• Anza
  • Iliyopita
  • 4 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 3156 / Pakua: 1761
Kiwango Kiwango Kiwango
NGUZO YA UCHAMUNGU

NGUZO YA UCHAMUNGU

Mwandishi:
Swahili

NGUZO YA UCHAMUNGU

Kimeandikwa na

Sayyid Ali Naqi Saheb

Kimetafsiriwa na

Maalim Dhikiri Omari Kiondo

Kimechapishwa na

Bilal Muslim Mission of Tanzania

S.L.P. 20033

Dar es Salaam - Tanzania

Kimetolewa juu ya web na timu ya

Ahlul Bayt Digital Islamic Library Project

1

NGUZO YA UCHAMUNGU

IMAMAH KATIKA QUR'ANI NA HADITHI

Mwenyezi Mungu Anasema: (Ewe mwanadamu! Ikumbuke) siku Tutakapowaita kila watu pamoja na Imamu wao; basi atakayepewa kitabu (chake cha Amali) kwa mkono wa kulia, hao watavisoma vitabu vyao (kwa furaha) (Bani Israeil, 17:71)

Mtukufu Mtume[s.a.w.w] Amesema: "Yeyote yule afaye pasi na kumjua Imamu wa zama zake, atakuwa kafa kifo cha ujinga."

Mtukufu Mtume[s.a.w.w] Amesema: "Hao (Ulul Amr watajwao mwenye Qur'ani 4:59) ni Makhalifa wangu na Maimamu wa Waislamu baada yangu. Wa kwanza ni Ali, kisha ni Hasan, kisha ni Husayn, kisha ni Ali bin Husayn, kisha ni Muhammad bin Ali, kisha ni Jaafar bin Muhammad, kisha ni Musa bin Jaafar, kisha ni Ali bin Musa, kisha ni Muhammad bin Ali, kisha ni Ali bin Muhammad, kisha ni Hasan bin Ali, kisha ni Muhammad bin Hasan (Mahdi)...." ("Kifayatul Athar" na "Rawdhatul Ahbab", vya Hafidh Jamaluddin Muhaddith).

SHUKRANI

Kitabu hiki kiliandikwa kwa lugha ya Urdu na Mtukufu Saiyadul Ulama Maulana Sayyid Ali Naqi Saheb, Mujtahid wa Chuo Kikuu cha Lucknow, Uhindi. Kimetafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza na Sayyid Hashim Raza Rizvi, B.A., B.T., Yadgar-e-Husaini H.S. School, AlIahabad, Uhindi, na kutolewa na Imamia Mission Lucknow, U.P., Uhindi. Kimetafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza na Sayyid Hashim Raza Rizvi, B.A., B.T., Yadgar-e-Husaini H.S. School, Allahabad, Uhindi na kutolewa na Imamia Mission Lucknow, U.P., Uhindi. Kimetafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili kutoka hiyo tafsiri ya Kiingereza na Bwana J. J. Shou wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (Tanzania) na kikachekiwa na kusahihishwa na Mwalimu Dhikiri (Zakir Ali) U.M. Kiondo, Edita wa "Sauti ya Bilal".

UTANGULIZI

Maisha ni nguvu isiyoonekana kwa macho na ambayo haipimiki kwa miaka isipokuwa kwa mkazo wa nguvu ya maendeleo iliyoko ndani yake. Maisha ya namna hii yanapotokea katika hali ya kawaida ya mambo ya ulimwengu yanaacha alama zisizofutika kuliko yale maisha ambayo yangekuwa na urefu wa miaka elfu moja. Maisha ya Imamu Muhammad Taqi[a.s] ni mfano wa maisha ya namna hiyo. Ingawa aliishi kwa muda wa miaka michache zaidi kuliko Imamu yeyote yule kati ya Maimamu hao kumi na wawili[a.s] , maisha yake ni muhimu kama yale ya Imamu yeyote yule mwingine kwani alikuwa na tabia sawa na Maimamu wengine, aliutangaza ujumbe ule ule na alikuwa ni Mwali wa Nuru ile ile.

JINA LA NASABA YAKE

Jina lake lilikuwa Muhammad, 'Kunyat' (jina Ia utoto) ni Abu Ja'far, na majina yake ya heshima ni Taqi (Muadilifu) na Jawad (Mkarimu), hivyo aliitwa Imamu Muhammad Taqi. Kama vile Imamu Muhammad Baqir [a] alivyojulikana kabla yake kwa jina la Abu Ja'far, yeye naye anajulikana katika vitabu kwa jina la Abu Ja'far wa pili. Pia anajulikana kwa jina la "Hadhrat Jawad". Baha yake alikuwa Imamu Ali Ridha[a.s] na mama yake alikuwa Bibi Sakinah Khatun.

KUZALIWA KWAKE

Alizaliwa mnamo tarehe kumi ya mwezi wa Rajab, mwaka wa 195 Hijiriya, mjini Madina wakati Amin, mwanawe Harun-AlRashid alikuwa akitawala mjini Baghdad (Iraq).

KULELEWA KWAKE

Ilimbidi Imamu Muhammad Taqi[a.s ] ajitayarishe mapema kuzikabili shida. Alikuwa na umri wa miaka mitano tu baba yake alipoondoka Madina kwenda Khurasan (Iran); na hakumwona tena baba yake maishani mwake kwani alifariki miaka mitatu baada ya kumwacha mwanawe huko Madina. Labda ulimwengu ulifikiria kuwa huenda nafsi ya Imamu Ja'far Sadiq[a.s] ingebakia wazi kwa vile Imamu kijana alikuwa bado hajaelimishwa ipasavyo. Lakini ulimwengu ulishangazwa kumwona mtoto mdogo, mara baadaye, akijadiliana na wanavyuoni wakuu wa siku zile katika baraza Ia Mfalme Mamun na wakaukubali ubora wake. Mshangao wao ulikuwa kitu cha kutegemewa maana hawakuamini kuweko kwa elimu ya Kimungu.

SAFARI YA KWANZA KWENDA IRAQ

Wakati Mfalme Mamun alipotangaza kuwa amemteua Imamu Ali Ridha[a.s] kuwa mrithi wake (wa kiti cha Ufalme) aliona ulazima wa kuwepo uhusiano bora na watu wa ukoo wa Bani Fatimah badala ya watu wa ukoo wa Bani Abbas; hivyo, kwa kujipendekeza kwa Mashia, alidhania kuwa itakuwa ni busara kuanzisha uhusiano mpya na watu wa ukoo wa Bani Fatimah, badala ya ule wa kiwahenga wa watu wa ukoo wa Bani Abbas na Bani Fatimah kuwa wote ni Bani Hashim.

Kwa hiyo katika hadhara hiyo hiyo alipotangaza kuwa yeye anamteua Imamu Ali Ridha kuwa atakuwa mrithi wake (wa kiti cha Ufalme) alimuozesha dada yake kwa Imamu Ali Ridha[a.s] na akatangaza ndoa kati ya binti wake na Imamu Muhammad Taqi[a.s] . Labda alifikiria kuwa kwa kufanya hivyo angeweza kumshawishi Imamu Ali Ridha[a.s] kumuunga mkono. Lakini baada ya muda mfupi tu aliona kuwa Imamu [a] alithamini zaidi ujumbe wa Uislamu na kazi yake ya Uongozi wa Dini, na kuwa hakubali jambo jingine liingilie Sheria.

Kwa hiyo aliyaona maisha yale mapya ya Imamu[a.s] akiwa jamaa ya mtawala huyo na wakati huo huo akichukua uzito wa kazi ya kuuhubiri Uislamu wa Kweli kuwa ni ya hatari kwa dola na utawala wake wa kijanja kuliko Madina. Kwa hiyo alimuuwa kwa kumpa sumu. Lakini sababu zilizomfanya amtangaze Imamu[a.s] kuwa ndiye mrithi wake wa baadaye bado zilikuwepo na bado anahitaji kuungwa mkono na Mashia na Mairani. Hivyo wakati alipojionyesha kuwa alikuwa na huzuni sana kwa kifo cha lmamu Ali Ridha[a.s] ili asijulikane kuwa alihusika na kifo hicho, ilimbidi pia aendelee na tangazo lake Ia kufunga ndoa kati ya binti wake na Imamu Muhammad Taqi[a.s] . Hivyo alimtaka Imamu Muhammad Taqi[a.s] kwenda Iraq kwa kuwa yeye pia alikwishahamia kwenye makao makuu ya zamani, Baghdad, akiwa na makusudio ya kuwaoza haraka.

MAJADILIANO KATI YAKE NA WANAVYUONI

Watu wa Ukoo wa Bani Abbas walikataa tangazo la Mfalme kumteua Imamu Ali Ridha[a.s] kuwa mrithi wake wa kiti cha Ufalme. Lakini walirithishwa kidogo na kuuawa kwa Imamu[a.s] kwa sumu. Hivyo basi walimlazimisha Mamun atangaze kuteuliwa kwa ndugu yake Mu'tamin kuwa mrithi wa kiti cha enzi. Zaidi ya hapo yale majoho meusi waliyokuwa wakiyavaa watu wa ukoo wa Bani Abbas yaliyokomeshwa na badala yake kutumiwa majoho ya kijani kama alivyoshauri Imamu Ridha[a.s] yalianza kutumika tena. Mambo haya yote yaliwahakikishia watu kimawazo, lakini sasa uamuzi wake wa kumuoza binti wake kwa Imamu Muhammad Taqi[a.s] , uliwakasirisha tena hivyo walingojea kuonyesha kutoridhika kwao na uamuzi wa Mamun kwamba mtoto mdogo apendelewe badala ya wanavyuoni wakuu wa zama hizo, na katika azima ya kutaka kumuoza binti wake kwa mtoto huyo (Imamu Taqi[a.s] ambapo ndoa kati ya dada yake na baba wa Imamu huyo haikutoa matokeo mazuri.

Mamun aliwajibu kuwa, ingawa yu mdogo kwa umri, Imamu Muhammad Taqi[a.s] alikuwa mrithi wa kweli wa baba yake na hakika alikuwa na elimu zaidi kuliko wanavyuoni wote na kama wana wasiwasi na jambo hili wanaruhusiwa kumleta mtu yeyote na kujadiliana naye na wataamini kuwa ni kweli. Walikwenda kumshawishi mmoja wa wanavyuoni mashuhuri wa Baghdad aitwaye Yahya bin Aksam kuja kujadiliana na Imamu[a.s].

Mamun alitayarisha mkutano mkubwa kwa ajili ya majadiliano hayo na watu wengi walialikwa. Kila mtu alikuwa na hamu ya kuona pambano hilo kati ya mtoto mdogo wa umri wa miaka tisa na mwanachuoni mwenye ujuzi wa siku nyingi na pia aliyekuwa kadhi mkuu wa nchi. Wanahistoria wameandika kuwa, achilia mbali wakuu wa baraza la Mfalme Mamun, viti mia tisa viliwekwa kwa ajili ya wanavyuoni.

Mamun aliweka kiti karibu naye kwa ajili ya lmamu[a.s] na kiti kingine mbele yake kwa ajili ya Yahya. Palikuwa kimya kabisa na mara Yahya alianza kusema kwa kuomba ruhusa ya Mfalme amuulize swali Imamu[a.s]. Mamun alimwambia Yahya aombe ruhusa kwa Imamu mwenyewe. Hapo alimgeukia Imamu na kumwomba ruhusa ya kumuuliza swali. Imamu [a] alimruhusu. Yahya aliuliza "Kama mtu akiwinda hali ya kuwa yu katika Hijah, Kafara yake ni nini? Swali hili lilionyesha kwamba Yahya alikuwa hajui kiasi cha elimu ya Imamu[a.s].

Katika kumjibu Yahya, Imamu[a.s] alilifafanua swali hilo katika kila uwezekano wake kwa utaratibu na uangalifu wa kitaalam mpaka wasikilizaji pamoja na Yahya mwenyewe waliweza kuielewa elimu ya Imamu kabla swali hilo halijajibiwa. Imamu[a.s] akasema, "Swali lako halieleweki. Ungelisema kama kitendo hicho kilitendwa ndani ya mipaka mitakatifu ya Kaabah au nje yake; kama mtu yule alifanya kitendo hicho akiwa anazijua sheria za jambo hilo au Ia; kama alimwua mnyama huyo makusudi au kwa bahati mbaya tu; kama mtu yule alikuwa mungwana au mtumwa, mtu mzima au mtoto; kama ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanya hivyo au vipi; kama aliua ndege au kwa kufanya hivyo au la; kama alifanya kitendo hicho usiku; au kwa siri au mchana na kama alikuwa anakwenda "Hajj" au "Umrah". Haiwezekani kutoa jibu kamili kwa swali hili mpaka mambo hayo yamefafanuliwa vizuri kwa sababu kafara ya kila kosa kati ya hayo itakuwa tofauti".

Yahya hakuwa na la kusema, hakujitayarisha ujibu maswali ya kiuchunguzi namna hiyo. Alama za kufadhaika zilionekana usoni mwake. Mamun alipoona hivyo, aliona kuwa ingelikuwa vema kumuomba Imamu[a.s] , "Ni vizuri uyaeleze wewe mwenyewe yote haya. Na hapo Imamu[a.s] alieleza kwa kirefu na kwa makini mambo yote aliyoyasema. Mamun sasa alitaka kufanya vichekesho kutokana na ujinga wa Yahya. Hivyo alimgeukia Imamu na kumwambia, "Sasa mwuulize Yahya swali lolote lile". Imamu alimgeukia Yahya na kuuliza. "Naomba nikuulize swali". Yahya sasa alikwishaelewa wazi kuhusu tofauti baina ya ujuzi wake na wa Imamu[a.s] , hivyo hakuwa na wasiwasi wa kujidanganya. Hivyo alijibu, "Ndiyo Bwana, kama nikiweza kulijibu swali lako nitalijibu la sivyo nitakuomba kulielezea".

Ndipo Imamu[a.s] alipomuuliza Yahya swali na mara moja Yahya alikiri kutoweza kwake kulijibu. Na Imamu akalielezea. Kisha Mamun akaanza kuwatangazia wale watu waliokuwepo akasema, "Sasa mmeona kuwa sikukosea niliposema kuwa ukoo huu unaelimishwa na Mwenyezi Mungu na hakuna mtu awezaye kuzungumza hata na watoto wao." Waliokuwepo wote walikubali ukweli wa jambo hilo.

Mamun alimuoza binti wake kwa Imamu[a.s] pale pale. Imamu[a.s] alitoa hotuba ambayo husomwa katika 'Nikah' (kusoma kanuni zilizowekwa na zilizothibitishwa kuonyesha maafikiano ya ndoa kati ya mume na mke) ya Waislamu. Mamun alionyesha ukarimu mkubwa siku hiyo na aligawa kiasi kikubwa cha pesa kwa raia wake.

2

NGUZO YA UCHAMUNGU

KURUDI MADINA

Baada ya ndoa, Imamu[a.s] alikaa Baghdad kwa muda wa mwaka mmoja hivi na halafu Mamun aliwaona wakiondoka kwenda Madina.

TABIA YAKE ADHIMU

Imamu Muhammad Taqi[a.s] alikuwa ni mmoja wa watu wa ukoo wa Mtume[s.a.w.w] na aIikuwa na tabia nzuri kama za wale wengine wa ukoo huo. Kumfanyia kila mtu upole, kutosheleza mahitaji ya kila mhitaji, kuweka maisha rahisi na usawa kuwa ni mambo muhimu zaidi, kuwasaidia maskini kwa siri, kuwatendea mema hata maadui, ukarimu mkubwa na kila wakati kuwakarihisha wale wapendao kujifunza vilikuwa sifa kubwa ziIizomtofautisha lmamu Taqi[a] .

Watawala wa koo za Bani Umayya na Bani Abbas hawakuwa na jambo Ia kufanya juu ya mtu wa ukoo wa Mtume[s.a.w.w] maana kwa sifa zao hizo walionyesha tofauti kubwa (iliopo kati yao na watu wengine) na kuonyesha ubaya wa watawala na majeshi yao. Kwa hiyo kila mara walijaribu kuivuruga senta ya Kidini ya Madina na jaribio la Yazid kumfanya Imamu Husain[a.s] awe upande wake jambo ambalo baadaye lilisababisha masaibu ya Karbala au tukichukua mfano mwingine, Mamun kumteua Imamu Ridha[a.s] kuwa mrithi wake wa kiti cha Ufalme kulikuwa ni njia tofauti ya kudhihirishia msimamo wao ule ule wa siku zote. Wakati fulani nguvu za uovu zilijitokeza kuushambulia UkweIi na mara nyingine walijaribu kuvishinda 'vipingamizi' kwa kumwua lmamu Ridha kwa sumu.

Sasa Mamun aIifikiria kuwa wakati huo ulifaa kwa kumgeuza mawazo mtoto mdogo mwenye umri wa miaka minane au tisa ambaye ametengwa na baba yake miaka mitatu iliyopita na hivyo hatari iliyokuwepo kila mara kwa utawala wa Bani Abbas itaondolewa. Mamun hakukuchukulia kushindwa kwake Imamu Ridha[a.s] kuwa iwe ndicho chanzo cha kukata tamaa kwake. Alifikiria kuwa haikuwa lazima kuwa ikiwa Imamu Ridha[a.s] hakuweza kushawishika (kwa sabahu alikwisha kuwa na tabia za kiutu uzima) mwanawe asingeliweza kufikiriwa kuwa si wa kumtumainia.

Lakini Mamun na watu wote wale ambao macho yao hayakuweza kuuona ukweli wa mambo, walistajaabu kuona kuwa mkwewe Mfalme wa ukoo wa Bani Abbas mwenye umri wa miaka tisa alikataa kukaa katika jumba la kifalme. Walimuona anashikilia kuendelea na tabia ya watu wa ukoo wake na walishangaa kuona kuwa alipokwenda Baghdad alikodisha nyumba ya kuishi badaIa ya kuishi katika majumba ya kifalme. Si hivyo tu, bali baada ya muda mfupi tu alikataa kuishi mjini Baghdad na kabla ya mwaka mmoja kwisha baada ya ndoa yake na binti wa mfalme, ilimbidi mfalme atengane na binti wake na kumruhusu aondoke na mumewe ambaye ilibidi matakwa yake yatiliwe na huyo mfalme mkuu na tena aliye baba mpenzi.

Huko Madina, Imamu[a.s] alirudia maisha yake ya zamani. Wakati wake mwingi aliutumia katika msikiti wa Mtukufu Mtume[s.a.w.w] ambamo wanafunzi wa Hadithi za Mtume[s.a.w.w] na Elimu ya dini walikwenda na kukuta kiti cha Imamu Ja'far al-Sadiq[a.s] kikiwa kimekaliwa tena na kiu yao ya kujifunza ikazimishwa.

Katika maisha yake ya faragha alikuwa na kawaida hiyo hiyo. Alimwekea mkewe Bibi UmmuI Fazl (bintiye Mamun) amri hizo hizo katika maisha yake kama alizowawekea wakeze wengine; baadaye kidogo alimwoa mwanamke mmoja tajiri wa ukoo wa Bwana Ammar bin Yasir (Mwenyezi Mungu na aiweke roho yake mahali pema Peponi) ambaye baadaye alikuwa mama wa lmamu Ali Naqi[a.s] . Ummul Fazl alimuandikia baba yake akimlalamikia juu ya jambo hilo. Hakika Mamun alikasirishwa sana kusikia hivyo lakini ilimbidi ajikaze. Kwa hiyo alimjibu akisema, 'sikukuoza kwa Abu Ja'far ili nimzuie asifanye yale aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu. Usinilalamikie juu ya mambo kama hayo tena.

b Jibu hili lilikuwa la kusawazisha mambo hasa. La sivyo, pamekwishakutokea mifano ambayo kuwapo mwanamke bora (kufuatana na imani) kuliweza kuzuia kufanyika kwa ndoa ya pili. Mtume[s.a.w.w] hakuoa mke mwingine wakati wa uhai wa Bibi Khadija na wakati wa uhai wa Bibi Fatimah[a.s] , Hadhrat Ali[a.s] pia hakuoa mke wa pili. Sasa Imamu Muhammad Taqi[a.s] aliona kuwa kwa vile Bibi Ummul Fazl akiwa binti wa Mfalme, alihitaji kutendewa tofauti na wake wengine. Imamu[a.s] alitaka kumuonyesha Bibi huyu kuwa mwenendo wa Uislamu haukutaka kuendekeza jambo hilo.

IMAMU MUHAMMAD TAQI [a.s] AKIWA MWALIMU WA DINI

Hotuba zake zilikuwa zinapendeza sana. Wakati mmoja wa Hija huko Makka alitoa hotuba juu ya amri za Dini kwa namna nzuri mno kiasi ambacho wanachuoni wakuu waliokuwepo walishangaa na walikubali kuwa walikuwa hawajapata kusikia hotuba nzuri kama hiyo. Wakati wa Imamu Ali[a.s] ilizuka madhehebu mpya ambayo ilikomesheza Uimamu kwa Imamu Musa Kadhim[a.s] na hawakuamini Uimamu wa Imamu Ali Ridha[a.s] .

Madhehebu haya yalijulikana kwa jina Ia "Wazifiyyah". lmamu Muhammad Taqi[a.s] alifaulu vizuri kuhubiria dhidi ya imani yao kiasi ambacho karibu kila mmoja wao alikubaliana naye na karibu wale wote walioifuata madhehebu hayo waliyotoka. Idadi kubwa ya wanavyuoni wakawa wanafunzi wake. Kama alivyoacha mhenga wake Hadhrat Ali[a.s] , Imamu Taqi[a.s] nae ameacha idadi kubwa ya Hadithi za kuaminika na zinazojulikana sana. Pia ameacha hotuba fulani nzuri sana.

SAFARI YAKE YA MWISHO KWENDA IRAQ

Katika mwaka wa 218 Hijiriya mfalme Mamun alifariki na nduguye Mu'tamin alirithi kiti cha ufalme akitumia jina Ia Mu'tasim Billah. Mara moja barua za malalamiko ambazo Bibi Ummul Fazl alimuandikia baba yake sasa zilianza tena kummiminikia baba yake hakuzitia maanani barua hizo kwa kuwa mwenyewe alimuozesha kwa Imamu[a.s] ingawa watu wa ukoo wa Bani Abbas walipinga, sasa huyu baba mdogo alianza kuzisikiliza.

Wakati wa ndugu yake Mamun, Mu'tamin aliwahi kukiwakilisha kikundi kilichopinga kuozwa kwa binti wa nduguye, Bibi Ummul Fazl kwa Imamu[a.s] . Zaidi ya hayo, alikuwa akiiogopa na kuihesabu sifa ya Imamu[a.s] ya uongozi wa dini kuwa si isiyokuwa na haki, chanzo cha hatari kwa utawala wake kama vile baba zake walivyofanya wakati wa enzi zao.

Kwa hiyo mnamo mwaka wa pili wa utawala wake alimwagiza Imamu[a.s] aende kwake na alimwandikia barua Gavana wa Madina, aitwaye Abdul Malik kuhusu jambo hiIo. Hivyo Imamu[a.s] alimuacha mkewe, mama yake Imamu Ali Naqi[a.s] akae na Abdul Malik na yeye akaondoka kwenda Baghdad.

KUFARIKI KWAKE

Kwa muda wa mwaka mmoja hivi baada ya kwenda Baghdad Imamu[a.s] hakusumbuliwa na Mu'tasim isipokuwa maisha ya Baghdad yalikuwa ya namna ya kifungo". Halafu silaha ile ile ya zamani (yaani ya kuuwa kwa sumu) ilitumika kwake na akapewa sumu akafa mnamo tarehe 22 Dhul-Qa'dah mwaka 220 Hijiriya. Alizikwa karibu na kaburi la Imamu Musa Kadhim[a.s] . Na mahali hapo pakajulikana kwa jina Ia Kadhimain (mji wa Kadhim wawili) na sasa kituo hicho kinaitwa Jawadain (mahali pa Jawad). Kimoja kati ya vyeo vya Imamu Muhammad Taqi[a.s] ni "Jawad".

MASAYYIDI WA UKOO WA RIDHAWI

Masayyidi (Masharifu) ambao wanajulikana kwa jina la Ridhawi wote wametokana na kizazi cha Imamu Muhammad Taqi[a.s] na wangekuwa wameitwa Taqawi kama pangekuwepo mfuatano wa ukoo wa Imamu Ridha[a.s] zaidi ya kupitia kwa Imamu Muhammad Taqi[a.s] ambao ungejulikana kwa jina Ia Ridhawi kwa kutofautishwa na wale wa ukoo waTaqawi. Lakini kizazi cha Imamu Ali Ridha[a.s] ni kile tu kilichotokana na lmamu Muhammad Taqi[a.s] na kwa kuwa Imamu Ali Ridha[a.s] alijulikana sana katika ulimwengu wa Kiislamu kwa sababu ya kuteuliwa kwake kuwa mrithi wa mfalme Mamun wa kiti cha ufalme, kizazi cha Imamu Muhammad Taqi[a.s] chote kiliitwa Ridhawi badala ya Taqawi.

HADITHI ZA IMAMU MUHAMMAD TAQI [a.s]

1. Yeyote yule amsaidiaye mshari (kwa namna yoyote ile) katika vitendo vyake ni mshiriki wake.

2. Siku ya "Uadilifu" (mdhuIumiwa kulipiziwa kisasi) ni ngumu zaidi kwa mshari (huyo aliyedhulumu) kuliko siku aliyomfanyia shari mdhulumiwa.

3. Mtu afanyaye kitu bila ya elimu ya kukifanyia kitu hicho, hukiharibu badala ya kukitengeneza.

4. Uchamungu huleta heshima, kujifunza ni hazina, ukimya humpa mtu hekima.

5. Hakuna kitu kibaya kwa dini kupita 'bid'at' (uzushi wenye maana mbaya) na hakuna kitu kiharibucho heshima kama tamaa.

6. Kuwatengeneza raia hutokana na mtawala na dua huzuia maovu.

7. Anayetumia maneno mabaya hulipwa maneno mabaya na afanyaye jambo bila akili huumia.

8. Mkarimu huwa mwangalifu kwa ukarimu wake kuliko wale wafaidikao kwa ukarimu huo. Ukarimu wake humlipa na humletea heshima na utukufu.

9. Yeyote ategemeaye upendeleo fulani toka kwa mtu mwingine pia humuogopa mtu huyo. Na yeyote asiyekielewa kitu fulani hukiona ni kibaya.

10. Kuachwa kwanza (kutoadhibiwa mara moja) ni kitu kipoteacho mara moja tu.

11. Anayetaka kuokoka lazima awe na moyo wa uvumilivu katika shida.

12. Ampandaye farasi wa uvumilivu huipata barabara ya kwendea kwenye uwanja wa ushindi.

13. Vitu vinne humuongoza mtu kwenye matendo mazuri, afya, utajiri, elimu na Neema za Mwenyezi Mungu.

14. Kumwamini Mwenyezi Mungu ni kuokokana na maovu yote na ni kinga kutokana na kila adui.

MAELEZO MACHACHE KUHUSU KABURI LA KADHIMAIN

Mtu yeyote anayeukaribia mji wa Baghdad kutokea upande wa Kaskazini au Magharibi atapendezwa kuona minara minne ya dhahabu katika mji wa Kadhimain, Kuba la Kadhim wawili ambao ni Maimamu Musa bin Ja'far[a.s] na Muhammad Taqi[a.s] . Kwenye lango kubwa lenye umbo la nusu mduara, kwenye ukuta unaolizunguka Kuba hilo pametundikwa mikufu mikubwa ambayo inaonyesha kwamba sehemu ile ni Takatifu.

Jengo la sasa lilijengwa mnamo mwanzoni mwa karne ya kumi na sita (ya zama za Ukristo), na limekuwa likitarizwa kwa nakshi nzuri nzuri. Jengo hili linakumbusha kujengwa kwake na Shah Isma'ili wa kwanza (tangu mwaka 1502 hadi 1524 Masihiya), ingawaje sultani wa Kituruki, Suleiman Mkuu aliyeuteka mji wa Baghdad na akakaa humo kwa muda wa miezi minne katika mwaka wa 1534 Masihiya alikwenda sehemu takatifu za Mashia na inasemekana aliyatia nakshi zaidi yale Makuba ya Kadhimain. Hata hivyo, vigae vya zege, viliwekwa mnamo mwaka 1796 Masihiya na Shah Muhammad Khan aliyekuwa Mfalme wa kwanza wa ukoo wa Qachar.

Mnamo mwaka 1870 Masihiya, mfalme Nasiruddin Shah Qachar aliviweka hivi vigae vya dhahabu katika Kuba moja na kwenye minara. Ni jambo la kufurahisha kuona kwamba tarehe zote za mabadiliko hayo zimeandikwa waziwazi. (Soma Kitabu cha maarifa yote kiitwacho "Encyclopaedia of Islam", chini ya kichwa cha habari "Kadhimain".

Hivyo ni wazi kwamba kuna miaka mia saba ya historia ya Kuba hili, kabla ya muda wa kutengenezwa kwa sasa kulikofanywa na Shah Ismail wa Kwanza. Maimamu wawili waliishi katika siku za awali za mji wa Baghdad ambapo kuta za Mji wa Mviringo wa mfalme Mansur katika upande wa Magharibi wa mto Tigris zilipokuwa bado zimesimama. Palikuwa na sehemu ya makaburi upande wa Kaskazini na Kaskazini ya magharibi zilizokuwa na majina kadhaa; likiwemo lile la Lango la Shamu, Ukoo wa Bani Abbas na lile la Lango la Majani Makavu, (Soma kitabu kiitwacho 'Tabaqat' cha Bwana Ibn Saad).

Maimamu hao wawili walizikwa karibu sana na kaburi la mwisho la upande wa Magharibi lakini wakati Bwana Ya'qubi, alipoandika kitabu chake cha Historia, sehemu yote ya Kaskazini ilikuwa imetengwa kwa ajili ya makaburi ya Maquraishi (Soma kitabu kiitwacho 'Tarikh') cha Bwana Yaqubi.

MWISHO

YALIYOMO

NGUZO YA UCHAMUNGU 1

NGUZO YA UCHAMUNGU 2

IMAMAH KATIKA QUR'ANI NA HADITHI 2

SHUKRANI 3

UTANGULIZI 3

JINA LA NASABA YAKE 3

KUZALIWA KWAKE 3

KULELEWA KWAKE 3

SAFARI YA KWANZA KWENDA IRAQ 3

MAJADILIANO KATI YAKE NA WANAVYUONI 3

NGUZO YA UCHAMUNGU 5

KURUDI MADINA 5

TABIA YAKE ADHIMU 5

IMAMU MUHAMMAD TAQI [a.s] AKIWA MWALIMU WA DINI 5

SAFARI YAKE YA MWISHO KWENDA IRAQ 5

KUFARIKI KWAKE 5

MASAYYIDI WA UKOO WA RIDHAWI 5

HADITHI ZA IMAMU MUHAMMAD TAQI [a.s] 5

MAELEZO MACHACHE KUHUSU KABURI LA KADHIMAIN 5

MWISHO 6