MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 60%

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA Mwandishi:
: AMIRALY M.H.DATOO
Kundi: Vitabu mbali mbali

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 17024 / Pakua: 3232
Kiwango Kiwango Kiwango
MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

Mwandishi:
Swahili

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

KIMEANDIKWA NA: 'AYATULLAH AL-'UDHMA NASIR MAKARIM SHIRAZI.

KIMETARJUMIWA NA :

AMIRALY M. H. DATOO

( Bukoba - Tanzania)

YALIYOMO

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 1

MANENO MAWILI YA MTARJUM 8

KWA JINA LA ALLAH SWT , AMBAYE NI RAHMAAN NA RAHIIM 8

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 10

SOMO LA 1: KUFIKIRIA, TAAMULI 10

SOMO LA 2: KIPIMO CHA MAJADILIANO 10

SOMO LA 3: WANAJALI VYAKULA VYA MIILI YAO LAKINI 10

SOMO LA 4 : KAZI YA KALAMU 11

SOMO LA 5 : BAINA YA WAJIBU KUBWA MBILI 11

SOMO LA 6 : SABABU ZA MAANGAMIZO YA JAMII 11

SOMO LA 7: UVIVU NA UMASIKINI 12

SOMO LA 8: ATHARI YA MVUA JUU YA MIOYO 12

SOMO LA 9: CHANZO CHA KIBURI NA UJEURI 12

SOMO LA 10: MAMBO 3 YENYE THAMANI MBELE YA ALLAH SWT 12

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 14

SOMO LA 11: KUUAWA SHAHIDI KWA AL-IMAM HUSSEIN IBN 'ALI IBN ABI TALIB A.S 14

SOMO LA 12: ALAMA MBILI ZA MWISLAMU WA KWELI 14

SOMO LA 13: MOTO WA GHADHABU 14

SOMO LA 14: VIANZIO VYA MALI 14

SOMO LA 15 : SHUGHULI MBAYA KABISA 15

SOMO LA 16 : BWANA NA MFUNGWA 15

SOMO LA 17 : UNAFIKI NA KIBURI 15

SOMO LA 18 : HUSUDA 16

SOMO LA 19 : ALIYENYIMWA NEEMA ZA ALLAH SWT 16

SOMO LA 20 : MARAFIKI WAOVU 16

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 17

SOMO LA 21 : UKAMILISHO WA KAZI 17

SOMO LA 22: MIKAKATI YA KUDUMU 17

SOMO LA 23: ADHABU KALI KABISA 17

SOMO LA 24: MAOVU YA MADENI 17

SOMO LA 25: MAISHA BORA YA KIJAMII 18

SOMO LA 26: UFUNGUO WA MAAFA 18

SOMO LA 27: ALAMA ZA WATU WA JANNAT ( PEPONI ) 18

SOMO LA 28: ALAMA ZA MNAFIKI 19

SOMO LA 29: USHAURI 19

SOMO LA 30: KUONGEA NA UKIMYA 19

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 21

SOMO LA 31: FURAHA YA USAMEHEVU 21

SOMO LA 32: ZAHID KATIKA MAANA SAHIHI 21

SOMO LA 33: KULINGANA NA MASHAHIDI 34 21

SOMO LA 34: WATU WALIO BORA 22

SOMO LA 35: IBADA ZA WATU WALIO HURU 22

SOMO LA 36: KILE KIVUNJACHO MGONGO WA MTU 22

SOMO LA 37: KUWA MSAFI 23

SOMO LA 38: HATIMA YA UJAHILI 23

SOMO LA 39: MISINGI YA MUONGOZO 23

SOMO LA 40: MASIKITIKO NI TABIA ZA UJAHILIYYAH 24

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 25

SOMO LA 4 1: KUJIPIMA MWENYEWE KILA SIKU 25

SOMO LA 4 2: NISHANI ZA IMANI NI NGUMU KULIKO CHUMA 25

SOMO LA 4 3: UHAKIKA WA UMOJA NA UADILIFU WA ALLAH SWT 25

SOMO LA 4 4: BAADHI Y ALAMA ZA IMANI 26

SOMO LA 4 5: ULIMWENGU SI MWISHO WETU BALI NI NJIA YA KUPITIA 26

SOMO LA 4 6: THAMANI YA MTU 27

SOMO LA 4 7: UKWELI NA UWONGO 27

SOMO LA 4 8: URITHI WENYE THAMANI MKUBWA WA WAARABU 27

SOMO LA 4 9: NINAWACHUKIA 28

SOMO LA 50: JITIHADA ZA WALIO WAOVU NA DHAIFU 28

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 29

SOMO LA 5 1: ALAMA ZA UKANDAMIZAJI 29

SOMO LA 5 2: HAKUNA UGONJWA USIOTIBIKA 29

SOMO LA 5 3: KWA NINI UPENDELEO HUTOKOMEA ? 29

SOMO LA 5 4: SHAHADA NA UHALISI 30

SOMO LA 5 5: WAJIPENDEAO KUJITOA MHANGA WENYEWE 30

SOMO LA 5 6: MWENYE BUSARA NA MPUMBAVU 30

SOMO LA 5 7: WAPO WACHAMUNGU WACHACHE 31

SOMO LA 5 8: UADILIFU MIONGONI MWA WATOTO 31

SOMO LA 5 9: WEWE UPO DAIMA UKIDHIBITIWA 31

SOMO LA 60: SI KUSIFU KWA KUDANGANYA, WALA SI WIVU 32

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 33

SOMO LA 6 1: DAIMA UWE TAYARI KWA AJILI YA NDUGU ZAKO 33

SOMO LA 6 2: MAKOSA MAISHANI 33

SOMO LA 63: DINI YA UISLAM ITAKUWA DINI YA ULIMWNEGU MZIMA 33

SOMO LA 6 4: USILICHUKULIE DHAMBI LOLOTE KUWA DOGO ! 34

SOMO LA 6 5: UTUKUFU WA ELIMU 34

SOMO LA 6 6: HAKI ZA WOTE 34

SOMO LA 6 7: TUMIA FEDHA KWA UTIIFU HAUTATENDA DHAMBI 35

SOMO LA 6 8: SOKO KUBWA LA KIBIASHARA 35

SOMO LA 6 9: WATU WALIOTUKUZWA 35

SOMO LA 70: KANUNI 3 ZA MISINGI YA JAMII 36

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 37

SOMO LA 7 1: HARAKA NA PUPA 37

SOMO LA 7 2: ZAHID 76 KWA HAKIKA 37

SOMO LA 7 4: MPANGO SAHIHI A DUNIA NA AKHERA 38

SOMO LA 7 5: ATHARI ZA DHAMBI 38

SOMO LA 7 6: SHI'A SAHIHI 38

SOMO LA 7 7: NI NANI TUMWULIZE ? 39

SOMO LA 7 8: NEEMA ILIYO BORA KABISA 39

SOMO LA 7 9: IMAM A.S. ASIYEONEKANA 39

SOMO LA 80: USIYASIKILIZE YALE YOTE YANAYOTAMKWA ! 40

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 41

SOMO LA 8 1: WATU MASHETANI 41

SOMO LA 8 2: FURAHA YA UHAKIKA 41

SOMO LA 8 3: MTAJI WENYE THAMANI 41

SOMO LA 8 4: VITU 2 HUSABABISHA MAANGAMIZO YA WATU 41

SOMO LA 8 5: HAKUNA WEMA ULIO MDOGO 42

SOMO LA 8 6: USITENDE DHAMBI HAUTAOMBA MSAMAHA 42

SOMO LA 8 7: MAISHA MAOVU KABISA 42

SOMO LA 8 8: AHADI ZETU NDIZO MADENI YETU 43

SOMO LA 8 9: MALI HARAMU 43

SOMO LA 90: USIMWOMBE MTU KITU CHOCHOTE 43

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 44

SOMO LA 9 1: AMELAANIWA MTU KAMA HUYU! 44

SOMO LA 9 2: TUSISULUHISHE MATATIZO KWA DHAMBI! 44

SOMO LA 9 3: KUTOSHEKA MWENYEWE ! 44

SOMO LA 9 4: NDUGU NA JAMAA WA KARIBU NA MBALI 44

SOMO LA 9 5: KUTUPILIA MBALI TABIA 45

SOMO LA 9 6: TUKIO LA KARBALA 45

SOMO LA 9 7: JE NI NANI ALIYE MWENYE BUSARA ? 45

SOMO LA 9 8: SABABU ZA UADUI 45

SOMO LA 9 9: UHALISI 46

SOMO LA 100 : MWENYE BARAKA 46

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 47

SOMO LA 101: MIKONO BORA KABISA 47

SOMO LA 102: OVU HATA KULIKO MAUTI 47

SOMO LA 103: UTAMBULISHO BAINA YA MUMINI NA MNAFIKI 47

SOMO LA 104: URITHI BORA KABISA 48

SOMO LA 105: KUHESHIMU UHURU WA FIKARA 48

SOMO LA 106: SIFA 6 ZISIZO NDANI MWA MUMIN 48

SOMO LA 107: USIVUNJE UHUSIANO WOTE 49

SOMO LA 108: IBADA SAHIHI 49

SOMO LA 109: USILISAHAU KOSA LAKO 49

SOMO LA 110: ADHABU KUBWA 50

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 51

SOMO LA 111: QURAN TUKUFU NI YA KILA ZAMA 51

SOMO LA 112: JITAHADHARISHE NA MATAMANIO 51

SOMO LA 113: NJIA MOJA TU YA KUWA SHI'A 51

SOMO LA 114: UHUSIANO WA MALI NA MATUMIZI! 52

SOMO LA 116: MAISHA NA KUENDESHA NYUMBA 52

SOMO LA 117: SAA NZIMA YA UADILIFU 53

SOMO LA 118: MGANGA WA KWELI 53

SOMO LA 119: MAKHALIFA WA MTUME S.A.W.W 53

SOMO LA 120: FURAHA YENEY MADHAMBI 54

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 55

SOMO LA 121: UFANYE KAZI ZINAZOZALISHA 55

SOMO LA 122: UREFU NA UFUPI WA MAISHA 55

SOMO LA 123: URAFIKI NA SHETANI! 55

SOMO LA 124: POKEA USHAURI ILI UONGOZWE ! 56

SOMO LA 125: SALAAM, KUSALIMIANA KIISLAMU 56

SOMO LA 126: KUTOKUKUBALIANA KWA IMANI NA MATENDO 56

SOMO LA 127: ADHABU ZA ALLAH SWT ! 57

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 59

SOMO LA 131: MILANGO ILIYOFUNGWA ITAFUNGULIWA 59

SOMO LA 132: JITAHADHARISHE NA WAOVU! 59

SOMO LA 133: VITA VIKUU 59

SOMO LA 134: GHAIBU IMAM MUHAMMAD MAHDI A.S 60

SOMO LA 135: CHANZO CHA MAOVU 60

SOMO LA 136: KUTIMIZA WAJIBU NDIYO IBADA KUU 60

SOMO LA 137: MAKAZI KATIKA SAYARI 61

SOMO LA 138: QUR'AN TUKUFU NA KANUNI YA UZITO 61

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 63

SOMO LA 14 1: LITABAKIA JINA TU KUTOKEA ISLAM 63

SOMO LA 14 2: KUTAMBUA UWEREVU NA UJAHILI 63

SOMO LA 14 3: ZAIDI YA NEEMA 63

SOMO LA 14 4: KUHUISHA SIRA ZA MA'ASUMIIN A.S 64

SOMO LA 14 5: SIRI NI AMANA 64

SOMO LA 14 6: ALAMA ZA IMANI YA DINI YA ISLAM 64

SOMO LA 14 7: SHARTI LA KWANZA KWA AJILI YA KILA KAZI 65

SOMO LA 14 8: UMUHIMU WA WAGENI 65

SOMO LA 1 4 9: HESHIMA NA MAPENZI 65

VITABU VILIVYOKUSANYWA NA KUTARJUMIWA NA AMIRALY M. H. DATOO 67

VITABU VILIVYOTAYARI 67

VITABU VINAVYOTAYARISHWA 68

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 70

MAREJEO (REFERENCES) 70

MANENO MAWILI YA MTARJUM

KWA JINA LA ALLAH SWT , AMBAYE NI RAHMAAN NA RAHIIM

Katika historia ya Dini ya Kislam na hususan Madhehebu ya Shi'a Ithna-Ashariyyah wamekuwapo na bado wapo Maulamaa ambao kwa hakika wametoa michango yao mikubwa katika kuuelemisha Ummah juu ya masuala mbalimbali yakiwemo ya kidunia, kijamii na kiroho vile vile.

Ni matumaini yangu kuwa kitabu hiki kitakuwa ni mwongozo katika mwelekeo na mwenendo wa Kiislamu katika masuala mbalimbali ya humu duniani na kutufaidisha Aakhera. Kazi ya awali ilikuwa katika lugha ya Kiajemi ambayo ilitarjumiwa katika Kiingereza na Ndg. Munir Shafe'i na ndipo nilipotarjumia katika Kiswahili.

Wabillahi tawfiq,

Amiraly M.H.Datoo

P. O. Box 838

Bukoba- Tanzania (E.Africa)

13 Ramadhaan al-Mubarak 1424 H (8 Novemba 2003 )

Barua Pepe : datooam@hotmail.com

Utapata hazina kubwa ya 'ilimu katika : www.dartabligh.org na

www.Alitrah.org na www.al-islam.org/kiswahili

UTANGULIZI

Mtaji wetu mkubwa baada ya Kitabu Kitakatifu, Qur'an Tukufu, ni Sunnah na Sirah za bwana wetu mtukufu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Ahlul Bayt(a.s) ya wanayumba wake, kwa hakika vitu hivi viwili ni vizito mno baada ya kifo chake na kwa hakika kwa kushikamana navyo kutawaokoa wanaadamu wasipotoke wala kukosea.

Kwa bahati mbaya, Ahadith hizi ambazo ni bahari ya sayansi na elimu, hazijajulikana vile ipasavyo. Kwa hakika zipo Ahadith nyingi mno katika kipimo kidogo ambamo kitabu cha maisha kipo kimejificha na kwa hakika kinaweza kutatua matatizo yote ambayo yanamkabili mwanadamu wa leo katika masuala mbalimbali.

Kitabu hiki ambacho ni mkusanyiko wa Ahadith na riwaya hizo zilizotarjumiwa pamoja na maelezo machache kwa mukhtasari. Kwa hakika Hadith hizi zilikuwa zikitolewa kila Siku ya Ijumaa katika Msikiti wa Imam Hussein(a.s) ( Teheran, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran) wakati wa mazungumzo na majadiliano ya Kidini na kisayansi, kwa hakika kila mmoja aliweza kuizingatia kwa muda wa juma zima kama ndilo somo lao, na wengi wa vijana, wavulana kwa wasichana, waliziihifdhi (walizikariri) mioyoni mwao.

Kwa hakika upokeo wake ulivyokuwa ukionekana na kuvutia, ilisababisha kuchapwa na kutolewa kila mahala. Hivyo kitabu hiki kidogo kitakuwa ni mwongozo kwa wale wote ambao wanataka kuuelewa Uislamu vyema kwa njia ya mafundisho madogo. Lakini jambo lililo la muhimu na maana ni kule kufuata na kutekeleza maamrisho na maongozo hayo.

Hivyo sote kwa pamoja tumwombe Allah swt atujaalie tawfiq ya kuelewa na kuweza kutekeleza kwa mujibu wa Ahadith hizi na hatimaye kuzingatia na kujipima. Qum, Nasir Makarim Shirazi, 1976

1

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 1: KUFIKIRIA, TAAMULI

Uwe tahadhari ! Elimu isiyo ambatana na ufikiriaji, haina faida. Uwe tahadhari ! Usomaji wa Qur'an Tukufu iwapo hautakuwa na ufikiriaji, basi hautakuwa na maana ! Uwe tahadhari ! 'Ibada isiyo na fikara ndani mwake, haina athari yake.1

Maelezo mafupi: Kuujaza ubongo wa mtu kwa kanuni za kisayansi, mantiki na kifalsafa, au na elimu yoyote itakuwa na athari ndogo sana hadi hapo itakapokuwa kwa misingi ya fikara sahihi, mtazamo wazi wa ulimwengu na kuzitambua misingi ya maisha ya mwanadamu. Ama usomaji wa Qur'an Tukufu utakuwa na athari ndogo iwapo haitaambatana na uchambuzi na kuzizingatia na kuzifikiria hizo Ayah zake, 'Ibada ambayo haina nuru ya ufikiriaji na busara ni sawa na mwili usio na roho, na kukosa athari za elimu ya hali ya juu.

SOMO LA 2: KIPIMO CHA MAJADILIANO

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema :

"Kuboresha hali ya maisha na uhusiano inawezekana kwa kutumia kipimo, sehemu mbili ya tatu ni kuwa makini na theluthi moja ni upuuziaji."

Maelezo mafupi: Hakuna kazi inayoanzishwa bila ya kufanyiwa utafiti, mpango au umakini, na vile vile hakuna kazi ambayo haimaliziki bila ya upuuzaji. Itakuwa wazi kusema vyema kuwa iwapo sisi tutataka kufanya kazi pasi na uchunguzi au utafiti na umakini, basi sisi kamwe hatutafanikiwa. Lakini iwapo sisi tutataka kung'ang'ania kila jambo linaloweza kutokea bila ya kutabiriwa wakati tufanyapo kazi, basi kamwe hatutaweza kufanya kazi zetu kwa uwepesi, na itatubidi tuishie miaka mingi katika kusomea tu kwa ajili ya kufanya jambo au kumchagua rafiki, mke na mambo kama hayo. Ndiyo maana inasemwa kuwa sehemu mbili ni za umakini na theluthi moja ni ya kutokuwa makini.

SOMO LA 3: WANAJALI VYAKULA VYA MIILI YAO LAKINI

Al-Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) anasema :"Ninastaajabishwa na wale ambao hufikiria vyakula kwa ajili ya miili yao tu, lakini hawafikirii vyakula kwa ajili ya Roho zao. Wao huondoa vyakula vinavyowasumbua kutokea matumbo yao, na papo hapo wa wanazijaza nyoyo zao kwa mambo yanayoangamiza nyoyo zao." 3

Maelezo mafupi : Kama vile Al-Imam Hassan ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. alivyosema, watu huwa wanajali mno vyakula vya kula, na hawali hadi wapo katika mwanga, na hawafungui vinywa vyao hadi pale macho yao yawapo wazi. Wao hujiepusha na vyakula vyote vyenye mashaka na wengi wao huzingatia maelfu ya hatua za afya na siha zao kwa ajili ya kuzilisha miili yao. Lakini, ama kuhusiana na vyakula vya Roho, wao, huku wakiwa wamefumba macho yao katika kiza kikali, wanajilisha vyakula vya nyoyo zao zenye kushukiwa, katika nyoyo zao. Wao kwa urahisi hukubalia maneno ya marafiki wasio wema, habari zisizo kweli na sahihi na usambazaji wenye sumu na mashaka, na kwa hakika haya ni yenye kushangaza mno.

SOMO LA 4 : KAZI YA KALAMU

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema :"Mimi sijamwona mfagiaji akiwa na tabasamu njema kabisa kama kalamu." 4

Maelezo mafupi: Kalamu inadhihirisha hisia za mwanadamu na kutarjumu busara ya mwanadamu. Kalamu ni mvumbuzi wa utamaduni na kuzungusha magurudumu ya jumuiya. Kalamu huelezea maumivu ya fikara za mwanadamu kwa kuendela kulia kwake, na vile vile husisimua mapenzi, kutamani maisha, maajabu ya maisha na maelfu kwa maelfu ya mema ambayo yamefichika katika kutabasamu ambayo huwapo baina ya midomo miwili. Lakini jambo la kusikitisha ni pale ambapo kalamu inapokuwa katika mikono ya watu ambao si mustahiki wake, machozi yake hubadilika kuwa matone ya damu, na ubashasha wake huwa ni aibisho kwa mema yote ya mwanadamu.

SOMO LA 5 : BAINA YA WAJIBU KUBWA MBILI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema :Muumini mwaminifu daima huwa na shauku ya mambo mawili : Madhambi yake yaliyopita ambapo hajui vile Allah swt atakavyomshughulikia kwayo, Maisha yake yaliyobakia hajui kile atakachokifanya ! 5

Maelezo mafupi: Dalili kuu ya udhihirisho wa imani ni kuhisi na kutambua wajibu wa mtu, kwa yale aliyoyatenda na wajibu na ufaradhisho wake kwa yale yanayotakiwa kutendwa. Ama kwa hakika wale wenye hisia hizi mbili, daima huwa wanafikiria vile watakavyoweza kufidia upuuzaji wao uliopita, na vile vile kutumia mustakbal kwa njia njema kabisa. Kwa hakika fikara hizi ndizo chachu za maendeleo na usongaji mbele wa mtu au taifa. Ama wale amabo hawafikirii matendo yao ya nyuma, wala wasiojali kujenga maisha yao ya mbeleni, huwa ni masikini na wenye shida wasio bahatika.

SOMO LA 6 : SABABU ZA MAANGAMIZO YA JAMII

Yapo mambo manne iwapo mojawapo likiingia katika nyumba yoyote, basi itaangamiza nyumba hiyo na kwayo baraka za Allah swt zitatokomea : udanganyifu, wizi, ulevi na zinaa. 6

Maelezo mafupi: Kwa hakika si majumbani mwetu tu bali hata kama maovu haya yataingia katika jumuiya au jamii, basi jumuiya au jamii hiyo itaangamia na kuteketea. Wakati udanganyifu, uhaini unapopenya katika jamii, ule moyo wa kujiamini unapotea kimoja.

Na wakati wizi unapoingia, katika sura zake mbalimbali, basi amani haitapatikana kamwe. Na wakati pombe na vinywaji haramu vitakapokuwa mashuhuri na kawaida miongoni mwa watu, basiwatadhoofisha fikara zao, watakuwa na vizazi vya vijana na watoto wasiofaa katika jamii. Na wakati watakapokuwa wamejitumbukiza katika zinaa, basi misingi ya kifamilia zitadhoofika na vizazi vyao vijavyo vitakuwa vya waasherati na waovu.

SOMO LA 7: UVIVU NA UMASIKINI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s) amesema :

Siku ambapo kila kitu kiliozeshwa na mwenzake, basi uvivu na umasikini zilifungamana kwa pamoja, na mtoto wao aliyezaliwa aliitwa ufukara. 7

Maelezo mafupi Kila kitu kinapatikana au kuvunwa kwa kutokana na jitihada na bidii. Na kwa hakika haya ndiyo yaliyo mafunzo makuu ya Dini ya Islam. Uvivu, kutokufanya kazi, udhaifu na kukwepa majukumu magumu na matatizo ndiyo mambo ambayo kamwe hayawezi kupatana na moyo huu wa imani. Kwani hakutakuwapo na matokeo yoyote isipokuwa umasikini katika kila jambo, ikiwemo kiuchumi, kimaadili na umasikini wa kiimani. Wakati huo huo Waumini halisi watakuwa wanajitosheleza kwa kila jambo na watakuwa ni watu wenye kutosheka katika kila jambo.

SOMO LA 8: ATHARI YA MVUA JUU YA MIOYO

Luqman mwenye hekim alisema :

Ewe mwanangu ! Allah swt huuisha nyoyo za watu kwa nuru ya elimu kama vile anavyohuisha ardhi iliyokufa kwa baraka za mvua kutokea mbinguni ! 8

Maelezo mafupi Moyo wa mtu kama ardhi sawa na bustani ambapo kila ya aina ya mimea, mbegu za maua, miche na miti imara huwa imeenea kila mahala, na lau itapatiwa maji kwa wakati wake, basi bustani hiyo itashamiri na kupendeza mno. Kwa hakika umwagiliaji wa bustani hiyo ya mioyo yetu huhitaji matone ya mvua ya sayansi na elimu. Hivyo nyoyo ambazo hazina elimu huwa zimekufa, zisizo na nuru wala mazao yoyote. Inatubidi sisi daima tuhuishe nyoyo zetu kwa nuru ya elimu.

SOMO LA 9: CHANZO CHA KIBURI NA UJEURI

Imeripotiwa kutokea Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) kuwa :

Hakuna mtu anayeweza kujivuna au kuwa na kiburi kwa wengine hadi pale yeye mwenyewe anapokuwa na hisia za kuwa chini undani mwake! 9

Maelezo mafupi: Siku hizi, utafiti wa kiakili na kifahamu umethibitisha kuwa ujeuri na kiburi si kitu kingine bali hali ya kujiona kwa mtu mwenyewe kuwa yu chini kuliko wengineo. Wale ambao wanakuwa wameambukizwa hayo, basi hujitwisha ubandia huu kwa kuficha kasoro zao hizo, na hivyo huongezea uchini wao kijamii na kujifanya wao wakachukia zaidi. Kwa mtazamo huu wa kiakili imetambulikana vyema kabisa kutokana na msemo wa Al- Imam Ja'afar as-Sadiq a.s. lakini kwa hakika Waumini halisi daima huwa ni watu ambao wanafanya kazi zao kwa heshima kubwa undani mwao.

SOMO LA 10: MAMBO 3 YENYE THAMANI MBELE YA ALLAH SWT

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema :

Yapo mambo matatu ambayo yanaondoa pazia na kukaribia Utukufu wa Allah swt : Sauti ya harakati za kalamu ya mwandishi wa kisayansi ! Sauti za mwendo wa wapiganaji wanapokuwa katika Vita vya Jihad ! Na sauti ya gurudumu la kusuka nyuzi la mwanamke mtoharifu ! 10

Maelezo mafupi: Kwa hakika maana na maelezo yenye nasiha kubwa! Kwa hakika zipo sauti tatu ambazo zinapenya kina cha uhai na kuendelea mbele katika maumbile yasiyoangamia wala kuteketea na kuelekea katika Ukuu na Utukufu wa Allah swt : sauti ya elimu na kalamu, ingawaje inaweza kuwa dhaifu na polepole, sauti ya Vita vitakatifu na kujitolea mhanga, na sauti ya jitihada, kuendelea na kufanya kazi hata kama itaonekana ndogo kiasi gani. Na kwa hakika, mambo haya matatu, elimu,Vita Vitakatifu, na kazi vinatengeneza msingi na jumuiya ya kibinadamu iliyoheshimika.

2

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 11: KUUAWA SHAHIDI KWA AL-IMAM HUSSEIN IBN 'ALI IBN ABI TALIB A.S.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) :Kuuawa Shahidi kwa Al-Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib (a.s) imeanza vuguvugu la joto katika nyoyo za Waumini ambavyo kamwe haitapoa. 11

Maelezo mafupi: Kwa hakika tumeviona vita vingi mno ulimwenguni ambavyo vinasahaulika kwa kupita kwa muda wa miezi na miaka. Hata vivyo, ukumbusho wa harakati na vuguvugu za wale waliojitolea mhanga katika njia ya Allah swt na kwa ajili ya uhuru wa wanaadamu na vile vile kwa ajili ya heshima na mema, kamwe havitasahaulika kwa sababu Allah swt, uhuru, heshima na mema kamwe hayatazeeka. Kwa hakika Al-Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib a.s. pamoja na wafuasi wake walikuwa ndio kitovu cha hayo kama wapiganaji kwa ajili ya imani.

SOMO LA 12: ALAMA MBILI ZA MWISLAMU WA KWELI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) :Usiheshimu tu wingi wa Sala, Saumu, Hijja, uchamungu na ukeshwaji wao katika ibada ( ingawaje hayo ni muhimu upande wao wenyewe ). Badala yake angalieni ukweli, uadilifu na uaminifu wao ! " 12

Maelezo mafupi Tukisoma nyaraka za Kiislamu, tunapambanuliwa bayana ukweli huu wa alama za Mwislamu halisi awe ni mkweli, mwadilifu na mwaminifu, na ingawaje katika Islam Sala, Saumu, Hajj ni ibada za hali ya juu, lakini hizo si dalili za Uislamu na badala yake zinatakiwa zitekelezwe pamoja na ukweli, uadilifu na uaminifu.

SOMO LA 13: MOTO WA GHADHABU

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) anasema :

Kwa hakika ghadhabu ni miale ya mioto ambayo huwashwa na Sheitani katika nyoyo za Wanaadamu . 13

Maelezo mafupi: Wakati mtu aliye katika hali ya ghadhabu (hasira) anapotenda kitu au kufanya uamuzi, mara nyingi imeonekana kuwa huja kujuta majuto na kusikitika kwa sababu mito ya ghadhabu imemsababisha yeye kutokuwa mwangalifu na makini kutokea fahamu na busara zake, na kwa ujumla, msisimko na hisia zake humwelekeza mahala ambapo hakutawezekana kufidia hasara hizo maishani mwake ! Inatubidi sisi tuweze kuuzima moto huu wa Kishetani kwa haraka iwezekanavyo na kwa uangalifu mkubwa. Ama sivyo, inawezekana ikateketeza maisha yetu na ya wengine.

SOMO LA 14: VIANZIO VYA MALI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema :

Tafuteni riziki yenu ndani mwa ardhi . 14 Maelezo mafupi Maagizo haya yalikuwa yametolewa na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) wakati ambapo kulipokuja kujulikana kuhusu machimbo ya vito vya thamani na mengineyo mengi ndani ya ardhi, ikimaanisha kuwa Waislamu inawabidi wapeleleze chini ya ardhi kwa ajili ya kujipatia riziki zao na kwa ajili ya mahitajio yao ya maishani. Kwa hakika maamrisho kama haya ni dalili za uzito wa maamrisho ya Kiislamu na vile vile ni somo la jitihada na juhudi na ni kwa ajili ya Waislamu kuishi maisha mema na yenye heshima!

SOMO LA 15 : SHUGHULI MBAYA KABISA

Na Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) vile vile amesema :

Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema kuwa:shughuli iliyo ovu kabisa ni ile ambayo imechangnyikana na riba . Vile vile Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) amesema :"Wakati Allah swt anapotaka kuuangmiza ummah, basi humo kutakuwa kumetokezea riba . 15

Maelezo mafupi Pamoja na kuwa na soko rahisi la riba kushamiri katika ulimwengu wa kisasa, na kutegemea mno kwa dunia ya kisasa juu ya riba katika sura mbalimbali, ni dhahiri kuwa riba inaangamiza taratibu zote za kifedha na kiuchumi za jamii na hatimaye kusababisha kulimbikizana kwa utajiri uliokithiri mikononi mwa matajiri wachache na taasisi, kwa hakika kuwapo kwa mgawanyo wa aina hii ndicho chanzo cha matatizo na maangamizo ya kijamii na ufisadi wa kimaadili.

SOMO LA 16 : BWANA NA MFUNGWA

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema :

Mfanyie fadhila mtu yeyote, nawe utakua bwana wake ! Usimwombe mtu yeyote, ama sivyo utakuwa kama yeye ! Kuwa na haja ya mtu yeyote, itakufanya wewe uwe mfungwa wake ! 16

Maelezo mafupi: Kanuni hii inaongoza kwa nguvu juu ya uhusiano wa kijamii wa mtu binafsi na mataifa, kuwa daima mikono yenye kutoa huwa daima ni mabwana na mikono inayopokea huwa ni duni. Mataifa au watu muhtaji kwa hakika ni watumwa ambao wametia saini zao za utumwa wao kwa kupitia msaada kutokea wengineo. Kwa hakika Mwislamu wa kweli hujaribu kuufanya uhusiano wake juu ya misingi ya maelewano, na wala si kuegemea msaada upande mmoja. Kwa hakika kutolewa kwa misaada ya shukuruani iwe imelengwa kwa wale walio mustahiki na dhaifu.

SOMO LA 17 : UNAFIKI NA KIBURI

Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) amesema :

Usitende matendo yako kwa kujionyesha au kiburi kwa watu ambao hawana uwezo juu ya maisha wala vifo yao, na ambao hawawezi kukutatulia matatizo yako. 17

Maelezo mafupi: Udhihirisho wote wa maisha ya wale ambao wamezoea kiburi na unafiki yanakuwa tupu. Wao wanakuwa na udhihirisho usio na moyo kutokea maendeleo, ufikirio na mazua zua kutokea uhai, hakuna umashuhuri kutokea furaha na utajiri, na maendeleo isipokuwa ni kutokana na Dini tu, na kwa hakika watu wenye kiburi hawajipatii chochote isipokuwa kujionyesha tu ! Kwa hakika ndiyo maana Dini ya Islam imekanusha kwa nguvu sifa hii mbaya na imesema kuwa hatima yako haipo chini ya watu hawa, sasa je kwa nini unajidai na kufanya kiburi ?

SOMO LA 18 : HUSUDA

Al-Imam Ja'afar as-Sadiq(a.s) amesema:

Mtu mwenye husuda hujifikishia hasara yeye mwenyewe kabla hajawafanyia wale anaowahusudu . 18

Maelezo mafupi: Moyo wa husuda ni ule ambao hauvumilii wengine wawapo na neema, na hujaribu kuwakosesha wao kutokana na neema hiyo, au kujaribu kuwapatia hasara kwa njia zinginezo. Kwa hakika, hasidi (mtu mwenye husuda) huwa ni mtu mwenye kurudi nyuma na kamwe si mwenye maendeleo.

Husuda kwa hakika ni ugonjwa mwovu kabisa wa kimaadili katika jamii na kwa mtizamo wa kiakili, mtu mwenye husuda huwa katika hasara zaidi na hufifia, hurudi nyuma na kudhalilika zaidi kuliko wengineo. Hivyo ni vyema kwa ajili yake kujaribu kujiendeleza kuliko kujishughulisha kuwarudisha nyuma wengineo.

SOMO LA 19 : ALIYENYIMWA NEEMA ZA ALLAH SWT

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s) amesema :

Yeyote yule aliye na maji na ardhi, na bado akabakia kuwa masikini na mwenye shida, basi huyo atakuwa amenyimwa neema za Allah swt ! 19

Maelezo mafupi: Kwa mujibu wa Ahadith na Riwaya za Dini ya Kiislamu, imesisitizwa mno kwa Waislamu ulimwenguni kote, kutumia vianzio mbalimbali kama ufugaji wa wanyama, kilimo, uchimbaji wa madini, vito na mali ghafi nyinginezo, ustadi, viwanda na biashara kwa ajili ya kupigana vita dhidi ya umasikini. Iwapo nchi yoyote itakuwa nacho chochote kati ya hizo, basi watumie kwa ajili ya kutimiza mahitaji yao ya kiuchumi. Sasa hebu fikiria kwa wale ambao wanavyo yote hayo. Ama sivyo watalaaniwa na kunyimwa neema za Allah swt na moyo wa Uislam. Kwa hakika tabia ya kuomba omba imelaaniwa vikali katika mtazamo wa Dini ya Islam.

SOMO LA 20 : MARAFIKI WAOVU

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema :

Marafiki zako waovu kabisa ni wale wanaokusifu na kuongea nawe maneno mengi kama maji na wanazificha aibu zako. 20

Maelezo mafupi: Kwa kukwepa uhakika wa maisha na kuficha ukweli, haya kamwe hayawezi kutatua matatizo yoyote, na wala haiwezekani kusemwa kuwa itaweza kumsaidia mtu yeyote. Kwa hivyo wale marafiki ambao hujaribu kuficha ukweli badala ya kukushutumu wewe kwa ajili ya kujirekebisha, na huficha makosa na kasoro za marafiki zao kwa kufurahika na udanganyifu, au wanaonyesha hivyo kama wema, si kwamba wao wameshindwa kuwa waaminifu katika urafiki wao, bali wametenda dhambi kubwa mno la udanganyifu na usaliti. Usaliti wao huo utaweza kuja kumharibia heshima, hadhi na mafanikio ya rafiki yao huyo.

9

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w) NA MA-IMAMU (a.s)

KUSEMA UONGO

498. Anas Ibn Maliki Khisal-i-Sadduq, Uk. 321: Anaelezea kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Chukueni mambo sita kutoka kwangu, na mimi nakubalia, na kutoa dhamana (Ya wewe kuingizwa Jannat)

1. Usiseme uongo

2.Unapo toa ahadi, usivunje

3. Unapo pewa amana na wengine, basi uwemuaminifu

4. Tazama chini ( usitende dhambi ).

5. Chunga heshima yako

6. Idhibiti mikono yako na ulimi wako.

499. Amesema Imam Al Hassan al-'Askari(a.s) : "Iwapo maovu yote yatawekwa katika nyunba moja, basi ufunguo ( wa milango yake ) itakuwa ni uongo ."[213] .

500. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Jiepusheni na kusema uongo hata kama ni uongo mgogo au mkubwa, kama kwa wadilifu au unasema kwa kdhihaki, kwasababu mtu anapo sema uongo mdogo basi anaweza kudiriki kusema uongo mkubwa pia.[214] .

501. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : Wakati mmoja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliulizwa kuhusu umbali baina ya ukweli na uongo naye akiwa akionyesha umbali huo baina ya macho yake na maskio yake kwa vidole vinne katika kutoa jibu hilo, "Kile majo yako yanayooonani ukweli na mengi na yale yanayo sikilizwa na maskio yako ni sehemu kubwa ni uongo."[215] .

502. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameyawekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[216]

503. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wasema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[217]

504. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameya wekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[218] .

505. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wa sema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[219] .

MARAFIKI NA URAFIKI

506. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Mtu anaathirika kwa imani ya marafiki zake. Kwa hivyo, muwe waangalifu kabisa katika urafiki wenu pamoja nao . " [220]

507. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) , Amesema: "Uwe rafiki wa yule ambaye atakuwa ndio heshima yako, si wewe uwe heshima yake. (Ufanye urafiki na wale walio juu yako ili wewe uweze kupata maendeleo kutokana na urafiki huo).[221] .

508. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Ndugu yangu mpenzi ni yule (anayenitambulisha) makosa na kasoro zangu.[222]

509. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kwa hakika kuna marafiki wa aina tatu kwa ajili ya Muislam:

1. Rafiki anayesema mimi niko pamoja nawe iwapo upo hai au umekufa: Na hili ndio matendo yake.

2. Rafiki anayesema mimi nipo rafiki wako hadi ukingoni mwa kaburi na nitakuacha:hawa ni watoto wake.

3. Rafiki anayesema mimi nitakuwa nawe hadi pale utakapo kufa:hii ni mali ambayo ataiacha humu duniani kwa warithi wake baada ya kifo chake.[223]

Tanbih Kutokana na riwaya hii, na kama hizi sisi tunaelewa kuwa kitu ambacho kitakuwa pamoja na huyo mtu aliye kufa na kuaga dunia hii katika siku ya Qiyamah imani na matendo yake mema. Na suala hili limezungumziwa katika ahadithi nyingi sana za Kiislam na vile vile katika ayah za Qur'an tukufu, kwa mfano:

510. Allah swt anatuambia: Wale walio amini na wakatenda mema watakuwa na raha na marejeo mazuri. (Qur'an, 13:29).

511. Allah swt anatuambia: Hakika wale walio amini na wakatenda mema - hakika Sisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema. (Qur'an,18: 30).

512. Allah swt anatuambi: Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi. (Qur'an, 18: 107).

513. Allah swt anatuambia:" Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi. (Qur'an,19: 96).

514. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Muwe waangalifu katika kutafuta marafiki wa kweli na mujaribu kuwafanyia majaribio, kwa sababu wao watakuwa ndio msaada wenu pale mnapokuwa katika hali nzuri na watetezi wenu pale mtapokuwa katika shida na matatizo."[224]

515. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Kukutana pamoja na wacha Mungut kunawaleteeni mema ."[225]

516. Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) . Amesema: "Jitahadharisheni na urafiki wa watendao madhambi, na kuwasaidia madhalimu ."[226]

MARAFIKI WASIO WEMA

517. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Anayetafuta uhusiano na marafiki wa wale wanao wadhalilisha wapenzi wa Allah swt basi watambue kuwa wao wamemuasi Allah swt ."[227]

518. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Mnapojulishwa kuhusu marafiki zenu wanapotenda maovu, nendeni mumwambie: Ewe fulani bin fulani ! Ama acha kutenda madhambi au ukae mbali nasi: Na hapo utengane naye hadi atakapo acha kutenda maovu.[228]

519. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili kutoka baba yake Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . ambaye Amesema kuwa baba yake Al Imam Hussein ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Ewe mwanangu! Jichunge na makundi matano na kamwe usifanye urafiki nao, wala usiongee nao na wala usifanye urafiki pamoja nao. Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . alimuuliza baba yake Je ni makundi gani hayo matano. Imam(a.s) . alimujibu: Jitahadharishe na wala usifanye urafiki pamoja na yule msema uongo kwa sababu yeye ni kama mazua mazua anaye kufanyia vitu vya mbali vikawa karibu, na anakifanya kiwe mbali kile ambacho kiko karibu nawe.[229]

Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na mtu ambaye hana tabia njema, kwa sababu atakuuza kwa thamani kwa tonge moja au hata chini ya hiyo. Jihadhari na wala usifanye uhusiano na bahili kwa sababu yeye atakunyima kutoka mali yake pale wewe utakapo hitaji hasa. Jihadhari na usifanye urafiki pamoja na mpumbavu, kwa sababu yeye atataka kukufaidisha wewe lakini kwa uhakika anakudhuru zaidi. Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na yule ambaye hawajali ndugu na maJama'a zake, kwa sababu mimi nimemona mtu kama huyo akilaaniwa katika kitabu cha Allah swt (yaani Qur'an Tukufu) katika sehemu tatu.

Nayo ni: Sura Al Baqarah, 2, Ayah ya 27; Wanao vunja ahadi ya Allah swt baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo amrisha Allah swt kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye Khasara. Sura Al-Raa'd, 13, ayah ya 25 Na wale wano vunja ahadi ya Allah swt baada ya kuzifunga, na wanakata aliy amrisha Allah swt yaungwe, na wanafanya fisadi katika nchi: Hao ndio watakao pata laana, na watapata Nyumba mbaya. Sura Muh'ammad, 47, ayah 22 Basi yanayo tarajiwa kwenu mkitawala ndio mfisidi katika nchi na mwatupe Jama'a zenu ?

520. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Ewe Kumail ! sema kile kilichopo katika hali yoyote ile. Uwe marafiki pamoja na wacha Allah swt na jiepushe na watendao maovu, jiweke mbali na wanafiki na usiwe pamoja na wadanganyifu na wahalifu na wahaini ."[230]

KUWAHUDUMIA WATU

521. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye mpuuzia ndugu yake Muislam mwenzake matatizo na shida za dunia hizi, basi Allah swt atampunguzia shida na matatizo yake huko Akhera ." [231]

522. Amesema Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Kwa hakika, maombi ya shida za watu zinazokuijia wewe ni miongoni mwa neema na baraka za Allah swt juu yako. Hivyo usisikitike kwa sababu ya neema na baraka hizi ."[232]

523. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Popote pale utakapoona ndugu yako Muislam ana shida, jaribu kuangalia kama utaweza kumusaidia. (Usimpuuze mpaka akutamkie shida zake.) "[233]

524. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa amenakili kutoka mababu zake(a.s) . ambao wamemnakili Mtume Muhammad(s.a.w.w) akisema: "Yeyote yule anayemlisha muumin aliye na njaa akashiba basi Allah swt atamlisha mpaka ashibe kutoka matunda ya Jannah; Na yeyote yule atakaye mvisha nguo yule aliye na shida za nguo, Allah swt atamvisha nguo zilizofumwa na za hariri, na yeyote yule atakaye mumalizia kiu muumin basi Allah swt atamjaalia kinywaji kilichopigwa lakiri; Na yeyote atakaye msaidia muumin kupunguza shida yake, basi Allah swt atamweka chini ya Arshi yake siku ya Qiyama siku ambayo hakutakuwa na kivuli chochote isipokuwa kivuli cha Arshi yake."[234]

525. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Watu wanamtegemea Allah swt kwa ajili ya riziki, kwa hiyo mpenzi miongoni mwa watu kwake Allah swt ni yule ambaye anawasaidia wale watu wanaomtegemea Allah swt na kuwafanya watu wa familia ya nyumbani wakawa na furaha."[235] .

526. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye wasaidia Waislam ndugu zake wakati wa shida, Allah swt atamwondolea shida na matatizo sabini na tatu, moja ambayo ni ambayo iko humu duniani na sabini na mbili zingine zitakazo kuwa wakati wa shida kubwa, ambapo watu watakuwa mashughuli katika mambo yao ya binafsi (katika Akhera) ." [236]

KUTOA MIKOPO

527. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayeijiwa na ndugu yake Muislam kwa ajili ya kukopa na kama yeye hampi mkopo, basi Allah swt atamharamishia kuingia Jannat siku ambayo waja mema watakuwa wakilipwa na kufidiwa ." [237]

528. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayetakiwa na ndugu yake Muislam kwa kukopeshwa na kama yeye hamkopeshi mkopo, Allah swt atamzuia kuingia Jannat siku ambayo waja wema watakuwa wakilipwa mema yao ." [238]

KUWASAIDIA WENYE SHIDA

529. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Waulizeni maswali walio elimika, muongee pamoja na wale wenye hekima, na mujihusishe pamoja na masikini."[239]

530. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Sababu mojawapo ya kuteketea na kupotea kwa mali na utajiri wa mtu ni kule kutowajali na kutowasaidia wale wenye shida."[240]

531. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mtume Muhammad (s.a.w.w) amemnakili Allah swt kwa kuameambiwa usiku wa Mi'raj: Ewe Ahamad! Mapenzi yangu ni kule kuwapenda masikini. Wafanye masikini wawe karibu nawe na uwaweke karibu nawe ili mimi niweze kukufikia wewe .."[241]

532. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Yeyote yule anayemmalizia muumin njaa yake kiasi kwamba akaridhika kikamilifu, basi hakuna binadamu yeyote miongoni mwetu au miongoni mwa Malaika wanaojua kiasi cha thawabu yake siku ya Qiyamah isipokuwa Allah swt mmiliki wa Malimwengu yote. Na aliongezea: Kumlisha Muislam aliye na njaa ni njia moja kubwa sana ya kuomba Tawba( usamehevu)."[242]

Baada ya hapo alisoma ayah ya Qur'an Tukufu Sura Al-Balad, 90, ayah 14 - 16. Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye Jama'a, Au masikini aliye vumbini.

ZAWADI NA KUWAFURAHISHA MUUMIN

533. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Wakati sadaka inapotolewa na mtu kutoka mikononi mwake, basi hiyo sadaka inasema: Mimi nilikuwa kitu cha kwisha, lakini wewe umenipa maisha; Mimi nilikuwa sina thamani sasa wewe umenifanya niwe na thamani kubwa; mimi nilikuwa ni adui nawe umenifanya mie kuwa rafiki; Wewe ulikuwa daima ukinilinda na kunihifadhi lakini sasa mimi nitakulinda na kukuhifadhi hadi siku ya Qiyamah ." [243]

534. Amesema Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) : "Yeyote yule atakaye mfurahisha Muumin, basi kwa hakika kwanza kabisa amemfurahisha Allah swt, na pili amemfurahisha Mtume Muhammad (s.a.w.w) na tatu ametufurahisha sisi Ahlul Bayt (a.s) "[244]

535. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Allah swt ameweka mahitaji ya wale wasio na uwezo katika mali ya matajiri. Kwa hivyo atakapokuwa mtu asiye na uwezo akabakia katika hali ya njaa basi ni kwa sababu matajiri wamemnyima haki yake ."[245] .

536. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Kwa kiapo cha Allah swt! Yeyote yule anayeizuia mali yake isiwasaidie Mumin wenye shida basi siku ya Qiyamah kamwe hawataonja chakula cha Jannat wala Kinywaji kilichopigwa Lakiri."[246]

SADAKA NA MISAADA

537. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah ."

538. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya ."

539. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema." Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akaendelea kusema: "Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika barak a."

540. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya .

541. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . katika kuelezea tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl, 92, Ayah ya 5 na 6: Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu. Ndipo amesema kuwa; Allah swt ndivyo anavyo walipa wale watendao mema, kwa mema yao mara kumi, au hata mara laki moja na hata zaidi ya hapo. Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi."

542. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa."

543. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka ."

544. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu ."

545. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjipatie riziki ."

546. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu. Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali kwa kile huyu mtu akitoacho katika mali yake ."

547. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu! Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi ".

548. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Kuwa mali halisi ya mtu ni ile ambayo yeye ametolea sadaka ."

549. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima ."

550. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam ."

551. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa akisema: "Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka ."

552. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . katika Nahjul Balagha amesema kuwa: "Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt ."

553. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima, "Awe na tabia njema, "Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa "Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo) " Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji (anaotoa katika njia ya Allah swt ).

554. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na nikawarudishia heshima yao miongoni mwa watu, basi mimi ninaona jambo hili ni afadhali na bora zaidi kuliko hata kwenda kuhiji Hijja sabini. "

555. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . aliijiwa na mtu mmoja na aliyeuliza, "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w)! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru ?"

556. Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimjibu kuwa: "Kuwa mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi."

557. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Siku moja Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Maimuna binti Harun, Je Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , 'Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi nimemfanya huru.' Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwambia "Iwapo kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea huruma basi ingekuwa afadhali zaidi."

558. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini ."

559. Siku moja walikuja wagonjwa wakilalamikia magonjwa yao mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ., naye akawaambia; "Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya ."

560. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . aliulizwa na Sahaba mmoja: "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo." Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . kamwambia: "Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo." Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alipomtembelea huyo mtu akamwambia, "Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata kama kitakuwa ni kipande kidogo tu. Utambue wazi kuwa kiasi chochote kile hata kikiwa kiasi gani kama kitatolewa kwa roho safi basi mbele ya Allah huwa ni kipenzi, kwani Allah swt ameelezea kuwa: Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! (Qur'an,99: 7 – 8).

561. Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alimwelezea kuwa: "Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Balad,90, Ayah11 - 16 Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? Kumkomboa mtumwa; Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye jamaa, Au masikini aliye vumbini

"Hivyo ewe Sahabi uelewe kuwa Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au watakao walisha yatima na masikini."

562. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu: "Toa Sadaka kwa niaba yake." Na mtu huyo akajibu kuwa "Sasa mtoto wake amekuwa na umri yaani amekuwa kijana." Basi Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimwambia kuwa "Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . kuwa: "Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo. Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza 'Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?' Kwa hayo mtoto akajibu "Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.' Kwa hayo baba yake akasema "Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo."

563. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia 'ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe."

564. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua ".

565. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) katika hadith zake amesema kuwa: "Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji ."

566. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Kuna aina tatu ya mikono wa " kwanza ni mkono ule wa Allah swt ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt, " mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na " mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt na musikalifishe nafisi zenu".

567. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.

Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt."

568. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa' ya tende, na kama sa' moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka. Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia 'Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe umejiandalia nini?' Na hapo wewe utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt."

569. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu." Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa katika mali yenu. Na miongoni mwa jamaa zenu wanapokuwa na shida muwasaidiapo hiyo siyo Sadaka bali hiyo ni wajibu wenu."

570. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka themanini. Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake. Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba. Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake. Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu."

571. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amesema kuwa; " Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi. Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba: 'Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.

Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt ni kwamba, Allah swt alimtuma Malaika Jibrail(a.s) kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili(a.s) . akamwambia 'Ewe bibi kizee! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake."

572. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: " Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka. Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo (mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana."

573. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa : "Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza, kama vile mwanadamu anavyowatunza watoto wake.

Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud, milima mikubwa sana."

574. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima ."

575. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima ."

576. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka ."

577. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s).! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri .

Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka hao haitakuwa ni Sadaka. Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .!Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka ."

578. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza mtu mmoja "Je leo umefunga Saumu?" Mtu huyo alijibu "La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza: "Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?" Naye akajibu: "Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.

579. Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza: "Je umemlisha masikini yeyote?" Naye akajibu: "Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) !" Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwambia huyo mtu: "Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee na uwe nao kwa mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka yako kwao."

580. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ambaye ameseama: "kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu."

581. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ili kutaka kuepukana na shari za madhalimu basi toeni Sadaka ."

582. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake : "Myahudi huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka. Myahudi huyo kama kawaida yake alikata kuni na alijitwisha kichwani mwake na akarud akiwa salama. Na tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini. Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali sana huku akiuma kuni. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Myahudi yule,'Je wewe leo umefanya jambo gani?' Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka. Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya."

583. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahaba wake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote. Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema: "Mimi nilipotoka nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za tende. Na kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa kama Sadaka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . akajibu "Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza."

584. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . siku mmoja alimwambia Sahabi wake Mayassari kuwa: "Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi."

585. Al Imam Hasan al-'Askary(a.s) . anasema kuwa: " Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . je tufanyeje sasa? Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: 'Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya mali yenu basi yeye kila siku atawarudishia pamoja na nyongeza yake. ' Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza : "Je ni nani huyo?" Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: "Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt." Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza kumkabidhi vipi mali zetu hizi? Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawaambia: Toeni Sadaka muwape wale wanaostahiki. Kwa kusikia hayo wakauliza ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Hapa tulipo tutawatoa wapi hawa masikini na mafakiri tutawatafuta wapi? Basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwajibu: munuie kuwa sehemu moja ya mali yenu mtatoa Sadaka basi na msiwe na wasiwasi Allah swt atailinda mali yenu yote.

"Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alivyowaambi,a na Imam(a.s) . akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao. Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi."

586. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema "mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue". Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia "Allah swt atakuzidishia" na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . na akamwambia Imam(a.s) . "Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa." Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam(a.s) . hakumpa chochote.

Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu mwingine kuja kuomba, na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alichota mikono ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia mtumwa wake kama tuna pesa zozote zile tulizo nazo kwetu mpe huyo. Na huyo mfanyakazi wa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa amri yake alimpa Dirham Ishirini alizokuwa nazo. Mwombaji akiwa anachukua Dirham akasema: 'Ewe Allah swt! Nakushukuru mno sana na hakuna mwingine wa kushirkishwa nawe. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . nguo aliyokuwa amejifunika akampa huyo mwombaji na huyo mwombaji baada ya kuivaa na kujifunika na hiyo nguo akamshukuru Allah swt ambaye amemjaalia nguo ya kujifunika. 'Ewe Aba 'Abdillah! Allah swt akulipe kila la heri. Na baada ya kusema hayo akaondoka zake. Kwa kuona haya Ma-sahaba wakamwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa kila alivyoendelea yeye kumsifu Allah swt ndivyo wewe ulivyoendelea kumpa na kama asinge omba kwa kutaja jina la Al Imam(a.s) . lazima angeendelea kumpa chochote zaidi ya hayo."

9

HADITH ZA MTUME (s.a.w.w) NA MA-IMAMU (a.s)

KUSEMA UONGO

498. Anas Ibn Maliki Khisal-i-Sadduq, Uk. 321: Anaelezea kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema: "Chukueni mambo sita kutoka kwangu, na mimi nakubalia, na kutoa dhamana (Ya wewe kuingizwa Jannat)

1. Usiseme uongo

2.Unapo toa ahadi, usivunje

3. Unapo pewa amana na wengine, basi uwemuaminifu

4. Tazama chini ( usitende dhambi ).

5. Chunga heshima yako

6. Idhibiti mikono yako na ulimi wako.

499. Amesema Imam Al Hassan al-'Askari(a.s) : "Iwapo maovu yote yatawekwa katika nyunba moja, basi ufunguo ( wa milango yake ) itakuwa ni uongo ."[213] .

500. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Jiepusheni na kusema uongo hata kama ni uongo mgogo au mkubwa, kama kwa wadilifu au unasema kwa kdhihaki, kwasababu mtu anapo sema uongo mdogo basi anaweza kudiriki kusema uongo mkubwa pia.[214] .

501. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : Wakati mmoja Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliulizwa kuhusu umbali baina ya ukweli na uongo naye akiwa akionyesha umbali huo baina ya macho yake na maskio yake kwa vidole vinne katika kutoa jibu hilo, "Kile majo yako yanayooonani ukweli na mengi na yale yanayo sikilizwa na maskio yako ni sehemu kubwa ni uongo."[215] .

502. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameyawekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[216]

503. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wasema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[217]

504. Amesema Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) : "Kwa hakika Allah swt ameya wekea maufuli maovu fulani, na ufunguo wake Allah swt ameweka katika pombe, lakinimaovu yatokanayo na kusema uongo ni zaidi hata kuliko pombe yenyewe ."[218] .

505. Amesema Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) : "Muwe wa sema ukweli na mujiepushe na usemaji uongo ."[219] .

MARAFIKI NA URAFIKI

506. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Mtu anaathirika kwa imani ya marafiki zake. Kwa hivyo, muwe waangalifu kabisa katika urafiki wenu pamoja nao . " [220]

507. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) , Amesema: "Uwe rafiki wa yule ambaye atakuwa ndio heshima yako, si wewe uwe heshima yake. (Ufanye urafiki na wale walio juu yako ili wewe uweze kupata maendeleo kutokana na urafiki huo).[221] .

508. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Ndugu yangu mpenzi ni yule (anayenitambulisha) makosa na kasoro zangu.[222]

509. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Kwa hakika kuna marafiki wa aina tatu kwa ajili ya Muislam:

1. Rafiki anayesema mimi niko pamoja nawe iwapo upo hai au umekufa: Na hili ndio matendo yake.

2. Rafiki anayesema mimi nipo rafiki wako hadi ukingoni mwa kaburi na nitakuacha:hawa ni watoto wake.

3. Rafiki anayesema mimi nitakuwa nawe hadi pale utakapo kufa:hii ni mali ambayo ataiacha humu duniani kwa warithi wake baada ya kifo chake.[223]

Tanbih Kutokana na riwaya hii, na kama hizi sisi tunaelewa kuwa kitu ambacho kitakuwa pamoja na huyo mtu aliye kufa na kuaga dunia hii katika siku ya Qiyamah imani na matendo yake mema. Na suala hili limezungumziwa katika ahadithi nyingi sana za Kiislam na vile vile katika ayah za Qur'an tukufu, kwa mfano:

510. Allah swt anatuambia: Wale walio amini na wakatenda mema watakuwa na raha na marejeo mazuri. (Qur'an, 13:29).

511. Allah swt anatuambia: Hakika wale walio amini na wakatenda mema - hakika Sisi hatupotezi ujira wa anaye tenda mema. (Qur'an,18: 30).

512. Allah swt anatuambi: Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi. (Qur'an, 18: 107).

513. Allah swt anatuambia:" Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi. (Qur'an,19: 96).

514. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Muwe waangalifu katika kutafuta marafiki wa kweli na mujaribu kuwafanyia majaribio, kwa sababu wao watakuwa ndio msaada wenu pale mnapokuwa katika hali nzuri na watetezi wenu pale mtapokuwa katika shida na matatizo."[224]

515. Amesema Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) : "Kukutana pamoja na wacha Mungut kunawaleteeni mema ."[225]

516. Al Imam Zaynul 'Abediin(a.s) . Amesema: "Jitahadharisheni na urafiki wa watendao madhambi, na kuwasaidia madhalimu ."[226]

MARAFIKI WASIO WEMA

517. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Anayetafuta uhusiano na marafiki wa wale wanao wadhalilisha wapenzi wa Allah swt basi watambue kuwa wao wamemuasi Allah swt ."[227]

518. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Mnapojulishwa kuhusu marafiki zenu wanapotenda maovu, nendeni mumwambie: Ewe fulani bin fulani ! Ama acha kutenda madhambi au ukae mbali nasi: Na hapo utengane naye hadi atakapo acha kutenda maovu.[228]

519. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili kutoka baba yake Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . ambaye Amesema kuwa baba yake Al Imam Hussein ibn Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Amesema: "Ewe mwanangu! Jichunge na makundi matano na kamwe usifanye urafiki nao, wala usiongee nao na wala usifanye urafiki pamoja nao. Kwa hayo Al Imam Muhammad al-Baquir(a.s) . alimuuliza baba yake Je ni makundi gani hayo matano. Imam(a.s) . alimujibu: Jitahadharishe na wala usifanye urafiki pamoja na yule msema uongo kwa sababu yeye ni kama mazua mazua anaye kufanyia vitu vya mbali vikawa karibu, na anakifanya kiwe mbali kile ambacho kiko karibu nawe.[229]

Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na mtu ambaye hana tabia njema, kwa sababu atakuuza kwa thamani kwa tonge moja au hata chini ya hiyo. Jihadhari na wala usifanye uhusiano na bahili kwa sababu yeye atakunyima kutoka mali yake pale wewe utakapo hitaji hasa. Jihadhari na usifanye urafiki pamoja na mpumbavu, kwa sababu yeye atataka kukufaidisha wewe lakini kwa uhakika anakudhuru zaidi. Jihadhari na usifanye uhusiano pamoja na yule ambaye hawajali ndugu na maJama'a zake, kwa sababu mimi nimemona mtu kama huyo akilaaniwa katika kitabu cha Allah swt (yaani Qur'an Tukufu) katika sehemu tatu.

Nayo ni: Sura Al Baqarah, 2, Ayah ya 27; Wanao vunja ahadi ya Allah swt baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo amrisha Allah swt kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye Khasara. Sura Al-Raa'd, 13, ayah ya 25 Na wale wano vunja ahadi ya Allah swt baada ya kuzifunga, na wanakata aliy amrisha Allah swt yaungwe, na wanafanya fisadi katika nchi: Hao ndio watakao pata laana, na watapata Nyumba mbaya. Sura Muh'ammad, 47, ayah 22 Basi yanayo tarajiwa kwenu mkitawala ndio mfisidi katika nchi na mwatupe Jama'a zenu ?

520. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Ewe Kumail ! sema kile kilichopo katika hali yoyote ile. Uwe marafiki pamoja na wacha Allah swt na jiepushe na watendao maovu, jiweke mbali na wanafiki na usiwe pamoja na wadanganyifu na wahalifu na wahaini ."[230]

KUWAHUDUMIA WATU

521. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye mpuuzia ndugu yake Muislam mwenzake matatizo na shida za dunia hizi, basi Allah swt atampunguzia shida na matatizo yake huko Akhera ." [231]

522. Amesema Al Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Kwa hakika, maombi ya shida za watu zinazokuijia wewe ni miongoni mwa neema na baraka za Allah swt juu yako. Hivyo usisikitike kwa sababu ya neema na baraka hizi ."[232]

523. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Popote pale utakapoona ndugu yako Muislam ana shida, jaribu kuangalia kama utaweza kumusaidia. (Usimpuuze mpaka akutamkie shida zake.) "[233]

524. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa amenakili kutoka mababu zake(a.s) . ambao wamemnakili Mtume Muhammad(s.a.w.w) akisema: "Yeyote yule anayemlisha muumin aliye na njaa akashiba basi Allah swt atamlisha mpaka ashibe kutoka matunda ya Jannah; Na yeyote yule atakaye mvisha nguo yule aliye na shida za nguo, Allah swt atamvisha nguo zilizofumwa na za hariri, na yeyote yule atakaye mumalizia kiu muumin basi Allah swt atamjaalia kinywaji kilichopigwa lakiri; Na yeyote atakaye msaidia muumin kupunguza shida yake, basi Allah swt atamweka chini ya Arshi yake siku ya Qiyama siku ambayo hakutakuwa na kivuli chochote isipokuwa kivuli cha Arshi yake."[234]

525. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Watu wanamtegemea Allah swt kwa ajili ya riziki, kwa hiyo mpenzi miongoni mwa watu kwake Allah swt ni yule ambaye anawasaidia wale watu wanaomtegemea Allah swt na kuwafanya watu wa familia ya nyumbani wakawa na furaha."[235] .

526. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule atakaye wasaidia Waislam ndugu zake wakati wa shida, Allah swt atamwondolea shida na matatizo sabini na tatu, moja ambayo ni ambayo iko humu duniani na sabini na mbili zingine zitakazo kuwa wakati wa shida kubwa, ambapo watu watakuwa mashughuli katika mambo yao ya binafsi (katika Akhera) ." [236]

KUTOA MIKOPO

527. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayeijiwa na ndugu yake Muislam kwa ajili ya kukopa na kama yeye hampi mkopo, basi Allah swt atamharamishia kuingia Jannat siku ambayo waja mema watakuwa wakilipwa na kufidiwa ." [237]

528. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Yeyote yule anayetakiwa na ndugu yake Muislam kwa kukopeshwa na kama yeye hamkopeshi mkopo, Allah swt atamzuia kuingia Jannat siku ambayo waja wema watakuwa wakilipwa mema yao ." [238]

KUWASAIDIA WENYE SHIDA

529. Amesema Mtume Muhammad(s.a.w.w) : "Waulizeni maswali walio elimika, muongee pamoja na wale wenye hekima, na mujihusishe pamoja na masikini."[239]

530. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Sababu mojawapo ya kuteketea na kupotea kwa mali na utajiri wa mtu ni kule kutowajali na kutowasaidia wale wenye shida."[240]

531. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Mtume Muhammad (s.a.w.w) amemnakili Allah swt kwa kuameambiwa usiku wa Mi'raj: Ewe Ahamad! Mapenzi yangu ni kule kuwapenda masikini. Wafanye masikini wawe karibu nawe na uwaweke karibu nawe ili mimi niweze kukufikia wewe .."[241]

532. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) : "Yeyote yule anayemmalizia muumin njaa yake kiasi kwamba akaridhika kikamilifu, basi hakuna binadamu yeyote miongoni mwetu au miongoni mwa Malaika wanaojua kiasi cha thawabu yake siku ya Qiyamah isipokuwa Allah swt mmiliki wa Malimwengu yote. Na aliongezea: Kumlisha Muislam aliye na njaa ni njia moja kubwa sana ya kuomba Tawba( usamehevu)."[242]

Baada ya hapo alisoma ayah ya Qur'an Tukufu Sura Al-Balad, 90, ayah 14 - 16. Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye Jama'a, Au masikini aliye vumbini.

ZAWADI NA KUWAFURAHISHA MUUMIN

533. Mtume Muhammad(s.a.w.w) Amesema: "Wakati sadaka inapotolewa na mtu kutoka mikononi mwake, basi hiyo sadaka inasema: Mimi nilikuwa kitu cha kwisha, lakini wewe umenipa maisha; Mimi nilikuwa sina thamani sasa wewe umenifanya niwe na thamani kubwa; mimi nilikuwa ni adui nawe umenifanya mie kuwa rafiki; Wewe ulikuwa daima ukinilinda na kunihifadhi lakini sasa mimi nitakulinda na kukuhifadhi hadi siku ya Qiyamah ." [243]

534. Amesema Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) : "Yeyote yule atakaye mfurahisha Muumin, basi kwa hakika kwanza kabisa amemfurahisha Allah swt, na pili amemfurahisha Mtume Muhammad (s.a.w.w) na tatu ametufurahisha sisi Ahlul Bayt (a.s) "[244]

535. Amesema Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) : "Allah swt ameweka mahitaji ya wale wasio na uwezo katika mali ya matajiri. Kwa hivyo atakapokuwa mtu asiye na uwezo akabakia katika hali ya njaa basi ni kwa sababu matajiri wamemnyima haki yake ."[245] .

536. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . Amesema: "Kwa kiapo cha Allah swt! Yeyote yule anayeizuia mali yake isiwasaidie Mumin wenye shida basi siku ya Qiyamah kamwe hawataonja chakula cha Jannat wala Kinywaji kilichopigwa Lakiri."[246]

SADAKA NA MISAADA

537. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Sadaka inalipia madeni na inaongezea katika barakah ."

538. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Sadaka inamwepusha mtu na ajali mbaya ."

539. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Mtu yeyote yule aliye mja wa Allah swt akiwa Mumin akatoa Sadaka, basi Allah swt baada ya kifo chake huyo mtu huwaweka vyema na kuwasaidia wananyumba yake katika hali njema." Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akaendelea kusema: "Faida ya kutoa Sadaka ni kwamba inamsaidia kulipia madeni na viile vile kuongezea katika barak a."

540. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kusaidia na kutoa sadaka vyote hivyo vinaondoa umasikini na hurefusha umri wa mtu. Na yule anayetoa huweza kuepukana na aina sabini za ajali mbaya .

541. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . katika kuelezea tafsiri ya aya, ya Qur'an Tukufu, Sura Al-Layl, 92, Ayah ya 5 na 6: Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali Ama mwenye kutoa na akamcha Mungu. Ndipo amesema kuwa; Allah swt ndivyo anavyo walipa wale watendao mema, kwa mema yao mara kumi, au hata mara laki moja na hata zaidi ya hapo. Na vile vile amesema kuwa: anayetoa katika njia ya Allah swt basi Allah swt humjaalia kila aina ya tawfiqi katika kazi hiyo ya khairi."

542. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Mtu yeyote yule ambaye anamwamimi Allah swt kuwa atamlipa na atamwongezea zaidi ya kile anacho kitoa basi huyo mtu kwa moyo mkunjufu na bila aina ya ubakhili wowote atatoa sadaka na misaada kwa wingi kabisa."

543. Amesema Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amemnakili Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Siku ya Qiyama ardhi itakuwa imepata moto kupita kiasi na mumin watakuwa katika kivuli na kivuli hicho itakuwa ni kile alicho kuwa akitoa Sadaka ."

544. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah moja kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Enyi watu! Toeni sadaka bila shaka sadaka inaongezea katika mali yenu, na hivyo mtoe sadaka na Allah swt atawarehemu ."

545. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjipatie riziki ."

546. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni sadaka mjiongezee riziki yenu. Bila shaka anayeamini kuwa Allah swt hulipa mambo yote. Basi yeye huwapa sadaka masikini kwa kupita kiasi. Allah swt humjaalia riziki kwa njia mbalimbali kwa kile huyu mtu akitoacho katika mali yake ."

547. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amenakili riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akisema kuwa: "Kuwa na akida ya Tawhid ni nusu ya sehemu ya dini, enyi watu! Toeni Sadaka ili mpate riziki zaidi ".

548. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . ametoa riwayah kutoka Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Kuwa mali halisi ya mtu ni ile ambayo yeye ametolea sadaka ."

549. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema ili balaa zisiwafikieni katika siku nzima ."

550. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Sadaka ni kinga dhidi ya moto wa Jahannam ."

551. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa akisema: "Enyi watu muwatibu wagonjwa wenu kwa kutoa Sadaka ."

552. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . katika Nahjul Balagha amesema kuwa: "Mnapoona riziki yenu inapungua na kuwa finyo basi muwe mkitoa sadaka ndivyo mtakuwa mkifanya biashara na Allah swt ."

553. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Imani ya muumini inakuwa na sifa nne za lazima, "Awe na tabia njema, "Awe mkarimu na mwepesi wa kutoa "Asizungumze zaidi ya yale yanayo takikana (hazungumzi mambo ovyo ovyo) " Hutumia kile kiasi kinacho takiwa ,siyo mfujaji (anaotoa katika njia ya Allah swt ).

554. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Iwapo mimi nitakwenda Hijja moja basi afadhali niwafanye huru watumwa kumi, lakini iwapo mimi nitajichukulia jukumu la kuwalisha familia ya Waislamu ambao wanashida ya chakula na ambao wanaishi kwa njaa nikawamalizia shida zao, nikawavalisha nguo wale ambao hawana nguo, na nikawarudishia heshima yao miongoni mwa watu, basi mimi ninaona jambo hili ni afadhali na bora zaidi kuliko hata kwenda kuhiji Hijja sabini. "

555. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . aliijiwa na mtu mmoja na aliyeuliza, "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w)! Mimi ninazo pesa na utajiri je ni jambo gani afadhali nitoe sadaka au nimnunue mtumwa na kumfanya huru ?"

556. Kwa hayo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimjibu kuwa: "Kuwa mimi ninaonelea kuwa kutoa Sadaka ni afadhali zaidi."

557. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Siku moja Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Maimuna binti Harun, Je Kijakazi wako amekuwaje? Akasema Maimuna kwa hayo alimjibu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , 'Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi nimemfanya huru.' Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwambia "Iwapo kama wewe ungelichukua jukumu la kumlisha, kumtunza, kumsaidia na kumwonea huruma basi ingekuwa afadhali zaidi."

558. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Muwatibu wagonjwa wenu kwa Sadaka, na muzuie maafa kwa kuomba dua na kutoa sadaka muongezee riziki zenu zipanuke, na kwamba Sadaka inawaepusheni na mitego ya mashetani sabini ."

559. Siku moja walikuja wagonjwa wakilalamikia magonjwa yao mbele ya Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) ., naye akawaambia; "Nendeni mtoe Sadaka kwa ajili ya magonjwa yenu na mtapona, iwapo mtu atatoa Sadaka kwa kile akitumiacho kwa siku dharura wake, basi Allah swt huahirisha hata kifo chake na vile vile humwepusha na ajali mbaya ."

560. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . aliulizwa na Sahaba mmoja: "Ewe mwana wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Mimi watoto wangu wawili wamefariki na amebakia mtoto wangu mdogo." Kwa hayo Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . kamwambia: "Basi toa Sadaka kwa niaba ya mtoto wako huyo." Na siku moja Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alipomtembelea huyo mtu akamwambia, "Mwambie mtoto wako huyo atoe Sadaka kwa mkono wake walau kiasi kidogo chochote kile au hata kama kitakuwa ni kipande kidogo tu. Utambue wazi kuwa kiasi chochote kile hata kikiwa kiasi gani kama kitatolewa kwa roho safi basi mbele ya Allah huwa ni kipenzi, kwani Allah swt ameelezea kuwa: Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! (Qur'an,99: 7 – 8).

561. Vile viel Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . alimwelezea kuwa: "Allah swt amesema katika Qur'an Tukufu, Surah Al-Balad,90, Ayah11 - 16 Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? Kumkomboa mtumwa; Au kumlisha siku ya njaa Yatima aliye jamaa, Au masikini aliye vumbini

"Hivyo ewe Sahabi uelewe kuwa Allah swt anaelewa wazi wazi kuwa si watu wote wenye uwezo wa kuwanunua na wenye kufanya huru watumwa hivyo yeye ameweka thawabu hizo hizo kwa wale watakao toa Sadaka au watakao walisha yatima na masikini."

562. Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alijiwa mtu mmoja mbele yake na kuelezea habari za mtoto wake, na kwa hayo Al Imam akamjibu: "Toa Sadaka kwa niaba yake." Na mtu huyo akajibu kuwa "Sasa mtoto wake amekuwa na umri yaani amekuwa kijana." Basi Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alimwambia kuwa "Mtoto wako atoe Sadaka kwa mkono wake, hata kama itakuwa ni kipande cha mkate, na hapo ndipo Al Imam Musa al-Kadhim(a.s) . alisema riwayah ya Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . kuwa: "Katika Israil alikuwa mtu mmoja aliyekuwa akimpenda mno mtoto wake, na akaona katika ndoto yake anaanmbiwa kuwa, mtoto wako huyo umpendaye mno atakufa usiku wa ndoa yake. Kulipowadia usiku wa arusi baba mzazi wa mtoto huyo, usiku kucha akawa katika wasiwasi na hakupata usingizi na kamwe hakupata raha usiku huo. Na kulipo pambazuka asubuhi na mtoto alipotoka chumbani mwake akiwa hai basi baba yeke alimwuliza 'Ewe mwanangu! Je katika usiku huu wako wa kuamukia leo umefanya mema yoyote?' Kwa hayo mtoto akajibu "Ewe baba yangu! hakuna jambo la maana sana lililotendeka, bali alitokezea masikini mmoja akaja mlangoni kuomba chakula, alikuwa na njaa na kile chakula walichokuwa wameniwekea, mimi nikampa chakula chote huyo mtu aliyekuja kuomba.' Kwa hayo baba yake akasema "Kwa sababu hii tu ndiyo Allah swt amekuondoshea balaa kubwa iliyokuwa ikupate wewe usiku huo."

563. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka kwa mkono wako mwenyewe basi unajiepusha na ajali mbaya, unajiepusha na balaa na maafa sabini na mitego ya mashetani sabini na ambamo kila shetani yuko anakwambia 'ewe fulani! Usitoe Sadaka kamwe."

564. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mgonjwa atoe Sadaka kwa mkono wake mwenyewe na anayempa amwambie amwombee dua ".

565. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) katika hadith zake amesema kuwa: "Mkono uliye juu yaani mtoaji ni afahali kuliko mkono ule ulio chini yake, yaani mpokeaji ."

566. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: "Kuna aina tatu ya mikono wa " kwanza ni mkono ule wa Allah swt ambao uko juu kabisa na kwa hakika neema zote ni za Allah swt, " mkono wa pili ni ule mkono wa yule mtu anaye toa, ambaye anatoa katika njia ya Allah swt na " mkono wa tatu ni wa yule anaye pokea ambao mkono uliochini wa yule anayetoa. Kwa hivyo enyi watu chochote kile kinachobakia miongoni mwenu mtoe katika njia ya Allah swt na musikalifishe nafisi zenu".

567. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alikuwa amemfanyia usia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) ; Ewe Ali! Ninakufanyia usia wa mambo mema machache na uyakumbuke vyema.

Ewe Allah swt umsaidie Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . Baada ya hapo wakati akifanya usia, Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alisema: Ama kuhusiana na sadaka tafadhali usiwe na mnunguniko wowote. Utoe kiasi kwamba mpaka uhisi kwamba wewe umefuja mali yako, lakini utambue wazi kuwa hiyo sio ufujaji bali hiyo umetoa katika njia ya Allah swt."

568. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa kuna riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa "Toeni Sadaka, angalau hata kwa sa' ya tende, na kama sa' moja hiyo hamnayo basi mtoe tende kwa kiganja kimoja na hata kama hivyo haitawezekana basi mtoe tende kiasi chochote kile na kama hivyo haitawezekana basi mtoe angalau kokwa moja ya tende, na kama hivyo pia haitawezekana basi yule masikini aliyekuja kuwaomba mumwambie maneno mazuri na matamu na maneno matakatifu katika kumwelezea kuwa hakuna chochote, na hayo pia ni sadaka. Kwa sababu isitokee Siku ya Qiyama kwamba Allah swt atakapo kuuliza hesabu ya neema alizokujaalia akakuambia 'Ewe mja! Mimi nilikupa mambo chungu nzima, sasa hebu angalia nafsini mwako je kwa kutumia neema hizo wewe umejiandalia nini?' Na hapo wewe utaangalia sehemu zote nne za dunia na utajawa na masikitiko, na utakuta hakuna jambo lolote lile litakalo kuokoa dhidi ya adhabu za Allah swt."

569. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Mtoe tende kiasi fulani kwani itawaokoa na moto wa Jahannam , mpanue riziki zenu na mteremshiwe riziki nyingi kwa kutoa Sadaka na kupitia dua mziondoe balaa na shida zenu." Mkumbuke kuwa kwa kutoa Sadaka hamtapungukiwa katika mali yenu. Na miongoni mwa jamaa zenu wanapokuwa na shida muwasaidiapo hiyo siyo Sadaka bali hiyo ni wajibu wenu."

570. Al Imam Muhammad al-Baqir(a.s) . amesema kuwa: "Kulikuwa na mja mmoja aliyekuwa akifanya ibada ya Allah swt kwa umri wake wa miaka themanini. Siku moja alimwona mwanamuke mmoja mzuri aliyekuwa akipendeza naye akawa ameingia katika mtego wake. Yeye alitimiza matamanio yake visivyo halali na mara akatokezea Malakul mauti (malaika anayetoa roho). Ulimi wake ulifunga kuongea na jasho lilianza kumtoka na kutokwa kwa roho na mara hapo alipita masikini akiomba. Basi mtu huyu ambaye alikuwa katika hali ya kukata roho alimwambia yule masikini kwa ishara kuwa mahala fulani kuna mkate hivyo auchukue hivyo aweze kula huyo masikini, na masikini huyo alivyoelekezwa akauchukua mkate akaondoka zake. Kwa hiyo ikatokea kwamba Allah swt aliibatilisha ibada zake za miaka themanini kwa sababu ya kuzini na ikatokea kwamba Allah swt akamsamehe madhambi yake yote kwa sababu ya kutoa Sadaka kwa moyo mkunjufu."

571. Al Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) . amesema kuwa; " Katika zama za Bani Israil kuliwahi kutokea baa la njaa ambao uliendelea kwa muda wa miaka mingi. Katika wakati huo ikatokezea kwamba bibi kizee mmoja akiwa amekabwa na njaa hali ya juu alikuwa ameketi akiwa na kipande kidogo cha mkate huku akitaka kukila kipande hicho, mara akasikia mlangoni sauti ikisema ya masikini aliyekuwa amekuja kuomba: 'Ewe mja wa Allah swt! Mimi nakufa kwa njaa naomba unisaidie, bibi kizee huyo akajiambia kwa hakika Sadaka ndiyo wakati huu muafaka wa kutoa, na kile alichokuwa akila akakitoa haraka akampa huyo aliyekuwa akiomba.

Bibi kizee huyo alikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa amekwenda porini na ghafla kule alishambuliwa na mnyama. Kwa kusikia sauti ya mtoto wake huyo bibi kizee ikimwita, alikimbia kumfukuza mnyama huyo na kwa muujiza wa Allah swt ni kwamba, Allah swt alimtuma Malaika Jibrail(a.s) kwenda kumwokoa mtoto huyo katika mdomo na mabano ya mnyama wa huyo muuwaji, na Malaika Jibraili(a.s) . akamwambia 'Ewe bibi kizee! Je umefurahi sasa? Kwa kile ulichokitoa sadaka basi Allah swt naye amekulipa mema yake."

572. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema kuwa: " Mfanye mema katika hali ya shida na ufakiri, na wema huo ni Sadaka. Toeni Sadaka kama itakuwa ni kiasi gani kwa udogo wake. Mnaweza kutoa kiasi cha tende mkajiokoa na Jahannam. Kwa hakika udogo huo siyo hoja na Allah swt ataulea udogo huo kama kwamba nyie mnavyo walea watoto wadogo wanaonyonya maziwa, na siku ya Qiyama wakati mema yenu hayo (mliyokuwa mkisema ni madogo) yatakapoletwa mbele yenu mtaona kuwa ni sawasawa na ukubwa wa milima mikubwa sana."

573. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameseama kuwa Allah swt anasema kuwa : "Hakuna kitu kingine mbali na Sadaka ambacho mtu anaweza kumpatia mtu mwingine kidhahiri, na kwa hakika mimi ndiye wakili wake musitahiki, na mimi ninayepokea kwa mikono Sadaka hiyo halafu hata ikiwa kama ni tende kidogo haidhuru mimi ndiye ninaitunza, kama vile mwanadamu anavyowatunza watoto wake.

Siku ya Qiyama huyo mtoa Sadaka atastaajabishwa mno kwa Sadaka zake ndogo alizokuwa akitoa zimekuwa kubwa kama milima ya Uhud, milima mikubwa sana."

574. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amenakili riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi na mapema kwa sababu kunaondoa balaa kwa siku nzima ."

575. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Kwa kutoa Sadaka asubuhi na mapema basi mtoa Sadaka huepukana na kila aina ya matatizo na mabaya yote kwa siku nzima ."

576. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . amesema kuwa: "Toeni Sadaka asubuhi, na kwa mapenzi kabisa, mwenyewe kutoa Sadaka amebahatika. Basi humwomba Allah swt amani kutokana na balaa zote zilizoko ardhini na mbinguni, na kwa hakika Allah swt humjaalia hivyo kwa sababu ya kutoa Sadaka ."

577. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) alimwusia Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ewe Al Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s).! Sadaka huondoa balaa ambazo lazima zitatokezea, na kwa kutenda mema pamoja na ndugu na majamaa kunarefusha umri .

Ya Ali! Iwapo jamaa na ndugu ni watu wenye shida, basi kuwapa Sadaka hao haitakuwa ni Sadaka. Ya Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) .!Kusema maneno bila vitendo ni ya bure hayana maana, na Sadaka bila kuwa na nia nayo haiwi Sadaka ."

578. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anasema kuwa: Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza mtu mmoja "Je leo umefunga Saumu?" Mtu huyo alijibu "La hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza: "Je leo umeshawahi kumtembelea aliye mgonjwa?" Naye akajibu: "Hapana! Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) " Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza naye aliendelea kumjibu hapana hakufanya hivyo.

579. Mwishoni Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) aliendelea kumwuliza: "Je umemlisha masikini yeyote?" Naye akajibu: "Hapana Ewe Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) !" Na hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwambia huyo mtu: "Nenda kwa wananyumba wako, nenda ukawatendee na uwe nao kwa mema na uwawie wema, basi hayo ndiyo yatakuwa Sadaka yako kwao."

580. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ambaye ameseama: "kwa baraka za Sadaka Allah swt humwondolea mwenye kutoa Sadaka balaa sabini, ambamo kuna magonjwa, madhara yatokanayo na moto, kuzama maji, kufunikwa na majumba mpaka kufa na atamwepusha ili asiwehuke au asiwe mwehu."

581. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . ameripoti riwayah kutoka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . kuwa: "Ili kutaka kuepukana na shari za madhalimu basi toeni Sadaka ."

582. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . anaelezea kuwa: Siku moja Myaudi mmoja likuwa akienda kukata miti porini na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwangalia na kuwaambia Ma-Sahaba wake : "Myahudi huyu leo ataumwa na nyoka na kifo chake kitasababishwa na sumu ya nyoka. Myahudi huyo kama kawaida yake alikata kuni na alijitwisha kichwani mwake na akarud akiwa salama. Na tena Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alipomwona Myahudi huyo akamwambia ateremshe mzigo wa kuni huo na auweke chini. Na Myahudi akafanya hivyo alivyoambiwa, na katika mzigo huo wa kuni wakaona kuna nyoka mweusi mwenye sumu kali sana huku akiuma kuni. Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alimwuliza Myahudi yule,'Je wewe leo umefanya jambo gani?' Myaudi huyo akasema: Mimi nimekata kuni na kuzifunga tu, lakini wakati nilivyokuwa nikirudi nilibakiwa na vipande viwili vya mkate na kipande kimoja mimi nikala na kipande kimoja nikampa masikini Sadaka. Hapo ndipo Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) akasema kwa kiapo cha Allah swt ni kwa sababu ya Sadaka ndiko balaa hii imekuondokea, kwa hakika Sadaka humwepusha mtu na ajali mbaya."

583. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . siku moja alikuwa pamoja na Ma-sahaba wake katika Masjid Nabawi, na upande mmoja wa ukuta ukaanguka chini. Kulikuwa na mtu mmoja hapo ambaye aliponea chupu chupu tu, kulianguka kizingiti kizito karibu na muguu wake. Lakini yeye bahati nzuri hakupata udhuru wowote. Hapo Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwaambia Ma-sahaba wake, hebu mwulizeni huyu mtu leo amefanya matendo gani? Na wakati alipoulizwa huyo mtu akasema: "Mimi nilipotoka nyumbani mwangu leo nilikuwa na kokwa chache za tende. Na kukatokezea na masikini mmoja akaniomba basi mimi nikampa kama Sadaka Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . akajibu "Basi kwa sababu hiyo tu leo, Allah swt amekuepusha na balaa hii ambayo ingekumaliza."

584. Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . siku mmoja alimwambia Sahabi wake Mayassari kuwa: "Ewe Mayassari je wajua kuwa wewe umeisha fikiwa na mauti mara nyingi, lakini Allah swt amekuongezea umri wako zaidi kwa sababu ya wewe kuwa mkarimu na kuwajali jamaa na ndugu zako umewawia wema ndio maanake umri wako umezidi."

585. Al Imam Hasan al-'Askary(a.s) . anasema kuwa: " Wakati mmoja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akiwa pamoja na wenzake walikuwa safari na wenzake hao walikuwa na mali nyingi sana. Na njiani wakapata habari kuwa wako majambazi wanaowapora matajiri mali zao. Kwa kusikia hayo hao matajiri walianza kutetemeka na wakaingiwa na hofu na wakaanza kumwuuliza Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . je tufanyeje sasa? Na kwa hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: 'Mkabidhini mali yenu yule ambaye ataweza kuifadhi mali yenu, na kwa kweli ataitunza sana na baada la kupungua hata itazidi pia, sio hayo tu na pale mutakapokuingiwa na shida ya mali yenu basi yeye kila siku atawarudishia pamoja na nyongeza yake. ' Kwa kusikia hayo hao wenzake aliokuwa nao katika safari wakamwuliza : "Je ni nani huyo?" Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawajibu: "Yeye ni miliki wa malimwengu zote Allah swt." Basi hao wenzake wakamwuliza je tunaweza kumkabidhi vipi mali zetu hizi? Hapo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akawaambia: Toeni Sadaka muwape wale wanaostahiki. Kwa kusikia hayo wakauliza ewe mjukuu wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ! Hapa tulipo tutawatoa wapi hawa masikini na mafakiri tutawatafuta wapi? Basi Al Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) . aliwajibu: munuie kuwa sehemu moja ya mali yenu mtatoa Sadaka basi na msiwe na wasiwasi Allah swt atailinda mali yenu yote.

"Wale waliokuwa naye pamoja safarini walinuia hivyo kama vile Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alivyowaambi,a na Imam(a.s) . akawaambia sasa nyie mko katika amani ya Allah swt, na wakiwa wanaendelea na safari majambazi hao walikumbana nao na kwa kudura za Allah swt wao wakawapita salama usalimini bila ya kudhurika na kusumbuliwa, hadi wakafika mwisho wa safari yao. Waliopofika tu mwisho wa safari yao wao wakatoa sehemu moja walizokuwa wamenuia kama Sadaka na sehemu iliyo bakia walifanyia biashara yao, na Allah swt akawajaalia baraka kiasi kwamba wakapata faida hata zaidi ya mara kumi."

586. Siku moja Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alikuwa Mina pamoja na Ma-sahaba wake wakila zabibu. Mara akatokezea mtu mmoja na akaomba. Basi Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa mkono wake akachukua fungu moja la zabibu akampa basi huyo akakataa kupokea, akisema "mimi sitaki zabibu hizi bali ninataka pesa tasilimu kama zipo ndio nichukue". Basi kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia "Allah swt atakuzidishia" na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . hakumpa chochote, baada ya muda si muda huyo mwombaji tena akarudi kwa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . na akamwambia Imam(a.s) . "Nipe zile zabibu ulizokuwa ukitaka kunipa." Na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia Allah swt atakutafutia njia yake, pamoja na hayo Imam(a.s) . hakumpa chochote.

Wakati bado wakiwa wamekaa akatokezea mtu mwingine kuja kuomba, na Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alitoa mbegu tatu tu za zabibu akampa huyo mwombaji. Mwombaji huyo alianza kumshukuru Allah swt kwa kumjaalia riziki hiyo na akaonyesha shukurani kwa ujumla. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . alichota mikono ya zabibu miwili akampa na hapo tena huyo mwombaji akaendelea kumshukuru Allah swt zaidi na zaidi. Kwa kusikia hayo tena Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . akamwambia mtumwa wake kama tuna pesa zozote zile tulizo nazo kwetu mpe huyo. Na huyo mfanyakazi wa Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kwa amri yake alimpa Dirham Ishirini alizokuwa nazo. Mwombaji akiwa anachukua Dirham akasema: 'Ewe Allah swt! Nakushukuru mno sana na hakuna mwingine wa kushirkishwa nawe. Kwa kusikia hayo Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . nguo aliyokuwa amejifunika akampa huyo mwombaji na huyo mwombaji baada ya kuivaa na kujifunika na hiyo nguo akamshukuru Allah swt ambaye amemjaalia nguo ya kujifunika. 'Ewe Aba 'Abdillah! Allah swt akulipe kila la heri. Na baada ya kusema hayo akaondoka zake. Kwa kuona haya Ma-sahaba wakamwambia Al Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) . kuwa kila alivyoendelea yeye kumsifu Allah swt ndivyo wewe ulivyoendelea kumpa na kama asinge omba kwa kutaja jina la Al Imam(a.s) . lazima angeendelea kumpa chochote zaidi ya hayo."


4

5