MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 0%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi: Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui, Al-Zenjibari.
Kundi:

Matembeleo: 59165
Pakua: 4782

Maelezo zaidi:

MUANDAMO WA MWEZI
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 59165 / Pakua: 4782
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

14

MUANDAMO WA MWEZI

SEHEMU YA KUMI NA NNE

UFAFANUZI WA AYA ISEMAYO : ATAKAYEUHUDHURIA MWEZI AFUNGE!

MUNASEMA

14.Ufafanuzi Wa Aya Isemayo:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atakayeuhudhuria mwezi afunge!" (2: 185)

Uchambuzi wa neno "shahida" na neno "Shahra"; baadhi ya watu wamedhani kwamba maana ya shahida ni 'kuona kwa macho' na neno Shahra wanadhani kuwa ni 'mwezi - muandamo.' Kwa mujibu wa Wafasirina takr iban wote wamelifasiri neno 'shahida' kwa maana ya "kuwepo" au "kuhudhuria" wala sio maana ya 'kuuona mwezi' hata Shaykh Muhammad 'Aliy Assaabuniy ameona ni makosa kitafsiri kulifasiri neno hilo kwa maana ya "Kuuona mwezi muandamo" kama alivyosema:: 27) "Na wala sio maana ya neno 'shahida' (liliyomo katika Aya hiyo) kwa maana ya kwamba: 'ameuona mwezi." Neno 'shahra' lililomo katika Aya hiyo linaleta maana ya 'mwezi - siku' yaani 'month' kwa lugha ya Kiingereza. Ni mwezi unaoashiria tarehe kuanzia 1 mpaka 29 au 30. Wala neno hilo halina maana ya 'mwezi-sayari' yaani 'crescent' au 'moon' kwa lugha ya Kiingereza.

JAWABU

Kama Shahida ina maana ya kuhudhuria tu, basi maana itakuwa "Atayekuwepo katika mji wa mwezi (month). Na kama ni hivyo, hii ni dalili kwamba kuna miji myengine bado hakuna mwezi (month) kwani Aya imekuja kwa njia ya mafhumu Al-Shati na mafhumu hii ni dalili katika dalili za Kisharia. Na kwa maana hio, itakuwa kuna sehemu mwezi bado haujaonekana; wanaoamrishwa kufunga ni wale ambao mwezi (month) umewaingilia kwa kuuona mwezi (Crecent). Tafsiri yenu inaupa nguvu msimamo wetu: si msimamo wenu. Pili wanavyuoni walioifasiri Aya hio kwa maana ya kuona wako wengi kama nilivyotaja baadhi yao katika kitabu na nitanukuu tena baadae.

MNASEMA

Kitu muhimu ni kuelewa kwamba maneno mawili hayo yaani 'shahida' na 'shahra' yaliyomo katika aya hiyo, yana maana tuliyoieleza hapo juu na ndivyo walivyoeleza Wafasirina wakubwa wote. Ni vyema mtu anapoingia katika mjadala kama huu atoe madondoo sahihi yenye kukubalika sio kuingiza fikra zake tu, hususan katika suala hili la tafsiri. Tukianza kutumia utamaduni huo wa kila mmoja kubuni tafsiri yake mwenyewe na tukaziacha tafsiri za Wanazuoni wenye kutegemewa, jambo hilo litatufanya tuwe na idadi kubwa ya wafasiri 'bandia' ambao sio wafasiri wa kweli.

JAWABU

Wafasirina bandia wamejaa sasa huko Zanzibar, ndio maana ikawa munanukuu kanuni za kiusuli na kuziweka si mwahala mwake bali hata kuzifasiri pia zinakushindeni munafasiri sivyo, halafu munataka kuingia katika mijadala ya elimu kama hii. Pili: Kinachotazamwa si tafsiri za wanavyuoni tu, hususan wasio Masahaba, bali kinachotazamwa ni dalili walizozitoa. Isipokuwa pale walipokubaliana ndio huwa kuna ulazima wa kufata: sio walipotafautiana. Tatu: Kama nilivyosema Wafasirina na Maulamaa wakubwa Mujtahidun walioifasiri Aya hio kwa maana ya kuona wako wengi kama tutavyonukuu maneno yao.

MNASEMA

Vile vile ukizingatia neno 'shahra'﴿ الشَّهْرَ﴾ utaliona katika herufi yake ya mwisho ambayo ni 'Re' imetiwa 'fat-ha' hio haina maana kwamba neno hilo lina maana ya 'mtendwa' kama wanavyodhania baadhi ya watu. Ingaw aje neno hilo limemalizikia 'fat-ha', lakini halina maana ya 'mtendwa' bali neno hilo linaashiria maana ya 'wakati'. Ni muda maalumu kama mfano mtu akisema: "Nitakuja mwezi wa Ramadhaan" hapa hakuna kitu chenye kuonekana bali muda au wakati tu Kinyume na akisema: "Nimeuona mwezi" hapa ndio itakuwa neno 'mwezi' ni 'mtendwa.' Kwa hiyo, wanaotumia Aya hiyo kwa maana ya 'kuuona mwezi kwa macho' sio sahihi kama alivyothibitisha hayo Mwanachuoni - Mufasir katika tafsiri ya 'Al-Kashaaf'. Na vile vile katika kitabu: 'Rawaaiul-Bayaan' yameelezwa hayo hayo.

Kinyume na maneno ya ndugu Juma aliposema: ((Aya hii inawezekana kuchukua tafsiri zote: kushuhudia kwa maana ya kuona na kushuhudia kwa maana ya kuwepo katika mji. Na zote zinakubalika kwa mujibu wa fani za tafsiriInasikitisha sana mar a nyingi kumuona ndugu yetu Juma anavyotoa tafsiri ya baadhi ya Aya za Qur-aan bila kuwapa nafasi Mashaykh wenye kutegemewa katika ulimwengu wa Kiislam. Anachokifanya yeye ni kuingiza fikra zake binafsi katika kufasiri Aya za Qur-aan tukufu. Kitendo ambacho hakikubaliki. Kwani ingekuwa inakubalika hali hiyo bila shaka kusingelikuwa na haja ya kutegemewa tafsiri yoyote, kwani kila mmoja wetu angelikuwa bingwa wa kubuni tafsiri aitakayo mwenyewe - jambo ambalo lingetufikisha pahala pabaya na baya zaidi ni kumsingizia uongo Mwenyezi Mungu katika Maneno Yake Matukufu. Wala hatukusudiwi kwamba hao wafasiri pekee walikuwa kama kwamba wakipata 'Wahyi' na kwamba maneno yao yalikuwa hayawezi kuwa na dosari au kupingwa. La hasha! Kinachokusudiwa ni kuwa anapoingia mtu yeyote katika mjadala wa kutetea hoja juu ya jambo fulani lazima aonyeshe madondoo sahihi yenye kuthibitisha dai lake hilo , sio kutoa fikra zake na zikakubalika. Kinachosisitizwa ni ule umuhimu wa kuonyesha madondoo ya tafsiri ya Aya za Qur-aan alizotegemea sio nafasi ya mtu kutumia akili yake katika maeneo hayo.

JAWABU

Wanavyuoni wa tafsiri hawakukubaliana juu ya suala hili kinyume na munavyodhani nyini. Wako waliosema kwamba neno 'shahra'﴿ الشَّهْرَ﴾ limetiwa fataha kwa kuwa ni dharfu-zaman kama mulivy onukuu nyinyi. Na kuna wengine wengi wanavyuoni wakubwa waliosema kuwa ni 'mtendwa'. Sasa nyinyi ilikuwa mutuoneshe ni ipi kauli sahihi tufate. Anasema Abu Hayyan - baada ya kuitaja hio irabu mulioitoa nyinyi - : "Na wakasema kwamba kunasibika ( kuingia fataha) kwa neno Sha-hr ni kwa kuwa ni (mtendwa). Nayo ni kwa msingi wa kuondoshwa mudhaf na maana ni atayeshuhudia - mtendwa wake akaondoshwa - naye ni mji (misr) au mji (balad)." Na haya yote nilikuelezeni lakini nyinyi hamutazami kilich osemwa: munatazama aliyesema. Kisha Abu Hayyaan akatoa muelekeo mwengine wa neno lililoondoshwa akasema: "Na ikasemwa kwamba kunasibika (kuingia fataha) kwa neno Sha-hr ni kwa kuondoa mudhaf nalo ni neno dukhul". Anasema Mahmud Safi: "(Neno) Al-Shar ni mtendwa, kwa (kukadiria) kuondoshwa mudhaf, na makadirio yake ni dukhulu Al-Shar (kuingia kwa mwezi).

Kwa ufupi ni kuwa wako wanavyuoni waliosema hivi na waliosema vile, tafauti na dhana za ndugu zetu kwamba wanavyuoni wote wamesema kitu kimoja. Na kila tafsiri moja inamuelekeo sahihi. Tafsiri ya kuwa mtendwa hasa ni mudhaf (kaondoshwa), mfano wake ni kama Aya:

﴿وَاسْأَلِ الْقَرْيَةَ الَّتِي كُنَّا فِيهَا وَالْعِيرَ الَّتِي أَقْبَلْنَا فِيهَا ۖ وَإِنَّا لَصَادِقُونَ

"Kiulize kijiji ambacho tulikuwamo ndani yake" . Sote tunajua kwamba kijiji hakiulizwi wala hakisemi. Hapa mten dwa pia kaondoshwa na asili yake ni : Waulize watu wa kijiji ambacho tulikuwemo ndani yake". Halkadhalika Aya﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ inawezekana ikawa maana yake ni"Ataye shuhudia miongoni mwenu uingiaji wa mwezi" yaani atayekuwepo katika mji wakati mwezi (month) unaingia. Tafsiri hii - kama nilivyosema - inatupa nguvu sisi. Au ikawa maana ni"Ataye shuhudia miongoni mwenu uingiaji wa mwezi" . Na kwa tafsiri hii, neno shahida litakuwa kwa maana ya kuona. Na - kama invyoleweka - kwamba kuweza kujua ni maana gani neno imekusudiwa, ni pale litapokuwa katika sentensi. Na kama neno sh ahida kwa asili halina maana ya kuona; je haliwezi kuwa na maana hio kwa misingi ya kimajazi zikiwepo Qarina?

MNASEMA

Takriban wafasirina wote wa Qur-aan tukufu wameifasiri Aya hiyo kwa maana ya 'atakayekuwa katika mji katika huu mwezi wa Ramadhaan afunge. Hakuna hata mmoja aliye Mwanachuoni wa kweli aliyeifasiri Aya hiyo kwa maana ya 'atakayeuona' au 'atakayeushuhudia' mwezi afunge. Wala hakuna khitilafu katika tafsiri za Wanavyuoni hao juu ya Aya hiyo. Khitilafu iliyopo ni moja tu: Je mwezi ukiandama sehemu moja duniani italazimu kufunga sehemu nyengine zilizobaki au kila sehemu na muandamo wake?

JAWABU

Kwanza: inaonekana hamukuyasoma maandishi yangu kwa makini wala hamujua mimi naeleza nini. Nilichokisema ni hiki: Wanavyuoni wengi wameifasiri Aya hii, kuwa maana yake ni "Atayeuhudhuria mwezi (Month) basi na-aufunge." Kisha wakabainisha kwamba maana ya atayeuhudhuria mwezi, ni atayekuwa katika makazi yake, yaani si msafiri. Nynyi munanijibu "Takriban wafasirina wote wa Qur-aan tukufu wameifasiri Aya hiyo kwa maana ya 'atakayekuwa katika mji katika huu mwezi wa Ramadhaan afunge". Sasa tafauti iko wapi?!

Kisha mukadai yale yale alioyadai Sheikh Nassor kwamba "Hakuna hata mmoja aliye Mwanachuoni wa kweli aliyeifasiri Aya hiyo kwa maana ya 'atakayeuona' au 'atakayeushuhudia' mwezi afunge". Nalo pia ni kosa kwani nakala za wanavyuoni walioifasiri Aya hio kwa maana ya kuona nimekupeni kwa wingi. Nimesema katika kitabu:

1) Abu Al-Suud - katika Maulamaa wa tafsiri - baada ya kuifasiri Aya hio kama alivyosisitiza Sheikh Nassor Bachoo, anasema: "Na ikasemwa kwamba (maana ya Aya hio ni) mwenye kuushuhudia hilala Al-shahri mwezi muandamo wa mwezi (wa Ramadhani) basi naafunge kama kauli yako (unaposema): 'Nimeshuhudia ijumaa yaani Sala yake (Sala ya ijumaa)." Mwisho wa kunukuu. Ni wazi kwamba kwa mujibu wa Abu Al-suud, kuna kauli ya pili juu ya tafsiri ya Aya hii, amba yo wengine wameshikana nayo. Na bila shaka Abu Al-suud hazungumzii watu wa Afrika ya Mashariki.

2) Ibn Al-arabiy. Anasema: "(Aya hii - yaani "Atayeushuhudia mwezi na-aufunge), inafasiriwa kwa kuushuhudia mwezi (month), nako ni kuuona mwezi muandamo, na vivyo hivyo kasema Mtume (s.a.w.): "Fungeni kwa kuuona na fungueni kwa kuuona." Mwisho wa kunukuu.

3) Ibn Baraka Al-bahlawiy, Al-umaniy, baada ya kuinukuu Aya hio inayosema:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Ataye ushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge." Akasema: "Na kushuhudia kuko kwa namna mbili: kushuhudia katika kuuona (mwezi muandamo) na kushuhudia kwa kujua kama kipofu na yule ambaye uoni wake amepungua kwa sababu ya kufichikana kwa (mwezi) au asiweze kuuona mwezi."

4) Abu Zahra kataja tafsiri ya Aya hio:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Ataye ushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" kwamba maana yake ni:"Atayeushuhudia miongoni mwenu mwezi muandamo wa mwezi (wa Ramadhani)."

5) Ibn Hazm baada ya kuinukuu Aya:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Ataye ushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" anasema: "Atayeuona basi kwa hakika kaushuhudia."

6) Al-Jassas Al-Razi, kaweka mlango aliouita : Babu kayfiyyati shuhudi al-shahri. Hapa Al-imamu Al-jassas, anazungumzia kuandama kwa mwezi ni vipi: nini dhana au mafhum (concept) ya kuandama kwa mwezi Kisheria? Akaanza kwa kunukuu Aya mbili:

Moja : ni Aya inayosema:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" .

Pili : ni Aya inayosema:﴿يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْأَهِلَّةِ ۖ قُلْ هِيَ مَوَاقِيتُ لِلنَّاسِ وَالْحَجِّ ۗ "Wanakuuliza kuhusu miezi miandamo, sema hivyo ni vipimo vya nyakati kwa ajili ya watu na hija" . Kisha akanukuu Hadithi ya Ibn Umar (r.a.), kisha akatoa maelezo mpaka akasema: (Likaonesha hilo kwamba kuuona mwezi muandamo ndio kuushuhudia mwezi (wa siku 29 au 30 yaani month ).

Ni wazi kwamba Al-jassas kaifasiri Aya hii kwa maana ya kuona kwa macho.

Na kabla ya hapa alisema: "Na hukumu zinazopatikana kutoka katika kauli yake (Allah S.W. inayosema):﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" ni kumlazimu kuufunga mwezi yule aliyeshuhudia miongoni mwao. Na kushuhudia kunagawika sehemu tatu: kuujua (kwamba mwezi umeandama), kuwepo katika mji, ..na ikamaanisha pia kwamba aliyeuona mwezi muandamo peke yake basi inampasa kuufu nga." Tazama uzuri maneno haya ya Al-imamu Al-jassas, utaona kwamba kakufasiri kushuhudia kulikotajwa katika Aya kwa tafsiri tatu: moja ya hizo ni kuona.

7) Anasema Al-Imamu Abu Muslim: "Na akauita Allah mwanzo wa mwezi kwa jina la mwezi mzima au pakadiriwe mudhafu (kilichotegemezwa ambacho kimeondoshwa nacho ni Hilal)." Bali Abu Muslim kabla ya hapa kanukuu kauli ya Al-zajjaj akisema "Shahru ni jina la Hilal (mwezi muandamo), ingawa kauli hii Al-imam baadae kaipinga.

8) Sheikh Al-Khalili na Prof Moh'd Bakr Ismail, utaona kwamba dhahiri ya maneno yao katika vitabu vyao ni kuwa Aya hio pia inafasirika kwa maana ya kuona kwa macho, ambapo Sheikh Al-khaliliy anasema hivi: "Na hoja gani basi iliothabiti zaidi na kubwa zaidi kuliko mtu kuuona mwezi muandamo kwa macho yake ambao wajibu wa funga au hukumu ya kufungua zimefungamanishwa nao. Mwenyezi Mungu anasema:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" 9) Ama Prof Moh'd Bakr Ismail yeye anasema kuhusu mtu aliyeuona mwezi peke yake: "Na saumu imemuajibikia peke yake katika hali hii, kwa sababu ya kauli yake Allah (S.W.):﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge".

10) Ibn Uthaimin alipokuwa akielezea tafsiri ya wale wenye msimamo kwamba kila mji na muandamo wake, alisema - kuhusu Aya hio inayosema:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" - maneno haya: "Na inajulikana kwamba haikusudiwi kwa (Aya) hio kw amba kila mtu auone peke yake, basi unatendewa kazi (muandamo huo) katika sehemu (mji) ulioonekana." 11) Al-Sayyid Ahmad Al-Hashimiy, alipokuwa akizungumzia darsa inayoitwa Al-istikhdam katika fani ya balagha, alitoa mfano wa Aya hio:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" kisha akasema: (Makusudio ya mwanzo ya neno Al-shahru (mwezi wa siku 29-30: month, katika Aya hii) ni Al-hilalu (Mwezi muandamo)." Mwisho wa kunukuu.

12) Anasema Dr. Wahbat Al-zuhailiy: "Mfano wa sababu ni kauli yake Allah Mtukufu﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" (basi) kuuona mwezi muandamo ndio sababu ya uwajibu wa kufunga." Je hao wote si wanavyuoni wa kweli? Ama kauli yenu: "Wala hakuna khitilafu katika tafsiri za Wanavyuoni hao juu ya Aya hiyo. Khitilafu iliyopo ni moja tu: Je mwezi ukiandama sehemu moja duniani italazimu kufunga sehemu nyengine zilizobaki au kila sehemu na muandamo wake". Jawabu ni kuwa khilafu ipo, lakini nyinyi munapenda kudai "Wamekubaliana" au "Maulamaa wote wamesema" n.k. Hili ndio tatizo lenu, na si nyinyi tu bali hata wale wenzenu walioko Saudia huo ndio mtindo wao. Hebu rejeeni hizo tafsiri mulizozitoa, kama ya Abu Suud, Abu Hayyan na wengine, mutazame je hamutooana waliosema kuwa maana ya Aya hio tunayoizungumzia hapa ni﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ "Ataye ushudia kati yune mwezi muandamo (crecent) wa mwezi (wa ramadhani" . Sasa kuushudia mwezi muandamo n i vipi?

MNASEMA

Mantiki hiyo ndiyo aliyotumia Shaykh Naaswir Bachuu kila anapotaja tafsiri ya Aya za Qur-aan tukufu huwa anaonesha pahala alipoitoa tafsiri hiyo. Kwa hivyo hakwenda kinyume na kanuni za kielimu na misingi sahihi ya Dini yetu. Alichosisitiza Shaykh Naaswir Bachuu katika Hadiyth isemayo:

(Fungeni kwa kuuona mwezi - muandamo) Ni kuwa Hadiyth hii ni 'aam - yaani ya ujumla, kwa hivyo popote mwezi utakapoonekana na habari hizo zikathibitishwa usahihi wake, basi watu wote wafunge. K adhalika wafungue kama ni mwezi wa kufungua. Pia Shaykh Naaswir ameonesha msimamo wa Wanazuoni juu ya masimulizi ya Kuraib kwamba hayawezi kuwa "hoja sahihi" katika mas-ala haya.

JAWABU

Ama Sheikh Nassor kenda kinyume na kanuni za elimu katika sehemu nyingi za kitabu chake. Kwanza katoa tafsiri na kupinga tafsiri bila kuonesha kwa mujibu wa kanuni za lugha, usuli na nyengine, usahihi wa tafsiri alioichagua: hakuonesha kifani kwanini kakipinga alichokipinga na kukisapoti alichokisapoti. Kwa hivyo, hakuwa na dalili za kielimu isipokuwa fulani kasema; wakati fulani kasema ni hoja ambayo kila kundi inalo. Kinachotakiwa ni kuonesha kuwa hoja hizi ndio sahihi kwa sababu kadha. Ama Hadithi(Fungeni kwa kuuona mwezi - muandamo), tumeshaielezea sana hatuna haja ya kuikariri mara kwa mara. Pia Hadithi ya Kuraib tumeshaielezea na kutoa majibu juu ya tafsiri sahihi ya Hadithi hio, hatuna haja ya kuikariri mara kwa mara.

MNASEMA

Ndugu Juma yeye amezitaja baadhi ya tafsiri za Quran na baadhi ya vitabu vilivyotaja Aya inayoelezewa:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ Akidhania kuwa tafsiri hizo zimeitafsiri Aya hiyo kuwa:"Atakayeushuhudia mwezi afunge." Ukichunguza vyema utaona kuwa ndugu Juma hakuelewa kinachokusudiwa katika tafsiri hizo. Kwanza utaona kuwa kila anapojaribu kulito lea tafsiri neno﴿ شَهِدَ﴾ 'shahida' huliwacha kama lilivyo kwa kusema 'atakayeushuhudia'. Ni kama kusema:"Atakayeushuhudia" maana yake"atakayeushuhudia."

JAWABU

Maana ya kuliwacha neno hilo kama lilivyo, ni kwa sababu wako waliofasiri Shahida kwa maana ya kuwepo; na wako waliofasiri Shahida kwa maana ya kuona. Kwa hivyo, baadhi ya mwahala - kutegemea nakusudia nini - ndio huliwacha kama lilivyo. Lakini kila aliyesoma kitabu changu kaelewa vyema nini nilichokieleza.

MNASEMA

Hebu na tuangalie Wanavyuoni walivyolifasiri neno shahida: Mwanachuoni Dr. Zuhaily ameeleza yafuatayo: "Kuuhudhuria mwezi wa Ramadhaan ni sababu ya kuwajibika kufunga (Swaum) kama ilivyoelezwa katika Qur-aan Tukufu:" Atakayekuwa katika mji katika huu mwezi (wa Ramadhaan) afunge" .

Dr Zuhaily aliendelea kutoa dalili ya kuonesha wajibu wa kufunga kwa kuonekana mwezi - muandamo kwa kuyanukuu maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pale aliposema:(Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo) Na jambo la kuonekana mwez i japo na mtu mmoja katika Hadiyth hiyo ni la wote ('aam). Wala hakuna Mwanachuoni yeyote aliyesema kuwa Hadiyth hii inaashiria kila pahala pafuate muandamo wake. Kutegemea maneno matupu ya mwanachuoni kama ni Khaas bila ya kuonyesha dalili zenye kuk ubalika kifani, huo utakuwa udhaifu.

JAWABU

kwanza : munatabia ya kutotoa marejeo. Ilikuwa ni jambo la busara munapotaja kauli ya mtu muoneshe kutoka wapi.

Pili : ikiwa Dr. Al-Zuhaili, katika sehemu moja kasema hivyo, sehemu nyengine kasema:"Atayeushudia mwezi na aufunge" . Kuuona mwezi muandamo ndio sababu ya wajibu wa kufunga. Kwa hivyo, Dr. Al-Zuhaili pia kaifasiri Aya hio kwa maana ya kuuona kwa macho. Cha kufahamu ni kuwa mwanachuoni anapotoa maelezo kisha akataja Aya au kinyume chake anapotaja Aya kisha akatoa maelezo, basi huwa maelezo hayo ndio anaifasiri Aya hio.

Ama kauli yenu: "Wala hakuna Mwanachuoni yeyote aliyesema kuwa Hadiyth hii inaashiria kila pahala pafuate muandamo wake. Kutegemea maneno matupu ya mwanachuoni kama ni Khaas bila ya kuonyesha dalili zenye kukubalika kifani, huo utakuwa udhaifu". Ninasema: munarejea kosa lile lile alililolifanya Sheikh Nassor la kudai hivyo, nami nimekunukulieni ushahidi k uwa wako wanavyuoni waliosema kwamba Hadithi hio "Fungeni kwa kuuona.." ni mahususi kwa watu maalumu nao ni wale waliouona. Anasema Ibn Hajar: (Na w ale ambao hawakuchukua kauli hio, wanasema kwa sababu kauli yake Mtume(s.a.w.w) aliposema:"Mpaka muuone" ni agizo kwa watu maalumu." Anasema Al-san'ani: "Na ikasemwa kwamba (Muandamo wa mbali) hauzingatiwi (mbali), kwa sababu kauli yake Mtume (s.a.w.w) aliposema:"Mukiuona" ni agizo kwa watu maalumu." Maelezo haya nyinyi mumeyafumbia macho kwani hamukuyapenda.

Ama kauli yenu: "Kutegemea maneno matupu ya mwanachuoni kama ni Khaas bila ya kuonyesha dalili zenye kukubalika kifani, huo utakuwa udhaifu" inanifanya nisijue mukitakacho. Ninanapokupeni ushahidi wa kifani juu ya tafsiri fulani, munasema Juma Mazrui anafasiri kwa rai yake wala hategemai mael ezo ya wanavyuoni; mukipewa maneno ya wanavyuoni munasema "Kutegemea maneno matupu ya mwanachuoni kama ni Khaas bila ya kuonyesha dalili zenye kukubalika kifani, huo utakuwa udhaifu". Sasa munataka vipi, hebu twambieni mutakavyo!

MNASEMA

Shaykh Al-Amin 'Aliy Mazrui: katika kuifasiri Aya isemayo:﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ ameeleza yafuatayo: "Basi mwenye kuwemo katika mwezi huu na afunge." Kisha akaendelea kusema: "Muradi wa 'mwenye kuwamo katika mwezi huu' ni ambaye hakuwa sa farini." (uk. 65)[9][9] Mwanachuoni Shaykh Al-Jassas katika kitabu chake Ahkamul-Qur-aan ameweka mlango unaitwa Kayfiyati Shuhudi Shahri "mlango unaolelezea namna ya kuhudhuria mwezi" Shaykh Al-Jassas akaanza kunukuu aya mbili, ya kwanza "Famman Shahida minkum na aya ya pili "Yas-alunaka 'anil-ahilah" Ifuatayo ni tafsiri sahihi ya aya hizo kama ilivyo katika vitabu vya tafsiri, tafsiri ya aya ya mwanzo:"Atakayekuwa katika Mji katika mwezi huu mwezi (wa Ramadhaan afunge" . Tafsiri ya aya ya pili:"wanakuuliza miezi miandamo sema hiyo ni (vielelezo vya) nyakati kwa ajili (ya mambo) ya watu na hija zao" .

JAWABU

Maneno ya Sheikh Al-Amin hayana upinzani. Na - kwa ujumla - maneno hayo na yalio mfano hayo yalikuwa hayana maana kwani mimi katika kitabu changu sijapinga kwamba kuna wanavyuoni walioifasiri Aya hio kwa maana ya kuwa katika mji. Bali nilisema: Wanavyuoni wengi wameifasiri Aya hii, kuwa maana yake ni "Atayeuhudhuria mwezi (Month) basi na-aufunge." Kisha wakabainisha kwamba maana ya atayeuhudhuria mwezi, ni atayekuwa katika makazi yake, yaani si msafiri.

Kwa hivyo, mimi nanachokipinga ni dai lenu kwamba hakuna mwanachuoni aliyefasiri shahida kwa maana ya kuona: wala sijapinga ukweli kwamba kuna wengi waliosema kwamba neno shahida katika Aya ni kwa maana ya kuwepo katika mji. Bali nilisema kwamba tafsi hii ndio yenye nguvu. Nilisema hivi: Tafsiri hii inapata nguvu kwa kutazama kukabiliana kimaana (Muqabala) - kuliopo katika sehemu ya kwanza ya Aya hii na sehemu yake ya pili. Aya hii inasema: "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu, basi na-aufunge." Neno "Kushuhudia" linatumika kwa maana ya kuhudhuria, na hutumika kwa maana hio na ziada nayo ni maana ya "Kuona" kwani kila muonaji huwa kahudhuria. Sasa "Kuushuhudia" mwezi inawezekana ikawa maana yake ni kuuona kwa macho na inaweza ikawa maana yake ni kuhudhuria kwa maana ya kuwepo katika mji. Sasa ilipokuja sehemu ya pili ya Aya, ikasema:

﴿مَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۗ

"Na atayekuwa mgonjwa au kuwa safarini, basi (afunge) idadi (ya siku asizozifunga" katika siku nyengine. " Hapa ikawa tumefahamu kwamba makusudio ya Aya inayosema:"Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu, basi na-aufunge" ni "Atayekuwa katika mji: yaani si msafiri." Na kwa tafsiri hii, Muqabala (opposite au kinyume) utakuwa umepatikana, na maana ya Aya itakuwa hivi: "Huyu ni wajibu kufunga kwa kuwa ni mzima na kwa kutokuwa safarini; na (kinyume chake) yule karuhusiwa kula kwa kuwa ni mgonjwa au kwa kuwemo safarini." Msingi huu wa Muqabala, dhahir ndio msingi wa wale walioifasiri Aya hio kuwa maana yake ni: Atayekuwa katika mji: yaani si msafiri" nao ni msingi madhubuti. Hatimae nikakuta katika tafsiri ya Ibn Jariri Al-ttabari akieleza hivyo hivyo Walillahi Al-hamdu.

Sasa munachokipinga ni nini? Inaonesha hamujui mukisemacho. Ama kuhusu Al-Imamu Al-Jassas Al-Razi, nilisema hivi: Al-jassas Al-raziy, kaweka mlango aliouita: Babu kayfiyyati shuhudi al-shahri. Hapa Al-imamu Al-jassas, anazungumzia kuandama kwa mwezi ni vipi: nini dhana au mafhum (concept) ya kuandama kwa mwezi Kisheri a? Akaanza kwa kunukuu Aya mbili:

Moja : ni Aya inayosema:

﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ

Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge).

Pili : ni Aya inayosema:﴿يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْأَهِلَّةِ ۖ قُلْ هِيَ مَوَاقِيتُ لِلنَّاسِ وَالْحَجِّ ۗ "Wanakuuliza kuhusu miezi miandamo, sema hivyo ni vipimo vya nyakati kwa ajili ya watu na hija" .

Kisha akanukuu Hadithi ya Ibn Umar (r.a.), kisha akatoa maelezo mpaka akasema:(Likaonesha hilo kwamba kuuona mwezi muandamo ndio kuushuhudia mwezi (wa siku 29 au 30 yaani month).

Ni wazi kwamba Al-jassas kaifasiri Aya hii kwa maana ya kuona kwa macho.

Nyinyi maneno:(Likaonesha hilo kwamba kuuona mwezi muandamo ndio kuushuhudia mwezi (wa siku 29 au 30 yaani month) , mumeyafumbia macho kama kawaida yenu, na badala yake mukasema: Mwanachuoni Shaykh Al-Jassas katika kitabu chake Ahkamul-Qur-aan ameweka mlango unaitwa Kayfiyati Shuhudi Shahri "mlango unaolelezea namna ya kuhudhuria mwezi" Shaykh Al-Jassas akaanza kunukuu aya mbili, ya kwanza "Famman Shahida minkum na aya ya pili "Yas-alunaka 'anil-ahilah" Ifuatayo ni tafsiri sahihi ya aya hizo kama ilivyo katika vitabu vya taf siri, tafsiri ya aya ya mwanzo:"Atakayekuwa katika Mji katika mwezi huu mwezi (wa Ramadhaan afunge" . Tafsiri ya aya ya pili:"wanakuuliza miezi miandamo sema hiyo ni (vielelezo vya) nyakati kwa ajili (ya mambo) ya watu na hija zao" . Mwisho wa kunukuu.

Bali kabla ya hapo Al-Jassas kasema kuhusu Aya hio kwamba ina maana tatu; moja yao alisema: "Na ikamaanisha kwamba atayeuona mwezi peke yake basi naafunge". Ni wazi kwamba Imamu huyu anakubali kwamba neno hilo au Aya hio pia inabeba maana ya kuona. Na akasema tena: "Na Waislamu wamekubaliana kwamba Aya hii na Hadithi hio kwamba maana yake ni kuuzingatia uoni wa mwezi muandamo". Yote haya nyinyi mumeyafumbia macho, kwani lengo lenu ni kunusuru rai. Kwa ujumla nilichokipinga si kwamba Aya hio ina maana ya kuwepo katika mji: hili sikulipinga bali nililitilia nguvu. Nilichokipinga ni dai kwamba; HAKUNA WANAVYUONI WALIOFASIRI AYA HIO KWA MAANA YA KUONEKANA MWEZI. Hili nililipinga na nikatoa ushahidi wa wanavyuoni wengi kama ilivyotangulia.

MNASEMA

Ufuatao ni ufafanuzi wa aya hizo. Tunaanza na aya ya mwanzo wanazuoni wengi sana wameitafsiri aya hiyo kwa maana iliyo hapo juu. Ingawa ukilichukua neno mojamoja katika aya hiyo na ukaliangalia katika makamusi ya Kiarabu utalikuta lina maana zaidi ya moja, utaratibu huu sio mgeni katika lugha ya Kiarabu, kanuni ya lugha inasema: "Neno halina maana (moja) mpaka liwemo ndani ya sentensi", kwa hivyo neno "Shahida" liliyomo ndani ya aya hiyo lina maana ya "Kuwepo" (sio maana ya kuona). Na neno "Shahri" lina maana ya mwezi siku, sio maana ya mwezi sayari hiyo ndiyo tafsiri sahihi ama kuitafsiri kwa maana ya "atakayeuona mwezi na afunge" hiyo ni tafsiri ya kuilazimisha.

JAWABU

Natukubaliane kuwa hio ndio tafsiri sahihi, japo kuwa hamukuonesha ushahidi wa elimu, tatizo ni kuwa tafsiri hio itawapa nguvu wale wenye kudai kwamba kila watu na muandamo wao. Kwani ikiwa tafsiri ya neno "Shahida" liliyomo ndani ya aya hiyo lina maana ya "Kuwepo" na tafsiri neno "Shahri" lina maana ya mwezi siku" maana itakuwa "Atayekuwepo katika mwezi siku naafunge" hii mufhumu mukhalafa yake - na kwa hapa ina nguvu kwani ni mafhumu Al-Shart - itakuwa yule ambaye hayupo katika mwezi siku basi asifunge - anayeamrishwa ni aliyepo. Na kusema hivi haiwezekani ila iwe kuna sehemu mwezi siku tayari umethibiti; na kuna sehemu bado haujathibiti. Na hili litawapa nguvu wapinzani wenu. Sijui munafahamu au munanukuu tu?!!!

MNASEMA

Ama uchambuzi wa aya ya pili kama ulivyo katika vitabu vingi vya tafsiri, kwanza wameeleza sababu ya kuteremshwa aya hiyo ni kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameulizwa na kama aya yenyewe inavyothibitisha tokeo hilo Na vilevile Wanazuoni hao wakaeleza kuwa kilichoulizwa hapo ni hali halisi ya mabadiliko ya miezi. Kwa maelezo zaidi rudi katika tafsiri, itakutosha tafsiri ya Dr. Zuhaily. Kwa mantiki hiyo hapa hapazungumziwi kuwepo miandamo mingi wala kuwepo muandamo wa kisheria, wala Aya hii maana ya kuwa kila nchi ifunge na ifunguwe kwa mujibu wa matlai yao , vile vile Aya hii haina maana ya kuwa ni "Khaas" katika zile Hadiyth zilizotaja kwa ujumla kuhusu suala la kufunga na kufungua.

JAWABU

Sasa munaanza kuchanganya mambo. Aya ambayo imesemwa kushuka kwa sababu hio ni Aya "Wanakuuliza kuhusu miezi miandamo": si Aya:"Atayeushudia mwezi" . Na maudhui yetu hapa ni kuhusu Aya"Atayeushudia mwezi" . Mara mumerukia kwengine. Kwa ufupi, ni kuwa tumeshajibu kwamba wanavyuoni hao wametegemea Hadith maudhui (Hadithi ya kutunga) kwa ushahidi tuliotoa wa sanad na kwa ushuhuda wa wanavyuoni wengine. Nakukumbusheni kaul i yenu muliposema: "Kutegemea maneno, matupu ya mwanachuoni kama ni Khaas bila ya kuonyesha dalili zenye kukubalika kifani, huo utakuwa ni udhaifu". Sasa nyinyi mulitumia fani gani hata mukaitegemea sababu hio ya kutremka Aya ambayo sanad ya riwaya y ake ina wapokezi waongo.

MNASEMA

Alichokisisitiza Shaykh Al-Jassas katika kitabu chake ni ule wajibu wa kufunga na kufungua kwa kuzingatia "Suala zima la kuonekana mwezi" Na ndio maana Shaykh Al-Jassas akanukuu Hadiyth zenye kutaja wajibu wa kufunga na kufungua kwa kuonekana mwezi. Na Hadiyth zote hizo zimetaja jambo hilo kwa njia ya Ujumla, yaani hukumu yake inawaenea Waumini wote popote walipo. Katika kuielezea kauli hii ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Shaykh Al-Jassas anasema: "ni jambo linaloeleweka kuwa kauli ya Mtume(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo:(Fungeni kwa kuonekana mwezi na Fungueni kwa kuonekana mwezi) ni ya ujumla haiwahusishi watu wa nchi moja peke yao pasi na wengine.

Na vilevile msimamo kama huu wa kufunga pamoja ameuweleza Dr. Zuhaily katika kitabu chake Al-Fiqhul- Islamiy.

JAWABU

Hatupingi kwamba kuna wanavyuoni waliosema hivyo, wala mimi katika kitabu chamgu sikupinga hilo; tunachodai ni kuwa hoja zao ni dhaifu ukilinganisha na hoja za kundi lapili. Na Hadithi hio tumeshaielezea, tusikariri yayo kwa yayo mara elfu.