MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 12%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 62348 / Pakua: 6747
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

16

MUANDAMO WA MWEZI

SEHEMU YA KUMI NA TANO

FUNGA YA 'ARAFAH

Katika sehemu hii, ni vyema kwanza nikanukuu yote nilioyasema kuhusu maudhui hii, kisha ndio nikanukuu jawabu niliojibiwa na kuijadili. Kuhusu suala hili nilisema: Anasema Sheikh Nassor Bachoo: "Jambo la kusikitisha ni kwamba ikiwa Waislamu watakubali kuwepo tafauti ya siku na tarehe baina yao, hapana shaka watakuwa wanafunga saumu ya Arafa siku tafauti na inavyotakiwa.

Kwa hivyo lengo na faida ya funga yenyewe litakuwa halikupatikana. Mbali na kukosekana huko Makka jambo baya zaidi ni kwamba watakuwa wanafunga siku ya pili yake ambapo watakuwa wanafunga siku ya 'Idul-Adh-ha'; siku ambayo ni Haramu kufunga.

Ni vyema tuzingatie kwamba funga hii ya Arafa pamoja na Iddi yake ni vitu ambavyo havina mahusiano na kuandama mwezi kutokana na kila nchi inavyoona mwezi wake. Bali chanzo cha funga ya Arafa ni uhusiano wa ile siku ambayo mahujaji wanaposimama katika uwanja wa Arafa. Na jambo la kusimama Arafa linapatikana sehemu moja tu ulimwenguni ambayo ni siku inayosadifu tarehe 9 Dhul-Hijjah huko mji wa Makka; sio tarehe tisa ya nchi nyengine yoyote ile. Kwa uthibitisho zaidi wa funga ya siku ya Arafa tunajifunza kuwa Mtume (s.a.w.) alipotueleza umuhimu wa siku hii, na kila alipotaja siku hii ya Arafa alitumia neno 'siku' wala hakutumia neno 'tarehe'.

Funga ya 'siku' ya Arafa." Mwisho wa kunukuu. Sasa tatizo moja linalowatatiza watu kuhusu suala zima la kuwa na miandamo tafauti ni tatizo hili la funga ya Arafa. Kwa kweli hili si tatizo lakini tatizo tunalo sisi wenyewe katika udha ifu wetu wa kukiweka kila kitu mahala pake na kutoa hukumu kwa mujibu wa misingi inavyotuelekeza. Siisahau kauli ya Dr. Al-zuhailiy yenye maana kwamba makosa mengi ya kifiq-hi yanatokana na kuwacha misingi yake ya kiusuli, na kwamba lau watu walikuwa wanaifata misingi hio, basi makosa yasingelitokea au ingelikuwa nadra sana kutokea.

Sasa suala tunaloulizwa ni kuwa kama muandamo kila watu wawe na wao, itakuwaje ikitokea siku ya Arafa kuwa kwetu ni mwezi nane, ilhali Arafa inakuwa mwezi tisa? Tukifunga tutakuwa tumefunga mwezi nane; tukifunga siku ya pili itakuwa Arafa imeshakwisha?

Jawabu ya suala hili: ni kuwa kwanza inatakiwa tujue kwanini tunafunga siku hio: nini sababu: je sababu ni Arafa au sababu ni mwezi muandamo? Tumeeleza huko nyuma nini illa ambayo, kwa Kiswahili, huwa tunaifasiri kuwa ni Sababu. Tukasema kwamba wengine wanatafautisha baina ya sababu na illa. Sababu - kwao - ni kitu kisicho na uhusiano na kitu chenye kupewa hukumu. Tukatoa mfano wa kutenguka kwa jua kuwa ni sababu ya kuwajibikiwa na Sala. Na illa ni kitu chenye uhusiano na kitu chenye kupewa hukumu, kama kuumwa ndio illa ya kuruhusika kula mchana wa mwezi wa Ramadhani.

Kwa maana hii, utakuwa umefahamu kwamba sababu ya:

1) Kutuwajibikia Sala ya Adhuri na Laasiri - kwa mfano - ni kutenguka jua. Ushahidi wake ni Aya inayosema: (Simamisha sala kwa kutenguka jua).

2) Sababu ya kufunga au kuwajibikiwa na funga ni kuuona mwezi. Kama ilivyo Hadithi inayosema:(Fungeni kwa kuuona) . Sasa hapa tuna mambo mawili: Moja: ni munasaba wa kufunga siku hio ya Arafa. Pili: ni sababu ya kufunga siku hio ya Arafa. Kisimamo cha Arafa ni Munasaba: wa kufunga siku hio: si sababu: Sababu: ya kufunga siku hio, ni muandamo wa mwezi wa mfunguo tatu. Wala usidhani kwamba tarehe tisa ya mwezi huo ndio sababu: "laa" (sio hivyo), bali tarehe tisa ni wakati wa kufunga: si sababu ya kufunga. Na hili linabainishwa zaidi na riwaya tuliotangulia kuinukuu huko nyuma, nayo ni riwaya ya Amiri wa Makka, yenye kusema: "Alituusia Mjumbe wa Allah - rehema na amani ziwe juu yake - tuabudu kwa kuuona, kama h atukuuona na wakashuhudia mashahidi wawili waadilifu, tuabudu kwa (kufata) ushahidi wao." Tumesema huko nyuma kwamba neno Nansuk (tuabudu) wengine wameifasiri ibada hii kuwa ni ibada ya hija nayo ndio tafsiri yenye muelekeo madhubuti zaidi, kwani neno hili hutumika sana kwa maana ya ibada ya hija, kama Allah (S.W.) anavyosema kuhusu ibada ya hija: Mukimaliza Nusuki (ibada) zenu (za hija). Na kwa hivyo imekuja katika "A'WNU AL-MA'ABUDI: SHARHU SUNANI ABI DAUD" kuhusu maana ya Hadithi hio tulioinukuu hapo juu kuwa maana yake inahusiana na ibada za hija. Anasema mwenye kusherehesha: "Na maana yake ni: 'Tuhiji kwa kuuona (mwezi), yaani mwezi muandamo wa mfunguo tatu." Ni wazi kwa maelezo haya au kwa mujibu wa Hadithi hii kwamba sababu ya ibada za hija - ikiwemo funga ya Arafa - ni kuandama kwa mwezi wa mfunguo tatu.

Sasa - tukirudi katika munasaba - ni kuwa munasaba si lazima kuwa mtu ausherehekee siku ile ile ya munnasaba huo. Kwa mfano, tunaposherehekea tokeo fulani lililotokea tarehe fulani katika historia, si lazima kuwa tuifanye sherehe yetu siku na tarehe ile ile: "Laa" tunaweza kuweka sherehe yetu siku nyengine. Sikusudii kufananisha sherehe yetu na mas-ala haya, ninachokusudia ni kukupa mfano utaoweza kufahamu kwawo tafauti baina ya Munasaba na Sababu.

Kwa hivyo, funga imeambatanishwa na muandamo wa mwezi, kama vile sala ilivyoambatanishwa na mtenguko wa jua. Utapolifahamu hili, utakuwa umefahamu kwamba, siku ya kufunga ni tarehe tisa mfunguo tatu, sawa siku hio imeafikiana na Arafa au imetafautiana, kwani sababu tayari imepatikana, na kilichotafauti ni kuafikana wakati wa tarehe ya baadhi ya sehemu na kuafikiana wakati mmoja wa Munasaba. Na Munasaba haufanywi kuw a ni illa wala haufanywi kuwa ni sababu ya hukumu. Hilo ni mosi.

Pili : ni kuwa: hata ikiwa kweli kilicho sahihi ni kwamba watu wakisimama Arafa na sisi tufunge hata ikiwa tarehe nane kwetu kwa mujibu wa muandamo wetu - tumeona kwamba kielimu hili ni kosa lakini tujaalie ni hivyo - basi elewa kwamba hili halijahalalisha kwamba na muandamo wa Ramadhani uwe mmoja. Ukitafakari kidogo hapa, utaona kwamba dai hili ni kujenga hoja juu ya Qiyas baina ya mambo mawili yaliotafauti. Arafa ni tokeo ambalo linatokea Makka tu, wakati Ramadhani ni tokeo la dunia nzima. Kwa hivyo, hata tukisema kwamba kilicho sahihi ni kufunga kwa ajili ya tokeo hilo au munasaba huo wa Arafa, basi itakuwa ni kwa sababu munasaba huo unatokea sehemu moja tu: kwetu hautokei. Kwa lugha nyengine, lau na sisi tulioko nje ya Makka ingelikuwa tunatakiwa tusimame Arafa yetu huko tuliko siku ya tarehe tisa, basi tungefanya hivyo kwa mujibu wa muandamo wetu, kama vile tunavyofunga kwa kufata muandamo wetu, na kusali kwa sababu ya mtenguko wetu wa jua. Wakati Ramadhani ni tokeo la dunia: watu wa Makka wanafunga na sisi tunafunga. Kwa hivyo, haya ni matokeo mawili tafauti huwezi kuyafanyia Qiyas kwani miongoni mwa masharti ya lazima ya Qiyas ni "Kupatikana usawa baina ya Shina na Tawi" na usawa hapa haupo. Kilicho sahihi, ni kufanya Qiyas cha Sala na funga. Kwani:

1) Wajibu wa Sala umefungamanishwa na kutenguka na kuzama kwa jua - kitu cha kimaumbile (Natural phenomenon). Kwa hivyo mtenguko wa jua ni sababu: si munasaba.

2) Wajibu wa funga umefungamanishwa na muandamo wa mwezi - kitu cha kimaumbile (Natural phenomenon). Kwa hivyo kuandama kwa mwezi ni sababu: si munasaba.

3) Jua - ambalo kutenguka kwake ndio sababu ya kuwajibikiwa na sala - likitenguka katika nchi moja, watu wa nchi nyengine hawawajibikiwi na sala. Kwa hivyo, Qiyas sahihi ni kuwa kuonekana kwa mwezi - ambayo ni sababu ya kuwajibika funga - katika nchi moja isiwe sababu ya kufunga kwa watu wa nchi nyengine. Hiki ni Qiyas sahihi. Ama kisimamo cha Arafa si Qiyas sahihi, kwani kisimamo cha Arafa ni Munasaba si Sababu wakati muandamo wa mwezi na kutenguka jua ndio Sababu. Au ukipenda kufanya Qiyas chengine sahihi, basi ni kile tulichotangulia kukinukuu kutoka kwa Sheikh Al-uthaimin, aliposema: "Na wakati wa mwezi ni kama wakati wa siku. Kama vile ambavyo miji inatafautiana katika kuanza kujizuia (na kula n a kunywa na jimai: yaani kuanza kufunga) na (inavyotafautiana katika) kufuturu kwa siku (daily au, basi vivyo hivyo inawapasa watafautiane katika kujizuia na kufuturu kwa mwezi (monthly au). Na (kama) inavyojulikana kwamba tafauti za kisiku zina athari zake kwa makubaliano ya Waislamu. (Watu) waliyo upande wa mashariki, hakika wao wanaanza kufunga kabla ya waliyo upande wa magharibi na wanafuturu kabla yao.

Wala haiwezekani mtu akasema kwamba kauli yake Allah (S.W. inayosema):"Sasa waingiliyeni (wake zenu) na tafuteni kile Allah alichokuandikiyeni, na kuleni na kunyweni mpaka ukubainikieni uzi mweupe kutokana na uzi mweusi wa alfajiri, kisha timizeni saumu hadi usiku." Na kauli yake (Mtume) s.a.w.:"Usiku ukitokeza kutoka hapa na mchana ukaondoka kutokea hapa na jua likatua, basi aliyefunga ameshafungua (au na-afungue)." (Haiwezekani mtu akasema kwamba Aya hio na Hadithi hii) kwamba ni za ujumla wa Wa islamu wote katika miji yote. Basi vivyo hivyo tunasema kuhusu ujumla wa kauli yake Allah (S.W.):﴿ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ (Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge).

Na kauli hii - kama unavyoona - ina nguvu yake kwa mujibu wa lafdhi (yake) na mtazamo sahihi na Qiyas sahihi vile vile: Qiyas cha wakati wa siku kwa (kuulinganisha) na wakati wa mwezi (month). Mwisho wa kunukuu.

Tatu : ni kuwa: kutokukiwahi kisimamo cha Arafa kwa baadhi ya Waislamu wa sehemu nyengine za dunia ni kitu cha lazima. Chukulia - kwa mfano - kuna nchi ambazo siku hio ya mwezi tisa, jua linatua Saudia kwao bado ni usiku au alfajiri ya siku hio hio. Ikiwa watafunga kwa munasaba wa Arafa, inakuwa Arafa haipo tena, labda wawe ni wenye kufata kauli ya wenye kujuzisha kusimama Arafa usiku ndio watakuwa nao wamefunga siku ya Arafa, lakini tatizo bado litabakia katika siku ya Idi.

Siku ya pili - tujaalie ni J/tatu - asubuhi watu wa miji ya Saudia wanasali Idi - wao kwao ni magharibi ya J/pili, na Idi haisaliwi magharibi. Hata wakifika asubuhi - J/tatu kwao - Makka tayari jua limetua, na kwa hivyo ni J/nne. Utaona kwamba mitazamo ya kiakili na hoja za kimaandiko zilizojengeka katika misingi imara ya kifani, inaonesha kwamba kufunga na kufungua - sawa ikiwa Ramadhani au Mwezi tisa mfunguo tatu - basi ni jambo linalofatana na miandamo ya mwezi. Na kilicho sahihi - kama tulivyobainisha - ni kuwa muandamo wa mbali usitendewe kazi mbali. Kwa hivyo, kufunga ni tarehe tisa, sawa imeafikiana na munasaba wa Arafa au haikuafikiana, na kwa kufata tarehe tisa watu wote wa dunia itawezekana kufunga na itawezekana kula Siku Kuu tarehe kumi. Ama tukifata munasaba wa kusimama Arafa, watu wa nchi nyengine hawatoweza kufunga kwani hakuna maafikiano ya wakati wa kufunga baina ya Makka na nchi zao, labda kwa wale wenye kufata kauli ya wenye kujuzisha kusimama Arafa usiku, lakini hata hivyo Idi wataikosa.

Ama tukirudi katika nadharia ya Sheikh Bachoo aliposema: " Ni vyema tuzingatie kwamba funga hii ya Arafa pamoja na Iddi yake ni vitu ambavyo havina mahusiano na kuandama mwezi kutokana na kila nchi inavyoona mwezi wake. Bali chanzo cha funga ya Arafa ni uhusiano wa ile siku ambayo mahujaji wanaposimama katika uwanja wa Arafa." Mwisho wa kunukuu. Tukirudi katika maelezo hayo tunakuta kuwa maelezo hayo yanaifanya ibada ya saumu ianzwe kabla ya kufika sababu yake, kwani Arafa inaanza tarehe tisa baada ya kutenguka jua Adhuhuri, wakati wafungaji huwa tayari wameshafunga tangu kabla ya Alfajiri. Jambo hili la kutangulia "Kilichosababishwa kabla ya kilichosababisha" halipo kamwe katika soko la elimu! Ilivyo ni kutangulia "Kilichosababisha kabla ya kilichosababishwa," kama unavyotangulia mtenguko wa jua au kuzama k wake (ambao ni sababu) halafu ndio ikafatia sala (ambacho ndicho kilichosababishwa).

Ama maneno ya Sheikh Nassor Bachoo aliposema: "Kwa uthibitisho zaidi wa funga ya siku ya Arafa tunajifunza kuwa Mtume (s.a.w.) alipotueleza umuhimu wa siku hii, na kila alipotaja siku hii ya Arafa alitumia neno 'siku' wala hakutumia neno 'tarehe'. Funga ya 'siku' ya Arafa." Mwisho wa kunukuu.

Tunasema kwamba: kuitwa siku hio kuwa ni siku ya Arafa na isiitwe siku ya mwezi tisa si hoja ya kuwa lazima tufunge sawa na Saudia, kwani mtegemezo huu ni kulitegemeza (neno hilo Arafa) kwa ajili ya kuitukuza ile ibada inayofanyika katika eneo hilo." Na hii ni kawaida ya Warabu kuyanasibisha majina ya siku kwa kuyapa majina ya sehemu ambazo kuna matokeo fulani adhimu yaliyotokea au yanatokea katika sehemu hizo. Siku ya vita vya Uhudi - kwa mfano - huiita Yawmu Uhud (Siku ya Uhudi), na Uhudi ni jina la sehemu. Halkadhalika vita vya Hunain: vinaitwa Yawmu H unain (Siku ya Hunain). Anasema Allah kuhusu vita hivyo: "Na siku ya Hunain wingi wenu ulipokupendezesheni." Na Hunain ni jina la mji. Halkadhalika vita vya Badr; Badr ni sehemu. Lakini tunaviita vita hiv yo "Yawmu Badri (Siku ya Badr). Anasema Sahaba Hassan bin Thabit, Mshairi wa Mtume(s.a.w.w):

Nyuso siku ya Badri zilimngojea Mwingi wa rehema alete ushindi. Tazama Sahaba Hassan: ameinasibisha siku hio kwa kuipa jina la sehemu ya Badr, kwa ajili ya utukufu wa yale yaliofanyika hapo. Kwa hivyo kunasibishwa siku ya Arafa na sehemu hio ya Arafa, si kwa sababu tufunge sawa sawa, bali ni kwa utukufu wa yale yanayotendeka. Na yanayotendeka hapo ni Munasaba wa kufunga si Sababu ya kufunga kama tulivyotangulia kubainisha. Na inampasa msomi - mwanachuoni na Talibu Al-ilm (mwanafunzi) - kutafautisha baina ya vitu viwili hivyo. Mwisho wa kunukuu nilioyasema katika kitabu.

JAWABU NILIOJIBIWA NI KAMA IFATAVYO

Baada ya kuyaeleza hayo nilioyaeleza, ndugu zangu walinijibu juu ya maudhui hio kama ifatavyo:

Funga Ya 'Arafah Neno 'Arafah au 'Arafah ni jina linalotokana na uwanja au viwanja maalum vilioko nje kidogo ya Mji Mtukufu wa Makkah. Mahujaji wote ambao wamehirimia kutekeleza Ibada ya Hijja hukusanyika katika viwanja hivyo. Jambo hilo la kwenda kusimama kwenye viwanja hivyo kwa kuomba dua na kumtaja Allaah ni katika nguzo kubwa ya ibada hiyo ya Hijja. Inampasa kila Hajji kusimama au kushiriki hata kwa muda mdogo katika mchana huo. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amebainisha hayo kwa kusema:

(Hijja ni 'Arafah) Jambo hilo linathibitisha kwamba mtu yeyote asiyetekeleza ibada ya kusimama 'Arafah anapokuwa Makkah, atakuwa hakuipata ibada hiyo ya Hijja. Watu humiminika na kusimama kwenye uwanja wa 'Arafah siku ya tarehe 9 - Dhul-Hijjah ya kila mwaka. Ikumbukwe kwamba tarehe 9 hiyo ni ya huko Makkah pahala ambapo inafanyika ibada ya Hijja wala siyo ya pahala pengine popote duniani. Ni vyema kuzingatia kwamba funga hii ya 'Arafah pamoja na 'Iyd yake ni vitu ambavyo havina mahusiano na kuandama kwa mwezi kutokana na kila nchi inavyoona mwezi wake. Chanzo cha funga hii ya 'Arafah ni ule uhusiano wa ile siku ambayo Mahujjaji wanaposimama katika uwanja wa 'Arafah. Ambapo jambo la kusimama 'Arafah linapatikana sehemu moja tu ulimwenguni ambayo ni siku inayosadifu tarehe 9 - Dhul-Hijjah huko mji wa Makkah, sio tarehe 9 ya nchi nyengine yoyote ile.

Kwa maneno mengine ni kuwa tutakapotofautiana katika kufunga Siku ya 'Arafah na 'Iydul-Hajj itakuwa kama kwamba kila nchi ina uwanja wake wa 'Arafah na Makkah yake. Kwa uthibitisho zaidi wa funga ya siku ya 'Arafah tunajifunza kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kila alipokuwa akieleza umuhimu wa siku hii alitumia neno "siku" wala hakutamka neno "tarehe." Ama kwa mujibu wa maelezo ya ndugu yetu Juma, kama kawaida yake yeye anaona kuitwa "Siku ya 'Arafah" haina maana kuwa lazima tufunge sawa na Saudia, bali anaona kuwa hiyo ni "Idhaafatu-Tashriif" (yaani kuitengeneza siku hiyo kwa ajili ya utukufu wa pahala hapo au kwa ajili ya utukufu wa tokeo lenyewe). Sisi kwa upande wetu tunamuuliza ndugu Juma, Je yapo maandiko yoyote ya kilugha au ya kisheria yanayotufunza kuwa pahala pakitumika "Idhaafatu-Tashriif" huwa haparuhusiki tena kutoa mafunzo mengine yaliyomo ndani ya "idhaafa" hiyo? Tujuavyo sisi zipo Aya nyingi za Qur-aan ambazo zimetumika ndani yake hiyo "Idhaafatu-Tashriif" lakini utakuta wanavyuoni wa tafsiri wametoa mafunzo mengine yapatikanayo katika "idhaafa" hizo.

Akaendelea ndugu Juma kutoa kikwazo ambacho anaona kuwa haiwezekani kufunga siku ya 'Arafah sawa na tokeo lenyewe huko Makkah kwa kisingizio cha kuwa kuna nchi zinazotofautiana kwa masaa mengi. Kisha akasema: (Na (kama) inavyojulikana kwamba tafauti za kisiku zina athari zake kwa makubaliano ya Waislamu. Waliyo upande wa mashariki, hakika wao wanaanza kufunga kabla ya waliyo upande wa magharibi na wanafuturu kabla yao). Kama ni hivyo tofauti ni nchi zilizo Magharibi kwa nchi zilizo za Mashariki zinatofautiana, sisi tunamuuliza ndugu Juma vipi tena kwa nchi zilizo jirani kama vile Omani na Dubai , au Omani ya Yemeni, Je! Kuna suala la Mashariki na Magharibi hapa? Au kama ni hivyo basi mbona Juma hakubali uwezekano wa kufunga pamoja nchi zote za Mashariki kwa wakati mmoja na zote za Magharibi kwa wakati mwengine?

JAWABU

Kwanza Kimsingi ni kuwa hamukujibu hoja zangu moja moja kama nilivyoeleza mimi. Mukhtasari wa nilioyaeleza ni kuwa:

a) Ibada za Hija zina Sababu yake.

b) Hadithi imeonesha kuwa sababu ya ibada hizo ni muandamo wa mwezi wa mfunguo tatu. Hadithi imesema: "Alituusia Mjumbe wa Allah - rehema na amani ziwe juu yake - tuabudu kwa kuuona, kama hatukuuona na wakashuhudia mashahidi wawili waadilifu, tuabudu kwa (kufata) ushahidi wao."

Tumesema katika kitabu kwamba neno Nansuk (tuabudu) wengine wameifasiri ibada hii kuwa ni ibada ya hija nayo ndio tafsiri yenye muelekeo madhubuti zaidi, kwani neno hili hutumika sana kwa maana ya ibada ya hija, kama Allah (S.W.) anavyosema kuhusu ibada ya hij a: Mukimaliza Nusuki (ibada) zenu (za hija). Na kwa hivyo imekuja katika "Awnu Al-Ma'abudi: Sharhu Sunani Abi Daud kuhusu maana ya Hadithi hio tulioinukuu hapo juu kuwa maana yake inahusiana na ibada za hija. Anasema mwenye kusherehesha: "Na maana yake ni: 'Tuhiji kwa kuuona (mwezi), yaani mwezi muandamo wa mfunguo tatu." Ni wazi kwa maelezo haya au kwa mujibu wa Hadithi hii kwamba sababu ya ibada za hija - ikiwemo funga ya Arafa - ni kuandama kwa mwezi wa mfunguo tatu.

c) Kwa hivyo, kwa mujibu wa Hadithi hii, sababu ya kuingia ibada ya hijja -funga yake ya mwezi 9 na idi yake mwezi 10, ni muandamo wa mwezi wa mfunguo tatu. Ama kisimamo cha Arafa nimejibu kwamba haiwezekani kuwa ndio sababu ya kufunga kwani, kisimamo kinakuwa baada ya kutenguka jua adhuhuri, wakati wafungaji wameshafunga tangu alfajiri, na sababu hutangulia kwanza kisha ndio kikaja kilichosababishwa; yaani kwa lugha nyengine sababu ya ibada huwa haitanguliwi na ibada yenyewe; bali kwanza hutangulia sababu kisha ndio ikaja ibada ambayo ndio iliosababishwa.

Kwa hivyo, ikiwa sababu ya ibada za hija kikiwemo kisimamo cha Arafa na funga yake ni muandamo wa mfunguo tatu, basi sisi tupo pale pale kwamba Hadithi sahihi ya Ibn Abbaas na Kuraib imethibisha kwamba muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali. Kwa hali hii, sisi Afrika Mashariki, na kwangine, hatuwezi kufunga kwa kufata mwezi tisa wa Saudia, kwani muandamo kila mtu ana wake; wala hatuwezi kufanya hivyo kwa kufata kisimamo cha Arafa kwani kisimamo cha Arafa sio sababu ya ibada za Hijja kikiwemo kifungo hicho; bali muandamo wa mwezi ndio sababu kama Hadithi ilivyosema.

MNASEMA

Ndugu Juma ni vyema aelewe kwamba upo uwezekano wa kufunga 'Arafah siku moja dunia nzima kama tulivyoelezea katika kurasa za nyuma za kitabu hichi kwamba dunia nzima inashirikiana katika mchana mmoja na inashirikiana katika usiku mmoja ingawaje kuna nchi zinazotanguliza na nyengine zinazofuatia. Mfano nchi zote za Afrika zinaweza kushirikiana kufunga siku moja kwani baadhi ya nchi za Afrika zinatofuatiana kwa masaa machache tu sio usiku mzima wala mchana mzima. Katika kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu imeandikwa kwamba tofauti iliyopo kwa nchi za Kiislamu zilizo Mashariki ya mbali kama Phillipines na Indonesia na zile zilizo Magharibi ya mbali kama Al-Maghrib yaani Morocco ni tofauti ya masaa 9 tu. Kwa hivyo upo uwezekano wa kitaalamu (Kijiografia) wa kuweza kufunga kwa pamoja katika siku hiyo hiyo moja. Tofauti iliyopo ni ya masaa tu. Tunafunga siku moja sio wakati mmoja wala sio dakika moja. Msisitizo upo katika kufunga siku moja sio kuanza wakati mmoja.

JAWABU

Ama kudai kwamba uko uwezekano wa kufunga Arafa duniani kote siku moja, hilo si da sahihi. Nimekupeni mfano wa mimi mwenye mwezi wa 5 na wa 6 2009 nilikuwa Hong Kong, nikampigia simu ndugu yangu aliye Marekani nikamuuliza ni saa ngapi huko kwenu akanijibu ni saa kumi jioni; wakati huo Hong Kong tumeshali Alfajiri tushatoka Msikiti baina ya saa 11 na nusu mpaka 12 au 12 kasoro kidogo. Tazama tafauti iliokuwepo hapo. Hii ina maana jua likitua U.S.A jioni baada ya masaa mawili, labda na nusu, Hong Kong watu wanaingia makazini asubuhi kweupe na jua liko juu. Utaona kwamba, Kiislamu, ikiingia Ijumaa Hong Kong, Marekani bado ni Alkhamisi. Waislamu walioko Hong Kong wakifunga Arafa mchana wa tarehe 9, Marekani bado ni usiku hawawezi kufunga; Waislamu wa Hong Kong wakifuturu jioni, Marekani ni wakati wa mwisho mwisho wa alfajiri au ni asubuhi. Kwa ufupi ni kuwa baadhi ya States za Amerika na Hong Kong, tafauti haipungui masaa kumi na mbili.

Kwa hivyo, dai hilo si sahihi. Na hapa inabainika kwamba kauli sahihi ni ya kufata tarehe 9 mfunguo tatu kwa mujibu wa muandamo wan chi zetu, kwani tukifanya hivyo Waislamu wote duniani wataweza kufunga tarehe 9 na kula siku kuu tarehe 10. Ama tukifata muandamo mmoja hilo halitowezekana kwani mchana wa mwezi 10 wa nchi moja, tuseme hio Hong Kong, ni usiku katika nchi nyengine tuseme hio Marekani; jua likitua Hong Kong itakuwa tayari Kisharia ni mwezi 11, wakati Marekani ndio kwanza wajitayarisha kwenda kusali idi bado kwao ni mwezi 10. Utaona Al-Nadhar, Athar na migawanyiko ya kijografia, yanatoa jawabu sawa kwamba kilicho sahihi ni kila watu kufata muandamo wao.

Ama baadhi ya nchi kama mulivyosema - Za Africa kwa mfano - sipingi kwamba kuna uwezekano, ninachopinga ni kuwa dalili ni tafauti na kitendo hicho. Kama Ibn Abbas kakataa kuchukua muandamo wa Sham wala tafauti baina yake na Madina haifiki masaa hayo ya masaa 9 na akatoa hoja kwamba "Hivi ndivyo alivyotufunza Mtume s.a.w.", basi vipi itawezekana Kisharia kwamba watu wa Africa nzima wafunge sawa sawa.

MNASEMA

Ndugu Juma anasema: (Utapolifahamu hili, utakuwa umefahamu kwamba, siku ya kufunga ni tarehe tisa mfunguo tatu, sawa siku hio imeafikiana na Arafa au imetafautiana,....) [uk. 141]

JAWABU

Nyinyi ndugu zangu munanukuu maneno "Utapolifahamu hili..?" Bila ya ku nukuu maelezo yenyewe yalionipelekea kusema "Utapolifahamu hili". Sasa msomaji atafahamu nini? Huu sio mjadala wa kielimu wenye lengo la kutafuta natija sahihi. Ilikuwa munukuu jawhari ya maneno yangu kasha ndio muyajibu.

MNASEM

a) Sisi tunamjibu kwamba: Sasa kama anaruhusu kutafautiana, tena kwanini imeitwa (Funga ya 'Arafah) isiitwe "Funga ya tarehe 9"? Kisha ndugu Juma anaamini kwamba: (Arafa ni tokeo ambalo linatokea Makka tu, wakati Ramadhani ni tokeo la dunia nzima.) Kama kawaida yake ndugu Juma anajikanganya kila mara, kama kweli anaamini kila nchi ifunge kwa muandamo wake na 'Arafah, kila nchi ifunge kivyake, inakuaje tena Ramadhaan iwe ni ya dunia nzima, 'Arafah iwe kila mtu na yake?

JAWABU

Ama kwanini imeitwa (Funga ya 'Arafah) isiitwe "Funga ya tarehe 9", nimeshakuelezeeni kwa urefu katika Kitabu. Nimesema: Tunasema kwamba: kuitwa siku hio kuwa ni siku ya Arafa na isiitwe siku ya mwezi tisa si hoja ya kuwa lazima tufunge sawa na Saudia, kwani mtegemezo huu ni kuli tegemeza (neno hilo Arafa) kwa ajili ya kuitukuza ile ibada inayofanyika katika eneo hilo." Na hii ni kawaida ya Warabu kuyanasibisha majina ya siku kwa kuyapa majina ya sehemu ambazo kuna matokeo fulani adhimu yaliyotokea au yanatokea katika sehemu hizo. Siku ya vita vya Uhudi - kwa mfano - huiita Yawmu Uhud (Siku ya Uhudi), na Uhudi ni jina la sehemu. Halkadhalika vita vya Hunain: vinaitwa Yawmu Hunain (Siku ya Hunain). Anasema Allah kuhusu vita hivyo: Na siku ya Hunain wingi wenu ulipokupendezesheni." Na Hunain ni jina la mji. Halkadhalika vita vya Badr; Badr ni sehemu. Lakini tunaviita vita hivyo "Yawmu Badri (Siku ya Badr). Anasema Sahaba Hassan bin Thabit, Mshairi wa Mtume(s.a.w.w) :

Nyuso siku ya Badri zilimngojea Mwingi wa rehema alete ushindi. Tazama Sahaba Hassan: ameinasibisha siku hio kwa kuipa jina la sehemu ya Badr, kwa ajil i ya utukufu wa yale yaliofanyika hapo. Kwa hivyo kunasibishwa siku ya Arafa na sehemu hio ya Arafa, si kwa sababu tufunge sawa sawa, bali ni kwa utukufu wa yale yanayotendeka. Na yanayotendeka hapo ni Munasaba wa kufunga si Sababu ya kufunga kama tulivyotangulia kubainisha. Na inampasa msomi - mwanachuoni na Talibu Al-ilm (mwanafunzi) - kutafautisha baina ya vitu viwili hivyo.

Ama kauli yenu: "Kama kawaida yake ndugu Juma anajikanganya kila mara, kama kweli anaamini kila nchi ifunge kwa muandamo wake na 'Arafah, kila nchi ifunge kivyake, inakuaje tena Ramadhaan iwe ni ya dunia nzima, 'Arafah iwe kila mtu na yake?" Mwisho wa kunukuu. Ninasema: hata hili pia nalo munalifanya kuwa ni hoja ya kielimu!!! Zote mbili - Ramadhani na Arafa - ni za dunia nzima, tafauti ni katika kuingia nyakati zake. Ramadhani ni refu Waislamu ni lazima watakutana kwani hakuna tafauti ya muandamo wa mwezi mzima; kuna tafauti ya siku moja mbili, Arafa ni tokeo la siku moja, inapotafautiana miandamo hupelekea kutafautiana kwa tarehe za kufunga na kula siku kuu.

MNASEMA

Hebu tuangalie hoja nyengine ya ndugu Juma katika uk 142 wa kitabu chake anapodai kunukuu maneno ya Shaykh Al-'Uthayminiy, anaposema: ("Na wakati wa mwezi ni kama wakati wa siku Kama vile ambavyo miji inatafautiana katika kuanza kujizuia (na kula na kunywa na jimai: yaani kuanza kufunga) na (inavyotafautiana katika) kufuturu kwa siku (daily) basi vivyo hivyo inawapasa watafautiane katika kujiz uia na kufuturu kwa mwezi (monthly)

a) Suala linakuja: Je! Kama anavyosema miji inatafautiana kufuturu kwa mwezi kama inavyotafautiana kwa siku. Sasa vipi katika nchi moja iliyo kubwa kama Tanzania ambayo ina mikoa inayotafautiana kuanza k ula na kunywa kama Dar es Salaam na Kigoma? Je! Mbona haitafautiani kwa mwezi? Inafunga kwa muandamo mmoja lakini Dar es Salaam na Kigoma zinatafautiana katika kuanza kula na kunywa (kufuturu) kwa zaidi ya dakika 45?

JAWABU

Hatuzungumzii watu wanatenda nini; tunazungumzia nini kinatakiwa Kisharia kitendwe. Watu wa Kigoma ikiwa muandamo kwao ni tafauti na Dar-es-Salam, basi ilivyo ni kuwa wafunge kwa mujibu wa Muandamo wao kama wanavyosali kwa mujibu wa mtenguko wao na kufuturu kwa mujibu wa kuzama jua kwao. Kinachotazamwa si tangazo au amri ya serikali, bali ni muandamo wa mwezi. Na hili - kama munavyojua - ni jambo ambalo wanavyuoni wamelizungumzia na wako walioeleza kama hivyo. Nchi kama Urusi, hasa kabla ya kugawanyika, vipi utamwambia mtu wa State moja ya mbali na iliotafauti kabisa na State nyengine kwamba wafunge sawa. Kinachozinagatiwa si suala la nchi moja bali ni umbali na tafati za matalai.

Pamoja na hayo, kama nilivyokuelezeni mara nyingi kwamba, suala la umbali gani watu wafunge sawa, linabakia kuwa ni uwanja wa ijtihad kwa kutokuwepo andiko lenye kuonesha umbali gani; ingawa andiko limeonesha kwamba muandamo wa mbali si hoja kwa walio mbali, kilichojificha ni umbali gani. Kwa hivyo, ukweli kwamba muandamo wa mbali si hoja kwa waliombali hili ni andiko ambalo lazima tusallim amri mbele yake; na je umabali huo uwe kiasi gani; hapa wenye elimu wana uwanja mpana wa kujitahidi na kutoa fat-wa na sisi tutatazama ilio na nguvu. Kwa hivyo, ikiwa watu wa Kigoma wamechukua ijtihad ya wanavyuoni wetu wakubwa waliotangulia wa Africa Mashariki, hilo linatoa nafasi kwani hapa uwanja wa ijtihad upo. Ama kutwambia kuwa dunia nzima tuwe na muandamo mmoja: hili ni kinyume na andiko na ni kinyume na maumbile yenyewe ya dunia.

MNASEMA

b) Kwa nini basi nchi kama Omani na Dubai zinatafautishwa katika kuangalia mwezi wakati ambapo nchi hizo hazina tofauti kubwa katika kuanza kula na kunywa? Wala hazina tofauti ya matlai wala masaa ya kuanza na kuingia kwa siku?

JAWABU

Imarati ni maamuzi ya serekali zao kufata Saudia; nalo ni kosa kwani wao na Oman ndio walio karibu zaidi na wana matalai sawa. Na nimekwambieni kuwa mjadala wetu si watu wanafanya nini: bali nini kinatakiwa kitedwe Kisharia. Vyenginevyo na mwengine anaweza kukuulizeni mbona Suudia wanafata muandamo wao; mbona Misr wanafata muandamo wao, n.k. Kwa hivyo, tuko pale pale kwamba hatuzungumzii nini watu wanafanya; bali tunazungumzia nini kinatakiwa kifanywe Kisharia.

MNASEMA

c) Tujuavyo sisi nchi zote za Uarabuni zinapata usiku wao mmoja na mchana wao mmoja, kwa hivyo hakuna shida yoyote katika kufunga 'Arafah siku moja kwa wote.

JAWABU

Sijakwambieni kuwa haiwezekani; nimesema kwamba ushihidi tulio nao ni kuwa:

1) Ibada za Hijja ikiwemo funga hio ya Arafa inategemea muandamo wa mwezi: si kisimamo cha Arafa. Kisimamo cha Arafa ni munasaba na muandamo wa mwezi ndio sababu ya ibada hizo.

2) Muandamo wa mbali si hoja kwa walio mbali.

MNASEMA

Shaykh Naaswir Khamiis 'Abdur-Rahmaan wa Mombasa Kenya ameandika kitabu chake "Mwezi Ko-Ongo" na amethibitisha tofauti ya masaa baina ya nchi mbali mbali mfano: "tofauti ya mji wa Mombasa na nchi ya magharibi ya mbali mwa Afrika kama Algeria ni masaa mawili na dakika ishirini na nane (2:28)" - uk 22. Katika jambo la kuonesha ufinyu aliokuwanao ndugu yetu Juma, ule wa kutokufanya uchunguzi wa kina katika mas-ala haya, yeye anaamini kwamba jambo hili limeanzishwa na Shaykh Naaswir Bachuu na wala halikuwepo ulimwenguni kama anavyodai mwenyewe kwa kauli yake ifuatayo: (Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja)

JAWABU

Jambo gani hilo ambalo nimedai kuzushwa na Sheikh Nassor Bachoo? Hebu ninukulieni hilo jambo. Fikra ninayosema kuwa kaja nayo Sheikh Nassor Bachoo Zanzibar ni fikra ya kututaka tufunge kwa muandamo mmoja. Kwa Zanzibar yeye ndiye aliyeitangaza, kuilingania na kuitungia kitabu. Wala sikusema kuwa katika dunia yeye ndiye muasisi wa fikra hio. Ama yale mulioyanukuu kutoka kwa Sheikh Nassor Khamis, sio yalionifanya mimi nikapigwa na mshangao huo: ((Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja). Kwa hivyo, musichanganye mambo. Mimi nilishagaa hivyo kwa sababu ya maneno haya ya Sheikh Nassor. Alisema Sheikh Nassor: "Pili kama ingalikuwa hakuna dhana ya kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge, Ibnu Abbas (r.a.) asingekuwa na haja ya kumuuuliza Kurayb juu ya habari za mwezi wa Sham kwa kusema:

"Kis ha (Ibn Abbas) akataja (habari) ya mwezi na akasema: "Ni lini mliuona mwezi?...akasema: "Wewe umeuona?" Hapo ndio nikashanga na nikasema: Hio ndio hoja nyengine ya Sheikh Bachoo, kwamba lau hakuna dhana ya kuwa mwezi ukionekana popote watu wafunge, basi Ibn Abbas asingekuwa na haja ya kumuuliza Kuraib "Lini mumeuona mwezi!!!" Ninasema: Enyi walimwengu wenzangu tazameni hoja za kielimu hizo!!!!!!! Kwani nyinyi Wazanzibari kabla ya kuja fikra hio ya Sheikh Nassor Bachoo ya kufunga kwa muandamo mmoja, mulikuwa hamuwaulizi watu wanaotoka nchi nyengine masuala kama hayo wanapokuja kwenu na nyinyi muko kati kati ya mwezi pamoja na kwamba nyote zamani mukifata muandamo wenu? Sasa kama nyinyi mulikuwa mukiuliza suala hilo hilo kwanini Ibn Abbas na yeye asiulize hata kama dhana hio haipo? Mimi binafsi nina kawaida ya kuwauliza wageni walioko nchi hii ninayoishi suala hilo, na natarajia kwamba pia nimewasikia watu wengi wenye kuwauliza wageni suala hilo. Kwa hakika shubuhati kama hizi hazifai katika kujadili mambo ya kielimu. Kwa ufupi ni kuwa hata kama dhana hio ilikuwepo, dhana hio inabomolewa na kukataa kwake - Ibn Abbas - kuukubali mwezi wa Sham, na kujenga hoja kwa Hadith marfu'u kwamba hayo ndio mafunzo ya Mtume(s.a.w.w) kwao. Sasa uko wapi uhusiano wa maneno yangu na nakala ya Sheikh Nassor Khamis?

MNASEMA

Sasa sisi tunataka kumtihibitishia ndugu Juma kuwa wapo watu wengi ambao pengine hawakuwafikiana na Shaykh Naaswir Bachuu katika baadhi ya mambo au misimamo lakini kwa bakhti nzuri katika hili suala la kufunga 'Arafah na kusali siku ya 'Iydul-Adh-ha wanafuata Makkah na wanaungana na ulimwengu mzima. Mfano mzuri kabisa ni ndugu zetu wa Tarika ya Kadiria, takriban wote wanafunga 'Arafah kwa kufuata tarehe 9 - Dhul-hijjah ya Saudia (Makkah). Hayo yanathibitishwa na aliyekuwa kiongozi wao Mkuu wa Tarika hiyo mwanachuoni maarufu Al-Marhuum Shaykh Muhammad Naaswir Abdulla Al-Qaadiry ambaye aliandika kitabu alichokiita: "Kitabu 'Arafah" na kuandika kwenye gamba la kitabu hicho kwamba: "Nguzo Kubwa Ya Hijjah Ni 'Arafah Tarehe Tisa Mfunguo Tatu Na Kuswali 'Iydul-Hajj Sawa Na Makkah." Katika uk 22 wa kitabu chake hicho pia ameandika kama ifuatavyo: "Waislamu wote ulimwenguni wafunge Sunnah ya 'Arafah sawa na 'Arafah ya Makkah."

Kisha katika uk 74 ameandika Fatwa zifuatazo: "'Arafah ya Makkah tarehe 9 mwezi wa Mfunguo Tatu (Dhul-Hajj) ndiyo 'Arafah ya Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) na ndiyo 'Arafah ya Waislamu wote popote walipo ulimwenguni." "Wananaokwenda Hijja, kwao ni haramu kufunga siku hiyo ya 'Arafah huko 'Arafaati (Makkah) na waliobaki majumbani, kwao ni Sunnah kubwa kufunga siku hiyo hiyo ya 'Arafah ya Makkah kokote waliko ulimwenguni." "Tarehe 10 Mfunguo Tatu (Dhul-Hajj) ndiyo siku ya 'Iyd ya Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) na 'Iyd ya dunia nzima kwa Waislamu wote. Kufunga siku hiyo yote kamili ni haramu. Anayeswali 'Iyd tarehe 10 ya Makkah amefanikiwa na ole wake yule anayeswali 'Iyd siku atakayo mwenyewe. Kwa ujumla kufunga tarehe 9 Mfunguo Tatu kwa Mahujaji 'Arafah ni Haramu. Na kufunga kwa Waislamu wote ulimwenguni tarehe 10, 11, 12 na 13 Mfunguo Tatu ni Haramu."

"Hivyo ni jambo baya kabisa na lenye kutia huzuni sana kuwaona baadhi ya ndugu zetu Waislamu wanaacha kufunga siku ya 'Arafah Aliyoiteua Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta'ala) na badala yake wanafunga siku ya kuchinja tarehe 10 (ya Makkah) wakisingizia kuwa ndiyo siku yao ya 'Arafah waitakayo wao waliyoichagua wao wenyewe ambayo kufunga siku hiyo ni haramu."

JAWABU

Haya! Hoja iko wapi humu! Je hii ni hoja kwamba alivyosema Sheikh Muhammad Nassor ni sahihi au ni hoja kwamba kuna watu wanaafikiana na nyinyi katika hilo? Ikiwa ndio munatoa hoja kwamba alivyosema Sheikh Muhammad Nassor ni sahihi; nitakutakeni dalili ya usahihi huo; ikiwa munatoa hoja kwamba kuna watu wanaafikiana na nyinyi katika hilo; hapo sikupingini. Lakini suala letu bado lipo: 1) Nini sababu ya kufunga Arafa.

2) Je sababu ni kisimamo cha Arafa.

3) Je ni muandamo wa mwezi wa mfunguo tatu.

4) Je tufate muandamo mmoja au kila mtu wake.

Mimi ushahidi nilio nao ni kuwa:

1) Sababu ya kufunga Arafa ni muandamo wa mfunguo tatu, kama ilivyonena Hadithi ya Amir wa Makka.

2) Kisimamo cha Arafa si sababu kwani sababu hutangulia kisha ndio kikija kilichosababishwa. Kama linavyotenguka jua ndio ukaingia wajibu wa kusali; au unavyoingia mwezi wa Ramadhani ndio ukaja wajibu wa Ramadhani. Ama kisimamo cha Arafa kinaanza baada ya kutenguka jua wakati wenye kufunga wanaanza kufunga tangu Alfajiri. Kwa hivyo, kisimamo cha Arafa ni munasaba ni sababu.

3) Kila watu wafate muandamo wao kwa mujibu wa Hadithi ya Ibn Abbas na Kuraib.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿الشَّهْرُ الْحَرَامُ بِالشَّهْرِ الْحَرَامِ وَالْحُرُمَاتُ قِصَاصٌ فَمَنِ اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ فَاعْتَدُوا عَلَيْهِ بِمِثْلِ مَا اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ ﴾

194.Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu; na vitu vitakatifu vina kisasi. Basi wanaowachokoza, pia nanyi wachokozeni kwa kadiri walivyowachokoza. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaomcha.

﴿وَأَنفِقُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَلَا تُلْقُوا بِأَيْدِيكُمْ إِلَى التَّهْلُكَةِ وَأَحْسِنُوا إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ﴾

195.Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamivu, na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema.

MIEZI MITAKATIFU

Aya 194 - 195

MAANA

Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu.

Miezi mitakatifu ni minne; mitatu inafuatana, nayo ni Dhul-Qaada, Dhul Hijja na Muharram (mfunguo pili, mfunguo tatu na mfunguo nne). Na mwezi mmoja uko pekee na ni (Rajab). Miezi hii imeitwa mitakatifu kwa sababu ya kuharamishwa kuuana ndani ya miezi hiyo. Katika wakati wa ujahiliya na wa Uislamu, ilikuwa mtu anaweza kukutana na mtu aliyemuua baba yake katika miezi hiyo na asimfanye chochote. Yameshatangulia maelezo kwamba Mtume na sahaba zake walitaka kufanya umra katika mwezi wa dhul-Qaada (mfunguo pili) mwaka wa sita (6 Hijriya), wakazuiwa na washirikina na wakatupiwa mishale na mawe; kisha waka-fanyiana suluhu kuwa Waislamu warudi mwaka utakaofutia. Lakini Waislamu wakaogopa washirikina wasije wakaanza kupigana katika mwezi mtakatifu; ndipo Mwenyezi Mungu akawapa idhini ya kupigana na washirikina na akabainisha kuwa lenye kukatazwa ni kuanza uadui wa kupigana na sio kujikinga. Kwa hivyo maana ya mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu ni kwamba mwenye kuihalalisha damu yenu enyi Waislamu katika mwezi huu, basi nanyi ihalalisheni damu yake katika mwezi huo huo.

Na vitu vitakatifu vina kisasi. Yaani mwenye kuvunja heshima ya Mwenyezi Mungu atalipizwa kisasi na atafanywa kama alivyofanya. Hiyo ndiyo asili kwa ujumla inayoondoa kila udhuru wa mwenye kuvunja heshima. Mwenye kuhalalilisha damu za watu, mali zao na heshima zao, naye atahalalishwa kwa kiasi kile alichowafanyia. Heshima kwa mtu mwingine inatokana na heshima ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kama akivunja heshima ya mwingine. Hapo itakuja haki ambayo daima inakuwa juu na wala haikaliwi. Hapa ndipo tunapata tafsiri ya:

Anayechokoza pia nanyi mchokozeni kwa kadiri alivyo wachokoza. Sharti la kulipiza ni kuwa sawa na kosa la aliyeanza bila ya kuzidisha au kupunguza. Hicho ndio kisasi hasa kilivyo. Unaweza kuuliza: Mwenye kuchokoza , yeye ni mchokozi bila ya wasiwasi wowote, lakini mwenye kulipiza kisasi bila shaka siye mchokozi. Kwa hiyo kuna wajihi gani kwa Mwenyezi Mungu kusema:Mchokozeni

Jibu : Makusudio ya kuwafanyia uchokozi, sio uchokozi hasa kwa maana yake, isipokuwa makusudio ni malipo ya uchokozi uliofanywa kwa kipimo chake bila ya kudhulumu. Hayo ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu(s.w.t.):

"Na malipo ya ubaya ni ubaya ulio sawa na (ubaya) huo..." (42:40)

KUTOA KATIKA NJIA YA MWENYEZI MUNGU

Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu. Kutoa katika njia yake Mwenyezi Mungu kunakuwa ni kwa masilahi ya umma; kama vile shule, hospitali na nyumba za kulea mayatima. Vile vile jihadi, sadaka kwa mafukara na masikini na kuwalisha watu wa nyumbani. Bora zaidi ya kutoa ni kule kunakohusika na kutia nguvu na kuieneza dini, kuthibitisha haki na kuibatilisha batili.

Wala msijitie, kwa mikono yenu, katika maangamivu

Mwenyezi Mungu ametumia neno mikono kwa maana ya mtu kujiingiza mwenyewe. Kama tukiangalia jumla hii peke yake tu bila ya kuangalia mfumo mzima wa maneno, ingelikuwa maana yake ni kuwa haijuzu kwa mtu kufanya lolote ambalo lina madhara na bila ya kuwako manufaa kwa ujumla. Lakini tukichunga mfumo wa maneno na kuja kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):"wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamivu" baada ya kusema:"Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu", basi maana yanakuwa, toeni katika mali zenu sio kwa ubahili wala ubadhirifu, kwa sababu yote hayo mawili yanaleta uangamivu. Kwa hivyo Aya kwa maana haya inakuwa kama ile Aya isemayo:

﴿ وَالَّذِينَ إِذَا أَنفَقُوا لَمْ يُسْرِفُوا وَلَمْ يَقْتُرُوا وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا ﴾

"Na wale ambao wanapotoa hawafanyi ubadhirifu wala ubahili, bali wanakuwa katikati ya hayo."( 25:67)

Inasemekana pia kwamba maana yake ni: Msijitie kwa mikono yenu kwenye maangamivu kwa kuacha kupigana jihadi na maadui wa dini na kutoa mali kwa ajili ya kuwaandaa wapigania jihadi, kwa sababu hilo litawaogopesha na atawaweza adui; muangamie na mdhalilike. Haya ndiyo yaliyothibitishwa na majaribio waliyoyapitia Waislamu. Wamekosa uhuru wao na heshima yao tangu walipoacha jihadi na kutoa mali kwa ajili ya kuinusuru haki na uadilifu. Hivyo akapata tamaa kila mnyang'anyaji na mnyakuzi; hata Wazayuni, vibaraka wa ukoloni, nao waliivamia Palestina mnamo 1948. Baada ya Waarabu kunyamaza na wasifanye jihadi. Baada ya miaka ishirini wakateka Sinai na ukanda wa Gaza Magharibi mwa mto Jordan; wakazikalia sehemu hizo kwa msaada wa Amerika, Uingereza na Ujerumani Magharibi. Wakawaua wanaume na kuwafukuza wanawake na watoto. Lau Waislamu wangefanya jihadi kabla yake, wangeliokoka na maangamizo haya na udhalili huu, na wala dola ya Israel isingekuwepo kabisa.Na fanyeni wema Kwa jihadi na kujitolea mali katika njia ya Mwenyezi Mungu na katika kila njia inayomridhisha Mungu na yenye sifa nzuri.

﴿ وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ وَلَا تَحْلِقُوا رُءُوسَكُمْ حَتَّىٰ يَبْلُغَ الْهَدْيُ مَحِلَّهُ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ بِهِ أَذًى مِّن رَّأْسِهِ فَفِدْيَةٌ مِّن صِيَامٍ أَوْ صَدَقَةٍ أَوْ نُسُكٍ فَإِذَا أَمِنتُمْ فَمَن تَمَتَّعَ بِالْعُمْرَةِ إِلَى الْحَجِّ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ تِلْكَ عَشَرَةٌ كَامِلَةٌ ذَٰلِكَ لِمَن لَّمْ يَكُنْ أَهْلُهُ حَاضِرِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴾

196.Na timizeni Hijja na Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Na kama mkizuiliwa, basi (chinjeni) wanyama walio wepesi kupatikana. Wala msinyoe vichwa vyenu mpaka wanyama hao wafike machinjioni mwao. Na ataka-yekuwa mgonjwa katika nyinyi au ana adha kichwani mwake, basi atoe fidia kwa kufunga au sadaka au kuchinja mnyama. Na mtakapokuwa salama, basi mwenye kujistarehesha kwa kufanya Umra, kisha akahiji, achinje mnyama aliye mwepesi kumpata. Na asiyepata, ni kufunga siku tatu katika Hijja na siku saba mtakaporudi; hizo ni siku kumi kamili. Hayo ni kwa yule ambaye watu wake hawako karibu na Msikiti Mtakatifu. Na mcheni Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

﴿ الْحَجُّ أَشْهُرٌ مَّعْلُومَاتٌ فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي الْحَجِّ وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ وَتَزَوَّدُوا فَإِنَّ خَيْرَ الزَّادِ التَّقْوَىٰ وَاتَّقُونِ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ﴾

197.Hijja ni miezi maalumu. Na anayejilazimisha kufanya Hijja katika miezi hiyo, basi hakuna kuchafua wala ufuska wala mabishano katika Hijja. Na heri yoyote mnayoifanya Mwenyezi Mungu anaijua. Na chukueni masurufu, na hakika masurufu bora ni takua; na nicheni Mimi, enyi wenye akili.

﴿ لَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَبْتَغُوا فَضْلًا مِّن رَّبِّكُمْ فَإِذَا أَفَضْتُم مِّنْ عَرَفَاتٍ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ عِندَ الْمَشْعَرِ الْحَرَامِ وَاذْكُرُوهُ كَمَا هَدَاكُمْ وَإِن كُنتُم مِّن قَبْلِهِ لَمِنَ الضَّالِّينَ ﴾

198.Si vibaya kwenu kutafuta riziki ya Mola wenu. Na mtakapomiminika kutoka Arafa, mtajeni Mwenyezi Mungu katika Mash'aril- Haram: Na mkumbukeni kama alivyowaongoza, ijapokuwa zamani mlikuwa miongoni mwa waliopotea.

﴿ ثُمَّ أَفِيضُوا مِنْ حَيْثُ أَفَاضَ النَّاسُ وَاسْتَغْفِرُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴾

199.Kisha miminikeni kutoka mahali wanapomiminika watu (wote), na mumwombe Mwenyezi Mungu maghufira; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kughufiria Mwenye kurehemu.

﴿ فَإِذَا قَضَيْتُم مَّنَاسِكَكُمْ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَذِكْرِكُمْ آبَاءَكُمْ أَوْ أَشَدَّ ذِكْرًا فَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا وَمَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ﴾

200.Na mmalizapo kuzitimiza ibada zenu, basi mtajeni Mwenyezi Mungu kama mlivyokuwa mkiwataja baba zenu; bali mtajeni zaidi. Na kuna baadhi ya watu wasemao: Mola wetu! Tupe duniani; nao katika Akhera, hawana lolote.

﴿ وَمِنْهُم مَّن يَقُولُ رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴾

201.Na miongoni mwao kuna asemaye; Mola wetu! Tupe mema duniani na (tupe) mema Akhera, na utulinde na adhabu ya Moto.

﴿ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ نَصِيبٌ مِّمَّا كَسَبُوا وَاللَّـهُ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴾

202.Hao ndio wenye fungu katika waliyoyachuma, na Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.

﴿ وَاذْكُرُوا اللَّـهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ فَمَن تَعَجَّلَ فِي يَوْمَيْنِ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ وَمَن تَأَخَّرَ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ لِمَنِ اتَّقَىٰ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّكُمْ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ﴾

203.Na mtajeni Mwenyezi Mungu katika siku zinazohisabiwa. Na mwenye kufanya haraka katika siku mbili, basi si dhambi juu yake; na mwenye kukawia pia si dhambi juu yake, kwa mwenye takua. Na mcheni Mwenyezi Mungu, na jueni kwamba nyinyi mtakusanywa Kwake.

TIMIZENI HIJJA NA UMRA

Aya 196 - 203

MAANA

Aya hizi zimeonyesha baadhi ya hukumu za Hijja, Mafaqihi wameweka vitabu maalumu vinavyohusu Hijja, nami nimetunga kitabu kwa jina Al- Hajj ala Madhahabil-Khamsa; kisha nikakiunganisha katika kitabu Al- Fiqh ala Madhahabil Khamsa wakati kiliporudiwa kuchapishwa kwa mara ya tatu. Vile vile nimeizungumza kwa urefu katika Juzuu ya pili ya kitabu Fiqh ul-Imam Jaffar Sadiq(a.s) Hijja imekuwa maarufu tangu zama za Nabii Ibrahim na Ismail(a.s) na iliendelea katika zama za ujahiliya; na Uislamu ukaithibitisha baada ya kuisafisha na mambo machafu, na kuongeza baadhi ya ibada.

Na timizeni Hijja na Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Maana ya Hijja kilugha, ni kukusudia, na kisharia ni ibada maalum katika mahali na wakati maalum. Umra kilugha ni ziara yoyote; na kisheria ni ziara katika Al-Kaaba kwa namna maalum, Hijja ni wajibu katika Quran, Hadith na Ijami. Bali wajibu wake umethubutu kwa dhahiri ya dini. Na mwenye kuikanusha sio Mwislamu, sawa sawa na aliyekanusha wajibu wa Saumu na Swala. Shia Imamiyya na Shafii wamesema Umra ni wajibu, Hanafi na Malik wamesema ni Sunna. Kusema kwake Mwenyezi Mungu Kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Yaani Hijini na fanyeni Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake na sio kwa makusudio ya kidunia. Kwani Waarabu walikuwa wakikusudia kuhiji kwa ajili ya kukutana, kujifaharisha, kutafuta mahitaji na kuhudhuria soko. Ndipo Mwenyezi Mungu akaamrisha Hijja iwe ni kwa makusudio yake Yeye kwa ibada safi yenye kutakasika na makusudio yoyote mengine.

Na kama mkizuiliwa, basi (chinjeni) wanyama walio wepesi kupatikana.

Yaani ikiwa mmeherimia Hijja, kisha mkazuilika kukamilisha ibada kwa njia yake ya kisheria kutokana na maradhi au adui na mengineyo, basi ni juu yenu kuchinja mnyama atakayepatikana kwa urahisi; kwa uchache awe ni mbuzi, wastani ni ng’ombe na wa juu zaidi ni ngamia.

Wala msinyoe vichwa vyenu mpaka wanyama hao wafike machinjioni mwao.

Msemo unaelekezwa kwa wale waliozuilika ambao hawakuweza kutimiza Hijja au Umra. Wao hawatakuwa wametoka katika ihram yao (miko ya Hijja) mpaka wajue kwamba mnyama amefika mahali pake pa kuchinjwa. Na mahali pa kuchinja ni Mina ikiwa ni Hijja; na kama ni Umra basi ni Makka. Hayo ni itakapokuwa kizuizi ni maradhi. Ama ikiwa kizuizi ni adui, basi mahali pa kuchinja ni pale mahali palipotokea kizuizi. Kwa sababu Mtume(s.a.w.w) alichinja mnyama katika Hudaybiya, alipozuiliwa na washirikina kuzuru nyumba ya Mwenyezi Mungu tukufu (Al Kaaba).

Na atakayekuwa mgonjwa katika nyinyi au ana adha kichwani mwake, basi atoe fidia kwa kufunga au sadaka au kuchinja mnyama.

Yaani ikiwa mwenye kuhirimia atanyoa kichwa chake kwa dharura, basi ni juu yake kutoa kafara, atakuwa na hiyari baina ya kufunga siku tatu, kuwalisha masikini sitini au kuchinja mnyama; kwa uchache awe ni mbuzi.

Na mtakapokuwa salama, basi mwenye kujistarehesha kwa kufanya Umra kisha akahiji, achinje mnyama aliyemwepesi kupatikana.

Yaani mtu asiyekuwa na kizuizi, akafanya Umra kisha akahiji baadae katika mwaka huo huo, basi ni juu yake kuchinja mnyama. Hii ndiyo aina ya Hijja inayojulikana kwa jina la Haj Tamattui (Hijja ya starehe) ambayo ni wajibu kwa wasiokuwa watu wa Makka.

Imeitwa Hijja ya starehe, kwa sababu mwenye kuhiji baada ya kumaliza amali za Umra anatoka kwenye miko ya Umra mpaka aje ahirimie Hijja.

Na asiyepata, ni kufunga siku tatu katika Hijja na siku saba mtakaporudi; hizo ni siku kumi kamili.

Imam Jaffar Sadiq(a.s) amesema;Mwenye kufanya Hajj Tamattu, asipopata mnyama atafunga siku tatu katika Hijja; siku ya saba, ya nane na ya tisa katika Dhul-Hijja (mfungu tatu) wala hakuna sharti la Iqama na siku saba atafunga atakaporudi kwa watu wake. Hizo ni siku kumi kamili za kutosheleza mnyama.

Hayo ni kwa yule ambaye watu wake hawako karibu na msikiti mtakatifu.

Mwenye Majmaul Bayan amesema kuwa hayo yaliyotangulia kutajwa katika Tamattui ya Umra kisha Hijja, sio kwa watu wa Makka na walio karibu yake. Isipokuwa ni kwa ambaye hayuko Makka, yule ambaye yuko mbali na Makka kwa zaidi ya maili kumi na mbili (12) kwa kila upande. Mafaqihi wa Kishia Imamiya wamesema Hajj Tamattui ni wajibu kwa walio mbali na Makka, wala haijuzu kwa aliyembali na Makka kuhiji Hijja Qiran na Ifrad, kwani hizo ni wajibu kwa watu wa Makka na wa kando kando yake; na wao haijuzu kwao kuhiji Hajj Tamattui. Kwa ufafanuzi zaidi angalia vitabu vya Fiqh.

Hijja ni miezi maalumu.

Nayo ni kuanzia Shawwal, Dhul-qaad na kumi la mwanzo la Dhul-Hijja. (mfunguo mosi, mfunguo pili na mfunguo tatu) Mwenye kuhirimia kabla yake Hijja yake haitaswihi na mwenye kuhirimia ndani ya miezi hiyo itaswihi na ataleta amali zilizobakia.

Na anayejilazimisha Hija katika miezi hiyo, basi hakuna kuchafua wala ufuska wala mabishano katika Hijja.

Makusudio ya uchafuzi hapa ni kujamii. Mtu akimjamii mkewe na huku amehirimia Hijja, basi Hijja yake imeharibika, sawa sawa na aliyejamii au kula huku akiwa amefunga. Kwa hiyo atakamilisha Hijja yake, kisha aje alipe mwaka ujao; kama ilivyo kwa mwenye kuiharibu Saumu. Makusudio ya ufuska, ni uongo na kutukana. Ama kuhusu kubishana riwaya za Ahlul Bait zinasema, hilo ni kusema mtu; Hapana wallahi au Kwa nini, wallahi n.k.

Si vibaya kwenu kutafuta riziki ya Mola wenu.

Kwa vile wakati wa ujahilia watu walikuwa wakifanya biashara na kuchuma siku za Hijja, kukadhaniwa kuwa ni haramu, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.), akaondoa tuhuma hii na akabainisha kwamba kuchuma hakupingani na ikhlasi katika amali za Hijja.

Na mtakapomiminika kutoka Arafa, mtajeni Mwenyezi Mungu katika Masharil Haram.

Arafa ni mahali maalum. Kumiminika kutoka Arafa ni kuondoka, Masharil-Haram ndipo pale panajulikana kama Muzdalifa na kutua hapo ni wajibu; kama ilivyo kwa Arafa.

Kisha miminikeni kutoka mahali wamiminikapo watu (wote). Inasemekana kuwa Maquraish walikuwa hawatui Arafa pamoja na watu wengine kwa kiburi tu, ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake kutua hapo na kutoka pamoja na watu ili abatilishe waliyokuwa wakiyafanya Maquraish.

Na mmalizapo kuzitimiza ibada zenu, basi mtajeni Mwenyezi Mungu zaidi.

Imepokuwa kutoka kwa Imam Baqir baba wa Imam Sadiq(a.s) kwamba watu walikuwa wanapomaliza Hijja wanakusanyika huko na kuwataja wazazi wao kwa fahari, ndipo Mwenyezi Mungu akawaamrisha kuliacha hilo na badala yake wamtaje Mwenyezi Mungu na jinsi alivyowaneemesha. Kwa sababu Yeye ndiye mwenye kuwaneemesha wao na mababa zao.

Na baadhi ya watu kuna asemaye: Mola wetu! Tupe duniani; nao katika akhera hawana lolote. Na miongoni mwao kuna asemaye: Mola wetu! Tupe mema duniani na (tupe) mema akhera, na utulinde na adhabu ya moto. Hao ndio wenye fungu katika waliyoyachuma, na Mwenyezi Mungu ni mwepesi wa kuhisabu.

Watu katika Hijja zao wako aina mbili. Aina ya kwanza ni yule asiyetaka lolote isipokuwa starehe ya dunia na hana makusudio yoyote isipokuwa dunia tu, na anapomwabudu Mwenyezi Mungu humwabudu kwa ajili ya dunia. Hawa ndio wenye kunyimwa neema ya Akhera. Ama aina ya pili ni yule anayetaka heri ya dunia na akhera na anafanya amali kwa ajili ya dunia yake na akhera yake. Huyu ndiye mwenye radhi mbele ya Mwenyezi Mungu kesho kwa kulipwa amali yake njema. Mwenye Tafsiri Rawhul Bayan amenukuu kutoka kwa Imam Ali bin Abi Twalib(a.s) kwamba wema katika dunia ni mwanamke mwema na katika akhera ni Hurulain. Ama adhabu ya moto makusudio yake ni mwanamke muovu.

Iwe ni sahih Hadith hiyo au la, lakini mimi najua kuna watu wanaohisi kwamba lau wao wangekuwa katika Jahanam kisha wakahiyarishwa kutoka katika Jahanam na warudi kwa wake zao waliokuwa nao duniani au wabaki Jahannam, basi wangelichagua kubaki katika Jahannam kuliko kuishi tena na wake zao hao.

Na mtajeni Mwenyezi Mungu katika siku zinazohisabiwa.

Makusudio yake ni siku tatu za Tashriq nazo ni; Tarehe kumi na moja, kumi na mbili na kumi na tatu katika mwezi wa Dhul-Hijja (mfungo tatu). Si wajibu kwa mwenye kuhiji kulala Mina usiku wa kumi na tatu, lakini kwa sharti ya kuwa atoke Mina siku ya kumi na mbili baada ya kupinduka jua na kabla ya Maghrib na awe hakuvunja mwiko wa kuwinda au kujamii. Kwa hali hiyo ndipo tunapopata tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na mwenye kufanya haraka katika siku mbili, basi si dhambi juu yake; na mwenye kukawia pia si dhambi juu yake kwa mwenye takua.

Yaani mwenye kuacha kuwinda na wanawake katika ihram yake. Ikiwa amevunja mwiko wa kulala na mke au kuwinda au alichelewa na jua siku ya kumi na mbili akiwa yuko Mina, basi itakuwa wajibu kwake kulala usiku wa kumi na tatu na kutupia mawe vikuta vitatu (shetani).

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿ وَمِنَ النَّاسِ مَن يُعْجِبُكَ قَوْلُهُ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَيُشْهِدُ اللَّـهَ عَلَىٰ مَا فِي قَلْبِهِ وَهُوَ أَلَدُّ الْخِصَامِ ﴾

204.Na katika watu kuna ambaye kauli yake inakupendeza katika maisha ya duniani, naye humshuhudiza Mwenyezi Mungu kwa yaliyo moyoni mwake na hali ni hasimu mkubwa kabisa.

﴿ وَإِذَا تَوَلَّىٰ سَعَىٰ فِي الْأَرْضِ لِيُفْسِدَ فِيهَا وَيُهْلِكَ الْحَرْثَ وَالنَّسْلَ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ الْفَسَادَ﴾

205.Na anapotawala hufanya bidii katika ardhi kufanya ufisadi, na huangamiza mimea na viumbe, na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi.

﴿ وَإِذَا قِيلَ لَهُ اتَّقِ اللَّـهَ أَخَذَتْهُ الْعِزَّةُ بِالْإِثْمِ فَحَسْبُهُ جَهَنَّمُ وَلَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴾

206.Na anapoambiwa. Mche Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kufanya dhambi. Basi Jahannam inamtosha, napo ni makao mabaya mno

﴿ وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْرِي نَفْسَهُ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ وَاللَّـهُ رَءُوفٌ بِالْعِبَادِ ﴾

207.Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni mpole kwa waja.

KAULI ZAO ZINAKUPENDEZA

Aya 204 – 207

MAANA

Baadhi ya wafasiri wapya wamejaza kurasa kwa maneno matamu katika kufasiri Aya hizi, lakini hawakuzidisha chochote zaidi ya kuwagawanya watu kwenye wema na uovu. Kwa dhahiri haya yanajulikana na wote, hayahitaji ubainifu wowote, sikwambii tafsiri ndefu tena. Unaweza kuuliza; Ikiwa kugawanyika watu kunajulikana na wote, basi kubainisha kunakuwa ni maelezo ambayo tayari yameshaelezwa na kufafanua lililofafanuliwa na yapasa kuyachukulia maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) vizuri? Jibu: Inawezekana kuwa makusudio ni kuongoza na kuelekeza kwamba mwenye akili anatakikana kutohadaliwa kwa mambo ya nje wala asimwamini mwenye kutegeneza maneno matamu. Kwa sababu wafisadi ni mabingwa wa kazi hiyo na kazi ya ria. Kwa hivyo ni juu yetu kutomtegemea yeyote isipokuwa baada ya kufanya majaribio na kupatikana dalili ya ukweli wake na usafi wake.

Hiyo ndiyo asili ya ujumla inayoenea katika hukumu nyingi za dini na za kidunia; kama kuchagua Hakimu, Kadhi, Naibu, Kadhi, Mufti na kila anayesimamia masilahi ya Umma. Ajabu ya maajabu ni kutakiwa shahada ya kielimu tu kwa mwenye kujitokeza kwa kazi muhimu ya mji au nchi na inayogusa maisha ya watu. Lakini haulizwi uaminifu wake na tabia yake, pamoja na kuwa hayo ndio msingi. Wengi wenye shahada wanazitumia kuwa ni zana za kuibia.

Na katika watu kuna ambaye kauli yake inakupendeza hapa duniani, naye humshuhudia Mwenyezi Mungu kwa yaliyomo moyoni mwake, na hali ni hasimu mkubwa kabisa.

Yaani wanadhihihirisha mapenzi na heri na hali wao ndio maadui zaidi wa heri na watu wa heri.

Na anapotawala hufanya bidii katika ardhi kufanya ufisadi.

Wamehitaliafiana wafasiri kuhusu neno Tawalla. Je makusudio ni kuondoka na maana yake kuwa ni, anapoondoka kwa yule aliyemdanganya, huhangaika katika ardhi kwa ufisadi. Au kwamba makusudio ni kutawala na usultani, na maana yawe, na atakapokuwa mtawala atafanya wanayoyafanya watawala waovu ya kuangamiza mimea na viumbe? Mwenye Tafsir Al manar amenakili kutoka kwa Ustadha wake Sheikh Muhammad Abduh kwamba ameyapa nguvu maana ya utawala kwa kuunganisha na kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

"Na anapoambiwa mche Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kufanya dhambi."

Kwa maana ya kuwa mtawala mkaidi anakuwa na kiburi kuongozwa kwenye maslahi au kupewa tahadhari ya mambo ya ufisadi, yeye hujiona yuko juu ya haki; kama vile alivyo juu ya watu wake anaowatawala, basi itawezekanaje kwa mtu kumwambia amwogope Mwenyezi Mungu.

Na huangamiza mimea na viumbe.

Mimea ni kilimo na viumbe ni wanyama. Makusudio ni maslahi yote ya kiuchumi katika kilimo, viwanda na ufugaji, mali ghafi, na mengineyo yanayohusika na uhai wa watu na maisha yao. Mwenyezi Mungu amehusisha kutaja kilimo na ufugaji kwa vile viwanda wakati huo havikuwa na umuhimu wowote kama ilivyo sasa. Uharamu wa mambo hayo kwa mtazamo wa Uislamu ni sawa na uharamu wa kumwaga damu; na mwenye kukusudia ubaya katika vitu hivyo, ndio amekusudia ubaya wa utu hasa; hata kama vitu hivyo ni milki ya adui anayepiga vita Waislamu. Mtume(s.a.w.w) amekataza kukata miti, kuharibu mimea na majengo na kutia sumu miji ya washirikina siku za vita, n.k. Lau tunailinganisha sharia ya Kiislamu na mambo yanayofanywa leo na dola za kikoloni na vita vyao vya silaha za kemikali kwenye mimea, watu na wanyama, na kuitia sumu anga kwa mabomu ya Atomic na kuyatupa kwa wanawake na watoto, lau hayo yote tunayaunganisha na Uislamu, basi tutajua huruma, uadilifu na utu wa Uislamu na unyama wa dola za Magharibi na jinsi zilivyopetuka mipaka katika dhulma na unyang'anyi.

Na Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hapendi ufisadi.

Hakuna uharibifu mkubwa zaidi kuliko kuzusha vita na kutumia silaha zenye kubomoa ili kuwatawala watu na kuwanyang'anya chakula na matunda ya jasho lao.

Na anapoambiwa mche Mwenyezi Mungu hupandwa na mori wa kufanya dhambi.

Mtu mwema wenye ikhlasi anakubali masahihisho na nasaha, bali huzitafuta na kuzikaribisha, kwa sababu yeye hana lengo jengine zaidi ya haki, wala hatafuti sifa; kwa sababu amali yake ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) sio umashuhuri.

Imam Amirul Muminin(a.s) anasema katika maneno anayowasifu wanaomcha Mwenyezi Mungu:"Hawaridhii na amali zao chache wala hawakioni kingi kilicho kingi; wao wanajituhumu na wao ni wenye kunyenyekea katika amali zao."

Katika hotuba yake siku za ukhalifa wake alisema: "Mtu hata kama ana cheo kikubwa katika haki na fadhila kubwa katika dini hawezi kuwa hahitajii kusaidiwa katika aliyobebeshwa na Mungu katika haki zake; wala si mwenye kutaka kujitukuza; wala mtu hata kama nafsi zinamfanya mdogo na kudharauliwa na macho sio kuwa hawezi kusaidia au kusaidiwa... Wala msinidhanie kuwa mimi ni mzito katika haki nitakayoambiwa, kwani mwenye kuifanya nzito haki atakayoambiwa au uadilifu atakaoonyeshwa, basi kwake kuitumia haki na uadilifu ni kuzito zaidi."

Hivyo ndivyo anavyotakikana mwanachuoni mwenye ikhlasi ya kweli. Ama mnafiki mwenye hiana, haki inakuwa nzito juu yake kwa sababu itamfedhehesha; na hununua sifa kwa thamani kubwa ili azibe upungufu wake na uovu wake.

Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu.

Yaani baadhi ya waumini wanaikabili Jihadi na wanapenda mauti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. sawa na wale wengine wanaopenda uhai. Hawana lengo jengine isipokuwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na thawabu Zake. Razi katika kutafsiri Aya hii anasema kuhusu sababu za kushuka kwake kuwa kuna riwaya tatu; Mojawapo ni kwamba Aya hii imeshuka kwa sababu ya Ali bin Abi Twalib(a.s) alipolala kwenye kitanda cha Mtume wakati wa Hijra, alisimama Jibril kichwani mwake, Mikail miguuni mwake na Jibril: Pongezi! Pongezi! ewe Ali akisema: Mwenyezi Mungu anajionea fahari kwako, mbele ya Malalika( [7] ).

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً وَلَا تَتَّبِعُوا خُطُوَاتِ الشَّيْطَانِ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ﴾

208.Enyi mlioamini! Ingieni katika usalama nyote, wala msifuate nyayo za Shetani. Kwa hakika yeye kwenu ni adui wa wazi.

﴿ فَإِن زَلَلْتُم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْكُمُ الْبَيِّنَاتُ فَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾

209.Na kama mkiteleza baada ya kuwafikia ubainifu, basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

﴿ هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ وَقُضِيَ الْأَمْرُ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴾

210.Hawangoji ila kuwafikia (adhabu ya) Mwenyezi Mungu katika vivuli vya mawingu na Malaika, na liishe jambo; na mambo yote hurudishwa kwa Mwenyezi Mungu.

INGIENI KATIKA USALAMA NYOTE

Aya 208 - 210

MAANA

Enyi Mlioamini! Ingieni katika usalama nyote.

Imesemekana kuwa makusudio ya neno Silmi hapa ni Uislamu, na kwamba msemo unawaelekea wanafiki ambao wameificha kufuru na kudhihirisha Uislamu. Na imesemekana kuwa msemo unawaelekea wenye kumwamini Mwenyezi Mungu katika Ahlul Kitab ambao hawakusilimu. Na ikasemekana kuwa unawaelekea Waislamu wote kwa hivyo maana yake yanakuwa ni kumtii Mwenyezi Mungu na kumnyenyekea katika hukumu Zake zote sio baadhi. Na pia imesemekana maana yake ni suluhu kwa maana kuwa ingieni katika suluhu nyote. Tuonavyo sisi ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemwamrisha mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu, kwa imani sahihi kuingia katika lile ambalo lina salama yake ya dunia na akhera. Na njia ya usalama inajulikana na wote, nayo ni kusaidiana, kuungana, na kuacha vita na uhasama. Vile vile kuyashinda matamanio na kuwa na ikhlasi katika kauli na vitendo.

Makusudio ya maneno hayo yanatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:Wala msifuate nyayo za shetani. Kwa hakika yeye kwenu ni adui wa wazi, Aliyoileta mara tu, baada ya kusema.Ingieni katika usalama nyote. Hapo Mwenyezi Mungu amezingatia kuwa nyayo za shetani kinyume chake ni usalama; na amemweka mtu mbele ya mambo mawili tu, hakuna la tatu; Ama kuingia katika usalama au kufuata nyayo za shetani ambazo ndio dhati ya uovu, ugomvi, shari na ufisadi.

Na kama mkiteleza baada ya kuwafikia ubainifu, basi jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye hekima.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuamrisha kuingia katika usalama na kukataza kufuatwa nyayo za shetani, amemhadharisha yule atakayehalifu amri yake na makatazo yake na akatishia kwa kusema: "Basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye hekima." Mwenye nguvu, hashindwi katika amri Yake wala hakimzuwii chochote kwa alilokusudia kulifanya. Mwenye hekima, humlipa mema mtiifu na humwadhibu mwasi. Razi anasema: "Huo ndio ukomo wa kiaga kwa sababu ni kuhofisha bila ya kutaja adhabu. Huenda mzazi akamwambia mtoto wake: "Ukiniasi basi wewe wanijua na wajua uwezo wangu kwako", basi maneno hayo yanakuwa ni makemeo ya ufasaha zaidi kuliko kutaja kipigo na mengineyo.

Hawangoji ila kuwafikia (adhabu ya) Mwenyezi Mungu katika vivuli vya mawingu na Malaika. Maana kwa ujumla ni kwamba wale wenye kukadhibisha na wakaasi watajiwa na adhabu kwa ghafla wala hawataokoka. Aya iko katika mwelekeo wa Aya inayosema:

﴿ فَهَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا السَّاعَةَ أَن تَأْتِيَهُم بَغْتَةً ﴾

"Na hawangoji ila saa ya Kiyama kiwajie kwa ghafla...?" (47:18).

Na lishe jambo; na mambo yote hurudishwa kwa Mwenyezi Mungu. Mauti ambayo hapana budi nayo, yakija na Kiyama kikija, kila kitu kitakuwa kimekwisha na hapatabakia mbele ya wenye makosa isipokuwa hisabu na mateso.

SIRI NA MATUKIO YA GHAFLA

Hakuna yeyote ajuaye yatakayomtokea mbele na siri ya wakati, heri au shari. Hawezi kuyajua hayo vyovyote atakavyokuwa na elimu au imani:

"Na nafsi yoyote haijui itachuma nini kesho." (31:34)

Mara nyingi mtu hujiwa na heri kwa ghafla wakati yeye anatazamia kupata shari; na hujiwa ghafla na shari wakati anapotazamia heri. Hakuna kitu kinachotia uchungu kama hicho cha kupata shari wakati wa kutazamia heri; kama vile ambavyo hakuna kitu kitamu kama kupata heri wakati wa kutazamia shari. Mwenye akili hawezi kughurika na alivyo navyo, bali hufikiria mzunguko wa zama; kama vile ambavyo hakati tamaa na lolote linalompata; kwani dunia inageuka milele; ndio maana ikasemwa; "Kudumu hali ni muhali na faraja inakuja kutokana na dhiki." Imam Ali(a.s) anasema:"Baada ya dhiki ni faraja. Anaendelea kusema Imam:"Hakika Musa bin Imran alitoka kuwatafutia watu wake moto akasemeshwa na Mwenyezi Mungu na akarudi akiwa Mtume." Mwenyezi Mungu anasema:

﴿ إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴾

"...Hawakati tamaa ya rehema ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri." (12:87).

Na amesema tena:

﴿ فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴾

... Hawajiaminishi na mipango ya Mwenyezi Mungu ila watu wenye hasara." (7:99).

Imeelezwa katika vitabu vya Historia na Sera kwamba Ibn Ziyat alikuwa waziri na mtu wa kutegemewa na Mu'utasim, naye alikuwa ni katika mataghuti wa hali ya juu na dhalimu mkubwa. Alitengeneza tanuri la chuma alilolijaza misumari yenye ncha pambizoni mwake. Anapomkasirikia mtu humtupa ndani, kila anavyojitingisha ndivyo misumari inavyomwingia mwilini mwake. Mutawakkil alipotawala alimshika Ibn Ziyat na akamfunga kwa chuma mikononi mwake na miguuni mwake kisha akamtupa katika tanuri hilo, na baadaye akafa. Kabla ya kufa alisikika akiimba shairi hili: Sifazake tulia, hebu nenda pole pole, Kigeugeu dunia, huenda nyuma na mbele.

﴿ سَلْ بَنِي إِسْرَائِيلَ كَمْ آتَيْنَاهُم مِّنْ آيَةٍ بَيِّنَةٍ وَمَن يُبَدِّلْ نِعْمَةَ اللَّـهِ مِن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُ فَإِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ﴾

211.Waulize wana wa Israil, ishara ngapi zilizo wazi tulizowapa? Na anayezibadilisha neema za Mwenyezi Mungu baada ya kumfikia, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.

﴿ زُيِّنَ لِلَّذِينَ كَفَرُوا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا وَيَسْخَرُونَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ اتَّقَوْا فَوْقَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَاللَّـهُ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴾

212.Wamepambiwa makafiri maisha ya duniani, na wanawafanyia maskhara wale walioamini. Na wale wenye takua watakuwa juu yao Siku ya Kiyama. Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hisabu

WAULIZE WANAWA ISRAIL

Aya 211 – 212

MAANA

Waulize wana wa Israil, ishara ngapi zilizo wazi tulizowapa?

Makusudio ya waulize hapa sio swali hasa la kihakika, kwa sababu Mtume(s.a.w.w) anajua hali zao, wala makusudio sio kuelezea hali waliyokuwa nayo; kama ilivyo katika Aya ya 49 na inayofuatia. Isipokuwa makusudio hasa ni kuwa Waislamu wazingatie na wapate funzo na hali ya Waisrail. Njia ya kupata funzo ni kuwa Waisrail walijiwa na Mtume Musa(a.s) kwa miujiza na hoja ambayo ni mkono kuwa mweupe, fimbo kugeuka nyoka na kupasuka bahari. Vile vile kufunikwa na wingu, kuteremshiwa Manna na Salwa na jabali kutoka maji. Pamoja na hayo yote waliasi na kukhalifu, ndipo Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa madhila na utwevu katika dunia na adhabu iumizayo katika Akhera. Na Waislamu nao wamejiwa na Muhammad(s.a.w.w) kwa miujiza na hoja zinazofahamisha ukweli wa Utume wake na kuswihi sharia yake; naye akawafikilizia habari kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwa waaingie katika Uislamu wote, kwani humo watapata heri na utengeneo wao; kama wakiasi kama walivyofanya Waisrail, basi yatawapata yaliyowapata Waisrail.

Na anayezibadilisha neema za Mwenyezi Mungu baada ya kumfikia, basi hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

Makusudio ya neema hapa ni dalili za haki, kwani hizo ni katika neema kubwa. Kwa sababu ndani yake mna uongofu na kuokoka na kuhiliki na upotevu. Makusudio ya kuzibadilisha ni kuziasi na kuziharibu. Kwa hiyo kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.)Na anayezibadilisha neema za Mwenyezi Mungu baada ya kumfikia ni sawa na kauli yake:

﴿ فَإِن زَلَلْتُم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْكُمُ الْبَيِّنَاتُ﴾

"Na kama mkiteleza baada ya kuwafikia ubainifu..." (2:209).

Vile vile kusema kwake:

﴿فَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾

"Basi hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu" (2:209) ni sawa na kusema Kwamba:Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye hekima."

Maana ni moja na lengo ni moja.

HAPANA IMANI BILA TAKUA (UCHA MUNGU)

Wamepambiwa makafiri maisha ya duniani.

Hapana tofauti kati ya mwenye kukanusha kuwapo Mwenyezi Mungu na yule mwenye kuamini kinadharia tu, lakini matendo yakawa ni tofauti. Hapana tofauti kati ya wawili hao. Kwa sababu kila mmoja ameathiriwa na dunia na vipambo vyake, ameathirika na kitu cha sasa hivi kuliko cha muda ujao; heri na manufaa ameyapima kwa kiwango cha manufaa yake, wala hakupima na mambo aliyoharamisha Mwenyezi Mungu wala na msimamo wa kibinadamu. Mimi kila ninavyozidi kuzama katika tafsiri ya Qur'an na kuangalia kwa undani Aya zake, basi huwa na yakini zaidi kwamba imani bila ya ucha Mungu haina maana yoyote; na kwamba kila anayeiangalia dunia kuwa ndio makusudio yake yote, basi atakuwa ameiweka mbali sharia ya haki na dini, atake asitake.

Imekuja Hadith Mutawatir kutoka kwa Mtume Mtukufu akisema: "Dunia na akhera zina madhara" yaani zinadhuriana kuhujumu moja yao nikuiacha nyingine( [8] ).

Imam Ali(a.s) anasema: "Hakika dunia na Akhera ni maadui wawili wanaotofautiana, na ni njia mbili tofauti. Mwenye kuipenda dunia ataichukia akhera na kuwa adui yake; zote mbili ni kama Mashariki na Magharibi, mwenye kutembea kati yao huwa mbali na nyingine kila anapokaribia moja wapo.

" Na wanawafanyia maskhara wale walioamini.

Ni kawaida wale wanaozichezea Hoja za Mwenyezi Mungu na hukumu zake wakihalalisha damu na mali ya haramu kuwadharau na kuwachezea wale wanaojilinda na maharamisho na kuvumilia tabu na mashaka kwa ajili ya kumridhisha Mungu.

Na wale wenye takua watakuwa juu yao siku ya Kiyama.

Amesema wenye takua wala hakusema wale walioamini, kwa sababu imani bila takua si lolote; kama tulivyobainisha. Maana yako wazi ni kuwa makafiri wakiwadharau waumini hivi sasa, basi mambo yatabadilika kesho. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قَالَ الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ إِنَّ الْخِزْيَ الْيَوْمَ وَالسُّوءَ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴾

"...Watasema walio pewa ilimu: Hakika hizaya na ubaya leo itawafika makafiri." (16:27).

﴿فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ﴾

"Basi leo wale ambao wameamini wanawacheka makafiri." (83:34)

Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hisabu.

Riziki ni mbili ya dunia na riziki ya Akhera. Riziki ya dunia inajulikana na riziki ya Akhera, ni neema isiyokatika na isiyokuwa na chembe ya huzuni au hofu. hataipata yeyote isipokuwa kwa imani na amali njema: Anasema Mwenyezi Mungu:

﴿وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

"Na wale walioamini na kutenda mema, hao ndio watu wa Peponi, humo watakaa milele." (2:82).

Kila mtu anaweza kupata riziki duniani, awe ni kafiri au Mumin, mwema au mwovu, na anayehangaika au asiyehan-gaika; kama vile urithi, zawadi, wasiya, n.k. Vile vile inaweza kupatikana kwa njia ya halali, au haramu, kama vile kunyang'anya, kughushi na utapeli. Mwenye Tafsir Al-Manar amenakili kutoka kwa mwalimu wake Sheikh Muhammad Abduh kwamba, amesema wakati wa kutafsiri Aya hii, kwamba riziki bila ya kuhangaika inaweza ikapatikana kwa baadhi ya watu. Ama kwa Umma ni muhali kujitosheleza isipoku-wa kwa kuhangaika na kufanya kazi. Huo ni ukweli ulio wazi kabisa.


10

11

12

13

14

15

16