MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA 0%

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA Mwandishi:
: AMIRALY M.H.DATOO
Kundi: Vitabu mbali mbali

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

Mwandishi: Kimeandikwa na: 'Ayatullah al-'Udhma Nasir Makarim Shirazi.
: AMIRALY M.H.DATOO
Kundi:

Matembeleo: 15897
Pakua: 2337

Maelezo zaidi:

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 15897 / Pakua: 2337
Kiwango Kiwango Kiwango
MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

Mwandishi:
Swahili

12

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 111: QURAN TUKUFU NI YA KILA ZAMA

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:

Allah swt hakuifanya Qur'an Tukufu kuwa kwa ajili ya zama fulani tu, wala si kwa ajili ya taifa fulani, hivyo daima huwa ni mpya na kwa ajili ya kila taifa ulimwenguni humu hadi siku ya Qiyama. 116

Maelezo mafupi: Al-Imam 'Ali ar-ridha a.s. alimjibu mtu mmoja ambaye alitaka kujua ni kwa nini Qur'an Tukufu haizeeki kwa kusomwa kila mara au kuchapwa ? Katika kusema huku kwa Al- Imam 'Ali ar-ridha a.s. amezungumzia kwa maana kamilifu kwa uhakika huu kuwa Qur'an Tukufu haikuumbwa na vitu vya dunia hii au haikutengenezwa na mwanadamu ambaye mwenyewe ataangamia na kuisha pamoja na mawazo yake yanayokaa yakibadilika. Hivyo vumbi hilo la kuzeeka haufuniki Qur'an Tukufu kwa kupita muda. Kwa hakika Qur'an Tukufu imetokea kutokana na sayansi na elimu ya Allah swt, ambaye kuwapo kwake kumekuwapo tangia mwanzoni na utakuwepo milele. Kila itakavyosomwa zaidi, ndivyo hivyo itakavyokuwa mpya na yenye kuvutia, na kwa hakika huu ndio mojawapo wa muujiza wa Qur'an Tukufu.

SOMO LA 112: JITAHADHARISHE NA MATAMANIO

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Ole wako kwa matamanio ya nafsi yako kama vile unavyojihadhari na maadui zako kwa sababu hakuna adui wako mkubwa kuliko matamanio yako na yale yanayotokana na ndimi zao. 117

Maelezo mafupi: Bila shaka maadui wa ndani ni hatari zaidi kuliko maadui wa nje. Kwa hivyo, matamanio ambayo humwathiri mwanadamu kwa undani, kwani huchukuliwa ni adui hatari kabisa wa mwanadamu. Upofu wa matamanio humfanya mtu akawa kiziwi na kipofu wa macho. Huondoa nuru ya busara, hugeuza nyuso za ukweli na hatimaye humwongoza katika maovu.

SOMO LA 113: NJIA MOJA TU YA KUWA SHI'A

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) alimwambia to jaber jofi:

Wafikishie salaam zangu kwa Mashi'a wetu na uwaambie kuwa wao hawatakuwa na uhusiano pamoja nasi na Allah swt ambapo njia moja tu iliyopo ni ya kujisalimisha kwa amri za Allah swt. 118

Maelezo mafupi: Kwa hakika wapo watu wengi ambao wanadai kuwa wao ni Mashi'a na mapenzi yao pamoja na Ahlul Bayt a.s. ndiyo yanayotosheleza kwa ajili ya uokovu wao Siku ya Qiyamah. Ati kwa kudhania kwao hivyo, wao wataingizwa katika ndugu na jamaa za Ahlul Bayt a.s., na kwamba watakuwa na uhusiano maalumu pamja na Allah swt, na hivyo kila kitu chao kitakuwa sawasawa kwa kuomba kwao. Kwa hakika uhusiano wa mwanadamu na Allah swt ni ule tu unaotokana na utiifu na kutimiza wajibu wake mtu. Yeyote yule anayejisalimisha mbele ya amri za Allah swt ndiye mtu wa karibu kabisa, na kwa hakika yeyote yule asiyemtii Allah swt kwa hakika amejiweka mbali mno na Allah swt, yeyote yule awaye.

SOMO LA 114: UHUSIANO WA MALI NA MATUMIZI!

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Yeyote yule anayechuma mali kwa njia ya haraam, ataitumia kwa njia ambayo haina baraka za Allah swt. 119

Maelezo mafupi: Inaaminiwa kwa kawaida kuwa si kila mali au milki inayopaswa kutumiwa kwa ajili ya wema wa jamii au njia nzuri na zilizo bora. Kwa hakika Hadith ya hapo juu ni uthibitisho mzuri kwa imani hii ya kawaida. Ni ukweli ulioonekana kwamba baadhi ya watu wamenuia kushiriki katika jambo jema kwa kutumia mali na milki yao, lakini ama wamesitisha wakiwa wamefikia katikati, au iwapo watakuwa wamekamilisha basi juhudi zao hizo hazitakuwa na ufanisi wa kutosha au itaonekana yenye matokeo yaliyogeuka. Kwa hakika wapo watu wengi mno ambao watoa huduma kubwa mno kwa moyo msafi na kwa mitaji yao midogo.

SOMO LA 115: MKWELI KABISA NA MWENYE BUSARA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Kila Ummah unao mtu aliye mkweli na mbainifu, na hivyo mkweli na mbainifu wa Ummah wangu ni Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib (a.s) 120

Maelezo mafupi: Kwa ajili yakutaka kukamilisha Dini halisi, Dini ya kudumu milele kama Islam, basi kunatakiwa kuwepo na mtu ambaye ni mzoefu na mwenye kujua masuala yote na undani wa Dini hiyo ili aweze kubainisha tofauti iliyopo baina ya ukweli na uwongo ( mstahikiwa jina la mbainishaji) baada ya kifo cha Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., sehemu kubwa ya Misheni yake ilipita katika magomvi mbalimbali pamoja na maadui wake. Inabidi yeye awe mkweli, mwaminifu, msemaji bora na msema ukweli ili aweze kuondoa kero zozote zinazowakera watu baada ya kiongozi wa kwanza. Kwa hakika wadhifa huu, kama ilivyo bayana hapo juu, ulikuwa umepewa Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) tu.

SOMO LA 116: MAISHA NA KUENDESHA NYUMBA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. alikuwa akikusanya na kuzichana kuni (kwa ajili ya nyumbani kwake) kutokea jangwani na kuchota maji na kufanya usafi kwa kufagia, na Bi. Fatimah az-Zahra a.s. alitayarisha unga na alikanda unga na kupika mikate. 121

Maelezo mafupi: Ukuu na utukufu wa ulimwengu mzima wa moyo na daraja kuu umefichika katika Hadith hii fupi kwa kuhusiana na Kiongozi Adhimu wa Islam, Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) na mfano mkubwa wa wanawake, Bi.Fatimah az-Zahra(a.s) kwani maisha yao kwa hakika yalikuwa ya kawaida na yenye kujaa uaminifu, uhalisi, kusaidiana na kushirikiana. Kufanya kazi haikuwa kudhalilika, na ushirikiano na kuelewana yalikuwa yakichukuliwa kuwa ni kipaumbele ya kimsingi, na kisichopendeza kulichukuliwa kama ndicho kipa umbele. Kwa hakika masuala haya hayapatikani tena majumbani mwetu na matokeo yake ni kwamba udugu na amani na mapenzi ndiyo maana yametoweka.

SOMO LA 117: SAA NZIMA YA UADILIFU

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Saa moja ya uadilifu ni bora kuliko ibada ya mwaka mzima. 122

Maelezo mafupi: 'Ibada ni uhusianao sawa wa viumbe pamoja na Muumba wao na 'uwezekano' pamoja na lazima na kuzingatia kwa uhusiano na muungano huu. Kwa hakika 'Ibada hizo ndizo zilizo mafunzo muhimu ambazo kwa hakika yanaathiri mno katika kurekebisha nafsi na akili ya mtu. Hata hivyo, sisi tunasoma katika Hadith hiyo hapo juu kuwa saa moja ya uadilifu ni bora na afadhali kuliko 'Ibada ya Sunnah ya mwaka mzima.

Na mahala pengine tunasoma kuwa saa moja ipitishwayo katika kufikiria na kutafakari, basi ni bora kuliko usiku mmoja ( au mwaka mmoja) upitishwao katika 'Ibada. Kwa hakika maneno haya yanaonyesha muhimu wa uadilifu ulivyo na fikara, kwani yote yana asili sawa. Popote pale ambapo hapatakuwa na uadilifu, basi hakutakuwa na ufikiriaji sahihi na busara.

SOMO LA 118: MGANGA WA KWELI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Kwa hakika mgamnga halisi ni Allah swt, na vitu ambavyo vikufaavyo vinaweza kuwa vyenye kumdhuru mtu mwingine. 123

Maelezo mafupi: Matukio yanayotokea katika maisha ya mwanadamu kwa mara nyingi hutokana na sera zake mbaya, uchaguaji au moyo wake na kwa hakika yapo matukio mengi mno kama haya yanayoumiza. Lakini mara nyingine matukio yasiyo mazuri hutokea si kwa kutokana na sababu hizo za juu, lakini kwa hakika hutokana na amri za Allah swt kama ndizo dawa kwa ajili ya waja wake. Dawa hizo mara nyingi huwa ni chungu, lakini huwa ni kama kengele ya kumwamsha na kumzindua mwanadamu, au kumtanabahisha juu ya udhaifu wake na au kuondoa kiburi na upotofu wake.

SOMO LA 119: MAKHALIFA WA MTUME S.A.W.W.

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Dini hii ya Allah swt daima itaheshimiwa na kuhifadhiwa kutokea maadui hadi hapo Makhalifa kumi na wawili (12) watakapoiongoza, na wote watatokana na Maqureish. 124

Maelezo mafupi: Hadith na Riwaya zilizo wazi na kujieleza zenyewe zimetolewa katika kuzungumzia Makhalifa 12 halisi wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) katika vitabu vinavyoheshimiwa na kuaminiwa katika Ahl as-Sunnah kama vile Sahih Bukhari, Sahih Muslim, Sahih Tirmidhi, Sahih Abu Dawud, Masud Ahmad na vitabu vingi vinginevyo, na jumla ya Hadith hizi zilizotolewa na Mashi'a na Masunni zinafikia idadi ya Ahadith 271! Ni jambo la kuvutia kuwa Ahadith hizo hazikubaliani na hata mmojawapo wa Waislamu waliongoza au kutawala baada ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) isipokuwa Maimamu 12 wa Mashi'a tu kwani makhalifa 4 wa kwanza, au wa-Bani Umayyah or Bani 'Abbas si wanaozungumziwa katika Hadith hii.

Kwa hivyo Masunni wameingia katika hali ngumu ya kutafsiri Hadith hii iliyo sahihi lakini kwa hakika tafsiri ya Hadith hii ipo wazi kabisa katika Ushi'a wa Ahlul bayt a.s. ya wananyumba wa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w)

SOMO LA 120: FURAHA YENEY MADHAMBI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Si haki kwa Waumini kushiriki katika hafla na sherehe ambamo kunatendwa maasi ambayo wao hawawezi kuzibadilisha. 125

Maelezo mafupi: Kushiriki katika karamu au sherehe zenye madhambi ni dhambi lenyewe, ingawaje mtu mwenyewe hatendi dhambi wala kushirikiana na washiriki katika karamu au sherehe hiyo. Kwa sababu kushiriki katika karamu au sherehe kama hizo kunachukuliwa ni kusaini dhambi, isipokuwa tu iwapo hatima ya mtu itakuwa ni kubadilisha hali hiyo na kutekeleza jukumu gumu kabisa la kuhubiri uwema na kukataza ubaya na maovu. Zaidi ya hayo, kujishughulisha na hali za madhambi, wakati kuwa tofauti na wao, kunaitia kiza nafsi ya mtu na kupunguza hali ya kujiepusha na madhambi na kumfanya mtu kuzoea madhambi.

13

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 121: UFANYE KAZI ZINAZOZALISHA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Lima na panda mti. Kwa kiapo cha Allah swt , watu hawajafanya tendo lolote lililo halisi zaidi ya hili. 126

Maelezo mafupi: Maisha ya mwanadamu yapo juu ya kazi zinazo zalisha, ikiwemo kilimo, na biashara mbalimbali, na hata wingi wa viwanda havitakuwa na maana bila ya kilimo kwani kwayo hujipatia mali ghafi. Kwa kuongezea, uovu na uzushi hauwezekani katika kilimo kama vile ilivyo kawaida katika mambo mengine. Kwani misingi yake ipo ni kawaida na kwa hakika faida yake ni kwa kutokana na jitihada za mtu. Kwa misingi hii, kilimo na upandaji wa miti kumeitwa kuwa ni kazi njema na halisi katika Hadith ya hapo juu.

SOMO LA 122: UREFU NA UFUPI WA MAISHA

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Kifo kinamwijia mtu mapema kuliko kawaida kwa kutokana na madhambi, na urefu wa maisha unatokana na uchamungu wake zaidi ya maisha ya kawaida. 127

Maelezo mafupi: Hakuna shaka kuwa wingi wa madhambi na tabia mbaya zinafupisha maisha moja kwa moja ( kama vile kulewa, kamari, husuda, wivu na shari na kutaka kulipiza kisasi) na nyingi zinafupisha maisha vinginevyo kwa kuathiri mivurugano ya kijamii na kuondoa amani na usalama wa kijamii na kuzuka kwa vita na mapigano ( kama vile riba, dhuluma na ukandamizaji).

Kwa upande wa pili, uchamungu ndio unaweza kuwa ndiyo sababu ya kurefuka kwa umri mrefu kwa kutokana na athari za utulivu wa nafsi na nyoyo na dhamira. Hivyo, madhambi, kutokujali athari zake mbaya, ni kichocheo kikubwa katika kufupisha maisha ya mwanadamu, ambapo kwa hakika uchamungu ni sababu kubwa katika kurefusha maisha pamoja mema yake yote.

SOMO LA 123: URAFIKI NA SHETANI!

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Usimlaani Shetani kidhahiri, wakati wewe ni rafiki yake kwa undani mwako. 128

Maelezo mafupi: Baadhi ya watu wanijiepusha na kuogopa kutokea maneno, maneno ya umasikini, unafiki, sheitani na kama hayo, wakati ambapo kimatendo wao wanakuwa wametumbukia ndani mwao. Sisi tunawajua baadhi ya matajiri ambao huishi maisha ya kimasikini kwa kuhofia umasikini. Sisi vile vile tunawajua wanafiki ambao kwa kurudia huwalaani wanafiki, lakini kwa hakika maisha yao yanakuwa yamejaa kwa unafiki.

Sisi vie vile tunawajua watu waovu ambao kwa udhahiri kabisa wanajiingiza katika kujinusuru kwa Allah swt dhidi ya Shetani, kwa maneno yao ya ulimini, lakini wao ni marafiki wa Shetani kwa undani mwao na hutilia mkazo na usisitizo juu ya mipango ya kishetani. Kwa hakika wao ni maadui kwa maneno na wala si kwa wa kweli kwa hisia au ukweli.

SOMO LA 124: POKEA USHAURI ILI UONGOZWE !

Al-Imam Hasan ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Hakuna mataifa yanayoshauriana miongoni mwao hadi pale wanapokuwa wameongozwa kwa mema na faida zao. 129

Maelezo mafupi: Kwa umoja daima imeilipa jamii neema, maendeleo na uboreshaji wao, hususan katika masuala ya kiakili na mipango ya maendeleo na utatuaji wa matatizo yao, kwa hakika kutekelezeka ushauriano na majadiliano kwa kimaajabu. Wale ambao wamezoea kujitolea mawazo yao wenyewe na kujitenga, mara nyingi kudhurika kwa makosa na hasara. Akili yoyote inayo mchocheo ambao haupo katika akili nyingineyo. Wakati vichocheo hivi vinapokutana na nyenzao, basi kutatokea mwanga ambao utang'arisha kiza wowote utakao kuwapo. Inatubidi sisi sote tuamue kuwa tutashauriana pamoja na watu walioelimika na wale walio makini.

SOMO LA 125: SALAAM, KUSALIMIANA KIISLAMU

Al-Imam Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Salaam (kusalimiana) zina thawabu 70, sehemu 69 za Salamu hiyo ni kwa ajili ya yule anayetoa Salaam na sehemu moja ni kwa ajili ya yule anayejibu Salaam hiyo. 130

Maelezo mafupi: Miongoni mwa kusalimiana katika mataifa ya ulimwenguni, Salaam, usalimio wa Kiislamu na kuamkiana, kwa hakika unao nuru ya ajabu, kwa sababu hiyo inamaanisha ukaribisho na amani, furaha na urafiki, na vile vile Dua ya amani na usalama na kheri kutokea Allah swt kwa mtu anayesalimiwa. Kwa sababu hizi, maamkizi ya wakazi wa Jannat ni Salaam, na Malaika wa Rahma huwapokea wachamungu na watendao mema kwa Salaam. Lakini kwa bahati mbaya, baadhi ya Waislamu wanaikataa amri hii ya Dini ya Islam kwa kujifakharisha kuwa kwa kutokusalimiana ndiko kunakoonyesha heshima zao na kwa kusalimiana hivyo kunawadhalilisha wao na kwa hakika wao ndio wenye hasara ya kukosa baraka, amani na Dua iliyopo katika Salaam kwa mujibu wa hadith hiyo ya hapo juu !

SOMO LA 126: KUTOKUKUBALIANA KWA IMANI NA MATENDO

Al-Imam Zainul 'Abidiin ibn Hussein ibn 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Wale watu wanaochukiwa na Allah swt ni wale ambao wameukubalia uongozi wa Imamu, lakini hawafuati matendo yake. 131

Maelezo mafupi: Mojawapo ya makosa makuu ya mwanadamu ni kutokukubaliana kwa imani yake pamoja na matendo yake. Yeye huamini kitu kingine, lakini hakuna ufuatio wa imani yake hiyo unaopatikana katika matendo yake. Yeye huamini katika Allah swt, lakini hukana katika matendo yake. Yeye huamini katika Mahakama Kuu ya Allah swt, lakini haonyeshi kujitayarisha kwayo. Yeye huamini kuwa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. ni Mtume Mkuu na kwamba Al- Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) kuwa ni kiongozi Mkuu, lakini utaona hawana sifa yoyote katika matendo yake yoyote. Hivyo tunasema kuwa matendo yake yapo upande mmoja na matendo yake yapo upande wa pili

SOMO LA 127: ADHABU ZA ALLAH SWT !

Al-Imam Muhammad al-Baqir(a.s) amesema:

Allah swt ameweka adhabu (kwa ajili ya madhambi na uasi) katika nyoyo na miili: 132 " Umasikini katika kipato " Uvivu katika 'Ibada Lakini Allah swt hajamwadhibu mja wake yeyote yule aliye na kitu kiovu kuliko moyo mgumu."

Maelezo mafupi: Adhabu za Allah swt kwa hakika ni matokeo ya matendo na matokeo ya madhambi ya mwanadamu mwenyewe. Kwa hakika baadhi ya nyakati hatima hizi mbaya huonekana kama nyakati mbaya katika maisha ya kidunia na nyakati zinginezo kama kunyimwa uhalisi katika 'Ibada na Dua pamoja na Muumba wetu. Lakini jambo lililo la muhimu na hatari kabisa ni kule kwa mwanadamu kudhihirisha maasi na makosa na matendo maovu kabisa kwa nyonyo ngumu na ukatili wa mwanadamu, kuondokana kutokea moyo wa mwandamu kwa hisia za kibinadamu na ukarimu, mapenzi na huruma, na kwa hakika moyo wa mwanadamu unaweza kuwa ndio chanzo kikuu cha madhambi na maasi mengi mno.

SOMO LA 128: UHAKIKA ULIO SAHAULIKA

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Allah swt ameumba yakini bila shaka kama mauti, lakini inaonekana kuwa shaka ndimo kamwe hakuna yakini. 133

Maelezo mafupi: Kwa hakika msemo huo ni wa kustaajabisha, na tafsiri bayana ya kutokujua kwa mwanadamu kuhusu hatima ya maisha na mauti. Mtu anaweza kusita katika kitu chochote kile na asiamini katika dini yoyote, lakini hasiti kwa kukiri kuwa maisha yatafikia mwisho wake tu na kuisha. Lakini yeye anaonekana hajui katika suala hili kama kwamba hakutakuwa na kifo ambacho ndicho kitakacho malizia maisha yake ! Hivyo, yeye hajitayarishi kwa kuikaribisha mauti na mwisho wake kwa imani, matendo mema, uhalisi na uchamungu. Hata hivyo, inatubidi sisi kwa lazima tuwe watu wenye uhakika na uhalisi katika kila hali na umri ili tusije tukajuta na kuaibika wakati wowote pale maisha yetu yatakapo malizika.

SOMO LA 129: NAFASI YA ELIMU NA BUSARA

Al-Imam Musa al-Kadhim(a.s) amesema:

Uoteshaji unakuwa katika ardhi laini, na wala si juu ya majiwe ! Na vile vile elimu na busra vinachomoza katika nyoyo za wachamungu, na kamwe si katika nyoyo za wadhalimu. 134

Maelezo mafupi: Hatua ya kwanza katika kutafuta elimu ni unyenyekevu, unyenyekevu kuelekea ukweli, unyenyekevu kuelekea mwalimu, na mtu yeyote anayejua zaidi kuliko sisi, na ambaye anaweza kutufundisha chochote. Kwa sababu hizi, ujahili na kiburi na ufidhuli yanakuwa yameambatana pamoja. Mfedhuli na mjauri kamwe hawezi kukubali kukiri kwa ujinga, na hata kama iwapo ukweli hautakuwa kwa mujibu wa nafsi yake ya kiburi na ufedhuli, si kwamba ati kuwa wao hukanusha hayo, bali hupinga pia. Wao hawakubali ukweli kutokea wale walio chini yao na mara nyingi hubakia kuwa wapumbavu kwa ukamilifu.

SOMO LA 130: MAJUKUMU MAZITO YA IMAM

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:

Imam ni Mwakilishi wa Allah swt juu ya ardhi hii na miongoni mwa waja wa Allah swt, na ni ushahidi kwa waja wake na mwenye kuwalingania watu kwake na mwenye mlinzi wa mipaka ya Allah swt dhidi ya yale yaliyoharamishwa. 135

Maelezo mafupi: Katika Hadith hii, ambayo ni sehemu ya Hadith ndefu katika kuzungumzia nafasi ya Uimamu, inazungumzia sehemu tano zilizo nzito za majukumu ya Imam(a.s)

1- Imam(a.s) ni mweka hazina na wakala wa Ufunuo na mhifadhi wa sayanzi zote, maamrisho na elimu za Dini.

2- Imam(a.s) ni sababu iliyohai na udhihirisho na mtambulishaji na mwendelezaji wa Dini ya Islam

3- Imam(a.s) ni mwakilishi mtakatifu wa Allah swt na mamlaka yake miongoni mwa watu

4- Imam(a.s) , hualika katika mema na kuzuia mabaya na ni Mjumbe mkuu wa Dini

5- Imam(a.s) ni mhifadhi wa mipaka ya Dini ya Islam dhidi ya uvamizi wa maadui wake. Na mtu kma huyo ndiye awenayo elimu ya Allah swt na daraja la utoharifu na hakuna mtu yeyote mwingine anayeweza kuwachagua hao Maimamu(a.s) isipokuwa ni Allah swt tu.

14

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 131: MILANGO ILIYOFUNGWA ITAFUNGULIWA

Al-Imam Muhammad at-Taqi(a.s) amesema:

Iwapo milango ya Jannat na ardhini zimefungwa kwa ajili ya mtu, na achaguapo uchamungu, Allah swt atamtoa humo. 136

Maelezo mafupi: Baadhi ya nyakati katika maisha, milango yote huwa inafungwa kwa ajili ya mwanadamu na popote pale anapogeukia, hukumbana na matatizo na magumu. Kwa hakika matukio kama hayo ni majukumu kwa ajili ya kumwamsha mwanadamu na kumfanya arejee kwa Allah swt, urejeo ulio sahihi na kubadilisha maisha na bahati yake. Wakati huu, iwapo yeye atajipatia usisitizo unaostahili kwa moyo wake wote, na kuomba msaada kutokea Allah swt, basi hakuna shaka kuwa msaada huo ataupata kutokea kwa Allah swt na upepo murua za baraka na rehema za Allah swt zitamkumba yeye na kwa hakika utakua ni muujiza mkubwa kwani milango yote iliyokuwa imefungwa itafunguka !

SOMO LA 132: JITAHADHARISHE NA WAOVU!

Al-Imam Muhammad at-Taqi (a.s) amesema:

Jitahadharishe na ugonjwa wa mtu yule ambaye hajistahi mwenyewe! 137

Maelezo mafupi: Kwa hakika, mojawapo ya hoja muhimu katika kuzuia ufisadi na uovu ni heshima au kuwa na hisia za heshima. Watu walioheshimika au wale wanaochukua heshima kwa ajili yao wenyewe, ingawaje wao inawezekana wasihesabike miongoni mwa walioheshimika katika mtazamo wa kijamii, wanajiepusha na mengi ya maovu na matendo mabaya kwa ajili ya kujitunzia nafasi yao. Lakini pale wao wanapohisi kuwa hawana heshima yoyote, jina au , basi wao hawatajali chochote. Hivyo Imam a.s. ametuonya tujitahadharishe na watu kama hao ! Na kwa misingi hiyo, mojawapo ya jambo lililo muhimu ni kuwaelimisha watoto au watu kwa ujumla ni kutengeneza heshima ndani mwao ili wao wawe na hisia ya kuwa na heshima maalum. Ama kwa upande mwingine, kinyume na hayo, kuwapunguzia watu heshima kwa hakika inayo athari mbaya kwa mtazamo wa kielimu na kuelimishana.

SOMO LA 133: VITA VIKUU

Al-Imam Hasan al-Askari(a.s) amesema:

Mtu aliye shupavu kabisa ni yule ambaye anaacha madhambi. 138

Maelezo mafupi: Sisi tunajua kuwa harakati dhidi ya matamanio ya maasi na za nafsi ndizo chanzo kikuu cha madhambi na inaitwa 'vita vikuu' katika Dini ya Islam, ikiwa kwa hakika harakati na vita vikali na vigumu hata kuzidi vita dhidi ya maadui. Kwa sababu vita hivi ni kwa ajili ya kujitakasisha kwa nafsi na hakutakuwa na ushindi wowote kwani kushindwa hutokea mara nyingi kwa sababu ya mipango na mikakati dhaifu. Katika jamii ambazo zilizojaa kwa madhambi, thamani ya vita hivi vinakuwa lazima na umuhimu wake katika kuboresha malengo na matakwa yake ya kijamii huwa yako wazi. Ushindi wa Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. katika mji mtukufu wa Madinah kwa hakika ulikuwa ndio uhitimisho wa utakasishaji wa nafsi na nyoyo, na harakati tukufu za Masahaba wake katika mji mtukufu wa Makkah.

SOMO LA 134: GHAIBU IMAM MUHAMMAD MAHDI A.S.

Al-Imam Muhammad Mahdi Sahib az-Zamaan(a.s)

amesema:

Katika matukio mengi yatakakayotokea katika kipindi hiki cha kuwa- ghaibu, rejea kwa wanaohadithia Hadith na Riwaya zetu. 139

Maelezo mafupi: Jamii za kibinadamu hazina mpangilio bila ya kuwa na kiongozi sawasawa. Na kwa sababu hizi, Allah swt kamwe hakuwaachia waja wake bila ya kiongozi na daima kumekuwapo viongozi wa Allah swt miongoni mwao. Hata katika kipindi cha kuwepo Ghaibu kwa Al-Imam Muhammad Mahdi Sahib az-Zamaan(a.s) kumekuwapo na wawakilishi wake mahsusi, na baada ya kusita kwa kipindi chao, aliwachagua wawakilishi wake wa kawaida kwa ajili ya kuwaongoza watu. Watu waliojitolea, waaminifu na watu walio makini ambao kwa hakika wanakuwa wameelimika vya kutosha kuhusu Kitabu Kitakatifu cha Waislamu, yaani Qur'an Tukufu, na vile vile Sunnah za Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Ahlul Bayt(a.s) tu ndio wanaopewa jukumu hili na yeyote yule mwingine ambaye anajidhania kuwa anaweza kulibeba jukumu hili, kwa hakika hukataliwa!

SOMO LA 135: CHANZO CHA MAOVU

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Jiepushe na pombe kwani hiyo ndiyo ufunguo (chanzo) cha maovu yote. 140

Maelezo mafupi: Ingawaje kunaandikwa vitabu na makala mbalimbali kuhusu athari na matokeo mabaya ya pombe na vileo, juu ya mishipa yetu ya fahamu, na mpangilio mzima wa kuivisha chakula tumboni na moyo, mishipa ya damu, maini na mafigo na kwa kifupi, sehemu zote za mwili zinatajwa na kwa hakika athari zake mbaya zinazozikumba jamii zimefanyiwa utafiti wa hali ya juu na wanasayansi na matokeo yao yanatisha, lakini sentenso hiyo fupi ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) haiwezi kupatikana popote kwani imeelezea uhakika wote katika sentenso (Hadith) moja tu. Naam, pombe kama maovu yote mengineyo, ni chanzo cha magomvi na balaa na shida za kila aina.

SOMO LA 136: KUTIMIZA WAJIBU NDIYO IBADA KUU

Yeyote yule atimizaye wajibu wake, basi atakuwa miongoni mwa wachamungu. 141

Maelezo mafupi: 'Ibada haijawekwa tu kwa ajili ya kuwahudumia watu, wala kusali na kufunga. Ambapo kwa hakika 'ibada kuu ni kule ambapo kila mmoja atatimiza wajibu wake sehemu yake. Je ni 'ibada ipi iliyo juu na bayana kuliko hiyo? Kwa hakika ni 'ibada ambayo inaweza kubadilisha jamii katika bustani ya maua na ambapo kunawza kupatikana mema na maendeleo. Kutimiza wajibu kuna imani kubwa ikiwemo wajibu wa kuabudu, zaidi ya wajibu wa kibinadamu na kijamii na hata huduma za kiuchumi, na hapo ndipo ubainisho sahihi wa wale walioacha wajibu zao zilizo za lazima na kujivunia na kuchunguza and kujidhania wao kuwa ni wafuasi wa Dini ya Islam, imebainishwa wazi.

SOMO LA 137: MAKAZI KATIKA SAYARI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Nyota hizi angani ni kama miji ilivyo juu ya ardhi, kila mji unakuwa umeunganishwa (na miji mingine) kwa kupitia mihimili ya mwanga. 142

Maelezo mafupi: NI jambo la ubinafsi kwa kuchukulia dunia yetu hii kuwa ni mahala pa kuishi tu na ambapo mamilioni ya sayari hazitumiki, zikiwa ati ni kimya bila ya viumbe vyenye uhai vinavyoishi humo. Leo wanasayansi wamepiga mahisabu yao kuhusiana na kuwapo maisha katika sayari zinginezo na wanao uhakika kuwa mamilioni ya sayari hizi zinazo viumbe vyenye uhai vinavyoishi humo, na kuna uwezekano mkubwa kuwa nyingi za sayari hizo zinamaendeleo makubwa hata kuliko sisi wakaazi wa sayari hii ya dunia kwa sababu maisha ya huko yameanza miaka maelfu ya mamilioni kabla dunia yetu hii. Hadith hiyo ya juu ni mojawapo ya muujiza wa kisayansi wa Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ambayo yeye ameizungumzia karne 14 zilizopita.

SOMO LA 138: QUR'AN TUKUFU NA KANUNI YA UZITO

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amemwambia mmoja wa marafiki zake:

Je Allah swt hasemi kuwa ameumba Jannat juu ya nguzo isiyoonekana ? Mimi nilimjibu : "Naam!" Naye (a.s) alinijibu : "Kwa hakika kuna nguzo ambayo nyinyi hamuioni." 143

Maelezo mafupi: Siku hizi, imethibitishwa kuwa sayari zimewekwa kwatika mizunguko yao, kwa hakika shukrani kwa uwiano sahihi wa uzito wa mvutano na nguvu zinazorudisha. Kwa hakika uvutio huo huvutiana kwa mfano wa mnyororo mkubwa, na nguvu za kurejesha huondoka kutokea nyenzake na uwiano wao upo sawasawa ambao umesababisha kubakia katika mzunguko wao bila ya kutokea badiliko au kulemea upande wowote, na kubakia imara katika nafasini mwao juu ya nguzo zao zisizoonekana. Je kuna maelezo yaliyo na nguvu kama ya hapo juu katika kuelezea ukweli huu katika zama hizo ambapo maajabu haya yalikuwa bado hayajavumbuliwa ? Je huu si muujiza mojawapo wa Viongozi wetu Wakuu?

SOMO LA 139: MAAJABU YA MILIMA!

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Mitikisiko na mienendo ya ardhi inadhibitiwa na milima. 144

Maelezo mafupi: Siku hizi, imethibitishwa kuwa mvuto wa Mwezi unaathari katika mwenendo wa maji ya mabahari na maji kujaa na kupwa kwa mara mbili kwa siku, kwa utofautisho wa mita 1 na hata zaidi ya mita 15 katika baadhi ya sehemu, vile vile inayo athari zake juu ya uso wa dunia (ardhi) na huiinua kwa zaidi ya sentimeta 30 na tena kuirudisha chini. Lakini kwa kutokana na ugumu halisi wa uso wa dunia kwa kutokana na kuwepo kwa milima, mizizi ambayo imeshikamana na nyenzake na kufanya mtandao kuuzunguka dunia ndio unaouponyesha athari zake zaidi. Kwa hakika, iwapo kusingalikuwapo na milima na gamba gumu la dunia lisingekuwa gumu kabisa, na kama kungalikuwapo na daima mwongezeko wa maji na kupwa, je kungalikuwapo na amani na usalama wetu ? Kwa hakika viongozi wetu wa Kiislamu wameyaelezea ukweli na uhakika huu karne 14 zilizopita.

SOMO LA 140: WANYAMA WADOGO KABISA

Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) amesema:

Sisi tunamwita Allah swt kuwa ni Mwerevu na Mwenye ustadi mwingi kwa sababu ameumba viumbe vidogo mno ambavyo sisi hatuwezi kuviona kwa sababu ya udogo wao, na wala mikono yetu haziwahisi hao. 145

Maelezo mafupi: Kile ukionacho hapo juu ni sehemu tu ya Hadith ndefu ambayo Fat'h Ibn yazid Gurgani ameihadithia kutokea Al-Imam 'Ali ar-ridha(a.s) , ambamo imeelezwa kuwa, 'wanyama hawa ni wadogo mno kiasi kwamba hawawezi kuhisiwa, na wapo wametawanyika katika mawimbi ya baharini na magamba ya miti, na majangwani na ardhi tambarare'. Hadith hii ambayo imeandikwa kiasi cha miaka elfu moja iliyopita imebakia kama ndiyo ukumbusho wa Al-Imam 'Ali ar-Ridha(a.s) na imetaja masuala haya miaka elfu zilizopita hata kabla ya kuvumbuliwa vifaa vya kuchunguzia na kukuzia viumbe vidogo kiasi hicho, na kwa hakika huu ni muujiza wa kisayansi.

15

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 14 1: LITABAKIA JINA TU KUTOKEA ISLAM

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Itawafikia watu zama ambapo herufi na maandishi kutokea Qur'an Tukufu na jina kutokea Islam yatakuwa yamebakia miongoni mwao. Misikiti ya Waislamu itakuwa ikiimarishwa kimajengo lakini yatakuwa yameteketea kwa mtazamo wa mwongozo na hidaya. 146

Maelezo mafupi: Sisi hatuwezi kusema kuhusu ubashiri huu wa kiajabu iwapo umekwisha dhihirika siku hizi au itahusika maishani mbele, lakini kwa hakika sisi tunashuhudia baadhi ya mifano yake hapa na pale na inashangaza kuwa Waislamu wanalalamikia kurudi nyuma kama kwamba kwao jina la Islam na mapicha ya Qur'an Tukufu tu vinatosha. Wao kamwe hawakuitumia Qur'an Tukufu kama ni Kitabu kifundishacho kwa ajili ya kumwelimisha mwanadamu na wala hawakuichukulia Islam kama ni shule yenye mpango wa kufundishia kiakili na kimatendo. Je wewe umeshashuhudia jamii halisi ya Kiislamu ambayo imerudi au kubakia nyuma au jamii ambayo haikutukuzwa au kuheshimiwa ulimwenguni ?

SOMO LA 14 2: KUTAMBUA UWEREVU NA UJAHILI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Ulimi ni utambulisho wa kukadiria kiasi cha ujahili na kupima uwerevu na busara. 147

Maelezo mafupi: Kwa hakika ulimi ni dirisha muhimu la nafsi na utu wake na kupima upeo wa fahamu za kila mtu. Ulimi ambao hufunua pazia kwa kupitia mizunguko yake ya kawaida na hivyo hudhihirisha vile ilipo na ilivyo nafsi ya mtu. Kwa misingi hii, mafunzo mengi mno ya Dini ya Islam yanazungumzia na kusisitiza usahihishwaji wa ulimi na maonyo na tahadhari zinakaa zikitolewa na hata viongozi wetu na ingawaje kusahihishwa kwa kikamilifu kwa ulimi hauwezekani bila ya kuirekebisha nafsi na akili na fahamu, lakini sisi tunaweza kudhibiti matokeo yanayoumiza kwa kutokwenda kwa ulimi katika mkondo sahihi kwa kukaa kimya au kujidhibiti na hiyo ndiyo njia ya kujiepusha na maovu yatokanayo na ulimi.

SOMO LA 14 3: ZAIDI YA NEEMA

imam hadi(a.s.) amesema:

"Yeyote yule anayeshukuru msaada, kuneemeka kwake kwa kushukuru kwake ni zaidi ya neema kwa ajili ya msaada, kwa sababu misaada ni mambo ya maisha ya humu duniani na shukurani ni mtaji wa humu duniani na Aakhera." 148

Maelezo mafupi: Tukichukulia ukweli huu kuwa shukrani si shukrani kwa mdomo tu, bali ni shukrani kwa uhakika na vile vile kwa kutumia msaada mahala panapostahiki, basi hapo ndipo inasemwa kuwa shukrani kwa msaada ina matokeo katika neema na mali yake kiasi kwamba msaada wenyewe si jambo kubwa kwa kulinganishwa nayo. Kwa kutumia misaada kwa uridhisho wa Allah swt na mahitaji ya waja Wake kwa hakika ni rasilimali na mtaji mkubwa kwa kuheshimika humu duniani na vile vile kwa neema kubwa huko Aakhera, wakati ambapo msaada unaweza kuwa ni neema cha kitu tu. Hivyo, shukurani ina thamani zaidi na zaidi ya msaada wenyewe.

SOMO LA 14 4: KUHUISHA SIRA ZA MA'ASUMIIN A.S.

Al-Imam 'Ali ar-Ridha (a.s) amesema:

Yeyote yule akaaye katika kikao au mkusanyiko ambapo huisha sira zetu, basi moyo wake hautakufa pale patakapo kufa nyoyo zingine. 149

Maelezo mafupi: Inafahamika wazi wazi kutokana na kauli ya hapo juu kuwa wajibu mkuu wa lazima juu ya wafuasi wa Ahlul Bayt(a.s) ya wananyumba ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni kuhuisha katika mikutano na mikusanyiko yao, kwa kujua imani na akida zao, kuelewa maana na ujumbe halisi kutokana na kauli na semi zao na kujizoesha na kufuata maamrisho yao na ni kusema kwamba mikutano na mikusanyiko yao iwe daima ni mikutano ya kusahihishana na kuwa tayari kwa maisha vile ipasavyo, na wala isiwe mikutano na mikusanyiko yao kwa ajili ya kuupoteza muda kwa starehe tu, kujiombea maslahi yao ya kibinafsi na kujifikiria mwenyewe na matatizo yake mwenyewe na matakwa yake mwenyewe bila kujali maslahi ya binadamu wengineo, imani na jamii kwa ujumla. Kwa hakika iwapo mikutano na mikusanyiko itakapokuwa vile tulivyofundishwa na Ahlul Bayt(a.s) basi nyoyo zetu zitahuika na vile vile fikara zetu zitakuwa njema zenye kuzaa matunda.

SOMO LA 14 5: SIRI NI AMANA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati mtu asemapo jambo lolote na kujitazama mwenyewe, basi mazungumzo yake hayo ni amana na siri kwetu (na inatubidi sisi kuitunza). 150

Maelezo mafupi: Kuamini katika Dini ya Islam ina sura nyingi, ikiwemo uaminifu katika kuweka na kutunza siri za watu. Jambo ili lina umuhimu mno katika Dini ya Islam kiasi kwamba kutoa siri za watu kumesemwa kuwa ni mojawapo ya Madhambi Makuu. Kwa ajili ya kutaka kuthibitisha jambo fulani kuwa siri, si lazima kwa msemaji kusema na kuomba na kusisitiza kuwapo kwa siri na kuitunza kwake. Na badala yake, ishara ndogo inatosheleza kuelewa uhakika huu. Iwapo mtu akijitazama mwenyewe na kujichambua mbele ya mtu mwingine basi inatosheleza kwake yeye kuweka mazungumzo ya ndugu yake Mwislamu kama siri yake.

SOMO LA 14 6: ALAMA ZA IMANI YA DINI YA ISLAM

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati matendo yako mema yanapokufurahisha na matendo yako maovu yanapokuhuzunisha, basi wewe ni Mumin. 151

Maelezo mafupi: Dini ya Islam inasema kuwa kila mtu huzaliwa akiwa katika maumbile yaliyo halisi na safi, imani halisi na mapenzi ya mema. Maovu na maasi ndiyo yanayokuja kuathiri nafsi yake na kuibadilisha na kuigeuza kabisa. Hata hivyo, hadi pale mwanadamu anapokuwa akipenda mema na kuchukia mabaya, nafsi yake ya imani na hali ya uhalisi wake bado unakuwapo hai ndani mwake. Watu walio waovu ambao wanakuwa wamekerwa kwa matendo yao maovu, na hujisikia fahari katika hali hiyo na au wanapojitolea mhanga, uwema, usamehevu na uadilifu huwa ni kero kwao, kwa hakika wao ni makafiri.

SOMO LA 14 7: SHARTI LA KWANZA KWA AJILI YA KILA KAZI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amemwambia Kumail ibn Ziyad:

Hakuna harakati wala kazi hadi pale utakapohitaji maarifa yake, uzoefu na elimu ya kutekeleza hivyo. 152

Maelezo mafupi: Iwapo sisi tutatafakari juu ya 'harakati zozote' zile, ndipo hapo sisi tutakuwa na uzoefu kwa mikakati na mipango ya Kiislamu na tutatambua hapo kuwa Dini ya Islam si mfuatilio wa 'ibada na dua tu na au inakosa mipango ya kimatendo. Badala yake inayo mipango na mikakati ya maisha ya mtu binafsi na vie vile masuala ya kijamii na vile vile hatua za maendeleo ya kibinadamu, jambo la kwanza ni akili na elimu ya uhakika. Islam inachukulia harakati na jitihada zote zisizo na matunda, ambazo zina elimu kidogo au mwongozo mdogo.

SOMO LA 14 8: UMUHIMU WA WAGENI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati Allah swt anapowatakia watu kheri na ukarimu, basi huwazawadia. Wao waliuliza: "Je ni zawadi ipi hiyo?" Kwa hayo Mtume (s.a.w.w) alijibu: "Mgeni." 153

Maelezo mafupi: Hayo ni ya kweli kabisa. Kwa hakika mgeni ni zawadi kutoka Allah swt , zawadi yenye heshima na thamani kubwa mno. Lakini katika ulimwengu ambamo mapenzi yote yameshapotea, mgeni hathaminiwi. Na badala yake ngeni anachukuliwa kusumbua na kutokupendwa. Hivyo, ni kwa nadra tu hutokea kwa mtu kumwalika mtu mwingine au kutembelewa isipokuwa kwa maada tu, kibiashara na uhusiano wa kisiasa. Wakati ambapo katika nchi za Kiislamu na familia ambazo bado utamaduni wa Kiislam upo hai, basi kwao mgeni huheshimiwa na kutukuzwa kama ni zawadi kutokea Allah swt hata kama hatakuwa na uhusiano wowote wa kijamaa pamoja nao.

SOMO LA 1 4 9: HESHIMA NA MAPENZI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Yeyote asiyewaheshimu wakubwa na wala kuwahurumia na kuwapenda wadogo, basi huyo si miongoni mwetu. 154

Maelezo mafupi: Jamii za binadamu ni kama msafara mkubwa ambao daima upo katika mwendo. Watoto wachanga huzaliwa na mama zao, na watoto hao hukua na wakubwa huwa wazee na wazee hufa na hakuna mtu ambaye asiyepitia msafara huu. Humu ndani, watu wazima ndio kwa kawaida wanakuwa na uzoefu zaidi na kuwa na mtazamo wa undani zaidi na wamekuwa ndio vianzio vya huduma mbalimbali katika maisha yao lau wao wangalikuwa watu wenye kutuonya kuhusu matendo yetu iwapo ni mema au mabaya, na mahisabu yote yanaonyesha kuwa wao waheshimiwe na vijana na mabarobaro waelewe heshima zao.

Na kwa kuwa watoto bado ni wapya na mwazoni mwa maisha yao, lazima wapendwe na misingi ya ukuaji wao lazima ijengwe na wakubwa kwa moyo halisi, na kwa hakika hivyo ndivyo ilivyo njia na utamaduni wa kibinadamu na jamii inayoendelea kimaendeleo.

SOMO LA 150: JICHUKULIE NJIA HII KWA AJILI YAKO

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Chochote kile kutokea kheri utakachokituma, kitahifadhiwa kwa ajili yako, na chochote kile utakachokiahirisha wewe, kitawafaidia wengineo ( na uwajibisho huo utakuwa mzigo juu yako). 155

Maelezo mafupi: Mali na utajiri unapatikana katika ulimwengu wetu wa leo kuliko kabla ilivyokuwapo bila ya kujali madhumuni muhimu na falsafa ya mali. Wale ambao hulimibikiza mali kama vichaa, na ambao hawajali ni njia zipi za halali, haraamu, haki au kudhulumu, kamwe hawafikirii kuwa wao kamwe hawataambatana pamoja na mali yao, na wala kuila yote kwa pamoja. Kwa hakika mzigo mzito upo juu ya mabega ya wenye kuimiliki mali hiyo; kulimbikiza, kuiacha na kuondoka na hatimaye kubeba wajibu wote juu yao.

VITABU VILIVYOKUSANYWA NA KUTARJUMIWA NA AMIRALY M. H. DATOO

BUKOBA - TANZANIA

Anwani ya pepe: datooam@hotmail.com

Hazina kubwa ya elimu inapatikana katika mtandao:

"www.alitrah.org

"www.dartabligh.org

"www.al-islam.org/kiswahili

VITABU VILIVYOTAYARI

1. AHADITH 2500 ZA MTUME S.A.W.W. NA MA-IMAMU A.S.

2. BWANA ABU TALIB (a.s) MADHULUMU WA HISTORIA

3. DALILI ZA QIYAMA NA KUDHIHIRI KWA IMAM MAHDI a.s.

4. DHAMBI KUU LA ISRAAF (UFUJAJI)

5. DHAMBI KUU LA KHIANA

6. DHAMBI KUU LA KUFICHA UKWELI

7. DHAMBI KUU LA KULA VIAPO VYA UONGO

8. DHAMBI KUU LA KUTOA USHAHIDI WA UONGO

9. DHAMBI KUU LA KUTOKUTIMIZA AHADI

10. DHAMBI KUU LA UCHAWI

11. DHAMBI KUU LA ULAWITI

12. DHAMBI KUU LA ULEVI

13. DHAMBI KUU LA KUTOKULIPA ZAKA, KHUMS NA SADAQAH

14. ELIMU KWA MADRASSAH : KITABU CHA KWANZA

15. FUNGUO ZA PEPONI - DUA MBALIMBALI

16. HADITHI ZA WATOTO ( PAMOJA NA PICHA )

17. HISTORIA YA ISLAM

18. HUKUMU ZILIZOTOLEWA NA IMAM 'ALI IBN ABI TALIB a.s.

19. IMAM ALI IBN ABI TALIB a.s. : FADHAIL NA HUKUMU

20. JANNAT NA JAHANNAM

21. JE MAKHARIJI NI NANI ?

22. KANUNI ZA SAUM

23. KESI YA FADAK

24. SADAKA : KUTOA NA KUPOKEA

25. MAANDISHI YA NAWHA 200 ZA 14 MASUMIIN a.s. (KATIKA LUGHA YA URDU )

26. MAELEZO NA KANUNI YA HAJJ

27. MAFUNZO 150 YA MAISHA

28. MAKALA MCHANGANYIKO No. 1

29. MAKALA MCHANGANYIKO No. 2

30. MAKHALIFA 4 BAADA YA MTUME MUHAMMAD MUSTAFA S.A.W.W.

31. MASIMULIZI KUTOKA QUR'AN TUKUFU

32. MKUSANYIKO WA FAHIRISTI YA AYAH ZA QUR'AN

33. MSAFARA WA IMAM HUSAYN IBN Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. MADINA - KARBALA

34. MWONGOZO KATIKA KUTENGENEZA USIA.

35. NAWHA, MARTHIYYAH 3100 ZA 14 MASUMIIN a.s. (SAUTI KATIKA LUGHA YA URDU)

36. TADHWIN AL-HADITH

37. TAJWID ILIYORAHISISHWA

38. TAWBA

39. USAMEHEVU KATIKA ISLAM

40. UWAHHABI - ASILI NA KUENEA KWAKE

41. VITA VILIVYOPIGANWA KATIKA ISLAM

42. WAANDISHI MASHI'A KATIKA SAHIH NA SUNAN ZA AHL SUNNA

43. WANYAMA WALIOTAJWA KATIKA QUR'AN TUKUFU

VITABU VILIVYOCHAPWA 44. DHAMBI KUU LA KAMARI

45. DHAMBI KUU LA RIBA

46. DHAMBI KUU LA UWONGO (juzuu ya kwanza )

47. DHAMBI KUU LA UWONGO (juzuu ya pili )

48. HEKAYA ZA BAHLUL

49. KITABU CHA TAJWID

50. NDOA KATIKA ISLAM

VITABU VINAVYOTAYARISHWA

1. DHAMBI KUU LA KUDHULUMU HAKI ZA WENGINE AU KUTOZITIMIZA

2. DHAMBI KUU LA KUDHULUMU MALI YA MAYATIMA

3. DHAMBI KUU LA KUIBIA UZITO

4. DHAMBI KUU LA KUKWEPA JIHAD

5. DHAMBI KUU LA KURUDIA UKAFIRI BAADA YA KUSILIMU

6. DHAMBI KUU LA KUTOKUJALI ADHABU ZA ALLAH swt

7. DHAMBI KUU LA KUTOKUWATII WAZAZI

8. DHAMBI KUU LA KUVUNJA UHUSIANO NA NDUGU NA JAMAA

9. DHAMBI KUU LA KUWASAIDI MADHALIMU

10. DHAMBI KUU LA KUWATUHUMU WATU KWA ULAWITI

11. DHAMBI KUU LA MAUAJI

12. DHAMBI KUU LA MUZIKI

13. DHAMBI KUU LA SHIRK

14. DHAMBI KUU LA UTUMIAJI WA KILICHO HARAMISHWA

15. DHAMBI KUU LA UWIZI

16. DHAMBI KUU LA ZINAA

17. DHAMBI KUU LA KUTOWASAIDIA WANYONGE

18. HIARI NA SHURUTISHO KATIKA ISLAM

19. MADHAMBI MAKUBWA NA MADHAMBI MADOGO

20. MAJINA YA WATOTO WAISLAMU

21. MASWALI NA MAJIBU MBALIMBALI

22. QUNUT

23. QURBAA-MAPENZI YA WANANYUMBA YA MTUME MUHAMMAD MUSTAFA S.A.W.W.

24. TAFSIRI YA JUZUU' 'AMMA

25. TAFSIRI YA SURAH AL-YA-SIIN

26. TAQWA

27. TUSIUPOTEZE WAKATI

28. USINGIZI NA NDOTO

29. YAAS