MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 0%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi: Juma Muhammad Rashid Al-Mazrui, Al-Zenjibari.
Kundi:

Matembeleo: 59156
Pakua: 4780

Maelezo zaidi:

MUANDAMO WA MWEZI
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 59156 / Pakua: 4780
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

9

MUANDAMO WA MWEZI

JAWABU NILILOJIBIWA

Ndugu zangu wakanijibu hivi:

10. Masimulizi Ya Kuraib Kama kawaida yake, Ndugu Juma ametoa dhana yake binafsi kwamba si lazima mwezi ukithibiti kuandama sehemu moja uwe umethibiti sehemu nyengine, na kwamba kwa mawazo yake ni lazima tusalim amri kwa hilo, yaani yeye anataka kila nchi ifunge kwa muandamo wake. Kwani aonavyo yeye katika jambo hilo kuna andiko. Hilo andiko je alinukuu? Alilolichukua yeye ni katika kisa cha Ibnu ''Abbas na Kuraib.[4]

JAWABU

Jamani! Nyinyi hamuoni haya kusema mambo ovyo ovyo?! Hivyo hii pia munaita rai yangu binafsi. Ivo mimi ndiye wa mwanzo kusema kuwa kila pahala na muandamo wao? Mimi ndiye wa mwanzo kuitumia Hadithi hii katika kuthibitisha hayo? Tena bado munaendelea kufanya makosa ya kifani kwa kudai kwenu: "Kwani aonavyo yeye katika jambo hilo kuna andiko. Hilo andiko je alinukuu? Alilolichukua yeye ni katika kisa cha Ibnu ''Abbas na Kuraib". Nakukumbusheni maneno yenu mazuri sahihi muliposema: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii", yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume (s.a.w.). Sasa bado munakana kuwa hilo si andiko, haya hizi ndio fani zenu mulizosoma?!

Munasema Sisi tunamfahamisha mambo yafuatayo kwamba:

1. Hakuna andiko Takatifu zaidi ya Qur-aan Tukufu, lakini bado Wanavyuoni wakubwa wametofautiana katika baadhi ya tafsiri za Aya nyingi pamoja na Hadiyth sahihi.

2. Maswahaba pia walitofautiana katika kufahamu tafsiri za Aya za Qur-aan na Hadiyth. (Angalia tafsiri ya Shaykh Ahmed Al-Khaliil J. 1)

3. Kama Wanavyuoni waliopita wangekuwa na msimamo kama wa ndugu Juma kwamba katika kisa cha Kuraib kuna andiko, basi kungekuwa hakuna mjadala. Kama ilivyo katika nyakati za Swala hazina tofauti kubwa, kila eneo linaswali kwa mitenguko yake ya jua.

4. Kama kisa chenyewe ni andiko, mbona ndugu Juma anatoa mawazo kwamba suala la umbali gani ndio linatakiwa Ijtihadi? Sasa tunakujibu kwamba hapa ndipo penye mjadala wote wa mwezi, maana mpaka leo hii hapakupatikana makubaliano ya kweli ya kisheria, isipokuwa kila eneo linafuata matakwa yake ya kisiasa na kifalme za nchi zao.

JAWABU

Mimi sijasema kuwa kuna andiko takatifu zaidi ya Qur-an. Pia mimi sijakataa kuwepo kwa khilafu katika tafsiri wala katika fiq-hi. Lakini pamoja na hayo, sisemi kuwa hakuna kauli sahihi na dhaifu. Wanavyuoni wote - mukiwemo nyinyi - wanakubali kuwa kauli ziko sahihi na dhaifu. Kwa hivyo, sisi tunadai kuwa kauli yenu ni dhaifu kwani haikujengeka katika fani za kielimu. Ama kauli yenu muliposema: "Kama Wanavyuoni waliopita wangekuwa na msimamo kama wa ndugu Juma kwamba katika kisa cha Kuraib kuna andiko, basi kungekuwa hakuna mjadala. Kama ilivyo katika nyakati za Swala hazina tofauti kubwa, kila eneo linaswali kwa mitenguko yake ya jua" inathibitisha yale tuliosema kwamba humujui munachokisema: watu wannena nasi twanena.

Kwani mumepata wapi nyinyi kwamba pakiwa na andiko watu huwa hawatafautiani. Si ndio nyinyi muliosema katika kifungu (1): "Hakuna andiko Takatifu zaidi ya Qur-aan Tukufu, lakini bado Wanavyuoni wakubwa wametofautiana katika baadhi ya tafsiri za Aya nyingi pamoja na Hadiyth sahihi". Na mukasema katika kifungu (2): "Maswahaba pia walitofautiana katika kufahamu tafsiri za Aya za Qur-aan na Hadiyth. (Angalia tafsiri ya Shaykh Ahmed Al-Khaliil J. 1)". Sasa Qur-ani si andiko kwa sababu wanavyuoni wametafautiana juu ya tafsiri ya baadhi ya Aya zake? Mimi nahisi hoja hio mumeijibu wenyewe. Halafu je Hadithi "Fungeni kwa kuuona" si andiko? Mbona wanavyuoni wamelifahamu tafauti? Ndugu zeu, hoja hamuna: muna vichekesho tu!!!

Pia tazameni kauli yenu: "Kama kisa chenyewe ni andiko, mbona ndugu Juma anatoa mawazo kwamba suala la umbali gani ndio linatakiwa Ijtihadi?". Nami nauliza ili iwe jawabu:

a) Kama Hadithi za Sala ya safari ni andiko, mbona wanatafautiana juu ya umbali gani ndio tusali safari?

b) Kama Hadithi hizo ni andiko mbona wanatafautiana je ni kwa muda wa siku ngapi safari inaendelea?

Enyi walimwengu! Hizi ndio hoja za kielimu tulizoahidiwa?! Hadithi za sala ya safari ni maandiko ya wazi juu ya mashru'iyya ya sala ya safari. Kilichokuwa hakiko wazi sana ni safari inaanza baada ya umbali gani na inadumu siku ngapi. Na kutokuwa wazi katika mas-ala haya, hayavunji asili ya sharia ya sala ya safari na usahihi wa maandiko yake, bali sala ya safari ni andiko la wazi juu ya sharia hio, na vipengele visivyo wazi ndio vinakuwa sehemu za ijtihad. Halkadhalika, ukweli kwamba wapi hadi wapi tufunge pamoja ni suala la ijtihadi, hakuvunji ukweli kwamba muandamo mmoja si hoja kwa dunia nzima.

MNASEMA

Sasa tunakujibu kwamba hapa ndipo penye mjadala wote wa mwezi, maana mpaka leo hii hapakupatikana makubaliano ya kweli ya kisheria, isipokuwa kila eneo linafuata matakwa yake ya kisiasa na kifalme za nchi zao.

JAWABU

Kitabu chenu au cha Sheikh wetu Bachoo, hakikusisitiza nukta hii, bali kinasisitiza usahihi wa kufunga kwa muandamo mmoja duniani. Anasema: Pia jambo la kuzingatia hapa ni kwamba ilivyokuwa mtu huyo alikuwa ni Bedui yaani mtu wa Majangwani, Mtume(s.a.w.w) angeweza kumuuliza anatoka wapi, lakini hakumuuliza kabisa suala hili jambo ambalo linathibitisha kuwa suala la umbali gani wa kuonekana mwezi Mtume(s.a.w.w) hakuwa akilizingatia hata kidogo!!! Mwisho wa kunukuu.

Na anasema: Ni kweli kwamba msimamo wa upande wetu ni kuwa mwezi ukiandama popote pale ulimwenguni watu wafunge. Nami nikamjibu katika kitabu changu hicho, kwamba hilo ni kinyume na Hadithi ya Kuraib, nayo ni Hadithi marfu'u kwa mujibu wa elimu ya Hadithi kama tulivyobainisha. Ama ukweli kwamba "Mpaka leo hii hapakupatikana makubaliano ya kweli ya kisheria, isipokuwa kila eneo linafuata matakwa yake ya kisiasa na kifalme za nchi zao". Narudia - mutanisamehe - kwamba tatizo lenu ni kutokujua mas-ala ya ijtihad na yasio ya ijtihad. Tumesema kwamba umbali gani au wapi hadi wapi watu wafunge pamoja, hili ni suala la ijtihad kwa sababu ya kutokuwepo andiko la wazi, lakini kufunga dunia nzima kwa muandamo mmoja, hili ni kinyume na andiko. Sasa tukirudi katika mas-ala ya ijtihad, ni kuwa mas-ala ya ijtihad si lazima watu waafikiane, bali mwenye kusibu hupata ujira mara mbili atayekosea hupata ujira wa ijtihad yake. Ama andiko, huwezi kulikwepa na kulipiga chenga hii na ile.

MNASEMA

Hapa chini tutaonyesha namna Wanavyuoni wenye kutegemewa ambao hawakukichukua kisa cha Kuraib kama ni hoja ya kwamba kila nchi au kila eneo lifunge au lifungue kwa muandamo wake. Wanavyuoni wamekhitalifiana kwa sababu kisa chenyewe cha Ibnu ''Abbas na Kuraib kina utata, hakikueleweka kwa mtazamo mmoja. Chambilecho alivyosema Shaykh Ahmed Al-Khaliil kwamba: "Hakuna madhehebu iliyosalimika." Habari hizi zimepatikana katika khutba yake iliyorikodiwa katika kanda (audio cassette) alipozungumza Shaykh Ahmed Al-Khaliil kwenye msikiti Istiqama Zanzibar iliyotafsiriwa na Shaykh Munir Sulayman 'Aziiz.

1. Rawdhatun-Nadiyyah: Kilichoandikwa na Shaykh Alqanuji

"Ama hoja ya aliyetegemea Hadiyth ya Kuraib iliyopokelewa na Muslim na wengineo, (hoja hiyo) sio sahihi kwa sababu Ibnu 'Abbas hakuelez a kama Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewakataza kufuata mwandamo wa nchi nyengine." Mwisho wa kunukuu.

JAWABU

Kwanza tungependa mufahamu kwamba katika kitu chenye khilafu, basi hakuna maneno ya mwanachuoni yeyote ambayo yanakuwa ndio hoja. Bali hoja huwa ni Qur-an, Hadithi na kanuni za tafsiri zilizokubalika. Pili: ikiwa kitu kuna mtu hakukifahamu pia haiwi hoja kwa vile wako waliokifahamu. Mara ngapi utakuta katika vitabu kwamba mwanachuoni mkubwa anadai kuwa kitu hiki hakipo au mimi sifahamu kakusudia nini, kisha mwengine akakibainisha kuwa kipo au kina maana gani. Chukua mfano kwamba Al-Mubarrad ni katika vigogo wa lugha ya Kiarabu. Lakini anadai kwamba kusema Lawlaya au lawlaka au laulahu n.k." anasema mf umo huu katika lugha ya Kiarabu haukupokewa kamwe. Wakati Sibawahi na wenziwe wameuthibitisha kuwepo kwa muundo huo kwa beit za Warabu wa kale kama:

Atutmi'u fiina man araq dimaana**Walawlaka lam ya'ar idh liahsabina hasan Na beit kama: Wakam matinin lawlaya tihta kama hawa**Biajramihi min qunnatin niqin munhawi Na beit kama: Awmat bi'aynayha minal h adaji**Lawlaka fid ha l'ami lam ahjuji Al-Mubarrad na ubingwa wake wote wa lugha hakujua kama kuna beit hizi. Mfano mwengine ni wa Al-Imamu Abu Hayyan. Anasema kuhusu beit isemayo: Fala Wallahi la yulfi Unasu n**Fatan hattaka ya Ibn Ziyad

Anasema Abu Hayyan, naye ni Imamu wa lugha na tafsiri,: "Na kumalizikia kwa ghaya katika hattaka sikufahamu; wala sijui kakusudia nini kwa (kusema) 'Hattaka', labda baiti hii ni ya kutunga (fabricated). Lakini aliyetia maelezo Sharhu Ibn 'Aqil kabainisha nini muradi wa kile ambacho Abu Hayyaan hakukifahamu. Kwa hivyo, kutokufahamu kwa Shaykh Alqanuji muradi wa Ibn Abbaas hakujakufanya kuwa Hadithi hio iwe batili, madamu wengine wamefahamu. Cha muhimu ni kuwa waliofahamu wamefahamu nini. Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib inasema:

"Kutoka kwa Kurayb (kasema) kwamba Ummu Al-fadhli bint Al-harith alimtuma Sham (Syria) kwa Muawiya. Akasema: 'Basi nikaenda Sham nikamkidhia haja yake.' Na ukaniindamia (mwezi wa) Ramadhani na mimi niko Sham. Basi nikauona mwezi usiku wa (kuamkia) ijumaa. Kisha nikaja Madina mwishoni mwa mwezi. Basi Abdullahi bin Abbas (r.a.) akaniuliza. Kisha akataja (habari za) mwezi muandamo akasema: 'Lini mumeuona mwezi muandamo?' Nikasema: 'Tumeuona usiku wa (kuamkia) Ijumaa.' Akasema: 'Wewe umeuona?' Nikasema: 'Ndio. Na Watu wameuona na wakafunga na Muawiya akafunga.' Akasema: 'Lakini hakika ya sisi tumeuona usiku wa (kuamkia) Juma Mosi, basi hatuachi kuendelea kufunga mpaka tutimize (siku) thalathini au tuuone.' Nikasema: 'Kwani wewe hutosheki na kuonekana na Muawiya na kufunga kwake?' Akasema: 'Laa' (Sio): Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w) ."

Kwa hivyo, Ibn Abbaas kasema "'Lakini hakika ya sisi tumeuona usiku wa (kuamkia) Juma Mosi, basi hatuachi kuendelea kufunga mpaka tutimize (siku) thalathini au tuuone". Ni wazi kwamba mwezi muandamo wa Sham hakuukubali kwani - kama tulivyoeleza katika kitabu - kwamba kutimiza kwa siku 30 kwa watu wa Madina ni kutimiza 31 kwa watu wa Sham, wakati hakuna mwezi wa siku 31. Hakuna ila tuseme kwamba muandamo wa Sham hakuukubali. Akaulizwa na Kuraib: "Kwani wewe hukutosheka na kuonekana kwa mwezi huko Sham" akajibu "Hapana" (Sikutosheka). Kisha akasema kwamba "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume(s.a.w.w) ".

Sasa kama Ibn Abbaas kakataa kuufata muandamo wa Sham kisha akajibu kwamba hivi (ninavyofanya mimi) ndivyo Mtume (s.a.w.) alivyofunza. Vipi mtu atadai kwamba: Ama hoja ya aliyetegemea Hadiyth ya Kuraib iliyopokelewa na Muslim na wengineo, (hoja hiyo) sio sahihi kwa sababu Ibnu 'Abbas hakueleza kama Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewakataza kufuata mwandamo wa nchi nyengine." Sasa Sheikh huyu alitaka Ibn Abbaas aeleze vipi tena zaidi ya hivi, naye kakataa kuufata muandamo huo na akasema kuwa hayo ndio mafunzo ya Mtume(s.a.w.w) kwao? Je hayo yanamaanisha kuwa dunia iwe na muandamo mmoja?! Kwa hivyo, nasi tunasema kuwa maelezo y Shaykh Alqanuji si sahihi, na ibara za Ibn Abbaas ziko wazi kabisa hata kwa mwanafunzi licha ya mwanachuoni.

MNASEMA

2. Aunul-Maabud, Sherhe Sunanu Abu-Daud: Yaani: aliposema: "hivi ndivyo alivyotuamrisha." kama anakusudia: Ametuamrisha kukubali ushahidi wa watu wawili sio mtu mmoja katika kufungua (siku ya 'Iydl-fitri). Aidha inawezekana pia kwamba anakusudia ametuamrisha tufungue kwa kufuata mwandamo wa nchi tuliyopo siyo nchi nyengine. Abu Daudi ameitegemea hii maana ya pili lakini Ibnul-Qayyim anaona kuwa maneno haya: "hivi ndivyo alivyotuamrisha" yana utata - yaani yanaweza kukusudiwa kwa maana ya kwanza au ya pili. Kwa maana hiyo, maneno hayo hayawezi kuwa hoja kwani hoja haitakiwi kuwa na utata (yaani maana zaidi ya moja). Wanavyuoni wa U sulil - Fiqhi wanasema hivi:

"Dalili ikiwa na maana (nyingi) zaidi ya moja, ushahidi wake huporomoka."

JAWABU

Kwanza naomba tuyanukuu maneno ya Aunul-Maabud, Sherhe Sunanu Abu-Daud kama yalivyo na tuyafahamu kama yalivyo, kwani hivyo mulivyoyaeleza nyinyi sivyo, bali hata hiyo tajama (translation) yake hapa ni mushkeli. Kitabu hicho kinasema: Kauli yake (Ibn Abbaas aliposema): "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume(s.a.w.w) , ina uwezekano kwamba makusudio kwayo ni k uwa yeye (Mtume(s.a.w.w) katuamuru tusiikubali shahada ya mtu mmoja katika kufuturu, au katuamuru kwamba tutegemee uoni wa mji wetu: wala tusitegemee uoni wa wengine. Na hii maana ya pili ndipo inapomili tarjama (yaani heading) ya mtunzi (wa kitabu hiki), lakini maana ya mwanzo ina uwezekano (huu na ule) basi ushahidi wake hauendi sawa kwani uwezekano wa namna tafauti unaifisidi dalili.

Hayo ndio maneno ya mwenye kitabu hicho akimnukuu Ibn Al-Qayyim. Utaona kuwa wenzetu hapa:

1) Wamefanya ghushi kama kawaida yao. Maneno tusiikubali shahada ya mtu mmoja katika kufuturu, wameyaondosha kwani hayakubaliani na lengo lao.

2) Maana ya maelezo yenyewe wameivuruga vuruga. Sijua hawajui au wanafanya kwa kukusudia?

Sasa kwa ufupi ni kuwa, anachokisema Ibn Al-Qayyim, ni kuwa Hadithi hii ina uwezekano wa aina mbili:

1) Tusiikubali shahada ya mtu mmoja katika kufuturu. Huu ndio uwezekano wa kwanza.

2) Tutegemee uoni wa mji wetu: wala tusitegemee uoni wa wengine. Huu ndio uwezekano wa pili.

Sasa Ibn Al-Qayyim anasema kwamba "Lakini maana ya mwanzo ina uwezekano (huu na ule) basi ushahidi wake hauendi sawa kwani uwezekano wa namna tafauti unaifisidi dalili". Kwa hivyo, anachokipinga Ibn Qayyim ni kuwa maneno ya Ibn Abbaas "Hivi ndivyo alivyotuamu Mtume s.a.w." yana uwezekano wa maana kwamba ushahidi wa mtu mmoja usikubalike, lakini maana hii si sahihi: maana hii yeye kaipinga. Ama maana ya pili ya kwamba: "Tutegemee uoni wa mji wetu: wala tusitegemee uoni wa wengine". Hii yeye hakuipinga na kakiri kuwa maana hio imo katika Hadithi hio. Sasa ikiwa ndugu zetu mumeshindwa kuyafahamu mabo simple (mepesi) kama haya, vipi mutaweza kujadili suala hili lenye kuhitaji fani hii na hile?! Ama kanuni: "Dalili ikiwa na maana nyingi basi ushahidi wake huporomoka" ni kanuni sahihi lakini ina sharti zake:

1) Iwe Maana nyingi zenyewe ziwe zinatokana na dalili.

2) Kusiwe na qarina (contex au dalili za nje) ambazo kwazo inawezekana kuipa uzito maana moja. Ama hapa katika Hadithi ya Ibn Abbaas, Qarina (context) inabainisha wazi nini muradi wa Ibn Abbaas kuyasema hayo. Qarina (context) yenyewe ni kukataa kwake kufata muandamo wa Sham na akasema: "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w.".

MNASEMA

3. Imamu Suyuti: Aliyesherehesha "Sunanun-Nisai" ametumia maneno yale yale ya Ibnul-Qayyim: Kwa hivyo Imamu Suyuti naye amekuja na msimamo ule ul e wa Ibnul-Qayyim wa kwamba maneno ya Ibnu ''Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu): "Hivi ndivyo alivyotuamrisha." Yana utata, kwa hivyo si hoja ya kutegemewa kisheria.

JAWABU

Al-Imamu Al-Suyuti ni kweli kasema kama alivyosema Al-Imamu Ibn Al-Qayyim. Maneno yake ni haya: Kauli yake (Ibn Abbaas aliposema): 'Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume(s.a.w.w) ,' ina uwezekano kwamba makusudio kwayo ni kuwa yeye katuamuru tu siikubali shahada ya mtu mmoja katika kufuturu, au katuamuru kwamba tutegemee uoni wa mji wetu: wala tusitegemee uoni wa wengine. Na hii maana ya pili ndipo inapomili tarjama (yaani heading) ya mtunzi (wa kitabu hiki), lakini maana ya mwanzo ina uwezekano (huu na ule) basi ushahidi wake hauendi sawa kwani uwezekano wa namna tafauti unaifisidi dalili, kana kwamba wameona kwamba chenye kufahamika akilini ni maana ya pili wakajenga dalili juu yake.

Hayo ndio maneno ya Al-Suyuti, nayo ni sawa na maneno ya Ibn Qayyum, nayo ni hoja yetu dhidi yenu. Lakini mulipolijua hilo, mukaona maneno ya Ibn Al-Qayyim muyaghushi: kipande mukikate; na maneno ya Al-Suyuti muyanukuu kipande kidogo tu kisemacho (Na kusema kwakwe (Ibn Abbaas) hivi ndivyo ali vyotuamuru!

Kwa hivyo, maneno ya Al-Imamu Al-Suyuti ni kama ya Ibn Al-Qayyim, kwamba maneno ya Ibn Abbaaas yana uwezekano wa aina mbili

1) Tusiikubali shahada ya mtu mmoja katika kufuturu, au katuamuru kwamba. Huu ndio uwezekano wa kwanza.

2) Tutegemee uoni wa mji wetu: wala tusitegemee uoni wa wengine. Huu ndio uwezekano wa pili.

Na kwamba uwezekano wa kwanza ni dhaifu na wa pili ndio wenye nguvu na ndio tegemeo - kule la Abu Dau; na huku - la Al-Nasai.

Munasema Baada ya kupimwa maneno ya Ibnu-'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) katika mezani ya Usul-Fiqhi na kuonekana kwamba hayaeleweki kwa maana moja, sasa tuyatie kwenye mezani ya Hadiyth ambapo tutaona maneno ya Ibnu-'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) aliyoyasema: "Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)," yanapewa 'Hukmu Arafi' yaani yanapewa nafasi sawa na Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika hukmu. Hapa mezani ya Mustwalahul-Hadiyth inatoa jawabu ifuatayo:

JAWABU

Ni mezani gani ya usulul-fiq-hi mulioitumia na ni kanuni gani ya usuli mulioitumia kuonesha kuwa maneno ya Ibn Abbaas hayaeleweki? Maneno ya Ibn Al-Qayyim mumeyaghushi; maneno ya Al-Suyuti mumeyabutua. Na yote yanakupingeni nyinyi: si yanakusapotini. Kanuni: "Dalili ikiwa na maana nyingi basi ushahidi wake huporomoka" hamukuifahamu, nayo pia hapa inaipa nguvu tafsiri yetu. Sasa nyinyi ni kanuni gani hio ya usuli mulioitumia hapa kuon esha kuwa maneno ya Ibn Abbaas hayaeleweki?! Pili munasema maneno ya Ibn Abbaas: "Yanapewa 'Hukmu Arafi' Haya ndio kama yale nilioyakuta ubaoni kwenu Al-Rajulu Jaa mukasema Al-Rajulu ni faa'il (mtenda)!!! Na hapa munatwambia: sijui huyu Raafi'u katoka wapi. Sijui na hili hamulijui au kalamu imekupokonyokeni pamoja wingi wenu! Mashekhe hii inaitwa bila ya Alif katika Al-Raa (Ree): sio Sasa kama nyinyi hata hizi istilahi (technical terms) hamuzij ui, ni kitu gani kinachokufanyeni mujitie katika mambo kama haya?! Lakini nakupeni udhuru, labda ni kosa la chapa!

MNASEMA

i. Katika kitabu cha kimeandika yafuatayo: "Itakapo gongana 'Marfuu-hukman' na 'Marfuu-Saraaha' hutangulizwa (katika hukmu) 'Marfuu-Saraaha."

ii. Pia katika tafsiri ya Qur-aan ifuatayo: 383) imeandikwa ifuatavyo: " "Marfuu-Saraa ha ni bora zaidi (aula) kutangulizwa (katika hukmu) kuliko Marfuu-hukman."

JAWABU

Munaendelea kunukuu mambo musioyajua mukijitia katika dhima na jukumu. Maana ya kugongana katika elimu ya Usulil-Fiqhi na usulil-Hadithi, ambako kunalifanya andiko moja liachwe, ni kuwa:

1) Andiko moja lisema hivi na la pili liseme kinyume chake. Wakati hapa hakuna mgongano baina Hadithi ya Ibn Abbaas "Fungeni kwa kuuona" na Hadithi yake: "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume(s.a.w.w) ". Kwani hadithi ya kwanza - kwa baadhi ya mazingatio yake ni Aam (ya ujumla) - na ya pili - kwa baadhi ya mazingatio yak e ni Khaas (specific). Na ujumla wenyewe uliomo katika Hadithi hio "Fungeni kwa kuuona" ni - kama tulivyoeleza katika kitabu Ushahidi Uliowekwa Wazi ni kuwa Hadithi hii ni ushahidi kwamba watu wote lazima wafunge kwa kuuona, wala haibanishi suala la ku wa je ukionekana mwezi na watu wan chi moja watu wan chi nyengine nao wafunge au wasifunge: hili katika hadithi hio halimo kwa mbali wala kwa karibu.

Ama mazingatio yenye kuifanya Hadithi yake: "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w.", ni ukweli kwamba Hadithi hii inaonesha kwa uwazi kwamba kila watu au kila mji na muandamo wao. Kanuni za kiusuli ni kuwa Aam (andiko la ujumla) likigongana na Khaas (andiko lenye kuvua baadhi ya mambo au specific exceptional), basi Khaas ndilo linalotangulizwa, kwani Khaas ni la hakika na Aam ni la dhana. Na kwa mazinagatio mengine, basi Hadithi "Fungeni kwa kuuona" ni mutlaq na Hadithi "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." ni muqayyad; kanuni ni kutanguliza muqayyad kabla ya mutlaq. Na kwa ba adhi ya mazingatio, Hadithi: "Fungeni kwa kuuona" ni mumal na Hadith "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." ni mubayyan. Kanuni ni kutanguliza mubayyan pasi na mujmal. Kwa hivyo, kiufupi ni kuwa hizi ni Hadithi mbili zenye kufasiriana: moja imeifasiri ya pili, wala hakuna mgongano.

Katika kitabu Ushahidi Uliowekwa Wazi, nilitoa maelezo yafuatayo:

a) Tumesema kwamba Hadithi hii ni mujmal (isiofafanuliwa) na kwamba mujmal hurejeshwa katika mubayyan. Kanuni hii ni kwa kuzingatia kwamba Hadithi hii haikubainisha je muandamo ni mmoja au kila watu wana muandamo wao? Bali imesema kwa ujumla tu "Fungeni kwa kuuona mwezi" kama Qur-an ilivyosema "Simamisha sala kwa kutenguka jua."

b) Tumesema pia kwamba Hadithi hii ni mutlaq na kwamba kanuni ni kulirejesha andiko mutlaq katika andiko muqayyad. Na tukasema kwamba ni lazima Hadithi hii ifungamanishwe na Hadithi ya Ibn Abbas. Hadithi ya Ibn Abbas ni muqayyad kwa hivyo ni lazima itangulizwe. Tumeiita Hadithi hii mutlaq kwa kuwa lafdhi yake haikufungamanishwa na sehemu yoyote, na tukaiita Hadithi ya Ibn Abbas kuwa ni muqayyad kwani lafdhi yake imefungamanishwa na sehemu moja pasi na nyengine.

b) Tumesema kuwa Hadithi hii ni Aam (ya ujumla). Ujumla huu ni kwa kuzingatiya wanaoambiwa au wanaohubiriwa (addressees). Na hii ni kuwa Hadithi inawataka Waislamu wote wafunge kwa kuuona mwezi. Lakini tumebainisha kwamba hii haina maana kuwa muandamo uwe mmoja, bali maana yake ni kuwa kila watu ni lazima wafunge kwa kuuona mwezi: sio kwa manazil wala kwa hisabu wala kufunga siku ya shaka. Hii ndio maana ya Hadithi hii, na hiyo ndio mielekeo ambayo kwayo nimezileta kanuni hizo za kiusuli.

2) Jambo la pili lenye kuyafanya maandiko yazingatiwe kuwa yanagongana ni kuwa maandiko hayo yote yawe sawa katika daraja zake.

3) Iwe hakuna njia ya kulipa uzito moja au kila moja kuliweka mahala pake. Kwa hapa kila andiko moja inawezekana kuliweka mahala pake na kuliweka kwenye muradi wake. Andiko: "Fungeni kwa kuuona mwezi" mahala pake ni kuwa kila watu wasifunge mpaka wauone; andiko "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." mahala pake ni kuwa mwezi wa mbali si hoja walio mbali. Ama yakitokea hayo, na isiwezekane kuyajumuisha au kulipa uzito moja au kila moja kuliweka mahala pake, huwa maandiko yanagongana, na yote huachwa. Kwa bahati Hadithi mbili hizo hazina mgongano huo, bali ni katika milango ya: Al-Mujmal na Al-Mubayyan; Al-'Aam na Al-Khas; Al-Mutlaq na Al-Muqayyad. Na huku si kugongana, bali ni kufasiriana kwa maandiko. Ama maneno ya Sahib Khabaril Wahid aliposema: "Itakapogongana 'Marfuu-hukman' na 'Marfuu-Saraaha' hutangulizwa (katika hukmu) 'Marfuu-Saraaha" inaonesha kuwa nyinyi wenyewe hamukuyafahamu. Nimekuelezeni wakatika gani andiko huambiwa kuwa limegongana. Nayo iwe:

1) Yote ni daraja moja kwa nguvu.

2) Isiwezekane kulipa uzito moja.

3) Isiwezekane kulifungamanisha moja na jengine na kuyapa tafsiri ya pamoja au kila moja kuliweka mahala pake. Wala haikusudiwi kwa kanuni hizo kugongana kwa:

1) Al-Mujmal na Al-Mubayyan.

2) Al-'Aam na Al-Khas.

3) Al-Mutlaq na Al-Muqayyad.

Vyenginevyo Aya za Qur-ani za ujumla huwa vile vile zinagongana na maandiko mengine. Aya za mirathi zimegongana na Hadithi "Mwenye kuua harithi". Katika Qur-ani hakuna "Mwenye kuua harithi" bali kuna mgao wa mafungu tu. Hadithi ya Mtume (s.a.w.) ikawatoa wenye kuua. Sasa kugongana huku hakuitwi kugongana; bali kunaitwa kubainisha andiko mujmal (andiko lisilofafanuliwa). Halkadhalika Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib ni kubainisha andiko mujmal (andiko lisilofafanuliwa) nalo ni Hadithi "Fungeni kwa kuuona".

MNASEMA

Ufafanuzi zaidi wa maelezo hayo ni kwamba Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) zilizotajwa hukmu ya kufunga na kufungua zimetaja hukmu hiyo kwa (saraaha) uwazi: "Fungeni kwa kuona mwezi." Hilo ni agizo la ujumla - yaani kwa watu wote. Lakini tukiyachunguza maneno ya Ibnu ''Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) tutayagundua ingawaje kayategemeza kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) bado hayako wazi - yana utatanishi.

JAWABU

Suala hili hili tumeshalijibu kwa urefu katika kitabu Ushahidi Uliowekwa Wazi. Na tunanukuu tena baadhi ya jawabu yetu. Nilisema: Jambo la pili: la kutazamwa katika Hadithi hii ni kuwa Khitabu (Agizo: kama alivyofasiri Sheikh Nassor Bachoo) ya Hadithi hii ni Aam (ya ujumla), kama Sheikh alivyonukuu kutoka katika kitabu cha Al-sayyid Saabiq. Na sisi tunajibu kwa jawabu mbili. Ya kwanza ni kuwa:

Ujumla wa agizo hilo, umehusishwa na Hadithi ya Ibn Abbas, na kanuni ya kiusuli inaeleza kwamba Al-khaas (Andiko maalumu au specific) nd io inayotangulizwa kuliko Al-aam (Andiko la ujumla), kwa kuwa kwake (hio Khaas) ni ya uhakika kinyume na Aam hakika yake ni (kitu) cha dhana. Kwa hivyo kanuni hapa inatutaka kuitanguliza Hadithi ya Ibn Abbas. Na natija ni kuwa ujumla jamala ulioba kia katika Hadithi "Fungeni kwa kuonekana mwezi na fungueni kwa kuonekana mwezi" na ambacho tunachotakiwa sote tukifanye kwa mujibu wa Hadithi hii, ni kuwa sote tufunge kwa kuuona mwezi. Ama je muandamo ni mmoja au kila watu wana muandamo wao, Hadithi hii haitoi jawabu hio. Jawabu ya pili ni ile tuliotangulia kuinukuu kutoka kwa Sheikh Ibn Uthaimin aliponukuu jawabu ya wale wenye kusema kwamba kila mji una muandamo wake, ambapo walisema kwamba ujumla uliomo katika Hadithi hio, ni sawa na ujumla uliomo katika Aya inayosema: "Sasa waingiliyeni ( wake zenu) na tafuteni kile Allah alichokuandikiyeni, na kuleni na kunyweni mpaka ukubainikieni uzi mweupe kutokana na uzi mweusi wa alfajiri, kisha timizeni saumu hadi usiku."

Je hapa Allah anazungumza na watu wote au na watu maalumu? Je kuzungumza huku na watu wote inamaanisha kwamba alfajiri ya nchi moja ikichomoza watu wa nchi zote wajizuie, au kila watu na alfajiri yao? Jawabu yako hapa ndio jawabu yetu kwa maneno ulioyanukuu kutoka katika kitabu cha Al-sayyid Saabiq kwamba Hadithi hiyo "Fungeni kwa kuuona" ni: " "Agizo la ujumla linalojumuisha umma wote (wa Kiislamu) kwa hivyo; yeyote miongoni mwao atakayeuona (mwezi) popote pale; kuone kana huko kutakuwa ni kuonekana kwa wote." Halkadhalika tunajibu ujumla huo kwa Hadithi inayosema: "Usiku ukitokeza kutoka hapa na mcha na ukaondoka kutokea hapa na jua likatua, basi aliyefunga ameshafungua (au na-afungue)." Na sisi tunauliza je hapa walikuwa wakiambiwa watu wa Makka tu, au wakiambiwa watu wa nchi zote? Kama walikuwa wakiambiwa watu wa nchi zote, je jua likitua Makka au katika mji wowote ule sote tufuturu? Kwa hakika kila aliyejaaliwa kuwa na mtazamo sahihi, anaona kwamba kujenga hoja kwa ujumla wa Hadithi "Fungeni kwa kuuona" kwamba ni ushahidi wa kuwepo muandamo mmoja, ni kujenga hoja juu ya msingi dhaifu sana. Na kwa maana hio, Ibn Uthaimin (Mwanachuoni wa Kiwahabi) akasema kwamba kauli ya kuwa kila watu wana muandamo wao: "Ina nguvu yake kwa mujibu wa lafdhi (yake) na mtazamo sahihi na Qiyas sahihi vile vile: Qiyas cha wakati wa siku kwa (kuulinganisha) na wakati wa mwezi (month). Mwisho wa kunukuu.

Kwa ufupi ni kuwa, ujumla wa Hadithi inayosema "Fungeni kwa kuuona" ni - kama tulivyotangulia kusema - kwamba watu wote ni lazima wafunge kwa kuuona: si kwa kalenda wala kwa jengine lolote. Huu ndio ujumla unaokusudiwa katika Hadithi hio, au ndio ujumla uliobakia baada ya kuhusishwa au kuvuliwa sehemu ya ujumla huo na Hadithi ya Ibn Abbas na Kuraib.

Jambo la tatu: la kutazamwa katika Hadithi hii, ni kuwa Hadithi hii ni Mutlaq (isiofungamanishwa na kitu) wakati Hadithi ya Ibn Abbas ni muqayyad (iliofungamanishwa). Kanuni ni kuitanguliza muqayyad kuliko mutlaq kama usuli unavyoeleza. Kwa hivyo, kila msingi utaoufata utaona kwamba Hadithi ya Ibn Abbas ndio inayotakiwa itangulizwe.

Ama waliosema kwamba tufunge kwa muandamo mmoja, ukweli ni kuwa wao waliitanguliza rai kuliko kanuni za tafsiri. Walitazama wakaona kuwa mwezi ni mmoja na unakamilisha safari yake mara moja na kwa hivyo muandamo utakuwa mmoja. Lakini tumeona kwamba huu si muandamo wa Kisharia bali ni muandamo wa Kifalaki: muandamo wa Kisharia tunaupata katika kuzijumisha Hadithi tafauti. Pili ni kuwa hio ni rai, na ya Ibn Abbas ni Hadithi; na rai haina uwezo wa kuipinga Hadithi. Kama walivyosema: "Rai haina nafasi mbele ya A ndiko."

Ama utata munaotaja nyinyi mara baada ya nyengine basi hata katika Hadithi "Fungeni kwa kuuona" pia upo; bali hapa upo zaidi kuliko katika Hadithi ya Kuraib na Ibn Abbaas; kwani Hadithi hii "Fungeni kwa kuuona" haikubainisha je tufunge kwa muandamo mmoja au kila watu na muandamo wao nayo Hadithi hio katika ujumla wake ni kama Aya "Simamisha Sala kwa kutenguka jua" na Hadithi "Usiku ukitokeza kutoka hapa na mchana ukaondoka kutokea hapa na jua likatua, basi aliyefunga ameshafungua (au na-afungue)." Zote zina ujumla sawa. Wakati - kwa upande wa pili - Hadithi ya Kuraib na Ibn Abbaas imebainisha kwamba mwezi wa mbali si hoja kwa walio mbali. Kwa hivyo, utata uko zaidi katika Hadithi "Fungeni kwa kuuona" kuliko Hadithi ya Kuraib na Ibn Abbaas.

MNASEMA

Baada ya kuyaona maneno ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) kwamba hayako wazi na kama mezani ya fani ya Hadiyth inavyojionesha - ni vyema kuwauliza Wanavyuoni ambao ni wapokezi wa Hadiyth: Je Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) hajawahi kupokea Hadiyth inayotaja kadhia hii ya miandamo ya mwezi nyengine isiyokuwa ile ya Kurayb? Wanavyuoni watajibu kuwa ipo riwaya iliyopokelewa na Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) mwenyewe juu ya suala hili la muandamo wa mwezi.

JAWABU

Hili tumeshalieleza kwamba hakuna kanuni laa ya kiusuli wala ya elimu ya Hadithi ilioifanya Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib kuwa isizingatiwe au iwe haifahamiki. Na kama kuna mtu hakuifahamu basi tatizo liko kwake si kwa Ibn Abbaas wala si katika riwaya yenye: riwaya iko wazi. Ibn Abbaas kaukataa muandamo wa Sham na akasema "Kuwa hivi ndivyo Mtume s.a.w. alivyotuamuru". Sasa alivyowaamuru ni vipi? Je kawaamuru kuwa wauzingatie muandamo wa mbali? Kama ni hivyo, vipi tena Ibn Abbaas asiufate naye ni mwanachuoni, sahaba mcha Mungu. Kwa hivyo, suala liko wazi na halitaki maelezo, lakini mtu akiwa kitu hakitaki huwa anatafuta kipengele dhaifu na shubuha hii na hile ili akikatae.

Ama suala: "Je Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) hajawahi kupokea Hadiyth inayotaja kadhia hii ya miandamo ya mwezi nyengine isiyokuwa ile ya Kurayb?" Jawabu ndio kapokea lakini je riwaya hio nyengine inabatilisha riwaya yake na Kuraib? Hili ndilo la kujiuliza?

Munasema Ifuatayo ndiyo riwaya yenyewe:

(Kutoka kwa Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) kwamba bedui mmoja alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Nimeuona mwezi." Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Unashuhudia kwamba hakuna anayepaswa kuabudiwa isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)?" akasema: "Ndio." Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Ewe Bilal watangazie watu kesho wafunge.")) (Muslim).

Kama tulivyoona kwamba Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ndiye aliyeipokea Hadiyth hiyo ya bedui na alivyokuja bedui huyo kumpa habari Bwana Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akazikubali habari hizi za kuambiwa. Jambo alilofanya ni kuzithibitisha tu kwamba yule aliyezileta habari zile ni Muislam. Wala hakumuuliza kwamba bedui yule anatokea wapi, wala pahala alipouona mwezi, wala kutokea masafa gani. Inawezekana kuwa alitokea maeneo ya karibu au vile vile inawezekana alitokea maeneo ya mbali na inaelekea kabisa kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwa akimjua bedui yule ndio maana akamtamkisha shahada ili kuhakikisha kama alikuwa ni Muislamu.

Ilivyokuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakumuuliza bedui jambo lolote katika hayo tuliyoyataja, Shari'ah ya 'Usulul-Fiqhi' Wanavyuoni wanasema yafuatayo: "Kuacha kuuliza pahala ambapo ilikuwa inayumkini kuuliza basi inamaanisha kuwa hii ni hukmu ya jumla ('aam) isiyokuwa na mipaka."

Habari hizi zimenukuliwa katika Tafsiri ya Qur-aan Tukufu: i. ii.

Na ndio njia inayoelekea kuwa sahihi kuliko kufuata jambo lenye utatanishi (ihtimaalati). Bora kushikamana na mafunzo sahihi ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambayo yako wazi na yaliyo mepesi. "Jambo la asli halihitaji (kuletewa) dalili, (lakini dalili inahitajika katika jambo lisilo la asili)."

Kwa hivyo ilivyokuwa Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) alipokea (Hadiyth) maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya kwamba alimkubali bedui bila ya kumuuliza anatokea wapi; halafu Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) huyu huyu hakuukubali mwezi ulionekana na Kuraib huko Sham, hapa inaonyesha wazi kwamba kitendo cha Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) kimetafautiana na yale aliyoyapokea kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

JAWABU

SANAD YA HADITHI

Katika kitabu changu Ushahidi Uliowekwa Wazi, niliikuu Hadithi hio ya Ibn Abbaas na nikatoa maelezo yafatayo: Hadithi hii - kama unavyoona - imepokewa na wapokezi tafauti. Lakini ina kasoro mbili: Moja ni mgongano katika sanad: wakati katika sanad nyengine Ikrima anaisimulia Hadithi hii mausulan (kwa kuifikisha) kutoka kwa Ibn Abbas kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) , katika sanad nyengine anaisimulia mursalan (bila kumtaja Ibn Abbas wala Sahaba yeyote). Na kwa hivyo, Al-nnasai anasema kwamba kauli ya kuwa Hadithi hii ni mursal (iliosimuliwa bila kutajwa Sahaba aliyeisikia Hadithi hio kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) : "Ndio inayoelekea zaidi kuwa sahihi."

Pia wanavyuoni wengine wakubwa wa Hadithi wanasema kwamba kundi (kubwa) la wasimulizi wameisimulia Hadithi hii kutoka kwa Ikrima kutoka kwa Mtume (s.a.w.) mursalan (bila kutajwa Ibn Abbas wala Sahaba yeyote). Miongoni mwa waliosema hivyo, ni Abu Daud kama ilivyo katika kitabu chake "AL-SUNAN" na akayanukuu maneno yake pia Al-bayhaqiy katika "AL-KUBRA". Na mfano wa maneno ya Abu Daud, ni maneno ya Ibn Majah katika "AL-SUNAN". Na akasema Al-tirmidhiy: "Hadithi ya Ibn Abbas ndani yake kuna khilafu: kaisimulia Sufyan Al-thauri na wengineo kutoka kwa Simak bin Harb kutoka kwa Ikrima kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) mursalan (bila kutajwa Ibn Abbas wala Sahaba yeyote), na wengi wa As-habu wa Simak wameisimulia (hivyo) kutoka kwa Ikrima kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) mursalan (bila kutajwa Ibn Abbas wala Sahaba yeyote)."

Ama Ibn Al-arabiy Al-malikiy yeye anasema: "Hilo kwetu halivunji usahihi wa kutoa habari (yaani usahihi wa kusimulia Hadithi) nayo ndio kauli ya Al-nadhaam kwani mpokezi wakati mwengine huiwasilisha (Hadithi kwa kumtaja Sahaba) na wakati mwengine huiachia (kwa kutokumtaja Sahaba), na (pia) wakati mwengine mpokezi mmoja huiwasilisha (Hadithi kwa kumtaja Sahaba) na mpokezi mwengine akaiachia (kwa kutokumtaja Sahaba)."

Kasoro ya pili ambayo kwayo imetiwa ila Hadithi hii, ni kuwa Hadithi hii kapwekeka nayo Simak bin Harb naye ni dhaifu, na kwa hivyo "Si ambaye anafanywa kuwa ni hoja katika Hadithi alizopwekeka nazo," kama alivyosema Al-nasai katika nakala ya Al-shaukaniy. Na bila shaka Simak bin Harb ni dhaifu. Anasema Abu Talib kutoka kwa Al-imamu Ahmad bin Hanbal akisema kwamba Simak bin Harb: "Hadithi zake zinagongana." Na "Alikuwa Shu'uba akimdhoofisha." Anasema Ibn Ammar: "(Wanavyuoni wa Hadithi) wanasema kwamba alikuwa akikosea." Anasema Ya'aqubu bin Abi Shaiba: "Nilimwambia Ibn Al-madiniy: (Vipi kuhusu) riwaya za Simak kutoka kwa Ibn Abbas? Akasema: "Ni zenye kugongana." Anasema Ibn Al-mubarak: "Simak ni dhaifu katika Hadithi." Anasema Ibn Hibban: "Anakosea." Na wako wengine waliomdhoofisha.

Kwa hivyo, kwa kuzingatia kwamba Hadithi hii, kapwekeka nayo Simak bin Harb kutoka kwa Ikrima, na Simak ni dhaifu, basi wanavyoni wa Hadithi wameihukumu Hadithi hii kuwa ni yenye sanad dhaifu, ingawa maana ya Hadithi hii wameikubali kwa kuzingatia kwamba inapata nguvu kwa Hadithi sahihi ya Ibn Umar ambayo tutainukuu katika sehemu inayofata Inshaa Allah. Anasema Al-shaukaniy kuhusu Hadithi hii ya bedui: "Nayo ni miongoni mwa kile ambacho hoja haisimami kwacho, kwa (sababu ya) kile kilichotangulia (kuelezwa) cha udhaifu wa yule aliyepwekeka nayo (naye ni Simak bin Harb)." Mwisho wa kunukuu.

Kisha baada ya hapo nikatoa tanbihi, nikasema: Jua kwamba udhaifu wa sanad ya Hadithi hii, haimaanishi udhaifu wa matn (text au maneno) ya Hadithi yenyewe. Maana ya Hadithi hii ni sahihi kwa vile kuna Hadithi nyengine - nayo ni Hadithi ya Ibn Umar - yenye kuafikiana na Hadithi hii kimaana. Na kwa hivyo wanavyuoni wengi wameitolea hoja Hadithi hii, na Ibn Hibban alipotaka kuisimulia Hadithi ya Ibn Umar tutayoinukuu baadae Inshaa Allah, alitumia lugha hii: "Kutaja habari (riwaya) yenye kubomoa kauli ya mwenye kudai kwamba habari (riwaya) hii (ya bedui) kapwekeka nayo Simak bin Harb na kwamba kuinasibisha kwake na Mtume(s.a.w.w) si sahihi." Kisha baada ya hapo, Ibn Hibban akasimulia riwaya hio ya Ibn Umar yenye maana sawa na riwaya ya bedui.

Kwa hivyo, ili muwe mumenijibu kwanza thibitisheni usahihi wa lafdhi hii ya Hadithi. Ama usahihi wa maana hauifanyi Hadithi kuwa ni hoja ikiwa ina sanad dhaifu. Kwa hivyo, kisanad, Hadithi hii si hoja na hilo wamelinena wanavyuoni wengi.