HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU23%

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU Mwandishi:
: AZIZI NJOZI
Kundi: Wanawake

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 33 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 47721 / Pakua: 5538
Kiwango Kiwango Kiwango
HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

Mwandishi:
Swahili

2

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

I- UISLAMU NA MAISHA YA KISASA

Suala la dini na maisha ya kisasa ni moja ya mambo ambayo hayawagusi Waislamu peke yao. Dini nyingine pia zilikumbana na tatizo hili. Watu wengi wenye kupendelea mabadiliko duniani, wameikana dini kwa sababu wanaamini kuwa dini na maisha ya sasa haviendi pamoja. Wanafikiri kuwa kudumaa, kutuama na kutobadilika ni sifa za lazima za mtu mshika dini. Kwa maneno mengine, wanafikiri kuwa kudumaa na ukinaifu unatokana na kutokuwepo kwa mabadiliko na kwamba kudumisha hali ya kizamani ndio tabia za dini.

Marehemu Bwana Nehru aliyekuwa waziri Mkuu wa India alikuwa na mawazo ya kisekula na hakuwa akiamini dini yoyote. Inaoinekana kutokana na kauli zake kuwa kilichomfanya asipende dini ni kutobadilika kwake na ukinaifu unaotokana na kutokuwepo kwa mabadiliko. Kuelekea kipindi cha mwisho cha maisha yake Nehru alihisi kuwa na uwazi moyoni mwake na aliamini kuwa uwazi ule ungezibwa na nguvu ya kiroho tu.

Lakini hakuelekea kuiamini dini yoyote kwa sababu aliamini kuwa hali ya ukinaifu na kutokuwepo kwa mabadiliko ilikuwepo katika dini zote. Mwandishi wa habari wa Kihindi, aitwaye Karanjia, alimhoji Nehru katika kipindi chake cha mwisho mwisho cha uhai wake (Nehru) na alivyoonekana haya yalikuwa ni mahojiano ya mwisho ambapo Nehru alitoa maoni yake juu ya matatizo ya jumla ya ulimwengu.

Alipokuwa akimzungumzia Gandhi, Karanjia alisema, "Baadhi ya wanaopendelea mabadiliko (liberals) na maendeleo wanaamini kuwa Gandhiji, kwa kupitia na kwa kutokana na utatuzi wake wa matatizo kwa hisia kali, unyofu na njia za kiroho, zimedhoofisha na kuitia ubaridi imani yako ya asili ya ujamaa wa kisayansi." Katika kulijibu hili, Nehru alisema; "Ni muhimu na vizuri kutumia fursa ya njia za kimaadili na kiroho.

Mara zote nimekubaliana na Gandhiji juu ya hili. Ninaamini kuwa ni muhimu zaidi kutumia fursa ya njia hizi, kwani sasa, kwa kiasi kikubwa kuliko ilivyokuwa huko nyuma, tunahitaji majibu ya kiroho na kimaadili juu ya maswali yanayotokana na pengo la kimaadili linalosababishwa na tamaduni za kisasa, ambazo zinazidi kuwa maarufu." Kisha Kiranjia aliuliza swali juu ya Ukomunisti.

Nehru alikiri mapungufu yake na katika majibu yake alionyesha baadhi ya mapungufu na ubovu wake (wa ukomunisti). Kwa mara nyingine tena alipendekeza suluhisho la kiroho juu ya matatizo ya dunia. Alipofika hapa Karanjia akasema; "Bwana Nehru, je dhana yako ya utatuzi wa matatizo ya kimaadili na kiroho haikufanyi uwe tofauti na Jawahanal wa jana? (Nehru mwenyewe enzi za ujana wake).

Ulichokisema kinaonyesha kuwa Bwana Nehru, katika kuelekea mwisho wa uhai wake, ameanza kumtafuta Mungu." Nehru alisema; "Ndiyo, nimebadilika. Msisitizo wangu juu ya unyofu na maadili ya kiroho na utatuzi wa matatizo sio wa bahati mbaya." Akaongeza kuwa; "Swali sasa ni jinsi ya kukuza maadili na imani ya kiroho katika daraja la juu zaidi.

Hapana shaka kwamba kwa ajili ya hili, dini zipo, lakini kwa bahati mbaya zimechukua mtazamo finyu na matendo yasiyobadilika na zimebaki kuwa taratibu rasmi lakini duni. Ni umbo lake la nje tu lililobaki, lakini ari na dhana yake ya kweli imetoweka." Uislamu na mahitaji ya wakati. Katika dini zote ni Uislamu tu unaojihusisha zaidi na vipengele vyote vya maisha ya mwanadamu.

Mafundisho yake hayajajikita katika matendo ya ibada na sala na mfumo wa ushauri wa maadili peke yake. Uislamu, kama ulivyoshughulikia uhusiano wa watu na Mwenyezi Mungu, ndivyo hivyohivyo ulivyoshughulikia mahusiano baina ya watu. Katika sura mbali mbali Uislamu umeshughulikia haki za watu binafsi na majukumu yao pia.

Hii ndio sababu swali kwamba mafundisho yake yanafaa kutumika au la katika mazingira yanayozidi kubadilika ni thabiti zaidi katika suala la Uislamu kuliko dini nyingine yoyote. Kwa bahati imetokea kwamba, wasomi wengi na waandishi wasiokuwa Waislamu wamezisoma sheria za kijamii na kiraia (za madai na za jinai) na wamezisifu kuwa ni chombo cha kisheria cha kimaendeleo na endelevu.

Wameusifu Uislamu kwa mapana na marefu, kuwa ni dini hai na itakayodumu milele, na wameuelezea uwezo na sifa za sheria hizi za Kiislamu wa kuweza kutumika nyakati zote na katika hali zote. Mwandishi maarufu sana wa Kiingereza aliyekuwa akipendelea msimamo wa wastani (liberal), Bernard Shaw amesema; "Mara zote nimekuwa nikiipa dini ya Muhammad heshima kubwa (daraja kubwa), kutokana na uhai wake wa ajabu.

Ni dini pekee inayoonekana kwangu kuwa na uwezo wa kunyumbulika na hivyo kuweza kutumika katika dunia inayobadilika na katika zama zote. Nimetabiri kuwa imani ya Muhammad itakubaliwa na Ulaya ya kesho, na dalili za hili zinajionyesha hata sasa. Makasisi wa zama za kati aidha kwa sababu ya ujinga au kwa sababu ya kung'ang'ania bila hoja imani zao waliupaka Uislamu rangi mbaya kabisa. Kwa kusema kweli walifundishwa kumchukia mtu huyu, Muhammad na dini yake. Kwao Muhammad alikuwa mpinga Kristo.

Mimi nimemsoma, mtu huyu wa ajabu, na kwa maoni yangu hakuwa mpinga Kristo kabisa na lazima aitwe mkombozi wa wanaadamu. Ninaamini kuwa kama mtu kama yeye angetwaa madaraka /uongozi wa dunia ya sasa angefanikiwa kutatua matatizo katika namna ambayo ingeleta amani na furaha, vitu ambavyo vinahitajika sana kwa sasa. Dr. Shibli Shama'il ni myakinifu wa Kiarabu wa Lebanoni. Kwa mara ya kwanza alitafsiri kitabu cha 'Darwin Kiitwacho 'Origin of Species' kwenda katika lugha ya Kiarabu, pamoja na sharhe ya mwanasayansi wa kijerumani aitwaye Boucher katika kitabu hicho akakipa jina la 'A weapon against religious belief.' ('Silaha dhidi ya imani za kidini.') Ingawa hamwamini Mwenyezi Mungu, haoni aibu kuusifu Uislamu na muasisi wake mtukuka. Ameusifu Uislamu kwa kusema kuwa ni dini hai inayoweza kutumika katika zama zote.

Mtu huyu, katika juzuu ya pili ya kitabu chake kiitwacho, 'Philosophy of Evolution' ambacho amekichapisha kwa Kiarabu, ameandika makala yenye kichwa cha cha habari 'Uislamu na Ustaarabu'. Ameandika makala hii kukanusha madai ya wasio Waislamu kwa kutoa madai kuwa Uislamu ndio uliosababisha kuporomoka kwa hali ya Waislamu. Shibli Shama'il amejaribu kuthibitisha kuwa jambo hasa lililosababisha kuporomoka kwa hali za Waislamu ni wao Waislamu kuyaacha (kuacha kutekeleza) mafundisho ya kijamii ya Uislamu.

Wale wazungu wanaoushambulia Uislamu aidha hawajui au wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kuwafanya watu wa Mashariki (Asia) wazitilie shaka sheria zao na mfumo wao ili kuwafanya wafuate mfumo wa Kimagharibi. Wakati wa zama zetu, suala la iwapo Uislamu unaafikiana na hali halisi ya maisha ya sasa au la limekuwa likiulizwa sana. Tunapata picha ya ndani ya watu hasa wale wanaotoka katika tabaka la wasomi na tunakuta kuwa swali hili linaulizwa zaidi kuliko maswali mengine.

PINGAMIZI

Wakati fulani watu hawa wanatoa hoja za kifalsafa juu ya suala hili kuwa vitu vyote hapa duniani lazima vibadilike. Hakuna kinachobaki vile vile bila kubadilika, na halikadhalika binadamu wanabadilika. Sasa inawezekanaje sheria za Kiislamu zibaki hivyo bila kubadilika kwa zama nenda rudi? Kama tukilitazama swala hili kwa mtazamo wa kifalsafa kabisa, jibu ni rahisi.

Ni vitu (maada) vinavyobadilika kila mara, ambavyo hukua na kuporomoka na ambavyo hupasika katika kugeuka na kuoza. Lakini sheria za ulimwengu hazibadiliki. Kwa mfano, viumbe vyote hai vimegeuka na vimeendelea kugeuka kwa mujibu wa utaratibu na kanuni fulani zilizoelezwa na wanasayansi. Hapana shaka kwamba viumbe hivi vinageuka na kubadilika lakini kanuni zinazotawala mabadiliko haya hazibadiliki. Na sasa tunazungumzia kanuni (sheria) hizi.

Katika hili, hakuna tofauti yoyote iwapo sheria hizi ni za asili au zimetungwa na kukusanywa, kwani inawezekana kwamba sheria ambazo zimetungwa zinaweza kuwa na asili kama chanzo chao na kuafikiana na mchakato wa mabadiliko ya mtu mmoja mmoja na halikadhalika jamii ya wanadamu kwa ujumla.

Hata hivyo, swali kuhusiana na kuafikina au kutoafikiana kwa Uislamu na mahitaji ya muda halina sura ya kiujumla na kifalsafa peke yake. Swali ambalo huulizwa zaidi ni kuwa kwa vile sheria huundwa kukidhi mahitaji ya wanaadamu na mahitaji yenyewe yanabadilika kila mara inawezekanaje sheria hizo za kijamii zibaki hivyo hivyo bila kubadilika? Ni swali zuri.

Na imetokea kuwa tabia za kimiujiza za Uislamu zimewezesha sheria zisizohitaji kubadilishwa kukidhi mahitaji yasiyobadilika ya mtu mmoja na jamii na sheria zinazobadilika badilika kwa mahitaji ya muda mfupi na yanayobadilika. Hii ni sifa ya kipekee ambayo Waislamu wote wajuzi wa mambo ya sheria za kiislamu na waliozisoma sheria zake wanajivunia. Tutalielezea hili vizuri zaidi baadaye. Je mabadiliko ya kijamii yanakwenda na wakati? Kabla ya kuliendea swali hili tungependa kuibua nukta mbili. Nukta ya kwanza ni kuwa watu wengi wanaoongelea maendeleo na mabadiliko ya hali wanadhani kuwa mabadiliko yoyote ya kijamii, hasa kama yametokea nchi za Kimagharibi, basi ni matokeo ya maendeleo.

Hili ni moja ya mawazo potofu liliyoendekezwa na kizazi hiki. Watu wanadhani kuwa kwa vile njia za maisha hubadilika siku hadi siku, zilizo duni hubadilishwa kwa zilizo bora zaidi na sayansi na viwanda vinaboreka kila siku, mabadiliko yote katika maisha ya binadamu ni aina ya maendeleo na kwa hiyo yanafaa kukaribishwa na kupokelewa kwa mikono miwili. Wanafikiri pia kuwa mabadiliko haya hayaepukiki na huja baada ya muda fulani.

Kwa kusema kweli sio kwamba mabadiliko yote ni matokeo ya maendeleo ya sayansi na viwanda wala sio kwamba hayaepukiki. Huku sayansi ikiendelea kukua, asili ya ubinafsi na unyama wa mwanadamu nayo hubaki bila kubadilika. Ujuzi (elimu) na busara humpeleka mtu katika ukamilifu na asili ya unyama wa mwanadamu humsukumia kwenye ufisadi na upotofu.

Asili ya unyama wa mwanadamu mara zote hujaribu kutumia ujuzi kama njia ya kupatia matamanio yake. Kwa kadiri muda unavyokwenda, kwa kadiri maendeleo na mabadiliko yanavyotokea, ufisadi na upotofu ndivyo unavyozidi kukua na kukomaa. Tunapaswa kwenda na wakati lakini wakati huo huo lazima tupige vita ufisadi pia. Mleta mabadiliko (mema) na mpinga mabadiliko (mema) wote wanapigana dhidi ya muda, tofauti yake ni kuwa mleta mabadiliko mema hupigana dhidi ya upotofu unaoletwa na mabadiliko ya muda na mpinga maendeleo (mabadiliko) hupigana dhidi ya mabadiliko (maendeleo halisi) yanayoletwa na mabadiliko ya muda.

Kama tunauchukulia muda na mabadiliiko yake kama kigezo cha mema yoyote na maovu yote, sasa ni kigezo gani cha kuupimia muda wenyewe? Kama kila kitu kitakwenda na wakati sasa je wakati wenyewe unapaswa kwenda na nini? Kama mwanadamu ataufuata muda na mabadiliko yake kwa utii mkubwa, sasa nini kitafanyika juu ya majukumu na nafasi ya utashi wa mwanadamu? Mwanadamu anaendesha gari la wakati, ambalo liko kwenye mwendo.

Lazima awe mwangalifu na aliongoze vyema gari lake. Vinginevyo atakuwa kama mtu aliyepanda farasi na akamwachia farasi wake aende popote atakapo. marekebisho au kuondoa kabisa? Nukta ya pili inayofaa kutajwa hapa ni kwamba baadhi ya watu wamelitatua tatizo gumu la Uislamu na mahitaji ya wakati kwa namna rahisi sana.

Wanasema kuwa Uislamu ni dini ya milele, na inaweza kurekebishwa ili kuafikiana na mahitaji ya kila zama na wakati. Lakini wanapoulizwa marekebisho haya yanafanyikaje na kanuni yake ni nini, mara moja wanasema kuwa hali ya maisha inapobadilika, sheria zilizopo hubatilishwa na kuwekwa nyingine. Wanatoa hoja kuwa sheria za msimu (muda mfupi) za kidini lazima ziwe na uwezo wa kurekebishwa na ziafikiane na maendeleo ya elimu na sayansi pamoja na kupanuka kwa utamaduni na ustaarabu. Kwa mujibu wao, uwezo huo wa sheria wa kuweza kurekebishwa ili kuafikiana na mahitaji ya wakati haupingani na Uislamu na sio kinyume na mafundisho yake.

Wanadai kuwa, kwa vile mahitaji ya wakati yanabadilika kila mara, basi kila zama huhitaji sheria mpya. Wanaendelea kudai kuwa sheria za kiraia na kijamii za Uislamu zinaafikiana na maisha rahisi ya Waarabu waliokuwa wakiishi kabla ya Uislamu, na ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa ni kwa mujibu wa mila na desturi zao.

Sasa kwa kuwa haziafikiani na maisha ya zama hizi zinatakiwa ziondolewe na ziwekwe nyingine mpya za kisasa. Watu hawa wanapaswa kuulizwa: Kama uwezo wa sheria kuweza kurekebishwa maana yake ni uwezo wa kubatilishwa na kufutwa, basi ni sheria gani ambayo haina sifa hii? Kuna sheria basi yeyote ambayo haiendi na wakati kwa mtazamo huu?

Tafsiri hii ya uwezo wa sheria kurekebishwa na kuweza kutumika katika zama zote ni sawa na kusema kuwa vitabu vyote na maktaba ndio njia bora kabisa za kufurahia maisha kwa sababu muda wowote mtu atakapotaka starehe, anaweza kuviuza na kutumia fedha zitakazopatikana kwa ajili ya kukidhi matamanio yake. Mwandishi wa Kiirani anasema kuwa mafundisho ya Uislamu yamegawanyika katika sehemu tatu.

Sehemu ya kwanza ina imani za msingi kama vile tauhidi (imani kuwa Mungu ni mmoja tu), Utume, Ufufuo n.k. Sehemu ya pili inahusiana na matendo ya ibada kama vile sala, saumu, udhu, tohara, hija n.k sehemu ya tatu ina sheria zinazohusiana na maisha ya watu. Kwa mujibu wake yeye ni sehemu mbili tu za mwanzo ambazo ni za lazima katika dini na ambazo zinafaa kuhifadhiwa milele.

Lakini sehemu ya tatu sio sehemu ya lazima ya dini kwa kuwa dini haihusiani na maisha ya kila siku ya watu. Mtukufu Mtume mwenyewe hakuamuru kuwa sheria hizi ziwe sehemu ya dini kwa vile hazikuhusiana na ujumbe wake yeye kama Mtume. Ilitokea tu kwamba akawa ni mkuu wa Dola, kwa hiyo akalazimika kuweka sheria pia. Vinginevyo dini haina lolote la kulazimisha katika maisha ya kidunia ya watu. Ni vigumu kuamini kuwa mtu anayeishi katika nchi ya Kiislamu anaweza kuwa mjinga wa mafundisho ya Uislamu kiasi hiki. Je, Qur'ani haijaelezea lengo la kuleta Mitume na Manabii? Je, Qur'ani haisemi wazi wazi kuwa:'Tumewaletea Mitume wetu na dalili za wazi na tumewaleta pamoja nao kitabu na vipimo, ili watu wahukumiane kwa haki. (Suratul Hadidi; 57:25). 35 Qur'ani imeuelezea uadilifu katika jamii kama lengo kuu la Mitume wote.

Kama unataka unaweza usiyafuate mafundisho ya Qur'ani, lakini kwa nini unatenda dhambi kubwa zaidi kwa kuusingizia na kuuzushia Uislamu na Qur'ani? Bahati yetu mbaya zaidi inatokana na ukweli kwamba maadili yetu na sheria vimepoteza chanzo pekee cha nguvu yake, yaani dini. Ni katika nusu karne tu tulipoanza kusikia watu wakipiga kelele kuwa Uislamu ni mzuri, ili muradi tu ubakie ndani ya majumba ya ibada, na usishughulike na jamii.

Kelele hii imepigwa kutoka ndani ya mipaka ya nchi za Waislamu na imeenezwa katika ulimwengu wote wa Kiislamu. Ili kuliweka lengo la kelele hizi wazi tunaweza kusema kuwa nia ni kuufanya Uislamu ubaki kuwa ni kikwazo cha kuzuia kuenea kwa ukomunisti lakini kama huu huu Uislamu utagongana na maslahi ya Magharibi basi upingwe vikali.

Kwa mtazamo wa watu wa Magharibi, matendo ya Uislamu lazima yaendelee, ili pindi ikitokea haja, Waislamu wahamasishwe kuupinga mfumo wa kikomunisti ambao hauamini mambo ya dini na Mungu, lakini sheria za kijamii za Uislamu ambazo zinatoa falsafa ya maisha ya Uislamu lazima ziondoshwe, kwa vile sheria hizi huwapa Waislamu uhuru fulani na kuwafanya wawe watu tofauti wanaojitegemea katika mfumo wao, jambo ambalo litawazuia kumezwa na nchi za Magharibi zenye tamaa kali. Kwa bahati mbaya, watetezi wa hoja kuwa Uislamu haujihusishi na maisha ya kila siku ya watu, wamesahau baadhi ya ukweli wa msingi. Awali miaka 1400 iliyopita, Uislamu ulipinga kanuni kuwa tunaamini baadhi ya mambo (baadhi ya mafundisho ya Uislamu) na tunayakataa mengine, na ukatamka kuwa kanuni na sheria za Uislamu hazibadiliki.

Pili tunaamini kuwa muda umefika ambapo Waislamu hawapaswi kupotoshwa na mbiu za uongo. Watu sasa pole pole wameanza kuamka na wameanza kutofautisha kati ya maendeleo ambayo ni matokeo ya kuchanua kwa vipaji vya kisayansi na kiakili, na kudhihiri kwa ufisadi na upotofu, kutoka nchi za Magharibi. Watu wa ulimwengu wa Kiislamu hivi sasa, kuliko kipindi kingine chochote, wameanza kufahamu thamani ya mafundisho ya Uislamu na wametambua kuwa wanaweza tu kuishi maisha huru kwa kuyafuata. Hawatayaacha, kwa gharama yoyote.

Waislamu makini wanafahamu kuwa propaganda dhidi ya sheria za kiislamu si chochote bali udanganyifu wa mabepari. Tatu, watetezi wa hoja hii wanapaswa kujua kuwa Uislamu unapokuwa na nguvu, hushinda mifumo mingine yote, iwe ya kikafiri au vinginevyo. Uislamu unataka kutawala maisha ya jamii kama falsafa ya maisha, na hautaki kubakia misikitini tu na sehemu nyingine za ibada. Uislamu ambao utabakia kwenye nyumba za ibada, utaacha nafasi kwa ajili ya mawazo ya Kimagharibi na halikadhalika mawazo yanayopingana na umagharibi na itikadi zake. Adhabu ambazo nchi za magharini zinatumikia, katika baadhi ya nchi za Waislamu ni matokeo ya kutoujua ukweli huu.

3

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

- II UISLAMU NA MAISHA YA KISASA

Mwanadamu sio kiumbe pekee anayeishi maisha ya kijamii. Wanyama wengi, na hususan wadudu hupenda kuishi pamoja na kushirikiana. Wanafuata kanuni za mgawanyo wa kazi, uzalishaji na ugavi na kutoa na kupokea amri. Nyuki, na baadhi ya wadudu jamii ya mchwa wana mfumo huu bora wa maisha, mfumo ambao utamchukua mwanadamu, anayejiona kuwa ni mfalme wa viumbe vyote, miaka au hata karne ili kufikia kiwango hicho cha ufanisi.

Ustaarabu wao (wadudu hawa) haujapitia vipindi kama vile zama za mwituni, zama za mawe na zama za nyuklia. Toka mwanzo wamekuwa na ustaarabu na mfumo wa namna moja kama tu walivyo leo. Ni mwanadamu aliyeanzia sifuri. Tazama : "Mwanadamu aliumbwa dhaifu ."Suratul Nisaa 4:28 Kwa upande wa wanyama, mahitaji yao ya maisha hayabadiliki. Kwao usasa na fasheni mpya havina maana. Ulimwengu wa kale na ulimwengu wa sasa kwao hauna tofauti yoyote.

Kwao sayansi haifanyi ugunduzi wowote ule. Bidhaa mpya kabisa nyepesi na nzito za viwanda hazikuingia katika soko lao; kwa nini? Kwa sababu wanaishi kwa silika na sio kwa akili (mantiki). Maisha ya kijamii ya mwanadamu mara zote yanabadilika. Kila karne ulimwengu unabadilika. Hapo ndio kuna siri ya mwanadamu kuwa mfalme wa viumbe vyote.

Mwanadamu ni mtoto wa maumbile aliyekomaa na kustahili heshima. Amefikia hatua ambayo hahitaji muongozo wa moja kwa moja wa ile nguvu ya ajabu iitwayo silika. Maumbile yanafahamu kuwa mwanadamu ni kiumbe aliyekomaa, na ndio maana yamemuacha huru. Yale ambayo wanyama wanayatekeleza kwa silika na kwa kufuata kanuni za maumbile ambazo hawawezi kuzivunja/kukiuka, wanaadamu wanatakiwa kuyatekeleza kwa kutumia akili na elimu na kwa kufuata sheria zilizopitishwa na zinazoonekana. Mwanadamu akiwa ni mwamuzi wa mwisho wa majaaliwa yake mara zote anaweza kupotoka na kuiacha njia ya maendeleo, na hapa ndio kuna siri ya kuteleza kwake, vipingamizi vyake (anavyokumbana navyo) kupotoka na kushindwa kwake.

Kama tu ilivyo kuwa maendeleo yapo wazi kwake, halikadhalika njia ya kuelekea upotofu, ufisadi na kushindwa haijafungwa. Wanaadamu wamefikia hatua ambayo kwa mujibu wa maneno ya Qur'ani wanaweza kubeba dhamana ambayo mbingu, ardhi na milima haviwezi kubeba; kwa maneno mengine, wanaweza kuishi maisha huru na wanaweza kuchukua majukumu ya kisheria, kitaalamu na mengineyo. Hii ndio sababu hawana kinga ya makosa, ubinafsi, ujinga na dhulma. Pale Qur'ani inapouelezea uwezo huu wa ajabu wa binadamu, mara moja unamtaja kuwa ni 'dhalimu na mjinga'.

Uwezo na sifa hizi mbili za mwanadamu, uwezo wa kuboreka (kuwa bora zaidi) na uwezo wa kupotoka havitenganishiki. Mwanadamu sio kama mnyama ambaye katika maisha yake ya kijamii, huwa haendi mbele wala nyuma, hageukii kulia wala kushoto. Lakini mwanadamu kwa upande wake, katika maisha yake wakati fulani huenda mbele na wakati fulani nyuma. Katika maisha ya wanadamu kama kuna mwendo na kasi, basi kuna kusimama na kupumzika pia. Kama kuna maendeleo na kubadilika kwenda katika hali bora zaidi basi kuna ufisadi na upotofu pia. Kama kuna haki na wema, basi kuna udhalimu na ushari pia.

Kama elimu na busara vimedhihiri basi ujinga na matamanio duni yamedhihiri pia. Inawezekana kwamba mabadiliko yanayotokea na hali mpya zinazoonekana vikawa ni vya kundi la pili (la mabaya). Wasiotaka kubadilishwa na waliopotoshwa. Ni moja ya tabia za mwanadamu kwamba wakati fulani hufanya jambo kupita kiasi na wakati fulani hufanya jambo kwa kiasi kidogo zaidi kuliko inavyohitajika. Kama akichagua kundi la kati na kati hufanya jitihada kutofautisha kati ya mabadiliko ya aina sahihi na mabadiliko ya aina potofu.

Hujaribu na hufanya jitihada kuusukuma muda mbele kwa msaada wa elimu na ubunifu wake na kujinasibisha na maendeleo huku akijaribu kuudhibiti upotofu na kuepuka kutangamana nao. Lakini kwa bahati mbaya, si mara zote mwanadamu huchagua njia hii. Anaandamwa na magonjwa mawili ya hatari, ugonjwa wa kutotaka kubadilika na ugonjwa wa ujinga. Ugonjwa wa kwanza matokeo yake ni kubaki bila mabadiliko na kujiepusha na maendeleo na matokeo ya ugonjwa wa pili ni upotofu wa kuangamia. Asiyetaka kubadilika huchukia kila jambo jipya na hawezi kuafikiana na kitu chochote isipokuwa cha zamani.

Kwa upande wa pili, limbukeni huona kila kitu kipya kuwa ni cha kisasa na maendeleo na hukiaona kuwa ndio hitajio la wakati. Kwa yule asiyetaka mabadiliko (rigid) kila maendeleo mapya kwake anaona ni ufisadi na upotofu wakati limbukeni anaona mambo yote mapya bila kubagua yote yana maana kupanuka kwa utamaduni na elimu. Asiyetaka mabadiliko hatofautishi kati ya pumba na kiini safi na kati ya njia na malengo. Kwa maoni yake kazi ya dini ni kuhifadhi yale yote ya kale na kuukuu hata kama hayatumiki.

Anafikiri kuwa Qur'ani iliteremshwa ili kudhibiti mwendo wa wakati na kuibakiza hali ya dunia iwe vile vile siku zote. Kwa mujibu wa mtazamo huu, mila za zamani na zilizopitwa na wakati, kama vile kuanza kusoma Qur'ani kuanzia mwisho, kuandikia kalamu za matete na wino wa kuchovya kunawia kwenye beseni la kituruki; kula kwa mikono, kutumia taa ya mafuta ya taa na kubakia bila ya kujua kusoma na kuandika ni mambo ya kidini ambayo lazima yahifadhiwe na kudumishwa. Kwa upande mwingine limbukeni huelekeza macho yake yote nchi za Magharibi ili aweze kuiga mtindo wowote mpya utakaotokea na kila mila mpya. Huiita hali hii kuwa ni kisasa na jambo la lazima kufuatwa lililoletwa na wakati. Wote wawili, wasiotaka mabadiliko na waliopotoka (wajinga) wanaamini kuwa mila na desturi zote za zamani ni kanuni/matendo ya kidini, tofauti ni kuwa asiyetaka mabadiliko anataka kuzihifadhi wakati mjinga anaona kuwa dini ni sawa na kudorora (bila mabadiliko yoyote).

Katika karne chache zilizopita suala la migongano kati ya dini na sayansi limekuwa likibishaniwa sana miongini mwa watu wa nchi za Magharibi. Wazo la migongano liliibuka kutokana na mambo mawili. Kwanza kanisa lilikuwa limezikubali baadhi ya dhana za kisayansi na kifalfasa kuwa ni imani za kidini, lakini maendeleo ya sayansi yakathibitisha uongo wa dhana hizo. Pili, sayansi imebadilisha muundo na hali za maisha. Wale wasiotaka mabadiliko, ambao wana muonekano wa kushika dini, wanataka kuufanya muonekano wa nje wa maisha ya kimaada kuwa sehemu ya dini, kama tu, bila ulazima wowote walivyoyapa sura ya kidini baadhi ya masuala ya kifalsafa.

Limbukeni nao wanaamini kuwa dini imeamuru muundo fulani wa maisha ya kimaada, na kwa vile sayansi imeamuru kuwepo kwa mabadiliko katika muundo huu, dini inapaswa kutupiliwa mbali. Kupinga mabadiliko kwa kundi moja, na ujinga wa kundi jingine, kumezua wazo la kubuni la mgogoro kati ya sayansi na dini. Hadith ya mafumbo katika Qur'ani Uislamu ni dini ya kimaendeleo na inataka wafuasi wake waendelee. Qur'ani imetumia hadith ya mafumbo (yenye mafundisho) kuwashawishi Waislamu wasonge mbele, chini ya nuru ya Qur'ani. Inasema kuwa wafuasi wa Mtume Muhammad(s.a.w.w) ni kama mbegu iliyopandwa katika ardhi. Kwanza matawi yake hutokeza kama majani laini ya mbegu. Kisha hukua na kuimarika sana kiasi cha kuweza kusimama katika kikonyo chake. Hakua haraka mno kiasi cha kuwashangaza sana wakulima.

Huu ni mfano wa jamii ambayo Qur'ani inaukusudia. Qur'ani inachokikusudia ni kukua. Qur'ani inataka kuweka msingi wa jamii ambayo mara zote itakuwa ikikua, ikiendelea na kupanuka. Will Durant anasema hakuna dini iliyowataka wafuasi wake kuwa na nguvu kama Uislamu ulivyofanya. Historia ya Uislamu wa awali inaonyesha ni kiasi gani Uislamu ulivyo na nguvu ya kuijenga upya jamii na kuisukuma mbele kimaendeleo. Uislamu unapingana na vyote viwili kutaka mabadiliko na ulimbukeni (ujinga) na unaviona vyote hivi viwili kuwa ni hatari. Uchakavu wa kiakili wa wasiotaka mabadiliko na kung'ang'ania kwao mila za zamani ambazo hazina uhusiano wowote na Uislamu, kumetoa kisingizio kwa limbukeni kuuona Uislamu kuwa unapingana na maisha ya kisasa (usasa).

Kwa upande mwingine kufuatana na kuiga mitindo mipya zaidi na namna za maisha za Magharibi kunakofanywa na limbukeni, imani yao kwamba kufuata utaratibu wa Kimagharibi kimwili na kiroho, kukubali kwao tabia, adabu na desturi za Magharibi, na kuiga kibubusa sheria za kiraia na kijamii kutoka katika nchi za Magharibi, kumetoa kisingizio kwa wasiotaka mabadiliko kukitazama kila kitu kipya kwa mashaka na kukiona kama tishio kwa dini yao, uhuru wao na kwa haiba ya kijamii ya jumuiya yao. Kwa sasa, Uislamu unagharamikia makosa ya makundi yote mawili.

Ung'ang'anizi wa wasiotaka mabadiliko umeacha uwanja wazi kwa limbukeni kufanya uharibifu na ujinga wa limbukeni umewafanya wasiotaka mabadiliko kuwa ving'ang'anizi zaidi katika imani zao. Inashangaza kuona kuwa hawa wanaojiita wameelimika na kustaarabika ingawa kiuhalisia ni watu wajinga, wanafikiri kuwa muda ni maasumu (haubebi dhambi). Ukweli ni kuwa mabadiliko yote yanaletwa na watu, na mwanadamu sio maasumu hata kidogo (hajaepukana na madhambi). Sasa vipi inaweza kufikirika kuwa mabadiliko ya muda mara zote huwa hayana makosa na matatizo. Kama ilivyo tu kuwa mwanadamu ana matakwa ya kupenda sayansi, maadili, sanaa na dini, na mara zote huchukua hatua mpya kwa maslahi ya wanadamu, pia ana baadhi ya tabia mbaya.

Ni mbinafsi, mwenye uchu wa madaraka na mwenye kupenda raha. Anapenda fedha na unyonyaji kama tu alivyo na uwezo wa kugundua mambo mapya na kutafuta njia bora zaidi za kufanya mambo pia ana dhamana ya kutenda makosa. Lakini limbukeni na waliopotoka hawajui mambo hayo. Wanarudia mahadhi yale yale kuwa ulimwengu wa kisasa upo hivi na vile. Kinachoshangaza zaidi ni kuwa wanalinganisha kanuni za maisha na vitu; kama vile viatu, kofia na gauni. Kwa vile vitu hivi hutafutwa na kuhitajika vinapokuwa vipya na kutupwa vinapochakaa, halikadhalika kwa mujibu wao, hali iwe hivyo hivyo kwa ukweli usiobadilika. Kwao, kizuri na kibaya havina maana zaidi ya kipya na cha zamani.

Ukabaila ni mbaya kwa sababu tu ni mfumo wa zamani na umepitwa na wakati. Vinginevyo ulikuwa mzuri kabisa wakati unaanzishwa duniani kwa mara ya kwanza. Halikadhalika unyonyaji wa wanawake ni mbaya tu kwa vile haupendwi na ulimwengu wa kisasa; vinginevyo hadi hivi majuzi, watu hawa hawa walikuwa hawampi mgao wa urithi. Walikuwa hawajaitambua haki yake ya kumiliki mali na walikuwa hawaheshimu ridhaa na maoni yake.

Kwa mujibu wa watu hawa, katika zama hizi, zikiwa ni zama za anga (kuruka na ndege n.k), kama ilivyokuwa tu haiwezekani kusafiri kwa punda na kuacha ndege, kuwasha kibatari na kuacha umeme, kushona nguo kwa mkono na kuandika kwa mkono huku ukiacha mashine kubwa za kisasa za kuchapishia, halikadhalika haiwezekani kuacha kwenda kwenye sherehe za muziki, sherehe ambazo watu wanavaa mavazi ya kuogelea, mialiko ya chakula cha usiku chenye nyama za kubanikwa, kutoshiriki katika vicheko vya ovyo, kutocheza karata, kutovaa visketi vifupu kwani vitu vyote hivi ni mitindo ya karne hii. Wanahofu kuwa wasiposhiriki katika mambo haya watarudi nyuma katika zama za kuendesha farasi. Wanadai kuwa hizi ni zama za nyukilia, zama za sayansi, zama za miezi ya kubuni na zama za makombora ya masafa marefu.

Hili ni jambo zuri! Sisi pia tunamshukuru Mungu kuwa tunaishi katika zama hizi na tunaomba kwamba tufurahie na kufaidika na sayansi na viwanda kwa kiwango cha juu kabisa. Lakini je, mambo yote haya yanasababishwa na sayansi tu? Je, hali zote za karne hii ni matokeo ya maendeleo ya kisasa ya sayansi? Je, sayansi inadai kuwa imedhibiti mambo yote hapa duniani? Sayansi haijawahi kudai hivyo hata siku moja.

Balaa la karne yetu ni kuwa kundi la wanasayansi kwa nia njema kabisa, huitumia sayansi kufanya ugunduzi mpya, lakini kundi jingine la wabinafsi na wenye uchu wa madaraka na wanaoabudu fedha huyatumia vibaya matunda ya jasho la wanasayansi ili kuyafikia malengo yao ya kiovu. Sayansi inalalamika kuwa inatumiwa vibaya na wanaadamu wakorofi na hii ndio bahati mbaya ya kizazi chetu. Sayansi inasonga mbele katika fani za fizikia na inagundua sheria za mwanga na kuakisi na kundi la wakorofi na wabinafsi wanaitumia kutengenezea filamu za bluu (ngono) za uharibifu na uovu. Kemia inaendelea na kugundua tabia za vitu mbali mbali na michanganyiko yake.

Baadhi ya watu wanaamua kutumia ugunduzi huu kutengeneza madawa ya kulevya, heroin ambayo ni laana kwa wanaadamu. Sayansi iligundua chanzo kizuri cha nishati ndani ya atom, lakini kabla ya ugunduzi haujatumika kwa manufaa ya wanaadamu, wenye tamaa ya madaraka walifanya haraka kutengeneza bomu la atomiki, na kuwadondoshea watu wasio na hatia. Mapokezi yalipoandaliwa, kwa ajili ya heshima ya Einstein, mwanasayansi mkubwa wa karne ya 20, yeye mwenyewe alipanda juu ya jukwaa na kusema, "Mnampa heshima mtu ambaye amechangia kwa namna fulani kutengenezwa kwa bomu la atomiki?"

Einsten mwenyewe hakutumia elimu yake kutengeneza bomu. Ni wengine waliotumia ugunduzi wake kwa lengo hili. Matumizi ya heroin, mabomu ya atomiki na filamu za matusi (bluu) haviwezi kuhalalishwa eti kwa madai kuwa ni mambo ya karne hii. Ikiwa ndege za kisasa kabisa za mabomu zinatumika kurushia mambomu bora kabisa kwa watu wa nchi nyingine, na watu walioelimika sana wanaajiriwa kufanya kazi hii, je, usasa huu unaweza kupuguza ushenzi wa kurithi wa tendo hili?

4

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

- III UISLAMU NA USASA

Hoja kuu ya wale ambao wanasema kuwa katika masuala ya haki za kifamilia tunapaswa kufuata mfumo wa Kimagharibi, ni kuwa muda umebadilika na mahitaji ya karne hii yanatutaka tufanye hivyo. Tunaonelea kuwa ni vizuri tuyaweke maoni yetu wazi juu ya nukta hii, kwa sababu bila kufanya hivyo, mjadala juu ya nukta yoyote hautakuwa kamili, ingawa kwa sababu ya uchache wa nafasi haiwezekani kulijadili suala hili kwa mitazamo yake yote, kifalsafa, kisheria, kijamii na kimaadili. Itatosheleza hapa kujadili nukta mbili tu. Nukta ya kwanza ni kwamba kuafikiana kwayo na kukubaliana na mabadiliko ya wakati sio suala rahisi sana kama baadhi ya watu wasiojua wanavyofikiri. Mabadiliko yanayoletwa na wakati, wakati fulani huwa ni ya kurudisha maendeleo nyuma.

Tunapaswa kwenda na mabadiliko ya wakati ya kimaendeleo na tunapaswa kuyapiga vita mabadiliko yanayoletwa na wakati ambayo ni ya kiharibifu. Ili kutofautisha aina hizi mbili za mabadiliko na kujua asili yake, tunapaswa kujua chanzo cha maendeleo (ugunduzi au mabadiliko) haya mapya na yameelekezwa katika mwelekeo gani. Tunapaswa kuangalia ni tabia gani za kibinadamu zimeyaleta (njema au mbaya) na ni matabaka gani ya watu yanatetea mambo haya mapya?

Tunapaswa kuangalia je yameletwa na tabia tukufu za mwanadamu au matamanio duni yanayofanana na wanyama, na kama yamekuja kama matokeo ya uchunguzi usio wa kibinafsi wa wanazuoni na wasomi, au yameletwa na matamanio duni ya wanaotumikia nafsi zao na tabia za kifisadi za jamii.

MNYAMBULIKO WA SHERIA ZA KIISLAMU

Nukta ya pili inayofaa kuwekwa wazi ni kuwa baadhi ya wasomi wa kiislamu wanaamini kuwa Uislamu una uwezo na sifa ambazo zinaupa uwezo wa kutumika zama zote. Kwa mujibu wa wasomi hawa, mafundisho ya Uislamu yanaafikiana na maendeleo ya wakati, kupanuka kwa utamaduni na matokeo ya mabadiliko haya. Hebu tuangalie asili, sifa na uwezo huu ambao Uislamu unao. Kwa maneno mengine hebu tuangalie ni vifaa gani vimewekwa katika jengo hili la dini, na ikiwa vimeipa sifa ya kuafikiana na hali zote zinazobadilika, bila kuwa na haja ya kuacha baadhi ya mafundisho yake na bila mgogoro wowote kati ya mafundisho yake na hali yoyote inayojitokeza ya kupanuka kwa elimu na ustaarabu.

Ingawa suala hili lina sura ya kiufundi, ili kuondoa shaka shaka ya wale wanaotilia shaka ukweli huu kuwa Uislamu una sifa hii, tunalielezea kwa kifupi hapa. Kwa undani zaidi juu ya suala hili, wasomaji wanaweza kusoma kitabu kiitwacho 'Tanbihul Ummah' cha hayati Ayatullah Naini au kitabu kingine kiitacho 'Marjaiyyat Wal Imamat cha mwanazuoni mkubwa wa zama hizi Allamah Tabatabai. Lakini vitabu vyote hivi vipo katika lugha ya kifursi. Kuna nukta nyingi, ambazo zinaunda siri ya Uislamu kuwa na uwezo wa kuafikiana na kupanuka kwa elimu na ustaarabu, na uwezo wa kutumika kwa sheria zake thabiti na imara katika hali mbali mbali za maisha. Hapa tutataja baadhi yake.

Msisitizo katika roho na kutojali sana kiwiliwili. Uislamu haujashughulikia maisha ya nje (kimwili) tu ambayo hutegemea kiwango cha maendeleo ya elimu ya mwanadamu. Mafundisho ya Uislamu hushughulikia roho pia na malengo ya maisha na hutoa njia bora kabisa ya kuyafikia malengo haya. Sayansi haijabadilisha roho na malengo ya maisha wala haijapendekeza njia yoyote nzuri zaidi, fupi zaidi na salama zaidi ya kuyafikia malengo haya. Imetoa tu njia bora zaidi na vifaa vya kukwamisha njia ya kuyafikia malengo haya. Uislamu, kwa kuhifadhi malengo tu katika himaya yake na kuacha muundo na mbinu kwenye himaya ya sayansi na teknolojia, umeepuka migongano dhidi ya utamaduni na ustaarabu.

Sio hivyo tu lakini pia kwa kuhimiza mambo yanayosaidia kupanuka kwa ustaarabu, yaani elimu, kazi, uchamungu, ridhaa, ujasiri na uvumilivu bila kukata tamaa, umejitolea kuwa kigezo kikuu cha kupanua ustaarabu. Uislamu umeweka alama za barabarani katika njia yote ya maendeleo ya mwanadamu. Alama hizi kwa upande mmoja zinaonyesha njia na kituo cha mwisho na kwa upande wa pili zinaonyesha makorongo na sehemu za hatari. Sheria zote za Kiislamu ni alama za barabara, aidha za aina ya kwanza au ya pili. Njia za maisha katika zama hutegemea juu ya kiwango cha elimu ya wanaadamu.

Kwa kadri elimu ya watu inavyopanuka, ndivyo njia bora zaidi za kujipatia kipato zinavyotokea na moja kwa moja zinachukua nafasi ya zile njia duni (za zamani). Mifumo ya nje na ya kimaada ya njia hizi (za kupatia riziki) haina utakatifu katika Uislamu, na Waislamu hawalazimiki kuzidumisha. Uislamu haujasema kifaa hiki na kile kitumike kwa ushonaji, ususi, kilimo, usafiri, vita au kazi nyingine. Hivyo hapawezi kuwa mgogoro wowote kati ya sayansi na Uislamu, pindi kifaa kinapopitiwa na wakati, cha kisasa zaidi kinaweza kutumika badala yake.

Uislamu haujaagiza kutumika kwa mtindo maalum ya viatu au nguo, wala haujapendekeza aina fulani ya ujenzi wa majengo. Halikadhalika hauhimizi juu ya mbinu fulani fulani za uzalishaji na ugavi. Hii ni moja ya sifa hizo za Uislamu, ambazo zimeuwezesha kuweza kutumika katika maendeleo yote ya wakati. Sheria madhubuti kwa mahitaji madhubuti na sheria zinazobadilika kwa mahitaji yanayobadilika. Sifa nyingine ya Uislamu, ambayo ina umuhimu mkubwa ni kuwa umeweka sheria madhubuti (zisizobadilika) kwa ajili ya mahitaji madhubuti (yasiyobadilika) na sheria zinazobadilika kwa mahitaji yanayobadilika. Mbali na mahitaji ya wanaadamu, mahitaji ya mtu mmoja mmoja na vikundi, yote yana asili ya kudumu.

Hayabadiliki kwa mujibu wa wakati. Kanuni za mifumo inayotawala silika za binadamu na mahusiano ya kijamii hazibadiliki. Tunazijua nadharia za 'Maadili husianishi' na 'Uadilifu husianishi' ambazo zina wafuasi wake, na tutatoa maoni yetu kuhusiana nao baadaye. Sehemu nyingine ya mahitaji ya mwanadamu ni ile ya mahitaji yanayobadilika, na hii huhitaji sheria zinazobadilika. Uislamu ulishayaona mahitaji hayo na umeyaunganisha na kanuni fulani ambazo zina sheria ndogo zinazobadilika kila hali inapobadilika. Kufafanua nukta hii hebu tuangalie mifano hii;'Andaeni majeshi kwa ajili yao (maadui)' (Suratul Anfal 8:60.) Wakati huo huo tunasoma hadith kadhaa za Mtume katika vitabu vya sheria za Kiislamu chini ya kichwa cha habari 'Kuendesha farasi na kurusha mishale.' Mtume aliwaelekeza Waislamu wajifunze kuendesha farasi na kurusha mishale na wawafundishe watoto wao pia. Haya yalikuwa ni sehemu ya mafunzo ya Kiislamu katika zama hizo.

Ni dhahiri kabisa hapa kuwa amri ya msingi ni 'Kuandaa majeshi.' Upinde na mshale, jambia na mkuki na farasi sio vya muhimu. Kilicho cha muhimu ni kuwa imara kijeshi dhidi ya maadui. Kuandaa majeshi ni amri ya kudumu ambayo imetokana na hitajio la kudumu. Hata hivyo ulazima wa kupata ujuzi katika kuendesha farasi na kurusha mishale sio wa kudumu, na hubadilika kutokana na wakati.

Kutokana na kubadilika kwa hali, ujuzi wa kufyatua risasi umechukua nafasi ya kurusha mishale. Mfano mwingine ni sheria ya kijamii inayohusu kubadilishana mali, iliyotajwa katika Qur'ani. Uislamu umetambua kanuni ya umiliki wa mali wa mtu binafsi. Hata hivyo umiliki huu unaotambuliwa na Uislamu ni tofauti na ule uliopo katika nchi za kibepari. Tabia ya umiliki wa mali wa watu binafsi katika Uislamu ni kanuni ya kubadilishana. Kwa utaratibu huu Uislamu umeweka sheria fulani.

Mojawapo imeelezwa na Qur'ani Tukufu katika maneno haya'Na msile mali zenu (kila mmoja kula za mwenzake) kwa batili' (Suratul Baqarah, 2:188).

Kwa maneno mengine katika mauzo ya biashara, fedha isitoke mkono mmoja kwenda mwingine isipokuwa kwa kubadilishana na kitu kingine cha halali chenye kuwa na mamlaka ya mwisho juu ya mali hiyo. Imelezwa na kufafanuliwa katika sheria ya Kiislamu mauzo na manunuzi ya vitu fulani yamekatazwa. Vitu hivyo ni pamoja na damu na kinyesi cha binadamu. Sababu ni kuwa vitu hivi havina thamani inayoviwezesha kuhesabika kuwa sehemu ya mali ya mwanadamu. Kanuni hii ni sawa ya mali ya mwanadamu. Kanuni hii ni sawa na ile iliyo katika Aya iliyonukuliwa hapo juu.

Ubatili wa mauzo na manunuzi ya damu na kinyesi cha binaadamu ni sehemu au mfano tu wa matumizi ya kanuni hiyo. Hata kama hakuna ubadilishaji uliofanyika, (wa bidhaa au bidhaa kwa fedha) fedha au mali inayomilikiwa na mtu fulani haiwezi kufujwa au kuliwa bure. Sheria inayokataza kula mali ya mtu mwingine bure (bila kufanya kazi) au kiwizi ni kanuni madhubuti na inatumika zama zote, na imetokana na hitajio la kudumu la jamii.

Lakini kanuni kuwa damu na kinyesi cha binadamu havihesabiki kama mali na haviruhusiwi kuuzwa, inahuisiana na wakati na kiwango cha ustaarabu. Kanuni hii inaweza kubadilishwa kutokana na mabadiliko ya hali, maendeleo ya sayansi na viwanda na uwezekano wa kuzitumia bidhaa hizi katika namna sahihi na yenye manufaa. Mfano mwingine; "Imam Ali(a.s) hakuwahi kuweka dawa kwenye nywele zake hata siku moja, ingawa zilikuwa zimekuwa za mvi katika miaka ya mwisho ya uhai wake.

Siku moja mtu mmoja alimwambia, 'Je Mtume hakuamrisha nywele za mvi ziwekwe dawa?" Ali alijibu 'Ndiyo aliamrisha' Sasa kwa nini huweki dawa kwenye nywele zako? Yule mtu aliuliza. Ali akasema; "Katika wakati ule ambao Mtume alitoa maelekezo haya, idadi ya Waislamu ilikuwa ndogo na kulikuwa wazee wengi waliokuwa wakishiriki vitani. Mtume aliwaamrisha wazipake dawa ili kuficha umri wao halisi, kwani kama adui angeona kuwa anapambana na kundi la wazee tu, hamasa yake ingeongezeka. Kwa kuwa Uislamu umeenea dunia yote, hali imebadilika. Kila mtu yupo huru kupaka dawa nywele zake au kuacha." Kwa maoni ya Imamu Ali, maelekezo ya Mtume hayakuwa ya kudumu wala haikuwa sheria ya kudumu.

Uislamu unajali muonekano wa nje na roho ya ndani pia. Lakini unataka pumba kwa ajili ya punje yenyewe na unataka nguo kwa ajili ya mwili. Suala la kubadilisha herufi Katika siku za hivi karibuni hapa Iran kumekuwa na ubishani juu ya kubadlisha herufi. Suala hili linaweza kuangaliwa katika pande mbili kwa mtazamo wa kanuni za Kiislamu, na kwa sura mbili. Kwanza ni iwapo Uislamu unapendelea herufi fulani na kuzibagua nyingine.

Je Uislamu unaziona herufi za sasa, ambazo ni za Kiarabu, kama zake, na herufi nyinginezo kama zile za kilatini zinazoonekana ni za kigeni? Uislamu ambao ni dini ya ulimwengu mzima unaziona herufi zote duniani kuwa ni sawa. Sura ya pili ni kuwa kiasi gani kubadilika kwa herufi kutachanganya utamaduni wa Taifa la Kiislamu na watu wengine na kutakuwa na madhara gani kwa utamaduni wa taifa hili. Na zaidi ya hayo, katika karne 14 zilizopita, vitabu vya Kiislamu na kisayansi vilivyozalishwa na Irani vimeandikwa katika herufi za sasa (za kiarabu), je kubadilisha herufi si kutazifuta (haribu) kazi zote hizi?

Swali jingine ni, 'Ni akina nani wanaopendekeza mabadiliko haya, na ni akina nani watakaoyatekeleza? Maswali yote haya ni thabiti.' Kuwategemea wengine ndio kumekatazwa, sio kofia ya kizungu Watu kama mimi mara nyingi wanakumbana na maswali, yanayoulizwa kwa dharau au kejeli. "Sheria ya Kiislamu inasemaje kuhusu kula ukiwa umesimama?' Ni vipi kuhusu kula kwa kijiko au uma?' Je kuvaa kofia ya kizungu kumekatazwa?' Je kutumia lugha za kigeni kumekatazwa?'" Katika kujibu maswali haya, tunasema kuwa Uislamu haujatoa maelekezo yoyote mahsusi juu ya hili. Uislamu haujawaelekeza wafuasi wake kula kwa mkono au kijiko. Ulichowaelekeza ni kuzingatia usafi.

Uislamu haujaelekeza matumizi ya mitindo ya aina fulani ya viatu, kofia au nguo. Kwa mtazamo wa Uislamu lugha zote Kiingereza, Kijapani, Kifursi, zina hadhi sawa. Hata hivyo, Uislamu unasema kitu fulani zaidi. Umesema kuwa imekatazwa mtu kupoteza utambulisho wake. Kuwaogopa wengine bila ulazima kumekatazwa, Kuwaiga wengine kumekatazwa, kuchekeshwa na kuvutiwa na wengine kama sungura anavyovutiwa na nyoka, kumekatazwa.

Kumchukulia punda mgeni aliyekufa kuwa ni farasi kumekatazwa. Kuingiza nchini upotofu na ukosefu wa maadili kutoka nje, kwa madai ni mambo ya kisasa ya karne hii, kumekatazwa. Kuamini kuwa Waislamu wanapaswa kufuata mila na utamaduni wa Kimagharibi ndani na nje, kimwili na kiroho, kumekatazwa. Kwenda nchi ya Kimagharibi kwa siku chache na baada ya kurudi, unaanza kutamka maneno yetu kama wao (wazungu) kumekatazwa. Muhimu na muhimu zaidi. Sura nyingine ya Uislamu inayoufanya uende na mahitaji ya wakati ni kukubaliana kwa mafundisho yake na akili/mantiki.

Uislamu umetangaza kuwa sheria zake zimezingatia maslahi makubwa zaidi. Na wakati huo huo, Uislamu wenyewe umetoa madaraja mbali mbali ya umuhimu wa maslahi haya. Hii inarahisisha kazi ya wataalamu wa sheria za Kiislamu katika fani hizo ambapo maslahi tofauti yanaonekana kugongana. Katika hali hizo, Uislamu umewaruhusu wataalamu wa sheria za Kiislamu kupima uzito wa maslahi tofauti, na kuzingatia mwongozo ambao Uislamu wenyewe umetoa, katika kuangalia ni maslahi gani hilo ni muhimu zaidi. Katika fani ya sheria za Kiislamu, hii huitwa suala la "muhimu na muhimu zaidi." Kuna mifano mingi ambapo kanuni hii ya maslahi ya juu na ya juu zaidi imepata kutumika.

Hata hivyo kwa sababu ya uchache wa nafasi, tunairuka sehemu hii Sheria yenye haki ya Turufu. Sifa nyingine ya Uislamu ambayo imeipa dini hii uwezo wa kuhamishika na kutumika katika hali mbali mbali na imeifanya kuwa dini inayoishi na ya kudumu milele ni kuwa ndani yake kuna chombo cha sheria ambacho kazi yake ni kudhibiti na kurekebisha sheria nyingine.

Mafakihi wanaziita kanuni hizi kuwa ni " kanuni za kuongozea." Kanuni ya 'Hakuna madhara' na 'Hakuna hasara' kwamba sheria haitatumika pale ambapo inaweza kusababisha ugumu au madhara kwa maslahi ya mtu asiye na hatia, imeuenea (imeutawala) mfumo mzima wa kisheria. Lengo la kanuni hizi ni kudhibiti na kurekebisha sheria nyingine. Kwa kusema kweli Uislamu umezipa nguvu ya turufu kanuni hizi ambazo hubadilisha kanuni nyingine.

Madaraka ya mtawala Kwa nyongeza kuna mfululizo mwingine wa kanuni za kuweka mambo katika mizania ambazo Mwenyezi Mungu ameipa dini hii ya mwisho. Ayatullah Na'ini na Allamah Tabatabai, juu ya hili, wametegemea madaraka ambayo Uislamu umeipa serikali ongofu ya Kiislamu. Kanuni ya ijtihadi Mshairi na mwanafalsafa wa Kipakistani anasema kuwa Ijtihadi (kuzalisha sheria kutoka vyanzo vyake vya asili) ni nguvu ya hamasa ya Uislamu. Yuko sawa kusema hivyo. Lakini kilicho muhimu zaidi ni kuwa Uislamu una sifa maalum ya kuruhusu Ijtihadi. Hakuna dini nyingine yenye sifa hii katika namna hii hii. Jengo la ndani la Uislamu limejengwa katika namna ambayo kwa msaada wa Ijtihadi, unaweza mara zote kwenda na mahitaji yanayobadilika katika maisha.

Abu Ali Ibn Sina (Avicenna) katika kitabu chake Al-Shifa, ameelezea haja ya Ijtihadi kuwa inatokana na kubadilika kila mara kwa mahitaji. Anasema kuwa hali za maisha mara zote zinabadilika. Matatizo mapya yanaibuka kila mara, lakini misingi ya Uislamu haibadiliki. Hivyo katika hali hii, lazima wawepo watu wanaojua sheria za kiislamu vizuri na mafundisho ya Kiislamu vizuri ili waweze kujibu maswali yote yanayoibuka katika kila zama na hivyo kukidhi mahitaji ya wakati. Katiba ya Iran inaamuru kuwa pawepo chombo cha mujtahidi wasiopungua watano (wanazuoni wakubwa wa Theolojia wanaoweza kufanya ijtihadi) kitakachokuwa kikichunguza sheria zinazopitishwa na serikali kila wakati.

Lengo hapa ni kuwa watu hawa (mujtahidi) kwa vile sio wapinga mabadiliko wala hawapingi maendeleo ya kisasa, wala sio limbukeni wala hawawafuati wengine kibubusa, waangalie na kudhibiti mfumo wa sheria wa nchi. Inapaswa kueleza kuwa ijtihad kwa namna halisi ina maana kubobea na inahitaji uelewa wa ndani sana wa misingi ya Uislamu na nguzo zake na elimu kubwa kabisa ya kanuni za fikihi ya Kiislamu, ambayo si kila mtu aliyesoma Uislamu kwa muda fulani anaweza kudai kuwa mujtahid.

Hapana shaka kuwa hii ni kazi ya umri mzima wa mtu ili kubobea katika kanuni na mafundisho ya Uislamu, na mbali na kipaji, nia na akili, inahitaji pia msaada wa Mungu. Mbali na kubobea (kwenye mchepuo maalum) na Ijtihad, baadhi ya watu wanaweza kupata elimu na kufikia kiasi kwamba maoni yao yanaweza kuchukuliwa kuwa ni fatwa. Historia ya Uislamu inawataja watu hao ambao licha ya elimu yao kubwa na maadili yao ya hali ya juu walikuwa na hadhari kubwa, walipokuwa wakitoa maoni yao, juu ya masuala ya kisheria.

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

Sura Ya Arubaini Na Tisa: Surat Al- Hujurat. Imeshuka Madina. Ina Aya 18.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure-hemu

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيِ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَاتَّقُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿١﴾

1. Enyi ambao mmeamini! Msitangulie mbele ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ ﴿٢﴾

2. Enyi mlioamini! Msinyanyue sauti zenu kuliko sauti ya Nabii, wala msiseme naye kwa kelele kama mnavyosemezana nyinyi kwa nyinyi, visije vitendo vyenu vikaanguka, na hali hamtambui.

إِنَّ الَّذِينَ يَغُضُّونَ أَصْوَاتَهُمْ عِندَ رَسُولِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ امْتَحَنَ اللَّـهُ قُلُوبَهُمْ لِلتَّقْوَىٰ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ عَظِيمٌ ﴿٣﴾

3. Kwa hakika ambao wanateremsha sauti zao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amezitia mtihani nyoyo zao kwa takua. Hao watakuwa na maghufira na ujira mkubwa.

إِنَّ الَّذِينَ يُنَادُونَكَ مِن وَرَاءِ الْحُجُرَاتِ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ ﴿٤﴾

4. Hakika ambao wanakuita nyuma ya vyumba, wengi wao hawana akili.

وَلَوْ أَنَّهُمْ صَبَرُوا حَتَّىٰ تَخْرُجَ إِلَيْهِمْ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٥﴾

5. Na lau wao wangelingojea mpaka uwatokee ingelikuwa kheri kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

MSINYANYUE SAUTI ZENU KULIKO SAUTI YA NABII

Aya 1 – 5

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawakumbusha waumini mambo haya yafutayo:-

1.Enyi ambao mmeamini! Msitangulie mbele ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Msifanye haraka kusema au kufanya tendo lolote linaoamabatana na dini na masilahi ya uma, mpaka alipitishe Mwenyezi Mungu kupitia Mtume wake mtukufu.

Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

Katika Nahjul-balagha imeandikwa: “Mche Mwenyezi Mungu kwa baad- hi ya takua hata kama ni kidogo. Na weka sitara baina yako na Mwenyezi Mungu hata kama ni nyembamba.”

Kwa uchache kabisa wa mtu kumcha Muumba wake ni kujizuia kusema: Lau Mwenyezi Mungu angelihalalisha hili ambalo ameliharamisha au angeliharamisha lile alilolilihalalisha. Au kusema afadhali Nabii angeli- fanya hivi au asingelifanya vile alivyofanya na mengineyo ya ujeuri na ujinga.

2.Enyi mlioamini! Msinyanyue sauti zenu kuliko sauti ya Nabii.

Si jambo zuri kuinua sauti bila ya dharura. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema: “Na uinamishe sauti yako. Hakika sauti mbaya zaidi ni ya punda.” Juz. 21 (31:19). Sikwambii tena ikiwa ni kuinua sauti mbele ya wakubwa na kwenye vikao vyao. Na Mtume mtukufu(s.a.w. w ) ni bwana wa manabii na mtukufu wa viumbe wote.

3.Wala msiseme naye kwa kelele kama mnavyosemezana nyinyi kwa nyinyi, visije vitendo vyenu vikaanguka, na hali hamtambui.

Mnapozungumza na Nabii msizungumze kama mnavyozungumza nyinyi. Mwenye kufanya hivyo atakuwa amebatilisha imani yake bila ya kutaka wala kujua. Na mwenye kubatilika imani yake ndio vimebatilika vitendo vyake na atakuwa mikononi mwa waliopata hasara.

Kwa hakika ambao wanateremsha sauti zao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amezitia mtihani nyoyo zao kwa takua – yaani amezisafisha nyoyo zao kwa matendo mema -Hao watakuwa na maghufira na ujira mkubwa.

Mwenyezi Mungu huwajaribu waja wake kwa aina mbalimbali ya mitihani, ili apate mawaidha mwenye kuwaidhika na ajikanye mwenye kukanyika. Mwenye kuwaidhika na akawa na subira Mwenyezi Mungu humtakasa, humuongoza njia ya usawa na humneemesha kwa maghufira na ujira wa wenye kuwa na subira.

Aya inaashiria kwamba kuzungumza kwa adabu na kwa inavyotakikana ni katika imani. Imam Ali(a . s) anasema:“Imani ya mja hainyooki mpaka unyooke moyo wake na moyo haunyooki mpaka unyooke ulimi wake.

Hakika ambao wanakuita nyuma ya vyumba, wengi wao hawana akili.

Mtume(s.a.w. w ) alikuwa na wake tisa, kila mmoja alikuwa na chumba chake kilichojengwa kwa makuti ya mtende, mlangoni kukiwa na pazia ya manyoya.

Wafasiri wanasema kuwa mabedui walikuja Madina na wakasimama nyuma ya vyumba vya Mtume wakaanza kuita kwa sauti: Ewe Muhammad(s.a.w. w ) tutokee! Mtume akangoja kidogo; kisha akawatokea. Mwenyezi Mungu amewataja kuwa wengi wao hawakujua walichokuwa wakikifanya, kutokana na ubedui na ushamba.

Na lau wao wangelingojea mpaka uwatokee ingelikuwa kheri kwao, kwa sababu kungoja na kutofanya haraka kuna malipo na thawabu, kumwdhimisha Mtume wa Mwenyezi Mungu na kuchunga adabu.

Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu. Rehema yake inaenea kwa washamba, walalahoi n.k.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَإٍ فَتَبَيَّنُوا أَن تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَىٰ مَا فَعَلْتُمْ نَادِمِينَ ﴿٦﴾

6. Enyi mlioamini! Akiwajia fasiki na habari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda.

AKIWAJIA FASIKI NA HABARI YOYOTE, ICHUNGUZENI

Aya 6

MAANA

Enyi mlioamini! Akiwajia fasiki na habari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda.

Imekuwa mashuhuri kwa wafasiri kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alimtuma Walid bin Uqba bin Abu Muit kwa Bani Mustaliq kuchukua Zaka, wakampokea kwa shangwe ya kumzunguka, lakini akadhania kuwa wanataka kumzuia.

Akarudi kwa Mtume(s.a.w. w ) na kumwambia: wamenizuia na kunifukuza. Basi Mtume(s.a.w. w ) akakasirika na baadhi ya swahaba zake wakamwambia tuwashambulie? Ndio ikashuka Aya hii kuwaondolea tuhuma Bani Mustaliq. Kuna sababu nyingine ya kushuka Aya hii.

Sisi hatutegemei lolote katika sababu za kushuka Aya ila ikithibiti kwa nukuu ya Qur’an au Hadith mutawatir. Zaidi ya hayo ni kuwa kudhania Walid shari hakuwezi kusababisha ufasiki; isipokuwa ni kukosea na kutatizika. Mwenye kukosea haitwi fasiki.

Vyovyote itakavyokuwa sababu za kushuka, lakini Aya haishilii kwenye sababu hiyo, bali inaenda mbali zaidi, kwa vile sababu haiwezi kuhusisha isipokuwa inaenea. Itakuwa sababu inatajwa kwa ajili ya jambo fulani ambalo halihusishi tamko. Kwa hiyo niwajibu kuichukulia dhahiri ya Aya, ambayo inafahamisha uharamu wa kuyachukulia maneno ya fasiki bila ya kuchunguza na kuthibitisha habari yake, kuhofia kuingia kwenye hatari; kama kuwadhuru wengine na kujuta, na majuto ni mjukuu.

Tunapata tafsiri ya Aya hii katika kauli ya Imam Ali(a . s) :“Mwenye kufuata njia iliyo wazi atakunywa maji, na mwenye kuacha atahangaika.”

Kundi la masheikh wa kisunni na kishia wameitumia Aya hii kuwa ni dalili ya wajibu wa kuchukulia kauli ya mwenye kutegemewa bila ya sharti la kuchunguza ukweli wake. Baadhi yao wameitolea dalili kwa maneno ya undani yaliyojifungafunga.

Iko wazi kuwa Aya imechukua msingi wa kiujumla wa kupima habari ambayo haifai kuitegema ila baada ya uthibitisho na hiyo ni habari ya fasiki. Vile vile habari inayotegemwa bila ya uthibitisho ambayo ni habari ya mwenye kutegemewa.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu ameshartiza kuitegemea habari ya fasiki kwa ubainifu na uthibitisho, lakini hakuitaja habari ya mwenye kutegemewa. Lau ingelikuwa ni wajib kuichunguza habari ya mwenye kuaminika basi angeliitaja. Kwa kuwa haikutajwa basi sharti hiyo haipo.

Tuanavyo sisi ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Akiwajia fasiki na habari yoyote, ichunguzeni,” inafahamisha tu wajibu wa kuichunguza na kuithibitisha habari ya fasiki wala haifahimishi wajibu huo kwa habri ya mwenye kuaminika. Sisi tuko na wale wasemao kuwa kuitegemea habari ya mwenye kuaminika bila ya uchunguzi ni njia wanayoitumia wenye akili wa kale na wa sasa.

Hata hivyo kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda,” inafahamisha kuwa habari yoyote ambayo hatuna wasiwasi nayo kuingia katika matatizo na haramu, basi inafaa kuitumia bila ya kumwangalia mtoaji habari.

Kimsingi ni kuwa tusiamini habari ila ikiwa inatoka kwa mwenye kuaminika au tuithibitishe na kuichunguza ikiwa inatoka kwa fasiki.

وَاعْلَمُوا أَنَّ فِيكُمْ رَسُولَ اللَّـهِ لَوْ يُطِيعُكُمْ فِي كَثِيرٍ مِّنَ الْأَمْرِ لَعَنِتُّمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ حَبَّبَ إِلَيْكُمُ الْإِيمَانَ وَزَيَّنَهُ فِي قُلُوبِكُمْ وَكَرَّهَ إِلَيْكُمُ الْكُفْرَ وَالْفُسُوقَ وَالْعِصْيَانَ أُولَـٰئِكَ هُمُ الرَّاشِدُونَ ﴿٧﴾

7. Na jueni kuwa yuko kati yenu Mtume wa Mwenyezi Mungu. Lau angeliwatii katika mambo mengi, bila ya shaka mngelitaabika. Lakini Mwenyezi Mungu amewapendezea Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na akauchukiza kwenu ukafiri, na upotovu, na uasi. Hao ndio walioongoka.

فَضْلًا مِّنَ اللَّـهِ وَنِعْمَةً وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ ﴿٨﴾

8. Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.

MWENYEZI MUNGU AMEWAPENDEKEZEA IMANI

Aya 7 – 8

MAANA

Na jueni kuwa yuko kati yenu Mtume wa Mwenyezi Mungu na mtukufu wa wa mwanzo na wa mwisho. Basi ni juu yenu kumwadhimisha wala msimpe habari isipokuwa ya ukweli.

Lau angeliwatii katika mambo mengi, bila ya shaka mngelitaabika.

Hii ni amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ikielekezwa kwa wau- mini kuwa wamsikilize Mtume na wamtii, wala wasimshauri lile analolijua kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ambalo wao hawalijui. Lau angeliwaitikia kwenye mambo mengi wanayomwambia wangelitaabika na kuingia kwenye tabu na dhambi.

Lakini Mwenyezi Mungu amewapendezea Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na akauchukiza kwenu ukafiri, na upotovu, na uasi. Hao ndio walioongoka.

Mwenyezi Mungu amewaamrisha waja wake wamwamini Yeye na wamtii, akawabainishia uzuri wa imani na utiifu, akatumia kila njia kuwahimiza hilo na akamwahidi malipo na thawabu kubwa mwenye kuamini na akatenda mema. Vile vile amewakataza ukafiri na uasi, akabainisha hasara zake na akamtishia kwa adhabu mwenye kukufuru na kuasi na akazisifia adhabu hizo kwa namna ambayo haiwezi kufikirika akilini ila baada ya kubainishwa. Ni mtu gani anayeweza kufikiria adhabu ambayo si mauti wala uhai.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewatuma Mitume wake kwa watu ili wafikishe amri, makatazo ahadi na kiaga chake. Kuna wale wanaoitikia kihaki na kiukweli, wengine wakapinga na kufanya inadi na kuna wale waliotikia kuhofia masilahi yao na tamaa ya ngawira.

Wale waliomwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume kihaki na kiukweli ndio aliowakusudia katika kauli yake: “Amewapendezea Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu.” Yaani ameipendekeza na kuipamba kutokana na kueleza uzuri wa imani na kivutio cha thawabu nyingi. Akauchukiza ukafiri kwa kueleza mabaya yake na tishio la adhabu chungu.

Unaweza kuuliza : Mwenyezi Mungu (s.w.t) amelibainisha hilo kwa waumini na makafiri, kwanini amehusisha kuwataja waumini, kinyume na wengineo?

Jibu : Ndio, lakini sio kila mwenye kusikia ubainifu wa Mwenyezi Mungu anauamini na kunufaika nao, wala sio kila mwenye kunasihiwa na Mwenyezi Mungu anakubali nasaha zake. Bali wema wamekubali na waovu wakakataa. Ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamtaja na kumsifu mwenye kusikia maneno akafuata mazuri yake na akampuuza mwenye kupinga na akaachana nayo.

Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kuchagua uongofu badala ya upotevu ana fadhila na malipo, lakini fadhila kubwa ni ya yule aliyemwandalia njia ya uongofu, akamwongoza na akampa uweza wa kuifuata. Walisema wakale: “Kama si sababu asingelifaulu msababishaji”

وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ ﴿٩﴾

9. Na ikiwa makundi mawili katika waumini yanapigana, basi yapatanisheni. Na likiwa moja la hayo linadhulumu jingine, basi lipigeni linalodhulumu mpaka lirejee kwenye amri ya Mwenyezi Mungu. Na likirejea basi yapatanisheni kwa uadilifu. Na hukumuni kwa haki. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanaohukumu kwa haki.

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٠﴾

10. Hakika Waumini tu ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mrehemiwe.

NA IKIWA MAKUNDI MAWILI KATIKA WAUMINI YANAPIGANA

Aya 9 – 10

MAANA

Na ikiwa makundi mawili katika waumini yanapigana, basi yapatanisheni.

Uaislamu una mafunzo na miongozo ya kujenga jamii na kuitengeneza; miongoni mwayo ni wajibu wa kumlinda binadamu damu yake, mali yake, hadhi yake na uhuru wake wa kusema na kutenda. Hakuna yeyote mwenye utawala wa hayo isipokuwa haki. Akitoka kwenye haki na akaingilia haki ya wengine, basi hapo atakuwa amejiondolea kinga ya hayo yeye mwenyewe. Mwenyezi Mungu anasema:

وَلَقَدْ كَرَّمْنَا بَنِي آدَمَ ﴿٧٠﴾

“Na hakika tumewatukuza wanadamau.” Juz. 15 (17:70).

Amesema tena kumwambia Mtume wake:

لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ ﴿٢٢﴾

“Wewe si mwenye kuwatawalia” (88:22).

Akasema tena:

إِنَّمَا السَّبِيلُ عَلَى الَّذِينَ يَظْلِمُونَ النَّاسَ وَيَبْغُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ ﴿٤٢﴾

“Bali njia ya lawama ipo kwa wale wanaowadhulumu watu, na wanafanya jeuri katika ardhi bila ya haki.” Juz. 25 (42:42).

Mafunzo mengine ya Uaislamu ni kuhurumiana na kusaidiana katika yale yaliyo na heri na masilahi kwa wote. Ikiwa itatokea uhasama baina ya makundi mawili ya waumini, basi wajibu wa waumini ni kusuluhisha kwenye misingi ya haki na uadilifu na kuchunga umoja usivunjike.

Kuna Hadith tukufu inayosema: “Je, niwaambie jambo lililo na daraja kubwa zaidi kuliko kufunga, kuswali na kutoa sadaka? Wakasema: Naam! Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: Ni kuwaunganisha waliotengana”

Na likiwa moja la hayo linadhulumu jingine, basi lipigeni linalodhulumu mpaka lirejee kwenye amri ya Mwenyezi Mungu.

Ikiwa kundi moja litakataa kurudi kwenye haki na likang’ang’ania uchokozi, basi ni juu ya waumini wengine kulihami na dhulma lile kundi linaloonewa, kwa hekima na mawaidha mazuri. Ikiwa lile kundi ovu halitakoma ila kwa vita, basi lipigeni katika mipaka ya sharia inayohakikisha amani ya wote.

Na likirejea basi yapatanisheni kwa uadilifu. Na hukumuni kwa haki. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanaohukumu kwa haki.

Likitubia lile kundi linaloonea na likaacha kabisa, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira mwenye kurehemu, na hakuna atakayeruhusiwa kulifanyia lolote. Lililobaki ni wajibu wa waumini, kwa juhudi zao waondoe, yaliyotokea kwenye nafsi za pande mbili.

Al-Jassas Al-Hanafi, anasema katika Kitabu Ahkamul-Qur’an akiwa anazungumzia Aya hii: “Ali Bin Abi Twalib alipigana na kundi ovu kwa upanga akiwa pamoja na maswahaba wakubwa wa Badr (Ahlu Badr) waliojulikana. Na alikuwa ni mwenye haki. Hakuna aliyehalifu katika kundi kabisa isipokuwa kundi ovu na wafuaisi wake aliokuwa akipigana nao.”

Na akasema Abu Bakr Al-Malik, Maaruf kwa jina la Ibn –Al-Arabi Al- Muafiri, katika Ahkamul - Qur’an: “Imethibiti kwa maulama wa Kiislamu na imethibiti kwa dalili ya dini kwamba Ali Bin Abu Twalib alikuwa Imam na kwamba kila mwenye kupigana naye ni muovu na kupambana na mtu huyo ni wajibu mpaka arudi kwenye haki.”

UDUGU WA KIDINI NA UDUGU WA KIBINADAMU

Hakika Waumini tu ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mrehemewe.

Hii ni kusisitiza kuleta suluhu baina ya pande mbili zilzigombana, pamoja na kuashiria kuwa upatanishi huu ni lazima kwa mfungamano wa udugu. Kuna Hadith isemayo: mwislamu ni ndugu wa mwislamu, hamdhulumu, hamtelekezi wala hamtii aibu.

Unaweza kuuliza: Kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t) amesema: Hakika waumini tu ni ndugu, na asiseme: Hakika watu wote tu ni ndugu. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) naye akasema:

“Mwislamu ni ndugu wa mwislamu.” Na asiseme: Mtu ni ndugu wa mtu? Tunajua kuwa Mola ni mmoja, asili ni moja, umbile ni moja na usawa baina ya watu ni wajibu. Kwa hiyo upendo unatakikana uwe ni wa jumla sio mahsusi; sawa na rehe- ma ambayo imekienea kila kitu?

Basi mgawanyo huu utakuwa na tofauti gani na ule unaowagawanya binadamu kwa misingi ya kiuchumi; walivyofanya wamarksi, au kuwagawanya kwa misingi ya kijinsia; kama walivyofanya wanazi au kwa misingi ya vita na silaha kama ilivyo siasa ya kimarekani?

Kisha nini kilichosababisha matatizo na maangamizi haya yanayomkabili binadamu leo, hadi kufikia kumalizana, baada ya binadmu kuweza kumiliki nguvu mbaya ya silaha za maangamizi? Je, hii imesabishwa na binadamu kama binadamu au imesabishwa na aina kwa aina za migawanyo?

Hatimaye sasa binadamu wasaidiane kwa misingi ya dini au asasi za kibanadamu?

Jibu : Maswali yote haya ni haki, na jibu lake ni moja tu litakoloweza kutosheleza maswali yote haya; nalo ni: Kusaidiana ni wajibu baina ya binadamu wote bila ya kubagua. Huu ndio mwito wa uaislamu hasa, unaofahamishwa na makumi ya Aya na riwaya. Tutatosheka kutaja Aya moja na riwaya moja.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema katika Aya ya 13 ya sura hii: “Enyi watu! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumewafanya mataifa na makabila ili mjuane. Hakika mtukufu zaidi yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi yenu.

Kwa hiyo mwito wake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Enyi watu!’ pamoja na kusema kwake: ‘Kutokana na mwanmmke na mwanamume’ na ‘aliye na takua zaidi’ ni dalili mkataa na wazi kuwa mwito wa Qur’an ni wa kiutu na wa mataifa, unamzingatia mtu ni ndugu wa mtu kwa namna yoyote itakvyokuwa itikadi yake, utaifa wake na jinsia yake.

Mfano wa Aya hii na ufafanuzi wake ni kauli yake Mtume mtukufu(s.a.w. w ) : “Watu wote wako sawa kama chane za shanuo. Jueni kuwa hakuna ubora wa mwarabu kwa mwajemi wala wa mwajemi kwa mwarabu, wala wa mwekundu kwa mweusi wala wa mweusi kwa mwekundu isipokuwa kwa takua … nyote mnatokana na Adamu na Adam ametokana na mchanga.”

Zaidi ya hayo katika Juz.21 (30:30) kuna Aya inayosema kuwa uislamu ni dini ya maumbile na katika Juz. 9 (8:24) kuna Aya inayofahamisha kuwa dini ya Mwenyezi Mungu ni dini ya maisha.

Kwa hali hiyo basi inatubainikia kuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna za Mtume wake zinazingatia kuamini utu ni sehemu inayokamilisha kumwamini Mwenyezi Mungu, mitume wake na Vitabu vyake.

Kwa hiyo Makusudio ya mumin katika Aya na mwislamu katika Hadith ni yule anayeamwamini Mwenyezi Mungu na mtu kwa kuwa ni mtu.

Kwa maneno mengine ni kuwa hakuna mzozo wala kupingana baina ya udugu wa kibinadamu na udugu wa kiislamu; huu wa kiislamu unauongeza nguvu ule wa kibinadamu.

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿١١﴾

11. Enyi ambao mmeamini! Kaumu isidharau kaumu nyingine, huenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake kwa wanawake wengine, huenda wakawa bora kuliko wao. Wala msitiane kasoro, wala msiitane majina ya kejeli. Na wasiotubu, hao ndio madhalimu.

KAUMU ISIDHARAU KAUMU NYINGINE

Aya 11

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Kaumu isidharau kaumu nyingine, huenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake kwa wanawake wengine, huenda wakawa bora kuliko wao.

Imesemekana kuwa neno Qawm, tulililofasiri kwa maana ya kaumu, kwa maana yake ya kiarabu huwa halitajwi ila kwa wanaume tu, kwa dalili ya kuunganishwa wanawake baada ya neno hilo.

Katika Juz. 19 (25:55-62) tulisema kuwa dhalimu kesho atachukuliwa na Mwenyezi Mungu kuwa ni kafiri ingawaje duniani anachukuliwa kuwa ni mwislamu kama akitamka shahada mbili.

Na mwenye kuwadharau wema atakuwa ni dhalimu na safihi.

Hili Mwenyezi Mungu amelikemea kwa ukali sana; kama aliposema:

فَيَسْخَرُونَ مِنْهُمْ سَخِرَ اللَّـهُ مِنْهُمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٩﴾

“…Wakawafanyia maskhara; Mwenyezi Mungu atawafanyia maskhara na wana wao adhabu iumizayo. “ Juz. 10 (9:79).

Pia kauli yake:

إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ ﴿٢٩﴾ وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ ﴿٣٠﴾ وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ ﴿٣١﴾ وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَـٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ ﴿٣٢﴾ وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ ﴿٣٣﴾ فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ﴿٣٤﴾

“Hakika wale walio na hatia walikuwa wakiwacheka wale ambao wameamini. Wakiwapitia wanakonyezana na wakirudi kwa watu wao walirudi wakishangilia. Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea. Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao. Basi leo wale ambao wameamini wanawacheka makafiri” (83: 29-34).

Vile vile amesema:

وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ ﴿١﴾

“Ole wake kila mtia kasoro mwenye kusengenya.” (104:1).

VIPI UTAPATA MARAFIKI?

Nimekumbuka, wakati nikifasiri Aya hii, kwamba kiasi cha mika 16 au zaidi iliyopita nilisoma tarjuma ya kitabu: How to win friends and influence people (vipi utapata marafiki na kuathiri nafsi) cha Dayl Karengi.

Vile vile nimekumbuka hekima ya hali ya juu ya Imam Zainul’abidin, inayohusiana na maudhui hii ambayo ina athari zaidi ya kitabu nilichokitaja pamoja na kuwa kimeenea sana na kufasiriwa kwenye lugha nyingi.

Imam, kwenye hekima yake, alikuwa akikusudia kauli yake Mwenyezi Mungu: “Kaumu isidharau kaumu nyingine, huenda wakawa bora kuliko wao.” Hekima yenyewe ni hii:

“Jihadhari na kuzungumza ambayo moyo unayakanya hata kama una udhuru. Kwani sio kila utakayemwambia shari unaweza kumfafanulia udhuru. Aliye mkubwa kuliko wewe muweke daraja ya mzazi, mdogo daraja ya mtoto, na aliye marika daraja ya kaka. Ni nani katika hawa unapenda kumvunjia heshima yake?

“Ikiwa shetani atakuingilia kujiona kuwa u mbora zaidi ya mwingine, angalia haya yafutayo: Ikiwa ni mkubwa zaidi yako, sema: amenitangulia kwa imani na matendo mema, kwa hiyo ni bora kuliko mimi. Ikiwa ni mdogo kuliko wewe, sema: nimemtangulia kwa maasi, kwa hiyo yeye ni bora kuliko mimi. Akiwa ni marika yako sema: mimi nina uhakika nimefanya dhambi, lakini nina shaka kuwa yeye amefanya dhambi, basi kwanini niache uhakika nichukue shaka?

“Ukiwaona watu wanakutukuza, sema: wamechukulia wema, na ikiwa wanakutenga, sema: kuna makosa nimefanya.”

Imam anaendelea kusema:“Ukiyafanya haya maisha yako yatakuwa mepesi, utakuwa na marafiki wengi na utakuwa na maadui kidogo, na utafurahi kwa wema wao wala hutasikitika kukutenga.”

Vyovyote watavyosema maulama na wenye hekima kuhisiana na maudhui haya, hawatazidisha kitu kwenye hekima hii fasaha ya hali juu.

Hilo si ajabu kwa vile aliyeisema ni mtoto wa wahyi, hazina ya ilimu ya wahyi na aliyekulia kwenye malezi yake.

Wala msitiane kasoro.

Msitiane ila wala msiwambie wengine lile ambalo hampendi kuambiwa.

Wala msiitane majina ya kejeli.

Mtu asimwite mwenzake kwa jina analolichukia. Mafaqihi wamesema kuwa ikiwa jina halikukusudiwa kasoro wala dharau na ni mashuhuri wa hilo, basi halina ubaya; kama vile Hassan Madafu, n.k.

Ni uovu kutumia jina baya baada ya imani.

Hapa kuna tafsiri mbili: Ya kwanza ni msimwite mumin ewe kafiri! Ya pili, ni uovu huko kumwita mwingine kwa jina asilolipenda. Tafsiri hii ina ngvuvu, kwa wafasiri wengi kuliko ile ya kwanza.

Na wasiotubu, hao ndio madhalimu.

Mwenye kutubia ni kama asiye na dhambi na mwenye kung’ang’ania dhambi atakuwa ameidhulumu nafsi yake. Kwa sababu Mwenyezi Mungu atawaadhibu wenye dhambi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ وَاتَّقُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ ﴿١٢﴾

12. Enyi ambao mmeamini! Jiepusheni na dhana nyingi. Hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Wala msipeleleze, wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je, anapenda mmoja wenu kuila nyama ya nduguye aliyekufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.

DHANA, UJASUSI NA KUSENGENYA

Aya 12

MAANA

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekataza dharau, kutia ila, kubeza na kuitana majina ya kuchukiza. Na akamkemea mwenye kufanya moja katika hayo. Katika Aya hii anakataza dhana mbaya, ujasusi na kusengenya. Ufafanuzi ndio huu ufuatao:-

DHANA

Enyi ambao mmeamini! Jiepusheni na dhana nyingi. Hakika baadhi ya dhana ni dhambi.

Sehemu hii ya Aya inawezekana kufanyiwa muhtasari kwa jumla moja tu: “Kila mtu hana hatia mpaka lithibitike kosa lake.”

Inawezekana jumla hii kuifafanua kwa urefu, tuweke mpaka wa linalopelekea asili ya dhana, kuwa je, inafaa kuichulia dhana au kuna wajibu wa kujieupusha wakati wote au wakati wa kuweko udhuru na wa kutokuweko ilimu? Na je, kuna udhuru wa kutojua au hakuna?

Ikiwa inafaa kuichukulia dhana, je, tuichukulie dhana vyovyote ilivyo sababu yake na mfungamano wake? Na ikiwa haifai kuichukulia dhana kwa namna yote ile, je ni nyenzo gani za ilimu kwenye hukumu ya sharia na mengineyo katika ilimu ya usul (misingi ya sharia) ambayo tumeimalizia miaka si kidogo kuisoma?

Ni vizuri tuchuke tafsiri ya wastani si kurefusha wala kufupiliza. Kabla ya lolote ni lazima tufanye maandalizi ya kujua toafauti baina ya shaka, dhana na ilimu. Shaka ni kuwa sawa uthibitisho na ukanusho. Dhana ni kuwa na nguvu upande mmoja baina ya hizo mbili, lakini bado kunakuwa na uwezekano kwa upande ule usio na nguvu. Ilimu ni kubainika upande mmoja unaofunga kabisa njia ya upande mwingine.

Unaweza kumdhania mtu heri au shari, ukawa umepatia au umekosea katika dhana yako. Hakuna ubaya kabisa ikiwa utamdhania mwenzako heri, iwe umepatia au umekosea; au iwe litajitokeza hilo kwenye kauli yako na vitendo vyako au lisijitokeze.

Mtume mtukufu(s.a.w. w ) anasema:“Wadhanieni waumini heri.” Imam Ali(a . s) anasema:“Liweke jambo la nduguyo kwenye heri.” Tazama Juz. 1 (2:83) kifungu cha ‘Kuchukia usahihi.’

Kwa hiyo basi inatubainikia maana ya kuwa kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t) amesema:“Jiepusheni na dhana nyingi,” na wala asisema ‘jiepusheni na kila dhana.’

Neno wingi huwa pia linatumiwa kwa maana ya baadhi; na haya ndiyo Makusudio yake kwenye Aya hii; yaani jiepusheni na dhana mbaya.

Dhana mbaya yenyewe sio haramu ikiwa haitajitokeza kwenye kauli au kitendo, wala mwenye dhana hiyo hana majukumu yoyote. Lakini ni lazima asiitolee maamuzi yoyote na aifanye kama haiko. Akiitolea uamuzi na ikajitokeza athari yake kwenye kauli au kitendo, basi atawajibika na atastahili lawama na adhabu.

Hii ndio dhana aliyoikusudia Mwenyezi Mungu aliposema: “Hakika baadhi ya dhana ni dhambi.”

Mtume mtukufu(s.a.w.w) anasema:“Mambo matatu hasalimiki nayo yeyote: Kisirani, hasadi na dhana: Ukiona kisirani endelea, ukiona husda usiitake, na ukidhania hakikisha. Kwa hiyo basi maana ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Jiepusheni na dhana nyingi’ nikuwa msizitolee maamuzi wala msizitumie; sawa na kauli yake “Asiwafitini shetani.”

UJASUSI

Wala msipeleleze.

Kupeleleza ni kuchunguza siri na makosa kwa njia ya kujificha. Ni haramu kwa Kitabu, Sunna, Ijmai (kongamano la maulama) na kiakili. Na kauli yake:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتًا غَيْرَ بُيُوتِكُمْ حَتَّىٰ تَسْتَأْنِسُوا ﴿٢٧﴾ فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فِيهَا أَحَدًا فَلَا تَدْخُلُوهَا حَتَّىٰ يُؤْذَنَ لَكُمْ... ﴿٢٨﴾

“Enyi ambao mmeamini! Msiingie nyumba zisizo nyumba zenu mpaka muombe ruhusa… na msipomkuta yeyote humo msiingie mpaka mpewe ruhusa.” Juz. 18 (24:27-28).

Katika Sunna ni Hadith ya Mtume mtukufu(s.a.w. w ) :“Mwenye kukuchungulia ukamtupia kijiwe na ukamtoboa macho yake, basi huna lawama.” Mafaqihi wamekubaliana kwa pamoja kuitumia Hadith hii. Ama akili inauona ujajusi ni vita dhidi ya maisha ya watu na kuingilia uhuru wao na mambo yao yanayowahusu katika mila na desturi.

Nimekumbuka, wakati nikiandika maneno haya, makala ndefu kuhusu maudhui haya, iliyotolewa na gazeti Al-Ahram la 27-6-1969, nililisoma wakati huo, kisha nikalihifadhi katika mafaili ya magazeti. Nililihifadhi na kuliweka akiba ya kulitumia nikilihitajia. Basi nikalisoma tena, mara nikaona mambo ambayo hata kuyawaza tu ni muhali; baadhi yake ni haya yafuatayo:

“Wamarekani hivi sasa wanajua kuwa sio kuwa kuta zao zina masikio tu, bali zina macho na mboni vile vile, kama lilivyosema gazeti la Times. USA wametengeneza kifaa kidogo cha ukubwa wa milimita, kinachoweza kusajili mazungumzo; na mtu anaweza kukiweka kwenye jaketi kama kifungo. Kila mtu anaweza kukitumia na kinagharimu kati ya dola 10 na 15.

Huko New York, wafanyabiashara wameweka matangazo ya biashara kwenye magazeti kuuza vifaa vya kurikodi mazungumzo ya watu majumbani mwao na wanaviuza madukani kama michezo ya watoto. Bei yake haizidi dola 18.

Mtu akiweka kifaa hiki kwenye gari kikielekezwa kwenye jengo basi kitarikodi kila neno linalosemwa kwenye jengo lile. Bali kuna kifaa cha kusikilizia maneno kisichozidi ukubwa wa punje ya choroko, kinachoweza kuwekwa kwenye kalamu nk, kinatumia betrii ya masaa 18 hadi 50.

Pia wametengeneza kifaa kidogo cha kutuma, kinachoweza kutangaza yanayopita kwenye majumba kwa umbali wa futi 50 na bei yake ni dola 400.

Ajabu ya yote ni kamera zinazopenya ukutani na kupiga picha mambo yote anayoyafanya mtu chooni na hata kwenye giza. Vile vile inawezekana kuchora chale (tattoo) katika mwili wa mtoto wakati anapozaliwa ambayo itafuatilia harakati zake katika maisha yake yote.

Kuna shirika katika Marekani yote linalokusanya habari na harakati binafsi za watu mashuhuri wa siasa, elimu, uandishi uchumi na wengineo na kurikodi maneno yao, na kupiga picha ya vitendo vyao, hata wanapofanya tendo la ndoa na wake zao na wengineo. Mtu anaweza kupata habari hizi kwa dola moja tu. Shirika hili linaitwa Benki ya habari.

Yote hayo yanatokea ikiwa serikali inajua kila kitu, bila ya kufanya lolote, kwa sababu imekuwa ni jambo la kawaida kama vile kuuza magazeti tu.” Mwisho wa nukuu ya gazeti.

Haya ni machache katika mengi. Watunzi wameandika vitabu maalum kuhusiana na maudhui haya. Lau wamarekani wangeliyafanya haya kwao tu wenyewe kwa wenyewe, tungeliwaambia wao na wanowatawala: “shauri yenu, kila mji una uhuru wa kujichagulia unavyotaka.” Lakini wamarekani wamevuka mipaka, wanafanya ujasusi kwenye nchi nyingine kwa ndege na satalaiti.

Usishangae msomaji. Marekani ni nchi ya maendeleo, demokarasia, bwana mkubwa wa uhuru, na polisi wa ulimwengu.

Tena zaidi ya hayo wanaamini Mwenyezi Mungu… Dalili kubwa kuwa wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho ni mauaji ya kinyama waliyoyafanya kwenye kijiji kimoja katika Vietnam ya kusini[6] , na kuwasheheneza silaha za kisasa mayahudi ili kuwamaliza wananchi wa Palestina, kuwaua watoto kwa ujumla na kutupa mabomu kwa kutumi ndege za Phantoum kwa watoto wa shule wa Misr! Kweli kabisa USA ni dola kubwa kwenye uwanja huu wa mauaji!

KUSENGENYA

Wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je, anapenda mmoja wenu kuila nyama ya nduguye aliye kufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.

Kusengenya ni kumtaja mtu kwa jambo asilolipenda. Mtume mtukufu(s.a.w. w ) anasema:“Kusengenya ni kumtaja ndugu yako kwa jambo analolichukia. Ikiwa jambo hilo analo huko ni kusengenya na ikiwa hana itakuwa ni kumsingizia.” Na kusingizia ni kukubwa zaidi kuliko kusengenya na kumeharamishwa kwa Kitabu Sunna na Ijmai (kongamano la maulama).

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemfananisha mwenye kusengenywa na maiti kwa vile anakuwa hayupo na akaifananisha hishima yake na nyama yake na kumtaja kwa uovu kuwa ndio kula.

Maana ya mnalichukia hilo ni kuwa ikiwa mnaona kinyaa kula nyama ya maiti basi pia muone kinyaa kumsengenya asiyekuwepo, kwa sababu yote mawili hayo yako sawa.

Hakuna jambo linalofahamisha kupungukiwa na udhalili kuliko kusengnya. Imam Ali(a . s) anasema:“Kusengenya ni juhudi ya asiyejiweza.” Na Mwenyezi Mungu hasamehi kusengenya mpaka asamehe aliyesengenywa. Mafaqihi wameuvua uharamu wa kusengenya kwa wafuatao:-

Mpagani, hakimu dhalimu, mwenye kuudhihirisha ufuska wake, kwa sababu mwenye kulitupa joho la haya hana cha kuficha, kumpa ushauri mwenye kutaka ushauri katika kushirikiana na mtu au kumwakilisha kwenye jambo muhimu, kumtengua shahidi kwa kadhi, na mwenye kudhulumiwa kwa yule aliyemdhulumu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

لَّا يُحِبُّ اللَّـهُ الْجَهْرَ بِالسُّوءِ مِنَ الْقَوْلِ إِلَّا مَن ظُلِمَ وَكَانَ اللَّـهُ سَمِيعًا عَلِيمًا ﴿١٤٨﴾

“Hapendi Mwenyezi Mungu maneno ya kutangaza uovu ila kwa aliyedhulumiwa.”

Juz. 6 (4:148).

Katika Kitabu Al-Makasib cha Sheikh Ansari, imesemwa kuwa sehemu zinazoondolewa uharamu wa kusengenya hazina idadi. Kwa sababu kusengenya kunakuwa haramu ikiwa kutangaza huko hakuna masilahi yenye nguvu. Vinginevyo, basi itakuwa wajibu kutangaza na kueneza kwa kuangalia masilahi yenye nguvu zaidi, kama ilivyo katika kila maasi ya haki za Mwenyezi Mungu na haki za binadamu.Tazama mwanzo wa Juz. 6.

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿١٣﴾

13. Enyi watu! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumewafanya mataifa na makabila ili mjuane. Hakika mtukufu zaidi yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi yenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye habari.

قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَـٰكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي قُلُوبِكُمْ وَإِن تُطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَا يَلِتْكُم مِّنْ أَعْمَالِكُمْ شَيْئًا إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٤﴾

14. Mabedui walisema: Tumeamini. Sema: Hamjaamini, lakini semeni: Tumesilimu. Kwani imani haijaingia katika nyoyo zenu. Na mkimtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hatawapunguzia chochote katika vitendo vyenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ لَمْ يَرْتَابُوا وَجَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ ﴿١٥﴾

15. Hakika Waumini ni wale tu waliomwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake tena wasiwe na shaka, na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao. Hao ndio wakweli.

قُلْ أَتُعَلِّمُونَ اللَّـهَ بِدِينِكُمْ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿١٦﴾

16. Sema: Je, mnamjulisha Mwenyezi Mungu Dini yenu, na hali Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi, na Mwenyezi Mungu anajua kila kitu?

يَمُنُّونَ عَلَيْكَ أَنْ أَسْلَمُوا قُل لَّا تَمُنُّوا عَلَيَّ إِسْلَامَكُم بَلِ اللَّـهُ يَمُنُّ عَلَيْكُمْ أَنْ هَدَاكُمْ لِلْإِيمَانِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿١٧﴾

17. Wanakusimbulia kuwa wamesilimu! Sema: Msinisimbulie kwa kusilimu kwenu. Bali Mwenyezi Mungu ndiye anayewasimbulia kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.

إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ غَيْبَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿١٨﴾

18. Hakika Mwenyezi Mungu anajua siri za mbingu na ardhi. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

MTUKUFU ZAIDI YENU NI MWENYE TAKUA ZAIDI

Aya 13 – 18

MAANA

Enyi watu! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumewafanya mataifa na makabila ili mjuane. Hakika mtukufu zaidi yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi yenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye habari.

Watu wanajua kuwa baba yao ni Adam na mama yao ni Hawa, lakini lengo la kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Tuewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke, ni kuwa watu wote wajue kwamba wao ni ndugu ni udugu wa usawa katika haki na wajibu.

Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu; “Ili mjuane,” ni kuwa Makusudio ya kutofautiana kwenu katika miji, nasaba na rangi, sio kuwa muwe vikundi, mchinjane na mjifaharishe kwa mataifa yenu, baba zenu na jinsi zenu, hapana! Sivyo kabisa.

Lengo ni muhurumiane na msaidiane katika yale yaliyo na heri yenu na masilahi yenu. Na mbora kabisa atakuwa yule anayemuogopa Mwenyezi Mungu zaidi na akawanufaisha waja wake.

Aya hii ni mwito kutoka kwenye Qur’an kuwa watu wawe umma mmoja wa kiutu na ulimwengu mmoja unaokusanywa na uadilifu na upendo. Ulimwengu huu ni tegemeo la wenye fikra safi na ni ndoto ya walio wema.

Tuna uhakika kuwa makubaliano ya haki za binadamu, yatabakia kwenye karatasi na yatakuwa ni nadharia tu, ikiwa hautapatikana umoja wa ubinadamu uliotolewa mwito na Qur’an, zaidi ya mika 1300 liliyopita. Amerika na Israil zilitia saini makubaliano ya haki za binadamu, lakini bado ndio za kwanza kuangamiza watu Vietnam na Palestina.

Leo ninapoandika maneno haya 22 April 1970, kamati ya umoja wa mataifa imehakikisha kuwa Israil imevunja haki za binadamu, ikasema waziwazi kuwa Israil imevunja majumba ya wakazi ikaacha miili ya wanaume, wanawake na watoto kwenye kifusi na ikakataa isizikwe. Pia imevunja sehemu takatifu na mahospitali[7] na kuwaadhibu wenyeji kwa umeme. Watu wazima wanawang’oa viungo, watoto wanawakata mikono na kupasua matumbo yao mbele ya baba zao na mama zao na mengineyo ya kinyama na mauji ya maangamizi.

Mabedui walisema: Tumeamini. Sema: Hamjaamini, lakini semeni: Tumesilimu. Kwani imani haijaingia katika nyoyo zenu. Na mkimtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hatawapunguzia chochote katika vitendo vyenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Makusudio ya uaislamu hapa ni kutamka shahada mbili. Katika Juz. 1 (2:82), tumetaja tofauti baina ya mumin na mwislamu. Hapa tutamnukuu Dkt Twaha Hussein katika kitabu Mir’atul-islama (Kioo cha uaislamu).

Yeye ni mwanafasihi anayefahamika kwa siri za fasihi, ninamnukuu: “Wakati wa Mtume kulikuweko waumini na waislamu. Basi, niipi tofauti baina imani na Uislamu? Imani kwa dhahiri ya Aya hii ni jambo lilio moyoni ambalo mihimili yake ni ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu na kusadikisha, kwa kina ndani ya dhamiri, kila aliloletewa wahyi Mtume.

Natija ya imani hii ni kumwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume katika kila wanalolitolea mwito, bila ya kigugumizi, kugwazagwaza, wala kutaradadi, kwa hali yoyote ile itakavyokuwa; iwe kuna matukio au majanga. Mhimili mwingine wa imani hii ni kumwogopa Mwenyezi Mungu kiundani kabisa likitajwa jina lake na kumtegemea kwa undani zinaposomwa Aya zake.

“Ama Uislamu ni twaa ya dhahiri ya kutekeleza wajibu na kujiepusha na yaliyokatwaza; hata kama haitafikia imani ya kweli. Kuna watu wanaosilimu kuhofia ubaya; kama walivyosilimu makuraishi walioachwa bila ya kutekwa nyara siku ya kutekwa Makka. Wengine walasilimu kwa hofu na tamaa; kama walivyofanya mabedui aliowataja Mwenyezi Mungu katika Aya hii.”

Hakika Waumini ni wale tu waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake tena wasiwe na shaka, na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao. Hao ndio wakweli.

Waumini wa kwelikweli kabisa ni wale wasiokuwa na shaka yoyote kwenye itikadi zao na wanaojitolea kihali na mali, kuihakikisha haki na kuibatilisha batili. Umetangulia mfano wake mara kadhaa; miongoni mwazo ni Juz. 10 (9:88).

Sema: Je, mnamjulisha Mwenyezi Mungu Dini yenu, na hali Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi, na Mwenyezi Mungu anajua kila kitu?

Mabedui walisema tumeamini, ndio Mwenyezi Mungu anawajibu, kuwa hivi mnamjulisha Mwenyezi Mungu imani yenu na hali Yeye anajua siri na yaliyofichika; kila kitu amekizunguka. Tena je imani inakuwa kwa kudai? Inatosha kuwa mtu ni mjinga kuwa hajui uweza wake Mwenyezi Mungu.

Wanakusimbulia kuwa wamesilimu! Sema: Msinisimbulie kwa kusilimu kwenu. Bali Mwenyezi Mungu ndiye anayewasimbulia kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.

Makusudio ya kusimbulia kwake Mwenyezi Mungu ni kuwafanyia hisani, kwa sababu Yeye amekataza masimbulizi, na hawezi kukataza jambo kisha alifanye. Makusudio ya kuongoza kwake kwenye imani ni kutoa mwongozo wa haki na kuipendekeza.

Maana ni kuwa mabedui na walio mfano wao wanaona kuwa wamemfanyia hisani Mola wao na mtume wao kwa dini yao na wanataka walipwe; hali yakuwa Mwenyezi Mungu ndiye aliyewafanyia hisani wao, pale alipowaongoza kwenye haki na kuwahimiza kupitia Mtume wake.

Kwa hiyo wao ndio wamshukuru kwa alivyowafanyia hisani na kuwaneemesha; sio wao wasimbulie na kutaka kulipwa; ikiwa kweli wameamini dini yao na wakafanya ikhlasi kwenye imani yao. Vinginevyo watakuwa wanastahili kutoka kwa Mwenyezi Mungu yale aliyowaandalia waongo na wahaini.

Hakika Mwenyezi Mungu anajua siri za mbingu na ardhi. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua imani ya kweli na ya uwongo na kuzipamabanua amali zilizokusudiwa dunia na zile zilizokusudiwa radhi ya Mwenyezi Mungu. Aina zote za amali pamoja na imani au kufuru ndio kipimo cha uadilifu wa hisabu na malipo.

MWISHO WA SURA YA ARUBAINI NA TISA: SURAT AL- HUJURAT

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

Sura Ya Arubaini Na Tisa: Surat Al- Hujurat. Imeshuka Madina. Ina Aya 18.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kure-hemu

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيِ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَاتَّقُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿١﴾

1. Enyi ambao mmeamini! Msitangulie mbele ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ ﴿٢﴾

2. Enyi mlioamini! Msinyanyue sauti zenu kuliko sauti ya Nabii, wala msiseme naye kwa kelele kama mnavyosemezana nyinyi kwa nyinyi, visije vitendo vyenu vikaanguka, na hali hamtambui.

إِنَّ الَّذِينَ يَغُضُّونَ أَصْوَاتَهُمْ عِندَ رَسُولِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ امْتَحَنَ اللَّـهُ قُلُوبَهُمْ لِلتَّقْوَىٰ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ عَظِيمٌ ﴿٣﴾

3. Kwa hakika ambao wanateremsha sauti zao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amezitia mtihani nyoyo zao kwa takua. Hao watakuwa na maghufira na ujira mkubwa.

إِنَّ الَّذِينَ يُنَادُونَكَ مِن وَرَاءِ الْحُجُرَاتِ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ ﴿٤﴾

4. Hakika ambao wanakuita nyuma ya vyumba, wengi wao hawana akili.

وَلَوْ أَنَّهُمْ صَبَرُوا حَتَّىٰ تَخْرُجَ إِلَيْهِمْ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٥﴾

5. Na lau wao wangelingojea mpaka uwatokee ingelikuwa kheri kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

MSINYANYUE SAUTI ZENU KULIKO SAUTI YA NABII

Aya 1 – 5

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawakumbusha waumini mambo haya yafutayo:-

1.Enyi ambao mmeamini! Msitangulie mbele ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Msifanye haraka kusema au kufanya tendo lolote linaoamabatana na dini na masilahi ya uma, mpaka alipitishe Mwenyezi Mungu kupitia Mtume wake mtukufu.

Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

Katika Nahjul-balagha imeandikwa: “Mche Mwenyezi Mungu kwa baad- hi ya takua hata kama ni kidogo. Na weka sitara baina yako na Mwenyezi Mungu hata kama ni nyembamba.”

Kwa uchache kabisa wa mtu kumcha Muumba wake ni kujizuia kusema: Lau Mwenyezi Mungu angelihalalisha hili ambalo ameliharamisha au angeliharamisha lile alilolilihalalisha. Au kusema afadhali Nabii angeli- fanya hivi au asingelifanya vile alivyofanya na mengineyo ya ujeuri na ujinga.

2.Enyi mlioamini! Msinyanyue sauti zenu kuliko sauti ya Nabii.

Si jambo zuri kuinua sauti bila ya dharura. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema: “Na uinamishe sauti yako. Hakika sauti mbaya zaidi ni ya punda.” Juz. 21 (31:19). Sikwambii tena ikiwa ni kuinua sauti mbele ya wakubwa na kwenye vikao vyao. Na Mtume mtukufu(s.a.w. w ) ni bwana wa manabii na mtukufu wa viumbe wote.

3.Wala msiseme naye kwa kelele kama mnavyosemezana nyinyi kwa nyinyi, visije vitendo vyenu vikaanguka, na hali hamtambui.

Mnapozungumza na Nabii msizungumze kama mnavyozungumza nyinyi. Mwenye kufanya hivyo atakuwa amebatilisha imani yake bila ya kutaka wala kujua. Na mwenye kubatilika imani yake ndio vimebatilika vitendo vyake na atakuwa mikononi mwa waliopata hasara.

Kwa hakika ambao wanateremsha sauti zao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amezitia mtihani nyoyo zao kwa takua – yaani amezisafisha nyoyo zao kwa matendo mema -Hao watakuwa na maghufira na ujira mkubwa.

Mwenyezi Mungu huwajaribu waja wake kwa aina mbalimbali ya mitihani, ili apate mawaidha mwenye kuwaidhika na ajikanye mwenye kukanyika. Mwenye kuwaidhika na akawa na subira Mwenyezi Mungu humtakasa, humuongoza njia ya usawa na humneemesha kwa maghufira na ujira wa wenye kuwa na subira.

Aya inaashiria kwamba kuzungumza kwa adabu na kwa inavyotakikana ni katika imani. Imam Ali(a . s) anasema:“Imani ya mja hainyooki mpaka unyooke moyo wake na moyo haunyooki mpaka unyooke ulimi wake.

Hakika ambao wanakuita nyuma ya vyumba, wengi wao hawana akili.

Mtume(s.a.w. w ) alikuwa na wake tisa, kila mmoja alikuwa na chumba chake kilichojengwa kwa makuti ya mtende, mlangoni kukiwa na pazia ya manyoya.

Wafasiri wanasema kuwa mabedui walikuja Madina na wakasimama nyuma ya vyumba vya Mtume wakaanza kuita kwa sauti: Ewe Muhammad(s.a.w. w ) tutokee! Mtume akangoja kidogo; kisha akawatokea. Mwenyezi Mungu amewataja kuwa wengi wao hawakujua walichokuwa wakikifanya, kutokana na ubedui na ushamba.

Na lau wao wangelingojea mpaka uwatokee ingelikuwa kheri kwao, kwa sababu kungoja na kutofanya haraka kuna malipo na thawabu, kumwdhimisha Mtume wa Mwenyezi Mungu na kuchunga adabu.

Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu. Rehema yake inaenea kwa washamba, walalahoi n.k.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَإٍ فَتَبَيَّنُوا أَن تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَىٰ مَا فَعَلْتُمْ نَادِمِينَ ﴿٦﴾

6. Enyi mlioamini! Akiwajia fasiki na habari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda.

AKIWAJIA FASIKI NA HABARI YOYOTE, ICHUNGUZENI

Aya 6

MAANA

Enyi mlioamini! Akiwajia fasiki na habari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda.

Imekuwa mashuhuri kwa wafasiri kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alimtuma Walid bin Uqba bin Abu Muit kwa Bani Mustaliq kuchukua Zaka, wakampokea kwa shangwe ya kumzunguka, lakini akadhania kuwa wanataka kumzuia.

Akarudi kwa Mtume(s.a.w. w ) na kumwambia: wamenizuia na kunifukuza. Basi Mtume(s.a.w. w ) akakasirika na baadhi ya swahaba zake wakamwambia tuwashambulie? Ndio ikashuka Aya hii kuwaondolea tuhuma Bani Mustaliq. Kuna sababu nyingine ya kushuka Aya hii.

Sisi hatutegemei lolote katika sababu za kushuka Aya ila ikithibiti kwa nukuu ya Qur’an au Hadith mutawatir. Zaidi ya hayo ni kuwa kudhania Walid shari hakuwezi kusababisha ufasiki; isipokuwa ni kukosea na kutatizika. Mwenye kukosea haitwi fasiki.

Vyovyote itakavyokuwa sababu za kushuka, lakini Aya haishilii kwenye sababu hiyo, bali inaenda mbali zaidi, kwa vile sababu haiwezi kuhusisha isipokuwa inaenea. Itakuwa sababu inatajwa kwa ajili ya jambo fulani ambalo halihusishi tamko. Kwa hiyo niwajibu kuichukulia dhahiri ya Aya, ambayo inafahamisha uharamu wa kuyachukulia maneno ya fasiki bila ya kuchunguza na kuthibitisha habari yake, kuhofia kuingia kwenye hatari; kama kuwadhuru wengine na kujuta, na majuto ni mjukuu.

Tunapata tafsiri ya Aya hii katika kauli ya Imam Ali(a . s) :“Mwenye kufuata njia iliyo wazi atakunywa maji, na mwenye kuacha atahangaika.”

Kundi la masheikh wa kisunni na kishia wameitumia Aya hii kuwa ni dalili ya wajibu wa kuchukulia kauli ya mwenye kutegemewa bila ya sharti la kuchunguza ukweli wake. Baadhi yao wameitolea dalili kwa maneno ya undani yaliyojifungafunga.

Iko wazi kuwa Aya imechukua msingi wa kiujumla wa kupima habari ambayo haifai kuitegema ila baada ya uthibitisho na hiyo ni habari ya fasiki. Vile vile habari inayotegemwa bila ya uthibitisho ambayo ni habari ya mwenye kutegemewa.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu ameshartiza kuitegemea habari ya fasiki kwa ubainifu na uthibitisho, lakini hakuitaja habari ya mwenye kutegemewa. Lau ingelikuwa ni wajib kuichunguza habari ya mwenye kuaminika basi angeliitaja. Kwa kuwa haikutajwa basi sharti hiyo haipo.

Tuanavyo sisi ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Akiwajia fasiki na habari yoyote, ichunguzeni,” inafahamisha tu wajibu wa kuichunguza na kuithibitisha habari ya fasiki wala haifahimishi wajibu huo kwa habri ya mwenye kuaminika. Sisi tuko na wale wasemao kuwa kuitegemea habari ya mwenye kuaminika bila ya uchunguzi ni njia wanayoitumia wenye akili wa kale na wa sasa.

Hata hivyo kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda,” inafahamisha kuwa habari yoyote ambayo hatuna wasiwasi nayo kuingia katika matatizo na haramu, basi inafaa kuitumia bila ya kumwangalia mtoaji habari.

Kimsingi ni kuwa tusiamini habari ila ikiwa inatoka kwa mwenye kuaminika au tuithibitishe na kuichunguza ikiwa inatoka kwa fasiki.

وَاعْلَمُوا أَنَّ فِيكُمْ رَسُولَ اللَّـهِ لَوْ يُطِيعُكُمْ فِي كَثِيرٍ مِّنَ الْأَمْرِ لَعَنِتُّمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ حَبَّبَ إِلَيْكُمُ الْإِيمَانَ وَزَيَّنَهُ فِي قُلُوبِكُمْ وَكَرَّهَ إِلَيْكُمُ الْكُفْرَ وَالْفُسُوقَ وَالْعِصْيَانَ أُولَـٰئِكَ هُمُ الرَّاشِدُونَ ﴿٧﴾

7. Na jueni kuwa yuko kati yenu Mtume wa Mwenyezi Mungu. Lau angeliwatii katika mambo mengi, bila ya shaka mngelitaabika. Lakini Mwenyezi Mungu amewapendezea Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na akauchukiza kwenu ukafiri, na upotovu, na uasi. Hao ndio walioongoka.

فَضْلًا مِّنَ اللَّـهِ وَنِعْمَةً وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ ﴿٨﴾

8. Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.

MWENYEZI MUNGU AMEWAPENDEKEZEA IMANI

Aya 7 – 8

MAANA

Na jueni kuwa yuko kati yenu Mtume wa Mwenyezi Mungu na mtukufu wa wa mwanzo na wa mwisho. Basi ni juu yenu kumwadhimisha wala msimpe habari isipokuwa ya ukweli.

Lau angeliwatii katika mambo mengi, bila ya shaka mngelitaabika.

Hii ni amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ikielekezwa kwa wau- mini kuwa wamsikilize Mtume na wamtii, wala wasimshauri lile analolijua kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ambalo wao hawalijui. Lau angeliwaitikia kwenye mambo mengi wanayomwambia wangelitaabika na kuingia kwenye tabu na dhambi.

Lakini Mwenyezi Mungu amewapendezea Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na akauchukiza kwenu ukafiri, na upotovu, na uasi. Hao ndio walioongoka.

Mwenyezi Mungu amewaamrisha waja wake wamwamini Yeye na wamtii, akawabainishia uzuri wa imani na utiifu, akatumia kila njia kuwahimiza hilo na akamwahidi malipo na thawabu kubwa mwenye kuamini na akatenda mema. Vile vile amewakataza ukafiri na uasi, akabainisha hasara zake na akamtishia kwa adhabu mwenye kukufuru na kuasi na akazisifia adhabu hizo kwa namna ambayo haiwezi kufikirika akilini ila baada ya kubainishwa. Ni mtu gani anayeweza kufikiria adhabu ambayo si mauti wala uhai.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewatuma Mitume wake kwa watu ili wafikishe amri, makatazo ahadi na kiaga chake. Kuna wale wanaoitikia kihaki na kiukweli, wengine wakapinga na kufanya inadi na kuna wale waliotikia kuhofia masilahi yao na tamaa ya ngawira.

Wale waliomwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume kihaki na kiukweli ndio aliowakusudia katika kauli yake: “Amewapendezea Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu.” Yaani ameipendekeza na kuipamba kutokana na kueleza uzuri wa imani na kivutio cha thawabu nyingi. Akauchukiza ukafiri kwa kueleza mabaya yake na tishio la adhabu chungu.

Unaweza kuuliza : Mwenyezi Mungu (s.w.t) amelibainisha hilo kwa waumini na makafiri, kwanini amehusisha kuwataja waumini, kinyume na wengineo?

Jibu : Ndio, lakini sio kila mwenye kusikia ubainifu wa Mwenyezi Mungu anauamini na kunufaika nao, wala sio kila mwenye kunasihiwa na Mwenyezi Mungu anakubali nasaha zake. Bali wema wamekubali na waovu wakakataa. Ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamtaja na kumsifu mwenye kusikia maneno akafuata mazuri yake na akampuuza mwenye kupinga na akaachana nayo.

Kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na neema zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye hikima.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kuchagua uongofu badala ya upotevu ana fadhila na malipo, lakini fadhila kubwa ni ya yule aliyemwandalia njia ya uongofu, akamwongoza na akampa uweza wa kuifuata. Walisema wakale: “Kama si sababu asingelifaulu msababishaji”

وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ ﴿٩﴾

9. Na ikiwa makundi mawili katika waumini yanapigana, basi yapatanisheni. Na likiwa moja la hayo linadhulumu jingine, basi lipigeni linalodhulumu mpaka lirejee kwenye amri ya Mwenyezi Mungu. Na likirejea basi yapatanisheni kwa uadilifu. Na hukumuni kwa haki. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanaohukumu kwa haki.

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٠﴾

10. Hakika Waumini tu ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mrehemiwe.

NA IKIWA MAKUNDI MAWILI KATIKA WAUMINI YANAPIGANA

Aya 9 – 10

MAANA

Na ikiwa makundi mawili katika waumini yanapigana, basi yapatanisheni.

Uaislamu una mafunzo na miongozo ya kujenga jamii na kuitengeneza; miongoni mwayo ni wajibu wa kumlinda binadamu damu yake, mali yake, hadhi yake na uhuru wake wa kusema na kutenda. Hakuna yeyote mwenye utawala wa hayo isipokuwa haki. Akitoka kwenye haki na akaingilia haki ya wengine, basi hapo atakuwa amejiondolea kinga ya hayo yeye mwenyewe. Mwenyezi Mungu anasema:

وَلَقَدْ كَرَّمْنَا بَنِي آدَمَ ﴿٧٠﴾

“Na hakika tumewatukuza wanadamau.” Juz. 15 (17:70).

Amesema tena kumwambia Mtume wake:

لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ ﴿٢٢﴾

“Wewe si mwenye kuwatawalia” (88:22).

Akasema tena:

إِنَّمَا السَّبِيلُ عَلَى الَّذِينَ يَظْلِمُونَ النَّاسَ وَيَبْغُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ ﴿٤٢﴾

“Bali njia ya lawama ipo kwa wale wanaowadhulumu watu, na wanafanya jeuri katika ardhi bila ya haki.” Juz. 25 (42:42).

Mafunzo mengine ya Uaislamu ni kuhurumiana na kusaidiana katika yale yaliyo na heri na masilahi kwa wote. Ikiwa itatokea uhasama baina ya makundi mawili ya waumini, basi wajibu wa waumini ni kusuluhisha kwenye misingi ya haki na uadilifu na kuchunga umoja usivunjike.

Kuna Hadith tukufu inayosema: “Je, niwaambie jambo lililo na daraja kubwa zaidi kuliko kufunga, kuswali na kutoa sadaka? Wakasema: Naam! Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akasema: Ni kuwaunganisha waliotengana”

Na likiwa moja la hayo linadhulumu jingine, basi lipigeni linalodhulumu mpaka lirejee kwenye amri ya Mwenyezi Mungu.

Ikiwa kundi moja litakataa kurudi kwenye haki na likang’ang’ania uchokozi, basi ni juu ya waumini wengine kulihami na dhulma lile kundi linaloonewa, kwa hekima na mawaidha mazuri. Ikiwa lile kundi ovu halitakoma ila kwa vita, basi lipigeni katika mipaka ya sharia inayohakikisha amani ya wote.

Na likirejea basi yapatanisheni kwa uadilifu. Na hukumuni kwa haki. Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wanaohukumu kwa haki.

Likitubia lile kundi linaloonea na likaacha kabisa, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira mwenye kurehemu, na hakuna atakayeruhusiwa kulifanyia lolote. Lililobaki ni wajibu wa waumini, kwa juhudi zao waondoe, yaliyotokea kwenye nafsi za pande mbili.

Al-Jassas Al-Hanafi, anasema katika Kitabu Ahkamul-Qur’an akiwa anazungumzia Aya hii: “Ali Bin Abi Twalib alipigana na kundi ovu kwa upanga akiwa pamoja na maswahaba wakubwa wa Badr (Ahlu Badr) waliojulikana. Na alikuwa ni mwenye haki. Hakuna aliyehalifu katika kundi kabisa isipokuwa kundi ovu na wafuaisi wake aliokuwa akipigana nao.”

Na akasema Abu Bakr Al-Malik, Maaruf kwa jina la Ibn –Al-Arabi Al- Muafiri, katika Ahkamul - Qur’an: “Imethibiti kwa maulama wa Kiislamu na imethibiti kwa dalili ya dini kwamba Ali Bin Abu Twalib alikuwa Imam na kwamba kila mwenye kupigana naye ni muovu na kupambana na mtu huyo ni wajibu mpaka arudi kwenye haki.”

UDUGU WA KIDINI NA UDUGU WA KIBINADAMU

Hakika Waumini tu ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mrehemewe.

Hii ni kusisitiza kuleta suluhu baina ya pande mbili zilzigombana, pamoja na kuashiria kuwa upatanishi huu ni lazima kwa mfungamano wa udugu. Kuna Hadith isemayo: mwislamu ni ndugu wa mwislamu, hamdhulumu, hamtelekezi wala hamtii aibu.

Unaweza kuuliza: Kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t) amesema: Hakika waumini tu ni ndugu, na asiseme: Hakika watu wote tu ni ndugu. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) naye akasema:

“Mwislamu ni ndugu wa mwislamu.” Na asiseme: Mtu ni ndugu wa mtu? Tunajua kuwa Mola ni mmoja, asili ni moja, umbile ni moja na usawa baina ya watu ni wajibu. Kwa hiyo upendo unatakikana uwe ni wa jumla sio mahsusi; sawa na rehe- ma ambayo imekienea kila kitu?

Basi mgawanyo huu utakuwa na tofauti gani na ule unaowagawanya binadamu kwa misingi ya kiuchumi; walivyofanya wamarksi, au kuwagawanya kwa misingi ya kijinsia; kama walivyofanya wanazi au kwa misingi ya vita na silaha kama ilivyo siasa ya kimarekani?

Kisha nini kilichosababisha matatizo na maangamizi haya yanayomkabili binadamu leo, hadi kufikia kumalizana, baada ya binadmu kuweza kumiliki nguvu mbaya ya silaha za maangamizi? Je, hii imesabishwa na binadamu kama binadamu au imesabishwa na aina kwa aina za migawanyo?

Hatimaye sasa binadamu wasaidiane kwa misingi ya dini au asasi za kibanadamu?

Jibu : Maswali yote haya ni haki, na jibu lake ni moja tu litakoloweza kutosheleza maswali yote haya; nalo ni: Kusaidiana ni wajibu baina ya binadamu wote bila ya kubagua. Huu ndio mwito wa uaislamu hasa, unaofahamishwa na makumi ya Aya na riwaya. Tutatosheka kutaja Aya moja na riwaya moja.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema katika Aya ya 13 ya sura hii: “Enyi watu! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumewafanya mataifa na makabila ili mjuane. Hakika mtukufu zaidi yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi yenu.

Kwa hiyo mwito wake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Enyi watu!’ pamoja na kusema kwake: ‘Kutokana na mwanmmke na mwanamume’ na ‘aliye na takua zaidi’ ni dalili mkataa na wazi kuwa mwito wa Qur’an ni wa kiutu na wa mataifa, unamzingatia mtu ni ndugu wa mtu kwa namna yoyote itakvyokuwa itikadi yake, utaifa wake na jinsia yake.

Mfano wa Aya hii na ufafanuzi wake ni kauli yake Mtume mtukufu(s.a.w. w ) : “Watu wote wako sawa kama chane za shanuo. Jueni kuwa hakuna ubora wa mwarabu kwa mwajemi wala wa mwajemi kwa mwarabu, wala wa mwekundu kwa mweusi wala wa mweusi kwa mwekundu isipokuwa kwa takua … nyote mnatokana na Adamu na Adam ametokana na mchanga.”

Zaidi ya hayo katika Juz.21 (30:30) kuna Aya inayosema kuwa uislamu ni dini ya maumbile na katika Juz. 9 (8:24) kuna Aya inayofahamisha kuwa dini ya Mwenyezi Mungu ni dini ya maisha.

Kwa hali hiyo basi inatubainikia kuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna za Mtume wake zinazingatia kuamini utu ni sehemu inayokamilisha kumwamini Mwenyezi Mungu, mitume wake na Vitabu vyake.

Kwa hiyo Makusudio ya mumin katika Aya na mwislamu katika Hadith ni yule anayeamwamini Mwenyezi Mungu na mtu kwa kuwa ni mtu.

Kwa maneno mengine ni kuwa hakuna mzozo wala kupingana baina ya udugu wa kibinadamu na udugu wa kiislamu; huu wa kiislamu unauongeza nguvu ule wa kibinadamu.

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿١١﴾

11. Enyi ambao mmeamini! Kaumu isidharau kaumu nyingine, huenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake kwa wanawake wengine, huenda wakawa bora kuliko wao. Wala msitiane kasoro, wala msiitane majina ya kejeli. Na wasiotubu, hao ndio madhalimu.

KAUMU ISIDHARAU KAUMU NYINGINE

Aya 11

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Kaumu isidharau kaumu nyingine, huenda wakawa bora kuliko wao; wala wanawake kwa wanawake wengine, huenda wakawa bora kuliko wao.

Imesemekana kuwa neno Qawm, tulililofasiri kwa maana ya kaumu, kwa maana yake ya kiarabu huwa halitajwi ila kwa wanaume tu, kwa dalili ya kuunganishwa wanawake baada ya neno hilo.

Katika Juz. 19 (25:55-62) tulisema kuwa dhalimu kesho atachukuliwa na Mwenyezi Mungu kuwa ni kafiri ingawaje duniani anachukuliwa kuwa ni mwislamu kama akitamka shahada mbili.

Na mwenye kuwadharau wema atakuwa ni dhalimu na safihi.

Hili Mwenyezi Mungu amelikemea kwa ukali sana; kama aliposema:

فَيَسْخَرُونَ مِنْهُمْ سَخِرَ اللَّـهُ مِنْهُمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٩﴾

“…Wakawafanyia maskhara; Mwenyezi Mungu atawafanyia maskhara na wana wao adhabu iumizayo. “ Juz. 10 (9:79).

Pia kauli yake:

إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ ﴿٢٩﴾ وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ ﴿٣٠﴾ وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ ﴿٣١﴾ وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَـٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ ﴿٣٢﴾ وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ ﴿٣٣﴾ فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ﴿٣٤﴾

“Hakika wale walio na hatia walikuwa wakiwacheka wale ambao wameamini. Wakiwapitia wanakonyezana na wakirudi kwa watu wao walirudi wakishangilia. Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea. Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao. Basi leo wale ambao wameamini wanawacheka makafiri” (83: 29-34).

Vile vile amesema:

وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ ﴿١﴾

“Ole wake kila mtia kasoro mwenye kusengenya.” (104:1).

VIPI UTAPATA MARAFIKI?

Nimekumbuka, wakati nikifasiri Aya hii, kwamba kiasi cha mika 16 au zaidi iliyopita nilisoma tarjuma ya kitabu: How to win friends and influence people (vipi utapata marafiki na kuathiri nafsi) cha Dayl Karengi.

Vile vile nimekumbuka hekima ya hali ya juu ya Imam Zainul’abidin, inayohusiana na maudhui hii ambayo ina athari zaidi ya kitabu nilichokitaja pamoja na kuwa kimeenea sana na kufasiriwa kwenye lugha nyingi.

Imam, kwenye hekima yake, alikuwa akikusudia kauli yake Mwenyezi Mungu: “Kaumu isidharau kaumu nyingine, huenda wakawa bora kuliko wao.” Hekima yenyewe ni hii:

“Jihadhari na kuzungumza ambayo moyo unayakanya hata kama una udhuru. Kwani sio kila utakayemwambia shari unaweza kumfafanulia udhuru. Aliye mkubwa kuliko wewe muweke daraja ya mzazi, mdogo daraja ya mtoto, na aliye marika daraja ya kaka. Ni nani katika hawa unapenda kumvunjia heshima yake?

“Ikiwa shetani atakuingilia kujiona kuwa u mbora zaidi ya mwingine, angalia haya yafutayo: Ikiwa ni mkubwa zaidi yako, sema: amenitangulia kwa imani na matendo mema, kwa hiyo ni bora kuliko mimi. Ikiwa ni mdogo kuliko wewe, sema: nimemtangulia kwa maasi, kwa hiyo yeye ni bora kuliko mimi. Akiwa ni marika yako sema: mimi nina uhakika nimefanya dhambi, lakini nina shaka kuwa yeye amefanya dhambi, basi kwanini niache uhakika nichukue shaka?

“Ukiwaona watu wanakutukuza, sema: wamechukulia wema, na ikiwa wanakutenga, sema: kuna makosa nimefanya.”

Imam anaendelea kusema:“Ukiyafanya haya maisha yako yatakuwa mepesi, utakuwa na marafiki wengi na utakuwa na maadui kidogo, na utafurahi kwa wema wao wala hutasikitika kukutenga.”

Vyovyote watavyosema maulama na wenye hekima kuhisiana na maudhui haya, hawatazidisha kitu kwenye hekima hii fasaha ya hali juu.

Hilo si ajabu kwa vile aliyeisema ni mtoto wa wahyi, hazina ya ilimu ya wahyi na aliyekulia kwenye malezi yake.

Wala msitiane kasoro.

Msitiane ila wala msiwambie wengine lile ambalo hampendi kuambiwa.

Wala msiitane majina ya kejeli.

Mtu asimwite mwenzake kwa jina analolichukia. Mafaqihi wamesema kuwa ikiwa jina halikukusudiwa kasoro wala dharau na ni mashuhuri wa hilo, basi halina ubaya; kama vile Hassan Madafu, n.k.

Ni uovu kutumia jina baya baada ya imani.

Hapa kuna tafsiri mbili: Ya kwanza ni msimwite mumin ewe kafiri! Ya pili, ni uovu huko kumwita mwingine kwa jina asilolipenda. Tafsiri hii ina ngvuvu, kwa wafasiri wengi kuliko ile ya kwanza.

Na wasiotubu, hao ndio madhalimu.

Mwenye kutubia ni kama asiye na dhambi na mwenye kung’ang’ania dhambi atakuwa ameidhulumu nafsi yake. Kwa sababu Mwenyezi Mungu atawaadhibu wenye dhambi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ وَاتَّقُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ ﴿١٢﴾

12. Enyi ambao mmeamini! Jiepusheni na dhana nyingi. Hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Wala msipeleleze, wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je, anapenda mmoja wenu kuila nyama ya nduguye aliyekufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.

DHANA, UJASUSI NA KUSENGENYA

Aya 12

MAANA

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekataza dharau, kutia ila, kubeza na kuitana majina ya kuchukiza. Na akamkemea mwenye kufanya moja katika hayo. Katika Aya hii anakataza dhana mbaya, ujasusi na kusengenya. Ufafanuzi ndio huu ufuatao:-

DHANA

Enyi ambao mmeamini! Jiepusheni na dhana nyingi. Hakika baadhi ya dhana ni dhambi.

Sehemu hii ya Aya inawezekana kufanyiwa muhtasari kwa jumla moja tu: “Kila mtu hana hatia mpaka lithibitike kosa lake.”

Inawezekana jumla hii kuifafanua kwa urefu, tuweke mpaka wa linalopelekea asili ya dhana, kuwa je, inafaa kuichulia dhana au kuna wajibu wa kujieupusha wakati wote au wakati wa kuweko udhuru na wa kutokuweko ilimu? Na je, kuna udhuru wa kutojua au hakuna?

Ikiwa inafaa kuichukulia dhana, je, tuichukulie dhana vyovyote ilivyo sababu yake na mfungamano wake? Na ikiwa haifai kuichukulia dhana kwa namna yote ile, je ni nyenzo gani za ilimu kwenye hukumu ya sharia na mengineyo katika ilimu ya usul (misingi ya sharia) ambayo tumeimalizia miaka si kidogo kuisoma?

Ni vizuri tuchuke tafsiri ya wastani si kurefusha wala kufupiliza. Kabla ya lolote ni lazima tufanye maandalizi ya kujua toafauti baina ya shaka, dhana na ilimu. Shaka ni kuwa sawa uthibitisho na ukanusho. Dhana ni kuwa na nguvu upande mmoja baina ya hizo mbili, lakini bado kunakuwa na uwezekano kwa upande ule usio na nguvu. Ilimu ni kubainika upande mmoja unaofunga kabisa njia ya upande mwingine.

Unaweza kumdhania mtu heri au shari, ukawa umepatia au umekosea katika dhana yako. Hakuna ubaya kabisa ikiwa utamdhania mwenzako heri, iwe umepatia au umekosea; au iwe litajitokeza hilo kwenye kauli yako na vitendo vyako au lisijitokeze.

Mtume mtukufu(s.a.w. w ) anasema:“Wadhanieni waumini heri.” Imam Ali(a . s) anasema:“Liweke jambo la nduguyo kwenye heri.” Tazama Juz. 1 (2:83) kifungu cha ‘Kuchukia usahihi.’

Kwa hiyo basi inatubainikia maana ya kuwa kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t) amesema:“Jiepusheni na dhana nyingi,” na wala asisema ‘jiepusheni na kila dhana.’

Neno wingi huwa pia linatumiwa kwa maana ya baadhi; na haya ndiyo Makusudio yake kwenye Aya hii; yaani jiepusheni na dhana mbaya.

Dhana mbaya yenyewe sio haramu ikiwa haitajitokeza kwenye kauli au kitendo, wala mwenye dhana hiyo hana majukumu yoyote. Lakini ni lazima asiitolee maamuzi yoyote na aifanye kama haiko. Akiitolea uamuzi na ikajitokeza athari yake kwenye kauli au kitendo, basi atawajibika na atastahili lawama na adhabu.

Hii ndio dhana aliyoikusudia Mwenyezi Mungu aliposema: “Hakika baadhi ya dhana ni dhambi.”

Mtume mtukufu(s.a.w.w) anasema:“Mambo matatu hasalimiki nayo yeyote: Kisirani, hasadi na dhana: Ukiona kisirani endelea, ukiona husda usiitake, na ukidhania hakikisha. Kwa hiyo basi maana ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Jiepusheni na dhana nyingi’ nikuwa msizitolee maamuzi wala msizitumie; sawa na kauli yake “Asiwafitini shetani.”

UJASUSI

Wala msipeleleze.

Kupeleleza ni kuchunguza siri na makosa kwa njia ya kujificha. Ni haramu kwa Kitabu, Sunna, Ijmai (kongamano la maulama) na kiakili. Na kauli yake:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتًا غَيْرَ بُيُوتِكُمْ حَتَّىٰ تَسْتَأْنِسُوا ﴿٢٧﴾ فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فِيهَا أَحَدًا فَلَا تَدْخُلُوهَا حَتَّىٰ يُؤْذَنَ لَكُمْ... ﴿٢٨﴾

“Enyi ambao mmeamini! Msiingie nyumba zisizo nyumba zenu mpaka muombe ruhusa… na msipomkuta yeyote humo msiingie mpaka mpewe ruhusa.” Juz. 18 (24:27-28).

Katika Sunna ni Hadith ya Mtume mtukufu(s.a.w. w ) :“Mwenye kukuchungulia ukamtupia kijiwe na ukamtoboa macho yake, basi huna lawama.” Mafaqihi wamekubaliana kwa pamoja kuitumia Hadith hii. Ama akili inauona ujajusi ni vita dhidi ya maisha ya watu na kuingilia uhuru wao na mambo yao yanayowahusu katika mila na desturi.

Nimekumbuka, wakati nikiandika maneno haya, makala ndefu kuhusu maudhui haya, iliyotolewa na gazeti Al-Ahram la 27-6-1969, nililisoma wakati huo, kisha nikalihifadhi katika mafaili ya magazeti. Nililihifadhi na kuliweka akiba ya kulitumia nikilihitajia. Basi nikalisoma tena, mara nikaona mambo ambayo hata kuyawaza tu ni muhali; baadhi yake ni haya yafuatayo:

“Wamarekani hivi sasa wanajua kuwa sio kuwa kuta zao zina masikio tu, bali zina macho na mboni vile vile, kama lilivyosema gazeti la Times. USA wametengeneza kifaa kidogo cha ukubwa wa milimita, kinachoweza kusajili mazungumzo; na mtu anaweza kukiweka kwenye jaketi kama kifungo. Kila mtu anaweza kukitumia na kinagharimu kati ya dola 10 na 15.

Huko New York, wafanyabiashara wameweka matangazo ya biashara kwenye magazeti kuuza vifaa vya kurikodi mazungumzo ya watu majumbani mwao na wanaviuza madukani kama michezo ya watoto. Bei yake haizidi dola 18.

Mtu akiweka kifaa hiki kwenye gari kikielekezwa kwenye jengo basi kitarikodi kila neno linalosemwa kwenye jengo lile. Bali kuna kifaa cha kusikilizia maneno kisichozidi ukubwa wa punje ya choroko, kinachoweza kuwekwa kwenye kalamu nk, kinatumia betrii ya masaa 18 hadi 50.

Pia wametengeneza kifaa kidogo cha kutuma, kinachoweza kutangaza yanayopita kwenye majumba kwa umbali wa futi 50 na bei yake ni dola 400.

Ajabu ya yote ni kamera zinazopenya ukutani na kupiga picha mambo yote anayoyafanya mtu chooni na hata kwenye giza. Vile vile inawezekana kuchora chale (tattoo) katika mwili wa mtoto wakati anapozaliwa ambayo itafuatilia harakati zake katika maisha yake yote.

Kuna shirika katika Marekani yote linalokusanya habari na harakati binafsi za watu mashuhuri wa siasa, elimu, uandishi uchumi na wengineo na kurikodi maneno yao, na kupiga picha ya vitendo vyao, hata wanapofanya tendo la ndoa na wake zao na wengineo. Mtu anaweza kupata habari hizi kwa dola moja tu. Shirika hili linaitwa Benki ya habari.

Yote hayo yanatokea ikiwa serikali inajua kila kitu, bila ya kufanya lolote, kwa sababu imekuwa ni jambo la kawaida kama vile kuuza magazeti tu.” Mwisho wa nukuu ya gazeti.

Haya ni machache katika mengi. Watunzi wameandika vitabu maalum kuhusiana na maudhui haya. Lau wamarekani wangeliyafanya haya kwao tu wenyewe kwa wenyewe, tungeliwaambia wao na wanowatawala: “shauri yenu, kila mji una uhuru wa kujichagulia unavyotaka.” Lakini wamarekani wamevuka mipaka, wanafanya ujasusi kwenye nchi nyingine kwa ndege na satalaiti.

Usishangae msomaji. Marekani ni nchi ya maendeleo, demokarasia, bwana mkubwa wa uhuru, na polisi wa ulimwengu.

Tena zaidi ya hayo wanaamini Mwenyezi Mungu… Dalili kubwa kuwa wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho ni mauaji ya kinyama waliyoyafanya kwenye kijiji kimoja katika Vietnam ya kusini[6] , na kuwasheheneza silaha za kisasa mayahudi ili kuwamaliza wananchi wa Palestina, kuwaua watoto kwa ujumla na kutupa mabomu kwa kutumi ndege za Phantoum kwa watoto wa shule wa Misr! Kweli kabisa USA ni dola kubwa kwenye uwanja huu wa mauaji!

KUSENGENYA

Wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je, anapenda mmoja wenu kuila nyama ya nduguye aliye kufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu.

Kusengenya ni kumtaja mtu kwa jambo asilolipenda. Mtume mtukufu(s.a.w. w ) anasema:“Kusengenya ni kumtaja ndugu yako kwa jambo analolichukia. Ikiwa jambo hilo analo huko ni kusengenya na ikiwa hana itakuwa ni kumsingizia.” Na kusingizia ni kukubwa zaidi kuliko kusengenya na kumeharamishwa kwa Kitabu Sunna na Ijmai (kongamano la maulama).

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemfananisha mwenye kusengenywa na maiti kwa vile anakuwa hayupo na akaifananisha hishima yake na nyama yake na kumtaja kwa uovu kuwa ndio kula.

Maana ya mnalichukia hilo ni kuwa ikiwa mnaona kinyaa kula nyama ya maiti basi pia muone kinyaa kumsengenya asiyekuwepo, kwa sababu yote mawili hayo yako sawa.

Hakuna jambo linalofahamisha kupungukiwa na udhalili kuliko kusengnya. Imam Ali(a . s) anasema:“Kusengenya ni juhudi ya asiyejiweza.” Na Mwenyezi Mungu hasamehi kusengenya mpaka asamehe aliyesengenywa. Mafaqihi wameuvua uharamu wa kusengenya kwa wafuatao:-

Mpagani, hakimu dhalimu, mwenye kuudhihirisha ufuska wake, kwa sababu mwenye kulitupa joho la haya hana cha kuficha, kumpa ushauri mwenye kutaka ushauri katika kushirikiana na mtu au kumwakilisha kwenye jambo muhimu, kumtengua shahidi kwa kadhi, na mwenye kudhulumiwa kwa yule aliyemdhulumu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

لَّا يُحِبُّ اللَّـهُ الْجَهْرَ بِالسُّوءِ مِنَ الْقَوْلِ إِلَّا مَن ظُلِمَ وَكَانَ اللَّـهُ سَمِيعًا عَلِيمًا ﴿١٤٨﴾

“Hapendi Mwenyezi Mungu maneno ya kutangaza uovu ila kwa aliyedhulumiwa.”

Juz. 6 (4:148).

Katika Kitabu Al-Makasib cha Sheikh Ansari, imesemwa kuwa sehemu zinazoondolewa uharamu wa kusengenya hazina idadi. Kwa sababu kusengenya kunakuwa haramu ikiwa kutangaza huko hakuna masilahi yenye nguvu. Vinginevyo, basi itakuwa wajibu kutangaza na kueneza kwa kuangalia masilahi yenye nguvu zaidi, kama ilivyo katika kila maasi ya haki za Mwenyezi Mungu na haki za binadamu.Tazama mwanzo wa Juz. 6.

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿١٣﴾

13. Enyi watu! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumewafanya mataifa na makabila ili mjuane. Hakika mtukufu zaidi yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi yenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye habari.

قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَـٰكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي قُلُوبِكُمْ وَإِن تُطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَا يَلِتْكُم مِّنْ أَعْمَالِكُمْ شَيْئًا إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٤﴾

14. Mabedui walisema: Tumeamini. Sema: Hamjaamini, lakini semeni: Tumesilimu. Kwani imani haijaingia katika nyoyo zenu. Na mkimtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hatawapunguzia chochote katika vitendo vyenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ لَمْ يَرْتَابُوا وَجَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ ﴿١٥﴾

15. Hakika Waumini ni wale tu waliomwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake tena wasiwe na shaka, na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao. Hao ndio wakweli.

قُلْ أَتُعَلِّمُونَ اللَّـهَ بِدِينِكُمْ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿١٦﴾

16. Sema: Je, mnamjulisha Mwenyezi Mungu Dini yenu, na hali Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi, na Mwenyezi Mungu anajua kila kitu?

يَمُنُّونَ عَلَيْكَ أَنْ أَسْلَمُوا قُل لَّا تَمُنُّوا عَلَيَّ إِسْلَامَكُم بَلِ اللَّـهُ يَمُنُّ عَلَيْكُمْ أَنْ هَدَاكُمْ لِلْإِيمَانِ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿١٧﴾

17. Wanakusimbulia kuwa wamesilimu! Sema: Msinisimbulie kwa kusilimu kwenu. Bali Mwenyezi Mungu ndiye anayewasimbulia kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.

إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ غَيْبَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاللَّـهُ بَصِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿١٨﴾

18. Hakika Mwenyezi Mungu anajua siri za mbingu na ardhi. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

MTUKUFU ZAIDI YENU NI MWENYE TAKUA ZAIDI

Aya 13 – 18

MAANA

Enyi watu! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumewafanya mataifa na makabila ili mjuane. Hakika mtukufu zaidi yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi yenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye habari.

Watu wanajua kuwa baba yao ni Adam na mama yao ni Hawa, lakini lengo la kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Tuewaumba kutokana na mwanamume na mwanamke, ni kuwa watu wote wajue kwamba wao ni ndugu ni udugu wa usawa katika haki na wajibu.

Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu; “Ili mjuane,” ni kuwa Makusudio ya kutofautiana kwenu katika miji, nasaba na rangi, sio kuwa muwe vikundi, mchinjane na mjifaharishe kwa mataifa yenu, baba zenu na jinsi zenu, hapana! Sivyo kabisa.

Lengo ni muhurumiane na msaidiane katika yale yaliyo na heri yenu na masilahi yenu. Na mbora kabisa atakuwa yule anayemuogopa Mwenyezi Mungu zaidi na akawanufaisha waja wake.

Aya hii ni mwito kutoka kwenye Qur’an kuwa watu wawe umma mmoja wa kiutu na ulimwengu mmoja unaokusanywa na uadilifu na upendo. Ulimwengu huu ni tegemeo la wenye fikra safi na ni ndoto ya walio wema.

Tuna uhakika kuwa makubaliano ya haki za binadamu, yatabakia kwenye karatasi na yatakuwa ni nadharia tu, ikiwa hautapatikana umoja wa ubinadamu uliotolewa mwito na Qur’an, zaidi ya mika 1300 liliyopita. Amerika na Israil zilitia saini makubaliano ya haki za binadamu, lakini bado ndio za kwanza kuangamiza watu Vietnam na Palestina.

Leo ninapoandika maneno haya 22 April 1970, kamati ya umoja wa mataifa imehakikisha kuwa Israil imevunja haki za binadamu, ikasema waziwazi kuwa Israil imevunja majumba ya wakazi ikaacha miili ya wanaume, wanawake na watoto kwenye kifusi na ikakataa isizikwe. Pia imevunja sehemu takatifu na mahospitali[7] na kuwaadhibu wenyeji kwa umeme. Watu wazima wanawang’oa viungo, watoto wanawakata mikono na kupasua matumbo yao mbele ya baba zao na mama zao na mengineyo ya kinyama na mauji ya maangamizi.

Mabedui walisema: Tumeamini. Sema: Hamjaamini, lakini semeni: Tumesilimu. Kwani imani haijaingia katika nyoyo zenu. Na mkimtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hatawapunguzia chochote katika vitendo vyenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Makusudio ya uaislamu hapa ni kutamka shahada mbili. Katika Juz. 1 (2:82), tumetaja tofauti baina ya mumin na mwislamu. Hapa tutamnukuu Dkt Twaha Hussein katika kitabu Mir’atul-islama (Kioo cha uaislamu).

Yeye ni mwanafasihi anayefahamika kwa siri za fasihi, ninamnukuu: “Wakati wa Mtume kulikuweko waumini na waislamu. Basi, niipi tofauti baina imani na Uislamu? Imani kwa dhahiri ya Aya hii ni jambo lilio moyoni ambalo mihimili yake ni ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu na kusadikisha, kwa kina ndani ya dhamiri, kila aliloletewa wahyi Mtume.

Natija ya imani hii ni kumwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume katika kila wanalolitolea mwito, bila ya kigugumizi, kugwazagwaza, wala kutaradadi, kwa hali yoyote ile itakavyokuwa; iwe kuna matukio au majanga. Mhimili mwingine wa imani hii ni kumwogopa Mwenyezi Mungu kiundani kabisa likitajwa jina lake na kumtegemea kwa undani zinaposomwa Aya zake.

“Ama Uislamu ni twaa ya dhahiri ya kutekeleza wajibu na kujiepusha na yaliyokatwaza; hata kama haitafikia imani ya kweli. Kuna watu wanaosilimu kuhofia ubaya; kama walivyosilimu makuraishi walioachwa bila ya kutekwa nyara siku ya kutekwa Makka. Wengine walasilimu kwa hofu na tamaa; kama walivyofanya mabedui aliowataja Mwenyezi Mungu katika Aya hii.”

Hakika Waumini ni wale tu waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake tena wasiwe na shaka, na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao. Hao ndio wakweli.

Waumini wa kwelikweli kabisa ni wale wasiokuwa na shaka yoyote kwenye itikadi zao na wanaojitolea kihali na mali, kuihakikisha haki na kuibatilisha batili. Umetangulia mfano wake mara kadhaa; miongoni mwazo ni Juz. 10 (9:88).

Sema: Je, mnamjulisha Mwenyezi Mungu Dini yenu, na hali Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi, na Mwenyezi Mungu anajua kila kitu?

Mabedui walisema tumeamini, ndio Mwenyezi Mungu anawajibu, kuwa hivi mnamjulisha Mwenyezi Mungu imani yenu na hali Yeye anajua siri na yaliyofichika; kila kitu amekizunguka. Tena je imani inakuwa kwa kudai? Inatosha kuwa mtu ni mjinga kuwa hajui uweza wake Mwenyezi Mungu.

Wanakusimbulia kuwa wamesilimu! Sema: Msinisimbulie kwa kusilimu kwenu. Bali Mwenyezi Mungu ndiye anayewasimbulia kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.

Makusudio ya kusimbulia kwake Mwenyezi Mungu ni kuwafanyia hisani, kwa sababu Yeye amekataza masimbulizi, na hawezi kukataza jambo kisha alifanye. Makusudio ya kuongoza kwake kwenye imani ni kutoa mwongozo wa haki na kuipendekeza.

Maana ni kuwa mabedui na walio mfano wao wanaona kuwa wamemfanyia hisani Mola wao na mtume wao kwa dini yao na wanataka walipwe; hali yakuwa Mwenyezi Mungu ndiye aliyewafanyia hisani wao, pale alipowaongoza kwenye haki na kuwahimiza kupitia Mtume wake.

Kwa hiyo wao ndio wamshukuru kwa alivyowafanyia hisani na kuwaneemesha; sio wao wasimbulie na kutaka kulipwa; ikiwa kweli wameamini dini yao na wakafanya ikhlasi kwenye imani yao. Vinginevyo watakuwa wanastahili kutoka kwa Mwenyezi Mungu yale aliyowaandalia waongo na wahaini.

Hakika Mwenyezi Mungu anajua siri za mbingu na ardhi. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua imani ya kweli na ya uwongo na kuzipamabanua amali zilizokusudiwa dunia na zile zilizokusudiwa radhi ya Mwenyezi Mungu. Aina zote za amali pamoja na imani au kufuru ndio kipimo cha uadilifu wa hisabu na malipo.

MWISHO WA SURA YA ARUBAINI NA TISA: SURAT AL- HUJURAT


4

5

6

7

8

9

10

11

12

13