MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 0%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi: Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui, Al-Zenjibari.
Kundi:

Matembeleo: 59150
Pakua: 4779

Maelezo zaidi:

MUANDAMO WA MWEZI
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 59150 / Pakua: 4779
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

15

MUANDAMO WA MWEZI

HOJA YA ABU AMMAR NASSIR AL-MAZRUI JUU YA MASIMULIZI YA KURAIB

MNASEMA

Hoja Ya Abu Ammar Nassir Al-Mazrui Juu Ya Masimulizi Ya Kuraib Katika kitabu cha ndugu Juma chapa ya pili uk 143 amenukuu hoja nyengine ambayo haikuwemo katika chapa yake ya kwanza. Katika hoja hiyo ya Abu Ammar imegundulika kwamba imejengeka katika msingi wa ibara isemayo: "inawezekana." Kwa hivyo ni ibara yenye utata (ihtimal) - yaani inawezekana hivi au kinyume na hivi. Ibara kama hizi zimeshaelezewa mara nyingi kuwa sio za kuzijengea hoja sahihi kama walivyothibitisha hayo Wanavyuoni wa Usulul-Fiqhi. Ingawa hoja hiyo imesemwa na Mwanachuoni mkubwa anayeheshimika sana na InshAllaah Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atamlipa kwa jitihada yake hiyo. Lakini kama alivyoandika ndugu Juma katika kitabu chake baada ya kuinukuu hoja moja ya Shaykh Naaswir Bachuu iliyomo ndani ya kitabu chake uk 37, hatimae kuonyesha mshangao katika hoja hiyo na kuandika hivi: (shubuhati kama hizi hazifai kujadili mambo ya kielimu.)

Nasi tunasema shubuhati kama hizi za kina Abu Ammar hazifai kujadili mambo ya kielimu.

JAWABU

Lakini kwa bahati mbaya hamukunukuu yote yaliosemwa. Mumenukuu kipande kidogo kisemacho "Inawezekana", kisha mukamuacha msomaji hajui kilichoanzia wala kilichokwishia. Nami nakunakilieni sehemu hio yote ili ijulikane Abu Ammar katoa hoja gani na kujibu nini na udhafu uko wapi. Maudhui ilianza hapa: UPINZANI WA TATU: Anaendelea Sheikh Bachoo na uchambuzi wake wa riwaya hio, anasema: "Pili kama ingalikuwa hakuna dhana ya kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge, Ibnu Abbas (r.a.) asingekuwa na haja ya kumuuuliza Kurayb juu ya habari za mwezi wa Sham kwa kusema: "Kisha (Ibn Abbas) akataja (habari) ya mwezi na akasema: "Ni lini mliuona mwezi?...akasema: "Wewe umeuona?"

Hio ndio hoja nyengine ya Sheikh Bachoo, kwamba lau hakuna dhana ya kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge, basi Ibn Abbas asingekuwa na haja ya kumuuliza Kuraib "Lini mumeuona mwezi!!!" Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja, mulikuwa hamuwaulizi watu wanaotoka nchi nyengine masuala kama hayo wanapokuja kwenu na nyinyi muko kati kati ya mwezi pamoja na kwamba nyote zamani mukifata muandamo wenu? Sasa kama nyinyi mulikuwa mukiuliza suala hilo hilo kwanini Ibn Abbas na yeye asiulize hata kama dhana hio haipo? Mimi binafsi nina kawaida ya kuwauliza wageni walioko nchi hii ninayoishi suala hilo, na natarajia kwamba pia nimewasikia watu wengi wenye kuwauliza wageni suala hilo. Kwa hakika shubuhati kama hizi hazifai katika kujadili mambo ya kielimu. Kwa ufupi ni kuwa hata kama dhana hio ilikuwepo, dhana hio inabomolewa na kukataa kwake - Ibn Abbas - kuukubali mwezi wa Sham, na kujenga hoja kwa Hadith marfu'u kwamba hayo ndio mafunzo ya Mtume(s.a.w.w) kwao.

Bali tunasema kwamba suala la Kuraib aliposema: "Je hutosheki kwa kuuona Muawiya na kufunga kwake" inawezekana ikawa na maana kinyume kabisa na fikra ya Sheikh Nassor, kwani inaweza ikawa ndio hasa inayomaanisha kwamba watu enzi hizo walikuwa hawazingatii muandamo wa mbali, au ikawa jambo hilo lilikuwa halijulikani kamwe, kwa sababu lau ingelikuwa Mtume(s.a.w.w) kafundisha kutendewa kazi muandamo wa mbali au ingelikuwa katika enzi hizo wanazingatia muandamo mmoja tu basi Kuraib asingelikuwa na haja ya kumuuliza Ibn Abbas suali hilo, bali angelimwambia: "Lipeni siku moja iliokupiteni ya muandamo wa Sham." Kwa hivyo, kumuuliza kwake suali hilo ni dalili ya wazi kwamba hakukuwa na dhana ilioenea kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge. Na kwa hivyo, Kuraib alikuwa hajui kamwe nini hukumu ya tokeo hilo.

Sasa sijui udhifu uko wapi katika hoja hio ya Abu Ammar?! Nyinyi baada ya kuchukua na kuijadili ile maana alioisema na ambayo inafahamika anapinga nini na anasapoti ni nini, munachukua ibara "Inawezekana" ndio mukaijadili. Mumewacha Jawhar (kiini) na mukag'an'gania Qushur (magamba).

MNASEMA

Ikumbukwe kuwa maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika jambo hili la kufunga na kufungua ni ya pamoja ('aam) kwa watu wote. Hakuna kabisa maneno mengine ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyo "sahihi" yenye kutufunza kuwa kila nchi ifunge na ifungue kwa muandamo wake. Kitu kilichoelezwa juu ya mas-ala haya ni upatikanaji wa mawasiliano ya habari za kuaminika katika utaratibu unaokubalika kishari'ah. Maneno ya Abu Ammar yasemayo: "Kwa sababu lau ingelikua Mtume(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kafundisha kutendewa kazi muandamo wa mbali." Hayo ni mane no dhaifu sana Hakuweza kutoa dalili sahihi isiyokua na utata inayoonesha kuwa amri hiyo ya kufunga na kufungua ina mipaka maalum, au ni ya watu maalumu au inahusisha nchi moja na kuacha nchi nyengine.

JAWABU

Dai lenu kwamba: "Hakuna kabisa maneno mengine ya Mtume(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyo "sahihi" yenye kutufunza kuwa kila nchi ifunge na ifungue kwa muandamo wake" si madai sahihi. Ibn Abbaas kaukataa muandamo wa mbali na kunena: "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w.". Nakukumbusheni maneno yenu muliposema: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) .

Ama kusema: "Kitu kilichoelezwa juu ya mas-ala haya ni upatikanaji wa mawasiliano ya habari za kuaminika katika utaratibu unaokubalika kishari'ah", pia yanahitaji muyafafanue. Ama ikiwa munakusudia kwamba mas-ala ya kupokea habari yamo katika riwaya, hilo ni kweli. Lakini riwaya hizo hazikutoa ufafanuzi wowote juu ya je tufunge kwa muandamo mmoja au kumi na moja. Faida inayopatikana katika habari hizo ni kuwa shahidi mmoja anatosha kuthibitisha muandamo. Ama istintaj yenu kwamba Mtume(s.a.w.w) hakuwauliza watowaji habari wapi wanatokea, si isimbat sahihi kwani:

a) Watoaji habari walikuwa wanajulikana watokapo, nalo ni jangwa la Madina.

b) Ni istimbat inayogongana na andiko la wazi, nayo ni Hadithi ya Ibn Abbaas aliposema "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w.".

Ama nakala yenu mulipomnukuu Abu Ammar akisema: "Maneno ya Abu Ammar yasemayo: "Kwa sababu lau ingelikua Mtume(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kafundisha kutendewa kazi muandamo wa mbali." Hayo ni maneno dhaifu sana Hakuweza kutoa dalil i sahihi isiyokua na utata inayoonesha kuwa amri hiyo ya kufunga na kufungua ina mipaka maalum, au ni ya watu maalumu au inahusisha nchi moja na kuacha nchi nyengine". Mwisho wa kunukuu. Kwanza ningekuombeni muikamilishe nakala hadi ilete maana kamili. Alichokisema ni:

Bali tunasema kwamba suala la Kuraib aliposema: "Je hutosheki kwa kuuona Muawiya na kufunga kwake" inawezekana ikawa na maana kinyume kabisa na fikra ya Sheikh Nassor, kwani inaweza ikawa ndio hasa inayomaanisha kwamba watu enzi hizo walikuwa hawazingatii muandamo wa mbali, au ikawa jambo hilo lilikuwa halijulikani kamwe, kwa sababu lau ingelikuwa Mtume(s.a.w.w) kafundisha kutendewa kazi muandamo wa mbali au ingelikuwa katika enzi hizo wanazingatia muandamo mmoja tu basi Kuraib asingelikuwa na haja ya kumuuliza Ibn Abbas suali hilo, bali angelimwambia: "Lipeni siku moja iliokupiteni ya muandamo wa Sham." Kwa hivyo, kumuuliza kwake suali hilo ni dalili ya wazi kwamba hakukuwa na dhana ilioenea kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge. Na kwa hivyo, Kuraib alikuwa hajui kamwe nini hukumu ya tokeo hilo.

Hoja hii kaitoa kujibu maelezo ya Sheikh Bacho aliposema: "Pili kama ingalikuwa hakuna dhana ya kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge, Ibnu Abbas (r.a.) asingekuwa na haja ya kumuuuliza Kurayb juu ya habari za mwezi wa Sham kwa kusema: "Kisha (Ibn Abbas) akataja (habari) ya mwezi na akasema: "Ni lini mliuona mwezi?...akasema: "Wewe ume uona?" Mukhtasar wa haya ni kuwa Sheikh Nassor kakufanya kule Ibn Abbaas kumuuliza Kuraib "Je wewe umeuona" kuwa ni dalili kwamba mwezi ukionekana popote watu wafunge. Na hili ndilo ambalo halina ushahidi, kwa bahati mbaya lisilo na ushahidi la Sheikh Bachoo hamukuliulizia ushahidi; lisilo ushahidi - kama mulivyo dai - la Abu Ammar mumeliulizia ushahidi - huu ni uchambuzi gani?! Kiufupi mimi nimejibu kwamba hata watu wan chi nyengine, huko kwetu Zanzibar na nchi nyengine, watu huulizana suala kama hilo hata kama wanafata miandamo yao. Sote tunajua kwamba hapo Zanzibar watu kabla ya kuanza fikra hio ya kufunga kwa muandamo mmoja, walikuwa wakiulizana hivyo. Kwa hivyo, hio si dalili ya kielimu. Ama jawabu ya Abu Ammar, ni kitu kisichohitaji ushahidi, kwani kama ilikuwa inaeleweka kwamba mwezi wa mbali utendewe kazi mbali, basi Kuraib angelimwambia Ibn Abbaas kwamba "Mwezi umeonekana Sham kabla yenu kwa siku kwa hivyo, muilipe siku moja". Sasa jawabu hii ina udhaifu gani na nyinyi munata watu wa Madina wafanyeje ikiwa siku moja ya Sham hawakuifunga: wasiilipe: iwe basi?!

Jambo ambalo mtu anaweza kulilahidh (kuliobserve) katika kitabu chenu, nikuwa hamunuu kitu kamili au chenye kuleta maana kamili. Wala hamunukuu jawabu zangu zote; munachagua zile muzitakazo mukanuuu kipande kidogo halafu munatoa jawabu zenu zilio mbali na elimu.

MNASEMA

Mwanachuoni Al-Jassas katika kitabu chake Ahkamul-Qur-aan J. 1, uk 305 katika kuieleza kauli hii ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema hivi: "Ni jambo linaloeleweka kuwa kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo: ((Fungeni kwa kuonekana mwezi -muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi-muandamo)) ni ya ujumla '(aam), inawahusisha watu wa pande zote za dunia na kwamba haihusu watu wa nchi moja peke yao pasi na wengine." Aidha Shaykh Sayyid Saabiq katika kitabu chake Fiqhus-Sunnah J. 1 uk 436 baada ya kuitaja kauli hiyo ya Mtume(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameandika hivi: "Na kauli hii ni agizo la ujumbe linalojumuisha umma wote (wa Kiislam), kwa hivyo yeyote miongoni mwao atakayeuona (mwezi-muandamo) popote pale; kuonekana huko kutakuwa ni kwa wote"

Kwa marejeo mengine zaidi kama haya angalia:-

1. Rawaaiul-Bayan J. 1, uk 211

2. Naylul-Awttar J. 4, uk 195

3. Sharhu Subulu Sawiyah Li Fiqhi Sunanil Marwiyah

4. Fatawa ya BAKWATA uk 110:.11 mada 14/70

JAWABU

Maelezo haya sijui munayanukuu mara ngapi! Maelezo hayo kayatoa Sheikh Bachoo na nimeyajibu nanyinyi munayakariri bila ya kutoa jawabu juu ya maelezo yangu. Nimesema: Jambo la pili: la kutazamwa katika Hadithi hii ni kuwa Khitabu (Agizo: kam a alivyofasiri Sheikh Nassor Bachoo) ya Hadithi hii ni Aam (ya ujumla), kama Sheikh alivyonukuu kutoka katika kitabu cha Al-sayyid Saabiq.

Na sisi tunajibu kwa jawabu mbili: Ya kwanza: ni kuwa: Ujumla wa agizo hilo, umehusishwa na Hadithi ya Ibn Abbas, na k anuni ya kiusuli inaeleza kwamba Al-khaas (Andiko maalumu au specific) ndio inayotangulizwa kuliko Al-aam (Andiko la ujumla), kwa kuwa kwake (hio Khaas) ni ya uhakika kinyume na Aam hakika yake ni (kitu) cha dhana. Kwa hivyo kanuni hapa in atutaka kuitanguliza Hadithi ya Ibn Abbas. Na natija ni kuwa ujumla jamala uliobakia katika Hadithi "Fungeni kwa kuonekana mwezi na fungueni kwa kuonekana mwezi" na ambacho tunachotakiwa sote tukifanye kwa mujibu wa Hadithi hii, ni kuwa sote tufunge kwa kuuona mwezi. Ama je muandamo ni mmoja au kila watu wana muandamo wao, Hadithi hii haitoi jawabu hio.

Jawabu ya pili: ni ile tuliotangulia kuinukuu kutoka kwa Sheikh Ibn Uthaimin aliponukuu jawabu ya wale wenye kusema kwamba kila mji una muandamo wake, ambapo walisema kwamba ujumla uliomo katika Hadithi hio, ni sawa na ujumla uliomo katika Aya inayosema:

﴿فَالْآنَ بَاشِرُوهُنَّ وَابْتَغُوا مَا كَتَبَ اللَّـهُ لَكُمْ ۚ وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ۖ ثُمَّ أَتِمُّوا الصِّيَامَ إِلَى اللَّيْلِ ۚ ﴾

"Sasa waingiliyeni (wake zenu) na tafuteni kile Allah alichokuandikiyeni, na kuleni na kunyweni mpaka ukubainikieni uzi mweupe kutokana na uzi mweusi wa alfajiri, kisha timizeni saumu hadi usiku."

Je hapa Allah anazungumza na watu wote au na watu maalumu? Je kuzungumza huku na watu wote inamaanisha kwamba alfajiri ya nchi moja ikichomoza watu wa nchi zote wajizuie, au kila watu na alfajiri yao? Jawabu yako hapa ndio jawabu yetu kwa maneno ulioyanukuu kutoka katika kitabu cha Al-sayyid Saabiq kwamba Hadithi hiyo"Fungeni kwa kuuona" ni: "Agizo la ujumla linalojumuisha umma wote ( wa Kiislamu) kwa hivyo; yeyote miongoni mwao atakayeuona (mwezi) popote pale; kuonekana huko kutakuwa ni kuonekana kwa wote."

Halkadhalika tunajibu ujumla huo kwa Hadithi inayosema: "Usiku ukitokeza kutoka hapa na mchana ukaondoka kutokea hapa na jua likatua, basi aliyefunga ameshafungua (au na-afungue)."

Na sisi tunauliza je hapa walikuwa wakiambiwa watu wa Makka tu, au wakiambiwa watu wa nchi zote? Kama walikuwa wakiambiwa watu wa nchi zote, je jua likitua Makka au katika mji wowote ule sote tufuturu? Kwa hakika kila aliyejaaliwa kuwa na mtazamo sahihi, anaona kwamba kujenga hoja kwa ujumla wa Hadithi "Fungeni kwa kuuona" kwamba ni ushahidi wa kuwepo muandamo mmoja, ni kujenga hoja juu ya msingi dhaifu sana. Na kwa maana hio, Ibn Uthaimin (Mwanachuoni wa Kiwahabi) akasema kwamba kauli ya kuwa kila watu wana muandamo wao: "Ina nguvu yake kwa mujibu wa lafdhi (yake) na mtazamo sahihi na Qiyas sahihi vile vile: Qiyas cha wakati wa siku kwa (kuulinganisha) na wakati wa mwezi (month). Mwisho wa kunukuu.

Kwa ufupi ni kuwa, ujumla wa Hadithi inayosema "Fungeni kwa kuuona" ni - kama tulivyotangulia kusema - kwamba watu wote ni lazima wafunge kwa kuuona: si kwa kalenda wala kwa jengine lolote. Huu ndio ujumla unaokusudiwa katika Hadithi hio, au ndio ujumla uliobakia baada ya kuhusishwa au kuvuliwa sehemu ya ujumla huo na Hadithi ya Ibn Abbas na Kuraib.

Jambo la tatu: la kutazamwa katika Hadithi hii, ni kuwa Hadithi hii ni Mutlaq (isiofungamanishwa na kitu) wakati Hadithi ya Ibn Abbas ni muqayyad (iliofungamanishwa). Kanuni ni kuitanguliza muqayyad kuliko mutlaq kama usuli unavyoeleza. Kwa hivyo, kila msingi utaoufata utaona kwamba Hadithi ya Ibn Abbas ndio inayotakiwa itangulizwe. Ama waliosema kwamba tufunge kwa muandamo mmoja, ukweli ni kuwa wao waliitanguliza rai kuliko kanuni za tafsiri. Walitazama wakaona kuwa mwezi ni mmoja na unakamilisha safari yake mara moja na kwa hivyo muandamo utakuwa mmoja. Lakini tumeona kwamba huu si muandamo wa Kisharia bali ni muandamo wa Kifalaki: muandamo wa Kisharia tunaupata katika kuzijumisha Hadithi tafauti.

Pili ni kuwa hio ni rai, na ya Ibn Abbas ni Hadithi; na rai haina uwezo wa kuipinga Hadithi. Kama walivyosema: "Rai haina nafasi mbele ya Andiko." Hii ndio jawabu yangu, nanyi mumeiruka kama mulivyoziruka sehemu kubwa za kitabu changu.

AINA ZA IJMA'

MNASEMA

Aina Za Ijma' Kuna baadhi ya watu kama ndugu yetu Juma ambao wamejenga hoja ya kuwepo miandamo mingi ya mwezi kwa vile maneno ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) katika kisa cha Kuraib yalinyamaziwa. Hakuna Sahaba yeyote aliyetoa kauli tofauti na ile ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu). Jambo hilo limechukuliwa kama ni hoja kwamba Masahaba wote walikubaliana na Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu).

JAWABU

Kwanza : mimi sikusema hivyo. Na ili nieleweke vyema, lazima munukuu maneno yote. Hapa kuna madai ya Sheikh Nassor na jawabu niliomjibu nainukuu ili nieleweke vyema nini nimekisema. Sheikh Nassor alidai kuwa msimamo wao ndio msimamo wa Makhalifa waongofu. Alisema hivi: "Kipindi chao cha ukhalifa kilichukua kiasi cha miaka 30 kabla ya kutokea utatanishi uliopatikana katika masimulizi ya Kurayb; ukijumuisha nyakati zote walizokamata ukhalifa Sayyidna Abu Bakr (r.a.) Sayyidna Omar (r.a.) Sayyidna Uthman (r.a.) Sayyidna Ally (r.a.), utagundua kwamba Uislamu ulikwishaenea sehemu kubwa ulimwenguni kaskazini mwa Afrika kama Misri na Maghrib (Morocco), baadhi ya nchi za Ulaya lakini haikuthibiti kwamba wao waliwahi kuzingatia suala la masafa au matalai katika suala la kuandama mwezi. Jambo la kujiuliza hapa je kwani wao walikuwa hawaelewi kwamba kulikuweko na nchi nyingi zilizokuwa mbali na Makka na Madina ambazo zilikuwa chini ya himaya zao? Mbona hawakueleza kuwa watu wa kila nchi wafunge kwa kuuona mwezi wao." Mwisho wa kunukuu.

Nami nikamjibu hivi: Jawabu ni kuwa: Hizi ni zile ambazo wataalamu huziita Shubuhati, nacho ni kitu ambacho kinaelekea lakini sio muradi. Kwa ufupi ni kuwa jawabu ya madai hayo ni kama inavyofata: Mosi ni kuwa: Kama ilivyokuwa hakuna ushahidi kwamba wao waliwaamrisha watu wasifate miandamo yao, pia hakuna ushahidi kwamba wao waliwakataza wasifate miandamo yao, au kwamba waliwaamrisha kufata muandamo wa Madina. Na kwa hivyo, Al-qutbu anasema: "Masahaba walikuwa hawawaamrishi watu wa miji ya mbali kufunga kwa kufata muandamo wa miji myengine."

Pili : ni kuwa: Marejeo ya Haya ni Hadithi za Mtume (s.a.w.), na tumesema kwamba Hadithi ya Ibn Abbas ndio iliomaanisha kwamba muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali. Na Hadithi ya Ibn Abbas sigha (form) yake ni ya raf'i (Ya kuinasibisha Hadithi hio na Mtume mwenyewe(s.a.w.w) . Kwa hivyo, ikiwa riwaya haikupokewa na Sahaba fulani, haidhurishi kitu madamu mwengine kaipokea na imethibiti. Na wala huu si mlango wa kuwa lazima Hadithi ipokelewe na kundi kubwa yaani iwe mutawatir. Hadithi mutawatir ni sharti katika itikadi: si katika matendo: katika matendo inatosha riwaya kuwa Ahadi, kama Jumhuri ilivyosema: "Hadithi Ahadi inawajibisha matendo wala haiwajibishi yakini (itikadi)." Tatu ni kuwa: Riwaya ya Ibn Abbas, hajulikani Sahaba aliyeipinga, pamoja na kuwa alikuwa Madina - mji wa Masahaba. Kwa hivyo, kunyamaza kwao kwa uchache iambiwe kuwa ni Al-ijmaa Al-su kutiy (Makubaliano ya kunyamaza), nayo ni makubaliano ambayo mmoja husema kitu wengine wakanyamaza wasimpinge. Kauli hii inaelekea zaidi, kuliko madai ya Sheikh Nassor Bachoo, kwani kusema hivi ni kuijenga kauli juu ya msingi unaokubalika Kisharia nao ni msingi wa kuzingatia Al-ijmaa Al-sukutiy (Makubaliano ya kunyamaza), ikiwa hajulikani aliyepinga katika watu wa zama hizo. Kwa hivyo, unapomjibu mtu kwanza uwe umemuelewa. Mimi sikudai kuwa Ijma' Sukutiy ni hoja waliokubaliana wanavyuoni, ba li ni hoja ambayo inafaa ukilinganisha na hoja ya Sh. Bachoo, kwani Ijma' Sukutiy wako wengi katika wanavyuoni, madhehebu na Maimamu ambao wameikubali, wakati madai ya Sheikh Nassor hayakuwa na tegemezi zozote zile.

MNASEMA

Ni vyema kuelewa kuwa Wanavyuoni wameigawa Ijma' kwenye sehemu mbili kuu:

i) Ijma' Sariyh.

ii) Ijma' Sukutii. Ijma' Sariyh Ni Ijma' ambayo Jamhuri ya Wanavyuoni wa Fiqhi wamekubaliana juu ya usahihi wake kwa vile iko wazi, haina utata wowote. Hoja ya Ijma' hii ni madhubuti na yenye kukubalika zaidi mbele ya Umma wa Kiislamu na wala hakuna khitilafu yoyote juu ya Ijma' hii. Katika kuielezea Ijma' hii, Imam Shaffi (Rahimahu Allaahu) anasema hivi: Anachosema Imam Shaffi hapa, juu ya umuhimu wa Ijma' hii kwa ufupi ni kuwa: "Hakuna yeyote atakayeweza kusema (juu ya umuhimu wa Ijma' hii Sariyh) kinyume na vile ambavyo Wanazuoni wote waliv yosema (kuhusu uzito wa Ijma' hii Sariyh). Kwa maneno mengine ni kuwa: "Mwanachuoni yeyote atakayeonana naye na kumuuliza uzito wa Ijma' hii Sariyh bila shaka jawabu ya Mwanachuoni huyo itakuwa ni ile yenye kuthibitisha umuhimu wa Ijma' - Sariyh, kuliko Ijma' - Sukutiy katika hoja."

JAWABU

Maneno yenu: "Wala hakuna khitilafu yoyote juu ya Ijma' hii" si sahihi. Nilikwambieni mara nyingi kwamba muache kusukuma; khilafu juu ya ijma'a hii pia ipo. Lakini mulikuwa museme tu kwamba kilicho sahihi ni kuwa ijma'a ya aina hii ni hoja yenye nguvu kwa mujibu wa dalili zake. Ama khilafu ipo. Pili: munaendelea na tatizo lenu la kunukuu kitu musichokifahamu. Al-Imamu Al-Shafi hasemi hivyo. Kwanza tafsiri mumeikosea: tafsiri ni: Hutosema wala (hatosema) yeyote miongoni mwa watu wa elimu (wanavyoni) kwamba kitu hiki kimekubaliwa na wote isipokuwa kile ambacho ukimkuta mwanachuoni yeyote milele atakwambi (hivyo hiv yo). Hio ndio tafsiri ya maneno hayo, lakini nyinyi - kama kawaida yenu - mumeyavuruga kichwa chini miguu juu halafu munajadili mambo ya elimu. Sasa baada ya hayo, je mumemfahamu nini Al-Imamu Al-Shafi?! Kwanza nataka mujue kwamba maudhui ya ijmaa ni pan asana na ina vipengele vingi sana. Anachokizungumzia Al-Imamu Al-Shafi ni kuwa ni vigumu mtu kudai kuwa jambo hili Umma umekubaliana. Kwani miji ya Kiislamu iko mingi na wanavyuoni ni wengi. Sisi tulio Zanzibar tukiwa na msimamo fulani hatujui kwamba je watu wote wanatusapoti au wako wasiokubaliana nasi. Lakini - anavosema Al-Shafi ni kuwa - unachoweza kudai kwamba haya ni makubaliano ya Umma ni kile kitu ambacho mwanachuoni yeyote ukimuuliza atakujibu hivyo hivyo. Kwa mfano je sala ni wajibu? Huna utayemuuliza ila atakwambia kwamba ni wajibu. Kwa mukhtasar, Al-Imamu Al-Shafi anazungumzia ugumu wa kuthibitisha ijmaa na hili limehusishwa na wengi hata Al-Imamu Ahmad inadaiwa kuwa kasema: "Atayedai ijmaa kasema uwongo".

MNASEMA

Ijma' - Sukutiy Ni makubaliano ambayo mmoja husema kitu na wengine wakanyamaza wasimpinge. Mtazamo Wa Wanavyuoni Juu Ya Ijma' Hii Sukutiy Takriban ukiviangalia vitabu vyote vya Usulul-Fiqh kuhusu Ijma' hii Sukutiy utaona kwamba ni Ijma' yenye khitilafu (mvutano) mkubwa, hakuna maafikiano ya pamoja. Tofauti na Ijma'-Sariyhi ambayo ina makubaliano yenye uzito wa hoja za kutegemewa katika misingi ya Shari'ah. Chanzo cha khitilafu hizi katika Ijma' Sukutiy ni kule kupatikana ndani yake utata; jambo ambalo huifanya hoja yake kuwa dhaifu. Kama kanuni ya Usulul-Fiqhi inavyosema: "Dalili inapokuwa ina maana nyingi huporomoka ushahidi wake." Shaykh Abu Zuhra amesema: Ifuatayo ni tafsiri kwa njia ya maana: "Ijma' Sukutiy (makubaliano ya kunyamaza) ina khitilafu kubwa mbele ya Wanavyuoni wa 'Usulul -Fiqhi.' Kwa kuwa Wanavyuoni wengi hawakuizingatia Ijma' hii ni dalili imara katika mas-ala ya kielimu. Al-Imam Shaffi ni miongoni mwa wale wasioizingatia Ijma' hii kuwa ni hoja, kama alivyoeleza hayo mwanachuoni M. Abu Zuhra katika kitabu chake cha Usulul-Fiqh. Sababu za msingi zilizoifanya Ijma' hii kutokuwa hoja imara - kwa mujibu wa maelezo ya Abu Zuhra ni kule kupatikana (ihtimaalat) tatanishi."

JAWABU

Na hapa naomba murekebishe tafsiri ya maneno ya Abu Zahra, kwani tafsiri muliodai kuwa ni njia ya maana imepoteza baadhi ya maana. Tafsiri ya maneno hayo ni Kwa hakika haifaii kuzingati kuwa kunyamaza ndio kuwafiki, kwani kunyamaza kuna uwezekano kwamba ni kunyamaza kwa kuwafiki; na kuna uwezekano kwamba yeye (mwenye kunyamaza) bado hajafanya ijtihad katika muwafaka, na inawezekana kwamba yeye ka jitahidi lakini ijtihada yake hakumpelekea kutoa (uamuzi wa) mkato kwa kitu chochote. Na kwa uwezekanu mwingi wa namna hii, haiwezekani kukazingatiwa kunyamaza kuwa ni hoja.

Nyinyi mumeongeza maneno Kwa kuwa Wanavyuoni wengi hawakuizingatia Ijma' hii ni dalili imara katika mas-ala ya kielimu. Wakati madhehebu mbili za Kisunni zimeikubali ijma'i hii na mbili zimeikataa. Kwa hivyo, kwa mujibu wa ufahamu wenu wa maana ya neno Jumhur, nusu ya Jumhur imeikubali ijma'i hio. Ukiongezea na madhehebu nyengine kama Ibadhi na wanavyuoni wengine waliotangulia kabla ya madhehebu nne za Kisuni, hutoweza tena kudai kwamba Kwa kuwa Wanavyuoni wengi hawakuizingatia Ijma' hii ni dalili imara katika mas-ala ya kielimu.

MUNASEMA

Shaykh Abu Zuhra baada ya kutaja udhaifu huo aliendelea kusema: "Kuwepo utata mwingi ndani ya Ijma' hii Sukutiy inaifanya Ijma' hii kutozingatiwa kuwa ni hoja." Kwa hivyo, Ijma' inayofaa kutangulizwa katika mjadala wa kielimu ni Ijma' -Sariyhi na wala sio Ijma'-Sukutiy. Ni vyema ieleweke pia, kwenda kinyume (kuikhalifu) Ijma'-Sukutiy sio makosa wala mtu haambiwi kuwa amefanya jambo la ufasiki kama alivyosema Shaykh Saalimiy: "Mwenye kukhalifu (kwenda kinyume na) Ijma' - Sukutiy haiambiwi kuwa ametenda kosa la ufasiki." 24 - 25) Naye Shaykh Abu Zuhra katika kueleza rai zilizopo juu ya Ijma'-Sukuty na kuonesha uzito wa hoja katika ljmai-Sariyhi amesema ifuatavyo: "Rai nyengine inasema (hii Ijmai-Sukuty) nayo ni Ijma' lakini sio sawa (katika uzito wa hoja) kama ilivyo Ijma'-Sariyhi. 205 - 206) Kutokana na miongozo sahihi ya Wanazuoni wa fani ya Usulul-Fiqhi tumeelewa kuwa: Ijma'-Sariyhi ndiyo yenye uzito wa hoja, na hakuna khitilafu juu ya jambo hilo. Pia tumejifunza kuwa kwa upande wa Ijma'-S ukutiy ni Ijma' yenye mzozo mbele ya Wanazuoni kutokana na kupatikana ndani yake tatanishi (Ihtmaalaat).

Kwa maana hiyo hapawezi kutegemewa Ijma'-Sukutiy kama ni hoja katika mjadala wa khitilafu za miandamo ya mwezi. Miongoni mwa Wanavyuoni ambao hawakuzingatia Ijma' hii kuwa ni hoja; mmoja wao ni Imam Shaffi (Radhiya Allaahu 'Anhu) kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Abu Zuhra.

JAWABU

Jawabu ya ujumla ni kuwa mengi mulioyasema hapa tunakubaliana: hatutafautiani. Suala ni kuwa je nyinyi mumenifahamu vipi mimi hata mukanijibu hivi? Mimi nilichokisema ni kuwa dai la Sheikh Nassor kwamba Masahaba walikubaliana kwamba kufunga ni kwa muandamo mmoja ni dai ambalo halina ushahidi wowote juu ya hilo. Kisha ndio nikamwambia kwamba Ibn Abbaas kasema kwa uwazi kwamba "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." yaani baada ya kuukataa muandamo wa Sham. Na hakuna ushahidi kwamba kuna sahaba alimpinga Ibn Abbaas kwa kusema hivi, bali ni wazi kwamba Masahaba waliokuwa Madina pia iliwafika habari hio ya Kuraib; haielekei kuwa Kuraib alimwambia Ibn Abbaas tu. Na pamoja na hayo hajulikani sahaba aliyepinga jambo hilo. Kwa hivyo, ndio nikasema:

Riwaya ya Ibn Abbas, hajulikani Sahaba aliyeipinga, pamoja na kuwa alikuwa Madina - mji wa Masahaba. Kwa hivyo, kunyamaza kwao kwa uchache iambiwe kuwa ni Al-ijmaa Al-sukutiy (Makubaliano ya kunyamaza), nayo ni ma kubaliano ambayo mmoja husema kitu wengine wakanyamaza wasimpinge. Kauli hii inaelekea zaidi, kuliko madai ya Sheikh Nassor Bachoo, kwani kusema hivi ni kuijenga kauli juu ya msingi unaokubalika Kisharia nao ni msingi wa kuzingatia Al-ijmaa Al-sukutiy (Makubaliano ya kunyamaza), ikiwa hajulikani aliyepinga katika watu wa zama hizo.

Yaani ukilinganisha madai ya Sheikh Bachoo na kauli hii, hii ni bora zaidi kwani Al-ijmaa Al-sukutiy (Makubaliano ya kunyamaza), hata kama hawakukuba liana wanavyuoni juu yake lakini wako wengi walioikubali. Anasema Dr. Wahbat Al-Zuhail"Wanavyuoni wana kauli tano kuhusu hio Al-ijmaa Al-sukutiy". Akataja wale wasioikubali. Kisha akataja wanaoikubali akasema kwamba hio ndio: " Madhehebu ya Hanafi wengi na Al-Imamu Ahmad (bin Hanbal) (wanasema kuwa hio) inazigatiwa kuwa ni hoja na makubaliano ya uhakika". Kwa hivyo, kwa ujumla Mahanafi na Mahanbali wanaona kuwa Al-ijmaa Al-sukutiy ni hoja ya Kisharia. Anasema Al-Imamu Al-Salimi: "Ama hukumu ya Al-ijmaa Al-sukutiy ni kuwa ni hoja ya dhana inayopelekea kutumika katika matendo wala haileti yakini ni kama vile Hadith Ahadi".

Maana ya maneno ya Al-Salimi "Ni hoja ya dhana" musijemukafikiria dhana kwa maana yake ya Kiswahili, bali anakusudia kwamba inafaa kutumika katika matendo: si katika itikadi. Kwa hivyo, kwa ujmla ni kuwa Al-ijmaa Al-sukutiy ni kitu kinachokubalika kwa vile ziko madhehebu waoikubali na wako wanavyuoni tafauti waliokubali. Kwa ufupi, mimi sikuwa hapa nikitoa hoja kwa Al-ijmaa Al-sukutiy kama mulivyodhania nyinyi; balili nilikuwa nalinganisha dai la Sheikh Nassor na kusema hivi; kwamba hli lina muelekeo zaidi kuliko dai la Sheikh Nassor.