MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI 18%

MUANDAMO WA MWEZI Mwandishi:
Kundi: Midahalo na majadiliano kielimu

MUANDAMO WA MWEZI
  • Anza
  • Iliyopita
  • 23 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 62345 / Pakua: 6746
Kiwango Kiwango Kiwango
MUANDAMO WA MWEZI

MUANDAMO WA MWEZI

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

4

10

MUANDAMO WA MWEZI

MATN YA HADITHI

Ama kuhusu matn ya Hadithi hii, na kuhusu madai yenu mulioyakariri bila ya kujibu nilioyasema, mimi nilisema hivi: Suala jengine muhimu katika Hadithi hii na ambalo linahusiana zaidi na mizozo na migogoro yetu ya mwezi muandamo katika Afrika ya Mashariki, ni kuwa je Hadithi hii inathibitisha usahihi wa dai la kwamba muandamo wa mji mmoja ni muandamo wa ulimwengu mzima? Katika kitabu chake Sheikh Nassor Abdallah Bachoo, baada ya kuinukuu Hadithi ya bedui, alitoa maelezo haya:

"Pia jambo la kuzingatia hapa ni kwamba ilivyokuwa mtu huyo alikuwa ni Bedui yaani mtu wa Majangwani, Mtume(s.a.w.w) angeweza kumuuliza anatoka wapi, lakini hakumuuliza kabisa suala hili jambo ambalo linathibitisha kuwa suala la umbali gani wa kuonekana mwezi Mtume(s.a.w.w) hakuwa akilizingatia hata kidogo!!!" Mwisho wa kunukuu.

Lakini nadharia hii ya Sheikh Nassor Bachoo, haikutokana na fikra sahihi. Labda tuulize suala ili iwe ndio jawabu ya madai haya ya Sh. Nassor Bachoo. Suala ni kuwa: je Sheikh Bachoo anadhani kwamba bedui huyo alitoka wapi mpaka akaweza kufika kwa Mtume(s.a.w.w) usiku huo huo wa muandamo wa mwezi na akampa habari hio? Je anadhani kuwa bedui huyo alitoka Sham, Misr, Yemen au Oman? Ni wazi kwamba bedui atayeweza kwenda kwa Mtume(s.a.w.w) kumpa habari hio usiku huo huo au hata usiku wa pili na wa tatu, basi atakuwa ni bedui wa jangwa la hapo hapo Madina. Na kwa hivyo Mtume(s.a.w.w) - naye ndiye mkamilifu wetu kwa akili na elimu - hakuwa na haja ya kumuuliza unatoka wapi. Ivo tuseme katika wakati ambao hapakuwa na ndege wala vyombo vyovyote vyenye kwenda kwa kasi akakujia mtu baada ya Isha akakwambia nimeuona mwezi, nawe upo Bumbwini au Mahonda, utahitaji kumuuliza anapotoka? Ni wazi kwamba mtu huyo atakuwa anatoka katika miji hio hio ya Zanzibar. Kwa hivyo, bedui alikuwa ni bedui wa Madina ndio maana akaweza kufika kwa Mtume(s.a.w.w) usiku huo huo. Na kwa hivyo Mtume(s.a.w.w) hakuhitaji kumuuliza anapotoka.

Lakini baada ya maelezo hayo ya kiakili ambayo yako wazi kwa kila mwenye kutafakari, ni bora tuwaachie wapokezi wa Hadithi watueleze bedui huyo alitokea wapi. Ikrima - mwanafunzi wa Ibn Abbas - anaeleza kwamba bedui huyo alikuwa akitokea Al-harrah nayo ni sehemu yenye mawe mawe katika eneo la Madina. Na kwa maelezo haya mafupi, unabainika udhaifu wa dai hilo la Sh. Bachoo la kukufanya kule Mtume(s.a.w.w) kutomuuliza bedui anapotoka, kuwa ni dalili ya kutozingatia masafa, a kitegemea Hadithi hio ya bedui, kwani bedui huyo anajulikana kwamba anatoka Madina: si mahala pengine.

Hayo ndio nilioyasema na yote haya nyinyi hamukuyajibu - si sanad wala si matn, bali mumekariri kitu kile kile ambacho nimeshakijibu, na huu sio mjadala wa kielimu. Mjadala wa kielimu ni kuwa nukta inayojibiwa kwa uwazi huwa haikaririwi tena bali hutazamwa mule ambamo hamukujibiwa. Lakini hayo, ni kwa wale wenye kujua nini maana ya debate. Ama kanuni isemayo: "Kuacha kuuliza pahala ambapo ilikuwa inayumkini kuuliza basi inamaanisha kuwa hii ni hukmu ya jumla ('aam) isiyokuwa na mipaka." Kanuni hii, haihusiani na riwaya hio ya Bedui. Kanuni hii - nayo ni ya Al-Imamu Al-Shafi kwa ninavyokumbuka - inazun gumzia kitu ambacho hakijulikani na hakikuulizwa; si kitu chenye kujulikana. Na asili ya kanuni hii imejengwa katika Hadithi zenye kusimulia Sahaba aliyesilimu naye ana wake wengi zaidi ya wane. Mtume (s.a.w.) akamuamuru awaache abakishe wane. Yule sahaba hakuuliza Mtume(s.a.w.w) je wa kuachwa ni waliolewa mwisho au wowote tu, na Mtume(s.a.w.w) naye hakumbainishia. Kwa hivyo, Maulamaa - nadhani wa mwanzo wao ni Al-Imamu Al-Shafi - ndio wakatoa kanuni hio kutoka katika Hadithi hio. Ama bedui aliyekwenda kwa Mtume(s.a.w.w) usiku wa muandamo au hata siku ya pili na ya tatu, basi ni badui wa jangwa hilo hilo la Madina: si bedui wa Oman, Yemen au Sham. Nadhani hili - ikiwa hamutaki ubishi - basi liko wazi. Juu ya hayo, riwaya yenyewe imesema kwamba huyo bedui alikuwa akitoka wapi. Ikrima - mwanafunzi wa Ibn Abbas - anaeleza kwamba bedui huyo alikuwa akitokea Al-harrah nayo ni sehemu yenye mawe mawe katika eneo la Madina. Sasa uko wapi uhusiano wa kanuni hii na hadithi ya bedui?!!!!!!!!

Ama kanuni isemayo: "Jambo la asli halihitaji (kuletewa) dalili, (lakini dalili inahitajika katika jambo lisilo la asili)" lau muliifahamu kanuni hii, musingeliniambia kuwa nilete ushahidi wa kuwepo kwa matalai ya mwezi, k wani jambo linalojulikana kwamba ndio lilivyo basi halihitaji ushahidi. Lakini nyinyi ndugu zangu hamusemi kitu kwa maarifa sahihi, bali muna msimamo wenu huo hamutaki kuuwacha na anayekupungeni huwa yeye si mtu wa msimamo. Munasema Je nini hukmu ya kadhia hii? Ni vyema tusogeze karibu mezani yetu ya Mustalahul-Hadiyth ili tuone kipimo sahihi na chenye uzito mkubwa kipo upande gani:

"Atakapokwenda kinyume mpokezi (wa Hadiyth) kwa kile alichokipokea; Je hutangulizwa (katika hukmu ya jambo hilo ) njia (madhehebu) ya mpokeaji (namna alivyofanya yeye) au itatangulizwa habari (yaani) kile alichokipokea? Jamhuri ya Wanavyuoni wa Usulul-Fiqhi na Wanavyuoni wa Fiqhi - wakiwemo Imamu Shafi na Abul-Hassan wameonelea kwamba kilicho wajibu kutendewa kazi ni ile habari aliyoipokea mpokeaji sio ile tafsiri (ya tendo) la mpokezi. Kwani chenye kuzingatiwa juu ya kadhia hii ni kile alichokipokea (Swahaba kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) sio kile anachokiona yeye katika rai yake au alichokitenda."

Habari hizi zinapatikana katika vitabu vifuatavyo: 1. Al - Ihkamu Fii Usulil-Ahkam J. 2

2. Irshadul-Fuhul.

3. Khabaril-Waahid Wahujjiyatuh.

4. Al-Fatawa-Swala, Zakka, Swaum wa Hajj - kitabu cha 1 uk 268.

Jawabu

Kanuni hio ni sahihi, lakini wapi Ibn Abbaas kenda kinyume na riwaya yake. Riwaya ya Ibn Abbaas - pamoja na udhaifu wa sanad yake - inasema: ((Kutoka kwa Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) kwamba bedui mmoja alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Nimeuona mwezi." Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Unashuhudia kwamba hakuna anayepaswa kuabudiwa isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)?" akasema: "Ndio." Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Ewe Bilal watangazie watu kesho wafunge.")). Haya iko wapi humu kwamba watu wafunge kwa muandamo mmoja, hata iwe Ibn Abbaas kenda kinyume na riwaya hii alipouacha muandamo wa Sham? Naona ndugu zangu munasema tu mambo bila hata ya kufikiri! Ama yale ya Mtume(s.a.w.w) kutokumuuliza bedui atokapo tumeshajibu.

MNASEMA

Baada ya kuona uzito uliopo katika mezani ya Mustalahul-Hadiyth. Ni vyema tuangalie tena mfano mwengine ufuatao:- Kuhusu Sahaba Abu Hurayra (Radhiya Allaahu 'Anhu) alivyopokea hukmu ya chombo kilichorambwa na mbwa. Sahaba huyu ndiye aliyepokea Hadiyth kutoka kwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba chombo kilichorambwa na mbwa kisafishwe kwa kuoshwa kwa maji mara saba; moja kati ya hizo isafishwe kwa mchanga. Katika mapokezi mengine Abu Hurayra (Radhiya Allaahu 'Anhu) huyu huyu ameshuhudiwa kutoka kwa Sa'iyd bin Musayab kwamba yeye Abu Hurayra alikiosha chombo mara tatu katika sehemu ambayo ilitiwa mdomo na mbwa.

Imeonekana kitendo hicho cha Abu Hurayra (Radhiya Allaahu 'Anhu) kimetofautiana na maneno aliyoyapokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa jambo hilo , Wanavyuoni wote wa Kishafi wamesema chombo kilichorambwa na mbwa kioshwe mara saba na wala sio mara tatu. Kwa mantiki hiyo wameona washike yale maneno yake Abu Hurayra aliyoyapokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na wameacha kushika kile kitendo chake. Kwa hivyo cha kuzingatia ni yale maneno yaliyopokewa na wala sio kitendo cha aliyepokea. Kwani huenda mpokeaji akaghafilika, lakini maneno yakabaki vile vile na ndiyo yanayostahiki kutendewa kazi. Haya ni kwa mujibu wa misingi ya Shari'ah, Qur-aan na Sunnah. Tokeo hili ni sawa katika hukmu na tokeo la Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) katika kisa cha Kuraib, kama vile Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) alipokea kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikubali habari za mwezi zilizoletwa na bedui asiyetambulika na bila ya kumuuliza anatokea wapi au mwezi aliuona wapi. Halafu Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) huyu huyu hakuukubali mwezi ulioonekana na Kuraib pamoja na watu wengine huko Sham.

JAWABU

Hivyo alivyofanya Abu Huraira ndio mpokezi kwenda kinyume na riwaya yake: sio yale yaliomo katika riwaya ya Ibn Abbaas na Kuraib kwa upande mmoja na riwaya ya Ibn Abbaas na bedui kwa upande wapili. Kule hakuna kwamba katika riwaya moja Ibn Abbaas kaambiwa fungeni kwa muandamo mmoja kisha katika riwaya ya pili akafunga kwa muandamo tafauti. Wala hili halifahamiki katika riwaya hio kamwe kama tulivyobainisha vya kutosha.

MNASEMA

Hapo ndipo tunapowajibika kushika yale maneno aliyoyapokea Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na kukiacha kitendo chake. Lililo bora ni kushika yale maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyo wazi kuwa mwezi ukionekana (popote) watu wafunge au wafungue na hivyo ndivyo alivyofanya mwenyewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) bila ya kuzingatia wapi umeonekana mwezi. Kauli yake ilikuwa kama ifuatavyo:"Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi - muandamo"

JAWABU

Ama kudai kwamba: "Hapo ndipo tunapowajibika kushika yale maneno aliyoyapokea Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na kukiacha kitendo chake. Lililo bora ni kushika yale maneno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyo wazi".

Hio ni dhana dhaifu sana. Kwa bahati tumekubaliana kwamba twende kwa mujibu wa kanuni. Utakumbuka kwamba riwaya ya Ibn Abbaas na Kuraib inasema: Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w) .. Kwa hivyo, kwa mujibu wa fani ya Hadithi 'Ulumul Hadith hii pia ni Hadithun Marfu'u sawa na Hadithi isemayo:"Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi - muandamo" . Na hivi ndivyo walivykobaliana wajuzi. Anasema Al-Suyuti alipokuwa akizungumzia Hadithun Marfu'u: "Akiwa (sahaba) atasema: 'Mtume s.a.w. katuamuru, basi hakuna khilafu ndani yake (hio ni Hadithun Marfu'u)'.

Kwa hivyo, kuifanya Hadithi (Fungeni kwa kuonekana mwezi - muandamo na fungueni kwa kuonekana mwezi - muandamo.) kuwa ndio Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) na Hadithi "Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w) " kuwa ni maneno ya Ibn Abbas ni kosa la kiminhaj (Methodolocal error); hilo halikubaliki katika elimu ya Hadithi. Zote hizo ni Hadithi za Mtume(s.a.w.w) , na kwa hivyo, kilichobaki ni kutafuta hii ina maana gani na hile ina maana gani. Tena nakukumbusheni kauli yenu muliposema: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w).

Tumesema: ama Hadithi"Fungeni kwa kuuona" ni andiko la wazi juu ya uwajibu wa kufunga kwa kuuona mwezi. Kw a hivyo, lazima tufunge kwa kuuona: si kwa kalenda wala si kufunga siku ya shaka. Hili ndilo linalothibitishwa na Hadithi hio:Fungeni kwa kuuona ." Lamu iliomo katika neno (Liru-uyatihi) ni H arfu Jarri li-tta'alil. Yaani ni harufu yenye kulitia neno kasra na kuonesha sababu ya maneno yaliotangulia au sababu ya hukumu iliotajwa. Kwa hivyo, maana ya haya ni kuwa kuuona mwezi iwe ndio sababu ya kufunga au kwa lugha nyengine sababu ya kufunga iwe ni kuuona mwezi. Hii ndio maana ya meneno"Fungeni kwa kuuona:" Hakuna hapa kinachoonesha mas-ala ya kufunga kwa muandamo mmoja au miandamo tafauti.

Ama Hadithi ya Ibn Abbaas na Kuraib, ambayo ndani yake tunapata kuwa Ibn Abbaas aliukataa kuufata muandamo wa Sham na kusema: Hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume(s.a.w.w ) Hadithi hii ni ushahidi kwamba muandamo wa mbali si hoja kwa walio mbali. Hivi ndivyo, taratibu za kifan i zinavyotutaka: tuyakusanye maandiko madamu inawezekana: sio moja tulitendee kazi jengine tulitupe. Kwa hivyo, natija ni kuwa:

a) Lazima tufunge kwa kuuona: si kwa kalenda wala si kufunga siku ya shaka. Hili linathibiti kwa Hadithi: Fungeni kwa kuuona."

b) Muandamo wa mbali hautendewi kazi mbali. Hili linathibiti kwa kitendo cha Ibn Abbas cha kuukataa muandamo wa Sham na kubainisha kwamba hicho ndicho alichokifunza Mtume(s.a.w.w) . Munasema Suala Jengine: Je masimulizi ya Kuraib na Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ndio yanakuwa makhsusi katika Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) zilizotaja habari za kufunga na kufungua? Ni vyema kuweka wazi kwamba Hadiyth zote za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aali hi wa sallam) ambazo ni nyingi mno (Mutawaatir) zilizotaja habari ya kufunga na kufungua mwezi wa Ramadhaan zote zimekuja kwa ujumla - ('aam) Bila kuhusisha watu wa nchi fulani, masafa au matlai ya aina yoyote. Angalia: Agizo hilo limekuja kwa watu wote. Masimulizi ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na Kuraib yalitokea zaidi ya miaka 30 baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kwamba Makhalifa wote wanne walikwishaondoka duniani. Kwa hivyo kuyafanya masimulizi hayo ya Kuraib kuwa ndiyo 'Khaas' katika Hadiyth hizo za kufunga na kufungua Swaum ni kinyume na kanuni za kifani. Ni vyema kuwaangalia Wanavyuoni wa fani ya Usulil-Fiqhi wanasema nini katika vitabu vyao kwenye huu mlango wa ('aam) - yaani maana ya ujumla na upamoja kwa watu wote:

JAWABU

1) Naam! Masimulizi ya Kuraib na Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ndio yanakuwa makhsusi, kwa kuwa yanawahusisha watu wa sehemu pasi na wengine; wakati katika masimulizi mengine hili hulipati.

2) Ama dai kwamba "Hadiyth zote za Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambazo ni nyingi mno (Mutawaatir) zilizotaja habari ya kufunga na kufungua mwezi wa Ramadhaan zote zimekuja kwa ujumla - ('aam)", si dai sahihi. Sasa riwaya zote zikija kwa uj umla - ('aam), ndio Hadithi ya Ibn Abbaas ishakuwa batili?!!! Au tufate kanuni kwamba andiko mahususi ndilo linalotangulizwa kuliko andiko la ujumla.

3) Pili: Je ujumla huo ni ujmla katika mazingato gani? Ujumla uliomo katika riwaya nyengine ni kama tulivyoeleza ni ujumla kwamba watu wote ni lazima wafunge kwa kuuona: wala hakuna katika Hadithi yoyote ujumla kwamba watu wote wafunge sawa. Suala je tufunge pamoja au tafauti halimo katika riwaya "Fungeni kwa kuuona" wala katika riwaya ziliokurubiana na hii kilafdhi. Bali riwaya hizi zinahimiza kwamba mfungo na mfunguo uwe kwa mujibu wa kuuona mwezi. Ama je muandamo wa mbali unakuwa hoja kwa walio mbali au haui, hilo linabainishwa na riwaya ya Ibn Abbas na Kuraib.

4) Ama dai kwamba: "Masimulizi ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na Kuraib yalitokea zaidi ya miaka 30 baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kwamba Makhalifa wote wanne walikwishaondoka duniani". Sijui dai hili linathibitisha nini? Kwani masimulizi yakiwa baada ya miaka 30 huwa yanabatilisha riwaya? Na kwani Makhalifa wakiondoka ndio riwaya huwa hazisimuliwi tena?! Masimulizi ya riwaya yana sharti zake zikitimia basi riwaya inazingatiwa.

5) Ama kudai: "Kwa hivyo kuyafanya masimulizi hayo ya Kuraib kuwa ndiyo 'Khaas' katika Hadiyth hizo za kufunga na kufungua Swaum ni kinyume na kanuni za kifani". Tunauliza: ni kinyume na fani gani hio? Tuleteeni hio fani inayoonesha kuwa kutegemea ri waya ya Ibn Abbaas na Kuraib ni kinyume na fani. Fani inasema kwamba "Kauli ya sahaba akisema Mtume s.a.w. katuamuru kadha au katukataza kadha" hio ni Hadithi ya Mtume. Kwa hivyo, hii ni Hadithi ya Mtume (s.a.w.). Sasa wapi umesikia kwamba au ni fani gani isemayo kwamba ni kosa kuuhusisha ujumla wa Hadithi moja kwa Hadithi nyengine?

MNASEMA

Ifuatayo ni tafsiri kwa njia ya maana bila ya kutafsiri neno kwa neno: "Ili khaas ikubalike katika misingi ya Shari'ah kama ni hoja sahihi lazima khaas hiyo iepukane na utata. Kuwepo kwa utata ndani ya khaas kutaifanya kukosa kuwekwa mbele kwenye safu za hoja. Kwa hivyo (kielimu) haitaweza kutegemewa kwa namna yoyote ile. Na badala yake itabakia kuwa ni ya ujumla ('aam) katika kuwajumuisha watu wot e popote walipo. Kwani kuwepo kwa utata ni tuhuma zisizo na ushahidi imara zinazoifanya khaas hiyo kwa mujibu wa kanuni za Usulil-Fiqh kutoweza kuzingatiwa.

JAWABU

Kwanza tafsiri yenu inataka kurekebishwa, pamoja kuwa mumejilinda kwa kusema: "Ifuatayo ni tafsiri kwa njia ya maana bila ya kutafsiri neno kwa neno". Na nadhani pia kuna kosa la chapa. Neno inavyoelekea munakusudia Wallahu A'alam. Na neno Ihtimal halina maana ya utata, bali maana yake ni uwezekano wa tafsiri hii na hile. Ama tafsiri ya maneno hayo ni hivi:

Ama (andiko la ujumla) kuwa lina uwezekano wa kuhusishwa (na andiko khaas specific) bila ya kuwepo dalili ya uwezekano huu, basi hilo ni katika yale yasiozingatiwa wala halitazamwi wala halitendewi kazi. Basi (hapo) ushahidi uliomo katika Aam (andiko la ujumla) unaendelea kubakia katika (ujumla wake wa) kukusanya sehemu zake za yakini. Wala kule kuwa kuna uwezakano tu (kwamba andiko Aam, andiko la ujumla) limehusishwa bila ya dalili hakuliathiri (kitu andiko hilo la Aam ujumla), kwani uwezekano huo ni katika kufikiri kitu kimakosa (illusion), na hakuna kuzingatia fikra ya kimakosa wala kufikiri kimakosa."

Hii ndio tafsiri ya maneno hayo. Sasa mumefahamu nini? Haitoshi mtu kufungua kitabu akatafuta kipande akanukuu ikiwa ile fani hajaisoma yote. Kinachozungumzwa hapa ni kuwa je ndiko Aam ni (la dhana) au ni (la uhakika na yakini)? Mahanafi wanasema ni (la uhakika na yakini); Jumhur wanasema ni (la dhana). Sasa wanaosema kuwa andiko hilo ni (la dhana) - nao ni Jumhur wanasema - wanajega hoja kwamba ndiko Aam linauwezekano wa kuwa limehusishwa kwani imesemwa kwamba hakuna ndiko Aam la ujumla ila huwa limehusishwa isipokuwa andiko kama "Hakika Allah ni Mjuzi wa k ila kitu" na yalio mfano wa hilo. Kwa hivyo, kwa kuzingatia kwamba maandiko Aam ya ujumla yote - taqriban - yamehusishwa, basi huwa hatuna yakini tunapolikuta andiko Aam la ujumla kwamba je ni kweli kila chenye kuhusiana na andiko hilo kimeingia au yameingia baadhi tu. Nikisema Wazanzibari ni wakarimu, je huwa kweli ni Wazanbari wote? Inawezekana ikawa wote na inawezekana ikawa si wote. Lakini kwa vile lafdhi Wazanzibari ni wakarimu inawaingiza wote, basi hapo ndio ikawekwa kanuni nyengine kwamba: "Andiko la ujumla linakwenda katika ujumla wake mpaka lipatikane andiko lenye kuhusisha." Nikikuta andiko jengine kwamba Mzanzibari si karimu, basi yeye huwa kahusiswa na andiko Khaas (specif ic au exceptional). Ama andiko khaas specific ni (la uhakika na yakini) kwa mujibu wa Jumhur. Na kwa hivyo, niksema Ali ni mkarimu, basi hili ni andiko la uhakika kwamba Ali kaingia katika ukarimu.

Ama wanaosema kwamba ndiko Aam la ujumla ni (la uhakika na yakini), nao ni Mahanafi, na kwamba andiko hilo linawaingiza wote wanaoingia katika lafdhi ya andiko hilo, ndio wanaosema hivyo: Ama (andiko la ujumla) kuwa lina uwezekano wa kuhusishwa (na andiko khaas specific) bila ya kuwepo dalili ya uweze kano huu, basi hilo ni katika yale yasiozingatiwa wala halitazamwi wala halitendewi kazi. Basi (hapo) ushahidi uliomo katika Aam (andiko la ujumla) unaendelea kubakia katika (ujumla wake wa) kukusanya sehemu zake za yakini. Wala kule kuwa kuna uwezakan o tu (kwamba andiko Aam, andiko la ujumla) limehusishwa bila ya dalili hakuliathiri (kitu andiko hilo la Aam ujumla), kwani uwezekano huo ni katika kufikiri kitu kimakosa (illusion), na hakuna kuzingatia fikra ya kimakosa wala kufikiri kimakosa." N a hao ni Mahanafi: si Jumhur. Kwa hivyo ni wazi kwamba ndugu zetu:

1) Hawakuyafahamu maana ya maneno walioyanukuu: wameyafasiri sivyo.

2) Hawakufahamu hii ni kauli ya akina nani.

3) Hawakufahamu muradi wake ni nini.

Kwa hivyo, maana ya maneno hayo si kwamba andiko lenye maana nyingi au lenye utata kama munavyoita nyinyi huwa halitumika kuhusisha ujumla. Hii sio maana ya maneno hayo. Bali hata ingelikuwa maana ya maneno hayo ni hivyo mulivyodhani nyinyi, basi hii ingekuwa dhidi yenu kwani Hadithi iliosemwa kuwa ina ihtimal uwezekano huu na hule ni Hadithi "fungeni kwa kuuona".

MNASEMA

Mukhtasari Wa Nukta Muhimu i). Kwa kuwa masimulizi ya Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) na Kuraib yana utatanishi - hayaeleweki kwa maana moja; hayawezi kuchukuliwa kama ni hoja kama walivyoeleza hayo Wanavyuoni wa Usulil-Fiqhi na Mustalahul-Hadiyth.

JAWABU

Tumejibu tayari kwamba hakuna utatanishi: utatanishi munao nyinyi. Bali Hadithi "Fungeni kwa kuuona" ndio yenye utata. Munasema

ii). Kwa kuwa Ibnu 'Abbas (Radhiya Allaahu 'Anhu) ameonyesha kinyume na vile alivyopokea Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakiwezi tena kuchukuliwa kitendo chake kama ni hoja.

Jawabu Tumejibu kwa hoja za kielimu kwamba Ibn Abbaas hakwenda kinyume na alichokipokea kutoka kwa Mtume (s.a.w.) bali kilichopo ni Hadithi moja kuifasiri nyengine, kwani zote mbili - kwa mujibu wa fani - ni Hadithi za Mtume(s.a.w.w) .

Munasema iii). Katika Hadiyth iliyopokelewa habari ya kuonekanwa mwezi muandamo na bedui ambapo ingeyumkinika kuulizwa aliuona wapi mwezi muandamo lakini hakuulizwa.

JAWABU

Bedui anajulikana anapotokea. Ikrima - mwanafunzi wa Ibn Abbas - anaeleza kwamba bedui huyo alikuwa akitokea Al-harrah nayo ni sehemu yenye mawe mawe katika eneo la Madina. Na hata pasitajwe anapotokea, inajulikana kuwa anatoka katika jangwa la Madina kwani hakuna uwezekano katika zama hizo mtu kutoka Sham au Misr akafika Madina usiku wa muandamo au hata baada ya wiki nzima.

MNASEMA

Jambo hilo linapewa hukmu ya 'aam ujumla katika fani ya Usulil-Fiqhi. Wanavyuoni wamekuwa wakisema haya yafuatayo: "Hakika chenye kuzingatiwa baina ya njia aliyopita Sahaba (katika kutenda jambo fulani) na kile alichokipokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam); jambo la k ufaa kuzingatiwa katika hukmu ni kile alichokipokea (wala sio kile alichokitenda). Hata kama kitendo chake hicho kimepata umaarufu na kujulikana sana ." Hiyo ndio maana ya maneno ya Wanavyuoni wa Shari'ah yasemayo: "Chenye kuzingatiwa ni kile alichokipokea Sahaba kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala sio kile alichokitenda kutokana na riwaya hiyo."

JAWABU

a) Maneno yenu na dalili mulioitoa ya kiusuli ni vitu viwili tafauti, jambo ambalo linathibitisha kwamba hamujui munasema nini. "Munasema: Jambo hilo linapewa hukmu ya 'aam ujumla katika fani ya Usulil-Fiqhi. Wanavyuoni wamekuwa wakisema haya yafuatayo".: Kisha mukataja kanuni isemayo: "Kikigongana kitendo cha Sahaba na riwaya yake inatangulizwa riwaya yake". Kanuni ina zungumzia mgongano wa rai na riwaya; nyinyi munaitumia kwamba ni dalili ya ujumla!!!

b) Ama ikiwa munakusudia kwamba Ibn Abbaas kenda kinyume na riwaya yake, hili tumelijibu kwamba si kinyume kwani zote ni Hadithi za Mtume(s.a.w.w) .

c) Katika Hadithi ya bedui hakuna kitu ujumla kamwe, ila vile kuwa bedui hakuulizwa atokapo ndiko mulikokudhania nyinyi kuwa hukumu yake ni ya ujumla. Lakini yeye hakuulizwa kwa sababu unajulikana anapotoka. Nimekuulizeni kama mimi niko Bumbwini katika zama za ngamia na punda ukanijia baada ya isha ukaniambia "Mwezi umeonekana", bado nitahitaji kukuuliza ulipoonekana. Si itakuwa umeonekana miji hio hio ya Unguja?

MNASEMA

iv). Ameandika mwanachuoni mmoja anayeitwa Shaykh Aadaud bin Ibrahim bin Umar kitabu cha Kiibadhi cha Usulul-Fiqh kinachosomeshwa mashuleni. Katika J. 2 uk 15 ameandika yafuatayo:

10. Kisha akafupisha kuandika kwenye Khulasa: Tafsiri yake ni kama ifuatavyo:- Atakapoeleza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya hukmu ya jambo (fulani) na hukmu hiyo ikawa ina utata (yaani ina tafsiri zaidi ya moja) kisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa s allam) akanyamaza bila ya kutoa ufafanuzi mwengine wowote juu ya hukmu ya jambo hilo; itakuwa hukmu ya jambo hilo ni 'aam - yaani ni hukmu ya jambo lenye kuwajumuisha Waumini wote kwa pamoja, pamoja na kuwa jambo hilo lina utata.

JAWABU

Nimeshakufahamisheni nini maana ya kanuni hii. Hii inaeleza kitu ambacho kina uwezekano mwingi na hakijulikani: si kitu chenye kujulikana. Bedui alikuwa akijulikana atoka wapi, kwa hivyo, Mtume (s.a.w.) kutokumuuliza anapotoka haina maana kuwa masafa hayazingatiwi, kwani mtu anajulikana anapotoka. Pili: ni kuwa kilichomuhimu kukifahamu ni kwamba hio yenu ni istimbat; na la Ibn Abbaas ni andiko; na istimbat haina uwezo wa kubomoa andiko. Na kwa hivyo, wamesema katika kawaida za fiq-hi Hakuna kuizingatia dalili (isio wazi) mbele ya andiko lililowazi. Ubainifu wa hili ni kuwa Ibn Abbaas kasema kwa uwazi kwamba "Hivi ndivyo alivyotuamuru Mtume s.a.w." wakati katika hadithi ya bedui hakuna uwazi huu kwamba muandamo ni mmoja, bali hayo munayoyadai nyinyi ni kwa njia ya istimbat na istimbat yunu yote ni makosa kama tulivyobainisha.

11

MUANDAMO WA MWEZI

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

MTAZAMO WA MASAHABA (RADHIYA ALLAAHU 'ANHU) JUU YA KADHIA YA KUFUNGA NA KUFUNGUA MTAZAMO WA MASAHABA

MNASEMA

Mtazamo Wa Masahaba (Radhiya Allaahu 'Anhu) Juu Ya Kadhia Ya Kufunga Na Kufungua Ndugu Juma amekuwa na mtazamo wake juu ya yale aliyoyasema Shaykh Naaswir Bachuu kwamba kwa muda wa miaka 30 ya Makhalifa waongofu hapakupatikana utatanishi wowote juu ya suala la muandamo wa mwezi. Haikuthibiti kwamba Masahaba waliwahi kuzingatia suala la masafa au matlai katika suala la kuandama kwa mwezi.

Ndugu Juma anasema: (Kama ilivyokuwa hakuna ushahidi kwamba wao waliwaamrisha watu wasifate miandamo yao, pia hakuna ushahidi kwamba wao waliwakataza wasifate miandamo yao, au kwamba waliwaamrisha kufata muandamo wa Madina.) Kwa upande wetu tunasema hivi: Ni kweli kuna uwezekano kwamba Masahaba hawakuwaamrisha watu wasifuate miandamo yao au waliwakataza watu kufuata miandamo yao.

Bila shaka jambo hilo linawezekana sana, kwani Masahaba hawana mamlaka ya kuwaamrisha au kuwakataza watu kwani wao hawakuwa wakipata Wahyi. Mwenye mamlaka hayo ni mwenyewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii." Juu yao Masahaba ni kumsikiliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anavyowaamuru na kumuuliza pale panapotokea mushkeli wowote. Kwa mantiki hiyo tunapenda kusema kuwa hakuna Riwaya hata moja iliyo Sahihi inayoeleza kuwa labda Masahaba walimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa tufunge vipi au wenzetu walioko mbali nao wafunge vipi na wafungue namna gani. Hii ina maana kwamba Masahaba walimuelewa vyema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika maagizo yake hasa katika suala hili la kufunga walielewa vyema kuwa agizo hili ni la Waumini wote, mahala popote walipo.

JAWABU

Dai lenu kwamba: "Kwa mantiki hiyo tunapenda kusema kuwa hakuna Riwaya hata moja iliyo Sahihi inayoeleza kuwa labda Masahaba walimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa tufunge vipi au wenzetu walioko mbali nao wafunge vipi na wafungue namna gani. Hii ina maana kwamba Masahaba walimuelewa vyema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika maagizo yake hasa katika suala hili la kufunga walielewa vyema kuwa agizo hili ni la Waumini wote, mahala popote walipo". Hili si dai sahihi. Utaona kwamba tunakariri yayo kwa yao. Tunasema kwamba kutokuwepo kwa riwaya kwamba aliulizwa, hakumaanishi kuwa hakuulizwa, bali kuna maanisha kuwa hakuna riwaya hii wala hile. Kwa hivyo, huenda ikawa aliulizwa huenda ikawa hakuulizwa - hakuna ithbati. Lakini hali hii haina uwezo wa kuibomoa riwaya iliothibiti kwa sanad sahihi kwamba mafunzo yake ni kutokuuzingatia muandamo wa mbali. Nakukumbusheni tena kauli yenu muliposema: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) . Kwa hivyo, natija ni kuwa:

1) Hakuna riwaya kwamba Mtume(s.a.w.w) kaulizwa hivi wala vile. Kwa hivyo, hapa hakuna hoja.

2) Kuna Hadithi kwamba Mtume kafunza kutokuuchukua muandamo wa mbali.

MNASEMA

Riwaya itegemewayo juu ya suala hili linalo zingatiwa matlai ni masimulizi ya Kuraib tu. Tukio lililotokea zaidi ya miaka 30 baada ya kufa Bwana Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Pia Makhalifa wote wanne walikwisha ondoka Duniani. Masimulizi ambayo yana utata mkubwa na hayana ufafanuzi wa kina, hususan yanapopimwa katika mezani mbili - mizani ya Usulul Fiqhi na mezani ya Mustalahul- Hadiyth. Baada ya kupimwa vizuri uzito wake katika mezani zote mbili, inabainika kwamba hapana uzito unaostahili kuchukuliwa kama ni hoja sahihi za kutegemewa katika mdahalo huu wa muandamo wa mwezi.

JAWABU

Naona tunaendelea kukariri. Ni mezani gani au ni kanuni gani ya Usulul Fiqhi au ya Mustalahul- Hadiyth muliotumia kubatilisha riwaya ya Kuraib na Ibn Abbaas. Nakukumbusheni tena mulioyasema punde: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) . Riwaya ya Ibn Abbaas iko hivyo. Sasa ni elimu gani ya Hadithi mulioitumia? Na kanuni zote za kiusuli kama nilivyobainisha katika kitabu zinaifanya Hadithi ya Kuraib na Ibn Abbaas itangulizwe.

MNASEMA

Ama tukichukua maneno sahihi ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliyoyasema:"Fungeni kwa kuuona mwezi muandamo" katika mezani, tutaona kina cha uzito wa maneno haya ni kikubwa mno. Ndio maana tukasema kushikamana na man eno ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni bora na ndiyo hasa Sheri'ah inavyotuagiza kuliko kushika maneno yenye utata na yenye khitilafu.

JAWABU

Nakukumbusheni tena maneno yenu: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume(s.a.w.w) . Riwaya ya Ibn Abbaas iko hivyo, kwa hivyo nayo ni mafunzo ya Mtume(s.a.w.w) musiyatoe kwenye uzito.

MNASEMA

Kama tukijadili uwezekano wa utekelezaji wa agizo hilo la kufunga na kufungua katika zama ambazo mawasiliano yalikuwa duni na hafifu sana; tungejiuliza, Masahaba wangewezaje kupeana taarifa za kuandama kwa mwezi katika nchi za mbali? Wengewezaje kwa pamoja kuamka wakiwa wamefunga na hasa pakizingatiwa kuwa taarifa zenyewe zinatakiwa ziwafikie wengine kabla ya kupambazukiwa na alfajiri? Bila shaka jambo hilo lilikuwa ni gumu kiutekelazaji hata katika nchi moja pekee. Lakini ni vyema kuelewa kwamba hilo lilikuwa ni jambo la dharura kwa wakati huo.

JAWABU

1) Illa ya kufunga kwa miandamo tafauti ni kutafautina miadamo: si kupatikana kwa teknolojia mpya katika zama zetu na kukosekana kwake hapo zamani. Kama vile ambavyo illa ya kusali katika nyakati tafauti ni kuingia nyakati hizo tafauti kwa mtenguko na mzamo wa jua. Na sharia haibadiliki isipokuwa kitu kiwe kina illa (sababu) fulani iliojulikana katika andiko kwa njia ya tasrih (uwazi) au istimbat, kisha illa (sababu) hiyo iwe haipo tena. Hapo hukumu pia hubadilika. Kama walivyosema wanavyuoni sababu ikiondoka na hukumu huondoka. Sasa nyinyi wenzetu mumepata wapi kwamba kutofika habari ndio sababu ya kufunga kwa miandamo tafauti ili iwe sasa kwa kupatikana teknolojia mpya t ayari illa (sababu) hio imeondoka na sasa hukumu imebadilika?

2) Pili ni kuwa suala hilo nimelijibu kwamba Ibn Abbas alisema: "Hatuachi kufunga mpaka tukamilishe idadi ya siku thalathini au tuuone mwezi." Sasa kama aliukubali muandamo wa Sham, basi asingelisema maneno hayo, kwani kwa hali yoyote ile ikifika siku ya mwezi 29 ya muandamo wa Madina ni lazima watu wa Madina wale idi siku ya pili, ((halafu ikiwa itawathibitikia kwamba Sham mwezi uliandama tarehe thalathini wao watu wa Madina wailipe siku moja)) kwani siku hio ya mwezi 29 wa Madina ni lazima Sham itakuwa ni siku ya tarehe 30 au tarehe mosi. Ikiwa ni tarehe 30 itakuwa Sham wamefunga siku 30, wakati Madina wamefunga siku 29, na Ikiwa Sham ni tarehe mosi siku hio, basi watakuwa wamo ndani ya siku kuu - kwa hali zote mbili, kama Ibn Abbas aliukubali muandamo wa Sham, basi ni lazima watu wa Madina waishie kufunga tarehe 29. Lakini tunamkuta Ibn Abbas anasema "Hatuachi kufunga mpaka tutimize (siku) thalathini au tuuone mwezi." Kusema "Mpaka tutimize (siku) thalathini". Kama ni hivyo, basi utaona hapa kwamba habari ya muandamo wa mwezi ilikwishafika Madana. Suala je ilitendewa kazi? Kwa hivyo, kufika na kutokufika kwa habari si sababu ya kuwepo kwa miandamo tafauti hapo kale, bali sababu ni umbali na kutafautiana kwa matalai. Na lau ilikuwa sababu ni kutofika habari, basi habari ikifika ingetendewa kazi. Lakini hapa habari imefika wala haikutendewa kazi.

MNASEMA

Msisitizo wetu mkubwa ni kuwa katika masimulizi ya Kuraib hapakupatikana maafikiano ya Wanavyuoni kwa hivyo si jambo la kutegemewa. Kama wanavyosema Wanavyuoni wa 'Usulil-fiqhi.' "Dalili ikiwa na maana (nyingi) zaidi ya moja, huporomoka ushahidi wake."

Jawabu Ikiwa kutokuafikiana kwa wanavyuoni ni sababu ya kuachwa kwa andiko, basi itatubidi tuiache Qur-ani yote ila Aya chache kwani Aya zote taqriban wametafautina kuzifasiri. Bismillahi itabidi tuitoe kwenye misahafu kwani wako wanaosema kuwa si Aya kabisa kama vile watu wa Mailk. Bali kwa mantiki hio pia tuiwache Hadithi "Fungeni kwa kuuona musifunge mpaka muuone.." kwani wanavyuoni pia hawakukubaliana juu ya maana yake. Anasema Ibn Hajar (Na wale ambao hawakuchukua kauli hio, wanasema kwa sababu kauli yake Mtume(s.a.w.w) aliposema) "Mpaka muuone" ni agizo kwa watu maalumu." Anasema Al-san'ani: "Na ikasemwa kwamba (Muandamo wa mbali) hauzingatiwi (mbali), kwa sababu kauli yake (Mtume(s.a.w.w) aliposema:"Mukiuona" ni agizo kwa watu maalumu."

Ama kanuni isemayo: "Dalili ikiwa na maana (nyingi) zaidi y a moja, huporomoka ushahidi wake" haihusiani na hapa. Nyinyi hiki kitabu chenu baada ya kukiandika hamukuwapitishia watu wa fani wakakichungulia?! Kanuni hio haina maana kuwa wanachuoni wakitafautiana basi dalili huporomoka. Basi tusisali sala ya safari, maana wametafautina masafa ya safari: wengine kilomita 12; wengine masafa ya siku 3 nk. Na pia muda wa siku ngapi sala ya safari inakwisha: zote hizi ni tafauti, kwa hivyo Waislamu wasisali sala ya safari!!! Maana ya kanuni hio ni kuwa dalili yenyewe (Aya au Hadithi) ikiwa ina uwezekano huu na ule wala hakuna Qarina yenye kuipa uzito maana moja, basi huwa huwezi kutoa ushahidi kwayo ukasema kuwa maana hii ndio ilikusudiwa madamu huna ushahdi.

MNASEMA

Ikumbukwe kuwa Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni (aula) bora kwa hali yoyote iwayo. Kinachotakiwa ni kuifuata sio kuibeza. Shaykh Al-Qanubiy wa Kiibadhi anasema katika kitabu chake kuwa: "Itakapogongana amri ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na amri nyengine yoyote, basi amri ya agizo la Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni (aula) bora zaidi kutangulizwa (mbele) na ku fuatwa." Shaykh Ahmed Al-Khaliil (Mufti Mkuu wa Omani) naye amesema: "Hakuna kuzingatiwa kauli itakayopingana na Hadiyth sahihi, kwani Sunnah ni hoja juu ya jambo la Kid ini, wala jambo jengine lolote haliwezi kuwa ni hoja dhidi ya Sunnah."

103) Anachokieleza Shaykh Ahmed Al-Khaliil ni kuwa: "Lazima marejeo y a asili (katika misingi ya Kidini) ni kila kilichoelezwa kwa (saraha) uwazi katika Qur-aan Tukufu na kilichoelezwa katika Sunnah Sahihi. "Walikuwa wanavyuoni wema wakionyesha kukereka kwao na hasira zao juu ya yule mtu ambaye anaipuuza (anaibeza) Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa (kuifuata) rai (ya mwanachuoni) au Qiyaas au mapende kezo ya Wanavyuoni au kauli ya mtu yeyote kwa kuipuuza Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)" Katika maudhui yetu hayo ya muandamo wa mwezi, katika kadhia ya kufunga na kufungua kwa kuonekana mwezi, ni vyema kuachana na vitu vyenye utata na kusisitiza kushikamana na maneno katika Hadiyth Sahihi ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo:"Fungeni kwa kuonekana mwezi -muandamo"

Jawabu Munahimiza kufata Hadithi ya Mtume (s.a.w.) kama wanavyohimiza wanavyuoni hao. Hilo hatutafautiani. Lakini tunasema kwamba riwaya zote mbili "Fungeni kwa kuuona" na "Hvi ndivyo alivyotuamu Mtume s.a.w." ni Hadithi. Nakukumbusheni maneno yenu: "Isipokuwa Sahaba akisema: "Tumeamrishwa kadha" au "Tumekatazwa kadha." Jambo hilo hupewa hukumu ya "Rafii" yaani hio inazingatiwa kuwa ni Hadithi ya Mtume (s.a.w.). Kwa hivyo, kinachotakiwa ni kuzijumuisha Hadithi hizo na kuzitazama zina maana gani: sio kuitendea kazi moja na kuiwacha moja: kuitendea kazi moja na kuiwacha moja ni kinyume na Al-Minhaj Al-Sahih (methodology) sahihi.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ تَفَرَّقُوا وَاخْتَلَفُوا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ وَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾

105.Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi; na hao ndio wenye adhabu kubwa.

﴿يَوْمَ تَبْيَضُّ وُجُوهٌ وَتَسْوَدُّ وُجُوهٌ فَأَمَّا الَّذِينَ اسْوَدَّتْ وُجُوهُهُمْ أَكَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴾

106.Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika. Na ama ambao nyuso zao zitasawijika, (wataambiwa): Je mlikufuru baada ya kuamini kwenu? Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha.

﴿وَأَمَّا الَّذِينَ ابْيَضَّتْ وُجُوهُهُمْ فَفِي رَحْمَةِ اللَّـهِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

107.Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, Wao humo watadumu.

﴿تِلْكَ آيَاتُ اللَّـهِ نَتْلُوهَا عَلَيْكَ بِالْحَقِّ وَمَا اللَّـهُ يُرِيدُ ظُلْمًا لِّلْعَالَمِينَ ﴾

108.Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki; na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe.

﴿وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴾

109.Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni; na kwa Mwenyezi Mungu hurejezwa mambo yote.

KUHITALIFIANA BAADA YA MTUME

Aya 105 - 109

MAANA

Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi.

Aya hii inamalizia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote" Makusudio ya wale waliofarakana ni watu wa Kitabu, Ambapo mayahudi walichangukana vikundi sabini na moja baada ya Mtume wao Musa, wakristo wakawa vikundi sabini na mbili baada ya Mtume wao Isa, Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu."Baada ya kuwajia hoja iliyo wazi" inafahamisha kwamba mtu haadhibiwi kwa kuiacha haki na kufuata batili, ila baada ya kubainishiwa hoja. Ama siri ya mkazo huu na kuupa kipaumbele muungano wa umma, ni kuwa utengano ndio kiini cha ufisadi na kwamba umma uliotengana hauwezi kuwa na maisha mazuri, wachilia mbali kuuita umma mwingine kwenye kheri. Pamoja na kuwapo Riwaya nyingi, na Hadith zinazohimiza muungano wa waislamu, lakini bado wamefarakana na kuwa vikundi mbali mbali, wamewazidi mayahudi kwa vikundi viwili zaidi na wakristo kikundi kimoja; kama ilivyoelezwa katika Hadith mashuhuri.

Kuna Hadithi nyingine isemayo: "Mtakuwa na desturi ile ile ya waliokuwa nayo kabla yenu." Akaulizwa: "Unakusudia mayahudi na manaswara ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Akasema: "Kumbe ninawakusudia kina nani? Utachanguka uthabiti wa waislamu" Katika kitabu Al-Jam'u Bainas-Sahihayni cha Hamid, kwenye Hadith Na. 131, anasema: Katika yaliyoafikianwa kutoka Musnad ya Anas bin Malik, amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) :"Watanijia watu miongoni mwa sahaba zangu kwenye hodhi, nitakapowaona na watakapokuwa wanaletwa kwangu watazuiwa ili wasinifikie. Hapo nitasema: 'Ewe Mola! Sahaba zangu, sahaba zangu! Nami nitaambiwa: 'Wewe hujui walizua nini baada yako" Katika kitabu hicho hicho Hadith Na. 267 anasema: "Katika yaliyaofikianwa kutoka Musnad ya Abu Huraira kutoka katika njia mbali mbali, ni kwamba Mtume amesema: "Wakati nikiwa nimesimama - siku ya Kiyama - litatokea kundi la watu mpaka nitakapowatambua, atatokea mtu baina yangu na yao na awambie: 'Haya twendeni.' Mimi nitauliza: Mpaka wapi? Naye aseme: 'Mpaka motoni' Nami niulize wana nini? Naye ajibu: 'Hakika wao walirtadi baada yako"

Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika.

Makusudio ya Siku, ni Siku ya Kiyama. Kung'aa uso, ni fumbo la kuonyesha furaha ya mumin kufurahia radhi za Mwenyezi Mungu na fadhila Zake. Kusawijika uso ni huzuni ya kafiri na fasiki kwa ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na ama ambao nyuso zao zitasawijika,(wataambiwa), je, mlikufuru baada ya kuamini kwenu?

Arrazi, Tabari na wafasiri wengine wengi wamenukuu kutoka kwa baadhi ya waliopita, kwamba makusudio ya watakaoambiwa hivyo ni Khawariji. Kwa sababu Mtume alisema kuwahusu:"Hakika wao watachomoka kutoka katika dini, kama unavyochomoka mshale kutoka katika uta (upinde)." Lakini dhahiri ya Aya inamkusanya kila mwenye kukufuru baada ya imani, wakiwemo Khawariji, watu wa bid'a na wenye maoni potofu. Kwa vile adhabu haihusiki tu na aliyekufuru baada ya imani bali inamuhusu kafiri yeyote, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Onjeni adhabu, kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha, Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, wao humo watadumu.

Rehma ya Mwenyezi Mungu ni Pepo. Kwa ufupi ni kwamba wale ambao wameshikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, na kufanya mambo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wakasaidiana kwenye mambo ya kheri na ya masilahi ya umma, basi watafufuliwa kesho wakiwa watukufu, wenye furaha na wenye kuridhia. Ama wale ambao wamehitalifiana kwa kuipupia dunia, wasiojishughulisha na dini wala umma au nchi, na ambao hawajishughulishi na lolote isipokuwa masilahi yao na ya watoto wao tu, basi wao watafufuliwa Siku ya Kiyama wakiwa madhalili, wenye hasara na makazi yao ni Jahanam, nayo ni marejeo mabaya kabisa. Ajabu ya maajabu ni kwamba baadhi ya wenye nyuso zilizosawijika wanadai kuwa wanamzungumzia Mungu na kutumia Jina lake, lakini mtu akiwaambia "Muogopeni Mungu" wao husema: "Umemkufuru Mwenyezi Mungu." Aliyewatangulia katika hilo ni Abdul Malik bin Marwan aliposema pale alipochukua Ukhalifa: "Kuanzia leo atakayeniambia muogope Mwenyezi Mungu nitamkata kichwa chake."

Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki.

Hizi, ni ishara ya Aya zinazoelekezea kuneemeshwa watu wema na kuadhibiwa makafiri. Msemo unamwelekea Muhammad(s.a.w.w) , muulizaji anaweza kuuliza: "Kuna faida gani katika habari hii, ikiwa Muhammad anajua kwa yakini kwamba Aya hizi ni haki na ni kweli?" Jibu: Ni kawaida ya Qur'an kulikariri hilo katika Aya kadhaa. Na makusudio sio kwa Muhammad hasa, bali ni kwa yule anayetia shaka na kudhani kwamba Aya hizi na mfano wake zinatoka kwa Muhammad, si kwa Mwenyezi Mungu.

﴿وَمَا كُنتَ تَتْلُو مِن قَبْلِهِ مِن كِتَابٍ وَلَا تَخُطُّهُ بِيَمِينِكَ إِذًا لَّارْتَابَ الْمُبْطِلُونَ﴾

"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wabatilifu" (29:48)

Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe, Kwa sababu dhuluma ni mbaya na Mwenyezi Mungu ameepukana nayo.

Aya hii ni dalili ya mkato kwamba Mwenyezi Mungu hakalifishi mja asiloliweza.

﴿كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَلَوْ آمَنَ أَهْلُ الْكِتَابِ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُم مِّنْهُمُ الْمُؤْمِنُونَ وَأَكْثَرُهُمُ الْفَاسِقُونَ﴾

110.Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu. Na lau watu wa Kitabu wangeliamini ingekuwa heri kwao. Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki .

﴿لَن يَضُرُّوكُمْ إِلَّا أَذًى وَإِن يُقَاتِلُوكُمْ يُوَلُّوكُمُ الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ ﴾

111.Hawatawadhuru isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia, kisha hawatasaidiwa.

UMMA WA MUHAMMAD

Aya 110 - 111

MAANA

Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu

Kuna njia kadhaa kuhusu Aya hii, kama ifuatavyo:

1) Katika makusudio ya umma, hakuna mwenye shaka kuwa makusudio ya umma hapa ni Umma wa Muhammad(s.a.w.w) , kwa dalili ya mfumo wenyewe wa maneno ulivyo na mtiririko wa misemo inayoelekezwa kwa waumini; kama vile; "Enyi ambao mmeamini mcheni Mwenyezi Mungu. Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu kwenu…" Mpaka kufikia kauli yake Mwenyezi Mungu:"Mmekuwa ni umma bora."

2). Je, makusudio ni waislamu wote katika wakati wote, au ni kuwahusu wale walio kuwa katika siku za kwanza za uislamu kama vile Masahaba na waliofuatia (tabiina)?

Jibu : Kuainisha makusudio ya umma hapa, kunahitaji kujua makusudio ya herufi kana (kuwa) ambayo ilivyo ni kuwa inahitaji isimu na habari yake. Pia hiyo kana inafahamisha kufanyika kitendo wakati uliopita, lakini haielezi ni wakati gani kimefanyika hicho kitendo wala kuwa kinaendelea au la.

Isipokuwa hilo linaweza kufahamika kutokana na vitu vingine vilivyo pamoja nayo kimaneno au hali ilivyo. Kwa mfano kusema, Zaid alikuwa ni mwenye kusimama. Hapo inachukuliwa kutendeka tendo la kusimama na kuisha bila kuendelea. Yaani Zaid, hakuwa ni mwenye kusimama, basi akasimama kipindi fulani bila ya kuendelea kusimama maisha. Lililofahamisha hilo ni neno mwenye kusimama, yaani hawezi kusimama maisha. Lakini kama tukisema Mwenyezi Mungu amekuwa ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu, hapo hali inafahamisha kudumu kwa tendo lenyewe, kwa sababu rehema na maghufira haviepukani na dhati yake Mwenyezi Mungu, na dhati yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ni ya milele na milele. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufungamanisha ubora wa umma na kumwamini kwake, na kuamrisha mema na kukataza maovu, basi maana ya Aya yanakuwa ni: Enyi waislamu! Msiseme tu sisi ni umma bora mpaka muamrishe na kukataza maovu; na kwamba sifa hii ya ubora itawaondokea mara tu mnapopuuza hilo.

Kwa hivyo basi kana hapa inakuwa ni kamilifu, sio pungufu; yaani haihitaji khabar. Kwa maana hayo makusudio ni waislamu wote([2] ) .

3).Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu 'mliotolewa kwa Watu' inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemleta Muhammad na umma wake(s.a.w.w) ushinde umma zote za mwanzo ukiwa umechukua Kitabu cha Mwenyezi Mungu mkono mmoja na Hadith za Mtume kwenye mkono mwingine, huku ukiwalingania vizazi vishikamane na vitu viwili hivyo na kuvitegemea kwa itikadi, sharia na maadili. Kwa sababu ndio marejeo pekee yanayoweza kuhakikisha ufanisi wa mambo yote, kudhamini maisha ya kila mtu na kufungua uwanja wa wenye uwezo wa kufanya ijitihadi kwa misingi ya usawa, amani na uhuru wa watu wote([3] ) .

Aya hii katika madhumuni yake inaafikiana na Aya isemayo:

﴿وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُمَّةً وَسَطًا لِّتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ وَيَكُونَ الرَّسُولُ عَلَيْكُمْ شَهِيدًا﴾

"Tumewafanya ni umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu na Mtume awe shahidi juu yenu." (2:143)

Ikiwa waislamu hawatafanya harakati zozote za kulingania kwenye kheri au kuamrisha mema na kukataza mabaya, basi sifa za uongozi zitawaondokea na watakuwa na haja ya kiongozi atakayewaamrisha mema na kuwakataza maovu. Ulikuwepo wakati ambapo waislamu walikuwa na harakati hizi. Wakati huo walikuwa wakistahili kuwa viongozi wa umma zingine; kisha wakapuuza; wakaendelea hivyo mpaka wakawa wanakataza mema na kuamrisha maovu; kama tuonavyo sasa. Leo vijana wamekuwa wanajivua kabisa na dini na hulka njema. Wakimwona mtu anaswali au kufunga husema kwa dharau: "Bado kuna Swala na Saumu katika karne ya ishirini?" Mwenye Tafsir Al-Manar, katika kufasiri Aya hii, anasema: "Kwa kweli hasa ninasema, haukuzimika ubora wa umma uliotolewa kwa watu, mpaka pale ulipoacha kuamrisha mema na kukataza mabaya. Na haukuacha hivyo kwa kupenda au kupuuza amri ya Mwenyezi Mungu, bali ni kwa kulazimishwa na ufedhuli wa Wafalme wa bani Umayya na waliofuata nyayo zao."

Kwa msingi vitu hutajwa kwa kinyume chake; kama ambavyo hutajwa kwa kifani chake, basi tutaleta Hadith tukufu aliyoitaja Hafidh Muhibbudin Attabari, amesema: "Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) 'Mfano wa Ahlu bait wangu, ni kama safina ya Nuh mwenye kuipanda ataokoka, na mwenye kushikamana nayo ataokoka, na mwenye kuachana nayo ataghariki'". Ama Hadith ya "Mimi nawaachia vizito viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kizazi changu - Ahlul bait wangu," imepokewa na wapokezi 35 katika Masahaba.

Na lau wangeliamini watu wa Kitabu, ingelikuwa heri kwao.

Yaani lau watu waliopewa Tawrat na Injil, wangelimwamini Muhammad(s.a.w.w) ingelikuwa imani yao hiyo ni heri yao katika muda wa sasa na ujao.

Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki.

Yaani katika watu wa Kitabu kuna waliomwamini Muhammad(s.a.w.w) ; kama vile Abdullah bin Salam na watu wake, na wengineo katika wanaswara, na wengi wao walibaki katika ukafiri.

Neno Fasiq na Kafir yanapokezana maana, hutumiwa Fasiq kwa maana ya Kafiri na Kafir kwa maana ya Fasiq. Na Fasiq hapa ina maana ya kafiri. Hawatawadhuru, isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia Madhara yako aina mbili:

Kwanza : ni kiasi cha huzuni na kusikia uchungu tu, ambako kadiri siku zinavyokwenda nayo yanafutika; kama vile inavyotokea katika nafsi kwa kusikia habari mbaya.

Pili : ni yale yanayogusa maisha na kuyumbisha; kama vile madhara yaletwayo na dola ya Israil ndani ya nchi ya Waarabu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewabashiria maswahaba wa Mtume(s.a.w.w) kwamba watu wa Kitabu:

Hawatawadhuru isipokuwa kwa maneno tu, kama vile uzushi na mabezo. Ama katika uwanja wa vita, nyinyi ndio washindi.

Amesema kweli Mwenyezi Mungu katika kiaga chake, Aliwapa ushindi waislamu wa mwanzo kwa wakristo na wengineo.

﴿ضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ أَيْنَ مَا ثُقِفُوا إِلَّا بِحَبْلٍ مِّنَ اللَّـهِ وَحَبْلٍ مِّنَ النَّاسِ وَبَاءُوا بِغَضَبٍ مِّنَ اللَّـهِ وَضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الْمَسْكَنَةُ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَانُوا يَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَيَقْتُلُونَ الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ﴾

112.Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana, isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki, hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

WAMEPIGWA CHAPA YA UDHALILI

Aya 112

MAANA

Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili.

Wafasiri wameafikiana kuwa, Aya hii imeshuka kwa ajili ya mayahudi; kama ambavyo wameafikiana kuwa makusudio yake ni kuwa Mwenyezi Mungu amewanyima utukufu na takrima, na akawaandikia udhalili tangu ulipoanza uislamu hadi siku ya mwisho. Kwa sababu wao katika ufisadi na kupetuka mipaka wamefikilia hatua ambayo hakuifikia na hataifikia yeyote. Baada ya wafasiri kuafikiana juu ya hilo, wametofautiana kuhusu aina ya udhalili na unyonge walio nao (Mayahudi ambayo iko kwa kila kizazi). Tofauti hiyo hasa inatokana na tofauti ya hali ya mayahudi wakati wa kufasiri, ambapo walikuwa wakitoa kodi kwa waislamu, yaani kauli ya mfasiri imekuja kuakisi na walivyokuwa wayahudi. Hiyo si ajabu maadam mtu anaathirikia kwa anachokisikia na kukiona, Na tafsiri yangu ya Aya hii inafuata desturi hii.

Vyovyote iwavyo, ninavyofahamu ni kwamba udhalili wa mayahudi uliokusudiwa na Aya ni huku kutawanyika kwao duniani, Mashariki na Magharibi, wakiwa wako kwenye nchi mbali mbali. Wao daima ni wafuasi na wala sio wanaofuatwa na kuhukumiwa katika dola yao. Wako peke yao katika mambo yao. Ama Israeli iliyoko Tel Aviv ni Dola ya jina tu, ilivyo hasa ni kambi tu ya kikoloni na ni kituo cha jeshi cha uchokozi. Hakika hii imedhihiri wazi wazi baada uchokozi wa Israel katika ardhi za Waarabu mnamo tarehe 5 Juni 1967. Ni uchokozi ambao wanaufanya waisrail ili kutekeleza mahitaji yao. Lau watauacha siku moja tu watanyang'anywa na waarabu.

Huo ndio udhalili hasa, kwa sababu mwenye heshima zake hutegemea nguvu zake mwenyewe na kujihami kwa mikono yake sio mikono ya wengine. Kwa hali hii, inatubainikia kuwa makusudio ya kamba ya watu, ni msaada wa kihali na mali utolewao na mataifa ya kikoloni kwa ajili ya kambi ya kikoloni ya Israel. Kwa hivyo basi tunaamini bila ya tashwish yoyote kwamba Dola ya Israil itaondoka tu kwa kuondoka ukoloni. Na ukoloni uko njiani kuisha iwe ni sasa au baadae. Wala maneno hayo sio ndoto, isipokuwa ni natija hasa itakayotokea, kama ilivyoeleza Hadith ya Mtume:"Hakitasimama Kiyama mpaka muwapige vita mayahudi na kwamba jiwe litasema: Ewe Mwislamu! Huyu hapa Yahudi nyuma yangu muue"([4] )

Ama Kamba ya Mwenyezi Mungu ni fumbo la matakwa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: yaani kwamba mayahudi wataendelea kuwa na udhalili mpaka atakapotaka Mwenyezi Mungu: ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu pia isemayo:

﴿قَالَ النَّارُ مَثْوَاكُمْ خَالِدِينَ فِيهَا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ﴾

"Moto ndio makazi yenu mtadumu humo milele ila apende Mwenyezi Mungu" (6:128)

Kisha baada ya hapo, Mwenyezi Mungu amebainisha sababu iliyowajibisha udhalili wao na ghadhabu yake kwao, kwa kusema:

Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki; hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Sura ya Baqara Aya 61.

Unaweza kuuliza : Kuna wasiokuwa Mayahudi katika mataifa mengine waliokanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua watu wema, kuasi na kupetuka mipaka; pamoja na hayo Mwenyezi Mungu hakuwapiga chapa ya udhalili na uduni. Je,kuna siri gani katika kuwahusisha Mayahudi?

Jibu : Mtu anaweza kupetuka mpaka kwa msukumo fulani unaotokana na masilahi yake na manufaa yake. Ama kupetuka mpaka si kwa lolote isipokuwa kwa kupendelea tu kufanya dhambi, hakujatokea kwa yeyote isipokuwa mayahudi tu, na pupa hii ya kupenda dhuluma na uovu iko ndani ya dini ya mayahudi. Wao wanaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu yuko na wao tu, sio wengineo; bali pia yuko dhidi ya maadui zao; na kwamba watu wote wameumbwa kwa ajili yao tu ili wawafanye vile watakavyo, sawa na mtu amfanyiavyo mnyama. Jambo linalofahamisha zaidi sera yao hiyo, zamani na sasa, ni fedheha yao katika Palestina, hasa waliyo yafanya huko Dayr Yasin, kuwachinja wanawake na watoto.

Mwanzo walikuwa wakiwaua Mitume wakati dunia ilipokuwa na Mitume. Ama leo, ambapo hakuna Mitume wanawaua wasuluhishaji; kama vile Bernadotte([5] ) , na wanawake na watoto. Kwa sababu, la muhimu katika itikadi yao na maumbile yao ni kuwaua watu wasiokuwa na hatia; wawe Mitume au wasuluhishi au watoto.

Tawrat yao imeandika uhalali wa kumwaga damu ya wanawake na watoto, na imelihimiza hilo. Kwa ujumla ni kwamba kuzikanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua wasuluhishi na watu wema wasio na hatia, na kufanya dhuluma na uchokozi, yote hayo ni dini na itikadi ya Mayahudi. Myahudi akimfanyia kosa mwengine asiyekuwa Myahudi basi anafanya kwa kujiburudisha tu, sio kwa haja fulani. Na kama akiacha kufanya hivyo, basi anaacha kwa kuogopa sio kwa kujistahi.

Hii ndiyo tofauti kati ya mayahudi na wasiokuwa mayahudi. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa Mwenyezi Mungu kuwawekea udhalili popote walipo.

Ama serikali habithi ya Israel ya sasa itaondoka tu, hakuna budi, Ushahidi mkubwa wa kwisha kwake ni kwamba imefungamana na ukoloni, ukoloni ukiondoka nayo inaondoka. Na ukoloni lazima uondoke tu, hata kama ni baada ya miaka. Maadam maumbile ya kibinadamu yanaukataa ukoloni na kuupinga kwa damu yake, basi utaondoka tu.

Yote haya tuliyoayataja yanakamilisha kifungu cha 'Mayahudi hawana mfano' katika tafsiri ya Sura Baqara (2) Aya63 na 66.

﴿لَيْسُوا سَوَاءً مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ﴾

113.Wote si sawa Katika watu wa Kitabu wamo walio na msimamo, wakasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku huku wakinyenyekea.

﴿يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَأُولَـٰئِكَ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴾

114. Wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wanaamrisha mema na wanakataza mabaya na wanaharakia mambo mema na hao ndio miongoni mwa watu wema.

﴿وَمَا يَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَلَن يُكْفَرُوهُ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ ﴾

115.Heri yoyote watakayoifayahaitakataliwa, Na Mwenyezi Mungu anawajua wamchao.

WOTE SI SAWA

Aya 113 -115

LUGHA

Mwenye Majmaul-bayan anasema: Tofauti kati ya neno Sura na Ajala ni kwamba Sura ni kufanya haraka linalojuzu kufanywa, Nako kunasifiwa. Na Ajala ni kufanya haraka jambo lisilofaa kufanywa, nako kunashutumiwa.

MAANA

Aya hizi tatu ziko wazi hazihitaji tafsir, Maana yake kwa ujumla ni kwamba watu wa Kitabu hawako sawa kwamba wote wamepotea, bali wako watu wema miongoni mwao. Wafasiri wengi wamechukulia sifa hii kwa aliyesilimu miongoni mwa watu wa Kitabu, na uzuri wa uislamu wake kimatendo na kiitikadi.

HUKUMU YA MWENYE KUACHA UISLAMU

Mwito wa kumwamini Muhammad kama Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa watu wa ulimwenguni bado upo mpaka Siku ya Mwisho. Nao unaelekezwa kwa watu wote, wa Mashariki na Magharibi. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا ﴾

"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote" (7:158).

Dalili ya ukweli wake ni mantiki ya kiakili, kuthibiti muujiza na kufaa dini kwa maisha. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema: "Msingi wa dini yangu ni akili" Na Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake Kitukufu:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ﴾

"Enyi ambao mmeamini muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume (wake) anapowaitia katika yale yatakayowapa maisha (8:24)

Lengo letu sio kutoa dalili za Utume wa Muhammad(s.a.w.w), ([6] ) isipokuwa lengo ni kubainisha kuwa je, asiyeamini Utume wa Muhammad anastahili adhabu: au hapana budi ya ufafanuzi? Kabla ya kumtofautisha mjuzi na asiye mjuzi na asiyemudu na mzembe, tutaonyesha msingi na vipimo vya kwanza vya kustahili adhabu au kutostahili; kutokana na hivyo, uhakika utafumbuka na kuwapambanua watu. Wote wameafikiana kwamba mtu, vyovyote awavyo, dini yoyote aliyo nayo, hastahili adhabu ila baada ya kusimamishiwa hoja. Na hoja haisimami ila baada ya kuweza yeye kufikia kwenye dalili ya haki na kuweza kwake kuitumia. Hapo akiacha hatakuwa na kisingizio. Ikiwa hakupata dalili ya haki yenye msingi au aliipata akashindwa kuifikia au aliifikia na akatekeleza mtazamo wake wa haki mpaka akafikia mwisho, lakini pamoja na hayo haki haikumdhihirikia, basi yeye atakuwa na udhuru, kwa sababu ya kutokamilika hoja juu yake. Kwa sababu, asiyethibitikiwa na haki haadhibiwi kwa kuiacha, ila ikiwa amezembea katika utafiti.

Vile vile miongoni mwa kawaida za msingi ambazo zinaambatana na utafiti huu ni ile ya "Adhabu kuepukwa na mambo yenye kutatiza." Kwa hiyo haijuzu kumhukumu mwenye kuiacha haki kuwa ni mwenye makosa anayestahili adhabu, maadamu tunaona kuwa kuna uwezekano kuwa anao udhuru katika kuacha kwake. Na kawaida hii inafungamana na watu wote, sio waislamu tu, Pia inakusanya aina zote za mipaka, Mfano kawaida ya 'Mwenye kukosea katika ijtihadi, basi kosa lake linasamehewa', Kawaida hii ni ya kiakili, haiwezekani kuihusisha na dini fulani tu, madhehebu, shina au tawi. Baada ya maelezo hayo hebu tuangalie hali hizi zifuatazo:

1) Kuishi binadamu mji ulio mbali na uislamu na waislamu; wala hakufikiliwa na mwito au hata kusikia jina la Muhammad(s.a.w.w) katika maisha yake yote. Pia awe hajawaza kwa karibu au mbali kwamba duniani kuna dini yenye jina la kiislamu na Mtume aitwaye Muhammad(s.a.w.w) . Hapana mwenye shaka kwamba huyu atasamehewa kwa kuwa hastahili adhabu. Maana akili ina hukumu ubaya wa adhabu bila ya ubainifu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na sisi si wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mitume" (17:15) Bila shaka akili ni Mtume wa ndani kwa ndani, ila tu yenyewe ni dalili ya kupatikana Mwenyezi Mungu tu. Ama dalili ya kuthibiti Utume wa Mtume, hapana budi kuwako na muujiza na udhihirishwe na yeye mwenyewe pamoja na akili kuhukumu kutowezekana kudhihiri kwa wasiokuwa Mitume.

2) Kuusikia mtu uislamu na Muhammad, lakini akawa hawezi kupambanua haki na batili, kwa sababu ya kushindwa kwake na kutoweza kufahamu dalili za haki na maarifa yake. Huyu pia anasamehewa, Kwa sababu yeye ni sawa na mtoto au mwenda wazimu. Mfano ni akitomwamini Muhammad(s.a.w.w) tangu udogo kwa kuwafuata wazazi wake na akajisahau alipokuwa mkubwa, akaendelea na itikadi yake bila ya kuitilia shaka yoyote, huyu atasamehewa. Kwa sababu kumkalifisha aliyejisahau asiye na uwezo ni sawa na kumkalifisha aliyelala. Amesema Muhaqqiq Al-Qummi: "Kujikomboa kutokana na kuiga wazazi ni jambo lisilofikiriwa na wengi, bali hata linakuwa zito aghlabu kwa wanavyuoni waliotosheka ambao wanadhani kuwa wamejivua kutokana na kuiga huko." Amesema tena: "Asiyeweza kung'amua wajibu wa kujua misingi, ni sawa na mnyama na mwedawazimu ambao hawana taklifa yoyote." Sheikh Tusi anasema: "Mwenye kushindwa kupata uthibitisho yuko katika daraja ya mnyama."

Hata hivyo, ikiwa aliyejisahau atakumbushwa wajibu wa maarifa, au kuambiwa na mtu: "Wewe uko au hauko sawa katika itikadi yako", lakini pamoja na hayo akang'ang'ania na wala asifanye utafiti na kuuliza, basi huyo atakuwa ni mwenye dhambi, kwa sababu atakuwa ni mzembe, na kutojua kwa mzembe si kisingizio.

3) Kutomwamini Muhammad(s.a.w.w) pamoja na kuwa anao uwezo wa kutosha wa kufahamu haki, lakini yeye alipuuza wala asijali kabisa: au alifanya utafiti pungufu na akauacha bila ya kuangalia mwisho wake; kama wafanyavyo wengi, hasa vijana wa kisasa. Basi huyu hatasameheka kwa sababu amekosea bila ya kujitahidi na alikuwa na uwezo wa kujua haki, lakini akapuuza. Ni wazi kuwa pia ataadhibiwa ambaye amefanya utafiti na akakinai, lakini pamoja na hayo akakataa kumwamini Muhammad(s.a.w.w) kwa ubaguzi na mali.

4).Kuangalia dalili na kuwa na mwelekeo wa kufuata haki kwa ikhlasi, lakini pamoja na hayo akakosa kuelekea kwenye njia ambayo itamwajibishia kumwamini Muhammad(s.a.w.w) ama kwa kushikamana kwake na mambo yenye kutatiza ya ubatilifu bila ya kuangalia ubatilifu wake, au kuchanganyikiwa na mengineyo ambayo yanazuia kuona haki. Huyu ataangaliwa hali yake, ikiwa atakanusha Utume wa Muhammad(s.a.w.w) kwa kauli ya mkato, basi yeye ataadhibiwa na kustahili adhabu. Kwa sababu yule ambaye imefichika kwake haki, haifai kwake kukataa moja kwa moja kukanusha haki. Inawezekana kuwa haki ipo lakini akazuiliwa, kuifika, na aghlabu huwa hivyo, kwa sababu mambo ya ulimwenguni yapo lakini tuyajuayo ni machache tu. Hali ni hivyo hivyo kuhusu kuwajua Mitume na wasuluhishi, Ni nani awezaye kujua kila kitu?

Watu wa mantiki wamelielezea hilo kwa ibara mbali mbali, miongoni mwazo ni: Kutokujua hakumaanishi kutokuwepo, kutopatikana hakumaanishi kuacha kupatikana, kuthibitisha na kukanusha kunahitaji dalili. Tumewaona wanavyuoni wengi wakiungana na hakika hii. Wanazituhumu rai zao na kujichunga katika kauli zao; wala hawajifanyi kuwa wao ndio kipimo cha ukweli. Hawawezi kusema: "Rai hii ni takatifu isiyo na shaka, na nyinginezo si chochote." Bali wao huipa mtazamo wa kujiuliza kila rai. Dalili kubwa zaidi ya kuwa mtu hana elimu, ni kule kujidanganya mwenyewe, kuiona safi elimu yake, na kudharau rai na itikadi za wengine.

Zaidi ya hayo kuacha kukinai mtu mmoja miongoni mwa watu kuhusu Utume wa Muhammad(s.a.w.w) hakumruhusu kukanusha Utume wa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) moja kwa moja. Na kama akifanya hivyo, basi atakuwa na jukumu. Hasa baada ya kuona idadi ya mabingwa ambao hawakuathiriwa na kurithi au mazingira, wakimwamini Muhammad na risala yake; si kwa lolote isipokuwa kuiheshimu haki na kuikubali hali halisi ilivyo([7] ) . Hayo ni ikiwa atapinga. Ama akiangalia dalili wala asikinai na pia asipinge; wakati huo huo akawa amenuia kwa moyo safi kuiamini haki wakati wowote itakapomdhihirikia; kama vile mwanafiqh mwadilifu ambaye hufutu jambo kwa nia ya kubadilisha mara tu ikimbainikia kuwa amekosea, basi huyu hatakuwa na jukumu, kwa sababu mwenye kukosea katika ijtihadi yake bila ya kufanya uzembe, hataadhibiwa kwa kukosea kwake; kama inavyohukumu akili na maandishi pia. Imepokewa kutoka kwa Imam Jafar Sadiq(a.s) , amesema:"Lau kama watu wasipofahamu (jambo) wakasimama na wala wasipinge, basi hawakukufuru" Katika Riwaya nyingine: "Hakika anakufuru tu akipinga"

Sheikh Ansari katika kitabu chake maarufu Arrasil mlango wa Dhana katika Usul, anasema: "Hadith nyingi zimefahamisha kuthibiti ukati na kati baina ya kufuru na imani" Ya kwamba mpingaji ni kafiri, mwenye kuitakidi ni Mumin, na mwenye shaka si kafiri wala Mumin. Katika Hadith zinazowezekana kuzitolea dalili ya kutoadhibiwa mwenye kufanya ijitihadi bila ya uzembe kama akikosea katika mambo ya itikadi, ni Hadith hii mashuhuri kwa sunni na shia:"Akijitahidi hakimu na akapata basi atalipwa mara mbili. Na akijitahidi akakosea, basi atalipwa mara moja" Kama mtu akisema kuwa Hadith hii inahusu mwenye kujitahidi katika matawi si katika masuala ya itikadi, kama walivyodai baadhi ya wanavyuoni, basi tutamjibu hivi: Linalomlinda, mwenye kujitahidi katika hukumu, asiadhibiwe ni kule kujichunga kwake na kutofanya uzembe katika utafiti, Na kinga hii inapatikana hasa katika masuala ya kiitikadi.

Zaidi ya hayo Mafaqihi wote wameafikiana kwa kauli moja kwamba mwenye kushindwa kuifikia itikadi ya kweli, anasamehewa. Miongoni mwao ni wale waliohusisha Hadith hii na matawi. Nasi hatuoni tofauti yoyote kati yake na yule mwenye kujitahidi, aliyetoa juhudi zake. Kwa sababu,wote wawili wameshindwa kujua maadam hawakuufikia uhakika. Kwa ufupi ni kwamba mwenye kuipinga, haki yoyote, basi ataadhibiwa, ni sawa awe amejitahidi au la, isipokuwa kama hana maarifa, kama mnyama. Kama akibakia kwenye msimamo wa kutopinga wala kuthibiti sawa, kujitahidi na kuangalia dalili au alifanya ijtihadi pungufu, basi ataadhibiwa. Ikiwa ameangalia dalili akajitahidi mpaka akafikia mwisho wake, basi yeye atasamehewa kwa sharti ya kubakia na mwelekeo wa haki kwa kuazimia kubadili msimamo wake wakati wowote itakapomdhihirikia haki.

Unaweza kuuliza : Umesema kuwa mwenye kushindwa kujua itikadi ya kweli - kama vile Utume wa Muhammad – atasamehewa, Vile vile mwenye kujitahidi ambaye hakuzembea katika jitihadi. Je, maana yake ni kuwa inajuzu kwetu kufanya naye muamala wa kiislamu, kama kuoa, kurithi n.k.

Jibu : Msamaha tunaoukusudia hapa ni kutostahiki adhabu akhera; ama kuoa na kurithi hapa duniani ni jambo jengine. Na kila asiyeamini utume wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) kwa hali yoyote atakayokuwa, haifai kuwa na muamala naye wa kiislam k.v. ndoa, urithi n.k. Ni sawa awe kesho atapona au ataangamia; kama ambavyo mwenye kusema "Laila ilaha illa llah Muhammad Rasulullah" anastahiki ya waislamu, ni juu yake yaliyo juu yao, hata kama alikuwa ni fasiki, bali hata mnafiki vile vile.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA NNE

﴿وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ تَفَرَّقُوا وَاخْتَلَفُوا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ وَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾

105.Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi; na hao ndio wenye adhabu kubwa.

﴿يَوْمَ تَبْيَضُّ وُجُوهٌ وَتَسْوَدُّ وُجُوهٌ فَأَمَّا الَّذِينَ اسْوَدَّتْ وُجُوهُهُمْ أَكَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ﴾

106.Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika. Na ama ambao nyuso zao zitasawijika, (wataambiwa): Je mlikufuru baada ya kuamini kwenu? Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha.

﴿وَأَمَّا الَّذِينَ ابْيَضَّتْ وُجُوهُهُمْ فَفِي رَحْمَةِ اللَّـهِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

107.Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, Wao humo watadumu.

﴿تِلْكَ آيَاتُ اللَّـهِ نَتْلُوهَا عَلَيْكَ بِالْحَقِّ وَمَا اللَّـهُ يُرِيدُ ظُلْمًا لِّلْعَالَمِينَ ﴾

108.Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki; na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe.

﴿وَلِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴾

109.Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo ardhini na vilivyomo mbinguni; na kwa Mwenyezi Mungu hurejezwa mambo yote.

KUHITALIFIANA BAADA YA MTUME

Aya 105 - 109

MAANA

Wala msiwe kama wale waliofarakana wakahitalifiana baada ya kuwajia wao dalili zilizo wazi.

Aya hii inamalizia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote" Makusudio ya wale waliofarakana ni watu wa Kitabu, Ambapo mayahudi walichangukana vikundi sabini na moja baada ya Mtume wao Musa, wakristo wakawa vikundi sabini na mbili baada ya Mtume wao Isa, Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu."Baada ya kuwajia hoja iliyo wazi" inafahamisha kwamba mtu haadhibiwi kwa kuiacha haki na kufuata batili, ila baada ya kubainishiwa hoja. Ama siri ya mkazo huu na kuupa kipaumbele muungano wa umma, ni kuwa utengano ndio kiini cha ufisadi na kwamba umma uliotengana hauwezi kuwa na maisha mazuri, wachilia mbali kuuita umma mwingine kwenye kheri. Pamoja na kuwapo Riwaya nyingi, na Hadith zinazohimiza muungano wa waislamu, lakini bado wamefarakana na kuwa vikundi mbali mbali, wamewazidi mayahudi kwa vikundi viwili zaidi na wakristo kikundi kimoja; kama ilivyoelezwa katika Hadith mashuhuri.

Kuna Hadithi nyingine isemayo: "Mtakuwa na desturi ile ile ya waliokuwa nayo kabla yenu." Akaulizwa: "Unakusudia mayahudi na manaswara ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?" Akasema: "Kumbe ninawakusudia kina nani? Utachanguka uthabiti wa waislamu" Katika kitabu Al-Jam'u Bainas-Sahihayni cha Hamid, kwenye Hadith Na. 131, anasema: Katika yaliyoafikianwa kutoka Musnad ya Anas bin Malik, amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) :"Watanijia watu miongoni mwa sahaba zangu kwenye hodhi, nitakapowaona na watakapokuwa wanaletwa kwangu watazuiwa ili wasinifikie. Hapo nitasema: 'Ewe Mola! Sahaba zangu, sahaba zangu! Nami nitaambiwa: 'Wewe hujui walizua nini baada yako" Katika kitabu hicho hicho Hadith Na. 267 anasema: "Katika yaliyaofikianwa kutoka Musnad ya Abu Huraira kutoka katika njia mbali mbali, ni kwamba Mtume amesema: "Wakati nikiwa nimesimama - siku ya Kiyama - litatokea kundi la watu mpaka nitakapowatambua, atatokea mtu baina yangu na yao na awambie: 'Haya twendeni.' Mimi nitauliza: Mpaka wapi? Naye aseme: 'Mpaka motoni' Nami niulize wana nini? Naye ajibu: 'Hakika wao walirtadi baada yako"

Siku ambayo nyuso zitang'aa na nyuso (nyingine) zitasawijika.

Makusudio ya Siku, ni Siku ya Kiyama. Kung'aa uso, ni fumbo la kuonyesha furaha ya mumin kufurahia radhi za Mwenyezi Mungu na fadhila Zake. Kusawijika uso ni huzuni ya kafiri na fasiki kwa ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na ama ambao nyuso zao zitasawijika,(wataambiwa), je, mlikufuru baada ya kuamini kwenu?

Arrazi, Tabari na wafasiri wengine wengi wamenukuu kutoka kwa baadhi ya waliopita, kwamba makusudio ya watakaoambiwa hivyo ni Khawariji. Kwa sababu Mtume alisema kuwahusu:"Hakika wao watachomoka kutoka katika dini, kama unavyochomoka mshale kutoka katika uta (upinde)." Lakini dhahiri ya Aya inamkusanya kila mwenye kukufuru baada ya imani, wakiwemo Khawariji, watu wa bid'a na wenye maoni potofu. Kwa vile adhabu haihusiki tu na aliyekufuru baada ya imani bali inamuhusu kafiri yeyote, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Onjeni adhabu, kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakanusha, Na ama ambao nyuso zao zitang'aa, watakuwa katika rehema ya Mwenyezi Mungu, wao humo watadumu.

Rehma ya Mwenyezi Mungu ni Pepo. Kwa ufupi ni kwamba wale ambao wameshikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, na kufanya mambo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wakasaidiana kwenye mambo ya kheri na ya masilahi ya umma, basi watafufuliwa kesho wakiwa watukufu, wenye furaha na wenye kuridhia. Ama wale ambao wamehitalifiana kwa kuipupia dunia, wasiojishughulisha na dini wala umma au nchi, na ambao hawajishughulishi na lolote isipokuwa masilahi yao na ya watoto wao tu, basi wao watafufuliwa Siku ya Kiyama wakiwa madhalili, wenye hasara na makazi yao ni Jahanam, nayo ni marejeo mabaya kabisa. Ajabu ya maajabu ni kwamba baadhi ya wenye nyuso zilizosawijika wanadai kuwa wanamzungumzia Mungu na kutumia Jina lake, lakini mtu akiwaambia "Muogopeni Mungu" wao husema: "Umemkufuru Mwenyezi Mungu." Aliyewatangulia katika hilo ni Abdul Malik bin Marwan aliposema pale alipochukua Ukhalifa: "Kuanzia leo atakayeniambia muogope Mwenyezi Mungu nitamkata kichwa chake."

Hizo ni Aya za Mwenyezi Mungu, tunakusomea wewe kwa haki.

Hizi, ni ishara ya Aya zinazoelekezea kuneemeshwa watu wema na kuadhibiwa makafiri. Msemo unamwelekea Muhammad(s.a.w.w) , muulizaji anaweza kuuliza: "Kuna faida gani katika habari hii, ikiwa Muhammad anajua kwa yakini kwamba Aya hizi ni haki na ni kweli?" Jibu: Ni kawaida ya Qur'an kulikariri hilo katika Aya kadhaa. Na makusudio sio kwa Muhammad hasa, bali ni kwa yule anayetia shaka na kudhani kwamba Aya hizi na mfano wake zinatoka kwa Muhammad, si kwa Mwenyezi Mungu.

﴿وَمَا كُنتَ تَتْلُو مِن قَبْلِهِ مِن كِتَابٍ وَلَا تَخُطُّهُ بِيَمِينِكَ إِذًا لَّارْتَابَ الْمُبْطِلُونَ﴾

"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wabatilifu" (29:48)

Na Mwenyezi Mungu hataki kuwadhulumu viumbe, Kwa sababu dhuluma ni mbaya na Mwenyezi Mungu ameepukana nayo.

Aya hii ni dalili ya mkato kwamba Mwenyezi Mungu hakalifishi mja asiloliweza.

﴿كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَلَوْ آمَنَ أَهْلُ الْكِتَابِ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُم مِّنْهُمُ الْمُؤْمِنُونَ وَأَكْثَرُهُمُ الْفَاسِقُونَ﴾

110.Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu. Na lau watu wa Kitabu wangeliamini ingekuwa heri kwao. Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki .

﴿لَن يَضُرُّوكُمْ إِلَّا أَذًى وَإِن يُقَاتِلُوكُمْ يُوَلُّوكُمُ الْأَدْبَارَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ ﴾

111.Hawatawadhuru isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia, kisha hawatasaidiwa.

UMMA WA MUHAMMAD

Aya 110 - 111

MAANA

Mmekuwa ni umma bora mliotolewa kwa watu, mnaaamrisha mema na kukataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu

Kuna njia kadhaa kuhusu Aya hii, kama ifuatavyo:

1) Katika makusudio ya umma, hakuna mwenye shaka kuwa makusudio ya umma hapa ni Umma wa Muhammad(s.a.w.w) , kwa dalili ya mfumo wenyewe wa maneno ulivyo na mtiririko wa misemo inayoelekezwa kwa waumini; kama vile; "Enyi ambao mmeamini mcheni Mwenyezi Mungu. Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu kwenu…" Mpaka kufikia kauli yake Mwenyezi Mungu:"Mmekuwa ni umma bora."

2). Je, makusudio ni waislamu wote katika wakati wote, au ni kuwahusu wale walio kuwa katika siku za kwanza za uislamu kama vile Masahaba na waliofuatia (tabiina)?

Jibu : Kuainisha makusudio ya umma hapa, kunahitaji kujua makusudio ya herufi kana (kuwa) ambayo ilivyo ni kuwa inahitaji isimu na habari yake. Pia hiyo kana inafahamisha kufanyika kitendo wakati uliopita, lakini haielezi ni wakati gani kimefanyika hicho kitendo wala kuwa kinaendelea au la.

Isipokuwa hilo linaweza kufahamika kutokana na vitu vingine vilivyo pamoja nayo kimaneno au hali ilivyo. Kwa mfano kusema, Zaid alikuwa ni mwenye kusimama. Hapo inachukuliwa kutendeka tendo la kusimama na kuisha bila kuendelea. Yaani Zaid, hakuwa ni mwenye kusimama, basi akasimama kipindi fulani bila ya kuendelea kusimama maisha. Lililofahamisha hilo ni neno mwenye kusimama, yaani hawezi kusimama maisha. Lakini kama tukisema Mwenyezi Mungu amekuwa ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu, hapo hali inafahamisha kudumu kwa tendo lenyewe, kwa sababu rehema na maghufira haviepukani na dhati yake Mwenyezi Mungu, na dhati yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ni ya milele na milele. Kwa kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufungamanisha ubora wa umma na kumwamini kwake, na kuamrisha mema na kukataza maovu, basi maana ya Aya yanakuwa ni: Enyi waislamu! Msiseme tu sisi ni umma bora mpaka muamrishe na kukataza maovu; na kwamba sifa hii ya ubora itawaondokea mara tu mnapopuuza hilo.

Kwa hivyo basi kana hapa inakuwa ni kamilifu, sio pungufu; yaani haihitaji khabar. Kwa maana hayo makusudio ni waislamu wote([2] ) .

3).Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu 'mliotolewa kwa Watu' inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemleta Muhammad na umma wake(s.a.w.w) ushinde umma zote za mwanzo ukiwa umechukua Kitabu cha Mwenyezi Mungu mkono mmoja na Hadith za Mtume kwenye mkono mwingine, huku ukiwalingania vizazi vishikamane na vitu viwili hivyo na kuvitegemea kwa itikadi, sharia na maadili. Kwa sababu ndio marejeo pekee yanayoweza kuhakikisha ufanisi wa mambo yote, kudhamini maisha ya kila mtu na kufungua uwanja wa wenye uwezo wa kufanya ijitihadi kwa misingi ya usawa, amani na uhuru wa watu wote([3] ) .

Aya hii katika madhumuni yake inaafikiana na Aya isemayo:

﴿وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُمَّةً وَسَطًا لِّتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ وَيَكُونَ الرَّسُولُ عَلَيْكُمْ شَهِيدًا﴾

"Tumewafanya ni umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu na Mtume awe shahidi juu yenu." (2:143)

Ikiwa waislamu hawatafanya harakati zozote za kulingania kwenye kheri au kuamrisha mema na kukataza mabaya, basi sifa za uongozi zitawaondokea na watakuwa na haja ya kiongozi atakayewaamrisha mema na kuwakataza maovu. Ulikuwepo wakati ambapo waislamu walikuwa na harakati hizi. Wakati huo walikuwa wakistahili kuwa viongozi wa umma zingine; kisha wakapuuza; wakaendelea hivyo mpaka wakawa wanakataza mema na kuamrisha maovu; kama tuonavyo sasa. Leo vijana wamekuwa wanajivua kabisa na dini na hulka njema. Wakimwona mtu anaswali au kufunga husema kwa dharau: "Bado kuna Swala na Saumu katika karne ya ishirini?" Mwenye Tafsir Al-Manar, katika kufasiri Aya hii, anasema: "Kwa kweli hasa ninasema, haukuzimika ubora wa umma uliotolewa kwa watu, mpaka pale ulipoacha kuamrisha mema na kukataza mabaya. Na haukuacha hivyo kwa kupenda au kupuuza amri ya Mwenyezi Mungu, bali ni kwa kulazimishwa na ufedhuli wa Wafalme wa bani Umayya na waliofuata nyayo zao."

Kwa msingi vitu hutajwa kwa kinyume chake; kama ambavyo hutajwa kwa kifani chake, basi tutaleta Hadith tukufu aliyoitaja Hafidh Muhibbudin Attabari, amesema: "Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) 'Mfano wa Ahlu bait wangu, ni kama safina ya Nuh mwenye kuipanda ataokoka, na mwenye kushikamana nayo ataokoka, na mwenye kuachana nayo ataghariki'". Ama Hadith ya "Mimi nawaachia vizito viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kizazi changu - Ahlul bait wangu," imepokewa na wapokezi 35 katika Masahaba.

Na lau wangeliamini watu wa Kitabu, ingelikuwa heri kwao.

Yaani lau watu waliopewa Tawrat na Injil, wangelimwamini Muhammad(s.a.w.w) ingelikuwa imani yao hiyo ni heri yao katika muda wa sasa na ujao.

Katika wao kuna wanaoamini na wengi wao ni wafasiki.

Yaani katika watu wa Kitabu kuna waliomwamini Muhammad(s.a.w.w) ; kama vile Abdullah bin Salam na watu wake, na wengineo katika wanaswara, na wengi wao walibaki katika ukafiri.

Neno Fasiq na Kafir yanapokezana maana, hutumiwa Fasiq kwa maana ya Kafiri na Kafir kwa maana ya Fasiq. Na Fasiq hapa ina maana ya kafiri. Hawatawadhuru, isipokuwa kuwaudhi tu, na wakipigana nanyi watawakimbia Madhara yako aina mbili:

Kwanza : ni kiasi cha huzuni na kusikia uchungu tu, ambako kadiri siku zinavyokwenda nayo yanafutika; kama vile inavyotokea katika nafsi kwa kusikia habari mbaya.

Pili : ni yale yanayogusa maisha na kuyumbisha; kama vile madhara yaletwayo na dola ya Israil ndani ya nchi ya Waarabu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewabashiria maswahaba wa Mtume(s.a.w.w) kwamba watu wa Kitabu:

Hawatawadhuru isipokuwa kwa maneno tu, kama vile uzushi na mabezo. Ama katika uwanja wa vita, nyinyi ndio washindi.

Amesema kweli Mwenyezi Mungu katika kiaga chake, Aliwapa ushindi waislamu wa mwanzo kwa wakristo na wengineo.

﴿ضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الذِّلَّةُ أَيْنَ مَا ثُقِفُوا إِلَّا بِحَبْلٍ مِّنَ اللَّـهِ وَحَبْلٍ مِّنَ النَّاسِ وَبَاءُوا بِغَضَبٍ مِّنَ اللَّـهِ وَضُرِبَتْ عَلَيْهِمُ الْمَسْكَنَةُ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَانُوا يَكْفُرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَيَقْتُلُونَ الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ﴾

112.Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana, isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki, hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

WAMEPIGWA CHAPA YA UDHALILI

Aya 112

MAANA

Wamepigwa na udhalili popote wanapokutanikana isipokuwa ni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu na kamba ya watu, Na wamestahili ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na wamepigwa na unyonge na udhalili.

Wafasiri wameafikiana kuwa, Aya hii imeshuka kwa ajili ya mayahudi; kama ambavyo wameafikiana kuwa makusudio yake ni kuwa Mwenyezi Mungu amewanyima utukufu na takrima, na akawaandikia udhalili tangu ulipoanza uislamu hadi siku ya mwisho. Kwa sababu wao katika ufisadi na kupetuka mipaka wamefikilia hatua ambayo hakuifikia na hataifikia yeyote. Baada ya wafasiri kuafikiana juu ya hilo, wametofautiana kuhusu aina ya udhalili na unyonge walio nao (Mayahudi ambayo iko kwa kila kizazi). Tofauti hiyo hasa inatokana na tofauti ya hali ya mayahudi wakati wa kufasiri, ambapo walikuwa wakitoa kodi kwa waislamu, yaani kauli ya mfasiri imekuja kuakisi na walivyokuwa wayahudi. Hiyo si ajabu maadam mtu anaathirikia kwa anachokisikia na kukiona, Na tafsiri yangu ya Aya hii inafuata desturi hii.

Vyovyote iwavyo, ninavyofahamu ni kwamba udhalili wa mayahudi uliokusudiwa na Aya ni huku kutawanyika kwao duniani, Mashariki na Magharibi, wakiwa wako kwenye nchi mbali mbali. Wao daima ni wafuasi na wala sio wanaofuatwa na kuhukumiwa katika dola yao. Wako peke yao katika mambo yao. Ama Israeli iliyoko Tel Aviv ni Dola ya jina tu, ilivyo hasa ni kambi tu ya kikoloni na ni kituo cha jeshi cha uchokozi. Hakika hii imedhihiri wazi wazi baada uchokozi wa Israel katika ardhi za Waarabu mnamo tarehe 5 Juni 1967. Ni uchokozi ambao wanaufanya waisrail ili kutekeleza mahitaji yao. Lau watauacha siku moja tu watanyang'anywa na waarabu.

Huo ndio udhalili hasa, kwa sababu mwenye heshima zake hutegemea nguvu zake mwenyewe na kujihami kwa mikono yake sio mikono ya wengine. Kwa hali hii, inatubainikia kuwa makusudio ya kamba ya watu, ni msaada wa kihali na mali utolewao na mataifa ya kikoloni kwa ajili ya kambi ya kikoloni ya Israel. Kwa hivyo basi tunaamini bila ya tashwish yoyote kwamba Dola ya Israil itaondoka tu kwa kuondoka ukoloni. Na ukoloni uko njiani kuisha iwe ni sasa au baadae. Wala maneno hayo sio ndoto, isipokuwa ni natija hasa itakayotokea, kama ilivyoeleza Hadith ya Mtume:"Hakitasimama Kiyama mpaka muwapige vita mayahudi na kwamba jiwe litasema: Ewe Mwislamu! Huyu hapa Yahudi nyuma yangu muue"([4] )

Ama Kamba ya Mwenyezi Mungu ni fumbo la matakwa yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: yaani kwamba mayahudi wataendelea kuwa na udhalili mpaka atakapotaka Mwenyezi Mungu: ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu pia isemayo:

﴿قَالَ النَّارُ مَثْوَاكُمْ خَالِدِينَ فِيهَا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ﴾

"Moto ndio makazi yenu mtadumu humo milele ila apende Mwenyezi Mungu" (6:128)

Kisha baada ya hapo, Mwenyezi Mungu amebainisha sababu iliyowajibisha udhalili wao na ghadhabu yake kwao, kwa kusema:

Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kuwaua Manabii pasi na haki; hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupetuka mipaka.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Sura ya Baqara Aya 61.

Unaweza kuuliza : Kuna wasiokuwa Mayahudi katika mataifa mengine waliokanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua watu wema, kuasi na kupetuka mipaka; pamoja na hayo Mwenyezi Mungu hakuwapiga chapa ya udhalili na uduni. Je,kuna siri gani katika kuwahusisha Mayahudi?

Jibu : Mtu anaweza kupetuka mpaka kwa msukumo fulani unaotokana na masilahi yake na manufaa yake. Ama kupetuka mpaka si kwa lolote isipokuwa kwa kupendelea tu kufanya dhambi, hakujatokea kwa yeyote isipokuwa mayahudi tu, na pupa hii ya kupenda dhuluma na uovu iko ndani ya dini ya mayahudi. Wao wanaitakidi kwamba Mwenyezi Mungu yuko na wao tu, sio wengineo; bali pia yuko dhidi ya maadui zao; na kwamba watu wote wameumbwa kwa ajili yao tu ili wawafanye vile watakavyo, sawa na mtu amfanyiavyo mnyama. Jambo linalofahamisha zaidi sera yao hiyo, zamani na sasa, ni fedheha yao katika Palestina, hasa waliyo yafanya huko Dayr Yasin, kuwachinja wanawake na watoto.

Mwanzo walikuwa wakiwaua Mitume wakati dunia ilipokuwa na Mitume. Ama leo, ambapo hakuna Mitume wanawaua wasuluhishaji; kama vile Bernadotte([5] ) , na wanawake na watoto. Kwa sababu, la muhimu katika itikadi yao na maumbile yao ni kuwaua watu wasiokuwa na hatia; wawe Mitume au wasuluhishi au watoto.

Tawrat yao imeandika uhalali wa kumwaga damu ya wanawake na watoto, na imelihimiza hilo. Kwa ujumla ni kwamba kuzikanusha dalili za Mwenyezi Mungu, kuwaua wasuluhishi na watu wema wasio na hatia, na kufanya dhuluma na uchokozi, yote hayo ni dini na itikadi ya Mayahudi. Myahudi akimfanyia kosa mwengine asiyekuwa Myahudi basi anafanya kwa kujiburudisha tu, sio kwa haja fulani. Na kama akiacha kufanya hivyo, basi anaacha kwa kuogopa sio kwa kujistahi.

Hii ndiyo tofauti kati ya mayahudi na wasiokuwa mayahudi. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa Mwenyezi Mungu kuwawekea udhalili popote walipo.

Ama serikali habithi ya Israel ya sasa itaondoka tu, hakuna budi, Ushahidi mkubwa wa kwisha kwake ni kwamba imefungamana na ukoloni, ukoloni ukiondoka nayo inaondoka. Na ukoloni lazima uondoke tu, hata kama ni baada ya miaka. Maadam maumbile ya kibinadamu yanaukataa ukoloni na kuupinga kwa damu yake, basi utaondoka tu.

Yote haya tuliyoayataja yanakamilisha kifungu cha 'Mayahudi hawana mfano' katika tafsiri ya Sura Baqara (2) Aya63 na 66.

﴿لَيْسُوا سَوَاءً مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ﴾

113.Wote si sawa Katika watu wa Kitabu wamo walio na msimamo, wakasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku huku wakinyenyekea.

﴿يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَأُولَـٰئِكَ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴾

114. Wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na wanaamrisha mema na wanakataza mabaya na wanaharakia mambo mema na hao ndio miongoni mwa watu wema.

﴿وَمَا يَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَلَن يُكْفَرُوهُ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ ﴾

115.Heri yoyote watakayoifayahaitakataliwa, Na Mwenyezi Mungu anawajua wamchao.

WOTE SI SAWA

Aya 113 -115

LUGHA

Mwenye Majmaul-bayan anasema: Tofauti kati ya neno Sura na Ajala ni kwamba Sura ni kufanya haraka linalojuzu kufanywa, Nako kunasifiwa. Na Ajala ni kufanya haraka jambo lisilofaa kufanywa, nako kunashutumiwa.

MAANA

Aya hizi tatu ziko wazi hazihitaji tafsir, Maana yake kwa ujumla ni kwamba watu wa Kitabu hawako sawa kwamba wote wamepotea, bali wako watu wema miongoni mwao. Wafasiri wengi wamechukulia sifa hii kwa aliyesilimu miongoni mwa watu wa Kitabu, na uzuri wa uislamu wake kimatendo na kiitikadi.

HUKUMU YA MWENYE KUACHA UISLAMU

Mwito wa kumwamini Muhammad kama Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa watu wa ulimwenguni bado upo mpaka Siku ya Mwisho. Nao unaelekezwa kwa watu wote, wa Mashariki na Magharibi. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قُلْ يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنِّي رَسُولُ اللَّـهِ إِلَيْكُمْ جَمِيعًا ﴾

"Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyote" (7:158).

Dalili ya ukweli wake ni mantiki ya kiakili, kuthibiti muujiza na kufaa dini kwa maisha. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema: "Msingi wa dini yangu ni akili" Na Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake Kitukufu:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ﴾

"Enyi ambao mmeamini muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume (wake) anapowaitia katika yale yatakayowapa maisha (8:24)

Lengo letu sio kutoa dalili za Utume wa Muhammad(s.a.w.w), ([6] ) isipokuwa lengo ni kubainisha kuwa je, asiyeamini Utume wa Muhammad anastahili adhabu: au hapana budi ya ufafanuzi? Kabla ya kumtofautisha mjuzi na asiye mjuzi na asiyemudu na mzembe, tutaonyesha msingi na vipimo vya kwanza vya kustahili adhabu au kutostahili; kutokana na hivyo, uhakika utafumbuka na kuwapambanua watu. Wote wameafikiana kwamba mtu, vyovyote awavyo, dini yoyote aliyo nayo, hastahili adhabu ila baada ya kusimamishiwa hoja. Na hoja haisimami ila baada ya kuweza yeye kufikia kwenye dalili ya haki na kuweza kwake kuitumia. Hapo akiacha hatakuwa na kisingizio. Ikiwa hakupata dalili ya haki yenye msingi au aliipata akashindwa kuifikia au aliifikia na akatekeleza mtazamo wake wa haki mpaka akafikia mwisho, lakini pamoja na hayo haki haikumdhihirikia, basi yeye atakuwa na udhuru, kwa sababu ya kutokamilika hoja juu yake. Kwa sababu, asiyethibitikiwa na haki haadhibiwi kwa kuiacha, ila ikiwa amezembea katika utafiti.

Vile vile miongoni mwa kawaida za msingi ambazo zinaambatana na utafiti huu ni ile ya "Adhabu kuepukwa na mambo yenye kutatiza." Kwa hiyo haijuzu kumhukumu mwenye kuiacha haki kuwa ni mwenye makosa anayestahili adhabu, maadamu tunaona kuwa kuna uwezekano kuwa anao udhuru katika kuacha kwake. Na kawaida hii inafungamana na watu wote, sio waislamu tu, Pia inakusanya aina zote za mipaka, Mfano kawaida ya 'Mwenye kukosea katika ijtihadi, basi kosa lake linasamehewa', Kawaida hii ni ya kiakili, haiwezekani kuihusisha na dini fulani tu, madhehebu, shina au tawi. Baada ya maelezo hayo hebu tuangalie hali hizi zifuatazo:

1) Kuishi binadamu mji ulio mbali na uislamu na waislamu; wala hakufikiliwa na mwito au hata kusikia jina la Muhammad(s.a.w.w) katika maisha yake yote. Pia awe hajawaza kwa karibu au mbali kwamba duniani kuna dini yenye jina la kiislamu na Mtume aitwaye Muhammad(s.a.w.w) . Hapana mwenye shaka kwamba huyu atasamehewa kwa kuwa hastahili adhabu. Maana akili ina hukumu ubaya wa adhabu bila ya ubainifu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na sisi si wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mitume" (17:15) Bila shaka akili ni Mtume wa ndani kwa ndani, ila tu yenyewe ni dalili ya kupatikana Mwenyezi Mungu tu. Ama dalili ya kuthibiti Utume wa Mtume, hapana budi kuwako na muujiza na udhihirishwe na yeye mwenyewe pamoja na akili kuhukumu kutowezekana kudhihiri kwa wasiokuwa Mitume.

2) Kuusikia mtu uislamu na Muhammad, lakini akawa hawezi kupambanua haki na batili, kwa sababu ya kushindwa kwake na kutoweza kufahamu dalili za haki na maarifa yake. Huyu pia anasamehewa, Kwa sababu yeye ni sawa na mtoto au mwenda wazimu. Mfano ni akitomwamini Muhammad(s.a.w.w) tangu udogo kwa kuwafuata wazazi wake na akajisahau alipokuwa mkubwa, akaendelea na itikadi yake bila ya kuitilia shaka yoyote, huyu atasamehewa. Kwa sababu kumkalifisha aliyejisahau asiye na uwezo ni sawa na kumkalifisha aliyelala. Amesema Muhaqqiq Al-Qummi: "Kujikomboa kutokana na kuiga wazazi ni jambo lisilofikiriwa na wengi, bali hata linakuwa zito aghlabu kwa wanavyuoni waliotosheka ambao wanadhani kuwa wamejivua kutokana na kuiga huko." Amesema tena: "Asiyeweza kung'amua wajibu wa kujua misingi, ni sawa na mnyama na mwedawazimu ambao hawana taklifa yoyote." Sheikh Tusi anasema: "Mwenye kushindwa kupata uthibitisho yuko katika daraja ya mnyama."

Hata hivyo, ikiwa aliyejisahau atakumbushwa wajibu wa maarifa, au kuambiwa na mtu: "Wewe uko au hauko sawa katika itikadi yako", lakini pamoja na hayo akang'ang'ania na wala asifanye utafiti na kuuliza, basi huyo atakuwa ni mwenye dhambi, kwa sababu atakuwa ni mzembe, na kutojua kwa mzembe si kisingizio.

3) Kutomwamini Muhammad(s.a.w.w) pamoja na kuwa anao uwezo wa kutosha wa kufahamu haki, lakini yeye alipuuza wala asijali kabisa: au alifanya utafiti pungufu na akauacha bila ya kuangalia mwisho wake; kama wafanyavyo wengi, hasa vijana wa kisasa. Basi huyu hatasameheka kwa sababu amekosea bila ya kujitahidi na alikuwa na uwezo wa kujua haki, lakini akapuuza. Ni wazi kuwa pia ataadhibiwa ambaye amefanya utafiti na akakinai, lakini pamoja na hayo akakataa kumwamini Muhammad(s.a.w.w) kwa ubaguzi na mali.

4).Kuangalia dalili na kuwa na mwelekeo wa kufuata haki kwa ikhlasi, lakini pamoja na hayo akakosa kuelekea kwenye njia ambayo itamwajibishia kumwamini Muhammad(s.a.w.w) ama kwa kushikamana kwake na mambo yenye kutatiza ya ubatilifu bila ya kuangalia ubatilifu wake, au kuchanganyikiwa na mengineyo ambayo yanazuia kuona haki. Huyu ataangaliwa hali yake, ikiwa atakanusha Utume wa Muhammad(s.a.w.w) kwa kauli ya mkato, basi yeye ataadhibiwa na kustahili adhabu. Kwa sababu yule ambaye imefichika kwake haki, haifai kwake kukataa moja kwa moja kukanusha haki. Inawezekana kuwa haki ipo lakini akazuiliwa, kuifika, na aghlabu huwa hivyo, kwa sababu mambo ya ulimwenguni yapo lakini tuyajuayo ni machache tu. Hali ni hivyo hivyo kuhusu kuwajua Mitume na wasuluhishi, Ni nani awezaye kujua kila kitu?

Watu wa mantiki wamelielezea hilo kwa ibara mbali mbali, miongoni mwazo ni: Kutokujua hakumaanishi kutokuwepo, kutopatikana hakumaanishi kuacha kupatikana, kuthibitisha na kukanusha kunahitaji dalili. Tumewaona wanavyuoni wengi wakiungana na hakika hii. Wanazituhumu rai zao na kujichunga katika kauli zao; wala hawajifanyi kuwa wao ndio kipimo cha ukweli. Hawawezi kusema: "Rai hii ni takatifu isiyo na shaka, na nyinginezo si chochote." Bali wao huipa mtazamo wa kujiuliza kila rai. Dalili kubwa zaidi ya kuwa mtu hana elimu, ni kule kujidanganya mwenyewe, kuiona safi elimu yake, na kudharau rai na itikadi za wengine.

Zaidi ya hayo kuacha kukinai mtu mmoja miongoni mwa watu kuhusu Utume wa Muhammad(s.a.w.w) hakumruhusu kukanusha Utume wa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) moja kwa moja. Na kama akifanya hivyo, basi atakuwa na jukumu. Hasa baada ya kuona idadi ya mabingwa ambao hawakuathiriwa na kurithi au mazingira, wakimwamini Muhammad na risala yake; si kwa lolote isipokuwa kuiheshimu haki na kuikubali hali halisi ilivyo([7] ) . Hayo ni ikiwa atapinga. Ama akiangalia dalili wala asikinai na pia asipinge; wakati huo huo akawa amenuia kwa moyo safi kuiamini haki wakati wowote itakapomdhihirikia; kama vile mwanafiqh mwadilifu ambaye hufutu jambo kwa nia ya kubadilisha mara tu ikimbainikia kuwa amekosea, basi huyu hatakuwa na jukumu, kwa sababu mwenye kukosea katika ijtihadi yake bila ya kufanya uzembe, hataadhibiwa kwa kukosea kwake; kama inavyohukumu akili na maandishi pia. Imepokewa kutoka kwa Imam Jafar Sadiq(a.s) , amesema:"Lau kama watu wasipofahamu (jambo) wakasimama na wala wasipinge, basi hawakukufuru" Katika Riwaya nyingine: "Hakika anakufuru tu akipinga"

Sheikh Ansari katika kitabu chake maarufu Arrasil mlango wa Dhana katika Usul, anasema: "Hadith nyingi zimefahamisha kuthibiti ukati na kati baina ya kufuru na imani" Ya kwamba mpingaji ni kafiri, mwenye kuitakidi ni Mumin, na mwenye shaka si kafiri wala Mumin. Katika Hadith zinazowezekana kuzitolea dalili ya kutoadhibiwa mwenye kufanya ijitihadi bila ya uzembe kama akikosea katika mambo ya itikadi, ni Hadith hii mashuhuri kwa sunni na shia:"Akijitahidi hakimu na akapata basi atalipwa mara mbili. Na akijitahidi akakosea, basi atalipwa mara moja" Kama mtu akisema kuwa Hadith hii inahusu mwenye kujitahidi katika matawi si katika masuala ya itikadi, kama walivyodai baadhi ya wanavyuoni, basi tutamjibu hivi: Linalomlinda, mwenye kujitahidi katika hukumu, asiadhibiwe ni kule kujichunga kwake na kutofanya uzembe katika utafiti, Na kinga hii inapatikana hasa katika masuala ya kiitikadi.

Zaidi ya hayo Mafaqihi wote wameafikiana kwa kauli moja kwamba mwenye kushindwa kuifikia itikadi ya kweli, anasamehewa. Miongoni mwao ni wale waliohusisha Hadith hii na matawi. Nasi hatuoni tofauti yoyote kati yake na yule mwenye kujitahidi, aliyetoa juhudi zake. Kwa sababu,wote wawili wameshindwa kujua maadam hawakuufikia uhakika. Kwa ufupi ni kwamba mwenye kuipinga, haki yoyote, basi ataadhibiwa, ni sawa awe amejitahidi au la, isipokuwa kama hana maarifa, kama mnyama. Kama akibakia kwenye msimamo wa kutopinga wala kuthibiti sawa, kujitahidi na kuangalia dalili au alifanya ijtihadi pungufu, basi ataadhibiwa. Ikiwa ameangalia dalili akajitahidi mpaka akafikia mwisho wake, basi yeye atasamehewa kwa sharti ya kubakia na mwelekeo wa haki kwa kuazimia kubadili msimamo wake wakati wowote itakapomdhihirikia haki.

Unaweza kuuliza : Umesema kuwa mwenye kushindwa kujua itikadi ya kweli - kama vile Utume wa Muhammad – atasamehewa, Vile vile mwenye kujitahidi ambaye hakuzembea katika jitihadi. Je, maana yake ni kuwa inajuzu kwetu kufanya naye muamala wa kiislamu, kama kuoa, kurithi n.k.

Jibu : Msamaha tunaoukusudia hapa ni kutostahiki adhabu akhera; ama kuoa na kurithi hapa duniani ni jambo jengine. Na kila asiyeamini utume wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) kwa hali yoyote atakayokuwa, haifai kuwa na muamala naye wa kiislam k.v. ndoa, urithi n.k. Ni sawa awe kesho atapona au ataangamia; kama ambavyo mwenye kusema "Laila ilaha illa llah Muhammad Rasulullah" anastahiki ya waislamu, ni juu yake yaliyo juu yao, hata kama alikuwa ni fasiki, bali hata mnafiki vile vile.


8

9

10

11

12

13

14

15

16