MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 18%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 62414 / Pakua: 6773
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

5

6

7

8

9

MAREJEO

1- Nilipeleka jawabu hii pamoja na kopi ya kitabu changu kwa wahusika.

2- Yaani katika jawabu hii nilipowapelekea.

3- Tamaza Tah-dhibu Tah-dhibu ya Imam Ibn Hajar Al Asqalani jalada la 3 uk 684-685 chapa ya Beirut. Tazama mahala pa herufi mimu] piya Taqribu Tah-dhibu jalada la 2 ukurasa 86.

4- Tazama Al Jarhu Wataadil cha Imam Ibn Abi Hatim jalada la 8 uk.68 chapa ya India.

5- Mudallis si maana yake mwongo; bali ni mwenye kughushi.

6- Sura 17, Aya 36.

7- Sura 7, Aya 33.

8- Sura 6, Aya 144.

9- Isipokuwa mpokezi wa kwanza ndio wasimulizi wametafautiana.

10 Tazama Tarjama ya Muhammad bin Abi Harmala katika Tahidhi Al-Tahdhib j. 10, uk. 96, tarjama na. 149.

11- J. 9, uk. 373, tarjama (biography) na. 690.

12- Al-Sunan Hadithi na.

13- Si Muhammad bin Kurayb.

14- Pia si Muhammad bin Kurayb, bali ni Kurayb, wala hakuna sanad yoyote ya riwaya hii ambayo ndani yake kuna Muhammad bin Kurayb.

15- Al-Sunan Hadithi na. 2329.

16 - Al-Sahih j. 2, uk. 924 Hadithi na. 1916.

17 - Al-Kubra j. 3, uk. 97, Hadithi na. 2432.

18 - Al-Kubra j. 6, uk. 294 Hadithi na. 8297.

19 - Tazama J. 2 uk 490.

20 - Sunna Za Mtume(s.a.w.w) yaani Hadithi zake zilizothibiti.

21- Qur-aan 4:59.

22- Al-Nawawi Taqribu Al-Nawawi kilicho pamoja na Tadribu Al-Rawi uk. 159-160.

23- Kitabu Ushahidi Uliowekwa Wazi nillikiambatanisha na jawabu kuwafikishia wahusika.

24 - Nassor Bachoo Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi uk. 2.

25 - Nassor Bachoo Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi uk. 162.

28 - Juma Mazrui Ushahidi Uliowekwa Wazi chapa ya kwanza 85, chapa ya pili uk. 97.

29 - Juma Mazrui Ushahidi Uliowekwa Wazi chapa ya kwanza 85, chapa ya pili uk. 97.

30 - J. 4, uk. 450, katika maelezo yake juu ya Hadithi na. 77/2599.

31 - Tazama Al-shaukaniy "AL-NAYLU" j. 3, uk. 212, katika maelezo juu ya Hadithi na. 1/1155 na 2/1156, katika "Babu Ikhtiyar Al-qasri Wa Jawazi Al-itmam."

32- Ibn Hisham Qatru Al-Nada uk. 357.

33 - Ibn Hisham Qatru Al-Nada uk. 361.

34 - Lakini Al-Hafidh Ibn Hajar kawakosoa waliosema kwa Hadithi hii imesimuliwa kutoka kwa Abu Sa'id Al-Khudri. Anasema Ibn Hajar: "Al-Ghazali na Al-Fakhr Al-Razi wakifatiwa na Al-Baydhawi wamekinasibisha kisa hiki kwa Abu Sa'id Al-Khudri nalo ni kosa, bali yeye (mwenye kisa hiki) ni Abu Sa'id Al-Mu'alla". Tazama Fat-hu Al-Bari j. 9, uk. 5076, katika sherehe ya Hadithi na. 4474. Ninasema: lakini maelezo hayo ya Ibn Hajar ya kuwakosoa Al-Ghazali, Al-Razi na Al-Baydhawi, bado ni maelezo ya kufirikiwa kwani kisa hiki kimesimuliwa pia na Muslim Hadithi na. 2201, na Abu Dawud Hadithi na. 3415 na wengine kutoka kwa Abu Sa'id Al-Khudri. Kwa hivyo, Al-Ghazali na wenziwe hawakukosea isipokuwa ikiwa Ibn Hajar anadai kuwa sanad hizo ni dhaifu na ya Al-Bukhari yenye kusema kuwa muhusika alikuwa ni Abu Sa'id Al-Mu'allah ndio sanad sahihi.

35 - Kati ya watu wa hilo kabila.

36 - Abu 'Ubaid Fadhailu Al-Qur-an uk. 224.

37 - Al-Bukhari Al-Sahih Haadithi na. 5006 na Hadithi na. 5736

38 - Al-Bukhari Al-Sahih Hadithi na. 5737.

39 - Nassor Bachoo Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi uk. 152.

40 - Sura ya 36 Aya 39.

41 - Sura ya 10 Aya ya 5.

42- Al-Tukhi Ahkamu Al-Hakim j. 1, uk. 55. Al-qurtubiy "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Al-zamakhshariy "AL-KASHAF" j. 4, uk. 19. Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10.

43 - Al-tukhiy "AHKAMU AL-HAKIM" j.1, uk. 55. Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10. Hizi ndizo buruji mashuhuri kwa wataalamu wa falaki hususan wa Kiarabu. Ama buruji inayoitwa Ophiuchus au kwa Kiarabu ?????? Al-hawiyya si mashuhuri kwao, na kwa hivyo utaona si aghlabu kuitaja: mara nyingi hutaja hizi kumi na mbili tu. Anasema Al-tukhiy Al-falakiy: "Jua kwamba katika anga kuna buruji - yaani nyota nyingi (ambazo) zinajengeka kutokana na hizo buruji kumi na mbili." Tazama "AHKAMU AL-HAKIM" j. 1, uk. 17.

44- Tazama majina hayo ya buruji katika Al-tukhiy "AHKAMU AL-HAKIM" j.1, uk. 158. Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10.

45 - Al-tukhiy "AHKAMU AL-HAKIM" j. 1, uk. 55. Al-qurtubiy "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10.

46 - Al-tukhiy "AHKAMU AL-HAKIM" j. 1, uk. 55. Al-qurtubiy "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10.

47 - Tazama majina ya vituo hivyo katika: Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10. Al-qurtubiy "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Al-zamakhshariy "AL-KASHAF" j. 4, uk. 19, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Al-tukhiy "AHKAMU AL-HAKIM" j. 1, uk. 55. Hata hivyo, majina ya manazili - kama tulivyotangulia kodokeza - si jambo ambalo wataalamu wameafikiana. Na kwa hivyo, utakuta huyu anayaita manazili fulani jina kadha, na mwengine anayaita manazili hayo hayo jina jengine. Kwa mfano, manazili ya Shartan wengine wanayaita Nat-hu. Tazama Al-tukhiy "AHKAMU AL-HAKIM" j. 1, uk. 56. Wengine hutaja Manazil Zabra kama ilivyo katika Al-zamakhshariy "AL-KASHAF" j. 4, uk. 19; wengine hawataji jina hilo kamwe, na badala yake hutaja jina la Al-kharatan kama ilivyo katika tafsiri ya Al-qurtubiy "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Lakini yote haya si muhimu: kilicho muhimu ni uhakika wa kitu: si jina. Lau mtu atayaita maji ulevi basi hayaharamiki; na lau atauita ulevi maji, basi hauhalalilki; kwani mazingatio yako katika uhakika wa kitu si katika jina lake.

48 - Wako wanaojiuliza: je kuna uhusiano gani baina ya mambo haya na Uislam? Sasa cha kufahamu ni kuwa sisi tunazungumzia uhakika (facts): hatuzungumzii dhana zisizokuwepo (illusion au (Nyota zipo tunaziona, na Allah katwambia kama zipo. Anasema Allah:"Na nyota zimetiishwa kwa amri yake." Sura 16 Aya 14. Na manazil yapo. Anasema Allah: "Na Mwezi tumeupimia manazil (vituo). Na buruji (constellations yaani mikusanyiko ya nyota) zipo. Anasema Allah: (Naapa kwa anga yenye buruji (mikusanyiko ya nyota). Al-allama Sheikh Al-farisy na Sheikh Ali bin Muhsin Al-barwaniy wameifasiri Aya hio hivi: "Naapa kwa mbingu yenye buruji." Lakini - ninavyoona mimi - ni bora kufasiri "Naapa kwa anga yenye buruji" kwani nyota ziko katika anga: si katika mbingu. Na neno al-samaa linafasirika kwa namna nyingi, moja ya hizo ni anga. Na kwa hivyo utaona kwamba Sheikh Al-farisy mwenyewe katika maelezo yake juu ya Aya ya 22 ya Sura ya 2, anasema: "Na samaa ni kila kilicho juu yako." Lakini labda neno "Mbingu" katika Kiswahili pia lina maana ya anga. Ikiwa ni hivyo, basi tafsiri ya Mashekhe wawili itakuwa haina mushkeli. Sasa tukirudi katika mas-ala ya falaki, nyota, manazil na buruji, ni kuwa kilichoharamishwa katika mambo haya ni kuamini kuwa mambo haya yanadhuru au yanafaa. Kuamini hivi ni shirki: ama kusoma myenendo ya sayari na nyota kwa ajili ya kujua hisabu na mengineo, haya sio yaliokatazwa kama Maulamaa wanavyosema. Ama yale majina walioyapa manazil na buruji hizo, sisi hayatudhuru kitu: cha muhimu kwetu ni kuwa uhakika wa kile kitu chenyewe kipo, na jina unaweza kuita unavyoona wewe.

49-. Al-qurtubiy "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36.

50 - J. 1, uk 55.

51- Uk. 57. Kumbuka kwamba maneno haya hapa mimi ninanukuu kwa ajili ya kutoa fikra mbali mbali za wataalamu tu: sisemi kuwa ni sahihi au ni makosa: nayanukuu kwa sababu yakiwa sahihi au si sahihi, basi hayaathiri kitu katika utafiti wetu huu. Lakini wasemaji hawa ni wenye kuaminika sana katika uwanja huu wafalaki kwa kadiri ninavyofahamu.

52 - Anasema Al-zamakhshariy katika "AL-KASHAF" j. 4, uk. 19, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36: "Unakaa mwezi katika kila moja ya hayo (manazili 28) kwa (muda wa) siku moja." Anasema Al-baghawiy katika "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10: "Basi unakaa mwezi katika kila moja ya hayo (manazili 28) kwa (muda wa) siku moja." Anasema Al-qurtubiy katika "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36: "Unakaa mwezi kila siku moja katika moja ya hayo (manazili 28)." Anasema Al-sabuni katika "SAFWAT AL-TAFASIR" j. 3, uk. 12: "Nayo ni manazili ishirini na nane, unakaa (mwezi) kila siku moja katika moja ya hayo (Manazili ishirini na nane)."

53 - Anasema Al-qurtubiy katika "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura 36: "Basi (Mwezi) unaikata falaki (Orbit) kwa muda wa siku ishirini na nane." Tazama pia maneno hayo katika: Al-zamakhshariy "AL-KASHAF" j. 4, uk. 19, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36. Anasema Al-tabtabai katika "AL-MIZAN" j. 17, uk. 90: "Manazil ni wingi wa (neno) manzil?..na dhahir ni kuwa makusudio ni manazil ishirini na nane ambayo mwezi unayakata katika (muda wa) siku ishirini na nane taqriban."

54 - Anasema Al-qurtubiy katika "AL-JAMI'U LIAHKAMI AL-QUR-AN" j. 15, uk. 30, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura 36: "Kisha (mwezi) hujificha; kisha huchomoza hali ya kuwa ni mwezi muandamo." Anasema Al-zamakhshariy katika "AL-KASHAF" j. 4, uk. 19, katika tafsiri ya Aya ya 40, ya Sura ya 36: "Kisha (mwezi) hujificha (kwa muda wa) siku mbili; au (kwa muda wa siku) moja ikiwa mwezi (month) ni mpungufu (Yaani ukiwa umeandama 29)." Anasema Al-baghawiy katika "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 2, uk. 410, katika tafsiri ya Aya ya 5, ya Sura ya 10: "Na hujificha (mwezi kwa muda wa) siku mbili ikiwa mwezi (month) ni siku thalathini; na ukiwa (mwezi: month) ni wa siku ishirini na tisa, basi (mwezi: moon) hufichika (kwa muda wa) siku moja."

54 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 5.

56 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 8.

57- Sura ya 10 Aya ya 5.

58 - Hii haina maana kwamba hakuna sababu nyengine za kuumbwa jua na mwezi, lakini iliotajwa hapa ni hio. Na Aya hii - kwa uoni wangu - inahitaji maelezo marefu sana. Mengine ni ya Kisharia; mengine ni ya kifalaki. Na yote yanahitaji wenyewe waliobobea katika fani hizo.

59 - Juma Mazrui Hoja zilizowekwa Wazi uk. 24, chapa ya pili na 24; chapa ya kwanza uk. 18.

60 - Tazama ukurasa wa 68-70, wa chapa ya pili ya kitabu Ushahidi uliowekwa wazi au uk. 58-59 wa kitabu hicho chapa ya kwanza.

61 - Aya yenyewe ni hii: "Yeye (Allah) Ndiye aliyelifanya jua kua muanga na mwezi kua nuru na akaupimia (huo mwezi) vituo, ili mujue idadi ya miaka na hisabu."

62- Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 5.

63- Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 8.

64- Tazama Ibn Uthaimin "FATAWA ULAMAI AL-BALADI AL-HARAM" uk. 194-195.

65 - Ibn Maja Al-Sunan Hadithi na. 17. 65

66- Sura ya 36 Aya 39.

67 - J. 1, uk 55.

68 - Wa kumi na tatu ni wa buruji inayoitwa Ophiuchus au kwa Kiarabu ?????? Al-hawiyya. Lakini hii si buruji mashuhuri kwa wanavyuoni wa Kiarabu, na kwa hivyo si aghlabu kuitaja: hutaja buruji 12 tu.

69 - Sura ya 85 Aya ya 1.

70 - Tazama Nassor Bachoo: "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI." Uk. 66.

71 - J. 1, uk 55.

72 - Wa kumi na tatu ni wa buruji inayoitwa Ophiuchus au kwa Kiarabu ?????? Al-hawiyya. Lakini hii si buruji mashuhuri kwa wanavyuoni wa Kiarabu, na kwa hivyo si aghlabu kuitaja: hutaja buruji 12 tu.

73 - Sura ya 85 Aya ya 1.

74 - Sheikh Al-mufassirin Badru Al-din Al-khaliliy "AL-HAQQU AL-DAMIGH" uk. 46.

75 - Ibn Mandhur "LISANU AL-ARAB" j. 8, uk. 183.

76 - Al-sabuniy "SAF-WATU AL-TAFASIR" j. 1, uk. 275, katika maelezo ya Aya ya 77 ya Sura ya 6.

77 - Sahihi ni "Mat-lail-Badri" si "Mat-lail-Badru".

78 - Ameipokea Al-hakim - katika "AL-MUSTADRAK" j. 1, uk. 584-585, Hadithi na. 1539, na Al-bayhaqiy katika "AL-KUBRA" j. 6, uk. 196, Hadithi na. 8022, na Abdul-Razzaq katika "AL-MUSANNAF" j. 4, uk. 122, Hadithi na. 7336, na Al-daraqutniy katika "AL-SUNAN" j. 2, uk. 163, Hadithi na. 29 .

79 - Abu Ghanim Al-khurasani "AL-MUDAWANA AL-SUGHRA" j. 1, uk. 168.

80 - Al-wahidiy "ASBABU AL-NNUZUL" uk. 98.

81 - Al-suyutiy "ASBABU AL-NUZUL" uk. 28.

82 - Bali Aya yenyewe inaonesha kwamba Hadithi hii ni ya kutunga. Tazama ukweli kwamba Aya inasema kwamba alichoulizwa Mtume (s.a.w.) ni miezi miandamo, wakati Hadithi inaonesha kwamba alichoulizwa ni hali tafauti za mwezi. Tena kama Hadithi hio ilikuwa sahihi, basi Qur-ani isingelitumia neno "Ahilla" (Miezi miandamo), bali ingetumia neno "Qamar" kwani neno "Hilal" - ambalo wingi wake ndio "Ahilla" - ni mahususi kwa maana ya (Mwezi muandamo), wakati Hadithi inaonesha kwamba alichoulizwa Mtume(s.a.w.w) ni hali ya mwezi kwa maana ya "Qamar," ndio maana akaulizwa kuhusu hatua (stages) unazopita za ukubwa na udogo. Kwa ufupi, ni kuwa kuna mgongano baina ya Hadithi na Aya; ukiongeza na udhaifu mkubwa uliopo wa sanad ya Hadithi hio, basi utakuwa umeongeza chumvi juu ya jaraha!

83- Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j. 9, uk. 387, tarjama na. 721.

84 - Al-suyutiy "ASBABU AL-NUZUL" uk. 6, katika maelezo juu ya Aya 14, ya Sura ya 2.

85- Tazama tafsiri ya Al-baghawiy "MAALIMU AL-TANZIL" j.1, uk. 144, katika maelezo ya chini yaliotiwa na Abdul-Razzaq Al-mahdiy.

86 - Hatimae ikanibainikia kwamba Hadithi hii ni ya kutunga tu, kwani Al-kalbiy kaisimulia kutoka kwa Abi Salih. Na Al-kalbiy kakiri kwamba riwaya zote alizozisimulia kutoka kwa Abi Salih ni za uwongo. Anasema Al-bukhari: "Katusimulia Yahya kutoka kwa Sufyan kasema: 'Kaniambia Al-kalbiy: 'Kila nilichokusimulia kutoka kwa Abi Salih ni uwongo." Tazama Al-dhahabiy "AL-MIZAN" j. 5, uk. 3, tarjama na. 7574.

87- Al-zarqaniy "MANAHILU AL-U'RFAAN" j. 2, uk. 17.

88 - Al-zarqaniy "MANAHILU AL-U'RFAAN" j. 2, uk. 17.

89 - Abdul-Razzaq katika maelezo yake juu ya Tafsiri ya Al-baghawiy "MA'ALIMU AL-TANZIL" j. 1, uk. 11.

90 - Tazama maelezo haya katika "AL-MAUDHUAT" (HADITHI ZA KUTUNGA) cha Ibn Al-jawziy, j. 1, uk. 240, milango yenye kuhusiana na Qur-an: mlango wa fadhila za Sura.

91 - Tazama maelezo ya Abdul-Razzaq Al-Mahdi katika Al-Kashaf j. 1, uk. 261.

92- Tazama maelezo ya Abdul-Razzaq Al-Mahdi katika Ma'alimu Al-Tanzil cha Al-Baghawi j. 1, uk. 234. Tazama pia maelezo ya Abdul-Razzaq Al-Mahdi huyo huyo katika Al-Jami'u cha Al-Qurtubi j. 2, uk. 339.

93 - Al-Alusi Ruhu Al-Ma'an j. 2, uk. 71.

94 - Tazama Al-Zarkashi Al-Burhan fii 'Ulumi Al-Qur-an j. 1, uk. 22.

95- Tazama Muslim "SAHIHU MUSLIM" katika Sharhu al-nawawiy ni j. 8, uk. 32, Hadithi na. 36- 2408, mlango kuhusu fadhila za Ali bin Abi Talib.

96 - Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j. 9, uk. 387, tarjama na. 721.

97- Al-suyutiy "ASBABU AL-NUZUL" uk. 6, katika maelezo juu ya Aya 14, ya Sura ya 2.

98 - Tazama tafsiri ya Al-baghawiy "MAALIMU AL-TANZIL" j.1, uk. 144, katika maelezo ya chini yaliotiwa na Abdul-Razzaq Al-mahdiy.

99 - Hatimae ikanibainikia kwamba Hadithi hii ni ya kutunga tu, kwani Al-kalbiy kaisimulia kutoka kwa Abi Salih. Na Al-kalbiy kakiri kwamba riwaya zote alizozisimulia kutoka kwa Abi Salih ni za uwongo. Anasema Al-bukhari: "Katusimulia Yahya kutoka kwa Sufyan kasema: 'Kaniambia Al-kalbiy: 'Kila nilichokusimulia kutoka kwa Abi Salih ni uwongo." Tazama Al-dhahabiy "AL-MIZAN" j. 5, uk. 3, tarjama na. 7574.

100 - Tazama maelezo ya Abdul-Razzaq Al-Mahdi katika Al-Kashaf j. 1, uk. 261.

101 - Tazama maelezo ya Abdul-Razzaq Al-Mahdi katika Ma'alimu Al-Tanzil cha Al-Baghawi j. 1, uk. 234. Tazama pia maelezo ya Abdul-Razzaq Al-Mahdi huyo huyo katika Al-Jami'u cha Al-Qurtubi j. 2, uk. 339.

102- Al-Alusi Ruhu Al-Ma'an j. 2, uk. 71.

103- Al-Sayyid Muhammad Rashid Ridhaa Al-Manar j. 2, uk. 143.

104 - Al-Tabatabai Al-Mizan j. 2, uk. 59.

105 - Hadithi hio kaipokea Muslim "SAHIHU MUSLIM" Hadithi na. 2523, j. 4, uk. 421 katika "Sharhu Al-nnawawi." Al-tirmidhiy "AL-SUNAN" uk. 207, Hadithi na. 693. Abu Daud "AL-SUNAN" uk. 400, Hadithi na. 2329. Al-nnasai "AL-KUBRA" j. 3, uk. 97-98, Hadithi na. 2432. Al-bayhaqiy "AL-KUBRA" j. 6, uk. 294-295. Ibn Khuzaima "AL-SAHIH" j. 2, uk. 924, Hadithi na. 1916. 106 - Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j 11, uk. 259, tarjama na. 479.

107- Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j.1, uk. 251, tarjama na. 533.

108 - Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j 9, uk. 96, tarjama na. 149.

109 - Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j. 8, uk. 388, tarjama na. 785. Jambo la kusikitisha ni kusema kitu bila ya ushahidi kutoka katika vitabu vyenye kutegemewa, ambapo Sheikh Bachoo alisema katika uk. 58 wa kitabu chake maneno haya: "Kisa cha Kuraib ni "MAJHUUL" yaani Kuraib ni mtu asiyeeleweka vyema katika wapokezi wa Hadithi." Sasa sijui Sheikh Bachoo maneno haya kayapata wapi?! Kuraib huyu ambaye ni Mawla wa Ibn Abbas katajwa katika: "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" cha Ibn Hajar tarjama (biography) na 785, na akasema Ibn Sa'ad ni "Mwenye kuaminika." Anasema Uthman Al-darimiy: "Nilimwambia Ibn Main: '(Riwaya za) Kuraib kutoka kwa Ibn Abbas ni bora zaidi kwako au (riwaya za) Ikrima (kutoka kwa Ibn Abbas?)" Akasema (Ibn Main): 'Wote wawili ni wenye kuaminika." Na Kuraib huyu katajwa pia na Ibn Hibban katika "AL-THIQAT" (Kitabu juu ya wapokezi wenye kuaminika), uk. 367, tarjama na. 5124. Tazama maelezo hayo pia katika "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j. 8, uk. 388 Kuraib katajwa pia na Al-bukhariy katika "AL-TAARIKHU AL-AWSAT" j. 1, uk. 371, tarjama na. 824, na akamtaja pia katika "AL-TAARIKHU AL-KABIR" j. 7, uk. 114, tarjama na. 10332. Na akatajwa na Ibn Sa'ad katika "AL-TABAQATU AL- KUBRA" j. 5, uk. 224, tarjama na. 905, na akasema kwamba ni "Mwenye kuaminika." Na akatajwa na Abu Hatim Al-raziy katika "AL-JARHU WA AL-TA'ADIL" j. 7, uk. 168, tarjama na. 955, na akanukuu kauli ya Ibn Main yenye kusema "Wao (Kuraib na Ikrima) ni waaminifu." Na wako wengine wengi waliomtaja Kuraib katika vitabu vya "TAARIKH" na vitabu vya wapokezi wa Hadithi. Tazama maelezo ya chini katika "AL-TAARIKHU AL-KABIR" cha Al-bukhari, j. 7, uk. 114 kilichohakikiwa na Mustafa Abdul-Qadir, utaona marejeo mengine 15 ya ziada ambayo sikuyataja hapa ambamo Kuraib katajwa. Kwa hivyo, kauli ya Sheikh Bachoo kwamba Kuraib hajulikani ni Mujazafa (Kusukuma): kauli hio haina thamani katika gulio la elimu.

110 - Al-shaukaniy "NAYLU AL-AWTAR." j. 4, uk. 200 katika sherehe ya Hadithi na. 1636.

111- Jawabu hii inapatikana katika darsa ya tafsiri ya Aya ya 189 ya Sura ya 2. Sehemu hii ya tafsiri ya Sheikh bado haijachapishwa lakini inapatikana katika kaseti za redio.

112 - Tazama Al-suyutiy: "TADRIBU AL-RAWI" uk. 161.

113- Al-shaukaniy "NAYLU AL-AWTAR." j. 4, uk. 200 katika sherehe ya Hadithi na. 1636.

114 - Wengine wanasema ni zaidi ya meli 700, kama ilivyo pia katika kitabu cha Sheikh Nassor Bachoo.

115 - Al-shaukaniy "NAYLU AL-AWTAR." j. 4, uk. 200 katika sherehe ya Hadithi na. 1636.

116 - Al-shaukaniy "NAYLU AL-AWTAR." j. 4, uk. 200 katika sherehe ya Hadithi na. 1636.

117 - Elewa kwamba ibara hii ya Al-shaukaniy aliposema: "Ikiwa andiko linajulikana" na aliposema: "Ikiwa andiko halijulikani" si ibara sahihi. Ibara hii msingi wake ni kuwa maneno ya Ibn Abbas aliposema: "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." ni ijtihadi yake Ibn Abbas. Nayo si kauli sahihi kama tulivyobainisha. Kwa hivyo, jawabu ni kuwa andiko linajulikana, nayo ni riwaya ya Ibn Abbas na Kuraib.

118 - Al-shaukaniy "NAYLU AL-AWTAR." j. 4, uk. 200 katika sherehe ya Hadithi na. 1636.

119 - Tazama kanuni hii katika Dr. Wahbat Al-zuhailiy "USULU AL-FIQ-HI" j. 1, uk. 637.

120 - Qiyas - kilugha - maana yake ni kipimo. Ama katika fani ya usulu Al-fiq-hi, Qiyas ni "Kukirejesha kitu ambacho hukumu yake haikutajwa, kwa kukilinganisha na kitu ambacho hukumu yake imetajwa, kisha ukakipa kitu ambacho hukumu yake haikutajwa hukumu sawa na ile ya kitu ambacho hukumu yake imetajwa, kwa ajili ya kuwepo illa (sababu) moja katika vitu viwili hivyo." Kwa hivyo, katika Qiyas, tuwe na mambo mane:

1) Aslu. Yaani asili au shina. Shina ni kile kitu ambacho hukumu yake imetajwa.

2) far'u. Yaani tawi. Tawi ni kile kitu ambacho hukumu yake haikutajwa.

3) Illah. Illa ni sababu ambayo ipo katika Aslu. (Shina) na ipo katika far'u (Tawi). Wengine wanatafautisha baina ya sababu na illa. Sababu - kwao - ni kitu kisicho na uhusiano na kitu chenye kupewa hukumu. Kama kutenguka jua kuwa ni sababu ya kuwajibikiwa na Sala. Na illa ni kitu chenye uhusiano na kitu chenye kupewa hukumu. Kama mgonjwa kuruhusiwa kula mwezi wa Ramadhani. Ugonjwa ni illa ya ruhusa hio, na uhusiano baina ya ugonjwa na kuruhusiwa kula uko wazi.

4) hukmu (hukumu) ni moja katika hukumu tano, nazo ni: wajibu, mandub (jambo litakiwalo kufanywa lakini si lazima), haramu, mubaha (ruhusa) na makruhu. Kwa hapa hukumu inaweza ikawa ima ni uharamu wa kuzingatia muandamo wa mbali; au wajibu wa watu wa kila mji kufata muandamo wao.

121 - Tazama darsa hii katika: Al-imamu Al-salimi "SHARHU TAL-ATI AL-SHAMS" j. 2, uk. 135. Dr. Wahbat Al-zuhaily "USULU AL-FIQ-HI AL-ISLAMI" j. 1, uk. 671. Sheikh Muhammad Al-khadhari " USULU AL-FIQ-HI" uk. 381.

122 - Kumbuka kwamba hapa tunafanya (Kuzikusanya sifa zinazoelekea kuwa illa (sababu) halafu kuzipima na kuchukua iliokuwa sahihi).

123 - Makusudio ya sababu isiovuuka mahala pake, ni sababu ambayo ndio iliosababisha kitu fulani kikapewa hukumu fulani, lakini sababu hio ikawa ipo katika kitu hicho tu: haipo katika kitu chengine. Sababu kama hii ni dhaifu, na kwa hivyo ikiwa kuna sababu nyengine ambayo ipo katika kitu hicho na pia ipo katika kitu au vitu vyengine - ambayo ndio huitwa kuwa ni sababu iliovuuka mahala pake - basi wanavyuoni huifanya sababu hio iliovuuka mahala pake kuwa ndio sababu ya hukumu. Si kwamba sababu isiovuuka mahala pake haifanywi kuwa ni sababu ya hukumu, "Laa" inafanywa kwa mujibu wa wanavyuoni wengi, lakini ikigongana na sababu inayovuuka mahala pake basi sababu hio inayovuuka mahala pake ndio ya kuzingatiwa. Na yote haya lau ingelikuwa neno "Sham" linafaa kuwa ni sababu, lakini hata kulifanya neno hilo kuwa ni sababu ya hukumu haiwezekani, kama ulivyoona humu katika maelezo yetu.

124 - Tazama: Sh. Nassor Bachoo: "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 32.

125 - "NAYLU AL-AWTAR." j. 4, uk. 200 katika sherehe ya Hadithi na. 1636.

126 - Neno "Punguzu" ndilo lililomo katika kitabu cha Sheikh Nassor, sijui kama kakusudia neno "Pungufu" au hili ndio neno sahihi kwa mujibu wa Sheikh Bachoo.

127 -Tazama "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 33.

128- Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 37.

129- Ibn Hajar "AL-FAT-HU" j. 5, uk. 2480, katika maelezo ya Hadithi na. 1911.

130 - Wau al-atfi ni wau yenye kuunganisha baina ya maneno mawili au zaidi au sentensi mbili au zaidi. Yaani ni Cojujuctional letter (Herufi ya kuuanganishia). Hii ni kama kusema katika Kishwahili: Ali na Saleh. Herufi "Na" ndio sawa na "Wau au wa" nayo imetumika kuunganisha baina ya maneno Ali na sale. Halkadhalika Wau al-atfi huunganisha maneno au sentensi.

131- Al-tirmidhiy "AL-SUNAN" katika tarjama ya mlango wa 9, maelezo ya Hadithi na. 693.

132- Ibn Khuzaima "SAHIHU" yake katika tarjama ya mlango na. 33, j. 2, uk. 924, Hadithi na. 1916.

133 - Tazama "SHARHU SAHIHI MUSLIM" ya Al-imamu Al-nnawawi, Hadithi na. 2523. Bali Sheikh Bachoo mwenyewe katika uk. 29 kayafasiri maneno hayo ya Ibn Abbas yasemayo: kuwa maana yake ni: "La (Hapana): hivi ndivyo alivyotuamrisha Mjumbe wa Mwenyezi Mungu." Halafu hapa kageuka na kuyafasiri maneno hayo hayo kuwa Ibn Abbas kasema "Anatosheka:" kule: "Laa" (Sio), huku: "Naam" (Ndio), na Hadithi ni ile ile na msemaji ni yule yule! Tazama pia katika uk. 109-110 uone upinzani alioutoa hapo halafu linganisha upinzani huo na upinzani alioutoa kabla ya hapo, utaona jinsi gani mwanamume alivyokuwa bingwa wa kubadilika! Na hili si jengine bali ni lile Waswahili wanalolisema: "Mfa maji hukamata maji." 134 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 37.

135- Hii ni hoja ya Abu Ammar, Nassir bin Mohd bin Rashid Al-mazrui, ambayo aliiongezea hapa. Nilisahau kuweka maelezo haya katika chapa ya kwanza. Na hapa nakamilisha wajibu wangu, kwa vile hoja hii si juhudi yangu, bali ni juhudi yake, nayo ni hoja sahihi, nzuri.

136- Tazama Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 17.

137- Tazama Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 152.

138 - Ibn 'Aqil Shar-hu Ibn 'Aqil j. 1, uk. 11.

139 - Ibn 'Aqil Shar-hu Ibn 'Aqil j. 1, uk. 11.

140 - Ibn 'Aqil Shar-hu Ibn 'Aqil j. 1, uk. 12.

141 - Ibn Hisham Qatru Al-Nada uk. 340.

142- Ibn 'Aqil Shar-hu Ibn 'Aqil j. 1, uk. 14.

143 - Ibn 'Aqil Shar-hu Ibn 'Aqil j. 1, uk. 14.

144 - Hadithi hio kaipokea Muslim "SAHIHU MUSLIM" Hadithi na. 2523, j. 4, uk. 421 katika "Sharhu Al-nnawawi." Al-tirmidhiy "AL-SUNAN" uk. 207, Hadithi na. 693. Abu Daud "AL-SUNAN" uk. 400, Hadithi na. 2329. Al-nnasai "AL-KUBRA" j. 3, uk. 97-98, Hadithi na. 2432. Al-bayhaqiy "AL-KUBRA" j. 6, uk. 294-295. Ibn Khuzaima "AL-SAHIH" j. 2, uk. 924, Hadithi na. 1916.

146 - Yaani Abu Daud, mpokezi wa Hadithi. Kwa hivyo, Abu Daud unasema kama tunavyosema sisi.

147 - Al-Adhim Abad A'wnu Al-Ma'abudi: Sharhu Sunani Abi Daud j. 6, uk. 454-455, katika sherehe ya Hadithi na. 2315.

148 - Yaani Al-Imamu Al-Nasai. Kwa hivyo, Al-Nasai na wengine pia wanawafikiana na sisi.

149- Maana ya kuwa andiko la ujumla ni la dhana na andiko maalum (specific au khaas) ni la uhakika, ni kuwa andiko la ujumla linakusanya vitu vyote vyenye kuhusiana na lafdhi ya andiko hilo, lakini hakuna uhakika kwamba kweli vyote vimeingia au vilivyoingia ni vingi tu, wakati katika andiko maalum (specific au khaas), tuna hakika kwamba kilichotajwa ndivyo kilivyo. Kufahamu hili vizuri, tazama mfano mtu anaposema Wazanzibari ni wakarimu. Andiko hili ni la ujumla linamuingiza kila anayeitwa Mzanzibari, lakini je kweli kila Mzanzibari ana sifa hiyo ya ukarimu? Ukitazama utaona si kweli kwamba Wazanzibari wote wako hivyo, labda hio ni sifa ya waliowengi tu. Lakini nikitumia lafdhi khaas (specific) nikasema Ali ni mkarimu, basi huwa ni kitu cha hakika kwa vile kinamuhusu mtu mmoja maalum. Kwa hivyo, andiko hili si la hakika. Lakini katika andiko maalum (specific au khaas) maneno huwa ni ya uhakika.

150 - Tazama Ibn Uthaimin "FATAWA ULAMAI AL-BALADI AL-HARAM" uk. 194-195.

151 - Al-salimiy "AL-JAWABAAT" j. 1, uk. 45.

152- Kama ilivyo katika "AL-NAYLU" cha Al-shaukaniy j. 4, uk. 192, katika maelezo ya Hadithi na. 1626.

153 - Abu Daud "AL-SUNAN" uk. 401 katika maelezo ya Hadithi na. 2338.

154 - Al-bayhaqiy "AL-KUBRA" j. 6, uk. 211, katika maelezo yake juu ya Hadithi na. 8069.

155- Ibn Majah "AL-SUNAN" uk. 278, katika maelezo yake juu ya Hadithi na. 1652.

156 - Al-tirmidhiy "AL-SUNAN" uk. 206, katika maelezo yake juu ya Hadithi na. 691.

157 - Al-nadhaam ni Ibrahim bin Sayyar, Sheikh wa madhehebu ya Mu'utazila.

158 - Ibn Al-arabiy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 120, katika tafsiri ya Aya inayosema: "Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu, basi na-aufunge."

159 - Kapwekeka maana yake kawa peke yake; na kupwekeka na Hadithi ni kuwa kaisimulia yeye tu: hakuna msimulizi mwengine aliyeisimulia. Lihifadhi neno hili kwa sababu limetumika katika sehemu nyengine nyingi za kitabu hiki. 160 - Al-shaukaniy "AL-NAYLU" j. 4, uk. 192.

161- Tazama "TAHDHIBU AL-TAHDHIB" j. 4, uk. 204, tarjama na. 405.

162 - Al-imamu Al-shaukaniy: "NAYLU AL-AWTAR" j. 4, uk. 193 katika maelezo ya Hadithi na. 1625-1626.

163 - Tazama Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 17.

164 - Katika uk. 17-18, Sheikh Bachoo anatoa hoja kwa Hadithi ya mabedui wawili na Hadithi ya Masahaba waliouona mwezi jana (yaani kwa mujibu wa siku waliokwenda kwa Mtume s.a.w.). Na jawabu yetu hapa ni hio hio kwamba watu hao wote walikuwa katika eneo la Madina. Ivo ni mtu gani katika zama za Mtume(s.a.w.w) atayetoka Sham au Oman au mji wowote ule wa mbali akafika kwa Mtume(s.a.w.w) kwa muda wa siku moja - usiku wa jana mpaka magharibi ya leo?! Kwa wakaazi wa Afrika ya Mashariki hili ni rahisi kuweza kulijua: waulizeni Wazanzibari waliokuja Oman zamani: walikuwa wakitoka Ruwi mpaka Niz-wa kwa muda gani? Amenisimulia mmoja wao kwamba walikuwa wakienda Niz-wa kwa punda na ngamia kwa muda wa wiki moja. Na hii kuna sehemu ambazo walikuwa wakipanda gari. Niz-wa kwa leo tunakwenda kwa gari kwa muda wa kama saa na nusu kutokea Ruwi. Ruwi na Niz-wa hapafiki k.m. 200. Ni masafa ya kama 180. Sasa wewe pima mwenyewe bedui huyo alikuwa wapi hata akaweza kufika kwa Mtume(s.a.w.w) - kwa ngamia au kwa punda - kwa muda wa siku moja au mbili au wiki, ikiwa watu hawa wamesafiri masafa ya k.m. mia na thamanini (180) kwa muda wa wiki?

165 - Kama ilivyo katika riwaya na. 8069 ya Al-bayhaqiy katika "AL-KUBRA" j. 6 uk. 211 na Al-hakim katika "AL-MUSTADRAK" j. 1, uk. 587 Hadithi na. 1546 na Abu Daud katika "AL-SUNAN" Hadithi na. 2338 na Al-daraqutniy katika "AL-SUNAN" j. 2, uk. 159 Hadithi na. 14.

166 - Kama ilivyo katika riwaya na. 8069 ya Al-bayhaqiy katika "AL-KUBRA" j. 6 uk. 211 na Al-hakim katika "AL-MUSTADRAK" j. 1, uk. 587 Hadithi na. 1546 na Abu Daud katika "AL-SUNAN" Hadithi na. 2338 na Al-daraqutniy katika "AL-SUNAN" j. 2, uk. 159 Hadithi na. 14.

167 - Al-Suyuti Tadribu Al-Rawi uk. 161.

168 - i. Ahkamul-Qur-aan Cha Al-Jaswas J. 1 uk 305. ii. Fiqhi-Sunnah Cha Sa'iyd Saabiq J. 1 uk 436.iii. Rawaaiul-Bayaan J. 1 uk 211. iv. Naylul-Awtaar J. 4 uk 195 v. Sharhu Subulu Sawiyyah Lifiqhi Sunanil - Marwiyyah vi. Fatawa Za BAKWATA uk 10 - 11 Mada 14/70

169 - Kanuni gani Yaa Nas!

170 - Tazama maudhui hii katika Dr. Al-Zuhaili Usulul Fiq-hi j. 1, uk 244-245. Al-Salimi Sharhu Tal'ati Al-Shams j. 1, uk. 105.

171- Kama ilivyo katika riwaya na. 8069 ya Al-bayhaqiy katika "AL-KUBRA" j. 6 uk. 211 na Al-hakim katika "AL-MUSTADRAK" j. 1, uk. 587 Hadithi na. 1546 na Abu Daud katika "AL-SUNAN" Hadithi na. 2338 na Al-daraqutniy katika "AL-SUNAN" j. 2, uk. 159 Hadithi na. 14.

172 - Ali Muhammad Al-Nadwi Al-Qawa'id Al-Fiqhiyya uk. 417. Muhammad Bakr Isma'il Al-Qawa'id Al-Fiqhiyya uk. 50.

173 - Lakini nyinyi Hadithi ya Ibn Abbaas na kuraib hamutaki kuiba hukumu hio, bali munaona ni kisa tu!!!

174 - Yaani Bismillahi zilio mwanzoni mwa sura: si Bismillahi ilio katikati ya Suratu Al-Naml.

175 - Ibn Hajar Al-Fat-Hu j. 5, uk. 2480, katika sherehe ya Hadithi na. 1907.

176- Al-San'ani Subulu Al-salam j. 1, uk. 415, katika maelezo ya Hadithi na. 610.

177 - Makusudio ya sababu isiovuuka mahala pake, ni sababu ambayo ndio iliosababisha kitu fulani kikapewa hukumu fulani, lakini sababu hio ikawa ipo katika kitu hicho tu: haipo katika kitu chengine. Sababu kama hii ni dhaifu, na kwa hivyo ikiwa kuna sababu nyengine ambayo ipo katika kitu hicho na pia ipo katika kitu au vitu vyengine - ambayo ndio huitwa kuwa ni sababu iliovuuka mahala pake - basi wanavyuoni huifanya sababu hio iliovuuka mahala pake kuwa ndio sababu ya hukumu. Si kwamba sababu isiovuuka mahala pake haifanywi kuwa ni sababu ya hukumu, "Laa" inafanywa kwa mujibu wa wanavyuoni wengi, lakini ikigongana na sababu inayovuuka mahala pake basi sababu hio inayovuuka mahala pake ndio ya kuzingatiwa. Na yote haya lau ingelikuwa neno "Sham" linafaa kuwa ni sababu, lakini hata kulifanya neno hilo kuwa ni sababu ya hukumu haiwezekani, kama ulivyoona humu katika maelezo yetu.

178 - Yaani Al-Imamu Al-Nasai. Kwa hivyo, Al-Nasai na wengine pia wanawafikiana na sisi.

179 - Au saba kwa mujibu wa Mahanafi.

180 - Rejea Ali Muhammad Al-Nadwi Al-Qawa'id Al-Fiqhiyya uk. 393. Muhammad Bakr Isma'il Al-Qawa'id Al-Fiqhiyya uk. 142.

181- Sehemu ya Aya isemayo: ilikuwa haimo kwa Kiarabu chake katika makala ya ndugu zetu. Hapa nimeiongeza kwani tafsiri yake kwa Kiswahili ilikuwemo.

182 - Tazama Juma Mazrui Ushahidi Uliowekwa Wazi Katika Suala La Miandamo Ya Mwezi uk 97 chapa ya pili, au uk. 85 chapa ya kwanza.

183 - Nassor Bachoo Ufafanuzi Wa Mgogoro Wa Kuandama Kwa Mwezi uk. 2.

184 - Tazama Al-qurtubiy: "BIDAYATU AL-MUJTAHID" j. 1, uk. 516.

185- Al-kaasaniy "BADAAIU AL-SANAI'I". J. 2, uk. 224-225

186- Al-imamu Abu Muslim "NITHARU AL-JAWHAR" J. 5, uk. 158.

187- Al-sayyid Saabiq "FIQ-HU AL-SUNNA" uk. 293

188 - Al-qurtubiy "BIDAYATU AL-MUJTAHID" j. 1, uk. 516

889 - Ibn Al-arabiy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 121.

190 - Al-qurtubiy "BIDAYATU AL-MUJTAHID" j. 1, uk. 516.

191 - Ramadhani ya mwakaa huu nilikusudia hasa kuwauliza wakazi wa nchi tafauti. Na jawabu ni kuwa: Watu wa jimbo la Kerla India wamefunga sawa na Oman, na Waislamu wa nchi hio wanafata madhehebu ya Shafi. Watu wa Pakistan, Bangladesh na India wamefunga siku ya pili baada ya Oman (ambayo ni siku ya tatu baada ya Saudia). Pakistan na Bangladesh asilimia kubwa ya wakazi wake ni Mahanafi.

192 - Tazama kanuni hii katika Dr. Wahbat Al-zuhailiy Usulu Al-Fiq-Hi j. 1, uk. 677, babu Qiyasi Al-Lugha.

193 - Tazama kanuni hii katika Dr. Wahbat Al-zuhailiy Usulu Al-Fiq-Hi j. 1, uk. 677, babu Qiyasi Al-Lugha.

194 - Tazama kanuni hii katika Dr. Wahbat Al-zuhailiy Usulu Al-Fiq-Hi j. 1, uk. 260..

195- Al-Jitali Al-Qawa'id j. 2, uk. 165.

196 - Al-Jitali Al-Qawa'id j. 2, uk. 56.

197 - Maelezo yake katika kitabu Al-Qawa'id cha Al-Jitali j. 2, uk. 70.

198 - Al-Khalili Al-Fatawa Al-Kitabu Al-Khamis uk. 357.

199- Kwa sasa siwezi kukunakilieni mifano mingi kwani ninapoisoma katika vitabu sidhanii kwamba kuna mtu ataihitaji, lakini hii mifano miwili itatosha kukupeni picha halisi, na nitapoitoa jawabu hii kama ni kitabu nitakunakilieni mifano ya ziada in shaa Allah.

200- Al-qurtubiy "BIDAYATU AL-MUJTAHID" j. 1, uk. 516.

201- Wafasina bandia na maulamaa bandia wamejaa tele leo Zanzibar; ndio maana tukawa na zogo hili. Wallahu Al-Musta'an!

202- Abu Hayyan Al-Bahr j. 2, uk. 47.

203 - Abu Hayyan Al-Bahr j. 2, uk. 47.

204 - Mahmud Safi I'irabu Al-Qur-an j. 2, uk. 371.

205- Tutaeleza kwa urefu katika kitabu inshaa Allah.

206 - Je kanuni hii nyinyi memeifata? Hao muliotolea ushidi katika kitabu chenu wote ni wanavyuoni wa kweli? Mwanachuoni wa kweli si Duktur, bali ni yule aliyefikia daraja ya ijtihad, na nyie munanukuu mpaka kutoka kwa watu wa kawaida! 207 - Abu Al-suud katika tafsiri yake j. 1, uk. 236.

208- Ibn Al-arabiy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 118.

209- Ibn Baraka "KITABU AL-JAMI'I" j. 2, uk. 5.

210- Abu Zahra "USULU AL-FIQ-HI". Kwa sasa ukurasa haunihudhurii kwa vile kitabu hiki sinacho mikononi

211 - Ibn Hazm "AL-MUHALLAH" j. 6, uk. 166.

212 - Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 278.

213- Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 279.

214 - Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 278.

215 - Maana ya maneno haya ya Abu Muslim aliposema: "Na akauita Allah mwanzo wa mwezi kwa jina la mwezi mzima" ni kuwa neno lililotumika katika Aya ni neno Shahr nalo lina maana ya mwezi kwa maana ya kipindi cha siku 29-30 (month), wakati makusudio ya Aya ni atayeushuhudia kwa maana ya kuuona, na unaoonekana ni mwezi ule wa sayari ulioko angani ambao kwa Kiarabu huitwa Qamar au huitwa Hilal unapokuwa muandamo, kwa maana hii itakuwa neno Shahr lililomo katika Aya hio, limetumika kwa maana ya Hilal. Au limetumika kwa maana yake hio hio ya Shahr lakini "Pakadiriwe mudhafu (kilichotegemezwa ambacho kimeondoshwa nacho ni Hilal). Na maana itakuwa "Hilalu Al-shahri" Mwezi muandamo wa mwezi (wa Ramadhani). Hii ndio maana iliomo katika maneno ya Sh. Abu Muslim.

216 - Abu Muslim "NITHARU AL-JAWHAR" j. 5, uk. 13.

217- Abu Muslim "NITHARU AL-JAWHAR" j. 5uk. 25.

218 - Sh. Al-khaliliy "AL-FATAWA" kitabu 1, uk. 309.

219- Prof Moh'd Bakr Ismail "AL-QAWAIDU AL-FIQ-HIYYA" uk 401.

220- Ibn Uthaimin "FATAWA ULAMAI AL-BALADI AL-HARAM" uk. 194.

221 - Al-sayyid Ahmad Al-hashimiy katika "JAWAHIRU AL-BALAGHA" uk. 389

222- Dr. Wahbat Al-zuhailiy "USULU AL-FIQ-HI" j. 1, uk. 43, au uk. 51 kwa chapa nyengine.

223 - Dr. Wahbat Al-zuhailiy "USULU AL-FIQ-HI" j. 1, uk. 43, au uk. 51 kwa chapa nyengine.

224 - Ibn Hajar Al-Fat-Hu j. 5, uk. 2480, katika sherehe ya Hadithi na. 1907.

225 - Al-San'ani Subulu Al-salam j. 1, uk. 415, katika maelezo ya Hadithi na. 610.

226 - Muqabala maana yake ni kusemwa kitu fulani katika sentensi moja kisha katika sentensi ya pili kukasemwa maneno yaliokinyume na yale yalio katika sentensi ya kwanza. Sasa ikiwa maana iliomo katika maneno ya kwanza imefichika, basi tunajiongozea kwa maneno ya pili kuufahamu muradi wa maneno ya kwanza. Tumetoa baadhi ya mifano miwili mitatu katika kitabu chetu: "HOJA ZENYE NGUVU" na si vibaya hapa tukainukuu tena mifano miwili, kwani huenda ikawa mtu kasoma kitabu hiki bila ya kusoma kile. Mfano wa muqabala ni kama Aya inayosema: "Anawahalalishia mambo mazuri na anawaharamishia mambo mabaya." Sura ya 7 aya 157. Na Aya inayosema: "Na wanatarajia rehema yake na wanaogopa adhabu yake." Sura ya 17 aya ya 57. Ukitazama hapa utaona kwamba kila sentensi ya pili ni kinyume na sentensi ya kwanza. Na huu ndio watu wa lugha ya Kiarabu wanaouita Muqabala, yaani opposite au sentensi ilio kinyume ya sentensi nyengine. Sasa kuna wakati inakuwa ni vigumu kuweza kujua maana iliokusudiwa katika sentensi ya kwanza lakini utapoitazama sentensi ya pili katika Muqabala wake, ndio inayokujuilisha muradi wa sentensi ya kwanza.

227- Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 278.

228 - Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 279.

229 - Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 278.

230- Al-jassas Al-raziy "AHKAMU AL-QUR-AN" j. 1, uk. 279.

231- Hii si kanuni muttarid. Neno linaweza kuwa tika sentensi na pia likawa na maana zaidi ya moja ikiwa maana hizo hazigongani. Neno "Sala" katika Aya: Hakika ya Allah na Malaika zake wanamsali Mtume?, lina maana mbili. Sala ya Allah ni maghfira nay a Malaika ni dua.

232 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 37.

133 - Hii ni hoja ya Abu Ammar, Nassir bin Mohd bin Rashid Al-mazrui, ambayo aliiongezea hapa. Nilisahau kuweka maelezo haya katika chapa ya kwanza. Na hapa nakamilisha wajibu wangu, kwa vile hoja hii si juhudi yangu, bali ni juhudi yake, nayo ni hoja sahihi, nzuri.

234 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 37.

235 - Maana ya kuwa andiko la ujumla ni la dhana na andiko maalum (specific au khaas) ni la uhakika, ni kuwa andiko la ujumla linakusanya vitu vyote vyenye kuhusiana na lafdhi ya andiko hilo, lakini hakuna uhakika kwamba kweli vyote vimeingia au vilivyoingia ni vingi tu, wakati katika andiko maalum (specific au khaas), tuna hakika kwamba kilichotajwa ndivyo kilivyo. Kufahamu hili vizuri, tazama mfano mtu anaposema Wazanzibari ni wakarimu. Andiko hili ni la ujumla linamuingiza kila anayeitwa Mzanzibari, lakini je kweli kila Mzanzibari ana sifa hiyo ya ukarimu? Ukitazama utaona si kweli kwamba Wazanzibari wote wako hivyo, labda hio ni sifa ya waliowengi tu. Lakini nikitumia lafdhi khaas (specific) nikasema Ali ni mkarimu, basi huwa ni kitu cha hakika kwa vile kinamuhusu mtu mmoja maalum. Kwa hivyo, andiko hili si la hakika. Lakini katika andiko maalum (specific au khaas) maneno huwa ni ya uhakika.

236- Tazama Ibn Uthaimin "FATAWA ULAMAI AL-BALADI AL-HARAM" uk. 194-195.

237- Al-salimiy "AL-JAWABAAT" j. 1, uk. 45.

238- Nassor Bachoo: "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 23.

239 - Kainukuu kauli hii Abu Muslim katika "NITHARU AL-JAWHAR" j. 5, uk. 159. Pia kauli hii utaipata katika Fatawa za Al-imamu Al-salimiy j. 2, uk. 114.

240 - Dr. Al-Zuhaili Usulu Al-Fiq-hi j. 1, uk. 521. Al-Qannubi Al-Tufan j. 3, sehemu ya kwanza uk. 23.

241 - Al-Qannubi Al-Tufan j. 3, sehemu ya kwanza uk. 23.

242 - Haya ndio maneno sahihi: sio mudai kwamba wamekubaliana juu ya ijma'i hii.

243 - Ikhtilafu katika Umma ipo, lakini hii ndio kauli yenye nguvu.

244 - Dr. Al-Zuhaili Usulul Fiq-hi j. 1, uk. 526.

245 - Dr. Al-Zuhaili Usulul Fiq-hi j. 1, uk. 527.

246- Al-imamu Al-salimi Sharhu Tal-Ati Al-Shams j. 2, uk. 135.

247- Suala: Je mwezi ukiandama Tanzania au nchi nyengine yoyote ile mwanzo kabla ya Saudia hoja yako kwamba: "Tarehe 9 Dhul-Hijjah huko mji wa Makka; sio tarehe tisa ya nchi nyengine yoyote ile" itakuwa na maana gani? Kumbuka kwamba Saudia haifati muandamo wa nchi nyengine. Kwa kufahamu zaidi, tazama maelezo ya chini (foot note) na. 223. 248- Tazama Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 113-114. 249 - Katika chapa ya kwanza nilisema hivi: "Tukatoa mfano wa kutenguka jua kuwa ni sababu ya kuingia wakati wa kusali." Kilichosahihi ni kusema: "Tukatoa mfano wa kutenguka jua kuwa ni sababu ya kuwajibikiwa na Sala."

250- Tumetaja walioipokea Hadithi hii katika uk. 54-56.

251 - Sura ya 2 Aya ya 200. Na mfano wake ni Hadithi inayosema: "Muhajir (akitaka kukaa Maka basi) akae siku tatu (tu) baada ya (kumaliza) nusuki (ibada) zake (za hija)." 252 - Katika chapa ya kwanza nimeandika "A'YNU" badala ya "A'WNU" basi sahihisha hapa; sahihi ni "A'WNU" si "A'YNU."

253 - Tazama "A'WNU AL-MA'ABUDI: SHARHU SUNANI ABI DAUD" j. 6, uk. 463.

254- Tazama Ibn Uthaimin "FATAWA ULAMAI AL-BALADI AL-HARAM" uk. 194-195.

255- Tatizo pia litabakia kwa wale ambao wakati kwao umetangulia kabla ya Saudia. Kwa mfano Arafa ni J/ane: ambapo alfajiri ya J/ane ikichomoza Saudia wao kwao jua linazama na kwa hivyo ni J/atano. Ikiwa watafunga mchana wa J/ane, basi watafunga kabla ya Arafa. Ikiingia Arafa Makka kwao ni usiku wa J/atano, na hakuna funga ya usiku. Kwa hali hii, ni wazi kwamba funga - yoyote iwayo - ni lazima ifungamanishwe na muandamo wa mwezi. Na kwa kufanya hivyo, Waislamu wote wa dunia wataweza kufunga Arafa mwezi tisa na kula Siku Kuu mwezi kumi.

256- Baada ya kuwa nimeimaliza kazi hii, alinisimulia mmoja wa Sahibu zangu kuhusu nukta alioitoa Sheikh mmoja wa Dar-es-salam katika kuwajibu wale wenye msimamo kwamba tufunge kwa muandamo mmoja. Sheikh aliwaambia watu hao kwamba tunajua kwamba Saudia haifuati muandamo wa nchi nyengine. Sasa suala: je ikiwa mwezi utaandama hapa kwetu kwanza je nyinyi mutafata wapi? Jawabu: Tutafata hapa hapa. Suala. Je ikiwa muko Makka na mwezi umeonekana huku kwanza mutasimama Arafa? Jawabu: Ndio, kwani hakuna Arafa ya mtu peke yake. Suala: Kwani kuna Arafa ya mwezi kumi? Arafa si mwezi tisa? Huoni kwamba ikiwa mwezi umeandama hapa kwanza na wao hawakufata muandamo wa hapa, itakuwa mwezi tisa hapa kule ni nane na tisa kule hapa ni kumi, kwa mujibu wa hisabu yao, wakati nyinyi mwezi munaouzingatia ni ule unaoandama kwanza? Jawabu: Kimya? Kwa hakika nukta hii fupi alioitoa Sheikh huyu inatosha kubainisha ukweli uko wapi.

257 - Kwa hivyo, ni wazi kwamba kisimamo cha Arafa si sababu ya kufunga siku hio bali sababu ni kuandama kwa mwezi wa mfunguo tatu ambao unatangulia kisha ndio zikaja ibada za hija kikiwemo kisimamo cha Arafa. Ama kisimamo hicho ni munasaba tu kama tulivyotangulia kubainisha.

258- Sura 9 Aya 25.

259- Mji uko karibu na Makka. Tazama Yaqut Al-rumi "MU'UJAMU AL-BULDAN" j. 1, uk. 190.

260- Tumetaja walioipokea Hadithi hii katika uk. 54-56.

261- Sura ya 2 Aya ya 200. Na mfano wake ni Hadithi inayosema: "Muhajir (akitaka kukaa Maka basi) akae siku tatu (tu) baada ya (kumaliza) nusuki (ibada) zake (za hija)."

262 - Katika chapa ya kwanza nimeandika "A'YNU" badala ya "A'WNU" basi sahihisha hapa; sahihi ni "A'WNU" si "A'YNU."

263- Tazama "A'WNU AL-MA'ABUDI: SHARHU SUNANI ABI DAUD" j. 6, uk. 463.

264 - Sura 9 Aya 25.

265 - Mji uko karibu na Makka. Tazama Yaqut Al-rumi "MU'UJAMU AL-BULDAN" j. 1, uk. 190.

266 - Anapodai au anaponukuu?!

267 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 37.

268 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 120-124.

269 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 123.

270- Al-imamu Abu Muslim: "NITHARU AL-JAWHAR" j. 5, uk. 157. Rudia pia uk. 194-195 wa kitabu "FATAWA ULAMMAI AL-BALADI AL-HARAM" cha wanachuoni wa Saudia uone walivyoeleza uhusiano wa matalai ya mwezi na matalai ya jua.

271 - Al-Imamu Badru Al-Din Al-Khalili Al-Fawa: Al-Sala, Al-Zaka, Al-Saum, Al-Haj uk. 314.

272- Al-nnawawi "SHARHU AL-MUHADHAB" j. 6, uk. 183.

273 - Nassor Bachoo "UFAFANUZI WA MGOGORO WA KUANDAMA KWA MWEZI" uk. 117-118.

274 - Ibn Hajar ana maelezo mazuri kuhusu Hadithi ya kufungwa mashetani. Tazama "AL-FAT-HU" katika sherehe ya Hadithi na. 1899.

275 - Na pia kwa kufata msingi wa kukamatana na hali ya mwanzo.

276 - Lakini pamoja na hayo tunasema kwamba ilikuwa ni juu ya Sheikh Bachoo kutotoa kabisa hoja hii, kwani Ramadhani inaingia pale tu jua linapotua siku ya mwezi 29 au 30 Shaabani. Sasa kama ni hivyo, vipi anahisi au nini rai yake pale jua linapotua Makka na Madina na ikawa Ramadhani imeingia na mashetani kufungwa, atawapa hukumu gani mashetani wa Marekani ambako ndio kwanza asubuhi au mchana - jua halijatua na Ramadhani haijaingia - je wao wataendelea kuvunja jungu? Au watakimbilia Saudia wakafungwe pamoja na wenzao?

277- Lakini pamoja na hayo tunasema kwamba ilikuwa ni juu ya Sheikh Bachoo kutotoa kabisa hoja hii, kwani Ramadhani inaingia pale tu jua linapotua siku ya mwezi 29 au 30 Shaabani. Sasa kama ni hivyo, vipi anahisi au nini rai yake pale jua linapotua Makka na Madina na ikawa Ramadhani imeingia na mashetani kufungwa, atawapa hukumu gani mashetani wa Marekani ambako ndio kwanza asubuhi au mchana - jua halijatua na Ramadhani haijaingia - je wao wataendelea kuvunja jungu? Au watakimbilia Saudia wakafungwe pamoja na wenzao?

278- Maana ya kuwa andiko la ujumla ni la dhana na andiko maalum (specific au khaas) ni la uhakika, ni kuwa andiko la ujumla linakusanya vitu vyote vyenye kuhusiana na lafdhi ya andiko hilo, lakini hakuna uhakika kwamba kweli vyote vimeingia au vilivyoingia ni vingi tu, wakati katika andiko maalum (specific au khaas), tuna hakika kwamba kilichotajwa ndivyo kilivyo. Kufahamu hili vizuri, tazama mfano mtu anaposema Wazanzibari ni wakarimu. Andiko hili ni la ujumla linamuingiza kila anayeitwa Mzanzibari, lakini je kweli kila Mzanzibari ana sifa hiyo ya ukarimu? Ukitazama utaona si kweli kwamba Wazanzibari wote wako hivyo, labda hio ni sifa ya waliowengi tu. Lakini nikitumia lafdhi khaas (specific) nikasema Ali ni mkarimu, basi huwa ni kitu cha hakika kwa vile kinamuhusu mtu mmoja maalum. Kwa hivyo, andiko hili si la hakika. Lakini katika andiko maalum (specific au khaas) maneno huwa ni ya uhakika.

279- Tazama Ibn Uthaimin "FATAWA ULAMAI AL-BALADI AL-HARAM" uk. 194-195.

280 - Al-salimiy "AL-JAWABAAT" j. 1, uk. 45.

281- Hadithi hio kaipokea Muslim "SAHIHU MUSLIM" Hadithi na. 2523, j. 4, uk. 421 katika "Sharhu Al-nnawawi." Al-tirmidhiy "AL-SUNAN" uk. 207, Hadithi na. 693. Abu Daud "AL-SUNAN" uk. 400, Hadithi na. 2329. Al-nnasai "AL-KUBRA" j. 3, uk. 97-98, Hadithi na. 2432. Al-bayhaqiy "AL-KUBRA" j. 6, uk. 294-295. Ibn Khuzaima "AL-SAHIH" j. 2, uk. 924, Hadithi na. 1916.

8

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA NANE

FITINA BANDIA ZA KISAYANSI

Watu wa maada wanasema kwamba kuasisiwa kwa kitivo chao cha fikra mnamo karne ya 18 na 19 kulihusiana moja kwa moja na maendeleo ya sayansi na kwamba ile mbinu pembuzi ilikuwa ni tunda ambalo lilichumwa kutoka kwenye mti uliostawi vizuri wa sayansi.

Wanaonyesha kila falsafa mbali na uyakinifu kama aina ya udhanifu, unaopingana na mbinu ya fikra ya kisayansi, na wanasisitiza kwamba msimamo wao ni wa kisayansi na endelevu. Kwa mujibu wa msimamo wao, uhalisia unategemea katika kukengeuka kutoka kwenye ukweli wa metafizikia; kila mtu anapaswa ategemeze falsafa yake ya maisha juu mantiki ya fahamu na majaribio na kuchagua uyakinifu. Lakini madai haya si lolote zaidi ya ndoto za kishabiki ambazo zimetegemezwa kwenye nadharia zisizothibitishwa. Mawazo kama haya yanakuja moja kwa moja kutoka kwenye mfumo wa fikra uliolenga kwenye uyakinifu; ambamo ndani yake, kila kitu kimeainishwa na kuwekewa mipaka kwa mujibu wa uyakinifu.

Imani kuhusu kitu cha kuabudu bila shaka ni mojawapo ya vyanzo vikuu vya utamaduni na elimu ya mwanadamu. Kupendekeza imani juu ya Mwenyezi Mungu kama msingi wa falsafa ya maisha kumesababisha mabadiliko makubwa katika misingi ya jamii na fikra katika historia yote ya binadamu. Sasa, pia, katika zama za sayansi na teknolojia, ambapo mwanadamu amekwishagundua kwenda angani, idadi kubwa ya wanasayansi wanao mtazamo wa kidini kama sehemu ya mfumo wa kisomi; wamekuja kuamini juu ya kuwepo kwa muumbaji, chanzo cha viumbe vyote, sio tu kwa njia ya moyo na dhamira, bali pia kupitia maamuzi na mantiki.

Kama uthibitisho wa wayakinifu juu ya falsafa yao ya maisha ungekuwa wa kweli, badala ya kutegemea kwenye ujuzi pungufu wa historia ya fikra za uyakinifu, panapaswa pawepo na uhusiano maalumu baina ya sayansi na mwelekeo kwenye uyakinifu; ni mawazo ya kiyakinifu tu yangewakilishwa kwenye nyanja ya kisayansi. Hivi kila mwana falsafa na msomi, katika kila kipindi, alishikilia falsafa ya maisha ya ukana-Mungu na akawa mtu wa kambi ya wayakinifu. Uchunguzi wa kisomi wa maisha na kazi za wanafikra wakubwa zitatosha kuonesha kwamba fulan kwamba kambi ya kidini kwa hali yoyote haina wanasayansi wa kweli, lakini pia kwamba wanafikra wa kisayansi wakubwa na watu wengine maarufu, wakiwa ni pamoja na waasisi wa nyingi ya sayansi ya wakati huu, wamekuwa na imani juu ya mungu mmoja.

Kwa nyongeza, itikadi za kiyakinifu na ukana-mungu kwa namna yoyote zimewekewa mipaka kwenye kipindi cha mageuzi na mendeleo ya sayansi, tangu nyakati za kale na kwa kweli wakati wote wa historia, wayakinifu wamebaki katika upinzani dhidi ya muungano wa umoja wa waumini. Leo hii hasa zaidi ni katika muundo wa Umarx uliorahisishwa kwamba bidhaa za sayansi zimegeuzwa kuwa chombo cha udanganyifu. Wale ambao mathalan wangekuwa wapange njia yao kwenye mwanga angavu wa elimu na kutathmini mambo yote kwa utambuzi na uchunguzi wa kina na wa kimantiki, katika hali ya kutokutawaliwa kabisa na ushabiki na ubaguzi wa haraka haraka - watu hawa hasa wamenaswa katika mtego wa kuvia na kuiga kijinga. Wamekataa kwa kuonyesha kiburi tu, maadili yote yaliyo bora zaidi kuliko akili na fikra, na hata wanajivunia ukanushaji wao wa kijinga.

Madai yao kwamba kuja kwa sayansi kumeondoa ile dhana ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni ufasaha wa usemaji tu na hauhusiani chochote na utaratibu wa kimantiki, kwa sababu hata maelfu ya majaribio ya kisayansi yasingeweza kwa hali yoyote ile kutosheleza kuonyesha kwam- ba hakipatikani kuwepo kiumbe au kitu chochote kisichokuwa cha kimaada. Uyakinifu ni itikadi ya ki-metafizikia, na kwa hiyo, lazima ithibitishwe au ikanushwe kwa mujibu wa utaratibu wa kifalsafa. Kwa sababu hii haswa, ukubalikaji wa uyakinifu hauwezi kufanywa kuwa ndio msingi kwa ajili ya ukanushwaji wa metafizikia. Kutafsiri uyakinifu kwa maana kama hiyo, ni katika uchambuzi wa mwisho utakuwa hauna maana kabisa; itakuwa ni dhana ya kishirikina ikihusisha upotoshaji ukweli, na kuifikiria kama ni ya kisayansi, kwa kweli itakuwa ni uhaini kwa sayansi.

Ni kweli kwamba mpaka hivi karibuni mwanadamu alikuwa kwa kiasi kikubwa hajui vyanzo vya asili na vipengele vinavyosababisha mambo na kwamba alikuwa na utambuzi mdogo sana wa matukio yaliyojitokeza karibu yake. Lakini imani yake haikutokana na ujinga, kwani endapo ingekuwa hivyo, ile misingi juu ya kumwamini Mwenyezi Mungu ingeporomoka pale mambo fulani yahusuyo dunia yalipovumbuliwa. Kinyume chake, tunaona katika zama hizi kwamba pamoja na uvumbuzi wa miujiza mingi kuhusu maumbile, imani juu ya Mwenyezi Mungu imepanuka zaidi. Sasa sayansi inanururisha eneo finyu sana; falsafa ya maisha ya kisayansi ni ujuzi wa sehemu moja, sio ujuzi wa kitu kizima.

Sayansi inashindwa kuonyesha hali na muundo wa maumbile yote. Lakini wakati huo huo, kwa vile mtindo wa utambuzi wa kisayansi ni sahihi na wa dhahiri, imani juu ya Mwenyezi Mungu inapata asili ya kisayansi zaidi na aina mpya ya mantiki kupitia maendeleo ya sayansi. Utambuzi wa mwanadamu hupatikana kupitia uelewa wake juu ya kisababisho na athari, na mtu anayeamini katika kisababisho kilichoko chini ya kitu haiwezekani kupuuza kirahisi wajibu wa jambo la msingi ambalo linafanya kazi juu, na kuzidi visababishi vingine vyote.

Hadi hivi karibuni, mwanadamu alidhani kuwepo kwake kulikuwa ni muundo tu wenye sehemu mbili na zinazowiana vizuri sana; alikuwa haitambui miujiza yenye utata iliyokuwemo kwenye maumbile yake. Leo hii amegundua ukweli wa kustajabisha sana na wenye athari nyingi kuhusu sehemu ya ndani ya mwili wake mdogo, akitambua kwamba kuna makumi ya mamilioni ya mabilioni ya chembe chembe hai mwilini mwake. Hali hii inawezesha kuwepo mazingatio maalum juu ya utukufu wa muumba anayehusika na matokeo-sanifu haya ambayo hayakuwezekana kufanyika zamani.

Je, kuna mantiki kusema kwamba imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni ya kipekee kwa wale wasiojua chochote kuhusu kubuniwa na kuumbwa kwa mwanadamu, na kwamba kinyume chake, mwana sayansi ambaye anatambua sheria za maumbile na mambo yanayohusiana na kukua na kuendelea kwa mwanadamu, ambaye anatambua kwamba sheria na mahesabu sahihi ndio yanaongoza hatua zote za uhai wa mwanadamu, analazimika kuamini kwamba mata, pamoja na kukosa utambuzi wote na fahamu, ndio chanzo cha sheria za kustaajabisha za maumbile? Hivi ugunduzi na ujuzi wa kisayansi unasababisha mwana sayansi kama huyo kuhitimisha kwamba mata ambayo haina utambuzi na ujuzi, ndiye muumbaji wa yeye na wa viumbe vingine vyote? Uyakinifu unaitazama dunia huku jicho moja likiwa limefumbwa na, matokeo yake ni kwamba, hauwezi kutoa majibu kwa mengi ya maswali.

Pia, sayansi haitoi jibu kwa lile swali la kama dunia inaweza kugawanyika katika sehemu mbili, ya kimaada na isiyo ya kimaada, au kwa swali la kama dunia ina lengo la kimaumbile. Maswali haya hayapo kwenye nyanja ya sayansi, elimu ya kisayansi inaweza kutufahamisha sisi - kwa kiwango fulani - kwamba ni nini, lakini haitaweza kutuonyesha mwelekeo katika uhai au kutuzindua na njia ya kufuatwa. Falsafa ya maisha, ya kisayansi, kwa hiyo, haiwezi kuwa msingi wa itika- di ya mwanadamu.

Tathmini ya ujuzi wa kisayansi zaidi ya yote ni ya kimatendo, kwa vile inamfanya mwanadamu aweze kutawala maumbile. Ni mifano na tathmini ya kinadharia ndio ambayo inahitajika kama msingi wa imani. Zaidi ya hayo, sayansi imeegemea kwenye majaribio na uchunguzi, na sheria zenye kuwa na majaribio juu ya msingi wao hulazimika kubadilika na kuyumba. Imani inahitaji msingi wenye umilele, ikiwa na kinga dhidi ya mabadiliko, na iwe na uwezo wa kujibu maswali kama vile asili na umbo la dunia kwa ujumla katika namna ya kuaminika na ya kudumu. Ni hapo tu ambapo mahitaji ya mwanadamu ya tafsiri na uchambuzi wa kina wa kuwa hai unaweza kutimia.

Kadiri anavyoelekea kwenye ukamilifu, mwanadamu anahitaji uwiano wa kiroho na kiakili; bila kuwa na lengo, atapotea na kwenye njia zisizo sahihi na kujihatarishia mabalaa. Mtu asiyeweza kupata lengo lake katika dini, atafuata lengo analolielewa yeye mwenyewe ambalo halitakuwa chochote isipokuwa maasi dhidi ya matakwa ya maumbile, halitahusiana na uendelevu au ukomavu wa akili.

Sababu za ukanushaji na kutoamini Vitabu juu ya historia ya dini hujaribu kufafanua kinaga ubaga mambo ambayo yamewavuta watu kwenye dini. Lakini majaribio kama hayo wanayoyafanya hayana maana yeyote na hayawezi kufichua ukweli wenyewe wa mambo. Ni muhimu kushabahia kwenye muelekeo wa asili wa mwanadamu kwenye imani ya mungu mmoja, ile sifa ya kiuhai ya jamii za wanadamu ambayo humpa mwanadamu - pamoja na tofauti zake zote ndani yake, fikira na matamanio yake - sehemu maalumu katika maumbile. Hapo ndipo inapowezekana kugundua mambo ambayo humwongoza mwanadamu kuikanyaga asili yake mwenyewe kwa kukataa dini, kwa viapo kabisa.

Mahusiano ya kidini ya mwanadamu ni matokeo ya asili yake, na uyakinifu ni kitu kinachopingana na maumbile yake. Kwa kulingana na tabia yake ya dhahiri, binadamu atajiumbia mungu wake mwenyewe kama hatamgundua Mungu wa kweli, na mungu anayemgundua yeye anaweza kuwa ni maumbile au mambo ya kihistoria yasiyoepukika. Na mungu huyu wa uwongo anachukua nafasi ya Mwenyezi Mungu wa kweli kwa kuzingatia ufahamu na mamlaka, kufaa kwa maagizo, na uwezo wa kumwongoza mtu kwenye njia fulani na kumsogeza mbele, bila kuzuiwa na matakwa ya mtu yeyote.

Huu ndio mwanzo wa kubadilishana miungu wa uwongo, ufuasi kwenye uabudu masanamu upya, ambao ungemtoa kafara Mwenyezi Mungu kikatili kwenye historia na kubadilisha lulu kwa shanga. Inasikitisha kwamba, watu wengi waliojiangamiza kwa unyonge waliojiingiza wenyewe wakawa wameinama chini mbele ya sanamu ambalo wameliunda wenyewe na kulifanya kuwa mungu! Wamempa kisogo muumba asiye na kifani na kwa hiari yao wakakubali fedheha inayochafua ya ibada iliyoongozwa vibaya kama hiyo.

Kama tukilichunguza jambo hili kwa ukaribu zaidi, tunaona kwamba kujitokeza kwa uyakinifu huko Ulaya kama kitivo cha fikra, ukatwaji wa uhusiano wa binadamu na kanuni ilioyo tukufu, kufungwa kwao kwenye nyororo za maada, kuchagua kuendekeza sayansi mahali pa dini - yote haya yalisababishwa na mlolongo wa mambo ya kijamii na kihistoria yaliyojitokeza katika nchi za magharibi.

Mojawapo ya mambo yaliyoamsha upingaji wa mabadiliko ulioenea katika Ulaya yote na kusababisha kutokeza kwa fikra zisizofuata dini na propaganda dhidi ya dini, ilikuwa shinikizo baya mno lililowekwa na mamlaka za kikanisa mwanzoni mwa kipindi cha mwamko-sanaa juu ya wasomi waliokuwa wanaleta mawazo mapya ya kisayansi. Kwa kuongezea kwenye mafundisho maalum ya kidini, kanisa pia liliwiwa shukrani kwa ajili ya kanuni fulani za kisayansi kuhusu mwanadamu na dunia ambazo lilizirithi kutoka kwa wanafalsafa wa kale - hasa wa Kigiriki - na ambazo ziliwekwa katika ulinganifu sawa na imani za dini. Nadharia yoyote iliyojitokeza kupingana na Biblia na hizi kanuni zilizorithiwa zilifikiriwa kama za uasi, na yeyote aliyezitetea angeadhibiwa vikali.

Upinganaji wa dhahiri baina ya dini na sayansi ulianzisha uadui wa pamoja katika pande hizi mbili. Wasomi na wanasayansi waliona kwamba Kanisa la Kikristo lilikuwa linazifunga akili na fikra, na kuzuia maendeleo huru ya mawazo; kupitia kwenye ufuasi wake wa mfumo unaoogofya wa fikra na desturi ya kwenda kinyume na akili, lilikuwa linatengeneza mazingira yenye kusonga kwa ajili ya mwanadamu wa zama hizo mpya. Hivyo, mabingwa walikimbilia kwenye kujitenga kunakohuzunisha kutoka kwenye dini.

Mashinikizo haya yaliyokuwa yakilimbikizana kwa siku nyingi, hatimaye yalisababisha majibu ya vurugu zilizoikumba Ulaya yote. Hapo ndipo nguvu na utawala wa Kanisa ulididimia na uonevu wake ulikoma, uhuru wa fikira za kimagharibi ulipatikana tena na ulionyesha hisia kali dhidi ya mipaka iliyokuwa imewekwa hapo mwanzoni. Wasomi waliondoa nyororo zote za taratibu za kizamani toka kwenye shingo zao na wakatoka kwenye dini. Maumivu na hasira zote walizokuwa wamezipata zilidhihiri kwenye wimbi kubwa la uadui dhidi ya dini. Hali ya wasi wasi mkubwa wa kiroho ilianza ambayo ilifikia kilele katika kutenganishwa sayansi na dini. Tamaa ya kisasi kisicho na mantiki dhidi ya dini kilisababisha kukanushwa kwa ukweli mwingi wa ki-Mungu na wa imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.

Ni kweli kwamba baadhi ya mafundisho yaliyounganishwa na dini hayakuwa na mantiki au hata msingi, yakiwa hayana uhusiano na ujuzi wa kidini uliothabiti. Lakini kulipiza kisasi juu ya Kanisa ni jambo moja na kuangukia kwenye chuki haraka na kwa makosa dhidi ya dini, kama hivyo, ni kitu kingine tofauti. Ni dhahiri kwamba kulipa kisasi, kukiwa ni jambo ambalo linatokana na hisia, halina uhusiano wowote na ufasaha wa kisomi.

Umasikini wa kiroho wa mwanadamu uliongezeka kwa kiwango kinacholingana na utajiri wake wa kisayansi na kiteknolojia. Jinsi alivyoendelea katika viwanda vingi, ndivyo maadili na nguvu yake ya kiroho vinazidi kupungua, hadi kufikia kiwango ambapo alikosa uwezo wa kimaadili wa kuweza kutumia inavyostahili ujuzi wake mpya alioupata. Ujuzi wa kisayansi haujishughulishi na maadili, mtu hawezi kuamua kazi za mwanadamu mwenye kuwajibika kwa kutumia kigezo cha sayansi. Sayansi hata ifike mbali vipi, bado haina uwezo wa kuona hata hatua moja mbele yake. Ujuzi wa kibinadamu hauwezi kufika kwenye chimbuko la dunia na kutambua kwa ufasaha yaliyomo, wala hauwezi kutabiri mustakabali wa baadaye wa mwanadamu.

Ni falsafa ya maisha ya Mungu Mmoja tu ambayo haijaribu kumfungia mwanadamu kwenye vipengele vya kimaada vya maisha yake. Kinyume chake kupitia kwenye ishara na dalili ambazo mwanadamu amepewa ili zimwongoze katika njia yake, imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, inaonyesha utukufu wa asili na mustakabali kwa ajili ya mwanadamu.

Mara tu mwanadamu anapoingia kwenye njia ya kumwamini Mwenyezi Mungu, hupata falsafa ya maisha pana ndani ya mfumo ambamo huweza kupata majibu kuhusu swali lake la msingi la ki-uchunguzi. Mara akishafikia hatua hii ya imani pana na yenye vipimo vingi, maisha yake mwanadamu huchukua juhudi mpya na maadili ambayo ndio matunda mazuri ya hiyo falsafa ya maisha huja kuwa kweli. Mapambano na kanisa yalikuwa kwa hiyo, kipengele kimoja katika kutenganisha sayansi na dini. Kundi lingine liliitekeleza dini na kukimbilia kwenye uyakinifu kwa sababu mawazo yaliyoshauriwa na Kanisa hayakuwa sahihi na hayaku- tosheleza, yaliyokosa na maadili yaliyo nje ya uwezo wa mwanadamu.

Mawazo haya kwa kawaida yalionekana kutokubalika na yasiyovutia kwa watu wenye akili. Kanisa lingemwonyesha Mwenyezi Mungu katika hali ya maada na kibinadamu kwa maana ambayo ilipingana na haja ya mwanadamu juu ya maadili kamili na kule kujitahidi kupenya na kuvuka mifumo yote yenye kuweka mipaka. Hapawezi kuwa na shaka kwamba endapo ukweli usiopingika unaingizwa kwenye ubongo wa mtu katika muundo wa hekaya wenye dosari, mtu huyo atakwenda kinyume nao mara tu atakapofika ukomavu wa kiakili.

Wakikabiliwa na taswira ya Mungu mwenye kupachikwa umbo la kibinadamu, iliyotengenezwa katika theolojia ya Ukristo, kutukuza imani zaidi kuliko matumizi ya akili na msisitizo kwamba imani lazima itangulie akili, watu walioelimika walitambua kwamba jitihada hizi zitokanazo na akili finyu, kwa lengo la kuzuia matumizi ya busara na sayansi katika ukiritimba wa theolojia ya Kikristo hazikuendana na kigezo cha mantiki na mbinu ya kisayansi. Kwa vile hazikuwa na chanzo thabiti ambacho kutokana nacho wangejifunza mafundisho ya kweli kuhusu Mwenyezi Mungu, yote yakiwa huru kabisa kutokana na taasisi za Kanisa na vitabu vyake vipotovu, na kwa kuwa hawakuwa na njia ya kuwafikisha kwenye mfumo ulio bora zaidi ambao ungeweza kutosheleza mahitaji yao ya kiroho na kimwili na kuwapa muundo unaofaa kwa ajili ya kuunganisha vipengele vyote muhimu vya maisha, vya kimwili na kiroho, hisia na kiakili, falsafa ya maisha ya uyakinifu iliota mizizi ndani yao, na kuwaelekeza kukana maadili yote yaliyo nje ya uwezo wa kibinadamu na yaliyo zaidi kinyume cha ubinadamu.

Walikuwa hawatambui kwamba ingawa kosa hupotosha dini wakati linapofuata njia ya ujinga, dini ya ukweli, isiyokuwa na uwongo wowote, ushirikina na upotovu inaweza kumkomboa mwanadamu kutoka kwenye utumwa wa visasili na ushirikina, na kumshikilia kwa umadhubuti kwenye mhimili wa imani ya kweli na kumpatia uelewa sahihi wa mafundisho yahusuyo Mwenyezi Mungu, ambayo hutosheleza akili yenye udadisi. Badala yake, wasomi wa nchi za Magharibi walitambua upande moja tu wa ushirikiana wa dini ya uwongo na jinsi mfumo ulioundwa wa imani wa dini, usio na kuswali, ulivyokosa kuwa na msingi wa kimantiki, kwa hiyo hawakusita kushutumu dini kwamba haina msingi wowote. Uamuzi wao uliegemezwa kwenye ile hali halisi ya kukatisha tamaa iliyomo kwenye dini yao wenyewe, na uamuzi huo haukuweza kushindwa kuwa wa haraka, usio wa kweli, usio na busara na mantiki.

Haya yamefafanuliwa ifuatavyo na msomi wa fiziolojia na biokemia: "Ukweli kwamba wasomi fulani hawakuongozwa, katika njia ya utafiti wao, kwenye utambuzi wa kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, una sababu nyingi sana. Hapa tunataja mbili miongoni mwa hizo. Kwanza; hali ya kisiasa iliyotengenezwa na udikteta, pamoja na hali zinazoambatana na mambo ya kijamii na kiutawala, zilielekea kumsababisha mwanadamu kukana kuwepo kwa Muumbaji. Pili, mawazo ya mwanadamu wakati wote yamekuwa yakivutiwa na njozi fulani na uwongo, na ingawa mwanadamu anaweza kuwa hana woga wa maumivu makali ya kiroho na kimwili, bado hana uhuru kamili wa kuchagua njia iliyonyooka.

"Katika familia za Kikristo, watoto wengi huamini kuwepo kwa Mwenyezi Mungu afananaye na mwanadamu, kana kwamba mwanadamu aliumbwa katika umbo la Mwenyezi Mungu. Wanapoanza kuingia kwenye nyanja ya sayansi na kujifunza na kutekeleza fikira za kisayansi, hawawezi tena kupatanisha dhana yao dhaifu ya kumpa Mwenyezi Mungu viungo vya mwanadamu na ushahidi wa kimantiki na mbinu za sayansi. Kwa hiyo baada ya muda fulani, wakati ambapo matumaini yote ya kupatanisha imani na sayansi yanatoweka, wanaitelekeza kabisa fikira yote ya Mwenyezi Mungu na kuifuta kabisa kwenye akili zao. "Sababu yake kubwa ni kwamba ushahidi wa mantiki na aina za sayansi hazirekebishi hisia na imani zao za mwanzoni, lakini badala yake, huwafanya wahisi kwamba walikosea katika imani yao ya mwanzo kuhusu Mwenyezi Mungu. Kwa mvuto wa hisia hizi, ikiunganishwa na mambo mengine ya kisaikolojia, wanashangazwa na upungufu wa fikra zao na huachana kabisa na majaribio ya namna yoyote ya kumjua Mwenyezi Mungu.[25] .

Kwa hiyo, wanasayansi, walijaribu, kwa kufafanua aina zote za sheria na fomyula na kutoacha nafasi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na dini katika kutafuta ufumbuzi wa maswali yanayogusa kuwepo uhai na maumbile. Walijaribu kukatisha matumaini ya wanadamu kutoka kwenye dini na kumweka kando Mwenyezi Mungu katika kuwa na wajibu wowote katika utendaji wa ulimwengu na mpango wa maumbile.

Kila walipofikia kukwama walijaribu kutafuta ufumbuzi wa tatizo kwa kutumia nadharia tete mbali mbali au kuahirisha ufumbuzi bayana wa tatizo hadi hapo utafiti mkubwa zaidi utakapokuwa umefanywa. Walidhani kwamba kwa njia hii walikuwa wanaepuka kujisalimisha kwenye fomyula isiyo ya kisayansi na ushirikina. Hivyo, ingawa waliepuka hatari ya kukubali ushirikina, kwa masikitiko walianza kupiga vita upagani na ukana-Mungu.

Ingawa imani juu ya Mwenyezi Mungu na kuamini katika kanuni ya uasilishaji ni jambo la kawaida na msingi kwa mwanadamu, haliwezi kulinganishwa na mahitaji ya kimaada ambayo mwanadamu wakati wote anajitahidi kuyapata. Liko tofauti kabisa na maisha ya kimaada, na kwa kuwa ni hitajio la ndani ya mwanadamu, linahusiana na namna tofauti kabisa. Zaidi ya haya, ni rahisi kukanusha kitu kisichoonekana kwa macho kuliko ilivyo kwa kukithibitisha, tukichukulia kutoweza kwetu kukielezea vya kutosha. Watu wanaokosa uwezo wa kiakili, kwa hiyo, huchagua njia rahisi na isiyo na usumbufu ya kukataa badala ya kujitahidi kutumia akili. Njia ya kukanusha aidha, haihusishi madhara yoyote yaliyodhahiri. Kwa kugeukia mbali na Mwenyezi Mungu, watu pole pole hujenga msimamo wa ukaidi na uadui kwenye dini, ulioathiriwa na ushabiki. Athari kubwa za msimamo kama huo zinaweza kuonekana kwa urahisi kwenye hoja zenye uovu za wale ambao wameipa mgongo dini.

Pia ni rahisi zaidi kukana kitu kisichoonekana kwa sababu kukithibitisha kuwepo kwake kutamaanisha wajibu mbali mbali kwa mwanadamu, wale wanaotaka kuzitupilia mbali wajibati hizo, kwa urahisi hukataa kuwepo kwa kanuni ya uanzishaji. Qur'anii inasema:

بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ ﴿٥﴾ يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ ﴿٦﴾ فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ ﴿٧﴾

"Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilizioko mbele yake. Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama? Basi jicho litapoduwaa." ( Qiyama:75: 5-7).

Mafundisho ya wale wataalamu wa kujihini, wajinga na wasio na mantiki pia hayawezi kutoonekana kama kipengele kinachosukuma vikundi fulani vya watu kuelekea kwenye uyakinifu. Zile silika zinazokuja kuwepo pamoja na maisha ya kawaida ya mtu ambazo zimefungamanishwa na uhai wake, si tu kwamba hazikosi maana na lengo; zenyewe pia ni nguvu ya kuumua na kuandaa takdiri, kipengele cha maendeleo na msogeo, ambacho ndio humsukuma mtu na kusonga mbele kuelekea kwenye lengo lililozingatiwa katika kuumbwa kwake. Ni kweli kwamba, mtu hatakiwi kuwa mtumwa aliyefunikwa macho kwenye silika zake kama mfungwa ambaye uhai wake wote na nyendo vinadhibitiwa na mwangalizi wa jela. Lakini, pia hapaswi kupigana vita na ukweli wa uhai wake mwenyewe na kutafuta kuzuia shughuli zote na nyendo kwa upande wa silika zake. Uhai wa mwanadamu wenye matunda mazuri, kwa kweli hutegemea juu ya kuwepo hai katika maisha yake kwa silika zake, zilizoenea kwa uwiano unaofaa; kuzuia silika kunasababisha utata na uharibifu wa haiba ya mtu.

Falsafa ya maisha iliyokuwepo kwenye Ukristo katika kipindi cha kati ilikuwa kwenye msingi wa maelekezo ya mazingira pekee ya Akhera ambayo yaliingiza na ushushaji thamani wa dunia ya kimaada. Sasa, matokeo yatakuwaje endapo mtu anakanusha uhalali wote wa nguvu za silika, kwa jina la Mwenyezi Mungu na dini, akajaribu hata kuziharibu kabisa; kama mtu anatukuza useja na maisha ya utawa na akakanusha hadharani ndoa na kuzaana kama ni uchafu, shughuli yenyewe hasa ambayo ndiyo inayolinda uhai wa spishi mbali mbali; na kama mtu anaona umasikini na kutojiweza kama ndio uhakikisho wa furaha ya hali ya juu? Je, kwa hiyo, itawezekana kutegemea dini kuchukua jukumu mashughuli na endelevu?

Jukumu halisi na kazi ya dini ni kusafisha, kuongoza na kudhibiti silika, kuwekea mpaka wa eneo la ushughulikaji wao, na kuzitakasa na upotofu na uovu wote. Sio kuziharibu na kuziondoa kabisa. Kwa kuzidhibiti silika na kujitahidi wakati wote kujinasua mwenyewe kutoka kwenye mtego unaoweza kuwepo, mwanadamu hujitengenezea hatima yake yenye lengo. Endapo mwanadamu anashindwa kufanya hivi, mgongano mkubwa wa silika ndani mwake ni mkubwa mno hivyo kwamba hawezi kuwa mdhibiti wa nafsi yake mwenyewe kwa urahisi. Kwa hiyo, anahitaji mfumo wenye maarifa mengi juu ya elimu ya maadili. Kwa upande moja binadamu anapatwa na mvuto wa shauku ya kidini, hali hii, humtiisha kwa siri na huzikusanya pamoja zile nguvu zake zilizotawanyika, kwenye mshiko wa uwezo wake, na kuzielekeza kwenye kupata maadili na manufaa. Kwa upande mwingine binadamu pia anapatwa na mvuto wa silika zake.

Katika jamii yoyote ambamo watu wakati wote wanaambiwa, kwa jina la Mwenyezi Mungu na dini, kwamba njia ya kwenye furaha ipo katika kuzikataa zawadi za dunia hii, mwanya unajitengeneza wenyewe kwa ajili ya maendeleo ya uyakinifu na umakinifu zaidi juu ya thamani ya vitu vya kimaada, ili kwamba zile fikra tukufu za dini, pamoja na athari zake zenye kufika mbali, zitoweke kwenye mazingira.

Lakini, hii haiwakilishi mantiki halisi ya dini. Dini za kweli huelekeza mazingatio ya mwanadamu kwenye maadili thabiti ya kiroho, yakijiegemeza katika imani juu ya muumbaji na kumpatia mtu mafundisho mapana na kanuni kwa ajili ya maisha yake. Maadili haya hupanua uwanja wa uoni wake hadi kwenye mipaka ya eneo la ki-mbingu, na kumtoa kutoka kwenye utumwa wa kuabudu matamanio yake mwenyewe na anasa za kidunia (uyakinifu), na wakati huo huo, yanamruhusu afurahie starehe za kidunia kwa kiasi cha kutosheleza tu.

Baadhi ya watu wanadhani kwamba starehe holela juu ya vitu fulani ambavyo vimepigwa marufuku na dini itawahakikishia kudumu furaha yao. Wanafikiri kwamba dini inapigana kwa ukaidi dhidi ya starehe zote na haiko tayari kukubaliana raha za dunia hii, kana kwamba Mwenyezi Mungu anamlazimisha mwanadamu kuchagua kati ya furaha ya hapa duniani na furaha ya Akhera. Mwelekeo huu kwenye dini ni wa unapotoshaji kabisa usiowezekana kuwa kweli. Ikiwa dini kuwajibika katika jitihada za binadamu na uchaguzi wake wa mwelekeo, ni kwa sababu kujiendekeza kusikozuilika kwenye matamanio, kujisalimisha bila masharti kwenye silika na hamu, na utiifu kwenye amri za umimi, hutia giza maisha ya mtu na humpeleka kwenye hali ya utumwa wa kutojitambua. Licha ya asili yake safi kimsingi, anaanguka kutoka kwenye daraja lake halisi na kukengeuka kutoka kwenye njia yake ya kweli. Kama kule kujiendekeza kiholela kwenye silika za matamanio kungekuwa sio sababu ya mateso ya milele na kujivunjia hadhi kuchungu, kusingeweza kukatazwa.

Ni fikira kama hizi ambazo zinafanya iwezekane kuelewa ni kwa nini dini imekataza mambo fulani na ni jinsi gani starehe ya dunia ilivyo na ulinganifu na furaha ya Akhera. Fikira kama hizi hutumika katika kumlazimisha wajibu fulani juu ya mwanadamu. Jaribio ya kutekeleza matendo ya faradhi ya ibada, kwa uaminifu na bila unafiki, huleta mabadiliko ya ndani kabisa mwa mtu, lengo la matendo haya kwa namna yoyote sio kupunguza furaha ya mtu ya kidunia.

Kuabudu ni sawa na tufani kali kwenye dimbwi (wangwa) tulivu la moyo, inayobadilisha tabia ya ndani ya mwanadamu na kigezo chake cha maamuzi. Ndiyo jiwe la pembeni ambapo msingi wa dini huimarishwa, mazoezi ya kuelimisha yenye manufaa yanayopenya kwenye vina virefu vya nafsi. Upanga wake mkali hukata fundo la upotofu na udhalili ndani ya binadamu na kumwezesha yeye kukimbilia eneo pana na safi, lisilo na mipaka. Kwa ufupi humwezesha mwanadamu kukua na kufikia ukomavu halisi.

Si tu kwamba hakuna mikinzano kati ya mambo ya maisha na yale ya kiroho; mambo ya kiroho yanafaa sana kwenye maisha ya furaha kubwa zaidi hapa duniani. Inaweza kuwa labda kwamba mafundisho yasiyoaminika na yasiyo na mantiki ya Ukristo yameathiri mielekeo ya kinyume na dini ya watu kama Betrand Russell. Kwa dhahiri aliamini kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni kujitakia huzuni, kama inavyodhihirika katik a maneno yafuatayo: "Mafundisho ya Kanisa yamefanya binadamu achague baina ya aina mbili ya mateso na umasikini. Ama mateso ya hapa duniani na kukosa starehe zake au mateso ya maisha ya akhera na kukosa furaha ya peponi.

Kuhusu Kanisa, mojawapo ya aina hizi mbili za mateso lazima na muhimu ivumiliwe. Ama mtu lazima ajisalimishe kwenye mateso ya hapa duniani na kuteseka kwa umasikini na upweke ili aweze kufurahia starehe za akhera, au, ikiwa mtu anataka kufurahia starehe za dunia hii lazima akubali kwamba atanyimwa starehe za akhera." Ueneaji wa maoni kama haya, ambayo yanadhihirisha ujinga mkubwa sana na wa kina falsafa ya maisha kidini, kunaweza kuamua hatima ya dini iliopo katika jamii fulani. Athari za maoni haya kwa itikadi na matendo ya binadamu ni nzito sana kuweza kupimwa vizuri, kwa mtazamo wa mpito wa juu juu. Muundo huu wa fikira umesababisha mazingatio ya mwanadamu kuelekezwa kipekee kwenye nyanja ya kimaada - awe anatambua au hatambui. Umakinifu unaojitokeza juu ya starehe na anasa umesababisha kudhoofika kwa mambo ya kiroho na maadili.

Dini haimshutumu mtu kuvumilia mojawapo ya aina mbili hizi za mateso. Inawezekana kabisa kuunganisha furaha ya dunia hii na ya Akhera. Kwa nini, Mwenyezi Mungu Ambaye hazina yake ya huruma na neema haipungui, asitake waja Wake wapate furaha kamili ambayo inakusanya dunia hii na Akhera? Hivi ndivyo kwa usahihi hasa anavyopenda Yeye.

Jambo lingine katika kuenea kwa fikira za kiyakinifu limekuwa ni uendekezaji wa tamaa na kuzama kwenye shimo la ashiki. Kila utambuzi wa kiakili na mawazo hufanya msingi wa baadhi ya matendo ya nje; njia ya matendo ya mwanadamu huchukua umbo la njia ya mvuto wa itikadi zake. Kinyume chake matendo na maadili ya mwanadamu pia huleta mabadiliko yenye ubora katika tabia yake ya kiakili na muundo wa fikira. Mtu anayeabudu matamanio yake polepole atapoteza mawazo yote matukufu kuhusu Mwenyezi Mungu. Mara tu anapochagua mhimili wa uhai wake kinyume na Mwenyezi Mungu na kudhania kwamba chochote kilichopo katika dunia hii, kimetupwa hivi hivi tu juu yake, bila madhumuni yoyote, hivyo kwamba wazo la kuwa na lengo katika maisha linakuwa halina maana kabisa, huanza kutoa uwezo wake wote wa kiakili katika kufanya starehe kwa wingi zaidi. Kutumbukia huku kunakofedhehesha, kwenye kiwango cha chini cha maisha, kunanyausha mizizi ya matumaini yote kwa ajili ya makuzi na maendeleo.

Mawazo ya kumwamini Mwenyezi Mungu; kwa kulinganisha, ni kama mbegu ambayo inahitaji udongo unaofaa ambamo inaweza kumea. Mbegu hiyo inaweza tu kustawi kwenye mazingira safi, mazingira ambamo mwanadamu anaweza kupata kwa haraka na urahisi kiwango cha ubora ambao ni wa kipekee kwake, kwa sababu ya muundo ambamo kanuni za maisha yake zimewekwa. Imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, haiwezi kustawi kwenye mazingira yaliyo jaa uovu.

Mojawapo ya vipingamizi vinavyo mzuia mtu asipate kumjua Mwenyezi Mungu na sababu za mwanadamu kukanusha kuweko huku, pamoja na kuwepo dalili zilizowazi na ushahidi wenye maamuzi ambao upo, kwa hiyo, ni kujisalimisha kwenye dhambi na kuendekeza matamanio. Imam Jafar as-Sadiq(a.s) alisema alipomjibu Mufadh'dhal ndani ya Risalah-yi Ahlija: "Ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba Mwenyezi Mungu hajashindwa kujijulisha Yeye kwa wasiomjua, kwani wanaona ushahidi dhahiri na ishara zisizo na shaka za Muumba katika mumbile Yake na wanatazama mambo ya ajabu katika Ufalme wa angani na duniani ambayo yanaelekeza kwa Muumba wao.

"Watu wajinga ni wale ambao wamefungua milango ya dhambi mbele yao na wakafuata njia ya kujiendekeza kwenye tamaa na ashiki. Matamanio ya nafsi zao yametawala nyoyo zao, na kwa sababu ya dhulma zao juu ya nafsi zao wenyewe shetani amechukua mamlaka juu yao. Mwenyezi Mungu amezipiga muhuri nyoyo za waovu."[26]

Tamaa ya starehe, ushindani, ubadhirifu, mantiki dhaifu ya waumini fulani wasio na elimu - hawa pia ni miongoni mwa vipengele vinayomlazimisha mwanadamu kukimbilia uyakinifu. Ghasia na mchafuko wa maisha, wingi wa bidhaa zinazozalishwa, utajiri na mamlaka, mielekeo ya maisha ya kisasa inayozuzua na kushughulisha, kuenea haraka kwa vitu vya anasa na starehe - yote haya yanawafunikiza kabisa watu walafi. Watu hawa wanajaribu kabisa kujitoa kwenye mazingira ya masuala ya kidini na hukataa kukubali mamlaka ya madaraka yoyote makubwa zaidi, kwani si tu kwamba hii isingewaletea manufaa yoyote ya kidunia, bali pia ingeshika hatamu kwenye mawimbi ya matamanio yao yaliyokomaa.

Kwenye mazingira ambayo watu wamezama kwenye dhambi, ufujaji, na uovu, na wakakataa kukubali mipaka yoyote inayotawala matendo yao, dini itabakia jina tu. Watu wanaojiendekeza na wayakinifu hawawezi kuwa wenye kumtafuta na kumwabudu Mwenyezi Mungu. Wakati ambapo mojawapo ya kanuni mbili zinazopingana; kanuni ya kusaka anasa na ile ya kumwamini Mwenyezi Mungu, inapokuwa imetawala nafasi ya akili ya mhusika, kanuni nyingine lazima iondoke humo. Mara tu moyo wa kuabudu unapokuwa katika maisha ya mwanadamu, huiondoa mielekeo yote ya kiyakinifu kwa kuzikata pingu imara za matamanio duni na wakati wote hutia msukumo juhudi ya mtu kupanda kuelekea kwenye lengo lake. Hivyo, muundo kamili wa uhuru wa binadamu wa kutoka kwenye utumwa na kuingia kwenye hali ya asilihujitokeza.

Jinsi lengo analojiwekea mtu mwenyewe linavyokuwa la juu na la mbali zaidi, ndivyo mwelekeo wa kuliendea utakavyo kuwa mkali zaidi na ndivyo jitihada inayohitajika ili kulifikia itakavyozidi kuwa kubwa zaidi na ya muda mrefu zaidi. Kwa hiyo, kama tunamchagua Mwenyezi Mungu kama lengo letu, tutakuwa tumechagua lengo la hali ya juu lisilo na ukomo, na njia inayoelekea kwenye mafanikio ya lengo hilo vivyo hivyo itakuwa haina ukomo, ingawa njia hiyo ni wazi na iliyonyooka wakti huo huo.

Ni lengo ambalo litajibu matatizo na maswali mengi, na kwa kuwa litatulazimisha kukataa udhalimu wa nafsi, utatupatia uhuru kamili juu yetu. Kama tukimkubali Mwenyezi Mungu kama ndio lengo letu, uhuru utapatanishwa na makuzi na maendeleo yetu. Juhudi zetu za kujiendeleza na kupiga hatua zitakuwa na maudhui na maana, kwa msaada wa silika za kiungu na tamaa ya uzima wa milele. Kwa ufupi, tamaa ya kupiga hatua na maendeleo, mara tu inaporekebishwa na ibada ya Mwenyezi Mungu, ama kwa hakika haipingani na uhuru wa binadamu wala haiishii kwenye yeye kuwa mtumwa.

Tunaweza kudai kuwa tumepata uhuru hapo tu tunapokuwa tunakwenda sambamba na kusonga mbele kwa ujumla kwa dunia yote kuelekea kwenye ukamilifu, kwa akili, na utambuzi kamili wa manufaa yatakayoletwa na hatua hii. Kufanya matendo kwa kutii hali ya asili au kwa kutoepukika kwa historia sio uhuru, kwani wakati mwanadamu anapoacha kujali ustawi wake mwenyewe kwa kufuata maamuru ya maumbile, hili si jingine mbali na utumwa au utii wa kijinga.

8

MWENYEZI MUNGU NA SIFA ZAKE

SOMO LA NANE

FITINA BANDIA ZA KISAYANSI

Watu wa maada wanasema kwamba kuasisiwa kwa kitivo chao cha fikra mnamo karne ya 18 na 19 kulihusiana moja kwa moja na maendeleo ya sayansi na kwamba ile mbinu pembuzi ilikuwa ni tunda ambalo lilichumwa kutoka kwenye mti uliostawi vizuri wa sayansi.

Wanaonyesha kila falsafa mbali na uyakinifu kama aina ya udhanifu, unaopingana na mbinu ya fikra ya kisayansi, na wanasisitiza kwamba msimamo wao ni wa kisayansi na endelevu. Kwa mujibu wa msimamo wao, uhalisia unategemea katika kukengeuka kutoka kwenye ukweli wa metafizikia; kila mtu anapaswa ategemeze falsafa yake ya maisha juu mantiki ya fahamu na majaribio na kuchagua uyakinifu. Lakini madai haya si lolote zaidi ya ndoto za kishabiki ambazo zimetegemezwa kwenye nadharia zisizothibitishwa. Mawazo kama haya yanakuja moja kwa moja kutoka kwenye mfumo wa fikra uliolenga kwenye uyakinifu; ambamo ndani yake, kila kitu kimeainishwa na kuwekewa mipaka kwa mujibu wa uyakinifu.

Imani kuhusu kitu cha kuabudu bila shaka ni mojawapo ya vyanzo vikuu vya utamaduni na elimu ya mwanadamu. Kupendekeza imani juu ya Mwenyezi Mungu kama msingi wa falsafa ya maisha kumesababisha mabadiliko makubwa katika misingi ya jamii na fikra katika historia yote ya binadamu. Sasa, pia, katika zama za sayansi na teknolojia, ambapo mwanadamu amekwishagundua kwenda angani, idadi kubwa ya wanasayansi wanao mtazamo wa kidini kama sehemu ya mfumo wa kisomi; wamekuja kuamini juu ya kuwepo kwa muumbaji, chanzo cha viumbe vyote, sio tu kwa njia ya moyo na dhamira, bali pia kupitia maamuzi na mantiki.

Kama uthibitisho wa wayakinifu juu ya falsafa yao ya maisha ungekuwa wa kweli, badala ya kutegemea kwenye ujuzi pungufu wa historia ya fikra za uyakinifu, panapaswa pawepo na uhusiano maalumu baina ya sayansi na mwelekeo kwenye uyakinifu; ni mawazo ya kiyakinifu tu yangewakilishwa kwenye nyanja ya kisayansi. Hivi kila mwana falsafa na msomi, katika kila kipindi, alishikilia falsafa ya maisha ya ukana-Mungu na akawa mtu wa kambi ya wayakinifu. Uchunguzi wa kisomi wa maisha na kazi za wanafikra wakubwa zitatosha kuonesha kwamba fulan kwamba kambi ya kidini kwa hali yoyote haina wanasayansi wa kweli, lakini pia kwamba wanafikra wa kisayansi wakubwa na watu wengine maarufu, wakiwa ni pamoja na waasisi wa nyingi ya sayansi ya wakati huu, wamekuwa na imani juu ya mungu mmoja.

Kwa nyongeza, itikadi za kiyakinifu na ukana-mungu kwa namna yoyote zimewekewa mipaka kwenye kipindi cha mageuzi na mendeleo ya sayansi, tangu nyakati za kale na kwa kweli wakati wote wa historia, wayakinifu wamebaki katika upinzani dhidi ya muungano wa umoja wa waumini. Leo hii hasa zaidi ni katika muundo wa Umarx uliorahisishwa kwamba bidhaa za sayansi zimegeuzwa kuwa chombo cha udanganyifu. Wale ambao mathalan wangekuwa wapange njia yao kwenye mwanga angavu wa elimu na kutathmini mambo yote kwa utambuzi na uchunguzi wa kina na wa kimantiki, katika hali ya kutokutawaliwa kabisa na ushabiki na ubaguzi wa haraka haraka - watu hawa hasa wamenaswa katika mtego wa kuvia na kuiga kijinga. Wamekataa kwa kuonyesha kiburi tu, maadili yote yaliyo bora zaidi kuliko akili na fikra, na hata wanajivunia ukanushaji wao wa kijinga.

Madai yao kwamba kuja kwa sayansi kumeondoa ile dhana ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni ufasaha wa usemaji tu na hauhusiani chochote na utaratibu wa kimantiki, kwa sababu hata maelfu ya majaribio ya kisayansi yasingeweza kwa hali yoyote ile kutosheleza kuonyesha kwam- ba hakipatikani kuwepo kiumbe au kitu chochote kisichokuwa cha kimaada. Uyakinifu ni itikadi ya ki-metafizikia, na kwa hiyo, lazima ithibitishwe au ikanushwe kwa mujibu wa utaratibu wa kifalsafa. Kwa sababu hii haswa, ukubalikaji wa uyakinifu hauwezi kufanywa kuwa ndio msingi kwa ajili ya ukanushwaji wa metafizikia. Kutafsiri uyakinifu kwa maana kama hiyo, ni katika uchambuzi wa mwisho utakuwa hauna maana kabisa; itakuwa ni dhana ya kishirikina ikihusisha upotoshaji ukweli, na kuifikiria kama ni ya kisayansi, kwa kweli itakuwa ni uhaini kwa sayansi.

Ni kweli kwamba mpaka hivi karibuni mwanadamu alikuwa kwa kiasi kikubwa hajui vyanzo vya asili na vipengele vinavyosababisha mambo na kwamba alikuwa na utambuzi mdogo sana wa matukio yaliyojitokeza karibu yake. Lakini imani yake haikutokana na ujinga, kwani endapo ingekuwa hivyo, ile misingi juu ya kumwamini Mwenyezi Mungu ingeporomoka pale mambo fulani yahusuyo dunia yalipovumbuliwa. Kinyume chake, tunaona katika zama hizi kwamba pamoja na uvumbuzi wa miujiza mingi kuhusu maumbile, imani juu ya Mwenyezi Mungu imepanuka zaidi. Sasa sayansi inanururisha eneo finyu sana; falsafa ya maisha ya kisayansi ni ujuzi wa sehemu moja, sio ujuzi wa kitu kizima.

Sayansi inashindwa kuonyesha hali na muundo wa maumbile yote. Lakini wakati huo huo, kwa vile mtindo wa utambuzi wa kisayansi ni sahihi na wa dhahiri, imani juu ya Mwenyezi Mungu inapata asili ya kisayansi zaidi na aina mpya ya mantiki kupitia maendeleo ya sayansi. Utambuzi wa mwanadamu hupatikana kupitia uelewa wake juu ya kisababisho na athari, na mtu anayeamini katika kisababisho kilichoko chini ya kitu haiwezekani kupuuza kirahisi wajibu wa jambo la msingi ambalo linafanya kazi juu, na kuzidi visababishi vingine vyote.

Hadi hivi karibuni, mwanadamu alidhani kuwepo kwake kulikuwa ni muundo tu wenye sehemu mbili na zinazowiana vizuri sana; alikuwa haitambui miujiza yenye utata iliyokuwemo kwenye maumbile yake. Leo hii amegundua ukweli wa kustajabisha sana na wenye athari nyingi kuhusu sehemu ya ndani ya mwili wake mdogo, akitambua kwamba kuna makumi ya mamilioni ya mabilioni ya chembe chembe hai mwilini mwake. Hali hii inawezesha kuwepo mazingatio maalum juu ya utukufu wa muumba anayehusika na matokeo-sanifu haya ambayo hayakuwezekana kufanyika zamani.

Je, kuna mantiki kusema kwamba imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu ni ya kipekee kwa wale wasiojua chochote kuhusu kubuniwa na kuumbwa kwa mwanadamu, na kwamba kinyume chake, mwana sayansi ambaye anatambua sheria za maumbile na mambo yanayohusiana na kukua na kuendelea kwa mwanadamu, ambaye anatambua kwamba sheria na mahesabu sahihi ndio yanaongoza hatua zote za uhai wa mwanadamu, analazimika kuamini kwamba mata, pamoja na kukosa utambuzi wote na fahamu, ndio chanzo cha sheria za kustaajabisha za maumbile? Hivi ugunduzi na ujuzi wa kisayansi unasababisha mwana sayansi kama huyo kuhitimisha kwamba mata ambayo haina utambuzi na ujuzi, ndiye muumbaji wa yeye na wa viumbe vingine vyote? Uyakinifu unaitazama dunia huku jicho moja likiwa limefumbwa na, matokeo yake ni kwamba, hauwezi kutoa majibu kwa mengi ya maswali.

Pia, sayansi haitoi jibu kwa lile swali la kama dunia inaweza kugawanyika katika sehemu mbili, ya kimaada na isiyo ya kimaada, au kwa swali la kama dunia ina lengo la kimaumbile. Maswali haya hayapo kwenye nyanja ya sayansi, elimu ya kisayansi inaweza kutufahamisha sisi - kwa kiwango fulani - kwamba ni nini, lakini haitaweza kutuonyesha mwelekeo katika uhai au kutuzindua na njia ya kufuatwa. Falsafa ya maisha, ya kisayansi, kwa hiyo, haiwezi kuwa msingi wa itika- di ya mwanadamu.

Tathmini ya ujuzi wa kisayansi zaidi ya yote ni ya kimatendo, kwa vile inamfanya mwanadamu aweze kutawala maumbile. Ni mifano na tathmini ya kinadharia ndio ambayo inahitajika kama msingi wa imani. Zaidi ya hayo, sayansi imeegemea kwenye majaribio na uchunguzi, na sheria zenye kuwa na majaribio juu ya msingi wao hulazimika kubadilika na kuyumba. Imani inahitaji msingi wenye umilele, ikiwa na kinga dhidi ya mabadiliko, na iwe na uwezo wa kujibu maswali kama vile asili na umbo la dunia kwa ujumla katika namna ya kuaminika na ya kudumu. Ni hapo tu ambapo mahitaji ya mwanadamu ya tafsiri na uchambuzi wa kina wa kuwa hai unaweza kutimia.

Kadiri anavyoelekea kwenye ukamilifu, mwanadamu anahitaji uwiano wa kiroho na kiakili; bila kuwa na lengo, atapotea na kwenye njia zisizo sahihi na kujihatarishia mabalaa. Mtu asiyeweza kupata lengo lake katika dini, atafuata lengo analolielewa yeye mwenyewe ambalo halitakuwa chochote isipokuwa maasi dhidi ya matakwa ya maumbile, halitahusiana na uendelevu au ukomavu wa akili.

Sababu za ukanushaji na kutoamini Vitabu juu ya historia ya dini hujaribu kufafanua kinaga ubaga mambo ambayo yamewavuta watu kwenye dini. Lakini majaribio kama hayo wanayoyafanya hayana maana yeyote na hayawezi kufichua ukweli wenyewe wa mambo. Ni muhimu kushabahia kwenye muelekeo wa asili wa mwanadamu kwenye imani ya mungu mmoja, ile sifa ya kiuhai ya jamii za wanadamu ambayo humpa mwanadamu - pamoja na tofauti zake zote ndani yake, fikira na matamanio yake - sehemu maalumu katika maumbile. Hapo ndipo inapowezekana kugundua mambo ambayo humwongoza mwanadamu kuikanyaga asili yake mwenyewe kwa kukataa dini, kwa viapo kabisa.

Mahusiano ya kidini ya mwanadamu ni matokeo ya asili yake, na uyakinifu ni kitu kinachopingana na maumbile yake. Kwa kulingana na tabia yake ya dhahiri, binadamu atajiumbia mungu wake mwenyewe kama hatamgundua Mungu wa kweli, na mungu anayemgundua yeye anaweza kuwa ni maumbile au mambo ya kihistoria yasiyoepukika. Na mungu huyu wa uwongo anachukua nafasi ya Mwenyezi Mungu wa kweli kwa kuzingatia ufahamu na mamlaka, kufaa kwa maagizo, na uwezo wa kumwongoza mtu kwenye njia fulani na kumsogeza mbele, bila kuzuiwa na matakwa ya mtu yeyote.

Huu ndio mwanzo wa kubadilishana miungu wa uwongo, ufuasi kwenye uabudu masanamu upya, ambao ungemtoa kafara Mwenyezi Mungu kikatili kwenye historia na kubadilisha lulu kwa shanga. Inasikitisha kwamba, watu wengi waliojiangamiza kwa unyonge waliojiingiza wenyewe wakawa wameinama chini mbele ya sanamu ambalo wameliunda wenyewe na kulifanya kuwa mungu! Wamempa kisogo muumba asiye na kifani na kwa hiari yao wakakubali fedheha inayochafua ya ibada iliyoongozwa vibaya kama hiyo.

Kama tukilichunguza jambo hili kwa ukaribu zaidi, tunaona kwamba kujitokeza kwa uyakinifu huko Ulaya kama kitivo cha fikra, ukatwaji wa uhusiano wa binadamu na kanuni ilioyo tukufu, kufungwa kwao kwenye nyororo za maada, kuchagua kuendekeza sayansi mahali pa dini - yote haya yalisababishwa na mlolongo wa mambo ya kijamii na kihistoria yaliyojitokeza katika nchi za magharibi.

Mojawapo ya mambo yaliyoamsha upingaji wa mabadiliko ulioenea katika Ulaya yote na kusababisha kutokeza kwa fikra zisizofuata dini na propaganda dhidi ya dini, ilikuwa shinikizo baya mno lililowekwa na mamlaka za kikanisa mwanzoni mwa kipindi cha mwamko-sanaa juu ya wasomi waliokuwa wanaleta mawazo mapya ya kisayansi. Kwa kuongezea kwenye mafundisho maalum ya kidini, kanisa pia liliwiwa shukrani kwa ajili ya kanuni fulani za kisayansi kuhusu mwanadamu na dunia ambazo lilizirithi kutoka kwa wanafalsafa wa kale - hasa wa Kigiriki - na ambazo ziliwekwa katika ulinganifu sawa na imani za dini. Nadharia yoyote iliyojitokeza kupingana na Biblia na hizi kanuni zilizorithiwa zilifikiriwa kama za uasi, na yeyote aliyezitetea angeadhibiwa vikali.

Upinganaji wa dhahiri baina ya dini na sayansi ulianzisha uadui wa pamoja katika pande hizi mbili. Wasomi na wanasayansi waliona kwamba Kanisa la Kikristo lilikuwa linazifunga akili na fikra, na kuzuia maendeleo huru ya mawazo; kupitia kwenye ufuasi wake wa mfumo unaoogofya wa fikra na desturi ya kwenda kinyume na akili, lilikuwa linatengeneza mazingira yenye kusonga kwa ajili ya mwanadamu wa zama hizo mpya. Hivyo, mabingwa walikimbilia kwenye kujitenga kunakohuzunisha kutoka kwenye dini.

Mashinikizo haya yaliyokuwa yakilimbikizana kwa siku nyingi, hatimaye yalisababisha majibu ya vurugu zilizoikumba Ulaya yote. Hapo ndipo nguvu na utawala wa Kanisa ulididimia na uonevu wake ulikoma, uhuru wa fikira za kimagharibi ulipatikana tena na ulionyesha hisia kali dhidi ya mipaka iliyokuwa imewekwa hapo mwanzoni. Wasomi waliondoa nyororo zote za taratibu za kizamani toka kwenye shingo zao na wakatoka kwenye dini. Maumivu na hasira zote walizokuwa wamezipata zilidhihiri kwenye wimbi kubwa la uadui dhidi ya dini. Hali ya wasi wasi mkubwa wa kiroho ilianza ambayo ilifikia kilele katika kutenganishwa sayansi na dini. Tamaa ya kisasi kisicho na mantiki dhidi ya dini kilisababisha kukanushwa kwa ukweli mwingi wa ki-Mungu na wa imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.

Ni kweli kwamba baadhi ya mafundisho yaliyounganishwa na dini hayakuwa na mantiki au hata msingi, yakiwa hayana uhusiano na ujuzi wa kidini uliothabiti. Lakini kulipiza kisasi juu ya Kanisa ni jambo moja na kuangukia kwenye chuki haraka na kwa makosa dhidi ya dini, kama hivyo, ni kitu kingine tofauti. Ni dhahiri kwamba kulipa kisasi, kukiwa ni jambo ambalo linatokana na hisia, halina uhusiano wowote na ufasaha wa kisomi.

Umasikini wa kiroho wa mwanadamu uliongezeka kwa kiwango kinacholingana na utajiri wake wa kisayansi na kiteknolojia. Jinsi alivyoendelea katika viwanda vingi, ndivyo maadili na nguvu yake ya kiroho vinazidi kupungua, hadi kufikia kiwango ambapo alikosa uwezo wa kimaadili wa kuweza kutumia inavyostahili ujuzi wake mpya alioupata. Ujuzi wa kisayansi haujishughulishi na maadili, mtu hawezi kuamua kazi za mwanadamu mwenye kuwajibika kwa kutumia kigezo cha sayansi. Sayansi hata ifike mbali vipi, bado haina uwezo wa kuona hata hatua moja mbele yake. Ujuzi wa kibinadamu hauwezi kufika kwenye chimbuko la dunia na kutambua kwa ufasaha yaliyomo, wala hauwezi kutabiri mustakabali wa baadaye wa mwanadamu.

Ni falsafa ya maisha ya Mungu Mmoja tu ambayo haijaribu kumfungia mwanadamu kwenye vipengele vya kimaada vya maisha yake. Kinyume chake kupitia kwenye ishara na dalili ambazo mwanadamu amepewa ili zimwongoze katika njia yake, imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, inaonyesha utukufu wa asili na mustakabali kwa ajili ya mwanadamu.

Mara tu mwanadamu anapoingia kwenye njia ya kumwamini Mwenyezi Mungu, hupata falsafa ya maisha pana ndani ya mfumo ambamo huweza kupata majibu kuhusu swali lake la msingi la ki-uchunguzi. Mara akishafikia hatua hii ya imani pana na yenye vipimo vingi, maisha yake mwanadamu huchukua juhudi mpya na maadili ambayo ndio matunda mazuri ya hiyo falsafa ya maisha huja kuwa kweli. Mapambano na kanisa yalikuwa kwa hiyo, kipengele kimoja katika kutenganisha sayansi na dini. Kundi lingine liliitekeleza dini na kukimbilia kwenye uyakinifu kwa sababu mawazo yaliyoshauriwa na Kanisa hayakuwa sahihi na hayaku- tosheleza, yaliyokosa na maadili yaliyo nje ya uwezo wa mwanadamu.

Mawazo haya kwa kawaida yalionekana kutokubalika na yasiyovutia kwa watu wenye akili. Kanisa lingemwonyesha Mwenyezi Mungu katika hali ya maada na kibinadamu kwa maana ambayo ilipingana na haja ya mwanadamu juu ya maadili kamili na kule kujitahidi kupenya na kuvuka mifumo yote yenye kuweka mipaka. Hapawezi kuwa na shaka kwamba endapo ukweli usiopingika unaingizwa kwenye ubongo wa mtu katika muundo wa hekaya wenye dosari, mtu huyo atakwenda kinyume nao mara tu atakapofika ukomavu wa kiakili.

Wakikabiliwa na taswira ya Mungu mwenye kupachikwa umbo la kibinadamu, iliyotengenezwa katika theolojia ya Ukristo, kutukuza imani zaidi kuliko matumizi ya akili na msisitizo kwamba imani lazima itangulie akili, watu walioelimika walitambua kwamba jitihada hizi zitokanazo na akili finyu, kwa lengo la kuzuia matumizi ya busara na sayansi katika ukiritimba wa theolojia ya Kikristo hazikuendana na kigezo cha mantiki na mbinu ya kisayansi. Kwa vile hazikuwa na chanzo thabiti ambacho kutokana nacho wangejifunza mafundisho ya kweli kuhusu Mwenyezi Mungu, yote yakiwa huru kabisa kutokana na taasisi za Kanisa na vitabu vyake vipotovu, na kwa kuwa hawakuwa na njia ya kuwafikisha kwenye mfumo ulio bora zaidi ambao ungeweza kutosheleza mahitaji yao ya kiroho na kimwili na kuwapa muundo unaofaa kwa ajili ya kuunganisha vipengele vyote muhimu vya maisha, vya kimwili na kiroho, hisia na kiakili, falsafa ya maisha ya uyakinifu iliota mizizi ndani yao, na kuwaelekeza kukana maadili yote yaliyo nje ya uwezo wa kibinadamu na yaliyo zaidi kinyume cha ubinadamu.

Walikuwa hawatambui kwamba ingawa kosa hupotosha dini wakati linapofuata njia ya ujinga, dini ya ukweli, isiyokuwa na uwongo wowote, ushirikina na upotovu inaweza kumkomboa mwanadamu kutoka kwenye utumwa wa visasili na ushirikina, na kumshikilia kwa umadhubuti kwenye mhimili wa imani ya kweli na kumpatia uelewa sahihi wa mafundisho yahusuyo Mwenyezi Mungu, ambayo hutosheleza akili yenye udadisi. Badala yake, wasomi wa nchi za Magharibi walitambua upande moja tu wa ushirikiana wa dini ya uwongo na jinsi mfumo ulioundwa wa imani wa dini, usio na kuswali, ulivyokosa kuwa na msingi wa kimantiki, kwa hiyo hawakusita kushutumu dini kwamba haina msingi wowote. Uamuzi wao uliegemezwa kwenye ile hali halisi ya kukatisha tamaa iliyomo kwenye dini yao wenyewe, na uamuzi huo haukuweza kushindwa kuwa wa haraka, usio wa kweli, usio na busara na mantiki.

Haya yamefafanuliwa ifuatavyo na msomi wa fiziolojia na biokemia: "Ukweli kwamba wasomi fulani hawakuongozwa, katika njia ya utafiti wao, kwenye utambuzi wa kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, una sababu nyingi sana. Hapa tunataja mbili miongoni mwa hizo. Kwanza; hali ya kisiasa iliyotengenezwa na udikteta, pamoja na hali zinazoambatana na mambo ya kijamii na kiutawala, zilielekea kumsababisha mwanadamu kukana kuwepo kwa Muumbaji. Pili, mawazo ya mwanadamu wakati wote yamekuwa yakivutiwa na njozi fulani na uwongo, na ingawa mwanadamu anaweza kuwa hana woga wa maumivu makali ya kiroho na kimwili, bado hana uhuru kamili wa kuchagua njia iliyonyooka.

"Katika familia za Kikristo, watoto wengi huamini kuwepo kwa Mwenyezi Mungu afananaye na mwanadamu, kana kwamba mwanadamu aliumbwa katika umbo la Mwenyezi Mungu. Wanapoanza kuingia kwenye nyanja ya sayansi na kujifunza na kutekeleza fikira za kisayansi, hawawezi tena kupatanisha dhana yao dhaifu ya kumpa Mwenyezi Mungu viungo vya mwanadamu na ushahidi wa kimantiki na mbinu za sayansi. Kwa hiyo baada ya muda fulani, wakati ambapo matumaini yote ya kupatanisha imani na sayansi yanatoweka, wanaitelekeza kabisa fikira yote ya Mwenyezi Mungu na kuifuta kabisa kwenye akili zao. "Sababu yake kubwa ni kwamba ushahidi wa mantiki na aina za sayansi hazirekebishi hisia na imani zao za mwanzoni, lakini badala yake, huwafanya wahisi kwamba walikosea katika imani yao ya mwanzo kuhusu Mwenyezi Mungu. Kwa mvuto wa hisia hizi, ikiunganishwa na mambo mengine ya kisaikolojia, wanashangazwa na upungufu wa fikra zao na huachana kabisa na majaribio ya namna yoyote ya kumjua Mwenyezi Mungu.[25] .

Kwa hiyo, wanasayansi, walijaribu, kwa kufafanua aina zote za sheria na fomyula na kutoacha nafasi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na dini katika kutafuta ufumbuzi wa maswali yanayogusa kuwepo uhai na maumbile. Walijaribu kukatisha matumaini ya wanadamu kutoka kwenye dini na kumweka kando Mwenyezi Mungu katika kuwa na wajibu wowote katika utendaji wa ulimwengu na mpango wa maumbile.

Kila walipofikia kukwama walijaribu kutafuta ufumbuzi wa tatizo kwa kutumia nadharia tete mbali mbali au kuahirisha ufumbuzi bayana wa tatizo hadi hapo utafiti mkubwa zaidi utakapokuwa umefanywa. Walidhani kwamba kwa njia hii walikuwa wanaepuka kujisalimisha kwenye fomyula isiyo ya kisayansi na ushirikina. Hivyo, ingawa waliepuka hatari ya kukubali ushirikina, kwa masikitiko walianza kupiga vita upagani na ukana-Mungu.

Ingawa imani juu ya Mwenyezi Mungu na kuamini katika kanuni ya uasilishaji ni jambo la kawaida na msingi kwa mwanadamu, haliwezi kulinganishwa na mahitaji ya kimaada ambayo mwanadamu wakati wote anajitahidi kuyapata. Liko tofauti kabisa na maisha ya kimaada, na kwa kuwa ni hitajio la ndani ya mwanadamu, linahusiana na namna tofauti kabisa. Zaidi ya haya, ni rahisi kukanusha kitu kisichoonekana kwa macho kuliko ilivyo kwa kukithibitisha, tukichukulia kutoweza kwetu kukielezea vya kutosha. Watu wanaokosa uwezo wa kiakili, kwa hiyo, huchagua njia rahisi na isiyo na usumbufu ya kukataa badala ya kujitahidi kutumia akili. Njia ya kukanusha aidha, haihusishi madhara yoyote yaliyodhahiri. Kwa kugeukia mbali na Mwenyezi Mungu, watu pole pole hujenga msimamo wa ukaidi na uadui kwenye dini, ulioathiriwa na ushabiki. Athari kubwa za msimamo kama huo zinaweza kuonekana kwa urahisi kwenye hoja zenye uovu za wale ambao wameipa mgongo dini.

Pia ni rahisi zaidi kukana kitu kisichoonekana kwa sababu kukithibitisha kuwepo kwake kutamaanisha wajibu mbali mbali kwa mwanadamu, wale wanaotaka kuzitupilia mbali wajibati hizo, kwa urahisi hukataa kuwepo kwa kanuni ya uanzishaji. Qur'anii inasema:

بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ ﴿٥﴾ يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ ﴿٦﴾ فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ ﴿٧﴾

"Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilizioko mbele yake. Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama? Basi jicho litapoduwaa." ( Qiyama:75: 5-7).

Mafundisho ya wale wataalamu wa kujihini, wajinga na wasio na mantiki pia hayawezi kutoonekana kama kipengele kinachosukuma vikundi fulani vya watu kuelekea kwenye uyakinifu. Zile silika zinazokuja kuwepo pamoja na maisha ya kawaida ya mtu ambazo zimefungamanishwa na uhai wake, si tu kwamba hazikosi maana na lengo; zenyewe pia ni nguvu ya kuumua na kuandaa takdiri, kipengele cha maendeleo na msogeo, ambacho ndio humsukuma mtu na kusonga mbele kuelekea kwenye lengo lililozingatiwa katika kuumbwa kwake. Ni kweli kwamba, mtu hatakiwi kuwa mtumwa aliyefunikwa macho kwenye silika zake kama mfungwa ambaye uhai wake wote na nyendo vinadhibitiwa na mwangalizi wa jela. Lakini, pia hapaswi kupigana vita na ukweli wa uhai wake mwenyewe na kutafuta kuzuia shughuli zote na nyendo kwa upande wa silika zake. Uhai wa mwanadamu wenye matunda mazuri, kwa kweli hutegemea juu ya kuwepo hai katika maisha yake kwa silika zake, zilizoenea kwa uwiano unaofaa; kuzuia silika kunasababisha utata na uharibifu wa haiba ya mtu.

Falsafa ya maisha iliyokuwepo kwenye Ukristo katika kipindi cha kati ilikuwa kwenye msingi wa maelekezo ya mazingira pekee ya Akhera ambayo yaliingiza na ushushaji thamani wa dunia ya kimaada. Sasa, matokeo yatakuwaje endapo mtu anakanusha uhalali wote wa nguvu za silika, kwa jina la Mwenyezi Mungu na dini, akajaribu hata kuziharibu kabisa; kama mtu anatukuza useja na maisha ya utawa na akakanusha hadharani ndoa na kuzaana kama ni uchafu, shughuli yenyewe hasa ambayo ndiyo inayolinda uhai wa spishi mbali mbali; na kama mtu anaona umasikini na kutojiweza kama ndio uhakikisho wa furaha ya hali ya juu? Je, kwa hiyo, itawezekana kutegemea dini kuchukua jukumu mashughuli na endelevu?

Jukumu halisi na kazi ya dini ni kusafisha, kuongoza na kudhibiti silika, kuwekea mpaka wa eneo la ushughulikaji wao, na kuzitakasa na upotofu na uovu wote. Sio kuziharibu na kuziondoa kabisa. Kwa kuzidhibiti silika na kujitahidi wakati wote kujinasua mwenyewe kutoka kwenye mtego unaoweza kuwepo, mwanadamu hujitengenezea hatima yake yenye lengo. Endapo mwanadamu anashindwa kufanya hivi, mgongano mkubwa wa silika ndani mwake ni mkubwa mno hivyo kwamba hawezi kuwa mdhibiti wa nafsi yake mwenyewe kwa urahisi. Kwa hiyo, anahitaji mfumo wenye maarifa mengi juu ya elimu ya maadili. Kwa upande moja binadamu anapatwa na mvuto wa shauku ya kidini, hali hii, humtiisha kwa siri na huzikusanya pamoja zile nguvu zake zilizotawanyika, kwenye mshiko wa uwezo wake, na kuzielekeza kwenye kupata maadili na manufaa. Kwa upande mwingine binadamu pia anapatwa na mvuto wa silika zake.

Katika jamii yoyote ambamo watu wakati wote wanaambiwa, kwa jina la Mwenyezi Mungu na dini, kwamba njia ya kwenye furaha ipo katika kuzikataa zawadi za dunia hii, mwanya unajitengeneza wenyewe kwa ajili ya maendeleo ya uyakinifu na umakinifu zaidi juu ya thamani ya vitu vya kimaada, ili kwamba zile fikra tukufu za dini, pamoja na athari zake zenye kufika mbali, zitoweke kwenye mazingira.

Lakini, hii haiwakilishi mantiki halisi ya dini. Dini za kweli huelekeza mazingatio ya mwanadamu kwenye maadili thabiti ya kiroho, yakijiegemeza katika imani juu ya muumbaji na kumpatia mtu mafundisho mapana na kanuni kwa ajili ya maisha yake. Maadili haya hupanua uwanja wa uoni wake hadi kwenye mipaka ya eneo la ki-mbingu, na kumtoa kutoka kwenye utumwa wa kuabudu matamanio yake mwenyewe na anasa za kidunia (uyakinifu), na wakati huo huo, yanamruhusu afurahie starehe za kidunia kwa kiasi cha kutosheleza tu.

Baadhi ya watu wanadhani kwamba starehe holela juu ya vitu fulani ambavyo vimepigwa marufuku na dini itawahakikishia kudumu furaha yao. Wanafikiri kwamba dini inapigana kwa ukaidi dhidi ya starehe zote na haiko tayari kukubaliana raha za dunia hii, kana kwamba Mwenyezi Mungu anamlazimisha mwanadamu kuchagua kati ya furaha ya hapa duniani na furaha ya Akhera. Mwelekeo huu kwenye dini ni wa unapotoshaji kabisa usiowezekana kuwa kweli. Ikiwa dini kuwajibika katika jitihada za binadamu na uchaguzi wake wa mwelekeo, ni kwa sababu kujiendekeza kusikozuilika kwenye matamanio, kujisalimisha bila masharti kwenye silika na hamu, na utiifu kwenye amri za umimi, hutia giza maisha ya mtu na humpeleka kwenye hali ya utumwa wa kutojitambua. Licha ya asili yake safi kimsingi, anaanguka kutoka kwenye daraja lake halisi na kukengeuka kutoka kwenye njia yake ya kweli. Kama kule kujiendekeza kiholela kwenye silika za matamanio kungekuwa sio sababu ya mateso ya milele na kujivunjia hadhi kuchungu, kusingeweza kukatazwa.

Ni fikira kama hizi ambazo zinafanya iwezekane kuelewa ni kwa nini dini imekataza mambo fulani na ni jinsi gani starehe ya dunia ilivyo na ulinganifu na furaha ya Akhera. Fikira kama hizi hutumika katika kumlazimisha wajibu fulani juu ya mwanadamu. Jaribio ya kutekeleza matendo ya faradhi ya ibada, kwa uaminifu na bila unafiki, huleta mabadiliko ya ndani kabisa mwa mtu, lengo la matendo haya kwa namna yoyote sio kupunguza furaha ya mtu ya kidunia.

Kuabudu ni sawa na tufani kali kwenye dimbwi (wangwa) tulivu la moyo, inayobadilisha tabia ya ndani ya mwanadamu na kigezo chake cha maamuzi. Ndiyo jiwe la pembeni ambapo msingi wa dini huimarishwa, mazoezi ya kuelimisha yenye manufaa yanayopenya kwenye vina virefu vya nafsi. Upanga wake mkali hukata fundo la upotofu na udhalili ndani ya binadamu na kumwezesha yeye kukimbilia eneo pana na safi, lisilo na mipaka. Kwa ufupi humwezesha mwanadamu kukua na kufikia ukomavu halisi.

Si tu kwamba hakuna mikinzano kati ya mambo ya maisha na yale ya kiroho; mambo ya kiroho yanafaa sana kwenye maisha ya furaha kubwa zaidi hapa duniani. Inaweza kuwa labda kwamba mafundisho yasiyoaminika na yasiyo na mantiki ya Ukristo yameathiri mielekeo ya kinyume na dini ya watu kama Betrand Russell. Kwa dhahiri aliamini kwamba kumwamini Mwenyezi Mungu ni kujitakia huzuni, kama inavyodhihirika katik a maneno yafuatayo: "Mafundisho ya Kanisa yamefanya binadamu achague baina ya aina mbili ya mateso na umasikini. Ama mateso ya hapa duniani na kukosa starehe zake au mateso ya maisha ya akhera na kukosa furaha ya peponi.

Kuhusu Kanisa, mojawapo ya aina hizi mbili za mateso lazima na muhimu ivumiliwe. Ama mtu lazima ajisalimishe kwenye mateso ya hapa duniani na kuteseka kwa umasikini na upweke ili aweze kufurahia starehe za akhera, au, ikiwa mtu anataka kufurahia starehe za dunia hii lazima akubali kwamba atanyimwa starehe za akhera." Ueneaji wa maoni kama haya, ambayo yanadhihirisha ujinga mkubwa sana na wa kina falsafa ya maisha kidini, kunaweza kuamua hatima ya dini iliopo katika jamii fulani. Athari za maoni haya kwa itikadi na matendo ya binadamu ni nzito sana kuweza kupimwa vizuri, kwa mtazamo wa mpito wa juu juu. Muundo huu wa fikira umesababisha mazingatio ya mwanadamu kuelekezwa kipekee kwenye nyanja ya kimaada - awe anatambua au hatambui. Umakinifu unaojitokeza juu ya starehe na anasa umesababisha kudhoofika kwa mambo ya kiroho na maadili.

Dini haimshutumu mtu kuvumilia mojawapo ya aina mbili hizi za mateso. Inawezekana kabisa kuunganisha furaha ya dunia hii na ya Akhera. Kwa nini, Mwenyezi Mungu Ambaye hazina yake ya huruma na neema haipungui, asitake waja Wake wapate furaha kamili ambayo inakusanya dunia hii na Akhera? Hivi ndivyo kwa usahihi hasa anavyopenda Yeye.

Jambo lingine katika kuenea kwa fikira za kiyakinifu limekuwa ni uendekezaji wa tamaa na kuzama kwenye shimo la ashiki. Kila utambuzi wa kiakili na mawazo hufanya msingi wa baadhi ya matendo ya nje; njia ya matendo ya mwanadamu huchukua umbo la njia ya mvuto wa itikadi zake. Kinyume chake matendo na maadili ya mwanadamu pia huleta mabadiliko yenye ubora katika tabia yake ya kiakili na muundo wa fikira. Mtu anayeabudu matamanio yake polepole atapoteza mawazo yote matukufu kuhusu Mwenyezi Mungu. Mara tu anapochagua mhimili wa uhai wake kinyume na Mwenyezi Mungu na kudhania kwamba chochote kilichopo katika dunia hii, kimetupwa hivi hivi tu juu yake, bila madhumuni yoyote, hivyo kwamba wazo la kuwa na lengo katika maisha linakuwa halina maana kabisa, huanza kutoa uwezo wake wote wa kiakili katika kufanya starehe kwa wingi zaidi. Kutumbukia huku kunakofedhehesha, kwenye kiwango cha chini cha maisha, kunanyausha mizizi ya matumaini yote kwa ajili ya makuzi na maendeleo.

Mawazo ya kumwamini Mwenyezi Mungu; kwa kulinganisha, ni kama mbegu ambayo inahitaji udongo unaofaa ambamo inaweza kumea. Mbegu hiyo inaweza tu kustawi kwenye mazingira safi, mazingira ambamo mwanadamu anaweza kupata kwa haraka na urahisi kiwango cha ubora ambao ni wa kipekee kwake, kwa sababu ya muundo ambamo kanuni za maisha yake zimewekwa. Imani ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, haiwezi kustawi kwenye mazingira yaliyo jaa uovu.

Mojawapo ya vipingamizi vinavyo mzuia mtu asipate kumjua Mwenyezi Mungu na sababu za mwanadamu kukanusha kuweko huku, pamoja na kuwepo dalili zilizowazi na ushahidi wenye maamuzi ambao upo, kwa hiyo, ni kujisalimisha kwenye dhambi na kuendekeza matamanio. Imam Jafar as-Sadiq(a.s) alisema alipomjibu Mufadh'dhal ndani ya Risalah-yi Ahlija: "Ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba Mwenyezi Mungu hajashindwa kujijulisha Yeye kwa wasiomjua, kwani wanaona ushahidi dhahiri na ishara zisizo na shaka za Muumba katika mumbile Yake na wanatazama mambo ya ajabu katika Ufalme wa angani na duniani ambayo yanaelekeza kwa Muumba wao.

"Watu wajinga ni wale ambao wamefungua milango ya dhambi mbele yao na wakafuata njia ya kujiendekeza kwenye tamaa na ashiki. Matamanio ya nafsi zao yametawala nyoyo zao, na kwa sababu ya dhulma zao juu ya nafsi zao wenyewe shetani amechukua mamlaka juu yao. Mwenyezi Mungu amezipiga muhuri nyoyo za waovu."[26]

Tamaa ya starehe, ushindani, ubadhirifu, mantiki dhaifu ya waumini fulani wasio na elimu - hawa pia ni miongoni mwa vipengele vinayomlazimisha mwanadamu kukimbilia uyakinifu. Ghasia na mchafuko wa maisha, wingi wa bidhaa zinazozalishwa, utajiri na mamlaka, mielekeo ya maisha ya kisasa inayozuzua na kushughulisha, kuenea haraka kwa vitu vya anasa na starehe - yote haya yanawafunikiza kabisa watu walafi. Watu hawa wanajaribu kabisa kujitoa kwenye mazingira ya masuala ya kidini na hukataa kukubali mamlaka ya madaraka yoyote makubwa zaidi, kwani si tu kwamba hii isingewaletea manufaa yoyote ya kidunia, bali pia ingeshika hatamu kwenye mawimbi ya matamanio yao yaliyokomaa.

Kwenye mazingira ambayo watu wamezama kwenye dhambi, ufujaji, na uovu, na wakakataa kukubali mipaka yoyote inayotawala matendo yao, dini itabakia jina tu. Watu wanaojiendekeza na wayakinifu hawawezi kuwa wenye kumtafuta na kumwabudu Mwenyezi Mungu. Wakati ambapo mojawapo ya kanuni mbili zinazopingana; kanuni ya kusaka anasa na ile ya kumwamini Mwenyezi Mungu, inapokuwa imetawala nafasi ya akili ya mhusika, kanuni nyingine lazima iondoke humo. Mara tu moyo wa kuabudu unapokuwa katika maisha ya mwanadamu, huiondoa mielekeo yote ya kiyakinifu kwa kuzikata pingu imara za matamanio duni na wakati wote hutia msukumo juhudi ya mtu kupanda kuelekea kwenye lengo lake. Hivyo, muundo kamili wa uhuru wa binadamu wa kutoka kwenye utumwa na kuingia kwenye hali ya asilihujitokeza.

Jinsi lengo analojiwekea mtu mwenyewe linavyokuwa la juu na la mbali zaidi, ndivyo mwelekeo wa kuliendea utakavyo kuwa mkali zaidi na ndivyo jitihada inayohitajika ili kulifikia itakavyozidi kuwa kubwa zaidi na ya muda mrefu zaidi. Kwa hiyo, kama tunamchagua Mwenyezi Mungu kama lengo letu, tutakuwa tumechagua lengo la hali ya juu lisilo na ukomo, na njia inayoelekea kwenye mafanikio ya lengo hilo vivyo hivyo itakuwa haina ukomo, ingawa njia hiyo ni wazi na iliyonyooka wakti huo huo.

Ni lengo ambalo litajibu matatizo na maswali mengi, na kwa kuwa litatulazimisha kukataa udhalimu wa nafsi, utatupatia uhuru kamili juu yetu. Kama tukimkubali Mwenyezi Mungu kama ndio lengo letu, uhuru utapatanishwa na makuzi na maendeleo yetu. Juhudi zetu za kujiendeleza na kupiga hatua zitakuwa na maudhui na maana, kwa msaada wa silika za kiungu na tamaa ya uzima wa milele. Kwa ufupi, tamaa ya kupiga hatua na maendeleo, mara tu inaporekebishwa na ibada ya Mwenyezi Mungu, ama kwa hakika haipingani na uhuru wa binadamu wala haiishii kwenye yeye kuwa mtumwa.

Tunaweza kudai kuwa tumepata uhuru hapo tu tunapokuwa tunakwenda sambamba na kusonga mbele kwa ujumla kwa dunia yote kuelekea kwenye ukamilifu, kwa akili, na utambuzi kamili wa manufaa yatakayoletwa na hatua hii. Kufanya matendo kwa kutii hali ya asili au kwa kutoepukika kwa historia sio uhuru, kwani wakati mwanadamu anapoacha kujali ustawi wake mwenyewe kwa kufuata maamuru ya maumbile, hili si jingine mbali na utumwa au utii wa kijinga.


13

14

15

16