MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 18%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 62343 / Pakua: 6745
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

1

2

5

MUANDAMO WA MWEZI

SEHEMU YA SABA

NDUGU JUMA ANACHANGANYA MAMBOKATIKA AYA YA QUR-AAN IFUATAYO

MNASEMA 7.

Ndugu Juma Anachanganya Mambo Katika Aya Ya Qur-aan Ifuatayo:

"Yeye (Mwenyezi Mungu) ndiye aliyelifanya jua (kutoa) mwangaza na mwezi (kuakisi) nuru na akaupangia (huo mwezi) vituo (vya kusafiria) ili mpate kujua idadi ya miaka na hesabu (ya nyakati"). (10: 5) Ndugu Juma anaona mwezi na jua ni vitu sawa sawa na kama kwamba vinafanya kazi moja kwa kuwa vimetajwa kwenye Aya moja ya Qur-aani. Huku akisisitiza kwamba: (Sasa utaona kwamba Aya hii imetaja vitu viwili: jua na mwezi. Na vyote hivi vinazunguka katika falaki (orbits) zake na vinapita katika manazil (vituo) yale yale na vinapita katika buruji (constellations) zile zile.) Pia anaona hukumu ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kusema kwamba ((Fungeni kwa kuuona mwezi)) ni sawa sawa na kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Aliposema kuwa:"Swalini kwa kutenguka jua" .

SISI TUNAJIBU HIVI:

a) Mwezi na jua ni vitu viwili tofauti vinavyofanya kazi tofauti katika huo wakati (time). Kila kimoja kinafanya kazi yake maalumu kwa kuashiria huo wakati maalumu uliopangiwa. Angalia pia: (36: 40), (2:187)

b) Hukumu ya ((Fungeni kwa kuona mwezi na Swalini kwa kutenguka jua)) ni vitu viwili tofauti kwa sababu zifuatazo: i. Hadiyth ya kufundisha nyakati za Swala aliteremka Sayyidna Jibriyl ('Alayhi swalaatu was-salaam) kuja kumfundisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala haina khitilafu ya mahala kwa Wanavyuoni karibu wote. Angalia pia Qur-aan Tukufu (17: 78).

ii. Hukumu ya mgonjwa au mtu aliye safarini anayo ruhusa ya kutokufunga hata kama ameona mwezi lakini hana ruhusa ya kutokuswali kabisa hata akiwa mgonjwa au aliye msafiri.

iii. iii) mashariki " jua nyakati za Ibada za watu. Yaani kuweza kujua wakati wa kufunga., kutaja "ikma hkani kabisa, Mwanamke aliye katika siku zake ambaye amepewa ruhusa ya kutofunga Swaum ya Ramadhaan na kutokuswali atakuja kulipa Swaum, lakini hatolipa Swala.

iv. Hutokezea (ijapo kwa Sadfa) watu wa eneo kubwa kama nchi zote za Kiarabu hufunga Swaum zao kwa siku moja kutokana na muandamo wa mwezi. Lakini hawaswali Swala zao za faradhi kwa wakati mmoja - kwa kufuata jua wala hilo halina pingamizi wala mjadala kama ilivyokuwa hakuna ikhtilafu katika kufuturu wakati wa kuzama jua. v. Kumbuka kilichozungumzwa ndani ya kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu pamoja na Wanavyuoni wote wakubwa waliokuja na hoja ya kufunga pamoja. Wameelezea uwezekano wa kufunga dunia nzima katika siku moja, sio dakika au saa moja ya siku. Kwa mfano, dunia nzima inaswali Swala ya Ijumaa siku moja ya Ijumaa. Hakuna Ijumaa mbili duniani bali kuna kupitana na kutanguliana na hayo yanakuwa hata katika nchi moja.[1]

vi. Nyakati za Swala zimetengenezewa Jadweli (Time table) zinazolingana na mitenguko ya jua lakini suala la kufunga (Swaum) halikubaliki kufanyiwa jadweli au kalenda za muandamo wa mwezi sharti mwezi uonekane japo kwa macho ya mtu mmoja. vii. Si sharti kuliona jua kwa macho hata kwa mtu mmoja wakati wa kuchomoza au kutua (kuzama) katika hukumu ya kuanza na kumaliza kufunga. Unahakikisha muda wake tu kama umefika.

viii. Mwezi una Manazil (vipimo maalumu kwa ajili ya mwezi peke yake sio jua). Angalia Qur-aan (36: 39). Mwezi: Umejaaliwa kuashiria hesabu ya masiku 1, 2 28, 29 au/na 30. Kuingia kwa siku iliyoashiriwa na muandamo wa mwezi ndio unaufanya Ummah wa Kiislamu ufunge au ufungue Ramadhaan. Jua: Limejaaliwa kuashiria hesabu ya sekunde , dakika, saa, siku, wiki, miezi (months), miaka pamoja na miongo (Seasons) kwa ujumla. Mwenendo wa jua ndio unaofafanua nyakati za Swala, kula daku na kufuturu. Wala huwezi kutumia mienendo ya mwezi au Manazil yake katika kuashiria nyakati za Swala, kula daku au kufutari. Kusema: (jua likitenguka Makka watu wa Zanzibar wasali?!) kama alivyosema ndugu Juma katika kitabu chake uk 20, hizo ndio hoja za mitaani anazozikataa, kisha akawa anazitumia mwenyewe. Sisi tunamjibu hivi: Basi wakiswali Dar es Salaam na Kigoma waswali? Nizwa wakiswali na Ruwi waswali? Maana wanafunga siku moja". Mwisho wa kunukuu.

Jawabu ya ujumla Aya isemayo:

"Yeye (Mwenyezi Mungu) ndiye aliyelifanya jua (kutoa) mwangaza na mwezi (kuakisi) nuru na akaupangia (huo mwezi) vituo (vya kusafiria) ili mpate kujua idadi ya miaka na hesabu (ya nyakati)" , imetaja khabari nayo ni maneno yasemayo: "Huwa Al-Ladhi Ja'ala" (Yeye ndiye aliyejaalia). Kisha ikaletwa Al-Lamu Al-Ta'aliliya Lita'alamu. Kisha ikaletwa Al-Ma'alul Aya ikasema: 'Adada Al-Sinina Wa Al-Hisab. Kwa hivyuo, kama mulikuwa nyinyi ni watu wa fani za elimu kama munav yodai mungelijua kwamba hapa mumesukuma bila ya elimu. Hii inamaanisha kuwa kujua idadi ya miaka na hesabu ndio sababuu ya kuumbwa jua na mwezi katika Aya hio. Na haya yametajwa katika Aya moja - mf anyaji ni mmoja na illa (sababu) iliotajwa ni moja. Kwa hivyo, Aya kama ilivyolihusisha jua ndivyo ilivouhusisha mwezi katika kazi zile zile.

Ama njia ya kufanya Qiyas baina ya jua na mwezi si kama mulivyodhania. Kumbukeni kuwa vitu viwili vinaweza kuwa vinatafautiana katika baadhi ya mitazamo (in some aspects) na vitawafikiana katika mitazamo myengine. Qiasi hufanywa katika zile sehemu zilizo sawa: si zile ziliotafauti. Wala si kwamba kitu kilichotomika kufantiwa qiasi kitu chengine huwa hakizingatiwi kabisa kwa sababu kuna shemu ziko tafauti kama mulivyodhani nyinyi. Tafadhali rejeeni vitabu vya usuli mujifunze kufanya Qiasi musisukume mukapoteza watu bila ya elimu. Waliofanya kiasi baina ya jua na mwezi, wametazama zile sehemu ambazo vitu viwili hivyo vimelingana. Nayo ni kama nilivyoeleza katika kitabu kwamba:

1) Wajibu wa Sala umefungamanishwa na kutenguka na kuzama kwa jua - kitu cha kimaumbile (Natural phenomenon). Kwa hivyo mtenguko wa jua ni sababu ya kuingia wajibu wa Sala.

2) Wajibu wa funga umefungamanishwa na muandamo wa mwezi - kitu cha kimaumbile (Natural phenomenon). Kwa hivyo kuandama kwa mwezi ni sababu ya kuingia wajibu wa wajibu wa funga.

4) Jua - ambalo kutenguka kwake ndio sababu ya kuwajibikiwa na sala - likitenguka katika nchi moja, watu wa nchi nyengine hawawajibikiwi na sala. Kwa hivyo, Qiyas sahihi ni kuwa kuonekana kwa mwezi - ambayo ni sababu ya kuwajibika funga - katika nchi moja isiwe sababu ya kufunga kwa watu wa nchi nyengine. Hiki ni Qiyas sahihi. Au ukipenda kufanya Qiyas chengine sahihi, basi ni kile tulichokinukuu kutoka kwa Sheikh Al-'Uthaimin, aliposema:

"Na wakati wa mwezi ni kama wakati wa siku Kama vile ambavyo miji inatafautiana katika kuanza kujizuia (na kula na kunywa na jimai: yaani kuanza kufunga) na (inavyotafautiana katika) kufuturu kwa siku (daily au basi vivyo hivyo inawapasa watafautiane katika kujizuia na kufuturu kwa mwezi (monthly). Na (kama) inavyojulikana kwamba tafa uti za kisiku zina athari zake kwa makubaliano ya Waislamu. (Watu) waliyo upande wa mashariki, hakika wao wanaanza kufunga kabla ya waliyo upande wa magharibi na wanafuturu kabla yao.

Wala haiwezekani mtu akasema kwamba kauli yake Allah (S.W. inayosema):"Sasa waingiliyeni (wake zenu) na tafuteni kile Allah alichokuandikiyeni, na kuleni na kunyweni mpaka ukubainikieni uzi mweupe kutokana na uzi mweusi wa alfajiri, kisha timizeni saumu hadi usiku." Na kauli yake Mtume (s.a .w.w):"Usiku ukitokeza kutoka hapa na mchana ukaondoka kutokea hapa na jua likatua, basi aliyefunga ameshafungua (au na-afungue)." (Haiw ezekani mtu akasema kwamba Aya hio na Hadithi hii) kwamba ni za ujumla wa Waislamu wote katika miji yote. Basi vivyo hivyo tunasema kuhusu ujumla wa kauli yake Allah (S.W.):"Atayeushuhudia mwezi miongoni mwenu na-aufunge" . Mwisho wa kunukuu.

Na kauli hii - kama unavyoona - ina nguvu yake kwa mujibu wa lafdhi (yake) na mtazamo sahihi na Qiyas sahihi vile vile: Qiyas cha wakati wa siku kwa (kuulinganisha) na wakati wa mwezi (month). Ama vifungu mulivyovileta vyote bado havijajibu hoja hizi. Kifungu cha kwanza kinasema: "a) Mwezi na jua ni vitu viwili tofauti vinavyofanya kazi tofauti katika huo wakati (time). Kila kimoja kinafanya kazi yake maalumu kwa kuashiria huo wakati maalumu uliopangiwa". Ninasema: nukta inayozungumzwa na wanavyuoni ni kuwa vyote viwili:

1) Ni vipimo vya nyakati

2) Kuingia kwake ni sababu za kuwajibika ibada.

3) Ni vitu vya kimaumbile (Natural phenomena).

Natija ni kuwa ikiwa tunakubaliana kwamba kutenguka jua nchi moja au katika watu wenye matalai moja ya jua si sababu ya kuingia wajibu was Sala katika nchi au matalai nyengine, basi vipi mwezi kuonekana katika matalai moja au nchi moja iwe ni sababu ya kufunga watu wa matalai au nchi nyengine?!

Kifungu (b) kinasema: b) Hukumu ya ((Fungeni kwa kuona mwezi na Swalini kwa kutenguka jua)) ni vitu viwili tofauti kwa sababu zifuatazo: i. Hadiyth ya kufundisha nyakati za Swala aliteremka Sayyidna Jibriyl ('Alayhi swalaatu was-salaam) kuja kumfundisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala haina khitilafu ya mahala kwa Wanavyuoni karibu wote. Angalia pia Qur-aan Tukufu (17: 78).

JAWABU

Sijui hata munasema nini!!! Kwanza mimi sikuzungumzia Hadithi ((Fungeni kwa kuona mwezi na Swalini kwa kutenguka jua)) na Hadithi ya Jibril ya nyakati za Sala. Bali nimezungumzia Hadithi hio, na Aya "Simamisheni sala kwa kutenguka jua". Na hoja nilioitoa ni kuwa katika Aya na Hadithi mwote kuna (ujumla) ulio sawa. Huku fungeni na kule Salini; huku kwa kuuona mwezi; kule kwa kutenguka jua - ujm la na illa (sababu) ni sawa katika maandiko yote mawili. Sasa ili iwe mumenijibu, basi inakubidini mujibu yale nilioyasema na muoneshe kuwa ujumla ulio huku na kule ni tafauti, sio mulete Hadithi ambayo mimi sikuitaja kamwe wala haihusiani na kile tunachokizungumza! Pili ni kuwa hata hio Hadithi munayoizungumzia nyinyi haijabatilisha niliyosema bali inayapa nguvu yale ninayosema kwamba kila watu na nyakati zao pamoja na kuwa andiko ni moja lile lile.

MNASEMA

"Hukumu ya mgonjwa au mtu aliye safarini anayo ruhusa ya kutokufunga hata kama ameona mwezi lakini hana ruhusa ya kutokuswali kabisa hata akiwa mgonjwa au aliye msafiri". iii. iii) mashariki " jua nyakati za Ibada za watu. Yaani kuweza kujua wakati wa kufunga., kutaja "ikma hkani kabisa,Mwanamke aliye katika siku zake ambaye amepewa ruhusa ya kutofunga Swaum ya Ramadhaan na kutokuswali atakuja kulipa Swaum, lakini hatolipa Swala.

JAWABU

Yametangulia maelezo kwamba vitu viwili huwa vinaoana katika baadhi ya mazingatio na kufarikiana katika mazingatio mengine. Wanavyuoni wanapofanya Qias baina ya vitu viwili hivyo, huwa hawadai kwamba vitu hivyo ni sawa katika kila kitu; bali huwa wanadai kuwa ni sawa katika zile sehemu walizozifanyia qias. Lau Mtume(s.a.w.w) - kwa mfano - alisema: "Musile samaki Fulani kwani ana sumu: anaua". Basi hapa hutafutwa illa (sababu) ya kukatazwa kula samaki huyo. Illa (sababu) ikipatikana na kwa hapa ni kuwa ana sumu, basi kila chenye sumu hupewa hukumu hio hio. Tukimkuta mnyama wa nchi kavu mwenye miguu mine ana sumu basi hupewa hukumu hio hio. Tukikuta tunda lina sumu hupewa hukumu hio hio. Huwezi tena kuda kwamba "Aa yule ni samaki anaishi baharini; huyu ni mnyama wa nchi kavu ana miguu miwili" au "Aa yule ni samaki anaishi baharini; hili ni tunda". Inayotazamwa ni illa (sababu), ikipatikana basi hukumu huthibiti palipotajwa hukumu na pasipotajwa. Huo ni mfano tu. Sasa tazama mambo ambayo wanavyuoni wameyafanyia Qiyas:

1) Imekuja Hadithi yenye kusema:"Kusengenya na kutia maneno mabaya baina ya watu, kunatoa udhu na kunavunja saumu" . Kama kawaida ya wanavyuoni huwa wanatafuta Illa (sababu) ya hukumu ikiwa Illa (sababu) hio haikutajwa kwa uwazi, kwani hukumu za kisharia ni zenye sababu. Hapa wakatafuta Illa (sababu) na wakaishia kwamba sababu ni kuwa matendo hay o ni katika madhambi makubwa. Kwa hivyo, wenye mtazamo huu wakasema kuwa kila dhambi kubwa inatengua udhu.

Wakati ukizitazama dhambi kubwa zenyewe ziko aina tafauti: kuzini ni tafauti na kulewa; kuiba ni tafauti na kuua n.k. Lakini kinachotazamwa ni kuungana kwa Illa (sababu) ndiko kunakovifanya vitu tafauti kuwa na hukumu moja. Ama ukitazama upande zilizotafautiana dhambi hizo, utaona kuiba hukumu yake ni kukatwa mkon; kuzini hukumu yake ni kupigwa mijeledi au kuuliwa; kuua hukumu yake ni kuuliwa. Lakini katika baadhi ya awajuh (aspects) zake, dhambi hizo ni sawa, nazo ni kuwa zote ni dhambi kubwa zenye kumpeleka mtu motoni kama hakutubia. Kwa hivyo, mfanyaji Qias huwa anatazama je ni katika mambo gani ya vitu viwili hivi mimi nayalinganisha. Ikiwa mambo hayo ni sawa, basi hukumu fulani itakuwa sawa. Na wala haina maana kuwa vitu viwe sawa katika hali zote. Bali hakuna hasa duniani vitu viliosawa katika hali zote, na kwa hivyo ingelikuwa kuna ufahamu huo mulio nao nyinyi, basi ingelikuwa hakuna kamwe kitu Qias.

2) Mtume(s.a.w.w) anasema:"Pombe imeharamishwa kwa sababu ya kulewesha kwake". Illa (sababu) ya kuharamishwa pombe ni hio iliotajwa. Kwa hivyo, kila penye Illa (sababu) hio hukumu inakuwa ni hio hio, ikiwa chenye kulewesha ni pombe au bangi au kokeni? Lakini ikiwa hujui Qias kinafanywa vipi, unaweza kutoa hoja kama hizo zenu ukasema:

a) Aa pombe inafanya kwa matunda mabovu (kwa Warabu wa kale inafanywa hasa hasa kutokana na zabibu) wakati bangi ni majani ya mmea unaoota.

b) Pombe inafanywa kutokana na matunda yaliooza, wakati bangi na kokeni ziko safi: haziozi! c) Pombe ni maji maji; wakati bangi na kokeni ni kavu.

Hivi ndivyo mtu asiyejua Qias kinafanywa vipi - kama nyinyi - anavyoweza kudai. Yaa Nas! Qias kinafanywa katika sehemu zilioafikiana baina ya vitu kwa sababu ya kuwepo sababu ilio sawa baina yao, wala haina maana kuwa vitu hivyo ni sawa katika kila kitu, zindukeni!

3) Mtume(s.a.w.w) alikataza kurembea mawe, kisha akataja Illa (sababu) ya kukataza huko, akasema:"Kwani haliwindi kiwindwa wala halimpigi na kumshinda adui, bali linavunja jino na kutofoa jicho" . Kwa hivyo, baada ya Mtume kutaja Illa (sababu) hizo, basi kinafanyiwa kiasi kila chenye kuwa na sifa hizo (chenye kuvunja jino, chenye kukata mguu, chenye kuvunja mkono) yaani vyenye kuweza kujeruhi: vyote vinaingia katika katazo. Wala huwezi kusema "Aa pigi (kwipi) ni tafauti na jiwe: pigi ni tawi la mti; jiwe limeundika katika ardhi". Tafauti hizi sizo zinazofanyiwa Qiasi: Qiasi kinafanyiwa zile sehemu zilio sawa. Kwa hivyo, vitu viwili vinaweza kuwa tafauti katika baadhi ya mitazamo yake (some aspects) na kuwa sawa katika mitazamo mingine, Qiyasi baina ya vitu hivyo hufanywa katika sehemu zenye kuwiyaana si zenye kufarikiana.

Kwa hivyo, kutafautiana kwa hukumu ya mgonjwa katika kusali na kufunga, na kuruhusika kwa mwanamke kutokulipa sala hakuvunji ukweli kwamba jua na mwezi viko sawa katika mas-ala ya nyakati. Katika mas-ala ya nyakati, kuingia kwa wajibu was ala kumefungamanishwa na jua - natural phenomenon (kitu cha kimaumbile); kuingia kwa wajibu wa saumu kumefungamanishwa na mwezi - natural phenomenon (kitu cha kimaumbile). Kutenguka kwa jua katika matlai fulani hakuwafanyi watu wa matlai mengine walazimikiwe na sala; kwa hivyo, kuandama kwa mwezi katika matlai fulani hakuwafanyi watu wa matlai mengine wawajibikiwe na funga.

Pili: ni kuwa hayo masuala mulioyasema, yamekuwa hivyo kwa sababu ya kuwepo ushahidi mwengine wa kimaandiko - yote yana dalili zake katika Hadithi. Na penye andiko huwa hakuna kufanya Qias kama kanuni zinavyoeleza. Yaani makusudio ya kuwa hapana Qias na andiko, ni kuwa huwezi kuleta Qiyas cha kubomoa andiko: si Qias chanye kuunga mkono andiko: Qias cha kuunga mkono andiko kimebarikiwa na kinatumika sana. Sisi suala letu ni kuwa je suala la kuzingatia matalai - tukiwacha kuwepo kwa maandiko (Hadithi ya Quraib) - je linapata nguvu katika Qiyas sahihi? Hili ndio suala. Nasi tunasema ndio, linapata nguvu ya Qias sahihi kama tulivyobainisha mara nyingi.

MNASEMA

Hutokezea (ijapo kwa Sadfa) watu wa eneo kubwa kama nchi zote za Kiarabu hufunga Swaum zao kwa siku moja kutokana na muandamo wa mwezi. Lakini hawaswali Swala zao za faradhi kwa wakati mmoja - kwa kufuata jua wala hilo halina pingamizi wala mjadala kama ilivyokuwa hakuna ikhtilafu katika kufuturu wakati wa kuzama jua.

JAWABU

1) Mimi sina kumbu kumbu ya nchi zote za Kiarabu kuonekana mwezi sawa au kufunga sawa. Kama nyinyi munazo munaweza kutupa.

2) Mimi katika kitabu changu, nilichokipinga ni kudai kuwa muandamo mmoja unatosha kwa dunia nzima na nikabainisha kuwa hili ni kinyume na Hadithi ya Kuraib. Ama eneo gani tufunge, nilikiri kuwa huu ni uwanja wa ijtihad. Kwa hivyo, kipengele hiki nacho pia kina mushkila.

MNASEMA

Kumbuka kilichozungumzwa ndani ya kitabu cha Shaykh Naaswir Bachuu pamoja na Wanavyuoni wote wakubwa waliokuja na hoja ya kufunga pamoja. Wameelezea uwezekano wa kufunga dunia nzima katika siku moja, sio dakika au saa moja ya siku. Kwa mfano, dunia nzima inaswali Swala ya Ijumaa siku moja ya Ijumaa. Hakuna Ijumaa mbili duniani bali kuna kupitana na kutanguliana na hayo yanakuwa hata katika nchi moja.

JAWABU

Nami napinga kwamba kuna uwezekano huo. Binafsi mwezi wa tano na wa sita 2009 nilikuwa Hong Kong. Nikampigia simu mtu aliyeko U.S.A, nikamuuliza kwenu saa ngapi? Akanambia saa kumi za jioni. Wakati huo mimi nilikuwa nishatoka msikitini kiasi cha saa kumi na moja na nusu au kumi na mbili kasoro kidogo au kumi na mbili. Hii ni kusema kuwa J/tatu asubuhi Hong Kong ni J/pili jioni U.S.A. Ikiingia alfajiri U.S.A, Hong Kong jua limeshatua kwa hivyo ni J/ane. Sasa uko wapi huo uwezekano wa dunia kufunga sawa?

Pili: je nyinyi si ndio muliokataa Qiasi cha Sala na funga, vipi tena hapa munalinganisha uwezekano wa kusali siku moja na uwezekano wa kufunga siku moja? Tatu: Kusali Ijumaa siku moja katika siku inayoitwa ijumaa, ni sawa kwani sababu imeshapatikana na wakati umeshafika, lakini suala letu ni je wanasali sawa sawa au kila mtu ni kwa mujibu wa wakati wake?

MNASEMA

Nyakati za Swala zimetengenezewa Jadweli (Time table) zinazolingana na mitenguko ya jua lakini suala la kufunga (Swaum) halikubaliki kufanyiwa jadweli au kalenda za muandamo wa mwezi sharti mwezi uonekane japo kwa macho ya mtu mmoja.

JAWABU

Na kusali pia ni sharti jua litenguke au lizame. Kusali kwetu kwa kufata jaduweli, ni kwa sababu tuna yakini kuwa wakati tayari: si kwa kutegemea jadueli. Lau na mwezi tulikuwa na yakini basi pia tungefanya hivyo hivyo. Ndio maana mwezi 30, tunafunga bila ya kuutazama kwani tuna yakini kwamba upo. Mas-ala hapa ni kuwepo yakini na kutokuwepo. Ama kwa kuzingatia asili ya amri, basi yote mawili - jua na mwezi - ni lazima vitazamwe.

Pili : jaduweli si jambo la kisharia tunaweza kuzikubali na tunaweza kuzikataa. Bali hio ni ijtihada ya watu tu: hakuna Aya wala Hadithi iliosema "Salini kwa kufata jadueli" bali "Salini kwa kutenguka jua". Tatu: ni kuwa yale niliokufahamisheni kwa urefu kwamba Qias baina ya mambo mawili si lazima kwamba yawe yameafikiana katika kila kitu bali yawe yameafikiana katika zile sehemu zinafantiwa Qias, zinafanya tafauti hii pia iwe haina umuhimu.

MNASEMA

Si sharti kuliona jua kwa macho hata kwa mtu mmoja wakati wa kuchomoza au kutua (kuzama) katika hukumu ya kuanza na kumaliza kufunga. Unahakikisha muda wake tu kama umefika.

JAWABU

Suala letu si mas-ala ya kuona au kutokuona, bali ni kuwa jua likitenguka katika nchi moja: si hoja kwa watu wan chi nyengine; basin a mwezi uwe hivyo hivyo kwani vyote ni vyombe vya kupimia wakati kwa ajili ya kuingia wajibu wa ibada.

MNASEMA

Mwezi una Manazil (vipimo maalumu kwa ajili ya mwezi peke yake sio jua). Angalia Qur-aan (36: 39).

Jawabu Aya ya 39 ya Sura ya 36 inasema:"Na Mwezi tumeupimia vituo mpaka ukarejea (kuwa mwembamba) kama karara kongwe (la mtende)" . Aya hii inathibitisha kwamba mwezi una manazil: haikanushi kwamba jua lina manazil. Wala hakuna mtaalamu yeyote aliyesema kuwa "Mwezi una Manazil (vipimo maalumu kwa ajili ya mwezi peke yake sio jua)" kama munavyosukuma nyinyi bila ya elimu. Nimebainisha katika kitabu changu na kunukuu maneno ya Al-Sayyid Al-Tukhi Al-Falaki kwamba: Manazil ni hizi nyota tunazoziona usiku, kama tulivyotangulia kunukuu maneno ya mtaalamu wa falaki Al-Tukhi kutoka katika kitabu chake kinachoitwa Ahkamu Al-Hakim Katika anga hii ya dunia kuna mijumuiko kumi nambili ya nyota ambayo inaitwa buruji. Kila mjumuiko mmoja ni buruji moja. Nazo ziko katika anga. Anasema Allah: (Naapa kwa anga yenye buruji (mikusanyiko ya nyota). Na kila buruji moja ina vituo ambavyo ndivyo vinavyoitwa manazil. Kwa hivyo, kama mwezi unavyopita katika buruji hizi, ndivyo jua, dunia na sayari nyenginezo zinavyopita: zote zinapita katika buruji zile zile na kwa hivyo zinapita katika manazil yale yale. Hii ni kusema kwamba jua na mwezi vyote viwili vina manazil. Fatilia kalenda zilizoandikwa na wataalamu wa falaki, utaona wanasema jua siku kadha liko katika buruji kadha, manzila (kituo) kadha daraja (degree) kadha. Na mwezi siku kadha uko katika buruji kadha, manzila kadha daraja kadha.

Nimekuelezeni katika kitabu kwamb kutoa ushahidi kwa Aya: "Na Mwezi tumeupimia vituo mpaka ukarejea (kuwa mwembamba) kama karara kongwe (la mtende)" kwamba jua halina manazil ni makosa, kwani ni kutoa ushahidi kwa njia ya Mafhumu Al-Llaqab nayo ni batili - taqriban - kwa makubaliano ya Umma mzima. Mafhumu Al-Llaqab ni kama mtu kusema: "Muhammad ni Mjumbe wa Mungu." Mwengine akasema "Basi Mussa si Mjumbe wa Mungu!" Huyu wa pili kajenga hoja yake kwa kutumia Mafhumu Al-Llaqab nalo ni kosa kwani kusemwa kwamba Muhammad ni Mjumbe wa Allah, haimaanishi kwamba hakuna Wajumbe wengine. Kwa hivyo, na hapa iliposemwa "Mwezi una manazil" nyinyi mukajibu: "Basi jua halina!!!!" Iliposemwa "Jua lina matalai" mukajibu "Basi mwezi hauna." Na haya ni makosa ya kifani. Kwani nikisema fulani alikuwa mwanachuoni wa Zanzibar inamaanisha kwamba yeye alikuwa mwanachuoni; wala haimaanishi kuwa mwengine hakuwa?! Au nikisema "Abu Bakr alikuwa muadilifu," maana yake ni kuwa Umar hakuwa?!

MNASEMA

"Mwezi: Umejaaliwa kuashiria hesabu ya masiku 1, 2 28, 29 au/na 30. Kuingia kwa siku iliyoashiriwa na muandamo wa mwezi ndio unaufanya Ummah wa Kiislamu ufunge au ufungue Ramadhaan. Jua: Limejaaliw a kuashiria hesabu ya sekunde, dakika, saa, siku, wiki, miezi (months), miaka pamoja na miongo (Seasons) kwa ujumla. Mwenendo wa jua ndio unaofafanua nyakati za Swala, kula daku na kufuturu. Wala huwezi kutumia mienendo ya mwezi au Manazil yake katika kuashiria nyakati za Swala, kula daku au kufutari".

JAWABU

Sawa! Lakini huo sio upande uliofanyiwa Qias baina ya vitu hivyo. Qias kimefanyiwa kwa mazingatio kwamba vitu vyote viwili hivyo ni vyombo vya kudhibiti wakati na ni kuingia kwake ni sababu ya kuwajibika ibada ya sala kwa upande wa jua; na kuwajibika kwa ibada ya saumu kwa upande wa mwezi. Jua likitenguka katika matalai moja au mji mmoja huwa si hoja kwa watu wa matalai au wa mji mwengine; kwa hivyo Qias ni kuwa na kuandama kwa mwezi katika matalai moja kusiwe hoja kwa watu wa matalai au wa mji mwengine. Tafadhali tazameni ni juu ya nukta gani Qias kimefanywa: sio mutafute tafauti katika sehemu ambazo sizo wanavyuoni wanazozifanyia Qias; angalieni mule walimofanyia Qias kasha ikiwa muna tafauti ndio mupinge.

Tumesema vitu viwili vinakuwa sawa katika mazingatio fulani kama pombe na bangi au kokeni kwa mazingatio kwamba vyote vinalevya; na vinakuwa tafauti katika mazingatio mengine kama tulivyobainisha kabla. Ukitaka kufanya Qias, kwanza unatazama hukumu unayotaka kuithibitisha. Kwa hapa ni uharamu. Pili unatazama sababu ya uharamu huo katika Aslu (Shina), kwa hapa ni kulewesha. Tatu unatazama je sababu hio ipo katika Far'u (tawi)? Jawabu ndio, bangi na kokeni nazo zinalewesha. Kwa hivyo, hukumu y a bangi na kokeni inakuwa sawa na pombe - vyote ni haramu kwa sababu ya kuungana katika Illa (sababu) ya uharamu. Wala hutazami tafauti za kuwa bangi ni majani; pombe ni maji maji; bangi haikuoza; pombe ni matunda yalioza. Hufanyi hivyo, kwani wewe lengo lako ni kutafuta nini kimesababisha pombe kuwa haramu, ukikipata unakitazama je katika bangi na kokeni kimo au hakimo. Hivi ndivyo Qias kinavyofanywa: sio hivyo mulivyodhania nyinyi. Halkadhalika mwezi na jua, kinachotazamwa ni kuwa jua ni kipimo cha ibada ya sala na ni sababu ya kuingia wajibu wake. Na mwezi pia ni kipimo cha ibada ya funga na ni sababu ya kuingia wajibu wake. Jua likitenguka mahala fulani haliwi sababu ya watu wa sehemu nyengine kusali; kwa hivyo, Qias sahihi ni kuwa kuandama kwa mwezi mahala Fulani isiwe sababu ya watu wa sehemu nyengine.

MNASEMA

Kusema: ((jua likitenguka Makka watu wa Zanzibar wasali?!)) kama alivyosema ndugu Juma katika kitabu chake uk. 20, hizo ndio hoja za mitaani anazozikataa, kisha akawa anazitumia mwenyewe. Sisi tunamjibu hivi: Basi wakiswali Dar es Salaam na Kigoma waswali? Nizwa wakiswali na Ruwi waswali? Maana wanafunga siku moja.

JAWABU

Hili ndilo tatizo lenu moja niliolizungumzia katika utangulizi: hamunukuu maneno yenye kuleta maana kamili. Suala je ilikuwaje hata mimi nikasema:"Jua likitenguka Makka watu wa Zanzibar wasali?! Je nilikuwa nadai kuwa watu wafanye hivyo au nilikuwa najibu hoja? Ufupisho wa kwanini nimesema hivyo, ni kuwa Sheikh Nassor aliichukua Aya isemayo:"Yeye (Allah) Ndiye aliyelifanya jua kua muanga na mwezi kua nuru na akaupimia (huo mwezi) vituo, ili mujue idadi ya miaka na hisabu," kuwa ni ushahidi juu ya muandamo mmoja duniani kote. Nami nikajibu - mukhtasari wake - kwamba Aya hii haina uhusiano na muandamo wa Kisharia, vyenginevyo Aya imetaja jua na mwezi kama ni vyombo vya nyakati. Kisha Aya ikataja illa (sababu) ya kuumbwa vitu hivyo nayo ni kujua idadi ya miaka na hesabu. Sasa nikamwambia Sheikh wangu kwamba, ikiwa yeye kaona kuwa Aya hii ni dalili ya muandamo wa Kisharia na kwamba muandamo mmoja - kwa mujibu wa Aya - unatosha dunia kote; basi Aya imetaja pia jua, kwa hivyo, nalo mtenguko wake mmoja na-utoshe duniani kote. Kwani Aya kama ilivyoutaja mwezi kuwa ni chombo cha kujua wakati ndivyo ilivyolitaja jua kwa lengo hilo hilo - illa ni moja na ma'alul ni moja. Hapa ndio nikasema kwamba, kwa mantiki yake hio ya kutoa ushahidi kwa Aya hii, basi na jua likitenguka Makka watu wa Zanzibar wasali kwani yeye katoa Aya hio kuthibitisha muandamo mmoja; na Aya imetaja jua na mwezi.

Hio ndio hoja yangu. Nyinyi kwa ufahamu wenu finyu au kwa ghushi zenu munakata kipande cha maneno yangu kisha munasema Juma kasema jua likitenguka Makka watu wa Zanzibar wasali!!! Fahamu ziko wapi: mimi sijasema hivyo.

Ama tafauti ya kufuturu Kigoma na Dar-es-salam na kuungana kwa kufunga, mumeikariri sana humu nami nimeieleza nukta hii katika sehemu nyengine kama mbili mutazikuta humu. Ama Niz-wa na Rui wanasali sawa na wanaona mwezi sawa.kuhusiana na jua na mwezi, ni kwamba humo mulimoona nyinyi kuwa muna tafauti simo mulimotumika kufanya Qias baina ya vitu viwili hivyo. Na inaposemwa kwamba vitu fulani vimefanyiwa Qias, haimaanishi kuwa vitu hivyo ni sawa katika pande zake zote; bali ina maanisha kwamba hukumu iliopo katika kitu ambacho hukumu yake imetajwa, inaingia katika kitu ambacho hukumu yake haikutajwa kwa sababu ya kuwepo illa jami'a sababu moja yenye kupelekea hukumu hio kuingia katika vitu viwili hivyo. Vyenginevyo, lau wanavyuoni wanatafautisha kama hivyo mulivyofanya nyinyi basi kusingelikuwepo na kitu Qiasi duniani kamwe kwani kuvikuta vitu viwili au zaidi vimeshabihiana katika pande zote ni muhali.

6

MUANDAMO WA MWEZI

SEHEMU YA NANE

KUTOKUTAJWA KWA MATLAI YA MWEZI NDANI YA QUR-AAN

Katika kitabu changu nilisema hivi: Anaendelea Sheikh Nassor Bachoo na maelezo yake kwa kusema: "Jambo jengine la kuzingatiwa ni kwamba wanavyuoni karibu wote wamekubaliana kuwa machomozo (matlai) yamehusiana na jua na kwamba kila eneo (pahala) linafata majira ya kuchomoza, kupinduka na kuzama kwa jua katika hukumu ya kusimamisha sala ndani ya siku hio hio moja kwa ulimwengu mzima. (Angalia: surat Al-israa (Banii Israil) 17: 78). Lakini hakuna aya hata moja katika Qur-an (bali hata hadithi moja, iliyokuja kujuzisha (kukubalisha) kuwepo kwa tafauti za matlai ya mwezi. Kwa hivyo basi hakuna hoja hata moja ya kisharia iliyokuja kukubalisha kuwepo kwa Matlai ya mwezi 'MATLAI-QAMAR' Neno MATLAI mara zote katika Qur-an limekuja likiambatanishwa pamoja na JUA, 'MATLAIL-SHAMS'. Zifuatazo ni baadhi ya Aya zilizotaja habari ya matlai:-

1)"Unaliona jua linapochomoza" AL-KAHF (18:17)

2)"Hata alipofika matokea ya jua AL-KAHF (18:90).

3)"Na umtukuze Mola wako pamoja na kumsifu kabla halijatoka jua" TAHA (20:130). Mwisho wa kunukuu. Kisha nami nikatoa maelezo yangu kama ifatavyo: Kwa hakika mimi kabla sijasoma kitabu cha Sheikh Nassor Bachoo, nilimsikia kijana mmoja akisema maneno hayo, n a yeye akaongezea kwa kusema: "Bali mwezi una manazil." Bila shaka aliikusudia - kwa usemi wake huo - Aya inayosema: "Na mwezi tumeupimia manazil" (vituo) .

Kwa hivyo watu hawa ni kwamba wametazama Aya ya Qur-an inayosema:"Na mwezi tumeupimia manazil" (vituo), na Aya kama:"Hata alipofiki machomozo ya jua" . Wakaona mwezi ndio wenye manazil na jua ndilo lenye matalai: mwezi hauna matalai wala jua halina manazil!!! Watu wangejua kwamba Qur-an haifasiriwi ila kwa fani zake, basi wangejua kwamba tafsiri yao hio wameijenga katika "MAFHUMU AL-LLAQAB," nayo ni batili - taqriban - kwa makubaliano ya Umma mzima, kama tulivyotangulia kueleza. Tumebainisha huko nyuma nini "MAFHUMU AL-LLAQAB," na kwamba hii ni kama mtu kusema: "Muhammad ni Mjumbe wa Mungu." Mwengine akasema "Basi Mussa si Mjumbe wa Mungu!" Huyu wa pili kajenga hoja yake kwa kutumia "MAFHUMU AL-LLAQAB," nalo ni kosa kwani kusemwa kwamba Muhammad ni Mjumbe wa Allah, haimaanishi kwamba hakuna Wajumbe wengine. Kwa hivyo, na hapa iliposemwa "Mwezi una manazil" wao wakajibu: "Basi jua halina!!!!" Walipoambiwa "Jua lina matalai" wakajibu "Basi mwezi hauna." Jamani! Kwani nikisema fulani alikuwa mwanachuoni wa Zanzibar inamaanisha kwamba mwengine hakuwa?! Au nikisema "Abu Bakr alikuwa muadilifu," maana yake ni kuwa Umar hakuwa?!

Kwa ufupi labda watu hawajui manazil ni nini. Manazil ni hizi nyota tunazoziona usiku, kama tulivyotangulia kunukuu maneno ya mtaalamu wa falaki Al-tukhi kutoka katika kitabu chake kinachoitwa "AHKAMU AL-HAKIM" Katika anga hii ya dunia kuna mijumuiko kumi nambili ya nyota ambayo inaitwa buruji. Kila mjumuiko mmoja ni buruji moja. Nazo ziko katika anga. Anasema Allah:"Naapa kwa anga yenye buruji" (mikusanyiko ya nyota). Na kila buruji moja ina vituo ambavyo ndivyo vinavyoitwa manazil.

Kwa hivyo, kama mwezi unavyopita katika buruji hizi, ndivyo jua, dunia na sayari nyenginezo zinavyopita: zote zinapita katika buruji zile zile na kwa hivyo zinapita katika manazil yale yale. Hii ni kusema kwamba jua na mwezi vyote viwili vina manazil. Fatilia kalenda zilizoandikwa na wataalamu wa falaki, utaona wanasema jua siku kadha liko katika buruji kadha, manzila (kituo) kadha daraja (degree) kadha. Na mwezi siku kadha uko katika buruji kadha, manzila kadha daraja kadha. Ama matalai, ni wingi wa neno, na maana yake ni kuchomoza au mahala pa kuchomoza. Kwa maana ya kwanza itakuwa ni (Jina lililoaanzia na mimu), kama linavyotumika neno Mi'iraj kwa maana ya Al-uruj (Kupaa). Na asili ya muundiko huu wa neno Mi'iraj hutumika kwa jina la chombo au zana kama Miftahu yaani chombo au zana ya kufungulia (ufunguo). Na kwa maana ya pili ya neno Matla'i ni (Jina la pahala). Kwa maana hii, jua na mwezi yote yana matalai, kwani yote yanachomoza na yana sehemu za kuchomoza. Na kwa sababu hii, wale wenye kujua Kiara bu sawa sawa hawakuona tabu - katika kumsifu Mtume(s.a.w.w) - kusema:

Mwezi umetalai kwetu (umechomoza). Na Mtume(s.a.w.w) hakuwambia kwamba mwezi hauchomozi. Sikusudii kusema kwamba Mtume(s.a.w.w) ni mwezi, laa: sio hivyo, lakin i kilichopo katika kasida hii ya Masahaba wa Madina ni kitu kilichofananishwa na kitu chengine: kimoja ni hakika cha pili ni majazi (metaphor au mithali). Lakini cha kufahamu ni kuwa katika kufanya tashbihi (kukifananisha k itu kimoja na chengine kwa maana ya mithali) basi kimoja ni lazima kiwe hakika ndivyo kilivyo. Halkadhalika hakuna aliyemkosoa Mshairi aliposema: Viumbe wote wanasubiri t unuko lake kama Mahujaji wanavyosubiri Mwezi muandamo uchomoze. Halkadhalika ukirudi katika kamusi la Kiarabu mashuhuri na lenye kutegemewa nalo ni Lisanu Al-Arab la Ibn Mandhur, utakuta alipokuwa akilielezea neno: Tala'a (kutalai au kuchomoza) ali sema: Chomoza: Limechomoza jua na mwezi na alfajiri na nyota.

Kwa hivyo jua na mwezi - yote mawili - yana matalai na manazil, na kutokutajwa matalai ya mwezi katika Qur-an haina maana kwamba hicho kitu hakipo kwani Qur-an haikutaja kila kitu kwa ufafanuzi, bali imetaja kila kitu kwa ujumla tu, na Allah kasema:"Alipouona mwezi unachomoza. "Anasema Al-sabuni katika tafsiri yake: "Bazighan ni Taalian: husemwa bazagha Al-qamaru (Mwezi umebazighi) unapoanza kuchomoza." Pili ni kuwa: suala la kuchomoza mwezi ni kitu cha maumbile tunachokishuhudia sote: hatuna haja ya kusubiri ushahidi wa Qur-an. Kwani nikisema kwamba binaadamu wanakwenda aridhini, huwa ninahitaji ushahidi wa Qur-an kuthibitisha maneno yangu? Mwisho wa kunukuu nilioyasema kitabuni.

JAWABU NILILOPATA

Kujibu hoja hio, ndugu zangu wakasema ifatavyo:

8. Kutokutajwa Kwa Matlai Ya Mwezi Ndani Ya Qur-aan Katika kuelezea mada hii Shaykh Naaswir Bachuu kwenye kitabu chake ameelezea kama ifuatavyo:- Lakini hakuna Aya hata moja katika Qur-aan (bali hata Hadiyth moja iliyokuja) kujuzisha (kukubalisha) kuwepo kwa tofauti za Matlai ya mwezi. Kwa hivyo basi hakuna hoja hata moja ya kisheria iliyokuja kukubalisha kuwepo kwa Matlai ya mwezi 'Matlial-Qamar'. Neno Matlai mara zote katika Qur-aan limekuja likiambatanishwa pamoja na Jua 'Matlai-shamsi'. Zifuatazo ni baadhi ya Aya zilizotaja habari za Matlai:"Unaliona jua linapochomoza...." (18: 17)"Hata ilipofika matokea ya jua " (18: 90)Na umtukuze Mola wako pamoja na kumsifu kabla halijatoka jua (Taha 20: 130)

" Na Mtukuze Mola wako kwa kumsifu, kabla ya kutoka jua..." (50: 39) Kwa upande wa Ndugu Juma, yeye anayaona maelezo hayo siyo sahihi, lakini kwa bahati mbaya kama kawaida yake hakuweza kutoa hata Aya moja kuthibitisha hoja yake. Tahamaki anajaribu kutoa hoja ya kuwepo "Matlail - Qamar" kwa hoja za mashairi, maneno ya kiarabu pamoja na kutukumbusha kipande cha Qasida maarufu. Sasa ukirejea tena katika maelezo ya Shaykh Naaswir Bachuu utakuta kuwa bado ndugu yetu Juma ana deni kubwa juu ya uthibitishaji wake katika mas-ala haya. Kwa kuwa Shaykh Naaswir ametulia katika misingi miwili imara ya Qur- aan na Sunnah. Ingetarajiwa Ndugu Juma naye angetoa hoja katika misingi hiyo hiyo lakini anaonesha umahiri wake katika kuhifadhi beti za Qasida wala Shaykh Naaswir hakusema hakuna aliyesema "Mat-lail-Badru" katika Qasida. Kwani Qasida au mashairi hata ndugu Juma anaweza kusema atakavyo wala hakatazwi. Alichosema Shaykh Naaswir ni kwamba hapakutajwa lafdhi ya "Matlail-Qamar" ndani ya Qur-aan lakini pametajwa: "Matlai-Shams."[2][2]

Kwa upande mwengine, Ndugu yetu Juma amejaribu kutaka kuonyesha kwamba yapo Matlai ya mwezi kwa kuinukuu Aya ya Qur-an isemayo:"Na alipouona mwezi unachomoza alisema: "Huu ndio Mola wangu." (6: 77) Hapa ingefaa aelezwe Ndugu Juma kama anakusudia kwamba ni dalili katik a Aya hiyo kuwepo kwa "Matlail - Qamar" basi kwa mujibu wa mtiririko wa Aya zilizotangulia kabla ya Aya hiyo, hazina uhusiano wowote katika masuala hayo. Wala hajulikani mfasiri hata mmoja aliyeifasiri hivyo Aya hiyo hata Ndugu Juma akapata kigezo hicho. Ama kama anakusudia kutujuulisha mtindo wa lugha ya Kiarabu kuhusu neno atakuwa amekwenda kinyume na kanuni, kwani tujuavyo sisi kitabu chake alichokiandika ni cha mas-ala ya mwezi wala hakihusiani na lugha". Mwisho wa kunukuu.

Nayo ni jawabu ya kuchekesha. Kwa ufupi nasema je nyinyi munapinga kwamba mwezi hauchomozi? Kama unachomoza je pale unapochomozea panaitwa vipi kwa Kiarabu na kwa Kiswahili? Na je kwani kitu kutokutajwa katika Qur-ani huwa hakipo? Au kitu kikithibiti katika ulimwengu wa hakika huwa kinatosha kuthibitishwa. Nakukumbusheni mulioyasema: "Jambo la asli halihitaji (kuletewa) dalili, (lakini dalili inahitajika katika jambo lisilo la asili)." Nikisema kuwa binaadamu wanakwenda kwa miguu aridhini huwa nahitaji ushahidi wa Qur-an kuthibitisha hilo? Na nani kakwambiyeni kwamba lugha ya Kiarabu sio msingi mama wa kuifasiri Qur-an hata mukakataa kutoa kwangu ushahidi wa kuwepo kwa matala ya mwezi kwa Aya isemayo:"Na alipouona mwezi unachomoza alisema: "Huu ndio Mola wangu." (6: 77) Ikiwa Aya hii inathibitisha kwamba mwezi unachomoza vipi tena utakataa kwamba mwezi una machomozo?! Hivi si vichekesho?! Pia nimekutajieni maelezo ya Shei kh Al-Sabuni akisema kuwa maana ya neno "Bazagha" ni kuchomoza; halafu munadai hakuna mwanachuoni aliyefasiri hivyo.

Halafu kwa kusukuma kwenu mambo ya elimu bila ya kuyarejesha katika fani zake zinazotumika kufasiria maandiko munasema: "Ingetarajiwa Ndugu Juma naye angetoa hoja katika misingi hiyo hiyo lakini anaonesha umahiri wake katika kuhifadhi beti za Qasida wala Shaykh Naaswir hakusema hakuna aliyesema "Mat-lail-Badru" katika Qasida. Kwani Qasida au mashairi hata ndugu Juma anaweza kusema atakavyo wala hakatazwi". Na munamnukuu Sheikh akisema: "Lakini hakuna Aya hata moja katika Qur-aan (bali hata Hadiyth moja iliyokuja) kujuzisha (kukubalisha) kuwepo kwa tofauti za Matlai ya mwezi". Ninasema: Aya nimekupeni:"Na alipouona mwezi unachomoza alisema" . Kilichobaki munambie ni maana ya kuchomoza katika Aya hii. Kumbukeni kwamba kinachozingatiwa si lafdhi bali ni maana, maana moja ya kitu inaweza kuwa na lafdhi nyingi. Thaub (nguo) inapotajwa kwa jina la libas (kivazi), huwezi kukataa ukasema nguo haikutajwa kwani maneno yote hayo yana maana moja. Ama Hadithi munayoidai, inaonesha hata hamujui Hadithi ni nini? Hadithi au Sunna zimegawika sehemu tatu:

1) Qawliyya (ya maneno). Yaani pale Mtume(s.a.w.w) anaposema au kuamuru au kukataza kitu.

2) Fi'iliyya (ya kimatendo). Yaani pale Mtume(s.a.w.w) anapotenda kitu.

3) Taqririyya (ya kukiri au kukubali). Yaani pale Mtume(s.a.w.w) anapokiona kitu kinatendwa au kinanenwa mbele yake naye asikikitaze.

Kwa hivyo, kama umelifahamu hilo basi utakuwa umeelewa kwamba kipande cha Qasida maarufu katika elimu ya Hadithi huwa kinaitwa Sunna taqririyya ni Hadithi ya kuona kitu ukakikubali. Sasa anayeomba Hadithi juu ya suala la matalai ya mwezi, kwanza na-akasome elimu ya Hadit hi. Kwa ufupi, nahisi sina haja ya kurefusha kwa vile munaonekana hamutaki ukweli bali munataka ushabiki, vyenginevyo musingeliukataa ushahidi wa wazi wa Qur-ani bila ya hoja sahihi. Bali suala lu kuwa mwezi una matala halitaki ushahidi wa Qur-ani kamwe kwani tunauona ukichomoza na sehemu unayochomoza.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ تَفَرَّقُوا وَاخْتَلَفُوا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ وَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾

105.Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi; na hao ndio wenye adhabu kubwa.

﴿يَوْمَ تَبْيَضُّ وُجُوهٌ وَتَسْوَدُّ وُجُوهٌ فَأَمَّا الَّذِينَ اسْوَدَّتْ وُجُوهُهُمْ أَكَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴾

106.Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika. Na ama ambao nyuso zao zitasawijika, (wataambiwa): Je mlikufuru baada ya kuamini kwenu? Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha.

﴿وَأَمَّا الَّذِينَ ابْيَضَّتْ وُجُوهُهُمْ فَفِي رَحْمَةِ اللَّـهِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

107.Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, Wao humo watadumu.

﴿تِلْكَ آيَاتُ اللَّـهِ نَتْلُوهَا عَلَيْكَ بِالْحَقِّ وَمَا اللَّـهُ يُرِيدُ ظُلْمًا لِّلْعَالَمِينَ ﴾

108.Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki; na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe.

﴿وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴾

109.Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni; na kwa Mwenyezi Mungu hurejezwa mambo yote.

KUHITALIFIANA BAADA YA MTUME

Aya 105 - 109

MAANA

Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi.

Aya hii inamalizia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote" Makusudio ya wale waliofarakana ni watu wa Kitabu, Ambapo mayahudi walichangukana vikundi sabini na moja baada ya Mtume wao Musa, wakristo wakawa vikundi sabini na mbili baada ya Mtume wao Isa, Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu."Baada ya kuwajia hoja iliyo wazi" inafahamisha kwamba mtu haadhibiwi kwa kuiacha haki na kufuata batili, ila baada ya kubainishiwa hoja. Ama siri ya mkazo huu na kuupa kipaumbele muungano wa umma, ni kuwa utengano ndio kiini cha ufisadi na kwamba umma uliotengana hauwezi kuwa na maisha mazuri, wachilia mbali kuuita umma mwingine kwenye kheri. Pamoja na kuwapo Riwaya nyingi, na Hadith zinazohimiza muungano wa waislamu, lakini bado wamefarakana na kuwa vikundi mbali mbali, wamewazidi mayahudi kwa vikundi viwili zaidi na wakristo kikundi kimoja; kama ilivyoelezwa katika Hadith mashuhuri.

Kuna Hadithi nyingine isemayo: "Mtakuwa na desturi ile ile ya waliokuwa nayo kabla yenu." Akaulizwa: "Unakusudia mayahudi na manaswara ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Akasema: "Kumbe ninawakusudia kina nani? Utachanguka uthabiti wa waislamu" Katika kitabu Al-Jam'u Bainas-Sahihayni cha Hamid, kwenye Hadith Na. 131, anasema: Katika yaliyoafikianwa kutoka Musnad ya Anas bin Malik, amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) :"Watanijia watu miongoni mwa sahaba zangu kwenye hodhi, nitakapowaona na watakapokuwa wanaletwa kwangu watazuiwa ili wasinifikie. Hapo nitasema: 'Ewe Mola! Sahaba zangu, sahaba zangu! Nami nitaambiwa: 'Wewe hujui walizua nini baada yako" Katika kitabu hicho hicho Hadith Na. 267 anasema: "Katika yaliyaofikianwa kutoka Musnad ya Abu Huraira kutoka katika njia mbali mbali, ni kwamba Mtume amesema: "Wakati nikiwa nimesimama - siku ya Kiyama - litatokea kundi la watu mpaka nitakapowatambua, atatokea mtu baina yangu na yao na awambie: 'Haya twendeni.' Mimi nitauliza: Mpaka wapi? Naye aseme: 'Mpaka motoni' Nami niulize wana nini? Naye ajibu: 'Hakika wao walirtadi baada yako"

Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika.

Makusudio ya Siku, ni Siku ya Kiyama. Kung'aa uso, ni fumbo la kuonyesha furaha ya mumin kufurahia radhi za Mwenyezi Mungu na fadhila Zake. Kusawijika uso ni huzuni ya kafiri na fasiki kwa ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na ama ambao nyuso zao zitasawijika,(wataambiwa), je, mlikufuru baada ya kuamini kwenu?

Arrazi, Tabari na wafasiri wengine wengi wamenukuu kutoka kwa baadhi ya waliopita, kwamba makusudio ya watakaoambiwa hivyo ni Khawariji. Kwa sababu Mtume alisema kuwahusu:"Hakika wao watachomoka kutoka katika dini, kama unavyochomoka mshale kutoka katika uta (upinde)." Lakini dhahiri ya Aya inamkusanya kila mwenye kukufuru baada ya imani, wakiwemo Khawariji, watu wa bid'a na wenye maoni potofu. Kwa vile adhabu haihusiki tu na aliyekufuru baada ya imani bali inamuhusu kafiri yeyote, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Onjeni adhabu, kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha, Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, wao humo watadumu.

Rehma ya Mwenyezi Mungu ni Pepo. Kwa ufupi ni kwamba wale ambao wameshikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, na kufanya mambo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wakasaidiana kwenye mambo ya kheri na ya masilahi ya umma, basi watafufuliwa kesho wakiwa watukufu, wenye furaha na wenye kuridhia. Ama wale ambao wamehitalifiana kwa kuipupia dunia, wasiojishughulisha na dini wala umma au nchi, na ambao hawajishughulishi na lolote isipokuwa masilahi yao na ya watoto wao tu, basi wao watafufuliwa Siku ya Kiyama wakiwa madhalili, wenye hasara na makazi yao ni Jahanam, nayo ni marejeo mabaya kabisa. Ajabu ya maajabu ni kwamba baadhi ya wenye nyuso zilizosawijika wanadai kuwa wanamzungumzia Mungu na kutumia Jina lake, lakini mtu akiwaambia "Muogopeni Mungu" wao husema: "Umemkufuru Mwenyezi Mungu." Aliyewatangulia katika hilo ni Abdul Malik bin Marwan aliposema pale alipochukua Ukhalifa: "Kuanzia leo atakayeniambia muogope Mwenyezi Mungu nitamkata kichwa chake."

Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki.

Hizi, ni ishara ya Aya zinazoelekezea kuneemeshwa watu wema na kuadhibiwa makafiri. Msemo unamwelekea Muhammad(s.a.w.w) , muulizaji anaweza kuuliza: "Kuna faida gani katika habari hii, ikiwa Muhammad anajua kwa yakini kwamba Aya hizi ni haki na ni kweli?" Jibu: Ni kawaida ya Qur'an kulikariri hilo katika Aya kadhaa. Na makusudio sio kwa Muhammad hasa, bali ni kwa yule anayetia shaka na kudhani kwamba Aya hizi na mfano wake zinatoka kwa Muhammad, si kwa Mwenyezi Mungu.

﴿وَمَا كُنتَ تَتْلُو مِن قَبْلِهِ مِن كِتَابٍ وَلَا تَخُطُّهُ بِيَمِينِكَ إِذًا لَّارْتَابَ الْمُبْطِلُونَ﴾

"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wabatilifu" (29:48)

Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe, Kwa sababu dhuluma ni mbaya na Mwenyezi Mungu ameepukana nayo.

Aya hii ni dalili ya mkato kwamba Mwenyezi Mungu hakalifishi mja asiloliweza.

﴿كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَلَوْ آمَنَ أَهْلُ الْكِتَابِ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُم مِّنْهُمُ الْمُؤْمِنُونَ وَأَكْثَرُهُمُ الْفَاسِقُونَ﴾

110.Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu. Na lau watu wa Kitabu wangeliamini ingekuwa heri kwao. Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki .

﴿لَن يَضُرُّوكُمْ إِلَّا أَذًى وَإِن يُقَاتِلُوكُمْ يُوَلُّوكُمُ الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ ﴾

111.Hawatawadhuru isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia, kisha hawatasaidiwa.

UMMA WA MUHAMMAD

Aya 110 - 111

MAANA

Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu

Kuna njia kadhaa kuhusu Aya hii, kama ifuatavyo:

1) Katika makusudio ya umma, hakuna mwenye shaka kuwa makusudio ya umma hapa ni Umma wa Muhammad(s.a.w.w) , kwa dalili ya mfumo wenyewe wa maneno ulivyo na mtiririko wa misemo inayoelekezwa kwa waumini; kama vile; "Enyi ambao mmeamini mcheni Mwenyezi Mungu. Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu kwenu…" Mpaka kufikia kauli yake Mwenyezi Mungu:"Mmekuwa ni umma bora."

2). Je, makusudio ni waislamu wote katika wakati wote, au ni kuwahusu wale walio kuwa katika siku za kwanza za uislamu kama vile Masahaba na waliofuatia (tabiina)?

Jibu : Kuainisha makusudio ya umma hapa, kunahitaji kujua makusudio ya herufi kana (kuwa) ambayo ilivyo ni kuwa inahitaji isimu na habari yake. Pia hiyo kana inafahamisha kufanyika kitendo wakati uliopita, lakini haielezi ni wakati gani kimefanyika hicho kitendo wala kuwa kinaendelea au la.

Isipokuwa hilo linaweza kufahamika kutokana na vitu vingine vilivyo pamoja nayo kimaneno au hali ilivyo. Kwa mfano kusema, Zaid alikuwa ni mwenye kusimama. Hapo inachukuliwa kutendeka tendo la kusimama na kuisha bila kuendelea. Yaani Zaid, hakuwa ni mwenye kusimama, basi akasimama kipindi fulani bila ya kuendelea kusimama maisha. Lililofahamisha hilo ni neno mwenye kusimama, yaani hawezi kusimama maisha. Lakini kama tukisema Mwenyezi Mungu amekuwa ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu, hapo hali inafahamisha kudumu kwa tendo lenyewe, kwa sababu rehema na maghufira haviepukani na dhati yake Mwenyezi Mungu, na dhati yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ni ya milele na milele. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufungamanisha ubora wa umma na kumwamini kwake, na kuamrisha mema na kukataza maovu, basi maana ya Aya yanakuwa ni: Enyi waislamu! Msiseme tu sisi ni umma bora mpaka muamrishe na kukataza maovu; na kwamba sifa hii ya ubora itawaondokea mara tu mnapopuuza hilo.

Kwa hivyo basi kana hapa inakuwa ni kamilifu, sio pungufu; yaani haihitaji khabar. Kwa maana hayo makusudio ni waislamu wote([2] ) .

3).Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu 'mliotolewa kwa Watu' inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemleta Muhammad na umma wake(s.a.w.w) ushinde umma zote za mwanzo ukiwa umechukua Kitabu cha Mwenyezi Mungu mkono mmoja na Hadith za Mtume kwenye mkono mwingine, huku ukiwalingania vizazi vishikamane na vitu viwili hivyo na kuvitegemea kwa itikadi, sharia na maadili. Kwa sababu ndio marejeo pekee yanayoweza kuhakikisha ufanisi wa mambo yote, kudhamini maisha ya kila mtu na kufungua uwanja wa wenye uwezo wa kufanya ijitihadi kwa misingi ya usawa, amani na uhuru wa watu wote([3] ) .

Aya hii katika madhumuni yake inaafikiana na Aya isemayo:

﴿وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُمَّةً وَسَطًا لِّتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ وَيَكُونَ الرَّسُولُ عَلَيْكُمْ شَهِيدًا﴾

"Tumewafanya ni umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu na Mtume awe shahidi juu yenu." (2:143)

Ikiwa waislamu hawatafanya harakati zozote za kulingania kwenye kheri au kuamrisha mema na kukataza mabaya, basi sifa za uongozi zitawaondokea na watakuwa na haja ya kiongozi atakayewaamrisha mema na kuwakataza maovu. Ulikuwepo wakati ambapo waislamu walikuwa na harakati hizi. Wakati huo walikuwa wakistahili kuwa viongozi wa umma zingine; kisha wakapuuza; wakaendelea hivyo mpaka wakawa wanakataza mema na kuamrisha maovu; kama tuonavyo sasa. Leo vijana wamekuwa wanajivua kabisa na dini na hulka njema. Wakimwona mtu anaswali au kufunga husema kwa dharau: "Bado kuna Swala na Saumu katika karne ya ishirini?" Mwenye Tafsir Al-Manar, katika kufasiri Aya hii, anasema: "Kwa kweli hasa ninasema, haukuzimika ubora wa umma uliotolewa kwa watu, mpaka pale ulipoacha kuamrisha mema na kukataza mabaya. Na haukuacha hivyo kwa kupenda au kupuuza amri ya Mwenyezi Mungu, bali ni kwa kulazimishwa na ufedhuli wa Wafalme wa bani Umayya na waliofuata nyayo zao."

Kwa msingi vitu hutajwa kwa kinyume chake; kama ambavyo hutajwa kwa kifani chake, basi tutaleta Hadith tukufu aliyoitaja Hafidh Muhibbudin Attabari, amesema: "Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) 'Mfano wa Ahlu bait wangu, ni kama safina ya Nuh mwenye kuipanda ataokoka, na mwenye kushikamana nayo ataokoka, na mwenye kuachana nayo ataghariki'". Ama Hadith ya "Mimi nawaachia vizito viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kizazi changu - Ahlul bait wangu," imepokewa na wapokezi 35 katika Masahaba.

Na lau wangeliamini watu wa Kitabu, ingelikuwa heri kwao.

Yaani lau watu waliopewa Tawrat na Injil, wangelimwamini Muhammad(s.a.w.w) ingelikuwa imani yao hiyo ni heri yao katika muda wa sasa na ujao.

Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki.

Yaani katika watu wa Kitabu kuna waliomwamini Muhammad(s.a.w.w) ; kama vile Abdullah bin Salam na watu wake, na wengineo katika wanaswara, na wengi wao walibaki katika ukafiri.

Neno Fasiq na Kafir yanapokezana maana, hutumiwa Fasiq kwa maana ya Kafiri na Kafir kwa maana ya Fasiq. Na Fasiq hapa ina maana ya kafiri. Hawatawadhuru, isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia Madhara yako aina mbili:

Kwanza : ni kiasi cha huzuni na kusikia uchungu tu, ambako kadiri siku zinavyokwenda nayo yanafutika; kama vile inavyotokea katika nafsi kwa kusikia habari mbaya.

Pili : ni yale yanayogusa maisha na kuyumbisha; kama vile madhara yaletwayo na dola ya Israil ndani ya nchi ya Waarabu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewabashiria maswahaba wa Mtume(s.a.w.w) kwamba watu wa Kitabu:

Hawatawadhuru isipokuwa kwa maneno tu, kama vile uzushi na mabezo. Ama katika uwanja wa vita, nyinyi ndio washindi.

Amesema kweli Mwenyezi Mungu katika kiaga chake, Aliwapa ushindi waislamu wa mwanzo kwa wakristo na wengineo.

﴿ضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ أَيْنَ مَا ثُقِفُوا إِلَّا بِحَبْلٍ مِّنَ اللَّـهِ وَحَبْلٍ مِّنَ النَّاسِ وَبَاءُوا بِغَضَبٍ مِّنَ اللَّـهِ وَضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الْمَسْكَنَةُ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَانُوا يَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَيَقْتُلُونَ الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ﴾

112.Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana, isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki, hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

WAMEPIGWA CHAPA YA UDHALILI

Aya 112

MAANA

Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili.

Wafasiri wameafikiana kuwa, Aya hii imeshuka kwa ajili ya mayahudi; kama ambavyo wameafikiana kuwa makusudio yake ni kuwa Mwenyezi Mungu amewanyima utukufu na takrima, na akawaandikia udhalili tangu ulipoanza uislamu hadi siku ya mwisho. Kwa sababu wao katika ufisadi na kupetuka mipaka wamefikilia hatua ambayo hakuifikia na hataifikia yeyote. Baada ya wafasiri kuafikiana juu ya hilo, wametofautiana kuhusu aina ya udhalili na unyonge walio nao (Mayahudi ambayo iko kwa kila kizazi). Tofauti hiyo hasa inatokana na tofauti ya hali ya mayahudi wakati wa kufasiri, ambapo walikuwa wakitoa kodi kwa waislamu, yaani kauli ya mfasiri imekuja kuakisi na walivyokuwa wayahudi. Hiyo si ajabu maadam mtu anaathirikia kwa anachokisikia na kukiona, Na tafsiri yangu ya Aya hii inafuata desturi hii.

Vyovyote iwavyo, ninavyofahamu ni kwamba udhalili wa mayahudi uliokusudiwa na Aya ni huku kutawanyika kwao duniani, Mashariki na Magharibi, wakiwa wako kwenye nchi mbali mbali. Wao daima ni wafuasi na wala sio wanaofuatwa na kuhukumiwa katika dola yao. Wako peke yao katika mambo yao. Ama Israeli iliyoko Tel Aviv ni Dola ya jina tu, ilivyo hasa ni kambi tu ya kikoloni na ni kituo cha jeshi cha uchokozi. Hakika hii imedhihiri wazi wazi baada uchokozi wa Israel katika ardhi za Waarabu mnamo tarehe 5 Juni 1967. Ni uchokozi ambao wanaufanya waisrail ili kutekeleza mahitaji yao. Lau watauacha siku moja tu watanyang'anywa na waarabu.

Huo ndio udhalili hasa, kwa sababu mwenye heshima zake hutegemea nguvu zake mwenyewe na kujihami kwa mikono yake sio mikono ya wengine. Kwa hali hii, inatubainikia kuwa makusudio ya kamba ya watu, ni msaada wa kihali na mali utolewao na mataifa ya kikoloni kwa ajili ya kambi ya kikoloni ya Israel. Kwa hivyo basi tunaamini bila ya tashwish yoyote kwamba Dola ya Israil itaondoka tu kwa kuondoka ukoloni. Na ukoloni uko njiani kuisha iwe ni sasa au baadae. Wala maneno hayo sio ndoto, isipokuwa ni natija hasa itakayotokea, kama ilivyoeleza Hadith ya Mtume:"Hakitasimama Kiyama mpaka muwapige vita mayahudi na kwamba jiwe litasema: Ewe Mwislamu! Huyu hapa Yahudi nyuma yangu muue"([4] )

Ama Kamba ya Mwenyezi Mungu ni fumbo la matakwa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: yaani kwamba mayahudi wataendelea kuwa na udhalili mpaka atakapotaka Mwenyezi Mungu: ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu pia isemayo:

﴿قَالَ النَّارُ مَثْوَاكُمْ خَالِدِينَ فِيهَا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ﴾

"Moto ndio makazi yenu mtadumu humo milele ila apende Mwenyezi Mungu" (6:128)

Kisha baada ya hapo, Mwenyezi Mungu amebainisha sababu iliyowajibisha udhalili wao na ghadhabu yake kwao, kwa kusema:

Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki; hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Sura ya Baqara Aya 61.

Unaweza kuuliza : Kuna wasiokuwa Mayahudi katika mataifa mengine waliokanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua watu wema, kuasi na kupetuka mipaka; pamoja na hayo Mwenyezi Mungu hakuwapiga chapa ya udhalili na uduni. Je,kuna siri gani katika kuwahusisha Mayahudi?

Jibu : Mtu anaweza kupetuka mpaka kwa msukumo fulani unaotokana na masilahi yake na manufaa yake. Ama kupetuka mpaka si kwa lolote isipokuwa kwa kupendelea tu kufanya dhambi, hakujatokea kwa yeyote isipokuwa mayahudi tu, na pupa hii ya kupenda dhuluma na uovu iko ndani ya dini ya mayahudi. Wao wanaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu yuko na wao tu, sio wengineo; bali pia yuko dhidi ya maadui zao; na kwamba watu wote wameumbwa kwa ajili yao tu ili wawafanye vile watakavyo, sawa na mtu amfanyiavyo mnyama. Jambo linalofahamisha zaidi sera yao hiyo, zamani na sasa, ni fedheha yao katika Palestina, hasa waliyo yafanya huko Dayr Yasin, kuwachinja wanawake na watoto.

Mwanzo walikuwa wakiwaua Mitume wakati dunia ilipokuwa na Mitume. Ama leo, ambapo hakuna Mitume wanawaua wasuluhishaji; kama vile Bernadotte([5] ) , na wanawake na watoto. Kwa sababu, la muhimu katika itikadi yao na maumbile yao ni kuwaua watu wasiokuwa na hatia; wawe Mitume au wasuluhishi au watoto.

Tawrat yao imeandika uhalali wa kumwaga damu ya wanawake na watoto, na imelihimiza hilo. Kwa ujumla ni kwamba kuzikanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua wasuluhishi na watu wema wasio na hatia, na kufanya dhuluma na uchokozi, yote hayo ni dini na itikadi ya Mayahudi. Myahudi akimfanyia kosa mwengine asiyekuwa Myahudi basi anafanya kwa kujiburudisha tu, sio kwa haja fulani. Na kama akiacha kufanya hivyo, basi anaacha kwa kuogopa sio kwa kujistahi.

Hii ndiyo tofauti kati ya mayahudi na wasiokuwa mayahudi. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa Mwenyezi Mungu kuwawekea udhalili popote walipo.

Ama serikali habithi ya Israel ya sasa itaondoka tu, hakuna budi, Ushahidi mkubwa wa kwisha kwake ni kwamba imefungamana na ukoloni, ukoloni ukiondoka nayo inaondoka. Na ukoloni lazima uondoke tu, hata kama ni baada ya miaka. Maadam maumbile ya kibinadamu yanaukataa ukoloni na kuupinga kwa damu yake, basi utaondoka tu.

Yote haya tuliyoayataja yanakamilisha kifungu cha 'Mayahudi hawana mfano' katika tafsiri ya Sura Baqara (2) Aya63 na 66.

﴿لَيْسُوا سَوَاءً مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ﴾

113.Wote si sawa Katika watu wa Kitabu wamo walio na msimamo, wakasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku huku wakinyenyekea.

﴿يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَأُولَـٰئِكَ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴾

114. Wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wanaamrisha mema na wanakataza mabaya na wanaharakia mambo mema na hao ndio miongoni mwa watu wema.

﴿وَمَا يَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَلَن يُكْفَرُوهُ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ ﴾

115.Heri yoyote watakayoifayahaitakataliwa, Na Mwenyezi Mungu anawajua wamchao.

WOTE SI SAWA

Aya 113 -115

LUGHA

Mwenye Majmaul-bayan anasema: Tofauti kati ya neno Sura na Ajala ni kwamba Sura ni kufanya haraka linalojuzu kufanywa, Nako kunasifiwa. Na Ajala ni kufanya haraka jambo lisilofaa kufanywa, nako kunashutumiwa.

MAANA

Aya hizi tatu ziko wazi hazihitaji tafsir, Maana yake kwa ujumla ni kwamba watu wa Kitabu hawako sawa kwamba wote wamepotea, bali wako watu wema miongoni mwao. Wafasiri wengi wamechukulia sifa hii kwa aliyesilimu miongoni mwa watu wa Kitabu, na uzuri wa uislamu wake kimatendo na kiitikadi.

HUKUMU YA MWENYE KUACHA UISLAMU

Mwito wa kumwamini Muhammad kama Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa watu wa ulimwenguni bado upo mpaka Siku ya Mwisho. Nao unaelekezwa kwa watu wote, wa Mashariki na Magharibi. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا ﴾

"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote" (7:158).

Dalili ya ukweli wake ni mantiki ya kiakili, kuthibiti muujiza na kufaa dini kwa maisha. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema: "Msingi wa dini yangu ni akili" Na Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake Kitukufu:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ﴾

"Enyi ambao mmeamini muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume (wake) anapowaitia katika yale yatakayowapa maisha (8:24)

Lengo letu sio kutoa dalili za Utume wa Muhammad(s.a.w.w), ([6] ) isipokuwa lengo ni kubainisha kuwa je, asiyeamini Utume wa Muhammad anastahili adhabu: au hapana budi ya ufafanuzi? Kabla ya kumtofautisha mjuzi na asiye mjuzi na asiyemudu na mzembe, tutaonyesha msingi na vipimo vya kwanza vya kustahili adhabu au kutostahili; kutokana na hivyo, uhakika utafumbuka na kuwapambanua watu. Wote wameafikiana kwamba mtu, vyovyote awavyo, dini yoyote aliyo nayo, hastahili adhabu ila baada ya kusimamishiwa hoja. Na hoja haisimami ila baada ya kuweza yeye kufikia kwenye dalili ya haki na kuweza kwake kuitumia. Hapo akiacha hatakuwa na kisingizio. Ikiwa hakupata dalili ya haki yenye msingi au aliipata akashindwa kuifikia au aliifikia na akatekeleza mtazamo wake wa haki mpaka akafikia mwisho, lakini pamoja na hayo haki haikumdhihirikia, basi yeye atakuwa na udhuru, kwa sababu ya kutokamilika hoja juu yake. Kwa sababu, asiyethibitikiwa na haki haadhibiwi kwa kuiacha, ila ikiwa amezembea katika utafiti.

Vile vile miongoni mwa kawaida za msingi ambazo zinaambatana na utafiti huu ni ile ya "Adhabu kuepukwa na mambo yenye kutatiza." Kwa hiyo haijuzu kumhukumu mwenye kuiacha haki kuwa ni mwenye makosa anayestahili adhabu, maadamu tunaona kuwa kuna uwezekano kuwa anao udhuru katika kuacha kwake. Na kawaida hii inafungamana na watu wote, sio waislamu tu, Pia inakusanya aina zote za mipaka, Mfano kawaida ya 'Mwenye kukosea katika ijtihadi, basi kosa lake linasamehewa', Kawaida hii ni ya kiakili, haiwezekani kuihusisha na dini fulani tu, madhehebu, shina au tawi. Baada ya maelezo hayo hebu tuangalie hali hizi zifuatazo:

1) Kuishi binadamu mji ulio mbali na uislamu na waislamu; wala hakufikiliwa na mwito au hata kusikia jina la Muhammad(s.a.w.w) katika maisha yake yote. Pia awe hajawaza kwa karibu au mbali kwamba duniani kuna dini yenye jina la kiislamu na Mtume aitwaye Muhammad(s.a.w.w) . Hapana mwenye shaka kwamba huyu atasamehewa kwa kuwa hastahili adhabu. Maana akili ina hukumu ubaya wa adhabu bila ya ubainifu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na sisi si wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mitume" (17:15) Bila shaka akili ni Mtume wa ndani kwa ndani, ila tu yenyewe ni dalili ya kupatikana Mwenyezi Mungu tu. Ama dalili ya kuthibiti Utume wa Mtume, hapana budi kuwako na muujiza na udhihirishwe na yeye mwenyewe pamoja na akili kuhukumu kutowezekana kudhihiri kwa wasiokuwa Mitume.

2) Kuusikia mtu uislamu na Muhammad, lakini akawa hawezi kupambanua haki na batili, kwa sababu ya kushindwa kwake na kutoweza kufahamu dalili za haki na maarifa yake. Huyu pia anasamehewa, Kwa sababu yeye ni sawa na mtoto au mwenda wazimu. Mfano ni akitomwamini Muhammad(s.a.w.w) tangu udogo kwa kuwafuata wazazi wake na akajisahau alipokuwa mkubwa, akaendelea na itikadi yake bila ya kuitilia shaka yoyote, huyu atasamehewa. Kwa sababu kumkalifisha aliyejisahau asiye na uwezo ni sawa na kumkalifisha aliyelala. Amesema Muhaqqiq Al-Qummi: "Kujikomboa kutokana na kuiga wazazi ni jambo lisilofikiriwa na wengi, bali hata linakuwa zito aghlabu kwa wanavyuoni waliotosheka ambao wanadhani kuwa wamejivua kutokana na kuiga huko." Amesema tena: "Asiyeweza kung'amua wajibu wa kujua misingi, ni sawa na mnyama na mwedawazimu ambao hawana taklifa yoyote." Sheikh Tusi anasema: "Mwenye kushindwa kupata uthibitisho yuko katika daraja ya mnyama."

Hata hivyo, ikiwa aliyejisahau atakumbushwa wajibu wa maarifa, au kuambiwa na mtu: "Wewe uko au hauko sawa katika itikadi yako", lakini pamoja na hayo akang'ang'ania na wala asifanye utafiti na kuuliza, basi huyo atakuwa ni mwenye dhambi, kwa sababu atakuwa ni mzembe, na kutojua kwa mzembe si kisingizio.

3) Kutomwamini Muhammad(s.a.w.w) pamoja na kuwa anao uwezo wa kutosha wa kufahamu haki, lakini yeye alipuuza wala asijali kabisa: au alifanya utafiti pungufu na akauacha bila ya kuangalia mwisho wake; kama wafanyavyo wengi, hasa vijana wa kisasa. Basi huyu hatasameheka kwa sababu amekosea bila ya kujitahidi na alikuwa na uwezo wa kujua haki, lakini akapuuza. Ni wazi kuwa pia ataadhibiwa ambaye amefanya utafiti na akakinai, lakini pamoja na hayo akakataa kumwamini Muhammad(s.a.w.w) kwa ubaguzi na mali.

4).Kuangalia dalili na kuwa na mwelekeo wa kufuata haki kwa ikhlasi, lakini pamoja na hayo akakosa kuelekea kwenye njia ambayo itamwajibishia kumwamini Muhammad(s.a.w.w) ama kwa kushikamana kwake na mambo yenye kutatiza ya ubatilifu bila ya kuangalia ubatilifu wake, au kuchanganyikiwa na mengineyo ambayo yanazuia kuona haki. Huyu ataangaliwa hali yake, ikiwa atakanusha Utume wa Muhammad(s.a.w.w) kwa kauli ya mkato, basi yeye ataadhibiwa na kustahili adhabu. Kwa sababu yule ambaye imefichika kwake haki, haifai kwake kukataa moja kwa moja kukanusha haki. Inawezekana kuwa haki ipo lakini akazuiliwa, kuifika, na aghlabu huwa hivyo, kwa sababu mambo ya ulimwenguni yapo lakini tuyajuayo ni machache tu. Hali ni hivyo hivyo kuhusu kuwajua Mitume na wasuluhishi, Ni nani awezaye kujua kila kitu?

Watu wa mantiki wamelielezea hilo kwa ibara mbali mbali, miongoni mwazo ni: Kutokujua hakumaanishi kutokuwepo, kutopatikana hakumaanishi kuacha kupatikana, kuthibitisha na kukanusha kunahitaji dalili. Tumewaona wanavyuoni wengi wakiungana na hakika hii. Wanazituhumu rai zao na kujichunga katika kauli zao; wala hawajifanyi kuwa wao ndio kipimo cha ukweli. Hawawezi kusema: "Rai hii ni takatifu isiyo na shaka, na nyinginezo si chochote." Bali wao huipa mtazamo wa kujiuliza kila rai. Dalili kubwa zaidi ya kuwa mtu hana elimu, ni kule kujidanganya mwenyewe, kuiona safi elimu yake, na kudharau rai na itikadi za wengine.

Zaidi ya hayo kuacha kukinai mtu mmoja miongoni mwa watu kuhusu Utume wa Muhammad(s.a.w.w) hakumruhusu kukanusha Utume wa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) moja kwa moja. Na kama akifanya hivyo, basi atakuwa na jukumu. Hasa baada ya kuona idadi ya mabingwa ambao hawakuathiriwa na kurithi au mazingira, wakimwamini Muhammad na risala yake; si kwa lolote isipokuwa kuiheshimu haki na kuikubali hali halisi ilivyo([7] ) . Hayo ni ikiwa atapinga. Ama akiangalia dalili wala asikinai na pia asipinge; wakati huo huo akawa amenuia kwa moyo safi kuiamini haki wakati wowote itakapomdhihirikia; kama vile mwanafiqh mwadilifu ambaye hufutu jambo kwa nia ya kubadilisha mara tu ikimbainikia kuwa amekosea, basi huyu hatakuwa na jukumu, kwa sababu mwenye kukosea katika ijtihadi yake bila ya kufanya uzembe, hataadhibiwa kwa kukosea kwake; kama inavyohukumu akili na maandishi pia. Imepokewa kutoka kwa Imam Jafar Sadiq(a.s) , amesema:"Lau kama watu wasipofahamu (jambo) wakasimama na wala wasipinge, basi hawakukufuru" Katika Riwaya nyingine: "Hakika anakufuru tu akipinga"

Sheikh Ansari katika kitabu chake maarufu Arrasil mlango wa Dhana katika Usul, anasema: "Hadith nyingi zimefahamisha kuthibiti ukati na kati baina ya kufuru na imani" Ya kwamba mpingaji ni kafiri, mwenye kuitakidi ni Mumin, na mwenye shaka si kafiri wala Mumin. Katika Hadith zinazowezekana kuzitolea dalili ya kutoadhibiwa mwenye kufanya ijitihadi bila ya uzembe kama akikosea katika mambo ya itikadi, ni Hadith hii mashuhuri kwa sunni na shia:"Akijitahidi hakimu na akapata basi atalipwa mara mbili. Na akijitahidi akakosea, basi atalipwa mara moja" Kama mtu akisema kuwa Hadith hii inahusu mwenye kujitahidi katika matawi si katika masuala ya itikadi, kama walivyodai baadhi ya wanavyuoni, basi tutamjibu hivi: Linalomlinda, mwenye kujitahidi katika hukumu, asiadhibiwe ni kule kujichunga kwake na kutofanya uzembe katika utafiti, Na kinga hii inapatikana hasa katika masuala ya kiitikadi.

Zaidi ya hayo Mafaqihi wote wameafikiana kwa kauli moja kwamba mwenye kushindwa kuifikia itikadi ya kweli, anasamehewa. Miongoni mwao ni wale waliohusisha Hadith hii na matawi. Nasi hatuoni tofauti yoyote kati yake na yule mwenye kujitahidi, aliyetoa juhudi zake. Kwa sababu,wote wawili wameshindwa kujua maadam hawakuufikia uhakika. Kwa ufupi ni kwamba mwenye kuipinga, haki yoyote, basi ataadhibiwa, ni sawa awe amejitahidi au la, isipokuwa kama hana maarifa, kama mnyama. Kama akibakia kwenye msimamo wa kutopinga wala kuthibiti sawa, kujitahidi na kuangalia dalili au alifanya ijtihadi pungufu, basi ataadhibiwa. Ikiwa ameangalia dalili akajitahidi mpaka akafikia mwisho wake, basi yeye atasamehewa kwa sharti ya kubakia na mwelekeo wa haki kwa kuazimia kubadili msimamo wake wakati wowote itakapomdhihirikia haki.

Unaweza kuuliza : Umesema kuwa mwenye kushindwa kujua itikadi ya kweli - kama vile Utume wa Muhammad – atasamehewa, Vile vile mwenye kujitahidi ambaye hakuzembea katika jitihadi. Je, maana yake ni kuwa inajuzu kwetu kufanya naye muamala wa kiislamu, kama kuoa, kurithi n.k.

Jibu : Msamaha tunaoukusudia hapa ni kutostahiki adhabu akhera; ama kuoa na kurithi hapa duniani ni jambo jengine. Na kila asiyeamini utume wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) kwa hali yoyote atakayokuwa, haifai kuwa na muamala naye wa kiislam k.v. ndoa, urithi n.k. Ni sawa awe kesho atapona au ataangamia; kama ambavyo mwenye kusema "Laila ilaha illa llah Muhammad Rasulullah" anastahiki ya waislamu, ni juu yake yaliyo juu yao, hata kama alikuwa ni fasiki, bali hata mnafiki vile vile.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ تَفَرَّقُوا وَاخْتَلَفُوا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ وَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾

105.Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi; na hao ndio wenye adhabu kubwa.

﴿يَوْمَ تَبْيَضُّ وُجُوهٌ وَتَسْوَدُّ وُجُوهٌ فَأَمَّا الَّذِينَ اسْوَدَّتْ وُجُوهُهُمْ أَكَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴾

106.Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika. Na ama ambao nyuso zao zitasawijika, (wataambiwa): Je mlikufuru baada ya kuamini kwenu? Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha.

﴿وَأَمَّا الَّذِينَ ابْيَضَّتْ وُجُوهُهُمْ فَفِي رَحْمَةِ اللَّـهِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

107.Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, Wao humo watadumu.

﴿تِلْكَ آيَاتُ اللَّـهِ نَتْلُوهَا عَلَيْكَ بِالْحَقِّ وَمَا اللَّـهُ يُرِيدُ ظُلْمًا لِّلْعَالَمِينَ ﴾

108.Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki; na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe.

﴿وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴾

109.Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni; na kwa Mwenyezi Mungu hurejezwa mambo yote.

KUHITALIFIANA BAADA YA MTUME

Aya 105 - 109

MAANA

Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi.

Aya hii inamalizia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote" Makusudio ya wale waliofarakana ni watu wa Kitabu, Ambapo mayahudi walichangukana vikundi sabini na moja baada ya Mtume wao Musa, wakristo wakawa vikundi sabini na mbili baada ya Mtume wao Isa, Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu."Baada ya kuwajia hoja iliyo wazi" inafahamisha kwamba mtu haadhibiwi kwa kuiacha haki na kufuata batili, ila baada ya kubainishiwa hoja. Ama siri ya mkazo huu na kuupa kipaumbele muungano wa umma, ni kuwa utengano ndio kiini cha ufisadi na kwamba umma uliotengana hauwezi kuwa na maisha mazuri, wachilia mbali kuuita umma mwingine kwenye kheri. Pamoja na kuwapo Riwaya nyingi, na Hadith zinazohimiza muungano wa waislamu, lakini bado wamefarakana na kuwa vikundi mbali mbali, wamewazidi mayahudi kwa vikundi viwili zaidi na wakristo kikundi kimoja; kama ilivyoelezwa katika Hadith mashuhuri.

Kuna Hadithi nyingine isemayo: "Mtakuwa na desturi ile ile ya waliokuwa nayo kabla yenu." Akaulizwa: "Unakusudia mayahudi na manaswara ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Akasema: "Kumbe ninawakusudia kina nani? Utachanguka uthabiti wa waislamu" Katika kitabu Al-Jam'u Bainas-Sahihayni cha Hamid, kwenye Hadith Na. 131, anasema: Katika yaliyoafikianwa kutoka Musnad ya Anas bin Malik, amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) :"Watanijia watu miongoni mwa sahaba zangu kwenye hodhi, nitakapowaona na watakapokuwa wanaletwa kwangu watazuiwa ili wasinifikie. Hapo nitasema: 'Ewe Mola! Sahaba zangu, sahaba zangu! Nami nitaambiwa: 'Wewe hujui walizua nini baada yako" Katika kitabu hicho hicho Hadith Na. 267 anasema: "Katika yaliyaofikianwa kutoka Musnad ya Abu Huraira kutoka katika njia mbali mbali, ni kwamba Mtume amesema: "Wakati nikiwa nimesimama - siku ya Kiyama - litatokea kundi la watu mpaka nitakapowatambua, atatokea mtu baina yangu na yao na awambie: 'Haya twendeni.' Mimi nitauliza: Mpaka wapi? Naye aseme: 'Mpaka motoni' Nami niulize wana nini? Naye ajibu: 'Hakika wao walirtadi baada yako"

Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika.

Makusudio ya Siku, ni Siku ya Kiyama. Kung'aa uso, ni fumbo la kuonyesha furaha ya mumin kufurahia radhi za Mwenyezi Mungu na fadhila Zake. Kusawijika uso ni huzuni ya kafiri na fasiki kwa ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na ama ambao nyuso zao zitasawijika,(wataambiwa), je, mlikufuru baada ya kuamini kwenu?

Arrazi, Tabari na wafasiri wengine wengi wamenukuu kutoka kwa baadhi ya waliopita, kwamba makusudio ya watakaoambiwa hivyo ni Khawariji. Kwa sababu Mtume alisema kuwahusu:"Hakika wao watachomoka kutoka katika dini, kama unavyochomoka mshale kutoka katika uta (upinde)." Lakini dhahiri ya Aya inamkusanya kila mwenye kukufuru baada ya imani, wakiwemo Khawariji, watu wa bid'a na wenye maoni potofu. Kwa vile adhabu haihusiki tu na aliyekufuru baada ya imani bali inamuhusu kafiri yeyote, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Onjeni adhabu, kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha, Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, wao humo watadumu.

Rehma ya Mwenyezi Mungu ni Pepo. Kwa ufupi ni kwamba wale ambao wameshikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, na kufanya mambo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wakasaidiana kwenye mambo ya kheri na ya masilahi ya umma, basi watafufuliwa kesho wakiwa watukufu, wenye furaha na wenye kuridhia. Ama wale ambao wamehitalifiana kwa kuipupia dunia, wasiojishughulisha na dini wala umma au nchi, na ambao hawajishughulishi na lolote isipokuwa masilahi yao na ya watoto wao tu, basi wao watafufuliwa Siku ya Kiyama wakiwa madhalili, wenye hasara na makazi yao ni Jahanam, nayo ni marejeo mabaya kabisa. Ajabu ya maajabu ni kwamba baadhi ya wenye nyuso zilizosawijika wanadai kuwa wanamzungumzia Mungu na kutumia Jina lake, lakini mtu akiwaambia "Muogopeni Mungu" wao husema: "Umemkufuru Mwenyezi Mungu." Aliyewatangulia katika hilo ni Abdul Malik bin Marwan aliposema pale alipochukua Ukhalifa: "Kuanzia leo atakayeniambia muogope Mwenyezi Mungu nitamkata kichwa chake."

Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki.

Hizi, ni ishara ya Aya zinazoelekezea kuneemeshwa watu wema na kuadhibiwa makafiri. Msemo unamwelekea Muhammad(s.a.w.w) , muulizaji anaweza kuuliza: "Kuna faida gani katika habari hii, ikiwa Muhammad anajua kwa yakini kwamba Aya hizi ni haki na ni kweli?" Jibu: Ni kawaida ya Qur'an kulikariri hilo katika Aya kadhaa. Na makusudio sio kwa Muhammad hasa, bali ni kwa yule anayetia shaka na kudhani kwamba Aya hizi na mfano wake zinatoka kwa Muhammad, si kwa Mwenyezi Mungu.

﴿وَمَا كُنتَ تَتْلُو مِن قَبْلِهِ مِن كِتَابٍ وَلَا تَخُطُّهُ بِيَمِينِكَ إِذًا لَّارْتَابَ الْمُبْطِلُونَ﴾

"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wabatilifu" (29:48)

Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe, Kwa sababu dhuluma ni mbaya na Mwenyezi Mungu ameepukana nayo.

Aya hii ni dalili ya mkato kwamba Mwenyezi Mungu hakalifishi mja asiloliweza.

﴿كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَلَوْ آمَنَ أَهْلُ الْكِتَابِ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُم مِّنْهُمُ الْمُؤْمِنُونَ وَأَكْثَرُهُمُ الْفَاسِقُونَ﴾

110.Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu. Na lau watu wa Kitabu wangeliamini ingekuwa heri kwao. Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki .

﴿لَن يَضُرُّوكُمْ إِلَّا أَذًى وَإِن يُقَاتِلُوكُمْ يُوَلُّوكُمُ الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ ﴾

111.Hawatawadhuru isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia, kisha hawatasaidiwa.

UMMA WA MUHAMMAD

Aya 110 - 111

MAANA

Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu

Kuna njia kadhaa kuhusu Aya hii, kama ifuatavyo:

1) Katika makusudio ya umma, hakuna mwenye shaka kuwa makusudio ya umma hapa ni Umma wa Muhammad(s.a.w.w) , kwa dalili ya mfumo wenyewe wa maneno ulivyo na mtiririko wa misemo inayoelekezwa kwa waumini; kama vile; "Enyi ambao mmeamini mcheni Mwenyezi Mungu. Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu kwenu…" Mpaka kufikia kauli yake Mwenyezi Mungu:"Mmekuwa ni umma bora."

2). Je, makusudio ni waislamu wote katika wakati wote, au ni kuwahusu wale walio kuwa katika siku za kwanza za uislamu kama vile Masahaba na waliofuatia (tabiina)?

Jibu : Kuainisha makusudio ya umma hapa, kunahitaji kujua makusudio ya herufi kana (kuwa) ambayo ilivyo ni kuwa inahitaji isimu na habari yake. Pia hiyo kana inafahamisha kufanyika kitendo wakati uliopita, lakini haielezi ni wakati gani kimefanyika hicho kitendo wala kuwa kinaendelea au la.

Isipokuwa hilo linaweza kufahamika kutokana na vitu vingine vilivyo pamoja nayo kimaneno au hali ilivyo. Kwa mfano kusema, Zaid alikuwa ni mwenye kusimama. Hapo inachukuliwa kutendeka tendo la kusimama na kuisha bila kuendelea. Yaani Zaid, hakuwa ni mwenye kusimama, basi akasimama kipindi fulani bila ya kuendelea kusimama maisha. Lililofahamisha hilo ni neno mwenye kusimama, yaani hawezi kusimama maisha. Lakini kama tukisema Mwenyezi Mungu amekuwa ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu, hapo hali inafahamisha kudumu kwa tendo lenyewe, kwa sababu rehema na maghufira haviepukani na dhati yake Mwenyezi Mungu, na dhati yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ni ya milele na milele. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufungamanisha ubora wa umma na kumwamini kwake, na kuamrisha mema na kukataza maovu, basi maana ya Aya yanakuwa ni: Enyi waislamu! Msiseme tu sisi ni umma bora mpaka muamrishe na kukataza maovu; na kwamba sifa hii ya ubora itawaondokea mara tu mnapopuuza hilo.

Kwa hivyo basi kana hapa inakuwa ni kamilifu, sio pungufu; yaani haihitaji khabar. Kwa maana hayo makusudio ni waislamu wote([2] ) .

3).Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu 'mliotolewa kwa Watu' inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemleta Muhammad na umma wake(s.a.w.w) ushinde umma zote za mwanzo ukiwa umechukua Kitabu cha Mwenyezi Mungu mkono mmoja na Hadith za Mtume kwenye mkono mwingine, huku ukiwalingania vizazi vishikamane na vitu viwili hivyo na kuvitegemea kwa itikadi, sharia na maadili. Kwa sababu ndio marejeo pekee yanayoweza kuhakikisha ufanisi wa mambo yote, kudhamini maisha ya kila mtu na kufungua uwanja wa wenye uwezo wa kufanya ijitihadi kwa misingi ya usawa, amani na uhuru wa watu wote([3] ) .

Aya hii katika madhumuni yake inaafikiana na Aya isemayo:

﴿وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُمَّةً وَسَطًا لِّتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ وَيَكُونَ الرَّسُولُ عَلَيْكُمْ شَهِيدًا﴾

"Tumewafanya ni umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu na Mtume awe shahidi juu yenu." (2:143)

Ikiwa waislamu hawatafanya harakati zozote za kulingania kwenye kheri au kuamrisha mema na kukataza mabaya, basi sifa za uongozi zitawaondokea na watakuwa na haja ya kiongozi atakayewaamrisha mema na kuwakataza maovu. Ulikuwepo wakati ambapo waislamu walikuwa na harakati hizi. Wakati huo walikuwa wakistahili kuwa viongozi wa umma zingine; kisha wakapuuza; wakaendelea hivyo mpaka wakawa wanakataza mema na kuamrisha maovu; kama tuonavyo sasa. Leo vijana wamekuwa wanajivua kabisa na dini na hulka njema. Wakimwona mtu anaswali au kufunga husema kwa dharau: "Bado kuna Swala na Saumu katika karne ya ishirini?" Mwenye Tafsir Al-Manar, katika kufasiri Aya hii, anasema: "Kwa kweli hasa ninasema, haukuzimika ubora wa umma uliotolewa kwa watu, mpaka pale ulipoacha kuamrisha mema na kukataza mabaya. Na haukuacha hivyo kwa kupenda au kupuuza amri ya Mwenyezi Mungu, bali ni kwa kulazimishwa na ufedhuli wa Wafalme wa bani Umayya na waliofuata nyayo zao."

Kwa msingi vitu hutajwa kwa kinyume chake; kama ambavyo hutajwa kwa kifani chake, basi tutaleta Hadith tukufu aliyoitaja Hafidh Muhibbudin Attabari, amesema: "Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) 'Mfano wa Ahlu bait wangu, ni kama safina ya Nuh mwenye kuipanda ataokoka, na mwenye kushikamana nayo ataokoka, na mwenye kuachana nayo ataghariki'". Ama Hadith ya "Mimi nawaachia vizito viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kizazi changu - Ahlul bait wangu," imepokewa na wapokezi 35 katika Masahaba.

Na lau wangeliamini watu wa Kitabu, ingelikuwa heri kwao.

Yaani lau watu waliopewa Tawrat na Injil, wangelimwamini Muhammad(s.a.w.w) ingelikuwa imani yao hiyo ni heri yao katika muda wa sasa na ujao.

Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki.

Yaani katika watu wa Kitabu kuna waliomwamini Muhammad(s.a.w.w) ; kama vile Abdullah bin Salam na watu wake, na wengineo katika wanaswara, na wengi wao walibaki katika ukafiri.

Neno Fasiq na Kafir yanapokezana maana, hutumiwa Fasiq kwa maana ya Kafiri na Kafir kwa maana ya Fasiq. Na Fasiq hapa ina maana ya kafiri. Hawatawadhuru, isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia Madhara yako aina mbili:

Kwanza : ni kiasi cha huzuni na kusikia uchungu tu, ambako kadiri siku zinavyokwenda nayo yanafutika; kama vile inavyotokea katika nafsi kwa kusikia habari mbaya.

Pili : ni yale yanayogusa maisha na kuyumbisha; kama vile madhara yaletwayo na dola ya Israil ndani ya nchi ya Waarabu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewabashiria maswahaba wa Mtume(s.a.w.w) kwamba watu wa Kitabu:

Hawatawadhuru isipokuwa kwa maneno tu, kama vile uzushi na mabezo. Ama katika uwanja wa vita, nyinyi ndio washindi.

Amesema kweli Mwenyezi Mungu katika kiaga chake, Aliwapa ushindi waislamu wa mwanzo kwa wakristo na wengineo.

﴿ضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ أَيْنَ مَا ثُقِفُوا إِلَّا بِحَبْلٍ مِّنَ اللَّـهِ وَحَبْلٍ مِّنَ النَّاسِ وَبَاءُوا بِغَضَبٍ مِّنَ اللَّـهِ وَضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الْمَسْكَنَةُ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَانُوا يَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَيَقْتُلُونَ الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ﴾

112.Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana, isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki, hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

WAMEPIGWA CHAPA YA UDHALILI

Aya 112

MAANA

Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili.

Wafasiri wameafikiana kuwa, Aya hii imeshuka kwa ajili ya mayahudi; kama ambavyo wameafikiana kuwa makusudio yake ni kuwa Mwenyezi Mungu amewanyima utukufu na takrima, na akawaandikia udhalili tangu ulipoanza uislamu hadi siku ya mwisho. Kwa sababu wao katika ufisadi na kupetuka mipaka wamefikilia hatua ambayo hakuifikia na hataifikia yeyote. Baada ya wafasiri kuafikiana juu ya hilo, wametofautiana kuhusu aina ya udhalili na unyonge walio nao (Mayahudi ambayo iko kwa kila kizazi). Tofauti hiyo hasa inatokana na tofauti ya hali ya mayahudi wakati wa kufasiri, ambapo walikuwa wakitoa kodi kwa waislamu, yaani kauli ya mfasiri imekuja kuakisi na walivyokuwa wayahudi. Hiyo si ajabu maadam mtu anaathirikia kwa anachokisikia na kukiona, Na tafsiri yangu ya Aya hii inafuata desturi hii.

Vyovyote iwavyo, ninavyofahamu ni kwamba udhalili wa mayahudi uliokusudiwa na Aya ni huku kutawanyika kwao duniani, Mashariki na Magharibi, wakiwa wako kwenye nchi mbali mbali. Wao daima ni wafuasi na wala sio wanaofuatwa na kuhukumiwa katika dola yao. Wako peke yao katika mambo yao. Ama Israeli iliyoko Tel Aviv ni Dola ya jina tu, ilivyo hasa ni kambi tu ya kikoloni na ni kituo cha jeshi cha uchokozi. Hakika hii imedhihiri wazi wazi baada uchokozi wa Israel katika ardhi za Waarabu mnamo tarehe 5 Juni 1967. Ni uchokozi ambao wanaufanya waisrail ili kutekeleza mahitaji yao. Lau watauacha siku moja tu watanyang'anywa na waarabu.

Huo ndio udhalili hasa, kwa sababu mwenye heshima zake hutegemea nguvu zake mwenyewe na kujihami kwa mikono yake sio mikono ya wengine. Kwa hali hii, inatubainikia kuwa makusudio ya kamba ya watu, ni msaada wa kihali na mali utolewao na mataifa ya kikoloni kwa ajili ya kambi ya kikoloni ya Israel. Kwa hivyo basi tunaamini bila ya tashwish yoyote kwamba Dola ya Israil itaondoka tu kwa kuondoka ukoloni. Na ukoloni uko njiani kuisha iwe ni sasa au baadae. Wala maneno hayo sio ndoto, isipokuwa ni natija hasa itakayotokea, kama ilivyoeleza Hadith ya Mtume:"Hakitasimama Kiyama mpaka muwapige vita mayahudi na kwamba jiwe litasema: Ewe Mwislamu! Huyu hapa Yahudi nyuma yangu muue"([4] )

Ama Kamba ya Mwenyezi Mungu ni fumbo la matakwa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: yaani kwamba mayahudi wataendelea kuwa na udhalili mpaka atakapotaka Mwenyezi Mungu: ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu pia isemayo:

﴿قَالَ النَّارُ مَثْوَاكُمْ خَالِدِينَ فِيهَا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ﴾

"Moto ndio makazi yenu mtadumu humo milele ila apende Mwenyezi Mungu" (6:128)

Kisha baada ya hapo, Mwenyezi Mungu amebainisha sababu iliyowajibisha udhalili wao na ghadhabu yake kwao, kwa kusema:

Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki; hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Sura ya Baqara Aya 61.

Unaweza kuuliza : Kuna wasiokuwa Mayahudi katika mataifa mengine waliokanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua watu wema, kuasi na kupetuka mipaka; pamoja na hayo Mwenyezi Mungu hakuwapiga chapa ya udhalili na uduni. Je,kuna siri gani katika kuwahusisha Mayahudi?

Jibu : Mtu anaweza kupetuka mpaka kwa msukumo fulani unaotokana na masilahi yake na manufaa yake. Ama kupetuka mpaka si kwa lolote isipokuwa kwa kupendelea tu kufanya dhambi, hakujatokea kwa yeyote isipokuwa mayahudi tu, na pupa hii ya kupenda dhuluma na uovu iko ndani ya dini ya mayahudi. Wao wanaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu yuko na wao tu, sio wengineo; bali pia yuko dhidi ya maadui zao; na kwamba watu wote wameumbwa kwa ajili yao tu ili wawafanye vile watakavyo, sawa na mtu amfanyiavyo mnyama. Jambo linalofahamisha zaidi sera yao hiyo, zamani na sasa, ni fedheha yao katika Palestina, hasa waliyo yafanya huko Dayr Yasin, kuwachinja wanawake na watoto.

Mwanzo walikuwa wakiwaua Mitume wakati dunia ilipokuwa na Mitume. Ama leo, ambapo hakuna Mitume wanawaua wasuluhishaji; kama vile Bernadotte([5] ) , na wanawake na watoto. Kwa sababu, la muhimu katika itikadi yao na maumbile yao ni kuwaua watu wasiokuwa na hatia; wawe Mitume au wasuluhishi au watoto.

Tawrat yao imeandika uhalali wa kumwaga damu ya wanawake na watoto, na imelihimiza hilo. Kwa ujumla ni kwamba kuzikanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua wasuluhishi na watu wema wasio na hatia, na kufanya dhuluma na uchokozi, yote hayo ni dini na itikadi ya Mayahudi. Myahudi akimfanyia kosa mwengine asiyekuwa Myahudi basi anafanya kwa kujiburudisha tu, sio kwa haja fulani. Na kama akiacha kufanya hivyo, basi anaacha kwa kuogopa sio kwa kujistahi.

Hii ndiyo tofauti kati ya mayahudi na wasiokuwa mayahudi. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa Mwenyezi Mungu kuwawekea udhalili popote walipo.

Ama serikali habithi ya Israel ya sasa itaondoka tu, hakuna budi, Ushahidi mkubwa wa kwisha kwake ni kwamba imefungamana na ukoloni, ukoloni ukiondoka nayo inaondoka. Na ukoloni lazima uondoke tu, hata kama ni baada ya miaka. Maadam maumbile ya kibinadamu yanaukataa ukoloni na kuupinga kwa damu yake, basi utaondoka tu.

Yote haya tuliyoayataja yanakamilisha kifungu cha 'Mayahudi hawana mfano' katika tafsiri ya Sura Baqara (2) Aya63 na 66.

﴿لَيْسُوا سَوَاءً مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ﴾

113.Wote si sawa Katika watu wa Kitabu wamo walio na msimamo, wakasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku huku wakinyenyekea.

﴿يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَأُولَـٰئِكَ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴾

114. Wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wanaamrisha mema na wanakataza mabaya na wanaharakia mambo mema na hao ndio miongoni mwa watu wema.

﴿وَمَا يَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَلَن يُكْفَرُوهُ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ ﴾

115.Heri yoyote watakayoifayahaitakataliwa, Na Mwenyezi Mungu anawajua wamchao.

WOTE SI SAWA

Aya 113 -115

LUGHA

Mwenye Majmaul-bayan anasema: Tofauti kati ya neno Sura na Ajala ni kwamba Sura ni kufanya haraka linalojuzu kufanywa, Nako kunasifiwa. Na Ajala ni kufanya haraka jambo lisilofaa kufanywa, nako kunashutumiwa.

MAANA

Aya hizi tatu ziko wazi hazihitaji tafsir, Maana yake kwa ujumla ni kwamba watu wa Kitabu hawako sawa kwamba wote wamepotea, bali wako watu wema miongoni mwao. Wafasiri wengi wamechukulia sifa hii kwa aliyesilimu miongoni mwa watu wa Kitabu, na uzuri wa uislamu wake kimatendo na kiitikadi.

HUKUMU YA MWENYE KUACHA UISLAMU

Mwito wa kumwamini Muhammad kama Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa watu wa ulimwenguni bado upo mpaka Siku ya Mwisho. Nao unaelekezwa kwa watu wote, wa Mashariki na Magharibi. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا ﴾

"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote" (7:158).

Dalili ya ukweli wake ni mantiki ya kiakili, kuthibiti muujiza na kufaa dini kwa maisha. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema: "Msingi wa dini yangu ni akili" Na Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake Kitukufu:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ﴾

"Enyi ambao mmeamini muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume (wake) anapowaitia katika yale yatakayowapa maisha (8:24)

Lengo letu sio kutoa dalili za Utume wa Muhammad(s.a.w.w), ([6] ) isipokuwa lengo ni kubainisha kuwa je, asiyeamini Utume wa Muhammad anastahili adhabu: au hapana budi ya ufafanuzi? Kabla ya kumtofautisha mjuzi na asiye mjuzi na asiyemudu na mzembe, tutaonyesha msingi na vipimo vya kwanza vya kustahili adhabu au kutostahili; kutokana na hivyo, uhakika utafumbuka na kuwapambanua watu. Wote wameafikiana kwamba mtu, vyovyote awavyo, dini yoyote aliyo nayo, hastahili adhabu ila baada ya kusimamishiwa hoja. Na hoja haisimami ila baada ya kuweza yeye kufikia kwenye dalili ya haki na kuweza kwake kuitumia. Hapo akiacha hatakuwa na kisingizio. Ikiwa hakupata dalili ya haki yenye msingi au aliipata akashindwa kuifikia au aliifikia na akatekeleza mtazamo wake wa haki mpaka akafikia mwisho, lakini pamoja na hayo haki haikumdhihirikia, basi yeye atakuwa na udhuru, kwa sababu ya kutokamilika hoja juu yake. Kwa sababu, asiyethibitikiwa na haki haadhibiwi kwa kuiacha, ila ikiwa amezembea katika utafiti.

Vile vile miongoni mwa kawaida za msingi ambazo zinaambatana na utafiti huu ni ile ya "Adhabu kuepukwa na mambo yenye kutatiza." Kwa hiyo haijuzu kumhukumu mwenye kuiacha haki kuwa ni mwenye makosa anayestahili adhabu, maadamu tunaona kuwa kuna uwezekano kuwa anao udhuru katika kuacha kwake. Na kawaida hii inafungamana na watu wote, sio waislamu tu, Pia inakusanya aina zote za mipaka, Mfano kawaida ya 'Mwenye kukosea katika ijtihadi, basi kosa lake linasamehewa', Kawaida hii ni ya kiakili, haiwezekani kuihusisha na dini fulani tu, madhehebu, shina au tawi. Baada ya maelezo hayo hebu tuangalie hali hizi zifuatazo:

1) Kuishi binadamu mji ulio mbali na uislamu na waislamu; wala hakufikiliwa na mwito au hata kusikia jina la Muhammad(s.a.w.w) katika maisha yake yote. Pia awe hajawaza kwa karibu au mbali kwamba duniani kuna dini yenye jina la kiislamu na Mtume aitwaye Muhammad(s.a.w.w) . Hapana mwenye shaka kwamba huyu atasamehewa kwa kuwa hastahili adhabu. Maana akili ina hukumu ubaya wa adhabu bila ya ubainifu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na sisi si wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mitume" (17:15) Bila shaka akili ni Mtume wa ndani kwa ndani, ila tu yenyewe ni dalili ya kupatikana Mwenyezi Mungu tu. Ama dalili ya kuthibiti Utume wa Mtume, hapana budi kuwako na muujiza na udhihirishwe na yeye mwenyewe pamoja na akili kuhukumu kutowezekana kudhihiri kwa wasiokuwa Mitume.

2) Kuusikia mtu uislamu na Muhammad, lakini akawa hawezi kupambanua haki na batili, kwa sababu ya kushindwa kwake na kutoweza kufahamu dalili za haki na maarifa yake. Huyu pia anasamehewa, Kwa sababu yeye ni sawa na mtoto au mwenda wazimu. Mfano ni akitomwamini Muhammad(s.a.w.w) tangu udogo kwa kuwafuata wazazi wake na akajisahau alipokuwa mkubwa, akaendelea na itikadi yake bila ya kuitilia shaka yoyote, huyu atasamehewa. Kwa sababu kumkalifisha aliyejisahau asiye na uwezo ni sawa na kumkalifisha aliyelala. Amesema Muhaqqiq Al-Qummi: "Kujikomboa kutokana na kuiga wazazi ni jambo lisilofikiriwa na wengi, bali hata linakuwa zito aghlabu kwa wanavyuoni waliotosheka ambao wanadhani kuwa wamejivua kutokana na kuiga huko." Amesema tena: "Asiyeweza kung'amua wajibu wa kujua misingi, ni sawa na mnyama na mwedawazimu ambao hawana taklifa yoyote." Sheikh Tusi anasema: "Mwenye kushindwa kupata uthibitisho yuko katika daraja ya mnyama."

Hata hivyo, ikiwa aliyejisahau atakumbushwa wajibu wa maarifa, au kuambiwa na mtu: "Wewe uko au hauko sawa katika itikadi yako", lakini pamoja na hayo akang'ang'ania na wala asifanye utafiti na kuuliza, basi huyo atakuwa ni mwenye dhambi, kwa sababu atakuwa ni mzembe, na kutojua kwa mzembe si kisingizio.

3) Kutomwamini Muhammad(s.a.w.w) pamoja na kuwa anao uwezo wa kutosha wa kufahamu haki, lakini yeye alipuuza wala asijali kabisa: au alifanya utafiti pungufu na akauacha bila ya kuangalia mwisho wake; kama wafanyavyo wengi, hasa vijana wa kisasa. Basi huyu hatasameheka kwa sababu amekosea bila ya kujitahidi na alikuwa na uwezo wa kujua haki, lakini akapuuza. Ni wazi kuwa pia ataadhibiwa ambaye amefanya utafiti na akakinai, lakini pamoja na hayo akakataa kumwamini Muhammad(s.a.w.w) kwa ubaguzi na mali.

4).Kuangalia dalili na kuwa na mwelekeo wa kufuata haki kwa ikhlasi, lakini pamoja na hayo akakosa kuelekea kwenye njia ambayo itamwajibishia kumwamini Muhammad(s.a.w.w) ama kwa kushikamana kwake na mambo yenye kutatiza ya ubatilifu bila ya kuangalia ubatilifu wake, au kuchanganyikiwa na mengineyo ambayo yanazuia kuona haki. Huyu ataangaliwa hali yake, ikiwa atakanusha Utume wa Muhammad(s.a.w.w) kwa kauli ya mkato, basi yeye ataadhibiwa na kustahili adhabu. Kwa sababu yule ambaye imefichika kwake haki, haifai kwake kukataa moja kwa moja kukanusha haki. Inawezekana kuwa haki ipo lakini akazuiliwa, kuifika, na aghlabu huwa hivyo, kwa sababu mambo ya ulimwenguni yapo lakini tuyajuayo ni machache tu. Hali ni hivyo hivyo kuhusu kuwajua Mitume na wasuluhishi, Ni nani awezaye kujua kila kitu?

Watu wa mantiki wamelielezea hilo kwa ibara mbali mbali, miongoni mwazo ni: Kutokujua hakumaanishi kutokuwepo, kutopatikana hakumaanishi kuacha kupatikana, kuthibitisha na kukanusha kunahitaji dalili. Tumewaona wanavyuoni wengi wakiungana na hakika hii. Wanazituhumu rai zao na kujichunga katika kauli zao; wala hawajifanyi kuwa wao ndio kipimo cha ukweli. Hawawezi kusema: "Rai hii ni takatifu isiyo na shaka, na nyinginezo si chochote." Bali wao huipa mtazamo wa kujiuliza kila rai. Dalili kubwa zaidi ya kuwa mtu hana elimu, ni kule kujidanganya mwenyewe, kuiona safi elimu yake, na kudharau rai na itikadi za wengine.

Zaidi ya hayo kuacha kukinai mtu mmoja miongoni mwa watu kuhusu Utume wa Muhammad(s.a.w.w) hakumruhusu kukanusha Utume wa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) moja kwa moja. Na kama akifanya hivyo, basi atakuwa na jukumu. Hasa baada ya kuona idadi ya mabingwa ambao hawakuathiriwa na kurithi au mazingira, wakimwamini Muhammad na risala yake; si kwa lolote isipokuwa kuiheshimu haki na kuikubali hali halisi ilivyo([7] ) . Hayo ni ikiwa atapinga. Ama akiangalia dalili wala asikinai na pia asipinge; wakati huo huo akawa amenuia kwa moyo safi kuiamini haki wakati wowote itakapomdhihirikia; kama vile mwanafiqh mwadilifu ambaye hufutu jambo kwa nia ya kubadilisha mara tu ikimbainikia kuwa amekosea, basi huyu hatakuwa na jukumu, kwa sababu mwenye kukosea katika ijtihadi yake bila ya kufanya uzembe, hataadhibiwa kwa kukosea kwake; kama inavyohukumu akili na maandishi pia. Imepokewa kutoka kwa Imam Jafar Sadiq(a.s) , amesema:"Lau kama watu wasipofahamu (jambo) wakasimama na wala wasipinge, basi hawakukufuru" Katika Riwaya nyingine: "Hakika anakufuru tu akipinga"

Sheikh Ansari katika kitabu chake maarufu Arrasil mlango wa Dhana katika Usul, anasema: "Hadith nyingi zimefahamisha kuthibiti ukati na kati baina ya kufuru na imani" Ya kwamba mpingaji ni kafiri, mwenye kuitakidi ni Mumin, na mwenye shaka si kafiri wala Mumin. Katika Hadith zinazowezekana kuzitolea dalili ya kutoadhibiwa mwenye kufanya ijitihadi bila ya uzembe kama akikosea katika mambo ya itikadi, ni Hadith hii mashuhuri kwa sunni na shia:"Akijitahidi hakimu na akapata basi atalipwa mara mbili. Na akijitahidi akakosea, basi atalipwa mara moja" Kama mtu akisema kuwa Hadith hii inahusu mwenye kujitahidi katika matawi si katika masuala ya itikadi, kama walivyodai baadhi ya wanavyuoni, basi tutamjibu hivi: Linalomlinda, mwenye kujitahidi katika hukumu, asiadhibiwe ni kule kujichunga kwake na kutofanya uzembe katika utafiti, Na kinga hii inapatikana hasa katika masuala ya kiitikadi.

Zaidi ya hayo Mafaqihi wote wameafikiana kwa kauli moja kwamba mwenye kushindwa kuifikia itikadi ya kweli, anasamehewa. Miongoni mwao ni wale waliohusisha Hadith hii na matawi. Nasi hatuoni tofauti yoyote kati yake na yule mwenye kujitahidi, aliyetoa juhudi zake. Kwa sababu,wote wawili wameshindwa kujua maadam hawakuufikia uhakika. Kwa ufupi ni kwamba mwenye kuipinga, haki yoyote, basi ataadhibiwa, ni sawa awe amejitahidi au la, isipokuwa kama hana maarifa, kama mnyama. Kama akibakia kwenye msimamo wa kutopinga wala kuthibiti sawa, kujitahidi na kuangalia dalili au alifanya ijtihadi pungufu, basi ataadhibiwa. Ikiwa ameangalia dalili akajitahidi mpaka akafikia mwisho wake, basi yeye atasamehewa kwa sharti ya kubakia na mwelekeo wa haki kwa kuazimia kubadili msimamo wake wakati wowote itakapomdhihirikia haki.

Unaweza kuuliza : Umesema kuwa mwenye kushindwa kujua itikadi ya kweli - kama vile Utume wa Muhammad – atasamehewa, Vile vile mwenye kujitahidi ambaye hakuzembea katika jitihadi. Je, maana yake ni kuwa inajuzu kwetu kufanya naye muamala wa kiislamu, kama kuoa, kurithi n.k.

Jibu : Msamaha tunaoukusudia hapa ni kutostahiki adhabu akhera; ama kuoa na kurithi hapa duniani ni jambo jengine. Na kila asiyeamini utume wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) kwa hali yoyote atakayokuwa, haifai kuwa na muamala naye wa kiislam k.v. ndoa, urithi n.k. Ni sawa awe kesho atapona au ataangamia; kama ambavyo mwenye kusema "Laila ilaha illa llah Muhammad Rasulullah" anastahiki ya waislamu, ni juu yake yaliyo juu yao, hata kama alikuwa ni fasiki, bali hata mnafiki vile vile.


6

7

8

9

10

11

12

13

14

15

16