ya Mola wangu hata kama tungelileta (bahari) kama hiyo kuongezea" (18:109)

﴿وَلَوْ أَنَّمَا فِي الْأَرْضِ مِن شَجَرَةٍ أَقْلَامٌ وَالْبَحْرُ يَمُدُّهُ مِن بَعْدِهِ سَبْعَةُ أَبْحُرٍ مَّا نَفِدَتْ كَلِمَاتُ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ﴾

"Na lau kama miti yote iliyomo katika ardhi ingelikuwa kalamu, na bahari hii (ikafanywa wino) na ikasaidiwa na bahari nyingine saba, maneno ya Mwenyezi Mungu yasingelikwisha. Bila shaka Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mwenye hekima" (31:27)

Pamoja na msisitizo huu Mtume (s.a.w) anataja majina na sifa 99 za Mwenyezi Mungu.

MAJINA 99 YA MWENYE EZI MUNGU

1. Allah Mwenyezi Mungu, Mola Mwenye kustahiki kuwepo. Hili ndilo jina la Dhati la Mungu Mmoja tu. 2. Ar-Rahmaanu Mwingi wa Rehema (huruma). 3. Ar-Rahiimu Mwenye kurehemu. 4. Al-Maliku Mfalme wa kweli wa milele. Mfalme wa Wafalme. 5. Al-Qudduusu Mtakatifu, Ametakasika na sifa zote chafu.

6. As-Salaamu Mwenye Kusalimika, Mwenye kuleta amani, Mwenye Salama. 7. Al-Mu'uminu Mtoaji wa amani. 8. Al-Muhayminu Mwangalizi wa mambo ya viumbe vyake (matendo yao, uhai wao, n.k) Mlinzi, Mchungaji. 9. Al-'Aziizu Mwenye Shani, shahidi katika mambo yake, Muhitajiwa na kila kitu na wala hahitaji kwa yeyote katika viumbe vyake. 10. Al-Jabbaaru Mwenye kuunga mambo yaliyovunjika. Mwenye kulazimisha viumbe wafanye analolitaka yeye bila ya wao kuwa na uwezo wala uhuru wa kumlazimisha yeye kufanya wanalotaka viumbe. 11. Al-Mutakabbiru Mwenye Kibri na Haki ya Kibri (Majestic, Suprem Pride). 12. Al-Khaaliqu Muumbaji, Mbora wa waumbaji. 13. Al-Baariu Mtengenezaji (The maker out of nothing). 14. Al-Muswawwiru Mfanyaji wa sura za namna namna (the Fashioner).15.Al-Ghaffaaru Msamehevu.Mwenye kusamehe.16.Al-Qahhaaru Mwenye Nguvu juu ya kila kitu (Irresistible). 17. Al-Wahhaabu Mpaji Mkuu (The Bestower) 18. Ar-Razzaaqu Mtoaji wa Riziki, Mwenye kuruzuku. 19. Al-Fattaahu Afungua kila kitu. 20. Al-Aliimu Ajuae, Mjuzi wa kila kitu. 21. Al-Qaabidhu Mwenye kuzuia, Mwenye kufisha na kusababisha kufa, Mwenye kunyima (kutia umaskini). 22. Al-Baasitwu: Mwenye kutoa,Mwenye kuhuisha, mwenye kuvipa viumbe uhai, mwenye kutajirisha. 23. Al-Khaafidhu Mfedhehesha waovu. 24. Ar-Raafiu Mpaji cheo, Mpandishaji daraja. 25. Al-Mui'zzu Mtoaji heshima kwa amtakaye. 26. Al-Mudhillu Mnyima heshima kwa amtakaye, mwenye kudhili. 27. As-Samiiu' Mwenye kusikia, Msikivu wa hali ya juu kabisa. 28. Al-Baswiiru Mwenye kuona, Muoni wa hali ya juu kabisa. 29. Al-Hakamu Mwenye kuhukumu, Mwenye kukata shauri,Mwamuzi. Muadilifu, mwenye kutoa ha30.Al-'Adluki asiye dhulumu.31.Al-Latwiifu Mpole, laini, mwenye huruma sana.32. Al-Khabiiru Mwenye khabari zote (mjuzi wa mambo yote). 33. Al-Haliimu Mpole sana, kabisa 34. Al-A'dhiimu Mkuu, Aliye Mkuu. 35.Al-Ghafuuru,Msamehevu.36.Ash-Shakuuru Mwenye shukrani.37.Al-'AIliyyu Aliye juu (The High). 38. Al-Kabiiru Mkubwa wa kuishi Mkongwe. 39. Al-Hafiidhu Haafidhi (The Preserver) Mwenye kuhifadhi kila kitu. 40. Al-Muqiitu Mlishaji (the Feeder), Mtoaji Riziki kwa kila kiumbe, Mwenye nguvu. 41. Al-Hasiibu Mwenye kuhesabu (The Reckoner), Mjuzi wa Hesabu. 42. Al-Jaliilu Mzuri wa hali ya juu (The majestic), Tajiri, Mtukufu, Mjuzi, Mtawala, mwenye Nguvu (yote haya yanajumuisha Al-Jaliil).(Mzuri wa hali zote) 43. Al-Kariimu Mtukufu mwenye ukarimu. 44. Ar-Raqiibu Muoni wa kila linalofanyika, Mwenye kuona yote yanayofanywa, anayaangalia yote yanayofanywa (The Watcher, The Watchful) 45. Al-Mujiibu Mpokeaji wa maombi ya waja wake.Mwenye kuona yote yanayofanywa, anayaangalia yote yanayofanywa. 46. Al-Waasiu Mwenye Wasaa, Mwenye kila kitu.47. Al-Hakiimu Mwenye Hikma (The wise). 48. Al-Waduudu Mwenye Upendo (The Loving), Mwenye kupenda kuwatakia mazuri watu. 49. Al-Majiidu Mtukufu (The Glorious), Mwenye kustahiki kutukuzwa. Jina hili lina changanywa kwa pamoja Al-Jaliil, Al-Wahaab na Al-Kariim. 50. Al-Baa'ithu Mwenye kufufua wafu. 51. As-Shahiidu Shahidi mwenye kushuhudia kila kitu (Witness). 52. Al-Haqqu Wa haki, Wa kweli hasa, Mkweli (The Truth), The True. 53. Al-Wakiilu Wakili (The Advocate), Mdhamini (The Trustee), Mlinzi mwenye kustahiki kuachiwa mambo ya watu.Anayeangalia na kulinda yote (The Representative). 54. Al-Qawiyyu Mwenye nguvu (the Strong). 55. Al-Matiinu,Aliye Madhubuti (The Firm), Asiyetingishika kwa lolote. 56. Al-Waliyyu Mwenye kusifika, kila sifa njema ni zake. 57. Al-Hamiidu Mhimidiwa, Mwenye kustahiki sifa zote nzuri. 58. Al-Muhswiy Mwenye kudhibiti (hesabu), Mwenye kuhesabu. 59. Al-Mubdiu Mwenye kuanzisha (The Producer, The Originator). 60. Al-Mu'iidu Mwenye kurejeza (The producer, The R'estorer). Angalia: Yeye Allah Ndiye Mwenye kuanzisha viumbe na kuvifanya vifu, kisha ndiye mwenye kuvirejesha tena kwenye maisha baada ya kufa.61. Al-Muhyi Mwenye kuhuisha. 62. Al-Hayyu Mwenye uhai wa milele (The Alive). 63. Al-Mumiitu Mwenye kufisha (The Causer of death, The Destroyer). 64. Al-Qayyumu Msimamia kila jambo, Mwendeshaji wa mambo yote. 65. Al-Waajidu Mwenye utaambuzi wa kila kitu.Utambuzi (The Perceiver). 66. Al-Maajidu Wa kuheshimiwa, Mtukufu (The Noble, illustrious). 67. Al-Waahidu,Mwenye kupwekeka, Mmoja tu (The One). 68. As-Swamadu Mwenye kukusudiwa kwa kuabudiwa, kuombwa na kutegemewa. 69. Al-Qaadiru Mwenye uwezo wa kufanya au kutofanya kila kitu, Muweza wa kufanya au kutofanya chochote. 70. Al-Muqtadiru Mwenye kudiriki kila kitu, mwenye uwezo wa pekee juu ya kila kitu (The Dominant, The Powerful).71.Al-Muqaddimu Mwenye kutanguliza, mwenye kumleta mja karibu naye. 72. Al-Muakhiru Mwenye kuakhirisha (The Postaponer). Mwenye kubakisha nyuma Mwenye kumpeleka mja mbali naye(The Deferer). 73. Al-Awwalu Wa mwanzo (The first). 74 Al Aakhiru Wa mwisho (The last). 75. Adh-Dhaahiru Wa dhahiri (The Outward). Haonekani kwa macho, wala hagusiki, wala haonjeki, ila anaonekana kwa akili na hoja zilizo wazi hapa ulimwenguni. 76. Al-Baatwinu Wa siri (The Inward). 77. Al-Waliyyu Gavana (The Governor), Mpanga Mipango ya watu na mwangalizi wa mipango yote. 78. Al-Muta'aali Mtukufu aliye juu (The High Exalted). 79. Al-Barru Mwema (The righteous). 80. At-Tawwaabu Mwenye kupokea Toba za waja wake. 81. Al-Muntaqimu Mwenye kuchukua kisasi, Mlipakisasi kwa waovu. 82. Al-'Afuwwu Mwenye kusamehe madhambi, mfuta madhambi ya waja wake (The Pardoner), Msamehevu. 83. Ar-Rauufu Mpole, Mwenye huruma (The compassionate). 84. Maalikal-Mulki Mwenye kumiliki ufalme wote, Mfalme wa 'Wafalme (The Owner of the Sovereignty) Mwenye kutumia mamlaka yake atakavyo. i85. Dhil-jalaali Wal-Ikraam Mwenye Utukufu na Heshima (The Lord of Majesty and Bounty). 86. Al-Muqsitu Mwenye kukamilisha usawa (The Equitable) Mwenye kutoa usawa, Mtoaji Haki sawa kwa kila anayestahiki. 87. Al-Jaamiu' Mkusanyaji (The gather or The Collector), Mkusanyaji viumbe siku ya mwisho (Kiyama). 88. Al-Ghaniyyu' Mwenye kujitosheleza (The self Sufficient), Hahitaji chochote kwa yeyote (The Independent, The absolute), Tajiri (The Rich). 89. Al-Mughnii Mwenye kutajirisha (The Enricher), mwenye kutosheleza viumbe kwa kila wanachohitajia. 90. Al-Maaniu' Mwenye kusalimisha viumbe kutokana na mabaya, mwenye kuzuia viumbe visidhurike, mwenye kunusuru (The Preventer, The Witholder). 91. Adh-Dhaarru Mwenye kuleta shari (Dhara), Mwenye kudhurisha (The Distresser). 92. An-Naafiu' Mwenye kuleta nafuu (Kheri), Mwenye kunufaisha (The Profitor). 93. An-Nuuru Nuru, Mwenye Nuru, Mwangaza (The Light).94.Al-Haadi Mwenye kuongoza waja wake katika kheri mbali mbali (Elimu, Riziki, n.k) Mwongozaji (The Guide). 95. Al-Badiiu' Mwasisi (The Originator). 96. Al-Baaqy Mwenye kubakia Milele, hana mwisho (The Everlasting, Enduring). 97. Al-Waarithu Mrithi, Mwenye Kurithi kila kitu (baada ya wenyewe kufa). 98. Ar-Rashiidu Mwenye kuongoa, mwenye kuongoa waja wake kuiendea njia ya kheri. 99. As-Swabuuru Mwenye kusubiri, mwenye subira (The Patient).

Katika Qur-an sifa za Mwenyezi Mungu zimeelezwa katika aya mbali mbali lakini si kwa mfululizo huu tulioupanga katika Hadith. Ayatul-Qurusiyyu (2:55)

﴿اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ﴾

"Mwenyezi Mungu hakuna Mola ila Yeye. Ndiye mwenye Uhai wa milele. Msimamizi wa kila jambo, kusinzia hakumshiki wala kulala. Ni vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na ardhini.Na nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyomo mbele yao viumbe na yaliyo nyuma yao; Wala (Hao viumbe) hawajui lolote katika ilimu yake, ila kwa alipendalo (mwenyewe). Enzi yake imeenea mbingu na ardhi, wala kuvilinda hivyo hakumshindi, na Yeye pekee ndiye aliye juu (ya kila kitu) na Ndiye Aliye Mkuu." (2:255)

﴿سَبَّحَ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١﴾ لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ يُحْيِي وَيُمِيتُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢﴾ هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣﴾هُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿٤﴾ لَّهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴿٥﴾ يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ وَهُوَ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٦﴾ آمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَأَنفِقُوا مِمَّا جَعَلَكُم مُّسْتَخْلَفِينَ فِيهِ فَالَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَأَنفَقُوا لَهُمْ أَجْرٌ كَبِيرٌ﴾

"Kinamtukuza Mwenyezi Mungu kila kilichomo mbinguni na ardhini, na Yeye ndiye mwenye Nguvu, Mwenye Hekima. Ufalme wa mbingu na ardhi ni wake, na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu. Yeye ndiye wa mwanzo na ndiye wa Mwisho, na ndiye wa Dhahiri na wa Siri, Naye ndiye Mjuzi wa kila kitu. Yeye ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi katika nyakati sita, kisha akatawala katika enzi yake. Anayajua yanayoingia katika ardhi na yanayotoka humo, na yanayoteremka kutoka mbinguni na yanayopanda humo. Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo na Mwenyezi Mungu anaona yote mnayoyatenda. Ufalme wa mbingu na ardhi ni wake na mambo yote yanarudishwa kwa Mwenyezi Mungu. Anaingiza usiku katika mchana na anaingiza mchana katika usiku.Na yeye anajua yaliyomo vifuani.Mwaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na toeni katika yale aliyokupeni. Basi wale walioamini miongoni mwenu na wakatoa, wana malipo makubwa." (57:1-7)

﴿هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ هُوَ الرَّحْمَـٰنُ الرَّحِيمُ ﴿٢٢﴾ هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٢٣﴾ هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ يُسَبِّحُ لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴾

"Yeye ndiye Allah.Ambaye hakuna aabudiwaye kwa haki ila Yeye tu. Ni Mjuzi wa yaliyofichikana na yaliyo Dhahiri. Mwingi wa Rehema, Mwenye kurehemu. Yeye Ndiye Allah, ambaye hakuna aabudiwaye kwa haki ila yeye tu.Ni Mfalme Mtakatifu, Mwenye Salama, Mtoaji wa Amani, Mwendeshaji wa mambo yake.Mwenye shani, mwenye kufanya alitakalo, Mkubwa (kuliko vyote vikubwa),Allah ametakasika na hao wanaomshirikisha naye.Yeye Ndiye Allah, Muumbaji, Mtengenezaji, Mfanyaji sura, Mwenye majina (sifa) mazuri.Kinamtukuza kila kilichomo mbinguni na ardhini.Naye ni mwenye nguvu mwenye Hikima." (59:22-24).

﴿قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾ اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ﴿٣﴾ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ﴾

Sema: Yeye ni Allah mmoja tu. Allah ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe vyote kwa kumuabudu, kumuomba na kumtegemea) Hakuzaa wala hakuzaliwa, wala hana anayefanana naye hata mmoja. (112:1-4)

UFAFANUZI WA SIFA ZA ALLAH (S.W)

Ukizichunguza kwa makini sifa zote hizi zilizoorodheshwa katika Qur-an na Hadith tunaona kuwa nyingi ya sifa hizi kama vile Ar-Rahmaan na Ar-Rahiim zinafanana au zinakaribia kufanana kwa kiasi ambacho wafasiri wengi wameshindwa kuzipambanua. Hii inadhihirisha ukamilifu wa sifa za Allah (s.w). Sifa hizi zinakienea kila kitu na kukifanya kila kitu katika mbingu na ardhi kiishi na kiwe kama kilivyo. Hapana mwanya wala nafasi iliyoachwa wazi bila ya kufunikwa na sifa za utendaji wa Allah (s.w).

Ni muhimu kwa kila muumini kuzifahamu sifa hizi kwa undani ili ziweze kumuathiri vilivyo katika utendaji wake wa kila siku. Ili kurahisisha kuzifahamu sifa hizi kwa undani, tumezigawanya sifa hizi katika mafungu yafuatayo:

(a) Sifa au majina ya Allah yanayoonesha kuwepo kwake na umoja wa Uungu wake.

(b) Majina ya Allah yanayoonesha ujuzi wake usio na mipaka.

(c) Majina ya Allah yanayoonesha upweke wake wa utawala na Utukufu wake.

(d) Sifa za Allah zinazoonesha Uadilifu wake usio na mipaka.

(e) Sifa za Allah zinazoonesha Urehemevu, Upendo na Usamehevu wake usio na mipaka.

(A) SIFA AU MAJINA YA ALLAH YANAYOONESHA KUWEPO KWAKE NA UMOJA WAKE, UUNGU WAKE NA UUMBAJI WAKE.

1. Allah Hili ni jina Dhati Pekee la Mungu Muumba Mmoja na Mpweke. Jina hili halifasiriki katika lugha yoyote.Mitume wote wamemtaja Mungu Muumba Mmoja Mpweke kwa jina hili la Allah.

2. Al-Waahid - Mmoja Pekee

3. Al-Ahad - Yeye ni Mmoja Sifa hizi zinasisitiza kuwa Allah (s.w) ni mmoja tu na hagawanyiki kama wanavyodai wakristo na Washirikina. Aya zifuatazo zinafafanua sifa hizi:

﴿وَمَا مِنْ إِلَـٰهٍ إِلَّا اللَّـهُ وَإِنَّ اللَّـهَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴾

"Hapana Mungu ila Allah.Hakika Allah ni mwenye nguvu na mwenye hekima" (3:62)

﴿ إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ ﴿٤﴾ رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ﴾

"Kwa yakini Mungu wenu ni Mmoja tu. Mola wa mbingu na ardhi na yaliyomo kati yake, na ni Mola wa mashariki (na Magharibi zote)". (37:4-5)

﴿قُلْ إِنَّمَا هُوَ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ وَإِنَّنِي بَرِيءٌ مِّمَّا تُشْرِكُونَ﴾

"Sema (ee Mtume): Yeye ni Mungu mmoja tu. Na hakika mimi ni mbali na hao mnaowashirikisha (naye)". (6:19)

4. As-Swamad- Mkusudiwa, Mstahiki kutegemewa na kila mtu. Kwake Yeye vinategemea vyote na Yeye ni mwenye kujitosheleza.Hategemei chochote.

5. Al-Haqq Mkweli, Yeye ni wa Haki. Msimamisha Haki.'

6. Al-Awwal Wa mwanzo, yeye ni mwanzo.

7. Al-Aa'Khir Wa mwisho, Yeye ni mwisho.

8. An-Nuur Yeye ni Nuru. Yeye ni mwanga.

9. Adh-Dhaahir Mdhihiri, Aliyedhihirika, Mdhihirishaji.

10. Al-Baatwin Msiri; Mjua yote ya siri. I

11. Al-Muhy Mwenye kutoa maisha, Mwenye kuhuisha.

12. Al-Hayy Aliye hai milele. Yeye ni Mhai.

13. Al-Qayyuum Mwenye Uhai wa maisha. Mwenye Kubakia Milele. Aya ifuatayo inaitaja sifa hii:

﴿ اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ﴾

"Mwenyezi Mungu hakuna Mola ila Yeye, Ndiye mwenye Uhai wa Maisha (wa kudumu) " (2:255)

14. Al-Waajid Mwenye kuwepo nyakati zote (hana mwanzo wala mwisho).

15. Al-Badiiu' Mwanzilishi (Mzushi) Pekee wa kila kitu. Aya zinazoidhihirisha sifa hii ya Allah:

﴿بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُ كُن فَيَكُونُ﴾

"Yeye ndiye mwanzilishi wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapotaka jambo basi huliambia tu "kuwa", nalo huwa" (2:117).

﴿ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ فَاعْبُدُوهُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ وَكِيلٌ﴾

"Huyo ndiye Allah, Mola wenu, hakuna anayeabudiwa kwa haki ila Yeye. Muumba wa kila kitu.Kwa hiyo mwabuduni Yeye (tu). Naye ni Mlinzi wa kila kitu" (6:102)

16. Al-Mubdiu Mwanzilishi wa kila kitu. Sifa hii inafafanuliwa vema na aya ifuatayo:

﴿أَوَلَمْ يَرَوْا كَيْفَ يُبْدِئُ اللَّـهُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ﴾

"Je,hawaoni jinsi (Mwenyezi Mungu) aanzishavyo viumbe,kisha atavirudisha (mara ya pili). Hakika kwa Mwenyezi Mungu hayo ni sahali" (29:19)

17. Al-Baaqii - Mwenye kubakia milele.Aya zifuatazo zinafafanua sifa hii ya Allah (s.w):

﴿كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ ﴿٢٦﴾ وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ﴾

"Kila kilicho juu yake (ardhi na mbingu) kitatoweka.Inabakia dhati ya Mola wako tu, Mwenye utukufu na heshima" (55:26-27)

﴿وَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ كُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ لَهُ الْحُكْمُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴾

"Wala usimuombe - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwingine, hakuna aabuduwaye kwa haki ila Yeye, kila kitu kitakufa isipokuwa Yeye tu. Hukumu ya mambo yote iko Kwake na Kwake mtarejeshwa (nyote)". (28:88)

18. Al-Khaaliq Muumbaji, mwanzilishi wa viumbe.

19. Al-Baariu Mtengenezaji, Mwanzilishi.

20. Al-Muswawwiru Mtengenezaji wa sura, muumbaji wa sura.

21. Al-Mu'iid Mwenye kurejeza. Aya ifuatayo inafafanua sifa hii ya Allah (s.w):

Marejeo yenu nyote ni kwake, na ahadi ya Allah ni haki. Hakika Yeye ndiye aliyeanzisha viumbe na ndiye atakayewarejeza, ili awalipe kiuadilifu wale waliamini na kufanya vitendo vizuri"(10:4)

22. Al-Muhyii Muhuishaji.Mwenye kuvifanya viumbe viishi kutoka kwenye ufu.

23. Al-Mumiitu Mfishaji, Mwenye Uwezo pekee wa kufisha vilivyo hai. Aya ifuatayo inafafanua:

﴿وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْيِي وَنُمِيتُ وَنَحْنُ الْوَارِثُونَ﴾

"Na sisi ndio tunaohuisha na tunaofisha, na sisi ndio warithi(wa vyote)".(15:23).

24. Al-Waarith Mrithi, Mrithishaji.

﴿وَكَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ بَطِرَتْ مَعِيشَتَهَا فَتِلْكَ مَسَاكِنُهُمْ لَمْ تُسْكَن مِّن بَعْدِهِمْ إِلَّا قَلِيلًا وَكُنَّا نَحْنُ الْوَارِثِينَ﴾

"Na tumeiangamiza miji mingapi iliyojifaharisha juu ya maisha yao! Hayo maskani yao yasiyokaliwa baada yao tena ila kidogo tu hivi, na sisi tumekuwa warithi (wa sehemu hizo)"(28:58)

25. Al-Baa'ith Mfufua wafu kutoka makaburini.

﴿وَأَنَّ السَّاعَةَ آتِيَةٌ لَّا رَيْبَ فِيهَا وَأَنَّ اللَّـهَ يَبْعَثُ مَن فِي الْقُبُورِ﴾

"Na kwamba Kiyama kitakuja hapana shaka ndani yake; na kwa hakika Mwenyezi Mungu atawafufua walio makaburini" (22:7)

26. Al-Jaamiu' Mkusanyaji wa watu wote siku ya Malipo.

﴿رَبَّنَا إِنَّكَ جَامِعُ النَّاسِ لِيَوْمٍ لَّا رَيْبَ فِيهِ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُخْلِفُ الْمِيعَادَ﴾

"Mola wetu! Wewe ndiye mkusanyaji wa watu siku isiyo na shaka ndani yake. Hakika Mwenyezi Mungu havunji miadi" (3:9)

27. Al-Muakh-khir Mwenye kuakhirisha, Mwenye kuchelewesha viumbe mpaka ufike muda wao.

28. Al-Muqaddim Mwenye kutanguliza, Mtangulizaji. Sifa zote hizi zinatupa picha kamili juu ya Allah (s.w) na uwezo wake wa Kiungu usiopatikana kwa kiumbe yeyote yule. Kwa muhtasari sifa hizi zinatufahamisha kuwa Allah (s.w) ni Mungu mmoja tu na Mpweke, ambaye hana mwanzo wala mwisho. Amekuwepo nyakati zote na atakuwepo milele. Hana mwanzilishi wake bali Yeye mwenyewe ni chanzo na vyote vimetokana na Yeye. Ni mwenye kujitegemea kwa kila kitu, na vyote vinategemea kwake kwa kila kitu kinachohusu kuwepo kwao, uhai wao na maisha yao kwa ujumla. Ndiye pekee anayemiliki maisha ya watu na viumbe vyote baada ya maisha ya hapa duniani.Ni dhahiri kwamba hapana kiumbe yeyote mwenye hata chembe ya sifa hizi. Hivyo kumtegemea kiumbe yoyote badala ya Allah ni ujahili wa hali ya juu.

(B) MAJINA YA ALLAH (S.W) YANAYOONESHA UJUZI WAKE USIO KIKOMO

29. Al-Baasitu Mkunjuaji, anakienea kila kiumbe. Sifa hii inafafanuliwa vyema katika aya ifuatayo:

﴿اللَّـهُ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ وَفَرِحُوا بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلَّا مَتَاعٌ﴾

"Allah hukunjua riziki kwa amtakaye na huidhikisha (kwa amtakaye)".(13:26)

30. Al-'Aliim Mjuzi wa kila kitu. Mjuzi wa yote.

31. Al-Hakiim Mwingi wa Hekima.

32. Al-Khabiiru Mwingi wa khabari, mwenye khabari zote.

33. As-Samiiu' Msikivu, Mwenye kusikia pasina mipaka.

34. Al-Baswiiru Mwenye kuona kila kitu; Mwenye kuona pasina mipaka. Usikivu na uoanaji wa Allah (s.w), hauna mipaka na ni wa kudumu milele.

35. Ash-Shahiid Shahidi, Mwenye kushuhudia kila kitu na kila tukio.

﴿إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَادُوا وَالصَّابِئِينَ وَالنَّصَارَىٰ وَالْمَجُوسَ وَالَّذِينَ أَشْرَكُوا إِنَّ اللَّـهَ يَفْصِلُ بَيْنَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ﴾

"Hapana jambo lolote linalotendeka bila Allah (s.w) kuwa shahidi juu ya jambo hilo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Shahidi juu ya kila kitu". (22:17).

36. Al-Mujiib Mwenye kujibu maombi.

37. Ar-Rashiid Mwenyezi Mungu Mwongozi wa njia ya sawa, mwenye kuelekeza katika mwenendo mzuri. Yeye ni mfundishaji na muongozaji. Yeye Mwenyewe ni mwongofu. Sifa hizi za Allah (s.w) zinatupa picha kamili juu ya ujuzi wake uso mipaka. Ni Allah (s.w) pekee anayestahiki kutegemewa kwa kila kitu kwani Ndiye pekee anayetujua fika tulivyo na ndiye pekee anayedhibiti kila tendo letu na kila tukio litokealo popote ardhini na mbinguni. Anatukumbusha hili katika aya zifuatazo:

﴿وَعِندَهُ مَفَاتِحُ الْغَيْبِ لَا يَعْلَمُهَا إِلَّا هُوَ وَيَعْلَمُ مَا فِي الْبَرِّ وَالْبَحْرِ وَمَا تَسْقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعْلَمُهَا وَلَا حَبَّةٍ فِي ظُلُمَاتِ الْأَرْضِ وَلَا رَطْبٍ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ﴾

"Na ziko kwake funguo za siri, hakuna azijuuaye ila Yeye tu, na Anajua yaliyomo barani na baharini. Na Halianguki jani ila analijua. Wala haianguki punje katika giza la ardhi (ila anaijua). Wala (hakianguki) kilichorutubika wala kilichoyasibika (ila anakijua). (Hapana chochote) ila kimo katika kitabu kidhihirishacho (kila jambo)" (6:59)

﴿أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ وَلَا خَمْسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمْ وَلَا أَدْنَىٰ مِن ذَٰلِكَ وَلَا أَكْثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمْ أَيْنَ مَا كَانُوا ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴾

"Je,huoni kwamba Allah anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini? Haupatikani mnong'ono wa watu watatu ila Yeye huwa wanne wao, wala wa tano ila yeye huwa ni wasita wao, wala wa wachache kuliko hao wala zaidi ila Yeye huwa pamoja nao popote walipo; kisha siku ya kiyama Atawaambia waliyoyatenda. Hakika Allah ni Mjuzi wa kila kitu" (58:7)

﴿وَرَبُّكَ يَعْلَمُ مَا تُكِنُّ صُدُورُهُمْ وَمَا يُعْلِنُونَ ﴾

"Na Mola wako Anayajua yanayoficha vifua vyao na wanayoyadhihirisha" (28:69)

﴿وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِ نَفْسُهُ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ الْوَرِيدِ ﴾

"Na bila shaka tumemuumba mtu, nasi tunajua yanayopita katika nafsi yake.Nasi tu karibu naye zaidi kuliko mshipa wa shingo (jugular vein) (50:16)

pamoja na aya hizi chache tulizozinukuu hapa, sifa hizi zimerejewa mahala pengi katika Qur-an ili kuonesha kwa uwazi ujuzi wa Allah (s.w) usio mipaka. Kwa muhtasari sifa hizi za Allah zinatuyakinishia kuwa Allah (s.w) ni Mjuzi wa kila kitu na ni Mwenye hekima isiyo na mipaka. Hakuna chochote kile kinachofichikana kwake, kiwe kimedhihirishwa kwa kusema au kwa kutenda au kiwe kimefichwa moyoni Allah (s.w) anakiona na anakijua. Hivyo muumini wa Allah (s.w) aliyeelewa fika sifa hizi anatarajiwa awe mkweli mno katika kila kipengele cha maisha yake ya kila siku kwani ana hakika kuwa hakuna siri mbele ya Allah (s.w) na ana uhakika kuwa Allah (s.w) atafichua siri zake zote kama si hapa duniani, huko akhera ni lazima.

(C) MAJINA YA ALLAH YANAYOONESHA UPWEKE WA UTAWALA, NGUVU NA UTUKUFU WAKE

38. Al-AziizMtukufu mwenye nguvu.

39. Al-Jabbaar Mwenye nguvu juu ya kila kitu.

40. Al-Mutakabbir Mwenye kumiliki nguvu zote, Mwenye haki ya kiburi.

41. Al-Maalik Mmiliki wa kila kitu na kila jambo.

﴿مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ ﴾

"Mwenye kumiliki siku ya malipo" (1:4)

42. Al-Malik Mfalme wa kila kitu.

43. Maalikul-Mulki Mmiliki wa Ufalme. Mmiliki wa Falme zote zilizomo mbinguni na ardhini. Tunapata ufafanuzi wa sifa hii katika aya ifuatayo:

﴿قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَاءُ بِيَدِكَ الْخَيْرُ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾

Sema (katika kumsifu Mwenyezi Mungu): "Ee Mola uliyemiliki Ufalme wote, humpa ufalme umtakaye, na humuondolea ufalme umtakaye, bila shaka Wewe ni Muweza juu ya kila kitu". (3:26)

44. Al-'Adhiim Mkuu, Mkubwa kwa utukufu, Mwenye enzi.

45. Al-'Aliyuu Mwenye daraja ya juu ya utukufu, Mtukufu wa watukufu.

46. Al-Qawiyyu Imara, Mwenye nguvu. Aya ifuatayo inafafanua sifa hizi

﴿اللَّـهُ لَطِيفٌ بِعِبَادِهِ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ وَهُوَ الْقَوِيُّ الْعَزِيزُ ﴾

Mwenyezi Mungu ni mpole kwa waja wake; anampa riziki amtakaye, naye ni mwenye nguvu, Mwenye kushinda". (42:19)

47. Al-Qahharu Mtenza nguvu. Mwenye nguvu juu ya kila kitu. Aya ifuatayo inafafanua vyema sifa hii:

﴿يَا صَاحِبَيِ السِّجْنِ أَأَرْبَابٌ مُّتَفَرِّقُونَ خَيْرٌ أَمِ اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴾

Enyi wafungwa wenzangu wawili! Je! Waungu wengi wanaofarikiana ndio bora au Mwenyezi Mungu mmoja Mwenye nguvu (juu ya kila kitu)" (12:39)

48. Al-Matiin Mwenye nguvu madhubuti, mwenye nguvu za kudumu, mwenye nguvu zisizokatika. Aya ifuatayo inadhihirisha sifa hii:

﴿إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ﴾

"Kwa yakini Mwenyezi Mungu ndiyo mtoaji wa riziki,mwenye nguvu madhubuti". (51:58).

49. Dhuljalaali-wal-Ikraam Bwana mtukufu, Mwingi wa Heshima.

﴿تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ ﴾

"Limetutuka jina la Mola wako Mwenye utukufu na heshima" (55:78)

50. Al-Jaliil Mtukufu na mwenye kuheshimika.

51. Al-Majiid Mtukufu, anayestahiki kutukuzwa. Wakasema (wale Malaika):

﴿قَالُوا أَتَعْجَبِينَ مِنْ أَمْرِ اللَّـهِ رَحْمَتُ اللَّـهِ وَبَرَكَاتُهُ عَلَيْكُمْ أَهْلَ الْبَيْتِ إِنَّهُ حَمِيدٌ مَّجِيدٌ﴾

"Je,unastaajabu amri ya Mwenyezi Mungu? Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka zake ziko juu yenu, enyi watu wa nyumba hii. Hakika Yeye ndiye anayestahiki kusifiwa na kutukuzwa" (11:73)

52. Al-Maajid Mtukufu anayestahiki kutukuzwa. 53. Al-Muta'al Mtukufu wa daraja. Aliye juu kwa daraja.

﴿عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْكَبِيرُ الْمُتَعَالِ ﴾

"Mjuzi wa siri na dhahiri, mkuu aliye juu" (13:9)

54. Al-Quddus Mtakatifu. Aliyetakasika na kila udhaifu.

55. Al-Kabiir Mkubwa kwa cheo na kwa kila kitu.

56. Al-Muqtadiru Mwenye uwezo juu ya kila kitu. Mwenye uwezo mkubwa na mwenye nguvu za kudiriki kila kitu na kila jambo. Aya ifuatayo inadhihirisha sifa hii:

﴿كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ ﴾

"Wakakadhibisha hoja zetu zote, kwa hiyo tukawatesa kama anavyotesa, Mwenye nguvu, mwenye uwezo". (54:42)

57. Al-Qaadiru Mwenye uwezo mkubwa wa kuendesha kila kitu kama inavyostahiki.

58. Al-Qadiiru Mwenye uwezo mkubwa na Mwenye nguvu. Sifa hizi za al- Qaadir na Al-Qadiiru zina maana sawa na ile ya Al-Muqtadir. Yote haya yanaonesha utawala na mamlaka ya Allah (s.w) juu ya kila kitu. Aya ifuatayo inafafanua:

﴿تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾

"Ametukuka yule ambaye mkononi mwake umo ufalme (wote): Naye ni mwenye uweza juu ya kila kitu". (67:1)

59. Al-Mu'izzu Mpandishaji wa daraja, mtunuki daraja na cheo.Hatukuki asiyemtukuza.

60. Al-Mudhillu Mwenye kudhili, mwenye kunyongesha, mwenye uwezo pekee wa kumdhalilisha asiyemtukuza. Kwa ufafanuzi wa sifa hizi mbili, hebu turejee tena aya ifuatayo:

﴿قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَاءُ بِيَدِكَ الْخَيْرُ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾

Sema: "Ee Mola uliomiliki ufalme wote! Humpa ufalme umtakaye, na humuondolea ufalme umtakaye, na humtukuza umtakaye, na humdhalilisha umtakaye, kheri imo mikononi mwako.Bila shaka wewe ni muweza juu ya kila kitu".(3:26)

61. Al-Khaafidhu Mfedheheshaji.

62. Ar-Raafi'u Mtukuzaji, Mpandishaji daraja. Sifa hizi mbili zinaonekana katika aya ifuatayo:

﴿إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ ﴿١﴾ لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ ﴿٢﴾ خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ ﴾

"Litakapotokea tukio (hilo la kiyama) ambalo kutokea kwake si uwongo.Lifedheheshalo (wabaya) na litukuzalo (wazuri)" (56:1-3)

Pia katika Qur-an Allah (s.w) amejitaja kwa jina la "Raafi'uddarajaat". Mpandishaji cheo na daraja.

﴿رَفِيعُ الدَّرَجَاتِ ذُو الْعَرْشِ يُلْقِي الرُّوحَ مِنْ أَمْرِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ لِيُنذِرَ يَوْمَ التَّلَاقِ﴾

"Yeye ndiye mwenye vyeo vya juu kabisa,Mwenye enzi. Hupeleka Wahyi wa amri yake kwa amtakaye miongoni mwa waja wake ili kuwaonya (viumbe) siku ya kukutana (naye)." (40:15)

63. Al-Walliyyu Mlezi wa kila kiumbe.

64. Al-Waaliy Muhifadhi wa viumbe vyote vilivyomo mbinguni na ardhini.

65. As-Salaam Chanzo cha amani na ukamilifu. Mtoa amani. 66. Al-Mu'min Mhifadhi na mlezi wa imani.

67. Al-Muhayminu Mwangalizi, mlezi, mchungaji wa usalama wa viumbe.

68. Ar-Raqiib Mwangalizi, Mchungaji. Sifa hii inadhihirishwa na aya ifuatayo:

﴿ مَا قُلْتُ لَهُمْ إِلَّا مَا أَمَرْتَنِي بِهِ أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ وَكُنتُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا مَّا دُمْتُ فِيهِمْ فَلَمَّا تَوَفَّيْتَنِي كُنتَ أَنتَ الرَّقِيبَ عَلَيْهِمْ وَأَنتَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ﴾

"Sikuwaambia lolote ila yale uliyoniamrisha ya kwamba: Mwabuduni Mwenyezi Mungu Mola wangu na Mola wenu'.Na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao, na uliponikamilishia muda wangu. Wewe ukawa mchungaji juu yao, na wewe shahidi juu ya kila kitu". (5:117)

69. Al-Wakiil, Mlinzi

﴿الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ ﴾

"Wale ambao watu (waliokodiwa na Makurayshi) waliwaambia (Waislamu): 'Watu wamekukusanyikieni. Kwa hiyo waogopeni'.Lakini maneno hayo yakawazidishia imani wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha.Naye ni mlinzi bora kabisa" (3:173).

70. Al-Haafidh Muhifadhi, Mlinzi.

71. Al-Hafiidh Muhifadhi, Mlezi, Mlinzi.

72. Al-Waasi'u Mwenye wasaa mkubwa.

73. Al-Muqiitu Mwongozi, Mwangalizi, Mtawala juu ya kila kitu.

74. Al-Muhsiy Mdhibiti wa kila kitu. Hapana jambo lolote linalofanywa na linalotendeka lililo nje ya udhibiti wake.

75. Al-Mughnii Mtajirishaji, mnawirishaji.

76. Al-Maani'u Mzuiliaji.

77. Al-Qaabidh Mwenye kuzuia, mwenye kunyima

78. Adh-dhaarru Mnyongeshaji, Mwenye kudhuru. Hapana anayedhuru, kudhuru Kwake na hapana yeyote anayeweza kuokoa chochote kilichodhuriwa na Allah. Aya ifuatayo inafafanua vyema:

﴿وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ لَيَقُولُنَّ اللَّـهُ قُلْ أَفَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ إِنْ أَرَادَنِيَ اللَّـهُ بِضُرٍّ هَلْ هُنَّ كَاشِفَاتُ ضُرِّهِ أَوْ أَرَادَنِي بِرَحْمَةٍ هَلْ هُنَّ مُمْسِكَاتُ رَحْمَتِهِ قُلْ حَسْبِيَ اللَّـهُ عَلَيْهِ يَتَوَكَّلُ الْمُتَوَكِّلُونَ﴾

"Na ukiwauliza: 'Na nani aliyeziumba mbingu na ardhi?" Bila shaka watasema: Ni Mwenyezi Mungu, Je mnawaonaje wale mnaowaomba kinyme cha Allah, kama Mwenyezi Mungu akitaka kunidhuru, wao wanaweza kuniondolea dhara yake?Au akitaka kunirehemu, je, wao wanaweza kuzuia rehema yake?" Sema:'Mwenyezi Mungu ananitosha, kwake wategemee wategemeao". (39:38)

Sifa zote hizi zinatupa picha kamili juu ya utalawa wa Allah (s.w) na uwezo wake juu ya kila kitu. Kutokana na sifa hizi tunafahamu kuwa Allah (s.w) Ndiye pekee aliyeumba mbingu na ardhi na vyote vilivyomo na ndiye pekee anayevilea, anayevilinda, anayevikuza na kuviendeleza na ndiye pekee anayeviongoza mpaka kufikia lengo la kuumbwa kwao. Allah (s.w) hahitaji msaada au ushauri kutoka kwa yeyote katika kutekeleza ridhaa yake juu ya viumbe vyake.Pia hahitaji zana au juhudi katika kulitekeleza alitakalo. Akitaka chochote kiwe ni kukiamrisha: "Kuwa" na kikawa pale pale na vile vile atakavyo.

Tukizingatia sifa hizi za Allah (s.w) tutaona kuwa, hapana yeyote anayestahiki kunyenyekewa, kuogopwa na kutegemewa kinyume na Allah (s.w). Ni wazi kuwa hapana yeyote mwenye uwezo wa kumdhuru yeyote, aliyepata hifadhi ya Allah (s.w). Kinyume chake hapana yeyote anayeweza kumnusuru aliyehukumiwa kudhurika na Allah (s.w). Kwa kufahamu hivi, muumini wa kweli hatarajiwi kumuogopa na kumchelea yeyote katika kutekeleza amri ya Allah (s.w). Historia inatuonesha kuwa Mitume wa Allah (s.w) na wale walioamini pamoja nao, hawakutetereka kamwe katika kutekeleza amri za Allah (s.w) kwa kuwa walifahamu kwa yakini kuwa hakuna yeyote atakayewasaidia dhidi ya adhabu ya Allah (s.w). Allah (s.w) anatukumbusha hili katika aya ifuatayo:

﴿قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا﴾

Sema: Waiteni wale mnaodai (kuwa wana uwezo) mkamwacha Yeye (Allah). Hawataweza kukuondosheeni shari wala kubadilisha (kuwa kheri). (17:56).

(D) SIFA ZA ALLAH (S.W) ZINAZOONESHA UADILIFU WAKE USIO NA MIPAKA

Pamoja na kwamba Allah (s.w) anatawala kila kitu na ana uwezo wa kufanya lolote apendalo dhidi ya kiumbe chochote, amejilazimishia uadilifu. Kila kiumbe anayestahiki kupata hiki au malipo fulani kutokana na ahadi yake, atamlipa kwa uadilifu. Sifa zifuatazo zinaonesha uadilifu wake katika kuwahukumu na kuwalipa waja wake.

79. Al-Hakamu Yeye ni Hakimu. Hakimu anayejitosheleza, asiyehitaji ushauri, msaada au ushahidi kutoka kwa yeyote. Ni hakimu aliyemjuzi kamili wa kesi anayoihukumu. Aya zifuatazo zinafafanua sifa hii:

﴿وَنَادَىٰ نُوحٌ رَّبَّهُ فَقَالَ رَبِّ إِنَّ ابْنِي مِنْ أَهْلِي وَإِنَّ وَعْدَكَ الْحَقُّ وَأَنتَ أَحْكَمُ الْحَاكِمِينَ ﴾

"Na Nuhu alimuomba Mola wake (alipomuona mwanawe anaangamia) akasema: "Ee Mola wangu! Mwanangu ni katika watu wa nyumbani kwangu (mbona anaangamia)? Na hakika ahadi yako ni haki, nawe ni mwenye kuhukumu kwa haki kuliko mahakimu (wote)" (11:45)

80. Al-'Adilu Mwadilifu

81. Al-Muqsit Mwenye kuhukumu kwa haki, Muadilifu.

82. Al-Fattaah Jaji Mkuu, Mbora wa mahakimu. Sifa hii inarejewa katika Qur-an kama ifuatavyo:

﴿رَبَّنَا افْتَحْ بَيْنَنَا وَبَيْنَ قَوْمِنَا بِالْحَقِّ وَأَنتَ خَيْرُ الْفَاتِحِينَ﴾

"Mola wetu! Hukumu baina yetu na baina ya wenzetu kwa haki, Nawe ndiye Mbora wa wanaohukumu" (7:89).

83. Al-Muntaqim Mwenye kulipa kisasi na kuwaadhibu waovu. Aya zifuatazo zinafafanua sifa hii:

﴿وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن ذُكِّرَ بِآيَاتِ رَبِّهِ ثُمَّ أَعْرَضَ عَنْهَا إِنَّا مِنَ الْمُجْرِمِينَ مُنتَقِمُونَ﴾

"Na nani dhalimu mkubwa kuliko yule anayekumbushwa kwa aya za Mola wake kisha akazikataa?Hakika sisi ni wenye kuchukua kisasi kwa wale wabaya". (32:22)

﴿وَاتَّقُوا فِتْنَةً لَّا تُصِيبَنَّ الَّذِينَ ظَلَمُوا مِنكُمْ خَاصَّةً وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴾

"Na iogopeni adhabu ambayo haitowasibu pekee yao wale waliodhulumu nafsi zao katika ninyi.Na mcheni Mwenyezi Mungu.Hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu" (8:25)

84. Al-Hasiib Mpweke katika kuhesabu. Tunapata ufafanuzi wa sifa hii katika aya ifuatayo:

﴿وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا ﴾

"Na mnapoamkiwa na maamkio yoyote yale, basi itikieni kwa yaliyo bora kuliko hayo, au rejesheni hayo hayo. Hakika Mwenyezi Mungu anafanya hisabu ya kila kitu" (4:86)

85. As-Sabuur Msubirifu, Mwingi wa subira. Tukizingatia sifa hizi za Allah (s.w) tunaona kwa yakini kuwa mja hana njia yoyote ya kuepa hukumu ya Allah (s.w). Hakimu atakuwa ni Allah (s.w) mwenyewe na hapana njia yoyote ya kupata upendeleo wowote mbele ya mahakama ya Allah (s.w). Muumini yeyote aliyeelewa vyema sifa hizi anatarajiwa awe muadilifu katika kila kipengele cha maisha yake yote na ahukumu kila jambo kwa haki. Kwani kila hukumu iliyopitishwa kinyume na haki, Mwenyezi Mungu ataihukumu kwa haki na kumlipa haki aliyestahiki na kumuadhibu vikali aliyeizuia haki.

(E) SIFA ZA ALLAH (S.W) ZINAZOONESHA UREHEMEVU, USAMEMEHEVU NA UPENDO WAKE KWA WAJA WAKE

Allah (s.w) pia ana sifa zifuatazo ambazo hukamilisha Uungu wake na kukidhi mahitajio yote ya viumbe. Pamoja na sifa za upweke wa Uungu wake, upweke wa uwezo wake wa kuumba, kukuza, kulea, kunawirisha, kuendeleza na kuvimiliki kwa udhibitifu mbingu na ardhi na vyote vilivyomo, na pamoja na upweke wa uadilifu wake katika kuwahukumu waja wake na kuwalipa malipo yanayostahiki, Allah (s.w) vile vile ni mwingi wa rehema, mwingi wa kusamehe, mwingi wa huruma na upendo kwa viumbe vyake. Hebu tuzingatie sifa zifuatazo:

86. Ar-Rahmaan Mwingi wa Rehema, Mwingi wa Ukarimu.

87. Ar-Rahiim Mwenye kurehemu, Mwingi wa Huruma. Sifa hizi zimewekwa pamoja, japo hatuoni tofauti kubwa katika tafsiri, ili kukamilisha sifa ya Urehemevu wa Allah (s.w). Hapana yeyote katika waja wake anayekirimu na kuhurumia viumbe vyake, mfano wa kukirimu na kurehemu kwake.

88. Al-Kariim Mkarimu, Mwingi wa Ukarimu.

89. Ar-Razzaaq Mwingi wa kuruzuku, Mruzuku pekee. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ndiye mtowaji wa riziki, Mwenye nguvu madhubuti (51:58) 90. Al-Mu-'utii Mwingi wa kutoa, Mpaji. Aya ifuatao inafafanua sifa hii:

﴿قَالَ رَبُّنَا الَّذِي أَعْطَىٰ كُلَّ شَيْءٍ خَلْقَهُ ثُمَّ هَدَىٰ ﴾

(Musa) akasema: "Mola wetu ni Yule aliyekipa kila kitu umbo lake kisha akakiongoza. (20:50)

91. Al-Wahhaab Mpaji mkuu.Mpaji pasina hesabu. Katika Qur-an tunafahamishwa:

﴿رَبَّنَا لَا تُزِغْ قُلُوبَنَا بَعْدَ إِذْ هَدَيْتَنَا وَهَبْ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحْمَةً إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ ﴾

Mola wetu! Usiache nyoyo zetu kupotea baada ya kuwa tayari umeziongoza, na utupe rehma kutoka kwako. Hakika Wewe ndiwe Mpaji mkuu.(3:8)

92. Al-Barru Mwema pekee. Mfadhili. Qur-an inaieleza sifa hii katika aya ifuatayo:

﴿إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ﴾

"Hakika sisi zamani tulikuwa tukimuabudu yeye (tu).Hakika Yeye Ndiye Mwema Mwenye rehma" (52:28)

93. An-Naafiu' Mwenye kunufaisha.

94. Ash-Shakuur Mwenye shukurani, Mshukuriwa. Sifa hii tunaipata katika aya zifuatazo:

﴿لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ ﴾

"Ili awape ujira wao kamili na kuwazidishia fadhila zake.Hakika Yeye ni mwingi wa msamaha, Mwenye shukurani" (35:30)

﴿وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي أَذْهَبَ عَنَّا الْحَزَنَ إِنَّ رَبَّنَا لَغَفُورٌ شَكُورٌ ﴾

"Na watasema (katika kushukuru kwao) sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliyetuondolea huzuni,kwa yakini Mola wetu ni mwingi wa msamaha, mwenye shukurani". (35:34)

95. Al-Ghaffaaru Msamehevu, Mwingi wa usamehevu. Tunaikuta sifa hii katika aya ifuatayo:

﴿وَإِنِّي لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا ثُمَّ اهْتَدَىٰ﴾

"Na hakika Mimi ni Mwenye kusamehe sana kwa anayetubia na kuamini na kutenda mema, tena akashika uongofu (bara bara)". (20:82)

96. Al-Ghafuuru Mwenye kusamehe, Mwingi wa Kusamehe.

97. At-Tawwaabu Mwenye kupokea toba.

98. Al-'Afuwwu Mwingi wa msamaha, Mtoaji msamaha.

99. Al-Haliimu Mpole.

100.Al-Waduud Mpenda, Aliyejawa na upendo.

101.Ar-Rauufu Mwingi wa upendo na huruma.

102.Al-Latiifu Mpole, Mwema sana, Laini kwa upole, Mwenye huruma sana.

103.Al-Haadii Mwongozaji.

104.Al-Hamiidu Mwenye kusifika, Mstahiki sifa pekee, Msifiwa. Hizi ndizo sifa za Allah (s.w) kama zinavyojitokeza kwenye Qur-an na Hadithi. Kila muumini hana budi kuzifahamu na kuzizingatia sifa hizi ili aweze kuishi maisha anayoyaridhia Allah katika kila hatua na kila kipengele cha maisha yake ya kila siku.

Mja anayemuamini Allah na kumfahamu vyema kwa sifa zake, anatarajiwa awe na msimamo madhubuti katika kutekeleza amri zote za Allah (s.w) na kusimamisha ufalme wake hapa ulimwenguni, kwani ana yakini kuwa mahitaji yake yote ikiwa ni pamoja na ulinzi, hifadhi, huruma, upendo na msamaha juu ya udhaifu wake yako mkononi mwa Allah (s.w) peke yake. Ana yakini kuwa akimtegemea yeyote kwa mahitaji hayo atakuwa amejiyumbisha na kujidhulumu mwenyewe nafsi yake, kujidhulumu kukubwa kusiko na kifani.

Maana ya Kumuamini Allah (s.w) katika Utendaji wa kila siku Hatua ya tatu na ya mwisho katika kuiendea Imani ya kweli juu ya Allah (s.w) ni hatua ya utendaji. Hivyo kiutendaji anayemuamini Allah (s.w) ni yule anayefuata maamrisho yake yote na kuacha makatazo yake yote pamoja na kuyaendea maisha yake ya kibinafsi na ya kijamii kwa kufuata mwongozo wake pekee - Rejea kurasa za mwanzo juu ya "Nani Muumini?" Aidha Muumini wa kweli ni yule atakayejitenga mbali na aina zote za shirk. Shirk ni kujaalia kinadharia au kiutendaji kuwa yupo mungu au miungu wengine pamoja na Allah (s.w) wanaosaidiana kuendesha nidhamu ya ulimwengu.

Kuna aina kuu nne za shirk:-

1.Shirk katika Dhati ya Allah (s.w). 2. Shirk katika sifa za Allah (s.w).

3. Shirk katika Hukumu za Allah (s.w)

4. Shirk katika Mamlaka ya Allah (s.w).

Shirk katika Dhati ya Allah (s.w) Kumshirikisha Allah (s.w) katika dhati yake ni kuchukua vitu au viumbe kama vile masanamu, hirizi, majabali, moto, ngombe, binadamu, n.k. na kuvinasabisha na Uungu na kuvielekea kwa unyenyekevu kwa kuviomba na kuvitegemea kama anavyostahiki kuombwa na kutegemewa Allah (s.w). Shirk katika Sifa za Allah (s.w) Kumshirikisha Allah (s.w) katika sifa zake ni kukinasibisha au kukipachika kiumbe chochote sifa anazostahiki kusifiwa kwazo Allah (s.w) pekee au kumdunisha Allah (s.w) kwa kumfananisha na viumbe vyake. Hata kumsifu Mtume kupita kiasi ni shirk kama tunavyotahadharishwa katika hadith ifuatayo:

"Imepokelewa kutoka kwa Umar (r.a) kuwa, Mtume (s.a.w.w) amesema: Msizidishe katika kunisifu kama walivyozidisha Wakristo (Manasara) katika kumsifu mwana wa Maryam (Isa (a.s). Mimi ni mja wa Allah tu kwa hiyo niiteni: "Mja wa Allah na Mtume wake" (Sahihi Bukhari).

Pia Waislam wanakatazwa kujisifu na kujitukuza au kuwasifu na kuwatukuza wengine kiasi cha kukiuka mipaka ya Allah (s.w) katika aya ifuatayo:

﴿الَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَائِرَ الْإِثْمِ وَالْفَوَاحِشَ إِلَّا اللَّمَمَ إِنَّ رَبَّكَ وَاسِعُ الْمَغْفِرَةِ هُوَ أَعْلَمُ بِكُمْ إِذْ أَنشَأَكُم مِّنَ الْأَرْضِ وَإِذْ أَنتُمْ أَجِنَّةٌ فِي بُطُونِ أُمَّهَاتِكُمْ فَلَا تُزَكُّوا أَنفُسَكُمْ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اتَّقَىٰ﴾

"... Yeye ndiye anayekujueni sana tangu alipokuumbeni katika ardhi na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase (msizisifu) nafsi zenu, yeye anamjua sana aliyetakasika" (53:32)

Waumini wa kweli pia wanatarajiwa wawe ni wenye kumtegemea Allah (s.w) pekee kwa kila jambo wanalolihitajia na kuomba moja kwa moja msaada wake, Baraka, Rehema zake, Msamaha wake n.k kwa kutumia sifa zake (majina yake) zinazolandana na yale tuyaombayo:

﴿ قُلِ ادْعُوا اللَّـهَ أَوِ ادْعُوا الرَّحْمَـٰنَ أَيًّا مَّا تَدْعُوا فَلَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ وَلَا تَجْهَرْ بِصَلَاتِكَ وَلَا تُخَافِتْ بِهَا وَابْتَغِ بَيْنَ ذَٰلِكَ سَبِيلًا﴾

"Sema; mwombeni (Allah) kwa jina la Allah au muombeni (kwa jina la) Rahman, kwa jina lolote mnalomwita (katika haya itafaa); kwani ana majina mazuri mazuri.." (17:110)

Shirk katika Hukumu za Allah (s.w) Kumshirikisha Allah (s.w) katika hukumu zake ni kutoa hukumu kinyume na alivyohukumu Allah (s.w) juu ya masuala mbali mbali. Kwa mfano Allah (s.w) anahukumu kuwa adhabu ya mwizi ni kukatwa kiganja chake cha mkono wa kulia; wazinifu wachapwe viboko mia, n.k. Pakitokea sheria inayotoa hukumu kinyume na Allah (s.w), itakuwa imemshirikisha Allah (s.w) katika hukumu zake. Inasisitizwa katika Qur-an kuwa wale wasiohukumu kwa kufuata sheria ya Allah (s.w) ni Makafiri, Madhalimu na Mafaasiq.

﴿وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ ﴾

"Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu basi hao ndio Makafiri.Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio Madhalimu.Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio Mafaasiq" (5:44- 47)

Shirk katika Mamlaka (Uongozi wa) ya Allah (s.w) Allah (s.w) ndiye aliyemuumba mwanaadamu kwa lengo na ndiye mwenye haki pekee ya kumuwekea mwanaadamu sharia na mwongozo wa maisha.

Akitokea mtu au kikundi cha watu kuchukua jukumu la kumtungia mwanaadamu sheria kinyume na ile ya Allah na kumtaka atii sheria hiyo ni kuchukua nafasi ya Allah (s.w). Hivyo atakayewaamrisha watu wamtii kinyume na sharia ya Allah (s.w) au atakaye waamrisha watu waishi kinyume na mwongozo wa Allah (s.w) atakuwa amechukua nafasi ya Uungu. Mayahudi na Wakristo wameshutumiwa katika Qur-an:

﴿اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا إِلَـٰهًا وَاحِدًا لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴾

"Wamewafanya wanazuoni wao na watawa wao kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu..." (9:31)

Mtume(s.a.w.w) katika kufafanua aya hii ameeleza kuwa kuwafanya wanazuoni au viongozi wengine kuwa mungu badala ya Allah (s.w) ni kuwatii kinyume na sharia ya Allah (s.w). Hivyo kukitii kiumbe chochote kinyume na utii kwa Allah (s.w) ni kukifanya kiumbe hicho mungu. Kina cha Uovu wa Shirk Shirk ni dhambi kubwa kuliko zote kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:

﴿إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا ﴾

"Hakika Allah hasamehi (dhambi ya) kushirikishwa na kitu na husamehe yasiyo haya kwa amtakaye. Na anayemshirikisha Allah bila shaka amebuni dhambi kubwa" (4:48)

﴿إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا ﴾

"Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi (dhambi ya) kushirikishwa na kitu na husamehe yasiyokuwa haya kwa amtakaye.Na anayemshirikisha Allah bila shaka yeye amepotea upotofu ulio mbali." (4:116)

Dhambi ya shirk hufuta mema yote aliyoyatenda mja kabla ya kushirikisha. "Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa wale waliokuwa kabla yako,kuwa "kama ukimshirikisha (Allah) bila shaka amali zako zitaruka patupu, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye khasara" (39:65)