HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU0%

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU Mwandishi:
: AZIZI NJOZI
Kundi: Wanawake

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

Mwandishi: Allamah Shahid Murtaza Mutahhari
: AZIZI NJOZI
Kundi:

Matembeleo: 45191
Pakua: 2957

Maelezo zaidi:

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 33 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 45191 / Pakua: 2957
Kiwango Kiwango Kiwango
HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

Mwandishi:
Swahili

6

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

DHANA ZA ASILI ZA HAKI YA FAMILIA

Tumesema kwamba mwanadamu hufaidi aina fulani ya heshima ya asili. Asili ya maumbile yake imempa haki kadhaa za msingi zisizoondosheka. Huu ndio msingi wa Azimio la haki za Binadamu kwa wote. Uislamu na falsafa za Mashariki (Asia) zinaunga mkono dhamira hii. Kisichofaa katika Azimio hili na kinachokwenda kinyume ni jinsi mifumo mbali mbali ya falsafa za Kimagharibi inavyoitafsiri asili na maumbile ya mwanadamu. Ni dhahiri kuwa chanzo pekee chenye mamlaka na kisicho na makosa juu ya elimu ya haki za binadamu ni kitabu adhimu na kitukufu cha maumbile. Ni kwa kuzirejea tu kurasa za kitabu hiki ndio tunaweza kuziona haki ambazo zinawahusu watu wote, na kupata hakikisho la nafasi linganishi za haki za mwanaume na mwanamke.

Inastaajabisha kwamba baadhi ya watu wenye mawazo finyu hawakijui chanzo hiki kitukufu. Kwa mujibu wao, chanzo pekee cha kuaminika ni chombo cha wale watu wachache wanaoitawala dunia waliopata nafasi ya kuliandika Azimio hili. Ingawa wao wenyewe wanaweza, kivitendo wasiyazingatie hayo waliyoyaandika lakini wengine hawana haki ya kupinga. Lakini sisi, kwa kutumia hizi hizi haki za binadamu, tunaamini kuwa tuna haki ya kutofautiana. Kwa maoni yetu, chanzo pekee ambacho hakiwezi kupingwa ni maumbile yenyewe ambayo yanaweza kuchukuliwa kuwa ni kitabu cha Mwenyezi Mungu.

Tunawaomba radhi wasomaji wetu, kwa sababu inatupasa tuibue baadhi ya masuala ambayo kwa kiasi fulani ni ya kifalsafa na hivyo yanaonekana makavu. Yanaweza pia kuwa yanakinaisha kwa baadhi ya wasomaji. Tungeweza kuwa tuliyaepuka masuala haya, lakini somo la haki za mwanamke linahusiana sana na masuala hayo hivyo haiwezekani kuyaachilia mbali moja kwa moja. Uhusiano kati ya haki za asili/msingi na malengo ya maumbile.

Kwa mtazamo wetu, haki za asili na za msingi zimeibuka kutokana na mpango wa Mungu, ambapo kwa mujibu wa mpango huu, utaratibu wa kibunifu, kwa kuzingatia malengo yake, huvisukuma mbele vitu vyote kuelekea katika hali ya ukamilikifu, uwezo ambao tayari umefichwa ndani ya maumbile yao. Kila uwezo wa kiasili ni msingi wa moja ya haki za asili na, wakati huo huo, ni mamlaka ya asili ya kuitekeleza haki hiyo. Kwa mfano kila mtoto wa mwanadamu ana haki ya kujifunza na kwenda shule, lakini mtoto wa kondoo hana haki hizo. Kwa nini iko hivyo? Ni kwa sababu mtoto wa binadamu ana uwezo wa kujifunza na kupata busara zaidi wakati mtoto wa kondoo hana uwezo huu. Utaratibu wa kibunifu umeweka mamlaka kwa ajili ya haki hii ndani ya umbile la mwanadamu, lakini mamlaka haya hayakuwekwa ndani ya kondoo. Mambo yako hivi hivi katika haki za kufikiri, kupiga kura na utashi.

Baadhi ya watu wanafikiri kuwa nadharia ya haki za asili na wazo kwamba maumbile yamempatia mwanadamu haki maalum ni madai ya kibinafsi na ya kipuuzi. Kwa kusema kweli hakuna tofauti kati ya haki za wanaadamu na viumbe wasiokuwa wanaadamu. Lakini huu sio uhalisia, vipawa vya kiakili ni tofauti. Maumbile yameiweka kila spishi (kiumbe) iliyopo ulimwenguni katika obiti yake maalum, na inaweza kuwa na mafanikio tu kama itasonga ndani ya mipaka yake. Muumba amefanya hivyo kwa malengo, na mpangilio huu sio wa bahati nasibu.

Msingi wa haki za kifamilia, ambalo ndilo jambo linalojadiliwa hapa, lazima litazamwe kiasili (kimaumbile) kama ilivyo kwa haki nyingine za asili. Kama tukitazama vipaji vya asili vya mwanaume na mwanamke, tunaweza kuona kwa urahisi, iwapo wanaweza kuwa na haki na wajibu unaofanana au la. Lazima ikumbukwe kuwa, kama tulivyoonyesha huko nyuma kuwa nukta inayohisabiwa ni kufanana kwa haki zao sio usawa wa haki zao. Haki za kijamii. Nafasi ya mwanadamu, kuhusiana na haki za kijamii zisizo za kifamilia, siku zote hazinafanani. Katika hali fulani huwa na haki zinazofanana lakini katika hali fulani nyingine haki zao huwa hazifanani lakini huwa na haki sawa. Katika jamii haki zote za msingi huwa sawa kwa watu wote. Kila mtu, kwa mfano, ana haki ya kutumia vipaji vyake kufanya kazi na kushiriki katika mashindano ya maisha, huwa mgombea katika nafasi fulani ya kijamii na kuipata katika njia za halali, kuonyesha uwezo wake kiakili na kivitendo.

Lakini usawa huu huu wa wote juu ya haki za msingi huwaweka katika nafasi zisizo sawa. Kwa mfano, kila mtu ana haki ya kufanya kazi na kushiriki katika ushindani wa maisha, lakini inapokuja katika utendaji wenyewe kivitendo, haiwezekani wote wakafanya kazi vizuri kwa ubora unaolingana. Wengine wanaweza sana na wengine kidogo. Halikadhalika wengine wana ufanisi mkubwa zaidi kuliko wengine. Tena wengine wana elimu zaidi wanamudu zaidi majukumu, wana ufanisi mkubwa zaidi na wanafaa zaidi kuliko wengine. Ni dhahiri kuwa haki zao walizojipatia haziwezi kufanana. Kujaribu kuzifanya haki zao walizojipatia kwa jitihada na vipaji vyao, zifanane haitakuwa kitu kingine isipokuwa dhulma iliyo wazi.

Sababu ambayo ni kwa nini wanaadamu wana haki sawa na zinazofanana ni kuwa uchunguzi wa masuala ya binadamu unathibitisha kuwa hakuna aliyeumbwa akiwa bwana mkubwa, au bwana mdogo. Hakuna aliyezaliwa akiwa mfanyakazi, fundi, mwalimu, ofisa, askari au waziri. Nafasi hizi na madaraja mbali mbali ni sehemu ya haki anazojipatia mtu kwa kipaji na jitihada zake binafsi. Watu wanapaswa kujitafutia haki hizi kwa mujibu wa uwezo, vipaji na jitihada zao.

Hapa ndipo ilipo tofauti kati ya maisha ya kijamii ya wanaadamu na yale ya wanyama wanaopenda kushirikiana kama vile nyuki. Muundo wa maisha ya nyuki ni wa asili/silika kwa asilimia mia moja. Majukumu na kazi mbali mbali zimegawiwa kwa kila mmoja wao na maumbile yenyewe. Baadhi yao wamezaliwa wakiwa machifu na wengine wamezaliwa wakiwa na vyeo vya chini. Baadhi yao huzaliwa wakiwa wahandisi, wengine wakiwa maafisa utawala na wengine wakiwa wafanya kazi wa kawaida. Lakini maisha ya mwanadamu yako tofauti kabisa. Hii ndio sababu baadhi ya wasomi wameikana kabisa ile nadharia ya kale ya kifalsafa inayosema kwamba mwanadamu ni kiumbe wa kijamii kimaumbile na wameonelea kuwa jamii ya wanaadamu ni ya kimkataba (kimaafikiano) kwa asilimia mia moja.

Haki za kifamilia Haya yote yalikuwa yanahusu jamii isiyo ya kifamilia. Sasa vipi kuhusu jamii ya kifamilia? Je, watu wote katika jamii ya familia pia wana nafasi inayofanana na ile ya haki zao wanazojipatia, au je, suala la jamii ya kifamilia, ambayo ina mke na mume, wazazi na watoto na kaka na dada ni tofauti, na je, kuna sheria maalum ya asili inayohusiana na haki za kifamilia? Katika suala hili kuna kuwepo na uwezekano wa mambo mawili. Mojawapo ni kuwa uhusiano kati ya mke na mume au kati ya wazazi na watoto ni kama mahusiano mengine yoyote ya kijamii. Ushirikiano wao ni sawa na ule wa chombo cha watu serikalini na kwenye makampuni. Mahusiano haya hayamaanishi kuwa baadhi ya watu kiasili wana nafasi maalumu.

Ni kutokana tu na sifa binafsi za mtu ndio inatokea kuwa mwingine ni bosi na mwingine ni wa cheo cha chini, mmoja hutoa amri na wengine hutii, mwingine kwa mwezi anapata mshahara mkubwa na mwingine mdogo. Kuwa mume au mke au kuwa baba, mama au mtoto pia haimaanishi kuwa kila mmoja katika hawa ana nafasi maalum. Ni sifa zao wanazojipatia ambazo huamua nafasi zao katika mahusiano yao. Nadharia ya kufanana kwa haki za kifamilia kati ya mwanaume na mwanamke (ambayo kwa makosa inaitwa usawa wa haki) imeegemea katika uwezekano huu.

Kwa mujibu wa nadharia hii, mwanaume na mwanamke hushiriki katika maisha ya kifamilia kwa uwezo sawa, mahitaji sawa na haki sawa za asili. Hivyo, haki zao za kifamilia lazima ziwekwe katika msingi wa kufanana. Kwa mujibu wa uwezekano mwingine, hata haki zao za msingi zinatofautiana. Mume ana haki na majukumu fulani na mke ana haki na majukumu yake fulani. Halikadhalika kwa baba, mama na mtoto.

Katika hali yoyote ile jamii ya kifamilia ni tofauti kabisa na taasisi nyingine za kijamii. Ni uwezekano huu, ambao kwawo dhana ya kutofanana kwa haki kati ya mwanamke na mwanaume imejengwa, na ambayo imekubaliwa na Uislamu. Sasa hebu tuangalie ni uwezekano upi kati ya aina hizi mbili hapo juu ni sahihi, na ni jinsi gani tunaweza kujua usahihi wake. Madai ya asili ya haki za kifamilia. Ili kufikia katika hitimisho sahihi wasomaji wanashauriwa kuzingatia nukta zifuatazo ambazo tayari tumeshazijadili katika suala hili: Haki za asili zimeibuka kutokana na ukweli kuwa maumbile yana lengo lililo wazi, na kuzingatia lengo hilo katika mtazamo, maumbile yamejaalia viumbe vyote hai uwezo fulani na kuweka juu yao haki fulani.

Mwanadamu kama alivyo anafaidi haki fulani zijulikanazo kama haki za binadamu, haki ambazo wanyama hawazifaidi. Ili kuzijua haki za asili na sifa zake, tunapaswa kuyatazama maumbile yenyewe. Kila uwezo wa asili ni mamlaka kwa ajili ya haki ya asili. Wanaadamu wote, kama wanajamii, wana haki za asili sawa na zinazofanana, lakini wanatofautiana katika haki walizojipatia wenyewe ambazo zinategemeana na kazi zao, sifa zao na ushiriki wao katika ushindani wa maisha. Sababu ambayo kwa nini wanaadamu wote katika jamii wana haki sawa na zinazofanana ni kwamba uchunguzi wa masuala ya wanaadamu umeweka wazi kuwa hakuna aliyezaliwa akiwa bwana mkubwa au akiwa na cheo cha chini, akiwa mwajiri au mwajiriwa, akiwa mtawala au mtawaliwa, au akiwa kamanda au askari wa kawaida.

Maisha ya mwanadamu ni tofauti na yale ya wanyama wanaopenda kushirikiana kama vile nyuki. Muundo wa maisha ya mwanadamu haukuamuliwa na maumbile wala maumbile hayakuwapangia watu kazi na vyeo mbali mbali. Nadharia ya kufanana kwa haki za kifamilia za mwanaume na mwanamke imejengwa juu ya dhana kuwa jamii ya kifamilia (wanafamilia) ni kama jamii nyingine ya watu. Wanafamilia wote wanaishi kwa uwezo sawa na mahitaji sawa. Maumbile yamewapa haki zinazofanana. Sheria ya maumbile haijawapangia muundo fulani maalumu, wala haijawapangia kazi na majukumu mbali mbali.

Ama nadharia ya kutofanana kwa haki za familia imejengwa juu ya dhana kuwa jamii ya kifamilia ni tofauti na jamii nyinginezo za kiraia. Mwanaume na mwanamke hawana uwezo na mahitaji sawa. Sheria ya uumbaji imewaweka katika nafasi zinazotofautiana na imepanga majukumu tofauti kwa kila mmoja. Sasa hebu tunagalie ni nadharia gani ni sahihi na kwa nini. Suala hili linaweza kuamuliwa kirahisi tukitumia kigezo ambacho tayari tumeshakitaja na kama tukitazama uwezo na mahitaji ya jinsia zote mbili, ambazo zinajenga mamlaka ya asili ya kudai haki za asili. Je, maisha ya kifamilia ni ya asili au ya kimkataba? Tumeshataja hapo awali kuwa kuna mitazamo miwili juu ya maisha ya kijamii ya mwanadamu. Baadhi wanaamini kwamba kwa asili mwanadamu ni jamii kwa maumbile, ambapo wengine wanashikilia kuwa maisha ya kijamii ni suala la kimkataba na maisha haya yamechaguliwa na mwanadamu kwa hiari yake chini ya ushawishi wa vipengele vinavyolazimisha. Lakini vipengele hivi ni vya nje sio vya ndani.

Hata hivyo, kama ambavyo maisha ya kifamilia yahusikavyo, hakuna mtazamo zaidi ya mmoja. Wote wanakubali kuwa maisha ya kifamilia ni ya asili kwa asilimia mia moja. Mwanadamu amezaliwa akiwa mwanafamilia kwa asili. Hakuwezi kuwa na rai mbili juu ya hili. Hata baadhi ya wanyama, kama vile njiwa na baadhi ya wadudu ambao wanaishi kwa jozi, japo hawaishi maisha ya kijamii kabisa lakini wana aina fulani ya ndoa. Hivyo, suala la maisha ya kifamilia ni tofauti na maisha ya kijamii. Maumbile yamechukua hatua fulani kuhakikisha kuwa mwanadamu na baadhi ya wanyama kwa silika wanakuwa na mwelekeo wa kupenda kuishi maisha ya kifamilia, kuunda familia na kuwa na watoto. Maisha ya mwanadamu wa kale, yawe ni ya kurithi mfumo jike au mfumo dume, lakini wakati wote aliishi maisha ya kifamilia. Nadharia ya vipindi vinne.

Kuhusiana na suala la umiliki wa mali jambo hili linakubaliwa na wote kuwa awali mali ilimilikiwa na jamii nzima (kwa pamoja) na kwamba kumiliki mali mtu mmoja mmoja kulikuja baadaye. Lakini hilo halijawahi kuwa suala la jinsia. Sababu ya umiliki mali binafsi mwanzoni kuwa na kipengele cha kijamii ni kwamba maisha wakati ule yalikuwa ni ya kikabila na kabila zima liliunda familia moja. Wanakabila ambao walikuwa wakiishi pamoja walikuwa na mawazo ya kuishi katika familia moja. Ndio maana mali ilikuwa ikimilikiwa na kabila zima. Katika jamii duni za kale hapakuwa na sheria wala mila ambayo ingeamua jukumu la mwanaume na mwanamke. Yalikuwa ni maumbile tu na hisia za asili ambazo ziliwafanya watekeleze majukumu fulani na waheshimu haki fulani. Hata katika hali hii hawakujiingiza katika ngono holela. Vile vile wanyama wale waliokuwa wakiishi katika jozi, japo hawakuwa na sheria ya kimkataba au kijamii walizingatia sheria ya asili ya haki na majukumu, na hivyo maisha yao ya ngono sio ya holela.

Mrs. Mehr Angiz Manuchehriyan katika dibaji ya kitabu chake, 'Maoni juu ya katiba na sheria ya kiraia ya Iran' anasema: Kwa mtazamo wa kisosholojia maisha ya mwanaume na mwanamke katika sehemu mbali mbali za dunia yanapitia katika moja ya hatua hizi nne. Hatua ya asili Hatua ya mwanaume kumtawala mwanamke hatua ya mwanamke kupinga kutawaliwa na mwanaume Hatua ya usawa wa haki kati ya mwanaume na mwanamke. Anaendelea kusema kuwa katika hatua ya mwanzo mwanamke na mwanaume walikuwa wanachanganyika bila kizuizi chochote. Sosholojia haikubaliani na mtazamo huu kabisa.

Kama kuna kikubwa zaidi sosholojia inachokikubali ni kuwa ilikuwa ni mila katika baadhi ya makabila duni (ya kijima) kwamba makaka kadhaa kwa pamoja walioa madada kadhaa. Na hao makaka wote walikuwa wakiwaingilia madada wote mchanganyiko na watoto walikuwa ni wa wote. Mila nyingine ni kuwa wavulana na wasichana kabla ya ndoa hawana kizuizi. Ni ndoa tu inayowawekea kizuizi. Hizi ni mila mbili tu zinazojulikana. Hata hivyo, kama kuna kabila la kijima linalokwenda zaidi ya mipaka hii na linaruhusu ngono holela basi suala lake ni la kipekee na sio la kawaida.

Will Durant katika kitabu chake, 'History of Civilization' Jalada la kwanza, anasema 'Ndoa ni ugunduzi wa wahenga (mababu) wetu waliokuwa wanyama. Katika baadhi ya ndege inaonekana kuwa ni ukweli kuwa kila ndege hubaki kushikamana na mke/mume wake maalum. Miongoni mwa sokwe na jamii ya nyani wakubwa kujamiiana kati ya dume na jike huendelea hadi mtoto aliyezaliwa anapokuwa mkubwa. Katika mambo mengine uhusiano huu unafanana na uhusiano kati ya mwanaume na mwanamke (watu). Jike linapojaribu kujisogeza kwa dume jingine, hufokewa vikali na lile dume -mume. Jamii ya nyani wanaishi katika familia yenye dume, jike na mtoto.

Ni kawaida kwa sokwe, baba na mama (sokwe) kukaa chini ya mti kula matunda wakati mtoto anakwea miti jirani yao. Historia ya mahusiano ya unyumba ni kongwe kuliko mwanadamu mwenyewe. Kuna jamii chache ambazo hazina mahusiano ya unyumba. Hata hivyo, mtu akijaribu kuzitafuta anaweza kupata chache sana. Tunachosisitiza hapa ni kuwa hisia za kifamilia ni za asili na za silika kwa wanaadamu, na sio zao la ustaarabu na tabia. Kuna wanyama wengi pia wenye hisia kama hizi kisilika. Hii ndio sababu, hakuna wakati wowote katika historia ambapo wanaume na wanawake waliishi pamoja bila kuwekeana mipaka ya ngono.

Hata wale wanaodai kuwepo kwa ukomunisti wa kifedha katika zama za ujima hawadai kuwepo kwa ukomunisti wa ngono. Nadharia ya vipindi vinne vya mahusiano ya mwanaume na mwanamke ni muigizo wa kitoto wa vipindi vinne vya umiliki wa mali, ambavyo wajamaa wanaamini. Wanashikilia kuwa katika suala la kumiliki mali, mwanadamu amepitia vipindi vinne, kipindi cha ujima, ukabaila, ubepari na ujamaa wa kisayansi, ambao ni kurudia kwa ujima lakini katika kiwango cha juu. Inachekesha kuona kuwa Mrs. Manushehriyan anakiita kipindi cha nne uhusiano kati ya mwanaume na mwanamke kuwa ni kipindi cha usawa wa haki na hakiiti kuwa ni kurudi kwa ujima. Katika hili hakufuata mfano wa wajamaa, ingawa anadai kuwa kuna mambo mengi yanayofanana kati ya kipindi cha nne na kipindi cha kwanza. Anasema kuwa kipindi cha nne kinafanana na kipindi cha kwanza kwa sababu katika zama zote hizi mbili mwanaume na mwanamke waliishi bila yeyote kati yao kuwa na madaraka juu ya mwenzake.

Bado hatuelewi anachokimaanisha hasa pale anaposema vipindi hivi (cha kwanza na cha nne) vinafanana kwa kiasi kikubwa. Kama anamaanisha kuwa katika kipindi cha nne vipingamizi vya kuchanganyika kiholela pole pole vitaondoka na familia haitakuwepo tena basi anachomaanisha juu ya usawa wa haki ambao yeye ni mtetezi wake mkubwa, ni tofauti kabisa na kile watetezi wengine wa haki za binadamu wanachokidai na wazo lake hili linaweza hata kuwakera wengine. Sasa hebu tugeuzie macho yetu kwenye asili ya hali za kifamilia za mwanaume na mwanamke. Katika hili lazima tuzingatie mambo mawili kichwani. Moja ni iwapo asili (maumbile) ya mwanamke ni tofauti na mwanaume au la kwa maneno mengine, kuangalia kama tofauti kati ya mwanaume na mwanamke ipo katika mfumo wa uzazi tu, au ina kwenda ndani zaidi.

Nukta ya pili ni kuwa iwapo kuna tofauti nyingine pia, je tofauti hizi zinaathiri haki na majukumu yao au la, au ni kama tofauti ya rangi na utaifa, mambo ambayo hayana uhusiano wowote na asili ya haki za binadamu? Mwanamke katika maumbile Kuhusiana na nukta ya kwanza, hatudhani kwamba ina ubishi. Kila mtu aliyesomasoma juu ya suala hili anajua kuwa tofauti kati ya mwanamke na mwanaume haibakii katika mfumo wa uzazi tu. Suala hapa ni iwapo tofauti hizi zinasababisha katika haki na majukumu yao au la. Wanasayansi na wachunguzi wa kizungu wameifanyia utafiti mkubwa nukta hii, na matokeo ya utafiti wao wa kibailojia, kisaikolojia na kisosholojia hayajaacha chembe yoyote ya shaka juu ya ukweli huu. Lakini ambacho wasomi hawa hawajakitupia macho vya kutosha ni kuwa tofauti hizi kati ya mwanamke na mwanaume zinasababisha kutofanana kwa haki zao na majukumu ya kifamilia, na kuwa tofauti hizi zinawaweka katika nafasi zinazofanana.

Msomi mashuhuri duniani wa kifaransa ambaye ni mwanasaikolojia, daktari wa upasuaji na mwanabaiolojia, Alexis Carrel, katika kitabu chake bora kabisa, 'Man, the Unkown being' (mwanadamu kiumbe asiyefahamika), anakiri kuwa, kwa mujibu wa sheria ya maumbile, mwanaume na mwanamke wameumbwa tofauti na kwamba tofauti zao zinafanya haki na majukumu yao kuwa tofauti. Katika kitabu chake ameweka sura moja yenye jina "Kazi za Kijinsia na Jenetiksi" katika sura hiyo anasema; korodani na ovari zina kazi nyingi sana. Viungo hivi havizalishi mayai na mbegu za uzazi na hivyo muungano wake kusababisha kuzaliwa kwa binadamu mpya peke yake, lakini pia huzalisha uowevu (fluid) ambao humwagwa katika damu na hivyo husababisha tabia za kike na kiume katika hisia zetu na katika tishu na viungo vyetu vya mwili.

Ni uoevu unaozalishwa na korodani ambao husababisha ukakamavu, ushujaa, moyo (thabiti) na kutoogopa. Ni sifa hizi zinazomtofautisha ng'ombe maksai na fahali. Ovari pia humuathiri mwanamke hivyo hivyo. Tofauti zilizopo kati ya mwanaume na mwanamke hazihusiani pekee na sura ya viungo vyao vya uzazi au mwanamke kuwa na tumbo la uzazi na kujifungua watoto na mfumo wao maalum wa elimu, bali ni matokeo ya sababu kubwa zaidi. Inatokana na kemikali zinazozalishwa na tezi za uzazi na kumwagwa katika damu.

Ni kutokana na kuipuuza nukta hii muhimu ndio baadhi ya watetezi wa harakati za wanawake wanafikiri kuwa jinsia zote mbili zinaweza kupata aina moja ya elimu na mafunzo na wanaweza kuchukua elimu na mafunzo ya aina moja na wanaweza kusomea aina moja ya fani/kazi na majukumu yanayofanana. Kwa kusema kweli mwanamke anatofautiana na mwanaume katika mambo mengi. Kila seli ya mwili wa mwanadamu na mifumo yote ya ogani, hasa mfumo wa misuli, ina alama ya jinsia. Sheria za fiziolojia pia, kama za unajimu ni thabiti na hazibadiliki. Tabia za watu haziwezi kuzibadilisha.

Tunapaswa kujaribu kuendeleza vipaji vyao katika mwelekeo unaoafikiana na haiba yao ya ndani, bila kuwaiga wanaume kibubusa. Ni jukumu lao kutoa mchango mkubwa zadi kuliko mwanaume katika maendeleo ya mwanadamu. Wasiyachukulie majukumu yao kiwepesi. Carrel, baada ya kuelezea kukua kwa manii na mayai na jinsi muungano wao unavyotokea anaonyesha kuwa kuwepo kwa mwanamke ni muhimu kwa uzazi lakini sio kuwepo kwa mwanaume.

Anaongeza kuwa mimba huukamilisha mwili na roho ya mwanamke. Mwisho wa sura anasema tusiwatazame/tusiwachukulie wasichana wadogo kwa mtazamo wa kufikiri aina moja ya maisha na namna moja ya ndoto na namna moja ya ukamilifu wao kama wavulana wadogo. Wataalamu wa masuala ya elimu na mafunzo wazingatie tofauti zao za ogani na kifiziolojia na majukumu ya asili ya mwanaume na mwanamke.

Zingatio la nukta hii ya msingi ni muhimu sana kwa mustakabali wa ustaarabu wetu. Kama ulivyoona, mwanasayansi huyu mkubwa anaweka msisitizo katika tofauti nyingi zilizopo kati ya mwanamke na mwanaume na anaamini kuwa tofauti hizi zinawaweka katika nafasi tofauti. Katika sura inayofuata pia, tutanukuu maoni ya wanasayansi juu ya nukta hii, na kisha tutafikia hitimisho kuwa ni maeneo gani ambayo mwanaume na mwanamke wana uwezo na mahitaji sawa na hivyo wanastahili haki na majukumu yanayofanana na ni katika maeneo gani wana nafasi tofauti na hivyo haki na majukumu yasiyofanana. Sehemu hiyo ya kitabu itakuwa muhimu sana kuliko nyingine zote juu ya somo na upangaji wa haki na majukumu ya kifamilia kati ya mwanaume na mwanamke.

7

HAKI ZA WANAWAKE KATIKA UISLAMU

TOFAUTI KATI YA MWANAMKE NA MWANAUME

Hii inaonekana kuwa sentensi isiyofaa. Inaonekana kuwa japo tupo katika karne hii, bado kuna baadhi ya watu, hapa na pale, ambao wana mawazo ya kizamani, na bado wanang'ang'ania wazo lililopitwa na wakati la tofauti kati ya mwanaume na mwanamke. Kama watu wa zama za kati (1500 A.D), watu hawa bado wanamuona mwanamke kuwa wa jinsia ya cheo cha chini na kwamba sio mwanadamu kamili na kamilifu. Yupo katikati si binaadamu wala si mnyama.

Hafai kuishi maisha ya kujitegemea na lazima aishi chini ya uangalizi na udhibiti wa wanaume. Lakini sasa tunajua kuwa mawazo yote haya yamepitwa na wakati na hayafai. Leo hii tunajua fika kuwa dai potofu la kudaiwa kuwa mwanamke sio mkamilifu lilizushwa na mwanaume katika enzi zile ambazo alikuwa anamtawala mwanamke. Sasa, habari iliyothibitishwa ni kwamba mwanamke anatokana na jinsia bora zaidi na mwanaume anatokana na jinsia duni. Haya hi maoni ya baadhi ya wa magharibi wa kisasa.

Kwa ukweli kabisa, maendeleo ya sayansi ya karne ya 20 yamethibitisha wazi wazi kuwepo kwa tofauti kati ya mwanaume na mwanamke. Kuwepo kwao sio uwasilishaji mbaya wa kijicho, bali ni ukweli wa kisayansi, uliotokana na uchunguzi na majaribio. Hata hivyo tofauti hizi hazipo ili kuthibitisha ni jinsia gani ni bora kuliko nyingine. Sheria ya maumbile imeziweka tofauti hizi ili mahusiano ya ndoa yawe imara zaidi na kuufanya msingi wa muungano kati ya mume na mke uwe mkubwa, imara na bora zaidi.

Maumbile yalitaka kugawa haki za kifamilia na majukumu yake baina yao kwa mikono yake (maumbile) yenyewe. Sheria ya maumbile umezifanya tofauti kati ya mwanaume na mwanamke sawa na tofauti ya viungo mbali mbali vya mwili. Imetoa nafasi mbali mbali kwa macho, masikio, mikono, nyayo na uti wa mgongo. Lakini haimaanishi kuwa imefanya dhulma na ubaguzi dhidi ya kiungo chochote.

Je ni uwiano au ukamilifu na kutokamilika? Inashangaza kwamba baadhi ya watu wanasisitiza kuwa tofauti katika nguvu za kimwili na kisaikolojia za mwanaume na mwanamke hutokana na ukamilifu wa mwanaume na kutokamilika kwa mwanamke. Wanashikilia kuwa, kwa sababu fulani nzuri, kwa makusudi kabisa mwanamke ameumbwa akiwa sio mkamilifu. Dhana ya kutokuwa mkamilifu kwa mwanamke imekuwa maarufu zaidi katika nchi za Magharibi kuliko Asia. Watu wa Magharibi wamemuonea. Wakati fulani wamekuwa wakitoa tafsiri mbaya ya maandiko ya kidini juu ya mwanamke, wanasema kwamba mwanamke ajione haya.

Wakati fulani wanasema, 'Mwanamke ni kiumbe mwenye nywele ndefu na ubongo usiofaa,' 'mwanamke ni nusu ya mnyama na nusu ya mtu'n.k. Bado inashangaza zaidi kuona kwamba baadhi ya watu wa Magharibi wamebadilisha mwelekeo wao kwa nyuzi 180, hivi karibuni wameanza kuleta hoja elfu na moja kuthibitisha kwamba kwa mujibu wa maumbile, mwanaume ni duni na sio mkamilifu na kwamba jinsia ya mwanamke ni bora na mkamilifu.

Kama umeshakisoma kitabu, "Woman, the Superior Sex,' cha Ashley Montague, unaweza kuona ni jinsi gani mwandishi huyu, kwa kupotosha ukweli na kuleta hoja zisikubaliana na ukweli alivyojaribu kuthibitisha kuwa mwanamke ni mkamilifu zaidi kuliko mwanaume. Katika fani za utabibu, saikolojia na takwimu za jamii kitabu hiki kinafaa sana, lakini pale mwandishi anapojaribu kutoa hitimisho lake kuthibitisha dai lake, ambalo ndio jina la kitabu anakwenda kwenye upuuzi mkubwa kabisa. Haifahamiki kwa nini ni lazima kwa watu wa Magharibi kwamba siku moja wamuumbue mwanamke na kumuadhiri ili siku ya pili warekebishe yale ya nyuma, wanalazimika kumuondolea mapungufu na udhaifu waliokuwa wamembandikia na badala yake wanambandikia hayo mwanaume.

Kuna umuhimu gani wa kuangalia tofauti kati ya mwanaume na mwanamke kwa matokeo ya ukamilifu wa jinsia mmoja na upungufu wa jinsia nyingine, ili kwamba wakati mwingine tulazimike kumuweka mwanaume upande na wakati mwingine mwanamke? Mwandishi wa kitabu hiki anasisitiza kuwa mwanamke ni bora kuliko mwanaume na anaona kuwa utukufu alionao (mwanaume) ni matokeo ya sababu za kihistoria na kijamii na sio matokeo ya sababu za asili. Kwa kusema kweli, tofauti kati ya mwanaume na mwanamke ni suala la uwiano sio ukamilifu na kutokamilika.

Sheria ya maumbile imeamua kuwa kwa kuwa mwanaume na mwanamke wameumbwa ili waishi pamoja, lazima wawe na uwiano mahususi wa vipaji vyao licha ya tofauti hizi. Nukta hii itafafanuliwa baadaye. Nadharia ya Plato. Suala la tofauti kati ya mwanamke na mwanaume sio jipya ambalo tunaweza kusema kuwa limeibuka katika zama zetu. Lina umri wa miaka zaidi ya 2400. Lilijadiliwa katika sura yake ya sasa, na Plato katika kitabu chake 'The Republic'. Kwa uwazi anaelezea kwamba wanaume na wanawake wana vipaji sawa, na wanawake wanaweza kufanya kazi za kiume na kupata haki kama zile za wanaume. Chanzo cha mawazo yote kuhusu mwanamke, ambayo yameibuka katika karne ya 20, na hata sehemu ya mawazo haya yanayoonekana kuwa ya ovyo na yasiyobadilika kwa watu wa karne ya 20, yamo katika mitazamo ya Plato.

Hii ndio sababu watu wanavutiwa naye sana na kumuita 'Baba wa falsafa'. Plato katika sura ya tano ya kitabu chake, 'The Republic' alizungumzia masuala kama vile ukomunisti wa wanawake na watoto, kuboresha kizazi (breed), kuwa hasi baadhi ya wanaume na wanawake, kuwaruhusu kuzaa wale tu wenye sifa zilizotukuka za kijenetiki, kulea watoto nje ya mazingira ya kifamilia na kuruhusu kuzaa katika miaka fulani tu ya uhai, katika kipindi ambacho nguvu (za uzazi) zipo kileleleni. Plato anaamini kuwa kama ilivyo kwa mwanaume, mwanamke anapaswa kupewa mafunzo ya kijeshi na kama mwanaume anavyoshiriki katika riadha, mwanamke ashiriki pia.

Hata hivyo, kuna mambo mawili ambayo Plato ameyasema. Moja ni kuwa anakiri kuwa kimwili na kiakili wanawake ni dhaifu kuliko wanaume. Kwa maneno mengine anaiona tofauti kati ya mwanaume na mwanamke kuwa ni ya kiasi (ukubwa), sio sifa (ubora) wa vipaji vyao. Anaamini kuwa wote mwanaume na mwanamke wana vipaji. Kitu pekee ni kuwa katika baadhi ya mambo mwanamke ni dhaifu kuliko mwanaume, lakini haoni sababu kwa nini awe na mfumo wa kipekee wa kuendesha mambo. Kwa vile Plato anamuona mwanamke kuwa dhaifu kuliko mwanaume, anamshukuru Mungu kuwa alizaliwa mwanaume. Anasema; "Namshukuru Mungu kwa kuzaliwa kwangu Mgiriki (myunani) na sio vinginevyo, kwa kuzaliwa kwangu nikiwa huru na sio mtumwa na kuzaliwa kwangu mwanume na sio mwanamke." Nukta ya pili ni kuwa yote aliyoyasema Plato ya kuhusu kuboresha ukoo (uzazi), vipaji vya jinsia zote mbili na ukomunisti wa mwanamke na watoto yanahusiana na tabaka tawala, yaani wanafalsafa watawala, kwa sababu kwa mujibu wake, ni tabaka hili tu ndio linafaa kuwa watawala.

Kama tunavyojua kisiasa, Plato alikuwa ni mpinga demokrasia na alikuwa akitetea utawala wa matabaka. Hivyo, alichokisema katika nukta hizo, kinahusiana na tabaka tawala. Kuhusiana na matabaka mengine, ana maoni tofauti. Aristole dhidi ya Plato. Mwanafunzi wa Plato, Aristole ni mwanafikra mwingine wa ulimwengu wa kale, ambaye maoni na mawazo yake tunayo. Ametoa maoni juu ya tofauti kati ya mwanamke na mwanaume na ameyapinga vikali maoni ya mwalimu wake. Anaamini kuwa mwanaume na mwanamke wanatofautiana sio kwa kiasi tu bali hata kwa sifa. Anasema kwamba jinsia hizi mbili zina vipaji vya aina tofauti na majukumu waliyopewa na sheria ya maumbile na haki walizopewa, vyote vinatofautiana sana. Kwa mujibu wa Aristole, kanuni zao za maadili pia zinatofautiana katika mambo mengi. Inawezekana kuwa sifa ya maadili ikawa bora kwa mwanaume lakini isiwe hivyo kwa mwanamke na kinyume chake.

Katika ulimwengu wa kale maoni ya Plato yaliondolewa, yakachukuliwa ya Aristole. Wasomi waliofuatia walipendelea maoni ya Aristole kuliko ya Plato. Mtazamo wa ulimwengu wa sasa. Hayo yalikuwa ya ulimwengu wa kale. Sasa hebu tuangalie ulimwengu wa sasa unavyosema. Ulimwengu wa sasa haubahatishi wala kukadiria. Unatumia njia za kisayansi. Hitimisho zake zimejengwa juu ya ukweli, takwimu na utafiti katika ulimwengu wa sasa.

Kama matokeo ya elimu kubwa na sahihi zaidi katika medani za utabibu, saikolojia na maarifa ya jamii, tofauti nyingi na kubwa, zaidi kati ya mwanamke na mwanaume, zilizokuwa hazijulikani katika ulimwengu wa kale, sasa zimegunduliwa. Watu wa kale walitathimini mwanaume na mwanamke kwa msingi wa kuwa mmoja ni mwenye kukwaruza sana, mrefu ana nywele nyingi zaidi mwilini, ana maungo makubwa zaidi na ana sauti nene zaidi wakati mwingine ana mwili nyororo zaidi, mfupi zaidi, na msafi zaidi, ana sauti nyembamba zaidi na ana maungo madogo zaidi. Waliozama zaidi walizingatia tofauti ya umri wao wa kukua (kubalehe na kuvunja ungo) na tofauti ya akili na hisa zao.

Walimchukulia mwanaume kama alama ya busara, na mwanamke kama alama ya upendo na mihemko. Lakini leo tofauti nyingi zaidi zinajulikana sasa kwamba ulimwengu wa mwanamke ni tofauti na ulimwengu wa mwanaume katika mambo mengi. Kwanza tutasimulia tofauti kati ya mwanaume na mwanamke, kwa mujibu wa tulivyozikusanya kutoka kwa wataalamu mabingwa wa fani hii. Kisha tutaeleza falsafa yake na tutaonyesha tofauti zipi ni za asili na zipi ni matokeo ya kihistoria, kiutamaduni na vipengele vya kijamii. Baadhi ya tofauti hizi ziko wazi mno kiasi cha kuwa huwezi kuzikana. Elimu ya wengine (juu ya hili) inaweza kupatikana kwa kusoma kidogo na uzoefu.