HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU15%

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU Mwandishi:
: AZIZI NJOZI
Kundi: Wanawake

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 33 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 47729 / Pakua: 5541
Kiwango Kiwango Kiwango
HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

18

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

NDOA YA MUDA (MUT'A)

Moja ya sheria tukufu za Uislamu kwa mtazamo wa sheria ya Ja'fari (Shia) ni kuwa kuna aina mbili za ndoa, ndoa ya kudumu na ndoa ya muda maalumu. Baadhi ya athari zinazotokana na aina hizi mbili za ndoa ni sawa (zinafanana) na nyingine ni tofauti. Kuna tofauti mbili za msingi tu kati ya ndoa hizi mbili. Moja ni kuwa katika ndoa ya muda, mwanaume na mwanamke huingia katika mkataba wa ndoa ya muda maalum. Muda ukiisha wanaweza kuongeza au kuachana.

Tofauti nyingine ni kuwa kuna uhuru mkubwa zaidi wa kuchagua katika ndoa ya muda. Wanaooana wanaweza kuwekeana masharti yoyote wanayopenda. Kwa mfano, katika ndoa ya kudumu mume anawajibika kumtunza mke wake na kumtimizia mahitaji yake ya kila siku. Pia anapaswa kumpatia mavazi, malazi na mahitaji mengine ya lazima kama vile matibabu. Lakini katika ndoa ya muda, kila kitu hutegemea masharti ya mkataba. Inawezekana kuwa mume anaweza kuwa hana uwezo au hayuko tayari kubeba gharana za mke wake, au mke anaweza asipende kutumia fedha za mume wake.

Katika ndoa ya kudumu mke anapaswa kumtambua mume wake kuwa ni mkuu wa familia na kumtii katika mambo ambayo yamo ndani ya mipaka ya familia, lakini katika ndoa ya muda hili linategemea masharti ya mkataba wa ndoa waliyowekeana. Katika ndoa ya kudumu, mke na mume wanarithiana, lakini katika ndoa ya muda hawarithiani.

Hata hivyo, katika ndoa ya muda, baada ya nikaha kusomwa, wanandoa hutambuliwa kuwa ni mume na mke halali na wanaweza kuingiliana lakini kabla ya hapo hawaruhusiwi kabisa kufanya hivyo (tendo la ndoa). Tofauti kuu kati ya ndoa ya muda na ndoa ya kudumu ni kuwa ndoa ya muda huweka masharti (majukumu) machache zaidi kwa wanandoa. Masharti yake hutegemea hiari, matakwa na makubaliano yao wao wenyewe. Kwa asili aina hii ya ndoa huwapa wanandoa uhuru fulani, na huwapa wao uhuru wa kuamua ni muda gani ndoa itadumu.

Katika ndoa ya kudumu si mume wala mke anayeweza kutumia njia za kuzuia mimba bila idhini ya mwenzake, lakini katika ndoa ya muda idhini sio jambo la lazima. Hii ni aina nyingine ya uhuru waliopewa mume na mke. Mtoto anayezaliwa katika ndoa ya muda ana hadhi sawa kisheria na mtoto aliyezaliwa ndani ya ndoa ya kudumu. Mahari: Mahari lazima ipangwe wakati wa ndoa, lakini malipo yake halisi yanaweza kutegemea makubaliano ya wanandoa wote wawili. Mahari ni ya lazima katika ndoa zote mbili ya muda na ya kudumu ingawa kuna tofauti kuwa kutopangwa kwa mahari katika ndoa ya muda huibatilisha ndoa hiyo, lakini kutopangwa kwa mahari katika ndoa ya kudumu hakubatilishi ndoa. Ikiwa mahari haikupangwa wakati wa kufunga ndoa, mke hustahili mahari ambayo imezoeleka eneo hilo.

Katika ndoa ya kudumu, mume amekatazwa kabisa kumuoa mama au binti wa mke wake na mke amekatazwa kuolewa na baba au mtoto wa mume wake. Hali iko hivi pia katika ndoa ya muda. Kama ilivyokuwa hairuhusiwi kutoa pendekezo la kumuoa mke aliyeolewa ndoa ya kudumu, halikadhalika hairuhusiwi kutoa pendekezo la kumuoa mwanamke aliye ndani ya ndoa ya muda.

Mtu akizini na mwanamke aliyeolewa ndoa ya kudumu hiki huwa ni kizuizi cha kudumu cha yeye kutokumuoa mwanamke huyo na halikadhalika mtu akizini na mke wa mtu aliye katika ndoa ya muda huwa amejiwekea kizuizi cha kudumu cha yeye kutokumuoa mwanamke huyo. Baada ya kupewa talaka, katika ndoa ya kudumu mke hupaswa kukaa eda, kipindi ambacho haruhusiwi kuolewa na mwanaume mwingine, halikadhalika katika ndoa ya muda baada ya ule muda waliokubaliana kuisha, mke anapaswa kukaa eda pia. Tofauti pekee ni kuwa kwa mke wa kudumu, eda ni miezi mitatu, ambapo kwa ndoa ya muda eda ni vipindi viwili vya hedhi, au siku 45.

Kuwaoa madada wawili kwa wakati mmoja hairuhusiwi katika ndoa zote mbili, ya muda na ya kudumu. Hii ndio maana ya ndoa ya muda kwa mujibu wa sheria ya Shia. Ni wazi kuwa tunaiunga mkono sheria hii kama itazingatia masharti yake. Ikiwa baadhi ya watu waliitumia vibaya huko nyuma au bado wanaitumia vibaya, hilo ni jambo ambalo liko nje ya sheria. Kufutwa kwa sheria hii, kama inavyopendekezwa na watu wa kisasa (modernist) hakuwezi kuwa na manufaa yoyote kwani kwa kuifuta maovu hayatakoma, isipokuwa tu yatachukua sura mpya. Vile vile, kufutwa kwa sheria hii kutasababisha kuzuka kwa maovu mengine mengi. Kinachotakiwa ni kuwa badala ya kutafuta dosari za sheria hii, watu wanapaswa kusaidiwa wajirekebishe na kuelimishwa.

Sasa hebu tuangalie kwanini ni muhimu kuwa na taasisi ya ndoa ya muda sambamba na ndoa ya kudumu. Ikiwa ndoa ya muda ni muhimu je inakubaliana na hali za sasa na mawazo ya kisasa ya maadili? Tunataka kulijadili swali hili chini ya vichwa viwili. Maisha ya sasa na ndoa ya muda. Dosari na uovu wa ndoa ya muda.

Maisha ya sasa na ndoa ya muda. Kama tulivyojifunza huko nyuma, ndoa ya kudumu huwapa majukumu mazito wanandoa wote wawili, mume na mke. Hata hivyo, hakuna mvulana au msichana ambaye wakati wa kupevuka, ambapo huwa katika shinikizo kubwa la hamu ya ngono, huwa amejiandaa kwa ndoa ya kudumu. Mahitaji ya zama hizi yameongeza urefu wa kitambo kati ya kupevuka kwa asili na kupevuka kijamii, ambapo mtu huwa na uwezo wa kujenga familia. Katika zama za kale, ambapo maisha yalikuwa rahisi, mvulana alikuwa anaweza kuanza kufanya kazi fulani toka kipindi cha awali kabisa cha kupevuka kwake na akaendelea nayo hadi mwisho wa uhai wake.

Lakini sasa hivi hili haliwezekani tena. Mvulana humaliza hatua mbali mbali za elimu akiwa na umri wa miaka 25, ikiwa hakufeli katika hatua yoyote. Hapo ndipo anapoweza kutarajiwa kuwa na kipato chake mwenyewe. Huchukua miaka mingine mitatu au minne ya kujiandaa na kuweza kuoa. Mambo yanakuwa hivi pia kwa msichana anayependa kupata elimu bora maishani. Mabarobaro na mihemko ya ngono.

Leo hii ukimuambia mvulana wa miaka 17, ambaye ndio anakuwa katika kilele cha hamu ya ngono, aoe, watu watakucheka. Hali itakuwa hivyo hivyo kwa msichana mwanafunzi wa miaka 16. Katika umri huu wote, wavulana na wasichana hawawezi kubeba majukumu ya ndoa ya kudumu, sio tu kwao kama mume na mke bali na kwa watoto wao pia watakaozaliwa. Kipi ni bora: utawa wa muda, Ukomonisti wa ngono, au ndoa ya muda? Tunajua maumbile yalivyo, lakini hali hiyo ya maisha katika ulimwengu wa sasa haituruhusu kuoa tukiwa na umri wa miaka 16 au 17.

Maumbile hayako tayari kuchelewesha upevukaji au hamu ya ngono hadi tutakapomaliza elimu yetu. Je vijana wetu wapo tayari kuishi maisha ya ubikra kwa muda hadi hapo watakapokuwa na uwezo wa kuoa ndoa ya kudumu? Hata kama kijana mwenyewe yuko radhi kustahamili, je, maumbile yapo tayari kumsamehe asipatwe na shinikizo na hitilafu za neva ambazo kwa kawaida matokeo yake ni kumfanya ajiepusha kutokana na tendo la kawaida la ngono, kama ilivyobainishwa na wataalamu wa kisasa wa sayansi ya akili? Sasa tumebakiwa na njia mbili tu.

Ya kwanza ni kumruhusu mvulana kushirikiana ngono na mamia ya wasichana, na msichana kushiriki katika uhusiano haramu na wavulana wengi, na kisha kutoa mimba nyingi. Hii inamaanisha kuwa kivitendo tunaruhusu Ukomonisti wa ngono. Kwa hakika, tukitoa uhuru usio na mipaka kwa wavulana na wasichana, tutakuwa tunakidhi matakwa ya Azimio la Haki za Binaadamu, kwa sababu kwa maoni ya watu wengi wenye akili finyu, Azimio linataka kuwa, ikiwa wanaume na wanawake wataenda motoni, basi waende pamoja mkono kwa mkono.

Lakini swali ni iwapo itawezekana kwa wavulana na wasichana hawa ambao watakuwa wamefanya ngono zisizo na idadi wakati wa kipindi chao cha masomo, kuishi maisha ya kawaida ya familia. Njia ya pili ni ndoa huru ya muda. Kwa kuanzia ndoa ya muda humpa kila mume mke mmoja kwa wakati mmoja. Ikiwa kila mwanamke ana mwanaume mmoja, ni wazi kila mwanaume atakuwa na mwanamke mmoja, isipokuwa pale ambapo jinsia moja itakuwa kubwa sana kuliko nyingine. Hivyo wavulana na wasichana wanaweza kupita katika kipindi chao cha masomo bila kupata madhara ya kuishi maisha ya utawa wa muda, au kuangukia katika lindi la Ukomonisti wa ngono. Ndoa ya majaribio. Kimsingi inawezekana kwa mwanaume na mwanamke wanaokusudia kuona ndoa ya kudumu wakawa kila mmoja hana imani ya kutosha juu ya mwenzake, hivyo wakaoana kwa majaribio kwa muda fulani.

Wakiwa wameaminiana vya kutosha, huendelea kuishi maisha ya ndoa, vinginevyo wanatengana. (kwa hiyo, tofauti kati ya mtindo wa Kimagharibi wa uhusiano pamoja na mwanamke na Uislamu ni kuwa kwa Wamagharibi hakuna dhana ya mfumo wa ndoa kati ya mwanamke na mwanaume ambapo katika Uislamu wenzi huhesabiwa kuwa mke na mume hata kama ni kwa muda). Nadharia ya Russell ya ndoa ya muda. Katika kitabu chake 'Matrimony and Morals' mwanafalsafa maarufu sana wa Kiingereza, Bertrand Russell, anasema kuwa malaya wanauhifadhi usafi wa kimaadili (kutozini) wa wake zetu na binti zetu. Mtazamo huu ulipotolewa kwa mara ya kwanza na Luckey katikati ya kipindi cha utawala wa Victoria watetea maadili walikereka sana, ingawa hata wao hawakujua kwanini.

Hata hivyo hawakuweza kuzivunja hoja za Luckey. Mantiki ya watetezi wa maadili ilikuwa, kama watu wangefuata maadili yao, malaya wasingekuwepo. Lakini walielewa fika kuwa hakuna aliyezingatia walichosema. Hii ndio kanuni ya kizungu ya kukabiliana na hatari inayoletwa na wanaume na wanawake wasioweza kufunga ndoa ya kudumu, na iliyotajwa hapo juu ni kanuni iliyopendekezwa na Uislamu.

Ikiwa kanuni hii ya kizungu itazingatiwa na jukumu hili likakabidhiwa kwa kundi fulani la wanawake wenye bahati mbaya, je hii itakuwa inaafikiana na heshima ya utu wa mwanadamu na staha ya mwanamke na kiini cha Azimio la haki za Binadamu? Bertrand Rusell, katika kitabu chake, ameingiza sura ya ndoa ya majaribio pia. Anasema kuwa Lindsay, ambaye kwa miaka mingi alikuwa jaji wa Denver, na kwa nafasi yake hiyo alikuwa na nafasi ya kutosha ya kuchunguza ukweli wa mwenendo wa maisha, alipendekeza kuwa iwepo 'ndoa ya wenzi' (companionship marriage).

Lakini kwa bahati mbaya jaji huyu alilazimika kupoteza kazi yake kwa kuwa alikuwa anajali maslahi ya vijana mno kuliko kuwajengea ndani yao hisia ya dhambi. Ili kuhakikisha anafukuzwa, mengi yalisemwa na kanisa Katoliki na Ku Klux Klan, (chama cha siri cha watu ambao hawataki watu weusi kushirikiana na watu weupe - wabaguzi wa rangi nchini Marikani). Ndoa ya wenzi ilipendekezwa na msomi anayependelea kuhifadhi mila za kale kwa nia ya kuweka jambo litakaloleta uimara katika mahusiano ya ngono. Lindsay alibaini kuwa tatizo kubwa la ndoa lilikuwa ni ukosefu wa fedha. Fedha haihitajiki kwa ajili ya watoto watakaozaliwa tu, lakini pia kwa sababu haimuwajibikii mwanamke kubeba gharama za matunzo ya familia. Anafikia hitimisho kuwa vijana wanapasa kufunga ndoa za wenzi (muda) ambazo ni tofauti na ndoa za kawaida katika njia tatu. Kwanza nia ya ndoa hii sio kuzaa watoto.

Pili: kwa vile mwanamke huwa hajazaa mtoto, kuachana muda unapokwisha huwa jambo rahisi. Tatu, katika suala la talaka, mwanamke hustahili kulipwa masurufu baada ya kuwa ameachwa. Hapana shaka kwamba mapendekezo ya Lindsay yanafaa na yanatekelezeka, kama yangekuwa yamekubaliwa kuwa sheria, yengetarajiwa kuwa na matokeo mazuri kwa maadili. Ambacho Lindsay na Russell wanakiita ndoa ya wenzi ni tofauti kidogo tu na ndoa ya muda katika Uislamu, lakini pendekezo hili linaonyesha kuwa wanafalsafa wa fani hii wamebaini kuwa ndoa ya kawaida ya kudumu haikidhi mahitaji yote ya jamii. Ndoa ya muda-II Tayari tumeshaeleza tabia ya ndoa ya muda, ulazima wa kuwepo kwake na ndoa ya kudumu kushindwa kukidhi mahitaji yote ya wanaadamu. Sasa hebu tuangalie upande wa pili wa shilingi na kuona hasara na dosari zake. Kabla ya kujadili hilo hebu tuangalie kitu kimoja.

Historia ya Imani. Katika masomo yote ambayo watu mbali mbali wameyatolea maoni, hakuna lililo tata na gumu kama historia ya mawazo, imani, mila na desturi za mwanadamu. Hii ndio sababu kuwa japo mada hii ni maarufu sana, maoni yaliyo mengi yanayotolewa juu ya hili yamekuwa ni upuuzi. Mtu yeyote mwenye elimu juu ya falsafa, mafundisho ya kumfikia Mungu kwa tafkira, irifan (mysticism) na falsafa ya uanazuoni (schalasticim) wa Kiislamu, na akasoma maandishi ya hivi karibuni katika nchi yetu juu ya masuala yanayohusiana na mada hii ataona kuwa mengi yanaazimwa kutoka kwa wageni au wananukuu na kuiga kila neno lao, pia anaweza kuelewa ninachomaanisha.

Waandishi wetu wa zama hizi wanarudia au kuziegemeza kazi zao na mustashirik, wakati inaonekana kuwa mustashirik hawa na vibaraka wao hawafanyi lolote katika kuyachambua masuala haya kwa kina. Kwa mfano, suala linalofahamika katika mafunzo ya Kiislamu ya irifan (mytcism) kama wahadat al-Wujud (Umoja wa Mwenyezi Mungu) limejadiliwa kutoka katika kila pembe, lakini hakuna jitihada ya maana iliyoelekezwa kufafanua maana halisi ya dhana (neno) hiyo wala kuelezea maoni ya vinara wa mafunzo haya ya irifan (Islamic Mysticism) kama vile Muhyiuddin ibn Arabi na Sadrul Muta'llihin Shiraz.

Hivi karibuni maoni yaliyotolewa juu ya ndoa ya muda katika gazeti la ki-Iran 'Zan-e-Imruz' au "mwanamke wa leo" yamenikumbusha mada ya 'Wahdat al-Wujud' Katika makala haya kila kitu kilizungumzwa juu ya ndoa ya muda, lakini nia hasa ya sheria hii iliachwa. Watu hawajali sheria hii kwa kuwa ni sehemu ya urithi wa Mashariki. Ingekuwa ni zawadi kutoka Magharibi mambo yangekuwa tofauti kabisa. Kama sheria hii ingekuwa inatoka Magharibi bila shaka makongamano na semina yangekuwa yanafanyika kutetea wazo kuwa ndoa ya kudumu haikidhi hali ya maisha ya karne hii na kwamba kizazi hiki hakiko tayari kubeba majukumu mazito ya ndoa ya kudumu.

Kizazi hiki kinataka kuwa huru. Kinataka kuishi maisha ya uhuru. Kinataka ndoa huru ambayo masharti yake yataamuliwa na wanandoa wenyewe. Sasa kwa kuwa tayari sauti zimeanza kupazwa huko Ulaya kuteteta ndoa ya muda na watu mashuhuri kama Bertrand Russel wanaihubiri kwa jina la ndoa ya wenzi inatarajiwa kuwa baada ya muda si mrefu ndoa ya muda itakuwa mashuhuri mno kiasi cha kuwa tutalazimika kuzindua kampeni za kutetea ndoa ya kudumu.

Pingamizi Yafuatayo ndiyo yanayosemwa kuwa ni ubaya na mapungufu ya ndoa ya muda. Msingi wa ndoa unapaswa kuwa wa kudumu tokea mwanzo wa mahusiano ya unyumba, mume na mke wanapaswa kujua kuwa kila mmoja ni mali ya mwenzake kwa kudumu. Wazo la kutengana halipaswi kuingi akilini mwao. Ndoa ya muda sio mkataba wa kudumu kati ya mume na mke. Ni kweli kuwa msingi wa ndoa unapaswa kuwa wa kudumu.

Hata hivyo, pingamizi hili linaweza kuwa sahihi tu kama tutaipinga ndoa ya kudumu na kuhimiza kuwa nafasi yake ichukuliwe na ndoa ya muda. Kama pande mbili zinaweza kuimudu ndoa ya kudumu na kila mmoja ana imani ya kutosha na mwenzake na wakaamua kuwa kwa kudumu kila mmoja awe mali ya mwenzake hapana shaka kuwa wanapaswa kufunga ndoa ya kudumu. Sheria ya ndoa ya muda imewekwa tu kwa vile ndoa ya kudumu peke yake haiwezi kukidhi mahitaji yote ya wanaadamu katika hali zote. Kuruhusu ndoa ya kudumu peke yake kutasababisha tu Ukomonisti wa ngono. Ni wazi kuwa hakuna mvulana au msichana ambaye ana rasilimali za kutosha kwa ajili ya ndoa ya kudumu anaweza kujiingiza katika mahusiano ya muda.

Wanawake na wasichana wa Kiirani, licha ya kuwa Shia, hawalipendi wazo la ndoa ya muda. Wanaliona kama tusi kwao. Hivyo maoni ya jumla ya Shia wenyewe yamelikataa. Tunaweza kujibu kuwa kulichukia wazo hilo kijumla kunatokana na wanaume waasherati kulitumia vibaya. Ni jukumu la serikali kuzuia kutumiwa kwake vibaya. Pili sio jambo la maana kutarajia ndoa ya muda kuwa mashuhuri kama ndoa ya kudumu, kwa sababu ndoa ya muda inakusudiwa kukidhi mahitaji ya wahusika ikiwa wote au mmoja wao hayuko tayari kufunga ndoa ya kudumu. Ndoa ya muda inashusha hadhi na utu wa mwanamke.

Ni sawa sawa na kuukodi mwili wa mtu, na hata kuhalalisha uuzaji wa watu. Ni kinyume na staha ya mwanamke kumuweka kwa ajili ya mwanaume yeyote kwa kubadilishana na fedha. Hili ni pingamizi linalostaajabisha zaidi. Kwanza ndoa ya muda, kama tulivyoeleza hapo awali, haina uhusiano wowote na uuzaji au ukodishaji. Je inaweza kuwa uuzaji au ukodoshaji kwa vile tu muda wa ndoa ni maalum? Je inakuwa ni kukodisha kwa kuwa mahari inapaswa kupangwa?

Tunataka kulijadili suala la mahari tofauti. Mafakihi wamekubaliana kuwa, kwa asili ya mkataba, hakuna tofauti kati ya ndoa ya kudumu na ndoa ya muda. Ni miundo miwili ya ndoa na mikataba yake inaweza kusihi tu kwa kuzingatia kanuni ya ndoa. Ikiwa mkataba wa ndoa ya muda utachukua sura ya uuzaji au ununuaji, basi itakuwa ni batili. Pili, tangu lini ada ya kukodi (kuajiri) watu ilipigwa marufuku? Mafundi cherehani, vionyozi, wapishi, hata wataalamu mabingwa, waajiriwa wote wa serikali kuanzia kwa Waziri Mkuu hadi kwa afisa wa cheo cha chini kabisa na wafanyakazi wote wa viwandani wote ni wa kukodiwa.

Mwanamke ambaye kwa hiari yake anaingia mkataba wa ndoa ya muda na mwanaume fulani sio mwanamke aliyekodishwa na hafanyi jambo la aibu kwa staha yake. Kama unataka kuona wanawake waliokodishwa na waliofanywa watumwa na unataka kujua maana halisi ya mwanamke aliyeajiriwa (kodiwa), unapaswa kwenda Ulaya na Marekani na utembelee makampuni ya filamu. Huko utaona miondoko ya viungo vya mwanamke, ishara zake na mikao ya kingono ikiuzwa. Tiketi za sinema na kumbi za starehe unazonunua ndiyo mishahara ya wanawake waliokodiwa.

Unatambua ni kiasi gani mwanamke anajidhalilisha ili kupata fedha? Analazimika kujifunza kwa miaka mingi sanaa ya kuamsha na kuchochea hamu ya ngono chini ya usimamizi wa wataalamu bingwa wa fani hiyo na wenye uzoefu. Analazimika kuuweka mwili wake, roho yake na haiba yake rehani kwenye makampuni ya biashara ili kuvutia wateja zaidi na zaidi. Ukitembelea mikahawa na mahoteli, unaweza kuona ni heshima gani mwanamke aliyopata, ni jinsi gani analazimika kuuza heshima na utu wake kwa ajili ya fedha kidogo ili kujaza masanduku ya fedha ya mabepari na jinsi gani analazimika kujiuza mbele ya wageni.

Wanawake waliokodiwa ni wale wasichana wa mauzo katika maduka makubwa ambao wanaitoa mhanga heshima na staha yao ili kukidhi tamaa ya waajiri wao. Wanawake waliokodiwa ni wale wasichana wanamitindo wanaoonekana katika TV wakitangaza bidhaa na wanaotumia mbinu zote kuwavutia wateja kwao. Nani asiyejua kuwa leo hii huko Magharibi uzuri wa mwanamke, mvuto wake wa kingono, sauti yake, sanaa yake, mwili wake, roho yake na zaidi ya yote, haiba yake vinatumika kama njia nyenyekevu za kutumikia maslahi ya ubepari wa Ulaya na Marekani?

Ninashangaa ni vipi mwanamke aliyeolewa na mwanaume fulani kwa hiari yake lakini kwa muda maalum anachukuliwa kuwa mwanamke aliyekodiwa (kufanya ngono) wakati mwanamke ambaye katika sherehe ya harusi au kwenye hafla ya jioni, mbele ya maelfu ya macho yenye tamaa ya wanaume, anaimba mpaka koo lake linauma, haonekani kuwa ni mwanamke aliyekodiwa (kufanya mambo machafu).

Kwa kuruhusu ndoa ya muda, Uislamu umemkinga mwanamke dhidi ya kunyonywa na mwanaume. Pia Uislamu umemkataza kutumia njia dhalili ili kujipatia riziki. Je, ni Uislamu uliomdhalilisha mwanamke au Ulaya ya karne hii? Ikiwa siku moja mwanamke atagundua mitego yote ambayo mwanaume wa karne hii ameiweka katika njia yake, bila shaka atapinga kwa nguvu zote uongo na udanganyifu huu. Hapo tu ndipo atakapobaini kuwa mlinzi pekee mwaminifu kwake na kimbilio lake ni Qur'ani.

Siku hiyo haiko mbali sana! Aidha, ndoa ya muda inahalalisha ndoa za mitala, ambazo ni mila mbaya. Kwa hiyo ndoa ya muda haifai. Mwisho wa sura hii tutaeleza ni kwa ajili ya nani sheria hii imewekwa. Na kuhusiana na ndoa za mitala, tutajadili hilo katika sura inayofuata. Ndoa ya muda haidumu. Huwaacha watoto watakaozaliwa wakiwa hawana makazi. Wanakuwa hawana mtu anayewajibika kwao. Wananyimwa uangalizi wa baba na upendo wa mama. Katika ndoa ya kudumu hakuna mwanandoa anayeweza kukwepa jukumu la kuzaa watoto, lakini katika ndoa ya muda, pande zote mbili ziko huru. Ni kweli kuwa mke hapaswi kumzuia mume wake kufurahia jimai, lakini anaweza kuchukua hatua za kuzuia mimba.

Tatizo hili limetatuliwa kabisa kutokana na maendeleo ya njia za kisasa za kuzuia mimba. Hivyo katika ndoa ya muda, ikiwa wote wawili, mume na mke wanapenda wanaweza kuzaa watoto, ikiwa wanalikubali jukumu la kuwalea. Ni wazi kuwa, kwa upande wa upendo wa asili, hakuna tofauti kati ya mtoto aliyezaliwa ndani ya ndoa ya kudumu na yule wa ndoa ya muda.

Ikiwa baba au mama watakataa kutekeleza jukumu lao, ni jukumu la mahakama kuwalazimisha kama vile tu inavyoingilia katika suala la talaka. Ikiwa mume na mke hawataki kuzaa watoto na nia yao ni kukidhi haja zao tu, wanapaswa wajiepushe kuzaa watoto. Kama tunavyojua, Kanisa haliruhusu njia za kuzuia mimba. Lakini kwa maoni ya Uislamu mume na mke wako huru kutumia njia za kuzuia mimba. Hata hivyo mimba ikishaingia hairuhusiwi kuitoa au kuiharibu.

Hili ndilo wanalolimaanisha mafakihi wa Kishia wanaposema kuwa lengo la ndoa ya kudumu ni kupata watoto na la ndoa ya muda ni kukidhi haja ya asili ya jimai. Ndoa ya muda maalum na nyumba ya wake wa mtu Moja ya mada, ambazo nchi za magharibi zinaitumia kama silaha ya kuonyesha uovu wa nchi za Mashariki na ambayo nchi za magharibi zimeandaa filamu na tamthilia kwa ajili yake ni suala la uundaji wa nyumba za wake (harems). Kwa bahati mbaya, mifano hii ni ukweli uliopata kuwepo katika historia.

Maisha ya baadhi ya makhalifa na masultani yanatoa mfano kamili wa muundo wa 'nyumba za wanawake' wao, ambazo huelezewa kuwa ni alama mashuhuri ya uasherati wa mwanaume wa Mashariki. Inadaiwa kuwa uhalali wa ndoa ya muda unafanana tu na uhalali wa nyumba ya wake, ambayo ni nukta dhaifu kwa upande wa nchi za Masharikii na imeleta aibu kwayo. Sio hivyo tu, bali pia ni sawa na kuhalalisha uasherati, miundo yote ambayo inakwenda kinyume na maadili na husababisha kuporomoka na kuangamia. Kitu hicho pia kimesemwa juu ya ndoa za mitala na zimetafsiriwa kuwa ni uhalalishaji wa nyumba za wanawake wengi (walio chini ya mwanaume mmoja). Tutalijadili suala la ndoa za mitala peke yake.

Hivi sasa tunabakia kwenye ndoa ya muda. Suala hili linapaswa kujadiliwa katika pembe mbili: Ni sababu gani za kijamii zilizosababisha uundwaji wa nyumba za wake (wa mtu mmoja) huko nyuma? Je, sheria ya ndoa ya muda ilikuwa na ushawishi katika hali hii? Je sheria ya ndoa ya muda inakusudia kutoa fursa kwa wanaume waasherati kuunda nyumba za wanawake wao? Sababu za kijamii za uundwaji wa nyumba za wake wa mtu (harems).

Kulikuwa na sababu mbili zilizosababisha kuwepo kwa nyumba hizi. Ya kwanza ilikuwa ni uchamungu na staha ya mwanamke. Nyumba hizi zinaweza kuundwa tu katika mazingira ambayo mwanamke hawezi kufanya tendo la ndoa na mwanaume zaidi ya mmoja. Katika hali hiyo mwanaume muasherati hana namna ila kuwakusanya wanawake wengi na kuunda 'nyumba ya wakeze' (harem). Ni wazi kuwa katika mazingira ambayo umuhimu hauwekwi katika staha na wanawake wapo wengi na bure hakuna anayeweza kuchukua taabu ya kuunda 'nyumba ya wake' kubwa kwa gharama kubwa na vifaa vingi. Sababu ya pili ilikuwa ni kutokuwepo kwa uadilifu wa kijamii.

Mazingira yanayofaa kwa uundaji wa 'nyumba za wake' ni kuwa wachache wame bobea katika kila aina ya starehe na raha, ambapo wengine hawawezi hata kupata mlo wa siku, na ambamo kuna wengi ambao hawawezi kumudu kuoa na kuwa na familia. Katika mazingira hayo, idadi ya wanawake ambao hawajaolewa huongezeka na hutengeneza mazingira mazuri ya uundwaji wa nyumba za wake.

Kwa upande mwingine, ikiwa kuna uadilifu wa kijamii na kuna uwezo wa kuunda familia na kuchagua mke/mume kwa wote, basi ni wazi kuwa kila mwanamke ataambatana na mume mmoja na kunakuwa hakuna fursa ya ufisadi na uundaji wa nyumba hizi. Ikiwa kila mtu mzima ana nafasi ya kuwa na mume/mke, ni wazi kuwa hapatakuwa na idadi kubwa ya wanawake wanaobaki kwa ajili ya matajiri kuunda nyumba za wake, kwani idadi ya wanawake kwa kawaida huwa sawa, huzidi au kupungua kidogo kuliko idadi ya wanaume.

Imekuwa ni mila kuwa historia inasimulia hadithi za nyumba hizi za makhalifa na masultani na kuelezea fahari na utajiri wa vitala (makazi na ofisi) vyao lakini hupuuzia kueleza dhiki, shida na taabu ya wale waliokufa katika tawala hizo na ambao hali zao hazikuwa zikiwaruhusu kuwa na mke. Mamia ya wanawake waliomalizia maisha yao katika nyumba hizi walikuwa ni haki ya asili ya wanaume hawa fukara waliolazimika kubakia bila kuoa mpaka walipokufa. Bila shaka katika jamii ambayo staha na usafi wa kimaadili upo na ambapo tendo la ngono haliwezekani isipokuwa ndani ya mipaka ya ndoa, zikiwemo zote mbili, ya muda na ya kudumu, uundaji wa nyumba za wake hauwezekani, hasa inapokuwa matabaka ya kijamii na kiuchumi yameondolewa na haki ya ndoa inapowekwa wazi kwa kila mtu mzima.

Tukiitazama historia kwa haraka haraka tutaona kuwa sheria ya ndoa ya muda haikuwa na ushawishi wowote katika uundwaji wa 'nyumba za wake' hata kidogo. Hakuna khalifa yeyote wa ukoo wa Abbas na masultani wa himaya ya Ottoman ambao hawa ndio walikuwa mashuhuri kwa kuwa na 'nyumba za wake' kubwa, aliyekuwa mfuasi wa Theolojia ya Shia na hivyo haitarajiwi kuwa yeyote kati yao angeweza kuwa alitumia fursa ya sheria ya ndoa ya muda. Masultani wa Kishia, japo wangeweza kuwa waliitumia sheria hii kama kisingizio kamwe hawakupata kufanya hivi kama makhalifa wa Ibn Abbasi na masultani wa himaya ya Ottomani. Hii inaonyesha wazi kuwa nyumba hizi zilisababishwa na sababu nyingine maalum za kijamii.

Je ndoa ya muda imehalalishwa ili kukidhi tamaa ya mwili? Hapana shaka kwamba dini zote za ki-mungu zinazuia kabisa uasherati na ukosefu wa maadili, kiasi cha kufikia baadhi ya wafuasi wake kuamua kuishi maisha ya utawa. Moja ya kanuni za wazi za Uislamu na zinazokubalika ni kupiga vita uzinifu, ambao umelinganishwa na shirki (kwa maneno ya Qur'ani).

Uislamu umemuelezea 'muonjaji' yaani anayetaka kufaidi kila aina ya wanawake, kuwa anashutumiwa na kuchukiwa na Allah. Tulipokuwa tukijadili suala la talaka, tulilizungumzia hili. Moja ya sifa (tabia) za Uislamu ni kuwa unapinga utawa na useja (kutooa) lakini hauruhusu uzinifu, kwa mujibu wa Uislamu, matamanio ya haja zote za asili, ikiwa ni pamoja na haja ya ngono yanatakiwa kukidhiwa ndani ya mipaka ya kisheria tu kwa kiasi cha mahitaji ya asili. Uislamu hauruhusu kuwasha moto wa matamanio na kuubadili kuwa kiu isiyokatika. Uislamu unapinga mambo yote yenye sura ya uasherati na dhulma.

Ni ukweli usio na shaka kuwa kamwe haikuwa nia ya Mtungaji wa sheria hii ya ndoa ya muda kutoa njia kwa washerati ya kukidhi matamanio yao yasiyokatika ya ngono na kuleta maafa na maangamizi kwa mwanamke na watoto wake wasio na hatia. Utiaji moyo mkubwa uliowekwa kwenye wazo la ndoa ya muda maalumu na Maimamu (wa Ahlul Bait) una falsafa maalumu, ambayo tutaieleza kwa kifupi. 'Nyumba za wake' na ulimwengu wa kisasa. Sasa hebu tuangalie jinsi ulimwengu wa kisasa ulivyolishughulikia suala la nyumba hizi. Ulimwengu wa kisasa unazitazana nyumba hizi kwa chuki na mila hii imeshaachwa.

Moja ya vipengele viwili vilivyosababisha kuwepo kwa nyumba hizo kimeshaondolewa. Lakini ni sababu ipi hiyo? Sio ile ya matabaka ya kijamii bali ile ya staha na uchamungu wa wanawake ndiyo imeondolewa. Mwanaume mzinifu wa zama hizi hahitaji tena kutaabika kuunda 'nyumba ya wake' na kubeba gharama kubwa za kuihudumia. Shukrani kwa utamaduni wa Kimagharibi kwamba kwa mwanaume wa karne hii 'nyumba ya wake' ipo katika kila sehemu.

BIli kuwafaidi wanawake wa rangi na mataifa mbali mbali, mwanaume wa sasa hahitaji kuwa na madaraka makubwa na fedha nyingi kama Harun al-Rashid au Fazl Ibn Yahya Barmaki. Anachohitaji ni gari tu na kipato cha elfu kiasi kila mwezi ili kuweza kufaidi ngono kwa kiasi ambacho hata Harun alRashid hakupata kuota.

Hoteli za kisasa, migahawa, na mikahawa mara zote zipo tayari kuhudumia (kutumiwa) kama nyumba za wanawake kwa wanaume. Wakati fulani uliopita kijana wa Kiiran, Adil Kutwali, wazi wazi alikiri kuwa na mabibi (mahawara) 22 wa maumbo na sura mbali mbali kwa wakati mmoja. Shukrani kwa utamaduni wa Kimagharibi kwamba mwanaume wa sasa anafurahia raha zote za nyumba hizi (harem) bila kuwa na hofu ya gharama kubwa ya kuihudumia. Kama shujaa wa 'alfu lela ulela' (masiku elfu moja na moja) angenyanyua kichwa chake kutoka mavumbini na kuona fursa tele za kufaidi ngono na urahisi wa bei pamoja na uwingi wa wanawake, asingefikiri tena haja ya kuwa na nyumba ya wake, na kubeba gharama zote za kuihudumia.

Angewashukuru watu wa magharibi kwa kumuokoa na gharama zote za kuunda nyumba ya wanawake na hapo hapo angetangaza kufutwa kwa ndoa za mitala na ndoa za muda, kwa sababu zinawapa wanaume mzigo wa majukumu juu ya wanawake. Ukiuliza ni nani aliyepoteza katika mchezo huu, kwa kuwa mshindi anajulikana toka zamani, tutasema kuwa kwa bahati mbaya mwanamke ndiye mara zote amekuwa mpotezaji. Kwa sababu ya kuamini kirahisi na kuwa rahisi, alipoteza jana na amepoteza leo.

Khalifa apiga marufuku ndoa ya muda maalum.

Ndoa ya muda inaruhusiwa na sheria ya Shia (Jafaria) peke yake. Madhehebu mengine ya Kiislamu hayaruhusu. Sikusudii kuingia katika ubishani wa Shia na Sunni. Napenda tu hapa kutaja kwa kifupi usuli wa kihistoria wa suala hili. Waislamu wote wanakubaliana kuwa katika kipindi cha awali cha Uislamu Mtukufu Mtume wakati akiwa safarini na ikawa Waislamu walikuwa mbali na wake zao na hivyo wakawa wanapata ugumu, aliwaruhusu kufunga ndoa za muda.

Inakubaliwa pia na Waislamu wote kuwa Khalifa wa pili, katika kipindi cha ukhalifa wake, aliipiga marufuku ndoa ya Mut'a kwa mujibu wa taarifa mashuhuri, alisema kuwa: "Leo ninapiga marufuku vitu viwili ambavyo vilikuwa halali wakati wa Mtume. Ni ndoa ya muda na kuhiji 'Hajj' na Umra kwa ihram mbili tofauti." Baadhi ya Sunni wanaamini kuwa Mtume mwenyewe aliipiga marufuku ndoa ya muda katika kipindi cha mwisho cha uhai wake na Khalifa wa pili alirudia kupiga marufuku ambayo tayari imeshawekwa na Mtume.

Lakini maneno ya Khalifa ambayo yamekuja kwetu yanaonyesha kitu tofauti na hiki. Maelezo sahihi juu ya hili ni yale yaliyotolewa na Allamah Kashif alGhita. Khalifa alipiga marufuku ndoa ya muda kwa sababu alifikiri kuwa jambo hili lilikuwa ndani ya mamlaka yake kikatiba kama Mkuu wa Dola, ambaye angeweza kutumia mamlaka yake maalum kutokana na mahitaji ya wakati. Kwa maneno mengine zuio la Khalifa lilikuwa ni la kisiasa sio la kisheria. Khalifa kamwe alikuwa hafichi wasi wasi wake juu ya kusambaa kwa masahaba wa Mtume katika nchi mpya zilizotekwa na kuchanganyika kwao na Waislamu wapya waliosilimu.

Katika muda wote wa uhai wake, alipinga vikali suala la Waislamu (masahaba) kuhama kutoka Madina. Pia hakutaka damu zao zichanganyike na Waislamu wapya waliosilimu, ambao imani yao ilikuwa bado haijawa kubwa. Ni wazi kuwa hii ilikuwa ni rai ya muda. Waislamu wa wakati ule waliikubali amri yake bila kuonyesha chuki, kwa sababu tu walijua kuwa ilikuwa ni ulazima wa kisiasa na sio sheria ya kudumu. Vinginevyo hailekei kwamba watu wangeridhika, kama wangeona Mtume aliamrisha hivi na Khalifa anaamrisha vinginevyo.

Lakini baadaye ambapo kama matokeo ya maendeleo fulani, maisha ya makhalifa wa mwanzo, hususan makhalifa wawili wa mwanzo, yalichukuliwa kama kiigizo, amri zao zilichukua sura ya sheria ya kudumu. Hivyo ndugu zetu wa kisunni wanapaswa kulaumiwa zaidi kuliko khalifa ambaye aliweka zuio la muda dhidi ya ndoa ya muda kwa sababu za kisiasa (kama ilivyokuwa kwa zuio la tumbaku nchini Iran katika mwanzo wa karne hii) Wengine wasingepaswa kulipa zuio hili sura ya sheria ya kudumu.

Ni dhahiri kuwa Allamah Kashif al-Ghita hakutoa maoni yoyote juu ya kitendo cha khalifa kama kilikuwa kinakubalika au la. Alieleza tu asili ya zuio hili na kwa nini halikupingwa na Waislamu. Hata hivyo ni kutokana na ushawishi huu na haiba (shaksia) ya Khalifa, kwamba watu waliacha kuifuata sheria hii na kwa sababu mila ya Uislamu ya ndoa ya kudumu ilidhaniwa ingeachwa basi ikawa ndoa ya muda imeachwa.

Ni katika hali hii kwamba kwa nia ya kuhakikisha kuwa desturi ya Kiislamu haisahauliki kabisa, Maimamu watukufu wa Ahlul Bait, ambao ni watetezi na walinzi wa imani walihimiza na kuitetea sana. Imam Jafar Sadiq(a.s) alikuwa akisema kuwa ndoa ya muda ni nukta ambayo hawezi kuificha kamwe. Mbali na faida nyingi za ndoa ya muda, jitihada ya kufufua desturi zilizokufa ilikuwa ni sababu nyingine ya Maimamu kuihubiri. Kwa maoni yetu, Maimamu walipowakataza watu kuoa kwa ndoa ya muda, walitaka iwe wazi kuwa ndoa hii haikuwa kwa wale wasioihitaji.

Imam Kadhim(as) alimwambia Ali ibn Yaqtin, 'Unataka ndoa ya muda ya nini? Allah amekuepusha na tatizo la kuihitaji." Alimwambia mtu mwingine kuwa 'ndoa ya muda, ni kwa yule asiye na mke au mwenye mke lakini mke wake yuko mbali." Muongozo na uhimizaji wa umma katika kuoa ndoa za muda ni hatua moja mbele katika "ufufuaji wa mila zilizoachwa" au desturi lakini uhimizaji peke yake kwa wale waliokuwa wakiihitaji haukuwa unatosha kuihuisha tena mila hii tuliyoruhusiwa na Mtume, kama inavyoonyeshwa wazi katika maandiko ya Kishia na vitabu vya hadithi.

Hata hivyo ni ukweli ulio wazi kuwa maana na lengo la Mtunzi wa sheria hii katika kuikuza (kuitetea) na maelezo ya sheria hii na lengo la Maimamu Maasumin la kuihimiza halikuwa na nia ya kuruhusu majaribio ya ngono, matamanio maovu na ujenzi wa nyumba za wake kwa ajili ya watu wenye tabia za wanyama wala kuwakandamiza na kuwatesa wanawake wasio na uwezo na waliokandamizwa pamoja na watoto yatima kwa wakati wowote. Mwandishi wa kimisri, Sheikh Muhammad Abu Zuhra, katika kitabu chake, 'Al-Ahwal al-Shakhsiya, amemnukuu Amirul Muuminina Ali(a.s) kuwa amesema, "Kama nikipata habari kwamba mtu mmoja mwenye mke amefunga ndoa ya muda, nitampiga mawe mpaka afe."

Hadith hii haina sanad (nyororo) ya wasimuliaji inayoeleweka. Hata hivyo usahihi wake unakubalika, inaunga mkono wazo kuwa ndoa ya muda inaruhusiwa tu kwa yule asiye na mke au ambaye mke wake yuko mbali. Kwa kifupi kwa nini tushikilie hadith hii moja ya mwanazuoni wa Kisunni (ambayo chanzo chake hakieleweki) na kuziacha hadithi nyingine nyingi za Amirul Muuminina Ali(a.s) zilizoripotiwa katika vitabu vyote vya kisunni na Kishia katika sura ya Mut'ah. Katika kauli zake nyingi za thamani Imam Ali (a.s), Amiri wa walioamini anasema, "Kama Umar asingeifuta ndoa ya muda, hakuna mtu ambaye angezini, isipokuwa wachache wenye maradhi ya ngono." Hii ni kuwa kama ndoa ya muda isingekuwa imepigwa marufuku, hakuna mtu ambaye angejenga tabia ya kuzini, ni wale tu ambao mara zote wanapenda kufanya mambo yaliyoharamishwa ndio wangefanya hivyo.

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Sura Ya Thelathini na Nne: Surat Saba. Imeshuka Makka. Ina Aya 54.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَلَهُ الْحَمْدُ فِي الْآخِرَةِ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ ﴿١﴾

1. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na sifa ni zake katika Akhera. Naye ni Mwenye hekima, Mwenye habari.

يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا وَهُوَ الرَّحِيمُ الْغَفُورُ ﴿٢﴾

2. Anayajua yanayoingia katika ardhi na yanayotoka humo, na yanayoteremka kutoka mbinguni na yanayopanda huko na Yeye ni Mwenye kurehemu, Mwingi wa maghufira.

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَأْتِينَا السَّاعَةُ قُلْ بَلَىٰ وَرَبِّي لَتَأْتِيَنَّكُمْ عَالِمِ الْغَيْبِ لَا يَعْزُبُ عَنْهُ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَلَا أَصْغَرُ مِن ذَٰلِكَ وَلَا أَكْبَرُ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ ﴿٣﴾

3. Na walisema wale ambao wamekufuru: Haitatufikia Saa. Sema: Ndio! Naapa kwa Mola wangu, itawafikia. Mjuzi wa ghaibu. Hapana kinachofichikana kwake hata chenye uzito wa chembe, si katika mbingu wala katika ardhi, wala kilicho kidogo katika hivyo wala kikubwa zaidi; ila vimo katika Kitabu chenye kubainisha.

لِّيَجْزِيَ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ ﴿٤﴾

4. Ili awalipe wale ambao wameamini na wakatenda mema. Hao watapata maghufira na riziki yenye heshima.

وَالَّذِينَ سَعَوْا فِي آيَاتِنَا مُعَاجِزِينَ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مِّن رِّجْزٍ أَلِيمٌ ﴿٥﴾

5. Na wale ambao wamehangaika kuzipinga ishara zetu wakiona watashinda, hao watapata adhabu mbaya yenye uchungu.

وَيَرَى الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ الَّذِي أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ هُوَ الْحَقَّ وَيَهْدِي إِلَىٰ صِرَاطِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿٦﴾

6. Na wale ambao wamepewa ilimu wanaona kuwa uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako ni haki na huongoza kwenye njia ya Mwenye nguvu, Mwenye kusifiwa.

SIFA NJEMA ZOTE NI ZA MWENYEZI MUNGU

Aya 1 – 6

MAANA

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na sifa ni zake katika Akhera. Naye ni Mwenye hekima, Mwenye habari.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye kustahiki kusifiwa kwa sifa njema katika nyumba mbili. Ni mmliki wa ulimwengu na mpangiliaji wake kwa vyote vilivyomo ndani yake, kulingana na elimu yake na hekima yake.

Kwenye Nahjul-Balagha, imesemwa: “Tunamsifu kwa ukubwa wa hisani yake na wema wa dalili yake na ziada ya fahila zake na neema zake. Sifa ambazo ni haki yake (sisi) kuzitekeleza na kulipa shukrani zake na kujikurubisha kwenye thawabu zake na kutaka ziada ya wema wake.”

Anayajua yanayoingia katika ardhi na yanayotoka humo na yanayoteremka kutoka mbinguni na yanayopanda huko na Yeye ni Mwenye kurehemu, Mwingi wa maghufira.

Maana ya Aya hii yamekaririka katika Aya kadhaa; ikiwemo Juz. 7 (6:59) na Juz. Juz. 11 (10:61). Ufupisho wake ni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

Na walisema wale ambao wamekufuru: Haitatufikia saa ya Kiyama. Sema: Ndio! Naapa kwa Mola wangu, itawafikia.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11(10:53).

Mjuzi wa ghaibu. Hapana kinachofichikana kwake hata chenye uzito wa chembe, si katika mbingu wala katika ardhi, wala kilicho kidogo katika hivyo wala kikubwa zaidi; ila vimo katika Kitabu chenye kubainisha.

Kitabu chenye kubainisha ni kinaya cha kuhifadhi. Maana ni kuwa hakuna anayejua wakati wa Kiyama isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake. Tazama Juz. 9 (7:187).

Ili awalipe wale ambao wameamini na wakatenda mema. Hao watapata maghufira na riziki yenye heshima. Na wale ambao wamehangaika kuzipinga ishara zetu wakiona watashinda, hao watapata adhabu mbaya yenye uchungu.

Huu ni ubainifu wa hekima ya ufufuo, ambayo ni kulipwa mema waliofanya wema na wale waliofanya uovu walipwe kwa uovu wao. Tazama Juz. 11 (10:3-4). Kifungu cha “Hisabu na malipo ni lazima.”

Na wale ambao wamepewa ilimu wanaona kuwa uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako ni haki na huongoza kwenye njia ya Mwenye nguvu, Mwenye kusifiwa.

Makusudio ya wale waliopewa ilimu ni kila mwenye ilimu aliye na insafu, wakati wowote na mahali potepote. Na makusudio ya uliyoteremshiwa ni Qur’an. Maana ni kuwa yeyote mwenye ilimu atakayeisoma Qur’an kiusahihi, lazima ataishia kuwa ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu; kwa sababu iko sawasawa kwenye itikadi yake, sharia yake na mafunzo yake yote.

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا هَلْ نَدُلُّكُمْ عَلَىٰ رَجُلٍ يُنَبِّئُكُمْ إِذَا مُزِّقْتُمْ كُلَّ مُمَزَّقٍ إِنَّكُمْ لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ ﴿٧﴾

7. Na wale ambao wamekufuru walisema: Je, tuwajulishe mtu anayewaambia mtakapocham- buliwa mapande mapande mtakuwa katika umbo jipya?

أَفْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا أَم بِهِ جِنَّةٌ بَلِ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ فِي الْعَذَابِ وَالضَّلَالِ الْبَعِيدِ ﴿٨﴾

8. Amemzulia Mwenyezi Mungu au ana wazimu? Bali wale ambao hawaamini akhera wamo adhabuni na upotofu wa mbali.

أَفَلَمْ يَرَوْا إِلَىٰ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِن نَّشَأْ نَخْسِفْ بِهِمُ الْأَرْضَ أَوْ نُسْقِطْ عَلَيْهِمْ كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّكُلِّ عَبْدٍ مُّنِيبٍ ﴿٩﴾

9. Je, hawaoni yaliyo mbele yao na nyuma yao ya mbingu na ardhi. Tungelipenda tungeliwadidimiza ardhini, au tungeliwateremshia vipande vya mbingu. Hakika katika hayo kuna ishara kwa kila mja aliyetubia.

WANAOPINGA SIKU YA MWISHO

Aya 7 – 9

MAANA

Na wale ambao wamekufuru walisema: Je, tuwajulishe mtu anayewaambia mtakapochambuliwa mapande mapande mtakuwa katika umbo jipya? Amemzulia Mwenyezi Mungu au ana wazimu?

Hivi ndivyo washirikina walivyomwambia Muhammad, ni muongo au mwendawazimu – Mungu apishie mbali. Kwa nini walisema neno la ukafiri kama hilo? Ni Kwa sababu Mtume aliwaambia kuwa mtu atafu- fuliwa baada ya mauti. Hawana dalili yoyote ya kupinga kwao huku isipokuwa kushangaa tu; kama walivyosema:

أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ ﴿٥﴾

“Amewafanya miungu wote kuwa ni mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.” (38: 5).

Hali yao hii, kama inavyonekana, inategemea vile wanavyofikiria. Maana yake ni kupinga hali halisi kwa fikra na mawazo; pamoja na kuwa fikra haiwi ya kweli ila ikiwa inaakisi hali halisi na kwamba yeyote anayeikum- batia nadharia yoyote hana budi kutafuta dalili ya ukweli wake kwa kuweko uhalisi unaoitafsiri, na haifai kukana uhalisi kwa fikra isiyokuwa na msingi wowote.

Katika hili Imam Ali(a.s) anaashiria kwa kusema:“Watu wanajulikana kwa haki, wala haki haijulikani kwa watu.”

Bali wale ambao hawaamini akhera wamo adhabuni na upotofu wa mbali.

Hao ni wajinga na wapotevu, kwa sababu wameipima haki na uhalisi kwa fikra zao na mawazo yao; na walitakiwa wapime fikra zao kwa haki na uhalisi.

Je, hawaoni yaliyo mbele yao na nyuma yao ya mbingu na ardhi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawaambia wakadhibishaji: Kuna ajabu gani ya kufufuliwa kwenu baada ya mauti:

أَوَلَيْسَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يَخْلُقَ مِثْلَهُم ﴿٨١﴾

“Kwani aliyeziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao?” (36:81).

Je, umbile hili halifahamishi umoja wake na ukamilifu wa uweza wake; ukiwemo kuwarudisha watu baada ya mauti?

Tumelizungumzia hilo mara nyingi. Tazama Juz. 1 (2:28 -29), Juz. 5 (4:85 – 87) na Juz. 11 (10:3–4).

Tungelipenda tungeliwadidimiza ardhini, au tungeliwateremshia vipande vya mbingu. Hakika katika hayo kuna ishara kwa kila mja aliyetubia.

Hayo ni ishara ya kuumba mbingu na ardhi. Kwa sabubu hilo, kwa mwenye akili, linafahamisha ukuu wa Mwenyezi Mungu na uweza wake wa kuipa uhai mifupa iliyochakafuka. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu:

‘Tungelipenda tungeliwadidimiza ardhini,’ ni karipio na makemeo kwa yule anayepinga siku ya mwisho, kwamba anaweza kumezwa na ardhi au kupigwa na kimondo kutoka mbinguni, kimuunguze.

وَلَقَدْ آتَيْنَا دَاوُودَ مِنَّا فَضْلًا يَا جِبَالُ أَوِّبِي مَعَهُ وَالطَّيْرَ وَأَلَنَّا لَهُ الْحَدِيدَ ﴿١٠﴾

10. Na kwa hakika tulimpa Daud fadhila kutoka kwetu. Enyi milima sabihini pamoja naye na ndege. Na tukamlainishia chuma.

أَنِ اعْمَلْ سَابِغَاتٍ وَقَدِّرْ فِي السَّرْدِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿١١﴾

11. Kwamba utengeneze nguo za chuma pana na kadiria sawa katika kuunganisha. Na tendeni mema. Hakika ninayaona mnayotenda.

وَلِسُلَيْمَانَ الرِّيحَ غُدُوُّهَا شَهْرٌ وَرَوَاحُهَا شَهْرٌ وَأَسَلْنَا لَهُ عَيْنَ الْقِطْرِ وَمِنَ الْجِنِّ مَن يَعْمَلُ بَيْنَ يَدَيْهِ بِإِذْنِ رَبِّهِ وَمَن يَزِغْ مِنْهُمْ عَنْ أَمْرِنَا نُذِقْهُ مِنْ عَذَابِ السَّعِيرِ ﴿١٢﴾

12. Na kwa Suleiman upepo. Safari yake ya asubuhi ni mwendo wa mwezi mmoja na safari yake ya jioni ni mwendo wa mwezi mmoja. Na tukamtiririshia chemchem ya shaba. Na katika majini kuna waliofanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mola wake. Na anayejitenga na amri katika wao tunamwonjesha adhabu ya moto unaowaka.

يَعْمَلُونَ لَهُ مَا يَشَاءُ مِن مَّحَارِيبَ وَتَمَاثِيلَ وَجِفَانٍ كَالْجَوَابِ وَقُدُورٍ رَّاسِيَاتٍ اعْمَلُوا آلَ دَاوُودَ شُكْرًا وَقَلِيلٌ مِّنْ عِبَادِيَ الشَّكُورُ ﴿١٣﴾

13. Wakimfanyia alipendalo, kama mihrabu na masanamu na sinia kubwa kama mahodhi, na masufuria makubwa yasiyoondoka mahali pake. Fanyeni amali enyi watu wa Daud kwa kushukuru. Ni wachache katika waja wangu wanaoshukuru.

فَلَمَّا قَضَيْنَا عَلَيْهِ الْمَوْتَ مَا دَلَّهُمْ عَلَىٰ مَوْتِهِ إِلَّا دَابَّةُ الْأَرْضِ تَأْكُلُ مِنسَأَتَهُ فَلَمَّا خَرَّ تَبَيَّنَتِ الْجِنُّ أَن لَّوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ الْغَيْبَ مَا لَبِثُوا فِي الْعَذَابِ الْمُهِينِ ﴿١٤﴾

14. Tulipomkidhia mauti, hapana aliyewajulisha mauti yake ila mnyama wa ardhi aliyekula fimbo yake. Alipoanguka majini walitambua lau kuwa wangelijua ya ghaibu wasingelikaa katika adhabu ya kufedhehesha.

DAUD NA SULEIMAN

Aya 10 – 14

MAANA

Na kwa hakika tulimpa Daud fadhila kutoka kwetu. Enyi milima sabihini pamoja naye na ndege. Na tukamlainishia chuma.

Katika Juz. 6 (4:163) Mwenyezi Mungu anasema: “Na Daud tukamapa Zaburi,” kwenye Juz. 19 (27:15) anasema: “Na hakika tulimpa Daud na Suleiman elimu” na kwenye Aya hii tuliyo nayo anaseama kuwa amempa neema ya sauti nzuri ambayo ilikuwa inakurubia kwenda sambamba na sauti ya milima na ndege.

Katika Juz. 17 (21:79) tulisema kuwa inawezekana kuwa tasbihi ya milima na ndege ni tasbihi halisi hasa pamoja na Daud, Kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu. Kuna msemaji aliyesema kuwa makusudio ya kusabihi milima na ndege pamoja na Suleimani ni kuwa ilikuwa ikimfanya asabihi; alipokuwa akiiona husema: “Subhana man khalaqa wa swawwara...” (Kutakasika ni kwa aliyeumba na akatia sura...).

Pia Mwenyezi Mungu alimneeemesha Daud kwa kukifanya chuma vile anavyotaka yeye bila ya kukitia motoni au kukigonga na nyundo. Inawezekana kuwa Mwenyezi Mungu alimfahamisha sababu na nyenzo za kukilainisha chuma.

Kwamba utengeneze nguo za chuma pana na kadiria sawa katika kuunganisha.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anamwambia Daud atengeneze deraya kutokana na chuma na atengeneze vizuri kuzuia panga mishale na mikuki na ziwe pana kwa namna ambayo mvaaji haitamzuia na harakati zozote.

Na tendeni mema. Hakika ninayaona mnayotenda.

Maneno yanaelekezwa kwa Daud na kizazi chake. Mwenyezi Mungu anawaamrisha wafanye mema na kuwa ameayaandalia malipo na thawabu. Umetangulia mfano wa Aya mbili hizi katika Juz. 17 (21:79 – 80).

Na kwa Suleiman upepo. Safari yake ya asubuhi ni mwendo wa mwezi mmoja na safari yake ya jioni ni mwendo wa mwezi mmoja.

Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa upepo ulikuwa ukimchukua Suleiman, anakotaka, kwa amri ya Mungu na kwamba masafa ya mwezi mzima kwa ngamia au kutembea kwa miguu alikuwa akienda kwa asubuhi moja na vile vile jioni.

Na tukamtiririshia chemchemi ya shaba.

Makusudio ya kumtiririshia hapa ni kumyeyushia. Yaani Mwenyezi Mungu Mtukufu alimyeyushia chuma Suleimani kama alivyomyeyushia baba yake Daud. Inawezekana kuwa Mwenyezi Mungu alimuongoza kwenye sababu za kuyeyusha.

Na katika majini kuna waliofanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mola wake. Na anayejitenga na amri katika wao tunamwonjesha adhabu ya moto unaowaka. Wakimfanyia alipendalo, kama mihrabu na masanamu na sinia kubwa kama mahodhi, na masufuria makubwa yasiyoondoka mahali pake.

Imetangulia pamoja na tafsiri yake katika Juz. 17 (21:82).

Fanyeni amali enyi watu wa Daud kwa kushukuru. Ni wachache katika waja wangu wanaoshukuru.

Ibn Al-arabi ameitaja Aya hii katika Futuhat Juz. 4, akasema: Shukrani ni kuiona neema kuwa imetoka kwa Mungu si kwa mwingine. Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimpa wahyi Musa akamwambia: Nishukuru kwa haki ya kushukuru. Akasema Musa: “Ni nani anayeweza hilo ewe Mola?” Akamwambia: “Ikiwa unaona neema imetokana na mimi basi umenishukuru.”

Tulipomkidhia mauti, hapana aliyewajulisha mauti yake ila mnyama wa ardhi aliyekula fimbo yake. Alipoanguka majini walitambua lau kuwa wangelijua ya ghaibu wasingelikaa katika adhabu ya kufedhehesha.

Aliyekidhiwa na mauti ni Suleiman. Mnyama wa ardhi ni mchwa anayekula miti. Maana ni kuwa Suleimani alifikiwa na mauti akiwa ameegemea fimbo yake; akabakia hivyo mpaka muda aliotaka Mwenyezi Mungu, majini na watu wakimwangalia na kumdhania kuwa yuko hai, mpaka pale mchwa walipokula fimbo yake kwa ndani, ikavunjika na Suleiman akaanguka; hapo wote wakajua kuwa amekufa; ikadhihirika kwa watu kuwa majini hawajui ghaibu. Kwa sababu lau wangelijua basi wasingelikuwa katika utumishi wa Suleiman akiwa ni maiti.

Ikiwa baadhi ya yaliyo katika Aya hii yanaonekana, kwa kawaida, ni vigumu kutokea, lakini kiakili inakubalika kutokea. Ndio maana tunayasadiki na kuyakubali; tukiwa tunaamini msingi wa wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwenda kwa Mtume(s.a.w. w ) wake mtukufu.

Tazama Juz. 3 (3:45 – 51) kifungu cha “Lisilowezekana kiakili na kidesturi.”

KUPINGA FIKRA YA KIDINI

Kutoka na kutajwa majini na mambo yasiyo ya kawaida katika Aya hii, ni vizuri tutaje yaliyoelezwa kwenye kitabu kilichotoka hivi karibuni, kina- choitwa Naqdu lfikri ddiniy. (Kupinga fikra ya kidini).

Hivi sasa tuko katika mwezi wa Novemba 1969. Yamezungumzwa mengi kuhusu kitabu hicho na mtungaji wake. Mwenye kusoma kitabu hicho mara moja atamhukumu mtungaji wake kuwa ana shaka na wasiwasi na dini zote. Hilo amelisema waziwazi kwenye Uk. 29, 77 na nyinginezo.

Lakini mwenye kukifuatilia kitabu na kuchukua dhahiri yake, ataona kuwa yaliyopelekea shaka na wasiwasi huu ni mambo yafutayo:

Kwanza : Kujaribu baadhi ya waumini kulazimisha kuoanisha nukuu za Qur’an na ugunduzi wa kisayansi, na kuzama sana kuleta taawili iliyo mbali na matamshi. Mtunzi wa kitabu hicho amelitolea ushahidi mwingi hilo, yakiwemo yale aliyoyanukuu katika Uk. 37, kwamba ugunduzi wa chembe za mwanga unafahamisha kuweko malaika na majini.

Mtungaji akielezea kauli hii alisema: “Sijui kuna uhusiano gani baina ya nadharia ya mwanga na kuweko majini.”

Pili : Mazoweya na nembo za kidini zilizoganda haziendani na maendeleo ya karne ya ishirini; kama anavyodai mwandishi.

Tatu: Baadhi ya wakuu wa dini kuunga mkono ukabaila na ukoloni kwa kutumia jina na Uislamu au Ukristo. Kitabu kimejaa ushahidi wa hilo; kama vile kwenye uk. 23: “Dini huko ulaya ilikuwa rafiki mkubwa wa serikali za kikabaila, hali ambayo inaendelea hadi sasa katika miji mbalimbali, hasa ndani ya miji ya kiarabu na nje, na vile dini inavyoungana moja kwa moja na ukoloni mambo leo unaongozwa na Marekani.”

Mtungaji aliongeza katika kupinga kitabu “Almasihiyya wal Islamu fi Lubnan” (Ukiristo na Uislmu Lebanon) ambacho ni mkusanyiko wa mihadhara ya Lebanon ya mwaka 1965, iliyotolewa na wakuu wa kidini wane: mmoja wa kisunni, mwengine wa kishia na wawili wa kikiristo.

Na wengine wane wa wasiokuwa na dini yoyote, lakini walizungungumza kwa niaba ya dini. Wote wakamwahidi Mwenyezi Mungu kuwa watafanya bidii ya kudumu kuondoa pingamizi zinazowekwa baina ya Uislamu na ukiristo.

Miongoni mwa aliyoyasema mtungaji huyu, katika kuwarudi wale waliotoa ahadi, ni yale yaliyo katika ukurasa wa 64, wa Kitabu chake hicho: “Lengo la kwanza la mihadhara na ahadi hizo ni wakristo kuunga mkono serkali ya Lebanon, kwa vile inawanufaisha wao zaidi kuliko waislamu walio na ufukara sana.

Baadhi ya waislamu nao wanaikubali serikali na kuungana na wakiristo, na kuaiachia serikali usimamizi wote wa kisiasa, kijamii na kiuchumi, si kwa lolote ila ni kwa kuwa wanapata manufaa fulani na faida kutoka serikalini. Kiasi ambacho maovu ya serikali yamesahaulika na kuelekea kwenye nembo ya mshikamano wa wakiristo na waislamu.”

Dalili mkataa kuwa malengo ni masilahi sio mshikamano wa kidini, mwandishi anaiweka wazi kwenye Uk. 60, katika kitabu chake, akisema: “Hakika Uislamu hauikubali Biblia, utatu, mhanga, kusulubiwa Bwana Masih, kuzikwa kwake na kutoka kwake kaburini n.k. Kama ambavyo wakiristo nao hawaikubali Qur’an wala utume wa Muhammad(s.a.w. w ) n.k. Sasa hawa wahadhiri na ahadi zao wataondoa vipi pingamizi hizi? Usawa hasa ni kufahamiana na kuelewena Walebanoni kwa uzalendo wao tu na misingi ya ushirikiano kwa masilahi yao, lakini dini aachiwe hiyari kila mtu kulingana na alivyokinai na mazoweya yake.”

Kutokana na kauli ya mwandishi huyu na wengineo wengi, katika kupinga fikra ya dini, inatubainikia kuwa siri ya upinzani wao, kama tulivyodokeza mwanzoni, imetokana na wakuu wa dini kuukumbatia ukoloni, udhalimu na ukandamizaji na kuupamba kwa jina la dini.

Lau wakuu wote wa dini wangeifanyia ikhlasi, wakaifahamisha kwa ufahamu sahihi na wakaibanisha kama alivyoiteremsha Isa na Muhammad na wasiiuze kwa thamani ndogo, basi wapinzani au washambulizi wa kulipwa wasingelipata mwanya wa kuituhumu au kuwa na shaka na dini ya kiislamu wala ya kikiristo.

Lakini jambo la kuvunja moyo ni kuwa watu wamelitumia jina la dini kwa uzushi na wengine wakasimama kuiharibu na kuingiza shaka baada ya kulipwa na maadui wa Mwenyezi Mungu; ndio ikawa radiamali hii kuto- ka kwa mwandishi huyu wa kitabu ‘Kupinga fikra ya dini’ na wengineo. Inasemekana pia mwandishi huyu ni katika wanaolipwa.

Hata hivyo, kwani dini itakuwa imekosea nini ikituhumiwa na wazushi na wenye upendeleo? Ilitakikana mwandishi aangalie ushahidi mwingi ulio katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu na suna za Mtume wake na pia katika historia ya Uislamu kuwa dini ni nguvu inayomwelekeza mtu kwenye maisha bora na kwamaba iko mbali na kila jambo lisiloingilika akilini na kugongana na hakika ya maisha.

Hakika hii wanakubaliana nayo wataalamu wengi wa mashariki na wa magharibi wasiokuwa waislamu. Tazama Juz. 1 (2:1-5) kifungu cha ‘Qur’an na Sayansi,’ Juz. 9 (8:24) kifungu cha ‘Dini na maisha,’ na Juz. 15 (17:9-12) kifungu cha ‘Uislamu ni dini ya maumbile.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

لَقَدْ كَانَ لِسَبَإٍ فِي مَسْكَنِهِمْ آيَةٌ جَنَّتَانِ عَن يَمِينٍ وَشِمَالٍ كُلُوا مِن رِّزْقِ رَبِّكُمْ وَاشْكُرُوا لَهُ بَلْدَةٌ طَيِّبَةٌ وَرَبٌّ غَفُورٌ ﴿١٥﴾

15. Hakika ilikuwa ishara kwa wasabaa katika maskani yaobustani mbili, kulia na kushoto. Kuleni katika riziki ya Mola wenu na mumshukuru. Mji mzuri na Mola mwenye maghufira.

فَأَعْرَضُوا فَأَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ سَيْلَ الْعَرِمِ وَبَدَّلْنَاهُم بِجَنَّتَيْهِمْ جَنَّتَيْنِ ذَوَاتَيْ أُكُلٍ خَمْطٍ وَأَثْلٍ وَشَيْءٍ مِّن سِدْرٍ قَلِيلٍ ﴿١٦﴾

16. Lakini wakaacha, basi tukawapelekea mafuriko makubwa na tukawabadilishia bustani zao kwa bustani nyingine mbili zenye matunda makali na mivinje na miti michache ya kunazi.

ذَٰلِكَ جَزَيْنَاهُم بِمَا كَفَرُوا وَهَلْ نُجَازِي إِلَّا الْكَفُورَ ﴿١٧﴾

17. Hayo tuliwalipa kwa vile walikufuru, nasi kwani tunamwadhibu isipokuwa anayekufuru?

وَجَعَلْنَا بَيْنَهُمْ وَبَيْنَ الْقُرَى الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا قُرًى ظَاهِرَةً وَقَدَّرْنَا فِيهَا السَّيْرَ سِيرُوا فِيهَا لَيَالِيَ وَأَيَّامًا آمِنِينَ ﴿١٨﴾

18. Na baina yao na miji mingine tuliyoibariki, tuliweka miji iliyo dhahiri na tukaweka humo vituo vya safari: Nendeni humo usiku na mchana kwa amani.

فَقَالُوا رَبَّنَا بَاعِدْ بَيْنَ أَسْفَارِنَا وَظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ فَجَعَلْنَاهُمْ أَحَادِيثَ وَمَزَّقْنَاهُمْ كُلَّ مُمَزَّقٍ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّكُلِّ صَبَّارٍ شَكُورٍ ﴿١٩﴾

19. Wakasema: Mola wetu, weka mwendo mrefu baina ya safari zetu. Na wakazidhulumu nafsi zao. Basi tukawafanya ni masimulizi na tukawatawanyatawanya. Hakika katika hayo, bila shaka kuna ishara kwa kila aliye na subira sana mwenye kushukuru.

وَلَقَدْ صَدَّقَ عَلَيْهِمْ إِبْلِيسُ ظَنَّهُ فَاتَّبَعُوهُ إِلَّا فَرِيقًا مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na hakika Ibilisi alisadikisha dhana yake juu yao. Na walimfuata isipokuwa kundi la waumini.

وَمَا كَانَ لَهُ عَلَيْهِم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا لِنَعْلَمَ مَن يُؤْمِنُ بِالْآخِرَةِ مِمَّنْ هُوَ مِنْهَا فِي شَكٍّ وَرَبُّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَفِيظٌ ﴿٢١﴾

21. Naye hakuwa na mamlaka yoyote juu yao, ila ni kwa sababu tujue ni nani mwenye kuamini Akhera na nani anayetilia shaka. Na Mola wako ni mwenye kuhifadhi kila kitu.

SABAA

Aya 15 – 21

LUGHA

Sabaa ni jina la kabila la waarabu, lililotokana na jina la baba ambaye kizazi chao kinatokana naye.

KISA KWA UFUPI

Katika Tarikh almas’ud imeelezwa kuwa mfalme wa kwanza wa Yemen alikuwa ni Sabaa bin Yashjab bin Ya’arab bin Qahtan. Jina lake hasa lilikuwa ni Abdu Shams. Aliitwa Sabaa kutokana na kuchukua kwake mateka[2] . Ardhi ya Sabaa ilikuwa ndio ardhi yenye rutuba na utajiri zaidi katika Yemen.

Kabla yake, ardhi hiyo, ilikuwa ikikumbwa na mafuriko yaliyoangamiza mimea na majengo. Basi akawakusanya wataalamu wa zama hizo kutafuta suluhisho la tatizo hilo. Wakaafikiana kujengwe ukuta baina ya milima miwili na kuweka mlango wa kuyafungulia maji kwa kiasi wanachokitaka.

Ukuta huu ulijulikana kwa jina la mji wa Maaribu uliokuwa karibu na ukuta. Kadiri siku zilivyoendelea kupita ndivyo maji nayo yalivyoongezeka, ukuta ukaharibika na maji yakavunja majumba na mashamba. Watu wakagura na wakatawanyika sehemu kadhaa za nchi. Hapa ndipo ilipochukuliwa mithali: ‘Mikono ya sabaa imetawanyika.’

Katika Tafsir At-Tabari na Majmaul-Bayan imeelezwa kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) kuhusu Sabaa, akasema: ‘Kulikuwa na mtu mmoja mwarabu aliyekuwa na watoto kumi, sita katika wao walikwenda upande wa Yemen na wane wakaenda upande wa Sham.

Waliokwenda upande wa Yemen ni: Kinda, Himyar, Azd, Ash’ar, Madh-hij na Anmar, miongoni mwao ni Khath’am na Bujayla. Ama wale waliokwenda upande wa Sham ni: Amila, Judham, Lakhmu na Ghassan.

Katika Tafsir Al-Ma raghi imeelezwa kuwa watafiti walikuwa wakitilia shaka jambo hili la ukuta, mpaka mgunduzi wa kifaransa Arno alipoweza kufika Maarib mnamo mwaka 1843 na akaona athari yake na kuweza kuchora picha iliyosambazwa kwenye magazeti ya ufaransa mwaka 1874. Baadaye Halevi na Glazr, wakatembelea sehemu hiyo, wakaafikiana na aliyoyasema.

MAANA

Hakika ilikuwa ishara kwa wasabaa katika maskani yaobustani mbili, kulia na kushoto. Kuleni katika riziki ya Mola wenu na mumshukuru. Mji mzuri na Mola mwenye maghufira.

Ishara ni dalili na alama ya neema za Mwenyezi Mungu zilizo nyingi katika mji huo. Bustani mbili kulia na kushoto, ni kinaya cha rutuba na mazao mengi yaliyopatikana kila pembe ya mji huo. Kila aliyepita ardhi ya Sabaa aliweza kuona mazao mengi kulia na kushoto.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaamrisha watu wa Sabaa, kupitia kwa manabii na Mitume wake, kuwa waneemeke na kheri zake na wamshukuru na wampwekeshe.

Lakini wakaacha, basi tukawapelekea mafuriko makubwa na tukawabadilishia bustani zao kwa bustani nyingine mbili zenye matunda makali na mivinje na miti michache ya mikunazi.

Neema ya Mwenyezi Mungu waliitumia kwa kumuuasi. Akawahadharisha kupitia Mitume wake, lakini halikuwafaa onyo wala kuzingatia mawaidha. Basi Mwenyezi Mungu akawapelekea mafuriko yaliyobomoa ukuta na kuharibu mimea. Mwenyezi Mungu akabadilisha bustani za matunda na konde za mazao kwa miti isiyoshibisha; kama vile: mikwaju, mikunazi na mingineyo inayomea jangwani ambayo wanakula wanyama wenye njaa au mtu aliyeishiwa kabisa.

Hayo tuliwalipa kwa vile walikufuru, nasi kwani tunamwadhibu isipokuwa anayekufuru?

Aliwalipa ufukara, ambao ni malipo ya kufedhehesha zaidi. Kuna Hadith isemayo: “Ufukara unakurubia kuwa ni ukafiri.” Nyingine inasema: “Ufukara unasawijisha uso duniani na akhera.” Imam Ali(a.s) alimwambia mwanawe Muhammad Al-Hanafiya: “Hakika ufukara unapunguza dini –yaani unampeleka mtu kumwasi Mwenyezi Mungu – unazubaisha akili na unaita mateso.”

Na baina yao na miji mingine tuliyoibariki, tuliweka miji iliyo dhahiri na tukaweka humo vituo vya safari: Nendeni humo usiku na mchana kwa amani.

Baina yao ni watu wa Sabaa. Makusudio ya miji ni Sham – kama walivyosema wafasiri-ambao Mwenyezi Mungu aliubariki kwa maji, miti, rutuba na matunda. Iliyodhahiri maana yake ni kuwa karibu ikijitokeza na kuonana.

Kuweka vituo vya safari baina ya mji mmoja na mwengine; kiasi ambacho msafiri anakuwa kwenye mji mmoja asubuhi na jioni anakuwa kwenye mji mwingine. Aya inausifia mji wa Sabaa kabla ya kuharibika. Maana yake ni kuwa miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake ni kuwa anayetaka kusafiri anakuwa kwenye amani ya nafsi yake na mali yake na hakuwa na haja ya kuchukua masurufu ya safari au kuhofia kiu wala njaa.

Lakini wakachoka na neema wakasema: Mola wetu weka mwendo mrefu baina ya safari zetu.

Yaani weka mbuga na nyika ili tutafute usafiri na tuchukue masurufu ya safari; sawa na walivyofanya wana wa israil walipochoka na Manna na Salwa na kumwambia Musa: “Basi tuombee

Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi miongoni mwa mboga zake, na matango yake na ngano yake na adesi zake na vitunguu vyake. Akasema: ‘Mnabadili vitu duni kwa vile vilivyo bora?” Juz.1(2:61).

Na wakazidhulumu nafsi zao kwa kupituka mipaka na kukufuru neema. Basi tukawafanya ni masimulizi na tukawatawanyatawanya. Hakika katika hayo, bila shaka kuna ishara kwa kila aliye na subira sana mwenye kushukuru.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwatawanya ardhini mpaka wakawa ni historia kwa vizazi na mazingatio kwa mwenye kuvumilia shida na akushukuru wakati wa raha.

Na hakika Ibilisi alisadikisha dhana yake juu yao. Na walimfuata isipokuwa kundi la waumini. Naye hakuwa na mamlaka yoyote juu yao.

Shetani aliwahadaa wamuasi Mwenyezi Mungu; wakamsikiliza na kumtii wale waliopetuka mipaka na kukufuru na wakamwasi wale walioamini na kuwa na takua. Aya hii inaashiria kauli ya Ibilisi aliposema:

وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٣٩﴾ إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ الْمُخْلَصِينَ ﴿٤٠﴾ قَالَ هَـٰذَا صِرَاطٌ عَلَيَّ مُسْتَقِيمٌ ﴿٤١﴾ إِنَّ عِبَادِي لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَانٌ إِلَّا مَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْغَاوِينَ ﴿٤٢﴾

“Na nitawapoteza wote; isipokuwa waja wako waliosafishwa. Akasema (Mwenyezi Mungu): Hii ni njia juu yangu mimi iliyonyooka. Hakika waja wangu hutakuwa na mamlaka nao, isipokuwa wale wapotofu waliokufua- ta.” Juz. 14 (15:39 – 42).

Ila ni kwa sababu tujue ni nani mwenye kuamini Akhera na nani anayetilia shaka.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawajua zaidi waja wake kuliko wao wenyewe, lakini anawajaribu kwa raha na dhiki na kwa matamanio na hawaa, ili awadhihirishe ulimwenguni na yaonekane makusudio yao na vitendo vyao ambavyo vinastahiki thawabu na adhabu.

Maana ya Aya hii yamekaririka mara nyingi, ikiwemo Juz. 4 (3: 140).

Na Mola wako ni mwenye kuhifadhi kila kitu.

Hakimpotei chochote kilichomo mbinguni wala ardhini. Kuna Hadith isemayo: “Mche Mwenyezi Mungu kama kwamba wewe unamuona; ukiwa humuoni basi Yeye anakuona.”

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ لَا يَمْلِكُونَ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَمَا لَهُمْ فِيهِمَا مِن شِرْكٍ وَمَا لَهُ مِنْهُم مِّن ظَهِيرٍ ﴿٢٢﴾

22. Sema: Waombeni hao mnaodai kuwa ni badala ya Mwenyezi Mungu. Hawamiliki hata chembe katika mbingu wala ardhini. Wala hawana ushirika wowote humo. Wala hawana msaidizi miongoni mwao.

وَلَا تَنفَعُ الشَّفَاعَةُ عِندَهُ إِلَّا لِمَنْ أَذِنَ لَهُ حَتَّىٰ إِذَا فُزِّعَ عَن قُلُوبِهِمْ قَالُوا مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ قَالُوا الْحَقَّ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ ﴿٢٣﴾

23. Wala hautafaa uombezi mbele yake ila kwa yule aliyempa idhini. Hata itakapoondolewa fazaa kwenye nyoyo zao, watasema: Kasema nini Mola wenu? Watasema: Haki, naye ndiye aliye juu, Mkubwa.

قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ وَإِنَّا أَوْ إِيَّاكُمْ لَعَلَىٰ هُدًى أَوْ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٢٤﴾

24. Sema: Ni nani anayewaruzuku kutoka mbinguni na ardhini? Sema, ni Mwenyezi Mungu! Na hakika sisi au nyinyi bila shaka tuko kwenye uongofu au upotofu ulio wazi.

قُل لَّا تُسْأَلُونَ عَمَّا أَجْرَمْنَا وَلَا نُسْأَلُ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٢٥﴾

25. Sema: Nyinyi hamtaulizwa kwa makosa tuliyoyafanya wala sisi hatutaulizwa kwa mnayoyatenda.

قُلْ يَجْمَعُ بَيْنَنَا رَبُّنَا ثُمَّ يَفْتَحُ بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَهُوَ الْفَتَّاحُ الْعَلِيمُ ﴿٢٦﴾

26. Sema: Mola wetu atatukusanya kisha atatuhukumu kwa haki, naye ndiye Hakimu, Mjuzi.

قُلْ أَرُونِيَ الَّذِينَ أَلْحَقْتُم بِهِ شُرَكَاءَ كَلَّا بَلْ هُوَ اللَّـهُ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٢٧﴾

27. Sema: Nionyesheni wale mliowaunganisha naye kuwa washirika. Hapana! Bali Yeye ni Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢٨﴾

28. Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mtoaji bishara na muonyaji, lakini watu wengi hawajui.

وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٢٩﴾

29. Na wanasema: Ni lini ahadi hii, ikiwa mnasema kweli?

قُل لَّكُم مِّيعَادُ يَوْمٍ لَّا تَسْتَأْخِرُونَ عَنْهُ سَاعَةً وَلَا تَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٠﴾

30. Sema: Mna miadi ya siku ambayo hamtaakhirisha saa wala hamtaitangulia.

SEMA WAITENI MNAODAI KUWA NI WAUNGU

Aya 22 – 30

MAANA

Sema: Waombeni hao mnaodai kuwa ni badala ya Mwenyezi Mungu.

Washirikina waliabudu Malaika na masanamu, Mtume(s.a.w. w ) akawakataza lakini hawakusikia, akawaambia kwa amri ya Mwenyezi Mungu: iko wapi dalili ya mnaowafanya kuwa ni miungu? Waombeni manufaa au kukinga madhara, muone kuwa wanasikia na kuwajibu?

Lengo la matakwa haya ni kusimamisha hoja isiyoshindwa. Ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا ﴿٥٦﴾

“Sema:“Waombeni hao mnaodai badala Yake hawawezi kuwaondolea madhara wala kuyabadilisha.” Juz. 25 (17:56).

Hawamiliki hata chembe katika mbingu wala ardhini. Wala hawana ushirika wowote humo. Wala hawana msaidizi miongoni mwao.

Maneno yanaelekezwa kwa washirikina. Hata chembe ni kinaya cha kuwa hawamiliki hata kitu kilicho kidogo na duni. Maana ni kuwa hana mshirika wala msaidizi.

Wala hautafaa uombezi mbele yake ila kwa yule aliyempa idhini.

Hii ni kuwarudi washirikina na kauli yao:

مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ ...﴿٣﴾

“Hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu.” (39:3).

Kwa maelezo zaidi Tazama Juz. 1 (47 – 48) kifungu cha ‘Shufaa.’

Hata itakapoondolewa fazaa kwenye nyoyo zao, watasema: Kasema nini Mola wenu? Watasema: Haki, naye ndiye aliye juu, Mkubwa.

Wafasiri wametofautiana kuhusu watakaoondolewa fazaa, watakaouliza na wataoulizwa.

Kauli yenye nguvu zaidi ni watakaoondolewa fazaa ni wote walioko mbinguni na ardhini; kwamba fazaa itawaenea wote isipokuwa atakaowataka Mwenyezi Mungu; kama ilivyoelezwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَيَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَفَزِعَ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَمَن فِي الْأَرْضِ إِلَّا مَن شَاءَ اللَّـهُ وَكُلٌّ أَتَوْهُ دَاخِرِينَ ﴿٨٧﴾

“Na siku itakapopuziwa parapanda, watafazaika waliomo mbinguni na waliomo ardhini, ila amtakaye Mwenyezi Mungu. Na wote watamfikia hali ya kuwa ni wanyonge.” Juz. 20 (27:87).

Mara kwa mara tumesema kuwa Qur’an inajifasiri yenyewe. Kwa hiyo maana yanakuwa kwamba wakati wa Kiyama, wa mbinguni na wa ardhini watagawanyika mafungu mawili: Kuna kundi litakalokuwa na fazaa kubwa na kundi jingine litakuwa na amani. Hawa ndio walioashiriwa na kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ila amtakaye Mwenyezi Mungu.” Kundi la kwanza ikitulia fazaa yake, watauliza kundil la pili: Mola wenu amesema nini na mwisho wetu ni upi? Watakoulizwa watajibu kuwa Mwenyezi Mungu amesema haki naye ndiye aliye juu, Mkubwa.

Jibu hili kwa ujumla linaashiria kuwa Mwenyezi Mungu hana mshirika wala msaidizi. Pia hakuna atakayeombea kwake isipokuwa aliyempa idhini.

Sema: Ni nani anayewaruzuku kutoka mbinguni na ardhini?

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume(s.a.w. w ) awaambie washirikina. Riziki ya kutoka mbinguni ni mvua na mwangaza na riziki ya ardhini ni mazao ya porini na yanayopandwa.

Sema : ni Mwenyezi Mungu, siyo masanamu au Malaika, wala sio Isa au Uzayr. Kwa vile hili ndio jibu pekee, ndio maana Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake mtukufu awajibie walioulizwa.

Na hakika sisi au nyinyi bila shaka tuko kwenye uongofu au upotofu ulio wazi.

Nabii ana uhakika kwamba yeye yuko kwenye uongofu na kwamba washirikina wako kwenye upotevu, lakini walipoukataa uwongofu na haki ndio akatumia mfumo huu wa hekima na kuwaambia kuwa mja wetu atakuwa kwenye haki na mwingine kwenye upotevu, basi zirudieni akili zenu muone ni nani aliye kwenye usawa?

Huu ndio mfumo wa Mtume wa uwongofu na rehema, kuongezea kuwa mwenye haki anajiamini hata wakimhalifu watu wote wa ardhini.

Sema: Nyinyi hamtaulizwa kwa makosa tuliyoyafanya wala sisi hatutaulizwa kwa mnayoyatenda.

Huu ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t):

وَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل لِّي عَمَلِي وَلَكُمْ عَمَلُكُمْ أَنتُم بَرِيئُونَ مِمَّا أَعْمَلُ وَأَنَا بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٤١﴾

“Na kama wakikukadhibisha, basi sema: Mimi nina amali yangu na nyinyi mna amali yenu. Nyinyi hamna jukumu kwa ninayoyatenda, na mimi sina jukumu kwa mnayoyatenda.” Juz. 11 (10:41).

Sema: Mola wetu atatukusanya kisha atatuhukumu kwa haki, naye ndiye Hakimu, Mjuzi.

Siku ya mwisho ina majina mengi; miongoni mwayo ni siku ya mkusanyiko. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

يَوْمَ يَجْمَعُكُمْ لِيَوْمِ الْجَمْعِ ﴿٩﴾

“Siku atakayowakusanya kwa ajili ya Siku ya mkusanyiko” (64:9).

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) atatukusanya sisi na na nyinyi ili tuangalie hisabu, malipo na matendo. Hapo pazia litafunuka na mtajua kundi gani ndio lililoelekea njia ya kunyooka.

Sema: Nionyesheni wale mliowaunganisha naye kuwa washirika.

Hapa kuna manaeno ya kukadiria kuwa nionyesheni dalili ya kuwa masanamu ni washirika wa Mwenyezi Mungu au watawajongeza kwa Mwenyezi Mungu.Hapana! Yeye hana mshirika wala msaidizi wala wa kuombea mbele yake isipokuwa aliyempa idhini.

Bali Yeye ni Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

Hakuna enzi wala nguvu isipokuwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Ama dalili za hekima yake na utukufu wake zinajitokeza katika kuumba ulimwengu na maajabu yake.

Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mtoaji bishara na muonyaji, lakini watu wengi hawajui.

Tazama Juz. 7 (6:92) na Juzuu hii tuliyo nayo (33:40) Kifungu cha ‘Kwanini utume umeishilia kwa Muhammad(s.a.w. w ) ?’

Na wanasema: Ni lini ahadi hii, ikiwa mnasema kweli?”

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 11 (10:48).

Sema: Mna miadi ya siku ambayo hamtaakhirisha saa wala hamtaitangulia.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu Mtukufu ameahidi ufufuo, hisabu na malipo, naye bila shaka, ni mwenye kutekelza miadi yake, lakini kwa wakati alioupanga yeye ambaye hekima yake imetukuka, hatanguliwi wala hacheleweshwi. Basi yasiwahade mliyo nayo enyi washirikina, kwa sababu yatakwisha tu, muda mfupi au mrefu, kisha marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu awajulishe yale mliyokuwa mkiyafanya.


6

7

8

9

10

11

12

13